Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeanza kupokea madai kwa njia ya mtandao tangu Aprili Mosi, 2024, Meneja wa PSSSF, Kanda ya Zanzibar,  Amina Kassim.

Aidha,  kufuatia mapinduzi hayo ya kidigitali katika kutoa huduma, Bi. Amina amewataka waajiri  kutumia mfumo huo ili kuwaondolea usumbufu wastaafu watarajiwa.

"Dunia ipo zama za teknolojia  hivyo PSSSF nayo haijaachwa nyuma, tumewarahisishia wanachama wetu kupata huduma mbalimbali kupitia mtandao.” Amefafanua.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Maonesho ya miaka 60 ya Muungano yanayofanyika katika viwanja vya Nyamanzi Wilaya ya Magharibi "A" Kisiwani Unguja, Zanzibar,  Amina ameeleza umuhimu wa Maonesho hayo kwamba ni alama ya kudumisha Muungano wa pande mbili, Bara na Visiwani.

“Kuna kila sababu ya kuendeleza muungano wa Tanganyika na Zanzibar ili kudumisha umoja na mshikamano ulioanzishwa na wasisi wetu. Kutokana na umuhimu huo ndio mana tumeamua kushiriki  maonesho haya ili kutoa huduma kwa wanachama wetu na wananchi kwa ujumla.” Alifafanua.

Akizungumzia huduma zitolewazo katika banda hilo, Amina alisema, pamoja na elimu ya hifadhi ya jamii, pia wanawaelimisha wanachama wao namna ya kutumia huduma za PSSSF Kiganjani.

“Huduma hii inatoa fursa kwa mwanachama kupata huduma mbalimbali za Mfuko kupitia Simu janja. Huduma hizo ni pamoja na kuangalia mwenedndo wa michango yake, mafao yatolewayo na Mfuko lakini kwa wastaafi anaweza kuhakiki taarifa zake.” Alifafanua.

Kaulimbiu ya Maonesho hayo ni “Miaka 60 ya Muungano tuna Shikamana, Tunaimarika kwa Maendeleo ya Taifa.”

“Sisi kama Mfuko tunaamini ushiriki wewtu unaakisi moja kwa moja kauli mbiu hiyo.” Alisema

Aidha alisema PSSSF imekuwa ikiimarisha utoaji huduma kwa wanachama popote walipo.

“Mwanachama wa PSSSF anaweza kufurahia mtandao wetu ambao ofisi zetu zimeenea nchi nzima Bara na Visiwani.”

 "Hivyo tunawakaribishwa wanachama wetu kwenye ofisi zetu za Zanzibar kwa hakika huku ndiko kushikamana vizuri kwa maendeleo ya taifa letu", alisema Amina. 

Meneja wa Ofisi ya PSSSF Zanzibar, Bi. Amina Kassim akimuelekeza Mkuu wa Polisi Jamii Zanzibar, Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP. Jonas Mdyanko Mahanga, namna ya kujisajili kwenye App ya PSSSF Kiganjani. Anayeangalia ni Afisa TEHAMA, Bilal Mlendela.

Meneja wa Ofisi ya PSSSF Zanzibar, Bi. Amina Kassim akimuelekeza Mkuu wa Polisi Jamii Zanzibar, Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP. Jonas Mdyanko Mahanga, namna ya kujisajili kwenye App ya PSSSF Kiganjani. Anayeangalia ni Afisa TEHAMA, Bilal Mlendela.





Share To:

Post A Comment: