MTOTO wa wanamuziki wa kishua wanaounda Kundi la Navy Kenzo, Emannuel Mkono ‘Nahreel’ na Aika Mareale waliompa jina la Gold, amegeuka kivutio kwa watu mbalimbali baada ya wawili hao kuachia picha yake mtandaoni.

Wanamuziki hao ambao ni kapo ya muda mrefu walionesha picha ya mtoto huyo kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii na kusababisha watu wengi kuichua na kuweka katika kurasa wakimsifia.

Mama wa Gold, Aika alimwambia ripota wetu kuwa  anafurahi kuona watu wengi wamefurahishwa na ujio wa mwanaye, jambo ambalo kwao ni baraka kubwa katika safari yao ya kimaisha.

Nahreel na Aika.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: