Na OWM - TAMISEMI, Lushoto


Mhe. Alhaji Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar,  amekubali ombi la Mbunge wa Jimbo la Lushoto Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa kutoa mchango wa Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya kuendeleza Kituo cha Elimu ya Kiislamu Irshaad (Irshaad Islamic Centre) kilichopo Lushoto, mkoani Tanga.

Fedha hizo zinatarajiwa kuwezesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kituo hicho, ikiwemo kuboresha Chuo cha Ufundi, kuanzisha bustani ya kisasa, kujenga madrasa yenye kukidhi mahitaji ya wanafunzi, kujenga nyumba za walimu, jengo la kupokelea wageni, hospitali pamoja na ukumbi wa kisasa wa kufanyia shughuli mbalimbali za kielimu na kijamii.

Prof. Shemdoe alitoa ombi hilo Julai 5, 2026 wakati wa Sherehe ya Maulidi ya Kumswalia Mtume Muhammad S.A.W iliyoandaliwa na Sheikh Sharrif Hussein Ahmad Badawiyy wa Kituo cha Irshaad Islamic Centre Lushoto, ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Dkt. Hussein Mwinyi amekubali ombi la Rais wa Kituo cha Irshaad Islamic Centre Lushoto Sheikh Sharrif Hussein Ahmad Badawiyy la kumwomba awe mlezi wa kituo hicho, ambapo Mhe. Dkt. Dkt. Hussein Mwinyi ameahidi kuendelea kushirikiana na viongozi pamoja na wadau mbalimbali katika kukiendeleza ili kiwe kitovu cha utoaji wa elimu bora na maadili mema.

Sanjari na hilo, Mhe. Rais Dkt.  Mwinyi ameridhia pia ombi la Rais wa Kituo hicho cha Irshaad Islamic Centre la kumtaka kuridhia jina la Hayati Alhaji Ali Hassan Mwinyi, litumike katika eneo la bustani linalotarajiwa kujengwa katika Chuo cha Ufundi kilichopo ndani ya kituo hicho, ikiwa ni sehemu ya kumuenzi na kutambua mchango wa maendeleo alioutoa Hayati Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiwa ni mlezi wa kituo hicho. 

Mhe. Prof. Shemdoe alimuunga mkono Mhe. Rais Dkt. Hussein Mwinyi kwa kuchangia Shilingi Milioni 20, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt. Batilda Burian  Milioni 5, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima Milioni 5, Mbunge wa Bumbuli Mhe. Mhandisi Ramadhani Hamza Milioni 5, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Bw. Rajab Abdallah Milioni 3 na Mbunge wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Abdullah Makame amechanga Milioni 5 na kufanya jumla ya fedha zilichangwa kuwa Milioni 248, hatua iliyoonyesha mshikamano wa viongozi hao katika kuunga mkono maendeleo ya elimu na ustawi wa jamii. 

Akizungumza mara baada ya hafla hiyo, Mhe. Prof. Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Mwinyi kwa kukubali ombi hilo, akieleza kuwa msaada huo utakuwa chachu ya kuinua viwango vya elimu, ustawi wa jamii na huduma zinazotolewa katika kituo hicho, ambacho kimeendelea kuwa nguzo muhimu ya malezi na elimu kwa vijana wa Lushoto na maeneo jirani.

Aidha, Wananchi na viongozi waliohudhuria hafla hiyo wamempongeza Mhe. Rais Dkt. Mwinyi kwa kukubali maombi yaliyowasilishwa na Mhe. Prof. Shemdoe, wakieleza kuwa uamuzi huo utaacha alama ya kudumu katika maendeleo ya Kituo cha Elimu ya Kiislamu Irshad Lushoto na kuongeza fursa za elimu, ujuzi na huduma za kijamii kwa vizazi vya sasa na vijavyo.














 


Kukamilika kwa ujenzi wa Barabara ya kutoka Longido - Samia Longido Girls Kijiji cha Oltepesi, Kata ya Orbomba, kunatarajiwa kuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa Wilaya ya Longido kwa kuboresha usafiri, mawasiliano, biashara na fursa za uwekezaji.

Hayo yameselwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang'onda, wakati akiweka Jiwe la Msingi  mradi wa barabara yenye urefu wa kilometa 0.84, mradi unaogharimu kiasi cha shilingi milioni 395.

" Kukamilika kwa barabara hiyo itarahisisha usafiri wa wananchi, kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii na kufungua fursa mpya za shughuli za kiuchumi kwa wakazi wa eneo hilo, hivyo mkandarasi unatakiwa kukamilisha kazi zilizobaki kwa kuzingatia viwango vya ubora vilivyowekwa". Amebainisha Mwang'onda

Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Longido, Mhandisi Lawrence Msemo, amesema barabara hiyo ina urefu wa jumla wa kilometa 0.84, ambapo awamu ya kwanza yenye urefu wa kilometa 0.3.

Ameeleza kuwa mradi huo ulianzishwa kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Longido Girls, huku kazi zilizobaki zikihusisha ujenzi wa mifereji ya maji.

Kwa mujibu wa Msemo, barabara hiyo inaunganisha Mji wa Longido na Shule ya Sekondari ya Wasichana Longido Girls, ambayo ni shule muhimu ya Mkoa wa Arusha, hivyo itarahisisha usafiri kwa wanafunzi, walimu na wananchi wa maeneo jirani.

Baadhi ya wananchi walieleza kufurahishwa na utekelezaji wa mradi huo. Mkazi wa eneo hilo, Losiana Lomayan, alisema barabara hiyo itachochea ukuaji wa uchumi wa wilaya, huku mwanafunzi Salome John akiishukuru Serikali kwa kuwajengea barabara ya lami.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Dk. Stephen Kiruswa, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara katika Wilaya ya Longido kulingana na bajeti zilizotengwa.









 


Katika siku ya nane (08) ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama SabaSaba, yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Wakala wa Vipimo (WMA) imeendeleza mkakati wake wa kuwatembelea wajasiriamali na kuwapatia elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo. 

Zoezi la utoaji elimu ya vipimo kwa wajasiriamali linaenda sambamba na kuhudumia wadau mbalimbali wanaotembelea banda la WMA katika Maonesho hayo ya SabaSaba. 

Lengo ni kuhakikisha elimu na huduma mbalimbali za ki-vipimo zinafikishwa kwa wadau wengi kadri iwezekanavyo.

Pichani ni matukio mbalimbali kuhusu utoaji elimu na huduma za ki-vipimo kwa wananchi na wadau, leo Julai 05, 2026.







. Amshukuru Rais Samia kwa kuidhinisha fedha hizo.


Na. OWM -TAMISEMI, Ulanga.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha huduma za afya msingi kwa kujenga na kukarabati  miundombinu ya zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya, ambapo Shilingi Bilioni 1.25 zimetolewa kuboresha utoaji wa huduma katika Hospitali ya Mahenge, wilayani Ulanga.

Prof. Shemdoe amesema hayo Julai 4, 2026, wakati wa muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kukagua na kuhimiza uwajibikaji alipotembelea hospitali ya Mahenge.

Prof. Shemdoe amesisitiza kuwa, Serikali imedhamiria kuendelea kuimarisha sekta ya afya kwa kuwezesha ujenzi wa   miundombinu bora itakayorahisisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Prof. Shemdoe amesema fedha hizo zilizoidhinishwa na kutolewa na Mhe. Rais zitatumika kujenga jengo la huduma za dharura, wodi ya wazazi, kliniki ya watoto pamoja na uzio wa hospitali utakaoimarisha usalama wa wananchi wanaofuata huduma na kuimarisha ulinzi wa miundombinu ya hospitali hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogor Iio, Mhe. Adam  Malima, amesema uwekezaji huo ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kuhakikisha huduma bora za afya zinawafikia wananchi.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Mhe. Salim Alaudin, amesema uboreshaji wa Hospitali ya Mahenge utawanufaisha wananchi wa Ulanga ambao hapo awali walilazimika kufuata huduma za dharura katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara, hali iliyokuwa ikisababisha adha kubwa kwa wananchi na  kusababisha  vifo vya baadhi ya wagonjwa.

Katika ziara hiyo, Prof. Shemdoe pia ametembelea, amekagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 11, ukiwepo mradi wa ujenzi wa Daraja la Mbuga  linalogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 2.35, ambalo linaunganisha barabara ya Mwaya, Iputi na Luhumbero.














Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, amewahimiza Watanzania wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutembelea Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake ili kupata elimu kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali.
-Aeleza umuhimu wa Mahusiano mema katika kuimarisha mshikamano wa Taifa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, leo Julai 4, 2026 Jijini Dar es Salaam amekutana na kufanya mazungumzo na Mchungaji Antony Thomas Lusekeleo maarufu kama Mzee wa Upako wa Kanisa la Gospel Revival Centre (GRC) pamoja na Mtume Crear Malisa wa King Dom Embassy Church, ambapo viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano wa Serikali na Taasisi za Dini katika kukuza ustawi wa jamii na mshikamano wa kitaifa.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Sangu amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ilianzisha Idara maalumu ya Mahusiano chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa lengo la kuimarisha uratibu wa masuala ya kijamii na kitaasisi, ikiwemo mahusiano ya kazi, mahusiano kati ya serikali na wadau wa kijamii, vyama vya siasa na taasisi za dini. Pia, kukuza amani, umoja na mshikamano katika jamii.

Waziri Sangu alibainisha kuwa mshikamano wa kijamii na maadili ni nguzo muhimu katika kulinda amani na utulivu wa taifa.

Kwa upande mwengine, Viongozi hao wa dini Mchungaji Antony Thomas Lusekeleo maarufu kama Mzee wa Upako wa Kanisa la Gospel Revival Centre (GRC) pamoja na Mtume Crear Malisa wa King Dom Embassy Church wameipongeza Serikali kwa kutoa kipaumbele kuhusu masuala ya mahusiano ya Serikali na makundi mbalimbali na kueleza utayari wa kushirikiana na serikali katika kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuendeleza maadili ya taifa.
Na: OWM (KAM)– Muleba, Kagera

Serikali imesema itaendelea kushirikiana na taasisi za dini katika kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii na kujenga jamii yenye maadili, amani na mshikamano huku ikizipongeza kwa mchango wake mkubwa katika kukuza maendeleo ya Taifa.
Ni mara chache sana mwanaume huingia mahali na kila mwanamke anageuka kumtazama. Lakini ndivyo ilivyokuwa kwa Brian mchungaji kijana, mchangamfu, mwenye hadhi ya kuvutia na uso wa kupendeza. 

Kila mara alipoingia kanisani au kwenye mkutano wowote wa kijamii, wanawake walitabasamu, wengine wakigombania nafasi ya kukaa jirani naye, wengine wakijitokeza kusaidia huduma yoyote tu ili kumvutia.

Nikiwa mmoja wa wasichana waliompenda kwa siri, nilijua wazi sina nafasi mbele ya wengine waliokuwa wakijitahidi kwa nguvu kumshawishi. Nilikuwa mwepesi wa maneno, lakini si wa kujiaminia kiasi cha kujitokeza wazi. Nilimpenda kwa moyo wangu wote, lakini kila mara nilijipa moyo kwamba huenda Mungu atanipa nafasi yangu muda ukifika.

Lakini wakati mwingine, kuwa na imani pekee hakutoshi ilifika wakati nikajua kuwa nina kazi ya ziada ya kufanya ili nionekane tofauti na wanawake wengine. Wengine walikuwa na magari, wengine walikuwa warembo wa kutupwa, na wengine walikuwa hata na nafasi kubwa kanisani mimi nilikuwa tu msichana wa kawaida. Hapo ndipo rafiki yangu alinifungua macho. SOMA ZAIDI.
Siku hiyo ilikuwa ya kawaida kama nyingine. Niliamka mapema, nikamvalisha mwanangu mdogo Brian mavazi safi, na tukaelekea sokoni Kariakoo kufanya manunuzi. Alikuwa na miaka minne tu, mwenye tabasamu tamu na mcheshi kiasi kwamba hata wafanyabiashara walimzoea.

Nikiwa kwenye kibanda cha mbogamboga, nilimwacha pembeni kidogo tu, macho yangu yakiwa kwa nyanya zilizopangwa vizuri. Haikuchukua hata dakika mbili nilipojigeuza, Brian alikuwa ametoweka. Panic ilinishika.

Nilimuita kwa sauti ya juu, nikakimbia huku na kule, nikawauliza watu waliokuwa karibu lakini hakuna aliyeona chochote. Masaa yaligeuka kuwa siku, siku zikawa wiki. Niliripoti polisi, wakachukua maelezo, wakaniambia nisubiri uchunguzi.

Nilizunguka kila kituo cha polisi, nikachapisha picha yake, nikatangaza hadi redioni, lakini kila siku iliisha bila jibu. Mume wangu alianza kunilaumu kwa uzembe. Familia ilianza kunitenga kana kwamba nilikuwa na mkono katika kupotea kwa mwanangu.

Hali ya ndoa ilianza kuyumba, na hata nilipojaribu kuwa na imani, ukweli ni kwamba nilianza kukubali kuwa huenda sitamwona tena Brian. Maisha yangu yalikuwa ya huzuni, machozi, na majuto. Hakukuwa na raha tena. Kila mtoto niliyemuona barabarani alinikumbusha mwanangu aliyepotea. SOMA ZAIDI.
Maisha yangu yalikuwa kama mzunguko wa kushindwa. Kila nilichogusa, kilikuwa kikishindwa. Nilikuwa nikiishi maisha ya maumivu na kukosa furaha kwa miaka mingi. 

Nilikutana na changamoto nyingi katika kila nyanja ya maisha yangu: kazi, familia, na hata uhusiano. Ilikuwa kama vile kila nilichofanya kilikuwa kikiharibika.

Nilikuwa na ndoto nyingi, lakini zilikuwa zikifeli moja baada ya nyingine. Kila nilijitahidi, ndivyo zilivyokuwa zikiendelea kushindwa. 

Wakati mwingine nilijikuta nikijiuliza, “Kwa nini mimi?” Nilijua kuwa nashindwa, lakini sikujua sababu ya kushindwa kwangu kila wakati. Niliamini kuwa ni hali tu ya maisha ambayo nilikuwa nimezingirwa nayo.

Nilijaribu kila njia ya kushinda changamoto hizi kutafuta kazi bora, kufanya kazi kwa bidii, kuwa na uhusiano mzuri na familia yangu lakini kila nililofanya lilionekana kuwa na mwishowe wa kushindwa. Wakati mmoja, nilijua kuwa lazima kuna kitu kilichokuwa kikizuia mafanikio yangu.

Nilijua kuwa kuna siri au nguvu fulani ambayo ilikuwa ikifanya niendelee kushindwa. Nilibaki nikijiuliza na kugumu kuelewa sababu ya haya yote. 

Hata nilipojaribu kuzungumza na familia yangu kuhusu hali yangu, walionekana kama watu waliojawa na huzuni na hawakuwa na msaada wa maana kwangu. SOMA ZAIDI.

 


Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga shilingi milioni 273.6 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme wa jua katika visiwa saba vya Wilaya ya Musoma ikiwemo Nyasaungu, Muroba, Kagongo, Nyamasanje, Rukuba na Iriga, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais, Mhe. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya umeme bila kujali eneo analoishi.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kutatua kero za wananchi katika Jimbo la Musoma Vijijini.

 Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa umeme ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo tayari vimefikiwa na huduma hiyo, huku hatua zinazofuata zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyosalia.

 Amebainisha kuwa kati ya vitongoji 374 vilivyopo, takribani 100 pekee ndivyo bado havijafikiwa na umeme huku zaidi ya vitongoji 50 vikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme.

Aidha, amesema Serikali imepokea maombi ya Mbunge wa Musoma Vijijini ya kuhakikisha vitongoji vyote ambavyo havina umeme vinafikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2027, akieleza kuwa lengo hilo linaendana na dhamira ya Serikali inayolenga kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.

Sambamba na hilo, Mhe. Salome amesema Wizara ya Nishati imeendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya uzalishaji mali, ikiwemo maeneo ya wachimbaji wa migodi wilayani Musoma Vijijini.

 Kuhusu  baadhi ya wananchi ambao miundombinu ya umeme imepita karibu na makazi yao lakini hawajaunganishwa na huduma hiyo,  amemuelekeza Meneja wa TANESCO Wilaya ya Musoma kuhakikisha wananchi hao wanaunganishiwa umeme.

Katika hatua nyingine, amewahimiza wananchi wa Musoma Vijijini kutumia nishati safi ya kupikia, akibainisha kuwa Serikali imetoa ruzuku ya zaidi ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ili kuyawezesha kupatikana kwa gharama nafuu.