Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan na Yoweri Museveni wa Uganda wameshuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano (MoU) ya kuendeleza ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta na Kitovu cha Nishati cha Kikanda Jijini Tanga, mradi unaotarajiwa kubadili taswira ya sekta ya nishati Afrika Mashariki.
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewataka vijana wanaoshiriki mpango wa Kujenga kesho bora (Building a Better Tomorrow (BBT) kutumia fursa ya urasimishaji wa biashara ili kuongeza thamani ya shughuli zao za kilimo na ufugaji, hatua itakayowawezesha kushindana katika masoko ya ndani na nje ya nchini.

Wito huo umetolewa leo Agosti 6,2026 jijini Dodoma na Afisa Usajili wa BRELA, Bw. Yusuph Mwasakafyuka,wakati akitoa mafunzo kwa vijana wa BBT, wanaoshiriki katika Maonesho ya 33 ya Kimataifa ya Kilimo (nanenane) Nzuguni jijini Dodoma. “Urasimishaji wa biashara ni nguzo muhimu ya kuwajengea uwezo wa kufanya kilimo cha kisasa kinachozalisha tija, badala ya kuendelea na mifumo ya jadi isiyo na ushindani wa kibiashara”. Amesema Mwasakafyuka.

Aidha amewaeleza vijana hao kuwa; wanapaswa kutambua kuwa mradi wa BBT hauwalengi tu kuwapa ujuzi wa uzalishaji wa mazao na mifugo, bali pia kuwajengea msingi wa kuwa wajasiriamali wenye biashara rasmi zinazotambulika kisheria. Alieleza kuwa kuongeza thamani ya mazao huanza kwa kusajili biashara au kampuni ili kuwapa nafasi ya kupanua shughuli zao na kuvutia masoko pamoja na wawekezaji.

Amefafanua kuwa BRELA imewapatia washiriki hao elimu kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo, ikiwemo usajili wa majina ya biashara, usajili wa makampuni, upatikanaji wa leseni pamoja na usajili wa alama za biashara, hatua ambazo zitawawezesha kulinda bidhaa na huduma zao dhidi ya matumizi yasiyo halali.

Aongeza kuwa elimu hiyo inalenga kuwahamasisha vijana kuanza mapema urasimishaji wa biashara wanazotaka kushughulika nazozao ili wanapohitimu mafunzo na kuanza uzalishaji wa kibiashara wawe tayari kushiriki kikamilifu katika uchumi rasmi, kupata fursa za mikopo, masoko na ushirikiano na taasisi mbalimbali za kifedha. Kwa upande wake Afisa Usajili Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bw. Nassoro Mtavu, amewahimiza vijana wajasiriamali kutambua umuhimu wa kusajili alama za biashara na huduma ili kulinda bidhaa na huduma zao dhidi ya matumizi yasiyo halali.

Amesema usajili wa alama za biashara pamoja na ulinzi wa hataza ni nyenzo muhimu zinazowezesha wabunifu na wajasiriamali kunufaika na kazi zao, kuongeza ushindani sokoni na kujenga chapa zenye kuaminika ndani na nje ya nchi.

Aidha, amewasisitiza vijana hao kutumia huduma zinazotolewa na BRELA mapema ili kuhakikisha bunifu na biashara zao zinalindwa kisheria, hatua itakayochochea ukuaji wa biashara, kuvutia uwekezaji na kuongeza thamani ya bidhaa za Kitanzania. Aidha, BRELA imeeleza itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo na programu mbalimbali za kuwawezesha vijana ili kuhakikisha elimu ya urasimishaji wa biashara inawafikia wananchi wengi zaidi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kujenga uchumi shindani unaochochewa na biashara rasmi, ubunifu na ongezeko la thamani katika sekta ya kilimo.

 

Kuishi bila kujua mwelekeo wa maisha yako ni sawa na kusafiri gerezani au gizani bila taa. Kwa miaka mingi, nilikuwa nikihangaika sana kufanya kazi mbalimbali na kujaribu biashara za kila aina, lakini kila nilipoweka juhudi na fedha zangu, matokeo yake yalikuwa ni kufilisika, kukata tamaa, na kurudi nyuma.

Nilibaki nikijiuliza ni kwa nini wenzangu niliosoma nao au kuanza nao maisha walikuwa wakifanikiwa kwa urahisi, wakati mimi kila mlango niliotamani kuufungua ulikuwa ukijifunga kwa kishindo.

​Nilianza kujiona kama mtu aliyelaaniwa. Nilibadili kazi zaidi ya mara tano na kujaribu Biashara tofauti tofauti kuanzia kilimo, uuzaji wa nguo, hadi usafirishaji lakini zote ziliishia kwenye madeni na msongo mkubwa wa mawazo.

Nilihisi kabisa kuwa kuna kitu kikubwa kilichokuwa kimefichika kuhusu maisha yangu ambacho nilikuwa sikijui, lakini sikuwahi kupata mtu wa kunifungua macho na kunionyesha njia sahihi ya kufuata ili nitoke kwenye giza hilo la umaskini na mahangaiko. SOMA ZAIDI.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri, akiwa ameambatana na wajumbe wengine wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, amepokelewa Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma, leo tarehe 6 Agosti 2026. Mapokezi hayo yaliyoandaliwa na CCM Mkoa wa Dodoma, yamehudhuriwa na wanachama, makada na viongozi mbalimbali wa CCM, akiwemo Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM (Bara), Mzee Philip Japhet Mangula.

 

Umaskini ni mzigo mzito unaoweza kumvua mwanadamu utu, heshima, na furaha ya maisha. Kwa miaka mingi, familia yangu ilikuwa ikipitia maisha ya dhiki ya kupindukia.

Kila siku ilikuwa ni vita ya kupata mlo mmoja tu wa jioni, huku madeni yakiniandama kutoka kila pembe. Nilibaki nikikopa hapa ili kulipa kule, lakini badala ya afadhali, mzunguko wa umaskini na madeni ulizidi kunisonga na kuninyima kabisa usingizi wa usiku.

​Kazi zozote nilizojaribu kufanya au biashara ndogo ndogo nilizozianzisha ziliishia kupata hasara na kufilisika ndani ya muda mfupi sana.

Nilibaki nikitazama watoto wangu wakikosa ada za shule na mahitaji ya msingi, huku majirani na ndugu wengine wakianza kunitenga na kunidharau kama mtu asiyekuwa na msaada wowote.

Hakuna maumivu makubwa kama kuona familia yako ikiteseka huku ukiwa huna uwezo wa kubadilisha hali hiyo, ukijua wazi kuwa unatia juhudi zote lakini matokeo yanakuwa ni sifuri. SOMA ZAIDI.

 

Kuitwa mama na kubeba kiumbe tumboni ni moja ya furaha kubwa na ndoto ya kila mwanamke aliyeko kwenye ndoa. Hata hivyo, kwangu mimi, miaka saba ya kwanza ya ndoa yangu iligeuka kuwa kipindi cha majuto, dhihaka, na machozi yasiyoisha.

Kila mwezi ulipopita bila kuona dalili za ujauzito, ndivyo matumaini yangu na mume wangu yalivyozidi kufifia. Tulitembea kwenye hospitali mbalimbali na kuonana na madaktari bingwa wa uzazi.

Nilitumia dawa za kila aina za kuweka homoni sawa na kusafisha kizazi, huku mume wangu naye akifanyiwa vipimo vilivyoonyesha hana tatizo lolote. Pamoja na vipimo vyote kuonyesha tuko salama, mimba haikutokea.

Nilianza kuona mabadiliko kutoka kwa ndugu wa mume wangu maneno ya chini chini, kebehi, na dharau zilianza kuelekezwa kwangu wakidai mimi ni “tumbo lisilobeba.”

Nilibaki nikilia usiku kucha, nikijifungia ndani kwa aibu na msongo mkubwa wa mawazo, nikihofia ndoa yangu ingevunjika muda wowote. SOMA ZAIDI.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, ametembelea banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma na kupongeza mchango wa benki hiyo katika kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limehimiza wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa wanaozalisha bure kwa gharama za Serikali, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na vikwazo vya kiabiashara.

  


Na John Walter -Babati 

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Hamidu Aweso, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Maji wa Vijiji vya Endamagay na Gidaboshka, uliopo katika Jimbo la Babati Vijijini. Mradi huo wenye thamani ya Shilingi bilioni 1.099 unalenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi 3,766 wa vijiji hivyo na maeneo ya jirani.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Mhe. Aweso alisema Serikali inaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maji ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati. 

Alibainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 30, 2026, huku utekelezaji wake ukiwa umefikia asilimia 87.

Katika ziara hiyo, Waziri Aweso aliambatana na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Baran Sillo.

Kufuatia hatua iliyofikiwa na mradi huo, Mhe. Aweso alitoa maelekezo kwa Wizara ya Maji kuhakikisha ndani ya kipindi kifupi inapatikana Shilingi 508,300,000 kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizosalia, ili mradi ukamilike kwa wakati na wananchi waanze kunufaika na huduma ya maji safi na salama kama ilivyopangwa.





 


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, amefurahishwa na uelewa mkubwa ulioonyeshwa na wanafunzi waliopata elimu ya vipimo katika banda la Wakala wa Vipimo - (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane.

Akizungumza leo Agosti 6, 2026 baada ya kuzungumza na wanafunzi hao aliowakuta katika Banda la WMA, Viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, Dodoma, Naibu Waziri ambaye pia alikuwa katika ziara ya kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho, alisema ni hatua nzuri kwa WMA kuanza kuwafundisha watoto umuhimu wa vipimo sahihi wakiwa wadogo.

“Nimefurahishwa sana. Watoto hawa wameelewa kuwa kipimo sahihi ni haki ya kila mtu. Hawa ndio Maafisa Vipimo wa kesho,” alisema.

Awali, Naibu Waziri Chande alipowakuta wanafunzi hao bandani aliwauliza maswali mbalimbali kuhusu vipimo na waliweza kujibu kwa ufasaha. 

Wanafunzi hao wa Shule ya Msingi Blessed Mabuba iliyopo jijini Dodoma, ambao waliongozana na mwalimu wao Irene Ketta, ambaye pia alipongeza WMA kwa kujielekeza katika utoaji elimu ya vipimo mashuleni hatua ambayo alisema imewawesha wanafunzi kueleza tofauti ya kipimo sahihi na kisicho sahihi, umuhimu wa kusoma lebo na jinsi ya kutumia mizani.

“Niwape pongezi WMA. Kama tutaendelea kuwapa elimu hii watoto wetu, tunajenga Taifa la wafanyabiashara waaminifu na walaji wenye ufahamu. Huu ndio msingi wa uchumi imara,” alisema Mwalimu Ketta.

WMA imeahidi kuhakikisha elimu ya vipimo inaenea kwa jamii nzima kupitia utoaji elimu kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi.







Na Mwandishi Wetu, Tabora

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kurahisisha upatikanaji wa Alama ya Ubora kwa kuanzisha mfumo wa kidijitali unaowezesha wajasiriamali na wazalishaji kuwasilisha maombi kwa njia ya mtandao, hatua inayolenga kuongeza idadi ya bidhaa zenye ubora unaokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.

 




Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameupongeza Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kwa maboresho makubwa ya utoaji wa huduma, hususan matumizi ya teknolojia yanayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Msonde amesema hayo leo, Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la TEMESA katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.

Dkt.Msonde Amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofikiwa na TEMESA, akieleza kuwa uimarishaji wa huduma za kidijitali pamoja na ongezeko la ubora wa mafundi umeongeza ufanisi wa wakala huo.


“Kilichonifurahisha zaidi ni uimarishaji wa mafundi. Sasa wanafanya kazi kwa weledi mkubwa na wanatengeneza magari kwa ubora. Kwa kweli TEMESA mmenifurahisha sana,hongereni sana” amesema Dkt. Msonde.

Aidha, amesema Serikali na wananchi wanaiamini TEMESA kutokana na mchango wake katika kulinda usalama wa magari ya Serikali na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za umma. Amewataka viongozi na watumishi wa wakala huo kuendelea kubuni na kuboresha huduma kwa kutumia teknolojia.

Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma- TEMESA, Bi. Martha Joachim, amesema miongoni mwa maboresho yaliyofanywa ni kuhuisha huduma ya ukodishaji wa mitambo kupitia Mfumo wa TIMIS, ambapo wateja sasa wanaweza kuwasilisha maombi ya ukodishaji kwa njia ya kidijitali, hatua iliyopunguza urasimu na muda wa kupata huduma.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050”, yanatarajiwa kuadhimishwa tarehe 8 Agosti, 2026.

Na.Mwandishi Wetu.

Serikali imewataka wawekezaji binafsi na taasisi mbalimbali nchini kutumia fursa zinazotolewa kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuwekeza katika ujenzi wa nyumba, majengo ya umma na makazi ya kisasa kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa makazi bora na kuharakisha maendeleo ya miundombinu nchini.

Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, baada ya kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, jijini Dodoma.Amesema Serikali imefanya maboresho ya sheria na kanuni zinazoiongoza TBA ili kuipa mamlaka mapana ya kushirikiana na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hatua itakayowezesha taasisi hiyo kuvutia mitaji na kuongeza kasi ya utoaji wa huduma.

Dkt. Msonde amesema tangu kuanzishwa kwake, TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi jukumu la kujenga na kusimamia majengo ya Serikali kwa viwango vya juu vya ubora, huku ikichangia kupunguza gharama za ujenzi na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya umma. Alisema majengo mengi ya Serikali yaliyopo nchini ni ushahidi wa uwezo na weledi wa taasisi hiyo katika sekta ya ujenzi.

Ameongeza kuwa pamoja na mafanikio hayo, TBA sasa ina nafasi kubwa zaidi ya kushiriki katika kutatua changamoto ya makazi kwa kujenga nyumba bora kwa gharama nafuu. Alisema taasisi hiyo inaweza kubuni na kutekeleza miradi ya makazi inayokidhi mahitaji ya wananchi wa kipato cha chini na cha kati, huku ikitumia maeneo yake ya kimkakati kuvutia uwekezaji na kuendeleza miradi ya kisasa.

Dkt. Msonde, amesema ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi kupitia TBA utaongeza uwekezaji, ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya ujenzi, huku ukiwezesha ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma, makazi ya biashara na miradi mingine ya maendeleo. Amewahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa hizo mapema kwa kuwa Serikali imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji na milango iko wazi kwa wote wenye nia ya kushirikiana na TBA.

Aidha, Dkt. Msonde ameipongeza TBA kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini, akisema utendaji wake umeendelea kuijengea Serikali imani kutokana na ubora wa kazi zake. Alisisitiza kuwa matarajio ya Serikali ni kuona taasisi hiyo ikitumia kikamilifu mamlaka mapya iliyopewa kupanua wigo wa huduma, kuongeza miradi ya kimkakati na kuwa chachu ya kuvutia uwekezaji utakaobadilisha sekta ya makazi na miundombinu nchini.

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameshiriki mapokezi ya Mhe. Dkt. Catherine Canute aliyemwakilisha Mwenyekiti wa UWT Taifa katika ziara ya kikazi Wilaya ya Chunya.

Ziara hiyo imelenga kukagua uhai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030 na namna miradi ya maendeleo inavyotekelezwa katika wilaya hiyo.

Akizungumza katika kikao cha kupokea na kujadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa kazi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), pamoja na taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Mhe. Dkt. Catherine Canute amewapongeza viongozi wa Chama, wakiwemo wabunge na viongozi wa Serikali, kwa ushirikiano wao katika kusimamia na kuharakisha maendeleo ya Wilaya ya Chunya.

Aidha, amempongeza Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo na juhudi zake katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi.

Pia amesisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanasimamia malezi bora kwa watoto na vijana ili kuwajenga katika maadili mema na kuwaandaa kuwa viongozi na wananchi wenye uwezo wa kuendeleza taifa imara la kesho.

Aidha, Mhe. Canute amempongeza Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo na jitihada zake katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuleta manufaa kwa wananchi.

Pamoja na hayo, amesisitiza wazazi na walezi kuendelea kusimamia malezi bora kwa watoto na vijana ili kuwajenga katika misingi sahihi itakayowawezesha kuwa chachu ya maendeleo na kuendeleza taifa lenye nguvu na imara.

Amesema ushirikiano wa viongozi pamoja na malezi bora kwa vijana ni nguzo muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji na maendeleo endelevu.

Kwa upande wake, Mhe. Mahundi ameendelea kusisitiza umuhimu wa mshikamano kati ya viongozi, Chama na wananchi katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaleta matokeo chanya kwa wananchi wa Chunya na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla.