Katika jamii ya Kimaasai, maisha ya mwanaume hupitia hatua mbalimbali za kimila zinazoonyesha ukuaji, Miongoni mwa hatua hizo muhimu ni kufanyiwa sherehe inayojulikana kwa jina la Orkiteng le Sirit ikimaanisha ni mwisho wa ujana na kuingia uzeeni.

Katika hatua hii ambapo mtu anatawazwa kuingia rika la uzee, wazee wa jamii hiyo huchagua Dume la rika ambalo lina afya njema na lililohasiwa tangu utoto wake, dume hili siku ya shughuli ndio hutolewa mwanzo kwenye boma lenye  Ng’ombe wengi na kumwagiwa maziwa kisha hunyongwa hadi kufa. 

Sherehe ya Orkiteng le Sirit , si sherehe ya kawaida bali ni tukio la heshima kubwa linalofanyika kwa kufuata mila na desturi za kale zilizorithishwa kutoka kizazi hadi kizazi. Kwa jamii ya Kimaasai, ni hatua ya ukamilifu wa mwanaume na uthibitisho kwamba ametimiza majukumu yake ya kifamilia na kijamii, kufanyiwa sherehe hii hakuangalii umri ila inazingatia jinsia kwa kuwa anayefanyiwa sherehe hii ni mwanaume pekee, vigezo vinavyoangaliwa ili mwanaume afanyiwe sherehe hii, ni lazima awe ameoa, awe na watoto wa kike na kiume na awe mtu mwema na maadili katika jamii.

Akizungumza wakati wa sherehe hiyo, Alaigwanani wa kabila la kimasai Maningo Rinjo amesema viongozi wa mila wa ukoo kama (Laizer, Mollel, Laitayo, Ngidong’i) ndio wenye jukumu la kumchagua dume atakayechinjwa baada ya kujiridhisha kuwa ana sifa zote zinazotakiwa kwa mujibu wa mila na desturi za Kimaasai ili kutekeleza jukumu hilo la kijamii ambalo linahudhuriwa na ndugu wote wa familia na jamii yote ya wamasai inayozunguka Kijiji hicho. 

“Si kila dume anaruhusiwa kutumika katika sherehe hii, sisi viongozi wa mila hukagua na kuthibitisha sifa zake kabla ya kutoa ruhusa ya kuchinjwa, dume wa kutekeleza sherehe hii lazima awe amehasiwa tangu utotoni, hajawahi kumpanda dume jike, pembe zake ziwe zimenyooka bila kupinda mithili ya pembe za mbogo, asiwe mgonjwa na sifa zingine za ndani ambazo viongozi wa kimila ndio huzichunguza kwa undani,” alisema Alaigwanani Maningo Rinjo.

Alaigwanani Olonyori Lemoyan kutoka Ukoo wa Laizer Kata ya Nainokanoka Ngorongoro alisisitiza kuwa si kila mwanaume anastahili kufanya sherehe ya Orkiteng le Sirit, moja wa masharti muhimu ili mwanaume afanyiwe tukio hilo kuwa

na familia yenye watoto wa kike na kiume, awe na mali na uelekeo wa maisha, mtu anayejali watu na awe ni rafiki wa ukoo wake na jamii inayomzunguka pamoja na kupata ridhaa ya ukoo wake kufanya sherehe hiyo. 

“Orkiteng le Sirit ni heshima kubwa katika jamii ya Kimaasai. Mwanaume lazima awe ametimiza wajibu wake wa kifamilia kwa kupata watoto wa kike na wa kiume. Bila kutimiza sharti hilo, hawezi kufikia hatua hii muhimu ya maisha,” alisema Alaigwanani Olonyori Lemoyan.

Wakati wa sherehe hizo baada ya dume kunyongwa na kutolewa nyama zake, mwanaume anayehitimu (anayepandishwa rika) pamoja na mke wake na mama yake mzazi wanatakiwa hukalia utumbo wa dume hilo kama ishara ya kuaga rasmi ujana na kuingia katika hatua ya uzee. Kitendo hicho hubeba maana kubwa ya kiutamaduni na kuashiria mwanzo wa jukumu jipya ndani ya jamii na kuachana na usharobaro na mambo yote ya ujana.

Baada ya taratibu hizo kukamilika, rika la Korianga huungana na mwenzao aliyeingia hatua ya uzee timilifu huimba nyimbo za furaha na heshima huku wakielekea bomani, wakimpongeza mwenzao kwa kufikia hatua hiyo adhimu. Nyimbo hizo huashiria kukubalika kwake rasmi katika kundi la wazee na kupewa nafasi ya kushiriki kikamilifu katika mila, desturi na maamuzi yanayohusu ustawi wa jamii.

Orkiteng le Sirit si tu sherehe ya kuchinja dume laa hasha, ni alama ya mafanikio ya maisha, uwajibikaji wa kifamilia na heshima ya kuwa mzee katika jamii ya Kimaasai. Hatua hii ni urithi wa kipekee unaoendelea kuunganisha vizazi na kuhifadhi utamaduni wenye thamani kubwa kwa jamii hiyo.







 Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema serikali imechukua hatua madhubuti kumaliza changamoto za kukatika kwa umeme zilizokuwa zikiathiri baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, hali iliyokuwa ikisababisha wilaya nzima kukosa umeme pindi hitilafu zinapotokea kwenye baadhi ya sehemu za mtandao.


Ndejembi amebainisha hayo leo wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Usambazaji Umeme (Switching Station) pamoja na transfoma mpya zilizojengwa kwa lengo la kuimarisha na kudhibiti mfumo wa usambazaji umeme katika wilaya hiyo.

Amesema uwepo wa miundombinu hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya mgao wa umeme wa ghafla, ambao hapo awali ulikuwa ukisababisha maeneo mengi ya Kongwa na wilaya jirani kuathirika pindi hitilafu inapotokea sehemu moja ya mfumo.

“Kwa muda mrefu, changamoto ya voltage ndogo na kukatika kwa umeme mara kwa mara ilikuwa kikwazo kikubwa kwa wananchi na wajasiriamali wadogo, hususan waliokuwa wakishindwa kuendesha shughuli za uzalishaji kama kusaga nafaka na kukamua mafuta kutokana na uhaba wa umeme wa uhakika,” amesema Ndejembi.

Ameongeza kuwa serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuliweka sekta ya nishati katika kipaumbele cha juu, hali iliyowezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuboresha maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Amesema zaidi ya shilingi bilioni 10 zimewekezwa katika eneo la Mbande kwa ajili ya ujenzi wa Switching Station hiyo, hatua ambayo itanufaisha wakazi wa wilaya za Kongwa, Kiteto, Gairo, Chamwino na Mpwapwa kwa kupata umeme wa uhakika na wa kutosha.

“Lengo letu siyo tu kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa kuwasha taa, bali ni umeme wa kuendesha viwanda na shughuli za uzalishaji. Hii itasaidia kukuza uchumi wa maeneo haya na kuongeza fursa za ajira,” ameongeza.

Uzinduzi wa mradi huo unatajwa kuwa sehemu ya jitihada za serikali kuboresha miundombinu ya nishati nchini na kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika unafika kwa wananchi wengi zaidi, hususan maeneo ya vijijini na pembezoni.







Na: OWM (KAM) – Dar es Salaam

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kutoa fursa za ajira zenye tija kwa wananchi na suala hilo limekuwa kipaumbele cha kitaifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano ya Kazi, Mheshimiwa Deus Sangu, wakati akizindua Maonesho ya Ajira ya Tano (5) kati ya Tanzania na China yaliyofanyika katika viwanja vya Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, leo Juni 16, 2026.

Aidha, Mheshimiwa Sangu amesema Serikali inatekeleza sera na programu zinazohamasisha viwanda, mafunzo ya ujuzi, ujasiriamali, ufanisi wa soko la ajira na kazi zenye staha kwa wote. Pia, amesema kupitia Dira ya Tanzania 2050, imewekwa wazi kuwa kila kijana nchini anapaswa kupata nafasi ya kujipatia ujuzi, kupata ajira yenye staha na kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya kiuchumi ya Taifa.

“Tanzania ni Taifa lenye vijana wengi, wameelimika, wana ndoto, wabunifu na wako tayari kuchangia katika maendeleo ya taifa,” amesema Waziri Sangu.

Ameongeza kuwa kupitia maonesho haya ya ajira, vijana wa Kitanzania wameunganishwa na waajiri, wameanzisha kazi zenye mafanikio na kupata uzoefu muhimu kupitia fursa zilizoundwa na jukwaa hilo.

Kadhalika, Waziri Sangu amesema makampuni ya Kichina yanayofanya kazi nchini Tanzania yamekuwa washirika muhimu kupitia uwekezaji katika miundombinu, viwanda, sekta ya madini, teknolojia ya habari, usafirishaji, nishati na sekta nyingine za kimkakati. Makampuni hayo yamechangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi na kutoa fursa za ajira kwa Watanzania.

Kwa upande mwingine, Mhe. Sangu amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano na Serikali ya China katika uhamishaji wa ujuzi, teknolojia, ubunifu na utaalamu ili kuongeza ushindani wa taifa katika uchumi wa dunia unaobadilika kwa kasi.

Naye, Balozi wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Chen Mingjian, amesema Maonesho ya Ajira yaliyoandaliwa na Chama cha Makampuni ya China yanayofanya shughuli nchini Tanzania yamekuwa jukwaa muhimu kwa makampuni hayo na wahitimu wa Kitanzania kukutana na kujadili kwa pamoja kuhusu fursa za ajira. Aidha, amezitaka kampuni hizo kuendelea kuwa daraja la ushirikiano kwa kutoa nafasi zaidi za ajira kwa Watanzania.

Zaidi ya kampuni 60 zinashiriki katika maonesho hayo kutoka sekta mbalimbali ikiwemo Uhandisi, Viwanda, Biashara, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Fedha pamoja na Huduma.

Maonesho ya Ajira ya Tano (5) kati ya China na Tanzania yamelenga kutangaza na kuwaunganisha vijana wahitimu na wenye ujuzi wa Kitanzania na makampuni ya Kichina, ili kuimarisha ajira, ubunifu na ushirikiano wa kiuchumi kwa manufaa ya pande zote mbili.

Na Mwandishi Wetu
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeanza kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yaliyoanza rasmi leo, tarehe 16 mpaka 23 Juni, yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma
Akizungumza kuhusu ushiriki wa EWURA katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa EWURA, Bi. Hawa Ramadhan Mniga, amesema maonesho hayo ni fursa muhimu kwa Mamlaka hiyo kuwafikia Watanzania na kuwapatia uelewa kuhusu majukumu yake katika usimamizi wa sekta za nishati na maji.
“Wananchi watakaotembelea banda la EWURA watapata fursa ya kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo mifumo mbalimbali ya kidijitali inayotumiwa na Mamlaka katika utoaji wa huduma kwa wateja, pamoja na maboresho yanayoendelea kufanyika kwa lengo la kuongeza ufanisi, kasi na ubora wa utoaji wa huduma,” amesema Bi. Mniga.
Ameongeza kuwa eneo lingine lililopatiwa kipaumbele ni uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kufanikisha lengo la Taifa la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Aidha, ametoa rai kwa wananchi, wadau wa sekta mbalimbali na washiriki wa maonesho hayo kutembelea banda la EWURA ili kupata elimu, kuuliza maswali na kufahamu kwa undani huduma zinazotolewa na Mamlaka hiyo.

 


Wadau mbalimbali waliotembelea Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika siku ya kwanza ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Juni 16, 2026 wamekiri kuvutiwa na elimu inayotolewa na timu ya wataalamu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Nadhifa Nyoni kutoka Mamlaka ya Maji (TANGA UWASA), Rose Mmary (JWTZ) na Janeth Matara, mwananchi mkazi wa Dodoma, wamepongeza kazi zinazofanywa na WMA na kukiri kuwa elimu waliyoipata kutoka kwa wataalamu imewaongezea uelewa kuhusu vipimo.

Kwa upande wake, Abbas Kayanda, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, pamoja na kupongeza kazi nzuri inayofanywa na WMA, ameshauri kuongeza nguvu katika utoaji elimu ya vipimo ili kuwapatia uelewa wananchi wengi zaidi hususan walioko vijijini.

Ufunguzi rasmi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026 yaliyoanza leo, Juni 16 katika uwanja wa Chinangali Dodoma, yatahitimishwa Juni 23.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Maendeleo Endelevu."

Biashara yangu ilikuwa ikiendelea vizuri kwa miaka kadhaa. Nilikuwa nimejenga jina zuri na kupata wateja wengi wa kudumu. 

Kila siku nilifungua biashara yangu nikiwa na matumaini kwa sababu nilijua watu walikuwa wanaamini huduma nilizokuwa nikitoa. Lakini mambo yalibadilika ghafla.

Siku moja nilianza kusikia maneno yasiyo ya kawaida kutoka kwa baadhi ya wateja. Wengine walikuwa wakisema wameambiwa huduma zangu si nzuri. 

Wengine walikuwa wakielezwa kwamba bidhaa nilizokuwa nauza hazikuwa na ubora kama zamani. Kwa kweli nilishangaa.
Tatizo kubwa lilikuwa kwamba taarifa hizo hazikuwa za kweli.

Hata hivyo, zilianza kuenea haraka. Ndani ya wiki chache, idadi ya wateja ilianza kupungua.
Biashara yangu ilianza kupata hasara. Kulikuwa na siku ambazo duka lilikaa karibu tupu kuanzia asubuhi hadi jioni. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu maisha yangu yalionekana kama yanakwama sehemu moja. Nilikuwa nafanya juhudi katika kila jambo nililolifanya, lakini matokeo hayakuwa mazuri kama nilivyotarajia. 

Kazi, biashara ndogo niliyokuwa nimeanza, na hata mipango yangu ya kifamilia vilikuwa vinachelewa kufanikiwa.

Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na kitu kibaya kinachoendelea maishani mwangu. Nilijaribu kubadilisha mbinu zangu. Nilisoma, nikashauriana na watu tofauti, na hata kujaribu fursa mpya. 

Lakini bado nilihisi kama kuna kizuizi kisichoelezeka kinachonifanya nisisonge mbele kama wengine. Kwa kweli ilianza kunichosha.

Siku moja nilipata pete ya kipekee ambayo ilinishangaza kwa namna fulani. Haikuwa ya kifahari sana kwa macho ya watu wengine, lakini nilihisi kama ina maana maalum kwangu. 

Niliamua kuivaa mara kwa mara bila kufikiria sana. Baada ya muda mfupi, nilianza kugundua mabadiliko madogo. SOMA ZAIDI.
Mwanaangu alikuwa mtoto mwenye akili nyingi.

Tatizo lilikuwa kwamba akili hizo hazikutumika kwenye mambo mazuri mara nyingi. Tangu akiwa mdogo, alikuwa na tabia ya kutotii maelekezo, kugombana na watoto wenzake, na kuingia matatizoni shuleni karibu kila wiki.
Mwanzoni niliamini ni hatua ya kawaida ya ukuaji.

Lakini kadri miaka ilivyopita, tabia zake zilianza kuwa mbaya zaidi. Simu kutoka shuleni zilikuwa za kawaida kwangu. 

Wakati mwingine niliitwa kwa sababu ya ugomvi, wakati mwingine kwa sababu ya kutoheshimu walimu, na mara nyingine kwa utundu uliowashangaza hata walimu wenye uzoefu. Kwa kweli nilichoka.

Nilijaribu kuzungumza naye kwa upole. Nilijaribu kumwadhibu alipokosea. Nilimpeleka kwa watu mbalimbali walioweza kumshauri. 

Kwa muda mfupi alionekana kubadilika, lakini baada ya siku chache mambo yalirudi kama zamani. Kilichoniumiza zaidi ni kusikia baadhi ya walimu wakisema walikuwa wamekata tamaa.SOMA ZAIDI.
Niliolewa nikiwa na matumaini ya kujenga familia yenye amani na furaha. Kwa miaka ya mwanzo, mambo yalikuwa mazuri. Lakini kadri muda ulivyopita, mume wangu alianza kutumia pombe kupita kiasi. Kile kilichoanza kama tabia ya mara chache kiligeuka kuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Nyumbani kwetu amani ilianza kupotea.
Alikuwa anarudi usiku sana, wakati mwingine bila maelezo yoyote. Ahadi za kuacha pombe zilikuwa nyingi, lakini baada ya siku chache alikuwa anarudia tabia ileile. Migogoro kati yetu iliongezeka na watoto wetu walianza kuathirika pia.

Kwa kweli nilichoka. Nilijaribu kuzungumza naye kwa upole. Nilimwomba afikirie familia yake na maisha yake ya baadaye. Wakati mwingine alikubali kuwa alikuwa na tatizo, lakini hakudumu kwenye uamuzi wake wa kubadilika. Miaka. SOMA ZAIDI.
Kwa miezi mingi, kijiji chetu kilikuwa kimekumbwa na wizi wa mara kwa mara. Watu walikuwa wanapoteza kuku, mbuzi, na hata mazao yaliyokuwa yamehifadhiwa baada ya mavuno. Kila mtu alikuwa na mashaka, lakini hakuna aliyekuwa anajua mwizi alikuwa nani.

Mimi pia nilikuwa miongoni mwa walioathirika.

Usiku mmoja nilikuta sehemu ya mazao yangu imeibiwa. Nilihuzunika sana kwa sababu nilikuwa nimefanya kazi kwa bidii kuyazalisha. 

Tulijaribu kupanga doria za usiku, lakini mwizi aliendelea kutoweka bila kuonekana. Kadri siku zilivyopita, hasira za wanakijiji ziliongezeka.
Watu wengi walikuwa wakituhumiana bila ushahidi.SOMA ZAIDI.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekifungia kiwanda cha SAN SHAN na BAI-LY PAPER CO. LTD kwa kukiuka sheria na taratibu za mazingira, hatua iliyochukuliwa baada ya timu ya ukaguzi wa mazingira uliofanyika katika Wilaya ya Mkuranga ukiongozwa na Meneja wa Utekelezaji wa Sheria wa NEMC, Mhandisi Luhuvilo Mwamila.
KAMPUNI ya Oryx Energies Tanzania imezindua kituo kipya cha mafuta eneo la Wazo jijini Dar es Salaam huku mkakati wa kampuni hiyo ukiwa ni kuendelea kusogeza huduma za nishati za mafuta na gesi karibu na wananchi.
SERIKALI imezitaka taasisi binafsi za elimu kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa mageuzi ya elimu yanayolenga kuimarisha ujuzi, sayansi na teknolojia, huku ikiipongeza Shule ya Kimataifa ya Luminous kwa mchango wake katika kukuza ubora wa elimu nchini.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

CHUO Cha Elimu ya Biashara (CBE) kimepanua wigo wa fursa za elimu ya juu nchini baada ya kupata ithibati kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kwa ajili ya kuendesha programu sita mpya zitakazoanza kupokea wanafunzi katika mwaka wa masomo 2026/2027.
Nilipoanza kazi katika kampuni niliyokuwa nikifanya kazi, nilikuwa na ndoto kubwa.

Nilitaka kujifunza, kukua kitaaluma, na siku moja kushika nafasi kubwa zaidi. Kwa hiyo nilijituma kwa bidii katika kila jukumu nililopewa. 

Nilifika kazini mapema, nilikamilisha kazi zangu kwa wakati, na nilijitahidi kufanya zaidi ya kile kilichotarajiwa.

Lakini miaka ilianza kupita bila mabadiliko yoyote. Watu waliokuja baada yangu walikuwa wakipandishwa vyeo huku mimi nikibaki kwenye nafasi ileile. 

Mara nyingi niliona mawazo yangu yakipuuzwa kwenye mikutano na mchango wangu kutotambuliwa hata nilipokuwa nimefanya kazi kubwa. Kwa kweli hali ile iliniumiza sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua uwezo wangu. Nilikuwa nikifanya kazi kwa bidii kuliko watu wengi waliokuwa wakinizunguka, lakini matokeo hayakuonekana. Kadri muda ulivyopita, nilianza kupoteza hamasa. 

Kulikuwa na siku nilijiuliza kama waajiri wangu walikuwa wanaona juhudi zangu. Wakati mwingine nilifikiria kuacha kazi na kuanza upya mahali pengine.

Lakini bado nilivumilia. Nilijikumbusha kwamba mafanikio wakati mwingine huchukua muda. Hata hivyo, moyoni nilitamani kuona siku ambayo juhudi zangu zingetambuliwa. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, nilihisi kama sauti yangu haikuwa na maana ndani ya familia yetu.

Kila kulipokuwa na kikao cha kifamilia, wazee na ndugu wengine walizungumza na kufanya maamuzi muhimu huku maoni yangu yakipuuzwa. Mara nyingi nilijaribu kutoa mawazo yangu, lakini watu walionekana kutoyapa uzito wowote.

Mwanzoni nilivumilia. Nilijiaminisha kwamba labda siku yangu ingefika. Lakini kadri miaka ilivyopita, hali haikubadilika. 

Wakati mwingine nilikuwa nikitoa wazo zuri ambalo lingesaidia familia, lakini hakuna aliyelisikiliza mpaka mtu mwingine aseme jambo lilelile.

Kwa kweli jambo hilo liliniumiza sana.
Nilianza kuhudhuria vikao vya familia bila hamasa. Nilijisikia kama mgeni badala ya sehemu ya familia ambayo nilikuwa nimeitumikia na kuijali kwa miaka mingi.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa nikijitahidi kuwasaidia ndugu zangu pale walipohitaji msaada. Lakini ilipofika wakati wa kufanya maamuzi, nilihisi kama mchango wangu haukuonekana kabisa.

Kadri muda ulivyopita, confidence yangu ilianza kupungua. Nilianza kukaa kimya hata nilipokuwa na mawazo mazuri kwa sababu tayari niliamini hakuna ambaye angesikiliza nilichokuwa nasema.SOMA ZAIDI.
Baada ya kupoteza kazi yangu, niliamini kwamba ningepata nyingine ndani ya muda mfupi.

Nilikuwa na uzoefu wa kazi, nilikuwa tayari kufanya kazi kwa bidii, na nilikuwa na matumaini kwamba waajiri wangetambua uwezo wangu. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyokuwa nimepanga. Miezi ilianza kupita.

Nilituma maombi ya kazi sehemu nyingi. Kila nilipoona tangazo la kazi, nilihakikisha nimetuma maombi yangu kwa wakati. Mara nyingine niliitwa kwenye usaili, lakini sikuwa nikichaguliwa. Mwaka mmoja ulipita. Kisha mwaka wa pili ukafika.

Kwa kweli hali ile ilianza kuniumiza sana. Niliona marafiki na watu niliokuwa nao wakipiga hatua maishani huku mimi nikiendelea kukaa nyumbani nikisubiri simu ambayo haikufika.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa mimi.

Baada ya kufeli usaili mara nyingi, confidence yangu ilishuka. Kila nilipoitwa kwenye interview mpya, nilikuwa naingia nikiwa tayari nimejiambia kwamba sitapata kazi. Kadri muda ulivyopita, matumaini yangu yalizidi kupungua.

Kulikuwa na siku nilizotaka kuacha kutuma maombi kabisa. SOMA ZAIDI.
Miaka miwili iliyopita, nilikuwa nikifanya biashara yangu kwa matumaini makubwa.

Biashara ilikuwa inaendelea vizuri na nilikuwa nimejijengea wateja wengi wa kudumu. Kwa sababu ya uaminifu tuliokuwa nao, mara nyingine nilikuwa nikiwaruhusu baadhi yao kuchukua bidhaa kwa mkopo na kulipa baadaye.

Mmoja wao alikuwa mteja niliyemwamini sana.
Tulikuwa tumefanya biashara kwa muda mrefu bila matatizo yoyote. Ndiyo maana sikuona shida aliponiomba bidhaa zenye thamani kubwa kwa ahadi kwamba angelipa ndani ya muda mfupi.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Siku za malipo zilipofika, simu zake zilianza kutopatikana. Ujumbe wangu haukujibiwa.

Nilijaribu kumtafuta kupitia marafiki na watu waliomfahamu, lakini sikufanikiwa. Kwa kweli nilihuzunika sana. 

Kiasi cha fedha alichokuwa anadaiwa kilikuwa kikubwa kwa biashara yangu. Hasara ile ilinifanya nipunguze baadhi ya mipango yangu na hata kushindwa kufanya manunuzi muhimu ya biashara kwa wakati.

Kadri miezi ilivyopita, matumaini yangu yalizidi kupungua. SOMA ZAIDI.

Kama mzazi, hakuna kitu kilichokuwa kinaniumiza zaidi kuliko kuona mtoto wangu akihangaika shuleni. Kwa miaka kadhaa, matokeo yake hayakuwa mazuri.

Kila muhula nilikuwa nikisubiri ripoti za shule kwa matumaini kwamba kungekuwa na mabadiliko, lakini mara nyingi nilibaki na maswali kuliko majibu.

Nilijaribu kila nilichoweza. Nilizungumza na walimu wake, nikamtafutia muda wa kusoma nyumbani, na nikajitahidi kumpa mazingira mazuri ya kujifunzia. Licha ya juhudi hizo zote, maendeleo yalikuwa madogo sana. Kwa kweli nilianza kuwa na wasiwasi.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua mtoto wangu alikuwa na uwezo. Alikuwa mwerevu na mwenye hamu ya kujifunza, lakini kwa sababu fulani matokeo yake hayakuonyesha uwezo huo.
Kadri miaka ilivyopita, confidence yake nayo ilianza kupungua.

Alianza kujilinganisha na wanafunzi wengine waliokuwa wakifanya vizuri zaidi. Wakati mwingine nilimwona akikatishwa tamaa na hata kuamini kwamba hangeweza kufanikiwa kama wenzake. 

Hali ile ilinivunja moyo. Nilitamani kuona mtoto wangu akiamini uwezo wake na kupata matokeo ambayo yangelingana na juhudi alizokuwa akiweka. SOMA ZAIDI.



Serikali imesema kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika ndani ya mwezi Septemba mwaka huu, hatua inayotarajiwa kuimarisha usafiri wa anga na kulipa hadhi zaidi jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya nchi.

Akizungumza wakati alipotembelea na kuona maendeleo ya mradi huo, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema ujenzi wa uwanja huo umefikia hatua za mwisho ambapo miundombinu mikubwa ikiwemo njia ya kuruka na kutua ndege pamoja na maeneo ya maegesho ya ndege imekamilika kwa kiwango kikubwa.

Mhe. Balozi Omar, alisema mradi huo ulianza kutekelezwa mwaka 2022 kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Mfuko wa Afrika Growing Together Fund (AGTF), ukiwa na lengo la kujenga uwanja wa kisasa utakaoendana na mahitaji ya Mji Mkuu wa nchi.

“Dodoma ni makao makuu ya nchi, hivyo ilikuwa muhimu kuwa na uwanja wa ndege wa kisasa unaoweza kukidhi ongezeko la shughuli za kiuchumi, kiserikali na kijamii,” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa, Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo iliyotolewa na watalaamu, sehemu ya kwanza inayohusisha miundombinu ya uwanja imefikia asilimia 86.73 ya utekelezaji, huku sehemu ya pili inayohusisha majengo muhimu ikiwemo jengo la abiria, mnara wa kuongozea ndege na jengo la zimamoto ikiwa imefikia asilimia 75.1.

“Uwanja huu utakuwa miongoni mwa viwanja vikubwa nchini, ukiwa na njia ya kuruka na kutua ndege yenye urefu wa kilomita 3.6 na upana wa mita 60, pamoja na maegesho makubwa ya ndege yatakayowezesha kuhudumia ndege nyingi kwa wakati mmoja” aliongeza Mhe. Balozi Omar.

Aidha Mhe. Balozi Omar, alisema Kukamilika kwa Uwanja huo kunatarajiwa kuufungua zaidi mji wa Dodoma kwa safari za ndani na kimataifa, huku ukiongeza mvuto wa uwekezaji, kuimarisha nafasi ya Tanzania katika sekta ya usafiri wa anga katika ukanda wa Afrika Mashariki, kwa kuwa jengo la abiria litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni 1.5 kwa mwaka, jambo linalotarajiwa kuongeza uwezo wa Dodoma kupokea wageni wa ndani na nje ya nchi pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Mradi huo pia unahusisha ujenzi wa mnara wa kisasa wa kuongozea ndege wenye urefu wa mita 56.2, jengo la zimamoto la kiwango cha kimataifa, majengo ya kuzalisha umeme na jengo la hali ya hewa lenye vifaa vya kisasa vya usimamizi wa usafiri wa anga.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Godfrey Kasekenya (Mb) alisema kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato ni miongoni mwa miradi muhimu ya kimkakati na ya kielelezo inayotekelezwa nchini chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Alisema mradi huo umebuniwa kwa mtazamo wa muda mrefu, ukiwa na uwezo wa kupanuliwa hatua kwa hatua kulingana na ongezeko la mahitaji ya usafiri wa anga nchini.

“Uwanja huu umejengwa kwa viwango vya kisasa vya kimataifa na unatarajiwa kuwa miongoni mwa viwanja vya ndege vya kisasa zaidi nchini mara utakapoanza kutumika” alisema Mhe. Kasekenya

Alisisitiza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika kwa wakati ili ahadi ya kuanza kwa shughuli za uwanja huo mwezi Septemba itimie, huku akibainisha kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha miundombinu ya usafiri na kukuza uchumi wa Taifa kupitia uwekezaji mkubwa wa kimkakati.

Katika Ziara hiyo Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, aliambatana na Naibu Mawaziri wake, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), Mhe. Laurent Luswetula, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha ambaye pia ni Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha ambaye pia ni Kamishna wa Idara ya Fedha za Nje, Bw. Rished Bade, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Balozi Mhandisi Aisha Amour pamoja na wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Fedha, Wizara ya Ujenzi wakiwemo Wakala wa Barabara nchini (Tanroads).