Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeendelea kutoa mafunzo kupitia kozi ndefu 49 zinazolenga kuzalisha wataalam mahiri watakaosaidia utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali nchini.
Serikali ya Tanzania ndani ya kipindi cha Miezi Mitatu ijayo inatarajiwa kuanza rasmi utekelezaji wa Mradi wa Kimkakati wa Liganga na Mchuchuma wenye uwekezaji wa Dola za Marekani Bilioni 2 hadi 3 baada ya mazungumzo kati ya Serikali na Mwekezaji kufikia zaidi ya asilimia 90.
Hayo yalibainishwa Mei 9, 2026 na Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika Shamba la Parachichi la Havira Farm Mkoani Njombe, pembeni mwa Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini, kinachotumika kama sehemu ya tathmini na kujipanga.
Alisema hatua hiyo inaashiria mwanzo wa utekelezaji wa mradi huo uliosubiriwa kwa miaka mingi ukitarajiwa kuongeza mapato ya Seikali, ajira kwa wananchi, kukuza sekta ya viwanda vya chuma na ustawi wa jamii inayozunguka mradi na taifa.
Aliongeza kwamba, mradi huo unatarajiwa kuzalisha tani milioni 2.9 za chuma ghafi kwa mwaka pamoja na tani milioni 1.1 za bidhaa za chuma kwa mwaka, huku ukitarajiwa kutoa zaidi ya ajira rasmi 6,500 na ajira zisizo rasmi zipatazo 26,000
‘’ Katika kipindi cha miaka 25 ya kwanza ya mradi, jumla ya mapato ya dola za Marekani 1,990,489,585,000 zinatarajiwa kupatikana ambapo kwenye miradi ya makaa ya mawe kiasi cha dola za Marekani 92,593,820; uchimbaji chuma kiasi cha dola za Marekani 910,781,519 na kiwanda cha chuma kiasi cha dola za Marekani 987,114,246,’’ alisema Msigwa.
Pia, aliongeza kwamba utekelezaji wa mradi huo utahusisha ujenzi wa msongo wa umeme wa Kilovoti 220 kati ya mchuchuma na na liganga na barabara kutoka Mchuchuma na Liganga ukiwemo mgodi wa makaa ya mawe mchuchuma wenye uwezo wa kuzalisha tani milioni 3 kwa mwaka na Kituo cha kufua umeme kwa megawati 600.
Msigwa alisema tayari Serikali imelipa zaidi ya shilingi bilioni 15 za fidia kwa wananchi ili kupisha utekelezaji wa mradi huo, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali kuhakikisha mradi huo unaanza kwa vitendo baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu.
Utekelezaji wa mradi wa Liganga na Mchuchuma unaashiria safari ya kuelekea Dira 2050 ambapo kupitia Sekta ya Madini imejipanga kufikia Uchumi wa Dola trilioni Moja ukiwa ni miongoni mwa miradi kielelezo iliyoanishwa kwenye mpango wa muda mrefu wa wa dira hiyo unaotarajiwa kuchochea sekta ya viwanda nchini.
Mbali na Sekta ya Madini, alisema Serikali inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Njombe ikiwemo barabara, maji na umeme kwa lengo la kuufungua zaidi mkoa huo kiuchumi na kijamii.
#LigangaMchuchuma #Madini ni Maishana Utajiri #TanzaniaSteelHub
#NjombeMpya #SafariyaViwanda #InvestInTanzania #MiningSector
#Mining4Development #MineralForGrowth
Viongozi mbalimbali wa Chama cha mapinduzi Mkoa na Wilayani wakiambatana na Viongozi wa Serikali mkoa wa Dodoma wameanza safari ya Kikazi kuelekea mkoani Mtwara kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Ushirika vya Msingi.
Viongozi hao wakingozana na Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma Ndg Joseph Chitinka na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Dodoma Bibi Theresia Nyoka wameanza ziara hiyo leo Mei 12, 2026 kutokea mkoani Dodoma kuelekea mkoani humo.
Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma ameeleza lengo la ziara hiyo ni kuwajengea uwezo, kujifunza utekelezaji wa Mfumo wa stakabadhi za ghala na kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Msingi Ushirika vya mkoa wa Mtwara na hivyo kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya kiushirika ndani ya Mkoa wa Dodoma.
Ziara hiyo inafanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Mei 13 hadi 14, 2026 na kuwahusisha Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa, Wenyeviti wa CCM Wilaya Mkoani Dodoma, Sekretariti ya Mkoa CCM, Baadhi ya Makatibu wa Chama wilaya na Wenezi,, Makatibu, Makatibu Tawala Uchumi na Uzalishaji Viwanda na Biashara na Kilimo.

Na OWM - TAMISEMI, Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewasisitiza washiriki wa Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Afua ya Uthibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, kuhakikisha suala usafi wa mazingira linakuwa ajenda ya kudumu katika vikao vyote vitakavyofanyika katika ngazi zote za Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuwezesha miji na majiji nchini kuwa masafi.
Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Mwaka wa Tathmini ya Afua ya Uthibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, unaofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Jiji- Mtumba, unaohudhuriwa na Maafisa Afya wa Mikoa, Maafisa Afya wa Halmashauri na Maafisa Mazingira wa Halmashauri.
“Nasisitiza suala la usafi wa mazingira liwe ajenda ya vikao vyenu. Vikao vya Kamati za Ushauri za Mikoa, Kamati za Ushauri za Wilaya, Kamati za Maendeleo za Kata, Mabaraza ya Madiwani, Kamati za Kudumu za Halmashauri pamoja na vya ALAT ngazi ya mkoa na taifa,” amesema Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe ameainisha kuwa, usafi wa mazingira ukizingatiwa katika ngazi zote za Mamlaka ya Serikali za Mitaa utapunguza milipuko ya magonjwa na matumizi ya fedha kwa ajili ya ununuzi wa madawa, na fedha zitakazookolewa zitaelekezwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hivyo amewataka maafisa hao kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kupunguza milipuko ya magonjwa na matumizi ya ununuzi wa dawa.
“Namshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuanzisha vitengo vya udhibiti wa taka ngumu ambavyo vinasaidia kuboresha zoezi la usafi wa mazingira nchini,” Prof. Shemdoe ameeleza.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Prof. Tumaini Nagu amesema uthibiti wa taka kwenye halmashauri ni jambo muhimu katika kuhakikisha kunakuwa na usafi wa mazingira na udhibiti wa magonjwa ya milipuko na kuongeza kuwa, takwimu za kisayansi zinaeleza kwamba uthibiti madhubuti wa taka ngumu unapelekea kupungua kwa asilimia 30 hadi 40 za magonjwa kama Malaria na mengineyo ambayo yanadhibitiwa kwa usafi wa mazingira.
Akizungumza kwa niaba ya washiriki, Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti taka ngumu wa Halmashauri ya wilaya Bahi Bw. William Mpangala amesema kuwa Serikali kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa inaendelea kushirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa afua za udhibiti wa taka ngumu kama za ukusanyaji na uchakataji wa taka ngumu, na kuongeza kuwa ushirikishwaji huo umeongeza ufanisi katika udhibiti wa taka kwenye halmashauri nchini.
Mkutano wa Mwaka huu una kaulimbiu isemayo “Taka ngumu ni Mali; tumia, rejeleza na Weka Miji katika hali ya usafi”.

Ujumbe wa wadau wa maendeleo ya elimu ukiwemo Global Partnership for Education (GPE) pamoja na Education Program for Results (EP4R) ukiongozwa na Morten Sigsgaard Mratibu wa Ushirika wa Nchi (GPE) umeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu inayotekelezwa katika Shule ya Msingi na Sekondari Buswelu, Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo Mei 11, 2026, Morten amesema miradi hiyo imeendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, hususan kwa wanafunzi wa elimu jumuishi.
Katika Shule ya Msingi Buswelu, inayohudumia wanafunzi 1,211 wakiwemo 176 wenye mahitaji maalumu, imefanikiwa kujenga bweni la wasichana wenye mahitaji maalumu kupitia ufadhili wa Serikali na GPE-LANES II.
Mradi huo9 umewezesha wanafunzi 80 kupata makazi salama ya bweni, huku huduma za bweni zikianza rasmi Mei 8, 2026 baada ya Serikali kuanza kutoa fedha za chakula.
Aidha, walimu na wanafunzi wameeleza mabadiliko chanya yaliyotokana na miradi hiyo, wakisema awali wanafunzi walikuwa wakisoma katika mazingira ya msongamano wa madarasa, lakini sasa wanapata nafasi ya kusoma katika mazingira bora na yenye nafasi ya kutosha, jambo lililoongeza umakini na ushiriki darasani.
Katika Shule ya Sekondari Buswelu, kupitia Programu ya EP4R, shule imepokea Shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa vyenye viti na meza 100, mradi ambao tayari umekamilika na unatumika.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wanasema awali walikuwa wakisoma wakiwa wamebanana kutokana na upungufu wa madarasa, hali iliyokuwa ikichangia usumbufu wakati wa masomo, lakini kwa sasa wanafurahia kusoma katika madarasa mapya yenye nafasi kubwa na mazingira rafiki ya kujifunzia.
Uongozi wa shule ulieleza kuwa miradi hiyo imechangia kuboresha ufaulu pamoja na kuongeza hamasa ya kujifunza.
Wadua wa maendeleo walitoa pongezi kwa Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya elimu na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kuboresha mazingira ya kujifunzia nchini.











📌 Vijana maeneo ya mradi wa umeme kwenye vitongoji kupewa kipaumbele kwenye ajira
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imetoa wito kwa wananchi kuwa walinzi wa kwanza wa miundombinu ya miradi ya kufikisha umeme vijijini inayotekelezwa na serikali, huku ikieleza kusikitishwa na matukio ya wizi wa vifaa vya umeme ikiwemo waya za mashine umba (transfoma) katika baadhi ya maeneo.
Wito huo umetolewa leo Mei 11, 2026 Mkoani Manyara na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu wakati akihitimisha ziara ya Bodi hiyo katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikiwa ni miradi ya nishati safi ya kupikia pamoja na miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji.
Balozi Kingu amesema serikali imetumia fedha nyingi kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda miundombinu hiyo dhidi ya vitendo vya hujuma na wizi vinavyoweza kuchelewesha maendeleo ya wananchi.
Katika ziara hiyo mkoani Manyara, Bodi ya REB imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji ambao ni kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom Tanzania pamoja na China Railway Seventh Group.
Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Msimamizi wa Miradi wa REA Mkoa wa Manyara, Mhandisi Geofrey Mkeni, amesema serikali kupitia REA imetenga zaidi ya shilingi bilioni 45.8 kwa ajili ya miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji 267 vya mkoa wa Manyara.
Mhandisi Mkeni amesema miradi hiyo inalenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme kwa wananchi wa vijijini ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Pia ametoa wito kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayofikiwa na miradi hiyo kuanza kufanya maandalizi ya miundombinu ya ndani ya nyumba ikiwemo wiring ili wawe tayari kuunganishiwa huduma ya umeme mara baada ya miradi hiyo kukamilika.
Kwa upande wao, wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo wameahidi kuhakikisha kazi zinakamilika kwa wakati huku wananchi wakinufaika kupitia ajira zinazotokana na utekelezaji wa miradi hiyo.
Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom Tanzania, Afisa Mahusiano ya Jamii na Mazingira, Oliver Charles, amesema miradi hiyo imefungua fursa mbalimbali za ajira kwa vijana wanaoishi katika maeneo yenye miradi ili wawe sehemu ya maendeleo yanayoletwa na serikali.
Naye Mhandisi wa Miradi kutoka kampuni ya China Railway Seventh Group, Estheria Fumbuka, amesema kampuni hiyo itaendelea kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati ili malengo ya serikali ya kuwafikishia wananchi huduma ya umeme vijijini yaweze kutimia.

Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) itaendelea kununua dawa zinazozalishwa na wawekezaji wa ndani ili kuimarisha uzalishaji wa ndani wa bidhaa za afya na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi.
Hayo yamesemwa Waziri wa Afya, Mohammed Mchengerwa leo Mei 11 2026 akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 Bungeni, Jijini Dodoma.
“Serikali imejipanga kuhakikisha MSD inanunua kwanza dawa zinazozalishwa ndani ya nchi zilizokidhi viwango vya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kabla ya kwenda kununua kutoka nje ya nchi, hatua inalenga kukuza viwanda vya ndani, kuongeza ajira na kuimarisha uchumi wa Taifa” amesema Waziri Mchengerwa
Amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, ikiwemo kuboresha upatikanaji wa ardhi, miundombinu muhimu pamoja na kuratibu uwekezaji katika sekta ya dawa na bidhaa za afya ili kuvutia uwekezaji zaidi nchini.
Waziri Mchengerwa amesema Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini kwa kutoa Shilingi trilioni 1.4 kupitia MSD ili kuhakikisha wananchi wanapata dawa na bidhaa muhimu za afya kwa wakati.
“Upatikanaji wa bidhaa muhimu za afya umeongezeka kutoka asilimia 58 mwaka 2021/22 hadi asilimia 88 mwezi Machi 2026” amesema Waziri Mchengerwa.
Amesema kuwa Wizara ya Afya itaendelea kuhamasisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi pamoja na kuwawekea mazingira rafiki na wezeshi, ikiwemo upatikanaji wa ardhi na miundombinu muhimu, ili kuwavutia kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya bidhaa za afya na kupunguza utegemezi.
Waziri Mchengerwa amesisitiza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya, dawa salama na huduma zenye ubora bila kuachwa nyuma.
-Wanufaika 463,228 waanza kupata huduma za matibabu.
Na Grace Michael, NHIF-Dodoma
Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kaya zisizo na uwezo kwa kutoa Shilingi bilioni 48.8 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi wa makundi maalum kupata huduma za afya kwa uhakika.
Kupitia utekelezaji huo, jumla ya kaya 172,297 tayari zimefikiwa na kuingizwa kwenye mpango huo, huku wanufaika 463,228 wakianza kupata huduma mbalimbali za matibabu katika vituo vilivyosajiliwa nchini.
Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya Fungu 52 kwa mwaka 2026/27 Waziri wa Afya Mhe. Omary Mchengerwa amesema kuwa, utekelezaji huu unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kujali hali yake ya kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya safari ya kuelekea huduma jumuishi za afya kwa wananchi wote.
Katika kuimarisha sekta ya afya sambamba na utekelezaji wa mpango huo, mabaraza na bodi za kitaaluma yameendelea kusimamia ubora wa huduma kwa kusajili wataalam wa afya 14,310, hatua inayoongeza nguvu kazi muhimu kwa utoaji wa huduma nchini.
Amesema kuwa kuhusu upatikanaji wa huduma za matibabu, jumla ya maduka ya dawa 330 yamesajiliwa pamoja na watarajali 3,004, huku vituo vya kutolea huduma za afya 3,643 vikisajiliwa ili kuongeza upatikanaji wa huduma karibu na wananchi.
Katika kuhakikisha taaluma na maadili yanaendelea kuzingatiwa hususan wakati huu wa kuhudumia wananchi wengi zaidi kupitia mfumo wa Bima ya Afya, vituo binafsi vya afya 654 vimekaguliwa ili kuhakikisha vinakidhi viwango na kutoa huduma salama kwa wananchi.
Mafanikio hayo yanaakisi hatua kubwa ya Serikali katika kujenga mfumo imara wa afya unaojali usawa, ubora na upatikanaji wa huduma kwa wote, huku Bima ya Afya kwa Wote ikiendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Na Hassan Kimweri, WAF - Dodoma
Sekta ya afya nchini imepata mafanikio makubwa katika kipindi cha awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yaliyoongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi kupitia ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa vifaa tiba, uoatikanaji wa dawa pamoja na huduma za kibingwa na za dharura nchini.
Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema hayo leo Mei 11, 2026 wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Spika wa Bunge Mhe. Mussa Azan Zungu.
"Eneo la vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoka elfu 10,153 mwaka 2021/22 hadi elfu 13,683 kufikia Machi 2026, sawa na ongezeko la vituo 3,530, Zahanati zimeongezeka kutoka elfu 7,189 hadi elfu 8,706 huku hospitali zikiongezeka kutoka mia 404 hadi mia 475 mwaka 2026," amesema Waziri Mchengerwa
Aidha, Waziri Mchengerwa amesema Serikali imeongeza majengo mapya katika hospitali mbalimbali zikiwemo Hospitali ya Muhimbili, KCMC, BMH, Bugando, Mirembe, pamoja na Kibong'oto huku ikiwa imejenga hospitali mpya 10 za rufaa za mikoa, kukarabati hospitali kongwe 50, kukamilisha maboma 980 ya zahanati na kujenga vituo vya afya 390.
Amesema, katika huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto, Serikali imeongeza wodi za watoto wachanga kutoka 80 hadi 438 pamoja na vituo vya upasuaji wa dharura kutoka 445 hadi 630 ambayo ni mafanikio yaliyochangia kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 556 mwaka 2016 hadi vifo 104 mwaka 2022 kwa kila vizazi hai 100,000.
"Katika huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa, Serikali imenunua na kusimika vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi bilioni 241.6 ambapo mashine za MRI zimeongezeka kutoka 7 hadi 13, CT Scan kutoka 12 hadi 45 pamoja na Digital X-ray kutoka 147 hadi 559," amesema Waziri Mchengerea
Kwa upande wa chanjo, amesema watoto waliopata chanjo ya Pentavalent dozi ya tatu wameongezeka kutoka watoto milioni 2,093,412 hadi milioni 3,186,979 huku kiwango cha chanjo kikiongezeka kutoka asilimia 93 hadi 96, juu ya lengo la kimataifa la asilimia 90.
"Upatikanaji wa dawa na bidhaa za afya umeimarika, Serikali imetoa Shilingi trilioni 1.4 kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba, viwanda vipya 11 vya dawa na vifaa tiba vimeanzishwa huku 'Tanzania Pharmaceutical Industries kikifufuliwa kwa ajili ya uzalishaji wa dawa za VVU nchini," amesema Waziri Mchengerea
Waziri wa Afya, Omary Mchenjgerwa amesema Serikali imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza kwa kuongeza huduma za matibabu, kinga na elimu kwa jamii, hatua iliyochangia kuongezeka kwa kliniki za kisukari na shinikizo la damu nchini.
Akizungumza leo Mei 11, 2026 bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mchenjgerwa amesema wizara imeendelea kuimarisha uratibu na utekelezaji wa afua za magonjwa ya kisukari, shinikizo la damu pamoja na magonjwa sugu ya mfumo wa upumuaji.
Amesema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, Serikali imeanzisha kliniki mpya 130 za huduma za kisukari na shinikizo la damu, na kufanya idadi ya kliniki hizo kufikia 168 kutoka kliniki 38 zilizokuwepo katika kipindi kama hicho mwaka 2025.
Kwa mujibu wa Waziri huyo, kliniki hizo zimepatiwa dawa muhimu, vifaa tiba pamoja na mafunzo kwa watumishi wa afya ili kuboresha upatikanaji na ubora wa huduma kwa wananchi wenye magonjwa yasiyoambukiza.
Aidha, amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za kinga na uchunguzi wa magonjwa hayo kupitia kampeni mbalimbali za afya ikiwemo upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza katika maeneo ya kazi, utoaji wa elimu kwa jamii pamoja na matembezi ya Kitaifa yanayohamasisha wananchi kufanya mazoezi.
Mchenjgerwa ameongeza kuwa Wizara pia imeendelea kutumia vyombo mbalimbali vya habari kutoa elimu ya uhamasishaji kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza, hatua inayolenga kupunguza ongezeko la wagonjwa na madhara yatokanayo na magonjwa hayo nchini.
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) leo Mei 10, 2026 imefanya ziara katika Kampuni zinazozalisha, kusambaza bidhaa za nishati safi ya kupikia katika Mkoa wa Arusha.
Bodi hiyo ikiwa imeongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu pamoja na Wajumbe wa Bodi hiyo, Mhe. Radhia Msuya na Mhandisi Sophia Mgonja waliweza kutembelea kampuni ya Ignate Energy Access yenye bidhaa za My Sol pamoja na kampuni ya HannyG Investment.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti Kingu, amezipongeza kampuni hizo kwa kuunga mkono kampeni ya Serikali ya Nishati Safi ya Kupikia kwa kuanza kutengeneza pamoja na kusambaza bidhaa za nishati safi ya kupikia huku akitoa wito kwa makampuni mengine kuendelea kuunga mkono kampeni hiyo ili malengo yaliyowekwa ya ifikapo 2034, Asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.
Awali akitoa taarifa ya utendaji wa kampuni ya My Sol, Meneja Uendeshaji wa Mitambo, Joe Chambua, amesema kuwa pamoja na huduma zingine zinatolewa na kampuni hiyo ikiwamo huduma ya ufungaji wa umeme jua, kampuni hiyo imeanza kutekeleza mradi wa nishati safi ya kupikia kwa kuja na teknolojia rahisi na ya gharama nafuu ya mtambo wa biogasi.
Amesema kuwa wamefanikiwa kufunga mitambo ya biogasi katika taasisi mbalimbali nchini ikiwemo Magereza.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni ya Hanny G Investment, Hanny Mbaria, ambao wanajishughulisha na utengenezaji wa majiko banifu pamoja na mkaa mbadala ameishukuru Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuipa kampuni hiyo kazi ya kusambaza majiko banifu na mkaa mbadala katika shule 53 Tanzania Bara.
Mbaria amesema licha ya mradi wa nishati safi ya kupikia kulinda mazingira lakini pia mradi huo umetoa ajira kwa vijana wengi.
“Kwa sasa kampuni yetu imekua zaidi na tumeajiri vijana wengi zaidi tofauti na hapo awali. Kwa sasa tuna wafanyakazi zaidi ya 120 wenye ajira za kudumu na wasio na ajira za moja kwa moja ni 1000,” amesema Mbaria.

NAIBU Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Longido Mkoani Arusha,Dkt Steven Kiruswa amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo cha uongozi wake anawiwa na kuhakikisha anatekeleza vipaumbele 16 katika kukamilisha miradi ya maendeleo katika Jimbo hilo.
Dkt Kiruswa alisema hayo katika mkutano wa hadhara wenye lengo la kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Longido kwa kukichagua chama chake cha Chama Cha Mapinduzi{CCM},Mgombea Urasi wa chama hicho Rais Samia Suluhu Hassan na Makamu wake Dkt Emmanuel Nchimbi,Mbunge na Madiwani wote wa chama hicho katika mkutano uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali katika ngazi ya tawi,kata na wilaya uliofanyika katika uwanja wa Longido Polisi.
Alisema moja ya vipaumbe ambavyo anataka kuvifanyia kazi katika kipindi miaka mitano ya ubunge wake ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa shule za msingi na sekondari katika kata zote za Jimbo hilo,kubuni miradi ya ajira kwa vijana,kukamilisha mradi wa maji wa chanzo cha Loormokerian Kijiji cha Oltepesi,kuchimba visima vya maji Kiseriani na Orkesumet.
Waziri Kiruswa alitaja kipaumbe kingine ni pamoja na ukarabati na ufunguaji wa barabara zilizo chini ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijni{TARURA} kwenye maeneo ynye vipaumbele,uendelezaji wa shule shikizi katika kata ambazo hazina ikiwa ni njia ya kupunguza umbali mrefu kwa watoto kwenda na kurudi shule na kujikinga na wanyama wakali.
Alisema ana uhakika ndani ya muda huo vipaumbele alivyovioanisha vitakuwa vimekamilika kwa kushirikiana na wananchini,serikali kuu,wadau wa maendeleo na wafadhili wa ndani na nje lengo kuu ni kutaka kuwapelekea huduma wananchi.
Aidha alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi kwa kumpa kura nyingi Rais Samia Suluhu Hassan na kuwa Rais awamu ya sita na kusema kuwa uamuzi walioufanya umeiheshimisha Longido kwani imekuwa wilaya ya kwanza kwa kutoa kura Nyingi Mkoani Arusha.
Waziri Kiruswa alisema kutokana na hali hiyo aliwaomba wananchi wa Longido kuwa wamoja na watulivu katika kuiletea maendeleo Longido na kumwombea afya njema Rais ili aweze kuendelea kuiongoza nchi kwa amani na upendo.
''Nawaomba wananchi wa Longido tuiombe nchi amani na tumwombee Rais wetu Samia Suluhu Hassan afya njema kwani amekuwa mstari wa mbele kuiendeleza Longido hivyo kila mmoja kwa imani yake ya kiislamu na kikrusto anapaswa kufanya hivyo''alisema Kiruswa
Naye Mkuu wa wilaya ya Longido,Salumu Kally amesema ni wakati wa wana Longido kushirikiana na Mbunge katika kuiletea maendeleo Jimbo hilo na kusema kuwa mifarakano mara nyingi hurudisha nyumba maendeleo hivyo hataki kuliona hilo likitokea.
Naye Mbunge wa Monduli,Joseph Isack na Mbunge wa Ngorongoro Yannick Ndoinyo wote waliwaomba wananchi wa Longido kushirikiana na Mbunge wao Kiruswa kwani mbunge huyo ni mpenda watu na mpenda maendeleo hivyo wasidhubutu kuipoteza lulu hiyo kwa namna yoyote ile kwani watakuwa wamefanya maksa makubwa sana,










.jpeg)
.jpeg)
