Imeelezwa kuwa mradi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Awamu ya Pili B (HEP 2B) unakwenda kuongeza  na kuchocchea uchakataji wa mazao ambayo kwa kiasi kikubwa wananchi wa mkoa wa Katavi wanazalisha mazao katika mkoa huo. 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi,  Mhe. Mwanamvua Mrindoto leo tarehe 6 Februari, 2026 mara baada ya kutambulishwa kwake mkandarasi Kampuni ya M/s ETDCO Ltd atakayetekeleza mradi wa HEP 2B wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 358 kwa wakazi zaidi ya 11,536 mkoani Katavi. 

"Kwa sasa  badala ya kuuza mazao ghafi tutaiza bidhaa, suala hili la kupatikana kwa umeme litakwenda kuipandisha bei za mazao kwa sababu yatachakatwa katika hali nzuri na zitauzwa bidhaa badala ya kuuza malighafi," Amesema RC. Mrindoto. 

Vilevile, ameongeza kuwa upatikanaji wa umeme wa uhakika kupitia mradi wa HEP 2B utakwenda kukuza uchumi, kukuza uwekezaji na kuleta ajira kwa vijana, wanawake, wazee na makundi mbalimbali katika mkoa huo.

"Nimsisitize mkandarasi kujipanga sawasawa uingie kazini kwa miguu yote miwili ukiwa na kasi kubwa kwa sababu wanachohitaji wananchi ni umeme wala sio maneno au ahadi, sio ratiba, sio michakato," Amesema RC Mrindoto. 

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Mussa Muze amesema lengo kuu la utekelezaji wa mradi wa HEP 2B ni kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi katika vitongoji vya mkoa wa Katavi na kusaidia maendeleo jumuishi ya kijamii na kiuchumi. 

Naye, Msimamizi wa Miradi ya REA mkoa wa Katavi, Mha. Gilbert Furia amesema, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kushiriki vema katika utekelezaji wa mradi, na kutumia fursa ya kuletewa umeme  kuweza kujiinua kiuchumi.

Pia, Mkandarasi kutoka Kampuni ya M/s ETDCO Ltd, Mha. Abdalah Mitenda amemueleza RC Mrindoto kuwa katika mradi huo wakandarasi watapewa kipaumbele kufanya shughuli mbalimbali zitakazokuwa zinafanyika katika mradi huo na kuwataka kuchangamkia fursa.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi,akizungumza wakati wa mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo.

Na.Mwandishi Wetu- KARIAKOO

Wafanyabiashara wameukubali mfumo wa Usimamizi wa Kodi za ndani (IDRAS) ,huku wakijiandaa kuupokea Jumatatu ya tarehe 9 Februari mwaka huu.

Akizungumza leo 6.2.2026 jijini Dar es salaam katika mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi amesema wapo tayari kuanza kuutumia mfumo huo kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mwenyekiti huyo amesema kupitia mafunzo ambayo wamepatiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanaamini mfumo utakuwa msaada kwao na kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo.

Amesema mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa yameondoa hofu iliyokuwepo awali na kuwapa uelewa wa pamoja kuhusu matumizi ya mfumo huo.

Bw. Mushi amesema wamejiandaa kuupokea mfumo wa IDRAS, akieleza kuwa jambo lolote jipya huwa linaogopesha kwa wanaolipokea.

Amebainisha kuwa mabadiliko ya kiteknolojia hayaepukiki katika dunia ya sasa, hivyo wafanyabiashara wanapaswa kuendana nayo ili kuboresha ufanisi wa ulipajikodi.

Hata hivyo, Mushi ametoa rai kwa TRA kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutatua changamoto ya mtandao katika baadhi ya maeneo ya biashara, hususani Kariakoo ili kuleta ufanisi wa matumizi mazuri ya mfumo mpya wa IDRAS kwa walipakodi.

Aidha, ametoa wito kwa wafanyabiashara wote kuwa tayari kuupokea mfumo wa IDRAS na kushirikiana na Serikali pamoja na TRA kwa karibu, akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kuhakikisha ulipaji wa kodi unakuwa rahisi na wenye tija.

“Tumejiandaa kuupokea mfumo kuanzia Jumatatu ya tarehe 9 mwezi huu Kikubwa ni kushirikiana na Serikali kuhakikisha tunalipa kodi na mifumo ya ulipaji iwe rahisi,” amesema Bw. Mushi.

Aidha,Mwenyekiti huyo amependekeza kuwepo kwa kipindi cha mpito cha mafunzo ili kuwapa wafanyabiashara nafasi ya kuuelewa mfumo huo Zaidi na kuleta ufanisi sahihi wa utekelezaji wake.

“Angalau miezi mitatu ya mwanzo iwe ni ya mafunzo na kuwaelimisha watu namna ya kutumia mfumo, watakapokuwa wameuelewa, tutakwenda pamoja,”- Bw. Mushi.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Frank Nkinda amekabidhi Hundi ya zaidi ya Bilioni moja kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu fedha zinazotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. 

Aidha, amekabidhi pia vitendea kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ambavyo ni cherehani pamoja na vifaa vya uchomeleaji.

Akizungumza wakati wa kukabidhi Hundi hiyo, DC Nkinda amevitaka vikundi hivyo kuitumia mikopo hiyo vizuri ili iweze kuwakwamua kiuchumi pamoja na kuhakikisha wanarudisha mikopo hiyo kwa wakati ili na wengine waweze kunufaika.

“Fedha hizi zimeletwa kwa lengo la kuwasaidia na kuwakwamua wananchi kiuchumi, fedha hizi zisiwe chanzo cha ugomvi miongoni mwenu, nendeni mkazitumie vizuri ili muweze kufikia malengo mliyojiwekea kama wanakikundi “ Amesema DC Nkinda

DC Nkinda amevitaka pia vikundi hivyo kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika Halmashauri hiyo ili pia ziweze kuwasaidia katika urejeshaji wa mikopo hiyo pamoja na kuvitaka vikundi hivyo kuhakikisha wanarudisha mikopo hiyo kwa wakati ili iweze kuwasaidia na wengine wanaohitaji.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Mhe. Ibrahim Six amevitaka vikundi hivyo kutumia fedha hizo vizuri ili viwe mfano kwa jamii inayowazunguka 

Bi. Rose Manumba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala amewasisitiza wanufaika hao wa Mkopo wa asilimia 10 kurejesha fedha kwa wakati kusudi waweze kukopa tena na kuweza kujikwamua zaidi.

Afisa Maendeleo ya jamii (W) Bw. Judica Sumari akisoma taarifa ya utoaji wa mikopo hiyo amesema mgawanyo wa fedha hizo ambao ni kiasi cha Shilingi 464,959,101 kimeenda kwa Wanawake, Shilingi 469,959,101 kwa vijana na watu wenye ulemavu ni Shilingi 232,479,550 

Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kupitia mikopo ya Asilimia 10 imeweza kutengeneza ajira 462 ikiwa wanawake ni 296, vijana 155 na  watu wenye ulemavu 11.









Habari zilianza kama uvumi. Watu hawakuamini. Lakini tiketi zilipoonyeshwa, ukimya ulitawala. Mwanamume huyo alidai kushinda bet mara 12 mfululizo. Sio siku moja. Sio wiki moja.

Bali kwa kipindi kilichowashangaza wengi. Kabla ya hapo, maisha yake hayakuwa mazuri. Alikuwa akifanya kazi ndogo ndogo. Mapato hayakuwa ya uhakika. Mara nyingi alikopa.

Alikuwa mmoja wa wale waliokuwa wakijaribu bahati bila mafanikio. Wengi walimjua kama mtu wa kawaida tu.
Ghughuli zilianza baada ya ushindi wa tatu mfululizo.

Marafiki waliinua nyusi. Baada ya ushindi wa sita, swali likaanza. Ilipofika ushindi wa kumi na mbili, mjadala ukalipuka. Wengine walimwonea wivu. Wengine walimshuku. Wengine walitaka kujua siri yake.

Alipoulizwa, hakutoa jibu la moja kwa moja. Alisema tu kuwa kulikuwa na kipindi aligundua mambo hayako sawa katika maisha yake. Kila alichogusa kilikuwa kinakwama.

Alijua tatizo halikuwa maarifa ya michezo. Kulikuwa na kitu kingine.
Ndipo aliposema alitafuta ushauri wa kina. Sio wa kubahatisha. Soma Zaidi.
Kwa muda mrefu, jina lake lilikuwa mfano wa kushindwa. Alikuwa na deni la zaidi ya Ksh2M. Benki zilikuwa zimemkataa. Marafiki walijitenga. Simu zilimlia kila siku. Alilala kwa mawazo. Aliamka kwa hofu.

Biashara yake ilikuwa imeanguka. Miradi ilifeli moja baada ya nyingine. Kila alipojaribu kuinuka, kitu kilimrudisha chini. Alianza kuuza mali zake. Alipoteza gari. Alipoteza heshima mbele ya familia.

Wengine walimshauri akubali kuwa ni mwisho. Wiki moja kabla ya mabadiliko, alitangaza wazi kuwa amechoka. Alisema hana tena la kufanya. Aliomba muda zaidi kwa wadai. Hakupata. Alikaa kimya.

Aliangalia maisha yake yakimponyoka.
Ndipo jambo lisilotarajiwa lilipotokea. Jamaa huyo alikutana na rafiki wa zamani. Walizungumza kwa kina. Alisimulia mzigo wa deni. Alisimulia kukwama kwake.

Rafiki alimshauri atafute usaidizi wa busara. Sio wa papara. Sio wa haraka.Soma Zaidi.
Kilio chake kilikatiza kimya cha mkutano wa ukoo. Machozi hayakuweza kuzuilika. Kwa miaka saba, alisema amebeba lawama nzito. Lawama ambazo hakuziomba. Lawama ambazo ziliharibu jina lake.

Alidaiwa kumroga mume wake. Bila ushahidi. Bila kusikilizwa. Mume wake alianza kubadilika taratibu. Biashara ikaanguka. Hasira ikaongezeka. Afya ikaanza kuyumba.

Kila jambo baya liligeuzwa lawama kwake. Ndugu wa mume wakaanza kunong’ona. Majirani wakaanza kujitenga. Amani ya nyumba ikapotea.
Alipelekwa kwa wazee wa ukoo mara kadhaa.

Alituhumiwa hadharani. Hakuna aliyesikiliza upande wake. Kila kilio chake kilichukuliwa kama mchezo. Alianza kuishi kwa hofu. Alianza kujilaumu. Ndoa ikawa gereza la kimya.

Kwa miaka yote hiyo, mume hakuwahi kupelekwa hospitali ya kina. Hakukuwa na uchunguzi wa kweli. Kila mtu aliridhika na jibu rahisi. Lawama zilipata mahali pa kukaa. Mwanamke akabaki na alama moyoni.

Hatimaye, baada ya hali kuwa mbaya zaidi, jamaa wa mbali aliingilia kati. Aliwashauri watafute msaada wa busara. Soma Zaidi.
Ilikuwa mwaka 2013 alipotea bila kuacha dalili yoyote. Jamaa huyo aliondoka nyumbani asubuhi kama kawaida. Hakurudi tena. Simu yake ilizimwa. Hakukuwa na ujumbe. Hakukuwa na maelezo.

Familia ilianza kumsaka kila mahali. Polisi walihusishwa. Marafiki waliulizwa. Miaka ikapita bila majibu.
Kadri siku zilivyogeuka kuwa miaka, matumaini yalififia. Mama yake aliugua kwa msongo wa mawazo.

Watoto wake walikua bila kumjua baba yao. Wengine walianza kusema huenda alikufa. Wengine walidai alikimbia kwa makusudi. Familia ilibaki katikati ya maumivu na maswali yasiyo na majibu.

Ghafla, mwaka huu, kilio kilisikika nyumbani. Jamaa huyo alisimama mlangoni. Alikuwa amechoka. Amebadilika sana. Lakini alikuwa hai. Familia ilishindwa kuamini macho yao. Wengine walilia.

Wengine walimkumbatia. Ilionekana kama ndoto. Lakini furaha ilichanganyika na maswali mengi mazito. Baada ya siku chache, ukweli ukaanza kujitokeza. Jamaa huyo alidai maisha yake yalivurugika ghafla.

Kila alipojaribu kurejea nyumbani, mambo yalizidi kuwa magumu. Alipoteza kumbukumbu kwa vipindi. Alijikuta akihama maeneo bila mpangilio.

Alisema nguvu zisizoeleweka zilikuwa zinamfanya ashindwe kurudi. Hapo ndipo familia ilipotafuta msaada wa nje. Soma Zaidi.
Tukio hili lililazua hofu na mshangao kiliibuka kijijini mmoja wa viongozi wa kanisa. Mchungaji maarufu aliopendwa na wengi alipatikana amekufa chooni. Habari hizo zilienea haraka, na kila mtu alikuwa na mashaka na maswali yasiyo na jibu.

Hali ilianza baada ya uvumi kuhusu msichana wa miaka 21 aliyehusishwa na matukio yasiyoeleweka ndani ya kanisa. Watu walijiuliza ni kweli au ni uvumi tu. Familia na waumini walikusanyika, lakini hofu ilitawala.

Hakuna aliyesema lolote kwa ujasiri.
Uchunguzi wa awali ulionyesha kuwa mchungaji alikula uroda iliyokuwa imechanganywa na kitu kisichoeleweka.

Sababu ya matokeo hayo bado haikuwa wazi. Polisi walipiga ripoti. Wanaume na wanawake walikaa wakitazama, wakiwa na hofu kubwa. Jamii ilikosa amani. Waumini walijilaumu kwa kushindwa kutambua hatari.

Familia ya mchungaji ililia kimya. Wengine waliogopa kuzungumza. Nyumba ya mchungaji ikawa kimya.Soma Zaidi.

 

Mbunge wa Jimbo la Kilombero, Abubakari Asenga, ameibua mjadala mzito bungeni baada ya kutoa kauli kali akiwataka Watanzania kuacha tabia ya kumkosoa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na familia yake kwa lugha ya kejeli kwenye mitandao ya kijamii. 

Kauli hiyo imekuja wakati ambapo mijadala mikali imekuwa ikiibuka mtandaoni, ikihusisha hata watu wa karibu na Rais, jambo lililoibua hisia tofauti miongoni mwa wananchi.

Akichangia hotuba ya Rais wakati wa ufunguzi wa Bunge la Kumi na Tatu, Asenga alisema wazi kuwa baadhi ya maneno yanayozungumzwa mitandaoni hayalengi kujenga Taifa. Kusoma Zaidi, bonyza hapa.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameongoza maelfu ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tabora, Munde Tambwe, yaliyofanyika Februari 4, 2026, nyumbani kwao Kata ya Cheyo, Manispaa ya Tabora. Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi wa Serikali, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wabunge, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi waliokuja kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi huyo.

Munde Tambwe alifariki dunia Februari 2, 2026, jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Baada ya taratibu za kitaifa na kifamilia kukamilika, mwili wake ulisafirishwa hadi mkoani Tabora na kuzikwa katika makaburi ya Sheikh Yahaya yaliyopo Kata ya Kidongo Chekundu.Kusoma Zaidi, Bonyza hapa.

Wakala wa Maendeleo ya Usimamizi wa Elimu (ADEM) kwa kushirikiana na VVOB – Education for Development umefikia hatua muhimu katika kuimarisha uongozi wa shule nchini Tanzania kufuatia utekelezaji wenye mafanikio wa Mradi wa LIT-LEAD.

 


Na OWM – TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe.  Tone Tinnes na kufanya mazungumzo ya namna ya kuboresha ushirikiano katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, ili kuikinga jamii dhidi ya majanga yanayoweza kuwakumba kutokana na mabadiliko ya tabianchi.

Prof. Shemdoe amekutana na Balozi Tinnes leo Februari 05, 2026 Jijini Dodoma katika ofisi ndogo za Wizara na kujadiliana masuala mbalimbali ili kuimarisha mahusiano ya kiutendaji baina ya OWM-TAMISEMI na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania.

Katika mzungumzo hayo wamekubaliana kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuwezezesha utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika sekta za afya na elimu msingi, miundombinu ya barabara na huduma nyinginezo za kijamii, ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Aidha, Prof. Shemdoe ameishukuru Serikali ya Norway kwakuwa mmoja wa wadau wa maendeleo katika kuimarisha mabadilikoyatabianchi, na kuiomba nchi hiyo kuendelea kuchangia maendeleo nchini kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inagusa maisha ya Watanzania.

Kwa upande wake, Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe.  Tinnes ameishukuru na kuipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Norway na Tanzania, ushirikiano ambao una tija katika maendeleo ya wananchi.

Katika kikao  hicho, Balozi huyo wa Norway aliambatana na Msaidizi wake Dkt. Lutgart Lenaerts pamoja na Mshauri Mwandamizi Dkt. Yassin Mkwizu.

๐Ÿ“ŒBima ya afya kwa wote yaguswa

Na Augusta Njoji

KAMATI ya Ushauri ya Wilaya ya Handeni (DCC) imepitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti ya Sh. bilioni 35 kwa mwaka wa fedha 2026/27 ya Halmashauri ya Mji Handeni, huku miongoni wa vipaumbele vilivyotajwa ni pamoja na kugharamia Bima ya Afya kwa Wote kwa wananchi wasio na uwezo kwa kutumia mapato ya ndani.

Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichofanyika leo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewaagiza Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wahudumu wa Afya kutoa elimu kwa wananchi kwa lugha rahisi ili wahamasike kujiunga na mpango huo wa bima ya afya.

Amesema serikali tayari imetangaza kuanza utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hivyo ni wajibu wa viongozi na watendaji kuhakikisha wananchi wanaelewa umuhimu wake ili wawe na uhakika wa matibabu wanapohitaji huduma za afya.

“Ni lazima wananchi waelimishwe kwa lugha wanayoielewa ili wajue faida za bima hii, kwani itawasaidia kupata huduma za matibabu kwa uhakika,” amesema Mhe. Nyamwese.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kubaini kama inatekelezwa kwa kuzingatia thamani halisi ya fedha, sambamba na kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema rasimu ya mpango na bajeti imeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi na mikakati ya maendeleo ya Halmashauri.

Ametaja vipaumbele vingine vitakavyotekelezwa kwa kutumia mapato ya ndani kuwa ni pamoja na kutenga Sh milioni 176 kwa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ujenzi wa fremu za maduka ili kuongeza vyanzo vya mapato, utekelezaji wa afua za lishe, ujenzi wa maabara katika shule moja ya sekondari pamoja na kuboresha miundombinu ya mifugo.

Awali, Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt. Hudi Muradi, amesema kwa mwaka wa fedha 2026/27 Sh milioni 30 zimetengwa katika mapato ya ndani kwa ajili ya kugharamia bima ya afya kwa wananchi wasio na uwezo na kwamba kwasasa serikali inaendelea na zoezi la uhakiki wa wananchi hao.

Ameongeza kuwa serikali imeimarisha miundombinu ya afya na kuajiri watumishi wapya 58 ili kuboresha utoaji wa huduma katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali imekwishabainisha na kufanya utafiti wa maeneo mbalimbali yanayofaa kuendelezwa kwa ajili ya miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo na jua, ikiwa ni pamoja na Zuzu-Dodoma, Same-Kilimanjaro na Manyoni-Singida.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Februari 05, 2026 bungenini jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mwera, Mhe. Suleiman Mohamed Rashid aliyehoji juu ya mpango wa Serikali wa kutumia vyanzo vya umeme na upepo juu vilivyopo nchini.

" Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 150 katika Wilaya ya Kishapu, Shinyanga ambapo awamu ya kwanza ya mradi huo wenye megawati 50 imekamilika na hatua za kuingiza umeme huo katika Gridi ya Taifa zimeanza," Amesema Mhe. Salome.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe Esther Malleko aliyehoji mkakati wa Serikali katika kumaliza usambazaji wa umeme kwenye vitongoji vilivyosalia mkoani humo, Mhe. Salome amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na kazi za utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro ambapo hadi kufikia Januari 2026 jumla ya vitongoji 2,032 kati ya 2,258 sawa na asilimia 90 vilipatiwa umeme na kusalia vitongoji 226 ambavyo vitapelekewa umeme kupitia miradi mbalimbali.





 



Na. Peter Haule. na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma


Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa mageuzi ya uchumi yataendelea kuwa ajenda ya muda mrefu yakilenga si tu kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi bali kuhakikisha ukuaji huo unachangia katika upatikanaji wa ajira na ustawi wa wananachi kwa ujumla.


Amebainisha hayo wakati wa kikao na Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa ya Moody’s Investor Service ikiongozwa na  Bw. John Walsh, kilichofanyika Ofisi za Treasury Square, jijini Dodoma.

 

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa uchumi wa nchi umeendelea kuimarika licha ya matukio kadhaa yaliyokwaza ustawi wa uchumi wa dunia ukiwemo uviko 19 ambapo katika kipindi cha mwaka jana uchumi ulikua kwa asilimia 5.4 na unatarajiwa kukua zaidi mwaka huu wa fedha 2025/26 hadi kufikia asilimia 6.

 

Aidha, alibainisha kuwa mahitaji ya uwekezaji yanaendelea kuwa makubwa hususani kwenye miundombinu ya kimkakati kama Bandari, Viwanja vya Ndege, Reli na mtandao wa Barabara ili kuchochea maendeleo.

 

Alieleza kuwa nchi inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli iendayo Kasi -SGR, Bwawa la uzalishaji wa umeme la Julius Nyerere na uimarishaji wa sekta nyingine za kijamii na kiuchumi hatua itakayochochea zaidi ukuaji na uimara wa uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.

 

Akizungumzia Mfumuko wa bei amesema kuwa, hali imeendelea kuwa tulivu ambapo kiwango cha mfumuko wa bei kimeendelea kubaki chini ya asilimia tano kwa miaka kadhaa, kikiwa kati ya asilimia 2.9 na 3.4.

 

Kwa upande wake Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa Moody’s,  Bw. John Walsh, alisema kuwa uamuzi wa kupandisha hadhi ya uwezo wa nchi kukopesheka na kuipa alama B1 yenye mtazamo thabiti ulitokana na uthabiti wa kiuchumi na kifedha ambao nchi imeuonesha licha ya changamoto za uchumi za dunia katika miaka ya karibuni.


Alisema kuwa Tanzania iliendelea kurekodi ukuaji thabiti wa uchumi licha ya athari za janga la UVIKO-19, mfumuko wa bei wa kimataifa na kupanda kwa viwango vya riba duniani.


“Uamuzi wa kupandisha hadhi kwa kiwango cha B1 ulitokana na uthabiti wa sera za uchumi jumla na mageuzi ya Serikali yanayotekelezwa chini ya Mpango wa Shirika la Fedha la Kimatafa (IMF), unaokaribia kukamilika”, alisema Bw. Walsh.


Alisema kuwa Serikali imepiga hatua muhimu katika kushughulikia changamoto za muda mrefu, ikiwemo ukusanyaji mdogo wa mapato ya ndani na mapungufu ya utekelezaji wa sera, hivyo Tathmini ya sasa inalenga kufuatilia mafanikio, changamoto zilizopo, na mwelekeo wa mageuzi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.


Aidha alieleza kuwa tathmini hiyo inalenga kupata taswira ya kina ya hali ya sasa ya uchumi wa Tanzania, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha ukuaji endelevu na uthabiti wa kifedha kwa muda mrefu.

Matokeo ya mapitio ya hivi karibuni ya Kampuni za Moody’s na Fitch ziliipa Tanzania daraja la B1 (stable outlook) na B+ (stable outlook), mtawalia ambayo yanaonesha kwamba Tanzania ni nchi salama kwa wawekezaji.

 


Serikali imetoa wito kwa wadau kutoka sekta ya fedha nchini kuanzisha huduma na bidhaa za kifedha zitakazowezesha ajenda ya nishati safi ya kupikia kusambaa zaidi, hususan kwa kuwawezesha wajasiriamali wadogo katika maeneo ya pembezoni na vijijini pamoja na wabunifu wa teknolojia za matumizi ya nishati hiyo.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba  tarehe 4 Februari 2026 wakati akimwakilisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi katika uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika shule ya sekondari Bunge Wasichana iliyopo mkoani Dodoma.

"Tanzania imepiga hatua kubwa katika ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, matumizi ya nishati hii yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 na kufikia asilimia 23.2 mwaka 2025. Hata hivyo, bado takribani asilimia 77 ya kaya nchini zinatumia nishati isiyo safi ya kupikia, hivyo natoa wito kwa sekta binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma ajenda hii kwa kuwezesha upatikanaji wa nishati mbalimbali safi za kupikia katika maeneo ya pembezoni na yale ya vijijini." Amesema Mhe. Salome

Aidha, Mhe. Salome amewasisitiza Wasambazaji wa gesi za mitungi kuongeza vituo vya usambazaji na ujazaji wa gesi za mitungi ili kurahisisha upatikanaji wake kwa watumiaji wengi zaidi, pia Wabunifu na vijana walioko vyuoni kufanya tafiti na kubuni nyenzo na teknolojia zitakazowezesha ajenda hii kusambaa na kuwafikia watu wengi. 

Kuhusu mradi wa nishati safi ya kupikia aliouzindua Mhe. Salome amesema kuwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali kwa taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za binadamu na kutunza mazingira.

Ameongeza kuwa mfumo huo  uliozinduliwa  utawezesha chakula kupikwa kwa usafi, kwa haraka, kwa ufanisi, kwa gharama nafuu na bila madhara ya moshi kwa wapishi na wanafunzi huku mazingira  yakiendelea kustawi.

Mhe. Salome ameeleza kuwa kuzinduliwa kwa mradi huo ni sehemu ya juhudi za kitaifa zinazoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034 ambapo mpaka sasa tayari asilimia 23.2 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia huku taasisi 1,136 zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku zikihamia katika matumizi ya nishati hiyo.

Akiwa katika shule hiyo ya Wasichana Bunge, Naibu Waziri amezindua pia Klabu ya Nishati Safi ya Kupikia  yaani Clean Cooking School Club ambayo ni ya kwanza kuzinduliwa kwa Tanzania ambayo itakuwa mfano wa kuigwa na shule nyingine nchini katika kueneza elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.

Wanafunzi watakaojiunga na klabu hiyo watakuwa Vinara  wa Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Champions) na watashirikiana na Wizara ya Nishati na wadau wengine katika kutoa elimu mashuleni na katika jamii pamoja na kubuni teknolojia za nishati safi ya kupikia zitakazolinda afya na mazingira.

Awali Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bunge Wasichana, Richard Msana  alisema shule hiyo yenye wanafunzi 555 imefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za nishati ya kupikia baada ya kuachana na matumizi ya kuni na kuhamia katika gesi.

Amesema kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2022, shule ilikuwa ikitumia takribani shilingi milioni 10.5 kwa kila miezi mitatu kununua kuni. Baadaye walipoanza kutumia mkaa mbadala, gharama zilishuka hadi kufikia shilingi milioni 2.7 na hivi sasa, kupitia mradi wa matumizi ya gesi, shule imenunua tani moja ya gesi iliyotumika kwa miezi miwili, ambapo matumizi ni wastani wa shilingi milioni 1.3 kwa mwezi, kiwango ambacho ni nafuu zaidi kiuchumi.








 


๐˜ผ๐™ž๐™ฉ๐™–๐™ ๐™– ๐™จ๐™š๐™ง๐™ž๐™ ๐™–๐™ก๐™ž ๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™š๐™ ๐™– ๐™ข๐™ž๐™ฅ๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ค ๐™ข๐™ž๐™ฏ๐™ช๐™ง๐™ž ๐™ฎ๐™– ๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™–๐™ž๐™ฃ๐™ช๐™– ๐™ซ๐™ž๐™Ÿ๐™–๐™ฃ๐™– ๐™ ๐™–๐™ฉ๐™ž๐™ ๐™– ๐™ ๐™ช๐™Ÿ๐™ž๐™ ๐™ฌ๐™–๐™ข๐™ช๐™– ๐™ ๐™ž๐™ช๐™˜๐™๐™ช๐™ข๐™ž.

๐˜ผ๐™จ๐™๐™–๐™ช๐™ง๐™ž ๐™†๐™ค๐™ฃ๐™œ๐™–๐™ฃ๐™ž ๐™ฏ๐™– ๐™‘๐™ž๐™ฌ๐™–๐™ฃ๐™™๐™– ๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™š๐™ ๐™ฌ๐™– ๐™ ๐™ž๐™ก๐™– ๐™จ๐™š๐™๐™š๐™ข๐™ช.

"๐™ˆ๐™ฅ๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ค ๐™๐™ช๐™ช ๐™ฌ๐™– ๐™ ๐™ค๐™ฃ๐™œ๐™–๐™ฃ๐™ž ๐™ฏ๐™– ๐™ซ๐™ž๐™ฌ๐™–๐™ฃ๐™™๐™– ๐™ช๐™จ๐™ž๐™ฌ๐™š ๐™ข๐™ฅ๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ค ๐™ฌ๐™– ๐™ข๐™–๐™š๐™ฃ๐™š๐™ค ๐™›๐™ช๐™ก๐™–๐™ฃ๐™ž ๐™๐™–๐™ก๐™–๐™›๐™ช ๐™ข๐™–๐™ฌ๐™–๐™ฏ๐™ค ๐™ฎ๐™–๐™ ๐™–๐™ฌ๐™– ๐™ฉ๐™ช๐™ฉ๐™–๐™›๐™ž๐™ ๐™ž๐™ง๐™ž๐™– ๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™š๐™ ๐™– ๐™ ๐™–๐™ฉ๐™ž๐™ ๐™– ๐™ ๐™ž๐™ก๐™– ๐™ฌ๐™ž๐™ก๐™–๐™ฎ๐™– ๐™—๐™–๐™ก๐™ž ๐™ ๐™ฌ๐™–๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™– ๐™๐™ช๐™ค ๐™ฃ๐™ž ๐™ข๐™ฅ๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ค, ๐™ฃ๐™ž๐™ฃ๐™œ๐™š๐™ค๐™ข๐™—๐™– ๐™ฉ๐™ช๐™Ÿ๐™ž๐™š๐™ก๐™š๐™ ๐™š๐™ฏ๐™š ๐™ ๐™ช๐™ฌ๐™š๐™ ๐™– ๐™ ๐™ค๐™ฃ๐™œ๐™–๐™ฃ๐™ž ๐™ฏ๐™– ๐™ซ๐™ž๐™ฌ๐™–๐™ฃ๐™™๐™– ๐™ ๐™ฌ๐™š๐™ฃ๐™ฎ๐™š ๐™ ๐™ž๐™ก๐™– ๐™š๐™ฃ๐™š๐™ค"

Hayo yameswa na Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mkoani Iringa, Mhe. ๐——๐—ถ๐—ฐ๐—ธ๐˜€๐—ผ๐—ป ๐—Ÿ๐˜‚๐˜๐—ฒ๐˜ƒ๐—ฒ๐—น๐—ฒ (๐—ฉ๐—ถ๐—น๐—น๐—ฎ) wakati akichangia kuhusiana na mpango wa serikali katika kujenga kongani za viwanda.

Mhe. Lutevele ameeleza kuwa ni muhimu kujenga kongani za viwanda kwa kila eneo kwa kile alichodai kuwa katika sekta ya viwanda wapo watu wengi walioajiriwa kufanya kazi na huwenda bado kama serikali haijawafikia.

Akitolea mfano jambo hilo, Mhe. Lutevele amesema "..๐˜ฌ๐˜ธ๐˜ข ๐˜ฎ๐˜ง๐˜ข๐˜ฏ๐˜ฐ ๐˜ฌ๐˜ข๐˜ต๐˜ช๐˜ฌ๐˜ข ๐˜ฏ๐˜ค๐˜ฉ๐˜ช ๐˜บ๐˜ฆ๐˜ต๐˜ถ ๐˜ฉ๐˜ข๐˜ต๐˜ข ๐˜ถ๐˜ฌ๐˜ช๐˜ต๐˜ฐ๐˜ฌ๐˜ข ๐˜ฏ๐˜ซ๐˜ฆ ๐˜ฉ๐˜ข๐˜ฑ๐˜ข ๐˜ด๐˜ข๐˜ด๐˜ข ๐˜ฉ๐˜ช๐˜ท๐˜ช ๐˜ถ๐˜ต๐˜ข๐˜ฌ๐˜ถ๐˜ต๐˜ข ๐˜ฌ๐˜ช๐˜ญ๐˜ข ๐˜ฃ๐˜ข๐˜ข๐˜ฅ๐˜ข ๐˜บ๐˜ข ๐˜ฎ๐˜ต๐˜ข๐˜ข ๐˜ฌ๐˜ถ๐˜ฏ๐˜ข ๐˜จ๐˜ฆ๐˜ณ๐˜ฆ๐˜ซ๐˜ช, ๐˜ท๐˜ช๐˜ซ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข ๐˜ธ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข๐˜ต๐˜ฆ๐˜ฏ๐˜จ๐˜ฆ๐˜ฏ๐˜ฆ๐˜ป๐˜ข ๐˜ฎ๐˜ข๐˜จ๐˜ข๐˜ณ๐˜ช, ๐˜ท๐˜ช๐˜ซ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข ๐˜ธ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข๐˜ง๐˜ข๐˜ฏ๐˜บ๐˜ข ๐˜ฌ๐˜ข๐˜ป๐˜ช ๐˜ป๐˜ข ๐˜ถ๐˜ง๐˜ถ๐˜ฏ๐˜ฅ๐˜ช ๐˜ด๐˜ฆ๐˜ญ๐˜ฆ๐˜ฎ๐˜ข๐˜ญ๐˜ข, ๐˜ธ๐˜ข๐˜ฎ๐˜ฐ ๐˜ฉ๐˜ถ๐˜ฎ๐˜ฐ ๐˜ญ๐˜ข๐˜ฌ๐˜ช๐˜ฏ๐˜ช ๐˜ฉ๐˜ข๐˜ธ๐˜ข ๐˜ท๐˜ช๐˜ซ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข ๐˜ฉ๐˜ข๐˜ต๐˜ถ๐˜ซ๐˜ข๐˜ธ๐˜ข๐˜ฌ๐˜ถ๐˜ด๐˜ข๐˜ฏ๐˜บ๐˜ข ๐˜ด๐˜ฆ๐˜ฉ๐˜ฆ๐˜ฎ๐˜ถ ๐˜ฎ๐˜ฐ๐˜ซ๐˜ข"

Akiwekea msisitizo jambo hilo, Mhe. Lutevele amelieleza Bunge kuwa kwa serikali kutofanya hivyo kunaathiri mambo makubwa mawili ambayo amesema ni kutokuwa na mpangilio mzuri katika miji Pamoja na kushindwa serikali kushindwa kukusanya mapato kwakuwa vijana hao hawajekewa mpango mzuri wa kurudi kuangalia maendeleo yao.

Aidha, ameeleza namna ambavyo mpango wa BBT ulivyoshindwa kufuzu katika kuleta matokeo chanya kwa ukubwa kwenye kuwainua vijana katika kujikwamua kiuchumi na kushauri namna bora ya kufanya.

#KaziNaUtuTunasongaMbele

Nilikuwa kwenye ndoa ambayo kwa nje ilionekana ya kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, hakukuwa na kelele. Lakini kulikuwa na tatizo moja lililonisumbua kimya kimya kila aliponikaribia, mwili wangu ulikataa kabisa.

Sikuwa najifanya, wala sikuwa namchukia. Ilikuwa ni kama mwili wangu na moyo wangu havikuelewana tena. Nilitembea hospitali kadhaa. Vipimo vikafanywa, majibu yakarudi yale yale: uko sawa.

Lakini nilijua ndani yangu kuna kitu hakiko sawa. Nilihisi hatia, huzuni, na hofu kuwa ndoa yangu ingeangamia kwa jambo ambalo sikuweza kulieleza vizuri hata kwa maneno.

Kadri siku zilivyopita, ukimya ukaingia kati yangu na mume wangu. Nilijitenga, nikajilaumu, na wakati mwingine nikajikuta nikilia peke yangu usiku. Madaktari walikuwa wamesema niko sawa, lakini kwa nini basi mwili wangu ulikataa?

Ndipo nilipopata ushauri wa kumtafuta mtu anayeelewa mahusiano, nafsi, na mizizi ya matatizo ya ndani. Soma Zaidi.
Baada ya harusi yangu, nilikuwa na furaha kubwa. Ndoa ilikuwa mpya, maisha yalionekana kuanza upya, na kila mtu alinitakia heri. Lakini baada ya wiki chache, kitu cha ajabu kilianza kutokea.

Nilianza kuota ndoto ileile mara kwa mara. Kila wiki, ndoto hiyo ilirudi bila kubadilika mandhari ileile, hisia ileile, na hofu ileile. Mwanzoni nilipuuzia.

Nilijiambia labda ni mawazo mengi au uchovu wa maandalizi ya harusi. Lakini ndoto zilipoendelea, nilianza kuona athari zake hata nikiwa macho.

Nilikuwa mchovu kila siku, moyo haukuwa na amani, na ndoa yangu ilianza kuingia ukimya usio wa kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, lakini furaha ile ya mwanzo ilianza kupotea polepole.

Nilipomweleza mume wangu, alicheka na kusema ni kawaida. Lakini moyoni nilijua kuna kitu hakiko sawa. Ndipo nikaanza kutafuta ushauri wa busara.Soma Zaidi.

Maisha yangu nyumbani yalikuwa hatari. Kila usiku, nilihisi kama kuna mtu anakuja. Hatua zisizoelezeka zilisikika nje ya mlango wangu. Wakati mwingine, niliona kivuli kisichoelezeka karibu na dirisha.

Familia yangu ilikuwa katika hofu. Hatukuwa na njia ya kujua ni lini hatari ingeibuka. Nilijaribu kuziba milango, kuacha kufanya kelele, na hata kulala na tahadhari. Lakini kila kitu kilionekana kushindwa.

Usiku ulikuwa mzito, na mawazo mabaya yalikuwa sehemu ya kila siku yangu. Nilihisi kama hatimaye maisha yangu yatakuwa hatarini.Soma Zaidi.