Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda (kulia) pamoja na Viongozi mbalimbali, wakionesha Mpango wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda mara baada ya kuuzindua katika hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 09 Februari 2026.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizindua Mpango wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda katika hafla iliyofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 09 Februari 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Mpango wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda uliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 09 Februari 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, akiwa na Viongozi mbalimbali katika picha ya pamoja na baadhi ya Waajiri, mara baada ya kuzindua Mpango wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda katika hafla iliyofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 09 Februari 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam kwaajili ya Uzinduzi wa Mpango wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda, leo tarehe 09 Februari 2026.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa na Viongozi mbalimbali wakati akishiriki Uzinduzi wa Mpango wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda uliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 09 Februari 2026.

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bw. David Lyamongi,akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa kibiashara wadau na wafanyabiashara wa mkoa wa Shinyanga iliyofanyika  katika Ukumbi wa Makindo, Shinyanga.

Na.Mwandishi Wetu-SHINYANGA

Baraza la Ushindani, kwa niaba ya Mwenyekiti wake, Mhe. Jaji Rose Ally Ebrahimu, limewashukuru wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Shinyanga kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika semina ya kuwajengea uwezo iliyofanyika  katika Ukumbi wa Makindo, Shinyanga.

Semina hiyo imelenga kuwaongezea wadau uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa kibiashara, haki zao kama wafanyabiashara pamoja na taratibu za kuwasilisha rufaa endapo hawataridhishwa na maamuzi ya mamlaka za udhibiti.

Akifungua semina hiyo, Bw. David Lyamongi, aliyemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, CP Salumu Hamduni, aliwataka wadau na wafanyabiashara kutumia vyema fursa hiyo ya kujifunza ili kuimarisha shughuli zao za kibiashara.

Aidha, aliishukuru Baraza la Ushindani kwa kuwaletea wakazi wa Shinyanga elimu muhimu inayolenga kulinda haki zao katika biashara na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.

Akizungumza katika semina hiyo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Mhe. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza la Ushindani ni chombo cha Serikali kilichoanzishwa kwa lengo la kusikiliza na kutatua migogoro ya ushindani wa kibiashara. Alisisitiza kuwa Baraza linaendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhakikisha wadau na wafanyabiashara wanalifahamu, kulifikia kwa urahisi na kulitumia ipasavyo wanapohitaji haki.

Kwa upande wake Mjasiriamali kutoka Mkoa wa Shinyanga , Bw. Dedani Rutazibwa,alipongeza Baraza la Ushindani kwa kuandaa semina hiyo ya kuwajengea uwezo wadau. Alisema kutokana na umuhimu wa chombo hicho, ameiomba Serikali kupitia Baraza la Ushindani kuendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali katika ngazi tofauti, ili wafanyabiashara waweze kufahamu haki zao pamoja na mamlaka sahihi za kuwasilisha rufaa zinazotokana na maamuzi ya mamlaka za udhibiti na Tume ya Ushindani.

Naye  Mkazi wa Shinyanga Mwl. Zezema Nyangaki, alisema kuwa elimu aliyopata kupitia semina hiyo imemfungua macho, akieleza kuwa awali hakuwa na uelewa kuhusu uwepo wa mamlaka za udhibiti zinazopokea malalamiko ya wafanyabiashara. Aliongeza kuwa mafunzo hayo yamemsaidia kufahamu kuwa endapo hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hizo, anaweza kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yake kwa mujibu wa sheria.


Wananchi wametakiwa kuwajali na kuachana na vitendo vya unyanyapaa dhidi ya wagonjwa wa kifafa, kwani asilimia kubwa ya wagonjwa hao hushindwa kupata ushirikiano kutoka kwa familia na jamii zinazowazunguka, jambo linalosababisha kuchelewa kupata matibabu na kufika hospitalini wakiwa katika hali mbaya zaidi kiafya.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kifafa Duniani yaliyofanyika leo Februari 06, 2026 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) amesema kuwa wizara inaandaa miongozo na taratibu mbalimbali kuhakikisha kuwa wagonjwa wa kifafa wanaishi katika mazingira salama na yenye staha.

"Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha kuwa watu takribani milioni 50 duniani wanaishi na kifafa, huku milioni 6 wakigundulika kila mwaka. Watu wenye kifafa wana hatari ya vifo mara tatu zaidi, huku Afrika ikiripoti viwango vya juu mara 4 hadi 6 zaidi. Zaidi ya asilimia 80 ya mzigo wa kifafa duniani unabebwa na nchi zenye kipato cha chini na cha kati, ikiwemo Tanzania.” amesema Dkt. Samizi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Dkt. Julieth Magandi, ameeleza kuwa Unyanyapaa bado ni changamoto kubwa kwa wagonjwa wa kifafa kwani baadhi ya jamii bado wanaamini kifafa kinarogwa, ni laana au ni ugonjwa wa kurithi, hali ambayo si ya kweli. Ameongeza kuwa kifafa ni ugonjwa unaotibika na kudhibitika kitaalamu, hivyo jamii inapaswa kuachana kabisa na mila potofu na badala yake kuwapa wagonjwa hawa msaada na heshima wanayostahili.

Aidha, akiwasilisha wasilisho lake katika mkutano huo, Rais wa Chama cha Kifafa nchini, Profesa William Matuja, amesema kuwa elimu kwa jamii ni silaha muhimu katika mapambano dhidi ya kifafa, akisisitiza kuwa endapo jamii itaelimishwa ipasavyo, wagonjwa wengi watajitokeza mapema kupata matibabu na kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine.






 


Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Shingi Bilioni 28 zilizorejesha tabasamu kwa wafanyabiashara wa Kariakoo ambazo zimetumika kujenga Soko Jipya la Kariakoo na kukarabati Soko la zamani la Kariakoo ambalo liliharibika kutokana na janga la moto  Oktoba 07, 2021.

Prof. Shemdoe ametoa shukrani hizo leo kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akitoa neno la utangulizi, wakati ya hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu Jipya la Kariakoo iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 

“Mhe. Rais natumia fursa hii kutoa shukrani za dhati kwa nia yako njema ya kurejesha tabasamu kwa wafanyabishara na wananchi, kwa kutoa fedha zaidi ya  Shilingi Bilioni 28 ili kujenga soko jipya na kukarabati lililoteketea kwa janga la moto la Oktoba 07, 2021”, ameeleza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, Soko la Kariakoo ni kitovu cha biashara ndani ya Jiji la Dar es Salaam na Taifa kwa ujumla, hivyo ofisi yake kwa kutambua hilo itahakikisha  soko hilo linatoa huduma bora na kwa ufanisi ili kuleta tija na kuakisi thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali.

Sanjali na hilo, Prof. Shemdoe amesema kuwa, Serikali inaendelea na utaratibu wa kuhakikisha barabara zote zinazozunguka Soko la Karikakoo na maeneo jirani zinafunguliwa ili ziweze kupitika wakati wote na kulifanya soko litoe huduma kwa wananchi masaa 24.

Aidha, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteu kuwa Waziri anayesimamia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na kumuahidi Mhe. Rais kwamba atafanya kazi kwa bidii na uadilifu mkubwa.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, katika eneo la jiwe la ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Wageni na viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Patrobas Katambi pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Doroth Gwajima wakiwa katika uzinduzi huo.