Kiongozi
 wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
 Mwambashi (wa pili kulia) akizungumza baada ya kuona uendelevu wa Mradi
 wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili 
katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na 
Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Shirika
 la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) leo Jumapili Julai 11,2021.
Kaimu
 Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola (kushoto) akimwelezea 
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni 
Josephine Mwambashi kuhusu Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala
 na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga 
unaotekelezwa na SHUWASA kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la 
Ujerumani (GIZ).
Mkuu
 wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Jasinta Mboneko akielezea jambo wakati 
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni 
Josephine Mwambashi  akiangalia uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa 
ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya 
Shinyanga
Viongozi
 mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta 
Mboneko wakifungua maji katika Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, 
Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Mmoja
 wa Wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, Koplo Rehema Haji akimtwisha 
ndoo ya maji Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na 
Ajira, Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini
 (CCM) baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 
mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi  kuangalia na kuridhishwa na 
uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji 
cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Naibu
 Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Patrobas 
Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini (CCM) 
akifurahia akiwa amejitwisha ndoo ya maji baada ya Kiongozi wa Mbio 
Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine 
Mwambashi kujionea na kuridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji katika 
mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa 
ya Shinyanga. Kulia ni mmoja wa Wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, Koplo Rehema Haji
Mwenge
 wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 ukiwa katika Mradi wa Maji katika mitaa ya 
Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya 
Shinyanga
Kiongozi
 wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
 Mwambashi (wa pili kulia) akiangalia sehemu ya bomba la maji katika 
moja ya kaya ya mwananchi anayeendelea na ujenzi wa nyumba  akitumia 
maji ya Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha 
Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Kiongozi
 wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
 Mwambashi (katikati) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. 
Jasinta Mboneko (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi 
Yusuph Katopola (kulia) akiangalia uendelevu wa Mradi wa Maji katika 
mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa 
ya Shinyanga.
Wafanyakazi
 wa SHUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji katika 
mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa 
ya Shinyanga baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru 
Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kuona uendelevu huo wa 
mradi wa maji.
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Kiongozi
 wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
 Mwambashi ameridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji Masekelo 
unaohudumia mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili 
katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na 
Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Shirika
 la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).
Akizungumza
 baada ya kuona uendelevu wa mradi huo wa maji leo Jumapili Julai 
11,2021 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Luteni Josephine 
Paul Mwambashi amesema mradi huo utasaidia kumtua mama ndoo kichwani kwa
 kusogeza huduma ya maji karibu na kuwapunguzia adha ya maji wananchi.
“Tumekuja
 hapa kuangalia uendelevu wa mradi wa maji ambao ambao jiwe lake la 
Msingi liliwekwa Julai 11,2019 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 
mwaka 2019, Ndugu Mzee Mkongea Ali. Tumeona uendelevu sasa wananchi 
wameweza kuunganishiwa maji katika kaya zao na hii ni hatua kubwa kwa 
sababu maji ni uhai na itasaidia kupunguza adha ya wananchi kufuata maji
 mbali na kutumia muda huo kufanya shughuli za uzalishaji mali”,amesema 
Luteni Josephine Mwambashi.
Kiongozi
 huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru amelishukuru Shirika la Maendeleo la 
Ujerumani (GIZ) kwa kufadhili mradi huo wa maji huku akiwataka wananchi 
kutunza mradi huo.
“Niwasihi
 wananchi kuendelea kutunza miundo mbinu ya maji ambayo inatupatia 
huduma hii muhimu ya maji ili yatumiwe na vizazi vijavyo.Ni matumaini 
yangu wananchi watatumia fursa hii kutumia maji safi na salama na 
kutunza mabomba ya maji”,ameongeza Luteni Josephine Mwambashi.
Akitoa
 taarifa kuhusu Mradi wa Maji Masekelo, Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, 
Mhandisi Yusuph Katopola amesema mradi huo umejengwa kwa ufadhili wa 
Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kwa kushirikiana na SHUWASA kwa 
gharama za shilingi 218,962,500/= ambazo zote zimetolewa na mfadhili 
huyo.
Amesema
 ujenzi wa mradi huo ulikamilika Mwezi Desemba 2020 ukihusisha ujenzi wa
 mtandao wa maji wenye urefu wa mita 11,225 na vituo 14 vya kuchotea 
maji (DP) na ufungaji wa dira 14 za malipo ya kabla.
“Ujenzi
 wa Mradi huu umezingatia mahitaji maalumu ya watu wenye mahitaji maalum
 kwa kujenga magati katika sehemu zinazofikika kwa urahisi. Mradi pia 
umeweza kuunganisha wateja wapya 230 hivyo kupelekea wakazi takribani 
1,380 kupata huduma ya maji moja kwa moja kwenye makazi yao”,amesema.
“Lengo
 la mradi huu wa maji ni kuwapunguzia adha ya maji wananchi, kumtua mama
 ndoo kichwani kwa kusogeza huduma ya maji safi maeneo ambayo yalikuwa 
hayajafikiwa na Mtandao wa maji ya Ziwa Victoria”,ameeleza Mhandisi 
Katopola.
Aidha,
 amesema SHUWASA itaendelea kuhakikisha mradi huo wa maji unakuwa 
endelevu kwa kuhakikisha mradi unatoa maji safi na salama kwa muda wa 
saa 24 kila siku isipokuwa wanapokuwa na matengenezo.
“SHUWASA
 inaendelea kuwasihi na itaendelea kuwashawishi wakazi wa maeneo ya 
Masekelo, Ndala na Ishoshandili kutumia maji safi na salama na hasa kwa 
kujiunga kwenye mtandao wa mabomba ili kila mwananchi aweze kupata maji 
katika mji wake”,ameongeza Mhandisi Katopola.
 
Post A Comment: