NA DENIS CHAMBI, TANGA.

JESHI la Polisi mkoa wa Tanga katika kukabiliana na  uhalifu ,wahalifu pamoja na kupiga  vita matumizi ya madawa ya kulevya limekuja na michauano ya mpira wa miguu kwa vijana waliopo ndani ya halmashauri ya jiji la Tanga inayotarajiwa kuanza kurindima ifikapo July 8, 2023.

Michauano hiyo inayotarajiwa kuzihusisha zaidi ya timu 20 kutoka katika mitaaa ya viunga vya jiji la Tanga ambapo itachezwa kwa mfumo wa mtoano na kwa upande  wa zawadi mbalimbali zitatangazwa hapo baadaye kwa bingwa wa mwaka huu 2023 pamoja na washindi wengine.

Akizungumza wakati wa kikao cha pamoja na wawakilishi  wakiwemo viongozi wa timu  zitakazo shiriki  michauano hiyo kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Tanga  Henry Mwaibambe amesema  wamelenga kupitia mashindano hayo ujumbe wa kupinga na kupiga Vita matumizi ya madawa ya kulevya umfikie kila mmoja popote pale alipo ili kizazi kijacho kiwe salama na kishiriki katika ujenzi wa Taifa 

Aidha alisema pamoja na kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya ni wajibu wa kila raia kuhakikisha anashiriki kikamilifu katika masuala mazima ya ulinzi na usalama wakishirikiana na vyombo vya dola katika kuwabaini wale wote wanaovunja sheria na waharifu  

" Mimi ni muumini sana wa usalama na lengo letu sisi hapa sote ni kwaajili ya usalama wetu, usalama wa maisha ya mwanadamu ndio kila kitu duniani athari za uhalifu  zinaweza kumkuta yeyote yule na mahali popote hivyo naomba sana kupitia mashindano haya tushirikiane  kuwabaini wahalifu" 

Akizungumza Polis jamii Frank Kipengele alisema ili kupata madhumuni na malengo ya ligi hiyo itachezwa mtaa husika wenye kila timu ili kuweza kuwafikia walengwa ambao ni wananchi na itakapofika siku ya fainali watachagua uwanja wenye watu wengi.

"Kwenye mechi ya ufunguzi tutatafuta kiwanja ambacho tutakiona kitakuwa na  washiriki wengi  na kitakuwa na watu wengi sana ambao tutaweza kuongeza nao kwenye siku ya ufunguzi  na viongozi tutawajulisha  lakini kwa mechi nyingine tutazipanga kwenye viwanja  ambavyo timu husika zinatoka na wala sii sehemu nyingine zozote "

" Utaratibu wa mashindano utakuwa ni wa mtoano mpaka tunafika robo fainali Kwenye fainali pia tutatafuta kiwanja ambacho kitakuwa na watu wengi kwaaajili ya kutangaza adhima ya mashindano haya  na kuhusu kiingilio tutakaa na viongozi tim husika  tunafanya viingilio ili timu zione thamani ya mashindano haya" alisema Kipengele


Share To:

Post A Comment: