MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha imewaachia huru watuhumiwa wote 24 katika kesi ya jinai inayohusu mauaji ya askari Koplo Ganus Mwita. Tukio hilo lilitokea katika Kijiji cha Orlolosokwani Tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro Juni 10, mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Mahakani hapo leo, Mkurugenzi wa Mashtaka ameiandikia Mahakama kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Kesi hiyo inajumuisha viongozi wa chama na serikali na ilianza kusikilizwa Mahakamani hapo Juni 16 kukiwa na watuhumiwa 27. Watuhumiwa watatu waliachiwa huru na kusalia watuhumiwa 24.

Share To:

Post A Comment: