Na. Josephine Majura na Peter Haule, WF, Dodoma

 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Devotha Minja, ameipongeza Wizara ya Fedha kwa kutekeleza Mradi wa Jengo jipya la Ofisi ya Wizara lililopo Mji wa Serikali Mtumba, kwa ufanisi, kwa kuwa mradi huo hauna maswali mengi ikilinganishwa na miradi mingine waliyoitembelea.

 

“Kazi ni nzuri, mmefanya kazi kubwa na taarifa zinazohitajika ziwasilishwe ili tuweza kuishauri vema Serikali”, alisema Mhe. Minja.

 

Aidha Mhe. Minja kwa niaba ya Kamati ameahidi kutoa ushirikiano katika maeneo mbalimbali yanayoihusu Wizara ya Fedha kwa Maendeleo ya Wananchi.

 

Akizungumza na Ujumbe wa Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge ya PAC, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula (Mb) alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la hilo lenye mvuto wa kipekee katika eneo hilo likiwa na urefu wa ghorofa tisa.

 

Mhe. Luswetula alisema kuwa jengo hilo lililofikia hatua ya asilimia 98 katika utekelezaji wake, anaimani watumishi wa Wizara ya Fedha wataongeza morali ya kazi kutokana na mazingira bora ya kazi katika jengo hilo lenye hadhi kubwa.

 

“Kwa mazingira haya majukumu ya Wizara ya Fedha yataenda vizuri ikiwa ni pamoja na utatuzi wa changamoto za wananchi wote kwa ujumla”, alisema Mhe. Luswetula.

 

Mhe. Luswetula alimhakikishia Mwenyekiti wa Kamati ya PAC kufanyia kazi ushauri na mapendekezo yote yaliyotolewa ikiwemo kuwasilisha taarifa za jengo hilo kwa ujumla wake.

 

Kamati ya Kudumu ya PAC imetembelea mradi wa Jengo hilo na kukagua Ofisi mbalimbali zikiwemo za Viongozi na Watumishi wa Wizara, Mifumo ya Fedha, usalama wa jengo, masuala ya Afya, kumbi za Mikutano na maeneo mengine.

 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), Akiongoza kikao na Uongozi wa Tume ya Pamoja ya Fedha, ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma, ambapo katika kikao hicho, aliiagiza Tume hiyo kushirikiana na Serikali kuchambua na kutoa mapendekezo ya namna bora ya kuboresha huduma kwa Watanzania kupitia mapato ya Serikali.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (Katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga (kulia), pamoja na Katibu Msaidizi, Idara ya Huduma za Kiufundi wa Tume hiyo, Bw. Jonas Nduttu, baada na kufanya mazungumzo, walipomtembelea Mhe, Balozi Omar (Mb), ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (kushoto), akiagana na Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo, baada ya Uongozi wa Tume hiyo, kumtembelea Mhe. Balozi Omar, ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma.
Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga, akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), na Uongozi wa Tume ya Pamoja ya Fedha, kilichofanyika Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, baada ya Uongozi huo kumtembelea Mhe. Balozi Omar.


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF – Dodoma)



Na. Asia Singano na Jordan Mbwambo, WF – Dodoma


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameiagiza Tume ya Pamoja ya Fedha (JFC), kushirikiana na Serikali kuchambua na kutoa mapendekezo ya namna bora ya kuboresha huduma kwa Watanzania kupitia mapato ya Serikali za Mitaa pamoja na uwezeshaji unaofanywa na Serikali Kuu kwenda Serikali za Mitaa.

Mhe. Balozi ametoa agizo hilo jijini Dodoma, alipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Tume ya Pamoja ya Fedha, ukiongozwa na Katibu wa Tume hiyo, Bw. Ernest Mchanga, walipomtembelea ofisini kwake Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, kwa ajili ya kujitambulisha.

Mhe. Balozi Omar alibainisha kuwa, pamoja na majukumu mengine ya kimuungano, Tume hiyo inapaswa kufanyia kazi masuala mengine ya kifedha hususani yale yasiyokuwa ya muungano ili kuboresha zaidi huduma za kijamii na kiuchumi.

“Kwa kutumia uzoefu wa Kimataifa tumewaagiza kufanya uchambuzi, tutakuja kukaa nao tutoe mapendekezo ya namna bora ambayo Serikali itaweza kuboresha huduma kwa Watanzania wote”. alibainisha Mhe. Balozi Omar (Mb).

Kwa upande wake Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga, alisema Taasisi hiyo itaendelea kushauri Serikali mbili za Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kuhusu Mfumo wa Fedha hususani katika mapato, matumizi pamoja na fedha nyingine zitakazowekwa na pande mbili za Muungano katika Akaunti ya Fedha ya Pamoja.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Fedha, akiwemo, Kamishina Msaidizi, Idara ya Sera, Bw. Wiliam Mhoja, pamoja na Kamishna Msaidizi, Idara ya Madeni, Bw. Omary Khama.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 19,2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Mafunzo hayo pia yameenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho hayo ni “Bidhaa Salama, Imani kwa Mlaji,” ikisisitiza umuhimu wa kuhakikisha bidhaa zote zinazotumiwa na wananchi zinakidhi viwango vya usalama na ubora.

Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC, Thecla Kitosi, amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wazuri wa elimu hiyo kwa jamii zinazowazunguka.

Aidha Bi.Kitosi amewaasa wanafunzi hao kuelewa haki zao kama walaji, pamoja na wajibu wao wa kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini au kuwa na mashaka kuhusu usalama wa bidhaa au huduma wanazotumia.

Hata hivyo amewahimiza wanafunzi kuwa mabalozi wazuri kwa jamii zao kwa kuwafahamisha wazazi na ndugu zao juu ya hatari za bidhaa bandia na namna ya kuzitambua.

"FCC itaendelea kutoa   elimu kwa makundi mbalimbali ya jamii, hususan wanafunzi, ni njia muhimu ya kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa, wanaoweza kujilinda dhidi ya bidhaa bandia na huduma zisizo na ubora."amesisitiza Bi.Kitosi

Kwa upande wake Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine, amieleza kuwa bidhaa bandia zinaweza kuwa na athari kubwa kiafya, kiuchumi na hata kijamii. Alifafanua kuwa baadhi ya bidhaa hizo, hususan vipodozi, dawa na vifaa vya umeme, vinaweza kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji kutokana na kutokidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa.

“Ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuwa makini na bidhaa tunazonunua. Hakikisheni mnachunguza nembo za ubora na kununua bidhaa kutoka kwa wauzaji wanaoaminika,” amesisitiza Bi. Diana.

Kwa upande wao, wanafunzi walionesha shauku kubwa kwa kuuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia. Walishukuru kwa elimu hiyo na kuahidi kuitumia ipasavyo katika maisha yao ya kila siku.

Elimu hii ni sehemu ya juhudi za FCC za kuendelea kulinda haki za mlaji pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na zenye ubora unaokubalika, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

 Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

   

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Maafisa kutoka Tume ya Ushindani(FCC) wakiwa katika picha ya pamoja na  Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Bunge  mara baada ya kukamilisha utoaji wa elimu kwa wanafunzi kuhusiana masuala ya kumlinda mlaji.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP), kwa kushirikiana na taasisi ya Sightsavers na YOWDO, umeandaa jukwaa maalumu la vijana na watu wenye ulemavu kwa lengo la kujadili fursa, changamoto na mikakati ya kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa nchi.


Serikali mkoani Kilimanjaro imeanza utekelezaji wa mkakati maalum wa kuwawezesha maafisa ugani kupitia mafunzo ya kitaalamu, ikiwa ni jitihada za kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo na kuongeza tija kwa wakulima.


Hatua hiyo inalenga pia kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuinua kipato cha wakulima katika mkoa huo.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wakati wa ufunguzi wa mafunzo yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), yaliyofanyika Machi 17, 2026 katika ukumbi wa Manispaa ya Moshi, Katibu Tawala Msaidizi wa Kilimo na Ufugaji, Dkt. Emmanuel Lema alisema maafisa ugani wanapaswa kutumia mbinu za kisasa na ubunifu ili kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi.

Alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo maafisa hao ili waweze kushauri matumizi sahihi ya mbegu bora, teknolojia za kisasa za kilimo pamoja na mbinu za kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.


Aidha, Dkt. Lema alibainisha kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha sekta ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji, kusambaza pembejeo na kuwapatia maafisa ugani vitendea kazi vinavyohitajika. Pia aliwataka maafisa hao kushiriki kikamilifu katika kudhibiti migogoro kati ya wakulima na wafugaji.


Kwa mujibu wa takwimu za mkoa, Kilimanjaro imezalisha tani 1,259,115 za mazao ya chakula katika mwaka wa kilimo 2024/2025, kiwango kinachozidi mahitaji ya tani 773,115.


Naye Afisa Kilimo kutoka COPRA, Bi. Paskalia Sitembela alisema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kutoa mafunzo yatakayochochea uzalishaji wa mazao yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko.


Maafisa ugani walioshiriki mafunzo hayo wameahidi kuyatumia ipasavyo ili kuwafikia wakulima katika maeneo yao na kuwapatia elimu sahihi ya kilimo, hatua itakayosaidia kuongeza uzalishaji wenye tija katika mkoa na taifa kwa ujumla.

 


Babati, Manyara: Sherehe ya kumbukizi ya kuzaliwa ya Mkurugenzi wa Mati Super Brands Ltd, Bilionea David Mulokozi, imegeuka kuwa somo la upendo na kuthaminiana baada ya mkewe, Doreen Mulokozi, kumuandalia tukio la kushtukiza lililogusa wengi.

Katika sherehe hiyo iliyofanyika Babati Mjini na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa, Doreen alimzawadia mumewe zawadi mbili kubwa—ikiwa ni pamoja na kumualika mwanamuziki anayempenda, Banana Zoro, ambaye aling’ara jukwaani kwa burudani ya hali ya juu na kukonga nyoyo za mwenyeji wa hafla pamoja na wageni wote.


Mbali na burudani hiyo iliyoongeza shamrashamra katika tukio hilo, Doreen alimkabidhi mumewe gari kama zawadi maalum ya kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa, hatua iliyodhihirisha mapenzi ya dhati na kuthamini mchango wake ndani ya familia.

Kwa upande wake, Banana Zoro alitoa shukrani zake za pekee kwa mwaliko huo, akieleza kuwa kushiriki katika hafla hiyo kumekuwa na maana kubwa kwake binafsi na kitaaluma.

Akizungumza kwa hisia na furaha, David Mulokozi alimshukuru mkewe kwa maandalizi hayo pamoja na zawadi ya kushtukiza, akieleza kuwa tukio hilo limekuwa moja ya kumbukumbu muhimu zaidi katika maisha yake.
“Kumbukizi yangu ya kuzaliwa alinifanyia mke wangu Doreen… kwangu vilikuwa vitu vya kipekee sana katika maisha yangu,” alisema Mulokozi.

Kwa utani, Mulokozi aliwataka pia wanawake wengine kuiga mfano huo kwa kuwapatia waume zao zawadi zenye thamani, badala ya zawadi ndogo ndogo za kawaida, jambo lililozua vicheko na furaha miongoni mwa wageni waliohudhuria.
Naye Doreen alimtakia mumewe baraka na mafanikio zaidi katika shughuli zake, huku akimuomba aitunze zawadi hiyo kama kumbukumbu muhimu ya upendo wao ili waendelee kuikumbuka hata watakapokuwa wazee.
Sherehe hiyo ilifanyika kwa mafanikio makubwa, ikijumuisha burudani, furaha na mshikamano wa kifamilia pamoja na marafiki, huku ikiakisi ujumbe mzito wa kuthaminiana, upendo wa kweli na umuhimu wa kusherehekea maisha pamoja.
Katika kuendeleza dhamira ya uwajibikaji kwa jamii, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limetembelea Kituo cha Watoto Yatima cha Umra Orphanage jijini Dar es Salaam, na kutoa msaada wa mahitaji muhimu sambamba na kuwapa faraja watoto wanaolelewa kituoni hapo, kuelekea sikukuu ya Idd.
NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) itaendelea kutoa fursa za mafunzo endelevu ya viongozi wa elimu wa ngazi mbalimbali na wadau wengine wa elimu ili waweze kuimarisha uongozi, usimamizi na uendeshaji wa shule kwa ajili ya utoaji wa elimu bora nchini. 

 




Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imetembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Utengamao cha Taifa unaotekelezwa na Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) katika eneo la Itega, jijini Dodoma.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 18 Machi 2026 na kuongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Edwin Swale ikiwa ni sehemu ya majukumu ya kamati ya kusimamia na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Swale amesema kuwa kamati imeridhishwa na hatua ya utekelezaji ambayo mradi umefikia kwani unaenda kutimiza dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kujali Utu na Ustawi wa Watanzania.

Sambamba na hilo, ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu kupitia Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za Kulevya kwa kubuni mbinu ya jinsi ya kusaidia waraibu watokanao na matumizi ya madawa za kulevya.

Awali,Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Mradi huo ni endelevu ikiwa ni juhudi ya Serikali katika mapambano dhidi ya Dawa za kulevya na kuahidi kuendelea kushirikiana na Taasisi binafsi katika mapambano dhidi ya matumizi ya Dawa za kulevya Nchini.

Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevya Bw. Aretas Lymo ameongeza kuwa kituo hiko kinatarajia kutoa huduma za matibabu, urekebishaji wa kitabia pamoja programu za kuwawezesha waathirika kurejea katika jamii wakiwa na uwezo wa kujitegemea.

Wakati huo huo, Makamu Mwenyekiti Mhe. Swale ameelekeza kuwa Ujenzi wa kituo hicho cha utengamao uzingatie Uwepo wa Miundombinu ya watu wenye mahitaji maalum na kutilia maanani malengo ya kituo ya kuwasaidia kiujuzi waraibu wa madawa ya kulevya .



 Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeingia katika mpango wa ushirikiano na kampuni ya Land Africa Safaris ili kukuza utalii wa ikolojia kupitia tukio la Cape to Cairo Arusha International Marathon linalotarajiwa kufanyika Mei 28 hadi 30, 2026 mkoani Arusha.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao kilichofanyika Machi 17, 2026 katika Ofisi ya Mhifadhi Mkuu wa Ziwa Duluti, Arumeru.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Mhifadhi Mkuu wa Ziwa Duluti, Peter A. Myonga, alisema ushirikiano huo ni fursa muhimu kwa TFS kutumia michezo kutangaza vivutio vya misitu na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea maeneo hayo.

Alisema tukio hilo linatarajiwa kuvutia zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi, hatua itakayochochea ongezeko la wageni, muda wa kukaa kwa watalii jijini Arusha na mapato yatokanayo na utalii.

Kwa mujibu wa Myonga, TFS imejipanga kushiriki kikamilifu katika mbio hizo ambapo vivutio vyake vya Napuru na Ziwa Duluti vitatembelewa na washiriki wa mbio hizo kwa ajili ya kutangaza utalii wa misitu na nyuki (api-tourism).

Aidha, alisema washiriki wa mbio hizo watapata fursa ya kutembelea vivutio vya misitu ikiwemo Shamba la Miti Meru na Ziwa Duluti kabla na baada ya tukio, huku mipango ikiwekwa kuhakikisha katika msimu ujao wa 2027 njia ya mbio inapita ndani ya hifadhi hizo ili kuongeza mvuto wa utalii.

Aliongeza kuwa TFS itanufaika pia kwa kuanzisha mabanda ya maonyesho, kutengeneza vifurushi vya utalii, huduma za kambi katika eneo la Napuru na kushiriki katika hafla ya Gala Dinner itakayotoa jukwaa la kuitangaza sekta ya misitu na nyuki.

Kwa upande wake, Haffy Mohamed  kutoka Land Africa Safaris alisema wataendelea kushirikiana na TFS kuhakikisha tukio hilo linakuwa chachu ya kukuza utalii wa michezo nchini.

Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuunganisha sekta ya michezo na utalii ili kuongeza mchango wa rasilimali za asili katika uchumi wa Taifa.