Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Na.Alex Sonna-DODOMA

BODI  ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imetangaza mafanikio makubwa katika mwaka wa fedha 2025/26 baada ya wakulima nchini kulipwa zaidi ya Shilingi trilioni 2.298 kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS), huku kiasi cha mazao yaliyouzwa kupitia mfumo huo kikiongezeka kwa asilimia 43.6 ndani ya mwaka mmoja.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 31,2026 jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa shughuli za bodi  hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026 na mwelekeo wa mwaka 2026/2027.

Amesema mfumo huo umeendelea kuwa chachu ya maendeleo ya sekta ya kilimo kwa kuwawezesha wakulima kupata masoko na bei zenye ushindani na malipo ya uhakika kupitia taasisi za fedha.

Bw.Bangu amesema  katika mwaka wa fedha 2025/26, jumla ya kilo bilioni 1.122 za mazao tisa, yakiwemo korosho, ufuta, kahawa, kakao, mbaazi, dengu, choroko, soya na chai, ziliuzwa kupitia minada ya kidijitali inayosimamiwa na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), ikilinganishwa na kilo milioni 781.6 mwaka uliotangulia.

"Ongezeko hili linaonyesha kuwa wakulima wengi zaidi wameendelea kuuamini Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuuona kuwa njia salama na yenye manufaa ya kuuza mazao yao," amesema  Bw. Bangu.

Amefafanua kuwa kutokana na mauzo hayo, Serikali za Mitaa zilikusanya zaidi ya Shilingi bilioni 61 kupitia ushuru wa mazao (CESS), huku thamani ya biashara yote iliyofanyika kupitia mfumo huo ikifikia Shilingi trilioni 2.679, hali inayodhihirisha mchango mkubwa wa mfumo huo katika kukuza uchumi wa Taifa.

Kwa mujibu wa Bw. Bangu, mfumo huo sasa unatekelezwa katika mikoa 23 na unahusisha mazao na bidhaa 18, tofauti na mwaka 2006 ulipoanza na zao moja pekee la korosho.

Amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika kuimarisha mfumo huo ambapo katika mwaka wa fedha 2025/26 ilitoa Shilingi milioni 950 zilizotumika kuboresha mifumo ya TEHAMA, kutoa elimu kwa wakulima, kuimarisha ukaguzi wa maghala na kununua vitendea kazi vya kuongeza ufanisi wa huduma.

Mbali na mafanikio hayo, WRRB ilibainisha kuwa mapato yake ya ndani yameongezeka kwa kasi kutoka Shilingi bilioni 1.998 mwaka 2023/24 hadi Shilingi bilioni 5.870 mwaka 2025/26, hatua iliyoifanya Bodi kujigharamia zaidi ya asilimia 67 ya bajeti yake na kupunguza utegemezi wa fedha za Serikali.

Aidha, mfumo huo ulizalisha jumla ya ajira 31,875 kupitia shughuli mbalimbali za ukusanyaji wa mazao, uhifadhi maghalani, usafirishaji, upimaji wa ubora na huduma nyingine katika mnyororo wa thamani wa biashara ya mazao.

Katika hatua nyingine, WRRB imetangaza mpango wa kupanua Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kutoka kwenye mazao ya kilimo kwenda katika sekta nyingine za uzalishaji, ambapo kwa mara ya kwanza sekta ya mifugo itaingizwa kwenye mfumo huo katika mwaka wa fedha 2026/27.

Bw. Bangu alisema mnada wa kwanza wa mifugo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala unatarajiwa kufanyika katika Wilaya ya Mvomero, huku bidhaa nyingine zikiwemo mwani, ngozi na mazao ya bustani zikitarajiwa kuingizwa kadri maandalizi ya kisera na kiutendaji yatakavyokamilika.

Ameongeza kuwa WRRB itaendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali kwa kuboresha mifumo ya WRMS na WRS-MIS, kuongeza matumizi ya stakabadhi za kielektroniki pamoja na kuunganisha huduma za leseni, ukaguzi, biashara na malipo katika mfumo mmoja.

Pia amesema Bodi itaendelea kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), NBC na taasisi nyingine za fedha ili kuongeza upatikanaji wa mikopo inayotumia Stakabadhi za Ghala kama dhamana, hatua itakayowawezesha wakulima na wafugaji kupata mitaji bila kuuza bidhaa zao kwa hasara.

Bw. Bangu amesema mafanikio hayo ni matokeo ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na usimamizi wa Wizara ya Viwanda na Biashara, akisisitiza kuwa WRRB itaendelea kutekeleza mikakati ya kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania, kuimarisha masoko ya wakulima na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Julai 31, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa bodi   hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.

Kariakoo, Julai 30, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa kikodi Kariakoo imeendesha semina maalum kwa wafanyabiashara ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kutoa elimu ya kodi na kuwajengea uelewa kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi yaliyoanza kutumika kwa mwaka 2026/2027.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mahusiano ya kidiplomasia kati ya Ufalme wa Morocco na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yameendelea kuimarika kwa kasi tangu ziara ya kihistoria ya Kiserikali ya Mfalme Mtukufu Mohammed VI nchini Tanzania mwaka 2016, huku ushirikiano katika sekta mbalimbali ukizidi kupanuka na kuleta manufaa kwa mataifa yote mawili.



Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania Bw. Burhan Kishenyi, akizungumza Julai 30, 2026 wakati akifungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
...........................................
Na Mwandishi Wetu Dodoma




Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania Bw. Burhan Kishenyi, leo tarehe 30.07.2026 amefungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, jijini Dodoma, na imewakutanisha washiriki kutoka taasisi mbalimbali za umma na wadau wanaoshughulika na masuala ya haki na ustawi wa watu wenye ulemavu.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Bw. Kishenyi amesema kuwa utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ni msingi muhimu katika kujenga jamii jumuishi inayotoa fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi.


Amesisitiza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inaweka msisitizo katika ushirikishwaji wa makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili kuchangia kikamilifu maendeleo ya kiuchumi na kijamii.


Aidha, amewataka washiriki kutumia warsha hiyo kujadili kwa kina wajibu wa kila taasisi katika kutekeleza matakwa ya sheria, kubadilishana uzoefu na kuibua mapendekezo yatakayosaidia kuondoa vikwazo vinavyokwamisha upatikanaji wa haki na huduma kwa watu wenye ulemavu.


Washiriki wa warsha hiyo wanatarajiwa kujengewa uwezo kuhusu tafsiri na utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, pamoja na namna ya kuoanisha utekelezaji wake na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kujenga Tanzania jumuishi, yenye usawa, haki na maendeleo endelevu kwa wananchi wote.


Kwa upande wake , Bw. Harold Sungusia, Rais Mstaafu wa TLS ambaye pia ni wakili wa kujitegemea alisisitiza umuhimu wa kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika mchakato wa maboresho ya sheria ili kuhakikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatekelezwa kwa misingi ya usawa, haki na ushirikishwaji.


Akizungumza katika mkutano uliojadili mwelekeo wa maboresho ya sheria na maendeleo ya taifa, Bw. Sungusia alisema kuwa sheria bora zinapaswa kuzingatia mahitaji ya makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili wasibaki nyuma katika safari ya maendeleo.


Alieleza kuwa ushiriki wa watu wenye ulemavu katika utoaji wa maoni na maamuzi kuhusu sheria ni muhimu kwa sababu unasaidia kutunga na kuboresha sheria zinazolinda haki zao na kuondoa vikwazo vinavyowazuia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa.


Aidha, alibainisha kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji mfumo wa sheria unaohakikisha fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote.


Bw. Sungusia alisema kuwa kujenga taifa lenye maendeleo endelevu kunategemea uwepo wa sheria jumuishi zinazolinda haki za kila mwananchi na kuweka mazingira yanayowawezesha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.


Washiriki wa mkutano huo walikubaliana kuwa ushirikishwaji wa makundi maalumu katika mchakato wa maboresho ya sheria ni nguzo muhimu ya kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kujenga jamii yenye usawa na haki kwa wote.
Wadau mbalimbali wakishiriki warsha hiyo.


Wadau wakichangia mada katika warsha hiyo.

Michango mbalimbali ikitolewa katika warsha hiyo.

Warsha hiyo ikiendelea

Michango ikiendelea kutolewa.

Taswira ya warsha hiyo.

 

Na.Mwandishi Wetu-Babati, Manyara

 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kaskazini imeendesha semina ya kuwajengea uwezo Maafisa wa Huduma kwa Wateja, Mahusiano na Sheria kutoka TANESCO na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira za Kanda ya Kaskazini kuhusu huduma kwa wateja na uzingatiaji wa matakwa ya kisheria.

Akifungua semina hiyo katika Hoteli ya White Rose, Babati, Meneja wa EWURA Kanda ya Kaskazini, Bw. George Mhina, aliwasisitiza washiriki kuyafahamu vyema majukumu yao ili waweze kutoa majibu sahihi, ya wakati na yanayozingatia sheria, hivyo kuboresha huduma kwa wateja.

Kwa niaba ya washiriki, Bi. Devotha Mayala kutoka Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tanga na Bw. Samwel Mandari kutoka TANESCO waliishukuru EWURA kwa mafunzo hayo, wakieleza kuwa yamewaongezea uelewa na uwezo wa kuwahudumia wateja kwa weledi zaidi.

Semina hiyo ni sehemu ya juhudi za EWURA za kuimarisha uwezo wa watoa huduma na kulinda haki za watumiaji wa huduma za nishati na maji kupitia Udhibiti wa Haki kwa Matokeo Chanya.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa mwaka 2026, yatakayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24 katika viwanja vya michezo vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga.

.......

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametangaza maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa mwaka 2026, yatakayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24 katika viwanja vya michezo vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga.

Akitangaza maadhimisho hayo amesema yatawakutanisha wadau kutoka wizara mbalimbali, vyuo vya elimu ya juu, vyuo vya ufundi na ufundi stadi, mashirika ya utafiti na sekta binafsi kwa ajili ya maonesho na mijadala ya kimkakati katika kuimarisha elimu, ujuzi na ubunifu nchini.

Prof. Mkenda amebainisha kuwa wananchi watapata fursa ya kushuhudia bunifu zilizobuniwa na vijana wa Kitanzania, ambazo zikovkatika hatua mbalimbali ikiwemo zilizo sokoni akitoleta mfano mashine ya kukamua mafuta ya parachichi (Avomero), mabegi ya shule yenye mfumo wa umeme jua (Soma Bags), na mita janja za maji (Smart Prepaid Water Meter).

Amesisitiza kuwa bunifu hizo ni ushahidi wa jitihada za serikali kuendeleza wabunifu na kuwezesha uwepo wa bidhaa hizo za ndani zinazotatua changamoto za kijamii na kiuchumi.

Aidha, Waziri Mkenda amesema zaidi ya bunifu 70 zipo katika hatua mbalimbali za kukuzwa ili ziwe biashara halisi na kuchangia uchumi wa taifa. Ameongeza kuwa Serikali imeanzisha mfuko maalum wa kusaidia wabunifu kupunguza gharama za uzalishaji na kuharakisha ukuaji wa biashara zao.

Pia ameeleza kuwa katika wiki ya ubunifu kutakuwa na Mashindano ya Kitaifa ya Ujuzi ambapo ni vigego vyake vya ushindani ni vya kimataifa na ikiwa ni maandalixi ya Nchi kushiriki katika mashindano ya kimataifa (World Skills Competition)

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, amesema serikali ipo katika hatua za kuhuisha Sera ya Taifa ya Sayansi, Teknolojia ili iendane na mabadiliko ya kidunia na mahitaji ya sasa.

Ameeleza kuwa sera mpya itakuwa mwongozo wa namna masuala yote ya sayansi, teknolojia na ubunifu yatakavyoshughulikiwa nchini, ikiwemo mashindano ya kitaifa ya ubunifu.

Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, Prof. Ladislus Mnyone, amesema serikali imekamilisha mkakati wa kuongeza ushiriki wa Watanzania wanaoishi nje ya nchi (diaspora) katika kuendeleza bunifu na teknolojia za ndani.

Aidha, amebainisha kuwa katika kuendelea kuibua wabunifu halmashauri 90 tayari zimeanzisha madawati ya sayansi na ubunifu, hatua inayowawezesha wabunifu kuwasilisha mawazo yao na kuunganishwa na taasisi ya COSTECH kwa ajili ya urndelezaji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, amepongeza jitihada za serikali katika kuhamasisha ubunifu nchini. Amesema banda maalum litakuwepo Tanga kuonyesha bunifu zilizofanikiwa kuingia sokoni ili kutoa ushuhuda wa mafanikio ya wabunifu wa Kitanzania.

Amesisitiza kuwa ushirikiano wa serikali, wadau na wananchi ni muhimu katika kuendeleza ubunifu na kuchochea maendeleo ya taifa.

Kauli mbiu ya mwaka huu: “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050”

Na Mwandishi Wetu

Hospitali ya Medinova Specialized Polyclinic imezindua rasmi huduma ya Tibamazoezi (Physiotherapy) ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupanua huduma za kibingwa na kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imesema imeendelea kuimarisha nafasi yake katika kufadhili sekta ya kilimo nchini baada ya mtaji wake kuongezeka kutoka Sh bilioni 60 hadi Sh bilioni 452.16, hatua iliyowezesha kupanua utoaji wa mikopo na huduma za kifedha kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.

 


Kupambana kwenye korido za sheria bila kupata haki ni moja ya mateso makubwa zaidi yanayoweza kukatisha tamaa na kuua roho ya mtu. 

Kwa zaidi ya miaka mitano, nilikuwa nikipambana mahakamani kutafuta haki yangu iliyopora na watu wenye fedha na ushawishi mkubwa.

Kila mara nilipowasilisha ushahidi na kufungua kesi, matokeo yalikuwa yale yale hukumu zilipotoshwa, ushahidi wangu ulipingwa, au kesi ilitupiliwa mbali kwa sababu zisizoeleweka.

Nilipoteza Rufaa baada ya Rufaa, huku nikitazama mali na jasho langu vikichukuliwa mchana kweupe. Gharama za mawakili na ada za mahakama zilitumia akiba yangu yote na kuniingiza kwenye madeni makubwa.

Watu wengi walianza kunidhiaki na kunipuuza, wakiamini kuwa nilikuwa nikipoteza muda kupambana na watu waliokuwa wameshikilia mfumo na kuwa na bahati isiyotikisika. Wasiwasi na msongo wa mawazo vilinikosesha amani na usingizi usiku. SOMA ZAIDI.

 

Kujituma kazini na kuonyesha matokeo bora ni lengo la kila mfanyikazi anayetaka kukua kitaaluma. Kwa zaidi ya miaka mitano, nilikuwa mfanyikazi wa mfano katika kampuni yetu.

Nilikuwa wa kwanza kuwasili ofisini, wa mwisho kuondoka, na miradi yote niliyopewa nilitekeleza kwa ufanisi wa hali ya juu. Hata hivyo, kila mwaka ulipowadia muda wa tathmini na kupandishwa vyo (promotions), jina langu lilipitwa kimyakimya.

Walikuwa wakipandishwa cheo watu niliowafundisha kazi au wale waliokuwa na uzoefu mdogo kabisa. Kila nilipojaribu kumuuliza mkurugenzi au idara ya rasilimali watu (HR), nilipewa ahadi hewa za “mwaka ujao ni zamu yako.”

Nilibaki nikijihisi nimekwama, nikiwa na majuto na msongo mkubwa wa mawazo huku nikiona juhudi zangu zote zikienda bure. SOMA ZAIDI.
Familia ndiyo kila kitu katika maisha ya mwanamume, na inapovunjika, unahisi kama dunia yote imekuporomokea. Kwa miaka mingi tulikuwa tukilinda na kuijenga ndoa yetu, tukipitia mengi na kupata watoto wazuri.

Hata hivyo, taratibu migogoro midogo midogo ilianza kuingia ndani ya nyumba yetu. Kila siku kulikuwa na maneno ya shombo, kutokuelewana, na hasira zisizo na msingi.

Siku moja baada ya ugomvi mkubwa, nilirudi nyumbani jioni na kukuta nyumba ipo tupu mke wangu alikuwa amebeba kila kitu, akachukua watoto, na kutoweka bila kuniambia anakokwenda.

​Nilibaki peke yangu kwenye nyumba iliyokuwa na baridi na ukimya wa kutisha. Nilijaribu kumtafuta kwa simu lakini alikuwa ameniziba (blocked) kila mahali, na ndugu zake walipokea simu zangu kwa dharau na kejeli wakidai kuwa sitamuona tena.

Wasiwasi, upweke, na maumivu ya kuwakosa watoto wangu viliniletea msongo mkubwa wa mawazo. Nilianza kujiona kama mwanamume niliyefeli kabisa. SOMA ZAIDI.

 

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, Julai 29, 2026

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza rasmi kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, yakilenga kuimarisha weledi, maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari wa Bongo FM jijini Dar es Salaam, redio dada ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya JAB, Tido Mhando, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kuelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, kwa kuzingatia weledi, maadili na uwajibikaji.

“Mafunzo haya ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari. Leo tumeanza rasmi na waandishi wa habari wa Bongo FM, tutaendelea kwa vyombo vingine pia kwa sababu, kutakuwa na mafunzo ya muda mfupi na ya muda mrefu. Hivyo, mafunzo haya yawe fursa ya kujenga uwezo na kuweka msingi imara wa kukuza na kulinda taaluma ya uandishi wa habari kwa kuongeza maarifa na weledi,” amesema Wakili Kipangula.

Akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, historia na uanzishwaji wake, katika mafunzo hayo yaliyoanza leo tarehe 29 Julai, 2026 katika ukumbi wa Bodi, Wakili Kipangula amesema sheria hiyo imeweka msingi wa kuimarisha taaluma ya habari kwa kubainisha viwango vya weledi, maadili na uwajibikaji

Amesisitiza kuwa JAB itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo kwa kuzingatia haki, uwazi na kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari, huku ikihakikisha taaluma ya habari inalinda maslahi ya umma..

Aidha, amewataka waandishi wa habari kuzingatia sheria na maadili katika kila hatua ya ukusanyaji, uchakataji na usambazaji wa habari ili kujiepusha na madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na ukiukaji wa taaluma.

Amesema kuzingatia misingi hiyo kunajenga weledi, kunalinda heshima ya taaluma na kuimarisha imani ya jamii kwa vyombo vya habari.
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.

Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

"Mafunzo haya yametupatia maarifa muhimu yatakayotusaidia kutekeleza majukumu yetu kwa kuzingatia maadili, sheria na viwango vya taaluma ya uandishi wa habari. Tunaamini yatachangia kuboresha utendaji wetu na kuongeza uwajibikaji katika kuhabarisha umma," wamesema washiriki hao.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.



📌PPRA Yatambua Ubora na Usimamizi .

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Tanga imeibuka miongoni mwa taasisi zilizofanya vizuri zaidi nchini katika usimamizi wa ununuzi wa umma baada ya kutwaa tuzo mbili katika Kongamano la 10 la Ununuzi wa Umma la mwaka 2026 linaloendelea jijini Arusha.

Tuzo hizo zilizotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) zinatokana na mafanikio ya TARURA Tanga katika kuzingatia kikamilifu matakwa ya Sheria ya Ununuzi wa Umma pamoja na kuonyesha ufanisi mkubwa katika utoaji wa mikataba.

Katika tuzo ya kwanza TARURA Tanga ilitambuliwa kwa kutekeleza kwa kiwango cha juu matakwa ya sheria yanayotaka asilimia 30 ya bajeti ya ununuzi kutengwa kwa ajili ya vikundi vya kijamii hatua iliyotajwa kuwa mfano bora wa utekelezaji wa sera za Serikali za kuwainua makundi yenye mahitaji maalum kiuchumi.

Tuzo ya pili ilitokana na mafanikio ya Wakala huo katika usimamizi wa mikataba baada ya kufanikisha utoaji wa mikataba 106 katika mwaka wa fedha 2025/2026, jambo lililoiweka miongoni mwa taasisi zilizofanya vizuri zaidi nchini.

Mafanikio hayo yanaendelea kuithibitisha TARURA kuwa miongoni mwa taasisi zinazosimamia kwa ufanisi matumizi ya fedha za umma kupitia uzingatiaji wa sheria, uwazi na uwajibikaji katika mchakato wa ununuzi nchini.