Na: OWM – TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara zinazoingia kwenye viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michezo na mazoezi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) jijini Dar es Salaam, huku wananchi wakifurahia hatua hiyo na kuipongeza Serikali kwa ujenzi wa miundombinu  itakayosaidia kutatua changamoto ya usafiri katika maeneo hayo.

Prof. Shemdoe amesema hayo Agosti 24, 2026, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu hiyo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, ikiwemo Kigamboni, Uwanja wa Taifa (Benjamin Mkapa), Leaders Club pamoja na eneo la Mbweni kuelekea Uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo.

Amesema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, akieleza kuwa ujenzi wa barabara za Kigamboni umefikia asilimia 75, barabara za Uwanja wa Taifa asilimia 20, Leaders Club asilimia 70, huku barabara za Mbweni kuelekea Uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo zikifikia asilimia 20. Kwa ujumla, Prof. Shemdoe amesema utekelezaji wa ujenzi wa barabara hizo umefikia wastani wa asilimia 50.

Prof. Shemdoe amesema ametoa maelekezo kwa wakandarasi katika maeneo yote yanayotekeleza miradi hiyo kuhakikisha wanaongeza kasi ya ujenzi na kufanya kazi kwa saa 24, ili kuongeza ufanisi na kuhakikisha ifikapo Agosti 30, 2026, utekelezaji unafikia wastani wa zaidi ya asilimia 60. 

Kwa upande wake, Mkazi wa Mbweni jijini Dar es Salaam na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Malindi Estate, Bi. Maria Bilia, amesema wananchi wa Mbweni wamefarijika kuona ujenzi wa barabara hizo ukiendelea, kwa kuwa utasaidia kupunguza changamoto ya usafiri katika eneo hilo.

Bi. Bilia amemuomba Prof. Shemdoe kufikisha salamu za pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuboresha miundombinu ya barabara kuelekea AFCON 2027.

Ameongeza kuwa ameshuhudia wakandarasi wakifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, hatua ambayo amesema inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Malindi Estate, Kata ya Mbweni, Manispaa ya Kinondoni, Bi. Selina Mkonye, amesema wananchi wa eneo hilo wanaunga mkono jitihada za Serikali kwa vitendo, ikiwemo kuwa na mpango mkakati wa miaka mitano wa ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 30 kwa kiwango cha lami na kilomita 60 kwa kiwango cha changarawe.

Bi. Mkonye amesema ujenzi wa barabara zinazotekelezwa kwa ajili ya maandalizi ya AFCON 2027 umekuja kuchagiza na kuimarisha mpango mkakati huo wa wananchi wa kuboresha miundombinu katika eneo lao.

Ujenzi wa barabara hizo unalenga kuboresha upatikanaji na mtiririko wa usafiri kuelekea viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michezo na mazoezi ya Fainali za AFCON 2027 jijini Dar es Salaam, sambamba na kuboresha miundombinu kwa manufaa ya wananchi.

Kwa sasa, miradi minne (4) inatekelezwa, ambayo ni ujenzi kwa kiwango cha zege wa Barabara ya Taifa yenye urefu wa kilomita 1.3, Litapwasi kilomita 0.43 na Sotele kilomita 0.2; ujenzi kwa kiwango cha zege wa Barabara ya Yanga yenye urefu wa kilomita 0.7; ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Dahomey yenye urefu wa kilomita 0.5; ujenzi wa Barabara ya Mbalizi yenye urefu wa kilomita 0.8, pamoja na uboreshaji wa maegesho ya VVIP katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo.


















Na Oscar Assenga, TANGA

BENKI ya NMB imesema uwekezaji katika elimu, ujuzi wa vitendo na ubunifu unaowawezesha Watanzania kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili nchi ni muhimu katika kufikia uchumi wa kipato cha juu.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Meneja Mwandamizi wa Maabara ya Ubunifu ya NMB, Maria Mwamyalla, alipokuwa akitoa salamu za wadhamini kwa niaba ya wadhamini wote katika maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yaliyofanyika mkoani Tanga.

Mwamyalla alisema kaulimbiu ya mwaka huu, “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” inaendana na mkakati wa NMB wa kuwekeza katika teknolojia, ubunifu, vijana na ujumuishaji wa kifedha.

Alisema kupitia Agenda 2030, benki hiyo imeweka teknolojia, ubunifu, uwekezaji kwa vijana na ujumuishaji wa kifedha kuwa sehemu muhimu ya mkakati wake wa ukuaji.

“Mwelekeo huo unaendana moja kwa moja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kujenga uchumi wa ushindani unaotumia maarifa, ujuzi na teknolojia,” alisema.

Alisisitiza kuwa teknolojia pekee haiwezi kuleta matokeo yanayotarajiwa bila kuwapo kwa watu wenye maarifa na ujuzi wa kuitumia ipasavyo.


NMB yawekeza Sh bilioni 2 kwa vijana

Mwamyalla alisema kupitia NMB Foundation, benki hiyo imeendelea kuwekeza katika elimu na malezi ya uongozi kwa vijana, hususan wanaotoka katika familia zenye uwezo mdogo kiuchumi.

Alisema kupitia programu ya Nuru Yangu Scholarship and Mentorship, NMB imewekeza zaidi ya Sh bilioni mbili tangu mwaka 2022, kwa ajili ya kuwafadhili wanafunzi 121 katika vyuo vikuu 11 nchini.

Kwa mujibu wa Mwamyalla, wanafunzi hao wamekuwa wakisaidiwa mahitaji mbalimbali yakiwamo ada, malazi na vitendea kazi kama kompyuta mpakato.

Alisema wanafunzi 21 tayari wameingia katika soko la ajira, huku wengine 42 wakitarajiwa kuhitimu mwaka huu.

“Tunatarajia kufungua dirisha la tatu la programu hii mwezi Septemba mwaka huu,” alisema.
Wabunifu wanufaika

Aidha, Mwamyalla alisema NMB inaendelea kutekeleza programu ya SEP kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Save the Children pamoja na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Alisema programu hiyo inalenga kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa kuwapatia vijana elimu ya vitendo katika maeneo mbalimbali, ikiwamo mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa na vyuo vya VETA.

Katika eneo la teknolojia na ubunifu, alisema NMB imewekeza zaidi ya Sh bilioni 232, huku sehemu kubwa ya suluhisho za kiteknolojia zikitengenezwa na wataalamu wazawa.

Alisema uwekezaji huo unalenga kujenga utaalamu wa Watanzania, kuimarisha usalama wa mifumo pamoja na kupunguza muda wa kupeleka bidhaa za kidijitali sokoni.

Alitaja miongoni mwa suluhisho hizo kuwa ni huduma ya NMB Mkononi, inayowawezesha wateja kupata huduma mbalimbali za kibenki kupitia simu zao za mkononi, ikiwamo kutuma na kupokea malipo ya kielektroniki.

Kwa mujibu wa Mwamyalla, huduma hizo zimechangia kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa zaidi ya wateja milioni 10 wa NMB.

Alisema kupitia programu ya PesaTek, iliyoanzishwa mwaka 2022, benki hiyo imezindua Innovation Sandbox na kuendelea kuwawezesha vijana pamoja na wabunifu katika sekta ya teknolojia kupima na kuendeleza suluhisho zao.

Mwamyalla alisema NMB itaendelea kushirikiana na Serikali na taasisi za elimu kuhakikisha elimu, ujuzi na ubunifu vinageuzwa kuwa suluhisho zinazochochea biashara na kuchangia maendeleo ya Taifa.

 


Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimeandika historia mpya mkoani Manyara kwa kuzindua rasmi utoaji wa programu Shahada (Degree) katika Kampasi ya Babati. 

Hafla hiyo ya uzinduzi wa 'Bachelor of Accountancy with Information Technology' na "Bachelor of Computer Science' imeongozwa leo Agosti 24, 2026 na Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo.

Mhe. Sillo amesema wahitimu wa programu hizo watakuwa sehemu ya kizazi kipya cha wabunifu watakaosadia kuimarisha matumizi ya Teknolojia katika sekta ya fedha, elimu, afya,biashara, kilimo, utalii, viwanda na utoaji wa huduma za serikali.

Mkuu wa Chuo IAA, Prof. Eliamani Sedoyeka amesema" hatua hii ni mkakati wa IAA kuunga mkono juhudi za Serikali kusogeza elimu bora kwa wananchi na kuhakikisha wanapata elimu inayokidhi mahitaji ya dunia ya sasa na baadaye".

Aidha, Prof. Eliamani Sedoyeka ametangaza kuwa wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza watapatiwa huduma ya hosteli bure  hatua inayolenga kupunguza gharama kwa wazazi na kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira salama na tulivu.

Kampasi ya Babati ilianza mwaka 2014 ikiwa na wanafunzi 272, sasa ina wanafunzi 728 na IAA  inalenga kuongeza idadi ya wanafunzi Babati hadi 6,000 ifikapo mwaka 2031.

Aidha, IAA inaandaa mkakati wa kuanzisha programu za  elimu inayozingatia ujuzi (skills-based curriculum) katika maeneo kama Kilimo biashara, Uchakataji wa chakula,Uchakataji wa ngozi,Uhandisi wa uchomeleaji.Lengo ni kuwaandaa vijana wenye ujuzi wa vitendo, kuongeza fursa za kujiajiri na kuajiriwa, na kuendana na mahitaji ya soko la ajira.

















Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, akitembelea Kikundi cha Ufugaji Nyuki na Utunzaji wa Mazingira cha Twikondele, kinachonufaika na uwezeshaji wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu.
Hospitali ya Taifa Muhimbili–Mloganzila kwa kushirikiana na wataalam kutoka Korea Kusini, imewapandikiza figo wagonjwa wanne na wengine 38 wamefanyiwa upasuaji wa kutengeneza na kurekebisha mishipa ya kuchuja damu katika kambi maalum iliyofanyika Agosti 15–19, 2026.

NA EMMANUEL MBATILO, PWANI

WAZIRI wa Afya, Mohamed Mchengerwa, amekabidhi gari la wagonjwa (ambulance) kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, likiwa na lengo la kuimarisha huduma za dharura katika Kituo cha Afya Magindu na maeneo ya jirani.


NA EMMANUEL MBATILO, PWANI

SERIKALI iko katika hatua za mwisho za kukamilisha mfumo wa kitaifa wa huduma za magari ya wagonjwa (ambulance), utakaoboresha uratibu wa huduma hizo, ufuatiliaji wa magari na kuziunganisha na namba ya dharura 115, inayopigwa bila malipo.
Na Mwandishi Wetu

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa fedha kwa wakulima na wajasiriamali, kuongeza uzalishaji na kuimarisha minyororo ya thamani ya kilimo Zanzibar.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga (Mb), Agosti 24, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo tofauti na Mabalozi wa Kenya na Afrika Kusini nchini, katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Kupendwa, kuposwa, na kuvaa shela la harusi ni ndoto ya kila mwanamke anayetamani kujenga familia yenye amani na heshima. 

Hata hivyo, pale ambapo kila mahusiano unayoingia yanafikia hatua ya uchumba kisha yanavunjika ghafla bila sababu ya msingi, maisha hugeuka kuwa aibu na kicheko mbele ya jamii.

Kwa zaidi ya miaka sita, nilipitia mikosi ya ajabu kwenye sekta ya mapenzi. Wanaume watatu tofauti waliniposa kwa mbwembwe nyingi, tukafanya mikutano ya familia, na kupanga tarehe za harusi. 

Lakini kila tulipobakiza wiki chache au siku chache kufanya harusi, mwanaume alibadilika ghafla, akaanza kunichukia bila kosa lolote, na hatimaye kutoroka na kukatisha ndoa.

​Nilibaki nikiwa na simanzi nzito, aibu mbele ya wazazi na ndugu zangu, na msongo mkubwa wa mawazo. Kila nilipojitazama kwenye kioo nilijiona mrembo, mwenye elimu na tabia njema, lakini kwenye macho ya wanaume nilionekana kama kiumbe cha kutisha.

Majirani na marafiki walianza kunisengenya na kunipa majina ya kejeli wakidai nina mikosi au nimerogwa nisiolewe kabisa.

Nilibaki nikijifungia ndani na kulia usiku kucha, nikipoteza kabisa matumaini ya kuwa na mume au kuitwa mama kwenye maisha yangu. SOMA ZAIDI.
Afya njema ndiyo nguzo kuu ya maisha na utafutaji wa kila siku, lakini pale unapoanza kupata maumivu makali mwilini kisha vipimo vya kisasa hospitalini vikakosa majibu, maisha hugeuka kuwa fumbo na mateso yasiyo na mwisho.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia kipindi kigumu mno cha afya yangu. Nilianza kuhisi vitu vikitembea mwilini, maumivu makali ya kichwa yasiyosikia dawa, na tumbo kuwaka moto kila usiku. Maumivu haya yalininyima kabisa uwezo wa kufanya kazi, kutoka nje, au hata kupata usingizi wa amani.

​Nilitembelea hospitali kubwa za mkoa na kutumia mamilioni ya fedha kufanya vipimo vya Ultra-sound, X-ray, na MRI. Hata hivyo, kila matokeo yalipotoka, madaktari waliniahidi kuwa vipimo vyote vilionyesha niko salama kabisa na sina ugonjwa wowote unaoonekana.

Waliponiandikia dawa za kupunguza maumivu, hazikusaidia kitu; hali ilizidi kuwa mbaya kila siku huku nikikonda, kupoteza muonekano wangu, na kuona kifo kikisogea karibu.

Nilibaki nikilia kwa uchungu kitandani, nikitazama akiba yangu yote ikiteketea hospitalini huku ndugu na marafiki wakianza kunitenga wakidhani nina ugonjwa wa ajabu usio na tiba. SOMA ZAIDI.
Kuingia kwenye ndoa na kuweka nia ya kujenga misingi thabiti ya kifedha na mumeo ni ndoto ya kila mwanamke, lakini pale ambapo mwanaume anapofanya kazi kwa bidii kisha anachukua mshahara wake wote na kuutumia na michepuko, maisha ya familia hugeuka kuwa mateso ya kila siku.

Kwa zaidi ya miaka minne, mume wangu alikuwa na tabia iliyostua na kuumiza sana. Kila mwisho wa mwezi ulipowadia na mshahara wake kuingia kwenye akunti, alibadilika ghafla. Hakurejea nyumbani kwa siku tatu au nne, na simu zake zote zilikuwa hazipatikani.

​Aliporejea, alikuja na mifuko mikavu bila hata shilingi mia moja ya matumizi. Pesa zote za mshahara alizimalizia kwenye hoteli za kifahari, baa, na kuwanunulia zawadi za ghali wanawake wa nje, huku mimi na watoto tukibaki bila chakula, tukidaiwa kodi ya nyumba, na watoto wakifukuzwa shuleni kwa kukosa ada.

Kila nilipojaribu kumhoji kwa uchungu, aliniletea vipigo, matusi ya nguoni, na kunitishia kunifukuza nyumbani. Nilibaki nikilia usiku na mchana, nikijiona sina thamani na nikitazama watoto wangu wakiteseka kwa ukata wakati baba yao anatapanya mamilioni ya fedha na michepuko mtaani. SOMA ZAIDI.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), CPA. Anthony Kasore, amesema ujuzi ndio msingi wa utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 kwa kuwawezesha wananchi kushiriki katika uzalishaji wa mali, bidhaa na huduma.

 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amezitaka Halmashauri zote nchini kutumia michezo kama nyenzo ya kuimarisha afya, ustawi, mshikamano na tija kwa watumishi, ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi. 

Prof. Shemdoe ametoa wito huo Agosti 23, 2026 jijini Mbeya wakati akifungua rasmi Mashindano ya Michezo ya Watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA), kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba.

Akizungumza katika ufunguzi huo, Prof. Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuyarejesha tena mashindano ya SHIMISEMITA mwaka 2023 baada ya  kusitishwa, akitambua kwamba michezo ni sehemu muhimu ya kujenga afya ya mwili na akili, kuimarisha mahusiano kazini na kukuza ushirikiano miongoni mwa watumishi kutoka Halmashauri mbalimbali nchini.

 “Leo hii mmekutana watumishi zaidi ya 5,000 kutoka katika Halmashauri 177. Kila mmoja anao wajibu wa kujenga mahusiano mazuri na watumishi wa Halmashauri nyingine, kwani michezo ni afya, michezo ni kiunganishi. Hivyo, tumieni fursa hii kujenga afya zenu na kuimarisha ushirikiano miongoni mwenu,” amesema.

Aidha, Prof. Shemdoe amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha ushiriki wa michezo unawahusisha watumishi kutoka maeneo mbalimbali, badala ya watumishi wa Makao Makuu pekee. Amesema watumishi kutoka ngazi za kata, vijiji na vitongoji wanapaswa kupewa fursa ya kushiriki, kwa kuwa michezo itawajengea ari na morali ya kutekeleza majukumu yao, ikiwemo ukusanyaji wa mapato, ikizingatiwa kuwa mtumishi mwenye afya njema ya mwili na akili atatekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amezitaka Halmashauri kuwaandaa na kuwajengea uwezo wananchi kutumia fursa zitakazotokana na Mashindano ya Soka kwa Timu za Taifa Barani Afrika (AFCON 2027). Amesema mashindano hayo si suala la michezo pekee, bali yatatoa fursa za kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na hususan katika sekta ya utalii, ambayo ni miongoni mwa sekta muhimu katika kuiingizia Tanzania fedha za kigeni.

Kutokana na umuhimu wa michezo kwa afya na utendaji wa watumishi wa umma, Prof. Shemdoe amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha michezo ya SHIMISEMITA inawekewa kifungu katika bajeti zao na kutengewa fedha ili kuwawezesha watumishi kushiriki kikamilifu. Amesema uwekezaji katika michezo ni uwekezaji katika afya ya mwili na akili za watumishi, jambo litakalosaidia kuongeza morali, ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, amemshukuru Prof. Shemdoe kwa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kuyaleta mashindano ya SHIMISEMITA mkoani Mbeya, na kuahidi kuwa uongozi wa mkoa umejipanga kuhakikisha usalama na ustawi wa wanamichezo wote wakati wa mashindano hayo. Aidha, Mhe. Malisa amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia mashindano ya SHIMISEMITA kuendelea kufanyika nchini.

Naye, Katibu Mkuu wa SHIMISEMITA, Bw. Henry Kapella, ameiomba Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, ikiwa mlezi wa SHIMISEMITA, kuendelea kuzihimiza Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya kuwawezesha watumishi kushiriki mashindano hayo kila mwaka. Ameshauri pia TAMISEMI kuweka kigezo cha uwepo wa fedha zilizotengwa kwa ajili ya michezo ya SHIMISEMITA katika mchakato wa kupitisha bajeti za Halmashauri, ili kuhakikisha watumishi wanapata fursa endelevu ya kushiriki michezo.

Mashindano ya SHIMISEMITA mwaka huu yamebeba kaulimbiu “Tuko Tayari kwa AFCON 2027,” ikiwa ni ujumbe unaosisitiza utayari wa Tanzania kutumia fursa za michezo, kuimarisha afya na mshikamano wa watumishi, pamoja na kunufaika na fursa za kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kiutalii zitakazotokana na AFCON 2027.

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi na washiriki wa Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu inayofanyika jijini Tanga kuhusu bunifu mbalimbali zinazozalishwa na watafiti na wabunifu wanaoshirikiana na taasisi hiyo.

Katika maadhimisho hayo, NM-AIST imewasilisha jumla ya bunifu 20, ambazo nyingi zimetokana na tafiti na kazi za watafiti wa ndani ya taasisi, huku nyingine zikiwa zimezalishwa na wabunifu wa nje wanaopatiwa malezi, mafunzo na mwongozo kupitia taasisi hiyo. Bunifu hizo zinaonesha jitihada za NM-AIST katika kuunganisha utafiti, ubunifu na mahitaji halisi ya jamii.

Aidha, taasisi hiyo imewashirikisha wawakilishi wa vikundi vya wanawake wanaopatiwa msaada na mwongozo katika kuboresha bidhaa zao na kuongeza thamani. Hatua hiyo inalenga kuwawezesha kutumia maarifa na teknolojia kuongeza ubora, tija na ushindani wa bidhaa zao sokoni.

Katika hatua nyingine, NM-AIST imewasilisha kampuni tatu zilizoanzishwa kutokana na bunifu na tafiti zilizofanyika ndani ya taasisi. Kampuni hizo ni Nano Filter, inayojihusisha na teknolojia ya uchujaji wa maji; AfriTech, inayotumia teknolojia inayotokana na mabaki ya korosho katika uchakataji wa ngozi; na Uji Chap Chap, inayolenga kuchangia afya bora kupitia bidhaa za lishe.

Ushiriki wa NM-AIST katika maonyesho hayo unaendelea kutoa fursa kwa wananchi kujifunza namna ambavyo matokeo ya utafiti na ubunifu yanaweza kubadilishwa kuwa bidhaa na huduma zenye manufaa kwa jamii. Aidha, ushiriki huo unaonesha mchango wa taasisi katika kukuza matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu kama nyenzo muhimu za maendeleo ya Tanzania.

NM-AIST inaendelea kuthibitisha dhamira yake ya kuifikia jamii, kuwatamia wajasiriamali na kukuza ubunifu kwa maendeleo endelevu.

 

Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Mhe. Omari Issa atunuku shahada za umahiri na uzamivu kwa wahitimi 138 katika Mahafali ya 12 ya Taasisi ya Nelson Mandela yaliyofanyika Leo tarehe 20 Agosti 2026, NM-AIST Tengeru Arusha.

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), Balozi Maimuna Tarishi, amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha tafiti, teknolojia na ubunifu unaozalishwa na Taasisi unatafsiriwa kuwa bidhaa, huduma na suluhisho halisi kwa changamoto za jamii, sambamba na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Akizungumza katika Mahafali ya 12 ya Taasisi (NM-AIST), Balozi Tarishi amesema ubunifu haupaswi kuishia kwenye makaratasi au usajili wa hati miliki, bali unapaswa kutumika kutatua changamoto katika sekta za kilimo, ufugaji, biashara, mazingira na uchumi.

“Ubunifu usiishie kwenye makaratasi wala usajili BRELA; twende tukautafsiri kwa vitendo ili kujibu changamoto mbalimbali za jamii,” amesema Balozi Tarish.

Aidha, amewataka wahitimu kutumia maarifa na ujuzi walioupata NM-AIST kujitolea kuitumikia jamii ya Tanzania na Afrika, badala ya kutumia elimu kwa manufaa binafsi pekee.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula, amesema jumla ya wahitimu 138 wamehitimu katika mahafali hayo, wakiwa wamezalisha machapisho 219 ya kisayansi na hati miliki saba.

Amesema NM-AIST itaendelea kuhamasisha wanafunzi na watafiti kuzalisha bidhaa, kufanya ugunduzi na kuchapisha tafiti katika majarida ya kimataifa. 

Pia, Profesa Maulilio Kipanyula amesema watafiti 19 wa NM-AIST wametambuliwa katika tuzo za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zinazohusisha machapisho katika majarida ya kisayansi yenye hadhi ya juu duniani.

NM-AIST inaendelea kubadili maarifa kuwa ubunifu, ubunifu kuwa bidhaa na huduma, na tafiti kuwa suluhisho la changamoto za jamii sambamba na utekelezaji wa Dira 2050.