Serikali, kupitia taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, imesisitiza kuendelea kuwadhibiti watu wanaoingiza bidhaa duni nchini kupitia njia haramu ikilenga kulinda afya za walaji na uchumi wa Taifa.


Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla Hamid, amefanya Kikao kazi na Kansela wa Chama Cha Kikomunisti (CPC), Ubalozi wa China nchini Tanzania Ndg. Xu Sujiang leo tarehe 16.04.2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Lengo la kikao hicho ni kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha uhusiano na itikadi za vyama hivyo.




Samia Suluhu Hassan amesema idadi ya hospitali zinazotoa huduma za upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu (neurosurgery) imeongezeka kutoka hospitali mbili hadi saba kufikia Aprili 2026, hatua inayoakisi uwekezaji mkubwa wa Serikali katika sekta ya afya.

Waziri Wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Na.Alex Sonna-Dodoma

Serikali imeandika historia mpya katika sekta ya uwekezaji baada ya kusajili miradi 915 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 10.95 mwaka 2025, ikiwa ni kiwango cha juu zaidi kuwahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa mfumo wa usajili wa miradi ya uwekezaji mwaka 1996.

Hayo yameelezwa leo Aprili 16,2026 bungeni jijini Dodoma na Waziri Wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Prof.Mkumbo amesema kuwa  mafanikio hayo yanaakisi ukuaji mkubwa wa sekta ya uwekezaji nchini, ambapo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, idadi ya miradi imeongezeka kutoka 256 mwaka 2021 hadi 915 mwaka 2025—sawa na ongezeko la asilimia 257.4.

Amesema  hatua hiyo ni ishara ya kuimarika kwa mazingira ya biashara na uwekezaji, sambamba na juhudi za makusudi za kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

"Tanzania pia imeanza kupanua uwekezaji wake nje ya mipaka. Takwimu za awali zinaonyesha kuwa kampuni za Kitanzania zimewekeza zaidi ya dola bilioni 3.1 katika nchi mbalimbali zikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Afrika Kusini, Japan na Qatar. Uwekezaji huo unalenga kupanua masoko, kuongeza ushindani na kuchochea uhamishaji wa teknolojia."amesema Prof.Mkumbo

Hata hivyo amesema kuwa Sekta zinazoongoza katika uwekezaji huo wa nje ni pamoja na viwanda vya chakula na vinywaji, nishati, usafirishaji, huduma za kifedha na vyombo vya habari.

Katika hatua nyingine, Serikali imekamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996 na kuandaa sera mpya ya mwaka 2026 inayosubiri kuidhinishwa. Sera hiyo inalenga kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kuweka mkazo kwenye upatikanaji wa ardhi, vivutio vya uwekezaji, ubunifu na ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi.

Sambamba na hilo, Mkakati wa Taifa wa Uwekezaji wa mwaka 2026–2031 umeandaliwa ili kutafsiri sera hiyo katika vitendo, kwa kuainisha vipaumbele na hatua mahsusi za kukuza uwekezaji wenye tija kwa uchumi wa taifa.

Katika kuimarisha ulinzi wa uwekezaji, Tanzania imeendelea kusaini mikataba ya kimataifa ya uwekezaji, ambapo hadi Machi 2026 jumla ya mikataba 20 ilikuwa imesainiwa, huku mingine ikiendelea kujadiliwa na nchi mbalimbali ikiwemo Japan, Canada na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Aidha, Serikali imeongeza kasi ya maendeleo ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi (SEZ), ambapo miradi 19 yenye thamani ya dola milioni 331.51 imesajiliwa na kutarajiwa kuzalisha ajira zaidi ya 11,700 pamoja na kuongeza mauzo ya nje.

Katika maeneo hayo, uwekezaji umeelekezwa kwenye viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, uzalishaji wa bidhaa za chuma, dawa na hata uunganishaji wa magari kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Serikali pia imeendelea kuboresha huduma kwa wawekezaji kupitia Kituo cha Pamoja cha Uwezeshaji Uwekezaji (OSFC), ambapo idadi ya taasisi zinazotoa huduma imeongezeka na kurahisisha upatikanaji wa vibali na nyaraka muhimu kwa wawekezaji.

Katika jitihada za kuimarisha uchumi, mapato yasiyo ya kodi kutoka mashirika ya umma yameongezeka na kufikia shilingi bilioni 773.37 hadi Machi 2026, ikiwa ni asilimia 85 ya lengo la kipindi hicho. Serikali pia imeongeza uwekezaji wake katika mashirika ya umma hadi kufikia shilingi trilioni 90.61.

Pamoja na mafanikio hayo, Serikali imeendelea kufanya mageuzi ya kimuundo kwa kufuta na kuunganisha baadhi ya mashirika ya umma ili kuongeza ufanisi na tija.

Hatua nyingine muhimu iliyochukuliwa ni kuboresha mazingira ya biashara kupitia mpango wa MKUMBI, ambapo sheria 28 zimefanyiwa mapitio na tozo 245 zimeondolewa au kupunguzwa ili kupunguza gharama kwa wafanyabiashara.

Serikali imesisitiza kuwa mageuzi haya yanalenga kujenga mazingira rafiki, yenye ushindani na yanayovutia uwekezaji zaidi, huku yakichochea ukuaji wa uchumi na ajira kwa Watanzania.

Amesema kuwa mwelekeo wa sasa unaonyesha kuwa Tanzania inaendelea kujijenga kama kitovu muhimu cha uwekezaji barani Afrika, huku mikakati mipya ikiweka msingi imara wa kufikia malengo ya maendeleo ya muda mrefu ifikapo mwaka 2050.

 

Na MWANDISHI WETU

SERIKALI imepokea rasmi hoja ya ajira za muda (part-time) kwa vijana iliyowasilishwa na Mbunge wa Kisarawe, Dk. Selemani Jafo, na kuanza mchakato wa kuichakata ili kubaini namna bora ya utekelezaji wake.

Akizungumza mara baada ya kupokea hoja hiyo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi, Sera, Bunge na Watu Wenye Ulemavu, Profesa Paramangamba Kabudi, amesema serikali inatambua uzito wa hoja hiyo na itaifanyia uchambuzi wa kina kabla ya kuchukua hatua stahiki.

Amesema hoja hiyo inalenga kutoa suluhisho la changamoto ya ajira kwa vijana, hivyo serikali itaipitia kwa makini ili kuona namna inavyoweza kutekelezwa kwa ufanisi na tija kwa taifa.

Aprili 9 mwaka huu, wakati akichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Jafo aliwasilisha hoja hiyo bungeni akipendekeza kuanzishwa kwa mpango maalumu wa ajira za muda mfupi kwa vijana nchini.

Katika hoja yake, Dk. Jafo alisema mpango huo utasaidia vijana kupata ajira za mikataba ya muda, kujenga uzoefu wa kazi na kupata kipato, sambamba na kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kuendelea kutoa ajira kwa vijana.

Alifafanua kuwa mpango huo unaweza kuanza kwa kuwahusisha vijana 50,000 wenye elimu ya stashahada na shahada, ambapo wa stashahada wangelipwa takribani Sh500,000 na wa shahada Sh700,000 kwa mikataba ya miaka mitatu.

Kwa mujibu wa maelezo yake, utekelezaji wa mpango huo unaweza kugharimu takribani Sh bilioni 396, huku ukilenga kupunguza tatizo la ajira na kuwajengea vijana uzoefu wa vitendo.

Aidha, alieleza kuwa hali ya sasa inaonesha vijana wengi wahitimu wanajikuta wakifanya kazi zisizoendana na taaluma zao, ikiwemo bodaboda, jambo alilosisitiza linahitaji hatua za haraka za kisera.

Pia alipendekeza utekelezaji wa mpango huo uanze kwa makundi maalumu yakiwemo walimu, wahudumu wa afya na vijana waliopo mitaani, huku ukiratibiwa kupitia mamlaka za serikali za mitaa ili kuongeza ufanisi.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

...

VIJANA nchini Tanzania wanaendelea kurasimisha shughuli zao za biashara kwa kasi, hali inayoashiria kuongezeka kwa ushiriki wao katika uchumi rasmi na mchango wao katika juhudi za maendeleo ya taifa.

Hayo yameelezwa leo Aprili 15,2026 na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw.Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma .

Bw.Nyaisa amesema takwimu za BRELA zinaonesha kuwa maelfu ya kampuni, majina ya biashara na alama za biashara na huduma (trade and service marks) zilizosajiliwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita zinamilikiwa na vijana. Hali hii inaonesha wazi kuongezeka kwa mchango wa vijana katika sekta za viwanda na biashara nchini.

"Kampuni 5,045 zimesajiliwa, ambapo 3,120 zinamilikiwa na vijana. Aidha, majina ya biashara 8,792 yamesajiliwa, kati ya hayo 4,938 ni ya vijana. Kwa upande wa alama za biashara, jumla ya 1,018 zimesajiliwa, nyingi zikiwa zinamilikiwa na vijana. Vilevile, leseni za biashara daraja la “A” 5,430 zimetolewa, ambapo takribani nusu yake zimekwenda kwa vijana."amesema Bw.Nyaisa

Amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo madiwani kuhusu taratibu za usajili wa biashara, utoaji wa leseni pamoja na ulinzi wa haki miliki, ili waweze kuwasaidia wafanyabiashara katika kata zao kwa ufanisi zaidi.

Hata hivyo amempongeza Meya wa Jiji la Dodoma kwa kushiriki mafunzo hayo, hatua hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya kuboresha mazingira ya biashara katika mji mkuu wa nchi. Pia ametambua mchango wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma chini ya uongozi wa Rosemary Senyamule kwa ushirikiano wake katika kutoa elimu ya biashara na msaada wa kitaalamu.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yanahusisha maeneo muhimu kama usajili wa kampuni, majina ya biashara, alama za biashara, hati miliki (patents), pamoja na utoaji wa leseni za viwanda na leseni za biashara daraja la “A”.

Aidha, amebainisha kuwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, BRELA imefanya maboresho mbalimbali ya kurahisisha mazingira ya kufanya biashara, ikiwemo kuanzisha mifumo ya kidijitali inayowezesha huduma kupatikana mtandaoni kupitia simu za mkononi.

Hata hivyo, Nyaisa ametaja changamoto ya utofauti katika utoaji wa leseni za biashara katika ngazi za serikali za mitaa. Alieleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara hupewa leseni daraja la “B” badala ya “A” kimakosa, hali inayosababisha mkanganyiko.

Amewataka madiwani kutumia mafunzo hayo kutatua changamoto hizo na kuwa mabalozi wa kuhamasisha urasimishaji wa biashara, hususan kwa vijana, wanawake na wajasiriamali wadogo.

“Baada ya mafunzo hayo, tunatarajia muwe mabalozi wazuri katika maeneo yenu na kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika ngazi za chini,” amesema.

Kwa upande wake, Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwona Chaula,amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuwajengea uwezo madiwani wanaofanya kazi kwa karibu na wananchi katika ngazi ya msingi. Aliongeza kuwa yatawasaidia kuelewa vyema taratibu za usajili na utoaji wa leseni za biashara ili waweze kuwasaidia wananchi katika shughuli zao za kila siku za kiuchumi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati mpana wa BRELA wa kujenga uchumi shindani na jumuishi kwa kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli rasmi za biashara nchini.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema ushiriki wa Tanzania kwenye Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP) upo kwenye biashara ya kusafirisha mafuta ghafi tu (transit nation) kutoka Kabaale Hoima hadi Chongoleani, Tanga na baadaye kupelekwa kwenye masoko ya kimataifa.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma leo Aprili 14, 2026 wakati akijibu swali la Mbunge wa Bahi, Mhe Kenneth Nollo aliyehoji Serikali ina mpango gani wa kuanza kusafirisha mafuta ghafi yanayotoka Uganda kupitia Bomba la Mafuta EACOP.

Mhe. Salome amesema mikataba ya mauzo hayo imeingiwa kati ya wabia wa mkondo wa juu nchini Uganda ambao ni Serikali ya Uganda na Makampuni ya Kimataifa (Totalenergies) kutoka Ufaransa na CNOOC kutoka China kwa kuzingatia vigezo vya usanifu wa kitaalam na uwezo wa uzalishaji wa visima.

" Mhe Spika naomba ifahamike pia, kwenye hii biashara tayari mikataba ya mauzo ya mafuta hayo imeshaingiwa kati ya wabia wa mkondo wa juu (upstreamers) na wanunuzi (masoko ya kimataifa)," Amesema Mhe Salome.


Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) Dkt. Benson Ndiege kushirikiana na Uongozi wa TCDC Sports Club wanunua vifaa vya michezo kwa wachezaji 42 kuelekea mashindano ya Michezo ya Meimosi mjini Njombe.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo Aprili 14, 2026 jijini Dodoma wakati wa kuwaaga wanamichezo wakielekea mjini Njombe.

Vifaa vilivyonunuliwa ni jezi za mprira wa miguu, viatu, mipira na vifaa vingine vya michezo.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amesema kuwa mkutano wa taasisi za ushindani barani Afrika umeleta pamoja wadau muhimu kutoka nchi mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto zinazoikumba sekta ya biashara. 
Ushirikiano kati ya VETA, Enabel na kiwanda cha Kasulu Sugar umeanza kuzaa matunda baada ya vijana 36 waliokuwa wakifanya kazi bila vyeti kutathminiwa na kupatiwa vyeti kupitia mfumo wa urasimishaji wa ujuzi (RPL).


Na Oscar Assenga, Lushoto

Kampuni ya Taifa Gas imeendelea kujipambanua kama kinara wa usambazaji wa gesi nchini Tanzania, ikiwa na takribani asilimia 51 ya ujazo wa gesi yote inayopatikana nchini.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo wakati wa Tamasha la NMB Kijiji Day lilofanyika Magamba wilayani Lushoto, Meneja wa Masoko wa kampuni hiyo, Oscar Shelukindo, amesema kuwa mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya kuhifadhi na kusambaza gesi, pamoja na dhamira ya dhati ya kuwahudumia Watanzania.

Ameeleza kuwa lengo kuu la kampuni hiyo ni kusaidia juhudi za taifa za kuhamasisha matumizi ya nishati safi, kwa kuwahamasisha wananchi kuachana na matumizi ya kuni na mkaa, ambayo yamekuwa na athari kubwa kwa afya na mazingira.

Kwa mujibu wa takwimu, zaidi ya Watanzania 33,000 hufariki kila mwaka kutokana na magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya nishati zisizo safi. 

Hali hiyo imeifanya Taifa Gas kuongeza juhudi za kuhakikisha gas inapatikana kwa urahisi na kwa gharama nafuu.

Katika hatua hiyo, kampuni hiyo inatoa mitungi ya gesi ya kilogramu 6 na 15 kwa bei nafuu, pamoja na huduma ya kujaza mitungi kwa wateja waliokwisha kuwa nayo, hatua inayolenga kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Aidha, Taifa Gas kwa kushirikiana na NMB Bank wanatarajiwa kushiriki katika Tamasha la Kijiji Day, ambapo watatoa huduma mbalimbali pamoja na elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi.

Juhudi hizi zinatajwa kuwa chachu ya mabadiliko chanya, zikilenga kuboresha afya za Watanzania na kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.


Serikali itahakikisha vipaumbele vya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) vinaakisi uhalisia wa mchango wa Sekta Binafsi, inayotarajiwa kuchangia takribani 70% ya Pato la Taifa (GDP) ifikapo mwaka 2050.

Hatua hiyo imebainishwa na Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dr. Blandina Kilama leo Aprili 13, 2026, wakati akifungua Warsha mahususi inayolenga kutoa fursa ya kujadili kwa kina, kukusanya maoni, uzoefu na mapendekezo ya wadau kutoka Sekta ya Umma, na Sekta Binafsi kuhusu maeneo sita (6) ya kipaumbele ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano, sambamba na mwelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“majadiliano haya yanalenga kuhakikisha kuwa mchango wa Sekta Binafsi unatambuliwa, unathaminiwa na kuingizwa kikamilifu katika uundaji na utekelezaji wa vipaumbele pamoja na mikakati ya maendeleo, ili kuimarisha ufanisi, kuongeza kasi ya utekelezaji wa FYDP IV, na kufikia matokeo yenye tija na endelevu kwa taifa” Amesema Dkt. Kilama.

Aidha, katika Warsha hiyo, washiriki watajadili mada mahususi zilizomo katika FYDP IV, ikiwemo Kujenga Uwezo wa Watu na Maendeleo ya Jamii, Kutumia Vichocheo vya Maendeleo, Mageuzi ya Sekta muhimu, Uadilifu wa Mazingira na Uhimilivu wa Tabianchi, Uchumi Imara, Jumuishi na Shindani na Kuimarisha Misingi ya Uendelevu wa Taifa.

Dkt. Kilama amesisitiza kuwa, matokeo ya warsha hiyo hayatabaki kuwa nadharia pekee, bali yatatumika katika kuboresha sera, mipango na mikakati ya maendeleo ya taifa.