Timu ya mpira wa miguu ya Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Sports Club imefanikiwa kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Championship msimu ujao 2026/2027 baada ya kufuzu kwa kupata sare ya goli 1-1 dhidi ya klabu ya African Sports kutoka Mkoani Tanga
Akizungumza baada ya kutamatika kwa mchezo Kocha Mkuu wa IAA SC Zulkifri Iddi amewapongeza wachezaji wake kwa kuipatia timu matokeo na kuthibitisha kuwa walifanikiwa kufuata maelekezo aliyowapa ndani ya dakika zote tisini, huku akiupongeza Uongozi wa Chuo IAA kwa sapoti kubwa walioitoa iliyopelekea kuandika historia hii kubwa kwa taasisi na jiji la Arusha
Akitoa pongezi Mwenyekiti wa mashindano chama cha soka Mkoa wa Arusha Emmanuel Antony ameisifu IAA SC kwa kuandika historia hii kubwa na kukiheshimisha chama cha soka Mkoa wa Arusha na kuahidi ushirikiano kwa timu kuhakikisha inafanya vizuri na kupiga hatua zaidi ili kufika hatua ya kushiriki Ligi kuu ya Tanzania
Kwa upande wake mchezaji wa IAA SC ambaye ndiye Mfungaji wa goli pekee la timu amewapongeza wachezaji wenzake, benchi la ufundi na Uongozi wa Chuo pamoja na mashabiki wao kwa kushirikiana kufanikisha kufikia mafanikio haya makubwa na kuahidi kuendelea kuipambania nembo ya IAA na jiji la Arusha msimu ujao kwenye mashindano ya Championship
IAA SC katika safari yake ya mafanikio haya ilifanikiwa kuibuka washindi wa ligi ya Wilaya ya Arusha, Ligi ya Mkoa, Ligi ya mabingwa wa Mikoa yote Tanzania na baadae Ligi daraja la pili (First League) na leo imefanikiwa kufuzu kutinga katika ligi daraja la kwanza (Championship) msimu wa mwaka 2026/2027

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika jengo la Kituo cha Polisi cha Kata ya Masasi, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.
Jengo hilo limejengwa na Bw. Iman Haule kupitia KUAMBIANA INVESTMENT COMPANY LIMITED ikiwa ni sehemu ya mchango wa sekta binafsi katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya usalama na kusogeza huduma za kipolisi karibu na wananchi.
Mhe. Naibu Waziri Mahundi amepongeza hatua hiyo, akieleza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya usalama unachangia kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao, kuongeza upatikanaji wa haki na kuleta mazingira wezeshi kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Wataalamu waanza kuwanoa wanafunzi, walimu na maafisa elimu kukabiliana na matokeo duni ya mitihani

Na Oscar Assenga, Tanga
MATOKEO duni ya mitihani ya Taifa katika baadhi ya shule za sekondari za Serikali jijini Tanga yameibua hatua mpya za kuwanufaisha wanafunzi kupitia mafunzo maalumu yanayolenga kuongeza ufaulu kwa kuwajengea uwezo wa kujifunza kwa ufanisi na kujiandaa vizuri kwa mitihani.
Mafunzo hayo yanatekelezwa na Taasisi ya Tanzania Centre for Education (TCE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Botnar foundation na Inovex kupitia mradi wa Tanga Yetu, unaohusisha shule 10 zilizobainika kuwa na changamoto ya matokeo hafifu kwa wanafunzi.
Akizungumza wakati wa kuanza kwa mafunzo hayo katika Shule ya Sekondari Nguvumali, Mkurugenzi Mtendaji wa TCE, Yusuf Ogutu, alisema kuboresha ufaulu ni hatua muhimu ya kuinua ubora wa elimu na kuwawezesha wanafunzi kufikia ndoto zao za kitaaluma na maisha ya baadae.

Alisema wanafunzi wengi hufanya mitihani bila kuelewa kwa kina mfumo wa maswali ya umahiri, uzito wa mada na mbinu sahihi za kujibu, hali inayochangia kushuka kwa matokeo licha ya kufundishwa darasani.
"Ndiyo maana tumeamua kuja na mafunzo haya ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa kuelewa, badala ya kukariri. Tunawafundisha namna ya kuchambua muhtasari wa masomo, kutambua mada zinazotiliwa mkazo katika mitihani na kuelewa matumizi ya vitenzi vinavyotumika katika maswali," alisema.
Aliongeza kuwa wanafunzi pia wanapatiwa mbinu za kupanga muda wa kujisomea, namna ya kujiandaa kabla,wakati na baada ya mtihani, jinsi ya kujibu maswali kwa ufanisi na namna ya kujitathmini baada ya kufanya mtihani.
Ogutu alisema mafanikio ya wanafunzi hayawezi kupatikana kwa juhudi za mwanafunzi pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa walimu, wazazi, viongozi wa elimu na wadau wa maendeleo.

"Tunataka kujenga utamaduni wa ufaulu. Mwanafunzi akielewa namna ya kujifunza na mwalimu akapata mbinu bora za kumwelekeza, matokeo mazuri yatapatikana," alisema.
Mbali na mafunzo hayo, alisema taasisi hiyo imeanza kufanya utafiti katika shule zote 27 za sekondari za Serikali za Jiji la Tanga ili kubaini sababu zinazochangia kushuka kwa ufaulu katika mitihani ya Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.
Alisema matokeo ya utafiti huo yatawezesha wadau wa elimu kuweka mikakati ya muda mrefu ya kuboresha ubora wa elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule za Serikali.

Kwa upande wake, Mratibu wa Elimu Kata ya Nguvumali, Lilian Shetua, alisema mafunzo hayo yanawasaidia wanafunzi kuendana na mahitaji ya mtaala ulioboreshwa unaowataka kuwa wabunifu, wachambuzi na wenye uwezo wa kutumia maarifa katika kutatua changamoto.
Alisema wanafunzi wengi wamekuwa wakifanya mitihani bila kuelewa muundo wake, lakini kupitia mafunzo hayo wanapata uelewa wa namna ya kujiandaa na kujibu maswali kwa kuzingatia matakwa ya Baraza la Mitihani.
"Ni matarajio yetu kwamba elimu hii itabadilisha mtazamo wa wanafunzi na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule yetu na nyingine zinazoshiriki mradi huu," alisema.

Naye Inspekta wa Polisi wa Kata ya Nguvumali, Sharifu Kiswamba, alisema pamoja na jitihada za kuboresha elimu, bado utoro wa wanafunzi na tabia ya kuzurura mitaani wakati wa masomo vinaendelea kuwa kikwazo kikubwa.
Aliwataka wazazi kuongeza usimamizi wa watoto wao na kushirikiana na walimu pamoja na viongozi wa kata ili kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria masomo na kutumia muda wao kujifunza.

Kwa upande wake, mwalimu wa Shule ya Sekondari Nguvumali, Venosa Massawe, alisema mafunzo hayo yamekuja wakati mwafaka kwani yanawasaidia walimu na wanafunzi kutafsiri kwa usahihi matakwa ya mtaala ulioboreshwa.

Hata hivyo, alisema mazingira magumu ya maisha ya baadhi ya wanafunzi, ikiwamo umaskini, malezi yasiyo ya karibu na changamoto za lishe, bado ni miongoni mwa sababu zinazochangia kushuka kwa kiwango cha ufaulu.

Alisema ushirikiano wa Serikali, wazazi, walimu na wadau wa maendeleo utaendelea kuwa nguzo muhimu katika kujenga mazingira bora ya kujifunza na kuongeza idadi ya wanafunzi wanaofaulu kwa viwango vya juu katika mitihani ya taifa.



Maisha yanaweza kuwa katili sana, hasa unapoona wadogo zako uliowasomesha wanakupita kimaendeleo wakati wewe umeshikilia karatasi za chuo zinazoliwa na mchwa. Mimi naitwa Mariam, mzaliwa wa Ilemela, jijini Mwanza.
Nilihitimu shahada yangu ya Uhasibu (Accounting) kwa kiwango cha juu, lakini mtaani niligeuka kuwa mtu wa dharau. Nilifikia hatua ya kukaa pembeni ya barabara nikisaidia mama yangu mdogo kushona viatu vya kimasai ili tu nipate mlo wa mchana.
Kila usaili niliokwenda, nilikuwa naonekana sifai, au nafasi inachukuliwa na mtu mwenye kujuana na wakubwa. Umri wangu wa kuelekea miaka 30 ulinifanya nikose amani; kila ndugu aliyeniona aliniuliza “Lini unaolewa?” au “Kazi mbona hupati?”. SOMA ZAIDI.
Kila asubuhi nilikuwa nawasha redio kubwa dukani kwangu ili kuvutia wateja, lakini watu walikuwa wakipita na kusikiliza muziki tu kisha wanaenda kununua kwa jirani yangu ambaye duka lake lilikuwa dogo na chafu.
Hali hii ilinitesa sana kisaikolojia. Nilianza kuonekana mwanaume niliyefeli mbele ya mke wangu na ndugu zangu, kwani kila mwezi nilikuwa nakopa pesa ya kulipa kodi ya pango. Nilihisi nina nuksi ya ajabu inayowafukuza watu wenye pesa na kuvuta watazamaji tu.
Nilijaribu kila mbinu; nilishusha bei hadi ya hasara, nilifanya matangazo kwa gari la spika mitaani, na hata kutoa zawadi kwa kila aliyenunua bidhaa, lakini wapi! Duka langu lilikuwa kama limepakwa dawa ya kufukuza watu. Nilikaribia kukata tamaa na kuuza kila kitu nikawe kondakta wa daladala.
Siku moja nilisafiri kwenda kijijini kwetu kwa ajili ya mazishi ya ndugu. Nikiwa nimekaa na wazee wa busara chini ya mwembe, tulianza kuzungumzia changamoto za kimaisha mjini. Mzee mmoja ambaye alikuwa ni rafiki wa marehemu, alinifuata pembeni na kuniambia, “Erick, kijana wangu, unahangaika bure na mbinu za kizungu. SOMA ZAIDI.
Nilijitosa kwenye michezo ya kubashiri (betting) nikiamini ndiyo njia pekee ya kuninasua kwenye umaskini, lakini badala yake niliishia kuwa ombaomba. Nilifikia hatua ya kulala kwenye mabenchi ya stendi ya mabasi baada ya kufukuzwa kwenye chumba nilichokuwa nimepanga kwa kukosa kodi ya miezi sita.
Kila nikiangalia umri wangu ukikaribia miaka 35, nilihisi moyo wangu unapasuka. Nilikuwa naona vijana wadogo wakishinda mamilioni kwenye betting, lakini mimi hata nikiweka mkeka wa timu mbili tu, lazima moja ingeharibu.
Nilihisi kuna kitu kimejifunga kwenye maisha yangu, maana hata bahati ndogo ya kuokota shilingi mia barabarani haikuwahi kunitokea. Nilikata tamaa kabisa na kuanza kuhisi labda nimerogwa na ndugu zangu wasiotaka nifanikiwe.SOMA ZAIDI.
Akizungumza na wananchi, Mbunge Mariam amesema mchango huo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na wananchi pamoja na wadau mbalimbali katika kuhakikisha shule hiyo inakamilika. Na OWM–TAMISEMI, Lilongwe, Malawi
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri wa Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe (SONGWECOM) kilichofanyika Julai 10, 2026 jijini Lilongwe, Malawi, kwa lengo la kujadili kuharakisha utekelezaji wa Mradi wa Maendeleo wa Bonde la Mto Songwe.
Mradi huo unatarajiwa kujengwa kwa pamoja na Serikali za Tanzania na Malawi na kuzalisha umeme wa megawati 180.2, huku ukiwa na manufaa makubwa katika sekta za umwagiliaji, usambazaji wa maji, uvuvi, utalii pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa nchi hizo mbili.
Kikao hicho kilijadili hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi, ikiwemo kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati, kwa manufaa ya wananchi wa pande zote za Bonde la Mto Songwe.
Miongoni mwa viongozi waliohudhuria kikao hicho ni Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde, Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola, pamoja na Naibu Waziri, Mhandisi Kasper Kasper Mmuya, na wataalamu mbalimbali kutoka Serikali za Tanzania na Malawi.
Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe (The Joint Songwe River Basin Commission – SONGWECOM) linaundwa na Mawaziri kumi kutoka Tanzania na Malawi wanaowakilisha sekta tano muhimu ambazo ni Maji, Nishati, Kilimo cha Umwagiliaji, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), pamoja na Ardhi, ndilo chombo cha juu cha maamuzi kinachosimamia shughuli za Kamisheni hiyo.
Kupitia kikao hicho, Tanzania na Malawi zimeendelea kudhihirisha dhamira ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika usimamizi endelevu wa rasilimali za Bonde la Mto Songwe, kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa nishati, kuimarisha usalama wa maji na chakula, na kuchochea maendeleo endelevu ya wananchi wa mataifa hayo mawili.






















.jpeg)
.jpeg)










