KAIMU Katibu Tawala Mkoa wa Pwani (RAS), Bi. Salvera Salvatory ameishauri Bohari ya Dawa (MSD) kuwa na mikakati endelevu ya kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya ili kuondoa malalamiko kwa wananchi ambayo kwa kiasi kikubwa yameanza kupungua.

Bi Salvatory ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa MSD Kanda ya Dar es Salaam na wadau wake wa Mkoa wa Pwani uliofanyika Kibaha Julai 6, 2023.

“Wananchi wanafarijika sana wanapofika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya wakapatiwa Dawa zote walizoandikiwa”

Kiongozi huyo amekiri kuvutiwa na MSD kuwa na kitengo cha Huduma kwa Wateja, ambao ndio hufanya mawasiliano kwa karibu na wadau na wateja, ambapo amewashauri kuhakikisha wanafuatilia malalamiko ya wateja na namna yanavyoshughulikiwa.

 Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji na Miradi wa MSD Victor Sungusia ameeleza kuwa usambazaji wa bidhaa za afya mara sita kwa mwaka umesaidia kuongeza hali ya upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Kwa upande wake Meneja wa Kanda ya MSD Betia Kaema ameahidi kufanyia kazi maazimio yote yaliyoazimiwa kwenye kikao hicho huku akisisitiza ushirikiano na mawasiliano ya mara kwa mara na wadau hao.


Wadau wa MSD wakiwa kwenye mkutano huo

Mkutano ukiendelea


Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji na Miradi wa MSD,  Victor Sungusia  akiwa kwenye mkutano huo

Wadau wakiwa kwenye mkutano huo.

 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: