Na Oscar Assenga,TANGA


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amezindua Kamati za Ushauri wa Kisheria ngazi ya mkoa na wilaya na kliniki ya Sheria bila malipo huku akieleza kwamba zitasaidia kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali kutokana na kukutanisha mawakili wa Serikali.

Aliyasema hayo leo kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga ambako kilifanyika uzinduzi wa Kamati hizo ambapo alisema pia wale wa taasisi mbalimbali na kuwasaidia wananchi wenye changamoto mbalimbali kupata ufumbuzi.

Alisema uwepo wa huduma hizo utawawezesha mawakili wa Serikali kusimamia utawala wa Sheria katika kushirikiana na wadau wengine katika kutatua kero za wananchi na kupunguza malalamikko ya kisheria kutoka kwa wananchi.

“Lakini pia kutoa elimu ya Sheria kwa umma katika kushughulikia changamoto mbalimbali katika maeneo yao pamoja na kutoa elimu kwa viongozi na maafisa wa Serikali waweze kutoa maamuzi kwa mujibu wa Sheria”Alisema






Aidha alisema pia itapunguza vitendo vya uonevu na vinavyovunja sheria na taratibu za nchi nah ii itawezesha mimi na wakuu wa wilaya kushughulikia masuala ya miradi ya maendeleo badala ya kuhangaika na migogoro ya wananchi .

“Lakini nanukuu katika kitabu cha Mathayo 5:9 Yesu anasema “Heri wapatanishi ,maana hao wataitwa wana wa Mungu”.Hii inaonyesha kuwa kazi ya kupatanisha ni ya Kiungu na inampendeza Mungu”

“Pia kwenye Qur’an inasititiza sana kutenda haki (Uadilifu)kama wajibu Mkuu wa kidini na kijami,ikiamrisha kusimamia haki hata kama ni dhidi ya nafsi zenu waziazi ,au jamaa (Quran 4:1:35,5.8).Uadilifu ni msingi wa imani,ukihimiza kulinda haki za wengine ,kuondoa chuki na kutoa fidia kwa wahasiriwa”Alisema

Aidha aliwataka wadau waelewe kuwa jukumu la kutatua migogoro katika maisha ya watanzania sio la Serikali pekee bali ni la wote wa maendeleo huku akieleza kazi kubwa Serikali iliyonayo ni pamoja na kutengeneza mazingira mamzuri yanayoweza kusaidia kamati hizo.

Alisema hilo linatokana na uwepo wa migogoro mingi katika jamii hasa migogoro ya ardhi na mirathi hivyo kamati hizo zinatakiwa kukaa kila mara kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake ya kusikiliza malalamiko ya ksiheria na kutoa elimu kwa umma kwa kushirikiana na ofisi za wakuu wa wilaya.

Hata hivyo alitoa rai kwamba kuna haja ya kuhakikisha kuwa kamati za mkoa na wilaya zinafanya mambo mbalimbali ili kukabiliana na migogoro ikiwemo kuendelea kuboresha kiwango cha utoaji wa huduma ya ushauri wa kisheria na kuongeza wigo na upatikanaji katika maeneo ambayo hayajafanikiwa kufikiwa hasa maeneo ya nje ya jiji.

Mkuu huyo wa mkoa alizitaka kujiwekea utaratibu wa kuandaa kliniki za kisheria bila malipo kwa utaratibu wa kuwafuata wananchi katika maeneo yaona hiyo inatokana na wapo wananchi wengine ambao wanaogopa kuingia kwenye ofisi za Serikali pamoja na wengine hawana uwezo wa kusafiri na kwenda kwenye ofisi hizo.

“Lakini hakikisheni mnapopokea malalamiko au migogoro mnaifuatilia mpaka mwisho ili kujiridhisha namna gani imemalizika na kuweka kumbukumbu ya kufungua na kufunga migogoro hii lengo likiwa kuzuia walalamikaji kurudi kuwasilisha malalamiko yaliyopita hasa pale anapoona uongozi umebadilika “Alisema

Hata hivyo nitoa wito kwa wananchi wote wa mkoa wa Tanga wenye migogoro kutumia nafasi hii kuwasilisha migogoro yenu katika kliniki ya Sheria bila malipo iliyoanza leo kwenye viwanja vya Tangamano mpaka Machi 15 mwaka huu .

Awali akzungumza akizungumza Mkurugenzi wa Uratibu na Huduma za Ushauri kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Neema Ringo alisema kwamba wamekuja mkoani Tanga kutoa huduma kwa wananchi za kisheria kwa maana yake kutekeleza wajibu wake katika kuwahudumia wananchi ambao ndio wanaipa mamlaka Serikali.

Alisema wakiwa mkoani Tanga watapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuweza kuzipatia ufumbuzi huku akiwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kuweza kupata huduma






Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Nicola Brennan na uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wamejadiliana namna ya kuimarisha utekelezaji wa mpango wa Samia Scholarship Extended DS/AI+ unaolenga kujenga wataalamu wa Akili Bandia (AI) na Sayansi ya Takwimu (Data Science) nchini.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo iliyofanyika tarehe 9 Machi 2026 katika Taasisi hiyo jijini Arusha, Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula, amesema katika awamu ya kwanza ya mpango huo wanafunzi 34 wa Kitanzania wamepata nafasi ya kusoma katika vyuo vikuu vya Ireland.

Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na NM-AIST inapanga kuandaa *bootcamp* maalum kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi watakaofuata kunufaika na mpango huo.

Kwa upande wake, Balozi Brennan ameipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira ya kuwekeza katika elimu ya juu katika fani za AI, Data Science na Sayansi shirikishi, akibainisha kuwa wanafunzi wa Kitanzania watapata elimu yenye viwango vya kimataifa katika vyuo vikuu vya Ireland.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wa wanawake katika masomo ya STEM na kuhimiza taasisi na wabunifu kuhakikisha matokeo ya tafiti yanafika sokoni ili kuchangia maendeleo ya uchumi, usalama wa chakula na ajira.

Katika ziara hiyo, Balozi Brennan pia alitembelea maabara, kituo cha kompyuta chenye uwezo mkubwa (HPC), Data Driven Institute (DDI) pamoja na vituo vya ubunifu vya NM-AIST ili kujionea mchango wa taasisi hiyo katika maendeleo ya sayansi na teknolojia nchini.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali inatarajia zaidi ya asilimia 70 ya fedha za utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano zitatoka katika sekta binafsi kupitia uwekezaji na mifumo ya ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP).

 


Na Munir Shemweta, Masasi

Mbunge wa Jimbo la Masasi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amekabidhi vifaa tiba katika Kituo cha Afya Mbonde kilichopo Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Dkt. Akwilapo amekabidhi vifaa hivyo leo, Machi 9, 2026, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha huduma za afya katika Wilaya ya Masasi na maeneo jirani ya wilaya hiyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Dkt. Akwilapo amesema utoaji wa vifaa tiba ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha taasisi za huduma za jamii kama vile hospitali na shule zinakuwa na miundombinu na vifaa vinavyowawezesha wataalamu kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Amesema, serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha sekta za afya na elimu zinaimarika ili wananchi waweze kupata huduma bora karibu na maeneo yao.

“Naishukuru serikali chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha siyo tu inajenga majengo ya hospitali na shule, bali pia inahakikisha kunapatikana vifaa pamoja na wataalamu watakaowezesha huduma kutolewa kwa ufanisi,” amesema Dkt. Akwilapo.

Ameongeza kuwa, kupatikana kwa vifaa tiba katika Kituo cha Afya Mbonde, ikiwemo mashine maalum ya kusaidia watoto waliozaliwa kabla ya muda, kutasaidia kuokoa maisha ya watoto hao.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mbonde, Dkt. Mohamed Abbas, amesema, vifaa vilivyopokelewa vitasaidia kuimarisha huduma mbalimbali ikiwemo huduma kwa watoto, chumba cha upasuaji pamoja na huduma za maabara.

Kwa mujibu wa Dkt Abbas, kituo hicho cha afya Mbonde kinahudumia zaidi ya wananchi 32,000 kutoka kata tatu za Sululu, Mtawale na Mwenge Mtapika. Pia kituo kinatoa huduma kwa wagonjwa wanaotoka Halmashauri za Masasi na Nanyumbu.

Dkt. Abbas ameongeza kuwa, kituo hicho kinatoa huduma mbalimbali zikiwemo upasuaji, huduma za kulaza wagonjwa, uzazi pamoja na maabara.

Katika hatua nyingine, Mbunge huyo wa Jimbo la Masasi na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo pia amekabidhi vitabu 3,667 kwa shule 12 za Halmashauri ya Mji Masasi kwa lengo la kusaidia shughuli za ufundishaji na ujifunzaji.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vitabu hivyo Machi 9, 2026, mara baada ya kukutana na watendaji wa sekta ya elimu katika halmashauri hiyo, Dkt. Akwilapo amesema vitabu ni nyenzo muhimu katika kuboresha elimu shuleni.

“Kama tunavyojua, ufundishaji unahitaji zana, na moja ya zana muhimu ni vitabu. Hii ni awamu ya kwanza ya msaada huu na tutakuja tena na awamu ya pili, lengo ni kuwapa walimu nafasi ya kufanya kazi kwa ufanisi zaidi,” amesema.

Amesema, hatua hiyo inalenga kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ili kuongeza ubora wa elimu kwa wanafunzi wa shule hizo.

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme wa Kilovoti 400 cha Iganjo mkoani Mbeya, ambao kwa sasa umefikia takribani asilimia 60 ya utekelezaji wake.

Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Machi 8, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika eneo la Iganjo jijini Mbeya ambao ni sehemu ya Mradi wa Njia kusafirisha Umeme kutoka mkoa wa Irunga hadi Mkoa wa Rukwa (TAZA).

“Kwa ujumla wake kazi hapa zinaenda vizuri sana. Niwapongeza Shirika la Umeme TANESCO kwa kazi ya usimamizi mzuri wa mradi huu,” amesema Mhe. Ndejembi

Akieleza faida za mradi huo amesema kuwa utaachangia kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Mbeya pamoja na mikoa jirani.

“Mradi huu utaongeza nguvu ya upatikanaji wa umeme kwa sababu kwa sasa Mkoa wa Mbeya unapata umeme kutoka kwenye njia ya kilovoti 220 lakini mradi huu utakua ni kilovoti 400. Wananchi watanufaika na mradi huu kwa sababu umeme utapoozwa na kusambazwa kwa Wananchi,” ameongeza Mhe. Ndejembi

Aidha, ameeleza kuwa serikali inayoongozwa na Rais wa awamu ya sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati ya nishati ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Tanzania - Zambia (TAZA) Mha. Elias Makunga amesema mradi wa kituo cha Iganjo unaendelea vizuri licha ya changamoto ndogo zilizojitokeza katika hatua za usambazaji wa vifaa.

“Mradi wa kituo cha Iganjo uko asilimia 60 ya utekelezaji, ujenzi wa misingi umekamilika kwa asilimia 89. Upande wa usambazaji wa vifaa kutoka China tuko asilimia 89, lakini tumekuwa na changamoto kidogo katika upande wa upokeaji wa vifaa unaohusiana na kuboresha mfumo wa TRA,” amesema Mha. Makunga

Mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Rukwa ukikamilika unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi muhimu katika kuimarisha Gridi ya Taifa na kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika katika ukanda wa Nyanda za Juu Kusini.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rosemary Senyamule, ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma kwa kusimamia vizuri upatikanaji wa fursa za Ununuzi wa Umma kwa makundi maalum, hususan wanawake, hatua ambayo imeendelea kuwasaidia kiuchumi na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo.

Akizungumza leo Machi 8, 2026 katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Mbande, Wilayani Kongwa Mkoa wa Dodoma, Bi. Senyamule amesema kuwa usimamizi mzuri wa PPRA umewezesha makundi ya wanawake kunufaika na zabuni mbalimbali za serikali kupitia mfumo wa kielektroniki wa Usimamizi wa Ununuzi -NeST.

Amesema kuwa hadi sasa vikundi vya wanawake vimefanikiwa kupata zabuni za serikali zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 16, hatua inayodhihirisha kuwa sera ya kutoa kipaumbele kwa makundi maalum inaleta matokeo chanya katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa zaidi ya vikundi 500 vya wanawake vimesajiliwa kwenye mfumo wa NeST, jambo linaloonesha mwitikio wa wanawake katika kutumia fursa za ununuzi wa umma zinazotolewa na Serikali.

Aidha, Bi. Senyamule amewataka wanawake wote nchini kuendelea kuunda vikundi vingi zaidi ili waweze kunufaika na fursa hizo za zabuni za serikali, akisisitiza kuwa serikali imeweka mazingira rafiki yanayowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa nchi.

“Ni muhimu wanawake mkajiunga katika vikundi na kujisajili katika mfumo wa NeST ili mpate nafasi ya kushiriki katika zabuni za serikali.

Fursa hizi zipo kwa ajili yenu na zinaweza kuwasaidia kukuza biashara na kuinua kipato chenu,” amesema.

Ameongeza kuwa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana katika kuwawezesha wanawake na kuhamasisha juhudi zaidi za kuhakikisha wanawake wanapata nafasi sawa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Msimizi wa Kituo cha Msaada wa Kitaalam kwa Wateja wa NeST - PPRA ( NeST Customer Technical Support Center) Bi. Asifiwe Makweta amesema Mamlaka ina shauku kuona vikundi vya kina Mama vonaongezeka siku hadi siku ili kuhakikisha fursa hizi za serikali zinawafikia walengwa kiyakinifu kwa makundi yote ikiwemo Wanawake ili kuleta uhai wa ushiriki wa makundi maalum bila kubaki nyuma kwa kundi lolote.

"Pamoja na kufikia idadi ya kusajili makundi 500 ya Wanawake kwenye mfumo wa NeST bado haijafikia idadi ya makundi tunayotamani kusajili kwenye Mfumo wa NeST ili kushiriki katika fursa hii ya asilimia 30 ya zabuni kwa makundi hayo ambayo ni Vijana, wanawake, Wazee na watu wenye ulemavu"amesema Bi. Makweta.


Na. Mwandishi Wetu , Dodoma


Wanawake kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Makao Makuu wameungana na wanawake wengine mkoani Dodoma kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani Machi 8, 2026, Jijini Dodoma

‎Katika kuadhimisha siku hii Wanawake hao wametoa msaada wa mahitaji mbalimbali katika Kituo cha Watoto Yatima cha Rahman kilichopo chang'ombe mkoani Dodoma, ili kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mahitaji hayo, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Bi. Subira Kaswaga, amesema kuwa mwaka 2026 mamlaka hiyo imeamua wanawake wa taasisi hiyo washiriki katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, ambayo hufanyika tarehe 8 Machi kila mwaka.

Aidha, amebainisha kuwa Mamlaka ya Serikali Mtandao inathamini wanawake na inahakikisha wanashiriki katika masuala mbalimbali ya kijamii ili kutoa motisha na hamasa kwa wanawake na wasichana kuwa na jitihada katika masomo yao pamoja na katika fani ya TEHAMA.Bi.Kaswaga amebainisha kuwa kabla ya kutoa msaada huo, walitembelea baadhi ya vituo vya watoto yatima ili kubaini mahitaji yaliyopo na kuamua kuchagua vituo vyenye uhitaji mkubwa zaidi.

Misaada hiyo ni vyakula mbalimbali ikiwemo mchele, sukari, na viazi, pamoja na taulo za kike, mafuta, nguo, na viatu kwa ajili ya watoto wanaoishi katika kituo hicho. Baadhi ya vitu vimetolewa na mamlaka na vingine vimechangwa na watumishi wa taasisi hiyo.Kwa upande wake, Katibu wa Kituo cha Rahman, Abdallah Said, amewapongeza na kuwashukuru wanawake kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa kutoa msaada huo kwa ajili ya kusaidia watoto wenye uhitaji, akibainisha kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka hasa katika kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Aidha, amebainisha kuwa kituo hicho kina jumla ya watoto 120 wanaopata huduma mbalimbali, huku kwa mujibu wa ustawi wa jamii, uwezo wa kituo kuwahifadhi watoto wanaolala ukiwa ni wa watoto wasio chini ya 46, ambapo watoto 74 hurudi katika kaya zao kwa bibi, babu, shangazi, au mjomba kutokana na uwezo mdogo wa kituo kuwahifadhi wote.

Maadhimisho ya mwaka 2026 yaliongozwa na kauli mbiu isemayo: “Haki kwa Wanawake na Wasichana: Msingi wa Maendeleo Jumuishi kuelekea Dira ya Taifa 2050.”‎