Majirani walidhani nina roho ya subira, lakini ukweli ni kwamba nilikuwa nimekufa ndani kwa ndani. Kwa miaka sita, nilibeba ndoa iliyojawa na fedheha, matusi, na kunyanyaswa. Mume wangu alikuwa mtu wa hasira za ghafla.
Angeweza kurudi usiku wa manane, anuke pombe, na anichape kwa sababu tu nilikuwa nimelala mapema. Hakuna aliyejua machungu yangu, maana nilijificha nyuma ya tabasamu.
Kila nikiomba ushauri kwa mama au dada zangu, walinambia “vumilia, ndoa ni uvumilivu.” Nilijaribu. Nilikaa kwa ajili ya watoto. Nilikaa kwa sababu sikuwa na kazi wala uwezo wa kujitegemea.
Lakini kilichoniumiza zaidi ni kwamba hata nilipojaribu kuzungumza naye, hakuwa tayari kusikiliza. Alikuwa akinidharau, akinita mjinga, na kila mara alinisuta kwa kusema mimi si kitu bila yeye. Soma zaidi hapa
Post A Comment: