Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameshiriki mapokezi ya Mhe. Dkt. Catherine Canute aliyemwakilisha Mwenyekiti wa UWT Taifa katika ziara ya kikazi Wilaya ya Chunya.

Ziara hiyo imelenga kukagua uhai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030 na namna miradi ya maendeleo inavyotekelezwa katika wilaya hiyo.

Akizungumza katika kikao cha kupokea na kujadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa kazi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), pamoja na taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Mhe. Dkt. Catherine Canute amewapongeza viongozi wa Chama, wakiwemo wabunge na viongozi wa Serikali, kwa ushirikiano wao katika kusimamia na kuharakisha maendeleo ya Wilaya ya Chunya.

Aidha, amempongeza Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo na juhudi zake katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi.

Pia amesisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanasimamia malezi bora kwa watoto na vijana ili kuwajenga katika maadili mema na kuwaandaa kuwa viongozi na wananchi wenye uwezo wa kuendeleza taifa imara la kesho.

Aidha, Mhe. Canute amempongeza Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo na jitihada zake katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuleta manufaa kwa wananchi.

Pamoja na hayo, amesisitiza wazazi na walezi kuendelea kusimamia malezi bora kwa watoto na vijana ili kuwajenga katika misingi sahihi itakayowawezesha kuwa chachu ya maendeleo na kuendeleza taifa lenye nguvu na imara.

Amesema ushirikiano wa viongozi pamoja na malezi bora kwa vijana ni nguzo muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji na maendeleo endelevu.

Kwa upande wake, Mhe. Mahundi ameendelea kusisitiza umuhimu wa mshikamano kati ya viongozi, Chama na wananchi katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaleta matokeo chanya kwa wananchi wa Chunya na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla.

 


 Na. WMA- Dodoma

Wakulima, wafugaji, wavuvi, wafanyabiashara na wananchi wameendelea  kutembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) Katika siku ya tano ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayoendelea jijini Dodoma, wakipatiwa elimu kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi ya vipimo.

Katika maonesho hayo, wananchi wamekuwa wakipata fursa ya kujifunza namna ya kutumia na kuhakiki vifaa vya vipimo, pamoja na kuelewa madhara yanayotokana na matumizi ya vipimo visivyo sahihi katika biashara za mbegu, pembejeo, maziwa, mazao na bidhaa nyingine.

Wataalamu wa WMA wamekuwa wakitoa elimu kwa vitendo na kujibu maswali ya wananchi kuhusu taratibu za uhakiki wa vipimo, hatua inayolenga kulinda haki za wakulima, wafanyabiashara na walaji.

WMA imesema itaendelea kutoa elimu hiyo bure kwa wananchi katika siku zote za maonesho hayo, ikiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya vipimo sahihi kwa ajili ya kuongeza tija na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kaulimbiu ya maonesho ya Nanenane Kitaifa 2026 ni: "Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050"

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (MB) (Mwenye Suti) akisikiliza maelezo ya Huduma zinazopatikana katika banda la Mfuko wa PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano,  Mh.Deus Sangu (MB) (wanne kushoto),  akipokea zawadi toka kwa Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw.  Jafari Merai Mgala, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini, Viwanja vya Nganga Mkoani Lindi Agosti 5, 2026.

Wananchi wakiwa kwenye banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, alipokuwa akizungumza kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini kwenye Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (MB) (Mwenye Suti) akiwasili kwenye Banda la PSSSF ndani ya maonesho ya Kilimo (Nanenane)  yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi, Agosti 5, 2026.

Lindi, Agosti 5, 2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema kaulimbiu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) ya "Tunalipa Jana" si kauli tu, bali inatekelezwa kwa vitendo na imeonyesha ukwasi wa Mfuko huo kupitia ulipaji wa mafao kwa wakati kwa wanachama wanaostaafu.

Mhe. Sangu ameyasema hayo Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi, ambapo alizungumza na wanachama, wastaafu na wananchi waliotembelea banda hilo.

"Wastaafu wengine wanashangaa kuona fedha zimeingia kwenye akaunti zao mara tu wanapotoka kazini na kujiuliza, 'Hizi fedha ni zangu kweli?' Hilo linaonesha wazi ukwasi wa Mfuko wa PSSSF na utekelezaji wa kaulimbiu ya Tunalipa Jana," amesema Mhe. Sangu.

Ameongeza kuwa hata wastaafu wanaopokea pensheni za kila mwezi hulipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi, na wakati mwingine hupokea malipo yao kabla ya watumishi walio bado kazini kupokea mishahara yao.

"Wastaafu wetu tumewapa kipaumbele. Mafanikio haya yametokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo yameuwezesha Mfuko kuendelea kukua na kutoa huduma bora kwa wanachama na wastaafu," amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Jafari Merai Mgala, amesema mafanikio ya utoaji wa huduma kwa haraka na kwa ufanisi yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na maboresho ya mifumo ya TEHAMA.

Amesema kwa sasa mwanachama au mstaafu anaweza kuwasilisha madai ya mafao akiwa mahali popote kupitia simu janja, kompyuta au kifaa kingine chenye uwezo wa kuunganishwa na intaneti, hatua iliyorahisisha upatikanaji wa huduma za Mfuko.

"Natoa wito kwa wanachama na wananchi wote wa Kanda ya Kusini kutembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Nanenane ili kupata elimu kuhusu huduma zetu pamoja na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na Mfuko," amesema Bw. Mgala.

Mwisho

Na; Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tanzania inatarajiwa kuingiza zaidi ya Sh bilioni 10 kutokana na mauzo ya biashara ya kaboni baada ya Serikali kuidhinisha miradi minne itakayouza tani milioni 4.2 za kaboni katika soko rasmi la kimataifa la biashara ya Kaboni.
SHIRIKA la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limesema linaendelea kuwasaidia wakulima na wajasiriamali kuongeza thamani ya mazao, kupunguza gharama za uzalishaji na kupata masoko kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa, maabara za ubora na suluhisho za nishati.

Serikali, kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.

Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.

“Mafuta yanapowasili nchini, Wakaguzi wa Mafuta hufuatilia hatua mbalimbali za upakuaji ili kuhakikisha yanakidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa,” amesema Mhandisi Makembe.

Ameeleza kuwa ufuatiliaji huo huanza mafuta yakiwa ndani ya meli na kuendelea wakati wa upakuaji na usafirishaji kupitia miundombinu maalumu, hadi yanapofikishwa kwenye maghala yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Kwa mujibu wa Mhandisi Makembe, Baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuidhinisha ubora wa bidhaa za mafuta kabla Meli haijaanza zoezi la Upakuaji ,Wakaguzi wa Mafuta wanajukumu la kuhakikisha kuwa taratibu za usalama na masharti ya upakuaji yanazingatiwa katika mchakato mzima wa upakuaji wa mafuta hayo. Hatua hiyo inalenga kulinda ubora wa mafuta na kuhakikisha shughuli za upakuaji zinafanyika kwa usalama.

Aidha, ukaguzi huo unalenga kubaini mapema changamoto zozote zinazoweza kuathiri ubora wa mafuta wakati wa upakuaji, usafirishaji au uhifadhi. Hatua hiyo husaidia kuhakikisha mafuta yanayopokelewa yanaendelea kuwa katika hali inayokubalika na TBS hadi yanapofikishwa kwenye maghala husika.

Meneja Msaidizi wa Idara ya Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Nasieku Kisambu akipokea Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa miradi ya CSR inayotekelezwa na mgodi huo.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Michael Mwang'onda (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele (kushoto mwenye skafu) wakifurahia uwekaji jiwe la msingi wa jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya Magoto kata ya Nyaikonga mradi unaogharamiwa na Barrick North Mara.

 


Na OWM – TAMISEMI, Morogoro

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wakulima, wafugaji na wavuvi kwa mchango wao mkubwa uliowezesha Tanzania kufikia utoshelevu wa chakula wa zaidi ya asilimia 120, hatua inayodhihirisha mafanikio ya uwekezaji unaoendelea kufanywa na Serikali katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Dkt. Mwigulu aliwasilisha pongezi hizo za Mhe. Rais Agosti 4, 2026, alipotembelea Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Nane Nane mkoani Morogoro.

 Katika ziara hiyo alijionea shughuli na ubunifu wa wakulima, wafugaji na wavuvi kutoka mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam, Pwani na Tanga.

Amesema maonesho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, "Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050," ambayo inawahimiza Watanzania kuzalisha kwa kuzingatia mahitaji ya soko, kutumia teknolojia za kisasa, kuongeza ubora wa bidhaa na kuimarisha mnyororo wa thamani ili kufanya kilimo kuwa biashara yenye tija na mchango mkubwa katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

"Kwa nilichojionea kupitia maonesho ya mwaka huu, ninaziona dalili zote kwamba ifikapo mwaka 2050 malengo ya Dira ya Taifa tuliyojiwekea yatakuwa yamefikiwa, kwa kuwa tuko kwenye hatua nzuri ya utekelezaji katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi," amesema Dkt. Mwigulu.

Ameongeza kuwa ameridhishwa na ubora wa mazao mbalimbali yaliyooneshwa, ikiwemo nyanya, bilinganya na bidhaa nyingine zinazokidhi viwango vya masoko ya kimataifa, yakiwemo ya Marekani na Ulaya, jambo linaloashiria kuwa Tanzania ipo kwenye mwelekeo sahihi wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani duniani.

Akizungumzia sekta ya mifugo na uvuvi, Dkt. Mwigulu amesema zimeendelea kuwa nguzo muhimu za uchumi wa taifa, akibainisha kuwa mchango wa sekta ya mifugo katika pato la taifa umeongezeka kutoka asilimia 2.3 hadi asilimia 6.2.

Ametoa mfano wa mafanikio ya wanaonufaika na sekta hiyo kwa kumtaja kijana mmoja mhitimu anayejihusisha na ufugaji wa kisasa, ambaye ameonesha ng'ombe mwenye uzito wa zaidi ya kilogramu 1,000 mwenye thamani ya takribani Shilingi Milioni 20. Aidha, amesema kijana huyo anafuga zaidi ya ng'ombe 200 na alipoulizwa na Waziri wa TAMISEMI kama anahitaji mkopo, alieleza kuwa hana uhitaji huo kutokana na mafanikio ya shughuli zake.

Awali, akitoa neno la utangulizi kabla ya Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi pamoja na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, alisema Waziri Mkuu alimpa jukumu la ulezi wa Mkoa wa Morogoro, hivyo alimkaribisha rasmi kama waziri mwenyeji wa mkoa huo, ambao ni mmoja wa mikoa inayounda Kanda ya Mashariki katika Maonesho ya Nane Nane.













 

Kilimo ni uti wa mgongo wa maisha na uwekezaji unaotegemewa na wengi kujenga hatua za maendeleo, lakini hakuna uchungu kama kutumia jasho na mtaji wako wote halafu ukaambulia patupu.

Baada ya kuwekeza akiba yangu ya miaka mingi, nilinunua shamba la hekari kumi na kuanza kilimo cha msimu. Nilipanda mbegu bora za kisasa, nikatumia mbolea za gharama, na kuhakikisha palizi inafanyika kwa wakati na umakini wa hali ya juu.

Hata hivyo, kile kilichotokea katika shamba langu kilikuwa ni maajabu yaliyomshaza kila mtu Kijijini. Wakati mashamba ya majirani zangu yaliyozunguka eneo langu yakistawi kwa kijani kibichi na kutoa mavuno tele, shamba langu lilikuwa likikauka ghafla.

Mimea ilianza kunyauka kuanzia chini, majani kubadilika rangi na kuwa ya njano, na matunda kupukutika kabla hayajakomaa. Nikaingia gharama za ziada kuleta wataalamu wa kilimo kupima udongo na dawa za wadudu, lakini hakuna kilichosaidia.

Kila msimu wa kuvuna ulipofika, nilikuwa nikiambulia hasara kubwa huku madeni ya pembejeo yakiniandama. Nilibaki nikijiuliza ni kwa nini ardhi ile ile, mvua ile ile, na huduma zile zile zinaleta matokeo tofauti kabisa kwangu. SOMA ZAIDI.

 

Kujenga familia na kuishi na mume unayempenda ni ndoto ya kila mwanamke, lakini pale hisia, uaminifu na heshima vinapotoweka ndani ya nyumba, ndoa inageuka kuwa uwanja wa mateso ya nafsi.

Baada ya kuishi na mume wangu kwa furaha na amani kwa miaka minne, ghafla mambo yalianza kubadilika kwa kasi ya ajabu. Mume wangu alibadilika tabia na kuanza kunichukulia kama mtu asiyekuwa na thamani yoyote mbele yake.

​Nia na hamu yake kwangu zilitoweka kabisa. Hakuwa akitaka kunigusa, kunibusu, wala kukaa karibu na mimi kama zamani. Kibaya zaidi, fedha zote alizokuwa akipata kazini na kwenye biashara zake alianza kuzitumbukiza nje kwa wanawake wa pembeni.

Huku mimi na watoto tukibaki bila hata pesa ya chakula na matumizi ya msingi ya nyumbani. Kila nilipojaribu kusema naye kwa upole au kulia, alipandwa na hasira kali, kunipigia kelele na kusema simvutii tena.

Nilibaki na majuto na msongo. SOMA ZAIDI.

 

Kutafuta fedha ni kazi ngumu inayohitaji jasho, muda, na akili nyingi, lakini hakuna maumivu makubwa kama kuona matunda ya kazi yako yakitoweka mikononi mwako kama moshi.

Kwa miaka kadhaa, nilikuwa nikifanya kazi kwa bidii na kupata mshahara pamoja na faida nzuri kwenye biashara zangu ndogo ndogo. Hata hivyo, maisha yangu ya kifedha yaligeuka kuwa fumbo la kutisha.

Kila pesa iliyoingia kwenye mikono yangu au akaunti yangu ya benki ilikuwa ikipotea kihasara na kwa njia za ajabu sana bila mimi kufanya la maana.

​Nikipokea fedha leo, kesho yake zingeibuka dharura zisizoelezeka simu au kifaa cha gharama kinaharibika ghafla, ugonjwa usiotarajiwa unaingia nyumbani, au kosa dogo linalogharimu fedha nyingi.

Hata pale nilipojaribu kuficha pesa taslimu kwenye kabati au pochi, nilikuta zimepungua bila mtu yeyote kugusa! Nilikuwa nikikaa na kuhesabu fedha zangu jioni, lakini kufika asubuhi nakuta kiasi kikubwa kimetoweka.

Nilibaki nikiwa na madeni yasiyotibika, nikikopa hapa na kurejesha pale, huku wenzangu niliowaingiza kwenye biashara wakipiga hatua na kujenga maisha yao. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu

WAMIKI wa vituo vya kulelea watoto nchini wamehimizwa kuwekeza katika mafunzo ya kitaalamu kwa walezi ili kuboresha ubora wa huduma za malezi na makuzi ya awali ya watoto, kufuatia kuongezeka kwa mahitaji ya wataalamu katika sekta hiyo.

 


‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara zinazoingia uwanja wa AFCON pamoja na maegesho ya magari huku ukiahidi kuhakikisha uwanja huo unafikika kwa barabara ya lami ndani ya muda uliokusudiwa.

‎Meneja wa TARURA mkoa wa Arusha, Mhandisi Nicholas Francis amesema mradi huo unahusisha ujenzi wa takribani kilomita 13 za barabara za lami zitakazorahisisha usafiri kwa wakazi wa maeneo hayo na wageni watakaohudhuria mashindano ya AFCON 2027.

‎Amefafanua kuwa mradi unajumuisha ujenzi wa barabara ya Essuri yenye urefu wa kilomita 2.45 kwa njia nne, barabara ya Lendita yenye kilomita 2.75 kwa njia nne, barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City yenye kilomita 5.5 kwa njia moja na kilomita 2.1 kwa njia nne pamoja na barabara za mzunguko zenye urefu wa kilomita 1.5 zinazojengwa kwa njia nne.

‎Mhandisi Francis amesema mradi ulianza rasmi tarehe 20 Aprili, 2026 na unatarajiwa kukamilika 20 Mei, 2027 ukiwa na muda wa utekelezaji wa miezi 13.

‎"Kwa sasa ujenzi umeelekezwa katika ujenzi wa barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City pamoja na barabara za mzunguko ili kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi Oktoba mwaka huu uwanja mpya wa michezo ufikike”amesema

‎Ameeleza kuwa utekelezaji wa barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City umefikia asilimia 53 huku mkandarasi akifanya kazi  usiku na mchana ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati. Aidha, katika eneo la daraja la barabara ya Essuri, kazi zinaendelea kwa saa 24 kila siku.

‎"Tunatarajia ifikapo mwisho wa mwezi Agosti mwaka huu utekelezaji wa Barabara ya Mateves utafikia asilimia 85 endapo hakutakuwa na changamoto kubwa hususan mvua", amesema.

‎Amesema baada  ya fidia kulipwa  kwa watu waliopitiwa na mradi huo, kasi ya utekelezaji imeongezeka kwa kiwango kikubwa. Tuna imani kwamba ifikapo mwezi Desemba mwaka huu ujenzi wa barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City utakuwa umekamilika kwa asilimia 100", amesema.

‎Kukamilika kwa mradi huo hakutasaidia tu kufanikisha maandalizi ya AFCON 2027 bali pia kutaimarisha mtandao wa barabara jijini Arusha, kupunguza msongamano wa magari, kuchochea shughuli za kiuchumi na kuacha urithi wa miundombinu bora itakayowanufaisha wananchi kwa vizazi vijavyo.








Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha kunakuwa na uwiano kati ya udhibiti wa taka za plastiki, ulinzi wa mazingira na ukuaji wa sekta ya viwanda ili uchumi wa nchi uendelee kuimarika.
 

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umefungua fursa mpya za uwekezaji katika sekta ya makazi, majengo ya biashara na maendeleo ya miji, hatua inayolenga kuboresha huduma kwa wananchi, kuvutia mitaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Meneja wa TBA Mkoa wa Dodoma, Qs. Emmanuel Wambura, amesema hayo katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.

Amesema TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi miradi mbalimbali ya Serikali katika sekta tofauti, ikiwemo ujenzi wa majengo ya Wizara ya Kilimo na taasisi zake, ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), vituo vya afya pamoja na taasisi nyingine za umma.

Kwa mujibu wa Qs. Wambura, utekelezaji wa miradi hiyo unalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha mazingira ya kazi katika taasisi za Serikali.

“TBA inaendelea kutekeleza dhamana yake ya kuhakikisha Serikali inapata majengo bora, salama na ya kisasa. Miradi mingi ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, huku mingine ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia miundombinu hiyo,” amesema Qs. Wambura.

Amesema mbali na miradi ya Serikali, TBA imeweka mkazo katika kuendeleza miradi ya makazi na miji ya kisasa, ikiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba 3,500 katika eneo la Nzuguni jijini Dodoma, ambao unaendelea kutekelezwa.

Amebainisha kuwa wakala huo umefungua fursa za uwekezaji kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), ambapo tayari baadhi ya wawekezaji, ikiwemo kampuni ya Fit Group kutoka Nigeria, wameonyesha nia ya kuwekeza katika mradi huo wa makazi.

Aidha, amesema TBA imeandaa maeneo yenye fursa kubwa za uwekezaji katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, ambapo wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika nyumba za makazi, majengo ya biashara, hoteli, ofisi na maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao.

Qs. Wambura amefafanua kuwa Mkoa wa Dodoma pekee una eneo la takribani hekta 630 lililoandaliwa kwa ajili ya uwekezaji, likiwa na miundombinu muhimu na mazingira rafiki kwa shughuli za biashara.

“Taratibu za uwekezaji ni wazi na rahisi. Tunawakaribisha Watanzania na wawekezaji kutoka nje ya nchi kushirikiana nasi katika kuendeleza miradi yenye tija kwa uchumi wa Taifa. Tunahitaji wawekezaji wenye uwezo na wanaozingatia sheria za nchi ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa,” amesema.

Katika hatua nyingine, amesema TBA imepanua wigo wa shughuli zake hadi kusimamia miradi ya ujenzi na ukarabati wa majengo ya ubalozi wa Tanzania nje ya nchi kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Amesema hatua hiyo inaonesha kuendelea kuaminiwa kwa uwezo wa kitaalamu wa wakala huo katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ndani na nje ya Tanzania.

Akizungumzia mchango wa TBA katika sekta ya kilimo, Qs. Wambura amesema wakala huo umeendelea kubuni na kusimamia ujenzi wa maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao, maabara za utafiti wa kilimo na miundombinu mingine muhimu inayosaidia kuongeza thamani ya mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kukuza ushindani wa sekta hiyo.

Amewakaribisha wananchi, taasisi na wawekezaji kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nanenane ili kupata taarifa kuhusu huduma zinazotolewa na wakala huo, ikiwemo usanifu wa majengo, ukadiriaji wa gharama za ujenzi, usimamizi wa miradi na fursa mbalimbali za uwekezaji.

“TBA ipo katika mikoa yote 26 ya Tanzania na itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga miundombinu ya kisasa, kuvutia uwekezaji na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” amesema Qs. Wambura.

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.