Mafunzo ya utoaji wa elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi yanaendelea kufanyika katika Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, yakilenga kuwaongezea wananchi uelewa kuhusu fursa za kupata mitaji na huduma za maendeleo ya biashara ili kukuza shughuli za kiuchumi.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Naibu Katibu  Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,Prof. Daniel Mushi,akizungumza wakati wa  kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma.
  
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,(hayupo pichani)  wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Na.Alex Sonna-DODOMA
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, ametoa maagizo matano kwa viongozi na watumishi wa sekta ya elimu nchini ili kuhakikisha sekta hiyo inaendana na mahitaji ya maendeleo ya taifa na mabadiliko ya dunia.
Prof.Nombo ametoa maagizo hayo leo Julai 13,2026 jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda.
Amesema mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu yametokana na ushirikiano na utendaji mzuri wa viongozi na watumishi wa wizara pamoja na taasisi zake, huku akisisitiza kuwa kikao hicho ni fursa muhimu ya kutathmini mafanikio na kupanga mwelekeo wa sekta kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
"Ndiyo maana tumeona ni muhimu kuwashirikisha wataalamu kutoka Tume ya Mipango ili kutusaidia kuona namna sekta ya elimu itakavyochangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Tunaamini dira hiyo ndiyo itakayotuongoza katika kukidhi mahitaji ya taifa kwa miaka ijayo," amesema Prof.Nombo
Prof.Nombo ameelekeza mapitio ya mara kwa mara ya kozi na programu za elimu ili ziendane na mahitaji ya sasa ya jamii, uchumi na soko la ajira. Amesema mjadala unaoendelea katika mitandao ya kijamii kuhusu uchaguzi wa kozi kwa wahitimu wa kidato cha sita unaonesha wazi kuwa kuna mahitaji mapya ya ujuzi na taaluma yanayopaswa kuzingatiwa.
"Mrejesho tunaoupata unatufanya tujitathmini na kuangalia aina ya kozi tunazotoa ili ziendane na mahitaji ya sasa ya jamii na uchumi. Tunahitaji kuongeza ubunifu na unyumbufu katika kuwapa wanafunzi fursa ya kusoma kozi zitakazochangia maendeleo ya taifa," amesema 
Kuhusu Mfumo wa Taarifa za Usimamizi wa Elimu (ESMIS), Prof.Nombo amesisitiza umuhimu wa kuwa na takwimu sahihi kwa ajili ya kufanya maamuzi yenye tija na kuagiza taasisi zote kuhakikisha mifumo yao ya TEHAMA inaunganishwa na mfumo huo.
Amesema hatua hiyo inatekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mifumo ya Serikali inasomana na kufanya kazi kwa pamoja, akibainisha kuwa wizara imeweka suala hilo kuwa kipaumbele.
Aidha, amehimiza kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika uwekezaji wa sekta ya elimu ili kuboresha huduma na miundombinu, pamoja na kutafuta mbinu mbadala za kugharamia sekta hiyo ili kuongeza fursa za wanafunzi wengi zaidi kuendelea na masomo.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Daniel Mushi, amewataka washiriki wa kikao kuendelea kueleza mafanikio yanayopatikana kupitia utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali za Serikali katika sekta ya elimu.
"Hatupaswi kusita kueleza mazuri ambayo Serikali inaendelea kuyafanya kwa wananchi kwa pamoja tunaweza kuijenga sekta ya elimu yenye ushindani, ubora na tija kwa maendeleo ya taifa," amesema  Prof Mushi
Katika kikao hicho, washiriki wamepokea na kujadili mawasilisho mbalimbali ikiwemo nafasi ya elimu, sayansi na teknolojia katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, umuhimu wa mifumo ya TEHAMA katika kuongeza ufanisi wa utoaji huduma.
Vilevile,matumizi ya mfumo wa ESMIS, pamoja na Mpango Mkakati wa Wizara wa mwaka 2026/27 hadi 2030/31 na utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/27.
Nilikuwa mkulima wa kawaida katika kijiji kimoja mkoani Mara. Maisha yangu yalitegemea kilimo na ufugaji mdogo wa samaki. 

Kwa miaka mingi nilikuwa nikijitahidi, lakini kila nilichokifanya kilionekana kutokwenda sawa. Mashamba yalikuwa yakikauka, biashara ndogo niliyokuwa nayo haikutoa faida, na nilikuwa nimeanza kukata tamaa.

Usiku mmoja nilipata ndoto ya ajabu sana. Niliota nimesimama kando ya mto mkubwa uliokuwa karibu na kijiji chetu. 

Maji yake yalikuwa meusi, na ghafla niliona maelfu ya samaki waliokufa wakielea juu ya maji. Nilihisi hofu kubwa katika ndoto hiyo. Kisha nikasikia sauti ikisema, “Kuna jambo kubwa linakaribia kutokea.”

Nilipoamka asubuhi, moyo wangu ulikuwa mzito. Sikuwa na amani kabisa. Saa chache baadaye nilipigiwa simu na kaka yangu aliyekuwa akiishi mjini.

 Aliniambia kuwa mtu mmoja wa familia yetu alikuwa ameugua ghafla na pia kulikuwa na mgogoro mkubwa kuhusu shamba la urithi ambalo lilikuwa limefichwa kwa miaka mingi. Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

Nilimuoa mke wangu nikiwa na matumaini makubwa ya maisha. Tulianza ndoa yetu tukiwa na mapenzi makubwa na ndoto nyingi. 

Wakati huo nilikuwa na duka la vifaa vya ujenzi lililokuwa linaendelea vizuri, na niliamini baada ya miaka michache tungejenga nyumba kubwa na kuwapa watoto wetu maisha mazuri.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Kila biashara niliyoanzisha ilianguka bila sababu ya kueleweka. Niliwahi kufungua duka la jumla, likafungwa baada ya miezi sita. Nikajaribu biashara ya mazao, nikapata hasara kubwa.

Hata nilipoingia kwenye biashara ya usafirishaji, gari langu liliharibika mara kwa mara hadi nikauza kwa hasara. Kilichonishangaza ni kwamba watu waliokuwa wanaanza biashara baada yangu walikuwa wakifanikiwa, lakini mimi nilikuwa narudi nyuma kila mwaka.

Madeni yaliongezeka, amani ikatoweka nyumbani, na mara kwa mara nilijikuta nikigombana na mke wangu. Miaka saba ilipita katika hali hiyo.

Siku moja, mke wangu alisafiri kwenda kumtembelea mama yake. Alisahau begi lake nyumbani. Nilipokuwa nikitafuta kitabu cha watoto ndani ya begi hilo, niliona bahasha ndogo iliyokuwa imefungwa.

Ndani yake kulikuwa na vitu vya ajabu picha yangu ndogo, vipande vya kitambaa nilivyokuwa nimevaa zamani na karatasi zilizoandikwa maneno nisiyoyafahamu. Nilishtuka sana. Mke wangu aliporudi, nilimuuliza kuhusu vitu hivyo.

Alianza kulia na baada ya muda mrefu alikiri ukweli. Aliniambia kwamba miaka mingi iliyopita, kabla hatujaoana, alienda kwa mganga kwa sababu aliogopa nitamuacha. Alipewa vitu hivyo na kuambiwa avihifadhi ili nibaki karibu naye milele.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.
Kwa miaka saba ya maisha yangu, maumivu ya mgongo yalikuwa sehemu ya maisha yangu ya kila siku. Kila nilipoamka asubuhi, nilihitaji dakika kadhaa kabla ya kusimama vizuri kutoka kitandani. 

Nilikuwa nikihisi maumivu makali kuanzia sehemu ya chini ya mgongo hadi miguuni. Wakati mwingine nilishindwa hata kuinama kuchukua kitu kilichoanguka chini.

Mwanzoni nilidhani ni uchovu wa kawaida kwa sababu nilikuwa nafanya kazi ya useremala. Lakini kadri miezi ilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya. 

Nilitembelea hospitali kadhaa na kufanyiwa vipimo tofauti. Madaktari walinipa dawa za maumivu na kunishauri nipumzike zaidi, lakini baada ya muda mfupi maumivu yalikuwa yanarudi tena.

Nilitumia pesa nyingi kutafuta matibabu. Wakati mwingine nililala chini kwa sababu sikuweza kupanda kitandani kutokana na maumivu. 

Familia yangu ilianza kuwa na wasiwasi, na biashara yangu ilianza kuyumba kwa sababu sikuweza kufanya kazi kwa muda mrefu kama zamani.

Mke wangu ndiye aliyekuwa akinisaidia kwa karibu kila kitu. Kuna siku nilishindwa hata kumbeba mwanangu mdogo kwa sababu mgongo wangu ulikuwa unauma sana. Nilijikuta nikipoteza matumaini na kuanza kuamini kwamba ningekaa na maumivu hayo maisha yangu yote.

Siku moja nilikutana na rafiki yangu wa zamani ambaye nilikuwa sijamuona kwa miaka kadhaa. Alinishangaa kuniona nikitembea kwa shida.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.

 

Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi  ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
















Na. OWM (KAM), Dar es Salaam

Kamishna wa Uhamiaji wa Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, CI Fakih Nyakunga, ameiomba Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) kupitia Idara ya Kazi kuhakikisha vibali vya kazi vinatolewa kwa raia wa kigeni wenye ujuzi ambao haupatikani nchini Tanzania ili kulinda ajira za wazawa.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa, amesimamisha shughuli za Kiwanda cha Hangjin Steel kinachojihusisha na uzalishaji wa nondo kwa kutumia vyuma chakavu, kilichopo Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, baada ya kubainika kukiuka masharti ya Sheria ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe, amewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya kumuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ufunguzi wa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Mafunzo hayo yatafanyika kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026 katika Manispaa ya Sumbawanga, yakiwa yameratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Prof. Shemdoe alipokelewa katika Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Makongoro Nyerere akiambatana na Mhe. Mhe. Jacqueline Mzindakaya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Kesho, Julai 13, 2026, Prof. Shemdoe atafungua rasmi mafunzo hayo katika Ukumbi wa Country Hotel, ambapo yanatarajiwa kuwakutanisha wananchi, wajasiriamali, vikundi vya wanawake na vijana, makundi yenye mahitaji maalum pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu fursa za mitaji, mikopo na huduma mbalimbali za uwezeshaji zinazotolewa na Serikali na taasisi zake, ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji, kukuza biashara, kuongeza ajira na kuinua kipato cha familia.

Mafunzo hayo pia yanatarajiwa kuwapa washiriki taarifa sahihi kuhusu namna ya kufikia huduma za kifedha na programu za uwezeshaji wa kiuchumi, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Rukwa kwa ujumla.














Kwa miaka mingi niliamini kuwa nilizaliwa chini ya nyota mbaya. Kila nilipopata kazi, mambo yalikuwa yanaenda vizuri kwa miezi michache, halafu matatizo ya ajabu yalianza. 

Wakati mwingine nilisingiziwa makosa ambayo sikufanya, wakati mwingine kampuni ilifunga ghafla, na mara nyingine nilifukuzwa bila maelezo yoyote.

Ndani ya miaka sita nilifukuzwa kazi mara nne. Hali hiyo ilinivunja moyo sana. Marafiki waliniona kama mtu asiye na bahati, na hata familia yangu ilianza kunipotezea imani.

Nilikuwa nimeoa na nilikuwa na watoto wawili, hivyo kila nilipopoteza kazi, maisha ya familia yangu yalizidi kuwa magumu.

Siku moja, nikiwa nimekata tamaa kabisa, nilikutana na mwanaume mmoja ambaye nilikuwa nimewahi kufanya naye kazi zamani. 

Nilimkuta anaendesha kampuni yake mwenyewe na maisha yake yalikuwa yamebadilika sana. 

Nilimweleza matatizo yangu, naye akaniambia kuwa wakati mwingine kuna vikwazo vya kiroho vinavyoweza kumfanya mtu ashindwe kudumu katika kazi au kufanikiwa.SOMA ZAIDI.
Nilianza ufugaji wa ng’ombe miaka saba iliyopita baada ya kustaafu kazi yangu ya udereva. Nilikuwa na ng’ombe 18 wa maziwa na biashara yangu ilikuwa inaendelea vizuri sana. Kila siku nilikuwa napata maziwa mengi na kuuza kwa hoteli na majirani.

Watu wengi walinipongeza kwa mafanikio yangu, na niliamini maisha yangu yalikuwa yamekaa sawa. Lakini ghafla mambo yalianza kubadilika. 

Ng’ombe mmoja aliugua na kufa bila sababu ya kueleweka. Baada ya wiki mbili, mwingine naye akafa. Ndani ya miezi mitatu nilikuwa nimepoteza ng’ombe sita.

Nilimuita daktari wa mifugo mara kadhaa. Aliwachunguza waliobaki na kuwapa dawa, lakini bado vifo viliendelea. 

Kilichonishangaza zaidi ni kwamba ng’ombe walikuwa wanaonekana wenye afya mchana, lakini asubuhi nilikuwa nakuta mmoja ameanguka na kufa.

Hasara ilianza kuwa kubwa. Nilishindwa kulipa ada za watoto na hata chakula cha mifugo kilianza kuwa tatizo. 

Watu kijijini walianza kunisema kuwa bahati yangu imeisha. Wengine waliniambia niuze ng’ombe waliobaki kabla wote hawajakufa.

Siku moja, mzee mmoja jirani yangu aliniuliza swali la ajabu. “Umeshawahi kukagua zizi lako usiku?” Nilimjibu hapana.

Aliniambia kuna mambo ambayo hayaonekani mchana. Alinieleza kuwa kuna watu wenye wivu wanaweza kutumia nguvu za giza kuharibu mifugo ya mtu anayefanikiwa. SOMA ZAIDI.
Nilikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho chuoni na nilikuwa nimebakiza wiki moja tu kufanya mitihani yangu ya mwisho.

Nilikuwa nimehangaika kwa miaka mitatu, nikifanya kazi ndogo ndogo ili kujilipia ada na mahitaji mengine. Ndoto yangu ilikuwa moja tu kuhitimu na kuibadilisha maisha ya familia yangu.

Siku moja nilipokuwa nikitoka darasani, niliitwa katika ofisi ya utawala. Nilidhani ni jambo la kawaida, lakini nilipoingia, nilikabidhiwa barua iliyosema kuwa nilikuwa nimefukuzwa chuo kutokana na deni la ada na madai ya ukiukaji wa kanuni za chuo.

Nilishangaa sana. Kwanza, nilikuwa nimebakiza kiasi kidogo sana cha ada ambacho nilikuwa nimeahidi kulipa baada ya mitihani. Pili, sikuwahi kuvunja sheria za chuo. Nilijaribu kujitetea lakini hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza.

Nilitoka ofisini nikiwa nimevunjika moyo. Nililia sana usiku huo. Niliona ndoto zangu zote zikifutika mbele ya macho yangu. Nilijiuliza ningewaambia nini wazazi wangu ambao walikuwa wamejitolea kila kitu ili nisome.

Rafiki yangu mmoja aliponiona katika hali hiyo, aliniambia nisikate tamaa. SOMA ZAIDI.

 

Katika kuonesha ujirani mwema Mbunge wa Kiteto Edward Ole Lekaita na Mbunge wa Kilindi Salehe Mhando wameamua kushirikiana kuhakikisha barabara ya Lengatei- Songe inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe na kupitika kwa mwaka mzima.

Mbali ya kushirikiana kusimamia Ujenzi wa barabara hiyo pia Wabunge hao wameshiriki shughuli ya uzinduzi wa shule ya awali na msingi Kijiji cha Lesiot Kata ya Lengatei Kiteto.