Katibu wa michezo kutoka Shirika la viwango Tanzania 'TBS' Nyabuchwenza Mitisela akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya timu yao ya mpira wa miguu kufanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali kwenye mashindano ya SHIMUTA yanayoendelea mkoani Tanga.
Mlinda mlango wa kikosi cha TBS Lukas Gula.
Na Denis Chambi Tanga.
SHIRIKA
la viwango Tanzania TBS kupitia timu yake ya mpira wa miguu
limefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali kwenye mashindano ya
Shimuta yanayoendelea mkoani Tanga baada ya kuwatapa nje wapinzani wao
mamlaka ya usimamizi wa wanayama pori Tanzania 'TAWA' kwa mikwaju ya
penati 5-4 mchezo uliochezwa november 25, 2022 kwenywe dimba la
Popatlal jijini Tanga.
Mchezo
huo ulilazimika kuamuliwa kwa mikwaju ya penati baada ya timu zote mbili
kumaliza mchezo wakitoshana nguvu ya goli 1-1 wakitangulia kupachika
bao TAWA mapema kabisa kunako dakika ya 3 ya mchezo huku TBS nao
wakisawazisha kwenye dakika ya 16 ya kipindi cha kwanza.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya ushindi huo Katibu wa michezo
kutoka Shirika la viwango Tanzania 'TBS' Nyabuchwenza Mitisela alisema
kuwa kila hatua waliyokuwa wakipiga mpaka hapo walipofikia ilikuwa ni
katika harakati za kutaka kutimiza malengo na matarajio walioelekezwa
na viongozi wao ya kuvuka robo fainali ambapo waliweza kufanikisha na
kupiga hatua zaidi.
"Mwaka
jana tuliishia robo fainali kwahiyo mwaka huu tukawa tumejiwekea
malengo kuwa ni lazima tufike nusu fainali tunashukuru Mungu malengo
yetu yametimia na tunafurahi wachezaji wetu wamejituma uwanjani na
wamecheza vizuri tunawapongeza sana" alisema
Katibu
huyo amewaomba mashabiki wao kuendelea kuwaombea kunako hatua ya nusu
fainali ikiwa ni pamoja na kuwatia motisha wachezaji huku akiwaahidi
kuipeleka timu hiyo kucheza fainali na hatimaye kuibuka mabingwa wa
mchezo huo kwa mwaka 2022.
"Nilikuwa
naiona robo fainali ni ngumu zaidi lakini niwaahidi tu wapenzi na
mashabiki wa timu yetu ya TBS kuwa tunaamini tutavuka nusu fainali na
Mungu akipenda kwenda kucheza fainali na kuibuka washindi" alisema
Mitisela.
Mlinda mlango
wa kikosi cha TBS Lukas Gula ambaye aliibuka kuwa shujaa wa mchezo huo
akiokoa mchomo mmoja wa penati na yeye kucheka na nyavu mara moja
alisema mwaka huu kwenye shimuta walijiuliza ni wapi walikosea mwaka
jana kulikowapelekea kuishia hatua ya robo fainali hivyo mwaka huu kuja
na mpango kazi kabambe wa kupiga hatua zaidi ambapo walifanikiwa na sasa
wakiwa wanaichungulia fainali.
"Siri
ya ushindi wa leo ni maandalizi mazuri na malengo ambayo tulijiwekea
katika michezo ya mwaka jana TBS ni miongoni mwa timu ambazo ziliingia
robo fainali lakini tuliondolewa kwa hatua ya matuta na TPDC ,
tulivyokuja mwaka huu tulijiandaa vizuri sana licha ya kwamba tulicheza
pungufu lakini tulifanikiwa kuhimili mchezo na kuwashinda wapinzani
wetu " alisema Gula.
"Timu
yetu imeonyesha timu nyingine kuwa sisi ni watu wa viwango na
tulijiwekea viwango mwaka huu kuwa lazima tufike fainali na tumefikia
katika malengo yetu kwahiyo ni funzo kwa timu nyingine ninaamini kwatika
hatua inayofuata na michezo mingine inayokuja kila mtu anaiogopa TBS
kwa sababu ni timu ambayo imejiweka katika viwango fulani" aliongeza
nyanda huyo.
Mashindano
hayo yaliyoanza kutimua vumbi November 15 yanahusisha timu za
watumishi kutoka mashirika ya umma , taasisi binafsi na makampuni 52
kote nchini na yanatarajiwa kutamatika November 29 mwaka huu kwa fainali
za michezo kucheza ikiwemo mpira wa miguu, Kikapu, Wavu, Pete ,
pamoja na michezo ya jadi ikiwemo Draft, Dats riadha huku
yakuliongozwa na kaulivmbiu ya 'Shimuta Familiya moja' .
Post A Comment: