Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu ametoa onyo kali kwa watu wanaojihusisha na udanganyifu na uchakachuaji wa taarifa katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kusisitiza itaendelea kuchukua hatua ili kuhakikisha misingi ya uadilifu na uwazi inazingatiwa ipasavyo.

Bangu,ametoa onyo hilo baada ya kufanya kikao kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro, kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Amesema mfumo huo unaendelea kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya uadilifu na uwazi, huku WRRB ikiendelea kushirikiana na mamlaka za mikoa, wilaya na halmashauri kusimamia utekelezaji wake.

“Moja ambalo nataka kuliweka wazi kwa Watanzania ni kwamba mfumo huu unafanya kazi kwa kuzingatia uadilifu. Kuna maeneo mengi mfumo unafanya vizuri, lakini tumeanza kuona baadhi ya watu wakiingiza taarifa zisizo sahihi kwenye mfumo kwa lengo la kujipatia fedha. Nataka nitoe onyo kali kwao kwamba tunasimamia mfumo huu kwa karibu na hatua stahiki zitachukuliwa,” amesema Bangu.

Ameeleza kuwa WRRB imeweka utaratibu wa kufanya uhakiki wa bidhaa zilizopo maghalani kabla ya kutolewa kwa katalogi za mauzo ili kuhakikisha wanunuzi wanapata taarifa sahihi kuhusu kiasi cha mazao yaliyopo.

Bangu pia amewahamasisha wakulima wa ufuta kuendelea kuuza mazao yao kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kupata masoko yenye ushindani na kuongeza kipato chao.

Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha mazingira ya biashara ya mazao kupitia mfumo huo, jambo linalowezesha wakulima kunufaika zaidi na jasho lao.

“Wilaya ya Malinyi imeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mfumo huu. Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto, lakini sasa tumeridhishwa na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wakulima wananufaika na mapato yao yanaongezeka,” amesema.

Katika hatua nyingine, WRRB imekabidhi msaada wa vifaa vya usafi na vyakula kwa Hospitali ya Wilaya ya Malinyi ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za uwajibikaji kwa jamii.

Akikabidhi msaada huo katika Wodi ya Wazazi ya hospitali hiyo, Bangu amesema WRRB itaendelea kushirikiana na jamii sambamba na kutekeleza majukumu yake ya kusimamia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala nchini.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Dk. Julius Nyasongo, aliyepokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Wakili Sebastian Waryuba, ameishukuru WRRB kwa msaada huo akisema utasaidia kuboresha ustawi wa akina mama wanaopata huduma hospitalini hapo.

“Msaada huu utakuwa na mchango mkubwa kwa akina mama wanaopata huduma katika hospitali yetu. Tunawashukuru WRRB kwa kuendelea kushirikiana na sekta ya afya na jamii kwa ujumla,” amesema Dk. Nyasongo.

     
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb) amelitaja Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa ni nguzo kuu ya kulinda afya za walaji na kuchochea ustawi wa viwanda nchini.

 



Na Oscar Assenga,TANGA


SERIKALI imekipongeza Chama cha Washauri wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TACOGA) kwa kuendelea kuandaa mafunzo yanayolenga kuimarisha uwezo wa kitaaluma na kiutendaji wa washauri wa wanafunzi, wanasihi na viongozi wa serikali za wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali nchini.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Tanga,Mkurugezi wa Maendeleo ya Jinsia kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Badru Abdnur alisema mafunzo hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kuwajengea washiriki uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanafunzi katika taasisi za elimu ya juu.

Alisema katika kipindi cha mafunzo hayo, washiriki walipata nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao, pamoja na kupata mbinu mpya zitakazowawezesha kuboresha huduma wanazozitoa kwa wanafunzi.

"Nawapongeza viongozi wa TACOGA kwa ubunifu na maono yao ya kuhakikisha mafunzo haya yanafanyika kila mwaka. Bila uongozi imara, kuandaa mafunzo ya aina hii si jambo rahisi," alisema.

Aliongeza kuwa hatua hiyo inaonesha utambuzi wa umuhimu wa maendeleo endelevu ya kitaaluma kwa watendaji wanaohusika na huduma za wanafunzi pamoja na viongozi wa serikali za wanafunzi.

Badru alibainisha kuwa mada zilizowasilishwa zimegusa maeneo nyeti yanayoathiri ustawi na maendeleo ya wanafunzi, ikiwemo afya ya akili, maadili, matumizi ya teknolojia na uongozi bora.

Alisema dunia ya sasa inabadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia, hali inayowafanya vijana kuwa miongoni mwa makundi yanayoathirika zaidi na mabadiliko hayo.

"Vijana wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo afya ya akili, matumizi mabaya ya teknolojia, matumizi ya dawa za kulevya na mmomonyoko wa maadili. Hivyo, kuna haja ya kuendelea kuwajengea uwezo na kuwapa mwongozo sahihi ili wawe raia wema na wazalendo," alisema.

Aidha, aliwakumbusha washiriki kuwa serikali na jamii kwa ujumla zinategemea sana mchango wa washauri na wanasihi katika kuwajenga wanafunzi. 

Alisema wazazi na walezi wana matumaini makubwa kwa maafisa hao kwa kuwa vijana wengi wanaojiunga na vyuo vikuu bado wana umri mdogo na wanahitaji mwongozo, uangalizi na malezi ya karibu.

Kwa mujibu wake, kutokana na nafasi hiyo muhimu, TACOGA ina wajibu mkubwa wa kuchangia mageuzi ya maendeleo ya taifa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Alitoa wito kwa chama hicho kuwekeza zaidi katika mifumo ya kiteknolojia ili kuendana na mazingira ya sasa ya kidijitali. Alisema ni muhimu kuanzisha mifumo ya kimtandao na programu za simu zitakazowezesha wanafunzi kupata huduma za ushauri kwa haraka na kwa urahisi bila kuathiri muda wao wa masomo.

Pia aliwataka kuendelea kujenga uwezo wa wanachama wao kupitia mafunzo endelevu ya saikolojia, unasihi na mbinu mpya za utoaji wa huduma ili kuwawezesha washauri na wanasihi kutoa suluhisho stahiki na la kisasa kwa changamoto zinazowakabili wanafunzi.

Vilevile, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha viashiria vya kupima matokeo ya kazi zinazofanywa na TACOGA kwa kuwekeza katika tafiti ndogo ndogo za kutathmini kama huduma zinazotolewa zinaleta matokeo chanya katika ufaulu wa wanafunzi na maendeleo yao ya kijamii na kitaaluma.

Mgeni rasmi huyo pia alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya ofisi za washauri wa wanafunzi na madawati ya jinsia pamoja na vitengo vya kuzuia ukatili wa kijinsia katika vyuo vikuu. Alisema kuna muunganiko mkubwa wa majukumu kati ya taasisi hizo, hivyo ushirikiano ukiimarishwa utasaidia kupunguza mzigo wa kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wanafunzi.

Alisema maarifa na stadi zilizopatikana kupitia mafunzo hayo zinatarajiwa kuwafanya washiriki kuwa mabalozi wa mabadiliko katika taasisi zao na kuchangia kufikiwa kwa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TACOGA, Sophia Nchimbi, alisema chama hicho kimeendelea kuandaa mafunzo hayo kwa lengo la kuwawezesha maafisa wa ofisi za washauri wa wanafunzi katika vyuo vikuu kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi.

Alisema washiriki walipata mafunzo yaliyohusu nidhamu chanya, usimamizi wa tabia, unasihi, matumizi salama ya mitandao ya kijamii, afya ya akili, malezi ya wanafunzi, uongozi bora na usimamizi wa madawati ya jinsia katika vyuo vikuu.

"Mafunzo haya yanatusaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbalimbali tunazokutana nazo katika maeneo yetu ya kazi. Maarifa tunayopata yanatupa uwezo wa kuwahudumia wanafunzi kwa ufanisi zaidi," alisema Nchimbi.

Alisema mada kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii zimewawezesha washiriki kuelewa namna bora ya kuwaelekeza wanafunzi kutumia teknolojia kwa manufaa ya elimu badala ya matumizi yasiyofaa.

Nchimbi alisema pia washiriki walipata elimu kuhusu namna ya kusimamia madawati ya jinsia ili kuhakikisha wanafunzi wanaokumbana na changamoto mbalimbali wanapata msaada kwa wakati na kwa usahihi.

Aliongeza kuwa TACOGA imekuwa ikifanikiwa kuendesha mafunzo hayo kutokana na ushirikiano mkubwa wa wanachama na wadau mbalimbali wanaochangia maendeleo ya huduma za ushauri kwa wanafunzi.

Jumla ya washiriki 94 kutoka vyuo mbalimbali nchini walishiriki mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Tanga.







Kwa zaidi ya miezi sita, nilikuwa nikikabiliana na tatizo ambalo lilikuwa linaninyima Amani. Mazao yangu yalikuwa yanipotea usiku. Mwanzoni nilidhani ni wanyama wa porini waliokuwa wanaingia shambani. SOMA ZAIDI/TAZAMA VIDEO.

Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kugundua kuwa baadhi ya mazao yalikuwa yanavunwa kwa utaratibu ambao haukuonyesha kazi ya wanyama. Mtu alikuwa anaiba. Kwa kweli iliniumiza sana.

Nilikuwa nimewekeza muda, nguvu, na fedha nyingi kwenye shamba lile. Kila nilipoenda kuvuna, niligundua sehemu ya mazao imepungua. Hasara iliongezeka mwezi baada ya mwezi. Nilijaribu kulinda shamba.

Niliweka walinzi mara kadhaa, nikabadilisha ratiba za kutembelea shamba, na hata kuwaomba majirani wanisaidie kufuatilia hali ya eneo hilo. 
Kwa muda mrefu, nilikuwa mfanyakazi ambaye kila mtu alijua kuwa mwenye Bidii. Nilifika kazini mapema, nilitimiza majukumu yangu kwa umakini, na nilijitahidi kuhakikisha kila kazi niliyopewa inakamilika kwa wakati. Niliamini kwamba juhudi zangu zingetambuliwa siku moja.SOMAZAIDI'TAZAMA VIDEO HAPA.

Lakini miaka ilipita bila mabadiliko. Kila mara nafasi mpya zilipofunguka, nilikuwa na matumaini kwamba safari hii ningechaguliwa. Badala yake, niliona wafanyakazi wengine wakipandishwa vyeo huku mimi nikibaki pale pale.

Kwa kweli iliniumiza Sana. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba baadhi ya watu waliokuwa wakitangulia walikuwa wamefika kazini muda mfupi kuliko mimi. Wakati mwingine nilijikuta nikijiuliza kama kazi yangu ilikuwa inaonekana au kama juhudi zangu zilikuwa zinapotea bure.

Polepole nilianza kupoteza hamasa. Nilikuwa bado nafanya kazi zangu, lakini moyo wangu haukuwa na furaha kama zamani. Nilihisi kama nilikuwa nimekwama katika sehemu moja huku miaka ikiendelea kusonga mbele.

Kulikuwa na kipindi nilifikiria kuacha Kazi. Lakini nilijua kwamba kufanya hivyo kwa hasira kungeweza kunigharimu zaidi. Nilihitaji sababu mpya ya kuendelea kupambana.
Kwa miaka mingi, nilitamani kupata mtu ambaye angenipenda kwa dhati na kunikubali jinsi nilivyo. Lakini safari yangu ya mapenzi haikuwa rahisi. SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO HAPA.

Kila nilipoingia kwenye uhusiano, nilikuwa na matumaini makubwa. Niliamini kwamba safari hii mambo yangekuwa tofauti. Cha kusikitisha ni kwamba mara nyingi mahusiano yale yaliishia kwenye maumivu, ahadi zilizovunjwa, na kuvunjika moyo.

Kwa kweli nilichoka. hKadri miaka ilivyopita, nilianza kupoteza imani katika mapenzi. Niliona marafiki zangu wakipata wenza, wakifunga ndoa, na kujenga familia, huku mimi nikiendelea kuanza upya kila baada ya kuvunjika moyo.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kuamini kuwa labda sikuwa nimekusudiwa kupata upendo wa kweli. Nilijitahidi kuonekana mwenye furaha mbele za watu, lakini moyoni nilikuwa na huzuni.

Wakati mwingine nilijiuliza kama kuna mtu ambaye angeniona wa thamani na kutaka kubaki maishani mwangu kwa dhati. Kulikuwa na kipindi nilikata tamaa kabisa.

Niliacha kutafuta mahusiano na kuamua kujikita kwenye shughuli zangu za kila siku. Nilijaribu kujikubali na kuendelea na maisha, ingawa sehemu ya moyo wangu bado ilitamani kupata mtu sahihi.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo sikuweza kukumbuka siku ambayo sikuwa nikikohoa. Mwanzoni nilidhani ilikuwa mafua ya kawaida ambayo yangepita yenyewe baada ya muda mfupi.TAZAMA VIDEO HAPA/ SOMA ZAIDI.

Lakini wiki zilipita, kisha miezi. Kikohozi kilibaki, na mara kwa mara nilikuwa nahisi maumivu kwenye kifua yaliyokuwa yananifanya niwe na wasiwasi. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Wakati mwingine niliamka usiku nikikohoa. Nilipozungumza kwa muda mrefu, koo lilichoka haraka. Watu wa karibu walikuwa wakiniuliza kwa nini sikuwa napona, lakini hata mimi sikuwa na jibu.

Kilichoniumiza zaidi ni kutokuwa na uhakika. Kila nilipohisi nafuu kidogo, dalili zilikuwa zinarudi tena. Nilianza kuogopa kwamba huenda kulikuwa na tatizo kubwa kuliko nilivyokuwa nikifikiria.

Hatimaye niliamua kutafuta msaada wa kitabibu. Nilifanyiwa uchunguzi na kupewa ushauri wa wataalamu wa afya. Pia nilielekezwa kuhusu umuhimu wa kufuata matibabu, kupumzika vya kutosha, na kuepuka vitu ambavyo vingesababisha hali yangu kuwa mbaya zaidi.

Lakini safari ya kupona haikuwa rahisi. Kulikuwa na siku nilihisi nimekata tamaa kwa sababu mabadiliko hayakuja haraka kama nilivyotarajia.
Kwa miaka minane, maisha yangu yalizunguka kesi moja ambayo ilinitesa kuliko jambo lolote nililowahi kupitia. Ilikuwa ni kesi ya ardhi ya familia yetu. Ardhi hiyo haikuwa tu kipande cha shamba. Ilikuwa sehemu ya historia yetu.  SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO.

Hapo ndipo wazazi wetu walilelewa, na hapo ndipo tulikuwa tumejenga matumaini ya vizazi vijavyo. Lakini siku moja mgogoro ulizuka. Kilichoanza kama kutokuelewana kidogo kiligeuka kuwa kesi kamili mahakamani.

Kila upande ulikuwa na madai yake, na ghafla familia yetu ikajikuta katika vita ya kisheria ambayo haikuonekana kuwa na mwisho. Kwa kweli ilikuwa safari ngumu sana.

Miaka ilipita huku kesi ikiendelea. Kulikuwa na vikao, nyaraka, na kusubiri maamuzi mbalimbali. Kila nilipoondoka mahakamani, nilibeba mzigo wa hofu moyoni mwangu.

Hofu ya kupoteza kila kitu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona wazee wa familia wakihangaika. Walikuwa wamewekeza matumaini yao yote kwenye ardhi hiyo, na kila siku waliishi kwa wasiwasi kuhusu hatima yake.

Kulikuwa na wakati nilikata tamaa. Baadhi ya watu waliniambia nikubali matokeo yoyote na kuacha kupambana. Wengine waliniambia kesi ile ingeendelea milele bila suluhisho.

Lakini moyoni sikuwa tayari kuacha. Siku moja rafiki yangu alinieleza kuhusu Kiwanga Doctors. Aliniambia waliwahi kumpa moyo wakati alikuwa akipitia changamoto kubwa iliyomfanya ahisi amefika mwisho wa safari.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

 


Na.Ashura Mohamed - Arusha.

Maonesho ya Karibu- KiliFair yamefunguliwa rasmi Jijini Arusha ambapo pamoja na kuchangia ukuaji wa pato la taifa Jukwaa hilo linatahwa kama kitovu cha kukutanisha wauzaji na waonenyeshaji kutoka mataifa mbali mbali barani Afrika

Maonesho hayo ambayo ambayo yanazidi kukua mwaka hadi mwaka yanawakutanisha wadau wa sekta ya utalii barani Afrika na Dunia kwa Ujumla kwa lengo la kutangeneza mnyororo wa Uchumi ndani ya sekta hiyo ili kuendelea kufanya vizuri zaidi,ambapo jukwaa hilo  huwakutanisha wadau wa ndani na nje ya nchi  ambao wameendelea kuwekeza na kuchagiza ongezeko la watalii katika Hifadhi za Taifa nchini.

Akifungua Maonesho hayo  Juni 05, 2026 katika Viwanja vya Magereza jijini Arusha, Mkurugenzi wa Utalii Dkt. Thereza Mugobi kwa niaba ya Waziri waMaliasili na Utalii alisema kuwa Karibu-KiliFair ni zaidi ya maonesho,ambao ni  uwekezaji wa kimkakati katika mustakabali wa utalii wa Tanzania. 

Dkt.Mugobi amesema kuwa Uhusiano huo wa kibiashara ulioanzishwa katika jukwaa hilo la Karibu KiliFair umezalisha ushirikiano mpya, kuongeza idadi ya watalii wanaowasili nchini, kuvutia uwekezaji, kutengeneza ajira, na kuimarisha maisha ya jamii zinazotegemea utalii. 

"Serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya utalii ikiwemo malazi, viwanja vya ndege, barabara ili kuboresha uzoefu wa watalii na kuwafikisha katika maeneo mbalimbali yenye vivutio kwa urahisi,pia Wizara itaendelea kutangaza vivutio vyake kupitia njia za kidijitali ili kuyafikia masoko mbalimbali duniani." Amesema Dkt. Mugobi.

Naye  mwakilishi kutoka “TATO” Wilbard Chambulo, amesema kuwa maonesho haya ni daraja linalounganisha wadau wa ndani ambao ni mawakala wa utalii na waongoza watalii pamoja na mawakala wa kimataifa kutoka katika mabara yote duniani.

Mkurugenzi Mwenza wa Karibu-KiliFair, Dominic Shoo, amesema ongezeko la washiriki kutoka mataifa mbalimbali ni ishara kuwa Tanzania imeendelea kujijengea heshima kama kitovu muhimu cha biashara ya utalii katika ukanda wa Afrika Mashariki

Shoo ameongeza kuwa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi utaendelea kuwa nguzo muhimu katika juhudi za kuitangaza Tanzania na kuongeza mchango wa utalii katika uchumi wa taifa

Karibu-KiliFair imeendelea kuwa moja ya maonesho makubwa zaidi ya utalii katika Afrika Mashariki, yakitoa nafasi kwa wadau kutangaza vivutio vya utalii, kujenga mitandao ya biashara na kuibua fursa mpya za uwekezaji ndani ya sekta hiyo.

Maonesho haya yatamalizika kesho Jumapili June 07 ambapo mwaka huu yamekutanisha zaidi ya watu 1000 kutoka mataifa mbali mbali.







Mradi wa uchorongaji wa visima vitatu vya gesi asilia unaoendelea katika Kitalu cha Mnazi Bay kilichopo Mkoani Mtwara umeleta manufaa makubwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kufuatia utekelezaji wenye mafanikio.

 



NA MWANDISHI WETU – SONGEA

Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki  maghala ya kuifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hii kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa  katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,

Ambao  umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga

Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika  katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.




Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.



 ‘Mkoa  hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.

Aidha Aliwaasa wanufaika wa Mradi huo kuwapatia wengine ujuzi walioupata na kuwa waaminifu wanapopata mikopo kupitia Bank ya Kilimo nchini TADB kwa kuirejesha kwa wakati kwa amendeleo ya Taifa.Afisa Uvuvi kutoka Cameroon Bi Audrely Tchoundi aliwapongeza wafugaji wa Tanzani kwa kuwa wabunifu katika eneo la ufungaji viumbemaji na ukulima wa mwani kwa kutumia mbinu mbadala akitolea mfano wakulima wa Mwani wa Kijiji cha Shuka Mkoani Lindi, pamoja na usimamizi mzuri wa mabwawa ya samaki.

Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana  Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.

Serikali imesisitiza kuwa uzingatiaji wa viwango na ubora wa bidhaa na huduma si jambo la hiari bali ni nguzo ya lazima katika kujenga uchumi wa viwanda wenye ushindani kitaifa na kimataifa.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa tuzo na vyeti kwa shule za Msingi zinazofanya vizuri katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika Mkoa wa Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika Kimkoa Juni 5, 2026 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, yakiongozwa na kauli mbiu isemayo, “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.”

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kampuni ya KPMG Tanzania imeamua kuendelea kudhamini shughuli mbalimbali zinazohamasisha utunzaji wa mazingira kwa vijana na wanafunzi ikiwa ni sehemu ya mchango wao katika kulinda mazingira nchini.

 


✅️ Sawa na Asilimia 105.8, Zikiwa Zimebaki siku 26 Kufunga Mwaka wa Fedha 2025/26

✅️ Watumishi Watakiwa Kuongeza Weledi Kufikia Sh Trilioni 1.4 Mwaka 2026/27

✅️ Watumishi  Watakiwa kuhudumia wananchi bila ubaguzi

WIZARA ya Madini imevuka lengo la ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 baada ya kukusanya Sh trilioni 1.27 hadi Juni 5, 2026, dhidi ya lengo la Sh trilioni 1.2, huku ikitarajia kufikia Sh trilioni 1.3 ifikapo  Juni 30, 2026.

Kutokana na mafanikio hayo, watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake wametakiwa kuondokana na uzembe, kuongeza bidii na kufanya kazi kwa weledi ili kufikia lengo jipya la ukusanyaji wa Sh trilioni 1.4 lililowekwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akizungumza katika kikao cha watumishi wote wa Wizara ya Madini na taasisi zake ambazo ni GST, TEITI, Tume ya Madini, STAMICO na TGC, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, amesema mafanikio yaliyopatikana yanapaswa kuwa chachu ya kuongeza juhudi katika usimamizi wa Sekta ya Madini kwa kuzingatia Sera, miongozo, kanuni na Sheria zilizowekwa.

Amesema watumishi wanapaswa kutambua kuwa wanapowahudumia wananchi wanatekeleza wajibu wenye thamani kubwa kwa taifa, hivyo wanapaswa kuwahudumia watu wote kwa usawa bila kujali itikadi, dini wala uraia wao.

“Wachache tuliokabidhiwa jukumu la kuhudumia sekta ya madini tunapaswa kuhakikisha watu wote wanahudumiwa kwa haki na uzalendo mkubwa ili kuendelea kujenga taifa letu,” amesema.

Amesema watumishi ndiyo injini ya Serikali katika sekta ya madini na kwamba mchango wao una nafasi muhimu katika kukuza uchumi wa nchi kupitia usimamizi bora wa rasilimali madini.

“Wito wangu ni kufanya kazi kwa bidii, weledi na kusimamia sera, miongozo, kanuni na sheria zilizowekwa ili sekta hii iendelee kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa,” amesema.

Katibu Mkuu huyo amesema watumishi wanapaswa kujiepusha na vitendo vya rushwa, uvivu na uzembe ambavyo vinaweza kuharibu imani ya wananchi kwa wizara, taasisi zake na Serikali kwa ujumla.

“Tusiharibu imani ya wananchi kwa rushwa, uvivu na uzembe. Mtu mmoja anayepokea rushwa anaweza kuchafua kazi za watumishi wengi waadilifu. Tufanye kazi kwa uzalendo mkubwa ili kuhakikisha hakuna mtu au wachache miongoni mwetu wanaochafua taswira ya wizara, taasisi zetu na Serikali kwa ujumla,” amesema.

Amesema watumishi wanapaswa kuchagua kuwa mwangaza badala ya kuwa kivuli na kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya wizara na taasisi zake kwa kuwa wote ni timu moja yenye malengo yanayofanana.

“Kazi ya mwenzako ikichelewa, mafanikio yako pia yanachelewa. GST ikichelewa kutekeleza majukumu yake, Tume ya Madini nayo itaathirika. Tusaidiane kwa pamoja kufikia malengo yetu,” amesema.

Katika salamu za Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, watumishi wamepongezwa kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Aidha, imeelezwa kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini imepangiwa kukusanya Sh trilioni 1.4, lengo ambalo linahitaji watumishi kuongeza uwajibikaji, uadilifu na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akizingumza katika Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani ( ILO), leo Juni 5, 2026, Jijini Geneva, Uswisi.

Kampuni ya Oryx Gas imeadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kufanya usafi katika Soko la Kimataifa la Samaki Feri jijini Dar es Salaam na kukabidhi vifaa vya usafi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi.
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetunukiwa Tuzo  leo tarehe 5 Juni 2026,  Siku ya Mazingira Duniani  kutokana na mchango wake mkubwa katika kuendeleza kilimo himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, matumizi endelevu ya rasilimali za asili na uwekezaji katika teknolojia rafiki kwa mazingira.