Na Oscar Assenga, TANGA

Programu ya Tanga Yetu imeendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa vijana na watoto wa Jiji la Tanga, kupitia miradi inayolenga kuimarisha elimu, ujuzi, teknolojia na ubunifu kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.

Akizungumza katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, Afisa Mawasiliano wa Programu ya Tanga Yetu, Cliford Sangai, alisema programu hiyo inayofadhiliwa na Foundation Botnar na kutekelezwa na Kampuni ya Innovate kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Tanga, imeshiriki maonyesho hayo kuonyesha matokeo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa jijini humo.

Alisema Tanga Yetu inatekeleza zaidi ya miradi 15 katika maeneo ya elimu, teknolojia na ubunifu, ikiwa na lengo la kuhakikisha watoto na vijana wanapata fursa za kukuza uwezo wao na kutumia maarifa kutatua changamoto zinazowakabili.

“Tumekuja kwenye wiki hii kuonyesha namna ambavyo Tanga Yetu imekuwa ikifadhili miradi mbalimbali katika elimu, ujuzi na ubunifu, pamoja na kuonyesha bidhaa na suluhisho zinazotokana na mawazo ya vijana wa Tanga,” alisema Sangai.

Kwa mujibu wa Sangai, baadhi ya miradi inayotekelezwa inalenga kukabiliana na changamoto ya watoto katika kujifunza kusoma na kuandika, huku matokeo ya mradi huo yakitumika katika kutengeneza mpango wa Kitaifa wa KKK.

Alisema programu hiyo pia imejikita katika kuwawezesha vijana kutumia vipaji na ujuzi wao katika teknolojia na ubunifu, akisisitiza kuwa vijana wa Tanga wana uwezo wa kubuni na kutengeneza bidhaa zinazoweza kutatua changamoto za jamii na hata kufikia soko la kitaifa.

“Vitu ambavyo tunaona vinafanyika katika miji mingine vinafanyika pia Tanga. Vijana wetu wamekuja na bidhaa walizobuni na kuzitengeneza wenyewe, jambo linaloonyesha uwezo mkubwa walionao,” alisema.

Sangai alisema katika eneo la ujuzi, Tanga Yetu imekuwa ikiwawezesha vijana kupata mafunzo mbalimbali yanayowaongezea uwezo wa kujiajiri na kuzalisha kipato kupitia teknolojia.

Alitaja baadhi ya mafunzo hayo kuwa ni Graphic Design, uchapishaji wa mabango na T-shirt, utengenezaji wa maudhui ya kidijitali (Content Creation), usimamizi wa mitandao ya kijamii (Social Media Management) pamoja na ujuzi mwingine wa kidijitali.

Alisema vijana wanaotembelea banda la Tanga Yetu katika maonyesho hayo wanaweza kuona miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo ya elimu, ujuzi na ubunifu, pamoja na namna inavyowasaidia vijana wa Tanga kujenga uwezo na kutengeneza fursa.

Sangai alisema Tanga Yetu pia imeanzisha Mfuko wa Ubunifu wa Tanga Yetu, ambao umewezesha vijana wanane kupata ufadhili wa kujaribu mawazo yao ya kibunifu yenye lengo la kutatua changamoto zinazoikabili jamii ya Jiji la Tanga.

Alisema miongoni mwa miradi hiyo ni mfumo unaolenga kuwasaidia wavuvi kufahamu maeneo yenye samaki pamoja na kufuatilia usalama wa vyombo vyao wanapokuwa baharini.

“Tumeshazoea wavuvi kuamka usiku na kwenda kuvua bila kujua samaki wapo wapi. Vijana wamekuja na mfumo unaoweza kumsaidia mvuvi kufahamu eneo ambalo samaki wapo na kwenda kuvua kwa ufanisi zaidi,” alisema.

Aliongeza kuwa mfumo huo pia unafuatilia mwenendo wa chombo cha uvuvi, hivyo iwapo kunapotokea  ajali baharini, watu waliopo nchi kavu wanaweza kufahamu eneo ambalo chombo hicho kimepata tatizo na kuchukua hatua kwa haraka.

Sangai alisema hatua hiyo inaonyesha namna ubunifu unavyoweza kutumika kama nyenzo ya kutatua changamoto zinazolikabili Jiji la Tanga na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Zainabu Msuya, mnufaika wa Mradi wa Kidijitali unaosimamiwa na Swahili Digital chini ya Programu ya Tanga Yetu, alisema amepata fursa ya kujifunza ujuzi mbalimbali wa teknolojia na sasa anaweza kutumia maarifa hayo kujiajiri na kuwawezesha vijana wengine.

Alisema mradi huo unatoa mafunzo katika maeneo ya Graphic Design, Artificial Intelligence (AI), Content Creation, Social Media Management na ujuzi wa kidijitali kwa ujumla.

Msuya alisema yeye ni mmoja wa wanufaika wa awamu ya kwanza ya mafunzo hayo na baadaye alipata nafasi ya kuwa mmoja wa wasimamizi katika awamu zilizofuata.

“Mradi huu umeweza kuwawezesha vijana wengi. Kwa awamu zilizofuata tulihusisha vijana 100 kwa kila awamu, na kwa ujumla vijana 300 wamepata mafunzo kupitia programu hii,” alisema.

Alisema mafunzo hayo yamewasaidia vijana kuongeza uelewa wa teknolojia na kupata uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii kama sehemu ya kujenga fursa za kiuchumi.

Naye Swahibu Bilal, msimamizi wa mradi wa kidijitali, alisema programu hiyo imekuwa ikiwafundisha vijana namna ya kutumia mitandao ya kijamii kwa ufanisi na kuitumia kama nyenzo ya kutengeneza kipato.

Alisema awali vijana wengi hawakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii kibiashara, lakini kupitia mafunzo hayo wameweza kujifunza namna ya kusimamia akaunti, kutengeneza maudhui na kutumia majukwaa hayo kukuza shughuli zao.

“Vijana wengi awali walikuwa hawaelewi namna ya kutumia mitandao ya kijamii kutengeneza kipato, lakini kupitia mafunzo haya sasa wanaweza kufanya mambo mbalimbali na kutumia ujuzi huo kujenga fursa zao,” alisema Bilal.

Programu ya Tanga Yetu inaendelea kushirikisha vijana katika elimu, ujuzi, teknolojia na ubunifu, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwaandaa kutumia maarifa na vipaji vyao katika kutatua changamoto za jamii na kuchangia maendeleo ya Jiji la Tanga na Taifa kwa ujumla.



Na Mwandishi Wetu - DAR ES SALAAM


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, ametoa maelekezo manne kwa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), akitaka Awamu ya Pili ya Mradi wa Faiba Mlangoni Kwako (FTTH) iwanufaishe wananchi kupitia huduma yenye ubora, uhakika na gharama nafuu.

Mhe. Kairuki alitoa maelekezo hayo wakati akizindua rasmi utekelezaji wa awamu hiyo katika Ukumbi wa Johari Rotana, Dar es Salaam, akisisitiza kuwa mafanikio ya mradi hayapaswi kupimwa kwa idadi ya Home Pass pekee, bali kwa idadi ya wananchi wanaounganishwa, ubora wa huduma, kasi ya intaneti na kiwango cha kuridhika kwa wateja.

Ametaka TTCL kupanua huduma ya faiba hadi maeneo yenye makazi yanayokua, masoko, maeneo ya biashara, viwanda, shule, vyuo, vituo vya afya na ofisi za Serikali Tanzania Bara na Zanzibar.

Pia ameagiza Shirika kudumisha ubora wa huduma na kuimarisha huduma kwa wateja, ikiwemo kushughulikia malalamiko kwa haraka na kwa ufanisi.

Waziri huyo amelitaka TTCL kuhakikisha huduma inapatikana kwa gharama nafuu kwa kuandaa vifurushi vinavyokidhi mahitaji ya familia, wanafunzi, vijana na wafanyabiashara wadogo na wa kati.

Katika agizo la nne, amesisitiza uwajibikaji na nidhamu ya kibiashara katika usimamizi wa mradi, akitaka wazabuni na wakandarasi wasimamiwe kwa ufanisi ili kazi zikamilike kwa wakati, kwa ubora na kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Amesema Faiba Mlangoni Kwako si mradi wa kujenga miundombinu ya mawasiliano pekee, bali ni hatua ya kimkakati ya kufungua fursa za elimu, biashara, ajira na ubunifu na kuchochea uchumi wa kidijitali.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, CPA Moremi Marwa, amesema Awamu ya Pili ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Biashara wa Miaka 10 wa Shirika wa 2025/26–2034/35.

Marwa amesema Awamu ya Kwanza imewezesha TTCL kujenga zaidi ya Home Pass 280,000 na kufikisha karibu 300,000 maungio ya huduma ya nyuzi za macho nchini.

Amesema katika Awamu ya Pili TTCL inalenga kuongeza zaidi ya Home Pass 400,000, huku ikiendelea kutumia teknolojia ya Gigabit Passive Optical Network (GPON) ili kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za uendeshaji na kuboresha ubora wa huduma.

Ameongeza kuwa utekelezaji unafanyika kwa ushirikiano na makandarasi wa ndani na wa kimataifa, wakiwemo Huawei, ZTT na Visoll.

Waziri Kairuki amewataka wananchi kutumia huduma hiyo katika kujifunza, kufanya biashara, kuongeza uzalishaji, kubuni ajira na kupata huduma za Serikali kidijitali, huku akiwataka pia kulinda miundombinu ya mawasiliano dhidi ya uharibifu na wizi.








Mameneja wa Kanda na Mikoa wa Taasisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) wameagizwa kuhakikisha hakuna bidhaa bandia na duni katika maeneo yao wanayoyasimamia kiutendaji.
Kariakoo, 20 Agosti, 2026

‎ Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeimarisha ushirikiano na uongozi wa Mabalozi Jengo kwa lengo la kuwafikia walipakodi na wadau mbalimbali kwa ufanisi zaidi.
Amani ya akili na usingizi mwanana usiku ni haki ya kila binadamu, lakini pale usiku unapogeuka kuwa uwanja wa mateso na ndoto za kutisha, maisha yote hugeuka kuwa jinamizi. Kwa zaidi ya miaka miwili, nilikuwa nikiteseka sana kila nilipoweka kichwa changu kitandani.

Nilikuwa nikoota ndoto za kufukuzwa na wanyama wakali, kuogelea kwenye maji machafu, kula chakula usiku, au kukabiliwa na watu waliokufa zamani waliokuwa wakinitisha na kuninyonga.

​Kila nilipoamka asubuhi, nilijikuta nikiwa na uchovu mwingi mwilini, maumivu ya viungo, na hofu kuu iliyoniletea msongo wa mawazo. Hali hii haikuishia kwenye usingizi tu; ndoto hizo zilianza kuniletea nuksi na mikosi kwenye maisha yangu ya kila siku.

Biashara zangu zilianza kufilisika, mahusiano yangu yakavunjika, na afya yangu ikaanza kudorora bila madaktari hospitali kuona ugonjwa wowote. Nilibaki nikihofu kufika usiku, nikiteseka kwa kukosa usingizi na kuona maisha yangu yakiangamia polepole. SOMA ZAIDI.
Kushirikiana vyema na majirani zako wa karibu ni msingi mkuu wa amani na usalama nyumbani, lakini pale unapozungukwa na majirani wenye chuki, maneno ya shombo, na fitna zisizo na msingi, nyumba yako hugeuka kuwa uwanja wa mateso.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia maisha ya ubaguzi na kelele zisizokwisha kutoka kwa majirani zangu wa mtaani. Kila nilipofanya maendeleo madogo iwe ni kukarabati nyumba, kununua chombo kipya, au hata watoto wangu kufanya vizuri shuleni vilizua chuki na maneno ya ushirikina dhidi yangu na familia yangu.

​Ugomvi ulitengenezwa bila sababu yoyote; walitupa taka mlangoni kwangu, wakatusingizia kashfa mbaya mtaani, na kunifanyia matusi ya wazi kila nilipopita mbele zao.

Nilitumia njia zote za kiustaarabu kwa kwenda kulalamika kwa wajumbe wa mtaa, wazee wa eneo hilo, na hata polisi, lakini kila walipoonywa, chuki yao iliongezeka na kuanza kutishia usalama wa watoto wangu.

Nilibaki nikinaikwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikipoteza kabisa amani ya kukaa kwenye nyumba yangu mwenyewe na kufikiria kuiweka sokoni ili nikimbie mateso hayo ya maneno. SOMA ZAIDI.

Kinshasa, 17 Agosti 2026: Airtel Africa imeandika historia baada ya kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano barani Afrika kuzindua kibiashara intaneti ya satelaiti kwa simu nchini Jamhuriya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ikifungua ukurasa mpya katika upatikanaji wa mawasilianokatika maeneo yasiyofikiwa na minara ya kawaida ya simu.
Uwekezaji kwenye kilimo na ufugaji unahitaji jasho, mtaji, na matumaini makubwa ya kuvuna matunda ya kazi yako. 

Hata hivyo, pale ambapo shamba lako linageuka kuwa uwanja wa magonjwa ya ajabu ya mifugo na uvamizi wa wizi wa kila siku, juhudi zako zote hugeuka kuwa hasara na simanzi kubwa.

Kwa zaidi ya msimu mitatu, niliwekeza mamilioni ya fedha kwenye kilimo cha mboga mboga na ufugaji wa kuku na ng’ombe wa maziwa. 

Lakini kila nilipokaribia kuvuna au kuuza mifugo, majanga yasiyoeleweka yalianza kutokea. Mazao yalikauka ghafla bila wadudu kuonekana, na mifugo yangu ilianza kufa mmoja baada ya mwingine.

​Kama vile haitoshi, majambazi na wezi wa mtaani walivamia shamba langu usiku wa manane na kuiba vifaa, mazao yaliyobaki, na ng’ombe wangu bora wa maziwa.

Nilitumia fedha nyingi kununua dawa za kisasa na kuweka walinzi, lakini hakuna kilichosaidia; wezi waliendelea kuingia na magonjwa yaliendelea kuangamiza mifugo.

Nilibaki nikiwa nimefilisika kabisa, nikitazama shamba langu likiwa uwanja wa vumbi na mifupa ya mifugo, huku madeni ya pembejeo yakiniandama na kunikosesha amani ya nafsi. SOMA ZAIDI.

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdulkarim amewataka watumishi kuhakikisha kuwa wanakuwa suluhu ya changamoto za wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo kwa kusikiliza, kutoa majawabu ya uhakika kwa wakati na kutoa mrejesho kwa wafanyabiashara hao kwa wakati na kuzingatia mkataba wa huduma kwa mteja.

 




Na: Julitha Mlay
Tanga, 20 Agosti 2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, leo Agosti 20, 2026 ametembelea Banda la Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa yanayoendelea jijini Tanga.

Katika ziara hiyo, Prof. Nombo amepata fursa ya kujionea shughuli na maudhui mbalimbali yanayotolewa na Tume katika kuelimisha umma kuhusu UNESCO, majukumu ya Tume na programu zake katika maeneo ya elimu, sayansi, utamaduni, mawasiliano na taarifa.

Prof. Nombo alikuwa ameambatana na Dkt. Fredrick Salukele, Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi, ambapo walipata fursa ya kufahamu zaidi namna Tume inavyotumia majukwaa ya kitaifa kuwafikia wananchi, wanafunzi, walimu, vijana na wadau wengine kwa taarifa kuhusu UNESCO na fursa zinazopatikana kupitia programu zake.

Ushiriki wa Tume katika Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha elimu na uelewa wa umma kuhusu UNESCO, pamoja na kuonesha mchango wa elimu, sayansi, utamaduni, mawasiliano na taarifa katika kukuza maarifa, ubunifu na maendeleo endelevu nchini.

Kupitia jukwaa hilo, Tume inaendelea kuwasogezea wananchi taarifa kuhusu kazi za UNESCO na maeneo mbalimbali yanayohusiana na utekelezaji wa programu zake nchini Tanzania, huku ikihamasisha ushiriki wa jamii katika kutumia maarifa na fursa zilizopo kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa yanaendelea jijini Tanga yakishirikisha taasisi na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu, ujuzi na ubunifu kwa lengo la kuelimisha jamii kuhusu fursa, huduma na jitihada zinazochangia maendeleo ya rasilimali watu nchini.

Kwa habari zaidi kuhusu shughuli, programu, matukio na fursa mbalimbali za Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, endelea kutufuatilia kupitia kurasa zetu rasmi za mitandao ya kijamii:

Facebook na Instagram: @unesconatcomtz
Tume ya Taifa ya UNESCO — Kuelimisha, Kuhamasisha na Kushirikisha Jamii.






 

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) nchini Tanzania, Ndugu Xu Sujiang, huku akisisitiza dhamira ya CCM ya kuendelea kuimarisha uhusiano wa kihistoria na wa kimkakati kati ya vyama hivyo viwili.









Kikao hicho kimefanyika leo Agosti 20,2026 katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma, ambapo Ndugu Xu ametumia nafasi hiyo kuaga rasmi kabla ya kuhitimisha majukumu yake nchini Tanzania

Na.Mwandishi Wetu- Dodoma

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake na kuitaka kuharakisha matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS) katika zao la parachichi ili kuongeza tija kwa wakulima.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, ametoa pongezi hizo leo Agosti 20, 2026 jijini Dodoma baada ya Kamati hiyo kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya WRRB kwa mwaka 2025/26.

Mhe. Mwanyika amesema Kamati imeridhishwa na utendaji kazi wa WRRB, hasa katika kushughulikia changamoto za wananchi, na kuitaka Bodi hiyo iongeze kasi katika utoaji elimu ili kuchochea matumizi ya mfumo huo katika maeneo mengine.

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wajumbe, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, ameahidi kufanyia kazi maelekezo ya Kamati hiyo na kuihakikishia kuwa ataendelea kulinda majukumu ya taasisi zilizo chini yake kwa mujibu wa sheria.

Awali, akiwasilisha taarifa kwa Kamati hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema kwa mwaka 2025/26, WRRB imetoa leseni kwa waendesha ghala 235, kusajili ghala 951, wanunuzi 390, waweka mali 2,667 na kutoa stakabadhi za ghala 214,170.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, kupitia Mwenyekiti wake Mhe.Deodatus Mwanyika, ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na taasisi zake kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi .

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo imeipongeza TBS kwa kutekeleza majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Deogratias Mwanyika kwaniaba ya kamati wakati wa kikao cha Kamati cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu,katika, ofisi za Bunge Jijini Dodoma mapema leo.

Mhe.Mwanyika amesema juhudi zinazofanywa na TBS katika kuhakikisha usalama na ubora wa bidhaa zinazotumiwa na Watanzania zinaonekana hata hivyo ametoa rai kwa TBS kuendelea kutoa elimu na kuongeza jitihada sambambana na kuwa na programu maalum za kushughulikia bidhaa zinazoingizwa nchini kwa njia zisizo rasmi.

Naye Mhe. Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga(Mb) ameishukuru kamati hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo na ushauri uliotolewa na kamati hiyo ili kuendelea kurahisisha utendaji kazi wa TBS.

Vile vile Mhe.Kapinga amesema lengo la Wizara kupitia TBS ni kuhakikisha kunakuwa na bidhaa zenye ubora na usalama katika soko zinazozalishwa ndani na zinazotoka nje ya nchi.