Jumuiya ya wanafunzi  Taasisi ya elimu ya juu Tanzania, vyuo vya kati na vyuo vikuu Mkoa wa Tabora wameiomba serikali kuendelea kutoa fursa za ajira, kutambua na kukuza vipaji vya watoto wenye ulemavu Nchini.

Kauli hiyo imetolewa na makamu wa Rais mstaafu wa serikali ya wanachuo katika chuo kikuu kishiriki cha Askofu mkuu Mihayo Tabora, Jojina  Nyamboko baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto wenye ulemavu wanaolelewa katika kituo cha Buhangija jumuishi katika Manispaa ya Shinyanga.

Akizungumza kwa niaba ya Rais wa jumuiya ya wanafunzi Taasisi ya elimu ya juu Bi. Maria Thomas, Jojina Nyamboko ambaye pia ni kamishna wa watu wenye mahitaji maalum TAHLISO ameiomba serikali kuwatambua watu wenye ulemavu kwa nafasi, vipaji  na uwezo wao hasa wale wanaohitimu katika vyuo mbalimbali Nchini.

“Ombi langu kwa serikali tujaribu kuwatambua watu wenye mahitaji maalum kwa nafasi zao na uwezo wao wapo watu wanamaliza vyuo wanauwezo kwahiyo namuomba mama yetu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akumbuke kwamba hawa watu wenye mahitaji maalum kwa vile wanavipaji tofauti tofauti hata anavyokuwa anatoa teuzi akumbuke pia kuwaweka watu wenye mahitaji maalum wakiwa pale ni mkuu wa Mkoa, mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wataendelea kuhamasisha watu wenye mahitaji maalum wengine kujitokeza na kuendelea kusoma ili wapate taaluma mbalimbali na kuendelea kuisaidia jamii”.Amesema Jojina

Ametaja malengo mbalimbali yaliyosababisha wanavyuo hao kufika na kutoa msaada katika kituo hicho kwamba ni pamoja na kuwahamasisha kuhusu umuhimu wa kusoma na kujifunza ili waweze kufikia malengo yao, kuwaonyesha upendo watoto hao, kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia katika kujenga jamii jumuishi.

Aidha kamishna wa watu wenye mahitaji maalum TAHLISO Georgina Nyamboko ametumia nafasi hiyo kuipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha miundominu ya elimu kwenye vituo vya wanafunzi wenye mahitaji maalum Nchini.

Wakizungumza na wanafunzi hao baadhi ya viongozi wa vyuo wametumia nafasi hiyo kuwasisitiza kuongeza juhudi katika masomo ili waweze kukabiliana na mazingira ya sasa yanayohitaji wasomi na wataakam waliobobea.

Katika ziara hiyo wameongozana na wanachuo wenye mahitaji maalum kutoka Mkoa wa Tabora ambapo pia pamoja na mambo mengine wametoa elimu ya namna ya kukabiliana na changamoto za mmomonyoko wa maadili ili kuepuka vitendo vya ukatili ikiwemo ubakaji na ulawiti.

“Tumeona pia tutoe elimu namna ya kukabiliana na changamoto ya kuporomoka kwa maadili hasa ya vijana, tumeona sahzi maporomoko ya maadili yamekuwa mengi hasa ubakaji, uvutaji wa madawa ya kulevya pamoja ya ushoga wao kama watu wenye changamoto unakuta mwengine haoni je anawezaje kuishi kwenye jamii hii ambayo imeporomoka kwenye maadili”.amesema Jojina

Akizungumza kwa niamba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga , Afisa elimu Halmashauri hiyo Mwalimu Wingwila Kitila ameshukuru na kuwapongeza wanachuo hao kwa kuguswa na changamoto zilizopo kwenye kituo cha Buhangija jumuishi.

Jumuiya ya wanafunzi  Taasisi ya elimu ya juu Tanzania, vyuo vya kati na vyuo vikuu Mkoa wa Tabora wamefanya ziara ya kuwatembelea wa shule ya msingi Buhangija ambapo wametoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo Sabuni, Dawa za mswaki, Madafutari, Taulo za kike, Viatu, Juice pamoja na kupanda miti 50 katika eneo la shule hiyo.

Kamishna wa watu wenye mahitaji maalum TAHLISO Jojina  Nyamboko ambaye pia ni makamu wa Rais mstaafu wa serikali ya wanachuo katika chuo kikuu kishiriki cha Askofu mkuu Mihayo Tabora akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo madaftari na Taulo za kike katika kituo cha watoto wenye mahitaji Buhangija mjini Shinyanga.

Kamishna wa watu wenye mahitaji maalum TAHLISO Jojina  Nyamboko ambaye pia ni makamu wa Rais mstaafu wa serikali ya wanachuo katika chuo kikuu kishiriki cha Askofu mkuu Mihayo Tabora akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo madaftari na Taulo za kike katika kituo cha watoto wenye mahitaji Buhangija mjini Shinyanga.

Akizungumza kwa niamba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga , Afisa elimu Halmashauri hiyo Mwalimu Wingwila Kitila ameshukuru na kuwapongeza wanachuo hao kwa kutoa msaada.

Hafla ya kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga ikiendelea.

Hafla ya kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga ikiendelea.

Hafla ya kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga ikiendelea.

Zoezi la  kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga likiendelea.

Zoezi la  kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga likiendelea.

Zoezi la  kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga likiendelea.

Zoezi la  kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga likiendelea.

Zoezi la  kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga likiendelea.

Picha ya pamoja baada ya kukabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji shule ya Buhangija Mjini Shinyanga.


Share To:

Misalaba

Post A Comment: