
Watu
wawili wanaodhaniwa kuwa ni wapenzi wamekutwa wamefariki huku chanzo
kikidaiwa kuwa walikunywa sumu katika Kitongoji cha Mlandizi kata ya
Mlandizi Tarafa ya Mlandizi Wilaya ya Kipolisi Mlandizi, mkoani Pwani.
Akizungumzia tukio hilo la kustaajabisha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amesema;
“Mnamo Tarehe 5 Septemba, 2021 asubuhi huko Mlandizi, watu wawili
wanaodaiwa kuwa ni wapenzi walikutwa wamefariki katika makazi yao baada
ya kunywa kitu kinachodhaniwa ni sumu.
“Watu
hao ni Godfrey Pius Mandai (48) ambaye alikuwa ni Dereva wa Kampuni na
Veronica Gerald (42), mfanyabiashara na mkazi wa Mtwara ambaye alisafiri
kutoka Mtwara na kumfuata mpenzi wake huyo Mlandizi.
“Imedaiwa
kuwa mwanaume yule alitengengeza juisi ambayo ndani yake ilikuwa na
sumu akampa Veronica akanywa na kufariki dunia, mwanaume hutyo alipoona
mpenzi wake amefariki na yeye akanywa ile juisi yenye sumu na akafariki
dunia.
“Inadaiwa kuwa chanzo cha tukio hili ni wivu wa mapenzi ambapo mwanaume alikuwa akimtuhumu Veronica kuwa anafanya usaliti.
“Kwenye
eneo la tukio tumekuta chupa yenye masalia ya sumu na tumekuta pia
karatasi ambayo inadhaniwa imeandikwa na mmoja wao ikiwa na maneno
yanayosomeka ‘HUU NI USALITI TU.’
Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi kutokana na tukio hilo,” amesema Kamanda Nyigesa.
Post A Comment: