Serikali imezitaka Wizara, Taasisi za Umma, Sekta Binafsi, Watafiti na Mashirika ya Kiraia kuchangamkia fursa ya Tanzania kuwa mwenyeji wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12).
Hayo yamesemwa leo Julai 2, 2026 Jijini Tanga na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu maandalizi ya Tanzania kuelekea Mkutano huo unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba mwaka huu.
Naibu Waziri Kwagilwa amesema katika Mkutano wa 11 wa Nchi Wanachama uliofanyika nchini Madagasca mwaka 2024, Tanzania ilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Mkataba wa Nairobi kwa kipindi cha miaka miwili hadi Disemba Mwaka 2026 pamoja na kuteuliwa kuwa mwenyeji wa COP12.
“Mkutano wa COP12 utajadili utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mkataba kwa kipindi cha mwaka 2024–2026 pamoja na kujadili masuala muhimu ikiwemo hifadhi na urejeshwaji wa mifumo ikolojia ya bahari kama mikoko, miamba ya matumbawe na nyasi bahari” amesema Mhe. Kwagilwa.
Ameongeza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuipa kipaumbele sekta ya mazingira na uhifadhi wa rasilimali za bahari ili kuimarisha uhifadhi wa rasilimali za bahari, mito, maziwa, maji chini ya ardhi na maeneo oevu.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri Kwagilwa, amesema Dira 2050 imeitambua sekta ya uchumi wa Buluu kuwa miongoni mwa sekta za kimkakati zinazokusudia kuleta mageuzi ya maendeleo endelevu na kuchangia ukuaji wa kijamii, kiuchumi na kiikolojia.
Amesema kuwa Tanzania ni nchi ya pwani yenye fursa kubwa ya kunufaika na sekta ya uchumi wa buluu kupitia uvuvi, nishati, usafirishaji, utalii, madini, mazingira na viwanda, hivyo mkutano huo utaliwezesha taifa kuwa katika nafasi bora ya kufikia maendeleo endelevu.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian amesema matokeo ya utafiti uliofanyika mkoani humo yanaonyesha athari za mabadiliko ya tabianchi zimeanza kuathiri kwa kiwango kikubwa shughuli za uvuvi na ukuzaji wa viumbe maji, hususan kilimo cha mwani.
Amesema utafiti uliofanyika kati ya mwaka 2021 na 2025 umebaini kuwa joto la bahari limeongezeka kutoka nyuzi joto 25.6 mwaka 2021 hadi kufikia nyuzi joto 28.39 mwaka 2024, hali inayobadili mfumo wa ikolojia wa bahari na kuathiri uzalishaji katika sekta ya uvuvi.
"Tumeshuhudia ongezeko la karibu nyuzi joto tatu baharini, huku siku za wavuvi kwenda kuvua zikishuka kutoka siku 221 mwaka 2021 hadi siku 170 kutokana na upepo mkali na hatari ya usalama baharini. Pia mavuno ya samaki yamepungua kwa wastani wa asilimia 25 hadi 30," amesema Dkt. Burian.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda amesema mkutano wa COP 12 utahusisha washiriki takribani 500-600 ikiwemo viongozi wa nchi, wataalamu na wadau mbalimbali.
Ameongeza kuwa lengo la tamko hilo la Serikali ni kuweka msingi wa maandalizi ya kina, ikiwa ni pamoja na kubainisha vipaumbele vya Taifa, na kupanga mikakati ya ushiriki ili kuhakikisha maandalizi yanafanyika kwa ufanisi na kwa wakati.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi mwanachama wa Mkataba wa Nairobi unaohusu Hifadhi, Usimamizi na Uendelezaji wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi.
Mkataba huu ulisainiwa tarehe 21 Juni 1985 na unatekelezwa chini ya usimamizi wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).
MWISHO

KATIKA hatua inayoashiria mabadiliko ya kimkakati katika usimamizi wa mazingira nchini, Serikali imeweka bayana mwelekeo mpya wa kuimarisha usafi wa mazingira kama nyenzo muhimu ya kupunguza magonjwa, kuongeza tija ya kiuchumi na kuharakisha maendeleo ya miji na vijiji.
Mkakati huo umeibuliwa jijini Dodoma leo July 2,2026 katika Kongamano la Kitaifa la Usafi wa Mazingira lililoambatana na uzinduzi wa mwongozo wa mpango jumuishi wa usimamizi wa huduma za usafi wa mazingira, ambalo limeweka msisitizo mpya wa kuunganisha huduma za usafi katika mfumo mmoja jumuishi unaolenga kuwafikia wananchi wote bila kuacha makundi yaliyo pembezoni.
Akizungumza katika kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Profesa Palamagamba Kabudi,amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira kuwa agenda ya kimkakati inayohitaji utekelezaji wa kisera, kitaasisi na kijamii kwa pamoja.
Amesema usafi wa mazingira sasa hautazamwi tena kama shughuli za kawaida za kijamii, bali ni sekta yenye mchango wa moja kwa moja katika afya ya umma, ustahimilivu wa miji na ukuaji wa uchumi.
Prof.Kabudi amesisitiza kuwa mkakati wa sasa unalenga kuhakikisha huduma jumuishi za usafi wa mazingira zinaimarishwa ili kupunguza tofauti za upatikanaji kati ya mijini na vijijini, pamoja na kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji na utupaji taka.
“Tunajenga mfumo ambao unafanya usafi wa mazingira kuwa huduma ya msingi inayofika kwa kila Mtanzania,” amesema Kabudi.
Ameongeza kuwa mafanikio ya mkakati huo yanategemea mabadiliko ya tabia kwa wananchi sambamba na uwekezaji katika miundombinu ya kisasa ya usafi wa mazingira.
Aidha, ametumia kongamano hilo kumpongeza Rais Samia kwa kuendelea kuongoza ajenda ya nishati safi ya kupikia, akisema ni sehemu muhimu ya mkakati mpana wa kulinda mazingira na kupunguza uchafuzi unaotokana na nishati chafu.
Katika hoja ya kiufundi, Kabudi ameonya juu ya kuendelea kwa tabia ya utupaji taka kwenye mitaro ya maji ya mvua, akisema vitendo hivyo vinadhoofisha mifumo ya miji na kuongeza hatari ya mafuriko na magonjwa ya mlipuko.
Amesisitiza kuwa uwekezaji katika usafi wa mazingira ni sehemu ya mkakati wa taifa wa kulinda afya ya umma na kupunguza gharama za matibabu zinazotokana na magonjwa yanayohusiana na mazingira.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha wa EWURA, Stanley Mahembe,aliyemwakilishi Mkurugenzi Mkuu amesema bado kuna pengo kubwa la kitaasisi katika usimamizi wa majitaka, akibainisha kuwa ni mamlaka 24 pekee kati ya 84 ndizo zilizo na mipango ya matibabu ya majitaka na tope la kinyesi.
Amesema hali hiyo inaonyesha umuhimu wa kuharakisha utekelezaji wa mwongozo mpya wa usimamizi wa mazingira uliozinduliwa katika kongamano hilo.
Naye Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA, Ngosi Mwihava, amesema kupitia bajeti ya shilingi trilioni 1.12 iliyopitishwa kwa ajili ya Wizara ya Maji, kuna matumaini makubwa ya kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya maji taka na usafi wa mazingira, ili kuendana na lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) namba 6 linalohusu upatikanaji wa maji safi na usafi wa mazingira kwa wote.
Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, Kunti Majala, amesema changamoto za mazingira zinaendelea kuchangia vifo vinavyoweza kuzuilika, hivyo kuhitaji mkakati wa elimu na usimamizi kuimarishwa zaidi.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, amesema ongezeko la kasi la watu katika mji wa Dodoma linahitaji mkakati madhubuti wa usafi wa mazingira unaoendana na ukuaji wa mji huo.
Kongamano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa dira mpya ya taifa ya kuimarisha mifumo ya usafi wa mazingira, kwa lengo la kujenga miji salama, yenye afya na endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Nilitabasamu kidogo na kupiga picha moja tu, halafu nikaangalia matokeo yake kabla sijaiweka hadharani.
Wote walionekana ni marefu na walikuwa wamevaa mavazi meusi, lakini cha kutisha zaidi ni kwamba nyuso zao zilikuwa zimefunikwa kwa kitambaa cheusi kama mazishi.
Tulikaa naye kwa miaka miwili, lakini kwa kipindi chote hicho nilijikuta nikilia kila siku.
Alininyima mapenzi ya kweli si tu kimwili bali hata kwa maneno.
Nilivumilia kwa sababu nilidhani labda siku moja atabadilika. Lakini siku zilisonga, na mateso yakawa kawaida yangu.
Lakini ndani ya miezi sita tu baada ya harusi, maisha yangu yakabadilika ghafla. Mke wangu alianza kuwa mtu tofauti kabisa na yule niliyempenda. Alianza kuwa mkali, mgumu kuelewana naye, na mara kwa mara alinituhumu kwa mambo ambayo hayakuwa ya kweli.
Mara nyingi alirudi nyumbani akiwa mlevi au aliingia chumbani akiwa mnyamavu kana kwamba hakutaka hata kuzungumza nami. Ilifikia hatua hata kula pamoja ilikuwa shida. Nilihisi kuna kitu kibaya, lakini sikuweza kukieleza. SOMA ZAIDI.
Tulisali, tulifunga, lakini hali ilizidi kuwa mbaya.
Kila mtu alikuwa anahisi hali hiyo si ya kawaida. Hata wageni waliokuja nyumbani walihisi hali ya baridi na uzito wa ajabu mara tu walipoingia mlangoni. Mmoja wa marafiki wa karibu wa familia yetu alituambia wazi kuwa huenda kuna mtu ametuloga au ametutendea jambo la kichawi.
Nilikuwa miongoni mwa watu ambao zamani nilikuwa siamini mambo haya lakini kilichokuwa kinaendelea kilinifanya nibadili msimamo wangu. Kwa mara ya kwanza, niliamua kutafuta msaada wa kitaalamu wa asili. SOMA ZAIDI.
Nilijaribu kulazimisha mazungumzo naye kuhusu hali hiyo, lakini alinijibu kwa maneno ya baridi, “Watoto wote ni baraka.”
Nilianza kusaka suluhisho kila mahali kwa madaktari wa kawaida, mitandaoni, na hata kupitia marafiki wa karibu. Lakini kila nilichopewa kilikuwa ushauri wa jumla tu. Hakuna kilichokuwa na uhakika.SOMA ZAIDI.
📌 Njia ya kV 400 yenye urefu wa km 345 kukamilika Agosti 21, 2026; kubeba umeme wa JNHPP na kuongeza uwezo wa Gridi ya Taifa.
Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma wenye urefu wa kilometa 345 umefikia asilimia 89 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 21, 2026. Kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha uwezo wa kusafirisha umeme, kuongeza uthabiti wa Gridi ya Taifa na kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini.
Akikagua maendeleo ya mradi huo Julai 1, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amesema mradi huo ni sehemu ya uwekezaji mkubwa wa kimkakati wa Serikali unaolenga kuimarisha miundombinu ya usafirishaji wa umeme ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya nishati nchini na kuifanya Gridi ya Taifa kuwa imara zaidi.
Mhe. Ndejembi amesema njia hiyo ya umeme ina umuhimu wa kipekee kwa kuwa itawezesha usafirishaji wa umeme unaozalishwa na Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) chenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 kwenda katika maeneo mbalimbali ya nchi, hivyo kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme kwa wananchi na sekta za uzalishaji.
“Serikali imeona mahitaji ya umeme nchini yanaendelea kuongezeka kutokana na ukuaji wa uchumi na ongezeko la wateja. Ujenzi wa njia hii ni muhimu kwa sababu utaongeza uwezo wa kusafirisha umeme na kuimarisha uthabiti wa Gridi ya Taifa,” amesema Mhe. Ndejembi.
Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuhakikisha Watanzania wanaendelea kupata huduma ya umeme wa uhakika inayochochea maendeleo ya viwanda, biashara na uchumi kwa ujumla.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Razalo Twange, amesema uwekezaji unaoendelea katika miundombinu ya umeme umewezesha Shirika kuongeza kwa kiasi kikubwa huduma kwa wananchi. Amesema katika mwaka wa fedha 2025/26, TANESCO imeandika historia kwa kuwaunganishia umeme zaidi ya wateja 800,000, idadi ambayo haijawahi kufikiwa tangu Tanzania ipate uhuru.
“Historia hii inaonesha wazi kuwa mahitaji ya umeme yanaongezeka kwa kasi, ndiyo maana tunaendelea kuwekeza katika miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuendana na ukuaji huo,” amesema Bw. Twange.









