Meneja wa Kanda ya Kaskazini (TBS),Mhandisi Yona Afrika akitoa elimu ya Viwango kwa wajasiriamali katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayoendelea jijini Arusha.

Na.Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limehimiza wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa wanaozalisha bure kwa gharama za Serikali, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na vikwazo vya kiabiashara.

Mbali na wito huo kwa wajasiriamali, shirika hilo limewataka wananchi kuhakikisha wananunua na kutumia bidhaa zilizothibishwa ubora na shirika hilo kwa kujenga utamaduni wa kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio.

Wito huo umetolewa na Meneja wa TBS Kanda ya Kaskazini,, Yona Afrika,. wakati akizungumza kwenye Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Arusha.

Alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa wajasiriamali katika kukuza uchumi wa Taifa na wao binafsi, ndiyo maana imebeba dhamana ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zao bure.

"Kwa hiyo tumeshiriki katika maonesho haya kwa sababu ni fursa ya kukutana na wadau mbalimbali na kuwaelezea shughuli zinazofanywa na TBS na fursa nyingine ambazo zinapatikana kama kuthibitisha bidhaa za wajasiriamali bure," alisema.

Alisema bidhaa zikishathibitishwa na TBS zinaingia masoko ya Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na ya kikanda bila vikwanzo vya biashara.

Alisema nchi za EAC zimeingia makubaliano, ambapo bidhaa zikishathitishwa na shirika la viwango la nchi husika,hazitakiwi kupimwa tena zinapopelekwa kwenye soko la nchi nyingine.

"Kwa hiyo TBS tumeshiriki maonesho haya kusudi kukutana na wadau mbalimbali, ambao tunawafikia na kuwapa taratibu za kufuata kuthibitisha ubora.

"Kwa kweli tunaishukuru Serikali kwa kuendelea kuandaa Maonesho haya ya Nanenane, kwani fursa muhimu ya kukutana na kutoa elimu kwa wadau.

Mfano tunawaambia kuwa wakipata barua ya utambulisho kutoka SIDO wakija kwetu utaratibu wa kuthibitisha ubora wa bidhaa unaanza mara moja, kwa wajasiriamali" alisema Afrika.

Kwa upande wa wananchi waliotembelea banda la TBS, walitakiwa kuhakikisha wanatumia bidhaa zilizothibitishwa ubora ili kulinda afya zao na kuona thamani ya fedha zao.

Alisema ni muhimu kusoma taarifa zilizopo kwenye vigungashio ili kujua kama zina ubora uliothititishwa na shirika pamoja na muda wake wa mwisho wa matumizi.



‎Waziri Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka ameipongeza Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa utekelezaji wa Mpango wa Matengenezo ya Barabara kwa Kutumia Vikundi vya Kijamii (CBRM) akieleza kuwa ni fursa muhimu ya kuwawezesha wananchi hususan vijana kushiriki katika shughuli za matengenezo ya barabara na kujiongezea kipato.
‎Mhe. Nanauka ametoa pongezi hizo alipotembelea banda la TARURA katika Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa ya Kilimo Nanenane yanayoendelea katika uwanja wa Dkt. John Malecela mkoani Dodoma.
‎Amesema kuna umuhimu wa kuwafikia wananchi kwa kuwapa elimu ya kutosha kuhusu fursa zinazotolewa kupitia mpango wa CBRM ili waweze kushiriki kikamilifu. Aidha, amependekeza kuwepo kwa ushirikiano wa karibu kati ya Wizara ya Maendeleo ya Vijana na TARURA katika utekelezaji wa mpango huo.
‎"Ni muhimu kuongeza kasi ya utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu fursa zilizopo katika mpango wa CBRM. Pia napendekeza kuwepo kwa vikao vya mara kwa mara kati ya Wizara ya Maendeleo ya Vijana na TARURA ili kuimarisha ushirikiano na kuhakikisha malengo ya mpango huu yanafikiwa", amesema Mhe. Nanauka.
‎Kwa upande wake, Mratibu wa mpango wa CBRM TARURA Makao Makuu, Mhandisi Richard Missa amemueleza Waziri huyo kuwa Wakala umeanza utekelezaji katika mkoa wa Tanga, Morogoro,Dodoma na Pwani ambapo barabara zaidi ya kilomita 1500 zinahudumiwa na vikundi 302 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
‎Aidha, amesema Wakala umejipanga kutekeleza mpango wa CBRM katika mikoa yote 25 ya Tanzania Bara kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ambapo zaidi ya kilomita 7000 za barabara zitafanyiwa matengenezo na vikundi 1100 vitapata fursa katika kazi hizo. 
‎Mhandisi Missa amesema mpango huo unalenga kuongeza ushiriki wa wananchi katika matengenezo ya kawaida ya barabara sambamba na kuchochea ajira na maendeleo ya kiuchumi katika jamii.
‎TARURA itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu utekelezaji na mafanikio ya mpango wa CBRM ili wananchi waendelee kunufaika na fursa zinazotokana na mpango huo.
‎Wakati huo huo, TARURA imewahimiza wananchi kuendelea kutembelea banda lake katika Maonesho ya Nanenane ili kupata elimu kuhusu majukumu ya Wakala, ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu miundombinu ya barabara pamoja na kujionea mafanikio ya miradi inayotekelezwa nchini kwa lengo la kuimarisha maendeleo endelevu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu,akiwahutubia washiriki wa mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na OSHA katika Mgodi wa Namungo uliopo Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.
 

Na Mwandishi Wetu

Meneja Kanda ya Kati wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bi. Hawa Lweno, ametoa wito kwa mafundi umeme kutembelea banda la Mamlaka hiyo katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya John Malecela jijini Dodoma, ili kupata elimu kuhusu umuhimu wa kupata leseni za ufundi umeme zinazotolewa na EWURA, pamoja na utaratibu wa kuomba leseni hizo.

Amesema kuwa leseni za ufundi umeme ni muhimu katika kuhakikisha huduma za ufungaji, ukarabati na matengenezo ya mifumo ya umeme zinafanywa na mafundi wenye sifa na wanaozingatia viwango vya ubora na usalama, hivyo kupunguza ajali zinazoweza kusababishwa na kazi za umeme zisizokidhi matakwa ya kitaalamu.

“Hili linaendana sambamba na wito kwa wananchi kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa mifumo yao ya umeme kila baada ya miaka mitano tangu mfumo huo ulipofungwa,” ameeleza.

Bi. Lweno amesema EWURA pia inatumia Maonesho ya Nanenane kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuongeza matumizi ya nishati safi kwa Watanzania.

Aidha, maeneo mengine yanayotolewa elimu ni pamoja na fursa za uwekezaji wa vituo vya mafuta katika maeneo ya vijijini, taratibu za kuwasilisha na kushughulikia malalamiko yanayohusu huduma zinazodhibitiwa na EWURA, pamoja na matumizi salama ya huduma za mafuta, umeme na gesi.

     

 


Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere leo imewaaga rasmi wajumbe wawili wa bodi ya Chuo hicho ambao wamemaliza muda wao tangu walipoteuliwa kushika nafasi hizo kwa kipindi cha miaka mitatu.

Wajumbe walioagwa ni pamoja na Prof. David Mfinanga na Ally Kibona ambao waliteuliwa Agosti 2023 na kuwa hadi Agosti 2026 wanatimiza miaka mitatu ya kutumikia nafasi hizo.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wajumbe hao, Mwenyekiri wa bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mhe. Stephen Wasira amewashukuru Wajumbe hao waliomaliza muda wao kwa utumishi wao na mchango walioutoa katika kuhakikisha masuala mbalimbali yanayohusu taasisi yanakwenda sawa.

Mhe. Wasira amesema Chuo kinathamini na kutambua michango yao waliyokuwa wanaitoa wakati wa kutimiza majukumu yao kupitia vikao na ziara mbalimbali za kikazi ambazo wamekuwa wakizifanya.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo amewapongeza na kuwashukuru kwa kipindi cha miaka mitatu kwa kutumikia nafasi zao kwa uaminifu, uadilifu na ushirikiano waliounesha kwa wajumbe wengine wa bodi hiyo kwa lengo la kuhakikisha Chuo kinatimiza malengo yake.

Nao Wajumbe waliomaliza muda wao ambao ni Prof. David Mfingana na Ally Kibona wamewashukuru wajumbe waliobakia kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakiupata kutoka kwenye bodi hiyo kwa muda wote waliokuwa wakitumikia nafasi zao, vilevile wamejifunza mengi kutoka kwa viongozi ambao walikuwa wakifanya nao kazi.

 

Imetolewa na

Kitengo cha Mawasilano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

7.08.2026



Na Munir Shemweta, Itilima

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amepongeza hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa Shule mpya ya Awali na Msingi Mwankola iliyopo Kijiji cha Lagangabilili, Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, huku akisisitiza kuwa elimu ni msingi muhimu wa maisha na maendeleo ya Taifa.

Dkt. Akwilapo amesema jamii inayowekeza katika elimu inaweka msingi imara wa maendeleo ya kizazi cha sasa na kijacho kwa kuwa elimu huwajengea watoto uwezo wa kujitambua, kupata maarifa na kujiandaa kushika nafasi mbalimbali za uongozi na kitaaluma.

Ametoa kauli hiyo Agosti 7, 2026 wakati wa ziara yake katika Kitongoji cha Mwankola, Kata ya Lagangabilili wilayani Itilima, ambako alikagua maendeleo ya mradi huo na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule hiyo.

Amesema wananchi wa Itilima wanapaswa kuendelea kuyapa umuhimu mkubwa masuala ya elimu na kuhakikisha watoto wanapata fursa ya kusoma katika mazingira bora, akieleza kuwa elimu ndiyo njia inayoweza kuwajengea vijana uwezo wa kuwa viongozi na wataalamu wenye mchango katika jamii.

‘’uwekezaji unaofanywa na Serikali katika miundombinu ya elimu unapaswa kuungwa mkono na wananchi, hususan wazazi na walezi, kwa kuhakikisha watoto wanahudhuria masomo na kupata mahitaji muhimu yatakayowawezesha kujifunza vizuri’’. Amesema Dkt Akwilapo

Akiwa katika eneo la mradi huo, Waziri Akwilapo aliwahimiza wazazi kutambua kuwa wao ni sehemu muhimu ya mafanikio ya elimu ya watoto wao, hivyo wanapaswa kushirikiana na Serikali na viongozi wa shule katika kuboresha mazingira ya ujifunzaji.

Pamoja na hilo, amesisitiza umuhimu wa wanafunzi kupata chakula shuleni, akibainisha kuwa upatikanaji wa chakula ni moja ya mambo yanayoweza kumsaidia mtoto kuwa katika mazingira mazuri ya kujifunza na kufuatilia masomo.

Amesema jitihada za kujenga madarasa na shule mpya zinapaswa kwenda sambamba na ushiriki wa wazazi katika ustawi wa wanafunzi ili uwekezaji unaofanywa na Serikali katika sekta ya elimu uweze kutoa matokeo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha amesema mkoa wake umepiga hatua katika sekta kubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo Afya na miundombinu.

Ameeleza kuwa hatua hizo zinatokana na juhudi kubwa zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Ziara hiyo ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuwapeleka mawaziri katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali iliyoahidiwa kwa wananchi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akiomba kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Kupitia ziara hizo, Serikali inafuatilia hatua za utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na changamoto zinazoweza kujitokeza ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma na miradi iliyokusudiwa kwa wakati.










 


Wakati Maonesho ya Nanenane yakiendelea kupamba moto katika maeneo mbalimbali nchini, Hifadhi ya Ngorongoro imeendelea kutanua mbawa zake na kuonesha vivutio vya utalii mubashara kupitia mitandao ya kijamii na luninga kubwa iliyofungwa kwenye banda la Wizara ya Maliasili na Utalii.

Watalii wanaotembelea maonesho hayo wameshuhudia vivutio vya wanyama mbalimbali kama Faru, Tembo, Pundamilia, Swala, Nyumbu, Simba wakiwa honeymoon, na makundi ya Nyati yakiwa yanajimbwafai katika maeneo yao ya asili.

Akiwa katika Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii, Meneja wa Idara ya Utalii na Masoko wa Ngorongoro SACC. Mariam Kobelo, ameeleza kuwa Ngorongoro imeendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya utalii na kuboresha huduma ili wageni waweze kushuhudia vivutio mubashara na kufurahia huduma zinazotolewa na Ngorongoro.

“Ngorongoro ikiwa ni eneo la kipekee, tumejipanga kuendelea kutumia teknolojia za kisasa kufikia watu na kuona maajabu na simulizi adhimu za kipekee.

 


Na WMA - DODOMA.


Wanafunzi wa Klabu ya Vipimo (Vipimo Club) kutoka Shule ya Msingi Mtemi Mazengo ya jijini Dodoma, wamegeuka walimu kwa siku moja baada ya kumpa elimu ya vipimo Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, katika banda la Wakala wa Vipimo (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane, Dodoma.

Leo Agosti 7, 2026, Naibu Waziri Londo alishangazwa na ufasaha wa wanafunzi hao walipomweleza umuhimu wa vipimo sahihi, kuandika kwa usahihi vifungashio katika bidhaa zilizofungashwa pamoja na madhara ya lumbesa.

“Nimefurahishwa sana. Watoto hawa ni mabalozi wazuri wa jamii. Uwekezaji wa WMA katika kizazi kijacho unaleta matokeo,” alisema.

Wanafunzi hao walikuwa katika ziara iliyoratibiwa na Wakala wa Vipimo ikiwa ni sehemu ya mpango wa elimu ya vipimo kwa vitendo.

Mkakati wa WMA ni kuwajengea wanafunzi uelewa wa vipimo kwa nadharia na vitendo ambapo leo wanafunzi hao wa Klabu ya Vipimo ndiyo walikuwa wakitoa huduma zote bandani ikiwemo kuelimisha, kuonyesha matumizi ya vipimo mbalimbali na kujibu maswali ya wananchi.

Naibu Waziri Londo ameonesha kufurahishwa na namna wanafunzi hao walivyojengewa uelewa mpana katika masuala ya vipimo na umahiri wao wa kutoa elimu hiyo kwake na kwa wananchi mbalimbali waliotembelea banda.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Vipimo, Francis Olwero amesema WMA imejipanga kikamilifu kuendeleza klabu za vipimo za wanafunzi ili kuwajengea uelewa wa kivipimo na kurahisisha zaidi usambazaji wa elimu ya vipimo kwa taifa zima wao wakiwa kama mabalozi. 

Amesema wanafunzi hao wamedhihirisha kuwa mbinu hiyo ya kuwaandaa wanafunzi kwa kuwapatia elimu ya vipimo ina tija.

Kiongozi wa Vipimo Club kutoka Mtemi Mazengo, Glory Enock ameishukuru WMA kuanzisha klabu hiyo na kuwapa elimu ya vipimo huku akibainisha kuwa ziara yao NaneNane ililenga pia kusaidia kujenga utamaduni wa “Pima kwa Haki, Pata Faida Halali”

 “Tumefundishwa, sasa tunafundisha wazazi na wafanyabiashara kutumia mizani sahihi,” alisema.

Wananchi waliotembelea banda la WMA waliipongeza na kuitaka iendelee kushirikisha shule nyingine kuanzisha Klabu za Vipimo.



 Na. Asia Singano na Josephine Majura, WF - Dodoma


Watumishi wa Wizara ya Fedha wanaotoa huduma kwa wananchi katika Maonesho ya 33 ya Kilimo ya Nanenane wamekumbushwa kuendelea kuzingatia weledi, uadilifu, uwajibikaji na maadili ya utumishi wa umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, sahihi na zenye kuakisi dhamira ya Serikali ya kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Wito huo ulitolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Wizara ya Fedha, Bw. Simbani Liganga, wakati alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha na taasisi zake katika Viwanja vya Maonesho ya Nanenane vya Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Alisema Maonesho ya Nanenane ni jukwaa muhimu kwa Wizara ya Fedha, kuimarisha mawasiliano na wananchi kwa kuwapatia elimu kuhusu majukumu ya Wizara, Sera za Fedha, mchakato wa maandalizi na usimamizi wa bajeti ya Serikali, usimamizi wa mali za Serikali, pamoja na huduma nyingine zinazotekelezwa na taasisi zake na kuwakaribisha wananchi kutembelea Banda hilo.

‘’Naendelea kutoa wito kwa wananchi kuwa, Wizara ya Fedha, bado inaendelea kushiriki katika Maonesho mbalimbali ikiwemo haya ya Nanenane kwa hiyo nawaalika wananchi kushiriki na kuja kwenye Banda hili ili kupata huduma zote zinazotolewa na Wizara ya Fedha na watumishi wa Wizara waliopo hapa’’ alisema Bw. Simbani.

Alieleza kuwa ubora wa huduma zinazotolewa katika Maonesho hayo unachangia kujenga taswira chanya ya Wizara ya Fedha na Serikali kwa ujumla, hivyo amewataka watumishi kuwapokea wananchi kwa heshima, kuwahudumia kwa haraka, kusikiliza changamoto zao na kutoa majibu sahihi yanayozingatia taaluma, sheria na miongozo ya Serikali.

"Kila mwananchi anayefika katika Banda letu anapaswa kuondoka akiwa amepata elimu, ameridhishwa na huduma aliyopewa na ameongeza uelewa kuhusu mchango wa Wizara ya Fedha katika maendeleo ya uchumi wa Taifa, ili kuyafikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na hiyo ndiyo dhima ya ushiriki wetu katika Maonesho haya" alisisitiza Bw. Simbani.

Aliongeza kuwa ushiriki wa Wizara ya Fedha katika Maonesho mbalimbali ya kitaifa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuwasogezea wananchi huduma, kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara, pamoja na kujenga uelewa wa umma kuhusu sera na mipango ya maendeleo inayoratibiwa na wizara hiyo.

Wizara ya Fedha imeendelea kutumia Maonesho ya Nanenane kama jukwaa la kutoa elimu ya fedha, kuhamasisha usimamizi mzuri wa rasilimali za umma na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wananchi, huku ikidhamiria kuendelea kushiriki maonesho mbalimbali ndani na nje ya nchi ili kuwafikia wananchi wengi zaidi, kutoa huduma zenye ubora na kuendelea kujenga jamii yenye uelewa mpana kuhusu masuala ya fedha na uchumi kwa maendeleo endelevu ya Taifa.






 


Na. Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.

Serikali imezindua Kielelezo cha Viwango vya Faida vya Dhamana za Serikali (Government Securities Yield Curve), hatua inayotarajiwa kuimarisha uwazi wa soko la fedha, kuongeza ufanisi wa maamuzi ya uwekezaji na kuvutia mitaji ya ndani na nje ya nchi.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amezindua Kielelezo hicho katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kilimanjaro, Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.

Bw. Tutuba alisema kupitia Kielelezo hicho wawekezaji wataweza kuona na kufuatilia mwenendo wa faida halisi katika soko la upili la Dhamana za Serikali, jambo litakalowasaidia kufanya maamuzi ya uwekezaji kwa kuzingatia taarifa sahihi na zinazoaminika.

‘‘Kielelezo hicho kitawawezesha wawekezaji wa ndani na wa kimataifa kulinganisha viwango vya faida vya Dhamana za Serikali ya Tanzania na fursa nyingine za uwekezaji ndani ya nchi, pamoja na masoko ya kikanda na kimataifa, hivyo kuongeza uwazi wa soko, kuvutia wawekezaji wa kigeni na kuimarisha ushindani wa soko la fedha nchini’’, alisema Bw. Tutuba.

Aidha Bw. Tutuba alisema Kielelezo hicho pia kitaakisi matarajio ya soko kuhusu ukuaji wa uchumi, mfumuko wa bei na mwelekeo wa sera ya fedha, hivyo kitakuwa nyenzo muhimu kwa Benki Kuu katika kuimarisha utekelezaji wa sera ya fedha inayotegemea viwango vya riba.

‘‘Soko letu limeshuhudia ukuaji mkubwa katika kipindi cha miaka 25, ambapo mwaka 2001, Dhamana za Serikali ambazo zilikuwa hazijaiva zilifikia shilingi bilioni 499, na kuongezeka mpaka kufikia shillingi trilioni 32.3 hivi sasa’’, alisema Bw. Tutuba.

Vilevile, alisema uthaminishaji wa Dhamana za Serikali zinazowasilishwa na mabenki ya biashara kama dhamana ya kupata mikopo kutoka Benki Kuu utafanyika kwa kutumia kielelezo hicho, hatua inayotarajiwa kuongeza usahihi na uwazi katika shughuli za kifedha.

‘‘Kwa upande wa sekta ya fedha, mabenki, mifuko ya hifadhi ya jamii, makampuni pamoja na wawekezaji binafsi watanufaika kwa kutumia taarifa za kielelezo hicho kama kiwango salama cha rejea katika kupanga viwango vya riba vya mikopo, mikopo ya nyumba, hatifungani za makampuni na bidhaa nyingine za uwekezaji’’, alifafanua Bw. Tutuba.

Bw. Tutuba aliwashukuru wadau wote wa soko kwa ushiriki wao ambao umeiwezesha Serikali kupata fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia Dhamana za Serikali pamoja na kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050.

Alisisitiza kuwa kuna umuhimu wa Benki Kuu na Serikali kwa ujumla kuendelea kutoa elimu ya uwekezaji ili kuhakikisha soko linaendelea kukua kwa kasi na kuongeza idadi ya wawekezaji kutoka 32,631 walioko sasa kwani idadi hiyo ni ndogo ikilinganishwa na idadi ya watu nchini.

Awali, akizungumza katika tukio hilo, Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Madeni, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, alisema kuwa soko la hisa limeendelea kukua ambapo
katika mwaka wa fedha 2025/26, thamani ya miamala iliyofanyika ilikuwa zaidi ya shilingi trilioni 6.7.

Alisema soko hilo ni fursa muhimu katika kuelekea utekelezaji wa Dira 2050 ambayo sehemu kubwa ya utekelezaji wake inatarajiwa itokane na sekta binafsi kwa takribani asilimia 70 hususani katika upatikanaji wa kitaji.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela, alisema kuwa Kielelezo hicho kitaongeza miamala na ukwasi katika soko la dhamana na kuchochea maendeleo ya aina nyingine za mali zinazouzwa katika soko la hisa.

Alipongeza Benki Kuu ya Tanzania kwa kuchapisha Kanuni za Marekebisho ya Udhibiti wa Fedha za Kigeni za mwaka 2026 na uzinduzi wa Kielelezo hicho kuwa hatua hiyo itaimarisha zaidi mfumo wa fedha nchini na kuweka mazingira yatakayowezesha Tanzania kuwa na soko la mitaji lenye ufanisi, uwazi na ushindani.

 

Kufanikiwa maishani ni matokeo ya juhudi, lakini kudumisha mafanikio hayo kunahitaji ulinzi na umakini mkubwa dhidi ya macho ya husuda. Kwa miaka mingi, nilikuwa miongoni mwa watu waliofanikiwa sana kijijini na mtaani kwetu.

Biashara zangu zilikuwa zikikuwa kwa kasi ajabu, nilimiliki majengo, na kila mradi niliogusa ulikuwa ukizaa matunda na kuniletea faida kubwa. 

Hata hivyo, bila kujua, mafanikio hayo ya haraka yalianza kuwajaza chuki na wivu watu wa karibu walioshindwa kuvumilia kuona nikipiga hatua kubwa.

​Katika hali niliyoshindwa kuielewa, mambo yalianza kubadilika ghafla kama ndoto ya kutisha. Ndani ya miezi michache tu, biashara zangu zote zilianza kuporomoka.

Wateja waliokuwa wakifurika kila siku walitoweka kabisa, pesa zikawa hazina baraka wala hazionekani zilipokwenda, na miradi yangu mipya ikaanza kufeli vibaya.

Nilibaki nikitazama mali zangu zikitoweka moja baada ya nyingine mpaka nikajikuta nimerudi chini kabisa kwenye umaskini wa kutupwa, huku wale waliozoea kunisifu wakianza kunitenga na kunicheka chini chini. SOMA ZAIDI.

 

Kila mwanamke anatamani kupata mwenza wa maisha anayejua thamani ya mapenzi, mwenye uaminifu, na anayeweza kumpa maisha ya amani na usalama wa kifedha.

Kwa miaka mingi, nilipitia maumivu makubwa kwenye mahusiano ya hapa nyumbani; niliahidiwa ndoa mara kadhaa lakini kila mara niliishia kuchezewa, kusalitiwa, na kuachwa nikiwa na maumivu ya moyo na madeni makubwa.

Nilitamani sana kupata mwenza kutoka nje ya nchi mpenzi wa kigeni au Mzungu mwenye upendo wa dhati ambaye angethamini mchango wangu na kunitoa kwenye msongo wa mawazo na maisha ya dhiki. Hata hivyo, kuipata ndoto hiyo haikuwa rahisi.

Nilijaribu kujiunga na mitandao mbalimbali ya kijamii na ya kutafuta wapenzi wa kigeni, lakini kila mwanamume niliyewasiliana naye alipoteza hamu au kukatisha mawasiliano ghafla kabla hata hatujakutana ana kwa ana.

Nilibaki nikijiuliza ni kwanini wenzangu walikuwa wakibahatika kupata wapenzi wa kigeni na kubadilisha maisha ya familia zao, wakati mimi kila mlango niliotaka kuufungua ulikuwa ukijifunga na kuniacha kwenye maumivu. SOMA ZAIDI.

 


Familia na watoto ni baraka kubwa sana maishani, lakini katika jamii zetu, tamaa ya kupata mtoto wa kiume wa kuendeleza ukoo na kurithi mali za familia ni jambo linalowagusa wazazi wengi. Mume wangu na mimi tulibarikiwa kupata mabinti wanne wazuri na wenye afya tele.

Pamoja na kuwapenda sana binti zetu, mume wangu alianza kuonyesha msongo mkubwa wa mawazo na wasiwasi kuhusu hatima ya jina la familia na biashara zetu kubwa ambazo ziliitaji mrithi wa kiume wa kuzisimamia.

​Maneno na shinikizo kutoka kwa ndugu wa mume wangu vilianza kuongezeka kila siku. Walianza kumshawishi achukue mke mwingine au atafute mwanamke wa nje atakayemzalia mtoto wa kiume.

Nilibaki nikihangaika kwenye maombi na kutembelea hospitali mbalimbali kuona kama kuna ushauri au tiba ya kisayansi inayoweza kusaidia, lakini kila mimba iliyofuata ilipopatikana, majibu na matokeo yalikuwa ni yale yale mtoto wa kike.

Ndoa yangu ilianza kuingia kwenye baridi kali, na hofu ya kupoteza mume wangu na nyumba yangu ikawa inaniandama kila siku. SOMA ZAIDI.



 Na. Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kuimarisha ushirikiano na Taasisi ya Africa50 pamoja na wanahisa wengine ili kuharakisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya miundombinu barani Afrika.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders’ Meeting-GSM) uliohitimishwa jana katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, ambapo alikuwa Mwenyekiti Mwenza wa mkutano huo.

Mhe. Balozi Omar, alieleza kuwa Tanzania, kama mwanahisa wa Africa50, inaiona taasisi hiyo kuwa chombo muhimu kinachounganisha Serikali, wawekezaji na taasisi za kifedha ili kubadilisha vipaumbele vya miundombinu kuwa miradi inayotekelezeka na yenye mvuto wa uwekezaji.

Aliongeza kuwa Tanzania, kama mwanahisa wa Africa50, inaiona taasisi hiyo kuwa chombo muhimu kinachounganisha Serikali, wawekezaji na taasisi za kifedha ili kubadilisha vipaumbele vya miundombinu kuwa miradi inayotekelezeka na yenye mvuto wa uwekezaji.

“Maono ya Africa50 yanaendana kikamilifu na dira ya maendeleo ya Tanzania ya mwaka 2050 (Dira 2050), inayolenga kuifikisha nchi katika uchumi wa kipato cha juu cha kati na kufikia uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aidha, aliwakaribisha washiriki kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika na kwingineko, akieleza kuwa Tanzania inajivunia kuwa mwenyeji wa mkutano huo muhimu unaoadhimisha miaka kumi ya mafanikio ya Africa50 tangu kuanza kwa shughuli zake.

“Tunawakaribisha kwa moyo mkunjufu hapa Dar es Salaam, Tunatumaini mtapata majadiliano yenye tija pamoja na kufurahia ukarimu wa Tanzania,” alisema Mhe. Balozi Omar.

Alisisitiza kuwa Miundombinu ni msingi wa kufikia azma hiyo, hususan katika sekta za nishati, usafirishaji na mifumo ya usafirishaji wa bidhaa, ambayo ni muhimu katika kukuza uzalishaji, biashara na uchumi kwa ujumla.

Mhe. Balozi Omar aliongeza kuwa Tanzania iko tayari kuendelea kushirikiana na Africa50 pamoja na wanahisa wengine katika kuvutia uwekezaji endelevu, kuendeleza miradi mikubwa ya kimkakati na kuimarisha uunganishwaji wa kikanda kwa manufaa ya wananchi wa Afrika.

“Nawashukuru washiriki wote kwa michango yenu yenye kujenga, na maamuzi yaliyofikiwa hapa yataisaidia Africa50 kuimarisha nafasi yake katika muongo ujao wa maendeleo ya miundombinu barani Afrika” alisema Mhe. Balozi Omar.

Mkutano huo umezikutanisha nchi wanahisa, taasisi za kifedha na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa lengo la kujadili namna bora ya kuendeleza na kufadhili miradi ya miundombinu barani Afrika.

JUBILEE Group Tanzania imezindua rasmi ukuta uliojengwa kuzunguka Shule ya Msingi Madenge iliyopo Temeke, Dar es Salaam, kwa lengo la kuimarisha usalama na kuondoa changamoto ya usumbufu uliokuwa ukisababishwa na wapita njia, hali iliyokuwa ikiathiri mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia.


Na Oscar Assenga,TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk. Batilda Burian, ametaka elimu ya kupinga rushwa ianze kutolewa kwa wanafunzi wa shule za msingi wakiwa na umri mdogo ili kuwajengea maadili ya uadilifu, uaminifu, uwajibikaji, uzalendo na kuipenda nchi yao.

Dk. Burian alitoa kauli hiyo Agosti 6, 2026, wakati wa fainali ya shindano la Chemsha Bongo Zuia Rushwa 2026 mkoani Tanga, lililofanyika katika Shule ya Ufundi Tanga (Tanga Technical Secondary School).

Alisema kuwafundisha wanafunzi masuala ya rushwa kuanzia wakiwa darasa la tatu kutawajengea msingi imara wa kuchukia na kukemea vitendo vya rushwa, hivyo kuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku.

Alisema wanafunzi tayari wanaonesha uelewa mkubwa kuhusu madhara ya rushwa kwa maendeleo ya taifa.

“Kama mlivyowasikia wanafunzi wakijieleza, wameonesha namna rushwa inavyodumaza maendeleo. Inaweza kusababisha kujengwa kwa madaraja mabovu kwa sababu ya kumpa kazi mkandarasi asiye na sifa. Mwisho serikali hudhani imetekeleza maendeleo, kumbe ni maendeleo ya magumashi,” alisema.



Dk. Burian, ambaye aliwakilishwa na Ofisa Elimu wa Mkoa wa Tanga, Emanuel Kisongo, alisema walimu wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa wanafunzi kwa kuwalea katika misingi ya maadili mema na kuwafundisha athari za rushwa kwa jamii na taifa.

Kwa upande wake, Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga, Ramadhan Ndwata, alisema shindano la Chemsha Bongo Zuia Rushwa 2026 linalenga kujenga kizazi chenye uadilifu kupitia wanafunzi wa shule za msingi.

Alisema maadili yanayojengwa kwa watoto yatawasaidia kukua wakiwa raia wanaochukia rushwa na kuzingatia misingi ya haki na uwajibikaji.

“Tunataka kujenga kizazi kitakachokuwa sehemu ya suluhisho la tatizo la rushwa badala ya kuwa sehemu ya tatizo. Vitendo vina nguvu kubwa katika kujenga maadili kuliko maneno pekee,” alisema.

Ndwata alisema kuanzishwa kwa klabu za wapinga rushwa katika shule za msingi kumeongeza uelewa wa wanafunzi kuhusu masuala ya rushwa.

Alisema wakati wa mashindano hayo wanafunzi walikuwa wakisahihishana wenyewe kuhusu masuala yanayohusu rushwa, jambo alilosema ni ishara ya mafanikio ya programu hiyo na kwamba wako tayari kuwaelimisha wengine.


Aidha, aliwataka wazazi kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuendeleza elimu dhidi ya rushwa, akisema familia ina nafasi kubwa katika kujenga maadili ya kizazi kijacho.

Mratibu wa mashindano hayo Frank Mapunda alisema Shule ya Msingi Kombezi iliibuka mshindi wa kwanza na kujinyakulia kombe kubwa pamoja na fedha taslimu Sh200,000.

Alisema mshindi wa pili alikuwa Klabu ya Wapinga Rushwa ya Shule ya Msingi Bombo iliyopata kombe dogo na Sh150,000, huku Shule ya Msingi Chumbageni ikishika nafasi ya tatu na kujishindia ngao ya glasi pamoja na Sh100,000.

Nafasi ya nne ilichukuliwa na Klabu ya Wapinga Rushwa ya Shule ya Msingi Nguvumali iliyopata ngao ya plastiki pamoja na Sh50,000.

Mwalimu wa Shule ya Msingi Mkwakwani Faraja Mwagike alisema kuanzishwa kwa klabu za wapinga rushwa kumewaongezea wanafunzi uadilifu, ujasiri na kuwajengea msingi wa kuwa raia wema watakaoheshimu sheria na kutenda haki.

Naye mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kisosora, Mariam Juma, alisema klabu hizo zimechangia kuwaelimisha wanafunzi kuhusu madhara ya rushwa kwa jamii na taifa.

“Ni muhimu wigo wa klabu hizi ukaongezwa ili wanafunzi wengi zaidi wanufaike na elimu hii na ujumbe uwafikie wote,” alisema.