-Magereza 12 Morogoro Yanufaika na Mradi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka REA     

Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro limeendelea kuhamasishwa matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya Mkakati wa Serikali kuhakikisha Asilimia 80 ya wanatumia wahamie kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya nishati safi ya kupikia kwa Jeshi la Magereza mkoani Morogoro, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu amesema kuwa lengo la taifa la kufikia matumizi makubwa ya nishati safi ya kupikia linawezekana kutokana na uwepo wa vyanzo mbalimbali vya nishati hiyo.

Amesema wananchi wana nafasi ya kuchagua aina ya nishati safi kulingana na mazingira wanayoishi, ikiwemo gesi, mkaa mbadala pamoja na matumizi ya umeme kwa ajili ya kupikia.

“Inawezekana ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi za kupikia maana zipo nyingi" amesema Mwenyekiti Kingu.

Aidha, ameeleza kuwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kupeleka huduma ya umeme katika Vijiji na Vitongoji jambo litakalowezesha wananchi wengi zaidi kutumia umeme kama chanzo cha nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Peter Anatory amesema mradi wa majiko ya nishati safi ya kupikia unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewezesha magereza 12 ya Mkoa wa Morogoro kunufaika na huduma hiyo.

Amesema kupitia mradi huo, magereza hayo yamepata majiko 15 yanayotumia mkaa rafiki kwa mazingira pamoja na tani 236 za mkaa huo, hali iliyosaidia kuongeza matumizi ya nishati safi katika taasisi za magereza.

“Mradi huu umekuwa kichocheo kikubwa kwa magereza katika kuhakikisha tunatumia nishati safi ya kupikia,” amesema Anatory.

Naye Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Samuel Aron Mwakatika amesema matumizi ya nishati safi yana mchango mkubwa katika kuboresha maisha ya wananchi, kulinda mazingira pamoja na kukuza uchumi wa taifa.

Amesema katika Chuo cha Udereva KPF Kingolwira, matumizi ya nishati safi yamesaidia kuokoa muda uliokuwa unapotea kwa wanafunzi kwenda kutafuta kuni.

“Katika chuo hiki tuna wanafunzi 381, hivyo zamani ilikuwa lazima kuwe na kundi la wanafunzi wanaokwenda kutafuta kuni jambo lililokuwa linapunguza muda wa kujifunza. Nishati safi imesaidia kuondoa changamoto hiyo,” amesema Mwakatika.

Aidha, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza (SSP), Nicostatus Magori amesema gereza hilo liliacha kutumia kuni kwa ajili ya kupikia chakula cha wafungwa tangu Desemba mwaka 2024 baada ya kuanza kutekelezwa kwa mradi huo wa kufungiwa mifumo ya nishati safi ya kupikia katika magereza. 





 

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unatarajia kujenga kiwanda kipya na uwekaji mitambo ya kisasa kwa ajili ya kuchakata mazao ya nyuki ili kuwezesha kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi la asali.

Kiwanda hicho kipya kitajengwa wilayani Manyoni, Mkoa wa  Singida ambako kuna kiwanda kidogo cha uchakataji kinachohudumia Kanda ya Kati inayojumisha mikoa ya Singida, Manyara na Dodoma ambacho kinatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh milioni 200 .

Mhifadhi Mkuu Daraja la Pili wa TFS , Claudia Kinabo amesema hayo alipozungumzia mikakati ya uzalishaji wa mazao ya nyuki ikiwemo asali katika kanda hiyo na namna ilivyojioanga kwenye maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani Mei 20 mwaka huu ambapo kitaifa ya kifanyika mkoani Tabora.

Kinabo ambaye ni msimamizi wa kitengo cha Ufugaji Nyuki Kanda ya Kati alisema Wakala huo umetenga bajeti kwa ajili ya kujenga kiwanda kikubwa zaidi ya ukataji wa mazao ya nyuki ambapo kwa sasa kipo kiwanda kidogo katika kituo cha Wilaya ya Manyoni.

“Ujenzi kwa maana ya upanuzi huu wa kiwanda cha Manyoni utakuwa na mchango mkubwa katika kukuza sekta ya asali na kuongeza uzalishaji katika eneo hili,” amesema Kinabo.

Kinabo amesema Kanda  yaKati unaendelea kuwa miongoni mwa maeneo yanayoongoza kwa uzalishaji wa asali chini ya TFS kwa sababu ina mazingira mazuri ya misitu yanayofaa kwa ufugaji nyuki.

Amesema kuwa Kanda hiyo una mashamba makubwa matano ya nyuki yaliyopo katika wilaya za Singida na Kondoa, maeneo yanayojulikana kwa mazingira mazuri ya ufugaji nyuki na uzalishaji wa asali bora.

Naye, Mhifadhi Nyuki Shamba la Nyuki Manyoni, Mrina Robert amesema kiwanda cha kuchakata mazao ya nyuki kimekuwa kikichakata mazao hayo kutoka wilaya mbalimbali za Kanda ya Kati pamoja na asali za wadau mbalimbali .

Mrina amesema kiwanda cha sasa licha ya kuendelea kuchakata mazao ya nyuki  kikiwa na uwezo wa kuchakata kilo 500 kwa saa nane  kwa siku.

Amesema kutokana na mahitaji makubwa na mtambo uliopo  ni mdogo pamoja na jengo, wakala katika bajeti yake umejipanga kujenga jengo kubwa la kiwanda na kuweka mitambo mikubwa nay a kisasa zaidi  ya kuchakata mazao ya nyuki kwa maana ya asali, nta na mengine.

Mrina amesema kiwanda hicho kipya kitachangia kuongeza kasi ya uchakataji wa asali  na kutoa ushawishi kwa wadau wenye mashamba ya nyuki kuleta mazao yao kuchakatwa.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu na Msaidizi wa Kamanda wa TFS Kanda ya Kati anayeshughulikia Dawati la Mipango na Masoko, Ignas Lupala alisema kwa mwaka wa fedha wa 2024/2025 lengo lilikuwa kuzalisha tani 20 za mazao ya nyuki na hadi kufikia msimu ulipomalizika zilizalishwa tani 16.5 za asali.

Lupala amesema kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Kanda hiyo imeweka lengo la kuvuna jumla ya tani 21 za asali na  bado msimu wa uvunaji unaendelea na mikakati mbalimbali imewekwa ya uzalishaji  mazao ya nyuki kwa wingi yanafikiwa kila mwaka.

Wataalam wa Tasnia ya Maziwa nchini wameonya juu ya matumizi holela ya dawa kwa mifugo ambayo husababisha uwepo wa masalia ya dawa katika maziwa, hali inayoweza kuhatarisha afya za walaji na kuathiri ubora wa bidhaa za maziwa.
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linaendelea kuimarisha ushirikiano na jamii kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya bomba la gesi asilia katika vijiji vya Mkwalia Kitumbo na Sunguvuni, wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

 


📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja TANESCO


📌 Asisitiza utoaji wa taarifa sahihi kwa wateja 


📌 Aagiza kuboreshwa kwa maslahi ya watoa huduma kuongeza ufanisi wa utendaji kazi 



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amewataka Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutumia kwa ufanisi mifumo ya kidigitali na akili mnemba ili kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia na kuongeza ufanisi wa huduma na mawasiliano kwa wateja.

Mhe. Makamba amesema hayo Mei 18, 2026 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao unaofanyika kwa siku tano katika Ukumbi wa Lavenda Hotel jijini Dodoma ukilenga kutathmini utendaji kazi, kutambua changamoto, kujadili mikakati ya kuboresha huduma kwa wateja na kuimarisha mawasiliano ya kimkakati ndani ya Shirika kwa mwaka ujao wa fedha.

“ Sote tunatambua, teknolojia ndiyo msingi wa utoaji huduma wa kisasa hivyo ni wajibu wenu Maafisa Huduma kwa Wateja kuhakikisha mifumo ya kidigitali ikiwemo akili mnemba inatumika kwa ufanisi ili wananchi wapate huduma bora na taarifa sahihi kwa wakati.” amesisita , Mhe. Salome Makamba

Katika hotuba yake, amesema Serikali inatambua jitihada za dhati zinazofanywa na TANESCO katika maboresho yaliyofanyika katika huduma kwa wateja na  mawasiliano ya kimkakati kupitia matumizi ya mitandao ya kijamii, makundi ya WhatsApp pamoja na utoaji wa elimu kuhusu matumizi salama ya umeme na Nishati Safi ya kupikia.

Aidha, ameitaka Menejimenti ya TANESCO kuboresha motisha kwa watoa huduma kwa wateja ili kuongeza ari na ufanisi wao kazini kwa kuzingatia kuwa wao ni watendaji wa mstari wa mbele katika kujenga taswira ya Shirika kwa wateja .

“ Kwa niaba ya Uongozi wa Wizara, nawapongeza watoa huduma kwa kujituma kwenu. Nimuombe Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO kusimamia uboreshaji wa maslahi yao ili waweze kutoa huduma bora na yenye uhakika kwa wateja,” amesema Mhe. Makamba.

Akizungumza kuhusu maboresho ya huduma kwa wateja, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ufanisi katika vituo vya huduma kwa wateja (Call Centers) ili kuhakikisha changamoto za wateja zinatatuliwa kwa wakati. 

“Nahimiza ushirikiano madhubuti kati ya TANESCO na wadau mbalimbali ili wateja waweze kupata taarifa sahihi kwa wakati. Aidha, kuna umuhimu mkubwa wa kuimarisha ushirikiano wa ndani kati ya Idara za TEHAMA na Huduma kwa Wateja kwa lengo la kufikia viwango bora zaidi vya utoaji huduma,” ameongeza .

Awali akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, Dkt. Lucy-Mary Mboma, amesema Bodi inaendelea kuthamini mchango wa Maafisa Huduma kwa Wateja na inatarajia kuona Shirika likiendelea kuimarisha taswira yake kupitia huduma bora na mawasiliano yenye tija.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Shirika limewekeza katika mifumo rasmi itakayowezesha kuhudumia zaidi ya wateja milioni sita kwa ufanisi mkubwa mara itakapoanza kufanya kazi hivi karibuni. Amesema hatua hiyo pia itasaidia kuokoa takribani shilingi milioni 400 zilizokuwa zikitumika kwenye mifumo ya nje.

“ TANESCO itaendelea kuwekeza katika mifumo ya kisasa ya utoaji huduma ili kuongeza ufanisi, kuhudumia kwa uhakika zaidi ya wateja milioni sita na kupunguza gharama za uendeshaji wa mifumo ya nje.” amebainisha, Bw. Twange. 

Mkutano huu wa mwaka wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja ni muendelezo wa utamaduni wa taratibu za Shirika wenye tija katika kuboresha utendaji kazi kwa maslahi ya Shirika, wateja na nchi kwa ujumla.

 

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Juma Homera amesema watu wanaoitukana Serikali, kufanya uchochezi na  vitendo visivyo vya maadili mitandaoni, majina yao yameshakabidhiwa kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ili Jeshi la Polisi ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Aliyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa siku wa mafunzo kwa mawakili wa serikali yaliyoandaliwa na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Arusha.

Dk. Homera alitoa kauli hiyo akijibu ombi la Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dk. Damas Ndumbaro aliyetaka mawakili wa serikali kuisaidia Serikali dhidi mashambulizi na upotoshaji unaofanywa mitandaoni.

Dk. Homera alisema majina ya wahusika wa uhalifu huo tayari yamekabidhiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa hatua za kisheria.

Alisema kuna Sheria ya Mitandao, sheria za Jeshi la Polisi na sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambazo zinadhibiti upotoshaji, uchochezi na uvunjifu wa maadili, hivyo serikali itahakikisha inazisimamia ili kukomesha uhali huo nchini.

"Serikali haikatai kukosolewa, lakini ikoselewa kwa jambo la haki na kweli na si jambo la uongo, na kutumia lugha ya matusi au uchochezi, hivyo wahusika watachukuliwa hatua za kisheria ili kuimarisha amani na usalama,"alisisitiza Dk Homera.

Aliongeza"Jeshi la Polisi limeanza kuchukua hatua dhidi ya wanaoitukana serikali, kufanya uchochezi na vitendo visivyo vya maadili mitandaoni."

Kuhusu mafunzo hayo, alisema yatawasaidia mawakili wa serikali kuishauri serikali ipasavyo na kwa weledi, kuwa na uelewa mpana wa masuala mbalimbali, kujengewa uelewa kuhusu miradi ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) na masuala mengine mbalimbali.

Alisema Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali inafanya kazi nzuri ya kuitetea serikali katika mashauri mbalimbali na kufanikiwa kuisadia serikali kuokoa zaidi ya shilingi trilioni moja kwa kushinda kesi hizo.

Naye Wakili Mkuu wa Serikali, Dk Ally Possi alisema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, kati ya mashauri 641, serikali ilishinda mashauri 595 sawa na asilimia 88.1 na kuokoa Sh bilioni 316.3 ambayo serikali ingelipa kama ingeshindwa mashauri hayo.

Kuhusu mashauri ya usuluhishi, alisema mashauri 18 yamekamilika na serikali kuokoa Sh bilioni 6.8 katika kipindi hicho.

"Kwa hiyo katika mashauri yote ya madai na usuluhishi kuanziaJulai 2025 hadi Aprili 2026, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali tumeisadia Serikali kuokoa shilingi trilioni 1.35,"alisema Dk Possi.

Aliongeza"Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ilianzishwa mwaka 2018, na moja ya mafanikio makubwa tuliyoyapata ni kuitetea serikali katika kesi ya kukamatwa kwa ndege yetu na kushinda."

Pia alisema mafunzo hayo kwa mawakili wa serikali yanalenga kulinda kila senti ya mlipakodi, kutetea rasilimali za serikali, kuongeza uwezo wa mawakili katika nyanja mbalimbali, kujinoa kitaaluma, na kuendesha mashauri kwa weledi na umahiri.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dk. Damas Ndumbaro alisema kuna haja kwa mawakili wa serikali kuja na mpango wa namna ya kuitetea serikali dhidi ya mashambulizi na upotoshaji mkubwa dhidi ya serikali.

"Nini nafasi ya mawakili wa Serikali katika jambo hili? Nashauri kupitia mafunzo haya jadilianeni nini cha kufanya ili kuihudumia nchi na jamii yetu kwa weledi,"alisema Dk. Ndumbaro

Pia alisema kwa kuwa asilimia 36 ya migogoro yote iliyoibuliwa na  timu ya Msaada wa Kisheria ya Samia imetokana na ardhi, hivyo alimuomba Wizara ya Katiba na Sheria kulifanyia utafiti jambo hilo ili kujua chanzo na kuja na suluhu ya kuikomesha migogoro hiyo.

Dk Ndumbaro aliwataka mawakili hao wa serikali kujifunza kwa vitendo kupitia mashauri mbalimbali wanayoshinda na kushindwa ili kufanya mabadiliko ya kisheria yanayohitajika kwa maslshi ya taifa na kuleta ufanisi katika sekta ya sheria.

Kwa mujibu wake, Februari 2018, Tanzania ilifanya mageuzi makubwa katika sekta ya sheria nchini kwa kupangilia upya nafasi tatu ikiwemo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).

Alisema mageuzi hayo yamesaidia kuleta ufanisi katika sekta ya sheria nchini.

Naye Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Alice Mtulo alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Mawakili wa serikali kuhusu uendedhaji wa mashauri ya madai na usuluhishi.

Alisema jumla ya washiriki 600 wanahudhuria mafunzo hayo wakiwemo mawakili kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, taasisi za serikali na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Samwel Maneno alisema mawakili wa serikali wanawajibu wa kuisaidia serikali kwa kutoa ushauri mzuri wa kisheria pale serikali inapoingia mikataba na sekta binafsi ambayo ni injini ya uchumi wa taifa.

Maneno alisema Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeshasajili mawakili zaidi ya 30 katika kitengo cha ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP) katika kutekeleza miradi ya ubia.

Naye Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Zanzibar, Shaaban Abdalla aliwataka mawakili hao wa serikali kusimamia mashauri ya madai na usuluhishi kwa weledi na uzalendo kupitia mafunzo wanayopewa.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama Tanzania, Profesa Elisante Ole Gabriel alisema kwa kuwa Mahakama ni chombo cha juu na cha mwisho katika kutoa haki, hivyo Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ni mdau muhimu katika jambo hilo.








NAIBU Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Jumanne Maghembe amesisitiza umuhimu wa vijana katika kuleta maendeleo endelevu na mabadiliko chanya kupitia teknolojia, diplomasia na ubunifu katika ngazi ya taifa na kimataifa.

 


Mbunge mstaafu na mdau wa masuala ya teknolojia na maendeleo ya kidijitali, Neema Lugangira, amepata heshima ya kuteuliwa tena na Katibu Mkuu wa United Nations kuhudumu katika Kamati ya Ushauri kuhusu masuala ya utawala wa mtandao duniani pamoja na maendeleo ya kidijitali.

Kamati hiyo ya kimataifa ina jukumu la kumshauri Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu namna bora ya kuimarisha ushirikiano wa kidijitali, usalama wa mtandao, upatikanaji wa teknolojia, pamoja na kuhakikisha maendeleo ya kidijitali yanawanufaisha watu wote duniani kwa usawa.

Akizungumzia uteuzi huo, wachambuzi wa masuala ya teknolojia wameeleza kuwa nafasi hiyo ni ishara ya kuongezeka kwa ushawishi wa Watanzania katika majukwaa ya kimataifa yanayojadili mustakabali wa dunia ya kidijitali.

Neema Lugangira amekuwa mmoja wa viongozi wanaosukuma ajenda ya matumizi ya teknolojia, ubunifu wa kidijitali pamoja na ujumuishaji wa wananchi katika uchumi wa kidijitali nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Uteuzi huo pia unatajwa kuwa fursa muhimu kwa Tanzania kuendelea kushiriki katika maamuzi na mijadala ya kimataifa kuhusu sera za teknolojia, mtandao na maendeleo ya kidijitali katika dunia inayobadilika kwa kasi.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeandaa mbio za marathon zijulikanazo kama ‘Viwango Marathon’ ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo, huku likihamasisha matumizi ya bidhaa zilizothibitishwa na TBS pamoja na kuimarisha afya kwa jamii kupitia michezo.

 


Mwenyekiti wa UVCCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida (MCC) amewasili mkoani Mtwara leo tarehe 18 Mei 2026 na kupokelewa katika Ofisi za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mtwara.

Ndugu Kawaida amepokea taarifa ya CCM mkoa wa Mtwara, taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM ambapo alifanya kikao cha ndani.

Akizungumza na Watendaji wa CCM ngazi ya mkoa wa Mtwara amewasihi kuendelea kuitangaza miradi inayotekelezwa kwa Wananchi na Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwenyekiti wa CCM.

Ndugu Kawaida amewataka watendaji wote kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na kutumia mitandao ya kijamii kueneza amani ya nchi.

Mwenyekiti Kawaida ataendelea na ziara ya kutembelea wanufaika wa miradi ya mikopo ya asilimia 4, kuzungumza na wananchi na kusikiliza maoni yao.












Na Mwandishi Wetu

Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) na Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL) wamesaini makubaliano ya kuwatafutia fursa mbalimbali za kilaaluma wanafunzi wa chuo hicho.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imesema itaendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini ili kuhakikisha wafanyabiashara wa Kariakoo wanakuwa na ushindani wa kikanda na kimataifa huku ikiitaja Kariakoo kuwa moyo wa biashara wa Tanzania na injini muhimu ya uchumi wa taifa.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Ilala kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ilala, JUZA, Care and Help, Chuo cha Maji, MUHAS pamoja na wadau mbalimbali wa mazingira wamefanya zoezi la usafi katika fukwe za Daraja la Salender zilizopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. 



Na Mwandishi wetu- MBEYA

Serikali imeendelea kuimarisha uwezo wa Kitaifa wa Kuzuia, Kujiandaa, Kukabiliana na Kurejesha hali baada ya maafa ili kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama ya  kuepuka madhara makubwa yatokanayo na maafa.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ofisi ya Mkoa wa Mbeya, Dkt. Noah Sikwese wakati akifunga mafunzo kwa Wajumbe Wateule wa Timu ya Kukabiliana na Dharura (RERT), Waatalamu wa Unendeshaji wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura (REOCC) katika Mkoa huo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa.

Dkt. Sikwese, amesema timu za kukabiliana na dharura zimejengewa msingi muhimu wa utendaji utakaowezesha Mkoa kuwa na uwezo wa kujiandaa na kukabiliana na matukio ya dharura kwa haraka  na ufanisi mkubwa .

“Timu hizi zitahusika katika kufanya tathmini za awali na za kina wakati wa maafa kubaini mahitaji halisi ya waathirika, pamoja na kuratibu upatikanaji wa rasilimali muhimu kwa ajili ya kukabiliana na athari za maafa,” alisema Dkt. Sikwese.


Pia, aliongeza kwamba mafunzo yamekuwa nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura.

“Kuanzishwa kwa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Mkoa wa Mbeya ni hatua muhimu katika kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa. Kituo hiki kitawezesha ufuatiliaji wa matukio  kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano miongoni mwa wadau,” alieleza.

Sambamba na hilo Dkt. Sikwese alifafanua kuwa, utekelezaji wa mafunzo hayo ulianza katika Mikoa a Mwanza, Arusha, Dodoma, ambapo hatua za kuanzisha Vituo vya Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu za kukabiliana  na maafa zilianza kutekelezwa.


“Ni matarajio yangu mafunzo haya yataongeza ufanisi, uwajibikaji, ustahimilivu dhidi ya majanga katika Mkoa wetu wa Mbeya,”aliongeza.

Aidha, alitoa wito kwa wataalamu wote waliopatiwa mafunzo kuendelea kuyafanyia kazi maarifa na stadi, kudumisha nidhamu ya kazi na kujenga utamaduani wa ushirikiano wa kitaalamu huku akiwasisitiza kuendelea kufanya mazoezi ya mara kwa mara ya uokoaji na  utoaji wa huduma ya kwanza kwa majeruhi au waliofikwa na maafa.

“Usimamizi wa maafa ni jukumu letu sote, kila mmoja ashiriki sasa na kuchukua hatua katika eneo lake ili kuokoa na kulinda maisha, mali na mazingira,” alisisitiza Dkt. Sikwese.


Ikumbukwe kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa yam waka 2004 (Toleo la 2025) pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 202 imeipa jukumu la kuratibu masuala yote ya usimamizi wa maafa nchini.






MWISHO

 


Katika jitihada za kuendeleza ustawi wa wananchi na kuchochea uchumi wa maeneo ya vijijni na vitongojini, Serikali inaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wilayani Kondoa kupitia mpango wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote vya wilaya hiyo.

 Mpaka sasa vitongoji 113 vina umeme huku kukiwa na mradi unaoendelea wa kupeleka umeme katika vitongoji 60.

Hayo yameelezwa leo Mei 16, 2026 na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kondoa, Dodoma.

Mhe. Salome ameeleza kwamba katika mradi wa umeme unaotekelezwa sasa wa kusambaza umeme katika vitongoji 60 zaidi ya shilingi billion 21 imetengwa kuhakikisha mradi huo unakamilika ambapo kukamilika kwake kutafanya  Kondoa kubakiwa na vitongoji 88 tu ambavyo havina umeme  vitakavyofikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2030.

Pia Mhe Salome ameeleza kwamba Serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 752 kwa ajili ya  kuhakikisha wananchi ambao miradi ya umeme inapita karibu na nyumba zao  wanafikiwa na huduma ya umeme katika kaya zao.

Ameongeza kuwa katika Wilaya ya Kondoa,  Wizara ya Nishati ina mpango wa kubadilisha nguzo zote chakavu na kupeleka nguzo za zege ili kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa na nishati ya umeme ya uhakika ili wananchi waendelee kufanya shughuli zao za kiuchumi kama vile uendeshaji wa viwanda vidogo na shughuli za kijamii.

Vilevile amesema Serikali ina mpango mahsusi kujenga laini kubwa ya umeme ili kuimarisha na kutatua changamoto ya nguvu ya umeme (Low Voltage katika Jimbo la Kondoa).

Katika hatua nyingine, Mhe. Salome amewaasa wananchi kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia akieleza kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na Wananchi Kondoa  kutunza misitu bado wanatakiwa kuilinda kwa kuachana na matumizi ya Kuni na mkaa na kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kama vile gesi, umeme na mkaa mbadala 

“Niwahakikishie wanakondoa sasa hivi Serikali imeweka ruzuku katika mitungi ya gesi, hivyo niwaombee sana tuanze kutumia Nishati safi kwa ajili ya kulinda  afya, mazingira na kuokoa muda wa kukaa jikoni ili tuweze kujiendeleza kiuchumi lakini pia tutumie nishati nyingine kama mkaa mbadala usiotoa moshi ambapo utatumia mkaa kidogo kupika chakula kingi na katika hali iliyo bora zaidi." Amesisitiza  Mhe Salome.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imezindua maabara za kompyuta katika Shule ya Sekondari Kimara pamoja na Shule ya Msingi Mkwawa jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya taasisi hiyo na jitihada za kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika sekta ya elimu.


Na Mwandishi Wetu

 

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Kongamano la 13 la Jukwaa la Miji Duniani (13th World Urban Forum) litakalofanyika Baku, Azerbaijan kuanzia tarehe 17-22 Mei 2026.

 

Kongamano hilo litakalofanyika katika Uwanja wa Olimpiki wa Baku kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Makazi Duniani (UN-Habitat), linabeba kaulimbiu isemayo: “Makazi kwa Dunia: Miji na Jamii Salama na Imara.”

 

Jukwaa hilo la Miji Duniani litazikutanisha nchi mbalimbali zikijadili na kuweka mikakati ya pamoja ya namna miji inavyoweza kuwa chachu ya kuchochea maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.

 

Aidha, Kongamano hilo la siku sita litahusisha ushiriki wa viongozi katika ngazi ya Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wataalamu mbalimbali watakaojadili changamoto za kimataifa za makazi pamoja na kukuza maendeleo endelevu ya miji.

 

Kupitia kongamano hilo la Miji Duniani kutakuwa na mawasilisho na mijadala kutoka kwa Mawaziri ambapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatarajia kutoa tamko  litakalotolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo.

 

Mawasilisho na mijada ya mawaziri katika kongamano hilo la Miji Duniani yatatoa fursa kwa Tanzania kujifunza kutoka nchi nyingine mbinu bora zinazoweza kuboresha utekelezaji wa sera mbalimbali za maendeleo pamoja na kutoa uzoefu wake.

 

Ujumbe wa Tanzania katika Kongamano hilo la Jukwaa la miji Duniani unahusisha pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Profesa Riziki Shemdoe,  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemera pamoja na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dkt. Asha-Rose Migiro, kwa nyakati tofauti amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi wawili wanaoziwakilisha nchi zao katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mbunge wa Jimbo la Mbinga vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta za elimu na afya hasa maeneo ya Jimbo hilo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.