Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi na washiriki wa Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu inayofanyika jijini Tanga kuhusu bunifu mbalimbali zinazozalishwa na watafiti na wabunifu wanaoshirikiana na taasisi hiyo.

Katika maadhimisho hayo, NM-AIST imewasilisha jumla ya bunifu 20, ambazo nyingi zimetokana na tafiti na kazi za watafiti wa ndani ya taasisi, huku nyingine zikiwa zimezalishwa na wabunifu wa nje wanaopatiwa malezi, mafunzo na mwongozo kupitia taasisi hiyo. Bunifu hizo zinaonesha jitihada za NM-AIST katika kuunganisha utafiti, ubunifu na mahitaji halisi ya jamii.

Aidha, taasisi hiyo imewashirikisha wawakilishi wa vikundi vya wanawake wanaopatiwa msaada na mwongozo katika kuboresha bidhaa zao na kuongeza thamani. Hatua hiyo inalenga kuwawezesha kutumia maarifa na teknolojia kuongeza ubora, tija na ushindani wa bidhaa zao sokoni.

Katika hatua nyingine, NM-AIST imewasilisha kampuni tatu zilizoanzishwa kutokana na bunifu na tafiti zilizofanyika ndani ya taasisi. Kampuni hizo ni Nano Filter, inayojihusisha na teknolojia ya uchujaji wa maji; AfriTech, inayotumia teknolojia inayotokana na mabaki ya korosho katika uchakataji wa ngozi; na Uji Chap Chap, inayolenga kuchangia afya bora kupitia bidhaa za lishe.

Ushiriki wa NM-AIST katika maonyesho hayo unaendelea kutoa fursa kwa wananchi kujifunza namna ambavyo matokeo ya utafiti na ubunifu yanaweza kubadilishwa kuwa bidhaa na huduma zenye manufaa kwa jamii. Aidha, ushiriki huo unaonesha mchango wa taasisi katika kukuza matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu kama nyenzo muhimu za maendeleo ya Tanzania.

NM-AIST inaendelea kuthibitisha dhamira yake ya kuifikia jamii, kuwatamia wajasiriamali na kukuza ubunifu kwa maendeleo endelevu.

 

Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Mhe. Omari Issa atunuku shahada za umahiri na uzamivu kwa wahitimi 138 katika Mahafali ya 12 ya Taasisi ya Nelson Mandela yaliyofanyika Leo tarehe 20 Agosti 2026, NM-AIST Tengeru Arusha.

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), Balozi Maimuna Tarishi, amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha tafiti, teknolojia na ubunifu unaozalishwa na Taasisi unatafsiriwa kuwa bidhaa, huduma na suluhisho halisi kwa changamoto za jamii, sambamba na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Akizungumza katika Mahafali ya 12 ya Taasisi (NM-AIST), Balozi Tarishi amesema ubunifu haupaswi kuishia kwenye makaratasi au usajili wa hati miliki, bali unapaswa kutumika kutatua changamoto katika sekta za kilimo, ufugaji, biashara, mazingira na uchumi.

“Ubunifu usiishie kwenye makaratasi wala usajili BRELA; twende tukautafsiri kwa vitendo ili kujibu changamoto mbalimbali za jamii,” amesema Balozi Tarish.

Aidha, amewataka wahitimu kutumia maarifa na ujuzi walioupata NM-AIST kujitolea kuitumikia jamii ya Tanzania na Afrika, badala ya kutumia elimu kwa manufaa binafsi pekee.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula, amesema jumla ya wahitimu 138 wamehitimu katika mahafali hayo, wakiwa wamezalisha machapisho 219 ya kisayansi na hati miliki saba.

Amesema NM-AIST itaendelea kuhamasisha wanafunzi na watafiti kuzalisha bidhaa, kufanya ugunduzi na kuchapisha tafiti katika majarida ya kimataifa. 

Pia, Profesa Maulilio Kipanyula amesema watafiti 19 wa NM-AIST wametambuliwa katika tuzo za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zinazohusisha machapisho katika majarida ya kisayansi yenye hadhi ya juu duniani.

NM-AIST inaendelea kubadili maarifa kuwa ubunifu, ubunifu kuwa bidhaa na huduma, na tafiti kuwa suluhisho la changamoto za jamii sambamba na utekelezaji wa Dira 2050.

23 Agosti 2026. | 📍Bagamoyo, Tanzania.

Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) umeendelea kutoa mafunzo maalum ya siku mbili kuhusu Uongozi na Usimamizi wa Utekelezaji wa Mtaala Ulioboreshwa, yakilenga kuimarisha uwezo wa Wakuu wa Shule za Sekondari katika kusimamia kwa ufanisi mabadiliko ya mtaala.

Na Cletus Sanga, WAF – Kibiti

Huduma za dharura nchini zimeendelea kuimarika kupitia hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuimarisha mfumo wa huduma za dharura, ikiwemo kuongeza na kuboresha magari ya wagonjwa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi wanaohitaji msaada wa haraka.
Mimi nilikuwa naishi peke yangu kwenye nyumba yangu kwa muda bila matatizo yoyote. Kila kitu kilikuwa cha kawaida, na nilikuwa nimezoea mazingira yangu vizuri. 

Lakini siku moja usiku, nilianza kusikia sauti za ajabu ndani ya nyumba. Nilidhani labda ni upepo au kitu cha kawaida.

Lakini kadri siku zilivyoenda, mambo yakaanza kuwa ya kutisha zaidi. Nilianza kuona kivuli kikisogea ukutani usiku. 

Kila nilipojaribu kuangalia vizuri, hakukuwa na kitu cha kueleweka. Hali hiyo ilinifanya nianze kuishi kwa hofu.

Usingizi wangu ulipotea.

Nilikuwa nikiamka mara kwa mara usiku, moyo ukipiga kwa kasi. Ilifika wakati nikashindwa kuvumilia tena.
Usiku mmoja hali ilizidi. Niliona kivuli hicho kwa uwazi zaidi na nikahisi hofu kali sana. Bila kufikiria sana, nilikimbia nje ya nyumba yangu na kwenda kwa jirani usiku huo huo.

Kesho yake nilimweleza rafiki yangu kilichotokea. SOMA ZAIDI......
Mimi nilikuwa kwenye uhusiano uliokuwa na maumivu mengi. Nilimpenda sana, lakini mara nyingi alinichukulia kawaida na kuniumiza kihisia. 

Nilijikuta nikivumilia mambo mengi kwa sababu ya mapenzi. Baada ya muda, nilichoka. Niliona siwezi kuendelea kuumia kila siku.

Uamuzi wa kuachana haukuwa rahisi, lakini nilijua ulikuwa wa lazima. Baada ya kuachana, nilibaki na huzuni kubwa. Nilihisi peke yangu, na wakati mwingine nilijilaumu kwa kila kitu kilichotokea. Ilikuwa ngumu sana kuanza upya.

Nilianza hata kupoteza imani ya kupata upendo wa kweli. Niliona kama kila kitu kimeharibika na sitapata mtu wa kunielewa tena. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI....
Mimi nilikuwa nimefanya kazi kwenye kampuni moja kwa muda mrefu lakini sikuwahi kupata nafasi kubwa. 

Nilikuwa nafanya kazi kwa bidii, lakini mara nyingi nilihisi kama juhudi zangu hazionekani. Kila mara nafasi za kupandishwa cheo zilipotoka, nilikuwa napuuzwa.

Hilo lilianza kunifanya nipoteze motisha na kujiamini. Nilianza kufikiria labda siwezi kufanikiwa zaidi kazini. 

Nilikuwa na hofu ya kuendelea kubaki sehemu moja bila mabadiliko yoyote. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa kazi kuhusu hali yangu. SOMA ZAIDI......
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu katika uzinduzi wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), unaofanywa leo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa jukumu la lake la kusimamia na kudhibiti masuala ya mazingira katika miradi ya maendeleo nchini.
Kulea mtoto kwa maadili mema na kumpa kila hitaji la msingi ni ndoto na furaha ya kila mzazi, lakini pale mwanao anapogeuka kuwa janga la familia, ukaidi unapotawala, na anapojiunga na magenge ya uhalifu na matumizi ya dawa za kulevya, maisha ya wazazi hugeuka kuwa msiba wa kila siku.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, mwanangu wa kiume aliyekuwa mwenye nidhamu na aliyefanya vizuri shuleni alibadilika ghafla. Alianza kutoroka shule, kuvuta bangi, na hatimaye kujiunga na kundi la vijana wa mtaani waliokuwa wakifanya wizi na kuwapiga watu nondo usiku.

​Kila nilipojaribu kuongea naye kwa wema, alinijibu kwa matusi, vitisho, na hata kutaka kunipiga. Nilitumia fedha nyingi kumpeleka kwenye vituo vya kuacha dawa za kulevya (rehab) na kumlipia dhamana mara kadhaa polisi pale alipokamatwa na uhalifu, lakini kila alipotoka alirudia tabia zile zile kwa kasi kubwa zaidi.

Nyumbani kwangu kuligeuka kuwa kero; alianza kuiba vyombo vya ndani, nguo, na vifaa vya elektroniki ili kwenda kuuza kwa bei ya kutupwa apate fedha za kununulia dawa za kulevya.

Nilibaki nikilia usiku na mchana, nikitarajia muda wowote kuletewa taarifa za kifo chake kutoka kwa wananchi wenye hasira kali au polisi, huku masimango ya majirani yakizidi kuwa makali. SOMA ZAIDI.

Kujenga ndoa na kuweka matumaini yako yote kwa mume ni hatua inayohitaji upendo na uaminifu mkubwa, lakini pale mwanaume uliyehangayika naye kuanzia chini anapokugeuka, kukutelekeza, na kumfuata mchepuko, maisha hugeuka kuwa jehanum.

Kwa zaidi ya miaka sita ya ndoa yetu, tuliaishi kwa amani na mafanikio na mume wangu. Hata hivyo, mambo yalibadilika ghafla pale alipopata uwezo wa kifedha na kuanza kuhusiana na mwanmke mwingine wa nje.

Mume wangu alibadilika tabia kabisa; akawa mkali, asiyelala nyumbani, na kuanza kuninyima matumizi ya familia.

​Siku mambo yalipofika kikomo, alikusanya nguo zake zote na kuondoka nyumbani akiniacha mimi na watoto wawili wadogo bila chakula wala pango la nyumba, huku akienda kupanga nyumba na huyo mchepuko mtaani.

Kila nilipompigia simu alinitukana, kunidhalilisha, na kuniambia nimsahau kabisa kwenye maisha yake. Nilibaki nikilia usiku na mchana, huku nikitazama watoto wangu wakiteseka kwa kukosa ada na mahitaji ya msingi.

Ndugu wa mume wangu walijaribu kuingilia kati lakini mwanaume huyo alikuwa amefungwa kabisa masikio na macho, asitake kuniona wala kunisikia. SOMA ZAIDI.
Kupoteza mzazi aliyekuwa nguzo ya familia ni pigo kubwa linaloacha simanzi nzito, lakini pale ambapo ndugu na jamaa wa karibu wanapotumia msiba huo kama fursa ya kukudhulumu eneo la urithi, uchungu na maumivu huongezeka mara dufu.

Baada ya msiba wa baba yangu mzazi, niliacha majukumu yangu yote na kurejea kijijini ili kusimamia ardhi na shamba la familia ambalo baba aliniachia mimi rasmi kabla ya kifo chake.

Hata hivyo, siku chache tu baada ya kumaliza taratibu za mazishi, wajomba na kaka zangu wa tumbo moja walianza kuonyesha sura zao halisi za uroho na chuki.

​Wakishirikiana na baadhi ya wazee wa ukoo waliopokea rushwa, walitengeneza nyaraka za uongo za ardhi na kudai kuwa baba hakuwa ameniachia eneo hilo.

Walitumia vitisho vya wazi, ushawishi wa fedha, na hata kuniletea majambazi nyumbani ili kunitisha niondoke kwenye ardhi ya baba yangu. Nilikwenda kwa serikali ya mtaa na baraza la ardhi la kijiji, lakini ndugu hao walitumia fedha zao na hila za kimila kufunga mdomo kila mtu aliyetaka kunitetea.

Nilibaki nikiwa sina msaada wowote, nikilia kwa uchungu na kuona jinsi jasho na urithi halali wa watoto wangu ukichukuliwa na watu wazima wenye tamaa mbaya. SOMA ZAIDI.
WAFANYAKAZI wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki wamefanya mazoezi ya kukimbia umbali wa takribani kilomita saba katika eneo la Coco Beach jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kujiweka katika hali nzuri ya kiafya na utayari wa kutekeleza majukumu yao.

 


Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewaasa viongozi katika Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuepuka migogoro miongoni mwao na baina yao na watumishi wanaowaongoza, akisisitiza kuwa migogoro mahali pa kazi inakwamisha ufanisi na azma ya Serikali ya kuwapelekea wananchi huduma bora.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo leo, Agosti 21, 2026, wakati akifunga Mkutano Mkuu wa 16 wa Mwaka wa Taasisi ya Maboresho katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA), uliofanyika kwa siku tatu kuanzia Agosti 19 hadi 21, 2026, katika Ukumbi wa Jiji  Mtumba, jijini Dodoma.

“Niwaase na kuwaomba sana muepuke migogoro miongoni mwenu; kati ya Mkurugenzi na Katibu Tawala, kati ya Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya, kati ya RAS na Mkuu  wa Mkoa, na kati ya kiongozi na watumishi unaowaongoza. Mahali penye migogoro hakuna ufanisi wa kazi na maendeleo,” amesema Prof. Shemdoe.

Amesema viongozi na watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wanapaswa kufanya kazi kwa kuheshimiana, akisisitiza kuwa hakuna sababu kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kupambana na Mwenyekiti wa Halmashauri au Mstahiki Meya.

Prof. Shemdoe amesema uzoefu wake katika uongozi umemfundisha umuhimu wa ushirikiano na kuheshimiana, akieleza kuwa alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hakuwahi kugombana na Mwenyekiti wa Halmashauri, na alipokuwa Katibu Tawala wa Mkoa hakuwahi kupishana lugha na Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Prof. Shemdoe amewataka viongozi hao kutumia maarifa, weledi na uzoefu wao katika kuwatumikia wananchi, akieleza kuwa Serikali za Mitaa ziko karibu zaidi na wananchi na hivyo ni kimbilio lao katika kupata huduma mbalimbali.

Amesema wananchi wanapopima mafanikio ya Serikali, kwa kiasi kikubwa huyapima kupitia huduma wanazozipata katika maeneo yao, zikiwemo huduma za afya ya msingi, elimu ya msingi, usafiri na usafirishaji.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuidhinisha na kuleta fedha kwa ajili ya uendeshaji wa Taasisi za Umma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Amesema fedha hizo zinaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kufanya shughuli za kiuchumi na kujiingizia kipato kwa ajili ya kuendesha maisha yao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya Maboresho katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA), Bw. Albert Gabriel Msovela, amemhakikishia Prof. Shemdoe kuwa wajumbe wa taasisi hiyo ni askari wake kiutendaji na kwamba TOA itaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi kwa mujibu wa Katiba.

Bw. Msovela amesema TOA itaendelea kushirikiana na Serikali katika kutekeleza malengo mbalimbali ya kitaifa, ikiwemo utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Mhe. Waziri, naomba nikuhakikishie kwamba kupitia Mkutano Mkuu huu wa 16 wa Mwaka wa TOA, tutatoka na mikakati, maazimio pamoja na mipango madhubuti ambayo tutakwenda kuwashirikisha wananchi katika utekelezaji wake kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo,” amesisitiza Bw. Msovela.

Mkutano Mkuu wa 16 wa Mwaka wa TOA uliowakutanisha Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Makatibu Tawala wa Wilaya, umefanyika chini ya Kaulimbiu isemayo: “Ugatuzi wa Madaraka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ni Nguzo Madhubuti ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”

NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Atupele Mwambene ametoa wito kwa walimu walioshiriki mafunzo ya somo la Elimu ya Biashara kuonesha ushirikiano kwa walimu wataowakuta katika vituo vyao vya kazi ili kuwasaidia watoto katika malezi pamoja na ujifunzaji.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeiomba Serikali kuongeza ruzuku kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ili kuwezesha kuongeza kasi ya ujenzi wa nyumba za makazi ya watumishi wa umma nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Selemani Kakoso, wakati wa ziara ya kukagua miradi ya nyumba za watumishi inayotekelezwa na TBA katika maeneo ya Kisasa na Nzuguni jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kutathmini utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini.

Kakoso amesema Kamati imejiridhisha na juhudi zinazofanywa na Serikali pamoja na TBA katika kukabiliana na changamoto ya makazi kwa watumishi wa umma, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya ujenzi kutokana na mahitaji makubwa ya nyumba nchini.

Amesema eneo la Nzuguni lenye takribani ekari 630 lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa makazi ni hatua muhimu katika kuendeleza mji mpya wa Serikali, kwa kuwa uwepo wa nyumba hizo utawasaidia watumishi, wakiwemo walio katika ngazi za chini, kupata makazi yaliyo karibu na maeneo yao ya kazi.

“Tunawapongeza Serikali kwa juhudi kubwa zilizofanyika na pia TBA kwa mipango mizuri ya kuandaa nyumba za makazi ya watumishi. Tumekagua eneo la Kisasa na tumeona maboresho makubwa katika nyumba zilizojengwa,” amesema Kakoso.

Hata hivyo, Kamati imeishauri Serikali kuharakisha upatikanaji wa wabia kupitia utaratibu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), ili kuongeza uwezo wa TBA kutekeleza miradi mikubwa ya nyumba kwa wakati na kukidhi mahitaji ya watumishi.

Kwa mujibu wa Kamati hiyo, ushirikishwaji wa sekta binafsi utawezesha kupatikana kwa mitaji na utaalamu zaidi, huku Serikali ikiendelea kusimamia miradi hiyo kuhakikisha inatoa huduma bora na nyumba zenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya watumishi.

Kuhusu huduma ya maji, Kamati imepongeza TBA kwa kuanzisha mfumo wake wa maji bila kutegemea kikamilifu huduma kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA).

Hata hivyo, imeitaka TBA kuongeza juhudi za kuchimba visima na kuimarisha mifumo ya majitaka ili kukidhi mahitaji ya eneo hilo kwa muda mrefu.

Aidha, Kamati imeishauri TBA kuangalia uwezekano wa kutumia nishati ya jua kama chanzo mbadala cha umeme, hatua ambayo itasaidia kupunguza utegemezi wa mfumo wa kawaida wa umeme na kuhakikisha huduma zinaendelea kupatikana wakati changamoto za umeme zinapotokea.

Vilevile, Kamati imeitaka Wizara ya Ujenzi kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI, TANROADS, TARURA pamoja na TBA katika ujenzi wa miundombinu bora ya barabara katika maeneo hayo, hususan barabara za lami, ili kuongeza mvuto wa makazi hayo na kurahisisha usafiri.

Kamati imesisitiza kuwa ujenzi wa nyumba za watumishi ni uwekezaji wa muda mrefu unaopaswa kuzingatia thamani ya fedha, ubora wa majengo na mahitaji ya wananchi, ili miundombinu hiyo iwe na tija kwa Serikali na kizazi cha sasa na kijacho.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Miliki wa TBA, Said Rajabu Mndeme, aliyemwakilisha Mtendaji Mkuu wa TBA, amesema mradi huo unatekelezwa katika eneo lenye takribani ekari 640, ambapo ujenzi wa nyumba 150 tayari umekamilika.

Amesema nyumba nyingine 110 zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi, zikiwemo nyumba 50 za chini zilizofikia hatua ya mwisho na zinatarajiwa kuanza kutumika. Aidha, majengo mawili ya ghorofa tano yako katika hatua ya msingi, ambapo kila jengo litakuwa na uwezo wa kuhudumia familia 30.

Kwa mujibu wa Mndeme, TBA imeanza kushirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa mradi huo baada ya eneo hilo kutangazwa na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuwasilisha mapendekezo ya kushirikiana na Wakala.

Amesema mradi huo umepangwa kuwa na huduma muhimu zikiwemo shule za awali, shule mbili za msingi, maeneo ya biashara pamoja na vyuo.

Mndeme amesema mahitaji ya nyumba katika Jiji la Dodoma ni makubwa, akifichua kuwa wakati ujenzi wa nyumba 150 za awali ulipokuwa ukiendelea, TBA ilipokea zaidi ya maombi 1,000 kutoka kwa watumishi waliokuwa wakihitaji makazi.

Amesema hadi sasa, Meneja wa TBA Mkoa wa Dodoma ana maombi zaidi ya 8,000 ya nyumba kutoka kwa watumishi na wananchi, hali inayoonyesha ukubwa wa changamoto ya makazi katika jiji hilo.

Mndeme ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita na Wizara ya Ujenzi kwa kuendelea kuiwezesha TBA kupitia ruzuku, akisema mradi huo ulioanza mwaka 2021 umeendelea kutekelezwa kwa ufadhili wa Serikali.

Amesema TBA sasa inalenga kuongeza kasi ya ushirikishwaji wa sekta binafsi ili kuharakisha ukamilishaji wa mpango wa ujenzi wa nyumba 3,500 na hivyo kupunguza changamoto ya makazi katika Jiji la Dodoma.