Wiki ya kwanza ilipita bila mafanikio. Familia yake ilimpigia simu mara nyingi lakini simu yake ilikuwa haipatikani.
Kadri siku zilivyoongezeka, huzuni ilitanda katika familia yote. Mama yake alikuwa akilia kila siku huku baba yake akijaribu kuficha maumivu aliyokuwa nayo.
Tulijaribu njia mbalimbali za kutafuta taarifa zake lakini hakuna kilichoonekana kufanya kazi. Hali hiyo iliwafanya ndugu na marafiki wake kuishi katika wasiwasi mkubwa. SOMA ZAIDI.
Tatizo lilianza pale muda wa kurejesha fedha ulipofika. Watu waliokuwa wakiniahidi kunilipa ndani ya wiki chache au miezi michache walibadilika ghafla.
Nilijikuta nikihitaji fedha hizo kwa ajili ya familia yangu na mipango mingine muhimu, lakini sikuwa na njia rahisi ya kuzipata.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Watu wengi walikuja kukiona kiwanja hicho. Wengine walionyesha nia kubwa ya kununua, wakapiga picha na kuuliza maswali mengi. Hata hivyo, baada ya hapo walipotea na hawakurudi tena. Miezi iligeuka kuwa miaka.
Kadri muda ulivyopita, nilianza kuvunjika moyo. Kila nilipopata simu kutoka kwa mtu aliyekuwa ameonyesha nia ya kununua, nilijawa na matumaini. Lakini mara nyingi mazungumzo yaliishia bila matokeo yoyote. Nilijaribu kupunguza bei.
Nilitangaza sehemu mbalimbali na hata kuwaomba marafiki wanisaidie kutafuta wanunuzi. Licha ya juhudi zote hizo, kiwanja changu kiliendelea kubaki bila mnunuzi.
Hali hiyo ilianza kuniathiri kifedha. Nilikuwa na mipango mingi iliyokuwa imesimama kwa sababu nilitegemea fedha za mauzo ya kiwanja hicho. SOMA ZAIDI.
Alikuwa mtiifu, mwenye bidii shuleni, na aliyeheshimu watu wote waliokuwa karibu naye. Kwa miaka mingi sikuwahi kupata malalamiko makubwa kuhusu tabia yake. Lakini mambo yalianza kubadilika ghafla.
Alianza kurudi nyumbani akiwa amechelewa bila sababu za kueleweka. Alikosa hamu ya kuzungumza na familia, na alionekana kuwa mkali kila nilipomuuliza maswali kuhusu marafiki zake wapya. Mwanzoni nilidhani ni hatua ya kawaida ya ukuaji.
Hata hivyo, kadri siku zilivyopita, nilianza kuona dalili ambazo zilinipa wasiwasi mkubwa. Matokeo yake shuleni yalianza kushuka, na baadhi ya walimu walinieleza kwamba alikuwa akijihusisha na wanafunzi waliokuwa na tabia zisizofaa. Nilihofia mustakabali wake.
Kila mzazi hutamani kuona mtoto wake akifanikiwa maishani. Nilijua kwamba kama nisingechukua hatua mapema, angeweza kuingia kwenye mkondo ambao ungeharibu ndoto zake na maisha yake kwa ujumla. Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa.
Wakati mwingine alisikiliza, lakini mara nyingi alionekana kutopenda ushauri wowote. Hali hiyo iliniumiza sana na kunifanya nikose usingizi. SOMA ZAIDI.
Familia yangu haikuwa na uwezo wa kugharamia masomo ya nje ya nchi, hivyo matumaini yangu yote yalikuwa kwenye kupata udhamini.
Kila nilipopokea ujumbe wa majibu, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa matumaini makubwa.
Lakini mara ya kwanza nilikataliwa.
Mara ya tatu ndiyo ilinivunja moyo zaidi.
Nilianza kujiuliza kama ndoto yangu ilikuwa kubwa kuliko uwezo wangu. Watu wengine walinishauri nikubali hali na kutafuta njia nyingine za kusoma karibu na nyumbani.
Zaidi ya wananchi 300 wametembelea banda la Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) tangu kuanza kwa Wiki ya Utumishi wa Umma, wakipata elimu na ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara katika maeneo yao, hatua hiyo imeendelea kuimarisha uhusiano kati ya wananchi na taasisi hiyo huku ikitoa fursa ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi moja kwa moja.
Akizungumza katika maonesho hayo, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa TARURA, Catherine Sungura, amesema wananchi wanaowasilisha kero zao huunganishwa moja kwa moja na mameneja wa maeneo husika ili kupata maelezo ya kina pamoja na ufumbuzi wa haraka, ameeleza lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu miradi inayotekelezwa na maendeleo yake.
Katika mwendelezo wa Wiki ya Utumishi wa Umma unaoendelea Jijini Dodoma hadi Juni 23, Sungura alieleza kuwa mwananchi kutoka eneo la Kimara amewasilisha maswali kuhusu maendeleo ya miundombinu ya barabara katika eneo lao , amesema TARURA imekuwa ikitoa ufafanuzi wa kina kwa kila mwananchi anayefika kwenye banda hilo.
Akizungumzia barabara ya King'ong'o iliyopo Kimara, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Sungura amesema ujenzi wa barabara ya zege unaoanzia eneo la TRA kuelekea King'ong'o unaendelea vizuri, amebainisha kuwa amewasiliana na Meneja wa TARURA Wilaya ya Ubungo na amewahakikishia wananchi kuwa kilomita 1.6 pekee ndizo zimebaki kukamilishwa, huku mita 800 zikitarajiwa kujengwa mwanzoni mwa mwaka mpya wa fedha kuanzia Julai na sehemu iliyobaki kukamilishwa katika awamu inayofuata.
Amesisitiza kuwa TARURA itaendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara inaboreshwa ili kurahisisha mawasiliano na usafiri kwa wananchi, huku akieleza kuwa barabara bora zinachochea upatikanaji wa huduma za kijamii, biashara na shughuli nyingine za maendeleo jambo ambalo ni muhimu katika kuinua ustawi wa jamii na kukuza uchumi wa maeneo mbalimbali nchini.
Meneja wa kampasi ya Dodoma ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Epaphra Manamba amesema katika kuendana na mahitaji ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 IAA itaendelea kuwekeza katika mitaala itakayojikita kwenye elimu – ujuzi (Competence based ) na ubunifu ili kuwaandaa wataalam watakaokuwa na uwajibikaji jumuishi katika kujenga Uchumi Jumuishi.
Prof. Manamba ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la IAA kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
“Dira ya Taifa ya 2050 imeipa sekta binafsi nafasi kubwa, tunapoongelea uwajibikaji jumuishi na uchumi jumuishi sekta binafsi inahusika kwa asilimia 100;sekta binafsi imepewa nguvu kwa sababu maendeleo ya nchi hii yatachangiwa na sekta binafsi na serikali itaandaa miundombinu ili kuiwezesha sekta binafsi kufanya kazi yake”
“Kozi za IAA zinamuandaa mwanafunzi si tu kwamba aende akaajiriwe bali aweze kujiajiri na kuajiri wengine.IAA ina Kiotamizi (Incubator) kazi yake ni kuwasaidia wanafunzi kuandaa mawazo ya biashara, kusimamia waweze kusajili biashara na kampuni zao, kuwaunganisha na wadau, wafadhili wakiwa bado chuoni; wengi wao wamefanikiwa kumaliza masomo yao tayari wakiwa wanamiliki kampuni zao na wanajipatia kipato,” amesema Prof. Manamba.
Mhitimu wa IAA ngazi ya Shaahda na Shahada ya Uzamili Bw. Justine Kitaja,amesema anajivunia kuwa sehemu ya mafaniko ya IAA anaipongeza IAA kwa ubinifu katika kuandaa mitaala yao na kuwawezesha wanafunzi kupata elimu bora inayoendana na mahitaji ambayo inawasaidia katika maeneo wanayofanyia kazi.











Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang'onda (wa pili kushoto) akizungumza kwenye mradi wa maji wa Mikocheni/Mkwaja. Kushoto kwake ni Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso na kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mhe Ayubu Sebabili
Na Mwandishi Wetu, PANGANI
WAZIRI wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ameagizi Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kuunganisha mtandao wa majisafi na salama kwenye makazi ya watu katika kijiji cha Mkwaja.
Mhe. Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Pangani, ameyasema hayo leo Juni 20, 2026 kijijini hapo, alipokaribishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa upanuzi mtandao wa maji kutoka ‘mradi mama’ uliopo kijiji cha Mikocheni.

Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Raiyan Mohamed Rashid, akimtishwa ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mkwaja wilayani Pangani, Mkoa wa Tanga kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji uliofika kijijini hapo kutokea kijiji jirani cha Mikocheni.
Mwenge wa Uhuru wenye kauli mbiu inayosema, “Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo” ulifika kwenye mradi huo wa kwanza baada ya kuingia katika Halmashauri ya Pangani kutokea Handeni.
Mhe. Aweso amesema, kwa vile Mwenge umechagiza maendeleo wilayani humo kwa vipindi tofauti, ipo haja ya kuendeleza hali hiyo kwa kuingiza maji kwenye makazi ya watu, badala ya kuishia kwenye vituo 12 vya kuchotea maji (DPs) vilivyopo Mkwaja.
Amesema, usambazaji majisafi na salama ni utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kumtua ndo mama kichwani.
Kwa mujibu wa Mhe. Aweso, kati ya vijiji 12,333 vilivyopo nchini, 10,758 vimefikiwa na huduma ya majisafi na salama wakati 1,575 vitafikiwa ifikapo 2030.
Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Pangani, Mhandisi Rajab Hussein, amesema upanuzi wa mradi wa Mikocheni ni matokeo ya upatikanaji maji kwa wastani wa lita 480,000 kwa siku, wakati mahitaji ya Mikocheni pekee ni lita 40,000.
Kwa mujibu wa Mhandisi Hussein, mahitaji yaliyobainika kwa matumizi katika kijiji cha Mkwaja ni lita 65,000 kwa siku na kufanya jumla yake kuwa lita 105, hivyo kuwa na lita 375,000 za ziada.

Ni picha ya uzinduzi wa mradi wa maji.
Amesema kupitia upanuzi wa mradi huo, RUWASA imejenga tenki lenye uwezo wa kuchukua lita 90,000 na kuwekwa kwenye mnara wa urefu wa mita sita, hivyo kuwa na uwezo wa kusambaza maji kijijini Mkwaji kupitia DPs zilizopo.
Naye Mwang’onda amesema agizo la Mhe. Aweso kwa RUWASA kuunganisha mtandao wa maji kwenye makazi ya watu ni kuuheshimisha Mwenge na kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mwang’onda amesema historia imeandikwa kwa Mhe. Rais Dkt Samia kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji majisafi na salama sehemu kubwa ya nchi.
Kwa hali, Mwang’onda, amehimiza wananchi kuwekeza zaidi katika amani, umoja na mshikamano, ili kufikia maono ya Mhe. Rais Dkt Samia kuwa na maendeleo endelevu.
MWISHO.

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linaendelea kushiriki kikamilifu katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Kitaifa yanayoendelea mkoani Dodoma, kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali kuhusu umuhimu wa kuzingatia viwango na ubora wa bidhaa zinazozalishwa na kutumika nchini.
Akizungumza katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa TBS, Julius Lwenje, amesema kuwa shirika hilo lina jukumu la kusimamia na kuhakikisha bidhaa mbalimbali zinazozalishwa, kuingizwa na kuuzwa nchini zinakidhi viwango vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria.
Amesema TBS inaendelea kutoa huduma za ukaguzi, upimaji na uthibitishaji wa ubora wa bidhaa mbalimbali, ikiwemo vyakula na vinywaji, kwa lengo la kulinda afya, usalama na maslahi ya watumiaji.
Lwenje amewahimiza wananchi kuendelea kutumia bidhaa zenye alama ya ubora ya TBS, akieleza kuwa alama hiyo ni uthibitisho kwamba bidhaa husika imefanyiwa ukaguzi na imekidhi viwango vinavyotakiwa.
“Tunawaomba wananchi kuwa makini wanaponunua bidhaa na kuhakikisha wanachagua bidhaa zenye alama ya ubora ya TBS, kwani hii ni ishara kwamba bidhaa hizo zimehakikiwa na kuthibitishwa kuwa salama kwa matumizi,” amesema.
Aidha, amesema ushiriki wa TBS katika maadhimisho hayo unatoa fursa kwa wananchi kupata elimu kuhusu huduma zinazotolewa na shirika hilo pamoja na kuelewa mchango wa viwango katika kukuza biashara, kulinda walaji na kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanawakutanisha taasisi mbalimbali za Serikali na wadau wake kwa lengo la kuonesha huduma wanazotoa na kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na wananchi.






Na Saidina Msangi na Asia Singano, WF - Dodoma
Wizara ya Fedha imeendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhakikisha wananchi wanapata ufafanuzi kuhusu masuala ya kodi, uchumi na sera mbalimbali za fedha na mchango wa kodi katika kugharamia huduma muhimu za kijamii kama vile miundombinu, elimu, afya, maji nishati na huduma nyingine muhimu.
Hayo yamebainishwa na Afisa Usimamizi wa Fedha Mkuu, Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. Abdul Dachi, wakati akitoa elimu kwa wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Bw. Dachi alisema kupitia Maonesho hayo, Idara imekuwa ikitoa taarifa kwa wananchi kwa lugha rahisi na inayoeleweka ili kuwawezesha kufahamu mchango wa Sera za Kodi na Uchumi katika maendeleo ya Taifa na ustawi wa jamii.
‘‘Miongoni mwa maeneo yanayotolewa elimu ni kuhusu mwenendo wa uchumi wa Taifa na namna Sera za Uchumi zinavyosaidia kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza fursa za ajira na kukuza uchumi kwa ujumla pamoja na namna hizo zinavyoandaliwa ili kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kwa ufanisi na kwa kuzingatia maslahi ya Taifa,’’, alisema Bw. Dachi.
Aliongeza kuwa Serikali inatumia taarifa za takwimu na tafiti mbalimbali zinazosaidia katika upangaji wa bajeti na utekelezaji wa mikakati ya maendeleo ya muda mfupi na mrefu pamoja na usimamizi wa mikataba ya kikodi kati ya Tanzania na mataifa mengine na ushirikiano wa kikanda na kimataifa unaolenga kulinda maslahi ya Taifa katika sekta ya kodi.
Alifafanua kuwa wananchi wanapatiwa elimu kuhusu namna Wizara inavyofanya tafiti za kisera na kuandaa mapendekezo ya kitaalamu yanayosaidia Serikali kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya nchi pamoja na namna Serikali inavyoshughulikia masuala ya kodi za kimataifa.
‘’Tumetumia fursa hii kueleza wananchi umuhimu wa sera za kodi na fedha katika kukuza uchumi na ustawi wa wananchi, mchango wa kodi katika maendeleo ya Taifa, pamoja na umuhimu wa uwazi na uwajibikaji katika mchakato wa utungaji wa sera nafasi ya Tanzania katika uchumi wa dunia na manufaa yanayotokana na ushirikiano wa kiuchumi na mataifa na taasisi mbalimbali za kimataifa’’, alifafanua Bw. Dachi.
Alisema kuwa ili kuhakikisha ujumbe unawafikia wananchi wengi zaidi, idara pia inatoa vipeperushi, vitabu vya elimu pamoja na mazungumzo ya ana kwa ana na wageni wanaotembelea Banda hatua inayochangia kuongeza uelewa wa umma na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wananchi katika maendeleo ya Taifa.
Tume ya Ushindani (FCC) imesema imeanza mpango wa kuanzisha klabu za elimu ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia katika shule za msingi, sekondari na taasisi za elimu ya juu ili kujenga kizazi chenye uelewa wa masuala hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari Juni 20, 2026, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema mpango huo utatekelezwa kupitia klabu zitakazojulikana kama Ushindani School Club.
Amesema lengo la mpango huo ni kuwafikia wanafunzi mapema na kuwajengea uelewa kuhusu ushindani, haki za mlaji na namna ya kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa au kupata huduma.
Feruzi amesema elimu hiyo itawasaidia wananchi kutambua bidhaa bandia, kulinda soko dhidi ya udanganyifu na kuwawezesha watumiaji kuchagua bidhaa salama na zenye ubora.
Ameeleza kuwa uelewa wa masuala ya ushindani na ulinzi wa mlaji utasaidia wananchi kufanya uchaguzi bora wa bidhaa na huduma, huku sekta binafsi ikiendelea kuchangia katika uzalishaji na ukuaji wa uchumi.
Aidha, amesema utoaji wa elimu hiyo utaendelea kupitia ofisi za kanda za FCC zilizopo Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma na Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha wananchi katika mikoa yote ya Tanzania Bara wanapata elimu hiyo.


Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA
Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.
Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.
Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.





Nilipotuma maombi yangu ya kwanza ya visa, niliamini kila kitu kilikuwa sawa. Nilikuwa nimeandaa nyaraka zote nilizohitaji na nilijitokeza kwenye mahojiano nikiwa na matumaini makubwa. Hata hivyo, maombi yangu yalikataliwa. Nilihuzunika sana.
Baada ya muda, nilijaribu tena. Safari hii nilijitayarisha zaidi na kuhakikisha kila kitu kiko sawa. Lakini kwa mshangao wangu, nilikataliwa tena. Mara ya pili ilinivunja moyo zaidi. Nilianza kuamini kwamba labda safari ya kwenda Marekani haikuwa sehemu ya maisha yangu. SOMA ZAIDI.
Maisha yangu yalibadilika ghafla siku mume wangu alipoondoka nyumbani. Mwanzoni nilidhani alikuwa amekasirishwa na migogoro ya kawaida ya ndoa na angerudi baada ya siku chache.
Habari hiyo ilinivunja moyo. Tulikuwa tumejenga maisha pamoja kwa miaka mingi na tulikuwa na watoto ambao walimhitaji baba yao. Kila nilipowaona watoto wakimuulizia, moyo wangu ulizidi kuumia.
Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa.
Wakati mwingine alipokea simu zangu, wakati mwingine hakujibu kabisa. Nilimwomba afikirie kuhusu familia yetu, lakini alionekana kuwa amefanya uamuzi wake. Kadri miezi ilivyopita, matumaini yangu yalianza kupungua.
Watu wengi walinishauri nikubali hali na kuendelea na maisha yangu. Ingawa nilisikiliza ushauri wao, bado nilitamani kuona familia yetu ikiungana tena. SOMA ZAIDI.
WANAFUNZI wanaofanya ubunifu wa matumizi ya teknolojia mbalimbali katika chuo cha ufundi Arusha (ATC), wametakiwa kusoma Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kuielewa na kuona fursa zilizopo ndani yake na kufanya bunifu zao kutokana na malengo ya dira hiyo.
Hayo yameelezwa Juni 19, 2026 na Mkuu wa chuo cha ufundi Arusha Profesa Musa Chacha katika hotuba yake ya kufungua wiki ya maonyesho ya ubunifu yanayoandaliwa kila mwaka chuoni hapo.
Profesa Chacha amesema dira ya Taifa 2050 imeainisha maeneo ambayo yanapaswa kuendelezwa kwaajili ya Maendeleo ya Watanzania hivyo wanafunzi wanaofanya bunifu chuoni hapo wanapaswa kuyasoma na kuyajua na kuyafanyia ubunifu.
Amesema kutokana na kazi nzuri ya ubunifu ambayo imekuwa ikifanywa na wanafunzi chuoni hapo, chuo kimepanga kujenga jengo maalum la ghorofa nne ambalo litatumika kwaajili ya shughuli za ubunifu.
“ Kwa kushirikiana na Serikali ya Italia hivi karibuni tunatarajia kujenga jengo kubwa la ghorofa nne ambalo litatumika kwaajili ya shughuli za ubunifu( innovation), hapa chuoni hatutaki hivi vipaji vyenu vipotee,” amesema.
Aidha Profesa Chacha amesema chuo kinaendelea na ujenzi wa karakana ( industrial workshop), ambayo itatumika kutengeneza mitambo bunifu itakayokuwa ikigunduliwa na wanafunzi chuoni hapo kwaajili ya kuuzwa na kwamba tayari mashine zitakazotumika katika karakana hiyo zipo njiani kufika chuoni hapo.
“ Hivi sasa tumeamua kuendeleza bunifu zote zitakazobuniwa na wanafunzi Kwa kuzizalisha na kuziingiza sokoni, tutakuwa na kiwanda hapa hapa chuoni na wote mnaofanya ugunduzi huu tutaendelea kuwafuatilia na kuona namna mnafaidika na bunifu zenu, tutawashika mkono popote mtakapoenda,” amesema Profesa Chacha.
Aidha amesema chuo kinakamilisha jengo la hospitali itakayokuwa ikitibia wanafunzi chuoni hapo lakini pia chuo kipi kwenye mikakati ya kujenga jengo litakalojulikana kama innovation center ambalo litakuwa maalum kwaajili ya ugunduzi na uzalishaji wa vifaa tiba vya hospitalini ( biomedical engineering).
Awali akimkaribisha mgeni rasmi Makamu mkuu wa chuo, Dkt Yusuph Mhando alisema katika maonyesho ya mwaka huu ambayo ni awamu ya tatu tangu kuanzishwa, jumla ya bunifu 75 ziliingia kwenye ushindani.
Amesema kati ya bunifu hizo, bunifu 20 zilihusiana na teknolojia ya habari na mawasiliano(Tehama), umeme 15, mitambo na magari 19, sayansi timizi 8, ujenzi na barabara13 na kwamba baada ya majaji kupitia bunifu hizo jumla ya bunifu 19 pekee ziliweza kuingia fainali.
Amesema mshindi wa kwanza ametoka katika fani ya mitambo aliyegundua mashine inayojulikana kama ( Energy trauma kit), akifuatiwa na Tehama ambaye amegundua mashine ya kupima uoni wa macho ( VR acute test),
Aidha amesema maonyesho hayo ni muhimu Kwa Taifa Kwa kuwa yamekuwa yakikuza ujuzi wa wanafunzi chuoni hapo Kwa kuweza kuonyesha Kwa vitendo kile ambacho wamekuwa wakifundishwa darasani.
“ Katika bunifu hizi, Kuna vijana wametengeneza mfumo wa kupiga kura wakati wa uchaguzi ukiwa nyumbani, teknolojia hii ikiweza kuboresha itaweza kusaidia sana katika eneo hili,” amesema.
Amesema ni tegemeo la chuo kuwa bunifu hizo zitafikia jamii na kutatua kero mbalimbali inazizikabili na hivyo chuo kitaendelea kuimarisha na kuendeleza vipaji vya wanafunzi hao.
Miaka ilipita katika hali hiyo. Biashara yangu ilikuwa ikiendelea kuwepo, lakini haikuwa inakua kwa kasi niliyokuwa nimeitarajia.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona washindani wangu wakipata mikataba mikubwa huku mimi nikibaki nikisubiri fursa ambazo hazikuonekana kuja.
Nilijaribu kuboresha huduma zangu na kutafuta masoko mapya. Ingawa kulikuwa na mabadiliko madogo, bado sikuweza kupata nafasi ambayo ingeibadilisha biashara yangu kwa kiwango kikubwa. SOMA ZAIDI.
Lakini kadri muda ulivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya. Kila wiki nilikuwa nikikuta bidhaa zimepungua bila maelezo ya kuridhisha. Nilipohesabu mauzo na kulinganisha na bidhaa zilizobaki, kulikuwa na tofauti kubwa ambayo sikuweza kuieleza. Nilianza kuwa na wasiwasi mkubwa.
Nilizungumza na wafanyakazi wangu na kuwauliza kama kuna jambo walilokuwa wamegundua. Wote walikana kujua chochote. Hata wateja wa kawaida hawakuonekana kuwa na taarifa yoyote kuhusu kilichokuwa kinaendelea. Hasara iliendelea kuongezeka.
Wakati mwingine nililala nikiwa nawaza jinsi biashara yangu ingeendelea kama wizi ule usingekoma. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba mwizi huyo hakuacha ushahidi wowote nyuma.
Nilijaribu njia mbalimbali za kumgundua. SOMA ZAIDI.





