Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni  Mapesa amewataka viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kutambua kuwa Uongozi ni utumishi wa kuwatumikia watu na si kutumikiwa, kwani kazi ya kiongozi ni kuwa tayari muda wote kutatua changamoto mbalimbali.

Mapesa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwapisha viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kwa mwaka 2026/27 pamoja na mambo mengine amepongeza Uongozi wa Serikali  iliyomaliza muda wake iliyokuwa ikiongozwa na Magashi Magina  kuwa walizingatia Weledi wa hali ya Juu.

Mkuu huyo wa Taasisi ameitaka Serikali mpya kuzingatia misingi ya Uongozi, na kuwa na namna bora ya kutatua changamoto ikiwa ni pamoja na kushirikiana vyema na Serikali ya Wanafunzi ambayo imemaliza muda wake, huku akiwaahidi ushirikiano wa dhati kutoka kwa Uongozi wa Chuo.

Kwa upande wake, Rais aliyemaliza muda wake Magashi Magina ameishukuru Menejimenti ya chuo kwa ushirikiano alioupata katika kipindi chote cha uongozi wake, ameeleza kuwa mafanikio yote yaliyopatikana yalitokana na uwazi na utayari wa Menejimenti kusikiliza na kutatua Changamoto mbalimbali za Wanafunzi jambo lililorahisisha utendaji kazi wa serikali yake.

Nao, Viongozi wapya walioapishwa kuiongoza Serikali ya Wanafunzi , Rais ni Samir Naseer na Makamu wa Rais  Julieth Mandia  wametoa shukrani za dhati kwa Wanafunzi wote kwa kuonyesha imani kwao na kuwachagua kuongoza Serikali ya wanafunzi ambapo wameahidi kuongozi kwa Uadilifu, Amani, mshikamano kwa  kushirikiana na Menejimenti ya Chuo pamoja na Serikali ya Wanafunzi iliyomaliza muda wake.

 

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

28.05.2026

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Maryprisca Mahundi amesema maonyesho ya Mbeya City Expo yameendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa Mkoa wa Mbeya kwa kuwakutanisha wananchi, taasisi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Akizungumza baada ya kutembelea mabanda mbalimbali katika maonyesho hayo yanayofanyika katika viwanja vya Uhindini, Jijini Mbeya, Eng. Mahundi amesema ameridhishwa na namna shughuli za kijamii na kiuchumi zinavyooneshwa kupitia maonyesho hayo.

Amesema Mbeya City Expo imekuwa jukwaa muhimu la kutoa elimu, kutangaza huduma na bidhaa pamoja na kuhamasisha fursa za maendeleo kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na maeneo ya jirani.

Aidha, amepongeza waandaaji wa maonyesho hayo kwa kutoa nafasi kwa wananchi kupata elimu na huduma mbalimbali zinazochochea maendeleo ya jamii pamoja na kukuza uchumi.

Katika hatua nyingine, Eng. Mahundi amesisitiza wananchi, hususan makundi maalum, kutumia vizuri mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na halmashauri ili kujikwamua kiuchumi na kuongeza kipato cha familia zao.

Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa najiona sifai kabisa. Nilikuwa mtu mwenye ndoto nyingi, lakini kadri muda ulivyopita nilianza kupoteza kujiamini. Kila nilipojaribu jambo jipya, kulikuwa na watu waliokuwa tayari kunikosoa au kunicheka.

Wengine walikuwa wakiniambia siwezi kufanikiwa, huku wengine wakinifanya nijihisi mdogo bila sababu. Kwa kweli iliniumiza sana. Polepole nilianza kujifungia ndani ya dunia yangu mwenyewe.

Nilianza kuogopa kuzungumza mbele za watu, kujaribu opportunities mpya, au hata kuvaa vile nilivyopenda kwa sababu nilihofia watu wangesema nini. 

Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wa rika langu wakisonga mbele huku mimi nikihisi kama nimesimama sehemu moja.

Kulikuwa na siku nilijiangalia kwenye kioo na kushindwa kuona kitu kizuri kuhusu mimi mwenyewe. 

Confidence yangu ilikuwa imeshuka sana kiasi kwamba hata watu walikuwa wanaanza kunichukulia kawaida. Nilianza kuamini maneno mabaya ya watu.SOMA ZAIDI.


Kulikuwa na kipindi ambacho nilikuwa karibu kukata tamaa kabisa kuhusu shamba langu. Nilikuwa nimewekeza nguvu nyingi sana kwenye kilimo. 

Kila siku nilikuwa naamka mapema kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Lakini ghafla nilianza kugundua mazao na vifaa vidogo vidogo vinaanza kupotea kwa njia isiyoeleweka.

Mwanzoni nilidhani ni makosa ya kawaida. Lakini kadri wiki zilivyopita, hasara ilianza kuongezeka. Mara napoteza mahindi yaliyokuwa tayari kuvunwa, mara vifaa vya kazi vinatoweka. 

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba kila nilipojaribu kuuliza watu wa karibu, hakuna aliyekuwa na taarifa yoyote.

Kwa kweli nilichanganyikiwa. Nilianza kufanya ulinzi wa usiku mara kadhaa lakini bado sikuweza kumkamata mtu yeyote. 

Wakati mwingine nilifika shambani asubuhi na kukuta dalili kuwa mtu alipita usiku lakini hakuna clue ya kueleweka.

Nilikuwa karibu kuvunjika moyo. Watu wengine waliniambia niache kupambana kwa sababu huenda singepata anayehusika. Lakini moyoni sikuwa tayari kuona jasho langu linaendelea kupotea.SOMA ZAIDI.


Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa karibu kufunga biashara yangu kwa maumivu makubwa. 

Nilikuwa nimeanzisha biashara yangu kwa juhudi nyingi sana. Nilikuwa naamka mapema kila siku, nikijituma kuhakikisha wateja wanapata huduma nzuri.

Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda sawa, na nilikuwa na matumaini makubwa ya kuona biashara yangu ikikua. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Biashara nyingine iliyokuwa karibu yangu ilianza kunizidi kwa namna ambayo sikuielewa. Wateja wangu wa kawaida wakaanza kupungua. Wengine walikuwa wanaenda upande mwingine ghafla bila maelezo.

Kilichoniumiza zaidi ni kusikia maneno yaliyokuwa yanaenezwa. Kulikuwa na watu waliokuwa wakisema biashara yangu haikuwa nzuri, bidhaa zangu hazikuwa na ubora, na huduma yangu haikuridhisha wakati nilikuwa najua nilikuwa najitahidi sana.

Polepole nilianza kuhisi kama mshindani wangu alikuwa akifanya kila kitu kuhakikisha ninapoteza wateja. Kwa kweli nilivunjika moyo. 

Kulikuwa na siku nilikaa dukani kwa masaa mengi bila mteja wa maana. Bills zilianza kuongezeka, stock ilianza kukaa sana, na nilianza kujiuliza kama ndoto yangu ilikuwa inaisha.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, maisha yangu yalikuwa ya hofu na wasiwasi kwa sababu ya pumu. Mwanzoni nilidhani ni hali ambayo ingeisha kadri muda ulivyopita. Lakini kadri nilivyokuwa nakua, mashambulizi ya pumu yakaanza kuwa ya mara kwa mara.

Kulikuwa na siku nilikosa pumzi ghafla usiku, nikaanza kukohoa sana, na familia yangu ikalazimika kunikimbiza hospitalini. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Nilikuwa naogopa hata mabadiliko ya hali ya hewa. Vumbi, baridi, moshi, au harufu kali vilikuwa vinanifanya niwe na wasiwasi. Wakati mwingine nilishindwa kushiriki shughuli za kawaida kwa sababu niliogopa kupata shida ya kupumua.

Kilichoniumiza zaidi ni kulazwa hospitalini mara kwa mara. Kulikuwa na nyakati nilihisi kama maisha yangu yalikuwa yamesimama. 

Nilifuata dawa nilizopewa hospitalini na kutumia inhaler kama nilivyoelekezwa, lakini bado nilikuwa napata changamoto za mara kwa mara.

Kulikuwa na kipindi nilianza kukata tamaa. Nilikuwa najiuliza kama ningewahi kuishi maisha ya kawaida bila hofu ya kushindwa kupumua ghafla.SOMA ZAIDI.


Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi kama kila kitu nilichorithi kutoka kwa wazazi wangu kilikuwa karibu kupotea. Baada ya baba yangu kufariki, aliacha kipande cha ardhi ambacho familia yetu ilikuwa ikikitegemea sana.

Tuliamini kila kitu kilikuwa sawa kwa sababu tulikuwa tunajua historia ya ardhi ile tangu zamani. Lakini ghafla mambo yalibadilika pale mtu mmoja alipojitokeza akidai sehemu ile ilikuwa yake.

Mwanzoni nilidhani ni misunderstanding ya kawaida. Lakini baada ya muda, jambo lile likafika hadi mahakamani. 

Nilishangaa kuona documents zikiletwa, madai tofauti tofauti yakitolewa, na watu ambao sikuwa nawafahamu wakihusika kwenye kesi ile.

Kwa kweli nilichanganyikiwa. Miaka ilianza kupita. Kila hearing ilikuwa inanipa stress kubwa. Mara kesi inaahirishwa, mara lawyer anahitaji gharama nyingine, mara napewa matumaini halafu mambo yanabadilika tena.

Wakati mwingine nilirudi nyumbani nikilia kimya nikihofia familia yangu ingepoteza kila kitu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wakianza kunizungumza vibaya.SOMA ZAIDI.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2026/2027 baada ya kujadili na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limetoa mafunzo maalumu kwa wafanyabiashara wa bidhaa za uokaji (bakary) Mkoa wa  Dar es Salaam ili kuongeza uelewa kuhusu masuala ya viwango, kuboresha usalama wa chakula na kuimarisha ushindani wa biashara zao sambamba na kulinda afya za watumiaji.

 


📌Yawasha umeme ukanda wa Nyasa kitongoji cha Nkanda

📌Yapongezwa kufikisha umeme kwenye mazingira magumu Njombe

📌Bodi ya REA yasisitiza wananchi kuchangamkia fursa uwepo wa nishati ya umeme


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijni (REA), unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa na watakaopewa zabuni ya kutekeleza miradi ili kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi.

Hayo yamebainishwa leo Mei 25, 2026 na Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), wakati wa hafla ya kukagua miradi, kutembelea na kuwasha umeme kitongoji cha Nkanda kilichopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe mradi uliokuwa unatekelezwa na Suma Jkt Electric Company Ltd. 

Mha. Ahmed Chinemba amesema kuwa, mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji vya mwambao wilayani Ludewa unatekelezwa na mkandarasi M/S SUMAJKT ELECTRIC COMPANY LTD kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2 ili wananchi wa mwambao wapate huduma ya umeme. 

"Mradi huu umelenga kuongeza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa kitongoji cha nkanda ukiwa na chachu ya kutoa fursa za kibiashara kwa kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kurahisiha upatikanaji wa huduma za kijamii na uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo kama mashine za kusaga, mashine za kuchana mbao pamoja na mashine za kuchomelea," Amesema Mha.  Chinemba.

Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Suma JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi, ameishukuru REA kwa kuwapatia kazi hiyo ya kufikisha umeme katika maeneo ya mwambao kikiwemo kitongoji hicho cha Nkanda ambapo kazi imekamilika kwa ubora. 

"Sisi Suma JKT tumefanisha kufikisha umeme kwenye mazingira magumu kama haya ambayo yalikuwa na changamoto nyingi lakini tumefanikiwa na sasa tunaona matunda yake, " Amesema Brigedia Jenerali Lupi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mha. Deogratius Nagu amesema katika kitongoji cha Nkanda takribani shilingi milioni 450 zimetolewa na Serikali kupitia REA ili kufikisha huduma ya umeme katika kitongoji hicho. 

Aidha, amewataka wananchi wa Nkanda kuchangamkia fursa ya uwepo wa umeme kwa kuhakikisha wanafanya wiring katika nyumba zao na kuunganisha umeme kwa wingi ili wanufaike na umeme huo katika kitongoji chao.

Naye, Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo hilo Bw. Stanslaus Gowele amesema ujio wa umeme maeneo ya mwambao yanakwenda kuongeza chachu ya Maendeleo kiuchumi na kijamii kwa wananchi hao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amelieleza Bunge kuwa Marekani na Uingereza zilifunga Ofisi Ndogo za Ubalozi Zanzibar kutokana na mabadiliko ya kisera katika uendeshaji wa ofisi zao ndogo duniani kote na si kwa Tanzania pekee na kwa sasa yaliyokuwa majukumu ya ofii hizo yanaendeshwa na Ofisi za Balozi zilizoko Dar es Salaam.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa lei Mei 25, 2026 akipanda mti aina ya mwembe katika eneo la Shule ya Sekondari ya Ndaoya, Mtaa wa Chongoleani jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026

....

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa amezitaka halmashauri, taasisi binafsi, mashirika mbalimbali pamoja na wananchi kuendelea kushirikiana na na Serikali katika kuhakikisha maeneo yanakuwa safi na salama.

Ametoa rai hiyo wakati akizungumza na wananchi mara baada ya kuongoza zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira jijini Tanga leo Mei 25, 2026 kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

Mhe. Kwagilwa alisema kuwa katika suala la usafi wa mazingira sekta binafsi ina nafasi kubwa ya kuwekeza katika teknolojia na mifumo bora ya usimamizi wa taka na urejelezaji ili kupunguza athari za taka kwa mazingira.

Alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha mazingira yanakuwa safi kuanzia nyumbani, maeneo ya biashara, taasisi, masoko hadi maeneo ya wazi huku akiwataka wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya mifumo ya ukusanyaji na utupaji wa taka pamoja na kuepuka vitendo vya uchafuzi wa mazingira.

“Mazingira machafu yana athari kubwa kwa afya na uchumi wa jamii. Uwepo wa taka ovyo, mifereji iliyoziba na uchafuzi wa mazingira huchangia kuenea kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu, malaria na magonjwa ya mlipuko. Hivyo, shughuli ya leo isiwe ya siku moja tu, bali iwe sehemu ya utamaduni wetu wa kila siku,” alisistiza.

Halikadhalika, Mhe. Kwagilwa alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa zitokanazo na taka ikiwemo uzoaji na urejelezaji wa taka ili kuzalisha mbolea, vyakula vya mifugo na bidhaa za viwandani.

Aliwapongeza wadau mbalimbali ambao wamebadilisha changamoto za taka kuwa fursa na kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika viwanda vya kurejeleza taka akisema kuwa hatua hiyo inachangia upatikanaji wa ajira, kuongeza kipato na kukuza uchumi kwa wananchi.

Pamoja na jitihada hizo za wadau, Naibu Waziri huyo alisema Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kupambana na uchafuzi wa mazingira kwa kuandaa na kutekeleza Mwongozo wa Usimamizi wa Taka Ngumu (Punguza, Tumia Tena na Rejeleza) wa Mwaka 2021.

Aliongeza kuwa sekta binafsi na asasi za kiraia zimeendelea kutekeleza mwongozo huo ambapo baadhi ya viwanda vinavyozalisha bidhaa zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki vimeungana pamoja katika kutekeleza Mpango wa Wajibu wa Wazalishaji wa Kusimamia Taka zinazotokana na bidhaa za wanzozalisha kwa kuondosha taka hizo kwenye Mazingira.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Dadi Kolimba Mhe. Dadi Kolimba alisema mkoa huo umeendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kufanya usafi katika maeneo yao.

Alisema kuwa wananchi wa Jiji la Tanga kila mwisho wa mwezi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hushiriki zoezi la usafi wa mazingira na kuondoa uchafu unaozalishwa katika mitaa ya jiji hilo.

Pia, Mhe. Kolimba alitumia nafasi hiyo kupongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuratibu shughuli za usafi na uhifadhi wa  mazingira kupitia zoezi la upandaji wa miti hususan kwa kila halmashauri kupanda miti milioni moja na nusu kila mwaka.

Itakumbukwa kwamba kilele cha Siku ya Mazingira kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026 na kaulimbiu ni ‘‘Dira 2050, Tuwajibike Kukijanisha Tanzania’’ ikilenga kuhamasisha jamii kushirki kikamilifu katika kuleta mageuzi na kuwajibika katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akiongoza zoezi la usafi wa mazingira lililohusisha uokotaji wa taka na kusafisha mifereji ya maji machafu katika eneo la Taifa Road ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa lei Mei 25, 2026 akipanda mti aina ya mwembe katika eneo la Shule ya Sekondari ya Ndaoya, Mtaa wa Chongoleani jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akizungumza na wananchi katika uwanja wa Tangamaano jijini Tanga mara baada ya zoezi la usafi wa mazingira lililohusisha uokotaji wa taka na kusafisha mifereji ya maji machafu katika eneo la Taifa Road ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian alipowasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa kabla ya zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAHITIMU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wametakiwa kutumia maarifa, ubunifu na teknolojia kuleta mabadiliko chanya katika jamii, huku wakihimizwa kuwa tayari kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa inayohitaji uadilifu, uwezo wa kuendana na mabadiliko pamoja na ujasiri wa kutatua matatizo halisi ya kijamii.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi, amesema taasisi hiyo imetoa mafunzo maalumu kwa wadau wanaojihusisha na uandaaji wa viazi vya kukaanga maarufu kama chipsi, kwa lengo la kuhakikisha chakula hicho kinakuwa salama kwa walaji.

 


Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amewataka Wafanyakazi wa MNMA kuendelea kufanya kazi kwa furaha, Uadilif na kuweka maslahi ya Taasisi mbele kwa kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa Wanafunzi na Watumishi kwa moyo na kufanya hivyo ni utumishi kama ilivyo utumishi wa Mungu, kwani kila kazi unayoifanya kwa ajili ya watu basi hiyo ni kazi ya Mungu.

Prof.Mapesa ameyasema hayo leo wakati wa kuwapongeza Watumishi hodari katika uwajibikaji wa utumishi wa umma kwa mwaka 2025/2026 kwa wale wote waliopata fursa ya kuwa Wafanyakazi bora, na kusisisitiza kuwa Watumishi waendelee kufanya kazi kwa kuzingatia Misingi ya utumishi wa umma na huo ndiyo uwe utamaduni wa kila siku.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaaluma Prof. Richard Kangalawe amesema Ushindi ni heshima huku akiwataka watumishi wengine kuendeela kuwajibika katika nafasi zao kwa lengo la kutimiza malengo ya Taasisi.



Naye Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Mipango, Fedha na Utawala Prof.Evaristo Haulle alisema mchakato wa kupata Mfanyakazi bora ulikuwa ni wa huru na haki ambapo vigezo mbalimbali vilizingatiwa ikiwemo Nidhamu ya mtumishi , Utendaji kazi wa mtumishi,(PEPMIS) na Mienendo mbalimbali, hivyo dosari zote zilizojitokeza zilishughulikiwa ipasavyo.

Nao viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Debora Donati wa THTU na kwa upande wa  RAAWU  Hashimu Mtongola  kwa pamoja wameipongeza Menejimenti kwa hafla hiyo fupi ambayo inatoa motisha na kuongeza morali ya kazi kwa Wafanyakazi na pia wameomba uongozi ufikirie kujumuisha Wafanyakazi wote kwa hafla ya namna hiyo wakati mwingine.



Wafanyakazi bora wa Taasisi kwa mwaka huu Filbert Nyakasi upande wa Wanataaluma  na Amedeus Mchau upande wa Waendeshaji wameshukuru uongozi kwa kutambua jitihada zao na mchango wao katika kutimiza majukumu ya kila siku na wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa Uadilifu, Nidhamu kwa  kushirikiana na Wafanyakazi wengine.


Wafanyakazi wote hodari wamentunukiwa vyeti vya kutambuliwa na zawadi ya fedha, ambapo zoezi limejumuisha Wafanyakazi wote bora wa Kampasi ya Kivukoni, Karume na Pemba.


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

ChUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

25.05.2026

 


Washiriki zaidi ya 300 wameshiriki mbio fupi za kilomita 5 katika  bonde la Olduvai Ngorongoro kwa lengo la kutangaza vivutio vya asili vya Olduvai na Laetoli ambapo historia ya Binadamu wa Kale ilianzia.

Akizungumza kwa Niaba ya Kamishna wa Uhifadhi kwenye tukio hilo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za Utalii na Masoko Mariam Kobelo ameeleza kuwa

Ngorongoro kwa kushirikiana na Cape to Cairo Marathon imefanya mbio hizo ili kuonesha utajiri wa utalii wa asili, historia, urithi wa utamaduni na  mambo kale uliopo Olduvai na Laetoli kama Nyumbani kwa asili ya Binadamu. Ameongeza kuwa Ngorongoro ni Nyumbani kwa Nyumbu wanaohama kwa kuwa pumzi ya kwanza ya ndama kupigwa mhuri kabla ya kuhamia maeneo mengine safari yao huanzia Ndutu Ngorongoro.

"Ngorongoro ni Nyumbani kwa asili ya binadamu kisayansi, Ni nyumbani kwa Nyumbu wanaohama kila mwaka, ni nyumbani kwa Spinshi ya Ndege zaidi ya 500, ni nyumbani kwa Wanyama wakubwa watano, kiufupi eneo la Ngorongoro ni Nyumbani kwa mkusanyiko wa Vitu vingi ndio maana tunawaambia wadau wote ndani na nje ya Nchi kuwa Wonders Are Calling" ameongeza Kamishna Kobelo.

 Mkurugenzi wa Cape to Cairo Arusha International Marathon, Timothy Mdinka ameeleza kuwa lengo la mbio hizo ni kutangaza mazao mapya  ya Utalii yaliyopo Tanzania na Bara la Africa kwa Ujumla kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo  Michezo kama mbio ambayo imefanyika leo Olduvai pamoja na marathon ya Cape to Cairo itakayofanyika tarehe 31 Mei, 2026.

Mbio hizo zimejumuisha wadau mbalimbali wakiwepo Ngorongoro, Cape to Cairo international Marathon, Karatu Runners,  Amani Collection, CRDB, UNDP, NHIF,  Diplomatic and Tourism Police Arusha

 


Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Isack Joseph Copriano amesimamisha uuzaji wa ardhi katika kata ya Esilale huku akita maeneo yote ya malisho kuhakikiwa upya na idara ya ardhi wilaya ya Monduli.

Yote hayo yanajiri mara baada kundi la wamama zaidi 200 kutoka majumbani kwao na kwenda kukaa eneo la Losirwa lililouzwa  kinyemela na kupaza sauti zao kuiomba  serikali kuingilia kati na ili kurejeshewa eneo lao muhimu la malisho.

Mhe.Isack amesisitiza kuwa amefanya hivyo kwasababu yeye ni mwakilishi wa wananchi nani mtu namba moja anayetetea  maslahi ya wananchi wake wa jimbo la Monduli.

“Ili kujiridhisha eneo hili ni mali ya wanakijiji kesho nendeni na wekeni Vibao vitakavyo onyesha eneo hili ni eneo  la Malisho na ogopa matapeli eneo hili haliuzwi!.

Nae Mwenyekiti wa sasa wa  kijiji hicho Bwana Yamat amesema anatambuq kuwa eneo hilo kama eneo la malisho na  kuwataka wananchi kijiji hicho kuwachukia watu waliouza eneo hilo la Malisho.

Hata hivyo wanachi hao walifikisha kero yao kwa Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Isack Joseph Copriano na  kumuomba awasaidie kurejesha eneo lililouzwa na watu wasio julikana.

Katika ziara hiyo Mbunge wa jimbo la Monduli amembatana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Monduli Mhe. Kisioki Moitiko.






 


Kumekuwa na mwitikio mkubwa wa watalii wa ndani kutembelea hifadhi ya Ngorongoro hii ikimaanisha wanarudi nyumbani eneo ambalo ndilo pekee lenye ushahidi wa kisayansi usiotiliwa shaka kuwa ndio chanzo cha binadamu wa kale.

Safari hii ni zamu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT ) chini ya Mchungaji Kiongozi wa Kanisa  hilo Usharika wa Kijitonyama jijini Dar es Salaam Rev, Dr. Elliona Kimaro aliyeongoza kundi la wanaume 300 kutoka mikoa mbalimbali nchini kutembea Makumbusho ya Jiopaki ya Ngorongoro-Lengai (Urithi Geopark) na vituo vya hifadhi vilivyopo Ngorongoro 

Akiwa na Ujumbe huo Dkt.  Kimaro amesema makundi mbalimbali kuhamasika kufanya utalii wa Ndani wanavutiwa na vitu mbalimbali ikiwemo kushuhudia uumbaji wa Mungu, kuona na kujifunza Chanzo cha asili ya Mwanadamu katika bonde la Olduvai na Laetoli, kuona Ikolojia ya hifadhi pamoja na utunzaji wa Mazingira kama vitabu vitakatifu vinavyohimiza.

"Tumekuja Nyumbani Ngorongoro kwenye asili ya Mwanadamu tukiwa na kundi la wanaume 300,  tumeshuhudia uumbaji wa Mungu, utunzaji wa Ikolojia, Mazingira, Misitu Wanyama wa kila aina ya vyote vilivyoumbwa kwa mfano wa Mungu" alisema  Dkt. Kimaro.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inawarudisha nyumbani binadamu wote ili kushuhudia asili yao ambapo binadamu alianza kutembea na kufanya shughuli zake kwa miguu miwili.






 

 Dar es Salaam

Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Jubilei ya Dhahabu ya miaka 50 ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), mwaka huu wadau wa biashara, wawekezaji, wabunifu na wananchi wanatarajiwa kushuhudia tukio la kipekee la kihistoria litakalojulikana kama “Sabasaba Golden Night”, Usiku wa Tuzo utakaofanyika tarehe 6 Julai 2026, usiku huu maalum wa dhahabu unalenga kusherehekea mafanikio, ubunifu na mchango wa maonesho hayo katika kukuza biashara na uchumi wa Tanzania kwa zaidi ya nusu karne.

Aidha,Uzinduzi wa Sabasaba Golden Night umebeba taswira mpya ya Maonesho ya Sabasaba ya mwaka 2026, ukiahidi burudani ya kiwango cha juu, mwangaza wa kipekee, maonesho ya kisasa, kutambua wadau waliotoa mchango mkubwa katika safari ya miaka 50 pamoja na kuunganisha sekta za biashara, uwekezaji na ubunifu chini ya jukwaa moja. Tukio hilo linatarajiwa kuwa moja ya vivutio vikubwa ndani ya Maonesho ya 50 ya Jubilei ya Dhahabu, yakiyotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 28 Juni hadi 13 Julai, 2026.

Akizungumza Mgeni Rasmi Mhe. Dennis Londo amesema Tuzo hizo zitakazotolewa Mwaka huu zinalenga kuonesha ni kwa namna gani Sekta ya Biashara imekua kupitia maonesho ya Biashara ya Sabasaba na namna ambavyo Maonesho haya yamekuza maelfu ya wafanyabiashara amba sasa ni wakubwa.

Aidha Dkt.Latifa Mohammed Khamis Mkurugenzi Mkuu wa Maendeleo ya Biashara Tanzania ameeleza kuwa “Usiku wa Dhahabu” si burudani pekee, bali ni ishara ya heshima kwa safari ya mafanikio ya Sabasaba tangu kuanzishwa kwake, sambamba na kufungua ukurasa mpya wa fursa za biashara, teknolojia na ushirikiano wa kimataifa. Wageni watakaohudhuria watapata nafasi ya kushuhudia historia ikikutana na ubunifu wa kizazi cha sasa katika mazingira yatakayobeba hadhi ya Jubilei ya Dhahabu. “Sabasaba 2026 KUBWA KULIKO