Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA, Mha. Ngosi Mwihava (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Ndg. Gerald Maganga (Kulia) wakimkabidhi Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mfano wa hundi kama ishara ya kukabidhi Hazina mchango wa kisheria wa taasisi hiyo wa Sh. 10.6 bilioni, kwa mwaka wa Fedha 2025/26, kwenye hafla iliyofanyika Ikulu jana.

 

 


● Yaligunduliwa kwa mara ya kwanza duniani mwaka 1959 katika Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma.

● Yana thamani kubwa katika elimu, utafiti wa kisayansi na utalii wa jiolojia.

● Ni sehemu ya urithi wa asili wa Tanzania.


Imeelezwa kuwa kuna umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti za kuhifadhi na kulinda madini adimu aina ya Yoderite yanayopatikana katika eneo la Mlima wa Mautia, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, ili kuhakikisha urithi huo wa kipekee wa kijiolojia unabaki salama kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Hayo yalisemwa Juni 30, 2026 na Meneja wa Jiolojia kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Solomon Maswi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea eneo hilo kwa ziara maalumu.

Maswi alisema kuwa uhifadhi wa Yoderite unaweza kuiwezesha Tanzania kuwa kitovu cha kimataifa cha tafiti kuhusu madini adimu, sambamba na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea maeneo yenye urithi wa jiolojia.

Aliongeza kuwa Yoderite ni miongoni mwa madini adimu yanayoifanya Tanzania kutambulika duniani kutokana na historia yake ya kugunduliwa kwa mara ya kwanza katika Mlima wa Mautia.

Aidha, alifafanua kuwa madini hayo yana mchango mkubwa katika tafiti za kisayansi kwa kusaidia kuelewa mchakato wa uundaji wa miamba na mazingira yenye shinikizo na joto la juu ndani ya ganda la dunia. Pia yana umuhimu mkubwa katika elimu ya jiolojia, maendeleo ya utalii wa jiolojia na uhifadhi wa urithi wa asili duniani.

Maswi alibainisha kuwa, kutokana na uchache wake na kupatikana katika maeneo machache sana duniani, madini ya Yoderite hayachimbwi kwa matumizi ya viwandani wala biashara. Badala yake, yanahifadhiwa kama urithi wa kipekee wa kijiolojia unaovutia watafiti, wanafunzi, wataalamu wa sayansi na watalii kutoka ndani na nje ya nchi. Hali hiyo inaipa Tanzania fursa ya kujijengea hadhi kama kitovu cha tafiti za kimataifa na utalii wa jiolojia unaotegemea urithi wa asili.

Taasisi za utafiti wa madini na vyuo vya Madini vimeshauriwa kutumia eneo hilo kwa mafunzo endelevu ya utafiti wa madini.

Madini ya Yoderite yaligunduliwa kwa mara ya kwanza duniani mwaka 1959 katika Milima ya Mautia, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma.

Kutokana na kuendelea kwa tafiti baada ya miaka 35 watafiti wa miamba na madini walifanikiwa kugundua aina hiyo ya madini nchini Zimbambwe.

Jina la Yoderite lilipewa kwa heshima ya mwanajiolojia mashuhuri wa Marekani, Hatten Yoder Jr., kutokana na mchango wake mkubwa katika tafiti za miamba na madini.







Nilipokuwa mdogo, nilikuwa na ndoto ya kuolewa na mwanamume mwenye huruma, anayejali, anayesikiliza na kunipa heshima kama mke.

Lakini kadri nilivyokua, niliingia kwenye uhusiano ambao ulivunja kabisa ndoto zangu. Nikiwa na umri wa miaka 23, nilipenda kwa moyo wangu wote, nikajitoa kwa mwanaume ambaye nilidhani ni mpenzi wa maisha yangu.

Tulikaa naye kwa miaka miwili, lakini kwa kipindi chote hicho nilijikuta nikilia kila siku.
Alininyima mapenzi ya kweli si tu kimwili bali hata kwa maneno. 

Hakuwa akinipa muda, hakuwahi kunipa sifa wala heshima, na mara nyingi aliniongelea vibaya mbele ya watu.

Nilivumilia kwa sababu nilidhani labda siku moja atabadilika. Lakini siku zilisonga, na mateso yakawa kawaida yangu. 

Nilijiona sifai, sina thamani, na sikustahili kupendwa. Wakati mwingine nilikuwa nikilala nikiwa nimejifunika na mto ili watoto wasisikie nikilia. Nilikuwa naumia sana, hasa kwa sababu sikuwahi kumkosea. SOMA ZAIDI.
Siku hiyo nilikuwa peke yangu nyumbani. Ilikuwa siku ya Jumamosi saa mbili usiku, nilikuwa nimekamilisha kazi za siku na nikajipumzisha kwenye kochi langu la sebuleni. 

Kama ilivyo kawaida yangu, nikachukua simu yangu kupiga picha ya selfie kwa ajili ya kupakia kwenye WhatsApp status.

Nilitabasamu kidogo na kupiga picha moja tu, halafu nikaangalia matokeo yake kabla sijaiweka hadharani. 

Ndipo nikaona jambo la kushangaza ambalo lilinifanya nitetemeke ghafla. Kwenye picha hiyo, nyuma yangu, kulionekana watu watatu wakiwa wamesimama karibu na mlango wa chumba cha kulala.

Wote walionekana ni marefu na walikuwa wamevaa mavazi meusi, lakini cha kutisha zaidi ni kwamba nyuso zao zilikuwa zimefunikwa kwa kitambaa cheusi kama mazishi. 

Hakukuwa na mtu mwingine nyumbani, milango yote ya chumba na nyumba ilikuwa imefungwa, na mimi mwenyewe nilikuwa nimehakikisha hilo kabla sijapiga selfie.

Moyo wangu ulianza kwenda mbio. Nilitetemeka mikono, nikahisi baridi kali ghafla licha ya kuwa ilikuwa jioni ya joto. 

Niliinuka taratibu, nikawasha taa zote za nyumba, nikafungua mlango wa nje na kutoka nje kwa haraka. Nilikaa kwa muda mrefu nje nikiwa sijaelewa kilichokuwa kimetokea.SOMA ZAIDI.
Niliwahi kuamini kuwa ndoa yetu ilikuwa imejengwa juu ya misingi ya upendo wa kweli. Tulikutana tukiwa chuoni, tukapendana kwa dhati, na baada ya miaka miwili ya uhusiano, tuliamua kuoana. Harusi yetu ilikuwa ya kupendeza sana, tulipendeza mbele ya watu, na kila mtu alitupongeza.

Lakini ndani ya miezi sita tu baada ya harusi, maisha yangu yakabadilika ghafla. Mke wangu alianza kuwa mtu tofauti kabisa na yule niliyempenda. 

Alianza kuwa mkali, mgumu kuelewana naye, na mara kwa mara alinituhumu kwa mambo ambayo hayakuwa ya kweli.

Mara nyingi alirudi nyumbani akiwa mlevi au aliingia chumbani akiwa mnyamavu kana kwamba hakutaka hata kuzungumza nami. Ilifikia hatua hata kula pamoja ilikuwa shida. Nilihisi kuna kitu kibaya, lakini sikuweza kukieleza.

Kilichonitatiza zaidi ni ndoto ambazo nilianza kupata nilikuwa naota moto, maiti, na mara nyingine nilimuona mke wangu akiwa na wanaume wengine. 

Hali hiyo ilinizidi nguvu. Nilipojaribu kuzungumza naye kuhusu hali yetu, alikasirika na kusema sina imani naye.

Niliendelea kuvumilia kwa matumaini kuwa labda ni msimu mgumu tu wa maisha ya ndoa, lakini hali ilizidi kuwa mbaya. 

Siku moja nilipokwenda kijijini kumtembelea babu yangu, nilikutana na mzee mmoja ambaye ni jirani yao. Baada ya kuzungumza naye kwa muda, aliniuliza maswali ya kushangaza kuhusu maisha yangu ya ndoa. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu familia yetu ilikuwa ikikumbwa na misukosuko isiyoelezeka. Kila aliyekuwa anafanikiwa kwao ghafla alianza kudorora. 

Watoto walifukuzwa shule kwa sababu zisizoeleweka, biashara za kaka zangu zilikufa ghafla, na hata afya ya mama yetu ilianza kuzorota pasipo ugonjwa halisi kujulikana.

Tulisali, tulifunga, lakini hali ilizidi kuwa mbaya.
Kila mtu alikuwa anahisi hali hiyo si ya kawaida. Hata wageni waliokuja nyumbani walihisi hali ya baridi na uzito wa ajabu mara tu walipoingia mlangoni. 

Mmoja wa marafiki wa karibu wa familia yetu alituambia wazi kuwa huenda kuna mtu ametuloga au ametutendea jambo la kichawi.

Nilikuwa miongoni mwa watu ambao zamani nilikuwa siamini mambo haya lakini kilichokuwa kinaendelea kilinifanya nibadili msimamo wangu. Kwa mara ya kwanza, niliamua kutafuta msaada wa kitaalamu wa asili. SOMA ZAIDI.
Hakuna kitu kilichokuwa kinaniumiza kama mume wangu kuonyesha dalili za kutojali mara baada ya kujifungua mtoto wa pili wa kike. 

Nilihisi kama sipendwi tena, hata kama hakuwahi kusema wazi. Alianza kuchelewa kurudi nyumbani, alikosa furaha nyumbani, na kila mara alipokuwa akizungumza na marafiki zake, alitaja jinsi anavyotamani kuwa na mtoto wa kiume.

Nilijaribu kulazimisha mazungumzo naye kuhusu hali hiyo, lakini alinijibu kwa maneno ya baridi, “Watoto wote ni baraka.” 

Ndiyo, nilielewa hilo, lakini moyo wa mwanamke unajua ukweli wa mambo. Nilijikuta nikianza kuishi kwa hofu na mashaka. Nilianza kujiona duni. Nilijiuliza kama ndoa yangu ingesalia imara bila kumpatia mtoto wa kiume.

Nilianza kusaka suluhisho kila mahali kwa madaktari wa kawaida, mitandaoni, na hata kupitia marafiki wa karibu. Lakini kila nilichopewa kilikuwa ushauri wa jumla tu. Hakuna kilichokuwa na uhakika.SOMA ZAIDI.
Wizara ya Afya imewataka waandishi wa habari na wadau wa mitandao ya kijamii kuendelea kutoa taarifa sahihi, kwa wakati na kutoka katika vyanzo rasmi ili kuimarisha uelewa wa wananchi na kuimarisha utayari wa taifa dhidi ya ugonjwa wa Ebola na dharura nyingine za afya ya umma.



Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amezindua rasmi Mfuko wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika Jimbo la Mtwara Mjini (UWEZO Program) na kusema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za uwezeshaji wa wanawake.

Akizungumza katika hafla hiyo Juni 30, 2026, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila kuyawezeaha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana.

Amesema ushiriki wa makundi maalum katika shughuli za kiuchumi ni hatua ya kujivunia na kuongeza kuwa mafanikio yatapatikana kwa makundi hayo kupatiwa mafunzo stahiki.

"Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila wananchi wake kuwa na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na hii ndiyo sababu kuwndelea kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake na vijana kupata fursa za kiuchumi kupitia sera na programu mbalimbali," alisema Naibu Waziri Mahundi.


Aidha, ameeleza kuvutiwa kwake na  Programu ya UWEZO kwa kuanza kutoa mikopo na kuwajengea wanawake uwezo kupitia mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, utunzaji wa kumbukumbu za biashara na uundaji wa vikundi, akieleza kuwa msingi huo utasaidia kuhakikisha mikopo inazalisha matokeo chanya na kuongeza maendeleo ya wanawake pamoja na familia zao.

Awali akitoa maelezo kuhusu Programu ya UWEZO, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, amesema wazo la kuanzisha mfuko huo limetokana na ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ya kuwawezesha wananchi kiuchumi. 

Amesema kupitia mfuko huo wenye mtaji wa shilingi milioni 150, wanawake zaidi ya 5,000 walitambuliwa kutoka kata zote 18 za jimbo hilo, wanawake 300 walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali na wanawake 81 wamekabidhiwa mikopo katika awamu ya kwanza.

"Mikopo hiii haina riba kutokana na ushirikiano kati ya Joel Nanauka Foundation na Benki ya Ushirika (Coop Bank), sababu lengo la programu hii si kutoa fedha pekee bali kujenga wanawake wajasiriamali wenye uwezo wa kujitegemea, kuongeza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Mtwara Mjini na Taifa kwa ujumla". alisema 
Waziri Nanauka.

Nao baadhi ya wanufaika wa Mkopo huo wameipongeza Serikali na kumpongeza Waziri Nanauka kwa maono na kutekeleza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni zake ambapo kwa sasa wataweza kujiendesha kiuchumi na kupunguza makali ya ugumu wa maisha na kuingizia taifa mapato. 








Habari njema kwa watumiaji wa mafuta nchini. Kuanzia Jumatano, tarehe 01 Julai 2026, bei kikomo za bidhaa za petroli zimeshuka kutokana na kupungua kwa bei za mafuta katika soko la dunia.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, imesema kutokana na kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia, bei za mafuta katika soko la hapa nchini zinashuka kwa Shilingi 96 kwa lita ya petroli, Shilingi 151 kwa lita ya dizeli na Shilingi 242 kwa lita ya mafuta ya taa.  

Kushuka huku kunatokana na mabadiliko katika soko la dunia, ikiwemo makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Marekani na Iran kuhusu vita inayoendelea eneo la Mashariki ya Kati, pamoja na kuruhusu meli za mafuta kupita katika Mlango Bahari wa Hormuz. Hatua hizo zimechangia kupunguza ugumu katika usafirishaji na upatikanaji wa mafuta duniani.

Hata hivyo, wastani wa bei katika soko la dunia bado haujarejea katika kiwango kilichokuwepo kabla ya kuanza kwa vita hiyo tarehe 28 Februari 2026.

Serikali imeahidi kuendelea kufanya mageuzi ya sera, sheria, kanuni na mifumo ya utoaji huduma ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, hatua inayolenga kuiwezesha sekta binafsi kuwa injini ya ukuaji wa uchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Rais wa Jamhuri ya Muungwana wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan (katikati)akikabidhiwa gawio la Sh.bilioni 15 kutoka kwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Tiper Balozi Mathias Chikawe(kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Tiper  Mohamed Mohamed (kulia) wakati wa hafla ya Siku ya Gawio iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam ambapo mashirika na taasisi mbalimbali ambazo Serikali inahisa wamekabidhi gawio serikalini.

 


. _Amshukuru Rais Samia kwa kuwezesha upatikanaji wa magari hayo_


. _Ataka magari hayo yasaidie kukuza utalii na ufuatiliaji wa mapato_

. _Aelekeza Halmashauri kushirikiana na TAWA, TANAPA na wadau wa utalii kukuza utalii_


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumanne Juni 30, 2026 amekabidhi magari mawili ya usimamizi na ufuatiliaji wa Utalii na mapato kwa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha upatikanaji wa magari hayo mawili yenye jumla ya thamani ya Shilingi 440,611,400.

Mhe. Makalla amekabidhi magari hayo wakati wa ziara yake Wilayani Monduli, akiagiza matumizi sahihi na yaliyokusudiwa kwa magari hayo ikiwa ni pamoja na kusaidia katika kukuza utalii Wilayani Monduli pamoja na ufuatiliaji na ukusanyaji wa mapato ya serikali.

Katika hatua nyingine, Mhe. Makalla akisisitiza kuhusu ukuzaji wa utalii Mkoani Arusha, ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Monduli kushirikiana na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na wadau wengine wa utalii katika kukuza utalii Wilayani Monduli sambamba na kuhifadhi vivutio vya utalii vilivyopo Wilayani Monduli.

Magari yaliyokabidhiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser Hardtop (5 door) likiwa na gharama ya Shilingi 235, 606,600 na Toyota Land Cruiser (Pick up) likiwa na gharama ya Shilingi 205, 004,800 pamoja na pikipiki aina ya Yamaha YBR iliyotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii, vyote kwa pamoja vikitajwa kuongeza chachu ya ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2026/27 na kuhakikisha doria za maliasili zinafanyika kikamilifu.

Awali katika maelezo yake Afisa mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bw. Jeofrey Mwambasi amemshukuru Rais Samia na Uongozi wa Halmashauri hiyo kwa kuwezesha kupatikana kwa magari hayo, akiahidi kuwa Halmashauri hiyo itayatunza magari na pikipiki hiyo pamoja na kuhakikisha yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na serikali katika ukusanyaji wa mapato pamoja na uhifadhi.






 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema ameridhishwa na kiwango cha utekelezaji wa maelekezo yake ya Januari, 2026 ya kutaka kukamilishwa kwa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro ifikapo Julai 26, 2026. 

Prof. Shemdoe amesema hayo Juni 29, 2026 mjini Morogoro, wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani humo ambayo ni sehemu ya muendelezo ufuatiliaji wa utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa ya ukamilishaji wa miradi ya mbalimbali ya maendeleo, yakiwepo ya utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. 

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa nimepata faraja kuona maendeleo ya ujenzi wa jengo hili lilofikia asilimia 90, Mhe. Mkuu wa Mkoa nikupongeze kwa ufuatiliaji na RAS kwa usimamizi wako mzuri,” ameeleza Prof. Shemdoe.

Kutokana na hatua nzuri ya ujenzi iliyofikiwa, Prof. Shemdoe amemtaka  Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Musa, kuhakikisha watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wanahamia katika jengo jipya la ofisi hiyo ndani ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2026/27. 

Aidha, Prof. Shemdoe amemsisitiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Musa kuhakikisha lifti inaletwa na kuwekwa kwa wakati, ikiwa ni pamoja na kufanya maandalizi ya kupata samani mpya zitakazotumiwa na watumishi wa ofisi hiyo. 

Kufuatia uwekezaji uliofanywa, Prof. Shemdoe amesema kwamba jengo hilo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa likikamilika, litakuwa limetumia bilioni 6.5 hivyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji huo mkubwa aliofanya kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa mkoa wa Morogoro.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema atasimamia utekelezaji wa maelekezo ya Prof. Shemdoe na kufafanua kuwa maelekezo hayo yanapaswa kutekelezwa na ofisi yake kabla ya tarehe 30 Septemba 2026 saa sita usiku na si ifikapo Septemba 30, 2026.

Jengo hilo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro linajengwa na Mkandarasi MCB Company LTD, Mbeya University of Science and Technology kwa usimamizi wa Mshauri Elekezi ambaye ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).











 


Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini.

Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini.

Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini ili Tanzania kuwa kitovu za usambazaji wa bidhaa hiyo barani Afrika.

“Lengo letu ni kuona wachimbaji wakubwa na wadogo hapa nchini wanapata bidhaa nyingi za kuzalisha madini pasipo kutegemea uagizwaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi," amesema Mavunde.

Naye, Mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Oriental Casting and Forging Ltd Bw. Hou Songcun amesema Kampuni yake ipo tayari kufanya uwekezaji mkubwa wa bidhaa za migodini nchini kwa kuwa Tanzania ni nchi ambayo ina mazingira mazuri ya uwekezaji na kwamba sekta ya madini inakua kwa kasi kubwa sana hivyo ni sehemu salama na rafiki ya kufanya uwekezaji ambao utakuwa suluhisho la upatikanaji wa bidhaa za migodini kwa urahisi zaidi.









Nilikuwa nimekata tamaa kabisa baada ya kukosa visa mara tatu mfululizo. Mara ya kwanza nilikataliwa kwa makosa madogo tu ya kiufundi, mara ya pili nikaambiwa sifai kifedha na mara ya tatu hata sikupewa nafasi ya mahojiano. Ilikuwa aibu kwa familia yangu na marafiki wangu.

Wengine walianza kuniambia niache kufikiria kwenda nje ya nchi kwa sababu labda haikuwa riziki yangu. Lakini ndoto yangu ya kuishi na kufanya kazi nje ya nchi ilikuwa kubwa kuliko maneno ya watu. Kila kukataliwa kuliniumiza moyo. Nilianza kupata msongo wa mawazo na hata kukosa usingizi.

Nilihisi kuna kitu kisicho cha kawaida kilichokuwa kinanizuia. Nilianza kuamini labda kuna watu walionionea wivu na kunifungia njia. Nilijaribu mara ya nne kuandaa nyaraka lakini nilihisi hofu na woga mkubwa. SOMA ZAIDI.
Nilipata kazi yangu ya ndoto baada ya kungoja kwa muda mrefu. Nilijua itakuwa nafasi ya kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Hata hivyo, mambo hayakuenda vile nilivyotarajia. Baada ya miezi michache nilianza kugundua bosi wangu hakuwa akinipenda.

Alionekana kunionea wivu kwa jinsi nilivyokuwa nafanya kazi vizuri na nilipata sifa kutoka kwa wafanyakazi wenzangu. Kila mradi nilipewa nilifanya kwa bidii, lakini kila mara alitafuta kosa dogo la kunilaumu mbele ya wenzangu.

Aliniweka kwenye shinikizo kubwa na aliniandikia barua ya onyo mara mbili kwa sababu ambazo hazikuwa na msingi. Nilihisi kama alitaka niachishwe kazi. Wafanyakazi wenzangu walinionea huruma lakini hakuna aliyethubutu kumkabili.

Nilianza kupoteza amani ya moyo. Kila asubuhi nilipokuwa nikiamka nilihisi kuchoka hata kabla ya kuingia ofisini. Niliwaza kuacha kazi lakini nilijua singeweza kumudu maisha bila kipato. Nilihitaji njia ya kubadilisha hali hii. SOMA ZAIDI.
Kila mtu katika familia yangu alijua kuna tatizo kubwa lakini hakuna aliyekuwa tayari kukubali. Kila siku ilianza na mabishano na ilimalizika kwa kelele. 

Baba na mama walikuwa wanagombana kwa sababu ndogo ndogo, watoto tulijikuta tukipigana wenyewe kwa sababu ya msongo.

Wageni walipoingia nyumbani waliona sura za hasira na kukaa kwetu pamoja mezani kuligeuka uwanja wa vita. 

Siku moja jirani alinieleza kuwa nyumbani kwetu kelele za matusi na ugomvi zilisikika hadi kwao. Nilijisikia aibu sana. Nilijua hali ile haikuwa ya kawaida.

Nilipojaribu kuzungumza na baba yangu hakutaka kunisikiliza. Mama alionekana amekata tamaa na ndugu zangu walikimbilia marafiki zao kila jioni ili wasikae nyumbani. 

Ilifika hatua nilihisi kama familia yetu ilivunjika. Nilipoona hali inazidi kuwa mbaya niliamua kutafuta suluhisho kwa siri.

Nilikuwa tayari kufanya lolote ilimradi amani irudi.SOMA ZAIDI.

Nilizaliwa katika familia iliyokumbwa na changamoto nyingi. Baba na mama walikuwa wakigombana mara kwa mara, na hata nilipokuwa mtu mzima, nilijikuta pia nikipitia matatizo kama hayo. 

Kila mara nilipojaribu kuanza biashara, iliniporomoka bila sababu ya kueleweka. Nilipoanzisha mahusiano, mara nyingi yalikuwa yakivunjika katikati ya furaha.

Watu wengi walinipa ushauri tofauti, wengine wakisema labda nilikuwa nimekumbwa na nuksi. Nilihisi nimeelemewa sana na niliamini labda maisha yangu yalikuwa yameandikwa kuwa ya mateso. Wengi walisema uchawi ni hatari, kwamba mtu akikimbilia huko anajiletea matatizo zaidi.

Kwa muda mrefu niliepuka hata kusikia neno hilo. Lakini nilipofikia hatua ya kukata tamaa kabisa, nilianza kutafuta njia mbadala. SOMA ZAIDI.