Wakala wa Vipimo (WMA) umetoa wito kwa Maafisa wanaosimamia  ununuzi na ugavi katika taasisi za umma na binafsi kuhakikisha vifaa vyote vinavyohusiana na vipimo vinawasilishwa WMA kwa ajili ya uhakiki kabla ya kupelekwa kwa watumiaji.

Akizungumza leo Septemba 2, 2026 katika Maonesho ya 21 ya  Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Uwanja wa Furahisha  jijini Mwanza, Afisa Ugavi wa WMA, Bi. Rehema Komba amesema ni vema taasisi zinapokamilisha ununuzi wa vifaa vya kivipimo,  zisivipeleke moja kwa moja kwa watumiaji bila kuhakikiwa, kwani inaweza lkupelekea hasara kwa serikali na wananchi.

"Tunasimamia mchakato wa manunuzi, lakini baada ya vifaa kufika, tuzikumbushe taasisi zetu kupeleka kwanza Wakala wa Vipimo kwa uhakiki. Msiogope kuchelewa kwa siku chache, bali ogopeni hasara ya miaka,"  amesema.

Akifafanua, Bi. Rehema ametoa mfano wa Mamlaka na Kampuni za Maji, ambapo amesema maafisa ugavi katika Mamlaka hizo  wanapaswa kushauri na kuhakikisha mita zote mpya za maji baada ya kununuliwa zinapita WMA kwa uhakiki  kabla ya kufungwa kwa wateja.

"Kama kila afisa ugavi atatoa ushauri huu mara baada ya kukamilisha manunuzi, tutakuwa tumepiga hatua kubwa kuhakikisha kuna biashara ya haki na ulinzi wa walaji nchini" ameongeza.

Mtaalamu huyo wa Ugavi amesema WMA ina mitambo ya kisasa inayowezesha kutoa huduma ya uhakiki wa haraka hali  inayoepusha usumbufu kwa taasisi wakati wa kutoa huduma.

Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yameanza tarehe  28 Agosti na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 6 Septemba, 2026.






Na Mwandishi Wetu

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amewataka wadau wa sekta ya umma na binafsi kuongeza ushirikiano katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia, akisema biashara hiyo inahatarisha uwekezaji, ushindani wa haki na usalama wa watumiaji.

Ngasongwa ameyasema hayo leo Septemba 2, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akimwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, katika Kongamano la Ulinzi dhidi ya Bidhaa Bandia na Uwekezaji lililoandaliwa na Kampuni ya NANOSILIKAN kwa kushirikiana na FCC, TISEZA, TCCIA na TPSF, katika Hoteli ya Johari Rotana.

Amesema bidhaa bandia haziathiri ushindani wa kibiashara pekee, bali pia zinawaumiza wazalishaji wanaofuata sheria ambao hulipa gharama za ubunifu, upimaji, viwango, usajili, ajira na kodi, wakati wazalishaji wa bidhaa bandia huepuka gharama hizo na hivyo kushindana kwa njia isiyo ya haki.

“Katika ushindani wa kawaida, mzalishaji bora au mwenye ufanisi zaidi ndiye anayeshinda. Lakini kwenye bidhaa bandia, anayeshinda ni yule anayekwepa gharama zinazofanya bidhaa iwe halali,” amesema

Ngasongwa amesema athari kubwa zaidi ya bidhaa bandia humwangukia mlaji, akitolea mfano mbegu bandia ambazo mkulima anaweza kugundua tatizo baada ya msimu kupita, dawa ambazo hazitibu ugonjwa uliokusudiwa na vipuri bandia vya magari ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa watumiaji. Alisema kwa kuwa madhara hayo yanaweza kujitokeza kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa, ni muhimu kuweka mifumo ya kuzuia bidhaa bandia kufika kwa mlaji.

Kwa mujibu wa Ngasongwa, utekelezaji wa sheria pekee hauwezi kumaliza tatizo hilo kwa kuwa maafisa wa ukaguzi hawawezi kuwepo katika kila duka na kila muamala nchini, hivyo ni muhimu kuwawezesha walaji kushiriki katika kuthibitisha uhalali wa bidhaa kabla ya kufanya manunuzi. Alisema njia hiyo inaweza kusaidia kuzuia madhara kabla hayajatokea, huku akisisitiza kuwa jukumu la Serikali la kusimamia sheria na kulinda walaji linaendelea.

Aidha, aliwataka wafanyabiashara na wazalishaji kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini bidhaa zao zikighushiwa, kusajili na kutunza kumbukumbu za alama za biashara zao pamoja na kushirikiana katika kutoa taarifa kuhusu wahusika wa biashara ya bidhaa bandia.

Kongamano hilo limewakutanisha wawakilishi wa Serikali, taasisi za udhibiti, sekta binafsi, wafanyabiashara, taasisi zinazohusika na haki miliki pamoja na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kujadili namna bora ya kulinda uwekezaji, wafanyabiashara na walaji dhidi ya athari za bidhaa bandia nchini.

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Ubungo jijini Dar es Salaam limeendelea na operesheni yake maalum ya kuwabaini na kuwachukulia hatua wateja ambao wanatumia umeme bila kulipia wakiwa wameunganishiwa umeme na vishoka mtaani kinyume na utaratibu.
Kuingia kwenye ndoa na kuishi na mume wako kwa miaka kumi bila kufanikiwa kupata mtoto ni jaribu zito linaloweza kuvunja moyo na kubomoa amani ya nyumba yoyote.

Kwa miaka yote hiyo, nilipitia maumivu makubwa ya nafsi, dharau kutoka kwa ndugu wa mume, na kejeli za majirani waliokuwa wakiniona kama mwanamke aliyelaaniwa.

Nilitembelea hospitali mbalimbali kubwa na kufanyiwa vipimo vya kila aina, lakini madaktari wote walibainisha kuwa mimi na mume wangu hatukuwa na tatizo lolote la kiafya.

Pamoja na majibu hayo mazuri ya hospitali, kila mwezi ulipopita bila kuona dalili za ujauzito, maumivu na kilio cha siri vilizidi kutawala maisha yangu huku ndoa yangu ikianza kutikisika na kutishia kuvunjika.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na nikikaribia kukata tamaa kabisa ya kuitwa mama, mama yangu mdogo alinitembelea na kunieleza ukweli ambao wanakijiji wengi wanaufahamu.

Aliniambia kuwa tatizo la kukosa mtoto huku vipimo vya hospitali vikiwa safi mara nyingi hutokana na tumbo la uzazi kufungwa kishirikina na watu wenye wivu, au nyota ya uzazi kufunikwa na ukungu wa giza. SOMA ZAIDI.
Kushtakiwa kwa uongo na kukabiliwa na kesi ya dhuluma mahakamani ni miongoni mwa majaribu mazito yanayoweza kuharibu maisha na amani ya mtu kwa muda mfupi.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia mateso makubwa ya nafsi baada ya wafanyabiashara fulani wenye fedha na ushawishi kunibambikizia kesi feki ya madai na fraud ili kuninyang’anya ardhi na uwekezaji wangu wa maisha yote.

Kila nilipofika mahakamani, mambo yalionekana kuniemea; mashahidi wa uongo walipangwa kunishuhudia vibaya, na mawakili wangu walionekana kuzidiwa nguvu.

Nilibaki nikikabiliwa na hofu kubwa ya kupoteza mali zangu zote na hata kufungwa jela kwa kosa ambalo sikuwahi kulifanya. SOMA ZAIDI.
Kumpoteza mtoto mdogo aliyetoka kucheza mlangoni kisha akatoweka kama moshi ni maumivu makubwa zaidi yanayoweza kumpata mzazi yeyote maishani. Siku hiyo ilianza kama siku nyingine zote za kawaida, lakini kufikia jioni, mwanangu wa miaka mitano hakuonekana tena eneo la nyumbani.

Tulitafuta kila kona ya mtaa, tukauliza majirani na ndugu, na hatimaye kutoa taarifa kituo cha polisi, lakini siku zilivyoenda ndivyo matumaini ya kumpata mtoto wangu wa pekee yalivyozidi kutoweka.

Kwa wiki mbili mtawalia, nyumba yetu ilitawaliwa na kilio na simanzi nzito, nikishindwa kula wala kulala huku mawazo mabaya ya kwamba huenda ameuawa au kuchukuliwa na watu wabaya yakinichoma sana moyoni.

​Nikiwa kwenye maumivu hayo makali na polisi wakiwa hawana majibu ya kueleweka, bibi mmoja wa mtaani kwetu alinitembelea na kuninong’oneza kuwa kutoweka kwa mtoto mazingira ya ajabu mara nyingi hutokana na mikono ya chuma ulete au wachawi wanaowatwaa watoto kishirikina. SOMA ZAIDI.



Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akizindua Programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) katika eneo la Nyamongo, mkoani Mara, inayolenga kupanua fursa za maeneo ya uchimbaji, taarifa za kijiolojia na leseni kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.













Helikopta ikifanya utafiti wa madini kwa njia ya anga katika eneo la Nyamongo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya MBT, hatua itakayosaidia kupata taarifa za kijiolojia kwa ajili ya utafiti wa kina na uchorongaji katika maeneo yaliyotengwa kwa wachimbaji wadogo.





 

 

  

Na Mwandishi Wetu.

 Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imekutana na kufanya mazungumzo na watangazaji na waandaaji wa kipindi cha Good Morning kinachorushwa na Wasafi FM, ambapo imewakumbusha umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya uandishi wa habari katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kikao hicho kimefanyika leo, Septemba 2, 2026, katika Makao Makuu ya JAB, Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam, kikilenga kuimarisha uelewa wa watangazaji hao kuhusu misingi ya weledi, uwajibikaji na matumizi sahihi ya majukwaa ya habari.

Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amefafanua matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229; Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Sura ya 306; pamoja na kanuni zake zinazopaswa kuzingatiwa katika utayarishaji na utangazaji wa maudhui.

Wakili Kipangula ameeleza kuwa kuzingatia sheria na maadili ni msingi wa kulinda heshima ya taaluma, haki za watu wanaohusika katika maudhui na imani ya jamii kwa Waandishi wa Habari.
Baada ya mazungumzo hayo, watangazaji wakongwe Gelard Hando na Hilary Mtuta, maarufu kama Zembwela, walikabidhiwa vitambulisho vyao vya ithibati ya uandishi wa habari baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Makabidhiano hayo yamekamilisha hatua ya kuwatambulisha rasmi kama Waandishi wa Habari wenye ithibati, wenye wajibu wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, maadili na uwajibikaji.








By Our Correspondent

ARUSHA: The future of education will not be shaped by technology alone, but by teachers who understand how to use it to improve the way learners are taught, assessed and supported.

This is the message emerging from a four-day training on the ICT Competency Standards for Teachers in Tanzania (ICT-CSTT) for teachers from Arusha City Council (Arusha CC) and Arusha District Council (Arusha DC), where participants are being challenged to look beyond traditional approaches and prepare for an increasingly digital education environment.





The training is being conducted through collaboration between the United Nations Educational, Scientific and Cultural Organisation (UNESCO), the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Tanzania Institute of Education (TIE), and the Prime Minister’s Office through TAMISEMI.

For Watson Gibson Mtewele, a Curriculum Developer for Computer Science at TIE, the purpose of such training goes beyond teaching teachers how to use individual digital applications.





He said it was about helping teachers understand how technology, including artificial intelligence (AI), can be used purposefully to strengthen teaching, learning and assessment.

Mr Mtewele said digital assessment tools such as Kahoot could make assessment more interactive and enable teachers to provide learners with immediate feedback.





“When teachers use these tools as assessment instruments, they can simplify teaching and learning, particularly by enabling learners to receive immediate feedback during assessment,” he said.

He explained that the value of such tools lies in the information they give teachers about learners’ understanding.





Instead of waiting until the end of a topic, term or examination period to discover that learners have struggled with a particular concept, a teacher can use assessment information to identify learning gaps earlier and provide additional support.

FROM ASSESSMENT TO ACTION

Mr Mtewele said teachers attending the training had also been introduced to Google Forms, enabling them to prepare questions, administer assessments, receive learners’ responses and follow up on their performance.

The information generated through such assessments, he said, can also help teachers communicate learners’ progress appropriately with parents and strengthen cooperation between schools and families.

This changes the role of assessment from simply recording marks to generating information that can guide teaching decisions.

A teacher can see what learners have understood, identify areas of difficulty and determine whether to reteach a concept, provide additional exercises or move forward with the lesson.





For teachers, therefore, digital competence can translate into more informed teaching, quicker feedback and better opportunities to support learners according to their needs.

THE TEACHER MUST KEEP LEARNING

But Mr Mtewele said technology alone would not transform education.

He challenged teachers to change their mindset and embrace continuous professional learning, particularly when many educational resources and learning opportunities are increasingly available online.

He warned that teachers who deliberately refuse to acquire new skills risk becoming less prepared for the changing learning environment.

“The learner of the coming years will not necessarily need the same teaching approaches that have been used in the past. Teachers must therefore be ready to change as the education environment changes,” he said.

He stressed that the growing use of AI and digital technologies should not be interpreted as replacing teachers.

Rather, he said, technology should strengthen the teacher’s ability to prepare lessons, assess learners, provide feedback, access educational resources and make informed decisions about instruction.

Teachers who embrace continuous learning, he said, stand to benefit from wider access to educational resources, improved digital confidence, more engaging assessment approaches and the ability to respond more quickly to learners’ needs.

Those who refuse to adapt, however, risk relying on approaches that may increasingly fail to respond to the changing needs of learners and the demands of the education system.

WHY THE TRAINING MATTERS

The training comes at a time when Tanzania is placing increasing emphasis on digital transformation in education.

The Education and Training Policy of 2014, 2023 Edition, together with the National Digital Education Strategy and the National Guidelines for Artificial Intelligence in Education, provides a policy and strategic direction for the growing role of technology in education. The Ministry of Education has officially published these documents alongside the ICT Competency Standards for Teachers in Tanzania.

The National Digital Education Strategy specifically identifies areas such as ICT integration in the curriculum, digital content, digital assessment and emerging technologies as requiring strengthened ICT competencies among teachers.

This places teachers at the centre of Tanzania’s digital education transformation.

For UNESCO and its Government partners, strengthening teachers’ capacity is therefore not simply about introducing technology into schools.

It is about ensuring that teachers have the knowledge and confidence to use technology responsibly and meaningfully to improve learning outcomes.

LOOKING TOWARDS VISION 2050

The importance of that preparation becomes even clearer when viewed against Tanzania Development Vision 2050, which places human development, science and technology and digital transformation among the drivers of the country’s long-term development.

The ICT Competency Standards for Teachers link teacher digital competence directly with the ambitions of Vision 2050, including the goal of having Tanzanians who are competent and confident creators and users of digital products and services.

For that vision to become a reality, digital competence cannot begin with learners alone.

It must begin with the people who guide their learning.

A teacher who continues to learn will be better positioned to guide learners through a world in which information, technology and AI are changing rapidly.

A teacher who refuses to learn risks facing tomorrow’s classroom with yesterday’s tools.

That, Mr Mtewele said, is why teachers should view digital training not as an additional burden, but as an investment in their profession and in the future of the learners they teach.

The challenge, therefore, is not whether technology will enter education.

It already has.

The more important question is whether teachers will be ready to use it wisely, responsibly and effectively.

For Tanzania’s journey towards 2050, the answer may begin with something as simple as a teacher deciding to learn one new digital skill today.