Clement akiwa na ng’ombe/eneo la malisho

*******************

MTANANA, KONGWA, DODOMA — Kwa miaka mingi, Clement Alfonce alifuga ng’ombe kwa kutegemea malisho ya asili. Ng’ombe wake walizunguka katika maeneo mbalimbali kutafuta malisho, hali iliyomweka katika migogoro ya mara kwa mara na majirani ambao mazao yao yaliathiriwa na mifugo hiyo.

Clement, mkazi wa Kijiji cha Mtanana katika Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, alikuwa na ng’ombe 56. Lakini kuwa na mifugo mingi hakukuwa na maana ya kuwa na ufugaji wenye uhakika.

Wakati wa ukame, malisho yalipungua na hali ya mifugo ilidhoofika. Baadhi ya ng’ombe walikufa kipindi cha ukame. Wakati mwingine mifugo iliingia katika mashamba ya majirani, na Clement alilazimika kulipa faini.

Changamoto hiyo ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Leo, hali imebadilika.

Clement amepunguza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa ufugaji wa kufuatana na ng’ombe kutafuta malisho. Ameuza ng’ombe wake 50 na kununua ng’ombe 16 wa maziwa anaowafuga kwa mfumo malisho bandani.

Mabadiliko hayo yameambatana na jambo jingine muhimu: sasa Clement analima malisho yake mwenyewe.

Shamba lake la malisho limekuwa sehemu muhimu ya mfumo wake mpya wa ufugaji, na ana matumaini makubwa kwamba uzalishaji huo utampa chakula cha kutosha cha mifugo hata wakati wa ukame.

Mabadiliko hayo yamechochewa kwa kiasi kikubwa na maarifa aliyoyapata kupitia utafiti shirikishi unaofanywa na watafiti wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa ufadhili wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

Utafiti huo, unaoongozwa na Dkt. Dorice Lutatenekwa, unahusisha tathmini ya aina mbalimbali za nyasi kwa lengo la kubaini uwezo wake wa kustahimili ukame na kutoa malisho yanayoweza kusaidia wafugaji katika mazingira yenye changamoto ya mabadiliko ya tabianchi.

Kwa Clement, ushiriki katika utafiti haukuwa suala la kusikia matokeo kutoka kwa wataalamu pekee. Alipata fursa ya kuona aina mbalimbali za malisho zikifanyiwa majaribio na kutathmini matokeo yake katika mazingira yake.

Kadiri alivyopata uelewa kuhusu uzalishaji wa malisho, ndivyo alivyobadilisha mtazamo wake kuhusu ufugaji.

Badala ya kujiuliza ng’ombe wake watapata wapi malisho, alianza kujenga uwezo wa kuzalisha chakula cha mifugo yake mwenyewe.

“Nilikuwa na ng’ombe wengi, lakini changamoto kubwa ilikuwa malisho, hasa wakati wa ukame. Mifugo ilikuwa ikiingia kwenye mashamba ya watu na nililazimika kulipa faini. Nilipojifunza kuhusu uzalishaji wa malisho na kuona matokeo ya utafiti, nikaona umuhimu wa kubadilisha mfumo wangu wa ufugaji.” Clement Alfonce, Mfugaji, Kijiji cha Mtanana B, Kongwa

Uamuzi wa Clement wa kuhamia kwenye ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kwa mfumo wa malisho bandani unaonyesha namna utafiti unavyoweza kusaidia katika kufanya maamuzi ya uzalishaji katika ngazi ya kaya.

Badiliko hilo halimaanishi tu kwamba idadi ya ng’ombe wake imeshuka kutoka 56 hadi 16.Maana yake kubwa iko katika mabadiliko ya mfumo wa ufugaji.

Ng’ombe waliokuwa wakitegemea malisho yanayopatikana kwa kutangatanga sasa wana mfumo maalumu wa kulishwa. Clement anaweza kupanga uzalishaji wa malisho, matumizi yake na mahitaji ya mifugo yake.

Hii pia inapunguza utegemezi wa malisho ya asili ambayo hupungua wakati wa ukame.

Utafiti wenye mantiki shambani

Maisha ya Clement inaonyesha changamoto kubwa inayokabili sayansi katika nchi nyingi, na namna ya kuhakikisha kwamba maarifa yanayozalishwa na watafiti yanafika kwa watu wanaohitaji kuyatumia.

Katika utafiti wa Mtanana, wafugaji wameshirikishwa katika mchakato wa kujifunza na kutathmini aina za malisho zinazofanyiwa majaribio.

Katika ziara ya kutathmini maendeleo ya utafiti huo, Dkt. Lutatenekwa alimweleza Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu, matokeo ya awali ya utafiti na namna wafugaji wanavyoshiriki katika mchakato huo.

Ziara hiyo ilitoa picha ya tofauti kati ya utafiti unaobaki kwenye ripoti na utafiti unaoanza kubadili namna watu wanavyozalisha.

Katika eneo la utafiti kulionekana malisho yanayofanyiwa tathmini, mashamba ya wakulima na wafugaji wanaojaribu kutumia maarifa hayo katika mifumo yao ya uzalishaji.

Kwa COSTECH, uzoefu huo unaendana na umuhimu wa kuwekeza katika utafiti unaozalisha maarifa yenye matumizi kwa jamii na uchumi.

Katika mahojiano yake waandishi wa habari wakati wa ziara hiyo, Dkt. Nungu alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha kuwa matokeo ya utafiti na teknolojia yanawafikia watumiaji wa mwisho na kusaidia kutatua changamoto halisi zinazowakabili wananchi.

“Tunataka utafiti uzalishe maarifa au utoe teknolojia ambazo zitakuwa suluhui kwa changamoto za watanzania. Mradi huo tumeona unavyobadili maisha ya Mfugaji Bw.Clement Alfonce, tunataka uwe na matokeo makubwa na chanya kwa wafugaji wote zaidi ya 1300 waliopo kwenye kata hii ya Mtanana” Dkt. Amos Nungu, Mkurugenzi Mkuu, COSTECH

Mabadiliko ya tabianchi yanabadilisha namna ya kufuga

Kongwa ni miongoni mwa maeneo ambayo wafugaji wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa malisho, hasa katika vipindi vya ukame.

Kwa mifugo inayotegemea malisho ya asili, ukame unaweza kumaanisha kupungua kwa chakula, kudhoofika kwa mifugo na hata vifo.

Katika mazingira hayo, uwezo wa mfugaji kuzalisha malisho yanayostahimili ukame unaweza kuwa sehemu ya mkakati mpana wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Ndiyo maana utafiti wa aina hii una umuhimu zaidi ya kutafuta aina nzuri ya nyasi. Unahusu usalama wa chakula cha mifugo, ustahimilivu wa mifumo ya uzalishaji na uwezo wa kaya za wafugaji kukabiliana na mabadiliko ya mazingira.

Kwa Clement, mwanga umeanza kuonekana.

Shamba lake la malisho linampa nafasi ya kupanga zaidi kuhusu chakula cha mifugo yake. Mfumo wa malisho bandani unapunguza hitaji la ng’ombe kuzunguka kutafuta malisho na hivyo kupunguza uwezekano wa migogoro inayotokana na mifugo kuingia kwenye mashamba ya wakulima.

Na muhimu zaidi, Clement sasa anaona ufugaji kama mfumo wa uzalishaji unaoweza kupangwa na kusimamiwa, badala ya kutegemea upatikanaji wa malisho ya asili.

Miaka 40 ya COSTECH: kipimo ni maisha yanayobadilika

Tanzania inapoadhimisha miaka 40 ya COSTECH, hadithi ya Clement inaibua swali muhimu kuhusu maana ya uwekezaji katika sayansi, teknolojia na ubunifu.

Matokeo ya utafiti hayaishii katika maabara, ripoti au machapisho ya kitaalamu.Thamani yake inaonekana zaidi pale ambapo maarifa yanatumiwa kufanya uamuzi mpya.

Kwa Clement, uamuzi huo ulikuwa kubadilisha mfumo wa ufugaji. Kutoka kuwa na ng’ombe 56 wanaozunguka kutafuta malisho, sasa ana ng’ombe 16 wa maziwa wanaofugwa ndani.Kutoka kutegemea zaidi malisho yanayopatikana kwenye nyanda za malisho, sasa analima malisho kwa ajili ya mifugo yake. Kutoka kukabiliana mara kwa mara na migogoro ya mifugo na wakulima, sasa ana mfumo wa ufugaji unaomruhusu kudhibiti zaidi mahitaji ya mifugo yake.

Na kutoka kukabili ukame bila uhakika wa chakula cha mifugo, sasa anajenga msingi wa uzalishaji wa malisho unaoweza kumsaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Hii ndiyo picha pana ya miaka 40 ya COSTECH: sayansi inapokuwa na maana pale inapobadilisha uwezo wa Mtanzania kutatua changamoto yake mwenyewe.

Katika Mtanana, mabadiliko hayo hayajaandikwa tu kwenye ripoti. Yanaonekana kwenye shamba.Yanaonekana kwenye malisho. Yanaonekana kwenye banda la ng’ombe. Na yanaonekana katika uamuzi wa mfugaji mmoja kubadilisha kabisa namna anavyofuga.

Clement hakubadilisha tu idadi ya ng’ombe alionao. Alibadilisha mfumo wa maisha unaowaendesha. Kutoka ng’ombe wa kuzunguka kutafuta malisho hadi ng’ombe wa kufugia ndani.Kutoka kutegemea malisho asili hadi kuanza kuzalisha chakula cha mifugo yake.

Na nyuma ya mabadiliko hayo kuna jambo moja: maarifa yaliyotokana na utafiti.

 

Mimi naitwa Elizabeth, natokea mkoani Dodoma, maeneo ya Area D. Maisha yangu ya ndoa yalikuwa kwenye kilele cha mafanikio kwa nje kwa sababu mume wangu ni mwanasiasa anayejulikana nchi nzima. Lakini siri iliyokuwa ndani ya nyumba yetu ilikuwa ni ya kusikitisha.

Kwa muda mrefu, nilikuwa napitia changamoto ya kukosa hamu ya tendo la ndoa na kuwa mkavu kiasi kwamba nikawa naogopa kumuona mume wangu akirudi nyumbani.

Ili kukwepa unyumba, nilianza tabia ya kujifanya nimevamiwa na “pepo la usingizi”, nikifika tu chumbani, najilaza sakafuni au kitandani na kuanza kukoroma kwa nguvu hata kama sijalala, ili tu mume wangu asiniguse.

Mume wangu alianza kuchoka na tabia yangu. Alisema, “Elizabeth, mbona kila nikirudi unakuwa umechoka kiasi hiki? Unafanya kazi gani Dodoma nzima mpaka ukorome kama trekta?”. Nilianza kukosa amani maana nilijua mume wangu anaweza kuanza kutafuta mwanamke mwingine nje, na hali hiyo ingeharibu sifa yetu kama familia ya kiongozi.

Nilienda kwa madaktari bingwa hapa Dodoma wakaniambia nina upungufu wa damu, lakini dawa walizonipa hazikurudisha hamu wala kuondoa ukavu uliokuwa unanichoma kama moto wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.

 

Naitwa Zaituni, mkazi wa jijini Arusha, maeneo ya mtaa wa Njiro. Maisha yangu ya ndoa yalifika mahali yakawa ni ya aibu na siri nzito ambayo ilikaribia kunivunjia heshima yangu mbele ya mume wangu na jamii inayotuzunguka.

Mume wangu ni mfanyabiashara mkubwa wa vito vya thamani kama Tanzanite, hivyo maisha yetu yalikuwa ni ya anasa, lakini ndani ya chumba chetu cha kulala, kulikuwa na “jangwa” la kutisha.

Kwa takriban miaka minne, nilipoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa na mwili wangu ukawa mkavu kiasi cha kutisha. Kila mume wangu alipojaribu kunigusa, nilihisi maumivu makali kama ninasuguliwa na msasa butu.

Katika hali ya kukata tamaa na kuogopa mume wangu asije kunitupa nje, nilianza kufanya kitendo cha hatari. Nilikuwa naiba mafuta ya kulainisha mashine (lubricants) kutoka kwenye gereji ya mume wangu na kuyaweka kwenye kopo la ‘lotion’ ili tu kumlainisha mume wangu wakati wa tendo.


Mimi naitwa Rehema, mkazi wa jijini Dar es Salaam, eneo la Sinza. Kwa miaka mingi, maisha yangu yalikuwa ni mzunguko wa maumivu na masikitiko. Licha ya kuwa na kazi nzuri na mwonekano unaovutia, suala la ndoa lilikuwa kama ndoto ya mchana.

Kila mwanaume aliyekuja kwangu alikuwa akitafuta starehe tu na kisha kutokomea. Nilifikisha umri wa miaka 38 nikiwa bado nipo nyumbani kwa wazazi, huku mdogo wangu wa mwisho akishabeba mtoto wake wa pili.

Kila sherehe ya kifamilia ilikuwa ni kero kwangu; ndugu walikuwa wakinitazama kwa jicho la huruma lililochanganyika na dhihaka. “Rehema, mbona hutuletei wifi?” au “Umri unaenda, utazaa lini?” yalikuwa maswali ya kila siku.

Nilijaribu kila mbinu, kuanzia mitandao ya kijamii hadi kuomba marafiki waniunganishe na watu, lakini wapi! Nilianza kuamini kuwa labda nimezaliwa kuwa mpweke maisha yangu yote. Hofu ya kukosa watoto ilinitesa sana usiku, nilikuwa nalia hadi mto unaloa maji. SOMA ZAIDI.

 


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) leo, Agosti 11, 2026, imeendelea na vikao vyake kwa kupitia na kuchambua taarifa za hesabu zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za Manispaa ya Shinyanga, Halmashauri za Wilaya za Kishapu na Msalala.

Uchambuzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa ratiba ya Kamati katika kufuatilia usimamizi wa rasilimali za umma katika Serikali za Mitaa na kuimarisha mifumo ya uwajibikaji, kuhakikisha wananchi wanapata huduma zinazoendana na thamani ya rasilimali zinazotengwa kwa ajili ya maendeleo yao.









 


Na: OWM - TAMISEMI


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeanza rasmi vikao vyake jijini Dodoma kwa kukutana na watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, kujadili utekelezaji wa shughuli za Serikali, hususan miradi ya miundombinu na utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa Nne wa Bunge unaotarajiwa kuanza Agosti 25, 2026.

Katika kikao hicho, Kamati imepokea na kujadili taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhusu ukarabati wa barabara zilizoharibiwa na mvua za masika nchini, pamoja na maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya BRT na mpango wa kuboresha huduma za usafirishaji zinazotolewa na UDART.

Katika vikao hivyo, Kamati pia inatarajia kupitia masuala mbalimbali yanayohusu utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwemo uimarishaji wa huduma za maji na lishe shuleni, utunzaji wa mazingira, ujenzi wa viwanja vya michezo pamoja na ajira za walimu wa michezo katika shule za msingi na sekondari.

Aidha, ratiba ya Kamati inaonesha kuwa itajadili masuala ya elimu, afya na mazingira, ikiwemo ujenzi wa shule na miundombinu yake, mikakati ya kukabiliana na viuadudu katika halmashauri, pamoja na mahitaji ya walimu na maandalizi ya utekelezaji wa mabadiliko ya mtaala wa elimu.













 



▪️ Lengo ni kurahisisha huduma kwa wateja

▪️ Kamati ya Bunge yaishauri Serikali kupunguza tozo zinazowaumiza wachimbaji wadogo

▪️ Dhahabu tani 67.8 zenye thamani ya Sh trilioni 18.4 zazalishwa kwenye viwanda vya usafishaji

▪️Waziri Mavunde aeleza mkakati wa kukuza biashara ya Tanzanite


Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameiagiza Tume ya Madini kuongeza muda wa uendeshaji wa masoko ya madini mpaka saa 3:00 usiku, hatua inayolenga kuongeza fursa za biashara na kuwahudumia wafanyabiashara na wauzaji wa madini kwa muda mrefu zaidi ili kuendana na mahitaji ya wadau na kuongeza ufanisi katika biashara ya madini.

Mavunde ametoa agizo hilo Agosti 11, 2026, wakati akijibu maswali ya Wabunge katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini jijini Dodoma, ambapo Wizara imewasilisha taarifa kuhusu hali halisi na maendeleo ya sekta ya madini nchini.

Mavunde amesema Serikali pia inaendelea kuimarisha udhibiti wa biashara ya madini na utoroshaji, huku ikisisitiza uongezaji thamani ndani ya nchi. Ameeleza kuwa katika eneo la Mirerani, serikali itatekeleza mkakati ambao imejiwekea wa kukuza biashara hiyo ya madini ya Tanzanite kwa kuhakikisha mfumo wa biashara ya madini hayo unapitiwa ili kusaidia kuchochea ukuaji wa biashara ya madini ya Tanzanite.

Kuhusu uwekezaji, amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua dhidi ya wenye leseni wanaoshikilia maeneo makubwa bila kuyaendeleza, akisisitiza kuwa maeneo yasiyoendelezwa kwa mujibu wa sheria yanaweza kuchukuliwa hatua, ikiwemo kufutwa kwa leseni. Aidha, Serikali inaendelea kushirikiana na Wizara ya Nishati kuhakikisha maeneo ya migodi yanapata umeme wa uhakika pamoja na kuzingatia miundombinu ya kimkakati katika mipango ya maendeleo.

Amesema Serikali pia inaendelea kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika uchumi wa madini kupitia mpango wa MBT unaolenga vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalum. Kwa upande mwingine, Serikali imesaini hati za makubaliano 14 na wawekezaji ambao miradi yao bado haijaanza uzalishaji, huku ikiendelea kuweka mazingira wezeshi kwa taasisi za fedha kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo wenye sifa.

Akitoa taarifa ya hali ya sekta hiyo, Kamishna wa Madini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, amesema madini yanaendelea kuwa sekta muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika mwaka wa fedha 2025/26, dhahabu iliongoza kwa uzalishaji baada ya kufikia tani 67.8 zenye thamani ya Sh trilioni 18.4. Aidha, kilogramu 28,701 za dhahabu ziliuzwa katika viwanda vitano vya kusafisha dhahabu nchini, ambapo kilogramu 21,710, sawa na asilimia 75.64, zilinunuliwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara kwa hatua zinazochukuliwa kuimarisha sekta hiyo, huku akisisitiza umuhimu wa kudhibiti utoroshaji wa madini na kupunguza tozo katika mnyororo wa biashara ya madini na kuitaka Serikali iangalie upya tozo kwa wachimbaji wadogo ambazo zimekuwa ni mzigo mkubwa.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amesema Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) na kuhakikisha shughuli za madini zinawanufaisha wananchi wanaozunguka maeneo ya migodi.

 


Na. Josephine Majura na Asia Singano, WF- Dodoma

Serikali imesema uchumi wa Tanzania unaendelea kuimarika na kwamba uwekezaji katika sekta mbalimbali, hususani madini, gesi, nishati, kilimo na miundombinu, unatarajiwa kutoa msukumo mkubwa kwa ukuaji wa uchumi.

Hayo yalielezwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akifungua mkutano na wataalamu wa Kampuni ya Kimataifa ya Tathmini ya Madeni ya (Fitch Ratings), uliofanyika kwa njia ya mtandao, ikiwa ni sehemu ya mchakato wa kufanya mapitio ya hali ya uchumi wa Tanzania.

Alisema Serikali imeendelea kuchukua hatua za kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, ikiwa ni pamoja na kufanyia kazi mapendekezo ya Tume ya Mageuzi ya Kodi iliyoundwa na Serikali, jambo ambalo limeendelea kukuza uchumi wa nchi.

‘’Upande wa ukuaji wa uchumi tumetoka asilimia 5, mwaka mwaka 2024, tumekwenda asilimia 5.9 mwaka jana, mwaka huu tunategemea uchumi utakuwa kwa asilimia 6.3 hatujafikia viwango ambavyo vilikuwa kabla ya COVID 19 lakini tunaendelea vizuri’’ alisema Mhe. Balozi Omar.

Alisema kuwa, moja ya maeneo muhimu yaliyojadiliwa na Fitch ni maendeleo makubwa yanayoendelea katika sekta ya madini na uchakataji wa madini, huku akieleza kuwa Tanzania ina miradi mikubwa ambayo ipo katika hatua mbalimbali za maandalizi na ikitekelezwa itakuwa na mchango mkubwa katika uchumi.

‘’Kuna miradi mingine mikubwa ukiwemo wa Nyanzaga wa uchimbaji wa dhahabu Mwanza ambao unatarajiwa kuwekeza zaidi ya dola milioni 500, kuna miradi mingine ambayo inaendelea upande wa aluminiam – Songea, Chuma- Liganga, Chuma -Dodoma, na miradi mingine kwa hiyo kwa ujumla kwenye sekta hii kuna uwekezaji mkubwa ambao unatarajiwa kuleta msukumo mkubwa katika uchumi wetu’’ Alisema Mhe. Balozi Omar (Mb).

Aliongeza kuwa kwa ujumla sekta ya madini inaendelea kuwa na nafasi kubwa katika kuchochea ukuaji wa uchumi, hasa kutokana na ongezeko la uwekezaji unaotarajiwa katika uchimbaji na uchakataji wa madini hapa nchini.

Alisema Mradi mkubwa wa gesi asilia iliyosindikwa (LNG), ni miongoni mwa miradi inayotarajiwa kuleta msukumo mkubwa katika uchumi, pamoja na mradi wa madini ya niobium ambao tayari umesainiwa na unatarajiwa kuvutia uwekezaji wa takribani dola milioni 442.

Aidha, alibainisha kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kupunguza athari za mabadiliko ya bei za mafuta na bidhaa nyingine muhimu kwa kutumia sera na mifumo mbalimbali ya kiuchumi.

Kwa upande wa Fitch, majadiliano yaliongozwa na mchambuzi Mkuu anayeshughulikia Tanzania, Bw. José Mantero, ambapo majadiliano hayo yalilenga kuwapa wachambuzi hao fursa ya kupata taarifa za kina kuhusu mwenendo wa uchumi wa Tanzania, utekelezaji wa sera za kibajeti na fedha, pamoja na mikakati ya Serikali katika usimamizi wa deni la Taifa.

Aidha, wachambuzi hao walijikita katika kutathmini athari za vita kati ya Iran katika uchumi wa Tanzania, hususan mwenendo wa bei za mafuta na mbolea, pamoja na hatua na mikakati inayochukuliwa na Serikali kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, Kamishna Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Deni la Taifa, Nuru Ndile, kwa njia ya mtandao.



 Na. Josephine Majura na Asia Singano, WF – Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, ameongoza Ujumbe wa Serikali ya Tanzania kwa niaba ya Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, katika kikao na Ujumbe wa Benki ya Dunia kilicholenga kuhitimisha maandalizi ya kitaalamu ya Programu ya Uendelezaji wa Ushoroba wa Kati wa Maendeleo ya Kiuchumi Utakaoongeza Ajira kwa Vijana (CATALYZING JOBS AND RESILIENT GROWTH IN THE CENTRAL CORRIDOR MULTIPHASE PROGRAMMATIC APPROACH 
(KAZI MPA).

Kikao hicho kilifanyika kwa lengo la kuwasilisha na kujadili matokeo ya maandalizi yaliyofanywa kwa pamoja kati ya Serikali na Benki ya Dunia, pamoja na kukubaliana hatua zinazofuata kuelekea kukamilisha maandalizi ya Programu hiyo, kilichofanyika, Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, pande hizo zilijadili kwa kina maeneo muhimu ya utekelezaji wa KAZI MPA, huku zikisisitiza umuhimu wa programu hiyo katika kuchochea mageuzi ya kiuchumi, kuongeza uwekezaji na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika kuchangia maendeleo ya uchumi wa Tanzania.

Aidha, KAZI MPA inalenga kuongeza fursa za ajira, hususan kwa vijana, pamoja na kuimarisha ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa kupitia kuendeleza miundombinu na mazingira wezeshi ya shughuli za kiuchumi katika Ushoroba wa Kati.

Utekelezaji wa programu hiyo unatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya jitihada za Serikali katika kutafsiri kwa vitendo malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, hususan katika kujenga uchumi wenye tija, jumuishi na stahimilivu, unaotoa fursa kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na biashara.

Ujumbe wa Serikali katika kikao hicho uliwahusisha pia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Bw. Adolf Ndunguru, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvivu Bi. Agness Meena, Kaimu Katibu Mkuu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubil Joshua, Naibu Makatibu Wakuu Wizara ya Kilimo, Prof. Peter Msoffe na Mhandisi Athumani Kilundumya pamoja na Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Taifa ya Mipango Bw. Sosthenes Kewe.

Kwa upande wa Ujumbe wa Benki ya Dunia ukiongozwa na Meneja wa Benki ya Dunia, Kitengo cha Utekelezaji wa Sekta ya Usafiri, Afrika Mashariki na Kusini, (Practice Manager for Transport in Eastern and Southern Africa), Bw. Binyam Reja.

Kikao hicho ni hatua muhimu kuelekea kukamilisha maandalizi ya KAZI MPA na kuweka msingi wa utekelezaji wa programu inayolenga kuchochea shughuli za kiuchumi, kuongeza fursa za ajira kwa vijana na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika uchumi wa kikanda na kimataifa.

 


Na. Benny Mwaipaja


Tanzania na Marekani zimeendelea kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika sekta mbalimbali zikiwemo madini adimu, nishati, afya, uwekezaji na maendeleo ya kiuchumi, pamoja na dhamira ya kuendeleza mazungumzo na ushirikiano wa kitaalamu kwa manufaa ya nchi hizo mbili.

Hayo yameafikiwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, walipokutana na kufanya mazungumzo ya katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo pia walieleza umuhimu wa kuendelea kutumia majadiliano ya kitaalamu na ushirikiano wa Serikali kwa Serikali katika kushughulikia maeneo yenye umuhimu wa kimkakati, ikiwemo maendeleo ya sekta ya Nishati ya Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas (LNG).

Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, alisisitiza kuwa mawasiliano ya karibu na ushirikiano kati ya wataalamu wa pande zote ni muhimu katika kuwezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

Aidha, walijadili fursa za kuendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini, ikiwemo miradi mikubwa ya madini na kuongeza thamani ya rasilimali nchini, ambapo walikubaliana kuhusu umuhimu wa kuwa na uratibu mzuri wa Serikali na wawekezaji ili kuhakikisha miradi ya kimkakati inatekelezwa kwa ufanisi na kutoa manufaa kwa uchumi na wananchi.

Kwa upande wa afya, alisema kuwa hivi karibuni, Marekani na Tanzaniaa zimesaini makubaliano ya kuendeleza sekta ya afya yatakayogharimu dola za Marekani bilioni 3.1 katika kipindi cha miaka mitano ijayo kwa ajili ya  kuimarisha mifumo ya afya, kukabiliana na magonjwa mbalimbali na kujenga uwezo wa ndani, kuelekea kwenye mifumo endelevu ya afya inayoongeza uwezo wa Tanzania kugharamia na kusimamia huduma za afya kwa muda mrefu, sambamba na kuimarisha uwezo wa kitaifa katika kinga, ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa.

“Tunatambua umuhimu wa uwekezaji katika miundombinu ya afya, uzalishaji wa bidhaa za afya nchini na kuimarisha taasisi zinazohusika na afya ya umma na Ushirikiano huu unalenga kuongeza uwezo wa Tanzania kukabiliana na changamoto za kiafya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu” alisema Mhe. Balozi Lentz

Kwa upande wake Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema kuwa kuna nafasi kubwa ya kubadilishana uzoefu kuhusu namna Serikali hizo zinavyoweza kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, kifedha na kitaalamu, na Serikali inatambua juhudi zinazoendelea za wataalamu wa pande zote mbili katika kuimarisha mifumo ya kifedha, ikiwemo maendeleo ya soko la dhamana za Serikali, ambazo zinatajwa kama mfano wa ushirikiano wa kitaalamu unaoweza kutoa manufaa ya muda mrefu kwa uchumi wa Tanzania.

“Kwa ujumla, mkutano huu umeonesha dhamira ya Tanzania na Marekani ya kuendeleza ushirikiano wa karibu katika maeneo ya kimkakati, na msisitizo mkubwa ukiwa katika kuimarisha uwekezaji, kujenga uwezo wa ndani, kuongeza thamani ya rasilimali na kuhakikisha ushirikiano huo unaleta matokeo chanya na endelevu kwa wananchi” alisema Mhe. Balozi Omar.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria Wizara ya Fedha, Bi. Mwantumu Sultan, Mshauri wa Siasa na Uchumi Ubalozi wa Marekani Nchini,  Bi. Rebecca Hunter, na wataalamu wengine wa Wizara ya Fedha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda, akifungua mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa wakaguzi wa Tume hiyo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama naAfya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwajengea uelewa wakaguzi hao wenye jukumu la kukagua uzingatiaji wa sheria na miongozo mbalimbali katika sekta ya umma.
Serikali imekusudia kukomesha uuzaji wa mazao ghafi kwani mfumo huo unamnyima mkulima zaidi ya nusu ya faida halisi na kubainisha kuwa mkakati uliopo ni kuongeza thamani ya mazao kama korosho kabla ya kuyaweka sokoni, hatua itakayoinua kipato cha wajasiriamali na wakulima wadogo mkoani humo.
Serikali imetoa agizo kwa wakandarasi na wasimamizi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji wa Masasi kuhakikisha miradi yote inakamilika ndani ya muda uliopangwa, na kusisitiza kuwa utamaduni wa kuongeza muda wa utekelezaji (extension) hauleti tija wala maendeleo kwa Taifa.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka watendaji wa Serikali na taasisi za udhibiti kuwa wawezeshaji wa biashara badala ya kufungia biashara, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kulinda mitaji na maslahi ya wananchi.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

WATANZANIA wameanza kunufaika na huduma za matibabu ya kibingwa zinazopatikana nchini, hali inayopunguza gharama na ulazima wa kusafiri nje ya nchi kutafuta matibabu.

 

Mimi naitwa Elizabeth, natokea mkoani Dodoma, maeneo ya Area D. Maisha yangu ya ndoa yalikuwa kwenye kilele cha mafanikio kwa nje kwa sababu mume wangu ni mwanasiasa anayejulikana nchi nzima. Lakini siri iliyokuwa ndani ya nyumba yetu ilikuwa ni ya kusikitisha.

Kwa muda mrefu, nilikuwa napitia changamoto ya kukosa hamu ya tendo la ndoa na kuwa mkavu kiasi kwamba nikawa naogopa kumuona mume wangu akirudi nyumbani.

Ili kukwepa unyumba, nilianza tabia ya kujifanya nimevamiwa na “pepo la usingizi”, nikifika tu chumbani, najilaza sakafuni au kitandani na kuanza kukoroma kwa nguvu hata kama sijalala, ili tu mume wangu asiniguse.

Mume wangu alianza kuchoka na tabia yangu. Alisema, “Elizabeth, mbona kila nikirudi unakuwa umechoka kiasi hiki? Unafanya kazi gani Dodoma nzima mpaka ukorome kama trekta?”. 

Nilianza kukosa amani maana nilijua mume wangu anaweza kuanza kutafuta mwanamke mwingine nje, na hali hiyo ingeharibu sifa yetu kama familia ya kiongozi.

Nilienda kwa madaktari bingwa hapa Dodoma wakaniambia nina upungufu wa damu, lakini dawa walizonipa hazikurudisha hamu wala kuondoa ukavu uliokuwa unanichoma kama moto wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.

 

Naitwa Zaituni, mkazi wa jijini Arusha, maeneo ya mtaa wa Njiro. Maisha yangu ya ndoa yalifika mahali yakawa ni ya aibu na siri nzito ambayo ilikaribia kunivunjia heshima yangu mbele ya mume wangu na jamii inayotuzunguka.

Mume wangu ni mfanyabiashara mkubwa wa vito vya thamani kama Tanzanite, hivyo maisha yetu yalikuwa ni ya anasa, lakini ndani ya chumba chetu cha kulala, kulikuwa na “jangwa” la kutisha.

Kwa takriban miaka minne, nilipoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa na mwili wangu ukawa mkavu kiasi cha kutisha. Kila mume wangu alipojaribu kunigusa, nilihisi maumivu makali kama ninasuguliwa na msasa butu.

Katika hali ya kukata tamaa na kuogopa mume wangu asije kunitupa nje, nilianza kufanya kitendo cha hatari. Nilikuwa naiba mafuta ya kulainisha mashine (lubricants) kutoka kwenye gereji ya mume wangu na kuyaweka kwenye kopo la ‘lotion’ ili tu kumlainisha mume wangu wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.

 

Mimi naitwa Rehema, mkazi wa jijini Dar es Salaam, eneo la Sinza. Kwa miaka mingi, maisha yangu yalikuwa ni mzunguko wa maumivu na masikitiko.

Licha ya kuwa na kazi nzuri na mwonekano unaovutia, suala la ndoa lilikuwa kama ndoto ya mchana.

Kila mwanaume aliyekuja kwangu alikuwa akitafuta starehe tu na kisha kutokomea. Nilifikisha umri wa miaka 38 nikiwa bado nipo nyumbani kwa wazazi, huku mdogo wangu wa mwisho akishabeba mtoto wake wa pili.

Kila sherehe ya kifamilia ilikuwa ni kero kwangu; ndugu walikuwa wakinitazama kwa jicho la huruma lililochanganyika na dhihaka. “Rehema, mbona hutuletei wifi?” au “Umri unaenda, utazaa lini?” yalikuwa maswali ya kila siku.

Nilijaribu kila mbinu, kuanzia mitandao ya kijamii hadi kuomba marafiki waniunganishe na watu, lakini wapi! Nilianza kuamini kuwa labda nimezaliwa kuwa mpweke maisha yangu yote. Hofu ya kukosa watoto ilinitesa sana usiku, nilikuwa nalia hadi mto unaloa maji. SOMA ZAIDI.