Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mha. Felchesmi Mramba, amefanya mazungumzo na wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kuhusu fursa za kuendeleza miradi ya jotoardhi na kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini Tanzania.

Mazungumzo hayo yamefanyika pembeni mwa Mkutano wa Dunia wa Jotoardhi (World Geothermal Congress – WGC 2026)  nchini Canada, ambapo Mha. Mramba alikutana na Bw. Yvan Champagne, Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Hewa Ukaa wa Kampuni ya CarbonAI. 

Katika kikao hicho viongozi hao wamejadiliana namna ya kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia pamoja na upatikanaji wa fedha kupitia mfumo wa hewa ukaa (carbon financing) kwa ajili ya kufadhili miradi hiyo.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mha. Mramba ameikaribisha CarbonAI kushirikiana na Serikali katika kutekeleza ajenda ya nishati safi ya kupikia na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

 Amesema Serikali ipo tayari kushirikiana na taasisi na kampuni zenye teknolojia na uzoefu utakaosaidia kufikiwa kwa malengo ya maendeleo endelevu katika sekta ya nishati.

Aidha, Mha. Mramba amefanya mazungumzo na wadau mbalimbali wa nishati jadidifu, hususan katika eneo la jotoardhi, kuhusu fursa za kuharakisha maendeleo ya miradi ya rasilimali hiyo nchini.

 Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuweka msisitizo mkubwa katika matumizi ya nishati jadidifu kama sehemu ya mkakati wa kuhakikisha asilimia 75 ya umeme nchini inazalishwa kutoka katika vyanzo vya nishati jadidifu ifikapo mwaka 2030.

Mkutano wa Dunia wa Jotoardhi (WGC 2026) umewakutanisha viongozi wa Serikali, Wataalam, wawekezaji na wadau wa Sekta ya Nishati kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa lengo la kujadili maendeleo ya teknolojia, sera na uwekezaji katika miradi ya jotoardhi.






 Na Hassan Kimweri, WAF – Tabora.

Jumla ya macho 996 yamefanyiwa uchunguzi kwa wagonjwa 823 wanaotarajiwa kufanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho katika kambi maalum ya madaktari bigwa iliyowekwa na Serikali kwa kushirikiana na Taasisi ya 'Helen Keller International' na wadau wengine wa sekta ya afya.  

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe. Elizabeth Rwegasila amesema hayo leo wakati wa ufunguzi wa kambi ya madaktari bingwa wa macho iliyowekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha afya ya macho na kuondoa tatizo la upofu kwa wananchi. 

"Idadi hii inaonesha ukubwa wa mahitaji ya huduma za macho kwa wananchi wa eneo hili, wanaonufaika na huduma hiyo wanapatiwa huduma mbalimbali muhimu ikiwemo usafiri kutoka majumbani mwao, malazi, chakula pamoja na huduma za matibabu kabla na baada ya upasuaji," amesema Mhe. Rwegasila

Aidha, amelishukuru Shirika la Helen Keller International kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za afya ya macho, akieleza kuwa mbali na kutoa huduma za matibabu, shirika hilo limechangia kuwajengea uwezo wataalamu wa afya ili kuendeleza huduma hizo hata baada ya mradi kukamilika.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wizara ya Afya Dkt. Greater Mande amesema mtoto wa jicho ni miongoni mwa sababu zinazosababisha upofu kwa wananchi wengi, kupitia kambi hiyo wagonjwa wengi wamepata fursa ya kurejeshewa uwezo wao wa kuona na kuendelea na shughuli zao za kila siku.

Pia, Dkt. Mande amewahimiza wananchi watakaonufaika na huduma hizo kuwa mabalozi kwa jamii zao kwa kutoa taarifa kwa watu wengine wenye changamoto za macho ili waweze kujitokeza kupata matibabu wanapopata fursa hiyo.

Nae, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Boniface Marwa amesema wataendelea kushirikiana na wadau ili huduma hiyo ya upasuaji na mtoto wa jicho inakua endelevu na wananchi waendelee kupata huduma hizo pamoja na kuwashukuru Helen Keller kwa kuwasimesha wataalam wa eneo hilo. 

Sambamba na hilo, Mkurugenzi wa Shirika ka Helen Keller International Dkt. Geogle kabona amesema msaada huo utaendelea kutolewa pamoja na kutoa huduma ya mafunzo kwa wataalamu wa eneo hilo pamoja na kutolewa kwa elimu ili jamii ipate uelewa huo. 

"Tutaendelea kushirikiana na Serikali katika juhudi za kupunguza upofu unaozuilika na kuhakikisha wananchi wengiz zaidi wanaoata huduma bira za afya ya macho," amesema Dkt. Kabona.






 Serikali imeendelea kuweka msukumo mkubwa katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi na mbadala nchini, hususan umeme na gesi asilia, katika sekta ya usafiri na matumizi ya majumbani, kupitia mapendekezo mapya ya hatua za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/27.


Akiwasilisha mapendekezo ya Serikali ya makadirio ya mapato na matumizi Bungeni, Waziri wa Fedha,Balozi Dkt Khamis Mussa Omar, amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kifedha na kodi zinazolenga kupunguza gharama za uwekezaji na kuongeza matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira.

Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, Serikali imeendelea kutoa msamaha wa ushuru wa bidhaa kwa magari yanayotumia umeme na gesi asilia kwa kuzingatia ukubwa wa injini, sambamba na msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) inayotumika kwenye magari.

Aidha, Serikali imeondoa VAT kwenye vifaa vinavyotumika katika miundombinu ya gesi asilia (CNG), ikiwemo compressors, vifaa vya kupimia, mitambo ya kuhifadhi gesi, magari maalum ya usafirishaji na pampu za kujazia gesi. Hatua hiyo pia inahusisha msamaha wa kodi katika mnyororo mzima wa uzalishaji wa CNG pamoja na vifaa vinavyotumika kubadili magari kutoka mafuta ya petroli kwenda kwenye gesi au umeme.

Katika sekta ya uzalishaji wa ndani, Serikali imeweka pia msamaha wa VAT kwenye malighafi zinazotumika kutengeneza mitungi ya gesi kwa matumizi ya majumbani na magari, pamoja na kutoa unafuu wa ushuru wa forodha kwa waunganishaji na wazalishaji wa vyombo vya moto vinavyotumia nishati safi nchini chini ya kanuni za Jumuiya ya Afrika Mashariki za mwaka 2025.

Kwa mwaka wa fedha 2026/27, Serikali inapendekeza hatua zaidi ikiwemo msamaha wa VAT kwa vifaa vya vituo vya kuchaji magari ya umeme (EV charging stations), pamoja na kupunguza ushuru wa forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 kwa magari yanayotumia umeme.

Pia, Serikali imependekeza msamaha wa VAT kwa mita janja za gesi ya kupikia (LPG smart meters) zitakazoingizwa nchini na kusambazwa na wasambazaji wa gesi pekee, sambamba na majadiliano ya kutoa unafuu wa kodi kwa waunganishaji wa magari ya umeme nchini ili kuchochea uzalishaji wa ndani.

Hatua hizo Serikali inasema, zinalenga kupunguza gharama za matumizi ya nishati safi, kuvutia uwekezaji katika sekta ya nishati mbadala, kuimarisha viwanda vya ndani, na hatimaye kulinda mazingira kupitia upunguzaji wa matumizi ya mafuta ya kisukuku.

Kwa ujumla, mkakati huu unaonekana kuwa sehemu ya mpango mpana wa Serikali wa kuhamia kwenye uchumi wa kijani unaotegemea nishati safi na endelevu nchini.

Kwa miezi 18 maisha yangu yalizunguka jambo moja tu kutafuta kazi. Kila asubuhi nilikuwa naamka mapema, kufungua simu au laptop yangu, na kutafuta matangazo mapya ya ajira.

Nilikuwa na ndoto ya kupata kazi nje ya nchi ili niweze kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Niliamini elimu na uzoefu wangu vingefungua milango mingi. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Nilituma CV kwa kampuni nyingi sana. Kila nilipoona tangazo jipya, nilihakikisha nimetuma maombi yangu kwa wakati. Wakati mwingine nilikuwa natumia saa nyingi kurekebisha CV na cover letter ili ziendane na nafasi husika.

Kilichoniumiza zaidi ni kutopata majibu. Wiki zikageuka miezi. Nilikuwa naangalia email kila siku nikitarajia mwaliko wa interview, lakini hakuna kilichokuwa kinatokea. Wakati mwingine nilipokea ujumbe wa kukataliwa, na mara nyingi sikupata jibu lolote.

Kwa kweli nilianza kukata tamaa. Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na tatizo kwenye qualifications zangu au kama ndoto yangu ilikuwa kubwa sana. Watu wengine walinishauri niache kufikiria kazi za nje na nijikite kwenye nafasi za karibu.SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa nimekata tamaa kabisa kuhusu mapenzi. Nilikuwa nimepitia mahusiano mengi yaliyoniacha nikiwa na maumivu makubwa.

Kila mara nilipoanza kumpenda mtu, mwishowe mambo yalikuwa yanaishia kuvunjika moyo. Nilianza kuamini labda mapenzi ya kweli hayakunihusu tena. Kwa kweli iliniumiza sana.

Nilikuwa nimejenga ukuta wa kujilinda. Sikutaka tena kuumizwa, na nilianza kuwa na hofu ya kuingia kwenye uhusiano mpya. Wakati mwingine hata nilipoona watu wakiwa na furaha kwenye mahusiano yao, nilihisi kama mimi niko tofauti.

Kulikuwa na siku nilijihisi mpweke sana. Nilianza kujitenga, nikapunguza kutoka, na hata kuacha kuamini kwamba ningepata mtu ambaye angenipenda kweli. Nilianza kufikiria labda niishie peke yangu tu.SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi biashara yangu ilikuwa karibu kuanguka kabisa. 

Nilikuwa nimeanzisha duka langu kwa juhudi nyingi sana. Nilijinyima mambo mengi ili nipate mtaji, nikajituma kuhakikisha biashara inakua.

Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri wateja walikuwa wanakuja, mauzo yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Nilianza kugundua pesa hazilingani. Kila nilipofanya hesabu za mwisho wa siku, kulikuwa na upungufu ambao sikuuelewa. Mwanzoni nilidhani labda ni makosa ya kawaida ya biashara. Lakini kadri wiki zilivyopita, hasara ilianza kuongezeka kwa namna iliyonipa hofu kubwa.

Kwa kweli nilichanganyikiwa. Niliongeza umakini kwenye stock na mauzo, lakini bado mambo hayakuwa yanaeleweka. Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara niliyokuwa nimeijenga kwa shida ikianza kudorora mbele ya macho yangu.

Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilianza kujiuliza kama nilikuwa nafanya kitu vibaya au kama kulikuwa na mtu aliyekuwa anaharibu biashara yangu kwa siri. Wakati mwingine nilifikiria hata kufunga duka kabla sijapoteza kila kitu. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi ndoa yangu ilikuwa karibu kuvunjika kabisa. 

Mwanzoni mume wangu alikuwa mtu wa furaha, mwenye kujali familia, na aliyekuwa karibu sana nasi. Lakini polepole mambo yakaanza kubadilika.

Kile kilichoanza kama kunywa mara moja moja kiligeuka tabia ya kila siku. Kwa kweli hali iliniumiza sana. 

Alianza kurudi nyumbani usiku sana, wakati mwingine akiwa amelewa kiasi cha kutoweza hata kuzungumza vizuri. Migogoro nyumbani ikaongezeka.

Watoto walikuwa wanaanza kumuogopa, na amani ya familia yetu ikaanza kupotea. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtu niliyemjua akibadilika mbele ya macho yangu.

Kulikuwa na siku hakutokea nyumbani kabisa, na nilikesha nikijiuliza maisha yetu yalikuwa yanaelekea wapi. Wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa nimebaki peke yangu kubeba kila jukumu la familia.

Nilijaribu kuzungumza naye mara nyingi. Mwanzoni aliahidi kubadilika, lakini baada ya muda alirudi kwenye tabia ile ile. Polepole nilianza kupoteza matumaini ya kuona ndoa yetu ikiimarika tena.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa naishi maisha ya kutafuta kazi kila siku bila mafanikio ya maana. Baada ya kumaliza masomo, nilikuwa na matumaini makubwa kwamba ningepata kazi nzuri haraka.

Nilikuwa na ndoto ya kusaidia familia yangu, kujitegemea, na kuishi maisha bora. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Nilianza kutuma applications kila mahali.

Mara nyingine nilikuwa nikiitwa interviews, lakini mwisho wa siku sikupata nafasi. Wakati mwingine hata sikupigiwa simu kabisa. Miezi iligeuka miaka, na nilijikuta nikifanya vibarua vya hapa na pale ili kujisitiri.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu niliomaliza nao shule wakisonga mbele huku mimi nikihangaika. Wakati mwingine nilianza kujiuliza kama nilikuwa nimekosea njia maishani.

Kulikuwa na siku nilikosa hata matumaini. Pressure ya familia, bills, na maisha kwa ujumla vilianza kunizidi. Watu wengine walikuwa wakiniambia labda sikuwa na connections za kupata kazi nzuri.SOMA ZAIDI.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali imesisitiza umuhimu wa kuimarisha elimu, utafiti na ubunifu kama nguzo muhimu za kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayolenga kujenga uchumi wa kisasa unaotegemea maarifa, teknolojia na ushindani wa kimataifa.

 


📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme

📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme kupitia LUKU


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limezindua mradi wa vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme pamoja na Mpango wa Ukopeshaji wa Majiko ya Umeme kwa Wateja (On-Bill Financing – OBF), hatua inayofungua ukurasa mpya wa matumizi ya umeme nchini na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya nishati safi.

Akizindua miradi hiyo jijini Dodoma, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb) leo tarehe 11 Juni, 2026 alisema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Tanzania kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya matumizi ya nishati safi duniani huku ikilenga kuboresha maisha ya wananchi na kukuza uchumi.

“Hatua hii inapanua matumizi ya umeme kutoka kupikia hadi usafiri, kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi, kupunguza gharama za maisha na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa,” alisema Mhe. Ndejembi.

Alisema Serikali imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya nishati, hali iliyowezesha uzalishaji wa umeme nchini kufikia zaidi ya megawati 4,000 na kuweka msingi wa matumizi mapana ya umeme katika sekta mbalimbali za uchumi.

Katika kuimarisha matumizi ya vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme, TANESCO kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) imepokea mashine 50 za kisasa za kuchajia vyombo hivyo kutoka kampuni ya AUTEL ya China. Mashine hizo zitafungwa katika maeneo mbalimbali ya kimkakati nchini ili kurahisisha huduma za uchaji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, alisema Shirika limejipanga kuongoza mageuzi ya matumizi ya umeme nchini kwa kutumia fursa ya upatikanaji wa umeme wa kutosha.

“Mtazamo wa awali kwamba umeme ni ghali na matumizi yake yanaishia kwenye mwanga pekee umebadilika kwa kiasi kikubwa. Leo, wananchi wengi wanatumia umeme katika kupikia na shughuli mbalimbali za kiuchumi, huku hatua ya kuzindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme ikifungua ukurasa mpya wa matumizi ya nishati safi nchini,” alisema Bw. Twange.

Kwa upande wa nishati safi ya kupikia, TANESCO imeanza kutekeleza Mpango wa On-Bill Financing (OBF) utakaowezesha wateja kupata majiko ya umeme kwa mkopo na kufanya marejesho kupitia manunuzi yao ya kawaida ya umeme wa LUKU.

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, ameipongeza TANESCO kwa hatua hiyo na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini.

“Nawapongeza TANESCO kwa hatua hii ya kimkakati inayofungua fursa mpya za matumizi ya nishati safi nchini. Ni muhimu kuendelea kuhamasisha wananchi kutumia nishati safi katika usafiri na kupikia ili kuharakisha maendeleo na kuhifadhi mazingira,” alisema Senyamule.

Uzinduzi wa miradi hiyo unaashiria hatua mpya ya kupanua matumizi ya umeme nchini kutoka matumizi ya kawaida ya majumbani hadi sekta za usafiri, kupikia na shughuli za uzalishaji mali, sambamba na juhudi za Taifa kuelekea uchumi wa kijani na maendeleo endelevu.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwa kushirikiana na Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa (ILO) limezindua Kituo cha Msaada kwa Wafanyakazi Wahamiaji Tanzania (TUCTA-MWRC) kwa lengo la kuwapatia taarifa, ushauri na msaada wafanyakazi wanaotafuta ajira ndani na nje ya nchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo amewasilisha Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27 akisisitiza vipaumbele vitano vya utekelezaji wake.

Akitaja vipaumbele hivyo, amesema mosi ni kuimarisha utawala bora, demokrasia, amani, na utulivu na pili ni kujenga uchumi imara, jumuishi na shindani na kipaumbele cha tatu ni, kuimarisha uwezo wa watu na maendeleo ya jamii.

Akiendelea kufafanua vipambele hivyo, Mhe. Waziri amesema kipaumbele cha nne ni kuimarisha uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu kwa mabadiliko ya tabianchi na cha tano kikiwa kusimamia utekelezaji wa vichocheo vya mageuzi ambavyo ni pamoja na nishati, miundombinu ya usafiri na usafirishaji, utafiti na maendeleo, na mageuzi ya kidigitali.

Prof Kitila amesesema utekelezaji wa vipaumbele hivyo ni hatua za kuyatekeleza malengo makuu ya Dira 2050, na vimezingatia Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/27 – 2030/31 wenye dhima ya “Mageuzi kwa ajili ya Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uzalishaji Ajira” ambao ni wa kwanza katika utekelezaji wa Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/27 – 2050/51.

Aidha katika kutekeleza maeneo ya vipaumbele hivyo, Serikali imepanga kuanza kutekeleza programu na miradi mbalimbali ikiwemo miradi shikizi 38 kati ya 51 iliyopo katika programu saba (7) za kielelezo zilizoainishwa katika Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.





MAGAVANA wa Benki Kuu za nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wamekutana jijini Dar es Salaam kujadili mikakati ya kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazoendelea kujitokeza duniani, huku migogoro ya kimataifa na mfumuko wa bei vikitajwa kuwa miongoni mwa vihatarishi vikubwa vya ukuaji wa uchumi wa ukanda huo.


Na Ashura Mohamed, ARUSHA

Naibu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalam kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha IAA, Dkt. Grace Temba, amezindua na kuweka msingi wa maandalizi ya kongamano la kimataifa la utalii linalotarajiwa kufanyika tarehe 25 Septemba, 2026 mkoani Arusha.

Tukio hilo la kongamano ni muhimu kwa taasisi hiyo na maalum kwa wadau wa utalii kutoka maeneo mbali mbali duniani likilenga wadau wa sekta ya utalii kwa dhima kubwa ya kuhamasisha utalii wa ndani ili kuendelea kuhamasisha idadi ya watalii kuongezeka.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo Dkt. Grace amesema kuwa lengo hasa ni kuhakikisha wadau mbali mbali wanashiriki na kufanya kongamano hilo kujumlisha watunga sera, wadau wa utalii kutoka ndani na nje ya nchi kujiandaa na kushiriki kwa ufanisi zaidi.

“Siku ya kongamano tunawaweka pamoja wadau mbali mbali tunatoa taarifa mbali mbali za utafiti zilizofanywa na wadau mbali mbali waliopo katika sekta ya utalii lakini pia Chuo cha Uhasibu Arusha, watunga sera wa taasisi na mlaji ili kuja na suluhisho na maboresho makubwa katika sekta ya utalii kwa lengo la kunufaisha pande zote,” alisema Dkt. Grace.

Aidha amesema kuwa kongamano hilo la nne linatarajiwa kuendelea kukuza na kutangaza nchi kimataifa kwa kuja na mawasilisho ambayo yatalenga wadau na watoa huduma kuendelea kujikuza kimasoko, miundombinu, na kuifanya sekta hiyo kuwa bobezi na kuchangia pato la taifa.

Nae Kaimu Mkuu wa Kitivo cha Biashara na Sayansi ya Jamii kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha IAA, Bi. Lorna Boniface Mwijarubi, amesema kuwa chuo hicho kinatarajia kushirikiana na taasisi mbali mbali na wadau wa utalii katika kuonyesha tafiti na bunifu ambazo zitaisaidia sekta ya utalii kuwa bora zaidi na kuendelea kuliingizia taifa kipato.

Amesema kuwa mafanikio yaliyopatikana kutokana na makongamano yaliyopita ni makubwa kwa kuwa yamekijengea chuo mashirikiano na wadau ambayo huwezesha wanafunzi wa kozi ya utalii na ukarimu kupata fursa ya kujifunza kwa vitendo katika maeneo mbali mbali nchini na kusaidia kupata ajira pamoja na taifa kupata mapato kupitia sekta hiyo.

Chuo cha Uhasibu Arusha IAA kimeendelea kuwa maarufu katika sekta mbali mbali kwa kutoa elimu bora yenye ushindani sokoni huku katika sekta ya utalii inatajwa kuwa ndio chuo pekee kinachotoa kozi ya utalii na ukarimu nchini ambayo inatajwa kuwa na mchango mkubwa katika kutangaza nchi na kuendelea kuifanya sekta hiyo kuwa bora zaidi nchini.











Kwa miaka mingi, nilijivunia biashara yangu.

Nilikuwa nimeijenga kwa juhudi kubwa na nilikuwa na imani kubwa kwa wafanyakazi wangu. Tulikuwa kama familia, na sikuwahi kufikiria kwamba mtu ambaye nilimwamini angeweza kuwa chanzo cha matatizo yaliyokuwa yananikabili. Tatizo lilianza polepole.

Kila mwisho wa wiki nilipokagua hesabu za biashara, niligundua kulikuwa na upungufu wa fedha. Mwanzoni nilidhani ni makosa ya kawaida ya mahesabu au matumizi ambayo hayakuwa yameandikwa vizuri. Lakini hali iliendelea kujirudia.

Wiki moja ikageuka mwezi, na miezi ikazidi kwenda. Kiasi cha fedha kilichokuwa kinapotea kilianza kuongezeka. 

Nilianza kupata wasiwasi kwa sababu biashara yangu ilikuwa ikipata hasara ambayo sikuweza kuieleza. Kwa kweli nilichanganyikiwa sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa siwezi kumshuku mtu yeyote. Wafanyakazi wote walionekana waaminifu na walikuwa wamefanya kazi nami kwa muda mrefu.
Nilianza kufuatilia kila kitu kwa karibu zaidi.

Nilikagua stakabadhi, mauzo, na matumizi ya kila siku. Hata hivyo, sikuweza kupata jibu la wazi kuhusu chanzo cha upotevu wa fedha.
Kadri muda ulivyopita, hasara ilizidi kuongezeka.

Kulikuwa na wakati nilifikiria kufunga biashara kwa sababu sikuona namna ya kuzuia hali ile.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, ndoto yangu kubwa ilikuwa kubeba mtoto wangu mikononi mwangu.

Nilipoolewa, niliamini kwamba baada ya muda mfupi ningekuwa mama. Nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu maisha yangu ya baadaye na familia niliyotamani kuijenga.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Mwezi mmoja ulipita, kisha mwingine. Baadaye mwaka mmoja ukapita bila kupata ujauzito. 

Kadri muda ulivyoendelea kwenda, wasiwasi ulianza kuingia moyoni mwangu. Nilitafuta ushauri wa kitabibu na kufanya vipimo mbalimbali.

Baadhi ya majibu niliyopata yalikuwa magumu kuyakubali. Niliambiwa kwamba kupata mtoto kungeweza kuwa changamoto kubwa kwangu na kwamba huenda ningehitaji uvumilivu mkubwa kuliko nilivyokuwa nikifikiria. Kwa kweli nilivunjika moyo.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wakipata watoto kwa urahisi huku mimi nikiendelea kusubiri. Kila nilipoalikwa kwenye sherehe za watoto au kuona familia mpya zikifurahia watoto wao, nilihisi maumivu makubwa moyoni. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na wakati niliamini kwamba mapenzi hayakuwa sehemu ya maisha yangu. Kwa miaka mingi, nilijaribu kujenga mahusiano ya kweli, lakini kila nilipofikiria nimepata mtu sahihi, mambo yaliishia tofauti. 

Nilivunjwa moyo mara kadhaa na hali ile iliniacha na maumivu makubwa ambayo sikutarajia.

Mwanzoni nilikuwa na matumaini. Kila nilipoanza uhusiano mpya, niliamini kwamba safari hii mambo yangekuwa tofauti. Lakini mara nyingi ndoto zangu ziliishia kuvunjika na kuniacha nikianza upya. Kadri miaka ilivyopita, nilianza kuchoka.

Niliona marafiki zangu wakifunga ndoa na kujenga familia zao huku mimi nikiendelea kuzunguka kwenye maumivu yale yale. 

Wakati mwingine nilijaribu kujifanya sina shida, lakini moyoni nilitamani kupata mtu ambaye angenipenda kwa dhati. Kwa kweli nilikata tamaa.

Nilifikia hatua ya kuamua kujikita kwenye kazi na maisha yangu binafsi. Nilijiambia kwamba huenda siku yangu ya kupata mwenza wa maisha isingewahi kufika. Lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mitatu, maisha yangu yalizunguka jambo moja tu. Kutafuta kazi. Kila asubuhi niliamka nikiwa na matumaini mapya. 

Nilifungua simu yangu na kutafuta matangazo ya kazi, nikatuma maombi, na kusubiri majibu ambayo mara nyingi hayakuwahi kufika.

Mwanzoni nilikuwa na matumaini makubwa.

Nilijiamini kuwa elimu yangu na uzoefu wangu vingekuwa vya kutosha kunisaidia kupata nafasi nzuri. Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kuona hali ikiwa tofauti na nilivyotarajia.
Miezi iligeuka miaka.

Nilituma maombi kwa kampuni nyingi sana. Wakati mwingine niliitwa kwa mahojiano lakini sikuchaguliwa. Mara nyingi sikupata hata majibu ya maombi niliyotuma. 

Kwa kweli hali ile ilinivunja moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona marafiki zangu wakipata kazi na kuendelea na maisha yao huku mimi nikiendelea kusubiri nafasi yangu.

Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na kitu nilichokuwa nakosea. Kadri miaka ilivyopita, confidence yangu ilianza kupungua. 

Kulikuwa na nyakati nilitaka kuacha kutuma maombi kabisa. Nilihisi kama kila juhudi niliyokuwa nikifanya hazikuwa na matokeo yoyote. Lakini sikuwa tayari kukata tamaa. SOMA ZAIDI.

Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo simu ikilia nilikuwa naogopa kuipokea.

Sababu ilikuwa moja tu. Nilikuwa na deni kubwa ambalo nilikuwa nimeshindwa kulilipa kwa muda mrefu.

Kila mwezi nilijitahidi kutafuta fedha za kulipa sehemu ya deni hilo, lakini mahitaji mengine ya maisha yalifanya hali kuwa ngumu zaidi.

Mwanzoni niliamini ningemaliza kulipa haraka.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyopanga. Biashara yangu ilipata changamoto, mapato yakapungua, na madeni yakaendelea kuongezeka. Kadri muda ulivyopita, presha ilizidi kuwa kubwa. Kwa kweli nilikuwa naishi kwa wasiwasi.

Kila nilipoona ujumbe au simu kutoka kwa wadai, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu. Wakati mwingine nilikosa usingizi nikifikiria jinsi nitakavyotoka kwenye hali ile.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa mtu mwenye bidii. Sikupenda kukwepa majukumu yangu, lakini nilijikuta katika hali ambayo sikuwa na uwezo wa kufanya kila kitu kwa wakati mmoja.

Miaka ilipita huku nikihangaika. Kulikuwa na nyakati nilikata tamaa na kuanza kuamini kwamba ningebeba mzigo wa deni hilo maisha yangu yote. Lakini moyoni bado nilikuwa na matumaini kwamba siku moja hali ingebadilika. SOMA ZAIDI.

 


Na; Mwandishi wetu – Chato


Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Louis Peter Bura Amepongeza Programu ya kuendeeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu kwa Uratibu wa Kituo cha kuendeleza ukuzaji Viumbemaji Rubambagwe Kilichopo wilayani Chato Mkoani Geita kinachosimamiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Ametoa Pongezi hizo Tarehe 10 Juni 2026 Wilayani Chato alipofanya ziara maalum ya kutembelea kituo hicho akiwa pamoja na timu ya wataalam waliokutana katika Wilaya hiyo wakiwa katika kazi maalum ya kufanya mapitio ya mpangokazi wa Program hiyo.



Mkuu wa Wilaya Bura, alisema kuwa Wilaya yake inawajibu wa kutoa elimu kwa wafugaji kupitia kituo cha Rubambagwe hivyo amewaasa wataalam kutoka katika sekta zinazotekeleza mradi kufanya kazi kwa ushirikianao na Wilaya hiyo, ili kuweza kuleta matokeo chanya katika uchumi wa Wilaya na Taifa kwa Ujumla na Kuongeza mnyororo wa thamani.


“Tutakuwa tunazalisha vifaranga vya samaki pale, haitatosha hiyo pia tutakuwa tunazalisha vyakula vya samaki, na hayo yote yamenipa mimi wakati mzuri na sababu ya kujifunza haya yote, na tunashukuru mradi huu kwenda kwa kasi na ni wakati sasa wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja . “Alibanisha

Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza ushirikishwaji mzuri baina ya sekta zinazotekeleza Programu hiyo nchini pamoja na Wilaya husika.’katika dhana nzima ya ushirikishwaji kuna mambo mengi ambayo Wilaya inaweza kuyasimamia na kuyatekeleza kwa ukaribu zaidi, hapa Chato wananchi wanajihusisha Zaidi na uuzaji wa samaki tuna soko kubwa la samaki hapa linaitwa Chato beach, wananchi wanapata chakula na pia wanauza sehemu nyingine nje ya Chato.’ Alifafanua.


Kwa upande wake Mratibu wa Programu Hiyo kutoka Ofisi ya waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Bw. Salimu Mwinjaka alisema pamoja na mambo Mengine kwa upande wa bahari kuu, Progamu hiyo inakusudia kujenga  viwanda vya samaki Tanzania Zanzibar katika eneo la Fungurefu na Wilayani Kilwa Mkoani Lindi na  kuweza kukabili hali ya upotevu wa mazao ya samaki baada ya kuvuna kwa kujenga vyumba vya ubaridi vya kuhifadhi mazao ya uvuvi, mitambo wa kuzalisha barafu, vichanja na mahema yakukaushia dagaa au samaki kwa kutumia mionzi ya jua. 


Akiongelea kuhusu ufugaji samaki, Bw. Mwinjaka alisema kupitia progamu hiyo kuna vituo vinne ambavyo vipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambavyo ni Pamoja na vituo vya kuendeleza ukuzaji viumbemaji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani Chato, Mwamapuli Wilayani Igunga, Kingolwira Wilayani Morogoro na kituo cha Ruhila Wilayani Songea.



Akiongea katika ziara hiyo, Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi Mkomanile Mahundi alisema kituo cha Kuendeleza Ukuzaji Viumbemaji Rubambagwe kitakuwa na kazi ya kuzalisha na kusambaza vifaranga bora vya samaki aina ya sato na kambale, pamoja na kutoa mafunzo kwa wakuzaji viumbemaji katika maeneo ya mikoa ya Geita, Mwanza, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Mara.


Aliongeza kusema pia, baada ya kituo kukamilika kitakuwa na uwezo wa kuchakata chakula cha samaki ambapo itapelekea wigo wa kuongeza ajira kwa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum.

“Wizara ya Mifugo na uvuvi kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) itawezesha uwepo wa dirisha maalum katika taasisi za kifedha kama vile Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa kuwawezesha wakuzaji viumbemaji kupata mkopo yenye riba nafuu ya pembejeo na zana za ukuzaji viumbemaji.” Alisem


Ujenzi wa Kituo hicho cha Rubambagwe umefikia Asilimia 85 mpaka sasa ambapo umehusisha Jengo la utawala, karakana, nyumba za wafanyakazi jengo la kitotoleshi cha samaki, ujenzi wa mabwawa ya kufugia samaki, chanzo cha maji yaani tenki maalum la kutunza maji, kuchuja na kusafirisha maji hayo kwenda kwenye mabwawa ya kufugia samaki, kitotoleshi pamoja na maeneo mengine yanayotumia maji kituoni hapo.


                                   xxxxx MWISHO xxxxxxxxx