





Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amezitaka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kushirikiana, kubadilishana uzoefu na kuimarisha juhudi za pamoja za kutunza maliasili zinazochangia katika maendeleo ya nchi hizo.
Ameyasema hayo leo Mei 20,2022 jijini Arusha katika Mkutano wa Nane wa Baraza la Sekta ya Mazingira na Maliasili .
“Afrika Mashariki ina utajiri wa maliasili ikiwemo misitu na wanyamapori ambao wanachangia katika maendeleo ya nchi za ukanda huo hivyo, usimamizi endelevu wa mazingira na maliasili ni muhimu ili kuhakikisha kwamba tunaendelea kunufaika” Mhe. Masanja amesisitiza.
Ameongeza kuwa Sekta ya Utalii, upatikanaji wa maji na usalama wa chakula pia ni mambo ya muhimu ya kuyajadili katika mkutano huo ili kuangalia namna ya kunufaika kwa pamoja.
Mhe. Masanja amesema mkutano huo ni fursa ya pekee ya kujadili mikakati ya pamoja ya kuhakikisha kuna usimamizi mzuri wa mazingira na maliasili katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Aidha, amesema kuwa mkutano huo utajadili mikakati ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi zinazoathiri maendeleo ya kiuchumi ya kijamii akitolea mfano wa ukame.
Mkutano huo uliotanguliw na kikao cha Makatibu Wakuu wa Jumuiya hiyo, umehudhuriwa na baadhi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania, Kenya na Uganda pamoja na nchi wanachama zilizoshiriki mkutano huo kwa njia ya mtandao ambazo ni Rwanda, Burundi na Sudan ya Kusini..
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Tulia Ackson amesema ukuaji mkubwa wa faida uliopata benki ya CRDB unastahili kuwa mfano wa kuigwa na taasisi zingine za fedha nchini.
Dkt Tulia ametoa pongezi hizo leo jijini Arusha wakati akifungua semina ya elimu ya fedha iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wanahisa wake na Watanzania kwa ujumla wakati wakijiandaa na Mkutano Mkuu wa 27 wa Wanahisa unaofanyika Mei 22 mwaka huu katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha AICC.
Amesema ukuaji huo umetokana na uwekezaji na usimamizi mzuri katika uendeshaji wa benki hiyo hivyo, kuwawezesha wanahisa kupata gawio ambalo sasa litaongezeka hadi kufikia asilimia 64 kwa hisa.
Dkt Tulia amesema benki hiyo imeendelea kudhihirisha kwa vitendo kuwa Benki kiongozi nchini kwani kila mwaka imekuwa ikitengeneza faida ya uwekezaji kwa wanahisa wake na kuzitaka taasisi nyingine za umma na binafsi kuiga mfano.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi benki hiyo, Dkt Ally Laay amesema wanajivunia kuendelea kukuza thamani ya uwekezaji wa wanahisa wake ikiwamo Serikali ambayo inamiliki asilimia 36 ya hisa.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema timu ya mawaziri wanane kutoka wizara shiriki inashughulikia migogoro mikubwa tu ya ardhi ambayo hulazimu kukutanisha wataalamu kutoka wizara husika.
Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Mei 19, 2022) Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbarali, Bw. Francis Mtega kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu ambaye aliuliza ni kwa nini baadhi ya maeneo yenye migogoro nchini hayajajumuishwa kwenye Kamati ya Mawaziri nane wa sekta husika.
“Migogoro hii ina ngazi mbalimbali za utatuzi na sisi Serikali tumeweka utaratibu. Kwanza, migogoro yote ya ardhi, inaratibiwa katika ngazi ya kijiji, na hii kamati ya kijiji inaweza kutatua migogoro kwa kukutanisha wenye migogoro. Baada ya hapo inaenda ngazi ya kata, wilaya na kisha ngazi ya mkoa.”
Amesema Kamati ya Mawaziri nane imeendelea kufanya kazi ya kubainisha maeneo tangu mwaka 2019 na tayari ilishapeleka taarifa Bungeni ya vijiji vilivyofikiwa na kubainisha vijiji vilivyokuwa na migogoro.
“Taarifa ilibainisha maeneo ya migogoro baina ya wakulima na wafugaji, wakulima na maeneo ya hifadhi. Kamati ya Mawaziri inaendelea kubaini maeneo yenye migogoro yenye tija na yasiyo na tija ili kila mmoja aendelee kufanya kazi yake, iwe ni ufugaji, kilimo au uvuvi. Pindi kazi hiyo ikikamilika, tutatoa taarifa ili Waheshimiwa Wabunge muwe na taarifa ya maeneo yenu,” amesema.
Amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imeridhia maeneo ya hifadhi yasiyo na tija na imeruhusu wananchi waendelee kufanya kazi zao.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kutoa ruzuku kwenye mazao yanayolimwa nchini kulingana na uhitaji uliopo na aina ya mazao.
“Upo mkakati wa Serikali wa kutoa ruzuku kwa mazao mbalimbali ikiwemo kahawa kutegemea na aina ya mazao husika. Ruzuku inategemea aina ya zao na mahitaji yake makubwa. Kuna mahitaji ya miche, dawa, mbegu, mbolea au ya maghala,” amesema.
Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Bi. Esther Malleko ambaye alitaka kujua Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa zao la kahawa linapatiwa ruzuku kwa vile halijawahi kuwekewa ruzuku ikilinganishwa na mazao mengine ya kimkakati.
“Juzi nilikuwa Bukoba kwenye kikao na wadau wa zao hilo. Kule wanahitaji zaidi miche na vyama vikuu vya msingi walisema wana upungufu wa maghala. Niliwahi kwenda Mbinga, wao wanahitaji zaidi mbolea kwa sababu kule bila mbolea, huwezi kukuza zao hilo.”
Waziri Mkuu amesema Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe wakati akihitimisha bajeti ya wizara yake, ameahidi kujenga maghala 300 kule Kagera kwa sababu tunajiandaa kuingia kwenye mfumo wa stakabadhi za mazao ghalani na bila maghala kuwepo huwezo kutumia mfumo huo.
Amemuahidi mbunge huyo kuwa ikifika zamu ya ruzuku kwa mkoa wa Kilimanjaro, yataangaliwa kwanza mahitaji yao ni yapi na utaangaliwa mpango wa Serikali kutoa ruzuku ukoje ili kuona kama unaendana na mahitaji yao.
Na Mwandishi Wetu
MWANAFUNZI wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Sandra Sommi kozi ya Uhandisi wa Komputa leo ameibuka mshindi wa kwanza katika kundi la vyuo vya kati katika mashindano ya Kimataifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU 2022).
Ushindi wa Sandra unatoka na ubunifu wake wa mashine ya kumsaidia watoto chini ya miaka mitano kupumua (bable CPAP).
Mshindi huyo amekabidhiwa na Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango hundi ya Sh milioni tano na cheti.
Dkt. Mpango alikua mgeni rasmi katika hafla ya kufunga maonesho hayo ya Kilele cha Wiki ya Ubunifu Kimataifa yanayofanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Jamhuri.
Katibu Tawala (DAS) wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Winfrida Funto, akizungumza na wakina mama waliofika kwenye uzinduzi huo (hawapo pichani)
Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Dk. Anthony Mwangolombe, akizungumza kwenye uzinduzi huo. |