Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, amesema Bodi inatarajia kuongeza bidhaa nyingine tano katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kuendelea kuwanufaisha watanzania katika sekta mbalimbali.

Akifungua kikao cha wadau cha kujadili na kupitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa WRRB wa miaka mitano (2026/27–2030/31) pamoja na kupokea maoni kuhusu maboresho ya Kanuni za Stakabadhi za Ghala, kilichofanyika Juni 26, 2026, mjini Morogoro, Bw. Bangu amesema mfumo huo umeendelea kukua kwa kasi na kuleta mafanikio makubwa.

Amesema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita mfumo huo ulikuwa unahusisha bidhaa mbili pekee, lakini kwa sasa unahusisha bidhaa 18, huku maandalizi yakiendelea kuongeza bidhaa nyingine tano ili kuimarisha uwazi, ushindani wa bei na kuongeza fursa za biashara ya mazao.

Bw. Bangu amebainisha kuwa pamoja na kuwanufaisha wakulima kwa kuwawezesha kuuza mazao yao kwa bei yenye ushindani, mfumo huo umechangia kuongeza mapato ya Serikali na kurahisisha Halmashauri kukusanya mapato yatokanayo na biashara ya mazao.

Aidha, amesema WRRB inaendelea na mazungumzo na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) pamoja na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) ili kuwezesha biashara ya mazao kufanyika kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, hatua itakayoongeza ufanisi na uwazi katika biashara hiyo.

Ameongeza kuwa Bodi itaendelea kuhamasisha matumizi ya mfumo huo kwa kuanzisha njia bunifu zitakazowasaidia wakulima kuepuka kuuza mazao yao mara tu baada ya mavuno, wakati bei zikiwa chini.

Kwa miaka mingi nilimchukulia rafiki yangu kama ndugu wa karibu. Tulishirikiana katika mambo mengi ya maisha.

Nilimwamini kwa siri zangu, mipango yangu ya biashara, na hata changamoto nilizokuwa napitia. Sikuwahi kufikiria kwamba angeweza kunitakia mabaya.

Lakini baada ya muda, mambo yalianza kwenda vibaya.

Biashara yangu ilianza kudorora bila sababu za kueleweka. Kila nilipopata nafasi nzuri, ghafla iliharibika. Marafiki wengine walianza kuniepuka, na hata baadhi ya mipango yangu muhimu ilivuja kabla haijatekelezwa. Nilijiuliza nilikuwa nakosea wapi. SOMA ZAIDI.
Nilipoajiriwa kwenye kampuni niliyokuwa nafanya kazi, niliahidi kufanya kila niwezalo ili niweze kupiga hatua. 

Nilikuwa nafika kazini mapema, nilikamilisha majukumu yangu kwa wakati, na nilijitahidi kufanya kazi kwa uaminifu. Kila mwaka niliamini kwamba juhudi zangu zingetambuliwa na ningepandishwa cheo.

Lakini miaka ilipita bila mabadiliko yoyote.
Niliona wafanyakazi wengine wakipata nafasi mpya huku mimi nikibaki kwenye nafasi ileile. Haikuwa kwamba sikuwa na uwezo, bali kila niliposubiri habari njema, siku ziliendelea kupita bila chochote kutokea.

Baada ya miaka minne nilianza kuvunjika moyo.
Nilijiuliza kama kweli kazi yangu ilikuwa ikionekana. Wakati mwingine nilifikiria kuacha kazi na kutafuta sehemu nyingine, lakini sikuwa na uhakika kama ningepata nafasi bora zaidi.
Nilihitaji mabadiliko. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto ya kuifanya ikue na kuwa moja ya biashara kubwa katika eneo letu. 

Nilifanya kazi kwa bidii kila siku. Nilihakikisha wateja wanapata huduma nzuri na bidhaa zenye ubora. Ingawa biashara iliendelea kuwepo, mapato yake yalitosha tu kulipa gharama za kawaida.

Nilihitaji mteja mkubwa ambaye angebadilisha hali yangu ya kifedha, lakini sikufanikiwa kumpata. Miaka miwili ilipita bila mafanikio.

Nilituma mapendekezo kwa kampuni mbalimbali na kuhudhuria mikutano mingi ya biashara. Mara nyingi niliahidiwa kwamba ningepigiwa simu, lakini majibu hayakuwahi kufika.

Wakati mwingine nilikaribia kupata mkataba, lakini dakika za mwisho nafasi hiyo ilipewa mtu mwingine. Nilianza kukata tamaa. Nilifikiria hata kufunga biashara na kuanza shughuli nyingine. Nilihisi juhudi zangu zote zilikuwa zimepotea bure. SOMA ZAIDI.
Nilikuwa kwenye mahusiano ambayo mwanzoni yalikuwa yenye furaha na upendo mkubwa.

Tulifanya kila kitu pamoja na tuliamini kwamba tungejenga maisha yetu ya baadaye kama familia. Lakini kadri muda ulivyopita, mambo yalianza kubadilika. Mawasiliano yalipungua na nilianza kuona mpenzi wangu akionyesha ukaribu usio wa kawaida na watu wengine.

Hali hiyo ilinivunja moyo. Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa lakini nilihisi kama alikuwa akizidi kuwa mbali nami. Nilianza kupoteza amani na kujiuliza kama mahusiano yetu yalikuwa yanafika mwisho. Sikutaka kuyaacha mapema. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa nikisafiri mara kwa mara kutokana na kazi yangu. Ingawa nilipenda kusafiri, kila safari iliniingia hofu. 

Nilikuwa nimeshuhudia ajali nyingi barabarani na mara kadhaa nilijikuta nikinusurika katika matukio yaliyoweza kunigharimu maisha. Hofu ilianza kutawala maisha yangu.

Kila nilipopanda gari, nilihisi wasiwasi. Familia yangu pia ilikuwa ikiishi kwa hofu kila nilipowaaga kwenda safari za mbali. Nilitamani kupata amani ya moyo ili niweze kufanya kazi zangu bila kuishi kwa hofu kila siku. SOMA ZAIDI.
Kariakoo, 26 Juni 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kariakoo imeendelea na maadhimisho ya miaka 30 ya TRA na maandalizi ya Tuzo za Rais kwa Walipakodi kwa kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii, ambapo leo imekabidhi vifaa tiba katika Hospitali ya Mnazi Mmoja. Msafara huo uliongozwa na Kaimu Meneja wa Mkoa wa Kikodi Kariakoo, Bw. Edson Issanya.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga vijana 400 wa Kitanzania waliopata fursa za ajira nje ya nchi iliyofanyika katika Ukumbi wa NSSF Mafao House jijini Dar es Salaam, tarehe 25 Juni, 2026.
CHUO Kikuu cha Mzumbe kimesema mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yatategemea kwa kiwango kikubwa ushiriki wa sekta binafsi, hususan katika kuzalisha ajira, kuvutia mitaji na kuharakisha ukuaji wa uchumi wa kisasa na wenye ushindani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC), David Kafulila amesema Tanzania haiwezi kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwa kutegemea kodi na mikopo pekee, akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ubia kati ya Serikali na sekta binafsi katika kugharamia na kuendesha miradi ya maendeleo.

Na Mwandishi Wetu 

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania kwa kushirikana na taasisi ya Kidodi Foundation wameingia makubaliano ya kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini kwa kulifiki kundi la watoa huduma za Saluni nchini.

 


Na OWM - TAMISEMI, Lushoto

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia wananchi wa Wilaya ya Lushoto Gari la kuhudumia wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo, ambalo limekabidhiwa kwa wananchi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bw. Wazo Mwang’onda.

Prof. Shemdoe ametoa shukrani hizo kwa Mhe. Rais kwa niaba ya wananchi wa Lushoto, leo Juni 26, 2026 wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru wilayani humo ukitokea wilaya ya Bumbuli, yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Kizala Lushoto.

“Tuna mshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia gari la kuhudumia wagonjwa katika hospitali ya wilaya, kwani gari lililokuwa likitumika katika hospitali hiyo lilipelekwa kata ya Mlola ambayo ni miongoni mwa kata 33 za wilaya ya Lushoto, ambayo ina vituo vya afya nane (8)  na kati ya hivyo ni vinne tu ndio vina magari ya kuhudumia wagonjwa,” ameeleza Prof. Shemdoe.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bw. Wazo Mwang’onda, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoendelea kusogeza huduma za afya msingi karibu na wananchi kupitia ujenzi wa vituo vya afya na zahanati, ikiwa ni pamoja na kupeleka magari ya kuhudumia wagonjwa katika vituo mbalimbali vya afya.

“Leo hapa tumeshuhudia gari jipya ambalo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amelileta Lushoto, nami nalikabidhi likawahudumie wananchi, na kuongeza kuwa Mwenge wa Uhuru umefurahishwa sana na huduma ambayo Mheshimiwa Rais ameileta kwa wananchi wa Lushoto,” amesema Bw. Mwang’onda.

Mwenge wa Uhuru katika wilaya ya Lushoto umeshakagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa barabara, ujenzi wa hoteli ya kitalii, ukarabati wa matenki ya maji,  umaliziaji wa madarasa, mradi wa vijana  pamoja na  wa kituo cha afya ambapo kesho asubuhi utakakabidhiwa katika wilaya ya Korogwe.














Nilipoolewa, nilikuwa na matumaini makubwa ya kuanzisha familia yenye watoto na furaha.

Mimi na mume wangu tulikuwa na ndoto za muda mrefu kuhusu jinsi tutakavyolea watoto wetu na kujenga maisha ya pamoja yaliyojaa upendo. Hata hivyo, miezi iligeuka kuwa miaka bila kupata ujauzito.

Miaka miwili ya kwanza tulichukulia kama kawaida. Lakini kadri muda ulivyoendelea, maswali kutoka kwa watu wa karibu yalianza kuongezeka. 

Kila mara tulikuwa tukikumbushwa jambo ambalo tayari lilikuwa linatugusa moyoni kwa kina. Nilijikuta nikikumbwa na huzuni kila nilipoona familia nyingine zikifurahia watoto wao.

Tulianza kutafuta ushauri wa kitabibu na njia mbalimbali za kupata msaada. Tulipitia vipimo, tukapata ushauri tofauti, na kila mara tulijaribu kubaki na matumaini. 

Hata hivyo, miaka ilizidi kwenda bila mabadiliko. Baada ya miaka saba, tulikuwa karibu kukata tamaa kabisa. Kulikuwa na siku ambazo nilijitenga kabisa na watu. SOMA ZAIDI.

Kwa muda mrefu, maisha yangu yalibadilika kutokana na tatizo ambalo sikulielewa vizuri.

Kila usiku nilikuwa nikienda kulala nikiwa na matumaini ya kupumzika, lakini mara nyingi nilikuwa naamka katikati ya usiku nikiwa na hofu kubwa. Nilikuwa naota ndoto za kutisha zilizokuwa zikijirudia mara kwa mara.

Kadri muda ulivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.
Nilianza kukosa usingizi wa kutosha. Kila asubuhi nilikuwa nimechoka, kichwa kikiwa kizito na mwili hauna nguvu. Kazini nilianza kushindwa kuzingatia kazi zangu na mara nyingi nilifanya makosa ambayo hayakuwa ya kawaida kwangu.

Hali hiyo ilinifanya niwe na wasiwasi mkubwa.
Nilijaribu njia mbalimbali za kawaida ili kupata usingizi, lakini hazikusaidia kwa muda mrefu. Wakati mwingine nililala kwa muda mfupi tu kisha nikashtuka tena nikiwa na hofu isiyoelezeka. Familia yangu ilianza kugundua mabadiliko yangu.SOMA ZAIDI.