Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.

...

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.

Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.

Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.

Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.

“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.

Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuongeza vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya  umeme ili kuongeza wigo wa utoaji huduma hiyo ambayo imeonekana kuleta mageuzi katika matumizi ya nishati safi.

Mhe. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma.

Waziri huyo mwenye dhamana ya Utumishi ametumia nafasi hiyo kuipongeza TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati safi kwa ajili ya  kupikia na katika vyombo vya usafiri.

‘’ TANESCO mnafanya kazi kubwa nawapongeza kwa mageuzi ya matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, natoa rai muongeze Vituo vya kuchajia vyombo hivyo ili kuongeza wigo wa utoaji huduma,’’ alisisitiza Mhe. Ridhiwani

Naye Meneja Masoko Bw. Fredrick Kalinga amesema TANESCO inashiriki katika Maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika ikiwemo maendeleo ya miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme, maboresho makubwa yaliyofanywa na Shirika kwenye mifumo ya kidigitali ya utoaji huduma kwa wateja pamoja na kuhamasisha jamii kutumia nishati safi ya umeme kupikia na katika vyombo vya usafiri kama magari, bajaji, guta, na pikipiki.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026  yenye kauli mbiu isemayo ‘’Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa huduma Endelevu’’ yameanza rasmi Juni 16, 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026










 


Serikali imeendelea kuimarisha jitihada za kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia upatikanaji wa mitaji, mafunzo na masoko ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya Taifa. 

Hayo yameelezwa leo Juni 17, 2026 bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga (Viti Maalum) aliyetaka kufahamu mipango maalum ya Serikali katika kuwawezesha wanawake.

Akijibu swali hilo, Mhe. Mahundi amesema Serikali inatumia mifumo mbalimbali ya uwezeshaji inayotekelezwa kupitia Wizara za kisekta pamoja na mamlaka za serikali za mitaa ikiwa na lengo la kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kujenga uwezo wa kiuchumi, kuongeza kipato na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Amefafanua kuwa miongoni mwa mipango hiyo ni utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri pamoja na Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake huku kabla ya kunufaika na mikopo hiyo, wanawake hupatiwa mafunzo ya kuongeza thamani ya bidhaa wanazozalisha kupitia ushirikiano kati ya Serikali, SIDO, VETA na taasisi mbalimbali zinazojihusisha na maendeleo ya wanawake.

Naibu Waziri huyo pia amesema Serikali inaendelea kutekeleza Programu ya Jenga Kesho Yako (BBT) katika sekta za kilimo, mifugo na ufugaji nyuki, ambayo imekuwa ikitoa fursa kwa wanawake kujikita katika shughuli za uzalishaji mali ambayo imeendelea kuwajengea uwezo wa kiufundi na kuwasaidia kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na sekta hizo muhimu.

Katika sekta ya madini, Mhe. Mahundi amesema Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) linaendesha programu maalum zinazowawezesha wanawake kushiriki katika shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa kuwapatia mafunzo, maarifa na kuwaunganisha na fursa mbalimbali za uwekezaji. Hatua hiyo inalenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta hiyo yenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

Aidha, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kuimarisha huduma jumuishi za kifedha zinazowawezesha wanawake kupata mitaji kupitia SACCOS na kuboresha mazingira ya uwezeshaji wa wanawake ili kuhakikisha wanapata mitaji, mafunzo na masoko ya uhakika yatakayowasaidia kukuza biashara zao na kuchangia kwa kiwango kikubwa zaidi katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.


















 


‎Wkala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia mradi wa RISE imeendelea kuimarisha ushiriki wa wananchi katika shughuli za matengenezo ya barabara kwa kutumia vikundi vya Kijamii vya Matengenezo ya Kawaida ya Barabara (CBRM) hatua inayolenga kuongeza ajira, kukuza uchumi wa wananchi na kuhakikisha barabara zinabaki katika hali nzuri mwaka mzima.

‎Akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu yanayoendelea jijini Arusha, Mtaalamu wa masuala ya  kijamii kutoka TARURA Makao Makuu, Bi. Mwanamisi Abdallah amesema mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa takwa la kisheria linaloelekeza asilimia 30 ya bajeti ya kazi za barabara kutengwa kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya barabara.

‎Amesema TARURA kupitia Mradi wa RISE imeamua kutumia fursa hiyo kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuunda na kuimarisha vikundi vya kijamii vyenye wanachama kati ya watano hadi ishirini ambavyo vitashiriki katika utekelezaji wa kazi mbalimbali za matengenezo ya barabara.

‎"Vikundi hivi vitapatiwa mikataba ya kufanya kazi za kusafisha mitaro, kuziba mashimo madogo, kuondoa vikwazo vinavyokatiza njia, kufyeka majani pamoja na shughuli nyingine ambazo hazihitaji matumizi ya mitambo mikubwa. Hii ni fursa kwa wananchi kupata ajira, kuongeza kipato na kushiriki moja kwa moja katika kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo yao", amesema Bi. Mwanamisi.

‎Kwa upande wake, Mratibu wa Kitaifa wa Programu kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. Dampu Ndenzako amesema ushirikiano kati ya ILO na TARURA unalenga kujenga uwezo kwa wataalamu na kuhakikisha vikundi vya kijamii vinatumika kikamilifu katika matengenezo ya barabara huku vikitoa manufaa ya kiuchumi kwa wananchi.

‎Amesema uzoefu unaonesha kuwa ushiriki wa wananchi katika matengenezo ya barabara hususan maeneo ya vijijini huongeza umiliki wa miundombinu hiyo, huimarisha huduma za usafiri na usafirishaji na kuhakikisha barabara zinapitika katika misimu yote ya mwaka huku wananchi wakinufaika kwa kupata ajira na kuongeza kipato.

‎Naye, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kongwa Mhandisi Peter Johnson, amesema wilaya hiyo imeanza kutekeleza mpango huo katika mwaka wa fedha 2025/26 ambapo imefanikiwa kuunda vikundi 34 vya CBRM, kati ya hivyo vikundi 31 tayari vimeanza kazi huku vingine vikiendelea kukamilisha taratibu za kuingia mikataba.

‎Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Bi. Hidaya Abdallah amesema mafunzo hayo yatawawezesha wataalamu wa maendeleo ya jamii kutambua, kuunda, kusajili na kuvijengea uwezo vikundi kwa kuzingatia miongozo na taratibu zilizowekwa huku wananchi wakipata fursa za ajira, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya miundombinu na uchumi wa jamii kwa ujumla.

‎Mafunzo hayo ya siku sita yanawakutanisha Wahandisi na Wataalamu wa Mazingira na Jamii kutoka TARURA Makao Makuu, Ofisi za Mikoa na Wilaya pamoja na Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi za Wakurugenzi wa Wilaya kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kusimamia utekelezaji wa mpango huo katika mwaka wa fedha 2026/27.











Nilipoolewa, niliamini ndoa yangu ingekuwa mahali pa furaha, amani, na upendo. Kwa miaka ya mwanzo mambo yalikuwa mazuri. 

Mimi na mume wangu tulikuwa karibu sana na tulifurahia muda wetu pamoja. Lakini kadri miaka ilivyopita, hali ilianza kubadilika taratibu.

Mazungumzo yetu yalipungua.

Tulianza kugombana kwa mambo madogo madogo. Wakati mwingine tungekaa siku nzima bila kuzungumza vizuri. 

Upendo ambao zamani ulikuwa wazi ulianza kupoa kiasi kwamba nilianza kuhisi kama tunaishi pamoja kama marafiki tu. Kwa kweli jambo hilo liliniumiza sana.

Nilijaribu kufanya kila nilichoweza ili kuboresha hali. Nilizungumza naye mara kadhaa kuhusu hisia zangu, lakini mazungumzo mengi yaliishia kwenye mabishano. Kadri muda ulivyopita, nilianza kuogopa kwamba ndoa yetu ilikuwa ikielekea mahali pabaya...SOMA ZAIDI.
Kwa muda fulani nilianza kuhisi mabadiliko katika ndoa yangu. Mke wangu ambaye zamani alikuwa mchangamfu na mkarimu alianza kubadilika. 

Alianza kutumia muda mwingi nje ya nyumba, simu yake ikawa na siri zaidi, na mazungumzo yetu yakapungua sana. Mwanzoni nilijaribu kujipa moyo.

Nilijiambia labda ni uchovu wa kazi au majukumu ya kawaida ya maisha. Lakini kadri siku zilivyopita, hisia zangu za wasiwasi zilianza kuongezeka. 

Nilianza kuona dalili ambazo zilinifanya nijiulize maswali mengi. Wakati mwingine alikuwa akirudi nyumbani akiwa na visingizio visivyoeleweka.

Simu yake ilikuwa haipatikani kwa muda mrefu, na mara nyingi alionekana kukasirika nilipomuuliza maswali madogo. 

Kwa kweli hali ile ilinichanganya sana. Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa, lakini hakutoa majibu ya kuridhisha. Badala yake, mazungumzo yetu yaligeuka kuwa mabishano. SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kuwa mtu wa kuamini sana katika ishara za hatari. Kwa miaka mingi nilikuwa nikiendesha gari na kusafiri mara kwa mara bila matatizo makubwa. 

Nilichukulia usalama kama jambo la kawaida ambalo halikuhitaji kufikiriwa sana. Lakini mwezi mmoja ulifika na kubadilisha mtazamo wangu kabisa.

Tukio la kwanza lilitokea nilipokuwa nikirejea nyumbani usiku. Gari moja lilitoka ghafla kwenye barabara ndogo bila kutoa ishara. Kwa sekunde chache nilidhani mgongano haukuwa unaweza kuepukika. Kwa bahati, nilifanikiwa kulikwepa.

Wiki moja baadaye, nilikuwa ndani ya gari la abiria lililopata hitilafu ya ghafla barabarani. Watu wengi walipata hofu, lakini dereva alifanikiwa kulisimamisha kabla ya kutokea madhara makubwa. Nilishukuru na kuendelea na maisha....SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu, nilikuwa nikiishi na tatizo ambalo sikuwa na ujasiri wa kulizungumzia na mtu yeyote. Mwanzoni nilidhani lilikuwa jambo la kawaida ambalo lingepita lenyewe. 

Lakini kadri miezi ilivyopita, niligundua hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya. Nguvu na hamu yangu ya mapenzi zilianza kupungua, jambo ambalo lilianza kuathiri mahusiano yangu.

Kwa kweli nilihangaika sana. Nilianza kupoteza kujiamini na nilikuwa nikiepuka mazungumzo yanayohusiana na suala hilo. 

Kila nilipoona hali haibadiliki, nilihisi wasiwasi zaidi. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mpenzi wangu akianza kuhisi kwamba simjali kama zamani.

Ingawa nilijaribu kueleza kwamba nilikuwa napitia changamoto, haikuwa rahisi kuelezea hisia nilizokuwa nazo. Hali ile ilianza kuleta umbali kati yetu na mara kwa mara kulikuwa na mabishano yaliyotokana na kutokuelewana.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kutafuta suluhisho. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kufanikiwa. Nilijituma kila siku kuhakikisha wateja wanapata huduma nzuri na bidhaa bora. 

Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda vizuri, lakini baada ya muda hali ilianza kubadilika. Washindani wapya waliingia sokoni.

Walikuwa na mitaji mikubwa, matangazo mengi, na ofa zilizovutia wateja. Polepole nilianza kuona idadi ya wateja wangu ikipungua. Mauzo yangu yakashuka mwezi baada ya mwezi. 

Kwa kweli nilihuzunika sana. Kulikuwa na siku ambazo biashara yangu ilikaa karibu tupu huku maduka ya washindani wangu yakiwa yamejaa watu.

Kila jioni nilihesabu mauzo na kuona jinsi faida ilivyokuwa ikizidi kupungua. Miezi kadhaa ilipita katika hali hiyo. Watu wengi waliniambia biashara yangu isingeweza kushindana na zile zilizokuwa zimejijengea nguvu sokoni. Baadhi walinishauri nifunge biashara na kutafuta kazi nyingine.

Lakini sikuwa tayari kukata tamaa. Nilijua nilikuwa nimewekeza muda, nguvu, na fedha nyingi katika biashara hiyo. Nilihitaji njia ya kuirudisha kwenye mafanikio....SOMA ZAIDI.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, amevutiwa na mfumo wa Kupanga na Kusimamia miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA). 

Mhe. Kikwete ameipongeza REA kwa kuja na mfumo huo mara baada ya kutembelea banda hilo kwenye ufunguzi wa Maadhimiaho ya Wiki ya Utumishi kwa Umma 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. 

Mfumo huo (*REA DIGITAL PLATFORM*) unaonyesha miradi yote inayotekelezwa na REA na kuweza kuisimamia kidijitali na kuwapa taarifa wadau popote walipo duniani kuhusiana na miradi ya Nishati vijijini.

Akimueleza Mhe. Kikwete, Afisa Upimaji Mwandamizi wa REA, Bw. Hussein Shamdas ameeleza kuwa kupitia mfumo huo mwananchi anaweza kujua mipango ya Wakala kwenye eneo lake na kufuatilia miradi inayotekelezwa na Wakala katika eneo husika.

 


Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwan Kikwete ameipongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi kwa Wananchi pamoja na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za nishati nchini.

Kikwete amesema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Aidha, amesisitiza Wizara pamoja na Taasisi zake kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ili Kila mmoja aifahamu kwa kina kwa manufaa ya kulinda Afya na mazingira.

" Hongerani Sana Nishati kwa kuendelea kuwasha Umeme na kuangaza Maisha ya Wananchi, tunaona Umeme upo wa kutosha" Alisema Kikwete 

Sambamba na hilo amesisitiza kuendelea kutangaza fursa zilizopo katika Sekta ya Nishati nchini kwa wananchi.

Ametembelea Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati ambazo ni TANESCO, REA, TPDC, EWURA, PURA,PBPA na EWURA CCC ambapo alipata fursa ya kujionea huduma zinazotolewa na taasisi hizo pamoja na mafanikio ya miradi mbalimbali inayotekelezwa.

 Airtel Tanzania imezindua minara miwili mipya ya mawasiliano ya 4G inayotumia umeme wa gridi ya taifa katika mikoa ya Geita na Dodoma, hatua inayotarajiwa kuboresha upatikanaji wa simu na intaneti kwa maelfu ya wananchi wa maeneo ambayo kwa muda mrefu yamekosa mawasiliano ya uhakika.

Minara hiyo imejengwa katika Kata ya Nyaruyeye, Wilaya ya Geita, na Kijiji cha Chinagali, Kata ya Zoissa, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, ikiwa na lengo la kuboresha mawasiliano, huduma za intaneti na huduma za kifedha kupitia simu kwa jamii zilizokuwa zikikabiliwa na changamoto za mtandao kwa miaka mingi.

Tofauti na minara mingine ya vijijini inayotegemea majenereta, minara hiyo imeunganishwa na umeme wa gridi ya taifa huku ikiwa na majenereta ya akiba, hatua inayopunguza gharama za uendeshaji na kuchangia uhifadhi wa mazingira kupitia kupunguza matumizi ya mafuta.

Katika Kata ya Nyaruyeye, zaidi ya wananchi 15,000 pamoja na wakazi wa Kata ya Nyarugusu na maeneo jirani wanatarajiwa kunufaika na maboresho hayo.

Uwekezaji huo unafuatia tathmini iliyofanywa na Airtel baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kuhusu changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo hayo.

Hatua hiyo inalenga kuimarisha mawasiliano, kuongeza ujumuishaji wa kifedha na kufungua fursa za kidijitali kwa jamii.

Viongozi wa maeneo husika wamesema minara hiyo itasaidia shughuli za elimu, biashara na utoaji wa huduma za umma, pamoja na kuchochea shughuli za kiuchumi, hususan katika maeneo yanayojishughulisha na kilimo na ufugaji kama Wilaya ya Kongwa.

Airtel imesema uwekezaji huo ni sehemu ya mkakati wake wa kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata fursa sawa katika uchumi wa kidijitali kupitia upatikanaji wa miundombinu ya mawasiliano ya uhakika