Na Mwandishi Wetu

JINHUA, CHINA — Taasisi za elimu ya juu kutoka Tanzania zikiwemo ADEM, MUCE, TIA, SUZA na UDSM zimeshiriki Kongamano la 3 la Marais wa Vyuo Vikuu kati ya China na Afrika lililofanyika jijini Jinhua kuanzia Aprili 14 hadi 20, 2026.

 



Na Oscar Assenga, Tanga

Kwa muda mrefu, gharama za pango zimekuwa mzigo usioonekana lakini mzito kwa taasisi nyingi nchini. 

Ni gharama ambazo zimezoeleka kiasi cha kukubalika kama sehemu ya kawaida ya uendeshaji, bila kuhojiwa kwa kina iwapo zinaweza kubadilishwa kuwa fursa.

Ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga, hali hiyo inaanza kuchukua mwelekeo mpya.

Fedha ambazo zilikuwa zikitumika kila mwaka kugharamia makazi ya watumishi sasa zinaelekezwa kwenye mkakati wenye dira tofauti ujenzi wa nyumba za watumishi katika kila wilaya ya mkoa.

Haya ni mabadiliko kutoka matumizi ya muda mfupi kwenda uwekezaji wa muda mrefu.

Upepo Mpya wa Ubunifu

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, anauelezea mkakati huo kama hatua ya kimkakati inayolenga kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuimarisha uwezo wa chama kuwekeza katika maendeleo mengine.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya chama mkoani humo, ikiwemo ujenzi wa nyumba za watumishi, Abdurhaman alionesha kuridhishwa na hatua nyumba hizo zilizofikiwa  katika maeneo mbalimbali mkoani humo , lakini zaidi akisisitiza thamani ya mshikamano uliowezesha mafanikio hayo.

“Kwa ujumla mmefanya kazi kubwa sana. Nawashukuru wadau wote walioshiriki, kwa sababu walichotoa si msaada tu, bali ni uwekezaji ambao utaendelea kuzaa matunda,” alisema kwa msisitizo.

Kauli hiyo inaakisi mwelekeo mpya wa fikra kutazama rasilimali si kama matumizi ya papo kwa papo, bali kama uwekezaji wa muda mrefu.

 

Kutoka Pango kwenda Uwekezaji

Kabla ya mradi huu kuanza, baadhi ya watumishi walikuwa wakilipa hadi shilingi 200,000 kwa mwezi kama pango, huku wengine wakilipa zaidi kulingana na eneo.

Kwa mwaka mmoja, gharama hizo zilijikusanya na kuwa mzigo mkubwa kwa chama—fedha ambazo, kwa mtazamo wa sasa, zingeelekezwa kwenye miradi mingine ya maendeleo.

Sasa picha inaanza kubadilika.

Kwa makadirio ya haraka, kukamilika kwa nyumba hizo katika wilaya zote za Mkoa wa Tanga kunatarajiwa kuiwezesha CCM kuokoa hadi shilingi milioni 90 kwa mwaka.

Fedha hizo, kwa mujibu wa uongozi wa chama, sasa zinageuka kuwa mtaji mpya wa maendeleo ya ndani.

“Fedha hizi zitasaidia kufanya shughuli nyingine za maendeleo ndani ya chama. Huu ni ubunifu ambao umehimizwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa pamoja na Kamati Kuu,” alieleza Abdurhaman.

Zaidi ya Takwimu: Ustawi wa Mtumishi

Licha ya faida za kifedha, mchango mkubwa zaidi wa mradi huu upo katika kuboresha ustawi wa watumishi.

Makazi bora, salama na yenye hadhi yanatarajiwa kuongeza ari, utulivu na ufanisi kazini—ambapo matokeo yake yanaonekana moja kwa moja katika utendaji wa kila siku.

Kwa lugha rahisi, mtumishi mwenye uhakika wa makazi ni mtumishi mwenye uhakika wa kazi bora.

Nidhamu ya Mali na Usimamizi wa Ardhi

Katika hatua nyingine, Abdurhaman alisisitiza umuhimu wa kulinda mali za chama kwa kuhakikisha maeneo yote yana hati miliki halali.

Alibainisha kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuzuia migogoro ya ardhi na kulinda uwekezaji wa muda mrefu wa chama.

Aidha, alihimiza upandaji wa miti ya kivuli na matunda katika maeneo ya chama, hatua inayolenga si tu kuboresha mazingira bali pia kuongeza thamani ya maeneo hayo na kulinda mipaka yake.


 

Wajibu wa Viongozi wa Wilaya

Viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya wamepewa jukumu la kuhakikisha sheria za ardhi zinazingatiwa kikamilifu, ikiwemo ulipaji wa kodi ya pango la ardhi na kufuata taratibu zote za umiliki.

Hii inaweka msisitizo kwenye uwajibikaji na nidhamu ya matumizi ya mali za umma na za chama.

 

Hitimisho: Gharama Zinapogeuka Fursa

Kwa ujumla, mkakati wa ujenzi wa nyumba za watumishi unaibuka kama mfano wa namna taasisi zinavyoweza kubadili changamoto kuwa fursa za kiuchumi na kijamii.

Ndani ya CCM Tanga, hatua hii si tu inaboresha maisha ya watumishi, bali pia inaweka msingi imara wa uendelevu wa kifedha na kiutendaji wa chama kwa siku zijazo.

Na zaidi ya yote, inaonesha kwamba maendeleo si suala la kuongeza matumizi—bali ni sanaa ya kuyabadilisha kuwa uwekezaji.

0714543839

Serikali imesisitiza umuhimu wa michezo kwa wafanyakazi kama sehemu muhimu ya kuimarisha afya na kuongeza ufanisi mahali pa kazi.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe.Rahma Kisuo, wakati akifungua rasmi Michezo ya Mei Mosi Kitaifa 2026 iliyofanyika Aprili 20, 2026 katika viwanja vya Sabasaba mkoani Njombe.

Amesema kuwa afya ya mfanyakazi ni mtaji mkubwa unaochangia maendeleo ya taasisi na taifa kwa ujumla, hivyo michezo inapaswa kupewa kipaumbele.

Aidha, Mhe.Kisuo amehimiza wafanyakazi kote nchini kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara badala ya kusubiri vipindi vya mashindano pekee. Amesisitiza kuwa mazoezi yawe sehemu ya maisha ya kila siku ili kuboresha afya na kuongeza tija kazini, huku akizitaka taasisi zote za umma na binafsi kuhakikisha zinatoa nafasi kwa wafanyakazi kushiriki shughuli za michezo.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Njombe Dkt. Stephane Nindi akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa, kufanyika kwa Maadhimisho ya Meimosi Njombe kumetoa fursa za kibiashara kwa wananchi wa mkoa huo.

Katika hatua nyingine, amewapongeza washiriki wa Michezo ya Mei Mosi na kuwataka kudumisha nidhamu, mshikamano na ushindani wa haki.

Amesisitiza kuwa michezo iwe chachu ya kuimarisha udugu na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi badala ya kuwa chanzo cha migogoro.

Kwa mwaka 2026, michezo hiyo inaongozwa na kauli mbiu isemayo, “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050,” huku watumishi na wachezaji wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) wakiwa miongoni mwa washiriki wa ufunguzi huo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Rulenge, Ngara. Harambee hiyo imefanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, Jijini Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Rulenge, Ngara. Harambee hiyo imefanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, Jijini Mwanza.

Viongozi na wageni mbalimbali wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipomwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Rulenge, Ngara, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, Jijini Mwanza.

Muhashamu Baba Askofu wa Jimbo la Rulenge Ngara, Severine Niwemugizi akieleza jambo wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Rulenge, Ngara, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach Arena,  Jijini Mwanza.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, akiongoza zoezi la harambee ya kuchangia Ujenzi wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Rulenge, Ngara katika ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, Jijini Mwanza.

Na: OWM (KAM) - Mwanza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema kuwa taasisi za dini zina mchango mkubwa katika kuimarisha ustawi wa jamii kwa kutoa huduma za kiroho, maadili na malezi bora, hatua inayochangia kwa kiasi kikubwa kuwa na maendeleo endelevu ya Taifa.

Aidha, amesema dhamira hiyo imedhihirishwa kwa vitendo na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikisha Taasisi za Dini katika masuala mbalimbali nchini.

Waziri Sangu amesema hayo alipomwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Rulenge, Ngara. Harambee hiyo imefanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, Jijini Mwanza.

Akisoma hotuba hiyo, Waziri Sangu amesema Mheshimiwa Waziri Mkuu amewaomba Viongozi wa dini kuendelea kuwalea kiroho vijana ili waendelee kuwa na maadili, tabia njema, wazalendo na wenye kupenda Taifa lao, malezi bora kwa lengo la kuwa na jamii tulivu na yenye amani.

Vilevile, amehamasisha ushirikiano baina ya Serikali na makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo Taasisi za Dini. Ameongeza kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameanzisha jukumu hili matamanio yake ni kuona Mahusiano baina ya Serikali na Makundi hayo ya Kijamii yanaendelea kuimarika kwa kudumisha tunu za Taifa ambazo ni amani, upendo, mshikamano na umoja wa Kitaifa.

Katika harambee hiyo, Mhe. Sangu amefanikiwa kuchangisha zaidi ya shilingi Milioni 114,982,000 ambapo katika pesa hiyo Waziri Mkuu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba amechangia Tsh. Milioni 30 taslimu.

Naye, Muhashamu Baba Askofu wa Jimbo la Rulenge Ngara, Severine Niwemugizi amesema ujenzi wa kanisa hilo hadi kukamilika utagharimu shilingi bilioni 7.7 ambazo zitahusisha gharama za ujenzi na ununuzi wa thamani za kanisa.

Kwa upande mwengine, ameipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za dini nchini, akieleza kuwa ushirikiano huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha ustawi wa jamii.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali imeendelea kuitambua sekta ya matukio na biashara za sherehe kama kichocheo muhimu cha ajira na ukuaji wa uchumi nchini, huku ikiwahimiza vijana na wanawake kuitumia kama jukwaa la kujiajiri na kuongeza kipato.
Rais wa zamani wa Liberia, Mheshimiwa Ellen Johnson Sirleaf ambaye pia ni Mlezi wa Mtandao wa Wanawake Viongozi barani Afrika African Women Leaders Network -AWLN) amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Aprili 19 hadi 22 Aprili 2026.
Watanzania wamehamasishwa kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kupata utulivu wa kuliongoza Taifa la Tanzania kwa amani, upendo na mshikamano.
Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Mtatifikolo, amesema kuwa taasisi za kidini zina nafasi kubwa katika kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania na wananchi wengine wanaoishi nchini huku akiomba wananchi na viongozi wa dini na serikali kupambana ma adui mmomonyoko wa maadili.
Mkaguzi wa Kata ya Milola, Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (A/INSP) Aloyce Andrew, kwa kushirikiana na wananchi wa kata hiyo, wamefanikiwa kumuua nyoka aliyekuwa akifugwa ambaye alisababisha taharuki kwa wakazi wa eneo la Mavimba, njia panda ya mnadani na wananchi wengine kushindwa kuendelea na shughuli zao kutokana na hofu.

 



Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wahitimu wa mahafali ya Kidato cha Sita katika Shule ya Wasichana Huruma jijini Dodoma kuzingatia  nidhamu, uzalendo na kutumia elimu yao kuleta maendeleo kwa taifa


Akizungumza katika mahafali hayo, Mhe. Mahundi amesema kuwa vijana ni rasilimali muhimu kwa maendeleo ya nchi na wanapaswa kujiandaa vyema kwa hatua inayofuata ya maisha yao kwa kuzingatia maadili na kuepuka vishawishi vinavyoweza kuharibu ndoto zao.

 “Katika hatua mnayoingia sasa, taifa linatarajia mengi kutoka kwenu; muwe vijana wenye uzalendo wa dhati, wanaozingatia nidhamu na maadili, na kutumia elimu yenu kutatua changamoto za jamii.”Alisema Mhe Mahundi


Aidha, amesisitiza kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira bora kwa vijana kupitia uwekezaji katika elimu, afya na ustawi wa jamii ili kuhakikisha hakuna mtoto anayeachwa nyuma katika kufikia mafanikio yake.


Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Huruma, Sr. Alfonsia Aloyce, amesema mahafali hayo ni tukio muhimu kwa wanafunzi waliomaliza masomo yao na kuwataka wahitimu kuendeleza nidhamu na maadili waliyojifunza shuleni wanaporejea nyumbani na kuanza maisha mapya.

“Baada ya kuhitimu, mtaenda kuishi bila usimamizi wa walimu na walezi, hivyo ni muhimu kujisimamia na kuzingatia maadili na mafundisho mliyoyapata ili yawasaidie katika maisha yenu ya baadaye.”alisema sr.Alfonsina

Mahafali hayo yamefanyika tarehe 18 Aprili 2026 katika Shule ya Wasichana Huruma, ambapo wahitimu wa Kidato cha Sita wamehitimisha rasmi safari yao ya elimu ya sekondari na kujiandaa na hatua inayofuata ya masomo na maisha.










Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

.... Zaidi ya shilingi bilioni 127.7 zimetumika kupeleka huduma ya nishati safi Vijijini Mkoa wa Mwanza hali iliyochochea ukuaji wa uchumi na kuboreka kwa huduma za kijamii vijijini.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) ambapo Wakala huo uliwasilisha mpango kazi pamoja na bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027.

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkoa wa Mwanza pekee imetoa jumla ya shilingi Bilioni 127.7 ili kutekeleza miradi ya kupeleka umeme hadi vitongojini. Mafanikio haya makubwa yamechangiwa pia na wabia wa maendeleo, tunawapongeza na kuwashukuru sana.

Niendelee kuwataka wananchi waendelee kulinda miundombinu ya umeme kwa kuwa serikali na wabia hawa wa maendeleo wanaweka fedha nyingi sana. Lakini pia niendelee kuwahimiza wabia wa maendeleo pamoja na REA kuendelea kuwekeza zaidi katika nishati safi ya kupikia,” amesema Mhe. Mtanda.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu amesema kuwa wabia hao wa maendeleo wamekuwa na imani kubwa na fedha wanazotoa katika utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini na ndio maana wanaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia REA katika utekelezaji wa miradi hiyo huku akiahidi kuwa Bodi yake itaendelea kuhakikisha kunakuwa na thamani ya fedha katika miradi inayotekelezwa na REA.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy amesema kuwa Wakala umewasilisha mipango na vipaumbele vyake kwa mwaka ujao wa fedha ili wabia hao waweze kuona maeneo wanayoweza kuendelea kushirikiana na Serikali kupitia REA katika kuendelea kuboresha maisha ya Wananchi.

“Pamoja na kazi kubwa inayofanyika katika kujenga miundombinu ya umeme, lakini lengo la msingi ni mwananchi wa kawaida aweze kuunganishiwa umeme na aweze kupata manufaa ya upatikanaji wa umeme.

Tumewasilisha mipango pamoja na vipaumbele katika bajeti yetu ijayo ambapo ni kuharakisha upatikanaji wa umeme kwenye vitongoji. Tumewapitisha pia wenzetu katika mpango wetu maalum wa kuwezesha na kuharakisha uunganishaji umeme majumbani,” amebainisha Mhandisi Saidy.

Mhandisi Saidy pia ameongeza baadhi ya mipango mingine iliyopangwa kutekelezwa na Wakala kwa mwaka ujao wa fedha ni pamoja na kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia vijijini, kuwezesha miradi ya nishati jadidifu na kuongeza ufanisi katika matumizi ya umeme na utumiaji wa umeme katika shughuli za maendeleo.

Mwenyekiti wa Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG), Robert Hovde ameipongeza Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa kufikisha umeme vijijini.

“Katika kipindi cha miongo kadhaa nyuma, Tanzania imekuwa na maendeleo makubwa katika kufikisha umeme vijijini yaliyotekelezwa na REA. Miundombinu ya umeme inaonekana hali inayotia matumaini kufikiwa kwa mpango wa kuunganisha umeme wananchi wote. Tunawatakia kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema Hovde.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG), Robert Hovde,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

 

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

 

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy,akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,mara baada ya kumalizika kwa  kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.