Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, ametembelea banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma na kupongeza mchango wa benki hiyo katika kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limehimiza wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa wanaozalisha bure kwa gharama za Serikali, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na vikwazo vya kiabiashara.

  


Na John Walter -Babati 

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Hamidu Aweso, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Maji wa Vijiji vya Endamagay na Gidaboshka, uliopo katika Jimbo la Babati Vijijini. Mradi huo wenye thamani ya Shilingi bilioni 1.099 unalenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi 3,766 wa vijiji hivyo na maeneo ya jirani.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Mhe. Aweso alisema Serikali inaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maji ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati. 

Alibainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 30, 2026, huku utekelezaji wake ukiwa umefikia asilimia 87.

Katika ziara hiyo, Waziri Aweso aliambatana na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Baran Sillo.

Kufuatia hatua iliyofikiwa na mradi huo, Mhe. Aweso alitoa maelekezo kwa Wizara ya Maji kuhakikisha ndani ya kipindi kifupi inapatikana Shilingi 508,300,000 kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizosalia, ili mradi ukamilike kwa wakati na wananchi waanze kunufaika na huduma ya maji safi na salama kama ilivyopangwa.





 


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, amefurahishwa na uelewa mkubwa ulioonyeshwa na wanafunzi waliopata elimu ya vipimo katika banda la Wakala wa Vipimo - (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane.

Akizungumza leo Agosti 6, 2026 baada ya kuzungumza na wanafunzi hao aliowakuta katika Banda la WMA, Viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, Dodoma, Naibu Waziri ambaye pia alikuwa katika ziara ya kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho, alisema ni hatua nzuri kwa WMA kuanza kuwafundisha watoto umuhimu wa vipimo sahihi wakiwa wadogo.

“Nimefurahishwa sana. Watoto hawa wameelewa kuwa kipimo sahihi ni haki ya kila mtu. Hawa ndio Maafisa Vipimo wa kesho,” alisema.

Awali, Naibu Waziri Chande alipowakuta wanafunzi hao bandani aliwauliza maswali mbalimbali kuhusu vipimo na waliweza kujibu kwa ufasaha. 

Wanafunzi hao wa Shule ya Msingi Blessed Mabuba iliyopo jijini Dodoma, ambao waliongozana na mwalimu wao Irene Ketta, ambaye pia alipongeza WMA kwa kujielekeza katika utoaji elimu ya vipimo mashuleni hatua ambayo alisema imewawesha wanafunzi kueleza tofauti ya kipimo sahihi na kisicho sahihi, umuhimu wa kusoma lebo na jinsi ya kutumia mizani.

“Niwape pongezi WMA. Kama tutaendelea kuwapa elimu hii watoto wetu, tunajenga Taifa la wafanyabiashara waaminifu na walaji wenye ufahamu. Huu ndio msingi wa uchumi imara,” alisema Mwalimu Ketta.

WMA imeahidi kuhakikisha elimu ya vipimo inaenea kwa jamii nzima kupitia utoaji elimu kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi.







Na Mwandishi Wetu, Tabora

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kurahisisha upatikanaji wa Alama ya Ubora kwa kuanzisha mfumo wa kidijitali unaowezesha wajasiriamali na wazalishaji kuwasilisha maombi kwa njia ya mtandao, hatua inayolenga kuongeza idadi ya bidhaa zenye ubora unaokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.

 




Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameupongeza Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kwa maboresho makubwa ya utoaji wa huduma, hususan matumizi ya teknolojia yanayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Msonde amesema hayo leo, Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la TEMESA katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.

Dkt.Msonde Amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofikiwa na TEMESA, akieleza kuwa uimarishaji wa huduma za kidijitali pamoja na ongezeko la ubora wa mafundi umeongeza ufanisi wa wakala huo.


“Kilichonifurahisha zaidi ni uimarishaji wa mafundi. Sasa wanafanya kazi kwa weledi mkubwa na wanatengeneza magari kwa ubora. Kwa kweli TEMESA mmenifurahisha sana,hongereni sana” amesema Dkt. Msonde.

Aidha, amesema Serikali na wananchi wanaiamini TEMESA kutokana na mchango wake katika kulinda usalama wa magari ya Serikali na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za umma. Amewataka viongozi na watumishi wa wakala huo kuendelea kubuni na kuboresha huduma kwa kutumia teknolojia.

Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma- TEMESA, Bi. Martha Joachim, amesema miongoni mwa maboresho yaliyofanywa ni kuhuisha huduma ya ukodishaji wa mitambo kupitia Mfumo wa TIMIS, ambapo wateja sasa wanaweza kuwasilisha maombi ya ukodishaji kwa njia ya kidijitali, hatua iliyopunguza urasimu na muda wa kupata huduma.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050”, yanatarajiwa kuadhimishwa tarehe 8 Agosti, 2026.

Na.Mwandishi Wetu.

Serikali imewataka wawekezaji binafsi na taasisi mbalimbali nchini kutumia fursa zinazotolewa kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuwekeza katika ujenzi wa nyumba, majengo ya umma na makazi ya kisasa kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa makazi bora na kuharakisha maendeleo ya miundombinu nchini.

Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, baada ya kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, jijini Dodoma.Amesema Serikali imefanya maboresho ya sheria na kanuni zinazoiongoza TBA ili kuipa mamlaka mapana ya kushirikiana na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hatua itakayowezesha taasisi hiyo kuvutia mitaji na kuongeza kasi ya utoaji wa huduma.

Dkt. Msonde amesema tangu kuanzishwa kwake, TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi jukumu la kujenga na kusimamia majengo ya Serikali kwa viwango vya juu vya ubora, huku ikichangia kupunguza gharama za ujenzi na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya umma. Alisema majengo mengi ya Serikali yaliyopo nchini ni ushahidi wa uwezo na weledi wa taasisi hiyo katika sekta ya ujenzi.

Ameongeza kuwa pamoja na mafanikio hayo, TBA sasa ina nafasi kubwa zaidi ya kushiriki katika kutatua changamoto ya makazi kwa kujenga nyumba bora kwa gharama nafuu. Alisema taasisi hiyo inaweza kubuni na kutekeleza miradi ya makazi inayokidhi mahitaji ya wananchi wa kipato cha chini na cha kati, huku ikitumia maeneo yake ya kimkakati kuvutia uwekezaji na kuendeleza miradi ya kisasa.

Dkt. Msonde, amesema ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi kupitia TBA utaongeza uwekezaji, ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya ujenzi, huku ukiwezesha ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma, makazi ya biashara na miradi mingine ya maendeleo. Amewahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa hizo mapema kwa kuwa Serikali imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji na milango iko wazi kwa wote wenye nia ya kushirikiana na TBA.

Aidha, Dkt. Msonde ameipongeza TBA kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini, akisema utendaji wake umeendelea kuijengea Serikali imani kutokana na ubora wa kazi zake. Alisisitiza kuwa matarajio ya Serikali ni kuona taasisi hiyo ikitumia kikamilifu mamlaka mapya iliyopewa kupanua wigo wa huduma, kuongeza miradi ya kimkakati na kuwa chachu ya kuvutia uwekezaji utakaobadilisha sekta ya makazi na miundombinu nchini.

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameshiriki mapokezi ya Mhe. Dkt. Catherine Canute aliyemwakilisha Mwenyekiti wa UWT Taifa katika ziara ya kikazi Wilaya ya Chunya.

Ziara hiyo imelenga kukagua uhai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030 na namna miradi ya maendeleo inavyotekelezwa katika wilaya hiyo.

Akizungumza katika kikao cha kupokea na kujadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa kazi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), pamoja na taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Mhe. Dkt. Catherine Canute amewapongeza viongozi wa Chama, wakiwemo wabunge na viongozi wa Serikali, kwa ushirikiano wao katika kusimamia na kuharakisha maendeleo ya Wilaya ya Chunya.

Aidha, amempongeza Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo na juhudi zake katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi.

Pia amesisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanasimamia malezi bora kwa watoto na vijana ili kuwajenga katika maadili mema na kuwaandaa kuwa viongozi na wananchi wenye uwezo wa kuendeleza taifa imara la kesho.

Aidha, Mhe. Canute amempongeza Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo na jitihada zake katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuleta manufaa kwa wananchi.

Pamoja na hayo, amesisitiza wazazi na walezi kuendelea kusimamia malezi bora kwa watoto na vijana ili kuwajenga katika misingi sahihi itakayowawezesha kuwa chachu ya maendeleo na kuendeleza taifa lenye nguvu na imara.

Amesema ushirikiano wa viongozi pamoja na malezi bora kwa vijana ni nguzo muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji na maendeleo endelevu.

Kwa upande wake, Mhe. Mahundi ameendelea kusisitiza umuhimu wa mshikamano kati ya viongozi, Chama na wananchi katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaleta matokeo chanya kwa wananchi wa Chunya na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla.

 


 Na. WMA- Dodoma

Wakulima, wafugaji, wavuvi, wafanyabiashara na wananchi wameendelea  kutembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) Katika siku ya tano ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayoendelea jijini Dodoma, wakipatiwa elimu kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi ya vipimo.

Katika maonesho hayo, wananchi wamekuwa wakipata fursa ya kujifunza namna ya kutumia na kuhakiki vifaa vya vipimo, pamoja na kuelewa madhara yanayotokana na matumizi ya vipimo visivyo sahihi katika biashara za mbegu, pembejeo, maziwa, mazao na bidhaa nyingine.

Wataalamu wa WMA wamekuwa wakitoa elimu kwa vitendo na kujibu maswali ya wananchi kuhusu taratibu za uhakiki wa vipimo, hatua inayolenga kulinda haki za wakulima, wafanyabiashara na walaji.

WMA imesema itaendelea kutoa elimu hiyo bure kwa wananchi katika siku zote za maonesho hayo, ikiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya vipimo sahihi kwa ajili ya kuongeza tija na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kaulimbiu ya maonesho ya Nanenane Kitaifa 2026 ni: "Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050"

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (MB) (Mwenye Suti) akisikiliza maelezo ya Huduma zinazopatikana katika banda la Mfuko wa PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano,  Mh.Deus Sangu (MB) (wanne kushoto),  akipokea zawadi toka kwa Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw.  Jafari Merai Mgala, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini, Viwanja vya Nganga Mkoani Lindi Agosti 5, 2026.

Wananchi wakiwa kwenye banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, alipokuwa akizungumza kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini kwenye Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (MB) (Mwenye Suti) akiwasili kwenye Banda la PSSSF ndani ya maonesho ya Kilimo (Nanenane)  yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi, Agosti 5, 2026.

Lindi, Agosti 5, 2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema kaulimbiu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) ya "Tunalipa Jana" si kauli tu, bali inatekelezwa kwa vitendo na imeonyesha ukwasi wa Mfuko huo kupitia ulipaji wa mafao kwa wakati kwa wanachama wanaostaafu.

Mhe. Sangu ameyasema hayo Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi, ambapo alizungumza na wanachama, wastaafu na wananchi waliotembelea banda hilo.

"Wastaafu wengine wanashangaa kuona fedha zimeingia kwenye akaunti zao mara tu wanapotoka kazini na kujiuliza, 'Hizi fedha ni zangu kweli?' Hilo linaonesha wazi ukwasi wa Mfuko wa PSSSF na utekelezaji wa kaulimbiu ya Tunalipa Jana," amesema Mhe. Sangu.

Ameongeza kuwa hata wastaafu wanaopokea pensheni za kila mwezi hulipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi, na wakati mwingine hupokea malipo yao kabla ya watumishi walio bado kazini kupokea mishahara yao.

"Wastaafu wetu tumewapa kipaumbele. Mafanikio haya yametokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo yameuwezesha Mfuko kuendelea kukua na kutoa huduma bora kwa wanachama na wastaafu," amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Jafari Merai Mgala, amesema mafanikio ya utoaji wa huduma kwa haraka na kwa ufanisi yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na maboresho ya mifumo ya TEHAMA.

Amesema kwa sasa mwanachama au mstaafu anaweza kuwasilisha madai ya mafao akiwa mahali popote kupitia simu janja, kompyuta au kifaa kingine chenye uwezo wa kuunganishwa na intaneti, hatua iliyorahisisha upatikanaji wa huduma za Mfuko.

"Natoa wito kwa wanachama na wananchi wote wa Kanda ya Kusini kutembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Nanenane ili kupata elimu kuhusu huduma zetu pamoja na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na Mfuko," amesema Bw. Mgala.

Mwisho

Na; Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tanzania inatarajiwa kuingiza zaidi ya Sh bilioni 10 kutokana na mauzo ya biashara ya kaboni baada ya Serikali kuidhinisha miradi minne itakayouza tani milioni 4.2 za kaboni katika soko rasmi la kimataifa la biashara ya Kaboni.
SHIRIKA la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limesema linaendelea kuwasaidia wakulima na wajasiriamali kuongeza thamani ya mazao, kupunguza gharama za uzalishaji na kupata masoko kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa, maabara za ubora na suluhisho za nishati.

Serikali, kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.

Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.

“Mafuta yanapowasili nchini, Wakaguzi wa Mafuta hufuatilia hatua mbalimbali za upakuaji ili kuhakikisha yanakidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa,” amesema Mhandisi Makembe.

Ameeleza kuwa ufuatiliaji huo huanza mafuta yakiwa ndani ya meli na kuendelea wakati wa upakuaji na usafirishaji kupitia miundombinu maalumu, hadi yanapofikishwa kwenye maghala yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Kwa mujibu wa Mhandisi Makembe, Baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuidhinisha ubora wa bidhaa za mafuta kabla Meli haijaanza zoezi la Upakuaji ,Wakaguzi wa Mafuta wanajukumu la kuhakikisha kuwa taratibu za usalama na masharti ya upakuaji yanazingatiwa katika mchakato mzima wa upakuaji wa mafuta hayo. Hatua hiyo inalenga kulinda ubora wa mafuta na kuhakikisha shughuli za upakuaji zinafanyika kwa usalama.

Aidha, ukaguzi huo unalenga kubaini mapema changamoto zozote zinazoweza kuathiri ubora wa mafuta wakati wa upakuaji, usafirishaji au uhifadhi. Hatua hiyo husaidia kuhakikisha mafuta yanayopokelewa yanaendelea kuwa katika hali inayokubalika na TBS hadi yanapofikishwa kwenye maghala husika.

Meneja Msaidizi wa Idara ya Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Nasieku Kisambu akipokea Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa miradi ya CSR inayotekelezwa na mgodi huo.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Michael Mwang'onda (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele (kushoto mwenye skafu) wakifurahia uwekaji jiwe la msingi wa jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya Magoto kata ya Nyaikonga mradi unaogharamiwa na Barrick North Mara.

 


Na OWM – TAMISEMI, Morogoro

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wakulima, wafugaji na wavuvi kwa mchango wao mkubwa uliowezesha Tanzania kufikia utoshelevu wa chakula wa zaidi ya asilimia 120, hatua inayodhihirisha mafanikio ya uwekezaji unaoendelea kufanywa na Serikali katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Dkt. Mwigulu aliwasilisha pongezi hizo za Mhe. Rais Agosti 4, 2026, alipotembelea Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Nane Nane mkoani Morogoro.

 Katika ziara hiyo alijionea shughuli na ubunifu wa wakulima, wafugaji na wavuvi kutoka mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam, Pwani na Tanga.

Amesema maonesho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, "Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050," ambayo inawahimiza Watanzania kuzalisha kwa kuzingatia mahitaji ya soko, kutumia teknolojia za kisasa, kuongeza ubora wa bidhaa na kuimarisha mnyororo wa thamani ili kufanya kilimo kuwa biashara yenye tija na mchango mkubwa katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

"Kwa nilichojionea kupitia maonesho ya mwaka huu, ninaziona dalili zote kwamba ifikapo mwaka 2050 malengo ya Dira ya Taifa tuliyojiwekea yatakuwa yamefikiwa, kwa kuwa tuko kwenye hatua nzuri ya utekelezaji katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi," amesema Dkt. Mwigulu.

Ameongeza kuwa ameridhishwa na ubora wa mazao mbalimbali yaliyooneshwa, ikiwemo nyanya, bilinganya na bidhaa nyingine zinazokidhi viwango vya masoko ya kimataifa, yakiwemo ya Marekani na Ulaya, jambo linaloashiria kuwa Tanzania ipo kwenye mwelekeo sahihi wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani duniani.

Akizungumzia sekta ya mifugo na uvuvi, Dkt. Mwigulu amesema zimeendelea kuwa nguzo muhimu za uchumi wa taifa, akibainisha kuwa mchango wa sekta ya mifugo katika pato la taifa umeongezeka kutoka asilimia 2.3 hadi asilimia 6.2.

Ametoa mfano wa mafanikio ya wanaonufaika na sekta hiyo kwa kumtaja kijana mmoja mhitimu anayejihusisha na ufugaji wa kisasa, ambaye ameonesha ng'ombe mwenye uzito wa zaidi ya kilogramu 1,000 mwenye thamani ya takribani Shilingi Milioni 20. Aidha, amesema kijana huyo anafuga zaidi ya ng'ombe 200 na alipoulizwa na Waziri wa TAMISEMI kama anahitaji mkopo, alieleza kuwa hana uhitaji huo kutokana na mafanikio ya shughuli zake.

Awali, akitoa neno la utangulizi kabla ya Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi pamoja na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, alisema Waziri Mkuu alimpa jukumu la ulezi wa Mkoa wa Morogoro, hivyo alimkaribisha rasmi kama waziri mwenyeji wa mkoa huo, ambao ni mmoja wa mikoa inayounda Kanda ya Mashariki katika Maonesho ya Nane Nane.