Ndani ya kipindi kifupi cha siku 100 za uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sekta ya Madini imeendelea kujiimarisha kama moja ya vielelezo bora vya mageuzi ya kiuchumi yanayoongozwa na maono, Sera thabiti na utekelezaji wenye mwelekeo wa kimataifa. Sekta ya Madini imepiga hatua kubwa si tu katika ukusanyaji wa mapato, bali pia katika uongezaji thamani wa madini, ushirikishwaji wa Watanzania (Local Content) maendeleo ya teknolojia na nafasi ya Tanzania katika ramani ya madini duniani.

Ukuaji wa Mapato na Mchango kwenye Uchumi wa Taifa

Takwimu zinaonesha mabadiliko Chanya na ya msingi, ndani ya miezi mitatu pekee (Novemba 2025 hadi Januari 25, 2026), Sekta ya Madini imekusanya kiasi cha Shilingi bilioni 311, sawa na asilimia 103 ya lengo ndani ya kipindi hicho, mwenendo huo unaakisi mageuzi ya mifumo ya usimamizi, udhibiti na uwazi katika shughuli za madini. Kwa ujumla, mapato ya Serikali kutoka sekta hiyo yameongezeka kutoka shilingi bilioni 526 Mwaka wa Fedha wa 2020/2021 hadi zaidi ya shilingi trilioni 1.071 mwaka 2024/2025, huku mwaka wa fedha uliopo wa 2025/2026 sekta ikiwekewa lengo la kukusanya shilingi trilioni 1.2.

Mafanikio haya yamechochea mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa (GDP) kuongezeka kutoka asilimia 10.1 hadi asilimia 12 ndani ya siku 100 pekee. Hatua hii inaipa Tanzania nafasi ya kipekee miongoni mwa nchi za Afrika zinazotumia rasilimali zao za madini kama kichocheo cha ukuaji wa uchumi jumuishi.

Local Content: Watanzania Kuwekwa Kwenye Moyo wa Sekta

Moja ya mafanikio makubwa yenye athari chanya ya kijamii na kiuchumi ni utekelezaji wa Sera na Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania (Local Content), kupitia marekebisho ya Kanuni za mwaka 2018, Serikali imeweka mfumo unaohakikisha ajira, manunuzi na huduma migodini zinawanufaisha Watanzania moja kwa moja. Matokeo yake, ajira za Watanzania migodini zimeongezeka kutoka 6,668 mwaka 2018 hadi kufikia zaidi ya 18,800 mwaka 2024, sawa na zaidi ya asilimia 97 ya ajira zote migodini.

Kwa upande wa manunuzi, mageuzi haya yamepunguza utegemezi wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi ambapo manunuzi ya ndani yameongezeka hadi asilimia 88 ya manunuzi yote ya migodini kufikia mwaka 2024, ikilinganishwa na asilimia 62 mwaka 2018. Hatua hiyo imesaidia kubakiza mzunguko mkubwa wa fedha ndani ya nchi na uchumi wa Taifa, kukuza viwanda vya ndani na kuongeza ajira katika sekta shirikishi kama ujenzi, usafirishaji, nishati na huduma za kitaalamu.

Uongezaji Thamani na Viwanda: Kuondoka kwenye Uchimbaji wa Malighafi

Katika utekelezaji wa Sera ya Madini ya mwaka 2009, Serikali imeongeza kasi ya ujenzi wa viwanda vya kusafisha na kuongeza thamani ya madini ambako Mkoa wa Dodoma umeibuka kama kitovu kipya cha uongezaji thamani, ukiwa na viwanda 9 vya uongezaji thamani wa madini pamoja na viwanda 4 vya madini ya metali kama shaba na nikeli. Aidha, kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kiwanda cha kusafisha chumvi kwa ajili ya mikoa ya Lindi na Mtwara kimekamilika kwa asilimia 99, hatua inayoongeza thamani ya rasilimali kabla ya kuingia sokoni.

Uwezeshaji wa Wachimbaji Wadogo: Mageuzi ya Uchumi wa Wananchi

Wachimbaji wadogo, wanaohusisha zaidi ya Watanzania milioni 6 kwenye mnyororo wa thamani wa madini, wamekuwa kitovu cha mageuzi ya kijamii. Ndani ya siku 100, Serikali imenunua mitambo 15 ya uchorongaji miamba, kutoa leseni 511 kwa vikundi vya wachimbaji wadogo Geita na Shinyanga, na kuwezesha mkopo wa Shilingi bilioni 30 kupitia taasisi za fedha. Sambamba na hilo, mpango wa kununua mitambo mikubwa ya CIP yenye uwezo wa kuchenjua tani 120 kwa saa, pamoja na kuanzishwa kwa mfuko wa dhamana, umefungua ukurasa mpya wa uchimbaji wa kisasa, salama na wenye tija.

Miradi Mikubwa na Hadhi ya Kimataifa

Katika hatua ya kihistoria, Tanzania inajiandaa kuingia rasmi kwenye uzalishaji wa Madini ya Ferro-Niobium kupitia mradi wa Songwe, Panda Hill, Mbeya, unaotarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi trilioni 1. Mradi huo utaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa wazalishaji wakuu wa kimataifa wa madini haya muhimu kwa viwanda vya chuma na teknolojia ya juu. Sambamba na hilo, maandalizi ya utafiti wa kina wa dhahabu (High Resolution Airborne Geo-Physical Survey) na kampuni ya kimataifa ya Barrick Gold katika Nzega na Kahama yanaashiria uwekezaji mpya wa kiwango kikubwa mara baada ya Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde kuzindua urushwaji wa helkopta kwa ajili wa utafiti huo.

Dhahabu, Nishati Safi na Masoko ya Ndani

Kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ununuzi wa zaidi ya tani 17 za dhahabu umeiweka Tanzania miongoni mwa nchi 10 bora barani Afrika kwa hifadhi ya dhahabu, jambo linaloongeza uthabiti wa uchumi na heshima ya kifedha kimataifa. Wakati huohuo, uzalishaji wa nishati safi ya kupikia ya ‘Rafiki Briquettes’ unaotokana na makaa ya mawe kupitia STAMICO unaunga mkono ajenda ya nishati safi, ukipunguza utegemezi wa kuni na mkaa ili kulinda mazingira.

Hitimisho

Kwa mtazamo wa kimkakati, siku 100 za uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia zimeifanya Sekta ya Madini kuwa chombo cha mageuzi ya uchumi, ajira na hadhi ya Taifa kimataifa. Tanzania inaendelea kujizatiti na kujiimarisha kuelekea kwenye uchumi wa uongezaji thamani, teknolojia na ushiriki mpana wa wananchi. Hayo si mafanikio ya kawaida, bali ni mapinduzi ya kimuundo yenye athari chanya za kudumu kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.














Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi,akizungumza na wadau leo Februari 02, 2026 jijini Dodoma.

....

Serikali imeelekeza wadau kuhakikisha uwekezaji unaofanyika karibu na kampasi mpya 16 za vyuo vikuu unazingatia mpangilio wa miji, usalama na viwango vya kitaifa ili kuzuia ujenzi holela na kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakidhi mahitaji ya wanafunzi, watumishi na jamii jirani.

Akizungumza Februari 02, 2026 jijini Dodoma, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi,amesema kuwa halmashauri na serikali za mitaa zinapaswa kutenga ardhi na kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi kwa kushirikiana na vyuo husika.

Prof. Mushi amesisitiza kuwa mipango hiyo lazima izingatie viwango vya kitaifa vya upangaji miji na kuondoa migongano ya matumizi ya ardhi.

Profesa Mushi pia amevielekeza vyuo vikuu kufungua milango ya ushirikiano na sekta binafsi kupitia ubia rasmi (PPP) katika ujenzi wa hosteli, vituo vya biashara na miundombinu maalum.

Amesema mashauriano ya mara kwa mara kati ya vyuo na serikali za mitaa ni muhimu ili kuoanisha mipango ya maendeleo na kuimarisha mazingira rafiki kwa uwekezaji.

Aidha, sekta binafsi imetakiwa kuhakikisha huduma wanazotoa zinajibu mahitaji halisi ya jamii kwa kuzingatia usalama, ubora na uwajibikaji wa kijamii.

Mratibu wa Mradi wa HEET Taifa, Dkt. Kenneth Hosea, amesema kuwa mbali na kutoa mafunzo ya programu za Shahada ya Kwanza na Shahada ya Pili, kampasi mpya pia zitalenga kutoa ujuzi wa vitendo kwa vijana, wanawake na makundi maalum. Hatua hii inalenga kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika maeneo ya pembezoni kupitia ujenzi wa miundombinu, upatikanaji wa huduma za msingi pamoja na fursa za ajira.

Aidha, Dkt. Hosea ameongeza kuwa kila kampasi inatarajiwa kudahili zaidi ya wanafunzi 1,000 mwanzoni, na idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka hadi kufikia takribani wanafunzi 7,000 kadri muda unavyosonga.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkinga, Rashid Karim Gembe, amesema kuwa kuanzishwa kwa kampasi mpya za elimu ya juu katika maeneo ya pembezoni kumeleta manufaa makubwa ya kiuchumi na kijamii

Amesema kuwa kutachochea ujenzi wa miundombinu kama barabara, maji na umeme, kuongeza upatikanaji wa huduma za msingi, pamoja na kutoa fursa za ajira kwa wananchi kupitia mahitaji ya walimu, wanafunzi na sekta binafsi, hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa ustawi wa jamii na maendeleo ya uchumi wa eneo husika.

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali imejipanga kuhakikisha wanawake wajasiriamali wanashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050, hususan katika nguzo za uchumi imara, jumuishi na shindani pamoja na maendeleo ya jamii.

Ameyasema hayo tarehe 02 Februari 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Janeth Elias Mahawanga, ambalo liliuliza kuwa “Je Serikali imejipangaje kuhakikisha wanawake wajasiliamali wanashiriki moja kwa moja kwenye utekelezaji wa dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050”?

Akijibu swali hilo Mhe. Mahundi amesema Serikali imeweka mikakati mbalimbali itakayowawezesha wanawake wajasiriamali kushiriki moja kwa moja katika maendeleo ya taifa kupitia shughuli za kiuchumi.

Mhe. Mahundi amesema mikakati hiyo inalenga kupunguza vikwazo vinavyowakabili wanawake katika upatikanaji wa mitaji na masoko ili kuongeza uzalishaji na ushindani wa bidhaa na huduma zao.

Mhe. Mahundi ameongeza kuwa Serikali inaendelea kubuni na kutekeleza jitihada mahsusi za kuwawezesha wanawake na wanaume kunufaika na fursa za kiuchumi, ikiwemo utekelezaji wa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi pamoja na kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali, matumizi ya teknolojia na viwanda vidogo na vya kati.

"Hatua hizo zitasaidia biashara za wanawake kukua, kuongeza ajira na kuchangia kikamilifu katika uchumi wa taifa kuelekea kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Maendeleo 2050." amesema Mhe. Mahundi 

Kila usiku, sauti za hatua zilinisumbua. Nilijua kuna mtu karibu, lakini kila niliposogea au kuangalia nje, hakuna mtu aliyeonekana. Mwili wangu ulikuwa na hofu, na usingizi wangu ulikuwa umekwama.

Nilijaribu kufikiria kuwa ni mawazo tu, au labda ni wanyama wa jirani, lakini moyo wangu ulijua kuna kitu tofauti.
Hali hiyo iliendelea kwa wiki kadhaa. Nilijaribu kuacha kufikiria, lakini kila usiku ulikuwa mbaya zaidi.

Hisia ya kutokuwa salama ilianza kuathiri maisha yangu ya kila siku hata kazi zangu zilipungua kwa sababu ya hofu. Siku moja, niliamua kuchunguza kwa umakini zaidi.

Nilipofuatilia kwa makini sauti hizo, nikashangaa kuona mtu aliyejaribu kuingia kwenye nyumba yangu kwa siri. Alikuwa mtu niliyemjua lakini hakutegemea kuwa atakuwa na nia mbaya. Nilihisi mchanganyiko wa hofu na kutoamini.Soma Zaidi.
Nilishuhudia maumivu makali yasiyo ya kawaida. Binti yangu alipewa kazi nje ya nchi kwa matumaini ya maisha bora, lakini badala yake alikumbana na mateso makali.

Mara nyingi alirudi nyumbani akiwa amelemaza kimwili na kihisia, akishindwa kueleza yote aliyopitia. Moyo wangu ulikosa pumzi kila niliposoma au kusikia alivyokuwa ameumia.

Nilijua lazima nifanye kitu. Hatua za kawaida za kisheria hazikutosha zilikuwa ngumu, zenye masharti mengi, na mara nyingine hazikutegemea haraka. 

Nilijitahidi kupata msaada sahihi, akitupa mwongozo na njia za kufanikisha haki bila hatari zaidi kwa binti yangu.Soma Zaidi.
Niligundua kwa hofu kubwa kwamba mume wangu alikuwa akihusiana kimya kimya na househelp yetu. Kila ishara ilionekana kuwa ni ya siri, na moyo wangu ulijaa hofu na hasira.

Nilijaribu kuzungumza naye kwa utulivu, lakini mara nyingi aligeuka kimya au kutoridhika na maneno yangu.
Nilijua lazima nifanye kitu cha busara, la hekima, na haraka sio kwa hasira, bali kuhakikisha ndoa yangu inapona.

Nilianza kukusanya ushahidi wa tabia yake bila kuingilia vibaya haki ya mtu yeyote. Kisha nikaanza kutumia mbinu za mawasiliano ya busara: kuzungumza kwa uwazi, kuweka mipaka, na kuonesha kuwa heshima na uaminifu ni msingi wa ndoa yetu.Soma Zaidi.
Nilipoanza biashara yangu ya garage, siku za mwanzo zilikuwa ngumu sana. Wateja hawakuonekana, pesa hazikuingia kama nilivyotarajia, na mara nyingi nilijisikia kama nitashindwa.

Nilijaribu matangazo madogo, kushirikiana na marafiki, hata kupunguza bei, lakini hakuna kilichobadilika. Siku moja, nilikumbuka kuwa kila biashara inahitaji njia za kipekee na za busara, sio tu kutegemea bahati.

Niliacha kufuata njia za kawaida tu na kuanza kuangalia kile wateja wanataka kweli: huduma haraka, matengenezo bora, na uangalifu kwa kila tatizo la gari.

Nilianzisha mpango wa kipekee: wateja wakija, wanapokea huduma ya haraka na kwa heshima, na walipokuwa wameridhika walikuwa wakiwataarifu marafiki zao.

Pia nilitumia mitandao ya kijamii kupandisha hadhi ya garage yangu, na kuonyesha matokeo halisi ya kazi zetu.Soma Zaidi.
Siku ile maisha yangu yalibadilika ghafla. Nilipokea habari kuwa nimeshingiziwa wizi niliokuwa sijufanya, na dunia yangu iliumia kwa hofu isiyoelezeka.

Kila mtu aliyeniuliza alinishauri kukubali hali hiyo, wakisema kesi hiyo ingeweza kuharibu heshima yangu na maisha yangu kabisa.

Nilihisi moyo wangu unaenda kwa kasi kila nikifikiria hatma yangu, na kila hatua niliyokuwa nikiichukua ilionekana kuwa hatari. Lakini sikuwa tayari kukubali kushindwa.

Nilijua lazima nitafute njia ya busara na ya haki kuhakikisha ukweli unadhihirika. Nilikusanya ushahidi kwa makini, nikazungumza na mashahidi wa kuaminika, na kushirikiana na wanasheria wenye uzoefu wa kesi ngumu kama hii.

Hatua kwa hatua, ulinganifu na ukweli ulianza kuibuka mbele ya mahakama, na hoja zangu zikawa na nguvu zaidi ya nilivyotarajia. Wale waliokuwa wakinisingizia wizi walijaribu kupinga, lakini ukweli haukupigwa chini.Soma Zaidi.

 

Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne, huku baadhi ya wanafunzi wakifutiwa matokeo yao kutokana na makosa ya utovu wa nidhamu, ikiwemo kuandika matusi katika karatasi za mitihani.

Wakati baadhi ya wanafunzi wakikumbana na adhabu hiyo, hali imekuwa tofauti kabisa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari FEZA Boys, ambapo matokeo yao yameleta furaha kubwa.

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa, jumla ya wanafunzi 71 walifanya mtihani wa Kidato cha Nne katika shule hiyo. Kati yao, wanafunzi 69 wamepata ufaulu wa Daraja la Kwanza (Division I), huku wanafunzi wawili pekee wakipata Daraja la Pili (Division II).

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Mwalimu wa Taaluma wa shule hiyo, Said Hassan, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa siri ya mafanikio hayo ni ushirikiano wa pamoja kati ya wazazi, walimu na wanafunzi, mkakati wanaouita “Utatu Mtakatifu (W3)”.

Alisema kuwa kwa upande wa shule, walimu hutimiza wajibu wao kwa kufundisha kwa bidii, huku wazazi wakipewa jukumu la kuhakikisha mahitaji muhimu ya wanafunzi yanapatikana kwa wakati, hali hiyo humwezesha mwanafunzi kupata muda wa ziada wa kujisomea.

Aidha, shule hiyo ina utaratibu wa kukaa na wanafunzi mmoja mmoja ili kufahamu changamoto zao, jambo linalosaidia kujenga urafiki kati ya mwalimu na mwanafunzi na hivyo kuongeza hamasa ya kupenda masomo.
Pia, shule hufanya mitihani ya mara kwa mara, ikiwemo kwa kushirikiana na shule jirani, hali inayowasaidia wanafunzi kuzoea mitihani na kuichukulia kama jambo la kawaida.

Kwa upande wa wanafunzi bora, Baraka Yunus, aliyepata alama A katika masomo yote, alisema mafanikio hayo yametokana na juhudi za pamoja kati ya shule na wazazi, aliongeza kuwa alipata muda wa kutosha wa kusoma akiwa shuleni na anatarajia kuwa mfanyabiashara baada ya kumaliza masomo yake.

Naye Chriss Mwingila, ambaye pia alipata alama A katika masomo yote, aliwashukuru walimu na wazazi kwa kuwawekea mazingira rafiki ya masomo yaliyowasaidia kupata muda wa kutosha wa kujifunza

Waalimu na wanafunzi wa shule ya Feza Boyz wakishangilia mara baada ya kupata matokeo ya kidato cha nne na kupata ufaulu wa alama A kwa darasa zima

Mwalimu wa taaluma wa shule ya Feza Boyz ,Said Hasan akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kidato cha nne jijini Dar es salaam.
Wanafunzi wa shule ya Feza Boyz wakishangilia kwa kuwabeba wanafunzi waliofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne na kupata ufaulu wa alama A kwa darasa zima

Ilikuwa usiku wa giza. Nilikuwa nikisafiri kwenda nyumbani baada ya mkutano wa kikazi. Barabara ilikuwa tupu, taa chache zikiwa zimethibitisha giza linaloweza kutisha.

Nilipokuwa nikitembea, ghafla nilipotea mwelekeo. Kila hatua ilinipa hisia ya kutisha, na mawazo yangu yalijaa hofu: “Huu ndio mwisho wangu?”
Nilijaribu kupiga simu, lakini hakuna ishara.

Nilijaribu kumuita mtu yeyote karibu hakuna aliyekuwa karibu. Kipindi hicho kilikuwa cha maumivu ya ndani, mwili wangu ukikosa nguvu, na moyo ukijaa hofu isiyo na kipimo. Nilihisi nitaanguka bila msaada, na hatari ya kukosa maisha ilikuwa karibu.

Nilikaa chini kujaribu kutuliza hisia zangu. Wakati huo, neno la rafiki yangu lilijitokeza: aliniambia nisikate tamaa, kulingana na uzoefu wake na wengine waliokuwa katika hali ngumu.Soma Zaidi.
Kila asubuhi ilikuwa vita. Mtoto wangu alianza kulia mara tu sare ya shule ilipotolewa. Alishika begi lake kwa mikono miwili na kusema hataki kurudi shule. Mwanzoni nilidhani ni uchovu wa kawaida au uvivu wa mtoto.

Lakini siku zilivyopita, machozi hayakuisha yaliongezeka. Nilijaribu kumlazimisha, nikamkemea, hata nikamwahidi zawadi. Hakubadilika.

Alianza kuumwa tumbo kila asubuhi, usingizi wake ukapotea, na tabasamu lake la kawaida likatoweka. Moyo wangu ulianza kunishtua: kuna kitu si sawa.

Siku moja nilikaa naye chini kwa upole nikamwambia aseme chochote bila kuogopa. Alilia sana ndipo akaniambia ukweli uliyonivunja kabisa. Shuleni alikuwa akidharauliwa, kuchekwa, na kutengwa kila siku.

Alikuwa anahisi hana thamani, na shule kwake ilikuwa mahali pa maumivu, si pa kujifunza. Nilikwenda shule mara kadhaa. Nilizungumza na walimu. Niliahidiwa mambo yangerekebishwa, lakini hali haikubadilika.

Mtoto wangu aliendelea kukosa amani, na mimi kama mzazi nilijihisi nimeshindwa. Nilikuwa nimejaribu kila njia ya kawaida lakini hofu ya mtoto wangu haikupungua.

Ni wakati huo rafiki yangu wa karibu alinishauri nisimame kidogo na nitafute msaada wa kina msaada wa kumjenga mtoto kisaikolojia na kurudisha ujasiri wake.Soma Zaidi.
Kulikuwa na siku niligundua kuwa ukimya unaweza kuumiza kuliko maneno. Mimi na mke wangu tulikuwa tunaishi nyumba moja, tunalala kitanda kimoja, lakini mioyo yetu ilikuwa mbali sana.

Hakukuwa na ugomvi mkubwa, wala kelele kulikuwa na kimya kizito kilichokuwa kikinikandamiza kila siku.
Nilijaribu kuanzisha mazungumzo, lakini kila nilipofungua mdomo nilikuta ukuta.

Macho yake yalikuwa na machozi ambayo hayakumwagika, nami nikabaki na maswali yasiyo na majibu. Ndoa yetu ilianza kukosa mwelekeo, na siku hadi siku matumaini yalizidi kupungua.

Siku moja nilichukua ujasiri kuuliza kwa upole kama kuna kitu kinachomsumbua. Hakujibu mara moja. Ilimchukua muda, kisha akaniambia kuna jambo la zamani lililokuwa linamuumiza moyoni jambo ambalo halikuwahi kusemwa kwa miaka mingi.

Ukweli huo ulinishtua, lakini pia ulinifanya nitambue kuwa kimya chetu kilikuwa kimejengwa juu ya maumivu yaliyofichwa. Tulijaribu kujitatulia wenyewe. Tulizungumza, tukasikiliza, tukajaribu kusamehe.

Lakini bado kulikuwa na mzigo ambao ulituzuia kusonga mbele kikamilifu. Nilihisi kama tunazunguka pale pale, bila suluhisho la kudumu.

Ni hapo niliposikia ushauri wa kutafuta msaada wa nje msaada wa watu waliokuwa wamesaidia wanandoa wengine waliokuwa kwenye hali kama yetu.Soma Zaidi.
Siku hiyo niliamka mapema kama kawaida, nikaoga na kujiandaa kwenda kazini bila kujua kuwa ingetakuwa siku ya mwisho. Nilipofika ofisini, nilikaa chini na kuitwa kwa haraka.

Maneno machache tu yakabadilisha maisha yangu: “Huduma zako hazihitajiki tena.” Hakukuwa na onyo, hakuna huruma, hakuna hata muda wa kujiandaa.

Nilirudi nyumbani nikiwa nimechanganyikiwa. Nilikuwa na kodi ya miezi miwili nyuma, watoto walihitaji karo, na simu yangu ilikuwa tayari imejaa madeni.

Jioni hiyo hiyo mwenye nyumba alinipigia akaniambia wazi kuwa kama sitapata pesa, nitatoka nje ya nyumba ndani ya siku chache. Hapo ndipo moyo wangu ulipoanguka kabisa. Usiku huo sikulala.

Nilikaa nikitazama dari nikijiuliza nitawaambia nini watoto wangu asubuhi. Nilijaribu kuomba kazi kwa marafiki, nikatuma CV kila mahali, nikajaribu hata kazi za mkono lakini hakuna kilichofunguka.

Kila mahali niligonga mlango, ulikuwa umefungwa. Siku ya pili, rafiki mmoja wa zamani alinipigia. 

Aliposikia hali niliyokuwa nayo, alinishauri nisimame kwanza, nitulie, na kutafuta msaada wa watu waliokuwa wamesaidia wengi waliokwama kama mimi. Soma Zaidi.
Kwa muda mrefu nilikuwa nakiishi na tatizo la tumbo kuvimba na kujaa gesi mara kwa mara. Haijalishi nilikula kidogo au chakula gani, baada ya muda mfupi tumbo langu lilijaa, likawa gumu na kunifanya nijisikie vibaya sana.

Wakati mwingine nilikuwa nikikosa raha ya kukaa na watu au hata kulala vizuri usiku. Mwanzoni nilipuuzia nikidhani ni tatizo la kawaida tu. Lakini siku zilivyopita hali haikubadilika.

Nilijaribu dawa za dukani, nilibadilisha chakula mara kadhaa, lakini nafuu ilikuwa ya muda mfupi tu. Ilifika wakati nikaanza kuchoka kimwili na hata kiakili. Nilijiuliza, “Kwa nini tumbo langu liko hivi kila siku?”

Siku moja nilimweleza rafiki yangu hali yangu. Akanisikiliza kwa makini kisha akanishauri nisikimbilie suluhisho la haraka, bali nitafute mwongozo wa asili na wa hekima. Soma Zaidi.

 



Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

 

Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme REA, Mha. Deogratius Nagu ametoa maelekezo hayo Januari 31, 2026 kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi katika Vitongoji vya Mlimani Park na Liuli Chini Wilaya ya Songea Mkoani wa Ruvuma.

 

"Kasi ya utekelezaji wa mradi huu hairidhishi kwani hadi sasa Mkandarasi yupo asilimia 56 wakati alipaswa kuwa ametekeleza kwa asilimia 80 kwa maana kwamba amewasha vitongoji 43 kati ya vitongoji 135 ambavyo alitakiwa kuwasha,” amefafanua Mha. Nagu.

 

Mhandisi Nagu amemuelekeza Mkandarasi kumbadilisha Meneja wa Mradi, kuhakikisha anaongeza timu za mafundi na wataalam katika maeneo yote ya mradi na aongeze usambazaji wa vifaa vya mradi ikiwemo transafoma na nyaya ili afanikishe kukamilisha mradi mapema zaidi.

 

“Tumeongeza nguvu ya ufuatiliaji hapa na tumemueleza haturidhishwi na kazi yake; ahakikishe anazingatia maelekezo yaliyotolewa leo, tumejipanga kumsimamia kwa karibu zaidi na tunaamini hadi mwezi wa sita atakuwa amekamilisha mradi,” amesema Mhandisi Nagu.

 

Kwa upande wake Mhandisi wa Mradi, Erick Njau akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Mradi, Li Hongli amesema kuchelewa kwa mradi kunatokana na kuchelewa kufika kwa vifaa vya mradi hata hivyo aliahidi kutekeleza maelekezo na kukamilisha mradi kwa wakati.

 

"Ni kweli hatuna changamoto zaidi ya hii ya kucheleweshewa vifaa na watoa huduma, tumepokea maelekezo na tunaahidi kuongeza kasi,” amesema Mha. Njau.

 

Aidha, akizungumza kwa niaba ya Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Zakaria Ng’okorome amesema mradi unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 14.56 na kwamba utanufaisha wateja wa awali zaidi ya 5,400.





MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani wa Halmashauri ya Mji Handeni, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi yaliyolenga kuwaimarisha katika masuala ya utawala bora, ufuatiliaji wa mapato na uelewa wa mipaka ya majukumu yao katika uendeshaji wa halmashauri.

Na Augusta Njoji

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka madiwani wa Halmashauri ya Mji Handeni, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi kuacha kutanguliza maslahi binafsi au ya kisiasa wanapotekeleza majukumu yao, na badala yake kuweka mbele maslahi ya wananchi na maendeleo ya halmashauri.

Nyamwese ametoa wito huo mjini Handeni wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani, yaliyolenga kuwaimarisha katika masuala ya utawala bora, ufuatiliaji wa mapato na uelewa wa mipaka ya majukumu yao katika uendeshaji wa halmashauri.

Amesisitiza kuwa serikali haitavumilia uzembe, hujuma wala vitendo vyovyote vinavyozorotesha maendeleo ya halmashauri, akiwataka madiwani kuwa macho na kutoa taarifa kwa wakati pindi wanapobaini mianya ya upotevu wa mapato.

“Tunaomba mkawe wabunifu na mzishauri halmashauri namna bora ya kuboresha na kusimamia vyanzo vya mapato. Nyie ndio mnaoishi na wananchi; mnapobaini kapu linavuja, tuambieni linavuja wapi na nani analivujisha ili hatua stahiki zichukuliwe,” amesema Nyamwese.

Ameongeza kuwa madiwani ni macho na masikio ya serikali katika maeneo yao, hivyo wanapaswa kusimamia nidhamu ya watumishi, kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kuchochea ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni, Margareth Killo, amesema mafunzo hayo yataongeza ufanisi na uwajibikaji wa madiwani katika kuwahudumia wananchi.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko, pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, Michael Chabai, wamesema mafunzo hayo yamewawezesha madiwani kufahamu vyema wajibu na mipaka yao, hali itakayopunguza migongano na kuongeza tija katika utendaji wa halmashauri.