
Picha haihusiani na habari hapa chini
Na Kadama Malunde 
Mfanyakazi
 wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Debora Rwekwama (34) mkazi wa 
Bushushu Mjini Shinyanga amefanyiwa ukatili kwa kushambuliwa kwa kupigwa
 sehemu mbalimbali za mwili wake  kisha kukatwa mkono wa kushoto kwa 
kisu na mme wake  aitwaye Jacobo Mwajenga (35) kutokana na kile 
kinachoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.
Kamanda
 wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando amesema tukio hilo 
limetokea Septemba 9,2021 usiku  katika mtaa wa Bushushu, Manispaa ya 
Shinyanga.
“Usiku
 wa Septemba 9,2021 Mfanyakazi wa Benki ya CRDB Debora Rwekwama (34) 
(Banker - CRDB)  mkazi wa Bushushu Manispaa ya Shinyanga alishambuliwa 
kwa kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake  na baada ya kupoteza fahamu
 alikatwa mkono wa kushoto kwa kisu na mme wake  aitwaye Jacobo Mwajenga
 (35)mkazi wa Bushushu”,amesema Kamanda Kyando.
"Huyu
 Jacob Mwajega inasemekana siku ya tukio mchana alienda pale Benki ya 
CRDB Mjini Shinyanga akakuta mke wake hayupo pale Benki isipokuwa Hand 
bag (Mkoba)  wake upo, huyu bwana akamsubiri mkewe, akiwa pale ukataka 
kutokea mzozo kidogo pale lakini watu wakaingilia kati kwamba haya mambo
 hayafai sehemu za kazi mtaenda kuyaongea huko nyumbani kwenu",ameeleza 
"Kwa
 hiyo usiku huo huyu bwana Jacobo Mwajenga akamshambulia huyo mke wake  
na kusababisha azimie na kumkata jeraha kubwa kweli kweli kwenye mkono 
wake wa kushoto na kusababisha mama huyu kuvuja damu nyingi",ameongeza
Baada
 ya kufanya tukio hilo, Bushushu Mjini Shinyanga Jacobo Mwajenga 
akambeba mke wake akiwa amezimia na kumpakia kwenye gari yao na 
kumpeleka hadi katika kituo cha Polisi Kahama.
"Alipofika
 katika kituo cha polisi Kahama akaripoti kwamba huyu mama amepata 
ajali, kutokana na hali aliyokuwa nayo mama huyo polisi hawakumhoji 
kwani alikuwa amezimia walichokifanya ni kumpa PF3 ili huyo bwana 
amkimbize mwanamke huyo hospitali na hawakujua kama ni mme wake",amesema.
"Huyu
 bwana akampeleka mama huyu hospitali ya wilaya ya Kahama. Sasa 
madaktari walivyokuwa wanamchunguza mama huyu hawakuona dalili ya ajali 
wakabaini kuwa mama ameshambuliwa wakatoa taarifa polisi na Polisi 
tukamkamata huyu bwana Jacobo akiwa hapo hospitali",amesema Kamanda Kyando.
Amesema chanzo cha tukio ni wivu wa mapenzi na kwamba tayari Jeshi la Polisi linamshikilia mtuhumiwa wa tukio hilo.
"Chanzo
 cha tukio hili ni wivu wa mapenzi. Huyu bwana yeye ni anafanya kazi ya 
Kuongoza watalii kule Arusha. Na kutokana na hii changamoto ya ugonjwa 
wa Corona inaonekana kazi yake imepata shida, muda mrefu yupo hapa 
Shinyanga anaishi na mke wake, hajishughulishi na kazi yoyote. Mama ni 
mfanyakazi wa Benki yeye yupo tu nyumbani,kwa hiyo nafikiri akajenga 
tabia ya wivu, na tumebaini chanzo cha tukio hili ni wivu wa mapenzi", ameeleza Kamanda Kyando.
Ameeleza kuwa hali ya majeruhi ni mbaya na amelazwa katika hospitali ya wilaya Kahama.
Kamanda
 Kyando amesema hivi sasa kuna matukio mengi ya vifo vinavyotokana na 
wivu wa mapenzi hivyo kutoa wito kwamba ukigundua kuwa mwenzako siyo 
mwaminifu kwenye mapenzi usijichukulie sheria mkononi,nenda kwa viongozi
 wa dini,serikali au vyombo vya dola kuliko kuchukua sheria mkononi 
kwani ni kosa la jinai na matokeo yake kuishia jela.
Post A Comment: