Kuanzisha kiwanda kidogo cha kusaga nafaka na kuzalisha unga ilikuwa hatua kubwa sana kwangu. Niloweka mitambo ya kisasa na kuajiri vijana wenye ujuzi ili kuhakikisha kazi inaenda vizuri.

Hata hivyo, miezi michache baada ya kuanza, nilikumbana na mtihani mzito uliotishia kufunga biashara yangu na kuniazima deni kubwa la benki.

Kila wiki, mashine zilikuwa zinaharibika bila sababu yoyote ya msingi. Mara mota ziungue, mara vipuri vikatike, au mifumo ya umeme ivurugike kabisa. Mafundi walikuja na kubadilisha vifaa vipya, lakini baada ya siku mbili au tatu, mtambo ule ule unajifunga tena.

Nilikuwa nikipoteza mamilioni ya fedha kwa ajili ya matengenezo na kununua vipuri, huku wateja wangu wakiondoka kwa kukosa bidhaa kwa wakati. Nilikuwa naingia hasara kila kukicha, na amani ya moyo ilitoweka kabisa. SOMA ZAIDI.
Kupotelewa na mtu unayempenda ni jeraha linalovuja damu kila siku bila kupona. Kaka yangu mkubwa, ambaye alikuwa tegemeo na kiongozi wa familia yetu, aliondoka nyumbani kwenda mijini kutafuta maisha miaka 18 iliyopita.

Tangu siku hiyo, hakurudi, na mawasiliano yalikatika kabisa. Tulimtafuta kila kona hospitalini, vituo vya polisi, na hata kwenye vyombo vya habari lakini hatukupata hata chembe ya matumaini.

​Mama yetu alizeeka kwa majonzi, kila kukicha akilia na kutazama mlangoni akihisi labda mwanaye angerudi. Miaka 18 ya upweke, sintofahamu, na simanzi ilianza kutufanya tuamini kuwa labda kaka yetu hayuko hai tena duniani. Furaha ilitoweka kabisa kwenye familia yetu. SOMA ZAIDI.
Siku niliyofukuzwa kazi itabaki kuwa moja ya siku zenye maumivu makubwa maishani mwangu. Nikiwa kama mfanyakazi mwaminifu niliyependa majukumu yangu, nilishitukizwa kwa tuhuma nzito za uongo za ubadhirifu wa fedha za kampuni.

Licha ya kujitetea kwa nguvu zote na kuonyesha ushahidi, uongozi ulikataa kunisikiliza na kunifukuza kazi mara moja bila hata kiinua mgongo.

​Maisha yalibadilika ghafla kuwa magumu mno. Ndani ya miezi sita, nilishindwa kulipa kodi ya nyumba, nikashindwa kuhudumia familia yangu, na marafiki niliokuwa nao kazini walinitenga wakiniogopa kama mhalifu.

Msongo wa mawazo ulinisonga sana nikijua sifa yangu ya miaka mingi imechafuka kwa uongo uliotengenezwa na maadui zangu wa kazini waliokuwa wakionea wivu mafanikio yangu. SOMA ZAIDI.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, akizungumza na wadau mbalimbali wa mazingira kabla ya kushiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yaliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.

 



•Prof. Shemdoe atoa wito kwa sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za watumishi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wananchi wa mvomero la kujengewa shule mbili za Sekondari katika Halmashauri ya Mvomero, ombi ambalo liliwasilishwa kwa niaba yao na Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe. Sara Msafiri pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro Mhe. Josephine Kapoma wakilenga kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji katika Halmashauri hiyo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 18, 2026 katika kijiji cha Mkindo, kata ya Mkindo, Halmashauri ya Mvomero Mkoa wa Morogoro, mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Mkindo, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma mkoani Morogoro.

"Mhe. Sara Msafiri akishirikiana na pacha wake Mhe. Josephine Kapoma waliniomba tujenge shule nne, nilipokea ombi hilo na kuliwasilisha kwa Mhe. Waziri Mkuu naye akaliwasilisha kwa Mhe. Rais ambaye ameridhia ombi hilo kwa kutoa Shilingi Bilioni 1.1 za kujenga shule mbili, na tayari fedha hizo zimeshaingizwa kwenye akaunti ya Halmashauri," amesema Prof. Shemdoe.

Katika kuhakikisha wananchi waliopo kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa wananufaika na shule hizo, Prof. Shemdoe ameelekeza zijengwe kwenye kata ya Dakawa na Mzumbe kama alivyoomba Mbunge wa Jimbo la hilo la Mvomero, Mhe. Msafiri, huku akitoa wito kwa sekta binafsi kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za walimu nchini.

Aidha, Prof. Shemdoe amesema kabla ya kufika shuleni hapo amekagua, ameweka jiwe la msingi na kuzindua huduma ya upasuaji katika jengo jipya la upasuaji la Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero lenye vifaa tiba vya kisasa, hatua itakayowawezesha wakazi wapatao 459,304 wa wilaya ya Mvomero na maeneo jirani kuwa na uhakika wa kupata huduma ya upasuaji katika hospitali hiyo.

Katika hatua ya kuboresha miundombinu ya elimu Mvomero, Prof. Shemdoe amesema pia ametembelea na kuzindua vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Miembeni yenye thamani ya Shilingi Milioni 115 ambayo imejengwa katika kijiji cha Mvomero, kata ya Mvomero wilayani Mvomero.

“Na sasa nipo hapa na nimeshiriki nanyi katika kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Mkindo katika kijiji hiki cha Mkindo kilichopo kata ya Mkindo, shule ambayo imejengwa baada ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa Shilingi Milioni 528 za ujenzi wa shule hii,” ameeleza Prof. Shemdoe.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Mhe.  Sara Msafiri, amemuomba Prof. Shemdoe kufikisha salamu za shukrani za wananchi wa Mvomero kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha ujenzi wa shule ya Sekondari ya Sayansi Mkindo, akisema shule hiyo itazalisha madaktari, wahandisi pamoja na walimu wa masomo ya sayansi.

Naye, Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Josephine Kapoma, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi wa miundombinu ya elimu katika maeneo ya vijijini hususani kwenye kijiji hicho cha Mkindo.

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeridhishwa na hatua, ubunifu na kasi ya mageuzi yanayotekelezwa na Gereza la Manyoni, mkoani Singida, katika kuachana na nishati isiyo safi na kuanza kutumia bidhaa na teknolojia za Nishati Safi ya Kupikia.
Kifo cha baba yangu kilikuwa pigo kubwa, lakini kilichofuata kilitesa moyo wangu hata zaidi. Siku ya kusomwa kwa wosia, nilipata mshtuko wa maisha yangu. Jina langu halikuwepo kabisa.

Kila kitu kuanzia mashamba, nyumba, hadi akaunti za benki kilikabidhiwa kwa ndugu zangu na mke wake mdogo. Nilifukuzwa kama mtu baki kwenye mali ambazo mimi mwenyewe nilisumbuka kuzitafuta pamoja na baba yangu.

​Ndugu walinitenga na kuniona sifai. Nilijaribu kwenda mahakamani, lakini kesi iligonga ukuta kwa sababu wosia ulikuwa umegongwa muhuri rasmi.

Nilijikuta nikiwa maskini wa kutupwa, ninaishi kwa dhiki, huku wale waliochukua urithi wangu wakicheka na kunisimanga kila siku. Nilijawa na kinyongo, upweke, na sonona kali. SOMA ZAIDI.
Kufungua saluni yangu mwenyewe ilikuwa ndoto ya maisha yangu. Nilitumia akiba yangu yote kukodisha fremu nzuri, kununua vioo vya kisasa, viti vya kifahari, na vifaa vyote vya ubora wa juu.

Nilijua kila aina ya mtindo wa nywele na urembo, lakini kuna kitu kimoja sikuwa nimekijua jinsi ya kupata wateja.

​Miezi tisa ya mwanzo ilikuwa jehanamu ya kiuchumi. Siku zote zilifanana; nilikaa kwenye kiti kuanzia asubuhi hadi jioni nikitazama mlango, lakini hakuna mtu aliyeingia. 

Kodi ilikuwa inakaribia kuisha, bili za umeme zilinishinda, na nilianza kufikiria kufunga biashara na kurudi kuajiriwa. Nilikosa amani, na kila usiku ulikuwa wa mawazo na machozi. SOMA ZAIDI.
Ndoa yetu ilianza kwa furaha na matumaini makubwa. Kama wanandoa wengine, ndoto yetu kuu ilikuwa kupata mtoto wa kutupa tabasamu na kuikamilisha familia yetu. Hata hivyo, miaka mitano ilipita bila mafanikio yoyote.

Kila mwezi ulikuwa wa maumivu, vilio vya chini kwa chini, na maswali yasiyokuwa na majibu kutoka kwa ndugu na marafiki. Tulijaribu kila njia ya hospitali. Tulitumia gharama kubwa kufanya vipimo na kununua dawa mbalimbali, lakini majibu yalibaki yale yale hakuna mabadiliko.

Upendo wetu ulianza kuingia kwenye majaribu makubwa, na matumaini yalianza kutoweka kabisa. Nilikua nikishuhudia wenzangu wakibeba mimba na kujifungua, huku mimi nikibaki na upweke na masikitiko moyoni. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu, Arusha

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha, Paul Christian Makonda, ameridhishwa na maboresho yanayoendelea katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center inayotoa huduma kwa ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, ALMC–JKCI Arusha.

 


Uwekezaji huo ni sehemu ya zaidi ya Shilingi Bilioni 100 zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita katika wilaya hiyo

Na. OWM–TAMISEMI, Gairo


Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza Shilingi bilioni 2.8 katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kituo cha Afya Chanjale, Barabara ya Confort Pub–Magoweko na Shule ya Amali Kwipipa, hatua iliyoboresha upatikanaji wa huduma za afya, kurahisisha usafiri na usafirishaji pamoja na kupanua fursa za elimu ya amali kwa wananchi wa wilaya ya Gairo.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 17, 2026 katika kijiji cha Kwipipa, kata ya Rubeho, wilaya ya Gairo, baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma.

Prof. Shemdoe amesema miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo wanayoishi kupitia uwekezaji unaogusa maisha yao ya kila siku.

"Leo nimekagua miradi mitatu muhimu. Mradi wa Kituo cha Afya Chanjale wenye thamani ya Shilingi Milioni 680, Barabara ya Confort Pub–Magoweko yenye thamani ya Shilingi Milioni 470 na Shule ya Amali Kwipipa yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.6.  Miradi hii ni matokeo ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi," amesema Prof. Shemdoe.

Akizungumzia Shule ya Amali Kwipipa, Prof. Shemdoe amesema shule hiyo imebobea katika mafunzo ya uhandisi na itakuwa chachu ya kuandaa wataalamu wenye ujuzi watakaoshiriki katika ujenzi wa taifa na maendeleo ya sekta mbalimbali za uzalishaji na amewataka wanafunzi wa shule hiyo kuitunza miundombinu yake ili idumu kwa muda mrefu na kuendelea kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Prof. Shemdoe ameainisha kuwa, uwekezaji huo ni sehemu ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita, akieleza kuwa tangu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aingie madarakani, Halmashauri ya Wilaya ya Gairo imepokea zaidi ya Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Gairo, Mhe. Ahmed Shabiby, amewapongeza wananchi wa kijiji cha Kwipipa kwa kujitolea eneo lililowezesha ujenzi wa shule ya Amali, yenye manufaa kwa wananchi wa Gairo na taifa kwa ujumla, Aidha ameipongeza TAMISEMI kwa kutenga bajeti ya chakula kwa wanafunzi wa shule hiyo, hatua itakayochangia kuboresha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia.

Naye, Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Josephine Kapoma, amesema Shule ya Amali Kwipipa itasaidia taifa kupata wahandisi wazawa wenye ujuzi na tija kwa taifa, hivyo amemuomba Prof. Shemdoe amfikishie salamu Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa wananchi wa Kwipipa wameipokea shule hiyo kwa furaha kutokana na mchango wake katika kuinua elimu ya ufundi nchini.



















Wazazi wametakiwa kutimiza wajibu wao katika malezi na ulinzi wa mtoto ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama yasiyo na vitendo vya ukatili.

Wito huo umetolewa na Mkaguzi Msaidizi Emmanuel Kisiri, ambaye ni Polisi wa Kata ya Ikoma, Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara,alipokuwa akitoa elimu ya Polisi Jamii katika nyumba ya Abwire Thomas hivi karibuni.

Mkaguzi Msaidizi Kisiri amesema wazazi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwalea, kuwafuatilia na kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuhatarisha ustawi wao.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya wazazi, jamii na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kujenga mazingira bora ya malezi na kuhakikisha haki za watoto zinazingatiwa.

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kufadhili mradi wa uzalishaji wa chumvi ya asili maarufu kama chumvi ya Kilyoma katika Kata ya Ntwike, Wilaya ya Iramba.

Kwa muda mrefu maisha yangu yaligeuka kuwa uwanja wa mateso makali. Nilikuwa nikishuhudia mambo ya ajabu ambayo sikuwahi kufikiria yangeweza kunipata.

Usiku nilipokuwa nikilala, nilisikia mizigo mizito ikinikandamiza kifua, nikashindwa kupumua na kushindwa hata kupiga kelele kuomba msaada.

Wakati mwingine nilikuwa nikiona vivuli vikizunguka chumbani kwangu, vikicheka kwa sauti ya kutisha, na mara nyingine nilihisi kama kuna mikono isiyoonekana ikinishika shingoni.

Wakati wa mchana hali haikuwa tofauti sana, nilikuwa nikihangaishwa na hofu isiyo na sababu, uchovu uliokithiri na migogoro isiyoisha katika maisha yangu.

Nilijua wazi kwamba haya yote yalikuwa matokeo ya uchawi uliokuwa unanifuata kila mahali. Kazi yangu ilianza kudorora kwa sababu nilikosa nguvu ya kufanya chochote. Ndugu na marafiki walianza kunitazama kama mtu asiye na msaada, na wengine walidhani nimechanganyikiwa.

Nilijitahidi kutafuta msaada wa kawaida kwa madaktari na hata kwa maombi yangu ya binafsi, lakini mambo yaliendelea kuwa mabaya zaidi. Usiku ulipokuwa ukiingia nilikuwa nikiingiwa na hofu kubwa, kwa sababu nilijua mzimu au nguvu mbaya ingenisumbua tena.

Nilijiona kama nimefungwa minyororo isiyoonekana ambayo haikuniruhusu kuishi maisha ya kawaida. Siku moja nilipokuwa nikisoma mtandaoni, nilikutana na ushuhuda wa watu waliokuwa wamepitia hali kama yangu lakini wakapata msaada. SOMA ZAIDI.

Niliposhitakiwa kwa kosa la ubakaji, nilihisi dunia imenigeuka. Majina yalinisakama mitaani, jirani na hata ndugu walinigeuka. 

Nilikuwa nikipita barabarani nikisikia minong’ono, wengine wakinicheka kwa siri na wengine wakinipa macho ya hukumu.

Niliona maisha yangu yote yakiporomoka ghafla, nikajua heshima yangu imefutwa milele. Mwanamke aliyenishitaki alijua fika hakuwa na ushahidi wowote. Lengo lake lilikuwa kunilazimisha nimpe pesa nyingi ili kunyamazisha kesi.

Alijua jina la ubakaji lingetisha na kunifanya nikubali masharti yake. Nilipoambiwa nitoe fedha ili nisionekane kortini, nilikataa. Nilihisi moyoni kuwa ningepoteza kila kitu iwapo ningekubali uongo huo.

Nilipoamua kusimama mahakamani, wengi waliniona kama mtu wa kujitakia maafa. Hata hivyo nilijua ukweli ulikuwa upande wangu. Nilichohitaji ni nguvu ya kusimama imara wakati huu mgumu. SOMA ZAIDI.

Usiku mmoja uliokuwa umesheheni giza na ukimya mzito, mjini kulizuka taharuki kubwa baada ya wezi kuvamia na kuvunja maduka yote kwenye barabara tuliyokuwa tunafanya biashara.

Kelele za kufuli zikivunjwa na milango ikipigwa ziliwafanya wenye maduka waliokuwa majumbani mwao kuamka kwa hofu, lakini hakuna aliyeweza kufika eneo la tukio kwa sababu wezi walikuwa wengi na wamejihami.

Asubuhi ilipofika, hali ya simanzi na hasira ilitanda miongoni mwa wafanyabiashara. Maduka yalikuwa yameachwa yakiwa wazi, rafu tupu, na hasara kubwa ikawa imewakumba.

Nilipofika dukani kwangu, majirani walikuwa wamejaa pale wakiwa na macho ya mshangao. Walidhani mimi pia ningekumbwa na masaibu yale yale. Lakini cha kushangaza ni kwamba lango langu lilikuwa limefungwa vilevile nilivyoacha jana usiku.

Hakuna kufuli lililovunjwa, hakuna mlango ulioguswa, na mali yangu yote ilikuwa salama kabisa. Wengine walishangaa wakajiuliza ni kwa nini wezi walipita kila duka lakini langu hawakuweza kulivunja.

Wengine walidhani nilikuwa nimeajiri mlinzi wa siri, kumbe ukweli ulikuwa tofauti kabisa. Siku chache kabla ya tukio hilo, nilikuwa nikipitia changamoto kubwa. Hali ya wizi katika eneo letu ilikuwa imeongezeka kwa kasi.

Wafanyabiashara wengi walikuwa wanalalamika kwamba kila wiki kulikuwa na duka lililoporwa. Mimi mwenyewe nilikuwa na wasiwasi mkubwa, hasa kwa sababu sikuwa na uwezo wa kumlipa mlinzi kila mwezi.

Ndipo nilipoamua kutafuta msaada wa kiroho ambao nilikuwa nimesikia watu wengi wakizungumza.SOMA ZAIDI.
Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Mhe. Eunje Ahn (kulia) akikabidhi zawadi kwa Kaimu Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi wa Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusinao  Bi. Alana Nchimbi, mara baada ya hafla ya mafunzo ya ukuzaji tija kwa vijana na wanawake walionufaika na programu za KOICA yaliyolenga kuimarisha utendaji wa kazi katika utumishi wa umma. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dodoma tarehe 16 Julai 2026.
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu, amezitaka kampuni za wazawa zinazotekeleza miradi ya kusambaza umeme vitongojini kufanya kazi kwa ufanisi na weledi ili kujijengea uwezo wa kushindana kimataifa na kupata miradi nje ya nchi.

 


Na Mwandishi wetu, Lushoto

Wananchi wa Jimbo la Lushoto Julai 16, 2026 wamemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa Barabara ya Malibwi–Kwekanga–Ngwelo, wakisema hatua hiyo imeondoa kero ya muda mrefu iliyokuwa ikikwamisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa mazao, na kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Lushoto Mhe. Prof. Riziki  Shemdoe, kwa kuifikisha Serikalini changamoto hiyo ambayo imepatiwa ufumbuzi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kwekanga, Bw. Salim Khamis Nyongo, amesema barabara hiyo inayojengwa inaunganisha Kata za Malibwi, Kwekanga, Kilole na Ngwelo pamoja na Jimbo la Mlalo, hivyo ni mhimili muhimu wa uchumi kwa wananchi wa eneo hilo ambao ni wakulima wa nyanya, viazi na karoti. 

“Kwa miaka mingi tumeshindwa kusafirisha mazao yetu kwa urahisi kutokana na ubovu wa barabara, hivyo tunamshukuru Rais Samia kwa kututatulia kero yetu ya barabara na tunampongeza Prof. Shemdoe kwa kuwasilisha kero yetu na hatimaye imetatuliwa,” amesema Bw. Nyongo.

Bi. Rukia Selemani, Mkazi wa Kijiji cha Kwekanga amesema kuwa kabla ya kuanza kwa ujenzi wa barabara hiyo walikuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kusafirisha mazao yao, lakini hata wakati ujenzi ukiendelea tayari wameanza kuona manufaa yake kwani imewarejeshea matumaini na kuwaletea tabasamu, hivyo wanamshukuru Prof. Shemdoe kwa kuhakikisha changamoto hiyo inafanyiwa kazi. 

Kwa upande wake, Bi. Fadhila Salehe ambaye pia ni mkazi wa kijiji cha Kwekanga amesema hapo awali magari yalikuwa yakiishia Malibwi, jambo lililowalazimu wananchi kubeba mizigo kichwani au kutumia pikipiki kwa gharama kubwa, hivyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa barabara hiyo na kumpongeza Mhe. Prof. Riziki Shemdoe kwa ufuatiliaji na usimamizi mzuri wa mradi huo.

Naye Bi. Biasina Shaban Mtari, Mkazi wa Kijiji cha Kwekanga amesema anashukuru kwa sasa magari kutoka Dar es Salaam, Arusha na Tanga yanafika kwenye makazi ya wananchi pasipo na kikwazo chochote, tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Mkazi Mwingine wa Kijiji cha Kwekaga, Bi. Shekela Ramadhan Mohamed amesema ujenzi wa barabara hiyo umeboresha pia maisha ya watoto wanaokwenda shule, kwani zamani walikuwa wakirejea nyumbani wakiwa wamechafuka kutokana na ubovu wa barabara, lakini sasa wanakwenda shuleni na kurejea nyumbani wakiwa wasafi.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi wa TARURA Wilaya ya Lushoto, Bi. Brand Joseph Nyaki, amesema Barabara ya Malibwi–Kwekanga–Ngwelo inarekebishwa kwa kiwango cha zege na Mkandarasi Ms. Broader Construction Company Ltd, ikihusisha tabaka la zege lenye unene wa milimita 150 kwa urefu wa kilomita 1.5.

Bi. Nyaki ameongeza kuwa, mradi huo umeleta manufaa ya kiuchumi kwa vikundi vya Songambele, Inuka na Mkombozi  vinavyonufaika na miradi ya vikundi kwa huduma wakati wa utekelezaji wa ujenzi huo wa mradi wa barabara, huku akimshukuru Mhe. Prof.  Shemdoe kwa kuendelea kusimamia upatikanaji wa miundombinu bora ya barabara inayofungua fursa za maendeleo na kuboresha maisha ya wananchi wa Jimbo la Lushoto.