Na Oscar Assenga, Muheza

WANANCHI 6,258 wa Kijiji cha Muungano, Wilaya ya Muheza, wanatarajiwa kunufaika na huduma bora za afya kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa Zahanati ya Muungano, mradi ambao umepokelewa na kuridhiwa na Mwenge wa Uhuru 2026 baada ya kukaguliwa na kupokea taarifa ya utekelezaji wake.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026 alisema kukamilika kwa zahanati hiyo kutasaidia kusogeza huduma za matibabu karibu na wananchi na kupunguza changamoto ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Alisema Serikali tayari imepeleka vifaa tiba pamoja na watumishi wa afya watakaotoa huduma katika zahanati hiyo, hatua inayoonesha dhamira ya kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, hususan katika maeneo ya vijijini.

“Mradi huu ni muhimu kwa wananchi wa Muungano na maeneo jirani kwa sababu unasaidia kuboresha upatikanaji wa huduma za afya na kuongeza ustawi wa jamii,” alisema.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa mafanikio ya mradi huo yametokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa maendeleo, hususan Taasisi ya Islamic Help, iliyochangia ujenzi wa zahanati hiyo, huku Serikali ikigharamia vifaa tiba na watumishi wa afya.

Aliwashukuru wadau wa maendeleo kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya kijamii, na kuwataka kuendeleza ushirikiano huo ili kusaidia kuboresha huduma muhimu kwa wananchi.

Aidha, aliwahimiza wananchi kuendelea kulinda amani na utulivu wa nchi, akisema kuwa mazingira hayo yanawezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuvutia wadau zaidi kushirikiana na Serikali.

Kwa upande wake, akitoa taarifa ya mradi huo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Dk. Fani Mussa, alisema ujenzi wa Zahanati ya Muungano ulianza Machi 2, 2025 na kukamilika kwa gharama ya Shilingi milioni 165.94.

Alieleza kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi milioni 141.55 zilitumika kwa ujenzi, huku Shilingi milioni 24.39 zikitumika kununua vifaa tiba.

Kwa mujibu wa Dk. Mussa, zahanati hiyo itahudumia wakazi 6,258 wa Kijiji cha Muungano, wakiwemo wanaume 3,089 na wanawake 3,169, na inatarajiwa kwa kiasi kikubwa kuboresha upatikanaji wa huduma za afya katika eneo hilo.

Baada ya ukaguzi huo, Mwenge wa Uhuru 2026 ulieleza kuridhishwa na ubora wa utekelezaji wa mradi huo, ukibainisha kuwa ni hatua muhimu katika kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuunga mkono jitihada za Serikali za kuimarisha sekta ya afya nchini.



Meneja wa Shirika  la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Kati, Hamisi Sudi Mwanasala,akizungumza na waandishi wa habari katika banda la TBS wakati wa  Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwenye Viwanja vya Chinangali  jijini Dodoma,

....

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kuonesha ubora wa huduma zake kwa wananchi kupitia ushiriki wake katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, huku mamia ya wananchi na wafanyabiashara wakifurika katika banda la taasisi hiyo kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa kwa njia ya kisasa.

Hayo yamesemwa leo Juni 23,2026 na Meneja wa TBS Kanda ya Kati, Hamisi Sudi Mwanasala, amesema mwitikio wa wananchi katika maonesho hayo umekuwa mkubwa kutokana na hamu ya kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu viwango, ubora wa bidhaa na taratibu za usajili.

Amesema TBS imetumia maonesho hayo kama jukwaa la kuwasogezea wananchi huduma muhimu zikiwemo utoaji wa vibali, usajili wa bidhaa na majengo ya biashara ya chakula na vipodozi pamoja na kupokea maombi ya leseni ya kutumia Nembo ya Ubora ya TBS.

"Tumeshuhudia mwamko mkubwa wa wananchi. Wengi wamekuja na maswali mbalimbali kuhusu huduma zetu na wamepata majibu ya kina. Kiu yao ya kupata taarifa sahihi imeweza kutimizwa kupitia wataalamu waliopo katika banda letu," amesema Mwanasala.

Amefafanua kuwa pamoja na kutoa huduma, TBS imeendelea kutoa elimu kwa wazalishaji, wafanyabiashara na waingizaji wa bidhaa kuhusu taratibu zinazopaswa kufuatwa ili kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa, kuingizwa au kuuzwa zinakidhi viwango vinavyotakiwa ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Mwanasala, maonesho ya mwaka huu yamekuwa na umuhimu wa kipekee kwa TBS kwani yanafanyika wakati Shirika hilo likiadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, safari ambayo imeambatana na mafanikio makubwa katika kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma nchini.

Amesema maadhimisho hayo yamekuwa fursa ya kukutana na wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara, wajasiriamali, taasisi za umma na wananchi wa kawaida ambao wametoa maoni na mapendekezo yatakayosaidia kuboresha zaidi huduma za Shirika hilo.

Katika hatua nyingine, Mwanasala amesema TBS imepiga hatua kubwa katika matumizi ya teknolojia ya kidijitali kwa kuweka mifumo inayorahisisha upatikanaji wa huduma bila wananchi kusafiri umbali mrefu kufika kwenye ofisi za Shirika hilo.

Ametaja mifumo hiyo kuwa ni Online Application System (OAS) pamoja na Integrated Standardization, Quality Assurance, Metrology and Testing System (ISQMT), ambayo inamwezesha mteja kufanya maombi ya usajili wa bidhaa, usajili wa maeneo ya biashara ya vipodozi na chakula na kupata leseni ya kutumia Nembo ya Ubora kwa njia ya mtandao.

"Leo hii mteja anaweza kuwasilisha maombi yake akiwa mahali popote alipo na kufuatilia hatua zote za maombi yake kidijitali hadi anapopata huduma anayohitaji. Hii imepunguza gharama, muda na usumbufu kwa wananchi," amesema 

Aidha, amebainisha kuwa jitihada za TBS katika kuboresha utendaji na utoaji wa huduma zimeendelea kutambuliwa kitaifa, baada ya Shirika hilo kushika nafasi ya tatu kati ya taasisi 47 za umma zilizoshindanishwa katika eneo la utawala bora kwenye utumishi wa umma mwaka huu, taasisi ya kwanza mwaka 2025 katika masuala ya udhibiti nchini na taasisi ya kwanza kwa mwaka 2023 Afrika.

Mwanasala amesema kuwa mafanikio hayo ni ishara ya dhamira ya TBS katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, huku akisisitiza kuwa Shirika hilo halitaridhika na mafanikio yaliyopatikana bali litaendelea kuboresha mifumo na huduma zake ili kukidhi mahitaji ya wananchi na wadau wa maendeleo.

Amewataka wananchi, wafanyabiashara na wazalishaji ambao hawajafika katika banda la TBS kutumia siku zilizobaki za maonesho hayo kutembelea banda hilo ili kupata elimu, ushauri na huduma mbalimbali zinazohusu ubora na usalama wa bidhaa.

"Tunawakaribisha wananchi wote kufika katika banda la TBS. Tunayo elimu, tunayo huduma na tunayo suluhisho la changamoto mbalimbali zinazohusu viwango. Lengo letu ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata bidhaa zenye ubora na salama," amesema

 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhe. Paschale Katambi Patrobas (Mb), aliyewakilishwa na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Afande Jeremiah Katungu Amewatunuku wafungwa 173 kati yao wanawake 6 na wanaume 167 vyeti vya mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara katika hafla ya mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara kwa ushirikiano wa Chuo Cha Uhasibu Arusha yaliyofanyika leo tarehe 22/June/2026 katika viwanja vya magereza kisongo mkoani Arusha.

Wakati wa utoaji wa vyeti hivyo Mhe. Katungu amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya marekebisho ya wafungwa kwa kuwekeza katika elimu na ujuzi unaowawezesha kuwa wananchi wenye tija wanaporejea katika jamii na kuongeza kuwa  mafunzo hayo yamekuwa nyenzo muhimu ya kuibua vipaji, kuongeza uwezo wa kujiajiri na kupunguza uwezekano wa kurudia vitendo vya uhalifu, huku akipongeza ushirikiano uliopo kati ya Jeshi la Magereza na Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika kufanikisha programu hiyo yenye manufaa makubwa kwa taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Joseph Mkude, amesema uwekezaji katika elimu ya ujasiriamali na stadi za biashara kwa wafungwa ni hatua muhimu ya kuwawezesha kujijengea maisha mapya yenye heshima na mchango chanya kwa jamii. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Profesa Eliamani Sedoyeka, amesema chuo hicho kinaendelea kutekeleza wajibu wake wa kijamii kwa kutoa elimu na mafunzo yanayolenga kuleta mabadiliko chanya kwa makundi mbalimbali ya jamii,na kuongeza kuwa mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara yaliyotolewa kwa wafungwa yamewajengea uwezo wa kubuni, kuanzisha na kusimamia shughuli mbalimbali za kiuchumi, hatua ambayo itawawezesha kujitegemea na kuwa sehemu ya nguvu kazi ya taifa baada ya kumaliza vifungo vyao. Profesa Sedoyeka ameongeza kuwa IAA itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali katika kutoa elimu inayojenga jamii jumuishi na yenye ustawi endelevu.

Utekelezaji wa mafunzo hayo kwa ushirikiano kati ya Jeshi la Magereza na Chuo cha Uhasibu Arusha unakwenda sambamba na azma ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayolenga kujenga uchumi shindani.










 


Wizara ya Nishati imesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo katika kufanikisha lengo la Taifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Wito huo umetolewa na Mjiolojia Mkuu wa Wizara ya Nishati, Bw. Ngereja Mgejwa, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, wakati akifungua Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia 2026 (Clean Cooking Expo 2026), Juni 23, 2026 katika Ukumbi wa EACLC jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika kongamano hilo, Bw. Mgejwa amesema nishati safi ya kupikia ni ajenda muhimu ya kitaifa inayohitaji ushirikiano wa wadau wote ili kuleta mabadiliko ya kudumu katika sekta ya nishati. Amesema matumizi ya nishati safi yana mchango mkubwa katika kulinda afya za wananchi, hususan wanawake na watoto, kuhifadhi mazingira, kuinua elimu kwa watoto wa kike na kuongeza tija ya kiuchumi.

Ameeleza kuwa kazi iliyopo mbele ni kuhakikisha wananchi wanapata nishati safi ya kupikia iliyo nafuu, salama na endelevu ikiwemo gesi oevu (LPG), majiko banifu, gesi asilia, umeme, bayogesi na bayoethanoli.

 Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya nishati safi pamoja na kutoa elimu kwa umma ili kubadili matumizi ya nishati za jadi kwenda kwenye nishati safi.

Bw. Mgejwa amepongeza Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TABWA) kwa kuandaa kongamano hilo, akisema majadiliano yatakayofanyika yataibua suluhisho na mapendekezo yatakayochochea ongezeko la matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

 Ameongeza kuwa kongamano hilo litahitimishwa kwa Mbio za Nishati Safi ya Kupikia zitakazotumika kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi kwa afya na uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa ya Wafanyabiashara Wanawake Tanzania(TABWA) Bi. Noreen Mawalla amesema maonesho hayo yameandaliwa chini ya kaulimbiu ya "Linda Afya, Hifadhi Mazingira, Okoa Muda kwa Uchumi Endelevu" kwa lengo la kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuunga mkono utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Amebainisha kuwa Clean Cooking Expo 2026 itafanyika kwa siku tatu na itajumuisha mafunzo, mijadala na maonesho ya teknolojia mbalimbali za nishati safi zitakazowakutanisha wadau kutoka sekta ya umma na binafsi. 

Amewakaribisha wananchi kutembelea mabanda ya maonesho ili kupata elimu na taarifa sahihi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, huku akieleza kuwa Mbio za Nishati Safi ya Kupikia zitafanyika Jumamosi na zinatarajiwa kuongozwa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi.








Kwa miaka miwili nilikuwa naishi maisha ya kukataliwa. Kila wiki nilikuwa natuma CV, nikajaza applications, na kwenda interviews nikiwa na matumaini makubwa. 

Wakati mwingine nilikuwa nafika hatua ya mwisho kabisa ya usaili, mpaka naambiwa, “Tutakupigia simu.” Lakini simu haikuwahi kuja.

Mwanzoni nilijipa moyo. Nilijua maisha si rahisi na kila mtu hupitia changamoto. Lakini kadri muda ulivyopita, hali ilianza kuniumiza zaidi.


Nilikuwa na qualifications nzuri, nilijitahidi kuvaa vizuri kwenye interviews, na hata kujifunza jinsi ya kujibu maswali kwa confidence.

.Lakini kila nilipokaribia kupata kazi, mambo yalikuwa yanaharibika ghafla bila kuelewa sababu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona marafiki niliomaliza nao shule wakianza maisha vizuri huku mimi nikiwa bado narudi nyumbani mikono mitupu. 

Wengine walikuwa hata wananishangaa, wakisema, “Inawezekanaje umefanya interviews nyingi hivi bila kazi?”

Polepole nilianza kupoteza kujiamini. Ilifika hatua nikaanza kuogopa hata kuona tangazo la kazi. Nilikuwa nimechoka psychologically. Kila niliposikia simu ikiita baada ya interview, moyo ulikuwa unapiga haraka, lakini mara nyingi ilikuwa disappointment nyingine. SOMA ZAIDI.
Nilipoolewa, nilikuwa na matumaini makubwa kuwa ningekuwa na uhusiano mzuri na familia ya mume wangu hasa mama yake. 

Mwanzoni kila kitu kilionekana sawa. Tuliongea vizuri, tulicheka pamoja, na nilihisi nimepokelewa vizuri ndani ya familia. Lakini kadri muda ulivyopita, mambo yakaanza kubadilika polepole.

Kulianza kuwa na kutokuelewana kwa mambo madogo madogo. Wakati mwingine nilihisi kama kila nilichofanya hakikuwa sawa machoni pake. 

Nikipika, kulikuwa na kasoro. Nikifanya jambo nyumbani, kulikuwa na maoni ya kuniumiza. Mwanzoni nilijitahidi kuvumilia nikidhani ni hali ya kawaida.

Lakini kadri miezi ilivyopita, hali ilizidi kuwa ngumu. Ilifika hatua hatukuweza hata kukaa sehemu moja kwa amani. Tulikuwa tunasalimiana kwa lazima tu. 

Kila ziara yake nyumbani ilikuwa inaniletea stress. Wakati mwingine nilikuwa hata naogopa kuzungumza ili nisije nikasema kitu kitakacholeta ugomvi mwingine.SOMA ZAIDI.
Maisha yetu yalikuwa ya kawaida lakini yenye amani. Mimi na mume wangu tulikuwa tunajitahidi pamoja kujenga familia yetu. Haikuwa maisha ya utajiri mkubwa, lakini tulikuwa tunatosheka na kile tulichokuwa nacho.

Kisha ghafla kila kitu kilibadilika. Siku moja mume wangu alirudi nyumbani akiwa kimya sana. Nilijua kuna kitu hakikuwa sawa.

Baadaye alinieleza kuwa alikuwa amepoteza kazi. Kwa kweli ilikuwa habari nzito kwetu.
Mwanzoni tulijaribu kujipa moyo kuwa ni kipindi tu kingepita haraka. Nilimfariji na kumwambia tutapambana pamoja. Lakini kadri wiki zilivyopita bila kazi mpya, mambo yakaanza kuwa magumu. Pesa zilianza kuwa shida.

Bills zilianza kujikusanya, kodi ikaanza kutusumbua, na mahitaji ya watoto yalikuwa yanaendelea kuongezeka. Polepole msongo wa mawazo ukaanza kuingia ndani ya nyumba yetu.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona mume wangu akibadilika. Mtu ambaye zamani alikuwa mchangamfu alianza kuwa mkimya sana.

Mara nyingine alikuwa anakasirika kwa mambo madogo. Alianza kujitenga, na wakati mwingine alikuwa anakaa peke yake kwa muda mrefu bila kuzungumza na mtu. Nyumbani kulianza kupoteza furaha. Tulianza kugombana mara kwa mara kwa sababu ya pressure ya maisha.

Wakati mwingine nilijikuta nikilia kimya usiku nikihofia familia yetu ingeanza kuvunjika kwa sababu ya hali ile. Ilifika hatua nikaanza kukata tamaa. SOMA ZAIDI.

Nilipitia kipindi kigumu sana baada ya kuachwa ghafla bila maelezo ya kueleweka. Mahusiano yetu yalionekana kuwa imara, tulikuwa na mipango ya pamoja, lakini siku moja alibadilika na kuondoka kimya kimya.

Mwanzoni nilijaribu kumtafuta ili kuelewa kilichotokea, lakini hakujibu simu wala ujumbe. Kadri siku zilivyopita, ukimya wake ulizidi kuniumiza.

Nilijikuta nikijiuliza maswali mengi bila majibu, nikitafuta makosa yangu bila kuyapata. Baada ya muda, nilichoka na kuamua kuacha kumfuatilia. 

Nilianza kujikita kwenye maisha yangu kujijenga upya, kurejesha kujiamini kwangu, na kujifunza kuishi bila yeye. Haikuwa rahisi, lakini nilijipa muda wa kupona.

Hata hivyo, ndani yangu bado kulikuwa na sehemu ndogo iliyotamani kujua ukweli wa kilichotokea. SOMA ZAIDI.

Siku ile ilianza kama kawaida, lakini haikuisha kama nilivyotarajia. Nilijikuta nimehusishwa na tukio ambalo sikuwa na uhusiano nalo kabisa.

Ghafla nilikuwa nimeshikiliwa na kuhojiwa kuhusu jambo ambalo sikulifanya. Nilijaribu kueleza ukweli wangu kwa utulivu, lakini ushahidi uliokuwa mbele yao ulikuwa unaonekana kunielekeza moja kwa moja.

Ilikuwa hali ya kutisha sana kuona kila kitu kikigeuka dhidi yangu bila mimi kuwa na njia ya kujitetea kikamilifu.

Siku zilivyopita, presha ilizidi. Nilianza kujiandaa kisaikolojia kwa matokeo mabaya zaidi, hata kama nilijua moyoni kuwa sikuwa na hatia. Familia yangu ilijaribu kunisaidia, lakini hali ilikuwa ngumu.

Baada ya kuona mambo yanaenda upande mbaya, niliamua kutafuta mwongozo wa ziada.SOMA ZAIDI.

 


Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) wameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuharakisha matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kusaidia upatikanaji wa fedha za uwekezaji zitakazochochea utekelezaji wa miradi mbalimbali ya nishati nchini.

Ahadi hiyo imetolewa na Kiongozi wa UNCDF, Pradeep Kurukulasuriya akiwa ameambatana na Kiongozi wa UNDP, Shijeki Komatsubava, wakati wa kikao na Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, jijini Dodoma kwa lengo la kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba amesema Serikali imeendelea kuweka mkazo katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wenye lengo la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanahamia kwenye nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. 

Amesema mwaka 2021 ni asilimia sita tu ya Watanzania waliokuwa wakitumia nishati safi ya kupikia, lakini kutokana na juhudi za Serikali, wadau wa maendeleo na sekta binafsi, kiwango hicho kimeongezeka na kufikia zaidi ya asilimia 28.

“Safari bado ni ndefu na inahitaji uwekezaji mkubwa pamoja na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo ili kufikia malengo tuliyojiwekea,” amesema Mhe. Salome Makamba.

Ameeleza kuwa, Serikali imeelekeza nguvu zaidi katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa wakati mmoja zikiwemo shule, vyuo, hospitali na hata majeshi, huku ikiendelea kutekeleza programu mbalimbali za kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Mhe. Salome Makamba amesema moja ya changamoto kubwa iliyopo ni upatikanaji wa rasilimali za kifedha zitakazowezesha wananchi na taasisi mbalimbali kupata teknolojia za nishati safi ya kupikia kwa urahisi zaidi, hususan katika maeneo ya vijijini ambako matumizi ya kuni na mkaa bado ni makubwa.

Kwa upande wake, Pradeep Kurukulasuriya amesema UNCDF ipo tayari kusaidia Tanzania kuvutia uwekezaji kupitia mifumo ya dhamana za mikopo, ruzuku za uwekezaji na mbinu nyingine za kifedha zinazolenga kupunguza hatari kwa wawekezaji na taasisi za fedha.

Amefafanua kuwa, Taasisi hiyo ina uzoefu wa kusaidia nchi mbalimbali kuvutia uwekezaji mkubwa kupitia mifumo ya ubunifu wa kifedha, ikiwemo matumizi ya dhamana za mikopo na fedha za kaboni, hatua ambayo inaweza kusaidia Tanzania kufikia malengo yake ya nishati safi ya kupikia kwa haraka zaidi.

"UNCDF iko tayari kufanya kazi kwa karibu na Wizara ya Nishati, Wizara ya Fedha pamoja na taasisi za fedha nchini ili kuandaa mpango maalumu wa kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya nishati safi ya kupikia". Amesema “Kurukulasuriya.

Kwa upande wake Shijeki Komatsubava amesema UNDP itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuweka mazingira wezeshi yatakayosaidia kuongeza uwekezaji na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia, hususan kwa wananchi wa maeneo ya vijijini na makundi yenye kipato cha chini.

Katika kikao hicho, pande hizo mbili zilijadiliana fursa za kutumia fedha za kaboni (carbon credits), kuimarisha ushiriki wa taasisi za fedha za ndani pamoja na kuandaa mifumo ya ubunifu wa kifedha itakayosaidia kuongeza upatikanaji wa teknolojia za nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Mhe. Salome ameishukuru UNCDF na UNDP kwa mchango wao katika kujenga uwezo wa wazalishaji wa teknolojia za nishati safi ya kupikia, kuandaa Mkakati wa Mawasiliano wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kubadilisha mitazamo ya wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi.

Pande hizo zimekubaliana kuendelea na majadiliano ya kitaalamu yatakayohusisha Wizara ya Nishati, Wizara ya Fedha, taasisi za fedha na wadau wengine muhimu ili kuandaa mpango wa pamoja wa kuharakisha upatikanaji wa rasilimali za kifedha kwa ajili ya utekelezaji wa agenda ya nishati safi ya kupikia nchini.









Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Selemani Mkomi, akisikiliza maelezo kutoka kwa timu ya wataalamu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), alipotembelea banda la maonesho kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea viwanja vya Chinangali Dodoma

NA EMMANUEL MBATILO, PWANI

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Kati limeteketeza tani 110 za bidhaa hafifu na zilizopigwa marufuku zenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 394 katika zoezi lililofanyika Juni 22, 2026, Mkuranga mkoani Pwani.



Na OWM - TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amazielekeza Halmashauri za wilaya ya Mkinga, Mafia, Mpwapwa, Kondoa, Chamwino, Mtwara, Mtama na Manispaa ya Kigamboni kutumia Bilioni 5.2 za programu ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (Local Climate Adaptive Facility-LoCAL) kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuwanufaisha wananchi.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo leo Juni 22, 2026 jijini Dodoma katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI, mara baada ya kukabidhiwa hundi yenye thamani ya Bilioni 5.2 za kitanzania na Katibu Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) Bw. Pradeep Kurukulasuriya, ambalo linafadhili utelelezaji wa programu ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (LoCAL).

“Katumieni fedha hizi kama zilivyoanishwa kwenye maelekezo ya mradi huu, kama ambavyo tumefanya vizuri katika utekelezaji wa awamu ya kwanza kwenye halmashauri za Chamwino, Kondoa na Mpwapwa,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameeleza kuwa, utekelezaji mzuri wa awamu ya kwanza ya mradi wa LoCAL katika Halmashauri hizo umewezesha kupatikana kwa mradi mpya wa SCALE wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambao unaotekelezwa katika halmashauri 54 nchini.

Katika kuongeza ufanisi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Prof. Shemdoe ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa maendeleo  kujitokeza ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuongeza kuwa milango ya Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI ipo wazi kwa mdau yeyote mwenye nia ya kuwasaidia wananchi kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, Diplomasia ya Uchumi ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndio inayofungua milango ya wadau mbalimbali kuja kushirikiana na Serikali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Mratibu wa Mradi wa LoCAL Wilaya ya Kondoa Bw. Laurence Robert Mogela amesema Halmashauri ya Kondoa imepokea dola za kimarekani 149,043 kwa ajili utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huo, utakaotekelezwa kwenye Kata ya Bumbuta kupitia kilimo cha kisasa kitakachoimarisha usalama wa chakula.

Kwa upande wake, Afisa Mazingira wa Wilaya ya Chamwino Bi. Elizabeth Solwa amesema wananchi wengi wa Wilaya ya Chamwino watanufaika na fedha za mradi wa LoCAL kwani wilaya itapokea milioni 500 kwa ajili ya kutekeleza awamu ya pili ya mradi huo katika kata mbili za Mtamalo na Mvumi Makulu.

Naye, Mratibu wa Mradi wa LoCAL Wilaya ya Mpwapwa Bw. Issa Abdallah Sepanja, amesema wilaya ya Mpwapwa imepokea Shilingi Milioni 491 kwa ajili ya kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa LoCAL ambazo zitatumika katika vijiji vya Godegode na Kitati kuchimba visima vya umwagiliaji na kujenga mfereji wa umwagiliaji wenye urefu wa mita 1200.

 



Na Oscar Assenga, Muheza

MWENGE wa Uhuru 2026 unatarajiwa kuingia Wilaya ya Muheza kesho saa 4:00 asubuhi na kukimbizwa kupitia miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.5, huku viongozi wa wilaya wakitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo.

Mwenge huo utapokewa katika eneo la Kilapura, Kijiji cha Muungano, Kata ya Mlingano na utapitia miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi inayolenga kuboresha maisha ya wananchi wa wilaya hiyo.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya ujio wa Mwenge huo, Mkuu wa wilaya ya Muheza Ayoub Sebabili alisema kati ya miradi saba itakayopitiwa, miwili itazinduliwa rasmi, miwili itawekewa mawe ya msingi na mitatu itatembelewa na kukaguliwa.

Alisema mradi wa kwanza ni Zahanati ya Muungano, ikifuatiwa na mradi wa maji wa Kijiji cha Magoda unaolenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi.

Pia Mwenge wa Uhuru utazindua mabweni ya Shule ya Sekondari Mangenya pamoja na kuweka jiwe la msingi katika darasa jipya linalojengwa kwa ajili ya maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2027.

Mbali na miradi hiyo, viongozi wa mbio za Mwenge watatembelea Klabu ya Wapinga Rushwa ya wanafunzi ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha maadili mema na mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa katika jamii.

Katika kuunga mkono juhudi za serikali za matumizi ya nishati safi, Mwenge wa Uhuru pia utashuhudia utoaji wa mitungi ya gesi kwa wananchi ili kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala na kulinda mazingira.

Ratiba hiyo itahusisha pia uzinduzi wa boksi kalavati katika Kijiji cha Tongwe, Kata ya Tongwe, kabla ya kutembelea kikundi cha vijana wa Kijiji cha Magila, Kata ya Genge, waliopata mkopo wa asilimia 10 kutoka mapato ya halmashauri kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Aidha, Mwenge huo utafungua rasmi Hoteli ya Harvest Inn, mradi wa uwekezaji wa mwananchi wenye thamani ya Sh milioni 950, unaotarajiwa kuongeza fursa za ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya utalii na huduma wilayani Muheza.

Baada ya shughuli za miradi kukamilika, mbio za Mwenge wa Uhuru zitahitimishwa katika viwanja vya Mkesha Jitegemee, ambapo kutafanyika maonesho mbalimbali ya utalii, biashara za wajasiriamali, burudani kutoka kwa wasanii wa ndani na nje ya wilaya pamoja na maonesho ya vipaji vya vijana.

Vilevile, wananchi watapata fursa ya kupatiwa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, maambukizi ya UKIMWI, malaria na masuala mengine ya kijamii yanayogusa maendeleo ya taifa.

Wananchi wa Muheza wametakiwa kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo za Mwenge wa Uhuru, zinazobeba kaulimbiu ya kuhamasisha uzalendo, uwajibikaji na maendeleo ya wananchi.

 

Na Mwandishi Wetu

WAFUGAJI nchini wamefurahishwa na mpango wa matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwenye sekta ya mifugo wakidai kuwa utaleta manufaa makubwa katika masoko na biashara shindani ya mifugo.

Akizungumza baada ya kutembelea banda la Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) katika Maonesho ya Mifugo na Mnada wa Kimataifa yanayofanyika katika Shamba la Mbogo, Chalinze mkoani Pwani, Mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji Tanzania (CCWT), Mrida Mshota, amesema mfumo huo utasaidia kutatua changamoto ya masoko ya mifugo nchini.

Amesema kupitia mpango huo wafugaji watapata fursa ya kujitangaza katika masoko ya kimataifa na kuuza mifugo yao kwa uhakika zaidi.

“Ukiwa na shamba lako na likasajiliwa na serikali sasa unakuwa na uhakika wa kuuza mifugo kwenye masoko makubwa ya kimataifa. Mpango huu ni mzuri na naiomba serikali iweke mkazo mkubwa kuhakikisha unaanza kutekelezwa haraka. Waziri Mkuu tayari alishasema jambo hili lishughulikiwe kwa haraka ili liwe na tija kwa wafugaji,” amesema Mshota.

Aidha, ameishauri Wizara ya Viwanda na Biashara kuweka mikakati madhubuti katika maeneo mbalimbali nchini ili utekelezaji wa mfumo huo uanze kabla ya mwaka huu kuisha.

“Sisi tuna kanda nane, hivyo tukitumia vizuri kanda zote serikali itakwenda kukusanya mapato bila kutumia nguvu kubwa. Kwa sasa utoroshaji wa mifugo ni mkubwa kwani baadhi ya wafugaji wanapeleka mifugo nje ya nchi bila utaratibu rasmi, lakini tukianza kutumia mfumo huu wenye masoko ya uhakika, tatizo hilo litapungua kwa kiasi kikubwa,” amesema.

Naye, Afisa Ubora wa WRRB, Bw. Anatolius Kabyemera, amesema mfumo huo utaleta uwazi katika biashara ya mazao na mifugo, kuongeza ushindani wa bei na kuhakikisha wafugaji pamoja na wakulima wanapata thamani halisi ya bidhaa zao.

Katika hatua inayoonyesha kuongezeka kwa mchango wa wataalamu wa Kitanzania katika majukwaa ya Kimataifa kampeni ya Perterms Consultancy Limited imetangazwa mshindi wa mchango wa Share My Story Initiative ulioandaliwa na Taasisi ya Basel Institute On Governance kupitia Mkutano wa Kimataifa wa Sita wa Hatua za Pamoja (Collective Action).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi akiwa na Mwenyekiti mwenza ambaye ni Naibu Balozi wa Finland Bw. Tomi Lounio, wameongoza Kikao cha Pili cha Bodi ya Usimamizi wa Mradi wa Maendeleo ya Matumizi ya Ardhi, Misitu na Mnyororo wa Thamani(FORLAND).
📍Bagamoyo, Tanzania

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ushauri ya ADEM, Dkt. Hillary A. Dachi, amewasili rasmi chuoni hapo na kuongoza kikao chake cha kwanza tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, ambapo Bodi ilikutana kujadili masuala mbalimbali ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa taasisi na kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu nchini.
Kijana mmoja kutoka familia ya jirani alitoweka ghafla bila kuacha taarifa yoyote. Mwanzoni, familia yake haikuwa na wasiwasi mkubwa. 

Walidhani alikuwa ameenda kwa marafiki au ndugu na angerudi baada ya muda mfupi. Lakini siku zilipopita bila habari zake, hofu ilianza kuongezeka.

Wiki ya kwanza ilipita bila mafanikio. Familia yake ilimpigia simu mara nyingi lakini simu yake ilikuwa haipatikani. 

Walizungumza na marafiki zake, walimuulizia maeneo aliyokuwa akitembelea mara kwa mara, lakini hakuna mtu aliyekuwa na taarifa za uhakika kuhusu alikokuwa.

Kadri siku zilivyoongezeka, huzuni ilitanda katika familia yote. Mama yake alikuwa akilia kila siku huku baba yake akijaribu kuficha maumivu aliyokuwa nayo. 

Kila mtu alitamani kusikia habari yoyote ambayo ingewapa matumaini. Baada ya wiki nne kupita, wengi walikuwa wameanza kukata tamaa.

Tulijaribu njia mbalimbali za kutafuta taarifa zake lakini hakuna kilichoonekana kufanya kazi. Hali hiyo iliwafanya ndugu na marafiki wake kuishi katika wasiwasi mkubwa. SOMA ZAIDI.
Nilikuwa nimekopesha watu mbalimbali fedha kwa miaka kadhaa kwa sababu niliamini katika kusaidiana. Baadhi walikuwa marafiki wa karibu, wengine ndugu, na wengine washirika wa biashara. 

Kila mmoja alikuwa na sababu iliyomfanya ahitaji msaada wa kifedha, na mara nyingi nilijitahidi kuwasaidia kadiri nilivyoweza.

Tatizo lilianza pale muda wa kurejesha fedha ulipofika. Watu waliokuwa wakiniahidi kunilipa ndani ya wiki chache au miezi michache walibadilika ghafla. 

Baadhi walikuwa hawapokei simu zangu, wengine walikuwa wakiahirisha tarehe za malipo kila mara. Kadri muda ulivyopita, kiasi cha fedha nilichokuwa nikidai kiliongezeka.

Nilijikuta nikihitaji fedha hizo kwa ajili ya familia yangu na mipango mingine muhimu, lakini sikuwa na njia rahisi ya kuzipata. 

Wakati mwingine nilisafiri kwenda kukutana na wadaiwa ana kwa ana, lakini bado nilirudi nyumbani bila mafanikio. Hali hiyo ilinivunja moyo sana. SOMA ZAIDI.