Articles by "KILIMANJARO"
Showing posts with label KILIMANJARO. Show all posts

 

MKUU wa Wilaya ya Rombo, Raymond Mwangwala, amesema kuwa endapo wananchi wataelewa umuhimu kulipa kodi na athari za biashara za magendo nchi itakuwa salama.

Hayo ameyasema hivi karibuni wakati wa ziara ya Maofisa wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) , idara ya forodha.

DC. Mwangwala amesema kuwa amewapa baraka maofisa hao kwenda kuwapa elimu wananchi.

"Elimu ni muhimu hatuzungumzii tu magendo , tunazungumzia mtu anaweza kuingiza silaha , mtu anaweza kuingia sumu ambayo itaathiti nchi yetu mtu anaweza wahamiaji harama ambao huwezi kuelewa ni maharamia au magaidi kwa hiyo tunapozungumzia kuangalia mipaka yetu hatuzungumzi kwenye muktadha wa kodi tu , tunazungumzia muktadha wa kiusalama, mapato , tunazungumzia mambo ambayo mwananchi akiyaelewa utakuwa msaada mkubwa kwa nchi yetu".

"Nendeni mtusaidie elimisheni watu waweze kuelewa tunakuwa tumeisaidia nchi yetu kwa kiasi kikubwa" .

Amependekeza kuwa elimu hiyo itolewe kwa Watendaji na wenyeviti wa vitongoji ambao hawa wako karibu na wananchi.

Amesema kuwa endapo mapato yakakusanywa vizuri basi nchi itapata maendeleo.

"Mnafanya hivyo lengo letu kuisaidia nchi , tunakuwa tuwasaidia Watanzania na tunakuwa tumemsaidia Rais wetu "

Amesema kuwa endapo wananchi wakaelewa umuhimu wa kodi na usimamizi ukawa nzuri basi nchi itajisimamia .

"Hakuna mtu atakayeweza kutunyanyasa kwa sababu tunakuwa na uwezo wa kujiendesha wenyewe ...mapato ya ndani tunaambiwa sasa yanafikia asilimia 70 kwa hiyo kama tumefika hatua hiyo tunaweza kujiendesha wenyewe".

Ametoa wito kwa maofisa wa TRA kufanya shughuli zao kwa uadilifu.

Ameitaja changamoto ya maeneo ya mipaka kutorasimishwa kwenye forodha kwa kuwa kuna njia zinazotumika kutoka ambapo haziwa mawakala wa forodha.

 MKUU wa wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, Mwanahamisi Munkunda amewataka wawekezaji kwenda kuwekeza katika wilaya hiyo kwani tatizo la maji ambalo lilikuwa kero kwao limeshapatiwa ufumbuzi wa kudumu.


Alitoa kauli hiyo jana alipofanya kikao na Wadau wa maji na menejimenti ya Mamlaka ya Maji Same Mwanga (Samwasa) mara baada ya kutembelea na kujionea mradi wa maji Mwanga - Same - Korogwe ambao awamu ya kwanza imeshakamilika na maji yanatoka katika wilaya ya Mwanga na Same.

Alisema kuwa, awali wawekezaji walikuwa wakishindwa kuwekeza katika wilaya hiyo kutokana na tatizo la maji lakini kwa sasa kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweza kukamilisha mradi huo.

"Tunatambua wawekezaji wengi walikuwa wakikataa kuja kuwekeza katika wilaya yetu kutokana na tatizo la maji tulilokuwa nalo lakini serikali imeonyesha kwa vitendo kuondoa changamoto zinazowakabili wananchi wake ambapo kwa sasa tunapata maji masaa 24" Alisema Mwanahamisi.

Alisema kuwa, mradi huo umeliliwa na wananchi kwa muda mrefu lakini Dkt. Samia amekuja kuumaliza na kutatua kiu ya Wanamwanga ambapo kwa sasa wanayo maji ya kutosha.

Mkuu huyo alidai kuwa, lengo la mradi huo ni kuifungua wilaya ya Mwanga kiuchumi na kimaendeleo na kuwataka kuwa walinzi wa mradi huo ili uweze kudumu muda mrefu.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa wilaya amewataka Watumishi wa Mamlaka ya maji Samwasa kubadilisha utendaji kazi na kuachana kufanya kazi kwa mazoea ili lengo la serikali na kuwahudumia wananchi wake liweze kutimia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Samwasa, Mhandisi Rashid Mwinjuma alisema kuwa, uhitaji wa maji kwa wilaya ya Mwanga na Same ni lita za ujazo milioni 8 kwa siku huku mradi huo ukiweza kuzalisha lita za ujazo milioni 55.5 kwa siku hivyo maji yapo ya kutosha.

Mhandisi Mwinjuma alisema kuwa, kwa sasa Mamlaka hiyo inazidai taasisi za serikali na watu binafsi milioni 149.23 kwa Mwanga na milioni 132.22 kwa Same ambapo amehimiza wananchi kuendelea kulipa Ankara zao pamoja na madeni.

Alisema kuwa, kwa sasa Mamlaka hiyo inakabiliwa na changamoto ya uchelewaji wa vifaa kama mabomba kea ajili ya maunganisho ya maji kwenye mtandao wa mradi, uhaba wa fedha inayopelekea kutomudu gharama za ujenzi wa miradi na uendeshaji.

"T inakabiliwa na changamoto ya baadhi ya wateja kutolipa Ankara zao kwa wakati ambapo kwa sasa tunadai zaidi ya milioni 281 lakini pia upotevu wa maji mkubwa kutokana na uchakavu wa miundombinu" Alisema Mhandisi Mwinjuma.







 MKUU wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni ameliagiza Jeshi la polisi kufanya msako na kuwakamata watu watatu wa familia moja wanaotuhumiwa na kwa maua ya Mwenyekiti wa kitongoji cha Kampimbi kata ya Ndungu, Charles Johnson Mkuruto(58).


Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa wilaya, mnamo Aprili 26 mwaka huu majira ya saa tano na nusu asubuhi huko kitongoji cha Kampimbi kijiji cha Ndungu kata ya Ndungu mtu mmoja aitwae Johnson Mkuruto(58) Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sinangoa 'A' aliuwawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya kichwani na nyuma ya bega la kulia.

Alisema kuwa, Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Ardhi kata ya Ndungu alikatwa na watu watatu ambao aliwataja kwa majina kuwa ni Mohamad Makundi, Hamad Makundi na Mnandi Makundi na kutoweka kusikojulikana.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa, sababu ya mauaji hayo ni mgogoro wa Ardhi uliopo Mahakama ya Ardhi ya Ndungu.

"Baraza la Ardhi jana lilienda eneo la mashamba yanayobishaniwa ndipo watuhumiwa walimvamia marehemu na kumkatakata na kitu chenye ncha kali kisha kukimbia" Alisema Kasilda. 

 


Na Elizabeth Joseph, Monduli.


WANANCHI wilayani Monduli wameshauriwa kuhakikisha wanatumia Mfumo mpya wa ukusanyaji Mapato ya ndani ya Halmashauri (TAUSI) ili kuongeza ufanisi kwenye ukusanyaji wa mapato.

Ushauri huo umetolewa na Ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bw,Abdallah Magambo wakati wa mahojiano na chombo hiki kuhusu mfumo huo wa Tausi.

Alisema toka kuanza kwa mfumo huo mnamo mwezi Machi mwaka huu mafanikio yameanza kuonekana ikiwa ni pamoja na kuepusha upotevu wa mapato ya Halmashauri na wananchi kutopoteza muda kufuatilia huduma  ikiwemo kulipa ushuru ama kuomba leseni ofisini kwakuwa mfumo huo unaruhusu kupata huduma popote walipo.

"Nature ya mfumo huu mtu mwenyewe anaweza kujisajiri kwa kuingiza taarifa zinazohitajika kwenye mfumo na hauhitaji kwenda kumsukuma mtu kila kitu anafanya huko alipo ikiwemo kupata control number na kulipia akiwa huko"aliongeza kusema Bw, Magambo.

Aidha aliwaomba wananchi kuhakikisha wao ndio wanajaza taarifa zinazohitajika na sio kumuagiza mtu kwakuwa katika usajiri itahitajika namba ya kitambulisho cha taifa (Nida),namba ya simu iliyosajiriwa kupitia Nida ambayo baadhi ya taarifa hutumwa kupitia namba hiyo.

"Changamoto inayojitokeza kupitia mfumo huu ni kuwa watu wengi hawana namba za Nida ama mwingine anakuwa namba ya Nida ila hana tena ile namba ya simu aliyoisajiri kwa Nida yake na mfumo unataka namba aliyosajiria Nida yake hivyo kujikuta walishindwa kumaliza kujaza taarifa zinazotakiwa ili kukamilisha maombi"alisema Ofisa hiyo.

Hata hivyo alifafanua kuwa katika kuhakikisha wananchi wa Monduli wanapata huduma hiyo tayari elimu kwa wadau na baadhi ya wataalam wa Halmashauri hiyo imetolewa ili kusaidia wananchi kujaza taafira kupitia mfumo huo ikiwemo watoa huduma za mtandao (internet services) katika maeneo ya Monduli mjini,Duka bovu,Lolkisale, Makuyuni,Mto wa mbu,Selela na Engaruka.

Naye mmoja wa wafanyabiashara ya saluni ya kike Bi,Stella Masanja akielezea mfumo huo alisema aliipongeza serikali kuanzisha mfumo huo na kusema unaongeza uaminifu kwa wananchi kwakuwa na uhakika wa mapato kuingia serikalini moja kwa moja.

Mfumo wa Tausi unamuwezesha mwananchi kuomba leseni,vibali na kulipa tozo,ushuru na faini mbalimbali kwa kutumia simu yenye uwezo wa kushika mtandao wa ama sehemu wanazotoa huduma za mtandao kupitia kompyuta huku lengo kuu la Serikali likiwa ni kuboresha ukusanyaji wa mapato Serikalini.


Naibu Waziri wa Uchukuzi Atupele Mwakibete akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, wakati Naibu Waziri huyo alipomtembelea Mkuu wa Mkoa huyo ofisini kwake hivi karibuni.
Imeelezwa kuwa upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Moshi mkoani
Kilimanjaro unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2023  ili kuruhusu ndege
zenye uwezo wakubeba abiria 40 za  binafsi na za biashara kuweza kuruka na
kutua kiwanjani hapo.

Akizungumza mkoani humo mara baada ya kukagua maendeleo ya upanuzi
huo, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete, amefafanua kuwa baada
ya filamu ya Royal Tour iliyofanywa na Rais wa Jamhuri wa Tanzania Mhe.
Samia Suluhu kumekuwa na ongezeko la watalii nchini hivyo dhamira ya
Serikali ni kuendeleza miundombinu ya viwanja vya ndege nchini ili
kutokwamisha matokeo ya filamu hiyo.

“Uzinduzi wa filamu ya royal tour umekuwa na matokeo chanya ambao
tunashuhudia idadi ya watalii inavyoongezeka kila siku, kwa ongezeko hilo
ndio maana mnaona tunajitahidi kuboresha viwanja vya ndege ili kuruhusu
watalii kuchagua popote wanapotaka kuruka na kutua," amefafanua Naibu
Waziri Mwakibete.

Aidha, Naibu Waziri huyo amezitaka Taasisi za Mamlaka ya Viwanja vya
Ndege nchini (TAA) na Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS)
kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi mzawa anayeboresha kiwanja hicho ili
akamilishe kazi hiyo kwa wakati na kwa viwango.

Mwakibete ameutaka uongozi wa TAA, TANROADS na Mkoa kukaa na
kumaliza changamoto zilizopo ikiwemo uvamizi wa eneo la kiwanja ili
kutomchelewesha mkandarasi kukamilisha mradi huo kwa wakati.

Naye, Meneja wa TANROADS mkoa wa Kilimanjaro, Eng. Motta Kyando,
ameeleza kuwa upanuzi wa kiwanja hicho unagharimiwa na fedha za ndani 
kiasi cha zaidi shilingi bilioni 12 na tayari Mkandarasi kampuni ya kizalendo ya
Rocktronic Limited ameanza kazi za awali za upanuzi ambapo mradi huo
utatekelezwa kwa muda wa miezi 12.

Eng. Motta ameongeza kuwa upanuzi huo utahusisha ujenzi wa barabara ya
kuruka na kutua ndege, barabara ya maegesho ya ndege, barabara za usalama
kiwanjani hapo kwa kiwango cha lami pamoja na uzio.

Kwa upande wake Meneja wa Kiwanja hicho, Yusufu Sood, amesema kwa sasa
kiwanja hicho kinahudumia ndege ndogo ambazo si za ratiba zinazoweza

kubeba abiria mpaka saba na helikopta za watu binafsi hivyo kukamilika kwa
maboresho hayo kutaongeza miruko ya ndege na idadi ya abiria.
Naibu Waziri Mwakibete yuko mkoani Kilimanjaro kwa ziara ya siku mbili
ambapo anakagua miradi ya miundombinu ambayo inatekelezwa na Wizara
kupitia Taasisi za Sekta ya Uchukuzi.
Naibu Waziri wa Uchukuzi Atupele Mwakibete akizungumza na Mhandisi wa Kampuni ya Costal Aviation, Boaz Onyango (kulia), wakati alipotembelea Kiwanja cha Ndege cha Moshi, Mkoani Kilimanjaro. Kushoto ni Meneja wa Kiwanja hicho Yusufu Sood na wa pili kushoto ni Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Motta Kyando.Naibu Waziri wa Uchukuzi Atupele Mwakibete akitoa maelekezo Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Motta Kyando wakati alipotembelea kiwanja cha Ndege cha Moshi hivi karibuni.Naibu Waziri wa Uchukuzi Atupele Mwakibete akitoa maelekezo Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Kilimanjaro Nchini (TANROADS) Mhandisi Motta Kyando na Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Moshi Yusufu Sood wakati alipotembelea kiwanja cha Ndege cha Moshi hivi karibuni.Muonekano wa sasa wa moja ya barabara ya kuruka na kutua yenye urefu wa Kilomita 1 nukta 2 ambayo kwa sasa imeanza kujengwa kujengwa kwa kiwango cha Lami. Mradi huo wa upanuzi unatekelezwa kwa fedha za ndani ambapo unatagharimu takribani shilingi bilioni 12 na unatekelezwa na Kampuni ya Rocktronic Limited na unatarajiwa kukamilika mwezi novemba mwaka 2023Kazi ya upanuzi wa Barabara ya Kuruka na kutua ndege ikiendelea katika Kiwanja cha Ndege cha Moshi. Mradi huo unatarajia kugharimu takribani kiasi cha shilingi bilioni 12 na unatekelekezwa kwa miezi 12 ambapo unatarajiwa kukamilika mwezi novemba mwakani. 



Naibu Waziri wa Maji Meryprisca Mahundi


Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Peter Mavunde


Naibu Waziri OR-TAMISEMI David Silinde



Kaya 255 za vijiji vitatu vya Igeleke, Usokami na Kibengu vilivyopo halmasauri ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa zitaondolewa eneo la hifadhi ya Shamba la Sao Hill.

Uamuzi huo umetangazwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula Oktoba 26, 2022 wakati Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta inayoshughulikia migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 ilipotembelea na kukutana na wananchi wa kijiji cha Kibengu kilichopo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

Dkt Mabula alisema uamuzi unaofanywa kuhusiana na eneo hilo una nia njema kwa mustakabali wa taifa na vizazi vijavyo kwa kuwa kaya hizo zimekuwa zikifanya shughuli za kibinadamu ndani ya hifadhi ikiwemo kilimo cha mazao ya kudumu na mazao ya msimu na kuharibu mazingira.

Alitaja idadi ya kaya kwa kila kijiji kuwa, ni kaya 4 za kijiji cha Igeleke kinachohusisha vitongoji vya Kihesa, Mdodi, Lwombogole na Igangilonga. Kaya nyingine ni 97 za kijiji cha Usokami zilizoko vitongoji vya Kidete, Msega, Mgwao, Ilamba, Nyamifwa na Uhwana pamoja na kaya 154 za kijiji cha Kibengu ambazo zote zitatakiwa kuondoka.

“Hiyo ni takwimu za kaya zinazoenda kuathirika na siyo kuhama eneo moja kwenda lingine lakini kwa utaratibu maalum na hakuna atakaye kuja kusema ondokeni leo” alisema Dkt Mabula.

“Mhe Samia amesema hamtaondoka bure na uthamini itafanyika kwa yoyote aliyetimiza masharti na kwa kuwa kijiji kimeandikishwa maana yake mmekidhi vigezo vya kulipwa, na kila mlichowekeza katika eneo husika hakuna atakayedhurika”

Baadhi ya mapendekezo ya wataalamu kuhusiana kaya zinazotakiwa kuondoka eneo la hifadhi ya msitu wa Sao Hill mkoani Iringa ni pamoja na kuwekwa ukomo kwa wananchi kuondoa miti ndani ya hifadhi sambamba na Hifadhi kutoa notsi ya kisheria kwa wananchi kuondoa miti yao kabla ya tarehe ya ukomo.

Mkoa wa Iringa unahusisha vijiji/mitaa 15 yenye migogoro ya matumizi ya ardhi ambapo vijiji hivyo vimeainishwa katika sehemu kuu sita kulingana na aina ya mgogoro na uamuzi uliotolewa na Baraza la Mawaziri.

Manaibu Mawaziri wa Wizara za Kisekta waliopo katika ziara hiyo kila mmoja alielezea umuhimu wa sekta yake katika kulinda na kuimarisha rasilimali za nchi kupitia sekta ya ardhi.

Khamis Hamza Chilo mbali na kupongeza upandaji miti ya biashara wilayani Mufindi alishauri wananchi kupanda miti ya kudumu ili kurithisha vizazi vijavyo.

‘’Nasema haya kwa sababu Tanzania kwa sasa inalia na kuathirika kwa mabadiliko ya tabia nchi na tuchukue tahadhari na kujitahidi kwa kutunza mazingira na kupanda miti ili mwisho wa siku tusilete athari kwa viumbe hai’’. Alisema Chillo

Kwa upande wake Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega alielezea umuhimu wa kuwa na ng’ombe wa maziwa na kushauri wananchi wa Mufindi kujitahidi kila mmoja kuwa na angalau ng’ombe wawili na kusisitiza kuwa, Wizara yake iko katika jitihada za kuimarisha shamba lake sehemu ya Sao hill.

Davida Silinde, Naibu Waziri OR-TAMISEMI alisema ofisi yake kuanzia sasa mchakato wa kusajili vijjji utafanyika kwa ushirikiano na wizara nyingine za kisekta ili kuepuka migogoro ya ardhi inayojitokeza mara kwa mara.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (kushoto) akimkabidhi zawadi ya picha Rawan Dakik (wa nne kutoka kushoto) ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika kutangaza Mlima Kilimanjaro, katika hafla fupi iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro . Mhe. Mary Masanja pia amemtangaza Rawan kama Balozi wa Hiari wa Mlima Kilimanjaro. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongella(wa nne kutoka kulia) wazazi wa Rawan, Mbunge wa Arusha Mjini,Mhe. Mrisho Gambo(wa tatu kutoka kulia),Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe.Jerry Muro (wa pili kutoka kulia) na Kaimu Mtendaji Mkuu wa TTB , Betrita Lyimo (kulia)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (kulia) akiteta jambo na wazazi wa Rawan kabla ya hafla fupi ya kumpokea iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Mhe. Mary Masanja pia amemtangaza Rawan Dakik kama Balozi wa hiari wa  Mlima Kilimanjaro.

Wizara ya Maliasili na Utalii imemteua Rawan Dakik kuwa balozi wa hiari wa Mlima Kilimanjaro ikiwa ni kutambua jitihada zake za kutangaza Mlima Kilimanjaro nchini baada ya kupanda  mlima Kilimanjaro kwa takriban mara tano na pia kuipeperusha bendera ya Tanzania katika kilele cha mlima mrefu zaidi duniani Everest uliopo bara la Asia.

Naibu Waziiri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja (Mb) ameyasema hayo leo wakati wa hafla fupi ya mapokezi ya Rawan Dakik iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro mkoani Kilimanjaro leo.

“Ni jambo la kujivunia sana leo hii kwa bendera yetu ya Tanzania kupeperushwa na si tu mwanamke wa kwanza kabisa Mtanzania lakini pia Mwanamke mwenye umri mdogo zaidi kufika kilele cha mlima Everest kutoka bara la Afrika”ameongeza Mhe. Masanja.

Mhe. Mary Masanja amesema kuwa Rawan Dakik amefanikiwa kufika katika kilele cha mlima Everest kutokana na jitihada binafsi alizojijengea baada ya kuanza kupanda Mlima Kilimanjaro tangu akiwa na umri wa miaka 13 kwa takriban mara tano.

”Mlima wetu wa Kilimanjaro umekuwa chachu ya mafanikio ya Rawan Dakik kwa kufika kilele cha mlima Everest kwa kuwa wataalam wanasema mlima Kilimanjaro ni moja ya kipimo muhimu cha kumuwezesha mtu kufanikiwa kupanda mlima Everest.” amesema Mhe. Mary Masanja.

Aidha, amesema mafanikio ya Rawan Dakik yatatoa hamasa kwa vijana wa Kitanzania hususan wasichana kutimiza ndoto zao.

 


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi, Juma Raibu ameagiza kukamtwa kwa wazabuni wanane wanaodaiwa kula fedha za Halmashauri zaidi ya Sh47 milioni pamoja na viongozi wa vikundi 45 vya asasi za kuweka na kukopa (Vicoba).

Viongozi hao wanadaiwa kuwa wameshindwa kurejesha zaidi ya Sh94 milioni walizokopa  tangu mwaka 2015.

Raibu ametoa agizo hilo alipowaita viongozi hao ofisini kwake kutaka kujua hatma ya fedha hizo ambazo walikopewa na Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.

“Wote hapa niliowaita mmehujumu fedha za serikali, hili jambo linakera sana haiwezekani tangu mwaka 2015 mpaka leo hamjarejesha fedha hizi mnazodaiwa na Halmashauri zaidi ya Sh94 milioni, hili halikubaliki nawakabidhi leo mikononi mwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mtuambie mnarejeshaje fedha hizi, Raibu

“Naomba muondoke na hawa watu watuambie tunapataje fedha zetu ambazo tuliwapa kwa upendo mkubwa, mimi sina mzaha kwenye fedha za serikali,” Raibu. “Takukuru naomba pia niwakabidhi wazabuni wanane waliokwapua fedha zetu  za  Halmashauri zaidi ya Sh47 milioni watuambie  wanazirejesha hizi fedha za serikali,” Raibu


Na Imma Msumba, Mwanga 

 Wanawake wa Halmashauri ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kutumia vizuri mikopo yao kwa kuwekeza kwenye shughuli  mbalimbali za maendeleo na zitakazo zalisha kwa wingi na kuwaletea mapato yakutosha katika familia zao.

Ameyasema hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mwanga  Mhe.Saleh Mkwizu alipokutana na vikundi vya kina mama wajasiriamali wadogo wadogo waliojiajiri katika masoko na minada katika Kata mbalimbali za Halmashauri hiyo.

Mhe. Mkwizu amewataka wanawake hao kuonyesha kuwa wanaweza kuinuka kiuchumi na kuacha utegemezi huku wakitekeleza majukumu yao katika ngazi za familia na jamii kwa ujumla.

“Mikopo hiyo mnayoenda kupewa ichukulieni kama mmepata tunda la embe katika mti wa miba,mkaitumie vizuri  mikopo hiyo na muache kwenda kununua vitu ambavyo havitawasaidia katika kujiletea maendeleo yenu na familia zenu"

Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan imelenga katika kuhakikisha matunda ya nchi yanaliwa na kila mtanzania,hivyo fursa hiyo ya wanawake kupatiwa mitaji kwa mikopo isiyo na riba nimkakati mzuri wakuendelea kutelekeza Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Halmashauri yangu ipo tayari kuwasaidia wakimama wote watakao fanikiwa kumaliza marejesho yao na nitawasaidia kupata mikopo mingine ya riba nafuu huku mkiwa katika vikundi vyenu,pia muendelee kutafuta fursa kubwa zaidi katika miradi mikubwa inayofanywa na serikali,ili muweze kukua katika biashara zenu.

Pia nipende kuipongeza Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa juhudi wanazozifanya za kusaida makundi maalumu ya vijana,wanawake na wenye ulemevu katika Halmashauri ya Mwanga.

Niwasihi wadau wa maendeleo Wilaya ya Mwanga na wenye mapenzi mema kwa Halmashauri yetu waendelee kusaidia akinamama katika nyanja ya kujikwamua kiuchumi ile pale wanapokosa usaidizi basi waweze kusimama wao kama wao na kuendesha maisha yao na wategemezi wao.