Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mkutano mkuu wa wanahisa wa Afrika50 na jukwaa la miundombinu Afrika, Agosti 03, 2026, Ofisi za Wizara ya Fedha, jijini Dar es salaam.

TANZANIA itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), yatakayofanyika Agosti 5 na 6, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Dar es Salaam.

Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mwenyeji na mwenyekiti wa hafla ya ufunguzi wa mkutano huo, ambao pia utahusisha taasisi mbalimbali za umma na sekta binafsi nchini, benki za biashara na maendeleo, taasisi za hifadhi ya jamii, masoko ya mitaji na wadau wa sekta za nishati, uchukuzi, reli, bandari, usafiri wa anga, maji, afya, madini, mafuta na gesi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, leo Septemba 03, 2026  Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema mkutano huo wa kimataifa unafanyika wakati Africa50 inatimiza miaka 10 tangu kuanza shughuli zake mwaka 2016, huku ukitarajiwa kukutanisha washiriki zaidi ya 1,200 kutoka Afrika na maeneo mbalimbali duniani.

Balozi Omar amesema Africa50 ilianzishwa mwaka 2013 kwa ushirikiano wa Serikali za Afrika na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ikiwa na lengo la kuharakisha maandalizi, uendelezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya miundombinu kupitia ubia kati ya Serikali na sekta binafsi katika sekta za nishati, uchukuzi, afya, elimu, TEHAMA na huduma za kifedha.

Amesema Tanzania ilijiunga rasmi na Africa50 Februari 14, 2023 kama mwanahisa wa kundi la “A” (African Sovereign States), hatua iliyopanua fursa za nchi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na ufadhili wa miradi mikubwa ya miundombinu.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, tangu kujiunga na taasisi hiyo, Tanzania imeanza kunufaika kupitia maandalizi ya miradi ya kimkakati ikiwemo maendeleo ya Bandari ya Mangapwani Zanzibar, Mradi wa Mini Liquefied Natural Gas (Mini LNG), miundombinu ya usafirishaji wa umeme na upanuzi wa huduma za usafishaji wa figo (dialysis) kupitia ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP).

Mkutano wa mwaka 2026 unafanyika chini ya kaulimbiu isemayo “A Decade of Economic Impact: From Ambition to Delivery.”

Balozi Omar amesema katika kipindi cha siku mbili za mkutano kutakuwa na Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50, Jukwaa la Miundombinu Afrika na hafla za kusaini makubaliano mbalimbali ya maandalizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya miundombinu.

Amesema kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo, Tanzania itapata fursa ya kuendelea kujitangaza kama kitovu cha uwekezaji na maendeleo ya miundombinu Afrika Mashariki, kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na taasisi za fedha za kimataifa, pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika miradi ya kimkakati yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

“Serikali inawahakikishia wananchi kuwa maandalizi yote yanaendelea vizuri kwa ushirikiano na Africa50 pamoja na taasisi mbalimbali za Serikali ili kuhakikisha mkutano huo unafanyika kwa mafanikio makubwa,” amesema Balozi Omar.

Ameongeza kuwa Serikali inawakaribisha wananchi kuendelea kutoa ushirikiano na kuwapokea wageni watakaofika nchini kwa ajili ya mkutano huo, ambao unatarajiwa kuwa miongoni mwa mikutano mikubwa ya kimataifa itakayofanyika nchini mwaka 2026.


 

Kusoma kwa miaka mingi na kupata shahada ya chuo kikuu ni hatua inayokupa matumaini makubwa ya kupata ajira nzuri na kujenga maisha yako. Baada ya kumaliza masomo yangu miaka mitano iliyopita, nilianza harakati za kuomba kazi za serikali na kwenye taasisi kubwa.

Nilikuwa na sifa zote zilizohitajika, viwango vya juu vya taaluma, na uwezo mkubwa wa kujieleza. Hata hivyo, maisha yangu ya utafutaji yaligeuka kuwa mfululizo wa maumivu na kukata tamaa kulikoingia akilini.

​Kila mara nilipoomba kazi, nilipita kwenye usahili wa mchujo (interview) kwa alama za juu sana. Lakini ajabu ni kwamba, ilipofika hatua ya mwisho ya kutoa majina ya waliopata ajira, jina langu lilipotelea hewani au kutupwa kimyakimya!

Watu niliowazidi uwezo na alama walikuwa wakichukuliwa, huku mimi nikibaki mtaani nikichekwa na kusaidiwa chakula na wazazi wangu.

Nilifanya usahili zaidi ya mara kumi na tano katika miaka hiyo mitano, lakini kila mara nilibaki ukingoni mwa mafanikio. Nilibaki nikijiuliza ni kwanini elimu na juhudi zangu hazikuwa zikizaa matunda.SOMA ZAIDI.

 

Kujenga nyumba ya kifahari na kuweka msingi imara wa maisha ni hatua inayompa kila mtafutaji heshima kubwa. 

Baada ya kufanya kazi kwa bidii ughaibuni na kuwekeza akiba yangu yote, nilipata kiwanja kizuri na kuanza ujenzi wa nyumba kubwa ya ghorofa moja kwa ajili ya familia yangu.

Mwanzo kila kitu kilienda kwa kasi na matumaini makubwa. Hata hivyo, mara tu kuta zilipoinuka na kuanza kuonekana kwa majirani na ndugu, vita vya chini kwa chini vilianza bila mimi kutarajia.

​Ujenzi ulianza kukumbana na ajali na mikosi isiyoelezeka. Mafundi bora niliowakodi walianza kuugua ghafla pindi tu walipokanyaga kwenye eneo la mradi, wengine wakipata majeraha ya ajabu na kukimbia kazi.

Vifaa vya ujenzi kama simenti na nondo vilikuwa vikiharibika au kupotea kimyakimya, na pesa nilizokuwa nikituma zilipotea kwenye dharura zisizotabirika.

Kumbe bila mimi kujua, baadhi ya ndugu zangu wa damu waliokuwa wakijifanya kunipongeza kwa nje, ndio waliokuwa wakizunguka usiku kufanya fitina na matambiko ya giza ili mradi wangu ufe na nifilisike!SOMA ZAIDI.

 


Kila mwanamume anapofikisha umri fulani na kufanikiwa kijamii, hamu yake kubwa ni kupata mke mwema wa kujenga naye familia na kuendeleza maisha.

Nikiwa na umri wa miaka 32, nikiwa na kazi nzuri na nyumba yangu mwenyewe, nilijiona nipo tayari kabisa kuoa.

Hata hivyo, maisha yangu ya mahusiano yaligeuka kuwa fumbo la kutisha na lenye kuumiza moyo kwa zaidi ya miaka minne.

Kila mara nilipompata binti mstaarabu, mwenye tabia njema na tukakubaliana kuoana, mambo yalianza kubadilika ghafla pindi tu alipokanyaga mlangoni kwangu.

Binti ambaye jioni tulikuwa na amani na furaha tele, ikifika usiku alipatwa na hofu isiyoelezeka, ndoto za kutisha za kuingiliwa na majitu, au maumivu makali ya mwili.

Ndani ya siku chache au wiki moja pekee, kila binti alifunganya virago vyake na kukimbia nyumba yangu huku akisema hawezi kuendelea kuishi pale.

Zaidi ya wasichana sita tofauti waliondoka kwa mtindo huo huo bila mimi kufanya kosa lolote, jambo lililonifanya nianze kuonekana kama mwanamume aliyelaaniwa au mwenye nuksi ya ajabu. SOMA ZAIDI.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ametembelea Banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) akiwa ameambatana na Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mhe. John Malechela, Nzuguni – Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafadh Ameir, amesisitiza nafasi muhimu ya wanawake wanataaluma katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026, Naibu Waziri amesema kuwa kauli mbiu ya hafla hiyo, “The Contribution of Women Professionals to the Implementation of Tanzania Development Vision 2050”, imeakisi mchango wa wanawake katika kujenga uchumi wa maarifa, ubunifu na teknolojia.

Ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu. Hatua zilizotekelezwa ni pamoja na maboresho ya sera na sheria, ujenzi wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika ufundishaji na ujifunzaji.

Aidha, amesisitiza kuwa mchango wa wanawake hauwezi kupuuzwa na kwamba Serikali ikiendelea kuimarisha usawa wa kijinsia, kuongeza ushiriki wa wanawake katika fani za STEM, kuzuia ukatili wa kijinsia na kuwekeza katika maendeleo ya kitaaluma ya walimu na wahadhiri kupitia mafunzo endelevu na tafiti.

Naibu Waziri ametoa wito kwa walimu, wakufunzi na wahadhiri kuendelea kuwa chachu ya mabadiliko ya Taifa kwa kuandaa kizazi chenye maadili, maarifa na ubunifu.

“Mustakabali wa Taifa upo mikononi mwa vijana na wanafunzi,” amesisitiza, akiwataka kutumia kikamilifu fursa za elimu zinazotolewa na Serikali ili kuleta suluhisho kwa changamoto za kijamii na kiuchumi." amesema Naibu Waziri

Naye Mbunge Viti Maalum Mwakilishi wa Vyuo Vikuu, Mhe. Asha Feruzi, amesema kuwa hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026 ni jukwaa la kujadili mustakabali wa elimu, ubunifu na teknolojia katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mhe. Feruzi amebainisha kuwa matokeo yanayotarajiwa kupitia ushirikiano huo ni kuimarika kwa tafiti, ubunifu na matumizi ya teknolojia za kisasa, hususan akili unde (Artificial Intelligence). Ameongeza kuwa vyuo vikuu na sekta binafsi vitaunganishwa ili kuzalisha suluhisho, bidhaa na huduma zinazochochea ukuaji wa uchumi shindani na endelevu.

 

Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limetangaza fursa 12 zitakazotokana na Tanzania kuwa mwenyeji mwenza wa Mashindano ya Mataifa ya Afrika AFCON 2027 ambazo zitafungua zaidi milango ya maendeleo ya uchumi, ajira, biashara, utalii na uwekezaji nchini.

Akizungumza kuhusu fursa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa BMT, Bw. Aminiel Aligaesha, amesema AFCON 2027 ni tukio la kihistoria litakalofanyika kwa mara ya kwanza Ukanda wa Afrika Mashariki na likiwa linatimiza miaka 70 mwakani tangu kuanzishwa kwake.

Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, fursa ya kwanza ni kuongezeka kwa biashara na shughuli za kiuchumi, ambapo hoteli, nyumba za kulala wageni, migahawa, maduka pamoja na wauzaji wa bidhaa zenye nembo za mashindano watanufaika kutokana na ongezeko la wageni na mashabiki.

Aidha, amesema sekta ya benki na huduma za kifedha itanufaika kupitia ongezeko la miamala ya kifedha, huduma za kubadilisha fedha za kigeni, udhamini wa matukio na utoaji wa bidhaa maalum za kifedha kwa wafanyabiashara watakaohudumia wageni.

Katika upande wa ajira, Bw. Aligaesha amesema vijana watapata nafasi za kazi katika sekta za ukarimu, usafiri, utalii, teknolojia, uandishi wa habari, uzalishaji wa maudhui na huduma nyingine, hali itakayowaongezea uzoefu wa kufanya kazi katika mazingira ya kimataifa.

Pia ametaja sekta ya usafiri kuwa miongoni mwa zitakazonufaika kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya usafiri wa anga, nchi kavu na majini, ikiwemo safari za ndani, huduma za teksi, mabasi, usafiri wa mtandaoni na vifurushi maalum vya safari za AFCON vinavyoweza kujumuisha utalii na malazi.

Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, AFCON 2027 pia itachochea maendeleo ya soka nchini kwa kuhamasisha uwekezaji katika akademi za vijana, ukocha, urefa na ukuzaji wa vipaji, huku sekta ya afya ikitarajiwa kunufaika kupitia utoaji wa huduma kwa wageni na kukuza utalii wa afya kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali.

Amesema mashindano hayo yatatoa jukwaa la kutangaza utamaduni wa Tanzania kupitia muziki, vyakula, sanaa, mavazi na lugha ya Kiswahili, sambamba na kuitangaza Tanzania (national branding) kwa mamilioni ya watazamaji duniani kupitia televisheni, mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya kimataifa.

Kuhusu sekta ya utalii, Bw. Aligaesha alisema wageni watakaokuja kushuhudia mashindano hayo watapata nafasi ya kutembelea vivutio mbalimbali ikiwemo Serengeti, Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro na Zanzibar, jambo litakaloongeza mapato ya sekta hiyo.

Ameongeza kuwa maandalizi ya AFCON tayari yamechochea maboresho makubwa ya miundombinu ikiwamo ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, ujenzi wa viwanja vipya Arusha na kule Zanzibar, pamoja na uboreshaji wa barabara, viwanja vya mazoezi na mifumo ya huduma za kidijitali ambayo itaendelea kutumika hata baada ya mashindano hayo kumalizika.

Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, mafanikio ya maandalizi na uendeshaji wa AFCON 2027 yataifanya Tanzania kuwa kitovu cha michezo barani Afrika, huku yakifungua milango ya kuandaa mashindano mengine ya kimataifa, kuvutia wawekezaji na kukuza uchumi wa michezo.

Aidha, amesema mashindano hayo yataimarisha diplomasia ya michezo na ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na kuimarisha uhusiano wa kikanda katika biashara, utalii, utamaduni na uwekezaji.

Akihitimisha, Bw. Aligaesha amewataka Watanzania kuendelea kufuatilia taarifa za BMT, akieleza kuwa utaratibu rasmi wa namna wananchi na wadau watakavyoweza kushiriki na kunufaika kupitia fursa hizo utatangazwa baadaye mwaka huu.

"Tunatoa wito kwa wananchi, wafanyabiashara na wadau wote kuanza kujiandaa mapema. AFCON 2027 ni mwanzo wa ukurasa mpya wa maendeleo ya michezo na uchumi wa michezo nchini, na muda si mrefu tutatangaza utaratibu wa namna fursa hizi zitakavyopatikana," amesisitiza Bw. Aligaesha

 

MC Mzungu Mweusi na Neema Naftari


Mwandishi wa habari na mshereheshaji maarufu nchini, Amos John, maarufu kama MC Mzungu Mweusi, ameanza rasmi maisha mapya ya ndoa baada ya kufunga ndoa takatifu na mpenzi wake, Neema Naftari, katika Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, Manispaa ya Shinyanga.

Ibada ya ndoa iliyofanyika Jumamosi, Agosti 1, 2026, ilihudhuriwa na ndugu, jamaa, marafiki, viongozi wa dini, Washereheshaji, waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali waliofika kushuhudia tukio hilo muhimu na kuwaombea wanandoa hao baraka katika maisha yao mapya.

Baada ya ibada hiyo, sherehe ya awali ilifanyika nyumbani kwa bwana harusi katika eneo la Kizumbi, Manispaa ya Shinyanga, kabla ya wageni kuelekea kwenye hafla ya mapokezi iliyofanyika katika Ukumbi wa Makindo Hotel, ambapo kulikuwa na burudani, pongezi na shamrashamra zilizoakisi furaha ya siku hiyo ya kipekee.

MC Mzungu Mweusi amejizolea heshima kubwa kupitia taaluma yake ya uandishi wa habari na umahiri wake wa kusherehesha matukio mbalimbali ya kitaifa na kijamii. 

Umahiri wake wa kuwasiliana na watu, uchangamfu na weledi wake vimemfanya kuwa miongoni mwa washereheshaji wanaoheshimika na kupendwa na wengi, hususan katika Kanda ya Ziwa na maeneo mengine nchini.

Mbali na taaluma yake, Amos John amekuwa akishiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na maendeleo, jambo lililomjengea taswira ya kiongozi mwenye moyo wa kujitolea na kuigusa jamii kupitia kazi zake.

Siku hiyo imebaki kuwa kumbukumbu muhimu kwa familia, marafiki na wadau wake, waliotumia nafasi hiyo kuwapongeza wanandoa hao na kuwatakia maisha marefu ya ndoa yenye upendo, amani, umoja na mafanikio.

Hongera Amos John (MC Mzungu Mweusi) na Neema Nasari kwa hatua hii muhimu ya maisha. Mungu awabariki na kuwaongoza katika safari yenu mpya ya ndoa.