Na lsmail Luhamba, Singida
WATENDAJI katika Wizara ya Nishati watakiwa kufanyakazi kwa bidii na
kuepuka vitendo vya Rushwa kama hatua ya kuongeza uaminifu kwa wananchi wanao
watumikia.
Ombi hilo limetolewa na Waziri wa Nishhati January Makamba wakati akihutubia Mkutano wa Baraza
la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kwa njia ya Mtandao unaofanyika mjini Singida.
Amesisitiza kuwa ubunifu na uwajibikaji mahali pa kazi ni jambo la msingi
ili kuendelea kutoa huduma bora na stahiki kwa wananchi Mijini na Vijijini.
Makamba alisema wizara hiyo itaendelea
kusimamia na kutelekeza miradi ya kimkakati ukiwemo mradi mkubwa wa kufua umeme
JNHPP ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 77.
Katika hatua nyingine amesema suala la kufikisha umeme wa gridi ya Taifa
mkoani Kigoma ni jambo la kupongezwa ambapo kwa sasa Serikali imepata fedha za
kutekeleza mradi wa kuzalisha umeme wa Kakono na miradi mingine ya kimkakati.
Waziri Makamba ameipongeza Menejimenti ya Wizara ya Wishati na Kamati
zilizofanikisha maandalizi ya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi na kusema kuwa
hicho ni kiashiria kizuri cha ushirikishwaji na uimarishwaji wa mahusiano
mazuri kati ya menejimenti na wafanyakazi, hatimaye kutambua mchango wa kila
mfanyakazi katika eneo lake la utumishi.
Hata hivyo imeelezwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ana imani kubwa na
Watendaji pamoja na Viongozi wa Wizara ya Nishati, hivyo watumishi hawana budi
kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili kuendelea kuienzi imani hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba amemhakikishia Waziri wa Nishati kuwa wataendelea kufanya kazi kwa weledi kwa kufuata kanuni ,taratibu na miongozo ili kuhakikisha Wizara inaendelea kutoa mchango mkubwa katika kukuza Pato la Taifa.
Post A Comment: