Articles by "MWENGEMAALUMUHURU2021"
Showing posts with label MWENGEMAALUMUHURU2021. Show all posts
Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Elirehema Doriye akizindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo.  Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Elirehema Doriye akizindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja  Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akizungumza katika uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja. Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akizungumza katika uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Elirehema Doriye akizungumza katika uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja.  Baadhi ya wadau wa NIC wakifuatilia uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC) imezindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba  3,2022 Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati akifungua huduma hiyo, Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto amewataka watumishi wa NIC kufuata ahadi iliyowekwa kwenye mkataba huo na asiwepo mtumishi yeyote wa kutenda kinyume na mkataba huo kwani atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria na Miongozo ya Utumishi wa Umma.

Amesema madhumuni ya mkataba huu ni kuboresha uhusiano baina ya Shirika na wateja wake lakini pia ukikusudia kuongeza uelewa kuhusu aina na ubora wa huduma zinazotolewa, haki na wajibu wa mteja na jinsi anavyoweza kuwasiliana.

"Mkataba wa Huduma kwa Mteja ni makubaliano kati yenu watoa huduma na mteja wenu ikiwa ni ahadi ya kutoa huduma bora kwa mteja, mkataba huu unaelekeza na kuainisha viwango vya huduma ambavyo wateja wenu wanatarajia kupata ili kufikia malengo yao". Amesema

Aidha amesema Ofisi ya Msajili wa Hazina na Serikali kwa ujumla ipo tayari kuwapa ushirikiano mnaostahili ikiwa tu mtaweka bidii katika kazi na kuboresha huduma zaidi ya zilivyo sasa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa NIC Dkt. Elirehema Doriye, amesema Shirika limekuwa likifanya mabadilikko kwenye kuwahudumia wateja ambapo wamekuwa wakiboresha huduma ili kuendana na ushindani ulioko sokoni jambo lililowavutia wateja kununua bidhaa zao za Bima na kuwafanya kuwa na ukuaji wa faida ya zaidi ya asilimia 100 katika miaka minne mfululizo.

"Mojawapo ya misingi inayotuongoza NIC yetu ni kutambua kuwa siku zote "Mteja Kwanza" yaani "Customer first" hii inamaanisha kwamba mteja kwetu ni kipaumbele namba moja katika utoaji huduma". Amesema Dkt.Doriye.

Aidha Dkt.Doriye amesema katika kuadhimisha wiki hii na kutambua umuhimu wa wateja, Shirika limezindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja "ikiwa ni ahadi yetu kwa wateja kuwa tutawapatia huduma inayostahili kulingana na ahadi tuliyowapa". Amesema

 

Watanzania wameaswa kujitokeza na kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa sahihi wakati wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 litakayofanyika nchi nzima Agosti 14, 2022.

Akizungumza jana mkoani Njombe wakati akizindua Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango alisema kuwa lengo la Serikali la kufanya zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ni kupata takwimu zitakazoisaidia katika uandaaji wa sera na mipango mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya wananchi.

“Ninawasihi sana Watanzania mjitokeze na kutoa ushirikiano wa kutosha ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa sahihi na taarifa zitakazokusanywa zitakuwa siri na zitatumika kwa ajili ya matumizi ya Sensa peke yake” Alisisitiza Makamu wa Rais

Aidha, Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Mpango amewataka waratibu na viongozi mbalimbali kuwaandaa wananchi nchi nzima ili waweze kushiriki zoezi la Sensa.

“Naamini wananchi wakiwa na uelewa wa kutosha watatoa ushirikiano unaohitajika, hivyo nawaomba viongozi wote wa Vyama vya Siasa, dini na Serikali muelimishe wananchi umuhimu wa kuhesabiwa” Alisisitiza Makamu wa Rais.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako alisema kuwa baada ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022 vijana sita waliondaliwa kutoka Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar, wataukimbiza Mwenge wa Uhuru katika mikoa 31 na halmashauri 195 nchini kwa siku 195.

“Mwenge wa Uhuru utafanya kazi ya kuhamasisha amani, umoja, upendo na mshikamano wa kitaifa pamoja na kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo katika maeneo yao ambapo ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu umezingatia, hoja, na vipaumbele vya Serikali ikiwa ni pamoja na umuhimu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 na kauli mbiu ya Mwenge mwaka huu ni Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo: Shiriki kuhesabiwa, tuyafikie Maendeleo ya Taifa”. Alisema Profesa Ndalichako.



 

 Na Amiri Kilagalila,Njombe


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2022 zitakazo fanyika mkoani Njombe tarehe mbili mwezi April.

Katibu mkuu ofisi ya waziri mkuu Prof. Jamal Katundu ametoa taarifa hiyo mkoani Njombe mara baada ya kukagua uwanja wa Sabasaba uliopo mjini Njombe kutakapofanyika sherehe hizo.

“Ukiangalia uwanja zaidi ya 90% umekamilika kwa hiyo nitumie nafasi hii kuwapongeza Njombe na kuwaomba wananchi mjitokeze kwa wingi tarehe mbili katika uzinduzi wa mbio za mwenge.tunategemea mgeni rasmi atakuwa makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Philip Mpango”alisema Katundu

Prof. Katundu amesema ameridhishwa na hali ya maandalizi inayoendelea ambapo amepongeza kamati za maandalizi za mkoa wa Njombe kwa kuandaa maonesho ya wajasiriamali ambayo yameanza ikiwa ni siku chache zimebaki kabla ya siku ya uzinduzi wenyewe.

“Kwa mara ya kwanza wanaNjombe wamejiongeza,kabla ya kufikia kilele watakuwa na shughuli mbali mbali za kibiashara tuwaombe pia watu wajitokeze kwenye hayo maonesho”aliongeza Katundu

Wakazi wa mkoa huu wameendelea na shughuli mbalimbali za maandalizi huku wakihamasishana kujitokeza kwa wingi. Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuzinduliwa Mkoani Njombe kwa mwaka huu 2022 ukiwa na kauli Mbiu “Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo Shiriki Kuhesabiwa Tuyafikie Maendeleo ya Taifa.”


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (kulia) akisisitiza jambo kwa Viongiozi wa Mkoa wa Njombe na Kamati ya Mkoa alipofanya ziara ya kukagua Maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Uwanja wa Sabasaba. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi. Judica Omari. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Kissa Kasongwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (wa pili kutoka kushoto) akiwa ameongozana na Viongiozi wa Mkoa wa Njombe na Kamati ya Mkoa alipofanya ziara ya kukagua Maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Uwanja wa Sabasaba Februari 23, 2022. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Mhandisi Marwa Rubirya.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (katikati) akikagua sehemu ya ukoka katika uwanja wa Sabasaba alipotembelea kwa lengo la kukagua Maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Mhandisi Marwa Rubirya (kulia) akifafanua jambo wakati walipokutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye UlemavU) Mhe. Prof. Joyce Ndalichako walipotembelea uwanja wa Sabasaba kwa lengo la kukagua Maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akivalishwa Skafu na vijana wa Halaiki alipowatembelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Mpechi. 
Sehemu ya vijana wa Halaiki wakiwa katika mazoezi katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Mpechi kuelekea katika uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na vijana wa Halaiki alipowatembelea katika Shule ya Sekondari Mpechi kwa lengo la kukagua maandalizi ya mazoezi yao kuelekea katika uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi. Judica Omari akitoa taarifa ya Mkoa kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa lengo la kukagua Maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amepongeza Kamati ya Maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa hatua nzuri waliyofikia kuelekea katika uzinduzi wa tukio hilo muhimu linalotarajiwa kufanyika Aprili 2, 2022 Mkoani Njombe.  

 

Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwenye kamati hiyo, Waziri Ndalichako alieleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi na kuipongeza kamati ya Mkoa kwa kuendelea kusimamia na kuratibu vyema shughuli hiyo ya maandalizi.

 

“Kwa namna maandalizi haya yanavyoendelea vizuri inadhihirisha kuwa tulifanya maamuzi sahihi kuteua Mkoa wa Njombe kuwa ni sehemu ambayo Mbio za Mwenge wa Uhuru zitazinduliwa,”

 

“Hongereni kwa maandalizi ambayo mmefanya mpaka sasa na niwapongeze kwa kuonyesha utayari wa kuhakikisha shughuli hii ya kitaifa inafana, maana maandalizi mazuri yataleta heshima kwa Mkoa huu, hivyo mzingatie masuala yote ya msingi yatakayofanya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Njombe una kuwa wa kihistoria,” alisema Waziri Ndalichako 

 

Aliongeza kuwa, kila mwaka Mwenge wa Uhuru hukimbizwa katika Mikoa, Wilaya na Halmashauri zote nchini ikiwemo Bara na Visiwani.

 

Waziri Ndalichako alifafanua kuwa Serikali imepanga kufanya Sensa ya Wat una Makazi mwezi Agosti 2022, hivyo kauli mbiu ya Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2022 ni; Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo; Shiriki Kuhesabiwa, Tuyafikie Maendeleo ya Taifa. 

 

Sambamba na hayo Mheshimiwa Ndalichako aliwasihi wajumbe wa Kamati hiyo ya Mkoa kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja ili kufanikisha utekelezaji wa majukumu yao katika shughuli hiyo ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani humo.

 

Pia, Waziri Ndalichako alipokeza Mkoa kwa namna umekuwa ukishirikisha wadau ili waweze kujitokeza na kuchangia ufanikishaji wa shughuli hiyo ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru. 

 

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Mhandisi Marwa Rubirya alisema kuwa Mkoa huo umejipanga vyema na maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru na aliahidi kusimamia shughuli zote za maandalizi kwa ufanisi na kukamilisha ndani ya muda uliopangwa.

 

“Nikuhakikishie uteuzi huu tutautendea haki na tutawezesha wananchi wa Mkoa wa Njombe wanashiriki katika tukio hilo muhimu na kutumia fursa hiyo ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kujitangaza kama Mkoa,” alisisitiza Mhe. Rubirya

Katika ziara hiyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako alitembelea Uwanja wa Sabasaba ambapo uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kufanyika, pia aliwatembelea vijana wa Halaiki katika Shule ya Sekondari Mpechi Mkoani Njombe.

 



PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

OWM - KVAW

 


Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Modest Mkude, kushoto, akimkabidhi Mwenge wa uhuru Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, Tayari kwa kukimbizwa wilayani humo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akiushika Mwenge wa Uhuru tayari kwa kukimbizwa wilayani humo leo.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, akiushika Mwenge wa Uhuru.
Mbunge wa Jimbo la Solwa Ahmed Salum, akiushika Mwenge wa Uhuru.
Mbunge wa Vitimaalum mkoani Shinyanga Christina Mzava, akiushika Mwenge wa Uhuru.
Mbio za Mwenge wa Uhuru zikianza wilayani Shinyanga kwa kukagua miradi na kuweka jiwe la msingi.
Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru Luten Josephine Mwambashi, akikagua ujenzi wa Maabara ya Sayansi katika shule ya Sekondari Mwalukwa.
Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru Luten Josephine Mwambashi, akiweka Jiwe la Msingi katika Zahanati ya Bushushu.
Muonekano wa Jengo la Zahanati ya Bushushu.
Kiongozi wa Mbio Maalum wa Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi, akiweka Jiwe la Msingi katika Nyumba za Watumishi mkoani Shinyanga zilizopo Negezi Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa nyumba za watumishi.
Kiongozi wa Mbio Maalum wa Mwenge wa Uhuru Luten Josephine Mwambashi, akiweka jiwe la msingi katika Jengo la Uthibiti ubora wa Shule Kanda ya Magharibi.
Muonekano wa Jengo la Uthibiti ubora wa Shule Kanda ya Magharibi.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vija na Ajira, akifungua maji katika mradi wa maji Masekelo wa mtandao wa Ziwa Victoria ambao ulitembelewa na Mwenge wa Uhuru kuona maendeleo yake ya utoaji huduma kwa wananchi.
Koplo Rehema Ali Haji ambaye ni Miongoni mwa viongozi wa Mbio Maalum wa Mwenge wa Uhuru, akimtwisha ndoo ya Maji Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, kwenye mradi huo wa maji wa Masekelo unotekelezwa na Mamlaka ya maji na usafi wa Mazingira mjini Shinyanga (SHUWASA.)
Ukaguzi wa mfumo wa TEHAMA katika Shule ya Sekondari Uhuru ukiendelea na viongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Awali Mkuu wa wilaya ya Shinyanga kushoto Jasinta Mboneko, akiwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi katikati wakiendelea na ukaguzi wa miradi.
 
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Luteni Josephine Mwambashi, ameweka mawe ya msingi na kuona miradi mbalimbali ya maendeleo Wilaya ya Shinyanga (Manispaa ya Shinyanga na wilaya ya Shinyanga), ambapo ameridhishwa na miradi hiyo na hakuna ambao ameukataa.

Zoezi la Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru kitaifa wilayani Shinyanga limefanyika leo Jumapili Julai 11,2021 mara baada ya Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Modest Mkude, kuukabidhi kwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko katika viwanja wa michezo Shule ya Sekondari Mwalukwa wilayani humo.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi yote sita Luteni Mwambashi amesema ameridhishwa na miradi hiyo ambayo imeendana na thamani ya fedha (Value for Money), huku kukiwa na salio la fedha kwenye baadhi ya miradi, na kuagiza ile ambayo haijakamilika kujengwa ikamilishwe haraka ili ianze kutoa huduma.

“Nimekagua miradi yote iko vizuri, na nimeweka jiwe la msingi, na ile ambayo nimetoa maelekezo yafanyiwe kazi, pamoja na kuikamilisha ile ambayo bado ipo kwenye hatua ya ujenzi ili itoe huduma haraka kwa wananchi,”amesema Luteni Mwambashi.

Pia amewapongeza wananchi wa Bushushu kwa kujitoa kuchangia ujenzi wa Zahanati, ambayo itawasaidia kuondokana na adha ya kufuata huduma za matibabu umbari mrefu.

Akitoa ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, amewataka Watanzania, kudumisha amani, kuendeleza mapambano ya Rushwa, madawa ya kulevya, virusi vya Ukimwi, Malaria, kuzingatia lishe bora kwa watoto, pamoja na Halmashauri kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato kwa njia ya kieletroniki.

Kwa upande wao Wabunge wa Shinyanga, akiwamo Mbunge wa Jimbo la Solwa Ahmed Salum, Patrobas Katambi Jimbo la Shinyanga mjini, pamoja na Christina Mzava wa viti maalum, kwa nyakati tofauti waliahidi kuendelea kuwaletea maendeleo wananchi, pamoja na kukamilisha maboma yaliyosalia kujengwa.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akisoma taarifa ya mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, amesema umekimbizwa Kilomita 136, pamoja na kukagua miradi sita yenye gharama ya Sh. milioni 855.

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni, Ujenzi Maabara ya Sayansi katika shule ya Sekondari Mwalukwa, Zahanati ya Bushusu, Nyumba nne za watumishi, Jengo la Uthibiti ubora wa shule Kanda ya Magharibi, chumba cha Tehama katika Shule ya Sekondari uhuru, pamoja na kuona maendeleo ya mradi wa maji Ziwa Victoria Masekelo.

Katika hatua nyingine Mboneko amewashukuru wananchi wa Shinyanga, kujitokeza kwa wingi kwenye mbio hizo za Mwenge wa uhuru, huku akiwataka kuendelea kushirikiana na Serikali kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo.

Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2021 inasema “Tehama ni msingi wa Taifa endelevu, Itumike kwa usahihi na uwajibikaji"
 


Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi (wa pili kulia) akizungumza baada ya kuona uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) leo Jumapili Julai 11,2021.
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola (kushoto) akimwelezea Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kuhusu Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na SHUWASA kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Jasinta Mboneko akielezea jambo wakati Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi akiangalia uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko wakifungua maji katika Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Mmoja wa Wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, Koplo Rehema Haji akimtwisha ndoo ya maji Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini (CCM) baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kuangalia na kuridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini (CCM) akifurahia akiwa amejitwisha ndoo ya maji baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kujionea na kuridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga. Kulia ni mmoja wa Wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, Koplo Rehema Haji
Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 ukiwa katika Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi (wa pili kulia) akiangalia sehemu ya bomba la maji katika moja ya kaya ya mwananchi anayeendelea na ujenzi wa nyumba akitumia maji ya Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi (katikati) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola (kulia) akiangalia uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Wafanyakazi wa SHUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kuona uendelevu huo wa mradi wa maji.
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
 
 
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi ameridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji Masekelo unaohudumia mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).

Akizungumza baada ya kuona uendelevu wa mradi huo wa maji leo Jumapili Julai 11,2021 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Luteni Josephine Paul Mwambashi amesema mradi huo utasaidia kumtua mama ndoo kichwani kwa kusogeza huduma ya maji karibu na kuwapunguzia adha ya maji wananchi.

“Tumekuja hapa kuangalia uendelevu wa mradi wa maji ambao ambao jiwe lake la Msingi liliwekwa Julai 11,2019 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndugu Mzee Mkongea Ali. Tumeona uendelevu sasa wananchi wameweza kuunganishiwa maji katika kaya zao na hii ni hatua kubwa kwa sababu maji ni uhai na itasaidia kupunguza adha ya wananchi kufuata maji mbali na kutumia muda huo kufanya shughuli za uzalishaji mali”,amesema Luteni Josephine Mwambashi.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru amelishukuru Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kwa kufadhili mradi huo wa maji huku akiwataka wananchi kutunza mradi huo.

“Niwasihi wananchi kuendelea kutunza miundo mbinu ya maji ambayo inatupatia huduma hii muhimu ya maji ili yatumiwe na vizazi vijavyo.Ni matumaini yangu wananchi watatumia fursa hii kutumia maji safi na salama na kutunza mabomba ya maji”,ameongeza Luteni Josephine Mwambashi.

Akitoa taarifa kuhusu Mradi wa Maji Masekelo, Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola amesema mradi huo umejengwa kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kwa kushirikiana na SHUWASA kwa gharama za shilingi 218,962,500/= ambazo zote zimetolewa na mfadhili huyo.

Amesema ujenzi wa mradi huo ulikamilika Mwezi Desemba 2020 ukihusisha ujenzi wa mtandao wa maji wenye urefu wa mita 11,225 na vituo 14 vya kuchotea maji (DP) na ufungaji wa dira 14 za malipo ya kabla.

“Ujenzi wa Mradi huu umezingatia mahitaji maalumu ya watu wenye mahitaji maalum kwa kujenga magati katika sehemu zinazofikika kwa urahisi. Mradi pia umeweza kuunganisha wateja wapya 230 hivyo kupelekea wakazi takribani 1,380 kupata huduma ya maji moja kwa moja kwenye makazi yao”,amesema.

“Lengo la mradi huu wa maji ni kuwapunguzia adha ya maji wananchi, kumtua mama ndoo kichwani kwa kusogeza huduma ya maji safi maeneo ambayo yalikuwa hayajafikiwa na Mtandao wa maji ya Ziwa Victoria”,ameeleza Mhandisi Katopola.

Aidha, amesema SHUWASA itaendelea kuhakikisha mradi huo wa maji unakuwa endelevu kwa kuhakikisha mradi unatoa maji safi na salama kwa muda wa saa 24 kila siku isipokuwa wanapokuwa na matengenezo.

“SHUWASA inaendelea kuwasihi na itaendelea kuwashawishi wakazi wa maeneo ya Masekelo, Ndala na Ishoshandili kutumia maji safi na salama na hasa kwa kujiunga kwenye mtandao wa mabomba ili kila mwananchi aweze kupata maji katika mji wake”,ameongeza Mhandisi Katopola.