Bodi ya Nishati Vijijini (REB) leo Mei 10, 2026 imefanya ziara katika Kampuni zinazozalisha, kusambaza bidhaa za nishati safi ya kupikia katika Mkoa wa Arusha.

Bodi hiyo ikiwa imeongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu pamoja na Wajumbe wa Bodi hiyo, Mhe. Radhia Msuya na Mhandisi Sophia Mgonja waliweza kutembelea kampuni ya Ignate Energy Access yenye bidhaa za My Sol pamoja na kampuni ya HannyG Investment.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti Kingu, amezipongeza kampuni hizo kwa kuunga mkono kampeni ya Serikali ya Nishati Safi ya Kupikia kwa kuanza kutengeneza pamoja na kusambaza bidhaa za nishati safi ya kupikia huku akitoa wito kwa makampuni mengine kuendelea kuunga mkono kampeni hiyo ili malengo yaliyowekwa ya ifikapo 2034, Asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Awali akitoa taarifa ya utendaji wa kampuni ya My Sol, Meneja Uendeshaji wa Mitambo, Joe Chambua, amesema kuwa pamoja na huduma zingine zinatolewa na kampuni hiyo ikiwamo huduma ya ufungaji wa umeme jua, kampuni hiyo imeanza kutekeleza mradi wa nishati safi ya kupikia kwa kuja na teknolojia rahisi na ya gharama nafuu ya mtambo wa biogasi.

Amesema kuwa wamefanikiwa kufunga mitambo ya biogasi katika taasisi mbalimbali nchini ikiwemo Magereza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni ya Hanny G Investment, Hanny Mbaria, ambao wanajishughulisha na utengenezaji wa majiko banifu pamoja na mkaa mbadala ameishukuru Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuipa kampuni hiyo kazi ya kusambaza majiko banifu na mkaa mbadala katika shule 53 Tanzania Bara.

Mbaria amesema licha ya mradi wa nishati safi ya kupikia kulinda mazingira lakini pia mradi huo umetoa ajira kwa vijana wengi.

“Kwa sasa kampuni yetu imekua zaidi na tumeajiri vijana wengi zaidi tofauti na hapo awali. Kwa sasa tuna wafanyakazi zaidi ya 120 wenye ajira za kudumu na wasio na ajira za moja kwa moja ni 1000,” amesema Mbaria.

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Halmashauri za Miji, Halmashauri za Wilaya, Shule za msingi, wadau wa mazingira pamoja na Mabalozi wa Mazingira, limepanda miche ya miti elfu arobaini katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwa Baraza hilo.



NAIBU Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Longido Mkoani Arusha,Dkt Steven Kiruswa  amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo cha uongozi wake anawiwa na kuhakikisha anatekeleza vipaumbele 16 katika kukamilisha miradi ya maendeleo katika Jimbo hilo.

Dkt Kiruswa alisema hayo katika mkutano wa hadhara wenye lengo la kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Longido kwa kukichagua chama chake cha Chama Cha Mapinduzi{CCM},Mgombea Urasi wa chama hicho Rais Samia Suluhu Hassan na Makamu wake Dkt Emmanuel Nchimbi,Mbunge na Madiwani wote wa chama hicho katika mkutano uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali katika ngazi ya tawi,kata na wilaya uliofanyika katika uwanja wa Longido Polisi.

Alisema moja ya vipaumbe ambavyo anataka kuvifanyia kazi katika kipindi miaka mitano ya ubunge wake ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa shule za msingi na sekondari katika kata zote za Jimbo hilo,kubuni miradi ya ajira kwa vijana,kukamilisha mradi wa maji wa chanzo cha Loormokerian Kijiji cha Oltepesi,kuchimba visima vya maji Kiseriani na Orkesumet.

Waziri Kiruswa alitaja kipaumbe kingine ni pamoja na ukarabati na ufunguaji wa barabara zilizo chini ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijni{TARURA} kwenye maeneo ynye vipaumbele,uendelezaji wa shule shikizi katika kata ambazo hazina ikiwa ni njia ya kupunguza umbali mrefu kwa watoto kwenda na kurudi shule na kujikinga na wanyama wakali.

Alisema ana uhakika ndani ya muda huo vipaumbele alivyovioanisha vitakuwa vimekamilika kwa kushirikiana na wananchini,serikali kuu,wadau wa maendeleo na wafadhili wa ndani na nje lengo kuu ni kutaka kuwapelekea huduma wananchi.

Aidha alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi kwa kumpa kura nyingi Rais Samia Suluhu Hassan na kuwa Rais awamu ya sita na kusema kuwa uamuzi walioufanya umeiheshimisha Longido kwani imekuwa wilaya ya kwanza kwa kutoa kura Nyingi Mkoani Arusha.

Waziri Kiruswa alisema kutokana na hali hiyo aliwaomba wananchi wa Longido kuwa wamoja na watulivu katika kuiletea maendeleo Longido na kumwombea afya njema Rais ili aweze kuendelea kuiongoza nchi kwa amani na upendo.

''Nawaomba wananchi wa Longido tuiombe nchi amani na tumwombee Rais wetu Samia Suluhu Hassan afya njema kwani amekuwa mstari wa mbele kuiendeleza Longido hivyo kila mmoja kwa imani yake ya kiislamu na kikrusto anapaswa kufanya hivyo''alisema Kiruswa

Naye Mkuu wa wilaya ya Longido,Salumu Kally amesema ni wakati wa wana Longido kushirikiana na Mbunge katika kuiletea maendeleo Jimbo hilo na kusema kuwa mifarakano mara nyingi hurudisha nyumba maendeleo hivyo hataki kuliona hilo likitokea.

Naye Mbunge wa Monduli,Joseph Isack na Mbunge wa Ngorongoro Yannick Ndoinyo wote waliwaomba wananchi wa Longido kushirikiana na Mbunge wao Kiruswa kwani mbunge huyo ni mpenda watu na mpenda maendeleo hivyo wasidhubutu kuipoteza lulu hiyo kwa namna yoyote ile kwani watakuwa wamefanya maksa makubwa sana,

 

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amewashauri Wamiliki wa Viwanda vipya Kutoa kipaumbele kwa wazawa katika ajira ili kukuza uchumi na mapato ya Taifa kwa ujumla.

Akizungumza Mei 09, 2026, wakati wa akifungua wa Kiwanda kipya cha kutengeneza tambi za papo hapo (Instant) cha Kura Food mkoani Pwani, amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya Biashara ikiwemo sera, miundombinu, na mifumo ili kuvutia Wawekezaji na wafanyabiashara na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.

Aidha, Wizara imefanya mapitio ya sheria na kanuni ili kuhakikisha zinajielekeza katika kuwezesha biashara na kuondoa vikwazo badala ya kudhibiti pekee. Lengo ni kushirikiana na wadau wa mnyororo wa thamani, kutumia teknolojia za kisasa zinazoongeza tija, uzalishaji, na ufanisi wa biashara nchini.

Naye, Mwenyekiti wa Kura Food, Bw. Wu Yeping, ameipongeza Serikali kwa kuweka mazingira rafiki yanayorahisisha uwekezaji,

Huku Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, akibainisha kuanza kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara na Reli ya Kisasa (SGR) kuanzia mwaka ujao ili kufungua zaidi fursa za kibiashara mkoani humo.

Naye Mbunge wa Kisarawe, Mhe. Selemani Jafo, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sera zake thabiti ambazo zimekuwa chachu ya kuvutia wawekezaji. Sera hizi zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa wananchi wa jimbo hilo kupitia kuanzishwa kwa viwanda vipya.

            
Na Mwandishi Wetu

Benki ya Ushirika (Coop Bank) mwishoni mwa wiki ilizindua rasmi tawi lake jipya Mtwara mjini ikiwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mkakati wa benki hiyo wa kupanua huduma za kifedha na kuimarisha uchumi jumuishi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa utekelezaji wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika kambi zake, huku akiwahamasisha kuelimisha jamii zinazozunguka kambi hizo nazo kutumia nishatia nishati safi ya kupikia.

Pongezi hizo zimetolewa leo Mei 9, 2026 wakati wa ziara ya Bodi hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inaayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Kambi ya JKT ya Oljoro Jijini Arusha.

Mradi huo unahusisha uzalishaji wa bayogesi kupitia mbolea ya ng’ombe, matumizi ya majiko ya gesi, majiko banifu na mashine za kutengenezea mkaa mbadala.

Mwenyekiti Kingu pia, amesisitiza juu ya vijana waliopo kwenye kambi hizo za JKT kupatiwa mafunzo ya namna ya kutengeneza mkaa mbadala ili waweze kutumia ujuzi huo kujiajiri na kuwa mawakala wa kutengeneza mkaa mbadala pindi watakapomaliza mafunzo yao.

Kwa upande wake, akimwakilisha Mkuu wa JKT, Kanali Projest Rutaihwa aliishukuru Bodi hiyo pamoja na Menejimenti ya REA kwa utekelezaji wa miradi nishati safi ya kupikia ambapo kambi 22 zimepata fedha kutoka REA za utekelezaji wa mradi huo ili kulinda mazingira pamoja na afya za wanaoandaa chakula.

Naye Kamanda wa Kikosi cha 833 KJ Oljoro, Kanali Victor Rutayuga Faustine, amesema mradi huo wa nishati safi ya kupikia umeleta mafanikio makubwa katika utunzaji wa mazingira na kupunguza matumizi ya kuni kambini hapo pamoja na kutumia muda mdogo kwenye kuandaa chakula cha vijana wanaopata mafunzo kambini hapo.

“Kabla ya mradi huu tulikuwa tunaagiza lori la kuni kutoka Mbeya kwa ajili ya kupikia chakula cha vijana wetu wa mafunzo hapa kambini. Lakini sasa matumizi ya nishati safi yamesaidia kupunguza utegemezi huo na kulinda mazingira,” amesema Kanali Faustine.

REA imetoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni 5.2 kwa ajili ya kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kambi za JKT ambapo fedha hizo pamoja na mambo mengine, zimewezesha kufungwa kwa mifumo ya nishati safi ya kupikia pamoja na ununuzi wa mashine za kutengenezea mkaa mbadala.

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imesema kuwa uwekezaji unaofanywa na Oryx Energies Tanzania Limited ni kielelezo cha mafanikio ya juhudi za Serikali katika kuimarisha sekta binafsi na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya taifa.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali imewataka wanamichezo na wadau wa sekta ya michezo nchini kutumia mfumo wa miliki ubunifu kulinda vipaji, majina na chapa zao ili kuongeza thamani ya kiuchumi ya shughuli zao na kujijengea maisha bora baada ya michezo.
Na Mwandishi Wetu 

WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa umma kufurahia utumishi wao na kupeleka furaha kwa wananchi.
Serikali imeendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa dawa na vifaa tiba barani Afrika kupitia uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya afya na matumizi ya teknolojia za kisasa.
Kituo cha Utamaduni cha Iran nchini Tanzania kimeanzisha mashindano ya uchoraji yanayolenga kuhamasisha jamii, hususan watoto na vijana, kueleza hisia zao kupitia sanaa kufuatia tukio la mlipuko lililotokea nchini Iran mwezi Februari mwaka huu, ambapo Shule ya Msingi ya Minaab ililipuliwa na kusababisha vifo vya wanafunzi 168.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amelielekeza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuhakikisha linalinda na kuthamini rasilimali za taasisi ili kuongeza ubora na ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan itaendelea kulinda ajira zilizopo na kuzalisha ajira mpya kupitia sekta ya viwanda na biashara kwa manufaa ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, leo tarehe 8 Mei, 2026 imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini katika Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kupata taarifa ya utekelezani wa miradi hiyo.

Mwenyekiti Kingu ambaye alikuwa ameongozana na Wajumbe wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Radhia Msuya na Mhandisi Sophia Mgonja walikutana na Kampuni ya Ceylex Engineering Limited na Derm Group Limited na ambao wanatekeleza miradi kwa Mkoa wa Kilimanjaro na pia walikutana na Kampuni ya Ceylex Engineering Limited na Nakuroi Investment Company Limited ambazo zinatekeleza miradi kwa Mkoa wa Arusha.

Mwenyekiti Balozi Meja Jenerali Mstaafu Kingu, amewatata wakandarasi hao kutekelezea miradi hiyo ndani ya muda wa mkataba waliosaini na kuhakikisha wanazingatia ubora unaotakiwa.

Kikao hicho ambacho kilihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu, Meneja Msimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mhandisi Michael Kyessi, Mhandisi Miradi kutoka REA, Isaac Sanga pamoja na Mameneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wa Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.