Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe, amewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya kumuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ufunguzi wa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.
Mafunzo hayo yatafanyika kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026 katika Manispaa ya Sumbawanga, yakiwa yameratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).
Prof. Shemdoe alipokelewa katika Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Makongoro Nyerere akiambatana na Mhe. Mhe. Jacqueline Mzindakaya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.
Kesho, Julai 13, 2026, Prof. Shemdoe atafungua rasmi mafunzo hayo katika Ukumbi wa Country Hotel, ambapo yanatarajiwa kuwakutanisha wananchi, wajasiriamali, vikundi vya wanawake na vijana, makundi yenye mahitaji maalum pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu fursa za mitaji, mikopo na huduma mbalimbali za uwezeshaji zinazotolewa na Serikali na taasisi zake, ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji, kukuza biashara, kuongeza ajira na kuinua kipato cha familia.
Mafunzo hayo pia yanatarajiwa kuwapa washiriki taarifa sahihi kuhusu namna ya kufikia huduma za kifedha na programu za uwezeshaji wa kiuchumi, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Rukwa kwa ujumla.
![]() |
Ndani ya miaka sita nilifukuzwa kazi mara nne. Hali hiyo ilinivunja moyo sana. Marafiki waliniona kama mtu asiye na bahati, na hata familia yangu ilianza kunipotezea imani.
Siku moja, nikiwa nimekata tamaa kabisa, nilikutana na mwanaume mmoja ambaye nilikuwa nimewahi kufanya naye kazi zamani.
Watu wengi walinipongeza kwa mafanikio yangu, na niliamini maisha yangu yalikuwa yamekaa sawa. Lakini ghafla mambo yalianza kubadilika.
Nilimuita daktari wa mifugo mara kadhaa. Aliwachunguza waliobaki na kuwapa dawa, lakini bado vifo viliendelea.
Hasara ilianza kuwa kubwa. Nilishindwa kulipa ada za watoto na hata chakula cha mifugo kilianza kuwa tatizo.
Siku moja, mzee mmoja jirani yangu aliniuliza swali la ajabu. “Umeshawahi kukagua zizi lako usiku?” Nilimjibu hapana.
Aliniambia kuna mambo ambayo hayaonekani mchana. Alinieleza kuwa kuna watu wenye wivu wanaweza kutumia nguvu za giza kuharibu mifugo ya mtu anayefanikiwa. SOMA ZAIDI.
Siku moja nilipokuwa nikitoka darasani, niliitwa katika ofisi ya utawala. Nilidhani ni jambo la kawaida, lakini nilipoingia, nilikabidhiwa barua iliyosema kuwa nilikuwa nimefukuzwa chuo kutokana na deni la ada na madai ya ukiukaji wa kanuni za chuo.
Nilishangaa sana. Kwanza, nilikuwa nimebakiza kiasi kidogo sana cha ada ambacho nilikuwa nimeahidi kulipa baada ya mitihani. Pili, sikuwahi kuvunja sheria za chuo. Nilijaribu kujitetea lakini hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza.
Nilitoka ofisini nikiwa nimevunjika moyo. Nililia sana usiku huo. Niliona ndoto zangu zote zikifutika mbele ya macho yangu. Nilijiuliza ningewaambia nini wazazi wangu ambao walikuwa wamejitolea kila kitu ili nisome.
Rafiki yangu mmoja aliponiona katika hali hiyo, aliniambia nisikate tamaa. SOMA ZAIDI.
Katika kuonesha ujirani mwema Mbunge wa Kiteto Edward Ole Lekaita na Mbunge wa Kilindi Salehe Mhando wameamua kushirikiana kuhakikisha barabara ya Lengatei- Songe inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe na kupitika kwa mwaka mzima.
Mbali ya kushirikiana kusimamia Ujenzi wa barabara hiyo pia Wabunge hao wameshiriki shughuli ya uzinduzi wa shule ya awali na msingi Kijiji cha Lesiot Kata ya Lengatei Kiteto.
Na. Mwandishi Wetu
TUME ya Ushindani (FCC) imeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wajasiriamali kutoka Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kuhusu namna ya kutambua bidhaa bandia, kulinda haki za walaji na biashara ili kuimarisha ushindani wa haki nchini.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema maonesho hayo yameiwezesha tume hiyo kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa kuwapa elimu kuhusu haki za walaji, ulinzi wa biashara pamoja na huduma mbalimbali zinazotolewa na FCC.
"FCC inaendelea kupokea na kushughulikia malalamiko ya wananchi, kusajili mikataba na kutoa huduma nyingine zinazolenga kulinda maslahi ya walaji na wafanyabiashara."amesema
Aidha FCC imewahimiza wananchi na wafanyabiashara kuendelea kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu, kuripoti bidhaa bandia na ukiukwaji wa haki za biashara ili kujenga mazingira ya ushindani wa haki na kulinda maslahi ya walaji nchini.
Kwa upande wake Afisa Ushirikiano wa TWCC, Bw. Nelson Clevary, ameipongeza na kuishikuru FCC kwa mafunzo hayo, akisema yamewasaidia wajasiriamali kutambua bidhaa bandia, kulinda bidhaa zao na kuelewa umuhimu wa kusajili majina na nembo za biashara.
Amesema ushirikiano wa miaka mitatu kati ya TWCC na FCC umeongeza uelewa wa wafanyabiashara kuhusu athari za bidhaa bandia na umuhimu wa kushirikiana na mamlaka husika katika kukabiliana na vitendo vya udanganyifu wa kibiashara.
Naye mjasiriamali kutoka Mwanza, Praxeda Mgyabuso, amesema elimu inayotolewa na FCC imewasaidia wafanyabiashara na wananchi kutofautisha bidhaa halisi na bandia pamoja na kuelewa umuhimu wa kulinda utambulisho wa biashara zao.
Amesema awali wengi walikuwa wakinunua bidhaa kwa kuangalia bei pekee, lakini sasa wanafahamu athari za bidhaa bandia kwa afya, uchumi na biashara, pamoja na umuhimu wa kusajili alama na nembo za biashara.

Timu ya mpira wa miguu ya Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Sports Club imefanikiwa kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Championship msimu ujao 2026/2027 baada ya kufuzu kwa kupata sare ya goli 1-1 dhidi ya klabu ya African Sports kutoka Mkoani Tanga
Akizungumza baada ya kutamatika kwa mchezo Kocha Mkuu wa IAA SC Zulkifri Iddi amewapongeza wachezaji wake kwa kuipatia timu matokeo na kuthibitisha kuwa walifanikiwa kufuata maelekezo aliyowapa ndani ya dakika zote tisini, huku akiupongeza Uongozi wa Chuo IAA kwa sapoti kubwa walioitoa iliyopelekea kuandika historia hii kubwa kwa taasisi na jiji la Arusha
Akitoa pongezi Mwenyekiti wa mashindano chama cha soka Mkoa wa Arusha Emmanuel Antony ameisifu IAA SC kwa kuandika historia hii kubwa na kukiheshimisha chama cha soka Mkoa wa Arusha na kuahidi ushirikiano kwa timu kuhakikisha inafanya vizuri na kupiga hatua zaidi ili kufika hatua ya kushiriki Ligi kuu ya Tanzania
Kwa upande wake mchezaji wa IAA SC ambaye ndiye Mfungaji wa goli pekee la timu amewapongeza wachezaji wenzake, benchi la ufundi na Uongozi wa Chuo pamoja na mashabiki wao kwa kushirikiana kufanikisha kufikia mafanikio haya makubwa na kuahidi kuendelea kuipambania nembo ya IAA na jiji la Arusha msimu ujao kwenye mashindano ya Championship
IAA SC katika safari yake ya mafanikio haya ilifanikiwa kuibuka washindi wa ligi ya Wilaya ya Arusha, Ligi ya Mkoa, Ligi ya mabingwa wa Mikoa yote Tanzania na baadae Ligi daraja la pili (First League) na leo imefanikiwa kufuzu kutinga katika ligi daraja la kwanza (Championship) msimu wa mwaka 2026/2027

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika jengo la Kituo cha Polisi cha Kata ya Masasi, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.
Jengo hilo limejengwa na Bw. Iman Haule kupitia KUAMBIANA INVESTMENT COMPANY LIMITED ikiwa ni sehemu ya mchango wa sekta binafsi katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya usalama na kusogeza huduma za kipolisi karibu na wananchi.
Mhe. Naibu Waziri Mahundi amepongeza hatua hiyo, akieleza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya usalama unachangia kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao, kuongeza upatikanaji wa haki na kuleta mazingira wezeshi kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.











































