Habari njema kwa watumiaji wa mafuta nchini. Kuanzia Jumatano, tarehe 01 Julai 2026, bei kikomo za bidhaa za petroli zimeshuka kutokana na kupungua kwa bei za mafuta katika soko la dunia.
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, imesema kutokana na kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia, bei za mafuta katika soko la hapa nchini zinashuka kwa Shilingi 96 kwa lita ya petroli, Shilingi 151 kwa lita ya dizeli na Shilingi 242 kwa lita ya mafuta ya taa.
Kushuka huku kunatokana na mabadiliko katika soko la dunia, ikiwemo makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Marekani na Iran kuhusu vita inayoendelea eneo la Mashariki ya Kati, pamoja na kuruhusu meli za mafuta kupita katika Mlango Bahari wa Hormuz. Hatua hizo zimechangia kupunguza ugumu katika usafirishaji na upatikanaji wa mafuta duniani.
Hata hivyo, wastani wa bei katika soko la dunia bado haujarejea katika kiwango kilichokuwepo kabla ya kuanza kwa vita hiyo tarehe 28 Februari 2026.
. _Amshukuru Rais Samia kwa kuwezesha upatikanaji wa magari hayo_
. _Ataka magari hayo yasaidie kukuza utalii na ufuatiliaji wa mapato_
. _Aelekeza Halmashauri kushirikiana na TAWA, TANAPA na wadau wa utalii kukuza utalii_
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumanne Juni 30, 2026 amekabidhi magari mawili ya usimamizi na ufuatiliaji wa Utalii na mapato kwa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha upatikanaji wa magari hayo mawili yenye jumla ya thamani ya Shilingi 440,611,400.
Mhe. Makalla amekabidhi magari hayo wakati wa ziara yake Wilayani Monduli, akiagiza matumizi sahihi na yaliyokusudiwa kwa magari hayo ikiwa ni pamoja na kusaidia katika kukuza utalii Wilayani Monduli pamoja na ufuatiliaji na ukusanyaji wa mapato ya serikali.
Katika hatua nyingine, Mhe. Makalla akisisitiza kuhusu ukuzaji wa utalii Mkoani Arusha, ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Monduli kushirikiana na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na wadau wengine wa utalii katika kukuza utalii Wilayani Monduli sambamba na kuhifadhi vivutio vya utalii vilivyopo Wilayani Monduli.
Magari yaliyokabidhiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser Hardtop (5 door) likiwa na gharama ya Shilingi 235, 606,600 na Toyota Land Cruiser (Pick up) likiwa na gharama ya Shilingi 205, 004,800 pamoja na pikipiki aina ya Yamaha YBR iliyotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii, vyote kwa pamoja vikitajwa kuongeza chachu ya ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2026/27 na kuhakikisha doria za maliasili zinafanyika kikamilifu.
Awali katika maelezo yake Afisa mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bw. Jeofrey Mwambasi amemshukuru Rais Samia na Uongozi wa Halmashauri hiyo kwa kuwezesha kupatikana kwa magari hayo, akiahidi kuwa Halmashauri hiyo itayatunza magari na pikipiki hiyo pamoja na kuhakikisha yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na serikali katika ukusanyaji wa mapato pamoja na uhifadhi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema ameridhishwa na kiwango cha utekelezaji wa maelekezo yake ya Januari, 2026 ya kutaka kukamilishwa kwa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro ifikapo Julai 26, 2026.
Prof. Shemdoe amesema hayo Juni 29, 2026 mjini Morogoro, wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani humo ambayo ni sehemu ya muendelezo ufuatiliaji wa utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa ya ukamilishaji wa miradi ya mbalimbali ya maendeleo, yakiwepo ya utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro.
“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa nimepata faraja kuona maendeleo ya ujenzi wa jengo hili lilofikia asilimia 90, Mhe. Mkuu wa Mkoa nikupongeze kwa ufuatiliaji na RAS kwa usimamizi wako mzuri,” ameeleza Prof. Shemdoe.
Kutokana na hatua nzuri ya ujenzi iliyofikiwa, Prof. Shemdoe amemtaka Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Musa, kuhakikisha watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wanahamia katika jengo jipya la ofisi hiyo ndani ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2026/27.
Aidha, Prof. Shemdoe amemsisitiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Musa kuhakikisha lifti inaletwa na kuwekwa kwa wakati, ikiwa ni pamoja na kufanya maandalizi ya kupata samani mpya zitakazotumiwa na watumishi wa ofisi hiyo.
Kufuatia uwekezaji uliofanywa, Prof. Shemdoe amesema kwamba jengo hilo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa likikamilika, litakuwa limetumia bilioni 6.5 hivyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji huo mkubwa aliofanya kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa mkoa wa Morogoro.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema atasimamia utekelezaji wa maelekezo ya Prof. Shemdoe na kufafanua kuwa maelekezo hayo yanapaswa kutekelezwa na ofisi yake kabla ya tarehe 30 Septemba 2026 saa sita usiku na si ifikapo Septemba 30, 2026.
Jengo hilo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro linajengwa na Mkandarasi MCB Company LTD, Mbeya University of Science and Technology kwa usimamizi wa Mshauri Elekezi ambaye ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini.
Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini.
Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini ili Tanzania kuwa kitovu za usambazaji wa bidhaa hiyo barani Afrika.
“Lengo letu ni kuona wachimbaji wakubwa na wadogo hapa nchini wanapata bidhaa nyingi za kuzalisha madini pasipo kutegemea uagizwaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi," amesema Mavunde.
Naye, Mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Oriental Casting and Forging Ltd Bw. Hou Songcun amesema Kampuni yake ipo tayari kufanya uwekezaji mkubwa wa bidhaa za migodini nchini kwa kuwa Tanzania ni nchi ambayo ina mazingira mazuri ya uwekezaji na kwamba sekta ya madini inakua kwa kasi kubwa sana hivyo ni sehemu salama na rafiki ya kufanya uwekezaji ambao utakuwa suluhisho la upatikanaji wa bidhaa za migodini kwa urahisi zaidi.
Wengine walianza kuniambia niache kufikiria kwenda nje ya nchi kwa sababu labda haikuwa riziki yangu. Lakini ndoto yangu ya kuishi na kufanya kazi nje ya nchi ilikuwa kubwa kuliko maneno ya watu. Kila kukataliwa kuliniumiza moyo. Nilianza kupata msongo wa mawazo na hata kukosa usingizi.
Nilihisi kuna kitu kisicho cha kawaida kilichokuwa kinanizuia. Nilianza kuamini labda kuna watu walionionea wivu na kunifungia njia. Nilijaribu mara ya nne kuandaa nyaraka lakini nilihisi hofu na woga mkubwa. SOMA ZAIDI.
Alionekana kunionea wivu kwa jinsi nilivyokuwa nafanya kazi vizuri na nilipata sifa kutoka kwa wafanyakazi wenzangu. Kila mradi nilipewa nilifanya kwa bidii, lakini kila mara alitafuta kosa dogo la kunilaumu mbele ya wenzangu.
Aliniweka kwenye shinikizo kubwa na aliniandikia barua ya onyo mara mbili kwa sababu ambazo hazikuwa na msingi. Nilihisi kama alitaka niachishwe kazi. Wafanyakazi wenzangu walinionea huruma lakini hakuna aliyethubutu kumkabili.
Nilianza kupoteza amani ya moyo. Kila asubuhi nilipokuwa nikiamka nilihisi kuchoka hata kabla ya kuingia ofisini. Niliwaza kuacha kazi lakini nilijua singeweza kumudu maisha bila kipato. Nilihitaji njia ya kubadilisha hali hii. SOMA ZAIDI.
Wageni walipoingia nyumbani waliona sura za hasira na kukaa kwetu pamoja mezani kuligeuka uwanja wa vita.
Nilipojaribu kuzungumza na baba yangu hakutaka kunisikiliza. Mama alionekana amekata tamaa na ndugu zangu walikimbilia marafiki zao kila jioni ili wasikae nyumbani.
Nilikuwa tayari kufanya lolote ilimradi amani irudi.SOMA ZAIDI.
Nilizaliwa katika familia iliyokumbwa na changamoto nyingi. Baba na mama walikuwa wakigombana mara kwa mara, na hata nilipokuwa mtu mzima, nilijikuta pia nikipitia matatizo kama hayo.
Watu wengi walinipa ushauri tofauti, wengine wakisema labda nilikuwa nimekumbwa na nuksi. Nilihisi nimeelemewa sana na niliamini labda maisha yangu yalikuwa yameandikwa kuwa ya mateso. Wengi walisema uchawi ni hatari, kwamba mtu akikimbilia huko anajiletea matatizo zaidi.
Kwa muda mrefu niliepuka hata kusikia neno hilo. Lakini nilipofikia hatua ya kukata tamaa kabisa, nilianza kutafuta njia mbadala. SOMA ZAIDI.
Mwanamke aliyenishitaki alijua fika hakuwa na ushahidi wowote. Lengo lake lilikuwa kunilazimisha nimpe pesa nyingi ili kunyamazisha kesi.
Nilihisi moyoni kuwa ningepoteza kila kitu iwapo ningekubali uongo huo. Nilipoamua kusimama mahakamani, wengi waliniona kama mtu wa kujitakia maafa.
📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba
📌 Kukamilika kwake kutaongeza ufanisi wa uzalishaji na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani
Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji.
Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.
Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani.
“Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi,” amesema Mhe. Ndejembi.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usambazaji Umeme TANESCO, Mhandisi Timoth Mgaya, amesema mradi huo unagharimu dola za Kimarekani milioni 24.81, sawa na takribani shilingi bilioni 64, na hadi sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji.
“Mradi huu unagharimu dola milioni 24.81 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 64. Hadi sasa utekelezaji umefikia asilimia 83, na tunaendelea kushirikiana na mkandarasi kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika ndani ya muda uliopangwa,” amesisitiza Mhandisi Mgaya.
Mradi wa ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho, kuboresha utegemevu wa uzalishaji wa umeme na kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika kwa wananchi.
Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale ni kituo cha kwanza cha kuzalisha umeme kwa kutumia maji nchini. Kilijengwa kati ya mwaka 1961 na 1964 na kina uwezo wa kuzalisha takribani megawati 21. Ukarabati unaoendelea unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho ili kiendelee kutoa mchango mkubwa katika Gridi ya Taifa kwa miaka ijayo.
📌Yasema ni matunda ya uzalendo wa Watanzania katika kulipa kodi
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi mzuri wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ikieleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 ambao umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na kuwa miongoni mwa miradi mikubwa barani Afrika.
Hayo yamebainishwa leo Juni 29, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu (Mb), wakati wa ziara ya Kamati hiyo katika Mradi wa Kufua Umeme wa JNHPP uliopo Rufiji, mkoani Pwani, kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo.
"Sisi kama Kamati tumeridhishwa na kazi kubwa iliyofanyika katika mradi huu hadi kukamilika kwake kwani mradi huu umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na unachangia takribani asilimia 45 ya umeme kwenye Gridi ya Taifa. Hivyo, nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza utekelezaji wa mradi huu wa kimkakati ambao umeleta suluhisho la kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini," amesema Mhe. Mgalu.
Aidha, Mhe. Mgalu amewashukuru wananchi kwa kulipa kodi ambazo zimepelekea mradi huo mkubwa kukamilika huku akisisitiza kuwa Kamati itaendelea kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa umeme wa uhakika wakati wote.
Amefafanua kuwa umeme unaozalishwa na JNHPP utaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme kupitia miradi mbalimbali ya usafirishaji wa umeme ikiwemo mradi wa Chalinze–Dodoma.
Vilevile, Mhe. Mgalu amesisitiza kuhusu kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuhakikisha umeme unaopatikana nchini unafika hadi ngazi ya vitongoji.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Umeme, Mhandisi Christopher Bitesigirwe, amesema ziara ya Kamati imelenga kujionea maendeleo ya mradi huo na imejiridhisha kuwa mitambo yote tisa imekamilika na inafanya kazi vizuri huku akiwahakikishia kukamilisha kwa wakati miradi yote ya usafirishaji na usambazaji wa umeme inayounganishwa na JNHPP.
Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Antony Mbushi, amesema TANESCO itaendelea kuhakikisha Kituo cha Kufua Umeme cha JNHPP kinaendeshwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwajengea uwezo wataalam wa Kitanzania wanaokisimamia ili kiendelee kuzalisha umeme wa uhakika kwa manufaa ya wananchi na maendeleo ya Taifa.























































