Na. Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC), Dkt. Aggrey Mlimuka, ametembelea banda la FCC katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Maonesho hayo yamewakutanisha washiriki mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, wakiwemo kampuni binafsi, taasisi na mashirika ya Serikali, yakitoa fursa ya kutangaza bidhaa, huduma na uwekezaji.

Akiwa katika banda la FCC, Dkt. Mlimuka ameipongeza Tume hiyo kwa kazi kubwa inayofanya katika kulinda ushindani wa haki sokoni na kuimarisha mapambano dhidi ya bidhaa bandia, hatua inayochangia kulinda maslahi ya walaji na kukuza mazingira bora ya biashara nchini.

Pia amempongeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, Menejimenti pamoja na watumishi wote wa Tume hiyo kwa kujituma, weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao na kuhakikisha taasisi hiyo inatimiza malengo yake kwa mafanikio.

FCC ina jukumu la kulinda na kuhimiza ushindani wa haki katika biashara, kulinda maslahi ya walaji, kupokea na kushughulikia malalamiko yanayohusu ukiukwaji wa sheria za ushindani, pamoja na kudhibiti uingizaji, usambazaji na uuzaji wa bidhaa bandia nchini.

Mbali na kutembelea banda la FCC, Dkt. Mlimuka pia alitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara ili kujionea shughuli na huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yenye kaulimbiu "Sabasaba Fahari ya Tanzania," yalianza rasmi Juni 28, 2026, na yanatarajiwa kuhitimishwa Julai 13, 2026 katika Viwanja vya Maonesho vya Julius Nyerere (Sabasaba Grounds), Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC) akipata maelezo kutoka kwa Bi. Roberta Feruzi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano - FCC wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa  yanayoendelea viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa FCC wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa  yanayoendelea viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Tanzania imepata heshima ya kutunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya WSIS Prizes 2026 kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano ulioongeza upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya vijijini na ambayo hayakuwa na huduma ya mawasiliano nchini.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Bw. Rashid Kassim Mchatta, amesema chanjo zinazozalishwa na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) zimeendelea kuthibitisha ubora wake kwa kusaidia kudhibiti magonjwa mbalimbali ya mifugo na kuongeza tija kwa wafugaji nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar.

Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar ambapo wamejadili kuhusu ushirikiano katika maeneo ya uwekezaji, ajira na maendeleo ya ujuzi.

Aidha, katika mazungumzo yao Mhe. Sangu alitumia fursa hiyo kumueleza Mwenyekiti wa Al Mansour Holding dhamira ya Serikali ya Tanzania katika kuendelea kuweka mazingira bora na rafiki kwa wawekezaji pamoja na kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Qatar.

Vilevile, Waziri Sangu ameipongeza kampuni ya Al Mansour Holding kwa kuendelea kuongeza wigo wa uwekezaji katika Mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania Bara na Zanzibar. Pia, amehamasisha kampuni hiyo kutumia wataalamu na nguvu kazi ya Watanzania katika shughuli zake nchini Qatar na katika masoko mengine ya kimataifa.

Kadhalika, ameihakikishia kampuni hiyo ushirikiano katika kukuza maendeleo ya rasilimali watu kupitia mafunzo, uhamishaji wa teknolojia na ujuzi ili kuchochea ajira na ukuaji wa uchumi.

Katika ziara hiyo, Waziri Sangu ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na wataalamu wengine kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar.

Mimi nilikuwa naishi na maumivu ya tumbo kwa muda mrefu sana. Kila siku nilikuwa naanza siku nikiwa sijisikii vizuri, na wakati mwingine maumivu yalikuwa yanazidi baada ya kula. Ilifika wakati nilianza kuogopa hata kula chakula kwa sababu sikujua kama nitapata maumivu tena.

Hali hii ilinifanya nipungue nguvu na hata uzito wangu ukaanza kushuka.
Nilitembelea vituo vya afya mara kadhaa, nikapewa dawa tofauti, lakini nafuu ilikuwa ya muda mfupi tu. Baada ya muda maumivu yalirudi tena kama kawaida.

Hali hii ilinichosha sana. Nilianza kukata tamaa na kuona kama nitakuwa na tatizo hili maisha yangu yote. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Baada ya miaka mingi ya majaribio bila mafanikio, Neema (si jina lake halisi) alikuwa amekata tamaa kuhusu ndoto yake ya kuwa mama. Licha ya kutafuta msaada katika vituo mbalimbali vya afya, changamoto ya kushika mimba iliendelea kuwa mzigo mkubwa kwake na familia yake.

Katika harakati za mwisho za kutafuta suluhisho, Neema alisikia kuhusu Kiwanga Doctors—wataalamu wa tiba za asili na jadi wanaosaidia watu kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiafya. Akiwa na matumaini kidogo yaliyosalia, aliamua kuwafikia na kupata ushauri wao.

Baada ya tathmini ya kina, Neema alipatiwa mwongozo na tiba za asili zilizolenga kuimarisha afya yake ya uzazi kwa ujumla. Kulingana na maelekezo aliyopatiwa, alianza kufuata matibabu hayo kwa nidhamu huku akizingatia pia ushauri wa mtindo bora wa maisha. SOMA ZAIDI.
Wakazi wa Karatina, Kaunti ya Nyeri, walijikuta katika hali ya mshangao baada ya tukio lisilo la kawaida kuripotiwa karibu na eneo la mahakama. Kundi la nyuki lilionekana kuvurugika, likasababisha taharuki ya muda mfupi huku watu wakikimbilia usalama.

Mashuhuda wanasema tukio hilo lilitokea ghafla, na baadhi yao walihusisha hali hiyo na mvurugiko wa mazingira au usumbufu wa makazi ya nyuki. Wataalamu wa mazingira wanaeleza kuwa nyuki huwa wakali wanapohisi tishio, hasa katika maeneo yenye kelele, mitikisiko au harakati nyingi.

Pamoja na tukio hilo, kumekuwa na mazungumzo miongoni mwa wakazi kuhusu umuhimu wa haki na uwazi katika jamii. Hata hivyo, wadau wa sheria wanasisitiza kuwa njia sahihi ya kushughulikia kutoridhishwa na maamuzi ya mahakama ni kupitia mifumo rasmi ya rufaa na taratibu za kisheria. SOMA ZAIDI.

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amekutana na kufanya kikao cha pembeni na wajumbe wa Kamati Tendaji (Steering Committee) ya Soko la Pamoja la Nishati Mashariki mwa Afrika (Eastern African Power Pool - EAPP), ya  kutoka Tanzania waliopo nchini Ethiopia. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kupokea ripoti na kupata uelewa wa kina wa masuala mbalimbali yaliyojadiliwa na kamati hiyo, ikiwa ni maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa Ngazi ya Mawaziri.

Kamati hiyo tendaji imekuwa nchini Ethiopia tangu Julai 7, ambapo ilikuwa ikitekeleza kikao chake cha 37 cha maandalizi. Kikao hiki cha Naibu Waziri na kamati kimekuja wakati muafaka kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 8 na 9 Julai, ambapo maazimio na mikakati mbalimbali ya sekta ya nishati inatarajiwa kujadiliwa na kupitishwa.

Hatua hizi zote ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea Mkutano wa 22 wa Baraza la Mawaziri la Soko la Pamoja la Nishati Mashariki mwa Afrika (Eastern African Power Pool - EAPP). Ushiriki wa Tanzania katika mikutano hii una umuhimu mkubwa katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda, kuuziana umeme, kuunganisha gridi za Taifa na kuhakikisha usalama wa nishati kwa nchi wanachama wa ukanda huo.







Serikali imeahidi kuendelea kuwaunga mkono wazalishaji wa ndani ili kuongeza uwezo wa uzalishaji na kukuza mauzo ya bidhaa nje ya nchi hatua inayolenga kuimarisha uchumi wa viwanda na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya kimataifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga(Mb), Julai 09, 2026 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya ziara yake katika Kiwanda cha Kamal Refinery kilichopo Bagamoyo mkoani Pwani kinachojihusisha na uchakataji wa mafuta machafu ya mitambo na magari (Waste/Used Lube Oil) ili kuyasafisha na kuzalisha mafuta mapya ya vilainishi (lubricants) na mafuta mazito ya viwandani (heavy fuel oil).

Aidha, amesema Sekta ya Viwanda na Biashara imeweka kipaumbele cha juu katika kuongeza minyororo ya thamani ya uzalishaji hapa nchini mkakati unaolenga kupunguza utegemezi na uingizaji wa bidhaa kutoka nje ambazo zina uwezo na sifa ya kuzalishwa kikamilifu na viwanda vya ndani.

Amesema uwekezaji huo umebainika kuwa na manufaa makubwa kimazingira, kwani unachangia kuweka mazingira katika hali ya usafi na usalama katika wakati ambao Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa kinara na “Champion” wa utunzaji wa mazingira.

Aidha, amesema ili kufanikisha azma hiyo, Sekta ya Viwanda na Biashara itashirikiana kwa karibu na Wizara yenye dhamana ya Mazingira, ambayo tayari ina uhusiano wa kikazi na kiwanda hicho ili kuhakikisha kiwanda hicho kinaongeza uzalishaji na kukuza biashara huku kikizingatia kikamilifu utunzaji endelevu wa ikolojia.

Vilevile, Amewasihi wadau mbalimbali kuunga mkono kiwanda hicho, kinachosaidia kulinda mazingira ya taifa kwa vizazi vijavyo huku akiwataka Watanzania kuendelea kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazojitokeza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho Bw. Sameer Santosh ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya biashara na kuwaunga mkono wazalishaji wa ndani.

Amesema kiwanda hocho kitaendelea kuongeza zaidi uwezo wa uzalishaji ili kupunguza uingizaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi.

Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa za kujenga kampuni ambayo ingenipa uhuru wa kifedha na kusaidia familia yangu. Kwa miaka ya mwanzo, mambo yalikuwa yanaenda vizuri. Wateja walikuwa wengi, mauzo yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu siku zijazo.

Lakini hali ilibadilika ghafla.

Mauzo yalianza kushuka mwezi baada ya mwezi. Wateja ambao walikuwa waaminifu kwa biashara yangu walianza kupungua, na baadhi yao walihamia kwa washindani wangu. Nilijaribu kupunguza bei za bidhaa na kuanzisha ofa mbalimbali, lakini matokeo hayakuwa yale niliyotarajia.

Hasara zilianza kuongezeka. Kila mwisho wa mwezi nilikuwa nikiangalia hesabu za biashara na kuona fedha zikizidi kupungua. Baadhi ya wafanyakazi walihofia kuhusu mustakabali wa biashara hiyo, na hata mimi mwenyewe nilianza kujiuliza kama ningelazimika kuifunga.
Usiku mwingi nilikosa usingizi.

Nilikuwa nikifikiria jinsi ya kulipa madeni, kuhifadhi biashara, na kuhakikisha familia yangu haipati matatizo kutokana na hali hiyo. Kadri muda ulivyopita, presha iliongezeka zaidi. SOMA ZAIDI.