Wahadzabe ni kabila linalopatikana mkabala na ziwa Eyasi pembezoni mwa hifadhi ya Ngorongoro na habari za maisha yao zimehifadhiwa katika makumbusho ya Urithi Jiopaki liyopo Karatu Mkoani Arusha.

Pamoja na mabadiliko ya ulimwengu na elimu kutolewa lakini kabila hili bado haliamini katika tohara kwa kijana wa kiume, kwao hiyo ni mwiko wakiamini binadamu anastahili kuwa kama alivyozaliwa.

Sababu kubwa ya kutokutahiriwa ni kuwa ukitahiriwa unapunguza nyama ya binadamu na kuizika wakati binadamu huyo akiwa hai, imani ni kwamba huwezi kata sehemu yoyote ya mwili wa binadamu aliye hai

Vilevile kabila  hili linaamini kwamba mwanaume akitahiriwa hupunguza ukubwa na utaalam wa mambo na kufanya  mwili wako kuwa na mapungufu hata wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Katika kuhakikisha kwamba mwanaume anakuwa na nguvu za kutosha wakati wa kushiriki tendo la ndoa hulazimika kula mizizi inayopatikana porini , matunda, asali ikiwa fresh na nyama pori ambayo inachomwa au kuchemshwa supu.

Kutokana na kutokutahiriwa Wahadzabe wanaamini kwamba miili yao huwa na nguvu ya kupambana na mnyama yoyote porini na hiyo ndiyo heshima ya mwanaume kamili ambaye hata anapochumbia kutaka kuoa hupimwa kwa uwezo wa kuwinda na kuleta chakula cha familia.

Hii ni sehemu ya maajabu ya maisha makabila wanaunda Ngorongoro Global Geopark ambapo licha ya Wahadzabe kuendelea kuishi katika ukanda huo lakini taarifa zao zinapatikana katika makumbusho ya Urithi Geopark.

Karibu Nyumbani Ngorongoro upate mshangao wa maajabu na uzoefu usiosahaulika.

 


Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma

Mkutano Mkuu wa 16 wa Mwaka wa Taasisi ya Maboresho katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA) unatarajiwa kujadili mchango wa ugatuzi wa madaraka katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku ukilenga kuweka mikakati itakayowezesha wananchi kunufaika zaidi na usimamizi wa maendeleo katika maeneo yao.

Mkutano huo utafanyika Agosti 19–21, 2026 katika Ukumbi wa Jiji la Dodoma, Mji wa Serikali Mtumba, ukiwa na Kaulimbiu isemayo: “Ugatuzi wa Madaraka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ni nguzo madhubuti ya kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa TOA, Bw. Albert Gabriel Msovela, ambaye amesema Mgeni Rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye atauzindua rasmi Agosti 19, 2026.

Bw. Msovela amesema mkutano huo unaendana na maelekezo ya Serikali yanayochagizwa na maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wananufaika na ugatuaji wa madaraka, hususan katika usimamizi wa miradi ya maendeleo na upatikanaji wa huduma bora za kijamii, kama zilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Mkutano huu ni fursa kwa wajumbe kujadili maeneo yaliyoainishwa kwenye Dira, na tutakuwa na mada mbalimbali zitakazowasilishwa na wabobezi. Ninawaomba wananchi waufuatilie mkutano huu utakaokuwa mubashara kupitia vyombo mbalimbali vya habari ili wajue ni kwa namna gani TOA itawashirikisha kwenye ubunifu na usimamizi wa miradi yote, ikiwemo ya afya, elimu na miundombinu ya barabara,” amesema Bw. Msovela.

Aidha, Bw. Msovela amesema mkutano huo unatarajiwa kutoa maazimio na mikakati ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya moja kwa moja kutokana na uwepo wa kikao hicho.

Ametoa wito kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu huo kuhudhuria na kushiriki kikamilifu katika mijadala itakayofanyika, akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kujenga mikakati yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Wajumbe watakaoshiriki katika Mkutano Mkuu huo wa TOA ni Makatibu Tawala wa Mikoa yote 26, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, zikiwemo Jiji, Manispaa na Halmashauri, pamoja na Makatibu Tawala wa Wilaya zote 136 nchini.

 


Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeandaa mtaala maalum wa kozi fupi za recycling kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika sekta ya taka na kuongeza thamani ya taka zinazoweza kurejelewa.

Hayo yameelezwa Agosti 15, 2026 jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Mohammed Omari, wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo katika Chuo cha VETA wilaya ya Bahi.

Amesema hatua hiyo imekuja baada ya tafiti kubaini kuwa baadhi ya vijana wanaojihusisha na shughuli za taka wanakabiliwa na changamoto za kiafya na kiusalama, hivyo kuhitajika kwa mtaala mahsusi utakaowawezesha kukabiliana na mazingira ya kazi.

Dkt. Omari amesema mtaala huo umeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya wadau katika mnyororo wa thamani wa taka, kuanzia ukusanyaji hadi uchakataji, kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, sekta binafsi, vyuo vya walimu na waajiri.

Aidha, amesema VETA inaendelea kushirikiana na wataalamu wa sekta mbalimbali kuunganisha ujuzi wa vitendo na mafunzo ya vyuoni. Ametolea mfano ushirikiano na mtaalamu wa samani, Edo Sama, anayerejeleza zaidi ya asilimia 50 ya mbao zilizokuwa zikitupwa na kuzitumia kutengeneza samani, hivyo kuongeza thamani ya taka na kupunguza upotevu wa rasilimali.

Ameongeza kuwa VETA inaendelea kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, ikiwemo kampuni ya Hans Paul ya Arusha inayotengeneza magari ya utalii, ili kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi wa vitendo. Amesema hatua hiyo inaendana na msisitizo wa Serikali wa kushirikisha sekta binafsi katika kukuza ujuzi na ajira kwa vijana.

 

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Aggrey Mwanri (MCC), leo Agosti 15, 2026, amekuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano wa Hadhara wa Jimbo la Ubungo, ulioandaliwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Prof. Kitila Mkumbo, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji.


Kabla ya kushiriki mkutano huo, Ndugu Mwanri alipokewa katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dar es Salaam na Sekretarieti ya CCM Mkoa, chini ya Katibu wa CCM Mkoa, Ndugu Mkandawire.

Aidha, alipokea taarifa fupi kuhusu utendaji wa Chama katika Mkoa huo na kuwashukuru viongozi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa usimamizi mzuri wa Chama na Serikali.

Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Mwanri amesisitiza umuhimu wa Wabunge, Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kufanya mikutano ya hadhara mara kwa mara ili kuwapa wananchi mrejesho kuhusu utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa Uchaguzi.

Aidha, amewasihi wananchi kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini.

Kwa upande wake, Prof. Kitila Mkumbo aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM mbele ya wananchi wa Jimbo la Ubungo, akieleza hatua zilizochukuliwa katika kuboresha miundombinu, hususan sekta ya barabara.

Prof. Kitila amesema ataendelea kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi na Serikali katika kuhakikisha wananchi wa Ubungo wanaendelea kupata huduma na maendeleo yanayostahili.

KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE.

Kutafuta pesa na kupambania maendeleo ni lengo la kila mtu, lakini pale unapotumbukia kwenye mtego wa michezo ya kubeti na kamari, maisha yote huanza kuporomoka kwa kasi ya ajabu.

Kwa miaka kadhaa, nilikabiliwa na uraibu mzito wa kamari uliyoanza kama mchezo mdogo wa kujiburudisha. 

Kila nilipoweka pesa na kushinda kiasi kidogo, tamani ya kupata pesa nyingi haraka ilitawala akili yangu, ikanifanya nianze kuweka kiasi kikubwa zaidi cha fedha kila siku.

​Taradibu, mchezo huo uligeuka kuwa janga lililomaliza akiba zangu zote za benki. Nilipoishiwa pesa, nilianza kuuza samani za nyumbani, kuchukua mikopo ya riba kubwa.

Na hatimaye niliuza kiwanja na nyumba yangu niliyojenga kwa jasho ili tu nipate pesa za kuendelea kubeti kwa matumaini ya kurejesha nilichopoteza.

Kila siku nilitoka nyumbani nikiwa na nia ya kuacha, lakini akili yangu ilikuwa ikivutwa kwa nguvu ya ajabu kurudi kwenye kumbi za kamari.

Nilibaki mfilisi, nikiwa na madeni kila kona, huku familia yangu ikiteseka kwa njaa na aibu kubwa mtaani. SOMA ZAIDI.
Afya ya ngozi na mwili ni nguzo muhimu inayompa mwanadamu kujiamini na amani ya moyo, lakini inapopatwa na magonjwa yasiyoeleweka, maisha yote huingia kwenye mateso makubwa.

Kwa miaka kadhaa, nilikabiliwa na ugonjwa mzito wa ngozi uliyoanza kama vipele vidogo mwilini kisha ukageuka kuwa vidonda vikubwa vilivyokuwa vikitoa maji, kuwasha vibaya sana, na kuacha madoa meusi mwili mzima.

Hali hiyo iliniletea aibu kubwa sana kiasi cha kushindwa kuvaa nguo fupi au kujichanganya na watu mtaani. Nilitumia fedha nyingi sana kutembelea hospitali mbalimbali na kumuona kila daktari wa ngozi niliyeelekezwa.

Nilitumia cream za kila aina, sindano, na dawa za kuzuia mzio (allergies), lakini kila nilipomaliza dozi, vidonda hivyo vilirudi kwa kasi zaidi na kuenea mwilini kote.

Vipimo vyote vya kisayansi vilionyesha sina ugonjwa wa hatari unaoeleweka, jambo lililowaacha hata madaktari wakiwa wamechanganyikiwa.

Nilibaki nikiteseka na maumivu na mwasho usiku kucha, nikipoteza kabisa matumaini ya kuwahi kupata ngozi laini na yenye afya tena. SOMA ZAIDI.
Kufanya kazi kwa bidii, uaminifu, na kujituma ni misingi inayotarajiwa kumletea kila mfanyakazi mafanikio na hatua mpya maishani. Hata hivyo, kwangu mimi, juhudi zangu zote za miaka mingi kazini zilikuwa kama kutwanga maji kwenye kinu.

Walioingia kazi juzi walipandishwa vyeo na kuongezewa mishahara, huku mimi nikiachwa kwenye nafasi ile ile ya chini kwa miaka na miaka. Kila nafasi ya upandaji cheo ilipojitokeza, majina yangu yalikatwa au kusahaulika ghafla, licha ya kwamba mimi ndiye niliyekuwa nikifanya kazi kubwa na ngumu zaidi.

​Hali hii iliniletea msongo mkubwa wa mawazo na unyonge wa nafsi. Mshahara wangu mdogo ulishindwa kukidhi mahitaji ya familia, huku nikishuhudia wenzangu wakinunua magari na kujenga nyumba.

Kila nilipojaribu kumfata bosi wangu kuulizia haki yangu, nilikutana na majibu ya mkato, baridi, na dharau. Nilianza kujiona sina bahati, nikipoteza kabisa hamu na morali ya kufanya kazi, huku nikihofia kustaafu nikiwa masikini bila mafanikio yoyote ya kujivunia. SOMA ZAIDI.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma, akifanya majumuisho ya michango ya Wajumbe wa Kamati katika kikao cha Kamati hiyo kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwakawa fedha 2025/2026.




Na Oscar Assenga, Kilindi


MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Crispian Chalamila amemuahidi Rais Samia Suluhu Hassan kuwa taasisi hiyo itaendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kuhakikisha vita dhidi ya rushwa nchini vinafanikiwa.

Chalamila alisema hayo wakati akizindua jengo jipya la ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Kilindi, mkoani Tanga, akisema Serikali imeendelea kuiwezesha taasisi hiyo kwa rasilimali watu, fedha na vitendea kazi ili kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa.



Alisema uwekezaji huo ni ishara ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia katika kuhakikisha TAKUKURU inakuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

“Kwa niaba ya menejimenti ya TAKUKURU, nitoe shukrani za dhati kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha taasisi hii kwa rasilimali watu, vitendea kazi na fedha,” alisema.

Chalamila alisema uwezeshaji huo umewezesha taasisi kujenga ofisi katika mikoa na wilaya mbalimbali, jambo linalowapa watumishi mazingira bora ya kufanyia kazi na wananchi kupata huduma kwa mazingira rafiki.

Ofisi 93 kufikia 2027

Chalamila alisema TAKUKURU imeweka mkakati wa kutenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa ofisi zake, huku akieleza kuwa taasisi hiyo ina ofisi 145 katika mikoa yote 26, wilaya 111 na vituo maalumu sita.



Alisema kati ya ofisi hizo, majengo 70 yanamilikiwa na TAKUKURU na yanapatikana katika mikoa 23, wilaya 46 na kituo maalumu kimoja.

“Majengo yanayoendelea kujengwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 na 2026/2027 ni 23, ambayo yanajumuisha ofisi tatu za mikoa na ofisi 20 za wilaya,” alisema.



Alisema kukamilika kwa miradi hiyo kutafanya hadi mwaka 2027 TAKUKURU kuwa na majengo 93 yanayomilikiwa na taasisi hiyo.

Hata hivyo, alisema bado kuna ofisi 52 ambazo hazijafikiwa na mpango huo wa ujenzi, zikiwa katika mikoa miwili, wilaya 45 na vituo maalumu vitano.

Kwa upande wa jengo la TAKUKURU Kilindi, Chalamila alisema limegharimu Sh450.7 milioni hadi kukamilika, ikiwa ni ongezeko la Sh3.1 milioni, sawa na asilimia 0.7 ya bajeti ya awali.

Alisema ongezeko hilo lilitokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi.

Aliwapongeza wataalamu wa TAKUKURU, Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Kilindi kwa kuhakikisha ujenzi wa jengo hilo unakamilika kwa wakati.

Pia aliwataka watumishi wa TAKUKURU katika wilaya ya Kilindi na maeneo mengine yenye majengo mapya kuyatunza pamoja na vitendea kazi walivyopewa ili yaweze kutumika kwa muda mrefu.

“Serikali imewawezesha kwa kiwango kikubwa. Hilo ni deni ambalo tunapaswa kulilipa kwa kufanya kazi kwa bidii na weledi zaidi ili dhamira ya Serikali ya kuitokomeza rushwa nchini itimie,” alisema.
DC aomba jenereta

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Hashim Mgandilwa, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuziwezesha taasisi zake kuwa na miundombinu bora inayorahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.



Mgandilwa alisema ujenzi wa jengo hilo ni hatua muhimu kwa wilaya hiyo, ambayo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya upungufu wa miundombinu ya ofisi.

Hata hivyo, aliomba TAKUKURU kuangalia uwezekano wa kuiwezesha ofisi hiyo kupata jenereta kutokana na changamoto ya kukatika kwa umeme katika eneo hilo.



“Jengo ni zuri, lakini haitakuwa na maana kama mwananchi akija kupata huduma anaambiwa umeme umekatika. Tunaomba muone namna ya kupata jenereta ili huduma ziendelee muda wote,” alisema.

Alisema Serikali tayari imeweka mpango wa kuimarisha umeme katika eneo hilo na imetenga Sh98 milioni kwa ajili ya ujenzi wa kituo kidogo cha kupoza umeme.


TAKUKURU Kilindi yapata ofisi baada ya miaka 20

Kwa upande wake, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhan Ndwatah, alisema kabla ya kupata jengo hilo, taasisi hiyo ilifanya kazi katika majengo ya kupanga kwa takribani miaka 20.



Alisema kuanzia mwaka 2005 hadi 2010 walikuwa katika majengo ya kupanga Kata ya Songe, kabla ya kuhamia Kata ya Bokwa, Kijiji cha Legeza Mwendo, ambako walikaa hadi mwaka 2026.



Ndwatah alisema hali hiyo ilisababisha changamoto mbalimbali, ikiwamo majengo kutokidhi mahitaji ya kisasa ya ofisi, changamoto za mawasiliano na ulazima wa kufanya ukarabati mara kwa mara.

Alisema pia kuwepo kwa ofisi katika majengo ya makazi ya watu kulikuwa kunawafanya baadhi ya wananchi kukosa uhuru wa kufika kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa utulivu.



“Tunamshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa uamuzi wa kutujengea jengo hili la kisasa. Litasaidia wananchi wa Kilindi kufika kwa uhuru na kupata huduma katika mazingira bora,” alisema.



Jengo hilo jipya linatarajiwa kuongeza ufanisi wa TAKUKURU Wilaya ya Kilindi katika kutekeleza majukumu yake, ikiwamo kupokea taarifa na malalamiko ya wananchi kuhusu vitendo vya rushwa.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Utafiti uliofanywa katika wilaya tatu nchini umebaini kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuathiri miundombinu ya shule, huku maeneo yanayokumbwa na mafuriko yakitajwa kuwa katika hatari kubwa ya kuharibika kwa madarasa, maktaba, maabara na miundombinu mingine ya shule.

Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Agosti 14, 2026 imepitia na kuujadili mkakati wa kuimarisha huduma za Maji, lishe, upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira kwenye shule za msingi na Sekondari nchini, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa Nne wa Bunge unaotarajiwa kuanza Agosti 25, 2026.

Katika kikao hicho, Kamati imejadili kwa kina namna bora ya uimarishaji wa huduma za maji , upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira kwenye Shule za msingi na sekondari nchini, pamoja na uimarishaji wa lishe katika shule za msingi nchini.  

Mara baada ya kuupitia mkakati huo, Kamati kupitia Mwenyekiti wake Mhe. Florent Kyombo, katika eneo la lishe imeitaka OWM - TAMISEMI kufanya utafiti wa kina ili kuwa na takwimu halisi za lishe mashuleni, kuimarisha somo la kilimo mashuleni ili kuwapatia ujuzi wa kilimo wanafunzi, ikiwa ni pamoja na kupata chakula cha kutosha mashuleni.

Kwa upande wa upandaji miti na utunzaji wa mazingira, Mhe. Kyombo ameitaka OWM - TAMISEMI kuhakikisha shule zinakuwa na vilabu mahususi za upandaji miti, kuwa na mkakati wa kupanda miti mashuleni na kila shule kupata  mgawo wa miche na kuongeza kuwa, shule ziwekewe ukomo wa idadi ya miti inayotakiwa kupandwa kila mwaka.

Ili kuimarisha huduma za maji mashuleni, Mhe.  Kyombo ameitaka OWM - TAMISEMI kuhakikisha miundombinu ya maji iliyopo mashuleni inatunzwa, kusimamia utaratibu wa ulipaji wa bili za maji mashuleni kwa wakati na kuongeza kuwa  kila shule kuwe na sharti au utaratibu wa kuchimba kisima au kuweka tanki la maji ili wanafunzi wawe na uhakika wa huduma ya maji. 


OWM-TAMISEMI ,Morogoro


Mkoa wa Morogoro umeanza kushuhudia shamrashamra za michezo baada ya Mashindano ya Michezo ya Wanafunzi wa Shule za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEASSA Games 2026) kuanza rasmi katika viwanja mbalimbali vya mkoa huo.

Mashindano hayo yameanza leo, Agosti 14, 2026, yakikutanisha maelfu ya wanamichezo chipukizi kutoka Tanzania na nchi mbalimbali za Afrika Mashariki, huku ushindani ukianza kushika kasi katika michezo mbalimbali.

Mapema asubuhi, viwanja mbalimbali vilianza kujaa wachezaji, makocha, waamuzi na mashabiki, hali iliyoifanya Morogoro kubadilika na kuwa kitovu cha michezo ya shule katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Katika mchezo wa mpira wa miguu wa wasichana uliochezwa Uwanja wa Jamhuri, Amus College ya Uganda ilianza kampeni yake kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Boni Consili Girls Vocational & Secondary School, katika mchezo uliokuwa miongoni mwa vivutio vya siku ya kwanza. 

Kwa upande mwingine, mchezo wa soka la wavulana nao umeanza kwa ushindani mkubwa, huku timu kutoka Tanzania, Uganda, Burundi na nchi nyingine zikianza safari ya kusaka ubingwa wa Afrika Mashariki. Miongoni mwa michezo ya siku ya kwanza, IPTEM Makamba ya Burundi ilitarajiwa kukutana na Nsumba ya Tanzania katika uwanja wa SUA. 

Mashindano ya mwaka huu yana sura ya kipekee kutokana na kuongezeka kwa michezo inayoshirikishwa, ikiwemo baseball, cricket, lacrosse, beach volleyball, chess, softball, beach football na scrabble, ambayo imeongezwa kwenye programu ya mashindano. 

Kwa ujumla, FEASSA Games 2026 imekusanya zaidi ya wanamichezo 6,000 ikifanya toleo hili kuwa miongoni mwa matoleo makubwa zaidi katika historia ya mashindano hayo. 

Mashindano yanaendelea katika maeneo mbalimbali ya Morogoro hadi Agosti 22, 2026, huku kila timu ikipigania heshima ya shule na nchi yake.