Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo (MOI) imesema itaendelea kuimarisha tafiti zinazolenga kuzalisha afua za matibabu zinazozingatia mazingira na vinasaba vya Watanzania, ili kuboresha huduma za matibabu ya magonjwa ya mifupa na mfumo wa fahamu.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, Jijini Dar es Salaam Julai 6, 2026, kwenye Maadhimisho ya Miaka 50 ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Amesema mara nyingi tiba zinazotumika hutokana na matokeo ya tafiti zilizofanyika katika nchi zilizoendelea pamoja na baadhi ya nchi za bara la Afrika, ambapo afua hizo zinaweza kuwa zimezingatia watu wenye vinasaba tofauti, hivyo wao wameona umuhimu wa kufanya tafiti zitakazozalisha afua zinazokidhi mazingira ya Tanzania.

Aidha, amesema MOI imetimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake na imeendelea kujikita katika maeneo makuu matatu ambayo ni kutoa huduma kwa wagonjwa wa mifumo ya ubongo na mifupa, kufundisha huduma hizo kwa wananchi na wataalam katika ngazi ya shahada ya kwanza, shahada ya pili na ubobezi, pamoja na kufanya tafiti.

Pia amesema taasisi hiyo imeweza kutoa mafunzo kwa wananchi na wataalam kutoka ndani na nje ya Tanzania, hususan katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati, Kusini na Magharibi, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha huduma za afya katika kanda hiyo.




 



Na Mwandishi Wetu
TUME ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) imesema Serikali imeanza maandalizi ya kuanzisha mpango wa kuzalisha umeme wa nyuklia, huku ikisisitiza kuwa utekelezaji wa mradi huo utafuata kikamilifu viwango vya kimataifa vya usalama ili kulinda wananchi, mazingira na kuhakikisha matumizi salama ya teknolojia hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la TAEC kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mkurugenzi Mkuu wa TAEC, Prof. Najat Kassim Mohammed, amesema Tanzania ipo katika hatua za awali za maandalizi kabla ya kuingia rasmi katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huo.

Alisema Serikali inaendelea kuimarisha mfumo wa kisheria, sera na taasisi zitakazosimamia matumizi ya teknolojia ya nyuklia ili kuhakikisha uzalishaji wa umeme unafanyika kwa kuzingatia viwango vya usalama vinavyokubalika kimataifa, sambamba na kujenga uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya nishati hiyo.

Prof. Najat alisema TAEC tayari imewaalika wataalamu wa kimataifa kufanya tathmini ya utayari wa Tanzania katika kutekeleza mpango huo.

Alieleza kuwa endapo tathmini hiyo itaridhisha, nchi itapata kibali cha kuendelea na hatua inayofuata ya utekelezaji.

Aidha, alisema Serikali inalenga ndani ya kipindi cha miaka saba kuanza kuzalisha umeme wa nyuklia, hatua inayotarajiwa kuongeza upatikanaji wa nishati ya uhakika, kuimarisha ukuaji wa uchumi na kuchochea maendeleo ya sekta ya viwanda.

Akizungumzia upatikanaji wa malighafi, Prof. Najat amesema Tanzania ina akiba ya madini ya Urani, ambayo ndiyo malighafi muhimu katika uzalishaji wa nishati ya nyuklia kuongeza kuwa madini ya urani lazima yachakatwe kwa teknolojia maalumu kabla ya kutumika kama mafuta ya nyuklia.

Alieleza kuwa katika hatua za mwanzo, urani itakayochimbwa nchini itasafirishwa kwenda nje ya nchi, ikiwemo Urusi, kwa ajili ya kuchakatwa, kisha kurejeshwa Tanzania kwa matumizi ya kuzalisha umeme.

Prof. Najat alisema mradi wa uchimbaji wa madini ya urani unatarajiwa kuanza katika eneo la Mkuju, mkoani Ruvuma, huku shughuli za utafiti zikiendelea katika maeneo mengine ili kubaini akiba zaidi zenye uwezo wa kuchimbwa kibiashara.

Pamoja na hayo, aliwataka wananchi kujenga uelewa sahihi kuhusu teknolojia ya nyuklia na kuondoa hofu zisizo na msingi, akisisitiza kuwa Serikali inatekeleza mpango huo kwa kuzingatia miongozo na viwango vya kimataifa vinavyolenga kuhakikisha usalama wa watu, mazingira na miundombinu.

Alisema matumizi ya teknolojia ya nyuklia yana mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa, siyo tu katika uzalishaji wa umeme, bali pia katika sekta za afya, kilimo, viwanda na utafiti wa kisayansi.

 


KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel Tanzania imeendelea kuimarisha mchango wake katika maendeleo ya jamii kwa kuunganisha ajenda za afya, ustawi wa wafanyakazi na uhifadhi wa mazingira kupitia udhamini wake wa mbio za ‘Great Ruaha Marathon 2026’, zilizofanyika hivi karibuni ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Ikiwa Mdhamini Rasmi kutoka sekta ya Mawasiliano, Airtel ilishiriki pamoja na mamia ya wakimbiaji katika tukio ambalo limeendelea kujijengea sifa kama moja ya mbio za kipekee nchini zinazochanganya michezo, utalii na juhudi za kuhifadhi mfumo wa ikolojia wa Mto Mkuu wa Ruaha.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo mkoani Iringa, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Airtel Tanzania, Bi. Stellah Kibaja, alisema ushiriki wa kampuni hiyo unaonyesha dhamira yake ya kuleta mchango chanya kwa jamii, hatua inayokwenda sambamba na shughuli zake za kibiashara.

"Airtel tunaamini kuwa mahusiano imara hayajengwi kupitia mtandao wetu pekee, bali kupitia watu, uzoefu wa pamoja na jamii zinazounganishwa na lengo moja. Ndiyo maana tunajivunia kuwa sehemu ya Great Ruaha Marathon, tukio linaloendana na maadili yetu ya kuhamasisha afya bora, kuunga mkono jamii na kushiriki katika mipango yenye manufaa ya kudumu," alisema Bi. Kibaja.

Katika kuonyesha mfano wa uongozi unaoshiriki kwa vitendo, Airtel iliwashirikisha wafanyakazi 20 katika mbio hizo, wakiwemo wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji ya kampuni hiyo.

Bi. Kibaja alibainisha kuwa kampuni hiyo inaamini afya ya wafanyakazi ndio msingi mkuu wa mafanikio ya taasisi yoyote inayotaka kupiga hatua.

"Watu wenye afya hujenga timu imara, timu imara hujenga biashara zenye mafanikio, na biashara zenye mafanikio huchangia zaidi maendeleo ya jamii. Uongozi hauonekani kwenye vikao pekee, bali pia katika kushiriki bega kwa bega na wafanyakazi na kuhamasisha wengine kupitia matendo," alisisitiza.

Aliongeza kuwa Airtel imeendelea kuwekeza katika programu za ustawi wa wafanyakazi zinazolenga kuimarisha afya ya mwili, akili na uwiano kati ya kazi na maisha binafsi, hatua inayosaidia kuongeza tija kazini na kuboresha huduma kwa wateja.

Mbali na michezo, Mkurugenzi huyo alieleza kuwa Airtel inaunganisha mamilioni ya Watanzania kila siku kupitia huduma za sauti, intaneti, intaneti ya nyumbani (Airtel Smart Box) na Airtel Money, huku ikizidi kupanua mtandao wake hadi vijijini.

"Mawasiliano ni zaidi ya kuunganisha watu; ni kufungua fursa. Iwe ni mwanafunzi anayesoma mtandaoni, mkulima anayepokea malipo kupitia Airtel Money, au mfanyabiashara anayekuza biashara yake kidijitali, kila muunganisho una nafasi ya kuboresha maisha ya Watanzania," alisema.

Akifunga maelezo yake kabla ya kuanza kwa mbio hizo, Bi. Kibaja aliwataka washiriki kuona mbio hizo kama jukwaa la kipekee la kuleta mabadiliko.

"Haijalishi unamaliza wa kwanza au wa mwisho. Kilicho muhimu ni kwamba umechagua kuwekeza katika afya yako, kuunga mkono uhifadhi wa mazingira na kuwa sehemu ya harakati zinazozalisha mabadiliko chanya kwa jamii," alihitimisha.

Mbio za Great Ruaha Marathon zimeendelea kukua na kuwa jukwaa muhimu linalovutia ushiriki wa sekta binafsi nchini katika kuhamasisha afya, kukuza utalii endelevu, na kuimarisha uhifadhi wa ikolojia ya Mto Mkuu wa Ruaha ambao ni uti wa mgongo wa hifadhi hiyo na nishati nchini.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amewaalika wafanyabiashara wa Ufaransa kuwekeza Tanzania, akisisitiza kuwa mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyopo nchini yanatoa fursa kubwa za kukuza biashara, kuzalisha ajira, kuhamisha teknolojia na ujuzi, pamoja na kuharakisha ujenzi wa uchumi wa viwanda wenye manufaa kwa Tanzania na Ufaransa.
Na Mwandishi Wetu

CHUO cha Benki Kuu ya Tanzania (BOT Academy) kimewahimiza Watanzania, hususani wahitimu wa elimu mbalimbali na watumishi wa sekta ya fedha, kujiunga na programu zake za mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi zinazolenga kuwajengea ujuzi wa vitendo unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na sekta ya fedha.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) imeeleza kuwa imejikita katika kutafuta rasilimali zitakazowezesha utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2023, kwa kuwekeza nguvu katika maeneo matatu ya kipaumbele ambayo ni ujenzi wa miundombinu kwa elimu ya lazima ya miaka 10, maendeleo ya mkondo wa amali pamoja na matumizi ya nishati safi na uhifadhi wa mazingira shuleni.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAFANYABIASHARA na wananchi kwa ujumla wametakiwa kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutembelea banda la Tume ya Ushindani (FCC) ili kupata huduma mbalimbali za papo kwa papo pamoja na elimu kuhusu ulinzi wa mlaji, ushindani wa biashara na udhibiti wa bidhaa bandia.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imesema ushiriki wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) unalenga kuelimisha wananchi kuhusu maboresho ya mitaala, kuhamasisha elimu jumuishi na kusogeza karibu huduma za vitabu vya kiada na ziada kwa wananchi.

 






>Asema kasi ya maendeleo chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amani, uchumi, afya, maji na miundombinu vimemshawishi kubadili msimamo wa kisiasa.

Baada ya zaidi ya miaka 30 ya kuwa mwanasiasa wa upinzani, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe, amefanya uamuzi mkubwa wa kisiasa kwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Jumbe, ambaye kwa muda mrefu alikuwa mmoja wa viongozi mashuhuri wa Chadema mkoani Tanga, amesema uamuzi wake umetokana na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na juhudi za Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha amani, umoja na ustawi wa wananchi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kumpokea ndani ya CCM iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, Jumbe alisema hakufanya uamuzi huo kwa papara, bali baada ya kutafakari kwa kina na kujiridhisha kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya taifa.


"Nilikuwa mpinzani kwa zaidi ya miaka 30, lakini leo nimeamua kuhitimisha safari hiyo. Kilichonishawishi zaidi ni kazi kubwa inayofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo na kuhakikisha amani ya nchi inalindwa," alisema.

Alieleza kuwa pia amevutiwa na utekelezaji wa falsafa ya 4R inayosisitiza maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya, akisema imeongeza mshikamano na kuimarisha mazingira ya maendeleo nchini.



Akizungumzia Mkoa wa Tanga, Jumbe alisema mabadiliko yanayoonekana katika sekta mbalimbali ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuufungua mkoa huo kiuchumi.

Alitaja kuongezeka kwa shughuli katika Bandari ya Tanga, ujenzi wa bandari kavu pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati kuwa miongoni mwa hatua zilizochochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za biashara.


"Nimekuwa nikipaza sauti kwa miaka mingi nikitaka Tanga ifunguliwe kiuchumi. Leo naona hilo limefanyika. Mizigo imeongezeka bandarini, bandari kavu zimejengwa na shughuli za biashara zinaendelea kukua," alisema.

Katika sekta ya afya, Jumbe alisema maboresho yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na ujenzi wa zahanati katika kata na mitaa mbalimbali vimempa imani kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma kwa wananchi.

Aidha, alisema upanuzi wa huduma za maji na umeme pamoja na utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni miongoni mwa hatua zinazoonyesha dhamira ya Serikali ya kuinua maisha ya Watanzania.




"Nilijiuliza ni hoja gani itanifanya nibaki upinzani wakati maendeleo yanaonekana wazi. Tanga ina amani, huduma zinaimarika na wananchi wanaendelea kunufaika na miradi ya maendeleo," alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, alisema chama hicho kinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano ili kuongeza uwezo wake wa kusimamia maendeleo na kuwatumikia wananchi.



Alisema tangu alipopewa dhamana ya kuongoza CCM mkoani humo, ameweka mkakati wa kuimarisha chama kupitia ushirikiano na wanachama pamoja na kuwakaribisha viongozi kutoka vyama vingine vya siasa.

Rajab alisema mkakati huo umeendelea kuzaa matunda, akieleza kuwa kujiunga kwa Rashid Jumbe ni ishara ya kuongezeka kwa imani ya baadhi ya viongozi wa upinzani kwa juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali.


"Jumbe alikuwa mmoja wa viongozi wakubwa wa upinzani katika Wilaya ya Tanga. Tuliahidi kwamba tutamshawishi aje kushirikiana nasi katika kujenga chama na kuwaletea wananchi maendeleo, na leo tumefanikiwa," alisema.
Maisha yangu yalikuwa yamejaa furaha na amani, lakini kama ilivyo kwa watu wengi, wapo ambao walikubali kuona wengine wakifa kwa hasira zao na chuki. 

Nilijua kuwa nilikuwa na maadui ambao hawakupenda kuona ninavyofanikiwa. Waliishi kwa kijicho, wakiwa na madhumuni ya kunivunja moyo na kuniharibia kila kitu kilichokuwa kikionekana kikienda sawa katika maisha yangu.

Walianza kunifanya nione kama mimi ni mtu asiye na thamani. Walikuwa wakijaribu kuniharibia jina langu, kuzusha maneno mabaya kuhusu mimi, na hata kufanyia kazi mambo ambayo yalionekana kama kutafuta namna ya kuniharibia kabisa. Hata hivyo, nilikuwa na imani kwamba hata maadui hawawezi kunizuia.

Lakini walipoona kwamba walikuwa wanashindwa kwa njia moja au nyingine, walijitahidi kuhamasisha nguvu za giza ili kuniletea madhara. Hali ilibadilika haraka. Maadui wangu walitumia njia za kishirikina kujaribu kuniharibia.

Nilijikuta nikikumbwa na maumivu yasiyoelezeka, huzuni kubwa, na wakati mwingine, nikiwa na wasiwasi kwamba nilikuwa nikipoteza kila kitu. 

Nilianza kuona dalili za mashambulizi ya kiroho ambayo yaliathiri kila upande wa maisha yangu. Familia yangu ilianza kupoteza imani kwangu, na hata marafiki walikuwa wakichukua upande wa maadui wangu.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

Sikuwahi kuelewa kwa nini maisha yangu yalikuwa na milima na mabonde. Nilikuwa nafanya juhudi nyingi kazini lakini hakuna kilichokuwa kinanyooka. 

Mahusiano yangu yalivunjika bila sababu za msingi, na hata marafiki wangu walionekana kufanikiwa wakati mimi nilikuwa nikijikokota. Nilianza kujiuliza, “Kuna nini kisichoeleweka kwenye maisha yangu?”

Nilihisi kama kuna kitu kilikuwa kimenifunika kisirisiri. Siku moja nilihudhuria kikao cha wanawake mahali fulani Mbezi Beach, na baada ya mada ya kawaida kumalizika, mgeni mmoja alisimama na kuzungumza kuhusu nyota za kuzaliwa. Alieleza jinsi tarehe yako ya kuzaliwa inaweza kufichua tabia zako, mafanikio yako, changamoto zako, na hata majira sahihi ya kufanya maamuzi makubwa.

Kwa kawaida, mimi si mtu wa kuamini mambo ya nyota au nguvu za angani, lakini alipoanza kueleza kuhusu watu waliozaliwa mwezi wa Novemba kama mimi, nilishtuka. Alisema, “Watu wa mwezi wa Novemba mara nyingi wana ndoto kubwa lakini hujikuta wanakwamishwa na nguvu zisizoonekana endapo hawajatambua nyota yao vizuri.”

Hapo hapo moyo wangu ulidunda. Alieleza mengi ambayo yalikuwa kama anaelezea maisha yangu kama vile nimewahi kumweleza. Niliposikia hilo, niliamua kufanya utafiti zaidi. Nilianza kwa kujifunza kuhusu nyota yangu nilizaliwa tarehe 11 Novemba, na hiyo inaangukia kwenye nyota ya Scorpio.

Nilijifunza kwamba watu wa Scorpio ni wenye hisia kali, wanapenda mambo ya undani, na wanaweza kuwa na bahati kubwa endapo watajua jinsi ya kuitumia nguvu ya nyota yao. Nilianza kuandika tabia zangu, vitu ninavyopenda, na mambo yanayonikera. Ghafla, maisha yangu yalianza kupata sura mpya.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

 BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imemkabidhi rasmi mwanautalii na mtangazaji wa vivutio vya utalii kutoka Oman, Khalid Hamed Al Barwani, Ubalozi wa Hiari wa Utalii wa Tanzania, ikiwa ni hatua ya kimkakati ya kuimarisha juhudi za kuitangaza Tanzania katika masoko ya kimataifa na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini.

Ubalozi huo umekabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa wa Al Barwani katika kuitangaza Tanzania kupitia majukwaa mbalimbali ya kimataifa.

Al Barwani alipata umaarufu mkubwa baada ya kuongoza kundi la Dream Team Explorers kutembelea Shamba la Miti la Sao Hill mwaka 2024, ambapo walijionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana katika eneo hilo, ikiwemo misitu ya kupandwa, mandhari ya kuvutia ya asili na eneo la Mto Ruaha. 

Maudhui waliyoyashiriki kupitia majukwaa yao ya kidijitali yalichangia kuongeza mwonekano wa Sao Hill na kuibua hamasa ya watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea eneo hilo.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi ubalozi huo, Mafuru alisema TTB itaendelea kushirikiana na watu mashuhuri, watengeneza maudhui na wadau wa kimataifa wenye ushawishi mkubwa katika masoko mbalimbali ili kuendelea kuitangaza Tanzania kama moja ya vivutio bora vya utalii duniani.

“Ubalozi huu ni kutambua mchango wa Khalid Al Barwani katika kuitangaza Tanzania na ni sehemu ya mkakati wetu wa kupanua wigo wa masoko ya utalii kupitia mabalozi wa hiari wanaotumia ushawishi wao kufikisha ujumbe wa Tanzania kwa mamilioni ya watu duniani,” alisema Mafuru.

Kwa upande wake, Al Barwani alishukuru kwa heshima hiyo na kuahidi kuendelea kuitangaza Tanzania kupitia majukwaa yake ya kimataifa, akieleza kuwa nchi ina vivutio vya kipekee vinavyostahili kufahamika zaidi duniani.

“Tanzania ni nchi yenye uzuri wa kipekee, kuanzia hifadhi za wanyamapori, misitu, fukwe, utamaduni hadi ukarimu wa wananchi wake. Nitaendelea kuwa balozi wa kuitangaza Tanzania kwa dunia,” alisema.

TTB inaendelea kutumia ushirikiano na wadau wa kimataifa pamoja na mabalozi wa hiari wa utalii kama sehemu ya mkakati wa kuongeza ushindani wa Tanzania katika soko la utalii duniani na kuunga mkono malengo ya taifa ya kukuza sekta ya utalii, kuongeza idadi ya wageni wa kimataifa na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya uchumi wa nchi.





Jina langu ni Joshua, na mimi ni mjasiriamali. Kwa muda mrefu, nilikuwa nikikabiliana na changamoto kubwa katika biashara yangu. Ilikuwa ni biashara ndogo ya kuuza bidhaa za vipodozi na huduma za uzuri, lakini kwa muda, wateja walikuwa wakipungua.

Nilijikuta nikikopa fedha nyingi kutoka kwa marafiki na familia yangu ili kuendesha biashara hii, lakini kila mara nilikuwa napata hasara. Nilijua kuwa hatua nilizokuwa nikichukua hazikufanikiwa, lakini sikujua ni wapi nilikosea.
Nilikutana na mshtuko mkubwa ulipokuja wazo la kumaliza biashara yangu.

Nilijua kuwa ikiwa nisingepata suluhisho haraka, nisingeweza kuendelea. Nilikuwa nimepoteza matumaini, lakini kimoja kilikuwa kinanifanya niwe na matumaini kidogo. 

Nilisikia kuhusu jinsi watu walivyokuwa wakitumia rituali za kiroho ili kuvutia wateja na kuimarisha biashara zao. Hii ilikuwa ni kitu ambacho nilikuwa najiuliza ikiwa kingeweza kutusaidia mimi pia.

Katika hali yangu ya kukata tamaa, nilijua kuwa nilihitaji msaada wa kiroho ili kubadilisha hali yangu.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

 Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imesema imetumia Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wadau kuhusu majukumu yake, fursa zilizopo katika sekta ya mbolea pamoja na mnyororo wa thamani wa uagizaji, utengenezaji na usambazaji wa mbolea nchini.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Julai 4, 2026, Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini wa TFRA, Joshua Ng’ondya, amesema mamlaka hiyo imefika kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, umuhimu wa upimaji wa udongo, pamoja na utaratibu wa kujisajili ili kunufaika na mpango wa mbolea za ruzuku.

Amesema kupitia maonesho hayo, wananchi na wafanyabiashara wanapata maelekezo ya namna ya kupata leseni za biashara, kusajili maeneo ya biashara na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa mbolea, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika biashara ya mbolea nchini.

Ng’ondya amesema TFRA ina jukumu la kudhibiti ubora wa mbolea za viwandani na mbolea hai zilizosajiliwa, pamoja na kuhakikisha zinakidhi viwango vinavyotakiwa kabla ya kuingia sokoni na katika mpango wa ruzuku kwa wakulima.

Aidha, ameeleza kuwa mamlaka hiyo inaendelea kutoa elimu kuhusu namna ya kutengeneza, kusajili na kuingiza mbolea sokoni kwa kufuata taratibu zilizowekwa, ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora, salama na zenye tija katika kuongeza uzalishaji wa mazao.

 

*Yawahamasisha Wananchi Kutumia Umeme kwa Ufanisi na gharama nafuu

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limewahimiza Watanzania kutembelea banda lake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) ili kujionea teknolojia mbalimbali za kisasa zinazolenga kuboresha matumizi ya umeme kwa usalama, ufanisi na gharama nafuu.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Irene Gowele, alisema maonesho ya mwaka huu yamebeba ubunifu unaowawezesha wananchi kujifunza namna teknolojia ya umeme inavyoweza kuboresha maisha yao ya kila siku.

Alisema mbali na shughuli za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme, TANESCO imejikita kuonesha thamani ya matumizi ya umeme katika sekta mbalimbali za maisha na uzalishaji.

Kivutio kikubwa katika banda hilo ni Nyumba Janja (Smart Home), ambayo imewekewa mfumo wa kisasa wa umeme wa kidijitali unaoongeza usalama wa nyumba dhidi ya majanga kama moto, huku ukimruhusu mmiliki kudhibiti vifaa vya umeme akiwa popote duniani kupitia simu ya mkononi.

Gowele alisema mfumo huo humwezesha mtumiaji kuwasha au kuzima vifaa vya umeme kwa njia ya programu maalumu pamoja na kufuatilia kiwango cha umeme kinachotumiwa na kila kifaa, hatua inayosaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na gharama za bili.

Aidha, alisema TANESCO inaendelea kuhamasisha matumizi ya vifaa vinavyotumia umeme kwa ufanisi mkubwa (energy efficient), ambapo nyumba hiyo imewekewa vifaa vinavyotumia kiwango kidogo cha umeme ili kuwaonesha wananchi namna wanavyoweza kupunguza matumizi ya nishati bila kuathiri huduma.

Pia aliwakumbusha wananchi kuhusu mpango wa TANESCO wa kukopesha majiko ya umeme, akisema wanaotembelea banda hilo wanaweza kupata majiko hayo kwa kununua au kwa mkopo kwa kutumia namba ya mita ya umeme pamoja na Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kwa ajili ya uhakiki.

Alieleza kuwa majiko hayo yana ufanisi mkubwa na yana uwezo wa kupika chakula cha Kitanzania kwa gharama ya chini ya shilingi 356 za umeme, hivyo kuwa mbadala wa gharama nafuu ukilinganisha na baadhi ya nishati nyingine za kupikia.

Katika maonesho hayo, wananchi pia wanapata fursa ya kujionea kwa teknolojia ya kidijitali miradi mikubwa ya uzalishaji umeme inayotekelezwa na TANESCO, ikiwemo Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere na Mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu mkoani Shinyanga unaozalisha megawati 50.

Vilevile, banda hilo linatoa elimu kuhusu matumizi ya umeme katika sekta ya usafiri kupitia magari, pikipiki na bajaji zinazotumia umeme, huku TANESCO ikisisitiza kuwa Tanzania ina umeme wa kutosha unaoweza kusaidia wananchi kupunguza gharama za usafiri na kuchangia utunzaji wa mazingira kwa kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa.

"TANESCO imekuja ki-smart Sabasaba mwaka huu. Tunawakaribisha wananchi wote kutembelea banda letu wajifunze, wajionee teknolojia hizi na namna zinavyoweza kuboresha maisha yao huku zikipunguza gharama za matumizi ya nishati," alisema Gowele.

 




Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limesema litaendelea kuimarisha huduma za mawasiliano nchini kwa kuendeleza matumizi ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, kupanua huduma za kidijitali na kuwekeza katika teknolojia za kisasa ili kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa kidijitali.

Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Moremi Marwa, amesema mafanikio yanayoendelea kupatikana ndani ya shirika hilo yametokana na maboresho ya kiutendaji na kibiashara yaliyofanyika katika kipindi cha hivi karibuni, hatua ambayo imewezesha TTCL kuongeza mapato, kupata faida na kuboresha huduma kwa wananchi.

Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Marwa alisema TTCL imeutumia mkutano huo kama jukwaa la kuonesha teknolojia na huduma mbalimbali zinazochochea maendeleo ya uchumi wa kidijitali kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano.

Alisema miongoni mwa huduma zinazotolewa ni intaneti ya kasi ya juu ya Supersonic Speed, kituo cha FTTX Experience Center kinachowawezesha wananchi kujionea matumizi ya teknolojia ya nyumba janja (Smart Home), pamoja na huduma za Cloud Computing kupitia Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data (National ICT Data Centre – NIDC).

Marwa alifafanua kuwa huduma za Cloud Computing zinazotolewa kupitia NIDC zinawapa wateja fursa ya kuhifadhi taarifa na mifumo yao kwa usalama wa hali ya juu bila kulazimika kuwekeza gharama kubwa katika miundombinu ya kuhifadhi data, jambo linalosaidia kuongeza ufanisi wa shughuli za taasisi na biashara.

Akizungumzia utendaji wa shirika hilo, alisema TTCL imepata faida ya takribani shilingi bilioni 23 katika mwaka wa fedha 2024/2025, huku matokeo ya awali ya mwaka wa fedha 2025/2026 yakionyesha kuongezeka kwa mapato, faida na idadi ya wateja wanaotumia huduma za shirika hilo.

Alisema mafanikio hayo yametokana na utekelezaji wa maboresho ya kimkakati yaliyofanywa kufuatia maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha TTCL linaendeshwa kwa misingi ya kibiashara, linaongeza mapato na kuondokana na utegemezi wa hasara.

Marwa alisisitiza kuwa TTCL itaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa na kuboresha miundombinu ya mawasiliano ili kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora, salama na za uhakika zinazochangia maendeleo ya uchumi wa kidijitali na Taifa kwa ujumla.

  Na Benny Mwaipaja, Banjul, Gambia


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amewasili Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.

Mhe. Omar alipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Banjul.

Mkutano huo utakaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha SDJK, jijini Banjul, utatoa jukwaa kwa nchi za Afrika kujadili masuala muhimu ya uchumi na maendeleo yanayoikabili Bara la Afrika, pamoja na kuweka msimamo wa pamoja katika kushirikiana na taasisi kubwa za kifedha duniani.

African Caucus ni jukwaa linalowakutanisha magavana wa Afrika katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Kundi la Benki ya Dunia, ambalo huzisaidia nchi za Afrika kuzungumza kwa sauti moja kuhusu masuala kama usimamizi wa madeni, fedha za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, maendeleo ya miundombinu, kupunguza umasikini, ajira, biashara, na mageuzi ya kiuchumi.

Gambia kuandaa mkutano huo wa mwaka 2026 ni fursa kubwa kwa nchi hiyo kushiriki kikamilifu katika mijadala ya bara na kuonesha vipaumbele vyake vya maendeleo.

Mkutano huo unaweza kuleta faida nyingi ikiwemo kuongeza mwonekano wa nchi hiyo katika ngazi ya Afrika na kimataifa, kuvutia mijadala kuhusu uwekezaji, na kuimarisha ushirikiano kati ya Gambia, nchi nyingine za Afrika, na washirika wa maendeleo.

Pia unaweza kuonesha juhudi za Gambia katika maeneo kama mageuzi ya uchumi, utalii, kilimo, uwezeshaji wa vijana, mabadiliko ya kidijitali, na maendeleo endelevu.

Mkutano wa 2026 unaweza pia kujikita katika changamoto zinazozikabili nchi za Afrika, zikiwemo ongezeko la madeni, mabadiliko ya tabianchi, uhaba wa chakula, ukosefu wa ajira, na umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda.

Masuala haya ni muhimu hasa kwa nchi ndogo kama Gambia, ambapo athari za mabadiliko ya tabianchi, rasilimali chache, na utegemezi wa sekta chache zinaweza kuathiri maendeleo ya Taifa na upitia African Caucus, nchi zinaweza kubadilishana uzoefu na kupendekeza suluhisho za vitendo linaloendana na hali halisi ya Afrika.

Kuandaa mkutano huu pia kunaweza kuwa na matokeo chanya kwa biashara za ndani na sekta ya utalii. Hoteli, huduma za usafiri, migahawa, waandaaji wa matukio, na vikundi vya sanaa na utamaduni vinaweza kunufaika kutokana na uwepo wa wajumbe na wageni.

Tukio hili linaweza kuitangaza Gambia kama nchi yenye amani, ukarimu, na uwezo wa kuandaa mikutano ya kimataifa na shughuli za kidiplomasia.

Kwa ujumla, Mkutano wa African Caucus wa 2026 nchini Gambia ni tukio lenye umuhimu mkubwa kwa Gambia na Bara la Afrika kwa jumla kwani unatoa nafasi kwa viongozi wa Afrika kujadili vipaumbele vya pamoja, kuimarisha ushirikiano, na kutetea haki zaidi kutoka kwa taasisi za kifedha duniani.

Kwa Gambia, huu ni wakati wa kuonesha uongozi, kutangaza malengo yake ya maendeleo, na kujitambulisha kama mshirika muhimu katika mustakabali wa uchumi wa Afrika.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kushoto), akisalimia na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, wakati alipowasili jijini Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kushoto), akiteta jambo na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, wakati alipowasili jijini Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kulia), akiwa katika picha na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, wakati alipowasili jijini Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WF, Banjul, Gambia)

 BODI ya Utalii Tanzania (TTB), imesema moja ya jukumu lake kubwa ni kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi, hivyo Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)yanayoendelea ni jukwaa muhimu la kuendelea kutangaza utalii wetu.


Aidha imesema kupitia maonesho hayo ya Sabasaba pia yamekuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha utalii wa ndani, kutangaza vivutio vya utalii na kuwaandaa wadau kunufaika na fursa mbalimbali ikiwemo mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kufanyika mwaka ujao.

Akizungumza katika maonesho hayo Naomi Mbilinyi ambaye ni Ofisa Utalii Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania amesema kupitia banda la TTB, wananchi wanapata taarifa kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya utalii, ikiwemo namna ya kuanzisha kampuni za utalii, kushiriki maonesho ya kimataifa na kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo nchini.

“TTB pia inatumia maonesho hayo kutangaza Swahili International Tourism Expo, yatakayofanyika mwezi Oktoba, ambapo wadau wanapata fursa ya kujisajili kama waoneshaji, wadhamini na washiriki wa maonesho hayo ya kimataifa.”

Ameongeza pia bodi hiyo inaendelea kujenga mfumo wa kidijitali utakaowezesha wadau wa utalii kusajili taarifa za biashara zao ili kutangaza huduma na vivutio vyao kwa urahisi katika masoko ya ndani na nje ya Tanzania.

Kwa mujibu wa Mbilinyi, banda la TTB pia limetenga eneo maalum la kutoa elimu kuhusu fursa zitakazotokana na mashindano ya AFCON, likiwaelimisha watoa huduma za malazi, usafiri na sekta nyingine jinsi ya kujiandaa kupokea wageni wengi watakaoingia nchini wakati wa mashindano hayo.

Amesema wageni wengi wanaotembelea banda hilo, hususan wakazi wa Dar es Salaam, huonyesha hamu ya kujifunza kuhusu maeneo ya utalii yaliyo karibu nao, ikiwemo fukwe, maeneo ya kihistoria, makumbusho na vivutio vingine vinavyoweza kutembelewa kwa safari za siku moja (city tour).

Pia amesema wananchi wengi huulizia gharama za kutembelea hifadhi za taifa na maeneo mengine ya utalii, ambapo TTB hushirikiana na taasisi mbalimbali za sekta hiyo kuwapa taarifa sahihi na kuwaelekeza kwenye mabanda husika.

Ametoa wito kwa wananchi, Mbilinyi aliwahimiza kutembelea banda la TTB katika Maonesho ya Sabasaba ili kupata taarifa mbalimbali ambazo si rahisi kuzipata sehemu nyingine, ikiwemo usajili wa mifumo ya kidijitali, taarifa kuhusu Swahili International Tourism Expo na maandalizi ya AFCON.

“Maonesho hayo yanatoa nafasi ya wananchi kuzungumza moja kwa moja na wataalamu wa utalii, kuuliza maswali, kutoa maoni na kupata mwongozo kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya utalii nchini.”






 


Na OWM - TAMISEMI, Lushoto


Mhe. Alhaji Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar,  amekubali ombi la Mbunge wa Jimbo la Lushoto Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa kutoa mchango wa Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya kuendeleza Kituo cha Elimu ya Kiislamu Irshaad (Irshaad Islamic Centre) kilichopo Lushoto, mkoani Tanga.

Fedha hizo zinatarajiwa kuwezesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kituo hicho, ikiwemo kuboresha Chuo cha Ufundi, kuanzisha bustani ya kisasa, kujenga madrasa yenye kukidhi mahitaji ya wanafunzi, kujenga nyumba za walimu, jengo la kupokelea wageni, hospitali pamoja na ukumbi wa kisasa wa kufanyia shughuli mbalimbali za kielimu na kijamii.

Prof. Shemdoe alitoa ombi hilo Julai 5, 2026 wakati wa Sherehe ya Maulidi ya Kumswalia Mtume Muhammad S.A.W iliyoandaliwa na Sheikh Sharrif Hussein Ahmad Badawiyy wa Kituo cha Irshaad Islamic Centre Lushoto, ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Dkt. Hussein Mwinyi amekubali ombi la Rais wa Kituo cha Irshaad Islamic Centre Lushoto Sheikh Sharrif Hussein Ahmad Badawiyy la kumwomba awe mlezi wa kituo hicho, ambapo Mhe. Dkt. Dkt. Hussein Mwinyi ameahidi kuendelea kushirikiana na viongozi pamoja na wadau mbalimbali katika kukiendeleza ili kiwe kitovu cha utoaji wa elimu bora na maadili mema.

Sanjari na hilo, Mhe. Rais Dkt.  Mwinyi ameridhia pia ombi la Rais wa Kituo hicho cha Irshaad Islamic Centre la kumtaka kuridhia jina la Hayati Alhaji Ali Hassan Mwinyi, litumike katika eneo la bustani linalotarajiwa kujengwa katika Chuo cha Ufundi kilichopo ndani ya kituo hicho, ikiwa ni sehemu ya kumuenzi na kutambua mchango wa maendeleo alioutoa Hayati Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiwa ni mlezi wa kituo hicho. 

Mhe. Prof. Shemdoe alimuunga mkono Mhe. Rais Dkt. Hussein Mwinyi kwa kuchangia Shilingi Milioni 20, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt. Batilda Burian  Milioni 5, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima Milioni 5, Mbunge wa Bumbuli Mhe. Mhandisi Ramadhani Hamza Milioni 5, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Bw. Rajab Abdallah Milioni 3 na Mbunge wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Abdullah Makame amechanga Milioni 5 na kufanya jumla ya fedha zilichangwa kuwa Milioni 248, hatua iliyoonyesha mshikamano wa viongozi hao katika kuunga mkono maendeleo ya elimu na ustawi wa jamii. 

Akizungumza mara baada ya hafla hiyo, Mhe. Prof. Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Mwinyi kwa kukubali ombi hilo, akieleza kuwa msaada huo utakuwa chachu ya kuinua viwango vya elimu, ustawi wa jamii na huduma zinazotolewa katika kituo hicho, ambacho kimeendelea kuwa nguzo muhimu ya malezi na elimu kwa vijana wa Lushoto na maeneo jirani.

Aidha, Wananchi na viongozi waliohudhuria hafla hiyo wamempongeza Mhe. Rais Dkt. Mwinyi kwa kukubali maombi yaliyowasilishwa na Mhe. Prof. Shemdoe, wakieleza kuwa uamuzi huo utaacha alama ya kudumu katika maendeleo ya Kituo cha Elimu ya Kiislamu Irshad Lushoto na kuongeza fursa za elimu, ujuzi na huduma za kijamii kwa vizazi vya sasa na vijavyo.