NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.
............
NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amewataka Maafisa Biashara nchini kutumia nafasi zao kikamilifu kuibua fursa za uwekezaji, kuongeza thamani ya mazao na kuboresha mazingira ya biashara katika halmashauri, hatua inayolenga kuchochea maendeleo ya kiuchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Londo ametoa kauli hiyo leo Agosti 17,2026 jijini Dodoma wakati wa Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara nchini, kilicholenga kuimarisha utekelezaji wa majukumu yao katika kukuza biashara, viwanda na uwekezaji.
Amesema Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchumi wa viwanda katika Afrika Mashariki na Kati, ikiwamo kufikia uchumi wa dola trilioni moja na kuongeza kipato cha Mtanzania hadi dola 7,000. Amesema kufikia malengo hayo kunahitaji uchumi imara, jumuishi na shindani unaotegemea sekta binafsi, sayansi na teknolojia, uwekezaji, utafiti pamoja na nguvu kazi yenye ujuzi.
"Maafisa Biashara wana jukumu la kuhakikisha halmashauri zinakuwa vituo vya uzalishaji, uwekezaji na biashara kwa kutambua fursa zilizopo, kuwaunganisha wazalishaji na masoko na kuhakikisha mazao yanaongezwa thamani. "amesema Mhe.Londo
Hata hivyo ametolea mfano wa mahindi, amesema wakulima wanapaswa kusaidiwa kuondokana na kuuza mazao ghafi na badala yake kuzalisha bidhaa kama unga wenye chapa na kuufikisha kwenye masoko, hatua itakayoongeza kipato na kuchangia kupunguza umaskini.
Aidha, amesema utekelezaji wa Dira 2050 unahitaji vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kushirikishwa kikamilifu katika uzalishaji, uwekezaji na biashara kupitia fursa za mikopo na uwezeshaji. Amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026, viwanda vikubwa vipya 25 vilijengwa katika sekta mbalimbali na kutoa ajira 39,000, zikiwamo ajira 7,600 za moja kwa moja na 31,000 zisizo za moja kwa moja.
Katika kuimarisha mazingira ya uwekezaji, Londo amezitaka mikoa kuhuisha kanzidata za viwanda, biashara, masoko, leseni, wawekezaji na maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kiuchumi, huku kila halmashauri ikiandaa wasifu wa fursa za uwekezaji unaoonyesha upatikanaji wa malighafi, miundombinu, masoko na maeneo ya uwekezaji. Pia amewataka Maafisa Biashara kuhakikisha Mabaraza ya Biashara yanafanya kazi kikamilifu na hoja za sekta binafsi zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.
Katika hatua nyingine, Londo amewataka Maafisa Biashara kuharakisha urasimishaji wa biashara zisizo rasmi kwa kutoa elimu kuhusu usajili wa biashara, leseni, TIN, viwango, vipimo na taarifa za umiliki.
Amesema urasimishaji utawawezesha wafanyabiashara kupata huduma za uwezeshaji, mitaji na masoko, huku akieleza kuwa halmashauri zimetengewa asilimia tano ya mapato ya ndani, yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 72 kwa mwaka wa fedha 2026/2027, kwa ajili ya kuwekeza katika miundombinu ya masoko, maeneo ya biashara na ujasiriamali.
Amesisitiza fedha hizo zitumike kwa ufanisi kwa kushirikisha sekta za ardhi, maji, nishati na barabara ili kuongeza tija kwa wafanyabiashara na kuvutia wawekezaji. Aidha, amewataka Maafisa Biashara kutumia nafasi zao kuboresha huduma na kuifanya Tanzania kuwa na mazingira bora zaidi ya biashara na uwekezaji, hatua ambayo ni muhimu katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum, amewataka Maafisa Biashara kuongeza udhibiti wa bidhaa feki na viwanda visivyo rasmi katika maeneo yao, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda afya na usalama wa wananchi, watumiaji pamoja na wazalishaji wanaofuata sheria.
Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa, amesema Maafisa Biashara ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wafanyabiashara katika kuhakikisha sera, sheria na kanuni za biashara zinatekelezwa na kuleta mabadiliko chanya katika mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.
Amesema kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, BRELA imeendelea kuboresha mifumo na sheria zinazosimamia usajili na utoaji wa leseni kwa lengo la kupunguza muda na gharama za kuanzisha na kuendesha biashara. Amesema kupitia BRELA Online System (ORS), huduma za wakala zimeunganishwa katika mfumo mmoja, huku mfumo huo ukiwezesha pia utoaji na usimamizi wa leseni za biashara kundi A na B.
Amesema mfumo huo unatoa fursa kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoa na kusimamia leseni za kundi B bila kuathiri mapato yao, kwani malipo yanayofanywa na mfanyabiashara yanaingia moja kwa moja katika akaunti ya halmashauri husika.
Aidha, ORS imeunganishwa na mifumo ya taasisi nyingine za Serikali ikiwamo NIDA na TRA, hatua inayowezesha taarifa muhimu kupatikana moja kwa moja bila mfanyabiashara kuwasilisha nyaraka ambazo tayari zipo kwenye mifumo hiyo.
Nyaisa,amesema kuwa maboresho hayo yameongeza uwazi na ufanisi, kupunguza urudufu wa taarifa, muda na gharama za kupata huduma, pamoja na kupunguza mianya ya uzembe katika utoaji wa huduma.
"BRELA itaendelea kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara, Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI, sekretarieti za mikoa na halmashauri katika kuwajengea uwezo Maafisa Biashara."amesema Nyaisa
Amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, BRELA imepanga kutoa mafunzo kwa Maafisa Biashara wote nchini kupitia kanda nne, yatakayolenga matumizi ya mifumo, utoaji na usimamizi wa leseni pamoja na utekelezaji wa sheria.
Pia amesema BRELA itaendelea kuboresha miunganiko ya mifumo ya kidijitali na kushirikiana na vyama vya Maafisa Biashara katika kutatua changamoto zao, huku akisisitiza kuwa maafisa hao ni mawakala muhimu wa uwekezaji nchini na wanapaswa kutambua kuwa jukumu lao ni kuwezesha biashara, si kuikwamisha, ili kujenga mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
Yalianza kama maumivu ya kawaida ya viungo na mgongo, lakini ndani ya muda mfupi, hali ilibadilika na kuwa mbaya zaidi miguu na mikono yangu ilipooza kabisa, na kuacha mwili wangu ukiwa hauna nguvu wala uwezo wa kujitikisa.
Nilitumia fedha zote za akiba na hata kuuza baadhi ya mali zangu ili kupata matibabu kwenye hospitali kubwa na kwa madaktari bingwa.
Hata hivyo, kila vipimo vya MRI, CT scan, na vipimo vya damu vilipofanyika, majibu yalikuja yakionyesha kuwa sina ugonjwa wowote unaoonekana kisayansi.
Nilibaki kitandani nikihudumiwa kila kitu kama mtoto mchanga, nikiteseka na maumivu makali ya ndani kwa ndani usiku kucha.
Nilianza kuona aibu na unyonge mkubwa, nikitazama familia yangu ikiteseka kwa kuniuza na kunisikitikia, huku nikipoteza kabisa matumaini ya kuwahi kusimama tena kwa miguu yangu. SOMA ZAIDI.
Nilitumia fedha nyingi sana kulipia ada za maombi ya Visa, mawakili wa usafiri, na vipimo vya afya, lakini kila nilipofika hatua ya mwisho ya usahili (interview) au kupokea majibu kutoka ubalozi, nilipokea barua za kukataliwa.
Mara ya kwanza nilijiambia ni bahati mbaya, lakini baada ya kukataliwa Visa mara ya nne mtawalia hata kwa safari ambazo nilikuwa na nyaraka zote halali na mwaliko rasmi ndipo nilipoanza kutambua kuna kitu kisichokuwa cha kawaida.
Kila mara nilipokaa mbele ya afisa wa ubalozi, nilipatwa na woga wa ajabu, ulimi ulikuwa mzito kujieleza, na sura yangu ilionekana kama ya mtu asiye na uaminifu mbele yao.
Nilibaki nikitazama marafiki zangu waliokuwa na nyaraka dhaifu kuliko zangu wakipata Visa kwa urahisi na kuondoka, huku mimi nikibaki nikiwa nimefilisika kwa gharama za safari zisizopatikana na kuchekwa na watu wa mtaani. SOMA ZAIDI.
Baada ya kuondokewa na wazazi wangu waliotutoka kwa pamoja, nilibaki mimi kama mtoto wa pekee nikiwa na matumaini ya kuendeleza mali zao ikiwemo nyumba ya familia na shamba kubwa la kilimo.
Hata hivyo, kabla hata ya siku arobaini kumalizika, mijomba na mashangazi zangu waligeuka ghafla. Walikaa kikao cha familia bila kunishirikisha, wakatengeneza nyaraka za uongo, na hatimaye walinifukuza kwenye nyumba na kupora shamba lote.
Nilibaki mtaani nikiwa sina mbele wala nyuma, nikilia kwa uchungu na unyonge. Nilitafuta msaada kwa viongozi wa mtaa na hata kujaribu kwenda polisi, lakini ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuziba pengo kila mahali.
Nilipojaribu kuwasogelea na kuwaomba wanihurumie, walinitishia kunifanyia vitendo vya kishirikina au hata kuniondoa duniani kama nitaendelea kufuatilia mali hizo.
Nilibaki nikiishi maisha ya uombaomba, nikiwa nimekonda kwa mawazo, huku nikitazama mali za wazazi wangu zikitumiwa na watu waliokosa huruma wala woga wa Mungu. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka na miaka, ukoo wetu ulikabiliwa na hali ya kusikitisha sana. Hakuna mtu yeyote kwenye familia yetu aliyewahi kufanikiwa kimaisha iwe ni kusoma na kupata kazi, kuanzisha biashara, au hata kudumu kwenye ndoa.
Kila kijana alipofikisha umri wa kuanza kujitegemea, alikumbana na mikosi mizito, magonjwa ya ajabu, au kufilisika ghafla na kurudi kijijini kuishi kwa unyonge.
Nilibaki nikitazama ndugu zangu wenye akili na uwezo mkubwa wakishindwa kabisa kupiga hatua, huku ukoo wetu ukichekwa na kudharaulika sana mtaani. Hali hii iliniletea huzuni na msongo mkubwa wa mawazo.
Kila nilipojaribu kupambana ili nikuze uchumi wangu na kuivusha familia, nilikutana na vizuizi visivyoeleweka na kupoteza fedha zangu zote.
Nilianza kuona wazi kuwa familia yetu ilikuwa kwenye kifungo cha giza na laana ya kurithishwa iliyokuwa ikinyonya mafanikio ya kila kizazi. SOMA ZAIDI.
Kwa miezi kadhaa, mtaa wetu ulikabiliwa na genge la majambazi na vibaka waliokuwa wakivunja nyumba na kuiba vitu vya thamani usiku wa manane. Kila siku tuliamka na kusikia nyumba ya jirani fulani imeingiliwa, watu wakipigwa, na mali zote kuondolewa.
Hali hii iliniletea hofu na msongo mkubwa wa mawazo. Kila jioni ilipowadia, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu, nikishindwa kupata usingizi usiku kucha huku nikisikiliza kila kishindo au mshindo wa nje.
Niliweka milango ya chuma, makufuli makubwa, na hata taa za usalama, lakini bado majambazi hao waliendelea kuvunja nyumba za majirani zetu waliokuwa na milango imara zaidi.
Nilibaki nikitetemeka kwa hofu ya zamu yetu kufika, nikihofia maisha ya mke wangu, watoto wangu, na mali tulizozitolea jasho kwa miaka mingi. SOMA ZAIDI.
Hata hivyo, pale unapotazama siku zikienda bila mteja hata mmoja kuingia dukani, huku kodi ya pango, bili, na madeni vikikuandama, maisha huanza kuwa chungu sana.
Kwa miezi kadhaa, nilikabiliwa na ukame mkubwa wa wateja kwenye duka langu la nguo na vipodozi. Nilikuwa nikiamka asubuhi na mapema, nikifungua duka kwa matumaini, lakini nilishinda nimeketi peke yangu mchana mzima huku maduka ya majirani zangu yakifurika watu kila dakika.
Hali hii iliniletea msongo mkubwa wa mawazo na unyonge. Nguo na bidhaa zilizopo dukani zilianza kuharibika na kupitwa na wakati, huku mtaji wangu ukiendelea kukatika kwa ajili ya kulipia pango la duka na gharama za usafiri.
Kila nilipojaribu kupunguza bei au kufanya matangazo, hakuna kilichobadilika watu walipita mbele ya duka langu wakitazama ndani na kuondoka bila kuingia.
Nilianza kukata tamaa na kufikiria kufunga duka hilo kwa aibu kubwa, nikiwa nimeingia kwenye madeni mazito na kupoteza akiba yangu yote ya maisha. SOMA ZAIDI.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka amewataka vijana kutumia michezo kama fursa ya kujipatia ajira na kujenga maisha yao, huku wakiepuka vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi na ukatili wa kijinsia.
Naibu Waziri Mahundi ameyasema hayo wakayi akikabidhi vifaa vya michezo kwa timu 13 za Kata ya Iwambi jijini Mbeya.
Amesema michezo inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kuwaweka vijana pamoja, kuwajengea vipaji na kuimarisha amani na mshikamano katika jamii huku akiwataka wananchi wa Iwambi kuunda timu moja imara itakayowakilisha kata hiyo katika mashindano mbalimbali na kuitangaza Iwambi kupitia michezo.
Aidha, amependekeza kuanzishwa kwa klabu ya mbio za pole (jogging) katika kata hiyo, akisema mazoezi ni muhimu katika kuimarisha afya na kusaidia jamii kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kwani michezo inapaswa kuwa chombo cha kuimarisha upendo na mshikamano ndani na nje ya Kata ya Iwambi, huku akitoa wito wa kushirikiana katika mapambano dhidi ya uhalifu.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Iwambi, Groria Ipopo Mwamajemba (Mchina), amemshukuru Mahundi kwa msaada huo, akisema amekuwa sehemu ya wakazi wa Iwambi na ameendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo katika kata hiyo.
Mwamajemba amesema kupitia michezo, vitendo vya uhalifu vimepungua kwa kiasi kikubwa katika Kata ya Iwambi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika michezo kwa vijana.
Mahundi ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya na Mkurugenzi wa Maryprisca Women Empowerment Foundation (MWEF), amekabidhi jozi mbili za vifaa vya michezo kwa kila timu pamoja na mpira mmoja kwa kila timu, katika hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Sekondari Iwambi ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Diwani wa Kata ya Iwambi, Groria Ipopo Mwamajemba maarufu kama Mchina, aliyeanzisha mashindano ya mpira wa miguu yaliyowakutanisha vijana kutoka mitaa mbalimbali ya kata hiyo.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana ana Rushwa nchini (TAKUKURU) imekabidhi vifaa muhimu vya kisasa kwa ajili ya kuimarisha huduma kwa watoto wachanga hususani waliozaliwa kabla ya wakati (njiti) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo.
Vifaa hivyo, ambavyo ni Phototherapy na Infant Warmer, vimetolewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini-TAKUKURU ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Hospitali ya Bombo katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi.
Akikabidhi vifaa hivyo katika hafla fupi iliyofanyika Hospitalini hapa, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini, Bw. Crispin Chalamila, amesema taasisi hiyo imeamua kutoa msaada huo baada ya kuona juhudi zinazofanywa na Hospitali ya Bombo katika kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Tanga wanapata huduma bora za afya.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo, Dkt. Husein Mangaa, ameishukuru TAKUKURU kwa msaada huo wa thamani kubwa na kwamba vitaongeza uwezo wa hospitali katika kutoa huduma kwa watoto wachanga wanaohitaji uangalizi maalum.
Naye Daktari Bingwa wa Watoto, Dkt. Mohamed Saleh, ameipongeza TAKUKURU kwa kuunga mkono juhudi za hospitali, akieleza kuwa vifaa hivyo vitasaidia wataalam kutoa huduma kwa ufanisi zaidi kwa watoto wachanga.
Uongozi wa Hospitali ya Bombo umeeleza kuwa upatikanaji wa vifaa hivyo ni hatua nyingine muhimu katika kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga na maeneo jirani.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Tanga na viongozi kutoka timu ya Afya ya mkoa wa Tanga ikiongozwa na Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa wa Tanga Bwana Imani Clemence.
Na Mwandishi wetu Idodi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe. Prof, Palamagamba Kabudi amesema Serikali itaendelea kuheshimu na kuthamini mchango wa kiuongozi uliotolewa na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu William Lukuvi.
Hayo ameyasema leo tarehe 15/08/2026 wakati wa maadhimisho ya ibada ya Misa Takatifu ya kumaliza Msiba iliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Idodi Mkoani Iringa na kuhudhuriwa na wananchi na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali.
Alisema, “Enzi za uhai wake Waziri Lukuvi alinisaidia kufahamu shughuli mbalimbali za Bunge na serikali na hivyo kupata weledi mzuri mambo mengi kutokana na uzoefu aliyokuwa nao,”
Aidha uwezo wake wa kusimamia nidhamu ipasavyo Bungeni ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na Bunge ilimfanya aendelee kuaminiwa katika kazi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu.
Kwa Upande Mama Germana Lukuvi Mjane wa Marehemu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe, Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushikamana na familia tangu walipopata msiba.
Awali Mbunge wa Isimani Mhe, Emanuela Mtatifikolo alisema Marehemu Lukuvi ataendelea kuishi kwenye mioyo ya wananchi wa Isimani, kwa mageuzi makubwa ya maendeleo aliyoyafanya.
“Uwakilishi wake kwa wananchi wa Jimbo la isimani na kwa kushirikiana na Serikali aliwezesha Jimbo la Isimani kunufaika na ujenzi wa barabara ya lami uimarishaji wa Huduma za afya na kuendelea kuboresha miundo mbinu ya elimu sambamba na umeme,” alibainisha
Wahadzabe ni kabila linalopatikana mkabala na ziwa Eyasi pembezoni mwa hifadhi ya Ngorongoro na habari za maisha yao zimehifadhiwa katika makumbusho ya Urithi Jiopaki liyopo Karatu Mkoani Arusha.
Pamoja na mabadiliko ya ulimwengu na elimu kutolewa lakini kabila hili bado haliamini katika tohara kwa kijana wa kiume, kwao hiyo ni mwiko wakiamini binadamu anastahili kuwa kama alivyozaliwa.
Sababu kubwa ya kutokutahiriwa ni kuwa ukitahiriwa unapunguza nyama ya binadamu na kuizika wakati binadamu huyo akiwa hai, imani ni kwamba huwezi kata sehemu yoyote ya mwili wa binadamu aliye hai
Vilevile kabila hili linaamini kwamba mwanaume akitahiriwa hupunguza ukubwa na utaalam wa mambo na kufanya mwili wako kuwa na mapungufu hata wakati wa kushiriki tendo la ndoa.
Katika kuhakikisha kwamba mwanaume anakuwa na nguvu za kutosha wakati wa kushiriki tendo la ndoa hulazimika kula mizizi inayopatikana porini , matunda, asali ikiwa fresh na nyama pori ambayo inachomwa au kuchemshwa supu.
Kutokana na kutokutahiriwa Wahadzabe wanaamini kwamba miili yao huwa na nguvu ya kupambana na mnyama yoyote porini na hiyo ndiyo heshima ya mwanaume kamili ambaye hata anapochumbia kutaka kuoa hupimwa kwa uwezo wa kuwinda na kuleta chakula cha familia.
Hii ni sehemu ya maajabu ya maisha makabila wanaunda Ngorongoro Global Geopark ambapo licha ya Wahadzabe kuendelea kuishi katika ukanda huo lakini taarifa zao zinapatikana katika makumbusho ya Urithi Geopark.
Karibu Nyumbani Ngorongoro upate mshangao wa maajabu na uzoefu usiosahaulika.
MKUTANO MKUU WA TOA WALENGA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050 ILI KUWANUFAISHA WANANCHI
Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma
Mkutano Mkuu wa 16 wa Mwaka wa Taasisi ya Maboresho katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA) unatarajiwa kujadili mchango wa ugatuzi wa madaraka katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku ukilenga kuweka mikakati itakayowezesha wananchi kunufaika zaidi na usimamizi wa maendeleo katika maeneo yao.
Mkutano huo utafanyika Agosti 19–21, 2026 katika Ukumbi wa Jiji la Dodoma, Mji wa Serikali Mtumba, ukiwa na Kaulimbiu isemayo: “Ugatuzi wa Madaraka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ni nguzo madhubuti ya kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa TOA, Bw. Albert Gabriel Msovela, ambaye amesema Mgeni Rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye atauzindua rasmi Agosti 19, 2026.
Bw. Msovela amesema mkutano huo unaendana na maelekezo ya Serikali yanayochagizwa na maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wananufaika na ugatuaji wa madaraka, hususan katika usimamizi wa miradi ya maendeleo na upatikanaji wa huduma bora za kijamii, kama zilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Mkutano huu ni fursa kwa wajumbe kujadili maeneo yaliyoainishwa kwenye Dira, na tutakuwa na mada mbalimbali zitakazowasilishwa na wabobezi. Ninawaomba wananchi waufuatilie mkutano huu utakaokuwa mubashara kupitia vyombo mbalimbali vya habari ili wajue ni kwa namna gani TOA itawashirikisha kwenye ubunifu na usimamizi wa miradi yote, ikiwemo ya afya, elimu na miundombinu ya barabara,” amesema Bw. Msovela.
Aidha, Bw. Msovela amesema mkutano huo unatarajiwa kutoa maazimio na mikakati ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya moja kwa moja kutokana na uwepo wa kikao hicho.
Ametoa wito kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu huo kuhudhuria na kushiriki kikamilifu katika mijadala itakayofanyika, akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kujenga mikakati yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Wajumbe watakaoshiriki katika Mkutano Mkuu huo wa TOA ni Makatibu Tawala wa Mikoa yote 26, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, zikiwemo Jiji, Manispaa na Halmashauri, pamoja na Makatibu Tawala wa Wilaya zote 136 nchini.
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeandaa mtaala maalum wa kozi fupi za recycling kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika sekta ya taka na kuongeza thamani ya taka zinazoweza kurejelewa.
Hayo yameelezwa Agosti 15, 2026 jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Mohammed Omari, wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo katika Chuo cha VETA wilaya ya Bahi.
Amesema hatua hiyo imekuja baada ya tafiti kubaini kuwa baadhi ya vijana wanaojihusisha na shughuli za taka wanakabiliwa na changamoto za kiafya na kiusalama, hivyo kuhitajika kwa mtaala mahsusi utakaowawezesha kukabiliana na mazingira ya kazi.
Dkt. Omari amesema mtaala huo umeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya wadau katika mnyororo wa thamani wa taka, kuanzia ukusanyaji hadi uchakataji, kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, sekta binafsi, vyuo vya walimu na waajiri.
Aidha, amesema VETA inaendelea kushirikiana na wataalamu wa sekta mbalimbali kuunganisha ujuzi wa vitendo na mafunzo ya vyuoni. Ametolea mfano ushirikiano na mtaalamu wa samani, Edo Sama, anayerejeleza zaidi ya asilimia 50 ya mbao zilizokuwa zikitupwa na kuzitumia kutengeneza samani, hivyo kuongeza thamani ya taka na kupunguza upotevu wa rasilimali.
Ameongeza kuwa VETA inaendelea kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, ikiwemo kampuni ya Hans Paul ya Arusha inayotengeneza magari ya utalii, ili kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi wa vitendo. Amesema hatua hiyo inaendana na msisitizo wa Serikali wa kushirikisha sekta binafsi katika kukuza ujuzi na ajira kwa vijana.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Aggrey Mwanri (MCC), leo Agosti 15, 2026, amekuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano wa Hadhara wa Jimbo la Ubungo, ulioandaliwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Prof. Kitila Mkumbo, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji.
Kabla ya kushiriki mkutano huo, Ndugu Mwanri alipokewa katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dar es Salaam na Sekretarieti ya CCM Mkoa, chini ya Katibu wa CCM Mkoa, Ndugu Mkandawire.
Aidha, alipokea taarifa fupi kuhusu utendaji wa Chama katika Mkoa huo na kuwashukuru viongozi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa usimamizi mzuri wa Chama na Serikali.
Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Mwanri amesisitiza umuhimu wa Wabunge, Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kufanya mikutano ya hadhara mara kwa mara ili kuwapa wananchi mrejesho kuhusu utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa Uchaguzi.
Aidha, amewasihi wananchi kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini.
Kwa upande wake, Prof. Kitila Mkumbo aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM mbele ya wananchi wa Jimbo la Ubungo, akieleza hatua zilizochukuliwa katika kuboresha miundombinu, hususan sekta ya barabara.
Prof. Kitila amesema ataendelea kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi na Serikali katika kuhakikisha wananchi wa Ubungo wanaendelea kupata huduma na maendeleo yanayostahili.
KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE.





























