Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekutana na kuzungumza na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam Aprili 21, 2026.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-Mzalendo blog-DODOMA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), leo 21 Aprili 2026, imetumia fursa ya Wiki ya Nishati kuwahamasisha waheshimiwa wabunge kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini pamoja na vituo vya CNG ili kuendelea kusogeza huduma kwa wananchi.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw. Wilfred Mwakalosi, alisema kuwa EWURA inatumia maonesho hayo kutoa elimu kuhusu namna inavyohakikisha upatikanaji wa huduma za nishati na maji kwa wakati na kwa gharama nafuu.

Amebainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi, hivyo kuwajengea uelewa kuhusu udhibiti, fursa za uwekezaji na utaratibu wa kupokea na kushughulikia migogoro na malalamiko kutawawezesha kuwasilisha taarifa sahihi kwa wananchi kuhusu juhudi za Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za umeme, mafuta na gesi asilia.

Akizungumza katika maonesho hayo, Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi, amesema elimu inayotolewa pia inalenga kuwafahamisha wananchi jinsi EWURA inavyosimamia upatikanaji wa huduma za mafuta nchini kwa kuzingatia ubora uliopitishwa na gharama sahihi.

Aidha, amewahamasisha wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta hiyo, hususan ujenzi wa vituo vya mafuta vya gharama nafuu vijijini na mijini pamoja vituo vya kujazia gesi asilia kwenye magari (CNG).

Kwa upande wake, Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,amesema  elimu inayotolewa imejikita katika kueleza namna EWURA inavyosimamia upangaji wa viwango vya bei za huduma za umeme, mafuta na gesi asilia. Aliongeza kuwa mamlaka hiyo huweka mizania kati ya maslahi ya watoa huduma na watumiaji, na kwamba wabunge waliopata elimu hiyo wataweza kuiwasilisha ipasavyo kwa wananchi katika maeneo yao.

Akizungumzia sekta ya gesi asilia, Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza, amesema  EWURA itaendelea kusimamia ubora wa miundombinu ya gesi asilia nchini na kuhamasisha matumizi yake, hususan katika magari.

Amebainisha kuwa hadi sasa vituo 18 vimepata leseni ya EWURA kutoa huduma ya gesi asilia, huku vituo sita vingine vikiwa katika hatua za mwisho za kupata leseni katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Aidha, mipango inaendelea kwa baadhi ya makampuni kusambaza gesi asilia iliyokandamizwa katika mikoa ya Morogoro na Dodoma.

Kwa upande wa sekta ya umeme, Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba, amewahamasisha wabunge na wadau wanaotembelea maonesho hayo kutumia mafundi umeme wenye leseni kutoka EWURA ili kuhakikisha usalama wa nyumba na mali zao. Alisema EWURA inaendelea kutoa leseni kwa mafundi umeme wenye sifa stahiki, ambapo zaidi ya leseni 1,000 zilitolewa katika mwaka wa fedha uliopita.

Naye Ofisa Rasilimali Watu Mkuu, Bi. Limi Kahabi, amesema EWURA ni mwajiri anayezingatia misingi ya usawa na haki katika mchakato wa ajira, akisisitiza kuwa taasisi hiyo huajiri kwa kuzingatia sifa, weledi na usawa kwa wote.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

 Ofisa Mkuu, Usimamizi wa Rasilimali Watu,Bi. Limi Kahabi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho  ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho  ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma






Na Oscar Assenga, Muheza

Mjumbe wa Kamati ya Hamasa Kanda ya Kaskazini wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Lukindo Mohamed, ametangaza rasmi kujiondoa ndani ya chama hicho na kueleza kuwa hatarajii kujiunga na chama kingine chochote cha siasa.

Lukindo, ambaye pia aliwahi kuwa Kaimu Katibu wa Baraza la Wazee Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Wilaya ya Muheza, amesema amefikia uamuzi huo kwa hiari yake mwenyewe ili aweze kuwa huru na kujikita katika shughuli zake binafsi, ikiwemo kilimo na malezi ya familia.

Akizungumza na waandishi wa habari  Lukindo alieleza kuwa moja ya sababu kubwa ya kujiondoa kwake ni kutoridhishwa na mwelekeo wa chama chake, hususan kuhimiza maandamano kama njia ya kutatua changamoto za kisiasa.

Alisema kuwa licha ya Tanzania kuwa nchi ya kidemokrasia inayoruhusu wananchi kuchagua viongozi kwa kura bado kumekuwa na msisitizo wa mara kwa mara wa kufanya maandamano, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara kwa wananchi, ikiwemo majeruhi na vifo.

“Naamini kabisa kuwa suluhu ya matatizo ya nchi yetu haiwezi kupatikana kupitia maandamano, bali kupitia mazungumzo na maridhiano ni muhimu viongozi wa vyama vya siasa kukaa pamoja na kujadiliana kwa lengo la kuijenga nchi,” alisema Lukindo.

Aliongeza kuwa hajashawishiwa na mtu yeyote kuchukua uamuzi huo, bali ametumia busara na uzoefu wake wa muda mrefu katika siasa, akieleza kuwa amehudumu ndani ya chama hicho tangu mwaka 1992 katika ngazi mbalimbali, ikiwemo Katibu wa Wilaya ya Muheza kuanzia mwaka 2010 hadi 2024.

Kwa upande wake, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Lushoto, Andrew Mjema, naye ametangaza kujiondoa ndani ya chama hicho, akieleza kuwa amechoshwa na kile alichokiita siasa za matamko na maandamano zisizo na tija kwa wanachama wa kawaida.

Mjema alisema kuwa mara nyingi viongozi wa juu wamekuwa wakitoa wito wa maandamano huku madhara yake yakiwakumba zaidi wanachama wa ngazi za chini, hali ambayo ameona si ya haki.

“Viongozi wanazungumza kuhusu maandamano lakini hawashiriki moja kwa moja, wanaoumia ni wanachama wa chini. Hii si sawa, ndiyo maana nimeamua kujiondoa na kuendelea na shughuli zangu za ufundi,” alisema Mjema.

Alisisitiza kuwa hatajiunga na chama chochote cha siasa, akiongeza kuwa anahitaji muda wa kujiendeleza kiuchumi na kuishi maisha yake binafsi nje ya siasa.

Wote wawili wamehitimisha kwa kushauri vyama vya siasa nchini kuweka mbele mazungumzo na maridhiano badala ya maandamano, wakiamini kuwa hiyo ndiyo njia sahihi ya kudumisha amani na kuleta maendeleo nchini.


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 21 Aprili 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mtandao wa Viongozi Wanawake wa Afrika (African Women Leaders Network - AWLN), ulioongozwa na Marais wastaafu wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, na Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia ya Ethiopia, Mhe. Sahle-Work Zewde, jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yalijikita katika hali ya kisiasa nchini pamoja na matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, yakihusisha pia umuhimu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.

Ujumbe huo upo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kufanya mashauriano na viongozi mbalimbali wa kitaifa kuhusu maendeleo ya kisiasa na juhudi zinazoendelea za kuimarisha demokrasia na utawala bora, ikiwa ni sehemu ya mchango wa wanawake viongozi wa Afrika katika kulinda amani na utulivu barani.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi,alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

.....

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio, amewaomba waheshimiwa wabunge na wadau mbalimbali kuendelea kutembelea maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma, ili kupata elimu juu ya shughuli za kimkakati zinazotekelezwa na taasisi zilizo chini ya wizara hiyo pamoja na kubaini fursa za uwekezaji zinazopatikana.

Akiwa akiwa katika banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. Mataragio amesema mamlaka hiyo imeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuhakikisha uwiano kati ya maslahi ya watoa huduma na watumiaji wa huduma zinazodhibitiwa, ikiwemo mafuta, gesi asilia na umeme.

“Tumeshuhudia jitihada kubwa zinazofanywa na EWURA katika kusimamia ubora wa huduma na bei stahiki, jambo ambalo linachangia kukuza uchumi na kulinda wananchi,” amesema Dkt. Mataragio.

Ameongeza kuwa uwepo wa EWURA katika maonesho hayo unatoa fursa kwa wananchi kupata elimu kuhusu haki na wajibu wao katika matumizi ya nishati, sambamba na kuelewa mifumo ya udhibiti inayolenga kuboresha huduma na fursa mbalimbali za uwekezaji.

Kwa upande wao, baadhi ya wabunge waliotembelea banda hilo pia waliipongeza EWURA kwa uwajibikaji wake, wakisema imekuwa mstari wa mbele kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi katika sekta ya nishati pamoja na kuhakilisha upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

Wiki ya Nishati 2026 imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati, zikiwemo taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati kwa lengo la kuonesha maendeleo na fursa zilizopo katika sekta hiyo muhimu kwa ustawi wa uchumi wa taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi,alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi,alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akisisitiza jambo kwa watumishi wa EWURA alipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Banda la EWURA kwenye Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio akipokea zawadi kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw.Wilfred Mwakalosi, mara baada ya kutembelea Banda la EWURA kwenye Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Wabunge mbalimbali wakipata elimu walipotembelea banda la EWURA  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia mafuta na gesi asilia, Dkt. James Mataragio,akizungumza mara baada ya kutembelea mabanda ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati  katika  maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (anayeshughulikia mafuta na gesi),Dkt. James Mataragio ameipongeza Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kwa kuhakikisha nchi inakuwa na mafuta ya kutosha wakati wote.
Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba kuunganishiwa huduma ya majisafi na salama, wakati mradi wa maji wa Kibosha Mnarani ukiendelea kukamilishwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameitaka TIRDO kushirikiana na Taasisi zingine kuhakikisha watanzania wanapata nishati safi rafiki na Kwa bei rahisi .
Na Mwandishi Wetu

JINHUA, CHINA — Taasisi za elimu ya juu kutoka Tanzania zikiwemo ADEM, MUCE, TIA, SUZA na UDSM zimeshiriki Kongamano la 3 la Marais wa Vyuo Vikuu kati ya China na Afrika lililofanyika jijini Jinhua kuanzia Aprili 14 hadi 20, 2026.

 



Na Oscar Assenga, Tanga

Kwa muda mrefu, gharama za pango zimekuwa mzigo usioonekana lakini mzito kwa taasisi nyingi nchini. 

Ni gharama ambazo zimezoeleka kiasi cha kukubalika kama sehemu ya kawaida ya uendeshaji, bila kuhojiwa kwa kina iwapo zinaweza kubadilishwa kuwa fursa.

Ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga, hali hiyo inaanza kuchukua mwelekeo mpya.

Fedha ambazo zilikuwa zikitumika kila mwaka kugharamia makazi ya watumishi sasa zinaelekezwa kwenye mkakati wenye dira tofauti ujenzi wa nyumba za watumishi katika kila wilaya ya mkoa.

Haya ni mabadiliko kutoka matumizi ya muda mfupi kwenda uwekezaji wa muda mrefu.


 

Upepo Mpya wa Ubunifu

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, anauelezea mkakati huo kama hatua ya kimkakati inayolenga kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuimarisha uwezo wa chama kuwekeza katika maendeleo mengine.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya chama mkoani humo, ikiwemo ujenzi wa nyumba za watumishi, Abdurhaman alionesha kuridhishwa na hatua nyumba hizo zilizofikiwa  katika maeneo mbalimbali mkoani humo , lakini zaidi akisisitiza thamani ya mshikamano uliowezesha mafanikio hayo.

“Kwa ujumla mmefanya kazi kubwa sana. Nawashukuru wadau wote walioshiriki, kwa sababu walichotoa si msaada tu, bali ni uwekezaji ambao utaendelea kuzaa matunda,” alisema kwa msisitizo.

Kauli hiyo inaakisi mwelekeo mpya wa fikra kutazama rasilimali si kama matumizi ya papo kwa papo, bali kama uwekezaji wa muda mrefu.

 

Kutoka Pango kwenda Uwekezaji

Kabla ya mradi huu kuanza, baadhi ya watumishi walikuwa wakilipa hadi shilingi 200,000 kwa mwezi kama pango, huku wengine wakilipa zaidi kulingana na eneo.

Kwa mwaka mmoja, gharama hizo zilijikusanya na kuwa mzigo mkubwa kwa chama—fedha ambazo, kwa mtazamo wa sasa, zingeelekezwa kwenye miradi mingine ya maendeleo.

Sasa picha inaanza kubadilika.

Kwa makadirio ya haraka, kukamilika kwa nyumba hizo katika wilaya zote za Mkoa wa Tanga kunatarajiwa kuiwezesha CCM kuokoa hadi shilingi milioni 90 kwa mwaka.

Fedha hizo, kwa mujibu wa uongozi wa chama, sasa zinageuka kuwa mtaji mpya wa maendeleo ya ndani.

“Fedha hizi zitasaidia kufanya shughuli nyingine za maendeleo ndani ya chama. Huu ni ubunifu ambao umehimizwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa pamoja na Kamati Kuu,” alieleza Abdurhaman.

 

Zaidi ya Takwimu: Ustawi wa Mtumishi

Licha ya faida za kifedha, mchango mkubwa zaidi wa mradi huu upo katika kuboresha ustawi wa watumishi.

Makazi bora, salama na yenye hadhi yanatarajiwa kuongeza ari, utulivu na ufanisi kazini—ambapo matokeo yake yanaonekana moja kwa moja katika utendaji wa kila siku.

Kwa lugha rahisi, mtumishi mwenye uhakika wa makazi ni mtumishi mwenye uhakika wa kazi bora.

Nidhamu ya Mali na Usimamizi wa Ardhi

Katika hatua nyingine, Abdurhaman alisisitiza umuhimu wa kulinda mali za chama kwa kuhakikisha maeneo yote yana hati miliki halali.

Alibainisha kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuzuia migogoro ya ardhi na kulinda uwekezaji wa muda mrefu wa chama.

Aidha, alihimiza upandaji wa miti ya kivuli na matunda katika maeneo ya chama, hatua inayolenga si tu kuboresha mazingira bali pia kuongeza thamani ya maeneo hayo na kulinda mipaka yake.


 

Wajibu wa Viongozi wa Wilaya

Viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya wamepewa jukumu la kuhakikisha sheria za ardhi zinazingatiwa kikamilifu, ikiwemo ulipaji wa kodi ya pango la ardhi na kufuata taratibu zote za umiliki.

Hii inaweka msisitizo kwenye uwajibikaji na nidhamu ya matumizi ya mali za umma na za chama.

 

Hitimisho: Gharama Zinapogeuka Fursa

Kwa ujumla, mkakati wa ujenzi wa nyumba za watumishi unaibuka kama mfano wa namna taasisi zinavyoweza kubadili changamoto kuwa fursa za kiuchumi na kijamii.

Ndani ya CCM Tanga, hatua hii si tu inaboresha maisha ya watumishi, bali pia inaweka msingi imara wa uendelevu wa kifedha na kiutendaji wa chama kwa siku zijazo.

Na zaidi ya yote, inaonesha kwamba maendeleo si suala la kuongeza matumizi—bali ni sanaa ya kuyabadilisha kuwa uwekezaji.

0714543839

Serikali imesisitiza umuhimu wa michezo kwa wafanyakazi kama sehemu muhimu ya kuimarisha afya na kuongeza ufanisi mahali pa kazi.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe.Rahma Kisuo, wakati akifungua rasmi Michezo ya Mei Mosi Kitaifa 2026 iliyofanyika Aprili 20, 2026 katika viwanja vya Sabasaba mkoani Njombe.

Amesema kuwa afya ya mfanyakazi ni mtaji mkubwa unaochangia maendeleo ya taasisi na taifa kwa ujumla, hivyo michezo inapaswa kupewa kipaumbele.

Aidha, Mhe.Kisuo amehimiza wafanyakazi kote nchini kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara badala ya kusubiri vipindi vya mashindano pekee. Amesisitiza kuwa mazoezi yawe sehemu ya maisha ya kila siku ili kuboresha afya na kuongeza tija kazini, huku akizitaka taasisi zote za umma na binafsi kuhakikisha zinatoa nafasi kwa wafanyakazi kushiriki shughuli za michezo.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Njombe Dkt. Stephane Nindi akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa, kufanyika kwa Maadhimisho ya Meimosi Njombe kumetoa fursa za kibiashara kwa wananchi wa mkoa huo.

Katika hatua nyingine, amewapongeza washiriki wa Michezo ya Mei Mosi na kuwataka kudumisha nidhamu, mshikamano na ushindani wa haki.

Amesisitiza kuwa michezo iwe chachu ya kuimarisha udugu na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi badala ya kuwa chanzo cha migogoro.

Kwa mwaka 2026, michezo hiyo inaongozwa na kauli mbiu isemayo, “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050,” huku watumishi na wachezaji wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) wakiwa miongoni mwa washiriki wa ufunguzi huo.