Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang'onda (wa pili kushoto) akizungumza kwenye mradi wa maji wa Mikocheni/Mkwaja. Kushoto kwake ni Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso na kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mhe Ayubu Sebabili


Na Mwandishi Wetu, PANGANI


WAZIRI wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ameagizi Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kuunganisha mtandao wa majisafi na salama kwenye makazi ya watu katika kijiji cha Mkwaja.


Mhe. Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Pangani, ameyasema hayo leo Juni 20, 2026 kijijini hapo, alipokaribishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa upanuzi mtandao wa maji kutoka ‘mradi mama’ uliopo kijiji cha Mikocheni.

Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Raiyan Mohamed Rashid, akimtishwa ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mkwaja wilayani Pangani, Mkoa wa Tanga kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji uliofika kijijini hapo kutokea kijiji jirani cha Mikocheni.



Mwenge wa Uhuru wenye kauli mbiu inayosema, “Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo” ulifika kwenye mradi huo wa kwanza baada ya kuingia katika Halmashauri ya Pangani kutokea Handeni.


Mhe. Aweso amesema, kwa vile Mwenge umechagiza maendeleo wilayani humo kwa vipindi tofauti, ipo haja ya kuendeleza hali hiyo kwa kuingiza maji kwenye makazi ya watu, badala ya kuishia kwenye vituo 12 vya kuchotea maji (DPs) vilivyopo Mkwaja.


Amesema, usambazaji majisafi na salama ni utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kumtua ndo mama kichwani.


Kwa mujibu wa Mhe. Aweso, kati ya vijiji 12,333 vilivyopo nchini, 10,758 vimefikiwa na huduma ya majisafi na salama wakati 1,575 vitafikiwa ifikapo 2030.


Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Pangani, Mhandisi Rajab Hussein, amesema upanuzi wa mradi wa Mikocheni ni matokeo ya upatikanaji maji kwa wastani wa lita 480,000 kwa siku, wakati mahitaji ya Mikocheni pekee ni lita 40,000.


Kwa mujibu wa Mhandisi Hussein, mahitaji yaliyobainika kwa matumizi katika kijiji cha Mkwaja ni lita 65,000 kwa siku na kufanya jumla yake kuwa lita 105, hivyo kuwa na lita 375,000 za ziada.

Ni picha ya uzinduzi wa mradi wa maji.

Amesema kupitia upanuzi wa mradi huo, RUWASA imejenga tenki lenye uwezo wa kuchukua lita 90,000 na kuwekwa kwenye mnara wa urefu wa mita sita, hivyo kuwa na uwezo wa kusambaza maji kijijini Mkwaji kupitia DPs zilizopo.


Naye Mwang’onda amesema agizo la Mhe. Aweso kwa RUWASA kuunganisha mtandao wa maji kwenye makazi ya watu ni kuuheshimisha Mwenge na kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mwang’onda amesema historia imeandikwa kwa Mhe. Rais Dkt Samia kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji majisafi na salama sehemu kubwa ya nchi.


Kwa hali, Mwang’onda, amehimiza wananchi kuwekeza zaidi katika amani, umoja na mshikamano, ili kufikia maono ya Mhe. Rais Dkt Samia kuwa na maendeleo endelevu.


MWISHO.

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linaendelea kushiriki kikamilifu katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Kitaifa yanayoendelea mkoani Dodoma, kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali kuhusu umuhimu wa kuzingatia viwango na ubora wa bidhaa zinazozalishwa na kutumika nchini.

Akizungumza katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa TBS, Julius Lwenje, amesema kuwa shirika hilo lina jukumu la kusimamia na kuhakikisha bidhaa mbalimbali zinazozalishwa, kuingizwa na kuuzwa nchini zinakidhi viwango vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria.

Amesema TBS inaendelea kutoa huduma za ukaguzi, upimaji na uthibitishaji wa ubora wa bidhaa mbalimbali, ikiwemo vyakula na vinywaji, kwa lengo la kulinda afya, usalama na maslahi ya watumiaji.

Lwenje amewahimiza wananchi kuendelea kutumia bidhaa zenye alama ya ubora ya TBS, akieleza kuwa alama hiyo ni uthibitisho kwamba bidhaa husika imefanyiwa ukaguzi na imekidhi viwango vinavyotakiwa.

“Tunawaomba wananchi kuwa makini wanaponunua bidhaa na kuhakikisha wanachagua bidhaa zenye alama ya ubora ya TBS, kwani hii ni ishara kwamba bidhaa hizo zimehakikiwa na kuthibitishwa kuwa salama kwa matumizi,” amesema.

Aidha, amesema ushiriki wa TBS katika maadhimisho hayo unatoa fursa kwa wananchi kupata elimu kuhusu huduma zinazotolewa na shirika hilo pamoja na kuelewa mchango wa viwango katika kukuza biashara, kulinda walaji na kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanawakutanisha taasisi mbalimbali za Serikali na wadau wake kwa lengo la kuonesha huduma wanazotoa na kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na wananchi.







Na Saidina Msangi na Asia Singano, WF - Dodoma

Wizara ya Fedha imeendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhakikisha wananchi wanapata ufafanuzi kuhusu masuala ya kodi, uchumi na sera mbalimbali za fedha na mchango wa kodi katika kugharamia huduma muhimu za kijamii kama vile miundombinu, elimu, afya, maji nishati na huduma nyingine muhimu.

Hayo yamebainishwa na Afisa Usimamizi wa Fedha Mkuu, Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. Abdul Dachi, wakati akitoa elimu kwa wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Bw. Dachi alisema kupitia Maonesho hayo, Idara imekuwa ikitoa taarifa kwa wananchi kwa lugha rahisi na inayoeleweka ili kuwawezesha kufahamu mchango wa Sera za Kodi na Uchumi katika maendeleo ya Taifa na ustawi wa jamii.

‘‘Miongoni mwa maeneo yanayotolewa elimu ni kuhusu mwenendo wa uchumi wa Taifa na namna Sera za Uchumi zinavyosaidia kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza fursa za ajira na kukuza uchumi kwa ujumla pamoja na namna hizo zinavyoandaliwa ili kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kwa ufanisi na kwa kuzingatia maslahi ya Taifa,’’, alisema Bw. Dachi.

Aliongeza kuwa Serikali inatumia taarifa za takwimu na tafiti mbalimbali zinazosaidia katika upangaji wa bajeti na utekelezaji wa mikakati ya maendeleo ya muda mfupi na mrefu pamoja na usimamizi wa mikataba ya kikodi kati ya Tanzania na mataifa mengine na ushirikiano wa kikanda na kimataifa unaolenga kulinda maslahi ya Taifa katika sekta ya kodi.

Alifafanua kuwa wananchi wanapatiwa elimu kuhusu namna Wizara inavyofanya tafiti za kisera na kuandaa mapendekezo ya kitaalamu yanayosaidia Serikali kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya nchi pamoja na namna Serikali inavyoshughulikia masuala ya kodi za kimataifa.

‘’Tumetumia fursa hii kueleza wananchi umuhimu wa sera za kodi na fedha katika kukuza uchumi na ustawi wa wananchi, mchango wa kodi katika maendeleo ya Taifa, pamoja na umuhimu wa uwazi na uwajibikaji katika mchakato wa utungaji wa sera nafasi ya Tanzania katika uchumi wa dunia na manufaa yanayotokana na ushirikiano wa kiuchumi na mataifa na taasisi mbalimbali za kimataifa’’, alifafanua Bw. Dachi.

Alisema kuwa ili kuhakikisha ujumbe unawafikia wananchi wengi zaidi, idara pia inatoa vipeperushi, vitabu vya elimu pamoja na mazungumzo ya ana kwa ana na wageni wanaotembelea Banda hatua inayochangia kuongeza uelewa wa umma na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wananchi katika maendeleo ya Taifa.

Tume ya Ushindani (FCC) imesema imeanza mpango wa kuanzisha klabu za elimu ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia katika shule za msingi, sekondari na taasisi za elimu ya juu ili kujenga kizazi chenye uelewa wa masuala hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari Juni 20, 2026, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema mpango huo utatekelezwa kupitia klabu zitakazojulikana kama Ushindani School Club. 

Amesema lengo la mpango huo ni kuwafikia wanafunzi mapema na kuwajengea uelewa kuhusu ushindani, haki za mlaji na namna ya kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa au kupata huduma.

Feruzi amesema elimu hiyo itawasaidia wananchi kutambua bidhaa bandia, kulinda soko dhidi ya udanganyifu na kuwawezesha watumiaji kuchagua bidhaa salama na zenye ubora.

Ameeleza kuwa uelewa wa masuala ya ushindani na ulinzi wa mlaji utasaidia wananchi kufanya uchaguzi bora wa bidhaa na huduma, huku sekta binafsi ikiendelea kuchangia katika uzalishaji na ukuaji wa uchumi.

Aidha, amesema utoaji wa elimu hiyo utaendelea kupitia ofisi za kanda za FCC zilizopo Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma na Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha wananchi katika mikoa yote ya Tanzania Bara wanapata elimu hiyo.



Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.

Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.

Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.




Kwa miaka mingi, nilikuwa na ndoto ya kusafiri kwenda Marekani. Nilitaka kutembelea nchi hiyo kwa sababu mbalimbali zilizokuwa muhimu kwangu. 

Kila nilipofikiria kuhusu safari hiyo, nilijawa na matumaini kwamba siku moja ndoto yangu ingetimia. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Nilipotuma maombi yangu ya kwanza ya visa, niliamini kila kitu kilikuwa sawa. Nilikuwa nimeandaa nyaraka zote nilizohitaji na nilijitokeza kwenye mahojiano nikiwa na matumaini makubwa. Hata hivyo, maombi yangu yalikataliwa. Nilihuzunika sana.

Baada ya muda, nilijaribu tena. Safari hii nilijitayarisha zaidi na kuhakikisha kila kitu kiko sawa. Lakini kwa mshangao wangu, nilikataliwa tena. Mara ya pili ilinivunja moyo zaidi. Nilianza kuamini kwamba labda safari ya kwenda Marekani haikuwa sehemu ya maisha yangu. SOMA ZAIDI.

Maisha yangu yalibadilika ghafla siku mume wangu alipoondoka nyumbani. Mwanzoni nilidhani alikuwa amekasirishwa na migogoro ya kawaida ya ndoa na angerudi baada ya siku chache. 

Lakini siku zikageuka kuwa wiki, na wiki zikageuka kuwa miezi. Baadaye niligundua kwamba alikuwa ameanza kuishi na mwanamke mwingine.

Habari hiyo ilinivunja moyo. Tulikuwa tumejenga maisha pamoja kwa miaka mingi na tulikuwa na watoto ambao walimhitaji baba yao. Kila nilipowaona watoto wakimuulizia, moyo wangu ulizidi kuumia.

Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa.
Wakati mwingine alipokea simu zangu, wakati mwingine hakujibu kabisa. Nilimwomba afikirie kuhusu familia yetu, lakini alionekana kuwa amefanya uamuzi wake. Kadri miezi ilivyopita, matumaini yangu yalianza kupungua.

Watu wengi walinishauri nikubali hali na kuendelea na maisha yangu. Ingawa nilisikiliza ushauri wao, bado nilitamani kuona familia yetu ikiungana tena. SOMA ZAIDI.

 WANAFUNZI wanaofanya ubunifu wa matumizi ya teknolojia mbalimbali katika chuo cha ufundi Arusha (ATC), wametakiwa kusoma Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kuielewa na kuona fursa zilizopo ndani yake na kufanya bunifu zao kutokana na malengo ya dira hiyo.


Hayo yameelezwa Juni 19, 2026 na Mkuu wa chuo cha ufundi Arusha Profesa Musa Chacha katika hotuba yake ya kufungua wiki ya maonyesho ya ubunifu yanayoandaliwa kila mwaka chuoni hapo.

Profesa Chacha amesema dira ya Taifa 2050 imeainisha maeneo ambayo yanapaswa kuendelezwa kwaajili ya Maendeleo ya Watanzania hivyo wanafunzi wanaofanya bunifu chuoni hapo wanapaswa kuyasoma na kuyajua na kuyafanyia ubunifu.

Amesema kutokana na kazi nzuri ya ubunifu ambayo imekuwa ikifanywa na wanafunzi chuoni hapo, chuo kimepanga kujenga jengo maalum la ghorofa nne ambalo litatumika kwaajili ya shughuli za ubunifu.

“ Kwa kushirikiana na Serikali ya Italia hivi karibuni tunatarajia kujenga jengo kubwa la ghorofa nne ambalo litatumika kwaajili ya shughuli za ubunifu( innovation), hapa chuoni hatutaki hivi vipaji vyenu vipotee,” amesema.

Aidha Profesa Chacha amesema chuo kinaendelea na ujenzi wa karakana ( industrial workshop), ambayo itatumika kutengeneza mitambo bunifu itakayokuwa ikigunduliwa na wanafunzi chuoni hapo kwaajili ya kuuzwa na kwamba tayari mashine zitakazotumika katika karakana hiyo zipo njiani kufika chuoni hapo.

“ Hivi sasa tumeamua kuendeleza bunifu zote zitakazobuniwa na wanafunzi Kwa kuzizalisha na kuziingiza sokoni, tutakuwa na kiwanda hapa hapa chuoni na wote mnaofanya ugunduzi huu tutaendelea kuwafuatilia na kuona namna mnafaidika na bunifu zenu, tutawashika mkono popote mtakapoenda,” amesema Profesa Chacha.

Aidha amesema chuo kinakamilisha jengo la hospitali itakayokuwa ikitibia wanafunzi chuoni hapo lakini pia chuo kipi kwenye mikakati ya kujenga jengo litakalojulikana kama innovation center ambalo litakuwa maalum kwaajili ya ugunduzi na uzalishaji wa vifaa tiba vya hospitalini ( biomedical engineering).

Awali akimkaribisha mgeni rasmi Makamu mkuu wa chuo, Dkt Yusuph Mhando alisema katika maonyesho ya mwaka huu ambayo ni awamu ya tatu tangu kuanzishwa, jumla ya bunifu 75 ziliingia kwenye ushindani.

Amesema kati ya bunifu hizo, bunifu 20 zilihusiana na teknolojia ya habari na mawasiliano(Tehama), umeme 15, mitambo na magari 19, sayansi timizi 8, ujenzi na barabara13 na kwamba baada ya majaji kupitia bunifu hizo jumla ya bunifu 19 pekee ziliweza kuingia fainali.

Amesema mshindi wa kwanza ametoka katika fani ya mitambo aliyegundua mashine inayojulikana kama ( Energy trauma kit), akifuatiwa na Tehama ambaye amegundua mashine ya kupima uoni wa macho ( VR acute test),

Aidha amesema maonyesho hayo ni muhimu Kwa Taifa Kwa kuwa yamekuwa yakikuza ujuzi wa wanafunzi chuoni hapo Kwa kuweza kuonyesha Kwa vitendo kile ambacho wamekuwa wakifundishwa darasani.

“ Katika bunifu hizi, Kuna vijana wametengeneza mfumo wa kupiga kura wakati wa uchaguzi ukiwa nyumbani, teknolojia hii ikiweza kuboresha itaweza kusaidia sana katika eneo hili,” amesema.

Amesema ni tegemeo la chuo kuwa bunifu hizo zitafikia jamii na kutatua kero mbalimbali inazizikabili na hivyo chuo kitaendelea kuimarisha na kuendeleza vipaji vya wanafunzi hao.

Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa za kufanikiwa na kubadilisha maisha ya familia yangu. Nilifanya kazi kwa bidii kila siku. 

Niliamka mapema, nilikutana na wateja, na nilijitahidi kuhakikisha kila huduma niliyotoa ilikuwa ya kiwango cha juu. Licha ya juhudi zote hizo, faida niliyokuwa napata haikutosha kufikia malengo yangu.

Miaka ilipita katika hali hiyo. Biashara yangu ilikuwa ikiendelea kuwepo, lakini haikuwa inakua kwa kasi niliyokuwa nimeitarajia. 

Wakati mwingine nilipata faida ndogo, na wakati mwingine nilihangaika hata kulipa baadhi ya gharama za kawaida za biashara.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona washindani wangu wakipata mikataba mikubwa huku mimi nikibaki nikisubiri fursa ambazo hazikuonekana kuja.

Nilijaribu kuboresha huduma zangu na kutafuta masoko mapya. Ingawa kulikuwa na mabadiliko madogo, bado sikuweza kupata nafasi ambayo ingeibadilisha biashara yangu kwa kiwango kikubwa. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miezi sita, nilikuwa nikipata hasara ambazo sikuweza kuzielewa. Nilimiliki duka la jumla ambalo lilikuwa likifanya vizuri katika eneo letu. Hata hivyo, nilianza kugundua kwamba baadhi ya bidhaa zilikuwa zinapotea mara kwa mara. Mwanzoni nilidhani ilikuwa ni makosa ya kawaida ya hesabu.

Lakini kadri muda ulivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya. Kila wiki nilikuwa nikikuta bidhaa zimepungua bila maelezo ya kuridhisha. Nilipohesabu mauzo na kulinganisha na bidhaa zilizobaki, kulikuwa na tofauti kubwa ambayo sikuweza kuieleza. Nilianza kuwa na wasiwasi mkubwa.

Nilizungumza na wafanyakazi wangu na kuwauliza kama kuna jambo walilokuwa wamegundua. Wote walikana kujua chochote. Hata wateja wa kawaida hawakuonekana kuwa na taarifa yoyote kuhusu kilichokuwa kinaendelea. Hasara iliendelea kuongezeka.

Wakati mwingine nililala nikiwa nawaza jinsi biashara yangu ingeendelea kama wizi ule usingekoma. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba mwizi huyo hakuacha ushahidi wowote nyuma.
Nilijaribu njia mbalimbali za kumgundua. SOMA ZAIDI.


Kwa miaka mingi, ndoto yangu kubwa ilikuwa kuwa mama. Nilikuwa nikitamani siku ambayo ningeshika mtoto wangu mikononi na kusikia akiniita mama. Baada ya kuolewa, mimi na mume wangu tulikuwa na matumaini makubwa kwamba tungepata watoto ndani ya muda mfupi.

Lakini mambo hayakwenda kama tulivyotarajia.

Mwaka wa kwanza ulipita bila kupata ujauzito. Kisha mwaka wa pili nao ukapita. Kadri miaka ilivyoendelea, watu wa karibu walianza kuuliza maswali ambayo yaliniumiza moyo. Nilijaribu kutabasamu mbele za watu, lakini ndani yangu nilikuwa nikiteseka.

Kila nilipoona familia nyingine zikifurahia watoto wao, nilijikuta nikitamani siku yangu ifike. Wakati mwingine nililia peke yangu usiku nikijiuliza kwa nini safari yangu ilikuwa ngumu kiasi hicho. Baadaye nilianza kutafuta ushauri kutoka sehemu mbalimbali.

Ingawa nilijitahidi kubaki na matumaini, kulikuwa na nyakati ambazo nilihisi kama ndoto yangu ilikuwa ikizidi kuwa mbali. Kilichoniumiza zaidi ni pale baadhi ya watu waliponiambia nisijiwekee matumaini makubwa. Maneno hayo yaliniumiza sana. SOMA ZAIDI.

  


Na. Farida Ramadhani na Chedaiwe Msuya, WF, Dodoma.

Serikali imeendelea kutumia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), kama nyenzo muhimu ya kuharakisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi, kuboresha huduma kwa wananchi na kuvutia uwekezaji nchini.

Hayo yameelezwa na Mchumi Mwandamizi wa Kitengo cha Ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi, Wizara ya Fedha, Bi. Josephina Melkiol wakati akizungumza na wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

Alisema katika kufanikisha hilo Serikali imefanya maboresho ya Sera, Sheria na Kanuni za PPP ili kuimarisha mazingira ya uwekezaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambapo hadi kufikia Juni 2026, jumla ya mikataba tisa (9) ya PPP imesainiwa katika sekta mbalimbali za maendeleo.

“Miradi iliyosainiwa ni pamoja na Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (DART) Awamu ya Kwanza na ya Pili wenye jumla ya mikataba minne, Mradi wa Ukaguzi wa Lazima wa Vyombo vya Moto, Mradi wa Ujenzi na Uendeshaji wa Jengo la Biashara Kariakoo, Mradi wa Ukarabati na Uendeshaji wa Reli ya TAZARA pamoja na miradi ya uboreshaji na uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam kupitia Kampuni za DP World na ADAN,” alibainisha Bi. Josephina.

Alieleza kuwa Serikali ilianzisha utekelezaji wa Programu ya PPP kupitia Sera ya Taifa ya PPP ya mwaka 2009, iliyolenga kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika utoaji wa huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha, alisema Sheria ya PPP ya mwaka 2010 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2011 ziliweka msingi wa mfumo wa kisheria na kitaasisi wa kusimamia miradi hiyo, huku marekebisho yaliyofanyika mwaka 2014, 2018 na 2023 yakilenga kuongeza ufanisi katika maandalizi ya miradi na mchakato wa kupata wabia.

Bi. Josephina alisema Serikali itaendelea kuimarisha matumizi ya mfumo wa PPP ili kuongeza uwekezaji katika sekta za kimkakati, kuboresha miundombinu na kuharakisha utekelezaji wa miradi yenye manufaa kwa wananchi.

Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi unaendelea kuwa chachu muhimu ya maendeleo kwa kuwezesha upatikanaji wa rasilimali, teknolojia na utaalamu unaohitajika katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kitaifa.






 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa vijana wa vyuo vikuu kuwa waadilifu na wazalendo pindi watakapoajiriwa Serikalini kuwatumikia wananchi au kupata fursa za uongozi wa kulitumikia taifa.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa vijana hao Juni 20, 2026, wakati akifungua Kongamano la Vijana (Youth Uongozi Forum) kwa niaba ya Mhe. Prof. Palamagamba John Aaidan Kabudi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) ambalo linalofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro, lililoandaliwa na taasisi ya Tanzania Leadership Foundation (TLF).

“Vijana wangu, watoto wangu, wadogo zangu mjitahidi sana kuwa waadilifu na wazalendo kwani mkishindwa kuwa waadilifu na wazalendo hamtaweza kudumu katika nafasi mtakazoaminiwa kuzitumikia,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka vijana hao kuwa wanyenyekevu watakapopata fursa ya kuwahudumia wananchi kwani haitowagharimu chochote kumsikiliza na kumuhudumia vizuri mwananchi anayefuata huduma, na kuongeza kuwa hakutakuwa na tija yoyote kwa kijana kuwa na majivuno pindi akipata nafasi ya kuutumikia umma.

Aidha, Prof. Shemdoe amewahimiza vijana wote nchini kutokata tamaa, kutokatishwa tamaa, kuchukua hatua mapema (pro-active) kwa jambo lolote wanaloliona linaweza kuwasaidia badala kusubiri kuambiwa walifanye na kuongeza kuwa, vijana wanapaswa kuilinda nchi kwa hali na mali kwani hakuna taifa lingine ambalo watajivunia zaidi ya taifa mama ambalo ni Tanzania.

Prof. Shemdoe amewahikikishia vijana kuwa, Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwajengea vijana mazingira bora kwa kuimarisha miundombinu ya elimu, mafunzo ya ujuzi pamoja na kuwawezesha kujikomboa kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri nchini, hivyo amewataka vijana kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo huku wakiwa wanaendelea na masomo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amewaasa vijana hao kutotegemea akili za watu wengine katika kujenga uwezo wao wa kufikiri bali watumie akili na uwezo wao binafsi katika kutafakari, kuchambua na kufanya maamuzi yenye mantiki, ili kujijenga na kuwa watu bora zaidi katika jamii.

Naye, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Taasisi ya Tanzania Leadership Foundation Mhe. Jabiri Makame ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe  amesema kuwa, msingi na dira ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni kutengeneza kizazi cha vijana viongozi ambao ni wazalendo, wenye maono, uwezo wa kujiongoza, kutoa uongozi katika taasisi za umma na sekta binafsi.












Katika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ili kuwawezesha wananchi, hususan vijana, kumudu kumiliki makazi.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TBA, Bi. Amina Lumuli, amesema kuwa TBA tayari imeanza kutekeleza miradi ya nyumba za gharama nafuu katika mkoa wa Dar es Salaam.

Bi. Lumuli ametaja Mradi wa Temeke Kota kuwa ni miongoni mwa miradi hiyo, akibainisha kuwa utekelezaji wa mpango huo utaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

"Tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi ili kwa pamoja tuweze kufanikisha lengo la Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 la kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu," amesema Bi. Lumuli.

Aidha, Bi. Lumuli amesema utekelezaji wa mradi huu unatokana na dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na yenye gharama nafuu.

Amesema TBA itaendelea kuhakikisha makundi yote, yakiwemo makundi maalum, yanafikiwa na kunufaika na programu hii ya nyumba za gharama nafuu.