Nilianza kuhisi kama safari yangu haitawahi kufanikiwa, licha ya juhudi zote nilizokuwa nafanya. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu changamoto yangu. SOMA ZAIDI.
Nilianza kuhisi kama safari yangu haitawahi kufanikiwa, licha ya juhudi zote nilizokuwa nafanya. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu changamoto yangu. SOMA ZAIDI.
Hakupenda tena mazungumzo marefu, hakutabasamu kama zamani, na mara nyingi alikuwa na msongo wa mawazo.
Nilijaribu kumuuliza kama kuna tatizo, lakini majibu yake yalikuwa mafupi au wakati mwingine hakuna majibu kabisa. Hali hii ilinifanya nijisikie kupotea ndani ya ndoa yangu.
Kadri siku zilivyopita, umbali kati yetu uliongezeka. Nilianza kuhisi kama tunaishi maisha mawili tofauti chini ya paa moja. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Nilianza kuhisi kama safari yangu haitawahi kufanikiwa, licha ya juhudi zote nilizokuwa nafanya. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu changamoto yangu. SOMA ZAIDI.
VIJANA nchini wametakiwa kupewa mafunzo ya uongozi tangu wakiwa katika umri mdogo ili kuwaandaa kuwa viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kuongoza katika nyanja mbalimbali, hatua inayolenga kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

DODOMA, September 7, 2026:
UNESCO, in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, has launched a programme to establish and strengthen Information and Communication Technology (ICT) Clubs in public schools in Dodoma and Morogoro, aimed at equipping girls with digital skills, confidence and knowledge to pursue education and careers in technology.

The initiative is being implemented under the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls,” which seeks to reduce the gender gap in digital education and expand opportunities for women and girls to participate fully in the technology sector.




Speaking during the official launch held today at Edema Conference Hall in Kisasa, Dodoma, UNESCO Tanzania Head of Education Sector, Dr Faith Shayo, said the initiative was designed to encourage girls to develop an interest in technology, build confidence and explore opportunities in ICT-related education and careers.
She said the ICT Clubs would provide students with opportunities for practical learning, innovation and the development of skills to use technology to address challenges in their communities.
Dr Shayo said the programme would also involve ICT teachers and student teachers, with the clubs serving as platforms for extracurricular activities that give students practical experience beyond regular classroom lessons.

She said challenges contributing to the digital divide included disparities in access to technology, digital skills and competencies, as well as limited opportunities for girls to gain first-hand knowledge of education and career pathways in technology-related fields.

The programme is being implemented in collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), and the Tanzania Institute of Education (TIE).
A total of 20 public schools are expected to participate, with 10 from Morogoro Municipality and 10 from Dodoma City. The programme will directly benefit 500 girls and 40 teachers.

The official launch marks the beginning of a series of activities under the programme, with a four-day ICT Innovation Bootcamp scheduled to begin tomorrow, September 8, at Msalato, and run through Friday, September 11, 2026.
The Bootcamp will provide students with opportunities for practical learning, digital skills development and innovation, including developing and showcasing digital ideas and projects aimed at addressing real-life challenges in their communities.

In Dodoma, participating schools include Dodoma, Kisasa, Nara, Ihumwa, Makole, Mnadani, Hazina, Mtumba and Msalato, all secondary schools.
Through the ICT Clubs, students will receive practical training in computer programming (coding), computational thinking and problem-solving, digital creativity, visual and audio content production, and the safe and responsible use of technology.
The girls will also be connected with women ICT professionals through mentorship programmes, enabling them to learn from their experiences and gain a broader understanding of education, employment and career opportunities in the technology sector.
PMO-RALG STRESSES COLLABORATION
Speaking on behalf of the Prime minister Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), Mr. Francis Gervas, from the Education Management Department, thanked UNESCO for partnering with the Government in implementing the initiative.
He stressed the importance of continued collaboration among stakeholders to ensure that the programme achieves its intended objectives and that the results and lessons generated are sustained beyond the implementation period.
Mr. Gervas also called for the initiative to be expanded to other parts of the country so that more girls could benefit, while urging participants and stakeholders to remain committed to its effective implementation.
TEACHER CALLS FOR ATTITUDE CHANGE
Meanwhile, Mr Godfrey Robin Mseti, a teacher at Mtumba, commended the Government and UNESCO for introducing the initiative, saying opportunities and training related to technology had for a long time been perceived as being more accessible to boys and men.
He said society needed to change the perception that ICT-related learning was mainly for boys, stressing that girls also had the ability and should be given equal opportunities to learn, participate in and benefit from technology.
Under the programme, the ICT Clubs are intended to provide safe and inclusive learning environments where students can develop their skills through learning, innovation, leadership and collaboration.
Girls are expected to account for at least 50 per cent of participation in the clubs, with stakeholders encouraged to promote even greater representation.
Overall, the initiative is expected to strengthen ICT Clubs in 20 schools and enable 500 girls to improve their digital skills, confidence, participation and leadership abilities, while increasing their awareness of education and career opportunities in ICT.
The programme seeks to ensure that girls acquire not only the skills to use technology, but also the confidence to view technology as a tool for innovation, education and building their future careers.

Na; Mwandishi wetu-Tanga.
Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa la Kuendeleza Kilimo (IFAD) na wataalamu kutoka katika sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) wamekutana Mkoani Tanga Tarehe 7 Septemba 2026 kwa lengo la kufanya mapitio ya Utekelezaji wa Programu hiyo.
Sambamba na hilo timu hiyo itatembelea maeneo yanayotekeleza Programu kwa Mkoa wa Tanga, ambapo kwa upande wa sekta ya kilimo timu hiyo itatembelea kata ya Msomela iliyopo katika Halmashauri ya Handeni Vijijini ambako programu imehamasisha na kutoa elimu ya kilimo bora kwa jamii ya kimasai ambao kiasili ni wafugaji ambapo wameweza kujishughulisha na kilimo cha mahindi chenye tija.

Programu imewezesha kuwepo kwa eneo la mashamba darasa (FFS) kwa mazao ya Alizeti, Mahindi na Maharage, na shamba Darasa hilo limeonesha mafanikio kwa kiasi kikubwa, ambapo hekta moja inaweza kuzalisha takribani magunia 20 ya kilo mia moja kila moja, na jamii ya wafugaji sasa inajishulisha na shughuli za Kilimo na kunufaika na upatikanaji wa mazao yanayolimwa.

Kwa upande wa Sekta ya Uvuvi, Programu inaendelea na ujenzi wa soko la kimataifa la Samaki Kipumbwi lililloko katika halmashauri ya Pangani ambapo mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 68% na linategemewa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.
Aidha, programu pia inaendelea na ujenzi wa vichanja 40 vya kukaushia dagaa ambavyo vinaweza kukausha takribani tani tano kwa za dagaa kwa wakati mmoja.

Kwa upande mwingine pia Programu ya AFDP inaendelea na ujenzi wa Ghala la baridi na mtambo wa barafu katika soko hilo kwa ajili ya kuhifadhi na kusafirisha samaki.

Awali Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la kimataifa la maendeleo ya Kilimo nchini (IFAD) Bw. Seth Meng alikutana na Kaimu Katibu tawala wa Mkoa wa Tanga Bw.Emmanuel Kisongo na kufanya mazungumzo kuhusiana na utekelezaji wa Programu katika Mkoa sambamba na mafanikio tarajiwa kwa wanachi wa maeneo husika ambapo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa alieleza kuwa Programu hiyo ni muhimu sana katika kuhamasisha maendeleo ya kilimo na uvuvi katika mkoa huo.
hi Aliishukuru IFAD kwa kuweza kuwafikia wananchi wa mkoa huo na kuwataka ikiwezekana kuongeza uwekezaji mkoani hapo.Kwa zaidi ya miaka kumi, nilikuwa nikifanya kazi katika kampuni moja kubwa, nikijitoa kwa kila hali na kufanya kazi ngumu zaidi ya wengine. Hata hivyo, jina langu lilikuwa likirukwa kila mara fursa za kupanda cheo au kuongezewa mshahara zilipojitokeza.
Wafanyakazi wapya waliingia na kupandishwa vyeo juu yangu, huku mimi nikibaki kwenye nafasi ile ile ya chini yenye mshahara mdogo usiotosheleza hata mahitaji ya msingi ya familia yangu.
Nilibaki nikidharaulika, nikipoteza kujiamini, na kuhisi kama juhudi zangu zote zilikuwa hazionekani.
Nikiwa kwenye majuto makubwa na nikifikiria kuacha kazi kwa uchungu na aibu, mfanyakazi mwenzangu mstaafu aliyekuwa akitambua uwezo wangu alinifuata kwa siri na kunieleza ukweli.
Aliniambia kuwa mara nyingi matatizo ya kutosahauwa au kukataliwa kazini hutokana na nyota yako kufunikwa na giza au kuwekewa vifungo vya husuda na watu wasiopenda maendeleo yako. SOMA ZAIDI.
Kila mradi au jambo la maendeleo nililoweka nia kulifanya lilikwama ghafla dakika za mwisho. Nikiwekeza fedha kwenye biashara, ilifilisika ndani ya miezi michache; nikipata miadi ya kazi au fursa za kifedha, watu waligeuka ghafla na kunikataa bila sababu za msingi.
Hali hii ilinirudisha nyuma sana kimaisha na kunifanya nionekane kama mtu wa mikosi mbele ya ndugu na marafiki. Nikiwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo na nikipitia umaskini uliotishia kuniletea aibu uzeeni, ndugu yangu mmoja aliyekuwa akitambua mateso yangu alinifuata kwa siri.
Aliniambia kuwa mikosi ya kujirudia na kukataliwa kila mahali mara nyingi hutokana na vifungo vya kishirikina kutoka kwa watu wenye wivu walioweka ukungu wa giza kwenye nyota yako ili usifanikiwe.SOMA ZAIDI.
Kuanzisha biashara kwa mtaji wako wote na matumaini makubwa ya kujiendeleza kisha kushuhudia duka au mradi wako ukikosa wateja siku hadi siku ni jaribu zito linaloweza kumvunja mtu moyo na kumuingiza kwenye madeni makubwa.
Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia nyakati ngumu sana katika biashara yangu ya duka la nguo na vipodozi. Kila asubuhi nilifungua duka mapema na kupanga bidhaa vizuri, lakini siku nzima ilipita bila kupata hata mteja mmoja wa kununua kitu cha mia tano.
Cha kusikitisha zaidi, maduka ya majirani zangu yaliyokuwa yakiuza bidhaa zinazofanana na zangu yalikuwa yakifurika wateja muda wote.
Nilibaki nikikaa dukani peke yangu kwa huzuni na aibu, nikishindwa kulipa kodi ya pango, kulipia umeme, au hata kurudisha mikopo niliyochukua kuanzisha biashara hiyo.
Nikiwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo na nikikaribia kufunga duka hilo kwa kufilisika, mfanyabiashara mmoja wa zamani aliyekuwa rafiki yangu alinitembelea na kunieleza ukweli ambao wengi hawautambui.
Aliniambia kuwa biashara kutosimama au kukosa wateja ghafla huku za majirani zikistawi mara nyingi hutokana na chuki za kibiashara, ambapo maadui huweka ukungu au vifungo vya kishirikina ili wateja wasione biashara yako. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu.
Uzinduzi huo ni hatua muhimu katika ushirikiano wa muda mrefu kati ya Benki ya CRDB na TRA SACCOS, na unaashiria awamu mpya ya mageuzi ya kidijitali katika utoaji wa huduma za kifedha kwa wanachama wa SACCOS hiyo.
Kupitia TRA SACCOS PESACARD, wanachama wataunganishwa na mfumo mpana wa malipo wa Visa na hivyo kuwa na uwezo wa kutoa fedha kupitia ATM pamoja na kufanya malipo katika vituo vya POS vinavyokubali Visa ndani na nje ya Tanzania.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo aliipongeza TRA SACCOS kwa kufikisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake, huku akiipongeza Benki ya CRDB kwa kuendelea kutumia uwezo wake wa kiteknolojia na kifedha kusaidia taasisi mbalimbali kupanua huduma za kisasa za kifedha.
“Miaka 20 ni hatua kubwa inayodhihirisha uimara, uaminifu na mchango wa TRA SACCOS katika kuboresha ustawi wa kifedha wa wanachama wake. Nawapongeza viongozi na wanachama kwa kuendelea kubadilika kulingana na mahitaji ya wakati, na Benki ya CRDB kwa kutumia uwezo wake wa kifedha na kiteknolojia kujenga ushirikiano unaorahisisha upatikanaji wa huduma. Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD unaonesha mafanikio tunayoweza kuyapata pale taasisi za fedha na vyama vya ushirika vinapounganisha nguvu katika kukuza ubunifu na ujumuishi wa kifedha.”
Pamoja na uzinduzi wa kadi hiyo, ushirikiano huo umewezesha kuunganishwa moja kwa moja kwa mifumo ya TRA SACCOS na mifumo ya Benki ya CRDB. Maboresho hayo yanamaanisha kuwa mwanachama anaweza kutumia akaunti yake iliyopo ndani ya mfumo wa TRA SACCOS kupata huduma zinazohusiana na PESACARD bila kulazimika kuwa na akaunti katika benki nyingine ya biashara.
Muunganiko huo pia unatarajiwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa mikopo kwa wanachama. Fedha za mikopo zitaweza kutolewa moja kwa moja kupitia mfumo wa TRA SACCOS, hatua inayopunguza michakato ya kuhamisha fedha kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine na hivyo kupunguza muda wa mwanachama kusubiri fedha baada ya mkopo wake kuidhinishwa.
Katibu wa Benki ya CRDB, Pascal Mihayo, alisema hatua hiyo inaakisi dhamira ya Benki ya kutumia teknolojia na ushirikiano wa kimkakati kutengeneza suluhisho zinazojibu mahitaji halisi ya wateja.
“Kwetu Benki ya CRDB, huu ni zaidi ya uzinduzi wa kadi. Ni uthibitisho wa namna ushirikiano wa muda mrefu unavyoweza kukua na kuzaa suluhisho zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja. Kupitia TRA SACCOS PESACARD na muunganiko wa mifumo yetu, tunawapa wanachama uhuru zaidi wa kupata na kutumia fedha zao, huku tukiiwezesha TRA SACCOS kuongeza kasi na ufanisi wa utoaji wa huduma. Haya ndiyo mageuzi ya kidigitali tunayoyasimamia, teknolojia inayorahisisha huduma, inayozisogeza karibu na wananchi na inayoongeza thamani halisi kwa mtumiaji.”
Miongoni mwa maboresho mengine muhimu ni kuunganishwa kwa huduma za TRA SACCOS na mtandao wa Mawakala wa CRDB. Hatua hiyo itawawezesha wanachama kuweka na kutoa fedha kupitia zaidi ya Mawakala 40,000 wa CRDB waliopo maeneo mbalimbali nchini, hivyo kupanua kwa kiasi kikubwa maeneo ambayo mwanachama anaweza kupata huduma.
Maboresho hayo yana umuhimu mkubwa hususan kwa wanachama waliopo nje ya maeneo yenye matawi ya benki, kwa kuwa yanapunguza utegemezi wa maeneo ya kawaida ya huduma za kifedha na kutumia mtandao mpana wa Benki ya CRDB kupeleka huduma karibu zaidi na mwanachama.
Kwa upande wake, Kamishnawa TRA, Yusuph Mwenda aliishukuru Benki ya CRDB kwa ushirikiano wake, akieleza kuwa PESACARD na muunganiko wa mifumo ni sehemu muhimu ya safari ya TRA SACCOS ya kuboresha na kufanya huduma zake kuwa za kisasa zaidi.
“Tunapoadhimisha miaka 20 ya TRA SACCOS, hatuangalii tu tulikotoka na mafanikio tuliyoyapata; tunaangalia pia tunakotaka kwenda na aina ya taasisi tunayotaka kuijenga kwa ajili ya wanachama wetu. TRA SACCOS PESACARD ni sehemu ya safari hiyo ya baadaye. Inawapa wanachama wetu urahisi, wigo mpana zaidi wa huduma na uwezo mkubwa wa kusimamia miamala yao. Tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kuamini maono yetu na kushirikiana nasi kuleta teknolojia inayoongeza uwezo wetu wa kuwahudumia wanachama vizuri zaidi.”
Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD pia unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya benki za biashara na taasisi za kifedha zinazomilikiwa na wanachama katika kuongeza ujumuishi wa kifedha. Kwa kuunganisha ukaribu wa TRA SACCOS na wanachama wake pamoja na teknolojia, miundombinu na uwezo wa malipo wa Benki ya CRDB, ushirikiano huo unalenga kuunda mazingira rahisi zaidi ya kupata huduma za kisasa za kifedha.
Kwa Benki ya CRDB, hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika teknolojia na kubuni suluhisho zinazoboresha uzoefu wa wateja na kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha. Benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na TRA SACCOS pamoja na taasisi nyingine katika sekta binafsi na umma kuleta mageuzi ya kidigitali na katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshiriki katika zoezi la ukusanyaji wa maoni ya awali ya wadau kuhusu maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi (General Management Plan – GMP) wa Hifadhi Hai na Mwanadamu ya Rufiji–Mafia–Kibiti–Kilwa (RUMAKI), ikiwa ni hatua muhimu katika kuweka msingi wa usimamizi endelevu na shirikishi wa eneo hilo.
Zoezi hilo limejikita katika kupata maoni, uzoefu na mapendekezo ya wadau kuhusu namna bora ya kuimarisha uhifadhi wa mazingira na bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali za asili pamoja na maendeleo ya jamii zinazozunguka na kutegemea rasilimali za RUMAKI.
RUMAKI, inayojumuisha Rufiji, Mafia, Kibiti na Kilwa, ni miongoni mwa Hifadhi Hai zilizotambuliwa na UNESCO na kuingizwa katika Mtandao wa Dunia wa Hifadhi Hai (World Network of Biosphere Reserves – WNBR) mwaka 2023, chini ya Mpango wa UNESCO wa Mwanadamu na Hifadhi Hai (Man and the Biosphere Programme – MAB).
Hifadhi hiyo ina mifumo mbalimbali muhimu ya ikolojia ya pwani na bahari, ikiwemo misitu ya mikoko, miamba ya matumbawe na nyasi bahari. Mifumo hiyo ina mchango mkubwa katika kuhifadhi bioanuai, kulinda mazingira ya pwani, kusaidia shughuli za kiuchumi za jamii na kuongeza uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Maoni ya wadau yaweka msingi wa mpango
Ukusanyaji wa maoni ya awali ni sehemu muhimu ya mchakato wa kuandaa Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa RUMAKI. Kupitia mchakato huo, wadau wanapata nafasi ya kueleza hali halisi ya eneo, changamoto zinazokabili uhifadhi na matumizi ya rasilimali, pamoja na fursa zinazoweza kuendelezwa kwa manufaa ya jamii na mazingira.
Miongoni mwa wadau wanaohusishwa katika mchakato huo ni viongozi wa Serikali za Mitaa na vijiji, taasisi za Serikali, jamii zinazozunguka Hifadhi Hai, wavuvi, Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe (Beach Management Units – BMUs), taasisi za utafiti, wataalamu na wadau wengine wa maendeleo.
Ushirikishwaji wa wadau katika hatua hii unalenga kuhakikisha kuwa mpango utakaotengenezwa unazingatia mahitaji ya uhifadhi pamoja na hali halisi ya maisha ya jamii zinazotegemea rasilimali za eneo hilo.
Kuunganisha uhifadhi na maendeleo ya jamii
Dhana ya Hifadhi Hai na Mwanadamu inalenga kuweka uwiano kati ya uhifadhi wa bioanuai na maendeleo ya jamii. Kwa mtazamo huo, uhifadhi wa RUMAKI unahitaji kwenda sambamba na matumizi endelevu ya rasilimali zinazosaidia maisha ya wananchi, huku ukihakikisha kuwa rasilimali hizo zinalindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Katika maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi, suala la mgawanyo wa maeneo ya Hifadhi Hai linatarajiwa kuwa miongoni mwa maeneo muhimu ya kuzingatiwa. Hii inahusisha maeneo ya msingi ya uhifadhi (Core Areas), maeneo yanayozunguka maeneo hayo (Buffer Zones) na maeneo ya mpito (Transition Areas), kwa kuzingatia malengo ya uhifadhi na maendeleo endelevu.
Mpangilio huo unalenga kuweka uelekeo unaoeleweka kuhusu shughuli zinazoweza kufanyika katika maeneo mbalimbali, namna ya kulinda maeneo yenye umuhimu mkubwa wa kiikolojia na jinsi ya kuwezesha shughuli za maendeleo zinazozingatia mazingira.
Nafasi ya Tume ya Taifa ya UNESCO
Ushiriki wa Tume ya Taifa ya UNESCO katika zoezi hili unaendana na nafasi yake katika kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa programu na shughuli za UNESCO nchini Tanzania, kwa kushirikiana na taasisi za Serikali na wadau husika.
Kupitia Mpango wa UNESCO wa Mwanadamu na Hifadhi Hai (MAB), Hifadhi Hai hutumika kama maeneo ya kujifunza na kuonesha namna uhifadhi wa bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali, maendeleo ya jamii, utafiti, elimu na ufuatiliaji vinavyoweza kuunganishwa katika eneo moja.
Kwa upande wa Tanzania, utekelezaji wa dhana hiyo katika RUMAKI unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya taasisi za Serikali, mamlaka za Serikali za Mitaa, jamii, wataalamu, taasisi za utafiti na wadau wengine wanaohusika na uhifadhi na maendeleo.
Hatua kuelekea usimamizi endelevu wa RUMAKI
Maoni yatakayokusanywa katika hatua hii yatatoa msingi wa kuendelea na mchakato wa kuandaa Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa RUMAKI. Mpango huo unatarajiwa kusaidia kuweka mwelekeo wa pamoja katika uhifadhi wa bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali, maendeleo ya jamii, utafiti, elimu na ufuatiliaji wa mazingira.
Kwa kuwa RUMAKI inahusisha maeneo ya nchi kavu, pwani na bahari pamoja na jamii zinazotegemea rasilimali hizo, usimamizi wake unahitaji mtazamo unaounganisha mahitaji ya uhifadhi na maendeleo.
Ushiriki wa wadau katika hatua za awali, hivyo, ni muhimu katika kujenga uelewa wa pamoja na kuweka msingi wa mpango unaozingatia mazingira halisi ya RUMAKI.
Maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa Hifadhi Hai na Mwanadamu ya RUMAKI yanaashiria hatua muhimu katika kuimarisha utekelezaji wa dhana ya UNESCO ya Mwanadamu na Hifadhi Hai, kwa lengo la kuhakikisha kuwa uhifadhi wa mazingira na bioanuai unaenda sambamba na maendeleo endelevu na ustawi wa jamii.
Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema zaidi ya wadau wa sekta ya afya 3000 kutoka nchi mbalimbali Duniani watashiriki katika Mkutano wa pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi (IPHCC), jijini Arusha.
Prof. Shemdoe amesema hayo mapema leo Septemba 06, 2026 akiwa jijini Dodoma, kabla ya kuelekea Arusha na kuwakaribisha washiriki hao kwenye mkutano huo utakaofanyika kuanzia tarehe 9 hadi 11 Septemba, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).
Prof. Shemdoe amesema, yeye binafsi atashiriki katika mkutano huo wenye tija katika kuboresha utoaji wa huduma za afya msingi nchini na afrika kwa ujumla.
Prof. Shemdoe amesema mkutano huo umelenga kutoa uzoefu wa Tanzania katika uboreshaji wa huduma za afya ya msingi, ikiwamo afua zilizopelekea kupunguza vifo vya akina mama na watoto ambapo Tanzania kupitia jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ni kinara katika eneo hilo barani Afika.
Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, mkutano huo umelenga pia kubadilishana uzoefu wa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika katika huduma za afya ya msingi duniani pamoja na kuandaa mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za afya ya msingi ili kufikia malengo ya kitaifa na Kimataifa, ikiwamo upatikanaji wa Huduma za Afya kwa wote na malengo endelevu ya maendeleo.
Mkutano huo wa kihistoria utawakutanisha washiriki zaidi ya 3000 kutoka Tanzania na mataifa mengine duniani wakiwamo; wataalam wa afya wanaofanya kazi ya kutoa huduma za afya ya msingi, watunga sera, wadau wa maendeleo, watafiti, wahadhiri, wanafunzi, asasi za kiraia na sekta binafsi, ambapo washiriki hao wamejisajiri kupitia tovuti ya https://iphcconference.tamisemi.go.tz .
Na: OWM – TAMISEMI, Uyui
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Shilingi Bilioni 13 kutumika kujenga daraja la Loya linalounganisha kata za Loya na Miswaki wilayani Uyui pamoja na wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
Amesema ujenzi wa daraja hilo utasaidia kuimarisha usafiri na usafirishaji wa mazao ya kilimo kwenda masokoni, kuongeza fursa za biashara kwa wananchi na muhimu zaidi, kuondoa changamoto ya wananchi kupoteza maisha na mali zao wanapovuka Mto Loya, hususan wakati wa mvua.
Prof. Shemdoe ameyasema hayo Septemba 5, 2026, alipotembelea eneo la Mto Mhwala, unaofahamika pia kama Mto Loya, ambako daraja hilo linatarajiwa kujengwa katika eneo lenye jiografia ya ardhi oevu.
Amesema ujenzi wa daraja hilo utakuwa suluhisho la muda mrefu kwa wananchi wa vijiji vya Loya, Miswaki, Isuli, Lutona, Mabeshi na Simbo-Igunga, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kukatika kwa mawasiliano ya barabara, hali inayowaathiri katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii.
Prof. Shemdoe amesema kati ya Shilingi Bilioni 13 zilizoidhinishwa, kiasi cha fedha zitatumika kumlipa Mhandisi Mshauri anayesimamia maandalizi ya michoro na kusimamia ujenzi kwa niaba ya Serikali, huku Shilingi Bilioni 10.4 zikitumika moja kwa moja katika ujenzi wa daraja hilo.
“Tumshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha na kuleta kiasi hicho cha Shilingi Bilioni 13 za ujenzi wa daraja la Loya, ambalo litaboresha biashara na usafirishaji wa mazao ya kilimo katika Kata za Loya na Miswaki wilayani Uyui pamoja na wilaya ya Igunga,” amesema Prof. Shemdoe.
Aidha, Prof. Shemdoe amesema ujenzi wa daraja hilo unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja baada ya kuanza kwa ujenzi, hatua ambayo itawaondolea wananchi gharama ya Shilingi 1,000 wanazolipa kwa kutumia kivuko kilichotengenezwa kwa juhudi za mwananchi aliyejitolea kujenga daraja la miti.
Akizungumzia hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya ujenzi huo, Prof. Shemdoe amesema Mhandisi Mshauri anatarajiwa kukamilisha kazi ya usanifu mwezi Septemba 2026, na kwamba mwezi Oktoba Serikali itatangaza zabuni ya kumpata mkandarasi atakayetekeleza mradi huo.
Amesema ujenzi rasmi unatarajiwa kuanza mwezi Desemba 2026 baada ya kusainiwa kwa mkataba, na utakamilika ndani ya mwaka mmoja, ifikapo Novemba 2027.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Igalula, Mhe. Juma Kawamba, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumtuma Prof. Shemdoe, ambaye amemtaja kuwa ni mchapakazi, kufikisha kwa wananchi habari njema ya ujenzi wa daraja la Loya.
Mhe. Kawamba amesema wananchi wa eneo hilo wamepoteza ndugu zao wengi kutokana na changamoto ya kuvuka eneo hilo, hivyo ujenzi wa daraja hilo utakuwa faraja kubwa na hatua muhimu ya kulinda maisha na mali zao.
Ametoa wito kwa wananchi kuwapokea na kushirikiana vizuri na wakandarasi watakaotekeleza mradi huo, pamoja na kulinda vitendea kazi na miundombinu itakayojengwa ili iweze kudumu na kunufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Loya ni wa kimkakati kwa kuwa, ukikamilika, utarahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao ya kilimo, kufungua fursa za biashara, kupunguza gharama za usafiri na kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kijamii kati ya wananchi wa Loya, Miswaki wilayani Uyui na maeneo ya wilaya ya Igunga, mkoani Tabora, sambamba na kulinda maisha na mali za wananchi.
Serikali imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kujipanga kikamilifu katika maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, hususan katika kuhakikisha wageni watakaofika nchini wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo.
Agizo hilo limetolewa l na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Florence Samizi (Mb.) ambaye amesema NHIF ina jukumu muhimu la kuratibu suala la bima ya afya wakati wa mashindano hayo ili kuhakikisha wageni wanapata huduma za matibabu kwa urahisi pindi wanapohitaji huduma hizo.
“Tuwape uhakika wa huduma bora ili waone fahari kuwapo hapa nchini katika kipindi chote cha mashindano hayo,” amesema Dkt. Samizi.
Amesema maandalizi ya huduma za matibabu yanapaswa kuzingatia pia huduma za dharura pamoja na huduma maalum, ikiwemo za moyo na mifupa, ili kukidhi mahitaji mbalimbali ya afya yatakayoweza kujitokeza wakati wa mashindano.
Aidha alidokeza kuwa tayari Wataalamu kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wamekagua Vituo vya kutolea huduma kwa alengo la kujiridhisha na wamefurahishwa na utayari unaoonyeshwa katika maandalizi ya huduma za matibabu jambo linaloonesha kuwa Tanzania inajiandaa kuhakikisha AFCON 2027 inafanyika katika mazingira salama na yenye huduma bora.
Ameitaka NHIF kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya, vituo vya kutolea huduma na wadau wengine kuhakikisha mfumo wa huduma za matibabu wakati wa mashindano hayo unakuwa imara, unaopatikana kwa wakati na unaokidhi viwango vinavyohitajika.
Akizungumzia hilo Mkurugenzi Mkuu waa NHIF, Dkt. Irene Isaka alisema kuwa tayari Mfuko umeshajipanga na umeandaa kifurushi maalumu kwa ajili ya wageni wote watakaokuja nchini kwa ajili ya mashindano hayo.
“Tayari tumejipanga na tuna kifurushi ambacho tutakileta Wizarani ili tupate baraka ya Wizara hivyo tunashukuru sana kwa maelekezo haya ambayo yanaboresha na kuhakikisha tunajipanga vyema,” alisema Dkt. Isaka.

NAIBU Waziri wa Afya, Mhe Dkt. Florence George Samizi (Mb), amelipongeza Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuwa moja ya mabaraza bora nchini. Amelitaka baraza kuhakikisha ajenda ya Bima ya Afya kwa wote inawafikia wananchi wengi zaidi.
Nimefurahi kusikia kwamba katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 Mfuko umeweza kufikia 10.7% ya Wananchi toka 8% ya wananchi iliyodumu kwa takriban miaka 10. Pamoja na pongezi hizo Mh. NAIBU WAZIRI ameutaka Mfuko kutumia TEHAMA na kusajili wanachama wengi zaidi ili kutimiza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wote huduma za bima ya afya. Hii itasaidia wananchi kuondokana na umaskini pale wanapopata maradhi. Dkt. Samizi ametoa maelekezo Hayo wakati wa mkutano wa nne wa wa Baraza la 4 wafanyakazi NHIF, Jijini Arusha, na kusisistiza menejimenti ya wafanyakazi wa NHIF kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu, weledi na uwajibikaji, huku wakisikiliza na kutatua kwa wakati kero za wananchi. Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya. Kutoa huduma bora na kuwa na mfumo wa kupokea mrejesho toka kwa wananchi. Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa NHIF, Dkt. Samizi amesema ni muhimu mfuko huo kuonesha mafanikio yaliyopatikana. Kuwepo kwa NHIF kumesaidia kuboresha huduma za Afya kwa kulipa madai na kutoa mikopo kwa vituo vya afya. Ni vema wanachi wakajulishwa hatua kubwa iliyofikiwa katika huduma za Afya na mchango wa NHIFkatika Sekta hii muhimu. Mlianza na vituo vichache sana mwaka 2001 hivi sasa yaani mwaka wa Fedha 2025/26 mmesajili zaidi ya vituo 10,600 nchi nzima. Ni vema kuonesha namna mlivyokabiliana na changamoto za wakati ule na namna zilivyowasaidia kuboresha Mfuko katika utoaji wa huduma. Amesema mafanikio hayo yanadhihirishwa na kujituma, ushirikiano, umoja na mshikamano miongoni mwa watumishi wa NHIF ili kufikia malengo ya mfuko kwa lengo la kutekeleza jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata bima ya Afya. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, ameeleza mafanikio yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa kilipa madai toka zaidi ya siku 90 hadi wastan wa siku 50 kwa mwaka wa Fedha 2025/2026. Vile vile alieleza kwamba Mfuko umeendelea kuimarika ambapo ziada imeongezeka kwa 57% Mfuko umepunguza matumizi kwa asilimia13% na uwekezaji umeongezeka kwa 106%.
Hii imewezesha Mfuko kuendeleza kifurushi cha wanafunzi, Toto Afya. Mfuko kusajili kifurushi cha tarangire, Mikumi, Ngorongoro, Serengeti Tanzanite na kifurushi cha vikundi yaani Umoja Afya ambacho ni sh. 60, 000 kwa matibabu ya mwaka mzima.
Vile vile alielezea mikakati inayotekelezwa na mfuko huo katika kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na matumizi ya TEHAMA kwenye usajili, uchakataji madai na kupambana na udanganyifu. Mfuko pia unashirikisha Sekta Binafsi katika usajili wa wanachama na katika huduma za matibabu. Mwakilishi wa chama Cha wafanyakazi TUGHE, Bw.Paul wamepongeza baraza Hilo kuzingati misingi ya Kazi stahiki za wafanyakazi kwenye taasisi hiyo. Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki semina elekezi ya siku mbili wamesema wamepata maarifa na mwelekeo mpya ambao utawasaidia kuboresha utendaji wao wa kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Bima ya Afya kwa wote! Jiunge sasa!


















