Na Oscar Assenga,TANGA

MKURUGENZI wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Dkt. Juma Mhina ametoa ahaidi ya kununua kila goli litakalofungwa na timu ya mpira wa Miguu ya Halmashauri hiyo wa kiasi cha 20,000 ikiwa ni kutoa motisha kwa wachezaji wa Halmahauri hiyo wanaoshiriki katika Michuano ya Shimisemita inayoendelea Jijini Tanga.

Aliyasema hayo leo mara baada ya kutembelea timu hiyo kabla ya kuanza mchezo wa mpira wa miguu dhidi yao na Halmasahauri ya Mpimbwe ikiwa ni michuano ya Shimisemita inayoendelea kwenye viwanja v ya Shule ya Sekondari Ufundi Mkoani Tanga

Alisema kwamba anaridhishwa na kiwango na mwenendo wa timu hiyo katika mashindano hayo hivyo akaendelea kutoa hamasa kwao kuhakikisha wanaendelea kufanya vizuri na kuibuka na ubingwa.

“Hongereni sana mmefanya kazi kubwa sana kwa kuendelea kufanya vizuri naomba tuendelea kuwa na nidhamu msichoke tupo pamoja na tutaendelea kuwasapoti “Alisema Mkurugenzi huyo

Hata hivyo aliwataka kuendelea kuhakikisha wanaendelea kupambana ili kuweza kusonga hatua nyengine kwenye mashindano hayo huku akisisitiza nidhamu na kujituma

Share To:

OSCAR ASSENGA

Post A Comment: