Baadhi yao waliniambia waziwazi kuwa hawawezi kuwa na mwanamke mwenye ulemavu. Nilipita katika aibu nyingi za hadharani na mara nyingine nililia usiku kucha nikiuliza Mungu kwa nini mimi.

Niliona marafiki zangu wakiolewa mmoja baada ya mwingine, wengine wakiposti mitandaoni maisha ya kifahari wakiwa na wake zao. Mimi nilibaki peke yangu, moyo wangu umevunjika. Nilipoteza imani kwamba ningepata mwanaume atakayenipenda kwa dhati.

Nilikuwa nimekubali kuishi maisha ya upweke hadi rafiki yangu mmoja aliniambia nisiache kupigania furaha yangu. Aliniambia kuna suluhisho na akanipendekeza nimtafute Doctor Kashiririka.

Nilipiga simu huku nikiwa na mashaka, nikamweleza yote niliyopitia. Nilishangazwa na jinsi alivyonisikiliza kwa upole na kunipa moyo. Aliniambia kuwa haijalishi hali yangu, bado naweza kuvutia upendo wa kweli.

Aliniandalia dawa za mitishamba maalum za kuvutia mapenzi ya kweli na kuondoa laana ya kukataliwa. Nilifuata maagizo yake kwa makini, nikiweka matumaini yangu yote kwenye tiba hiyo. Soma zaidi hapa 

  


Nilikuwa mtu mwenye furaha, kazi nzuri na familia yenye upendo, lakini ghafla maisha yangu yalibadilika. Nilianza kupoteza kila kitu bila sababu ya kueleweka. Kwanza nilifutwa kazi ghafla bila kosa lolote. Baada ya hapo, biashara ndogo niliyokuwa nimewekeza ikaanguka.

Ndoa yangu nayo ikayumba, mume wangu akaanza kuwa mkali na hatimaye akaniacha. Watu waliokuwa marafiki zangu wakaanza kuniepuka kana kwamba mimi ndiye nilikuwa chanzo cha matatizo yote. Nilihisi dunia imenipoteza na sikujua la kufanya.

Nilipojaribu kuanza upya, kila hatua ilikuwa inakwama. Nilikuwa nikipata kazi mpya, lakini ndani ya miezi michache nilifutwa tena. Afya yangu nayo ilianza kudorora, nilikuwa mgonjwa kila mara bila madaktari kupata tatizo maalum.

Nilijikuta nikiwa mpweke, sina msaada, na sina cha kutegemea. Nilihisi kama kuna nguvu isiyoonekana inayonifuatilia na kuhakikisha sipigi hatua yoyote ya kimaisha. Woga na huzuni vilinifanya nisiamini tena mtu yeyote, na nilikaribia kukata tamaa kabisa. Soma zaidi hapa 

 

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza leo  Septemba 16, 2025, wakati wa ziara yake ya kukagua athari za moto uliotokea alfajiri ya Septemba 15 katika soko la Kawe.

...

SERIKALI  imetenga shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa soko la muda kwa wafanyabiashara waliokumbwa na janga la moto katika soko la Kawe, huku ikiahidi kukamilisha ujenzi huo ndani ya wiki mbili.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo, ametoa  kauli hiyo leo  Septemba 16, 2025, wakati wa ziara yake ya kukagua athari za moto uliotokea alfajiri ya Septemba 15 katika soko hilo.

Dkt.Jafo amesema kuwa  ujenzi wa soko hilo la muda utafanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers, na kumtaka Mhandisi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha kazi hiyo inakamilika kwa muda uliopangwa ili wafanyabiashara waweze kurejea kazini.

“Serikali imejipanga kuhakikisha shughuli za biashara zinaanza tena haraka. Wafanyabiashara wataendelea kutumia soko la muda wakati Serikali ikiendelea na mpango wa kujenga soko la kudumu la kisasa litakalokuwa na miundombinu bora na bima dhidi ya majanga,” amesema  Dkt. Jafo.

Aidha, ametoa  onyo kali dhidi ya kuingilia mchakato wa upangaji wa maeneo katika soko la muda, akisisitiza kuwa ni wafanyabiashara halali pekee ndio watakaopangiwa nafasi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Saad Mtambule, amethibitisha kuwa mbali na shilingi milioni 400 zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko la muda, Serikali pia imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara walioathirika na moto huo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Bi Hanifa Hamza, amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) imedhamiria kujenga soko jipya la kisasa litakalokuwa na mpangilio bora, uzio, na miundombinu ya kisasa ikiwemo bima ya majanga.

  

Sikuwa na amani usiku ule nilipoamka ghafla saa tisa usiku nikakuta geti langu liko wazi. Nilipotoka nje, niligundua kuwa gari langu halipo. Nilihisi miguu ikiniisha nguvu na nikaketi chini nikilia.

Hilo ndilo gari pekee ambalo nilikuwa nimenunua kwa miaka mingi ya kujinyima na kulipa mkopo. Usiku huo nilipiga simu kwa jirani na hata polisi lakini waliniambia uchunguzi ungefanyika kesho asubuhi. Nilihisi kama siku hiyo haingeisha.

Asubuhi ilipofika, polisi walikuja, wakapima eneo la tukio lakini waliniambia mambo haya huchukua muda. Nilihisi kama walikuwa hawaelewi maumivu niliyokuwa nayo.

Gari langu lilikuwa ndiyo tegemeo la familia yangu na kazi yangu, na sasa niliona ndoto zangu zikivunjika mbele ya macho yangu. Nilianza kuwa na hofu kubwa, nikaona kana kwamba maisha yangu yanazidi kuwa magumu.

Nikiwa nimeishiwa na mbinu, jirani yangu mmoja aliniambia kuwa tatizo kama hili linaweza kusuluhishwa kwa njia za kitamaduni. Kwanza nilisita kwa sababu sikuwahi kujaribu jambo kama hilo. Soma zaidi hapa 

 


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amewaeleza wananchi wa Bukombe kuwa maendeleo yaliyopatikana jimboni humo yametokana na upendo wa Rais Samia Suluhu Hassan kwao, hivyo wajitokeze kuwapigia kura wagombea wa CCM ifikapo Oktoba 29 mwaka huu ili waendelee kupata maendeleo.

Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 16, 2025 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Runzewe Magharibi wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Amesema katika kipindi cha miaka mitano ya Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan chini ya CCM imefanya kazi kubwa ya kuleta miradi ya maendeleo katika Kata hiyo ambayo miundombinu yake imefunguka zikiwemo ujenzi wa barabara, shule, miradi ya maji. Ameutaja  mradi wa Msasa ambao upo mbioni kupanuliwa ili kuhudumia wananchi wengi zaidi.

Ameongeza kuwa katika kipindi hicho wamejenga Ofisi mpya ya Halmashauri ya Wilaya, soko na stendi ya kisasa ili kusogeza na kuboresha huduma za jamii.

“Wilaya yetu ina shule tano za kidato cha tano na sita, tunajenga Chuo Kikuu kimoja Bukombe, tumejenga maghala. Nataka niwaambie mkituchagua tunaongeza sekondari nyingine ili watoto wanaozaliwa hapa wapate elimu katika ngazi zote”amesema Dkt. Biteko

Amesisitiza “ Kazi yenu wananchi ni kupiga kura ili mtudai maendeleo, Rais Samia anatupenda wananchi wa Runzewe, anatupenda wananchi wa Bukombe hivyo, tarehe 29 Oktoba tujitokeze kwa wingi na tumchague yeye katika nafasi ya urais,”

Naye, Mgombea wa Udiwani Kata ya Runzewe Magharibi, Patrick Isongolo amesema Rais Samia na Dkt. Biteko wamefanya jitihada kubwa ya kuleta maendeleo katika Kata hiyo hivyo Oktoba 29 wananchi wakawachague wagombea wa CCM.

“Mwaka jana Biteko amechangia ujenzi wa kituo cha afya, tulikuwa na changamoto kubwa sana ya barabara na daraja pale kwa Sae, Dkt. Biteko na Serikali ya CCM wamesaidia kuhamasisha na kutuletea maendeleo tunayoyashuhudia,” amesema Isongolo

Katika hatua nyingine,  akizungumza  katika Kata ya Runzewe Mashariki Dkt. Biteko  amesema  Rais Samia angependa kuona wananchi wanapata maendeleo ya haraka katika viwango vya juu.

Amefafanua kuwa Rais Samia alitoa fedha za kukamikisha ujenzi wa zahanati na Kituo cha Afya cha Msonga pamoja na kujenga kituo kingine cha afya na shule.

“Nasimama hapa kuwatangazia barabara ya pale kona nne tutakarabati ili watu wapite vizuri, ninemwambia diwani atafute eneo tununue ili tujenge shule watoto wapate mahali pa kusoma,” amesema Dkt. Biteko

Ameongeza kuwa wamedhamiria kufikisha umeme katika kila kitongoji cha Kata hiyo ya Runzewe Mashariki.

Aidha, amewaasa kuwa hakuna maendeleo yatakayotokea bila wao kujitokeza na kupiga kura kumchagua mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, mbunge Biteko na Mary diwani.

“Wapiga kura waliopo hapa ni 17,006, uchaguzi huu ningeomba twende wote tukapige kura,” amesema Dkt. Biteko.

Naye, Diwani wa Kata ya Runzewe Mashariki, Mary Nchiba amewaomba wananchi wa Kata hiyo kuwapigia kura wagombea wa CCM kwa kuwa wamefanya kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo.

 


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Simanjiro, James Ole Millya, ameahidi kuwaunganisha wananchi wa wilaya hiyo na kuhakikisha wanashirikiana na serikali kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili, ikiwemo migogoro ya ardhi.

Millya aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni zake uliofanyika katika mji wa Orkesument, tukio lililohudhuriwa na wananchi pamoja na makada wa CCM.

Amesema wananchi wa Simanjiro hawana sababu ya kuendelea kuwa maskini ilhali wanamiliki rasilimali nyingi, ikiwemo nguvu kazi na ardhi ya kutosha, na kwamba kinachohitajika ni kiongozi sahihi wa kuwaunganisha na kuongoza juhudi hizo.

“Kazi hiyo nitaiifanya kwa nguvu zangu zote endapo mtanipa ridhaa ya kuwa Mbunge wenu, tukashirikiane na Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na madiwani wa CCM kuharakisha maendeleo ya Simanjiro,” alisema Millya.

Kwa upande wao, baadhi ya makada wa chama hicho akiwemo Lembris Kitiri na Sendew Laiser, walisema wana imani kubwa na Millya wakimtaja kama kiongozi mwenye uwezo wa kushirikisha wananchi na kuleta maendeleo ya kweli katika Jimbo la Simanjiro.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi mkoa wa Manyara Janes Darabe amewaasa wana Simanjiro kuhakikisha kura za mheshimiwa rais mbunge na madiwani zinapatikana za kishindo pamoja na madiwani.


 


Na; Mwandishi Wetu - Handeni


Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imevitaka vyama vyote vya siasa katika Wilaya ya Handeni kuhakikisha vinazingatia kanuni, taratibu na sheria zilizowekwa wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, uwazi na kwa mujibu wa sheria.


Akizungumza katika kikao kazi na wawakilishi wa vyama vya siasa katika Wilaya ya Handeni, Bi. Edna Assey kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa alisema kuwa jukumu la vyama vya siasa ni kuhakikisha vinashiriki uchaguzi kwa kuzingatia misingi ya kidemokrasia na kuepuka vitendo vinavyoweza kuhatarisha uhalali wa mchakato mzima.



"Vyama vya siasa haviruhusiwi kujihusisha na vitendo vya rushwa kama kutoa fedha, mikopo, zawadi au hata ahadi za vyeo kwa lengo la kushawishi wapiga kura. Kitendo hicho ni kinyume cha sheria na kinaweza kupelekea hatua kali za kisheria kuchukuliwa,” alisema Bi. Edna

Aidha, aliwakumbusha viongozi wa vyama kuzingatia haki na wajibu wao wakati wa kampeni, ikiwemo kuendesha kampeni za kistaarabu, kuheshimiana na kuepuka kutumia lugha za matusi, kejeli, uchochezi au vitisho dhidi ya vyama vingine.


Ofisi ya Msajili imeeleza kuwa uchaguzi ni zoezi la kitaifa linalohusu mustakabali wa taifa lote, hivyo vyama vyote vinapaswa kushiriki kwa kuonyesha mfano bora wa uongozi unaojali maslahi mapana ya wananchi na taifa.

Bi. Edna Assey alisisitiza kuwa kuzingatia taratibu na sheria zilizowekwa kutasaidia kujenga mshikamano wa kitaifa, kuimarisha demokrasia na kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumu kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu.

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa pia imewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi kwa kutumia haki ya kupiga kura na kufanya maamuzi kwa uhuru bila kushawishiwa kwa rushwa au vitisho. Wananchi wamehimizwa kutanguliza amani na mshikamano na wa kitaifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.



 


Wakati ndoa yangu ilianza kuyumba, nilihisi kama dunia imenigeuka na kuanza kunikandamiza. Mume wangu, ambaye zamani alikuwa rafiki yangu wa karibu, mshauri wangu na mtu wa kwanza kumweleza siri zangu, alianza kubadilika taratibu.

Mara alianza kurudi nyumbani usiku wa manane, simu yake akaanza kuweka kwa vibration na kuibeba kila mahali. Nilipomuuliza kwa upole, alinijibu kwa hasira kana kwamba mimi ndiye nilikuwa tatizo.

Nilihisi uchungu mwingi hasa nilipogundua alikuwa na mpango wa kando. Nilipata mshtuko na nilipoteza nguvu za kuendelea na maisha kawaida. Nilianza kukosa usingizi, nilikonda ghafla na hata jirani zangu waligundua kuna jambo baya linaendelea.

Kila nilichojaribu kilionekana kupotea bure. Nilijaribu kuzungumza naye kwa upole, kumshirikisha familia zetu ili watushauri, hata nilijitahidi kusali kila usiku nikiomba mabadiliko, lakini hali ilizidi kuwa mbaya.

Alizidi kuwa mbali nami kiakili na kihisia, na nilijiona kama mgeni ndani ya nyumba yangu mwenyewe. Nilianza hata kufikiria kuondoka, lakini moyoni nilijua singeweza kuvunja familia kwa sababu ya mwanamke wa nje. Nilimwangalia mtoto wangu na nilijua lazima nipambane hadi mwisho kuokoa ndoa yangu. Soma zaidi hapa 

 


Vienna, Austria.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Mha.Felchesmi Mramba ameshiriki mkutano wa 69 wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki -IAEA  jijini Vienna Austria ambao unawashirikisha wadau mbalimbali wanaotumia nishati ya nyuklia kama chanzo cha umeme.

Mha. Mramba anashiriki  mkutano huo wa kimataifa unaowakutanisha wadau mbalimbali na mataifa makubwa yanayotumia nyuklia kama chanzo kimojawapo cha kuzalisha umeme.

Mkutano huo unakuja kipindi ambacho Wizara ya Nishati imepewa jukumu kubwa na  Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan, la kuhakikiaha TANESCO inaaza kuzalisha umeme kwa kutumia madini ya Uranium yanayopatikana Namtumbo mkoa wa Ruvuma.

Tanzania inatarajia kutumia vema fursa ya mkutano huo wa 69 wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kuzalisha umeme kwa nguvu ya nyuklia pamoja na kuangalia fursa za uwekezaji kwenye miradi ya umeme .

Ujumbe wa Tanzania unaongozwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo.

Wajumbe Wengine walioshiriki Mkutano huo ni pamoja na Balozi wa Tanzania na Mwakilishi wa Kudumu Nchini Austria, Mhe. Naimi S. H. Aziz, Mha. Joseph John Kirangi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Maji na Ardhi ya Zanzibar, Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati Mha. Innocent Luoga  pamoja na Viongozi Waandamizi na Wataalam kutoka Kamisheni ya Nguvu za Atomi (TAEC).

Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Mzee Yusuf Makamba amewaomba wananchi wa Jimbo la  Bumbuli mkoani Tanga kumchagua mgombea urais wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan, mgombea ubunge wa jimbo hilo, Mhandisi Ramadhani Singano na madiwani wote wa chama hicho.

Makamba amesema hayo leo Septemba 15, 2025 kwa njia ya simu kwenye mkutano wa kampeni za mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho, Dk Emmanuel Nchimbi uliofanyika Lushoto eneo la Soni.

Mzee makamba amesema anaimani na wagombea wote wa CCM na alipenda kuhudhuria mkutano huo ila tatizo ni changamoto ya afya yake.

Dk Nchimbi alimpigia simu Mzee Makamba akiwa jukwaani ndipo alipozungumza na kuwaombea kura wagombe wote huku akiwaomba wananchi wa mkoa wa Tanga wasimuangushe katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 29, 2025.