Home
Kitaifa
WANAFUNZI 196 WANUSURIKA KUFA KWA MOTO BWENINI MKOANI PWANI
 
 
WANAFUNZI wasichana wapatao 196 wa shule
 ya sekondari ya Moreto iliyopo kata ya Lugoba tarafa ya Msoga Jimbo la 
Chalinze mkoani Pwani, wamenusurika kufa baada ya bweni lao kuteketea 
kwa moto jana asubuhi. 
Mbunge
 wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ametoa msaada ya magodoro 50 yenye 
thamani ya Sh milioni 2.2 kwa kuwa mali zote wasichana zimeteketea. 
“Tumshukuru
 Mungu pamoja na kutokea kwa hasara ya kuteketea kwa mali, lakini hakuna
 madhara kwa wanafunzi yaliyotokea,” amesema Ridhiwani. 
Amewapa pole walimu na wanafunzi na kuwaomba wadau wengine, kujitokeza kwenda kusaidia pale watakapojaaliwa. 
Mkuu
 wa Shule hiyo , Justine Lyamuya, amesema, ajali hiyo ni ya Oktoba 5, 
asubuhi ambako walianza kuona moshi mzito katika bweni mojawapo 
wanaloishi wasichana wa shule hiyo. 
Alisema wakati moto huo unazuka, wanafunzi hao walikuwa kwenye masomo yao darasani. 
"Tulifuatilia
 na kukuta moto umeshashika kwenye bweni hilo na jitihada za kuuzima 
zilishindikana,” alisema Lyamuya na kuongeza kuwa mali zote za wanafunzi
 wanaolala kwenye bweni hilo zimeteketea kwa moto hivyo kwa sasa 
wanafanya tathmini kujua kiwango cha hasara. 
Polisi mkoani Pwani inafanya uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha moto huo. 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Boniventure Mushongi amesema, jengo hilo linatumia nishati ya umeme wa jua. 
Amesema uchunguzi wa kina utafanyika kujua kiini cha kuzuka kwa moto huo. 
Amesema bweni hilo linakadiriwa kuwa na wanafunzi 196. 
Kamanda Mushongi amesema thamani za mali za wanafunzi zilizoteketea katika moto huo, bado haijafahamika.
 
Chanzo-Habarileo 
 Kama Una Habari,Picha,Tangazo n.k Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp +255762 561 399
 
 
 
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 Back To Top
 
Post A Comment: