Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akiwasalimia na kuwapa pole manusura wa chakula kinachosadikika kuwa na sumu.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akiwasalimia na kuwapa pole manusura wa chakula kinachosadikika kuwa na sumu.
Na Edina Malekela,Singida
Mkuu
wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amewatembelea wananchi
waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa huo baada kula chakula
kinachosadikika kuwa na sumu ambapo katika tukio mtoto mmoja mwenye
umri wa miaka 7 amefariki dunia huku watu wengine 50 wakinusurika kifo.
Wakazi
hao wa Kata ya Unyambwa kijiji cha Kisasida katika Manispaa ya Singida
mkoani Singida walifikishwa hospitalini hapo jana baada ya hali zao kuwa
mbaya kutokana na kula chakula kilichoandaliwa katika shughuli za
ufunguzi wa Madrasa kijijini hapo.
Dkt.
Mahenge amewapongeza madaktari wa Hospitali hiyo kwa jitihada za
kuhakikisha wananusuru maisha ya wananchi hao ambapo kwa sasa hali zao
zinaendelea vizuri na kuipongeza Serikali kwa kuweka miundombinu mizuri
ya huduma katika sekta ya afya.
Ametoa
wito kwa Viongozi wa Serikali na Dini kuwajibika kikamilifu katika
kutoa elimu ya namna ya kuandaa chakula pamoja na kusimamia inapotokea
sherehe mbalimbali kwenye maeneo yao ili kuepuka madhara ya namna hiyo.
Kwa
mujibu wa Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa Banuba Deogratius
amesema walipokea jumla ya wagonjwa 50,kati yao Wanawake 34 na Wanaume
16 ambapo hali zao zinaendelea vizuri na wanaanza kuwaruhusu baadhi yao
kurudi nyumbani kuendelea na majukumu yao.
Aidha
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida Stella Mutabihirwa amesema
wanawashikilia washukiwa 7 walioshiriki kuandaa chakula hicho kwa ajili
ya uchunguzi na tayari wamechukua chakula hicho kwa uchunguzi zaidi.
Katika tukio hilo Kamanda amesema mtoto mmoja mwenye umri wa miaka (7) ambaye amefahamika kwa jina la Fahad Masudi amefariki dunia kabla ya kufikishwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Post A Comment: