Mkuu wa mkoa wa Rukwa mh. Joachim Wangabo ametoa
ushauri kwa wadau wa michezo nchini kuona namna ya kuimarisha mbinu za kuibua
vipaji vya wanamichezo kuanzia ngazi ya shule za msingi katika mashindano ya
UMITASHUMTA na UMISETA ili kuweza kuwa na vijana watakaoweza kubeba jina la
Tanzania katika michezo.
Amesema kuwa yeye ni miongoni mwa watu waliochelewa
kulala ili kuangalia mechi baina Tanzania maarufu kama Taifa Starts na jirani
zetu Kenya maarufu kama Harambee Strars ambapo hadi kumalizika kwa mchezo huo Harambee
Stars iliibuka kidedea kwa kuilaza Taifa Stars mabao 3 kwa 2.
“Kuna ambao wamelala alfajiri na wengine wapo humu
ambao wamelala leo, tunaomboleza kufungwa huku, tungeshinda jana tungekuwa na
mwanga wa kusonga mbele, sasa ni kinyume na yalivyokuwa matarajio yetu lakini
ndugu wana Rukwa tusikate tamaa, tuendelee kuiunga mkono timu yetu hii ya
Taifa, Kufungwa ni kujifunza, tuendelee kujipanga vizuri hasa kwa vijana
kuanzia UMISHAMTA huku mpaka UMISETA na kwenye “academy” hizi,” alieleza.
Aidha, alibainisha kasoro kadhaa zinazojitokeza
katika ligi yetu ya Tanzania hasa kwa upande wa timu vinara zinazopata nafasi
za kwenda kucheza makombe ya Kalbu Bingwa Afrika pamoja na Kombe la Shirikisho
kuona namna ya kutoa fursa kwa wachezaji wa kitanzania ili wapate ujuzi wa kimataifa
na sio kuwajenga wachezaji wa nje ambao wanakwenda kutumikia nchi zao.
“Hizi timu zetu za Yanga na Simba pamoja na Azama
zinafanya vizuri kwasababu zina wachezaji wengi wa kigeni matokeo yake timu ya
Taifa inapokwenda kwenye mashindano wachezaji wetu wanabaki wenyewe, angalieni
Emanuel Okwi anavuma kule Uganda lakini tumemuwezesha sisi hapa Tanzania,”
Alisema.
Post A Comment: