Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini.

Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini.

Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini ili Tanzania kuwa kitovu za usambazaji wa bidhaa hiyo barani Afrika.

“Lengo letu ni kuona wachimbaji wakubwa na wadogo hapa nchini wanapata bidhaa nyingi za kuzalisha madini pasipo kutegemea uagizwaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi," amesema Mavunde.

Naye, Mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Oriental Casting and Forging Ltd Bw. Hou Songcun amesema Kampuni yake ipo tayari kufanya uwekezaji mkubwa wa bidhaa za migodini nchini kwa kuwa Tanzania ni nchi ambayo ina mazingira mazuri ya uwekezaji na kwamba sekta ya madini inakua kwa kasi kubwa sana hivyo ni sehemu salama na rafiki ya kufanya uwekezaji ambao utakuwa suluhisho la upatikanaji wa bidhaa za migodini kwa urahisi zaidi.









Nilikuwa nimekata tamaa kabisa baada ya kukosa visa mara tatu mfululizo. Mara ya kwanza nilikataliwa kwa makosa madogo tu ya kiufundi, mara ya pili nikaambiwa sifai kifedha na mara ya tatu hata sikupewa nafasi ya mahojiano. Ilikuwa aibu kwa familia yangu na marafiki wangu.

Wengine walianza kuniambia niache kufikiria kwenda nje ya nchi kwa sababu labda haikuwa riziki yangu. Lakini ndoto yangu ya kuishi na kufanya kazi nje ya nchi ilikuwa kubwa kuliko maneno ya watu. Kila kukataliwa kuliniumiza moyo. Nilianza kupata msongo wa mawazo na hata kukosa usingizi.

Nilihisi kuna kitu kisicho cha kawaida kilichokuwa kinanizuia. Nilianza kuamini labda kuna watu walionionea wivu na kunifungia njia. Nilijaribu mara ya nne kuandaa nyaraka lakini nilihisi hofu na woga mkubwa. SOMA ZAIDI.
Nilipata kazi yangu ya ndoto baada ya kungoja kwa muda mrefu. Nilijua itakuwa nafasi ya kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Hata hivyo, mambo hayakuenda vile nilivyotarajia. Baada ya miezi michache nilianza kugundua bosi wangu hakuwa akinipenda.

Alionekana kunionea wivu kwa jinsi nilivyokuwa nafanya kazi vizuri na nilipata sifa kutoka kwa wafanyakazi wenzangu. Kila mradi nilipewa nilifanya kwa bidii, lakini kila mara alitafuta kosa dogo la kunilaumu mbele ya wenzangu.

Aliniweka kwenye shinikizo kubwa na aliniandikia barua ya onyo mara mbili kwa sababu ambazo hazikuwa na msingi. Nilihisi kama alitaka niachishwe kazi. Wafanyakazi wenzangu walinionea huruma lakini hakuna aliyethubutu kumkabili.

Nilianza kupoteza amani ya moyo. Kila asubuhi nilipokuwa nikiamka nilihisi kuchoka hata kabla ya kuingia ofisini. Niliwaza kuacha kazi lakini nilijua singeweza kumudu maisha bila kipato. Nilihitaji njia ya kubadilisha hali hii. SOMA ZAIDI.
Kila mtu katika familia yangu alijua kuna tatizo kubwa lakini hakuna aliyekuwa tayari kukubali. Kila siku ilianza na mabishano na ilimalizika kwa kelele. 

Baba na mama walikuwa wanagombana kwa sababu ndogo ndogo, watoto tulijikuta tukipigana wenyewe kwa sababu ya msongo.

Wageni walipoingia nyumbani waliona sura za hasira na kukaa kwetu pamoja mezani kuligeuka uwanja wa vita. 

Siku moja jirani alinieleza kuwa nyumbani kwetu kelele za matusi na ugomvi zilisikika hadi kwao. Nilijisikia aibu sana. Nilijua hali ile haikuwa ya kawaida.

Nilipojaribu kuzungumza na baba yangu hakutaka kunisikiliza. Mama alionekana amekata tamaa na ndugu zangu walikimbilia marafiki zao kila jioni ili wasikae nyumbani. 

Ilifika hatua nilihisi kama familia yetu ilivunjika. Nilipoona hali inazidi kuwa mbaya niliamua kutafuta suluhisho kwa siri.

Nilikuwa tayari kufanya lolote ilimradi amani irudi.SOMA ZAIDI.

Nilizaliwa katika familia iliyokumbwa na changamoto nyingi. Baba na mama walikuwa wakigombana mara kwa mara, na hata nilipokuwa mtu mzima, nilijikuta pia nikipitia matatizo kama hayo. 

Kila mara nilipojaribu kuanza biashara, iliniporomoka bila sababu ya kueleweka. Nilipoanzisha mahusiano, mara nyingi yalikuwa yakivunjika katikati ya furaha.

Watu wengi walinipa ushauri tofauti, wengine wakisema labda nilikuwa nimekumbwa na nuksi. Nilihisi nimeelemewa sana na niliamini labda maisha yangu yalikuwa yameandikwa kuwa ya mateso. Wengi walisema uchawi ni hatari, kwamba mtu akikimbilia huko anajiletea matatizo zaidi.

Kwa muda mrefu niliepuka hata kusikia neno hilo. Lakini nilipofikia hatua ya kukata tamaa kabisa, nilianza kutafuta njia mbadala. SOMA ZAIDI.
Niliposhitakiwa kwa kosa la ubakaji, nilihisi dunia imenigeuka. Majina yalinisakama mitaani, jirani na hata ndugu walinigeuka.....SOMA ZAIDI.

Nilikuwa nikipita barabarani nikisikia minong’ono, wengine wakinicheka kwa siri na wengine wakinipa macho ya hukumu. Niliona maisha yangu yote yakiporomoka ghafla, nikajua heshima yangu imefutwa milele.

Mwanamke aliyenishitaki alijua fika hakuwa na ushahidi wowote. Lengo lake lilikuwa kunilazimisha nimpe pesa nyingi ili kunyamazisha kesi. 

Alijua jina la ubakaji lingetisha na kunifanya nikubali masharti yake. Nilipoambiwa nitoe fedha ili nisionekane kortini, nilikataa.

Nilihisi moyoni kuwa ningepoteza kila kitu iwapo ningekubali uongo huo. Nilipoamua kusimama mahakamani, wengi waliniona kama mtu wa kujitakia maafa. 

Hata hivyo nilijua ukweli ulikuwa upande wangu. Nilichohitaji ni nguvu ya kusimama imara wakati huu mgumu.

 


📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba

📌 Kukamilika kwake  kutaongeza ufanisi wa uzalishaji na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani


Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji.

Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.

Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani.

“Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi,” amesema Mhe. Ndejembi.

Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usambazaji Umeme TANESCO, Mhandisi Timoth Mgaya, amesema mradi huo unagharimu dola za Kimarekani milioni 24.81, sawa na takribani shilingi bilioni 64, na hadi sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji.

“Mradi huu unagharimu dola milioni 24.81 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 64. Hadi sasa utekelezaji umefikia asilimia 83, na tunaendelea kushirikiana na mkandarasi kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika ndani ya muda uliopangwa,” amesisitiza Mhandisi Mgaya.

Mradi wa ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho, kuboresha utegemevu wa uzalishaji wa umeme na kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika kwa wananchi.

Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale ni kituo cha kwanza cha kuzalisha umeme kwa kutumia maji nchini. Kilijengwa kati ya mwaka 1961 na 1964 na kina uwezo wa kuzalisha takribani megawati 21. Ukarabati unaoendelea unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho ili kiendelee kutoa mchango mkubwa katika Gridi ya Taifa kwa miaka ijayo.











NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali ya Ireland imesisitiza kuendelea kuunga mkono juhudi za kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake katika taasisi za elimu ya juu nchini Tanzania, ikieleza kuwa elimu jumuishi ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye usawa.

 



📌Yasema ni matunda ya  uzalendo wa Watanzania katika kulipa kodi


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi mzuri wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ikieleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 ambao umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na kuwa miongoni mwa miradi mikubwa barani Afrika.

Hayo yamebainishwa leo Juni 29, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu (Mb), wakati wa ziara ya Kamati hiyo katika Mradi wa Kufua Umeme wa JNHPP uliopo Rufiji, mkoani Pwani, kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo.

"Sisi kama Kamati tumeridhishwa na kazi kubwa iliyofanyika katika mradi huu hadi kukamilika kwake kwani mradi huu umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na unachangia takribani asilimia 45 ya umeme kwenye Gridi ya Taifa. Hivyo, nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza utekelezaji wa mradi huu wa kimkakati ambao umeleta suluhisho la kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini," amesema Mhe. Mgalu.

Aidha, Mhe. Mgalu amewashukuru wananchi kwa kulipa kodi ambazo zimepelekea mradi huo mkubwa kukamilika huku akisisitiza kuwa Kamati itaendelea kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa umeme wa uhakika wakati wote.

Amefafanua kuwa umeme unaozalishwa na JNHPP utaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme kupitia miradi mbalimbali ya usafirishaji wa umeme ikiwemo mradi wa Chalinze–Dodoma.

 Vilevile, Mhe. Mgalu amesisitiza kuhusu kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuhakikisha umeme unaopatikana nchini unafika hadi ngazi ya vitongoji.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Umeme, Mhandisi Christopher Bitesigirwe, amesema ziara ya Kamati imelenga kujionea maendeleo ya mradi huo na imejiridhisha kuwa mitambo yote tisa imekamilika na inafanya kazi vizuri huku akiwahakikishia kukamilisha kwa wakati miradi yote ya usafirishaji na usambazaji wa umeme inayounganishwa na JNHPP.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Antony Mbushi, amesema TANESCO itaendelea kuhakikisha Kituo cha Kufua Umeme cha JNHPP kinaendeshwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwajengea uwezo wataalam wa Kitanzania wanaokisimamia ili kiendelee kuzalisha umeme wa uhakika kwa manufaa ya wananchi na maendeleo ya Taifa.
















 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius J. Ndejembi amesema mradi wa kimkakati wa kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani, mkoani Tanga nchini Tanzania wa EACOP (East African Crude Oil Pipeline), umefikia asilimia 86 ya utekelezaji, huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 2026.

Waziri Ndejembi ametoa kauli hiyo leo, Juni 29, 2026, wakati akikagua utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) katika eneo la Chongoleani, mkoani Tanga.

Mhe.  Ndejembi amesema kuwa kutokana na kasi nzuri ya utekelezaji wa mradi huo, meli ya kwanza inatarajiwa kuchukua mafuta ghafi kutoka Chongoleani mwezi Januari 2027, hatua muhimu inayosubiriwa kwa hamu.

Akitoa maelekezo kuhusu changamoto zilizobainishwa na mkandarasi, Waziri Ndejembi amemtaka mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa njia ya umeme itakayotumika katika uendeshaji wa mitambo kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo ifikapo mwanzoni mwa mwezi Agosti.

“Changamoto ndogo ndogo tulizozikuta ni kama umeme bado line hazijafika na nimemtaka mkandarasi kupitia Shirika letu la TANESCO kuhakikisha mpaka ifikapo tarehe ya mwisho wa mkataba wake awe amekamilisha kazi yake,” amesisitiza Waziri Ndejembi.

Amesema mradi huu ni miongoni mwa miradi ya mfano nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla, ukiwa umegharimu Dola za Marekani Bilioni 6.02. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechangia Dola za Marekani Milioni 374, sawa na asilimia 15 ya mchango wa wanahisa.

Kadhalika, Waziri Ndejembi ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutumia vizuri na kuchangamkia fursa zinazotokana na mradi huo. Amesema katika kipindi cha ujenzi, jumla ya ajira 10,000 zimezalishwa, ambapo ajira 7,500 sawa na asilimia 75 zimenufaisha Watanzania.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian, ametoa pongezi kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha utekelezaji wa mradi huo nchini Tanzania kwa ushirikiano na Uganda. Amesema kati ya mikoa nane inayopitiwa na mradi huo, Mkoa wa Tanga umefaidika kwa kiwango kikubwa kupitia fursa mbalimbali za ajira na maendeleo kwa wananchi, hususan vijana.