Articles by "afy"
Showing posts with label afy. Show all posts

 


Kamishna wa Madini Nchini Dkt. Abdul Rahmani  Shaban Mwanga kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa amefanya ziara ya kikazi Kituo cha Jemolojia Tanzania  (TGC) na kukutana na timu ya Menejimenti ya Kituo hicho huku akielezea madhumuni ya ziara hiyo ikiwa ni kujitambulisha.

Dkt.Mwanga amekipongeza kituo hicho kwa kuendelea kutoa mafunzo ya uongezeaji thamani madini nchini na kuhamasisha watanzania kuendelea kupeleka wanafunzi kujiunga na kituo hicho.

Sambamba na hilo Dkt. Mwanga ameagiza uongozi wa Kituo hicho kuongeza juhudi katika kukifanya Kituo hicho kuzidi kutambulika Kimataifa na kuvutia wateja na wadau wa sekta ya madini kutoka ndani na nje ya nchi.

Pia amekitaka Kituo cha Jemolojia Nchini (TGC) kuendelea kutoa huduma zinazoendana na soko la madini Duniani kama vile huduma za Kimaabara za utambuzi wa madini ya vito pamoja na bidhaa za usonara.

Kwa upande wake Mratibu wa Kituo cha Jemolojia Daniel Kidesheni
amesema kuwa, Kituo hicho kinatoa huduma mbalimbali za uongezaji thamani madini kwa wadau ikiwa ni pamoja na utambuzi wa madini ya vito, usanifu madini pamoja na uchongaji wa vinyago vya miamba.

 

 

 

Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Jiji la Arusha katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid ambapo amewataka vijana kutambua kuwa anawahangaikia kwani wao Ni nguvu kazi ya Taifa.



Rais wa jamburi ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemuagiza mkuu wa wa mkoa wa Arusha John Mongela kwenda wilaya ya Ngorongoro kuangalia tofati zilizopo Kati ya wananch wanaoishi  ndani ya hifadhi  na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ili kuangalia namna ya kutatua

Mhe.Rais alisema kuwa  huko awali kulikuwa na migogoro mingi Sana, kwani vijiji vingi vimeingia kwenye hifadhi ,lakini wakaangalia migogoro hiyo kwa undani zaidi ya vijiji 100 wameamua kuviacha vilipo, kwani wakivihamisha hakuna pa kuvipeleka

Aidha alimshukuru Leigwanani Kisongo kwa kumwambia kwamba Serikali ikikaa pamoja na wafugaji wanaoishi ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, mgogoro huo utatatulika,hivyo Rais wameahidi kumtuma mkuu wa mkoa kutafuta Suluhu.

"Vijiji zaidi ya Mia moja tumeviacha vibakie vilipo ,tukiviahamisha hatuna pa kuvipeleka,Ila nakushukuru Sana Leigwanani Kisongo kwamba umetuambia tukikaa na sisi mgogoro utatatuta,nataka nikuahidi namleta mkuu wa mkoa aje kukaa na ninyi yakimshinda nitaingia mwenyewe" Alisema Rais.

Wakati huohuo Mhe.Rais amempa miezi 3 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya karatu Rajabu Karia Magara kuhakikisha anakamilisha  ujenzi wa hospital hiyo ili kumaliza tatizo la wqgonjwa kukosa huduma ya matubabu 

  Karatu Kuna hospitali ya wilaya ambayo imeanzwa kujengwa kuanzia mwaka 2019 fedha yote umetolewa ipo pale iqna hospitali haijaisha, nakupa miezi mitatu kwasababu fedha yote unayo sioni kwanini hospital haijaisha Ina mwaka wa pili Sasa haijaisha"Alisema Mhe.Samia

Amemtaka kuhakikisha kuwa  hospitali hiyo inamalizika kwa muda alioutoa ili akienda  Karatu nikute imemalizika nije niifungie na wannachi wapate huduma 
 tukiviahamisha hatuna mahali pa kuvipeleka

Akizungumza juu ya ujenzi wa Stendi Jiji la Arusha Mhe.Rais Alisema kuwa hlmshauri Jiji ipeleke mchoro kwani Serikali inamradi wanaandaa wa kuomba fedha hivyo zikipatikana watazileta kwaajili ya ujenzi wa Stendi hiyo

Kuhusu suala la machinga. Alisema kuwa hawawezi kuruhusu sir za mjini kuharibiwa Ila utatafutwa utaratibu Maalum ili kuhakikisha wanpatiwa maeneo ya kufanya biashara zao

Kuhusiana na masuala ya mikopo kwaajili ya kuinua uchumi alisema kuwa mikopo yenye masharti nafuu kwaajili ya manufaa ya Taifa ataiileta Ila mikopo kichefuchefu hatoweza kunichukua kwasababu inawasogeza watanzania inaleta Maendeleo hivyo hataogopa kuichukua

Nataka kuwaahidi watanzania nitaangalia mikopo yenye unafuu kwa nchi yetu, inayoleta faida kwa nchi yetu hiyo nitaichukua, mikopo chechefu sitaichukua lakini ile ambayo inaleta nafuu kwa nchi yetu, inatusogeza watanzania inaleta maendeleo hiyo sitaogopa nitaichukua,”- Rais Samia Suluhu Hassan.
Watu 27 waliofanyiwa uchunguzi kama wameambukizwa ugonjwa wa corona, akiwepo dereva wa taxi ambaye alimbeba mgonjwa wa kwanza Isabella Mwampamba wamebainika hawana virusi vya ugonjwa huo.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi msaidizi wa kitengo cha ufuatiliaji wa magonjwa ya mlipuko katika Wizara ya Afya, Dk Janeth Mghamba akiwa na mtaalam wa majanga wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dk Faraja Msemwa. 

Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha, maafisa hao wa Wizara ya Afya nchini Tanzania, wamesema watu hao 27 walichukuliwa sampuli baada ya kubainika kuwa walikutana na dereva wa teksi ambaye alimbeba mgonjwa wa kwanza wa  Corona nchini Tanzania.

"Watu hawa walikuwa karibu na dereva na baada ya kuchukuliwa vipimo na kupelekwa maabara kuu iliyopo jijini Dar es Salaam wamebainika hawajaambukizwa." Amesema Dk Mghamba. 

Pamoja na hayo amesema kuwa watu hao, wataendelea kufuatiliwa hadi vitakapofanyika vipimo vya mara tatu kama ambavyo Shirika la Afya Duniani WHO imeagiza.