Jiji lote lilijua kesi yangu ya talaka. Ilikuwa gumzo mitaani na hata kazini. Siku ya hukumu nilihisi dunia imenipotea. Nilipoteza nyumba yangu, magari, na hata biashara yangu ikagawanywa kwa mume wangu wa zamani. Nilipokea makaratasi ya hukumu nikiwa nimekaa kimya, machozi yakinibubujika, nikijiuliza nitaanzia wapi tena. Majirani waliniangalia kwa huruma, wengine wakinong’ona kwamba maisha yangu yalikuwa yamefika mwisho.

Mali niliyojenga kwa miaka mingi ya jasho ilipotea kwa dakika chache tu za kusoma hukumu. Nililazimika kuondoka kwenye nyumba niliyoinunua kwa mikopo na kwenda kukaa na shangazi yangu kwa muda. Nilikuwa nimevunjika moyo na kila nilichokiona kilinikumbusha maisha yangu ya ndoa. Nilipoteza hamu ya kula, nilianza kupoteza uzito, na hata kuzungumza na watu nikawa sina nguvu.

Kesi ya rufaa niliyojaribu kufungua haikusaidia chochote kwa sababu upande wa mume wangu ulikuwa na nguvu na wakili wao alikuwa na ujuzi mkubwa.

Nilianza kuamini kwamba huu ndio ulikuwa mwisho wangu. Marafiki walinambia nianze upya maisha, lakini nilijua haki yangu ilikuwa haijapatikana. Nilikuwa na ushahidi kwamba nilichochangia katika kujenga mali ile kilikuwa kikubwa kuliko chake, lakini mahakama haikuzingatia. Soma zaidi hapa 



Na Denis Chambi, Tanga.


MGOMBEA wa nafasi ya Urais kupitia chama cha Alliance Democratic Change (ADC) Wilson Elias Mulumbe ameahidi Serikali atakayoiongoza itahakikisha inarejesha viwanda vyote vilivyobinafsishwa pamoja na kufufua vilivyokufa ili viweze kuzalisha na hatimaye  kuwapatia wananchi ajira za kudumu hatua ambayo itainua uchumi wa mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.


Akizungumza katika mwendelezo wa kampeni zake mkoani Tanga Mulumbe amesema kuwa kutokana na ubinafsishwaji wa viwanda na vingine vikashindwa kuendelea kuzalisha kumechangia kwa kiasi kikubwa ukosefu wa ajira hususani kwa vijana ambao ndio Nguvu kazi ya Taifa.


Ameongeza kuwa pamoja na kuvirejesha viwanda hivyo ikiwemo vilivyokuwepo mkoani Tanga pia atahakikisha anajenga kiwanda cha kuchakata Samaki  ambao watakuza soko la ndani na nje ya nchi huku akiahidi kukaa upya na wawekezaji ambao walifunga viwanda vyao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kodi kuwataka wavifungue ili waweze kuzalisha ajira kwa watanzania.

" Wenzetu baada ya kubinafsisha viwanda hivi walitakiwa kuvisimamia lakini mwisho wa siku waliwaachia  mabepali ambao waliviua,  ahadi yetu kwa wananchi ni kwamba sasa tunaenda kuvifufua  na kuvirudisha mikononi mwa Serikali  na vijana wetu wataenda kufanya kazi"


"Viwanda vingi hapa Tanga vilifungwa kutokana na wingi wa kodi ambazo wawekezaji wameshindwa kulipa kwenye mamlaka  lakini sisi tutakapoingia madarakani tutawaita na kukaa nao wawekezaji wote ambao walifunga viwanda vyao  waendelee kufanya kazi ili kuzalisha ajira kwa watanzania" amesema na kuongeza


"Naomba mtuchague chama cha ADC ili viwanda vingi vilivyokufa ikiwemo kiwanda Cha Amboni  tutakifanya kuwa kiwanda Cha kuchakata minofu ya Samaki  na kutengeneza nyenzo za uvuvi wa Samaki ili kila mwezi tuweze kuvua tani 40 za Samaki ambazo zitachakatwa  na kupelekwa kwa walaji wa ndani na nje ya nchi yetu" amesema Mulumbe.


Mbali na hayo Mulumbe ameahidi endapo atachaguliwa October 29 kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Serikali yake itahakikisha inawalipa mishahara wenyeviti wa Serikali za mitaa ,vijiji na vitongoji ili kuwawezesha na kuwapa motisha ya kufanya kazi.

"Hata wenyekiti wetu wa Serikali za mitaa tutaweza kuwalipa mishahara mbali na kazi kubwa wanayoifanya lakini bado Serikali iliyopo madarakani haiwalipi chochote endapo mkitupa ridhaa ya kuiongoza hii nchi kuanzia mwishoni mwa mwaka huu wa 2025 tutaanza kuwalipa  mishahara hapo ndio wakati ambapo watafanya kazi kwa uadilifu  na kuweza kuwasaidia wananchi wetu" ameongeza mgombea huyo.


Awali akizungumza mwenyekiti wa Alliance Democratic Change 'ADC' Taifa Shabani Itutu ameeleza kero za wananchi ambazo zimekuwa zikielekezwa kwa Mahakama ma Jeshi la Polisi nchini ambapo  amesema kuwa utoaji wa haki umekuwa ukighubikwa na vitendo vya rushwa jambo ambalo limekuwa likiwanyima haki wanaostahili.


"Kuna malalamiko mengi ya wananchi juu ya Jeshi la Polisi unapopelekwa kituo chochote cha Polisi huwezi kutoka bila ya chochote hii sii haki kabisa wengine ni watu wa Mahakama  shida imekuwepo kwenye utoaji wa hukumu  watu wengi wenye maisha ya chini wanalalamika  hawapati haki mpaka watoe rushwa  tuwaambie tu kwamba nchi hii inafuata misingi ya sheria  na katiba ya nchi dhamana ni haki ya kila mtu na kupata haki ni haki ya kila mtu"


Aidha chama hicho cha Alliance Democratic Change (ADC) kimetumia kampeni hizo kumnadi mgombea ubunge kupitia chama cha Wananchi CUF wa Jimbo la Tanga Mussa Mbarouk  ikiwa ni ishara ya kumuunga mkono na kumuombea kura kwa wananchi ifikapo October 29 mwaka huu kwenye uchaguzi mkuu wa madiwani ,wabunge na Rais.


MWISHO.

 


Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) jana tarehe 16 Septemba, 2025 lilifanya mafunzo ya usalama na utunzaji wa mazingira majini kwa wadau wa usafiri majini  katika Mwalo wa Matema wilayani Kyela mkoani Mbeya. 

Elimu hiyo ililenga kuimarisha usalama wa usafiri majini katika Ziwa Nyasa ili kupunguza ajali na kulinda maisha ya wananchi wanaotegemea usafiri huo kwa biashara na shughuli zao za kila siku.

Akizungumza katika kikao cha uhamasishaji kilichofanyika ufukweni mwa Ziwa hilo, Afisa Mfawidhi wa TASAC Mkoa wa Mbeya, Naho. David Chiragi aliwataka wamiliki wa vyombo vidogo vya usafiri majini kuhakikisha wanazingatia kanuni na taratibu za uendeshaji wa vyombo hivyo kwa mujibu wa leseni zao.

“Tuzingatie matakwa ya leseni zetu ikiwemo kutofanya safari za usiku, safari zianze saa 12 asubuhi na kumalizika jioni ili kuepusha ajali zinazoweza kutokea gizani," alisema Naho. Chiragi. 

Aliongeza kuwa abiria wanatakiwa kuvaa jaketi okozi muda wote wa safari, na kusisitiza kuwa katika usafiri majini hakuna ajali za bahati mbaya, bali ni uzembe na kutozingatia kanuni.

Kwa upande wake, Mkuu wa Bandari ya Matema, Bw. Beat Haule, aliwataka waendeshaji na wamiliki wa maboti kuhakikisha wanatimiza masharti yote yaliyowekwa na TASAC ili kufanya kazi kwa usalama na ufanisi.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Maboti, Wilaya ya Kyela, Bw. Macarus Gowele, aliiomba Serikali kuwajengea miundombinu ya huduma katika maeneo yao ikiwemo vyoo na sehemu za kulala endapo wakikwama njiani hasa wakati wa mvua .

Wananchi na wamiliki wa vyombo vya usafiri majini walioshiriki kikao hicho waliipongeza TASAC kwa kutoa elimu hiyo, wakisema itasaidia kuimarisha usalama wa abiria na mizigo, kukuza biashara na kuendeleza shughuli za utalii katika eneo la fukwe ya Matema.

 

Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege,akizungumza kwenye kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WADAU wa zao la Tumbaku nchini wamekutana jijini Dodoma na kuweka mkakati wa pamoja wa kuhakikisha wakulima wanapata bima ya zao hilo kupitia vyama vyao vya ushirika, ili kuwalinda dhidi ya majanga na hasara zinazoweza kuathiri uzalishaji.

Kikao hicho maalum kimewaleta pamoja Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Shirikisho la Vyama vya Ushirika (TFC), Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Konsotia ya Bima za Kilimo (TAIC), taasisi za kifedha na wakuu wa wilaya za mkoa wa Tabora.

Lengo  la mkutano huo ulikuwa  kutafuta suluhu ya changamoto zinazowakabili wakulima wa tumbaku, hususan uhakika wa kipato wanapokumbana na majanga ya asili au mazingira yasiyotabirika, pamoja na utoroshaji wa mazao.

Akizungumza kwenye kikao hicho Lleo Septemba 17,2025 jijini Dodoma, Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege, amesema kuwa hatua hiyo ni mwanzo wa kuhakikisha kila mkulima wa tumbaku anakuwa na bima ya mazao kabla ya kuanza msimu mpya wa kilimo.

“Usajili wa wakulima wa tumbaku utaanza mara moja na takwimu zao zitakusanywa kwa manufaa ya wakulima wenyewe, taasisi za kifedha na kampuni za bima. Tunataka mfumo wa bima uwe na tija na kulinda kipato cha mkulima,” amesema  Dkt. Ndiege.

Aidha ameongeza kuwa bima kwa wakulima kwa sasa ni jambo la lazima kwa kuwa inawalinda wanapokumbwa na majanga, huku akibainisha kuwa Serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha kila mkulima anakuwa na bima ya mazao.

"Kupitia ushirika, wakulima wataweza kupata huduma ya bima kwa urahisi zaidi, huku taasisi za kifedha na kampuni za bima zikihakikisha mfumo huo unakuwa endelevu."amesema Dkt. Ndiege.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Dkt. Khamis Mkanachi, amesema kuwa usajili na bima kwa wakulima ni hatua ya kudhibiti mianya ya utoroshaji wa tumbaku na kuhakikisha mkulima anakua na maslahi ya moja kwa moja kupitia chama chake cha ushirika.

Dkt.Mkanachi, amesema kuwa usajili wa wakulima ni hatua muhimu na ya haraka, kwani bila ya zoezi hilo uhalali na utambuzi wa wakulima unabaki kuwa fumbo.

 "Kukamilika kwa usajili huo kutasaidia kudhibiti vitendo vya utoroshaji wa tumbaku, kwa kuwa mkulima atakayekopeshwa na benki kupitia chama cha ushirika atalazimika kuuza tumbaku yake kupitia chama hicho na si vinginevyo."amesema Dkt.Mkanach

Wadau hao wameeleza kuwa bima ya mazao ni nguzo muhimu katika kulinda ustawi wa wakulima na kuongeza tija ya kilimo, jambo litakalosaidia sekta ya tumbaku kuchangia ipasavyo katika pato la taifa.

Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege,akizungumza kwenye kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Kamishna wa Bima  Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) - Dkt. Baghayo Saqware,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

 Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Dkt. Khamis Mkanachi,akichangia mada  wakati wa kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Dkt Gerald Mongella,akichangia mada  wakati wa kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Wadau mbalimbali wakisikiliza hotuba ya Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege,(hayupo pichani) wakati wa  kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Wadau mbalimbali wakisikiliza hotuba ya Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege,(hayupo pichani) wakati wa  kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Wadau mbalimbali wakisikiliza hotuba ya Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege,(hayupo pichani) wakati wa  kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

Wadau mbalimbali wakisikiliza hotuba ya Mrajis na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege,(hayupo pichani) wakati wa  kikao cha wadau wa Tumbaku kwa ajili ya kupitisha utaratibu wa utekelezaji na utoaji wa Bima ya Zao la Tumbaku kwa wakulima kupitia Ushirika kilichofanyika leo Septemba 17,2025 jijini Dodoma.

 

 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akifuatilia maelezo ya Mhandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Rashid Mtamila (wa tatu kutoka kushoto) walipotembelea uwanja wa Sokoine leo Septemba 17, 2025, kukagua maandalizi ya uwanja huo kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.

Na; Mwandishi wetu- Mbeya

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus amekagua maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zitakazofanyika jijini Mbeya.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mkoa kuhusu maandalizi leo 17 Septemba 2025, Naibu Katibu Mkuu Zuhura Yunus alieleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi na kuipongeza kamati ya Mkoa kwa kuendelea kusimamia na kuratibu vyema shughuli hiyo.

Katika ziara hiyo, Naibu Katibu Mkuu huyo aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo kukagua uwanja wa Uhindini kutakapofanyika maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa, uwanja wa Sokoine kwa ajili ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na kukagua mazoezi ya vijana wa halaiki.

Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa mwaka 2025 zinaongozwa na kauli mbiu isemayo “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa waka 2025 kwa Amani na Utulivu”.

Mbio hizo zilizinduliwa rasmi Aprili 2, 2025 Kibaha, Mkoani Pwani na kilele chake kitafanyika Mkoani Mbeya Oktoba 14, 2025, ambapo Mwenge wa Uhuru unakimbizwa katika mikoa 31 na Halmashauri 195 zikiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Mkoa wa Mbeya wakati wa ziara yake Septemba 17, 2025 ya kukagua maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru zitakazofanyika jijini Mbeya.

Wajumbe wa Kamati Elekezi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakifuatilia taarifa ya mkoa wa Mbeya kuhusu maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025.

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo akieleza hatua zilizofikiwa na mkoa kuhusu maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akikagua moja ya mabango ya hamasa kuhusu kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru yaliyaondaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya leo Septemba 17, 2025, jijini Mbeya.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akikagua maeneo mbalimbali katika uwanja wa Sokoine wakati wa ziara yake ya kufuatilia Maendeleo ya maandalizi ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025, jijini Mbeya.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akifuatilia maelezo ya Mhandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Rashid Mtamila (wa tatu kutoka kushoto) walipotembelea uwanja wa Sokoine leo Septemba 17, 2025, kukagua maandalizi ya uwanja huo kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.

 

Sikuwahi kufikiria siku moja ningefutwa kazi bila hata kupewa sababu. Ilikuwa siku ya Ijumaa asubuhi nilipoitwa ghafla ofisini kwa meneja. Nilipofika, nilikabidhiwa barua na kuambiwa huduma zangu hazihitajiki tena. Nilihisi dunia inazunguka, moyo ukasita kupiga kwa sekunde kadhaa. Nilishindwa hata kuuliza kwa nini. Niliondoka ofisini nikiwa na machozi yakinitiririka, nikihisi aibu na huzuni kubwa.

Wiki ya kwanza nyumbani ilikuwa mbaya zaidi. Niliamka kila asubuhi nikijiuliza kosa langu lilikuwa lipi. Niliogopa kukutana na majirani au marafiki kwani sikutaka kuulizwa maswali. Kila usiku nililala nikiwa na mawazo mazito, nikijiuliza maisha yangu yangeendeleaje bila kipato.

\Nilikuwa nimezoea maisha yenye ratiba na mshahara wa kila mwezi. Mara ghafla nikawa sina kazi, sina mpango, na sina uhakika wa kesho.

Nilijaribu kutuma maombi ya kazi mtandaoni na kwa rafiki zangu lakini sikupata majibu yoyote. Hali yangu ya kiakili ilianza kuwa mbaya.

Nilianza hata kufikiria pengine nililaaniwa au kuna mtu alikuwa hanitakii mema. Ilikuwa kama kila kitu kilikuwa kikinipita, na wenzangu wa zamani kazini walionekana kufurahia maisha. Hapo ndipo nilipoamua sitakaa chini nione maisha yangu yakiharibika. Soma zaidi hapa 

 


 Na; Mwandishi Wetu - Kilindi 

 Vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mkuu nchini mwaka 2025,katika Jimbo la Kilindi vimetakiwa kufanya kampeni za kistaarabu ili kuendeleza utulivu na amani iliopo nchini. 

Wito huo umetolewa na Afisa mwandamizi kutoka ofisi ya msajili wa vyama vya siasa Bi. Edna Assey katika kikao cha mafunzo na vyama vya siasa vyenye wagombea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, katika jimbo la Kilindi kilichofanyika tarehe 17/09/2025 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya wilaya ya Kilindi. 

 “wakati wa kufanya kampeni zenu acheni sera ziongee” alisema Afisa mwandamizi Bi Assey na kuvitaka vyama vya siasa kunadi sera zao ili zieleweke kwa wananchi na kuacha kutumia maneno na vitendo ambavyo vinaweza kuhatarisha kuvunjika kwa amani na utulivu. 

 Aliongeza kusema kuwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ina majukumu mbalimbali ikiwemo kusimamia utekelezaji wa sheria ya vyama vya siasa sura ya 258 na kuvitaja vitendo vinavyokatazwa na sheria ya vyama vya siasa kuwa ni pamoja na Kunadi sera zinazopingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Katiba ya Zanzibar na Sheria nyingine za nchi, Kuunda kikundi cha ulinzi na usalama cha aina yeyote au kuwa na taasisi inayolenga kufanya majukumu ya jeshi la polisi au vikosi vingine vya ulinzi na usalama wa nchi.

 Kuratibu,kuendesha au kufadhili mafunzo yeyote ya kutumia nguvu au silaha kwa wananchama wake au kwa mtu yeyote Kuhamasisha udini,ukabila na ukanda ,kuhamasisha kuvunjika kwa Muungano wa Tanzania au kuwa na lengo la kufanya siasa upande mmoja wa Muungano Vitendo vingine vinavyokatazwa na sheria ya vyama vya siasa ni kuruhusu au kuhamasisha matumizi ya nguvu kama njia ya kufikia malengo ya kisiasa.

 Kuruhusu viongozi au wananchama wake kutumia maneno ya matusi,dhihaka,kashfa na uchochezi yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani Kupeperusha bendera ya chama,kufanya siasa au kufungua tawi katika maeneo ya kazi,shule,vyuo,ibada
,majengo ya serikali au umma Kutoa matamshi,kuandaa machapisho,kuharibu au kufanya kitendo chochote chenye dhamira ya kudhalilisha au kudhihaki bendera ya chama kingine na kufanya mikutano au maandamano bila kufuata utaratibu wa kisheria.


 Kwa upande wao viongozi wa vyama vya siasa Wilayani Kilindi waliipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kwa maandalizi mazuri ya uchaguzi na kuomba kuendeleza ushirikiano mzuri kati ya serikali na vyama vya siasa. 




 


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa Watanzania kudumisha amani na utulivu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa uchaguzi siyo vita bali ni tendo la demokrasia.

Akihutubia leo, Jumatano Septemba 17, 2025, katika kijiji cha Kajengwa, Makunduchi, Visiwani Zanzibar, Dkt. Samia amesema amani ni msingi wa maendeleo ya Taifa na inapaswa kulindwa kwa gharama yoyote, hususan wakati huu wa uchaguzi.

“Ndugu zangu, tunaingia kipindi cha uchaguzi. Mwanzo nilipokuja kujitambulisha, ahadi kubwa niliyoitoa ni kuifanya Tanzania iwe na amani na utulivu. Sasa tunapoelekea Uchaguzi Mkuu, nawaomba sana tudumishe amani na utulivu. Uchaguzi si vita, ni tendo la demokrasia. Nenda weka kura yako, kisha rudi nyumbani ukatulie ili nchi ibaki salama,” amesema Dkt. Samia.

Dkt. Samia ameonya dhidi ya vitendo vya vurugu na matumizi ya silaha za aina yoyote, akisema havileti suluhisho la maana kwa Taifa. Amesisitiza kuwa utulivu na mshikamano wa kitaifa unapaswa kupewa kipaumbele na kila Mtanzania.

Aidha, Dkt. Samia amesema vyombo vya ulinzi na usalama nchini vimejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira salama na ya amani, Bara na Visiwani.

KIGODA Cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere katika Taaluma za Umajumui wa Afrika (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam) kwa kushirikiana na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP Centre), limeandaa kongamano kubwa la kujadili Uchumi Jumuishi kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

 

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeandaa kikao cha Waratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 15–19 Septemba 2025  ambacho kimeshirikisha taasisi 22 kwa lengo la kujadili maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimeshiriki kama moja ya taasisi nufaika ya mradi huu.

Akifungua kikao hicho Mratibu wa Mradi wa HEET KitaifaDkt. Kenneth Hosea amewataka waratibu hao kutumia kikao hicho kubadilishana uzoefu katika kuboresha utekelezaji wa mradi huo, ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 74.3 hali inayoonesha kasi nzuri ya shughuli zilizopangwa kutekelezwa katika mradi huo

 Akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Mratibu wa Mradi HEET IAA, Mratibu Msaidizi wa Mradi wa HEET IAABw. Emmanuel Pallangyo amesema, IAA kupitia mradi huu IAA inaendelea na ujenzi wa majengo ya TEHAMA, taaluma, utawala, maktaba na maabara ya kompyuta katika kampasi za SongeaBabati na Arusha ambayo yatachangia kuboresha mazingira ya ufundishaji, ujifunzaji na kuongeza udahili wa wanafunzi.

Aidha, Pallangyo amesema ujenzi wa majengo hayo umezingatia miundombinu wezeshi kwa watu wenye mahitaji maalum, huku akibainisha kuwa jumla ya wananchi 1055 wamepata ajira za muda katika ujenzi unaoendelea  ikiwemo ujenzi, utoaji wa huduma za chakula na ufundi mbalimbali, ambazo zinawasaidia kujipatia kipato kwa ajili ya kujikimu kimaisha. 

Pamoja na ujenzi wa miundombinu, Pallangyo amesema mradi wa HEET umewezesha IAA kuhuisha jumla ya mitaala 08 ili kuendana na mahitaji ya soko la ajira, kutoa mafunzo ( Shahada ya Uzamivu) kwa watumishi 22 , kuimarisha ushirikiano wa kisekta katika ya Chuo na wadau ikiwemo sekta binafsi na kuongeza uelewa wa masuala ya jinsia na elimu jumuishi katika utoaji wa elimu.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mradi huu  imetenga jumla ya shilingi bilioni 48 kwa  ajili ya IAA ili kuwezesha ujenzi na uboreshaji wa miundombinu, mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa watumishi, kuimarisha ushirikiano wa kisekta na kuimarisha masuala ya jinsia na elimu jumuishi.