Jamii  imeaswa  kupanda miti yenye kutunza uoto wa asili na kuhifadhi mazingira kwa ujumla ilikuendana na mabadiliko ya  tabia nchi  yanayo endelea kuikumba dunia kwa ufanyaji  wa shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya vyanzo vya maji na yaliyo hifadhiwa ambapo shughuli hizo za kibinadamu zinazofanywa husababisha athari za kimazingira kama ukosefu wa mvua na ukame katika maeneo mengi ya nchi. 

Mkuu wa wilaya ya Mafia Mkoani pwani Injinia Martine Ntemo  ameyasema hayo alipo tembelea banda la wakala wa huduma za misitu Tanzania  katika maonyesho ya wakulima , wavuvi na wafugaji  nanenane kanda ya mashariki yenye mikoa minne ya Tanga, Pwani , Dar es salaam na mwenyeji Morogoro. 

Dc Martine  Ntemo  amewataka wakala wa huduma za misitu tanzania (TFS)  kuendelea  kutoa elimu kwa wananchi  juu ya  utunzaji na uhifadhi  wa mazingira  kwa  upandaji wa miti  ilikuepukana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ya nayoendelea kuikumba dunia kwa sasa.

Pia amewaomba wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) kuendelea kuhamasisha upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali ya nchi  na uhifadhi wa mazingira kwa kutunza vyanzo vya maji ilikuepukana na mabadiliko ya tabia nchi yaliyo sababishwa na shughuli za kibina damu.  

Kwa upande wa Meneja msaidizi  kanda ya Mashariki msimamizi wa rasilimali  za misitu  amesema wao kama wakala wa  huduma za misitu tanzania wanaendelea kupanda miti katika mashamba yao na kuzalisha miti ambayo  hutolewa kwa wananchi  ilikupanda katika maeneo yao  hivyo amewaom ba wananchi luendelea kutunza   mazingira kwa kupanda miti  katika maeneo yao.     

Share To:

Post A Comment: