📌Yasema ni matunda ya  uzalendo wa Watanzania katika kulipa kodi


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi mzuri wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ikieleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 ambao umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na kuwa miongoni mwa miradi mikubwa barani Afrika.

Hayo yamebainishwa leo Juni 29, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu (Mb), wakati wa ziara ya Kamati hiyo katika Mradi wa Kufua Umeme wa JNHPP uliopo Rufiji, mkoani Pwani, kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo.

"Sisi kama Kamati tumeridhishwa na kazi kubwa iliyofanyika katika mradi huu hadi kukamilika kwake kwani mradi huu umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na unachangia takribani asilimia 45 ya umeme kwenye Gridi ya Taifa. Hivyo, nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza utekelezaji wa mradi huu wa kimkakati ambao umeleta suluhisho la kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini," amesema Mhe. Mgalu.

Aidha, Mhe. Mgalu amewashukuru wananchi kwa kulipa kodi ambazo zimepelekea mradi huo mkubwa kukamilika huku akisisitiza kuwa Kamati itaendelea kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa umeme wa uhakika wakati wote.

Amefafanua kuwa umeme unaozalishwa na JNHPP utaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme kupitia miradi mbalimbali ya usafirishaji wa umeme ikiwemo mradi wa Chalinze–Dodoma.

 Vilevile, Mhe. Mgalu amesisitiza kuhusu kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuhakikisha umeme unaopatikana nchini unafika hadi ngazi ya vitongoji.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Umeme, Mhandisi Christopher Bitesigirwe, amesema ziara ya Kamati imelenga kujionea maendeleo ya mradi huo na imejiridhisha kuwa mitambo yote tisa imekamilika na inafanya kazi vizuri huku akiwahakikishia kukamilisha kwa wakati miradi yote ya usafirishaji na usambazaji wa umeme inayounganishwa na JNHPP.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Antony Mbushi, amesema TANESCO itaendelea kuhakikisha Kituo cha Kufua Umeme cha JNHPP kinaendeshwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwajengea uwezo wataalam wa Kitanzania wanaokisimamia ili kiendelee kuzalisha umeme wa uhakika kwa manufaa ya wananchi na maendeleo ya Taifa.
















 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius J. Ndejembi amesema mradi wa kimkakati wa kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani, mkoani Tanga nchini Tanzania wa EACOP (East African Crude Oil Pipeline), umefikia asilimia 86 ya utekelezaji, huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 2026.

Waziri Ndejembi ametoa kauli hiyo leo, Juni 29, 2026, wakati akikagua utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) katika eneo la Chongoleani, mkoani Tanga.

Mhe.  Ndejembi amesema kuwa kutokana na kasi nzuri ya utekelezaji wa mradi huo, meli ya kwanza inatarajiwa kuchukua mafuta ghafi kutoka Chongoleani mwezi Januari 2027, hatua muhimu inayosubiriwa kwa hamu.

Akitoa maelekezo kuhusu changamoto zilizobainishwa na mkandarasi, Waziri Ndejembi amemtaka mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa njia ya umeme itakayotumika katika uendeshaji wa mitambo kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo ifikapo mwanzoni mwa mwezi Agosti.

“Changamoto ndogo ndogo tulizozikuta ni kama umeme bado line hazijafika na nimemtaka mkandarasi kupitia Shirika letu la TANESCO kuhakikisha mpaka ifikapo tarehe ya mwisho wa mkataba wake awe amekamilisha kazi yake,” amesisitiza Waziri Ndejembi.

Amesema mradi huu ni miongoni mwa miradi ya mfano nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla, ukiwa umegharimu Dola za Marekani Bilioni 6.02. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechangia Dola za Marekani Milioni 374, sawa na asilimia 15 ya mchango wa wanahisa.

Kadhalika, Waziri Ndejembi ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutumia vizuri na kuchangamkia fursa zinazotokana na mradi huo. Amesema katika kipindi cha ujenzi, jumla ya ajira 10,000 zimezalishwa, ambapo ajira 7,500 sawa na asilimia 75 zimenufaisha Watanzania.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian, ametoa pongezi kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha utekelezaji wa mradi huo nchini Tanzania kwa ushirikiano na Uganda. Amesema kati ya mikoa nane inayopitiwa na mradi huo, Mkoa wa Tanga umefaidika kwa kiwango kikubwa kupitia fursa mbalimbali za ajira na maendeleo kwa wananchi, hususan vijana.

















NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) imewahimiza wananchi na wadau wa maendeleo kutembelea banda lake katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) ili kupata huduma mbalimbali na elimu kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake.
Na Mwandishi Wetu

NDOTO za vijana wa Tanzania wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali nje ya nchi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 zimeingia hatua muhimu baada ya Global Education Link kuwakutanisha wanafunzi hao pamoja na wazazi na walezi wao kwa ajili ya kuhakiki nyaraka na kukamilisha maandalizi ya safari.
Siku nilipogundua kwamba mume wangu alikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine, nilihisi dunia yangu imeporomoka. 

Tulikuwa tumekaa kwenye ndoa kwa miaka kadhaa na niliamini tulikuwa tunajenga maisha mazuri pamoja. Kugundua ukweli huo kuliniacha na maumivu makubwa, hasira, na maswali mengi ambayo sikuwa na majibu yake.

Mwanzoni nilitaka kukabiliana nao kwa hasira.
Nilifikiria kumpigia simu mwanamke huyo na hata kwenda kumtafuta ili tuzungumze. Lakini kila nilipotulia, niliona kwamba ugomvi usingeweza kujenga ndoa yangu upya. Nilihitaji suluhisho ambalo lingeokoa familia yangu.SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha kampuni yangu, nilikuwa na ndoto ya kuifanya ikue na kushindana na kampuni kubwa zilizokuwa sokoni. 

Tulifanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kila mteja anapata huduma bora. Hata hivyo, ili kampuni iweze kupiga hatua kubwa, tulihitaji kupata zabuni kubwa ambayo ingetupa nafasi ya kukua. Haikuwa rahisi.

Mara kadhaa niliwasilisha maombi ya zabuni katika taasisi mbalimbali, lakini kila mara nilipokea taarifa kwamba kampuni nyingine ndiyo ilikuwa imechaguliwa. 

Kila kushindwa kuliniongezea maumivu na kunifanya nipoteze matumaini. Baada ya muda, hali ya kifedha ya kampuni ilianza kuwa mbaya.

Mapato yalipungua na baadhi ya miradi ilisimama kutokana na ukosefu wa fedha. Nilianza kuogopa kwamba ningelazimika kufunga kampuni ambayo nilikuwa nimeijenga kwa miaka mingi. Nilikuwa karibu kukata tamaa. SOMA ZAIDI.

Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kufanikiwa. Nilichagua eneo zuri, nikahakikisha bidhaa zangu zina ubora, na nilihudumia kila mteja kwa heshima. Mwanzoni biashara ilikuwa inaenda vizuri, lakini baada ya muda idadi ya wateja ilianza kupungua.

Kila siku nilifungua duka nikiwa na matumaini.
Lakini mara nyingi nilimaliza siku bila kuuza chochote cha maana. Wakati mwingine nilikaa kwa saa nyingi nikisubiri mteja mmoja tu aingie dukani. Gharama za kodi, umeme na bidhaa ziliendelea kuongezeka huku mapato yakizidi kushuka.

Nilijaribu kila nilichoweza. Nilitangaza biashara yangu, nikapunguza bei za bidhaa na hata nikaanzisha ofa maalumu, lakini bado hali haikubadilika. Nilianza kufikiria kufunga biashara kwa sababu hasara zilikuwa zimekuwa nyingi. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miaka sita, niliishi nikipigania ardhi ambayo nilijua ilikuwa yangu halali. Nilikuwa nimeinunua kwa fedha nilizozitafuta kwa jasho, lakini muda mfupi baadaye watu wengine walianza kuidai. 

Kila nilipofikiri mgogoro umeisha, changamoto mpya iliibuka. Nilizunguka katika ofisi mbalimbali nikitafuta haki yangu, lakini sikuona mwisho wa matatizo hayo.

Hali hiyo ilininyima amani. Sikuweza kuendeleza mipango yangu ya kujenga nyumba kwa sababu sikuwa na uhakika kama ningebaki na ardhi hiyo. 

Watu wengi walinishauri niikate tamaa na nitafute sehemu nyingine, lakini moyo wangu haukukubali kupoteza mali yangu. SOMA ZAIDI.
Dada yangu alikuwa mtu wa karibu sana katika maisha yangu. Tulikulia pamoja, tukashirikiana katika kila hatua ya maisha, na tuliamini hakuna jambo ambalo lingeweza kututenganisha. Lakini baada ya kutokea mgogoro wa kifamilia, kila mmoja alichukua upande wake na mawasiliano yakakatika kabisa.

Mwaka mmoja ukawa miwili. Miaka miwili ikawa mitano, na kabla hatujagundua, miaka kumi ilikuwa imepita bila kuonana wala kuzungumza. Kila mmoja aliendelea na maisha yake kana kwamba mwenzake hakuwahi kuwepo. Nilikuwa nikimuona kwenye sherehe za kifamilia mara chache.

Lakini kila mmoja aliepuka mwenzake. Hakukuwa na salamu, hakukuwa na mazungumzo, na hali hiyo iliwaumiza hata wazazi wetu ambao walitamani kutuona tukipatana tena. Kadri miaka ilivyozidi kusonga, nilianza kuona pengo kubwa lililokuwa limejitokeza ndani ya familia yetu. SOMA ZAIDI.

 


Awataka kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa wanafunzi walioshiriki mashindano ya UMISSETA mwaka 2026 kuendeleza vipaji vya michezo na Sanaa walivyonavyo kwani vitawasaidia katika maisha yao ya baadaye, huku akiwataka kuzingatia nidhamu na kusoma kwa bidii ili  kufikia ndoto zao na kutoa mchango katika maendeleo ya taifa.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa wanafunzi leo Juni 28, 2026 mjini Iringa katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Lugalo, wakati akifunga mashindano ya UMISSETA kwa mwaka wa 2026.

“Nina wasihi muendelee kuwa na nidhamu, kujituma katika masomo yenu na kuendeleza vipaji vyenu vya michezo na sanaa, msiviache vipaji vyenu kwani hata mimi juzi tulipokuwa tunapokea Mwenge wa Uhuru Lushoto nilijikuta nikikumbushia kipaji changu cha kupiga ngoma za utamaduni na kuimba kwa umahiri,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amewahakikishia wanafunzi hao kuwa, Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kuhakikisha vipaji vya wanafunzi vinaibuliwa, vinatambuliwa, vinakuzwa ili kuwanufaisha na kulinufaisha taifa kupitia ushiriki wao katika kuliwakilisha taifa kwenye mashindano ya michezo na Sanaa ndani na nje ya nchi.

Aidha, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu, michezo, sanaa na maendeleo ya vijana kwenye ajenda kuu ya taifa na kuongeza kuwa, uwekezaji huo unaendelea kuweka msingi imara wa kuibua na kuendeleza vipaji vya watoto na vijana wa Tanzania.

 Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Bw. Atupele Mwambene amesema kuwa, ushiriki wa wanafunzi katika michezo mbalimbali ya UMITASHUMTA na UMISSETA umeendelea kuwa jukwaa muhimu la kitaifa la kuibua vipaji, kuimarisha afya, kujenga urafiki na kuendeleza umoja wa kitaifa miongoni mwa wanafunzi. 

Naye Mwakilishi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Leah Kihimbi amemuhakikishia Prof. Shemdoe kuwa wizara yake itatekeleza ipasavyo jukumu la kuibua kuendeleza vipaji na vipawa vinavyotokana na mashindano hayo ya sanaa na michezo shuleni. 

Mwakilishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ambaye ni Afisa Mdhamini Bw. Mohamed Nassoro Salimu amesema Zanzibar inakwenda kujipanga ili kuleta ushindani mkubwa katika mashindano ya mwakani, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kufanya mageuzi katika sekta ya michezo.

Akitoa neno la shukrani, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru amewashukuru maafisa elimu, wakuu wa shule, walimu, waratibu wa michezo na walezi wa wanafunzi, kwa kazi kubwa walioifanya ya kuwaandaa na kuwaleta wanafunzi katika mashindano ambayo yamewawezesha kujifunza thamani ya nidhamu, ushindani wa haki, uvumilivu, uzalendo na mshikamano wa kitaifa.















NAIBU Waziri wa Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Longido Mkoani Arusha, Dkt Steven Kiruswa amewataka wananchi wa jimbo hilo kujenga umoja  na wananchi wa nchi jirani ya Kenya kwani viongozi wa juu ya nchi hizo wanamahusiano mazuri na hivyo nao wanapaswa kufuata nyayo hizo. 

Kiruswa alisema hayo juzi katika kijiji cha Kimwat kilichopo kata ya Sinonik wilayani Longido ambacho kipo mpakani mwa Kenya wakati akizindua miradi miwili ya maendeleo ikiwemo mradi wa Zahanati na mradi wa maji vyote vikiwa na gharama ya zaidi ya shilingi milioni 188.3 miradi hiyo imetekelezwa kwa mchango wa Mbunge Kiruswa , nguvu za wananchi,shirika lisilo la kiserikali la Pingo's na fedha kutoka serikali kuu.

Alisema kijiji hicho na kata kwa ujumla walikuwa wakipata huduma ya maji ,elimu na afya katika nchi jirani ya Kenya kutokana na mahusiano mazuri waliyajenga na wananchi wa nchi hizo lakini awamu ya sita ya uongozi wa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan huduma hiyo inapatikana nchini na sasa wananchi wa Kenya wanakuja kupata huduma hizo hapa nchini.

Kiruswa alisema kutokana na uhusiano mzuri na wananchi wa Kenya na Tanzania ndio màana Uzinduzi wa miradi hiyo umehudhuriwa wananchi wa nchini humo wakiongozwa na viongozi wao akiwemo  Afisa Mtendaji Kijiji cha Meto,Peter Milia na Joseph Kink Afisa Mtendaji wa Kata ya Meto.

Alisema mradi wa Zahanati ulianza kujengwa june 2023 na kukamilika mwaka huu yeye binafsi amechangia kiasi cha shilingi milioni 5,michango ya wananchi sh milioni 11 na fedha toka serikali kuu zilipelekwa shilingi milioni 80 na sasa Zahanati hiyo inahudumia wananchi wa Kijiji cha Kimwat na wananchi wa nchi jirani.

Naibu Waziri kiruswa aliipongeza Pingo’s kwa kusimamia na kutoa fedha shilingi milioni 70 ,michango ya wananchi shilingi milioni 2.3 na Mbunge shilingi milioni 20 na kusema kuwa mradi huo utasaidia wananchi na wananchi na mifugo na utekelezaji huo ni kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) kufikisha huduma karibu na wananchi.

Naye Mkuu wa wilaya ya Longido ,Salumu Kally amewaomba wananchi wa Longido kumpa ushirikiano Mbunge Kiruswa kwani kiongozi mwenye upendo na wananchi wake na amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha huduma zote muhimu ikiwemo miradi ya Maji ,Afya ,elimu ,umeme na Barabara inakamilika kwa maslahi ya wananchi wake hivyo hapasŵi kupotezwa katika uongozi wake.

Naye Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kimwat Rosemary Mbogho wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi Kiruswa alisema kijiji kinakabiliwa na changamoto ikiwemo upungufu wa watumishi wa Zahanati,nyumba za watumishi ,madarasa ,barabara na umeme katika vitongoji na Mbunge Kiruswa aliahidi yeye na marafiki zake kujenga nyumba ya watumishi na suala la barabara alimwagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini(TARURA) kutekeleza hilo kwani bajeti fedha hizo zipo.