Articles by "MICHEZO"
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts

 

 


Na Oscar Assenga,TANGA

MKURUGENZI wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Dkt. Juma Mhina ametoa ahaidi ya kununua kila goli litakalofungwa na timu ya mpira wa Miguu ya Halmashauri hiyo wa kiasi cha 20,000 ikiwa ni kutoa motisha kwa wachezaji wa Halmahauri hiyo wanaoshiriki katika Michuano ya Shimisemita inayoendelea Jijini Tanga.

Aliyasema hayo leo mara baada ya kutembelea timu hiyo kabla ya kuanza mchezo wa mpira wa miguu dhidi yao na Halmasahauri ya Mpimbwe ikiwa ni michuano ya Shimisemita inayoendelea kwenye viwanja v ya Shule ya Sekondari Ufundi Mkoani Tanga

Alisema kwamba anaridhishwa na kiwango na mwenendo wa timu hiyo katika mashindano hayo hivyo akaendelea kutoa hamasa kwao kuhakikisha wanaendelea kufanya vizuri na kuibuka na ubingwa.

“Hongereni sana mmefanya kazi kubwa sana kwa kuendelea kufanya vizuri naomba tuendelea kuwa na nidhamu msichoke tupo pamoja na tutaendelea kuwasapoti “Alisema Mkurugenzi huyo

Hata hivyo aliwataka kuendelea kuhakikisha wanaendelea kupambana ili kuweza kusonga hatua nyengine kwenye mashindano hayo huku akisisitiza nidhamu na kujituma

 







Na Oscar Assenga,TANGA

TIMU ya Mpira wa Miguu ya Halmashauri  ya Wilaya ya Muheza imebamiza Halmashauri ya wilaya ya Bumbuli mabao 3-2 katika michuano ya Shirikisho la Michezo la Mamlaka za Serikali za Mitaa kaika mchezo uliochezwa kwenye viwanja vya Shule ya Ufundi Tanga.

Shirikisho hili la Michezo linahusisha watumishi waliopo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ( Halmashauri) waliopo kwenye idara na vitengo mbalimbali.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa na upinzani mkubwa kutokana na kila timu kutaka kupata ushindi lakini Halmashauri ya wilaya ya Muheza iliweza kuhimili na kuutawala vyema mchezo huo na hatimaye kuweza kuibuka na kidedea
Mashindano ya Shirikisho la Serikali za Mitaa Tanzania ( SHIMISEMITA) yalianza rasmi Agosti 15, 2025 na yanatarajiwa kukamilika Agosti 29, 2025 huku yakilenga kuwakutanisha watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, kushirikiana pamoja, kufahamiana, kubadilishana mawazo, kujenga Afya za watumishi ili kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo kisukari na shinikizo la damu.
Michezo hii inaendelea katika Viwanja mbalimbali vya Michezo vilivyopo Jijini Tanga huku yakiwa yamebeba Kauli mbiu ya SHIMISEMITA 2025  " Jitokeze kupiga Kura kwa maendeleo ya Michezo".

 



Na Oscar Assenga, TANGA


USHIRIKI wa Watumishi katika michezo umetajwa kwamba ni njia nzuri ya kujenga amani na mshikamano ambao unaweza kuboresha afya zao na hivyo kuongeza ufanisi na tija mahala pa kazi.

Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumia Huduma ya Maji nchini (ATAWAS) Mhandisi Geofrey Hilly wakati akifungua Fainali za Mashindano ya Sekta ya Maji maarufu kama Maji Cup yanayoendelea kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani Jijini Tanga.

Mhandisi Hilly alisema watumishi wanaposhiriki michezo wanatekeleza maelekezo ya Serikali kuhakikisha wafanyakazi wanashiriki michezo kadri inavyowezekana ili kuimarisha afya zao lakini na kuongeza ufanisi kazini

Alisema kwamba wanafanya hivyo ili kuhakikisha wanakuwa na afya njema na kufanya kazi zao kwa tija kutokana na kwamba wanaposhiriki michezo inaweza kuwaondolea mambo mbalimbali ikiwemo msongo wa mawazo.

“Tunafanya michezo yetu tufahamiane vizuri Mamlaka na Mamlaka ili tuweze kupeana changamoto na
utatuzi kwenye maeneo yetu tunayofanya kazi.

Aidha alisema kwamba mamlaka hiyo imeonyesha mfano bora wa kuweza kutafuta fedha nje ya njia zilizozoeleka ya kufanya miradi ya maendeleo wanaishukuru serikali kuwapa sapoti na kutoa ruhusa ya kufanikisha jambo hilo walitoa hati fungani yenye thamani ya Bilioni 53.12.

Alisema kutokana na hilo walifanikiwa na Taasisi ya kwanza ya umma Afrika Mashariki na kati kutoa hati fungani kama taasisi ya serikali ni miongoni mwa mafanikio ya serikali.

Mhandisi Hilly alisema kwamba katika michezo hiyo ya mwaka huu walivyoanza mpaka sasa wanaangalia mafanikio ya serikali ya awamu ya sita katika sekta ya maji chini ya Rais Dkt Samia Suluhu .

Alisema katika ilani ya CCM walipanga kuwafikishia huduma ya maji asilimia 85 vijijini na 95 mijini sasa wanavyozungumza licha ya miradi mingi inayoendelea nchini asilimia 83 vijijini na asilimia 93 mijini hivyo miradi inayoendelea ifikapo mwezi Desemba watakuwa zaidi ya asilimia 85 vijijini na mijini zaidi 95.

Hata hivyo alisema kwamba katika utekeleza ilani miradi ya maendeleo umefanyika vizuri wanatoa pongezi kwa viongozi huku akieleza namna Waziri wa Maji Jumaa Aweso anavyopambana na kwa juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu wamefanikisha.

Awali akizungumza Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Watumia Huduma ya Maji nchini (ATAWAS) Constantino Chiwaligo alisema mashindano hayo yana umuhimu mkubwa kutokana na sehemu ya kuongeza hamasa,mshikamano na kubadilishana uzoefu.

Alisema tokea mashindano hayo yalipoanzishwa mwaka 2021 na Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye alitoa maelekezo ya kuwaeleza wajaribu kushirikisha jamii katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na utoaji wa huduma ya maji na usafi wa mazingira.


Alisema pale wanaposhiriki jamii watumie michezo kupeleka huo ujumbe ikiwemo kuwapa maelekezo ya kuwaeleza waanzisha Michezo ya Maji Cup na wamekuwa waktekeleza pale na kutoa kauli mbiu kila mwaka.

Huu ni mwaka wa tano katika mashindano hayo na mwaka huu ujumbe wa mwaka huu ni kuangalia mafanikio ya sekta ya maji serikali ya awamu ya sita na wakaanza maji cup lig na kushirikisha timu kutoka kanda nane Tanzania na wametembea Tanzania nzima

Hata hivyo afisa Raslimali watu wa Tanga Uwasa Benard Wambura alisema kuwa jumla ya taasisi 14 zimeweza kushiriki katika michuano hiyo katika mpira wa miguu kwa wanaume na na netball kwa wanawake.

“ushiriki wa timu hizo ulikuwa kwa mfumo wa kanda na sasa wapo kwenye fainali ili kutafuta mshindi katika ligi hiyo ambayo imehusisha na mamlaka za maji zilizopo Tanzania bara na visiwani”alisema Wambura






 


NA DENIS MLOWE IRINGA 

TIMU za soka za Spana fc na BBC Fc zimekuwa timu za kwanza kufuzu hatua ya 8 bora katika mashindano ya kugombea kombe la Vunjabei baada ya michezo ya marudiano baina ya yao na timu za Migori Fc na Tanesco. 

Katika mchezo wa kwanza baina ya Spana fc na Migori timu ya Spana ilichezea kipigo cha goli 1 bila na mechi ya marudiano Spana fc waliondoka na ushindi wa goli 2 0 hivyo kufuzu moja kwa moja hatua ya nane bora. 

Wakati Spana wakifuzu timu ya BBC nayo imefanikiwa kufuzu hatua hiyo baada ya kutoka sare katika mchezo wa marudiano kwa matokeo ya 1 - 1 dhidi ya Tanesco wakati mchezo wa awali BBC walishinda goli 1.

Mashindano hayo yanaendelea leo ambapo zitapatikana timu mbili nyingine kufuzu hatua ya 8 bora kwenda kuwania kitita cha milioni 10 kinachotolewa na mdhamini wa mashindano hayo kampuji ya Vunja Bei chini ya Mkurugenzi wake Fred Ngajilo aka Fred Vunjabei .

Katika michezo ya leo Timu ya Isakalilo itakuwa mgeni katika uwanja wa shule ya Msingi Mlandege ambapo wenyeji wao watakuwa Viwengi ambapo katika mchezo wa kwanza timu ya Isakalilo ambayo hadi sasa haijawahi poteza mchezo itaingia na faida ya goli 5 ilizopata mechi ya kwanza.

Katika uwanja wa shule ya msingi Ipogoro kutakuwa ba mchezo mwingine katika ya Mti pesa dhidi ya Viwengi fc dhidi ya Kising’a fc ambapo timu mwenyeji anapewa nafasi kubwa kuingia hatua ya 8 bora baada ya ushindi katika mchezo wa kwanza.

Katika mashindano hayo mchezaji Barnaba Carlo amezidi kuwaacha mbali wapinzani wake katika kushindania mfungaji bora wa mashidano hayo baada ya kuwa na magoli 8 akifuatiwa na Osca Evaristo mwenye magoli matano.

Mashindano ya kombe la Vunjabei yamekuwa chachu ya mabadiliko ya soka mkoani Iringa na Nyanda za Juu Kusini kutokana na zawadi kubwa iliyowekwa kuliko mashindano yote kuanzishwa mkoani Iringa hivyo timu nyingi kuonyesha nia ya kuzinyaka fedha hizo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakati wa hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakati wa hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.



Wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (kulia) akimpatia mpira mmoja wa wawakilishi wa wachezaji wa timu za mpira kwa ajili ya mashindano ya ligi Samia Cup yanayotarajiwa kufanyika katika Kata ya Chipogolo.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyevaa miwani) akisalimiana na baadhi ya wananchi wa Kata ya Chipogolo wakati alipowasili kwa ajili ya hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa hafla ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyeshika mpira) akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Chipogolo, Bw. Msafiri Mgonela (wa kwanza kulia) wakati wa hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (wa tatu kutoka kulia) akifurahia jambo wakati wa hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup. Kulia kwake ni Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na mmoja wa wawakilishi wa timu ya mpira ya wanawake wakati wa hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.



Wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa hafla ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na mwananchi wa Kata ya Chipogolo aliyehudhuria hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.


Na. Mwandishi Wetu-Chipogolo


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe ameunga mkono mashindano ya ligi Samia Cup na kugawa vifaa vya michezo huku akiahidi kutoa zawadi kwa mshindi wa kwanza kiasi cha fedha shilingi 500,000/=, mshindi wa pili 250,000/= na mshindi wa tatu 150,000/= kuelekea mashindano ya ligi Samia Cup yanayotarajiwa kufanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Kata Chipogolo.

Mhe. Simbachawene ameunga mkono mashindano hayo alipokuwa mgeni rasmi kwenye hafla maalum iliyolenga kugawa vifaa hivyo vilivyonunuliwa na Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika.

Mhe. Diwani ninakupongeza sana, kwenye baadhi ya maeneo mimi ndiye ninayeombwa kutoa vifaa vya michezo, lakini leo ni tofauti na nilivyozoea nimekuja kugawa vifaa hivi vilivyonunuliwa nawe, hongera kwa kujitolea na huo ndio uongozi, nami nitaongeza fedha kuanzia mshindi wa kwanza hadi wa tatu. Amesema Waziri Simbachawene.

Akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Chipogolo, Waziri Simbachawene ametoa pongezi kwa Mhe. Diwani Kayanda kwa kutoa vifaa hivyo na kutumia fursa ya Mashindano ya Ligi Samia Cup kuwafahamisha wananchi maendeleo ambayo yamefanyika katika kipindi cha miaka mitano chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo kujengwa kwa vituo vya afya, usambazaji wa umeme, kutatua changamoto ya maji na miundombinu ikiwemo ujenzi wa Barabara kwenye baadhi ya maeneo.

Aidha, Waziri Simbachawene amesema michezo inatoa ajira, inaimarisha afya, inajenga undugu na inaleta furaha kwa jamii hivyo ni vema wananchi wa Chipogolo wakashiriki kwa wingi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kukubali kuwa mgeni rasmi na kugawa vifaa hivyo vya michezo na kuunga mkono mashindano hayo kwa kutoa fedha kwa washindi.


Vilevile, Mhe. Kayanda amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kushughulikia masuala mbalimbali ya maendeleo katika Kata ya Chipogolo.