Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Siuluhu Hassan, akizungumza alipotembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia), akimsikiliza Meneja wa Ofisi ya Zanzibar ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Mariam Saleh, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026 (Kizimkazi Festival 2026) Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kushoto), akimsikiliza Meneja wa Ofisi ya Zanzibar ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Mariam Saleh, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026 (Kizimkazi Festival 2026) Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.


Zanzibar, Agosti 12, 2026


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) katika Maonesho yanayoambatana na Tamasha la 10 la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.


Katika ziara hiyo, Mhe. Rais Samia amepongeza PSSSF kwa kushiriki katika maonesho hayo na kutoa huduma pamoja na elimu kwa wanachama na wananchi wanaotembelea banda la Mfuko.


Mhe. Rais Samia alipokelewa na Meneja wa PSSSF Ofisi ya Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, ambaye alimueleza kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko, pamoja na namna wanachama na wananchi wanavyonufaika na huduma hizo kupitia banda hilo.


Mhe. Rais Samia ameupongeza Mfuko kwa utoaji wa huduma na kusisitiza umuhimu wa kusikiliza na kushughulikia kwa wakati changamoto zinazowasilishwa na wananchi na wanachama.


“Nawapongeza sana kwa huduma nzuri. Kama kuna malalamiko, yakusanyeni na muyafanyie kazi,” ameagiza Mhe. Rais Samia.


Ushiriki wa PSSSF katika Tamasha la Kizimkazi unalenga kuendelea kuwafikia wanachama na wananchi kwa kuwapatia elimu kuhusu hifadhi ya jamii, huduma zinazotolewa na Mfuko pamoja na kuwawezesha kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu mafao na huduma za PSSSF.

Mwisho

 

Na Mwandishi Wetu

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, ameanza ziara ya kikazi mkoani Mwanza kwa lengo la kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia na kukuza ushindani wa haki katika soko.

Katika ziara hiyo, iliyofanyika leo Agosti 12, 2026, Bi. Ngasongwa amekutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Ndugu Balandya Elikana, ambapo wamejadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika kudhibiti uingizaji, uzalishaji na usambazaji wa bidhaa bandia.

Akizungumza katika kikao hicho, Balandya amesema udhibiti wa bidhaa bandia ni muhimu katika kuhakikisha bidhaa halali zinapata fursa sawa ya kushindana katika soko, hatua ambayo itasaidia kuchochea shughuli za kiuchumi na kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa.

"Kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia kutasaidia kuwalinda wafanyabiashara wanaofuata sheria, kuongeza imani ya wananchi kwa bidhaa zinazouzwa sokoni na kuchochea ukuaji wa uchumi."amesema Balandya

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema Tume itaendelea kuchukua hatua dhidi ya uingizaji, uzalishaji na usambazaji wa bidhaa bandia ili kuhakikisha bidhaa halali zinapata mazingira bora ya ushindani katika soko.

Bi.Ngasongwa amesema kuwa  hatua hizo ni sehemu ya jitihada za FCC za kulinda ushindani wa haki, kuwalinda wafanyabiashara wanaozingatia sheria na kuhakikisha shughuli za kibiashara zinafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.

  

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma Mchafu (kushoto) akizungumza na Wajumbe wa Kamati hiyo, Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, pamoja na Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya utendaji wa OSHA katika kipindi cha Mwaka wa fedha 2025/2026, Bungeni, Jijini Dodoma leo tarehe 12 Agosti, 2026. Kulia ni Katibu wa Kamati hiyo, Bw. Pius Katabinzi.

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wametoa elimu kwa wafanyabiashara na wachongaji wa vinyago katika eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam kuhusu sheria, kanuni na taratibu za uvunaji, usafirishaji na biashara ya mazao ya misitu, ikiwemo taratibu za kusafirisha bidhaa hizo nje ya nchi.

 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha-Rose Migiro, amefungua rasmi Tawi la CCM Kibuteni, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja, leo tarehe 12 Agosti 2026.

Tawi hili lina historia kubwa tangu nyakati za ASP na TANU, na ni jambo la kujivunia kuona sasa lina sura mpya inayokwenda sambamba na mahitaji na hadhi ya Chama.

Dkt. Migiro amewahimiza viongozi na wanachama kuhakikisha Tawi hilo linakuwa kituo cha uhai wa Chama, mshikamano, mafunzo, vikao na utekelezaji wa shughuli za Chama.

Pia, Katibu Mkuu amewashukuru wana-CCM wa Kibuteni kwa mapokezi mazuri, upendo na zawadi.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Zanzibar, Bi. Mariam Saleh Tuzo ya shukran kutokana na mchango wa Mfuko huo kuwa miongoni mwa Taasisi zilizofanikisha kufanyika kwa Kongamano hilo ambalo ni sehemu ya Tamasha la 10 la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar usiku wa kuamkia leo Agosti 12, 2026.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Taasisi zilizopatiwa tuzo

Rais wa Zaznibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Kushoto) na mkewe Mama Mariam Mwinyi (mwenye raba nyekundu), wakitembelea mabanda ya Maonesho baada ya kuzindua Tamasha la Kizimkazi Agosti 12, 2026



Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, akiwa na Tuzo ya shukrani baada ya kukabidhiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kukabidhiwa



Zanzibar, Agosti 12, 2026


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameutunuku Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) tuzo ya kutambua mchango wake katika kuwezesha kufanyika kwa Mdahalo wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, usiku wa kuamkia leo, Agosti 12, 2026.


Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, kwa niaba ya Mfuko, ikiwa ni sehemu ya utambuzi kwa taasisi na wadau walioshiriki katika kuwezesha mdahalo huo, uliofuatiwa na Maonesho ya Picha za Tamasha la Kizimkazi.


Mdahalo huo umefanyika sambamba na Tamasha la 10 la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026), linalofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo tamasha hilo limeanza rasmi leo kwa matembezi pamoja na uzinduzi uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.


Ushiriki wa PSSSF katika mdahalo huo unaakisi dhamira ya Mfuko ya kushirikiana na Serikali, taasisi na wadau mbalimbali katika kuunga mkono mijadala yenye umuhimu kwa jamii, mazingira na maendeleo endelevu.


Aidha, PSSSF inawakaribisha wanachama na wananchi kutembelea banda la Mfuko katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayoanza leo, Agosti 12, 2026, kwa ajili ya kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko, amesema Afisa Uhusiano Mkuu wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady.

Mwisho


 


📌Asema wajibu wa kila Mtanzania ni kuhakikisha mafanikio yanakuwa endelevu

Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaendelea kuwa endelevu.

Dkt. Biteko amesema hayo wakati akishiriki mjadala kuhusu “Uongozi wa Kimkakati wa Tanzania katika Kuharakisha Mabadiliko ya Nishati Endelevu na Jumuishi”, uliofanyika katika Mdahalo wa Nishati Safi ulioandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF), Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Amesema uwepo wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia ni sehemu ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuipa msukumo ajenda hiyo katika ngazi mbalimbali za uongozi wake na kuifikisha hadi katika majukwaa ya kimataifa.

Dkt. Biteko amesema umuhimu wa kuendelea kuipa kipaumbele ajenda hiyo unatokana na ukubwa wa athari za matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia, ikiwemo uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa, ambapo takribani hekta 470,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini.

Aidha, amesema zaidi ya watu 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa wakati wa kupika, hali inayoonesha umuhimu wa kuongeza kasi ya mpito kuelekea matumizi ya nishati safi.

Ameongeza kuwa matumizi ya nishati isiyo safi yana athari za kijinsia, hususan kwa wanawake ambao hutumia muda mwingi kutafuta kuni badala ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.

Amesema athari hizo pia zinawagusa watoto, ambapo baadhi yao hukosa muda wa kutosha wa kuhudhuria masomo kutokana na kulazimika kusaidia familia zao kutafuta kuni kwa ajili ya kupikia.

Katika mjadala huo, Dkt. Biteko amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini za mara kwa mara ili kubaini kiwango cha uendelevu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan baada ya wananchi kuwezeshwa kupata teknolojia na miundombinu husika.

Amesema tathmini hizo zitasaidia Serikali na wadau kubaini changamoto zilizopo, kupima matokeo yaliyofikiwa na kuweka mikakati madhubuti zaidi ya kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Pia, Dkt. Biteko ameipongeza Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuwa miongoni mwa taasisi zinazochangia utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia shughuli mbalimbali, ikiwemo kusaidia upatikanaji wa miundombinu pamoja na kuendesha midahalo inayowakutanisha wadau kujadili namna bora ya kuharakisha matumizi ya nishati safi, salama na endelevu nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kuhusu mkakati na mpango kazi wa Taifa wa hifadhi ya bioanuai, taarifa hiyo ameiwasilisha Bungeni Agosti 11, 2026.
Clement akiwa na ng’ombe/eneo la malisho

*******************

MTANANA, KONGWA, DODOMA — Kwa miaka mingi, Clement Alfonce alifuga ng’ombe kwa kutegemea malisho ya asili. Ng’ombe wake walizunguka katika maeneo mbalimbali kutafuta malisho, hali iliyomweka katika migogoro ya mara kwa mara na majirani ambao mazao yao yaliathiriwa na mifugo hiyo.

Clement, mkazi wa Kijiji cha Mtanana katika Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, alikuwa na ng’ombe 56. Lakini kuwa na mifugo mingi hakukuwa na maana ya kuwa na ufugaji wenye uhakika.

Wakati wa ukame, malisho yalipungua na hali ya mifugo ilidhoofika. Baadhi ya ng’ombe walikufa kipindi cha ukame. Wakati mwingine mifugo iliingia katika mashamba ya majirani, na Clement alilazimika kulipa faini.

Changamoto hiyo ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Leo, hali imebadilika.

Clement amepunguza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa ufugaji wa kufuatana na ng’ombe kutafuta malisho. Ameuza ng’ombe wake 50 na kununua ng’ombe 16 wa maziwa anaowafuga kwa mfumo malisho bandani.

Mabadiliko hayo yameambatana na jambo jingine muhimu: sasa Clement analima malisho yake mwenyewe.

Shamba lake la malisho limekuwa sehemu muhimu ya mfumo wake mpya wa ufugaji, na ana matumaini makubwa kwamba uzalishaji huo utampa chakula cha kutosha cha mifugo hata wakati wa ukame.

Mabadiliko hayo yamechochewa kwa kiasi kikubwa na maarifa aliyoyapata kupitia utafiti shirikishi unaofanywa na watafiti wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa ufadhili wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

Utafiti huo, unaoongozwa na Dkt. Dorice Lutatenekwa, unahusisha tathmini ya aina mbalimbali za nyasi kwa lengo la kubaini uwezo wake wa kustahimili ukame na kutoa malisho yanayoweza kusaidia wafugaji katika mazingira yenye changamoto ya mabadiliko ya tabianchi.

Kwa Clement, ushiriki katika utafiti haukuwa suala la kusikia matokeo kutoka kwa wataalamu pekee. Alipata fursa ya kuona aina mbalimbali za malisho zikifanyiwa majaribio na kutathmini matokeo yake katika mazingira yake.

Kadiri alivyopata uelewa kuhusu uzalishaji wa malisho, ndivyo alivyobadilisha mtazamo wake kuhusu ufugaji.

Badala ya kujiuliza ng’ombe wake watapata wapi malisho, alianza kujenga uwezo wa kuzalisha chakula cha mifugo yake mwenyewe.

“Nilikuwa na ng’ombe wengi, lakini changamoto kubwa ilikuwa malisho, hasa wakati wa ukame. Mifugo ilikuwa ikiingia kwenye mashamba ya watu na nililazimika kulipa faini. Nilipojifunza kuhusu uzalishaji wa malisho na kuona matokeo ya utafiti, nikaona umuhimu wa kubadilisha mfumo wangu wa ufugaji.” Clement Alfonce, Mfugaji, Kijiji cha Mtanana B, Kongwa

Uamuzi wa Clement wa kuhamia kwenye ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kwa mfumo wa malisho bandani unaonyesha namna utafiti unavyoweza kusaidia katika kufanya maamuzi ya uzalishaji katika ngazi ya kaya.

Badiliko hilo halimaanishi tu kwamba idadi ya ng’ombe wake imeshuka kutoka 56 hadi 16.Maana yake kubwa iko katika mabadiliko ya mfumo wa ufugaji.

Ng’ombe waliokuwa wakitegemea malisho yanayopatikana kwa kutangatanga sasa wana mfumo maalumu wa kulishwa. Clement anaweza kupanga uzalishaji wa malisho, matumizi yake na mahitaji ya mifugo yake.

Hii pia inapunguza utegemezi wa malisho ya asili ambayo hupungua wakati wa ukame.

Utafiti wenye mantiki shambani

Maisha ya Clement inaonyesha changamoto kubwa inayokabili sayansi katika nchi nyingi, na namna ya kuhakikisha kwamba maarifa yanayozalishwa na watafiti yanafika kwa watu wanaohitaji kuyatumia.

Katika utafiti wa Mtanana, wafugaji wameshirikishwa katika mchakato wa kujifunza na kutathmini aina za malisho zinazofanyiwa majaribio.

Katika ziara ya kutathmini maendeleo ya utafiti huo, Dkt. Lutatenekwa alimweleza Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu, matokeo ya awali ya utafiti na namna wafugaji wanavyoshiriki katika mchakato huo.

Ziara hiyo ilitoa picha ya tofauti kati ya utafiti unaobaki kwenye ripoti na utafiti unaoanza kubadili namna watu wanavyozalisha.

Katika eneo la utafiti kulionekana malisho yanayofanyiwa tathmini, mashamba ya wakulima na wafugaji wanaojaribu kutumia maarifa hayo katika mifumo yao ya uzalishaji.

Kwa COSTECH, uzoefu huo unaendana na umuhimu wa kuwekeza katika utafiti unaozalisha maarifa yenye matumizi kwa jamii na uchumi.

Katika mahojiano yake waandishi wa habari wakati wa ziara hiyo, Dkt. Nungu alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha kuwa matokeo ya utafiti na teknolojia yanawafikia watumiaji wa mwisho na kusaidia kutatua changamoto halisi zinazowakabili wananchi.

“Tunataka utafiti uzalishe maarifa au utoe teknolojia ambazo zitakuwa suluhui kwa changamoto za watanzania. Mradi huo tumeona unavyobadili maisha ya Mfugaji Bw.Clement Alfonce, tunataka uwe na matokeo makubwa na chanya kwa wafugaji wote zaidi ya 1300 waliopo kwenye kata hii ya Mtanana” Dkt. Amos Nungu, Mkurugenzi Mkuu, COSTECH

Mabadiliko ya tabianchi yanabadilisha namna ya kufuga

Kongwa ni miongoni mwa maeneo ambayo wafugaji wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa malisho, hasa katika vipindi vya ukame.

Kwa mifugo inayotegemea malisho ya asili, ukame unaweza kumaanisha kupungua kwa chakula, kudhoofika kwa mifugo na hata vifo.

Katika mazingira hayo, uwezo wa mfugaji kuzalisha malisho yanayostahimili ukame unaweza kuwa sehemu ya mkakati mpana wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Ndiyo maana utafiti wa aina hii una umuhimu zaidi ya kutafuta aina nzuri ya nyasi. Unahusu usalama wa chakula cha mifugo, ustahimilivu wa mifumo ya uzalishaji na uwezo wa kaya za wafugaji kukabiliana na mabadiliko ya mazingira.

Kwa Clement, mwanga umeanza kuonekana.

Shamba lake la malisho linampa nafasi ya kupanga zaidi kuhusu chakula cha mifugo yake. Mfumo wa malisho bandani unapunguza hitaji la ng’ombe kuzunguka kutafuta malisho na hivyo kupunguza uwezekano wa migogoro inayotokana na mifugo kuingia kwenye mashamba ya wakulima.

Na muhimu zaidi, Clement sasa anaona ufugaji kama mfumo wa uzalishaji unaoweza kupangwa na kusimamiwa, badala ya kutegemea upatikanaji wa malisho ya asili.

Miaka 40 ya COSTECH: kipimo ni maisha yanayobadilika

Tanzania inapoadhimisha miaka 40 ya COSTECH, hadithi ya Clement inaibua swali muhimu kuhusu maana ya uwekezaji katika sayansi, teknolojia na ubunifu.

Matokeo ya utafiti hayaishii katika maabara, ripoti au machapisho ya kitaalamu.Thamani yake inaonekana zaidi pale ambapo maarifa yanatumiwa kufanya uamuzi mpya.

Kwa Clement, uamuzi huo ulikuwa kubadilisha mfumo wa ufugaji. Kutoka kuwa na ng’ombe 56 wanaozunguka kutafuta malisho, sasa ana ng’ombe 16 wa maziwa wanaofugwa ndani.Kutoka kutegemea zaidi malisho yanayopatikana kwenye nyanda za malisho, sasa analima malisho kwa ajili ya mifugo yake. Kutoka kukabiliana mara kwa mara na migogoro ya mifugo na wakulima, sasa ana mfumo wa ufugaji unaomruhusu kudhibiti zaidi mahitaji ya mifugo yake.

Na kutoka kukabili ukame bila uhakika wa chakula cha mifugo, sasa anajenga msingi wa uzalishaji wa malisho unaoweza kumsaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Hii ndiyo picha pana ya miaka 40 ya COSTECH: sayansi inapokuwa na maana pale inapobadilisha uwezo wa Mtanzania kutatua changamoto yake mwenyewe.

Katika Mtanana, mabadiliko hayo hayajaandikwa tu kwenye ripoti. Yanaonekana kwenye shamba.Yanaonekana kwenye malisho. Yanaonekana kwenye banda la ng’ombe. Na yanaonekana katika uamuzi wa mfugaji mmoja kubadilisha kabisa namna anavyofuga.

Clement hakubadilisha tu idadi ya ng’ombe alionao. Alibadilisha mfumo wa maisha unaowaendesha. Kutoka ng’ombe wa kuzunguka kutafuta malisho hadi ng’ombe wa kufugia ndani.Kutoka kutegemea malisho asili hadi kuanza kuzalisha chakula cha mifugo yake.

Na nyuma ya mabadiliko hayo kuna jambo moja: maarifa yaliyotokana na utafiti.

 

Mimi naitwa Elizabeth, natokea mkoani Dodoma, maeneo ya Area D. Maisha yangu ya ndoa yalikuwa kwenye kilele cha mafanikio kwa nje kwa sababu mume wangu ni mwanasiasa anayejulikana nchi nzima. Lakini siri iliyokuwa ndani ya nyumba yetu ilikuwa ni ya kusikitisha.

Kwa muda mrefu, nilikuwa napitia changamoto ya kukosa hamu ya tendo la ndoa na kuwa mkavu kiasi kwamba nikawa naogopa kumuona mume wangu akirudi nyumbani.

Ili kukwepa unyumba, nilianza tabia ya kujifanya nimevamiwa na “pepo la usingizi”, nikifika tu chumbani, najilaza sakafuni au kitandani na kuanza kukoroma kwa nguvu hata kama sijalala, ili tu mume wangu asiniguse.

Mume wangu alianza kuchoka na tabia yangu. Alisema, “Elizabeth, mbona kila nikirudi unakuwa umechoka kiasi hiki? Unafanya kazi gani Dodoma nzima mpaka ukorome kama trekta?”. Nilianza kukosa amani maana nilijua mume wangu anaweza kuanza kutafuta mwanamke mwingine nje, na hali hiyo ingeharibu sifa yetu kama familia ya kiongozi.

Nilienda kwa madaktari bingwa hapa Dodoma wakaniambia nina upungufu wa damu, lakini dawa walizonipa hazikurudisha hamu wala kuondoa ukavu uliokuwa unanichoma kama moto wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.

 

Naitwa Zaituni, mkazi wa jijini Arusha, maeneo ya mtaa wa Njiro. Maisha yangu ya ndoa yalifika mahali yakawa ni ya aibu na siri nzito ambayo ilikaribia kunivunjia heshima yangu mbele ya mume wangu na jamii inayotuzunguka.

Mume wangu ni mfanyabiashara mkubwa wa vito vya thamani kama Tanzanite, hivyo maisha yetu yalikuwa ni ya anasa, lakini ndani ya chumba chetu cha kulala, kulikuwa na “jangwa” la kutisha.

Kwa takriban miaka minne, nilipoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa na mwili wangu ukawa mkavu kiasi cha kutisha. Kila mume wangu alipojaribu kunigusa, nilihisi maumivu makali kama ninasuguliwa na msasa butu.

Katika hali ya kukata tamaa na kuogopa mume wangu asije kunitupa nje, nilianza kufanya kitendo cha hatari. Nilikuwa naiba mafuta ya kulainisha mashine (lubricants) kutoka kwenye gereji ya mume wangu na kuyaweka kwenye kopo la ‘lotion’ ili tu kumlainisha mume wangu wakati wa tendo.


Mimi naitwa Rehema, mkazi wa jijini Dar es Salaam, eneo la Sinza. Kwa miaka mingi, maisha yangu yalikuwa ni mzunguko wa maumivu na masikitiko. Licha ya kuwa na kazi nzuri na mwonekano unaovutia, suala la ndoa lilikuwa kama ndoto ya mchana.

Kila mwanaume aliyekuja kwangu alikuwa akitafuta starehe tu na kisha kutokomea. Nilifikisha umri wa miaka 38 nikiwa bado nipo nyumbani kwa wazazi, huku mdogo wangu wa mwisho akishabeba mtoto wake wa pili.

Kila sherehe ya kifamilia ilikuwa ni kero kwangu; ndugu walikuwa wakinitazama kwa jicho la huruma lililochanganyika na dhihaka. “Rehema, mbona hutuletei wifi?” au “Umri unaenda, utazaa lini?” yalikuwa maswali ya kila siku.

Nilijaribu kila mbinu, kuanzia mitandao ya kijamii hadi kuomba marafiki waniunganishe na watu, lakini wapi! Nilianza kuamini kuwa labda nimezaliwa kuwa mpweke maisha yangu yote. Hofu ya kukosa watoto ilinitesa sana usiku, nilikuwa nalia hadi mto unaloa maji. SOMA ZAIDI.

 


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) leo, Agosti 11, 2026, imeendelea na vikao vyake kwa kupitia na kuchambua taarifa za hesabu zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za Manispaa ya Shinyanga, Halmashauri za Wilaya za Kishapu na Msalala.

Uchambuzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa ratiba ya Kamati katika kufuatilia usimamizi wa rasilimali za umma katika Serikali za Mitaa na kuimarisha mifumo ya uwajibikaji, kuhakikisha wananchi wanapata huduma zinazoendana na thamani ya rasilimali zinazotengwa kwa ajili ya maendeleo yao.









 


Na: OWM - TAMISEMI


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeanza rasmi vikao vyake jijini Dodoma kwa kukutana na watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, kujadili utekelezaji wa shughuli za Serikali, hususan miradi ya miundombinu na utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa Nne wa Bunge unaotarajiwa kuanza Agosti 25, 2026.

Katika kikao hicho, Kamati imepokea na kujadili taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhusu ukarabati wa barabara zilizoharibiwa na mvua za masika nchini, pamoja na maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya BRT na mpango wa kuboresha huduma za usafirishaji zinazotolewa na UDART.

Katika vikao hivyo, Kamati pia inatarajia kupitia masuala mbalimbali yanayohusu utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwemo uimarishaji wa huduma za maji na lishe shuleni, utunzaji wa mazingira, ujenzi wa viwanja vya michezo pamoja na ajira za walimu wa michezo katika shule za msingi na sekondari.

Aidha, ratiba ya Kamati inaonesha kuwa itajadili masuala ya elimu, afya na mazingira, ikiwemo ujenzi wa shule na miundombinu yake, mikakati ya kukabiliana na viuadudu katika halmashauri, pamoja na mahitaji ya walimu na maandalizi ya utekelezaji wa mabadiliko ya mtaala wa elimu.