📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme
📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme kupitia LUKU
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limezindua mradi wa vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme pamoja na Mpango wa Ukopeshaji wa Majiko ya Umeme kwa Wateja (On-Bill Financing – OBF), hatua inayofungua ukurasa mpya wa matumizi ya umeme nchini na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya nishati safi.
Akizindua miradi hiyo jijini Dodoma, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb) leo tarehe 11 Juni, 2026 alisema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Tanzania kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya matumizi ya nishati safi duniani huku ikilenga kuboresha maisha ya wananchi na kukuza uchumi.
“Hatua hii inapanua matumizi ya umeme kutoka kupikia hadi usafiri, kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi, kupunguza gharama za maisha na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa,” alisema Mhe. Ndejembi.
Alisema Serikali imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya nishati, hali iliyowezesha uzalishaji wa umeme nchini kufikia zaidi ya megawati 4,000 na kuweka msingi wa matumizi mapana ya umeme katika sekta mbalimbali za uchumi.
Katika kuimarisha matumizi ya vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme, TANESCO kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) imepokea mashine 50 za kisasa za kuchajia vyombo hivyo kutoka kampuni ya AUTEL ya China. Mashine hizo zitafungwa katika maeneo mbalimbali ya kimkakati nchini ili kurahisisha huduma za uchaji.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, alisema Shirika limejipanga kuongoza mageuzi ya matumizi ya umeme nchini kwa kutumia fursa ya upatikanaji wa umeme wa kutosha.
“Mtazamo wa awali kwamba umeme ni ghali na matumizi yake yanaishia kwenye mwanga pekee umebadilika kwa kiasi kikubwa. Leo, wananchi wengi wanatumia umeme katika kupikia na shughuli mbalimbali za kiuchumi, huku hatua ya kuzindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme ikifungua ukurasa mpya wa matumizi ya nishati safi nchini,” alisema Bw. Twange.
Kwa upande wa nishati safi ya kupikia, TANESCO imeanza kutekeleza Mpango wa On-Bill Financing (OBF) utakaowezesha wateja kupata majiko ya umeme kwa mkopo na kufanya marejesho kupitia manunuzi yao ya kawaida ya umeme wa LUKU.
Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, ameipongeza TANESCO kwa hatua hiyo na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini.
“Nawapongeza TANESCO kwa hatua hii ya kimkakati inayofungua fursa mpya za matumizi ya nishati safi nchini. Ni muhimu kuendelea kuhamasisha wananchi kutumia nishati safi katika usafiri na kupikia ili kuharakisha maendeleo na kuhifadhi mazingira,” alisema Senyamule.
Uzinduzi wa miradi hiyo unaashiria hatua mpya ya kupanua matumizi ya umeme nchini kutoka matumizi ya kawaida ya majumbani hadi sekta za usafiri, kupikia na shughuli za uzalishaji mali, sambamba na juhudi za Taifa kuelekea uchumi wa kijani na maendeleo endelevu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo amewasilisha Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27 akisisitiza vipaumbele vitano vya utekelezaji wake.
Akitaja vipaumbele hivyo, amesema mosi ni kuimarisha utawala bora, demokrasia, amani, na utulivu na pili ni kujenga uchumi imara, jumuishi na shindani na kipaumbele cha tatu ni, kuimarisha uwezo wa watu na maendeleo ya jamii.
Akiendelea kufafanua vipambele hivyo, Mhe. Waziri amesema kipaumbele cha nne ni kuimarisha uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu kwa mabadiliko ya tabianchi na cha tano kikiwa kusimamia utekelezaji wa vichocheo vya mageuzi ambavyo ni pamoja na nishati, miundombinu ya usafiri na usafirishaji, utafiti na maendeleo, na mageuzi ya kidigitali.
Prof Kitila amesesema utekelezaji wa vipaumbele hivyo ni hatua za kuyatekeleza malengo makuu ya Dira 2050, na vimezingatia Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/27 – 2030/31 wenye dhima ya “Mageuzi kwa ajili ya Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uzalishaji Ajira” ambao ni wa kwanza katika utekelezaji wa Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/27 – 2050/51.
Aidha katika kutekeleza maeneo ya vipaumbele hivyo, Serikali imepanga kuanza kutekeleza programu na miradi mbalimbali ikiwemo miradi shikizi 38 kati ya 51 iliyopo katika programu saba (7) za kielelezo zilizoainishwa katika Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.






Na Ashura Mohamed, ARUSHA
Naibu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalam kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha IAA, Dkt. Grace Temba, amezindua na kuweka msingi wa maandalizi ya kongamano la kimataifa la utalii linalotarajiwa kufanyika tarehe 25 Septemba, 2026 mkoani Arusha.
Tukio hilo la kongamano ni muhimu kwa taasisi hiyo na maalum kwa wadau wa utalii kutoka maeneo mbali mbali duniani likilenga wadau wa sekta ya utalii kwa dhima kubwa ya kuhamasisha utalii wa ndani ili kuendelea kuhamasisha idadi ya watalii kuongezeka.
Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo Dkt. Grace amesema kuwa lengo hasa ni kuhakikisha wadau mbali mbali wanashiriki na kufanya kongamano hilo kujumlisha watunga sera, wadau wa utalii kutoka ndani na nje ya nchi kujiandaa na kushiriki kwa ufanisi zaidi.
“Siku ya kongamano tunawaweka pamoja wadau mbali mbali tunatoa taarifa mbali mbali za utafiti zilizofanywa na wadau mbali mbali waliopo katika sekta ya utalii lakini pia Chuo cha Uhasibu Arusha, watunga sera wa taasisi na mlaji ili kuja na suluhisho na maboresho makubwa katika sekta ya utalii kwa lengo la kunufaisha pande zote,” alisema Dkt. Grace.
Aidha amesema kuwa kongamano hilo la nne linatarajiwa kuendelea kukuza na kutangaza nchi kimataifa kwa kuja na mawasilisho ambayo yatalenga wadau na watoa huduma kuendelea kujikuza kimasoko, miundombinu, na kuifanya sekta hiyo kuwa bobezi na kuchangia pato la taifa.
Nae Kaimu Mkuu wa Kitivo cha Biashara na Sayansi ya Jamii kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha IAA, Bi. Lorna Boniface Mwijarubi, amesema kuwa chuo hicho kinatarajia kushirikiana na taasisi mbali mbali na wadau wa utalii katika kuonyesha tafiti na bunifu ambazo zitaisaidia sekta ya utalii kuwa bora zaidi na kuendelea kuliingizia taifa kipato.
Amesema kuwa mafanikio yaliyopatikana kutokana na makongamano yaliyopita ni makubwa kwa kuwa yamekijengea chuo mashirikiano na wadau ambayo huwezesha wanafunzi wa kozi ya utalii na ukarimu kupata fursa ya kujifunza kwa vitendo katika maeneo mbali mbali nchini na kusaidia kupata ajira pamoja na taifa kupata mapato kupitia sekta hiyo.
Chuo cha Uhasibu Arusha IAA kimeendelea kuwa maarufu katika sekta mbali mbali kwa kutoa elimu bora yenye ushindani sokoni huku katika sekta ya utalii inatajwa kuwa ndio chuo pekee kinachotoa kozi ya utalii na ukarimu nchini ambayo inatajwa kuwa na mchango mkubwa katika kutangaza nchi na kuendelea kuifanya sekta hiyo kuwa bora zaidi nchini.
Nilikuwa nimeijenga kwa juhudi kubwa na nilikuwa na imani kubwa kwa wafanyakazi wangu. Tulikuwa kama familia, na sikuwahi kufikiria kwamba mtu ambaye nilimwamini angeweza kuwa chanzo cha matatizo yaliyokuwa yananikabili. Tatizo lilianza polepole.
Kila mwisho wa wiki nilipokagua hesabu za biashara, niligundua kulikuwa na upungufu wa fedha. Mwanzoni nilidhani ni makosa ya kawaida ya mahesabu au matumizi ambayo hayakuwa yameandikwa vizuri. Lakini hali iliendelea kujirudia.
Wiki moja ikageuka mwezi, na miezi ikazidi kwenda. Kiasi cha fedha kilichokuwa kinapotea kilianza kuongezeka.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa siwezi kumshuku mtu yeyote. Wafanyakazi wote walionekana waaminifu na walikuwa wamefanya kazi nami kwa muda mrefu.
Nilianza kufuatilia kila kitu kwa karibu zaidi.
Nilikagua stakabadhi, mauzo, na matumizi ya kila siku. Hata hivyo, sikuweza kupata jibu la wazi kuhusu chanzo cha upotevu wa fedha.
Kadri muda ulivyopita, hasara ilizidi kuongezeka.
Kulikuwa na wakati nilifikiria kufunga biashara kwa sababu sikuona namna ya kuzuia hali ile.SOMA ZAIDI.
Nilipoolewa, niliamini kwamba baada ya muda mfupi ningekuwa mama. Nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu maisha yangu ya baadaye na familia niliyotamani kuijenga.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Mwezi mmoja ulipita, kisha mwingine. Baadaye mwaka mmoja ukapita bila kupata ujauzito.
Baadhi ya majibu niliyopata yalikuwa magumu kuyakubali. Niliambiwa kwamba kupata mtoto kungeweza kuwa changamoto kubwa kwangu na kwamba huenda ningehitaji uvumilivu mkubwa kuliko nilivyokuwa nikifikiria. Kwa kweli nilivunjika moyo.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wakipata watoto kwa urahisi huku mimi nikiendelea kusubiri. Kila nilipoalikwa kwenye sherehe za watoto au kuona familia mpya zikifurahia watoto wao, nilihisi maumivu makubwa moyoni. SOMA ZAIDI.
Mwanzoni nilikuwa na matumaini. Kila nilipoanza uhusiano mpya, niliamini kwamba safari hii mambo yangekuwa tofauti. Lakini mara nyingi ndoto zangu ziliishia kuvunjika na kuniacha nikianza upya. Kadri miaka ilivyopita, nilianza kuchoka.
Niliona marafiki zangu wakifunga ndoa na kujenga familia zao huku mimi nikiendelea kuzunguka kwenye maumivu yale yale.
Nilifikia hatua ya kuamua kujikita kwenye kazi na maisha yangu binafsi. Nilijiambia kwamba huenda siku yangu ya kupata mwenza wa maisha isingewahi kufika. Lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti.SOMA ZAIDI.
Mwanzoni nilikuwa na matumaini makubwa.
Nilijiamini kuwa elimu yangu na uzoefu wangu vingekuwa vya kutosha kunisaidia kupata nafasi nzuri. Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kuona hali ikiwa tofauti na nilivyotarajia.
Miezi iligeuka miaka.
Nilituma maombi kwa kampuni nyingi sana. Wakati mwingine niliitwa kwa mahojiano lakini sikuchaguliwa. Mara nyingi sikupata hata majibu ya maombi niliyotuma.
Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na kitu nilichokuwa nakosea. Kadri miaka ilivyopita, confidence yangu ilianza kupungua.
Sababu ilikuwa moja tu. Nilikuwa na deni kubwa ambalo nilikuwa nimeshindwa kulilipa kwa muda mrefu.
Mwanzoni niliamini ningemaliza kulipa haraka.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyopanga. Biashara yangu ilipata changamoto, mapato yakapungua, na madeni yakaendelea kuongezeka. Kadri muda ulivyopita, presha ilizidi kuwa kubwa. Kwa kweli nilikuwa naishi kwa wasiwasi.
Kila nilipoona ujumbe au simu kutoka kwa wadai, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu. Wakati mwingine nilikosa usingizi nikifikiria jinsi nitakavyotoka kwenye hali ile.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa mtu mwenye bidii. Sikupenda kukwepa majukumu yangu, lakini nilijikuta katika hali ambayo sikuwa na uwezo wa kufanya kila kitu kwa wakati mmoja.
Miaka ilipita huku nikihangaika. Kulikuwa na nyakati nilikata tamaa na kuanza kuamini kwamba ningebeba mzigo wa deni hilo maisha yangu yote. Lakini moyoni bado nilikuwa na matumaini kwamba siku moja hali ingebadilika. SOMA ZAIDI.

Na; Mwandishi wetu – Chato
Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Louis Peter Bura Amepongeza Programu ya kuendeeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu kwa Uratibu wa Kituo cha kuendeleza ukuzaji Viumbemaji Rubambagwe Kilichopo wilayani Chato Mkoani Geita kinachosimamiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
Ametoa Pongezi hizo Tarehe 10 Juni 2026 Wilayani Chato alipofanya ziara maalum ya kutembelea kituo hicho akiwa pamoja na timu ya wataalam waliokutana katika Wilaya hiyo wakiwa katika kazi maalum ya kufanya mapitio ya mpangokazi wa Program hiyo.
Mkuu wa Wilaya Bura, alisema kuwa Wilaya yake inawajibu wa kutoa elimu kwa wafugaji kupitia kituo cha Rubambagwe hivyo amewaasa wataalam kutoka katika sekta zinazotekeleza mradi kufanya kazi kwa ushirikianao na Wilaya hiyo, ili kuweza kuleta matokeo chanya katika uchumi wa Wilaya na Taifa kwa Ujumla na Kuongeza mnyororo wa thamani.
“Tutakuwa tunazalisha vifaranga vya samaki pale, haitatosha hiyo pia tutakuwa tunazalisha vyakula vya samaki, na hayo yote yamenipa mimi wakati mzuri na sababu ya kujifunza haya yote, na tunashukuru mradi huu kwenda kwa kasi na ni wakati sasa wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja . “Alibanisha
Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza ushirikishwaji mzuri baina ya sekta zinazotekeleza Programu hiyo nchini pamoja na Wilaya husika.’katika dhana nzima ya ushirikishwaji kuna mambo mengi ambayo Wilaya inaweza kuyasimamia na kuyatekeleza kwa ukaribu zaidi, hapa Chato wananchi wanajihusisha Zaidi na uuzaji wa samaki tuna soko kubwa la samaki hapa linaitwa Chato beach, wananchi wanapata chakula na pia wanauza sehemu nyingine nje ya Chato.’ Alifafanua.
Kwa upande wake Mratibu wa Programu Hiyo kutoka Ofisi ya waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Bw. Salimu Mwinjaka alisema pamoja na mambo Mengine kwa upande wa bahari kuu, Progamu hiyo inakusudia kujenga viwanda vya samaki Tanzania Zanzibar katika eneo la Fungurefu na Wilayani Kilwa Mkoani Lindi na kuweza kukabili hali ya upotevu wa mazao ya samaki baada ya kuvuna kwa kujenga vyumba vya ubaridi vya kuhifadhi mazao ya uvuvi, mitambo wa kuzalisha barafu, vichanja na mahema yakukaushia dagaa au samaki kwa kutumia mionzi ya jua.

Akiongelea kuhusu ufugaji samaki, Bw. Mwinjaka alisema kupitia progamu hiyo kuna vituo vinne ambavyo vipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambavyo ni Pamoja na vituo vya kuendeleza ukuzaji viumbemaji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani Chato, Mwamapuli Wilayani Igunga, Kingolwira Wilayani Morogoro na kituo cha Ruhila Wilayani Songea.
Akiongea katika ziara hiyo, Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi Mkomanile Mahundi alisema kituo cha Kuendeleza Ukuzaji Viumbemaji Rubambagwe kitakuwa na kazi ya kuzalisha na kusambaza vifaranga bora vya samaki aina ya sato na kambale, pamoja na kutoa mafunzo kwa wakuzaji viumbemaji katika maeneo ya mikoa ya Geita, Mwanza, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Mara.
Aliongeza kusema pia, baada ya kituo kukamilika kitakuwa na uwezo wa kuchakata chakula cha samaki ambapo itapelekea wigo wa kuongeza ajira kwa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum.
“Wizara ya Mifugo na uvuvi kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) itawezesha uwepo wa dirisha maalum katika taasisi za kifedha kama vile Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa kuwawezesha wakuzaji viumbemaji kupata mkopo yenye riba nafuu ya pembejeo na zana za ukuzaji viumbemaji.” Alisem
Ujenzi wa Kituo hicho cha Rubambagwe umefikia Asilimia 85 mpaka sasa ambapo umehusisha Jengo la utawala, karakana, nyumba za wafanyakazi jengo la kitotoleshi cha samaki, ujenzi wa mabwawa ya kufugia samaki, chanzo cha maji yaani tenki maalum la kutunza maji, kuchuja na kusafirisha maji hayo kwenda kwenye mabwawa ya kufugia samaki, kitotoleshi pamoja na maeneo mengine yanayotumia maji kituoni hapo.
xxxxx MWISHO xxxxxxxxx
ZIARA YA RAIS SAMIA YAIMARISHA USHIRIKIANO WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA KATI YA TANZANIA NA URUSI
Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesaini hati tatu za makubaliano ya ushirikiano wa kielimu na Urusi zitakazowezesha kubadilishana wataalamu, kuendeleza tafiti za pamoja na kuongeza fursa za elimu ya juu kwa wanafunzi wa nchi hizo mbili.
Akitoa taarifa hiyo kwa Waandishi wa Habari Juni 10, 2026 jijini Dodoma Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya ziara ya kihistoria nchini humo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo imeleta mafanikio katika nyanja za elimu, sayansi na teknolojia
Waziri Mkenda ametaja makubaliano yaliyofanyika ya kwanza ni kati ya Wizara ya Elimu ya Tanzania na Wizara ya Elimu ya Urusi yanayolenga kubadilishana walimu na wataalamu, kuendesha semina za pamoja na kufundisha lugha za Kiswahili na Kirusi.
Makubaliano ya pili ambayo Wizara imeingia yamehusisha Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) na Chuo Kikuu cha RUDN, ambapo wanafunzi wa kitanzania watapata fursa ya kusoma shahada ya kwanza ya Teknolojia ya Anga kupitia mfumo wa shahada pacha, wakisoma miaka miwili Tanzania na miaka miwili nchini Urusi
“Kupitia programu hii, wanafunzi watatumia mtaala wenye viwango vya kimataifa, kusoma kwa lugha ya kingereza nchini Tanzania na kujifunza lugha ya Kirusi kabla ya kuendelea na masomo yao nchini Urusi. Hatua hii itaongeza uwezo wa taifa katika sayansi, teknolojia na uhandisi.” Amesema Waziri Mkenda
Hati ya tatu ya makubaliano kati ya DIT na Chuo Kikuu cha RUDN inalenga programu za shahada ya uzamili, ambapo wanafunzi watapata nafasi ya kusoma katika nchi zote mbili na kutunukiwa shahada zinazotambulika kimataifa, huku ushirikiano huo ukifungua milango mipya ya utafiti na ubunifu.
"Chuo Kikuu cha RUDN kimeahidi kutoa ufadhili wa masomo (scholarships) kumi kwa wanafunzi wa Kitanzania. Ufadhili huu, utawawezesha Watanzania kusoma nje ya nchi kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended DS/AI+" amesema Prof Mkenda.
Mafanikio haya yanafuatia ziara ya kihistoria ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, nchini Urusi mapema mwezi huu yakilenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kielimu kati ya Tanzania na Urusi, huku akipata heshima ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima kutoka Chuo Kikuu cha RUDN, kutambua mchango wake katika uongozi na maendeleo ya kimataifa.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina (kushoto) Kamishna wa Kazi, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Suzan Mkangwa (kulia) na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda (katikati) wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Bw. Gilbert Houngbo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tempus, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tarehe 9 Juni, 2026, Geneva, Uswizi.
Na: OWM (KAM) - Geneva, Uswizi
Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeungana na mataifa mengine katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika tarehe 9 Juni, 2026 katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Geneva, Uswisi.
Aidha, ujumbe huo wa Tanzania uliongozwa na Kamishna wa Kazi, Suzan Mkangwa ambaye aliambatana na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi Zanzibar, Rashid Khamis Othman, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Wataalamu na Wawakilishi wa Waajiri (ATE) pamoja na Wawakilishi kutoka Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA).
Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), Gilbert F. Houngbo ametoa wito kwa jamii ya Kimataifa na Wadau wa Utatu kutekeleza kwa vitendo Mipango na Maadhimio ya Mkutano wa Marrakesh uliofanyika nchini Morocco, Februari 2026 kwa lengo la kupinga utumikishwaji wa Mtoto.
Vilevile, alisisitiza juu ya jitihada za makusudi zinazotakiwa kuchukuliwa na nchi wanachama wa ILO, katika kukuza kazi za staha na utekelezaji wa sera ya elimu bure.
Kwa upande wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kudhihirisha mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya kazi na ajira, hasa hatua madhubuti zilizochukuliwa katika kutokomeza ajira za watoto nchini ni kama zifuatazo:- Utekelezaji wa Mradi wa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Brazil kwa kushirikiana na ILO mradi huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa elimu kuhusu utumikishwaji wa mtoto na madhara yake.
Pia, kuhuishwa kwa Mkakati wa Taifa wa Kutokomeza Utumikishwaji wa Mtoto 2024/25–2028/29, unaolenga kuunganisha nguvu za wadau wote wa maendeleo, mashirika ya kiraia na jamii kwa ujumla. Kadhalika, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya Haki Kazini kupitia Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA). Vyombo hivi vimekuwa vikitimiza vyema wajibu wake wa kutafsiri sheria na kutoa haki, hususani ulinzi kwa mtoto; Kuadhimisha Siku ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto Kitaifa kila tarehe 12 Juni. Wadau kutoka Tanzania Bara na Zanzibar hushiriki na kupokea mikakati ya Serikali ya kukabiliana na tatizo hili; pamoja na Kutoa elimu kwa Umma kwa kuwa utumikishwaji wa mtoto ni jukumu la jamii nzima, hivyo ushirikiano baina ya Wizara, wadau wa maendeleo, kaya, na kila mwananchi unahitajika ili kufafanua tafsiri ya utumikishwaji wa mtoto, kazi za shuruti, na kazi hatarishi kwa afya na maendeleo ya mtoto.
Siku ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto uadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Juni na Shirika la Kazi Duniani (ILO) pamoja na nchi wanachama kwa lengo la kuhamasisha nguvu ya pamoja baina ya Serikali, Vyama vya Waajiri, na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi katika kukuza ajira zenye staha na kutokomeza utumikishwaji wa watoto unaowanyima fursa za kijamii, hususan haki ya elimu.
Maadhimisho hayo kwa mwaka huu 2026 yataongozwa na Kaulimbiu isemayo: “Red Card to Child Labour” ikimaanisha wito kwa wadau wote wa maendeleo kutoonesha uvumilivu wowote kwa vitendo vinavyochochea au kusababisha utumikishwaji wa mtoto katika sekta zote za kijamii na kiuchumi.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina (kushoto) Kamishna wa Kazi, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Suzan Mkangwa (kulia) na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda (katikati) wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Bw. Gilbert Houngbo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tempus, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tarehe 9 Juni, 2026, Geneva, Uswizi.

Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Bw. Gilbert Houngbo akihutubia wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Utumikishwaji wa Mtoto yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tempus, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, tarehe 9 Juni, 2026, Geneva, Uswizi.

Lakini miaka ilipita bila mabadiliko yoyote.
Wafanyakazi wengine walikuwa wakipandishwa vyeo au kuongezewa mishahara, huku mimi nikiendelea kufanya kazi kwa kiwango kilekile cha mshahara.
Kwa kweli iliniumiza sana.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua nilikuwa nikitoa mchango mkubwa kazini. Mara nyingi nilifanya kazi za ziada na kusaidia pale ambapo wengine walishindwa, lakini juhudi zangu zilionekana kama hazionekani kabisa.
Kadri muda ulivyopita, nilianza kupoteza hamasa.
Kulikuwa na siku nilijiuliza kama kulikuwa na umuhimu wa kuendelea kujituma kiasi kile. Wakati mwingine nilifikiria kutafuta kazi nyingine, lakini sikuwa na uhakika kama ningepata fursa bora zaidi.



















