![]() |
Kaimu Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mahusiano kwa
Umma- TAWA ,Twaha Twaibu akizungumza na waandishi wa habari |
NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
MAMLAKA ya
Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imeshiriki kwenye mkutano wa 17
wa maafisa habari ,Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali mkoani Tanga kwa
lengo la kutumia fursa hiyo kutangaza vivutio vya utalii
vinavyopatikana kwenye mapori ya akiba na Mapori tengefu nchini.
Mkutano
huo ulifunguliwa juzi na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya
Habari Mhe. Nape Nnauye (Mb) ambapo akizungumza wakati wa mkutano huo
alitumia
fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais na Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassan
kwa jitihada zake za dhati za kufungua sekta ya Utalii nchini.
Pia
Waziri huyo aliwataka Maafisa Habari na Mawasiliano kuhakikisha tovuti
na mitandao ya kijamii ya Taasisi inatumia fursa hiyo kutangaza vivutio
vya utalii na habari nyingine za Taasisi zinazoisemea.
Naye
kwa upande wake, Kaimu Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mahusiano kwa
Umma- TAWA ,Twaha Twaibu amesema TAWA inashiriki kwenye mkutano huu kwa
lengo kubwa la kuendelea kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana
kwenye maeneo yao .
Alisema hiyo ni kama
jitihada za kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan wa
kutangaza vivutio nchini kwa kupitia filamu maalumu ya "Royal Tour"
iliyozinduliwa hivi karibuni.
Akizungumzia kauli ya Waziri Nape ya kutoa siku 14 kwa Maafisa Habari kutumia tovuti na mitandao ya Kijamii, alisema TAWA imepokea maelekezo hayo na itaendelea kutumia mitandao ya kijamii na tovuti za Taasisi kama nyenzo muhimu ya kujitangaza.
Katika mkutano huo mkubwa umeshirikisha wadau
wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kutoka Taasisi mbalimbali
za serikali zilizopo Tanzania Bara na Visiwani.
Post A Comment: