NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewahimiza wawekezaji wazawa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya viwanda, ikisisitiza kuwa imeendelea kuboresha na kurahisisha mazingira ya biashara ili kuongeza uwekezaji wa ndani.

Na Augusta Njoji

Timu ya wataalamu wa afya kutoka Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni imeanza rasmi mpango wa utoaji elimu kwa jamii ili kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa na kuboresha ustawi wa wananchi.

Utoaji wa elimu hiyo imejikita katika afua za kuzuia malaria, lishe bora, bima ya afya kwa wote pamoja na huduma za mama na mtoto, ikiwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha jamii inakuwa na afya bora.

Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Ofisa Afya wa Halmashauri na Mratibu wa Elimu ya Afya kwa Umma, Jonas Mkondya, amesema wamejipanga kutembelea kila mtaa katika kata zote 12 za Halmashauri ya Mji Handeni ili kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapatia elimu sahihi ya afya.

Ameeleza kuwa elimu hiyo itasaidia kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na magonjwa, kuboresha lishe pamoja na umuhimu wa kujiunga na bima ya afya kwa wote ili kupata huduma kwa urahisi.

Kata zitakazofikiwa katika ziara hiyo ya wataalamu wa afya ni Konje, Mabanda, Kwenjugo, Malezi, Chanika, Mlimani, Mdoe, Vibaoni, Kwediyamba, Kideleko, Msasa na Kwamagome.

Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sports Club imeonyeshana ubabe na Timu ya Mpira wa miguu ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT) baada ya kutoka sare ya goli mbili kwa mbili katika mechi ya kirafiki iliyochezwa leo Aprili 24, 2026 katika viwanja vya Chai mkoani Njombe.

Hapo Aprili 22, 2026 TCDC Sports Club ilikubali kipigo cha bao moja bila 1- 0 kutoka Timu ya Mpira wa miguu ya TANWART katika mechi ya kirafiki iliyochezwa viwanja vya Kibena mkoani humo.

TCDC Sports Club inaendelea kushiriki Michezo ya kirafiki mkoani humo baada ya kushindwa kuvuka hatua za makundi kwenye Mashindando ya Michezo ya Meimosi inayoendelea mkoani humo.

 

Katika kuelekea Kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani ( Meimosi) ambayo kitaifa inafanyika mkoani Njombe, Timu ya Pooltable ya TCDC Sports Club imeshiriki mashindando ya mchezo huo Aprili 23, 2026 ndani ya African Club mjini humo.

Mchezaji Mbasso John ameiwakilisha TCDC Sports Club katika mchezo huo huku akishinda mechi ya kwanza kati ya TCDC na Ulinzi na ,mechi ya pili akicheza na Arusha DC na kutoka moja moja na kupoteza mchezo wa mwisho baada ya kufungwa na timu ya Mahakama.

Kwa hatua hiyo TCDC Sports Club haijafanikiwa kuingia nusu fainali katika mchezo wa Pooltable katika Mashindando ya Michezo ya Meimosi.

Wanamichezo wa TCDC Sports Club wameshiriki mashindano ya riadha (mbio) katika Michezo ya kitaifa Meimosi inayoendelea mkoani Njombe.

Wachezaji walioshiririki mbio hizo ni Mbaso John aliyekimbia Mita 100 na kuibuka mshindi wa tatu (3) katika round ya kwanza, na baadae kupoteza nafasi ya ushindi katika hatua ya nusu fainali.

Mchezaji mwingine ni William Valentine aliyeshiriki riadha mbio za Mita 800 na kutofaninikiwa kupata ushindi baada ya kuzidiwa na wanariadha kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI na Wizara ya Mambo ya ndani.

Kwa upande wake Noel Steven ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCDC Sports Club ameshiriki mchezo wa Draft ambapo kwa mzunguko wa kwanza TCDC Sports Club ilishinda mechi mbili na mzunguko wa pili kupata draw na hivyo kutofanikiwa kuvuka hatua za makundi baada ya kuzidiwa kete na TRA na Wizara ya Kilimo.

Michezo hiyo yote imechezwa Aprili 21, 2026 katika viwanja vya Njombe Sekondari na Viwanja vya sabasaba (77) mkoani humo.

 


Na Mwandishi Wetu, Lusaka

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unashiriki Kongamano la Kimataifa la Nishati Endelevu ya Kuni na Mkaa (Sustainable Woodfuel Forum) linaloendelea Lusaka, Zambia, likiwa jukwaa la kimataifa la kubadilishana uzoefu na mbinu bora za usimamizi wa misitu na nishati ya miti.

Kongamano hilo linafanyika chini ya Programu ya Dryland Sustainable Landscapes Impact Programme (DSL-IP) kwa ufadhili wa Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF) na kuratibiwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa kushirikiana na Serikali ya Zambia.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mhifadhi Mkuu TFS, Kassim Ally, amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati ya kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema hatua hiyo ni sehemu ya azma ya Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ifikapo mwaka 2034.

Ally amesema juhudi hizo zinajumuisha utekelezaji wa sera, uwekezaji katika nishati mbadala na kampeni za elimu kwa umma ili kubadilisha tabia ya matumizi ya nishati.

Ameeleza kuwa hatua hizo zitasaidia kupunguza ukataji miti hovyo, kulinda misitu na kuboresha afya za wananchi dhidi ya athari za moshi wa majumbani.

Kwa mujibu wa Ally, ushiriki wa TFS unafanyika kupitia mradi wa Integrated Landscape Management in Dry Miombo Woodlands of Tanzania unaolenga kurejesha mifumo ikolojia na kupunguza upotevu wa bioanuwai.

Amesema mradi huo pia unalenga kuimarisha ustahimilivu wa uzalishaji katika maeneo ya Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame katika Mkoa wa Tabora (Wilaya za Kaliua, Sikonge na Urambo) na Wilaya ya Mlele mkoani Katavi kupitia usimamizi shirikishi wa misitu.

Ameongeza kuwa kupitia mradi huo, jamii zinashirikishwa moja kwa moja katika uhifadhi huku zikipewa fursa za kunufaika kiuchumi kupitia matumizi endelevu ya rasilimali.

Kongamano hilo linawakutanisha wadau kutoka nchi mbalimbali za ukanda wa Miombo-Mopane kujadili mahitaji ya nishati ya kuni na mkaa hadi mwaka 2050 na athari zake kwa uchumi na mazingira.

Katika maonesho yanayoambatana na kongamano hilo, TFS imewasilisha teknolojia za nishati safi ya kupikia na mbinu mbadala za matumizi ya kuni na mkaa.

Maji ya kimataifa ni moja ya rasilimali inayoleta amani katika nchi mbalimbali zinazonufaika na wananchi wake.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso ( Mb) akifungua kikao cha 13 cha  Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (ZAMCOM) jijini Dar es salaam amesema maji hayana mpaka na yanakusanya watu kwa maendeleo yao.

Mhe. Aweso ambaye katika mkutano huo ni Mwenyekiti ameainisha kuwa umoja wa wananchi na nchi walizopo umeletwa na maji ya kimataifa, maji yanayovuka mipaka ya nchi zao.

Amesema ni muhimu kuwa na rasilimali za kutosha ili kuleta maendeleo na wananchi wanashirikishwa kutunza rasilimali za maji ili kuleta maendeleo katika sekta nyingine za uchumi.

Mhe. Aweso amesisitiza kwa wajumbe wa mkutano huo kuwa maji ni muhimu na yanahitajika kuleta maendeleo kwa wananchi.

ZAMCOM inagusa maisha ya kila wananchi zaidi ya milioni 51 na imekusanya nchi za Tanzania, Angola, Zambia, Malawi, Namibia, Botswana, Zimbabwe, na Msumbiji.





‎Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff, amefungua mafunzo ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uelewa wataalamu wa TARURA kutoka TAMISEMI, ofisi ya Makao Makuu, Mikoa, Wilaya, Mhandisi Mshauri pamoja na Mkandarasi katika kutekeleza mradi wa Sanifu na Jenga wa barabara zinazoingia uwanja wa AFCON jijini Arusha.

‎Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhandisi Seff alisema lengo kuu ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa miradi ya sanifu na jenga ili kuimarisha uzingatiaji wa taratibu, kushughulikia changamoto kwa wakati na kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa mafanikio.

‎Alifafanua kuwa mafanikio hayo yanapaswa kuzingatia misingi ya usalama, masuala ya kijamii na kimazingira, muda, gharama, thamani, ubora pamoja na mahitaji ya kiutendaji.

‎Mhandisi Seff alibainisha kuwa tangu kuanzishwa kwa TARURA, Wakala huo haujawahi kupata mradi mkubwa kama huo, hivyo mafunzo hayo ni fursa muhimu ya kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani ili wawe tayari kushughulikia miradi mikubwa zaidi ijayo.

‎Aliwataka washiriki wa mafunzo kujifunza kwa umakini na kuuliza maswali yatakayowaongezea uelewa, akisisitiza kuwa jukumu walilonalo ni kubwa na linahitaji umakini wa hali ya juu katika kila hatua ya utekelezaji.

‎Aidha, aliwakumbusha wasimamizi wa mradi kuzingatia muda akieleza kuwa barabara hizo zinatakiwa kukamilika ifikapo Mei 2027 bila nyongeza ya muda.

‎“Serikali imeiamini TARURA kwa kuipatia jukumu hilo kwa manufaa ya Taifa hivyo hamna budi kufanya kazi usiku na mchana”.



Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Serikali inaendelea kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na upatikanaji wa umeme nchini, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka 2026/2027. 

Amesema hayo Aprili 23, 2026  Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja za wabunge mara baada ya kuwasilishwa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati ya Mwaka 2026/2027.

Akijibu hoja hizo amesema Rais wa Jamuhurinya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia, akilenga kufikisha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia  ifikapo mwaka 2034 huku akifafanua kuwa matumizi hayo yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi zaidi ya asilimia 28 kwa sasa, huku jitihada hizo zikilenga kulinda mazingira na afya za wananchi.

Aidha, ameeleza kuwa Serikali imesambaza zaidi ya kilomita 56.4 za mabomba ya gesi asilia, mitungi ya gesi zaidi ya laki tatu, majiko ya gesi zaidi ya elfu 49 na majiko ya umeme zaidi ya elfu saba ambapo  zaidi ya taasisi 55 zimepatiwa majiko ya nishati safi, huku mpango ukiwa kufikia taasisi zaidi ya 400.

Katika kuhakikisha upatikanaji wa umeme vijijini  zaidi ya visiwa 120 kati ya 143 tayari vimepata umeme wa sola kwa ruzuku ya asilimia 45 hadi 75  hatua inayolenga kuwaondoa wananchi katika matumizi ya vibatari na kuboresha maisha yao kwa ujumla.








Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) pamoja na Menejimenti ya NEEC, tarehe 23 Aprili 2026 walifanya ziara maalum ya kutembelea mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) katika maeneo ya Ntondo mkoani Singida na Sojo mkoani Tabora.

 


📌Ni shilingi trilioni 2.53

📌Serikali kuja na mradi wa kuunganisha umeme kwa sh.27,000 katika maeneo ya Mjini yenye sura ya Vijiji

📌Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2000 kwa makaa ya mawe mbioni

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha kwa kishindo shilingi trilioni 2.53 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Nishati 2026/2027.

Kati ya fedha hizo, Shilingi trilioni 2.46 sawa na asilimia 97.5 ya bajeti yote  imeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 2.5 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Akihitimisha hoja kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2026/2027 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi alilieleza Bunge kuwa Wizara ya Nishati itaendelea kuhakikisha kwamba maono ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi na mwelekeo uliowekwa kwenye Dira 2050 yanatekelezwa kwa vitendo na kwa haraka.

Kutokana na hilo alieleza kuwa lengo lililowekwa kwa Wizara la kuzalisha umeme  wa megawati 8000 ifikapo 2030 litatekelezwa kwani Wizara ya Nishati imeshajipanga kuzalisha kiasi hicho cha umeme huku ikidhamiria kuzalisha megawati 70,000 ifikapo 2050.

"Ili kutekeleza lengo hili tutatumia vyanzo vyote vinavyopatikana kwenye Taifa letu ikiwemo vyanzo vya maji kama vile Malagarasi (49.5MW), Kakono (87MW), Ruhudji (358), Rumakali (222MW),  Jeothemo na makaa ya mawe.." Alisema Mhe. Ndejembi

Akifafanua kuhusu mradi wa uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe, Mhe. Ndejembi alisema Tanzania ina hifadhi kubwa ya makaa hayo na sasa Serikali inashirikiana na Sekta binafsi ili kuhakikisha kuwa inaanza uzalishaji wa megawati zaidi ya 2000 kwa kutumia nishati hiyo.

Aliongeza kuwa miradi mingine  itakayowezesha kufikia lengo la uzalishaji wa megawati 8000 ifikapo 2030 ni pamoja na miradi ya umeme Jua ikiwemo  ya Kishapu, Manyoni, Zuzu, miradi ya upepo ya Same, Makambako pamoja na kuzalisha umeme kwa kutumia urani.

Aidha, Mhe. Ndejembi aligusia suala la kufikisha umeme kwenye maeneo ya wananchi akieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha umeme unatoka kwenye vyanzo vya uzalishaji na kufikia maeneo ya wananchi na ya uzalishaji kama vile migodi viwanda n.k

Katika jitihada hizo za kufikisha umeme kwa wananchi alisema mradi wa kufikisha umeme wa gridi mikoa ya Mtwara na Lindi  kupitia ujenzi wa njia ya umeme ya kV 220 ya Songea- Tunduru- Masasi-Mahumbika unaendelea huku mkandarasi akiwa ameshalipwa shilingi bilioni 83 kwa ajili ya kuendelea na kazi.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Nishati aliiagiza TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) kuwasiliana na Wabunge wote ambao wana maeneo ambayo ni Manispaa/Majiji/ Halmashauri za Mji lakini yana sura ya vijiji ambayo wananchi wake wanalipa zaidi ya shilingi 27,000  kuunganisha umeme ili kuvitambua vijiji hivyo na kuja na mradi utakaohakikisha  wananchi katika vijiji hivyo wanaunganishiwa umeme kwa shilingi 27,000 tu ndani ya mwaka mmoja. 

" Serikali hii ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu na haiwezi kuweka matabaka ya wananchi, mtu amekaa ng'ambo moja analipa 27,000 na ng'ambo nyingine analipa 320,000 hili halikubaliki, Serikali imesikia changamoto hii na inaifanyia kazi, tutahakikisha umeme unawaka katika vijiji ambavyo vipo ndani ya miji." Alisema Mhe. Ndejembi

Kuhusu suala la kufikisha umeme kwenye Taasisi kama vile shule, zahanati n.k aliitaka REA kufanya tathmini ili kutambua taasisi ambazo hazijapelekewa umeme katika vijiji vyenye umeme ili ziweze kuunganishiwa.

Aidha, kuhusu suala la mafuta alisema kufungwa kwa mlango  bahari wa Hormuz kunaleta changamoto kubwa ya upatikanaji mafuta duniani kwani asilimia 20 ya nishati ya mafuta inatoka katika mlango bahari huo lakini kutokana na Serikali ya Tanzania kujali wananchi wake, nchi ina mafuta ya kutosha na hakuna kituo ambacho kimefungwa kwa kukosa nishati hiyo tofauti na baadhi ya maeneo mengine duniani.

Vilevile kuhusu bei ya mafuta alieleza kuwa Serikali inafanya kila jitihada ili ziwe himilivu huku ikihakikisha mafuta yanapatikana muda wote na  hifadhi mpya ya mafuta inayojengwa jijini Dar es Salaam eneo la Kigamboni ikitoa hakikisho la uhifadhi wa mafuta.

Vilevile alieleza kuwa, ili kurahisisha upatikanaji wa mafuta katika maeneo mbalimbali  nchini Serikali inajenga bomba la kusafirisha mafuta safi kutoka Dar es Salaam hadi Ndola, Zambia litakokuwa na matoleo na matenki ya kuhifadhi mafuta katika mikoa ya Morogoro, Njombe na Songwe na hivyo kupunguza msongamano jijini Dar es Salaam na kuondoa mzigo barabarani.

Katika Gesi Asilia, Mhe. Ndejembi alisema Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linafanya kazi kubwa kuhakikisha Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia inazidi kuimarika na sasa Shirika hilo linaendelea na miradi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa bomba la gesi la km 34 kutoka Ntorya hadi Madimba, wanachimba kisima kingine cha gesi katika eneo la Mnazi Bay ambacho kimeonekana kina hifadhi kubwa ya gesi mara mbili ya makisio ya awali, vilevile Shirika hilo linaendelea na  utafutaji wa mafuta katika kitalu cha Eyasi Wembere.

Aidha kuhusu mradi mkubwa wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika ( LNG)  alisema kuwa kwa sasa Serikali imefikia hatua za mwisho kuweza kuanza mradi na kwamba makubaliano ya kibiashara na kikodi yamekamilika na hatua inayoendelea sasa ni makubaliano ya kisheria.

Aliongeza kuwa, katika mradi wa LNG tayari  kuna kazi ambazo tayari zimeshaanza kama vile ulipaji fidia na ujenzi wa shule ya Likong'o.

Ili kuhakikisha wazawa wanashiriki ipasavyo katika mradi wa LNG alisema Serikali imeielekeza TPDC  kwenda mkoa wa Lindi kutoa elimu ya fursa zitakazopatikana huku Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) ikitakiwa kuwajengea uwezo wazawa ili mradi utakapoanza waweze kushiriki katika nyanja  mbalimvali ikiwemo utoaji wa huduma. ‎<This message was edited>

 


-Moshi, Kilimanjaro

Katika hatua kubwa inayolenga kuleta mapinduzi kwenye soko huria na kumlinda Mlaji. Mamlaka ya Ushindani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCA) zimekutana Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro leo Aprili 23, 2026 na kuwaapisha rasmi wajumbe wapya wanne kutoka Nchi za Tanzania, Somalia, Uganda na DRC ambao watasimamia mazingira mazuri ya ushindani wa biashara na walaji kwa Jumuiya hiyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewataka waajiri na wafanyakazi nchini kuyatazama upya mazingira ya kazi ili kuhakikisha yanakuwa salama na rafiki kwa afya, hususan afya ya akili.

Na Oscar Assenga, Tanga

Katika kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia duniani, Shule ya Sekondari Coastal High School imetangaza mpango kabambe wa kuanzisha programu ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) ifikapo Januari 2027.

Mpango huo unalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kisasa utakaowawezesha kushindana katika soko la ajira la Kimataifa.

Akizungumza wakati wa mahafali ya Kidato cha Sita yaliyofanyika jijini Tanga, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Isack Dastan Kifwete  alisema kuwa tayari wameanza kuchukua hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa mpango huo.


Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kufanikisha upatikanaji wa huduma ya intaneti kupitia Kampuni ya TTCL, pamoja na kuwepo kwa mtaalamu wa TEHAMA shuleni hapo.

Hata hivyo, alibainisha kuwa bado kuna changamoto kadhaa zinazokwamisha utekelezaji wa mpango huo kwa ufanisi unaohitajika.

Alizitaja changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vifaa muhimu kama kompyuta za kisasa, ubao janja (smart board), pamoja na miundombinu ya chumba maalumu kitakachotumika kufundishia programu ya AI.

Mbali na hilo, shule pia ina mpango wa kuanzisha programu ya Habari na Mawasiliano ya Umma, unaolenga kuwajengea wanafunzi uwezo wa uandishi wa habari, mawasiliano, pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa katika tasnia ya habari.

Tayari maandalizi ya awali, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya studio, yameanza kufanyika.

Pamoja na jitihada hizo, Mwalimu Mkuu alieleza kuwa shule bado inahitaji vifaa muhimu ili kukamilisha studio hiyo.

Vifaa vinavyohitajika ni pamoja na kamera za kisasa, meza ya matangazo, vifaa vya kuzuia kelele, vinasa sauti, vipaza sauti pamoja na kompyuta zenye uwezo wa kisasa.

Aidha, alitaja changamoto nyingine zinazoikabili shule kuwa ni pamoja na baadhi ya wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati kutokana na hali ngumu ya kiuchumi, pamoja na ushiriki mdogo wa wazazi na walezi katika masuala ya kitaaluma na malezi ya wanafunzi.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule umetoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia jitihada hizo ikiwemo kuwaomba wadau msaada wa vifaa kwa ajili ya kuanzisha studio ya habari, pamoja na kuunganishwa na taasisi au watu binafsi wanaoweza kusaidia upatikanaji wa kompyuta za kisasa.

Kwa ujumla, mpango huu unaonesha dhamira ya dhati ya shule katika kuwajengea wanafunzi msingi imara wa elimu ya kisasa ili kuwaandaa kukabiliana na dunia inayoendeshwa na teknolojia kwa kasi kubwa.

Awali, akizungumza katika mahafali hayo,Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar (CCM), Ussi Salum Pendeza, alisema kuwa atashirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha baadhi ya changamoto zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka.

Alisema kuwa ataanza mwenyewe kuchangia upatikanaji wa baadhi ya vifaa muhimu, ikiwemo kompyuta za kisasa na ubao janja, sambamba na kuhamasisha wadau wengine kushiriki.

“Katika hili la ubao janja na baadhi ya kompyuta, nitaanza mimi mwenyewe. Pia nitahakikisha michango inapatikana na kuwashirikisha wengine. Nachukua nafasi hii kuwashukuru walimu na Bodi ya Shule ya Coastal kwa ushirikiano wao katika kuhakikisha shule inafanya vizuri na matokeo yanakuwa mazuri,” alisema.

Ussi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Taasisi ya Pendeza Foundation, alisema anajivunia kuiongoza shule hiyo na ameahidi kuendelea kuisimamia ili iweze kufanya vizuri zaidi na kujulikana kitaifa.