Serikali imedhamiria kubadilisha maisha ya wananchi vitongojini kupitia usambazaji wa umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi wamehimizwa kuchangamkia kuunganishiwa umeme kwenye vitongoji vilivyofikiwa.



NAIBU Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya, amezungumzia umuhimu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), kushirikiana na sekta binafsi na taasisi za elimu ya uhandisi katika kuendesha maabara zake za kisasa.

Hatua hiyo itaiwezesha TANROADS kuongeza mapato, kuimarisha huduma za kitaalamu na kuifanya Taasisi hiyo kuwa kitovu cha umahiri katika upimaji wa vifaa vya ujenzi wa barabara nchini na ukanda wa Afrika Mashariki.

Eng. Kasekenya amesema hayo leo wakati wa ziara yake kukagua maendeleo ya ujenzi wa Makao Makuu ya TANROADS jijini Dodoma.

Ameitaka TANROADS  kuhakikisha viongozi wake wakuu na watumishi wanaopaswa kuhamia Makao Makuu ya nchi wanakamilisha uhamisho wao ifikapo mwisho wa Agosti mwaka huu.

Amemtaka Mkandarasi CRJE East Africa Ltd. anayejenga jengo hilo ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 85 kuongeza kasi ili likamilike kwa wakati.

"Tunapoelekea katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ni muhimu Taasisi za umma kuangalia namna ya kushirikiana na sekta binafsi ili kuongeza tija kwa umma hivyo TANROADS ina maabara za kisasa ambazo zinaweza kutumika kutoa huduma za kibiashara na kitaalamu kwa taasisi mbalimbali ndani na nje ya nchi," amesisitiza Naibu Waziri Kasekenya.

Aliongeza kuwa ushirikiano, ubunifu, uadilifu na moyo wa kujituma kutaifanya TANROADS kuwa kituo cha umahiri katika upimaji wa vifaa vya ujenzi wa barabara na kuongeza uwezo wa wataalamu wa ndani kupitia ubadilishanaji wa uzoefu na teknolojia.

Eng. Kasekenya amesema  Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejidhatiti  kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa ili kuimarisha uwezo wa Taasisi za Serikali kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

"Serikali imehakikisha TANROADS inapata eneo kubwa pamoja na majengo na maabara za kisasa zinazokwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia duniani," amesema Eng. Kasekenya.

 Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma, Eng. Zuhura Amani, amesema mradi huo wenye thamani ya Shilingi bilioni 49.72 unatekelezwa na kampuni ya CRJE East Africa Limited chini ya usimamizi wa Tanzania Building Agency (TBA)
















Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amefungua mafunzo ya tatu ya Bespoke kwa Mawakili wa Serikali, yalioandaliwa na kuratibiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambayo yameanza tarehe 15 Julai, 2026 na yatahimishwa tarehe 17 Julai, 2026 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Arusha (AICC) Jijini Arusha.
Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Usimamizi Rasilimali Watu katika Taasisi za Umma-Ofisi ya Msajili wa Hazina, Bw. Hussein Kakurwa, akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Bodi ya Ushauri katika mafunzo elekezi ya Bodi ya OSHA yaliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha Mkoani Pwani.

 


▪️Tanzania yajipanga kuwa kitovu cha huduma bora za Maabara ya madini kusini mwa Jangwa la Sahara


■ Waziri Mavunde amshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia kwa uamuzi wa ujenzi wa maabara


■ Amtaka Mkandarasi kukamilisha ujenzi kwa wakati


■ Ujenzi wa Maabara kugharimu zaidi ya Bilioni 14.3


Kufuatia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa maabara ya kisasa ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), hatua hiyo inakwenda kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za maabara ya madini kusini mwa Jangwa la Sahara.

Hayo yamesemwa leo tarehe 15 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maabara ya GST uliopo Kizota, Jijini Dodoma.

"Tunamshukuru Rais wetu Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha za utekelezaji wa mradi huu wa kisasa, unaokwenda kuifanya Nchi yetu kuwa kinara na mahiri katika utoaji wa huduma za maabara za madini", amesema.

"Mradi huu pia unakwenda kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za maabara kwa Nchi za Afrika ya Mashariki na Kati, kutokana na ubora wa huduma hizo kuwa za kimataifa" ameeleza Waziri Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa kwa muda mrefu wachimbaji wadogo wamekuwa wakipata changamoto ya upimaji wa sampuli zao kwenye maabara, hali iliyopelekea kushindwa kufanya shughuli zao kiufanisi.

Mavunde amesitiza kuwa ujio wa maabara hiyo ya kisasa unakwenda kuwa mwarobaini wa changamoto za wachimbaji ikiwa ni pamoja na kuhudumia wachimbaji wengi zaidi kwa ubora wa kimataifa.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Madini Tanzania, Mhandisi Ally Samaje ameeleza kuwa ujenzi wa mradi huo wa maabara unagharimu shilingi bilioni 14.3 na upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo unataraji kukamilika ifikapo Mwezi Septemba, 2027. 

Aidha, ameongeza kuwa maabara hiyo ikikamilika itakuwa ni ya kisasa na inakwenda kuhudumia wateja wengi wa ndani na nje ya Nchi.












Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Tanzania imezindua kitabu cha Mwongozo wa Matumizi Salama ya Gesi ya LPG na kusaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu na Chama cha Skauti Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha elimu ya matumizi salama ya gesi ya kupikia kwa wananchi kupitia mtandao wa vijana wa Skauti nchini.
Na Mwandishi Wetu

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimeandika historia mpya baada ya kuingia kwa mara ya kwanza katika orodha ya QS World University Rankings (QS WUR) 2027, hatua inayokitambulisha rasmi miongoni mwa vyuo vikuu bora duniani na kuiweka Tanzania katika ramani ya kimataifa ya elimu ya juu, utafiti na ubunifu.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Mahmoud Thabit Kombo leo Julai 14, 2026 amekabidhiwa rasmi kombe kutoka kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Ngwaru Maghembe linalotokana na ushindi wa timu ya Wanadiplomasia katika Bonanza Kuu la Bunge la Benki ya CRDB lililofanyika tarehe 20 Juni 2026 katika Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Zaidi ya wananchi 5,000 kutoka vijiji vitatu vya kata ya Endamaghaay, Wilaya ya Babati mkoani Manyara, wameanza kunufaika na mradi wa maji safi na salama ulitekelezwa na wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) uliolenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji wenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilion 1.9.
Na mwandishi wetu Arusha.

Zaidi ya wananchi 8,000 kutoka Mkoa wa Arusha na maeneo mengine nchini wamepata huduma za uchunguzi na matibabu bila malipo katika siku mbili za kwanza za kambi maalumu ya afya inayofanyika jijini Arusha.

 


📌 Majiko banifu 5,776 kusambazwa mkoani Lindi


Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema Mkoa wa Lindi umeanza kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya juhudi za kufikia lengo la kitaifa la kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Bi. Omary amesema hayo leo, Julai 15, 2026, alipokutana na Afisa Mshauri Mwandamizi wa Masuala ya Kiufundi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Deusdedit Malulu, aliyeambatana na uongozi wa Kampuni ya Tango Energy Limited, inayotekeleza usambazaji wa majiko banifu mkoani Lindi.

“Nawapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Tunamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na tutaendelea kutoa elimu ili iwafikie wananchi wote,” amesema Bi. Omary.

Kwa upande wake, Mha. Malulu amesema jumla ya majiko banifu 5,776 yameanza kusambazwa na Kampuni ya Tango Energy Limited katika maeneo ya Lindi, Ruangwa, Nachingwea, Liwale na Kilwa.

Mha. Malulu amewataka wananchi katika maeneo hayo kuchangamkia fursa ya kupata majiko banifu kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 7,600 tu kwa jiko.

Naye, Meneja wa Mauzo wa Tango Energy Limited, Bw. Emmanuel Ibrahim, amesema mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kiasi kidogo cha kuni na mkaa, hatua inayolenga kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi unaotokana na matumizi ya majiko ya kawaida.

Kupitia mradi huo, Tango Energy Limited itasambaza jumla ya majiko banifu 5,776 kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Bei halisi ya jiko moja ni TZS 50,847.46, lakini Serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85, hivyo mwananchi atanunua jiko kwa TZS 7,600 tu.









 




Na Denis Chambi, Tanga .

JUMUIYA YA  Afrika Mashariki (EAC) umezipongeza nchi za Tanzania na Kenya kwa kuendelea kuimarisha mifumo ya usimamizi wa forodha ambao umeweza kuchangia ongezeko la ukusanyaji wa kodi kupitia mamlaka zake za Tanzania Revenue Authority 'TRA' na Kenya Revenue Authority 'KRA' pamoja na kuboresha miundombinu inayotumika.

Hatua hiyo pia  imeweza kuwapa uelewa mpana na kuwasaidia  wafanyabiashara  hususani wajasiramali wadogowadogo waliopo katika nchi hizo kujua umuhimu wa kulipa kodi kwa wakati pamoja na kuwapa fursa ya kuuza bidhaa zao ndani ya Afrika Mashariki hatua ambayo imewawezesha kukuza mitaji yao.

Akitoa pongezi hizo mara baada ya kutembelea  kituo cha  Horohoro kwa upande wa Tanzania na kile cha  Lungalunga kwa upande wa Kenya Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya Afrika ya  Mashariki (EAC) Annet Semwamba amesema kuwa malengo ya kuanzishwa kwa umoja huo yameendelea kukua katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara  huku wakiendelea kutatua  changamoto nyingine  zilizopo ambazo bado zimeendelea kuwa kikwazo baina ya nchi wanachama




"Tumefurahi sana kuona kwamba mapato yameongezeka kwa upande wa TRA na KRA ambapo pesa mnazokusanya zinakwenda moja kwa moja katika kuboresha na kutoa huduma za kijamii na hivyo kugusa maisha ya wananchi wa hali ya chini tunaona barabara zimejengwa , hospitali,  elimu na kadharika" amesema Semwamba.


"Lakini pia tumefurahi kuona kuwa miundombinu ambayo ipo inatumika ipasavyo kwa sababu yapo baadhi ya maeneo ipo miundombinu kama hii lakini haitumiki kama vile ambacho inatakiwa" ameongeza.


Moja wapo ya malengo ya pango wa Umoja wa Afrika 'EAC' ni kuhakikisha  kuwa nchi zote nane  zilizopo ndani ya Umoja huo zinatumia sarafu moja  ili kuwawezesha na kuwasaidia wafanyabishara kupata urahisi wa kuuza na kuzitangaza biashara zao ndani na nje. 


Semwamba amezitaka nchi zote wananchama kupitia wimbo wa Afrika Mashariki kuuishi kwa vitendo kupitia tungo na maneno yaliyotumika  hatua ambayo itawezesha kufikia malengo ya kuanzishwa kwa Umoja huo.

Awali akizungumza  Afisa mfawidhi kutoka katika kituo Cha Horohoro Shadrack Mbona ameeleza  kuwa  kumekuwa na mafanikio  yaliyochangiwa na ushirikiano baina ya vituo hivyo ambapo kwa upande wa Tanzania kupitia kituo cha Horohoro ukusanyaji wa mapato umeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 306 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 hadi Bilioni 548  kwa mwaka 2024/2025.


"Ufanyaji wa biashara umekuwa ukikuwa mwaka hadi mwaka  kwa mfano kwa mwaka wa fedha 2022/2023 sisi kama kituo cha Horohoro tuliweza  kukusanya Bilioni 306 mwaka unaofuata imeenda adi Bilioni 408 mwaka unaofuata imeenda hadi Bilioni 548 kuna ongezezo la Bilioni 100 kila mwaka  na hii jnawezekana kwa sababu tunaboresha huduma" amesema.


Aisha Mbonea ameoeleza kuwepo kwa   utaratibu wa kutoa elimu kwa wafanyabiahara wadogowadogo  kuhusu jinsi ya kuwasaidia kuhusu taratibu za kufuata wakati anapohitaji huduma ya kwenda kuuza ama kununua bidhaa kwa upande wa Tanzania na Kenya.


"Tumekuwa na utaratibu wa kupitia kwenye masoko yaliyopo mipakani kwetu na kutoa elimu kwa wafanyabiahara  kuhusu hatua ambazo wanatakiwa kuzifuata na sasa Wana uelewa wa kutosha na imekuwa na mafanikio makuba sana na sisi tutaendelea na utaratibu huu" amesema


Amesema kuwa badokatika kituo hicho  kuna uhitaji mkubwa wa matumizi ya kifaa ya kisasa ya utambuzi wa mizigo 'Scanner machine' kwaajili ya kutambua na kubaini bidhaa ambazo zinapitushwa na wafanyabishara wa  nchi zote mbili.


"Maendeleo haya yanahitsji vituo vya kisasa zaidi kwa sababu  mahitaji yanaongezeka  kuna mizigo mingi ambayo  kwa kukagua moja moja unaweza kutumia muda mrefu hivyo kumekuwa na changamoto ya ukaguzi ambayo inahitaji sasa kuwepo kwa matumizi ya Scanner ili kupunguza muda wa ukaguzi na kuimarisha ulinzi na tutahakikisha usalama wa nchi zote mbili" amesema Mbonea.

Sikuwahi kufikiria kuwa siku moja ningepitia hali kama hii kwenye ndoa yangu. Mume wangu alianza kubadilika taratibu alikuwa anachelewa kurudi nyumbani, simu yake imekuwa siri, na alikosa muda kabisa wa familia. Nilijaribu kumuuliza mara kadhaa, lakini kila wakati alikuwa na majibu ya kunizungusha.

Moyoni nilijua kuna kitu kinaendelea, lakini sikuwa na ushahidi. Siku moja nilimweleza rafiki yangu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilijikuta kwenye hali ngumu sana baada ya kusingiziwa kesi ambayo sikuwa na uhusiano nayo kabisa. 

Ilianza ghafla, na kabla sijajua, nilikuwa tayari nahusishwa na jambo ambalo sikulifanya. Nilishangaa sana kuona watu wakianza kunitazama tofauti.

Wengine walinihukumu bila hata kusikiliza upande wangu. Hofu ya kifungo ilinijaa moyoni, na sikuweza kupata amani. 

Nilijaribu kujitetea, lakini ushahidi uliokuwa unaonekana haukuwa upande wangu. Ilikuwa kama kila kitu kilikuwa kinanigeuka. SOMA ZAIDI.
Naitwa Miriam, mmoja wa watu wa familia ya marehemu. Kifo cha ndugu yetu kilitupata kama pigo kubwa sana, lakini kilichotuumiza zaidi ni kwamba mazingira ya kifo chake yalikuwa ya kutatanisha na yasiyoeleweka kirahisi.

Kwa muda mrefu tulibaki na maswali mengi bila majibu.

Familia ilianza kugawanyika kwa mashaka na huzuni, huku kila mmoja akitaka kujua ukweli wa kilichotokea.SOMA ZAIDI.

 MWENGE wa uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye wodi ya wanawake na watoto katika kituo cha afya Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, iliyojengwa na kampuni ya Chusa Mining LTD.

Kampuni ya Chusa Mining LTD chini ya Mkurugenzi wake Joseph Damasi Mwakipesile imejenga wodi hiyo ya wanawake na watoto kwa gharama ya shilingi milioni 230 kupitia mchango wao kwa jamii (CSR).

Kiongozi wa mbio za mwenye wa uhuru kitaifa mwaka 2026 Wazo Mwang'onda ameipongeza Chusa Mining LTD kwa kujenga wodi hiyo ambayo wanawake na watoto watalazwa na kupata huduma za afya katika kituo hicho cha afya pindi wakiugua.

Amesema mdau huyo wa maendeleo amejenga jengo hilo kutokana na jitihada za dhati za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu kuweka mazingira rafiki kwa wachimbaji kufanya kazi, nao kutoa kiasi kwa jamii.

"Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kwa sisi wakristo tunaamini kuwa Mungu anakujaribu pale unapotoa kwani amesema nijaribuni kupitia majitoleo na atakubariki pale ulipotoa hongera sana mdau wa maendeleo kwa kujitolea," amesema Mwang'onda.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Ole Millya ambaye pia ni Mbunge wa Simanjiro amesema hatua ya Chusa Mining LTD kuwjenga wodi hiyo ni maendeleo makubwa.

Ole Millya amesema Chusa Mining wamekuwa msaada mkubwa kwa jamii kwani wanakwenda kumaliza changamoto ya upungufu ya wodi ya kulaza wanawake na watoto.

Mkurugenzi wa kampuni ya Chusa Mining LTD, Joseph Mwakipesile ametoa shukrani kwa Serikali kupitia Wizara ya Madini kwa namna wanavyotoa ushirikiano katika kazi zao.

Mwakipesile amesema wamejenga jengo hilo baada ya kusikia changamoto ya wodi ya wanawake na watoto ili kurudisha kidogo wanachokipata kwa jamii.

"Tunashukuru leo hii mwenge wa uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye mradi huu wa wodi ya wanawake na watoto katika kituo cha afya Mirerani," amesema Mwakipesile.

Mganga mfawidhi wa kituo cha afya Mirerani Dkt Namnyaki Lukumay akisoma taarifa ya mradi huo amesema umegharimu shilingi milioni 230 na kujengwa na kampuni ya Chusa mining LTD.

Dkt Namnyaki amesema lengo kuu la mradi huo ni kuboresha upatikanaji wa huduma bora na rafiki za afya kwa wanawake na watoto na kuboresha afya ya familia na jamii kwa ujumla.

Amesema mradi huo ukikamilika utahudumia wanawake 5,000 na watoto zaidi ya 7,000 kwa mwaka katika kituo cha afya cha Mirerani.

"Sisi wananchi wa Simanjiro tunaishukuru Serikali ya awamu inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha huduma za afya, kwa heshima na taadhima tunaomba utembee, kukagua na kuweka jiwe la msingi mradi wetu wa jengo la msingi mradi wetu wa jengo la wodi ya wanawake na watoto katika kituo cha afya Mirerani," amesema. 


 

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy, leo Julai 14, 2026, amepokea tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (Government Institutions Exhibitor), ambayo REA ilitwaa katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.

Tuzo hiyo imewasilishwa kwake na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya watumishi walioshiriki katika maonesho hayo.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mha. Saidy amewapongeza watumishi wa Wakala kwa juhudi, kujituma na ushirikiano wao ulioiwezesha REA kutwaa tuzo hiyo.

Aidha, amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na ushirikiano katika kutekeleza miradi ya REA vijijini na vitongojini, ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma za nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

New York, Marekani

Spika wa Bunge Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb) amesema Bunge la Tanzania limechukua hatua madhubuti za kuhimiza matumizi ya magari ya umeme pamoja na gesi.

Amesema hatua hizo zimelenga kuimarisha utekelezaji wa mipango ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Mheshimiwa Spika ameyasema hayo leo Julai 14, 2026 wakati akiwasilisha taarifa ya Bunge la Tanzania kuhusu matumizi ya Nishati Safi kwenye  Jukwaa la Kibunge katika Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (HLPF) 2026.

Mkutano huo umefanyika  katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN), jijini New York, nchini Marekani.

Amesema Bunge la Tanzania limepitisha marekebisho ya sera na sheria za kodi yaliyopunguza ushuru wa magari ya umeme kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 na kwamba misamaha mbalimbali ya ushuru na kodi kwa baadhi ya magari yanayotumia umeme na gesi imetolewa ili kuongeza matumizi ya usafiri rafiki kwa mazingira.

"Hatua hizi zinalenga kuwahamasisha wananchi kutumia magari ya umeme na yanayotumia gesi, kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa, kupunguza utegemezi wa uagizaji wa mafuta ya petroli kutoka nje ya nchi na kulinda mazingira," alisema Mheshimiwa Zungu

Aidha, amesema Tanzania imeendelea kuimarisha mifumo ya kitaasisi ya kushughulikia masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa kuanzisha vitengo maalumu vya usimamizi wa masuala hayo, kuimarisha uhifadhi wa vyanzo vya maji na kuweka mfumo wa kitaifa wa ufuatiliaji wa kaboni.

"Hatua hizi zinaonesha dhamira ya Tanzania ya kujenga uchumi unaozingatia maendeleo endelevu huku ikichangia juhudi za dunia za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi," amesema.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Zungu ameialika Jumuiya ya Kimataifa kushiriki Mkutano wa 153 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) utakaofanyika jijini Arusha, akisisitiza kuwa Tanzania ni nchi salama na ipo tayari kuwakaribisha wajumbe kutoka mataifa mbalimbali.

"Ninawakaribisha nyote Tanzania kushiriki Mkutano wa 153 wa IPU jijini Arusha. Hakuna changamoto za kiafya zinazopaswa kuwapa wasiwasi wageni wanaokuja Afrika Mashariki, hususan Tanzania, karibuni mfurahie Mlima Kilimanjaro na visiwa vya marashi ya karafuu,  Zanzibar," alisema Mheshimiwa Zungu.

 


Jackline Minja, WMJJWM -  Kigoma

Ushirikiano wa jamii, viongozi wa dini, taasisi mbalimbali na vyombo vya dola umetajwa kuwa nguzo muhimu katika kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyoendelea kuhatarisha usalama, haki na ustawi wa wanawake, watoto pamoja na makundi mengine yaliyo katika mazingira hatarishi.

Akizungumza wakati wa Kongamano la Kupinga Ukatili wa Kijinsia lililofanyika katika Ukumbi wa NSSF mkoani Kigoma, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia hayawezi kufanikiwa bila ushirikiano wa Serikali, viongozi wa dini, viongozi wa mila, taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla, huku akisisitiza kila mmoja kutimiza wajibu wake katika kulinda haki na usalama wa wahanga wa vitendo hivyo. 

“Ukatili wa kijinsia si jambo la kawaida wala sehemu ya utamaduni, hivyo hakuna mila, desturi au sababu yoyote inayoweza kuhalalisha kumuumiza, kumdhalilisha au kumnyima mtu haki zake za msingi niwaombe wananchi kuacha kuficha matukio ya ukatili na badala yake kutoa taarifa kwa vyombo husika ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria na kuzuia madhara kuendelea kutokea kwa waathirika wengine”. amesema Naibu Waziri Mahundi

Aidha, amesema Serikali itaendelea kuimarisha utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia pamoja na kuimarisha huduma za ulinzi kwa waathirika huku amekiwataka wazazi na walezi kuzingatia malezi chanya kwa watoto, huku akiwahimiza viongozi wa dini na mila kuendelea kutumia nafasi zao kuelimisha jamii na kukemea vitendo vya ukatili vinavyoathiri maendeleo ya familia na taifa.

"Hakuna atakayefanya vitendo vya ukatili na akabaki bila kuchukuliwa hatua wote watakaobainika kutenda vitendo hivyo watachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria, ikiwemo vifungo vya muda mrefu na pale sheria inapotoa nafasi, vifungo vya maisha, ili iwe fundisho kwa wengine basi serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu kila tukio kwa sababu tunataka kujenga jamii ya watu wa mfano wanaoheshimu haki na utu wa wenzao maana tumeona baadhi ya adhabu hazijawa kikwazo cha kutosha kwa wahalifu, hivyo hatutasita kuhakikisha sheria zinasimamiwa ipasavyo," amesema Naibu Waziri  Mahundi

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, amesema ukatili wa kijinsia bado ni changamoto kubwa wilayani humo kutokana na kuendelea kuripotiwa kwa matukio mengi yanayohusisha wanawake na watoto, akibainisha kuwa viongozi wa dini, Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi na maafisa ustawi wa jamii wamekuwa na mchango mkubwa katika kutoa elimu na kuwasaidia waathirika kupata haki zao.

"Katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia lazima tuliseme jambo hili kila siku. Mimi nalisemea kila siku kwa sababu kesi nyingi zinakuja sana pale ofisini kwangu. Matukio ni mengi na yanatia huzuni sana. Niwapongeze viongozi wa dini, Dawati la Jinsia na maafisa ustawi wa jamii kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuendelea kuelimisha jamii na kusimama na waathirika wa vitendo hivi" amesema Dkt. Chuachua.