Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeendelea kuvuna matunda ya uwekezaji katika utalii wa misitu, huku idadi ya watalii wanaotembelea vivutio vinavyosimamiwa na taasisi hiyo ikifikia 377,116 mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko kubwa kutoka watalii 46,533 mwaka 2020.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Utalii TFS, PCO Someni Mteleka, ongezeko hilo linaenda sambamba na kuimarika kwa mchango wa utalii katika mapato ya taasisi, ambapo mwaka 2020 TFS ilirekodi watalii mapato ya zaidi ya Sh 159 milioni kutokana na utalii wa ikolojia na kuongezeka hadi Sh 3.5 bilioni mwaka 2025/2026

Akizungumza jana Septemba 15, 2026 jijini Dodoma wakati wa mafunzo ya utangulizi kwa watumishi wapya wa TFS, Mteleka alisema taasisi hiyo inaendelea kuendeleza bidhaa mbalimbali za utalii zinazotokana na misitu, mashamba ya miti, mikoko na maeneo ya kihistoria, hatua inayolenga kuongeza fursa za utalii na manufaa ya kiuchumi.

Alisema TFS kwa sasa inasimamia maeneo 35 ya utalii yanayotoa shughuli mbalimbali, zikiwemo matembezi ya misituni, kuangalia ndege na wanyama, kupanda na kutalii milimani, utalii wa nyuki, baiskeli, kuendesha mitumbwi na kayak, kambi, picnic, pamoja na kutembelea maeneo ya kihistoria na kitamaduni.

Mteleka alisema ukuaji wa utalii umechangiwa pia na kuongezeka kwa maeneo ya hifadhi za misitu ya kitaifa (NFRs), ambayo yameongezeka kutoka maeneo matano mwaka 2015 hadi kufikia 25 mwaka 2025, huku utalii wa ikolojia ukiwa miongoni mwa shughuli kuu za kiuchumi zinazoruhusiwa katika maeneo hayo kwa kuzingatia uhifadhi na athari ndogo kwa mazingira.

Alisema mbali na hifadhi za misitu, TFS inaendelea kutumia mashamba ya miti na misitu ya mikoko kuendeleza bidhaa mpya za utalii zisizohitaji uvunaji wa rasilimali, ikiwemo utalii wa michezo kama mbio za magari, marathoni na shughuli za kuendesha farasi, pamoja na shughuli za utalii katika maeneo ya mikoko.

Kwa mujibu wa Mteleka, TFS pia inasimamia vituo sita vya maeneo ya kale, vikiwemo Mji Mkongwe wa Bagamoyo, Magofu ya Kaole, Tongoni, Michoro ya Miamba ya Kondoa ambayo ni eneo la Urithi wa Dunia la UNESCO, pamoja na maeneo yanayohusishwa na Dk. David Livingstone na Jengo la Afya.

Alisema TFS inaendelea kushirikiana na taasisi za Serikali, washirika wa maendeleo, mashirika yasiyo ya Serikali, jamii na sekta binafsi katika kuboresha miundombinu, huduma na upatikanaji wa vivutio, huku ikiendelea kutangaza bidhaa zake kupitia vyombo vya habari vya jadi na kidijitali ili kuongeza watalii na kuchangia lengo la taifa la kufikia watalii milioni nane kwa mwaka ifikapo 2030.




 Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilaya ya Chamwino imefungua barabara ya Manda–Mafurungu yenye urefu wa kilomita 25 hatua ambayo imebadili hali ya usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa kijiji cha Mafurungu baada ya kukabiliwa na changamoto ya muda mrefu ya kutokuwa na barabara.


‎Akizungumza kuhusu maendeleo ya mradi huo, Meneja wa TARURA wilaya ya Chamwino Mhandisi Richard Sanga amesema, barabara hiyo imefunguliwa ikiwa ni jitihada za serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunganisha wananchi na kurahisisha shughuli za kiuchumi na kijamii.

‎Amesema TARURA wilaya ya Chamwino inahudumia mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 1,297 huku ujenzi wa barabara ya Manda–Mafurungu ukiwa ni muhimu kwa wananchi wa vijiji vya Manda na Mafurungu kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya na elimu, kupunguza gharama za usafiri na kufungua fursa za kiuchumi.

‎"Awali barabara hii haikuwepo kabisa lakini baada ya kupata fedha tumeweza kuifungua, mkandarasi tayari ameshafungua kilomita zote 25 huku kazi zinazoendelea ni ujenzi wa makalavati, uwekaji wa kifusi katika maeneo korofi na maandalizi ya uchongaji wa mifereji kwa ajili ya kudhibiti na kuondoa maji ya mvua barabarani", amesema.

‎Ameeleza kuwa kutokana na umuhimu wa barabara hiyo katika bajeti ya mwaka huu wa fedha wataweka changarawe katika baadhi ya maeneo korofi huku mpango wa mwaka ujao wa fedha ukiwa ni kuweka kifusi barabara yote na kumalizia makalavati ili kuhakikisha barabara inapitika kwa urahisi na kwa uhakika kipindi chote cha mwaka.

‎Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kitongoji cha Machimbo, Bw. Mrisho Ally amesema kabla ya barabara hiyo wananchi wa Mafurungu wakitaka kusafiri hadi Dodoma mjini safari ya kwenda na kurudi walikuwa wakitumia nauli zaidi ya Sh. 100,000/= hali iliyowalazimu kutumia muda mwingi na gharama kubwa.

‎Amesema kwa sasa gharama hiyo imeshuka hadi Sh. 24,000/= kwa safari ya kwenda na kurudi huku magari yakiwa yanafika moja kwa moja kijijini ambapo imepunguza gharama na muda wa usafiri.

‎Ameongeza kuwa eneo hilo lina shughuli kubwa za uchimbaji wa madini ya dhahabu zinazochangia uchumi wa wilaya ya Chamwino hivyo ameiomba serikali kuendelea kuboresha barabara hiyo ili iweze kutoa huduma kwa wananchi na wafanyabiashara katika kipindi cha mwaka mzima.

‎Naye, Bw. Zabroni Matonya mkazi wa Mafurungu na mwekezaji katika shughuli za uchimbaji madini amesema, barabara hiyo imekuwa mkombozi kwa wachimbaji na wawekezaji kutokana na kurahisisha usafirishaji wa vifaa na malighafi kwani awali ubovu wa barabara uliwafanya kutumia muda mrefu kusafirisha malighafi zao mjini hivyo ameishukuru serikali kwa barabara hiyo.

‎Mkazi wa Mafurungu Bi. Salma Mtacha amesema kabla ya barabara wanafunzi walikuwa wakitembea umbali mrefu kufika shuleni hali iliyokuwa ikiwatia hofu wazazi lakini sasa barabara imefunguka wanafunzi wanafika shuleni bila shida pia wananchi wanafika katika vituo vya afya na hospitali bila changamoto jambo ambalo limeongeza usalama na ustawi wa jamii.

‎Naye, Selemani Bundala mkazi wa Mafurungu amesema awali safari ya kutoka kijijini hadi Dodoma mjini kwa pikipiki ilikuwa ikigharimu hadi Sh. 100,000/= lakini baada ya barabara kufunguliwa hali imebadilika na mabasi sasa yanafika moja kwa moja kijijini.

‎Amesema wananchi wanathamini jitihada za serikali katika kufungua barabara hiyo na ameomba kazi ya uboreshaji iendelee hadi barabara hiyo iweze kupitika mwaka mzima.




 

Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie, akizungumza wakati wa kufungua Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Na. Asia Singano, WF – Dodoma.

Wizara ya Fedha imeendelea kuandaa na kuboresha miongozo mbalimbali inayolenga kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya ukaguzi na kuongeza ufanisi wa kazi hiyo, ili kuendelea kulinda fedha za umma na kukuza uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie, wakati akifungua Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Mhandisi Nindie alisema kuwa mwongozo huo unahusisha hatua mbalimbali za mchakato wa ukaguzi, na kwamba baadhi ya vipengele vyake vinapitia hatua ya uhakiki ili kuhakikisha vinaendana na mahitaji na viwango vinavyotakiwa.

"Tunachukua baadhi ya vipengele kwa ajili ya kuvithibitisha, ambapo ni muhimu kupitia na kuthibitisha miongozo hiyo kabla ya kuanza kutumika kikamilifu. alisema Mhandisi Nindie.

Alieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa miongozo inayotumika katika kazi za ukaguzi ina ubora, inaeleweka na inawasaidia watendaji kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa watumishi kuwa na vyeti vya kitaaluma (certification), kwakuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuongeza ufanisi na ubora wa utekelezaji wa majukumu yao.

"Suala la kuwa na vyeti vya kitaaluma limekuwa sehemu muhimu ya mipango ya kuimarisha uwezo wa watumishi. Natambua kuwa tangu mwaka 2021 kulikuwa na mpango uliolenga kuongeza idadi ya watumishi wenye vyeti hivyo," alisema Mhandisi Nindie.

Alibainisha kuwa kuendelea kuwekeza katika ujuzi na taaluma za watumishi ni hatua muhimu katika kuboresha utendaji kazi na kuhakikisha majukumu ya taasisi yanatekelezwa kwa viwango vinavyohitajika.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Wizara ya Fedha, kupitia Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali yakiwakutanisha Wakaguzi wa Ndani kutoka taasisi za umma na kutoka Wizara ya Fedha, ili kuwaongezea uelewa katika utekelezaji wa majukumu yao

 


📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb.) aipongeza TANESCO kwa kutekeleza Mradi kwa kutumia wataalamu wa ndani

📌 MD Twange asema mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme umefikia asilimia 82 ya utekelezaji wake


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amekagua ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Imalilo mkoani Simiyu ambapo ameeleza kukamilika kwa mradi huo kutafungua fursa za uwekezaji na kuboresha huduma ya upatikanaji wa umeme kwa wananchi. 

Mhe. Mwigulu ameyasema hayo leo Septemba 14, 2026 katika eneo la mradi wa Imalilo wakati akikagua utekelezaji wake. 

"Nawapongeza sana Wizara ya Nishati kwa kutekeleza mradi huu kupitia TANESCO kwa kutumia wataalamu wa ndani hongereni sana" amesema Mhe. Dkt. Mwigulu 

Dkt. Mwigulu akizungumzia kuhusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Ibadakuli, Shinyanga hadi Imalilo, Simiyu, Dkt. Mwigulu amesema Serikali itatoa fedha kuhakikisha mradi huo unakamalika na kuwa na tija kwa Taifa. 

Awali, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Bw. Lazaro Twange amesema mradi umetekelezwa kwa kutumia wataalamu wa ndani na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja. 

"Mhe. Waziri Mkuu mradi huu umefikia asilimia 82 ya utekelezaji wake na utakamilkika katika muda ambao tumeupanga" amesema Bw. Twange. Aidha amesema gharama ya utekelezaji wa mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme umegarimu shilingi bilioni 27, ambapo mpaka sasa Serikali imetumia shilingi bilioni 15 na kazi zote za msingi zimekamilika na ujenzi unaendelea. 

Mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Imalilo unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya umeme katika mikoa ya Simiyu, Mara na maeneo jirani.











 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika kinga, uchunguzi na matibabu ya saratani kutokana na uwekezaji unaofanywa na Serikali chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akihutubia Jukwaa la Kisayansi la IAEA mjini Vienna, Austria, amesema Tanzania inalenga kuwa kitovu cha utaalamu na mafunzo ya tiba ya saratani kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ni ongezeko la chanjo ya HPV kwa wasichana wenye miaka 9–14 kutoka asilimia 58 mwaka 2018 hadi asilimia 98 mwaka 2026, huku vituo vya tiba ya saratani kwa mionzi vikiongezeka kutoka vitatu mwaka 2020 hadi sita mwaka 2026. Serikali pia imeongeza teknolojia za kisasa za uchunguzi na matibabu, ikiwemo PET-Scan, MRI, LINAC, CT Scan na mammography, na inalenga kuwa na vituo tisa vya huduma jumuishi za saratani katika kanda sita za kimkakati Tanzania Bara na Zanzibar ifikapo 2030.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa IAEA na washirika wa kimataifa kuendelea kuiunga mkono Tanzania kupitia mpango wa Rays of Hope, pamoja na kuiteua Taasisi ya Saratani Ocean Road kuwa Kituo cha Umahiri cha Saratani kwa ajili ya mafunzo na kujenga uwezo wa wataalamu wa Afrika. Hatua hiyo inalenga kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha huduma, utaalamu na teknolojia za kisasa za tiba ya saratani katika ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Tanzania imetumia mkutano huo kueleza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano na IAEA katika matumizi mengine ya teknolojia ya nyuklia, ikiwemo kilimo na maandalizi ya muda mrefu ya programu ya nishati ya nyuklia.
 
Kwa Tanzania, mkutano huo unatoa fursa ya kuunganisha hatua ambazo tayari zimepigwa na mahitaji ya awamu inayofuata ya kuongeza vituo vya saratani, kujenga wataalamu, kupata teknolojia zaidi na kuimarisha ushirikiano wa kisayansi na kifedha.
 
Jukwaa hilo la siku mbili linafanyika chini ya kaulimbiu “Rays of Hope: Delivering on the Promise of Cancer Care,” likiwakutanisha viongozi, wanasayansi, wataalamu wa afya na wadau wengine kujadili namna ya kupunguza pengo la upatikanaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya saratani duniani.

 




 Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Africa Tourism Private Sector Alliance (ATPSA) Tourism Roadshow Tanzania 2026, jukwaa litakalowakutanisha wafanyabiashara wa utalii, wanunuzi na wadau kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika kwa ajili ya kukuza biashara na ushirikiano katika sekta hiyo.

Roadshow hiyo itafanyika Zanzibar Septemba 27, 2026, katika Hotel Verde Zanzibar, kabla ya kuhamia Arusha Septemba 30, 2026, katika Gran Meliá Arusha.

Tukio hilo linafanyika wakati Tanzania ikiendelea kuimarisha nafasi yake katika sekta ya utalii barani Afrika, baada ya kutambuliwa kuwa Africa’s Leading Destination 2026, huku Bodi ya Utalii Tanzania ikishinda tuzo ya Africa’s Leading Tourist Board 2026 kwa mwaka wa tano mfululizo.

Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Dr. Thereza Mugobi, amesema Roadshow hiyo ni fursa kwa Tanzania kutangaza vivutio vyake, lakini pia kushiriki katika kujenga soko la utalii la Afrika kwa Waafrika.

Kwa upande wake, Madam Devotha Mdachi, Mjumbe wa Bodi na Mwakilishi Rasmi wa Africa Tourism Partners (ATP) na Africa Tourism Private Sector Alliance (ATPSA) kwa ukanda wa Afrika Mashariki, amewataka wadau wa utalii nchini kutumia fursa hiyo kujenga masoko mapya na ushirikiano wa kibiashara.

Washiriki kutoka nchi mbalimbali zikiwemo Botswana, Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Uganda, Namibia, Nigeria, Rwanda na Afrika Kusini, pamoja na India na Belgium, wanatarajiwa kushiriki katika mikutano hiyo.

Msingi wa Roadshow utakuwa ni mikutano ya biashara kwa biashara (B2B), ambapo washiriki watatumia mfumo wa ATPSA B2B Appointment Platform kupanga mikutano na washirika wao wa biashara. Kila mshiriki atapata nafasi ya kufanya hadi mikutano 15 iliyopangwa kabla.

Kaulimbiu ya Roadshow hiyo ni “Meet. Connect. Trade. Grow Africa.”, ikiwa na lengo la kuimarisha biashara ya utalii, ushirikiano wa sekta binafsi na kukuza utalii wa ndani ya Afrika.

ATPSA inaeleza kuwa mustakabali wa utalii barani Afrika unahitaji nchi, biashara na watu kuunganishwa zaidi ili kujenga soko imara la utalii ndani ya bara.









 


Mwenyekiti wa Vijana wa CCM Wilaya ya Moshi Vijijini, CPA (T) Yuvenali Shirima, amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kujiandaa mapema kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua kubwa zinazotarajiwa katika msimu wa Vuli 2026.

Shirima amewataka wananchi kufuatilia taarifa rasmi zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kuzingatia maelekezo ya Serikali na wataalamu, pamoja na kuepuka maeneo hatarishi kama mabonde, maeneo ya mito na sehemu zenye miteremko mikali.

Aidha, ameipongeza Serikali kwa hatua mbalimbali inazochukua katika kujiandaa na kukabiliana na athari za El Niño, akisisitiza kuwa maandalizi ya mapema ni muhimu katika kulinda maisha, mali na miundombinu.

Katika pongezi hizo, amemtaja pia Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Godfrey Eliakimu Mzava, kwa juhudi zake za kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kuchukua tahadhari. Amesema katika matukio mbalimbali, Mhe. Mzava amekuwa akitoa elimu kwa wananchi, kuitisha vikao na kuwakutanisha wadau mbalimbali ili kuhakikisha jamii inaelewa namna ya kukabiliana na changamoto zinazoweza kusababishwa na mvua hizo.

“Tunampongeza Mkuu wa Wilaya kwa kuwa karibu na wananchi na kuendelea kutoa elimu. Elimu, tahadhari na maandalizi ya mapema vinaweza kusaidia kuokoa maisha na mali za wananchi,” amesema Shirima.

Amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali, kutoa taarifa za viashiria vya hatari na kuhakikisha wanachukua hatua stahiki kabla ya madhara kutokea.







Nilikuwa naishi kwenye huzuni kubwa kwa muda mrefu. Kila kitu kilibadilika baada ya tukio moja ambalo liliniacha nikiwa na maumivu ya ndani ambayo sikuweza kuyaeleza kwa mtu yeyote.

Nilijaribu kuendelea na maisha kama kawaida, lakini moyoni nilikuwa nimevunjika.

Nilikuwa napoteza hamu ya kufanya mambo niliyokuwa napenda. Hata kukutana na watu kulikuwa kunanichosha.

Watu wengi walidhani niko sawa kwa sababu nilikuwa natabasamu mbele yao, lakini ukweli ni kwamba nilikuwa naumia kimya kimya kila siku.

Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Naitwa James kutoka Nyandarua. Kwa muda mrefu nilikuwa mfanyabiashara mdogo nikijitahidi kujenga maisha yangu kupitia duka la bidhaa za kila siku. Mwanzoni biashara yangu ilikuwa ikienda vizuri, lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Bidhaa zilianza kukwama sokoni, wateja wakapungua, na mara nyingine nilikuwa napata hasara bila kuelewa chanzo.
Nilijaribu kubadilisha bidhaa, kupunguza bei, na hata kubadili eneo la mauzo, lakini bado hali haikubadilika. Kila wiki ilikuwa kama napoteza zaidi kuliko ninavyopata.

Hali hiyo ilinifanya niingie kwenye msongo wa mawazo. Nilianza kujiuliza kama biashara siyo sehemu yangu kabisa. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu changamoto zangu. SOMA ZAIDI.
Naitwa Samuel kutoka Webuye. Sikuamini kabisa kuwa siku moja ningeweza kupata pikipiki yangu iliyoibiwa kwa njia ambayo ingeniacha nikiwa na mshangao mkubwa na pia funzo la maisha. Siku hiyo pikipiki yangu ilipotea mchana kweupe.

Nilihisi kuchanganyikiwa sana na hasira kwa wakati mmoja, kwa sababu ilikuwa ndiyo tegemeo langu la kila siku kwenye shughuli zangu za kujipatia kipato. Nilianza kuitafuta kila mahali bila mafanikio. Nilizungumza na watu kadhaa, lakini hakuna aliyekuwa na taarifa sahihi.

Kadri muda ulivyozidi kwenda, ndivyo nilivyozidi kukata tamaa na kuhisi kama pikipiki yangu imepotea kabisa bila matumaini ya kuipata tena. SOMA ZAIDI.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

JIJI la Dar es Salaam limezindua Jukwaa la Mifumo ya Chakula litakalokuwa chombo cha kuunganisha wadau mbalimbali katika kuboresha upatikanaji wa chakula salama, bora na chenye lishe kwa wakazi wa jiji hilo.

Na.Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani ya Somali  imefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza uzoefu na mbinu zinazotumiwa na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika kusimamia ushindani wa kibiashara, kudhibiti bidhaa bandia na kulinda maslahi ya walaji.

Ziara hiyo imefanywa na Mkurugenzi wa Masuala ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na Kamishna wa Mamlaka ya Ushindani ya Afrika Mashariki (EACA), Bw. Ahmed Warsame pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Upatikanaji wa Masoko wa Wizara ya Biashara na Viwanda ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Bw. Abdihalim Osman.

Katika ziara hiyo, ujumbe huo umekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, pamoja na uongozi wa Tume, ambapo walipata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kukuza na kulinda ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, uongozi wa ujumbe wa Somalia umepongeza utendaji wa FCC, ukieleza kuwa uzoefu wa Tanzania katika kusimamia ushindani na kulinda mlaji ni muhimu kwa Somalia katika kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa soko na kukuza mazingira bora ya biashara.

Ujumbe huo umeeleza kuwa kujifunza kutoka FCC kutasaidia kuongeza uelewa na uwezo wa taasisi za Somalia katika kukabiliana na changamoto zinazohusu ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwadhuru walaji.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema  kuwa Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na taasisi za Somalia na nchi nyingine katika kubadilishana uzoefu, maarifa na mbinu bora za usimamizi wa ushindani na ulinzi wa walaji.

Ziara hiyo ya siku moja imekuwa fursa muhimu kwa Somalia kujifunza uzoefu wa Tanzania katika eneo la ushindani wa kibiashara, udhibiti wa bidhaa bandia na ulinzi wa mlaji, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi na kuchangia katika ujenzi wa masoko yenye ushindani wa haki na biashara endelevu.