Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 376 vya mkoa huo utawezesha uongezaji thamani wa mazao ya kilimo kupitia uanzishwaji na uendelezaji wa viwanda vidogo vidogo katika maeneo ya wananchi.

Mhe. Dendego aliyasema hayo wakati wa hafla ya kumtambulisha rasmi mkandarasi wa mradi huo, Kampuni ya China Railway No. 4 Engineering Group Ltd kutoka Jamhuri ya Watu wa China, kampuni iliyoshinda zabuni ya kusambaza umeme katika vitongoji hivyo na kuongeza kuwa mradi huo unatarajiwa kufikia kaya 13,259 mara utakapokamilika.

Amesema kuwa upatikanaji wa umeme si anasa bali ni nyenzo muhimu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, na kwamba Mkoa wa Singida umeendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo kutokana na uwepo wa viwanda vidogo hadi ngazi ya vitongoji.

“Upatikanaji wa umeme utaongeza thamani ya mazao ya kilimo kupitia viwanda vidogo vidogo. Wananchi wa Mkoa wa Singida wana mahitaji makubwa ya umeme, hivyo idadi ya awali ya wananchi 13,000 ni mwanzo tu, na tunatarajia mahitaji yataongezeka zaidi,” amesema Mheshimiwa Dendego.

Aidha, Mkuu wa Mkoa huyo amemtaka mkandarasi kuhakikisha anatoa kipaumbele cha ajira za muda mfupi kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yatakayopitiwa na mradi huo.

Mhe. Dendego alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kipaumbele katika upatikanaji wa nishati ya umeme vijijini kwa kuidhinisha jumla ya shilingi bilioni 45.6 kwa ajili ya kusambaza umeme katika vitongoji 376 vya Mkoa wa Singida.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Umeme Vijijini (REA), Mhandisi, Thomas Mmbaga, amesema kuwa Serikali kupitia REA imemtambulisha rasmi mkandarasi ili kuanza utekelezaji wa mradi huo kwa mkataba wa miaka mitatu. Ameeleza kuwa wateja wa awali 13,259 wanatarajiwa kuunganishwa na huduma ya umeme katika wilaya za Ikungi, Mkalama, Itigi, Iramba, Singida na Manyoni.

Naye mwakilishi wa Kampuni ya China Railway No. 4 Engineering Group Ltd, Mhandisi, Baraka Mhagama, amesema kuwa kampuni hiyo imejipanga kutekeleza mradi ndani ya kipindi cha miaka miwili licha ya mkataba kuruhusu utekelezaji kwa miaka mitatu. Ameahidi kushirikiana kwa karibu na REA, TANESCO pamoja na viongozi wa Mkoa wa Singida ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kuleta tija iliyokusudiwa.

  


Na. Chedaiwe Msuya na Jordan Mbwambo WF, Dodoma.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti mikopo yenye riba kubwa ili kulinda wananchi dhidi ya mikopo hatarishi, ikiwemo kuimarisha usimamizi wa sekta ya fedha kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mhe. Munde alitoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Mhe. Nyakisa Sanga, aliyetaka kufahamu hatua zinazochukuliwa na Serikali kuhakikisha wananchi, hususan wafanyakazi, hawabebeshwi mzigo wa riba kubwa za mikopo.

Alieleza kuwa Serikali kwa kushirikiana na BoT imeendelea kusimamia kwa karibu taasisi za fedha ili kuhakikisha zinazingatia sheria, kanuni na miongozo ya utoaji wa mikopo.

Akijibu swali la msingi lililoulizwa kuhusu wakati ambao wafanyakazi wa Tanzania watapunguziwa riba za mikopo na kufikia asilimia 7 au 8, Mhe. Munde alisema kuwa kwa mujibu wa sera za uchumi wa nchi, riba za mikopo zinazotolewa na taasisi za fedha huamuliwa na nguvu za soko, hivyo Serikali haiwezi kuelekeza moja kwa moja taasisi hizo kuweka viwango maalum vya riba kwa kundi fulani la wakopaji.

“Riba za mikopo nchini huamuliwa na soko. Serikali ikielekeza taasisi za fedha kuweka kiwango maalum cha riba kwa wafanyakazi au mkopaji yeyote, itakuwa inakinzana na mwelekeo wa sera ya soko huria,” alisema Mhe. Munde.

Mhe. Munde alifafanua kuwa taasisi za fedha zina uhuru wa kuweka viwango vya riba vya chini ikiwemo asilimia 7 au pungufu endapo zitaona inafaa kufanya hivyo.

Aidha, wafanyakazi binafsi au kupitia waajiri wao wana fursa ya kufanya majadiliano na benki husika ili kukubaliana juu ya viwango vya riba vinavyoweza kutolewa.

Mhe. Munde alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kifedha nchini kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu na yenye tija kwa wananchi, huku ikilinda misingi ya sera ya soko huria inayotumika nchini
Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dar es Salaam Dalmia Mikaya amezindua rasmi mradi wa Elimu ya Mirathi Mashuleni ulio chini ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Mirathi Tanzania (MITA)lengo likiwa kuipeleka elimu hiyo kwa jamii ya Wilaya hiyo na Watanzania kwa ujumla.

Na Job Karongo

HALMASHAURI ya Mji Handeni imeendelea kuonyesha mafanikio katika utekelezaji wa mpango wa lishe shuleni baada ya jumla ya wanafunzi 28,047 kati ya 30,898, sawa na asilimia 91, wanaosoma shule za msingi na sekondari kuendelea kupata chakula wakiwa shule.

Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Handeni, Esther Herman, wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe kwa Robo ya Pili ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za lishe kilichohudhuriwa na viongozi wa halmashauri pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Amesema kuwa mpango huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha afya za wanafunzi, kuongeza mahudhurio shuleni pamoja na kuinua kiwango cha ufaulu kutokana na wanafunzi kuwa na umakini zaidi darasani.

Amebainisha kuwa utoaji wa chakula shuleni ni sehemu ya mkakati wa halmashauri wa kuboresha lishe kwa watoto wa umri wa shule, huku ukilenga pia kupunguza tatizo la utoro na kuongeza motisha ya wanafunzi katika masomo.

Kwa mujibu wa Afisa Lishe huyo, mafanikio ya mpango huo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya halmashauri, uongozi wa shule, wazazi na wadau wa maendeleo ambao kwa pamoja wamekuwa wakichangia upatikanaji wa chakula shuleni.

Hata hivyo, ametoa wito kwa shule na jamii kwa ujumla kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha wanafunzi wote waliosalia wanafikiwa na huduma ya chakula shuleni, kwa lengo la kufikia asilimia 100 ya wanafunzi wote katika halmashauri hiyo.

 



📌Mradi unatekelezwa kwa Miaka Mitatu


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi kabambe wa shilingi bilioni 69 wa kusambaza umeme katika vitongoji 634 utakaonufaisha wateja wa awali 20,328 Mkoani Ruvuma.


Meneja Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme wa REA, Mhandisi Deogratius Nagu amebainisha hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy Februari 02, 2026 Mkoani Ruvuma wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi watakaotekeleza mradi Kampuni ya mzawa ya Energy Services Ltd na Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Kusafirisha na Kusambaza Umeme (ETDCO) kwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Brigedia Jenerali Ahmed Abasi Ahmed.


“Tunamshukuru Rais Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi cha shilingi 69,134,982,657.9576 kitumike kusambaza umeme katika vitongoji 634 mkoani hapa na leo hii tumefika hapa kumtambulisha Mkandarasi na maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi yameanza,” amesema Mhandisi Nagu.


Akizungumza wakati wa utambulisho wa wakandarasi hao, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Ahmed ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza dhamira na maono ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vitendo na kuwataka wakandarasi hao kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.


Amesema umeme unakwenda kuongeza chachu ya maendeleo na kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi na metoa wito kwa wananchi maeneo ya mradi kuchangamkia fursa zitokanazo na mradi lakini pia kuwa waadilifu kwa kulinda na kutunza miundombinu ya umeme na pia kuwapatia ushirikiano wakandarasi.


“Tuwahakikishie Mkoa unao wataalam walio tayari kufanya kazi muda wowote, hivyo tunawahakikishia ushirikiano wa kutosha na ni wajibu wetu kuhakikisha ulinzi na usalama lakini pia wkandarasi mnapaswa kuwa waadilifu na mjikague wenyewe kwa wenyewe,” ameelekeza Brigedia Jenerali Ahmed.


Akizungumzia hali ya usambazaji umeme mkoani humo, Mhandisi Nagu amesema kuwa vijiji vyote 551 vimefikishiwa umeme na kwamba hadi sasa vitongoji 2,107 vimefikishiwa umeme kati ya vitongoji 3,691 na kwamba kazi inaendelea ya kusambaza umeme katika vitongoji 731.


Mha. Nagu amefafanua kuwa ETDCO atatekeleza mradi kwenye vitongoji 262 katika Wilaya za Mbinga na Nyasa kwa gharama ya shilingi bilioni 37.9 na huku Energy Services akitekeleza kwenye vitongoji 372 kwa gharama ya shilingi bilioni 31.2 katika Wilaya za Songea, Namtumbo na Tunduru


Amesema, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.


Pia, Mhandisi Nagu amesema mradi unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu na ameiomba Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kushirikiana na REA kufikisha elimu na taarifa sahihi kwa wananchi sambamba na kuhamasisha wananchi kuunganishiwa umeme.


Aidha, kwa upande wao wakandarasi wa mradi huo walimhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa watatekeleza mradi kwa uaminifu, uadilifu na uzalendo kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za Serikali. 






 

Stakeholders Laud Transparent Indicative Pricing System as Small Scale Output Soars


Singida

Mineral sector stakeholders in Singida Region have hailed the Singida Mineral Market as a game changer, citing significant improvements in transparency, fairness and efficiency driven by the adoption of a digital indicative pricing system.

Artisanal miners, mineral processors and traders operating in the region say the market has revolutionized mineral trade by safeguarding miners against price exploitation and quality manipulation, while strengthening trust among sector players.

Speaking at the market, a geologist from the Singida Resident Mines Office,  Mbeleye David, said the establishment of the mineral market has yielded substantial benefits for small-scale miners and traders by introducing systems that protect them from fraud related to gold quality and unfair pricing.

 David noted that before the establishment of mineral markets, Singida Region was recording very low volumes of officially traded mineral production between 100 and 200 grammes. However, through the operational mineral markets, the region is now coordinating between 50 and 60 kilogrammes of mineral output from small-scale miners, reflecting increased efficiency and stakeholder confidence in the system.

He explained that the government has put in place a robust indicative pricing mechanism aimed at protecting artisanal miners from selling minerals at undervalued prices.

“The market is equipped with a modern X-Ray Fluorescence (XRF) machine for testing gold purity, ensuring that minerals are traded based on accurate quality standards and their true market value,” said David.

He added that unlike in the past, when indicative prices were provided only for raw gold, the current system uses a digital display board showing indicative prices for various minerals, including gold, copper and silver an innovation that has enhanced transparency and eliminated loopholes for malpractice in mineral trade.

“This technology has streamlined market operations, including mineral valuation and the issuance of mineral transportation permits for both domestic and international markets, which are now processed faster and more efficiently,” he said.

Meanwhile, mineral trader   Abubakari Omary said that despite the notable progress, continuous education on the use of indicative prices is essential for miners and traders to avoid misunderstandings and disputes during transactions.

“Education remains critical to ensure every stakeholder understands their rights and obligations and conducts business based on actual market prices,” said Omary.

Stakeholders also commended the new mineral market framework for allowing unlicensed artisanal miners to register and sell their minerals directly at the markets without being required to use a trader’s licence a move that has removed a major barrier that previously limited participation in the formal mineral trade.

Overall, the Singida Mineral Market has been described as a key driver of growth in the region’s mineral sector by enhancing transparency, improving trade security and increasing government revenue through the control and prevention of mineral smuggling.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda,akizungumza wakati wa kikao cha kumtambulisha mkandarasi TIBEA Company Limited pamoja na White City International Contractors ambao wamepewa dhamana ya kusambaza huduma hio katika Vitongoji 619 vya Mkoa huo kwa kipindi cha Miaka Mitatu.

Na.Mwandishi Wetu-MWANZA

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia Bil. 66.7 kupeleka umeme katika Vitongoji 619 ambapo Kaya 19,878 zitafikiwa na Huduma hio ya Umeme wa REA.

Hayo yamesemwa leo tarehe 02/02/2026 Jijini Mwanza na Mhe. Mtanda wakati wa kikao cha kumtambulisha mkandarasi TIBEA Company Limited pamoja na White City International Contractors ambao wamepewa dhamana ya kusambaza huduma hio katika Vitongoji 619 vya Mkoa huo kwa kipindi cha Miaka Mitatu.

Mhe. Mtanda amesisitiza Mradi huu ni Mkubwa hivyo Matumaini yake kwa Wananchi wa Ukerewe,Misungwi,Magu,Sengerema na Kwimba wanakwenda kunufaika na Mradi huu hivyo amewataka wakandarasi waliopewa kazi hio kufanya kazi kwa weledi na kuepuka Vitendo vya Rushwa wakati wa kuwaunganishia Wananchi Umeme kitendo ambacho sio kizuri kwani kinaharibu taswira ya Kampuni yao na endapo itabainika Sheria itachukua Mkondo wake ikiwemo kutokupewa kazi nyingine yoyote.

“Ni Vizuri mkafanya kazi kwa Uadilifu, Mkaepuke Rukwa wakati wa kuwaunganishia Umeme Wananchi,Amesisitiza Mhe. Mtanda”.

Aidha, Mhe. Mtanda ameomba Wananchi watakaofikishiwa huduma hio ya Umeme kuwapokea Vizuri Wakandarasi, Amesisitiza ni muhimu Wakandarasi hao kushirikisha ngazi zote za Serikali mpaka kwa Walengwa Wananchi kwani itarahishisha kazi, Pia ametaka Wananchi waelezwe sifa za Mradi, utaratibu wa kuweka umeme kwenye Nyumba zao upoje ili kuepuka usumbufu na Mazingira ya Uwepo wa Rushwa hivyo ni muhimu kuwaelimisha Wananchi nia ya Serikali ni kuwahudumia wote

Kwa upande wake, Mhandisi, Seif Abduli, Mhandisi wa Miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amesema TIBEA Company Limited atahudumia Vitongoji 313 kwa Wilaya ya Sengerema na Kwimba huku gharama yake ikiwa Bil. 33.7, Kwa upande wa White City International Contractors atahudumia Vitongoji 306 Wilaya ya Ukerewe,Misungwi pamoja na Magu ambapo gharama yake ni Bil 32.7.

Mhandisi Seif amesisitiza Mradi huu ni Mkubwa na wakimkakati lengo likiwa Watanzania wanapata Umeme hivyo Serikali imeweka jitihada kubwa ambapo imeleta kifaa Maalum kinachoitwa OMETA ambapo kitawasaidia wananchi waishio Vijijini wasio na uwezo wa Kufanya Wiring kuunganishiwa umeme kupitia kifaa ili asitokee Mwananchi atakaye achwa nyuma na Huduma ya Umeme Vitongojini.

Kila mwaka nilisubiri kwa hamu kupata promotion kazini, lakini kila mwaka nilinyimwa bila sababu za kweli. Nilijisemea labda ni bahati mbaya, labda sikutosha.

Lakini baada ya muda nilianza kuona kuwa tatizo lilikuwa kubwa zaidi kulikuwa na vizuizi vilivyokuwa vikinyamazisha juhudi zangu, na wengi hawakuwa tayari kuona uwezo wangu.

Nilihisi kuchanganyikiwa, na mara nyingine hata kutojiamini.
Nilijaribu kufanya kazi kwa bidii zaidi, kushirikiana na wenzangu, na kuonyesha uwezo wangu mara kwa mara, lakini promotion bado haikujia.

Hii ilifanya moyo wangu uwe mzito, na kila siku nilipofika kazini, nilihisi kuchukuliwa kidogo. Hata hivyo, moyo wangu haukukubali kushindwa kwa urahisi.

Siku moja, niliamua kubadilisha mkondo: badala ya kusubiri watu wengine wakithamini kazi yangu, nikaamua kuanzisha jambo langu binafsi. Nilijifunza mbinu, kutafuta mwongozo, na kuwekeza muda wangu kwa hekima na busara. Soma Zaidi.
Nilimpenda kwa dhati. Nilimwamini kabisa. Nilifikiri tupo pamoja hadi mwisho. Lakini ghafla, aliniondokea. Aliniaibisha mbele ya marafiki na familia. Nilijihisi sifai, na aibu ilitupa kila kona ya moyo wangu.

Nililia, lakini hatimaye nikajikusanya. Sikupiga kelele, sikutafuta kugomana naye. Badala yake, nilijijenga kimya kimya. Nilijipenda tena. Nilijipa heshima.

Nilijaribu kuondoa maumivu yangu bila kuonyesha udhaifu kwa wengine.Soma Zaidi.
Siku ile ilianza kama nyingine yoyote. Mwanamke huyu alikuwa akihisi upweke na huzuni, lakini hakuwahi kufikiria kuwa maisha yake yangebadilika ghafla.

Bwana wa jirani wake, ambaye walikuwa marafiki wa karibu, alianza kuonyesha umakini usio wa kawaida. Mara moja, mahusiano yao yalipita mipaka isiyoelezeka.

Baada ya tukio hilo la usiku mmoja, mwanamke huyo alianza kupata ishara za ajabu. Mwili wake ulianza kubadilika kwa njia ambazo hakuweza kuelezea. Kila siku alipoamka, alijikuta akiona vitu visivyo vya kawaida, na hofu ikaanza kumshika.

Alianza kuogopa kuzungumza na familia au marafiki, kwa sababu alihisi kuwa wengine hawawezi kuelewa kilichomkuta. Hali ikawa mbaya zaidi alipogundua kuwa baadhi ya sehemu za mwili wake zilikua tofauti.

Alishindwa kuamini macho yake. Huu ulikuwa uonyesho wa jambo lisilo la kawaida, la kishirikina.Soma Zaidi.
Kwa muda mrefu, nilikuwa nikiteseka kutokana na ndoto mbaya ambazo zilirudia kila usiku. Kila ndoto ilinileta hofu, maumivu, na kuacha usiku zikiwa mbaya kuliko awali.

Nilijaribu kumshirikisha kanisa, lakini mara zote waliniambia ni sala tu au kuzisali ndoto hizi zitapita. Nilihisi kutopewa msaada halisi, na hofu ikazidiwa kila siku.

Nilijaribu njia tofauti: kutafakari, kusoma vitabu vya dini, na kujaribu kuondoa mawazo mabaya. Lakini hakukuwa na matokeo.

Ndoto zilikuwa zinapita kwa nguvu, zikiharibu usingizi wangu na hata hali ya akili yangu siku nzima. Nilihisi kama niko peke yangu, na hakuna mtu anayejua jinsi nilivyotesek. Soma Zaidi.
Nilipokuwa na ndoto ya kuanzisha biashara yangu, kila kitu kilionekana kuwa sawa mwanzoni. Nilipanga, kuwekeza muda na pesa, na kila hatua niliyochukua ilinipa matumaini.

Lakini mara kwa mara, kila jaribio langu lilishindikana. Pesa zilizopotea, mikataba iliyopotea, na wateja waliokimbia nilijikuta nikiwa na kuchanganyikiwa na kuchukizwa.

Nilijaribu kuelewa tatizo. Nilijaribu kuboresha bidhaa zangu, kushirikiana na watu sahihi, na kufanya kila jambo kwa uangalifu. Lakini kila hatua mpya ilikuwa na kizuizi.

Nilihisi kuna nguvu isiyoonekana ikipinga kila juhudi yangu. Hali hiyo iliniondaka hofu na hasira. Hatimaye, nilijua lazima nifuate njia nyingine.

Nilianza kuangalia kwa makini kila mtu aliye karibu nami. Ndipo nilipogundua ukweli wa kutisha: kulikuwa na mtu aliyekuwa akinipinga kinyume, bila mimi kujua.

Wengine waliokuwa karibu na mimi walikuwa wakijaribu kunishusha kwa siri. Kila hatua niliyokuwa nikichukua ili kusonga mbele, walikuwa wakihakikisha inashindikana.

Sikurudia makosa yale. Nilijua lazima nipate mwongozo sahihi. Soma Zaidi.



Na Mwandishi Wetu - Dodoma


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea ugeni wa viongozi wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomu Duniani (IAEA) ukiongozwa na Bwana Gashaw Gebeyehu Wolde, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kiufundi kwa Afrika, pamoja na Bi. Azza Kashlan, Afisa wa Usimamizi wa Programu.

Ziara hiyo inalenga kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na IAEA katika sekta za viwanda, afya, elimu, kilimo na chakula.

Ugeni huo, ukiwa na mwenyeji wake Profesa Najat Kassim Mohammed, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), ulianza ziara yake jijini Dodoma kwa kutembelea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ambapo walikutana na Katibu Mkuu, Mhe. Balozi Dkt. Samweli William Shelukindo.

Mazungumzo hayo yalihusu nafasi ya Tanzania katika ushirikiano wa kimataifa wa nyuklia kwa maendeleo endelevu.


Baadaye, viongozi hao walitembelea Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu, Profesa Daniel Mushi, kuhusu mafanikio ya miradi inayotumia teknolojia ya nyuklia nchini.


Aidha, walijadili maendeleo ya programu za elimu zilizoanzishwa kwa msaada wa IAEA, ambazo zinalenga kuongeza idadi ya wataalamu wa fizikia ya tiba ili kuimarisha huduma za saratani nchini.


Naibu Katibu Mkuu alibainisha kuwa ushirikiano wa Tanzania na IAEA ni wa muda mrefu na umeleta matokeo ya vitendo kupitia Programu ya Ushirikiano wa Kiufundi. Kikao hicho kilikumbusha mafanikio ya hivi karibuni, yakiwemo miradi ya kitaifa ya TC inayoendelea katika awamu ya mwaka 2025–2026 na kiwango cha juu cha maendeleo kilichoripotiwa kufikia mwisho wa Desemba 2025.


Miradi hiyo inahusu sekta za viwanda, afya, kilimo na usalama wa chakula, ikiwemo; Mradi wa kituo cha mionzi cha matumizi mbalimbali (multipurpose irradiator facility), Upanuzi wa huduma za tiba ya nyuklia na radiotherapy, Uzalishaji wa mbegu kwa njia ya mionzi (mutation breeding) kwa pamba na maharage ya kawaida, Kuimarisha uwezo wa maabara ya usalama wa chakula Zanzibar.


Katika kikao hicho, Profesa Mushi aliwasilisha mapendekezo kwa awamu ijayo ya ushirikiano, ikiwemo; Kusaidia Tanzania katika matumizi ya teknolojia za nyuklia na atomu kama sehemu ya mpango wa muda mrefu wa usambazaji wa umeme, Kuimarisha na kusasisha mitaala ya shule na elimu ya juu katika sayansi ya nyuklia na fani zinazohusiana, Kuendeleza na kuimarisha miundombinu ya maabara na uwezo wa kiufundi, Kupanua vyanzo vya nishati ili kuendana na mahitaji ya ukuaji wa taifa, Kuendelea kutoa mwongozo wa kiufundi kwa matumizi salama na yenye uwajibikaji ya teknolojia ya nyuklia.




Naibu Katibu Mkuu alisisitiza Kuimarisha ushirikiano kwenye mifumo na miundombinu, hususan katika: Uchambuzi wa uwezekano wa utekelezaji wa Mitambo Midogo ya Nyuklia (Small Modular Reactors – SMRs), Kupanua huduma za tiba ya mionzi ya saratani (radiotherapy) kwenda katika mikoa mingine, Matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika chakula na kilimo, na Usalama na ulinzi, ikijumuisha uboreshaji wa miundombinu ya usimamizi wa taka za mionzi (radioactive waste management facilities).




Naye Mkurugenzi Gashaw kutoka Wakala wa Nguvu za Atomu Duniani alipongeza mapendekezo hayo na kuthibitisha kuendelea kwa ushirikiano. Walisisitiza kuwa Tanzania imekuwa na uhusiano wa muda mrefu na shirika hilo, na sasa imefikia hatua ya ukomavu katika programu zake, huku ikichukua nafasi ya kuwa kitovu cha kikanda katika kujenga uwezo wa kitaalamu.


Mambo muhimu yaliyosisitizwa ni pamoja na; Kuendelea kuunga mkono vipaumbele vya kitaifa kupitia Programu ya Ushirikiano wa Kiufundi, Hatua za awali katika mchakato wa kuanzisha mradi wa nyuklia, ikiwemo kuimarisha taasisi, mifumo na rasilimali watu, Kutambua uongozi wa Tanzania na mchango wake katika kujenga uwezo wa kikanda, Kuendeleza matumizi ya kituo cha mionzi cha matumizi mbalimbali, Kupanua matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya taifa, Kuweka usalama na ulinzi kama msingi wa matumizi ya nyuklia, Kuendeleza rasilimali watu kupitia mafunzo ya muda mrefu katika tiba ya nyuklia na fani nyingine maalumu, huku wakihimiza wataalamu wa Kitanzania kuchangamkia nafasi zinazotolewa na IAEA.




Ugeni huo pia ulitembelea Wizara ya Nishati, ambapo ulipokelewa na Katibu Mkuu Mhandisi Felichism Mramba. Mazungumzo yalihusu hatua zilizofikiwa katika mchakato wa Tanzania kuelekea kuanzisha mradi wa umeme wa nyuklia, hatua inayolenga kuongeza vyanzo vya nishati safi na salama kwa maendeleo ya uchumi wa taifa.


Mnamo tarehe 4 Februari 2026, ugeni huo utatembelea Chuo cha Nelson Mandela cha Sayansi na Teknolojia Afrika (NM-AIST) Jijini Arusha, ambapo watajionea maendeleo ya mradi wa Green House for Beans (RAF5059). Mradi huo unatumia mbinu za nyuklia kuboresha uzalishaji wa mazao ya jamii ya kunde, ukilenga kuongeza usalama wa chakula na kipato kwa wakulima wadogo.


Ziara ya viongozi wa IAEA nchini Tanzania inaendelea kuthibitisha dhamira ya serikali ya kuendeleza ushirikiano wa kimataifa katika matumizi salama na endelevu ya teknolojia ya nyuklia. Kupitia miradi hii, Tanzania inalenga kuimarisha huduma za afya, kuongeza rasilimali watu wenye ujuzi wa kisayansi, kukuza kilimo, na kuandaa mazingira ya kuanzisha nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya taifa.