Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salumu, akiongoza ujumbe wa jumuiya hiyo kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Septemba 2026, kufuatia kufiwa na mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar, tarehe 7 Septemba 2026.
WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, ameshiriki utiaji saini mikataba ya kiutendaji kati ya Wizara ya Maji na Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), hatua inayolenga kubadili utendaji kutoka mazoea hadi mfumo unaopimika na wenye uwajibikaji.


KAMPUNI ya Kimataifa ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Barrick Gold kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Kiseriani kata ya Engikaret wilyani Longido Mkoani Arusha,Mbunge wa Jimbo hilo,Dkt Steven Kiruswa na serikali wamefanikiwa kujenga shule shikizi kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 230.

Akizungumza katika uzinduzi wa shule hiyo Kijiji hapo ,Meneja Mkazi wa Barrick{Country Manager} Tanzania ,Melkiory Ngido alisema uamuzi wa kampuni hiyo kuchangia msaada ni kufuatia maombi ya Kiruswa ambaye ni Naibu Waziri wa Madini na kujionea wenyewe hali ya changamoto za wanafunzi kutembea km 32 kwenda na kurudi shule  hali inayoleta hatari kwa wanafunzi hao kwa wanyama wakali.

Ngido aliwaahidi wananchi Kiseriani na Longido kwa ujumloa kuwa Barrick Gold itashirikiana na wananchi katika kujenga miundombinu ya elimu kwa kuwa wananchi wameonyesha nia ya dhati na ushirikiano na uadilifu mkubwa katika ujenzi wa madarasa mawili na 0fisi ya mwalimu kwani kampuni hiyo imechangia zaidi ya shilingi milioni 180 na zimetumika kama ilivyokusudiwa.

Alisema elimu ni msingi wa maisha na wananchi wa Kijiji cha Kiseriani ambao wengi wao ni wa jamii ya kifugaji ya Kimasai kuamua wenye kujitoa na kujenga madarasa mawili na ofisi ya mwalimu ni uamuzi unaopaswa kuungwa mkono kwa kuwa jamii hiyo imeamua kujitoa na kuwajali wanafunzi wa jamii hiyo na kujali elimu zaidi na sio vinginevyo.

‘’Barrick Gold Mining imeaamua kujitoa zaidi Longido kuhakikisha elimu inasogezwa zaidi katika maeneo ya makazi ya watu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miundombinu ya elimu ikiwemo madarasa,ofisi na nyumba za walimu zinajengwa kwa maslahi ya watoto wa jamii hiyo’’alisema Ngido

Naye Kiruswa aliishukuru kampuni hiyo kwa uamuzi wa ujenzi wa madarasa na ofisi ya mwalimu na kuahidi ushirikiano zaidi na kusema kuwa uamuzi huo unapaswa kupongezwa na wananchi wote wa Longido na kusema kuwa uadilifu ni jambo muhimu katika kuwashawishi wafadhili wengine kujitoa katika kutoa misaada ya miundombinu ya elimu,maji na barabara.

Alisema uamuzi wa ujenzi wa madarasa mengine mawili ulioazwa na wananchi kwa kusomba mawe,mchanga na kokote ni uamuzi wenye busara kubwa na yeye ataunga mkono kwa hilo kwa kutoa mifuko 100 ya simenti na kumalizia upauaji.

Waziri Kiruswa alisema na kuwaomba wana Kiseriani na Longido kwa ujumla kujitoa katika shughuli za kijamii ikiwemo ujenzi wa miundoimbinu ya elimu na kusema kuwa yeye kwa hilo atakuwa mstrari wa mbele katika kuchangia na kusaka wafadhili zaidi .

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi{CCM} wilaya ya Longido ,Papa Nakuta amempongeza Kiruswa kwa jinsi anavyojitoa kwa maendeleo ya wananchi wa longido na kuwataka wananchi kumuunga mkono mbunge huyo ambaye ameenda bungeni kufanya kazi na sio kulala kwani kila mradi mchango wake upo kama sio yeye basi analeta marafiki zake na kufanya ushawishi kwa serikali kuendelea kupeleka fedha za miradi Jimbo hapo.














Shirika la Viwango Tanzania (TBS) imekabidhi cheti cha ubora wa huduma kwa wakala wa maji na usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ikiwa ni Ishara ya utoaji huduma bora ya maji nchini.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb), ametembelea kiwanja kinachotarajiwa kujengwa Viwango House eneo la Mateves, Mkoani Arusha.

 



OWM –TAMISEMI, Dar es Salaam  


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi leo Septemba 11, 2026 amezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika na majanga kuchukua hatua za haraka kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba hadi Desemba 2026. 

 

Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo kwa taasisi hizo katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam, ambapo kwa upande wa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI yamepokelewa na Waziri Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, mara baada ya ofisi yake na taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka, kuwasilisha taarifa ya utayari na maandalizi ya Serikali katika kukabiliana na madhara ya mvua hizo, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.


Katika kikao kazi hicho, Makamu wa Rais, Mhe. Ndejembi ameagiza wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo kuhakikisha zinafanya kampeni maalum ya usafi katika miundombinu ya barabara na mifereji ya maji.


“Ifanyike kampeni ya haraka, mikondo na mifereji ya maji izibuliwe, na barabara ziandaliwe,” amesisitiza Makamu wa Rais.

 

Aidha, Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi, ameelekeza taka, tope na udongo unaotolewa baada ya kuzibua mitaro na mifereji katika maeneo mbalimbali kuondolewa mara moja na kutupwa katika maeneo yaliyotengwa, badala ya kuachwa kandokando ya barabara ambako taka, tope na udongo huo zinaweza kurejea kwenye mifereji wakati mvua zinapoanza.

 

Makamu wa Rais pia amezitaka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo, kufanya kazi kwa pamoja ya kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.



Akipokea maagizo hayo kwa ajili ya utekelezaji, Waziri wa Nchi, OWM – TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemueleza Mhe. Makamu wa Rais kuwa ofisi yake imeshaanza kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha usafi wa mazingira katika majiji aliyoyatoa Septemba 02, 2026 wakati akiwaapishwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.


Prof. Shemdoe amemtaarifu Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi kuwa, Septemba 07, 2026 alifanya kikao kazi na Wakuu wa Mikoa yenye majiji, viongozi wa majiji na manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka kuhakikisha wanatekeleza kampeni maalum ya wiki mbili ya usafi wa mazingira katika majiji ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais.


Akianisha namna ofisi yake itakavyotekeleza maelekezo ya Makamu wa Rais ya kujiandaa na kukabiliana na athari za mvua za El Niño, Prof. Shemdoe amewasilisha kwa Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi, mkakati wa ofisi yake kupitia TARURA ulioandaliwa kwa ajili ya kujiaanda, kuzuia na kupambana na madhara ya uharibifu wa miundombinu ya barabara unaoweza kutokana na mvua za El Niño, ambao umeanisha namna utakavyotekelezwa.

Kariakoo, 11 Septemba, 2026

Wafanyabiashara wa vipodozi katika Mtaa wa Vipodozi Kariakoo, Dar es Salaam, wamepata elimu kuhusu masuala ya kodi na huduma zinazotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia ziara ya maafisa wa mamlaka hiyo iliyoongozwa na Kaimu Meneja wa Mkoa wa Kodi Kariakoo, Edson Issanya.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), akichangia hoja kuhusu uwekezaji katika sekta ya afya wakati wa Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya, linalofanyika jijini Nairobi, Kenya.
Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, ndugu Saddy Sevingi akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua mafunzo kuhusu uelewa wa usalama wa kimtandao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Tanzania imepata nafasi 150 za ufadhili wa masomo nchini Algeria kwa wanafunzi waliofanya vizuri, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuongeza fursa za elimu ya juu nje ya nchi.
Mimi nilikuwa kwenye mahusiano ambayo yalinivunja moyo vibaya sana. Nilimpenda mtu kwa dhati, nikajitoa kwa kila hali, lakini mwisho wake niligundua nilikuwa natumiwa tu. Alikuwa ananihitaji pale tu alipokuwa na shida.

Nilipokuwa nikihitaji upendo au msaada, hakuwa karibu. Hilo liliniumiza sana, lakini nilivumilia kwa sababu nilikuwa na matumaini mambo yangebadiika.

Baada ya muda, ukweli ulijitokeza wazi. Nilijikuta nimeachwa na maumivu makubwa ya moyo.

Ilikuwa ngumu sana kuamini tena au hata kufikiria kuanza upya. Nilikaa kwa muda mrefu nikiwa peke yangu. Nilikuwa na hofu ya kuingia kwenye mahusiano mengine. Nilihisi kama kila mtu angeweza kuniumiza tena. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.

Mimi nilikuwa kwenye kesi ambayo ilinichukua karibu miaka mitano. Ilianza kama jambo dogo, lakini baadaye ikageuka kuwa vita kubwa ya kisheria iliyokuwa inaninyima amani kila siku.

Kila nilipoenda kusikilizwa kwa kesi, nilirudi nyumbani nikiwa nimechoka na kukata tamaa.

Ilionekana kama haki haikuwa upande wangu, hata pale nilipojua ukweli uko wazi. Gharama ziliongezeka, muda ulienda, na nilianza kupoteza matumaini kabisa. Ilifika wakati nilihisi kama nitaacha kila kitu na kukubali kushindwa. SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kufikiria kama siku moja ningepitia tukio ambalo lingebadilisha maisha yangu kwa sekunde chache tu. Ilianza kama siku ya kawaida kabisa, nikiwa nimechoka baada ya shughuli za mchana. Nilirudi nyumbani mapema bila kumpa taarifa yoyote.

Nilipoingia, nilihisi kuna hali ya tofauti ukimya usio wa kawaida na mlango ambao haukuwa katika hali niliyoacha asubuhi. Nilipoelekea ndani, nilianza kusikia sauti ndogo kutoka chumbani. Moyo wangu ulianza kupiga kwa kasi bila kuelewa kinachoendelea. Kila hatua niliyopiga iliongeza wasiwasi na mashaka.

Nilipofika mlangoni, niliganda kwa muda. Nilichokishuhudia kilikuwa kitu ambacho sikuwahi kukitarajia kutoka kwa watu wawili niliowaamini zaidi maishani mwangu. Mke wangu na rafiki yangu wa karibu walikuwa katika hali iliyonifanya nisemeze chochote kwa muda mrefu.

Ukimya mzito uliingia chumbani mara moja baada ya kuniona. Hisia zilichanganyika hasira, maumivu, na mshangao mkubwa. Sikuweza kuendelea kubaki pale kwa muda mrefu, hivyo niliondoka nikiwa nimevurugika kabisa kiakili.

Siku zilizofuata zilikuwa ngumu sana kwangu. Nilijikuta nikifikiria sana kilichotokea, nikikosa amani na hata mwelekeo wa maisha. SOMA ZAIDI.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) akisalimiana na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

Na William Bundala-Kahama Shinyanga

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kata ya Majengo manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga imeishukuru na kuipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya barabara katika kata hiyo.

 1789036939464 (1).jpg



Technology is not only for boys.

Girls belong in technology too.

Inside the UNESCO–BNU Closing the Digital Divide Project Boot Camp, girls are gaining

hands-on experience with technology—learning, exploring, collaborating and building their

digital skills.

But this is about more than learning how to use computers.

It is about challenging the belief that technology is a space for boys.

When girls are given the opportunity to learn, participate and explore technology, they can

build confidence, discover their potential and begin to see themselves as creators,

innovators and future leaders.

Let’s break the stereotypes.

Let’s open equal opportunities.

Let’s empower girls to shape the digital future.

GIRLS BELONG IN TECH.

UNESCO–BNU: Closing the Digital Divide Project

#GirlsInTech

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), akizungumza na wajumbe kutoka Tanzania watakaoshiriki Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika Sekta ya Afya, alipowasili jijini Nairobi, Kenya.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kusogeza huduma na elimu kuhusu viwango, ubora na usalama wa bidhaa karibu na wananchi kupitia Kliniki ya Viwango, hatua inayolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo na kuwawezesha wafanyabiashara kuzingatia matakwa ya viwango.
PEMBA — Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bw. Khamis Abdulla Said, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kuendelea kufadhili miradi ya maendeleo ya elimu Unguja na Pemba, akisema hatua hiyo inasaidia kuboresha mazingira ya ujifunzaji na kuinua ubora wa elimu visiwani humo.