Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza rasmi utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kuimarisha usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wake zinatatuliwa bila kurudi kwenye biashara holela ya mazao.

Akitoa taarifa baada ya kutembelea mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Morogoro na Iringa ikiwa ni utekelezaji wa maagizo hayo aliyoyatoa kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi hiyo Mei 19, 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema katika ziara hiyo amekutana na viongozi wa mikoa, wilaya na Kamati za Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kujionea namna mfumo huo unavyotekelezwa kwenye zao la ufuta.

“Nimeridhishwa na namna serikali za mikoa zinavyoendelea kushirikiana na WRRB katika kuhakikisha mfumo unasimamiwa vizuri. Viongozi wote tuliokutana nao wameonesha utayari mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa mfumo huu na kushughulikia changamoto zinazojitokeza,” amesema.

Amesema moja ya maelekezo makubwa yaliyotolewa na Waziri Mkuu ni kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika mfumo huo hazitumiki kama sababu ya kurejea katika biashara holela ya mazao, bali zitafutiwe ufumbuzi kwa wakati.

Kwa mujibu wa Bw. Bangu, changamoto zilizotajwa na Waziri Mkuu zinahusisha miundombinu ikiwamo ujenzi wa maghala, matengenezo ya barabara na uwepo wa mazingira bora ya kurahisisha usafirishaji wa mazao yanayopitia katika mfumo huo. Amesema WRRB imeweka mikakati mahsusi ya kuhakikisha ubora wa mazao unaimarishwa kwa kushirikiana na wakuu wa mikoa na wilaya ili bidhaa zote zinazopelekwa maghalani zikidhi viwango vinavyotakiwa.

“Tumewaelekeza waendesha maghala kuzingatia kikamilifu miongozo iliyotolewa na taasisi husika. Kwa sasa zao lililo sokoni ni ufuta na tayari miongozo ya utekelezaji imetolewa na COPRA,” amesema.

Kuhusu upungufu wa maghala, Bw. Bangu amesema tayari WRRB imeanza mazungumzo na halmashauri mbalimbali ili kuona namna ya kutumia fursa ya uwekezaji katika miundombinu ya maghala ambayo itaongeza ufanisi wa mfumo huo na kuwafikisha wakulima karibu zaidi na minada.

Kadhalika, amesema WRRB kwa kushirikiana na COPRA pia imeanza kuangalia uwezekano wa kuongeza mazao mengine kwenye mfumo ikiwamo karanga, njugu mawe na choroko ili kuongeza idadi ya wanufaika.

Akizungumzia changamoto ya mdororo wa bei, Bangu amesema wananchi wamekuwa wakilinganisha bei za sasa na zile za miaka mitatu iliyopita bila kuzingatia mabadiliko ya soko la dunia, hivyo WRRB imeendelea kutoa elimu kuhusu mwenendo wa bei katika masoko ya kimataifa.

Pia amesema baadhi ya maeneo yamekumbwa na upungufu wa uzalishaji kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na ukosefu wa mbegu bora, na kwamba WRRB imeanza mazungumzo na Jeshi la Magereza ili kutumia mashamba yake kuongeza uzalishaji wa mbegu.

“Niwahakikishie wananchi kuwa mfumo huu ni imara na tunaendelea kutatua changamoto zote zinazojitokeza. Tukishirikiana na wadau wote, tutamkomboa mkulima wa Tanzania na kuhakikisha anapata thamani halisi ya mazao yake,” alisema.



 Na. Josephine Majura, WF, Dodoma.


Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) zimekubaliana kuharakisha hatua za kukamilisha mikataba ya ufadhili wa Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Jiji la Mwanza Awamu ya Pili (LV WATSAN II), unaolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za maji safi na usafi wa mazingira kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza na maeneo jirani.

Hayo yamejiri Jijini Dodoma baada ya Kamishna Msaidizi wa Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Robert Mtengule, kwa niaba ya Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu E-maamry Mwamba, alipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) ulioongozwa na Mkuu wa Kitengo kinachoratibu Mahusiano ya Nchi na Sekta ya Umma kwa Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, Bw. Christian Elias.

Mazungumzo hayo yalitoa fursa kwa pande zote mbili kufanya tathmini ya ushirikiano uliopo na kubaini maeneo mapya ya ushirikiano yatakayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

Katika kikao hicho, pande zote zilijadili maendeleo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea nchini kupitia ufadhili wa Benki hiyo pamoja na fursa za ufadhili wa miradi mipya katika sekta za maji na usafiri, ambazo ni muhimu katika kuboresha huduma za kijamii na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Aidha, pande hizo zilijadili hatua za mwisho za kukamilisha mkataba wa ufadhili wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka wa Dar es Salaam Awamu ya Nne na Tano (BRT IV & V), unaotarajiwa kuimarisha huduma za usafiri wa umma na kupunguza changamoto za msongamano wa magari jijini Dar es Salaam.

Mbali na Sekta za Maji na Usafiri, mazungumzo hayo yaligusia maeneo mengine ya kipaumbele kwa maendeleo ya Taifa, ikiwemo miradi ya nishati,  mawasiliano na ya habari na (TEHAMA), pamoja na programu za uwezeshaji wa wajasiriamali kupitia mikopo inayotolewa EIB kwa benki za biashara hapa nchini.

Akizungumza katika kikao hicho, Kamishna Msaidizi wa Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Robert Mtengule alisema Serikali inathamini mchango wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) katika kusukuma mbele ajenda za maendeleo nchini.

“Ushirikiano huu ni muhimu katika kuharakisha utekelezaji wa miradi na programu zinazochangia maendeleo endelevu ya nchi yetu,” alisema Bw. Mtengule.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo kinachoratibu Mahusiano ya Nchi na Sekta ya Umma kwa Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB), Bw. Christian Elias, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa mapokezi mazuri pamoja na ushirikiano unaotolewa na timu ya wataalamu katika kuendeleza ajenda hizo muhimu.

“Tunatazamia kukamilisha hatua zinazofuata, ikiwemo kusainiwa kwa mikataba ya ufadhili ya miradi ya BRT IV & V na LV WATSAN na kuanza utekelezaji wa miradi hiyo,” alisema Bw. Elias.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Bajeti, Bi. Vicky Jengo; Kaimu Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Madeni, Bw. Mulesi Manyama; Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya, Bw. Jonathan Mpuya; pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Fedha na Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB).
Nilipoamua kugombea kiti cha uongozi katika eneo letu, nilijua ushindani ungekuwa mkali.

Wapinzani wangu walikuwa na majina makubwa, walifahamika na watu wengi, na walionekana kuwa na ushawishi mkubwa zaidi kuliko mimi. Kadri kampeni zilivyoendelea, ilionekana wazi kwamba walikuwa wakivutia umati mkubwa kila walipofanya mikutano yao.

Hali hiyo ilianza kunipa wasiwasi. Ingawa nilikuwa nikifanya kila niwezalo kuwafikia wananchi, bado nilihisi kama nilikuwa nyuma. Kila niliposikia watu wakizungumza kuhusu uchaguzi, mara nyingi walikuwa wakiwataja wapinzani wangu kama washindi watarajiwa.
Baadhi ya wafuasi wangu walikata tamaa.

Wengine walinieleza wazi kwamba ushindi ungekuwa mgumu sana. Kadri siku za uchaguzi zilivyokuwa zikisogea, presha ilizidi kuongezeka.
Nilijitahidi kubaki imara. Niliendelea kuzunguka katika vijiji na mitaa mbalimbali nikisikiliza wananchi na kueleza mipango yangu.

Hata hivyo, ukweli ni kwamba sikuwa na uhakika kama juhudi zangu zingetosha kubadilisha hali iliyokuwa imejitokeza. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa za kujenga kampuni ambayo ingenipa uhuru wa kifedha na kusaidia familia yangu. Kwa miaka ya mwanzo, mambo yalikuwa yanaenda vizuri. Wateja walikuwa wengi, mauzo yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu siku zijazo.

Lakini hali ilibadilika ghafla.

Mauzo yalianza kushuka mwezi baada ya mwezi. Wateja ambao walikuwa waaminifu kwa biashara yangu walianza kupungua, na baadhi yao walihamia kwa washindani wangu. Nilijaribu kupunguza bei za bidhaa na kuanzisha ofa mbalimbali, lakini matokeo hayakuwa yale niliyotarajia.

Hasara zilianza kuongezeka. Kila mwisho wa mwezi nilikuwa nikiangalia hesabu za biashara na kuona fedha zikizidi kupungua. Baadhi ya wafanyakazi walihofia kuhusu mustakabali wa biashara hiyo, na hata mimi mwenyewe nilianza kujiuliza kama ningelazimika kuifunga.
Usiku mwingi nilikosa usingizi.

Nilikuwa nikifikiria jinsi ya kulipa madeni, kuhifadhi biashara, na kuhakikisha familia yangu haipati matatizo kutokana na hali hiyo. Kadri muda ulivyopita, presha iliongezeka zaidi.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, ndoa yangu ilikuwa mfano wa furaha kwa watu wengi waliotuzunguka. Mimi na mume wangu tulielewana vizuri na tulijitahidi kujenga familia yenye upendo na heshima. 

Hata hivyo, mambo yalianza kubadilika taratibu. Migogoro iliongezeka, mawasiliano yakapungua, na kila mmoja wetu alianza kuishi kama mtu anayejitegemea badala ya mwenzi wa maisha.

Kadri miezi ilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.
Tulikuwa tunazungumza kwa shida na wakati mwingine siku ziliweza kupita bila kuwa na mazungumzo ya maana. Watu wa karibu nasi walianza kugundua kwamba kulikuwa na tatizo kubwa ndani ya ndoa yetu.

Baadhi yao walikuwa tayari wamekata tamaa.
Kulikuwa na uvumi kwamba talaka ilikuwa karibu na kwamba ndoa yetu isingeweza kuokolewa. Hata mimi mwenyewe nilianza kujiuliza kama kweli kulikuwa na njia ya kurekebisha mambo. Maumivu hayo yaliniathiri sana.

Nilihisi kama nilikuwa napoteza mtu ambaye nilikuwa nimempenda na kushirikiana naye kwa miaka mingi. Nilijaribu njia mbalimbali za kutatua tofauti zetu lakini kila nilipoona matumaini, changamoto nyingine ilijitokeza. SOMA ZAIDI.

Baada ya kuhitimu masomo yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kupata kazi nzuri na kuanza kujitegemea. 

Nilituma maombi kwa kampuni nyingi, mashirika mbalimbali, na hata biashara ndogo ndogo zilizokuwa zinatafuta wafanyakazi. Kila nilipoitwa kwenye usaili, nilijiambia kwamba safari hii ndiyo nafasi yangu ya mwisho ya kubadilisha maisha.

Lakini majibu yalikuwa yale yale. Mara kwa mara nilipokea ujumbe wa kukataliwa. Wakati mwingine nilifika hatua za mwisho za usaili na kuambiwa nisubiri majibu, lakini siku zote nafasi hiyo ilipewa mtu mwingine. Miaka mitatu ilipita katika hali hiyo.

Akiba yangu ilianza kuisha na nilianza kutegemea msaada wa familia katika baadhi ya mahitaji yangu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu niliomaliza nao shule wakipiga hatua kubwa maishani huku mimi nikibaki sehemu ileile. Nilianza kukata tamaa. SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningesimama mahakamani nikitetea uhuru wangu kwa kosa ambalo sikuwa nimelifanya.

Maisha yangu yalikuwa ya kawaida hadi pale tukio moja lilipotokea na jina langu kuhusishwa nalo. Ghafla nilijikuta nikitajwa katika uchunguzi wa kesi iliyokuwa imezua mjadala mkubwa katika eneo letu.

Mwanzoni niliamini ukweli ungejitetea wenyewe. Lakini kadri uchunguzi ulivyoendelea, hali ilianza kuwa mbaya zaidi. Baadhi ya ushahidi ulionekana kunielekezea mimi. Watu ambao walikuwa wakinifahamu walianza kunitazama tofauti, na hata baadhi ya marafiki walijitenga nami. Familia yangu iliteseka sana.

Kila siku tulikuwa tunaishi kwa hofu ya kile ambacho kingetokea baadaye. Nilijua moyoni kwamba sikuwa na hatia, lakini kadri kesi ilivyokuwa ikiendelea, matumaini yangu yalikuwa yakipungua. Hatimaye siku ya kusikilizwa kwa kesi ilifika.

Nilikaa mahakamani nikisubiri uamuzi ambao ungeweza kubadilisha maisha yangu milele. Dakika zilionekana kusonga polepole huku mawazo mengi yakipita akilini mwangu.SOMA ZAIDI.

 


📌Washiriki Nishati Safi expo wafurahishwa na miradi ya REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeshiriki Maonesho na Kongamano la Nishati Safi expo 2026 yanayofanyika katika ukumbi wa Ubungo EACLC jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba. 

Akizungumza katika kongamano hilo leo Juni 24, 2026, Msimamizi wa miradi ya REA, Mha. Francis Manyama amesema kuwa, upatikanaji wa umeme vijijini umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza matumizi ya nishati zinazochafua mazingira na kuongeza matumizi ya nishati safi.

Ameongeza kuwa, miradi ya usambazaji wa umeme vijijini imewezesha wananchi kuachana na matumizi ya majenereta na vyanzo vingine vya nishati vinavyotumia mafuta, hali inayosaidia kupunguza uzalishaji wa hewa chafuzi.

Halikadhalika, REA inaendelea na mradi wa kufunga mifumo ya umeme jua katika visiwa mbalimbali nchini, ambapo mifumo 20,000 inatarajiwa kufungwa ili kuongeza upatikanaji wa nishati safi katika maeneo yasiyofikika kirahisi na gridi ya taifa.

Mbali na hilo, amesema wakala unasaidia wazalishaji wadogo wa umeme wanaotumia maporomoko ya maji ili kuongeza matumizi ya nishati jadidifu na kupunguza utegemezi wa vyanzo vya nishati vinavyoharibu mazingira.

Katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, REA inaendelea kufunga miundombinu ya majiko ya kisasa katika taasisi mbalimbali za umma na binafsi zikiwemo shule, vyuo na taasisi za huduma za jamii.

Amesema katika awamu ya kwanza, pili na tatu za utekelezaji wa mradi huo, taasisi 454 zinazohudumia zaidi ya watu 100 zitafikiwa na miundombinu hiyo ambayo inafungwa bila gharama kwa taasisi husika.

Aidha, amesema REA inatoa ruzuku ya asilimia 50 kwa mitungi ya gesi ya kilo sita pamoja na ruzuku ya asilimia 80 hadi 85 kwa majiko banifu ili kuwezesha wananchi wa vijijini kupata nishati safi kwa gharama nafuu.

Mha. Manyama amesema wakala umefunga mifumo ya nishati safi ya kupikia katika magereza nchini na kambi 22 za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) zilizopo katika mikoa 14, hatua inayochangia kupunguza matumizi ya kuni na mkaa pamoja na kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.











 


Aelekeza kijana mlemavu Joseph kupewa ajira ya kudumu


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemuelekeza Katibu Mkuu - UTUMISHI Bw. Juma Selemani Mkomi kufanya tathmini ya kubaini Maafisa Utumishi waliozembea kukamilisha mchakato wa Watumishi wa Umma kupandishwa madaraja kwa mwaka wa fedha 2025/26 na kuwachukulia hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria, Taratibu, Kanuni na  Miongozo ya Utumishi wa Umma. 

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Juni 23, 2026 kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka, wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

“Kuna Maafisa Utumishi kwa uzembe wamesababisha watumishi kutopandishwa madaraja mwaka 2025/26, Katibu Mkuu UTUMISHI kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi nakuelekeza kufanya tathmini ya kubaini maafisa waliokwamisha upandishaji wa madaraja na kuchukua hatua ya kuwaondoa katika nafasi zao,” amesisitiza Prof. Shemdoe. 

Prof. Shemdoe amewataka Wakuu wa Taasisi za Umma na Maafisa Utumishi nchini kushughulikia kwa wakati kero na malalamiko ya watumishi wanaowaongoza, kwani nafasi walizonazo ni kwa ajili ya kuwatumikia watumishi hao ili nao waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

Pia, Prof. Shemdoe amemuelekeza Katibu Mkuu UTUMISHI kumpatia ajira ya kudumu kijana mlemavu aliyemkuta kwenye banda la VETA ambaye hana mikono lakini ana ujuzi wa kusanifu majengo na samani kwa kutumia miguu yake kupitia kompyuta mpakato.

Aidha, Prof. Shemdoe kwa niaba ya watumishi wa umma nchini amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapandisha madaraja watumishi wa umma, kulipa madai ya muda mrefu ya watumishi wa umma, ikiwa ni pamoja na kuajiri watumishi wengi wa kada mbalimbali wakiwemo walimu na wa sekta ya afya.  

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amezipongeza taasisi za kifedha zikiwemo CRDB, NMB, AZANIA, NBC na nyinginezo zilizoshiriki maonesho ya Wiki ya Wiki ya Utumishi wa Umma kutokana na kuhitajika kwa taasisi hizo kwa watumishi wa umma, ambako kunawapa wigo watumishi kuchagua benki wanayoona inafaa kuchukua mkopo wa kuwezesha shughuli zao binafsi za kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Selemani Mkomi amesema kupitia maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu, wananchi wamepata huduma za moja kwa moja kutoka katika taasisi za umma na kuongeza kuwa, taasisi za umma zimepata fursa ya kubadilishana uzoefu kiutendaji ikiwa ni pamoja na kuiwezesha Serikali kupata mrejesho utakaoiwezesha kuborsha utoaji wa huduma.

Katika maadhimisho ya mwaka huu, jumla ya Taasisi za Umma 226 zimetoa elimu na huduma mbalimbali kwa watumishi wa umma na wananchi ikiwemo matumizi ya mifumo ya utoaji wa huduma katika Utumishi wa Umma, hati za viwanja, vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho vya taifa na huduma za kitabibu za kibingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Benjamini Mkapa, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Taasisi ya Mifupa (MOI) na Hospitali ya Bugando.











Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) imeendelea kuimarisha kampeni ya utoaji elimu kwa umma kuhusu madhara ya biashara ya bidhaa bandia, ikisisitiza kuwa utengenezaji, usambazaji na uuzaji wa bidhaa hizo ni kosa la jinai linaloadhibiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Akizungumza leo Juni 22, 2026, katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema bidhaa bandia zina athari kubwa kwa uchumi, afya na usalama wa wananchi, huku zikidhoofisha ushindani wa haki katika biashara.

Amesema watu watakaobainika kujihusisha na biashara ya bidhaa bandia wanaweza kukabiliwa na adhabu ya kifungo cha kati ya miaka minne hadi 15 jela pamoja na faini inayofikia kati ya Shilingi milioni 10 na milioni 50, kulingana na masharti ya sheria husika.

Bi. Feruzi ameeleza kuwa FCC inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za ndani na kimataifa katika kudhibiti bidhaa bandia ili kuhakikisha haziingii nchini, hazisambazwi katika soko la ndani, wala kutumiwa kama njia ya kupitishwa kwenda mataifa mengine kupitia mifumo ya usafirishaji.

Amebainisha kuwa nafasi ya Tanzania kama lango muhimu la biashara na usafirishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki inaifanya nchi kuwa miongoni mwa maeneo yanayoweza kutumiwa na wahalifu kusafirisha bidhaa bandia, hali inayohitaji ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi na wananchi katika kupambana na tatizo hilo.

Kwa mujibu wa Bi. Feruzi, biashara ya bidhaa bandia si changamoto ya Tanzania pekee, bali ni tatizo la kimataifa linalosababishwa na watu wasio waaminifu wanaotafuta faida kwa kutumia kazi, ubunifu na alama za biashara za wengine kinyume cha sheria.

Ametoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara kuwa makini wanaponunua au kuuza bidhaa, huku akiwahimiza kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini uwepo wa bidhaa zinazohisiwa kuwa bandia.

Vilevile, amesema Tanzania itaadhimisha Siku ya Kitaifa ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Juni 25, 2026, yakiwa na  kauli mbiu isemayo: "Linda Maisha na Masoko Dhidi ya Pombe, Vilainishi na Sigara Bandia" ambapo maadhimisho hayo yatatumika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu athari za bidhaa bandia na kuimarisha juhudi za kitaifa na kimataifa za kupambana na biashara hiyo haramu.

Amesisitiza kuwa mafanikio ya vita dhidi ya bidhaa bandia yanategemea ushirikiano wa wadau wote, ikiwemo Serikali, wafanyabiashara , wazalishaji na wananchi, ili kulinda uchumi wa taifa, afya za watumiaji na mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki.



Na Benny Mwaipaja, Dodoma

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limepitisha kwa kishindo Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2026/27 kwa asilimia 97.66 baada ya wabunge 385 kupiga kura ya ndio kuunga mkono Bajeti hiyo.

Akitangaza matokeo ya kura ya wazi iliyopigwa bungeni jijini Dodoma, Spika wa Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu alisema kuwa kati ya kura hizo 393 zilizopigwa, kura 8 zimekataa kuunga mkono bajeti hiyo na wabunge wengine nane 8 hawakupiga kura kwa sababu hawakuwepo bungeni.

Akihitimisha hoja baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Sheria kwa ajili ya kuidhinisha Serikali kuanza kutekeleza Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2026/2026 (zaidi ya shilingi trlilioni 62.33) kutoka katika Mfuko Mkuu wa Hazina, Mhe. Spika Zungu alimpongeza Waziri wa Fedha, Mhe. Ballozi Khamis Mussa Omar (Mb) wasaidizi wake, watendaji wa Wizara kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya na Wabunge wote kwa michango yao yenye tija kwa Taifa.

“Kura zimepigwa na Serikali imeruhusiwa kuzitumia pesa kuanzia sasa, mkazitumie pesa hizi kama Kamati za Bunge zilivyoelekeza, kuhakikisha maslahi ya watu kwanza yanazingatiwa kabla ya mambo mengine. Bunge hili litaendelea kufuatilia utekelezaji wake na kuhakikisha kuwa miradi yote iliyoainishwa inazingatiwa na kuleta furaha kwa wananchi” alisisitiza Mhe. Zungu.

Kupitia kwa Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), Serikali ililiomba Bunge lipitishe Bajeti ya shilingi trilioni 62.33 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo katika Mwaka wa Fedha 2026/2027, ikiwa ni ongezeko la asilimia 10.3 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2025/26. 

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, mapato yalitarajiwa kuwa shilingi trilioni 46.79 ambapo mapato ya kodi ni shilingi trilioni 36.99, mapato mengine ni shilingi trilioni 9.24 (ikijumuisha mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 1.977) na misaada kutoka kwa washirika wa maendeleo shilingi bilioni 563.1.

Aidha aliongeza kuwa ili kuendana na dhamira ya kujitegemea katika uendeshaji wa Serikali na maendeleo, takribani robo tatu ya bajeti yote ya mwaka 2026/27, sawa na asilimia 74.2 itagharamiwa na mapato ya ndani.

Matumizi na uwekezaji katika mali zisizo za kifedha yalikadiriwa kuwa shilingi trilioni 54.50 pasipo kujumuisha malipo ya mtaji wa deni la Serikali ambapo kati ya kiasi hicho, stahiki za watumishi ikijumuisha michango ya pensheni ni shilingi trilioni 10.13.

“Gharama za bidhaa na huduma itakuwa shilingi trilioni 5.22, malipo ya riba ni shilingi trilioni 6.86, ruzuku shilingi trilioni 25.32, mafao na misaada ya kijamii shilingi trilioni 1.01, uwekezaji katika mali zisizo za kifedha shilingi trilioni 2.33 na gharama nyingine shilingi trilioni 3.63.” alisema Mhe. Balozi Omar

Aliongeza kuwa kulingana na makadirio ya mapato na matumizi hayo, kunajitokeza nakisi kwenye bajeti ya shilingi trilioni 7.71 na Serikali itaendelea kugharamia nakisi ya bajeti hiyo kwa kutumia mikopo kutoka vyanzo vya ndani na nje kwa kuzingatia Mkakati wa Muda wa Kati wa Kusimamia Deni la Serikali (2025/26 – 2027/28).

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, katika mwaka 2026/27, Serikali inatarajia kukopa jumla ya shilingi trilioni 15.54 ambapo kati ya kiasi hicho, mikopo ya ndani itakuwa shilingi trilioni 6.56, mikopo ya nje yenye masharti nafuu shilingi trilioni 6.55 na mikopo ya nje yenye masharti ya kibiashara shilingi trilioni 2.43.
Aidha, Serikali inakadiria kulipa malipo ya mtaji kwa mikopo iliyoiva shilingi trilioni 7.84.

Baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo, Bunge linatarajia kupokea, kujadili na kupitisha Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2026 ( The Finance Bill,2026) tarehe 24 Juni, 2026

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu haki na wajibu wao katika sekta za nishati na maji, sambamba na kuhamasisha uwekezaji wa vituo vya mafuta vijijini ili kuongeza upatikanaji wa huduma salama na kukomesha biashara holela ya mafuta.

Hatua hiyo ni sehemu ya mafanikio ya ushiriki wa EWURA katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma, ambapo maelfu ya wananchi wamefika katika banda la mamlaka hiyo kupata elimu na ufafanuzi kuhusu huduma mbalimbali zinazodhibitiwa na EWURA.

Akizungumza katika maonesho hayo, Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Wilfred Mwakalosi, amesema kwa siku nane mfululizo mamlaka hiyo imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusu sekta za mafuta, umeme, gesi asilia na maji, pamoja na kupokea na kushughulikia maswali na changamoto mbalimbali zinazowakabili watumiaji wa huduma hizo.

Amesema wananchi wengi walitumia fursa hiyo kupata ufahamu kuhusu namna ya kuwasilisha malalamiko wanapokumbana na changamoto za huduma, huku mada ya uwekezaji katika vituo vya mafuta vijijini ikiwa miongoni mwa masuala yaliyoibua maswali mengi zaidi.

“Wananchi wengi walitaka kufahamu taratibu na fursa zilizopo za kuanzisha vituo vya kisasa vya mafuta vijijini ili kuondokana na biashara ya mafuta inayofanyika kwa kutumia chupa, ndoo na magaloni, ambayo mara nyingi huhatarisha usalama wa watu na mali,” amesema Mwakalosi.

Ameeleza kuwa Serikali kupitia EWURA imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji kwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za vibali na leseni kwa wawekezaji wa vituo vya mafuta vijijini.

Kwa mujibu wa EWURA, ada ya kibali cha ujenzi wa kituo cha mafuta katika maeneo ya vijijini imepunguzwa kutoka Shilingi 500,000 zinazotozwa maeneo ya mijini hadi Shilingi 50,000, huku ada ya leseni ikishushwa kutoka Shilingi milioni moja hadi Shilingi 100,000.

Mbali na punguzo hilo, EWURA imepunguza baadhi ya masharti ya uwekezaji kwa kuruhusu matumizi ya nyaraka za uthibitisho wa umiliki wa ardhi zinazotolewa na serikali za vijiji badala ya hati kamili za ardhi zinazohitajika katika maeneo ya mijini.

Hatua hiyo inalenga kuvutia wawekezaji wengi zaidi katika maeneo ya vijijini na kuongeza upatikanaji wa mafuta kwa njia salama, nafuu na inayozingatia viwango vya usalama.

Katika maonesho hayo, wananchi pia walipata ufafanuzi kuhusu namna EWURA inavyosimamia ukokotoaji wa bei za mafuta, viwango vya huduma za maji na umeme, pamoja na taratibu za kuwasilisha malalamiko pale wanaporidhika au kutoridhika na huduma zinazotolewa na watoa huduma.

Aidha, Mwakalosi amewahimiza wananchi kusoma na kuelewa mikataba ya huduma kwa wateja inayotolewa na taasisi za maji, umeme na nishati, akieleza kuwa mikataba hiyo inaainisha kwa uwazi haki, wajibu na viwango vya huduma vinavyopaswa kutolewa kwa mteja.

Amesisitiza kuwa wananchi wenye uelewa wa mikataba hiyo wanakuwa na uwezo mkubwa wa kudai huduma bora, kufuatilia utekelezaji wa haki zao na hata kudai fidia pale ambapo watoa huduma watashindwa kutekeleza viwango walivyoahidi.

Vilevile, EWURA imewahakikishia wananchi kuwa nchi inaendelea kuwa na hali nzuri ya upatikanaji wa umeme, gesi na maji kutokana na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa na Serikali katika sekta hizo.

Mwakalosi ametaja ongezeko la uzalishaji wa umeme kupitia Bwawa la Mwalimu Nyerere kuwa miongoni mwa hatua zilizochangia kuimarika kwa huduma za nishati nchini, huku EWURA ikiendelea kusimamia upatikanaji endelevu wa huduma za maji na nishati kwa manufaa ya wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.