Na Lusungu Helela, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini.

Mhe. Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi Jama Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo.

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mhe. Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao.

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho, Mhe.Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia.

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira.

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.








Hakuna jaribu zito kimaisha kama kukabiliwa na tuhuma za uongo mahakamani, ambazo si tu kwamba zinatishia kukupotezea uhuru wako, bali pia zinaharibu kabisa heshima na hatima ya familia yako.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia mateso makubwa ya kisheria na kisaikolojia. Jirani yangu mmoja aliyekuwa na wivu na chuki binafsi alishirikiana na watu wenye ushawishi kutunga kesi nzito ya bandia dhidi yangu, wakinituhumu kwa makosa ya ujambazi wa kutumia silaha na uharibifu wa mali.

​Kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani, mashahidi wa uongo walipangwa kwa umahiri mkubwa na ushahidi wa kughushi uliwasilishwa ili kuhakikisha ninahukumiwa kifungo cha miaka ishirini jela.

Kila nilipohudhuria vipindi vya mahakama, niliona jinsi haki yangu ilivyokuwa ikikandamizwa. Nilitumia fedha nyingi kulipa mawakili mbalimbali, lakini kila hatua tuliyopiga, hakimu na waendesha mashitaka walionekana kupendekeza upande wa walionishtaki.

Nilibaki nikikabiliwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikishindwa kulala usiku, huku mke wangu na watoto wangu wakilia kila siku wakihofia kunipoteza kwa miaka mingi jela. SOMA ZAIDI.
Kila mwanamke anapoingia kwenye ndoa, tamani lake kubwa ni kubeba mtoto wake mwenyewe mkononi na kushuhudia furaha ya familia ikikua. Hata hivyo, pale miaka inapopita bila kupata mtoto, ndoa hugeuka kuwa chungu na chenye machozi yasiyoisha.

Kwa zaidi ya miaka kumi ndani ya ndoa yangu, nilipitia mateso makubwa ya kisaikolojia na kijamii. Nilitengwa na ndugu wa mume wangu, wakinibeza na kunipa majina ya kejeli kama “tasa” na “mwanamke asiye na faida.”

​Kila mkutano wa familia ulipofanyika, nilionekana kama kiumbe kisicho na thamani. Mume wangu, ambaye mwanzoni alikuwa akinipenda sana, anza kubadilika taratibu; alianza kuchelewa kurudi nyumbani, kunipazia sauti, na hata kutishia kumleta mwanamke mwingine nyumbani ili amzalie watoto.

Nilitembelea madaktari bingwa mbalimbali wa afya ya uzazi na kutumia dawa nyingi za hospitali, lakini vipimo vyote vilionyesha sina tatizo lolote linaloonekana. Nilibaki nikilia usiku kucha na kuomba miracle, nikiona ndoa yangu ya miaka kumi ikienda kuvunjika kabisa. SOMA ZAIDI.
Kujenga maisha na mume wako kwa miaka mingi ni safari inayohitaji juhudi, uvumilivu, na upendo wa dhati. 

Hata hivyo, pale msiba unapotokea na mume wako kufariki dunia, kisha ndugu zake wanapogeuka kuwa maadui na kukuvua kila kitu ulichokipigania, maisha hugeuka kuwa jehanum ya papo hapo.

Baada ya mume wangu kufariki ghafla, nilijikuta kwenye mateso makubwa yasiyoelezeka. Wajomba na kaka zake walipanga safu ya kunivua haki zote za ujane.

​Siku chache tu baada ya mazishi, ndugu hao walivamia nyumba yetu ya familia, wakachukua nyaraka zote za viwanja, magari, na kadi za benki, kisha wakaniamuru niondoke mimi na watoto wangu wawili wadogo bila kubeba kitu chochote.

Kila nilipojaribu kutafuta msaada wa kisheria na serikali za mitaa, ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuziba mianya yote na kunitishia maisha yangu na ya watoto wangu.

Nilibaki nikilia kwa uchungu na simanzi nzito, nikiwa hana hifadhi wala kipato cha kulisha watoto wangu, huku nikitazama jasho la mume wangu likifaidiwa na watu waliomtelekeza wakati wa uzima wake. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Viongozi wapya wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) wameapishwa rasmi jijini Dar es Salaam, huku wakitakiwa kusimamia Katiba ya chama, kulinda maslahi ya wanachama na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uwajibikaji na mshikamano.

Uapisho huo umefanyika leo, Agosti 26, 2026, katika hafla iliyowakutanisha viongozi wa chama, wanachama pamoja na wageni mbalimbali, ikiwa ni hatua muhimu ya kuanza rasmi kwa kipindi kipya cha uongozi wa TAPSEA.

Akizungumza wakati wa kuwaapisha viongozi hao, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, aliwataka viongozi hao kuzingatia Katiba ya TAPSEA na kuitumia kama msingi wa kuwaongoza wanachama pamoja na kufanya maamuzi yenye maslahi kwa chama.
Mhe. Kiswaga amesema uongozi wa chama unahitaji umakini, hekima na uwezo wa kusimamia tofauti zinazoweza kujitokeza miongoni mwa wanachama, akisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuhakikisha changamoto zinatatuliwa kwa kufuata Katiba na taratibu zilizowekwa.

Amesema TAPSEA ni chama kikubwa chenye wajibu wa kuwatumikia wanachama wake, hivyo viongozi wapya wanapaswa kuwa imara katika kutetea na kusimamia maslahi yao, huku wakihakikisha chama kinaendelea kukua na kufikia malengo yaliyowekwa.

“Niwaombe viongozi mnapotoka hapa mkasimamie vyema Katiba yenu ili kuweza kuondoa migogoro itakayojitokeza,” amesema Kiswaga.
Aidha, Mhe. Kiswaga amewataka viongozi hao kuwa mfano kwa wanachama katika utekelezaji wa majukumu yao, akieleza kuwa uongozi bora hujengwa kupitia uwazi, ushirikishwaji na kuheshimu taratibu zinazokubalika ndani ya chama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa TAPSEA, Leah Mwamba, amewashukuru wanachama kwa kumpa dhamana ya kuwaongoza na kuahidi kufanya kazi kwa kushirikiana nao ili kuhakikisha chama kinafikia malengo yake.

Mwamba amesema tukio la uapisho ni hatua muhimu katika safari ya uongozi wa TAPSEA na kwamba dhamana waliyopewa viongozi hao inahitaji ushirikiano wa wanachama pamoja na wadau mbalimbali.
“Ninatoa shukrani zangu za pekee kwa wote walioungana nasi katika historia hii. Jambo hili la uapisho ni kubwa sana, hivyo tunaomba mzidi kutuombea tufanye vyema katika uongozi,” amesema Mwamba.

Amesema uongozi mpya utaendelea kusikiliza maoni ya wanachama na kutafuta njia zitakazosaidia kuimarisha umoja, mshikamano na maendeleo ya chama, huku ukizingatia majukumu na wajibu uliowekwa kupitia Katiba ya TAPSEA.

Naye Katibu Mkuu wa TAPSEA, Hellen Magati, amewashukuru wageni na wadau waliohudhuria hafla hiyo, akiahidi kuwa uongozi mpya utashirikiana na wanachama katika kutekeleza majukumu yake.
Magati amesema ushirikiano wa viongozi na wanachama ni muhimu katika kuhakikisha mipango ya chama inatekelezwa kwa ufanisi na changamoto zinazojitokeza zinapata ufumbuzi kwa wakati.

Amesisitiza kuwa uongozi mpya utazingatia misingi ya ushirikiano katika kuendeleza shughuli za TAPSEA na kuhakikisha wanachama wanapata nafasi ya kutoa maoni na kushiriki katika masuala yanayohusu maendeleo ya chama.

Viongozi wengine walioapishwa ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Halima Twaha Mgulo, Makamu Mwenyekiti, Zainab Ibrahim Ally, Mweka Hazina, Nyanza Msongela, pamoja na wajumbe wengine waliochaguliwa katika uongozi huo.
Uapisho huo unatajwa kuwa hatua ya kukamilisha mchakato wa uchaguzi na kuweka rasmi uongozi mpya katika nafasi zao za kuwahudumia wanachama, huku matarajio yakiwa ni kuona chama kinaendelea kuimarisha umoja na kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Viongozi hao walioapishwa leo, Agosti 26, 2026, walichaguliwa katika Mkutano Mkuu wa 13 wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) uliofanyika mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Ngurdoto, mkoani Arusha.