Na. Veronica Mwafisi-Dodoma


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III) na kutoa maelekezo ya kuendeleza misingi ya utekelezaji wenye ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika kufikia walengwa waliokusudiwa na kutimiza malengo ya PSSN III.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amezungumza hayo leo tarehe 14 Agosti, 2026 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro ameipongeza TASAF kwa utekelezaji mzuri wa Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya. 

Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi nyingi kwa ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri katika mpango wa kunusuru kaya maskini, lakini pia mnatekeleza vizuri Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya, mnamwakilisha vizuri Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa miradi hii Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III), Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amesema, PSSN III iliidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Dunia tarehe 10 Aprili 2026, na kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi kabla ya kuanza utekelezaji.


Naibu Waziri Qwaray amesema kuwa, katika maandalizi ya utekelezaji wa PSSN III, hatua muhimu zimekamilika ikiwemo kukamilisha usanifu wa Mpango, kuandaa nyaraka mbalimbali za utekelezaji, miongozo ya kiutendaji na kuimarisha mifumo ya TEHAMA inayosimamia shughuli za Mpango. 

Aidha ameongeza kuwa, mchakato wa utambuzi wa Mamlaka za Maeneo ya Utekelezaji yatakayoshiriki kwenye utekelezaji wa Mpango unaendelea na unaojumuisha timu ya wataalamu kutoka TASAF, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), pamoja na wataalamu wa mazingira ambapo uchambuzi na uchakataji huo utazingatia viwango vya umaskini katika ngazi ya Halmashauri pamoja na viashiria vya athari za kimazingira, ikiwemo uwezekano wa maeneo kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi na majanga mbalimbali.

Vilevile, Mhe. Qwaray amesema kupitia mpango huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa kaya maskini na zilizo katika mazingira hatarishi kukabiliana na changamoto za kiuchumi, kijamii na kimazingira, kuongeza ujuzi na taaluma kwa vijana kutoka kaya maskini na zinazoishi katika mazingira hatarishi zitakazoweza kujiajiri na kuajiriwa, kuwa na masijala ya kitaifa (kanzi data) yenye taarifa muhimu ya kaya maskini na zilizopo katika mazingira hatarishi pamoja na urasimishwaji wa TASAF kama taasisi ya umma ya kutekeleza na kusimamia utoaji wa huduma za msaada ya kijamii itakayohakikisha uendelevu, ufanisi na uratibu wa utoaji wa huduma hizo nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray ameishukuru Kamati hiyo kwa maoni na ushauri mbalimbali ambao wameutoa na kuahidi kufanyia kazi ili kuimarisha na kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.



Na Mwandishi Wetu - Zanzibar


Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kujenga mazingira wezeshi kwa uchumi wa kidijitali Zanzibar kwa kuwezesha huduma ya intaneti katika mradi wa makazi wa Amani Residency, uliopo Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, kupitia huduma yake ya Faiba Mlangoni Kwako.

Mradi huo wa kisasa wa makazi ulizinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ukiwa ni sehemu ya uwekezaji unaolenga kuongeza fursa za makazi bora, biashara na utalii pamoja na kuchochea shughuli za kiuchumi Zanzibar.

Akizungumza kuhusu uwezeshaji huo, Meneja wa TTCL Zanzibar, Bi. Nasra Mugheiry, alisema TTCL imeweka mazingira ya mawasiliano ya kisasa katika Amani Residency ili kuwawezesha wakazi kupata huduma ya intaneti karibu na makazi yao na kutumia fursa mbalimbali zinazotokana na uchumi wa kidijitali.

“TTCL kupitia huduma ya Faiba Mlangoni Kwako imeweka mazingira wezeshi ya mawasiliano katika Amani Residency, kwa lengo la kuwawezesha wakazi kutumia intaneti katika shughuli zao za kila siku, ikiwemo kazi, biashara, elimu, mawasiliano na huduma mbalimbali za kidijitali. Tunataka kuhakikisha kwamba makazi ya kisasa yanaendana na mahitaji ya kisasa ya mawasiliano,” alisema Bi. Mugheiry.

Huduma hiyo inatarajiwa kuongeza thamani ya mradi huo kwa kuwawezesha wakazi kufanya shughuli mbalimbali kwa urahisi wakiwa majumbani. Kwa wakazi wanaofanya kazi kwa njia ya mtandao, wafanyabiashara, wanafunzi na familia, upatikanaji wa intaneti ya nyumbani utarahisisha matumizi ya mikutano ya mtandaoni, kujifunza, kufanya biashara kupitia majukwaa ya kidijitali, mawasiliano pamoja na huduma za Serikali mtandao.

Amani Residency, unaojengwa katika eneo la ekari 11, una jumla ya nyumba 82, zikiwemo villa 18 na apartment 64, pamoja na huduma mbalimbali za burudani na mapumziko. Uwepo wa huduma ya Faiba Mlangoni Kwako unaifanya miundombinu ya mawasiliano kuwa sehemu muhimu ya mazingira ya makazi hayo, sambamba na mahitaji ya maisha ya kisasa.

Kwa upande wa biashara, intaneti inayopatikana katika makazi inaweza kuwapa wakazi fursa ya kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa kutumia teknolojia, ikiwemo biashara za mtandaoni, masoko ya kidijitali, huduma za kifedha na mawasiliano ya kibiashara. Hali hiyo inaendana na juhudi za TTCL za kuchochea matumizi ya teknolojia na kuunganisha wananchi na fursa za uchumi wa kidijitali.

Aidha, uwezeshaji huo unaimarisha dhamira ya TTCL ya kusogeza huduma za mawasiliano kwa wananchi katika maeneo wanayoishi na kufanya shughuli zao, kwa kuzingatia kwamba intaneti imekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku na kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kwa TTCL, kuwezesha Amani Residency kwa huduma ya Faiba Mlangoni Kwako ni zaidi ya kuunganisha makazi na intaneti; ni hatua ya kujenga mazingira ambayo yanawawezesha wananchi kuishi, kufanya kazi, kujifunza, kuwasiliana na kufanya biashara kwa kutumia teknolojia, sambamba na juhudi za taifa za kujenga uchumi unaotegemea zaidi huduma na fursa za kidijitali.





Wananchi wa Mkoa wa Tanga na mikoa jirani wanahamasishwa kushiriki katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ubunifu na Ujuzi, itakayofanyika kuanzia tarehe 15 - 24 Agosti 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, ili kujifunza, kubadilishana maarifa na kutumia fursa mbalimbali za elimu, ujuzi na ubunifu.
Na Mwandishi Wetu ,Zanzibar

ORYX Gas Zanzibar imeeleza hatua mbalimbali inazochukua kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na katika Tamasha la Kizimkazi kampuni hiyo imetoa mitungi ya gesi 200 huku mkakati kwasasa ni kutoa majenerata yanatotumia gesi ya LPG katika hoteli na viwanda visiwani Zanzibar.

Wananchi wa Mkoa wa Tanga na mikoa jirani wanahamasishwa kushiriki katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ubunifu na Ujuzi, itakayofanyika kuanzia tarehe 15 - 24 Agosti 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, ili kujifunza, kubadilishana maarifa na kutumia fursa mbalimbali za elimu, ujuzi na ubunifu.

Akizungumza Agosti 14, 2026, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Kassim Mchata, amesema maonyesho hayo yatashirikisha taasisi zaidi ya 300 pamoja na wadau wa sekta ya elimu, sayansi na teknolojia. Aidha, kutakuwa na mashindano ya ubunifu na ujuzi katika fani mbalimbali ikiwemo ushonaji, ususi, umeme na mengineyo, ambapo washindi wa kitaifa watapata nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa.

Mchata ameongeza kuwa wadhamini mbalimbali wakiwemo mabenki wamejitokeza kudhamini miradi ya ubunifu na kuunga mkono wajasiriamali chipukizi.

Kwa upande wake, Prof. Ladislaus Mnyone, Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, alisema lengo kuu la wiki hiyo ni kuwaleta pamoja wadau kujadili na kuweka mikakati ya pamoja kuhusu elimu, ujuzi na ubunifu.

Amebainisha kuwa matukio makuu yatakuwa ni maonesho ya teknolojia yanayoonyesha mchango wa sayansi katika sekta mbalimbali, pamoja na kongamano la elimu na ubunifu litakalojadili utekelezaji wa Dira 2050.

Prof. Mnyone amefafanua kuwa kongamano hilo litaangazia nyenzo tano kuu: utafiti na maendeleo, sayansi na ubunifu, teknolojia za kidijitali, nishati, na usafirishaji funganishi.

Kupitia mijadala na maonesho hayo, Wizara inalenga kufanikisha malengo ya taifa ikiwemo kufikia uchumi wa dola trilioni 1 ifikapo mwaka 2050, kipato cha wastani cha mtu mmoja kati ya Dola za Marekani 7,000 - 12,000, na ajira zenye staha kwa angalau asilimia 50 ya Watanzania.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wanaohudhuria mafunzo maalum ya diplomasia nchini India wametembelea Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini New Delhi.
Kujaribu na kujituma maishani ni hatua ya kila mtu anayepambania maendeleo, lakini pale kila unachogusa kinapoharibika na kukutana na ukuta, maisha huanza kuwa mzigo mzito.

Kwa miaka kadhaa, nilikabiliwa na mfululizo wa nuksi na mikosi ya ajabu. Kila mradi au wazo jipya nililojaribu kuanzisha iwe ni biashara ndogo, kilimo, au mchakato wa kusafiri lilikuwa likisambaratika dakika za mwisho kabisa bila sababu yoyote ya msingi.

​Nilibaki nikitazama maisha yangu yakirudi nyuma kila siku, huku watu wenzangu niliotafuta nao wakipiga hatua na kufanikiwa.

Pesa zilizoingia mkononi mwangu zilitoweka bila kufanya la maana, marafiki na watu wa karibu walianza kujitenga nami, na kila mlango wa fursa niliogonga ulijifunga kwa kishindo.

Nilianza kujiona kama mtu aliyelaaniwa, nikipoteza kabisa matumaini ya maisha na kuishi kwa huzuni na msongo mkubwa wa mawazo. SOMA ZAIDI.
Kuhusishwa kwenye kesi au mgogoro wa kisheria usio na msingi ni moja ya mtihani mkubwa na wa kutisha zaidi maishani. Kwa miaka kadhaa, maisha yangu yaliingia kwenye giza na hofu kubwa baada ya kusingiziwa kesi nzito ya uongo mahakamani.

Watu waliokuwa na pesa, ushawishi, na chuki binafsi dhidi yangu walishirikiana na mashahidi wa uongo kutengeneza tuhuma bandia ili kunifunga jela na kupora mali zangu tulizozitolea jasho na familia yangu.

​Kila mara nilipohudhuria vipindi vya mahakama, nilijikuta nikipatwa na tumbo la moto na msongo mkubwa wa mawazo. Upande wa mashtaka ulileta mashahidi waliokula kiapo na kusema uongo wa waziwazi bila woga, huku mawakili wao wakitumia mbinu za kila aina kupindisha ukweli.

Nilibaki nikitazama maisha yangu, uaminifu wangu, na familia yangu zikielekea kuporomoka. Hofu ya kwenda jela kwa kosa ambalo sikutenda ilininyima kabisa usingizi na amani ya nafsi, nikishuhudia fedha zote nilizokuwa nazo zikiishia kwenye gharama za kesi na mawakili bila matumaini ya kupona. SOMA ZAIDI.
Kujaribu na kujituma maishani ni hatua ya kila mtu anayepambania maendeleo, lakini pale kila unachogusa kinapoharibika na kukutana na ukuta, maisha huanza kuwa mzigo mzito. Kwa miaka kadhaa, nilikabiliwa na mfululizo wa nuksi na mikosi ya ajabu.

Kila mradi au wazo jipya nililojaribu kuanzisha iwe ni biashara ndogo, kilimo, au mchakato wa kusafiri lilikuwa likisambaratika dakika za mwisho kabisa bila sababu yoyote ya msingi.

​Nilibaki nikitazama maisha yangu yakirudi nyuma kila siku, huku watu wenzangu niliotafuta nao wakipiga hatua na kufanikiwa.

Pesa zilizoingia mkononi mwangu zilitoweka bila kufanya la maana, marafiki na watu wa karibu walianza kujitenga nami, na kila mlango wa fursa niliogonga ulijifunga kwa kishindo.

Nilianza kujiona kama mtu aliyelaaniwa, nikipoteza kabisa matumaini ya maisha na kuishi kwa huzuni na msongo mkubwa wa mawazo. SOMA ZAIDI.

 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (wa pili kushoto) akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA Kizimkazi, Zanzibar, linalotarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026. Wengine katika Picha ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fefha, Bw. Nsubili Joshua (wa pili kushoto), Kamishna Mkuu wa TRA, CPA. Yusuph Juma Mwenda (wa tatu kulia), Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha (kulia), na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini, Mhe. Othman Ali Maulid (wa pili Kulia).
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akipanda mti mara baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA Kizimkazi, Zanzibar, linalotarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiambatana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, Kamishna Mkuu wa TRA, CPA. Yusuph Juma Mwenda na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini, Mhe. Othman Ali Maulid, wakisikiliza maelezo ya Meneja wa Usimamizi wa Majengo na Mali wa TRA, Mhandisi Rwambali Mtete, kuhusu wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA Kizimkazi, Zanzibar, ambalo linatarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026, kuhusu utekelezaji wa ujenzi unavyoendelea hadi sasa.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA Kizimkazi, Zanzibar, linalotarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026, ambapo pamoja na mambo mengine alisema Serikali itaendelea kuboresha na kuimarisha miundombinu ya Ofisi za TRA katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo maeneo ya mipakani, ili kuimarisha huduma, kurahisisha biashara, kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, kuwawezesha watumishi kufanya kazi katika mazingira bora, na kuongeza uwezo wa Serikali kukusanya mapato kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, akizungumza wakati akimkaribisha Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani) kuzungumza wakati wa hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA Kizimkazi, Zanzibar, linalotarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026.
Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati aliyeketi), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua (Kulia aliyeketi), Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda (wa pili kushoto aliyeketi), Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha (kushoto), na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini, Mhe. Othman Ali Maulid (wa pili kulia aliyeketi) Wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa TRA Zanzibar wakati wa hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA Kizimkazi, Zanzibar, linalotarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026.
Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati aliyeketi), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua (Kulia aliyeketi), Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda (wa pili kushoto aliyeketi), Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha (kushoto), na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini, Mhe. Othman Ali Maulid (wa pili kulia aliyeketi), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA Kizimkazi, Zanzibar, linalotarajiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma mwezi Novemba mwaka huu 2026.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Kizimkazi, Zanzibar)


Na. Benny Mwaipaja, Kizimkazi, ZANZIBAR


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameimwagia sifa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA kwa utendaji uliotukuka uliowezesha Mamlaka hiyo kuendelea kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato kila mwezi na kueleza imani yake kwamba kwa kushirikiana na alipakodi, wataweza kuvuka lengo walilopangiwa la kukusanya zaidi ya shilingi trilioni 42 katika Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Mhe. Balozi Omar, ametoa pongezi hizo wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya TRA, Kizimkazi, Zanzibar, litakalokuwa na ghorofa moja, ambapo hadi kukamilika kwake linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.6.

Sifa hizo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, zinafuatia maelezo ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA Bw. Yusuph Mwenda ambapo alisema katika mwezi Julai mwaka huu, Mamlaka yake imevuka malengo kwa kukusanya shilingi trilioni 3.2 ikilinganishwa na malengo waliyopangiwa ya kukusanya shilingi trilioni 2.

Alisema kuwa mafanikio ya TRA katika ukusanyaji wa mapato yanatokana na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, Bunge na wadau wa kodi, ambapo mwezi Julai pekee, Mamlaka ilikusanya zaidi ya Shilingi trilioni 3.245 ikilinganishwa na lengo la mwezi la kukusanya shilingi trilioni 2.971, sawa na ufanisi wa asilimia 109 ya lengo, na ukuaji wa asilimia 21.

“Kutokana na usimamizi wako mzuri Mhe. Waziri wa Fedha, na ushirikiano na walipakodi, tunakuhakikishia tutavuka lengo hilo na kupita, ishara inayoonesha kwamba tumeanza mwaka wa fedha kwa nguvu kubwa, na tuna imani tutafikia na kuvuka malengo tuliyowekewa” alisema Bw. Mwenda.

Aidha, CPA Mwenda alisema kuwa katika kipindi hicho cha Julai, 2026, TRA imefanikiwa kukusanya shilingi bilioni 325, fedha mabazo ni asilimia 70 ya makusanyo yote na kuzipeleka moja kwa moja kwenye Mifuko 11 ya ujenzi wa miundombinu katika sekta mbalimbali zikiwemo Barabara, maji, utalii na sekta nyingne.

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa Ofisi za TRA, Kizimkazi-Unguja Zanzibar inayojengwa na Kampuni ya CRJE ya China, ni sehemu ya ujenzi wa Ofisi kama hizo 49 zinazojengwa nchi nzima zikitarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 32 kwa ajili ya kuboresha mazingira ya ulipaji kodi na kusogeza huduma karibu na wananchi.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) aliwahakikishia watanzania kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa inajitegemea kwa kutumia mapato yake ya ndani kutekeleza miradi yake ya maendeleo ambapo katika Mwaka wa Fedha 2026/2027, imepanga kujitegemea kwa zaidi ya asilimia 74.

Alisema kuwa ujenzi wa Ofisi za TRA Kizimkazi na maeneo mengine nchini, ni mikakati ya Serikali ya kuimarisha huduma, kurahisisha shughuli za biashara, kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato na kuwawezesha watumishi kufanya kazi katika mazingira bora kwa ajili ya kuongeza mapato yanayowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo barabara, nishati, maji, kuimarisha huduma za afya na kuwekeza katika elimu.

Mhe. Balozi Omar ameuagiza Uongozi wa TRA kuhakikisha kuwa wanashirikiana na Mamlaka ya Mapato Zanzibar ZRA kutumia miundombinu ya Ofisi hizo na nyingine zitakazo jengwa Visiwani Zanzibar, ili wadau wa kodi wapate huduma kikamilifu, jambo ambalo Kamishna wa TRA Bw. Mwenda aliahidi kulifanyia kazi.

Aidha aliwataka wafanyabiashara na wananchi kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa wakati, kwa ukamilifu na kwa hiari, akisisitiza kuwa ulipaji wa kodi unapaswa kuwa jambo la fahari kwa kila mwananchi anayewajibika na Serikali itaendelea kushirikiana na wafanyabiashara katika kuboresha huduma za kodi na kupunguza changamoto zinazowakabili, huku ikitarajia wafanyabiashara nao kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini, Mhe. Othman Ali Maulid, alitoa wito kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) kuendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato kwa ufanisi na kuzingatia utoaji wa huduma bora kwa wananchi, lakini pia kusikiliza changamoto za wananchi na wafanyabiashara.

Akiongea kwa niaba ya Wafanyabishara wa sekta ya hoteli na utalii Zanzibar, Bw. Henry Kaunda, aliishukuru TRA na ZRA kwa kushirikina na wafanyabiashara na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili hatua iliyochangia ulipaji kodi kwa hiari na kuomba elimu zaidi ya mlipakodi iendelee kutolewa kwa wafanyabiashara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameweka jiwe la msingi na kupanda mti katika Skuli ya Sekondari ya Ufundi Kizimkazi Mkunguni, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.

 


Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO

Jumla ya wanafunzi 10 waliomaliza kidato cha sita na kupata alama za juu katika tahasusi za PCM, PGM na PMC, wamepata ufadhili wa kwenda kusoma katika Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN University) kilichopo jijini Moscow, nchini Urusi.

Ufadhili huo umepatikana kufuatia ziara rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoifanya  nchini humo mnamo mwezi Juni, 2026 ambapo chuo hicho ndicho kilichomtunuku Shahada ya Uzamivu ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa).

Akizungumza na Waandishi wa Habari Agosti 13, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa wanafunzi hao wamepata ufadhili huo kupitia utaratibu wa Samia Scholarship Extended.

"Wanafunzi hao wanatarajiwa kufanya kambi ya mafunzo nchini Urusi kwa takriban miezi 10, Serikali ya Urusi itagharamia mafunzo hayo kwa asilimia 80 na Serikali ya Tanzania itagharamia asilimia 20, watakapoanza mafunzo ya chuo kikuu mnamo Septemba 2027, Serikali ya Urusi itagharamia kwa asilimia 100", amesema Prof. Mkenda.

Akifafanua juu ya upatikanaji wa wanafunzi hao, Mhe. Prof. Mkenda amesema kuwa wamechukua wale waliofaulu vizuri baada ya wale 50 wa mwanzo, hivyo wamechukua kuanzia mwanafunzi wa 51 hadi 60 ambapo kati yake, wanafunzi nane wametoka katika shule za serikali na wanafunzi wawili wametoka katika shule za binafsi.

Akizungumza kuhusu wanafunzi 50 waliochaguliwa hivi karibuni, amesema kuwa wote wamekubali kupokea ufadhili huo wa kusoma nje ya nchi na wanatarajia kuanza kambi ya mafunzo mnamo Septemba 14, 2026 kwa muda usiozidi miezi 10 katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela - Arusha (NM-AIST) kabla ya kwenda katika vyuo hivyo vya nje ya nchi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkenda ametoa rai kwa wanafunzi wanaopata ufadhili wa kusoma nje ya nchi kufanya vizuri kwenye masomo yao ili kuongeza ushawishi kwa nchi hizo kutoa ufadhili kwa wanafunzi wengine zaidi hali itakayosaidia mikopo ya elimu ya juu inayotolewa kwa wanafunzi nchini kuwafikia wanafunzi wengi zaidi.

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe.Salome Makamba,akipata maelezo mara baada ya kutembelea  banda la Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA) katika Maonesho ya Kizimkazi yanayoendelea katika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar.

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba, amehimiza umma kupata taarifa sahihi kuhusu hali ya sekta ndogo ya umeme nchini, huku akitoa wito kwa Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuendelea kutoa elimu na taarifa kwa wananchi kuhusu jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuboresha huduma za umeme.

Mhe. Makamba ametoa wito huo leo, tarehe 13 Agosti 2026, alipotembelea banda la EWURA katika Maonesho ya Kizimkazi yanayoendelea katika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, amesema ni muhimu wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu kuongezeka kwa uzalishaji na upatikanaji wa umeme nchini na hivyo kukidhi mahitaji tuliyonayo.

“Gharama ya umeme nchini Tanzania ni nafuu ikilinganishwa na nchi jirani, na Serikali inaendelea na juhudi za kuboresha na kuimarisha miundombinu ya umeme ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo kwa uhakika, hatua itakayochochea maendeleo ya kiuchumi nchini,” aliongeza.

Katika banda la EWURA, Mhe. Makamba alifahamishwa Mamlaka imetumia fursa ya Maonesho hayo kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya udhibiti ikiwemo mikataba ya huduma kwa wateja, matumizi sahihi na salama ya huduma za bidhaa za gesi ya mitungi, gesi asilia, umeme na maji, fursa za uwekezaji katika sekta na mengineyo.

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe.Salome Makamba,akisaini kitabu  mara baada ya kutembelea  banda la Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA) katika Maonesho ya Kizimkazi yanayoendelea katika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar.

 

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe.Salome Makamba,akipata maelezo mara baada ya kutembelea  banda la Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA) katika Maonesho ya Kizimkazi yanayoendelea katika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar.





Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb.), ametembelea mabanda ya Wizara ya Nishati na taasisi zake katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayoendelea Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Akiwa katika mabanda hayo, Mhe. Salome amezungumza na wataalam pamoja na kujionea namna wanavyotoa elimu kwa wananchi kuhusu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Serikali katika Sekta ya Nishati.

Mhe. Salome amewapongeza watendaji wa Wizara na taasisi zake kwa kutumia maonesho hayo kuwaelimisha wananchi kuhusu juhudi zinazofanywa na Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha Sekta ya Nishati na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Amesema Serikali inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati katika Sekta ya Nishati, ambapo baadhi ya miradi imekamilika ukiwemo mradi wa Julius Nyerere wa megawati 2,115 na mradi wa umeme jua Kishapu ambao awamu yake ya kwanza imekamilika na kuzalisha megawati 50.

Amesema kuwa miradi mingine inaendelea kutekelezwa, ikiwemo Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), pamoja na miradi ya umeme, gesi asilia na nishati safi ya kupikia.

Katika nishati safi ya kupikia amesema Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wanachi ili kuhamasisha matumizi ya nishati hiyo huku ikiendelea kusambaza teknolojia na miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa taasisi na wananchi.

Katika maonesho hayo amewataka wataalam kuendelea kutoa elimu  ili wananchi wafahamu hatua zinazopigwa na Serikali katika Sekta ya Nishati, manufaa ya miradi inayotekelezwa pamoja na fursa zinazopatikana katika sekta hiyo.

Wizara ya Nishati na taasisi zake zinashiriki Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, kuanzia Agosti 12 hadi 14, 2026.

Naitwa Benson, mkazi wa zamani wa jijini Arusha. Kwa miaka mitano baada ya kuhitimu chuo, nilijikita kwenye kutoa huduma za mafunzo ya ziada (tuition) kwa wanafunzi wa sekondari. Pamoja na akili yangu na bidii ya kufundisha, maisha yangu yalikuwa ya duni kiasi cha kutisha.

Nilikuwa naishi kwenye chumba kimoja ambacho hata mvua ikinyesha navuja, na chakula changu kikuu kilikuwa ni ugali wa ngano na chumvi, hali iliyonifanya nionekane kama mgonjwa mbele ya watu.

Kila nikijaribu kufungua kituo changu cha kudumu, wamiliki wa majengo walikuwa wananitimua kwa kukosa kodi. Nilihisi nina nuksi ambayo imeziba kila tundu la mafanikio yangu.

Nilianza kuona wadogo zangu niliowasomesha wakifanikiwa na kunipita kimaisha, huku mimi nikiishia kuwa “mwalimu wa mtaani” asiye na heshima. Nilikata tamaa na kuanza kuwaza kuwa labda nimezaliwa kuwa maskini wa kudumu. SOMA ZAIDI.
John Nyakundi, mfanyabiashara wa nguo mjini Kisii, anasema alifika hatua ya kukata tamaa baada ya biashara yake kuanza kuporomoka ghafla. Kwa zaidi ya mwaka mmoja, alikuwa akipata hasara mfululizo licha ya kujaribu mbinu tofauti za kuvutia wateja.

Kwa mujibu wake, wateja walipungua kwa kiasi kikubwa na hata wale waliokuwa wa kudumu walianza kupotea. Bidhaa zilikaa dukani kwa muda mrefu bila kuuzwa na gharama za uendeshaji zikazidi kuwa kubwa.

“Nilikuwa nafungua duka kila siku lakini hakuna mabadiliko. Ilifika mahali nikahisi kufunga kabisa,” alisema John.

Hali hiyo ilimuweka kwenye presha kubwa ya kifedha kwani alikuwa pia na madeni aliyokuwa anapaswa kulipa. SOMA ZAIDI.
Biashara iliyokuwa ikiyumba kila mwezi

Samuel Kiptoo, mfanyabiashara wa bidhaa za jumla mjini Eldoret, anasema maisha yake ya biashara yalikuwa ya kupanda na kushuka kwa muda mrefu. Kila mwezi alijikuta akifunga duka kwa hasara licha ya kuwekeza mtaji mkubwa.

Kwa mujibu wake, hali hiyo ilianza ghafla. Wateja walipungua bila sababu ya wazi, bidhaa zilikaa muda mrefu bila kuuzwa na mara kwa mara alipata hasara hata wakati wa msimu wa biashara.

“Niliwahi kufikiria kufunga kabisa. Nilikuwa naingia kazini asubuhi lakini moyo haukuwa na matumaini,” alisema.

Alijaribu kubadilisha mbinu za biashara, kupunguza bei na hata kuongeza aina ya bidhaa, lakini hakuna kilichosaidia. SOMA ZAIDI.

Wananchi mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya huduma za afya, hatua iliyowarahisishia upatikanaji wa huduma hizo bila kulazimika kusafiri umbali mrefu.

 


KIZIMKAZI, ZANZIBAR


Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake imetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufanikisha Mdahalo wa Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Agosti 2026.

Tuzo hiyo imetolewa usiku wa kuamkia tarehe 12 Agosti 2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kupokelewa kwa niaba ya Wizara ya Nishati na taasisi zake na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba.

Mdahalo huo, uliokuwa na lengo la kujadili namna ya kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia iliyo endelevu, salama na nafuu kwa wananchi na taasisi, uliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka Serikalini, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, taasisi za fedha, wanateknolojia, watafiti na asasi za kiraia.

Mdahalo huo uliandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation (MIF), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha na kuchagiza hatua za pamoja katika kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Katika Mdahalo huo, Serikali iliendelea kusisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, taasisi za fedha na wadau wengine.

Tuzo hiyo ni ishara ya kutambua mchango na ushirikiano wa Wizara ya Nishati na taasisi zake katika kufanikisha Mdahalo huo, unaolenga kuchagiza mjadala na hatua madhubuti kuelekea kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.