Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amewashauri Wamiliki wa Viwanda vipya Kutoa kipaumbele kwa wazawa katika ajira ili kukuza uchumi na mapato ya Taifa kwa ujumla.

Akizungumza Mei 09, 2026, wakati wa akifungua wa Kiwanda kipya cha kutengeneza tambi za papo hapo (Instant) cha Kura Food mkoani Pwani, amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya Biashara ikiwemo sera, miundombinu, na mifumo ili kuvutia Wawekezaji na wafanyabiashara na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.

Aidha, Wizara imefanya mapitio ya sheria na kanuni ili kuhakikisha zinajielekeza katika kuwezesha biashara na kuondoa vikwazo badala ya kudhibiti pekee. Lengo ni kushirikiana na wadau wa mnyororo wa thamani, kutumia teknolojia za kisasa zinazoongeza tija, uzalishaji, na ufanisi wa biashara nchini.

Naye, Mwenyekiti wa Kura Food, Bw. Wu Yeping, ameipongeza Serikali kwa kuweka mazingira rafiki yanayorahisisha uwekezaji,

Huku Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, akibainisha kuanza kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara na Reli ya Kisasa (SGR) kuanzia mwaka ujao ili kufungua zaidi fursa za kibiashara mkoani humo.

Naye Mbunge wa Kisarawe, Mhe. Selemani Jafo, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sera zake thabiti ambazo zimekuwa chachu ya kuvutia wawekezaji. Sera hizi zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa wananchi wa jimbo hilo kupitia kuanzishwa kwa viwanda vipya.

            
Na Mwandishi Wetu

Benki ya Ushirika (Coop Bank) mwishoni mwa wiki ilizindua rasmi tawi lake jipya Mtwara mjini ikiwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mkakati wa benki hiyo wa kupanua huduma za kifedha na kuimarisha uchumi jumuishi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa utekelezaji wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika kambi zake, huku akiwahamasisha kuelimisha jamii zinazozunguka kambi hizo nazo kutumia nishatia nishati safi ya kupikia.

Pongezi hizo zimetolewa leo Mei 9, 2026 wakati wa ziara ya Bodi hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inaayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Kambi ya JKT ya Oljoro Jijini Arusha.

Mradi huo unahusisha uzalishaji wa bayogesi kupitia mbolea ya ng’ombe, matumizi ya majiko ya gesi, majiko banifu na mashine za kutengenezea mkaa mbadala.

Mwenyekiti Kingu pia, amesisitiza juu ya vijana waliopo kwenye kambi hizo za JKT kupatiwa mafunzo ya namna ya kutengeneza mkaa mbadala ili waweze kutumia ujuzi huo kujiajiri na kuwa mawakala wa kutengeneza mkaa mbadala pindi watakapomaliza mafunzo yao.

Kwa upande wake, akimwakilisha Mkuu wa JKT, Kanali Projest Rutaihwa aliishukuru Bodi hiyo pamoja na Menejimenti ya REA kwa utekelezaji wa miradi nishati safi ya kupikia ambapo kambi 22 zimepata fedha kutoka REA za utekelezaji wa mradi huo ili kulinda mazingira pamoja na afya za wanaoandaa chakula.

Naye Kamanda wa Kikosi cha 833 KJ Oljoro, Kanali Victor Rutayuga Faustine, amesema mradi huo wa nishati safi ya kupikia umeleta mafanikio makubwa katika utunzaji wa mazingira na kupunguza matumizi ya kuni kambini hapo pamoja na kutumia muda mdogo kwenye kuandaa chakula cha vijana wanaopata mafunzo kambini hapo.

“Kabla ya mradi huu tulikuwa tunaagiza lori la kuni kutoka Mbeya kwa ajili ya kupikia chakula cha vijana wetu wa mafunzo hapa kambini. Lakini sasa matumizi ya nishati safi yamesaidia kupunguza utegemezi huo na kulinda mazingira,” amesema Kanali Faustine.

REA imetoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni 5.2 kwa ajili ya kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kambi za JKT ambapo fedha hizo pamoja na mambo mengine, zimewezesha kufungwa kwa mifumo ya nishati safi ya kupikia pamoja na ununuzi wa mashine za kutengenezea mkaa mbadala.

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imesema kuwa uwekezaji unaofanywa na Oryx Energies Tanzania Limited ni kielelezo cha mafanikio ya juhudi za Serikali katika kuimarisha sekta binafsi na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya taifa.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali imewataka wanamichezo na wadau wa sekta ya michezo nchini kutumia mfumo wa miliki ubunifu kulinda vipaji, majina na chapa zao ili kuongeza thamani ya kiuchumi ya shughuli zao na kujijengea maisha bora baada ya michezo.
Na Mwandishi Wetu 

WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa umma kufurahia utumishi wao na kupeleka furaha kwa wananchi.
Serikali imeendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa dawa na vifaa tiba barani Afrika kupitia uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya afya na matumizi ya teknolojia za kisasa.
Kituo cha Utamaduni cha Iran nchini Tanzania kimeanzisha mashindano ya uchoraji yanayolenga kuhamasisha jamii, hususan watoto na vijana, kueleza hisia zao kupitia sanaa kufuatia tukio la mlipuko lililotokea nchini Iran mwezi Februari mwaka huu, ambapo Shule ya Msingi ya Minaab ililipuliwa na kusababisha vifo vya wanafunzi 168.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amelielekeza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuhakikisha linalinda na kuthamini rasilimali za taasisi ili kuongeza ubora na ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan itaendelea kulinda ajira zilizopo na kuzalisha ajira mpya kupitia sekta ya viwanda na biashara kwa manufaa ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, leo tarehe 8 Mei, 2026 imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini katika Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kupata taarifa ya utekelezani wa miradi hiyo.

Mwenyekiti Kingu ambaye alikuwa ameongozana na Wajumbe wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Radhia Msuya na Mhandisi Sophia Mgonja walikutana na Kampuni ya Ceylex Engineering Limited na Derm Group Limited na ambao wanatekeleza miradi kwa Mkoa wa Kilimanjaro na pia walikutana na Kampuni ya Ceylex Engineering Limited na Nakuroi Investment Company Limited ambazo zinatekeleza miradi kwa Mkoa wa Arusha.

Mwenyekiti Balozi Meja Jenerali Mstaafu Kingu, amewatata wakandarasi hao kutekelezea miradi hiyo ndani ya muda wa mkataba waliosaini na kuhakikisha wanazingatia ubora unaotakiwa.

Kikao hicho ambacho kilihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu, Meneja Msimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mhandisi Michael Kyessi, Mhandisi Miradi kutoka REA, Isaac Sanga pamoja na Mameneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wa Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.