Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, ameshiriki kilele cha Maonesho ya 33 ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane, yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt.John Malecela Nzunguni Jijini Dodoma yakilenga kuimarisha tija, uzalishaji na upatikanaji wa masoko kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wadau wa sekta ya kilimo nchini.

Maonesho hayo yaliyoongozwa na kaulimbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya 2050”, yamefungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, huku yakitoa fursa kwa taasisi za Serikali, sekta binafsi na wadau mbalimbali kuonesha huduma, bidhaa na fursa zinazolenga kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo.

Akizungumza mara baada ya kushiriki kilele hicho, Bi. Ngasongwa amesema ushiriki wa FCC katika maonesho hayo ulikuwa sehemu ya jitihada za kuifikisha elimu ya ushindani kwa wananchi, wazalishaji na wafanyabiashara ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika shughuli za kiuchumi.

Amesema FCC imeendelea kutumia majukwaa mbalimbali kama Nane Nane kutoa elimu kuhusu madhara ya bidhaa bandia na umuhimu wa wananchi kuwa makini wakati wa kununua bidhaa, kwa kuwa matumizi ya bidhaa zisizo halisi yanaweza kuathiri usalama wa watumiaji, ubora wa uzalishaji na ushindani wa biashara.

Bi.Ngasongwa amesisitiza kuwa elimu kwa wananchi ni muhimu katika kujenga soko lenye ushindani wa haki, ambapo wazalishaji na wafanyabiashara wanapata mazingira bora ya kushindana huku watumiaji wakilindwa dhidi ya vitendo vinavyoweza kuathiri maslahi yao.

Amesema FCC itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuimarisha uelewa wa sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.

Ushiriki wa FCC katika Maonesho ya Nane Nane unaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kujenga uchumi shindani na wenye tija, kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu na uelewa unaowawezesha kufanya maamuzi sahihi katika soko, huku wafanyabiashara wakihimizwa kuzingatia sheria, ubora wa bidhaa na ushindani wa haki.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (kushoto), akizungumza na watendaji kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) jijini Dar es Salaam Agosti 8, 2026.

.Baadhi ya Watendaji kutoka Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano za PSSSF, NSSF na OSHA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na watendaji kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) jijini Dar es Salaam Agosti 8, 2026.



Dar es salaam, Agosti 8, 2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu (Mb) leo (Jumamosi, Agosti 8, 2026) amefanya vikao kazi jijini Dar es salaam na Menejimenti za taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utendaji.

Katika vikao kazi hivyo, Waziri Sangu, kwa nyakati tofauti amekutana na Menejimenti za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Mashirika ya Umma (PSSSF); Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF); Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF); na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA).

Waziri Sangu amepokea taarifa za utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo kutoka kwa watendaji wake wakuu na kuelekeza taasisi hizo kuendelea kuongeza ufanisi hususan katika matumizi ya teknolojia ya Habari na mawasiliano (TEHAMA) katika utendaji na utoaji huduma kwa wananchi.


“Nawaelekeza kuongeza utoaji wa elimu ya matumizi ya kidijitali katika mifumo yetu ili kuwawezesha wale wasio na elimu ya kidijitali kupata huduma zetu kwa urahisi na haraka,” amesema Waziri Sangu.


Vikao hivyo vilihudhuriwa na Mkurugenzi wa Hifadhi ya Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Festo Fute, Wakurugenzi Wakuu wa PSSSF, NSSF, WCF na OSHA pamoja na wajumbe wa Menejimenti za taasisi hizo.


Mhe. Sangu ameendesha vikao kazi hivyo baada ya jana kukamilisha ziara yake ya siku saba katika wilaya zote za mkoa wa Lindi iliyolenga kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali mkoani humo.


Mwisho

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini limeendelea kutumia Maonesho ya Nanenane 2026 kutoa elimu kwa wazalishaji, wajasiriamali na wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa kuzingatia viwango ili kuongeza tija na kupanua masoko ndani na nje ya Tanzania.
RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kuimarisha upatikanaji wa mitaji kwa wadau wa sekta ya kilimo kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), huku mtaji wa benki hiyo ukiongezeka kutoka Sh bilioni 60 mwaka 2020/21 hadi Sh bilioni 452.

 


Fursa za kupanda cheo na kufanikiwa kazini ni hamu ya kila mwajiriwa anayejituma na kutimiza wajibu wake kwa uaminifu. Hata hivyo, kwangu mimi, miaka kumi iliyopita ilikuwa ni kipindi cha vilio, maumivu, na kuvunjika moyo.

Pamoja na kuwa na elimu ya kutosha, utendaji wa hali ya juu, na nidhamu ya mfano kazini, nilijikuta nikisalia kwenye nafasi ile ile ya chini, huku watu niliowafundisha kazi na wengine waliokuja miaka mingi baada yangu wakiniruka na kupandishwa vyeo vya juu na kuongezewa mshahara.

​Kila mara nafasi ya uongozi au usimamizi ilipojitokeza na kufanyiwa usahili, jina langu lilikuwa likionolewa dakika za mwisho bila sababu za msingi.

Nilianza kuona dharau kutoka kwa wafanyakazi wenzangu, na maneno ya kebehi yalianza kuenea yakidai mimi ni mtu asiyekuwa na bahati wala nyota ya uongozi.

Msongo mkubwa wa mawazo ulinipata, mshahara wangu mdogo ulishindwa kukidhi mahitaji ya familia, na nilianza kufikiria kuacha kazi kwa aibu na kukata tamaa kabisa na maisha. SOMA ZAIDI.

 


Amani na utulivu wa usiku ni haki ya kila mwanadamu, lakini kwangu mimi, muda wa kulala ulikuwa ni mwanzo wa mateso makubwa na hofu isiyoelezeka.

Kwa miezi mingi, kila nilipoweka kichwa changu kitandani, nilikuwa nikikabiliwa na ndoto za kutisha za kufukuzwa na wanyama wakali, kuogelea kwenye maji marefu ya giza, au kulishwa vitu vya ajabu usingizini.

Hali hii ilipozidi, nilianza kuhisi uzito mkubwa kifuani kana kwamba kuna mtu aliyekuwa akinikandamiza usiku kucha na kuninyima kabisa uwezo wa kupumua au kupiga kelele.

​Mateso haya yalianza kuathiri afya yangu ya mwili na akili. Nilikuwa nikiamka asubuhi nikiwa nimechoka sana, mwenye maumivu makali ya viungo na msongo mkubwa wa mawazo.

Hali hii ilileta hofu kubwa hata kwa familia yangu; watoto wangu walishtushwa na kelele na vilio nilivyokuwa nikipiga usiku kucha wakati wa ndoto hizo mbaya.

Nilitembea kwenye hospitali mbalimbali na kutumia dawa za kutuliza mfumo wa fahamu na usingizi, lakini vipimo vyote vya kisayansi vilionyesha sina ugonjwa wowote, huku mateso ya usiku yakiendelea kunilaza macho. SOMA ZAIDI.

 


Hakuna jambo linaloweza kukutoa machozi na kukunyima amani ya nafsi kama kukabiliwa na shtaka la uongo ambalo hulijui wala kushingiliana nalo.

Kwa miezi mingi, maisha yangu yaliingia kwenye giza nene baada ya kushitakiwa mahakamani kwa kosa la dhuluma lililobuniwa na watu wenye chuki na husuda waliotaka kunipora ardhi na mali zangu.

Nilibaki nikihangaika kutoka chombo kimoja cha sheria hadi kingine, nikitumia pesa nyingi kuwalipa mawakili, lakini kila siku kesi ilivyoendelea, mambo yalianza kunielekea vibaya na kila kiashiria kilionyesha nilikuwa hatarini kufungwa jela miaka mingi.

​Msongo wa mawazo ulitawala maisha yangu na familia yangu. Nilitazama mke na watoto wangu wakilia kila siku wakihofia hatima yao mara nitakapopelekwa gerezani.

Mashahidi wa uongo walipangwa kunikabili, na nyaraka za kughushi zilitengenezwa kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha napoteza haki yangu na kuozea jela.

Nilihisi kabisa kuwa mfumo mzima na maamuzi vilikuwa vimeharibiwa na nguvu za giza za maadui zangu waliotaka kunimaliza kabisa. SOMA ZAIDI.


Na Peter Ngamilo- TAEC


Katika safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kisasa na wa viwanda, sekta za kilimo, mifugo na viwanda zinaendelea kuwa nguzo muhimu za maendeleo ya Taifa. Hata hivyo, ukuaji wa sekta hizo hauwezi tena kutegemea mbinu za jadi pekee, hasa katika kipindi ambacho dunia inakabiliwa na changamoto za ongezeko la watu, mabadiliko ya tabianchi, kupungua kwa rutuba ya ardhi, uhaba wa maji pamoja na kuongezeka kwa magonjwa ya mimea na mifugo.

Mataifa mbalimbali duniani yameamua kukabiliana na changamoto hizo kwa kuwekeza katika sayansi na teknolojia. Miongoni mwa teknolojia zinazobadili taswira ya uzalishaji wa chakula na usimamizi wa rasilimali ni teknolojia ya nyuklia, ambayo kwa miongo kadhaa imekuwa ikitumika kuongeza tija katika kilimo, kuboresha uzalishaji wa mifugo, kusimamia rasilimali za maji, kuimarisha tafiti za kisayansi na kuongeza ushindani wa bidhaa katika masoko ya ndani na kimataifa.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC), Peter Ngamilo, bado kuna uelewa mdogo miongoni mwa wananchi kuhusu mchango wa teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya kila siku.

“Watu wengi wakisikia neno nyuklia hufikiria uzalishaji wa umeme au silaha. Ukweli ni kwamba sehemu kubwa ya teknolojia hii duniani inatumika kuboresha maisha ya wananchi kupitia kilimo, mifugo, maji, afya na viwanda. Hii ndiyo elimu ambayo TAEC inaendelea kuifikisha kwa wananchi kupitia Maonesho ya Nanenane,” anasema Ngamilo.


Anasema ushiriki wa TAEC katika Maonesho ya Nanenane haulengi tu kuonesha shughuli za Tume, bali pia kuwajengea wananchi uelewa kwamba teknolojia ya nyuklia ni nyenzo ya maendeleo inayoweza kuongeza uzalishaji wa chakula, kupunguza gharama za uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao na kuchochea ukuaji wa uchumi.

KILIMO KISICHOTEGEMEA BAHATI, BALI SAYANSI

Sekta ya kilimo ni miongoni mwa nguzo kuu za uchumi wa Tanzania. Hata hivyo, uzalishaji wake bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo wadudu waharibifu, magonjwa ya mimea, matumizi yasiyo sahihi ya mbolea na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Katika nchi mbalimbali duniani, baadhi ya changamoto hizo zimepatiwa suluhisho kupitia matumizi ya teknolojia ya nyuklia, ikiwemo mbinu ya mutation breeding, inayotumika katika kuboresha mbegu ili kupata aina za mazao zenye uwezo wa kustahimili ukame, magonjwa na wadudu, huku zikitoa mavuno bora.

Kwa mujibu wa taarifa za mashirika ya kimataifa yanayohusika na matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika kilimo, zaidi ya aina 3,400 za mazao yaliyoboreshwa kwa kutumia mbinu za mutation breeding zimesajiliwa katika zaidi ya nchi 75 duniani.

Nchi kama China, India na Vietnam ni miongoni mwa zilizopata mafanikio katika matumizi ya mbinu hizo, ambapo aina mbalimbali za mazao zimeboreshwa kwa lengo la kuongeza uzalishaji na kukabiliana na changamoto za mazingira.

Ngamilo anasema Tanzania ina sababu ya kuwekeza zaidi katika matumizi ya teknolojia hiyo.

“Tanzania imejaliwa kuwa na ardhi kubwa, rasilimali za maji na mazingira yanayofaa kwa uzalishaji wa mazao mbalimbali. Tukichanganya rasilimali hizi na teknolojia ya kisasa, ikiwemo teknolojia ya nyuklia, tunaweza kuongeza uzalishaji wa mazao ya kimkakati, kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ushindani wa bidhaa zetu katika masoko ya kikanda na kimataifa,” anasema.

KUPAMBANA NA WADUDU BILA KUHARIBU MAZINGIRA

Kila mwaka wakulima hupoteza sehemu ya mazao kutokana na wadudu waharibifu, hali inayosababisha hasara na kupunguza tija ya kilimo.

Moja ya matumizi muhimu ya teknolojia ya nyuklia katika kudhibiti wadudu ni Sterile Insect Technique (SIT), mbinu inayohusisha uzalishaji na kuachiliwa kwa wadudu wa kiume waliotiwa utasa ili wanapopandana na majike wasiweze kuzalisha kizazi kipya.

Mbinu hiyo imekuwa ikitumika katika maeneo mbalimbali duniani kudhibiti wadudu waharibifu, wakiwemo baadhi ya aina za nzi wanaoshambulia matunda na mazao mengine.

Kwa Tanzania, matumizi ya teknolojia hiyo yanaweza kuwa na mchango katika kudhibiti wadudu waharibifu, kuongeza uzalishaji wa matunda na mboga, kupunguza utegemezi wa viuatilifu na kusaidia kulinda mazingira.

“Teknolojia ya nyuklia inatufundisha kuwa si kila tatizo la kilimo linahitaji matumizi makubwa ya kemikali. Sayansi imetupa mbinu mbadala zinazoweza kusaidia kulinda mazingira na wakati huo huo kuongeza uzalishaji wa mazao,” anasema Ngamilo.

MIFUGO: KUBORESHA AFYA NA KUONGEZA UZALISHAJI

Sekta ya mifugo ina mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania, lakini bado inakabiliwa na changamoto za magonjwa, uzalishaji, uzazi na lishe.

Teknolojia ya nyuklia inaweza kutumika katika uchunguzi na udhibiti wa magonjwa, utafiti wa lishe ya mifugo pamoja na kufuatilia namna virutubisho vinavyotumika mwilini, hatua inayoweza kusaidia kuboresha uzalishaji wa maziwa na nyama.

Mfano unaotajwa katika matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika kudhibiti magonjwa ya mifugo ni Zanzibar, ambako matumizi ya Sterile Insect Technique yalichangia katika udhibiti wa nzi tsetse na kupunguza tatizo la trypanosomiasis.

Ngamilo anasema uzoefu huo unaonesha kwamba Afrika inaweza kutumia sayansi na teknolojia kutatua changamoto zinazolikabili bara hilo.

“Mfano wa Zanzibar unaonesha wazi kuwa teknolojia ya nyuklia inaweza kutoa suluhisho la changamoto ambazo kwa miaka mingi zilionekana kuwa ngumu na zenye gharama kubwa kuzitatua. Huu ni ushahidi kwamba teknolojia hii inaweza kuleta matokeo yanayogusa maisha ya wananchi,” anasema.

MAJI: RASILIMALI INAYOHITAJI SAYANSI

Katika kipindi ambacho mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuathiri upatikanaji na usalama wa maji, teknolojia ya nyuklia inaweza kuwa nyenzo muhimu katika usimamizi wa rasilimali hiyo.

Kupitia matumizi ya Isotope Hydrology, wataalamu wanaweza kupata taarifa kuhusu chanzo cha maji, umri wa maji yaliyopo chini ya ardhi, mwelekeo wa mtiririko wake na namna yanavyorejea kwenye mifumo ya asili.

Taarifa hizo zinaweza kusaidia katika kupanga matumizi endelevu ya maji kwa ajili ya kilimo, mifugo, viwanda na matumizi ya binadamu.

“Kilimo cha kesho kitategemea siyo tu upatikanaji wa maji, bali pia uwezo wa kuyatumia kwa ufanisi. Teknolojia ya nyuklia inatupa maarifa ya kisayansi yanayotuwezesha kuelewa na kupanga matumizi bora ya rasilimali hiyo muhimu,” anaeleza Ngamilo.

SAYANSI INAYOENDESHA TAFITI NA VIWANDA

Mbali na kilimo, mifugo na maji, teknolojia ya nyuklia ina nafasi katika tafiti zinazolenga kuboresha rutuba ya udongo, matumizi sahihi ya mbolea na kuongeza ufanisi wa uzalishaji wa mazao.

Katika sekta ya viwanda, teknolojia hiyo inaweza kutumika katika upimaji wa ubora wa bidhaa, ukaguzi wa miundombinu bila kuiharibu pamoja na kuboresha ufanisi wa michakato mbalimbali ya uzalishaji.

Kwa mujibu wa Ngamilo, maendeleo ya viwanda hayawezi kutenganishwa na maendeleo ya kilimo na mifugo kwa sababu viwanda vinahitaji malighafi bora na za kutosha.

“Viwanda vinahitaji malighafi bora. Malighafi bora zinatokana na kilimo na mifugo yenye tija. Hivyo, teknolojia ya nyuklia inaunganisha mnyororo mzima wa thamani, kuanzia shambani hadi kiwandani na hatimaye sokoni,” anasema.

NANENANE: KUWEKEZA KATIKA MAARIFA

Katika Maonesho ya Nanenane mwaka 2026, TAEC inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama na yenye manufaa ya teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Ngamilo anasema wananchi wanaotembelea banda la TAEC wamekuwa wakionesha hamu ya kufahamu namna teknolojia hiyo inavyoweza kutumika kutatua changamoto zinazowakabili katika shughuli zao za kila siku.

“Tunataka wananchi waondoke katika banda la TAEC wakiwa na uelewa kwamba teknolojia ya nyuklia si teknolojia ya mbali. Ni teknolojia inayoweza kumsaidia mkulima kuongeza mavuno, mfugaji kuongeza uzalishaji wa maziwa na nyama, mtafiti kupata majibu sahihi na Taifa kujenga uchumi imara,” anasema.

TANZANIA INA FURSA YA KUONGOZA

Kwa kuwa na ardhi kubwa, rasilimali za maji, mifugo na nguvu kazi ya vijana, Tanzania ina fursa kubwa ya kutumia sayansi na teknolojia kuongeza uzalishaji wa chakula, kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza thamani ya mazao, kukuza mauzo ya nje na kuharakisha ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Hata hivyo, fursa hiyo inahitaji uwekezaji zaidi katika tafiti, miundombinu, wataalamu na uhamasishaji wa matumizi ya teknolojia hiyo miongoni mwa wakulima, wafugaji, wafanyabiashara na wadau wengine.

Ngamilo anasisitiza kwamba teknolojia ya nyuklia si mbadala wa mkulima au mfugaji, bali ni nyenzo inayoweza kuongeza tija, ubora na ushindani wa bidhaa zao.

“Safari ya kuelekea Tanzania yenye uchumi wa kisasa haitategemea rasilimali tulizonazo pekee, bali namna tutakavyozitumia kwa kutumia sayansi na teknolojia. Teknolojia ya nyuklia ni moja ya zana muhimu zitakazotuwezesha kufikia azma hiyo. Huu ndio ujumbe tunaoupeleka kwa Watanzania kupitia Maonesho ya Nanenane 2026,” anahitimisha Ngamilo.




 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, amepongeza hatua madhubuti zinazochukuliwa na Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake katika kuhamasisha na kusambaza nishati safi ya kupikia nchini.

Mhe. Mgalu ametoa pongezi hizo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutambuliwa kuwa Kinara wa Nishati Safi Afrika, iliyoandaliwa na Taasisi ya Women and Youth Future Initiative (WYFI).

Amesema Wizara ya Nishati na taasisi zake, ikiwemo Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), zimeendelea kutekeleza hatua mbalimbali zinazolenga kuhakikisha nishati safi ya kupikia inawafikia wananchi wengi zaidi.

Mhe. Mgalu amebainisha kuwa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unalenga kuhakikisha takriban asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi na salama ya kupikia ifikapo mwaka 2034, huku Serikali ikijipanga kutumia takriban shilingi trilioni 24.6 katika uwekezaji na utekelezaji wa miundombinu ya nishati safi nchini.

Ameongeza kuwa, katika kuwezesha upatikanaji wa nishati mbadala na nafuu kwa wananchi, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza uzalishaji wa mkaa mbadala unaotokana na makaa ya mawe, ambao unapatikana kwa bei nafuu. Aidha, kiwanda cha Kisarawe kinazalisha mkaa na majiko mbadala, huku kukiwa na takriban viwanda vitano vinavyofanya kazi katika mikoa mbalimbali na mipango ya kufungua kiwanda kipya mkoani Dodoma ikiendelea.

Mhe. Mgalu ametoa wito kwa Watanzania kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, akisisitiza kuwa hatua hiyo inalinda mazingira na afya ya jamii, inapunguza changamoto zinazowakabili wanawake kutokana na matumizi ya nishati zisizo safi na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Aidha, ameahidi kuwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini itaendelea kuishauri na kuisimamia Serikali kwa karibu ili kuhakikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia inatekelezwa kikamilifu kwa manufaa ya Watanzania wote.

Kwa upande wake, Meneja wa Elimu kwa Walipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), CPA Paul Walalaze, amesema Serikali imeendelea kutoa misamaha mbalimbali ya kodi, hususan Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), kwa baadhi ya vifaa vinavyotumika katika nishati safi ya kupikia, ikiwemo mitungi ya gesi, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji na matumizi ya nishati hiyo nchini.









Na WMA- Dodoma


Wakala wa Vipimo (WMA) umetakiwa kupanua mpango wa kuanzisha klabu za vipimo shuleni hadi katika shule za sekondari, ili kuongeza wigo wa elimu ya vipimo na kuhakikisha uelewa wa matumizi sahihi ya vipimo unafika hadi ngazi ya kaya.

Wito huo umetolewa na Mhadhiri wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Patroba Chaulo, ambaye amepongeza WMA kwa kuanzisha klabu hizo katika shule za msingi, akisema matumizi ya wanafunzi kama mabalozi wa elimu ya vipimo ni mkakati wenye tija kubwa kwa jamii.

Amesema mpango huo unatoa fursa ya kutumia mfumo wa elimu wa “mtoto kwa mtoto” (child-to-child), ambapo wanafunzi huweza kufikisha elimu na ujumbe kwa wenzao kwa urahisi zaidi, na hatimaye kuwafikishia wazazi na familia zao.

Kwa mujibu wa Chaulo, njia hiyo inaweza kuwa na ufanisi mkubwa kwa sababu wanafunzi wana nafasi kubwa ya kushirikiana na kuwasiliana na wenzao kwa lugha rahisi na inayoeleweka, jambo linalorahisisha uenezaji wa elimu ya vipimo.

“Mtoto anaweza kumwelewesha mtoto mwenzake kwa urahisi zaidi kuliko mtu mzima anapojaribu kumwelewesha mwanafunzi. Hii inafanya mfumo wa child-to-child kuwa fursa muhimu katika kueneza elimu ya vipimo,” amesema.

Ameeleza kuwa umuhimu wa mpango huo hauishii shuleni pekee, bali unaweza kusaidia elimu ya vipimo kufika hadi ngazi ya kaya, kwa kuwa wanafunzi wanaotoka katika klabu hizo wanaishi katika familia na jamii mbalimbali.

Amesema kupitia wanafunzi hao, WMA inaweza kuwa na mtandao mpana wa mabalozi ambao utasaidia kufikisha ujumbe kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi katika maeneo ambayo ni vigumu kwa Wakala kufika moja kwa moja.

“WMA haiwezi kufika katika kila nyumba, lakini wanafunzi hawa wanatoka katika kaya mbalimbali. Hivyo, wanakuwa kiungo muhimu cha kufikisha elimu hii kutoka shuleni hadi katika familia na jamii kwa ujumla,” amesisitiza.

Chaulo amesema elimu hiyo ni muhimu katika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya vipimo sahihi na vilivyothibitishwa, hususan katika shughuli za kila siku zinazohusisha biashara na miamala mbalimbali.

Amesema jamii yenye uelewa kuhusu vipimo inaweza kutambua umuhimu wa kuhakikisha bidhaa zinapimwa kwa vipimo sahihi na kulinda haki za watumiaji pamoja na wafanyabiashara.

Kwa msingi huo, amependekeza WMA kuendelea kuimarisha klabu hizo katika shule za msingi na kuzitanua hadi shule za sekondari ili kuwafikia vijana wengi zaidi na kujenga kizazi chenye uelewa mpana kuhusu viwango na vipimo.

Ameongeza kuwa uwekezaji katika elimu ya vipimo kupitia shule ni hatua muhimu ya kujenga utamaduni wa matumizi sahihi ya vipimo nchini, huku wanafunzi wakitumiwa kama sehemu ya suluhisho la kufikisha elimu hiyo katika jamii.

Mpango huo pia unatarajiwa kuongeza uelewa wa Watanzania kuhusu umuhimu wa kuwa na viwango na vipimo sahihi na vilivyothibitishwa (standards in measurements) katika maisha ya kila siku, hususan katika shughuli zinazohusisha biashara, ununuzi na uuzaji wa bidhaa.



Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam  katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro

 


Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Moshi Vijijini umewaalika vijana na wananchi wote kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani yatakayofanyika Agosti 12, 2026, katika Viwanja vya UVCCM Himo, kuanzia saa 4:00 kamili asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Moshi Vijijini, Yuvenali Ole Rafaeli Shirima, amesema maadhimisho hayo yanalenga kuwaunganisha vijana, kuimarisha mshikamano, uzalendo na kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya Taifa.

Amesema maadhimisho hayo yatawakutanisha vijana kutoka maeneo mbalimbali pamoja na viongozi wa Serikali, Chama, taasisi na wadau wa maendeleo kwa ajili ya kujadili nafasi ya vijana katika ujenzi wa Taifa na kuhamasisha matumizi ya fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Shirima ametoa wito kwa vijana wa Wilaya ya Moshi Vijijini, Mkoa wa Kilimanjaro na maeneo mengine kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maadhimisho hayo, akisisitiza kuwa vijana ni nguvu muhimu katika kulinda amani na kuharakisha maendeleo ya nchi.

Maadhimisho ya mwaka huu yatafanyika chini ya kaulimbiu isemayo:

“Vijana ni Nguvu ya Taifa; Tushirikiane Kulinda Amani kwa Maendeleo ya Taifa Letu.”

#SikuYaVijanaDuniani2026 #UVCCMMoshiVijijini #VijanaNiNguvuYaTaifa #Kilimanjaro

Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza mazungumzo na wazalishaji wa parachichi katika wilaya za Mufindi na Njombe kwa lengo la kuanzisha mfumo wa ubunifu utakaoruhusu shamba kutumika kama ghala la bidhaa hai ili kuongeza ufanisi wa biashara ya zao hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema hayo katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma wakati akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo, aliyetembelea banda la WRRB.

Bw. Bangu amesema utaratibu huo utahakikisha matunda yanayovunwa ni yale tu yaliyofikia viwango vinavyohitajika na wanunuzi, jambo litakalopunguza upotevu wa mazao baada ya mavuno, kuhifadhi ubora wa bidhaa na kuongeza thamani ya biashara ya parachichi.

Aidha, amesema WRRB inatarajia kushirikiana na Shirika la Posta Tanzania ili kuunganisha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na huduma za kidijitali za biashara pamoja na usafirishaji wa bidhaa.

Amesema ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza ufanisi wa biashara, kurahisisha miamala na kuimarisha imani ya wanunuzi katika soko.

Awali, Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu Huduma wa WRRB, Bw. Mwita Thomas, amesema mfumo huo unaendelea kupanuliwa kutoka kwenye mazao ya kilimo pekee na sasa unahusisha pia bidhaa zisizo za kilimo, zikiwamo mifugo hai, mwani na samaki wanaofugwa kwenye vizimba.

 


 Wakala wa Vipimo (WMA) umetakiwa kupanua mpango wa kuanzisha klabu za vipimo shuleni hadi katika shule za sekondari, ili kuongeza wigo wa elimu ya vipimo na kuhakikisha uelewa wa matumizi sahihi ya vipimo unafika hadi ngazi ya kaya.

Wito huo umetolewa na Mhadhiri wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Patroba Chaulo, ambaye amepongeza WMA kwa kuanzisha klabu hizo katika shule za msingi, akisema matumizi ya wanafunzi kama mabalozi wa elimu ya vipimo ni mkakati wenye tija kubwa kwa jamii.

Amesema mpango huo unatoa fursa ya kutumia mfumo wa elimu wa “mtoto kwa mtoto” (child-to-child), ambapo wanafunzi huweza kufikisha elimu na ujumbe kwa wenzao kwa urahisi zaidi, na hatimaye kuwafikishia wazazi na familia zao.

Kwa mujibu wa Chaulo, njia hiyo inaweza kuwa na ufanisi mkubwa kwa sababu wanafunzi wana nafasi kubwa ya kushirikiana na kuwasiliana na wenzao kwa lugha rahisi na inayoeleweka, jambo linalorahisisha uenezaji wa elimu ya vipimo.

“Mtoto anaweza kumwelewesha mtoto mwenzake kwa urahisi zaidi kuliko mtu mzima anapojaribu kumwelewesha mwanafunzi. Hii inafanya mfumo wa child-to-child kuwa fursa muhimu katika kueneza elimu ya vipimo,” amesema.

Ameeleza kuwa umuhimu wa mpango huo hauishii shuleni pekee, bali unaweza kusaidia elimu ya vipimo kufika hadi ngazi ya kaya, kwa kuwa wanafunzi wanaotoka katika klabu hizo wanaishi katika familia na jamii mbalimbali.

Amesema kupitia wanafunzi hao, WMA inaweza kuwa na mtandao mpana wa mabalozi ambao utasaidia kufikisha ujumbe kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi katika maeneo ambayo ni vigumu kwa Wakala kufika moja kwa moja.

“WMA haiwezi kufika katika kila nyumba, lakini wanafunzi hawa wanatoka katika kaya mbalimbali. Hivyo, wanakuwa kiungo muhimu cha kufikisha elimu hii kutoka shuleni hadi katika familia na jamii kwa ujumla,” amesisitiza.

Chaulo amesema elimu hiyo ni muhimu katika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya vipimo sahihi na vilivyothibitishwa, hususan katika shughuli za kila siku zinazohusisha biashara na miamala mbalimbali.

Amesema jamii yenye uelewa kuhusu vipimo inaweza kutambua umuhimu wa kuhakikisha bidhaa zinapimwa kwa vipimo sahihi na kulinda haki za watumiaji pamoja na wafanyabiashara.

Kwa msingi huo, amependekeza WMA kuendelea kuimarisha klabu hizo katika shule za msingi na kuzitanua hadi shule za sekondari ili kuwafikia vijana wengi zaidi na kujenga kizazi chenye uelewa mpana kuhusu viwango na vipimo.

Ameongeza kuwa uwekezaji katika elimu ya vipimo kupitia shule ni hatua muhimu ya kujenga utamaduni wa matumizi sahihi ya vipimo nchini, huku wanafunzi wakitumiwa kama sehemu ya suluhisho la kufikisha elimu hiyo katika jamii.

Mpango huo pia unatarajiwa kuongeza uelewa wa Watanzania kuhusu umuhimu wa kuwa na viwango na vipimo sahihi na vilivyothibitishwa (standards in measurements) katika maisha ya kila siku, hususan katika shughuli zinazohusisha biashara, ununuzi na uuzaji wa bidhaa.






 


Na OWM–TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amemhakikishia Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa Ofisi yake itatekeleza kikamilifu jukumu la kuisimamia Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), kwa lengo la kuhakikisha sera na mipango ya Serikali ya kuboresha usafiri wa umma jijini Dar es Salaam inafanikiwa.

Prof. Shemdoe ametoa kauli hiyo leo, Agosti 7, 2026, jijini Dar es Salaam, alipotoa salamu za OWM–TAMISEMI kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mbele ya wananchi, mara baada ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufungua rasmi Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka, Awamu ya Pili (BRT II), unaohusisha barabara za Kilwa, Chang’ombe, Sokoine na Kawawa.

“Mheshimiwa Rais, kazi uliyotupa ya kuisimamia Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) tutaifanya kwa bidii, weledi na moyo wa uzalendo ili kufanikisha utekelezaji wa sera na mipango ya Serikali ya kuboresha usafiri wa umma,” amesema Prof. Shemdoe.

Akizungumzia mchango wa wadau katika kufanikisha mradi huo, Prof. Shemdoe amewashukuru wadau mbalimbali, wakiwemo Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), TANROADS, wakandarasi, washauri elekezi na watoa huduma, kwa ushirikiano wao uliowezesha kukamilika na kuzinduliwa kwa BRT II.

Amesema mradi huo unalenga kupunguza changamoto za usafiri kwa wakazi wa Dar es Salaam wanaotumia barabara za Kilwa, Chang’ombe, Sokoine na Kawawa, pamoja na kuboresha ufanisi wa usafiri wa umma jijini humo.

Akieleza faida za mabasi ya kisasa ya mwendokasi kwa wananchi na mazingira, Prof. Shemdoe amesema mabasi 60 yaliyoanza kutoa huduma katika njia ya Mbagala–Posta yamechangia kupunguza msongamano wa magari yanayoelekea katikati ya jiji, baada ya kuondoa daladala 400 kati ya daladala 1,627 zilizokuwa zikihudumia wakazi wa eneo hilo.

Amesema hatua hiyo si tu inaboresha usafiri kwa wananchi, bali pia inachangia kupunguza uzalishaji wa hewa yenye kiwango kikubwa cha gesi ya kaboni dioksidi (CO₂), inayozalishwa wakati injini za magari zinapochoma mafuta ya petroli na dizeli.

Kwa hatua hiyo, Serikali inaendelea kuimarisha usafiri wa umma wenye ufanisi na unaozingatia mahitaji ya wananchi, huku ikiweka mkazo katika kupunguza msongamano wa magari na athari za uzalishaji wa hewa ukaa jijini Dar es Salaam.