Na Ferdinand Shayo ,Arusha .


Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC) kimetoa mafunzo ya utengenezaji wa majiko ya nishati safi pamoja na miundombinu yake kwa Maafisa wa Jeshi la Magereza kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania ili kuwawezesha kutumia nishati hiyo na kuondokana na matumizi ya mkaa na kuni ambayo yanasababisha uharibifu wa mazingira .

Akizungumza katika hafla ya kufunga Mafunzo hayo ,Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Magereza Tanzania ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha Felichisim Masawe amempongeza Mkuu wa Jeshi hilo kwa kutoa Maafisa waliopatiwa mafunzo na CAMARTEC ili waweze kutengeneza majiko yanayotumia gesi ya bayogesi pamoja na sufuria.


Masawe amesema kuwa Jeshi hilo limekua mstari wa mbele kutekeleza agenda ya nishati safi kwa kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Samia Suluhu Hassan ya kuzitaka taasisi zenye watu Zaidi ya 100 kuanza kutumia nishati safi ambapo magereza wameanza tangu mwaka 2024.

Kaimu Mkurugenzi wa CARMATEC Boniface Chatila amelitaka Jeshi la Magereza kuendelea kushirikiana na kituo hicho ili kupata mahitaji yote muhimu ya mitambo ya nishati safi pamoja na kutoa ujuzi kwa Maafisa Magereza ili kueneza Teknolojia hizo.

Kwa upande wake Mratibu wa Mafunzo CAMARTEC Peter Mtoba amesema kituo hicho kimesaini makubaliano ya kutengeneza majiko Zaidi ya 300 ya nishati safi yatakayosambazwa kwenye magereza mbali mbali nchini ili kuhakikisha wanatumia nishati safi na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa.


NAIBU Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Peter Msofe,akizungumza na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mara baada ya kutembelea makao makuu ya Baraza hilo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo.

Na.Mwandishi Wetu

NAIBU Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Peter Msofe, amepongeza utendaji kazi na uwajibikaji wa watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Mazingira nchini.

Prof.Msofe ametoa pongezi hizo alipotembelea makao makuu ya Baraza hilo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo.

“NEMC pamoja na changamoto mnazokabiliana nazo, bado mmepiga hatua kubwa katika usimamizi wa mazingira. Mnafanya kazi inayotambulika na kuonekana na wananchi. Endeleeni kujituma kwa ajili ya maslahi ya Taifa, huku mkilinda afya zenu dhidi ya mazingira hatarishi,” amesema Prof. Msofe.

Aidha Prof. Msofe amesisitiza maeneo matano ya msingi kwa watumishi wa NEMC ili kuboresha zaidi utekelezaji wa majukumu yao.

Ametaja Maeneo hayo ni kuweka uwiano kati ya vihatarishi binafsi na vya mazingira ya kazi,Kujifunza na kushirikishana maarifa ya kitaalamu,Kushirikiana kwa karibu katika utekelezaji wa majukumu,Kuwa wabunifu katika masuala ya mazingira pamoja na Kufanya kazi kwa kuendana na mahitaji ya dunia ya sasa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, ameeleza kuwa Baraza hilo bado linakumbana na changamoto ya kutokuwa na mamlaka kamili ya utekelezaji wa baadhi ya majukumu.

"Tunaendelea na mchakato wa kulifanya Baraza kuwa mamlaka kamili ya mazingira. Kwa sasa, tunategemea vyombo vya ulinzi na usalama katika kutekeleza baadhi ya kazi kutokana na kukosekana kwa sheria inayotoa mamlaka hiyo kwa NEMC," amesema Dkt. Semesi.

NAIBU Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Peter Msofe,akizungumza na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mara baada ya kutembelea makao makuu ya Baraza hilo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo.

NAIBU Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Peter Msofe,akizungumza na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mara baada ya kutembelea makao makuu ya Baraza hilo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo.

NAIBU Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Peter Msofe,akizungumza na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mara baada ya kutembelea makao makuu ya Baraza hilo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo.

NAIBU Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Peter Msofe,akizungumza na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mara baada ya kutembelea makao makuu ya Baraza hilo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo.

Na.Mwandishi Wetu.
BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma, likitoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda na kuhifadhi mazingira kupitia kilimo rafiki kwa mazingira.
Kupitia banda lake, NEMC inatoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya mazingira, ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) kabla ya kuanzisha miradi ya kilimo, ujenzi na shughuli nyingine za kiuchumi.
Aidha, elimu nyingine inayotolewa ni kuhusu,Katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki,Athari za uchafuzi wa vyanzo vya maji,Umuhimu wa kuzingatia kilimo hifadhi,Ulipaji wa ada za mazingira kwa mujibu wa sheria na Elimu ya urejelezaji wa taka kwa ajili ya kulinda mazingira na kuongeza kipato. Maonesho ya Nanenane mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo "Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi." NEMC imesisitiza kuwa uchaguzi wa viongozi wenye maono katika sekta hizo ni msingi wa utekelezaji wa sera na sheria za mazingira kwa maendeleo endelevu. Baraza hilo limewahimiza wakulima, wafugaji, wavuvi na wananchi wote wanaotembelea maonesho hayo kutembelea banda la NEMC ili kupata elimu sahihi juu ya mbinu bora za kilimo na uzalishaji zinazozingatia utunzaji wa mazingira. “Ustawi wa kilimo na uchumi wetu unategemea sana afya ya mazingira yetu. Tunawahamasisha wananchi kufika kujifunza na kushirikiana nasi katika kulinda mazingira kwa kizazi cha sasa na kijacho,” imesema NEMC. Maonesho ya Nanenane kitaifa yameanza rasmi Agosti 1 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Agosti 8, 2025.

Kila mwanamke ana ndoto ya kuolewa na mume mzuri ampendaye ambaye anaona anamfaa kuanzisha naye familia na kuishi maisha mazuri ya upendo, furaha, kujaliana na kuthaminiana.

Vigumu kusema kuna mwanamke asiyekuwa na malengo hayo ingawa kuna wachache ambao wanaweza kuwa kinyume na hilo kutokana na sababu mbalimbali ambazo muda mwingine zinakuwa nje ya uwezo wa wao au sababu za kimazingira.

Jina langu ni Salma, kwa sasa nina miaka 46, naishi Temeke, niliolewa miaka mitatu iliyopita, yaani nikiwa na umri wa miaka 43 jambo ambalo mwenyewe sikuamini hata familia yangu tayari ilikuwa imeshanikatia tamaa. Soma zaidi hapa 

   

Nilikuwa nimezoea maisha ya kawaida ya umaskini. Siku zote nilipambana kuendesha maisha yangu, nikitafuta vibarua vya hapa na pale mjini Mbeya ili nipate pesa ya chakula na kodi.

Nilikuwa na marafiki wengi wa karibu hasa wanawake tuliokuwa tukisaidiana kila mara mambo yalipoenda kombo. Tulikuwa kama dada; nilifikiri urafiki wetu ungekuwa wa milele.

Lakini maisha yangu yalibadilika ghafla baada ya kupata mwelekeo mpya wa kibiashara. Katika kipindi cha chini ya miezi mitatu, nilikuwa nimefungua duka la vifaa vya ujenzi, nikamiliki gari aina ya Toyota Vanguard, na nikaanza kuishi kwenye nyumba ya vyumba vitatu, nikiwa na samani za kisasa. Badala ya kushangilia mafanikio yangu, marafiki wangu wote walianza kunitenga.

Walikuwa wakinisengenya mitandaoni na kusema nimejiingiza kwenye biashara haramu au nimeolewa na mzee wa pesa. Wengine walidai ninafanya mambo ya kichawi.

Iliniuma sana kwa sababu sikutarajia watu niliowategemea kuwa nguzo yangu wawe wa kwanza kunipiga kwa maneno na chuki. Soma zaidi hapa 

 


Na Mwandishi Wetu - Rufiji.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Rufiji ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo anayemaliza muda wake Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema siasa anazozifanya ni za maendeleo, ambazo dhamira yake ni kuwakomboa wananchi wa Rufiji kwa kuwaimarisha kiuchumi pamoja na kuwajengea miundombinu bora ya afya, elimu na barabara. 

Mhe. Mchengerwa amesema hayo kwa nyakati tofauti wakati akiomba kura kwa wajumbe wa Chama cha Mapinduzi wa Kata za Mkongo, Ngorongo, Kipugira na Mwasemi zilizopo katika Jimbo la Rufiji.

“Siasa zangu ni siasa za maendeleo, nimedhamiria kuwakomboa ndio maana nikilala na kuamka nawaza maendeleo ya Rujiji hivyo ninaomba kura zenu wanarufiji kwani sitowaangusha,” Mhe. Mchengerwa alisisitiza.

Mhe. Mchengerwa amewathibitishia wananchi wa Rufiji kuwa, kupitia Miradi ya Benki ya Dunia kiasi cha bilioni 30 zitatumika kujenga barabara kwa kiwango cha lami, stendi za kisasa na masoko ya kisasa.

“Moyoni mwangu ipo Rufiji hivyo mapenzi yangu kwa Rufiji hayajifichi, ninawaomba wanarufiji wenzangu mniamini kwani sitowasaliti,” Mhe. Mchengerwa ameeleza bayana.

Sanjari na hilo, Mhe. Mchengerwa amewataka wananchi wa Rufiji waendelee kumuamini kwani amejenga shule za Sekondari 22 kutoka 4 alizozikuta, amejenga shule za msingi 63 kutoka 20 alizozikuta, amejenga vituo vya afya 9 kutoka 3 vilivyokuwepo hivyo anaamini miaka 5 ijayo hakutakuwa na kata isiyo na kituo cha afya.

Mhe. Mchengerwa amehimiza kuwa, yuko tayari kuendeleza dhana yake ya mapinduzi ya fikra ya miaka 10 ya uongozi wake akiwa Mbunge wa Jimbo la Rufiji, hivyo amewaomba wananchi wa Rufiji wamuunge mkono kwa kumpa kura nyingi ili aendelee kuwatumikia na kuwaletea maendeleo.

Mhe. Mchengerwa amepata fursa ya kuomba kura kwa wajumbe wa Kata za Mkongo, Ngorongo, Kipugira na Mwasemi ikiwa ni sehemu ya Mchakato wa Kura za Maoni ndani CCM, ambapo aliambatana na wagombea wenzie wanne ambao ni Salma Ponga, Hamisa Kisoma na Seleman Mhekela ambao Julai 28, 2025 waliteuliwa na Kamati Kuu ya CCM.







Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno amefanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Mawakili ya Curtis ( Curtis, Mallet-Prevost,Colt&Mosle LLP Law firm) kwa nia ya kuanzisha fursa za ushirikiano katika maeneo mbalimbali kati ya Kampuni hiyo na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 

Hakuna ubishi kuwa kila binadamu ana ndoto kubwa za kufanikiwa kimaisha, lakini ukweli ni kwamba sio kila mwenye ndoto inaweza kutimia na pengine inaweza kutimia ila kwa kuchelewa sana.

Ndivyo maisha yalivyo, wakati mwingine hayakupi kile unachota na wakati mwingine yanakupata ambacho hukutarajia, ndilo fumbo kubwa ambalo lipo katika maisha ya kila siku hapa duniania.

Jina langu Musa, mwaka 2017 nilipata kazi katika kampuni mmoja ya kimaaifa ya kuuza vinywaji baridi, kwa hakika kazi hii ilikuwa ni nzuri na yenye mashahara mzuri ajabu.

Nilikuwa najisemea kimoyo moyo kuwa endapo nitafanya kazi hii kwa miaka miwili tu, basi nitaweza kujenga nyumba hata mbili, kununua gari na mambo mengine makubwa ya kimaendeleo.

Hata hivyo, miezi saba tu katika ajira ile, mambo yalianza kubadiika, kuna wafanyakazi wenzangu ambao walikuwa ni rafiki zangu, walianza kunipiga vita ya chini kwa chini. Soma zaidi hapa 

 

Naweza kusema hakuna furaha anayokuwa nayo mwanamke kama kuitwa Mama, daima siwezi kuisahau siku ambayo nilimshika kwa mikono yangu mtoto wangu wa kwanza kwa mara ya kwanza.

Chozi la furaha lilinitoka bila mwenyewe kujua, nilijikuta nalia tu kwa furaha niliyokuwa nayo, moyo wangu ulihemewa kwa furaha ambayo ni vigumu kuelezeka na kueleweka.

Nasema hivyo kwa sababu kuu mbili; kwanza kujifungua salama mtoto wangu wa kwanza akiwa na afya tele, pili ni kwamba niliangaika sana kutafuta mtoto hadi ukafikia wakati wa kuanza kukataa.

Jina langu kwa sasa naitwa Mama Anna, ni mkazi wa Malindi nchini Kenya, katika ndoa yangu nilikaa miaka zaidi ya mwili bila kujaliwa mtoto ingawa nilikuwa na kiu sana kumzalia mume wangu. Soma zaidi hapa 

  

Kwa zaidi ya miaka minne, nilitembea kila hospitali niliyoweza kufika nikitafuta tiba ya maumivu makali ya tumbo yaliyokuwa yananisumbua. Kila siku ilikuwa mateso. Maumivu hayo hayakuwa ya kawaida.

Yalianza taratibu kama kiungulia, kisha yakawa yanakata tumbo kwa nguvu kila baada ya kula au wakati wa usiku. Nilikuwa naishi kwa kutumia dawa za kupunguza maumivu tu, lakini shida haikuwa inakwisha.

Nilifanya vipimo vingi ultrasound, endoscopy, hata CT scan lakini kila daktari alinambia sina shida yoyote kubwa. Walikuwa wananipa antibiotics, dawa za kuondoa gesi, na chakula cha kufuata, lakini hakuna kilichobadilika.

Kuna wakati nilianza kufikiria labda ni laana, au kuna mtu alinilaani kwa sababu nilianza kupoteza uzito, nilikonda, na uso wangu ukaanza kukosa nuru. Soma zaidi hapa 

NA EMMANUEL MBATILO DAR ES SALAAM

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendela kutoa hamasa kwa washiriki wa Tuzo za Ubora kwa mwaka 2025/26 kufanya maombi ambapo wadau wameaswa kuzingatia mwisho  wa tarehe ya kutuma maombi ya ushiriki ambayo ni Julai 31, 2025, kwa vipengele vyote vilivyotangazwa, katika pande zote za Muungano wa Tanzania.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka kampuni ya Kimataifa ya uwakili ya Clyde & Co Afrika kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kufungua fursa ya mafunzo kwa Mawakili wa Serikali.

  


Nilikuwa msichana mrembo, mwenye maadili na roho ya kupenda kweli. Lakini kwa miaka mingi, kila mwanaume aliyekuja maishani mwangu aliniacha nikiwa na moyo uliovunjika.

Walikuwa wananitumia, kuniahidi ndoa, kisha baada ya kunipata, walinigeuka kana kwamba mimi si chochote. Nilijaribu kubadilika, kujifunza kutoka kwa makosa yangu, hata kufunga na kuomba lakini haikubadilika chochote. Ilikuwa kana kwamba nililaaniwa kwenye mapenzi.

Marafiki zangu walinicheka. Waliniita “malkia wa heartbreak.” Mama yangu aliniambia pengine najaribu sana. Kila nilipojaribu kuelezea uchungu wangu, walidhani labda mimi ndiye tatizo.

Nilipoingia kwenye uhusiano na kijana mmoja wa kanisani ambaye kila mtu alimwona kama mtakatifu, nilidhani labda huyu ni wa mwisho. Lakini hata yeye alinilaghai, alinitumia kisha akaoa msichana mwingine bila kuniambia. Hapo ndipo moyo wangu ulivunjika kabisa. Soma zaidi hapa 

NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imefungua mafunzo ya siku tatu ya Uongozi na Usimamizi wa Shule pamoja na Utawala Bora wa Elimu kwa Maafisa Elimu kutoka mikoa yote 26 na Halmashauri zote 184 za Tanzania Bara yakiwa na lengo la kuongeza ufanisi na kuimarisha usimamizi wa sekta ya elimu nchini.

  

Hii ni simulizi yangu ya kweli, na kama mwanaume, ilikuwa ni aibu kuu kukiri kuwa nilikuwa nimeishiwa nguvu za kiume. Nilianza kwa kupuuza, nikidhani ni stress au uchovu wa kawaida.

Lakini miezi ilivyopita, hali haikubadilika badala yake, ilizidi kuwa mbaya. Nikiwa na miaka 34, mke wangu alianza kuonekana mwenye huzuni. Alikuwa mpole lakini mbali. Sikuhitaji kuuliza kujua kwamba alikata tamaa.

Tulijaribu kila kitu. Nilinunua virutubisho vya bei ghali, nilifuata mazoezi ya mtandaoni, nikabadilisha chakula changu. Nilijaribu hata kunywa vitu vya ajabu nilivyoshauriwa na marafiki asali ya tembo, mzizi wa mti fulani kutoka Kilimanjaro, hata supu ya pweza!

Lakini haikusaidia. Mke wangu, ambaye alinivumilia kwa upole na heshima, alianza kujifungia zaidi. Alikubali hali kimya kimya lakini macho yake yaliniambia kila kitu alikuwa karibu kuniondoka. Soma zaidi hapa 

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL) wamesaini mkataba wa makubaliano na Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways) katika uboreshaji wa viwango vya uendeshaji na kuongeza ushindani katika soko la usafiri wa anga la kikanda na kimataifa.

 

Nakumbuka tangu utotoni mwangu nilitaka kuwa mfanyabiashara anayeheshimika nchini Kenya, nilikua na ndoto hizo ila sikuwahi kujua wakati mmoja ndoto hii ingekuja kutumia kwa kuwa nilitoka familia isiyona fedha.

Nilipomaliza Chuo Kikuu niliaamua kujitosa katika biashara, hivyo niliweza kuzungumza na wazazi wangu na kuwaomba waweze kunipa usaidizi wa kifedha kwa kuwa nilizokuwa nazo kwenye akiba yangu hazikuwa zinatosha.

Wazazi wangu walikua na ugumu kidogo kuzitoa fedha hizo lakini walikuja wakazitoa baadaye hivyo nikaanza biashara za kuuza nguo katikati mwa jiji.

Nilikua na matumaini mengi ya biashara hiyo kuweza kufanikiwa, nilipofungua biashara hiyo kulikuwepo na biashara nyingine kama yangu, kwa upande wangu nilinunua bidhaa zenye dhamani ya Sh2,000,000 na kuingia katika soko la ushindani. Soma zaidi hapa 

 


๐Ÿ“ŒYanahusisha ushiriki wa ajira kwa wazawa, mapato kwa nchi na utoaji huduma EACOP

๐Ÿ“Œ Atembelea ujenzi wa kiwanda cha kuweka mifumo ya upashaji na utunzaji joto kwenye mabomba ya EACOP kilichoko Sojo

๐Ÿ“Œ Apongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa utashi wake kutekeleza mradi wa EACOP

๐Ÿ“Œ Dola za kimarekani Bilioni 5.65 kutumika ujenzi wa bomba la EACOP hadi kukamilika


Na Neema Mbuja, Nzega

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Sekta ya Mafuta na Gesi Wizara ya Nishati, Dkt James Mataragio, amesema utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP)  unazingatia maslahi mapana ya nchi ikiwemo upatikanaji wa ajira kwa wazawa, kuongezeka kwa pato la Taifa na ushirikishwaji wa kampuni za wazawa kutoa huduma kwenye utekelezaji wa mradi wa EACOP.

Dkt.  Mataragio ameyasema hayo leo tarehe 28 Julai, 2025 wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara yake ya kutembelea na kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa EACOP hususani utekelezaji wa makubaliano kwenye mradi huo.

Akiwa kwenye kiwanda cha kuweka mifumo ya upashaji na utunzaji wa joto(Thermal Insulation System )Dkt.Mataragio alijionea namna mabomba yatakayotumika kusafirisha mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga yanavyoandaliwa na kuwekwa teknolojia maalumu ya kudhibiti kutu eneo la Sojo wilaya ya Nzega mkoa wa Tabora.

‘’ Wizara ya Nishati ndio mwenye dhamana ya kusimamia maslahi ya Serikali chini ya TPDC na tumeridhika na maendeleo ya utekelezaji wa mradi  kwa kuzingatia sheria na mikataba iliyopo, ambapo mpaka sasa fedha zote za mradi wa EACOP zimepatikana kwa asilimia mia moja’’ Amesema Dkt Mataragio

Ameongeza kuwa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki unaendelea kwenye mikoa ya Kagera, Geita, Tabora,Singida,Dodoma,Manyara,na Tanga na utahusisha pia ujenzi wa vituo 4 vya kuongeza msukumo wa mafuta(Pump Stations) na vituo viwili vya kupunguza msukumo wa mafuta(Pressure reduction Stations) ambao umekamilika kwa asilimia 55

‘’ Ujenzi wa bomba la Mafuta ghafi la EACOP kwa sasa umefikia asilimia 65  na utagharimu kiasi cha Dola za kimarekani Bilioni 5.65 na jambo la kufurahisha ni kwamba ajira za wazawa takribani 9,194 zimezalishwa katika kipindi cha ujenzi wa mradi  na kati ya hizo asilimia 75 zimenufaisha wazawa’’ Amesistiza Dkt Mataragio

Amesema mpaka sasa jumla ya shilingi bilioni 60 zimepatikana kutokana na manufaa ya utekelezaji wa mradi wa EACOP ikiwemo 

Makusanyo ya pango la ardhi, ushuru wa huduma na usajili wa vibali mbalimbali kwenye halmashauri.

Ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki unatekelezwa na nchi mbili za Tanzania na Uganda ambapo kila moja ina hisa asilimia 15, ambapo UNOOC ya China asilimia 8 na Total Energies asilimia 62 ambapo mradi unatarajia kukamilika mwezi Julai, 2026.