Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama (aliyekaa meza kuu) akimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (aliyesimama) alipokuwa akitoa shukrani kwa kamati hiyo baada ya kumaliza kikao kazi kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo na taasisi zake kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akitoa ufafanuzi wa hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Taasisi ya UONGOZI ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024 kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba akijibu hoja ya taasisi yake kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akijibu hoja ya taasisi yake kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shedrack Mziray akitoa ufafanuzi wa hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Mick Lutechura Kiliba akitoa ufafanuzi wa hoja iliyowasilishwa kwa taasisi anayoisimamia wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo na taasisi zake kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma, Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi akijibu hoja ya taasisi yake kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akifafanua hoja ya taasisi yake kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Capt. Budodi Budodi akijibu hoja ya taasisi anayoisimamia kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Sehemu ya Watendaji wa Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.


Na. Veronica Mwafisi-Dodoma


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia taasisi iliyopo chini yake ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kwa kusanifu na kusimamia mifumo mingi ya TEHAMA nchini ili kuboresha utoaji huduma kwa taasisi za umma.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama ametoa pongezi hizo leo jijini Dodoma kwa niaba ya kamati yake wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na Taasisi ya UONGOZI iliyolenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa tassisi hizo.

Mhe Mhagama amesema ni wazi kuwa kwa sasa taasisi zote za serikali zinatumia mifumo ya TEHAMA hivyo, eGA ina wajibu wa kuzisaidia taasisi hizo ili kutimiza malengo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwa na serikali ya kidijitali itakayokidhi mahitaji na viwango vikubwa katika kutoa huduma bora kwa wananchi.
Tunafahamu kuwa kila taasisi ya serikali inatumia mifumo ya TEHAMA, niwasihi endeleeni kushirikiana ili kuleta tija na manufaa katika utendaji kazi kwa lengo la kutimiza malengo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwa na serikali ya kidijitali kwa maendeleo ya nchi yetu. Dkt. Mhagama amesisitiza

Akizungumzia maeneo ambayo jiografia yake haipo vizuri, Mhe. Dkt. Mhagama amesema maeneo hayo yanapaswa kuwa na miundombinu ya TEHAMA itakayowezesha upatikanaji wa huduma za kimtandao uliosanifiwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) ili kuwasaidia watumishi wa umma kuendelea kutekeleza majukumu yao bila kuwa na changamoto ya kimtandao.
Katika hatua nyingine, Mhe. Dkt. Mhagama ameipongeza Taasisi ya UONGOZI kwa kuendesha mafunzo ya mara kwa mara kwa viongozi jambo ambalo linawasaidia watumishi katika taasisi mbalimbali kuwajibika kwa ufasaha kupitia mafunzo ambayo wamekuwa wakipatiwa kutoka katika taasisi hiyo.

Ameisisitiza taasisi hiyo kuendelea kuwajengea uwezo viongozi waliopo ili kuwa na viongozi bora na wazalendo kwa nchi yetu.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kwa kutoa ushauri, maoni na miongozo mbalimbali ambayo ofisi yake imekuwa ikiifanyia kazi na kwa asilimia kubwa imeisaidia ofisi hiyo kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Mhe. Mwenyekiti, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora inajivunia kusimamiwa na Kamati yako kwani mmekuwa mkitupatia ushauri, maoni na miongozo mbalimbali ambayo yameleta tija kwetu na kutufanya tutekeleze majukumu yetu kikamilifu na kwa ufanisi mkubwa sana. Mhe. Simbachawene amesema.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imemaliza kikao kazi chake cha siku mbili kwa kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na baadhi ya taasisi zake ikiwemo TASAF, eGA na Taasisi ya UONGOZI.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Adinan Mpyagila akikabidhi zawadi ya cheti mwanafunzi wa shule ya sekondari Lionja wakati wa mahafali ya 15 ya shule hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Adinan Mpyagila akizungumza na wazazi juu ya umuhimu wa elimu kwa watoto wao pamoja jitihada za serikali kuinua elimu hiyo wilaya ya Nachingwea 


Na Fredy Mgunda, Nachingwea, Lindi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Adinan Mpyagila ametangaza kutatua changamoto ya choo cha walimu hadi kufikia 30/11/2024 ili waalimu waendelee kutoa elimu bora kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Lionja.

Akizungumza wakati wa mahafali ya 15 ya shule ya sekondari Lionja, Mpyagila alisema kuwa walimu wanatakiwa kuwa na choo bora ambacho kitakuwa mbali na choo cha wanafunzi ili kulinda heshima ya mwalimu awapo shuleni na nyumbani.

Kufuatia changamoto hiyo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Adinan Mpyagila alifanya harambee ya ujenzi wa choo hicho na kufanikiwa kukusanya Kiasi cha shilingi 1,553,950 ambayo itasaidia ujenzi wa hadi kufikia tarehe 30/12024.

Mpyagila aliahidi kutoa mpira, jezi, mafuta,unga wa wangano na sukari kwa wanafunzi wa kidato cha nne ili kuwaongezea morali kufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne itakayofanyika hivi karibuni 

Aliwataka wazazi kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto wao katika kipindi ambapo dunia ipo kwenye mageuzi ya sayansi na teknolojia kwa faida ya familia zao na taifa kwa ujumla na aliwapongeza walimu kwa ufaulu wa asilimia 100 katika matokeo ya kidato cha nne na pili.

Aidha Mpyagila alikumbuka changamoto za shule, ikiwemo ukosefu wa mwalimu wa kike, na aliahidi kuchukua hatua za haraka kutatua tatizo hilo ili wanafunzi wa kike waweze kupata mwalimu anayeweza kutatua changamoto zao.

Katika hatua nyingine mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Adinan Mpyagila aliwasihi wananchi kujitokeza kupiga kura na kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa kuongoza miaka mitano ijayo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akiongoza kikao kazi cha kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akitoa ufafanuzi wa moja ya hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024 kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Abeid Ramadhani (katikati) akichangia hoja wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka akitoa ufafanuzi wa hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa ufafanuzi wa hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Naibu Katibu Mkuu, Bw. Xavier Daudi (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bw. Musa Magufuli (kushoto) kabla ya kuingia katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024 kilichofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria pamoja na Watendaji wa Ofisi hiyo kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Sehemu ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo kwa mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Sehemu ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na taasisi zake kwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuhakikisha huduma bora inatolewa kwa wananchi kwa wakati sahihi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama ametoa pongezi hizo jijini Dodoma kwa niaba ya kamati yake wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Aprili hadi Septemba 2024.

“Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imesheheni wabobezi wa sekta zote jambo linalowafanya watendaji wa ofisi hii pamoja na taasisi zilizopo chini yake kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Mhe. Dkt. Mhagama amesema.

Aidha Dkt. Mhagama ameishukuru Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa kamati hiyo kwani wajumbe wake wamekuwa wakipatiwa uelewa mpana juu ya utekelezaji wa majukumu ya kila taasisi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Dkt. Mhagama ameishauri Ofisi ya Rais- UTUMISHI na Utawala Bora kutoa mrejesho mara kwa mara kwa wananchi juu ya hatua mbalimbali ambazo imekuwa ikizichukua na kuzifanyia kazi baada ya kupokea malalamiko au changamoto ya masuala mbalimbali ili kuonesha namna ambavyo ofisi hiyo imekuwa ikiwajibika na kutekeleza majukumu yake kwa kiwango kikubwa.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria itapokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kwa siku mbili, tarehe 21 na 22 Oktoba, 2024.

 Na Denis Chambi, Tanga.

Naibu waziri wa nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia Dkt James Mataragio ameeleza kuwa wizara hiyo ipo kwenye mpango wa kuendelea kuitangaza Tanzania kimataifa ambapo inatarajia kuvinadi vitalu vya utafutaji wa mafuta sambamba na kuingia makubaliano ya uzalishaji na makampuni ya nje ya nchi.

Akizungumza hayo Dkt Mataragio baada ya kufungua kikao cha pili cha mkutano wa baraza la wafanyakazi ‘PURA’ amesema kuwa itakuwa ni awamu ya tano inayotarajiwa kufanyika mwaka 2025 itakayokwenda sambamba na mkutano wa kimataifa wa East Afrika Petroli conference Exhibition ukijumuisha nchi zote za Afrika Mashariki.

Aliongeza kuwa ikiwa tayari zimeshafanyika  hatua nne toka mwaka  2000 Tanzania inazidi kufunguka kiuchumi kupitia gesi asilia kutokana na kuvutia wawekezaji wengi wa ndani na nje ya nchi hali ambayo inakwenda kuongeza pato la Taifa na kumuinua mtanzania mmoja mmoja.

Alisema kuwa mkutano huo unatazamiwa kufanyika Machi 5 mwaka 2025 mkoani Dar es Salaam na wanatarajia mgeni rasmi atakuwa Rais Dkt Samia Suluhu  kwa ajili ya kuzindua vitalu na watavinadi vitalu 24 ambavyo wanapanga kuvinadi huku wakiwakaribisha wawekezaji kutoka nchi mbalimbali kuja kuangalia vitalu.

Aidha alisema kwamba wameingia mkataba na kampuni ya TGS ambao wameingia mkataba wa kufanya masoko ya vitalu na Serikali imejipanga vizuri na kikubwa kuwa na uwazi na utayari na wizara imejipanga kushirikiana na Pura ambao ndio  msimamizi wapo nao pamoja katika zoezi la kunadi vitalu hivyo.

“Tunategemea katika jitihada zinazofanywa sasa tunaanza kuitangaza nchi kwenye sekta ya mafuta na hivi karibu mtaona makapuni mengi yanakuja Tanzania na tuna miradi mikubwa ya kuchakata gesi unaofanyika Lindi ni miradi tunayoitangaza”Alisema

Alisema kwamba hiyo yote inaonyesha mazingira bora yaliyopo nchini ya uwekezaji kwa sababu mwekezaji anaposikia nchi ina mradi wa Dola Bilioni 42 ambao unataka kufanyika Tanzania anakuwa na imani kwamba sheria zetu,vivutio vyetu vya kifedha, taasisi zetu zinauwezo hivyo wawekezaji wakija nchini na kuwekeza uwekezaji wao utakuwa salama.

“Kwa muda mrefu tumekuwa tukinadi vitalu vyetu na kujitahidi kuhakikisha kunadi vitalu pamoja na kuingia makubaliano ya uzalishaji na makampuni ya nje mara ya mwisho tulinadi vitalu 2013 na kukaa muda mrefu bila ya kufanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali ikwemo ni takwa ya kisheria”Alisema

Alisema kwa sababu njia ya sharaingi ya mwaka 2013 ilikuwa haisomani na sheria ya mafuta ya mwaka 2015na sasa walichokifanya kama wizara wamebadilisha mkataba wa mauzo wa mfumo wa uzalishaji ambao itasadia kwenda kujadili mikataba mbalimbali ya uwekezaji kwenye upande wa mafuta na itatoa vivutio vyingi itakayowasaidia kampuni za kimataifa za mafuta kuja kuwekeza Tanzania,

Awali akizungumza wakati wa mkutano huo Mkurugenzi wa PURA Mhandisi Charles Jimmy na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la PURA alisema kwamba watanadi vitalu na ambacho kinachofanyika kwa mujibu wa sheria na wao wanasimamia kwa sasa Tanzania ukichukua eneo lake la kilomita za mradi 947,000 kiasi cha eneo la mraba 534,000 zinaonyesha viashiria vya kuwa na mafuta au gesi asilia.

Aidha alisema kati ya hizo ni 534,000 wana 162,000 ambazo tayari zimeshafanyiwa kazi sawa na asilimia 30 na vitalu 21 vitatoka bahari kuu na vitatu vitatu vitatoka upande wa Ziwa Tanganyika na watavitangaza na watu watatoa mapendekezo ya kuvifanyia kazi.



Alisema kwamba watazingitia vigezo vilivyowekwa pamoja na nchi itapata nini kutokana na mapendekezo yao na baadae watachagua aliyebora wampe vitalu kimoja, viwili au vitatu ili aendelee kufanya utafiti na wao watasimamia hizo tafiti ili baadae akigundua.

 



Ferdinand Shayo ,Arusha.


Mkuu wa Wilaya ya Karatu Dadi Kolimba amekipongeza Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia vijijini (CAMARTEC) kwa kusambaza teknolojia na mashine mbali mbali za kulima ,kuvuna na kuchakata mazao pamoja na kuyaongezea thamani ili yaweze kupata bei nzuri katika masoko ya ndani na nje ya nchi hivyo kuwakomboa wakulima.

Akizungumza mara baada ya kutembelea kituo kihandisi cha Teknolojia za Kilimo kilichoanzishwa na CAMARTEC katika kijiji cha Gongali Wilayani Karatu ambapo amejionea zana mbali mbali ikiwemo mashine za Kupukuchua mahindi,maharage,alizeti na matrekta ,Mkuu wa Wilaya hiyo amesema kuwa kituo hicho kitawasaidia wakulima kulima kwa kisasa na kuchakata mazao yao kwa kutumia zana za kisasa.

Kolimba ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuiwezesha Camartec kufungua kituo kijijini hapo na kuwafikia wakulima wengi na kuongeza kuwa uhitaji wa mashine hizo bado ni mkubwa kwa wilaya hiyo yenye wakulima wengi zaidi.

Kaimu Mkurugenzi wa CARMATEC Mhandisi Godfrey Mwinama amesema wataendelea kufanya utafiti na kutengeneza mashine ambazo zitakua mkombozi kwa wakulima kwa kuwokolea muda na gharama lunwa walizokuwa wakitumia kutokana na teknolojia duni.

"Tunaishukuru sana Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dr
Samia Suluhu Hassan kwa kutuwezesha kuwasogezea wakulima wa vijijini mashine mbali mbali " Anaeleza Godfrey Mwinama Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa CARMATEC.

Kwa upande wao wakulima wakiwemo Rogati Israel na Musa Hussein wamesema kuwa mashine walizozipata kutoka CAMARTEC Zimewasaidia kupukuchua mahindi na maharage kwa muda mfupi bila kuharibu ubora wa mazao hayo.






 


Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu  ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa shughuli za utafiti wa Wanyamapori ambazo zina tija katika  sekta ya uhifadhi na utalii  ambayo inachangia asilimia 17% ya pato la Taifa.

Akizungumza  jijini Arusha wakati wa kikao na Menejimenti ya TAWIRI, Bw. Mchechu  amesema Ofisi ya msajili wa Hazina  itaendelea kushauri vyema katika kuimarisha Mashirika ya Umma yaweze kujiendesha kwa tija.

“nawapongeza kwa utendaji mzuri, nitoe wito kuendelea kuwa wabunifu kutumia  rasimali mlizo nazo kujiendesha kwa ufanisi” amehimiza  Bw.Mchechu

Naye, Mkurugenzi Mkuu TAWIRI Dkt, Eblate Mjingo amesema TAWIRI ni taasisi ya kimkakati  ambayo mbali na kutokuonekana  ikizalisha  fedha moja kwa moja ina mchango  mkubwa katika mapato yatokanayo na utalii nchini ambapo takwimu na taarifa za tafiti ndizo zinazonadi utalii na kuimarisha uhifadhi

 


Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, leo Oktoba 21, 2024, imetiliana saini makubaliano ya uwekezaji na mafunzo na Kampuni ya Huduma za Mawasiliano ya Kielekroniki ya China (CECIS LTD) ambapo kupitia makubaliano hayo, zaidi ya makampuni 600 ya vifaa vya kompuya yataweza kuwekeza nchini.

Lengo la uwekezaji huo ni kuongeza ujuzi kwa vijana na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utengenezaji wa kompuya kimataifa.

Makubaliano hayo yamesainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Mohammed Abdulla na Mwenyekiti wa Kampuni ya Huduma za Mawasiliano ya Kielekroniki ya China CECIS Bw. Guo Zhaoping na kushuhudiwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Maryprisca Mahundi ambaye amesema Tanzania inakwenda kupiga hatua kubwa katika masuala ya uchumi wa kidijitali.

"Makubaliano haya ni matokeo ya ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini China aliyoifanya hivi karibuni, Kampuni hii ni wabobezi wa masuala ya usalama wa mitandao hivyo elimu waliyonayo itawawezesha vijana kujifunza kwani tunahitaji wataalam wengi zaidi wa TEHAMA nchini" amesema Mhe. Mahundi.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Mohammed Abdulla amesema uwekezaji huo utatoa fursa kwa watanzania kujifunza na kupata ajira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kampuni ya huduma za mawasiliano ya kielekroniki ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Sayansi na Teknolojia wa Kamati ya Kampuni hiyo Bw. Guo Zhaoping amesema uwekezaji huo umefuata misingi ya nchi za Tanzania na China na kwamba unalenga kuchochea maendeleo ya uchumi wa kidijitali.

"Kampuni yetu inafanya uwekezaji katika mambo makuu matano ikiwepo sekta ya kompuya na usalama wa mitandao ambapo pamoja na kufanya shughuli za kibiashara pia tunalenga kukuza uchumi wa kidijitali baina yetu na nchi zingine, kwa hapa Tanzania tutafanya kazi kulingana na mahitaji" amesema Bw. Zhaoping.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Dkt. Nkundwe Moses Mwasaga amesema pamoja na mambo mengine, pia wamekubaliana kuvutia makampuni mbalimbali ya Kielekroniki kuwekeza nchini ambapo mwaka 2025 kutakuwa na maonesho makubwa ya utengenezaji wa vifaa vya kompuya Afrika ambapo Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kupitia Tume yake watakuwa wenyeji wa maonesho hayo.

Makubaliano hayo yamesainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Mohammed Abdulla na Mwenyekiti wa Kampuni ya huduma za Mawasiliano ya Kielekroniki ya China (CECIS) Bw. Guo Zhaoping.