Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amekitaka Chama cha Wazee Wanaume Tanzania (CCWWT) kutokuwa chama cha harakati, bali kutumia nafasi yake katika kutoa ushauri, kupatanisha jamii, kulea watoto na vijana, pamoja na kuhifadhi mila na desturi za Kitanzania.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo Agosti 29, 2026, katika Ukumbi wa St. Gaspar jijini Dodoma, wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa CCWWT kwa mwaka 2026, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

Amesema wazee wana nafasi ya kipekee katika jamii ya Kitanzania kutokana na heshima na hadhi waliyonayo, akieleza kuwa wamekuwa walinzi wa mila na desturi, washauri, wapatanishi na walezi wa watoto, vijana na jamii kwa ujumla.

“Wazee mna kazi kubwa na ya msingi ya kuhifadhi mila na desturi za Kitanzania, kuwa washauri na wapatanishi wazuri katika jamii, ikiwa ni pamoja na walezi wa jamii ya Kitanzania, hivyo, tekelezeni majukumu ya chama chenu kwa mujibu wa katiba yenu,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua wazee kama rasilimali na hazina kubwa katika maendeleo ya taifa, akibainisha kuwa uwepo wa Tanzania kama taifa ni kielelezo cha mchango mkubwa uliotolewa na wazee katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Prof. Shemdoe amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha maisha ya wazee nchini, sambamba na kuimarisha mifumo ya utoaji huduma kwa makundi yote bila ubaguzi. Ametaja miongoni mwa hatua hizo kuwa ni kuwekwa kwa mifumo ya kisheria inayolenga kuimarisha upatikanaji wa huduma, ikiwemo kutungwa kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote Na. 13 ya Mwaka 2023.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amesema Tanzania imefikia hatua ilipo leo kutokana na mchango mkubwa wa wazee ambao ni tunu ya taifa.

Amesema wazee wamejenga familia, wamelea watoto, wamefundisha vijana, wamejenga taasisi na kulitumikia taifa, hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya nchi. Kwa msingi huo, amesema taifa linapaswa kutumia ipasavyo maarifa, uzoefu na hekima walizonazo wazee kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Akizungumza kwa niaba ya wazee, Katibu Mkuu wa CCWWT, Bw. Flavianus Lughuyu, amesema licha ya wazee kuacha alama kubwa katika historia ya taifa, bado kuna haja ya kujenga mifumo imara ya kuwaenzi na kutambua mchango wao.

Amesema historia na uzoefu wa wazee vinapaswa kutumika kama nyenzo ya kujenga maadili kwa vijana, ili kutambua kuwa kulitumikia taifa kwa uaminifu kuna thamani hata baada ya mtu kustaafu.

Mkutano huo umebeba Kaulimbiu isemayo: “Wazee ni Tunu, Tuwatunze kwa Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii.”

Kaulimbiu hiyo imekuja wakati muafaka ambapo Tanzania imeanza utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, sambamba na utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Wazee ya Mwaka 2003, Toleo la Mwaka 2024.














Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija Nassir Ali, amewataka wananchi wa Mkuranga kuhakikisha wanalinda miundombinu ya gesi asilia iliyojengwa katika maeneo yao ili iweze kudumu na kuwanufaisha wananchi pamoja na taifa kwa ujumla.

Na Mwandishi Wetu, MOROGORO WANANCHI waliotembelea banda la Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) katika Maonesho ya Utamaduni, wameeleza kufurahishwa na elimu wanayoipata kuhusu majukumu ya Wakala katika kuratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.

Wananchi hao wamesema maonesho hayo yamekuwa fursa muhimu kwao kupata uelewa kuhusu Mfumo wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (Bulk Procurement System – BPS), namna mafuta yanavyoagizwa nchini na nafasi ya PBPA katika kuratibu mchakato huo.

Bi. Maria Ngilisho, mmoja wa waliotembelea banda hilo, alisema elimu hiyo imemsaidia kuelewa mchakato wa upatikanaji wa mafuta nchini, ambao awali hakuwa na ufahamu wa kutosha kuuhusu.

“Nimefurahi kupata elimu hii kwa sababu tumekuwa tukitumia mafuta kila siku, lakini hatukuwa tunafahamu mchakato unaofanyika hadi mafuta yanapofika nchini. Sasa nimeelewa kuwa kuna taasisi kama PBPA inayoratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja,” alisema Ngilisho.

Naye, Bw. Michael Maganga, alisema mawasiliano ya ana kwa ana na watumishi wa PBPA yamewapa wananchi nafasi ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa moja kwa moja kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mafuta.

“Elimu tunayopata hapa ni muhimu sana kwa sababu tunapata nafasi ya kuuliza maswali yanayotuhusu kama watumiaji wa mafuta na tunapata majibu kutoka kwa wataalamu. Ni vizuri PBPA kuendelea kutumia maonesho haya kuwafikia wananchi,” alisema Maganga.

Kwa mujibu wa PBPA, miongoni mwa majukumu ya Wakala ni kukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, kuendesha zabuni za kimataifa za ununuzi wa mafuta kwa wingi, pamoja na kuratibu upokeaji na uwasilishaji wa bidhaa hizo nchini. Ushiriki wa PBPA katika maonesho mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Wakala za kuwaelimisha

Ushiriki wa PBPA katika maonesho mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Wakala za kuwaelimisha wananchi kuhusu majukumu yake na nafasi yake katika sekta ya mafuta, huku ukitoa fursa kwa wananchi kupata ufafanuzi kuhusu mchakato wa uagizaji wa mafuta na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa hizo unaendelea kuwa wa uhakika nchini.

Nilikuwa naishi maisha ya maumivu kwa muda mrefu sana. Kila siku nilikuwa naamka nikiwa na uchovu, maumivu ya mwili, na hali ya kutokuwa sawa bila kuelewa chanzo chake.

Nilizunguka hospitali nyingi nikitafuta majibu.

Vipimo vilifanyika, dawa nikapewa, lakini hali haikubadilika. Wakati mwingine nilihisi nafuu kidogo, lakini baadaye maumivu yalirudi tena. Maisha yangu yalibadilika kabisa. Nilishindwa kufanya kazi vizuri, hata mambo madogo yalikuwa magumu kwangu.

Nilianza kukata tamaa na kuona kama hii ndiyo hali yangu ya maisha milele.
Siku moja nilimweleza jirani yangu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa kwenye maumivu makubwa baada ya kuachwa na mtu niliyempenda kwa moyo wangu wote. Ilikuwa ni miaka mingi ya ukimya, maumivu, na maswali yasiyo na majibu.

Nilijaribu kusonga mbele, lakini kila mara nilijikuta nikikumbuka yale tuliyokuwa nayo.

Ilikuwa ngumu sana kumtoa kabisa moyoni mwangu. Baada ya muda, nilianza kukubali kwamba labda mambo yameisha kabisa na sina tena nafasi ya kurekebisha chochote. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu hisia zangu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilianza biashara yangu ndogo nikiwa na matumaini makubwa sana. Nilikuwa na ndoto ya kuibadilisha familia yangu kupitia juhudi zangu mwenyewe. 

Lakini mambo hayakuenda kama nilivyotarajia. Kila nilipoanza kitu kipya, kilikuwa kinaanza vizuri lakini baadaye kinaporomoka ghafla.

Nilijikuta nikirudia mwanzo mara kwa mara bila mafanikio. Hali hiyo ilinifanya niwe na huzuni na kukata tamaa. 

Wakati mwingine nilijiuliza kama nilichagua njia sahihi maishani. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu changamoto yangu. SOMA ZAIDI.

 


Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za Msingi na Sekondari jijini Mwanza wameomba Wakala wa Vipimo (WMA) kuanzisha Klabu za Vipimo katika shule za Mkoa huo.

Ombi hilo wamelitoa leo Jumamosi, Agosti 29, 2026 walipotembelea banda la WMA katika Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea viwanja vya Furahisha, Jijini Mwanza.

Ili kuthibitisha kiu yao ya elimu ya vipimo, mwanafunzi mmoja kutoka Shule ya Msingi Ghana, Ibrahim Omary, alijitolea na kupewa fursa ya kutoa elimu ya vipimo kwa wanafunzi wenzake na wananchi waliotembelea banda hilo. Aliifanya kazi hiyo kwa ufasaha mkubwa na kupata pongezi.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Ibrahim alisema: 

“Tuliona kwenye vyombo vya habari wanafunzi wenzetu jijini Dodoma ambao wako katika Klabu za Vipimo wakitoa elimu ya vipimo, tukavutiwa sana. Nasi tunaomba WMA waanzishe klabu hizo kwa shule za Mwanza ili nasi tupate elimu hiyo kwa kina.”

Wanafunzi hao wameahidi kuwa mabalozi wa WMA katika jamii zao kwa kuelimisha wenzao, familia na majirani kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi ya vipimo. Wengi wao wamesema ndoto yao ni kuwa Maafisa Vipimo.

Akijibu ombi hilo, Meneja Mawasiliano wa WMA, Bi. Veronica Simba amewaahidi wanafunzi hao kuwa Wakala utaanzisha Klabu za Vipimo katika shule za Mkoa wa Mwanza na hatua kwa hatua katika mikoa mingine yote nchini.

“Lengo letu ni kufikisha elimu ya vipimo kwa watoto tangu awali. Kupitia klabu hizi tunajenga kizazi cha wafanyabiashara na watumiaji wanaojali haki na usawa katika biashara,” amesema Bi. Simba.

Wanafunzi na wananchi wengine wameendelea kufurika katika banda la WMA katika siku ya pili ya maonesho hayo. Wamesema wameridhishwa na elimu wanayopata kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi ya vipimo.

Maonesho hayo yameanza tarehe 28 Agosti 2026 na yanahitimishwa tarehe 6 Septemba 2026 yakiwa na  kaulimbiu "Usalama na Amani ni Kichocheo cha Biashara na  Uwekezaji hapa Nchini".  

Katika  Maonesho hayo, WMA inatumia kaulimbiu isemayo “Vipimo Sahihi ni Msingi wa Usalama, Amani na  Uwekezaji wa Biashara ”.

KAHAMA

Baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi (NEEC) limetoa wito kwa wananchi wa manispaa ya Kahama hususan wakazi wa kata ya Mwendakulima kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo katika kituo cha mafunzo ya kilimo kilichopo kata ya mwendakulima wilayani Kahama mkoani Shinyanga kilicholenga kuwainua wananchi katika sekta ya kilimo.
Na Mwandishi Wetu

MKAZI wa mtaa wa Unyasini katika Kata ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam Yahaya Kizenga amemuomba Rais DK.Samia Suluhu Hassan kupitia kwa Mkuu wa mkoa huo Albart Chalamila kuwasaidia kupata haki ya eneo la aridhi ambalo kuna watu wamevamia wakitaka kuwadhulumu.


Na TAEC
Dodoma


Kila mwaka tarehe 29 Agosti, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Majaribio ya Nyuklia (International Day against Nuclear Tests), ikiwa ni fursa ya kutafakari madhara yaliyosababishwa na majaribio ya silaha za nyuklia na kuendelea kuhimiza juhudi za kujenga dunia yenye amani na usalama.

Siku hii ilianzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2009 kupitia Azimio Na. 64/35, kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu madhara ya majaribio ya silaha za nyuklia na umuhimu wa kuyasitisha. Tarehe 29 Agosti pia ina umuhimu wa kihistoria kutokana na kufungwa kwa eneo la majaribio ya nyuklia la Semipalatinsk nchini Kazakhstan mwaka 1991.

Tangu jaribio la kwanza la silaha ya nyuklia mwaka 1945, zaidi ya majaribio 2,000 yamefanyika duniani, yakiacha historia ya madhara kwa afya ya binadamu, mazingira na usalama wa dunia.

Katika kuadhimisha siku hii, Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) inaungana na jumuiya ya kimataifa kupinga majaribio ya silaha za nyuklia na kusisitiza matumizi salama, yenye uwajibikaji na ya amani ya sayansi na teknolojia ya nyuklia.

Ni muhimu kuelewa kuwa kupinga majaribio ya silaha za nyuklia si kupinga teknolojia ya nyuklia. Teknolojia hii inapotumika kwa madhumuni ya amani na chini ya mifumo madhubuti ya usalama na udhibiti, ina mchango mkubwa katika kuboresha maisha na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Nchini Tanzania, TAEC ina jukumu la kusimamia na kudhibiti matumizi salama ya vyanzo vya mionzi pamoja na kuhamasisha matumizi ya amani ya teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, kilimo, mifugo, viwanda, migodi, maji, utafiti, mazingira na nishati.

Katika afya, teknolojia ya mionzi inatumika katika uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali; katika kilimo na mifugo inachangia katika utafiti, uboreshaji wa uzalishaji na udhibiti wa baadhi ya wadudu na magonjwa. Mbinu za nyuklia pia zina matumizi muhimu katika tafiti za rasilimali za maji, viwanda, migodi na maeneo mengine ya maendeleo.

Kwa msingi huo, tunapaswa kutofautisha kati ya matumizi ya nyuklia kwa madhumuni ya kijeshi na matumizi yake kwa madhumuni ya amani. Hofu inayotokana na madhara ya silaha za nyuklia isiwe sababu ya kuiona teknolojia yote ya nyuklia kama tishio.

TAEC itaendelea kuhakikisha matumizi ya vyanzo vya mionzi nchini yanafanyika kwa kuzingatia sheria na viwango vya usalama ili kuwalinda wafanyakazi, wagonjwa, wananchi na mazingira. Tutaendelea pia kutoa elimu kwa umma ili kuondoa dhana potofu na kuongeza uelewa kuhusu manufaa ya matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia.

Tunapoadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Majaribio ya Nyuklia, tunatoa wito kwa wananchi kuendelea kupata taarifa sahihi na kuunga mkono matumizi salama na ya amani ya teknolojia ya nyuklia kwa manufaa ya Taifa na ustawi wa binadamu.

Ujumbe wetu ni wazi: HAPANA kwa majaribio ya silaha za nyuklia; NDIYO kwa matumizi salama na ya amani ya teknolojia ya nyuklia kwa maendeleo ya Taifa.

“Mionzi kwa Matumizi Salama na Teknolojia ya Nyuklia kwa Maendeleo ya Taifa.”
Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Magharibi limeteketeza tani 3.4 za unga wa mahindi uliokuwa chini ya kiwango, wenye thamani ya takribani Sh. milioni 3.5, baada ya vipimo vya maabara kubaini kuwa haukidhi viwango vya usalama kwa matumizi ya binadamu.

 

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umeeleza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja umeendelea kuhakikisha Tanzania inapata bidhaa za mafuta kwa uhakika, kwa wakati na kwa gharama shindani.

Akizungumza katika Maonesho ya Nne ya Kitaifa ya Utamaduni yanayoendelea mkoani Morogoro, Mchumi wa PBPA, Bw. Henry Kilenga, amesema mfumo huo unahusisha ukusanyaji wa mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta nchini kabla ya kutangazwa kwa zabuni za kimataifa.

Amesema PBPA hukusanya mahitaji hayo na kuyaunganisha ili mafuta yaagizwe kwa pamoja kwa kiwango kikubwa. Utaratibu huo huiwezesha nchi kunufaika na ununuzi wa pamoja na kupata gharama shindani za uagizaji na usafirishaji.

“PBPA hukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, huandaa zabuni na kuwashindanisha wazabuni waliokidhi vigezo. Utaratibu huu unasaidia kuhakikisha nchi inapata mafuta kwa uhakika na kwa gharama shindani,” amesema Kilenga.

Amefafanua kuwa zabuni hizo hushirikisha kampuni za kimataifa zilizohakikiwa na kukidhi vigezo vilivyowekwa na PBPA. Wazabuni hushindanishwa kwa uwazi, huku tathmini ikizingatia bei zilizowasilishwa, uwezo wa kusambaza mafuta na masharti mengine ya zabuni.

Kwa mujibu wa Kilenga, baada ya kukamilika kwa tathmini, kampuni zilizokidhi vigezo na kuwasilisha bei nzuri huchaguliwa kuleta mafuta nchini kulingana na kiasi na muda uliopangwa.

Kilenga amesema uwazi na ushindani katika uendeshaji wa zabuni unalenga kulinda maslahi ya taifa, kuongeza ufanisi na kuhakikisha bidhaa za mafuta zinaendelea kupatikana kwa ajili ya wananchi na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Amesisitiza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja una mchango mkubwa katika kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Katika umri wa utu uzima, utulivu wa ndoa na furaha ya mke na mume ni nguzo kuu ya amani ya familia. 

Hata hivyo, pale uwezo wa kutimiza tendo la ndoa unapotoweka ghafla na kukuacha ukiwa huna nguvu wala uwezo wa kumridhisha mwenza wako, heshima na kujiamini kama mwanamume husambaratika kwa kasi kubwa.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia maumivu makubwa ya nafsi na fedheha ya siri ndani ya nyumba yangu. 

Mwanamume niliyestahiwa na jamii na kupata mafanikio ya kimaisha, nilijikuta ghafla nikishindwa kabisa kutimiza wajibu wangu wa ndoa.

Kila nilipojaribu kusogelea kitanda cha mke wangu, mwili ulilegea na kukosa ushirikiano kabisa. Mke wangu, ambaye mwanzoni alijitahidi kuwa mvumilivu, alianza kubadilika taratibu; alianza kunionyesha dharau, kunipazia sauti kwa mambo madogo, na mara kwa mara kunipigia pasi za maskhara zilizoniumiza sana chembe za moyo.

Nilitumia dawa mbalimbali za viwandani na hospitali zilizokuwa zikaniongezea tu mapigo ya moyo bila kutoa suluhu ya kudumu. Nilibaki nikikabiliwa na msongo mkubwa wa mawazo na hofu ya kuachwa au kusalitiwa. SOMA ZAIDI.
Katika umri wa utu uzima, furaha kuu ya mzazi ni kushuhudia watoto uliowalea kwa shida na tabu wakikua kwa nidhamu, heshima, na kuwa nguzo ya familia.

Hata hivyo, pale mtoto wako wa kwanza ambaye ndiye tegemeo na mfano kwa wadogo zake anapogeuka ghafla, kuanza kukudharau, na kutumbukia kwenye matumizi ya dawa za kulevya, amani ya nyumba hutoweka kabisa.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia maumivu makubwa ya nafsi kutoka kwa mwanangu mkubwa aliyekuwa na umri wa miaka 24.

​Kijana aliyekuwa na nidhamu ya hali ya juu na aliyefaulu masomo yake kwa kiwango kizuri, alianza kubadilika kwa kasi ya ajabu.

Alijiunga na makundi mabaya ya mtaani, akaanza kuvuta bangi na kutumia dawa kali za kulevya. Kila nilipojaribu kukaa naye na kumshauri kama mzazi, alinijibu kwa matusi makali, kunipazia sauti, na hata kutishia kunipiga.

Numba yetu iligeuka kuwa chumba cha mateso; alipoteza kazi yake, akaanza kuiba vitu vya nyumbani na kuuza ili apate fedha za kununulia dawa hizo.

Nilibaki nikilia usiku na mchana, nikiona maisha ya mwanangu yakisambaratika na heshima ya familia yetu ikipotea mbele ya jamii. SOMA ZAIDI.
Uwekezaji katika majengo ya kupanga na biashara za nyumba ni miongoni mwa malengo makubwa ya kiutu uzima yanayotoa uhakika wa kipato na usalama wa kimaisha katika uzee.

Hata hivyo, pale unapoweka akiba zako zote za maisha na kujenga jengo la kifahari, kisha linakaa wazi miaka miwili bila mpangaji hata mmoja kujitokeza, maisha hugeuka kuwa chanzo cha msongo mkubwa wa mawazo na madeni yasiyolipika.

Baada ya kustaafu na kumaliza ujenzi wa jengo langu la ghorofa lenye vyumba vya biashara na makazi, nilikuwa na matumaini makubwa ya kuanza kuvuna matunda ya jasho langu.

​Hata hivyo, mambo yalikwenda tofauti kabisa na matarajio yangu. Kwa zaidi ya miaka miwili, hakuna mpangaji aliyetaka kupanga kwenye jengo hilo. 

Watu wengi walikuwa wakipita na kuangalia, wengine wakiulizia bei na kuahidi kurudi, lakini walipotoka tu hapo hawakurejea tena.

Wakati huo huo, majengo mengine ya majirani yaliyokuwa ya kizee na yasiyo na miundombinu mizuri yalikuwa yakipata wapangaji kila siku.

Nilibaki nikilipa kodi za ardhi na ulinzi kutoka mfukoni mwangu bila kuingiza hata sarafu moja, huku madeni ya benki yakianza kunisonga na kutishia kupiga mnada uwekezaji wangu wote. SOMA ZAIDI.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Dkt. Evaline Munisi (wa tatu kutoka kushoto) akizindua rasmi Ughaibuni Loan wakati wa hafla ya kuwaaga Watanzania wanaokwenda kufanya kazi nje ya  nchi, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB, Palm Beach Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Agosti, 2026.
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar imeupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kazi kubwa inayofanya katika kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za bima ya afya nchini, pamoja na ushirikiano wake na Mfuko wa Huduma za Afya Zanzibar (ZHSF).

Pongezi hizo zimetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mariam Hamis Said, wakati Kamati hiyo pamoja na Menejimenti za ZHSF na NHIF ilipotembelea Makao Makuu ya NHIF kwa ajili ya kujifunza namna Mfuko huo unavyoendesha na kutoa huduma kwa wanachama.

Mhe. Mariam amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa, kwa kuwa Kamati imepata fursa ya kuelezwa na kujionea kwa vitendo mifumo na huduma zinazotolewa na NHIF, kupitia ziara kwenye Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH).

Pamoja na kutoa pongezi kwa NHIF, Kamati hiyo ilipata fursa ya kutaka kufahamu kwa kina masuala mbalimbali yanayohusu uendeshaji na maendeleo ya Mfuko, ikiwemo namna NHIF inavyopambana na udanganyifu, utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wanachama wanapata huduma bora na kwa wakati.

Aidha, Kamati ilitaka kufahamu namna matumizi ya TEHAMA yameboresha utendaji wa NHIF na kusaidia kupunguza gharama za uendeshaji, pamoja na namna uwekezaji unavyosaidia kuimarisha Mfuko.

Masuala mengine yaliyotiliwa mkazo ni pamoja na vyanzo vya mapato ya Mfuko, viashiria vinavyotumika kupima mafanikio na uendelevu wa NHIF, pamoja na mafunzo na uzoefu ambao Mfuko umeupata katika kipindi cha miaka 25 ya utekelezaji wa majukumu yake.

Amesema ushirikiano kati ya NHIF na ZHSF umeleta matokeo makubwa katika hatua mbalimbali za uanzishaji na uendelezaji wa ZHSF, huku akieleza kuwa uzoefu na msaada uliotolewa na NHIF umeiwezesha Zanzibar kuanza na kuendelea vizuri katika safari ya kuimarisha huduma za bima ya afya.

“Kamati inapongeza NHIF na ZHSF kwa mashirikiano makubwa wanayoyafanya ambayo yamewezesha ZHSF kuanza na kuendelea vizuri,” amesema Mhe. Mariam.

Ameongeza kuwa kazi iliyofanywa na NHIF katika kusaidia uanzishaji wa ZHSF ilihitaji uvumilivu na kujitolea kwa kiwango kikubwa, akieleza kuwa Zanzibar imenufaika na uzoefu wa NHIF katika kujenga mfumo wa bima ya afya.

“Kazi iliyofanywa na NHIF ni kazi iliyofanyika kwa uvumilivu mkubwa, lakini kwa kutubeba Zanzibar katika uanzishaji wa Mfuko wetu,” amesema.

Aidha, Mhe. Mariam ameipongeza Menejimenti ya NHIF kwa kuwawezesha kutembelea Hospitali ya Benjamin Mkapa, ambako wamejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa.

Amesema ziara hiyo imewapa fursa ya kuona kwa vitendo ubora wa huduma zinazotolewa, hususan huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, ambayo ni mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha huduma za afya nchini.

“Tumejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa. Hakika kazi hii ni kubwa na nzuri ambayo kwa ujumla tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, ambapo huduma za kibingwa na kibingwa bobezi zinapatikana hapa nchini,” amesema. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, amesema Mfuko utaendelea kushirikiana kwa karibu na ZHSF ili kuhakikisha wananchi na wanachama wanapata huduma bora za afya kwa wakati na kwa ufanisi.

Dkt. Isaka amesema NHIF itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa ZHSF, hususan katika maeneo ya uzoefu, mifumo ya utoaji huduma na masuala mengine ya kitaalamu, kwa lengo la kuimarisha huduma za bima ya afya kwa wananchi wa Zanzibar.

Amesema ushirikiano huo ni sehemu ya dhamira ya NHIF ya kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa wananchi popote walipo nchini, huku mifuko hiyo ikiendelea kujifunza na kubadilishana uzoefu katika kuboresha huduma kwa wanachama.

Ziara hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu baina ya taasisi zinazohusika na utoaji wa huduma za bima ya afya Tanzania Bara na Zanzibar.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!