Na WMJJWM-Dodoma


Wazee nchini wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha huduma muhimu kwa Ustawi wa Wazee ikiwemo huduma za Afya, Msaada wa Kisaikolijia na kuboresha Miundombinu ya Makazi ya Wazee wenye changamoto nchini.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Taifa Lameck Sendo Januari 20, 2025 alipokutana na kuzungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu ofisini kwake jijini Dodoma.

Aidha, Mzee Sendo ameipongeza Wizara kwa kuratibu vyema mchakato wa Mapitio ya Sera ya Wazee ya mwaka 2003 toleo la 2023 ambayo ipo katika hatua za mwisho ili iweze kuanza kutumika na baadae kuwezesha mchakato wa utungwaji wa Sheria ya Wazee nchini.

“Kwa kweli Wizara inafanya kazi kubwa kwenye eneo la kuimarisha Ustawi wa Wazee na ni imani yetu kwamba Serikali hii itaendelea kuwatambua Wazee na kuwapatia Huduma Bora za Afya ikiwemo Bima na kuwashirikisha katika masuala yanayowahusu kama vile uchumi, siasa, familia na Jamii kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho" amesema Mzee Sendo

Pia Mzee Sendo ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wao na kuwashirikisha katika kutoa maoni kwenye mchakato wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amesema Serikali ya Awamu sita inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhakikisha wazee wanapata huduma bora katika maeneo yao pia na wale waliopo katika makazi ya wazee ikiwemo matibabu, lishe na ulinzi.

Aidha Dkt. Jingu amesema katika kuboresha zaidi ustawi wa Wazee nchini, Serikali itaendelea kupokea maoni na ushauri wa Wazee juu ya namna njema ya kuboresha Huduma na Ustawi wa wao kwa ujumla.

Dkt. Jingu ametoa wito kwa Jamii kuendelea kuwalinda Wazee, kwani wao ni Tunu muhimu na kutumia maarifa waliyonayo katika masuala mbalimbali ikiwemo malezi na Makuzi ya Watoto, kupambana na vitendo vya ukatili na mmomonyoko wa maadili.

 


Katibu Mkuu Viwanda na Biashara amshukuru Rais kutumia vyema fedha za Watanzania

✅Akagua ujenzi Jengo la WMA na kukiri kuridhishwa

✅Mtendaji Mkuu WMA asema litakamilika Februari 10

✅Litakuwa na Maabara ya kisasa yenye kuhifadhi vipimo kiwango cha kimataifa

 Na Veronica Simba – WMA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah amempongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kuwezesha ujenzi wa Jengo la Ofisi Kuu ya Wakala wa Vipimo (WMA) jijini Dodoma akisema ni matumizi mazuri ya fedha za Watanzania.

Ameyasema hayo leo Januari 20, 2025 baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo hilo ambalo limegharimu shilingi bilioni 6.2 na liko katika hatua za mwisho kukamilika.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dkt. Abdallah amesema kuwa lengo la ujenzi wa jengo hilo ni kuhakikisha utoaji huduma katika sekta ya biashara hususan katika bidhaa zinazotoka viwandani unaboreshwa.

Akifafanua, amesema kuwa maboresho ya kutoa huduma bora katika sekta ya biashara na katika uendelezaji wa viwanda ni pamoja na kuwa na mazingira mazuri kwa wafanyakazi na yale ya utoaji wa huduma hizo.

“Na katika hili, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mambo mengi makubwa, mojawapo ikiwa ni ujenzi wa jengo hili ambalo tunakwenda kulizindua hivi karibuni,” amesisitiza.

“Ninyi wenyewe ni mashahidi; fedha za Watanzania zinaenda kukamilisha ujenzi huu ili tuweze kutoa huduma bora katika jamii ya wafanyabiashara ili tuweze kuleta maendeleo na tija katika sekta ya viwanda,” ameongeza Katibu Mkuu.

Kuhusu mtazamo wake kutokana na maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo, Katibu Mkuu Hashil ameeleza kuwa kwa mujibu wa maelezo na uthibitisho uliotolewa pamoja na kujionea kwa macho kazi inavyoendelea, ni dhahiri Mkandarasi atakamilisha kazi ndani ya muda ulioafikiwa ambao ni Februari 10 mwaka huu.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Alban Kihulla, pamoja na kuunga mkono pongezi na shukrani kwa Rais Samia kuwezesha ujenzi wa jengo hilo, pia amebainisha kuwa ujenzi umefikia asilimia 95.2 na kwamba kukamilika kwake siyo tu kutaboresha mazingira ya wafanyakazi wa Wakala bali pia kwa Serikali kwa ujumla.

Akidadavua baadhi ya faida zitakazopatikana kutokana na kukamilika kwa jengo hilo, Mtendaji Mkuu ameeleza kuwa maabara ya kisasa ndani yake itawezesha kuhifadhi vifaa ambavyo kitaalamu vinajulikana kama vyenye usahihi wa kati au kwa lugha ya kigeni ‘secondary standards’

“Niwakumbushe tu kuwa, Wakala wa Vipimo ndiyo umepewa jukumu la kuhifadhi vipimo vyenye usahihi wa kati, kwa maana pale ndiyo tunalinganishwa kimataifa na ndipo unaleta ongezeko la imani kwa wawekezaji kuja kuwekeza nchini wakijua kwamba usahihi wa vipimo unafuatiliwa kutoka ngazi ya mfanyabiashara mpaka ngazi ya kimataifa.”

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, mwakilishi wa Mkandarasi anayejenga jengo hilo kutoka Kampuni ya Mohamed Builders, Bwana Burhan Hamza pamoja na Mshauri Elekezi kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Bi Rachel Lista wamethibitisha kuwa jengo litakamilika na kukabidhiwa kwa WMA Februari 10, 2025.

Ujenzi wa Jengo la Ofisi Kuu ya Wakala wa Vipimo, lililopo eneo la Medeli jijini Dodoma ulianza Julai 2, 2022 na matarajio ilikuwa likamilike Desemba 30, 2024 lakini Mkandarasi aliomba kuongezewa siku 40 kutokana na changamoto ndogondogo alizokutana nazo.

Hadi sasa Mkandarasi amelipwa jumla ya shilingi bilioni 5.8 kati ya shilingi bilioni 6.2 ambayo ni gharama ya utekelezaji wa Mradi huo.






 


Nimekuja kubaini katika maisha unaweza kufanya kazi kwa bidii sana na kujituma lakini ikawa ni vigumu kwa wewe kufanikiwa kwa sababu unakuwa anapambana katika eneo ambalo sipo riziki yako ilipo.

Jina langu ni Ramadhani mkazi wa Mombasa, Kenya, tangu nikiwa kijana mdogo niliamua kujishughulisha na uvivu maana nilipenda sana safari za majini, kazi hiyo niliifanya kwa miaka mingi hadi kila mtu mtaani kwetu alikuwa akinitambu kama mvuvi mashahuri sana.

Changamoto yangu ilinza pale ambapo nilikuwa nafanya kazi sana na kutambulika na kila mtu na kusifiwa sana lakini hakuna maendeleo yoyote niliyoyapata kwenye maisha yangu kutokana na kazi yangu.

Nilianza kupata msongo wa mawazo, kwani nilitaka kuoa maana tayari nilikuwa na mchumba lakini nilishindwa endapo nitaoa ni jinsi gani nitamtunza mke wangu wakati sina maendelo yoyote yale.

Wazo lilinijia nikatazama nyota yangu ya mafanikio ipo wapi maana kama ni uvuvi nimeshafanya kwa zaidi ya miaka 10 sina chochote cha maana nachoweza kujisifia.

Nilitafuta mtaandaoni wataalam wazuri wa masuala ya nyota hadi pale ambalo nilikutana na mtandao wa Dr Bokko ambaye nathubutu kumuita shujaa wa maisha yangu.

Katika tovuti yake hiyo nilichuka namba yake, +255618536050 na kumpigia, alinialika ofisini kwake.

Baada ya kufika na kutazama kwa utaalamu wake, aliniambia nyota yangu ya mafanikio haipo katika uvuvi bali ni kununua samaki toka wavuvi na kuuza kwa wateja.

Hatimaye nikaondoka kuelekea nyumbani, sikuwa na mtaji ila nilisema kwa vile wavuvi wengi ni rafiki zangu nitakuwa nakopa halafu nauza nikipata fedha nawalipa deni lao mimi nabakia na faida.

Nakumbuka nilifanya hivyo kwa muda wa wiki moja pekee tayari nikawa na mtaji wangu wa kununua samaki wa kutosha, biashara hii imenipa mafanikio hadi nimeweza kujenga na sasa nina watoto watatu na wote wanasoma shule nzuri.

Binafsi tangu wakati huo nimekuwa nikiamini sana katika nyota, hata rafiki zangu ambao wamekuwa wanapata ugumu wa maisha mara kadhaa nimekuwa nikiwashauri kwenda kutazama nyota za kwa Dr Bokko ambaye ndiye mtaalamu wa kuaminika zaidi kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki.

 


📌 ataka miundombinu ya umeme ilindwe

Katika kuunga mkono kampeni ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ya kuhamasisha wananchi kuunganisha umeme kwenye nyumba zao, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai amewalipia gharama za kuunganisha umeme wazee na wenye ulemavu katika Kijiji cha Nzogolo Kata ya Nzega ndogo.

Mkuu huyo wa Wilaya alitoa ahadi hiyo wakati wa kampeni inayoendelea Mkoa wa Tabora inayotekelezwa na REA ya kutoa elimu kwa umma na kuhamasisha wananchi waliofikiwa na miradi ya umeme vijijini wanaunganisha nyumba zao na umeme.

“Tunampongeza na kumshkuru sana Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea umeme vijijini na sasa anapeleka kwenye vitongoji. Ni jukumu langu mimi na wewe kutumia fursa hii adhimu kuunganisha umeme. Na mimi kama mwakilishi wa Mhe. Rais nitawawekea wazee wangu wa hapa wawili, kuna mama nimetoa fedha pia awekewe umeme,” amesema Mhe. Tukai.

Mhe. Tukai pia amewahamasisha wananchi kutumia umeme huo kujiletea maendeleo kwa kufanya shughuli zitakazowaongezea kipato kupitia uwepo wa umeme huo huku akiwataka kutunza miundombinu hiyo ya umeme.

Kwa upande wake Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Tabora, Mha. Oscar Migani amesema Serikali kupitia REA imetumia zaidi ya Shilingi Bilioni 53.97 kutekeleza miradi mbalimbali ya nishati vijijini katika Wilaya ya Nzega.

Katika Mkutano huo, Mbunge wa Nzega Mjini ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe aliahidi kuwalipia wananchi 10 ili waunganishiwe umeme kwa lengo la kuhamasisha shughuli za maendeleo katika Kata hiyo.








 



Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua rasmi Mwenyekiti na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa mgombea wa urais kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Uamuzi huu wa kihistoria unaonyesha imani kubwa na matumaini makubwa ambayo CCM inayo kwa uongozi thabiti na wa kimkakati wa Rais Samia, pamoja na dhamira yake isiyotetereka ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Katika kipindi chake cha uongozi, Tanzania imeshuhudia mafanikio makubwa katika ukuaji wa uchumi, ujenzi wa miundombinu, maboresho ya huduma za afya, na kukuza demokrasia kupitia falsafa yake ya “4Rs.”

Akiwa Rais wa kwanza mwanamke katika historia ya Tanzania, Rais Samia si tu kwamba amevunja vikwazo vya kijinsia, bali pia ameweka viwango vipya vya uongozi shirikishi na wa maono.

Uteuzi wa CCM ni hatua muhimu ya kuhakikisha maendeleo yanayoendelea na mustakabali wa neema kwa Watanzania wote.











 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Yusuf  Nzowa,akipeperusha béndera kama ishara ya kuzindua mbio za Kilimanjaro Premium Lager International Marathon 2025 katika hoteli ya Salinero-Kilimanjaro huku wadhamini wa mbio hizo na wadau wengine wakishuhudia uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Khensani Mkhombo akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Yusuf Nzowa akizungumza wakati wa tukio hilo.


MSIMU wa 23 wa mbio za kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager International Marathon 2025 umezinduliwa mkoani Kilimanjaro hafla iliyowakutanisha wadau mbalimbali wa michezo.

Mbio hizo zimezinduliwa mwishoni mwa wiki hii katika Hoteli ya Salinero mkoani humo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Kiseo Yusuf Nzowa, akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu,ametoa pongezi nyingi kwa wadhamini, wandaaji na wadau wengine wa michezo kwa kufanya mashindano hayo kuwa endelevu, jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kuweka Mkoa wa Kilimanjaro katika ramani ya dunia.

Yusuf anasema mbali na kukuza afya za watu, mbio hizo ambazo sasa ni maarufu Barani Afrika zinachangia kukuza uchumi wa mkoa na Taifa kwa ujumla kupitia sekta ya utalii kila mwaka, kutokana na washiriki wa ngazi zote kuwepo mkoani humo kipindi chote cha mbio hizo.

“Tunajivunia mbio za Kilimanjaro Premium Lager International Marathon ambazo zimeendelea kuwa maarufu kila mwaka; tukio hili kwa sasa limekuwa maarufu huku likishirikisha zaidi ya watu 12,000 na idadi kama hiyo ya mashabiki wanaokuja mkoani kwetu kwa ajili ya kufuatilia”, amesema 

Ameongeza, "tukio hili linawaleta pamoja watu kutoka takribani nchi 56 jambo ambalo linayafanya mashindano hayo kuwa ya kipekee ukanda wa Afrika Mashariki na Kati,"

Yusuf alitoa rai kwa wadau wote wa michezo kushirikiana kwa karibu na waandaaji wa mbio hizo ili ziendelee kuleta manufaa zaidi ya kiuchumi kwa Mkoa, Taifa na kwa mtu mmoja mmoja kutokana na ukweli kwamba mashindano hayo yanazidi kukua na sambamba na umaarufu wake kuendelea kukua kila mwaka.

"Mbio hizi huandaliwa kila mwaka na mwaka huu ni msimu wake wa 23, manafuaa yake kiuchumi yanaonekana wazi kwa jamii yote ya Watanzania, kutokana pamoja na mambo mengine ikiwemo kukua kwa biashara mbalimbali katika mji wa Moshi; nitoe wito kwa wafanyabiashara wote wa Moshi na Mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla kuhakikisha wanazingatia ubora katika kutoa huduma zao ili kulinda heshima ya Mkoa katika nyanja za kibiashara”, amesema.

“Nichukue fursa hii kuwapongeza wadhamini wote wa mbio hizi wakiongozwa na mdhamini mkuu Kilimanjaro Premium Lager ambao wanadhamini mbio za kilomita, kampuni ya YAS ambao wanadhamini mbio za kilomita 21 (Yas Half Marathon) pamoja na Benki ya CRDB ambao wanadhamini mbio za kilomita 5”, amesema 

Anaongeza, “Napenda pia kuwaponegza wadhamini wengine ambao wanaunga mkono mbio hizo ambao ni pamoja na kampuni ya saruji ya Simba (Simba Cement), Kilimanjaro Water, TotalEnergies, kampuni ya TPC Sugar Ltd, Wasambazaji rasmi GardaWorld, CMC Automobiles, Salinero- Kilimanjaro, Kibo Palace Hotel na Keys Hotel, ambao ushiriki wao umechangia kuendelea kukua kwa mbio hizi”.

Akiongea katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Khensani Mkhombo, amesema kuwa kampuni hiyo inajivunia kuwa wadhamini wa mbio hizo kwa miaka 23 iliyopita kupitia Bia ya Kilimanjaro Premium Lager na kuifanya kampuni hiyo kuwa mmoja wa wadhamini wa muda mrefu kwenye tukio moja la kimichezo hapa nchini.


“Kutokana na mbio hizi kuzidi kupata umaarufu, Mwaka huu, kamati ya maandalizi ya mbio hizi imekuja na mkakati mpya unaolenga kufanya matamasha ya utangulizi ambayo yatafanyika siku za mwisho wa wiki kuelekea mbio hizi, ambapo matamasha hayo yataanza Ijumaa na kumalizika Jumapili ambayo ndiyo siku ya mbio hizo”, amesema 

Akizungumzia  zawadi zilizoandaliwa kwa msimu wa 2025, Mkhombo amesema kuwa Kilimanjaro Premium Lager imetenga jumla ya shilingi milioni 30, ambapo washidi wa kilomita 42 kwa wanaume na wanawake kila mmoja anatarajiwa kupata zawadi shilingi milioni 5.5, ambapo wanariadha wa Kitanzania ambao watashika nafasi ya kwanza katika mbio za kilomita 42watapata bakshishi ya 550,000/- kila mmoja.

Akizungumzia mafaniko mengine, Mkhombo amesema mbali na kukuza sekta ya michezo, mashindano hayo pia yameimarisha ushirikiano wa muda mrefu kati ya wadhamini, wandaaji, chama cha riadha nchini RT pamoja na jamii yote kwa ujumla.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Biashara YAS, Isack Nchunda amesema, "Mwaka huu tunaadhimisha na kujivunia kuwa sehemu ya udhamini wa mbio hizi maarufu Barani Afrika kwa muongo wa kumi sasa, kupitia udhamini wetu wa mbio za kilomita 21 maarufu kama Yas Half Marathon, ambapo kitengo hiki kinawaleta washiriki takribani 6,500, wakiwemo wanariadha maarufu Barani Afrika”.

Amesema mwaka huu, wakimbiaji na washiriki wengine wa pembeni kwa maana ya mashabiki wa mbio hizo watarajie kuona mambo mazuri kwenye mbio za kilomita 21 kutokana na uzoefu walionao wadhamini wambio hizo ambao ni Yas, ambapo alitoa rai kwa washiriki wa mbio hizo kujitokeza mapema ili kuwahi nafasi zao kabla mbio hizo hazijaanza siku ya tukio hilo.

Kwa upande wake, Meneja Biashara wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, David Peter, amesema kampuni hiyo inajivunia kuwa mmoja wa washiriki wa Karibu wa mbio hizo maarufu kupitia udhamini wake katika mbio za kilomita 5 za mashindano ya Kilimanjaro Marathon ambayo yanalenga kuboresha afya za watu sambamba na kukuza uchumi wa Mkoa wa Kilimanjaro na Taifa kwa ujumla.

“Kwetu hili ni jukwaa sahihi la kuitangaza benki yetu kwani tunatarajia kuwafikia Watanzania wengi wa Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro pamoja na wale Mikoa ya jirani kupitia udhamini wetu wa mbio za Kilomita 5 za Benki ya CRDB,” amesema na kuongeza, nitoe wito kwa washiriki kujisajili kwa wingi ili waweze kushiriki kitengo cha mbio za CRDB Bank kilomita 5.”

Kwa upande wao kamati ya waandaaji wa mbio hizo wamewashukuru wadhamini wakuu wa Kilimanjaro Premium Lager na YAS kwa kutenga kitita cha jumla ya shilingi milioni 53 ambazo zitatolewa kama zawadi ya Mbio za kilomita 42 na kilomita 21, pamoja na vitengo vinmgine mbalimbali.

Waandaaji hao pia wamesema kuwa tukio hilo mwaka huu, pia linalenga kuchangia asilimia 5 ya kila malipo ya kiingilio kwa ajili ya msaada kwa Shirika la Tumaini la Maisha (TLM), msaada ambao wamesema unalenga kuwahudumia watoto wanaougua ugonjwa wa saratani ili wapate matumaini mapya baada ya kupata matibabu ya ugonjwa huo.

“Pesa zote ambazo zitachangwa kwa ajili ya msaada huo mwaka huu, zitaelekezwa kwenye Kituo cha Matibabu ya saratani wka watoto kilihcoko katika hospitali ya rufaa ya kanda ya KCMC (KCMC ZRH) iliyoko Moshi, mkoani Kilimanjaro”, imesema sehemu ya taarifa ya wandaaji hao.

Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager Marathon zinatarajiwa kufanyika Jumapili ya Februari 23, 2025, katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), ambapo mbio hizo zimeadnaliwa na kampuni ya Kilimanjaro Marathon na kuratibiwa hapa nchini na kampuni ya Executive Solutions Limited, ambapo kampuni ya Wild Frontiers ndiyo inawajibika na matayarisho yote ya usafiri pamoja na maswala yote ya masoko yanayohusiana na tukio hilo muhimu.



Na John Walter -Babati

Mahakama ya Mwanzo Babati imewahukumu kifungo cha miezi miwili gerezani vijana wawili, Abubakari Semburi (18) na Abdul Hamza (18), wakazi wa Maisaka, kwa kosa la kuharibu mali ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA).

Washitakiwa hao walikutwa na hatia ya kuharibu mita za maji za BAWASA na kuziuza kama chuma chakavu katika kesi iliyowasilishwa na mlalamikaji, Sebastian Honorath, ambaye ni Meneja wa Ufundi wa BAWASA. 

Hukumu hiyo ilitolewa Januari 10, 2025, na Mheshimiwa Hakimu Kangida Kalembo, kwa mujibu wa kifungu cha 326(1) cha Sheria ya Kanuni za Adhabu, sura ya 16, marejeo ya mwaka 2022.

Wawili hao walikutwa na mita hizo  Desemba 24, 2024, majira ya saa saba mchana, katika maeneo ya Maisaka, mjini Babati.

Meneja wa Huduma kwa Wateja wa BAWASA, Rashidi Chalahani, amesema wamekuwa wakifuatilia kwa muda mrefu visa vya wizi wa mita za maji kutoka kwa wateja wao ambapo uchunguzi walioufanya ulipelekea kugundua mita hizo zikiwa zimeuzwa kwenye eneo la biashara ya chuma chakavu, hatua iliyosababisha kufunguliwa kwa kesi hiyo mahakamani.

Bw. Chalahani ametoa wito kwa jamii kutambua kuwa mita za maji ni mali ya umma na zinapaswa kuheshimiwa na kutunzwa. 

Aidha, amewataka wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo wataona uharibifu au uhujumu wa miundombinu ya maji. 

Amesema vitendo kama hivyo vinakwamisha juhudi za serikali za kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi wote.

Hukumu hii ni onyo kwa wale wanaojihusisha na uharibifu wa miundombinu ya umma, huku ikisisitiza umuhimu wa kushirikiana katika kulinda rasilimali za taifa.

 

Katika kutafuta mke wa kumuoa kuna wakati nilifikia kipindi na kusema huwenda nina mikosi katika maisha yangu, hiyo ni kutokana kila mwanamke ambaye nilikuwa namtongoza alikuwa akinikatalia ombo langu.

Sikujua sababu ni nini hasa maana kama ni mvuto wa sura ninao, nina kazi ya kunipa kipato kizuri tu cha kijikimu na kuendeleza maisha yangu na hata kumuhudumia mwanamke ambaye nitakuwa naye katika mahusino.

Jina langu ni Yona toka Dodoma mkoani Tanzania, nina miaka 30 sasa nikiwa ni Baba wa watoto wawili na mke mmoja ambaye na mpenda sana na yeye ameonyesha kunipenda tangu siku ya kwanza tunaanza mahusiano yetu.

Mke wangu ni raia wa Marekani, alikuja Tanzania kutalii na ndipo aliweza kukutana na mimi na kuanzisha mahusiano, kukutana kwetu kulikuja baada ya mimi kuhaingaika sana kutafuta dawa za mvuto wa kimapenzi ambazo nilikuja kuzipata kwa mtu aitwaye Dr Bokko.

Mtu huyu nilikutana naye kupitia mitandao ya kijamii ambapo kwenye group moja la Facebook linalohusu mambo ya uchumba, dada mmoja alituma namba zake +255618536050 na kueleza Dr Bokko alifanikiwa lengo lake la kupata mume.

Nikiwa katika hali ya kukata tamaa, niliamua kupiga moyo konde na kumtumia Dr Bokko ujumbe mrefu kupitia WhatsApp nikimueleza kuhusu shida yangu.

Haikuchukua muda ujumbe wangu ukawa umejibiwa na mchakato wa kutumiwa dawa ukawa umeanza.

Baada ya kupata dawa zangu nilianza kuzitumia nikiwa na matumaini tele, sasa siku moja nikiwa nakatiza maeneo ya mjini nilikutana na dada mmoja wa kizungu ambaye alikuwa anahitaji nyumba ya kufikia wageni, kutokana mimi nilikuwa ni mwenyeji wa pale, nilimsaidia kupata nyumba hiyo mara moja.

Aliniomba namba yangu ya simu na kuniambia atanitafuta siku inayofuata, sikuwa na mawazo kuwa anaweza kuja kuwa mpenzi wangu, nilikuwa najua tu anaweza kunipa kazi za hapa na pale na baadaye kupata fedha.

Basi akanipigia tukakutana na kuzungumza sana, tukala na kunywa, tuliendelea kuzoeana hadi ikafika hatua za yeye kuonyesha dalili kuwa ananipenda.

Nilisita kumwambia kuhofia kuwa naweza kuharibu urafiki wetu, mwenyewe uvumilivu ulimshinda na kunitumia SMS kuwa ananipenda ana angependa niwe mume wake.

Hatimaye tulianza mahusiano hadi kuja kufunga ndoa na sasa tumejaliwa kupata watoto wawili wa kiume, maisha ni mazuri sana, nashukuru kwa tiba ya Dr Bokko ambaye ameweza kubadilisha maisha yangu kabisa.

 


Wataalam sekta za Wanyamapori na Misitu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Wizara ya Maliasili na Utalii  na Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakutana Jijini Arusha, kujadili utekelezaji wa mashirikiano baina ya pande mbili kwa ustawi wa uhifadhi na kukuza utalii nchini.

Wakizungumza wakati wa kikao hicho viongozi wa pande zote mbili, Bi. Kay Kagaruki, Mkurugenzi Msaidizi Matumizi Endelevu ya Wanyamapori , Kutoka Wizara ya Malisili na Utalii, Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Bw. Said Juma Ali Mkurugenzi wa Misitu, Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamesema  mashirikiano hayo yameleta tija katika sekta ya uhifadhi wa wanyamapori, Misitu na Utalii.

Aidha, Miongoni mwa mada zilizojadiliwa katika kikao  kazi hicho ambacho kimefanyika makao Makuu ya TAWIRI, ni pamoja na utekelezaji wa Mikataba ya Kikanda na Kimataifa, udhibiti wa ujangili, utoroshwaji wa nyara, usimamizi wa rasilimali za misitu, nyuki na wanyamapori, utafiti na biashara katika sekta za misitu, nyuki na wanyamapori na uendelezaji Utalii.









Wananchi wanaotumia barabara ya Same – Mkomazi wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa haraka wa daraja lililovunjika katika kijiji cha Mpirani, Same mapema mwezi huu kutokana na mvua. 

Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti, wananchi hao wameeleza kwamba kukatika kwa daraja hilo kulikata mawasiliano ya barabara kati ya Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro hadi Mkomazi kulisababisha usumbufu mkubwa kwao.

“Tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa kumtuma Waziri wa Ujenzi kuja hapa kuangalia hali na kutoa maelekezo. Tunashukuru kwamba daraja linapitika na tunaweza kuendelea na kazi zetu kama kawaida,” alisema Hassan Mkayanda ambaye ni mkazi wa Same.

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, alitembelea eneo hilo wiki iliyopita na kuagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kujenga daraja hilo usiku na mchana ili liweze kupitika tena na kuruhusu shughuli za kijamii na kiuchumi zirejee katika hali ya kawaida.

Barabara hiyo muhimu katika upande wa Kaskazini mwa Tanzania ni miongoni mwa zilizoathiriwa na mvua ambazo Waziri Ulega alizifanyika ukaguzi katika maeneo tofauti nchini katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.