Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amewaomba Wakristo na Waislamu mkoani Mbeya kuendelea kutenda mema, kuishi kwa upendo, umoja na amani hata baada ya kumalizika kwa vipindi vya mfungo wa Kwaresma na Ramadhani.
Ameyasema hayo katika futari (Iftari) iliyoandaliwa na Taasisi ya Maryprisca Women Foundation iliyowakutanisha viongozi wa serikali, Jeshi la Polisi, vyama vya siasa, taasisi za kidini pamoja na wananchi wa Kata ya Iwambi na kata jirani, Mahundi amesema waumini wanapaswa kuyaishi mafundisho ya vitabu vitakatifu hata baada ya kumaliza ibada za mfungo na kuendelea kuiombea nchi.
“Ni wajibu wetu kuyaishi yale yote tunayofundishwa katika vitabu vitakatifu vya dini zetu. Tusiache kuiombea nchi yetu ya Tanzania ili iendelee kuwa na amani na upendo kwa sababu hiyo ndiyo lugha yetu na utamaduni wetu kama taifa,ni wasihi tuendelee kuiamini serikali na kuendelea kudumisha mshikamano maana hii ni tunu yetu watanzania wote ” amesema Mahundi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Josephine Manase, alimpongeza Mhe. Mahundi kwa moyo wake wa upendo kwa jamii na kuwataka viongozi wa dini kuendelea kuwajali watoto yatima pamoja na watu wasiojiweza katika jamii maana hiyo ndio ibada kuu katika maisha ya mwanadamu.
“Katika ibada mnazozifanya msisahau kuwahudumia watoto yatima na wale wasiojiweza kwa sababu kuwahudumia wao ni sehemu ya ibada kubwa na kumbukumbu isiyofutika mbele za Mwenyezi Mungu lakini pia tuendelee kumuombea Rais wetu ili aweze kuendelea kufanya kazi ya kutuletea maendeleo” amesema Manase.
Salamu za Serikali ya Wilaya ya Mbeya zilizowasilishwa na Afisa Tawala wa Wilaya hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Devotha Chacha, zimemhakikishia Mhe. Mahundi ushirikiano wa kutosha katika shughuli zake za kijamii. ambapo Serikali ya Wilaya ya Mbeya itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi hiyo kwani kazi wanazozifanya ni huduma kwa jamii na ni wito kutoka kwa Mwenyezi Mungu"amesema Devotha
Kwa upande wao viongozi mbalimbali wa dini waliohudhuria iftari hiyo wamempongeza Mhe. Mahundi kwa kuendelea kudumisha utaratibu wa kuwakutanisha wananchi wa dini tofauti katika futari hiyo wakisema hatua hiyo inaimarisha upendo, mshikamano na amani katika jamii.
"Utaratibu huu wa kuwakutanisha watu wa dini mbalimbali ni jambo jema linaloendelea kuimarisha upendo na umoja katika jamii, na tunaona mabadiliko kila mwaka kwa kuwa wananchi wanaendelea kuungana zaidi,” wamesema viongozi hao wa dini.























.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




