Sheria kuanzisha Bodi ya Wajiolojia kusimamia na kuratibu taaluma nchini

Serikali kutenga asilimia 10 ya mapato ya madini kwa utafiti wa jiosayansi

Taarifa sahihi za jiolojia kuimarisha uwekezaji na kuwalinda wadau wa madini


Wizara ya Madini imewasilisha pendekezo la kuanzishwa kwa Sheria ya Usimamizi wa Wajiolojia nchini katika Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri, hatua inayolenga kuweka mfumo madhubuti wa kusimamia taaluma hiyo na kuhakikisha taarifa za jiosayansi zinazotolewa nchini zinakuwa sahihi na zenye kuaminika.

Hayo yamebainishwa leo, Septemba 16, 2026, jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya ya Wajiolojia Tanzania (TGS).

Dkt. Kiruswa amesema endapo Sheria hiyo itapitishwa, itaanzishwa Bodi ya Wajiolojia itakayokuwa na jukumu la kusimamia, kuratibu na kuimarisha taaluma hiyo, ikiwemo kuweka viwango vya kitaaluma na kuhakikisha wataalamu wanaohusika na shughuli za jiosayansi wanatambulika na kuwajibika ipasavyo.

Amesema hatua hiyo ni muhimu kutokana na umuhimu wa taarifa za jiosayansi katika shughuli za utafutaji, uchimbaji na uwekezaji katika sekta ya madini, huku akieleza kuwa kumekuwa na baadhi ya taarifa zisizo sahihi zinazotolewa na watu wasio waaminifu au wasiokuwa na weledi na ujuzi unaohitajika, hali ambayo imekuwa ikisababisha hasara kwa baadhi ya wadau wa sekta hiyo.

“Ni muhimu kuwa na chombo kitakachosimamia taaluma hii ili kuhakikisha taarifa za jiosayansi zinazotokana na tafiti zinazofanywa nchini zinakuwa za uhakika na zinatolewa na wataalamu wenye sifa, weledi na uwajibikaji,” amesema Dkt. Kiruswa.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa amesema Serikali imefanya uamuzi wa kutenga asilimia 10 ya makusanyo yatokanayo na mapato yasiyo ya kodi katika sekta ya madini kwa ajili ya shughuli za utafiti wa madini nchini, ambapo fedha hizo zinakadiriwa kufikia takribani Sh bilioni 140.

Amesema fedha hizo zitawezesha Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuongeza kasi ya tafiti za jiosayansi na kuzalisha taarifa nyingi na sahihi zitakazosaidia kubainisha rasilimali zilizopo nchini na kuweka msingi imara wa uwekezaji katika sekta ya madini.

Dkt. Kiruswa amesema Wizara ya Madini itaendelea kushirikiana na Jumuiya ya Wajiolojia Tanzania katika kuimarisha taaluma hiyo na kuhakikisha wataalamu wa ndani wanashiriki kikamilifu katika tafiti na shughuli za jiosayansi zinazolenga kuongeza manufaa ya rasilimali za madini kwa Taifa.

Ameeleza kuwa hatua hiyo inakwenda sambamba na vipaumbele vya Wizara vinavyotokana na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050 na Sera ya Madini, ambavyo ni pamoja na kuongeza utafiti na upatikanaji wa taarifa sahihi za jiolojia, kuongeza thamani madini, kuunganisha sekta ya madini na sekta nyingine za uchumi, kurasimisha na kuboresha uchimbaji mdogo, pamoja na kuimarisha usimamizi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Kwa upande wake, Rais wa Jumuiya ya Wajiolojia Tanzania, Prof. Alisante Mshiu, amesema Mkutano Mkuu wa Mwaka ulianza Septemba 14, 2026, ukiwa na dhima ya “Matumizi ya Suluhisho za Jiosayansi kwa Ukuaji wa Viwanda, Uhakika wa Upatikanaji wa Nishati, Kuelekea Matumizi ya Nishati Safi na Maendeleo Stahimilivu Tanzania.”

Amesema mkutano huo umelenga kutoa fursa kwa wataalamu kubadilishana uzoefu na maarifa katika nyanja mbalimbali za jiosayansi, kwa lengo la kuongeza matumizi ya taaluma hiyo katika kutatua changamoto za maendeleo, kukuza uchumi na kuongeza manufaa yatokanayo na rasilimali zilizopo nchini.


















Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Mkandarasi KIKIM Contractors Limited kwa kushirikiana na mbia wake AMACO Enterprises katika Manispaa ya Lindi.

Miradi hiyo inahusisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 5.3, Stendi ya Mabasi Mitwero, Soko Kuu la Matopeni na Ofisi ya Mradi, inayotekelezwa na Serikali kupitia Mradi wa Ustawishaji Miji Tanzania (TACTIC).

Prof. Shemdoe ameeleza kutoridhishwa kwake na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo Septemba 15, 2026, mara baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Mitwero na Soko Kuu la Matopeni, ambapo alibaini kuwa utekelezaji wake umefikia asilimia 23, huku ikiwa imesalia miezi mitano kabla ya muda wa kukamilisha na kukabidhi miradi hiyo.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, kuhakikisha suala la utekelezaji wa mikataba hiyo linashughulikiwa kwa mujibu wa masharti ya mikataba, ili kuharakisha utekelezaji na kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, hawa wanaotukwamisha ni wakandarasi wazawa ambao usipowapa kazi wanalalamika. Hivyo, Mheshimiwa RC, hawa wana mikataba, shughulikia suala hili kwa mujibu wa mkataba, kwani wakandarasi hawa wanaonekana ni wababaishaji,” amesema Prof. Shemdoe.

Aidha, Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi kukutana na wakandarasi hao ili wampe mpango mkakati wa kukamilisha miradi hiyo haraka iwezekanavyo, na kuwasilisha kwake mpango kazi huo ifikapo Septemba 23, 2026.Vilevile, ameelekeza kuwa kila baada ya wiki mbili apatiwe mrejesho wa utekelezaji wa mpango huo, ili kufahamu hatua zinazochukuliwa na maendeleo ya miradi hiyo.

Akieleza chanzo cha kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mwakilishi wa Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya Interconsult Ltd, ambaye pia ni Mhandisi Mkazi, Mhandisi Rashidi Abdallah, amesema changamoto hiyo imetokana na mkandarasi kutokuwa amejipanga vyema kiutendaji, kutokuwa na rasilimaliwatu ya kutosha na kutumia vibaya fedha za awali alizolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi.

Naye mmoja wa Wakurugenzi wa kampuni zilizopewa kandarasi hizo, John Daniel, amekiri kuwa wamechelewa kutekeleza miradi hiyo kutokana na uzembe, huku akieleza kuwa wamejipanga kufanya kazi usiku na mchana baada ya kuzifanyia kazi changamoto zilizokuwa zikikwamisha utekelezaji. 

Bw. Daniel ameomba kukutana na Mkuu wa Mkoa wa Lindi ili kuwasilisha mpango kazi wao, huku akimuomba Mkuu wa Mkoa kuwawekea malengo ya muda mfupi yatakayowawezesha kukamilisha kandarasi yao kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema atakutana na wakandarasi hao ili wamueleze mkakati wanaokuja nao wa kukamilisha miradi yote ndani ya miezi mitano iliyobaki.

Mhe. Malima amewataka wakandarasi hao, wakati wa kikao hicho, kuwa tayari kuridhia kutoa mkataba mdogo (sub-contract) kwa mkandarasi mwingine kutekeleza sehemu ya mradi endapo wataona hawana uwezo wa kuikamilisha kwa wakati.

Katika ziara yake ya Septemba 15, 2026, Prof. Shemdoe alitembelea na kukagua pia utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Daraja la Ng’uni katika Kata ya Nanganga, ujenzi wa shule mpya ya msingi eneo la Shule ya Sekondari Kitandi, ujenzi wa Kituo cha Afya Chiola Nachingwea, pamoja na kufanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mtuha, Nachingwea DC.

















NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa wito wa kujenga mifumo itakayowezesha ubunifu na fursa za mazingira kugeuzwa kuwa miradi inayotekelezeka, inayoweza kufadhiliwa na kukua.
Jina langu ni Baraka. Kujenga ndoa na familia kwa miaka mingi kisha kushuhudia nyumba yako ikijaa ugomvi, matusi, na baridi la mahusiano ni jambo linaloumiza moyo na kunyonga nafsi.

Kwa muda mrefu, mimi na mwenzangu wa maisha tulikuwa tukiishi kama maadui waliokutana nyumba moja. Kila siku ilikuwa ni sababu za kelele na mizozo hata kwa mambo madogo yasiyo na msingi.

Mapenzi, heshima, na mazungumzo ya amani vilitoweka kabisa, na badala yake paka mweusi wa ugomvi akatawala nyumba yetu.

Hali hii ilileta msongo mkubwa wa mawazo kwa watoto na kunifanya nishinde na hofu ya kuwa ndoa yetu iliyodumu kwa miaka mingi ingeishia kwenye talaka na aibu kubwa katika umri wetu huu wa ukubwani.

​Nikiwa kwenye simanzi na nikionekana kukosa matumaini ya kuokoa ndoa yangu, ndugu yangu wa karibu alinitembelea na kunikuta nikiwa kwenye huzuni nzito. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Godfrey. Kuwekeza mtaji wako wote kwenye biashara kisha kutazama duka lako likifa taratibu huku ukipata hasara kila siku ni jaribu zito linaloweza kumfanya mtu akate tamaa ya maisha.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikuwa nikimiliki duka la bidhaa mbalimbali ambalo hapo awali lilikuwa likiniingizia faida nzuri.

Hata hivyo, ghafla mambo yalianza kubadilika vibaya sana; wateja waliokuwa wakija kila siku walitoweka kwa awamu, na hata wale waliopita mbele ya duka langu walionekana kama hawalioni kabisa.

Bidhaa zilikaa kwenye rafu mpaka kuharibika, kodi ya pango ilianza kuniletea migogoro na mwenye nyumba, na madeni ya wauzaji wa jumla yalianza kunisonga kila upande.

Nikiwa kwenye simanzi nzito na msongo mkubwa wa mawazo nikifikiria kufunga duka na kukimbia mji, mfanyabiashara mwenzangu wa siku nyingi alinitembelea. SOMA ZAIDI.


Jina langu ni Joseph. Kupoteza uwezo wa kiume na kushindwa kumtimizia mwenzako wa maisha haki yake ya ndoa ni jambo linaloweza kumvua mwanamume heshima, kujiamini, na amani ya nafsi.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilikuwa nikiteseka na tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume na mwili kukosa hamu kabisa. Kila nilipojaribu kumsogelea mke wangu, nilijikuta nikiishia njiani na kuondoka nikiwa nimejaa aibu kubwa.

Hali hii ilileta baridi kali katika ndoa yetu; mke wangu alianza kunitazama kwa dharau, mazungumzo ya amani yalitoweka, na hofu ya yeye kutoka nje ya ndoa au kuniacha kabisa ilikuwa ikinikesha usiku kucha nikiwa na msongo mkubwa wa mawazo.

Nikiwa kwenye simanzi na majuto makubwa, rafiki yangu wa miaka mingi alinitembelea na kunikuta nikiwa mwenye huzuni nzito. SOMA ZAIDI.


 

Kigoma, Septemba 16, 2026

Wadau mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji wamekutana mjini Kigoma katika kikao cha siku moja kilichoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kwa lengo la kujadili fursa na changamoto zinazohusiana na usafirishaji wa mizigo na namna ya kuimarisha biashara katika ukanda wa Magharibi na Maziwa Makuu.

Kikao hicho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka katika sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji, ambapo Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano miongoni mwa wadau katika kuimarisha ufanisi wa usafirishaji na kukuza biashara ya kikanda.

Kwa upande wa TPA, Naibu Mkurugenzi Mkuu, Mha. Dkt. Baraka Mdima, ameshiriki kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, akiwakilisha uongozi wa Mamlaka katika majadiliano yaliyolenga kubaini maeneo ya kimkakati ya kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji kupitia Bandari ya Kigoma.

Majadiliano katika kikao hicho yamejikita katika kubaini changamoto zinazokwamisha mtiririko wa mizigo, zikiwemo vikwazo visivyo vya kiforodha, ucheleweshaji na gharama za usafirishaji, pamoja na kutafuta suluhu za pamoja zitakazoboresha mazingira ya biashara na kuongeza ushindani wa njia za usafirishaji.

Aidha, wadau wamejadili umuhimu wa kuimarisha matumizi ya Bandari ya Kigoma kama lango muhimu la biashara katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kupitia Ushoroba wa Kati (Central Corridor) unaoiunganisha Tanzania na nchi jirani.

Kikao hicho pia kimekuwa fursa ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wengine wa mnyororo wa usafirishaji katika kuboresha huduma, kupunguza muda na gharama za usafirishaji, na kuweka mazingira rafiki zaidi kwa biashara ya ndani na ya kikanda.

Kwa ujumla, kikao hicho kimeendelea kuonesha umuhimu wa majadiliano ya pamoja katika kutatua changamoto za usafirishaji na kutumia fursa zilizopo katika ukanda wa Magharibi, huku Bandari ya Kigoma ikiendelea kuwa sehemu muhimu ya kuunganisha biashara ya Tanzania na masoko ya nchi za Maziwa Makuu.












RIYADH, SAUDI ARABIA: 

Tanzania imesisitiza umuhimu wa kujenga na kutumia akili unde (Artificial Intelligence – AI) inayozingatia lugha, utamaduni, mazingira na mahitaji ya jamii, huku ikieleza dhamira ya kuimarisha uwezo wa ndani wa nchi katika teknolojia hiyo na kuongeza nafasi ya Kiswahili katika ulimwengu wa akili unde.

Msisitizo huo umetolewa katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde linalofanyika mjini Riyadh, Saudi Arabia, ambapo Tanzania imeshiriki katika mjadala wa kimataifa kuhusu hatua za vitendo zinazoweza kuchukuliwa na nchi ili kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanaenda sambamba na maadili, uwajibikaji, usalama na maendeleo jumuishi.

Katika mchango wake kwenye mjadala huo, mwakilishi wa Tanzania aliishukuru UNESCO na Serikali ya Saudi Arabia kwa kuandaa jukwaa hilo, akieleza kuwa majadiliano hayo yana umuhimu mkubwa katika kuzipa nchi nafasi ya kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la pamoja kuhusu fursa na changamoto zinazoletwa na maendeleo ya akili unde.

Aidha, Tanzania iliishukuru UNESCO kwa kuiunga mkono Serikali katika kutekeleza Mbinu ya Tathmini ya Utayari wa Akili Unde (Readiness Assessment Methodology – RAM) mwaka 2024, ambayo matokeo yake yalizinduliwa mwaka 2025.

Tathmini hiyo iliisaidia Tanzania kubaini maeneo mbalimbali yanayohitaji kuimarishwa ili kujenga mazingira wezeshi kwa maendeleo na matumizi salama, jumuishi na yenye maadili ya akili unde.

TANZANIA YASISITIZA KUJENGA UWEZO WA NDANI

Akieleza baadhi ya mapengo yaliyobainika, mwakilishi wa Tanzania alitaja umuhimu wa kuhakikisha lugha mbalimbali zinapata nafasi katika mifumo ya akili unde, akisisitiza kuwa nchi zinahitaji kujenga uwezo wa ndani ili teknolojia hiyo iweze kuakisi mazingira na mahitaji ya jamii zao.

Alieleza kuwa utegemezi mkubwa wa mifumo ya akili unde iliyotengenezwa nje unaweza kuibua changamoto zinazohusiana na uwakilishi wa tamaduni, usalama na umiliki wa data, pamoja na ulinganifu wa mifumo hiyo na sheria na maadili ya nchi husika.

Kwa msingi huo, Tanzania imeona umuhimu wa kuwekeza katika uwezo wa ndani wa kutengeneza na kutumia mifumo ya akili unde inayozingatia lugha na mazingira ya Tanzania, sambamba na kuimarisha miundombinu ya data na mifumo ya kitaifa ya usimamizi wa teknolojia hiyo.

Mwelekeo huo unaendana na hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuimarisha mageuzi ya kidijitali nchini. Serikali imetangaza mageuzi ya kidijitali kuwa miongoni mwa vipaumbele katika Bajeti ya mwaka 2026/2027, huku ikiendelea na maandalizi ya Mkakati wa Taifa wa Akili Unde.

KISWAHILI KUPATA NAFASI KATIKA MAPINDUZI YA AI

Moja ya hoja muhimu iliyowasilishwa na Tanzania Riyadh ni umuhimu wa kuendeleza mfumo mkubwa wa lugha (Large Language Model – LLM) wa Kiswahili, ili kuwezesha lugha hiyo kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya teknolojia za akili unde.

Tanzania imeeleza nia ya kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo UNESCO, katika kuendeleza mfumo huo, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa teknolojia kuelewa na kutumia Kiswahili kwa ufasaha na kwa kuzingatia mazingira ya watumiaji wake.

Kiswahili kinachukua nafasi muhimu katika maisha ya Watanzania na ni miongoni mwa lugha zinazotumika na idadi kubwa ya watu barani Afrika. Kwa hiyo, uwekezaji katika teknolojia inayoweza kuelewa na kutumia Kiswahili una umuhimu katika kupanua ushiriki wa wananchi katika mapinduzi ya kidijitali.

Hatua hii pia inaendana na mwelekeo wa Serikali wa kuendeleza rasilimali na zana za lugha ya Kiswahili kwa ajili ya mifumo ya akili unde na uchakataji wa lugha asilia.

MAGEUZI YA KIDIJITALI KUELEKEA TANZANIA YA MAENDELEO

Mjadala wa Tanzania katika jukwaa hilo unaakisi mwelekeo mpana wa Serikali katika kutumia teknolojia za kisasa kama kichocheo cha maendeleo ya Taifa.

Katika hatua mbalimbali, Serikali imeendelea kuweka mazingira ya matumizi ya akili unde, ikiwemo kuimarisha sera na mifumo ya kidijitali, kulinda taarifa binafsi na kujenga uwezo wa rasilimali watu katika teknolojia zinazochipukia.

Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Kidijitali wa 2024–2034 pamoja na hatua zinazoendelea katika eneo la akili unde vinaweka msingi wa kutumia teknolojia za kisasa katika kuongeza ufanisi wa huduma, kukuza ubunifu na kuchochea shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wa elimu, Serikali pia imeendelea kuweka msisitizo katika matumizi sahihi ya teknolojia mpya, ikiwemo akili unde, katika ufundishaji, ujifunzaji, utafiti na ujenzi wa uwezo wa walimu na wanafunzi.

TANZANIA NA AJENDA YA AI BARANI AFRIKA

Katika mjadala huo wa kimataifa, Tanzania imeendelea kuangazia pia nafasi ya Afrika katika mapinduzi ya akili unde, ikisisitiza umuhimu wa bara hilo kuongeza uwezo wake katika sayansi, teknolojia, utafiti, ubunifu na ujuzi wa kidijitali.

Kwa Tanzania, Afrika inapaswa kuwa zaidi ya mtumiaji wa teknolojia hiyo; inahitaji pia kujenga uwezo wa kuzalisha maarifa, data, mifumo na ubunifu unaozingatia mazingira ya Kiafrika.

Hii inamaanisha kuongeza uwekezaji katika wataalamu, taasisi za utafiti, miundombinu ya kidijitali na rasilimali za lugha za Kiafrika ili kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanawanufaisha wananchi na kuchangia maendeleo ya bara.

UNESCO NA TANZANIA ZASHIRIKI KUJENGA AI YENYE MAADILI

Ushiriki wa Tanzania katika jukwaa la Riyadh unaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na UNESCO katika eneo la teknolojia zinazochipukia na matumizi yake yenye uwajibikaji.

Kupitia Tathmini ya Utayari wa Akili Unde, Tanzania imepata fursa ya kutathmini mazingira yake ya kitaifa na kubaini maeneo yanayohitaji kuimarishwa katika sera, mifumo ya kitaasisi, uwezo wa watu, miundombinu na matumizi ya teknolojia hiyo.

Kwa upande mwingine, ushiriki katika mijadala ya kimataifa kama ya Riyadh unaipa Tanzania nafasi ya kushirikisha uzoefu wake, kujifunza kutoka kwa nchi nyingine na kuendelea kujenga ushirikiano wa kimataifa katika eneo la akili unde.

Hatua hizi zinaendana na dhamira ya Serikali ya kutumia mageuzi ya kidijitali, sayansi, teknolojia na ubunifu kama nyenzo za kuongeza fursa za maendeleo na kujenga Tanzania inayokwenda sambamba na mabadiliko ya kiteknolojia duniani.

TANZANIA YAANGALIA MUSTAKABALI WA TEKNOLOJIA

Kwa ujumla, ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde umeweka mkazo katika kujenga teknolojia inayozingatia watu, lugha na mazingira yao.

Kupitia mjadala huo, Tanzania imeendelea kuonyesha umuhimu wa kuunganisha maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya jamii, huku ikisisitiza kuwa akili unde inapaswa kutumika kwa kuzingatia maadili, usalama, haki, utofauti wa lugha na tamaduni, pamoja na vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.

Ushiriki huo unaendelea kuifanya Tanzania kuwa sehemu ya mjadala wa kimataifa kuhusu mustakabali wa akili unde, wakati Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kujenga mazingira wezeshi ya mageuzi ya kidijitali na matumizi ya teknolojia kwa maendeleo ya Taifa.

Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde linaendelea mjini Riyadh, Saudi Arabia, likiwakutanisha viongozi, wataalamu, watafiti, watunga sera na wadau kutoka sehemu mbalimbali duniani kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na utawala wa akili unde unaozingatia maadili na uwajibikaji.

 Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeendelea kuvuna matunda ya uwekezaji katika utalii wa misitu, huku idadi ya watalii wanaotembelea vivutio vinavyosimamiwa na taasisi hiyo ikifikia 377,116 mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko kubwa kutoka watalii 46,533 mwaka 2020.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Utalii TFS, PCO Someni Mteleka, ongezeko hilo linaenda sambamba na kuimarika kwa mchango wa utalii katika mapato ya taasisi, ambapo mwaka 2020 TFS ilirekodi watalii mapato ya zaidi ya Sh 159 milioni kutokana na utalii wa ikolojia na kuongezeka hadi Sh 3.5 bilioni mwaka 2025/2026

Akizungumza jana Septemba 15, 2026 jijini Dodoma wakati wa mafunzo ya utangulizi kwa watumishi wapya wa TFS, Mteleka alisema taasisi hiyo inaendelea kuendeleza bidhaa mbalimbali za utalii zinazotokana na misitu, mashamba ya miti, mikoko na maeneo ya kihistoria, hatua inayolenga kuongeza fursa za utalii na manufaa ya kiuchumi.

Alisema TFS kwa sasa inasimamia maeneo 35 ya utalii yanayotoa shughuli mbalimbali, zikiwemo matembezi ya misituni, kuangalia ndege na wanyama, kupanda na kutalii milimani, utalii wa nyuki, baiskeli, kuendesha mitumbwi na kayak, kambi, picnic, pamoja na kutembelea maeneo ya kihistoria na kitamaduni.

Mteleka alisema ukuaji wa utalii umechangiwa pia na kuongezeka kwa maeneo ya hifadhi za misitu ya kitaifa (NFRs), ambayo yameongezeka kutoka maeneo matano mwaka 2015 hadi kufikia 25 mwaka 2025, huku utalii wa ikolojia ukiwa miongoni mwa shughuli kuu za kiuchumi zinazoruhusiwa katika maeneo hayo kwa kuzingatia uhifadhi na athari ndogo kwa mazingira.

Alisema mbali na hifadhi za misitu, TFS inaendelea kutumia mashamba ya miti na misitu ya mikoko kuendeleza bidhaa mpya za utalii zisizohitaji uvunaji wa rasilimali, ikiwemo utalii wa michezo kama mbio za magari, marathoni na shughuli za kuendesha farasi, pamoja na shughuli za utalii katika maeneo ya mikoko.

Kwa mujibu wa Mteleka, TFS pia inasimamia vituo sita vya maeneo ya kale, vikiwemo Mji Mkongwe wa Bagamoyo, Magofu ya Kaole, Tongoni, Michoro ya Miamba ya Kondoa ambayo ni eneo la Urithi wa Dunia la UNESCO, pamoja na maeneo yanayohusishwa na Dk. David Livingstone na Jengo la Afya.

Alisema TFS inaendelea kushirikiana na taasisi za Serikali, washirika wa maendeleo, mashirika yasiyo ya Serikali, jamii na sekta binafsi katika kuboresha miundombinu, huduma na upatikanaji wa vivutio, huku ikiendelea kutangaza bidhaa zake kupitia vyombo vya habari vya jadi na kidijitali ili kuongeza watalii na kuchangia lengo la taifa la kufikia watalii milioni nane kwa mwaka ifikapo 2030.




 Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilaya ya Chamwino imefungua barabara ya Manda–Mafurungu yenye urefu wa kilomita 25 hatua ambayo imebadili hali ya usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa kijiji cha Mafurungu baada ya kukabiliwa na changamoto ya muda mrefu ya kutokuwa na barabara.


‎Akizungumza kuhusu maendeleo ya mradi huo, Meneja wa TARURA wilaya ya Chamwino Mhandisi Richard Sanga amesema, barabara hiyo imefunguliwa ikiwa ni jitihada za serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuunganisha wananchi na kurahisisha shughuli za kiuchumi na kijamii.

‎Amesema TARURA wilaya ya Chamwino inahudumia mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 1,297 huku ujenzi wa barabara ya Manda–Mafurungu ukiwa ni muhimu kwa wananchi wa vijiji vya Manda na Mafurungu kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya na elimu, kupunguza gharama za usafiri na kufungua fursa za kiuchumi.

‎"Awali barabara hii haikuwepo kabisa lakini baada ya kupata fedha tumeweza kuifungua, mkandarasi tayari ameshafungua kilomita zote 25 huku kazi zinazoendelea ni ujenzi wa makalavati, uwekaji wa kifusi katika maeneo korofi na maandalizi ya uchongaji wa mifereji kwa ajili ya kudhibiti na kuondoa maji ya mvua barabarani", amesema.

‎Ameeleza kuwa kutokana na umuhimu wa barabara hiyo katika bajeti ya mwaka huu wa fedha wataweka changarawe katika baadhi ya maeneo korofi huku mpango wa mwaka ujao wa fedha ukiwa ni kuweka kifusi barabara yote na kumalizia makalavati ili kuhakikisha barabara inapitika kwa urahisi na kwa uhakika kipindi chote cha mwaka.

‎Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kitongoji cha Machimbo, Bw. Mrisho Ally amesema kabla ya barabara hiyo wananchi wa Mafurungu wakitaka kusafiri hadi Dodoma mjini safari ya kwenda na kurudi walikuwa wakitumia nauli zaidi ya Sh. 100,000/= hali iliyowalazimu kutumia muda mwingi na gharama kubwa.

‎Amesema kwa sasa gharama hiyo imeshuka hadi Sh. 24,000/= kwa safari ya kwenda na kurudi huku magari yakiwa yanafika moja kwa moja kijijini ambapo imepunguza gharama na muda wa usafiri.

‎Ameongeza kuwa eneo hilo lina shughuli kubwa za uchimbaji wa madini ya dhahabu zinazochangia uchumi wa wilaya ya Chamwino hivyo ameiomba serikali kuendelea kuboresha barabara hiyo ili iweze kutoa huduma kwa wananchi na wafanyabiashara katika kipindi cha mwaka mzima.

‎Naye, Bw. Zabroni Matonya mkazi wa Mafurungu na mwekezaji katika shughuli za uchimbaji madini amesema, barabara hiyo imekuwa mkombozi kwa wachimbaji na wawekezaji kutokana na kurahisisha usafirishaji wa vifaa na malighafi kwani awali ubovu wa barabara uliwafanya kutumia muda mrefu kusafirisha malighafi zao mjini hivyo ameishukuru serikali kwa barabara hiyo.

‎Mkazi wa Mafurungu Bi. Salma Mtacha amesema kabla ya barabara wanafunzi walikuwa wakitembea umbali mrefu kufika shuleni hali iliyokuwa ikiwatia hofu wazazi lakini sasa barabara imefunguka wanafunzi wanafika shuleni bila shida pia wananchi wanafika katika vituo vya afya na hospitali bila changamoto jambo ambalo limeongeza usalama na ustawi wa jamii.

‎Naye, Selemani Bundala mkazi wa Mafurungu amesema awali safari ya kutoka kijijini hadi Dodoma mjini kwa pikipiki ilikuwa ikigharimu hadi Sh. 100,000/= lakini baada ya barabara kufunguliwa hali imebadilika na mabasi sasa yanafika moja kwa moja kijijini.

‎Amesema wananchi wanathamini jitihada za serikali katika kufungua barabara hiyo na ameomba kazi ya uboreshaji iendelee hadi barabara hiyo iweze kupitika mwaka mzima.