Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Na.Alex Sonna-,Kisarawe

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ametangaza kuanza kutolewa kwa Tuzo ya Jafo ya Ufanisi wa Juu kwa Mradi wa Maendeleo, ikiwa ni mpango wa kutambua na kuhamasisha utendaji bora, ubunifu na uwajibikaji miongoni mwa Wenyeviti wa Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe.

Akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wilayani humo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo, Dkt. Jafo amesema tuzo hiyo (JAFO’s High Perfomance Development Project Award), inalenga kukuza ufanisi wa juu katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, kuongeza uwajibikaji na kuibua ushindani chanya miongoni mwa wenyeviti hao.

Amesema tuzo hiyo itatolewa kila mwaka ili kumtambua na kumzawadia Mwenyekiti au Mwakilishi wa Kijiji aliyeonesha utendaji wa hali ya juu, ubunifu na matokeo yanayopimika katika kusimamia mradi ndani ya Halmashauri hiyo

“Tuzo hii ni kwa Mwenyekiti wa Kijiji au mwakilishi wa kijiji atakayeng’ara kwa mafanikio ya kipekee katika kuibua, kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kasi, hususan ile yenye athari chanya katika sekta za afya, elimu, kilimo, biashara, michezo na miundombinu, ninalenga kuhamasisha viongozi wetu wa vijiji kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uwazi zaidi. Tunataka kuona matokeo halisi yanayogusa maisha ya wananchi,” amesema Dkt. Jafo.

Mbunge huyo ameongeza kuwa tathmini ya mshindi wa tuzo hiyo itazingatia vigezo mbalimbali, ikiwemo utekelezaji wa miradi yenye athari kubwa ndani ya muda uliopangwa, maboresho yanayopimika katika utoaji wa huduma, usimamizi bora wa rasilimali, ushiriki wa wananchi na wadau pamoja na uendelevu wa miradi iliyotekelezwa.

Amesema pia tuzo hiyo itahusishwa moja kwa moja na mradi au mpango mahsusi wa maendeleo, ambapo ushahidi wa matokeo kama ongezeko la ufanisi, ubora wa huduma na kuridhika kwa wananchi utatumika kama msingi wa tathmini.

Awali, Dkt. Jafo amepongeza mchango mkubwa wa Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji, akisema wao ni kiungo muhimu katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya serikali ngazi ya msingi.

Ameeleza kuwa mkutano huo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wake wa uongozi wa miaka 2025–2030, akisisitiza dhamira ya kufanya kazi kwa kasi ya ‘chaka kwa chaka’ ili kuharakisha maendeleo vijijini.

Amebainisha kuwa kupitia usimamizi bora wa viongozi wa vijiji, azma ya kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati ifikapo mwaka 2030, pamoja na kuimarisha sekta ya elimu na shughuli za kiuchumi, itawezekana kwa vitendo.

“Ndani ya miaka mitano ijayo tunahitaji kufanya kazi kwa mchakamchaka, kuanzia ukusanyaji wa mapato hadi matumizi yake, ili miradi ya maendeleo isimamiwe kwa ufanisi na kuleta matokeo yanayoonekana kwa wananchi,” amesisitiza.

Nao baadhi ya wenyeviti wa vijiji na vitongoji wamempongeza Dkt Jafo kwa ubunifu huo, wakisema kuwa utaongeza hamasa na ushindani chanya wa kimaendeleo katika Halmashauri ya Kisarawe.

Wamesema tayari wamejipanga kikamilifu kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao ili kuongeza ufanisi na hatimaye kuibuka washindi wa tuzo hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,aakiwasili katika ukumbi wa halmashauri wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuzungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo ya  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Nyahori Mahumbwe,wakati ,akizungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare,,wakati ,akizungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Afisa Utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Bi.Sabra Mwankenja wakati ,akizungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.




Na Oscar Assenga, LUSHOTO.

MATEMBEZI Maalumu ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Mazingira Asilia Magamba (Magamba Forest Walkathon and Andventure Season 111) yenye lengo la kutangaza na kuhamasisha utalii zinatarajiwa kufanyika Desemba 17 -20 katika mji wa Lushoto mkoani Tanga huku maandalizi yakielezwa kukamilika kwa asilimia 85.

Akizungumza na Mtandao huo Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Misitu ya Mazingira Asilia Magamba, Christoganus Vyokuta amesema kwamba kuelekea mbio hizo wadau mbalimbali wa uhifadhi na utalii watapata fursa ya kujitangaza na kuonesha huduma na bidhaa zao mjini Lushoto.

Alisema kilele cha mbio hizo kitafanyika Desemba 20 ambapo washiriki watashiriki katika matembezi maalumu ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Magamba ikiwa ni sehemu ya kutangaza pia vivutio vya utalii vilivyopo ndani ya hifadhi ya Mazingira Asilia ya Magamba wilayani humo

Mhifadhi huyo alisema pia lengo jingine la mbio hizo za Magamba Forest Walkathon and Adventure Season III ni kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi wa mazingira na kukuza utalii ikolojia ikiwemo kuhamasisha Watanzania kutembelea vivutio vya asili vilivyopo nchini.

Mhifadhi huyo amewataka wananchi na wadau wa sekta ya utalii kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo huku akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kulinda rasilimali za asili na kuhakikisha uhifadhi endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema kuwa sekta ya Elimu, hususan elimu ya Juu ina mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa, kutokana na kuzalisha nguvukazi inayoshiriki kutoa huduma katika sekta mbalimbali.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe alipokutana nao kwa ajili ya kuzungumzia maendeleo ya kisarawe pamoja na kuwashukuru kwa kuchaguliwa katika uchaguzi uliomalizika.

Na Alex Sonna, Kisarawe

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewaambia Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kuwa kipindi cha miaka mitano ijayo kitakuwa cha mchakamchaka wa maendeleo, akisisitiza kuwa wana jukumu kubwa la kuwatumikia wananchi kwa ufanisi na mshikamano.

Akizungumza katika kikao cha kuwashukuru na kuomba ushirikiano wa madiwani hao, Dkt. Jafo amesema amejipanga kuhakikisha anatafuta rasilimali fedha zitakazosaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata zote za wilaya hiyo.

Amesema matarajio ya wananchi ni makubwa, hivyo madiwani wanapaswa kutambua uzito wa dhamana waliyopewa na wananchi.

“Chaguzi zote zimekwisha. Tulianza na kura za maoni, tukapita kwenye uchaguzi mkuu na uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri. Kila uchaguzi huwa na makundi, lakini sasa ni wakati wa kuungana na kushirikiana kwa ajenda moja ya maendeleo,” amesema Dkt. Jafo.

Mbunge huyo ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Baraza la Madiwani ili liweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, akibainisha kuwa tayari ameshawasilisha maombi mbalimbali serikalini yanayohusu ujenzi wa shule mpya na kuboresha miundombinu ya shule zilizopo.

“Nitahangaika kwa kila hali kuhakikisha tunasonga mbele kama halmashauri. Maombi ya ujenzi wa shule mpya na miundombinu ya elimu yameshapokelewa na serikali,” amesema.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha sasa atakuwa karibu zaidi na wananchi kwa kufanya ziara nyingi vijijini, kutoa taarifa na kusikiliza changamoto zao, huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano.

“Tusikubali kugawanywa, kwa sababu tukiruhusu hilo tutaleta udhaifu. Tufanye kazi kama timu, tushirikiane na tupendane, wote tuwe kitu kimoja,” amesema.

Kwa upande wa sekta ya afya, Dkt. Jafo amesema amejipanga kuweka historia mpya kwa kuhakikisha kila kijiji katika Wilaya ya Kisarawe kinakuwa na zahanati, ili kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Aidha, amewataka madiwani kusimamia kwa karibu matumizi ya mapato ya ndani ili yatumike kwa usahihi na kuleta matokeo yanayo onekana.

“Haiwezekani mwaka ukapita bila kuwa na kitu kinacho onekana kimefanyika. Lazima fedha tunazo kusanya ziwe na matunda kwa wananchi,” amesema.

“Nikuhakikishie Mwenyekiti, miradi ya maendeleo tutahangaika nayo kwa ujumla wake. Tunaahidi mengi vijijini, hivyo ushirikiano na kupendana ni jambo la msingi ili tufanikiwe,” amesema.

Amewahimiza madiwani hao kwenda kuwashukuru wananchi waliowaamini na kuwachagua, akisisitiza kuwa mafanikio ya safari ya miaka mitano ijayo yatategemea namna watakavyoanza na kuendeleza kazi ya kuwatumikia wananchi kwa bidii na uadilifu.

   

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewahimiza watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kufanya kazi kwa weledi, bidii na kwa kushirikiana kwa karibu na Baraza la Madiwani ili kuchochea maendeleo ya wilaya hiyo na kuboresha utoaji wa huduma za msingi kwa wananchi.

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo, ambapo amesema lengo la kikao hicho lilikuwa ni kuwashukuru kwa kazi wanazozifanya na kuwaomba waendelee kutoa ushirikiano katika kuwatumikia wananchi wa Kisarawe.

“Ni muhimu kupendana na kushirikiana kama watumishi wa Serikali. Fanyeni kazi bila kuchoka, kwa kuwa mnalipwa mshahara wakati wapo wananchi wengi bado hawana ajira. Fanyeni kazi kama ibada; mkifanya hivyo kwa moyo wote mtapata mafanikio makubwa,” amesema Dkt. Jafo.

Ameongeza kuwa watumishi wanapaswa kujiepusha na utendaji wa mazoea na badala yake wafanye kazi kwa ubunifu na uwajibikaji, huku wakiacha alama chanya katika maeneo wanayoyahudumia.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutafuta rasilimali fedha na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za miradi ili miradi hiyo iwe na tija na kuleta manufaa kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Nyahori Mahumbwe, ameahidi kumpa ushirikiano Mbunge huyo katika kuwatumikia wananchi na kutekeleza ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi.

“Tupo tayari kufanya kazi mchana na usiku kuwatumikia wananchi na kutekeleza ahadi mlizozitoa wakati wa uchaguzi. Watekelezaji wa mkataba ule ni sisi watumishi wa Serikali, hivyo tutahakikisha tunashirikiana kikamilifu kutekeleza Ilani ya Uchaguzi,” amesema Mahumbwe.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare, amesema madiwani wapo tayari kufanya kazi kwa weledi na mshikamano katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Sehemu ya watumishi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,wakati akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Nyahori Mahumbwe,wakati ,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza KMwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare,wakati ,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Afisa Utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Bi.Sabra Mwankenja,wakati ,akizungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Sehemu ya watumishi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo (hayupo pichani) ,wakati akizungumza na watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo ,akiwa katika picha ya pamoja ,mara baada ya kuzungumza na watumishi  wa Halmashauri hiyo  wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya katika wilaya hiyo.