Katika siku ya nane (08) ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama SabaSaba, yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Wakala wa Vipimo (WMA) imeendeleza mkakati wake wa kuwatembelea wajasiriamali na kuwapatia elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo.
Zoezi la utoaji elimu ya vipimo kwa wajasiriamali linaenda sambamba na kuhudumia wadau mbalimbali wanaotembelea banda la WMA katika Maonesho hayo ya SabaSaba.
Lengo ni kuhakikisha elimu na huduma mbalimbali za ki-vipimo zinafikishwa kwa wadau wengi kadri iwezekanavyo.
Pichani ni matukio mbalimbali kuhusu utoaji elimu na huduma za ki-vipimo kwa wananchi na wadau, leo Julai 05, 2026.
. Amshukuru Rais Samia kwa kuidhinisha fedha hizo.
Na. OWM -TAMISEMI, Ulanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha huduma za afya msingi kwa kujenga na kukarabati miundombinu ya zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya, ambapo Shilingi Bilioni 1.25 zimetolewa kuboresha utoaji wa huduma katika Hospitali ya Mahenge, wilayani Ulanga.
Prof. Shemdoe amesema hayo Julai 4, 2026, wakati wa muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kukagua na kuhimiza uwajibikaji alipotembelea hospitali ya Mahenge.
Prof. Shemdoe amesisitiza kuwa, Serikali imedhamiria kuendelea kuimarisha sekta ya afya kwa kuwezesha ujenzi wa miundombinu bora itakayorahisisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Prof. Shemdoe amesema fedha hizo zilizoidhinishwa na kutolewa na Mhe. Rais zitatumika kujenga jengo la huduma za dharura, wodi ya wazazi, kliniki ya watoto pamoja na uzio wa hospitali utakaoimarisha usalama wa wananchi wanaofuata huduma na kuimarisha ulinzi wa miundombinu ya hospitali hiyo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogor Iio, Mhe. Adam Malima, amesema uwekezaji huo ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kuhakikisha huduma bora za afya zinawafikia wananchi.
Naye, Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Mhe. Salim Alaudin, amesema uboreshaji wa Hospitali ya Mahenge utawanufaisha wananchi wa Ulanga ambao hapo awali walilazimika kufuata huduma za dharura katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara, hali iliyokuwa ikisababisha adha kubwa kwa wananchi na kusababisha vifo vya baadhi ya wagonjwa.
Katika ziara hiyo, Prof. Shemdoe pia ametembelea, amekagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 11, ukiwepo mradi wa ujenzi wa Daraja la Mbuga linalogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 2.35, ambalo linaunganisha barabara ya Mwaya, Iputi na Luhumbero.
Nikiwa mmoja wa wasichana waliompenda kwa siri, nilijua wazi sina nafasi mbele ya wengine waliokuwa wakijitahidi kwa nguvu kumshawishi. Nilikuwa mwepesi wa maneno, lakini si wa kujiaminia kiasi cha kujitokeza wazi. Nilimpenda kwa moyo wangu wote, lakini kila mara nilijipa moyo kwamba huenda Mungu atanipa nafasi yangu muda ukifika.
Lakini wakati mwingine, kuwa na imani pekee hakutoshi ilifika wakati nikajua kuwa nina kazi ya ziada ya kufanya ili nionekane tofauti na wanawake wengine. Wengine walikuwa na magari, wengine walikuwa warembo wa kutupwa, na wengine walikuwa hata na nafasi kubwa kanisani mimi nilikuwa tu msichana wa kawaida. Hapo ndipo rafiki yangu alinifungua macho. SOMA ZAIDI.
Nikiwa kwenye kibanda cha mbogamboga, nilimwacha pembeni kidogo tu, macho yangu yakiwa kwa nyanya zilizopangwa vizuri. Haikuchukua hata dakika mbili nilipojigeuza, Brian alikuwa ametoweka. Panic ilinishika.
Nilimuita kwa sauti ya juu, nikakimbia huku na kule, nikawauliza watu waliokuwa karibu lakini hakuna aliyeona chochote. Masaa yaligeuka kuwa siku, siku zikawa wiki. Niliripoti polisi, wakachukua maelezo, wakaniambia nisubiri uchunguzi.
Nilizunguka kila kituo cha polisi, nikachapisha picha yake, nikatangaza hadi redioni, lakini kila siku iliisha bila jibu. Mume wangu alianza kunilaumu kwa uzembe. Familia ilianza kunitenga kana kwamba nilikuwa na mkono katika kupotea kwa mwanangu.
Hali ya ndoa ilianza kuyumba, na hata nilipojaribu kuwa na imani, ukweli ni kwamba nilianza kukubali kuwa huenda sitamwona tena Brian. Maisha yangu yalikuwa ya huzuni, machozi, na majuto. Hakukuwa na raha tena. Kila mtoto niliyemuona barabarani alinikumbusha mwanangu aliyepotea. SOMA ZAIDI.
Nilikuwa na ndoto nyingi, lakini zilikuwa zikifeli moja baada ya nyingine. Kila nilijitahidi, ndivyo zilivyokuwa zikiendelea kushindwa.
Nilijaribu kila njia ya kushinda changamoto hizi kutafuta kazi bora, kufanya kazi kwa bidii, kuwa na uhusiano mzuri na familia yangu lakini kila nililofanya lilionekana kuwa na mwishowe wa kushindwa. Wakati mmoja, nilijua kuwa lazima kuna kitu kilichokuwa kikizuia mafanikio yangu.
Nilijua kuwa kuna siri au nguvu fulani ambayo ilikuwa ikifanya niendelee kushindwa. Nilibaki nikijiuliza na kugumu kuelewa sababu ya haya yote.
Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga shilingi milioni 273.6 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme wa jua katika visiwa saba vya Wilaya ya Musoma ikiwemo Nyasaungu, Muroba, Kagongo, Nyamasanje, Rukuba na Iriga, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais, Mhe. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya umeme bila kujali eneo analoishi.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kutatua kero za wananchi katika Jimbo la Musoma Vijijini.
Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa umeme ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo tayari vimefikiwa na huduma hiyo, huku hatua zinazofuata zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyosalia.
Amebainisha kuwa kati ya vitongoji 374 vilivyopo, takribani 100 pekee ndivyo bado havijafikiwa na umeme huku zaidi ya vitongoji 50 vikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme.
Aidha, amesema Serikali imepokea maombi ya Mbunge wa Musoma Vijijini ya kuhakikisha vitongoji vyote ambavyo havina umeme vinafikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2027, akieleza kuwa lengo hilo linaendana na dhamira ya Serikali inayolenga kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.
Sambamba na hilo, Mhe. Salome amesema Wizara ya Nishati imeendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya uzalishaji mali, ikiwemo maeneo ya wachimbaji wa migodi wilayani Musoma Vijijini.
Kuhusu baadhi ya wananchi ambao miundombinu ya umeme imepita karibu na makazi yao lakini hawajaunganishwa na huduma hiyo, amemuelekeza Meneja wa TANESCO Wilaya ya Musoma kuhakikisha wananchi hao wanaunganishiwa umeme.
Katika hatua nyingine, amewahimiza wananchi wa Musoma Vijijini kutumia nishati safi ya kupikia, akibainisha kuwa Serikali imetoa ruzuku ya zaidi ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ili kuyawezesha kupatikana kwa gharama nafuu.
Imeelezwa kuwa Serikali inaendelea na maandalizi ya kuufanya Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, kuwa mfano wa matumizi ya nishati safi kupitia mradi wa usambazaji wa gesi asilia.
Miundombinu hiyo itaunganisha gesi asilia katika majengo ya Wizara, ofisi za Ubalozi, taasisi za Serikali, majengo ya biashara, hoteli, migahawa pamoja na makazi ya eneo la Mtumba.
Hayo yameelezwa na Mjiolojia kutoka Wizara ya Nishati, Nuru Helambili wakati akitoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Helambili amesema mradi huo unalenga kujenga kituo cha kupokelea gesi (Gas receiving terminal) itakayokuwa ikisafirishwa kwa magari maalum kutoka Kituo Mama cha CNG kilichopo Mlimani City, Dar es Salaam.
Amefafanua kuwa mradi huo utahusisha pia ujenzi wa kituo cha kupunguza mgandamizo wa gesi, mtandao wa usambazaji na kituo cha kujazia gesi asilia kwenye magari.
Helambili ameeleza kuwa katika mwaka 2026/2027 Serikali itakamilisha tathmini ya athari kwa mazingira na jamii na kuanza taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo, huku Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) likitenga shilingi bilioni 14.40 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli hizo.
• Akagua miradi ya maendeleo, ahimiza ikamilike kwa wakati.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu, amewaletea wananchi wa Mlimba kiasi cha Shilingi Bilioni 1.2 za kitanzania kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili za msingi zitakazoongeza fursa za elimu na kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.
Prof. Shemdoe amesema hayo Julai 3, 2026 katika Uwanja wa Tandare, Kata ya Igima, wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi hao, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji wa watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba.
"Leo nimekuja na habari njema kutoka kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaletea Shilingi
Bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa Shule za Msingi Mgeta na Nganyangira. Nimejiridhisha kuwa fedha hizo tayari zimeingizwa kwenye akaunti ya halmashauri ili utekelezaji uanze mara moja," ameeleza Prof. Shemdoe.
Katika ziara hiyo, Prof. Shemdoe amezindua mabasi mawili ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, amefungua Shule ya Msingi Ngajengwa na kukabidhi vipaza sauti kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii ili kuimarisha utoaji wa elimu kwa wananchi katika maeneo yao.
Aidha, Prof. Shemdoe amekagua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba saba za watumishi, kukagua ujenzi wa wodi mbili za upasuaji katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, pamoja na kutembelea barabara inayojengwa ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikisababisha usumbufu kwa wananchi.
"Nimetembelea daraja kubwa linalojengwa katika Kata ya Mgeta ambalo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Shilingi Bilioni 1.7 kwa ajili ya ujenzi wake. Vilevile, kuna daraja lingine limepatiwa
Shilingi Bilioni 1.7. Huu ni uwekezaji mkubwa unaoonyesha dhamira ya Mhe. Rais ya kuwaletea wananchi maendeleo," amesema Prof. Shemdoe.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima amesema Wilaya ya Mlimba ndiyo kinara wa uzalishaji katika mkoa huo, huku akibainisha kuwa mapato ya halmashauri hiyo yanaendelea kuongezeka kwa kasi kuliko halmashauri nyingine kutokana na kuimarika kwa shughuli za uzalishaji na ukusanyaji wa mapato.
Naye, Mbunge wa Jimbo la Mlimba, Mhe. Dkt. Kellenrose Rwakatare amesema Serikali inaendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kujenga na kuimarisha miundombinu ya shule, ikiwemo kukamilisha majengo yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi, hatua inayochangia kuwapatia wanafunzi mazingira bora ya kujifunzia.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeelekeza kuwa wananchi wote ambao wamepitiwa na miundombinu ya umeme lakini bado hawajaunganishiwa huduma hiyo waunganishiwe kwa gharama ya Shilingi 27,000 tu.
Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Julai 3, 2026, katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Butiama, mkoani Mara, katika ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Mwigulu Nchemba.
Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Salome amemuelekeza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara pamoja na Meneja wa TANESCO Wilaya ya Butiama kubaini maeneo yote ambayo nyaya za umeme zimepita juu ya kaya za wananchi lakini bado hawajaunganishwa na huduma husika ili hatua stahiki zichukuliwe, ikiwemo kufunga transfoma katika maeneo yenye uhitaji.
Amesisitiza kuwa umeme ni nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi, akieleza kuwa unachochea ukuaji wa uchumi, huboresha huduma za afya na kuinua ustawi wa wananchi, hivyo Serikali itaendelea kuhakikisha wananchi wote wanaostahili wanafikiwa na huduma hiyo.
Aidha, amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga zaidi ya Shilingi bilioni 38 kwa ajili ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini katika Mkoa wa Mara. Fedha hizo zitawezesha kuendelea kusambaza umeme katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Ameongeza kuwa, kufuatia maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali itahakikisha vitongoji 51 ambavyo havina umeme mkoani Mara vinafikiwa na nishati hiyo.
Kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, Mhe.Salome amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Amesema katika Mkoa wa Mara tayari Serikali imesambaza majiko ya gesi zaidi ya 19,000 na majiko banifu zaidi ya 8,000 ili kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kulinda afya za wananchi na kuhifadhi mazingira.
Katika mkutano huo wa hadhara, wananchi waliwasilisha jumla ya kero sita, ambapo kero tatu zilipatiwa ufumbuzi papo hapo, huku hatua za kushughulikia kero zilizobaki zikiendelea kuchukuliwa na Serikali.



















































