Kwa zaidi ya miaka minne, nilikuwa nikimiliki duka kubwa la vifaa vya ujenzi na bidhaa za nyumbani katika mji wetu. Biashara hii ilikuwa ndiyo tegemeo langu kuu na chanzo cha rizki kwa familia na wafanyikazi wangu sita.

Niliwekeza mamilioni ya fedha na mtaji wangu wote ili kuhakikisha duka langu linakuwa na kila aina ya bidhaa zenye ubora wa hali ya juu. Hata hivyo, kuanzia katikati ya mwaka jana, mambo yalianza kubadilika ghafla kwa njia ya kutatanisha sana.

​Duka langu lilikuwa katikati ya mji ambapo watu wengi wanapita, lakini ajabu ni kwamba wateja walikuwa wakipita mlangoni na kuingia kwenye maduka ya jirani yaliyokuwa na bidhaa chache kuliko zangu.

Siku zilipita bila kuuza hata bidhaa moja ya maana. Akiba yangu ya benki ilisha kabisa, madeni ya wauzaji wa jumla yalianza kunilundikia, na wafanyikazi wangu walishindwa kupata mshahara kwa miezi mitatu mfululizo.

Nilibaki nikiketi dukani kuanzia asubuhi hadi jioni nikiwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikitazama biashara yangu ya mamilioni ikiporomoka kuelekea kufilisika kabisa. SOMA ZAIDI.

 

Jina langu ni Baraka. Kuna siku moja katika maisha yangu ambayo sitaisahau kamwe.

Ilikuwa siku ambayo kosa dogo la kutuma pesa lilibadilisha maisha ya familia yangu.

Mama yangu alikuwa amelazwa hospitalini katika hali mbaya sana. Madaktari walihitaji malipo ya haraka ili kuendelea na matibabu yake.

Nyumbani kulikuwa na hofu kubwa. Kila mtu alikuwa akipiga simu kutafuta msaada. Ndugu walichangia walichoweza.

Baada ya kuhangaika kwa muda, hatimaye nilifanikiwa kupata TSh 1,850,000. Kwangu mimi, hiyo haikuwa pesa tu.

Ilikuwa matumaini. Ilikuwa nafasi ya kumuokoa mama yangu. SOMA ZAIDI.

Takribani wakulima wadogo 1,000 kutoka mikoa ya Morogoro, Dodoma na Arusha wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kuondokana na matumizi ya viuatilifu hatarishi katika shughuli zao za kulimo. Idadi hiyo ya wakulima itawagusa moja kwa moja wakulima wa mbogamboga, vitunguu, mbogamboga na pamba waliopo kwenye wilaya za Karatu, Chamwino, Mvomero na Meru. Hatua hiyo inayolenga kuwahamasisha wakulima kuachana na matumizi ya viuatilifu hatarishi ili kupunguza madhara ya kiafya yanayosababishwa na kemikali hizo kuanzia kwa mkulima mpaka kwa mlaji.

Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa Asasi Isiyo ya Kiserikali ya AGENDA For Environment and Responsible Development, Dorah Swai, mkoani Morogoro wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa kilimo bora na mazingira kutoka katika taasisi za serikali na binafsi. Bi. Swai amesema kuwa mradi huo uliofadhiliwa na mfuko wa Global Frame Work (GFC) unahusisha nchi tatu za ukanda wa Mahariki mwa Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya na Ethiopia na kila nchi imejiwekea malengo ya kufikia angalau wakulima 1000. Amesema dhamira kuu ya mradi huo wa kuondoa viuatilifu hatarishi ukanda wa Mashariki mwa Afrika una lengo la kuangalia namna bora ya kuwawezesha wakulima wadogo 3,000 watakaokuwa vinara wa mabadiliko katika matumizi ya viuatilifu mbadala kwa wenzao.

Katika warsha hiyo, Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Joseph Kiwango, amesema serikali iko tayari kushiriukiana na wadau wote wenye nia ya kuwainua Watanzania kupitia sekta ya kilimo kinachozingatia utunzaji wa mazingira na afya za binadamu. Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya Mwavuli wa Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Bakari Mongo, pamoja na Afisa Programu Mkuu wa Agenda, Silvani Mng’anya, kila mmoja kwa nyakati tofauti amesema suala la kupambana na viuatilifu hatarishi halipaswa kuwa la mtu mmoja au kikundi Fulani, kwani madhara ya viuatilifu hatarishi hayaishii kwa mtu mmoja. “Jukumu la kuondoa viuatilifu hatarishi halipaswa kuwa la mtu mmoja, ni jukumu letu sote katika kuhakikisha mlaji wa mwisho analindwa dhidi ya madhara yatokanayo na viuatilifu hatarishi.”amesema Mongo.

 

 

Na. Mtemi Sona

Dodoma. Mwenyekiti wa Ujenzi Sports Club, Arch. Ibrahim Chatila, amesema uongozi mpya umejipanga kuijenga timu hiyo kuwa ya kisasa, imara na yenye ushindani mkubwa katika mashindano yote itakayoshiriki.

Akizungumza kuhusu mikakati ya kuiboresha klabu hiyo iliyo chini ya Wizara ya Ujenzi, Chatila amesema lengo kuu ni kuunda kikosi chenye ubora wa hali ya juu kitakachokuwa na uwezo wa kushindana na timu mbalimbali nchini.

Amesema hatua za awali zitahusisha usajili wa wachezaji bora pamoja na kuimarisha benchi la ufundi kwa kuwashirikisha makocha wenye uwezo na sifa zinazohitajika ili kuongeza ushindani wa timu.

"Tunataka kuunda timu yenye wachezaji watakaoweza kuleta ushindi na ambao watazingatia weledi, nidhamu na taaluma katika kila mashindano tutakayoshiriki," amesema Chatila.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa uongozi mpya uliochaguliwa umeazimia kuijenga upya Ujenzi Sports Club kwa misingi ya umoja, utawala bora na uwajibikaji kuanzia kwa viongozi, benchi la ufundi, wachezaji hadi wanachama.

Kwa mujibu wa Chatila, mafanikio ya timu hayatategemea ubora wa kikosi pekee, bali pia uimara wa mifumo ya uendeshaji wa klabu.

Mbali na masuala ya kiufundi, amesema uongozi wake umeweka mkazo katika kuimarisha uchumi wa klabu kwa kutafuta wadhamini na wadau mbalimbali watakaosaidia kuiendesha timu kwa kiwango cha kisasa.

"Lengo letu ni kuwa na klabu inayojitegemea kiuchumi, yenye uwezo wa kujiendesha na kushiriki mashindano kwa ushindani mkubwa," amesema.

Arch. Ibrahim Chatila ni Mbunifu Majengo kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ambayo ni moja ya taasisi zinazounda Ujenzi Sports Club. Pia ni kocha mwenye leseni ya CAF na amewahi kuwa mjumbe wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Singida kwa kipindi cha miaka minne.

Yeye ni miongoni mwa viongozi wapya waliochaguliwa hivi karibuni kuiongoza Ujenzi Sports Club, klabu inayoundwa na taasisi 10 zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi.

Klabu hiyo hushiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, netiboli, riadha, kuvuta kamba na michezo mingine ya ushindani.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Takribani watoto 10,000 nchini wanahusishwa na shughuli za uchimbaji mdogo wa dhahabu zinazotumia zebaki  hali inayowaweka katika hatari  ya kupata madhara ya kiafya kutokana na sumu ya kemikali hiyo. Mbali na watoto, wanawake  kati ya asilimia 20 hadi 30  katika sekta ya uchimbaji mdogo wa madini pia wanakabiliwa na athari kubwa za kiafya zinazotokana na matumizi ya zebaki, ikiwemo madhara ya mfumo wa fahamu na afya ya uzazi. Hali hiyo imechochea wadau wa mazingira kutaka biashara ya zebaki duniani ikomeshwe na matumizi yake katika uchimbaji mdogo kusitishwa ifikapo mwaka 2032. Akizungumza leo Julai 30, 2026 jijini Dodoma katika Warsha ya Mradi wa Marekebisho ya Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki unaotekelezwa na AGENDA kwa kushirikiana na IPEN,Afisa Programu wa AGENDA, Angel Shaniva amesema mbali na kuhusisha watoto, sekta ya uchimbaji mdogo wa dhahabu (ASGM) inakadiriwa kuajiri moja kwa moja zaidi ya watu milioni 1.2 huku zaidi ya watu milioni 7.2 wakitegemea shughuli zake kwa njia zisizo za moja kwa moja. Shaniva amesema jamii inapaswa kuachana na matumizi ya zebaki (mercury) ili kuwalinda wanawake na watoto dhidi ya athari za kiafya na kimazingira.  Amesema mradi huo unalenga kuongeza uelewa na kujenga ushirikiano kati ya wadau wote ili kuharakisha utekelezaji wa Mkataba wa Minamata na kuunga mkono marekebisho yanayolenga kukomesha biashara ya zebaki duniani pamoja na kuweka tarehe rasmi ya kusitisha matumizi yake katika uchimbaji mdogo wa dhahabu. Amesema AGENDA imekuwa ikifanya kazi katika maeneo ya mazingira, mabadiliko ya tabianchi, elimu na jinsia, ambapo kupitia zaidi ya miradi 140 iliyotekelezwa imeendelea kukuza ushirikiano na kuongeza uelewa kuhusu masuala ya maendeleo endelevu. Kwa upande wake Afisa Program wa AGENDA, Clara Benjamin, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi 153 wanachama wa Mkataba wa Minamata unaolenga kulinda afya ya binadamu na mazingira dhidi ya madhara ya zebaki, lakini bado biashara ya kemikali hiyo inaendelea huku kukiwa hakuna tarehe rasmi ya kusitisha matumizi yake katika uchimbaji mdogo wa dhahabu. Amesema takwimu zinaonyesha biashara ya zebaki duniani imeongezeka kutoka tani 1,200 mwaka 2017 hadi tani 1,700 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 40, huku sekta ya uchimbaji mdogo wa dhahabu ikiendelea kutumia zaidi ya tani 2,000 za zebaki kila mwaka bila dalili za kupungua. Kwa mujibu wake, maeneo yenye matumizi makubwa ya zebaki nchini ni Geita, Shinyanga, Mbeya na Mara ambako kemikali hiyo hutumika kutenganisha dhahabu, lakini matumizi hayo yameendelea kusababisha uchafuzi wa ardhi, mito na samaki pamoja na madhara makubwa ya kiafya ikiwemo uharibifu wa mfumo wa fahamu na kuhatarisha usalama wa chakula. Amesema matumizi ya zebaki pia yanahusishwa na biashara haramu ya dhahabu, kuikosesha Serikali mapato na kudhoofisha usimamizi wa sekta ya madini. Amesema marekebisho yanayopendekezwa katika Mkataba wa Minamata yanataka biashara ya kimataifa ya zebaki ipigwe marufuku isipokuwa kwa matumizi yanayokubalika kimazingira pamoja na kuweka mwaka 2032 kuwa mwisho wa matumizi ya zebaki katika uchimbaji mdogo wa dhahabu. Kwa upande wake, Afisa Mazingira Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Ahmad Hassan Mbwana, amesema Serikali kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na wadau wengine imeendelea kutekeleza miradi ya kupunguza matumizi yasiyo salama ya zebaki kupitia utoaji wa elimu katika mikoa saba ikiwemo Mwanza na Geita. Amesema wachimbaji wadogo wameendelea kuelimishwa kuhusu madhara ya zebaki, matumizi ya teknolojia salama na umuhimu wa kufanya tathmini za athari kwa mazingira kabla na wakati wa shughuli za uchimbaji. Mbwana amesema elimu hiyo imechangia kuongeza uelewa kuhusu uhifadhi wa mazingira na pia kuongeza tija ya uzalishaji kwa wachimbaji wanaotumia teknolojia salama, huku uratibu wa wadau na mapitio ya sheria mbalimbali ukiendelea kuboreshwa. Hata hivyo amesema bado ipo changamoto ya baadhi ya wachimbaji kutokuwa na anuani rasmi za maeneo yao ya kazi, hali inayofanya kuwa vigumu kuwafikia kwa ajili ya ukaguzi wa usalama, utoaji wa elimu na ufuatiliaji wa matumizi ya kemikali hatarishi. Naye Mkaguzi wa Usalama Mahali pa Kazi (OSHA), Thadei Mwasamila, amesema ni muhimu kuimarisha ukaguzi wa mara kwa mara katika migodi midogo, kubaini vihatarishi na kuhakikisha wachimbaji pamoja na waajiri wanazingatia viwango vya afya na usalama kazini. Amesema OSHA itaendelea kusisitiza matumizi sahihi ya vifaa vya kinga binafsi, uhifadhi salama wa kemikali na usimamizi wa taka zenye zebaki ili kupunguza madhara ya muda mrefu kwa wachimbaji na jamii zinazozunguka maeneo ya migodi. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NESODO, Alfred Lugela, amesema kupanda kwa bei ya dhahabu duniani kumeongeza matumizi ya zebaki katika uchimbaji mdogo, huku akieleza kuwa udhibiti wa biashara ya kemikali hiyo unaweza kuhamasisha matumizi ya teknolojia mbadala zilizo salama. Kutokana na hayo Mhandisi wa Migodi kutoka Wizara ya Madini, Yusuf Yusufu, amesema usimamizi madhubuti wa shughuli za uchimbaji mdogo pamoja na matumizi ya teknolojia mbadala kama gravity concentration na borax ni muhimu katika kulinda afya za wananchi, mazingira na kuongeza tija katika sekta ya madini. Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Tawfiq Halfan, amesema mafanikio ya kupunguza matumizi ya zebaki yatategemea ushirikiano wa Serikali, wadau wa mazingira, wachimbaji na jamii kwa ujumla ili kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika bila kuhatarisha afya za wananchi na mazingira. Kwa mujibu wa wadau hao, kuungwa mkono kwa marekebisho ya Mkataba wa Minamata kutaiwezesha Tanzania kupunguza matumizi ya zebaki, kuimarisha usimamizi wa sekta ya madini na kulinda afya za wachimbaji, wanawake, watoto na vizazi vijavyo.
            
 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza Julai 31, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua Kikao cha Kamati Elekezi ya Programu ya Pili ya Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi (ESPJ II)

Na.Mwandishi Wetu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema Programu ya Pili ya Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi (ESPJ II) ni hatua ya kimkakati inayolenga kuongeza ajira zenye tija na kuimarisha ustawi wa jamii.

Akizungumza Julai 31, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua Kikao cha Kamati Elekezi ya Programu hiyo, Prof. Nombo amesema kuwa programu hiyo inalenga kuzalisha rasilimali watu wenye umahiri wa kisasa kwa sekta za viwanda, teknolojia, ubunifu na sekta binafsi, ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Prof. Nombo amebainisha kuwa Programu imeandaliwa katika misingi ya Mkakati wa Pili wa Taifa wa Kuendeleza Ujuzi, Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023, pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa matokeo makuu yanayotarajiwa ni kuongeza fursa za mafunzo kwa vijana wasio na ajira na wanaotoka katika mazingira magumu, kuimarisha mfumo wa kusimamia Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (TVET), na kushirikisha sekta binafsi katika kuboresha ubora wa mafunzo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Programu ya Pili ya Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi, Dkt. Erick Mgaya, amesema utekelezaji wa Programu hiyo ni wa miaka sita wenye thamani ya Shilingi bilioni 780 sawa na Dola za Kimarekani milioni 300 unatarajiwa kunufaisha zaidi ya Watanzania milioni moja.

Amefafanua kuwa programu hii inatekelezwa na Taasisi 19 pamoja na wizara mbalimbali ikiwemo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Afya, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, pamoja na taasisi za mafunzo zikishirikiana na Sekta binafsi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Na.Alex Sonna-DODOMA

BODI  ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imetangaza mafanikio makubwa katika mwaka wa fedha 2025/26 baada ya wakulima nchini kulipwa zaidi ya Shilingi trilioni 2.298 kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS), huku kiasi cha mazao yaliyouzwa kupitia mfumo huo kikiongezeka kwa asilimia 43.6 ndani ya mwaka mmoja.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 31,2026 jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa shughuli za bodi  hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026 na mwelekeo wa mwaka 2026/2027.

Amesema mfumo huo umeendelea kuwa chachu ya maendeleo ya sekta ya kilimo kwa kuwawezesha wakulima kupata masoko na bei zenye ushindani na malipo ya uhakika kupitia taasisi za fedha.

Bw.Bangu amesema  katika mwaka wa fedha 2025/26, jumla ya kilo bilioni 1.122 za mazao tisa, yakiwemo korosho, ufuta, kahawa, kakao, mbaazi, dengu, choroko, soya na chai, ziliuzwa kupitia minada ya kidijitali inayosimamiwa na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), ikilinganishwa na kilo milioni 781.6 mwaka uliotangulia.

"Ongezeko hili linaonyesha kuwa wakulima wengi zaidi wameendelea kuuamini Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuuona kuwa njia salama na yenye manufaa ya kuuza mazao yao," amesema  Bw. Bangu.

Amefafanua kuwa kutokana na mauzo hayo, Serikali za Mitaa zilikusanya zaidi ya Shilingi bilioni 61 kupitia ushuru wa mazao (CESS), huku thamani ya biashara yote iliyofanyika kupitia mfumo huo ikifikia Shilingi trilioni 2.679, hali inayodhihirisha mchango mkubwa wa mfumo huo katika kukuza uchumi wa Taifa.

Kwa mujibu wa Bw. Bangu, mfumo huo sasa unatekelezwa katika mikoa 23 na unahusisha mazao na bidhaa 18, tofauti na mwaka 2006 ulipoanza na zao moja pekee la korosho.

Amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika kuimarisha mfumo huo ambapo katika mwaka wa fedha 2025/26 ilitoa Shilingi milioni 950 zilizotumika kuboresha mifumo ya TEHAMA, kutoa elimu kwa wakulima, kuimarisha ukaguzi wa maghala na kununua vitendea kazi vya kuongeza ufanisi wa huduma.

Mbali na mafanikio hayo, WRRB ilibainisha kuwa mapato yake ya ndani yameongezeka kwa kasi kutoka Shilingi bilioni 1.998 mwaka 2023/24 hadi Shilingi bilioni 5.870 mwaka 2025/26, hatua iliyoifanya Bodi kujigharamia zaidi ya asilimia 67 ya bajeti yake na kupunguza utegemezi wa fedha za Serikali.

Aidha, mfumo huo ulizalisha jumla ya ajira 31,875 kupitia shughuli mbalimbali za ukusanyaji wa mazao, uhifadhi maghalani, usafirishaji, upimaji wa ubora na huduma nyingine katika mnyororo wa thamani wa biashara ya mazao.

Katika hatua nyingine, WRRB imetangaza mpango wa kupanua Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kutoka kwenye mazao ya kilimo kwenda katika sekta nyingine za uzalishaji, ambapo kwa mara ya kwanza sekta ya mifugo itaingizwa kwenye mfumo huo katika mwaka wa fedha 2026/27.

Bw. Bangu alisema mnada wa kwanza wa mifugo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala unatarajiwa kufanyika katika Wilaya ya Mvomero, huku bidhaa nyingine zikiwemo mwani, ngozi na mazao ya bustani zikitarajiwa kuingizwa kadri maandalizi ya kisera na kiutendaji yatakavyokamilika.

Ameongeza kuwa WRRB itaendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali kwa kuboresha mifumo ya WRMS na WRS-MIS, kuongeza matumizi ya stakabadhi za kielektroniki pamoja na kuunganisha huduma za leseni, ukaguzi, biashara na malipo katika mfumo mmoja.

Pia amesema Bodi itaendelea kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), NBC na taasisi nyingine za fedha ili kuongeza upatikanaji wa mikopo inayotumia Stakabadhi za Ghala kama dhamana, hatua itakayowawezesha wakulima na wafugaji kupata mitaji bila kuuza bidhaa zao kwa hasara.

Bw. Bangu amesema mafanikio hayo ni matokeo ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na usimamizi wa Wizara ya Viwanda na Biashara, akisisitiza kuwa WRRB itaendelea kutekeleza mikakati ya kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania, kuimarisha masoko ya wakulima na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Kariakoo, Julai 30, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa kikodi Kariakoo imeendesha semina maalum kwa wafanyabiashara ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kutoa elimu ya kodi na kuwajengea uelewa kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi yaliyoanza kutumika kwa mwaka 2026/2027.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mahusiano ya kidiplomasia kati ya Ufalme wa Morocco na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yameendelea kuimarika kwa kasi tangu ziara ya kihistoria ya Kiserikali ya Mfalme Mtukufu Mohammed VI nchini Tanzania mwaka 2016, huku ushirikiano katika sekta mbalimbali ukizidi kupanuka na kuleta manufaa kwa mataifa yote mawili.



Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania Bw. Burhan Kishenyi, akizungumza Julai 30, 2026 wakati akifungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
...........................................
Na Mwandishi Wetu Dodoma




Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania Bw. Burhan Kishenyi, leo tarehe 30.07.2026 amefungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, jijini Dodoma, na imewakutanisha washiriki kutoka taasisi mbalimbali za umma na wadau wanaoshughulika na masuala ya haki na ustawi wa watu wenye ulemavu.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Bw. Kishenyi amesema kuwa utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ni msingi muhimu katika kujenga jamii jumuishi inayotoa fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi.


Amesisitiza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inaweka msisitizo katika ushirikishwaji wa makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili kuchangia kikamilifu maendeleo ya kiuchumi na kijamii.


Aidha, amewataka washiriki kutumia warsha hiyo kujadili kwa kina wajibu wa kila taasisi katika kutekeleza matakwa ya sheria, kubadilishana uzoefu na kuibua mapendekezo yatakayosaidia kuondoa vikwazo vinavyokwamisha upatikanaji wa haki na huduma kwa watu wenye ulemavu.


Washiriki wa warsha hiyo wanatarajiwa kujengewa uwezo kuhusu tafsiri na utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, pamoja na namna ya kuoanisha utekelezaji wake na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kujenga Tanzania jumuishi, yenye usawa, haki na maendeleo endelevu kwa wananchi wote.


Kwa upande wake , Bw. Harold Sungusia, Rais Mstaafu wa TLS ambaye pia ni wakili wa kujitegemea alisisitiza umuhimu wa kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika mchakato wa maboresho ya sheria ili kuhakikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatekelezwa kwa misingi ya usawa, haki na ushirikishwaji.


Akizungumza katika mkutano uliojadili mwelekeo wa maboresho ya sheria na maendeleo ya taifa, Bw. Sungusia alisema kuwa sheria bora zinapaswa kuzingatia mahitaji ya makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili wasibaki nyuma katika safari ya maendeleo.


Alieleza kuwa ushiriki wa watu wenye ulemavu katika utoaji wa maoni na maamuzi kuhusu sheria ni muhimu kwa sababu unasaidia kutunga na kuboresha sheria zinazolinda haki zao na kuondoa vikwazo vinavyowazuia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa.


Aidha, alibainisha kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji mfumo wa sheria unaohakikisha fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote.


Bw. Sungusia alisema kuwa kujenga taifa lenye maendeleo endelevu kunategemea uwepo wa sheria jumuishi zinazolinda haki za kila mwananchi na kuweka mazingira yanayowawezesha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.


Washiriki wa mkutano huo walikubaliana kuwa ushirikishwaji wa makundi maalumu katika mchakato wa maboresho ya sheria ni nguzo muhimu ya kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kujenga jamii yenye usawa na haki kwa wote.
Wadau mbalimbali wakishiriki warsha hiyo.


Wadau wakichangia mada katika warsha hiyo.

Michango mbalimbali ikitolewa katika warsha hiyo.

Warsha hiyo ikiendelea

Michango ikiendelea kutolewa.

Taswira ya warsha hiyo.