Msajili wa Baraza la Ushindani (FCT), Mhe. Mbegu Kaskasi,akizungumza wakati akifungua mafunzo kwa wadau na wafanyabiashara mkoani Arusha ya kuwajengea uwezo kuhusu matumizi ya mfumo wa usajili wa mashauri kwa njia ya kielektroniki (e-filing).

ARUSHA:

Baraza la Ushindani (FCT) limewahimiza wadau na wafanyabiashara mkoani Arusha kutumia kikamilifu mfumo wa usajili wa mashauri kwa njia ya kielektroniki (e-filing), lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kupunguza gharama katika uwasilishaji wa mashauri.

Akizungumza katika mafunzo hayo Msajili wa Baraza hilo, Mhe. Mbegu Kaskasi, alisema mfumo huo wa kisasa umeundwa ili kurahisisha usajili wa mashauri na rufaa bila wadau kulazimika kufika katika ofisi za FCT, hatua ambayo itaokoa muda na kuongeza ufanisi.

“Mfumo huu utaimarisha uwazi, kasi ya utoaji haki na kupunguza usumbufu kwa wadau,” alisema Mhe. Kaskasi, akibainisha kuwa hatua hiyo inakwenda sambamba na msukumo wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma."amesema Mhe.Kaskasi

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw. Moses Pesha, amelipongeza Baraza kwa kuendelea kutoa elimu kwa wanaohusika na wananchi kwa ujumla, akisema hatua hiyo imeongeza uelewa na kuimarisha imani ya wananchi katika mifumo ya utoaji haki.

Naye Afisa TEHAMA wa FCT, Ndg. Athumani Kanyegezi, amesema mfumo wa e-filing unaimarisha usalama wa taarifa na kuongeza urahisi wa kuzifikia ndani ya muda mfupi, tofauti na mfumo wa zamani wa kuhifadhi mafaili kwa mikono.

Katika upande wa wadau, mfanyabiashara wa jijini Arusha, Bi. Jonia Karumuna, ameipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara, kwa kuwezesha taasisi kama Baraza la Ushindani kuendelea kulinda haki za wafanyabiashara na kusikiliza rufaa zinazotokana na migogoro kutoka Tume ya Ushindani (FCC) na mamlaka mbalimbali za udhibiti ikiwemo EWURA, LATRA, TCRA, TCAA na PURA.

Amesema uwepo wa Baraza hilo umeongeza imani kwa wafanyabiashara kutokana na mchango wake katika kuhakikisha haki inatolewa kwa wakati na kwa kuzingatia misingi ya ushindani wa haki nchini.

 


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe, leo amepokea mpango mkakati wa ukamilishaji wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kutoka kwa  Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa (Mshitiri), Msanifu Majengo Justine Katabalo wa Kampuni ya MCB Company Ltd (Mkandarasi) pamoja na Mhandisi Khamadu Kitunzi kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (Mshauri Elekezi), ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo yake aliyoyatoa Januari 17, 2026 mjini Morogoro wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo.

Prof, shemdoe ameridhishwa na mpango mkakati uliowasilishwa ambao utawezesha jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kukamilia ifikapo Juni 07, 2026 tofauti na maelekezo ya awali ambapo ilipaswa jengo hilo kukamilika mwezi Julai 2026.

Awali, Prof. Shemdoe alielekeza ndani ya wiki moja Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mkandarasi kampuni ya MCB Company LTD na Mshauri Elekezi Wakala wa Majengo (TBA) kukutana na kuandaa mpango mkakati wa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo na kuuwasilisha ofisini kwake leo.

Prof. Shemdoe alilazimika kutoa maelekezo hayo baada ya kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo, licha ya kutokuwa na changamoto ya fedha. Ujenzi  wa jengo hilo  ulianza kutekelezwa Mei 27, 2022 na ulitakiwa kukamilika Mei 26, 2024.











Nilipoachwa ghafla, nilihisi dunia imenigeuka. Ndoa yangu ilivunjika bila onyo, na nilibaki na maswali mengi yasiyo na majibu. 

Watu waliniona kama mwanamke aliyeshindwa, baadhi wakinionea huruma, wengine wakinicheka nyuma ya pazia.

Usiku nililala kwa mawazo mazito; mchana nilitembea nikiwa sina mwelekeo. Nilijaribu kuanza upya, lakini kila nilipoinuka, moyo ulivunjika tena. 

Mateso yalizidi nilipopoteza hata heshima yangu. Nilijihisi peke yangu, nikilaumiwa kimya kimya kwa mambo ambayo sikuyafanya.

Nilijaribu mazungumzo ya busara, nikatafuta ushauri wa kifamilia, hata nikavumilia ukimya. Hakuna kilichobadilika. 

Nilifika mahali nikahisi tumaini lote limeisha, na maisha yangu yamewekwa kwenye kona isiyoonekana.

Siku moja, tukio la kushangaza lilitokea na kujaa vichwa vya habari mitaani. Kulikuwa na simulizi zilizopotoshwa zikisema kuwa nilimteka mwanaume fulani. 

Ukweli ni kwamba nilijikuta katikati ya hali isiyoeleweka, maneno yakichanganywa, na hofu ikitawala.

Nilijua kuwa kulikuwa na nguvu zisizoeleweka zilizokuwa zikicheza na hisia na uamuzi wa watu. Nilitambua wazi kuwa bila msaada wa kweli, ningezidi kupotea. Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mwanamke-mmoja-ashangaza-baada-ya-kumteka-jamaa-mmoja-na-kumfanya-mume-kisa-kuachwa/
Nilizaliwa kwenye familia ya kawaida sana, bila jina, bila mtaji, na bila mtu wa kunisukuma mbele. Wakati wenzangu walionekana kuwa na mwelekeo maishani, mimi nilikuwa napambana na umaskini, kejeli na kukataliwa kila mahali nilipojaribu.

Shuleni nilidharauliwa, mitaani nilionekana kama asiye na maana, na hata nyumbani nilionekana kama mzigo. Kila nilipoonyesha ndoto zangu, watu walicheka. Mateso yangu hayakuishia hapo. Nilipofika utu uzima, nilipitia kushindwa mara kwa mara.

Kazi nilikosa, miradi ilifeli, marafiki walinigeuka. Nililala njaa siku kadhaa, nikihama makazi mara kwa mara, nikiishi kwa msaada wa watu. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa na kipaji, lakini kilionekana kama kimefungwa.

Nilijitahidi kwa nguvu zangu zote, lakini kila nilipojaribu kusonga mbele, kitu kisichoonekana kilinirudisha nyuma. Nilifika mahali nikaanza kujiuliza maswali mazito: kwa nini ni mimi? Kwa nini juhudi zangu hazizai matunda?

Nilianza kukata tamaa, nikaacha hata kuwaambia watu ndoto zangu. Usiku nililala nikiwa na mawazo mazito, mchana nilitembea bila mwelekeo. Ilifika wakati nilihisi kabisa kuwa maisha yangu yamefikia mwisho kabla hata hayajaanza.

Mabadiliko yalianza baada ya kukutana na mtu mmoja aliyenisikiliza bila kunihukumu. Aliniambia ukweli ambao nilikuwa nikiuhisi muda mrefu moyoni: kwamba wakati mwingine mateso ya muda mrefu hayatokani na uvivu au laana ya kawaida, bali nyota ya mtu inaweza kufungwa. Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/kijana-apitia-mateso-mazito-lakini-akaja-kuwa-mtu-maarufu-duniani/
Nilianza kuona ndoto zile bila kuelewa maana yake. Kila usiku karibu saa ile ile, mwanaume yule yule alinitokea. 

Sikuwa namjua, lakini alionekana kama mtu wa karibu sana nami. Ndoto hizo zilikuwa na hisia kali kiasi cha kuniacha nikiwa nimechanganyikiwa nilipoamka.

Nilikuwa nikijiuliza kwa nini ndoto zinajirudia, na kwa nini moyo wangu ulikuwa ukimsikia mtu nisiyemjua. 

Kadri siku zilivyopita, ndoto ziliongezeka. Nilijaribu kupuuza, kujiambia ni mawazo tu, labda uchovu au msongo wa mawazo. Lakini hapana.

Kila nilipozidi kujaribu kuzisahau, zilirejea kwa nguvu zaidi. Nilianza kupoteza usingizi, nikahisi kama kuna kitu kisicho cha kawaida kinanifuata. Hapo ndipo hofu ilianza. Nilihisi kama nimefungwa na jambo nisilolielewa.

Nilizungumza na marafiki wachache, baadhi waliinicheka, wengine waliniambia niombe au nipumzike. Hakuna aliyenisaidia. 

Nilianza kukata tamaa, nikaogopa hata kulala. Ndipo siku moja jambo la kushangaza likatokea.

Nikiwa kwenye shughuli zangu za kawaida, nilikutana uso kwa uso na mwanaume niliyekuwa nikimuona kwenye ndoto. Alikuwa yuleyule, sura, sauti, hata namna ya kunitazama. Nilisimama kama nimerogwa.

Tulipoanza kuzungumza, ilionekana kana kwamba tulikuwa tukifahamiana kwa muda mrefu. Nilitetemeka. Nilijua wazi kuwa hili halikuwa jambo la kawaida. Hapo ndipo nilipoamua kutafuta msaada wa kweli.Soma Zaidi...

https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mdada-afanya-mapenzi-na-mwanaume-kwa-ndoto-ashtuka-kupatana-naye-live/
Sikuwahi kufikiria kuwa kazi ingetuingiza kwenye hali ya ajabu kiasi hiki. Nilikuwa mfanyakazi wa kawaida, nikifanya bidii ili kutimiza malengo yangu. Boss wangu alikuwa mkali, mwenye sauti kubwa na hakuamini mtu kirahisi.

Kila siku nilijitahidi kuonyesha uwezo wangu, lakini licha ya juhudi zote, nilionekana kupuuzwa. Ilifika wakati nilianza kuamini labda sifai, au kuna jambo linafanyika kisiri dhidi yangu. Kadri muda ulivyopita, hali ilizidi kuwa ngumu.

Kila nilipokaribia kupata nafasi au kupendekezwa, jambo lilibadilika ghafla. Wenzangu walinipita, na mimi nilibaki nikijiuliza kosa langu ni nini. Nilihisi kama nyota yangu ya kazi imezimwa, na matumaini yakaanza kupotea. Nilijaribu kubadilisha idara, kuongeza bidii, hata kujinyenyekeza, lakini bado hakuna kilichobadilika.

Nilipokuwa karibu kukata tamaa, nilipata ushauri kutoka kwa mtu niliyemwamini aliyeniambia ukweli mchungu: wakati mwingine si bidii pekee inayohitajika, bali kurekebisha mvuto na bahati ya mtu. Soma Zaidi....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mwanaume-mmoja-ampa-mapenzi-boss-wake-sasa-apagawa-kila-muda-anamuita-kwake/
Nilipoachwa, dunia yangu ilionekana kusimama. Mwanamke niliyempenda kwa moyo wangu wote alinigeuka ghafla na kuniacha bila maelezo ya kueleweka. Nilidharauliwa, nikachekwa, na hata baadhi ya marafiki walijitenga nami wakiamini maisha yangu yamefika mwisho.

Kila mahali nilipopita nilihisi macho ya watu yananiona kama mtu aliyeshindwa kimaisha na kimapenzi. Nilijaribu kuanza upya. Nilijaribu kujiamini tena, kuzungumza na watu wapya, hata kuomba na kujipa moyo.

Lakini kila nilipojaribu kusonga mbele, jambo fulani lilikuwa linanirudisha nyuma. Nilikuwa na biashara ndogo, nayo ilianza kudorora. Bahati ilinipotea, mapenzi hayakutokea, na siku zikawa nzito kama miezi.

Mara nyingi nilikaa peke yangu nikijiuliza kama nililaaniwa au kama kuna mtu alikuwa amefunga nyota yangu.Soma Zaidi....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jamaa-aliyeachwa-apata-bahati-ya-kupendwa-na-kufanya-harusi-ya-kitaifa/

 


Ujenzi wa mabweni ya wasichana katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli umefikia asilimia 58, hatua inayotarajiwa kuongeza fursa ya makazi kwa zaidi ya wanafunzi 500 pindi mradi huo utakapokamilika.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea mradi huo chuoni hapo, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema kukamilika kwa mabweni hayo kutasaidia kulinda usalama wa wanafunzi wa kike na kuwawezesha kusoma katika mazingira salama na tulivu.

“Watoto wakike wako kwenye hatari zaidi wanapolazimika kuishi nje ya maeneo ya Chuo. Kukamilika kwa mabweni haya kutapunguza changamoto za kiusalama na kuwapa wasichana wetu nafasi ya kusoma kwa utulivu na kuzingatia ndoto zao,” amesema Mhe. Mahundi.

Mhe. Mahundi amesema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira rafiki ya kujifunzia, hususan kwa masomo ya ufundi na ujuzi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli, Boniface Daniel amesema fedha walizopokea hivi karibuni zitasaidia kuingia awamu ya nne ya ujenzi wa mabweni hayo, hatua itakayoharakisha kukamilika kwa mradi huo.

“Fedha tulizopokea zitatuwezesha kuendelea na awamu ya nne ya ujenzi. Lengo letu ni kuhakikisha mabweni haya yanakamilika kwa wakati ili wanafunzi wengi zaidi wanufaike,” amesema Mkuu wa Chuo Boniface Daniel.

Nao baadhi ya wanafunzi wa Chuo hicho wamepongeza jitihada za Serikali katika ujenzi wa mabweni hayo, wakisema yatasaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza morali ya masomo, hasa katika kozi za ufundi.

Katika ziara yake chuoni hapo, Naibu Waziri Mhandisi Maryprisca Mahundi ametembelea madarasa ya ushonaji, eneo la ujenzi wa mabweni hayo pamoja na kufanya mazungumzo na wanafunzi, akiwahimiza kuzingatia nidhamu na kutumia fursa za elimu ya ufundi zinazotolewa na Serikali.













 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya ameanza ziara ya kikazi Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha ukiwa ni muendelezo wa kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

Awali Mhandisi Maryprisca Mahundi amefika ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM)Wilaya ya Monduli kwa ajili ya utambulisho.

Akiongea na uongozi CCM wa Wilaya ya Monduli Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameahidi kutekeleza majukumu kwa lengo la kumsaidia Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

Waziri na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Wanawake na Makundi Maalumu wanafanya ziara nchi nzima kukagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa mabweni ya wasichana katika vyuo vya Maendeleo ya jamii.