Wakala wa Barabra za mijini na Vijini TARURA  wanatarijia zaidi ya bilioni mbili kukamilisha Ujenzi wa Barabara ya TCA Levolisi,CCM, Kaloleni-KwaBenson na TRA Hadi East Africa Zenye Urefu wa Kilomita 2.241 na zitakazojegwa kwa kiwango Cha Lami. 

Hayo yamesemwa wakati Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 ulipotembelea na kuweka jiwe la Msingi Katika Mradi huo ambapo Akisoma Taarifa ya Ujenzi huo Mbele ya Kiongozi Wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Wilaya ya Arusha Mhandisi Godfrey Bwire Amesema Mradi huo unaulianza Tarehe 28.06.2024 huku ikitarajia kukamilika Mwaka huu. 

Meneja huyo wa Tarura Amesema Ujenzi huo wa Barabara unalenga  kusogeza Huduma  ya Miundombinu ya Barabara Kwenye Makazi ya Watu ili kurahisisha Huduma za Usafirishaji kwa kupunguza Gharama za Maisha. 

Akizungumza kabla ya kuweka Jiwe la Msingi Katika Barabara hiyo Kiongozi Wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  Kitaifa Ismail Ali Ussi  ameipongeza Tarura kwa kuendelea kumwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza Ahadi za kuboresha Miundombinu pamoja na Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi wa Barabara kuwa na Ubora unatakiwa.

Aidha Barabara zinazojengwa kwa kiwango Cha Lami ni TCA 0.655km,Levolisi 0.187km,CCM 0.129km,Kaloleni Hadi Kwa Benson 1.0km na TRA Hadi East Afrika 0.27km.









 






Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Mizengo Pinda amehimiza viongozi waliopewa dhamana ya mamlaka ya kusimamia mchakato wa uteuzi wa wagombea kuhakikisha wanatenda haki kwa wale wote waliojitokeza kwenye kinyang’anyiro hicho .

Pinda aliyasema hayo leo mara baada ya kutembelea ukarabati wa ofisi ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga ambao umefikia asilimia 99 uliofanywa ikiwa ni ndoto za Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo Rajab Abduhaman kuona jengo hilo linakuwa na muonekana mzuri kwa ajili ya kuwahudumia wana CCM.

Akiwa katika eneo hilo mara baada ya kutembelea ukarabati wa jingo hilo aliupongeza uongozi wa CCM kutokana na kazi nzuri walioifanya ya kukarabati jengo hilo na hivyo kuwa na muonekana mpya.

Alisema wakati nchi ikielekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu Octoba mwaka huu tayari maandalizi yameshaanza na waliochukua fomu Udiwani na Ubunge wameshafanya na kazi ya chama ni kuhimiza viongozi waliopewa dhamana ya mamlaka ya kusimamia mchakato watende haki.

“ Bahati nzuri kamati yenu mlisimamie kikamilifu ili mtu asipate sababu ya kupiga kelele wakati hakuna sababu ya kufanya hivyo kwa wananchi tunaomba wakati wa kupiga kura tumieni haki yenu tena kwa uhuru wenu wenyewe”Alisema

Aidha alisema pia kupitia utaratibu uliowekwa kabla ya kutoka kwenda kupambana na vyama vyengine lazima wampate mgombea wa chama atakayekwenda kupambana na vyama vyengine vya siasa tumieni haki yenu vizuri mtupe mgombea ambaye mnaamini anaweza kutuvusha kwa haraka zaidi.

Hata hivyo Waziri Mkuu Mstaafu Pinda alisema kwamba wanaendelea kumshukuru Rais Dkt Samia Suluhu na kumpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya nchi ipo kwenye utulivu na amani na mambo yanasonga mbele.

“Tanga kuna maneno nimesikia Rais hana deni na sisi na octoba tunatiki niombeni wana Tanga na wana CCM hilo jambo lipo mbele yenu na Tanga mlikuwa wapambanaji sana lazima jitihada kuhakikisha mnaongoza kwenye kura za Rais na Ubunge kwenye chaguzi zijazo”Alisema

Pinda aliwataka viongozi wa mkoa huo kuendelea kuchapa kazi pamoja na mshikamano kwa kuhakikisha wanaendelea kudumisha amani na ulitulivu ambao wanao mpaka sasa kutokana na kwamba haukudondoka tu angani bali umejengwa hivyo waendelee kumuomba mwenyezi Mungu aendelee kuisimamia.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman amesema ukarabati wa ofisi hiyo ni maelekezo ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Dkt Samia Suluhu kuhakikisha mali za chama yakiwemo majengo ya chama ya ofisi na menginevyo wanayalinda na kuyafanyia ukarabati mkubwa ili yaendelee kutumika miaka mingi kadri inavyowezekana.

Aidha alisema kwamba alifanya ziara kwenye mkoa wa Tanga na katikati pita pita yake aliona jengo lao namna lilivyokuwa na kutoa maelekezo kuhakikisha jengo hilo linafanyiwa ukarabati mkubwa na hayo ni matunda ya Mwenyekiti wa Taifa na maelekeo yake.

“Tulipopata maelekezo hayo tukasema lazima tufanye kwa sababu haki na heshima ya CCM kwenye nchi na mkoa wa Tanga ni kubwa haiwezekani viongozi wa CCM wanaovyoonekana uzuri lakini mahali wanapofanyia kazi hapafanani na nasi tukasema hapana lazima watii maelekezo hayo na tunashukuru wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa na Kamisaa wao kwa umoja na mshikamano wao ndio umewezesha kutekeleza maelekezo hayo ya Rais”Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi ,Dkt Batilda Burian amesema wa wamefarijika uwepo wa Waziri Mkuu huyo na wanamshukru Mwenyekiti Taifa kwa kazi kubwa aliyoifanya wakati wa ziara yake na wana Tanga wanaendelea kumshukuru kwa mambo mengi makubwa ya kimaendeleo aliyofanya kwa mkoa huo.

“Kutokanana na hilo tunasema kwamba Mama Hana deni na Octoba tunatiki na kura zitajaa na kumwagika kutokana na kasi kubwa ya maendeleo aliyoyafanya katika mkoa wa Tanga na hivyo kuufungua kiuchumi”Alisema

Hata hivyo,Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Mfaume Kizigo alisema chama hicho kimepata kiongozi wa kwelikweli na kinachoonekana hapo ni sehemu ya maendeleo makubwa yaliyofanywa na Mwenyekiti huyo kutokana na kila wilaya amejenga byumba za watumishi kuanzia chama na Jumuiya zake zote na amefanya hivyo kila alipokwenda kuishauri kamati ya siasa.



Mwisho.



Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) wamesaini makubaliano ya ushirikiano wa matibabu ya ubingwa bobezi wa magonjwa ya moyo kwa kutumia uwezo wa wataalamu wa ndani ya nchi.

Makubaliano hayo yalisainiwa jana katika Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) iliyopo jijini Dodoma na Wakurugenzi watendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na BMH.

Akizungumza mara baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama alisema ni jambo la kupendeza kuona wataalamu waliopo ndani ya nchi wanasaini makubaliano ya kujengeana uwezo wao kwa wao na kutotegemea wataalamu kutoka nje ya nchi.

Mhe. Mhagama alisema siku za nyuma walikuwa wanawategemea wataalamu kutoka nje ya nchi kuja kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani ya nchi lakini sasa hivi mambo yamebadilika wataalamu wa ndani wanajengeana uwezo wao kwa wao na kuna wataalamu wanatoka nje ya nchi wanakuja kujengewa uwezo hapa nchini.

“Tunaishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwekeza katika majengo, vifaa tiba vya kisasa na kusomesha wataalamu wa afya kitu kilichosababisha huduma za matibabu ya ubingwa bobezi kupatikana hapa nchini”, alisema Mhe. Mhagama.

Aidha Waziri huyo wa Afya alisema kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika katika sekta ya Afya na Tanzania kupokea wagonjwa kutoka nje ya nchi ambao wanakuja kutibiwa, wakati umefika sasa kwa Hospitali zinazotoa huduma za ubingwa bobezi kuimarisha Utalii Tiba na kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa kufuata miongozi ya afya kwa wagonjwa wanaowahudumia.

“Nimepokea ripoti ya kambi maalumu ya matibabu iliyofanyika Visiwani Comoro ambayo ilishirikisha wataalamu kutoka JKCI, BMH, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) na Taasisi ya Saratani Ocean Road, ninawaomba muendelee kuungana  kwa pamoja kama mlivyofanya Comoro muende katika nchi nyingine kutoa huduma za ubingwa bobezi ili wale mtakaowakuta na shida waje kutibiwa hapa nchini”,alisema Mhe. Jenista.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema ushirikiano uliokuwepo baina yao na BMH umesaidia kuimarika kwa upatikanaji wa huduma ya matibabu ya moyo hapa nchini.

“Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wamekuwa wakiwajengea uwezo wataalamu wa magonjwa wa moyo waliopo BMH kwa kufanya hivi upatikanaji wa huduma ya matibabu ya kibingwa ya moyo umeongezeka na kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa uharaka”, alisema Dkt. Kisenge.

Akikabidhi taarifa ya kambi maalumu ya matibabu ya ubingwa bobezi wa magonjwa mbalimbali iliyofanyika Visiwani Comoro Dkt. Kisenge ambaye alikuwa mratibu wa kambi hiyo alisema waliona zaidi ya wagonjwa 2700 na wagonjwa zaidi ya 400 walishafika hapa nchini kutibiwa na wameingiza zaidi ya shilingi bilioni 3.

“Mwishoni mwa mwaka jana tulienda Visiwani Comoro kuwatibu wenzetu ambao wanatutegemea Tanzania kupata huduma za ubingwa bobezi, tukiwa nchini humo tuliwajengea uwezo wataalamu wao na kujenga ushirikiano baina ya hospitali zao na zetu”, alisema Dkt. Kisenge.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Prof. Abel Makubi alisema ushirikiano wa BMH na JKCI ulianza miaka mingi iliyopita lakini sasa hivi wameona wauweke katika maandishi.

“Tutaendelea kushirikiana katika kufanya tafiti za magonjwa ya moyo, kutoa mafunzo kwa wataalamu wetu na kubadilishana ujuzi wa kazi hii ikiwa ni pamoja na kufanya matibabu ya pamoja”, alisema Prof. Makubi.

Katika hafla hiyo ya utiaji saini makubaliano hayo ambayo ilikwenda sambamba na uzinduzi wa kliniki ya wagonjwa wa kimataifa, wagonjwa maalumu na uchunguzi wa afya katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama alimteua Dkt. Peter Kisenge Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kuwa Mwenyekiti wa kamati ya Utalii Tiba nchini.

 


SERIKALI ya Tanzania imeendelea kuchukua hatua thabiti za kuboresha upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na kuchochea ukuaji wa uchumi, kupitia mradi mkubwa wa usafirishaji wa umeme kutoka Chalinze hadi Kituo cha Kinyerezi III wenye urefu wa kilomita 135 na uwezo wa kusafirisha hadi megawati 1,000.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko, amesema hayo leo Julai 10, 2025 jijini Dar es Salaam alipokuwa akikagua miradi mbalimbali ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, I Extension na Kinyerezi II.

Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameeleza kuwa ujenzi wa njia hiyo mpya ya umeme ni sehemu ya mpango wa Serikali kuhakikisha nishati ya uhakika inafika katika maeneo ya viwanda, hususan katika mikoa ya pwani na magharibi, ambayo awali ilikuwa inakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa umeme wa kutosha.

 “Maeneo kama Mkuranga yana viwanda vingi yanayohitaji umeme wa kutosha. Hali hii inatufanya tuongeze uwezo wa vituo vya kuzalisha, mfano Kinyerezi III kutoka megawati 600 hadi 1,000 ili kukidhi mahitaji yanayoendelea kuongezeka,” amesema Dkt. Biteko.

Akizungumzia maendeleo ya upatikanaji wa umeme nchini, Dkt. Biteko amesema mafanikio yaliyopatikana hadi sasa yanatokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Mhe. Rais Samia amewekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya nishati. Kwa mwaka huu wa fedha, tumetenga Shilingi trilioni 2.3 kwa ajili ya kuendeleza miradi ya umeme na kuimarisha miundombinu ya usambazaji,” amesema Dkt. Biteko.

Aidha, Dkt. Biteko amesisitiza kuwa sekta ya nishati ni uti wa mgongo wa uchumi wa taifa, na ndio msingi wa maendeleo ya viwanda, biashara, elimu, na huduma za afya.

Amepongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa maboresho makubwa ya huduma zake kwa wananchi, ikiwemo kuondoa gharama za simu kwa wateja wanaotaka msaada wa haraka na kuimarisha usikivu na ufuatiliaji wa changamoto za wateja.

Kwa mujibu wa taarifa ya hali ya uchumi ya mwaka 2024, sekta ya nishati imekuwa kwa asilimia 14, ikishika nafasi ya pili nyuma ya sekta ya Sanaa, Utamaduni, Michezo na Habari ambayo imekua kwa asilimia 17.

Dkt. Biteko amehitimisha kwa kutoa wito kwa wananchi kushiriki katika ulinzi wa miundombinu ya umeme na kulipa gharama za matumizi kwa wakati, ili kuendeleza juhudi za Serikali katika kujenga taifa lenye nishati ya uhakika kwa wote.

Kwa Upande wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Endward Mpogolo amesema kuwa ziara hiyo ni ya muhimu sana kwa kuwa inatoa mwanga wa wazi kuhusu hali ya uzalishaji wa nishati nchini, hasa wakati huu ambapo mahitaji ya umeme yanaongezeka kufuatia ukuaji wa viwanda, hasa katika Wilaya ya Kigamboni.

"Ni hatua muhimu katika kuhakikisha huduma ya umeme inaimarishwa ili kuendana na kasi ya maendeleo," amesema Mpogolo.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya alitumia fursa hiyo kupeleka salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa kushughulikia kwa vitendo changamoto ya maji jijini Dar es Salaam.

"Tupelekee salamu kwa Mheshimiwa Rais kwa kuleta zaidi ya Shilingi bilioni 37 ambazo zimewezesha ujenzi wa tanki kubwa la maji lililopo Bangulo, Wilaya ya Ilala. Tenki hilo litakuwa sehemu muhimu ya kusaidia upatikanaji wa maji kwa wakazi wa jiji na pia litachangia katika upatikanaji wa umeme," ameongeza.

Vilevile, ameeleza shukrani kwa Serikali kwa kuendelea kupeleka fedha za maendeleo katika wilaya mbalimbali za Dar es Salaam, jambo ambalo limechochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kuchangia ustawi wa nchi kwa ujumla.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akizungumza wakati wa ziara ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko (wa tatu kulia) akikagua maendeleo ya miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension na Kinyerezi II leo, Julai 10, 2025, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Lazaro Twange akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko wakati akiwasili katika miradi ya kuzalisha umeme leo, Julai 10, 2025, jijini Dar es Salaam.
  Mitambo ya miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension na Kinyerezi II.
  
Matuki mbalimbali.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa wito kwa nchi za Afrika kuwekeza michango ya wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii katika miradi ya maendeleo.

Amezungumza hayo katika Mkutano wa 14 wa Kimataifa wa Watunga Sera wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Barani Afrika Leo Julai 10, 2025 uliofunguliwa na Mhe. Dkt. Philip Mipango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanyika katika kituo cha mikutano AICC jijini Arusha

Mhe. Kikwete amesema mkutano wa nchi wanachama unatoa nafasi ya kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati ya pamoja kwa ajili ya kukuza mifuko hiyo na kuchochea maendeleo ya miundombinu barani Afrika.

Kauli mbiu ya mkutano huo ni “Mifuko ya Hifadhi ya Jamii: Chachu ya Maendeleo ya Miundombinu na Ukuaji wa Kiuchumi na Kijamii Barani Afrika.”






Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amefanya ziara ya kutembelea maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Jijini Dar es Salaam, tarehe 10 Julai, 2025
NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

KATIKA kipindi cha uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu-ADEM imeendesha programu za mafunzo ya uongozi na usimamizi wa elimu pamoja na uthibiti ubora wa ndani wa shule kwa viongozi wa elimu 89,716 kwa upande wa Tanzania Bara na viongozi 1,197 kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Viongozi na wasimamizi wa Elimu waliopatiwa mafunzo hayo ni Maafisa Elimu wa Mikoa, Halmashauri na Maafisa Elimu Kata. Hii imejumuisha pia walimu wakuu, wajumbe wa kamati na Bodi za shule, wathibiti ubora wa elimu na wajumbe wa Bodi za vyuo vya ualimu.

Ameyasema hayo jana Julai 9,2025 Bagamoyo mkoani Pwani Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo wakati akitoa taarifa kuhusu mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwenye eneo la uongozi na usimamizi wa elimu nchini.

Amesema mafunzo hayo yalilenga kuimarisha usimamizi wa sekta ya elimu nchini ili kuendana na mabadiliko na maboresho ya sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023.

Aidha Prof. Nombo amesema kupitia Mradi wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji kwa Elimu Msingi-BOOST, ADEM ilipatiwa kiasi cha shilingi bilioni 16,163,065,800.00 kwaajili ya utekelezaji ambapo fedha hizo zimetumika kwaajili ya kuendesha mafunzo ya walimu wakuu pia uandaaji na uchapishaji wa vitabu vya Kiongozi cha Mwalimu Mkuu "School Management Manual" na kitabu cha Utawala Bora wa Elimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ("LGA's Education Good Governance Manual" ).

"Vitabu hivi ni mwongozo wa Utawala Bora katika Elimu wenye kujumuisha uwekaji wa mipango ya maendeleo ya shule, usimamizi wa shule, ukaguzi wa ndani, Usimamizi wa ujenzi, ushirikishwaji wa jamii na ushughulikiaji wa malalamiko katika elimu". Amesema Prof. Nombo.

Amesema kuwa baada ya kuandaa miongozo hiyo ADEM iliendesha mafunzo ya Uongozi na Usimamizi fanisi wa shule kwa walimu wakuu 17,817 katika Mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

Amesema kupitia mradi huo wa BOOST, Wakala unaendelea kuendesha mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Maafisa Elimu Kata 3,956, Maafisa Elimu wa Mikoa 26 na Maafisa Elimu kutoka katika Halmashauri zote 184 nchini kwa upande wa Tanzania Bara.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi amewataka walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Ganako Wilayani Karatu kutunza miundombinu ya shule ili kuhakikisha wanafunzi wanasoma kwa utulivu sanjari na kuhamasisha klabu za kupinga rushwa zinaendelezwa zaidi

Alisema endapo miundombinu ya shule ikitunzwa vema itawezesha wanafunzi kufaulu kutokana na uhalisia wa utulivu uliopo na kusisitiza walimu kusimamia maadili sanjari na kuhamasisha klabu za wapinga rushwa zinaendelezwa ili wanafunzi wajue mbinu mbalimbali za kupambana na rushwa wakiwa mitaani na maeneo mengine. 

"Endeleeni kulinda miundombinu ya elimu sanjari na kupinga rushwa kwa wanafunzi lakini naipongeza halmashauri ya wilaya hii kwa kutenga fedha sh, milioni 30 kama mapato ya ndano kwaaajili ya ujenzi wa darasa shule ya msingi Ganako pia endeleeni kujenga na kukarabati madarasa mengine zaidi"

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ganako, Lucy Yamay aliishukuru halmashauri ya wilaya hiyo kutoa sh, milioni 30 kwaaajili ya ujenzi wa chumba kimoja cha darasa kwani mradi huo utawezesha wanafunzi kusoma kwenye mazingira rafiki ikiwemo kupunguza msongamano wa wanafunzi darasa ni

Sambamba na hilo pia alimshukuru Rais Samia Hassan Suluhu kwakuendelea kuboresha miundombinu ya elimu ikiwemo utatuzi wa changamoto mbalimbali katika sekta ya elimu , awali Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk, Lameck Ng'ang'a akipokea mwenge huo kutokea wilayani Ngorongoro alisema jumla ya miradi nane ya Bil. 4.6 itazinduliwa, kuwekwa mawe ya msingi sambamba na miradi mingine kutembelewa ikiwemo lishe na matumizi ya nishati safi ya kupikia.

NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeendelea kuimarisha uongozi na usimamizi wa elimu nchini kwa kutoa mafunzo ya uongozi, usimamizi na utawala bora kwa walimu wakuu wa shule za awali na msingi pamoja na maafisa elimu kata kutoka Tanzania Bara.

 


📌Mkurugenzi Mkuu REA abainisha hatua zinazochukuliwa

📌Amshukuru Rais Samia kwa kuwezesha

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.


Amebainisha hayo Julai 07, 2025 katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam ndani ya Banda la Maonesho la Wakala wa Nishati Vijijini (REA).


“REA inalo jukumu la kuhakikisha maeneo yote ya vijijini yanapata aina zote za nishati safi zinazotumika nchini ikiwemo; umeme, nishati safi ya kupikia pamoja na bidhaa za mafuta ya petroli na dizeli na hili linafanyika kupitia miradi mbalimbali ambayo baadhi imekamilika na mingine ipo katika hatua tofauti tofauti za utekelezaji,” amebainisha Mha. Saidy.


Alisema Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia umeelekeza ifikapo mwaka 2034; angalau 80% ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia na REA ni miongoni mwa taasisi zilizopewa jukumu la kuhakikisha lengo hilo linafikiwa.
Alibainisha kuwa kwa sasa takriban asilimia 96 ya wananchi maeneo ya vijijini wanatumia kuni na mkaa kupikia na kwamba jukumu lililopo ni kuhakikisha wananchi hao wanaachana na matumizi ya nishati zisizo salama na kuanza kutumia nishati safi na salama.


Alitaja hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na REA ikiwemo uhamasishaji na uelimishaji wananchi kufahamu athari za kutumia nishati isio salama pamoja na kuwafahamisha faida za kutumia nishati safi ya kupikia, kuwarahisishia wananchi upatikanaji wa bidhaa za nishati safi jirani na maeneo yao na kuwezesha teknolojia za nishati yenyewe.


“Kuna dhana imejengeka kwamba nishati safi ya kupikia ni gharama kuliko nishati zingine dhana ambayo haina ukweli kwa 100% kwani kwa sasa kuna teknolojia zilizoboreshwa ambazo zinazuia upotevu wa nishati wakati wa kupika hivyo kuwapunguzia gharama watumiaji," alifafanua Mha. Saidy


Aliongeza kuwa watu wengi hawaangalii gharama nyingine kama muda wanaotumia kusaka kuni na madhila mengine wanayokutana nayo huko porini wakati wakisaka kuni.


Alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha REA kutekeleza jukumu la kusimamia upatikanaji wa nishati safi ya kupikia hasa ikizingitiwa kuwa yeye ni kinara wa nishati safi ya kupikia.


Alibainisha baadhi ya mafanikio ambayo yamepatikana tangu kuanza kutekeleza mkakati huo wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo ni pamoja na kuwezesha wananchi maeneo mbalimbali vijijini kuhama kupitia ruzuku iliyotolewa ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ya kilo 6 na vichomeo vyake.


“Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Samia ilitoa ruzuku ya 50% kwenye mitungi ya gesi ya kupikia ipatayo 452,000 ambayo imeshaanza kusambazwa kwenye mikoa yote Tanzania Bara na zoezi linaendelea; sambamba na mitungi 110,000 ambayo ilisambazwa mwaka juzi kupitia Wabunge kwenye majimbo yao,” alisema Mhandisi Saidy.


Sambamba na hilo, Mha. Saidy alibainisha kuwa REA imewezesha Jeshi la Magereza ambapo kwa sasa magereza zote 129 zimehama kutoka kwenye matumizi ya nishati zisizo salama, na hivi karibuni REA imekuja na mpango wa kuwezesha Maafisa wa Jeshi la Magereza nao kutumia nishati safi ya kupikia katika familia zao.


“Kama mtakumbuka Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alielekeza taasisi zinazohudumia zaidi ya watu 100 zianze kutumia nishati safi ya kupikia na hili tunatekeleza na tunatarajia kuzifikia zaidi ya taasisi 400 katika mwaka huu wa fedha. Tulianza na Jeshi la Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na takriban shule 53,” alibainisha Mha. Saidy.


Mhandisi Saidy vilevile alibainisha mradi wa mikopo nafuu wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vya mafuta ya petroli na dizeli ulioanzishwa na REA ambao umelenga kuwasogezea wananchi wa vijijini huduma kwa gharama nafuu na ubora unaokubalika.

 


Apatiwa elimu juu ya utekelezaji wa mkakati wa Taifa wa  Nishati safi ya kupikia

 Wizara ya Nishati kuendelea kuweka mazingira mazuri kwa tasisi zake kutekeleza majukumu yake kikamilifu


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi leo 7 Julai, 2025 ametembelea banda la Wizara ya Nishati  kwenye maonesho ya biashara ya kimataifa maarufu kama sabasaba jijini Dar es salaam

Akiwa kwenye banda la Wizara ya Nishati Mhe Mwinyi alipokelewa na Mkuu wa kitengo cha  Mawasiliano Serikalini Bi Neema Chalila Mbuja, ambapo alimweleza juu ya hatua za utekelezaji zilizofikiwa kwenye utekelezaji wa mkakati wa Taifa wa nishati safi ya kupikia na kuongeza kuwa ajenda hiyo ni utekelezaji wa azimio la Mhe Rais Samia kama kinara wa nishati safi ya kupikia.

Amesema Wizara ya Nishati kupitia taasisi zilizopo chini ya Wizara zimekuwa zikitekeleza kwa vitendo ajenda hiyo kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambae ni kinara wa nishati safi ya kupikia kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia.

Wizara ya nishati tayari imezindua mikakati miwili ya nishati safi ya kupikia na ule wa mawasiliano ili kuwezesha utekelezaji wa ajenda ya nishati safi ya kupikia kwa vitendo





 


Wizara ya Fedha imeibuka na tuzo ya Mshindi wa Tatu wa jumla kwa upande wa Wizara zilizoshiriki Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

Tuzo hizo zimetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Seleman Jaffo ambapo kwa upande wa Wizara ya Fedha Tuzo hiyo imepokelewa na Afisa Habari Mwandamizi, Bw. Ramadhan Kissimba, kwa niaba ya Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bw. Benny Mwaipaja, ambapo ushindi huo umetokana na Wizara zilizotoa huduma bora kwa wananchi katika Maonesho hayo.

Wizara ya Fedha inatoa huduma katika Maonesho hayo kupitia Idara, Vitengo na Taasisi zilizochini ya Wizara ya Fedha ikiwa ni pamoja na Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), Mfuko wa Dhamana na Uwekezaji Tanzania (UTT AMIS), Mfuko wa Self Microfinance, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

Taasisi nyingine ni pamoja na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Benki ya Maendeleo TIB na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Hazina SACCOS, Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Mamlaka ya Rufaa za Zabuni za Umma (PPAA) na Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA).

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ali Ussi amezitaka Taasisi za elimu nchini wakiwemo VETA kuhakikisha wanatunza mazingira sambamba na uoteshaji miti katika maeneo yao hayo yamejiri wakati wa ukaguzi wa mradi wa kuhifadhi mazingira na upandaji wa miti katika Chuo cha VETA Longido. 

Ussi alisisitiza taasisi  za elimu ikiwemo shule za msingi na sekondari kutunza mazingira ikiwemo upandaji wa vitalu vya miche ya aina mbalimbali ili kuhakikisha maeneo yaliyopo yanakuwa na uoto wa asili ikiwa ni kampeni ya Rais Samia Hassan Suluhu ya kuhakikisha Tanzania inakuwa ya kijani

"Endeleeni kupanda miti ili kuhakikisha Tanzania inakua ya kijani ikiwemo kuhakikisha vitalu vua miti ya aina mbalimbali lakini napongeza VETA kwa kuanzisha mradi huu unaowapa fursa za ajira vijana"

Awali akisoma taarifa ya mradi huo,Ofisa Ufugaji Nyuki halmashauri ya Longido,Remna Rombola alisema jumla ya miti 1000 imepandwa ikiwemo miche ya vitalu 8,000 ambayo imepandwa kwa gharama ya sh, milioni 4.3 ambapo halmashauri ya Longido imetoa sh, milioni 1.5 huku miti 1000 ikitolewa na  Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) 

"Mradi huu utasaidia unoreshaji wa mazingira kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo upunguzaji wa hewa ukaa"

Awali Mkuu wa Wilaya ya Longido Salum KalLi amesema mwenge wa Uhuru ukiwa wilayani hapo utakimbizwa kilomita 222.4 na kupitia jumla ya miradi saba ya bilioni 2.2