Articles by "mbulu"
Showing posts with label mbulu. Show all posts


Na John Walter-Mbulu

Mkuu wa wilaya ya Mbulu Komred Kheri James, amewataka wakulima wilayani humo kuweka akiba ya chakula Cha kutosha ajili ya matumizi ya familia ili kuepuka changamoto ya njaa inayoweza kutokea kutokana na mabadiliko ya Tabia ya Nchi.                                          

Ameyaeleza hayo akiwa katika ziara ya kikazi katika Kata ya Bargish, Daudi na Marang ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake katika kusikiliza na kutatua kero za Wananchi.

Aidha amewahimiza na wafugaji kuhakikisha katika pesa wanayo pata katika mauzo ya mifugo yao, watumie kiasi cha fedha hizo kununua chakula na kuweka akiba.    

Pamoja na mambo mengine Komred Kheri James ameitumia ziara hiyo kukagua miradi ya maendeleo, kuhamasisha shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za Wananchi.                                   

Kwa upande wa utekelezaji wa miradi Komred Kheri James ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Mbulu kwa usimamizi wa miradi ya Elimu, na ameelekeza Halmashauri iwekeze nguvu za kutosha kukamilishwa miradi ilio anzishwa na wananchi ili iweze kukamilika na kutumika. 

Mkuu wa wilaya ya Mbulu Kheri James akizungumza na wananchi wa kata ya Bargish.

  

 


Na John Walter-Mbulu

Baraza la madiwani halmhauri ya mji wa Mbulu Mkoani Manyara limeketi na kujadili matumizi ya halmashauri na kupitisha bajeti ya zaidi ya shilingi billioni 24 kwa mwaka 2023-2024.

 

Bajeti hiyo imepitishwa baada ya kikao kilichoketi siku mbili kwa ajili ya kujadili mapato na matumizi ya halmashauri hiyo.

 

Akitangaza kupitishwa kwa bajeti hiyo , mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa mbulu Yefred Muyenzi amelishukuru baraza kwa kupitisha bajeti hiyo.

 

Aidha Mkurugenzi Muyenzi , amewataka wakuu wa idara kusimamia fedha hizo zitumike kama zilivyoidhinishwa na baraza.


Kwa upande wake katibu tawala wa wilaya ya Mbulu Bi Sara Sanga, ametumia kikao hicho cha baraza la madiwani kutoa wito kwa wazazi na walezi wa kuhakikisha wanafuzni wote wenye sifa za kwenda shule wanapata haki hiyo.

 

Aidha amewataka wazazi kuhakikisha wanachangia gharama za chakula kwa watoto wao ili kuwawezesha kusoma kwa utulivu.