Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe, amewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya kumuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ufunguzi wa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Mafunzo hayo yatafanyika kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026 katika Manispaa ya Sumbawanga, yakiwa yameratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Prof. Shemdoe alipokelewa katika Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Makongoro Nyerere akiambatana na Mhe. Mhe. Jacqueline Mzindakaya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Kesho, Julai 13, 2026, Prof. Shemdoe atafungua rasmi mafunzo hayo katika Ukumbi wa Country Hotel, ambapo yanatarajiwa kuwakutanisha wananchi, wajasiriamali, vikundi vya wanawake na vijana, makundi yenye mahitaji maalum pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu fursa za mitaji, mikopo na huduma mbalimbali za uwezeshaji zinazotolewa na Serikali na taasisi zake, ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji, kukuza biashara, kuongeza ajira na kuinua kipato cha familia.

Mafunzo hayo pia yanatarajiwa kuwapa washiriki taarifa sahihi kuhusu namna ya kufikia huduma za kifedha na programu za uwezeshaji wa kiuchumi, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Rukwa kwa ujumla.














Kwa miaka mingi niliamini kuwa nilizaliwa chini ya nyota mbaya. Kila nilipopata kazi, mambo yalikuwa yanaenda vizuri kwa miezi michache, halafu matatizo ya ajabu yalianza. 

Wakati mwingine nilisingiziwa makosa ambayo sikufanya, wakati mwingine kampuni ilifunga ghafla, na mara nyingine nilifukuzwa bila maelezo yoyote.

Ndani ya miaka sita nilifukuzwa kazi mara nne. Hali hiyo ilinivunja moyo sana. Marafiki waliniona kama mtu asiye na bahati, na hata familia yangu ilianza kunipotezea imani.

Nilikuwa nimeoa na nilikuwa na watoto wawili, hivyo kila nilipopoteza kazi, maisha ya familia yangu yalizidi kuwa magumu.

Siku moja, nikiwa nimekata tamaa kabisa, nilikutana na mwanaume mmoja ambaye nilikuwa nimewahi kufanya naye kazi zamani. 

Nilimkuta anaendesha kampuni yake mwenyewe na maisha yake yalikuwa yamebadilika sana. 

Nilimweleza matatizo yangu, naye akaniambia kuwa wakati mwingine kuna vikwazo vya kiroho vinavyoweza kumfanya mtu ashindwe kudumu katika kazi au kufanikiwa.SOMA ZAIDI.
Nilianza ufugaji wa ng’ombe miaka saba iliyopita baada ya kustaafu kazi yangu ya udereva. Nilikuwa na ng’ombe 18 wa maziwa na biashara yangu ilikuwa inaendelea vizuri sana. Kila siku nilikuwa napata maziwa mengi na kuuza kwa hoteli na majirani.

Watu wengi walinipongeza kwa mafanikio yangu, na niliamini maisha yangu yalikuwa yamekaa sawa. Lakini ghafla mambo yalianza kubadilika. 

Ng’ombe mmoja aliugua na kufa bila sababu ya kueleweka. Baada ya wiki mbili, mwingine naye akafa. Ndani ya miezi mitatu nilikuwa nimepoteza ng’ombe sita.

Nilimuita daktari wa mifugo mara kadhaa. Aliwachunguza waliobaki na kuwapa dawa, lakini bado vifo viliendelea. 

Kilichonishangaza zaidi ni kwamba ng’ombe walikuwa wanaonekana wenye afya mchana, lakini asubuhi nilikuwa nakuta mmoja ameanguka na kufa.

Hasara ilianza kuwa kubwa. Nilishindwa kulipa ada za watoto na hata chakula cha mifugo kilianza kuwa tatizo. 

Watu kijijini walianza kunisema kuwa bahati yangu imeisha. Wengine waliniambia niuze ng’ombe waliobaki kabla wote hawajakufa.

Siku moja, mzee mmoja jirani yangu aliniuliza swali la ajabu. “Umeshawahi kukagua zizi lako usiku?” Nilimjibu hapana.

Aliniambia kuna mambo ambayo hayaonekani mchana. Alinieleza kuwa kuna watu wenye wivu wanaweza kutumia nguvu za giza kuharibu mifugo ya mtu anayefanikiwa. SOMA ZAIDI.
Nilikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho chuoni na nilikuwa nimebakiza wiki moja tu kufanya mitihani yangu ya mwisho.

Nilikuwa nimehangaika kwa miaka mitatu, nikifanya kazi ndogo ndogo ili kujilipia ada na mahitaji mengine. Ndoto yangu ilikuwa moja tu kuhitimu na kuibadilisha maisha ya familia yangu.

Siku moja nilipokuwa nikitoka darasani, niliitwa katika ofisi ya utawala. Nilidhani ni jambo la kawaida, lakini nilipoingia, nilikabidhiwa barua iliyosema kuwa nilikuwa nimefukuzwa chuo kutokana na deni la ada na madai ya ukiukaji wa kanuni za chuo.

Nilishangaa sana. Kwanza, nilikuwa nimebakiza kiasi kidogo sana cha ada ambacho nilikuwa nimeahidi kulipa baada ya mitihani. Pili, sikuwahi kuvunja sheria za chuo. Nilijaribu kujitetea lakini hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza.

Nilitoka ofisini nikiwa nimevunjika moyo. Nililia sana usiku huo. Niliona ndoto zangu zote zikifutika mbele ya macho yangu. Nilijiuliza ningewaambia nini wazazi wangu ambao walikuwa wamejitolea kila kitu ili nisome.

Rafiki yangu mmoja aliponiona katika hali hiyo, aliniambia nisikate tamaa. SOMA ZAIDI.

 

Katika kuonesha ujirani mwema Mbunge wa Kiteto Edward Ole Lekaita na Mbunge wa Kilindi Salehe Mhando wameamua kushirikiana kuhakikisha barabara ya Lengatei- Songe inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe na kupitika kwa mwaka mzima.

Mbali ya kushirikiana kusimamia Ujenzi wa barabara hiyo pia Wabunge hao wameshiriki shughuli ya uzinduzi wa shule ya awali na msingi Kijiji cha Lesiot Kata ya Lengatei Kiteto.



Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mhe. Petro Magoti ameipongeza Taasisi ya Elimu Tanzania kwa namna ilivyofanya maboresho ya mitaala ya Elimu nchini yenye lengo la kumfanya muhitimu kuweza kujiajiri au kuajiriwa mara anapomaliza masomo yake.

Mhe. Magoti ameyasema hayo leo tarehe 13/7/2026 katika maonesho ya Sabasaba ambapo amesema kuwa TET inafanya kazi nzuri ya kuboresha elimu nchini.

"Kwa kweli nawapongeza kwa kazi nzuri ya kuboresha Elimu nchini hasa hivi karibuni katika maboresho ya mitaala yaliyofanyika, ni tumaini langu kwamba wanafunzi nchi nzima wataendelea kufanya vyema, "amesema mhe. Magoti.

Pia ameeleza, anafurahia namna wanafunzi wanaendelea kupatiwa vitendea kazi kama vitabu vinavyowapelekea kuendele kufanya vyema wakati wa masomo yao na kuendelea kuipongeza TET kwa uratibu mzuri na upatikanaji wa vitabu mashuleni.

TET inashiriki katika maonesho ya Kimataifa ya biashara maarufu kama Sabasaba yaliyoanza tarehe 28,Juni ambapo yanatarajiwa kufungwa hapo kesho,Julai 13.

Na. Mwandishi Wetu

TUME ya Ushindani (FCC) imeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wajasiriamali kutoka Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kuhusu namna ya kutambua bidhaa bandia, kulinda haki za walaji na biashara ili kuimarisha ushindani wa haki nchini.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema maonesho hayo yameiwezesha tume hiyo kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa kuwapa elimu kuhusu haki za walaji, ulinzi wa biashara pamoja na huduma mbalimbali zinazotolewa na FCC.

"FCC inaendelea kupokea na kushughulikia malalamiko ya wananchi, kusajili mikataba na kutoa huduma nyingine zinazolenga kulinda maslahi ya walaji na wafanyabiashara."amesema

Aidha FCC imewahimiza wananchi na wafanyabiashara kuendelea kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu, kuripoti bidhaa bandia na ukiukwaji wa haki za biashara ili kujenga mazingira ya ushindani wa haki na kulinda maslahi ya walaji nchini.

Kwa upande wake Afisa Ushirikiano wa TWCC, Bw. Nelson Clevary, ameipongeza na kuishikuru FCC kwa mafunzo hayo, akisema yamewasaidia wajasiriamali kutambua bidhaa bandia, kulinda bidhaa zao na kuelewa umuhimu wa kusajili majina na nembo za biashara.

Amesema ushirikiano wa miaka mitatu kati ya TWCC na FCC umeongeza uelewa wa wafanyabiashara kuhusu athari za bidhaa bandia na umuhimu wa kushirikiana na mamlaka husika katika kukabiliana na vitendo vya udanganyifu wa kibiashara.

Naye mjasiriamali kutoka Mwanza, Praxeda Mgyabuso, amesema elimu inayotolewa na FCC imewasaidia wafanyabiashara na wananchi kutofautisha bidhaa halisi na bandia pamoja na kuelewa umuhimu wa kulinda utambulisho wa biashara zao.

Amesema awali wengi walikuwa wakinunua bidhaa kwa kuangalia bei pekee, lakini sasa wanafahamu athari za bidhaa bandia kwa afya, uchumi na biashara, pamoja na umuhimu wa kusajili alama na nembo za biashara.

 

Na Mwandishi Wetu.

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa Kisheria wa Utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa Waandishi wa Habari Wakongwe, hatua inayolenga kutambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari waliolitumikia Taifa kwa muda mrefu na kwa utumishi uliotukuka katika maendeleo ya sekta ya habari nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo, Julai 11, 2026, wakati wa maadhimisho ya JAB Day yaliyofanyika katika Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Kupitia hotuba yake iliyosomwa na Dkt. Egbert Mkoko, Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Bw. Tido Mhando, alisema mwongozo huo umeandaliwa kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa Bodi chini ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 pamoja na Kanuni zake, ili kuweka utaratibu wa utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa waandishi wa habari wakongwe waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya taaluma hiyo.

Alisema mwongozo huo unawahusu waandishi wa habari ambao wakati Sheria ya Huduma za Habari ilipoanza kutumika mwaka 2016 walikuwa na umri wa miaka 50 au zaidi na walikuwa tayari wametoa mchango mkubwa katika sekta ya habari, lakini hawakupata fursa ya kujiendeleza hadi kufikia sifa za kitaaluma zinazohitajika kwa mujibu wa sheria.

"Mwongozo huu unalenga kuhifadhi historia ya tasnia ya habari, kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe na kuhakikisha uzoefu wao unaendelea kuwa sehemu ya urithi wa taaluma ya uandishi wa habari nchini," ilieleza sehemu ya hotuba ya Mwenyekiti.

Bw. Mhando alisisitiza kuwa mwongozo huo hauondoi wala haupunguzi masharti ya msingi yaliyowekwa na Sheria ya Huduma za Habari kuhusu sifa za kupata ithibati kwa waandishi wa habari, bali unaweka utaratibu wa kutekeleza mamlaka ambayo sheria imeipa Bodi kuhusu utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa watu wenye utumishi uliotukuka na waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya sekta ya habari.

Aidha, aliipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuendelea kuiwezesha Bodi kutekeleza majukumu yake na kuimarisha ushirikiano unaolenga kukuza weledi, uwajibikaji na maadili katika taaluma ya uandishi wa habari.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alisema uzinduzi wa mwongozo huo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari na unaonesha dhamira ya Bodi ya kuimarisha viwango vya taaluma huku ikitambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe waliolitumikia Taifa kwa uaminifu, uzalendo na weledi.

Sambamba na uzinduzi huo, JAB iliendesha mdahalo uliowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari kujadili maendeleo ya sekta ya habari nchini, utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari pamoja na mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika mwaka mmoja wa utekelezaji wa mfumo wa utoaji wa ithibati kwa waandishi wa habari waliokidhi vigezo vya sheria.

 


Timu ya mpira wa miguu ya Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Sports Club imefanikiwa kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Championship msimu ujao 2026/2027 baada ya kufuzu kwa kupata sare ya goli 1-1 dhidi ya klabu ya African Sports kutoka Mkoani Tanga 

Akizungumza baada ya kutamatika kwa mchezo Kocha Mkuu wa IAA SC Zulkifri Iddi amewapongeza wachezaji wake kwa kuipatia timu matokeo na kuthibitisha kuwa walifanikiwa kufuata maelekezo aliyowapa ndani ya dakika zote tisini, huku akiupongeza Uongozi wa Chuo IAA kwa sapoti kubwa walioitoa iliyopelekea kuandika historia hii kubwa kwa taasisi na jiji la Arusha 

Akitoa pongezi Mwenyekiti wa mashindano chama cha soka Mkoa wa Arusha Emmanuel Antony ameisifu IAA SC kwa kuandika historia hii kubwa na kukiheshimisha chama cha soka Mkoa wa Arusha na kuahidi ushirikiano kwa timu kuhakikisha inafanya vizuri na kupiga hatua zaidi ili kufika hatua ya kushiriki Ligi kuu ya Tanzania 

Kwa upande wake mchezaji wa IAA SC ambaye ndiye Mfungaji wa goli pekee la timu amewapongeza wachezaji wenzake, benchi la ufundi na Uongozi wa Chuo pamoja na mashabiki wao kwa kushirikiana kufanikisha kufikia mafanikio haya makubwa na kuahidi kuendelea kuipambania nembo ya IAA na jiji la Arusha msimu ujao kwenye mashindano ya Championship

IAA SC katika safari yake ya mafanikio haya ilifanikiwa kuibuka washindi wa ligi ya Wilaya ya Arusha, Ligi ya Mkoa, Ligi ya mabingwa wa Mikoa yote Tanzania na baadae Ligi daraja la pili (First League) na leo imefanikiwa kufuzu kutinga katika ligi daraja la kwanza (Championship) msimu wa mwaka 2026/2027


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MKURUGENZI wa Idara ya Elimu Mbadala na Elimu ya Watu Wazima Zanzibar, Mashavu Ahmada Fakih, ameipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha sekta ya elimu nchini, huku akiwataka wadau wa maendeleo na wananchi kuendelea kuchangia Mfuko wa Elimu ili kuongeza ubora wa elimu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imezitaka taasisi za maendeleo, sekta binafsi na wananchi wenye uwezo kujitokeza kuchangia Mfuko wa Taifa wa Elimu ili kuongeza rasilimali zitakazowezesha kuboresha miundombinu ya elimu na kuimarisha uwekezaji katika elimu ya amali nchini.

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Wasafi Media, Nasib Abdul maarufu Diamond Platnumz, amesema utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari unaweka mazingira bora ya kukuza uwekezaji katika sekta ya habari kwa kuhakikisha vyombo vya habari vinaendeshwa kwa kuzingatia sheria, weledi na viwango vya taaluma.

Diamond alitoa kauli hiyo tarehe 11 Juni, 2026 alipotembelea Banda la Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), kufuatia mwaliko wa Bodi hiyo ili kujionea huduma na elimu inayotolewa kwa waandishi wa habari pamoja na wananchi.

Alisema uwekezaji katika sekta ya habari unahitaji nidhamu, maono, subira na uongozi unaozingatia sheria, akibainisha kuwa usimamizi unaofanywa na JAB unasaidia wawekezaji kuelewa matakwa ya kisheria na namna ya kuyazingatia bila kuhisi kuwa biashara zao zinakwamishwa.

"Utekelezaji na usimamizi wa Sheria ya Huduma za Habari unaonesha ni kwa kiwango gani Serikali inaunga mkono uwekezaji wa vijana katika sekta ya habari. Kazi ya Bodi si kuzuia watu kufanya biashara, bali kuwaelekeza kufuata matakwa ya sheria na kuwahamasisha kuongeza elimu na kukidhi vigezo vinavyotakiwa," alisema Diamond.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa sheria unahitaji busara, maarifa na uwezo wa kuwaelimisha wadau ili waelewe mabadiliko ya taratibu bila kujenga hofu au kuona kuwa wanawekewa vikwazo.

"Kazi hii inahitaji busara na maarifa ya kuwafundisha watu, kuwaelekeza na kuwafanya waelewe taratibu mpya pasipo kuona kwamba wameharibiwa biashara zao. Nimeona Bodi ina timu nzuri inayounga mkono maono ya uongozi wake katika kusimamia sekta hii," alisema Diamond.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alimpongeza Diamond kwa uwekezaji wake katika sekta ya habari na kwa Wasafi Media kuendelea kuzingatia matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari.

Alisema JAB itaendelea kushirikiana na wamiliki wa vyombo vya habari na wadau wengine kuhakikisha sheria inatekelezwa kwa njia inayokuza weledi, uwajibikaji na maendeleo ya sekta ya habari, huku ikitoa elimu na ushauri unaowawezesha wadau kutekeleza matakwa ya sheria kwa ufanisi.

Ziara ya Diamond katika Banda la JAB ilikuwa sehemu ya maadhimisho ya JAB Day yaliyofanyika ndani ya Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, ambapo Bodi imekuwa ikitoa huduma za ithibati, elimu kuhusu Sheria ya Huduma za Habari na ushauri kwa waandishi wa habari, wamiliki wa vyombo vya habari na wananchi.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika jengo la Kituo cha Polisi cha Kata ya Masasi, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.

Jengo hilo limejengwa na Bw. Iman Haule kupitia KUAMBIANA INVESTMENT COMPANY LIMITED ikiwa ni sehemu ya mchango wa sekta binafsi katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya usalama na kusogeza huduma za kipolisi karibu na wananchi.

Mhe. Naibu Waziri Mahundi amepongeza hatua hiyo, akieleza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya usalama unachangia kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao, kuongeza upatikanaji wa haki na kuleta mazingira wezeshi kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.