Na.Mwandishi Wetu-Geneva
Tanzania imetoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano wa kimataifa ili kuhakikisha maendeleo ya kasi ya Akili Unde (AI) yanasimamiwa kupitia mifumo ya kimataifa iliyo jumuishi, yenye uwazi na usawa, ikitahadharisha kuwa nchi zinazoendelea hazipaswi kuachwa nyuma wakati teknolojia hiyo ikiendelea kubadili uchumi na jamii.
Akizungumza mbele ya zaidi ya wajumbe 190 wanaowakilisha serikali, mashirika ya kimataifa, sekta binafsi na jamii ya teknolojia duniani katika mdahalo wa Kimataifa kuhusu Utawala wa Akili Unde (Global Dialogue on AI Governance), Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki (Mb), aliwasilisha dira ya Tanzania ya kutumia Akili Unde kama kichocheo cha maendeleo ya taifa huku ikiimarisha mifumo ya kuhakikisha matumizi yake yanakuwa ya kuwajibika.
Waziri alisema Tanzania inaichukulia Akili Unde kuwa nguzo muhimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kichocheo muhimu cha uchumi wa kidijitali unaochipukia. Alieleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mageuzi ya kina ya sera na mifumo ya udhibiti ili kuweka mazingira imara yanayochochea ubunifu huku yakilinda haki za wananchi na kujenga imani ya umma.
“Tanzania inaamini kuwa Akili Unde ina uwezo wa kuleta mageuzi katika sekta za kilimo, afya, elimu, huduma za kifedha na utawala wa umma,” alisema Mhe. Kairuki. “Hivyo, matumizi yake yanapaswa kuwa salama, jumuishi na yalenge kuhakikisha wananchi wote wananufaika.”
Alieleza hatua zinazotekelezwa kuimarisha utawala wa Akili Unde, ikiwemo kuandaa mifumo ya udhibiti, kuboresha mifumo ya usimamizi wa data, kuimarisha ulinzi wa faragha na usalama wa mtandao, pamoja na kuandaa miongozo ya kitaifa ya matumizi ya Akili Unde katika sekta za kimkakati kama elimu na afya.
Waziri pia alieleza uwekezaji unaoendelea wa Serikali katika miundombinu ya kidijitali, akitaja upanuzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) pamoja na maendeleo ya Miundombinu ya Umma ya Kidijitali (Digital Public Infrastructure – DPI) kuwa msingi muhimu wa kupanua mawasiliano ya kidijitali na kuwezesha wananchi wengi zaidi kupata huduma zinazotumia Akili Unde nchini kote.
Mbali na mageuzi ya ndani ya nchi, Mhe. Angellah Kairuki alisisitiza kuwa utawala madhubuti wa Akili Unde unahitaji ushirikiano endelevu wa kimataifa.
Alithibitisha dhamira ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana kwa karibu na Umoja wa Kimataifa wa Mawasiliano (ITU), Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Mawasiliano Afrika (ATU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ili kuendeleza mifumo ya kidijitali inayoweza kushirikiana, inayorahisisha ubunifu, biashara na huduma za kuvuka mipaka huku ikilinda mamlaka ya nchi na usalama wa data.
Akihitimisha hotuba yake, Waziri Kairuki alitoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano wa kimataifa katika uhamishaji wa teknolojia, maendeleo ya ujuzi, ushirikiano wa tafiti, ubunifu na uwekezaji katika miundombinu ya kidijitali. Alisisitiza kuwa kuziba pengo la kidijitali kutahitaji hatua za pamoja ili kuhakikisha manufaa ya Akili Unde yanagawanywa kwa usawa kati ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
Mdahalo wa Kimataifa kuhusu Utawala wa Akili Unde unawakutanisha watunga sera, viongozi wa serikali, wataalamu wa teknolojia na wadau wa sekta binafsi kutoka duniani kote kwa lengo la kujenga mifumo ya kimataifa ya utawala wa Akili Unde na kujadili namna teknolojia hiyo inavyoweza kuchangia maendeleo jumuishi na endelevu.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo (MOI) imesema itaendelea kuimarisha tafiti zinazolenga kuzalisha afua za matibabu zinazozingatia mazingira na vinasaba vya Watanzania, ili kuboresha huduma za matibabu ya magonjwa ya mifupa na mfumo wa fahamu.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, Jijini Dar es Salaam Julai 6, 2026, kwenye Maadhimisho ya Miaka 50 ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Amesema mara nyingi tiba zinazotumika hutokana na matokeo ya tafiti zilizofanyika katika nchi zilizoendelea pamoja na baadhi ya nchi za bara la Afrika, ambapo afua hizo zinaweza kuwa zimezingatia watu wenye vinasaba tofauti, hivyo wao wameona umuhimu wa kufanya tafiti zitakazozalisha afua zinazokidhi mazingira ya Tanzania.
Aidha, amesema MOI imetimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake na imeendelea kujikita katika maeneo makuu matatu ambayo ni kutoa huduma kwa wagonjwa wa mifumo ya ubongo na mifupa, kufundisha huduma hizo kwa wananchi na wataalam katika ngazi ya shahada ya kwanza, shahada ya pili na ubobezi, pamoja na kufanya tafiti.
Pia amesema taasisi hiyo imeweza kutoa mafunzo kwa wananchi na wataalam kutoka ndani na nje ya Tanzania, hususan katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati, Kusini na Magharibi, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha huduma za afya katika kanda hiyo.
>Asema kasi ya maendeleo chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amani, uchumi, afya, maji na miundombinu vimemshawishi kubadili msimamo wa kisiasa.
Baada ya zaidi ya miaka 30 ya kuwa mwanasiasa wa upinzani, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe, amefanya uamuzi mkubwa wa kisiasa kwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Jumbe, ambaye kwa muda mrefu alikuwa mmoja wa viongozi mashuhuri wa Chadema mkoani Tanga, amesema uamuzi wake umetokana na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na juhudi za Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha amani, umoja na ustawi wa wananchi.
Akizungumza wakati wa hafla ya kumpokea ndani ya CCM iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, Jumbe alisema hakufanya uamuzi huo kwa papara, bali baada ya kutafakari kwa kina na kujiridhisha kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya taifa.
"Nilikuwa mpinzani kwa zaidi ya miaka 30, lakini leo nimeamua kuhitimisha safari hiyo. Kilichonishawishi zaidi ni kazi kubwa inayofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo na kuhakikisha amani ya nchi inalindwa," alisema.
Alieleza kuwa pia amevutiwa na utekelezaji wa falsafa ya 4R inayosisitiza maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya, akisema imeongeza mshikamano na kuimarisha mazingira ya maendeleo nchini.
Akizungumzia Mkoa wa Tanga, Jumbe alisema mabadiliko yanayoonekana katika sekta mbalimbali ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuufungua mkoa huo kiuchumi.
Alitaja kuongezeka kwa shughuli katika Bandari ya Tanga, ujenzi wa bandari kavu pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati kuwa miongoni mwa hatua zilizochochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za biashara.
"Nimekuwa nikipaza sauti kwa miaka mingi nikitaka Tanga ifunguliwe kiuchumi. Leo naona hilo limefanyika. Mizigo imeongezeka bandarini, bandari kavu zimejengwa na shughuli za biashara zinaendelea kukua," alisema.
Katika sekta ya afya, Jumbe alisema maboresho yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na ujenzi wa zahanati katika kata na mitaa mbalimbali vimempa imani kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma kwa wananchi.
Aidha, alisema upanuzi wa huduma za maji na umeme pamoja na utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni miongoni mwa hatua zinazoonyesha dhamira ya Serikali ya kuinua maisha ya Watanzania.
"Nilijiuliza ni hoja gani itanifanya nibaki upinzani wakati maendeleo yanaonekana wazi. Tanga ina amani, huduma zinaimarika na wananchi wanaendelea kunufaika na miradi ya maendeleo," alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, alisema chama hicho kinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano ili kuongeza uwezo wake wa kusimamia maendeleo na kuwatumikia wananchi.
Alisema tangu alipopewa dhamana ya kuongoza CCM mkoani humo, ameweka mkakati wa kuimarisha chama kupitia ushirikiano na wanachama pamoja na kuwakaribisha viongozi kutoka vyama vingine vya siasa.
Rajab alisema mkakati huo umeendelea kuzaa matunda, akieleza kuwa kujiunga kwa Rashid Jumbe ni ishara ya kuongezeka kwa imani ya baadhi ya viongozi wa upinzani kwa juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali.
"Jumbe alikuwa mmoja wa viongozi wakubwa wa upinzani katika Wilaya ya Tanga. Tuliahidi kwamba tutamshawishi aje kushirikiana nasi katika kujenga chama na kuwaletea wananchi maendeleo, na leo tumefanikiwa," alisema.
Walianza kunifanya nione kama mimi ni mtu asiye na thamani. Walikuwa wakijaribu kuniharibia jina langu, kuzusha maneno mabaya kuhusu mimi, na hata kufanyia kazi mambo ambayo yalionekana kama kutafuta namna ya kuniharibia kabisa. Hata hivyo, nilikuwa na imani kwamba hata maadui hawawezi kunizuia.
Lakini walipoona kwamba walikuwa wanashindwa kwa njia moja au nyingine, walijitahidi kuhamasisha nguvu za giza ili kuniletea madhara. Hali ilibadilika haraka. Maadui wangu walitumia njia za kishirikina kujaribu kuniharibia.
Nilijikuta nikikumbwa na maumivu yasiyoelezeka, huzuni kubwa, na wakati mwingine, nikiwa na wasiwasi kwamba nilikuwa nikipoteza kila kitu.
Sikuwahi kuelewa kwa nini maisha yangu yalikuwa na milima na mabonde. Nilikuwa nafanya juhudi nyingi kazini lakini hakuna kilichokuwa kinanyooka.
Nilihisi kama kuna kitu kilikuwa kimenifunika kisirisiri. Siku moja nilihudhuria kikao cha wanawake mahali fulani Mbezi Beach, na baada ya mada ya kawaida kumalizika, mgeni mmoja alisimama na kuzungumza kuhusu nyota za kuzaliwa. Alieleza jinsi tarehe yako ya kuzaliwa inaweza kufichua tabia zako, mafanikio yako, changamoto zako, na hata majira sahihi ya kufanya maamuzi makubwa.
Kwa kawaida, mimi si mtu wa kuamini mambo ya nyota au nguvu za angani, lakini alipoanza kueleza kuhusu watu waliozaliwa mwezi wa Novemba kama mimi, nilishtuka. Alisema, “Watu wa mwezi wa Novemba mara nyingi wana ndoto kubwa lakini hujikuta wanakwamishwa na nguvu zisizoonekana endapo hawajatambua nyota yao vizuri.”
Hapo hapo moyo wangu ulidunda. Alieleza mengi ambayo yalikuwa kama anaelezea maisha yangu kama vile nimewahi kumweleza. Niliposikia hilo, niliamua kufanya utafiti zaidi. Nilianza kwa kujifunza kuhusu nyota yangu nilizaliwa tarehe 11 Novemba, na hiyo inaangukia kwenye nyota ya Scorpio.
Nilijifunza kwamba watu wa Scorpio ni wenye hisia kali, wanapenda mambo ya undani, na wanaweza kuwa na bahati kubwa endapo watajua jinsi ya kuitumia nguvu ya nyota yao. Nilianza kuandika tabia zangu, vitu ninavyopenda, na mambo yanayonikera. Ghafla, maisha yangu yalianza kupata sura mpya.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.
BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imemkabidhi rasmi mwanautalii na mtangazaji wa vivutio vya utalii kutoka Oman, Khalid Hamed Al Barwani, Ubalozi wa Hiari wa Utalii wa Tanzania, ikiwa ni hatua ya kimkakati ya kuimarisha juhudi za kuitangaza Tanzania katika masoko ya kimataifa na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini.
Ubalozi huo umekabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa wa Al Barwani katika kuitangaza Tanzania kupitia majukwaa mbalimbali ya kimataifa.
Al Barwani alipata umaarufu mkubwa baada ya kuongoza kundi la Dream Team Explorers kutembelea Shamba la Miti la Sao Hill mwaka 2024, ambapo walijionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana katika eneo hilo, ikiwemo misitu ya kupandwa, mandhari ya kuvutia ya asili na eneo la Mto Ruaha.
Maudhui waliyoyashiriki kupitia majukwaa yao ya kidijitali yalichangia kuongeza mwonekano wa Sao Hill na kuibua hamasa ya watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea eneo hilo.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi ubalozi huo, Mafuru alisema TTB itaendelea kushirikiana na watu mashuhuri, watengeneza maudhui na wadau wa kimataifa wenye ushawishi mkubwa katika masoko mbalimbali ili kuendelea kuitangaza Tanzania kama moja ya vivutio bora vya utalii duniani.
“Ubalozi huu ni kutambua mchango wa Khalid Al Barwani katika kuitangaza Tanzania na ni sehemu ya mkakati wetu wa kupanua wigo wa masoko ya utalii kupitia mabalozi wa hiari wanaotumia ushawishi wao kufikisha ujumbe wa Tanzania kwa mamilioni ya watu duniani,” alisema Mafuru.
Kwa upande wake, Al Barwani alishukuru kwa heshima hiyo na kuahidi kuendelea kuitangaza Tanzania kupitia majukwaa yake ya kimataifa, akieleza kuwa nchi ina vivutio vya kipekee vinavyostahili kufahamika zaidi duniani.
“Tanzania ni nchi yenye uzuri wa kipekee, kuanzia hifadhi za wanyamapori, misitu, fukwe, utamaduni hadi ukarimu wa wananchi wake. Nitaendelea kuwa balozi wa kuitangaza Tanzania kwa dunia,” alisema.
TTB inaendelea kutumia ushirikiano na wadau wa kimataifa pamoja na mabalozi wa hiari wa utalii kama sehemu ya mkakati wa kuongeza ushindani wa Tanzania katika soko la utalii duniani na kuunga mkono malengo ya taifa ya kukuza sekta ya utalii, kuongeza idadi ya wageni wa kimataifa na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya uchumi wa nchi.
Jina langu ni Joshua, na mimi ni mjasiriamali. Kwa muda mrefu, nilikuwa nikikabiliana na changamoto kubwa katika biashara yangu. Ilikuwa ni biashara ndogo ya kuuza bidhaa za vipodozi na huduma za uzuri, lakini kwa muda, wateja walikuwa wakipungua.
Nilijikuta nikikopa fedha nyingi kutoka kwa marafiki na familia yangu ili kuendesha biashara hii, lakini kila mara nilikuwa napata hasara. Nilijua kuwa hatua nilizokuwa nikichukua hazikufanikiwa, lakini sikujua ni wapi nilikosea.
Nilikutana na mshtuko mkubwa ulipokuja wazo la kumaliza biashara yangu.
Nilijua kuwa ikiwa nisingepata suluhisho haraka, nisingeweza kuendelea. Nilikuwa nimepoteza matumaini, lakini kimoja kilikuwa kinanifanya niwe na matumaini kidogo.
Katika hali yangu ya kukata tamaa, nilijua kuwa nilihitaji msaada wa kiroho ili kubadilisha hali yangu.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.
Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imesema imetumia Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wadau kuhusu majukumu yake, fursa zilizopo katika sekta ya mbolea pamoja na mnyororo wa thamani wa uagizaji, utengenezaji na usambazaji wa mbolea nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Julai 4, 2026, Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini wa TFRA, Joshua Ng’ondya, amesema mamlaka hiyo imefika kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, umuhimu wa upimaji wa udongo, pamoja na utaratibu wa kujisajili ili kunufaika na mpango wa mbolea za ruzuku.
Amesema kupitia maonesho hayo, wananchi na wafanyabiashara wanapata maelekezo ya namna ya kupata leseni za biashara, kusajili maeneo ya biashara na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa mbolea, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika biashara ya mbolea nchini.
Ng’ondya amesema TFRA ina jukumu la kudhibiti ubora wa mbolea za viwandani na mbolea hai zilizosajiliwa, pamoja na kuhakikisha zinakidhi viwango vinavyotakiwa kabla ya kuingia sokoni na katika mpango wa ruzuku kwa wakulima.
Aidha, ameeleza kuwa mamlaka hiyo inaendelea kutoa elimu kuhusu namna ya kutengeneza, kusajili na kuingiza mbolea sokoni kwa kufuata taratibu zilizowekwa, ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora, salama na zenye tija katika kuongeza uzalishaji wa mazao.
Na Benny Mwaipaja, Banjul, Gambia
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amewasili Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.
Mhe. Omar alipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Banjul.
Mkutano huo utakaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha SDJK, jijini Banjul, utatoa jukwaa kwa nchi za Afrika kujadili masuala muhimu ya uchumi na maendeleo yanayoikabili Bara la Afrika, pamoja na kuweka msimamo wa pamoja katika kushirikiana na taasisi kubwa za kifedha duniani.
African Caucus ni jukwaa linalowakutanisha magavana wa Afrika katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Kundi la Benki ya Dunia, ambalo huzisaidia nchi za Afrika kuzungumza kwa sauti moja kuhusu masuala kama usimamizi wa madeni, fedha za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, maendeleo ya miundombinu, kupunguza umasikini, ajira, biashara, na mageuzi ya kiuchumi.
Gambia kuandaa mkutano huo wa mwaka 2026 ni fursa kubwa kwa nchi hiyo kushiriki kikamilifu katika mijadala ya bara na kuonesha vipaumbele vyake vya maendeleo.
Mkutano huo unaweza kuleta faida nyingi ikiwemo kuongeza mwonekano wa nchi hiyo katika ngazi ya Afrika na kimataifa, kuvutia mijadala kuhusu uwekezaji, na kuimarisha ushirikiano kati ya Gambia, nchi nyingine za Afrika, na washirika wa maendeleo.
Pia unaweza kuonesha juhudi za Gambia katika maeneo kama mageuzi ya uchumi, utalii, kilimo, uwezeshaji wa vijana, mabadiliko ya kidijitali, na maendeleo endelevu.
Mkutano wa 2026 unaweza pia kujikita katika changamoto zinazozikabili nchi za Afrika, zikiwemo ongezeko la madeni, mabadiliko ya tabianchi, uhaba wa chakula, ukosefu wa ajira, na umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Masuala haya ni muhimu hasa kwa nchi ndogo kama Gambia, ambapo athari za mabadiliko ya tabianchi, rasilimali chache, na utegemezi wa sekta chache zinaweza kuathiri maendeleo ya Taifa na upitia African Caucus, nchi zinaweza kubadilishana uzoefu na kupendekeza suluhisho za vitendo linaloendana na hali halisi ya Afrika.
Kuandaa mkutano huu pia kunaweza kuwa na matokeo chanya kwa biashara za ndani na sekta ya utalii. Hoteli, huduma za usafiri, migahawa, waandaaji wa matukio, na vikundi vya sanaa na utamaduni vinaweza kunufaika kutokana na uwepo wa wajumbe na wageni.
Tukio hili linaweza kuitangaza Gambia kama nchi yenye amani, ukarimu, na uwezo wa kuandaa mikutano ya kimataifa na shughuli za kidiplomasia.
Kwa ujumla, Mkutano wa African Caucus wa 2026 nchini Gambia ni tukio lenye umuhimu mkubwa kwa Gambia na Bara la Afrika kwa jumla kwani unatoa nafasi kwa viongozi wa Afrika kujadili vipaumbele vya pamoja, kuimarisha ushirikiano, na kutetea haki zaidi kutoka kwa taasisi za kifedha duniani.
Kwa Gambia, huu ni wakati wa kuonesha uongozi, kutangaza malengo yake ya maendeleo, na kujitambulisha kama mshirika muhimu katika mustakabali wa uchumi wa Afrika.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kushoto), akisalimia na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, wakati alipowasili jijini Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kushoto), akiteta jambo na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, wakati alipowasili jijini Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb)(kulia), akiwa katika picha na Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anayesimamia pia shughuli za kibalozi nchini Gambia, Mhe. Balozi Selestine Kakele, wakati alipowasili jijini Banjul nchini Gambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, utakaofanyika kuanzia jumatatu tarehe 6 Julai, 2026, unatarajiwa kuwa tukio muhimu litakalowakutanisha viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WF, Banjul, Gambia)




.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)
