Ikiwa ni hatua ya kuwaongezea watanzania wigo wa uwekaji akiba na uwekezaji kupitia ununuzi wa dhahabu, Serikali ipo mbioni kuanzisha uuzaji wa Sarafu ya dhahabu nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 17 Mei, 2025 na Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb) akiwa Mkoani Geita aliposhiriki katika uzinduzi wa tawi la benki ya Stanbic Geita.

"Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Dkt. Samia S. Hassan amefanya makubwa katika sekta yetu ya madini, na ndiyo maana tumeweza kuchangia katika pato la Taifa kufikia asilimia 10.1 kwa mwaka 2024, mwaka mmoja kabla ya mwaka 2025 kama ilivyokuwa imeelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi na Mpango wa Maendeleo wa miaka 5.

Wizara kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzanania(BOT) tunajadiliana namna bora  ya uanzishwaji wa Sarafu za dhahabu(𝙜𝙤𝙡𝙙 𝙘𝙤𝙞𝙣𝙨) ili kuongeza umiliki wa dhahabu miongoni mwa wananchi, kuimarisha soko la ndani la dhahabu na mzunguko wa fedha ndani ya nchi yetu.

Hatua hiyo ya uanzishwaji wa uuzaji wa Sarafu ya dhahabu ni sehemu ya maboresho ya mpango wa ununuzi wa dhahabu kupitia Benki Kuu ya Tanzania ili kufikia malengo tarajiwa ya kuwa na ununuzi wa dhahabu endelevu na wenye tija nchini.

Nawapongeza Benki ya STANBIC kwa kusogeza huduma  rafiki ya kibenki kwa wananchi wa Geita hususani wadau wa madini na hivyo kuzitaka Benki nyingine kuiangalia sekta ya madini kwa upekee ili kuwezesha mitaji kwa watanzania ili washiriki katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini, kwani sekta hiyo ina utofauti mkubwa na sekta nyingine za uzalishaji nchini” Alisema Mavunde

Awali, akitoa maelezo kuhusu uanzishwaji wa Tawi hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Stanbic, Bw. Fredrick Maxi aliishukuru Serikali kwa kuweka mazingira mazuri ya biashara na kubainisha kuwa Benki ya Stanbic kwa sasa ina matawi 15 nchini na inaendelea kufungua matawi mengine mengi kwenye maeneo ya uchimbaji ili kuwafikia wadau wengi zaidi kwenye sekta ya madini,na pia Benki inakuja na mpango maalum wa kutoa riba ndogo isiyo ya kibiashara kwa sekta ya madini ili kuchochea shughuli za madini nchini ambapo kwa sasa wachimbaji wadogo wanaweza kuchukua mikopo isiyozidi Tsh 115,000,000 bila kuwa na dhamana.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mh. Martin Shigela aliishukuru benki ya Stanbic kwa kuleta Tawi Mkoani Geita na kusisitiza kwamba, ni matokeo ya kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwezesha sekta za uzalishaji zinazochochea ukuaji wa biashara na kuzifanya benki za biashara kuchangamkia fursa zinazoendelea kuibuka mkoani hapo na kuwataka wananchi wa Geita kuchangamkia huduma zitolewazo na taasisi hizo za fedha katika kujiimarisha kimtaji.










 


Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA kupitia Mradi wa HEET wamehitimisha Mafunzo ya siku tatu ya kujenga uelewa wa mradi huo kwa watumishi wa ajira mpya kada za Taaluma na Utawala yaliyofanyika katika Jengo la Ofisi ya Atomic Energy Commission Njiro jijini Arusha

Akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Kitivo cha Biashara IAA Dkt. Martin Dome ameushukuru uongozi wa Chuo Pamoja na Mradi wa HEET kwa kufanikisha mafunzo hayo ambayo yatawawezesha watumishi hao wapya kupata muongozo wa utendaji kazi wao huku wakizingatia maalidi

Dkt.Dome amewataka watumishi hao kuyatumia vyema mafunzo na kuhakikisha wanakuwa wazalendo, watunzaji wazuri wa nyaraka za serikali, Pamoja na kuzingatia mifumo ya sheria zinazowaongoza wakiwa kazini

“Hakikisheni mnaenda kufanya kazi kwa kuzingatia maadili kwani itakuwa nyenzo muhumu na itapekekea kuipa sifa nzuri taasisi kutokana na ubora mtakaouonyesha mkiwa mnatekeleza majukumu yenu” amesema Dkt. Dome

Nae Afisa Takukuru Mkoa wa Arusha Gipson Isaya amesema utumishi wa umma ni dhamana hivyo amewahasa watumishi hao kuhakikisha wanaisaidia serikali kutoa huduma kwa wananchi bila la kujihusisha na masuala ya rushwa kwani ni hatari kwao na kwa taifa kwa ujumla

Chrispina Ntanga Mkufunzi msaidizi IAA kampasi ya Dar es salaam ni moja ya watumishi walioshiriki mafunzo, amesema elimu aliyoipata inaenda kumsaidia kufanya kazi kwa kuzingatia maadili Pamoja na kuendelea kupinga suala la rushwa kama mtumishi wa umma

Mafunzo haya yamefanyika kwa siku tatu na kuhudhuriwa na wadau kutoka taasisi mbalimbali waliohusika kutoa mafunzo, na mwisho washiriki ambao ni watumishi wapya IAA wamekula kiapo cha uadilifu kwa watumishi wa umma.

















WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ameagiza kupelekewa taarifa kamili za wasimamizi na mshauri mwelekezi wa ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) Awamu ya Nne baada ya kushuhudia uzembe unaosababisha usumbufu zaidi barabarani kinyume na malengo ya mradi huo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kufanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi huo unaotoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuelekea Mwenge hadi Tegeta, sambamba na tawi la kutoka Mwenge hadi Ubungo, Ulega alieleza kushangazwa na jinsi wasimamizi na mshauri mwelekezi wa mradi huo wanavyoonekana kufumbia macho uzembe huo.

Mojawapo ya maeneo ambayo yalimkera waziri huyo jana ilikuwa ni katika eneo la Palm Beach, Upanga ambako alikuta shimo kubwa limechimbwa na mkandarasi, pasipo kukamilisha kwanza kazi ya muhimu zaidi katika maeneo ya awali kutoka Morocco hadi Mwenge hadi Kaunda.

“Mimi nimepita kukagua. Kazi ambazo nimeaminiwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni za barabara na madaraja. Rais hapendi na hafurahishwi na msongamano mkubwa hapa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini. Hisia hizo hajawahi kuzificha,” alisema Waziri Ulega.

Ameongeza kuwa alipohoji sababu ya kuchimba eneo jipya kabla ya kukamilisha maeneo ya awali, alielezwa kuwa ni mkandarasi huyo huyo ambaye bado hajamaliza kazi sehemu ya mwanzo.

“Nini kimemfanya awe na haraka ya kuja kutifua huku wakati kule hajakamilisha? Hii ndiyo hoja yangu na ugomvi wangu hapa,” alisema.

Waziri Ulega amesema amebaini tatizo kubwa liko kwa upande wa wasimamizi wa mradi pamoja na Mshauri Elekezi. 

“Hii ni barabara ya umma, si mali ya mkandarasi. Mkandarasi hawezi kuvamia na kuchimba kiholela. Hapa shida si mkandarasi peke yake, ni wasimamizi na mshauri elekezi,” alisema kwa msisitizo.













 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa rai kwa Benki Kuu pamoja na Umoja wa Mabaneki Tanzania (TBA) kupitia sheria na kanuni zinazosimamia sekta ya fedha kimataifa na kiinchi ili kulinda na kuepuka hatari ya kupoteza rasilimali.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Maadhimisho ya Miaka 30 ya Benki ya CRDB pamoja Semina ya Wanahisa wa Benki hiyo inayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). Amesema matumizi makubwa ya teknolojia yanaondoa mipaka ya kijiografia na hivyo kuunganisha huduma za fedha duniani hivyo ni muhimu kuwepo na menejimenti ya vihatarishi na hitaji la kuzingatia kanuni za kifedha za kimataifa.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa Benki ya CRDB kuweka mkazo zaidi katika udhibiti wa tishio la uhalifu wa kimtandao ili kujenga imani ya wateja na kulinda heshima ya benki hiyo. Amesema Benki ya CRDB haina budi kujihami mapema na wakati wowote kwa sababu, kukua kwa matumizi ya teknolojia kumeleta wimbi la matukio ya uhalifu wa kimtandao unaohatarisha mitaji ya benki duniani na kuongeza gharama za kukabiliana nao.

Aidha Makamu wa Rais amesema ni vema kuendelea kufanya mageuzi ya kiteknolojia kwa kuongeza matumizi ya huduma za kimtandao ili kuongeza ufanisi, usalama, na ushindani.  Amewasihi kufanya ushirikiano  na wadau wa teknolojia ya fedha ili kubuni bidhaa na huduma zenye ubora. Amesema kuwekeza kwenye Teknolojia kutapunguza gharama za uendeshaji, kuwafikia wateja wengi zaidi kwa muda mfupi hususan walio vijijini na maeneo yasiyo na matawi na kwa watu wenye kipato cha chini au wasioweza kufungua akaunti za kawaida.

Katika kulinda mazingira, Makamu wa Rais ametoa rai kwa mabenki kuangalia uwezekano wa kuunganisha nguvu kwa kuwa na miradi ya pamoja na Taasisi nyingine za fedha, ili kupata kiwango kikubwa zaidi cha fedha na kuziba pengo la ufadhili wa miradi ya mazingira ambalo bado ni kubwa mno. 

Makamu wa Rais amesema Serikali imejizatiti kuhakikisha kuwa sekta ya fedha inaendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi. Amesema Serikali imeboresha sera na kuweka mifumo madhubuti, imejenga miundombinu wezesha na imeendelea kukuza uchumi wa nchi na kipato cha wananchi.

Ameongeza kwamba, Serikali ilipitisha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ili kuweka msingi imara wa kisheria kwa uendeshaji wa benki na taasisi nyingine za kifedha nchini. Kadhalika, Serikali imetengeneza sera mbalimbali zikiwemo,  Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2000,  Mpango wa Taifa wa Huduma  Jumuishi za Fedha  (Awamu ya Kwanza 2014-2016, Awamu ya Pili 2018-2022 na Awamu ya Tatu 2023-2028), Mpango wa Taifa wa Elimu ya Fedha (2016-2020), Programu ya Kutoa Elimu ya Fedha kwa Umma (2021/22 – 2025/26),  Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha  ya mwaka 2017, Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha (2020/21 -2029/30) pamoja  na Sheria ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018. 

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali imepokea kwa furaha ujenzi wa shule ya sekondari ya mfano itakayojengwa na Benki ya CRDB katika Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam ambayo pamoja na ubora wa miundombinu ya ufundishaji inayotarajiwa kuwa dira kwa shule zingine za umma na binafsi. Amesema zawadi hiyo ni ya kipekee kutoka kwa benki kwenda kwa jamii. 

Prof. Mkenda ameihakikishia Benki ya CRDB kwamba Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itaendelea kushirikiana kwa karibu na benki hiyo kwa maslahi ya Taifa na kwa maendeleo ya Elimu kwa mustakabali wa vizazi vya sasa na vijavyo.  

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt. Ally Laay ameishukuru Serikali, wadau, wanahisa, wateja, washirika kwa kuendelea kuiamini Benki ya CRDB na kushirikiana katika kipindi cha miaka 30. Amesema miaka 30 iliyopita imekuwa na mafanikio makubwa na wanatarajia kuifikisha banki hiyo katika viwango vya juu zaidi.

Dkt. Laay amesema Benki ya CRDB itaendelea kuwa mshiriki namba moja wa maendeleo kwa Serikali, wadau wa maendeleo pamoja na wateja wote. 

Awali akitoa taarifa ya historia na maendeleo ya Benki ya CRDB, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Abdulmajid Nsekela amesema katika kipindi cha miaka 30 Beki hiyo imefanya mageuzi makubwa na kuwa benki mwanzilishi wa huduma mbalimbali za kifedha nchini. Ameongeza kwamba Benki imeendelea kubuni huduma mahususi kwa makundi mbalimbali kwa kuzingatia idadi kubwa ya wanawake na vijana ambao wapo katika sekta isiyo rasmi. 

Nsekela amesema Benki hiyo inajivunia kuwa mstari wa mbele katika utekelezaji wa sera za mazingira, jamii na utawala bora. Amesema mwaka 2019 ilikuwa Benki ya kwanza Afrika mashariki na kati kusahiliwa na shirika kubwa duniani la mazingira la GCF na kupewa daraja la kati kusimamia miradi yenye kiwango cha zaidi ya dola milioni 200.





Na Mwandishi Wetu-Dodoma

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kuhamasisha watanzania kuwa na desturi ya kujenga miundombinu na kuvuna maji ya mvua kwa kila msimu wa mvua ili kuwa na uhakika wa maji kwa kipindi cha mwaka mzima hususani kipindi cha kiangazi.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt James Andilie amesema hamasa hiyo inalenga kuwafanya wananchi kuona umuhimu wa kuvuna maji ya mvua ambayo yanaweza kutumiwa kumwagilia mimea, kunywesha wanyama na watu.

“Uvunaji wa maji ya mvua ni mbinu ambayo inazuia maji ya mvua kutiririka hovyo, badala yake tunaweza kuyakusanya na kuyahifadhi kwa matumizi mbalimbali”. Alisisitiza.
EWURA hudhibiti mamlaka za majisafi na usafi wa mazingira nchini ambapo moja ya jukumu lake ni kuhakikisha zinaimarisha hali ya uzalishaji na usambazaji wa maji nchini ikiwa ni pamoja kusimamia utekelezaji wa mikakati na miongozo mbalimbali ya kuboresha huduma .

Vilevile, Dk. Andilile amesisitiza kuwa, uvunaji wa maji ya mvua unaweza kuleta uhakika wa maji na kuwa chanzo mbadala cha maji kwa mamlaka. EWURA ilianza kuhamasisha uvunaji maji ya mvua Mei, 2023.

Mwekezaji Wa sekta ya usafirishaji jijini Arusha Patrick Petro mulokozi amelalamikia Jeshi la Polisi Mkoa Wa Arusha kushindwa kumpa ushirikiano Wa kufungua mashitaka ili apate Mali zake ambazo ni mabasi mawili aina ya costa aliyekuwa ameyakodisha kwa kampuni ya Impala shato  inayofanya usafirisha wa abiria na mizigo kwenda nchi jirani 

‎Kijana Patrick anaeleza kuwa amesumbuka kwa zaidi ya mwaka mmoja kwenye kituo Cha polisi Cha Cental Arusha kufungua mashitaka lakin Kila alipoenda alichukuliwa maelezo na hakuna chochote kilichoendelea ikiwa nipamoja na upelelezi kufanyika na watuhumiwa wake kukamatwa

‎Hakuishia hapo Patrickanaeleza kuwa kuna baadhi ya maafisa Wa NGAZI za juu Wa Jeshi la Polisi na wasaidizi Wa ofisi ya mkuu Wa mkoa aliwaomba msaada katika kupa Mali zake  na Kila walipotaka kumsaidia walimweleeza walipigiwa kutoka ngazi za juu na kuwaeeleza waachane na swala Hilo 

‎Patrick ameeleza kuwa mtu anamlalamikia kuchukua mabasi yake bwana Edimundi Koka ni Mdogo Wake na Mbunge Wa Jimbo la Kibaha Silvester Koka ambae kaka yake huyo anatumia nafasi yake ya ubunge kuwapigia viongozi wakubwa simu na yeye kukandamizwa asipatiwe haki yake 

‎Patrick anamuomba Rais Dkt Samia na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda wamsaidie kupata haki yake 

‎Juhudi za kumpata anae lalamikiwa zimefanyika ikiwa ni pamoja na Kufika Ofisini kwake na baada ya Kufika na kuwaona waandishi Wa Habari alikataa Kuzungumza chochote na kumuagiza mtoto wake kueleza hajupo tayari Kuzungumza na waondoke 

Juhudi ya kulipata Jeshi la Polisi ziligonga mwamba huku msaidizi Wa Kamanda Wa polisi Mkoa wa Arusha aliyepokea simu alieleza kuwa  Kamanda yupo bize kwenye misafara ya viongozi iliyopo Mkoani Arusha

 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Namibia Mhe  Caesar Chacha Waitara, amemwakilisha Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso (Mb), Waziri wa Maji katika Mkutano wa 12 wa Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (Zambezi Watercourse Commission-ZAMCOM) uliofanyika tarehe 15 Mei 2025 jijini Windhoek, Namibia.

Katika mkutano huo wa ZAMCOM unaojumuisha nchi nane za Tanzania, Angola, Botswana, Malawi, Msumbiji, Namibia, Zambia na Zimbabwe, Waziri wa Maji, Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso (Mb) amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa ZAMCOM katika kipindi cha mwaka 2025/2026.