Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salum Kalli, ameitembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana Lekule mnamo Mei 7, 2025, ambapo alipata fursa ya kujionea maendeleo ya shule hiyo pamoja na kuzungumza na wanafunzi.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Kalli aliwahimiza wanafunzi hao kusoma kwa bidii na kuwa na nidhamu wawapo shuleni, akisisitiza kuwa elimu ndiyo njia pekee ya kufikia mafanikio ya maisha. Aliwataka kuepuka kabisa vitendo vya mimba za utotoni ambavyo vinaweza kuwa kikwazo kikubwa katika safari yao ya kielimu na kuwakatisha ndoto zao za baadae.

Aidha, kama sehemu ya kuwatia moyo, Mkuu huyo wa Wilaya aliwazawadia wanafunzi hao nyama ya ng’ombe kwa ajili ya chakula, jambo lililopokelewa kwa shangwe na furaha kubwa.

Akizungumza kwa niaba ya shule hiyo, Mkuu wa Shule Mwalimu Anna Wenseslausi alimshukuru sana Mkuu huyo wa Wilaya kwa ujio wake na zawadi aliyoitoa.













Share To:

Post A Comment: