Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) katika miaka mitatu ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kinajivunia mafanikio kadha wa kadha ikiwemo ongezeko la udahili wa wanafunzi ziadi ya 3800, kutoka wanafunzi 13,0199 mwaka 2021 hadi wanafunafu 17, 084.

Katika ongezeko hilo wanafunzi 105 kutoka nje ya mipaka ya Tanzania, 22 kati yao wanasoma Shahada za Awali na 83 Shahada za Juu huku  kwa upande wa watanzania, wanaume 10, 255 na wanawake 6, 829 kati yao wanafunzi 16,023 wanasoma Shahada za Awali na 1, 061 Shahada za Juu. 

Akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda amesema, ongezeko kubwa la idadi ya wanafunzi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania limetokana na mashirikiano mazuri, kuimarika kwa  Diplomasia, kazi kubwa inayofanywa na Dkt. Samia ndani ya miaka yake mitatu ya uongozi.

Pia ongezeko la mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu pamoja na ufadhili wa wanafunzi kupitia mradi wa wa Samia Scholarship kwa wanafunzi wa Sayansi ikizingatiwa SUA ni moja ya Chuo Kikuu  chenye kozi na fani ya Sayansi hapa nchini.

 Ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia, SUA imeimarisha mashirikiano na Taasisi za Mataifa mbalimbali kwa uchache, SUA imeingia mkataba wa mashirikiano na Chuo Kikuu cha Artemisa cha Jamhuri ya Cuba makataba utakao saidia kuinua taaluma na ujuzi kwa wataalamu wa nchi hizi mbili.

Mnamo Novemba 17, 2023 SUA ilisaini mkataba wa ushirikiano na Waziri wa  nchi wa Masula ya Dunia na mikakati ya Kidiplomasia wa Romania Mhe. Traiana Leurentiu Hristea hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo Romania ilitoa ufadhili wa masomo  kwa  wanafunzi 10 wa kitanzania.

Pia SUA imeingia mkataba wa makubaliano na Shirika  la Maendeleo la Japan (JICA) ya kutekeleza mradi wa kudhibiti na kuzuia maambukizi ya magonjwa yatokayo kwa wanyama kwenda kwa binadamu na kutoka kwa binadamu kwenda kwa wanyama. 

Katika Mradi huo SUA imejikita katika magonjwa mawili ya Kifua kikuu (TB – Zoonotic Tuberculosis) na ugonjwa wa kutupa mimba ( Brucellosis)

Prof. Chibunda ameendelea kuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kukiwezesha Chuo kikuu SUA kwa kukipatia fedha kwa jili ya Tafiti mbalimbali ambazo zimekuwa zikitoa majawabu ambayo yanatatua changamoto katika jamii  hasa katika Sekta za  Kilimoa, Mifugo, Uvuvu na Afya.

“Hivi karibuni watafiti wawili Dkt. Makarius Lalika na Dkt. Ramadhani Majubwa wamepewe fedha shilingi milioni 240 na Serikali ya Dkt. Samia kupitia Tume ya Taifa Sayansi na Teknolojia ( COSTECH) kwa ajili ya kufanya tafiti. Rais Samia amefanya mambo makubwa sana katika miaka yake hii mitatu hapa SUA”  amesema Prof. Chibunda

 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) imesikitishwa na kutotumika kwa majengo ya Hospitali ya Manispaa ya Bukoba kutokana na kukosa usajili.

 

Kauli hiyo imetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Stansalau Mabula wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo.

 

Alisema licha ya kwamba majengo manne kati ya sita yamekamalika tangu mwaka 2021 lakini majengo hayo hadi sasa hayajaanza kutumika kutokana na kuchelewa kuomba usajili kutoka Zahanati kuwa Hospitali ya Wilaya.

 

“Kamati  hii inakagua thamani ya fedha na kuona kama imefanya kazi iliyokusudiwa, lakini kama majengo yamekamilika lakini hayatumiki thamani yake bado haionekani,” alisema.

 

Alisema kwa tathimini iliyofanywa na Kamati mpaka sasa majengo hayo yanatumika kwa asilimia 10 tu ya malengo yalikusudiwa ya kujenga hospitali hiyo.

 

“Miaka mitatu nyuma mliomba fedha mletewe hospitali ya wilaya, lakini pamoja na kumaliza majengo toka mwaka 2021, mwaka jana Desemba ndio mlipeleka maombi ya kusajili Hospitali ya Wilaya kutoka kwenye zahanati.

 

“Vifaa vimepelekwa na MSD (Bohari ya Dawa), tunajisikiaje kama hatutavitumia kwa wakati, vitaharibika, wiki mbili zijazo wataleta vingine vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 400, vitaharibika,” alisema

 

Aliutaka watendaji wa Manispaa hiyo wawe na uchungu na fedha za Serikali zinazopelekwa kwa ajili ya kuweka miundombinu na kuwawapelekea wananchi  huduma bora. 

 

Aidha, kamati iliagiza kufanyika marekebisho iliyoyainisha katika majengo ya hospitali hiyo ikiwemo sakafu hasa katika chumba cha upasuaji.

 




 Tanzania tayari imeanza kunufaika na mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 4, kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Balozi Ombeni Sefue.

Akizungumza katika ziara ya Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), inayoongozwa na Mbunge wa Jimbo la Kwela, Deus Clement Sangu, Balozi Sefue alisema pamoja na utekelezaji wa mradi huo kufikia asilimia 27, ushiriki wa nchi katika mradi huo unaleta manufaa mengi yanayoonekana. .

Balozi Sefue alitaja baadhi ya faida hizo kuwa ni zaidi ya trilioni 2.4 zinazokadiriwa kupatikana kutokana na mradi huo, pamoja na ajira za Watanzania 4,968 tangu kuanzishwa kwa mradi huo mwaka 2021.

“Hii imechochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika mikoa inayohusika na mradi huo,” alibainisha. Alibainisha kuwa mradi huo umeajiri wazawa 385 katika Jiji la Tanga kati ya 539 katika eneo la ujenzi wa jengo hilo. “Kadhalika mkandarasi wa ujenzi wa tanki la mafuta amelipa gharama za huduma kiasi cha 53.15M/ Halmashauri ya Jiji la Tanga hadi sasa,” alisema Balozi Sefue.

Balozi Sefue pia alitaja faida nyingine kuwa ni pamoja na watoa huduma mbalimbali kunufaika na Dola za Kimarekani milioni 171.71 zilizotolewa kwa wakandarasi wa ndani, ambapo jumla ya Dola milioni 462 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa huduma na bidhaa mbalimbali.

Kuhusu hali ya utekelezaji wa mradi huo, wajumbe wa Kamati ya PIC pia walielezwa kuwa mambo kadhaa ya mradi huo, kama vile ujenzi wa kambi na kuhifadhi mabomba yamekamilika kwa asilimia 100.

“Ujenzi wa Kiwanda cha Kupitishia Mifumo ya joto (TIS) umefikia asilimia 61, na mtambo huo uko tayari kwa majaribio,” alisema na kuongeza kuwa mabomba yenye uwezo wa kulazwa kwa umbali wa kilomita 280 yamefika katika kiwanda cha TIS, tayari kwa kufungwa. na mfumo wa kuhifadhi mafuta kabla ya kazi ya kuwekewa bomba kuanza Mei mwaka huu.

Matenki yatakayopelekwa katika kituo cha kupokea na kuhifadhi mafuta cha Chongoleani (MST) yapo katika hatua ya ujenzi, huku asilimia 32 ya kazi ikiwa imekamilika, huku gati ya kupakia mafuta ikiwa imekamilika kwa asilimia 36.

Balozi Sefue aliupongeza mradi huo kwa kuwa ni Ubia wa kweli wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) si tu Tanzania bali hata katika mataifa hayo mawili washirika, na kueleza kuwa yanadhihirisha jinsi diplomasia inavyoweza kusogeza mbele michakato.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Musa Makame, alieleza kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania tayari imepata 30 billion kutokana na mradi huo na watoa huduma wengine na inatarajia kukusanya zaidi kadri ujenzi unavyoendelea hadi kukamilika.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deus Clement Sangu, alieleza kuridhishwa na Tanzania kuwa imeanza kufaidika na mradi huo ambao umekuwa na upinzani mkubwa kimataifa.

Alieleza kuridhishwa na Tanzania kupitia TPDC, kama mwanahisa, inaendelea kushirikiana na wanahisa wengine kuhakikisha mradi huo unafikia malengo yake. Alieleza kuwa alifahamishwa kuwa hadi Machi 15, mwaka huu, TPDC ilichangia jumla ya dola za Marekani milioni 268.78, ambayo ni asilimia 87 ya Dola za Marekani milioni 308 ambazo Tanzania ilipangwa kuchangia kama mtaji.

Wawekezaji binafsi wanatekeleza mradi huo kwa ushirikiano na serikali ya Tanzania na Uganda. TPDC na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) zinamiliki asilimia 15 kila moja, TotalEnergies ya Ufaransa inamiliki asilimia 62, na Shirika la Mafuta la China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) linamiliki asilimia 8.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Chongoleani, Ambari Mabruki Hoza, ambaye pia ni Maalim Ashraf Mabano, aliipongeza Serikali kwa kuanzisha mradi huo ambao alieleza kuwa umeanza kutoa zawadi. Hata hivyo, ameitaka EACOP kuangalia namna ya kuwajengea wananchi vifaa vya kisasa vya uvuvi na ufugaji utakaoboresha maisha yao.

Naye Diwani wa Kata ya Chongoleani Kassim Mbega ameihimiza serikali au mradi huo kufikiria kujenga kituo cha afya kwa manufaa ya jamii na watendaji wa mradi huo. Alieleza kuwa inasikitisha kuwa tangu kuanza kwa mradi huo mamlaka husika hazijafikiria kupanua huduma ya afya ambayo leo inakabiliwa na ongezeko kubwa la watu.



 

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (katikati) na Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde (kulia) wakikata utepe wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick.



Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde, ameipongeza Kampuni ya Dhahabu ya Barrick ambayo inaendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals, kwa kufanya uwekezaji unaoendelea kuchangia kukuza uchumi na kufanikisha miradi ya kijamii ambayo inaendelea kuboresha maisha ya wananchi.

Mh. Mavunde ametoa pongezi hizo leo Jumatatu Machi 18,2024 wilayani Kahama wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick chenye hadhi ya kimataifa kijulikanacho kama Barrick Academy, katika mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama ambao umefungwa ambacho kitakuwa kinatoa mafunzo kwa wafanyakazi wa Barrick wa nchini na nje ya nchi kupata utaalamu wa kuendesha shughuli zao kwa weledi.

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde.


Waziri Mavunde amesema ulimwengu wa sasa ni wa sayansi na teknolojia hivyo chuo hicho kimeanzishwa katika wakati muafaka ambapo sekta ya madini nchini inakua kwa kasi sana na kuhitaji wataalamu wa kutosha.


Ametoa wito kwa uongozi wa Barrick kuangalia uwezekano wa kuanzisha kozi za kuwasaidia wachimbaji wadogo wadogo nao wapate maarifa ya kuendesha kazi zao kwa maarifa.

“Barrick mmeanza kwa kufungua chuo katika eneo hili la Ukanda Maalum wa Kiuchumi la Buzwagi la Serikali, nina imani wawekezaji wengi watajitokeza kujenga viwanda ili kuziba athari za kiuchumi zilizotokana na kufungwa kwa mgodi wa Buzwagi”,amesisitiza.

Kwa upande wake, Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow, amesema Barrick itaendelea kufanya kazi na Serikali kuhakikisha ubia wake unanufaisha pande zote na kuchangia kukuza uchumi wa nchi.

Bristow amesema Barrick, inalipa umuhimu kubwa suala la elimu na itaendelea kuwekeza katika sekta hiyo ili kuhakikisha watanzania wanapata elimu na ndio maana imeamua kufungua chuo kikubwa cha kimataifa cha Barrick Academy nchini.

“Tutaendelea kuhakikisha kuwa ubia wetu na Serikali ya Tanzania unakuwa wa kuigwa katika sehemu mbalimbali duniani kwa kufanikisha kuleta mafanikio na maendeleo chanya kwa wananchi”, amesisitiza Bristow.

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow.

Bristow amesema Chuo cha Barrick kimebuniwa na Barrick ili kutoa programu maalumu za mafunzo zinazoandaliwa kulingana na mahitaji zinazolenga kuandaa mameneja wa mstari wa mbele wa Barrick ili wakue kama watu binafsi na viongozi katika nyanja zao huku kozi hizo zikiwapa ujuzi wa kusimamia timu zao kwa ufanisi zaidi na kuboresha utendaji.

“Chuo cha Barrick kitakuwa kikitoa mafunzo kwa mafomeni, wasimamizi na warakibu zaidi ya 2,000 kutoka Kannda ya Afrika Mashariki na Kati katika kipindi cha miezi 24 ijayo. Tukiwa na maono ya mbele, tunajitayarisha pia kuwajumuisha Wakandarasi wetu na kupanua mtaala ili kufikia taaluma nyingi zaidi ikiwa ni pamoja na kutoa kozi za uongozi katika masuala ya fedha, ujuzi wa ngazi ya juu wa Kompyuta na katika masuala ya usalama”,ameongeza Bristow.

Ameeleza kuwa, ufunguzi wa chuo cha Barrick unafuatia ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja wa ndege wa Buzwagi Kahama mnamo mwezi Januari 2024 lililofungua fursa kwa ajili ya huduma za ndege zilizopangwa ambalo linaweza kuhudumia zaidi ya abiria 200 kwa wakati mmoja ambapo jengo hilo linatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji uchumi katika Manispaa ya Kahama.

Muokano sehemu ya majengo katika Chuo cha mafunzo cha Barrick


Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Barrick katika Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, Sebastiaan Bock amesema uwanja wa ndege na Chuo katika mgodi uliofungwa wa Buzwagi ni sehemu ya mpango wa Barrick wa kuibadili Buzwagi kuwa Ukanda Maalum wa kiuchumi.

“Upembuzi yakinifu uliofanyika mwaka 2021 ulionesha kuwa uundwaji wa Kanda maalumu ya kiuchumi ulikuwa na uwezo wa kuchukua nafasi ya mgodi wa Buzwagi kama kichocheo cha uchumi wa eneo hili na unaweza kutengeneza ajira zipatazo 3,000 kila mwaka, kuzalisha zaidi ya dola 150,000 kila mwaka kutokana na tozo za huduma kwa Manispaa ya Kahama na kutoa takribani dola milioni 4.5 kwa mwaka kama kodi ya ajira”,amesema Sebastiaan.

Amesema Serikali ya Tanzania iliidhinisha ubadilishaji wa mgodi wa Buzwagi kuwa ukanda maalum wa kiuchumi (SEZ) kupitia tangazo la Serikali ilitolewa mwezi Februari 2024 na tayari Wawekezaji wameanza mchakato wa kuanzisha viwanda katika eneo hilo.

Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Barrick katika Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, Sebastiaan Bock.

“Namna tunavyofunga migodi yetu ni muhimu kwetu kama ambavyo tunaijenga na kuiendesha. Mgodi wetu wa Buzwagi ulikuwa kitovu cha uchumi katika ukanda huu kwa takribani miaka 15 kabla ya kutoa dhahabu yake ya mwisho mwaka 2021. Hata hivyo, mtazamo wetu huo siyo mwisho wa hadithi hii kwa Buzwagi tunapoibadilisha kuwa mali mbadala yenye tija ambayo itahudumia jamii kwa miongo kadhaa ijayo”,amesema Bock.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) Charles Itembe ameipongeza Kampuni ya Barrick kwa kubuni wazo la kuanzisha Chuo cha Barrick huku akiwaomba wawekezaji mbalimbali kujitokeza kuwekeza katika eneo hilo ili kuongeza thamani ya madini na vitu vingine kwenye eneo la Buzwagi ambako kutakuwa na viwanda zaidi ya 100 na mpaka sasa kuna wawekezaji wanane.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita amesema kuanzishwa kwa Chuo cha Barrick ni matokeo mazuri ya ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ili kukuza uwekezaji nchini.

Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini Mhe. Jumanne Kishimba amewapongeza Barrick kuwa wawekezaji wa kwanza katika Mgodi uliofungwa wa Barrick huku akiomba chuo hicho pia kitumike kutoa mafunzo ya madini kwa wachimbaji wadogo na jinsi ya kufanya biashara ya madini huku Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kahama Thomas Muyonga akisema uwekezaji unaofanyika katika eneo hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kukuza uwekezaji nchini.


ANGALIA PICHA HAPA CHINI

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde akizungumza leo Jumatatu Machi 18,2024 wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick 'Barrick Academy' chenye hadhi ya kimataifa katika mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick chenye hadhi ya kimataifa katika mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Barrick katika Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, Sebastiaan Bock akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick chenye hadhi ya kimataifa katika mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (katikati) na Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde wakikata utepe wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick chenye hadhi ya kimataifa katika mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde (katikati) akiwa ndani ya moja ya madarasa katika Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Muonekano ndani ya moja ya madarasa katika Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde (katikati) akiteta jambo na Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow (kushoto) katika Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Muokano sehemu ya majengo katika Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Muokano sehemu ya majengo katika Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Muokano sehemu ya majengo katika Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.
Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga

Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini Mhe. Jumanne Kishimba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kahama Mhe. Thomas Muyonga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga



Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) Charles Itembe akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick kwenye mgodi wa zamani wa Buzwagi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde (katikati) akizungumza na viongozi mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Chuo cha mafunzo cha Barrick

Waziri wa Madini, Mhe. Antony Mavunde akipiga picha ya pamoja na viongozi mbalimbali

 


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii imesema kuwa, haijaridhishwa na urejeshaji mikopo ya fedha za mradi wa kupanga, kupima na kumilikisha ardhi (KKK) unaofanyika kwenye halmashauri mbalimbali nchini.


Hayo yamebainishwa na Kamati hiyo wakati ilipotembelea na kukagua utekelezaji mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi (KKK) katika eneo la Msolwa katika halmashauri ya wilaya ya Chalinze mkoa wa Pwani.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe, Timotheo Mzava ameeleza kuwa, mbali na Kamati yake kuridhishwa na mradi wa KKK kwa ujumla lakini hawajaridhishwa na namna mikopo hiyo inavyorejeshwa na halmashauri.

Akitolea mfano wa Halmashauri ya Chalinze katika mkoa wa Pwani, Mhe, Mzava amesema pamoja na halmashauri hiyo kukopeshwa kiasi cha shilingi Bilioni 2.5 kwa ajili ya mradi wa KKK lakini imeshindwa kurejesha fedha kwa wakati.

‘’Kama Kamati bado hatujaridhishwa kabisa namna ya kasi ya urejeshaji fedha hizi na wito na msisitizo wetu zifanyike kila aina ya jitihada kuhakikisha fedha zinarudi ili zikasaidie maeneo mengine yenye uhitaji ili dhamira ya Rais ya kutoa fedha hizo iweze kufikiwa’’ alisema Mzava

Kwa mujibu wa Mhe, Mzava, hadi Machi 2024 kwa ujumla wizara imepokea marejesho ya shilingi bilioni 22.7 kati ya shilingi bilioni 50 sawa na asilimia 45 kutoka kwenye halmashauri na taasisi mbalimbali zilizonufaika na mkopo huo.

Amesema, fedha zinazotolewea kama mkopo usio na riba kwa halmashauri zikirejeshwa zitasaidia kukopesha halmashauri nyingine na hivyo kuisaidia kutatua changamoto za sekta ya ardhi nchini na kuboresha katika maeneo mengine.

Hata hivyo, ametaka kufanyika jitihada mbalimbali ili kusaidia katika urejeshaji mikopo hiyo na kuweza kuzisaidia halmashauri nyingine ili ziweze kuondoa changamoto za sekta ya ardhi nchini.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda amebainisha kuwa, mpaka sasa halmashaurii zilizorejesha kiasi chote cha fedha ya mkopo ni 12 huku zile zilizorejesha sehemu ya fedha zikiwa ni 43.

Mhe, Pinda amesema, Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi (KKK) ni program ya miaka kumi inayotekelezwa na wizara yake kwa kushirikiana na halmashauri mbalimbali nchini.

Ameongeza kuwa, utekelezaji wa Programu hiyo ulianza mwaka 2018/2019 na unatarajiwa kukamilika 2028/2029. Lengo la Programu ya KKK ni Kupanga miji na kuhakikisha makazi holela yanaondolewa kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Programu hiyo inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri ambazo ni mamlaka za upangaji na sekta binafsi ambapo program hiyo inagharimiewa na serikali kupitia fedha za ndani za bajeti ya maendeleo.

Serikali ilitoa mtaji wa shilingi Bilioni 50 kwa ajili ya utekelezaji wa program ya KKK kwa utaratibu wa kuzikopesha halmashauri na taasisi ambapo wizara kwa kushirikiana na wizara ya fedha na Ofisi ya Rais TAMISEMI ziliweka utaratibu kwa kuweka vigezo vya kutoa mkopo huo bila riba kwa ajili ya utekelezaji wa program.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe, Timotheo Mzava akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon mara baada ya Kamati yake kuwasili mkoa wa Pwani kukagua utekelezaji Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika halmashauri ya Chalinze mkoa wa Pwani tarehe 18 Machi 2024. Katikati ni Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Chalinze na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe, Ridhiwani Kikwete wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii katika halmashauri ya wilaya ya Chalinze Machi 18, 2024.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe, Timotheo Mzava na Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda wakimsikiliza Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze Deo Msilu (wa pili kulia) kuhusu mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi unaotekelezwa katika eneo la Msolwa Halmashauri ya Chalinze Machi 18, 2024.
Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze Deo Msilu akisisitiza jambo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ilipokwenda kukagua mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika eneo la Msolwa Chalinze Machi 18, 2024.
Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze Deo Msilu (Kulia) akielezea matumizi ya kifaa cha upimaji mbele ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ilipokwenda kukagua mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika eneo la Msolwa Chalinze Machi 18, 2024.
Mbunge wa jimbo la Chalinze na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe, Ridhiwani Kikwete akimkabidhi Hati Milki ya Ardhi mmoja wa wananchi wa Chalinze wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ilipokwenda kukagua mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi eneo la Chalinze machi 18, 2024.


Na Joel Maduka ,Kahama Shinyanga….


Wanawake Halamashauri ya Msalala Wilayani Kahama wametakiwa kuwa wabunifu na kujenga tabia ya kukimbilia fursa mbalimbali zinapojitokeza ambazo zitawasaidia kujinyanyua kiuchumi na kuepukana na tabia ya kuendelea kuwa wategemezi kwa wanaume.


Wito huo umetolewa na mgeni rasmi  ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Msalala Iddi Kassim Iddi wakati akizungumza kwenye tamasha la Mwanamke Mwekezaji ambalo limefanyika kwenye Kijiji cha Kakola Kata ya Bulyanhulu.


Mbunge Iddi amesema ni vyema kwa wakina mama wakatumia fursa zilizopo kwenye Halmashauri ya Msalala kwaajili ya kuinuka kiuchumi kwani tayari miradi mbalimbali imeendelea kuwekezwa na kwamba wao kama wanawake kupitia vikundi vyao wanaweza kunufaika na miradi hiyo mikubwa  ya kimakakati ikiwemo ya ujenzi wa Barabara pamoja na fedha za CSR ambazo zimekuwa zikitangaziwa tenda.


“Tulikuwa ziara Mkoani Mara tumeona mradi mkubwa wa mboga mboga na matunda tayari tumeongea na mgodi kuomba kupitia fedha za CSR tunakuwa na mashamba ambayo watapaitia vikundi ambavyo vitalima mbogamboga na matunda na kusambaza kwenye mgodi wetu wa Bulyanhulu pamoja na kwa makampuni yaliyomo ndani ya mgodi najua ukijiunga na kuanzisha vikundi mtakuwa wanufaika wakubwa wa mradi huu”Iddi Kassim Iddi Mbunge Jimbo la Msalala.


“Kuna mradi mkubwa wa ujenzi wa Barabara ya Kilomita 73 niwaombe wakina mama msibaki nyuma kuchukua tenda kwani ni mradi ambao utadumu kwa miaka miwili nitashangaa kuona wanawake wengine wanatoka maeneo tofauti na wanapatiwa tenda nyie nawaomba muwe mstari wa mbele kuomba tenda nia yangu nataka kuwaona wanawake wa msalala mnanyanyka kichumi”Iddi Kassim Iddi Mbunge jimbo la Msalala.


Aidha kwa upande Mwingine Mbunge Iddi amewaunga wanawake hao kiasi cha Sh,Milioni moja ambacho kitasaidia kutunisha mfuko wa kikundi huku akiwahahidi kufadhili tamasha hilo kwa mwezi wa nane liweze kuwakutanisha wanawake wengi zaidi ambao watapatiwa elimu namna bora ya matumizi ya fedha na utunzaji wa fedha na mbinu za kuanzisha vikundi.


“Nataka kuona baada ya kuwa mmefundishwa na wawezeshaji ambao mmewataka wakina Nanauka nataka kuona yale ambayo mmeyazungumza mnayafanyia utekelezaji hili tunapokutana tusiwe watu wa kupiga  porojo na kuachana na hapa nimetajiwa vikundi vinne najua kuna tatizo la ajira  sasa kupitia kikundi cha Women Talk Group tunaomba wakinamama watano ambao wanauwitaji tutawaomba wapatiwa ajira  na kampuni ya KASIPILIAN”Iddi Kassim Iddi Mbunge jimbo la Msalala.


Naye Mdau wa maendelo wa kata ya Bulyanhulu  Mapungo Paschal Mapungo amesema chanzo kikubwa cha kuwawezesha wanawake ni kutokana na jitihada zao ambazo wamekuwa wakizifanya katika kujitafutia kipato cha kila siku ambacho nia yao ni kuinua maisha yao






 


Jumla ya hati 8,325 zimesajliwa na kutolewa kwa wananchi waliofika kupata huduma katika Klinik za Ardhi mkoa wa Dar es Salaam.


Aidha, wananchi 18,224 wamefika katika klinik ya ardhi kupata huduma mbalimbali mkoani humo.

Hayo yamebainishwa tarehe 17 Machi 2024 na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Jerry Silaa wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi Maliasili na Utalii kukagua utekelezaji mradi wa uboreshaji Usalama wa Milki za ardhi (LTIP) katika mkoa wa Dar es Salaam.

Amsema, katika Klinik Hiyo migogoro mbalimbali imetatuliwa ikiwemo migogoro ya mipaka, mirathi, matumizi ya ardhi pamoja na migogoro ya umiliki wa ardhi.

Kwa mujibu wa Silaa, Serikali kupitia wizara ya ardhi imeendelea kuchukua hatua za makusdi ili kuhakikisha kuwa utoaji wa huduma za ardhi unaboreshwa kupitia mradi wa uboreshaji Usalama wa Milki za ardhi.

Amezitaja hatua zinazochukuliwa kuwa ni kuunda timu za wataalamu wa ardhi katika ngazi za mitaa kwa ajili ya kukwamua kazi za urasimishaji wa makazi katika maeneo yaliyopangwa pamoja na kuendesha Klinik za ardhi katika maeneo mbalimbali.

Hatua nyingine ni kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya ardhi kupitia vipindi vya redio na telebisheni, mikutano ya wananchi katika mitaa yao sambamba na kuunda timu za kushughulikia kero na migogoro ya ardhi.

Mhe, Silaa ameweka wazi kuwa, azma ya wizara yake ni kuendelea kufanya mageuzi kwenye sekta ya ardhi yanayolenga kuboresha huduma za ardhi kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Akielezea zaidi kuhusu Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP), Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema, mradi huo ni miongoni wa nyenzo muhimu zilizoonesha mafanikio makubwa katika kuongeza usawa wa kijinsia katika umiliki wa ardhi.

‘’Kati ya Hatimiliki 8325 zilizosajiliwa katika mkoa wa Dar es Salaam Hatimiliki 2,461 sawa na asilimia 29.6 no za wanawake’’ alisema Mhe, Silaa

Amefafanua kuwa, mradi huo wa uboreshaji milki za ardhi umewezesha kuongezeka kwa idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi nchini kutoka asilimia 25 hadi asilimia 41 huku idadi ya hati za pamoja baina ya wana ndoa zikiongezeka na kufikia asilimia 10 ya hati zilizotolewa.

Aidha, amesema Klinik za Ardhi zinazoendeshwa kupitia mradi wa LTIP zimekuwa jukwaa muhimu la kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa wanawake kumililki ardhi.

Kwa upande wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii kupitia Mwenyekiti wake Mhe, Timotheo Mzava mbali na kuridhishwa na utekelezaji mradi wa LTIP imeipongeza Wizara ya Ardhi kwa kazi nzuri ya kutekeleza miradi ya uboreshaji miliki za ardhi hususan katika klinik za ardhi.

‘’Mnafanya kazi nzuri na sisi kama kamati tunaridhika na kazi inayofanyika na ki ukweli ni kazi ni nzuri na tunataka iendeleee’’ alisema Mhe, Silaa

Aidha, Kamati imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anaayoifanya ikiwemo kuwezesha upatikanaji fedha za mradi wa LTIP ili kusaidia utatuzi wa changamoto katika sekta ya ardhi.

Aidha, amemtaka Waziri wa Ardhi kuijenga taasisi ili muelekeo alio nao uende mpaka kwa watumishi wa chini kwa kuwa haitatosha maono aliyo nayo kubaki kwa viongozi pekee. ‘’Huwezi kuwa kila mahali lazima kuwemo mfumo wa kitaasisi utakaoshuka mpaka kwa watendaji wa chini na wimbo uende mpaka ngazi za chini na likifanikiwa hilo tutakwenda vizuri sana’’. Alisema Mhe, Mzava

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii mbali na kukagua utekelezaji mradi wa uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) ilishiriki pia kwenye utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa wananchi wa eneo la Bunju Dar es Salaam.

 


NAIBU  Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi amemuagiza Meneja wa RUWASA  Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga,  kuhakikisha anapeleka huduma ya maji kwenye vitongoji ambavyo bado havina huduma ya maji.

Mhandisi Mahundi ametoa maagizo hayo leo Machi 17, 2024  akiwa katika muendelezo wa ziara ya kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Maji Mkoani Ruvuma 

Akiwa ziarani pia Mhandisi Mahundi ametoa rai kwa wananchi kuendelea kutunza vyanzo vya maji ili miradi ya maji iwe endelevu.

Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira  Mhe.Jackson Kiswaga ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa usimamizi na utekelezaji wa miradi. 

"Mradi huu ukamilike kwa wakati pia wananchi muweze kutunza Miundombinu yake ili mradi uwe endelevu. Lakini chombo cha watumiaji maji katika  jamii kiundwe ili kiweze kukusanya fedha na kufanya matumizi mazuri ya ukarabati wa mradi pindi  inapotokea mradi umeharibika"amesema Mhe.Kiswaga

Akitoa taarifa ya  utekelezaji wa mradi wa maji  Malungu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa Mhandisi  Masoud Samila amesema mradi wa  Malungu unatekelezwa  kwa gharama  ya Shilingi Bilioni 1.2 

Mhandisi  Samila amesema kukamilika kwa mradi huo kunalenga kuwanufaisha wananchi wapatao 9,659 kutoka vijiji vya Malungu na Tingi vilivyopo katika kata ya Tingi.

" Mradi pia utasaidia kupunguza magonjwa mbalimbali ya mlipuko kwa jamii. Vilevile kutokana na kuimarika kwa huduma ya maji, jamii itapata muda wa kufanya shughuli za maendeleo"amesema Mhandisi Samila