Tanzania imeandika ukurasa mpya katika historia ya elimu ya ufundi kwa kupeleka walimu 150 wa Amali za Kihandisi nchini India.

Hatua hii kubwa ya kimkakati siyo tu safari ya mafunzo, bali ni uwekezaji wa kitaifa katika mustakabali wa elimu na uchumi wa viwanda, ikilenga kuongeza umahiri wa walimu na kuandaa kizazi cha wataalamu watakaoshindana kimataifa katika nyanja za teknolojia na uhandisi.

Katika hafla ya kuwaaga walimu hao Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesisitiza kuwa mpango wa mafunzo hayo ni utekelezaji wa sera ya elimu ya lazima ya miaka 10, unaolenga kujenga umahiri wa ufundishaji na kuandaa kizazi cha wataalamu wenye ushindani wa kimataifa. Ameeleza kuwa safari ya mageuzi ya elimu inaendelea na haitarudi nyuma, huku akiwataka walimu watambue nafasi yao kama daraja kati ya sera na utekelezaji darasani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe amewataka walimu hao kudumisha nidhamu na maadili, kujifunza kwa bidii na wakirudi wasambaze maarifa kwa wenzao ili kuharakisha mageuzi ya elimu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia walimu hao fursa ya mafunzo, akisisitiza kuwa ni ishara ya dhamira ya dhati ya kuendeleza mageuzi ya elimu, huku akipongeza mshirikiano wa viongozi wa wizara za kisekta katika kulitekeleza kwa ufanisi.

Kamishna wa Elimu Dkt. Lyabwene Mtahabwa ameeleza kuwa mafunzo hayo ya mwezi mmoja yamewahusisha walimu kutoka mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na viongozi wa ngazi ya elimu mkoa kutoka mikoa tisa ili kusimamia kikamilifu uendelevu wa mafunzo warudipo nchini.

Wanufaika wa mafunzo hayo, akiwemo Mwalimu Judith Faustine wa Uhandisi Ujenzi katika Shule ya Sekondari Mwadui Ufundi na Mwalimu Jacob Mwalyego wa fani ya Uashi katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Mbogwe, wameishukuru Serikali kwa kuwapatia nafasi hii ya kipekee. Wamesema ni heshima kubwa na fursa ya kuongeza maarifa yatakayowawezesha kuendeleza mageuzi ya elimu nchini.

 


Na Oscar Assenga, TANGA

BODI ya Wakurugenzi ya Bonde la Pangani leo wamefanya ziara ya kukagua maeneo vyanzo vya maji ikiwemo Bwawa la Mabayani na Mtambo wa Kutibu Maji wa Mowe na kujiridhisha kuhusiana na kazi zinazotelezwa na menejimenti pamoja na wateja wao namna wanavyopokea huduma.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bonde la Pangani,Mhandisi Ruth Koya alisema kwamba bodi hiyo na menejimenti wamefanya ziara hiyo kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa maelekezo na majukumu wanayowalekeza menejimenti kwamba wanayafuatilia na kuyafanya kwa uhakika.



Katika ziara hiyo Bodi hiyo wametembelea Bwawa la mabayani wamejionea shughuli Zinazofanyika ikiwemo utunzwaji wa Bwawa la mabayani pamoja na kumtembelea mteja wao mkubwa Tanga Uwasa wameona yupo vizuri na kazi inafanyika kwa waledi

Alisema kwamba wameona bwawa limewekwa alama na wameipokea taarifa kwamba wananchi nao wanashirikishwa kutokana na uwepo wa jumuiya za watumia maji ambao wamekuwa chachu kubwa kuhakikisha vyanzo hivyo vinalindwa na kutunzwa.

Aidha alitoa wito kwa watumishi na kusisitiza kuwasimamia wadau wao wakiwemo Tanga Uwasa ili kuendelea kutunza chanzo cha maji kikubwa ambacho ni muhimu kwa ajili ya Jiji la Tanga na kushirikiana na wadau Tanga Uwasa na wengineo .

Alisema kwamba lakini wamepata taarifa Tanga Uwasa wanazidi kupanua uzalishaji maji hadi kufikia lita milioni 70 ina maana utunzaji ni nzuri ndio maana wameweza kuwekeza zaidi kupitia hat fungani yao walioipata hivi karibuni.

Awali akizungumza Mkurugenzi wa Bonde la Pangani Segule segule alisema kwamba ziara ya Bodi hiyo ni kutembelea maeneo ya uwandani na kukakgua maeneneo mbalimbali na kujiridhisha kuhusiana na kazi zinazotekelzwa na menejimenti lakini kupata kujua kuhusu wateja wao mbalimbali wanavyopokea huduma zao.

Alisema kwamba bodi imeona ipite kwenye eneo la mnufaika mkubwa wa maji Mto Zigi ambao ni wenzao wa Tanga Uwasa ambapo wametembelea maeneo mbalimbali ambayo Tanga Uwasa wanafaidika nayo wamenza ikiwemo Bwawa la Mabayani ambalo wao ndio wamiliki na yeye ndio mteja wao.

Aidha alisema kwamba wamejionea mazingira yanavyotunzwa na wametumia fursa hiyo kupata maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Tanga Uwasa kuhusiana na mradi wa Hati Funfani ambao unatumia chanzo kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji Tanga .

Alieleza kwamba na ziara ilitoa fursa kwa wajumbe wa bodi,menejimenti kuona mchango wao kama bonde mchango wao kwenye mradi Hatifungani kwamba wakitunza vyanzo vyema wenzao wa Tanga Uwasa wataweza fikia matarajio yao na kwa gharama walizokadiria.

Aliongeza kwamba bwawa hilo wanalitunza na moja walishaanza kuweka alama za mipaka kuainisha mita 500 na kama sheria za usimamizi rasilimali za maji zinaelekeza mita 60 za chanzo lakini wanatoa mamlaka kwa taasisi na wao kama mabonde kuomba nyongeza kwa bwawa la mabayani wamehifadhi mita 500 .

Alieleza kwa sasa hiyo inatoa fursa hata nyongeza za miradi kutokana na mahitaji ya maji wanaweza kuhifadhi hivyo mkakakati wao ni kuendelea kuimraisha baada ya kuweka alama za mipaka katika yale maeneo walioweka mipaka watu wasifanye shughuli za kibinadamu ili kupunguza uchafuzi kwenda kwenye bwawa.

Aliongeza kwamba lakini upande wa juu wa bwawa wanaendelea kuimarisha utunzaji wa jumuiya za watumiaji maji ambao wote wanakuwa watumiaji maji na mkakati wa kuziimarisha huku wenzao Tanga Uwasa wameimarisha utunzaji wa vyanzo vya maji .

Hata hivyo alisema kwamb hali ya vyanzo vya maji ukilinganisha na miaka ya nyuma ni nzuri changamoto zipo lakini hawajafika wakati wa kusema hali iliyopo imehataraisha vyanzo kukauka na kushindwa kuwahudumua watu.

Aliongeza kwamba lazima waendelee kuimarisha na shughuli zinaongezeka kutokana na mahitaji ya ardhi kuna jitihada kubwa za watu kutokana na uhaba wa ardhi na watu wanaongezeka na kutaka kusogelea vyanzo wao wanaendelea kuimarisha jumuiya za watumiaji maji ili kuweza kuhakikisha vyanzo vya maji vilivyopo vinatunzwa na kuvilindwa.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly alisema kwamba ameshiriki katika ziara hiyo ya Bodi ya Bonde la Pangani ambao wanatembelea kuangalia vyanzo vya maji vinavyotunzwa ikiwemo bwawa la mabayani ambalo ndio chanzo kikubwa wanachotumia Tanga Uwasa katika kusambaza maji kinahudumia Tanga, Muheza na Mkinga .

Mhandisi Hilly alisema wameongeza uzalishaji wa maji kuhakikisha wanawafikia vema wananchi ili kutekeleza malengo yao mbalimbali ya nchi ifikapo 2030 watu wote wawe wamepata maji mijini na Tanga Uwasa na wenzao Ruwasa wananchi waweze kupata maji.

Alisema kwa hiyo mahitaji na matumizi ni makubwa wao kwa kushirikiana na Bodi la Bonde la Mto Pangani wanaweka juhudi kubwa katika utunzaji chanzo cha maji kutokana na kuwa wanufaika wakubwa wa bonde hilo.

Alieleza hivyo wana wajibu kuhakikisha chanzo hicho kinalindwa na kutunzwa wanashirikiana kwenye maeneo mbalimbali ya mto,bwawa la mabayani wana mpaka kamati za uhifadhi na utunzaji wa mazingira ikiwemo uwamakizi kuhakikisha vinaendelea kuwa imara.

“Kwa mfano mradi wa hati fungani miongoni mwa fedha zinakwenda kwenye chanzo cha maji na sasa wana mkakati wa kupanda miti laki moja katika maeneo hayo na mpaka sasa wamepanda miti zaidi 50,000”Alisema

Hata hvyo alieleza pia wameendelea na mradi wa hati fungani kuongeza uzalishaji maji huku wakieleza mipango yao ni kuongeza uwezo bwawa tuta eneo la kupita utoro wa maji na kazi za mazingira zitafanyika na hivyyo itawasadia kuwa na uhakika wa usambazaji wa maji hata ikitokea mabadiliko ya tabia ya nchi na wakati wa ukame.

TUME  ya Ushindani (FCC) kupitia Kanda ya Ziwa imeendelea kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kutoa elimu ya ulinzi wa mlaji kupitia Kliniki ya Mlaji inayofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo, Manispaa ya Musoma.

Katika kuimarisha uelewa wa wadau mbalimbali, FCC haikuishia kwa wananchi pekee bali pia ilifanya ziara maalum kwa baadhi ya taasisi zinazotoa huduma ndogo za fedha katika manispaa hiyo, kwa lengo la kuzielimisha juu ya wajibu wao wa kuzingatia sheria na kanuni katika utoaji wa huduma.

Akiongoza zoezi hilo, Mkuu wa Kanda ya Ziwa,Bw. Frank Mdimi, akishirikiana na Afisa Biashara wa Manispaa ya Musoma, Joshua Mlole pamoja na maafisa wengine, walitembelea taasisi za Enokwe, Pongeza na Ohura na kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na watoa huduma hao.

Katika ziara hiyo, maafisa wa FCC wamesisitiza umuhimu wa kuandaa mikataba ya huduma kwa uwazi na haki, wakielekeza taasisi hizo kuzingatia matakwa ya  Sheria ya Ushindani inasimamia na kudhibiti Mikataba ya Mlaji inayoandaliwa na watoa huduma

Watoa huduma kutoka taasisi hizo walionesha utayari mkubwa wa kupokea maelekezo hayo, wakieleza kufurahishwa kwao na hatua ya FCC kuwafuata na kuwapatia elimu kwa vitendo. Wamesisitiza kuwa elimu hiyo itawasaidia kuboresha huduma zao na kujenga uaminifu kwa wateja wao.

Aidha, taasisi hizo zimeahidi kushirikiana kwa karibu na FCC kwa kuhakikisha zinazingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali, pamoja na kudumisha mawasiliano ya mara kwa mara ili kuboresha zaidi sekta ya huduma ndogo za fedha.

Zoezi la utoaji elimu kupitia Kliniki ya Mlaji linaendelea Machi 27, ambapo wananchi wataendelea kupatiwa elimu kuhusu haki zao, wajibu wao na namna bora ya kujilinda wanapotumia huduma mbalimbali sokoni.

Na Emma Kigombe

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Tanga, Mwalimu Joseph Shayo, amewataka wanamichezo wote walioshiriki mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa kuendelea kudumisha nidhamu na kuongeza juhudi katika mazoezi ili kujiimarisha zaidi.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa mashindano hayo ya mkoa, Mwalimu Shayo alisema ni muhimu kwa wanamichezo hao kuendelea kufanya mazoezi kwa bidii ili waweze kuwa katika kiwango bora kitakachowawezesha kufanya vizuri zaidi katika mashindano yajayo.

Alieleza kuwa kambi ya maandalizi kwa wanamichezo waliochaguliwa inatarajiwa kuanza tarehe 25 Mei hadi 5 Juni 2026, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mashindano ya kitaifa ya UMITASHUMTA. Hata hivyo, alibainisha kuwa bado kutakuwa na mchujo zaidi katika ngazi ya mkoa ili kupata timu bora zaidi itakayoiwakilisha Tanga.

“Msibweteke, endeleeni kufanya mazoezi ya kutosha. Tunahitaji timu imara itakayoweza kushindana na kufanya vizuri katika ngazi ya taifa,” alisisitiza.


Kwa upande mwingine, Mwalimu Shayo aliwatia moyo wanamichezo ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na timu ya mkoa, akiwataka kutovunjika moyo bali kuendelea kujituma. Aliwapongeza kwa kufikia hatua ya kushiriki mashindano ya ngazi ya mkoa na kueleza kuwa ushindani ulikuwa mkubwa.



Naye Afisa Michezo Mkoa wa Tanga, Digna Tesha, alisema mashindano hayo yalihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, mpira wa mikono, mpira wa kikapu, mpira wa wavu pamoja na michezo mingine, yakihusisha wavulana, wasichana na makundi maalum.

Alifafanua kuwa jumla ya wanamichezo 1,200 kutoka halmashauri zote 11 za mkoa walishiriki, ambapo kati yao wanamichezo 120 wamechaguliwa kuuwakilisha mkoa wa Tanga katika mashindano ya UMITASHUMTA kitaifa yatakayofanyika mkoani Iringa mwaka 2026.

Aidha, aliwataka wanamichezo hao watakaopata nafasi ya kuiwakilisha Tanga kujituma kwa hali ya juu ili waweze kufanya vizuri na hatimaye kupata nafasi ya kushiriki mashindano ya michezo ya shule za msingi na sekondari kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEASSA), yatakayofanyika mwaka huu mkoani Morogoro.

Alisisitiza kuwa mafanikio katika mashindano hayo yatategemea nidhamu, maandalizi na ushirikiano kati ya wanamichezo na walimu wao.

Mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa yamebebwa na kauli mbiu isemayo “Michezo na Sanaa Shuleni, daraja la Ajira, Afya na Ushindani Kimataifa”

Wananchi wa Wilaya ya Chato mkoani Geita wamepata fursa ya kupata nishati safi ya kupikia kwa urahisi zaidi kufuatia uzinduzi wa duka jipya la kuuza mitungi na majiko ya gesi la kampuni ya Oryx Gas Tanzania.

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Maryprisca Mahundi, ametoa rai ya kuimarishwa kwa uzalendo na utunzaji wa miundombinu ya chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale ili iweze kudumu na kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mdahalo wa maadili na uzalendo uliofanyika chuoni hapo, Mahundi amesema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha anailinda na kuitunza miundombinu ya umma, akisisitiza kuwa maadili na uzalendo ni msingi muhimu wa maendeleo ya Taifa.

“Uzalendo ni hali ya mtu kuipenda nchi yake, kulinda rasilimali za Taifa, kuwajibika na kufanya kazi kwa bidii kwa manufaa ya wote. Bila maadili thabiti, uzalendo wa kweli hauwezi kujengeka,” amesema Mahundi.

Aidha, amewataka vijana na jamii kwa ujumla kujiepusha na vitendo vinavyoharibu maadili na badala yake kuwa mstari wa mbele katika kulinda tunu za Taifa, huku akisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuboresha miundombinu ya taasisi za elimu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilman Ndile, amesema mdahalo huo ni jukwaa muhimu litakalosaidia kujenga uelewa mpana wa masuala ya maadili na uzalendo kwa wanafunzi na wananchi.

Naye Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale, Luciana Mvula , amesema chuo hicho kinaendelea kutekeleza programu za maendeleo ya ujuzi kwa wanafunzi kwa lengo la kuhakikisha kinazalisha wahitimu wenye uwezo wa kujiajiri na kuajirika, sambamba na kuchangia maendeleo ya jamii.

Amesema pamoja na mafanikio yaliyopo, chuo kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya miundombinu, hivyo ameomba kuendelea kupatiwa ushirikiano ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Kwa upande wao, washiriki wa mdahalo huo wamesema mada zilizowasilishwa zimekuwa na manufaa makubwa kwao na zimewajengea uelewa mpana kuhusu maadili na uzalendo, huku wakiahidi kuifikisha elimu hiyo kwa wengine ambao hawakupata fursa ya kushiriki.

“Mada hizi zimeeleweka vizuri na zimetupa mwanga mkubwa, hivyo tutaenda kuwa mabalozi kwa wengine ili kuhakikisha jamii inakuwa na maadili mema na uzalendo kwa Taifa letu,” wamesema baadhi ya washiriki.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 26, 2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam kuhusu kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Akizungumza na wanafunzi hao,Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bi.Techla Kitosi,amesisitiza umuhimu wa watumiaji kuwa na uelewa wa haki zao wanaponunua bidhaa au huduma. Ameeleza kuwa mlaji ana haki ya kupata bidhaa bora, salama na zenye ubora unaokubalika.

Aidha ameonya dhidi ya ununuzi wa bidhaa bandia ambazo zinaweza kuhatarisha afya na usalama wa mtumiaji.

“Ni muhimu sana kwa kila mmoja wenu kujifunza kutambua bidhaa halisi na bandia. Msikubali kudanganywa na bei ndogo bila kuangalia ubora wa bidhaa,” amesema Bi.Kitosi

Kwa upande wake, Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi, Magdalena Hall, ameeleza wajibu wa mlaji kuwa ni pamoja na kusoma maelekezo ya matumizi ya bidhaa, kuhifadhi stakabadhi za manunuzi na kutoa taarifa pale wanapokutana na bidhaa zisizo na viwango.

Hata hivyo Bi.Hall ,amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wa ulinzi wa mlaji katika jamii zao kwa kutoa elimu kwa familia na marafiki kuhusu madhara ya bidhaa bandia.

Wanafunzi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali na kupewa majibu ya kina, jambo lililosaidia kuongeza uelewa wao kuhusu masuala ya ulinzi wa mlaji.

Elimu  hiyo ni sehemu ya jitihada za Tume ya Ushindani kuendelea kutoa elimu kwa umma, hususan vijana, ili kujenga jamii yenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa na huduma.

Mafunzo hayo ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Wanafunzi Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.