Siku zote nilijua ninataka kuwa mama. Nililelewa kwenye familia ya upendo, na ndoto yangu kubwa baada ya ndoa ilikuwa ni kulea mtoto wetu mwenyewe. Lakini mume wangu hakuwa na mtazamo huo.

Alinieleza mapema kabla ya ndoa kwamba kwa sasa hataki mtoto, na labda hata hana mpango wa kuwa mzazi kabisa. Nilidhani angetulia baada ya ndoa, lakini sikujua kwamba kauli hiyo ilikuwa ya kweli kabisa.

Tulipooana, mwaka wa kwanza ulipita na nilipojaribu kuleta mada ya mtoto, alikwepa. Mwaka wa pili, alikua mkali zaidi. Alisema wazi: “Mimi sitaki mtoto. Nisingependa kulea dunia hii ilivyo.” Maneno hayo yalinichoma.

Kila nikiona watoto wa rafiki zangu, kila ninapoona diaper kwenye duka, au baby shower kwenye Instagram, moyo wangu ulikua unazimia kwa ndani. Nilianza kuwa na huzuni isiyoisha.

Marafiki zangu walinijulisha kuwa huenda kuna jambo la ndani zaidi. Moja alinieleza: “Wanaume wengi wanaweza kubadilika, lakini kuna baadhi huwa wamefungwa kiroho wakiwa na sababu zisizoeleweka au mapingamizi ya maisha ya familia.” Akanishauri niwasiliane na watu walio na maarifa ya kusaidia kwenye masuala ya ndoa kiroho. Soma zaidi hapa.

 


Lengo ni Kuchochea Maendeleo, Usalama na Utunzaji wa Mazingira kwa Vizazi Vijavyo

Serikali kupitia Tume ya Madini imezindua mpango maalum wa “Uchimbaji Bora na Endelevu kwa Kizazi Kijacho”, unaolenga kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchimbaji madini nchini. Mpango huu unatoa fursa ya kuanzisha vikundi, kupata mikopo, pamoja na leseni za uchimbaji kwa lengo la kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika mafunzo kwa wachimbaji wadogo yaliyofanyika katika vijiji vya Utaho A na Isalanda, Kata ya Kituntu na Puma mkoani Singida, Mjiolojia kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Mutagwa, amebainisha kuwa mpango huo pia unalenga kuhakikisha kuwa shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa usalama na kuzingatia utunzaji wa mazingira.

“Uchimbaji salama ni msingi wa maendeleo. Tunawafundisha wachimbaji si tu kuhusu mbinu bora za uchimbaji, bali pia umuhimu wa kulipa kodi ya serikali kama vile mrabaha wa asilimia 4 kwa madini ya ujenzi,” amesema Mutagwa.

Aidha, amewaonya wanaojihusisha na ununuzi wa madini bila kulipa kodi, akisisitiza kuwa mfumo wa malipo ya kodi unapatikana kupitia POS katika ofisi za madini. 

Amesisitiza kuwa kila mchimbaji ana wajibu wa kutoa taarifa za ukwepaji kodi kwa mujibu wa Kifungu cha 87 cha Sheria ya Madini, Sura ya 23, ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Kwa upande wake, Mkaguzi wa Migodi na Baruti kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Eng. Lameck Maduhu, amesisitiza umuhimu wa usalama katika maeneo ya kazi.

“Fedha tunazopata zitakuwa hazina maana kama hatutajilinda. Ni lazima kuvaa vifaa kinga muda wote –  safety boots, kofia ngumu, suruali maalum na barakoa. Ndala hazihusiki kabisa kwenye machimbo,” ameeleza kwa msisitizo.

Ameongeza kuwa uchimbaji unaozingatia matumizi ya baruti unapaswa kufanywa kwa njia ya kitaalam na kwa uangalifu mkubwa ili kuzuia uharibifu wa mazingira, akihimiza wachimbaji kuacha tabia ya kukata na kuchoma miti kiholela.

Mchimbaji wa madini ya ujenzi kutoka Kijiji cha Utaho A, Jenifa Mtandu, ameishukuru Tume ya Madini kwa elimu waliyopewa, akisema imewapa maarifa ya kujilinda, umuhimu wa vikundi, na fursa za kupata mikopo kwa maendeleo ya shughuli zao.

“Mafunzo haya yametufungua macho. Tunajua sasa umuhimu wa leseni, kuwa na vikundi na mikopo. Tunaiona kesho yetu ikiwa salama zaidi,” amesema Mtandu kwa furaha.

Mpango huu umewezeshwa kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa lengo la kusaidia wachimbaji wadogo wa madini ya ujenzi hususan kokoto, ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya miundombinu, kuongeza kipato na kuchangia mapambano dhidi ya umasikini katika jamii.

Mpango huu unatarajiwa kuwa chachu ya mageuzi makubwa katika Sekta ya Madini nchini kwa kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa weledi, uadilifu, na kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.





Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira amewakumbusha watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo kushirikiana na Wanahabari ili wananchi waweze kufahamu mambo mbalimbali yahusuyo Uchaguzi.

  


Naitwa David, tangu nilipoanza kufanya kazi katika shirika ambalo ninafanya kazi sasa, sikuwahi kupata nafasi ya kumvutia Bosi wangu, alikuwa mtu mgumu sana, kwa hivyo wakati mwingine ilikuwa vigumu kwangu kuelewana naye.

Kwa bahati wale ambao alioelewana naye ndio waliopatana nafasi ya kupandishwa daraja au kupata nyongeza ya mshahara, nilihisi kwamba hakuniona hata kidogo licha ya kazi nzuri nilizokuwa nafanya.

Niliamua kuwa mfanyakazi bora kwa kwenda kazini mapema, kufanya kazi zaidi na kufanya kazi hata masaa ya ziada lakini baada ya miezi michache, alimpandisha daraja mtu mwingine na kuniambia kuwa bado sijafika hatua hiyo.

Nilijisikia vibaya sana baada ya kusema hivyo, nilifikiria kuacha kazi kwa sababu nilikuwa nimefanya kazi katika kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu. Soma zaidi hapa.

Ujumbe kutoka Benki ya Dunia wakiongozwa na Bi. Gemma Todd wamefika ADEM Bagamoyo kufanya ufuatiliaji wa namna mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa yanayoendeshwa kwa Maafisa Elimu Kata nchini yanavyoendeshwa.

Wataalamu hao pia wamepata fursa ya kufanya kikao Mkakati na Mtendaji Mkuu Dkt. Maulid J. Maulid ambapo wamejadiliana mambo muhimu kuhusu namna ADEM inavyoweza kunufaika na miradi kutoka Benki ya Dunia hususani uwezeshwaji katika eneo la Kuimarisha Miundombinu ya Mifumo ya TEHAMA itakayosaidia kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi mbalimbali wa elimu nchini.

Vilevile, Wataalamu hao wamepata fursa ya kuzungumza na washiriki wa mafunzo hayo wapatao 246 kutoka Mkoa wa Iringa na Singida na kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kufanya usimamizi fanisi wa shughuli za elimu katika maeneo yao ili kufanikisha malengo ya programu ya BOOST ya kuboresha utoaji elimu ya Awali na Msingi nchini.

 -Serikali kupunguza ada ya kodi ya pango kwa mwaka kwa Leseni ya chumvi


-Rais Samia apongezwa kwa kiwanda cha kusafisha chumvi Lindi

-Wazalishaji wa chumvi wafurahia kuanza kwa kodi ya zuio

-Serikali kudhibiti uingizaji wa chumvi kiholela nchini

Dar es Salaam

Katika kuwajengea uwezo wazalishaji wa chimvi nchini,Serikali imekuja na mikakati mbalimbali kufikia azma hiyo ikiwemo upunguzaji wa ada ya pango kwa mwaka ya leseni (Annual Rent) za uchimbaji mdogo wa chumvi nchini ili kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuchochea uzalishaji wa wingi wa chumvi nchini.

Hayo yamesemwa jana tarehe 15 Julai, 2025 na Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb) Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga Kikao cha wadau wa sekta ndogo ya chumvi chini ya Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA).

"Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutubeba sekta ya madini na wachimbaji kwa ujumla. Ni yeye aliyetuelekeza kusikiliza kilio chenu na kutatua changamoto zinazowakabili ili mnufaike na shughuli mnazofanya"

"Ametuelekeza Wizara ya Madini tuliridhie ombi lenu na kupunguza ada ya pango ya mwaka ya leseni ya uchimbaji mdogo kutoka Shilingi 45,000 mpaka Shilingi 20,000 kwa hekta, hili linakwenda kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ubora wa chumvi ya mzalishaji mdogo" alieleza Mhe. Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ikiwemo udhibiti wa chumvi inayoingizwa kutoka nje ya nchi, zimepelekea bei ya chumvi ghafi kuongezeka na hivyo kuwanufaisha zaidi wazalishaji wadogo wa chumvi nchini.

Uanzishwaji wa kodi ya zuio ya asilimia mbili (2%) kwenye mauzo ya chumvi ghafi kwa wazalishaji wenye leseni za PML imekuwa ni neema na manufaa kwao badala ya utaratibu wa awali wa kufanyiwa makadirio ya kodi ya mapato, ambao ulikuwa ni kero kubwa kwa wazalishaji wadogo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde alieleza kuwa Kiwanda cha kuzalisha chumvi cha STAMICO kipo hatua za mwisho, na kuagiza Shirika hilo kuhakikisha kabla ya mwezi wa Agosti kuisha kiwe kimekamilika na kuanza uzalishaji wa chumvi ili kupanua wigo wa soko la chumvi ya wazalishaji wadogo.

Awali, akitoa taarifa ya utendaji wa Taasisi yao, Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA), Bi. Hawa Ghasia aliishukuru Serikali kwa kushughulikia changamoto zilizokuwa zinaikabili sekta ndogo ya chumvi nchini ambazo zimepelekea bei ya chumvi kupanda na kuwanufaisha zaidi wazalisha chumvi nchini.



 




Airtel Tanzania leo imezindua rasmi huduma ya Airtel Chapakazi, suluhusho jipya lililoundwa kuchochea ukuaji wa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo kote nchini. Uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika Makao makuu ya Airtel Tanzania jijini Dar es Salaam, ulionyesha dhamira ya Airtel katika kukuza maendeleo jumuishi ya kidijitali na kuunga mkono ajenda ya kukuza uchumi wa Tanzania.

Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kulingana na takwimu za kitaifa, asilimia 15 tu ya biashara ndogo ndogo na za kati nchini Tanzania kwa sasa zinapata zana rasmi za masoko ya kidijitali, pengo ambalo Airtel Chapakazi inalenga kuziba. Airtel Chapakazi ni suluhisho la kibunifu linaloenda kuwapa wafanyabiashara wadogo uwezo sawa wa kidijitali unaotumiwa na makampuni makubwa.

Huduma ya Airtel Chapakazi inapatikana katika vifurushi vitano (05) vilivyoundwa kulingana na ukubwa na mahitaji na utofauti wa biashara:

● SME chap pack (TZS 100,000): Inajumuisha laini 2 za simu, kila moja ikiwa na GB10 ya data, SMS 1,000, na dakika 1,000 kwa mitandao yote. Pia kifurushi hiki kinajumuisha router ya intaneti ya bure kwa ajili ya matumizi ya ofisi yenye kasi ya 10 Mbps

● Kifurushi cha SME Bomba (TZS 150,000): Inajumuisha laini 3 za simu, kila moja ikiwa na 10GB ya data, SMS 1,000, na dakika 1,000 kwa mitandao yote. Pia kifurushi hiki kinajumuisha router ya intaneti ya bure kwa ajili ya matumizi ya ofisi yenye kasi ya 20 Mbps.

● Fahari Pack (TZS 200,000): Inajumuisha laini 5 za simu, kila moja ikiwa na 10GB ya data, SMS 1,000, na dakika 1,000 kwa mitandao yote. Pia kifurushi hiki kinajumuisha router ya intaneti ya bure kwa ajili ya matumizi ya ofisi yenye kasi ya Mbps 30 na SMS 5,000.

● Supa Pack (TZS 300,000): Inatoa laini 9 za simu zenye data sawa, SMS, na manufaa ya sauti, router ya ofisi ya bure ya Mbps 30, na SMS 10,000 kwa wingi.

● Max Pack (TZS 400,000): Inatoa laini 14 za simu, router ya ofisi ya bure yenye kasi ya Mbps 50, na SMS 15,000 — zinazofaa kwa timu kubwa yenye watu wengi au yenye ukuaji wa kasi ya juu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Tanzania, Joseph Muhere, alisema Airtel Chapakazi inadhihirisha dhamira ya Airtel kusaidia biashara ndogo ndogo na za kati kupitia huduma suluhishi za kidijitali.

"Kwa kutumia Airtel Chapakazi, wateja watapata msaada wa karibu kutoka kwa mawakala wetu kuanzia hatua ya mwanzo hadi kupakua programu kutoka Play Store. Baada ya taarifa hizo kuthibitishwa, mteja atapokea ujumbe mfupi wa kiunganishi wa kupakua programu ya Airtel Chapakazi kutoka Play Store, mteja atapakua programu hiyo, kuchagua kifurushi: Fahari, Supa, au Max, na kukamilisha malipo ili kuwezesha huduma.” Alieleza Muhere.

Muhere alisisitiza juu ya umuhimu wa biashara ndogo ndogo na za kati katika uchumi wa Tanzania, akibainisha kuwa kundi hilo la wafanyabiashara wajasiriamali linashikilia zaidi ya asilimia 95 ya biashara zote, limeajiri zaidi ya watu milioni 8, na linachangia takriban asilimia 35 kwenye Pato la Taifa, ilhali wengi bado hawajafikiwa na zana za kijiditali ambazo zinaweza kukuza biashara zao kwa kiasi kikubwa.

"Kwa kipindi kirefu, Airtel Tanzania ilikuwa na dhamira ya kuanzisha suluhisho la kidijitali ambalo litaboresha sekta ya biashara na kuchangia katika kukuza uchumi wa nchi na sasa ndoto hiyo imetimia kwa kupitia Airtel Chapakazi," aliongeza Muhere.

Uzinduzi wa Airtel Chapakazi ni sehemu ya dhamira kubwa ya Airtel Tanzania katika kukuza maendeleo jumuishi, yanayoendeshwa na teknolojia nchini kote kwa kuwapa wafanyabiashara wanazohitaji ili kustawi katika zama za kidijitali.
Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Joseph Muhere (katikati), akizungumza na waadishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya Airtel Chapakazi jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kushoto ni Mkuu wa Huduma za Wajasiriamali, Bw. Charles Banduka na Meneja Mahusiano wa Kampuni hiyo, Bw. Jackson Mmbando.Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzani, Bw. Jackson Mmbando (kulia), akizungumza na waadishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya Airtel Chapakazi jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kushoto ni Mkuu wa Huduma za Wajasiriamali, Bw. Charles Banduka na Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel, Bw. Joseph Muhere.
Mkuu wa Huduma za Wajasiriamali wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Banduka (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati wa uzinduzi wa huduma ya Airtel Chapakazi jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kushoto kwake Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel, Bw. Joseph Muhere na Meneja Mahusiano wa kampuni hiyo, Bw. Jackson Mbando.

 

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula( kulia) akimsikiliza mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya St. Joseph akielezea kuhusu ubunifu wa ndege nyuki (drone) yenye uwezo wa kupanda mbegu shambani kwa kutumia mfumo wa kisasa unaopima ukubwa wa shamba na kusambaza mbegu kwa usahihi na haraka wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela Julai 16,2025.

Na.Mwandishi Wetu_Arusha 

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imeadhimisha Wiki ya Ubunifu kwa lengo la kuendeleza maono ya Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela, aliyetamani bara la Afrika lijitegemee kielimu na kiteknolojia kwa kuzalisha wataalamu wake wa ndani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo Julai 16,2025 katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo, Makamu Mkuu wa Taasisi hiyo, Profesa Maulilio Kipanyula, alisema Wiki ya Ubunifu inalenga kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa sayansi, uhandisi, teknolojia na ubunifu kama nguzo kuu za maendeleo ya kweli.

“Maendeleo hayawezi kupatikana bila sayansi na teknolojia. Tumejikita pia katika matumizi ya sayansi shirikishi, hasa akili bandia (AI), kama sehemu ya kukuza maarifa ya vijana wetu,” alisema Prof. Kipanyula.

Shughuli hiyo imeambatana na mihadhara ya kitaalamu kutoka kwa wazungumzaji wa kitaifa na kimataifa, pamoja na maonesho ya bunifu kutoka kwa wanafunzi wa shule za sekondari na vyuo vya ufundi. Kila kundi lilipewa nafasi kuonesha vipaji vyao kupitia uvumbuzi unaolenga kutatua changamoto za kijamii.

Miongoni mwa bunifu zilizovutia wengi ni drone iliyoundwa na wanafunzi wa shule ya sekondari ya St. Joseph, ambayo ina uwezo wa kupanda mbegu shambani kwa kutumia mfumo wa kisasa unaopima ukubwa wa shamba na kusambaza mbegu kwa usahihi na haraka.

“Nimefurahishwa sana na ubunifu huu. Teknolojia hii ni msaada mkubwa kwa wakulima wetu kwani inapunguza gharama, muda, na upotevu wa mbegu. Ni aina ya bunifu zinazofaa kuendelezwa,” aliongeza Prof. Kipanyula.

Kwa upande wake, Naibu Makamu Mkuu wa Taasisi anayeshughulika na Taaluma, Utafiti na Ubunifu, Prof. Anthony Mshandete, alisema taasisi hiyo inaendelea kuibua vipaji kuanzia shule za sekondari hadi vyuo vikuu kwa lengo la kukuza teknolojia zinazoibuka na kuliletea taifa maendeleo.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mandela Wiki, Prof. Linus Munishi, alisema wiki ya ubunifu imehusisha wadau kutoka ngazi mbalimbali kuanzia shule za sekondari, vyuo vya kati na vikuu, hadi mashirika ya umma, sekta binafsi, wajasiriamali na viwanda.

“Tunapenda kuona kizazi cha ubunifu kinaanza kuibuliwa mapema kabisa, ndiyo maana tumeshirikisha hata shule za awali na zile zilizoko karibu na taasisi,” alieleza Prof. Munishi.

Maadhimisho hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kukuza mawazo mapya na kushirikisha jamii katika safari ya mabadiliko ya kiteknolojia, kwa kuzingatia dira ya Hayati Nelson Mandela ya Afrika yenye kujitegemea kielimu na kisayansi.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula akizungumza na wanafunzi, wabunifu na wasayansi wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela Julai 16,2025.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula( kulia) akimsikiliza Dkt Esther Kimaro ( kushoto) akielezea kuhusu miradi ya ushirikishwaji wa jamii kwa ajili ya usimamizi endelevu wa magonjwa ya mifugo katika jamii za wafugaji wakatinwa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela Julai 16,2025.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula( kulia) akimsikiliza mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya St. Joseph akielezea kuhusu ubunifu wa ndege nyuki (drone) yenye uwezo wa kupanda mbegu shambani kwa kutumia mfumo wa kisasa unaopima ukubwa wa shamba na kusambaza mbegu kwa usahihi na haraka wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela Julai 16,2025.

  

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula akitembelea wabunifu mbalimbali walikuwa wakionyesha bunifu na Teknolojia ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela julai 16,2025.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula( kushoto ) akipokea zawadi kutoka kwa waalimu shule ya Sekondari ya Shepherd wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela Julai 16,2025.

   

Wahudhuriaji wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu ya Nelson Mandela ikiwa ni wiki ya kuonyesha ubunifu katika masuala ya sayansi na teknolojia kwa lengo la kumbukizi ya aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini Hayati Nelson Mandela inayoadhimishwa katika wiki ya kuazimishwa siku yake ya kuzaliwa na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela.

 


📌Wananchi wampongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mafanikio ya ujenzi wa Mradi, wafikia asilimia 64.2

📌 Timu ya wataalamu wa SULUHU wakutana na Uongozi wa Mkoa wa Tanga, kueleza mafanikio ya mradi

📌 Ajira kwa wazawa kipaumbele cha mradi kwa asilimia 80

📌Mradi  watumia Bilioni 10.4 kulipa fidia kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga


Na Neema Mbuja, Tanga

Wananchi waishio kwenye vijiji vinavyopakana na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki, EACOP wamesema Serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa ya kubadili maisha ya wananchi kiuchumi kupitia mradi wa bomba la EACOP kwa kufungua fursa za kiuchumi kwenye maeneo hayo.

Wananchi hao wameyasema hayo leo 16 Julai, 2025 kwa nyakati tofauti wakati walipokuwa wakielezea mafanikio ya utekelezaji wa mradi huo na kueleza namna ambavyo maisha ya mtu mmojammoja wamefanikiwa kufuatia uwepo wa mradi wa EACOP.  

“ Sijawahi kuona mradi ambao umetoa manufaa makubwa ya kiuchumi na kubadili naisha ya wananchi wake kama huu wa EACOP na tunaishukuri sana Serikali ya Tanzania kukubali mradi huu kutekeleza” Alisema Bw. Loita Naftali mkazi wa kata ya Chongoleani

Amesema licha ya kujengewa nyumba, kupatiwa fedha za kujikimu kiasi cha shilingi 500,000 kwa mwezi,  bado walipatiwa elimu ya ujasiriamali, Kilimo na ufugaji wa kisasa ili kuinua hali ya uchumi.

Naye, Kassim Mwavezo Mbega amesema tangu kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki EACOP mkoa wa Tanga umeimarika kiuchumi na mzunguko wa fedha kuwa mkubwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali na kuongeza kuwa kwa sasa wimbi la ujenzi wa nyumba za wageni na za binafsi pamoja na taasisi za fedha umekuwa mkubwa kutokana na mkoa kupokea wageni wengi wa mradi wa EACOP. 

Kwa upande wake, Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa EACOP kutoka TPDC Asiadi Mrutu amesema wakati wa zoezi la awali la kuwafidia wananchi hao Mradi ulitekeleza  mpango maalumu chini ya taratibu za Kimataifa  wenye lengo la  kuwapatia elimu ya ujasirimali na kuendeleza kilimo na ufugaji wa kisasa ili wajiendeshe kibiashara sambamba na elimu ya utunzaji wa fedha.

Amesema kupitia programu hii, imeboresha sana maisha yao na familia zao sambamba na upatikanaji wa ajira kwa wananchi wanaozunguka eneo la mradi. 

Awali kabla ya kuzungumza na wananchi wanufaika wa mradi wa EACOP timu ya wataalamu kutoka Wizara ya Nishati,na TPDC ,na TBC  kwa ajili ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa EACOP na mafanikio yaliyopatikana kwa Serikali ya awamu ya sita, ilifika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga na kupokelewa na Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Tanga Bi Amina Kibunde Said na kuieleza timu hiyo kuwa mradi wa EACOP ni miongoni mwa miradi ya kimkakati na yq mfqno kitekelezwa hapa nchini kutokana na uwazi wa uendeshaji wa mradi huo.

Amesema uchumi wa Mkoa wa Tanga kwenye Wilaya zake 6 zinazopitiwa na mradi huo zimenufaika pia na miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo maji, umeme na wananchi mmojammoja. na kuishukuru Serikali kwa kazi nzuri inayofanya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

“ Niahidi kuwa mkoa utaendelea kutoa ushirikiano kwenye utekelezaji wa mradi huu kwani viijana wengi wamenufaika na mradi wa EACOP kwa kiasi kikubwa “ Alisema Bi. Amina

Amewashukuru Wizara ya Nishati kupitia TPDC kwa kuhakikisha wananchi wote wanafidiwa isipokuwa kwa wale 12 ambao wana changamoto binafsi ikiwemo za kifamilia na mirathi ambapo jumla ya shilingi Bilioni 10.4 zimetumika kulipa fidia sawa na asilimia 99.3.











Uongozi thabiti na wenye mwelekeo wa pamoja ni nguzo kuu katika utendaji na utekelezaji wenye tija katika katika kufanikisha malengo mapana ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 16 Julai, 2025 katika mafunzo maalum kwa Viongozi wa Wizara hiyo yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha, Mkoani Pwani.

Akifungua mafunzo hayo Naibu Katibu Mkuu anaeshughulikia Sayansi Teknolojia na Elimu ya Juu Prof. Daniel Mushi amesema malengo makuu ya mafunzo ni kukuza uwezo wa kiungozi na utawala, kujenga mshikamano, kujenga misingi ya utendaji katika mwaka mpya wa fedha ulioanza ili kuongeza tija katika kufikia malengo ya kutekeleza mageuzi ya elimu na malengo ya kitaifa ya kuhakikisha kila mtoto anapata Elimu na ujuzi.