MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha imewaachia huru watuhumiwa wote 24 katika kesi ya jinai inayohusu mauaji ya askari Koplo Ganus Mwita. Tukio hilo lilitokea katika Kijiji cha Orlolosokwani Tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro Juni 10, mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Mahakani hapo leo, Mkurugenzi wa Mashtaka ameiandikia Mahakama kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.
Kesi hiyo inajumuisha viongozi wa chama na serikali na ilianza kusikilizwa Mahakamani hapo Juni 16 kukiwa na watuhumiwa 27. Watuhumiwa watatu waliachiwa huru na kusalia watuhumiwa 24.
Ndege ya Precision Air imepata ajali katika Ziwa Victoria Bukoba, Kagera asubuhi hii ambapo Mashuhuda wanasema ajali hii imetokana na Ndege hiyo kupata hitilafu wakati ikitua,RPC Kagera amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na wanaendelea na juhudi za uokozi.
Tatizo hili linatokana na Mifumo ya Google kubadilika na kusababisha Baadhi ya mitandao ya simu kushindwa kutoa Data zinazo weza kuonyesha Picha katika Blog yetu
Kwa watumiaji wa Voda na Tigo hawakukubwa na tatizo hili ila kwa watumiaji wa Halotel na Airtel ndio walikubwa na tatizo hili.
Ila kwa sasa tumeweza kufanikisha kutatua tatizo hilo kwa upande wa mitandao yote na Tatizo hili limekwisha
Kwa Maoni au maswali wasiliana nasisi kupitia namba hizi 0758767077 - 0762561399

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Dkt. Zainab Chaula akipokea kitabu cha Mkurugenzi wa Taasisi ya Azaria Foundation Audax Abeli kinachoelezea maisha yake ya mtaani chenye lengo la kuisaidia Jamii kuwaondoa watoto katika mazingira hatarishi. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Amon Mpanju na wajumbe wa Menejimenti ya Wizara mara baada ya kikao cha Menejimenti Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Dkt. Zainab Chaula akiongoza kikao cha Menejimenti ya Wizara hiyo na Taasisi ya Azaria Foundation kujadili namna ya kuwaondoa watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani, kilichofanyika Jijini Dodoma

Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha leo imeahirisha
usikillizaji wa ushahidi wa shahidi namba saba upande wa Jamhuri wa kesi
ya jinai namba 105 ya mwaka 2021 ya unyang'anyi wa kutumia silaha
inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai
Ole Sabaya na wenzake wawili kutokana na Mshtakiwa namba Moja Lengai Ole
Sabaya kutokufika mahakamani kutokana na sababu za kiafya.
Akiahirisha
shauri Hilo Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo amesema shauri hilo
litaendelea kusikilizwa tena hapo kesho Agosti 05 asubuhi kwa kuendelea kusikiliza ushahidi wa
shahidi namba saba Mratibu Msaidizi wa Polisi ASP Gwakisa Minga ambaye
ni Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya Arusha.
Waziri Mkuu Kaasim Majaliwa ameishukuru Benki ya Afrika (BOA) kwa jitihada zake za kuendelea kuisaidia Tanzania katika Sekta mbalimbali za maendeleo.
Ametoa kauli hiyo jana (Jumatano Julai 14, 2021) wakati alipozungumza na Rais wa benki hiyo Othman Benjelloun kwenye hoteli ya Sofitel, Rabat Nchini Morocco.
Amesema kuwa uwepo wa Benki hiyo nchini Tanzania umewawezesha wananchi kunufaika na huduma mbalimbali zinazotolewa na Benki hiyo, "kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tunaishukuru Benki ya Afrika kwa jitihada hizi".
Aidha, Waziri Mkuu alimshauri Rais Benjelloun kuendelea kupanua wigo wa huduma za benki hiyo nchini ili kuwafikia watanzania wengi zaidi hasa katika sekta za Elimu, Kilimo, Mifugo na Madini.
Waziri Mkuu aliahidi kuwa ataandaa utaratibu wa kuukutanisha uongozi wa Benki hiyo na sekta binafsi nchini Tanzania ili kuona namna watakavyoweza kushirikiana katika kuwahudumia Watanzania.
Kwa upande wake, Rais Benjelloun amesema lengo la benki hiyo ni kuendelea kukuza uwekezaji wake nchini Tanzania. "Sisi tupo tayari kuwekeza katika maeneo mbayo viongozi wa taifa la Tanzania watatushauri lengo likiwa ni kutoa mchango wetu katika kujenga uchumi".
Naye, Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda alisema kuwa benki hiyo isaidie kukuza mahusiano ya Tanzania na Morocco katika sekta ya kilimo hasa kwenye mazao kama vile Mchele, Tumbaku, kahawa na mazao mengine.
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar Leila Muhamed Mussa amesema yapo maeneo ya fukwe ambayo hayajawekezwa mpaka sasa hivyo ni fursa kwa wawekezaji kuyatumia na kwamba Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi amefungua milango kwa wawekezaji.
Pia aliiomba benki hiyo kuona namna ya kuwawezesha wakulima wa viungo ili waweze kufanya shughuli zao kwa tija.
Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa, amefafanua taarifa ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa hivi karibuni kuhusu kufunguliwa kwa vyombo vya habari vilivyofungiwa.
Msigwa amesema Rais Samia Suluhu Hassan, ameelekeza Televisheni za Mtandaoni (Online Tv) tu ndio zifunguliwe na sio vyombo vya habari vingine yakiwemo Magazeti yaliyofungwa kwa mujibu wa Sheria.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amesema uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya elimu na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk John Magufuli ndio siri iliyopelekea shule nane za serikali kuingia kwenye kumi bora katika matokeo ya kidato cha sita 2020.
Na.
|
Jina la Kiwanda
|
Malengo ya Uzalishaji (tani)
|
Kiasi kilichozalishwa (tani)
|
Uzalishaji (%)
|
1
|
Kilombero Sugar Co. Ltd
|
120,183
|
103,122
|
85.8
|
2
|
TPC Ltd
|
90,815
|
88,968
|
98.0
|
3
|
Kagera Sugar Ltd
|
95,000
|
79,403
|
83.6
|
4
|
Mtibwa Sugar Estates Ltd
|
33,513
|
20,705
|
61.8
|
5
|
Manyara Sugar Co. Ltd
|
5,785
|
6,750
|
116.7
|
JUMLA
|
345,296
|
298,949
|
86.6
|
NA.
|
MKOA
|
BEI YA KILO (Tsh)
|
IRINGA
|
2,900
| |
MBEYA
|
3,000
| |
RUKWA
|
3,200
| |
KATAVI
|
3,200
| |
RUVUMA
|
3,200
| |
NJOMBE
|
2,900
| |
LINDI
|
2,800
| |
MTWARA
|
2,800
| |
ARUSHA
|
2,700
| |
KILIMANJARO
|
2,700
| |
MANYARA
|
2,700
| |
TANGA
|
2,700
| |
DAR ES SALAAM
|
2,600
| |
PWANI
|
2,700
| |
MOROGORO
|
2,700
| |
KAGERA
|
3,000
| |
MWANZA
|
2,900
| |
SIMIYU
|
2,900
| |
SHINYANGA
|
2,900
| |
GEITA
|
2,900
| |
MARA
|
3,000
| |
KIGOMA
|
3,200
| |
SINGIDA
|
2,900
| |
TABORA
|
2,900
| |
DODOMA
|
2,900
| |
SONGWE
|
3,000
|
























