Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa pili kushoto), akiwasili katika viwanja vya shule ya Msingi Katesh B Wilayani Hanang’, mkoani Manyara, katika kilele cha siku ya maadhimisho ya Idadi ya Watu Duniani, wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Makongoro Nyerere.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya watu na Makazi itakayfanyika tarehe 23 Agostu, 2022 ili kupata takwimu sahihi za idadi ya watu ili kurahisisha mipango ya maendeleo, wakati wa kilele cha siku ya maadhimisho ya Idadi ya Watu Duniani, Wilayani Hanang’, mkoani Manyara.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiteta jambo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), Bw. Mark Bryan Schreiner, wakati wa kilele cha siku ya maadhimisho ya Idadi ya Watu Duniani, ikliyofanyika kitaifa Wilayani Hanang’, mkoani Manyara.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Frederick Sumaye, wakiangalia alizeti iliyozalishwa kwa kutumia mbegu ya kisasa, wakati wa kilele cha siku ya maadhimisho ya Idadi ya Watu Duniani, iliyofanyika kitaifa Wilayani Hanang’, mkoani Manyara.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akicheza ngoma ya kikundi cha utamaduni cha kabila la Kibarbaig cha Gehandu kutoka Wilaya ya Hanang mkoani Manyara, wakati wa maadhimishi ya kilele cha siku ya Watu Duniani, iliyofanyika kitaifa Wilayani Hanang mkoani Manyara.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Lawrence Mafuru, wakifurahia jambo na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Mipango ya Kitaifa wa Wizara hiyo, Bw. Royal Lyanga, wakati wa kilele cha siku ya maadhimisho ya Idadi ya Watu Duniani,iliyofanyika Wilayani Hanang’, mkoani Manyara.
Share To:

Post A Comment: