​Na. OWM (KAM) Mwanga

​Serikali imezitaka taasisi na viongozi wa dini nchini kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhubiri maadili mema, mshikamano na uvumilivu ili kujenga jamii yenye amani, utulivu na uchaji wa Mungu.

 


Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) limeendelea kuvutia makundi mbalimbali ya wananchi katika Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza, ikiwa ni siku ya tatu, Agosti 30, 2026.

Makundi hayo yameonesha kuvutiwa na elimu ya vipimo tofauti tofauti.

Wakiwa bandani hapo, wengi wa wanafunzi na vijana wameonesha kuvutiwa zaidi na elimu ya matumizi  ya mizani za kielektroniki na pampu za kupimia mafuta.

 Wamesema elimu hiyo inawapa uelewa wa kuwa mabalozi wa vipimo shuleni na majumbani mwao huku wengine wakidai ndoto yao ni kuwa Maafisa Vipimo wa baadae.

Kwa upande wa akina mama wajasiriamali, wengi  wamejikita kujifunza kuhusu matumizi sahihi ya mizani  inayotumika masokoni na waliuliza maswali mengi kuhusu namna ya kutambua ujazo wa mtungi wa gesi ya kupikia wanapoenda kununua.

 Wengi wameipongeza WMA kwa kuwaelimisha jinsi ya kuepuka hasara na kuhakikisha mteja anapata haki yake.

Askari na wazee waliotembelea Banda la WMA wameonesha kuvutiwa na elimu ya vipimo katika sekta ya mafuta ya petroli, saruji na bidhaa nyingine za ujenzi. Askari wamesema elimu hiyo itawasaidia katika doria za kuhakikisha biashara inafanyika kwa haki, wakati wazee wamesema wamepata uelewa mpya wa kulinda familia zao dhidi ya udanganyifu.

Wananchi wote waliotembelea banda hilo wamepongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kuwa na Wakala wa Vipimo nchini. Wamesema uwepo wa WMA umesaidia kulinda haki za walaji na kuweka mazingira bora ya biashara yanayosadifu kaulimbiu ya maonesho isemayo “Usalama na  Amani ni Kichocheo cha Biashara na Uwekezaji".

Kujenga familia na mume wako kwa miaka mingi ni safari inayohitaji juhudi na upendo wa dhati, lakini pale ambapo mwanamke mwingine anapoingilia ndoa yako na kumng’oa mume wako nyumbani, maumivu yake ni mazito mno.

Kwa miezi sita, nilipitia kipindi kigumu zaidi maishani mwangu baada ya mume wangu wa ndoa kufungasha virago na kunitelekeza mimi na watoto wetu. Alihamia kabisa kwa mwanamke mwingine aliyekuwa akimfanyia hila za kishirikina.

Mume wangu alibadilika ghafla; akaacha kutoa matumizi ya nyumbani, akakata mawasiliano na sisi, na hata nilipojaribu kumtafuta alinijibu kwa matusi makali na kusema hanitaki tena. Nilibaki nikilia usiku kucha huku watoto wakiniuliza baba yao yuko wapi, nikiwa sina wa kunisaidia.

​Nikiwa kwenye simanzi hiyo na nikikaribia kukata tamaa ya kuiokoa ndoa yangu, jirani yangu mmoja alinijia na kunieleza kuhusu njia za kiasili za kurejesha upendo na kumvuta mume aliyetoroka.

Alinishauri kwa dhati kuwasiliana na Kiwanga Doctors, wataalamu mashuhuri wanaosifika kwa kurudisha mapenzi kwenye ndoa, kuvunja michepuko na nyumba ndogo, na kumrudisha mume au mke aliyetoroka nyumbani ndani ya muda mfupi. SOMA ZAIDI.

Kufanya kazi kwa bidii na kujinyima kwa miaka mingi ili kuweka akiba ya maisha ni hatua inayotoa matumaini ya kuwa na maisha ya baadae yenye usalama.

Hata hivyo, pale mtu unayemwamini anapokugeuka, akachukua fedha zako zote na kukuacha ukiwa huna hata sarafu moja mfukoni, maumivu yake hayaelezeki.

Mfanyabiashara mmoja niliyemuchukulia kama ndugu alinishawishi kuwekeza fedha zangu zote kwenye biashara yake kwa ahadi ya kuanza kugawana faida.

Baada ya kumkabidhi mamilioni ya shilingi niliyokuwa nimejikusanyia kwa jasho na damu, alianza kunikimbia. 

Kila nilipomfuata anidai au anirudishie mtaji wangu, alinikejeli, kunitishia na hata kunicheka mbele ya watu akidai sina lolote la kumfanya kwani anafahamu watu wengi wenye ushawishi.

​Nilibaki nikiteseka na msongo mkubwa wa mawazo, nikishindwa kulipa kodi ya nyumba na hata kununua chakula cha familia yangu.

Nikiwa kwenye machungu hayo, rafiki yangu wa karibu alinishauri nitafute msaada wa kiasili ili kumtia adhabu mtu huyo na kumlazimisha arudishe haki yangu. SOMA ZAIDI.
Kufikisha umri wa miaka arobaini nikiwa bado nipo peke yangu bila mume au familia ilikuwa ni chanzo cha maumivu makubwa na msongo wa mawazo katika maisha yangu.

Kila siku niliwatazama rafiki zangu wa rika moja, wadogo zangu, na hata majirani wakifunga ndoa na kujenga familia zenye furaha, huku mimi nikibaki nikilia kwa siri nyumbani kwangu.

Kila mwanamume aliyekuja kwenye maisha yangu na kuonyesha nia ya kunioa, pindi tu alipokaribia kuchukua hatua za kutambulishwa nyumbani, alitoweka ghafla bila sababu yoyote ya msingi au kuanzisha migogoro ya ajabu na kuondoka.

Nilibaki nikidharaulika mtaani, nikipewa majina ya kejeli na ndugu, huku nikianza kukubaliana na matokeo kuwa labda nimezaliwa niishi peke yangu hadi uzee.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito, shangazi yangu aliyekuwa akifahamu mateso yangu alinitembelea na kunieleza kuwa matatizo ya kukataliwa na kukosa mume katika umri mkubwa mara nyingi hutokana na nyota ya mahaba kufungwa na maadui au kuvishwa ukungu wa kishirikina unaowafanya wanaume waone huna mvuto. SOMA ZAIDI.

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) uko kwenye mchakato wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Sura ya 395, kwa lengo la kupanua wigo wa wanachama, kuendana na mahitaji ya sasa ya huduma za afya na kuimarisha uendelevu wa Mfuko.

Marekebisho hayo pia yanalenga kuimarisha udhibiti wa matumizi mabaya ya Mfuko, ikiwemo udanganyifu unaoweza kufanywa na baadhi ya wanachama, waajiri na watoa huduma za afya lakini kwenda sambamba na sheria Mama ya Bima ya Afya kwa Wote.

Akizungumza  katika ukumbi wa mikutano wa NHIF, Kinondoni, Dar es Salaam, wakati wa kupokea maoni ya wadau kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya sheria hiyo, Meneja wa Huduma za Sheria wa NHIF, Matamus Fungo, amesema sheria hiyo iliyotungwa mwaka 1999 inahitaji maboresho ili iendane na mabadiliko yaliyopo katika sekta ya afya na mwelekeo wa utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.

“Tunataka sheria yetu iweze kuboreshwa ili iwezeshe watu wengi zaidi kujiunga na pia kuziba mianya ya matumizi mabaya ya kadi yanayofanywa na baadhi ya wanachama wasio waaminifu” amesema.

Amesema marekebisho hayo yanatarajiwa kuongeza idadi ya wanachama, kuimarisha uendelevu wa Mfuko na kuweka mifumo madhubuti zaidi ya kudhibiti udanganyifu na matumizi yasiyofaa ya huduma za bima ya afya.

Kuzingatia Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote

Kwa upande wake, Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Mwenda Tulalemwa, amesema marekebisho ya sheria yanapaswa kuzingatia mahitaji ya makundi mbalimbali ya wananchi pamoja na kuendana na Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, ili kuhakikisha hakuna mgongano wa kisheria.

Amesema wadau waliotoa maoni wamependekeza maboresho katika maeneo mbalimbali, ikiwemo mfumo wa malipo kwa vituo vya kutolea huduma za afya, huduma kwa watu wasio na uwezo na watu wenye ulemavu.

Aidha, miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa ni kuongeza umri wa watoto wanaotambuliwa kama wategemezi kutoka miaka 21 hadi 25, hatua inayolenga kuendana na mahitaji ya familia na mazingira ya sasa.

Naye Wakili wa Mahakama Kuu na mwanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Ferdinand Makole, amesema marekebisho ya sheria yanaweza kuwa fursa muhimu ya kuongeza urahisi, ufanisi na ubora wa huduma zinazotolewa na NHIF.

Amesema sheria inapaswa kuweka mazingira yatakayowezesha Mfuko kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wanachama na wananchi kwa ujumla, huku ikizingatia uendelevu wa Mfuko.

Kwa upande wake, Mwanasheria wa Bohari ya Dawa (MSD), Brighton Mtigani, amesema ushirikishwaji wa wananchi na wadau mbalimbali ni muhimu katika kuhakikisha sheria inayoandaliwa inaendana na mahitaji yanayobadilika ya jamii.

Amesema ushirikishwaji huo utasaidia kujenga mfumo unaozingatia usawa katika upatikanaji wa huduma za afya na kuhakikisha makundi mbalimbali yanapata huduma bila vikwazo visivyokuwa vya lazima.

Maoni ya wadau kuchangia maboresho ya rasimu

Naye Ofisa Sheria Mwandamizi kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Japhes Daudi, amesema maoni yaliyotolewa na wadau yamechukuliwa na yataendelea kutumika katika kuboresha rasimu ya mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Kwa ujumla, mchakato huo unalenga kuhakikisha Sheria ya NHIF inaendana na mazingira ya sasa ya utoaji wa huduma za afya na mwelekeo wa Serikali wa kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya kupitia mfumo wa Bima ya Afya kwa Wote.

Marekebisho hayo yanatarajiwa kupanua wigo wa wananchi wanaoweza kunufaika na bima ya afya, kuimarisha udhibiti wa matumizi ya Mfuko, kuboresha huduma kwa wanachama na kuimarisha uendelevu wa NHIF, sambamba na kuchangia utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote nchini.

 

*Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge sasa*

 

WALIMU 328 kutoka shule 10 za Sekondari katika Jiji la Tanga wanapigwa msasa kupitia semina maalumu inayolenga kuwaongezea ujuzi na mbinu za ufundishaji, hatua inayolenga kuongeza ufaulu wa wanafunzi wa Kidato cha Pili na Nne.

Semina hiyo inaendeshwa na Taasisi ya Tanzania Centre For Education kupitia mradi wa Tanga Yetu, unaofadhiliwa na Foundation Botnar na kutekelezwa kwa kushirikiana na Innovex, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kukuza ufaulu katika shule za Jiji la Tanga.

Akizungumza wakati wa semina hiyo iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Nguvumali,   Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Centre for Education Yusuf Ogutu  alisema mafunzo hayo ni mwendelezo wa semina zilizolenga kuwajengea uwezo walimu katika masomo mbalimbali.
Alisema katika hatua hiyo walimu wa masomo ya Historia, Jiografia, Business Studies na Bookkeeping wamepatiwa mafunzo, huku awali semina ikiwa imefanyika katika Shule ya Sekondari Kihere kwa walimu wa Civics, Kiswahili, Kiingereza, Historia ya Tanzania na Maadili.

Ogutu alisema mpango huo unalenga kuhakikisha walimu wanakuwa na uelewa na lugha moja katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanafunzi na hatimaye kuboresha ufaulu.

“Tunawapatia walimu maarifa na mafunzo, pamoja na kuwawezesha gharama za usafiri kutoka walikotoka na kurejea. Hii ni sehemu ya mpango mpana wa kuhakikisha kampeni ya kukuza ufaulu katika Jiji la Tanga inafikia malengo,” alisema.
Alisema kampeni hiyo inatekelezwa kwa hatua mbalimbali, ambapo awamu ya kwanza iliwahusisha wanafunzi, hatua ya pili ni walimu na awamu inayofuata itawahusisha waratibu wa elimu ngazi ya kata, maafisa elimu wa wilaya pamoja na kamati za malezi na wazazi.

Kwa mujibu wa Ogutu, mpango huo unalenga kuwafanya wadau hao kuwa na uelewa unaofanana katika kuhakikisha wanashirikiana kutafuta suluhisho la changamoto zinazoathiri ufaulu wa wanafunzi.

Alisema hadi sasa walimu 85 tayari wamefikiwa kupitia mafunzo hayo, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka hadi kufikia walimu 100 katika awamu inayoendelea, kabla ya kukamilishwa kwa mafunzo ya walimu wa masomo ya sayansi.
Ogutu alisema jumla ya walimu 328 katika shule 10 wanatarajiwa kunufaika na mpango huo, ambao unalenga kutoa mchango katika kuboresha matokeo ya wanafunzi wa Jiji la Tanga.

Wakufunzi kutoka shule bora
Aidha, alisema walimu wanaopatiwa mafunzo hayo wanafundishwa na wakufunzi wenye uzoefu kutoka baadhi ya shule zilizofanya vizuri kitaifa, hatua inayolenga kuwapatia mbinu bora za ufundishaji.

Alizitaja baadhi ya shule hizo kuwa ni Mzumbe, Marian Boys na Feza Boys, ambazo zimekuwa zikifanya vizuri katika mitihani ya kitaifa.
Alisema pia kuna wakufunzi kutoka Canossa pamoja na shule mbalimbali za Serikali zilizowahi kufanya vizuri kitaifa.

“Tunawaamini sana walimu kwa sababu wao ndiyo injini ya matokeo. Ukiwapiga msasa walimu na kuwaongezea uwezo, unakuwa umeweka msingi mzuri wa kuboresha ufaulu wa wanafunzi,” alisema.
Alisema katika semina hizo walimu wanapata nafasi ya kujadili changamoto mbalimbali za ufundishaji, ikiwemo mada ambazo zimekuwa zikiwasumbua, ili kupata ufumbuzi na kuhakikisha wanakuwa na uelewa unaofanana katika ufundishaji.

Alisema kupitia mpango huo, matarajio ni kuona walimu wakiboresha namna ya kufundisha na wanafunzi wakipata uelewa mzuri wa masomo, jambo litakalosaidia kuongeza ufaulu katika mitihani ya Kidato cha Pili na Nne.
Mpango huo ni sehemu ya juhudi za Tanga Yetu za kuwaunganisha wanafunzi, walimu, wazazi na wadau wengine wa elimu katika kutafuta njia za kuboresha kiwango cha ufaulu katika shule za Jiji la Tanga.
Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe. Louis Peter Bura akifungua mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na OSHA kwa kikundi cha mafundi wanaojihusisha na uchomeleaji vyuma na useremala katika Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyamirembe, Wilaya ya Chato Mkoani Geita.



Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amekitaka Chama cha Wazee Wanaume Tanzania (CCWWT) kutokuwa chama cha harakati, bali kutumia nafasi yake katika kutoa ushauri, kupatanisha jamii, kulea watoto na vijana, pamoja na kuhifadhi mila na desturi za Kitanzania.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo Agosti 29, 2026, katika Ukumbi wa St. Gaspar jijini Dodoma, wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa CCWWT kwa mwaka 2026, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

Amesema wazee wana nafasi ya kipekee katika jamii ya Kitanzania kutokana na heshima na hadhi waliyonayo, akieleza kuwa wamekuwa walinzi wa mila na desturi, washauri, wapatanishi na walezi wa watoto, vijana na jamii kwa ujumla.

“Wazee mna kazi kubwa na ya msingi ya kuhifadhi mila na desturi za Kitanzania, kuwa washauri na wapatanishi wazuri katika jamii, ikiwa ni pamoja na walezi wa jamii ya Kitanzania, hivyo, tekelezeni majukumu ya chama chenu kwa mujibu wa katiba yenu,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua wazee kama rasilimali na hazina kubwa katika maendeleo ya taifa, akibainisha kuwa uwepo wa Tanzania kama taifa ni kielelezo cha mchango mkubwa uliotolewa na wazee katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Prof. Shemdoe amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha maisha ya wazee nchini, sambamba na kuimarisha mifumo ya utoaji huduma kwa makundi yote bila ubaguzi. Ametaja miongoni mwa hatua hizo kuwa ni kuwekwa kwa mifumo ya kisheria inayolenga kuimarisha upatikanaji wa huduma, ikiwemo kutungwa kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote Na. 13 ya Mwaka 2023.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amesema Tanzania imefikia hatua ilipo leo kutokana na mchango mkubwa wa wazee ambao ni tunu ya taifa.

Amesema wazee wamejenga familia, wamelea watoto, wamefundisha vijana, wamejenga taasisi na kulitumikia taifa, hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya nchi. Kwa msingi huo, amesema taifa linapaswa kutumia ipasavyo maarifa, uzoefu na hekima walizonazo wazee kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Akizungumza kwa niaba ya wazee, Katibu Mkuu wa CCWWT, Bw. Flavianus Lughuyu, amesema licha ya wazee kuacha alama kubwa katika historia ya taifa, bado kuna haja ya kujenga mifumo imara ya kuwaenzi na kutambua mchango wao.

Amesema historia na uzoefu wa wazee vinapaswa kutumika kama nyenzo ya kujenga maadili kwa vijana, ili kutambua kuwa kulitumikia taifa kwa uaminifu kuna thamani hata baada ya mtu kustaafu.

Mkutano huo umebeba Kaulimbiu isemayo: “Wazee ni Tunu, Tuwatunze kwa Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii.”

Kaulimbiu hiyo imekuja wakati muafaka ambapo Tanzania imeanza utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, sambamba na utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Wazee ya Mwaka 2003, Toleo la Mwaka 2024.














Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija Nassir Ali, amewataka wananchi wa Mkuranga kuhakikisha wanalinda miundombinu ya gesi asilia iliyojengwa katika maeneo yao ili iweze kudumu na kuwanufaisha wananchi pamoja na taifa kwa ujumla.

Na Mwandishi Wetu, MOROGORO WANANCHI waliotembelea banda la Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) katika Maonesho ya Utamaduni, wameeleza kufurahishwa na elimu wanayoipata kuhusu majukumu ya Wakala katika kuratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.

Wananchi hao wamesema maonesho hayo yamekuwa fursa muhimu kwao kupata uelewa kuhusu Mfumo wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (Bulk Procurement System – BPS), namna mafuta yanavyoagizwa nchini na nafasi ya PBPA katika kuratibu mchakato huo.

Bi. Maria Ngilisho, mmoja wa waliotembelea banda hilo, alisema elimu hiyo imemsaidia kuelewa mchakato wa upatikanaji wa mafuta nchini, ambao awali hakuwa na ufahamu wa kutosha kuuhusu.

“Nimefurahi kupata elimu hii kwa sababu tumekuwa tukitumia mafuta kila siku, lakini hatukuwa tunafahamu mchakato unaofanyika hadi mafuta yanapofika nchini. Sasa nimeelewa kuwa kuna taasisi kama PBPA inayoratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja,” alisema Ngilisho.

Naye, Bw. Michael Maganga, alisema mawasiliano ya ana kwa ana na watumishi wa PBPA yamewapa wananchi nafasi ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa moja kwa moja kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mafuta.

“Elimu tunayopata hapa ni muhimu sana kwa sababu tunapata nafasi ya kuuliza maswali yanayotuhusu kama watumiaji wa mafuta na tunapata majibu kutoka kwa wataalamu. Ni vizuri PBPA kuendelea kutumia maonesho haya kuwafikia wananchi,” alisema Maganga.

Kwa mujibu wa PBPA, miongoni mwa majukumu ya Wakala ni kukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, kuendesha zabuni za kimataifa za ununuzi wa mafuta kwa wingi, pamoja na kuratibu upokeaji na uwasilishaji wa bidhaa hizo nchini. Ushiriki wa PBPA katika maonesho mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Wakala za kuwaelimisha

Ushiriki wa PBPA katika maonesho mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Wakala za kuwaelimisha wananchi kuhusu majukumu yake na nafasi yake katika sekta ya mafuta, huku ukitoa fursa kwa wananchi kupata ufafanuzi kuhusu mchakato wa uagizaji wa mafuta na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa hizo unaendelea kuwa wa uhakika nchini.