Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Halmashauri ya Mji Handeni imejipanga kutekeleza shughuli mbalimbali ikiwamo uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya maadhimisho hayo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema halmashauri hiyo inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Amesema Machi 5, 2026 kutafanyika kongamano la wanawake litakaloenda sambamba na uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi la Halmashauri ya Mji Handeni, linalolenga kuwaunganisha wanawake ili kubadilishana uzoefu, kupata taarifa za fursa za kiuchumi na kuimarisha shughuli zao za ujasiriamali.

Ukwaju amesema kongamano hilo pia litaambatana na maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wanawake wajasiriamali, hatua inayolenga kuonesha ubunifu wao pamoja na juhudi wanazofanya katika kujikwamua kiuchumi.

Ameongeza kuwa katika kongamano hilo litakalofanyika katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Handeni, washiriki watapatiwa elimu mbalimbali ikiwemo masuala ya umiliki wa ardhi na mirathi, malezi na makuzi ya watoto, ujasiriamali na biashara, elimu ya ushirika na SACCOS pamoja na kilimo bora na ufugaji wa kisasa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, Machi 6, 2026 halmashauri itatoa msaada kwa baadhi ya kaya zinazoishi katika mazingira hatarishi ikiwa ni sehemu ya kuonesha mshikamano na kusaidia jamii zenye uhitaji.

Kadhalika amesema kilele cha maadhimisho hayo kwa ngazi ya Halmashauri kitafanyika Machi 7, 2026 katika viwanja vya Shule ya Msingi Kwenjugo, ambapo kutafanyika ugawaji wa taulo za kike kwa wanafunzi wa kike pamoja na utoaji wa vyeti kwa vikundi vinne vya wanawake vilivyotekeleza miradi yao kwa mafanikio na kurejesha mikopo ya asilimia 10 kwa wakati. Amesema mgeni rasmi katika shughuli hizo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese.

Ukwaju amesema maadhimisho hayo yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050,” huku halmashauri ikiendelea kuhamasisha wananchi wote kushiriki kikamilifu katika kuimarisha usawa wa kijinsia na kuchochea maendeleo jumuishi kwa wanawake na wasichana.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameutaka uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mzenga, kilichopo Kata ya Mzenga, Wilaya ya Kisarawe, kuhakikisha kinatoa mafunzo katika fani zinazoendana na shughuli za kiuchumi za eneo hilo.

Mhe. Wanu ametoa agizo hilo Machi 03, 2026, wilayani Kisarawe wakati wa ziara ya ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na Wizara katika wilaya hiyo.

Amewataka viongozi wa wilaya na wananchi wa eneo hilo kuona umuhimu wa mafunzo ya ujuzi na hivyo kuhamasisha vijana kujiunga na chuo hicho ili kupata ujuzi utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.

Amesema chuo hicho, pamoja na vyuo vingine vya maendeleo ya wananchi, vinapaswa kuzingatia mahitaji halisi ya kiujuzi ili vijana waweze kujiunga kwa wingi.

“Mmesema hapa mnazalisha zao la korosho, ufuta na mihogo; kwa nini sasa msianzishe kozi ya kusindika mazao hayo? Hii itawamasisha vijana kujiunga na chuo kwa kuwa wanasoma kile wanachofanyia kazi,” amesema Mhe. Wanu.

Aidha, ameutaka uongozi wa chuo hicho kusimamia ipasavyo mifumo ya usimamizi wa watumishi ili kuimarisha uwajibikaji.

Akiwa wilayani humo, Mhe. Wanu pia amekagua ujenzi wa VETA Kisarawe na kusema kuwa Serikali inaendelea kujipanga kupata rasilimali fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa chuo hicho ili malengo ya kutoa ujuzi kwa wananchi yafikiwe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mhe. Petro Magoti, amemuhakikishia Naibu Waziri Wanu ushirikiano katika kusimamia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa, ikiwemo kuhakikisha huduma za umeme na maji zinafika katika eneo la chuo ili kurahisisha hatua inayofuata ya ujenzi.



Na OWM - TAMISEMI, GEITA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameelekeza Maafisa Lishe na Maendeleo ya Jamii wanaosimamia utekelezaji wa Mradi Jumuishi wa Lishe katika Mkoa wa Geita, Tabora na Iringa kupatiwa vyombo vya usafiri ili waweze kwenda kutoa huduma kwenye maeneo yanayokabiliwa na matatizo ya lishe kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Prof. Shemdoe ametoa maelelezo hayo leo Machi 03, 2026, wakati akizindua Mradi Jumuishi wa Lishe katika Mkoa wa Geita, ambao utawawezesha watoto wa  mkoa wa Geita kukua vizuri kimwili na kiakili, na kuwa na nguvu na afya bora. 

“Katibu Mkuu na wataalam mnaosimamia mradi huu, hakikisheni kupitia bajeti za mradi mnawapatia Maafisa Lishe na Maendeleo ya Jamii vyombo vya usafiri katika halmashauri zote zinazotekeleza mradi huu ili waweze kutoka sehemu moja kwenda nyingine kuwahudumia watoto,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amesema, kipekee anashukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake ambazo zimewezesha kupatikana kwa mradi huo jumuishi wa lishe, “Mwaka 2022 akiwa Jijini Washington, nchini Marekani akihudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, alikutana na kukubaliana na Mama Jamie Cooper, Rais wa Taasisi ya Big Win Philanthropy kuanzisha ushirikiano uliowezesha kupatikana kwa mradi huu”.

Mkuu wa Mkoa Geita Mhe. Martine Shigela amemshukuru Mhe. Rais kwa kuelekeza na kuhakikisha kwamba kila kijiji kuna kuwa na siku ya afya na lishe na amemhakikishia Prof. Shemdoe kuwa mkoa wake utaendelea kutekeleza kampeni hiyo ya siku ya afya na lishe ili kupunguza changamoto ya utapia mlo.

Naye, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI anayeshughulikia afya, Prof. Tumaini Nagu, amesema Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI ina imani kubwa kuwa, ushirikiano thabiti wa Wakuu wa Mikoa na Wilaya wa mikoa ya Geita, Tabora na Iringa utawezesha kufikia malengo ya mradi jumuishi wa lishe ambao umezinduliwa na Prof. Shemdoe.

Pia, Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Bw.  Mohammed Gombati amesema kuwa, kama lililivyo jina la mradi jumuishi, wamekusanyika watumishi kutoka idara zote ili kwa pamoja waweze kujipanga katika kutekeleza mradi huo jumuishi wa lishe.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Bw. Luitfrid Nnally amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara katika suala la lishe kwa kuleta mkataba wa lishe tangu akiwa Makamu wa Rais, kitendo ambacho kimepelekea Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutoa kipaumbele katika suala la lishe.

Taasisi ya Big Win Philanthropy ya Nchini Uingereza inafadhili Mradi huo Jumuishi wa Lishe, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kukabiliana na matatizo ya lishe kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Prof.Riziki Shemdoe, amewaelekeza Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri kuanza maandalizi ya mapema kwa ajili ya kupokea makundi rika mawili (double cohort) ya wanafunzi wa Darasa la Sita na la Saba watakaohitimu masomo yao mwaka 2027 na kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2028 kwa pamoja.

Prof. Shemdoe ameyasema hayo  Machi 2, 2026 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 12 wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri Tanzania Bara unaofanyika katika Ukumbi wa Lush Garden Hotel, jijini Arusha.

“Tuanze maandalizi ya mapokezi ya Darasa la Sita na  la Saba ambao wataingia Kidato cha Kwanza kwa pamoja  Januari 2028,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Ameeleza kuwa Maafisa Elimu wanazo takwimu sahihi za wanafunzi hao, hivyo wanapaswa kuziandaa kwa umakini na kuziwasilisha Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuwezesha maandalizi maalumu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa, upatikanaji wa madawati na ajira ya walimu wa kutosha.

Aidha, amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kwa kushirikiana na madiwani, wazazi na walezi kuendelea kuhakikisha wanafunzi wa elimu ya awali, msingi na sekondari wanapata chakula shuleni ili kuboresha mahudhurio na ufaulu wao.

Na Emmanuel Mbatilo, Dar es Salaam

Tume ya Ushindani (FCC) imetangaza kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Haki ya Mlaji Duniani kwa kuendesha kampeni maalum ya utoaji elimu kwa walaji na wafanyabiashara ili kuongeza uelewa wa haki na wajibu wao katika soko.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu wa Ofısi hiyo Bi, Leila Mavika akitoa hotuba ya Mgeni Rasmi katika kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofısi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Mwanaamani Mtoo akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa utayari wake katika utekelezaji wa majukumu yaliyokasimiwa katika kuimarisha afya na ustawi wa Taifa wakati wa kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera Afisa Ustawi wa jamii Mwandamizi Bi. Juliana Ntukey akiwasilisha mada kuhusu Mwongozo na Waraka wa kudhibiti VVU, UKIMWI na MSY 2014 wakati wa kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti magonjwa hayo ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera. Washiriki wa Kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu Ofısi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi, Leila Mavika akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya kitaifa ya kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza baada ya Mgeni Rasmi kufungua kikao cha Afua kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera Washiriki wa Kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu Ofısi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi, Leila Mavika akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya kitaifa ya kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza baada ya Mgeni Rasmi kufungua kikao cha Afua kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera

Na. Antonia Mbwambo - Kagera Mwakilishi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Leila Mavika amewaelekeza Wajumbe wa Kamati ya Kitaifa na waratibu ngazi ya Wizara, Taasisi zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza majukumu yao kwa weledi ili kujenga Utumishi wa Umma wenye afya, tija na unaoendana na matarajio ya wananchi. Bi. Mavika ameyasema hayo leo tarehe 02 Machi, 2026 wakati akifungua kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa. Aidha Bi. Mavika amezipongeza Taasisi za Umma ambazo zimekuwa zikifanya vizuri katika kusimamia afua za VVU, UKIMWI na MSY hasa kwenye Kuratibu kampeni za upimaji wa hiari wa VVU na utoaji wa elimu ya lishe bora, mazoezi na afya ya akili.
“Haya mafanikio ni ya kujivunia, lakini bado tunayo safari ya kwenda kufikia malengo tuliyojiwekea pamoja na mafanikio hayo” Bi. Mavika alisema. Vilevile Bi. Mavika amesisitiza kuwa ushirikiano wa Wadau na Taasisi simamizi za Kudhibiti VVU UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza ikiwemo Wizara ya Afya, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), na wadau wengine ni muhimu katika kuhakikisha utekelezaji wa afua hizo unaendana na miongozo ya kitaifa.
Amehitimisha kwa kuwataka Wajumbe wa Kamati ya Kitaifa na waratibu kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kuweka vipaumbele vinavyoendana na hali halisi ya watumishi na kuhakikisha kuwa kila taasisi ina mpango kazi unaotekelezeka.Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Mwanaamani Mtoo amemshukuru Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa utayari wake katika utekelezaji wa majukumu yaliyokasimiwa katika kuimarisha afya na ustawi wa Taifa. Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Bw. Bwai Biseko akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, amewashukuru waratibu kwa namna ambavyo wameshiriki kikamilifu katika kikao hicho na kutoa wito kwa kila mshiriki kuzingatia na kutekeleza yote yaliyoshauriwa.
 

 Na Munir Shemweta, WANMM

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, ameutumia uzinduzi wa “Samia Ardhi Kliniki” jijini Dar es Salaam kutangaza msimamo mkali wa Wizara dhidi ya vitendo vya uzembe na ucheleweshaji wa huduma kwa wananchi.

 

Katika hafla hiyo, Waziri Akwilapo amesema Wizara imeamua “kujivua gamba” na kuanza ukurasa mpya wa uwajibikaji, akisisitiza kuwa kauli za watumishi kudai mafaili kupotea au kutoonekana hazitavumiliwa tena.

 

“Hakuna kitu kama faili kupotea. Ofisi zetu zina mifumo thabiti, na mafaili hayana miguu ya kutoroka. Kauli hizi nimezipiga marufuku rasmi,” alisisitiza.

 

Waziri huyo alieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mageuzi yanayolenga kurejesha imani ya wananchi kwa sekta ya ardhi, ambayo imekuwa ikikabiliwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusu urasimu na usumbufu usio wa lazima.

 

Alisema Wizara haitasita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa watumishi watakaobainika kukwamisha huduma kwa maslahi binafsi, akisisitiza kuwa ardhi ni rasilimali ya Taifa na watumishi ni wasimamizi tu, si wamiliki.

 

Uzinduzi wa “Samia Ardhi Kliniki” umefanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Kliniki hiyo itafanyika nchi nzima kuanzia Machi 2 hadi 7, 2026, ikitoa huduma za msaada wa kisheria, utoaji wa hatimiliki na elimu ya taratibu za umilikishwaji wa ardhi.

 

Mbali na kuhimiza wanawake kujitokeza kunufaika na huduma hizo, Waziri Akwilapo aliwataka wanaume na viongozi wa kaya kuachana na mila potofu zinazowanyima wanawake haki ya kumiliki ardhi.

 

Kwa mujibu wa Waziri, idadi ya wanawake wenye hatimiliki imeongezeka hadi wastani wa asilimia 28 kutoka chini ya asilimia 10 miaka ya nyuma, hatua aliyoitaja kuwa ni mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita.

 

Kauli mbiu ya zoezi hilo ni: “Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,” ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kuhakikisha usawa wa kijinsia na kuimarisha uchumi wa familia na Taifa kwa ujumla.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw Edward Mpogolo akimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila mbali na kuipongeza Wizara ya Ardhi kwa kuanzisha Samia Ardhi Kliniki amesema, kuna baadhi ya changamoto zilizoanza kujitokeza kwa wale wanaopata hati miliki za ardhi kufunga barabara zinazotumika kwa jamii.

 

Ameomba utaratibu wa fomu za kuthibitishwa na majirani katika maeneo yaliyorasimishwa kuzingaitiwa kwa kupitishwa katika ngazi husika na kusimamiwa ili kuepuka changamoto kama hizo.

 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemnera amesema huduma kubwa zinazotolewa kupitia Samia Ardhi Kliniki ni elimu hususan ya haki za umiliki kwa wanawake, ushauri wa mambo mbalimbali ya sekta ya ardhi, utoaji hati kwa waliokamilisha taratibu pamoja na huduma nyingine. 

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa Kuzindua Samia Ardhi Kliniki jijini Dar es Salaam tarehe 2 Machi 2026
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akimkabidhi hati milki ya ardhi mmoja wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakati wa Samia Ardhi Kliniki tarehe 2 Machi 2026.
Naibu Katibu Mkuu Bi. Lucy Kabyemera akimkabidhi hati Miliki ya Ardhi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Edrward Mpogolo katika tukio la uzinduzi wa Samia Ardhi Kliniki jijini Dar es Salaam tarehe 2 Machi 2026. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi Dkt Upendo Matotola.
Sehemu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakipata huduma kupitia Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam
Sehemu ya watumishi wa sekta ya ardhi wanawake wakitoa huduma katika Samia Ardhi Kliniki inayofanyika jijini Dar es Salaam
 
Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Upendo Matotola akimkabidhi mwanamama mkazi wa jiji la Dar es Salaam  Hati Milki ya ardhi katika Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam.Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA, MICHUZI TV)
 
 
 
 
 

Serikali kuendelea kuweka mazingira salama kwa wenye Viwanda vinavyofanya kazi na kutatua changamoto kwa wakati ili kuendelea kulinda ajira za Watanzania na kuongeza mzunguko wa fedha kwa jamii na wananchi kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb) wakati wa ziara ya kikazi Machi 2, 2026 mkoani Morogoro.

Londo amemshauri Katibu Tawala mkoani Morogoro kuweka utaratibu kwa mikopo ya asilimia 10 kuwafikia walengwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogo (SIDO) ili kuleta maana ya utoaji wa mikopo kwa jamii nchini.

Londo ametembelea viwanda vinne katika Manispaa ya Morogoro ikiwemo SIDO, Mkwawa, Cotex na Mazava katika ziara yake ya siku moja mkoani hapa.

Pia amesema ikiwa wajasiliamali hao watapata mikopo wakiwa hapo ambako wamezungukwa na aina mbalimbali za ujasiriamali itawasaidia kupata namna ya kujengwa na kuwa wajasiriamali wazuri na hivyo kuwa na uhakika wa kurejesha mikopo hiyo.

Uwepo wa gundi inayozalishwa kwenye viwanda hivyo vidogo vilivyopo kwenye eneo la viwanda SIDO Morogoro ambapo ameiomba serikali ya mkoa kusimamia uzalishaji huo na kufanya masoko makubwa ya gundi kuanzia ndani ya mkoa na kisha nje ya mkoa Taifa hadi nje ya nchi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa SIDO, Mhandisi Profesa Sylvester Mpanduji anasema wanajipanga kuhakikisha wanaboresha eneo la viwanda la SIDO Morogoro ili kufanya wajasiriamali kulitumia kama kongani la viwanda na kuleta maana

Hata hivyo, Meneja wa SIDO Morogoro, Bi.Joan Nangawe anasema wametengeneza ajira zaidi ya 115 baada ya kutoa elimu, kuwakusanya wajasiriamali kwenye eneo la viwanda na kutoa mikopo ya shilingi Milioni 62.5.

Anasema katika siku 100 za Rais Samia Suluhu Hassan jumla ya wajasiriamali ambao ni vijana wanatarajia kupata mikopo ya shilingi Milioni 250 kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.

Mmoja wa wajasiriamali anayetengeneza Gundi kwenye eneo la viwanda SIDO Marry Hassan anasema licha ya kuwa na uhakika wa soko la ndani kwa mikoa ya Morogoro na Dar es salaam lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa masoko ya nje ambayo yanaweza kuwapa nafasi kubwa katika kuongeza uzalishaji na kukua kiuchumi.

Na.Alex Sonna-Dodoma

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanzisha  kliniki maalum iitwayo Samia Ardhi Kliniki nchi nzima kwa lengo la kuongeza idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi, ambapo kwa sasa ni asilimia 28 tu.

Hatua hiyo inalenga kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha huduma za ardhi zinatolewa kwa wananchi kwa kuzingatia misingi ya usawa wa kijinsia.

Akizungumza leo Machi 2,2026 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa kliniki hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Mhandisi Anthony Sanga, amesema mpango huo utaendeshwa nchi nzima na unatarajiwa kuhitimishwa Machi 7 mwaka huu, kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Mhandisi Sanga amesema kuwa  lengo kuu la Samia Ardhi Kliniki ni kuongeza asilimia ya umiliki wa ardhi kwa wanawake nchini kupitia utoaji wa elimu, hati za umiliki na utatuzi wa migogoro ya ardhi.

 "Takwimu zinaonesha kuwa ni takriban asilimia 28 pekee ya wanawake nchini wanamiliki ardhi, jambo linaloonesha umuhimu wa kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha ushiriki wao katika masuala ya umilikishaji."amesema Mhandisi Sanga

Mhandisi Sanga amefafanua kuwa Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 iliweka msingi wa usawa wa kijinsia katika umiliki wa ardhi kati ya wanaume na wanawake. Hata hivyo, amesema changamoto zilijitokeza katika utekelezaji, hasa kwenye masuala ya mirathi na urithi ambapo mila na desturi zilichangia kuwabagua wanawake.

“Tamko la sera ya mwaka 1995 lilielekeza kuzingatia mila na desturi, lakini katika sera mpya iliyozinduliwa mwaka 2025 na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, haki ya umiliki wa ardhi kwa wote—wanaume na wanawake imewekewa usawa bayana,” amesema Mhandisi Sanga

Aidha amesisitiza kuwa katika sera hiyo mpya, masuala ya urithi na mirathi yameainishwa kwa kuzingatia usawa wa kijinsia, hivyo kuweka mazingira rafiki kwa wanawake kumiliki na kurithi ardhi bila ubaguzi.

"Kupitia Ardhi kliniki hiyo maalum, wanawake watapatiwa hati za umiliki wa ardhi, kusaidiwa kutatua migogoro ya ardhi pamoja na kupewa elimu kuhusu haki na taratibu za umiliki wa ardhi."amesema

Amesema mpango huo unalenga kuhakikisha changamoto zinazowakabili wanawake katika sekta ya ardhi zinatatuliwa kwa wakati, huku ukichochea ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla.

Hata hivyo amewataka kuwa watulivu wakati zoezi hilo likiendelea ili waweze kuhudumiwa kikamilivu na kwa weledi.

Kwa upande wake, Mthamini Mkuu wa Serikali wa Wizara hiyo, Bi. Evelyn Baruti Mugasha, amesema hadi majira ya mchana wanawake zaidi ya 160 walikuwa wamejitokeza kupata hati, huku wengine wakiendelea kujitokeza.

Bi. Mugasha amewataka wanawake wa Mkoa wa Dodoma kutumia fursa ya kliniki hiyo kupata elimu, ushauri na huduma mbalimbali, huku akitoa wito kwa wanaume kutoa ushirikiano ili kuwawezesha wanawake kushiriki kikamilifu.

“Kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi ni hatua muhimu katika kuimarisha uchumi wa familia na taifa kwa ujumla,” amesema Bi. Mugasha.

Nao, wanachi wa Mkoa wa Dodoma wamempongeza Rais Samia  kwa kuwapa kipaumbele wanawake katika suala la hati ili kuhakikisha hawabaki nyuma.

Naye mkazi wa Chidachi, Bi. Veronica Hamisi, amesema amefurahi kupata hati aliyokuwa akiifuatilia kwa takribani miaka mitatu ndani ya siku moja.

Kwa upande wake, mkazi wa Miyuji, Getruda Mathias, amesema amehangaika kwa miaka mitano kupata hati, lakini anamshukuru Rais kwa kutoa kipaumbele kwa wanawake kilichomwezesha kupata hati ndani ya saa moja bila usumbufu.

“Nawasihi wanawake wenzangu tujitokeze kwa wingi kuchangamkia fursa hii ambayo itahitimishwa Machi 7 mwaka huu,” amesema.

Mkazi wa Ilazo, Zena Hamis, pia amemshukuru Rais kwa kuwapa kipaumbele wanawake na kuwasihi wale ambao bado hawajajitokeza kufanya hivyo ili kunufaika na huduma hiyo.

 


Mjua kwao hapotei njia, na mwenda pole hajikwai, unaweza ukafikiri utani kumbe inaelekea ni hivyo wale wote wanaopambana Kariakoo, Gaza, Teheran na kwingineko inaaminika kuwa asili yao ni Bonde la Olduvai lililoko eneo la hifadhi ya Ngorongoro.

Bonde la Olduvai linafahamika kama eneo la kipekee duniani kupatikana masalia ya jamii za binadamu wa kale na zana za mwanzo za mawe yanayowakilisha hatua muhimu za awali katika chimbuko la binadamu kuanzia miaka milioni 2 iliyopita hadi sasa.

Kupitia eneo hili ndio ulimwengu ulipoanza kujua historia ya safari ya mabadiliko ya mwanadamu baada ya ugunduzi wa fuvu maarufu la Zinjanthropus mwaka 1959 ambalo lilibadilisha uelewa na mtazamo wa wanasayansi kuhusu mchango wa Tanzania katika masuala ya asili ya binadamu.


Bonde Olduvai limehifadhi visukuku, historia na chimbuko la binadamu katika mtiririko uliokamilika.