Kiongozi
wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
Mwambashi (wa pili kulia) akizungumza baada ya kuona uendelevu wa Mradi
wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili
katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Shirika
la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) leo Jumapili Julai 11,2021.
Kaimu
Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola (kushoto) akimwelezea
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni
Josephine Mwambashi kuhusu Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala
na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
unaotekelezwa na SHUWASA kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la
Ujerumani (GIZ).
Mkuu
wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Jasinta Mboneko akielezea jambo wakati
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni
Josephine Mwambashi akiangalia uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa
ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya
Shinyanga
Viongozi
mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta
Mboneko wakifungua maji katika Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo,
Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Mmoja
wa Wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, Koplo Rehema Haji akimtwisha
ndoo ya maji Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na
Ajira, Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini
(CCM) baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa
mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kuangalia na kuridhishwa na
uendelevu wa Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji
cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Naibu
Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Patrobas
Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini (CCM)
akifurahia akiwa amejitwisha ndoo ya maji baada ya Kiongozi wa Mbio
Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
Mwambashi kujionea na kuridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji katika
mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa
ya Shinyanga. Kulia ni mmoja wa Wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2021, Koplo Rehema Haji
Mwenge
wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 ukiwa katika Mradi wa Maji katika mitaa ya
Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya
Shinyanga
Kiongozi
wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
Mwambashi (wa pili kulia) akiangalia sehemu ya bomba la maji katika
moja ya kaya ya mwananchi anayeendelea na ujenzi wa nyumba akitumia
maji ya Mradi wa Maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha
Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Kiongozi
wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
Mwambashi (katikati) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe.
Jasinta Mboneko (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi
Yusuph Katopola (kulia) akiangalia uendelevu wa Mradi wa Maji katika
mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa
ya Shinyanga.
Wafanyakazi
wa SHUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji katika
mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa
ya Shinyanga baada ya Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru
Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi kuona uendelevu huo wa
mradi wa maji.
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya mradi wa maji katika mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili katika Manispaa ya Shinyanga.
Kiongozi
wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine
Mwambashi ameridhishwa na uendelevu wa Mradi wa Maji Masekelo
unaohudumia mitaa ya Masekelo, Ndala na kitongoji cha Ishoshandili
katika Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na
Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Shirika
la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).
Akizungumza
baada ya kuona uendelevu wa mradi huo wa maji leo Jumapili Julai
11,2021 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Luteni Josephine
Paul Mwambashi amesema mradi huo utasaidia kumtua mama ndoo kichwani kwa
kusogeza huduma ya maji karibu na kuwapunguzia adha ya maji wananchi.
“Tumekuja
hapa kuangalia uendelevu wa mradi wa maji ambao ambao jiwe lake la
Msingi liliwekwa Julai 11,2019 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru
mwaka 2019, Ndugu Mzee Mkongea Ali. Tumeona uendelevu sasa wananchi
wameweza kuunganishiwa maji katika kaya zao na hii ni hatua kubwa kwa
sababu maji ni uhai na itasaidia kupunguza adha ya wananchi kufuata maji
mbali na kutumia muda huo kufanya shughuli za uzalishaji mali”,amesema
Luteni Josephine Mwambashi.
Kiongozi
huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru amelishukuru Shirika la Maendeleo la
Ujerumani (GIZ) kwa kufadhili mradi huo wa maji huku akiwataka wananchi
kutunza mradi huo.
“Niwasihi
wananchi kuendelea kutunza miundo mbinu ya maji ambayo inatupatia
huduma hii muhimu ya maji ili yatumiwe na vizazi vijavyo.Ni matumaini
yangu wananchi watatumia fursa hii kutumia maji safi na salama na
kutunza mabomba ya maji”,ameongeza Luteni Josephine Mwambashi.
Akitoa
taarifa kuhusu Mradi wa Maji Masekelo, Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA,
Mhandisi Yusuph Katopola amesema mradi huo umejengwa kwa ufadhili wa
Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kwa kushirikiana na SHUWASA kwa
gharama za shilingi 218,962,500/= ambazo zote zimetolewa na mfadhili
huyo.
Amesema
ujenzi wa mradi huo ulikamilika Mwezi Desemba 2020 ukihusisha ujenzi wa
mtandao wa maji wenye urefu wa mita 11,225 na vituo 14 vya kuchotea
maji (DP) na ufungaji wa dira 14 za malipo ya kabla.
“Ujenzi
wa Mradi huu umezingatia mahitaji maalumu ya watu wenye mahitaji maalum
kwa kujenga magati katika sehemu zinazofikika kwa urahisi. Mradi pia
umeweza kuunganisha wateja wapya 230 hivyo kupelekea wakazi takribani
1,380 kupata huduma ya maji moja kwa moja kwenye makazi yao”,amesema.
“Lengo
la mradi huu wa maji ni kuwapunguzia adha ya maji wananchi, kumtua mama
ndoo kichwani kwa kusogeza huduma ya maji safi maeneo ambayo yalikuwa
hayajafikiwa na Mtandao wa maji ya Ziwa Victoria”,ameeleza Mhandisi
Katopola.
Aidha,
amesema SHUWASA itaendelea kuhakikisha mradi huo wa maji unakuwa
endelevu kwa kuhakikisha mradi unatoa maji safi na salama kwa muda wa
saa 24 kila siku isipokuwa wanapokuwa na matengenezo.
“SHUWASA
inaendelea kuwasihi na itaendelea kuwashawishi wakazi wa maeneo ya
Masekelo, Ndala na Ishoshandili kutumia maji safi na salama na hasa kwa
kujiunga kwenye mtandao wa mabomba ili kila mwananchi aweze kupata maji
katika mji wake”,ameongeza Mhandisi Katopola.
Post A Comment: