Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, akiongoza Kikao cha Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, wakati wa kuwapokea na kuwatambulisha wajumbe walioteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), hivi karibuni. Katika kikao hicho kilichofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, leo Jumamosi, tarehe 1 Agosti 2026, pia Balozi Dkt. Migiro alishuhudia makabidhiano ya ofisi na majukumu kati ya viongozi wapya na wanaoondoka 

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Aggrey Mwanri akipokewa na kusalimiana kwa tabasamu na bashasha na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Ndugu John Mongella, leo Jumamosi, tarehe 1 Agosti 2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, wakati wa mapokezi ya Wajumbe wa Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, walioteuliwa hivi karibuni.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati) akishuhudia makabidhiano ya ofisi na majukumu, kati ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Komredi Aggrey Mwanri (kushoto pichani) na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Komredi John Mongella (kulia pichani), yaliyofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, leo Jumamosi, tarehe 1 Agosti 2026.





Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa HIfadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) jijini Dar es Salaam, Agosti 1, 2026.


Ataka Uwekezaji wenye Tija

Na: Mwandishi Wetu - Dar eś Salaam 

Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imeelekezwa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali ili kuhakikisha mfuko unaendelea kuwa imara, endelevu na wenye uwezo wa kutoa huduma bora kwa wanachama.

Amesema hayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Mfuko huo wa PSSSF iliyofanyika leo Agosti 1, 2026, PSSSF Commercial Complex, Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Mhe. Sangu amesema jukumu kuu la bodi ni kusimamia shughuli za mfuko kama ilivyoainishwa katika Sheria ya PSSSF, kifungu cha 11 hususan katika maeneo makuu ya usimamizi ikiwemo huduma kwa wanachama, ukusanyaji wa michango, uwekezaji wa rasilimali za mfuko na ulipaji wa mafao.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (Katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa PSSSF jijini Dar es Salaam Agosti 1, 2026

Vile vile, amesisitiza kuwa katika kutekeleza majukumu hayo, bodi inapaswa kuzingatia kikamilifu sheria, kanuni na miongozo ya Serikali pamoja na Mpango Mkakati wa PSSSF, ambao umeanza kutekelezwa pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Wajumbe mmeingia katika kipindi muhimu ambapo mfuko umeanza kutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano. Huu ndio utakaokuwa mwongozo wa utekelezaji wa majukumu na kufanikisha malengo ya mfuko,” amesema.



Kadhalika, amewataka wajumbe kuzingatia misingi ya uadilifu, uwajibikaji, uwazi na ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao, akibainisha kuwa Serikali ina matarajio makubwa kwa PSSSF katika kuhakikisha mfuko huo unakuwa imara.

Kuhusu uwekezaji, Waziri alisema fedha za wanachama zinapaswa kuwekezwa kwa umakini na weledi ili kulinda thamani yake na kuhakikisha zinazalisha faida itakayowezesha mfuko kutimiza wajibu wa kulipa mafao kwa wakati, hata baada ya miongo kadhaa.

Viongozi waliohudhuria hafla hiyo


“Fedha za wanachama zinawekwa leo kwa matarajio ya kulipa mafao miaka ijayo. Hivyo, ni muhimu ziwekezwe katika miradi yenye tija, salama na inayozingatia miongozo ya uwekezaji iliyowekwa na Serikali,” alisisitiza.

Viongozi waliohudhuria hafla hiyo

Dar es Salaam | 31 Julai 2026

Kwa wiki kadhaa, swali moja limekuwa likiulizwa kila sehemu—mitandaoni, kwenye WhatsApp, hata pale unapokutana na marafiki kwenye baa.

Watu wamekuwa wakiuliza: "Kwa nini mitishamba inazungumzwa sana hivi karibuni?"

 


Wakala wa Vipimo (WMA) umeanza kutoa elimu ya vipimo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi katika siku ya kwanza, (Agosti 1, 2026) ya Maonesho ya Wakulima Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya John Malecela, eneo la Nzuguni jijini Dodoma.

Kwenye banda lake lenye kaulimbiu 

"Usahihi wa Vipimo vya Mbegu, Pembejeo, Mazao  na Bidhaa Sokoni ni Msingi wa Tija na Utekelezaji wa Dira 2050," Maafisa Vipimo wa WMA wanatoa elimu ya vipimo na majukumu ya Wakala kwa ujumla katika kulinda haki za wakulima, wafugaji, wavuvi na wanunuzi.  

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa WMA Bi. Veronica Simba alisema lengo ni kuhakikisha kila mkulima, mfugaji na mvuvi anaelewa umuhimu wa kutumia mizani na vipimo vingine vilivyohakikiwa na WMA. 

“Kama unauza mahindi, mbolea au maziwa, na kama unanunua pembejeo za mifugo au samaki, kipimo sahihi ndiyo msingi wa faida. Tunataka kila mtu atoke hapa Nane Nane akiwa na uelewa wa kutambua na kudai kipimo sahihi,” alisisitiza Bi. Veronica.

Bi. Veronica aliwataka wakulima, wafugaji, wavuvi na wananchi kwa ujumla kutembelea banda la WMA katika kipindi chote cha maonesho hayo. “Wataalamu wetu wapo hapa kutoa elimu bure. Njoo ujifunze, uulize maswali na hata kutoa maoni yako,” aliongeza.

WMA imesema itatumia kipindi chote cha maonesho hayo kuhamasisha matumizi ya vipimo sahihi kama njia moja ya kutekeleza Kauli Mbiu ya Taifa ya  NaneNane 2026 "Tambua Soko, Ongeza Tija, Kutekeleza Dira 2050" na kuhakikisha sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi inakuwa na ushindani na uhakika wa soko.







Mkurugenzi wa Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mbolea Tanzania, Lameck Borega,akizungumza na waandishi wa habari kwenye Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt.John Samuel Malecela jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imewahimiza wakulima nchini kuachana na dhana potofu kuhusu matumizi ya mbolea, ikisisitiza kuwa kilimo cha kisasa kinahitaji matumizi sahihi ya mbolea ili kuongeza uzalishaji na tija mashambani.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mbolea Tanzania, Lameck Borega, wakati wa Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt.John Samuel Malecela jijini Dodoma.

Bw.Borega amesema TFC, ambayo inamilikiwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imefika katika maonesho hayo ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa wakulima kuhusu umuhimu wa kutumia mbolea bora na zinazokidhi mahitaji ya mazao pamoja na aina mbalimbali za udongo.

Amesema kampuni hiyo inasambaza mbolea za aina mbalimbali ikiwemo DAP kwa ajili ya kupandia, Urea na CAN kwa ukuaji wa mazao, pamoja na NPK na SA zinazosaidia kukomaza mazao, huku akisisitiza kuwa uchaguzi wa mbolea unapaswa kuzingatia mahitaji halisi ya udongo na zao husika.

"Kilimo bila mbolea ni kilimo kisicho na tija. Ili mkulima apate mavuno mengi na yenye ubora ni lazima atumie mbolea sahihi," amesema Borega.

Amefafanua kuwa maafisa wa TFC wanaendelea kuwafikia wakulima katika mikoa yote nchini kwa kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, sambamba na kuwasaidia kuelewa aina za mbolea zinazofaa kwa maeneo yao.

Aidha, amesema maonesho ya Nane Nane yamekuwa jukwaa muhimu la kuonesha tofauti ya uzalishaji kati ya mashamba yanayotumia mbolea na yale yasiyotumia kupitia mashamba darasa (demo plots) yaliyoandaliwa na kampuni hiyo.

"Anayetembelea banda letu anaweza kujionea mwenyewe tofauti ya ukuaji wa mazao yaliyotumia mbolea na yale ambayo hayajatumia. Huo ni ushahidi wa moja kwa moja wa faida za matumizi ya mbolea," amesema

Borega pia amewataka wakulima kupuuza imani kwamba mbolea huharibu udongo, akieleza kuwa udongo hutofautiana kwa kiwango cha virutubisho na kwamba mbolea huongeza virutubisho vinavyokuwa vimepungua kutokana na matumizi ya muda mrefu na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Amekumbusha kuwa Kampuni ya Mbolea Tanzania ilianzishwa mwaka 1968, miaka minane baada ya Uhuru, ikiwa na dhamira ya kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

"Tunawaalika wakulima wote kutembelea banda letu katika maonesho ya Nane Nane na kufika katika vituo vyetu vilivyopo nchini kote ili kupata mbolea bora zilizothibitishwa na mamlaka husika kwa ajili ya kilimo chenye tija," amesema  Borega.

Na Alex Sonna– Dodoma

Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imeanza utekelezaji wa mpango mkubwa wa kuongeza upatikanaji wa mbolea nchini kwa kuagiza tani 200,000 za mbolea kwa msimu wa kilimo wa mwaka huu, sambamba na uwekezaji katika viwanda vya kuchanganya mbolea na uchakataji wa chokaa ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao.

Mkurugenzi Mkuu wa TFC, Samuel Ahadi Mshote, amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora kwa wakati, kuongeza matumizi ya pembejeo na kuimarisha usalama wa chakula pamoja na uchumi wa kilimo nchini.

Akizungumza leo Agosti 1,2026 kwenye Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt.John Samuel Malecela jijini Dodoma, Mshote amesema TFC ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa mbolea zenye ubora unaokidhi mahitaji ya wakulima, huku ikijiandaa kuanza uzalishaji wa mbolea zinazochanganywa kulingana na afya ya udongo na mahitaji ya mazao mbalimbali.

Amesema katika awamu ya kwanza kampuni imeagiza tani 70,000 za mbolea, ambapo tani 35,000 za mbolea aina ya DAP tayari zimewasili nchini na zinafungashwa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kusambazwa kwa wakulima kupitia utaratibu wa pembejeo zenye ruzuku ya Serikali.

Aidha, amesema tani nyingine 40,000 za mbolea aina ya Urea zinatarajiwa kuwasili ndani ya muda mfupi ili kuendelea kukidhi mahitaji ya msimu wa kilimo unaoanza.

"Tunataka kuhakikisha hakuna mkulima anayekosa mbolea kwa sababu ya upungufu wa usambazaji. Ndiyo maana tumejipanga kuongeza uagizaji na kuimarisha mtandao wa usambazaji nchini kote," amesema  Mshote.

Amesema TFC imepanua mtandao wake wa huduma kwa kuongeza vituo vya mauzo kutoka nane hadi 26 vilivyopo katika mikoa 22 ya Tanzania Bara, hatua iliyorahisisha wakulima kupata mbolea karibu na maeneo yao.

Mbali na vituo hivyo, kampuni hiyo inashirikiana na zaidi ya mawakala 600 wa pembejeo za kilimo, vyama vya ushirika 29 (AMCOS) pamoja na halmashauri mbalimbali ili kuhakikisha mbolea zinawafikia wakulima hadi ngazi ya vijiji.

Kwa mujibu wa Mshote, tangu TFC ilipoanza kusambaza mbolea mwaka 2022, tayari zaidi ya tani 350,000 za mbolea za ruzuku zimesambazwa kwa wakulima wanaojihusisha na uzalishaji wa mpunga, mahindi, mboga mboga, vitunguu na mazao mengine ya biashara.

Katika hatua nyingine, amesema kampuni hiyo inakamilisha ufungaji wa mtambo wa kisasa wa kuchanganya mbolea katika jiji la Dar es Salaam, ambao utakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 300,000 za mbolea kwa mwaka kulingana na mahitaji ya udongo na mazao husika.

Amesema uwekezaji huo utapunguza utegemezi wa uagizaji wa mbolea kutoka nje ya nchi na kuongeza upatikanaji wa mbolea maalumu kwa mazao ya kimkakati kama vitunguu, ufuta, parachichi na mazao mengine yenye thamani kubwa kiuchumi.

Sambamba na hilo,amesema  TFC imeanza kutekeleza mradi wa uchimbaji na uchakataji wa chokaa mkoani Tanga baada ya kupatiwa eneo na Halmashauri ya Jiji la Tanga. Chokaa hicho kitatumika kurekebisha tindikali kwenye udongo pamoja na kuwa malighafi muhimu katika uzalishaji wa mbolea.

Mshote amesema mafanikio ya utekelezaji wa mpango wa ruzuku ya mbolea yameongeza matumizi ya pembejeo nchini kutoka tani 300,000 hadi zaidi ya tani milioni 1.2 kwa mwaka, huku takribani asilimia 80 ya wanufaika wakiwa ni wakulima wadogo.

Amesema ongezeko hilo limechangia kuimarika kwa uzalishaji wa mazao na kuiwezesha Tanzania kufikia kiwango cha zaidi ya asilimia 130 cha kujitosheleza kwa chakula.

Aidha, matumizi ya mbolea kwa hekta yameongezeka kutoka kilo 16 hadi kilo 24, huku Serikali na wadau wa sekta hiyo wakilenga kufikia kiwango cha kilo 30 kwa hekta kama kinavyoelekezwa na Azimio la Abuja kuhusu matumizi ya mbolea barani Afrika.

Amesema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, sekta binafsi, taasisi za umma na wananchi ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati na kwa ufanisi.

Ameeleza kuwa dhamira ya Serikali ni kuona Tanzania inafikia uchumi shindani, wenye tija na jumuishi ifikapo mwaka 2050, huku akiahidi kuwa wataendelea kusimamia kwa dhati utekelezaji wa mipango na vipaumbele vilivyowekwa ili kuhakikisha maono hayo yanageuka kuwa matokeo yanayoonekana kwa manufaa ya Watanzania wote.

Mshote amewataka wakulima kutembelea banda la TFC katika Maonesho ya Nane Nane ili kupata elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea na kufahamu aina zinazofaa kwa mazao na mazingira yao, akisisitiza kuwa matumizi ya pembejeo bora ndiyo msingi wa kuongeza tija, kipato cha mkulima na ukuaji wa sekta ya kilimo nchini.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Bi. Khadija Ngasongwa,akizungumza na wadau wakati wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.

DURBAN - AFRIKA KUSINI

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amezishauri nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuwekeza zaidi katika maendeleo ya viwanda na miundombinu ili kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji.

Bi. Ngasongwa ametoa wito huo jijini Durban, Afrika Kusini, wakati akishiriki Mkutano wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC unaoendelea nchini humo.

"Ushiriki wa FCC katika wiki hii unalenga kuhakikisha sera na miongozo ya ushindani wa haki inazingatiwa katika maendeleo ya viwanda. Tunataka kuona viwanda vya ukanda wetu vinakuwa na ushindani, vinatoa fursa kwa wanawake na vijana, na vinatoa bidhaa zenye ubora kwa walaji," alisema Bi. Ngasongwa.

Ameongeza kuwa uwekezaji katika viwanda vya kuongeza thamani ya malighafi utasaidia kuwainua kiuchumi wanawake na vijana, kupanua masoko ya bidhaa za nchi za SADC na kuongeza mapato ya fedha za kigeni.

Akizungumzia ushiriki wa Tanzania, Bi. Ngasongwa amesema mkutano huo unaendana na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania hususan katika sekta za madini, kilimo, bidhaa za afya, miundombinu na ubunifu.

"Ushiriki wa Tanzania una umuhimu mkubwa kwa sababu unajikita katika kuimarisha mnyororo wa thamani. Ni maeneo muhimu katika safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa viwanda na kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," alisema.

Bi. Ngasongwa pia amewataka wadau wa fedha waliopo katika mkutano huo ikiwemo TIB, Exim Bank, BADEA na Nedbank kushirikiana katika kuhamasisha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya miradi ya maendeleo na uwekezaji nchini.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa na madini ya kimkakati na rasilimali nyingine. Hivyo ni muhimu kuyachakata ndani ya nchi badala ya kuuza malighafi ili kuongeza thamani, kuzalisha ajira na kuchochea ukuaji wa viwanda.

Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC ulifunguliwa rasmi Julai 27, 2026 na ulihitimishwa Julai 31, 2026 na umetoka na maazimio ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika biashara, uwekezaji na maendeleo ya viwanda kama sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa 46 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2026 Jijini Durban, Afrika Kusini.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Bi. Khadija Ngasongwa, akizungumza na wadau wakati wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki kutoka Tanzania wakati wa Mkutano wa 9 wa Wiki ya Viwanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Industrialisation Week), unaofanyika jijini Durban, Afrika Kusini.

 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma, Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na FCC kwa baadhi ya wadau waliotembelea Banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.

 

Kushuhudia mtoto wako wa pekee akiteseka bila kupata msaada ni jambo linaloweza kumvunja moyo mzazi yeyote. Kwa zaidi ya miaka miwili, binti yetu mwenye umri wa miaka kumi na mbili alipatwa na hali ya kutatanisha sana.

Alianza kulalamika maumivu makali ya kichwa na tumbo kila ilipofika jioni, na mwili wake ulipoteza nguvu kabisa hadi kushindwa kutembea au kwenda shuleni. Usiku uliingia akiwa anapiga makelele ya kutisha, akidai kuona watu waliovaa nguo nyeusi wakimnyonya damu na kumtishia maisha.

​Nilimtembeza kwenye hospitali kubwa na za kifahari nchini. Madaktari walifanya vipimo vya kila aina kuanzia vipimo vya damu, MRI, hadi Scan za kichwa lakini majibu yote yalikuja kuwa yuko salama na hana ugonjwa wowote wa kibinadamu!

Pamoja na majibu hayo, mtoto alizidi kukonda na kudhoofika siku hadi siku. Tilitumia akiba yetu yote kununua dawa za kutuliza maumivu ambazo hazikusaidia kitu.

Nilibaki nikilia usiku na mchana, nikitazama binti yangu akipotea mikononi mwangu huku tukiamini alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa nadra usio na tiba. SOMA ZAIDI.

 

Nyumba yenye furaha na amani inaweza kubadilika ghafla na kuwa uwanja wa dhiki na mateso pindi janga la uraibu linapoingia. Kwa zaidi ya miaka mitatu, mume wangu alitumbukia kabisa kwenye mtego wa michezo ya bahati nasibu (gambling).

Kila mwezi alipopokea mshahara wake, badala ya kuleta nyumbani kwa ajili ya chakula, kodi ya nyumba, na ada za watoto, alielekeza pesa zote kwenye kubashiri matokeo ya mpira na kucheza michezo ya mtandaoni kwa matumaini ya kupata faida ya haraka.

​Matokeo yake yalikuwa ni maafa makubwa kwa familia yetu. Aliuza vifaa vya nyumbani kimyakimya, alikopa fedha kwa majirani na taasisi za mikopo, na kila mara alirudi nyumbani akiwa na hasira, dharau, na migogoro mikubwa baada ya kupoteza kila senti.

Watoto wetu walifukuzwa shule mara kwa mara kwa kukosa ada, na madeni yalitukabili kila kona. Nilibaki nikilia usiku kucha nikiwa na hofu kwamba tungeshia mtaani bila makazi wala chakula, huku mume wangu akionekana kupoteza kabisa akili ya uongozi wa familia. SOMA ZAIDI.

 

Kusafiri kwenda nje ya nchi kwa ajili ya masomo au kazi ndoto ambayo kila kijana anayepambana anatamani kuitimiza. 

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikuwa nikihangaika usiku na mchana kupata fursa ya kwenda kufanya kazi Ulaya baada ya kupata mwaliko rasmi kutoka kwa kampuni moja kubwa.

Kila kitu kilikuwa kikienda vizuri upande wa waajiri wangu, lakini ajabu ni kwamba kila nilipofika kwenye hatua za mwisho za kukamilisha pasipoti na mchakato wa Visa, vikwazo visivyoeleweka vilianza kujitokeza.

​Nyaraka zangu zilikuwa zikipotea kimyakimya maofisini, majina yangu yalikosewa mara kwa mara kwenye mifumo, au maombi yangu yalikataliwa bila sababu za msingi. Nilibaki nikishangaa na kuumia moyoni huku nikishuhudia fursa zangu za dhahabu zikiyeyuka.

Kumbe bila mimi kujua, baadhi ya ndugu zangu wa karibu waliokuwa wakionyesha kunifurahia kwa nje, ndio waliokuwa mstari wa mbele kufanya fitina chini kwa chini ili nisifanikiwe kutoka kimaisha! SOMA ZAIDI.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Mark Kihulla amewatembelea na kuzungumza na watumishi wa Wakala huo Mkoa wa Arusha tarehe 31 Julai 2026.

Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa kusikiliza changamoto za watumishi, kuwapongeza kwa utendaji wao, na kuwapa mwelekeo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wakala.

Akizungumza na watumishi hao, Afisa Mtendaji Mkuu aliipongeza Ofisi ya Mkoa kwa kazi nzuri ya uhakiki wa vipimo wanayoendelea kufanya.

Alisema mafanikio ya WMA yanategemea uadilifu, umahiri na nidhamu ya kila mtumishi.

Aidha, aliwataka watumishi kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi na kuzingatia maadili ya kazi. “Tuwe mabalozi wazuri wa WMA. Kila mteja tunayemhudumia ni fursa ya kujenga taswira nzuri ya Wakala,” alisisitiza.

Kwa upande wao, watumishi wa Mkoa wa Arusha walimshukuru Mtendaji Mkuu kwa uongozi wake wenye 'kuonesha njia' na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Katika ziara hiyo ya Afisa Mtendaji Mkuu, watumishi walipata nafasi ya kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali ya kuboresha utoaji huduma ya vipimo katika Mkoa huo.


 

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi, akizungumza wakati wa semina maalum ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.


*Mmoja atoa ushuhuda wa ‘Tunalipa Jana’


*Bunge: tunawashukuru PSSSF kwa elimu


Morogoro, Julai 31, 2026


Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.

Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.

“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Bi. Angelina Sanga.

Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.

Katika semina hiyo Mtumishi Mstaafu wa Bunge Bw. Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.


Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Bw. Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine

“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Bw. Hajji Moshi.

Kwa upande wake, Bw. Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.

Mtumishi kutoka Ofisi ya Bunge, Bi. Angelina Sanga (kushoto), akiwa na Afisa Matekelezo kutoka PSSSF, Bi. Upendo Chilewa, wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bi. Sanga alipokuwa akijisajili kaaika huduma ya mifumo ya kidijitali.

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi (kushoto), akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto (kulia), mara baada ya kuhitimishwa kwa semina ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto, akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa ajili ya Makatibu wa Kamati za Bunge mjini Morogoro.

Mtumishi Mstaafu wa Bunge, Bw. Gerald Magili, akitoa ushuhuda wake wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bw. Magili aliipongeza PSSSF kwa kulipa mafao yake kwa wakati
Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kwa umakini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajj Moshi (kulia), wakati wa semina ya kujenga uelewa wa Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Denis Londo, amesema ubora wa bidhaa ni nguzo muhimu katika kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kwenye soko la kimataifa na kufanikisha azma ya nchi ya kujenga uchumi wenye thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050.
Kariakoo, 31 Julai, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeendelea kuimarisha ushirikiano na walipakodi kupitia mikutano ya ana kwa ana (Outreach) inayolenga kusikiliza, kutatua changamoto na kutoa elimu ya kodi ili kuwawezesha walipakodi kutekeleza wajibu wao kwa hiari.
Kuingia kwenye ndoa ni matumaini ya kila mwanamke kwamba atapata mume atakayempenda, kumheshimu, na kuilinda familia yao. Hata hivyo, mara tu baada ya harusi yetu, ndoa yangu iligeuka kuwa uwanja wa maumivu na dharau kubwa.

Mume wangu alibadilika ghafla na kuanza kuendesha nyumba yetu kwa maelekezo ya mama yake mzazi pekee. Kila uamuzi uliotakiwa kufanywa kuanzia matumizi ya fedha, chakula kinachopikwa, hadi malezi ya watoto ulipaswa kupitishwa na mama mkwe wangu kwanza.

​Kila nilipojaribu kutoa maoni yangu au kushauri kama mke wa ndani, mume wangu alinisukuma pembeni, kunitusi, na kuniambia kuwa mimi ni mgeni tu aliyetoka mbali ambaye sina haki ya kupinga kauli ya mama yake.

Mama mkwe alitumia fursa hiyo kunidharau waziwazi na kunifanyia vitimbi vya kila aina ili nionekane sifai. Nilibaki nikiwa sina sauti wala thamani kwenye nyumba yangu mwenyewe, nikilia usiku kucha kwa uchungu wa kuonekana kama mjakazi na sio mke halali.SOMA ZAIDI.

 

Kwa zaidi ya miaka minne, nilikuwa nikimiliki duka kubwa la vifaa vya ujenzi na bidhaa za nyumbani katika mji wetu. Biashara hii ilikuwa ndiyo tegemeo langu kuu na chanzo cha rizki kwa familia na wafanyikazi wangu sita.

Niliwekeza mamilioni ya fedha na mtaji wangu wote ili kuhakikisha duka langu linakuwa na kila aina ya bidhaa zenye ubora wa hali ya juu. Hata hivyo, kuanzia katikati ya mwaka jana, mambo yalianza kubadilika ghafla kwa njia ya kutatanisha sana.

​Duka langu lilikuwa katikati ya mji ambapo watu wengi wanapita, lakini ajabu ni kwamba wateja walikuwa wakipita mlangoni na kuingia kwenye maduka ya jirani yaliyokuwa na bidhaa chache kuliko zangu.

Siku zilipita bila kuuza hata bidhaa moja ya maana. Akiba yangu ya benki ilisha kabisa, madeni ya wauzaji wa jumla yalianza kunilundikia, na wafanyikazi wangu walishindwa kupata mshahara kwa miezi mitatu mfululizo.

Nilibaki nikiketi dukani kuanzia asubuhi hadi jioni nikiwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikitazama biashara yangu ya mamilioni ikiporomoka kuelekea kufilisika kabisa. SOMA ZAIDI.

 

Jina langu ni Baraka. Kuna siku moja katika maisha yangu ambayo sitaisahau kamwe.

Ilikuwa siku ambayo kosa dogo la kutuma pesa lilibadilisha maisha ya familia yangu.

Mama yangu alikuwa amelazwa hospitalini katika hali mbaya sana. Madaktari walihitaji malipo ya haraka ili kuendelea na matibabu yake.

Nyumbani kulikuwa na hofu kubwa. Kila mtu alikuwa akipiga simu kutafuta msaada. Ndugu walichangia walichoweza.

Baada ya kuhangaika kwa muda, hatimaye nilifanikiwa kupata TSh 1,850,000. Kwangu mimi, hiyo haikuwa pesa tu.

Ilikuwa matumaini. Ilikuwa nafasi ya kumuokoa mama yangu. SOMA ZAIDI.

Takribani wakulima wadogo 1,000 kutoka mikoa ya Morogoro, Dodoma na Arusha wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kuondokana na matumizi ya viuatilifu hatarishi katika shughuli zao za kulimo. Idadi hiyo ya wakulima itawagusa moja kwa moja wakulima wa mbogamboga, vitunguu, mbogamboga na pamba waliopo kwenye wilaya za Karatu, Chamwino, Mvomero na Meru. Hatua hiyo inayolenga kuwahamasisha wakulima kuachana na matumizi ya viuatilifu hatarishi ili kupunguza madhara ya kiafya yanayosababishwa na kemikali hizo kuanzia kwa mkulima mpaka kwa mlaji.

Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa Asasi Isiyo ya Kiserikali ya AGENDA For Environment and Responsible Development, Dorah Swai, mkoani Morogoro wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa kilimo bora na mazingira kutoka katika taasisi za serikali na binafsi. Bi. Swai amesema kuwa mradi huo uliofadhiliwa na mfuko wa Global Frame Work (GFC) unahusisha nchi tatu za ukanda wa Mahariki mwa Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya na Ethiopia na kila nchi imejiwekea malengo ya kufikia angalau wakulima 1000. Amesema dhamira kuu ya mradi huo wa kuondoa viuatilifu hatarishi ukanda wa Mashariki mwa Afrika una lengo la kuangalia namna bora ya kuwawezesha wakulima wadogo 3,000 watakaokuwa vinara wa mabadiliko katika matumizi ya viuatilifu mbadala kwa wenzao.

Katika warsha hiyo, Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Joseph Kiwango, amesema serikali iko tayari kushiriukiana na wadau wote wenye nia ya kuwainua Watanzania kupitia sekta ya kilimo kinachozingatia utunzaji wa mazingira na afya za binadamu. Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya Mwavuli wa Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Bakari Mongo, pamoja na Afisa Programu Mkuu wa Agenda, Silvani Mng’anya, kila mmoja kwa nyakati tofauti amesema suala la kupambana na viuatilifu hatarishi halipaswa kuwa la mtu mmoja au kikundi Fulani, kwani madhara ya viuatilifu hatarishi hayaishii kwa mtu mmoja. “Jukumu la kuondoa viuatilifu hatarishi halipaswa kuwa la mtu mmoja, ni jukumu letu sote katika kuhakikisha mlaji wa mwisho analindwa dhidi ya madhara yatokanayo na viuatilifu hatarishi.”amesema Mongo.