Na MWANDISHI WETU

SERIKALI imepokea rasmi hoja ya ajira za muda (part-time) kwa vijana iliyowasilishwa na Mbunge wa Kisarawe, Dk. Selemani Jafo, na kuanza mchakato wa kuichakata ili kubaini namna bora ya utekelezaji wake.

Akizungumza mara baada ya kupokea hoja hiyo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi, Sera, Bunge na Watu Wenye Ulemavu, Profesa Paramangamba Kabudi, amesema serikali inatambua uzito wa hoja hiyo na itaifanyia uchambuzi wa kina kabla ya kuchukua hatua stahiki.

Amesema hoja hiyo inalenga kutoa suluhisho la changamoto ya ajira kwa vijana, hivyo serikali itaipitia kwa makini ili kuona namna inavyoweza kutekelezwa kwa ufanisi na tija kwa taifa.

Aprili 9 mwaka huu, wakati akichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Jafo aliwasilisha hoja hiyo bungeni akipendekeza kuanzishwa kwa mpango maalumu wa ajira za muda mfupi kwa vijana nchini.

Katika hoja yake, Dk. Jafo alisema mpango huo utasaidia vijana kupata ajira za mikataba ya muda, kujenga uzoefu wa kazi na kupata kipato, sambamba na kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kuendelea kutoa ajira kwa vijana.

Alifafanua kuwa mpango huo unaweza kuanza kwa kuwahusisha vijana 50,000 wenye elimu ya stashahada na shahada, ambapo wa stashahada wangelipwa takribani Sh500,000 na wa shahada Sh700,000 kwa mikataba ya miaka mitatu.

Kwa mujibu wa maelezo yake, utekelezaji wa mpango huo unaweza kugharimu takribani Sh bilioni 396, huku ukilenga kupunguza tatizo la ajira na kuwajengea vijana uzoefu wa vitendo.

Aidha, alieleza kuwa hali ya sasa inaonesha vijana wengi wahitimu wanajikuta wakifanya kazi zisizoendana na taaluma zao, ikiwemo bodaboda, jambo alilosisitiza linahitaji hatua za haraka za kisera.

Pia alipendekeza utekelezaji wa mpango huo uanze kwa makundi maalumu yakiwemo walimu, wahudumu wa afya na vijana waliopo mitaani, huku ukiratibiwa kupitia mamlaka za serikali za mitaa ili kuongeza ufanisi.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

...

VIJANA nchini Tanzania wanaendelea kurasimisha shughuli zao za biashara kwa kasi, hali inayoashiria kuongezeka kwa ushiriki wao katika uchumi rasmi na mchango wao katika juhudi za maendeleo ya taifa.

Hayo yameelezwa leo Aprili 15,2026 na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw.Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma .

Bw.Nyaisa amesema takwimu za BRELA zinaonesha kuwa maelfu ya kampuni, majina ya biashara na alama za biashara na huduma (trade and service marks) zilizosajiliwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita zinamilikiwa na vijana. Hali hii inaonesha wazi kuongezeka kwa mchango wa vijana katika sekta za viwanda na biashara nchini.

"Kampuni 5,045 zimesajiliwa, ambapo 3,120 zinamilikiwa na vijana. Aidha, majina ya biashara 8,792 yamesajiliwa, kati ya hayo 4,938 ni ya vijana. Kwa upande wa alama za biashara, jumla ya 1,018 zimesajiliwa, nyingi zikiwa zinamilikiwa na vijana. Vilevile, leseni za biashara daraja la “A” 5,430 zimetolewa, ambapo takribani nusu yake zimekwenda kwa vijana."amesema Bw.Nyaisa

Amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo madiwani kuhusu taratibu za usajili wa biashara, utoaji wa leseni pamoja na ulinzi wa haki miliki, ili waweze kuwasaidia wafanyabiashara katika kata zao kwa ufanisi zaidi.

Hata hivyo amempongeza Meya wa Jiji la Dodoma kwa kushiriki mafunzo hayo, hatua hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya kuboresha mazingira ya biashara katika mji mkuu wa nchi. Pia ametambua mchango wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma chini ya uongozi wa Rosemary Senyamule kwa ushirikiano wake katika kutoa elimu ya biashara na msaada wa kitaalamu.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yanahusisha maeneo muhimu kama usajili wa kampuni, majina ya biashara, alama za biashara, hati miliki (patents), pamoja na utoaji wa leseni za viwanda na leseni za biashara daraja la “A”.

Aidha, amebainisha kuwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, BRELA imefanya maboresho mbalimbali ya kurahisisha mazingira ya kufanya biashara, ikiwemo kuanzisha mifumo ya kidijitali inayowezesha huduma kupatikana mtandaoni kupitia simu za mkononi.

Hata hivyo, Nyaisa ametaja changamoto ya utofauti katika utoaji wa leseni za biashara katika ngazi za serikali za mitaa. Alieleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara hupewa leseni daraja la “B” badala ya “A” kimakosa, hali inayosababisha mkanganyiko.

Amewataka madiwani kutumia mafunzo hayo kutatua changamoto hizo na kuwa mabalozi wa kuhamasisha urasimishaji wa biashara, hususan kwa vijana, wanawake na wajasiriamali wadogo.

“Baada ya mafunzo hayo, tunatarajia muwe mabalozi wazuri katika maeneo yenu na kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika ngazi za chini,” amesema.

Kwa upande wake, Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwona Chaula,amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuwajengea uwezo madiwani wanaofanya kazi kwa karibu na wananchi katika ngazi ya msingi. Aliongeza kuwa yatawasaidia kuelewa vyema taratibu za usajili na utoaji wa leseni za biashara ili waweze kuwasaidia wananchi katika shughuli zao za kila siku za kiuchumi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati mpana wa BRELA wa kujenga uchumi shindani na jumuishi kwa kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli rasmi za biashara nchini.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema ushiriki wa Tanzania kwenye Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP) upo kwenye biashara ya kusafirisha mafuta ghafi tu (transit nation) kutoka Kabaale Hoima hadi Chongoleani, Tanga na baadaye kupelekwa kwenye masoko ya kimataifa.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma leo Aprili 14, 2026 wakati akijibu swali la Mbunge wa Bahi, Mhe Kenneth Nollo aliyehoji Serikali ina mpango gani wa kuanza kusafirisha mafuta ghafi yanayotoka Uganda kupitia Bomba la Mafuta EACOP.

Mhe. Salome amesema mikataba ya mauzo hayo imeingiwa kati ya wabia wa mkondo wa juu nchini Uganda ambao ni Serikali ya Uganda na Makampuni ya Kimataifa (Totalenergies) kutoka Ufaransa na CNOOC kutoka China kwa kuzingatia vigezo vya usanifu wa kitaalam na uwezo wa uzalishaji wa visima.

" Mhe Spika naomba ifahamike pia, kwenye hii biashara tayari mikataba ya mauzo ya mafuta hayo imeshaingiwa kati ya wabia wa mkondo wa juu (upstreamers) na wanunuzi (masoko ya kimataifa)," Amesema Mhe Salome.


Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) Dkt. Benson Ndiege kushirikiana na Uongozi wa TCDC Sports Club wanunua vifaa vya michezo kwa wachezaji 42 kuelekea mashindano ya Michezo ya Meimosi mjini Njombe.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo Aprili 14, 2026 jijini Dodoma wakati wa kuwaaga wanamichezo wakielekea mjini Njombe.

Vifaa vilivyonunuliwa ni jezi za mprira wa miguu, viatu, mipira na vifaa vingine vya michezo.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amesema kuwa mkutano wa taasisi za ushindani barani Afrika umeleta pamoja wadau muhimu kutoka nchi mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto zinazoikumba sekta ya biashara. 
Ushirikiano kati ya VETA, Enabel na kiwanda cha Kasulu Sugar umeanza kuzaa matunda baada ya vijana 36 waliokuwa wakifanya kazi bila vyeti kutathminiwa na kupatiwa vyeti kupitia mfumo wa urasimishaji wa ujuzi (RPL).


Na Oscar Assenga, Lushoto

Kampuni ya Taifa Gas imeendelea kujipambanua kama kinara wa usambazaji wa gesi nchini Tanzania, ikiwa na takribani asilimia 51 ya ujazo wa gesi yote inayopatikana nchini.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo wakati wa Tamasha la NMB Kijiji Day lilofanyika Magamba wilayani Lushoto, Meneja wa Masoko wa kampuni hiyo, Oscar Shelukindo, amesema kuwa mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya kuhifadhi na kusambaza gesi, pamoja na dhamira ya dhati ya kuwahudumia Watanzania.

Ameeleza kuwa lengo kuu la kampuni hiyo ni kusaidia juhudi za taifa za kuhamasisha matumizi ya nishati safi, kwa kuwahamasisha wananchi kuachana na matumizi ya kuni na mkaa, ambayo yamekuwa na athari kubwa kwa afya na mazingira.

Kwa mujibu wa takwimu, zaidi ya Watanzania 33,000 hufariki kila mwaka kutokana na magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya nishati zisizo safi. 

Hali hiyo imeifanya Taifa Gas kuongeza juhudi za kuhakikisha gas inapatikana kwa urahisi na kwa gharama nafuu.

Katika hatua hiyo, kampuni hiyo inatoa mitungi ya gesi ya kilogramu 6 na 15 kwa bei nafuu, pamoja na huduma ya kujaza mitungi kwa wateja waliokwisha kuwa nayo, hatua inayolenga kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Aidha, Taifa Gas kwa kushirikiana na NMB Bank wanatarajiwa kushiriki katika Tamasha la Kijiji Day, ambapo watatoa huduma mbalimbali pamoja na elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi.

Juhudi hizi zinatajwa kuwa chachu ya mabadiliko chanya, zikilenga kuboresha afya za Watanzania na kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.


Serikali itahakikisha vipaumbele vya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) vinaakisi uhalisia wa mchango wa Sekta Binafsi, inayotarajiwa kuchangia takribani 70% ya Pato la Taifa (GDP) ifikapo mwaka 2050.

Hatua hiyo imebainishwa na Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dr. Blandina Kilama leo Aprili 13, 2026, wakati akifungua Warsha mahususi inayolenga kutoa fursa ya kujadili kwa kina, kukusanya maoni, uzoefu na mapendekezo ya wadau kutoka Sekta ya Umma, na Sekta Binafsi kuhusu maeneo sita (6) ya kipaumbele ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano, sambamba na mwelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“majadiliano haya yanalenga kuhakikisha kuwa mchango wa Sekta Binafsi unatambuliwa, unathaminiwa na kuingizwa kikamilifu katika uundaji na utekelezaji wa vipaumbele pamoja na mikakati ya maendeleo, ili kuimarisha ufanisi, kuongeza kasi ya utekelezaji wa FYDP IV, na kufikia matokeo yenye tija na endelevu kwa taifa” Amesema Dkt. Kilama.

Aidha, katika Warsha hiyo, washiriki watajadili mada mahususi zilizomo katika FYDP IV, ikiwemo Kujenga Uwezo wa Watu na Maendeleo ya Jamii, Kutumia Vichocheo vya Maendeleo, Mageuzi ya Sekta muhimu, Uadilifu wa Mazingira na Uhimilivu wa Tabianchi, Uchumi Imara, Jumuishi na Shindani na Kuimarisha Misingi ya Uendelevu wa Taifa.

Dkt. Kilama amesisitiza kuwa, matokeo ya warsha hiyo hayatabaki kuwa nadharia pekee, bali yatatumika katika kuboresha sera, mipango na mikakati ya maendeleo ya taifa.

▪︎ Asisitiza Vijana kuomba udahili na ufadhili*

▪︎ Asisitiza Uwazi na Ushindani*

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametangaza rasmi kutolewa kwa ufadhili kupitia Samia Scholarship Exender AI/DS wa masomo ya Uzamili (Masters) katika Sayansi ya Data, Akili Unde na fani zinazohusiana.

Akizungumza Aprili 13, 2026 jijini Dar es Salaam amesema kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika kuandaa rasilimali watu wenye uwezo wa kushindana kimataifa katika sayansi na teknolojia na kuwashawishi vijana wenye vigezo kuomba udahili na ufadhili.

Prof. Mkenda ameeleza kuwa Samia Scholarship extended DS/AI+ ilianza kufadhili wanafunzi wa shahada ya kwanza waliobobea katika sayansi, uhandisi, tiba na hisabati, ambapo tayari wanafunzi 16 wamepelekwa nchini Afrika Kusini na wengine 34 watakwenda nchini Ireland.

Ameongeza kuwa ufadhili wa sasa unalenga kuongeza idadi ya vijana wa kitanzania wenye ujuzi na taaluma katika maeneo hayo.

"Ufadhali huu ni kwa waombaji watakaosoma shahada ya Uzamili katika Taasisi ya Indian Institute of Technology (IIT) Madras – Kampasi ya Zanzibar," amesisitiza Prof. Mkenda

Waziri Mkenda amesema kuwa masharti ni ya wazi ambapo mwombaji awe Mtanzania, mwenye umri usiozidi miaka 35, awe na daraja la kwanza katika masomo ya sayansi ya kidato cha sita, GPA ya angalau 3.8 katika shahada ya kwanza, na awe amepata udahili katika IIT Madras, Zanzibar.

Amesisitiza kuwa hatua ya kwanza ni kuomba udahili chuoni kabla ya Aprili 15, kisha kuwasilisha maombi ya ufadhili kuanzia Juni 1 hadi Juni 30 na kwamba Kamati huru itapitia maombi kwa uwazi na ushindani, kuhakikisha wanafunzi bora zaidi wanapata nafasi.

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikiwa kukamata kilogramu 101.2 za dawa za kulevya aina ya mirungi katika eneo la Tabata Kibo jijini Dar es Salaam, zikiwa zimefichwa ndani ya basi la abiria.

 


 Mbunge wa Jimbo la Hanang Mkoani Manyara ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mhe. Asia Halamga, amekabidhi mifuko ya mbegu za dengu kwa viongozi na wananchi mbalimbali wilayani Hanang  ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha sekta ya kilimo na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa mbegu hizo Mbunge huyo amesema kuwa lengo la kutoa mbegu hizo ni kuongeza tija kwa wakulima na kuinua kipato chao kupitia kilimo cha kisasa hususani baada ya mvua nyingi za mwaka huu kuharibu mazao ya maharage shambani

Asia ameendelea kueleza kuwa  kuwa utoaji wa mbegu hizo utasaidia kurejesha uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula kwa wakazi wa Hanang kwani mbegu za dengu ni mkakati wa kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara yenye soko la uhakika ndani na nje ya nchi.

Kwa upande Mkuu wa Wilaya ya Hanang Almishi Issa Hazali amemshukuru Mbunge Asia Halamga kwa kuwakumbuka wananchi wa Jimbo hilo na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi

“Hatua hii ni ya kupongezwa kwani inaenda moja kwa moja kugusa maisha ya wananchi wetu na sisi kama Serikali tutaendelea kushirikiana na Mbunge sambamba na viongozi wengine wote wenye nia njema ya kuleta maendeleo katika Jimbo letu hili,” Amesema Almishi

Hata hivyo wananchi hao wamemshukuru sana Mbunge huyo kwa msaada huo ambao utaleta mapinduzi makubwa katika sekta ya kilimo.