
Kampuni ya kuzalisha vinywaji changamshi ya Mati Super Brands Limited yenye makao Makuu mjini Babati mkoani Manyara imetoa zawadi ya fedha Taslimu kwa madereva wa Bajaji waliobandika matangazo ya kinywaji cha Tanzanite Royal Gin kinachozalishwa na kampuni hiyo kama njia mojawapo ya kuunga mkono juhudi za vijana wanaojikwamua kiuchumi na kuiunga mkono kampuni hiyo ya wawekezaji wazawa.
Wakikabidhi zawadi kwa madereva wa bajaji ikiwa ni muendelezo wa kutoa zawadi baada ya Mkurugenzi wa Kampuni hiyo David Mulokozi kukabidhi zawadi ya Bajaji mpya kwa kijana aliyeweka picha yake na picha ya bidhaa ya Strong Dry Gin kwenye bajaji yake julai mwaka 2024.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited Gwandumi Mpoma amesema kuwa kampuni hiyo itaendelea kutoa zawadi kwa madereva wa bajaji ambao ni wabunifu na wamekua wakiweka picha ya bidhaa zinazozalishwa na kampuni hiyo katika bajaji zao kutokana na mapenzi mema waliyonayo kwa kampuni hiyo.
“Tumekua tukipishana na Bajaji zenye picha ya kinywaji cha Tanzanite Royal Gin hapa mjini baada ya kufuatilia kwa kipindi kirefu tumegundua hawa vijana wana damu ya Mati Super Brands Limited hivyo tutaendelea kuwaunga mkono kila mara ,tunatoa wito kwa madereva wengine kuendelea kutuunga mkono” Anaeleza Mpoma.
Meneja Chapa wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited Izack Piganio amesema kuwa wamewakabidhi madereva wa bajaji fedha za mwezi mzima ambazo wamekua wakirejesha kwa wamiliki wa bajaji ili fedha wanazozipata wazitumie kwa maendeleo yao binafsi kama faida kwao .
Piganio amesema kuwa kampuni hiyo inatambua na kuthamini mchango wa madereva wa bajaji katika kutangaza bidhaa bora zinazozalishwa na kampuni hiyo zenye viwango vya kitaifa na kimataifa.












Na Munir Shemweta, WANMM NGARA
Tanzania na Rwanda zimetiliana saini Hati ya Makubaliano (MoU) ya Uimarishaji mpaka wa Kimataifa baina ya nchi hizo.
Makubaliano hayo yamefikiwa Juni 12, 2025 mara baada ya kukamilika kwa Kikao cha Kamati ya Pamoja cha Wataalamu (JTC) kati ya Tanzania na Rwanda kilichofanyia katika mji wa Ngara mkoa wa Kagera.
Utiaji saini makubaliano hayo umefanywa kati ya Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Hamdouny Mansour na Bw. Abel Buhungu ambaye ni kiongozi wa ujumbe kutoka nchini Rwanda
Akizungunza mara baada ya utiaji saini makubaliano hayo, Bw. Hamdouny Mansour, ameshukuru kwa hatua iliyofikiwa ya kutiwa saini makubaliano ya uimarishaji mpaka wa kimataifa kati ya Tanzania na Rwanda na kueleza kuwa, ni matumaini yake maazimio yaliyofikiwa yatatekelezwa kama walivyokubaliana.
Naye kiongozi wa ujumbe wa Rwanda ambaye ni Mkuu wa Ubalozi wa Rwanda nchini Sudan Mhe. Abel Buhungu ameshukuru serikali ya Tanzania kwa kuialika nchi yake kushiriki kikao cha pamoja cha uimarishaji mpaka wa kimataifa kwa nchi hizo mbili na kueleza kuwa, hana mashaka kwa kazi iliyofanyika muda si mrefu watafikia malengo yaliyokusudiwa.
Wakati wa kikao cha JTC wajumbe walipata fursa ya kukagua mpaka wa wa kimataifa wa Tanzania na Rwanda ambapo ukaguzi ulianzia katika alama ya mpaka ya Mafiga Matatu (Kasange) mahali ambapo mto Kagera/Akagera unakutana na mto Mwidu kisha kuelekea Rusumo mahali ambapo mto kagera unakutana na mto Ruvuvu/Ruvubu.
Lengo la ukaguzi wa mpaka ni kubaini hali halisi ya mpaka ulivyo, maendelezo yanayoyafanyika na yale yaliyofanyika pamoja na shughuli za kibinadamu zinazofanyika.
Mpaka wa Tanzania na Rwanda una urefu wa takriban km 230.
Zoezi la uimarishaji mipaka ya kimataifa ni utekelezaji wa makubaliano ya umoja wa Afrika kuwa ifikapo mwaka 2027 mipaka baina ya nchi za Afrika iwe imeimarishwa

Na Okuly Julius _ DODOMA
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na kukabidhi magari 19 kwa ajili ya ofisi za makao makuu na wilaya mbalimbali nchini.
Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, Waziri Aweso alisema RUWASA ilianzishwa kutokana na changamoto kubwa ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini, jambo lililopelekea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuona umuhimu wa kuanzishwa kwa wakala huo.

“Leo hii suala la ujenzi wa miradi ya maji vijijini siyo tatizo tena. Namshukuru sana Rais Samia kwa kuwa ujenzi wa taasisi hii unaenda sambamba na mazingira bora ya kazi kwa watumishi,” alisema Waziri Aweso.
Ameeleza kuwa Rais Samia alitoa kiasi cha Shilingi bilioni 24 kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya RUWASA, na kupongeza juhudi hizo akisema: “Hakika Rais wetu ni mjenzi. Yote aliyotufanyia tutamlipa kwa kufanya kazi kwa bidii, kwani amefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa miradi ya maji nchini.”
Ameongeza kuwa watahakikisha wanamfuatilia mkandarasi kwa karibu ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati, na fedha zitatolewa kwa wakati ili kuondoa changamoto au malalamiko yoyote.
“Ujenzi bora wa miradi ya maji unaendana na usimamizi makini na ufuatiliaji wa karibu. Nitahakikisha RUWASA wanapata ushirikiano wote wanaouhitaji ili kukamilisha yote waliyokusudia,” alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya RUWASA, Bi. Ruth Koya, alimshukuru Waziri Aweso kwa kuonesha uangalizi wa kipekee kwa taasisi hiyo, akisema magari 19 yaliyotolewa yataongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya RUWASA.
“Rais Samia Suluhu Hassan aliahidi kumtua mama ndoo kichwani na anaendelea kutekeleza hilo kwa vitendo. Waziri wa Maji naye anatekeleza wajibu wake kwa dhati. Magari haya yatasaidia kufanikisha lengo la Ilani ya CCM ya kuhakikisha huduma ya maji vijijini inafikia asilimia 85 ifikapo mwaka 2025,” alisema.

Katika kikao hicho, Mkuu wa Kitengo cha Ushauri Elekezi wa mradi huo, Bw. Peter Salyeem, aliwasilisha taarifa ya maendeleo ya ujenzi, akieleza kuwa mchakato ulianza Machi 2022 kwa maandalizi ya michoro, tathmini ya gharama na mazingira. Ujenzi ulianza rasmi Novemba 2023.
Alieleza kuwa mradi huo unagharimu Shilingi bilioni 24.9, huku gharama za ushauri elekezi zikiwa Shilingi milioni 499. Fedha zote zinatolewa na Serikali Kuu kupitia Wizara ya Maji.
“Mradi huu unahusisha ujenzi wa jengo kuu la ofisi ya RUWASA, kazi za nje, majengo saidizi kama mgahawa, kibanda cha mlinzi, jengo la jenereta pamoja na uzio wa eneo lote la kiwanja,” alisema.
Alibainisha kuwa mkandarasi wa mradi ni kampuni ya China Jiangxi International Economic and Technical Company Limited, huku mshauri elekezi akiwa ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA). Mradi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 12, kuanzia Novemba 2023 hadi Desemba 31, 2024, na hadi sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji.

Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka RUWASA, Bw. Titus Mkapa, alithibitisha kuwa magari yaliyokabidhiwa ni 19 na yataelekezwa kwenye ofisi za makao makuu pamoja na wilaya ili kuongeza ufanisi wa shughuli za utoaji huduma za maji vijijini.





Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amezindua Ushirika wa waendesha Pikipiki na Bajaj Dodoma na kuwataka wasafirishaji hao kutumia fursa hiyo kujiimarisha kiuchumi kupitia mikopo mbalimbali.
“Ninawapongeza kwa uamuzi huu wa kuanzisha SACCOS yenu,ni wakati muafaka sasa kuwaona vijana mkimiliki vyombo vya usafiri vya kwenu wenyewe.
Kupitia SACCOS hii vijana wengi watabadilisha maisha yao na kujijenga kiuchumi.
Nitoe rai kwa viongozi wa SACCOS kuhakikisha mnatumia vizuri mkopo wa asilimia 10 wa mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma ambapo mpaka sasa zimetengwa shilioni Bilioni 7 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya wakina mama,vijana na watu wenye ulemavu”Alisema Mavunde
Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri anewataka maafisa wasafirishaji hao kutumia SACCOS kutatua changamoto za msingi za kiuchumi za vijana wengi na kuahidi kwamba serikali itakuwa nao bega kwa bega kuhakikisha inaweka mazingira rafiki ya ufanyaji wa shughuli zao.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma SACP George Katabazi amewataka maafisa wasafirishaji hao kuzingatia sheria za usalama barabarani na kwamba Jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana nao kwa karibu kama wadau muhimu wa usalama katika jamii.
Akitoa shukrani zake Mwenyekiti wa UMAPIDO Ndg. Marwa Chacha Nyagate ameshukuru Mh. Rais Dkt. Sania S. Hassan kwa kuwajengea ofisi za chama hicho mkoani Dodoma na pia kumshukuru Mbunge Mavunde kwa mchango wa Tsh 15,000,000 kuiwezesha SACCOS yao kuanzishwa na kuahidi kwamba wataitumia SACCOS kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa vijana wote waliopo kwenye tasnia hiyo.
Mwenyekiti Marwa pia alisisitiza umuhimu wa vijana hao kushiriki uchaguzi mkuu 2025 ili kutimiza takwa la kikatiba.
Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya kama njia ya kujiandaa na changamoto za kiafya, ikiwemo gharama kubwa za matibabu ya magonjwa kama saratani.
Wito huo umetolewa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mhe. Ester Matiko (Viti Maalum), ambaye alitaka kufahamu kama Serikali haioni haja ya kuweka kifurushi cha saratani kwenye bima ya afya ya chini ili kuwezesha wananchi wa kawaida kupata huduma, kutokana na gharama kubwa za matibabu ya ugonjwa huo.
Akijibu swali hilo, Dkt. Mollel amesema jamii inapaswa kubadilika na kuwekeza kwenye bima ya afya ili kuimarisha afya zao.
"Watu wako tayari kuchangisha Milioni 100 kwa ajili ya harusi, lakini mtoto anapozaliwa hakuna anayechangia hata kwa ajili ya matibabu. Hii inaonyesha kwamba jamii inathamini sherehe kuliko afya,” amefafanua Dkt. Mollel.
Aidha, Dkt. Mollel amebainisha kuwa Serikali imetenga zaidi ya Shilingi Bilioni 200 kwa ajili ya msamaha wa matibabu, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wananchi, hususan wasio na uwezo, wanapata huduma za afya bila vikwazo vya kifedha.
Naibu Waziri amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mifumo ya bima ya afya ili kuhakikisha huduma za afya, zikiwemo za magonjwa yasiyoambukiza kama saratani, zinapatikana kwa wote kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa bima ya afya kwa wote unaotarajiwa kuimarika zaidi katika utekelezaji wa sera mpya ya afya.
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Prof. Haruni Mapesa ameitaka Serikali mpya ya Wanafunzi wa Chuo (MASO), kuzingatia, kujifunza kwa weledi na kuyatumia mafunzo watakayoyapata katika semina elekezi ya kuwajengea uwezo ili wawe viongozi bora na wa kuigwa katika kipindi chote cha uongozi wao.
Hayo ameyasema Mkuu wa Chuo Prof. Mapesa Wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo serikali mpya ya wanafunzi kwa mwaka 2025/26 yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Kampasi ya Kivukoni.
Prof. Mapesa amesema mafunzo watakayoyapata wakayatumie katika kufanya kazi kwa bidii na kuendelea kuishi viapo vyao walivyoapa baada ya kuteuliwa kuongoza serikali ya wanafunzi wa chuo hicho.
“ Serikali ya wanafunzi (MASO) ni daraja kati ya wanafunzi na Menejimenti ya Chuo katika kuwasilisha maoni, kero, changamoto zinazowakabili wanafunzi hapa chuoni, hivyo mafunzo haya yatawajenga katika kutambua misingi ya sheria na taratibu za kufuata katika kuwasilisha mambo mbalimbali katika menejimenti”, Alisisitiza Prof. Mapesa.
Mkuu huyo wa Chuo pia ameitaka Serikali ya wanafunzi kuwa mfano wa kuigwa kwa wenzao katika kuwashawishi kusoma kwa bidii ili kujiepusha na vitendo vya udanganyifu katika kipindi cha mitihani, kuwashawishi wanafunzi wenzao katika ulipaji wa ada pamoja na michango mbalimbali ya chuo, na kujiepusha na makundi ya migogoro katika muda wao ili waweze kuyafikia malengo ya kumaliza chuo kwa pamoja.
Baadhi ya mada zitakazowasilishwa ni pamoja na Dhana ya Uongozi na Utawala Bor. Kanuni, Taratibu na Matumizi ya Fedha za Umma. Migogoro, Utatuzi, na Wajibu wa Serikali ya Wanafunzi.
Mada nyingine zitakazowasilishwa ni Uongozi Bora, Maadili, Haki na Wajibu wa Kiongozi Bora, Mawasiliano na Matumizi ya Muda, na Kazi za Dawati la Jinsia.
Semeni hiyo elekezi kwa Serikali mpya ya Wanafunzi ni maalumu katika kuwajengea uwezo viongozi wa serikali hiyo ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi na weledi katika muda wote wa uongozi wao.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE
Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini katika kuunnga juhudi za Rais awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo imefanikiwa kuanzisha mradi wa mgahawa ikiwa kama ni moja ya kitega uchumi kwa ajili ya kuweza kujikwamua kiuchumi pamoja na mradi wa ujenzi wa nyumba ya Katibu wa jumuiya hiyo.
Hayo yamebainishwa na Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Cecilia Ndaru wakati wa kikao cha kikanuni cha baraza hilo ambacho kimeweza kukutana kwa lengo la kujadili masuala mbali mbali ya kimaendeleo, kujiandaa katika kuelekea uchaguzi mkuu, mapokezi ya Mwenyekiti wa UTW Taifa sambamba na kupokea taarifa ya utekelezaji wa ilani ya chama kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2020 hadi 2025 kutoka kwa madiwani wa viti maalumu.
Katibu Ndaru amesema kwamba lengo lao kubwa ni kuweka mikakati madhubuti ya kuendelea kubuni na kunzisha miradi mipya ambayo itaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa jumuiya hiyo kuweza kujiongezea kipato pamoja na kuweka misingi imara ya kuweza kuimarisha jumuiya hiyo kuanzia ngazi za chini.
Katika kikao hicho cha baraza ambacho kilifunguliwa na Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka ambaye alikuwa mgeni rasmi amewataka wanawake hao kuhakikisha wanakuwa naa umoja na mshikamano hasa katika kioindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Nyamka katika baraza hilo amewahimiza wanawake kuchangamkia fursa za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ikiwemo katika nafasi ya udiwani pamoja na ubunge na kuwaomba wanampa kura nyingi za kishindo cha hali ya juu Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi huo mkuu amebainisha kwamba lengo la chama ni kuhakikisha wanashinda katika nafasi zote.
"Nawapongeza sana wanawake wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini kwa kuweza kuchapa kazi kwa bidii na mimi nimefaarijika sana kuona meweza kusimamia vemaa utekelezaji wa ilani ya chama na pia mmeweza kuanzisha mradi wa mgahawa amabo utaweza kuwa ni chachu ya kujikwamua kuchumi sambamba na ujenzi wa nyumba ya katibu kwa hivyo kitu kikubwa mfanye kazi na viongozi ambao bado wapo madarakani achanane na kampeni amabzo hazina faida kwa kipindi hiki,"amebainisha Nyamka.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu kwa kuweza kutenga fedha nyingi ambazo zimekwenda katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu, afya, maji,miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyingine za kijamii.
Aidha Mgonja amemshukuru Mbungu wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe. Silvestry Koka pamoja na mke wake Mama Selina Koka kwa kuweza kuwa mstari wa mbele kupambana katika kuwasaidia kwa hali na mali kufanikiwa ujenzi wa mradi wa mgahawa pamoja na mradi wa ujenzi wa nyumba ya katibu wa UWT kwa kushirikiana na wadau na viongozi wengine wa chama pamoja na jumuiya zake.
Naye mlezi wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini ambaye pia ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka amewahimiza wanawake wote kuwa na umoja na mshikamano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kuwaomba kuwa mstari wa mbele katika kupiga kura lengo ikiwa ni kuweza kushika katika nafasi zote za udiwani, ubunge, pamoja na nafasi ya urais.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka ambaye amefunga rasmi kikao cha baraza hilo ameishukuru kwa dhati jumiya hiyo ya wanawake kwa kuweza kumpa ushirikiano na sapoti kubwa katika kipindi chote ambacho aliingia madarakani na kuahidi kuendelea kushirikiano nao katika masuala mbali mbali ya kimaendeleo na kutatua changamoto ambazo wanakumbana nazo.
Koka amebainisha kwamba tangu aingie madarakani mnamo mwaka 2010 ameweza kuwa bega kwa bega na jumuiya ya UWT ambapo wameweza kushirikiana katika baadhi ya miradi mbali mbali ikiwemo ujenzi wa mradi wa nyumba ya Katibu pamoja naa kiteega uchumi cha mgahawa sambamba na kushirikishwa katika vikao mbali mbali vyebye kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo ikiwemo kutatua kero na changamoto za wananchi.
Wananchi wa Kijiji cha Mvuleni na vijiji vya jirani katika Kata ya Nyamato,Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani wamenufaika na Huduma bora ya afya baada ya Ujenzi wa Kituo kipya cha Afya cha Mvuleni kilichogharimu Shilingi Milioni 559.
Kituo hicho kinachotoa Huduma za Wagonjwa wa nje,Huduma za Maabara,Upasuaji na Huduma za Uzazi, kimepunguza umbali kwa Wananchi kufata Huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga.
Akizungumza wakati alipotembelea Kituo hicho,Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Ndg. Zainab Khamis Shomari (MNEC) amewataka Wananchi wa Kata ya Nyamato kuiunga Mkono Serikali ya Dkt. Samia Suluhu katika Juhudi zake za kuwaletea Maendeleo Watanzania.
"Katika maeneo yote tuliyozunguka tumekuta Vituo vya Afya,Zahanati na Maji Safi na Salama,hii ndio kazi inayofanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongwa na Rais Samia Suluhu Hassan,lengo ni kusogea huduma muhimu kwa Wananchi"
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bw. Shigeki Komatsubara, amefanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Njombe yenye lengo la kutembelea na kujionea fursa za uwekezaji zilizopo Mkoanj Njombe, hasa zile zilizojikita zaidi kwenye mazao ya kilimo na kuongeza thamani.
Mara baada ya kuwasili, Bw. Komatsubara alipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, ambaye alitumia nafasi hiyo kumkaribisha mkoani Njombe na kumweleza fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta mbalimbali.
“Mkoa wa Njombe una ardhi nzuri na yenye rutuba, mazingira rafiki kwa uwekezaji, na wananchi wachapakazi. UNDP mnayo nafasi ya kipekee ya kushirikiana nasi katika kuinua kilimo, viwanda na ajira kwa vijana wetu,” alisema Mhe. Mtaka.
Katika ziara hiyo, Bw. Komatsubara alitembelea viwanda mbalimbali vikiwemo cha kuchakata mafuta ya parachichi cha AVO Afrika, kiwanda cha kufungasha parachichi Makambako, kiwanda cha mbao cha EAST KELIN WOOD, pamoja na viwanda vya chai vya Kibena na TANWAT.
Akiwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, alipewa taarifa ya fursa za uwekezaji zilizopo mkoani humo, hasa katika sekta ya kilimo, viwanda vidogo na huduma za kijamii.
Akizungumza mwishoni mwa ziara yake, Bw. Shigeki Komatsubara jana tarehe 11, 2025 alisema:
“Nimefurahishwa sana na mapokezi niliyoyapata Njombe. Ardhi yenye rutuba, mazingira mazuri na watu wa kujituma vinaufanya mkoa huu kuwa na fursa kubwa sana za maendeleo. Bila shaka, nitarejea tena Njombe kuona namna bora ya kushirikiana katika utekelezaji wa miradi ya pamoja.”
Ziara hii inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya UNDP na Serikali ya Mkoa wa Njombe katika kuchochea maendeleo endelevu kupitia uwekezaji, ubunifu, na matumizi bora ya rasilimali zilizopo.