Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) pamoja na Menejimenti ya NEEC, tarehe 23 Aprili 2026 walifanya ziara maalum ya kutembelea mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) katika maeneo ya Ntondo mkoani Singida na Sojo mkoani Tabora.

 


๐Ÿ“ŒNi shilingi trilioni 2.53

๐Ÿ“ŒSerikali kuja na mradi wa kuunganisha umeme kwa sh.27,000 katika maeneo ya Mjini yenye sura ya Vijiji

๐Ÿ“ŒMradi wa kuzalisha umeme megawati 2000 kwa makaa ya mawe mbioni

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha kwa kishindo shilingi trilioni 2.53 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Nishati 2026/2027.

Kati ya fedha hizo, Shilingi trilioni 2.46 sawa na asilimia 97.5 ya bajeti yote  imeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 2.5 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Akihitimisha hoja kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2026/2027 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi alilieleza Bunge kuwa Wizara ya Nishati itaendelea kuhakikisha kwamba maono ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi na mwelekeo uliowekwa kwenye Dira 2050 yanatekelezwa kwa vitendo na kwa haraka.

Kutokana na hilo alieleza kuwa lengo lililowekwa kwa Wizara la kuzalisha umeme  wa megawati 8000 ifikapo 2030 litatekelezwa kwani Wizara ya Nishati imeshajipanga kuzalisha kiasi hicho cha umeme huku ikidhamiria kuzalisha megawati 70,000 ifikapo 2050.

"Ili kutekeleza lengo hili tutatumia vyanzo vyote vinavyopatikana kwenye Taifa letu ikiwemo vyanzo vya maji kama vile Malagarasi (49.5MW), Kakono (87MW), Ruhudji (358), Rumakali (222MW),  Jeothemo na makaa ya mawe.." Alisema Mhe. Ndejembi

Akifafanua kuhusu mradi wa uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe, Mhe. Ndejembi alisema Tanzania ina hifadhi kubwa ya makaa hayo na sasa Serikali inashirikiana na Sekta binafsi ili kuhakikisha kuwa inaanza uzalishaji wa megawati zaidi ya 2000 kwa kutumia nishati hiyo.

Aliongeza kuwa miradi mingine  itakayowezesha kufikia lengo la uzalishaji wa megawati 8000 ifikapo 2030 ni pamoja na miradi ya umeme Jua ikiwemo  ya Kishapu, Manyoni, Zuzu, miradi ya upepo ya Same, Makambako pamoja na kuzalisha umeme kwa kutumia urani.

Aidha, Mhe. Ndejembi aligusia suala la kufikisha umeme kwenye maeneo ya wananchi akieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha umeme unatoka kwenye vyanzo vya uzalishaji na kufikia maeneo ya wananchi na ya uzalishaji kama vile migodi viwanda n.k

Katika jitihada hizo za kufikisha umeme kwa wananchi alisema mradi wa kufikisha umeme wa gridi mikoa ya Mtwara na Lindi  kupitia ujenzi wa njia ya umeme ya kV 220 ya Songea- Tunduru- Masasi-Mahumbika unaendelea huku mkandarasi akiwa ameshalipwa shilingi bilioni 83 kwa ajili ya kuendelea na kazi.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Nishati aliiagiza TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) kuwasiliana na Wabunge wote ambao wana maeneo ambayo ni Manispaa/Majiji/ Halmashauri za Mji lakini yana sura ya vijiji ambayo wananchi wake wanalipa zaidi ya shilingi 27,000  kuunganisha umeme ili kuvitambua vijiji hivyo na kuja na mradi utakaohakikisha  wananchi katika vijiji hivyo wanaunganishiwa umeme kwa shilingi 27,000 tu ndani ya mwaka mmoja. 

" Serikali hii ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu na haiwezi kuweka matabaka ya wananchi, mtu amekaa ng'ambo moja analipa 27,000 na ng'ambo nyingine analipa 320,000 hili halikubaliki, Serikali imesikia changamoto hii na inaifanyia kazi, tutahakikisha umeme unawaka katika vijiji ambavyo vipo ndani ya miji." Alisema Mhe. Ndejembi

Kuhusu suala la kufikisha umeme kwenye Taasisi kama vile shule, zahanati n.k aliitaka REA kufanya tathmini ili kutambua taasisi ambazo hazijapelekewa umeme katika vijiji vyenye umeme ili ziweze kuunganishiwa.

Aidha, kuhusu suala la mafuta alisema kufungwa kwa mlango  bahari wa Hormuz kunaleta changamoto kubwa ya upatikanaji mafuta duniani kwani asilimia 20 ya nishati ya mafuta inatoka katika mlango bahari huo lakini kutokana na Serikali ya Tanzania kujali wananchi wake, nchi ina mafuta ya kutosha na hakuna kituo ambacho kimefungwa kwa kukosa nishati hiyo tofauti na baadhi ya maeneo mengine duniani.

Vilevile kuhusu bei ya mafuta alieleza kuwa Serikali inafanya kila jitihada ili ziwe himilivu huku ikihakikisha mafuta yanapatikana muda wote na  hifadhi mpya ya mafuta inayojengwa jijini Dar es Salaam eneo la Kigamboni ikitoa hakikisho la uhifadhi wa mafuta.

Vilevile alieleza kuwa, ili kurahisisha upatikanaji wa mafuta katika maeneo mbalimbali  nchini Serikali inajenga bomba la kusafirisha mafuta safi kutoka Dar es Salaam hadi Ndola, Zambia litakokuwa na matoleo na matenki ya kuhifadhi mafuta katika mikoa ya Morogoro, Njombe na Songwe na hivyo kupunguza msongamano jijini Dar es Salaam na kuondoa mzigo barabarani.

Katika Gesi Asilia, Mhe. Ndejembi alisema Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linafanya kazi kubwa kuhakikisha Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia inazidi kuimarika na sasa Shirika hilo linaendelea na miradi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa bomba la gesi la km 34 kutoka Ntorya hadi Madimba, wanachimba kisima kingine cha gesi katika eneo la Mnazi Bay ambacho kimeonekana kina hifadhi kubwa ya gesi mara mbili ya makisio ya awali, vilevile Shirika hilo linaendelea na  utafutaji wa mafuta katika kitalu cha Eyasi Wembere.

Aidha kuhusu mradi mkubwa wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika ( LNG)  alisema kuwa kwa sasa Serikali imefikia hatua za mwisho kuweza kuanza mradi na kwamba makubaliano ya kibiashara na kikodi yamekamilika na hatua inayoendelea sasa ni makubaliano ya kisheria.

Aliongeza kuwa, katika mradi wa LNG tayari  kuna kazi ambazo tayari zimeshaanza kama vile ulipaji fidia na ujenzi wa shule ya Likong'o.

Ili kuhakikisha wazawa wanashiriki ipasavyo katika mradi wa LNG alisema Serikali imeielekeza TPDC  kwenda mkoa wa Lindi kutoa elimu ya fursa zitakazopatikana huku Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) ikitakiwa kuwajengea uwezo wazawa ili mradi utakapoanza waweze kushiriki katika nyanja  mbalimvali ikiwemo utoaji wa huduma. ‎<This message was edited>

 


-Moshi, Kilimanjaro

Katika hatua kubwa inayolenga kuleta mapinduzi kwenye soko huria na kumlinda Mlaji. Mamlaka ya Ushindani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCA) zimekutana Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro leo Aprili 23, 2026 na kuwaapisha rasmi wajumbe wapya wanne kutoka Nchi za Tanzania, Somalia, Uganda na DRC ambao watasimamia mazingira mazuri ya ushindani wa biashara na walaji kwa Jumuiya hiyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewataka waajiri na wafanyakazi nchini kuyatazama upya mazingira ya kazi ili kuhakikisha yanakuwa salama na rafiki kwa afya, hususan afya ya akili.

Na Oscar Assenga, Tanga

Katika kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia duniani, Shule ya Sekondari Coastal High School imetangaza mpango kabambe wa kuanzisha programu ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) ifikapo Januari 2027.

Mpango huo unalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kisasa utakaowawezesha kushindana katika soko la ajira la Kimataifa.

Akizungumza wakati wa mahafali ya Kidato cha Sita yaliyofanyika jijini Tanga, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Isack Dastan Kifwete  alisema kuwa tayari wameanza kuchukua hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa mpango huo.


Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kufanikisha upatikanaji wa huduma ya intaneti kupitia Kampuni ya TTCL, pamoja na kuwepo kwa mtaalamu wa TEHAMA shuleni hapo.

Hata hivyo, alibainisha kuwa bado kuna changamoto kadhaa zinazokwamisha utekelezaji wa mpango huo kwa ufanisi unaohitajika.

Alizitaja changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vifaa muhimu kama kompyuta za kisasa, ubao janja (smart board), pamoja na miundombinu ya chumba maalumu kitakachotumika kufundishia programu ya AI.

Mbali na hilo, shule pia ina mpango wa kuanzisha programu ya Habari na Mawasiliano ya Umma, unaolenga kuwajengea wanafunzi uwezo wa uandishi wa habari, mawasiliano, pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa katika tasnia ya habari.

Tayari maandalizi ya awali, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya studio, yameanza kufanyika.

Pamoja na jitihada hizo, Mwalimu Mkuu alieleza kuwa shule bado inahitaji vifaa muhimu ili kukamilisha studio hiyo.

Vifaa vinavyohitajika ni pamoja na kamera za kisasa, meza ya matangazo, vifaa vya kuzuia kelele, vinasa sauti, vipaza sauti pamoja na kompyuta zenye uwezo wa kisasa.

Aidha, alitaja changamoto nyingine zinazoikabili shule kuwa ni pamoja na baadhi ya wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati kutokana na hali ngumu ya kiuchumi, pamoja na ushiriki mdogo wa wazazi na walezi katika masuala ya kitaaluma na malezi ya wanafunzi.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule umetoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia jitihada hizo ikiwemo kuwaomba wadau msaada wa vifaa kwa ajili ya kuanzisha studio ya habari, pamoja na kuunganishwa na taasisi au watu binafsi wanaoweza kusaidia upatikanaji wa kompyuta za kisasa.

Kwa ujumla, mpango huu unaonesha dhamira ya dhati ya shule katika kuwajengea wanafunzi msingi imara wa elimu ya kisasa ili kuwaandaa kukabiliana na dunia inayoendeshwa na teknolojia kwa kasi kubwa.

Awali, akizungumza katika mahafali hayo,Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar (CCM), Ussi Salum Pendeza, alisema kuwa atashirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha baadhi ya changamoto zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka.

Alisema kuwa ataanza mwenyewe kuchangia upatikanaji wa baadhi ya vifaa muhimu, ikiwemo kompyuta za kisasa na ubao janja, sambamba na kuhamasisha wadau wengine kushiriki.

“Katika hili la ubao janja na baadhi ya kompyuta, nitaanza mimi mwenyewe. Pia nitahakikisha michango inapatikana na kuwashirikisha wengine. Nachukua nafasi hii kuwashukuru walimu na Bodi ya Shule ya Coastal kwa ushirikiano wao katika kuhakikisha shule inafanya vizuri na matokeo yanakuwa mazuri,” alisema.

Ussi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Taasisi ya Pendeza Foundation, alisema anajivunia kuiongoza shule hiyo na ameahidi kuendelea kuisimamia ili iweze kufanya vizuri zaidi na kujulikana kitaifa.

Baraza kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) limekutana kujadili na kuweka mwelekeo wa vipaumbele vya Mamlaka kuelekea mwaka wa fedha 2026/2027, likilenga kuimarisha utoaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi.
Naibu Katibu Mkuu (Taaluma) Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt. Mwanakhamis Ameir (kulia) na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha (kushoto) wakisaini mkataba maalum kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya elimu visiwani Unguja na Pemba.

 



#Ataka kazi zikamilike ifikapo Mei 2027

Arusha

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara zinazoingia katika uwanja utakaotumika kwa mashindano ya AFCON jijini Arusha.

Mhandisi Seff amesema kwamba ziara hiyo imelenga kujionea hatua za utekelezaji wa mradi wa barabara zenye urefu wa kilomita 21.4 ambapo kazi tayari zimeanza katika sehemu ya barabara ya Essuri.

Amesema serikali imejipanga kuhakikisha miundombinu hiyo inakamilika kwa wakati na kuongeza kuwa maeneo ambayo bado hayajaanza yanasubiri kukamilisha taratibu za fidia kwa wananchi watakaoathiriwa na mradi huo huku mkakati ukiwa ni kuendelea kuzungumza nao ili kutoa ushirikiano na kuruhusu kazi ziendelee bila vikwazo.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha barabara hizi zinakamilika ifikapo Mei mwaka 2027 ili ziwe tayari kabla ya mashindano ya AFCON,” amesema Mhandisi Seff.

Aidha, amesema mradi huo unatekelezwa kwa utaratibu wa Sanifu na Jenga (Design and Build) unaotumika pale ambapo muda ni mchache huku hatua zote za ununuzi tayari zikikamilika.

Ameeleza kuwa TARURA itaendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha mkandarasi anakamilisha kazi kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa sanjari na ratiba ya mashindano hayo makubwa ya Mataifa ya Afrika.

Ameongeza kuwa kwa sasa Mkandarasi M/s China Railway Construction Engineering Group tayari ameanza kazi ambapo ameanza na barabara ya Essuri yenye urefu wa kilomita 2.45 pia kutajengwa daraja lenye urefu wa mita 100.

Kwa upande wa barabara ya Lendita yenye kilomita 2.75, Mhandisi Seff amesema barabara hiyo itajengwa pamoja na daraja katika awamu ya pili ya mradi huku barabara hiyo ikitarajiwa kuwa ya njia nne.

Ameongeza kusema pia barabara ya Mateves yenye kilomita 6.5 itajengwa kwa sehemu mbili ambapo kilomita 5.5 zitakuwa njia mbili na kilomita 1 itakuwa njia nne.

Mtendaji Mkuu huyo amesema kukamilika kwa mradi huo kutaleta mafanikio makubwa kwa Taasisi hiyo kwa kupata uzoefu wa kusimamia miradi ya Sanifu na Jenga, huku wananchi wakinufaika kwa kuondokana na changamoto ya miundombinu katika maeneo hayo.

Vilevile, amesema wakazi wa maeneo yanayozunguka mradi huo watapewa kipaumbele cha ajira na amewataka vijana kujitokeza kupata ajira na kutumia fursa hiyo kujiongezea kipato pamoja na uzoefu wa kazi.

Kwa upande mwingine amewataka wasimamizi wa mradi huo kusimamia kwa karibu utekelezaji wake kwani mashindano hayo yanatarajiwa kuanza Julai mwakani.

Naye, Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya M/s Afrisa Construction Engineering Group Bw. Idephonce Karol amesema mradi huo ulianza rasmi tarehe 1 Aprili, 2026 na kwa sasa hatua za awali zinaendelea vizuri.

Amesema tayari wamehamasisha timu ya wataalamu, kufanya upimaji wa maeneo yote matatu ya barabara, uchunguzi wa udongo, tathmini ya vifaa vya ujenzi pamoja na kusafisha sehemu ya barabara ya Essuri urefu wa kilomita 1.8.

“Tumejipanga kikamilifu na tunafahamu umuhimu wa mradi huu hivyo tutafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha unakamilika kwa wakati,” amesema Karol.














Na Oscar Assenga,TANGA

MKURUGENZI wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani Segule Segule amewataka wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kauli hiyo ameitoa baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.



Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.



Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.



Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.



Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.

Wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Onyo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Segule Segule, baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.

Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.

Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekabidhi tuzo kwa Mkoa wa Njombe ikiwa ni Mshindi wa Jumla wa Shindano la Afya na Usafi wa Mazingira kwa Mwaka 2024.

WITO umetolewa kwa viongozi wa Serikali za Mitaa nchini kuimarisha ushirikiano na Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mifuko ya Elimu ya Halmashauri ili kuongeza kasi ya maendeleo ya sekta ya elimu.
Afisa Masoko wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Bw. Fihiri Mbawala, akitoa ufafanuzi kwa Bi. Rauhya Omary, muuzaji wa duka la pembejeo za mifugo la Manispaa ya Lindi, tarehe 22 Aprili 2026, kuhusu mbinu bora za kuhakikisha mazingira ya uhifadhi wa chanjo yanazingatia viwango vinavyotakiwa ili kudumisha ubora na ufanisi wake, wakati wa ziara ya utoaji elimu ya matumizi sahihi ya chanjo zilizofanyika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Moremi Marwa akifungua Mkutano Maalumu wa Baraza la Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam uliofanyika leo Aprili 22, 2026  Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius  Ndejembi, akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, leo, tarehe 22 Aprili 2026, Bunge jijini Dodoma.

....

Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kuimarisha usimamizi na udhibiti wa shughuli za bidhaa za mafuta ya petroli nchini, hatua inayolenga kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa nishati, usalama wa miundombinu pamoja na ubora wa huduma kwa wananchi.Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo Aprili 22,2026 bungeni Dodoma. Akieleza mafanikio ya utekelezaji huo hadi Machi 2026, EWURA imefanikiwa kutoa jumla ya leseni 636 kwa biashara mbalimbali katika sekta ndogo ya mafuta na gesi. Leseni hizo zinahusisha vituo vya mafuta mijini na vijijini, maghala ya kuhifadhia mafuta, pamoja na biashara ya usambazaji na uuzaji wa gesi ya kupikia (LPG) na vilainishi. "Takwimu zinaonesha kuwa vituo vya mafuta mijini vimeongoza kwa kupata leseni nyingi zaidi, huku pia juhudi zikielekezwa katika maeneo ya vijijini ili kupanua huduma na kuongeza upatikanaji wa nishati kwa wananchi wa maeneo hayo. Hatua hii inaakisi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha huduma za mafuta zinawafikia wananchi wote bila kujali maeneo yao."amesema Mhe.Ndejembi Katika kuimarisha miundombinu ya sekta hiyo, EWURA pia ilitoa vibali 288 vya ujenzi wa miundombinu ya mafuta, ambapo vibali 137 vilihusu maeneo ya mijini na 143 vijijini. Vibali vingine vilihusisha maghala ya kuhifadhi mafuta na gesi, pamoja na miundombinu ya matumizi ya viwandani na migodini. Sambamba na utoaji wa leseni na vibali, EWURA imeendelea kusimamia kwa karibu taratibu za uagizaji na usambazaji wa mafuta nchini. Katika ukaguzi wa ubora wa bidhaa, jumla ya sampuli 648 zilipimwa, ambapo sampuli 608 sawa na asilimia 93.83 zilikidhi viwango vinavyotakiwa. Vituo 22 vilivyobainika kuuza mafuta yasiyokidhi viwango vilichukuliwa hatua za kisheria, ikiwemo kufungiwa na kutozwa faini. Aidha, ukaguzi wa miundombinu ya mafuta ulifanyika katika vituo 544, ambapo asilimia 86.95 ya miundombinu hiyo ilikidhi viwango vya ubora, ikiwa ni pamoja na masuala ya afya, usalama na mazingira. Wamiliki wa vituo 95 ambavyo havikukidhi vigezo walielekezwa kufanya maboresho ili kuendana na viwango vilivyowekwa. Kwa ujumla, hatua hizi zinaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha sekta ya mafuta inakuwa salama, yenye ufanisi na inachangia kikamilifu katika ukuaji wa uchumi wa Taifa, huku ikilinda maslahi ya watumiaji na mazingira.

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius  Ndejembi, akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, leo, tarehe 22 Aprili 2026, Bunge jijini Dodoma.

..

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imekagua jumla ya vituo 672 vya mafuta kote nchini katika jitihada za kuimarisha udhibiti wa ubora wa mafuta na kulinda maslahi ya watumiaji.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo Aprili 22,2026 bungeni Dodoma.

Katika ukaguzi huo, vituo 50 sawa na asilimia 7.44 vilibainika kuuza mafuta yasiyokidhi viwango vilivyowekwa, hatua iliyochochea mamlaka hiyo kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika. Hatua hizo zilijumuisha kufungiwa kwa vituo husika, kutozwa faini pamoja na kuwasilishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kulipa kodi walizokwepa.

Mbali na ukaguzi wa ubora, EWURA pia ilifanya operesheni maalum ya kufuatilia mwenendo wa usambazaji wa mafuta, ambapo ilibaini vituo vitatu vilivyokuwa vimeficha mafuta kwa makusudi vikisubiri mabadiliko ya bei. Serikali ilichukua hatua za haraka kwa kuvifungia vituo hivyo na kutoa adhabu kwa mujibu wa sheria zilizopo.

Hata hivyo amesema kuwa Serikali imeendelea kuimarisha usimamizi wa sekta ya mafuta nchini kupitia utekelezaji wa programu ya uwekaji vinasaba kwenye mafuta, hatua inayolenga kudhibiti ubora wa bidhaa hiyo pamoja na kuhakikisha ukusanyaji sahihi wa mapato ya kodi.

Amesema  Kupitia EWURA utekelezaji wa mpango huo umeonesha mafanikio makubwa kufikia Machi 2026, ambapo jumla ya lita bilioni 1.51 za petroli na lita bilioni 2.02 za dizeli ziliwekewa vinasaba. Kiasi hicho kinaonesha ongezeko la asilimia 14 kwa petroli na asilimia 10 kwa dizeli ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka wa fedha 2024/25.

Hata hivyo, kwa upande wa mafuta ya taa, kiasi kilichowekewa vinasaba kilifikia lita milioni 2.80, ikiwa ni pungufu la asilimia 40, hali inayotafsiriwa kuwa na mabadiliko ya mwenendo wa matumizi au usambazaji wa bidhaa hiyo sokoni.

Hatua hizi zinaakisi dhamira ya Serikali ya kuhakikisha sekta ya mafuta inasimamiwa kwa uwazi na ufanisi, huku ikihakikisha haki kwa watumiaji na kuongeza mapato ya Taifa. Aidha, juhudi hizo zinasaidia kudhibiti vitendo vya udanganyifu vinavyoweza kuhatarisha uchumi na ustawi wa wananchi.

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius  Ndejembi, akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, leo, tarehe 22 Aprili 2026, Bunge jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna,Mzalendo blog-DODOMA

Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kuimarisha usimamizi na udhibiti wa shughuli za gesi asilia katika mkondo wa kati na chini, hatua inayolenga kuhakikisha usalama wa miundombinu, upatikanaji wa huduma bora pamoja na kukuza matumizi ya nishati safi nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 leo Aprili 22,2026 bungeni Dodoma.

Amesema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, EWURA ilifanya kaguzi 68 katika miundombinu ya gesi asilia iliyopo katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam. Miundombinu hiyo inahusisha mitambo minne ya uchakataji, miwili ya usafirishaji, mtandao wa usambazaji wenye urefu wa kilomita 243 pamoja na vituo 18 vya kujazia gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) kwa magari. Taarifa zinaonesha kuwa miundombinu yote iliyokaguliwa ilikidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa.

Katika kuendeleza sekta hiyo, EWURA ilitoa vibali tisa vya ujenzi wa vituo vya CNG katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Ruvuma. Maeneo yaliyopata vibali katika mkoa wa Dar es Salaam ni pamoja na Mbezi Beach, Mbagala, Kigamboni, Buguruni, Mwenge, Kinyerezi na Gongolamboto, huku Morogoro (Msamvu) na Ruvuma (Tunduru) kila mmoja ukipata kibali kimoja.

Aidha, vibali viwili vilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kupokelea gesi asilia iliyoshindiliwa kwa matumizi ya viwanda vilivyopo Kibaha mkoani Pwani, hatua inayotarajiwa kuongeza matumizi ya nishati hiyo katika uzalishaji wa viwandani.

Katika sekta ya usafirishaji na usambazaji, EWURA ilitoa vibali saba vya ujenzi wa mabomba ya gesi asilia, ikiwemo mabomba ya kuunganisha gesi kwenye viwanda, taasisi, migahawa na majumbani, pamoja na mabomba ya kuhudumia vituo vya CNG. Kibali kingine kilihusu ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Ntorya hadi Madimba mkoani Mtwara.

Sambamba na hilo, jumla ya leseni 17 zilitolewa kwa ajili ya uendeshaji na usafirishaji wa gesi asilia, zikiwemo leseni za vituo vya CNG na usambazaji wa gesi katika mkoa wa Pwani. Ongezeko la utoaji wa vibali na leseni linaonesha mwitikio mkubwa wa sekta binafsi kushiriki katika mnyororo wa thamani wa gesi asilia.

Serikali imeeleza kuwa itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuvutia wawekezaji zaidi katika sekta hiyo, hasa katika mikoa ya kimkakati kama Morogoro, Dodoma, Mbeya na Tanga. Wito umetolewa kwa sekta binafsi kuchangamkia fursa zilizopo, kufuatia ongezeko la matumizi ya gesi asilia katika usafiri, viwandani na matumizi ya majumbani.

Hatua hizi zinaakisi dhamira ya Serikali ya kuhakikisha gesi asilia inakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi, huku ikichangia upatikanaji wa nishati safi, nafuu na salama kwa wananchi.

Na Mwandishi wetu Itigi, Singida

Timu kutoka Uganda ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii, Wanyamapori na Malikale Bi. Doreen S. Katusiime yafanya ziara ya mafunzo Itigi.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameibuka na hoja nzito wakichangia bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), wakitaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupewa mamlaka kamili pamoja na rasilimali za kutosha ili liweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imetoa seti 200 za mitungi ya Oryx kwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono Mpango wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekutana na kuzungumza na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam Aprili 21, 2026.