Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo amewasilisha Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27 akisisitiza vipaumbele vitano vya utekelezaji wake.

Akitaja vipaumbele hivyo, amesema mosi ni kuimarisha utawala bora, demokrasia, amani, na utulivu na pili ni kujenga uchumi imara, jumuishi na shindani na kipaumbele cha tatu ni, kuimarisha uwezo wa watu na maendeleo ya jamii.

Akiendelea kufafanua vipambele hivyo, Mhe. Waziri amesema kipaumbele cha nne ni kuimarisha uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu kwa mabadiliko ya tabianchi na cha tano kikiwa kusimamia utekelezaji wa vichocheo vya mageuzi ambavyo ni pamoja na nishati, miundombinu ya usafiri na usafirishaji, utafiti na maendeleo, na mageuzi ya kidigitali.

Prof Kitila amesesema utekelezaji wa vipaumbele hivyo ni hatua za kuyatekeleza malengo makuu ya Dira 2050, na vimezingatia Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/27 – 2030/31 wenye dhima ya “Mageuzi kwa ajili ya Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uzalishaji Ajira” ambao ni wa kwanza katika utekelezaji wa Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/27 – 2050/51.

Aidha katika kutekeleza maeneo ya vipaumbele hivyo, Serikali imepanga kuanza kutekeleza programu na miradi mbalimbali ikiwemo miradi shikizi 38 kati ya 51 iliyopo katika programu saba (7) za kielelezo zilizoainishwa katika Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.





MAGAVANA wa Benki Kuu za nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wamekutana jijini Dar es Salaam kujadili mikakati ya kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazoendelea kujitokeza duniani, huku migogoro ya kimataifa na mfumuko wa bei vikitajwa kuwa miongoni mwa vihatarishi vikubwa vya ukuaji wa uchumi wa ukanda huo.


Na Ashura Mohamed, ARUSHA

Naibu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalam kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha IAA, Dkt. Grace Temba, amezindua na kuweka msingi wa maandalizi ya kongamano la kimataifa la utalii linalotarajiwa kufanyika tarehe 25 Septemba, 2026 mkoani Arusha.

Tukio hilo la kongamano ni muhimu kwa taasisi hiyo na maalum kwa wadau wa utalii kutoka maeneo mbali mbali duniani likilenga wadau wa sekta ya utalii kwa dhima kubwa ya kuhamasisha utalii wa ndani ili kuendelea kuhamasisha idadi ya watalii kuongezeka.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo Dkt. Grace amesema kuwa lengo hasa ni kuhakikisha wadau mbali mbali wanashiriki na kufanya kongamano hilo kujumlisha watunga sera, wadau wa utalii kutoka ndani na nje ya nchi kujiandaa na kushiriki kwa ufanisi zaidi.

“Siku ya kongamano tunawaweka pamoja wadau mbali mbali tunatoa taarifa mbali mbali za utafiti zilizofanywa na wadau mbali mbali waliopo katika sekta ya utalii lakini pia Chuo cha Uhasibu Arusha, watunga sera wa taasisi na mlaji ili kuja na suluhisho na maboresho makubwa katika sekta ya utalii kwa lengo la kunufaisha pande zote,” alisema Dkt. Grace.

Aidha amesema kuwa kongamano hilo la nne linatarajiwa kuendelea kukuza na kutangaza nchi kimataifa kwa kuja na mawasilisho ambayo yatalenga wadau na watoa huduma kuendelea kujikuza kimasoko, miundombinu, na kuifanya sekta hiyo kuwa bobezi na kuchangia pato la taifa.

Nae Kaimu Mkuu wa Kitivo cha Biashara na Sayansi ya Jamii kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha IAA, Bi. Lorna Boniface Mwijarubi, amesema kuwa chuo hicho kinatarajia kushirikiana na taasisi mbali mbali na wadau wa utalii katika kuonyesha tafiti na bunifu ambazo zitaisaidia sekta ya utalii kuwa bora zaidi na kuendelea kuliingizia taifa kipato.

Amesema kuwa mafanikio yaliyopatikana kutokana na makongamano yaliyopita ni makubwa kwa kuwa yamekijengea chuo mashirikiano na wadau ambayo huwezesha wanafunzi wa kozi ya utalii na ukarimu kupata fursa ya kujifunza kwa vitendo katika maeneo mbali mbali nchini na kusaidia kupata ajira pamoja na taifa kupata mapato kupitia sekta hiyo.

Chuo cha Uhasibu Arusha IAA kimeendelea kuwa maarufu katika sekta mbali mbali kwa kutoa elimu bora yenye ushindani sokoni huku katika sekta ya utalii inatajwa kuwa ndio chuo pekee kinachotoa kozi ya utalii na ukarimu nchini ambayo inatajwa kuwa na mchango mkubwa katika kutangaza nchi na kuendelea kuifanya sekta hiyo kuwa bora zaidi nchini.











Kwa miaka mingi, nilijivunia biashara yangu.

Nilikuwa nimeijenga kwa juhudi kubwa na nilikuwa na imani kubwa kwa wafanyakazi wangu. Tulikuwa kama familia, na sikuwahi kufikiria kwamba mtu ambaye nilimwamini angeweza kuwa chanzo cha matatizo yaliyokuwa yananikabili. Tatizo lilianza polepole.

Kila mwisho wa wiki nilipokagua hesabu za biashara, niligundua kulikuwa na upungufu wa fedha. Mwanzoni nilidhani ni makosa ya kawaida ya mahesabu au matumizi ambayo hayakuwa yameandikwa vizuri. Lakini hali iliendelea kujirudia.

Wiki moja ikageuka mwezi, na miezi ikazidi kwenda. Kiasi cha fedha kilichokuwa kinapotea kilianza kuongezeka. 

Nilianza kupata wasiwasi kwa sababu biashara yangu ilikuwa ikipata hasara ambayo sikuweza kuieleza. Kwa kweli nilichanganyikiwa sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa siwezi kumshuku mtu yeyote. Wafanyakazi wote walionekana waaminifu na walikuwa wamefanya kazi nami kwa muda mrefu.
Nilianza kufuatilia kila kitu kwa karibu zaidi.

Nilikagua stakabadhi, mauzo, na matumizi ya kila siku. Hata hivyo, sikuweza kupata jibu la wazi kuhusu chanzo cha upotevu wa fedha.
Kadri muda ulivyopita, hasara ilizidi kuongezeka.

Kulikuwa na wakati nilifikiria kufunga biashara kwa sababu sikuona namna ya kuzuia hali ile.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, ndoto yangu kubwa ilikuwa kubeba mtoto wangu mikononi mwangu.

Nilipoolewa, niliamini kwamba baada ya muda mfupi ningekuwa mama. Nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu maisha yangu ya baadaye na familia niliyotamani kuijenga.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Mwezi mmoja ulipita, kisha mwingine. Baadaye mwaka mmoja ukapita bila kupata ujauzito. 

Kadri muda ulivyoendelea kwenda, wasiwasi ulianza kuingia moyoni mwangu. Nilitafuta ushauri wa kitabibu na kufanya vipimo mbalimbali.

Baadhi ya majibu niliyopata yalikuwa magumu kuyakubali. Niliambiwa kwamba kupata mtoto kungeweza kuwa changamoto kubwa kwangu na kwamba huenda ningehitaji uvumilivu mkubwa kuliko nilivyokuwa nikifikiria. Kwa kweli nilivunjika moyo.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wakipata watoto kwa urahisi huku mimi nikiendelea kusubiri. Kila nilipoalikwa kwenye sherehe za watoto au kuona familia mpya zikifurahia watoto wao, nilihisi maumivu makubwa moyoni. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na wakati niliamini kwamba mapenzi hayakuwa sehemu ya maisha yangu. Kwa miaka mingi, nilijaribu kujenga mahusiano ya kweli, lakini kila nilipofikiria nimepata mtu sahihi, mambo yaliishia tofauti. 

Nilivunjwa moyo mara kadhaa na hali ile iliniacha na maumivu makubwa ambayo sikutarajia.

Mwanzoni nilikuwa na matumaini. Kila nilipoanza uhusiano mpya, niliamini kwamba safari hii mambo yangekuwa tofauti. Lakini mara nyingi ndoto zangu ziliishia kuvunjika na kuniacha nikianza upya. Kadri miaka ilivyopita, nilianza kuchoka.

Niliona marafiki zangu wakifunga ndoa na kujenga familia zao huku mimi nikiendelea kuzunguka kwenye maumivu yale yale. 

Wakati mwingine nilijaribu kujifanya sina shida, lakini moyoni nilitamani kupata mtu ambaye angenipenda kwa dhati. Kwa kweli nilikata tamaa.

Nilifikia hatua ya kuamua kujikita kwenye kazi na maisha yangu binafsi. Nilijiambia kwamba huenda siku yangu ya kupata mwenza wa maisha isingewahi kufika. Lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mitatu, maisha yangu yalizunguka jambo moja tu. Kutafuta kazi. Kila asubuhi niliamka nikiwa na matumaini mapya. 

Nilifungua simu yangu na kutafuta matangazo ya kazi, nikatuma maombi, na kusubiri majibu ambayo mara nyingi hayakuwahi kufika.

Mwanzoni nilikuwa na matumaini makubwa.

Nilijiamini kuwa elimu yangu na uzoefu wangu vingekuwa vya kutosha kunisaidia kupata nafasi nzuri. Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kuona hali ikiwa tofauti na nilivyotarajia.
Miezi iligeuka miaka.

Nilituma maombi kwa kampuni nyingi sana. Wakati mwingine niliitwa kwa mahojiano lakini sikuchaguliwa. Mara nyingi sikupata hata majibu ya maombi niliyotuma. 

Kwa kweli hali ile ilinivunja moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona marafiki zangu wakipata kazi na kuendelea na maisha yao huku mimi nikiendelea kusubiri nafasi yangu.

Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na kitu nilichokuwa nakosea. Kadri miaka ilivyopita, confidence yangu ilianza kupungua. 

Kulikuwa na nyakati nilitaka kuacha kutuma maombi kabisa. Nilihisi kama kila juhudi niliyokuwa nikifanya hazikuwa na matokeo yoyote. Lakini sikuwa tayari kukata tamaa. SOMA ZAIDI.

Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo simu ikilia nilikuwa naogopa kuipokea.

Sababu ilikuwa moja tu. Nilikuwa na deni kubwa ambalo nilikuwa nimeshindwa kulilipa kwa muda mrefu.

Kila mwezi nilijitahidi kutafuta fedha za kulipa sehemu ya deni hilo, lakini mahitaji mengine ya maisha yalifanya hali kuwa ngumu zaidi.

Mwanzoni niliamini ningemaliza kulipa haraka.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyopanga. Biashara yangu ilipata changamoto, mapato yakapungua, na madeni yakaendelea kuongezeka. Kadri muda ulivyopita, presha ilizidi kuwa kubwa. Kwa kweli nilikuwa naishi kwa wasiwasi.

Kila nilipoona ujumbe au simu kutoka kwa wadai, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu. Wakati mwingine nilikosa usingizi nikifikiria jinsi nitakavyotoka kwenye hali ile.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa mtu mwenye bidii. Sikupenda kukwepa majukumu yangu, lakini nilijikuta katika hali ambayo sikuwa na uwezo wa kufanya kila kitu kwa wakati mmoja.

Miaka ilipita huku nikihangaika. Kulikuwa na nyakati nilikata tamaa na kuanza kuamini kwamba ningebeba mzigo wa deni hilo maisha yangu yote. Lakini moyoni bado nilikuwa na matumaini kwamba siku moja hali ingebadilika. SOMA ZAIDI.

 


Na; Mwandishi wetu – Chato


Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Louis Peter Bura Amepongeza Programu ya kuendeeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu kwa Uratibu wa Kituo cha kuendeleza ukuzaji Viumbemaji Rubambagwe Kilichopo wilayani Chato Mkoani Geita kinachosimamiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Ametoa Pongezi hizo Tarehe 10 Juni 2026 Wilayani Chato alipofanya ziara maalum ya kutembelea kituo hicho akiwa pamoja na timu ya wataalam waliokutana katika Wilaya hiyo wakiwa katika kazi maalum ya kufanya mapitio ya mpangokazi wa Program hiyo.



Mkuu wa Wilaya Bura, alisema kuwa Wilaya yake inawajibu wa kutoa elimu kwa wafugaji kupitia kituo cha Rubambagwe hivyo amewaasa wataalam kutoka katika sekta zinazotekeleza mradi kufanya kazi kwa ushirikianao na Wilaya hiyo, ili kuweza kuleta matokeo chanya katika uchumi wa Wilaya na Taifa kwa Ujumla na Kuongeza mnyororo wa thamani.


“Tutakuwa tunazalisha vifaranga vya samaki pale, haitatosha hiyo pia tutakuwa tunazalisha vyakula vya samaki, na hayo yote yamenipa mimi wakati mzuri na sababu ya kujifunza haya yote, na tunashukuru mradi huu kwenda kwa kasi na ni wakati sasa wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja . “Alibanisha

Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza ushirikishwaji mzuri baina ya sekta zinazotekeleza Programu hiyo nchini pamoja na Wilaya husika.’katika dhana nzima ya ushirikishwaji kuna mambo mengi ambayo Wilaya inaweza kuyasimamia na kuyatekeleza kwa ukaribu zaidi, hapa Chato wananchi wanajihusisha Zaidi na uuzaji wa samaki tuna soko kubwa la samaki hapa linaitwa Chato beach, wananchi wanapata chakula na pia wanauza sehemu nyingine nje ya Chato.’ Alifafanua.


Kwa upande wake Mratibu wa Programu Hiyo kutoka Ofisi ya waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Bw. Salimu Mwinjaka alisema pamoja na mambo Mengine kwa upande wa bahari kuu, Progamu hiyo inakusudia kujenga  viwanda vya samaki Tanzania Zanzibar katika eneo la Fungurefu na Wilayani Kilwa Mkoani Lindi na  kuweza kukabili hali ya upotevu wa mazao ya samaki baada ya kuvuna kwa kujenga vyumba vya ubaridi vya kuhifadhi mazao ya uvuvi, mitambo wa kuzalisha barafu, vichanja na mahema yakukaushia dagaa au samaki kwa kutumia mionzi ya jua. 


Akiongelea kuhusu ufugaji samaki, Bw. Mwinjaka alisema kupitia progamu hiyo kuna vituo vinne ambavyo vipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambavyo ni Pamoja na vituo vya kuendeleza ukuzaji viumbemaji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani Chato, Mwamapuli Wilayani Igunga, Kingolwira Wilayani Morogoro na kituo cha Ruhila Wilayani Songea.



Akiongea katika ziara hiyo, Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi Mkomanile Mahundi alisema kituo cha Kuendeleza Ukuzaji Viumbemaji Rubambagwe kitakuwa na kazi ya kuzalisha na kusambaza vifaranga bora vya samaki aina ya sato na kambale, pamoja na kutoa mafunzo kwa wakuzaji viumbemaji katika maeneo ya mikoa ya Geita, Mwanza, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Mara.


Aliongeza kusema pia, baada ya kituo kukamilika kitakuwa na uwezo wa kuchakata chakula cha samaki ambapo itapelekea wigo wa kuongeza ajira kwa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum.

“Wizara ya Mifugo na uvuvi kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) itawezesha uwepo wa dirisha maalum katika taasisi za kifedha kama vile Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa kuwawezesha wakuzaji viumbemaji kupata mkopo yenye riba nafuu ya pembejeo na zana za ukuzaji viumbemaji.” Alisem


Ujenzi wa Kituo hicho cha Rubambagwe umefikia Asilimia 85 mpaka sasa ambapo umehusisha Jengo la utawala, karakana, nyumba za wafanyakazi jengo la kitotoleshi cha samaki, ujenzi wa mabwawa ya kufugia samaki, chanzo cha maji yaani tenki maalum la kutunza maji, kuchuja na kusafirisha maji hayo kwenda kwenye mabwawa ya kufugia samaki, kitotoleshi pamoja na maeneo mengine yanayotumia maji kituoni hapo.


                                   xxxxx MWISHO xxxxxxxxx

Shirika la Masoko ya Kariakoo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) na Halmashauri ya Jiji ya Dar es Salaam wameshirikiana kuzibua mitaro ya maji taka inayozunguka Soko Kuu la Kariakoo.

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesaini hati tatu za makubaliano ya ushirikiano wa kielimu na Urusi zitakazowezesha kubadilishana wataalamu, kuendeleza tafiti za pamoja na kuongeza fursa za elimu ya juu kwa wanafunzi wa nchi hizo mbili.

Akitoa taarifa hiyo kwa Waandishi wa Habari Juni 10, 2026 jijini Dodoma Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya ziara ya kihistoria nchini humo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo imeleta mafanikio katika nyanja za elimu, sayansi na teknolojia

Waziri Mkenda ametaja makubaliano yaliyofanyika ya kwanza ni kati ya Wizara ya Elimu ya Tanzania na Wizara ya Elimu ya Urusi yanayolenga kubadilishana walimu na wataalamu, kuendesha semina za pamoja na kufundisha lugha za Kiswahili na Kirusi.

Makubaliano ya pili ambayo Wizara imeingia yamehusisha Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) na Chuo Kikuu cha RUDN, ambapo wanafunzi wa kitanzania watapata fursa ya kusoma shahada ya kwanza ya Teknolojia ya Anga kupitia mfumo wa shahada pacha, wakisoma miaka miwili Tanzania na miaka miwili nchini Urusi

“Kupitia programu hii, wanafunzi watatumia mtaala wenye viwango vya kimataifa, kusoma kwa lugha ya kingereza nchini Tanzania na kujifunza lugha ya Kirusi kabla ya kuendelea na masomo yao nchini Urusi. Hatua hii itaongeza uwezo wa taifa katika sayansi, teknolojia na uhandisi.” Amesema Waziri Mkenda

Hati ya tatu ya makubaliano kati ya DIT na Chuo Kikuu cha RUDN inalenga programu za shahada ya uzamili, ambapo wanafunzi watapata nafasi ya kusoma katika nchi zote mbili na kutunukiwa shahada zinazotambulika kimataifa, huku ushirikiano huo ukifungua milango mipya ya utafiti na ubunifu.

"Chuo Kikuu cha RUDN kimeahidi kutoa ufadhili wa masomo (scholarships) kumi kwa wanafunzi wa Kitanzania. Ufadhili huu, utawawezesha Watanzania kusoma nje ya nchi kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended DS/AI+" amesema Prof Mkenda.

Mafanikio haya yanafuatia ziara ya kihistoria ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, nchini Urusi mapema mwezi huu yakilenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kielimu kati ya Tanzania na Urusi, huku akipata heshima ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima kutoka Chuo Kikuu cha RUDN, kutambua mchango wake katika uongozi na maendeleo ya kimataifa.




Serikali imesema Bajeti Kuu ya mwaka wa fedha 2026/27 ni ya kipekee kwa kuwa ndiyo bajeti ya kwanza itakayotumika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/27–2030/31) pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025-2030.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwelekeo wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, katika Ukumbi wa Kambarage, Treasury Square jijini Dodoma, Bajeti ambayo itasomwa Bungeni Dodoma Siku ya Alhamisi, tarehe 11 juni 2026.
 
Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, Serikali inatarajia kutumia jumla ya shilingi trilioni 62.3 katika mwaka wa fedha 2026/27, ambapo sehemu kubwa ya fedha hizo itaelekezwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kimkakati inayochochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
 
“Fedha hizi zitaelekezwa katika kuendelea na ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), kuboresha mtandao wa barabara, kuimarisha huduma za maji, kuendeleza miradi ya nishati pamoja na uwekezaji katika rasilimali watu na maendeleo ya ujuzi,” alisema Mhe. Balozi Omar.
 
Aidha, alisema kuwa bajeti hiyo imeandaliwa kwa lengo la kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii, kuongeza ajira, kuvutia uwekezaji na kuimarisha ustawi wa wananchi na Serikali inatarajia kukusanya mapato ya ndani ya shilingi trilioni 46.8 ili kugharamia sehemu kubwa ya matumizi yaliyopangwa katika bajeti hiyo.
 
Mhe. Balozi Omar aliongeza kuwa, kabla ya kuwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka 2026/27, Serikali itatoa tathmini ya utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2025/26, akibainisha kuwa ukusanyaji wa mapato ya ndani umeendelea kufanya vizuri na kufikia malengo yaliyowekwa.

Aliongeza kuwa, Serikali imeendelea kushirikisha wadau mbalimbali katika mchakato wa maandalizi ya bajeti kupitia Kamati ya Wataalam wa Maboresho ya Kodi (Task Force on Tax Reforms) pamoja na Kamati ya Ushauri ya Ngazi ya Juu ya ‘Think Tank’, hatua ambayo imeongeza uwazi na ushirikishwaji katika maamuzi ya sera za kodi.
 
“Upande wa maboresho ya kodi, Serikali imepokea jumla ya mapendekezo 727 kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo sekta binafsi, taasisi za elimu, jumuiya za wafanyabiashara, mashirika yasiyo ya kiserikali na wananchi binafsi, ambapo kati ya mapendekezo hayo, 125 yalikubaliwa kama yalivyowasilishwa, 121 yalifanyiwa maboresho na kukubaliwa, huku 295 yakikataliwa baada ya kufanyiwa uchambuzi wa kina” alisema Mhe. Balozi Omar
 
Mhe Balozi Omar aliongeza kuwa, Lengo la maboresho hayo ni kukuza uchumi, kuongeza ajira, kupanua wigo wa kodi kwa kuvutia uwekezaji zaidi na wakati huo huo kupunguza mzigo wa kodi kwa walipakodi.
 
Mhe. Balozi Omar, alitumia fursa hiyo kuwapongeza waandishi wa habari kwa mchango wao mkubwa katika kuhabarisha umma kuhusu masuala ya maendeleo na kusisitiza umuhimu wa wananchi kuendelea kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati.
 
“Tunajenga Taifa letu kwa pamoja. Serikali itaendelea kuhakikisha fedha zinazokusanywa zinatumika kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya kwa wananchi,” alisema Mhe. Balozi Omar.

Alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania kufuatilia kwa makini uwasilishaji rasmi wa Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/27 utakaofanyika Bungeni jijini Dodoma Juni 11, 2026, akisema bajeti hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia matarajio ya wananchi na mahitaji ya maendeleo ya taifa.
Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt Maulid J. Maulid leo umefungua Mafunzo ya Uongozi wa Kimkakati (Strategic Leadership) kwa viongozi wa shule za sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, yakiwakutanisha washiriki 44 wakiwemo Wakuu wa Shule za Sekondari 22 na Makamu Wakuu wa Shule 22. 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Mwigulu Nchemba akimsikiliza Mbunge wa jimbo la Kilindi Mhe.Salehe Mbwana Mhando leo Jumatano Juni 10,2026 bungeni jijini Dodoma.




 

Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kipo katika mchakato wa kupitia na kuhuisha mitaala tisa ya masomo ili iendane na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 (Toleo la 2023), pamoja na mahitaji ya sasa ya soko la ajira nchini.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina (kushoto) Kamishna wa Kazi, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Suzan Mkangwa (kulia) na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda (katikati) wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Bw. Gilbert Houngbo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tempus, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tarehe 9 Juni, 2026, Geneva, Uswizi.

Na: OWM (KAM) - Geneva, Uswizi

Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeungana na mataifa mengine katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika tarehe 9 Juni, 2026 katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Geneva, Uswisi.

Aidha, ujumbe huo wa Tanzania uliongozwa na Kamishna wa Kazi, Suzan Mkangwa ambaye aliambatana na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi Zanzibar, Rashid Khamis Othman, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Wataalamu na Wawakilishi wa Waajiri (ATE) pamoja na Wawakilishi kutoka Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA).

Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), Gilbert F. Houngbo ametoa wito kwa jamii ya Kimataifa na Wadau wa Utatu kutekeleza kwa vitendo Mipango na Maadhimio ya Mkutano wa Marrakesh uliofanyika nchini Morocco, Februari 2026 kwa lengo la kupinga utumikishwaji wa Mtoto.

Vilevile, alisisitiza juu ya jitihada za makusudi zinazotakiwa kuchukuliwa na nchi wanachama wa ILO, katika kukuza kazi za staha na utekelezaji wa sera ya elimu bure.

Kwa upande wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kudhihirisha mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya kazi na ajira, hasa hatua madhubuti zilizochukuliwa katika kutokomeza ajira za watoto nchini ni kama zifuatazo:- Utekelezaji wa Mradi wa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Brazil kwa kushirikiana na ILO mradi huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa elimu kuhusu utumikishwaji wa mtoto na madhara yake.

Pia, kuhuishwa kwa Mkakati wa Taifa wa Kutokomeza Utumikishwaji wa Mtoto 2024/25–2028/29, unaolenga kuunganisha nguvu za wadau wote wa maendeleo, mashirika ya kiraia na jamii kwa ujumla. Kadhalika, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya Haki Kazini kupitia Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA). Vyombo hivi vimekuwa vikitimiza vyema wajibu wake wa kutafsiri sheria na kutoa haki, hususani ulinzi kwa mtoto; Kuadhimisha Siku ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto Kitaifa kila tarehe 12 Juni. Wadau kutoka Tanzania Bara na Zanzibar hushiriki na kupokea mikakati ya Serikali ya kukabiliana na tatizo hili; pamoja na Kutoa elimu kwa Umma kwa kuwa utumikishwaji wa mtoto ni jukumu la jamii nzima, hivyo ushirikiano baina ya Wizara, wadau wa maendeleo, kaya, na kila mwananchi unahitajika ili kufafanua tafsiri ya utumikishwaji wa mtoto, kazi za shuruti, na kazi hatarishi kwa afya na maendeleo ya mtoto.

Siku ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto uadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Juni na Shirika la Kazi Duniani (ILO) pamoja na nchi wanachama kwa lengo la kuhamasisha nguvu ya pamoja baina ya Serikali, Vyama vya Waajiri, na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi katika kukuza ajira zenye staha na kutokomeza utumikishwaji wa watoto unaowanyima fursa za kijamii, hususan haki ya elimu.

Maadhimisho hayo kwa mwaka huu 2026 yataongozwa na Kaulimbiu isemayo: “Red Card to Child Labour” ikimaanisha wito kwa wadau wote wa maendeleo kutoonesha uvumilivu wowote kwa vitendo vinavyochochea au kusababisha utumikishwaji wa mtoto katika sekta zote za kijamii na kiuchumi.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina (kushoto) Kamishna wa Kazi, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Suzan Mkangwa (kulia) na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda (katikati) wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Bw. Gilbert Houngbo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tempus, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tarehe 9 Juni, 2026, Geneva, Uswizi.

Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Bw. Gilbert Houngbo akihutubia wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tempus, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tarehe 9 Juni, 2026, Geneva, Uswizi.

Kwa miaka mingi, nilifanya kazi yangu kwa moyo wote. Nilifika kazini mapema, nilitimiza majukumu yangu kwa umakini, na nilijitahidi kuhakikisha kila kazi niliyopewa inakamilika kwa wakati. Niliamini kwamba bidii yangu ingetambuliwa siku moja. SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO HAPA.

Lakini miaka ilipita bila mabadiliko yoyote.
Wafanyakazi wengine walikuwa wakipandishwa vyeo au kuongezewa mishahara, huku mimi nikiendelea kufanya kazi kwa kiwango kilekile cha mshahara.

Kila mwisho wa mwezi nilijitahidi kulipa bili na kuhudumia familia yangu, lakini hali ya maisha iliendelea kuwa ngumu.
Kwa kweli iliniumiza sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua nilikuwa nikitoa mchango mkubwa kazini. Mara nyingi nilifanya kazi za ziada na kusaidia pale ambapo wengine walishindwa, lakini juhudi zangu zilionekana kama hazionekani kabisa.
Kadri muda ulivyopita, nilianza kupoteza hamasa.

Kulikuwa na siku nilijiuliza kama kulikuwa na umuhimu wa kuendelea kujituma kiasi kile. Wakati mwingine nilifikiria kutafuta kazi nyingine, lakini sikuwa na uhakika kama ningepata fursa bora zaidi.
Hakuna maumivu makubwa kwa mzazi kama kuona mtoto wake akiwa karibu naye, lakini mioyo yenu ikiwa mbali sana. Hicho ndicho nilichokuwa napitia na mwanangu kwa miaka kadhaa. SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO.

Tulikuwa tunaishi nyumba moja, tulionana kila siku, lakini hatukuwa tunazungumza kama baba na mwana.

Kila mmoja alikuwa akiendelea na maisha yake kana kwamba mwenzake hayupo. Kilichoanza kama kutokuelewana kidogo kilikua na kuwa ukimya mkubwa uliotutenganisha. 

Mwanzoni niliamini hali ile ingepita yenyewe. Nilidhani baada ya siku chache angerudi na kuzungumza nami kama zamani.

Lakini siku zikageuka wiki, wiki zikageuka miezi, na hatimaye miaka ikaanza kupita bila mabadiliko yoyote. Kwa kweli hali ile ilinivunja moyo. 

Kila nilipomwona akizungumza kwa furaha na watu wengine huku akinikwepa mimi, nilihisi maumivu makubwa ndani yangu.

Wakati mwingine nilitaka kumuita na kuanzisha mazungumzo, lakini kiburi, hasira, na maumivu ya yaliyopita yalikuwa yamejenga ukuta kati yetu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona familia yetu ikikosa furaha tuliyokuwa nayo zamani.

Kulikuwa na nyakati nilijiuliza kama tungewahi kuwa karibu tena.

Kwa miaka mingi, ndoto yangu kubwa ilikuwa kuwa mzazi. Nilipofunga ndoa, niliamini kwamba ndani ya muda mfupi ningekuwa nikiwabeba watoto wangu mikononi mwangu. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. SOMA ZAIDI/TAZAMA VIDEO.

Miezi iligeuka miaka bila kupata ujauzito.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kupata maswali kutoka kwa ndugu, marafiki, na hata majirani. Kila mtu alitaka kujua ni lini ningepata mtoto. 

Ingawa walikuwa na nia njema, maswali hayo yalikuwa yananiumiza moyo. Nilitafuta msaada wa kitabibu na kufanya vipimo mbalimbali.

Baadhi ya majibu niliyopata yalinitia hofu. Niliambiwa kwamba nafasi yangu ya kupata mtoto ilikuwa ndogo kuliko nilivyokuwa nikitarajia. Kusikia maneno hayo kulinifanya nilie kwa siku nyingi. Kwa kweli nilikata tamaa.

Kulikuwa na nyakati nilihisi kama ndoto yangu ya kuwa mzazi ilikuwa ikinitoroka.

Kila nilipoona familia zikiwa na watoto wao, nilitamani siku moja ningepata furaha hiyo pia.
Licha ya maumivu hayo, sikuacha kuamini.