Nahodha wa timu ya mpira wa miguu kutoka  Mamlaka ya usimamizi wa wanayama pori Tanzania  'TAWA' Ernest Carlos akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya timu yao kutolewa kwenye mashindano ya SHIMUTA hatua ya robo fainali na  shirika la viwango  Tanzania TBS kwa mikwaju ya penati 4-5.

 Kocha wa timu ya mpira wa miguu ya Mamlaka ya usimamizi wa wanayama pori Tanzania  'TAWA' Abdallah Msauka akizungumza mara baada ya mchezo wao wa robo fainali ya mashindano ya SHIMITA waliocheza dhidi ya  timu ya shirika la viwango  Tanzania 'TBS'..

 Na Denis Chambi,  Tanga.

TIMU ya mpira wa miguu kutoka  Mamlaka ya usimamizi wa wanayama pori Tanzania  'TAWA' imetupwa nje ya mashindano ya Shimuta kwa njia ya mkwaju ya penati 4-5 kwenye mchezo wa hatua ya robo fainali walipokutana kutafuta tiketi ya kuwania nafasi ya nusu fainali na wapinzani wao  Shirika la viwango Tanzania 'TBS' katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Popatlal jijini Tanga.


Licha ya kuyaaga mashindano hayo lakini bado timu hiyo inajipongeza kwa hatua ya kuvuka malengo walilokuwa wamejiwekea ambapo walizamilia kuvuka hatua ya 16 bora ambayo walifanikiwa na hatimaye kuja kugonga mwamba kwenye robo fainali huku wakiwa na rekodi nzuri kwenye michezo waliyocheza ambapo hawajapoteza hata mechi moja.

Katika mchezo huo ulioamuliwa na mikwaju ya penati zilimalizika dakika zote ndani ya uwanja  kwa droo ya 1-1  TAWA wakitangulia kupata bao la mapema kabisa kunako dakika ya tatu  kwenye kipindi cha kwanza ambapo haikuchukuwa muda  TBS nao wakasawazisha kunako dakika ya 16.

Nahodha wa timu hiyo  Ernest Carlos alisema malengo ya  mamlaka ya usimamizi wa wanayamapori  Tanzania TAWA ilikuwa ni kuvuka hatua ya 16 bora ambayo walifanikiwa kuitimiza  na kufanikiwa kupiga hatua moja mbele kitu ambacho  wanajivunia  licha ya kuwa  walitamani kucheza fainali  za mashindano hayo kwa mwaka huu wa 2022.

"Malengo ya mamlaka ya usimamizi wa Wanayama pori 'TAWA' ilikuwa ni kuvuka hatua ya 16 bora,  tumefanikiwa lengo  limetimia tumecheza robo fainali ilikuwa ni zaidi ya lengo tulilokusudia" alisema Carlos.

Alisema mbali na kushiriki michuano hiyo  walikuja na ujumbe maalumu kwa wananchi na Tanzania kwa ujumla wa kutunza mazingira na wanyama wote ambao wapo nje ya hifadhi za taifa ambapo amewataka kushirikiana na mamlaka hiyo katika kuhakikisha wanalinda na kutunza   hifadhi  zote zilizopo hapa nchini.

 "Lakini pia lengo la taasisi lilikuwa ni kuleta motisha kwa wafanyakazi pamoja na kuitangaza mamlaka ya usimamizi wa wanayamapori  kuwajulisha wananchi kuwa kuna mamlaka kama hiyo ambayo inahusika na wanyama pori wote ambao wako nje ya hifadhi za taifa zote,   kikubwa tushirikiane wote kulinda mazingira yetu kutunza wanyama wetu ili tuweze kuwarithisha vizazi vijavyo" alisema Carlos.

Akitoa tathmini ya mchezo huo kocha anayekiongoza kikosi cha timu ya TAWA  Abdallah Msauka amesema kuwa  siku zote hatua ya kuamua mchezo kwa njia ya penati haina mwenyewe licha ya kuwa waliweza kutawala mchezo huo kwa dakika zote,  huku akijivunia ubora wa timu yake ambayo ni mara ya pili kushiriki michuano hiyo.

"Mchezo ulikuwa ni mzuri tulifanikiwa kupata goli dakika ya tatu wenzetu  wakaja kusawazisha dakika ya 16,  kipindi cha pili pia tumecheza kila mmoja alikuwa anatafuta nafasi ya kupata goli lakini hatukufanikiwa tumekwenda kwenye penati wenzetu wametuzidi penati moja kwahiyo ndio sehemu ya mchezo hapa tulipofikia kwa hatua hii kwenye mashindano yajayo tuna kitu cha kuanzia" 

"Ndani  ya mchezo sijazidiwa ila penati ndio ziliamua na ilikuwa lazima mmoja akose ili mwingine apite lakini kikubwa namshukuru Mungu kwasababu timu ilikuja kwenye mashindano ikiwa ni  mara ya pili kushiriki lakini kuna timu ambazo ni uzoefu zimeondoka kabla yetu kwahiyo kwa mimi mwalimu  kuwa na timu ya TAWA  kwa mara ya kwanza naona kabisa  ni hatua nimepiga" alisema Msauka.

Mashindano hayo  yaliyoanza kutimua vumbi November 15 yanahusisha  timu za  watumishi kutoka mashirika  ya umma,  taasisi binafsi na makampuni kote nchini na yanatarajiwa kutamatika November 29 mwaka huu kwa fainali za michezo ya  mpira wa miguu,  Kikapu,  Wavu,  Pete ,   pamoja na michezo ya jadi ikiwemo Draft,  Dats  riadha yakibebwa na kauli mbiu isemayo 'Shimuta familiya moja' . 





Share To:

Post A Comment: