Na: OWM – TAMISEMI, Kilwa – Lindi
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amezielekeza Wilaya na Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinafanya kazi ya kuzibua mitaro na mifereji ya maji ili kujiandaa na kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kunyesha kuanzia mwezi Oktoba 2026 hadi Februari 2027, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.
Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Septemba 13, 2026 akiwa Somanga, wilaya ya Kilwa, katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Lindi, yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhimiza uwajibikaji kwa viongozi na watumishi wa umma katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za maendeleo.
Prof. Shemdoe amewataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Mameneja wa TARURA Wilaya nchini kote, kuhakikisha wanashirikiana na taasisi nyingine katika kujiandaa na kuwa na utayari wa kukabiliana na athari za mvua za El Niño kwa kuhakikisha miundombinu ya kupitisha maji inakuwa katika hali nzuri na inakidhi mahitaji.
“Nimuelekeze Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kushirikiana na wananchi kuzibua mifereji ya maji iliyoziba ili kipindi cha mvua za El Niño maji yasipate nafasi ya kuchepuka na kuvamia makazi ya wananchi na kuleta madhara, Mkuu wa Wilaya ya Kilwa simamia jambo hili,” amesisitiza Prof. Shemdoe.
Katika hatua nyingine, akijibu ombi la wananchi wa kata ya Kinjumbi la kujengewa kwa kiwango cha lami
barabara ya Kinjumbi yenye urefu wa kilomita 30, Prof. Shemdoe amesema ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami utachukua muda mrefu, hivyo amemuelekeza Meneja wa TARURA kufanya tathmini ya gharama za kuikarabati kwa kiwango cha changarawe na kuwasilisha gharama hizo ofisini kwake ili bajeti ya fedha za matengenezo itumike kuikarabati na kuiwezesha kutumika muda wote.
Maelekezo ya Prof. Shemdoe kwa wilaya na halmashauri kujiandaa kukabiliana na athari za mvua za El Niño ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa katika kikao kazi Septemba 11, 2026 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, aliyezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka za kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba 2026.
Aidha, maelekezo hayo ya Prof. Shemdoe kwa wilaya na halmashauri kujiandaa kukabiliana na athari za mvua za El Niño ni muendelezo wa hatua za utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha usafi wa mazingira katika miji na majiji, aliyoyatoa Septemba 2, 2026 wakati akiwaapisha Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Somanga, mkazi wa kata ya Somanga, wilaya ya Kilwa, Bw. Hashimu Omary Changadua, ameishukuru na kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mbili za sekondari, soko la kimkakati na kituo cha afya, pamoja na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.
Mara baada ya kuzungumza na wananchi wa Somanga, Prof. Shemdoe aliendelea na ziara yake kwa kutembelea na kukagua ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao linalojengwa na halmashauri ya Kilwa, pamoja na ujenzi wa soko la wajasiriamali wadogo katika kijiji cha Njianne, kata ya Tingi, katika halmashauri hiyo.
Ikiwa taifa liko katika juhudi za kujenga jamii yenye maadili, amani, mshikamano na uwajibikaji, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limetakiwa kuendelea kutumia nafasi yake katika kuimarisha misingi hiyo na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rose Mary Senyamule, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 6 wa Wachungaji wa KKKT unaofanyika katika Ukumbi wa Chimwaga, jijini Dodoma.
Senyamule amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa KKKT katika maendeleo ya taifa, ikieleza kuwa kwa miaka mingi kanisa hilo limekuwa mshirika muhimu katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii.
Amesema huduma hizo ni pamoja na elimu, afya, malezi ya vijana, huduma kwa watu wenye mahitaji maalum pamoja na misaada ya kijamii na juhudi za kupambana na umaskini.
Senyamule amesema pamoja na huduma za kijamii, KKKT imeendelea kuwa mdau katika shughuli za kiuchumi na uwekezaji, huku viongozi wa dini wakiwa na nafasi ya kipekee katika kujenga maadili mema, kudumisha amani na kuimarisha umoja wa kitaifa.
“Viongozi wa dini tunatambua kuwa mnaaminika sana na wananchi kuliko taasisi na watu wengine. Kwa sababu hiyo, mafundisho na matendo yenu yanaweza kuleta mabadiliko makubwa katika familia, jumuiya na taifa kwa ujumla,” amesema.
Amesema taifa linahitaji viongozi wa dini wanaoweza kuwa sauti ya matumaini na faraja kwa wananchi, hususan wale wanaopitia changamoto mbalimbali za maisha.
Senyamule amewataka wachungaji na viongozi wa dini kwa ujumla kuendelea kuwa sauti ya faraja kwa wenye huzuni, matumaini kwa waliokata tamaa na msaada kwa watu walio katika mazingira magumu.
Katika eneo la malezi, amesema kuna umuhimu wa kuimarisha malezi ya kiroho na kimaadili, hasa kwa watoto na vijana, ili kuwaandaa kuwa kizazi chenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.
Aidha, amewataka wachungaji kuendelea kutoa elimu inayowajenga wananchi katika nyanja za kiroho, kijamii na kiuchumi, huku wakihimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, kutumia fursa zilizopo na kushiriki katika shughuli halali za maendeleo.
“Imani iendelee kusambaa sambamba na matendo yanayoleta ustawi wa mtu binafsi, jamii na taifa kwa ujumla,” amesema.
Mkutano Mkuu wa 6 wa Wachungaji wa KKKT umehusisha wachungaji kutoka Dayosisi 28 za KKKT na umefunguliwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Alex Malalusa.
Mkutano huo unatarajiwa kuendelea hadi Septemba 17, 2025, ukiwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayohusu huduma ya kanisa, malezi ya kiroho na nafasi ya kanisa katika jamii na maendeleo ya taifa.
Mashindano ya Soka ya Kiruswa Jimbo Cup yanayoandaliwa kila mwaka na Naibu Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Longido Mkoani Arusha,Dkt Steven Kiruswa yameingia msimu wa sita na kuendelea kufana kila mwaka na mwaka huu timu 51 zimeshiriki mashindano hayo kutoka katika tarafa nne wa wilaya hiyo yenye wakazi wengi vijana wa jamii ya kifugaji ya Kimasai.
Naibu Waziri huyo alisema hayo baada ya uzinduzi rasmi wa mashindano ya Kiruswa Jimbo Cup mwaka huu na kusema kuwa mwaka yatafanikiwa zaidi kwani waandaji wamejipanga kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa na vijana kuchukuliwa kwenda katika ligi za madaraja mengine ya juu timu za huko ili waweze kuiwakilisha vema Longido.
"Sasa mwakani ntakuja kivingine nataka iwatoe vijana wa kiume na kike wa hapa Longido kwenda kupata fursa za kimaisha kupitia michezo na kujikita katika michezo zaidi na kuacha mara moja kujikita katika ujambazi, madawa na ulevi"alisema Kiruswa
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Wilaya ya Longido(LDFA) Obeid Mollel amesema Kiruswa Jimbo Cup ni mashindano yanayokuwa mwaka hadi mwaka na vijana wengi wamefanikiwa kusajili katika timu za ngazi mbalimbali Mkoa na ligi daraja la pili na kwanza baada kuonyesha vipaji vyao katika mashindano hayo.
Mollel alisema timu zote shiriki zimepewa seti moja ya jezi na mpira na washindi watapata zawadi ya fedha taslimu na medali ila mwakani utaratibu utabadilika kwa kuongeza zawadi ya fedha kuwa nono na timu zilizoshika nafasi tatu za juu zitapewa jezi na mpira na sio timu zote kama ilivyokuwa sasa hiyo ni kuongeza ushindani katika soka.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Longido ,Salumu Kally amesema kuwa Kiruswa Jimbo Cup ni mashindano muhimu katika wilaya yake kwani yanawapa ubize vijana kujikita katika soka na kuacha kujikita katika uhalifu,madawa na ulevi hivyo Mbunge anastahili pongezi na kuungwa mkono kwa hali na mali.
Naye Maenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Papa Nakuta amesema michezo ni ilani ya chama hicho inayosisitiza kuendeleza michezo na anachofanya Kiruswa ni utekelezaji wa ilani ya chama katika kukuza michezo katika Jimbo la Longido na vijana wanafurahia mashindano hayo ambayo yanaonyesha ushindani mkubwa mwaka hadi mwaka.
Nilikuwa na hasira kubwa ndani yangu. Wakati mwingine nilifikiria kulipiza kisasi kwa njia za haraka, lakini nilijua hilo lingeweza kuniletea matatizo makubwa zaidi, hasa ya kisheria. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu hali hiyo. SOMA ZAIDI.
Tulijaribu kupambana kwa njia mbalimbali kwa miaka mingi, lakini hakuna kilichobadilika. Kila hatua tuliyochukua ilionekana kugonga mwamba. Hali hii ilinichosha sana. Ilikuwa sio tu kupoteza mali, bali pia historia na heshima ya familia yetu.
Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali hiyo. SOMA ZAIDI.
Nilishutumiwa kwa makosa ambayo sikuwa nimeyafanya, na bila nafasi ya kujitetea kwa ufasaha, nikafukuzwa kazi kwa aibu kubwa. Siku ile nilihisi kama dunia imenigeuka. Niliondoka kazini nikiwa na maswali mengi kichwani na maumivu makubwa moyoni.
Watu waliokuwa wananijua walishangaa na wengine walianza kunidharau. Siku zilizofuata zilikuwa ngumu sana. Nilianza kujifungia ndani, nikikosa hamu ya kufanya chochote. Nilihisi kama maisha yangu yamefikia mwisho wa safari. SOMA ZAIDI.
Afya yangu ilianza kudhoofika kwa magonjwa ya ajabu yasiyorekodiwa vipimo vya hospitali, biashara yangu ikapoteza wateja wote, na migogoro isiyoisha ikaanza kuibuka nyumbani kwangu.
Nilijua wazi kuwa kuna maadui waliokuwa wakinitazama kwa jicho la husuda na kunirushia mishale ya kishirikina ili kunidondosha kabisa na kuniharibia maisha.
Nikiwa kwenye majuto na hofu kubwa ya kupoteza kila kitu nilichochuma kwa jasho langu, mzee mmoja wa heshima katika kijiji chetu alinitembelea.
Baada ya kumsimulia mateso na majanga yaliyokuwa yakiniandama, alinieleza kwa huruma kuwa ulinzi wa kawaida hautoshi pale unapokabiliwa na maadui wenye roho mbaya na uchawi wa waziwazi. SOMA ZAIDI.
Mateso haya hayakuishia ndotoni pekee; mchana nilikuwa nikihisi uzito mkubwa mabega, maumivu ya kichwa yasiyoonekana hospitali, na kila mpango wangu wa maendeleo ulikuwa ukiharibika ghafla.
Nilibaki nikijitenga na watu, nikiteseka na vifungo vya kishirikina vilivyotaka kuniangamiza. Nikiwa kwenye majuto na kukata tamaa kabisa, ndugu yangu mmoja aliyekuwa akijua hali yangu alinitembelea.
Baada ya kushuhudia jinsi nilivyokuwa nikidhoofika kwa kukosa usingizi na amani, alinieleza kwa huruma kuwa maumivu na ndoto za namna hiyo ni ishara za wazi za vifungo vya giza na uchawi uliotegwa ili kuniharibia maisha. SOMA ZAIDI.
Kwa miezi mingi, nilikuwa nikiona mabadiliko makubwa kwa mwenzangu; simu zilifungwa maneno ya siri, alirudi nyumbani usiku wa manane akiwa na visingizio visivyo na msingi, na mapenzi yote na heshima kwangu vilipungua.
Kila nilipojaribu kumuuliza kwa ukweli, alipandisha hasira, kunifokea, na kunifanya nionekane mwenye wivu usio na maana. Hali hii iliniletea msongo mkubwa wa mawazo, nikiishi kwa hofu na wasiwasi huku nikitazama mahusiano yetu yakitumbukia kwenye shimo la usaliti.
Nikiwa kwenye simanzi na nikitafuta njia ya kupata ukweli bila kuendelea kudanganywa na kuonekana mjinga, rafiki yangu wa karibu alinishauri kutafuta suluhisho la kienyeji badala ya kuendelea kugombana bila ushahidi.
Alinieleza kuwa wapo wataalamu wa kiasili wenye uwezo wa kufanya visomo vinavyoweza kumfanya mtu anayecheat afumanishe mwenyewe au kunaswa papo kwa papo bila kukana. SOMA ZAIDI.
Kizimkazi, Kusini Unguja — Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Hamisi Masanja Malebo, ameungana na viongozi wengine wa Wizara katika kumtembelea na kumpa pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.
Ziara hiyo imefanyika tarehe 11 Septemba 2026 nyumbani kwa Rais Samia, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo ujumbe huo ulifika kutoa pole na faraja kwa Rais pamoja na familia yake katika kipindi hiki cha maombolezo.
Prof. Malebo, akiwa sehemu ya ujumbe huo wa viongozi, aliungana na viongozi wengine wa Wizara kuwasilisha salamu za pole kwa Rais Samia na familia yake kufuatia msiba wa Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 7 Septemba 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar.
Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaungana na Rais Samia, familia, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huo katika kipindi hiki cha huzuni na maombolezo.
Tume inatoa pole kwa Rais Samia na familia yake, huku ikiwaombea nguvu, faraja na moyo wa subira katika kipindi hiki cha majonzi.
Tume ya Taifa ya UNESCO inaendelea kuungana na familia katika kuomboleza msiba huo na kuenzi kumbukumbu ya Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.
GEITA: Kwa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu, kukosa ajira si lazima kuwe na maana ya kukosa kabisa fursa za kufanya kazi; wakati mwingine changamoto kubwa ni kukosa maarifa na ujuzi unaowawezesha kuzitambua na kuzitumia fursa zilizopo.
Hilo ndilo linalolenga kushughulikiwa na Mradi wa BRIDGE Tanzania, unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini, kwa kuwapatia vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu elimu ya msingi na ujuzi wa vitendo unaoweza kuwawezesha kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi.
Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, vijana 210 tayari wamepatiwa mafunzo kupitia mradi huo, huku baadhi yao wakianza kutumia ujuzi walioupata katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, zikiwemo sabuni za miche, sabuni za maji na vyakula vya mifugo.
Mafunzo hayo pia yanahusisha kusoma, kuandika, kuhesabu na ujasiriamali, yakilenga kuwajengea vijana uwezo unaoweza kutumika katika maisha yao na katika mazingira ya soko.
Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya (District Steering Committee) ya Mradi wa BRIDGE Tanzania kilichofanyika Nzera, Geita, Mratibu Msaidizi wa Kitaifa wa mradi huo, Adriano Adrian Hyera, alisema hadi sasa vijana 210 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita wamepatiwa mafunzo.
Alisema mradi huo unaweka mkazo katika kuwapa vijana fursa ya kupata maarifa na ujuzi ambao unaweza kuwasaidia kujenga uwezo wa kujitegemea.
“Lengo si kuwapa vijana mafunzo pekee, bali kuwajengea uwezo ambao wataweza kuutumia baada ya mafunzo ili kujipatia kipato na kujitegemea,” alisema Hyera.
Kwa mujibu wa muundo wa mradi, vijana ambao hawakupata fursa ya kukamilisha elimu ya msingi hupewa nafasi ya kujenga uwezo katika kusoma, kuandika na kuhesabu, kabla ya kuendelea na mafunzo ya ujuzi wa vitendo unaoendana na mazingira yao na fursa zinazopatikana katika soko.
Mtazamo huo unaweka msisitizo katika kuunganisha elimu na ujuzi wa vitendo, ili kijana anapomaliza mafunzo asiishie kuwa na maarifa ya darasani pekee, bali awe na uwezo wa kutumia ujuzi huo katika shughuli za uzalishaji na kujiajiri.
Katika utekelezaji wake Geita, mradi unawawezesha vijana kujifunza kwa vitendo na pia unatoa vifaa na mahitaji muhimu kwa ajili ya mafunzo, ili kuwapa nafasi ya kufanya mazoezi ya uzalishaji wakati wa kujifunza.
Baadhi ya vijana walionufaika na programu hiyo wamesema mafunzo yamewajengea uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji na kuwapa mtazamo mpya kuhusu namna wanavyoweza kutumia ujuzi wao kama njia ya kujipatia kipato.
Ujuzi huo unawapa pia nafasi ya kutengeneza bidhaa ambazo zinaweza kutumika katika jamii na, kwa kuzingatia ubora na mahitaji ya soko, kuwa sehemu ya shughuli zao za kiuchumi.
Kutoka elimu ya msingi hadi ujuzi wa soko
Kwa mtazamo wa mradi, elimu na ujuzi haviwekwi katika maeneo mawili tofauti, bali vinaunganishwa ili kumjengea kijana uwezo wa kutumia maarifa yake katika mazingira halisi.
Baada ya kujenga msingi wa kusoma, kuandika na kuhesabu, kijana hupewa ujuzi wa vitendo unaozingatia eneo analotoka na fursa zinazopatikana katika soko.
Hii inalenga kuwapa vijana ambao hawakumaliza elimu rasmi nafasi ya kupata ujuzi unaoweza kuwasaidia kushindana katika shughuli za kiuchumi pamoja na vijana wengine waliopitia njia rasmi za elimu na mafunzo ya ufundi.
Kwa maana hiyo, BRIDGE Tanzania inalenga kujenga daraja kati ya elimu, ujuzi na soko, badala ya kuishia katika utoaji wa mafunzo pekee.
Vijana wahimizwa kutumia fursa za mikopo
Akizungumzia hatua zinazofuata baada ya mafunzo, Hyera aliwashauri vijana kujiunga katika vikundi vya watu watano ili waweze kuchangamkia fursa za mikopo zinazotolewa na Halmashauri.
Alisema ushiriki katika vikundi unaweza kuwasaidia vijana kutumia ujuzi walioupata katika shughuli za kiuchumi na kutafuta fursa za kukuza shughuli zao.
Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa mafunzo wanayopata vijana yanaunganishwa na fursa za mitaji na uzalishaji, ili kuongeza uwezekano wa ujuzi huo kuleta matokeo katika maisha yao.
Majaribio yenye matarajio ya kupanuka
BRIDGE Tanzania ni mpango wa majaribio unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Kaskazini A Unguja.
Mradi una lengo la kuwafikia vijana 3,000 katika kipindi cha miaka mitano, sawa na takribani vijana 600 kila mwaka.
Majaribio hayo yanatoa nafasi ya kutathmini namna ya kuwaunganisha vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu na elimu ya msingi, ujuzi wa vitendo na fursa za kiuchumi.
Matokeo na uzoefu unaopatikana katika maeneo ya utekelezaji utasaidia katika kutathmini namna mfumo huo unavyoweza kuimarishwa na, baada ya tathmini, kupanuliwa katika maeneo mengine nchini.
Tume ya UNESCO katika utekelezaji
Utekelezaji wa BRIDGE Tanzania unaenda sambamba na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuwawezesha vijana kupata maarifa, ujuzi na fursa za kushiriki katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa.
Kupitia Tume ya Taifa ya UNESCO, ushirikiano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini umegeuzwa kuwa fursa ya kuwafikia vijana ambao kwa sababu mbalimbali hawapo katika mfumo rasmi wa elimu.
Tume ya Taifa ya UNESCO, kwa jukumu lake la kuratibu, kutathmini na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za UNESCO nchini, inaendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kuhakikisha programu zinazotekelezwa zinachangia mahitaji na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania.
Kwa BRIDGE Tanzania, msisitizo ni kuhakikisha kijana aliye nje ya mfumo rasmi hapotezi fursa ya kujenga uwezo. Badala yake, anapewa nafasi ya kujifunza, kupata ujuzi na kuutumia katika kujenga maisha yake.
Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya kilichofanyika Nzera, Geita, kilitoa nafasi kwa wadau kupitia utekelezaji wa mradi, mafanikio, changamoto na hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kuongeza manufaa yake kwa vijana.
Kwa vijana hao 210 wa Geita, safari inaanzia katika kujenga msingi wa elimu na ujuzi; lakini lengo kubwa ni kuwawezesha kutumia uwezo huo katika ulimwengu halisi wa kazi, uzalishaji na kujitegemea. https://www.instagram.com/reel/DczGOqpqA74/?igsi=ZHVqMjQwemwyYTU=
KAMPUNI ya Kimataifa ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Barrick Gold kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Kiseriani kata ya Engikaret wilyani Longido Mkoani Arusha,Mbunge wa Jimbo hilo,Dkt Steven Kiruswa na serikali wamefanikiwa kujenga shule shikizi kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 230.
Akizungumza katika uzinduzi wa shule hiyo Kijiji hapo ,Meneja Mkazi wa Barrick{Country Manager} Tanzania ,Melkiory Ngido alisema uamuzi wa kampuni hiyo kuchangia msaada ni kufuatia maombi ya Kiruswa ambaye ni Naibu Waziri wa Madini na kujionea wenyewe hali ya changamoto za wanafunzi kutembea km 32 kwenda na kurudi shule hali inayoleta hatari kwa wanafunzi hao kwa wanyama wakali.
Ngido aliwaahidi wananchi Kiseriani na Longido kwa ujumloa kuwa Barrick Gold itashirikiana na wananchi katika kujenga miundombinu ya elimu kwa kuwa wananchi wameonyesha nia ya dhati na ushirikiano na uadilifu mkubwa katika ujenzi wa madarasa mawili na 0fisi ya mwalimu kwani kampuni hiyo imechangia zaidi ya shilingi milioni 180 na zimetumika kama ilivyokusudiwa.
Alisema elimu ni msingi wa maisha na wananchi wa Kijiji cha Kiseriani ambao wengi wao ni wa jamii ya kifugaji ya Kimasai kuamua wenye kujitoa na kujenga madarasa mawili na ofisi ya mwalimu ni uamuzi unaopaswa kuungwa mkono kwa kuwa jamii hiyo imeamua kujitoa na kuwajali wanafunzi wa jamii hiyo na kujali elimu zaidi na sio vinginevyo.
‘’Barrick Gold Mining imeaamua kujitoa zaidi Longido kuhakikisha elimu inasogezwa zaidi katika maeneo ya makazi ya watu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miundombinu ya elimu ikiwemo madarasa,ofisi na nyumba za walimu zinajengwa kwa maslahi ya watoto wa jamii hiyo’’alisema Ngido
Naye Kiruswa aliishukuru kampuni hiyo kwa uamuzi wa ujenzi wa madarasa na ofisi ya mwalimu na kuahidi ushirikiano zaidi na kusema kuwa uamuzi huo unapaswa kupongezwa na wananchi wote wa Longido na kusema kuwa uadilifu ni jambo muhimu katika kuwashawishi wafadhili wengine kujitoa katika kutoa misaada ya miundombinu ya elimu,maji na barabara.
Alisema uamuzi wa ujenzi wa madarasa mengine mawili ulioazwa na wananchi kwa kusomba mawe,mchanga na kokote ni uamuzi wenye busara kubwa na yeye ataunga mkono kwa hilo kwa kutoa mifuko 100 ya simenti na kumalizia upauaji.
Waziri Kiruswa alisema na kuwaomba wana Kiseriani na Longido kwa ujumla kujitoa katika shughuli za kijamii ikiwemo ujenzi wa miundoimbinu ya elimu na kusema kuwa yeye kwa hilo atakuwa mstrari wa mbele katika kuchangia na kusaka wafadhili zaidi .
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi{CCM} wilaya ya Longido ,Papa Nakuta amempongeza Kiruswa kwa jinsi anavyojitoa kwa maendeleo ya wananchi wa longido na kuwataka wananchi kumuunga mkono mbunge huyo ambaye ameenda bungeni kufanya kazi na sio kulala kwani kila mradi mchango wake upo kama sio yeye basi analeta marafiki zake na kufanya ushawishi kwa serikali kuendelea kupeleka fedha za miradi Jimbo hapo.

















































