Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Siuluhu Hassan, akizungumza alipotembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia), akimsikiliza Meneja wa Ofisi ya Zanzibar ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Mariam Saleh, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026 (Kizimkazi Festival 2026) Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kushoto), akimsikiliza Meneja wa Ofisi ya Zanzibar ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Mariam Saleh, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026 (Kizimkazi Festival 2026) Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.
Zanzibar, Agosti 12, 2026
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) katika Maonesho yanayoambatana na Tamasha la 10 la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Katika ziara hiyo, Mhe. Rais Samia amepongeza PSSSF kwa kushiriki katika maonesho hayo na kutoa huduma pamoja na elimu kwa wanachama na wananchi wanaotembelea banda la Mfuko.
Mhe. Rais Samia alipokelewa na Meneja wa PSSSF Ofisi ya Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, ambaye alimueleza kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko, pamoja na namna wanachama na wananchi wanavyonufaika na huduma hizo kupitia banda hilo.
Mhe. Rais Samia ameupongeza Mfuko kwa utoaji wa huduma na kusisitiza umuhimu wa kusikiliza na kushughulikia kwa wakati changamoto zinazowasilishwa na wananchi na wanachama.
“Nawapongeza sana kwa huduma nzuri. Kama kuna malalamiko, yakusanyeni na muyafanyie kazi,” ameagiza Mhe. Rais Samia.
Ushiriki wa PSSSF katika Tamasha la Kizimkazi unalenga kuendelea kuwafikia wanachama na wananchi kwa kuwapatia elimu kuhusu hifadhi ya jamii, huduma zinazotolewa na Mfuko pamoja na kuwawezesha kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu mafao na huduma za PSSSF.
Mwisho




Post A Comment: