Na. Mwandishi Wetu
TUME ya Ushindani (FCC) imeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wajasiriamali kutoka Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kuhusu namna ya kutambua bidhaa bandia, kulinda haki za walaji na biashara ili kuimarisha ushindani wa haki nchini.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema maonesho hayo yameiwezesha tume hiyo kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa kuwapa elimu kuhusu haki za walaji, ulinzi wa biashara pamoja na huduma mbalimbali zinazotolewa na FCC.
"FCC inaendelea kupokea na kushughulikia malalamiko ya wananchi, kusajili mikataba na kutoa huduma nyingine zinazolenga kulinda maslahi ya walaji na wafanyabiashara."amesema
Aidha FCC imewahimiza wananchi na wafanyabiashara kuendelea kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu, kuripoti bidhaa bandia na ukiukwaji wa haki za biashara ili kujenga mazingira ya ushindani wa haki na kulinda maslahi ya walaji nchini.
Kwa upande wake Afisa Ushirikiano wa TWCC, Bw. Nelson Clevary, ameipongeza na kuishikuru FCC kwa mafunzo hayo, akisema yamewasaidia wajasiriamali kutambua bidhaa bandia, kulinda bidhaa zao na kuelewa umuhimu wa kusajili majina na nembo za biashara.
Amesema ushirikiano wa miaka mitatu kati ya TWCC na FCC umeongeza uelewa wa wafanyabiashara kuhusu athari za bidhaa bandia na umuhimu wa kushirikiana na mamlaka husika katika kukabiliana na vitendo vya udanganyifu wa kibiashara.
Naye mjasiriamali kutoka Mwanza, Praxeda Mgyabuso, amesema elimu inayotolewa na FCC imewasaidia wafanyabiashara na wananchi kutofautisha bidhaa halisi na bandia pamoja na kuelewa umuhimu wa kulinda utambulisho wa biashara zao.
Amesema awali wengi walikuwa wakinunua bidhaa kwa kuangalia bei pekee, lakini sasa wanafahamu athari za bidhaa bandia kwa afya, uchumi na biashara, pamoja na umuhimu wa kusajili alama na nembo za biashara.

Timu ya mpira wa miguu ya Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Sports Club imefanikiwa kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Championship msimu ujao 2026/2027 baada ya kufuzu kwa kupata sare ya goli 1-1 dhidi ya klabu ya African Sports kutoka Mkoani Tanga
Akizungumza baada ya kutamatika kwa mchezo Kocha Mkuu wa IAA SC Zulkifri Iddi amewapongeza wachezaji wake kwa kuipatia timu matokeo na kuthibitisha kuwa walifanikiwa kufuata maelekezo aliyowapa ndani ya dakika zote tisini, huku akiupongeza Uongozi wa Chuo IAA kwa sapoti kubwa walioitoa iliyopelekea kuandika historia hii kubwa kwa taasisi na jiji la Arusha
Akitoa pongezi Mwenyekiti wa mashindano chama cha soka Mkoa wa Arusha Emmanuel Antony ameisifu IAA SC kwa kuandika historia hii kubwa na kukiheshimisha chama cha soka Mkoa wa Arusha na kuahidi ushirikiano kwa timu kuhakikisha inafanya vizuri na kupiga hatua zaidi ili kufika hatua ya kushiriki Ligi kuu ya Tanzania
Kwa upande wake mchezaji wa IAA SC ambaye ndiye Mfungaji wa goli pekee la timu amewapongeza wachezaji wenzake, benchi la ufundi na Uongozi wa Chuo pamoja na mashabiki wao kwa kushirikiana kufanikisha kufikia mafanikio haya makubwa na kuahidi kuendelea kuipambania nembo ya IAA na jiji la Arusha msimu ujao kwenye mashindano ya Championship
IAA SC katika safari yake ya mafanikio haya ilifanikiwa kuibuka washindi wa ligi ya Wilaya ya Arusha, Ligi ya Mkoa, Ligi ya mabingwa wa Mikoa yote Tanzania na baadae Ligi daraja la pili (First League) na leo imefanikiwa kufuzu kutinga katika ligi daraja la kwanza (Championship) msimu wa mwaka 2026/2027

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika jengo la Kituo cha Polisi cha Kata ya Masasi, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.
Jengo hilo limejengwa na Bw. Iman Haule kupitia KUAMBIANA INVESTMENT COMPANY LIMITED ikiwa ni sehemu ya mchango wa sekta binafsi katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya usalama na kusogeza huduma za kipolisi karibu na wananchi.
Mhe. Naibu Waziri Mahundi amepongeza hatua hiyo, akieleza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya usalama unachangia kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao, kuongeza upatikanaji wa haki na kuleta mazingira wezeshi kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Wataalamu waanza kuwanoa wanafunzi, walimu na maafisa elimu kukabiliana na matokeo duni ya mitihani

Na Oscar Assenga, Tanga
MATOKEO duni ya mitihani ya Taifa katika baadhi ya shule za sekondari za Serikali jijini Tanga yameibua hatua mpya za kuwanufaisha wanafunzi kupitia mafunzo maalumu yanayolenga kuongeza ufaulu kwa kuwajengea uwezo wa kujifunza kwa ufanisi na kujiandaa vizuri kwa mitihani.
Mafunzo hayo yanatekelezwa na Taasisi ya Tanzania Centre for Education (TCE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Botnar foundation na Inovex kupitia mradi wa Tanga Yetu, unaohusisha shule 10 zilizobainika kuwa na changamoto ya matokeo hafifu kwa wanafunzi.
Akizungumza wakati wa kuanza kwa mafunzo hayo katika Shule ya Sekondari Nguvumali, Mkurugenzi Mtendaji wa TCE, Yusuf Ogutu, alisema kuboresha ufaulu ni hatua muhimu ya kuinua ubora wa elimu na kuwawezesha wanafunzi kufikia ndoto zao za kitaaluma na maisha ya baadae.

Alisema wanafunzi wengi hufanya mitihani bila kuelewa kwa kina mfumo wa maswali ya umahiri, uzito wa mada na mbinu sahihi za kujibu, hali inayochangia kushuka kwa matokeo licha ya kufundishwa darasani.
"Ndiyo maana tumeamua kuja na mafunzo haya ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa kuelewa, badala ya kukariri. Tunawafundisha namna ya kuchambua muhtasari wa masomo, kutambua mada zinazotiliwa mkazo katika mitihani na kuelewa matumizi ya vitenzi vinavyotumika katika maswali," alisema.
Aliongeza kuwa wanafunzi pia wanapatiwa mbinu za kupanga muda wa kujisomea, namna ya kujiandaa kabla,wakati na baada ya mtihani, jinsi ya kujibu maswali kwa ufanisi na namna ya kujitathmini baada ya kufanya mtihani.
Ogutu alisema mafanikio ya wanafunzi hayawezi kupatikana kwa juhudi za mwanafunzi pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa walimu, wazazi, viongozi wa elimu na wadau wa maendeleo.

"Tunataka kujenga utamaduni wa ufaulu. Mwanafunzi akielewa namna ya kujifunza na mwalimu akapata mbinu bora za kumwelekeza, matokeo mazuri yatapatikana," alisema.
Mbali na mafunzo hayo, alisema taasisi hiyo imeanza kufanya utafiti katika shule zote 27 za sekondari za Serikali za Jiji la Tanga ili kubaini sababu zinazochangia kushuka kwa ufaulu katika mitihani ya Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.
Alisema matokeo ya utafiti huo yatawezesha wadau wa elimu kuweka mikakati ya muda mrefu ya kuboresha ubora wa elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule za Serikali.

Kwa upande wake, Mratibu wa Elimu Kata ya Nguvumali, Lilian Shetua, alisema mafunzo hayo yanawasaidia wanafunzi kuendana na mahitaji ya mtaala ulioboreshwa unaowataka kuwa wabunifu, wachambuzi na wenye uwezo wa kutumia maarifa katika kutatua changamoto.
Alisema wanafunzi wengi wamekuwa wakifanya mitihani bila kuelewa muundo wake, lakini kupitia mafunzo hayo wanapata uelewa wa namna ya kujiandaa na kujibu maswali kwa kuzingatia matakwa ya Baraza la Mitihani.
"Ni matarajio yetu kwamba elimu hii itabadilisha mtazamo wa wanafunzi na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule yetu na nyingine zinazoshiriki mradi huu," alisema.

Naye Inspekta wa Polisi wa Kata ya Nguvumali, Sharifu Kiswamba, alisema pamoja na jitihada za kuboresha elimu, bado utoro wa wanafunzi na tabia ya kuzurura mitaani wakati wa masomo vinaendelea kuwa kikwazo kikubwa.
Aliwataka wazazi kuongeza usimamizi wa watoto wao na kushirikiana na walimu pamoja na viongozi wa kata ili kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria masomo na kutumia muda wao kujifunza.

Kwa upande wake, mwalimu wa Shule ya Sekondari Nguvumali, Venosa Massawe, alisema mafunzo hayo yamekuja wakati mwafaka kwani yanawasaidia walimu na wanafunzi kutafsiri kwa usahihi matakwa ya mtaala ulioboreshwa.

Hata hivyo, alisema mazingira magumu ya maisha ya baadhi ya wanafunzi, ikiwamo umaskini, malezi yasiyo ya karibu na changamoto za lishe, bado ni miongoni mwa sababu zinazochangia kushuka kwa kiwango cha ufaulu.

Alisema ushirikiano wa Serikali, wazazi, walimu na wadau wa maendeleo utaendelea kuwa nguzo muhimu katika kujenga mazingira bora ya kujifunza na kuongeza idadi ya wanafunzi wanaofaulu kwa viwango vya juu katika mitihani ya taifa.



Maisha yanaweza kuwa katili sana, hasa unapoona wadogo zako uliowasomesha wanakupita kimaendeleo wakati wewe umeshikilia karatasi za chuo zinazoliwa na mchwa. Mimi naitwa Mariam, mzaliwa wa Ilemela, jijini Mwanza.
Nilihitimu shahada yangu ya Uhasibu (Accounting) kwa kiwango cha juu, lakini mtaani niligeuka kuwa mtu wa dharau. Nilifikia hatua ya kukaa pembeni ya barabara nikisaidia mama yangu mdogo kushona viatu vya kimasai ili tu nipate mlo wa mchana.
Kila usaili niliokwenda, nilikuwa naonekana sifai, au nafasi inachukuliwa na mtu mwenye kujuana na wakubwa. Umri wangu wa kuelekea miaka 30 ulinifanya nikose amani; kila ndugu aliyeniona aliniuliza “Lini unaolewa?” au “Kazi mbona hupati?”. SOMA ZAIDI.
Kila asubuhi nilikuwa nawasha redio kubwa dukani kwangu ili kuvutia wateja, lakini watu walikuwa wakipita na kusikiliza muziki tu kisha wanaenda kununua kwa jirani yangu ambaye duka lake lilikuwa dogo na chafu.
Hali hii ilinitesa sana kisaikolojia. Nilianza kuonekana mwanaume niliyefeli mbele ya mke wangu na ndugu zangu, kwani kila mwezi nilikuwa nakopa pesa ya kulipa kodi ya pango. Nilihisi nina nuksi ya ajabu inayowafukuza watu wenye pesa na kuvuta watazamaji tu.
Nilijaribu kila mbinu; nilishusha bei hadi ya hasara, nilifanya matangazo kwa gari la spika mitaani, na hata kutoa zawadi kwa kila aliyenunua bidhaa, lakini wapi! Duka langu lilikuwa kama limepakwa dawa ya kufukuza watu. Nilikaribia kukata tamaa na kuuza kila kitu nikawe kondakta wa daladala.
Siku moja nilisafiri kwenda kijijini kwetu kwa ajili ya mazishi ya ndugu. Nikiwa nimekaa na wazee wa busara chini ya mwembe, tulianza kuzungumzia changamoto za kimaisha mjini. Mzee mmoja ambaye alikuwa ni rafiki wa marehemu, alinifuata pembeni na kuniambia, “Erick, kijana wangu, unahangaika bure na mbinu za kizungu. SOMA ZAIDI.

























