Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amempongeza Dkt. Rose Mbwete aliyekuwa Mkurugenzi wa kamapsi ya Karume –Zanzibar kwa kufanya kazi nzuri iliyozingatia kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma kwa kipindi cha miaka saba (2018- 2025) akiwa Mkurugenzi wa kampasi ya karume Zanzibar.

Profesa mapesa ameyasema hayo leo wakati wa kikao kazi cha Menejimenti cha kumuaga Dkt. Mbwete na Kumkaribisha Mkurugenzi mpya Dkt. Sifuni Lusiru, ambapo pamoja na mambo mengine Dkt Mbwete amepongezwa kwa kujenga mahusiano mazuri kati ya Chuo na Taasisi nyingine za Serikali zilizopo Zanzibar, pia amekuwa mvumilivu , amejenga umoja na mshikamano miongoni mwa Wafanayakazi wa kampasi ya karume.

Prof. Mapesa amemsihi Mkurugenzi mpya Dkt. Lusiru kuhakikisha anayaendeleza  na kudumisha yale yote ambayo Dkt. Mbwete aliyasimamia kwa maslahi mapana ya Taasisi, ametakiwa pia kushirikisha Menejimenti ya Chuo na Watumishi anawaowasimia pale inapobidi.

Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Richard Kangalawe amesema kwa sasa Kampasi ya karume imekuwa huwezi kulinganisha na miaka ya nyuma kwa maana  kozi zinazofundishwa zimeongezeka, idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa imeongezeka, idadi ya wanafunzi wanaohitimu imeongezeka na  hata idadi ya Watumishi imeongezeka.

Kwa upande wa Naibu Mkuu wa Chuo, Mipango, Fedha na Utawala Prof. Evaristo Haulle amesema ni jambo la kufurahia pamoja kumpongeza Dkt. Mbwete kwa utumishi wake mwema, ulioleta tija kwa Taasisi hivyo kukutana pamoja na kumpongeza anaponaliza muda wake kunatoa fursa kwa viongozi wengine kufanya tafakuri ya kina ya namna bora ya kuendeleza Taasisi.

Dkt.Rose Mbwete Mkurugenzi aliyemaliza muda wake amekiri kuwa kufanikiwa kwake kutimiza majukumu ya taasisi ni pamoja na ushirikiano wa dhati aliupata kutoka kwenye bodi ya Chuo, Menejimenti na Watumishi aliokuwa anawasimami, hivyo anaamini kuwa ushirikiano ni jambo la muhimu, Uvumilivu, Hekima na kuzingatia Tamaduni za aneo husika.

Mbwete amesema changamoto zipo lakini lazima kuwe na namna bora ya kuzitatua. Kwa kuweka maslahi ya Taasisi mbele Umoja Ndiyo nguvu yetu na umoja ni ushindi.

Naye Dkt. Sifuni Lusiru ameahidi kuendeleza yale yote ambayo Dkt Mbwete aliyasimamia kwa mustakbali wa Taasisi, ameahidi kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, taratibu, sheria na miongozo ya Utumishi wa umma.

Imetolewa na ;

Kitengo cha mawasiliano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

26.01.2026

 


Na OWM -TAMISEMI 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM- TAMISEMI) Mhe. Sospeter Mtwale amewataka watendaji wa Sekretarieti za Mikoa kutafakari na kutathmini maeneo ya utendaji kazi yanayohitaji kufanyiwa maboresho pamoja na kujenga timu za utendaji kazi zenye kuleta tija.

Mhe. Mtwale ametoa rai hiyo leo Januari 26, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa St Gasper Dodoma, wakati akifungua mafunzo ya uongozi kwa makatibu tawala wa mikoa sehemu ya elimu na mafunzo ya ufundi, wakuu wa vitengo vya uhasibu na fedha, ukaguzi wa ndani na maendeleo ya jamii kutoka katika sekretarieti za mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

Amesema TAMISEMI imeona umuhimu wa kutoa mafunzo ya uongozi kwa watendaji hao ili kuongeza ufanisi na tija katika sekretarieti za mikoa na kuwa awamu hii inahitimisha mafunzo kwa watendaji wa sekretarieti hizo ambapo tayari mafunzo yameshatolewa kwa wakuu na sehemu na vitengo vingine.

"Sitarajii ushiriki hafifu, matarajio ya TAMISEMI baada ya mafunzo ni kuwa mtaweza kusimamia watumishi pamoja na ninyi wenyewe kuwa vioo katika kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na pia mtadhibiti uvujaji wa siri za serikali, mtasimamia vema rasilimali za umma na kuepuka migogoro isiyo ya lazima," amesisitiza Mhe. Mtwale.

Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa, OWM-TAMISEMI Angelista Kihaga amesema mafunzo hayo ni ya uongozi sio ya taaluma na kuongeza kuwa baada ya mafunzo hayo watafanya tathmini kuona endapo kuna mabadiliko.

Bi. Angelista amewataka watendaji hao wanaopata mafunzo kuwa chachu ya mabadiliko ya uongozi kwa watendaji na watumishi wenzao kwani baadhi ya mada watakazofundishwa ni pamoja na usimamizi wa miradi, rasilimali watu na kufanya kazi kama timu moja.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Tawala za Mikoa, OWM-TAMISEMI Beatrice Kimoleta amesema mafunzo hayo yalianza kutolewa mwezi Mei 2025 kwa baadhi ya viongozi wa sekretarieti za mikoa kwa kushirikiana vizuri na Taasisi ya Uongozi.

Ameongeza kuwa kupitia mafunzo hayo wamelenga kuwajengea uwezo watendaji hao ili wawe washauri wazuri kwa viongozi wa sekretarieti za mikoa kwani hapo awali mafunzo ya uongozi yalikuwa yakitolewa kwa viongozi pekee na kutowashirikisha washauri wao.

Akizungumza kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Emmanueli Tesua ameishukuru OWM-TAMISEMI kwa kuwashirikisha katika kutoa mafunzo hayo kwa viongozi wote wa Sekretarieti za Mikoa.



Na Munir Shemweta, WANMM

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeingilia kati mgogoro wa matumizi ya ardhi unaomhusisha mwekezaji Rashid Kwanzibwa, aliyedaiwa kubomoa baadhi ya majengo yaliyokuwa kwenye maeneo ya serikali na kuanzisha miradi bila utaratibu katika eneo la Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro, Geita.

Akitolea ufafanuzi kuhusu suala hilo leo, tarehe 26 Januari, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amesema wizara yake inaungana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhakikisha mgogoro unafanyiwa kazi na kukamilika.

Mhe. Dkt Akwilapo amewakumbusha wamiliki wa maeneo yote nchini kuzingatia matumizi yaliyokusudiwa katika hati miliki zao, na endapo mmiliki ana mpango wa kuendeleza eneo lake kwa matumizi tofauti na yaliyotolewa katika hati, ni lazima apate kibali cha mabadiliko ya matumizi kama sheria inavyoelekeza.

''Hatua hiyo itahakikisha maeneo yanaendelezwa kwa kuzingatia mpango, na hivyo kuondoa migongano ya matumizi, kutunza mazingira, na kuweka nadhifu miji yetu''. Amesema

Kwa mujibu wa Dkt. Akwilapo, uendelezaji wowote unaofanyika sharti uzingatie sheria za uendelezaji miji, ikiwa ni pamoja na kupata vibali vyote vinavyotolewa na mamlaka zote za serikali. Kwa sasa, wataalamu wa Wizara wameungana na TAMISEMI kushughulikia suala hilo, na baada ya uchunguzi kukamilika, kutatolewa taarifa rasmi ya pamoja.

Uamuzi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuingilia kati sakata hilo unafuatia kusambaa kwa picha mjengeo katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ikionesha Kamati ya Fedha na Uchumi ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ikilazimika kusimamisha shughuli za mradi wa ujenzi wa vibanda vya maduka kwenye eneo la viwanja vya CCM Katoro, huku ikidaiwa mwekezaji kuingia mipaka ya serikali ya kijiji katika Kitongoji cha Katoro Center kilichopo mji mdogo wa Katoro mkoani Geita.

Katika maisha ya kila siku, kuna matukio ambayo huwezi kuyatarajia hata katika ndoto zako mbaya. Mimi, mwanamke mmoja aliyetambulika kama Slay Queen, nilijikuta katika tukio ambalo lilibadilisha maisha yangu kwa mshangao mkubwa.

Baada ya kumchukua mume wa mwanamke mwingine Nairobi, nilidhani maisha yangu yatakuwa ya raha na furaha, lakini ukweli ulikuwa tofauti kabisa.

Siku chache baada ya kitendo hicho, tabia zangu zilianza kubadilika ghafla. Nilianza kuogopa kila kona, kushindwa kulala, na mawazo ya huzuni na hofu yakitawala akili yangu.

Wakati mwingine nilijikuta nikiongea peke yangu bila maana, nikihisi nimepoteza udhibiti wa akili yangu. Majirani na rafiki walishangaa kuona mabadiliko haya, na wengi walidhani kuwa nilikuwa nimekwenda “pale mbali” kiakili.

Hali hiyo ilinionyesha wazi kuwa nilihitaji msaada wa haraka. Nilihitaji mtu mwenye hekima na mbinu za busara ili kunisaidia kurekebisha hali hii, kuondoa huzuni na hofu, na kurejesha amani ya akili yangu.Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/slay-queen-atokwa-wazimu-baada-ya-kumchukua-mume-wa-mwanamke-mwingine-nairobi/
Maisha ya kijijini si rahisi, hasa pale kipato kinapokuwa kidogo. Katika eneo letu, watu wengi waliwahi kujipatia riziki kupitia shughuli ndogo ndogo za jadi. 

Hata hivyo, mambo yalibadilika ghafla pale mamlaka zilipoanza msako mkali dhidi ya pombe haramu.

Kila siku kulikuwa na habari za watu kukamatwa, kufungiwa familia zao, na mali kunyakuliwa. Hofu ilitanda kijijini.
Familia yangu ilijikuta katikati ya presha kubwa.

Kulikuwa na vitisho visivyoeleweka, tetesi za majirani, na hofu kwamba siku yoyote tungejikuta mikononi mwa polisi bila hata kuelewa kosa letu vizuri. Nilihisi kama kiongozi wa familia, na mzigo huo ulinilemea sana.

Usiku sikulala, nikijiuliza nitawalinda vipi watu ninaowapenda. Nilijaribu njia nyingi za kawaida kushauriana na marafiki, kusikiliza ushauri wa watu wa karibu lakini kila mtu alikuwa na hofu yake.

Hakukuwa na suluhisho la uhakika. Soma Zaidi.....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-nilivyolinda-familia-yangu-dhidi-ya-kukamatwa-wakati-polisi-walipolenga-pombe-haramu-kijijin/

Nilipoanza kuhisi maumivu makali ya kifua na kichefuchefu kila siku, sikujua kuwa ni ishara ya tatizo kubwa. 

Mara kwa mara nilikuwa nikiwa na homa, kukohoa damu kidogo, na kushindwa kupata nguvu za kutosha.

Kila siku ilikuwa ni changamoto; hata kupanda ngazi ndogo kulikuwa mgumu. Marafiki na familia walikuwa na wasiwasi, na mara nyingine walinieleza ni lazima niangalie afya yangu kwa haraka.

Baada ya kupimwa kwa mara kadhaa, madaktari walitupa matokeo yaliyochanganya akili zangu TB! Nilihisi dunia yangu imevunjika. Kwa mara ya kwanza, hofu na woga vilijaza kila kona ya maisha yangu.

Nilijua TB ni hatari sana, na wazo la kutokupona liliniogopesha sana. Nilijaribu dawa za kawaida, milo bora, na kupumua kwa uangalifu, lakini hali yangu haikuwa bora. Kila hatua ilionekana kuchosha mwili wangu na kuathiri moyo wangu.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/tb-ilikua-kituo-cha-hatari-maishani-mwangu-hii-ndiyo-njia-nilivyopona-ndani-ya-siku-chache-baada-ya-kutembelea-daktari-maalum/
Kila mtu ana siri yake, lakini kuna baadhi ya matukio ambayo huwezi kufikiria kutokea hata katika ndoto zako mbaya zaidi. 

Mimi, mfanyabiashara wa Nakuru, nilikuwa nikijisikia nafsi yangu ikiwa huru na furaha katika maisha yangu ya kila siku.

Lakini siku moja, tukio la kushangaza lilitokea ambalo lilibadilisha kila kitu.
Nilikuwa nikiwa na mapenzi na mwanamke niliyejua kuwa ni hatari kidogo pesa zake na sifa yake zilikuwa zikitishia.

Tulipokuwa ndani ya gari langu, tukishiriki wakati wa karibu, ghafla alikumbana na tatizo ambalo halikutarajiwa alikwama! Nilijikuta nikiwa na hofu, nikishangaa jinsi jambo hili lingetokea.

Sauti za wasiozunguka zilisikika, na hofu ya kudhihirika hadharani ilinifanya nikose utulivu. Nilihisi aibu kubwa, na woga wa kupoteza heshima yangu ulianza kunitawala.

Nilijaribu kwa kila njia kumsaidia, lakini kila jaribio lilitengeneza woga zaidi. Nilihisi sina njia. Nilijua kuwa tukio hili lingebadilisha hadhi yangu katika biashara na maisha ya kibinafsi.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mfanyabiashara-wa-nakuru-akwama-na-msichana-wakati-wa-mapenzi-ndani-ya-gari-yake-suluhisho-la-ajabu-lilirudisha-heshima-yake/

Miaka michache iliyopita, mke wangu na mimi tulikabiliana na tatizo kubwa sana la kifedha. Deni la Sh. 3 Milioni lilikuwa limekusanyika, na kila siku tulihisi uzito mkubwa wa wasi wasi na hofu.

Kila mara tulipofikiria jinsi ya kuligharamia, tunapata vizuizi visivyoonekana, masharti ya benki yaliyokuwa magumu, na hata hofu ya kupoteza kila kitu tulichojenga kwa pamoja.

Kila siku nyumbani ilikuwa yenye hofu. Tulikuwa tunapata usingizi mgumu, mawazo ya kupoteza kila kitu yalituzunguka kila kona. Watu walituuliza “mnafanya nini na deni?” na maneno hayo yaliongeza hofu yetu.

Tulijaribu njia za kawaida kuongea na benki, kuomba marekebisho, hata kujaribu kuchanganya pesa zetu za dharura lakini kila njia ilitupotezea matumaini zaidi.

Nilihisi kama kila kitu kilikuwa kikienda mbaya zaidi, na wenzangu waliniona nikiwa nimevunjika kimoyo. Siku moja, tukijaribu tena kuwasiliana na benki, tukashangaa. Wengine walinidhihaki, wengine wakishangaa.

Lakini ukweli ulitushangaza zaidi benki ilikuwa “imepoteza” hati zetu zote! Hatua moja hii ilikuwa kama mwangaza wa tumaini. Hata hivyo, tulijua hatuwezi kutegemea bahati pekee.

Tulihitaji mwongozo sahihi wa kulinda mali zetu na kuhakikisha kuwa tunepata haki yetu bila madhara yoyote.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/tulikuwa-tukiwa-na-deni-la-sh-3-milioni-benki-ilinipotezea-hati-zake-sasa-ukiangalia-utashangaa-jinsi-tulivyoepuka-hasara-kubwa/

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia (Diaspora), katika hoteli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 25 Januari, 2026.

Na: OWM (KAM) – Riyadh, Saudi Arabia

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu, amewahimiza Watanzania wanaoishi nje ya nchi (Diaspora) kuitambua na kuielewa kwa kina Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ili waweze kubaini fursa zilizopo na kuchangia kikamilifu maendeleo ya Taifa.

Amesema Dira hiyo inaeleza mwelekeo wa Taifa ambalo Tanzania inalenga kujenga, hivyo ni muhimu kwa Diaspora kuitumia kama mwongozo wa kutambua na kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta za uwekezaji, ajira, ujuzi, ubunifu na matumizi ya teknolojia, kwa lengo la kukuza uchumi na kuongeza Pato la Taifa.

Mhe. Sangu ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi nchini Saudi Arabia, ambapo pamoja na mambo mengine, anatarajiwa kushiriki Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaojadili masuala ya soko la ajira duniani.

Katika ziara hiyo, Waziri Sangu pia amekutana na Watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchini Saudi Arabia tarehe 24 Januari, 2026, kwa lengo la kujadiliana, kubadilishana uzoefu na kusikiliza changamoto pamoja na fursa zilizopo kwa Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi.

Alieleza kuwa, Serikali inatambua mchango mkubwa wa Diaspora katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia fedha wanazozituma nyumbani (remittances), uwekezaji, pamoja na kuhamasisha maarifa na ujuzi walioupata nje ya nchi.

Aidha, Waziri Sangu amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi wanalindwa, wanaheshimiwa na wananufaika ipasavyo na fursa za ajira za kimataifa.

“Tumeimarisha ushirikiano na Serikali ya Saudi Arabia kupitia makubaliano ya ajira, kuboresha mifumo ya usimamizi wa mawakala binafsi wa ajira, pamoja na kuanzisha mafunzo ya kabla ya kuondoka nchini ili kuwaandaa Watanzania wetu kikamilifu,” amesema Waziri Sangu

Kadhalika, amewahakikishia Diaspora kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Kitengo cha Huduma za Ajira itaendelea kuratibu na kusimamia fursa za ajira kwa Watanzania ili kuhakikisha zinakuwa za staha, salama na zenye haki.

Kwa upande mwingine, Waziri Sangu amesema Serikali kupitia Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) imeanzisha mafao yatakayowawezesha Watanzania walioajiriwa katika sekta binafsi pamoja na waliojiajiri kunufaika na huduma za hifadhi ya jamii hata wanapokuwa nje ya nchi.

Pia Waziri Sangu ameipongeza Saudi Arabia kwa mahusiano mazuri na mashirikiano na Tanzania kwani kupitia mkataba wa mashirikiano umewezasha Watanzania 1,049 kupata ajira Nchini Saudi Arabia.

Naye, Mwenyekiti wa Diaspora nchini Saudi Arabia, Dkt. Zidikheri Msechu, amesema Diaspora wako tayari kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Pia amewahimiza Watanzania wanaopata fursa za ajira nje ya nchi kufuata taratibu rasmi na kutumia mawakala wanaotambulika na Serikali kabla ya kwenda kufanya kazi nje ya nchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia (Diaspora), katika hoteli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 25 Januari, 2026.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akipokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Watanzania wanaofanya kazi nchini Saudi Arabia (Diaspora), Dkt. Zidikheri Msechu walipokutana katika hotrli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu,akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Watanzania wanaoishi nchini Saudi Arabia (Diaspora), katika hoteli ya Ritz Carlton, Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 25 Januari, 2026.


Nilipoajiriwa kazini, nilikuwa na ndoto kubwa. Nilifanya kazi kwa bidii, nilikuwa mtu wa kwanza kufika na wa mwisho kutoka. Kila jukumu nililopewa nililitekeleza kwa uaminifu na kujituma.

Nilitarajia juhudi zangu zingeonekana, lakini mwaka wa kwanza ulipita bila mabadiliko yoyote. Nilijipa moyo nikijua labda muda wangu ulikuwa bado haujafika.

Mwaka wa pili ukaanza, na hali ikawa ile ile. Watu niliowafundisha wakaanza kupandishwa vyeo. Wengine waliokuwa na muda mfupi kazini wakawa wakubwa wangu. Nilikuwa nashangaa, nilikuwa naumia kimya kimya.

Kila nilipouliza, niliambiwa “endelea kujituma, muda wako utafika.” Lakini ndani yangu nilihisi kuna kitu kinazuia maendeleo yangu. Nilianza kupoteza motisha. Nilijiuliza kama kweli nilikuwa na thamani kazini pale.

Heshima yangu kazini ilianza kushuka, na hata nyumbani mawazo yalinizidi. Nilikuwa nafanya kazi, lakini matunda ya kazi hayakuonekana. Ilifika hatua nikahisi kama ninafungwa, kana kwamba kuna mkono usioonekana unaozuia maendeleo yangu. Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilifanya-kazi-kwa-miaka-mbili-bila-kupata-promotion-ila-nilijitafutia-hiyo-promotion-mwenyewe/
Kipindi nilipokuwa shule, nilijulikana kama mwanafunzi “anayejaribu lakini hafanikiwi.” Kila muhula ulipofika mwisho, majina yaliposomwa darasani, langu halikuwahi kukaribia orodha ya wanaofanya vizuri.

Walimu waliniona kama aliyekata tamaa. Wenzangu walinicheka, wengine wakinionea huruma. Kila niliporudi nyumbani, nilikuwa na mzigo mkubwa moyoni hisia kwamba nimewaangusha wale waliokuwa wananiamini.

Nilijitahidi kusoma. Nilikaa masaa mengi usiku, lakini kichwa kilionekana kizito, kumbukumbu ikikataa kukaa. Kila jaribio lilionekana kuishia pale pale.

Nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa mimi, au kulikuwa na kitu kingine kinachonizuia. Kicheko cha watu kilinifanya nijione mdogo, na siku moja nilijikuta nikisema, “labda shule sio kwa ajili yangu.”

Lakini ndani yangu kulikuwa na sauti ndogo iliyokataa kuniruhusu kuacha. Niliamua kuwa hata nikipambana peke yangu, sitakubali kushindwa.

Nilizungumza na mtu aliyenielewa na akanishauri nijilinde kiakili na kiroho, niondoe hofu, wivu, na mizigo ya maneno niliyokuwa nikiambiwa kila siku.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nachekwa-na-watu-kwa-kufeli-darasani-lakini-niliamua-liwe-liwalo-nikatafuta-kinga-sasa-nahitimu/
Nilikuwa nikijaribu bahati yangu kwenye betting kwa muda mrefu, kila wiki nikipoteza pesa bila kuonekana na hakuna sababu dhahiri. Kila mara nilijikuta nikihisi nimechoka, kuchanganyikiwa, na wakati mwingine kushuka moyo.

Rafiki zangu walinipa ushauri, lakini kila mbinu waliyojaribu ilikuwa ile ile—kupoteza tena. Nilihisi labda betting si kwaajili yangu, na mara nyingi nilijiuliza kama nilikuwa nikifanya kitu kisicho na maana.

Hali hiyo ilinifanya nisahau sababu niliyoanza betting furaha na ndoto ya kupata faida ya haraka. Nilijaribu kuongeza dau, kuchanganya mbinu, hata kubashiri kwa kutumia hisia zangu, lakini matokeo hayakuwa tofauti.

Machozi na hofu vilijaa kila mara nilipoona matokeo mabaya. Nilihisi nipo kwenye mzunguko usio na mwisho wa kushindwa. Baada ya muda, niliamua kuwa lazima nibadilishe mtazamo wangu.Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-nilishinda-mita-na-football-bet-moja-safi/

Kwa muda mrefu, maisha ya ndoa yangu yalikuwa kama kupigana bila mwisho. Kila siku ilikuwa changamoto nyingine, mabishano madogo yakipandishwa na majanga makubwa. Nilihisi kuwa hakuna furaha tena.

Mke wangu au mume wangu, mara zote walionekana kukosa kuvumiliana. Shida ndogo ndogo zilipandishwa na kuwa mabishano makubwa, na nyumba ilijaa huzuni. Nilijaribu njia zote nilizoona kwenye familia na marafiki, nikitafuta suluhisho la haraka.

Nilijaribu kuzungumza, kuandika, hata kusamehe kilichopita, lakini kila hatua ilikuwa ya muda mfupi. Mara nyingi nilihisi mapenzi yalikuwa hayana ladha tena. Nilihisi nimechoka na kujiuliza kama ndoa yetu ilikuwa bado na thamani yoyote.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/tulipigana-kila-siku-nyumbani-ndoa-ikakosa-ladha-lakini-nilipata-suluhisho-kamili-la-kurejesha-penzi/
Nilipoanza kupata shinikizo la damu juu, maisha yangu yaligeuka kuwa changamoto kila siku. Nilikuwa nikihisi kichefuchefu, maumivu ya kichwa, na wakati mwingine kupoteza nguvu ghafla.

Watu walianza kuniona nikikosa nguvu, na mara nyingine walinilaumu kwa kula vibaya au kutojali afya yangu. Nilijaribu kutumia dawa za kawaida, kubadilisha lishe, hata kupunguza stress, lakini hakuna kilichonipa faraja ya kudumu.

Hali ilinionyesha wazi kuwa tatizo ni kubwa zaidi ya nilivyodhani. Wengi walinieleza tu “angalau jaribu kupumua vizuri au punguza msongo wa mawazo,” lakini hakuna kilichobadilika.

Nilihisi kuhuzunika kila siku, nikijua afya yangu iko hatarini. Nilikuwa nikihitaji suluhisho sahihi, la kudumu, na lisilo na madhara, ili kurekebisha shinikizo langu la damu.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipata-shinikizo-la-damu-juu-lakini-hatua-moja-ya-busara-ilirejesha-afya-yangu/

 




Na Oscar Assenga,TANGA

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman amesema ana dhamira ya dhati kurejesha timu ya mpira wa miguu, African Spots ya jijini humo ili kurejesha heshima ya timu hiyo kongwe pamoja na Dabi ya Tanga iliyokuwa na upinzani mkubwa hapa nchini.



Alisema timu hiyo imekuwa ikisuasua kupanda daraja kwa muda mrefu kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo basi la kuwasafirisha wachezaji pamoja na benchi la ufundi hivyo uwepo wa basi hilo utasaidia kuwawezesha kuondokana nazo


Aliyasema hayo Januari 24 mwaka huu katika hafla ya kuukabidhi uongozi wa timu hiyo gari Jipya aina ya TATA lililogarimu takribani shilingi Milioni 170, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Klabu hiyo barabara 12 Jijini Tanga .

Rajabu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) alisema kwamba kurudi kwa timu hiyo kongwe hapa nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1936 kutarejesha heshima ya Mkoa wa Tanga kutokana na kwamba bila African Spots hakuna Coastal Union inayochangiwa na utani wa jadi timu hizo kama ilivyokuwa Simba na Yanga za Jijini Dar es Salaam.


Mbali ya kununua basi na kukabidhi, Mwenyekiti ameahidi kusaidia timu hiyo na kuiinua hadi kufikia kucheza ligi kuu ambapo ataipambania na kujenga Jengo la Ofisi la Gorofa tatu ikiwa ni pamoja na kununua gari kubwa zaidi wakati gari iliyokabidhiwa kubaki kuwa ya kuwapeleka wachezaji mazoezini.



Sambamba na kukabidhi gari hilo mwenyekiti huyo pia alitoa kiasi cha shilingi Milioni 30 na kukabidhi kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kwa ajili ya kutatua changamoto kadhaa zinazowakabili.


Awali akizungumza katika Halfa hiyo Rais wa TFF Walles Karia aliwasihi wanachama kushirikiana na vionhozi ili kufanya maamuzi pamoja na kujitokeza uwanjani pindi timu zitakapokuwq zancheza kwani ndio jambo sahihi la kuvuta wawekezaji.


Lakini pia aliwasihi viwanja vya michezo vilivyopo Myanjani Technically Center, "kile kituo kipo na kinafanya vizuri sana lakini kinanufaisha vijana walioko nje ya Tanga, niwasiji kwamba mpeleke vijana pale ili timu zetu zipate wachezaji bora" alisema Karia.

Katika hafla hiyo alikuwepo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) ambaye alisisitiza suala la wanachama kushirikiana na vionhozi wa timu hiyo na kuchangia kipato kwenye timu matokeo yataonekana.

"Kama tutakuwa na timu mbili (2) zinazoenda ligi kuu, hata uchumi wa Tanga utaimarika kupitia michezo, tuchangie timu kwa kwenda uwanjani na hata kununua jezi, kwa kufanya hivyo kutaimarisha timu zetu na wachezaji kuwa na ari uwanjani" alisema.

Katika kuinua timu hizo Naibu Waziri Mwana FA alitoa kiasi cha shilingi Milioni 10 ambapo kila timu imekabidhiwa kwa vionhozi wa timu zote mbili kiasi cha shilingi Milioni 5.

Rais Karia amewahakikishia Watanzania kwamba timu ya African Spots ikismama imara kama awali na Coastal Union ndiyo timu pekee ambazo zina uwezo wa kusimamishana na Simba na Yanga na siyo timu nyingine.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi, Dk. Batilda Buriani aliwataka vionhozi wa timu za mipira na wanamichezo wote kutumia fursa ambazo zipo mkoani humo katika kuimarisha timu na kuleta manufaa katika Mkoa.

"Mradi wa Bomba la mafuta nao una fursa katika michezo, kule Uganda wamesaidia kujenga uwanja wa mpira, na hata timu yetu ya Coastal Union imeshapeleka maombi yake tunasubiri utekelezaji mwengine uendelee"

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru mkoani Arusha na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa chuoni hapo, ikiwemo ujenzi wa jengo la Utawala, kituo cha uhifadhi wa machapisho yanayohusu  wanawake, mabweni ya wanafunzi pamoja na Kituo cha Ubunifu wa Kidigitali na Huduma Tandaa (JODIC).

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la Utawala, Mhe. Mahundi amesema serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya vyuo vya maendeleo ya jamii ili kuimarisha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma.

 “Miradi inayoletwa hapa chuoni inapaswa kusimamiwa kwa viwango vinavyokubalika ili thamani ya fedha itumike ipasavyo na kwa ubora unaostahili kwa manufaa ya wanafunzi na taasisi kwa ujumla,” amesema Mhe. Mahundi.

Aidha , Mhe. Mahundi amepata fursa ya kuzungumza na wanafunzi wa taasisi hiyo ambapo amewahimiza kutumia elimu wanayoipata chuoni hapo kwenda kuitumikia jamii kwa vitendo kwa kuwa  elimu ya maendeleo ya jamii inapaswa kuwa chachu ya mabadiliko chanya katika jamii na siyo kubaki darasani pekee. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru, Dkt. Bakari George, ameishukuru serikali kwa kuendelea kuiunga mkono taasisi hiyo kupitia utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. 

“Hili  jengo la Utawala na miradi mingine inaongeza ufanisi wa kiutendaji na kuboresha huduma kwa wanafunzi, Uwekezaji huu unaofanywa na serikali ni kielelezo cha dhamira yake ya kuimarisha elimu ya maendeleo ya jamii nchini,” amesema Dkt. George.

Ziara hiyo ya Naibu Waziri Mahundi katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru imekuwa sehemu ya juhudi za serikali katika kuimarisha elimu ya maendeleo ya jamii nchini, kwa lengo la kuhakikisha vyuo vinaendelea kuzalisha wataalamu wenye ujuzi, ubunifu na maadili watakaotumia elimu yao kutatua changamoto za kijamii, kuendeleza ustawi wa wananchi na kuchangia maendeleo endelevu ya Taifa.