Na mwandishi wetu

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju amesema mradi wa jengo la wagonjwa Mahututi katika Hospitali ya Halmashauri hiyo litakapokamilika litaondoa adha kwa wananchi kusafiri takribani kilomita 160 kufuata huduma hizo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga.

Akisoma taarifa ya mradi huo kwa Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Handeni, Ukwaju amesema uwepo wa jengo hilo ni juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya na kuwataka watendaji kuhakikisha miundombinu hiyo inatumika ipasavyo kuokoa maisha ya wananchi.

"Uwepo wa ICU hii utaondoa changamoto iliyokuwa inawakabili wagonjwa mahututi waliolazimika kusafirishwa umbali mrefu kupata huduma, hali iliyokuwa ikiongeza hatari kwa maisha yao pamoja na gharama kwa familia," amesema.

Awali, amefafanua kuwa Mradi wa ujenzi wa jengo la ICU ulianza Mei 6, 2024 na kukamilika Mei 25, 2025 kwa gharama ya zaidi ya Sh. milioni 426, ukitekelezwa na kampuni ya SWASH Construction Co. Limited kwa kushirikiana na CAREMED Gas Limited waliotekeleza mfumo wa gesi ya oksijeni.

Amesema Halmashauri tayari imelipia vifaa tiba vya awali vyenye thamani ya Sh. milioni 200 kupitia Bohari ya Dawa (MSD), huku ununuzi wa vifaa tiba vingine pamoja na awamu ya pili ya mfumo wa gesi ya oksijeni ukitarajiwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2026/2027.

Ujenzi wa jengo hilo ni sehemu ya maboresho ya miundombinu ya afya yaliyowezeshwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo alitoa Sh. milioni 900 kwa awamu ya pili kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa majengo mbalimbali ya hospitali hiyo.

Nao, wananchi wa Handeni wameeleza matumaini yao kuwa kuanza kwa huduma za ICU kutasaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wengi, kuongeza ufanisi wa huduma za afya na kupunguza msongamano katika hospitali za rufaa za mkoa.


Na: OWM (KAM) - Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu amezindua Programu ya Nchi ya Kazi za Staha Awamu ya Tatu ya Mwaka 2025/2026 – 2029/2030 na Mkakati wa kukuza Kazi za Staha Kwa wafanyakazi wa nyumbani.

 


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 12, 2026 amekagua na kuweka jiwe la msingi la Mradi wa ujenzi kituo cha kupokea na kupoza umeme cha MVA 60 Mkatata Tanga na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa  kilovolti 33.

Akiweka jiwe la msingi mradi huo, Dkt. Mwigulu amesema kutekelezwa kwa mradi huo ni jitihada za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika. 

"Nitoe rai kwa Wizara ya Nishati kuhakikisha kasi ya ukamilishwaji wa mradi huo na unakamilika kwa wakati ". Amesisitiza Mhe. Waziri Mkuu. 

Katika hatua nyingine ameiagiza Wizara ya Nishati kuwasiliana na Wizara ya Fedha ili kukamilisha malipo ya fidia kwa Wananchi takribani shilingi bilioni moja.

Ujennzi wa mradi huo ni shilingi bilioni 44 na unahusisha ujenzi wa vituo viwili vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme vyenye uwezo wa MVA 60 huku kila kimoja kikiwa na MVA 30,  pamoja na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa kilovoti 33 kutoka kituo cha Mkata hadi kwa Msisi.

Kwa upande wake Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwezisha upatikanaji wa fedha zitakazo tumika katika utekelezaji wa mradi huo.

“Utekelezaji wa mradi huu unakwenda kuondoa changamoto za umeme katika Wilaya za Handeni na Kilindi ambazo zinapata umeme kutokea Tanga mjiani ambapo ni umbali mrefu". Amesema Mhe. Ndejembi. 

Amefafanua kuwa kupitia miundombinu hiyo mipya, umeme utasafirishwa kutoka Mkata kwenda Msisi kwa umbali wa kilomita 45, hatua itakayoongeza uwezo wa usambazaji na kuimarisha huduma katika maeneo hayo.

Kuimalika kwa huduma ya umeme Wilaya za Handeni na Kilindi kutachochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii.













 


Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi amesema mradi wa kimkakati wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme katika eneo la Mkata wilayani Handeni utagharimu shilingi bilioni 44.14 mpaka kukamilika kwake na utaimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Wilaya ya Handeni.

Akizungumza Februari 13, 2026 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi, Waziri wa Nishati Mhe. Ndejembi amesema fedha hizo pia zitatumika kujenga njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 45 kutoka kituo cha Mkata hadi kijiji cha Kwamsisi.


Alieleza kuwa kwa muda mrefu wakazi wa Handeni walikuwa wakipata umeme kutoka Tanga, hali iliyosababisha upotevu mkubwa wa umeme njiani kutokana na umbali mrefu pamoja na kupungua kwa nguvu ya umeme. Kupitia mradi huu, sasa umeme utatoka Chalinze ambako ni karibu zaidi na Handeni, jambo litakaloongeza uthabiti wa huduma hiyo na kupunguza changamoto za kukatika mara kwa mara.

Kwa mujibu wa Waziri Ndejembi, kukamilika kwa kituo hicho kutaimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika wilaya za Handeni na Kilindi, kuchochea shughuli za uchimbaji wa madini ya graphite, kuvutia wawekezaji wapya na kuongeza mapato ya Shirika la Umeme kupitia wateja wakubwa watakaojiunga baada ya mradi kukamilika. Aidha, ajira zipatazo 120 zinatarajiwa kunufaisha wananchi wa eneo hilo.

Mradi huo unatekelezwa na kampuni ya TBEA kutoka China na utekelezaji wake ulianza Agosti 17, 2023 na unatarajiwa kukamilika Novemba 16, 2026.

Kwa upande wake, mkazi wa Kwamsisi, Rashid Hamza amesema awali ilikuwa vigumu kuendesha shughuli za kiuchumi kwa kutegemea umeme kutokana na kukatika mara kwa mara. Alisema matarajio yao ni kuona mradi huo ukikamilika kwa wakati ili kuwawezesha kuongeza uzalishaji na kipato kupitia matumizi ya nishati ya umeme.

Jiwe la msingi la mradi huo limewekwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mwigulu Nchemba kama dhamira ya Serikali ya kuendelea kuimarisha miundombinu ya nishati kwa maendeleo ya wananchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb), akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Dhahabu Duniani (WGC), Bw. David Tait, pamoja na Waheshimiwa Mawaziri baada ya mazungumzo ya kimkakati.
Majadiliano hayo yamelenga kuboresha mnyororo wa thamani wa sekta ya dhahabu nchini, hususani katika kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo ili kukuza mchango wao katika uchumi wa taifa.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Katika kutekeleza sera ya kutosafirisha madini bila kuongeza thamani, serikali imekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Dhahabu Duniani (World Gold Concil) Bw. David Tait juu ya kuendeleza sekta ya dhahabu nchini.

Mazungumzo hayo yamefanyika leo Februari 13, 2026 jijini Dar es Salaam ambapo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb.) ameongoza Mawaziri wanne, Mawaziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Maendeleo ya Vijana Mhe. Joel Nanauka, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dorothy Gwajima katika mazungumzo hayo.

Mazungumzo hayo yameangazia namna ya kuirasimisha sekta ya wachimbaji wa dhahabu wadogo ili kuhakikisha wanafanya uchimbaji wenye faida bila kuathiri mazingira.

Aidha, wamejadili namna ambavyo baraza hilo litashiriki kuiwezesha Tanzania kuvutia wawekezaji zaidi katika kuongeza thamani ya madini yanayozalishwa nchini ikiwa ni utekelezaji wa sera na sheria za sasa ambazo haziruhusu kuuza na kusafirisha madini bila kuongeza thamani.

Waziri wa Madini Mhe. Antony Mavunde amesema kuwa Baraza la madini duniani limevutiwa na namana serikali invyojenga mfumo mzuri wa kuwawezesha wachimbaji wadogo ambao huchangia uzalishaji wa madini kwa asilimia 40, huvyo kulifanya baraza hilo kuiona Tanzania ikiwa ni sehemu salama ya kufanya ushirikiano katika kukuza sekta hiyo.

Kwa upande wake Bw. Tait Amesema kuwa Baraza la Dhahabu duniani linavutiwa na namna serikali ya Tanzania inavyowawezesha wachimbaji wadogo, na hivyo ushirikia baina ya shirika hilo utakuwa ni kitovu na kielelezo cha namna sekta ya inavyoweza kukua na kuongeza tija.



 

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw. Abdul-Razaq Badru ameongoza kikao cha kimkakati kilichojumuisha waheshimiwa Madiwani,  Viongozi wa Mila, watendaji wa kata, wenyeviti wa Vijiji na watendaji wa vijiji kwa lengo la kudumisha mahusiano na uboreshaji wa huduma za kijamii na uboreshaji wa shughuli  za Uhifadhi shirikishi.

Kamishna Abdul-Razaq Badru ameeleza kuwa kikao hicho ni sehemu ya mkakati wa Mamlaka hiyo kukutana na makundi mbalimbali kujadili uboreshaji wa shughuli za kijamii na huduma za wananchi kama Maji, shule, Malisho, barabara, mawasiliano, afya na mengineyo.

"Viongozi na Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro ni wadau muhimu katika hifadhi, tunakutana nao kama sehemu ya kuboresha uhusiano na kuwaeleza mikakati ya Serikali dhidi yao. 

 kwa sasa tunaboresha miundombinu ya huduma za maji, ujenzi wa Barabara kwa tabaka gumu kutoka Loduare hadi Golini, kujenga minara mipya ya mawasiliano 9 ndani ya hifadhi ili kufikisha huduma kwa wananchi na wadau mbalimbali" amefafanua Kamishna Badru.

Kwa upande wa Viongozi waheshimiwa Madiwani, viongozi wa Mila wameiomba Serikali kupitia Mamlaka hiyo kuendelea kuboresha mahusiano, huduma za kijamii kama  miundombinu ya Maji, barabara, ukarabati wa vituo vya afya na shule, mahitaji  ya baraza la wafugaji, chunvi za mifugo na mpango wa malisho ya mifugo hawa wakati wa kiangazi.











 

Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati) akiwa na viongozi wengine wa wa Serikali, Bunge, na Benki ya CRDB wakipata maelezo kutoka mwanzilishi wa kampuni ya Aquafresh iliyoshiriki katika maonesho ya biashara changa bunifu za vijana katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati) akipokelewa na kikundi cha ngoma za asili vacati alipowasili katika uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Wengine pichana ni kushoto kwake ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wapili kushoto) akipata maelezo kutoka kampuni ya Kana Wine iliyoshiriki katika maonesho ya biashara changa bunifu za vijana katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (watatu kulia), Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Dkt. Donald Mmari (wapili kulia), Mwenyekiti wa CRDB Bank Foundation, CPA Osward Urassa (wakwanza kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wapili kushoto) akiwasili katika katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Alioongozana nao ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wakwanza kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Kitila Mkumbo, ameipongeza CRDB Bank Foundation pamoja na CRDB Bank kwa kuanzisha programu ya Go Green na IMBEJU, akisema ni hatua ya kimkakati inayounganisha ajenda ya Serikali ya uchumi wa kijani na uwezeshaji wa vijana nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, Profesa Mkumbo alisema mpango huo unaendana na Dira ya Taifa 2050 inayolenga kujenga uchumi jumuishi, shindani na himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, huku vijana wakitambuliwa kuwa nguvu kazi kuu ya maendeleo.

Alisema Serikali imeweka mkazo katika kukuza ubunifu wa vijana, uchumi wa kijani na ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi, akibainisha kuwa miradi ya vijana inayolinda mazingira ni utekelezaji wa moja kwa moja wa dira ya maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Abdulmajid Nsekela, alisema Go Green na IMBEJU ni daraja linalounganisha fedha za kimataifa za tabianchi na vijana wabunifu wanaokosa dhamana au historia ya mikopo katika mifumo ya kawaida ya kifedha. Alieleza kuwa kupitia programu ya TACATDP yenye thamani ya dola milioni 200 kwa ushirikiano na Green Climate Fund, zaidi ya Sh bilioni 100 tayari zimetolewa kufikia takribani wanufaika 600,000 kote nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Tully Esther Mwambapa, alisema maombi ya programu yatafanyika kidijitali kupitia jukwaa la FursaHub kuanzia Februari 12 hadi Machi 11, 2026, yakilenga kuchuja miradi yenye uwezo wa kujiendesha kibiashara na kurejesha mitaji nafuu. Alibainisha kuwa mitaji itatolewa kuanzia Sh 500,000 hadi Sh milioni 500, huku miradi bora zaidi ikipata ruzuku ya kati ya Sh 500,000 hadi Sh milioni 10 kuongeza kasi ya ukuaji.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Naibu Spika wa Bunge, Daniel Sillo, alisema Bunge limeweka msingi wa kisheria unaounga mkono ulinzi wa mazingira na uchumi wa kijani, akitaja programu hiyo kuwa mfano halisi wa kuunganisha sera, mitaji na ubunifu wa vijana.

Kwa niaba ya vijana wanufaika, Irene Vambi, mwanzilishi wa Mrembo Naturals, alisema programu ya IMBEJU imemwezesha kubadili wazo la biashara kuwa uzalishaji unaokua na kutoa ajira kwa vijana wengine, akiwahimiza vijana nchini kutumia fursa hiyo kujenga mustakabali wao kiuchumi.

Uzinduzi wa Go Green na IMBEJU unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa mitaji nafuu, kuimarisha biashara bunifu za vijana na kuchochea uchumi wa kijani nchini, huku ukiongeza mchango wa sekta binafsi katika maendeleo endelevu ya taifa.

Ukitaka, naweza pia kukuandalia kichwa cha habari kikali cha ukurasa wa mbele, au toleo fupi la mtandaoni.

 


Na Munir Shemweta, WANMM

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani mwaka huu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi itaendesha Kliniki Maalum ya Ardhi kwa ajili ya wanawake itakayojulikana kwa jina la "Samia Ardhi Week."

Kiniki hiyo itashughulikia changamoto za ardhi kwa wanawake na itafanyika kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026 katika mikoa yote ya Tanzania Bara ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake ambayo huadhimishwa tarehe 8 Machi kila mwaka ambapo kwa mwaka huu inaongozwa na Kaulimbiu "Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050"

Akizungumza jijini Dodoma tarehe 12 Februari 2026 wakati wa kuahirisha Kliniki Maalum ya Maombi ya Hati, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema, wanawake wote wenye changamoto za ardhi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi katika maeneo ambayo kliniki hizo zitafanyika.

"Wanawake wote wenye shida za masuala ya ardhi wanatakiwa kujitokeza katika mikoa ya Tanzania Bara ambayo kliniki hizo zitafanyika" amesema Mhe Dkt. Akwilapo.

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nia ya wizara yake kuanzisha kliniki za ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ni kuwafikia wananchi wenye shida zinazohusiana masuala ya ardhi.

Akizungumzia Kliniki Maalum ya Maombi ya Hati aliyoiahirisha, Mhe. Dkt Akwilapo amesema, kliniki hiyo imekuwa na mafanikio makubwa ambapo hadi kufikia tarehe 12 Februari 2026 wananchi 4,597 wamehudumiwa huku Hatimilki 3,878 zikiwa zimeandaliwa.

"Kumbe kupata hati inawezekana, katika hati 3,878 zilizoandaliwa jumla ya hati 1,508 zimechukuliwa na wahusika huku hati 2,370 zikiwa bado hazijachukuliwa", amesema Dkt. Akwilapo.

Ametoa rai kwa wananchi ambao wamepata huduma na hati zao zimekamilika wafike ofisi za ardhi kwa ajili ya kuzichukua kwa kuwa hati hizo za ardhi ni mali yao.

Kliniki Maalum ya Maombi ya hati ilianza januari 28, 2026 katika viwanja vya Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Dodoma na kuhitimishwa tarehe 12 Februari 2026.