Na Oscar Assenga,TANGA

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman amesema ana dhamira ya dhati kurejesha timu ya mpira wa miguu, African Spots ya jijini humo ili kurejesha heshima ya timu hiyo kongwe pamoja na Dabi ya Tanga iliyokuwa na upinzani mkubwa hapa nchini.



Alisema timu hiyo imekuwa ikisuasua kupanda daraja kwa muda mrefu kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo basi la kuwasafirisha wachezaji pamoja na benchi la ufundi hivyo uwepo wa basi hilo utasaidia kuwawezesha kuondokana nazo


Aliyasema hayo Januari 24 mwaka huu katika hafla ya kuukabidhi uongozi wa timu hiyo gari Jipya aina ya TATA lililogarimu takribani shilingi Milioni 170, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Klabu hiyo barabara 12 Jijini Tanga .

Rajabu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) alisema kwamba kurudi kwa timu hiyo kongwe hapa nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1936 kutarejesha heshima ya Mkoa wa Tanga kutokana na kwamba bila African Spots hakuna Coastal Union inayochangiwa na utani wa jadi timu hizo kama ilivyokuwa Simba na Yanga za Jijini Dar es Salaam.


Mbali ya kununua basi na kukabidhi, Mwenyekiti ameahidi kusaidia timu hiyo na kuiinua hadi kufikia kucheza ligi kuu ambapo ataipambania na kujenga Jengo la Ofisi la Gorofa tatu ikiwa ni pamoja na kununua gari kubwa zaidi wakati gari iliyokabidhiwa kubaki kuwa ya kuwapeleka wachezaji mazoezini.



Sambamba na kukabidhi gari hilo mwenyekiti huyo pia alitoa kiasi cha shilingi Milioni 30 na kukabidhi kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kwa ajili ya kutatua changamoto kadhaa zinazowakabili.


Awali akizungumza katika Halfa hiyo Rais wa TFF Walles Karia aliwasihi wanachama kushirikiana na vionhozi ili kufanya maamuzi pamoja na kujitokeza uwanjani pindi timu zitakapokuwq zancheza kwani ndio jambo sahihi la kuvuta wawekezaji.


Lakini pia aliwasihi viwanja vya michezo vilivyopo Myanjani Technically Center, "kile kituo kipo na kinafanya vizuri sana lakini kinanufaisha vijana walioko nje ya Tanga, niwasiji kwamba mpeleke vijana pale ili timu zetu zipate wachezaji bora" alisema Karia.

Katika hafla hiyo alikuwepo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) ambaye alisisitiza suala la wanachama kushirikiana na vionhozi wa timu hiyo na kuchangia kipato kwenye timu matokeo yataonekana.

"Kama tutakuwa na timu mbili (2) zinazoenda ligi kuu, hata uchumi wa Tanga utaimarika kupitia michezo, tuchangie timu kwa kwenda uwanjani na hata kununua jezi, kwa kufanya hivyo kutaimarisha timu zetu na wachezaji kuwa na ari uwanjani" alisema.

Katika kuinua timu hizo Naibu Waziri Mwana FA alitoa kiasi cha shilingi Milioni 10 ambapo kila timu imekabidhiwa kwa vionhozi wa timu zote mbili kiasi cha shilingi Milioni 5.

Rais Karia amewahakikishia Watanzania kwamba timu ya African Spots ikismama imara kama awali na Coastal Union ndiyo timu pekee ambazo zina uwezo wa kusimamishana na Simba na Yanga na siyo timu nyingine.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi, Dk. Batilda Buriani aliwataka vionhozi wa timu za mipira na wanamichezo wote kutumia fursa ambazo zipo mkoani humo katika kuimarisha timu na kuleta manufaa katika Mkoa.

"Mradi wa Bomba la mafuta nao una fursa katika michezo, kule Uganda wamesaidia kujenga uwanja wa mpira, na hata timu yetu ya Coastal Union imeshapeleka maombi yake tunasubiri utekelezaji mwengine uendelee"

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru mkoani Arusha na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa chuoni hapo, ikiwemo ujenzi wa jengo la Utawala, kituo cha uhifadhi wa machapisho yanayohusu  wanawake, mabweni ya wanafunzi pamoja na Kituo cha Ubunifu wa Kidigitali na Huduma Tandaa (JODIC).

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la Utawala, Mhe. Mahundi amesema serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya vyuo vya maendeleo ya jamii ili kuimarisha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma.

 “Miradi inayoletwa hapa chuoni inapaswa kusimamiwa kwa viwango vinavyokubalika ili thamani ya fedha itumike ipasavyo na kwa ubora unaostahili kwa manufaa ya wanafunzi na taasisi kwa ujumla,” amesema Mhe. Mahundi.

Aidha , Mhe. Mahundi amepata fursa ya kuzungumza na wanafunzi wa taasisi hiyo ambapo amewahimiza kutumia elimu wanayoipata chuoni hapo kwenda kuitumikia jamii kwa vitendo kwa kuwa  elimu ya maendeleo ya jamii inapaswa kuwa chachu ya mabadiliko chanya katika jamii na siyo kubaki darasani pekee. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru, Dkt. Bakari George, ameishukuru serikali kwa kuendelea kuiunga mkono taasisi hiyo kupitia utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. 

“Hili  jengo la Utawala na miradi mingine inaongeza ufanisi wa kiutendaji na kuboresha huduma kwa wanafunzi, Uwekezaji huu unaofanywa na serikali ni kielelezo cha dhamira yake ya kuimarisha elimu ya maendeleo ya jamii nchini,” amesema Dkt. George.

Ziara hiyo ya Naibu Waziri Mahundi katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru imekuwa sehemu ya juhudi za serikali katika kuimarisha elimu ya maendeleo ya jamii nchini, kwa lengo la kuhakikisha vyuo vinaendelea kuzalisha wataalamu wenye ujuzi, ubunifu na maadili watakaotumia elimu yao kutatua changamoto za kijamii, kuendeleza ustawi wa wananchi na kuchangia maendeleo endelevu ya Taifa.





















Maisha yangu yalikuwa gumu sana. Nilihisi naliachwa peke yangu na kila mtu: marafiki walinigeukia, familia ilikuwa mbali, na hata watu wa karibu walinidharau. Kila jaribio langu la kujiinua au kupata msaada liligonga mwamba.

Nilijiona nimefungwa ndani ya hali isiyokuwa na mwanga. Machozi na huzuni vilijaza kila siku yangu, na moyo wangu ulikuwa mzito. 

Nilihisi kama kila mtu alikuwa amepoteza imani yangu na mimi mwenyewe nilianza kujiuliza kama maisha yangu yangewahi kubadilika.

Nilijaribu kila njia ya kawaida ya kurekebisha maisha yangu: kazi mpya, biashara ndogo, kujitahidi kuzungumza na wengine, lakini kila jambo lilikuwa bure. 

Kila mtu alionekana kufanikisha maisha yake huku mimi nikianguka.Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/niliachwa-na-kila-mtu-lakini-njia-hii-ilinirudishia-heshima-yangu-hadharani/

Miaka mitano ya maisha yangu yalikuwa ni machungu. Kila nilipojaribu kusonga mbele, watu walinicheka, wakiniona kama mtu wa kushindwa. Kila jaribio langu la biashara, mapenzi, na hata kazi lilibaki bila matokeo.

Nilijikuta nikiwa peke yangu, nikiogopa kushirikiana na mtu yeyote kwa sababu kila mara nilipokuwa na matumaini, nilipoteza tena. Machozi, hasira na huzuni vilichanganyika ndani ya moyo wangu, nikijiuliza kama siku moja maisha yangu yangebadilika.

Nilijaribu kila njia: madaktari, mitambo ya kazi, ushauri wa rafiki, kila kitu. Lakini kila jitihada ilishindwa. Nilihisi kama dunia ilikuwa ikinicheka nyuma ya pazia, na mimi sina nguvu ya kuibadilisha.

Nilijaribu kuacha kuota ndoto kubwa, lakini moyo wangu haukuridhika; kila mara nilijitahidi kuishi kwa ndoto ndogo, nikijitahidi kuendelea bila matumaini makubwa. Nilijua kile nilichotaka kilikuwa kubwa, lakini kila njia ilikataa kuniruhusu kufika. Soma Zaidi...

https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilichekwa-kwa-miaka-mitano-leo-wananiomba-namba-ya-mganga-baada-ya-maisha-yangu-kubadilika-kabisa/
Maisha ya binti huyu yalikuwa ya kawaida mwanzoni. Alikuwa msichana wa kawaida, anayefurahia shule, marafiki, na ndoto zake za maisha. Lakini kwa ghafla, mambo yalibadilika ghafla. 

Alianza kuishi hali ya kushangaza: mwili wake na akili yake vilianza kushindwa kufanya kazi kwa usawa.

Nilipojaribu kuzungumza naye, alionekana kama alikuwa kimya kimya, akiwa na huzuni isiyoelezeka. 

Baada ya uchungu zaidi, familia iligundua kuwa binti huyu alikuwa amepatwa na kitu kisichoelezeka. Alikuwa kapewa yai na mtu asiyemjua, na ndani ya muda mfupi hali yake ilibadilika ghafla.

Alianza kuonyesha dalili za uchawi: usingizi wa kushangaza, nguvu kupungua, na hali ya kuogopa kila mtu karibu naye. 

Wote walijaribu njia za kawaida madaktari, dawa za kawaida, hata mazungumzo lakini hakuna kilichokuwa kikiwasaidia. Hali hiyo ilizidisha hofu na huzuni kwa familia nzima.

Wakati huo, walihisi kila kitu kilikuwa kimemalizika. Binti huyu alipoteza furaha, afya yake ilishuka, na kila siku ilikuwa vita ya kuishi. 

Familia ilijikuta ikikata tamaa, wakiwa na shaka kama atarudi kuwa sawa tena. Machozi na kukata tamaa vilijaa nyumbani kwao.Soma Zaidi...

https://kiwangadoctor.com/kiswahili/binti-kapewa-yai-na-mtu-asiyemjua-kumbe-kalishwa-uchawi-lakini-arudi-sawa-baada-ya-kupata-usaidizi-huu/

Maisha kazini mara nyingine huwa na changamoto zisizo za kawaida, lakini siku hiyo, mimi sikuwahi kufikiria kuwa mambo yangekuwa mabaya kiasi hiki. 

Nilijua kuwa mke wa boss wangu alikuwa na maisha yake ya kimapenzi, lakini hakukuwa na dalili yoyote ya shida.

Kila kitu kilionekana kuwa kawaida. Hata hivyo, ndani ya ofisi, baadhi ya watu walikuwa wakianza kuona mwenendo wa ajabu, na mapenzi yasiyo ya kawaida yakianza kuibuka kimyakimya. 

Siku moja, tukio lililotisha lilitokea. Penzi la mlinzi wa nyumba lilianza kuonekana wazi mbele ya kila mtu.

Kwa mara ya kwanza, hakuweza kuficha hisia zake, na hali hiyo ilileta hofu, kutokuwa na amani, na kuchanganya hisia za kila mtu. 

Watu walianza kuzungumza kimyakimya, wengine wakidhani ni wivu wa kawaida, wengine wakidhani ni bahati tu ya ajabu.

Lakini mimi nilijua kuna kitu kingine kilichokuwa kinaficha nyuma ya tabia hizi.
Mke wa boss alijikuta kwenye hali ngumu, akidhani kuwa hakuna mtu anayeona. Lakini kila siku, hofu na wasiwasi viliongezeka.

Nafsi zetu zote zilidhani mambo yangeendelea hivi bila suluhisho, lakini ndani ya moyo wangu, nilihisi lazima nisuluhishe kwa njia ambayo haiwezi kuumiza au kushusha heshima ya mtu yeyote.Soma Zaidi.....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mke-wa-boss-anogewa-na-penzi-la-mlinzi-kilichotekea-baada-ya-kufumaniwa-nichakushangaza/
Siku hiyo haikuwahi kutoka kwenye kumbukumbu za maisha yake. Ilikuwa ni siku ya huzuni nzito, machozi yasiyokauka, na maumivu ya kumpoteza mtoto. Alijifungua mapacha wawili, lakini furaha ile iligeuka haraka kuwa kilio.

Madaktari walitangaza kwa masikitiko kuwa mmoja wa mapacha hao hakunusurika. Bila maswali mengi, bila muda wa kuhoji, waliambiwa mtoto amekufa. Kwa moyo uliojaa maumivu, familia ilifanya mazishi. Mtoto yule mdogo alizikwa, na maisha yakalazimika kuendelea.

Pacha aliyebaki alikua chini ya uangalizi mkubwa, lakini kila siku mama yake aliishi na kovu moyoni. Kila alipomtazama mtoto wake aliyesalia, alijiuliza kimya kimya: “Je, pacha wake angekuwa vipi leo?”

Miaka ilipita. Mtoto alikua, akaanza shule, akakomaa. Maisha yalipata sura mpya, ingawa kumbukumbu ya yule pacha aliyedhaniwa kufa haikuwahi kupotea kabisa. Ilikuwa ni simulizi ya huzuni iliyofunikwa na wakati.

Ajabu ilianza siku moja mjini, alipokwenda kwenye shughuli zake za kawaida. Akiwa njiani, macho yake yalivutwa na kijana mmoja aliyepita karibu naye. 

Moyo wake uliruka. Alisimama ghafla. Uso ule, macho yale, hata mwendo… vilifanana kupita kawaida. Soma Zaidi....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/alizika-pacha-mmoja-akidhani-amekufa-ajabu-alikuja-kumuona-tena-akiwa-mtu-mzima/

 


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) zimeingia makubaliano yaliyolenga kufikisha umeme katika vitongoji na jamii ambazo zimepitiwa na bomba hilo la mafuta kwa upande wa Tanzania.

Mkataba huo wa ushirikiano ambao utatekelezwa kwa miaka mitano, umesainiwa leo Januari 23, 2026 Jijini Dar es Salaam kati ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa EACOP, Guillaume Dulout.

Akizungumza baada ya kusainiwa kwa mkataba huo, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Saidy amesema kuwa makubaliano hayo yatahakikisha jamii zinazoishi pembezoni mwa mradi wa bomba la mafuta kutoka Mkoa wa Kagera mpaka Mkoa wa Tanga zinafikiwa na kunufaika na mradi huo kwa kufikishiwa huduma ya umeme.

Mhandisi Saidy ameongeza kuwa ushirikiano huo pamoja na manufaa mengine unalenga kuimarisha huduma za kijamii kama shule, vituo vya afya na miradi ya maji, pamoja na kuchochea matumizi ya umeme kwa shughuli za uzalishaji mali na kukuza biashara maeneo ya vijijini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa EACOP, Dulout amesema kuwa utekelezwaji wa mradi huo ni muendelezo wa EACOP kuboresha maisha ya jamii zinazopitiwa na mradi wa bomba la mafuta.

Kwa Tanzania, mradi wa bomba la mafuta linapita katika mikoa 8, halmashauri 27 na vijiji 231, hivyo kugusa moja kwa moja maisha ya jamii nyingi za vijijini na utekelezwaji wa makubaliano kati ya REA na EACOP, ni hatua muhimu katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo kando kando ya na mradi wa bomba la mafuta zinanufaika moja kwa moja na upatikanaji wa umeme.












Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dennis Londo amelipongeza Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) kwa kutekeleza ahadi ya siku 100 ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutoa mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa wajasiriamali ili kuendeleza miradi mbalimbali ya viwanda nchini.

Baraza la Ushindani (FCT) limeendesha mafunzo ya uwezeshaji kwa wadau mbalimbali jijini Moshi, mkoani Kilimanjaro,katika ukumbi wa Kiringe. Mafunzo hayo yaliwahusisha wafanyabiashara na wananchi kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu masuala ya ushindani, haki za kibiashara na mifumo ya kisasa ya utoaji wa haki.

Mafunzo hayo yalijibiwa kwa mwitikio mkubwa, ishara kuwa kuna mahitaji makubwa ya elimu kuhusu taratibu za kisheria na huduma zinazotolewa na Baraza la Ushindani.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Msajili wa Baraza, Mhe. Mbegu Kaskasi, amewashukuru wadau wa Moshi kwa kujitokeza kwa wingi na kuonesha hamasa ya kujifunza, akisema hatua hiyo inaonyesha utayari wa jamii kuimarisha mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki.

Mhe. Kaskasi amebainisha kuwa Baraza linaendelea kuboresha mifumo yake ili kurahisisha upatikanaji wa haki, ikiwemo mfumo wa kielektroniki wa uwasilishaji wa mashauri ya rufaa (e-filing), ambao umepunguza gharama na kuondoa usumbufu wa kusafiri kwa wale waliokuwa wakilazimika kufika ofisini moja kwa moja.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo walieleza kunufaika na elimu waliyoipata, wakisema imewasaidia kuelewa haki zao, wajibu wao na hatua za kufuata wanapohitaji kuwasilisha mashauri yao.