Serikali imeendelea kuweka mazingira bora ya kuishi kwa wazee nchini kupitia uboreshaji wa Sera, huduma za afya na ukarabati wa makazi ya wazee ili kuhakikisha wanaishi kwa heshima, usalama na utu.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, Julai 14, 2026, alipotembelea Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Kibirizi mkoani Kigoma kwa lengo la kujionea hali ya utoaji wa huduma za ustawi wa jamii kwa wazee wanaoishi katika makazi hayo. 

"Serikali inatambua wazee kuwa ni tunu, hazina ya hekima na msingi wa maadili ya Taifa letu. Tunathamini mchango wao mkubwa katika ujenzi wa familia, jamii na Taifa, hivyo tutaendelea kuhakikisha wanaishi kwa heshima, usalama na utu, Makazi ya wazee yanapaswa kuwa suluhisho la mwisho pale ambapo mazingira ya kifamilia hayatoi fursa ya kuwahudumia wazee, huku jamii ikiendelea kuthamini na kuwalea wazee ndani ya familia zao " alisema Naibu Waziri Mahundi. 

Aidha, Naibu Waziri Mahundi amesema Wizara imetenga jumla ya shilingi milioni 400 kwa ajili ya ukarabati wa Makazi ya Wazee nchini, ambapo kati ya fedha hizo shilingi milioni 100 zimetengwa kwa ajili ya kuboresha Makazi ya Wazee Kibirizi ili kuendelea kuwapatia wazee mazingira salama na huduma bora zaidi. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, amewapongeza watumishi wanaotoa huduma katika Makazi ya Wazee Kibirizi kwa kujitolea kuwalea na kuwahudumia wazee kwa upendo na heshima na kuhakikisha vituo hivi vinakuwa sehemu salama ambapo wazee wanaishi bila unyonge na wanapata huduma zote stahiki

“Hii ni Wizara inayogusa moja kwa moja maisha na utu wa wananchi niwapongeza watumishi wote wa makazi haya kwa kazi kubwa mnayoifanya ya kuwalea na kuwahudumia wazee wetu, Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imeendelea kufanya kazi kubwa kuhakikisha vituo hivi vinakuwa sehemu salama ambapo wazee wanaishi bila unyonge na wanapata huduma zote stahiki kwakua  Hii ni Wizara inayogusa moja kwa moja maisha na utu wa wananchi" amesema Mkuu wa Wilaya Chuachua.

Awali akiwasilisha taarifa ya Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Kibirizi, Mfawidhi wa Makazi hayo, Binura Joshua, amesema makazi hayo ni miongoni mwa makazi 13 yanayosimamiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, ambapo  huduma bora za ustawi wa jamii kwa wahudumiwa wake zinatolewa kikamilifu, zikiwemo huduma za chakula, malazi, afya  na ushauri nasaha wa kijamii pia makazi  yanashirikiana na Wadau mbalimbali katika kuhakikisha kuwa wahudumiwa wanapata huduma zinazokidhi mahitaji yao ya msingi na kuboresha ustawi wao.

Wakizungumza kwa niaba ya wenzao, wazee wanaoishi katika Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Kibirizi wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kuendelea kuwajali na kuwapatia huduma muhimu zinazowawezesha kuishi kwa amani na heshima.

"Tunamshukuru sana Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Maendeleo ya Jamii kwa kutukumbuka na kuendelea kutuhudumia, Pamoja na changamoto za mazingira zilizopo, hatukosi chakula, matibabu na malezi ya upendo kutoka kwa watumishi wa makazi Tunajisikia kuwa sehemu ya familia na tunaendelea kuishi kwa matumaini," wamesema wazee hao.










Nilifungua duka langu la nguo nikiwa na matumaini makubwa. Nilikuwa nimeweka akiba ya miaka mingi na hata kukopa fedha kutoka kwa ndugu ili kuhakikisha biashara inaanza vizuri. Nilikuwa na imani kwamba ndani ya miezi michache ningekuwa nimeanza kupata faida.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Kila siku nilikuwa nafungua duka mapema asubuhi na kulifunga jioni bila kuuza hata bidhaa chache. 

Wakati maduka yaliyokuwa jirani yangu yalikuwa yamejaa wateja, kwangu watu walikuwa wanapita tu bila hata kuingia.

Nilianza kushangaa ni kwa nini hali ilikuwa hivyo ilhali nilikuwa na bidhaa nzuri na bei za ushindani. Baada ya miezi sita, nilikuwa nimeanza kupata hasara kubwa.

Nilishindwa kulipa kodi ya fremu kwa wakati, madeni yakaanza kuongezeka na hata familia yangu ilianza kunishauri nifunge biashara. Nilihisi ndoto yangu ilikuwa imefika mwisho.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

 

Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningekamatwa na polisi kwa kosa ambalo sikuwahi kulifanya. 

Nilikuwa mfanyabiashara mdogo wa vifaa vya umeme, nikiishi maisha ya kawaida na kuheshimika katika jamii.

Siku moja, nilipokuwa dukani kwangu, polisi walifika na kuniambia nilikuwa nahusishwa na wizi mkubwa uliotokea kwenye kampuni moja usiku uliotangulia.

Nilibaki nimeshtuka. Sikuwahi hata kufika eneo ambalo walidai wizi ulifanyika. Licha ya kueleza ukweli, nilikamatwa na kupelekwa kituoni. Habari zilienea haraka, na watu wengi wakaanza kuniona kama mwizi kabla hata ya kesi kusikilizwa.

Baada ya kufikishwa mahakamani, nilikana mashtaka yote. Hata hivyo, upande wa mashtaka ulidai kuwa ulikuwa na mashahidi walioniona karibu na eneo la tukio.

Nilihisi dunia imenigeuka. Nilijua sikuwa na kosa, lakini sikuwa na uwezo wa kuthibitisha nilikokuwa muda huo.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

 

Nilipokuwa na miaka 25, niliamini kwamba kabla sijafikisha miaka 30 ningekuwa tayari nimeolewa na kuwa na watoto. Lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti.

Kila uhusiano niliouanzisha uliishia njiani. Wanaume walikuwa wakiniahidi ndoa, lakini muda ulipofika walibadilika ghafla au waliniondoka bila maelezo.

Kadiri miaka ilivyokuwa ikisonga, shinikizo kutoka kwa familia na jamii liliongezeka. Kila nilipohudhuria harusi, watu waliniuliza, “Wewe ni lini?” Maswali hayo yalinivunja moyo.

Wengine waliniambia nilikuwa nimechelewa, na kwamba nafasi yangu ya kupata familia ilikuwa imepungua.

Nilijaribu kila njia. Nilijiunga na vikundi mbalimbali vya kijamii, nikakubali kutambulishwa kwa wanaume tofauti, lakini hakuna uhusiano uliodumu. 

Wakati mwingine mwanaume alikuwa akionyesha mapenzi makubwa mwanzoni, lakini baada ya muda mfupi alikuwa anakata mawasiliano kabisa. Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

 


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekuletea mashindano ya Wazo Bunifu yanayolenga kupata suluhisho za kibunifu zitakazochangia kuboresha mfumo wa kodi nchini. Hii ni fursa yako ya kuwasilisha wazo lenye tija na kushindania zawadi ya hadi Shilingi Milioni 50.

Mawazo yatakayowasilishwa yanapaswa kulenga eneo moja au zaidi kati ya yafuatayo ; kupanua wigo wa kodi, kurahisisha ukadiriaji na ulipaji wa kodi kwa biashara ndogo ndogo, kuimarisha huduma za kodi za kidijitali, kupunguza gharama za ukusanyaji wa mapato, kutumia teknolojia za kisasa kama AI, Big Data na Blockchain katika usimamizi wa kodi, pamoja na kuboresha utatuzi wa migogoro ya kodi ili kuwa wa haraka, wazi na wenye kuaminika zaidi.

Kutuma Wazo lako ingia tovuti ya TRA, Bonyeza kitufe cha innovation portal fuata hatua zinazofuata, Mwisho wa kutuma wazo lako bunifu ni julai 31, 2026.

MWISHO WA SHINDANO HILI NI MWEZI HUU WA 7 NI HATARII


 


📌 Miradi mipya ya kusafirisha umeme kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar

📌 Serikali yawekeza Dola za Marekani milioni 282 kuongeza upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Katika ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, Mhe. Dkt. Mwinyi alipata fursa ya kujionea miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme, teknolojia za matumizi bora ya umeme ikiwemo majiko sanifu yanayotumia umeme kwa ufanisi, huduma ya Luku Janja pamoja na mfumo wa Smart House unaomwezesha mtumiaji kufuatilia matumizi ya umeme kupitia simu ya mkononi.

Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa kujenga njia mpya tatu za kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar kupitia nyaya zitakazopita chini ya bahari.

Ameeleza kuwa njia hizo zitajumuisha Dar es Salaam–Unguja, Tanga–Pemba na Kisiju–Mafia, na kwamba kukamilika kwake kutaongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na uwezo wa kuhudumia ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ukuaji wa viwanda, sekta ya utalii, uwekezaji na shughuli nyingine za kiuchumi visiwani Zanzibar.

Bw. Twange amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 282, ambapo Dola milioni 6 zimetengwa mahsusi kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea katika sekta ya umeme. Kupitia mradi huu wa Dola za Marekani milioni 282, tunaendelea kuimarisha miundombinu ya umeme, huku sehemu ya fedha hizo ikielekezwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na ZECO,” amesema Bw. Twange.

Aidha, amesema TANESCO imeendelea kuleta ubunifu wa kidijitali kupitia mfumo wa Smart House, unaomwezesha mwananchi kufuatilia matumizi ya umeme wa nyumba yake kupitia simu ya mkononi, hatua inayosaidia matumizi bora na yenye tija ya umeme.

Vilevile, Bw. Twange amesema mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme umefikia mafanikio makubwa, ambapo zaidi ya asilimia 90 ya wananchi waliopata majiko hayo wanaendelea kuyalipia kwa utaratibu wa makato kupitia ununuzi wa umeme wa LUKU, hatua inayorahisisha wananchi kumudu gharama za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Jitihada hizo ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme ya uhakika na kutumia nishati safi katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, ikiwemo katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115, umeendelea kuweka msingi wa upatikanaji wa umeme wa kutosha unaowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.












Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amemkabidhi mfanyabiashara mwenye ulemavu, Bi.Esther Mashaka Msengi, mashine ya kusagia viungo ili kuongeza uzalishaji, kupunguza gharama za biashara na kuboresha kipato chake.

Akikabidhi mashine hiyo  katika Viwanja vya Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), amesema aliguswa na changamoto za Esther aliyekuwa akitumia muda na fedha nyingi kusafirisha viungo kwenda kusagwa kabla ya kuvifungasha na kuviuza. 

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi zake kuhakikisha anaimarisha biashara yake, huku akiitaka BRELA kukamilisha usajili wa nembo ya bidhaa zake, TBS kumsaidia kupata ithibati ya ubora na SIDO kuendelea kumjengea uwezo.

Aidha, amelishukuru Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania TEMDO kwa kuwezesha upatikanaji wa mashine hiyo na kueleza kuwa hatua hiyo inaunga mkono maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha wajasiriamali kuongeza tija.

Kwa upande wake, Bi. Esther Msengi amesema mashine hiyo itapunguza gharama za uzalishaji na kumwezesha kupanua biashara yake. 

Mwakilishi wa Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO), Mhandisi. Elisante Mjema, amesema mashine hiyo inaweza kusaga kilo 10 za viungo kwa saa moja na kuongeza uzalishaji hadi kufikia mauzo ya takribani shilingi milioni 1.5 kwa siku endapo kutakuwa na malighafi za kutosha.

 


Na OWM–TAMISEMI, Sumbawanga

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amempongeza Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa juhudi zake za kuwaunganisha wadau mbalimbali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, uongozi wa mkoa wa Rukwa na halmashauri zake, hatua iliyowezesha kufanyika kwa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi mkoani Rukwa.

Prof. Shemdoe ametoa pongezi hizo Julai 13, 2026 katika Ukumbi wa Country Hotel mjini Sumbawanga wakati akifungua mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, mafunzo ambayo yameratibiwa na Mbunge huyo kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Prof. Shemdoe amesema kuwa, anaamini mafunzo hayo yatafungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa, akiwataka washiriki kutumia elimu watakayopata kuanzisha biashara mpya, kuimarisha biashara walizonazo, kuongeza uzalishaji na kuongeza thamani ya bidhaa na mazao wanayozalisha, na kuongeza kwamba mafunzo hayo yameandaliwa kwa lengo la kuwafikia wananchi wa makundi yote, wakiwemo watu wenye ulemavu.

Aidha, Prof. Shemdoe amezielekeza ofisi za mikoa na halmashauri nchini kutenga nafasi za ofisi kwa ajili ya vituo vya uwezeshaji kiuchumi vitakavyohudumia vijana, wanawake, watu wenye ulemavu na makundi mengine maalum yanayojishughulisha na kilimo, ufugaji, uvuvi, umachinga, bodaboda, ufundi na ujasiriamali, ili kujenga taifa lenye uchumi imara, shindani na jumuishi.

"Ninazielekeza ofisi zote za mikoa na halmashauri nchini kuiga mfano wa mkoa wa Rukwa kwa kutenga ofisi za vituo vya uwezeshaji kiuchumi, vitakavyowawezesha wananchi kupata taarifa, ushauri na kuunganishwa na fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji ili wananchi wajikwamue kiuchumi," amesema Prof. Shemdoe.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhe. Makongoro Nyerere, amemshukuru Prof. Shemdoe kwa kukubali kumwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika ufunguzi wa mafunzo hayo, akisema uwepo wake unaonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha kiuchumi vijana, wanawake, watu wenye ulemavu na makundi mengine maalum.

Kwa upande wake, Mhe. Mzindakaya amesema uwepo wa Prof. Shemdoe akimuwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika ufunguzi wa mafunzo hayo, ni ishara ya namna Serikali inavyothamini jitihada za kuwawezesha wananchi kiuchumi. 

Naye Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bw. Gwakisa Bapala, amesema mafunzo hayo yatawawezesha wananchi kunufaika na huduma za mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji kwa ajili ya kuanzisha miradi mipya, kukuza biashara zilizopo, kuongeza thamani ya mazao na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Rukwa na Taifa kwa ujumla.

Mafunzo hayo yanayofanyika katika halmashauri zote nne za mkoa wa Rukwa kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026, yamelenga kuwafikia wananchi zaidi ya 1,000 na kuwapa maarifa yatakayowawezesha kutumia kikamilifu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji kwa maendeleo yao na ya Taifa, fursa ambazo zinatoka katika mifuko na taasisi 15 ikijumuisha NMB, CRDB, Azania Bank, TADB, AGITF, Self MF, BOT, Machinga Fund, YDF, SIDO, Pass Trust, Pass Leasing, EFTA, TaFF na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa.












Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Mha. Wolta Kirita, amesisitiza umuhimu wa kushirikisha Vyombo vya Utoaji wa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) katika mipango na programu zote zinazolenga kuboresha huduma za maji vijijini ili kuhakikisha huduma hizo zinakuwa endelevu na wananchi wanaendelea kunufaika na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali.
Mafunzo ya utoaji wa elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi yanaendelea kufanyika katika Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, yakilenga kuwaongezea wananchi uelewa kuhusu fursa za kupata mitaji na huduma za maendeleo ya biashara ili kukuza shughuli za kiuchumi.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Naibu Katibu  Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,Prof. Daniel Mushi,akizungumza wakati wa  kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma.
  
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Na.Alex Sonna-DODOMA
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, ametoa maagizo matano kwa viongozi na watumishi wa sekta ya elimu nchini ili kuhakikisha sekta hiyo inaendana na mahitaji ya maendeleo ya taifa na mabadiliko ya dunia.
Prof.Nombo ametoa maagizo hayo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda.
Amesema mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu yametokana na ushirikiano na utendaji mzuri wa viongozi na watumishi wa wizara pamoja na taasisi zake, huku akisisitiza kuwa kikao hicho ni fursa muhimu ya kutathmini mafanikio na kupanga mwelekeo wa sekta kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
"Ndiyo maana tumeona ni muhimu kuwashirikisha wataalamu kutoka Tume ya Mipango ili kutusaidia kuona namna sekta ya elimu itakavyochangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Tunaamini dira hiyo ndiyo itakayotuongoza katika kukidhi mahitaji ya taifa kwa miaka ijayo," amesema Prof.Nombo
Prof.Nombo ameelekeza mapitio ya mara kwa mara ya kozi na programu za elimu ili ziendane na mahitaji ya sasa ya jamii, uchumi na soko la ajira. Amesema mjadala unaoendelea katika mitandao ya kijamii kuhusu uchaguzi wa kozi kwa wahitimu wa kidato cha sita unaonesha wazi kuwa kuna mahitaji mapya ya ujuzi na taaluma yanayopaswa kuzingatiwa.
"Mrejesho tunaoupata unatufanya tujitathmini na kuangalia aina ya kozi tunazotoa ili ziendane na mahitaji ya sasa ya jamii na uchumi. Tunahitaji kuongeza ubunifu na unyumbufu katika kuwapa wanafunzi fursa ya kusoma kozi zitakazochangia maendeleo ya taifa," amesema 
Kuhusu Mfumo wa Taarifa za Usimamizi wa Elimu (ESMIS), Prof.Nombo amesisitiza umuhimu wa kuwa na takwimu sahihi kwa ajili ya kufanya maamuzi yenye tija na kuagiza taasisi zote kuhakikisha mifumo yao ya TEHAMA inaunganishwa na mfumo huo.
Amesema hatua hiyo inatekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mifumo ya Serikali inasomana na kufanya kazi kwa pamoja, akibainisha kuwa wizara imeweka suala hilo kuwa kipaumbele.
Aidha, amehimiza kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika uwekezaji wa sekta ya elimu ili kuboresha huduma na miundombinu, pamoja na kutafuta mbinu mbadala za kugharamia sekta hiyo ili kuongeza fursa za wanafunzi wengi zaidi kuendelea na masomo.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Daniel Mushi, amewataka washiriki wa kikao kuendelea kueleza mafanikio yanayopatikana kupitia utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali za Serikali katika sekta ya elimu.
"Hatupaswi kusita kueleza mazuri ambayo Serikali inaendelea kuyafanya kwa wananchi kwa pamoja tunaweza kuijenga sekta ya elimu yenye ushindani, ubora na tija kwa maendeleo ya taifa," amesema  Prof Mushi
Katika kikao hicho, washiriki wamepokea na kujadili mawasilisho mbalimbali ikiwemo nafasi ya elimu, sayansi na teknolojia katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, umuhimu wa mifumo ya TEHAMA katika kuongeza ufanisi wa utoaji huduma.
Vilevile,matumizi ya mfumo wa ESMIS, pamoja na Mpango Mkakati wa Wizara wa mwaka 2026/27 hadi 2030/31 na utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/27.