Mchezaji wa timu ya mamlaka ya mapato Tanzania  'TRA' kushoto akiwania mpira dhidi ya mchezaji   wa chuo kikuu cha Dar es salaam 'UDSM' wakati wa mchezo wao wa nusu fainali uliochezwa juzi katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga ambapo TRA walishinda kwa vikapu 51-45 na kufanikiwa kuingia fainali ya Shimuta.
Kikosi cha timu ya mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania 'TPA' kitakachocheza fainali za SHIMUTA mwaka 2022 dhidi ya mamlaka ya mapato Tanzania  'TRA'.

 Na Denis Chambi,  Tanga.

Kesho November 27,  2022 inasubiriwa  kwa hamu kubwa na wapenzi,  mashabiki na wadau  wa mchezo wa mpira wa kikapu  wakitaka kushuhudia ni nani mbabe atakayeibuka bingwa wa mchezo huo kati ya timu ya mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania  'TPA' dhidi ya mamlaka ya mapato Tanzania  'TRA' zilizofanikiwa kutinga hatua ya fainali ya mchezo huo kwenye mashindano ya Shimuta mwaka huu.

Timu ya mamlaka ya mapato Tanzania  TRA ilifanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali hizo  baada ya  kuwafunga  mahasimu wa  shirika la umeme Tanzania 'TANESCO' kwa vikapu 51-45 huku Bandari wao wakiwatembezea kipigo wapinzani wao chuo kikuu cha Dar es salaam 'UDSM'  kwa kuwafunga vikapu  71 -53 katika hatua ya nusu fainali mechi zote zikichezwa katika  uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga.

Akizungumza  mara baada ya kutinga hatua ya fainali katibu wa michezo kutoka TRA Kamna Shomari alisema  kuwa  mwaka huu wana jambo lao ambalo lazima walitimize hususani katika mchezo  wa mpira wa kikapu wakipanga kutawadhwa kuwa mabingwa kwa mwaka huu wa 2022.

"Mwaka huu tumekuja na adhima moja tu ya kuhakikiaha kwamba linakufa jitu na tunachukuwa hili kombe la Basketball mpaka sasa hivi sisi hatuhesabu kwamba haya ni mafanikio sisi malengo yetu makubwa  ni kuchukuwa ubingwa wala hatuna jambo lingine lolote" alisema

Shomari alikiri wazi kuwa haikuwa rahisi kwao kuwafunga Tanesco kwenye mchezo wa wa nusu fainali ambao wana uzoefu na historia nzuri kwenye shimuta hii ikionyesha kuwa upinzani ulikuwa ni mkubwa kutoka kwao lakini uimara wa kikosi chake uliweza kuamua matokeo   na kuibuka washindi huku wakifurahia kuwafunga vigogo wa kundi lao wakiwemo UDSM.

"Upinzani ulikuwa ni mkali Tanesco wenzetu  wanahistoria nzuri kwenye  michezo hii ,  ukiangalia wametupa upinzani mkubwa  lakini mwishoni wa mchezo  kwa sababu sisi ni bora  tukaweza kufanikiwa kuwafunga" alisema Shomari

Aidha alilipongeza shirikisho linalo simamia  michezo hiyo maarufu  kama Shimuta kwa kuwaletea mashindano hayo kila mwaka ambapo mbali na kukutana na  upinzani kwenye michezo umewajengea ukaribu ushirikiano baina yao wafanyakazi  wa taasiai mashirika na makampuni mbalimbali yanayoshiriki  michuano hiyo.

"Kwa ujumla tunawapongeza waandaaji halmashauri kuu ya shimuta kwa  kusimamia na kuongoza michezo yote ambayo inahusisha taasisi 52 sio jambo rahisi hata kidogo,  tunaomba michezo  hii iendelee kuwepo na kuboreshwa zaidi ina manufaa makubwa kwetu  mbali na kutukutanisha kimichezo lakini imekuwa ni sehemu yetu wafanyakazi kubadilishana mawazo kujenga na kuimarisha mahusiano baina ya taasisi na taasisi"  alisema katibu  huyo.

Mashindano hayo  ya Shimuta  yanayofanyika kitaifa mkoani Tanga kwa mara ya pili mfululizo  yalinza kutimua vumbi katika viwanja mbalimbali tangu November 15 yakibebwa na kauli mbiu ya mwaka huu 'Shimuta Familiya moja' na yanatarajiwa kufungwa rasmi November 29 ,  2022.

Shimuta mwaka huu inajumuisha michezo ya  mpira wa miguu,  Mpira wa pete,   wavu,  kikapu ,  riadha pamoja na michezo ya jadi ikiwemo  Draft,  Dats vishale  na Pooltable   yakivunja rekodi kubwa mwaka huu  kwa kushirikisha  timu mbalimbali zapatazo 52 kutoka  mashirikaya umma  taasisi binafsi  na makampuni.
Share To:

Post A Comment: