Serikali imesema udanganyifu katika mitihani ya kitaifa umepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kuimarishwa kwa usimamizi wa mitihani nchini.

Kauli hiyo imetolewa Septemba 7, 2026 mkoani Ruvuma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Prof. Carolyne Nombo, alipofika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na kuazungumzia utekelezaji wa masuala mbalimbali ya elimu ikiwemo maandalizi ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba unaotrajia kufanyika nchini kote Septemba 9 na 10, 2026.

Ameeleza kuwa mitihani ya kitaifa ni suala nyeti linalohitaji usimamizi madhubuti, hivyo viongozi wa elimu katika ngazi zote wanapaswa kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinafuatwa.

“Udanganyifu umepungua kwa kiasi kikubwa, nawasihi wanafunzi wa darasa la saba manaotarajia kufanya mitihani yenu kutojiingiza katika udanganyifu wowote wa mitihani, tuzingatie taratibu zote za mitihani,” amesisitiza Prof. Nombo

Aidha, amezitaka kamati za mitihani za mikoa na viongozi wa elimu kuendelea kushirikiana katika kusimamia mitihani, huku akiwapongeza kwa hatua ambazo tayari zimechukuliwa katika kupunguza udanganyifu.

Amebainisha kuwa, Serikali itaendelea kuchukua hatua pale inapobaini vitendo vya udanganyifu, hasa vile vinavyohusisha kupanga kwa pamoja kati ya wanafunzi, walimu au wasimamizi wa mitihani.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Songea Mhe. Wilman Kapenjama amesema mkoa umejiandaa vema katika kusimamia mtihani huo kwa hali ya usalama bila changamoto yoyote.



Na Boniphace John, OKULY BLOG - DODOMA


Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) umewaagiza Mameneja wa Mikoa yote 26 nchini kufanya ukaguzi wa miundombinu ya barabara, madaraja, makalavati na maeneo mengine hatarishi, ili kuchukua hatua za haraka kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.

Wito huo umetolewa jijini Dodoma Septemba 7,2026 na Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa barabara ya Ntyuka–Mvumi–Kikombo pamoja na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mhandisi Besta amesema TANROADS inapaswa kuwa makini kwa kutambua mapema maeneo yanayoweza kuathiriwa na mvua na kuhakikisha hatua stahiki zinachukuliwa kabla ya mvua kuanza.

Amesema ukaguzi huo ni muhimu kutokana na changamoto zilizowahi kujitokeza katika baadhi ya maeneo wakati wa mvua, akitoa mfano wa Daraja la Mutikila ambalo Desemba mwaka jana liliathiriwa na mvua na kusababisha usafiri wa magari na wananchi kukwama.

 “Natoa rai kwa mameneja wote wa mikoa 26 waende wakafanye ukaguzi na kuangalia ni namna gani wanaweza kupunguza athari zinazoweza kutokana na mvua za El Niño,” amesema Mhandisi Besta.

Amesema pamoja na Daraja la Mutikila, TANROADS inahakikisha kazi katika madaraja ya Mangungo na Kikombo, pamoja na madaraja mengine yanayotekelezwa katika mradi huo, zinakamilishwa kwa wakati ili yaweze kupitika wakati wa mvua.

Mhandisi Besta pia amemtaka mkandarasi wa mradi huo kuongeza kasi ya utekelezaji wa kazi ili kukamilisha sehemu iliyobaki na kuwawezesha wananchi kunufaika na barabara hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Zuhura Amani, mradi huo una urefu wa jumla ya kilomita 76 na unatekelezwa kwa awamu mbili.

Amesema awamu ya kwanza inayotekelezwa sasa inahusisha kilomita 25 na imefikia asilimia 67.9 ya utekelezaji.

Kati ya kilomita hizo, kilomita 8.6 ziko upande wa Ntyuka kuelekea Mvumi, huku upande wa Kikombo ukiwa na kilomita 14.4, ikiwemo kilomita tano zinazounganisha barabara hiyo na barabara inayoelekea Makao Makuu ya Jeshi.

Mhandisi Amani amesema mkandarasi wa mradi huo ni CHICO, ambaye tayari amekamilisha ujenzi wa sehemu kubwa ya barabara, ambapo kilomita 23.2 kati ya 25 zimefikia kiwango kinachohitajika.

Amesema kazi kubwa zilizobaki ni pamoja na kujaza tuta la barabara, kuunganisha maeneo ya madaraja na kukamilisha miundombinu ya kupitisha maji katika maeneo ya Mutikila, Mangungo na Kikombo, pamoja na daraja la reli ya MGR.

Amesema TANROADS tayari imeanza kuimarisha maeneo ya madaraja yaliyokuwa yakileta changamoto wakati wa mvua kwa kutumia kifusi, kuimarisha kingo za matuta na kufungua njia za mito, hatua inayolenga kuhakikisha watumiaji wa barabara wanaendelea kupita kwa usalama.

Kwa mujibu wa Mhandisi Amani, TANROADS inatarajia madaraja ya Mutikila, Mangungo na Kikombo kukamilika na kufikia hatua ya kupitika kabla ya kuanza kwa mvua, hatua ambayo itasaidia kupunguza usumbufu kwa wananchi na watumiaji wengine wa barabara.












Vyama vya siasa nchini vimetakiwa kutumia majukwaa yao kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote, kwa kuwa afya ni haki ya kila mwananchi bila kujali itikadi, umri, jinsia au nafasi yake katika jamii.

Wito huo umetolewa na Kaimu Waziri wa Afya Dkt. Saada Mkuya Salum na Mbunge wa Welezo, wakati wa semina iliyowakutanisha wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa na wataalamu kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa ajili ya kuwajengea uelewa kuhusu Bima ya Afya kwa Wote.

Dkt. Mkuya alisema wanasiasa wana mtandao mpana wa kuwafikia wananchi kuanzia ngazi ya jamii hadi taifa, hivyo wana nafasi muhimu ya kuwa mabalozi wa elimu kuhusu afya na bima ya afya.

Alisema ushiriki wa vyama vya siasa katika kutoa elimu hiyo unaweza kusaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya na namna inavyoweza kusaidia kulinda afya na ustawi wa familia.

“Bima ya afya inalinda mwananchi na familia dhidi ya gharama kubwa za matibabu. Hili si suala la chama cha siasa, bali ni suala la maisha na ustawi wa wananchi,” alisema Dkt. Mkuya.

Aliongeza kuwa wanasiasa wanapokutana na wananchi katika maeneo mbalimbali, ikiwemo mikutano ya hadhara na majukwaa mengine, wanaweza kutumia fursa hizo kutoa elimu sahihi kuhusu umuhimu wa bima ya afya.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Juma Ally Khatib, alisema elimu iliyotolewa katika semina hiyo itawafikia viongozi wa vyama vya siasa kuanzia ngazi ya taifa, mikoa, wilaya na kata, pamoja na wanachama wao.

Alisema viongozi hao watakuwa na jukumu la kuifikisha elimu hiyo kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini, ili kuongeza uelewa na ushiriki katika mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.

“Tunachojifunza hapa hakitaishia kwa wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa. Tutakwenda kuwaelimisha viongozi wetu wa kitaifa, mikoa, wilaya, kata na wanachama, ambao nao wataifikisha elimu hii kwa wananchi,” alisema Khatib.

Naye Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mohamed Ahmed, alisema semina hiyo inalenga kuwawezesha viongozi na wawakilishi wa vyama vya siasa kupata uelewa sahihi kuhusu mifumo ya bima ya afya nchini, ili waweze kutoa elimu sahihi kwa wananchi.

Alisema uelewa wa viongozi wa kisiasa ni muhimu kwa kuwa wana nafasi kubwa ya kuhamasisha wananchi kushiriki katika mipango mbalimbali ya Serikali inayolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya.

Akizungumza katika semina hiyo, Dkt. David Mwanesano kutoka NHIF, alisema Serikali imeanza kutekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa awamu, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha wananchi wanapata kinga dhidi ya changamoto za gharama za matibabu.

Alisema hadi sasa jumla ya kaya 276,400 zimekwishaandikishwa katika mpango huo na kuanza kupata huduma za afya.

Alisisitiza kuwa ushirikiano wa wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa kisiasa, ni muhimu katika kufanikisha azma ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma za matibabu bila kukabiliwa na mzigo mkubwa wa gharama za matibabu.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa


Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa,akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 8,2026 jijini Dodoma  kuhusu kukamilika kwa awamu ya kwanza na kufunguliwa kwa awamu ya pili ya udahili wa shahada ya kwanza kwa mwaka wa masomo 2026/2027/.

Na.Alex Sonna-DODOMA 
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetangaza kukamilika kwa Awamu ya Kwanza ya udahili wa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na programu za Shahada ya Kwanza kwa mwaka wa masomo 2026/2027 na kuanza kwa Awamu ya Pili ya udahili kuanzia leo, Septemba 8 hadi 21, mwaka huu.
Hayo yamesemwa leo Septemba 8,2026 jijini Dodoma na Katibu Mtendaji wa TCU, Prof. Charles Kihampa, amesema jumla ya waombaji 149,645 waliwasilisha maombi ya kujiunga na vyuo 93 vilivyoidhinishwa kudahili wanafunzi wa Shahada ya Kwanza katika mwaka wa masomo 2026/2027.
Prof. Kihampa amesema katika mwaka huo wa masomo, vyuo vimeongeza programu za Shahada ya Kwanza kutoka 894 mwaka 2025/2026 hadi kufikia 1,019, sawa na ongezeko la programu 125, huku nafasi za udahili zikiongezeka kutoka 205,652 hadi 227,555.
Amesema ongezeko hilo la nafasi 21,903 ni sawa na asilimia 10.7, hatua inayolenga kuongeza fursa kwa vijana wanaohitaji kuendelea na elimu ya juu nchini.
Aidha, ameeleza kuwa katika Awamu ya Kwanza, waombaji 117,334, sawa na asilimia 78.4 ya waombaji wote, wamepata nafasi za udahili katika vyuo walivyoviomba, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka baada ya kukamilika kwa Awamu ya Pili.
 "Waombaji waliopata udahili katika vyuo zaidi ya kimoja wametakiwa kuthibitisha chuo kimojawapo kuanzia Septemba 8 hadi 21, 2026, kwa kutumia namba maalum ya siri iliyotumwa kupitia ujumbe mfupi wa simu au barua pepe waliotumia wakati wa kuomba udahili."amesema Prof. Kihampa
Aidha, TCU imewataka waombaji ambao hawakupata nafasi katika Awamu ya Kwanza, pamoja na wale ambao hawakuweza kuwasilisha maombi, kutumia fursa ya Awamu ya Pili kwa kutuma maombi katika vyuo na programu wanazozipenda. Vyuo pia vimeelekezwa kutangaza programu ambazo bado zina nafasi.
"Tume imewakumbusha waombaji kuwa masuala yote yanayohusu udahili na uthibitisho wa nafasi yanapaswa kuwasilishwa moja kwa moja katika vyuo husika, huku vyuo vikielekezwa kushughulikia changamoto za waombaji kwa haraka kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya udahili," amesisitiza.

 

DODOMA, September 8, 2026: 

Efforts to prepare Tanzanian girls for the rapidly expanding digital economy are taking a new direction, with UNESCO calling for gender to be placed at the centre of digital skills education to ensure that girls are not left behind in the country’s digital transformation.

The call comes as Tanzania, through collaboration with UNESCO and Beijing Normal University (BNU), implements the “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls” project, an initiative aimed at strengthening digital skills while addressing barriers that continue to limit girls’ participation in technology and innovation.

Gender specialist Dr Rosemarie N. Mwaipopo said digitalisation was no longer simply a matter of access to computers or the internet, but an increasingly important pathway to education, employment, innovation and wider socio-economic development.

She said the country’s digital transformation would have greater impact if girls were given deliberate opportunities to acquire digital skills, participate in innovation and develop the confidence needed to pursue technology-related education and careers.

“Digitalisation is a major influence in societal development, enhancing access to opportunities,” Dr Mwaipopo said, while emphasising the need to confront the persistent gender gap in digital participation.

She questioned why the gap continued to exist globally and in Tanzania despite various innovations, programmes and interventions designed to expand access to technology and digital skills.

According to her, the challenge was not only about whether technology was available, but also about who had the skills, confidence, opportunity and enabling environment to use that technology and turn it into meaningful solutions.

She said this was where the UNESCO-BNU project could make an important contribution by introducing a gender perspective into digital skills education.

CREATING A CRITICAL MASS OF GIRLS IN ICT

Dr Mwaipopo said the project would deliberately select female students to participate in ICT innovation training as part of an affirmative action approach aimed at creating a critical mass of girls with digital knowledge and skills.

She said increasing the number of girls exposed to technology and innovation would help challenge the long-standing perception that ICT and STEM-related fields were predominantly for boys.

The approach, she explained, was intended to create more girls who could confidently engage with technology, develop innovations and eventually pursue careers in the digital sector.

“This is not simply about teaching girls how to use technology. It is about creating opportunities for them to become knowledgeable, confident and active participants in the digital future,” she said.

She said a growing pool of digitally skilled girls could also provide role models for younger generations and contribute to changing community perceptions about the role of women in technology.

CHANGING THE WAY GIRLS LEARN

Dr Mwaipopo said teachers would be equally important in achieving this transformation.

She called for teachers to be equipped with gender-transformative pedagogy, enabling them to recognise and challenge attitudes, practices and social norms that may discourage girls from participating fully in ICT and STEM education.

She said teachers needed to create classrooms where girls felt confident to experiment, ask questions, solve problems and develop technological innovations.

The objective, she said, was to move beyond simply providing equal access to boys and girls towards creating learning environments capable of transforming the conditions that have historically limited girls’ participation.



She said teachers and students would also need greater awareness of gender equality, gender barriers, enabling factors and intersectionality to understand why girls may experience digital education differently depending on their social and economic circumstances.

INNOVATION THAT WORKS FOR EVERYONE

Dr Mwaipopo further challenged students to think about gender when developing ICT solutions.
She said female students should be equipped to apply a gender lens in ICT processes and innovation, ensuring that digital products and solutions were accessible, sensitive to different needs and inclusive.

She explained that successful digital innovation should not only answer the question of whether a technology works, but also consider who can access it, who can use it and who ultimately benefits from it.

Such an approach, she said, would enable girls to see technology as more than computers and coding, but as a powerful tool for addressing real challenges facing families, communities and the country.

BUILDING TANZANIA’S DIGITAL GENERATION

The gender-transformative approach is being implemented alongside efforts to establish and strengthen ICT Clubs in public schools, providing girls with practical opportunities to develop digital skills, participate in innovation and explore technology-related career pathways.

The broader UNESCO-BNU initiative is being implemented in collaboration with the Government of the United Republic of Tanzania, reflecting the importance of partnerships in strengthening digital education and expanding opportunities for women and girls.

Through the project, teachers and female students are expected to gain skills and approaches that can contribute to more inclusive digital learning environments.

For Tanzania, the initiative comes at a time when digital skills are increasingly becoming essential for education, employment, entrepreneurship and innovation.
Its significance therefore extends beyond the classroom.

By deliberately investing in girls’ digital skills today, the country is building a generation capable of participating in and contributing to tomorrow’s technology-driven economy.

The ultimate ambition is to ensure that Tanzanian girls are not merely users of technology, but creators, innovators, entrepreneurs and future leaders in the digital economy.

And by ensuring that no girl is excluded from the digital transformation, Tanzania can strengthen its human capital and build a more inclusive digital future in which every girl has an opportunity to learn, innovate and shape the country’s development.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), katika Kongamano la 5 la Kimataifa la Uchumi wa Buluu, limejipambanua katika sekta ya mazingira kwa kusisitiza umuhimu wa matumizi endelevu ya rasilimali za bahari, mito, maziwa na maeneo ya pwani, sambamba na uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira.
Mimi nilikuwa na ndoto ya kusafiri nje ya nchi kwa muda mrefu. Niliandaa kila kitu, lakini kilichonishinda zaidi ilikuwa kupata visa.

Kila nilipojaribu, nilikumbana na ucheleweshaji na wakati mwingine kukataliwa. Hali hii ilinifanya nikate tamaa kidogo.

Nilianza kuhisi kama safari yangu haitawahi kufanikiwa, licha ya juhudi zote nilizokuwa nafanya. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu changamoto yangu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa kwenye ndoa ambayo mwanzoni ilikuwa na furaha na maelewano. Tulikuwa tunazungumza, kucheka, na kushirikiana kila kitu bila shida. Lakini baada ya muda, mabadiliko yakaanza. Mke wangu alianza kujitenga kimya kimya.

Hakupenda tena mazungumzo marefu, hakutabasamu kama zamani, na mara nyingi alikuwa na msongo wa mawazo.
Nilijaribu kumuuliza kama kuna tatizo, lakini majibu yake yalikuwa mafupi au wakati mwingine hakuna majibu kabisa. Hali hii ilinifanya nijisikie kupotea ndani ya ndoa yangu.

Kadri siku zilivyopita, umbali kati yetu uliongezeka. Nilianza kuhisi kama tunaishi maisha mawili tofauti chini ya paa moja. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa na ndoto ya kusafiri nje ya nchi kwa muda mrefu. Niliandaa kila kitu, lakini kilichonishinda zaidi ilikuwa kupata visa. 

Kila nilipojaribu, nilikumbana na ucheleweshaji na wakati mwingine kukataliwa. Hali hii ilinifanya nikate tamaa kidogo.

Nilianza kuhisi kama safari yangu haitawahi kufanikiwa, licha ya juhudi zote nilizokuwa nafanya. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu changamoto yangu. SOMA ZAIDI.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

VIJANA nchini wametakiwa kupewa mafunzo ya uongozi tangu wakiwa katika umri mdogo ili kuwaandaa kuwa viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kuongoza katika nyanja mbalimbali, hatua inayolenga kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.




DODOMA, September 7, 2026:


UNESCO, in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, has launched a programme to establish and strengthen Information and Communication Technology (ICT) Clubs in public schools in Dodoma and Morogoro, aimed at equipping girls with digital skills, confidence and knowledge to pursue education and careers in technology.


The initiative is being implemented under the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls,” which seeks to reduce the gender gap in digital education and expand opportunities for women and girls to participate fully in the technology sector.








Speaking during the official launch held today at Edema Conference Hall in Kisasa, Dodoma, UNESCO Tanzania Head of Education Sector, Dr Faith Shayo, said the initiative was designed to encourage girls to develop an interest in technology, build confidence and explore opportunities in ICT-related education and careers.


She said the ICT Clubs would provide students with opportunities for practical learning, innovation and the development of skills to use technology to address challenges in their communities.

Dr Shayo said the programme would also involve ICT teachers and student teachers, with the clubs serving as platforms for extracurricular activities that give students practical experience beyond regular classroom lessons.



She said challenges contributing to the digital divide included disparities in access to technology, digital skills and competencies, as well as limited opportunities for girls to gain first-hand knowledge of education and career pathways in technology-related fields.



The programme is being implemented in collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), and the Tanzania Institute of Education (TIE).

A total of 20 public schools are expected to participate, with 10 from Morogoro Municipality and 10 from Dodoma City. The programme will directly benefit 500 girls and 40 teachers.



The official launch marks the beginning of a series of activities under the programme, with a four-day ICT Innovation Bootcamp scheduled to begin tomorrow, September 8, at Msalato, and run through Friday, September 11, 2026.

The Bootcamp will provide students with opportunities for practical learning, digital skills development and innovation, including developing and showcasing digital ideas and projects aimed at addressing real-life challenges in their communities.



In Dodoma, participating schools include Dodoma, Kisasa, Nara, Ihumwa, Makole, Mnadani, Hazina, Mtumba and Msalato, all secondary schools.

Through the ICT Clubs, students will receive practical training in computer programming (coding), computational thinking and problem-solving, digital creativity, visual and audio content production, and the safe and responsible use of technology.



The girls will also be connected with women ICT professionals through mentorship programmes, enabling them to learn from their experiences and gain a broader understanding of education, employment and career opportunities in the technology sector.

PMO-RALG STRESSES COLLABORATION

Speaking on behalf of the Prime minister Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), Mr. Francis Gervas, from the Education Management Department, thanked UNESCO for partnering with the Government in implementing the initiative.

He stressed the importance of continued collaboration among stakeholders to ensure that the programme achieves its intended objectives and that the results and lessons generated are sustained beyond the implementation period.

Mr. Gervas also called for the initiative to be expanded to other parts of the country so that more girls could benefit, while urging participants and stakeholders to remain committed to its effective implementation.

TEACHER CALLS FOR ATTITUDE CHANGE
Meanwhile, Mr Godfrey Robin Mseti, a teacher at Mtumba, commended the Government and UNESCO for introducing the initiative, saying opportunities and training related to technology had for a long time been perceived as being more accessible to boys and men.

He said society needed to change the perception that ICT-related learning was mainly for boys, stressing that girls also had the ability and should be given equal opportunities to learn, participate in and benefit from technology.

Under the programme, the ICT Clubs are intended to provide safe and inclusive learning environments where students can develop their skills through learning, innovation, leadership and collaboration.
Girls are expected to account for at least 50 per cent of participation in the clubs, with stakeholders encouraged to promote even greater representation.

Overall, the initiative is expected to strengthen ICT Clubs in 20 schools and enable 500 girls to improve their digital skills, confidence, participation and leadership abilities, while increasing their awareness of education and career opportunities in ICT.

The programme seeks to ensure that girls acquire not only the skills to use technology, but also the confidence to view technology as a tool for innovation, education and building their future careers.