Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kukamilisha ujenzi wa majengo ya kituo cha mafunzo ya  Uongezaji thamani madini ya vito kwa kuongeza nguvukazi na kufanya kazi kwa masaa 24 ili kukamilisha ujenzi wa jengo kwa muda mfupi.

Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Desemba 12, 2025 mkoani Arusha  wakati wa ziara yake ya  kukagua mradi wa kituo hicho  ulioanza ujenzi rasmi ambapo katika maelekezo yake amemtaka mkandarasi kuzingatia ujenzi bora wenye kukidhi vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba.

Waziri Mavunde amefafanua kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais.Dkt. Samia Suluhu Hassan  inatekeleza mikakati yake kwenye mnyororo mzima wa uongezaji thamani madini ya vito kama Sera ya Madini ya Mwaka 2009 inavyoelekeza.

Sambamba na hapo, Waziri Mavunde amesisitiza kuwa,  kuanza kwa ujenzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akihutubia Bunge la 13 jijini Dodoma.

Waziri Mavunde amebainisha kuwa,  kukamilika kwa  kituo hicho , kutaleta faida mbalimbali ikiwa pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi watakao jiunga kwenye kituo, kuongezeka kwa wataalamu wa uongezaji thamani madini ya vito, kufungua fursa za ajira kwa vijana na wafanyabiashara wa madini , pamoja na kutosafirishwa kwa madini ghafi nje ya nchi hivyo kutachagiza  ongezeko la  mapato kwa taifa.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Mavunde ametoa siku 7 kwa Katibu Mkuu Wizara ya Madini kukutana na wakandarasi ,TGC na Taasisi za serikali kwa ajili ya upatikanaji vibali muhimu vya kuendeleza ujenzi.

Kwa upande wake , Mkuu wa Wilaya Arusha Mhe. Joseph Mkude ameahidi kuendelea kufuatilia maendeleo ya ujenzi ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kama Serikali inavyotaka.

Mkude ameongeza kuwa, kukamilka kwa kituo hicho itakuwa moja ya sehemu ya uwekezaji mkubwa wa serikali  husasan kwenye Sekta ya Madini mkoani Arusha.

Awali, akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi, Mkuu wa kituo cha TGC Mhandisi. Ally Maganga ameeleza kuwa, ujenzi wa majengo pacha hayo ya ghorofa 8 utagharimu Tsh Bilioni 33 na kukamilika kwake kutaongeza fursa ya vijana wengi kupata ajira kupitia ujuzi wa uongezaji thamani madini ya vito.

Naye, Meneja Mradi Mhandisi Robert Lubuva ameahidi kuhakikisha kama wakandarasi wataongeza nguvu ya rasilimali watu na vifaa ili mradi uweze kukamilika na kuwahudumia watanzania kwa wakati.







๐Ÿ“Œ Utaimarisha upatikanaji wa umeme Mbagala na Gongo la Mboto

๐Ÿ“Œ Majaribio yameanza ; Shukurani kwa Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme cha Kinyerezi 1 Extension umekamilika rasmi, ikiwa ni pamoja na kufungwa kwa Transfoma yenye uwezo wa MVA 175.

Amesema hatua hii ni muhimu kwa kuboresha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Jiji la Dar es Salaam, hususan maeneo ya Mbagala na Gongo la Mboto, ambayo yamekuwa yakikumbwa na changamoto za kukatika kwa umeme kutokana na ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi.

Mhe. Salome amesema hayo Desemba 11, 2025, wakati wa ziara yake katika vituo vya uzalishaji umeme vya Kinyerezi I, Kinyerezi II, Ubungo I, Ubungo II na Ubungo III akiongeza kuwa mradi tayari umeanza majaribio (testing).

“Tunamshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa. Transfoma zimefungwa, majaribio yanaendelea, na wananchi wa Gongo la Mboto na Mbagala sasa watapata umeme wa uhakika,” Mhe. Salome.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Shirika linaendelea kuboresha miundombinu yake ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka.

Amebainisha kuwa katika eneo la Kinyerezi kumefungwa Transfoma kubwa ya MVA 175, huku maeneo ya Gongo la Mboto na Mbagala yakiwekewa Transfoma ya MVA 120 ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya umeme.

Amesisitiza kuwa idadi ya watu imekuwa ikiongezeka Jiji la  Dar es Salaam, hivyo miundombinu ya umeme lazima iboreshwe mara kwa mara ili kuendana na uhitaji uliopo. 

"Lengo la Kinyerezi 1 Extension lilikuwa kuongeza uwezo wa kusambaza umeme unaozalishwa kuwafikia wateja wetu kwa kiwango kinachostahili," amesema Bw. Twange.







 



✔️ _Dkt. Kiruswa Asisitiza kuwa Huo Ndio Mwelekeo Mpya wa Sekta ya Madini Nchini_


✔️ _Mining For A Brighter Tomorrow-MBT Kuwasha Moto wa Maendeleo: Vijana na Wanawake Wachimbaji Kunyanyuliwa_


✔️ _Serikali Kuendelea Kufyeka Leseni Zisizofanyiwa Kazi Ili Kutoa Nafasi kwa Wachimbaji Wengine_


๐Ÿ“ _Rombo- Kilimanjaro,_


Serikali imeeleza kujivunia hatua kubwa zinazopigwa na Wachimbaji Wadogo nchini, wakiwemo wanaochimba Madini ya Pozzolana pamoja na wakataji wa matofali ya volcano (volcanic blocks) katika Kata ya Holili, Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, hatua inayoendelea kuonesha kasi ya ukuaji wa Sekta ya Madini siku hadi siku.

Kauli hiyo imetolewa leo Desemba 11, 2025 na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji wilayani Rombo, ambapo amesisitiza kuwa Sekta ya Madini imekuwa mhimili unaochochea na kuunganisha sekta nyingine kama ujenzi, viwanda, biashara, kilimo, maji na maeneo mengine ya uchumi.

Dkt. Kiruswa amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini imeanzisha Programu ya Mining for A Brighter Tomorrow – MBT yenye lengo la kuwawezesha vijana na wanawake wanaojihusisha na uchimbaji mdogo kwa kuwapatia leseni za uchimbaji pamoja na vifaa vya kisasa ili kuboresha uzalishaji wao na kuongeza tija.

 “Programu hii ni sehemu ya dhamira ya Serikali kuhakikisha wachimbaji wadogo wanapiga hatua na kuwa sehemu pana ya uchumi wa taifa,” amesema Dkt. Kiruswa.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini itaendelea kufuta leseni za uchimbaji na utafiti ambazo hazifanyiwi kazi, ili kuhakikisha rasilimali madini zinawanufaisha Watanzania kikamilifu na kuondoa vizuizi vinavyochelewesha maendeleo ya sekta.

Kwa upande, Mkuu wa Wilaya ya Rombo,  Mhe. Raymond Mwangwala amesema kuwa uwepo wa madini ya Pozzolana umesaidia kutangaza Wilaya hiyo sambamba na kuongeza mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Rombo huku vijana wakinufaika na ajira kupitia uwepo wa madini hayo yatokanayo na volcano na miamba ya volcano inayotumika kutengenezea matofali imara.

Kwa upande wake Afisa Madini Mkazi wa Mkoa Kilimanjaro Mhandisi Abel Madaha ameeleza kuwa makusanyo ya maduhuli kutoka Sekta ya Madini katika Mkoa wa Kilimanjaro yamefikia shilingi bilioni 1.63 kuanzia Julai hadi Novemba 2025, ikiwa ni asilimia 45 ya lengo la mwaka la kukusanya shilingi bilioni 4.2 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua imayoashiria mwitikio mzuri wa wachimbaji na usimamizi madhubuti unaoendelea kufanywa na Wizara ya Madini ili kuhakikisha rasilimali za nchi zinachangia kikamilifu kwenye maendeleo ya taifa.

Pozzolana ni aina ya madini ujenzi yenye asili ya udongo au majivu ya volkano ambayo, ikichanganywa na chokaa na maji, huunda saruji yenye uimara mkubwa na hutumika kwa wingi katika viwanda vya saruji hapa nchini.






 


Na James K. Mwanamyoto - Dodoma

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ametembelea Soko la Majengo jijini Dodoma na kukagua maendeleo ya ukarabati wa soko hilo, ambapo amemuelekeza mkandarasi Kampuni ya Azhar Construction kukamilisha ukarabati huo ifikapo Mwezi Februari 2026 ili wafanyabiashara waanze kulitumia.

Katika kuhakikisha maelekezo yake yanatekelezwa, Dkt. Mwigulu amemtaka Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko kufanya makubaliano ya kimaandishi na mkandarasi huyo kuwa, hakutakuwa na nyongeza ya muda wa ukarabati wa soko hilo ifikapo Mwezi Februari, 2026.

“Serikali inataka ukarabati wa Soko ukamilike kwa wakati ili kukidhi mahitaji ya wakazi wa Jiji la Dodoma, ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira wezeshi ya kuendelea kukuza uchumi wa wafanyabiashara,” Dkt. Nchemba amesisitiza.

Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe akimkaribisha Mhe. Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ukarabati wa soko hilo la Majengo unatekelezwa kupitia fedha za Mradi wa Uendelezaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC).

Akieleza historia ya soko hilo la Majengo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema kuwa, soko hilo linalokarabatiwa ni la muda mrefu lilojengwa kipindi cha uhuru (1960’s) hivyo lilikuwa chakavu kiasi cha kutokidhi mahitaji ya sasa kwa muundo wake.

Mhe. Senyamule amefafanua kuwa, ukarabati wa soko hilo ulianza Mwezi Machi 2025 na ukarabati wake unategemewa kukamilika ifikapo Machi 25, 2026, hivyo ofisi yake inaendelea na juhudi za kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati licha ya maendeleo ya utekelezaji wake kutoendana na muda uliopangwa kimkataba.

Naye, mmoja wa wafanyabiashara katika Soko la Majengo, Bw. Abubakari Athuman amemshukuru Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kwa kufanya ukaguzi wa ukarabati katika Soko la Majengo na kumuelekeza mkandarasi akamilishe ukarabati kwa wakati ili waweze kulitumia soko hilo kwani hivi sasa wanafanya biashara katika mazingira ambayo sio rafiki kibiashara.

Kwa upande wake, mfanyabisahara mwingine Bi. Khadija Abdallah amesema kufuatia maelekezo ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Mchemba, wafanyabiashara wamepata faraja kuwa mkandarasi atakamilisha ukarabati wa soko ili waanze kulitumia, ikizingatiwa kwamba mvua za masika zitaanza muda si mrefu.

  


Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amewataka Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Chuo hicho kuhakikisha wanafuata Kanuni, Taratibu na Sheria za Chuo kama zilivyo na zinavyoelekezwa.


Prof. Mapesa ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa kwanza 2025/2026 kwenye kikao kilicholenga kuwakaribisha rasmi wanafunzi hao ambapo pamoja na mambo mengine alielezea historia ya Chuo, Mipango na Maendeleo ya Taasisi kwa Ujumla wake.



Mkuu huyo wa Chuo amewataka Wanafunzi kuwa na nidhamu kwa kufuata sharia na kanuni za ufanyaji wa mitihani, nidhamu katika Mavazi, kuheshimiana baina yao, lakini pia kuwa na nidhamu kwa Wafanyakazi wanaohudumu katika Taasisi hiyo.


Pia Prof. Mapesa amewasihi sana Wanafunzi wa Chuo hicho kujiepusha na matendo maovu ikiwemo kujihusisha na makundi yasiyofaa, kujiepusha na utumiaji wa dawa za kulevya, pamoja na kuhakiksiha changamoto walizonazo wanaziwasilisha sehemu husika ili zipatiwe ufumbuzi kwa wakati badala ya kufanya vurugu.


“ Jukumu lililowaleta Chuoni ni kusoma kwa bidii na kuhakikisha mnafaulu vyema mitihani kwani ndiyo kipimo cha uelewa wa kile ambacho mtakuwa mmefundishwa, lengo likiwa ni kufikia malengo na matarajio mliyojiwekea  katika kutimiza ndoto zenu mlizojiwekea katika maisha.”alisisitiza Prof. Mapesa.


Prof. Mapesa amewataka Wanafunzi hao kuzingatia na kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho muda wote wanapokuwa Chuoni, kuhakikisha wanakamilisha Usajili, kutunza Mazingira pamoja na Miundombinu mbalimbali iliyopo Chuoni.



Kwa upande wake Rais wa Serikali ya Wanafunzi Magashi Magina  amewataka Wanafunzi wenzake kuzingatia yale yote yaliyoelekezwa na Mkuu wa Taasisi, ili kujiepusha na usumbufu usio wa lazima.


Kupitia kikao hicho, Wanafunzi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali ambayo yalipatiwa majibu na viongozi kupitia kikao hicho,Kikao hicho kimehudhuriwa na Menejimenti ya Chuo, Serikali ya Wanafunzi, Wafanyakazi Waendeshaji na Wanataaluma.


Imetolewa na:


Kitengo cha Mawasiliano na Masoko


CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE


11.12.2025

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Viongozi Chipukizi wakati wa uzinduzi wa Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine ni wageni waalikwa. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wakwanza kulia) akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo (hayupo pichani) wakati akitoa maelezo ya awali kuhusu taasisi hiyo kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri huyo kuzindua rasmi Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifurahia jambo wakati Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) alipokuwa akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wapili kutoka kulia) akiwa katika uzinduzi wa Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo. Wengine ni Watendaji wa taasisi hiyo. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati waliokaaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi Chipukizi mara baada ya Naibu Waziri huyo kuzindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine ni wageni waalikwa. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.

Na Veonica Mwafisi-Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ametoa wito kwa Viongozi kuendelea kujifunza siku kwa siku ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia na kitamaduni yatakayowezesha kubuni mikakati mbalimbali ya kuboresha utendaji kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Qwaray ameyasema hayo leo tarehe 11 Disemba, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Viongozi Chipukizi kabla ya kuzindua Programu ya Viongozi hao.

Amesema ili mtu aweze kuwa kiongozi mzuri, ni lazima aendelee kujifunza kila siku kwa lengo la kuweza kukabiliana na changamoto za kiuongozi ikiwemo kubuni mbinu mbalimbali za kusimamia mabadiliko ya kimfumo, kiutawala, kiuchumi, kiteknolojia na kitamaduni yanayojitokeza kila siku.

Mhe. Qwaray amewashukuru na kuwapongeza washirika kutoka Finland na HAUS kwa kukubali kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI kubuni na kuandaa programu hii maalumu kwa viongozi na taifa kwa ujumla kwani ina umuhimu wa pekee katika kuendeleza viongozi nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Aidha, amewasisitiza Viongozi kushirikiana na watumishi walio chini yao kwa kuwaelekeza kazi badala ya kuwaacha na kuwaona ni tatizo katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kiongozi usiwe mchoyo kufundisha walio chini yako, tuwafundishe, tunakua, tutengeneze viongozi wa baadae, tusishikilie madaraka, tutengeneze viongozi wengi kadri tuwezavyo, Kiongozi hutakiwi kushikilia kila kitu, shirikisha wenzio ili upate mawazo mapya, kuboresha utendaji na kufikia malengo mahususi yaliyowekwa kwa ustawi wa taifa, Mhe. Qwaray amesisitiza.

Amesema Tanzania inaendelea kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs 2030), Ajenda ya Maendeleo ya Afrika (Agenda 2063) na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na malengo hayo yameweka bayana kuwa mabadiliko ya kiuongozi ni muhimu kwani ndiyo nguzo kuu ya kufikia malengo yaliyowekwa huku akitolea mfano Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kuwa imeweka malengo ya kuwa na uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

“Ni dhahiri hatuwezi kufikia lengo hili kama tusipojipanga na kuweka mikakati madhubuti ya kutuwezesha kufikia malengo yetu.”

Ametaja moja ya mikakati hiyo ni pamoja na kuwa na nguvu kazi yenye uwezo na motisha pamoja na kuwajengea uwezo viongozi kupitia mafunzo kama haya.

Programu hii ni muhimu sana kwani itasaidia Serikali kuwa na viongozi watakaotimiza matarajio ya wananchi.

“Nina imani kuwa maarifa na ujuzi utakaotolewa kwa washiriki wa programu hii utawapa msingi bora na utayari kuongoza na kutoa huduma bora kwa wanachi.

Mhe. Qwaray amewashauri viongozi kujifanyia tathmini ili kutambua uwezo na udhaifu wao kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuboresha utendaji hasa kwenye eneo la mapungufu.

Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri kuzindua Programu hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo amesema Taasisi yao imekuwa ikitoa mafunzo mbalimbali ya uongozi ili kuwa na viongozi bora katika taifa.

“Kunaweza kukawa na mifumo mizuri lakini viongozi sio wazuri, hivyo mafunzo tunayoyatoa yanasaidia kuwajenga viongozi kuendana na mifumo mizuri iliyopo, Bw. Kadari ameongeza.

 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amekutana na Balozi wa Falme za Kiarabu Saudi Arabia, Mhe. Yahya Bin Ahmed Okeish, ambapo wamejadili kuimarisha ushirikiano katika sekta ya elimu pamoja na kuongeza fursa za skolashipu kwa vijana.

Prof. Mkenda ameishukuru Saudi Arabia kwa kuongeza nafasi za ufadhili masomo ya jelimu ya juu kutoka 90 hadi 127 kwa wanafunzi wa watanzania, na ameahidi kuwa Serikali itazitumia kikamilifu fursa hizo ili kuwawezesha vijana kupata elimu chini humo.

Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha vijana wanapata elimu stahiki katika maeneo ya kimkakati, ikiwemo Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, Sayansi ya Takwimi na Akili Unde.

Kwa upande wake, Mhe. Okeish amesema Saudi Arabia inajivunia ushirikiano wake na Tanzania katika sekta ya elimu na itaendeleza ushirikiano huo katika kutekeleza mikakati ya kuendeleza elimu na ujuzi kwa vijana wa Kitanzania kulingana na vipaumbele vya taifa.

Aidha, ameipongeza Wizara ya Elimu kwa kuwa na Sera Bora ya Elimu na pia mipango yake ya kufanya ziara nchini Saudi Arabia kutembelea vyuo mbalimbali, kubadilisha a uzoefu na kupanua fursa za elimu kwa vijana wa mataifa yote mawili ikiwemo suala la kuimarisha ufundshaji lugha ya kiarabu.

   

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI na Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Disemba 11, 2025 wamekutana jijini Dodoma kujadili kwa pamoja mikakati ya kuimarisha ushirikiano katika kuwawezesha vijana wa Tanzania kupata fursa za elimu, ujuzi na ajira.

Kikao hicho kimeongozwa na Prof. Carolyne Nombo, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na Jenifa Omolo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana.

Viongozi hao wamejadili njia za kuhakikisha vijana wanapata taarifa sahihi kuhusu fursa za elimu na kuwezeshwa ili kukidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Prof. Nombo amesema kuwa Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 Toleo la 2023 pamoja na mitaala iliyoboreshwa vinaendelea kumwandaa kijana wa Kitanzania kupata ujuzi unaohitajika katika ulimwengu wa kazi.

Amesisitiza kuwa sera hiyo inatoa nafasi kwa vijana wote, wakiwemo walioacha shule awali, kurejea na kupata elimu kupitia mfumo rasmi na usio rasmi, ikiwemo programu ya IPOSA.

Aidha, Prof. Nombo amebainisha kuwa Serikali inaendelea kupanua fursa za ufundi na mafunzo ya ufundi stadi, mikopo ya elimu, pamoja na ufadhili kupitia Samia Skolashipu, ili kuongeza wigo wa vijana kupata elimu na ujuzi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo, ameipongeza Wizara ya Elimu kwa kuanzisha programu nyingi zinazolenga kuwawezesha vijana kujitegemea na kushindana katika soko la ajira. Amesema programu hizo ni muhimu katika kuchochea ushiriki wa vijana katika uchumi wa taifa.

Katika kikao hicho, viongozi hao wamekubaliana kuimarisha upatikanaji wa taarifa za fursa mbalimbali kwa vijana, kutafuta rasilimali fedha kwa ajili ya kugharamia mafunzo mahususi, pamoja na kuratibu programu zitakazowaunganisha vijana na viwanda ili kupata mafunzo kwa vitendo.