NA DENIS CHAMBI, TANGA.


WASHINDI  kupitia maonesho ya  Elimu ujuzi na ubunifu yanayoendelea kufanyika  kitaifa mkoani Tanga  wanatarajiwa kuiwakilisha Tanzania katika maonesho ya kidunia  kwenda kuonesha ujuzi ,ubunifu na maarifa yao.


Hayo yameelezwa na  katibu mtendaji kutoka baraza la Taifa la elimu  ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET) Mwajuma Lingwanda wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho hayo ambapo amesema jumla ya washiriki 49  waliopatikana kwenye mchujo uliofanyika katika ngazi ya Kanda watashindanishwa  kwenye vipengele 9 ambapo kila  mshidi atakata tiketi ya kwenda kuiwakilisha Tanzania kimataifa.

"Mashindano haya yalianza katika ngazi ya Kanda ambapo tulikiwa na washiriki  katika maeneo 9 ya ujuzi  na baada ya hapo tumefikia kwenye maonesho ya kitaifa na tuna washiriki 49 kutoka kwenye taasisi mbalimbali waamuzi wako tayari  wale watakaofanikiwa kufaulu na kuwa washindi wa kwanza  watapata nafasi ya kushiriki kwenye mashindano ya kimataifa  mwaka huu"amesema Lingwanda.


Fani hizo zitakazoshindaniwa ni pamoja na mapishi , mekatroniksi, ujenzi, ujuzi wa mitandao,  uchomeleaji wa vyuma , uhandisi, ushonaji wa nguo, na urembo.

Akizungumza Mkurugenzi  mdhibiti ubora kutoka NACTVET Geoffrey Oleke amesema kuwa  ujuzi katika nyanja mbalimbali ni una umuhimu husasani kwa rika la vijana ambao ndio tegemeo na Taifa la kesho hivyo Taifa linapaswa kuwekeza katika elimu ya sayansi.


Amesema mchakato wa kuwapata washiriki wa maonesho hayo ulianza juni 2026 ambapo vyuo vyote vya sayansi vilishiriki katika mchakato katika fani 15 ambapo kati ya hizo  fani 9 zilipata washiriki wengi hivyo kupewa kipaumbele kwa washiriki wa mwaka huu kitaifa ambapo kila fani ina washiriki watano watakaochuana kuonyesha maarifa na ujuzi wao.


"Bila ujuzi kwa Hakika hakuna nchi inaweza ikaendelea kwahiyo na sisi kama nchi tunashiriki kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunakuza ujuzi wa vijana wetu katika shule za sekondari na vyuo ili tupate nguvu kazi iliyo imara ambayo itaisaidia nchi yetu katika kuchochea maendeleo yake" amesema  Oleke.


Maonesho hayo ambayo kwa mwaka huu wa 2026 yamebebwa na kauli mbiu isemayo Elimu ujuzi na ubunifu , njia ya kufikia dira 2050 yameanza kufanyika August 16 yakifunguliwa  rasmi na waziri wa elimu Prof. Adolfu Mkenda huku yakitarajiwa kufungwa August 24 na waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba




NA DENIS CHAMBI, TANGA.


TAASISI za elimu zilizopo hapa nchini zimetakiwa kuendana na  dira ya Taifa ya 2050  katika kupitia masomo tafiti na ujuzi mbalimbali wanaoutoa kwa wanafunzi  wanaosoma ngazi mbalimbali ili kuendana na maendeleo ya teknolojia..


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani wakati alipotembelea na kukagua maandalizi ya maonesho ya wiki ya kitaifa ya Elimu ujuzi na ubunifu yanayoendelea katika viwanja ya shule ya sekondari Usagara ambapo yanayotarajiwa kuzinduliwa rasmi na waziri wa elimu Prof Adolfu Mkenda  17 august 2026.


Dkt.Buriani amesema kuwa Kila taasisi  za elimu Zina wajibu wa kuwaelimisha wananchi juu ya mwelekeo wa kitaifa wa dira ya 2050 ili kutoa ufahamu juu ya malengo ya serikali katika maendeleo  kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo za kielimu.


kaimu mkuu wa kitengo Cha mawasiliano na masoko kutoka katika chuo cha maji  kilichopo mkoani Dar es salaam chini ya wizara ya maji Godfrey Kituli wakati akizungumza na Msumba Blog katika maonesho ya Elimu , sayansi na ubunifu yanayoendelea kufanyika kitaifa mkoani Tanga ambapo ameeleza kuwa katika kuunga mkono jitihada za serikali juu ya umuhimu wa utunzaji wa vyanzo vya maji wameweza kupanda miti zaidi ya 1500 katika chuo hicho.


"Kumekuwa na uharibifu wa vyanzo mbalimbali vya maji  kutokana na shughuli za kibinadamu  tunaendelea kufanya tafiti na kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha vyanzo vya maji  vinalindwa na kutunzwa, tunaiunga mkono moja kwa moja  serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu juu ya utunzaji wa mazingira hususani vyanzo vya maji vinavyowazunguka katika maeneo yao". Amesema Kituli.


Maonesho hayo ambayo yanajumuiaha zaidi ya taasisi 300  kwa mwaka 2026 yamebebwa na kauli mbiu isemayo Elimu , ujuzi na ubunifu njia  ya kufikia dira ya 2050 yanatarajiwa kufungwa rasmi august 24 na waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba.

Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS, Bw.Habakuki Kalebo,akiwasilisha mada wakati wa kikao kilichoandaliwa na BRELA cha Maafisa Biashara pamoja na Wakuu wa Idara za Viwanda na Biashara kinachofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA 

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limesisitiza umuhimu wa kusajili maeneo yote yanayohusika na uuzaji, usambazaji na uhifadhi wa bidhaa za chakula na vipodozi, likieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na bora, kulinda afya zao.

Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS, Bw.Habakuki Kalebo, amesema hayo wakati wa kikao kilichoandaliwa na BRELA cha Maafisa Biashara pamoja na Wakuu wa Idara za Viwanda na Biashara, akieleza kuwa TBS inashirikiana na Ofisi ya Rais–TAMISEMI kupitia mamlaka za serikali za mitaa katika kusimamia usajili wa maeneo hayo.

Kalebo amesema usajili huo unalenga kuhakikisha bidhaa zinazouzwa, kusambazwa au kuhifadhiwa ni salama, bora na zimethibitishwa na TBS, huku mazingira yanayotumika kuhifadhi na kuuza bidhaa yamekidhi masharti ya usalama na usafi. Amesema kwa bidhaa za chakula, hatua hiyo inasaidia kuzuia uchafuzi kwa kuhakikisha chakula hakihifadhiwi au kuchanganywa na bidhaa nyingine zinazoweza kuhatarisha ubora wake.

Aidha, amesema usajili huo unasaidia kudhibiti usalama wa vipodozi vinavyoingizwa sokoni, kwa kuhakikisha havina viambata vyenye madhara kwa watumiaji. Ameongeza kuwa ukaguzi katika maeneo hayo pia husaidia kubaini na kuondoa bidhaa zilizomaliza muda wake kabla hazijawafikia wananchi, hivyo kupunguza hatari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya bidhaa zisizofaa.

 "Mfumo wa usajili pia una umuhimu katika ufuatiliaji wa bidhaa sokoni, kwani pale changamoto inapojitokeza, TBS inaweza kubaini bidhaa husika zilipo, kiasi kilichopo na kuchukua hatua za haraka za kuziondoa sokoni. Amesema utaratibu huo unaimarisha udhibiti wa bidhaa na kuongeza uwezo wa Serikali kulinda afya na usalama wa wananchi."amesema Bw.Kalebo 

Amesema ushirikiano kati ya TBS, Maafisa Biashara na Mamlaka za serikali za mitaa ni muhimu katika kuhakikisha wafanyabiashara wanaelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria na Viwango vya bidhaa. 

Kalebo amesisitiza kuwa ulinzi wa afya ya wananchi unapaswa kuwa sehemu muhimu ya usimamizi wa biashara, akieleza kuwa mtu mwenye afya njema ana uwezo mkubwa wa kushiriki katika shughuli za uzalishaji na kuchangia uchumi wa taifa.

Amesema matumizi ya bidhaa salama hupunguza hatari za magonjwa na gharama za matibabu, hivyo usajili na udhibiti wa maeneo ya biashara ya chakula na vipodozi ni hatua muhimu katika kulinda afya ya jamii na kuongeza tija ya Taifa.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, amesema ushirikiano kati ya Serikali, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania na wadau mbalimbali ni muhimu katika kugeuza ubunifu, teknolojia na utafiti kuwa chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Dkt. Kida amesema hayo kuelekea Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026, inayotarajiwa kufanyika Agosti 31 hadi Septemba 4, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.



Amesema jukwaa hilo litasaidia kuunganisha mawazo bunifu, utafiti, teknolojia, sera, mitaji, masoko na uwekezaji, ili kuchochea suluhisho zenye kuongeza tija, kuzalisha ajira na kuboresha maisha ya wananchi.

“Hatuhitaji ubunifu unaobaki katika mawazo au maabara. Tunahitaji kuugeuza kuwa bidhaa, huduma na suluhisho zinazoongeza tija, kuzalisha ajira, kuvutia uwekezaji na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Dkt. Kida.

Aidha, Amesema ushirikiano wa Serikali, sekta binafsi, taasisi za elimu na utafiti, wabunifu, wajasiriamali, wawekezaji na washirika wa maendeleo utakuwa muhimu katika kujenga mazingira yatakayowezesha mawazo bunifu kufikia hatua ya utekelezaji na soko.

Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026, yenye kaulimbiu “Kutoka Kwenye Matarajio hadi Mabadiliko; Kutumia Ubunifu katika Kuelekea Tanzania yenye Ustawi wa Pamoja,” itajumuisha mijadala ya kisera, maonesho ya ubunifu, shughuli za vijana na majadiliano ya uwekezaji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo anatarajiwa kuzindua Jukwaa hilo, litakalohusisha mjadala wa Mawaziri kuhusu Ubunifu na Utekelezaji, utakaojadili namna ubunifu na teknolojia vinavyoweza kuimarishwa katika mipango na utekelezaji wa maendeleo ya Taifa.

Unaweza kujisajili sasa kupitia https://summitpoint.co.tz/events/iwtz-2026




SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeteketeza tani 39 za bidhaa za chakula zisizokidhi matakwa ya viwango, zenye thamani ya takribani Sh milioni 149, ikiwa ni hatua ya kuwalinda wananchi dhidi ya matumizi ya bidhaa zisizo salama.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

............

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amewataka Maafisa Biashara nchini kutumia nafasi zao kikamilifu kuibua fursa za uwekezaji, kuongeza thamani ya mazao na kuboresha mazingira ya biashara katika halmashauri, hatua inayolenga kuchochea maendeleo ya kiuchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Londo ametoa kauli hiyo leo Agosti 17,2026 jijini Dodoma  wakati wa Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara nchini, kilicholenga kuimarisha utekelezaji wa majukumu yao katika kukuza biashara, viwanda na uwekezaji.

Amesema Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchumi wa viwanda katika Afrika Mashariki na Kati, ikiwamo kufikia uchumi wa dola trilioni moja na kuongeza kipato cha Mtanzania hadi dola 7,000. Amesema kufikia malengo hayo kunahitaji uchumi imara, jumuishi na shindani unaotegemea sekta binafsi, sayansi na teknolojia, uwekezaji, utafiti pamoja na nguvu kazi yenye ujuzi.

"Maafisa Biashara wana jukumu la kuhakikisha halmashauri zinakuwa vituo vya uzalishaji, uwekezaji na biashara kwa kutambua fursa zilizopo, kuwaunganisha wazalishaji na masoko na kuhakikisha mazao yanaongezwa thamani. "amesema Mhe.Londo

Hata hivyo ametolea mfano wa mahindi, amesema wakulima wanapaswa kusaidiwa kuondokana na kuuza mazao ghafi na badala yake kuzalisha bidhaa kama unga wenye chapa na kuufikisha kwenye masoko, hatua itakayoongeza kipato na kuchangia kupunguza umaskini.

Aidha, amesema utekelezaji wa Dira 2050 unahitaji vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kushirikishwa kikamilifu katika uzalishaji, uwekezaji na biashara kupitia fursa za mikopo na uwezeshaji. Amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026, viwanda vikubwa vipya 25 vilijengwa katika sekta mbalimbali na kutoa ajira 39,000, zikiwamo ajira 7,600 za moja kwa moja na 31,000 zisizo za moja kwa moja.

Katika kuimarisha mazingira ya uwekezaji, Londo amezitaka mikoa kuhuisha kanzidata za viwanda, biashara, masoko, leseni, wawekezaji na maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kiuchumi, huku kila halmashauri ikiandaa wasifu wa fursa za uwekezaji unaoonyesha upatikanaji wa malighafi, miundombinu, masoko na maeneo ya uwekezaji. Pia amewataka Maafisa Biashara kuhakikisha Mabaraza ya Biashara yanafanya kazi kikamilifu na hoja za sekta binafsi zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Londo amewataka Maafisa Biashara kuharakisha urasimishaji wa biashara zisizo rasmi kwa kutoa elimu kuhusu usajili wa biashara, leseni, TIN, viwango, vipimo na taarifa za umiliki.

Amesema urasimishaji utawawezesha wafanyabiashara kupata huduma za uwezeshaji, mitaji na masoko, huku akieleza kuwa halmashauri zimetengewa asilimia tano ya mapato ya ndani, yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 72 kwa mwaka wa fedha 2026/2027, kwa ajili ya kuwekeza katika miundombinu ya masoko, maeneo ya biashara na ujasiriamali.

Amesisitiza fedha hizo zitumike kwa ufanisi kwa kushirikisha sekta za ardhi, maji, nishati na barabara ili kuongeza tija kwa wafanyabiashara na kuvutia wawekezaji. Aidha, amewataka Maafisa Biashara kutumia nafasi zao kuboresha huduma na kuifanya Tanzania kuwa na mazingira bora zaidi ya biashara na uwekezaji, hatua ambayo ni muhimu katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum, amewataka Maafisa Biashara kuongeza udhibiti wa bidhaa feki na viwanda visivyo rasmi katika maeneo yao, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda afya na usalama wa wananchi, watumiaji pamoja na wazalishaji wanaofuata sheria.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa, amesema Maafisa Biashara ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wafanyabiashara katika kuhakikisha sera, sheria na kanuni za biashara zinatekelezwa na kuleta mabadiliko chanya katika mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Amesema kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, BRELA imeendelea kuboresha mifumo na sheria zinazosimamia usajili na utoaji wa leseni kwa lengo la kupunguza muda na gharama za kuanzisha na kuendesha biashara. Amesema kupitia BRELA Online System (ORS), huduma za wakala zimeunganishwa katika mfumo mmoja, huku mfumo huo ukiwezesha pia utoaji na usimamizi wa leseni za biashara kundi A na B.

Amesema mfumo huo unatoa fursa kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoa na kusimamia leseni za kundi B bila kuathiri mapato yao, kwani malipo yanayofanywa na mfanyabiashara yanaingia moja kwa moja katika akaunti ya halmashauri husika.

Aidha, ORS imeunganishwa na mifumo ya taasisi nyingine za Serikali ikiwamo NIDA na TRA, hatua inayowezesha taarifa muhimu kupatikana moja kwa moja bila mfanyabiashara kuwasilisha nyaraka ambazo tayari zipo kwenye mifumo hiyo.

Nyaisa,amesema kuwa  maboresho hayo yameongeza uwazi na ufanisi, kupunguza urudufu wa taarifa, muda na gharama za kupata huduma, pamoja na kupunguza mianya ya uzembe katika utoaji wa huduma.

"BRELA itaendelea kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara, Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI, sekretarieti za mikoa na halmashauri katika kuwajengea uwezo Maafisa Biashara."amesema Nyaisa

Amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, BRELA imepanga kutoa mafunzo kwa Maafisa Biashara wote nchini kupitia kanda nne, yatakayolenga matumizi ya mifumo, utoaji na usimamizi wa leseni pamoja na utekelezaji wa sheria.

Pia amesema BRELA itaendelea kuboresha miunganiko ya mifumo ya kidijitali na kushirikiana na vyama vya Maafisa Biashara katika kutatua changamoto zao, huku akisisitiza kuwa maafisa hao ni mawakala muhimu wa uwekezaji nchini na wanapaswa kutambua kuwa jukumu lao ni kuwezesha biashara, si kuikwamisha, ili kujenga mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji.

Afya bora ndiyo msingi mkuu wa kila utafutaji wa riziki, lakini pale mwili unapofungwa na kuteseka kwa magonjwa ya ajabu, maisha yote husimama ghafla. Kwa zaidi ya miaka miwili, nilikabiliwa na mtihani mzito uliotishia kukatisha kabisa ndoto zangu.

Yalianza kama maumivu ya kawaida ya viungo na mgongo, lakini ndani ya muda mfupi, hali ilibadilika na kuwa mbaya zaidi miguu na mikono yangu ilipooza kabisa, na kuacha mwili wangu ukiwa hauna nguvu wala uwezo wa kujitikisa.

​Nilitumia fedha zote za akiba na hata kuuza baadhi ya mali zangu ili kupata matibabu kwenye hospitali kubwa na kwa madaktari bingwa.

Hata hivyo, kila vipimo vya MRI, CT scan, na vipimo vya damu vilipofanyika, majibu yalikuja yakionyesha kuwa sina ugonjwa wowote unaoonekana kisayansi.

Nilibaki kitandani nikihudumiwa kila kitu kama mtoto mchanga, nikiteseka na maumivu makali ya ndani kwa ndani usiku kucha.

Nilianza kuona aibu na unyonge mkubwa, nikitazama familia yangu ikiteseka kwa kuniuza na kunisikitikia, huku nikipoteza kabisa matumaini ya kuwahi kusimama tena kwa miguu yangu. SOMA ZAIDI.
Kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya masomo, kazi, au fursa za kimaisha ni ndoto ya kila kijana anayetaka kubadilisha mfumo wa maisha yake na wa familia yake. 

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikabiliwa na kizingiti kizito na cha ajabu sana kila nilipojaribu kukamilisha mchakato wa kusafiri kwenda ng’ambo.

Nilitumia fedha nyingi sana kulipia ada za maombi ya Visa, mawakili wa usafiri, na vipimo vya afya, lakini kila nilipofika hatua ya mwisho ya usahili (interview) au kupokea majibu kutoka ubalozi, nilipokea barua za kukataliwa.

​Mara ya kwanza nilijiambia ni bahati mbaya, lakini baada ya kukataliwa Visa mara ya nne mtawalia hata kwa safari ambazo nilikuwa na nyaraka zote halali na mwaliko rasmi ndipo nilipoanza kutambua kuna kitu kisichokuwa cha kawaida.

Kila mara nilipokaa mbele ya afisa wa ubalozi, nilipatwa na woga wa ajabu, ulimi ulikuwa mzito kujieleza, na sura yangu ilionekana kama ya mtu asiye na uaminifu mbele yao.

Nilibaki nikitazama marafiki zangu waliokuwa na nyaraka dhaifu kuliko zangu wakipata Visa kwa urahisi na kuondoka, huku mimi nikibaki nikiwa nimefilisika kwa gharama za safari zisizopatikana na kuchekwa na watu wa mtaani. SOMA ZAIDI.
Msiba wa wazazi ni pigo kubwa linalomuachia kila mtoto simanzi na ukiwa, lakini inapojitokeza hali ambapo ndugu wa damu wanatumia fursa hiyo kukudhulumu na kukupora urithi wako, maumivu yake huwa mazito mno kuvumilika.

Baada ya kuondokewa na wazazi wangu waliotutoka kwa pamoja, nilibaki mimi kama mtoto wa pekee nikiwa na matumaini ya kuendeleza mali zao ikiwemo nyumba ya familia na shamba kubwa la kilimo.

Hata hivyo, kabla hata ya siku arobaini kumalizika, mijomba na mashangazi zangu waligeuka ghafla. Walikaa kikao cha familia bila kunishirikisha, wakatengeneza nyaraka za uongo, na hatimaye walinifukuza kwenye nyumba na kupora shamba lote.

​Nilibaki mtaani nikiwa sina mbele wala nyuma, nikilia kwa uchungu na unyonge. Nilitafuta msaada kwa viongozi wa mtaa na hata kujaribu kwenda polisi, lakini ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuziba pengo kila mahali.

Nilipojaribu kuwasogelea na kuwaomba wanihurumie, walinitishia kunifanyia vitendo vya kishirikina au hata kuniondoa duniani kama nitaendelea kufuatilia mali hizo.

Nilibaki nikiishi maisha ya uombaomba, nikiwa nimekonda kwa mawazo, huku nikitazama mali za wazazi wangu zikitumiwa na watu waliokosa huruma wala woga wa Mungu. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imeombwa kuzipa kipaumbele kampuni binafsi zenye uwezo wa kuzalisha oksijeni ya tiba kwa ajili ya matumizi hospitalini, badala ya kuwekeza zaidi katika uzalishaji wake, ili kutumia kikamilifu uwezo uliopo nchini.
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imewakumbusha Jamii juu ya umuhimu wa kulinda miundonbinu ya Maji ili kujenga jumuiya inayothamini huduma ya Maji kwa vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.
Kujituma kwa bidii na kutafuta maendeleo ni lengo la kila familia, lakini pale unapoona familia nzima, ndugu, na ukoo mzima unateseka kwa umaskini wa kutupwa na mikosi ya aina moja, inakuwa wazi kuwa tatizo ni kubwa zaidi ya juhudi za kibadamu.

Kwa miaka na miaka, ukoo wetu ulikabiliwa na hali ya kusikitisha sana. Hakuna mtu yeyote kwenye familia yetu aliyewahi kufanikiwa kimaisha iwe ni kusoma na kupata kazi, kuanzisha biashara, au hata kudumu kwenye ndoa.

Kila kijana alipofikisha umri wa kuanza kujitegemea, alikumbana na mikosi mizito, magonjwa ya ajabu, au kufilisika ghafla na kurudi kijijini kuishi kwa unyonge.

​Nilibaki nikitazama ndugu zangu wenye akili na uwezo mkubwa wakishindwa kabisa kupiga hatua, huku ukoo wetu ukichekwa na kudharaulika sana mtaani. Hali hii iliniletea huzuni na msongo mkubwa wa mawazo.

Kila nilipojaribu kupambana ili nikuze uchumi wangu na kuivusha familia, nilikutana na vizuizi visivyoeleweka na kupoteza fedha zangu zote.

Nilianza kuona wazi kuwa familia yetu ilikuwa kwenye kifungo cha giza na laana ya kurithishwa iliyokuwa ikinyonya mafanikio ya kila kizazi. SOMA ZAIDI.
Kujenga au kupanga nyumba na kuweka vitu vyako vya thamani ni hatua kubwa ya maendeleo, lakini pale eneo lako linaposhambuliwa na wimbi la wizi na uvamizi, amani ya familia yote huchukuliwa ghafla.

Kwa miezi kadhaa, mtaa wetu ulikabiliwa na genge la majambazi na vibaka waliokuwa wakivunja nyumba na kuiba vitu vya thamani usiku wa manane. Kila siku tuliamka na kusikia nyumba ya jirani fulani imeingiliwa, watu wakipigwa, na mali zote kuondolewa.

​Hali hii iliniletea hofu na msongo mkubwa wa mawazo. Kila jioni ilipowadia, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu, nikishindwa kupata usingizi usiku kucha huku nikisikiliza kila kishindo au mshindo wa nje.

Niliweka milango ya chuma, makufuli makubwa, na hata taa za usalama, lakini bado majambazi hao waliendelea kuvunja nyumba za majirani zetu waliokuwa na milango imara zaidi.

Nilibaki nikitetemeka kwa hofu ya zamu yetu kufika, nikihofia maisha ya mke wangu, watoto wangu, na mali tulizozitolea jasho kwa miaka mingi. SOMA ZAIDI.
Kuanzisha biashara na kuwekeza mtaji wako wote kwa matumaini ya kupata faida ni hatua kubwa ya kuelekea kwenye mafanikio ya kifedha.

Hata hivyo, pale unapotazama siku zikienda bila mteja hata mmoja kuingia dukani, huku kodi ya pango, bili, na madeni vikikuandama, maisha huanza kuwa chungu sana.

Kwa miezi kadhaa, nilikabiliwa na ukame mkubwa wa wateja kwenye duka langu la nguo na vipodozi. Nilikuwa nikiamka asubuhi na mapema, nikifungua duka kwa matumaini, lakini nilishinda nimeketi peke yangu mchana mzima huku maduka ya majirani zangu yakifurika watu kila dakika.

​Hali hii iliniletea msongo mkubwa wa mawazo na unyonge. Nguo na bidhaa zilizopo dukani zilianza kuharibika na kupitwa na wakati, huku mtaji wangu ukiendelea kukatika kwa ajili ya kulipia pango la duka na gharama za usafiri.

Kila nilipojaribu kupunguza bei au kufanya matangazo, hakuna kilichobadilika watu walipita mbele ya duka langu wakitazama ndani na kuondoka bila kuingia.

Nilianza kukata tamaa na kufikiria kufunga duka hilo kwa aibu kubwa, nikiwa nimeingia kwenye madeni mazito na kupoteza akiba yangu yote ya maisha. SOMA ZAIDI.

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka amewataka vijana kutumia michezo kama fursa ya kujipatia ajira na kujenga maisha yao, huku wakiepuka vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi na ukatili wa kijinsia.

Naibu Waziri Mahundi ameyasema hayo wakayi akikabidhi vifaa vya michezo kwa timu 13 za Kata ya Iwambi jijini Mbeya.

Amesema michezo inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kuwaweka vijana pamoja, kuwajengea vipaji na kuimarisha amani na mshikamano katika jamii huku akiwataka wananchi wa Iwambi kuunda timu moja imara itakayowakilisha kata hiyo katika mashindano mbalimbali na kuitangaza Iwambi kupitia michezo.

Aidha, amependekeza kuanzishwa kwa klabu ya mbio za pole (jogging) katika kata hiyo, akisema mazoezi ni muhimu katika kuimarisha afya na kusaidia jamii kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kwani michezo inapaswa kuwa chombo cha kuimarisha upendo na mshikamano ndani na nje ya Kata ya Iwambi, huku akitoa wito wa kushirikiana katika mapambano dhidi ya uhalifu.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Iwambi, Groria Ipopo Mwamajemba (Mchina), amemshukuru Mahundi kwa msaada huo, akisema amekuwa sehemu ya wakazi wa Iwambi na ameendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo katika kata hiyo.

Mwamajemba amesema kupitia michezo, vitendo vya uhalifu vimepungua kwa kiasi kikubwa katika Kata ya Iwambi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika michezo kwa vijana.

Mahundi ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya na Mkurugenzi wa Maryprisca Women Empowerment Foundation (MWEF), amekabidhi jozi mbili za vifaa vya michezo kwa kila timu pamoja na mpira mmoja kwa kila timu, katika hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Sekondari Iwambi ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Diwani wa Kata ya Iwambi, Groria Ipopo Mwamajemba maarufu kama Mchina, aliyeanzisha mashindano ya mpira wa miguu yaliyowakutanisha vijana kutoka mitaa mbalimbali ya kata hiyo.













Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa pili kulia), akifurahi kuzindua mradi wa jengo la utawala la Shule ya Sekondari Mjini Kati uliotekelezwa kwa fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kutoka mgodi wa Barrick North Mara. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele na viongozi wengine wa wilaya.

 




TAASISI ya Kuzuia na Kupambana ana Rushwa nchini (TAKUKURU) imekabidhi vifaa muhimu vya kisasa kwa ajili ya kuimarisha huduma kwa watoto wachanga hususani waliozaliwa kabla ya wakati (njiti) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo.

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo Leo Agosti 15,2026 imepokea vifaa muhimu vya kisasa kwa ajili ya kuimarisha huduma kwa watoto wachanga, hususan waliozaliwa kabla ya wakati.

Vifaa hivyo, ambavyo ni Phototherapy na Infant Warmer, vimetolewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini-TAKUKURU ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Hospitali ya Bombo katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Akikabidhi vifaa hivyo katika hafla fupi iliyofanyika Hospitalini hapa, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini, Bw. Crispin Chalamila, amesema taasisi hiyo imeamua kutoa msaada huo baada ya kuona juhudi zinazofanywa na Hospitali ya Bombo katika kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Tanga wanapata huduma bora za afya.

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo, Dkt. Husein Mangaa, ameishukuru TAKUKURU kwa msaada huo wa thamani kubwa na kwamba vitaongeza uwezo wa hospitali katika kutoa huduma kwa watoto wachanga wanaohitaji uangalizi maalum.

Naye Daktari Bingwa wa Watoto, Dkt. Mohamed Saleh, ameipongeza TAKUKURU kwa kuunga mkono juhudi za hospitali, akieleza kuwa vifaa hivyo vitasaidia wataalam kutoa huduma kwa ufanisi zaidi kwa watoto wachanga.

Uongozi wa Hospitali ya Bombo umeeleza kuwa upatikanaji wa vifaa hivyo ni hatua nyingine muhimu katika kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga na maeneo jirani.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Tanga na viongozi kutoka timu ya Afya ya mkoa wa Tanga ikiongozwa na Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa wa Tanga Bwana Imani Clemence.