
Na Mwandishi Wetu - Tanga
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, ameitaka Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) kuongeza nguvu katika utoaji wa elimu kwa umma ili kujenga uelewa sahihi kuhusu teknolojia ya nyuklia na kuondoa hofu pamoja na dhana potofu miongoni mwa wananchi wanaohusisha teknolojia hiyo na utengenezaji wa mabomu ya nyuklia.
Prof. Nombo ametoa maelekezo hayo leo, Agosti 20, 2026, alipotembelea banda la TAEC katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga.
Amesema pamoja na hatua zinazochukuliwa katika kuendeleza sayansi na teknolojia nchini, bado kuna haja ya kuongeza elimu kwa wananchi ili wanaposikia neno nyuklia wasifikirie silaha au mabomu pekee, bali watambue mchango mkubwa wa teknolojia hiyo katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Kwa mujibu wa Prof. Nombo, TAEC ikiwa taasisi yenye dhamana ya kusimamia matumizi salama ya mionzi na kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya nyuklia nchini, ina nafasi muhimu ya kuhakikisha taarifa sahihi zinawafikia wananchi kwa lugha rahisi na kupitia majukwaa mbalimbali.
Amesema elimu hiyo ni muhimu zaidi katika kipindi ambacho Tanzania inaendelea kujenga uwezo wake katika sayansi na teknolojia na kuangalia namna teknolojia mbalimbali za kisasa zinavyoweza kutumika katika kukabiliana na changamoto za maendeleo.
“TAEC mnapaswa kuweka nguvu kubwa katika kutoa elimu kwa wananchi. Bado kuna watu wakisikia masuala ya nyuklia wanafikiria mabomu, wakati teknolojia hii ina matumizi mengi ya amani yanayoweza kusaidia maendeleo ya nchi,” amesema Prof. Nombo.
Teknolojia ya nyuklia ina matumizi mapana katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo, mifugo, maji, viwanda, migodi, nishati na utafiti wa kisayansi. Katika sekta ya afya, kwa mfano, mionzi na mbinu za nyuklia hutumika katika uchunguzi na matibabu ya baadhi ya magonjwa, wakati katika kilimo na mifugo teknolojia hiyo inaweza kusaidia katika tafiti, udhibiti wa wadudu na magonjwa pamoja na kuongeza tija katika uzalishaji.
Prof. Nombo pia ameitaka TAEC kutumia nafasi yake kuwafikia wanafunzi na kuwahamasisha kupenda na kusoma masomo ya sayansi, akieleza kuwa maendeleo ya teknolojia yanahitaji nchi kuwa na wataalamu wa kutosha wenye maarifa katika fani za sayansi, teknolojia, uhandisi na maeneo mengine yanayohusiana.
Amesema Serikali imeendelea kufungua fursa kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo ya sayansi kupitia programu mbalimbali za ufadhili wa masomo, ikiwemo Samia Scholarship na Samia Scholarship Extended, hatua inayolenga kuongeza idadi ya wataalamu katika maeneo ya kimkakati yanayohitajika kwa maendeleo ya Taifa.
Kwa mtazamo wake, uwepo wa fursa hizo unapaswa kuwa kichocheo kwa wanafunzi kuongeza juhudi katika masomo yao na kujenga msingi imara wa taaluma zitakazowawezesha kutumia fursa zinazotolewa na Serikali kujiendeleza katika elimu ya juu ndani na nje ya nchi.
Amesisitiza kuwa uwekezaji katika elimu ya sayansi hauishii katika kuongeza idadi ya wahitimu pekee, bali ni sehemu ya maandalizi ya muda mrefu ya Taifa kuwa na wataalamu wenye uwezo wa kusimamia na kutumia teknolojia zinazoendelea kubadilika kwa kasi duniani.
Ziara ya Prof. Nombo katika banda la TAEC imekuja wakati Tume hiyo ikiendelea kutumia Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya mionzi na namna teknolojia ya nyuklia inavyoweza kuchangia maendeleo katika sekta mbalimbali.
Katika banda hilo, wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali wamekuwa wakipata maelezo kuhusu majukumu ya TAEC, usimamizi wa vyanzo vya mionzi pamoja na matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa madhumuni ya amani. Wanafunzi pia wanapata fursa ya kufahamu taaluma zinazohusiana na sayansi na teknolojia ya nyuklia na njia wanazoweza kupitia kuingia katika fani hizo.
Maelekezo ya Prof. Nombo yanaweka mkazo katika umuhimu wa elimu kwa umma kwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia. Kadiri Tanzania inavyoendelea kupanua matumizi ya sayansi na teknolojia katika shughuli za maendeleo, ndivyo inavyokuwa muhimu kwa wananchi kuelewa teknolojia hizo, matumizi yake na mifumo iliyowekwa kuhakikisha zinatumika kwa usalama.
Kwa TAEC, jukumu hilo lina maana ya kwenda zaidi ya usimamizi wa matumizi salama ya mionzi na kuendelea kujenga daraja la uelewa kati ya sayansi na jamii, ili teknolojia ya nyuklia isitazamwe kwa hofu, bali kwa uelewa wa fursa zake, matumizi yake ya amani na mchango wake katika maendeleo ya Taifa.
Kupata mpenzi sahihi wa kujenga naye maisha na kuanzisha familia ni ndoto ya kila mwanamke, lakini pale kila mahusiano yanapovunjika ghafla hasa unapokaribia hatua ya ndoa, maisha hugeuka kuwa mateso na aibu kubwa.
Kwa zaidi ya miaka saba, nilijikuta kwenye mzunguko wa ajabu na wa kikatili. Nilianzisha mahusiano na wanaume tofauti, wote wakionyesha nia ya dhati ya kunioa.
Lakini kila tulipofikia hatua ya kutambulishana ukweni, kupanga tarehe ya harusi, au kutoa mahari, mambo yaliharibika ghafla bila sababu za msingi. Mwanaume alibadilika, akawa mkali, au akatokomea kabisa na kukata mawasiliano.
Mara ya kwanza nilidhani ni bahati mbaya, lakini ilipotokea kwa mwanaume wa tatu na harusi ikavunjika wiki mbili kabla ya siku yenyewe, nilichanganyikiwa kabisa.
Nilibaki na magauni ya harusi ndani, kadi zikiwa zimeshagawiwa, na familia yangu ikiingia kwenye aibu nzito mtaani. Nilianza kujitenga na marafiki zangu waliokuwa wakiolewa mmoja baada ya mwingine, nikiumia moyoni na kuhisi nina gundu au nimelaaniwa nisipate mume.
Masimango ya majirani na ndugu yalinizidia, wengine wakisema labda nina tabia mbaya zilizojificha zinazowakimbiza wanaume, jambo ambalo halikuwa kweli. Nilianza kupoteza ujasiri wa kupenda tena, nikiamini kabisa kuwa nimezeekea nyumbani. SOMA ZAIDI.
Hata hivyo, pale unapojikuta umekwama kwenye nafasi ile ile ya chini kwa miaka nane bila kuongezewa mshahara wala kupandishwa cheo, maisha ya kazi hugeuka kuwa unyonge na mateso ya kisaikolojia.
Katika oparesheni za kila siku za ofisi yetu, mimi ndiye niliyekuwa nikibeba mizigo mikubwa ya kazi, nikikaa muda wa ziada (overtime), na kuhakikisha kila mradi unakamilika kwa wakati.
Pamoja me juhudi zote hizo, kila msimu wa upandishwaji vyeo na ongezeko la mshahara ulipowadia, jina langu lilipuuzwa kabisa.
Nilibaki nikitazama vijana wapya waliotoka vyuo juzi wakiajiriwa na kupandishwa vyeo juu yangu ndani ya miezi michache, huku wakipewa mishahara minono na marupurupu kibao.
Kila nilipojaribu kuongea na mabosi wangu au kuomba mapendekezo ya kupanda cheo, nilipokea ahadi za uongo na visingizio visivyoeleweka.
Nilibaki nikijisikia vibaya na kupatwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikiona kama elimu na jasho langu vilikuwa vikitumiwa vibaya bila thamani yoyote. SOMA ZAIDI.
Nilifungua duka langu la nguo na vipodozi nikitarajia kupata faida kubwa ya kuendesha maisha yangu na familia. Hata hivyo, miezi michache baada ya kufungua, mambo yalibadilika ghafla.
Mtaani kwetu kulikuwa na watu wengi, lakini kila aliyepita mbele ya duka langu alitazama tu na kupita bila kuingia ndani. Kwa miezi mitano mtawalia, nilikuwa nikiamka asubuhi na mapema, kufungua duka, na kukaa siku nzima hadi usiku bila kuuza hata kitu cha shilingi mia.
Nguo zilianza kushika vumbi na kuharibika, kodi ya fremu ikawa inanilundikia, na wamiliki wa bidhaa waliaza kunidai kwa shinikizo kubwa.
Nilibaki nikilia peke yangu ndani ya duka lililokosa wateja, nikitazama maduka ya majirani zangu yakiwa yamefurika wateja kila siku huku langu likionekana kama limepakwa mikosi au kusahaulika.
Nilianza kupata msongo mkubwa wa mawazo, nikifikiria kufunga duka na kukimbia madeni yaliyokuwa yakinikabili. SOMA ZAIDI.
Na OWM – TAMISEMI, Dodoma
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kuhusu kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi inayosimamiwa na Ofisi hiyo.
Katika kikao hicho, pande hizo zimejadili maeneo ya ushirikiano, hususan matumizi ya utaalamu, teknolojia na uzoefu wa kitaasisi katika kuhakikisha miradi ya miundombinu inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa, kwa wakati na kuleta thamani halisi kwa wananchi.
Mhandisi Mativila amesisitiza umuhimu wa taasisi za Serikali kushirikiana na vyuo vikuu katika kupata suluhisho za kitaalamu zitakazosaidia kuongeza ufanisi na ubora wa miradi ya ujenzi inayotekelezwa nchini.
Kwa upande wake, Mkuu wa Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Innocent Macho, alisema Chuo hicho kina uwezo na uzoefu mkubwa wa kutoa huduma za kitaalamu kupitia kampuni yake ya ushauri, The Bureau for Industrial Cooperation (BICO), ambayo imeshiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini.
Pande hizo zimekubaliana kuendelea na majadiliano ili kuweka mazingira madhubuti ya ushirikiano yatakayochangia utekelezaji bora na endelevu wa miradi ya miundombinu chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI.
Na Mwandishi wetu -IRINGA
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Nderiananga amewapongeza watu wenye ulemavu kwa kushiriki shughuli za kiuchumi na kuongeza pato lao na Taifa kwa ujumla.
Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na watu wenye ulemavu katika Kituo cha wenye ulemavu cha Neema Craft kilichopo Manispaa ya Iringa Mh. Ummy alisema kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira yatakayowawezesha watu wenye ulemavukupata elimu, mafunzo ya ufundi na mitaji ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji.
Pia aliongeza kuwa watu wenye ulemavu wanapopata elimu ya fani mbalimbali huwajengea hali ya kujiamini, kuwa tayari kuonyesha uwezo wao na kuwa wabunifu hatimaye kupunguza wimbi la utegemezi.
" Nikipongeze Kituo hiki cha Neema Craft kwa hatua kubwa waliopiga katika kuwawezesha wenye ulemavu kwenye ujuzi mbalimbali kama tulivyoona kuna ufundi seremala, ufumaji, ushonaji, upishi na fani nyingine nyingi ambapo zote hizi zinafanywa na watu wenye ulemavu kwetu kama Serikali ni furaha kubwa," Alipongeza Mhe. Ummy
Hata hivyo amewataka watu wenye ulemavu kutumia fursa za mikopo, mafunzo na uwezeshaji zinazotolewa na Serikali ili kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi zitakazowasaidia kujitegemea.
"Wananchi wanaponufaika na mikopo hii ni heshima kubwa kwa Mbunge pia Mkuu wa Mkoa kaka yangu Kheri James nawapongeza sana kwa namna mnavyopambana kwa ajili ya watu wenye ulemavu," alisema.
Vile vile Mhe. Ummy alifafanua kwamba baadhi ya watu wenye ulemavu wameonyesha uwezo mkubwa katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, zikiwemo samani, mikoba, mikeka na mazulia, huku bidhaa hizo zikiuzwa katika hoteli na masoko mbalimbali.
Alisema mafanikio hayo yanaonesha kuwa watu wenye ulemavu wana uwezo wa kufanya shughuli zenye tija endapo watapata uwezeshaji unaostahili.
"Nimetembelea hapa Neema Craft nimejionea namna watu wenye ulemavu wanavyofanya shughuli zao za ujasirimali wanabuni na kutengeneza bidhaa nzuri ambazo hata watu wazima hawawezi na bidhaa hizo mara nyingi tunaziona katika mahoteli makubwa ambayo huwezi kuzania kwamba watu wenye ulemavu ndio wametengeneza,"Alieleza.
Aidha aliwataka wazazi na walezi kutowaficha ndani watoto wenye ulemavu badala yake kuwapeleka shule au vyuo vya ufundi na vituo vinavyotoa mafunzo ya ujuzi hatua itakayosaidia kujikwamua kiuchumi hatimaye kutoka katika hali ya kuwa omba omba mitaani.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Neema Crafts mkoani Iringa Bwa. Joseph Adams alisema kituo hicho kilianzishwa mwaka 2003 ikiwa ni mradi wa kijamii unaolenga kutoa mafunzo na ajira kwa watu wenye ulemavu kama vile wasiyosikia ( viziwi) na wenye ulemavu wa viungo ili kuwapa heshima na kuwaepusha na kuomba barabarani.
"Kituo hiki kinajumuisha kazi nyingi sana na zote wanafanya wao wenyewe na kuzalisha bidhaa ambazo tunaziuza kama vile Karakana za kazi za mikono, Mgahawa unaoendeshwa na viziwi na Nyumba ya wageni (Guesthouse),"Alisema Mkurugenzi huyo.
Aidha aliipongeza Serikali kwa kuendelea kuonyesha upendo kwa wenye ulemavu bila ubaguzi huku akiiomba kuboresha sekta ya wakalimani kuwasaidia wenye ulemavu kupata huduma muhimu kama hospitali, taasisi za fedha, nyumba za ibada na nyinginezo.
MWISHO
✅ Viwanda vya KEDA, GoodWill Vyachochea Kasi
✅ Wilaya yatenga Hekari 15 ujenzi wa Bandari Kavu
✅ Dkt.Kiruswa Ahimiza uzingatiaji Bei Elekezi za Madini
Kutokana na kuongezeka kwa Kasi ya uwekezaji ya shughuli za uongezaji thamani madini nchini huku ikizidi kujifungamanisha zaidi na sekta nyingine za uchumi, Sekta ya Madini imeendelea kuweka Msingi wa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kujenga uchumi wa Dola Trilioni 1, kupitia viwanda.
Hayo yalibainishwa Agosti 19, 2026 wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, Wilayani Mkuranga iliyolenga kufuatilia shughuli za madini, kubaini changamoto na kutoa maelekezo muhimu.
Katika ziara hiyo , Dkt. Kiruswa alitembelea viwanda vikubwa vya KEDA Tanzania Float Glass kinachozalisha vioo kwa ajili ya maghorofa, magari na matumizi mbalimbali, pamoja na Kiwanda cha GoodWill Ceramic Co.Ltd kinachozalisha vigae vya sakafu na ukutani pamoja na vifaa vya usafi wa majumbani na vyooni na kueleza kuwa, ni jambo la kujivunia kuona Tanzania inaweza kuzalisha bidhaa zinazoweza kuuzwa kwenye mataifa makubwa duniani kama Marekani.
Dkt.Kiruswa alisisitiza uzingatiaji wa bei elekezi zinazotolewa na Serikali kwa madini yanayotumika viwandani, pamoja na kumuagiza Afisa Madini Mkazi Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kwa kushirikiana na Wilaya hiyo kuandaa semina kwa wamiliki wa viwanda na leseni za uchimbaji kuhusu uwajibikaji kwa jamii, utunzaji wa mazingira na masuala mengine ya msingi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mhe. Hadija Nasri Ally, alisema Wilaya hiyo inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa uwekezaji, ikiwemo kutenga ekari 15 kwa ajili ya ujenzi wa Bandari Kavu itakayorahisisha uhifadhi na usafirishaji wa bidhaa zinazozalishwa wilayani humo,
Alisema Mkuranga ina viwanda 275, ambapo 39 vinatumia madini kuzalisha bidhaa mbalimbali, huku shughuli za madini zikichangia shilingi bilioni 3.2 katika mwaka wa fedha 2025/26.
Naye, Meneja Biashara wa KEDA Tanzania, Ruby Zhu, alieleza kuwa, asilimia 98 ya malighafi ya kiwanda hicho inatoka Mkuranga, huku kiwanda kikizalisha takribani tani 600 za vioo kwa siku, vinavyosafirishwa katika masoko mbalimbali duniani ikiwemo Marekani.
Kwa upande wake, Meneja Biashara wa GoodWill, Justin Xie alieleza kwamba, asilimia 90 ya malighafi zinazotumiwa na kiwanda hicho zinatoka Tanzania na kuongeza kuwa, kampuni hiyo imepanua uzalishaji wa bidhaa za majumbani, ikiwemo sinki za kunawia, vifaa vya vyooni na bafu huku bidhaa zao zikiuzwa mataifa mbalimbali ikiwemo nchi za Ulaya na Marekani.
Kuhusu ajira, Xie alisema kiwanda kimetoa ajira za moja kwa moja kwa watanzania zipatazo 3,000 na zisizo za moja kwa moja 12,000.
"Tumeweka mizizi nchini Tanzania, tunaweza kujitolea kubadilisha rasilimali za madini za ndani kuwa bidhaa za usafirishaji nje zenye thamani kubwa, na kuleta ajira zaidi na kodi na kushiriki na idara zote kuzungumzia vizuizi katika mnyororo wa usambazaji wa madini, na kwa pamoja kuendeleza ujenzi wa viwanda nchini Tanzania," alisema Justin Xie.
Kwa mujibu wa Afisa Madini wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, Mhandisi Lameck Gabote, Mkuranga ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa madini ya ujenzi na viwandani yanayohudumia kwa kiasi kikubwa Mkoa wa Dar es Salaam na mikoa jirani.

Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) inaendelea kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga, ikitumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya mionzi na fursa zinazotokana na teknolojia ya nyuklia katika kuchochea maendeleo ya Taifa.
Maonesho hayo, yanayoratibiwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, yanawakutanisha taasisi za Serikali, taasisi za elimu na utafiti, wabunifu, wanafunzi, wataalamu pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu, sayansi na teknolojia.
Katika banda la TAEC, wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali wanaendelea kupata elimu kuhusu jukumu la Tume la kusimamia na kudhibiti matumizi salama ya mionzi nchini, pamoja na mchango wa teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, kilimo, mifugo, maji, viwanda, migodi, utafiti na nishati.
Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo pia unatoa fursa kwa wanafunzi na vijana kufahamu taaluma mbalimbali zinazohusiana na teknolojia ya nyuklia na umuhimu wa kujikita katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM) ili kujenga kizazi cha wataalamu kitakachosaidia Taifa kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Akifungua rasmi maonesho hayo Agosti 18, 2026, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisisitiza umuhimu wa elimu, ujuzi, sayansi, teknolojia na ubunifu katika kujenga uchumi wa kisasa na kuongeza uwezo wa Taifa kutumia maarifa na teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo.
Katika muktadha huo, ushiriki wa TAEC unaunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha sayansi na teknolojia zinatumika moja kwa moja katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Teknolojia ya nyuklia ina matumizi mapana yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo katika uchunguzi na tiba ya magonjwa, kuongeza tija katika kilimo na mifugo, usimamizi wa rasilimali za maji, shughuli za viwandani na migodini, utafiti wa kisayansi pamoja na sekta ya nishati.
Wananchi wanaotembelea banda la TAEC pia wanapata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na wataalamu, kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu usalama wa mionzi, udhibiti wa vyanzo vya mionzi na matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa madhumuni ya amani na maendeleo.
TAEC itaendelea kutoa elimu na kuhamasisha matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia kwa maendeleo endelevu ya Taifa.
“Mionzi kwa Matumizi Salama na Teknolojia ya Nyuklia kwa Maendeleo ya Taifa.”








Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
Msimamizi wa Mradi wa Tanzania FAST Health, Japhet Daud, akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.






















.jpeg)





















































