Articles by "MWENGE2022"
Showing posts with label MWENGE2022. Show all posts

 


Na Mwandishi wetu ,Mbeya


MBUNGE wa  Jimbo la Lupa Wilayani Chunya ,Masache Kasaka amesema kuwa  uwepo  wa Mwenge wa uhuru  wilayani humo umeleta fursa za kiuchumi kwa wananchi na wafanyibiashara katika kuchochea maendeleo katika kufanya shughuli mbali mbali  ambazo huwaongezea kipato.

Kasaka amesema hayo jana` wakati  akizungumza na  mtandao huu mara baada ya kukabidhi Mwenge wa uhuru kwa  Wilaya ya Mbeya  Mjini ukitokea wilaya ya Chunya .

Mbunge huyo amesema kuwa mara nyingi Mwenge wa uhuru unapokuja unachochea maendeleo kwa wilaya ya chunya hivyo ni fursa tosha kwa kila mtu mwenye uwezo kuweza kufanya ujasiliamali wa aina mbali mbali .

“Mwenge wa uhuru ulifika Chunya Septemba nane mwaka huu na kupita miradi yote ya maendeleo  kwa kuanzia kata ya Chalangwa kuzindua Zahanati ya Itumba ambayo tayari imeanza kufanya kazi kuna baadhi ya vitu vichache vilivyoonekana vimetolewa maelekezo na kufanyiwa kazi  na mradi mwingine wa Sangambi  kuzinduliwa na wananchi wameanza kutumia maji ,maeneo mengine ni sehemu ya miundo mbinu”amesema Mbunge Masache.

Kasaka amesema kwamba mradi wa Daraja la Nselele ambalo daraja hilo kwa kipindi kirefu kulikuwa na changamoto hasa kipindi cha mvua kulikuwa na changamotio  wananchi walikuwa wanashindwa kupita na watu kadhaa walifariki kipindi cha mvua hivyo kwa ujumla Mwenge umepita vizuri hakukuwa  na shida yeyote mpaka kukabidhiwa wilaya ya Mbeya mjini .

Hata hivyo Kasaka alitaja miradi iliyozinduliwa kuwa ni minne ambapo kati hiyo , mradi mmoja  ulitembelewa  na kuwa mradi kwanza  ni Zahanati , Maji ,Daraja pamoja  na kiwanda cha kuchenjua dhahabu.

Rose Akimu ni mkazi Itumba amesema ujio wa Mwenge wa Uhuru mara nyingi wananchi walio wengi hasa wanawake hujishughulisha masuala ya ujasiliamali wa kupika chakula ambao huwapatia kipato cha kuendesha maisha yao,


“Wanawake tukipata taarifa kutoka kwa viongozi wa maeneo yetu huwa tunafurahi uwepo wa Mwenge wa uhuru maana baadhi yetu tuna vikundi ambavyo hutusaidia kufanya ujasiliamali wa pamoja siku ya mkesha wa Mwenge ,hivyo tunawaambia wanawake wenzetu ambao hawajishughulishi wafanye hivyo pindi Mwenge unapokesha kwenye maeneo yao wafanye biashara wasibweteke kusubiri kupewa fedha na waume zao “amesema Akimu.




Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma, akiweka Jiwe la Msingi katika ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Ushetu.

Na Marco Maduhu, USHETU

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma, amezindua na kuweka jiwe la msingi kwenye Miradi ya maendeleo Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama.

Mwenge huo wa Uhuru umekimbizwa jana Julai 31, 2022 katika Halmashauri ya Ushetu umbali wa Kilomita 70 na kupitia Miradi ya maendeleo Mitano yenye thamani ya Sh. bilioni 1.2.

Akizungumza wakati uzinduaji na kuweka mawe ya Msingi kwenye Miradi hiyo ya maendeleo, Geraruma  amepongeza utekelezaji wake, na kubainisha kuwa ile ambayo ameitolea maagizo ukamilishwe haraka na kutoa huduma bora kuwa wananchi.

"Kuna baadhi ya Miradi ambayo nimeitolea maagizo ya kufanyiwa marekebisho naomba utekelezaji wake ufanyike haraka sana," amesema Geraruma.

Katika hatua nyingine Geraruma, amewasisitiza Wananchi wa Ushetu, kuwa siku ya kuhesabiwa Sensa ya watu na Makazi Agost 23 mwaka huu wajitokeze kwa wingi kuhesabiwa na kutimiza Malengo ya Serikali kupata idadi ya watu kamili.

Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, Lino Pius Mwageni, amesema Mwenge huo wa Uhuru ,utazindua ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa katika Shule ya Sekondari Dakama.

Ametaja Miradi mingine ambayo umewekewa Jiwe la Msingi, kuwa ni ujenzi wa Barabara ya Nyamilangano kwa kiwango cha Lami Kilomita Moja, Utanuzi wa Mradi wa Majisafi na salama.

Miradi mingine ni uwekaji Msingi ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Ushetu, pamoja na kiwanda kidogo cha kuchakata nafaka kilichopo Uyogo.

Aidha, Mwenge huo wa Uhuru ukiwa mkoani Shinyanga kuanzia Julai 26 mwaka huu, umepitia Jumla ya Miradi ya Maendeleo 38 yenye thamani ya Sh. bilioni 43.1 ambapo leo umekabidhiwa Mkoani Tabora.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma akizungumza wakati wa kupitia Miradi ya Maendeleo.

Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga akizungumza kwenye Mbio za Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Ushetu.

Mbunge wa Jimbo la Ushetu Emmanuel Cherehani akizungumza kwenye Mbio za Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Ushetu.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma akizundua Mradi wa vyumba vya Madarasa katika Shule ya Sekondari Dakama.

Vyumba vya Madarasa katika Shule ya Dakama Halmashauri ya Ushetu.

Ukaguzi ukiendelea katika vyumba vya Madarasa katika Shule ya Sekondari Dakama.

 

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma akizindua Mradi wa Maji katika kijiji cha Bugwandege Manispaa ya Shinyanga, ambao umetekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA).

Na Marco Mduhu, SHINYANGA

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa  Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma, amefungua  Mradi wa Maji katika kijiji cha Bugwandege Manispaa ya Shinyanga, ambao umewaondolea wananchi adha ya kutumia Maji Machafu.
 
Mradi  uliotekelezwa na SHUWASA  chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko -19 umefunguliwa  Julai 27, 2022.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Shinyanga (SHUWASA) Mhandisi Yusuph Katopola, amesema walipokea fedha za UVIKO-19 jumla ya Sh. milioni 469 kwa ajili ya kutekeleza Miradi mbalimbali ya Maji kwa Wananchi wa Bugwandege, Magwata, Bugimbagu, Didia na Iselamagazi  lakini wametumia Sh.milioni 406 na Miradi yote inatoa huduma ya Majisafi kwa wananchi, ukiwemo mradi huu  wa Bugwandege ambao utanufaisha wananchi 6,900 na kwa Maeneo yote idadi ya wanufaika ni 21,536.
 
Naye Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, amesema Mradi huo wa Maji safi na Salama umekuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi hao wa Bugwandege, ambao wameondokana na adha ya kutumia maji machafu pamoja na hofu ya Wanyama wakali kwa kufuata maji umbali mrefu.
 
“Tumpongeza Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kwa kutuletea pesa hizi na kutekeleza miradi ya Maji safi na salama kwa wananchi na sasa mnakunywa Maji safi,”amesema Mboneko.
 
Aidha, Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu, amesema kipindi cha kampeni cha uchaguzi mkuu mwaka 2020 waliahidi kupeleka Maji kijijini humo lakini sasa maji yapo na kumpongeza Rais Samia kuitekeleza ilani ya uchaguzi kwa vitendo.
 
Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022 Sahili Nyanzabara Geraruma, ameupongeza Mradi huo na kutoa msemo kuwa popote mama alipo Maji yamemfikia na kumtua ndoo kichwani.
 
Pia ametoa wito kwa wananchi wa kijiji hicho cha Bugwandege kuitunza miundombinu ya mradi huo wa maji, pamoja na kuvuta maji majumbani mwao na kuacha kuchota kwenye vituo vya kuchotea maji.
 
Kauli Mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu (2022) inasema “Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo, Shiriki kuhesabiwa kwa Maendeleo ya Taifa.

 

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma, akizungumza alipofika kuzindua Mradi wa Maji safi na Salama katika Kijiji cha Bugwandege Manispaa ya Shinyanga, uliotekelezwa na (SHUWASA).
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza kwenye uzinduzi wa Mradi wa Maji kijiji cha Bugwandege.

Mkurugenzi Mtendaji wa (SHUWASA) Mhandisi Yusuph Katopola, akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Maji katika kijiji cha Bugwandege na miradi mingine ambayo inatokana na fedha za UVIKO-19.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma, (kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa (SHUWASA) Mhandisi Yusuph Katopola.

Ukaguzi Mradi wa Maji ukiendelea katika Kijiji cha Bugwandege.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma akizundua Mradi wa Maji katika kijiji cha Bugwandege Manispaa ya Shinyanga, ambao umetekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA).
Wajumbe wa Bodi Mamlaka ya Maji Shinyanga (SHUWASA) wakishuhudia uzinduzi wa Mradi wa Maji katika Kijiji cha Bugwandege-Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

 


KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2022,Sahili Geraruma amewataka viongozi kusimamia na kufuatilia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

Kauli hiyo ameitoa wakati mwenge huo ukiwa wilayani Karatu mkoani Arusha kuzindua, kutembelea na kuweka mawe ya msingi katika baadhi ya miradi.

Bw. Geraruma alisema kuwa, kumekuwa na tabia iliyozoeleka kwa baadhi ya viongozi wa Serikali hasa idara ya manunuzi kwa kuidhinisha fedha kwa ajili ya miradi bila ufuatiliaji ili kujua matumizi halali ya fedha zilizoidhinishwa jambo ambalo husababisha miradi mingi kuwa chini ya kiwango.

Alisema kuwa, ni jukumu la wataalamu kutembelea miradi mara kwa mara ili kujua ubora wake na kuweza kurekebisha kabla mradi haujafia mbali kuepuka miradi isiyo na tija.

Kiongozi huyo wa mbio za mwenge aliwataka madiwani pamoja na uongozi mzima wa wilaya kuipa vipaumbele miradi inayoibuliwa na wananchi kwa kutoa michango ili kuwapa moyo wananchi kuchangia miradi.

"Wananchi wanachanga michango wanaanza utekelezaji wa mradi,lakini halmashauri mnakaa muda mrefu kuweka mchango wa halmashauri,"alisema kiongozi huyo.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Dadi Kolimba alisema kuwa Mwenge wa Uhuru wilayani Karatu umeweza kuzindua,kufungua na kuweka mawe ya miradi nane yenye thamani ya shilingi bilioni 3.6 ikiwemo michango ya Serikali Kuu,halmashauri ya wilaya pamoja na nguvu za wananchi.

Alifafanua kuwa, kati ya miradi hiyo miradi miwili ilifunguliwa,mitatu ilizinduliwa na miwili ilitembelewa ambapo mradi moja ulitolewa maelekezo.










Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Mwaka 2022, Sahili Geraruma Ameiagiza Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha pamoja na wataalamu katika halmashauri za mkoa huo kuhakikisha wanatumia namna bora ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye lengo la kuzisaidia jamii.

ametoa maagizo hayo wilayani Monduli wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika shule mpya ya sekondari Mswakini huku akisisitiza wataalamu wa Halmashauri kusimamia vema wakandarasi wanao tekeleza miradi ya Serikali katika maeneo yao.


Ukaguzi pamoja na kuzinduliwa miradi ya maendeleo kwa wananchi na Mwenge wa Uhuru mkoani Arusha unaendelea ikiwa ni kuhakikisha thamani halisi ya fedha inaonekana na huduma iliyokusudiwa inaifikia jamii Kwa wakati.

Hata hivyo kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amemtaka mkandarasi anaye tekeleza mradi wa shule ya sekondari ya Mswakini kuyafanyia kazi mapungufu yote yaliyo jitokeza haraka iwezekanavyo.

kwa Upande wake Mkuu wa wilaya ya Monduli Frank Mwaisumbe amesema amepokea maelekezo ya Mwenge wa Uhuru na ipo tayari kuyafanyia kazi.














 


Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 umeanza kukimbizwa leo katika Halmashauri ya mji wa Babati.

Ukiwa Mjini Babati unatarajiwa kuweka mawe ya msingi Katika miradi mitatu na kuzindua mitatu yenye thamani ya Bilioni 14.6.

Mwenge wa Uhuru mjini Babati utakimbizwa Kwa umbali wa kilomita 87.

Kauli mbiu ya mwenge wa uhuru mwaka 2022 "Sensa ni msingi wa Mipango ya maendeleo,shiriki kuhesabiwa tuyafikie maendeleo endelevu ya taifa".




Na John Walter-Kiteto

Mwenge wa Uhuru Kitaifa umeweka Jiwe la msingi kwenye mradi wa maji  Majengo mapya Kaloleni wilayani Kiteto mkoani Manyara kwa lengo la kuwezesha wananchi kuendelea kupata huduma ya maji safi. 

Mradi huo ambao uliibuliwa na wakala wa maji na usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa kushirikiana na jamii na halmashauri ya wilaya ya Kiteto kutokana na changamoto ya mahitaji ya upatikanaji maji katika kata hiyo, unatekelezwa kupitia fedha za uviko 19 kwa kuchimba kisima chenye urefu wa mita 160 ambao kina uwezo wa kuzalisha maji lita 18,000 kwa saa.

Akiongea wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe hilo kwenye mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa,Sahili Geraruma amesema ameridhika na utekelezaji wa mradi huo na kwamba utanufaisha wakazi wengi wa Kaloleni na maeneo ya jirani.

"Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan anawapenda wakazi wa Kiteto na ndio maana amewezesha mradi huu kutekelezwa kwa kasi ili kumtua mama ndoo ya maji kichwani," amesema

Ameongeza kuwa hii ni sehemu ya nia njema ya Rais Samia aliyonayo ya kuhakikisha wananchi wote wanapata majisafi ipasavyo.

Ameitaka RUWASA kuhakikisha huduma ya maji inakua endelevu na wananchi wanapata majisafi muda wote.

Taarifa kuhusu mradi huo kutoka RUWASA inaeleza kuwa mradi huo umefikia asilimia 89 ya utekelezaji na unatarajia kukamilika Juni 30 mwaka huu kwa gharama ya shilingi milioni 445,043,973.38.

"Pia mradi umehusisha uwekaji wa mtandao wa kusambaza na kulaza bomba za maji kwa kwa umbali wa mita 10,627.," imeeleza.

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mbaraka Al Haji Batenga ametoa shukrani kwa Serikali kwa kuona umuhimu wa mradi huo na kutoa fedha kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa mradi huu kwa kasi.

Mradi wa Maji Kaloleni utakapokamilika utahudumia wananchi takribani 2,838.

Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2022, Sensa ni msingi wa mipango ya maendeleo,shiriki kuhesabiwa,tuyafikie maendeleo ya taifa.

Msimamizi wa Mradi wa uendelezaji wa Miundombinu ya Maji Safi Mhandisi Violet Kazumba akitoa maelezo kwa kiongozi wa mbio za mwengi mwaka 2022 Sahili Nyanzabara Geraruma alipotembelea ikiwemo kushiriki kuwaunganishia huduma ya maji safi wakazi wa Kata ya Maweni wawili ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa maunganisho ya maji safi kwa mradi huo

 

Msimamizi wa Mradi wa uendelezaji wa Miundombinu ya Maji Safi Mhandisi Violet Kazumba akitoa maelezo kwa kiongozi wa mbio za mwengi mwaka 2022 Sahili Nyanzabara Geraruma alipotembelea ikiwemo kushiriki kuwaunganishia huduma ya maji safi wakazi wa Kata ya Maweni wawili ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa maunganisho ya maji safi kwa mradi huo

MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima kulia akipokea mwenge wa Uhuru 2020 leo
Kiongozi wa mbio za mwengi mwaka 2022 Sahili Nyanzabara Geraruma akikagua mradi huo

kiongozi wa mbio za mwengi mwaka 2022 Sahili Nyanzabara Geraruma akikawa mikono mara baada ya kufanya kazi ya ukaguzi wa mradi huo



NA OSCAR ASSENGA, TANGA.

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2022 Sahili Nyanzabara Geraruma ameipongeza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga Uwasa kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhakikisha wanawapatia maji safi wananchi na hivyo kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu.

Geraruma aliyasema hayo leo wakati alipotembelea mradi wa uendelezaji wa Miundombinu ya Maji Safi ikiwemo kushiriki kuwaunganishia huduma ya maji safi wakazi wa Kata ya Maweni wawili ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa maunganisho ya maji safi kwa mradi huo.

Alisema kwamba wametembelea mradi huo na kuona namna mamlaka hiyo ilivyofanya kazi nzuri kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo muhimu kwa ustawi wa maisha yao ya kila siku.

“Kwa kweli niwapongeze Tanga Uwasa kwa kazi nzuri mnayoifanya kuhakikisha mnapaelekea wananchi maji hivyo hakikisheni wananchi wanapolipia huduma hiyo wanaipata kwa wakati ”Alisema

Kiongozi huyo aliitaka mamlaka hiyo kuhakikisha wanafikisha maji kwa haraka kwa wananchi ikiwemo kutekeleza majukumu yao kwa wakati pamoja na wananchi wanapolipia waweze kuunganishiwa kwa muda muafaka ili kuepusha malalamiko yasiyokuwa na tija.

“Ndugu zangu watumishi kama wakati mwengine kuna changamoto muwe mnawaeleza wananchi badala ya kusubiri mpaka walalamike na kuilaumu serikali hii “Alisema Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge.

Hata hivyo aliwakumbusha wananchi kuhakikisha wanajiandaa na kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi kwani ni muhimu kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi yetu.

Awali akitoa taarifa kuhusu mradi huo, Msimamizi wa Mradi huo Mhandisi Violet Kazumba alisema kwamba mamlaka hiyo inatekeleza mradi wa uendelezaji wa miundombinu ya maji safi katika Jiji la Tanga kupitia Fedha za Uviko zilizotolewa na Serikali ya Tanzania kwa lengo la kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Uviko 19.

Mhandisi Violet alisema mamlaka hiyo imeweza kusimammia mradi wa uendelezaji wa miundombinu ya majai safi Tanga unaogharimu kiasi cha Sh.512,832,602.80 hadi kukamilika wenye urefu wa kilomita 17,640 katika maeneo ya MSD (Mita 4,000),Kichangani-Mji Mwema (Mita 5,125) Mwahako Neema (Mita 3,000),Masiwani Mbugani (Mita 3,300) na Pongwe kusini (Mita 2,215).

Aidha alisema katika utekelezaji wa mradi huo ulioanza Novemba 2021 na kukamilika Mei 17,2022 ambapo kazi zilizofanyika katika mradi huo ni pamoja na upanuzi na ununuzi wa mabomba ya urefu wa mita 17,640,Ujenzi wa Chemba 46 na usimikaji wa alama 353 za kuonesha miundombinu ya maji ambapo kazi zote zimekamilika kwa asilimia 100 na fedha iliyolipwa ni Sh.Milioni 468,366,302 sawa na asilimia 84.



Mradi huo umekusudiwa kuunganisha matawi ya wateja wapatao 1,200 ambapo jumla ya wakazi 7,200 watanufaika na hadi sasa wateja 15 wameshaunganishwa kwenye mtandao wa maji na wameshaanza kupata huduma ya maji safi na salama majumbani mwao.


 Mradi mkubwa wa ujenzi wa mabwawa ya ufugaji samaki TANLAPIA Ltd, uliopo Nianjema ,Bagamoyo, Mkoani Pwani ukikamilika unalenga kusaidia wafugaji wa samaki aina ya Sato nchini na Ukanda wa Sahara , kwani utatumia teknolojia ya kisasa kuongeza uzalishaji na kupunguza athari za Mazingira.


Mradi huo wa kimkakati unatarajia kugharimu dollar milioni 19 sawa na sh.Bilioni 44.6 fedha ya kitanzania Hadi kukamilika kwake.

Akisoma taarifa kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahir Geraruma, wakati alipoweka jiwe la msingi kwenye mradi huo ,Meneja wa Mradi ,Farida Bozohera alisema ,Hadi kufikia mwezi April mwaka huu mradi umeshatumia sh.bilioni 11.5 .

"Mradi huu ukikamilika tutatumia teknolojia ya kisasa inayolenga kuongeza uzalishaji na kupunguza athari za Mazingira, kwa wafugaji wa samaki aina ya sato katika nchi zilizo Kusini mwa Ukanda wa Sahara.:;"alisema Farida.

Awali akipokea Mwenge huo ukitokea Halmashauri ya Chalinze, kwenye viwanja vya shule ya msingi Fukayose, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Shauri Selenda alisema, Jumla ya miradi 11 yenye thamani ya sh.Bilioni 46.308.2 katika kata nne imetembelewa.

Nae Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallah alieleza ,miradi 25 yenye thamani ya Bilioni 47.2 imepitiwa na mwenge huo katika Halmashauri mbili za wilaya hiyo.

Alieleza ,wilaya hiyo ina Halmashauri hizo mbili ambapo Halmashauri ya Chalinze imetembelewa miradi 14 iliyogharimu milioni 937.8 na Bagamoyo miradi 11 yenye thamani ya Bilioni 46.3.

Akielezea kuhusu mradi huo wa ufugaji samaki Zainab alibainisha ,Ni uwekezaji mkubwa katika Halmashauri ya Bagamoyo, Afrika Mashariki na kati na Ukanda wa Sahara.

Miradi mingine iliyopitiwa ni pamoja na mradi wa upanuzi wa maji kijiji cha Fukayose, kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la upasuaji na wodi ya wazazi na barabara kiwango cha Pavement blocks mita 880.

Mwenge wa Uhuru uliingia Mkoani Pwani,"; Mei mosi na kutembelea miradi 111 yenye thamani ya sh.Bilioni 69.2 ,kwenye Halmashauri Tisa ambapo Mei 10 mkoa huu utaukabidhi Mwenge huo Jijini la Dar es Salaam.