Na John Walter-Babati

Mkuu wa wilaya wa Babati  Lazaro Twange amesema kuwa haridhishwi na utendaji kazi  wa Mratibu wa sensa aliepo sasa kutokana na utendaji wake dhaifu wa kazi katika kuhamasisha watu kushiriki vyema katika sensa ya mwaka huu.

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya mji wa Babati Twange ameiagiza Halmashauri hiyo kuona hatua zinazofaa kuchukuliwa ila yeye hayupo tayari kufanya kazi na mratibu huyo.

Serikali imepanga kufanya sensa ya watu na makazi ifikapo tarehe 23  Agosti 2022 ambapo kitaifa  hufanyika kila baada ya miaka 10  ambapo  mara ya mwisho kufanyika sensa ni mwaka 2012 .

Amesema kuwa Sensa ya watu na makazi itaisaidia serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidi mchakato wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025 pamoja  na ufuatiliaji wa ajenda za maendeleo  za kimataifa .

Pia amesema takwimu sahihi  za sensa zinahitajika kwa ajili ya ugawaji  wa majimbo ya uchaguzi kwa ufanisi  pamoja na  kurekebesha mipaka ya kiutawala katika serikali za mitaa katika wilaya ya Babati.

Amewataka wananchi wa wilaya hiyo kujiandaa kuhesabiwa ifikapo mwezi Agosti na kutoa ushirikiano kwa maafisa watakaokuwa wanapita kuchukua taarifa kwenye maeneo yao.


Share To:

Post A Comment: