Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu na Ubora wa WRRB, Bw. Mwita Thomas,akizungumza wakati wa ufungaji mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika Morogoro.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.
Na.Mwandishi Wetu-MOROGORO
Watumishi na wasimamizi wa shughuli za ghala nchini wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji ili kuimarisha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuongeza ufanisi katika biashara ya mazao ya kilimo.
Wito huo umetolewa na Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, alipokuwa akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo.
Bi. Chatta amesema uadilifu wa watendaji wa mfumo ni msingi wa kujenga imani kwa wakulima, wanunuzi na taasisi za fedha, huku akisisitiza kuwa Mfumo huo umeendelea kuwa nyenzo muhimu ya kuhakikisha biashara ya mazao inafanyika kwa uwazi, ubora na ushindani.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhimiza matumizi ya Mfumo huo pamoja na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) ili kuongeza thamani ya mazao, kupanua fursa za masoko yenye ushindani na kuongeza manufaa kwa wakulima.
Aidha, amewataka washiriki kutumia maarifa waliyoyapata kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kuendana na mabadiliko ya teknolojia na kuhakikisha taarifa za mazao zinakuwa sahihi na kwa wakati.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu na Ubora wa WRRB, Bw. Mwita Thomas, amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kuzingatia sheria, kanuni na taratibu walizofundishwa ili kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji, pamoja na kulinda hadhi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.
Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na WRRB yamefanyika kwa siku tano na yamehudhuriwa na washiriki 103 kutoka kampuni za uendeshaji wa ghala na wadau mbalimbali wa Mfumo huo.
Siku zote alikuwa miongoni mwa wale wanaopinga imani yoyote inayohusiana na mambo ya kiroho au usaidizi wa kipekee nje ya hospitali na sheria za kawaida.
Lakini maisha ni walimu wakubwa kuliko vitabu. Na wakati mwingine, hata wasioamini, hupata sababu ya kufikiri upya. Brian alikuwa kwenye uhusiano wa muda mrefu na msichana aitwaye Hellen. Walikuwa kama mfano wa wapenzi bora mitandaoni. Picha za mapenzi, safari, zawadi ilikuwa ni hadithi ya kisasa ya upendo.
Hata hivyo, mambo yalianza kubadilika mwaka jana, pale Brian alipogundua kwamba Hellen alikuwa akiongea kwa karibu sana na jamaa mmoja wa kazini kwake. Awali alipuuzia, akiamini ni wivu tu wa kawaida. Lakini alipoanza kuona ujumbe mfupi wa siri, mazungumzo ya sauti usiku wa manane, na safari za ghafla zisizoelezeka, alijua kuna jambo. SOMA ZAIDI.
Nilijaribu njia nyingi za kujitibu, nikitembelea madaktari na kutumia dawa za hospitali, lakini hakuna kilichobadilika. Nilikuwa nikikosa usingizi na kujikuta nikiishi na hofu ya kila wakati. Hali hii ilianza kuathiri maisha yangu ya kila siku, hata kazi yangu.
Nilikuwa mchovu, mwenye huzuni, na nashindwa kuendelea mbele. SOMA ZAIDI.
Nilijaribu kila njia. Nilihudhuria kliniki za kibingwa, nikatumia dawa za gharama kubwa, nilijaribu hata mashine maalum za mazoezi ya nyonga. Madaktari walinitia moyo kuwa inaweza kuisha kwa muda, lakini mwaka ulipita baada ya mwingine, hali haikubadilika.
Nilijiepusha na mahusiano ya karibu, nikaacha safari za usiku, na hata kazi zilizoitaji kulala nje niliziacha all kwa sababu ya haya. Mara moja nikiwa kazini, niliitwa kwenye kikao cha wafanyakazi cha kusafiri nje ya jiji. Kwa kisingizio cha afya, niliomba nisiende.
Lakini macho ya baadhi ya wenzangu yalinielekea kwa mashaka. Nilihisi kama watu walikuwa wakianza kugundua kuwa kuna kitu kisicho cha kawaida kwangu. Ukweli ni kwamba nilikuwa nimechoka kujificha. Nilihitaji mabadiliko. SOMA ZAIDI.
Wafugaji nchini wanatarajiwa kunufaika na biashara ya kisasa ya mifugo baada ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kuanza kuingiza mifugo katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, utakaounganisha taarifa za mifugo kidijitali na kuwawezesha wanunuzi kushindana kwa uwazi kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).
Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema baada ya mafanikio ya kusimamia bidhaa 18 za mazao ya kilimo kupitia mfumo huo, sasa bodi imepanua huduma zake kwa kujumuisha mifugo.
Amesema hatua hiyo inatokana na mahitaji ya wafugaji waliokuwa wakihoji kwa nini mfumo huo unawanufaisha wakulima pekee huku sekta ya mifugo ikibaki nje.
"Tumekuja na bidhaa mpya ambazo zimeongezwa kwenye mfumo, na kubwa zaidi tumewafikia wafugaji. Tulikuwa tunasimamia bidhaa 18 za mazao ya kilimo, lakini sasa tumeingia rasmi kwenye bidhaa za mifugo," amesema.
Bw. Bangu amesema WRRB inalenga kuunganisha biashara ya mifugo na TMX, ambapo taarifa za kila mnyama zitawekwa kidijitali ili wanunuzi waweze kuzifikia kwa urahisi, kushindana kwa uwazi na kufanya maamuzi ya ununuzi kwa kutumia taarifa sahihi badala ya makadirio.
Ameeleza kuwa mfumo huo utatumia taarifa zinazopatikana kupitia hereni za utambuzi wa mifugo zilizozinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ambazo zina namba maalumu zinazobeba taarifa za kila mnyama.
"Tunafahamu Mheshimiwa Rais Samia miaka miwili iliyopita alizindua uwekaji wa hereni kwenye mifugo. Sisi kama WRRB tunapiga hatua zaidi kwa kutumia taarifa zilizopo kwenye hereni hizo kuingiza mifugo kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala. Hereni hiyo ndiyo itakuwa msingi wa stakabadhi kwa kuwa ina namba na taarifa zote za mnyama," amesema.
Amefafanua kuwa mfumo huo utawanufaisha wafugaji wanaojishughulisha na unenepeshaji wa mifugo kwa kuwa mifugo yao itahifadhiwa katika maeneo maalumu yatakayokuwa yanatambulika kama ghala, huku wafugaji wakipewa stakabadhi zitakazowawezesha kupata mikopo kutoka taasisi za fedha.
Kwa mujibu wa Bangu, WRRB tayari imefikia makubaliano na Benki ya NBC ambayo imekubali kutoa mikopo kwa wafugaji watakaoweka mifugo yao kwenye ghala.
"Wengi wanauliza ghala litakuwaje. Kwa upande wa mifugo, zizi ndilo litakuwa ghala. Mifugo itatunzwa katika maeneo maalumu yenye chakula na huduma za matibabu, huku mfugaji akiwa na stakabadhi inayomwezesha kupata fedha bila kulazimika kuuza mifugo yake mapema," amesema.
Bangu amesema hatua nyingine muhimu ni kuondoa utaratibu wa kupanga bei kwa kutazama mwonekano wa mnyama pekee, badala yake mifugo itapimwa kwa uzito ili bei iweze kuamuliwa kwa kuzingatia kilo halisi za mnyama.
"Leo hii kwenye minada mingi ng'ombe anapimwa kwa macho, anaonekana mnene au mwembamba ndipo bei inawekwa. Sisi tunataka mifugo ipimwe kwa uzito ili bei iwe ya haki kwa mfugaji na mnunuzi. Hii itakuwa mkombozi mkubwa kwa wafugaji na pia itarahisisha upatikanaji wa taarifa zinazohitajika katika masoko ya ndani na kimataifa," amesema.


Serikali imewaagiza wazalishaji wote nchini kutumia alama ya 'Made in Tanzania' ili kuongeza imani kwa bidhaa zinazozalishwa nchini na kuimarisha ushindani wake katika masoko ya kimataifa.
Agizo hilo limetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Immanuel Nchimbi, kwenye kilele cha Usiku wa Jubilei ya Dhahabu (Miaka 50) ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), uliofanyika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam. Sherehe hizo zilienda sambamba na utoaji wa tuzo kwa washirika muhimu wa mamlaka hiyo. Udhibiti wa Viwango na Huduma za Kifedha.
Aidha, Makamu wa Rais amezitaka taasisi zinazosimamia viwango na huduma za kifedha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha bidhaa za Tanzania zinakidhi viwango vya kimataifa. Alisema matumizi ya alama ya 'Made in Tanzania' yataongeza utambulisho wa bidhaa zenye ubora na kuimarisha heshima ya taifa katika biashara za kimataifa.
"Nazipongeza taasisi za fedha kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa viwanda vidogo na vya kati, akisema hatua hiyo imeendelea kupunguza changamoto za upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali na kuchochea ukuaji wa uzalishaji nchini."amesema Balozi Nchimbi
Amesema Serikali itaendelea kuweka sera rafiki, kuboresha miundombinu na kuimarisha sekta binafsi ili kujenga uchumi wa viwanda wenye ushindani. Ameongeza kuwa maadhimisho ya Jubilei ya Dhahabu ya TANTRADE ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana, ikiwemo kuongezeka kwa viwanda, uzalishaji, ajira na upanuzi wa masoko ya bidhaa za Tanzania duniani.
Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga (Mb), amesisitiza kuwa manufaa makubwa ya rasilimali zilizopo nchini yatapatikana Tanzania itakapowekeza katika kuchakata na kuzalisha bidhaa za mwisho zenye ubora wa juu badala ya kuuza malighafi ghafi nje ya nchi.
Waziri Kapinga amebainisha kuwa hatua hiyo itafungua masoko mapya, itaongeza thamani ya mauzo ya nje, na kuinua uchumi wa wananchi kwa ujumla.
Mhe. Kapinga ameeleza kuwa, ili kujenga uchumi imara wa viwanda na wenye ushindani, kuna haja ya kubadili mtazamo wa kibiashara kwa kuhakikisha mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi, misitu na madini yanageuzwa kuwa bidhaa zilizofungashwa vizuri na kukidhi viwango vya kimataifa.
Amesisitiza kuwa uwekezaji mkubwa katika teknolojia za kisasa una mchango mkubwa katika kuongeza kiwango cha uzalishaji, kuboresha ubora wa bidhaa zinazotengenezwa nchini, kupunguza gharama za uendeshaji, na kuzipa bidhaa za Tanzania uwezo mkubwa wa kushindana katika soko la kimataifa.

Kukamilika kwa ujenzi wa Daraja la Upinde la Mawe katika Mto Mmbaga, Wilaya ya Ngorongoro, kunatarajiwa kufungua fursa za kijamii na kiuchumi kwa kurahisisha usafiri na usafirishaji, kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii pamoja na kuchochea biashara kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo jirani.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa daraja hilo katika mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang'onda, amesema kuwa mradi huo umeondoa adha ya muda mrefu iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa maeneo hayo, hususan kipindi cha msimu wa mvua ambapo ilikuwa changamoto kubwa kuvuka Mto Mmbaga.
Amesisitiza kuwa, Serikali ya awamu ya sita imeendelea kuboresha miundombinu ya barabara kwa kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika ujenzi wa barabara na madaraja ili kuimarisha miundombinu na kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.
"Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitambua changamoto zilizokuwa zinawakabili wananchi wa eneo Oldonyosambu na majirani zake na kuelekeza fedha zitolewe kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili, ambalo sasa limekuwa mkombozi kwa jamii, tuendelee kulitunza na kulitulitumia kwa usafirishaji wa watu na bidhaa, kupanua fursa za biashara na kuimarisha shughuli za kiuchumi kwa maendeleo yetu na Taifa letu," Amesema Mwang'onda.
Mwang'onda amesisitiza kuwa, Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini huku akiwahimiza wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu, ambayo ni msingi wa maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, Yanick Ndoinyo, alipokea kwa furaha kukamilika kwa daraja hilo akisema linahudumia kata za Sale, Pinyinyi na Oldonyosambu kupitia Masusu hadi Jema
Alimshukuru Rais Dk,Samia Suluhu Hassan kwa kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Ngorongoro kwa kutoa fedha za Mfuko wa Barabara zilizowezesha ujenzi wa daraja hilo, akieleza kuwa ni hatua muhimu katika kuboresha mawasiliano, usafiri na maisha ya wananchi wa wilaya hiyo.
Na.Mwandishi Wetu-Geneva
Tanzania imetoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano wa kimataifa ili kuhakikisha maendeleo ya kasi ya Akili Unde (AI) yanasimamiwa kupitia mifumo ya kimataifa iliyo jumuishi, yenye uwazi na usawa, ikitahadharisha kuwa nchi zinazoendelea hazipaswi kuachwa nyuma wakati teknolojia hiyo ikiendelea kubadili uchumi na jamii.
Akizungumza mbele ya zaidi ya wajumbe 190 wanaowakilisha serikali, mashirika ya kimataifa, sekta binafsi na jamii ya teknolojia duniani katika mdahalo wa Kimataifa kuhusu Utawala wa Akili Unde (Global Dialogue on AI Governance), Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki (Mb), aliwasilisha dira ya Tanzania ya kutumia Akili Unde kama kichocheo cha maendeleo ya taifa huku ikiimarisha mifumo ya kuhakikisha matumizi yake yanakuwa ya kuwajibika.
Waziri alisema Tanzania inaichukulia Akili Unde kuwa nguzo muhimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kichocheo muhimu cha uchumi wa kidijitali unaochipukia. Alieleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mageuzi ya kina ya sera na mifumo ya udhibiti ili kuweka mazingira imara yanayochochea ubunifu huku yakilinda haki za wananchi na kujenga imani ya umma.
“Tanzania inaamini kuwa Akili Unde ina uwezo wa kuleta mageuzi katika sekta za kilimo, afya, elimu, huduma za kifedha na utawala wa umma,” alisema Mhe. Kairuki. “Hivyo, matumizi yake yanapaswa kuwa salama, jumuishi na yalenge kuhakikisha wananchi wote wananufaika.”
Alieleza hatua zinazotekelezwa kuimarisha utawala wa Akili Unde, ikiwemo kuandaa mifumo ya udhibiti, kuboresha mifumo ya usimamizi wa data, kuimarisha ulinzi wa faragha na usalama wa mtandao, pamoja na kuandaa miongozo ya kitaifa ya matumizi ya Akili Unde katika sekta za kimkakati kama elimu na afya.
Waziri pia alieleza uwekezaji unaoendelea wa Serikali katika miundombinu ya kidijitali, akitaja upanuzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) pamoja na maendeleo ya Miundombinu ya Umma ya Kidijitali (Digital Public Infrastructure – DPI) kuwa msingi muhimu wa kupanua mawasiliano ya kidijitali na kuwezesha wananchi wengi zaidi kupata huduma zinazotumia Akili Unde nchini kote.
Mbali na mageuzi ya ndani ya nchi, Mhe. Angellah Kairuki alisisitiza kuwa utawala madhubuti wa Akili Unde unahitaji ushirikiano endelevu wa kimataifa.
Alithibitisha dhamira ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana kwa karibu na Umoja wa Kimataifa wa Mawasiliano (ITU), Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Mawasiliano Afrika (ATU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ili kuendeleza mifumo ya kidijitali inayoweza kushirikiana, inayorahisisha ubunifu, biashara na huduma za kuvuka mipaka huku ikilinda mamlaka ya nchi na usalama wa data.
Akihitimisha hotuba yake, Waziri Kairuki alitoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano wa kimataifa katika uhamishaji wa teknolojia, maendeleo ya ujuzi, ushirikiano wa tafiti, ubunifu na uwekezaji katika miundombinu ya kidijitali. Alisisitiza kuwa kuziba pengo la kidijitali kutahitaji hatua za pamoja ili kuhakikisha manufaa ya Akili Unde yanagawanywa kwa usawa kati ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
Mdahalo wa Kimataifa kuhusu Utawala wa Akili Unde unawakutanisha watunga sera, viongozi wa serikali, wataalamu wa teknolojia na wadau wa sekta binafsi kutoka duniani kote kwa lengo la kujenga mifumo ya kimataifa ya utawala wa Akili Unde na kujadili namna teknolojia hiyo inavyoweza kuchangia maendeleo jumuishi na endelevu.









