Na Oscar Assenga, Tanga
Katika kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia duniani, Shule ya Sekondari Coastal High School imetangaza mpango kabambe wa kuanzisha programu ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) ifikapo Januari 2027.
Mpango huo unalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kisasa utakaowawezesha kushindana katika soko la ajira la Kimataifa.
Akizungumza wakati wa mahafali ya Kidato cha Sita yaliyofanyika jijini Tanga, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Isack Dastan Kifwete alisema kuwa tayari wameanza kuchukua hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa mpango huo.
Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kufanikisha upatikanaji wa huduma ya intaneti kupitia Kampuni ya TTCL, pamoja na kuwepo kwa mtaalamu wa TEHAMA shuleni hapo.
Hata hivyo, alibainisha kuwa bado kuna changamoto kadhaa zinazokwamisha utekelezaji wa mpango huo kwa ufanisi unaohitajika.
Alizitaja changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vifaa muhimu kama kompyuta za kisasa, ubao janja (smart board), pamoja na miundombinu ya chumba maalumu kitakachotumika kufundishia programu ya AI.
Mbali na hilo, shule pia ina mpango wa kuanzisha programu ya Habari na Mawasiliano ya Umma, unaolenga kuwajengea wanafunzi uwezo wa uandishi wa habari, mawasiliano, pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa katika tasnia ya habari.
Tayari maandalizi ya awali, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya studio, yameanza kufanyika.
Pamoja na jitihada hizo, Mwalimu Mkuu alieleza kuwa shule bado inahitaji vifaa muhimu ili kukamilisha studio hiyo.
Vifaa vinavyohitajika ni pamoja na kamera za kisasa, meza ya matangazo, vifaa vya kuzuia kelele, vinasa sauti, vipaza sauti pamoja na kompyuta zenye uwezo wa kisasa.
Aidha, alitaja changamoto nyingine zinazoikabili shule kuwa ni pamoja na baadhi ya wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati kutokana na hali ngumu ya kiuchumi, pamoja na ushiriki mdogo wa wazazi na walezi katika masuala ya kitaaluma na malezi ya wanafunzi.
Kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule umetoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia jitihada hizo ikiwemo kuwaomba wadau msaada wa vifaa kwa ajili ya kuanzisha studio ya habari, pamoja na kuunganishwa na taasisi au watu binafsi wanaoweza kusaidia upatikanaji wa kompyuta za kisasa.
Kwa ujumla, mpango huu unaonesha dhamira ya dhati ya shule katika kuwajengea wanafunzi msingi imara wa elimu ya kisasa ili kuwaandaa kukabiliana na dunia inayoendeshwa na teknolojia kwa kasi kubwa.
Awali, akizungumza katika mahafali hayo,Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar (CCM), Ussi Salum Pendeza, alisema kuwa atashirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha baadhi ya changamoto zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka.
Alisema kuwa ataanza mwenyewe kuchangia upatikanaji wa baadhi ya vifaa muhimu, ikiwemo kompyuta za kisasa na ubao janja, sambamba na kuhamasisha wadau wengine kushiriki.
“Katika hili la ubao janja na baadhi ya kompyuta, nitaanza mimi mwenyewe. Pia nitahakikisha michango inapatikana na kuwashirikisha wengine. Nachukua nafasi hii kuwashukuru walimu na Bodi ya Shule ya Coastal kwa ushirikiano wao katika kuhakikisha shule inafanya vizuri na matokeo yanakuwa mazuri,” alisema.
Ussi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Taasisi ya Pendeza Foundation, alisema anajivunia kuiongoza shule hiyo na ameahidi kuendelea kuisimamia ili iweze kufanya vizuri zaidi na kujulikana kitaifa.

Na Oscar Assenga,TANGA
MKURUGENZI wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani Segule Segule amewataka wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Kauli hiyo ameitoa baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.
Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.
.jpg)
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.
“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.
Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.
“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.
Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.
Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.
.jpg)
Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.
Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.
Wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Onyo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Segule Segule, baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.
Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.
“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.
Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.
Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.
“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.
Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.
Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.
Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.
Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, leo, tarehe 22 Aprili 2026, Bunge jijini Dodoma.
....
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, leo, tarehe 22 Aprili 2026, Bunge jijini Dodoma.
..
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imekagua jumla ya vituo 672 vya mafuta kote nchini katika jitihada za kuimarisha udhibiti wa ubora wa mafuta na kulinda maslahi ya watumiaji.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo Aprili 22,2026 bungeni Dodoma.
Katika ukaguzi huo, vituo 50 sawa na asilimia 7.44 vilibainika kuuza mafuta yasiyokidhi viwango vilivyowekwa, hatua iliyochochea mamlaka hiyo kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika. Hatua hizo zilijumuisha kufungiwa kwa vituo husika, kutozwa faini pamoja na kuwasilishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kulipa kodi walizokwepa.
Mbali na ukaguzi wa ubora, EWURA pia ilifanya operesheni maalum ya kufuatilia mwenendo wa usambazaji wa mafuta, ambapo ilibaini vituo vitatu vilivyokuwa vimeficha mafuta kwa makusudi vikisubiri mabadiliko ya bei. Serikali ilichukua hatua za haraka kwa kuvifungia vituo hivyo na kutoa adhabu kwa mujibu wa sheria zilizopo.
Hata hivyo amesema kuwa Serikali imeendelea kuimarisha usimamizi wa sekta ya mafuta nchini kupitia utekelezaji wa programu ya uwekaji vinasaba kwenye mafuta, hatua inayolenga kudhibiti ubora wa bidhaa hiyo pamoja na kuhakikisha ukusanyaji sahihi wa mapato ya kodi.
Amesema Kupitia EWURA utekelezaji wa mpango huo umeonesha mafanikio makubwa kufikia Machi 2026, ambapo jumla ya lita bilioni 1.51 za petroli na lita bilioni 2.02 za dizeli ziliwekewa vinasaba. Kiasi hicho kinaonesha ongezeko la asilimia 14 kwa petroli na asilimia 10 kwa dizeli ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka wa fedha 2024/25.
Hata hivyo, kwa upande wa mafuta ya taa, kiasi kilichowekewa vinasaba kilifikia lita milioni 2.80, ikiwa ni pungufu la asilimia 40, hali inayotafsiriwa kuwa na mabadiliko ya mwenendo wa matumizi au usambazaji wa bidhaa hiyo sokoni.
Hatua hizi zinaakisi dhamira ya Serikali ya kuhakikisha sekta ya mafuta inasimamiwa kwa uwazi na ufanisi, huku ikihakikisha haki kwa watumiaji na kuongeza mapato ya Taifa. Aidha, juhudi hizo zinasaidia kudhibiti vitendo vya udanganyifu vinavyoweza kuhatarisha uchumi na ustawi wa wananchi.
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27, leo, tarehe 22 Aprili 2026, Bunge jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna,Mzalendo blog-DODOMA
Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kuimarisha usimamizi na udhibiti wa shughuli za gesi asilia katika mkondo wa kati na chini, hatua inayolenga kuhakikisha usalama wa miundombinu, upatikanaji wa huduma bora pamoja na kukuza matumizi ya nishati safi nchini.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 leo Aprili 22,2026 bungeni Dodoma.
Amesema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, EWURA ilifanya kaguzi 68 katika miundombinu ya gesi asilia iliyopo katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam. Miundombinu hiyo inahusisha mitambo minne ya uchakataji, miwili ya usafirishaji, mtandao wa usambazaji wenye urefu wa kilomita 243 pamoja na vituo 18 vya kujazia gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) kwa magari. Taarifa zinaonesha kuwa miundombinu yote iliyokaguliwa ilikidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa.
Katika kuendeleza sekta hiyo, EWURA ilitoa vibali tisa vya ujenzi wa vituo vya CNG katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Ruvuma. Maeneo yaliyopata vibali katika mkoa wa Dar es Salaam ni pamoja na Mbezi Beach, Mbagala, Kigamboni, Buguruni, Mwenge, Kinyerezi na Gongolamboto, huku Morogoro (Msamvu) na Ruvuma (Tunduru) kila mmoja ukipata kibali kimoja.
Aidha, vibali viwili vilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kupokelea gesi asilia iliyoshindiliwa kwa matumizi ya viwanda vilivyopo Kibaha mkoani Pwani, hatua inayotarajiwa kuongeza matumizi ya nishati hiyo katika uzalishaji wa viwandani.
Katika sekta ya usafirishaji na usambazaji, EWURA ilitoa vibali saba vya ujenzi wa mabomba ya gesi asilia, ikiwemo mabomba ya kuunganisha gesi kwenye viwanda, taasisi, migahawa na majumbani, pamoja na mabomba ya kuhudumia vituo vya CNG. Kibali kingine kilihusu ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Ntorya hadi Madimba mkoani Mtwara.
Sambamba na hilo, jumla ya leseni 17 zilitolewa kwa ajili ya uendeshaji na usafirishaji wa gesi asilia, zikiwemo leseni za vituo vya CNG na usambazaji wa gesi katika mkoa wa Pwani. Ongezeko la utoaji wa vibali na leseni linaonesha mwitikio mkubwa wa sekta binafsi kushiriki katika mnyororo wa thamani wa gesi asilia.
Serikali imeeleza kuwa itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuvutia wawekezaji zaidi katika sekta hiyo, hasa katika mikoa ya kimkakati kama Morogoro, Dodoma, Mbeya na Tanga. Wito umetolewa kwa sekta binafsi kuchangamkia fursa zilizopo, kufuatia ongezeko la matumizi ya gesi asilia katika usafiri, viwandani na matumizi ya majumbani.
Hatua hizi zinaakisi dhamira ya Serikali ya kuhakikisha gesi asilia inakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi, huku ikichangia upatikanaji wa nishati safi, nafuu na salama kwa wananchi.
Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna-Mzalendo blog-DODOMA
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), leo 21 Aprili 2026, imetumia fursa ya Wiki ya Nishati kuwahamasisha waheshimiwa wabunge kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini pamoja na vituo vya CNG ili kuendelea kusogeza huduma kwa wananchi.
Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw. Wilfred Mwakalosi, alisema kuwa EWURA inatumia maonesho hayo kutoa elimu kuhusu namna inavyohakikisha upatikanaji wa huduma za nishati na maji kwa wakati na kwa gharama nafuu.
Amebainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi, hivyo kuwajengea uelewa kuhusu udhibiti, fursa za uwekezaji na utaratibu wa kupokea na kushughulikia migogoro na malalamiko kutawawezesha kuwasilisha taarifa sahihi kwa wananchi kuhusu juhudi za Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za umeme, mafuta na gesi asilia.
Akizungumza katika maonesho hayo, Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi, amesema elimu inayotolewa pia inalenga kuwafahamisha wananchi jinsi EWURA inavyosimamia upatikanaji wa huduma za mafuta nchini kwa kuzingatia ubora uliopitishwa na gharama sahihi.
Aidha, amewahamasisha wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta hiyo, hususan ujenzi wa vituo vya mafuta vya gharama nafuu vijijini na mijini pamoja vituo vya kujazia gesi asilia kwenye magari (CNG).
Kwa upande wake, Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,amesema elimu inayotolewa imejikita katika kueleza namna EWURA inavyosimamia upangaji wa viwango vya bei za huduma za umeme, mafuta na gesi asilia. Aliongeza kuwa mamlaka hiyo huweka mizania kati ya maslahi ya watoa huduma na watumiaji, na kwamba wabunge waliopata elimu hiyo wataweza kuiwasilisha ipasavyo kwa wananchi katika maeneo yao.
Akizungumzia sekta ya gesi asilia, Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza, amesema EWURA itaendelea kusimamia ubora wa miundombinu ya gesi asilia nchini na kuhamasisha matumizi yake, hususan katika magari.
Amebainisha kuwa hadi sasa vituo 18 vimepata leseni ya EWURA kutoa huduma ya gesi asilia, huku vituo sita vingine vikiwa katika hatua za mwisho za kupata leseni katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Aidha, mipango inaendelea kwa baadhi ya makampuni kusambaza gesi asilia iliyokandamizwa katika mikoa ya Morogoro na Dodoma.
Kwa upande wa sekta ya umeme, Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba, amewahamasisha wabunge na wadau wanaotembelea maonesho hayo kutumia mafundi umeme wenye leseni kutoka EWURA ili kuhakikisha usalama wa nyumba na mali zao. Alisema EWURA inaendelea kutoa leseni kwa mafundi umeme wenye sifa stahiki, ambapo zaidi ya leseni 1,000 zilitolewa katika mwaka wa fedha uliopita.
Naye Ofisa Rasilimali Watu Mkuu, Bi. Limi Kahabi, amesema EWURA ni mwajiri anayezingatia misingi ya usawa na haki katika mchakato wa ajira, akisisitiza kuwa taasisi hiyo huajiri kwa kuzingatia sifa, weledi na usawa kwa wote.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Ofisa Mkuu, Usimamizi wa Rasilimali Watu,Bi. Limi Kahabi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma























