Articles by "Habari"
Showing posts with label Habari. Show all posts

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela ameendelea na ziara zake katika baadhi ya matawi ya jijini Dar es Salaam kukutana na wateja ikiwa ni siku chache baada ya Benki kukamilisha maboresho makubwa ya mfumo wake mkuu wa utoaji huduma (Core Banking System).

Akiwa katika tawi la CRDB TPA lililopo katika jengo la Bandari jijini Dar es Salaam alikozungumza na mameneja wa matawi ya Kanda ya Dar es Salaam na Pwani pamoja na wanahabari, Nsekela alipata fursa pia ya kuzungumza na wateja waliokuwa wakihudumiwa. Aliwashukuru wateja kwa ushirikiano na uvumilivu wao katika kipindi cha mabadiliko huku akiwahakikishia kuwa huduma za Benki zinaendelea kuimarika kila siku tangu kuanza kutumika kwa mfumo mpya.

“Kuanzia tarehe 8 Septemba tulihamia kwenye mfumo mkuu wa utoaji huduma za benki ambapo, kwa ukubwa wa mabadiliko yaliyofanyika, baadhi ya wateja wetu walipata changamoto katika akaunti zao na baadhi ya miamala kutofanikiwa. Juhudi za wataalamu wetu zimefanyika usiku na mchana, na hadi jana akaunti zilizokuwa na changamoto zilirudi katika hali yake ya kawaida. Aidha, wateja ambao miamala yao ilikwama walirudishiwa fedha katika akaunti zao na miamala kuendelea kufanyika kwa ufanisi,” amesema Nsekela.

Aidha, Nsekela amebainisha kuwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika mfumo huu mpya umezingatia mahitaji ya sasa na ya baadaye ya wateja, na mabadiliko hayo yametekelezwa katika nchi zote ambako Benki ya CRDB inafanya biashara yaani Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) - huduma zinaendelea vizuri. Vilevile, ameongeza kuwa mageuzi hayo yanaweka msingi wa Benki kujitanua kimataifa, ambapo hivi karibuni Benki ya CRDB imepata leseni ya kuanzisha ofisi Dubai.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa pamoja na mabadiliko yaliyotokea, Benki bado imeendelea kufanya vizuri kibiashara ikithibitisha imani kubwa ya wateja waliyonayo kwa Benki yao. Vilevile ametumia fursa hiyo kuwashukuru wafanyakazi wote kwa kujitoa kwao katika kipindi hiki cha mabadiliko na akawahimiza kuendelea kusimamia weledi katika utoaji huduma ili kuhakikisha mfumo mpya unaleta matokeo yaliyokusudiwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela (kushoto) akihudumia na kupokea maoni ya wateja kuhusu maboresho ya mfumo mkuu wa uendeshaji wa huduma yaliyofanyika hivi karibuni katika tawi la Benki ya CRDB TPA lililopo katika Jengo la bandari jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) akiangalia namna huduma zinavyotolewa kwa wateja kupitia mfumo mkuu wa uendeshaji wa huduma ulioanza kutumika hivi karibuni. Amefanya ukaguzi huo katika tawi la Benki ya CRDB TPA lililopo katika Jengo la bandari jijini Dar es Salaam alikotembelea kusikiliza na kupokea maoni ya wateja kuhusu maboresho ya yaliyofanyika hivi karibuni.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) akimsikiliza Lella Mushi, mmoja wa mawakala wanaotoa huduma za Benki ya CRDB alipomkuta katika tawi la Benki ya CRDB TPA lililopo katika Jengo la bandari jijini Dar es Salaam alikotembelea ili kusikiliza na kupokea maoni ya wateja kuhusu maboresho ya mfumo mkuu wa uendeshaji wa huduma yaliyofanyika hivi karibuni.

Timu ya watalaamu kutoka TEITI ikitembelea baadhi ya miradi ya CSR, ikiwemo ya elimu katika vijiji vilivyo jirani na mgodi wa North Mara
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko, akizungumza na watalaamu kutoka TEITI waliotembelea mgodi huo.
**

Na Mwandishi Wetu, Tarime

Timu ya wataalamu wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikali katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) ilitembelea Mgodi wa Dhahabu wa North Mara Septemba 11, 2025 kujionea mchango wake kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

 

 

BODI  ya Wakurugenzi ya Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) imetoa wito kwa taasisi zote zinazohusika na usimamizi wa mafuta nchini kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha taratibu za upakiaji na upakuaji mafuta zinafuatwa kwa kuzingatia usalama wa watu na uhifadhi wa mazingira.

Wajumbe wa Bodi hiyo wametoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kukagua huduma za shehena za mafuta katika Bandari za Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma. Walisema kuwa upakiaji wa mafuta bila kutumia mifumo rasmi ni hatari, kwa kuwa unaweza kuharibu mazingira na kuhatarisha maisha ya wananchi.

Mwenyekiti wa Bodi ya PBPA, Dkt. Lutengeno Mwakahesya, alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuhakikisha miundombinu yote ya kusafirisha mafuta inazingatia viwango vya usalama na heshima kwa mazingira.

“Kushusha mafuta moja kwa moja kutoka kwenye malori hadi melini bila kutumia terminal ni hatari. Tunashauri TPA iangalie uwezekano wa kujenga matenki mapya ya kuhifadhia mafuta au kuboresha yaliyopo kupitia maboresho yanayoendelea ya Bandari ya Kigoma,” alisema.

Aliongeza kuwa ni vyema TPA ikaweka utaratibu wa bei sawa (equal pricing) kwa shughuli zote za kushusha na kusafirisha mafuta kupitia Kigoma ili kurahisisha matumizi ya terminal, kupunguza gharama kwa wadau na kuongeza usalama wa shughuli hizo.

Awali akiwasilisha taarifa ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) Kigoma, Meneja wa Bandari za Ziwa Tanganyika, Edward Mabula, alisema kwa sasa bandari hiyo inatumia mfumo wa dipping system, huku maandalizi yakiendelea ili kuanza kutumia flow meter system yenye ufanisi zaidi.

Mabula alisema biashara ya mafuta katika bandari hiyo imekuwa ikikua mwaka hadi mwaka. “Kwa mfano, mapokezi ya mafuta yameongezeka kutoka tani 32,826 mwaka 2023 hadi tani 52,367 mwaka 2024. Hii inaonyesha jinsi uhitaji wa huduma unavyoongezeka,” alisema. Alifafanua kuwa mafuta hayo huhudumiwa kupitia cargo terminal na kusafirishwa kwa meli ya Sangara kwenda nchi jirani za Burundi na Congo. TPA, alisema, imejipanga kuhakikisha uhitaji unaoongezeka unakidhiwa kwa wakati.

Mabula aliongeza kuwa wakati wa upakiaji wa mafuta, taasisi za zimamoto huhakikisha zipo eneo la bandari kama hatua ya tahadhari ya kulinda usalama wa watu na mazingira. Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika Bandari ya Kigoma, Mohamed Mnonda, alisema taasisi yake kwa kushirikiana na TPA, EWURA na wadau wengine inasimamia kwa karibu mizigo yote inayosafirishwa nje ya nchi kupitia Kigoma.

“TRA inahakikisha mizigo yote inapimwa na kusajiliwa ipasavyo ili kuepusha upotevu wa mapato ya Serikali na kulinda usahihi wa takwimu za biashara,” alisema.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya GBP Tanzania Bw. Rashid Seif aliomba Serikali kuruhusu tena biashara ya mafuta ya kusafirisha nje (export) kupitia bandari za Ziwa Tanganyika. Alisema kufungwa kwa mfumo huo kumesababisha makampuni mengi kufunga depoti zao, lakini kama mfumo huo ukifunguliwa upya, makampuni yatatumia tena matenki yao, jambo litakaloongeza mapato ya Serikali na kuchochea ajira kwa wananchi wa Kigoma.

Serikali kwa sasa inaendelea na maboresho ya Bandari ya Kigoma na zingine za Ziwa Tanganyika, lengo likiwa ni kuongeza uwezo wa kuhudumia shehena kubwa za mafuta na bidhaa nyingine. Maboresho hayo yanatarajiwa kuongeza ushindani wa bandari za Tanzania katika ukanda wa Maziwa Makuu na kusaidia kukuza biashara na usafirishaji kwenda nchi jirani za Burundi, Congo na Zambia.

 

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt Hashil Abdalah amesema ujio wa ujumbe wa wafanyabishara kutoka nchini Oman utazidi kuitangaza Tanzania kimataifa hususani katika sekta ya viwanda na biashara hali itakayoongeza wawekezaji kutoka nje ya Tanzania ‎Dkt Abdallah ameyasema Septemba 07, 2025 wakati wa Ziara ya Ujumbe huo katika Kiwanda cha Union Meat Group kinachojihusisha na uchakataji wa nyama ya mbuzi na kondoo pamoja na Kongani ya Viwanda ya Kasasa (KAMAKA ) vilivyopo Mkoani Pwani.

Naye, Mjumbe wa Baraza la Nchi na Mwenyekiti wa Chama cha Biashara na Viwanda cha Oman Mkoa wa Al Wusta na Kiongozi wa Ujumbe huo Dkt. Salem bin Salim Al-Junaibi amesema ujumbe huo ulivutiwa na kufurahishwa na uwezo wa Kiwanda cha Union Meat kwa kuzingatia viwango vya juu kutoka kwenye usafi na weledi wa wafanyakazi hadi uzingatiaji wa viwango vya Halal.

"Ushirikiano huu unakuja kwa wakati unaofaa, tunapobadilisha uchumi wetu na kuimarisha ushirikiano katika biashara na uwekezaji wa kimkakati katika vifaa, bandari, kilimo, utalii, nishati pamoja na usalama wa chakula." Bw. Al-Junaibi alisema

‎Akizungumza kwa niaba ya ujumbe kutoka Oman Bw. Zahran Al Aras ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji na kuahidi kuendelea kununua nyama kutoka Tanzania kwa kuwa ina radha nzuri. ‎Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bi Mariam Gw'hwani ameuhakikishia ujumbe huo Kuwa Union Meat itaendelea kuzingatia viwango vya kimataifa vya afya, usafi, na utii wa Halal na kuwa Kiwanda chake kina uwezo wa kuchinja na nyama ya mbuzi na kondoo 3500 wanachinjwa kiwandani hapo kwa siku na

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa chemba ya wafanyabiashara wenye viwanda na wakulima nchini TCCIA Bw. Oscar Kissanga amesema faida ya ujio wa ujumbe huo nchini kuimarisha uhusiano wa kibiashara baina ya nchi hizo na Kuwa taasisi yake iko tayari kutumia fursa zitakazotokana na uhusiano huo. ‎Ujumbe huo wa wafanyabishara zaidi ya 15 umetembelea pia eneo la uwekezaji wa viwanda la KAMAKA lililopo Kibaha Pwani huku ukitarajiwa kuwepo nchini kwa siku tano na kutembelea miradi mbalimbali.

Katika kujenga mshikamano wa kikanda, viongozi wa serikali, wataalamu wa masuala ya bahari na uvuvi, viongozi wa jamii na wanaharakati wa uhifadhi wa mazingira ya pwani wameweka saini makubaliano ya kihistoria ya kuimarisha ushirikiano katika mapambano dhidi ya Uvuvi Haramu, Usioripotiwa na Usiodhibitiwa katika maji ya Afrika Mashariki.


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ali Ussi (kushoto) akizindua jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule ya Kharumwa

 

MOROGORO

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa Mfumo wa Usimamizi wa Kodi za Ndani ujulikanao kama IDRAS, ambao unalenga kuleta mapinduzi makubwa katika ukusanyaji na usimamizi wa kodi nchini.

Hayo yameelezwa leo Mkoani Morogoro na Meneja wa Mradi wa IDRAS, Bw.Frank Mwaselela, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Vinara 105 wa Usimamizi wa Mabadiliko kutoka Tanzania Bara na Visiwani.

Bw. Mwaselela amesema mfumo huo utarahisisha kazi ya ukusanyaji wa kodi kwa kuiunganisha taratibu zote za kodi za ndani kwenye jukwaa moja la kidijitali.

“IDRAS ni mfumo ambao utarahisisha upatikanaji wa taarifa, uwasilishaji wa taarifa za kodi, na ufuatiliaji wa malipo. Unalenga kuleta urahisi wa matumizi kwa watumiaji wa ndani wa TRA, hasa maofisa wa ukusanyaji,” amesema Bw. Mwaselela.

Ameeleza kuwa katika hatua za ujenzi wa mfumo huo, TRA imeshirikiana kwa karibu na wadau wa ndani na nje ya taasisi ili kuhakikisha kuwa mfumo huo unajengwa kulingana na mahitaji halisi ya watumiaji katika ulimwengu wa kisasa wa Usimamizi wa kodi, sheria na taratibu za kodi.

“Tumeweza kuyapitia mahitaji mbalimbali ya wadau ili kuhakikisha tunajenga mfumo unaokidhi matakwa ya sasa ya kiteknolojia na kiutendaji. Kwa sasa tupo kwenye hatua ya mwisho ya ujenzi,” aliongeza”, Bw. Mwaselela .

Kwa mujibu wa Mwaselela, hatua muhimu kabla ya mfumo kuanza kutumika ni kuwaandaa watumiaji wa ndani na nje kwa kuwajengea uwezo juu ya namna ya kutumia mfumo huo.

“Kwa sasa tupo kwenye tukio maalum ambalo linawaleta pamoja watumiaji wa ndani kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani, zaidi ya 105. Lengo ni kuwapa mafunzo na kuwawezesha kuwa mabalozi wa mfumo huu katika maeneo yao ya kazi,” amesema.

Vile vile amesema kuwa mfumo huo mpya utachukua nafasi ya utaratibu wa zamani wa usimamizi wa kodi uliokuwa ukifanyika kwa njia zisizo za kielektroniki. Kwa sasa, taratibu zote zitaendeshwa kwa njia ya kidijitali, jambo ambalo litaongeza uwazi, ufanisi na uwajibikaji.

“Mabadiliko haya ni makubwa na yanahitaji maandalizi ya kina kwa watumiaji. Tumeanza na kuwanoa mabalozi wa ndani, na baadaye tutafikia makundi mengine wakiwemo watumiaji wa nje ya taasisi,” ameeleza Bw. Mwaselela.

 

 

Na.Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Positive Cooker imeunga mkono juhudi za Serikali za kuondoa matumizi ya nishati chafu ya kupikia kwa kuendesha kampeni ya elimu kwa wananchi wa Dodoma juu ya matumizi ya majiko janja yanayotumia umeme katika kupikia.

Akizungumza katika kampeni hiyo leo Septemba 2,2025 jijini Dodoma  Meneja wa Positive Cooker Kanda ya Kati, Bw. Eliud Swai, amesema  lengo ni kuhamasisha wananchi kutumia majiko janja ya umeme kupikia, ikiwa ni sehemu ya mchango wa kampuni hiyo katika kuunga mkono ajenda ya kitaifa ya matumizi ya nishati safi.

Bw. Swai amesema kuwa kampeni hiyo inalenga kuwashawishi Watanzania kuachana na mila potofu kuhusu matumizi ya umeme kupikia na badala yake kuanza kuamini kuwa ni nishati rafiki, nafuu na salama.

“Lengo letu ni kufanya kampeni ya kutunza mazingira. Tunahamasisha wananchi watumie umeme kwa sababu hivi sasa kila nyumba ya Mtanzania ina umeme, lakini wengi wanauhusisha zaidi na mwanga, friji au kuchaji simu. Tunataka watambue kuwa umeme ni nishati nafuu jikoni kwako,” amesema Bw. Swai

Aidha amebainisha kuwa majiko hayo janja yanatumia wastani wa nusu uniti hadi uniti moja kwa saa moja ya kupika, sawa na shilingi 180 hadi 350, hali inayothibitisha ufanisi wake wa gharama.

Hata hivyo amesema kuwa  ujio wa teknolojia hiyo mpya utasaidia kuondoa utegemezi wa mkaa na kuni, hivyo kulinda afya za watumiaji na kuokoa misitu.

“Lengo letu ni kutoa elimu kwa kila Mtanzania ili aache kutumia mkaa na kuni. Hii ni sehemu ya jitihada za kuunga mkono kampeni ya nishati safi ya kupikia na kumsaidia mama wa nyumbani apike bila kero wala gharama kubwa kwa kutumia majiko ya umeme,” ameongeza Bw. Swai.

Nao Baadhi ya wananchi waliohudhuria kampeni hiyo wamesema kuwa  elimu waliyopewa imekuwa ya msaada mkubwa, ikiwakumbusha madhara ya matumizi ya nishati chafu na faida za kutumia umeme kupikia.

“Elimu tuliyopewa ni nzuri, inatukumbusha umuhimu wa kutumia majiko haya ya umeme. Zamani tulipokuwa tunatumia kuni na mkaa tulipata changamoto nyingi, ikiwemo kuchelewa kuiva kwa chakula, lakini sasa majiko janja yanaongeza kasi na urahisi wa kupika,” wamesema 

Iwapo familia nyingi zitatumia majiko hayo, kasi ya ukataji miti itapungua na hivyo kuimarisha uhifadhi wa misitu, hatua itakayosaidia Tanzania kufikia malengo yake ya kupunguza hewa ya ukaa.




Na Oscar Assenga, TANGA



SERIKALI imesema kwamba ina mpango wa kuendelea kufanya uwekezaji katika Bandari ya Tanga kwa kuongeza sehemu ya kutoa huduma mara mbili kutoka mita 450 hadi kufikia mita 900 ili kuendelea kuongeza ufanisi wa kuhudumia shehena



Hayo yalibainishwa Septemba 1,2025 na Msajili wa Hazina Nehemiah Mchechu wakati alipofanya ziara katika Bandari ya Tanga kuona uwekezaji uliofanywa na Serikali wa Sh.Bilioni 429.1, huku akiridhishwa na maboresho yaliyofanyika ambayo yameiwezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi.

Alisema kwamba uwekezaji katika Bandari hiyo utaendelea kuwa chachu ya kuongeza matokeo ya wazi ya kiuchumi kutokana na kuchangia uwepo wa shughuli mbalimbali za kiuchumi na hivyo kuchangia maendeleo ya mkoa na Taifa kwa ujumla.

Aidha alisema kwamba katika sehemu ya kutolea huduma kuna mita 450 na kina mita 3 na kinaenda kuwa mita 13 ikiwemo lango la kuingilia limepanuliwa na kufikia upana mita 135 kwa kina cha mita 13 lakini bado kuna mipango inafanyika kuongeza ifike mita 900.

“Tunaiona Bandari hii ikichangamka tayari Serikali inakwenda kufanya uwekezaji mara mbili kutoka mita 450 mpaka mita 900 maana yake ni mita ni 1800 sasa unapokuwa unaangalia maeneo ya Bandari uwekezaji huo na ule uwekezaji wa Chongoleni kwa ajili ya mafuta ukiangalia gati inayotengenezwa kwa ajili ya Meli kubwa zinazokuja kusafirisha mafuta ghafi yanayotoka nchini Uganda huu ni uwekezaji mkubwa ”Alisema



Aliongeza kwamba maana tayari eneo la Tanga litakuwa ni kitovu cha biashara pamoja na eneo ambalo kila mtu kutoka mataifa mbalimbali atakuwa anaifahamu na kuwa na uwekezaji mkubwa na kuleta nafasi kubwa za kiuchumi sio kwa mkoa bali nchi nzima.

“Kimsingi mimi kama Msimamizi wa Mashirika na Mmiliki kwa niaba ya Serikali ninafarijika na huduma zinazotolewa na TPA na utulivu tunauona uimara wa huduma maana yake ni muunganiko wa vitu viwili uongozi inayofahamu kazi yake na watumishi wanaofanya kazi yao kwa ustawi wa juu”Alisema



Alisema kwamba wanazidi kuwa na matumaini makubwa sana kwa sababu Bandari asilimia kubwa ya mapato yake yanayokusanywa na TRA wanatoka Bandari na wanafikiria ni muhimu kuendelea kuitazama Bandari kwa jicho la Pekee.

“Lakini niwasihi wafanyakazi wa Bandari tuone ufahari tupo sehemu ambayo ni jicho na mboni ya Serikali katika uchumi wa nchi kwa hivyo lazima tuichukulie kama sehemu muhimu inayohitaji huduma zilizobora na tija kwa ajili ya maendeleo”Alisema



Hata hivyo alisema kwamba jambo jingine ni kuendelea kuhakikisha sekta binafsi na umma zinaungana lakini mali inabaki kuwa ni ya Bandari na zitabali kuwa mali ya nchi na wananchi kwa ujumla.

“Tunachokizungumza hapo ni na wanachokizungumza ni wawekezaji ambao watakuja kuziendesha na watapata mapato lakini baada ya muda kile kitu ni mali yetu na hakiondoki na maana yake tunakuwa na ushindani na ufanisi na huduma zitaendelea kuwa bora hivyo ni jambo la msingi na watanzania waendelea kujiunga na kujifunza kwa waliokuja kuwekeza”Alisema



Awali akizungumza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Plasduce Mbossa alisema uwekezaji wa viwanda huo umesaidia kuhudumia meli kwa urahisi na gharama nafuu kutokana na kuimarika miundombinu ya Bandari ya Tanga



“Sisi tumekusanya Bilioni 75 ambazo tunatumia kulipa wafanyakazi,vifaa na kufanya ukarabati tunatumia fedha hizo Tanga kuna ukuaji mkubwa wa viwanda na kichosabababisha ni Bandari sasa tunaweza kuhudumia meli kwa urahisi na bei nafuu ndio inapeleka uwekezaji wa viwanda”Alisema

Hata hivyo alisema ujenzi viwanda vilivyo vinasababisha ukuaji wake kuimarika kwa Bandari ikiwemo maboresho walioyafanya na ukuaji wa uchumi na mahitaji na maendeleo yanazidi kufanywa ikiwemo upanuzi zaidi na watajenga mita 900 zaidi.

“ Leo utaona kuna meli mbili zinahudumiwa na meli tatu nje zinasubiri hivyo tunahitaji kupanua miundombinu ili kuweza kuzihudumia meli zote kwa wakati na kuwasaidia wafanyabiashara na wakulima kulifikia soko kupitia Bandari ya Tanga”Alisema

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha alimhakikishia Msajili huyo kuwa huduma katika Bandari ya tanga itazidi kuimarika kwa maana ya kwamba meli zitakapokuwa zinakuja watazihudumia sio kwa zaidi ya siku tatu meli inaondoka huku akitoa wito kwa watumiaji wa Bandari hiyo waendelee kuitumia