Na Munir Shemweta, WANMM

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, ameutumia uzinduzi wa “Samia Ardhi Kliniki” jijini Dar es Salaam kutangaza msimamo mkali wa Wizara dhidi ya vitendo vya uzembe na ucheleweshaji wa huduma kwa wananchi.

 

Katika hafla hiyo, Waziri Akwilapo amesema Wizara imeamua “kujivua gamba” na kuanza ukurasa mpya wa uwajibikaji, akisisitiza kuwa kauli za watumishi kudai mafaili kupotea au kutoonekana hazitavumiliwa tena.

 

“Hakuna kitu kama faili kupotea. Ofisi zetu zina mifumo thabiti, na mafaili hayana miguu ya kutoroka. Kauli hizi nimezipiga marufuku rasmi,” alisisitiza.

 

Waziri huyo alieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mageuzi yanayolenga kurejesha imani ya wananchi kwa sekta ya ardhi, ambayo imekuwa ikikabiliwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusu urasimu na usumbufu usio wa lazima.

 

Alisema Wizara haitasita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa watumishi watakaobainika kukwamisha huduma kwa maslahi binafsi, akisisitiza kuwa ardhi ni rasilimali ya Taifa na watumishi ni wasimamizi tu, si wamiliki.

 

Uzinduzi wa “Samia Ardhi Kliniki” umefanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Kliniki hiyo itafanyika nchi nzima kuanzia Machi 2 hadi 7, 2026, ikitoa huduma za msaada wa kisheria, utoaji wa hatimiliki na elimu ya taratibu za umilikishwaji wa ardhi.

 

Mbali na kuhimiza wanawake kujitokeza kunufaika na huduma hizo, Waziri Akwilapo aliwataka wanaume na viongozi wa kaya kuachana na mila potofu zinazowanyima wanawake haki ya kumiliki ardhi.

 

Kwa mujibu wa Waziri, idadi ya wanawake wenye hatimiliki imeongezeka hadi wastani wa asilimia 28 kutoka chini ya asilimia 10 miaka ya nyuma, hatua aliyoitaja kuwa ni mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita.

 

Kauli mbiu ya zoezi hilo ni: “Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,” ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kuhakikisha usawa wa kijinsia na kuimarisha uchumi wa familia na Taifa kwa ujumla.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw Edward Mpogolo akimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila mbali na kuipongeza Wizara ya Ardhi kwa kuanzisha Samia Ardhi Kliniki amesema, kuna baadhi ya changamoto zilizoanza kujitokeza kwa wale wanaopata hati miliki za ardhi kufunga barabara zinazotumika kwa jamii.

 

Ameomba utaratibu wa fomu za kuthibitishwa na majirani katika maeneo yaliyorasimishwa kuzingaitiwa kwa kupitishwa katika ngazi husika na kusimamiwa ili kuepuka changamoto kama hizo.

 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemnera amesema huduma kubwa zinazotolewa kupitia Samia Ardhi Kliniki ni elimu hususan ya haki za umiliki kwa wanawake, ushauri wa mambo mbalimbali ya sekta ya ardhi, utoaji hati kwa waliokamilisha taratibu pamoja na huduma nyingine. 

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa Kuzindua Samia Ardhi Kliniki jijini Dar es Salaam tarehe 2 Machi 2026
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akimkabidhi hati milki ya ardhi mmoja wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakati wa Samia Ardhi Kliniki tarehe 2 Machi 2026.
Naibu Katibu Mkuu Bi. Lucy Kabyemera akimkabidhi hati Miliki ya Ardhi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Edrward Mpogolo katika tukio la uzinduzi wa Samia Ardhi Kliniki jijini Dar es Salaam tarehe 2 Machi 2026. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi Dkt Upendo Matotola.
Sehemu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakipata huduma kupitia Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam
Sehemu ya watumishi wa sekta ya ardhi wanawake wakitoa huduma katika Samia Ardhi Kliniki inayofanyika jijini Dar es Salaam
 
Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Upendo Matotola akimkabidhi mwanamama mkazi wa jiji la Dar es Salaam  Hati Milki ya ardhi katika Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam.Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA, MICHUZI TV)
 
 
 
 
 

Serikali kuendelea kuweka mazingira salama kwa wenye Viwanda vinavyofanya kazi na kutatua changamoto kwa wakati ili kuendelea kulinda ajira za Watanzania na kuongeza mzunguko wa fedha kwa jamii na wananchi kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb) wakati wa ziara ya kikazi Machi 2, 2026 mkoani Morogoro.

Londo amemshauri Katibu Tawala mkoani Morogoro kuweka utaratibu kwa mikopo ya asilimia 10 kuwafikia walengwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogo (SIDO) ili kuleta maana ya utoaji wa mikopo kwa jamii nchini.

Londo ametembelea viwanda vinne katika Manispaa ya Morogoro ikiwemo SIDO, Mkwawa, Cotex na Mazava katika ziara yake ya siku moja mkoani hapa.

Pia amesema ikiwa wajasiliamali hao watapata mikopo wakiwa hapo ambako wamezungukwa na aina mbalimbali za ujasiriamali itawasaidia kupata namna ya kujengwa na kuwa wajasiriamali wazuri na hivyo kuwa na uhakika wa kurejesha mikopo hiyo.

Uwepo wa gundi inayozalishwa kwenye viwanda hivyo vidogo vilivyopo kwenye eneo la viwanda SIDO Morogoro ambapo ameiomba serikali ya mkoa kusimamia uzalishaji huo na kufanya masoko makubwa ya gundi kuanzia ndani ya mkoa na kisha nje ya mkoa Taifa hadi nje ya nchi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa SIDO, Mhandisi Profesa Sylvester Mpanduji anasema wanajipanga kuhakikisha wanaboresha eneo la viwanda la SIDO Morogoro ili kufanya wajasiriamali kulitumia kama kongani la viwanda na kuleta maana

Hata hivyo, Meneja wa SIDO Morogoro, Bi.Joan Nangawe anasema wametengeneza ajira zaidi ya 115 baada ya kutoa elimu, kuwakusanya wajasiriamali kwenye eneo la viwanda na kutoa mikopo ya shilingi Milioni 62.5.

Anasema katika siku 100 za Rais Samia Suluhu Hassan jumla ya wajasiriamali ambao ni vijana wanatarajia kupata mikopo ya shilingi Milioni 250 kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.

Mmoja wa wajasiriamali anayetengeneza Gundi kwenye eneo la viwanda SIDO Marry Hassan anasema licha ya kuwa na uhakika wa soko la ndani kwa mikoa ya Morogoro na Dar es salaam lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa masoko ya nje ambayo yanaweza kuwapa nafasi kubwa katika kuongeza uzalishaji na kukua kiuchumi.

Na.Alex Sonna-Dodoma

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanzisha  kliniki maalum iitwayo Samia Ardhi Kliniki nchi nzima kwa lengo la kuongeza idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi, ambapo kwa sasa ni asilimia 28 tu.

Hatua hiyo inalenga kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha huduma za ardhi zinatolewa kwa wananchi kwa kuzingatia misingi ya usawa wa kijinsia.

Akizungumza leo Machi 2,2026 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa kliniki hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Mhandisi Anthony Sanga, amesema mpango huo utaendeshwa nchi nzima na unatarajiwa kuhitimishwa Machi 7 mwaka huu, kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Mhandisi Sanga amesema kuwa  lengo kuu la Samia Ardhi Kliniki ni kuongeza asilimia ya umiliki wa ardhi kwa wanawake nchini kupitia utoaji wa elimu, hati za umiliki na utatuzi wa migogoro ya ardhi.

 "Takwimu zinaonesha kuwa ni takriban asilimia 28 pekee ya wanawake nchini wanamiliki ardhi, jambo linaloonesha umuhimu wa kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha ushiriki wao katika masuala ya umilikishaji."amesema Mhandisi Sanga

Mhandisi Sanga amefafanua kuwa Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 iliweka msingi wa usawa wa kijinsia katika umiliki wa ardhi kati ya wanaume na wanawake. Hata hivyo, amesema changamoto zilijitokeza katika utekelezaji, hasa kwenye masuala ya mirathi na urithi ambapo mila na desturi zilichangia kuwabagua wanawake.

“Tamko la sera ya mwaka 1995 lilielekeza kuzingatia mila na desturi, lakini katika sera mpya iliyozinduliwa mwaka 2025 na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, haki ya umiliki wa ardhi kwa wote—wanaume na wanawake imewekewa usawa bayana,” amesema Mhandisi Sanga

Aidha amesisitiza kuwa katika sera hiyo mpya, masuala ya urithi na mirathi yameainishwa kwa kuzingatia usawa wa kijinsia, hivyo kuweka mazingira rafiki kwa wanawake kumiliki na kurithi ardhi bila ubaguzi.

"Kupitia Ardhi kliniki hiyo maalum, wanawake watapatiwa hati za umiliki wa ardhi, kusaidiwa kutatua migogoro ya ardhi pamoja na kupewa elimu kuhusu haki na taratibu za umiliki wa ardhi."amesema

Amesema mpango huo unalenga kuhakikisha changamoto zinazowakabili wanawake katika sekta ya ardhi zinatatuliwa kwa wakati, huku ukichochea ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla.

Hata hivyo amewataka kuwa watulivu wakati zoezi hilo likiendelea ili waweze kuhudumiwa kikamilivu na kwa weledi.

Kwa upande wake, Mthamini Mkuu wa Serikali wa Wizara hiyo, Bi. Evelyn Baruti Mugasha, amesema hadi majira ya mchana wanawake zaidi ya 160 walikuwa wamejitokeza kupata hati, huku wengine wakiendelea kujitokeza.

Bi. Mugasha amewataka wanawake wa Mkoa wa Dodoma kutumia fursa ya kliniki hiyo kupata elimu, ushauri na huduma mbalimbali, huku akitoa wito kwa wanaume kutoa ushirikiano ili kuwawezesha wanawake kushiriki kikamilifu.

“Kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi ni hatua muhimu katika kuimarisha uchumi wa familia na taifa kwa ujumla,” amesema Bi. Mugasha.

Nao, wanachi wa Mkoa wa Dodoma wamempongeza Rais Samia  kwa kuwapa kipaumbele wanawake katika suala la hati ili kuhakikisha hawabaki nyuma.

Naye mkazi wa Chidachi, Bi. Veronica Hamisi, amesema amefurahi kupata hati aliyokuwa akiifuatilia kwa takribani miaka mitatu ndani ya siku moja.

Kwa upande wake, mkazi wa Miyuji, Getruda Mathias, amesema amehangaika kwa miaka mitano kupata hati, lakini anamshukuru Rais kwa kutoa kipaumbele kwa wanawake kilichomwezesha kupata hati ndani ya saa moja bila usumbufu.

“Nawasihi wanawake wenzangu tujitokeze kwa wingi kuchangamkia fursa hii ambayo itahitimishwa Machi 7 mwaka huu,” amesema.

Mkazi wa Ilazo, Zena Hamis, pia amemshukuru Rais kwa kuwapa kipaumbele wanawake na kuwasihi wale ambao bado hawajajitokeza kufanya hivyo ili kunufaika na huduma hiyo.

 


Mjua kwao hapotei njia, na mwenda pole hajikwai, unaweza ukafikiri utani kumbe inaelekea ni hivyo wale wote wanaopambana Kariakoo, Gaza, Teheran na kwingineko inaaminika kuwa asili yao ni Bonde la Olduvai lililoko eneo la hifadhi ya Ngorongoro.

Bonde la Olduvai linafahamika kama eneo la kipekee duniani kupatikana masalia ya jamii za binadamu wa kale na zana za mwanzo za mawe yanayowakilisha hatua muhimu za awali katika chimbuko la binadamu kuanzia miaka milioni 2 iliyopita hadi sasa.

Kupitia eneo hili ndio ulimwengu ulipoanza kujua historia ya safari ya mabadiliko ya mwanadamu baada ya ugunduzi wa fuvu maarufu la Zinjanthropus mwaka 1959 ambalo lilibadilisha uelewa na mtazamo wa wanasayansi kuhusu mchango wa Tanzania katika masuala ya asili ya binadamu.


Bonde Olduvai limehifadhi visukuku, historia na chimbuko la binadamu katika mtiririko uliokamilika.

 

Waziri Mkuu Mstaafu, Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025, Luhaga Joelson Mpina (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi )  walipokutana katika mazishi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Yuda Thadei Ruwaichi akisalimiana na 
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina walipokutana katika mazishi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Mhashamu Renatus Nkwande akisalimiana na 
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025,(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Luhaga Joelson Mpina walipokutana katika mazishi ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026

Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo,(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi) Luhaga Joelson Mpina pamoja na Maaskofu Katoliki katika mazishi Mwadhama Askofu Mstaafu Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina pamoja na Mwenyekiti wa Zamani wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia  katika mazishi ya Askofu Mkuu  Mstaafu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisalimiana na Waziri Msaafu wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Profesa Anna Kajumulo Tibaijuka mara baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kumuombea Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026

Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisalimiana na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee  wa CHADEMA, Suzan Lyimo mara baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kumuombea Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026

Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisaini kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amelitaka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuongeza kasi katika utafiti wa upatikanaji wa maeneo mapya ya uchimbaji wa visima vipya vya gesi asilia ili kuongeza upatikanaji wa gesi kwa matumizi mbalimbali pamoja na kufanikisha agenda ya matumizi ya nishati safi nchini.

Ndejembi ameeleza hayo tarehe 27 Februari 2026 mkoani Mtwara wakati akizindua mradi wa uchimbaji wa visima vitatu ambapo viwili ni kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay na kimoja kwa ajili ya utafutaji huku utekelezaji umefikia asilimia 58.

“Rai yangu kwenu TPDC ni kuongeza kasi ya uchimbaji wa gesi katika maeneo mengine na kuhakikisha mashapo yaliyopo yanaanza kuzalisha tunapozindua kitalu hiki hapa mipango ya kuanza kuchimba sehemu nyingine ianze mara moja” amesisitiza Ndejembi.

Ndejembi ameeleza kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan iliamua kuwekeza fedha kupitia TPDC kwani mahitaji ya gesi yanaongezeka kutokana na nchi inavyoendelea kukua na kusababisha mahitaji ya gesi kuongezeka kwa ajili ya uzalishaji wa umeme matumizi ya viwandani na taasisi nishati kwenye vyombo vya usafiri pamoja na matumizi ya majumbani.

Ndejembi ameipongeza TPDC kwa kushirikiana na Kampuni ya Maurel & Prom katika kutekeleza mradi wa uchimbaji wa visima hivyo ambavyo vitaongeza uzalishaji wa gesi na kuchochea kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi.

Kadhalika Ndejembi ameitaka TPDC kuendelea kuyawezesha makampuni na wataalamu wazawa ikiwa ni pamoja na kuweka mpango wa kuendelea kuwajengea uwezo wataalamu waliopo katika maeneo ya utekelezaji wa miradi ili nao wanufaike na kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi yao.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt James Mataragio ameeleza kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika nishati ya gesi ambapo katika mradi huo pekee itatumika zaidi ya shilingi bilioni 235.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Mussa Makame amesema Serikali kupitia TPDC inamiliki Kitalu cha Mnazi Bay kwa asilimia 40 na Kampuni ya Maurel & Prom inamiliki asilimia 60 na kubainisha kuwa uzalishaji umeendelea kuongezeka ambapo kwa sasa uzalishaji katika kitalu hicho umefikia futi za ujazo milioni 100 kwa siku.


Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dkt. Khamis Said 'kushoto', akimkabidhi cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mwalimu Dkt. Alexius Revocatus Kaganze, alipotunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa) katika Ustawi wa Jamii na Uongozi wa Biashara kutoka Christian Ministerial Training University (CMTU) ya nchini Zambia katika hafla iliyofanyika Februari 28, 2026 Mkoa wa Shinyanga. Kulia ni Mwenyekiti Mwanzilishi wa Greeling Global Peace Organization na mmiliki wa CMTU, Profesa Askofu Kennedy Songwe.

...................................

Na Dotto Mwaibale, Shinyanga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mwalimu Alexius Revocatus Kaganze, ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa) katika Ustawi wa Jamii na Uongozi wa Biashara kutoka Christian Ministerial Training University (CMTU) ya nchini Zambia.

Mbali na tuzo hiyo, pia ameteuliwa kuwa Balozi wa Amani Duniani (Peace Ambassador – AMB) na Greenling Peace Foundation kwa kutambua mchango wake katika kuhimiza amani, mshikamano na maendeleo ya kijamii.

Tuzo hizo zilitolewa Februari 27, 2026, mkoani Shinyanga katika maadhimisho ya Siku ya Amani na Upendo Duniani yaliyofanyika kitaifa, yakihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wanaharakati wa amani na wageni kutoka ndani na nje ya nchi. Maadhimisho hayo yaliandaliwa na Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO).

Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dkt. Khamis Said, ambaye alisema amani ni nguzo kuu ya maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

Alieleza kuwa UNESCO ilianzishwa baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia kwa lengo la kujenga utamaduni wa amani kupitia elimu, sayansi na utamaduni, ili kuzuia migogoro na kuhakikisha dunia inabaki katika mshikamano wa kudumu.

“Tunampongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga kwa uteuzi wake wa kuwa Balozi wa Amani. Hii ni ishara kuwa viongozi wa ngazi zote wana wajibu wa kueneza ujumbe wa amani, uvumilivu na mshikamano wa kitaifa,” alisema Dkt. Said.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti Mwanzilishi wa Greeling Global Peace Organization na mmiliki wa CMTU, Profesa Askofu Kennedy Songwe, alisema wakati dunia ikiadhimisha siku ya amani, Mwalimu Kaganze ametambuliwa kwa juhudi zake za kuunganisha jamii kupitia haki na umoja.

Alisema shirika hilo linafanya kazi katika zaidi ya mataifa 30 likilenga kuinua kizazi cha viongozi wenye maono ya kuleta amani endelevu.

Naye Profesa Stephano Nzowa wa African Graduate University alisema Tanzania imejijengea sifa ya kuwa “Kisiwa cha Amani,” hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kuilinda na kuienzi amani hiyo kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Safari ya Utumishi wa Miaka 15

Mwl. Alexius Kaganze alizaliwa Machi 3, 1986, na kwa zaidi ya miaka 15 amelihudumia Taifa katika nyadhifa mbalimbali serikalini, zikiwemo:

Mwalimu

Afisa Elimu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga (kuanzia 2021)

Mchango Wake Katika Sekta Mbalimbali

1. Elimu:

Amehimiza ubora wa elimu, akisisitiza walimu kuwa nguzo ya maarifa, maadili na ujenzi wa amani. Amesimamia ujenzi wa madarasa, mabweni na miundombinu ya shule za msingi na sekondari, pamoja na kuhakikisha utekelezaji sahihi wa sera ya elimu bila malipo.

 

2. Ajira na Uwezeshaji Vijana:

Amekuwa mstari wa mbele kuhimiza nidhamu ya kazi, maadili na kujiajiri kwa vijana, huku akisimamia miradi ya miundombinu inayochochea uchumi wa manispaa.

3. Biashara:

Amehamasisha utoaji wa mitaji kwa wafanyabiashara wadogo na kukutana na wadau wa sekta ya nyumba za kulala wageni ili kuboresha huduma na kukuza uchumi wa eneo hilo.

5. Michezo:

Ameunga mkono michezo kama chachu ya kukuza vipaji, afya na nidhamu kwa vijana.

6. Miundombinu:

Amesimamia miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa barabara za lami zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.6, kituo kipya cha mabasi Katunda, pamoja na miradi ya elimu na afya yenye thamani ya mabilioni ya shilingi.

Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stella Joel ndiye aliyemuibua Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga baada ya kupewa taarifa kuhusu anavyojitoa kwa jamii kuwatumikia baada ya hapo ulianza mchakato wa kujua jinsi anavyofanya kazi na hatimaye kutambulika na kutunukiwa shahada hiyo ya udaktari wa heshima.

“Tuzo ambazo amepata nataka kuwahakikishiaWanashinyanga na Watanzania kwa ujumla wao kuwa tumepata mtu ambaye atalisaidia taifa hivyo tumuombee kwani watu wa namna yake ni wachache,” alisema Joel.

Mkazi wa Shinyanga kwa zaidi ya miaka 20, Charles Luchagula, alisema mkurugenzi huyo amekuwa karibu na jamii kwa kusaidia mikopo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, pamoja na kuchangia maendeleo ya shule na michezo.

Kwa upande wake, Daud Moses, mmiliki wa Hope Conscious Pre and Primary School, alisema alipata msaada wa haraka katika mchakato wa usajili wa shule yake baada ya kuwasiliana na ofisi ya mkurugenzi huyo.

Akizungumza baada ya kutunukiwa tuzo hiyo, Dkt. Kaganze alishukuru CMTU kwa kutambua mchango wake akiwa hai, akisema tuzo hiyo itamhamasisha kuongeza bidii katika kuwatumikia wananchi.

“Tuzo hii inanipa nguvu mpya ya kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu na kujituma zaidi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa Shinyanga na Taifa kwa ujumla,” alisema.

Kwa ujumla, tuzo hiyo ni uthibitisho wa mchango wake katika kuimarisha utawala bora, kuhamasisha amani na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Manispaa ya Shinyanga.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mwalimu Dkt. Alexius Revocatus Kaganze, akionesha cheti baada ya kutunukiwa tuzo hizo.

Profesa Stephano Nzowa wa African Graduate University, akimvika kofia ikiwa ni ishara ya kumtunuku Mwalimu Dkt. Alexius Revocatus Kaganze, alipotunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa) katika Ustawi wa Jamii na Uongozi wa Biashara. 

Mwenyekiti Mwanzilishi wa Greeling Global Peace Organization na mmiliki wa CMTU, Profesa Askofu Kennedy Songwe, akimpongeza Mwalimu Dkt. Kaganze.

Mwalimu Dkt. Kaganze akiwapungia mkono wananchi wa Manispa ya Shinyanga 'hawapo pichani wakati alipokuwa akienda kutunukiwa tuzo hizo'
Mwalimu Dkt. Kaganze akiwa kwenye gari maalumu wakati akielekea ukumbi wa Level One kutunukiwa tuzo hizo.

Picha ya pamoja.

Wapiga matarumbeta wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania 'KKKT' Mkoa wa Shinyanga wakinoesha hafla hiyo.


Ndugu , jamaa na marafiki wa Mwalimu Dkt. Kaganze wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mwalimu Mlemwa Msusi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Shinyanga akitafsiri kwa vitendo mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea katika hafla hiyo kwa ajili ya wenzetu wenye usikivu hafifu.
Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu.
Wadau wakiwa kwenye hafla hiyo.
Bi. Editha Alex akiwa na mtoto wake, Joleene Joel kwenye hafla hiyo.
Ndugu zake Mwalimu Kaganze wakiwa kwenye hafla hiyo. Kutoka kushoto ni Mwalimu Autalia Sukari, Beatrice George na Linda Joel.
Viongozi wakiwa meza kuu.
Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stella Joel akionesha furaha kwenye hafla hiyo. Kushoto ni Mlezi wa TAMUFO, Dkt. Frank Mbuli.. 
Afisa Program wa Tume ya Taifa UNESCO, Edelfrida Tibaija 'kushoto' akiwaelekeza jambo Mlezi wa TAMUFO na Katibu wa TAMUFO, Stella Joel katika hafla hiyo.
Katibu wa TAMUFO, Stella Joel akiteta jambo na Mwenza wake Mwalimu Dkt. Kaganze, Safina Kaganze.
Mmoja wa uratibu wa hafla hiyo, Joel Komba,  akipokea maelekezo ya viongozi katika hafla hiyo
Mwalimu Dkt. Kaganze akiteta jambo na Mwenza wake Safina..
Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dkt. Khamis Said akiwasalimia washiriki wa hafla hiyo.
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Nesta Sanga, akiwavika Beji maalumu washiriki wa hafla hiyo.
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Nesta Sanga, akimvika beji maalumu Balozi wa Amani, Mess Chengula ambaye pia ni kiongozi wa wchimba madini.
Nesta aakiendelea na kuwavika Beji Maalumu washiriki katika hafla hiyo

Mama mzazi wa Mwalimu Dkt. Kaganze Christina Gafisa akivikwaa beji maalumu
Baba Mzazi wa Mwalimu Dkt. Kaganze Mathias Fungamake, akivikwa Beji.
Mama Mkwe wa Mwalimu Dkt. Kaganze akivikwa Beji.
Afisa Program wa Tume ya Taifa UNESCO, Edelfrida Tibaija akivikwa Beji.
Mkurugenzi wa Maalula TV, Daniesa Malula, akionesha furaha yake wakati wa hafla hiyo.
Mratibu wa hafla hiyo Dkt. Christina Ngereza akizungumza katika hafla hiyo.
Mwalimu Luhunga akizungumzia kazi mbalimbali alizofanya Balozi Dkt. Kaganze
Daud Moses, mmiliki wa Hope Conscious Pre and Primary School, akizungumza.
Katibu wa TAMUFO Stella Joel akizungumza.
Ndugu waa Mwalimu Dkt. Kaganze wakiwa katika foleni ya kwenda kumpongeza ndugu yako kwa kutunukiwa tuzo