Bunge wa viti maalum mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) DR Ritta Kabati akitoa msaada wa vifaa vya walemavu wa viongo lengo likiwa ni kuunga mkono Bunge wa viti maalum mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) DR Ritta Kabati. (PICHA KUTOKA MAKTABA)
Na
Fredy Mgunda,Iringa.
BUNGE
wa viti maalum mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) DR Ritta
Kabati amesema kuwa Mheshimiwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaheshimisha
wanawake kwa utendaji wake wa kazi katika kuliongoza Taifa la Tanzania.
Akizungumza
na blog hii mbunge huyo DR Kabati alisema kuwa toka ameteuliwa kuwa Rais wa
Tanzania amefanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo na kuonyesha kuwa yeye ni
kiongozi bora ambaye anaweka kulifikisha taifa hili katika nchi ya ahadi.
Dr
Kabati alisema kuwa Rais Samia toka ameingia madarakani amefanikiwa kuwaamini
wanawake katika utendaji wa nyazifa za ngazi ya juu na wanawake hao wamekuwa
wanafanya kazi hizo vizuri tofauti na ilivyokuwa kwenye fikra za watanzania
wengi.
“Lakini
Mheshimiwa Rais mwanamke huyu ametupa upendeleo na ametuamini sana wanawake
wenzie na ametoa nafasi nyingi za upendeleo kwa wanawake ambao wanauwezo wa
kuongoza nafasi hizo na wanamsaidia kweli kweli” alisema Dr Kabati
Alisema
kuwa kuna mawazi wengi wanawake ambao wamekuwa wanafanya kazi kubwa ya kuleta
maendeleo kwenye wizara zao kama vile waziri wa ulinzi,waziri wa afya,waziri wa
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na
manaibu mawaziri wengi kwenye wizara mbali mbali na wanafanya kazi vizuri.
DR
Kabati alisema kuwa kuna wakuu wa wilaya,wakuu wa mikoa, maneja na wakurugenzi wanawake wengi na wamekuwa
wanafanya kazi nzuri ya kumsaidia Mheshimiwa Rais kuleta maendeleo kwa
watanzania.
Alisema
kuwa katika maeneo ambayo wanawake wamepewa nafasi ya kuongoza kumekuwa na
mabadiliko ya haraka ya kimaendeleona yanaonekana kutokana na wanawake wengi
wamezaliwa kuwa viongozi toka wakiwa kwenye ngazi ya familia.
Dr
kabati alisema kuwa watanzania wanatakiwa kuendelea kumuamini na kumuunga mkono
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta
maendeleo kwa wananchi wa Tanzania.
Alisema kuwa kwa kipindi cha
mwaka mmoja wa madaraka yake amefanikisha miradi mingi na mikubwa ya
kimaendeleo kwa wananchi na kuwapunguzia adha ya kuchangia maendeleo kwa kiasi
kikubwa.
Dr Kabati alimazia kwa kusema
kuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa
mwaka mmoja tu amefanya mabadiliko makubwa ya kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzania
na atakiwa kuendelea kupewa heshima anayostahili.
Alisema kuwa Rais Samia ameondoa mateso ya Bodi ya
Mikopo uliowatesa wafanyakazi kwa miaka kadhaa kwa kuondoa tozo ya kutunza
thamani ya mkopo ambayo ilikuwa inaongeza mkopo kila mwaka badala ya
kupunguza.
Dr Kabati alisema kiburi cha madaraka kwa wakuu na
watendaji wa taasisi kimepungua, kuongezeka kwa amani na utulivu ofisini mwa
wafanyakazi kutokana na mabadiliko hayo.
“Awali, wafanyakazi wengi walikuwa katika hali ya
uoga na njia panda kutokana na vitisho, pia kufufuka kwa matumaini ya maboresho
ya mishahara iliyosimamishwa kupandishwa kwa miaka mitano iliyotangulia, hii ni
baada ya kutoa ahadi ya kuboresha maslahi ya mishahara katika sherehe za Mei
Mosi jijini Mwanza mwaka 2021,”amesema.
Dr kabati amesema kuendelea kulipwa malimbikizo ya
mishahara na maslahi mengine kwa awamu mbalimbali na kuongeza kwa umri wa
wanufaika wa Bima ya Afya kutoka miaka 18 hadi 21
Na
ikumbukwe kuwa Mwishoni mwa juma hili itakuwa ni mwaka mmoja tangu Samia Suluhu
Hassan ambae alikuwa Makamu wa rais wa Tanzania aliposhika hatamu za nchi hiyo
kufuatia kifo cha mtangulizi wake hivyo kuwa mwanamke wa kwanza kuongoza taifa
hilo.
Aliapishwa,
katikati ya kipindi cha janga la corona, mwezi Machi baada ya mtangulizi wake
John Magufuli alipofariki ghafla alipokuwa madarakani. Na mara tu aliposhika
uongozi, alinukuliwa akisema kuwa ‘‘yeye na Magufuli walikuwa kitu kimoja.’’
Post A Comment: