Ndege mbili za kivita za Marekani
zenye uwezo wa kubeba silaha za nyuklia, B-1 Lancer, zimepaa juu ya anga
ya Korea Kusini, siku chache baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio
la tano la silaha za nyuklia.
Marekani imeitahadharisha Korea Kaskazini kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi ya taifa hilo baada ya kufanyika kwa majaribio hayo ya bomu Ijumaa.
Jaribio hilo la Pyongyang ndilo kubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na taifa hilo.
'Ndege aina ya B-1 zina uwezo wa kubeba makombora yenye mabomu ya nyuklia au mabomu ya nyuklia yenyewe yenye uwezo wa kuharibu hata mahandaki.
Operesheni hiyo ya kupaa kwa ndege ilikuwa imepangiwa kufanyika Jumatatu lakini ikacheleweshwa kutokana na hali mbaya ya hewa Guam, eneo ambalo ndege hizo hukaa.
Post A Comment: