LICHA ya wafanyabiashara wa Soko la Sabasaba Jijini  kutishia kuandamana hadi kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Ili kumfikishia kilio chao cha kuondolewa katika eneo hilo, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru ameendelea  kuwataka wafanyanishara hao kupisha ukarabati wa soko hilo huku akieleza lengo la serikali ni jema kwa maslahi ya wafanyabaishara hao na siyo vinginevyo.


Hayo yanajiri ikiwa ni hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka kuagiza Jiji la Dodoma kufanya mkakati wa Uboreshaji wa Soko hilo kwa kuwaorodhesha wafanyabiasha wote katika mfumo maalum ili kuweza kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza hapo baadaye.


Akiongea na waandishi wa habari leo Aprili 20, 2022 Ofisini kwake amesema lengo la Jiji ni kuwahamisha kwa muda wafanyabiashara hao ili kufanya ukarabati wa soko hilo na baada ya ujenzi huo kukamilika watawarudisha kuendelea na shughuli zao kama kawaida.


"Zoezi hili tunalifanya kwa uwazi,tuliwashirikisha wafanyabiashara wote na kilichobaki sasa ni kuhakiki ili kuwatambua nani anamiliki nini na anafanya nini na kuwaondoa hofu kuwa tunakwenda kuwahamisha kwa muda ili kupisha ujenzi wa eneo hilo kwa muda wa mwaka mmoja au miwili kulingana na mchoro wetu”amesema Mafuru


Aidha amesema soko hilo ni la historia na limechakaa kutokana na kuwa  ni la muda mrefu tangu mwaka 1996 halijafanyiwa ukarabati wa miundominu yake hivyo ni wakati muafaka wa kuhakikisha linakarabatiwa kisasa zaidi kulingana na mahitaji na kuweza kuhudumia zaidi ya wafanyabiashara 7000 .


"Lengo la jiji ni kuboresha mazingira ya wafanyabiashara na si kuwadhulumu,imefika wakati wafanyabiashara kuelewa Dodoma Sasa ni Jiji na ndiyo Makao makuu ya nchi na soko la Sabasaba limekuwa halina hadhi lazima tufanye ukarabati,"amefafanua na kuongeza;


Mvua ikinyesha pale Sabasaba watu wanashindwa kufanya shughuli zao kwa utaratibu  tope linakuwa la kutisha na nimekuwa nikipokea  malalamiko mengi kuwa tunachukua ushuru lakini hatufanyi ukarabati”amesema Mafuru


Amesema jiji halina lengo la kuwaonea wafanyabiasahara bali kinachotakiwa ni kuwashirikisha kila hatua ili kuweza kupata uelewa wa pamoja na kila mtu kuridhika na maamuzi hayo.


Hata hivyo amesema malalamiko ambayo wamekuwa wakiyapata yanaonyesha kuwa wafanyabiashara hao hawana imani na jiji katika kutekeleza mpango huo hivyo Kutoa nafasi ya kuwahudumia huku akitoa maelekezo kwa  wapangaji waliojimilikisha zaidi ya kibanda kimoja kuwa  watamiliki kibanda kimoja tu ili kuwapa nafasi watu wengine .


"Kuna baadhi ya wafanyabiashara wamejimilikisha zaidi ya vibanda 20 na kuvipangisha kwa watu wengine kwa bei ya juu niseme wazi kuwa baada ya ukarabati huo Kila mfanyabiashara atakuwa na haki ya kumiliki kibada kimoja ili kila mfanya biashara awe na fursa,"amesema


Naye Afisa biashara wa Jiji la Dodoma Donatila Vedasto amesema lengo la  kuwahamisha kwa muda wafanyabiashara ni kupisha uboreshaji wa miundombinu na kwamba mpango huo ni wa kitambo lakini haukutekelezwa kwa wakati kutokana na ufinyu wa bajeti uliokuwepo.



Amesema ili kupata kauli moja wanapanga kuendelea na vikao vya kujadilina baina ya jiji na uongozo wa soko hilo ili kupata namna bora ya kufikia mwafaka.


“Kuna watu wanahofu kupoteza vibanda vyao hasa wale wenye maeneo zaidi ya moja lakini ni wahakikishie kuwa kupitia mazungumzo tutafikia mwafaka na hakuna atakaye poteza haki yake waelewe tuu tunafanya uhakiki ili kujilidhisha na idadi ya wafanyabiasahara iliyopo”amesema


Amesema "Soko la sababasa miundombini yake imechakaa na hata ukienda sasa hivi kuko wazi lakini pia hili ni jiji na makao makuu hatuwezi kuwa na soko la aina ile  kama jiji tukasema kuwe na kitu cha kufanya kuboresha soko kama hadhi ya jiji na kuendana na makao makuu ya nchi,


Tukawaza kuweka mkakati kwa maana katika mradi huu tutanza ujenzi mwezi wa saba na  huwezi kuanza bila kuwashirikisha wadau ,vikao vimeanza tangu mwaka jana kuhusiana na changamoto kikubwa miundombinu vikao vya kuanza kujenza tumeanza mwezi wa kwanza wtaalam walikuja tukawashirikisha," amesema Afisa huyo wa Biashara .


Share To:

Post A Comment: