Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amewatunuku  vyeti na kuwakabidhi zawadi ya Fedha taslimu watumishi  20  ambao wameshinda nafasi na kuwa Wafanyakazi bora katika mwaka wa fedha 2024/2025, Wafanyakazi hao ni  kutoka  katika  Kurugenzi, Idara na Vitengo kwa kampasi zote za Chuo hicho .

Akizungumza na Menejimenti na Wafanyakazi hao Prof.Mapesa amewapongeza kwa ushindi huo na amewataka Watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidi, nidhamu na Uzalendo ili kufikia Malengo ya Taasisi na Taifa kwa ujumla.

Prof. Mapesa amesema teknolojia inazidi kukua hivyo amewataka  Watumishi kuona namna bora ya kutumia E- Learning,  na kuona ni namna gani vifaa na mifumo ya Kisasa  viitaweza kutumika ili kuwafikie wadau wengi. 

Prof. Mapesa amesema  ni wajibu wa kila Mtumishi  kufanya mahala Pa kazi kuwa mahala Pa furaha,  Amani,  na sehemu salama kwa kuwa muda mwingi  mtumishi anatumia muda wake akiwa kazini.

“ Nawasisitiza sana Kwa upande wa Wanataaluma kuhakikisha tafiti zinafanyika, na Ushauri wa kitaalamu unatolewa, jipangeni kuandika na kuchapisha ikiwa ni pamoja na kuhakikisha tunatoa huduma bora kwa wateja (Customer care), kujali wateja ni jambo la msingi sana,”alisisitiza Profesa Mapesa.

Katika hatua nyingine Prof. Mapesa ameungana na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan katika kuomboleza kifo cha Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Cleopa David Msuya ambapo amesema Taifa limepoteza mtu muhimu kwa namna moja ama nyingine  kwa kuwa Mzee  Msuya alikuwa ni miongoni mwa Wazee walioshirikiana na baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere katika kukijenga Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Mipango, Fedha na Utawala Dkt. Evaristo Haulle alivitaja  vigezo vilivyotumika kumpata Mfanyakazi bora kuwa ni sharti awe Mtumishi wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa Zaidi ya mwaka mmoja, awe na mahusiano mazuri na viongozi  na Wafanyakazi wenzake, asiwe mtu wa Majungu na awe tayari kulinda Uchumi na kudumisha Amani.

Katika hafla hiyo fupi ambayo ilishirikisha viongozi wa vyama vya Wafanyakazi, Chama cha Wafanyakazi wa Taaasisi, Elimu ya juu, Sayasni, Teknolojia, Ufundi Stadi, Habari na Utafiti (RAAWU), Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu (THTU) na MNIMASA.

Kwa upande wa Wafanyakazi bora waliowakilisha Chuo Dkt. Willy Maliganya upande wa Wanataaluma,  na Bwana. Atanas Limbu upande wa Waendeshaji wameushukuru Uongozi wa Chuo na kusema kuwa zawadi zilizotolewa zinatoa motisha kwa Wafanyakazi kujituma na kufanya vizuri na kuwa ushindi uliopatikana siyo wa kwao peke yao bali ni wa Chuo kizima.







Share To:

Post A Comment: