Na. Josephine Majura, WF, Dodoma

Wizara ya Fedha imezitaka kampuni na taasisi zinazotoa bidhaa na huduma kwa Wizara kuendelea kuzingatia viwango vya ubora, uaminifu, uwazi na masharti ya mikataba ili kuhakikisha Serikali inapata thamani halisi ya fedha katika matumizi ya rasilimali za umma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tathmini ya Mwaka 2025/26 cha Utendaji wa Wazabuni na Watoa Huduma kwa Wizara ya Fedha kilichofanyika katika Ukumbi wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha, Bw. Lusius Mwenda, alisema kuwa Wizara inatarajia kuona maboresho makubwa katika utoaji wa bidhaa na huduma, hususan katika maeneo ya ubora, ufanisi na matumizi ya teknolojia za kidijitali.

Alisema kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa mikataba mbalimbali, bado kuna umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara na watoa huduma ili kukabiliana na changamoto zinazojitokeza na kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali.

“Tunatarajia wazabuni na watoa huduma kuendelea kuzingatia viwango vya ubora vilivyokubalika, kuwasilisha bidhaa na huduma kwa wakati, pamoja na kuzingatia maadili ya kitaaluma na taratibu zote za ununuzi wa umma,” alisema Bw. Mwenda.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kujenga na kudumisha uhusiano wa kikazi unaozingatia uaminifu na uwazi, akieleza kuwa misingi hiyo ndiyo msingi wa mafanikio katika utekelezaji wa mikataba ya Serikali.

Wizara pia imeeleza kuwa itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wazabuni na watoa huduma ili kuhakikisha mikataba inatekelezwa kwa ufanisi na changamoto zinazojitokeza zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi, Wizara ya Fedha, Bw. Boaz Ntembanda, alisema lengo la kikao hicho ni kufanya tathmini ya utekelezaji wa mikataba ya wazabuni na watoa huduma, kubaini changamoto zilizojitokeza na kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha utoaji wa bidhaa na huduma kwa wakati, kwa ubora unaotakiwa na kwa kuzingatia masharti yaliyokubaliwa.

 

Naye mmoja wa wwaakilishi wa wazabuni wanaotoa huduma Wizara ya Fedha, Bi. Happiness Kategile, aliipongeza Wizara kwa kuwakutanisha pamoja wazabuni na watoa huduma, akisema hatua hiyo imefungua fursa ya kujadiliana kwa uwazi, kubadilishana uzoefu na kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa mikataba.

Katika kikao hicho, washiriki walipata fursa ya kujadili utekelezaji wa mikataba, ubora wa huduma zilizotolewa, matumizi ya TEHAMA katika mifumo ya ununuzi na ugavi, pamoja na masuala ya mazingira, jamii na utawala bora katika shughuli za ununuzi wa umma.










 

Na: OWM – KAM, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu amewataka waajiri nchini kuzingatia viwango vya kima cha chini cha mshahara vilivyowekwa na Serikali ili kuhakikisha wafanyakazi katika sekta binafsi wanapata stahiki zao kwa mujibu wa sheria hatua itakayosaidia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Mhe. Sangu ametoa wito huo Juni 25, 2026, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 67 wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) uliofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam ambapo amesema ulipaji wa mishahara inayokidhi viwango vya chini vilivyowekwa kisheria ni wajibu wa kila mwajiri ambapo inaongeza motisha kwa wafanyakazi na kuimarisha uzalishaji katika maeneo ya kazi.

Waziri Sangu amesema ili sekta ya kazi kuendelea kuwa na mafanikio ni jambo muhimu kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ili kuhakikisha nguvu kazi ya wafanyakazi inalindwa na wakati huo huo kuhakikisha kuwa mazingira ya biashara yanabaki rafiki, shindani na endelevu.

Amesema Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waajiri watakaobainika kukiuka masharti ya mishahara kwa kuwalipa wafanyakazi kiwango cha chini ya kile kilichoainishwa katika sheria na kanuni za kazi.

Sambamba na hilo, Waziri Sangu amewataka waajiri wote kuendelea kuzingatia sheria za kazi kwa kuwasilisha kwa wakati michango ya wafanyakazi katika mifuko ya hifadhi ya jamii ikiwemo NSSF, PSSSF pamoja na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) bila kuchelewa au kukiuka taratibu zilizowekwa.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza mahusiano mazuri kazini kupitia majadiliano na ushirikiano kati ya waajiri na wafanyakazi ili kuimarisha tija, amani na maendeleo katika maeneo ya kazi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Sangu amepongeza Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kuingia makubaliano na NSSF akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuongeza uelewa na uzingatiaji wa sheria za kazi, hususan katika masuala ya kinga ya jamii, mishahara na utoaji wa ajira zenye staha.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bw. Oscar Mgaya amesema mkakati mpya wa miaka mitano wa chama hicho unalenga kuimarisha uwezo wa waajiri kuboresha huduma kwa wanachama na kuongeza mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya taifa ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Waajiri ni nguzo muhimu katika kukuza uchumi, kuongeza ajira zenye staha na kuchangia mapato ya Serikali, hivyo ushirikiano kati ya Serikali, Waajiri na Wafanyakazi utaendelea kuimarishwa kupitia majadiliano ya kijamii yenye tija ili kutatua changamoto za maeneo ya kazi kwa wakati,” amesema Mgaya.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Bw. Hery Mkunda amesema TUCTA na ATE zimeendelea kushirikiana katika kutekeleza miradi mbalimbali yenye lengo la kuongeza tija kwa wafanyakazi na waajiri.

Miongoni mwa miradi hiyo ni programu za ukuzaji ujuzi na uanzishwaji wa kituo kinachotoa taarifa sahihi na huduma kwa Watanzania wanaokwenda kufanya kazi nje ya nchi pamoja na raia wa kigeni wanaokuja kufanya kazi nchini.

Mkunda amewakumbusha waajiri kuendelea kuimarisha ushirikiano na wafanyakazi kwa kuwashirikisha katika masuala ya maeneo ya kazi na kuondoa dhana kwamba wafanyakazi ni wapinzani wa waajiri.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bw. Masha Mshomba akizungumza mara baada ya kusaini hati ya makubaliano ya ushirikiano wa taasisi yake na ATE amesema utaongeza wigo mpana wa kufanikisha shughuli za NSSF ikiwa ni mkakati wa kuanza kutekeleza Dira ya 2050 kupitia wigo wa hifadhi ya jamii.

 

 

 


📌Apongeza juhudi za REA kusambaza Nishati Safi ya kupikia vijijini


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba leo tarehe 25 Juni, 2026 amefunga rasmi Maonesho na Kongamano la Nishati Safi Expo 2026  yaliyofanyika katika ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam

Akiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ameipongeza REA kwa kuendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. 

"Naipongeza REA kwa kazi kubwa mnayoifanya katika kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na naendelea kuwahimiza wananchi kuendelea kutumia teknolojia mpya za nishati safi ili kulinda afya, mazingira na kuboresha ustawi wa jamii, " Ameongeza Mhe. Makamba. 

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha malengo ya Taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yanafikiwa kwa manufaa ya Watanzania wote.

Aidha, Mhe. Makamba ameelezwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanahama kutoka katika matumizi ya nishati zisizo safi na zisizo salama kwenda kwenye teknolojia bora za nishati safi ya kupikia.

Vilevile, Mha wa miradi Francis Manyama amemfafanulia  kuwa kupitia maonesho hayo, REA imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuonesha teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya kuni mbadala, majiko banifu, majiko ya umeme na teknolojia nyingine rafiki kwa mazingira.

Alieleza kuwa washiriki mbalimbali wakiwemo baba lishe, mama lishe, washiriki kutoka asasi za kirai, na mashirika ya binafisi, walimu na wadau wengine walitembelea banda la REA na kupata elimu pamoja na kujionea teknolojia hizo zinazochochea matumizi ya nishati safi nchini.

Aidha, Mha. Manyama alimueleza Mhe. Makamba kuwa REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo usambazaji wa majiko banifu 200,000 katika mikoa 25 ya Tanzania Bara pamoja na usambazaji wa mitungi ya gesi ya LPG ya kilo sita ipatayo 3,255 kwa kila Wilaya kwa lengo la kurahisisha upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Vilevile, alibainisha kuwa Wakala unatekeleza mradi wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa siku, ambapo utekelezaji wake unafanyika kwa ushirikiano na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na Jeshi la Magereza.

Katika hatua nyingine, alieleza kuwa REA kupitia TPDC imetekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia ya kupikia katika kaya zilizopo mikoa ya Lindi na Pwani, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi wa maeneo hayo. Pia alieleza kua Wakala kupitia STAMICO utawezesha usimikaji wa mashine ya kuzalisha mkaa mbadala katika mkoa wa Geita ili kurahisha upatikanaji endelevu wa nishati ya kupikia kwa wingi na wakati.










Mwanangu alikuwa mmoja wa wanafunzi waliokuwa wakifanya vizuri sana shuleni.

Kwa miaka mingi alikuwa mwenye bidii, alihudhuria masomo yake vizuri, na walimu wake walikuwa na matumaini makubwa kuhusu mustakabali wake. Kama mzazi, nilijivunia maendeleo yake na niliamini angefikia ndoto zake.

Lakini hali ilibadilika ghafla. Alianza kupoteza hamu ya kwenda shule. Matokeo yake yakaanza kushuka, na mara nyingi alikuwa akitafuta sababu za kutohudhuria masomo. Mwanzoni nilidhani ilikuwa changamoto ya muda mfupi ambayo ingepita yenyewe.

Badala yake, mambo yalizidi kuwa mabaya.
Kadri miezi ilivyopita, mwanangu alianza kujitenga na familia. Hakutaka kuzungumza kuhusu kile kilichokuwa kinamsumbua. Nilijaribu kumshauri na kumtia moyo, lakini kila juhudi niliyofanya zilionekana kutofika kwake.
Hatimaye aliacha masomo kabisa. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miezi minane, familia yetu ilikuwa ikiishi kwa hofu. Kulikuwa na mwizi ambaye alikuwa akiingia nyumbani kwetu na wakati mwingine kwa majirani zetu bila kuacha ushahidi wa kutosha. Kila alipofanya wizi, alionekana kutoweka kana kwamba hakuna mtu ambaye angeweza kumgundua.

Mwanzoni tulidhani ni tukio la kawaida. Lakini kadri matukio yalivyoendelea kujirudia, tuliweza kuona kwamba mtu huyo alikuwa akifahamu vizuri mienendo ya watu katika eneo letu. Mara nyingi aliiba vitu vya thamani na kuondoka bila kuonekana. Hasira na hofu viliongezeka.

Tulijaribu kuwa makini zaidi. Tulibadilisha ratiba zetu, tukaongeza ulinzi, na hata kuwahusisha baadhi ya watu wa eneo letu katika jitihada za kumtafuta. Hata hivyo, mwizi huyo aliendelea kutusumbua. Watu wengi walianza kukata tamaa. SOMA ZAIDI.

Kwa muda mrefu, nilikuwa na ndoto ya kusafiri nje ya nchi. Nilitaka kuona dunia, kujifunza mambo mapya, na kufungua milango ya fursa ambazo sikuweza kuzipata nilipokuwa nyumbani. Kila nilipofikiria kuhusu safari hiyo, nilijawa na matumaini makubwa. Tatizo lilikuwa kupata visa.

Mara ya kwanza nilipotuma maombi, niliamini kila kitu kingekwenda sawa. Nilikuwa nimeandaa nyaraka zangu vizuri na nilijitokeza kwa mahojiano nikiwa na matumaini makubwa. Lakini maombi yangu yalikataliwa. Nilihuzunika, lakini sikuacha kujaribu.

Baada ya muda nilituma maombi tena. Mara ya pili nilikataliwa. Mara ya tatu hali ilikuwa ileile. Nilipojaribu mara ya nne na kupata jibu lilelile, nilihisi kama ndoto yangu ilikuwa imefika mwisho. Watu wengi waliniambia niache kupoteza muda na fedha. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa nimewekeza nguvu, muda, na fedha nyingi katika biashara yangu.

Mambo yalikuwa yanaenda vizuri mwanzoni. Wateja walikuwa wengi na nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu maisha yangu ya baadaye. Nilifanikiwa kupanua biashara na hata kuajiri wafanyakazi wachache ili kunisaidia kuhudumia wateja.

Lakini hali ilibadilika ghafla. Mauzo yalianza kushuka mwezi baada ya mwezi. Gharama za uendeshaji ziliongezeka huku mapato yakizidi kupungua. Nilijitahidi kutafuta njia za kuokoa biashara yangu, lakini kila hatua niliyochukua ilionekana kutokuleta matokeo.

Baada ya muda mfupi, nilikuwa nimepoteza karibu kila kitu. Madeni yaliongezeka, baadhi ya mali zililazimika kuuzwa, na biashara ambayo nilikuwa nimeijenga kwa miaka mingi ilionekana kuelekea kufungwa kabisa. Watu wengi waliniambia nikubali hali na nianze maisha mapya mahali pengine. SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningesikia mke wangu akinitajia neno talaka kwa uzito mkubwa. Tulikuwa tumefunga ndoa kwa miaka kadhaa na tulikuwa tumepitia mengi pamoja. 

Kama familia nyingine nyingi, tulikuwa na changamoto zetu, lakini sikuamini kwamba mambo yangefika hatua ya kutaka kuachana kabisa.

Mabadiliko yalianza taratibu. Mawasiliano yetu yalipungua, migogoro midogo ikawa ya mara kwa mara, na furaha iliyokuwa ndani ya nyumba yetu ilianza kupotea. 

Kila mmoja wetu alikuwa akibeba maumivu yake kimya kimya. Siku moja mke wangu aliniambia jambo ambalo lilinishtua sana.

Alisema alikuwa amechoka na hali ya ndoa yetu na alikuwa anafikiria kuomba talaka. Nilihisi kama dunia yangu ilisimama kwa muda. 

Nilijua kwamba kama nisingechukua hatua, familia yetu ingeweza kuvunjika. Kwa wiki kadhaa nilihangaika sana. Nilijiuliza ni wapi tulikosea na ni kwa nini tulifika hatua hiyo.SOMA ZAIDI.

 


Mamlaka ya Umeme Vijijini (REA) kutoka nchini Zambia yapongeza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini inayotekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Pongezi hizo zimetolewa leo Juni 24, 2026 na Mtendaji Mkuu wa REA Zambia, Mhandisi Alex Mbumba wakati wa ziara ya viongozi hao walipotembelea miradi ya umeme vijijini katika Kijiji cha Vikonje Mkoani Dodoma.

“Tumekuja Tanzania kujifunza na kujionea namna miradi ya umeme vijijini inavyotekelezwa baada ya mafanikio makubwa yaliyofikiwa ya kufikisha umeme kwenye vijiji vyake vyote.

Tumekuwa na vikao na uongozi wa REA Tanzania toka tulivyowasili nchini kwa ajili ya kujifunza. Leo tumekuja kuona miradi ya umeme inavyotekelezwa na namna ilivyonufaisha na kuboresha maisha ya wananchi vijijini. Tumeona REA Tanzania inavyotekeleza miradi yake kwa ubora na viwango vya Kimataifa,” amesema Mhandisi Mbumba huku akiwahamasisha wananchi kutumia umeme kujiletea maendeleo.

Kwa upande wake Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya kupeleka Umeme Vijijini kutoka REA Tanzania, Mhandisi Deogratius Nagu amesema kuwa ujio wa ugeni huo kutoka REA Zambia ni ishara ya kutambuliwa kwa mafanikio yaliyofikiwa nchini katika kupeleka huduma ya umeme kwa wananchi vijijini.

“Tanzania ni moja kati ya nchi chache Barani Afrika zilizofanikiwa kufikisha umeme katika vijiji vyake vyote, hivyo basi wenzetu wa Zambia wameona waje wajifunze ni kwa namna gani tumefanikiwa kutekeleza miradi yetu na kufikia mafanikio ya kufikisha umeme vijiji vyote vya Tanzania Bara,” amesema Mhandisi Nagu.













Na John Mapepele, WAF – Kilimanjaro

Tanzania imeandika ukurasa mpya katika mapambano dhidi ya saratani baada ya Serikali kuzindua rasmi Jengo la Tiba Mionzi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC), hatua inayotarajiwa kuwanufaisha maelfu ya wagonjwa wa Kanda ya Kaskazini na nchi jirani.

 

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026. Picha na Kadama Malunde
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga

Na Kadama Malunde -

Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga imewataka vijana wake kuendelea kulinda amani, kujiepusha na mijadala ya matusi kwenye mitandao ya kijamii na badala yake kujikita katika kueleza mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita, kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi kama njia bora ya kujibu hoja za wapinzani.

Wito huo umetolewa leo Juni 24, 2026 na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, wakati akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga, ambapo amesisitiza kuwa vijana wa CCM wanapaswa kuwa mabalozi wa amani, maendeleo na mshikamano wa taifa.

Werema amesema vijana wa UVCCM, ambao ni sehemu ya chama kinachoiongoza serikali, wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwahudumia wananchi bila ubaguzi, kusikiliza changamoto zao na kuzifikisha katika mamlaka husika, sambamba na kuhamasisha vijana kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotolewa na serikali.


"Vijana wa Mkoa wa Shinyanga tusijibu matusi mtandaoni. Tueleze mambo makubwa yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan. Tuwaambie vijana kuwa serikali haijalala. Wapinzani wanajaribu kuharibu taswira ya serikali kwa kutumia matusi badala ya hoja, lakini sisi tuwaeleze wananchi kuhusu fursa zilizopo na maendeleo yanayoendelea kutekelezwa," amesema Werema.

Ametaja baadhi ya miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa mkoani Shinyanga kuwa ni pamoja na Mradi wa Umeme wa Jua Kishapu, ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga pamoja na miradi mingine katika sekta mbalimbali, akisisitiza kuwa hayo ndiyo yanapaswa kuwa ajenda kuu za vijana wa CCM wanapozungumza na wananchi.

"Tusitumie muda mwingi kuhangaika na matusi. Tuwajibu wapinzani kwa vitendo, kwa kueleza mafanikio ya serikali na kwa kusikiliza pamoja na kutatua kero za wananchi," ameongeza.

Werema amesema UVCCM itaendelea kuwa nguzo ya kulinda amani, utulivu na mshikamano wa taifa huku ikiunga mkono juhudi za serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

"Tupo tayari kuipigania serikali dhidi ya wanaotaka kuharibu taswira ya nchi yetu. Vijana tutaendelea kuhubiri amani na hatutakuwa tayari kushiriki vitendo vya kuvuruga utulivu wa nchi. Ni jukumu letu kulinda serikali, kulinda taifa letu na kushirikiana kutatua changamoto za wananchi. Amani tuliyonayo lazima tuilinde," amesema.

Katika hatua nyingine, amesisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila amani na kuwataka vijana kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kuilinda.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga.

"Naomba tutunze amani ya nchi. Hatuwezi kufanya maendeleo bila amani. Tuwaambie wale wenye nia ya kuvuruga amani kuwa sisi tunahitaji amani. Sisi vijana hatuna muda wa kuvuruga amani, bali tuna jukumu la kushiriki katika maendeleo ya taifa," amesema.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amesema UVCCM ni tanuru la kuandaa viongozi wa taifa na nguzo muhimu katika kuimarisha uhai wa Chama Cha Mapinduzi.

Mhita amesema vijana wanapaswa kutumia nafasi waliyopewa ndani ya jumuiya hiyo kujifunza misingi ya uongozi, uzalendo na uwajibikaji ili waweze kuwa viongozi bora wa kesho.

"Jumuiya ya Vijana ni tanuru la kuoka viongozi. Hapa ndipo viongozi wengi wanapoandaliwa na kujengwa. UVCCM ni hazina ya viongozi wa taifa letu," amesema Mhita.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita.

Amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kuwawezesha vijana kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa fursa mbalimbali za kiuchumi.

"Dkt. Samia ni kiongozi anayewapenda vijana. Ni lazima vijana wawe na nidhamu. UVCCM ni jeshi la CCM ambalo lipo tayari kukitetea chama na kuunga mkono juhudi za Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Dkt. Samia Suluhu Hassan," amesema.

Mhita amesema Mkoa wa Shinyanga umeendelea kunufaika na uwekezaji mkubwa wa serikali katika kipindi cha uongozi wa Rais Samia ambapo zaidi ya shilingi trilioni 1.7 zimeelekezwa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
"Katika kipindi hiki cha uongozi wa Rais Samia, Mkoa wa Shinyanga umepokea zaidi ya shilingi trilioni 1.7 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Miradi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na imeendelea kuboresha huduma kwa wananchi," amesema.

Aidha, amewataka viongozi wa UVCCM na vijana kwa ujumla kuwa mabalozi wa maendeleo kwa kuwaelimisha wenzao kuhusu fursa zinazotolewa na serikali, hususan mikopo ya vijana inayotolewa kupitia halmashauri.

"Vijana waendelee kufuatilia na kutumia fursa zilizopo. Serikali imetoa fursa nyingi kwa vijana kuanzia ngazi ya halmashauri. Ninyi ndiyo wasemaji na watetezi wa vijana, waelekezeni namna ya kunufaika na fursa hizo na wahamasisheni kuchukua mikopo na kuirejesha kwa wakati," amesema.

Mhita pia amewapongeza vijana wa CCM Mkoa wa Shinyanga kwa nidhamu, ushiriki wao katika ziara mbalimbali za chama na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, akisema juhudi hizo zimeendelea kuimarisha chama na kuongeza idadi ya wanachama wapya.

"Nawapongeza vijana wa CCM Mkoa wa Shinyanga kwa nidhamu yenu, kwa kufanya ziara na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Mnaifanya CCM iendelee kuwa hai na kuendelea kupata wanachama wapya," amesema.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, amewataka vijana wa UVCCM kuendelea kukijenga chama kwa umoja, mshikamano na nidhamu huku akiwahimiza kujiepusha na makundi yasiyo na tija ambayo yanaweza kudhoofisha nguvu na umoja wa chama.

Batimayo amesema vijana wanapaswa kuwa na maono makubwa ya uongozi na kujiandaa kuwa viongozi wa baadaye kwa kufanya kazi kwa bidii, kujituma na kutanguliza maslahi ya chama na wananchi.

"Naomba tuepuke makundi ndani ya chama. Kila mmoja awajibike kwa nafasi yake, tuwaunge mkono viongozi wetu na tuendelee kuimarisha mshikamano ndani ya CCM," amesema Batimayo.

Ameongeza kuwa umoja, nidhamu na uwajibikaji vitasaidia chama kuendelea kuwa imara na kuandaa viongozi bora watakaoendeleza dhamana ya kuwatumikia wananchi siku zijazo.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Benson Werema, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026. Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Katibu wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Salama Mhampi akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Katibu wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Salama Mhampi akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Katibu wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Salama Mhampi akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika leo Juni 24, 2026.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, akizungumza katika kikao cha Baraza la UVCCM Mkoa wa Shinyanga