Serikali imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha sekta ya elimu kwa kuongeza miaka ya elimu ya lazima, kupanua fursa za elimu ya sekondari na kuimarisha mafunzo ya ufundi ili kuwapa vijana uwezo wa kushiriki kikamilifu katika soko la ajira.

Akizungumza Septemba 02, 2026 jijini Dodoma na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema maandalizi ya utekelezaji wa miaka 10 ya elimu ya lazima kuanzia mwaka 2028 yanaendelea, hatua itakayohitaji miundombinu, walimu na nafasi za kutosha katika shule za sekondari.  

Prof. Mkenda amebainisha kuwa mpango huo utasababisha ongezeko kubwa la wanafunzi watakaoingia sekondari, hivyo Serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha wanafunzi wote wanaostahili wanapata nafasi ya kuendelea na masomo.  

Aidha, ameongeza kuwa  Serikali inaendelea kuimarisha mfumo wa elimu wenye mikondo ya elimu ya jumla na elimu ya amali, ili wanafunzi wapate maarifa na stadi zinazowawezesha kuajirika au kujiajiri.  

Katika mazungumzo hayo, Prof. Mkenda ameeleza kuwa Serikali inajenga vyuo vya ufundi katika maeneo mbalimbali na kuimarisha mafunzo ya ufundi ili kukidhi mahitaji ya vijana na uchumi wa Taifa.  

Prof. Mkenda ameongeza kuwa Serikali inawekeza katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati pamoja na teknolojia mpya kama akili bandia (AI), ujifunzaji wa mashine na usalama wa mtandao, ili kuandaa wataalamu wa kisasa.  

Amesisitiza  umuhimu wa ushiriki wa sekta binafsi katika kupanua fursa za elimu, hususan katika ujenzi wa miundombinu na utoaji wa elimu ya amali.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa Serikali inatazama uwezekano wa kuboresha vivutio vya kisera vitakavyoongeza uwekezaji wa sekta binafsi katika elimu.  

Naye Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Marianne Young, amepongeza juhudi za Tanzania na kuahidi kuendeleza ushirikiano katika elimu na na mafunzo ya  ufundi, ikiwemo kuunganisha taasisi za Tanzania na vyuo vikuu vya Uingereza katika maeneo ya teknolojia ya kisasa na mazingira.

 


Na Denis Chambi, Tanga.


KUTOKANA na kasi ya ukuaji na maendeleo ya mkoa wa Tanga inayotokana na uwekezaji wa Serikali kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo Bomba la Mafuta ghafi pamoja na uboreshaji wa Bandari  Shirika la Nyumba Tanzania  'NHC' linaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa nyumba za Makazi pamoja na biashara ili kuweza kukidhi ongezeko la watu na uhitaji.

Akizungumza ofisni kwake Meneja wa Shirika la Nyumba Tanzania 'NHC' Mkoa wa Tanga Mhandishi Mussa Kamendu amesema kuwa kumekuwa na ongezeko wa watu  wakiwemo watumishi wa umma , taasisi na sekta binafsi  hali ambayo inaonyesha kuwepo na uhitaji wa Makazi pamoja na nyumba za biashara kadiri miaka inavyokwenda hii ikichangiwa zaidi na kasi ya maendeleo ya mkoa huo ambao unazidi kukua kiuchumi.

"Tumekuwa tukitekeleza  miradi kadhaa  ambayo ni sehemu ya kukabliana na ongezeko la watu kwa maana ya mahitaji ya nyumba, tunafanya miradi hiyo kutokana na mabadiliko maendeleo na fursa mbalimbali ambazo zipo katika mkoa wa Tanga kwa sasa"

"Tunazo nyumba 20 za Makazi ambazo tumeshaziuza mradi huu upo hatua ya mwisho  tunategemea utakamilika mwanzoni mwa mwaka ujao wa fedha  tunazo nyumba  nyingine ambazo zina sehemu za ofisi , Benki pamoja na biashara"amesema Kamendu.

Amesema kwa sasa Shirika hilo lina zaidi ya wapangaji 900 lakini kutokana na  kuwa ujio wa mradi wa Bomba la Mafuta ghafi linalotoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga Tanzania umechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la watu hususani kutoka nje ya nchi.

"Kutokana na maendeleo Mkoa wa Tanga kuna watu wengi wanaamua kuhamia mkoa wa Tanga kwa sababu ya fursa zilizopo kwa sasa ambao wote hawa wanahitaji nyumba kwa sababu hiyo sisi kama Shirika tumeendelea kujipanga" amesema

Aidha Kamendu ameongeza kuwa pamoja na ujenzi wa makazi hayo Shirika hilo linaendelea kuboresha na kukarabati nyumba zake zote  zinazoendelea kutumiwa na wapangaji kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma.

"Nyumba pia zilizopo tunafanya juhudi ya kuzikarabati kwa lengo la kufanya nyumba za wapangaji wetu ziweze kuwa katika hali bora na bado tunaendelea na zoezi hilo la kukarabati ambao unahusisha  kupaka rangi, kubadilisha mifumo ya umeme na maji " amesema Mhandishi Kamendu.

Kauli mbiu ya Serikali ya mkoa wa Tanga chini ya Mkuu wa mkoa huo Balozi Dkt Batilda Buriani isemayo "Tanga lango kuu la uchumi Afrika Mashariki na SADC' inaonyesha Tanga kuwa miongoni mwa Mikoa hapa nchini inayotazamwa na kuwavutia wawekezaji wa kutoka ndani na nje ya nchi.

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetekeleza Mradi wa Usambazaji Umeme katika maeneo 582 ya wachimbaji wadogo, kilimo na viwanda Tanzania Bara, kwa gharama ya Shilingi bilioni 115.

Mhe. Makamba ameyasema hayo leo Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mhe. Mwanahamisi Athumani, Mbunge wa Viti Maalumu, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatekeleza Mpango Mkakati Maalumu wa kuhakikisha maeneo ya wachimbaji wadogo yanafikishiwa umeme wa kutosha kwa lengo la kupunguza gharama za uzalishaji.

Akijibu swali hilo, Mhe. Makamba amesema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa Aprili, 2023 na kwa sasa umefikia hatua za mwisho za utekelezaji.

Aidha, amesema Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Wizara ya Madini inaendelea kuainisha maeneo ya kipaumbele yatakayofikishiwa huduma ya umeme katika hatua zinazofuata, kwa kuzingatia upatikanaji wa fedha.

Sambamba na hilo, Mhe. Makamba amesema Serikali kupitia TANESCO, kwa kutumia fedha za ndani, inaendelea kutekeleza miradi ya kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme pamoja na ujenzi na uboreshaji wa vituo vya kupoza umeme katika mikoa mbalimbali nchini, hususan maeneo yenye changamoto ya low voltage.

Amesema hatua hizo ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha maeneo yote ya uzalishaji yanafikiwa na huduma ya umeme ya kutosha na ya uhakika.

Mhe. Makamba amesisitiza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha wachimbaji wadogo, wakulima, viwanda na maeneo mengine ya uzalishaji yanapata umeme wa kutosha na wa uhakika wakati wote, ili kupunguza gharama za uzalishaji, kuongeza tija na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi nchini.

 


Na. Peter Haule na Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam


Serikali imetoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania kuwa mitaji ya uwekezaji yenye tija, itakayochochea uzalishaji, kuongeza ajira, mauzo ya nje na kukuza uchumi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati alipokuwa Mgeni Rasmi katika halfa ya Mjadala wa Bodi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt) unaofanyika kila Mwezi” Board of Directors and Members of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt) Monthly Dialogue”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wenye thamani ya takribani dola za Marekani trilioni moja, huku pato la mtu mmoja mmoja likitarajiwa kuvuka dola 7,000 ifikapo mwaka 2050, lakini pia uchumi wa viwanda, jumuishi na unaoongozwa na sekta binafsi.

“Utekelezaji wa Dira 2050 kupitia Mpango wa Muda Mrefu wa Maendeleo na Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) umeweka msisitizo mkubwa kwa sekta binafsi, ambapo mfumo wa uwekezaji wa uwiano wa asilimia 70 kwa 30 unaiweka sekta binafsi kama injini kuu ya ukuaji na ufadhili wa maendeleo” alisema
Mhe. Balozi Omar

Aliongeza kuwa Utekelezaji wa FYDP IV unahitaji uwekezaji unaokadiriwa kufikia takribani Shilingi trilioni 477, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kugharamia takribani asilimia 70, sawa na Shilingi trilioni 324.49.

Mhe. Balozi Omar, alisisitiza kuwa takwimu hizo zinaonesha wazi kuwa Tanzania haiwezi kufikia malengo yake ya maendeleo kwa kutegemea bajeti ya Serikali, mikopo ya nje au misaada ya maendeleo pekee, bali inapaswa kuongeza uwezo wa kukusanya na kutumia mitaji ya ndani na ya sekta binafsi.

Akizungumzia Mfumo wa fedha, Mhe. Balozi Omar alisema sekta ya fedha nchini imeendelea kuwa imara licha ya changamoto na misukosuko ya uchumi duniani, ikiwa imechangiwa na misingi imara ya uchumi na shughuli endelevu za kiuchumi na mageuzi mbalimbali katika sekta hiyo yameendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa sekta huku mikopo kwa sekta binafsi ikikua kwa wastani wa zaidi ya asilimia 20 na mikopo chechefu ikiendelea kudhibitiwa chini ya kiwango kinachopendekezwa cha asilimia tano.

“Mchango wa sekta ya fedha katika Pato la Taifa umeongezeka hadi kufikia asilimia 4.3, huku ujumuishaji wa kifedha kwa watu wazima ukifikia asilimia 76, Maendeleo haya yanatoa msingi mzuri wa kuongeza uwezo wa mfumo wa fedha katika kukusanya akiba na kuzielekeza kwenye uwekezaji wenye tija” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aidha, alisema Serikali inakamilisha mchakato wa kuidhinisha awamu ya pili ya Blueprint for Regulatory Reforms (MKUMBI II), ambayo inalenga kuendana na mabadiliko ya sasa ya kiuchumi, kiteknolojia na kibiashara sambamba na kuendelea kufanya mageuzi ya kisheria, kiutawala na kitaasisi yanayolenga kurahisisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Alisisitiza umuhimu wa kuongeza uwekezaji wa ndani, akieleza kuwa pamoja na uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDI) umeongezeka kutoka dola milioni 1,656 mwaka 2024 hadi dola milioni 1,718 mwaka 2025, sawa na ongezeko la asilimia 3.7, kuwa muhimu katika kuleta mitaji, teknolojia, utaalamu na masoko ya kimataifa, Watanzania wanapaswa kuwezeshwa kushiriki zaidi katika kuwekeza ndani ya uchumi wao wenyewe.

“Nawasisitiza umuhimu wa kuimarisha na kuongeza ushiriki katika masoko ya mitaji nchini, akieleza kuwa masoko yenye kina na ukwasi yanaweza kuwa chanzo muhimu cha mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya uwekezaji na Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kisheria na udhibiti yatakayowezesha kuibuka kwa bidhaa mbalimbali za masoko ya mitaji, huku ushiriki wa wananchi katika hati fungani za Serikali, mifuko ya uwekezaji na soko la hisa ukiendelea kuhamasishwa” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa Tanzania tayari ina msingi mzuri wa kifedha unaojumuisha mfumo wa benki unaokua, mifuko ya pensheni na taasisi za fedha zenye mali zinazoongezeka, ushiriki mkubwa wa wananchi katika bidhaa rasmi za uwekezaji, masoko ya mitaji yanayopanuka pamoja na sekta binafsi yenye nguvu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt), Bw. David Tarimo, alisema mjadala huo umejikita katika namna ya kubadilisha akiba zilizopo nchini kuwa mtaji wa kukuza uchumi na kuongeza upatikanaji wa mtaji wa ndani.

Alisema mjadala huo pia umeangazia malengo makubwa yaliyowekwa kupitia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Miaka 50, ambayo kwa kiasi kikubwa yanategemea ushiriki na uwekezaji wa sekta binafsi, na Mpango wa Tano wa Maendeleo wa Miaka Mitano umeweka msisitizo mkubwa zaidi katika uwekezaji wa sekta binafsi ikilinganishwa na mipango ya miaka iliyopita.

Bw. Tarimo amesema kikao hicho kimewapa wadau fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuimarisha mazingira ya uwekezaji na kuongeza uwezo wa sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa.

“Jukwaa hili lmepata fursa ya kusikiliza mipango ya Serikali kuhusu utekelezaji wa Dira hiyo, huku wajumbe nao wakitoa mawazo na mapendekezo yanayolenga kusaidia kufanikisha malengo hayo” alisema Bw. Tarimo

Aliongeza kuwa CEOrt itaendelea kushirikiana na Serikali kubaini maeneo yanayohitaji maboresho na kuunga mkono mageuzi katika kanuni na taratibu, ili kujenga mazingira ya biashara yaliyo rafiki, rahisi na yenye gharama nafuu, hususan kwa wafanyabiashara wadogo.

 


Wakala wa Vipimo (WMA) umetoa wito kwa Maafisa wanaosimamia  ununuzi na ugavi katika taasisi za umma na binafsi kuhakikisha vifaa vyote vinavyohusiana na vipimo vinawasilishwa WMA kwa ajili ya uhakiki kabla ya kupelekwa kwa watumiaji.

Akizungumza leo Septemba 2, 2026 katika Maonesho ya 21 ya  Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Uwanja wa Furahisha  jijini Mwanza, Afisa Ugavi wa WMA, Bi. Rehema Komba amesema ni vema taasisi zinapokamilisha ununuzi wa vifaa vya kivipimo,  zisivipeleke moja kwa moja kwa watumiaji bila kuhakikiwa, kwani inaweza lkupelekea hasara kwa serikali na wananchi.

"Tunasimamia mchakato wa manunuzi, lakini baada ya vifaa kufika, tuzikumbushe taasisi zetu kupeleka kwanza Wakala wa Vipimo kwa uhakiki. Msiogope kuchelewa kwa siku chache, bali ogopeni hasara ya miaka,"  amesema.

Akifafanua, Bi. Rehema ametoa mfano wa Mamlaka na Kampuni za Maji, ambapo amesema maafisa ugavi katika Mamlaka hizo  wanapaswa kushauri na kuhakikisha mita zote mpya za maji baada ya kununuliwa zinapita WMA kwa uhakiki  kabla ya kufungwa kwa wateja.

"Kama kila afisa ugavi atatoa ushauri huu mara baada ya kukamilisha manunuzi, tutakuwa tumepiga hatua kubwa kuhakikisha kuna biashara ya haki na ulinzi wa walaji nchini" ameongeza.

Mtaalamu huyo wa Ugavi amesema WMA ina mitambo ya kisasa inayowezesha kutoa huduma ya uhakiki wa haraka hali  inayoepusha usumbufu kwa taasisi wakati wa kutoa huduma.

Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yameanza tarehe  28 Agosti na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 6 Septemba, 2026.






Na Mwandishi Wetu

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amewataka wadau wa sekta ya umma na binafsi kuongeza ushirikiano katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia, akisema biashara hiyo inahatarisha uwekezaji, ushindani wa haki na usalama wa watumiaji.

Ngasongwa ameyasema hayo leo Septemba 2, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akimwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, katika Kongamano la Ulinzi dhidi ya Bidhaa Bandia na Uwekezaji lililoandaliwa na Kampuni ya NANOSILIKAN kwa kushirikiana na FCC, TISEZA, TCCIA na TPSF, katika Hoteli ya Johari Rotana.

Amesema bidhaa bandia haziathiri ushindani wa kibiashara pekee, bali pia zinawaumiza wazalishaji wanaofuata sheria ambao hulipa gharama za ubunifu, upimaji, viwango, usajili, ajira na kodi, wakati wazalishaji wa bidhaa bandia huepuka gharama hizo na hivyo kushindana kwa njia isiyo ya haki.

“Katika ushindani wa kawaida, mzalishaji bora au mwenye ufanisi zaidi ndiye anayeshinda. Lakini kwenye bidhaa bandia, anayeshinda ni yule anayekwepa gharama zinazofanya bidhaa iwe halali,” amesema

Ngasongwa amesema athari kubwa zaidi ya bidhaa bandia humwangukia mlaji, akitolea mfano mbegu bandia ambazo mkulima anaweza kugundua tatizo baada ya msimu kupita, dawa ambazo hazitibu ugonjwa uliokusudiwa na vipuri bandia vya magari ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa watumiaji. Alisema kwa kuwa madhara hayo yanaweza kujitokeza kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa, ni muhimu kuweka mifumo ya kuzuia bidhaa bandia kufika kwa mlaji.

Kwa mujibu wa Ngasongwa, utekelezaji wa sheria pekee hauwezi kumaliza tatizo hilo kwa kuwa maafisa wa ukaguzi hawawezi kuwepo katika kila duka na kila muamala nchini, hivyo ni muhimu kuwawezesha walaji kushiriki katika kuthibitisha uhalali wa bidhaa kabla ya kufanya manunuzi. Alisema njia hiyo inaweza kusaidia kuzuia madhara kabla hayajatokea, huku akisisitiza kuwa jukumu la Serikali la kusimamia sheria na kulinda walaji linaendelea.

Aidha, aliwataka wafanyabiashara na wazalishaji kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini bidhaa zao zikighushiwa, kusajili na kutunza kumbukumbu za alama za biashara zao pamoja na kushirikiana katika kutoa taarifa kuhusu wahusika wa biashara ya bidhaa bandia.

Kongamano hilo limewakutanisha wawakilishi wa Serikali, taasisi za udhibiti, sekta binafsi, wafanyabiashara, taasisi zinazohusika na haki miliki pamoja na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kujadili namna bora ya kulinda uwekezaji, wafanyabiashara na walaji dhidi ya athari za bidhaa bandia nchini.

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Ubungo jijini Dar es Salaam limeendelea na operesheni yake maalum ya kuwabaini na kuwachukulia hatua wateja ambao wanatumia umeme bila kulipia wakiwa wameunganishiwa umeme na vishoka mtaani kinyume na utaratibu.
Kuingia kwenye ndoa na kuishi na mume wako kwa miaka kumi bila kufanikiwa kupata mtoto ni jaribu zito linaloweza kuvunja moyo na kubomoa amani ya nyumba yoyote.

Kwa miaka yote hiyo, nilipitia maumivu makubwa ya nafsi, dharau kutoka kwa ndugu wa mume, na kejeli za majirani waliokuwa wakiniona kama mwanamke aliyelaaniwa.

Nilitembelea hospitali mbalimbali kubwa na kufanyiwa vipimo vya kila aina, lakini madaktari wote walibainisha kuwa mimi na mume wangu hatukuwa na tatizo lolote la kiafya.

Pamoja na majibu hayo mazuri ya hospitali, kila mwezi ulipopita bila kuona dalili za ujauzito, maumivu na kilio cha siri vilizidi kutawala maisha yangu huku ndoa yangu ikianza kutikisika na kutishia kuvunjika.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na nikikaribia kukata tamaa kabisa ya kuitwa mama, mama yangu mdogo alinitembelea na kunieleza ukweli ambao wanakijiji wengi wanaufahamu.

Aliniambia kuwa tatizo la kukosa mtoto huku vipimo vya hospitali vikiwa safi mara nyingi hutokana na tumbo la uzazi kufungwa kishirikina na watu wenye wivu, au nyota ya uzazi kufunikwa na ukungu wa giza. SOMA ZAIDI.
Kushtakiwa kwa uongo na kukabiliwa na kesi ya dhuluma mahakamani ni miongoni mwa majaribu mazito yanayoweza kuharibu maisha na amani ya mtu kwa muda mfupi.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia mateso makubwa ya nafsi baada ya wafanyabiashara fulani wenye fedha na ushawishi kunibambikizia kesi feki ya madai na fraud ili kuninyang’anya ardhi na uwekezaji wangu wa maisha yote.

Kila nilipofika mahakamani, mambo yalionekana kuniemea; mashahidi wa uongo walipangwa kunishuhudia vibaya, na mawakili wangu walionekana kuzidiwa nguvu.

Nilibaki nikikabiliwa na hofu kubwa ya kupoteza mali zangu zote na hata kufungwa jela kwa kosa ambalo sikuwahi kulifanya. SOMA ZAIDI.
Kumpoteza mtoto mdogo aliyetoka kucheza mlangoni kisha akatoweka kama moshi ni maumivu makubwa zaidi yanayoweza kumpata mzazi yeyote maishani. Siku hiyo ilianza kama siku nyingine zote za kawaida, lakini kufikia jioni, mwanangu wa miaka mitano hakuonekana tena eneo la nyumbani.

Tulitafuta kila kona ya mtaa, tukauliza majirani na ndugu, na hatimaye kutoa taarifa kituo cha polisi, lakini siku zilivyoenda ndivyo matumaini ya kumpata mtoto wangu wa pekee yalivyozidi kutoweka.

Kwa wiki mbili mtawalia, nyumba yetu ilitawaliwa na kilio na simanzi nzito, nikishindwa kula wala kulala huku mawazo mabaya ya kwamba huenda ameuawa au kuchukuliwa na watu wabaya yakinichoma sana moyoni.

​Nikiwa kwenye maumivu hayo makali na polisi wakiwa hawana majibu ya kueleweka, bibi mmoja wa mtaani kwetu alinitembelea na kuninong’oneza kuwa kutoweka kwa mtoto mazingira ya ajabu mara nyingi hutokana na mikono ya chuma ulete au wachawi wanaowatwaa watoto kishirikina. SOMA ZAIDI.



Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akizindua Programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) katika eneo la Nyamongo, mkoani Mara, inayolenga kupanua fursa za maeneo ya uchimbaji, taarifa za kijiolojia na leseni kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.













Helikopta ikifanya utafiti wa madini kwa njia ya anga katika eneo la Nyamongo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya MBT, hatua itakayosaidia kupata taarifa za kijiolojia kwa ajili ya utafiti wa kina na uchorongaji katika maeneo yaliyotengwa kwa wachimbaji wadogo.





 

 

  

Na Mwandishi Wetu.

 Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imekutana na kufanya mazungumzo na watangazaji na waandaaji wa kipindi cha Good Morning kinachorushwa na Wasafi FM, ambapo imewakumbusha umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya uandishi wa habari katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kikao hicho kimefanyika leo, Septemba 2, 2026, katika Makao Makuu ya JAB, Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam, kikilenga kuimarisha uelewa wa watangazaji hao kuhusu misingi ya weledi, uwajibikaji na matumizi sahihi ya majukwaa ya habari.

Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amefafanua matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229; Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Sura ya 306; pamoja na kanuni zake zinazopaswa kuzingatiwa katika utayarishaji na utangazaji wa maudhui.

Wakili Kipangula ameeleza kuwa kuzingatia sheria na maadili ni msingi wa kulinda heshima ya taaluma, haki za watu wanaohusika katika maudhui na imani ya jamii kwa Waandishi wa Habari.
Baada ya mazungumzo hayo, watangazaji wakongwe Gelard Hando na Hilary Mtuta, maarufu kama Zembwela, walikabidhiwa vitambulisho vyao vya ithibati ya uandishi wa habari baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Makabidhiano hayo yamekamilisha hatua ya kuwatambulisha rasmi kama Waandishi wa Habari wenye ithibati, wenye wajibu wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, maadili na uwajibikaji.