Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa 21 wa Baraza la Mawaziri wa Nishati wa Ukanda wa Mashariki mwa Afrika, uliofanyika Aprili 29, 2026 jijini Cairo, Misri, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya umeme.

Katika mkutano huo wa nchi wanachama wa Umoja wa Nishati Mashariki mwa Afrika (EAPP), uamuzi muhimu umefikiwa wa kuichagua rasmi Jamhuri ya Kiarabu ya Misri kuwa mwenyeji wa kudumu wa kituo cha uendeshaji wa soko la umeme la pamoja  kwa nchi wanachama.

Mkutano huo uliongozwa na Waziri wa Umeme na Nishati Jadidifu wa Misri, Mhe. Dkt. Mahmoud Esmat, ambaye pia ni mwenyekiti anayemaliza muda wake,  uliwakutanisha Mawaziri wa Nishati kutoka nchi 13 wanachama kwa lengo la kukamilisha mfumo wa kiutawala na kiuendeshaji wa soko la umeme la pamoja na endelevu.

Mbali na kuichagua Misri, Baraza hilo pia limepitisha nyongeza ya muda wa miezi miwili kwa nchi wanachama kukamilisha mchakato wa kuridhia hati za makubaliano ya ushirikiano baina ya serikali na mashirika ya umeme.

Aidha, mkutano huo umeridhia Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasi ya Ethiopia kuchukua nafasi ya uenyekiti wa Baraza la Mawaziri, kufuatia kumalizika kwa muda wa uongozi wa sasa, kwa mujibu wa katiba ya umoja huo inayotaka uongozi kuzunguka kwa wanachama kila mwaka.

Akihitimisha mkutano huo, Mwenyekiti wa EAPP, Mhe. Dkt. Esmat, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza umoja, ushirikiano, uwazi na kuheshimiana miongoni mwa nchi wanachama ili kufikia malengo ya kuwa na soko la umeme la kikanda lenye tija.

Akizungumza kuhusu mkutano, Mhe. Salome amesema maazimio yaliyofikiwa ni hatua muhimu katika kuleta mageuzi makubwa katika biashara ya umeme na kuimarisha soko la nishati la pamoja kwa nchi za ukanda huo.

Katika mkutano huo, Mhe. Makamba ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Misri, Meja Jenerali Richard Makanzo, Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO anayeshughulikia uzalishaji umeme, Mhandisi Anthony Mbushi, pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati, TANESCO na EWURA.














Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza wakati akifungua  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza wakati akifungua  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda (hayupo pichani) wakati wa  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema utekelezaji wa mageuzi ya elimu unaoendelea nchini ni sehemu ya dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha vijana wanapatiwa ujuzi, maarifa na uwezo unaowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa taifa.

Ameyasema hayo leo  Aprili 29, 2026 katika Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo, Prof. Mkenda amesisitiza kuwa sekta ya elimu inabeba wajibu mkubwa katika maendeleo ya nchi na kwamba, wajibu wa Wizara ni kuhakikisha mipango yote inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kasi.

Waziri Mkenda ameongeza kuwa kuanzishwa kwa Wizara maalum ya maendeleo ya vijana ni uthibitisho wa umuhimu wa kundi hilo katika maendeleo ya taifa na kuwa elimu ya ufundi kupitia VETA, ni msingi wa kuwaandaa vijana kuzalisha na kushiriki katika uchumi wa kisasa.  "Utekelezaji wa elimu ya miaka 10 ya lazima na uimarishaji wa shule za Sekondari na shule za amali unatekelezwa kwa ushirikiano wa karibu na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, na hata sekta binafsi hasa katika kuhakikisha upatikanaji wa shule karibu na makazi ya wananchi na ununuzi wa vifaa vya kisasa kwa ajili ya mafunzo ya ufundi."amesema Prof. Mkenda Katika kuhimiza ubunifu na uwajibikaji, Prof. Mkenda amewataka watumishi wa Wizara kuendeleza kasi ya utendaji na kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa kuhusu utekelezaji na mafanikio ya serikali katika maeneo ya sekta ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,amesema Serikali inaendelea kuimarisha usimamizi wa ajira na rasilimaliwatu kwa kuzingatia malengo na maono ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hususan katika utekelezaji wa Kifungu cha 73 cha Sheria ya Ajira kinachohusu uhusiano kazini.

Prof. Nombo amesema kuwa kupitia mkutano huo, wajumbe watapitia mpango na bajeti ya wizara pamoja na masuala ya utawala na usimamizi wa rasilimali watu pamoja na kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuboresha afya na usalama mahali pa kazi. Prof. Nombo amesisitiza kuwa mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ubora na uaminifu katika utendaji kazi,  "Dhamira ya Wizara ni kuona watumishi wanafanya kazi kwa bidii, kwa uadilifu na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuendeleza mageuzi yanayoendelea katika elimu."amesema Prof. Nombo Aidha, amewashukuru wajumbe wa Baraza hilo kwa ushirikiano wao na amewataka kuendekeza juhudi za kuimarisha mifumo ya usimamizi ndani ya Wizara.

Kampuni ya GASCO imeeleza kuwa usalama na ustawi wa mfanyakazi ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa shughuli zake za kila siku, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya kuhakikisha mazingira salama, rafiki na yenye kuchochea tija kazini.
Na Mwandishi wetu

Katika dunia inayokabiliwa na changamoto kubwa za mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la uchafuzi wa mazingira na kupungua kwa rasilimali asilia, hadithi ya Tanzania inajitokeza kama mfano wa matumaini, uthabiti na maamuzi ya kimkakati. Maadhimisho ya miaka 40 ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) si tukio la kawaida—ni kielelezo cha dhamira ya Taifa kulinda uhai wake huku likiendeleza uchumi wake.



‎Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) unaolenga kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe mkoani Tanga.

‎Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw.  Burhan Ngulungu ambapo amesema kuwa takribani shilingi Bilioni 19 kupitia mradi wa TACTIC zitatumika katika ujenzi wa barabara za lami Km 10.4 na mifereji ya maji ya mvua itakayosaidia kuondoa maji katikati ya mji na kupeleka eneo la mto Pangani.

‎"Kuna barabara itaunganisha stendi ya Kijazi na soko la Kilole, hivyo barabara ikikamilika licha ya kupendezesha mji, wananchi pia wataweza kupata huduma za usafiri na usafishaji, mazingira bora ya kufanyia biashara kwa wajasiriamali na wafanyabiashara na pia kuongeza mapato ya halmashauri ya mji wa Korogwe", amesema.

‎Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Korogwe mjini CPA. Charles Njama amesema mradi huo unaotarajiwa kujenga barabara katika kata za Bagamoyo, Mgombezi, Mtonga, Manundu, Masuguru na Magunga unakwenda kuleta tabasamu la kudumu kwa wananchi wa Korogwe.

‎"Tunamshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mradi huu, barabara ya NMB-Magunga ni muhimu kwa wananchi wa Korogwe, Handeni, Lushoto na maeneo mengine kwasababu inapeleka wagonjwa hospitali ya Magunga, ikikamilika kwa kiwango cha lami itasaidia wagonjwa kufika hospitali bila usumbufu", amesema.

‎Naye, Mhandisi Charles Kamugisha Mratibu mradi wa TACTIC Korogwe Mji, ameeleza kuwa mradi unatarajiwa kukamilika tarehe 23 Januari, 2027 ambapo unahusisha ujenzi wa barabara ya NMB-Magunga Km 2.7, Bagamoyo-Mgombezi-Kibo Km 6.5, Kijazi Bus Stand-Kilole sokoni Km 1.2 pamoja na mifereji ya maji ya mvua Km 1.43 fedha za mkopo nafuu toka Benki ya Dunia. 

‎Vilevile, Mhandisi Zakayo Magoro Meneja wa TARURA wilaya ya Korogwe amesema kuwa TARURA ina mtandao wa barabara za lami Km 16.1 kupitia mradi wa TACTIC zitaongezeka hadi kufikia Km 26.5 ambapo zikikamilika zitapendezesha mji, thamani ya ardhi itapanda na itapunguza gharama za matengenezo ya mara kwa mara. 

‎Naye, Bw. Mohamed Dachi mkazi wa kata ya Mgombezi ambaye ni mkulima ameishukuru serikali kwa ujenzi wa barabara ya Bagamoyo hadi Kibo ambapo ikikamilika itaongeza fursa za kibiashara na kiuchumi kwani watasafirisha mazao yao sokoni kwa urahisi.

‎Bw. Salmin Sadala mkazi wa kata ya Manundu ambaye ni mfanyabiashara ndogondogo amesema kuwa baada ya kukamilika kwa mradi huo licha ya mji wa Korogwe kupendeza pia taa zikiwekwa watafanya biashara hadi usiku na kuchochea kukua kwa shughuli za kiuchumi kwa wananchi.

Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP Centre) kimesema mafanikio ya utekelezaji wa ajenda ya ubia nchini yameongeza kwa kiasi kikubwa thamani ya miradi ya maendeleo, huku kikitoa wito wa kufanyiwa maboresho kwa Sheria ya Utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji na kulinda maslahi ya walipa kodi.

Naibu Waziri wa Nishati,Mhe. Salome Makamba ametembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Misri, ambapo alipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini humo, Richard Makanzo.

Katika mazungumzo yao, Balozi Makanzo alieleza majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na ubalozi huo, pamoja na kuainisha fursa zilizopo katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo, umeme, uchukuzi na biashara. 

Balozi Makanzo alieleza kuwa ushirikiano kati ya Serikali za Tanzania na Misri katika sekta hizo unalenga kuwanufaisha wananchi na kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.

Mhe. Salome alimpongeza Balozi Makanzo kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na timu yake, hususan katika kuendeleza mahusiano si tu kati ya Tanzania na Misri, bali pia na balozi za nchi nyingine zilizopo nchini humo.

 Mhe. Salome yupo nchini Misri kwa ajili ya kushiriki mkutano wa East African Power Pool, utakaofanyika Aprili 29, 2026 jijini Cairo. 

Mkutano huo utajadili masuala muhimu ya sekta ya nishati miongoni mwa nchi wanachama, ikiwemo uunganishaji wa gridi za taifa na biashara ya umeme baina ya nchi hizo.

Mkutano huo umetanguliwa na vikao vya wataalamu kutoka sekta ya nishati katika nchi wanachama, vikilenga kuweka msingi wa majadiliano ya viongozi.










Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Maji (Water Institute) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dr. Maulid J. Maulid wamekutana Aprili 28, 2026 jijini Dar Es Salaam kwa kikao cha 46 cha Bodi hiyo kujadili masuala ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utoaji wa huduma za kitaaluma na miradi ya maendeleo itakayoboresha ufundishaji na ujifunzaji.

 Na Farida Mangube Morogoro


Bodi ya Maji ya Bonde la Wami-Ruvu imewatoa hofu wakazi wa Manispaa ya Morogoro kuwa maji ya Bwawa la Mindu ni salama, kwani kemikali iliyomwagika haikufikia chanzo cha maji.

Wasiwasi huo ulizuka kufuatia ajali ya lori lililokuwa likisafirisha kemikali aina ya sulphur kuacha njia na kugonga miti mita 300 kutoka bwawa la Mindu mtaa wa mikoroshini Kata ya Mindu barabara kuu ya Morogoro–Iringa.

Mkurugenzi wa Bonde la Maji bonde la Wami-Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmasi, amesema hatua za haraka zilizochukuliwa na wataalamu zilisaidia kuzuia kemikali hiyo kusambaa hadi kwenye chanzo cha maji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA), CPA Sais Kyejo, amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa hakuna madhara yaliyobainika katika ubora wa maji yanayosambazwa.

“Wananchi waendelee kutumia maji bila hofu,” amesema Kyejo.

Naye Meneja wa Kanda ya Kati wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Bi Magdalena Mtenga, amesema hadi sasa hakuna madhara yaliyoripotiwa kwa wananchi, licha ya kemikali hiyo kuwa hatarishi endapo itashughulikiwa bila tahadhari.

Ameeleza kuwa sulphur ina sifa ya kuwaka na hata kulipuka, pamoja na kusababisha muwasho wa ngozi au koo, lakini hali hiyo haikutokea wakati wa operesheni ya kuiondoa katika eneo la ajali.

Taasisi mbalimbali zikiwemo Bonde la Wami-Ruvu, MORUWASA, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) pamoja na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji zilishiriki kuondoa kemikali hiyo kwa usalama.

Meneja wa NEMC Kanda ya Morogoro na Rufiji, Arnold Mapinduzi, amesema kemikali hiyo itateketezwa kwa mujibu wa sheria ili kulinda mazingira.

Ajali hiyo ni ya tatu ndani ya mwezi mmoja kuhusisha usafirishaji wa kemikali aina ya sulphur Barabara kuu ya Morogoro - Iringa hali inayochochea haja ya kuimarisha usalama wa usafirishaji wa kemikali hatarishi.





 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi ameitaka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuzingatia mambo 10 vya msingi huku akisisitiza nidhamu, haki, weledi na uadilifu katika utekelezaji wa majukumu na wajibu wa wizara wa kulinda raia na mali zao.

Ametoa maagizo hayo makati akifungua Kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambacho kimefanyika leo,jijini Dodoma ambapo kilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Ally Senga Gugu,Wakuu wa Idara na Vitengo wa wizara,Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Katungu, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF John Masunga, Kamishna wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas, Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, CP Kombo Khamis Kombo,Wawakilishi wa Idara ya Uhamiaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) na wawakilishi wa watumishi wa wizara.

“Naomba tuzingatie yafuatayo; Moja, kusimamia na kuhakikisha mpango mkakati, mipango dira, dhima na majukumu ya wizara yanatekelezwa kwa ufanisi ili kufikia malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, mbili, kuzingatia miongozo mbalimbali ya kisera ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa.

Tatu;kuhakikisha watumishi wote wanaostahili wanapandishwa vyeo kwa wakati.” amesema Waziri Katambi

Katika hotuba yake hiyo ya kufungua Baraza,Waziri Katambi ametaja agizo lingine la nne kuwa ni kulipa madai ya wastaafu, uhamisho, likizo, stahiki, madeni na madai mbalimbali ya watumishi kwa wakati ili kuipunguzia serikali malimbikizo ya madeni.

Tano ni kuhakikisha watumishi wa wizara wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, haki, maadili na taratibu bila kutumia madaraka au mamlaka yao vibaya ili kuhakikisha kwamba   dhana ya uwajibikaji na utawala bora inaendelea kuzingatiwa na kuleta tabasamu ambalo  Rais wa nchi, Dkt.Samia Suluhu Hassan amekusudia.

Sita ni ufanisi na utendaji utakaosaidia uwajibikaji na nidhamu kazini, utekelezaji kwa wakati  na tathmini ambayo itapima malengo na kufuatilia kile ambacho tunakifanya na kupima malengo kama yamefikiwa kwa kuyafanyia tathmini na kufuatilia eneo gani linastahili marekebisho.

Saba ni kuzingatia maslahi na haki za watumishi ikiwemo pia kuwapa fursa ya mafunzo ili kuwaongezea ujuzi na weledi, huku akisisitiza haitakiwi kufanya kazi kwa kujuana, kuviziana wala kwa kutegena,ambapo aliwataka kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na mahusiano yaliyo mema na tija kwa taifa.

Nane ni mafunzo huku akisisitiza wale wanaostahili kwenda mafunzo ikiwa ni programu fupi,warsha,ujuzi au weledi huku akikisitiza lizingatiwe kwa kuwa linaongeza ufanisi na kurahisisha majukumu 

Tisa ni kuzingatia usalama na maadili ya kazi na Kumi  ni kuimarisha mawasiliano ya ndani ya taasisi ili kuweza kurahisisha utendaji kazi katika kuwahudumia wananchi, ikiwemo mahusiano kati ya ofisi moja na nyingine, ikiwemo masuala ya kuandikiana barua pepe kati ya ofisi moja na nyingine akisisitiza kuwepo mazungumzo kwanza ya ana kwa ana ili kuweza kurahisisha maamuzi ambayo baadae wayaweke katika maandishi ambapo pia alisisitiza utunzaji wa siri.

Waziri Katambi alimalizia kwa kusisitiza uwepo utaratibu wa kufanya tathmini ya bajeti na rasilimali zilizopo ili kuleta matokeo chanya katika kuwahudumia wananchi ikiwemo ulinzi wa mali na maisha yao.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI ya Belarus imeendelea kutoa fursa za ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa Tanzania, hususan katika fani ya tiba kwa mwaka wa masomo 2026/2027, hatua inayotokana na kuimarika kwa ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Daniel Mushi, amesema upatikanaji wa mabasi ya watumishi yatasaidia sana katika kuweka mazingira salama na wezeshi ya utendaji.

Amesema hatua hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kujali watumishi na kuboresha mazingira ya kazi.

Amesisitiza kuwa watumishi ni nguzo kuu ya kufikia malengo kwani ndio watekekezaji wa mipango na maono wizara hivyo, Wizara inaendelea kuweka mazingira stahiki na jumuishi kwa watumishi wote.

"Rais wetu amesisitiza kazi iende sambamba na kujali utu, na hivi ndio tunatekeleza kauli mbiu ya Kazi na Utu tunasonga mbele kwa kuweka mazingira yanayovutia utendaji kwa watumishi" amesema Prof. Mushi.

Prof. Mushi amewahimiza watumishi kutumia mabasi hayo na kuyatunza ili yaweze kurahisisha utendaji kazi na kutumika kwa muda mrefu.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Edith Rwiza amesema ununuzi wa mabasi matatu (3) mapya kwa ajili ya usafiri wa watumishi ni hatua muhimu ya kuboresha mazingira ya kazi kwa Wizara.

Akizungumza jijini Dodoma Aprili 28, 2026 katika uzinduzi wa mabasi ya watumishi, Mkurugenzi huyo amesema mabasi hayo yamenunuliwa na Wizara kwa kushirikiana na Mradi wa Kuimarisha na Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi Tanzania Bara (BOOST) kwa zaidi ya Shilingi milioni 500 kwa lengo la kuwezesha watumishi katika safari za kila siku za kwenda kazini na kurudi nyumbani pamoja na ziara za kikazi.

"Kabla ya hatua hii, watumishi walilazimika kutumia kati ya shilingi 10,000 hadi 15,000 kwa siku kufika ofisini hali iliyoleta ugumu wa maisha na kupunguza morali ya kazi" amesema Dkt. Rwiza

Mkurugenzi Rwiza amesema upatikanaji wa mabasi haya ni sehemu ya jitihada za wizara kuhakikisha watumishi wanafanya kazi katika mazingira bora na yenye ufanisi.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikalin na Afya (TUGHE), Bw. Moshi Kisinga ameushukuru uongozi wa Wizara hiyo kwa kununua magari kwa ajili ya watumishi.

"Kwa niaba ya watumishi wenzangu tumepokea magari haya kwa furaha na hakika tumeondokana na changamoto kubwa ya usafiri", amesema Kisinga.

Ametoa rai kwa watumishi kufanya kazi kwa juhudi na maarifa akisisitiza uwajibikaji katika majukumu ya kila siku.