Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni  Mapesa amewataka viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kutambua kuwa Uongozi ni utumishi wa kuwatumikia watu na si kutumikiwa, kwani kazi ya kiongozi ni kuwa tayari muda wote kutatua changamoto mbalimbali.

Mapesa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwapisha viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kwa mwaka 2026/27 pamoja na mambo mengine amepongeza Uongozi wa Serikali  iliyomaliza muda wake iliyokuwa ikiongozwa na Magashi Magina  kuwa walizingatia Weledi wa hali ya Juu.

Mkuu huyo wa Taasisi ameitaka Serikali mpya kuzingatia misingi ya Uongozi, na kuwa na namna bora ya kutatua changamoto ikiwa ni pamoja na kushirikiana vyema na Serikali ya Wanafunzi ambayo imemaliza muda wake, huku akiwaahidi ushirikiano wa dhati kutoka kwa Uongozi wa Chuo.

Kwa upande wake, Rais aliyemaliza muda wake Magashi Magina ameishukuru Menejimenti ya chuo kwa ushirikiano alioupata katika kipindi chote cha uongozi wake, ameeleza kuwa mafanikio yote yaliyopatikana yalitokana na uwazi na utayari wa Menejimenti kusikiliza na kutatua Changamoto mbalimbali za Wanafunzi jambo lililorahisisha utendaji kazi wa serikali yake.

Nao, Viongozi wapya walioapishwa kuiongoza Serikali ya Wanafunzi , Rais ni Samir Naseer na Makamu wa Rais  Julieth Mandia  wametoa shukrani za dhati kwa Wanafunzi wote kwa kuonyesha imani kwao na kuwachagua kuongoza Serikali ya wanafunzi ambapo wameahidi kuongozi kwa Uadilifu, Amani, mshikamano kwa  kushirikiana na Menejimenti ya Chuo pamoja na Serikali ya Wanafunzi iliyomaliza muda wake.

 

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

28.05.2026

Share To:

Post A Comment: