Na Mwandishi Wetu

WANAFUNZI wanaosoma mkondo wa elimu ya amali katika Shule ya Sekondari Dar es Salaam wameeleza kuwa ufadhili wa vifaa vya ushonaji uliotolewa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) umeleta mapinduzi makubwa katika utoaji wa mafunzo ya vitendo, hatua inayowajengea uwezo wa kujiajiri na kuanzisha biashara mara baada ya kuhitimu masomo yao.

Kiwanga Doctors wanaendelea kujijengea jina miongoni mwa watu wanaotafuta msaada wa kushughulikia changamoto zinazowakabili katika maisha ya kila siku. Kwa mujibu wa wateja mbalimbali waliowahi kutafuta huduma zao, wamekuwa wakipata ushauri na mwongozo unaowasaidia kurejesha matumaini katika nyanja tofauti za maisha.

Baadhi ya wateja wanasema walifika Kiwanga Doctors wakikabiliwa na migogoro ya ndoa iliyokuwa imechukua muda mrefu bila kupata suluhisho. Kwa mujibu wao, baada ya kufuata ushauri walioupokea, mahusiano yao yalianza kuimarika na familia zao kurejea katika hali ya maelewano.

Katika upande wa biashara, wapo wafanyabiashara wanaodai walikuwa wakipitia kipindi kigumu cha kushuka kwa mauzo na hasara za mara kwa mara. Wanasema walipopata ushauri kutoka Kiwanga Doctors walirejea kufanya biashara kwa ari mpya, jambo ambalo, kwa mujibu wao, liliwasaidia kuona mabadiliko chanya katika shughuli zao za kila siku.SOMA ZAIDI.
MKwa watu wengi, changamoto za mahusiano zinaweza kuleta maumivu makubwa, hasa pale penzi linapovunjika au mwenza anapoondoka bila matarajio ya kurejea. Hata hivyo, baadhi ya wateja wanasema walipata mwongozo uliowapa matumaini mapya wakati walipokuwa wamekata tamaa.

Kwa mujibu wa ushuhuda wao, baadhi yao walikuwa wameachwa na wenza wao, ndoa zilikuwa ukingoni kuvunjika, huku wengine wakidai walikuwa wamepoteza mawasiliano kabisa na watu waliowapenda. Wanasema baada ya kufuata ushauri walioupokea, mahusiano yao yalianza kuboreka hatua kwa hatua, mawasiliano yakarejea na katika baadhi ya matukio walifanikiwa kupatana tena na wapenzi wao.

Wengine pia wanasema walikuwa wakikabiliwa na migogoro ya mara kwa mara ndani ya ndoa, ukosefu wa maelewano na kutokuaminiana. Kwa mujibu wao, walipata mwongozo uliowasaidia kujenga upya mahusiano yao na kurejesha ut. SOMA ZAIDI.
Kupata ajira ni changamoto inayowakabili watu wengi, hasa baada ya kutuma maombi mengi bila kuitwa kwenye usaili. Hata hivyo, baadhi ya wateja wanasema walipata matumaini mapya baada ya kutafuta ushauri walipokuwa wamekata tamaa.

Kwa mujibu wa ushuhuda wao, baadhi yao walikuwa wamekaa kwa muda mrefu bila kazi licha ya kuwa na elimu na uzoefu unaohitajika. Wanasema walipopata mwongozo na kufuata ushauri walioupokea, walianza kuona mabadiliko, ikiwa ni pamoja na kuitwa kwenye usaili na baadaye kupata nafasi za ajira walizokuwa wakizitafuta.

Wengine wanadai walikuwa wakikosa mafanikio ya mara kwa mara katika maombi ya kazi, huku wengine wakisema walikuwa wakikwama katika hatua za mwisho za usaili. Kwa mujibu wao, walirejea na ushuhuda wakisema walipata fursa zilizowabadilisha maisha yao.

Baadhi ya wateja pia wanasema walipata maendeleo katika biashara, ongezeko la wateja na kuimarika kwa shughuli zao za kiuchumi baada ya kupata ushauri. Wengine wanadai walifanikiwa kurejesha kujiamini na mtazamo chanya uliowasaidia kufuatilia malengo yao kwa bidii zaidi. SOMA ZAIDI.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka Watanzania kuendelea kutembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), akisema maonesho ya mwaka huu 2026 yameonesha mafanikio makubwa ya maendeleo ya viwanda, ubunifu wa teknolojia na ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini.

Akizungumza Julai 08, 2026 baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho hayo, Kapinga amesema mwitikio wa wananchi ni mkubwa kiasi kwamba Serikali inatafakari kuongeza siku moja ya maonesho ili kutoa nafasi kwa wananchi wengi zaidi kushiriki na wafanyabiashara kuendelea kufanya biashara.

Amesema ukubwa wa maonesho hayo unamlazimu kuyatembelea mara kwa mara kwa kuwa haiwezekani kuona mabanda yote kwa siku moja, huku akieleza kuridhishwa na namna waoneshaji walivyojiandaa na ubora wa bidhaa zinazooneshwa.

Waziri Kapinga amesema maonesho ya mwaka 2026 yamebeba teknolojia mbalimbali za kisasa, ikiwemo magari yanayotumia umeme, magari ya mseto (hybrid), magari yanayotumia gesi asilia (CNG) kwa asilimia 100 pamoja na mitambo ya kisasa inayotumia umeme, hatua inayoonesha ukuaji wa sekta ya viwanda na matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira.

Aidha, amesema bidhaa za ndani zimeendelea kuongezeka ubora, hususan katika thamani na vifungashio, jambo linalodhihirisha mafanikio ya uwekezaji wa Serikali katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kukuza uzalishaji wa ndani.

"Wananchi waendelee kujitokeza kutembelea Sabasaba. Fursa zilizopo mwaka huu ni nyingi zaidi, hivyo ni wakati mzuri wa kujifunza, kufanya biashara na kuona maendeleo ya viwanda vya Tanzania," amesema Kapinga.

Ameongeza kuwa iwapo uamuzi wa kuongeza siku moja ya maonesho utapitishwa, utalenga kuwapa wananchi, hasa wanaokuwa kazini siku za kawaida, nafasi zaidi ya kutembelea maonesho hayo na kunufaika na fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa kaitika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Zanzibar

KIZIMKAZI Kumenoga! Hiyo ndio kauli mbiu iliyobeba Tamasha la Kizimkazi 20226 linatarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 12 hadi Agosti 14 mwaka huu likiwa limesheheni fursa lukuki .
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa Maonesho ya Sabasaba yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Alice Mtulo (aliyesimama katikati) akiwa pamoja na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Na.Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Mazungumzo ya Viongozi hao yamelenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar katika sekta ya kazi na ajira, hususan eneo la kukuza maendeleo ya rasilimali watu, ulinzi na haki za wafanyakazi pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania.

Vilevile, wamejadili kuhusu Mkutano wa Uhamaji wa Wafanyakazi (Labour Mobility Dialogue) utakaowakutanisha nchi wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Nchi za Ghuba (GCC), Jordan, Lebanon na nchi za Afrika zinazotuma wafanyakazi nje ya nchi chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika (African Union). Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Oktoba 2026 Tanzania, jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na kupanua fursa za ajira salama na zenye staha kwa wananchi wa nchi shiriki.

Katika kikao hicho, Waziri Sangu aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Jane Songoro.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akimkabidhi tuzo Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, tuzo ya kutambua ushirikiano katika ya Tanzaniana Qatar katika masuala ya Ajira, leo Julai 8, 2026, katika Ofisi za Wizara hiyo ya Kazi Jijini Doha, nchini Qatar.

 


Munir Shemweta, Misungwi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo amewatahadharisha viongozi wa vijiji nchini kuacha kujihusisha moja kwa moja na uuzaji wa ardhi bila kufuata taratibu za kisheria, akisema tabia hiyo imekuwa chanzo kikubwa cha migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini.

Dkt. Akwilapo ametoa onyo hilo Julai 6, 2026 wilayani Misungwi mkoani Mwanza wakati wa hafla ya kukabidhi hati 668 za hakimiliki za kimila kwa wananchi wa vijiji vya Ndinga na Lubuga. Alisisitiza kuwa viongozi wa vijiji, wakiwemo wenyeviti, ni wasimamizi wa ardhi na si wauzaji, hivyo maamuzi ya kuuza ardhi ya kijiji yanapaswa kufanywa kwa kufuata sheria kupitia mikutano ya vijiji na kupata ridhaa ya halmashauri husika.

"Mnapotaka kuuza ardhi kwa watu lazima kijiji kupitia mikutano ya kijiji na halmashauri kikubaliane na hilo. Asije akawa mwenyekiti anaingia kwenye makubaliano peke yake. Tunapiga vita suala hilo kwa sababu limetuingiza kwenye matatizo mengi katika maeneo mbalimbali," alisema Dkt. Akwilapo, akibainisha kuwa kauli hiyo inawahusu viongozi wa vijiji kote nchini na si Misungwi pekee.

Waziri huyo pia alisisitiza kuwa Serikali haitavumilia ubaguzi wa aina yoyote katika umiliki wa ardhi, ikiwemo ubaguzi wa kijinsia, kikabila au kwa misingi mingine. Alieleza kuwa sera na sheria za ardhi zinatambua haki sawa kwa wananchi wote kumiliki ardhi, huku wataalamu wa sekta hiyo wakitakiwa kuendelea kuzisimamia ipasavyo ili kuhakikisha haki inatendeka kwa kila Mtanzania.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Bi. Johari Simizi alisema wilaya hiyo kwa sasa ndiyo eneo linalopokea kasi kubwa ya ukuaji wa makazi kutoka maeneo mengine ya Mkoa wa Mwanza, hali inayohitaji upangaji bora wa matumizi ya ardhi.

Alisema wananchi wa Misungwi wanahitaji mji uliopangwa vizuri kupitia umilikishwaji rasmi wa ardhi ili kuondoa makazi holela na kuifanya wilaya hiyo kuwa na mwonekano unaovutia.

Naye Mbunge wa Jimbo la Misungwi, Mhe. Silvery Salvatory aliitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuongeza elimu kwa wananchi kuhusu matumizi na umuhimu wa nyaraka za umiliki wa ardhi, akisema baadhi ya wanufaika wa hati bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu haki na wajibu unaoambatana na nyaraka hizo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Mwanza, Bw. Wilson Luge aliwapongeza wananchi wa Misungwi kwa mwitikio mkubwa wa kushiriki zoezi la urasimishaji wa ardhi, akisema hatua hiyo imeifanya wilaya hiyo kuwa mfano wa kuigwa na maeneo mengine katika juhudi za kupunguza migogoro ya ardhi kupitia upimaji na utoaji wa hati za umiliki.

Kwa niaba ya wanufaika, Bw. Shije Mashaka aliishukuru Serikali kwa kuwawezesha wananchi kumiliki ardhi kwa hati za hakimiliki za kimila, akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa migogoro ya mipaka iliyokuwa ikiwasumbua kwa muda mrefu.

Katika utekelezaji wa mradi wa upangaji na upimaji ardhi, Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoa wa Mwanza iliipa kampuni ya GMS Geo Tech Consultancy Co. Ltd kazi ya kupima vijiji vya Ndinga na Lubuga, ambapo jumla ya hati 668 zilitolewa kwa wananchi katika awamu ya kwanza ya mradi huo.





 



Na.Ashura Mohamed-Arusha 

Maonesho ya Sanaa ya  Kazi za Ufundi,Uchoraji na Uchongaji yanatarajia kukutanisha zaidi ya wasanii 1500 duniani  lengo likiwa ni kutangaza na kukuza saana ya Ufundi nchini ikiwa ni pamoja na kuwafungulia Masoko ya kimataifa wasanii hao.

Akizungumza Jijini Arusha na Waandishi wa Habari kuhusiana na Maonesho hayo,Makurugenzi mwenza wa Tanzania International Tourism Festival bwana Ibrahim Jama amesema wanalenga kutangaza utalii na utamaduni pamoja na vivutio vilivyo ndani ya nchi ya Tanzania.

"Katika kudumisha utalii,sanaa na utamaduni  Wetu ni maonyesho  haya yatakuwa yenye vivutio vya sanaa ya uchongaji na pia kutakuwa na warsha ya kuelekeza kuhusu sanaa nzima ya uchongaji yenye maelekezo ya elimu na Maendeleo na kulinda sanaa ya uchongaji."Alisisitiza Ibrahim 

Pia amesema kuwa wasanii hao watapata fursa ya kupata ya kupata elimu kuhusu sanaa nzima mwenendo halisi wa soko la sanaa  ndani ya nchi katika uchongaji na uchoraji na michezo kujua wajibu wao katika kuingiza kipato kikubwa haswa fedha za. kigeni.

Aidha Wadau ambao watashiriki mkutano huo watapata fursa ya kutembelea vivutio vilivyopo katika Mkoa wa Arusha ili kuendelea kuiunga Mkono  serikali katika kuendeleza utalii wa ndani pamoja na maonyesho ya bidhaa za Uchoraji na Uchongaji yatakayofanyika kwa siku tatu.

Bi Rukia Walele ni Raisi wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA ) amesema kuwa Shirikisho hilo linaundwa na wachoraji,wachongaji,wasusi,wanaofuma vitambaa,Wanamitindo na wabunifu wa Mavazi na Viatu   ambapo lengo ni kutoa elimu Maalum ya sekta ya Utalii ili kutumia majukwaa hayo kupata elimu zaidi na ushiriki wa kundi hilo bado sio wa kuridhisha.

Kupitia maonyesho hayo watawezeshwa kuingia katika mfumo rasmi wa kupata kipato na kupata Maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na kuliingizia Taifa fedha za kigeni.






 


Na OWM–TAMISEMI, Ifakara

Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ifakara wanatarajia kunufaika na huduma za kulaza wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Ifakara mara baada ya Serikali kuahidi kutoa Shilingi Milioni 700 ndani ya mwezi Julai, 2026 kwa ajili ya kukamilisha miundombinu muhimu itakayowezesha hospitali hiyo kuanza kutoa huduma hiyo kwa wagonjwa.

Ahadi hiyo ya Serikali imetolewa na Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Julai 6, 2026 akiwa kata ya Kiberege, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo, ambapo alipokea taarifa za utekelezaji wa miradi ya nyumba nne za Wakuu wa Idara, majengo matatu ya Hospitali ya Wilaya na Soko la Kiberege na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo. 

Prof. Shemdoe amesema Serikali itapeleka Shilingi Milioni 700 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la utawala, chumba cha kuhifadhia maiti pamoja na njia za kupita (walkways) katika Hospitali ya Wilaya ya Ifakara, ili kuwezesha hospitali hiyo kuanza rasmi huduma za kulaza wagonjwa na kupunguza adha iliyokuwa ikiwakabili wananchi kutafuta huduma hizo mbali na maeneo yao.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, fedha hizo zinaakisi dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuimarisha huduma za afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na makazi yao na kuongeza kuwa, wananchi wanapaswa kuendelea kulinda amani na utulivu uliopo ili Serikali iendelee kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya umma na taifa.

"Fedha hizi ni ishara ya upendo wa Rais Samia kwa wananchi wa Ifakara. Anawapenda na ameazimia kuona huduma za afya zinaboreshwa na maisha ya wananchi yanabadilika kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo," amesema Prof. Shemdoe.

Mbali na sekta ya afya, Prof. Shemdoe amesema Serikali itatoa Shilingi Milioni  330 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mkasu kama ilivyotoa  Shilingi Milioni 191 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa soko la Kiberege, miradi inayolenga kuboresha huduma ya usafiri na usafirishaji, biashara  pamoja na kuinua uchumi wa wananchi.

Akizungumzia utekelezaji wa ujenzi wa barabara zenye urefu kilomita 10,   Prof. Shemdoe amemuelekeza Mhe. Sultan Kwanja, Diwani wa Kata ya Kiberege kuweka kipaumbele katika ujenzi wa barabara zinazoelekea kwenye maeneo yenye shughuli za kilimo ili kurahisisha usafirishaji wa mazao na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi. 

Kwa upande wake, Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, amesema ziara ya Mhe. Prof. Shemdoe imelenga kutatua changamoto za wananchi na si kufanya ziara zenye mlengo wa kuwahadaa wananchi.

"Waziri wa TAMISEMI hajaja kufanya sanaa; amekuja kushughulikia changamoto za wananchi, ndiyo maana aliposikia changamoto ya barabara ameambatana na Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro pamoja na Meneja wa TARURA Wilaya ya Ifakara ili kuhakikisha suala hilo linapatiwa ufumbuzi," amesema Mhe. Malima.

Naye, Mhe. Abubakari Asenga, Mbunge wa Jimbo la Ifakara, amewahakikishia wananchi kuwa ujenzi wa barabara za mitaa utasimamiwa kwa karibu chini ya uongozi wa Prof. Shemdoe, akibainisha kuwa mafanikio yaliyopatikana katika upatikanaji wa fedha za soko la Kiberege yanaonesha dhamira ya Serikali ya kutekeleza pia miradi mingine ya maendeleo.

Akiwa wilayani Ifakara, Prof. Shemdoe amekagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo nyumba nne za wakuu wa idara, majengo matatu ya hospitali ya wilaya ya Ifakara na soko la Kiberege, ikiwa ni pamoja na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma.

Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema Tanzania na Qatar zimeendelea kushiurikiana kwa karibu katika sekta mbalimbali, ikiwemo masuala ya ajira ambapo tangu nchi hizo ziliposaini makubaliano ya ushirikiano wa ajira mwaka 2018 mafanikio makubwa yameonekana katika kuongezeka kwa fursa za ajira kwa Watanzania.

Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu na Ubora wa WRRB, Bw. Mwita Thomas,akizungumza wakati wa ufungaji mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika Morogoro.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufunga  mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Na.Mwandishi Wetu-MOROGORO

Watumishi na wasimamizi wa shughuli za ghala nchini wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji ili kuimarisha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuongeza ufanisi katika biashara ya mazao ya kilimo.

Wito huo umetolewa na Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, alipokuwa akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo.

Bi. Chatta amesema uadilifu wa watendaji wa mfumo ni msingi wa kujenga imani kwa wakulima, wanunuzi na taasisi za fedha, huku akisisitiza kuwa Mfumo huo umeendelea kuwa nyenzo muhimu ya kuhakikisha biashara ya mazao inafanyika kwa uwazi, ubora na ushindani.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhimiza matumizi ya Mfumo huo pamoja na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) ili kuongeza thamani ya mazao, kupanua fursa za masoko yenye ushindani na kuongeza manufaa kwa wakulima.

Aidha, amewataka washiriki kutumia maarifa waliyoyapata kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kuendana na mabadiliko ya teknolojia na kuhakikisha taarifa za mazao zinakuwa sahihi na kwa wakati.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu na Ubora wa WRRB, Bw. Mwita Thomas, amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kuzingatia sheria, kanuni na taratibu walizofundishwa ili kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji, pamoja na kulinda hadhi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na WRRB yamefanyika kwa siku tano na yamehudhuriwa na washiriki 103 kutoka kampuni za uendeshaji wa ghala na wadau mbalimbali wa Mfumo huo.


Siku zote alikuwa miongoni mwa wale wanaopinga imani yoyote inayohusiana na mambo ya kiroho au usaidizi wa kipekee nje ya hospitali na sheria za kawaida.

Jina lake ni Brian, na alikuwa rafiki yangu wa karibu tangu chuo kikuu. Mcheshi, mwenye akili nyingi, lakini mwenye misimamo mikali isiyoyumba hasa linapokuja suala la imani zisizo za kisayansi.

Lakini maisha ni walimu wakubwa kuliko vitabu. Na wakati mwingine, hata wasioamini, hupata sababu ya kufikiri upya. Brian alikuwa kwenye uhusiano wa muda mrefu na msichana aitwaye Hellen. Walikuwa kama mfano wa wapenzi bora mitandaoni. Picha za mapenzi, safari, zawadi ilikuwa ni hadithi ya kisasa ya upendo.

Hata hivyo, mambo yalianza kubadilika mwaka jana, pale Brian alipogundua kwamba Hellen alikuwa akiongea kwa karibu sana na jamaa mmoja wa kazini kwake. Awali alipuuzia, akiamini ni wivu tu wa kawaida. Lakini alipoanza kuona ujumbe mfupi wa siri, mazungumzo ya sauti usiku wa manane, na safari za ghafla zisizoelezeka, alijua kuna jambo. SOMA ZAIDI.
Kila usiku nilikuwa na hofu. Niliozidi kulala na mapambano ya kiakili. Kila nilipolala, niliona jini likinifuatilia. 

Hii haikuwa ndoto tu, bali ilikua ni hali ya kutisha, na nilijua kuwa nilihitaji msaada wa haraka. Nilijua kwamba siyo ugonjwa wa akili, bali jambo la kiroho.

Nilijaribu njia nyingi za kujitibu, nikitembelea madaktari na kutumia dawa za hospitali, lakini hakuna kilichobadilika. Nilikuwa nikikosa usingizi na kujikuta nikiishi na hofu ya kila wakati. Hali hii ilianza kuathiri maisha yangu ya kila siku, hata kazi yangu.

Nilikuwa mchovu, mwenye huzuni, na nashindwa kuendelea mbele. SOMA ZAIDI.
Saa nane usiku, kelele za maji zikimiminika chini ya godoro zilinifanya nijishtukie tena. Nilikuwa mtu mzima, lakini nilijikuta nimelowa kitandani kwa mara nyingine tena. 

Nililia kimoyomoyo, nikajiuliza ni lini hali hii ya kuaibisha ingeisha. Nikiwa na miaka 35, bado nilikuwa nikikumbwa na tatizo la kujikojolea usingizini hali iliyokuwa imenifanya niishi kwa siri, aibu na fedheha tangu nilipokuwa msichana mdogo.

Nilijaribu kila njia. Nilihudhuria kliniki za kibingwa, nikatumia dawa za gharama kubwa, nilijaribu hata mashine maalum za mazoezi ya nyonga. Madaktari walinitia moyo kuwa inaweza kuisha kwa muda, lakini mwaka ulipita baada ya mwingine, hali haikubadilika.

Nilijiepusha na mahusiano ya karibu, nikaacha safari za usiku, na hata kazi zilizoitaji kulala nje niliziacha all kwa sababu ya haya. Mara moja nikiwa kazini, niliitwa kwenye kikao cha wafanyakazi cha kusafiri nje ya jiji. Kwa kisingizio cha afya, niliomba nisiende.

Lakini macho ya baadhi ya wenzangu yalinielekea kwa mashaka. Nilihisi kama watu walikuwa wakianza kugundua kuwa kuna kitu kisicho cha kawaida kwangu. Ukweli ni kwamba nilikuwa nimechoka kujificha. Nilihitaji mabadiliko. SOMA ZAIDI.