Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewahimiza wazazi na walezi kuimarisha malezi ya watoto wao na kutoa taarifa mapema kwa maafisa ustawi wa jamii pale wanapobaini changamoto zinazoweza kuhatarisha ustawi wa mtoto.
Mhe. Mahundi ametoa wito huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Martha Festo Mariki leo Juni 19, 2026 bungeni Dodoma, ambapo amebainisha kuwa Serikali imeendelea kuimarisha mikakati mbalimbali ya kukabiliana na tatizo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani nchini, ikiwemo kutoa elimu kwa wazazi na walezi, kuimarisha uchumi wa kaya na kuboresha huduma za ustawi wa jamii.
Amesema Serikali imeweka mkazo katika kuelimisha wazazi na walezi kuhusu wajibu wao wa kuwalea na kuwatunza watoto ili kuwazuia kukimbilia maisha ya mitaani.
"Serikali inaendelea kutoa elimu kwa walimu na jamii kwa ujumla kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola mara mtoto anapopotea nyumbani au shuleni, hatua ambayo imekuwa ikisaidia kuzuia watoto wengi kuingia katika mazingira ya kuishi mitaani." Amesema Mahundi
Katika hatua nyingine, Mhe. Mahundi amesema Serikali imeanzisha Madawati ya Huduma za Ustawi wa Jamii katika vituo vya usafirishaji nchini kwa lengo la kuwabaini na kuwasaidia watoto wanaotoroka majumbani kuelekea mitaani ambapo Madawati hayo yanasaidia kubaini watoto walio katika hatari na kuwaunganisha na familia zao kabla hawajaingia katika maisha mtaani aidha kuimarisha uchumi wa kaya ni sehemu muhimu ya suluhisho la changamoto hiyo, kwani umasikini ni miongoni mwa sababu zinazochangia baadhi ya watoto kuondoka nyumbani.
Takwimu zinaonesha kuwa kati ya Julai 2025 na Februari 2026, jumla ya watoto 6,182 waliokolewa kutoka mitaani, huku watoto 5,663 kati yao wakiunganishwa tena na familia zao na wengine kupatiwa huduma mbalimbali kulingana na mahitaji yao.
Hata hivyo Serikali imesisitiza kuwa itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha tatizo la watoto wa mtaani linapungua na hatimaye kutokomezwa kabisa nchini.
Na. Jordan Mbwambo, WF, Dodoma.
Wizara ya Fedha imewahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika minada ya hadhara ya mali chakavu, ziada na sinzia za Serikali inayoendeshwa na Wizara ya Fedha kupitia Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali.
Wito huo umetolewa na Msimamizi wa Mali za Serikali Mwandamizi, Wizara ya Fedha, Bw. George Killo, wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, ambapo wananchi wamekuwa wakipatiwa elimu kuhusu taratibu za usimamizi na uondoshaji wa mali za Serikali.
Alifafanua kuwa, mali zinazokuwa zimechakaa, zimepitwa na wakati au kutokuwa na matumizi tena katika taasisi za umma huondoshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo husika kabla ya kuuzwa kupitia minada ya wazi inayowapa wananchi wote fursa sawa ya kushiriki.
“Tunawahimiza wananchi kufuatilia matangazo rasmi ya minada hiyo yanayotolewa kupitia vyombo mbalimbali vya habari na mifumo ya Serikali ili kupata taarifa sahihi kuhusu aina ya mali zinazouzwa, masharti ya ushiriki pamoja na ratiba za minada husika”, alisema Bw. Killo
Aliongeza kuwa, ushiriki mpana wa wananchi katika minada ya Serikali huongeza ushindani, huimarisha uwazi katika mchakato wa mauzo na huchangia katika uongezaji wa mapato katika Mfuko wa Mikopo wa Watumishi (PSAF).
Bw. Killo, alifafanua kuwa, minada hiyo huendeshwa kwa kuzingatia misingi ya usawa, haki na uwazi, ambapo kila mwananchi anayekidhi vigezo vilivyowekwa anaruhusiwa kushiriki.
Aidha, elimu inayotolewa kwa wananchi kuhusu minada ya Serikali inalenga kuongeza uelewa wa taratibu za ushiriki na kuwawezesha kutumia ipasavyo fursa zinazopatikana.
Kwa upande wa Wananchi waliotembelea Banda la Wizara katika Maonesho hayo wamepongeza juhudi za kutoa elimu kuhusu minada ya Serikali, wakieleza kuwa zimewaongezea uelewa kuhusu fursa zilizopo na kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika minada hiyo kwa kuzingatia taratibu na masharti yaliyowekwa.
Katibu Mtendaji wa Mamlaka ya Rufani za Zabuni za Umma (PPAA), Bw. James Sando, akiscan msimbo kupata Jarida la Hazina Yetu, linaloandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, wakati alipotembelea Banda la Wizara katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Afisa Huduma Mwandamizi wa Hazina Saccos, Bi. Leah Nkinda, akitoa elimu kuhusuhuduma zinazotolewa na ushirika huo, kwa wananchi waliotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Na Mwandishi Wetu - Dodoma
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amelipongeza Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC), kwa mchango wake katika kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya watumiaji wa huduma za nishati na maji, hatua inayosaidia huduma zinazodhibitiwa na EWURA ikiwemo huduma ya umeme kuboreshwa kwa maslahi ya wananchi.
Bw. Twange ametoa pongezi hizo leo, Juni 19, 2026, baada ya kutembelea banda la EWURA CCC katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Akizungumza katika banda hilo, Bw. Twange amesema kazi inayofanywa na EWURA CCC ya kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya huduma za umeme imekuwa chachu ya maboresho ya huduma hiyo, ikiwemo kupungua kwa baadhi ya changamoto zilizokuwa zikilalamikiwa mara kwa mara.
"Tunatambua mchango mkubwa wa EWURA CCC katika kuwawakikisha wananchi na kufuatilia utatuzi wa changamoto zao. Malalamiko mnayotupatia yanatusaidia kutambua maeneo yanayohitaji maboresho na kuchukua hatua stahiki ili kuendelea kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi," amesema Bw. Twange.
Kwa upande wake, Afisa Huduma kwa Wateja Mwandamizi wa EWURA CCC, Bw. Amani Mbogo, amesema idadi ya malalamiko yanayohusu TANESCO imeendelea kupungua ikilinganishwa na miaka iliyopita, ambapo sehemu kubwa ya malalamiko hayo yalihusiana na huduma za kuunganishiwa umeme.
EWURA CCC inaendelea kutekeleza majukumu yake ya kulinda na kutetea watumiaji wa huduma za nishati na maji kwa kutoa elimu kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji, kupokea malalamiko ya watumiaji na kuwaelekeza utaratibu wa utatuzi wake.
Aidha, EWURA CCC imekuwa ikifuatilia malalamiko hayo ili kuhakikisha yanatatuliwa kwa wakati na mamlaka husika kwa ustawi wa watumiaji na kufanya huduma ziwe bora na endelevu.
Serikali imeeleza mikakati mbalimbali inayotekelezwa ili kuondoa changamoto za watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani, ikiwa ni pamoja na hatua za kinga, uokoaji na uimarishaji wa ustawi wa jamii katika ngazi ya familia na jamii kwa ujumla.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Martha Festo Mariki, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mikakati ya kina yenye lengo la kuhakikisha watoto wanapata malezi bora na kuepuka kuingia katika maisha ya mitaani.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, baadhi ya hatua zinazochukuliwa na Serikali ni pamoja na kutoa elimu kwa wazazi na walezi kuhusu umuhimu wa malezi bora na usimamizi wa watoto ili kuzuia hali zinazoweza kuwasukuma watoto kukimbilia mitaani.
Aidha, Serikali imeendelea kuhamasisha wazazi na walezi kutoa taarifa kwa maafisa ustawi wa jamii pale inapojitokeza changamoto zinazoweza kuhatarisha ustawi wa watoto ndani ya familia, ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa.
Katika kuimarisha usalama wa watoto, wazazi, walezi pamoja na walimu wanahimizwa kutoa taarifa mara moja katika vituo vya polisi au mamlaka husika pindi mtoto anapopotea nyumbani au shuleni, ili kusaidia ufuatiliaji wa haraka.
Serikali pia imeweka mkazo katika kuboresha uchumi wa kaya, hatua inayolenga kuhakikisha familia zinakuwa na uwezo wa kuwapatia watoto mahitaji yao ya msingi na hivyo kupunguza uwezekano wa watoto kuingia mitaani kutokana na changamoto za kiuchumi.
Vilevile, Serikali imeanzisha Madawati ya Huduma za Ustawi wa Jamii katika vituo vya usafirishaji nchini, yakiwa na jukumu la kubaini, kuzuia na kuwasaidia watoto wanaotoroka nyumbani na kuingia katika maisha ya mitaani.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, jumla ya watoto 6,182 waliokuwa wakiishi au kufanya kazi mtaani wameokolewa. Kati yao, watoto 5,663 wameunganishwa tena na familia zao, huku wengine waliobaki wakipatiwa huduma stahiki kulingana na mahitaji yao ya ustawi wa jamii.
Serikali imesisitiza kuwa itaendelea kuimarisha mikakati hiyo ili kuhakikisha kila mtoto anapata haki ya kuishi katika mazingira salama, yenye malezi bora na yenye kumlinda dhidi ya changamoto za maisha ya mitaani.

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea kujivunia mafanikio ya matumizi ya Moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa kieletroniki kupitia mfumo Mfumo wa Ununuzi wa Umma wa Tanzania (NeST).
Mafanikio hayo yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando alipotembelea banda la Mamlaka hiyo kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, Jijini Dodoma.
Bw. Sando amesema kuwa moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa ilianzishwa ili kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zinajitokeza kwenye utatuzi wa migogoro kwenye michakato ya ununuzi wa umma.
“Changamoto tulizoziondoa kwa wazabuni na taasisi nunuzi ni pamoja kuokoa muda, gharama, uwazi na uwajibikaji pamoja na kumbukumbu sahihi za malalamiko na rufaa zinazowasilishwa na wazabuni,” amesema Bw. Sando.
Bw. Sando amebainisha kuwa ili PPAA iweze kufanya maamuzi kuhusu shauri lililowasilishwa kwa Mamlaka hiyo ni lazima kuwa na kumbukumbu sahihi za shauri hilo, hivyo kupitia moduli PPAA imeweza kupata nyaraka mbalimbali zinazohitajika kwa wakati.
“Kwa Mwaka wa fedha 2025/26 hadi sasa malalamiko takribani 157 yamewasilishwa kupitia moduli hiyo kwa taasisi nunuzi, na kati ya malalamiko hayo mashauri 37 yamewasilishwa PPAA na kutolewa uamuzi, hivyo matumizi ya moduli yanaendelea vyema,” ameongeza Bw. Sando
PPAA inampango wa kuunganisha sekta ya utoaji haki katika ununuzi wa umma na mfumo wa utoaji haki wa Mahakama ya Tanzania kwa mwaka wa fedha ujao ili kuongeza uwazi na uwajibikaji zaidi.

Kadri siku za mazishi zilivyokaribia, uvumi ulienea kila kona ya kijiji. SOMA ZAIDI.
Nilijaribu kuvumilia nikiamini kwamba ni changamoto za kawaida za maisha.
Lakini hali ilibadilika nilipoanza kuona mambo yakiwagusa watoto wangu pia.
Kama mzazi, niliumia sana kuona watoto wangu wakipitia hali ambazo sikuweza kuzielewa.
Nilianza kuwa na wasiwasi mkubwa. Kadri siku zilivyopita, nilihisi kama kila kitu kizuri kilichokuwa karibu kutokea katika familia yangu kilikuwa kinakwama ghafla. Watu wa karibu walinipa ushauri tofauti, lakini bado sikupata amani moyoni. SOMA ZAIDI.
Kadri muda ulivyopita, nilianza kukata tamaa.
Marafiki zangu wengi walikuwa wamepata wenza wao na wengine walikuwa wameanzisha familia.
Nilijaribu kujiweka bize na kazi na shughuli nyingine, lakini moyoni bado nilitamani kupata mwenza wa kweli. Sikuhitaji utajiri au sifa, nilihitaji upendo wa kweli na mtu ambaye angekuwa mwaminifu kwangu.SOMA ZAIDI.
Lakini mwaka mmoja uligeuka kuwa miaka.
Kila nilipoona marafiki na ndugu wakipata watoto, nilifurahi kwa ajili yao lakini moyoni nilibeba huzuni kubwa. Maswali kutoka kwa watu kuhusu lini ningepata mtoto yalizidi kuniumiza kadri muda ulivyopita.
Nilijaribu kutafuta msaada sehemu mbalimbali.
Nilifuata ushauri niliokuwa nikipewa na nikajitahidi kubaki na matumaini. Hata hivyo, baada ya muda mrefu kupita bila mafanikio, nilianza kuhisi kuchoka na kuvunjika moyo.
Kilichoniumiza zaidi ni kusikia watu wakisema huenda nisingepata mtoto kabisa.
Wakati mwingine nililia peke yangu nikijiuliza kwa nini safari yangu ilikuwa ngumu kiasi hicho. Mume wangu alinipa moyo, lakini nilijua naye pia alikuwa akitamani kuona familia yetu ikipanuka.SOMA ZAIDI.
Maumivu yalikuwa makubwa. Mama yetu alikuwa akilia mara kwa mara akijiuliza alikokuwa mtoto wake.
Tulitafuta kupitia marafiki, ndugu wa mbali, na maeneo mbalimbali ambayo tulidhani angeweza kuwa.
Na Mwandishi Wetu
Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imesema matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika sekta ya mifugo yataimarisha masoko na kuongeza ushindani wa bei ya bidhaa hiyo nchini.
Akizungumza Juni 19, 2026 katika Maonesho ya Mifugo na Mnada wa Kimataifa yanayofanyika katika Shamba la Mbogo, Chalinze mkoani Pwani, Afisa Ubora wa WRRB, Anatolius Kabyemera, amesema bodi hiyo imeingia kwenye sekta hiyo kwa lengo la kuwawezesha wafugaji kuuza mifugo yao kupitia mfumo rasmi na wenye tija.
Amesema mfumo huo utasaidia wafugaji kuimarisha ufugaji na kuongeza kipato chao ambapo mifugo itahifadhiwa kwenye eneo maalumu lililosajiliwa kama ghala ya mifugo wakati wakisubiri mnada.
“Mfumo huu utawezesha mifugo kuletwa kwenye ghala ambalo ni eneo teule lenye maji, malisho na wataalamu wa mifugo, litahesabika kuwa ghala la mifugo. Baada ya mfugaji kuingiza mifugo yake katika ghala akisubiri mnada, atapatiwa stakabadhi itakayomwezesha kupata mkopo kupitia taasisi za fedha ambazo tumeshaingia nazo makubaliano, kwa mfano NBC,” amesema Kabyemera.
Kwa upande wake, mmoja wa wafugaji waliotembelea banda la WRRB katika maonesho hayo, Moringe Gasper, ameipongeza bodi hiyo kwa kutoa elimu kuhusu matumizi ya mfumo huo katika sekta ya mifugo.
Amesema wafugaji wengi wako tayari kuona utekelezaji wa mfumo huo unaanza haraka ili nao waweze kunufaika kama ilivyo kwa wakulima wanaotumia mfumo wa stakabadhi za ghala kwa sasa.

Na Mwandishi Wetu
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhan Kailima, amepongeza ufanisi na uwazi wa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unaosimamiwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, akieleza kuwa mfumo huo umechangia kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.
Bw. Kailima alitoa pongezi hizo Juni 18, 2026 alipotembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Akizungumza baada ya kupata maelezo kuhusu utekelezaji wa mfumo huo, alisema kuwa umejengwa katika misingi ya uwazi na ushindani, jambo linalosaidia kupunguza gharama za uagizaji wa mafuta na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Akitoa ufafanuzi kwa mgeni huyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, alisema kuwa katika mfumo wa uagizaji mafuta kwa pamoja, ushindani hujikita katika gharama za usafirishaji wa mafuta (Premium).
Alieleza kuwa wazabuni hushindanishwa kwa kuwasilisha bei za usafirishaji wa bidhaa za petroli, dizeli na mafuta ya taa, ambapo mzabuni mwenye gharama nafuu zaidi hupatiwa zabuni husika.
“Utaratibu huu umetuwezesha kuhakikisha upatikanaji wa mafuta ya kutosha nchini wakati wote na wakati huohuo kuipa Serikali taarifa sahihi za kiasi cha mafuta na hivyo kuwezesha ukusanyaji wa mapato yatokanayo na biashara ya mafuta,” alisema.
Aliongeza kuwa mikataba ya uagizaji wa mafuta husainiwa mapema kabla ya bidhaa kuwasili nchini, jambo linaloiwezesha Serikali kufanya makadirio sahihi ya mapato yatokanayo na sekta hiyo.
Kwa mujibu wa Mwitazy, mafanikio ya mfumo huo yameifanya PBPA kuwa kitovu cha huduma za uagizaji mafuta kwa nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zikiwemo Malawi, Rwanda, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambazo huleta mahitaji yao kupitia mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja.
Ziara ya Bw. Kailima katika banda la PBPA ni sehemu ya shughuli za Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayolenga kuonesha mafanikio, huduma na ubunifu unaotekelezwa na taasisi za umma katika kuwahudumia wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa.

Serikali imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa mikopo yenye masharti nafuu inayotolewa kwa wafanyabiashara ndogondogo ili kuhakikisha fedha hizo zinawanufaisha walengwa na kudhibiti upotevu wa fedha za umma.
Kauli hiyo imetolewa Juni 18, 2026 bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Tamima Haji Abass, aliyehoji kuhusu uwepo wa mwongozo na utaratibu wa kusimamia mikopo hiyo.
Mhe. Mahundi amebainisha kwamba, Serikali imeingia makubaliano na Benki ya NMB kusimamia utoaji wa mikopo yenye riba nafuu ya asilimia saba kwa mwaka kwa wafanyabiashara ndogondogo wanaokidhi vigezo vilivyowekwa, ikiwemo kuwa na kitambulisho cha kidijitali.
Amefafanua kuwa kabla ya mkopo kutolewa, biashara husika hutembelewa na kutathminiwa ili kujiridhisha kama inakidhi masharti ya kupata mkopo. Baada ya hapo, waombaji hupatiwa mafunzo ya usimamizi wa fedha na biashara kabla ya kupokea mkopo, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa matumizi ya fedha hizo na kuimarisha uwezo wa kurejesha mikopo kwa wakati.
“Marejesho ya mikopo hiyo yanafuatiliwa na maafisa wa Benki ya NMB kwa karibu ili kuhakikisha fedha za Serikali zinaendelea kuzunguka na kuwafikia walengwa wengi zaidi. Mfumo huo umewekwa mahsusi kuimarisha uwajibikaji na kupunguza changamoto za ucheleweshaji au kutorejeshwa kwa mikopo" amesema Mhe. Mahundi
Aidha, amesema utaratibu huo umeainishwa katika Mwongozo wa Utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa Wafanyabiashara ndogondogo kupitia Taasisi za Fedha wa mwaka 2024, ambao umeweka misingi ya utoaji na usimamizi wa mikopo hiyo nchini. Mwongozo huo unalenga kujenga mfumo endelevu wa uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia sekta ya biashara ndogo ndogo.
Hatua hizo zinaendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo nafuu huku ikiimarisha mifumo ya usimamizi na ufuatiliaji wa fedha za umma ili ziweze kuleta matokeo chanya kwa walengwa na maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla.
Na. Jordan Mbwambo, WF, Dodoma.
Serikali imeanza kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, hatua inayolenga kufungamanisha na kuboresha usimamizi wa shughuli za Mnyororo wa Ugavi nchini ili kuongeza ufanisi, matumizi bora ya rasilimali na kupata thamani halisi ya fedha za umma.
Hayo yalibainishwa na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Usimamizi wa Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi. Anne Swila, wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Alisema kuwa Sera hiyo inalenga maeneo sita makuu, yakiwemo Ununuzi wa Umma, Ugomboaji na Uondoshaji wa Mizigo ya Serikali, Upokeaji na Urejeshaji, Utunzaji na Uhifadhi, Usambazaji, pamoja na uhifadhi wa Mazingira na Utawala Bora.
‘‘Kwa miaka mingi tumekuwa na sheria nzuri za ununuzi, lakini hazikuwa zimeunganishwa kwa msingi mmoja wa kisera, Sera hii sasa inakwenda kuziba pengo hilo na kuhakikisha kila shilingi ya umma inatumika kwa thamani yake halisi, kwa kuhakikisha mikakati ya utekelezaji inajumuisha kuimarisha udhibiti wa bei, uchaguzi wa wazabuni, na kuendeleza Kada ya Ununuzi na Ugavi Serikalini " alieleza Bi. Swila.
Alisisitiza kuwa ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wa Sera hii itaongeza ushindani na kuwapa fursa wazabuni wazawa, sekta binafsi na makundi maalum ya kijamii, hatua itakayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi na kuchochea ukuaji wa ajira.
Bi. Swila alisema Sera hiyo pia inatarajiwa kuimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki na rasilimali za ndani, kuvutia uwekezaji katika miundombinu ya uhifadhi na usambazaji, na hivyo kuifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
‘‘Miongoni mwa mafanikio yanayotarajiwa ni kuongezeka kwa ufanisi, udhibiti bora wa gharama, kuimarika kwa ubora wa huduma kwa wananchi, ongezeko la ajira, uzingatiaji wa uhifadhi wa mazingira, na kuwa na mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini utakaohakikisha utekelezaji wa sera unaleta tija iliyokusudiwa’’, alifafanua Bi Swila.
Aidha, alisema kuwa Sera hiyo itawezesha kuwepo kwa mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini, hatua itakayoifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kuchangia kupunguza umasikini nchini.
Sera hiyo inatarajiwa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2026 hadi 2036 na tathmini ya utekelezaji itafanyika kila baada ya miaka mitano ya utekelezaji
“Sasa najua ni nini ninapaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua sukari au hata ninaponunua gesi ya kupikia.” Ni kauli ya Bw. Bilson Vedastus, mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.
Banda hilo limekuwa kitovu cha msongamano siku ya tatu ya maonesho, Juni 18, 2026 huku wananchi wakijitokeza kwa wingi kujifunza jinsi Serikali kupitia WMA inavyohakikisha kila kipimo kinachotumika kibiashara na katika huduma ni sahihi. Maonesho yalianza tarehe 16 Juni na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 23 Juni 2026.
Baada ya kupata maelezo ya hatua kwa hatua kutoka kwa wataalamu, wengi wameahidi kuwa mabalozi wa Wakala wa Vipimo katika maeneo yao.
“Tumeona jinsi pampu, mizani na vifaa vingine vinavyohakikiwa kuhakikisha vinapima kwa usahihi. Sasa hatuwezi kukaa kimya tukiona mteja anadhulumiwa. Tutawaeleza jirani zetu na kuripoti udanganyifu popote tutakapouona,” alisema Bi. Asha Siyaya.
Wataalamu wa WMA, Albogast Kajungu, Mbwana Amani na Said Ibrahim waliwaeleza wananchi kuwa uhakiki wa vipimo unagusa sekta zote zinazowahusu moja kwa moja kila siku. Katika sekta ya mafuta, pampu zote huhakikiwa na kuwekewa stika ya uthibitisho. Sokoni na madukani, mizani inayotumika kupimia sukari, mchele na mboga hufanyiwa ukaguzi ili mteja asipoteze pesa.
Sekta ya maji na umeme nayo haikuachwa nyuma. Mita za maji na umeme zinazotumika nyumbani na kwenye biashara ndogo huhakikiwa na kuthibitishwa ili kuhakikisha mteja analipia matumizi halisi na si makadirio au idadi isiyo sahihi. Vile vile mitungi ya gesi ya kupikia, bidhaa zilizofungashwa kama unga na sabuni, pamoja na mizani za barabarani zote huhakikiwa mara kwa mara.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Meneja Mawasiliano wa Wakala wa Vipimo, Bi Veronica Simba amesema lengo ni moja: kuhakikisha mwananchi anapata thamani kamili ya kila shilingi anayolipa, na amewahamasisha wananchi wengi zaidi kutembelea banda hilo kabla ya maonesho kuhitimishwa.





























