Kupata mpenzi sahihi wa kujenga naye maisha na kuanzisha familia ni ndoto ya kila mwanamke, lakini pale kila mahusiano yanapovunjika ghafla hasa unapokaribia hatua ya ndoa, maisha hugeuka kuwa mateso na aibu kubwa.

Kwa zaidi ya miaka saba, nilijikuta kwenye mzunguko wa ajabu na wa kikatili. Nilianzisha mahusiano na wanaume tofauti, wote wakionyesha nia ya dhati ya kunioa.

Lakini kila tulipofikia hatua ya kutambulishana ukweni, kupanga tarehe ya harusi, au kutoa mahari, mambo yaliharibika ghafla bila sababu za msingi. Mwanaume alibadilika, akawa mkali, au akatokomea kabisa na kukata mawasiliano.

​Mara ya kwanza nilidhani ni bahati mbaya, lakini ilipotokea kwa mwanaume wa tatu na harusi ikavunjika wiki mbili kabla ya siku yenyewe, nilichanganyikiwa kabisa.

Nilibaki na magauni ya harusi ndani, kadi zikiwa zimeshagawiwa, na familia yangu ikiingia kwenye aibu nzito mtaani. Nilianza kujitenga na marafiki zangu waliokuwa wakiolewa mmoja baada ya mwingine, nikiumia moyoni na kuhisi nina gundu au nimelaaniwa nisipate mume.

Masimango ya majirani na ndugu yalinizidia, wengine wakisema labda nina tabia mbaya zilizojificha zinazowakimbiza wanaume, jambo ambalo halikuwa kweli. Nilianza kupoteza ujasiri wa kupenda tena, nikiamini kabisa kuwa nimezeekea nyumbani. SOMA ZAIDI.

 

Kufanya kazi kwa uaminifu, kujituma, na kujitoa kwa kampuni kwa miaka mingi ni jambo linalopaswa kumletea mfanyakazi yeyote matunda na maendeleo.

Hata hivyo, pale unapojikuta umekwama kwenye nafasi ile ile ya chini kwa miaka nane bila kuongezewa mshahara wala kupandishwa cheo, maisha ya kazi hugeuka kuwa unyonge na mateso ya kisaikolojia.

Katika oparesheni za kila siku za ofisi yetu, mimi ndiye niliyekuwa nikibeba mizigo mikubwa ya kazi, nikikaa muda wa ziada (overtime), na kuhakikisha kila mradi unakamilika kwa wakati.

​Pamoja me juhudi zote hizo, kila msimu wa upandishwaji vyeo na ongezeko la mshahara ulipowadia, jina langu lilipuuzwa kabisa.

Nilibaki nikitazama vijana wapya waliotoka vyuo juzi wakiajiriwa na kupandishwa vyeo juu yangu ndani ya miezi michache, huku wakipewa mishahara minono na marupurupu kibao.

Kila nilipojaribu kuongea na mabosi wangu au kuomba mapendekezo ya kupanda cheo, nilipokea ahadi za uongo na visingizio visivyoeleweka.

Nilibaki nikijisikia vibaya na kupatwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikiona kama elimu na jasho langu vilikuwa vikitumiwa vibaya bila thamani yoyote. SOMA ZAIDI.

 

Kuanzisha biashara na kuwekeza mtaji wako wote ni hatua kubwa ya kujitafutia maendeleo, lakini pale biashara hiyo inapodorora na kukaa miezi kibao bila kupata mteja hata mmoja, maisha hugeuka kuwa mzigo mzito wa madeni.

Nilifungua duka langu la nguo na vipodozi nikitarajia kupata faida kubwa ya kuendesha maisha yangu na familia. Hata hivyo, miezi michache baada ya kufungua, mambo yalibadilika ghafla.

Mtaani kwetu kulikuwa na watu wengi, lakini kila aliyepita mbele ya duka langu alitazama tu na kupita bila kuingia ndani. Kwa miezi mitano mtawalia, nilikuwa nikiamka asubuhi na mapema, kufungua duka, na kukaa siku nzima hadi usiku bila kuuza hata kitu cha shilingi mia.

Nguo zilianza kushika vumbi na kuharibika, kodi ya fremu ikawa inanilundikia, na wamiliki wa bidhaa waliaza kunidai kwa shinikizo kubwa.

Nilibaki nikilia peke yangu ndani ya duka lililokosa wateja, nikitazama maduka ya majirani zangu yakiwa yamefurika wateja kila siku huku langu likionekana kama limepakwa mikosi au kusahaulika.

Nilianza kupata msongo mkubwa wa mawazo, nikifikiria kufunga duka na kukimbia madeni yaliyokuwa yakinikabili. SOMA ZAIDI.

Morogoro

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta ya Maji, Afya na Usafi wa Mazingira, umeanza rasmi mchakato wa kuandaa Mkakati wa RUWASA wa Menejimenti ya Tope Kinyesi (Faecal Sludge Management Strategy), unaolenga kuweka mfumo madhubuti, salama na endelevu wa menejimenti ya tope kinyesi katika maeneo ya vijijini.

 



Na OWM – TAMISEMI, Dodoma


Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kuhusu kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi inayosimamiwa na Ofisi hiyo.

Katika kikao hicho, pande hizo zimejadili maeneo ya ushirikiano, hususan matumizi ya utaalamu, teknolojia na uzoefu wa kitaasisi katika kuhakikisha miradi ya miundombinu inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa, kwa wakati na kuleta thamani halisi kwa wananchi.

Mhandisi Mativila amesisitiza umuhimu wa taasisi za Serikali kushirikiana na vyuo vikuu katika kupata suluhisho za kitaalamu zitakazosaidia kuongeza ufanisi na ubora wa miradi ya ujenzi inayotekelezwa nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Innocent Macho, alisema Chuo hicho kina uwezo na uzoefu mkubwa wa kutoa huduma za kitaalamu kupitia kampuni yake ya ushauri, The Bureau for Industrial Cooperation (BICO), ambayo imeshiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini.

Pande hizo zimekubaliana kuendelea na majadiliano ili kuweka mazingira madhubuti ya ushirikiano yatakayochangia utekelezaji bora na endelevu wa miradi ya miundombinu chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI.

 

 



Na Mwandishi wetu -IRINGA

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,  Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe.  Nderiananga amewapongeza watu wenye ulemavu kwa kushiriki shughuli za kiuchumi na kuongeza pato lao na Taifa kwa ujumla.


Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na watu wenye ulemavu  katika Kituo cha wenye ulemavu cha Neema Craft kilichopo Manispaa ya Iringa Mh. Ummy alisema kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira yatakayowawezesha watu wenye ulemavukupata elimu, mafunzo ya ufundi na mitaji ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji.

Pia aliongeza kuwa watu wenye ulemavu wanapopata elimu ya fani mbalimbali huwajengea hali ya kujiamini, kuwa tayari kuonyesha uwezo wao na kuwa wabunifu hatimaye kupunguza wimbi la utegemezi.

" Nikipongeze Kituo hiki cha Neema Craft kwa hatua kubwa waliopiga katika kuwawezesha wenye ulemavu kwenye ujuzi mbalimbali kama tulivyoona kuna ufundi seremala, ufumaji, ushonaji, upishi na fani nyingine nyingi ambapo zote hizi zinafanywa na watu wenye ulemavu kwetu kama Serikali ni furaha kubwa," Alipongeza Mhe. Ummy


Hata  hivyo amewataka watu wenye ulemavu kutumia fursa za mikopo, mafunzo na uwezeshaji zinazotolewa na Serikali ili kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi zitakazowasaidia kujitegemea.

"Wananchi wanaponufaika na mikopo hii ni heshima kubwa kwa Mbunge pia Mkuu wa Mkoa kaka yangu Kheri James nawapongeza sana kwa namna mnavyopambana kwa ajili ya watu wenye ulemavu," alisema.

Vile vile Mhe. Ummy alifafanua kwamba baadhi ya watu wenye ulemavu wameonyesha uwezo mkubwa katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, zikiwemo samani, mikoba, mikeka na mazulia, huku bidhaa hizo zikiuzwa katika hoteli na masoko mbalimbali.

Alisema mafanikio hayo yanaonesha kuwa watu wenye ulemavu wana uwezo wa kufanya shughuli zenye tija endapo watapata uwezeshaji unaostahili.

"Nimetembelea hapa Neema Craft nimejionea namna watu wenye ulemavu wanavyofanya shughuli zao za ujasirimali wanabuni na kutengeneza bidhaa nzuri ambazo hata watu wazima hawawezi na bidhaa hizo mara nyingi tunaziona katika mahoteli makubwa ambayo huwezi kuzania kwamba watu wenye ulemavu ndio wametengeneza,"Alieleza.

Aidha aliwataka wazazi na walezi kutowaficha ndani watoto wenye ulemavu badala yake kuwapeleka shule au vyuo vya ufundi na vituo vinavyotoa mafunzo ya ujuzi hatua itakayosaidia kujikwamua kiuchumi hatimaye kutoka katika hali ya kuwa omba omba mitaani.

Kwa upande wake Mkurugenzi  wa Kituo cha Neema Crafts mkoani Iringa Bwa. Joseph Adams alisema kituo hicho kilianzishwa mwaka 2003 ikiwa ni  mradi wa kijamii unaolenga kutoa mafunzo na ajira kwa watu wenye ulemavu kama vile wasiyosikia ( viziwi)  na wenye ulemavu wa viungo ili kuwapa heshima na kuwaepusha na kuomba barabarani. 


"Kituo hiki kinajumuisha kazi nyingi sana na zote wanafanya wao wenyewe na kuzalisha bidhaa ambazo tunaziuza kama vile Karakana za kazi za mikono, Mgahawa  unaoendeshwa na viziwi na  Nyumba ya wageni (Guesthouse),"Alisema  Mkurugenzi huyo.

Aidha aliipongeza Serikali kwa kuendelea kuonyesha upendo kwa wenye ulemavu bila ubaguzi huku akiiomba kuboresha sekta ya wakalimani kuwasaidia wenye ulemavu kupata huduma muhimu kama hospitali, taasisi za fedha, nyumba za ibada na nyinginezo.


MWISHO

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekutana na ujumbe wa waandaaji wa Tanzania Green Summit (TGS), inayotarajiwa kufanyika Septemba 15–16, 2026 Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kujadili mikakati ya kuhakikisha unaleta tija katika ajenda ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi.

 


Viwanda vya KEDA, GoodWill Vyachochea Kasi

✅ Wilaya yatenga Hekari 15  ujenzi wa Bandari Kavu

✅ Dkt.Kiruswa Ahimiza uzingatiaji  Bei Elekezi za Madini

Kutokana na kuongezeka kwa Kasi ya uwekezaji ya  shughuli za uongezaji thamani madini nchini huku ikizidi kujifungamanisha zaidi na sekta nyingine za uchumi, Sekta ya Madini imeendelea kuweka Msingi wa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kujenga uchumi wa Dola Trilioni 1, kupitia viwanda.

Hayo yalibainishwa Agosti 19, 2026  wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, Wilayani Mkuranga iliyolenga kufuatilia shughuli za madini, kubaini changamoto na kutoa maelekezo muhimu.

Katika ziara hiyo , Dkt. Kiruswa alitembelea viwanda vikubwa vya KEDA Tanzania Float Glass kinachozalisha vioo kwa ajili ya maghorofa, magari na matumizi mbalimbali, pamoja na Kiwanda cha GoodWill Ceramic Co.Ltd kinachozalisha vigae vya sakafu na ukutani pamoja na vifaa vya usafi wa majumbani na vyooni na kueleza kuwa, ni jambo la kujivunia kuona Tanzania inaweza kuzalisha bidhaa zinazoweza kuuzwa kwenye mataifa makubwa duniani kama Marekani.

Dkt.Kiruswa alisisitiza uzingatiaji wa bei elekezi zinazotolewa na Serikali kwa madini yanayotumika viwandani, pamoja na kumuagiza Afisa Madini Mkazi Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kwa kushirikiana na Wilaya hiyo kuandaa semina kwa wamiliki wa viwanda na leseni za uchimbaji kuhusu uwajibikaji kwa jamii, utunzaji wa mazingira na masuala mengine ya msingi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mhe. Hadija Nasri Ally, alisema Wilaya hiyo inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa uwekezaji, ikiwemo kutenga ekari 15 kwa ajili ya ujenzi wa Bandari Kavu itakayorahisisha uhifadhi na usafirishaji wa bidhaa zinazozalishwa wilayani humo,

Alisema Mkuranga ina viwanda 275, ambapo 39 vinatumia madini kuzalisha bidhaa mbalimbali, huku shughuli za madini zikichangia shilingi bilioni 3.2 katika mwaka wa fedha 2025/26.

Naye, Meneja Biashara wa KEDA Tanzania, Ruby Zhu, alieleza kuwa, asilimia 98 ya malighafi ya kiwanda hicho inatoka Mkuranga, huku kiwanda kikizalisha takribani tani 600 za vioo kwa siku, vinavyosafirishwa katika masoko mbalimbali duniani ikiwemo Marekani.

Kwa upande wake, Meneja  Biashara wa GoodWill, Justin Xie alieleza kwamba, asilimia 90 ya malighafi zinazotumiwa na kiwanda hicho zinatoka Tanzania na kuongeza kuwa, kampuni hiyo imepanua uzalishaji wa bidhaa za majumbani, ikiwemo sinki za kunawia, vifaa vya vyooni na bafu huku bidhaa zao zikiuzwa  mataifa mbalimbali ikiwemo nchi za Ulaya na Marekani.

Kuhusu ajira, Xie alisema kiwanda kimetoa  ajira za moja kwa moja kwa  watanzania  zipatazo 3,000 na zisizo za moja kwa moja 12,000.

"Tumeweka mizizi nchini Tanzania, tunaweza kujitolea kubadilisha rasilimali za madini za ndani kuwa bidhaa za usafirishaji nje zenye thamani kubwa, na kuleta ajira zaidi na kodi na kushiriki na idara zote kuzungumzia vizuizi katika mnyororo wa usambazaji wa madini, na kwa pamoja kuendeleza ujenzi wa viwanda nchini Tanzania," alisema Justin Xie.

Kwa mujibu wa Afisa Madini wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, Mhandisi  Lameck Gabote, Mkuranga ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa madini ya ujenzi na viwandani yanayohudumia kwa kiasi kikubwa Mkoa wa Dar es Salaam na mikoa jirani.










 



Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) inaendelea kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga, ikitumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya mionzi na fursa zinazotokana na teknolojia ya nyuklia katika kuchochea maendeleo ya Taifa.

Maonesho hayo, yanayoratibiwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, yanawakutanisha taasisi za Serikali, taasisi za elimu na utafiti, wabunifu, wanafunzi, wataalamu pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu, sayansi na teknolojia.

Katika banda la TAEC, wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali wanaendelea kupata elimu kuhusu jukumu la Tume la kusimamia na kudhibiti matumizi salama ya mionzi nchini, pamoja na mchango wa teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, kilimo, mifugo, maji, viwanda, migodi, utafiti na nishati.

Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo pia unatoa fursa kwa wanafunzi na vijana kufahamu taaluma mbalimbali zinazohusiana na teknolojia ya nyuklia na umuhimu wa kujikita katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM) ili kujenga kizazi cha wataalamu kitakachosaidia Taifa kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Akifungua rasmi maonesho hayo Agosti 18, 2026, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisisitiza umuhimu wa elimu, ujuzi, sayansi, teknolojia na ubunifu katika kujenga uchumi wa kisasa na kuongeza uwezo wa Taifa kutumia maarifa na teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo.

Katika muktadha huo, ushiriki wa TAEC unaunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha sayansi na teknolojia zinatumika moja kwa moja katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Teknolojia ya nyuklia ina matumizi mapana yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo katika uchunguzi na tiba ya magonjwa, kuongeza tija katika kilimo na mifugo, usimamizi wa rasilimali za maji, shughuli za viwandani na migodini, utafiti wa kisayansi pamoja na sekta ya nishati.

Wananchi wanaotembelea banda la TAEC pia wanapata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na wataalamu, kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu usalama wa mionzi, udhibiti wa vyanzo vya mionzi na matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa madhumuni ya amani na maendeleo.

TAEC itaendelea kutoa elimu na kuhamasisha matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

“Mionzi kwa Matumizi Salama na Teknolojia ya Nyuklia kwa Maendeleo ya Taifa.”






 

Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa akisaini Kitabu wakati alipotembelea Banda la TIA katika Wiki ya Elimu Kitaifa ,Ujuzi na Ubunifu inayoendelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara,Jijini Tanga.
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa akipata maelezo kutoka Mkuu wa Sehemu - Ukuzaji na Uendelezaji wa wanafunzi kitaaluma na kitaalam wa TIA Imani  Matonya  kuhusiana na bunifu mbalimbali wa wanafunzi na wahitimu was TIA  walizoleta katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu ,Ujuzi na Ubunifu  Kwakati Mkuu wa Chuo hicho  alipotembelea Banda la TIA katika Wiki ya Elimu Kitaifa ,Ujuzi na Ubunifu inayoendelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara,Jijini Tanga.
Baadhi ya Wahitimu na Wanafunzi wa TIA  ambao wenye bunifu ambazo zimesimamiwa TIA kwenye maonesho ya Wiki ya Elimu Kitaifa ,Ujuzi na Ubunifu inayoendelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara,Jijini Tanga.

 




Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa, amesema maonyesho ya elimu, ujuzi na ubunifu ni jukwaa muhimu kwa taasisi za elimu kuonyesha kazi zinazofanywa na wanafunzi pamoja na kuwafungulia vijana fursa mbalimbali za kujifunza na kuendeleza vipaji vyao.

Profesa Mapesa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kuhusu ushiriki wa chuo hicho katika maonyesho ya elimu, ujuzi na ubunifu yanayoendelea mkoani Tanga, akimpongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, pamoja na Wizara hiyo kwa kuendelea kusimamia maonyesho hayo na kuwa na mafanikio.

Amesema maonyesho hayo yamekuwa na umuhimu kwa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa kuwa yanatoa nafasi ya kuonyesha programu zinazotolewa na chuoni ikiwemo mafunzo yanayohusiana na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), pamoja na kazi za ubunifu zinazofanywa na wanafunzi.

“Tunajivunia kupata fursa ya kuonyesha kazi za vijana wetu, ubunifu wao katika sayansi, teknolojia na maeneo mbalimbali. Ubunifu huu umekuwa na mguso mkubwa na tunaamini siku zijazo utakuwa na matokeo makubwa zaidi,” amesema Profesa Mapesa.

Amesema chuo kina mpango wa kuendeleza ubunifu wa wanafunzi kwa kuunganisha kazi hizo na watumiaji na wadau wakubwa ili zitumike zaidi katika shughuli za uzalishaji na kuchangia maendeleo ya uchumi.

Profesa Mapesa amesema maonyesho hayo pia yamekuwa fursa kwa vijana wanaotaka kujiunga na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kupata taarifa kuhusu programu mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho, huku baadhi yao wakipata huduma za usajili na maelekezo ya kujiunga na programu hizo moja kwa moja katika banda la chuo.

Ameeleza kuwa chuo kinatoa programu za umahiri, shahada ya kwanza, pamoja na diploma, huku akiwataka wananchi wa Tanga kutembelea maonyesho hayo, hususan banda la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, ili kupata fursa ya kujifunza zaidi kuhusu huduma na programu zinazotolewa na taasisi hiyo.

Aidha, amesema chuo hicho kina nafasi ya kipekee katika kuhifadhi na kutangaza historia ya Muasisi wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kupitia machapisho, kumbukumbu na hotuba zake ambazo, amesema, zimekuwa na mchango mkubwa katika historia ya Tanzania na Afrika.

Profesa Mapesa amewashukuru waandaaji wa maonyesho hayo pamoja na vyombo vya habari kwa kuendelea kuhabarisha umma kuhusu shughuli za maonyesho na kazi zinazofanywa na taasisi za elimu. Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusisitiza umuhimu wa elimu, ujuzi na ubunifu katika maendeleo ya taifa.

Amesema uwekezaji unaoendelea katika elimu, ujuzi na ubunifu ni muhimu katika kujenga Taifa lenye vijana wenye uwezo wa kutumia maarifa na teknolojia kutatua changamoto na kuchangia maendeleo ya Tanzania.

 

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THP S katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026. 
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi wa Miradi THPS, Dkt. Benedicta Masanja, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Msimamizi wa Mradi wa Tanzania FAST Health, Japhet Daud, akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Msimamizi wa Mradi wa Tanzania FAST Health, Japhet Daud, akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mratibu wa Miradi THPS, Dkt. Mariana Mubelwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Dkt. Baraka Msumi akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.


Tanzania Health Promotion Support (THPS) imetambulisha rasmi Mradi wa Tanzania FAST Health katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, unaolenga kuimarisha huduma za VVU kwa watoto, vijana, wanawake wajawazito na wanaonyonyesha.

Mradi huo unaofadhiliwa na ViiV Positive Action, utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Juni 2026 hadi Juni 2029 katika Manispaa ya Kahama na Halmashauri ya Muheza.

Mradi unatekelezwa na THPS kwa kushirikiana na Serikali, pamoja na Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na VVU (National Council of People Living with HIV - NACOPHA) na Mtandao wa Vijana Wanaoishi na VVU -Network of Young People Living with HIV (NYP+), kwa lengo la kuziba mapengo katika upimaji, utambuzi wa mapema, matibabu na mwendelezo wa huduma kwa watu wanaoishi na VVU.

Akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo mjini Kahama leo, Agosti 19, 2026, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, amesema ujio wa FAST Health ni fursa muhimu kwa Serikali kuendelea kuimarisha huduma za VVU, hususan kwa watoto na vijana ambao bado wanakabiliwa na changamoto katika kufikiwa na huduma.

Dkt. Rutatinisibwa amesema kwa mujibu wa takwimu za Tanzania HIV Impact Survey (THIS) 2022–2023, kiwango cha maambukizi ya VVU kwa watu wenye umri wa miaka 15 na zaidi katika Mkoa wa Shinyanga ni takribani asilimia 5.6, hali inayosisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha kinga, upimaji, utambuzi wa mapema, matibabu na ufuatiliaji wa wagonjwa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa.

Amesema Mkoa wa Shinyanga umefanya vizuri katika kufikia malengo ya UNAIDS ya 95-95-95, ambapo umefikia asilimia 96.5, 99.2 na 98.9, lakini bado kuna haja ya kuendelea kuziba mapengo, hasa katika kuwafikia watoto na vijana.

Ameeleza kuwa baadhi ya changamoto bado ni kuchelewa kutambua watoto wenye VVU, upimaji kutowafikia watoto na wanafamilia wote wanaostahili, unyanyapaa, changamoto za usafiri na kiuchumi pamoja na baadhi ya wagonjwa kupotea katika mwendelezo wa huduma.

“Hakuna mtoto au kijana anayestahili huduma za VVU anayepaswa kuachwa nyuma. Tunapaswa kujua watoto wetu wako wapi, kuwafikia, kuwapima wanaostahili kupimwa, kuwaunganisha mara moja katika huduma pale wanapogundulika kuwa na VVU na kuwasaidia kufikia na kudumisha ufubazaji wa virusi,” amesema Dkt. Rutatinisibwa.

Amesema kupitia Mradi wa Tanzania FAST Health, Serikali inatarajia kuimarishwa kwa utafutaji hai wa watoto na vijana wenye VVU, ikiwemo matumizi bora ya index testing, kuongeza utambuzi wa mapema na kuhakikisha wanaobainika kuwa na VVU wanaunganishwa na huduma na matibabu kwa wakati.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa.

Aidha, amesema mradi unapaswa kuimarisha huduma zinazomlenga mtoto, kijana na familia kwa ujumla, kuongeza ufuasi wa dawa na kuhakikisha watu wanaoishi na VVU wanaendelea na matibabu hadi kufikia na kudumisha ufubazaji wa virusi.

Dkt. Rutatinisibwa amesisitiza kuwa Mradi wa Tanzania FAST Health haipaswi kufanya kazi kama mradi unaojitegemea, bali inapaswa kuunganishwa kikamilifu katika mifumo ya Serikali ili matokeo yake yawe endelevu hata baada ya kipindi cha ufadhili kumalizika.

“RHMT, CHMT, vituo vya kutolea huduma za afya, THPS, jamii na wadau wengine tunapaswa kufanya kazi kama timu moja. Tunatarajia kila afua itakayotekelezwa iwe na umiliki wa Serikali na jamii, matumizi sahihi ya takwimu na mpango wa uendelevu,” amesema.

Ametoa wito kwa watoa huduma kuhakikisha wanatoa huduma bora, rafiki, zenye usiri na zinazozingatia mahitaji ya watoto, vijana na familia, huku akizitaka THPS na washirika wake kuendelea kujenga uwezo wa mifumo ya Serikali badala ya kuanzisha mifumo sambamba.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miradi THPS, Dkt. Benedicta Masanja, akimwakilisha Mkurugenzi wa THPS, Dkt. Redempta Mbatia, amesema Mradi wa Tanzania FAST Health unalenga kutumia mbinu zenye ushahidi kuwafikia watoto, wanawake wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na vijana wanaohitaji huduma za VVU.
Mkurugenzi wa Miradi THPS, Dkt. Benedicta Masanja.

Amesema mradi huo unalenga kuongeza mahudhurio ya wajawazito na wanaonyonyesha katika kliniki, kuimarisha upimaji wa watoto, kupunguza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na kuhakikisha watu wanaoishi na VVU wanaendelea kupata huduma na matibabu.

Dkt. Masanja amesema mradi utatumia Mama Vinara 35, vijana rika na klabu za vijana katika kuongeza uelewa na kuwafikia wananchi, huku ukisisitiza umuhimu wa kupunguza unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na VVU.

Amesema utekelezaji wa mradi huo katika halmashauri ya Muheza na  Halmashauri ya Manispaa ya Kahama unalenga kuimarisha huduma zilizopo na kujenga mifumo endelevu kwa kushirikiana na Serikali, NACOPHA na NYP+.

Naye Mratibu wa Miradi THPS, Dkt. Mariana Mubelwa, amesema Mradi wa Tanzania FAST Health unalenga kuziba mapengo katika utoaji wa huduma za VVU kwa watoto na vijana wenye umri wa miaka 0 hadi 19, huku ikiimarisha ufuatiliaji wa wanaopata huduma na kupunguza kukatisha au kuacha matibabu.
Mratibu wa Miradi THPS, Dkt. Mariana Mubelwa.

Amesema afua zitakazotekelezwa ni pamoja na upimaji wa VVU katika jamii, index testing, mpango wa Mama Walezi (Mentor Mothers), kuanzisha na kuimarisha klabu za vijana, elimu rika na vikundi vya msaada wa kisaikolojia.

Dkt. Mubelwa amesema mradi pia utaimarisha mifumo ya afya kupitia matumizi ya takwimu, kuongeza uwezo wa watumishi wa afya, kuunganisha huduma na kuongeza ushiriki wa jamii.
Unyanyapaa bado changamoto

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa Tanzania FAST Health, Japhet Daud, amesema mradi huo umebuniwa kuchagiza utatuzi wa changamoto zilizopo katika huduma za VVU, ikiwemo unyanyapaa ambao bado unaendelea kuwa kikwazo kwa baadhi ya watu kujitokeza kupima, kuanza na kuendelea na matibabu.

Amesema moja ya malengo ya mradi ni kuboresha afya ya mama kwa kuwahamasisha wanawake wajawazito na wanaonyonyesha kuhudhuria kliniki, kuimarisha huduma za upimaji wa VVU kwa watoto na kuhakikisha watu wanaoishi na VVU wanaendelea kupata huduma na matibabu.
Msimamizi wa Mradi wa Tanzania FAST Health, Japhet Daud.

Japhet amesema mradi pia utashirikiana na Serikali na wadau wengine kuimarisha mifumo ya afya ili huduma zinazotolewa ziwe endelevu hata baada ya mradi kukamilika.

Amesema Mama Vinara 35, vijana rika na klabu za vijana watatumika katika kutoa elimu, kuhamasisha matumizi ya huduma na kupunguza unyanyapaa katika jamii.

Ameongeza kuwa jamii itaelimishwa kuhusu umuhimu wa watu wanaoishi na VVU kuendelea na matibabu na kufikia ufubazaji wa virusi, akisisitiza ujumbe kwamba mtu anayetumia dawa ipasavyo na kufikia kiwango cha virusi kutokomea mwilini haambukizi VVU kwa njia ya ngono.

Havionekani, haviambukizi,” amesema Japhet, akieleza kuwa ujumbe huo unalenga kuongeza uelewa kuhusu matibabu na kupunguza hofu na unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na VVU.

Mradi wa Tanzania FAST Health ulianza Juni 2026 na unatarajiwa kukamilika Juni 2029, ukiwa tayari umetambulishwa katika Halmashauri ya Muheza mkoani Tanga, na sasa umetambulishwa rasmi katika Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mkurugenzi wa Miradi THPS, Dkt. Benedicta Masanja, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mkurugenzi wa Miradi THPS, Dkt. Benedicta Masanja, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.



Back To Top