NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Zainab Katimba amesisitiza kuwa uchangiaji katika sekta ya elimu usitumike kumuadhibu mwanafunzi ambaye mzazi wake kashindwa kutoa mchango.

Mhe.Katimba ameyasema hayo leo Julai 26, 2024 akiwa katika ziara ya kukagua miundombinu ya sekta ya elimu katika mamlaka za serikali za mitaa.

Katimba amesema michango yenye kiwango kikubwa inaondoa dhana ya serikali ya elimu bila malipo, hivyo halmashauri zote zinatakiwa kufuata miongozo ya uchangishaji shuleni.

“Nimeona hapa mnautaratibu wa kuchangisha wanafunzi na mmesema mnawachangisha laki sita kwa mwaka, hiki ni kiwango kikubwa, na kimsingi kinaondoa tafsiri ya elimu bila malipo.”

“Huwezi ukamwambia mzazi au ukamwambia mtanzania kwamba elimu bila malipo, anamleta mtoto shule anakutana na mchango mikubwa na sio kila mzazi atakuwa na uwezo wa kutoa."

Kuhusu changamoto ya ukosefu wa kichomea taka na uzio, Mhe.Katimba aliielekeza halmashauri ya Mji Nzega kutumia mapato ya ndani kutatua changamoto hiyo.

Amesema dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wanapata haki ya kumaliza mzunguko wao wa elimumsingi tena bila malipo.

“Masharti ya michango hii ni kwamba wale wazazi watakaoshindwa kwasababu fulani kutoa michango hii watoto wao wasiadhibiwe kwa kuwambiwa watoto wao wasiingie shuleni. Mchango haimaanishi mtoto akose haki ya kwenda shule kwasababu amekosa mchango wakati amelipiwa ada na Mheshimiwa Dk Samia Suluhu Hassan.

Kuhusu changamoto ya uzio na kichomea taka, Katimba aliiagiza halmashauri ya Nzega kutenga fedha kupitia mapato ya ndani ili kutatua changamoto hiyo.

Naye Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji wa Nzega, Lulu Nchiha alisema wazazi wanachangia chakula chenye thamani ya Sh laki sita.










Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amewataka watumishi wa sekta ya ardhi nchini kuongeza uadilifu na kutenda haki katika utekelezaji wa majukumu yao sambamba na kuongeza kasi katika utendaji kazi.

Mhe. Ndejembi namesema, suala la ardhi ni gumu na linahitaji watumishi kuwa makini ambapo amesisitiza kuwa ni lazima watumishi wa sekta ya ardhi watende haki huku wakizingatia kuwa kuna sheria, kanuni na miongozo inayowaoongoza katika utendaji kazi.

Aidha, Mhe. Ndejembi amesema, yale yote mazuri yaliyofanywa na mtangulizi wake ikiwemo Klinik za Ardhi atayaendendeleza kwa lengo la kuleta ufanisi wa wizara.

‘’Sikuja kutengua torati, yote aliyoyaanzisha mtanguluzi wangu ikiwemo klinik za ardhi zitaendelea na vile vile anayehisi jambo lake limekwama ajitokeze na atahudumiwa’’ amesema Mhe. Ndejembi.

Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo tarehe 26 Julai 2024 wakati akizungumza na viongozi pamoja na watumishi wa Wizara ya Ardhi mkoa wa Dar es Salaam mara baada ya kutoka kuapishwa kushika nafasi hiyo kutoka kwa mtangulizi wake Mhe. Jerry Silaa.

Sambamba na hayo Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametaka kuimarishwa kwa mifumo ndani ya wizara ili migogoro ya ardhi isiendelee kujitokeza.

Mhe. Ndejembi ameapishwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akitokea Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Watu wenye ulemavu).

PIX%2B1%2B%25286%2529
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akizungumza wakati akifungua Kikao cha Watumishi wa Wizara ya Fedha kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani), kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo amewaagiza watumishi kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa mapato na kuratibu upatikanaji wa fedha ili kutoa fedha kwa wakati kwa miradi yote iliyoidhinishwa na Bunge.
PIX%2B2%2B%25285%2529
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo, akizungumza wakati akimkaribisha Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) kufungua Kikao cha Watumishi wa Wizara, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo ameeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kushirikishana masuala mbalimbali ya kiutendaji pamoja masuala mengine yanayogusa maisha ya watumishi nje ya utumishi wa Umma.
PIX%2B3%2B%25284%2529
Watumishi wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (hayupo pichani), wakati akifungua Kikao cha Watumishi wa Wizara ya Fedha kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani), kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma.
PIX%2B4%2B%25286%2529
Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa, akizungumza kwa niaba ya viongozi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha, wakati wa Kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo ameipongeza Wizara kwa kufanikisha kikao hicho kikijumuisha kwa mara ya kwanza viongozi wa Taasisi za Wizara na kutoa rai kuwa vikao hivyo vijumuishe watumishi wote wa Taasisi za Wizara ili kuwa na uelewa wa pamoja katika utekelezaji wa majukumu.
PIX%2B5%2B%25283%2529
Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali (IAG), Bw. Benjamin Magai, akizungumza jambo wakati wa Kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo ameupongeza uongozi wa Wizara kwa kuitisha kikao hicho kwa kuwa kitachochea ufanisi wa kazi.
PIX%2B6%2B%25284%2529
Mwandishi Mwendesha Ofisi Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Mwamanga, akichangia jambo wakati wa majadiliano ya Kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo kilijumuisha Menejiment ya Wizara, Wakuu wa Taasisi za Wizara a Fedha, Hazina Ndogo za Mikoa, pamoja na watumishi wa Wizara kwa ajili ya kushauriana na kubadilishana uzoefu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Wizara, Taasisi na Serikali kwa ujumla.
PIX%2B7%2B%25283%2529
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (Katikati), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo (watatu kushoto), wakifuatilia majadiliano na maswali kutoka kwa watumishi wa Wizara ya Fedha, wakati wa Kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo kilijumuisha Menejiment ya Wizara, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakuu wa Hazina Ndogo za Mikoa, pamoja na watumishi wa Wizara kwa ajili ya kushauriana na kubadilishana uzoefu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Wizara, Taasisi na Serikali kwa ujumla. Wengine katika picha ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali (IAG), Bw. Benjamin Magai (wa kwanza kushoto), Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa (wa pili kushoto), Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Madeni, Bw. Japhet Justine (wa tatu kulia), na Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), Prof. Hozen Mayaya.
PIX%2B8%2B%25281%2529
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (Katikati), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo (watatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Menejimenti ya Wizara ya Fedha, baada ya kumalizika kwa Kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo kilijumuisha Wakuu wa Hazina Ndogo, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na watumishi wa Wizara hiyo kwa ajili ya kushauriana na kubadilishana uzoefu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Wizara, Taasisi na Serikali kwa ujumla.
PIX%2B9
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (Katikati), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo (watatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Fedha, baada ya kumalizika kwa Kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo kilijumuisha Menejimenti ya Wizara, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakuu wa Hazina Ndogo, na watumishi wa Wizara kwa ajili ya kushauriana na kubadilishana uzoefu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Wizara, Taasisi na Serikali kwa ujumla.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)

Na. Saidina Msangi na Farida Ramadhani, WF, Dodoma



Watumishi wa Wizara ya Fedha wameagizwa kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa mapato na kuratibu upatikanaji wa fedha ili kutoa fedha kwa wakati kwa ajili ya kutekeleza miradi yote iliyoidhinishwa na Bunge.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Fedha kwa niaba ya Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati akifungua kikao cha watumishi na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma.

Alisema kuwa ni muhimu watumishi hao kutekeleza majukumu yao na maelekezo yanayotolewa na Serikali kwa wakati ikiwa ni pamoja na kufanyia kazi kwa wakati yatokanayo na mjadala wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2024/25.

‘‘Ni muhimu kuwa mfano katika kuzingatia miongozo ya usimamizi wa mali na fedha za Umma, hususan katika kufungamanisha mahitaji yetu na bajeti iliyoidhinishwa na Bunge pamoja na kuimarisha mfumo wa ushirikishaji, uratibu na kufanya kazi kwa karibu na wadau wetu ili kuongeza ubora wa huduma zetu kwa wateja wa ndani na nje ”, alisisitiza Mhe. Chande.

Aliwaelekeza watumishi hao kutumia taaluma zao katika kushauri na kufanya maamuzi kwa wakati kwa maslahi mapana ya Taifa pamoja na kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo ili kuimarisha mfumo wa utawala bora na utawala wa sheria.

Aidha, aliwaagiza Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, kuendelea kusimamia majukumu waliyopewa katika Taasisi wanazoongoza na kuongeza ubunifu na weledi ili kuweza kuchangia fedha katika mfuko Mkuu wa Serikali.

Alisema ni muhimu kusimamia majukumu yao kwa kuzingatia sheria na kanuni, mali na fedha za Serikali ikiwemo kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za Umma katika Ununuzi. 

‘‘Nendeni mkatekeleze kwa ufanisi Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023 na Kanuni zake pamoja na kutumia Mfumo wa NeST, tutimize viapo na wajibu wetu katika suala la usimamizi wa mali na fedha za Umma,’’aliagiza Mhe. Chande.

Mhe. Chande alitoa wito kwa watumishi hao kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na kushiriki katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura ili kuweze kutumia haki zao wakati wa uchaguzi mkuu kuchagua viongozi wanaowataka na kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo katika Taifa letu ili shughuli za kiuchumi na kijamii ziendelee kuimarika.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Naibu Katibu wa wizara hiyo Bi. Jenifa Christian Omolo alisema kuwa lengo la kikao hicho ni kushirikishana masuala mbalimbali ya kiutendaji pamoja masuala mengine yanayogusa maisha ya watumishi nje ya utumishi wa Umma.

‘‘Lengo la kujumuisha masuala ya maisha ya watumishi nje ya utumishi wa Umma ni kukumbushana kuwa sisi watumishi ni sehemu ya Umma, na pia inawezekana leo ni watumishi wa Umma lakini kesho tukawa raia kama raia wengine nje ya utumishi wa Umma’’alieleza Bi Omolo.

Akizungumzia utekelezaji wa majukumu ya wizara Bi. Omolo alisema kuwa Wizara imeendelea kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa mpango na bajeti ya 2023/24, bila kusahau changamoto mbalimbali zilizosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Alisema wizara imeendelea kutoa huduma kwa wateja kwa mujibu wa muundo na mgawanyo wa majukumu ya Serikali, kubuni na kusimamia utekelezaji wa Sera za Uchumi jumla, Fedha na Ununuzi wa Umma pamoja na kusimamia ukusanyaji wa mapato na utaratibu wa upatikanaji wa fedha kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo.

‘‘Tumeendelea kuratibu upatikanaji wa fedha na kuimarisha uhusiano wa masuala ya fedha kwa Taasisi za kikanda na Kimataifa, kutekeleza maelekezo ya viongozi na kushiriki katika shughuli mbalimbali za pamoja za kitaifa ikiwemo michezo ya Mei Mosi, SHIMIWI, maonesho ya SABASABA, Nanenane n.k;’’, alifafanua Bi. Omolo.

Kikao hicho cha wafanyakazi kilijumuisha Wakuu wa Hazina Ndogo, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na watumishi wa wizara hiyo kwa ajili ya kushauriana na kubadilishana uzoefu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Wizara, Taasisi na Serikali kwa ujumla.

Naye Mtakwimu Mkuu wa Serikali Bi. Albina Chuwa ameipongeza wizara kwa kufanikisha kikao hicho kikijumuisha viongozi wa Taasisi za wizara na kutoa rai kuwa vikao hivyo vijumuishe watumishi wa Taasisi za wizara ili kuwa na uelewa wa pamoja katika utekelezaji wa majukumu.



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karatu Ndg.Juma Hokororo amekemea uzembe wa muhandisi, mafundi pamoja na wasimamizi wazembe wa miradi inayotekelezwa katika kituo cha afya buger baada ya kusuasua kwa miradi hiyo.

Mkurugenzi ametoa maelekezo hayo akizungumza na wakuu wa idara katika eneo la kituo hicho alipofika kukagua utekelezaji wa miradi hiyo ambayo ni jengo la mama na mtoto, vyoo matundu matatu, kichomea taka pamoja na mnara wa tenki. 

Ambapo akikagua miradi hiyo amebaini kuwa uzembe mkubwa unafanyika katika jengo la mama na mtoto ambalo lilitakiwa kukamilika mapema lakini mpka sasa lionekana kutofikia hatua ya kuridhisha.

Amemuelekeza Mhandisi wa halamshauri pamoja na Msimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanamtafuta fundi mwingine haraka ili kukamilisha mradi huo kwa ubora na kwa wakati. 

Miradi hiyo inayotekelezwa katika kituo hicho cha afya ni fedha kutoka mradi wa miundombinu ya maji SWASH pamoja na fedha za ndani kutoka halmashauri ambapo ni zaidi ya milion 250 za kitanzania.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa ameelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri wasitoke katika vituo vyao vya kazi wakati wa vikao vya Kamati ya Fedha, Bajeti pamoja na vile vya Usalama ili kusimamia kikamilifu masuala muhimu ya maamuzi na kudhibiti upatikanaji wa hati chafu katika Halmashauri.

Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo wakati wa kikao kazi chake na wakuu wa wilaya wote nchini kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha mkoani Pwani.

“Inaonekana sababu kubwa ya halmashauri nyingi kupata hati chafu ni kitendo cha baadhi ya Wakurugenzi kushindwa kusimamia masuala ya fedha na kutelekeza jukumu hilo kwa maafisa wa fedha na kukaimisha Ofisi kila wakato, hivyo kuanzia sasa mkurugenzi yeyote asitoke kwenye kituo chake cha kazi wakati wa vikao vya masuala ya fedha,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Mhe. Mchengerwa amewataka Wakuu wa Wilaya kutoa taarifa iwapo Mkurugenzi yeyote atatoka katika kituo chake cha kazi wakati wa vikao vya kujadili masuala muhimu ya mipango na bajeti vikiendelea na hasa kwenye vikao vya kamati za fedha pamoja na vya kamati za usalama.

“Katibu Mkuu sitegemei kusikia Mkurugenzi wa Halmashauri anatoka kituoni bila kumpatia taarifa Mkuu wa Wilaya kwani Mkurugenzi anapaswa kushirikiana kiutendaji na Mkuu wa Wilaya, hivyo naamini hilo halitatokea baada ya kikao hiki,” Mhe. Mchengerwa amehimiza.

Aidha, Mhe. Mchengerwa amewataka Wakuu wa Wilaya hao kuzingatia mipaka ya madaraka yao kwani wao ni kiungo muhimu cha kuimarisha ushirikiano miongoni mwa viongozi na watendaji wa taasisi zote zilizopo katika ngazi ya wilaya na halmashauri.

“Katika kutekeleza majukumu yenu mnapaswa kuzingatia mipaka yenu ya utendaji kazi na hatua mtakazochukua zizingatie Kanuni, Sheria, Miongozo na Taratibu zilizopo katika Utumishi wa Umma ili mjiepushe na changamoto ya ulevi wa madaraka,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amefanya kikao kazi cha siku mbili na Wakuu wa Wilaya zote nchini katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani ambacho kilicholenga kuhimiza uwajibikaji kwa viongozi hao.

 2B9A8831

Mshauri wa Ubora wa Huduma za Afya Mradi wa Afya Hatua THPS Makao Makuu, Agnes Kirato (kushoto) akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha kuhusu huduma za afya zinazotolewa na THPS
2B9A8878
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha (kushoto) akiipongeza THPS kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuimarisha afya za wananchi pamoja na kuwapatia elimu ya kujikinga na maradhi mbalimbali alipotembelea Banda la THPS wakati wa maadhimisho ya kampeni ya "Afya Yangu, Haki Yangu" iliyopewa jina la Afya Code Clinic Mkoani Shinyanga yaliyofanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga Julai 25,2024. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
2B9A8839
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha (kushoto) akizungumza alipotembelea Banda la THPS 
2B9A8852
Meneja Programu wa THPS Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Amos Scott  akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha (kushoto) kuhusu huduma za afya zinazotolewa na THPS


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Siku ya Afya Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 7 Aprili. Mwaka huu, wadau wanaadhimisha siku hiyo kwa kuendesha kampeni ya "Afya yangu, Haki yangu"  ili kupigania haki ya kila mtu kupata huduma bora za afya.

Mkoani Shinyanga shughuli za kuadhimisha siku hiyo zinafanyika katika viwanja vya Kambarage kuanzia tarehe 24 hadi 27 Julai 2024 kupitia Kampeni iliyopewa jina la Afya Code Clinic iliyoandaliwa na kuratibiwa na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga  kwa kushirikiana na wadau wa afya.

Kupitia mradi wa Afya Hatua unaofadhiliwa na Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR), kupitia Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Marekani (CDC), Tanzania Health Promotion Support (THPS) inashiriki katika maadhimisho hayo kwa kutoa elimu na huduma za afya kwa wakazi wa Shinyanga.

Akizungumza wakati wa Maadhimisho hayo yanayoratibiwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Meneja Programu wa THPS Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Amos Scott amesema maadhimisho hayo yanayoshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo watoa huduma za afya, watekelezaji wa miradi na vyuo vya afya yanalenga kuhamasisha tabia ya kutafuta huduma za afya na kutoa huduma bora za afya kwa wakazi wa Shinyanga.

Dkt. Scott amesema katika maadhimisho hayo,THPS inatoa huduma za kupima VVU, afua za kinga, uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
2B9A8704
Meneja Programu wa THPS Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Amos Scott.

Dkt. Scott amesema THPS katika Mkoa wa Shinyanga inahudumia zaidi ya Wapokea huduma za VVU 71,183 katika vituo 92 vya Tiba na Matunzo ambapo asilimia 99% kati yao wameweza kufubaza Virusi vya UKIMWI lakini pia THPS kwa Kushirikiana na Serikali katika kipindi cha Oktoba 2023 - Juni 2024 imetoa huduma ya upimaji wa VVU kwa watu 211,763 na kati yao zaidi ya 4077 walikutwa na maambukizi ya VVU na wote wamewaunganisha katika huduma za tiba na matunzo.

Ameeleza kuwa katika kipindi cha Oktoba 2023 hadi Juni 2024, wapokea huduma 21,759 walipimwa saratani ya mlango wa kizazi, ambapo 563 waligundulika kuwa na viashiria vya saratani hiyo na 552 kati yao walipatiwa matibabu.

“Tunaendelea kuwaokoa akina mama dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi. Tunaomba wanawake wajenge tabia ya kupima afya zao kwani saratani nyingi zikiweza kufanyiwa uchunguzi wa awali zinatibika, isipotibiwa mapema ni ngumu kutibiwa”,amesema Dkt. Scott.

Kadhalika, amesema THPS hutoa huduma za afya mahususi kwa vijana. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Juni 2024, mradi wa Afya Hatua umetoa huduma kwa vijana 4,027 wanaoishi na VVU ambapo 3,082 ni wanawake na 1,125 ni wanaume. THPS inafanya kazi na vituo mbali mbali vya kutolea huduma za afya ili kuhakikisha matumizi sahihi ya dawa za kufubaza VVU kwa wapokea huduma.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, akiwa katika banda la THPS, amewapongeza wadau hao kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuimarisha afya za wananchi pamoja na kuwapatia elimu ya kujikinga na maradhi mbalimbali.
2B9A8849
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha.

"Kwanza niwapongeze kwa kazi kubwa mnayofanya na sisi tunawashukuru , ni vizuri kuwa na maeneo kama haya kwa maana ya kwamba tunataka watu wakimbilie kwenye maeneo yanayotoa elimu kwa sababu elimu ndiyo tiba ya kwanza halafu kupima ni tiba ya pili halafu inayofuata kushauriwa ya tatu ni matibabu. Kama watu wangetumia muda mwingi kupata elimu mambo mengi tungeweza kuyaepuka",amesema Mhe. Macha.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga amewakumbusha wananchi kuwa ugonjwa wa UKIMWI bado upo na magonjwa mengine yanayoambukizwa kwa njia ya ngono ikiwemo Homa ya Ini yapo hivyo vijana wawe makini wachukue hatua za kujikinga lakini pindi wanapobainika kuwa na maambukizi ya VVU wazingatie matumizi ya dawa za kufubaza makali ya VVU.

"Nimeona THPS mnafanya huduma ya Tohara Kinga kwa wanaume. Ndugu zangu Tohara Kinga siyo jambo la siri wananchi jitokezeni kupata tohara Kinga",amesema Mhe. Macha.


Kuhusu THPS

Tanzania Health Promotion Support (THPS) ni asasi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa mwaka 2011, chini ya Sheria ya asasi zisizo za kiserikali nambari 24 ya 2002.

THPS inafanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara za Afya za Tanzania Bara na Zanzibar; Wizara ya Jinsia, Vijana, Wazee na Makundi Maalum; Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Kwa ufadhili wa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Misaada ya UKIMWI (PEPFAR) kupitia Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (U.S. CDC), THPS inatekeleza afua mbalimbali za VVU/UKIMWI; Kifua Kikuu; kuzuia ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto; huduma za afya ya uzazi, uzazi, watoto wachanga, watoto na vijana; mifumo ya habari ya maabara na usimamizi wa afya, na UVIKO-19.

Kuhusu mradi wa CDC/PEPFAR Afya Hatua (Oktoba, 2021- Septemba, 2026)

Mradi huu unalenga kutoa huduma jumuishi katika vituo vya afya (Kigoma, Pwani, Shinyanga na Tanga) na katika jamii (Kigoma, Pwani na Tanga).

Huduma hizi ni pamoja na matibabu na matunzo ya watu wanaoishi na VVU, huduma za kitabibu za tohara kwa wanaume katika mikoa ya Kigoma na Shinyanga na programu ya DREAMS kwa wanawake katika mkoa wa Shinyanga.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
2B9A8837
Mshauri wa Ubora wa Huduma za Afya Mradi wa Afya Hatua THPS Makao Makuu, Agnes Kirato (kulia) akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha kuhusu huduma za afya zinazotolewa na THPS
2B9A8833
Mshauri wa Ubora wa Huduma za Afya Mradi wa Afya Hatua THPS Makao Makuu, Agnes Kirato (kulia) akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha kuhusu huduma za afya zinazotolewa na THPS
2B9A8907
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda la THPS linalotoa huduma rafiki kwa vijana ikiwemo upimaji wa VVU, uchunguzi wa magonjwa ya ngono, utoaji wa dawa Kinga (PrEP), uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza na uchunguzi wa kifua kikuu
2B9A8905
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda la THPS linalotoa huduma rafiki kwa vijana ikiwemo upimaji wa VVU, uchunguzi wa magonjwa ya ngono, utoaji wa dawa Kinga (PrEP), uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza na uchunguzi wa kifua kikuu
2B9A8895
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda la THPS linalotoa huduma rafiki kwa vijana ikiwemo upimaji wa VVU, uchunguzi wa magonjwa ya ngono, utoaji wa dawa Kinga (PrEP), uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza na uchunguzi wa kifua kikuu
2B9A8896
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda la THPS linalotoa huduma rafiki kwa vijana ikiwemo upimaji wa VVU, uchunguzi wa magonjwa ya ngono, utoaji wa dawa Kinga (PrEP), uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza na uchunguzi wa kifua kikuu
2B9A8886
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda ya THPS linalotoa huduma za upimaji wa VVU
2B9A8892
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda ya THPS linalotoa huduma za upimaji wa VVU
2B9A8883
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa katika banda ya THPS linalotoa huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama
2B9A8690
Wananchi wakiendelea kupata huduma kwenye banda ya THPS linalotoa huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama
2B9A8683
Huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama zikiendelea katika Banda la THPS
2B9A8678
Huduma za afya zikiendelea kutolewa katika Banda la THPS
2B9A9000