Serikali, kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.

Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.

“Mafuta yanapowasili nchini, Wakaguzi wa Mafuta hufuatilia hatua mbalimbali za upakuaji ili kuhakikisha yanakidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa,” amesema Mhandisi Makembe.

Ameeleza kuwa ufuatiliaji huo huanza mafuta yakiwa ndani ya meli na kuendelea wakati wa upakuaji na usafirishaji kupitia miundombinu maalumu, hadi yanapofikishwa kwenye maghala yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Kwa mujibu wa Mhandisi Makembe, Baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuidhinisha ubora wa bidhaa za mafuta kabla Meli haijaanza zoezi la Upakuaji ,Wakaguzi wa Mafuta wanajukumu la kuhakikisha kuwa taratibu za usalama na masharti ya upakuaji yanazingatiwa katika mchakato mzima wa upakuaji wa mafuta hayo. Hatua hiyo inalenga kulinda ubora wa mafuta na kuhakikisha shughuli za upakuaji zinafanyika kwa usalama.

Aidha, ukaguzi huo unalenga kubaini mapema changamoto zozote zinazoweza kuathiri ubora wa mafuta wakati wa upakuaji, usafirishaji au uhifadhi. Hatua hiyo husaidia kuhakikisha mafuta yanayopokelewa yanaendelea kuwa katika hali inayokubalika na TBS hadi yanapofikishwa kwenye maghala husika.

Meneja Msaidizi wa Idara ya Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Nasieku Kisambu akipokea Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa miradi ya CSR inayotekelezwa na mgodi huo.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Michael Mwang'onda (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele (kushoto mwenye skafu) wakifurahia uwekaji jiwe la msingi wa jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya Magoto kata ya Nyaikonga mradi unaogharamiwa na Barrick North Mara.

 


Na OWM – TAMISEMI, Morogoro

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wakulima, wafugaji na wavuvi kwa mchango wao mkubwa uliowezesha Tanzania kufikia utoshelevu wa chakula wa zaidi ya asilimia 120, hatua inayodhihirisha mafanikio ya uwekezaji unaoendelea kufanywa na Serikali katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Dkt. Mwigulu aliwasilisha pongezi hizo za Mhe. Rais Agosti 4, 2026, alipotembelea Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Nane Nane mkoani Morogoro.

 Katika ziara hiyo alijionea shughuli na ubunifu wa wakulima, wafugaji na wavuvi kutoka mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam, Pwani na Tanga.

Amesema maonesho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, "Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050," ambayo inawahimiza Watanzania kuzalisha kwa kuzingatia mahitaji ya soko, kutumia teknolojia za kisasa, kuongeza ubora wa bidhaa na kuimarisha mnyororo wa thamani ili kufanya kilimo kuwa biashara yenye tija na mchango mkubwa katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

"Kwa nilichojionea kupitia maonesho ya mwaka huu, ninaziona dalili zote kwamba ifikapo mwaka 2050 malengo ya Dira ya Taifa tuliyojiwekea yatakuwa yamefikiwa, kwa kuwa tuko kwenye hatua nzuri ya utekelezaji katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi," amesema Dkt. Mwigulu.

Ameongeza kuwa ameridhishwa na ubora wa mazao mbalimbali yaliyooneshwa, ikiwemo nyanya, bilinganya na bidhaa nyingine zinazokidhi viwango vya masoko ya kimataifa, yakiwemo ya Marekani na Ulaya, jambo linaloashiria kuwa Tanzania ipo kwenye mwelekeo sahihi wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani duniani.

Akizungumzia sekta ya mifugo na uvuvi, Dkt. Mwigulu amesema zimeendelea kuwa nguzo muhimu za uchumi wa taifa, akibainisha kuwa mchango wa sekta ya mifugo katika pato la taifa umeongezeka kutoka asilimia 2.3 hadi asilimia 6.2.

Ametoa mfano wa mafanikio ya wanaonufaika na sekta hiyo kwa kumtaja kijana mmoja mhitimu anayejihusisha na ufugaji wa kisasa, ambaye ameonesha ng'ombe mwenye uzito wa zaidi ya kilogramu 1,000 mwenye thamani ya takribani Shilingi Milioni 20. Aidha, amesema kijana huyo anafuga zaidi ya ng'ombe 200 na alipoulizwa na Waziri wa TAMISEMI kama anahitaji mkopo, alieleza kuwa hana uhitaji huo kutokana na mafanikio ya shughuli zake.

Awali, akitoa neno la utangulizi kabla ya Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi pamoja na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, alisema Waziri Mkuu alimpa jukumu la ulezi wa Mkoa wa Morogoro, hivyo alimkaribisha rasmi kama waziri mwenyeji wa mkoa huo, ambao ni mmoja wa mikoa inayounda Kanda ya Mashariki katika Maonesho ya Nane Nane.













 

Kilimo ni uti wa mgongo wa maisha na uwekezaji unaotegemewa na wengi kujenga hatua za maendeleo, lakini hakuna uchungu kama kutumia jasho na mtaji wako wote halafu ukaambulia patupu.

Baada ya kuwekeza akiba yangu ya miaka mingi, nilinunua shamba la hekari kumi na kuanza kilimo cha msimu. Nilipanda mbegu bora za kisasa, nikatumia mbolea za gharama, na kuhakikisha palizi inafanyika kwa wakati na umakini wa hali ya juu.

Hata hivyo, kile kilichotokea katika shamba langu kilikuwa ni maajabu yaliyomshaza kila mtu Kijijini. Wakati mashamba ya majirani zangu yaliyozunguka eneo langu yakistawi kwa kijani kibichi na kutoa mavuno tele, shamba langu lilikuwa likikauka ghafla.

Mimea ilianza kunyauka kuanzia chini, majani kubadilika rangi na kuwa ya njano, na matunda kupukutika kabla hayajakomaa. Nikaingia gharama za ziada kuleta wataalamu wa kilimo kupima udongo na dawa za wadudu, lakini hakuna kilichosaidia.

Kila msimu wa kuvuna ulipofika, nilikuwa nikiambulia hasara kubwa huku madeni ya pembejeo yakiniandama. Nilibaki nikijiuliza ni kwa nini ardhi ile ile, mvua ile ile, na huduma zile zile zinaleta matokeo tofauti kabisa kwangu. SOMA ZAIDI.

 

Kujenga familia na kuishi na mume unayempenda ni ndoto ya kila mwanamke, lakini pale hisia, uaminifu na heshima vinapotoweka ndani ya nyumba, ndoa inageuka kuwa uwanja wa mateso ya nafsi.

Baada ya kuishi na mume wangu kwa furaha na amani kwa miaka minne, ghafla mambo yalianza kubadilika kwa kasi ya ajabu. Mume wangu alibadilika tabia na kuanza kunichukulia kama mtu asiyekuwa na thamani yoyote mbele yake.

​Nia na hamu yake kwangu zilitoweka kabisa. Hakuwa akitaka kunigusa, kunibusu, wala kukaa karibu na mimi kama zamani. Kibaya zaidi, fedha zote alizokuwa akipata kazini na kwenye biashara zake alianza kuzitumbukiza nje kwa wanawake wa pembeni.

Huku mimi na watoto tukibaki bila hata pesa ya chakula na matumizi ya msingi ya nyumbani. Kila nilipojaribu kusema naye kwa upole au kulia, alipandwa na hasira kali, kunipigia kelele na kusema simvutii tena.

Nilibaki na majuto na msongo. SOMA ZAIDI.

 

Kutafuta fedha ni kazi ngumu inayohitaji jasho, muda, na akili nyingi, lakini hakuna maumivu makubwa kama kuona matunda ya kazi yako yakitoweka mikononi mwako kama moshi.

Kwa miaka kadhaa, nilikuwa nikifanya kazi kwa bidii na kupata mshahara pamoja na faida nzuri kwenye biashara zangu ndogo ndogo. Hata hivyo, maisha yangu ya kifedha yaligeuka kuwa fumbo la kutisha.

Kila pesa iliyoingia kwenye mikono yangu au akaunti yangu ya benki ilikuwa ikipotea kihasara na kwa njia za ajabu sana bila mimi kufanya la maana.

​Nikipokea fedha leo, kesho yake zingeibuka dharura zisizoelezeka simu au kifaa cha gharama kinaharibika ghafla, ugonjwa usiotarajiwa unaingia nyumbani, au kosa dogo linalogharimu fedha nyingi.

Hata pale nilipojaribu kuficha pesa taslimu kwenye kabati au pochi, nilikuta zimepungua bila mtu yeyote kugusa! Nilikuwa nikikaa na kuhesabu fedha zangu jioni, lakini kufika asubuhi nakuta kiasi kikubwa kimetoweka.

Nilibaki nikiwa na madeni yasiyotibika, nikikopa hapa na kurejesha pale, huku wenzangu niliowaingiza kwenye biashara wakipiga hatua na kujenga maisha yao. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu

WAMIKI wa vituo vya kulelea watoto nchini wamehimizwa kuwekeza katika mafunzo ya kitaalamu kwa walezi ili kuboresha ubora wa huduma za malezi na makuzi ya awali ya watoto, kufuatia kuongezeka kwa mahitaji ya wataalamu katika sekta hiyo.

 


‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara zinazoingia uwanja wa AFCON pamoja na maegesho ya magari huku ukiahidi kuhakikisha uwanja huo unafikika kwa barabara ya lami ndani ya muda uliokusudiwa.

‎Meneja wa TARURA mkoa wa Arusha, Mhandisi Nicholas Francis amesema mradi huo unahusisha ujenzi wa takribani kilomita 13 za barabara za lami zitakazorahisisha usafiri kwa wakazi wa maeneo hayo na wageni watakaohudhuria mashindano ya AFCON 2027.

‎Amefafanua kuwa mradi unajumuisha ujenzi wa barabara ya Essuri yenye urefu wa kilomita 2.45 kwa njia nne, barabara ya Lendita yenye kilomita 2.75 kwa njia nne, barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City yenye kilomita 5.5 kwa njia moja na kilomita 2.1 kwa njia nne pamoja na barabara za mzunguko zenye urefu wa kilomita 1.5 zinazojengwa kwa njia nne.

‎Mhandisi Francis amesema mradi ulianza rasmi tarehe 20 Aprili, 2026 na unatarajiwa kukamilika 20 Mei, 2027 ukiwa na muda wa utekelezaji wa miezi 13.

‎"Kwa sasa ujenzi umeelekezwa katika ujenzi wa barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City pamoja na barabara za mzunguko ili kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi Oktoba mwaka huu uwanja mpya wa michezo ufikike”amesema

‎Ameeleza kuwa utekelezaji wa barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City umefikia asilimia 53 huku mkandarasi akifanya kazi  usiku na mchana ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati. Aidha, katika eneo la daraja la barabara ya Essuri, kazi zinaendelea kwa saa 24 kila siku.

‎"Tunatarajia ifikapo mwisho wa mwezi Agosti mwaka huu utekelezaji wa Barabara ya Mateves utafikia asilimia 85 endapo hakutakuwa na changamoto kubwa hususan mvua", amesema.

‎Amesema baada  ya fidia kulipwa  kwa watu waliopitiwa na mradi huo, kasi ya utekelezaji imeongezeka kwa kiwango kikubwa. Tuna imani kwamba ifikapo mwezi Desemba mwaka huu ujenzi wa barabara ya Mateves AFCON–Bondeni City utakuwa umekamilika kwa asilimia 100", amesema.

‎Kukamilika kwa mradi huo hakutasaidia tu kufanikisha maandalizi ya AFCON 2027 bali pia kutaimarisha mtandao wa barabara jijini Arusha, kupunguza msongamano wa magari, kuchochea shughuli za kiuchumi na kuacha urithi wa miundombinu bora itakayowanufaisha wananchi kwa vizazi vijavyo.








Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha kunakuwa na uwiano kati ya udhibiti wa taka za plastiki, ulinzi wa mazingira na ukuaji wa sekta ya viwanda ili uchumi wa nchi uendelee kuimarika.
 

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umefungua fursa mpya za uwekezaji katika sekta ya makazi, majengo ya biashara na maendeleo ya miji, hatua inayolenga kuboresha huduma kwa wananchi, kuvutia mitaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Meneja wa TBA Mkoa wa Dodoma, Qs. Emmanuel Wambura, amesema hayo katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.

Amesema TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi miradi mbalimbali ya Serikali katika sekta tofauti, ikiwemo ujenzi wa majengo ya Wizara ya Kilimo na taasisi zake, ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), vituo vya afya pamoja na taasisi nyingine za umma.

Kwa mujibu wa Qs. Wambura, utekelezaji wa miradi hiyo unalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha mazingira ya kazi katika taasisi za Serikali.

“TBA inaendelea kutekeleza dhamana yake ya kuhakikisha Serikali inapata majengo bora, salama na ya kisasa. Miradi mingi ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, huku mingine ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia miundombinu hiyo,” amesema Qs. Wambura.

Amesema mbali na miradi ya Serikali, TBA imeweka mkazo katika kuendeleza miradi ya makazi na miji ya kisasa, ikiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba 3,500 katika eneo la Nzuguni jijini Dodoma, ambao unaendelea kutekelezwa.

Amebainisha kuwa wakala huo umefungua fursa za uwekezaji kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), ambapo tayari baadhi ya wawekezaji, ikiwemo kampuni ya Fit Group kutoka Nigeria, wameonyesha nia ya kuwekeza katika mradi huo wa makazi.

Aidha, amesema TBA imeandaa maeneo yenye fursa kubwa za uwekezaji katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, ambapo wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika nyumba za makazi, majengo ya biashara, hoteli, ofisi na maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao.

Qs. Wambura amefafanua kuwa Mkoa wa Dodoma pekee una eneo la takribani hekta 630 lililoandaliwa kwa ajili ya uwekezaji, likiwa na miundombinu muhimu na mazingira rafiki kwa shughuli za biashara.

“Taratibu za uwekezaji ni wazi na rahisi. Tunawakaribisha Watanzania na wawekezaji kutoka nje ya nchi kushirikiana nasi katika kuendeleza miradi yenye tija kwa uchumi wa Taifa. Tunahitaji wawekezaji wenye uwezo na wanaozingatia sheria za nchi ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa,” amesema.

Katika hatua nyingine, amesema TBA imepanua wigo wa shughuli zake hadi kusimamia miradi ya ujenzi na ukarabati wa majengo ya ubalozi wa Tanzania nje ya nchi kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Amesema hatua hiyo inaonesha kuendelea kuaminiwa kwa uwezo wa kitaalamu wa wakala huo katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ndani na nje ya Tanzania.

Akizungumzia mchango wa TBA katika sekta ya kilimo, Qs. Wambura amesema wakala huo umeendelea kubuni na kusimamia ujenzi wa maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao, maabara za utafiti wa kilimo na miundombinu mingine muhimu inayosaidia kuongeza thamani ya mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kukuza ushindani wa sekta hiyo.

Amewakaribisha wananchi, taasisi na wawekezaji kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nanenane ili kupata taarifa kuhusu huduma zinazotolewa na wakala huo, ikiwemo usanifu wa majengo, ukadiriaji wa gharama za ujenzi, usimamizi wa miradi na fursa mbalimbali za uwekezaji.

“TBA ipo katika mikoa yote 26 ya Tanzania na itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga miundombinu ya kisasa, kuvutia uwekezaji na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” amesema Qs. Wambura.

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Na. Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi kilicholenga kujadili utendaji wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka -BRT leo 04 Agosti, 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam.

Serikali kupitia Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imewahakikishia wakulima nchini upatikanaji wa mbolea ya kutosha kwa msimu wa kilimo wa mwaka huu, ikitangaza kuanza kwa usambazaji wa tani 33,000 za mbolea ya kupandia aina ya DAP zilizowasili nchini kupitia Bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza leo Agosti 4,2026 katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Lameck Borega, amesema kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa wakati, kwa bei nafuu na katika maeneo yote ya nchi.

Amesema TFC, ambayo ni kampuni inayomilikiwa kwa asilimia 100 na Serikali chini ya Wizara ya Kilimo, ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa mbolea kwa wakulima wote ili kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Bw.Borega amesema kwa msimu wa mwaka huu kampuni imepanga kusambaza takribani tani 200,000 za mbolea za aina mbalimbali, huku meli ya MV Aurora ikiwa tayari imewasili na tani 33,000 za mbolea ya DAP ambazo zimeanza kusafirishwa kwenda vituo vya TFC na kwa mawakala wake nchini kote.

"Mbolea hii imewasili kwa wakati muafaka wakati wakulima wengi wanaendelea kuandaa mashamba yao kwa ajili ya msimu mpya wa kilimo. Lengo letu ni kuhakikisha hakuna mkulima anayekosa mbolea kutokana na ucheleweshaji wa usambazaji," amesema Borega.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kubeba sehemu kubwa ya gharama za mbolea kupitia mpango wa ruzuku ili kupunguza mzigo kwa wakulima. Alifafanua kuwa mfuko mmoja wa kilo 50 wa mbolea ya DAP ungegharimu karibu shilingi 200,000 bila ruzuku, lakini kutokana na msaada wa Serikali mkulima analipa karibu nusu ya gharama hiyo huku Serikali ikigharamia sehemu iliyobaki.

Amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwa kuhakikisha pembejeo muhimu zinapatikana kwa gharama zinazomuduwa na wakulima.

Bw.Borega ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa usambazaji wa mbolea ya kupandia, Serikali inatarajia kuingiza nchini tani 40,000 za mbolea ya kukuzia aina ya Urea mwezi Septemba, hatua itakayowezesha wakulima kupata pembejeo zote muhimu katika kipindi sahihi cha uzalishaji.

"Niwaondoe wasiwasi wakulima wote nchini Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakati na kwa mfumo wa ruzuku ili kila mkulima aweze kunufaika na kuongeza uzalishaji wa mazao," amesema 

Sambamba na hilo,Bw. Borega amewataka wakulima wanaotembelea Maonesho ya Nanenane kutembelea  banda la TFC ili kupata elimu ya matumizi sahihi ya mbolea, namna ya kunufaika na mfumo wa ruzuku na mahali pa kupata mbolea hizo.

Amesema TFC pia inaendelea kushiriki maonesho ya Nanenane katika kanda mbalimbali nchini ikiwemo Mbeya, Arusha, Mwanza, Simiyu, Iringa na Morogoro, ambako wakulima wanaendelea kupewa elimu ya kitaalamu kuhusu matumizi bora ya mbolea na njia rahisi za kuzipata kupitia mtandao wa vituo na mawakala wa kampuni hiyo.

Hata hivyo amesisitiza kuwa matumizi sahihi ya mbolea ni nguzo muhimu ya kuongeza tija ya kilimo, hivyo akawataka wakulima kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu itakayowawezesha kuongeza uzalishaji na kuinua kipato chao.




RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA UMOJA WA MABUNGE DUNIANI (IPU) JIJINI ARUSHA

Zaidi ya washiriki 2,000 kutoka nchi mbalimbali duniani wanatarajiwa kuhudhuria Mkutano wa 153 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) utakaofanyika Oktoba 5-9, 2026 jijini Arusha.

Taarifa hiyo imetolewa na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 4, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC) Jijini Arusha kuhusu utayari wa Bunge kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

Mheshimiwa Spika amesema miongoni mwa watakaoshiriki mkutano huo ni Maspika wa Bunge, Wabunge, maafisa wa Bunge, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na kikanda, wanadiplomasia, washirika wa maendeleo, mashirika ya kiraia, taasisi za Elimu ya juu pamoja na vyombo vya habari.

Ameitaja Kauli Mbiu ya Mkutano kuwa “Kuimarisha Utawala Bora na Kuiwezesha Jamii kupitia Ushirikishwaji, Imani na Fursa kwa Wote" na kwamba ufunguzi rasmi utafanywa na Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan 05 Oktoba, 2026.

Amesema Bunge la Tanzania lipo tayari kikamilifu kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa kihistoria na kwamba ni heshima kubwa kwa nchi na ni uthibitisho wa imani ambayo jumuiya ya kimataifa ya mabunge inayo kwa Tanzania.

"Hii inathibitisha dhamira yetu ya muda mrefu katika kudumisha demokrasia, amani, ushirikiano wa kimataifa na diplomasia ya kibunge" amesema Mheshimiwa Spika.

Mheshimiwa Spika amesema ana imani mkutano huo utaleta mchango mkubwa katika kutatua changamoto zinazokabili dunia kwa sasa ikiwemo Mabadiliko ya Tabianchi, migogoro ya kimataifa na ugumu wa maisha.

 Mbali na ratiba rasmi, amesema mkutano huo utaimarisha ushirikiano wa Kimataifa, kukuza ushirikiano wa kimkakati na kutoa fursa adhimu kwa sekta za utalii, usafirishaji na huduma nchini.

“Pia utatoa fursa ya kuionesha dunia utajiri wa utamaduni wa Tanzania, fursa za uwekezaji na vivutio vya utalii vinavyotambulika duniani,” amesema

Awali akizungumza baada ya kukagua Ukumbi wa AICC, Mheshimiwa Zungu amesema mandaliziyanaendelea vizuri kupitia ushirikiano wa karibu kati ya Bunge, Serikali, Sekretarieti ya IPU na wadau wengine.

Amewakaribisha washiriki wote Jijini Arusha katika mkutano huo.
Urafiki wa kweli ulipata nafasi ya kuadhimishwa kwa namna ya kipekee wakati wanawake kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam walipokutana katika hafla ya Girlfriends Circle, iliyoandaliwa na kampuni ya Eventfully kwa kushirikiana na Serengeti Premium Apple.

 


Na Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.

 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Africa50 Bw. Alain Ebobisse, amebainisha kuwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), ni fursa ya kuonesha mafanikio ambayo Tanzania imeyapata katika sekta ya miundombinu, kutangaza fursa zinazopatikana ikiwa ni ushahidi kuwa uwekezaji katika miundombinu ya Afrika una tija, unalipa na unaweza kufadhiliwa.

 

Bw. Ebobisse alisema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi, Khamis Mussa Omar (MB), katika kikao cha pamoja cha maandalizi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.

 

Bw. Ebobisse alibainisha kuwa ajenda kuu ya mkutano huo itakuwa ni ujenzi wa uchumi wa viwanda barani Afrika kupitia uongezaji thamani wa rasilimali za ndani, jambo linalotegemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa nishati ya uhakika huku akipongeza dira ya uongozi wa Tanzania katika kuvutia mtaji wa sekta binafsi.

 

"Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana maono makubwa ya kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi katika sekta ya miundombinu nchini Tanzania. Sisi Africa50 ni mojawapo ya nyenzo zinazosaidia kutekeleza maono hayo kwa kushirikiana katika utekelezaji wa miradi, ambapo miundombinu mbalimbali ikiwemo nishati ni muhimu katika maendeleo ya viwanda na kutuma ujumbe kuwa Afrika iko tayari kwa uwekezaji," alisema Bw. Ebobisse.

 

Bw. Ebobisse aliongeza kuwa Africa50 imeweka kipaumbele kikubwa katika miundombinu ya gesi asilia ikiwemo mabomba na mitambo ya uchakataji ili kuelekeza gesi zaidi kwenye maeneo ya viwanda nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla ili kuongeza thamani ya rasilimali na kuimarisha uchumi wa Afrika.

 

Alisisitiza kuwa licha ya uwepo wa kundi kubwa la wawekezaji tayari wenye hamasa ya kushiriki, huo ulikuwa wakati muafaka wa kutuma ujumbe kwa Tanzania, Afrika na dunia nzima kwamba Bara la Afrika liko tayari na ni eneo salama na la kimkakati kwa uwekezaji wa miundombinu.

 

Naye Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi, Khamis Mussa Omar (MB), alisema kuwa Serikali imekamilisha maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Jukwaa la Miundombinu Afrika unaolenga kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi katika miundombinu ya kimkakati, ikiwemo gesi asilia, umeme na viwanda barani Afrika.

 

Alisema Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Dar es Salaam unatarajiwa kufunguliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

 

"Tunatarajia kusaini hati tatu za mashirikiano katika afya hasa usafishaji wa damu (dialysis), tumefanya tathmini ya maendeleo ya miradi ya kimkakati ikiwemo mradi wa gesi asilia, miundombinu ya usafirishaji wa nishati, pamoja na masuala mengine ya nishati yanayolenga kuharakisha maendeleo ya uchumi wa viwanda, " alisema Mhe. Balozi Omar.

 

Balozi Omar alithibitisha kuwa Serikali imejiridhisha kuwa maandalizi yote muhimu ya mkutano huo unaotarajiwa kukutanisha viongozi wa kitaifa, marais wa taasisi za kifedha, na wawekezaji wakubwa wa kimataifa yako tayari ili kuhakikisha mkutano huo wa siku mbili unapata mafanikio makubwa na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

 Waswahili husema nyumba njema haikosi wageni na hii imedhihirika leo tarehe 4 Agosti, 2026 baada ya Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar mhe Zubeir Ali Maulid kutembelea eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Akiwa katika geti la Loduare Spika Maulid alipata taarifa ya vivutio vya eneo hilo iliiyotolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Mariam Kobelo ambapo alielezwa kuendelea kuimarika kwa shughuli za uhifadhi,utalii na maendeleo ya jamii.

Aidha, haitoshi Spika Zubeir alielezwa kuhusiana na maajabu ya mchanga unaohama uliopo eneo la Olduvai ambapo mamia ya watu ambao mapenzi yao yamelega lega humiminika katika eneo hilo kuimarisha mapenzi.

Kwa mujibu wa simulizi za kihistoria kutokana na mchanga huo kuwa na asili ya sumaku wapendao wakifika mahali hapo penzi huwa motomoto na kuimarika.

Akizungumza baada ya ziara hiyo Spika Zubeir ametoa wito kwa watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii ili kujifunza na kupata utulivu.

Spika Zubeir ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kufanya kazi usiku na mchana katika kulinda uhifadhi, kusimamia utalii na maendeleo ya jamii.