Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua rasmi Nyenzo za Utekelezaji wa Dira 2050 Juni 29, 2026 jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt Tausi Kida wakati akitoa elimu kwa wananchi mbalimbali juu ya utekelezaji wa Dira 2050 katika maonesho ya wiki ya utumishi wa umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park-Jijini Dodoma.

Akiwa katika viwanja hivyo kwenye Banda la Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Kida aliwaambia waandishi wa Habari kuwa Tume hiyo imekamilisha nyenzo za utekelezajiwa wa Dira 2050 sambamba na Mfumo wa kitaifa wa kusimamia mipango na miradi ya maendeleo unaojulikana kama e-Delivery.

“Tumekamilisha nyenzo zote za utekekezaji wa Dira 2050, ikiwa ni pamoja na Mipango ya utekelezaji, Miongozo na Mifumo ya Usimamizi na Ufuatiliaji na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan atazindua Nyenzo hizo tarehe 29 Juni, 2026” amesema Dkt. Kida.

Aidha, amefafanua kuwa nyenzo zitakazozindualiwa ni pamoja na Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/27-2050/51, Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2026/27-2030/31 pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2026/27 pamoja na Mfumo wa kitaifa wa kusimamia mipango na miradi ya maendeleo unaojulikana kama e-Delivery.




Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imesema matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika sekta ya mifugo yataimarisha masoko na kuongeza ushindani wa bei ya bidhaa hiyo nchini.

Akizungumza Juni 19, 2026 katika Maonesho ya Mifugo na Mnada wa Kimataifa yanayofanyika katika Shamba la Mbogo, Chalinze mkoani Pwani, Afisa Ubora wa WRRB, Anatolius Kabyemera, amesema bodi hiyo imeingia kwenye sekta hiyo kwa lengo la kuwawezesha wafugaji kuuza mifugo yao kupitia mfumo rasmi na wenye tija.

Amesema mfumo huo utasaidia wafugaji kuimarisha ufugaji na kuongeza kipato chao ambapo mifugo itahifadhiwa kwenye eneo maalumu lililosajiliwa kama ghala ya mifugo wakati wakisubiri mnada.

“Mfumo huu utawezesha mifugo kuletwa kwenye ghala ambalo ni eneo teule lenye maji, malisho na wataalamu wa mifugo, litahesabika kuwa ghala la mifugo. Baada ya mfugaji kuingiza mifugo yake katika ghala akisubiri mnada, atapatiwa stakabadhi itakayomwezesha kupata mkopo kupitia taasisi za fedha ambazo tumeshaingia nazo makubaliano, kwa mfano NBC,” amesema Kabyemera.

Kwa upande wake, mmoja wa wafugaji waliotembelea banda la WRRB katika maonesho hayo, Moringe Gasper, ameipongeza bodi hiyo kwa kutoa elimu kuhusu matumizi ya mfumo huo katika sekta ya mifugo.

Amesema wafugaji wengi wako tayari kuona utekelezaji wa mfumo huo unaanza haraka ili nao waweze kunufaika kama ilivyo kwa wakulima wanaotumia mfumo wa stakabadhi za ghala kwa sasa.

NA Oscar Nkembo

Msimamizi wa Dawati la Ukaguzi wa Kemikali wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Kati, Suitbert Sinduhije amesema Mamlaka imedhibiti Kemikali ya Sulphur iliyomwagika eneo la Mikumi na amewataka Madereva kuzingatia mafunzo wanayopata huku akiwasihi Wananchi kutoa taarifa kwa Mamlaka pindi ajali za Kemikali zinapotokea.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linaendelea kuhimiza ushiriki wa wadau mbalimbali katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira, likieleza kuwa mafanikio katika sekta hiyo yanategemea ushirikiano wa wananchi, taasisi za umma, sekta binafsi na washirika wa maendeleo.
Kariakoo, 18 Juni, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imewapongeza walipakodi wa eneo la Mchikichini kwa mchango wao mkubwa ambao umekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Mamlaka, katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.
Na OWM-KAM, Mwanza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu, amepongeza waajiri nchini wanaotekeleza wajibu wao kwa kuzingatia sheria za kazi, ikiwemo kuwasilisha michango ya wafanyakazi katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa lengo la kulinda maslahi ya wafanyakazi dhidi ya madhara yanayotokana na kazi.
 

Na Mwandishi Wetu

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhan Kailima, amepongeza ufanisi na uwazi wa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unaosimamiwa na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, akieleza kuwa mfumo huo umechangia kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.

Bw. Kailima alitoa pongezi hizo Juni 18, 2026 alipotembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kupata maelezo kuhusu utekelezaji wa mfumo huo, alisema kuwa umejengwa katika misingi ya uwazi na ushindani, jambo linalosaidia kupunguza gharama za uagizaji wa mafuta na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.

Akitoa ufafanuzi kwa mgeni huyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, alisema kuwa katika mfumo wa uagizaji mafuta kwa pamoja, ushindani hujikita katika gharama za usafirishaji wa mafuta (Premium).

Alieleza kuwa wazabuni hushindanishwa kwa kuwasilisha bei za usafirishaji wa bidhaa za petroli, dizeli na mafuta ya taa, ambapo mzabuni mwenye gharama nafuu zaidi hupatiwa zabuni husika.

“Utaratibu huu umetuwezesha kuhakikisha upatikanaji wa mafuta ya kutosha nchini wakati wote na wakati huohuo kuipa Serikali taarifa sahihi za kiasi cha mafuta na hivyo kuwezesha ukusanyaji wa mapato yatokanayo na biashara ya mafuta,” alisema.

Aliongeza kuwa mikataba ya uagizaji wa mafuta husainiwa mapema kabla ya bidhaa kuwasili nchini, jambo linaloiwezesha Serikali kufanya makadirio sahihi ya mapato yatokanayo na sekta hiyo.

Kwa mujibu wa Mwitazy, mafanikio ya mfumo huo yameifanya PBPA kuwa kitovu cha huduma za uagizaji mafuta kwa nchi kadhaa za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zikiwemo Malawi, Rwanda, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambazo huleta mahitaji yao kupitia mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja.

Ziara ya Bw. Kailima katika banda la PBPA ni sehemu ya shughuli za Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayolenga kuonesha mafanikio, huduma na ubunifu unaotekelezwa na taasisi za umma katika kuwahudumia wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa.

 


Serikali imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa mikopo yenye masharti nafuu inayotolewa kwa wafanyabiashara ndogondogo ili kuhakikisha fedha hizo zinawanufaisha walengwa na kudhibiti upotevu wa fedha za umma.

Kauli hiyo imetolewa Juni 18, 2026 bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi wakati  akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Tamima Haji Abass, aliyehoji kuhusu uwepo wa mwongozo na utaratibu wa kusimamia mikopo hiyo.

Mhe. Mahundi  amebainisha kwamba, Serikali imeingia makubaliano na Benki ya NMB kusimamia utoaji wa mikopo yenye riba nafuu ya asilimia saba kwa mwaka kwa wafanyabiashara ndogondogo wanaokidhi vigezo vilivyowekwa, ikiwemo kuwa na kitambulisho cha kidijitali.

Amefafanua kuwa kabla ya mkopo kutolewa, biashara husika hutembelewa na kutathminiwa ili kujiridhisha kama inakidhi masharti ya kupata mkopo. Baada ya hapo, waombaji hupatiwa mafunzo ya usimamizi wa fedha na biashara kabla ya kupokea mkopo, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa matumizi ya fedha hizo na kuimarisha uwezo wa kurejesha mikopo kwa wakati.

“Marejesho ya mikopo hiyo yanafuatiliwa na maafisa wa Benki ya NMB kwa karibu ili kuhakikisha fedha za Serikali zinaendelea kuzunguka na kuwafikia walengwa wengi zaidi. Mfumo huo umewekwa mahsusi kuimarisha uwajibikaji na kupunguza changamoto za ucheleweshaji au kutorejeshwa kwa mikopo" amesema Mhe. Mahundi

Aidha, amesema utaratibu huo umeainishwa katika Mwongozo wa Utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa Wafanyabiashara ndogondogo kupitia Taasisi za Fedha wa mwaka 2024, ambao umeweka misingi ya utoaji na usimamizi wa mikopo hiyo nchini. Mwongozo huo unalenga kujenga mfumo endelevu wa uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia sekta ya biashara ndogo ndogo.

Hatua hizo zinaendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo nafuu huku ikiimarisha mifumo ya usimamizi na ufuatiliaji wa fedha za umma ili ziweze kuleta matokeo chanya kwa walengwa na maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla.

 


Na. Jordan Mbwambo, WF, Dodoma.

Serikali imeanza kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, hatua inayolenga kufungamanisha na kuboresha usimamizi wa shughuli za Mnyororo wa Ugavi nchini ili kuongeza ufanisi, matumizi bora ya rasilimali na kupata thamani halisi ya fedha za umma.

Hayo yalibainishwa na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Usimamizi wa Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi. Anne Swila, wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Alisema kuwa Sera hiyo inalenga maeneo sita makuu, yakiwemo Ununuzi wa Umma, Ugomboaji na Uondoshaji wa Mizigo ya Serikali, Upokeaji na Urejeshaji, Utunzaji na Uhifadhi, Usambazaji, pamoja na uhifadhi wa Mazingira na Utawala Bora.

‘‘Kwa miaka mingi tumekuwa na sheria nzuri za ununuzi, lakini hazikuwa zimeunganishwa kwa msingi mmoja wa kisera, Sera hii sasa inakwenda kuziba pengo hilo na kuhakikisha kila shilingi ya umma inatumika kwa thamani yake halisi, kwa kuhakikisha mikakati ya utekelezaji inajumuisha kuimarisha udhibiti wa bei, uchaguzi wa wazabuni, na kuendeleza Kada ya Ununuzi na Ugavi Serikalini " alieleza Bi. Swila.

Alisisitiza kuwa ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wa Sera hii itaongeza ushindani na kuwapa fursa wazabuni wazawa, sekta binafsi na makundi maalum ya kijamii, hatua itakayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi na kuchochea ukuaji wa ajira.

Bi. Swila alisema Sera hiyo pia inatarajiwa kuimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki na rasilimali za ndani, kuvutia uwekezaji katika miundombinu ya uhifadhi na usambazaji, na hivyo kuifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

‘‘Miongoni mwa mafanikio yanayotarajiwa ni kuongezeka kwa ufanisi, udhibiti bora wa gharama, kuimarika kwa ubora wa huduma kwa wananchi, ongezeko la ajira, uzingatiaji wa uhifadhi wa mazingira, na kuwa na mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini utakaohakikisha utekelezaji wa sera unaleta tija iliyokusudiwa’’, alifafanua Bi Swila.

Aidha, alisema kuwa Sera hiyo itawezesha kuwepo kwa mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini, hatua itakayoifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kuchangia kupunguza umasikini nchini.

Sera hiyo inatarajiwa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2026 hadi 2036 na tathmini ya utekelezaji itafanyika kila baada ya miaka mitano ya utekelezaji


 


“Sasa najua ni nini ninapaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua sukari au hata ninaponunua gesi ya kupikia.” Ni kauli ya Bw. Bilson Vedastus, mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.

Banda hilo limekuwa kitovu cha msongamano siku ya tatu ya maonesho, Juni 18, 2026 huku wananchi wakijitokeza kwa wingi kujifunza jinsi Serikali kupitia WMA inavyohakikisha kila kipimo kinachotumika kibiashara na katika huduma ni sahihi. Maonesho yalianza tarehe 16 Juni na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 23 Juni 2026.

Baada ya kupata maelezo ya hatua kwa hatua kutoka kwa wataalamu, wengi wameahidi kuwa mabalozi wa Wakala wa Vipimo katika maeneo yao. 

“Tumeona jinsi pampu, mizani na vifaa vingine vinavyohakikiwa kuhakikisha vinapima kwa usahihi. Sasa hatuwezi kukaa kimya tukiona mteja anadhulumiwa. Tutawaeleza jirani zetu na kuripoti udanganyifu popote tutakapouona,” alisema Bi. Asha Siyaya.

Wataalamu wa WMA, Albogast Kajungu, Mbwana Amani na Said Ibrahim waliwaeleza wananchi kuwa uhakiki wa vipimo unagusa sekta zote zinazowahusu moja kwa moja kila siku. Katika sekta ya mafuta, pampu zote huhakikiwa na kuwekewa stika ya uthibitisho. Sokoni na madukani, mizani inayotumika kupimia sukari, mchele na mboga hufanyiwa ukaguzi ili mteja asipoteze pesa.

Sekta ya maji na umeme nayo haikuachwa nyuma. Mita za maji na umeme zinazotumika nyumbani na kwenye biashara ndogo huhakikiwa na kuthibitishwa ili kuhakikisha mteja analipia matumizi halisi na si makadirio au idadi isiyo sahihi. Vile vile mitungi ya gesi ya kupikia, bidhaa zilizofungashwa kama unga na sabuni, pamoja na mizani za barabarani zote huhakikiwa mara kwa mara.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Meneja Mawasiliano wa Wakala wa Vipimo, Bi Veronica Simba amesema lengo ni moja: kuhakikisha mwananchi anapata thamani kamili ya kila shilingi anayolipa, na amewahamasisha wananchi wengi zaidi kutembelea banda hilo kabla ya maonesho kuhitimishwa.






NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA

SERIKALI imesema Tanzania bado haina mgonjwa wa Ebola na hali ya usalama wa afya nchini inaendelea kuwa nzuri, huku ikieleza kuwa imeimarisha hatua mbalimbali za kuzuia ugonjwa huo kuingia nchini kutokana na mlipuko unaoendelea katika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uganda.

Biashara yangu ilianza vizuri sana. Mwanzoni nilikuwa napata wateja kila siku na mauzo yalikuwa yakiongezeka. Lakini baada ya muda, mambo yalibadilika ghafla. Wateja wakapungua, bidhaa zikaanza kukaa muda mrefu bila kununuliwa, na gharama zikaanza kunizidi.

Nilijaribu kila njia niliyoweza kupunguza bei, kubadilisha bidhaa, hata kubadilisha eneo la biashara. Lakini bado hakuna kilichobadilika. Kila siku nilikuwa nikikumbana na hasara zaidi, na polepole nikaanza kupoteza matumaini.
Ilifika hatua nikaanza kufikiria kufunga kabisa biashara.

Ilikuwa vigumu kukubali kushindwa, lakini hali ilikuwa inanilazimisha kuona ukweli. Baada ya muda wa mawazo mengi, niliamua kutafuta mwongozo wa ziada. SOMA ZAIDI.
Maisha yetu yalibadilika ghafla pale ndugu yangu alipoanza kubadilika tabia. Alikuwa mtu mchangamfu, mwenye ndoto na malengo, lakini polepole akaanza kujitenga, kupoteza mwelekeo, na hatimaye kuingia kwenye matumizi mabaya ya dawa za kulevya.

Mwanzoni tulidhani ni hatua ya muda tu, lakini hali ilizidi kuwa mbaya. Alianza kupoteza heshima, afya yake ilidhoofika, na hata mawasiliano ndani ya familia yakavunjika. Kila tulipojaribu kumshauri, alionekana kama hataki kusikiliza.

Ilinivunja moyo kumuona akizama zaidi kila siku. Nilihisi kama tunampoteza polepole, na hakuna aliyekuwa na jibu la kumsaidia. Familia ilianza kukata tamaa, lakini mimi sikuweza kuacha kuamini kwamba bado kulikuwa na njia ya kumrudisha. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi nilikata tamaa kabisa na masomo. Nilikuwa nimeanza vizuri, lakini kadri muda ulivyopita, nikapoteza mwelekeo. Alama zilianza kushuka, motisha ikaisha, na hatimaye nikajikuta nimeacha kabisa kile nilichokuwa nimeanza.

Watu wengi walinishauri nirudi shuleni, lakini ndani yangu sikuwa na nguvu wala hamasa ya kuanza tena. Nilihisi kama nimechelewa, na hata nikirudi, singeweza kufanikiwa kama mwanzo. Hali hiyo ilinifanya nibaki pale pale bila maendeleo.

Kadri siku zilivyopita, nilianza kuona athari za uamuzi wangu. Maisha yalikuwa yanakwama, na nilianza kujilaumu kwa kuacha masomo. Ndani yangu kulikuwa na sauti ndogo iliyoniambia bado naweza kubadilisha hali hiyo, lakini sikuwa najua nianzie wapi. SOMA ZAIDI.

Maumivu ya usaliti yameendelea kuwa moja ya changamoto kubwa inayotikisa mahusiano mengi katika jamii ya sasa. 

Watu waliowahi kuamini kwa dhati hujikuta wakibeba huzuni, hasira na maswali mengi baada ya kugundua kuwa walisalitiwa na wale waliowapenda. Kutokana na hali hiyo, wengi sasa wameanza kutafuta njia salama za kujijenga upya na kulinda mapenzi yao yasivunjike tena.

Wataalamu wa mahusiano wanasema uponyaji wa penzi lililoumizwa huanza kwa mazungumzo ya kweli. Kukaa chini na kueleza hisia bila kuficha jambo husaidia kuondoa mizigo ya moyoni. Wenzi wanaoweza kuzungumza kwa uwazi kuhusu kilichotokea, sababu zake na matarajio ya baadaye huwa na nafasi kubwa ya kurejesha uelewano. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu nilikuwa naingia kwenye mahusiano yaliyoanza vizuri lakini yakavunjika ghafla. Kila mara ilikuwa ni hadithi ile ile mwanzo mzuri, matumaini makubwa, halafu mwisho usioeleweka. Nilijikuta nikibaki na maumivu na maswali mengi yasiyo na majibu.

Nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa kwangu.

Nilijaribu kubadilika, kuwa mvumilivu zaidi, na kujitahidi kuelewa wenzi wangu. Lakini licha ya jitihada hizo zote, matokeo hayakubadilika. Ilikuwa kama mzunguko unaojirudia bila mwisho. Kadri muda ulivyopita, nilianza kupoteza imani na mahusiano kabisa.

Nilihisi kama upendo haukuwa na nafasi katika maisha yangu. Hali hiyo ilinifanya nijitenge kihisia ili kuepuka maumivu zaidi.SOMA ZAIDI.


‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imewakutanisha wahandisi na wataalamu wa sekta ya barabara katika mafunzo maalum yanayolenga kuimarisha usalama wa watumiaji wa barabara wakati wa usanifu, ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara nchini.

‎Mafunzo hayo yanayofanyika mkoani Morogoro yanalenga kuongeza uelewa na uwezo wa wataalamu katika kuzingatia viwango vya usalama barabarani ili kupunguza ajali na kulinda maisha ya watumiaji wote wa barabara.

‎Akizungumza katika mahojiano maalum, Mratibu Msaidizi wa Mradi wa RISE, Mhandisi Lwitiko Mwandobo, amesema mafunzo hayo yameandaliwa mahsusi kuwajengea uwezo wahandisi na kuwakumbusha wajibu wao wa kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara unazingatiwa tangu hatua ya usanifu hadi utekelezaji wa miradi.

‎"Tunataka kuhakikisha kwamba kila mradi wa barabara unazingatia usalama kwa kuweka alama zote muhimu, miundombinu rafiki kwa watumiaji na hatua nyingine za kinga zitakazosaidia kupunguza ajali zinazoweza kuepukika. Hii ni sehemu ya juhudi za kulinda maisha ya wananchi na mali zao", amesema Mhandisi Mwandobo.

‎Kwa upande wake, Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema usalama wa watumiaji wa barabara ni jukumu la pamoja linalohitaji ushirikiano wa wadau wote ili kufikia lengo la kupunguza kwa kiwango kikubwa ajali za barabarani na pia kuna umuhimu wa kuendelea kuimarisha mifumo ya kisheria na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya barabara.

‎"Tukizingatia usalama katika kila hatua ya ujenzi wa barabara, kuimarisha elimu kwa umma na kuhakikisha miundombinu inakidhi viwango vinavyotakiwa, tutapunguza kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani na madhara yake kwa jamii",  amesema Mhandisi Mkinga.

‎Naye, Mratibu wa Masuala ya Usalama Barabarani kutoka (TARURA), Mhandisi Faizer Mbange, amesema mwelekeo wa sasa katika ujenzi wa barabara unalenga kuhakikisha mahitaji ya makundi yote ya watumiaji wa barabara yanazingatiwa ikiwemo waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, bodaboda, bajaji pamoja na watumiaji wa vyombo vingine vya usafiri.

‎Amesema tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo usanifu wa barabara ulijikita zaidi katika magari, sasa miundombinu ya barabara inapaswa kuwa jumuishi na salama kwa kila mtumiaji bila kujali aina ya usafiri anaotumia.

‎Mafunzo hayo yamewakutanisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za sekta ya barabara na usafiri zikiwemo Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Ofisi ya Waziri Mkuu– TAMISEMI, TARURA na Mfuko wa Barabara (Road Fund).






Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Jakaya Kikwete (Mb), amefungua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, yanayofanyika kuanzia Juni 16 hadi 23, 2026 yakibeba kaulimbiu isemayo, "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu."

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, ameipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa huduma mbalimbali inazotoa kwa wananchi na kuitaka kuongeza juhudi za kuelimisha umma kuhusu hatua na mafanikio ya Serikali katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Ridhiwani alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la Mamlaka ya Elimu Tanzania katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, ambapo alipata fursa ya kujionea huduma na shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo.

Akizungumza alipotembelea banda hilo la TEA, Ridhiwani alisema taasisi hiyo ina mchango mkubwa katika maendeleo ya elimu nchini kupitia usimamizi wa Mfuko wa Elimu wa Taifa, hivyo ni muhimu wananchi wakaendelea kupata taarifa sahihi kuhusu miradi na mafanikio yanayotekelezwa kwa manufaa yao.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania, Eliafile Solla, alisema ushiriki wa TEA katika maadhimisho hayo unalenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu na shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na mamlaka hiyo kupitia Mfuko wa Elimu wa Taifa.

Ametaja majukumu makuu mawili yya TEA ambayo ni kutafuta rasilimali fedha na vifaa kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo na kisha kugawa rasilimali hizo katika shule na taasisi za elimu kwa lengo la kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia nchini.

“Tunatumia maonesho haya kuwafikia wananchi moja kwa moja ili waelewe namna TEA inavyoshirikiana na wadau mbalimbali katika kuimarisha sekta ya elimu kwa kutoa rasilimali zinazosaidia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu pamoja na upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia,” amesema Solla.

Ameongeza kuwa watumishi wa TEA walioshiriki maonesho hayo wamejipanga kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo, sambamba na kuendelea kutekeleza jukumu la kutafuta rasilimali fedha na vifaa vitakavyosaidia kuimarisha juhudi za Serikali za kuboresha mazingira ya elimu nchini.

Serikali ya Tanzania imefafanua uamuzi wake wa kuweka akiba ya fedha za kigeni ikiwemo dola za Marekani na dhahabu, ikieleza kuwa hatua hiyo inatokana na mabadiliko ya kiuchumi yanayoendelea kuikumba dunia.


Kauli hiyo imetolewa leo bungeni Dodoma na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, aliyetaka ufafanuzi kuhusu sera ya serikali ya ununuzi na uuzaji wa dhahabu pamoja na maslahi mapana ya taifa.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa dhahabu sasa imejumuishwa rasmi katika mfumo wa akiba ya fedha za kigeni, kama ilivyo kwa dola za Marekani, na si bidhaa ya biashara ya kawaida inayotumika kwa matumizi ya kila siku ya kiuchumi.

Amefafanua kuwa mpango wa ununuzi wa dhahabu umeendelea vizuri na hadi sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na takribani tani 27 za dhahabu kama sehemu ya akiba yake ya taifa.

Aidha, Waziri Mkuu huyo amesisitiza kuwa dhahabu ya taifa haiuzwi kiholela, na akabainisha kuwa utaratibu wa uuzaji wake, pale inapobidi, hufanywa kupitia taasisi rasmi za fedha au kwa tangazo la umma kupitia magazeti ya serikali, si kwa watu binafsi.

Dkt. Mwigulu amewahakikishia wabunge kuwa hakuna uuzaji holela wa dhahabu unaofanyika, bali mfumo uliowekwa unalenga kulinda maslahi ya taifa na kuimarisha uthabiti wa uchumi wa nchi.