WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa{TAMISEMI}Professa  Riziki Shemdoe amesema kuwa fedha za mradi wa shilingi Bilioni 82.5 za ujenzi wa Miundombinu ya barabara inayozunguka uwanja wa AFCON ni fedha za mapato ya ndani hivyo wananchi wa Mkoa wa Arusha wametakiwa kuitunza miundombinu hiyo.

Professa Shemdoe alisema hayo jana Jijini Arusha wakati wa utiaji saini kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini{TARURA} na Mkandarasi wa mradi huo kampuni ya CRJE ya Nchini China shughuli iliyofanyika eneo la karibu ya uwanja na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi{CCM}ngazi ya kata hadi Mkoa,viongozi wa serikali,viongozi wa dini na wananchi wa Mkoa wa Arusha.

Alisema mashindano ya AFCON ni mashindano muhimu sana Afrika na yanaangaliwa na mamia ya watu wengi Duniani na hivyo basi Miundombinu yeke ya kuzunguka uwanja huo yanapaswa kuwa yenye ubora mzuri wenye kuwafutia watu wote wataokwenda kuangalia mashindano hayo na ndio maana Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia utolewaji wa fedha hizo kutoka mapato ya ndani.

Waziri alisema kutokana na umuhimu ulionyeshwa na Rais wa kutoa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa  Miundombinu inayozunguka uwanja huo,wananchi wote wa Mkoa wa Arusha wanapaswa kuwa walinzi wa Miundombinu hiyo kwa maslahi ya Umma na mradi huo unapaswa kukamilika mapema mwezi Mei mwakani na kusiwe na visingizio.

Alisema viongozi wa Chama,serikali na wananchi wa Mkoa wa Arusha wanapaswa kumshukuru Rais kwa  kujitoa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo ambao kwa sasa ujenzi wake umefikia asilimia 75 na pia kutoa fedha nyingine kwa ajili ya Mindombinu ya Barabara inayozunguka uwanja hyuo kwani uamuzi huo unapaswa kupongezwa na kila mmoja.

''Utekelezaji wa mradi huu ni jitihada za serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan za kutaka mashindano ya AFCON kuchezwa katika mazingira mazuri na yenye mvuto sambamba na Miundombinu ya barabara kuwa katika hali ya ubora na kuvutia''alisema Shemdoe

''Wananchi wote wote Mkoani Arusha na Mikoa ya jirani wanatakiwa kuwa wasimamizi wa mradi huu na maradi unaposuasua wanapaswa kutoa taarifa sehemu husika ili hatua ziweze kuchukuliwa kwani mradi huu ni wetu sote''alisema 

Naye Mtendaji Mkuu wa Tarura,Mhandisi Victor Seif alisema ujenzi wa Miundombinu ya Barabara za kuelekea na kuzunguka uwanja wa mpira utakaotumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2027 katika Jiji la Arusha umegharimu kiasi hicho cha fedha na Barabara ya km 19.9  ambayo itakuwa na njia nne na mbili.

Mhandisi Seif alisema kuwa ujenzi wa uwanja umefikia zaidi ya asilimia 75 sambamba na ujenzi wa Miundombinu muhimu yenye umbali wa zaidi ya km 19.9 kwa kiwango cha lami kuelekea kwenye uwanja huo kutokea Barabara Kuu ya Arusha-Babati na Arusha Bypass na kuzunguka uwanja huo Mateves-Bondeni km 6.5,Km 1.5 njia nne na km 5 njia mbili kutoka barabara kuu Arusha -Babati,barabara ya Lendita km 2.75 njia nne ,barabara ya Essari km 2.45 2.45 njia nne zote kutoka barabara kuu ya Arusha Bypass na km 1.5 barabara kuzunguka uwanja.

Alisema baada ya mchakato wa ununuzi kukamilika,Kampuni ya M/s China Railway Construction Engineering Group kushinda zabuni na kupewa kazi hiyo ya ujenzi wa barabara kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 82.5 kwa muda wa miezi 13 na kazi inapaswa kuanza aprill mosi mwaka huu na usimamizi wa ujenzi wa barabara hiyo utasimamiwa na kampuni ya M/s Afrisa Consulting ya Jijini Dar es Salaam kwa mkataba wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.4

Naye Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini na Waziri wa Habari,Sanaa ,Michezo na Utamaduni,Poul Makonda alisema kuwa Jiji la Arusha lina kiu kubwa na barabara za lami kwani ni Jiji la mwisho kuwa na barabara za lami kwani Majiji yote Tanzania yana barabara za lami hivyo aliiomba Tarura kuhakikisha inafanya kila jitihada kutekeleza ahadi zake za ujenzi wa barabara za kiwango cha lami ili wananchi waweze kupitia kwa nyakati zote.

Makonda alisema na kumshukuru Rais kwa uamuzi wake wa kuridhia kutoa fedha shilingi Bilioni 82.5 kwa ajili ya Miundombinu ya kuzunguka uwanja wa AFCON na kusema kuwa uamuzi huo unapaswa kupongezwa na kuwataka wakazi wa Arusha kushukuru kwa hilo na kuwasihi wananchi watakaolipwa fidia kupokea fedha hizo bila kuleta manung'uniko.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla ameahidi kuwasimamia wakandarasi wa ujenzi wa Miundombinu ya kuzunguka uwanja huo ili waweze kuimaliza kwa wakati na kuwataka wananchi kuwa mstari wa mbele kutoa taarifa pindi mkandarasi atakaonekana anafanaya kazi kwa kusuasua katika kutekeleza majukumu yake.















  

 

 

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa mkono wa Eid kwa wazee wanaoishi katika Kata ya Ilemi, jijini Mbeya, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Eid al-Fitr.

Akiwasililisha zawadi hizo Kwa niaba ya Rais, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali inayoongozwa na Rais Samia katika kuwajali wazee na makundi maalum, hususan katika nyakati za sikukuu.

“Mheshimiwa Rais amewakumbuka wazee wa Ilemi katika kipindi hiki cha Eid, na ameona ni vyema kuwafikishia mkono wa upendo ili nao waweze kusherehekea kwa furaha kama Watanzania wengine,” amesema Mahundi.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuthamini mchango wa wazee katika jamii na kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha ustawi wao unaimarika siku hadi siku.

Baadhi ya wazee waliopokea msaada huo wamemshukuru Rais Samia pamoja na Naibu Waziri Mahundi kwa kuwajali, wakisema msaada huo umewaletea faraja na kuwatia moyo katika kipindi hiki cha sikukuu.

Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi wa serikali za mitaa pamoja na wananchi wa eneo hilo.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

TUME ya Ushindani (FCC) kanda ya Nyanda za Juu Kusini  imetoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa mpana ili waweze kufanya maamuzi sahihi wanaponunua na kutumia bidhaa mbalimbali  ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Akitoa elimu hiyo Mkoani Njombe, Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) Nyanda za Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga, amesisitiza umuhimu wa kila mlaji kufahamu haki zake za msingi.alieza kuwa haki hizo ni pamoja na kupata bidhaa bora, kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa, pamoja na haki ya kulalamika pale mlaji anapodhulumiwa.

Aidha, Bw. Mbanga ameeleza madhara makubwa yatokanayo na matumizi ya bidhaa bandia, akibainisha kuwa bidhaa hizo zinaweza kusababisha athari za kiafya, kupoteza fedha, na kudhoofisha uchumi wa nchi. Amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii zao ili kupunguza matumizi ya bidhaa hizo hatarishi.

“FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi.”amesema Bw. Mbanga

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameacha alama chanya kwa wanafunzi wa FDC Njombe, ambapo wengi wao wameeleza kuwa elimu hiyo imewafungua macho na kuwapa nguvu ya kusimamia haki zao kama walaji, huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia nchini.

Kupitia mafunzo hayo, walikumbushwa kuwa mlaji ana nafasi kubwa katika kulinda afya yake na uchumi wa taifa kwa kuchagua bidhaa zilizo salama na zenye ubora unaokubalika.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) Mkoani Njombe wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia yaliyotolewa  na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

 

Na WMA – Dodoma

Watumishi wa Wakala wa Vipimo (WMA), wameitikia wito wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaowataka watanzania kupitia makundi mbalimbali kupanda miti katika maeneo yao ili kuhifadhi mazingira.

Akiongoza zoezi la upandaji miti katika eneo ilipo Ofisi Kuu ya WMA Medeli jijini Dodoma, mapema leo Machi 20, 2026 Meneja Utawala na Rasilimali Watu, Charles Mavunde amewasisitiza watumishi wa Wakala hiyo nchi nzima kuzingatia maelekezo ya Serikali kwa kupanda miti na kuitunza ili kulinda mazingira.

Amesema kuwa, Mheshimiwa Rais Samia amekuwa akisisitiza mara kwa mara kuhusu upandaji miti katika maeneo mbalimbali na kwamba yeye mwenyewe ameonyesha mfano kwa kuwa kinara wa upandaji miti, hivyo WMA imeona ni vyema pia iitikie wito huo.

“Mtakumbuka kwamba, hata Mheshimiwa Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimwakilisha Mhe. Rais katika maadhimisho ya siku ya upandaji miti duniani na maadhimisho ya upandaji miti kitaifa, jana Machi 19, 2026 kule Lindi aliagiza kuwa makundi mbalimbali ya watanzania waendeleze utamaduni wa kupanda miti,” ameeleza Mavunde na kuhitimisha kuwa WMA imeyachukulia kwa uzito maelekezo ya viongozi hao na itayatekeleza kikamilifu.

Viongozi na watumishi mbalimbali wa WMA Makao Makuu wameshiriki zoezi hilo la upandaji miti akiwemo Mkurugenzi wa Huduma za Biashara Phanuel Mtuki, Meneja Sehemu ya Fedha, CPA Ibrahim Mbinga, Meneja Mkoa wa Dodoma Said Ibrahim na Meneja Mawasiliano Veronica Simba.

Wengine walioshiriki ni watumishi kutoka Idara mbalimbali wakiwemo maafisa, maafisa usafirishaji na wasaidizi wa ofisi.

WMA ni wakala ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara yenye jukumu kuu la kumlinda mlaji kupitia usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo katika sekta mbalimbali.

 




Na Mwandishi wetu- DAR ES SALAAM


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambaye pia ni Mbunge wa

Arumeru Magharibi Mhe. Johannes Lukumay ameipongeza  Serikali kuendelea kusaidia kundi la Watu waishio na Maamubikizi Virusi vya 

UKIMWI kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Lukumay ameyasema  hayo tarehe 19 Machi 2026 mara baada ya ziara ya kutembelea Baraza la Watu waishio na maambukizi ya Virusi vya  UKIMWI akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika ( Konga ya Jiji) iliyofanyika   katika Viwanja vya Pugu Mnadani Jijini Dar es Salaam.

 Amesema kuwa watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni sawa na watu wengine hivyo yapaswa kuwapa kipaumbele katika fursa mbalimbali za kimaendeleo.

Pia Mwenyekiti huyo amelipongeza kundi hilo kwa namna

wanavyojituma katika kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini hivyo  kuziagiza  sekta husika kusaidia katika kuwatafutia masoko kwa ajili ya bidhaa zao.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wataendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuongeza nguvu zaidi kwa Wanakonga ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Nderiananga amempongeza Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Wilaya pamoja na Katibu Tawala wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na timu nzima kwa kuwawezesha Wanakonga katika fursa mbalimbali na kuwataka kuendelea na desturi hiyo ya kuwawezesha kwani mwaka huu wa fedha bado haujamalizika.

Aidha  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Elihuruma Mabelya amesema kuwa moja ya eneo waliloliwekea nguvu ni Konga hiyo kwa kuunga mkono shughuli zao za  kiuchumi ili kuhakikisha

wanainuka na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo.





Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha mara baada ya kuwapatia elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

KATIKA harakati za kuimarisha uelewa wa haki za walaji nchini, Tume ya Ushindani (FCC) leo Machi 19, 2026 imetoa elimu kwa wanachuo wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Elimu hiyo ilitolewa na FCC kwa lengo la kuwajengea uelewa wanachuo kuhusu haki zao wanapokuwa wanatumia bidhaa na huduma mbalimbali. Wanachuo walipata nafasi ya kujifunza mambo muhimu ambayo mara nyingi huyapuuzia katika maisha yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo,Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,amewaeleza wanachuo kuwa wengi wao huingia katika mikataba bila kusoma masharti yake, hali inayoweza kusababisha hasara au kunyimwa haki zao bila wao kutambua.

Amefafanua kuwa mikataba mingi hasa ya huduma za simu, mikopo na manunuzi ya mtandaoni huwa na vifungu vinavyohitaji umakini mkubwa kabla ya kukubaliwa. Hivyo aliwataka wanachuo kujenga utamaduni wa kusoma na kuelewa kila wanachosaini.

Aidha, amesema  kuwa mlaji ana haki ya kupata bidhaa bora, taarifa sahihi na huduma stahiki. Pale haki hizo zinapokiukwa, mlaji anatakiwa kuchukua hatua za kisheria au kuripoti kwa mamlaka husika.

"FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi."amesema Bi.Hall

Kwa ujumla, mafunzo hayo yamewajengea wanachuo uelewa mkubwa na kuwahamasisha kuwa mabalozi wa haki za walaji, huku yakichangia mafanikio ya maadhimisho ya Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha mikataba halisi na feki  mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha mara baada ya kuwapatia elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.