Serikali kupitia Wizara ya Fedha imetangaza vipaumbele vinane (8) vya kimkakati kwa mwaka wa fedha 2026/27, vyenye lengo la kukuza uchumi, kuimarisha nidhamu ya matumizi ya rasilimali za umma, na kulipa madeni.
Vipaumbele hivyo vimewasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akisoma mapendekezo ya mpango na bajeti ya wizara hiyo.Sera na mikakati hiyo mikuu imegawanyika katika maeneo yafuatayo:
1. Ukuaji wa Uchumi na Kudhibiti Mfumuko wa BeiWizara imepanga kusimamia uchumi jumla ili ufikie ukuaji wa asilimia 6.3 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2026. Aidha, jitihada zitawekwa ili kudhibiti mfumuko wa bei ubaki kwenye viwango vya tarakimu moja (wastani wa asilimia 3.0 hadi 5.0), huku akiba ya fedha za kigeni ikitunzwa kukidhi uagizaji wa bidhaa na huduma kwa angalau miezi minne (4).
2. Nidhamu ya Matumizi na Ukusanyaji MapatoIli kuhakikisha thamani halisi ya fedha za umma inaonekana, serikali itaimarisha nidhamu ya bajeti (fiscal discipline). Hatua hii itahusisha usimamizi madhubuti wa ununuzi wa umma na kupunguza tabia ya kuhamisha fedha kutoka fungu moja kwenda jingine (reallocation between votes).
3. Kuvunja Rekodi ya Mapato (Tsh Bilioni 55,200.75)Katika bajeti kuu ya serikali ya jumla ya shilingi bilioni 62,334.19, Wizara ya Fedha inalenga kuboresha mifumo ya kodi, misaada, na mikopo ili kuchangia shilingi bilioni 55,200.75 kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina. Hii ni sawa na asilimia 88.6 ya bajeti yote.
4. Kulipa Madeni na Kuaminika KimataifaSerikali imetenga shilingi bilioni 15,102.80 kwa ajili ya kulipa kwa wakati riba na mitaji ya madeni yanayotarajiwa kuiva. Hatua hii inalenga kulinda mikataba na kuendelea kujenga imani kwa wawekezaji katika masoko ya fedha ya kikanda na kimataifa.
5. Mabilioni ya Kulipa Watumishi na WakandarasiHabari njema kwa wadau wa ndani ni kwamba serikali itakuwa ikitoa shilingi bilioni 100.00 kila mwezi. Fedha hizi zitasaidia kulipa madeni ya watumishi wa umma, wakandarasi, wazabuni, na watoa huduma mbalimbali ili kuchochea mzunguko wa fedha.
6. Usawa wa Mgawanyo wa Fedha kwa HalmashauriKutakuwa na maboresho makubwa kwenye ugawaji wa rasilimali fedha kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa (Halmashauri). Mgawanyo huo utazingatia tafiti za kitaalamu ili kuondoa urudufu wa majukumu na kuleta uwiano wa kimaendeleo nchini.
7. Mageuzi ya Mfumo wa Bajeti (PBB)Serikali itafanya tathmini ya kina ya usimamizi wa bajeti kwa kutumia Mfumo wa Programu (Programme Based Budgeting – PBB). Lengo ni kuwezesha maamuzi sahihi ya kimabadiliko katika upangaji wa bajeti unaoleta matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi.
8. Matumizi ya Akili Unde (AI) na Utawala BoraKatika kwenda na wakati, wizara itajenga uwezo wa watumishi wake kuhusu masuala ya Mazingira, Jamii na Utawala Bora (ESG). Kubwa zaidi, serikali itaanza kuingiza matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) katika usimamizi wa fedha za umma na uchumi ili kuongeza ufanisi na uwazi.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, leo tarehe 2 Juni, 2026 amekutana na Balozi wa Australia nchini Tanzania anayemaliza muda wake wa uwakilishi, Mhe. Jenny Da Rin, kwa mazungumzo ya kumuaga yaliyofanyika jijini Dodoma.
Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kiruswa amempongeza Mhe. Jenny Da Rin kwa kumaliza muda wake wa uwakilishi nchini kwa mafanikio makubwa, huku akitambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Australia, hususan katika maendeleo ya Sekta ya Madini.
Amesema Tanzania na Australia zimeendelea kushirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo imekuwa na matokeo chanya katika kukuza sekta ya madini na kuchangia maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa Serikali ya Tanzania imeendelea kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya rasilimali madini kwa kuwashirikisha kikamilifu katika shughuli za madini, huku ikitambua mchango wa wawekezaji wa kimataifa, wakiwemo kutoka Australia, katika maendeleo ya sekta hiyo.
Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano na Australia katika maeneo ya utafiti wa madini, uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na maendeleo ya rasilimali watu ili kuongeza uzalishaji na kuifanya sekta ya madini kuwa na tija zaidi kwa Taifa.
“Sekta ya madini inaendelea kukua kwa kasi na inahitaji uwekezaji wa kutosha katika teknolojia, ujuzi na tafiti ili kuongeza uzalishaji na manufaa ya kiuchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla,” amesema Dkt. Kiruswa.

Kwa upande wake, Mhe. Jenny Da Rin ameishukuru Serikali ya Tanzania na Wizara ya Madini kwa ushirikiano mkubwa alioupata katika kipindi chote cha utumishi wake nchini.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa Watanzania kutumia kikamilifu fursa za elimu, mafunzo na semina zinazotolewa na Australia, akibainisha kuwa maarifa na ujuzi unaopatikana kupitia programu hizo unachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sekta mbalimbali, ikiwemo Sekta ya Madini.
Mhe. Jenny Da Rin ameongeza kuwa moja ya malengo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Australia ni kuhamasisha wawekezaji na wafanyabiashara wa Australia kuja kuwekeza nchini Tanzania pamoja na kuendeleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa pande zote mbili.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutatua changamoto zinazoweza kuathiri mazingira ya uwekezaji ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kukuza maendeleo ya nchi hizo mbili.



WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema vijana wanapaswa kutumia fursa zinazotolewa na Serikali kwa kukuza ubunifu, kuongeza bidii katika kazi, kutumia teknolojia na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi hususan zilizo rafiki kwa Mazingira.
Mhe. Masauni amesema hayo katika Kongamano la Vijana lililofanyika jijini Dar es Salaam, Juni 2, 2026 ambalo ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambapo kilele chake kitaifa yanafanyika Juni 5, 2026 mkoani Dodoma.
Amesema, kongamano hilo ni jukwaa muhimu linalowaunganisha vijana na maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kwa kuwapa nafasi ya kushiriki katika mijadala, kujifunza kutoka kwa wataalam, kubadilishana uzoefu na kuibua suluhisho bunifu zinazoweza kutekelezwa kwa vitendo katika jamii zao.
“Ninyi ndio nguvu kazi ya Taifa na nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, vijana ni zaidi ya asilimia 64 ya nguvu kazi ya Taifa. Hii ina maana kuwa mchango wenu ni muhimu sana katika kulinda mazingira, kukuza uchumi wa kijani na kuhakikisha maendeleo endelevu ya Taifa letu.”
Aidha ameongeza kuwa ni vyema vijana wakatambua changamoto za kimazingira pia zinaweza kuwa fursa kubwa za kiuchumi, takwimu za kimataifa zinaonesha kuwa mpito kuelekea uchumi wa kijani unaweza kuzalisha ajira milioni 8.4 kwa vijana duniani ifikapo mwaka 2030.
Aidha, amesema uchumi endelevu duniani unakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola trilioni 12 na uwezo wa kuzalisha zaidi ya ajira milioni 380 duniani kote.
“Hii inaonesha dhamira ya pamoja ya Taifa katika kulinda mazingira na kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho”.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi, amesema kuwajengea uwezo vijana kupitia programu za kujitolea ni mkakati muhimu wa kuandaa kizazi kitakachosimamia agenda za maendeleo endelevu, uhifadhi wa mazingira na uchumi wa kijani.
Amesema programu za kujitolea zinawawezesha vijana kupata uzoefu wa kazi unaohitajika katika soko la ajira, huku zikizisaidia taasisi kupata kundi la vijana wenye maarifa, ubunifu na uwezo wa kutumia teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo.
“Afrika ina hazina kubwa ya rasilimali watu, ambapo takribani asilimia 40 ya vijana wa dunia wanaishi katika bara hilo, jambo linalotoa fursa kubwa ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kiteknolojia endapo vijana hao watapatiwa elimu, ujuzi na nafasi za kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.” Amesema Dkt. Muyungi.
Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Suzan Mkangwa (kulia), Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda na Mkurugenzi wa CMA, Usekelege Mpulla wakifuatilia agenda mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi leo Juni 2, 2026 ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaofanyika Jijini Geneva, Uswisi.
Na: OWM (KAM)
Tanzania imeshiriki kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi kinachoendelea jijini Geneva, Uswisi, ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Katika kikao hicho kilichifanyika leo Juni 2, 2026 wajumbe wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa viwango vya kazi, ikiwemo mjadala wa jumla kuhusu ripoti kuu ya Kamati ya Mkutano na maadhimisho ya miaka 100 ya ajenda ya Kazi zenye Staha, Tathmini ya Jumla, pamoja na wajibu wa nchi wanachama katika kuwasilisha taarifa na kutekeleza majukumu mengine yanayohusiana na viwango vya kazi.
Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho ulijumuisha Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Kazini, Suzan Mkangwa, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), Khadija Mwenda, pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Usekelege Mpulla.
Tanzania, ambayo ni mwanachama wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) na mjumbe wa Bodi ya Magavana inayowakilisha nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki, inaendelea kushiriki Mkutano Mkuu wa 114 wa shirika hilo unaowakutanisha wawakilishi wa Serikali, Waajiri na Wafanyakazi kutoka nchi wanachama 187.

Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Suzan Mkangwa (kulia), Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda na Mkurugenzi wa CMA, Usekelege Mpulla wakifuatilia agenda mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi leo Juni 2, 2026 ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaofanyika Jijini Geneva, Uswisi.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina akifuatilia agenda mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi leo Juni 2, 2026 ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaofanyika Jijini Geneva, Uswisi.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetangaza kuwa jumla ya walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Nne la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Awali na Msingi pamoja na Shindano la Pili la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Sekondari Tanzania Bara,ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuendelea kuimarisha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 2, 2026, jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, amesema kuwa hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo itafanyika Juni 6, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Amesema mashindano hayo yanatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao wa kitaaluma, ubunifu na matumizi ya mbinu bora za ufundishaji darasani, huku yakitumika pia kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA).
"Kati ya walimu 3,153 waliosajiliwa kupitia Mfumo wa National Teaching Skills Competition System (TSCS), walimu 1,263 walitimiza masharti yote ya ushiriki kwa kuwasilisha video za ufundishaji pamoja na maandalio ya masomo kwa ajili ya tathmini."amesema Mhe.Ameir
Amesema mchakato wa tathmini umekamilika na tayari orodha teule ya walimu watano bora imepatikana katika kila eneo la ushindani, huku mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa zawadi akitarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.
Mhe. Ameir ameeleza kuwa mshindi wa kwanza katika kila kundi atazawadiwa Shilingi milioni 2.5, cheti cha pongezi, cheti cha ushindi pamoja na kompyuta mpakato. Aidha, shule anayofundisha mshindi huyo itapatiwa projekta kwa ajili ya kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.
Katika hatua nyingine, amesema shule zitakazotoa washindi wa kwanza katika maeneo ya Kusoma kwa Darasa la Awali, Kiingereza kwa Darasa la Kwanza na Ufaraguzi wa Zana kwa Darasa la Pili zitapatiwa vibao vya kielektroniki 100 vyenye thamani ya Shilingi milioni tano.
Serikali inaendelea kutumia mashindano hayo kama nyenzo ya kuhamasisha ubunifu, kuongeza ari ya utendaji kwa walimu na kuibua mbinu bora za ufundishaji zitakazochangia kuinua viwango vya elimu nchini.
Kaulimbiu ya shindano la mwaka huu ni “UFUNDISHAJI BORA, TAIFA IMARA.

Mimi pia nilitamani furaha hiyo, lakini kila uhusiano niliouanzisha uliishia njiani. Kwa kweli iliniumiza sana.
Wakati mwingine nilicheka mbele za watu, lakini moyoni nilikuwa na huzuni kubwa. Kilichoniumiza zaidi ni kuona matumaini yangu yakipungua mwaka baada ya mwaka.
Nilijaribu mahusiano mbalimbali, lakini hayakudumu. Baadhi yaliishia kwenye kuvunjika moyo, mengine yalikufa kabla hata hayajafika mbali.
Kwa miaka kadhaa alikuwa akirudi nyumbani na matokeo ambayo hayakuwa mazuri. Walimu walikuwa wakisema hakuwa makini darasani, wengine wakisema hakupenda kusoma. Kadri muda ulivyopita, watoto wengine walikuwa wakimpita huku yeye akibaki nyuma.
Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kusikia baadhi ya watu wakimuita mzembe. Mimi nilijua alikuwa mtoto mwenye akili, lakini nilikuwa nashindwa kuelewa kwa nini hakufanya vizuri kama wengine.
Matokeo yalipozidi kushuka, hali ikawa ngumu zaidi. Mtoto wangu alianza kupoteza confidence. Wakati mwingine alikuwa anakataa hata kuonyesha report form yake. Nilimuona akianza kuamini maneno mabaya aliyokuwa akiyasikia kutoka kwa watu.
Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda vizuri, lakini baada ya muda hali ilianza kubadilika. Wateja walipungua.
Kwa kweli nilianza kuchoka. Kilichoniumiza zaidi ni kuona madeni yakiongezeka huku mapato yakipungua.
Lakini siku moja kila kitu kilibadilika. Kulitokea tukio la wizi katika eneo letu, na ghafla jina langu likaanza kutajwa.
Kwa kweli nilivunjika moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu ambao walikuwa wakinisalimia kila siku wakianza kuniepuka.
Nilijaribu kueleza ukweli. Lakini ilionekana kama hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza. Watu walikuwa tayari wameunda maoni yao kuhusu mimi. Hata baadhi ya ndugu zangu walionekana kuwa na mashaka.
Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini jambo lile lilikuwa limenitokea. Nilihofia kupoteza kabisa heshima niliyokuwa nimeijenga kwa miaka mingi. Kulikuwa na wakati nilitaka kuondoka kijijini.
Tulidhani labda alikuwa amesafiri au alikuwa na matatizo aliyohitaji kuyatatua peke yake. Lakini siku zikageuka wiki. Wiki zikageuka miezi. Na miezi ikageuka miaka. Kwa kweli ilikuwa kipindi kigumu sana kwa familia yetu.
Mama yangu alikuwa akikesha akiomba na kutamani kusikia sauti yake tena. Kila simu iliyopigwa kutoka namba ngeni ilitupa matumaini kwamba huenda alikuwa amepatikana. Lakini mara nyingi tulibaki na maswali kuliko majibu.
Tulijaribu kutafuta taarifa kupitia marafiki zake, watu aliokuwa akifanya nao kazi, na hata ndugu wa mbali. Wakati mwingine tulipata taarifa zilizotupa matumaini, lakini zilikuja kuonekana si za kweli.
Kadri miaka ilivyopita, maumivu hayakuondoka.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za Dini nchini kuimarisha maadili kwa jamii na kukuza maemdeleo.
Mhe. Sangu amesema hayo alipomwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika hafla ya kumsimika uaskofu mchungaji Daniely Liyaseke wa Kanisa la The Charismatic Episcopal Church of Tanzania, Dayosisi mpya ya Ukanda wa Tanzanite One, iliyofanyika Mei 31, 2026 Kijiji cha Terat, Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Sangu amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa makanisa katika kuimarisha maadili, mshikamano wa kijamii na maendeleo ya Taifa na itaendeleza ushirikiano huo. Ameongeza kuwa kauli mbiu ya kanisa hilo “Kwa neema ya Mungu, tunajenga Huduma kwa vizazi vya sasa na vijavyo” inaakisi dhamira ya kuwekeza kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Vile vile, Mhe. Sangu alisisitiza mambo matatu muhimu kwa Taasisi za dini ziendelee kuombea amani, mshikamano na afya njema kwa viongozi wakuu wa nchi akiwemo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kadhalika, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na tasasisi za dini katika malezi ya vijana ili kujenga Taifa lenye maadili, upendo na uwajibikaji, pia kuendeleza ushirikiano katika utoaji wa elimu na huduma za kijamii kwa kizazi chenye uzalendo na uwajibikaji.
Aidha, Mhe. Sangu aliongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa, Ofisi na ununuzi wa gari, ambapo katika harambee hiyo Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amechangia Shilingi Milioni 15 na Waziri Sangu amechangia Shilingi Milioni 5.
Naye, Askofu Daniely Liyaseke aliwashukuru viongozi wa Serikali, viongozi wa dini na waumini kwa mshikamano na ushirikiano, akisisitiza kuwa “ukiona kobe yupo juu ya mti, ujue kuna aliyempandisha.”
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. James Millya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mhe. Fakih Lulandala, walipongeza uongozi wa Askofu Liyaseke na kusisitiza kuwa uwepo wa Dayosisi hiyo ni nguzo ya mshikamano wa kijamii na maendeleo ya kiroho.

MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum leo Juni 1,2026 bungeni jijini Dodoma.

MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum leo Juni 1,2026 bungeni jijini Dodoma.
......
MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameitaka Serikali kuboresha mazingira ya kazi kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini ikiwemo kuwapatia magari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bungeni, Dkt. Jafo amesema maafisa hao ni nguzo muhimu katika kusukuma maendeleo ya jamii na wanastahili kuwezeshwa kwa vitendea kazi vinavyokidhi mahitaji ya kazi zao.
Amesema Maafisa Maendeleo ya Jamii ni mawakala wa mabadiliko katika jamii kwa kuwa karibu kila programu ya maendeleo inayotekelezwa nchini inahitaji ushiriki wao wa moja kwa moja, hivyo ni muhimu kupewa heshima na mazingira bora ya kufanyia kazi.
Dkt. Jafo ameeleza kuwa pamoja na magari, maafisa hao wanapaswa kuwa na ofisi zenye hadhi na rasilimali za kutosha zitakazowawezesha kuwafikia wananchi kwa urahisi na kutoa huduma stahiki.
Aidha, ameishauri Serikali kuanzisha vitengo vya Maendeleo ya Jamii katika wizara zote na taasisi za umma zaidi ya 325 ili kuhakikisha masuala ya maendeleo ya jamii yanapewa kipaumbele na kuratibiwa kwa ufanisi katika sekta mbalimbali.
Pia amependekeza kuanzishwa kwa Kitengo cha Uratibu wa Sekta ndani ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii kitakachosaidia kuunganisha taarifa za maendeleo kutoka wizara na taasisi mbalimbali, hatua ambayo alisema itaiwezesha nchi kuwa na mfumo imara wa kufuatilia maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 246,197 wakiwemo wasichana 114,102 na wavulana 132,095 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2026 wanatakiwa kuripoti shuleni kuanzia Julai 04, 2026 hadi Julai 31, 2026 kwakuwa muhula wa kwanza wa masomo utaanza Julai 06, 2026.
Prof. Shemdoe amesema hayo leo Juni 01, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo ya Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Magogoni Jijini Dar es Salaam, wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi kwa mwaka 2026.
“Wanafunzi 172,114 sawa na asilimia 69.9 wakiwemo wasichana 85,987 na wavulana 86,127 wenye sifa wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule za sekondari za Serikali 856 zikiwemo shule za bweni 825, kutwa 25 na kutwa na bweni sita (06),” amefafanua Prof. Shemdoe.
Aidha, Prof. Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 74,083 sawa na asilimia 30.1 wakiwemo wasichana 28,115 na wavulana 45,968 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.
“Wanafunzi 3,144 wakiwemo wasichana 1,170 na wavulana 1,974 wamechaguliwa kujiunga na fani mbalimbali katika vyuo 04 vya elimu ya ufundi, vyuo hivyo ni Chuo cha Ufundi cha Arusha (ATC), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) na Chuo cha Maendeleo ya Maji (WMDI),” ameeleza Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe amesisitiza kwamba, uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi umefanyika kwa kuzingatia ufaulu na nafasi zilizopo katika shule; hivyo, hakutakuwa na fursa ya kufanya mabadiliko yoyote ya Shule kutokana na ukosefu wa nafasi.
Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi zilizotumika kujenga miundombinu bora ya shule za kidato cha tano na vyuo vya kati ambayo itatumika kuwahudumia wanafunzi 246,197 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi mwaka 2026.
Na Oscar Assenga,TANGA
Fedha hizo zilikabidhiwa kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, katika hatua inayodhihirisha dhamira ya chama ya kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa viongozi wake wa ngazi za wilaya.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Rajab alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kwamba utakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa watumishi pamoja na shughuli za chama katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Alieleza kuwa mradi huo una thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5, huku fedha zote zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wake zikiwa tayari zimepatikana kupitia michango ya wanachama, viongozi na wadau mbalimbali wa chama.
"Mradi huu unagharimu jumla ya shilingi bilioni 2, milioni 500 na laki 250. Fedha hizi zimepatikana kupitia michango mbalimbali ikiwemo milioni 56 zilizotolewa awali, milioni 10 kutoka kwa MNEC pamoja na michango iliyokusanywa kutoka wilaya zote za mkoa," alisema Rajab.

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kutatua changamoto za makazi kwa baadhi ya viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya, jambo litakaloongeza utulivu wa kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Alisema nyumba hizo si tu kwamba zitakuwa makazi ya viongozi, bali pia ni uwekezaji wa muda mrefu wa chama katika kujenga taasisi imara yenye uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kuwahudumia wanachama wake.

"Tunajenga misingi ya chama kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Viongozi wanaweza kubadilika, lakini miundombinu tunayojenga leo itaendelea kulitumikia chama kwa miaka mingi ijayo," alisisitiza.
Rajab aliongeza kuwa ujenzi wa chama ni jukumu endelevu linalohitaji mshikamano wa wanachama wote, akisisitiza kuwa maendeleo ya chama hayawezi kupatikana bila ushiriki wa pamoja wa wanachama wake.

Kutokana na hilo, aliwataka wana-CCM wa Mkoa wa Tanga kuendelea kuchangia kwa hali na mali, kutumia elimu na uzoefu wao pamoja na nguvu kazi katika kukiimarisha chama.
Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, alisema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa chama wa kuimarisha utendaji wake katika ngazi za wilaya kwa kuhakikisha viongozi wanapata mazingira bora ya kazi na makazi.
Alifafanua kuwa kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo zitatumika na viongozi muhimu wa chama na jumuiya zake.

"Kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo ni nyumba ya Katibu wa CCM wa Wilaya, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Vijana, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na nyumba ya Katibu wa UWT," alisema Kizigo.

Alieleza kuwa uwepo wa nyumba hizo utasaidia kupunguza gharama za upangaji wa makazi, kuimarisha upatikanaji wa viongozi katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za chama na jumuiya zake.
Kwa mujibu wa Kizigo, kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuijengea CCM Mkoa wa Tanga miundombinu imara itakayosaidia kuendeleza shughuli zake za kisiasa, kiutawala na kijamii kwa ufanisi zaidi katika miaka ijayo.
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Benezeth Lutege, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness K. Meena. Warsha hiyo imefanyika leo Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha.

Mkurugenzi Msaidizi wa Epidemiolojia na Magonjwa ya Mifugo Yanayovuka Mipaka (TADs) akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Habari II wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Chiku Makwai, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Sheria I wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Denis Ukaka, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Na Chiku Makwai – ARUSHA
Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo.
Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika.
Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapema kabla hayajasababisha athari kubwa kwa uzalishaji, biashara ya mifugo na afya ya jamii.
“Mkakati huu utaweka msingi wa kuwa na mfumo mmoja wa kitaifa wa mawasiliano ya dharura utakaoongoza utoaji wa taarifa, ushirikishwaji wa wadau na usimamizi wa mawasiliano wakati wa matukio ya milipuko ya magonjwa ya mifugo,” amesema Dkt. Lutege.
Aidha, amebainisha kuwa magonjwa mbalimbali ya mifugo, ikiwemo Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever), yanahitaji uratibu madhubuti wa mawasiliano ili kuhakikisha wananchi na wadau wanapata taarifa sahihi zitakazowawezesha kuchukua hatua stahiki kwa wakati.
Warsha hiyo imewakutanisha wataalamu wa mifugo, afya ya wanyama, mawasiliano na wadau wengine kutoka taasisi za Serikali pamoja na mashirika ya kimataifa kwa lengo la kujadili mbinu bora za mawasiliano ya hatari, usimamizi wa taarifa za dharura na mikakati ya kuimarisha mwitikio wakati wa milipuko ya magonjwa.
Washiriki pia wanatarajiwa kujadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa taarifa pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya afya ya wanyama na afya ya binadamu kwa kuzingatia dhana ya Afya Moja (One Health).
Kupitia warsha hiyo, Tanzania inatarajia kuwa na mkakati madhubuti wa mawasiliano ya dharura utakaosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema, kuongeza mwitikio wa haraka wakati wa matukio ya dharura na kulinda ustawi wa mifugo sambamba na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.



