Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa Serikali inawetegemea wanasayansi na wahandisi ili kufanikisha dhamira ya Tanzania ya kujenga uchumi wa viwanda, amesisitiza kuwa kundi hilo lina mchango katika kuendeleza ubunifu, kuongeza tija na kuleta maendeleo endelevu nchini.

Prof. Mkenda amesema hayo Disemba 5, 2025 jijini Dar es Salaam katika Mahafali ya 19 ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT), akisema katika kutimiza azma hiyo Serikali imeendelea kuongeza fursa za mafunzo na Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi ili kusimamia ubora wa elimu sambamba na utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, Toleo la 2023.

"Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuleta mageuzi ya elimu, kwa kuwawezesha watanzania hususan vijana kupata maarifa, stadi na ujuzi ili kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi" Amesema Waziri Mkenda.

Amebainisha kuwa, Serikali kupitia mkopo nafuu wa Benki ya Dunia imewekeza jumla ya Dola za Marekani milioni tisini (90) ambapo kupitia fedha hizo Taasisi ya DIT, imeanzisha Kituo cha Umahiri cha Kikanda cha Mafunzo ya TEHAMA (RAFIC) katika Kampasi ya Dar es Salaam na Kituo cha Umahiri cha Uchakataji bidhaa za ngozi (CELPAT) kampasi ya Mwanza.

Ameipongeza DIT kwa kuendelea kutoa mafunzo bora, sambamba na kutambua, kujenga, kukuza na kuendeleza bunifu. Amesema kuwa Serikali inajivunia juhudi hizo na ameisisitiza kuendelea kusimamia majukumu yake kikamilifu.

Mkuu wa Taasisi ya DIT, Profesa Preksedis Ndomba, amesema kuwa Taasisi hiyo imejikita katika dhana ya ufundishaji inayotilia mkazo mafunzo kwa vitendo pamoja na ziara za mafunzo viwandani, ambayo imewasaidia wanafunzi kuwa wabunifu na kufikia viwango vya kuanzisha makampuni.

Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi hiyo, Dtk. Richard Masika ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga zaidi ya Sh. Bilioni mbili katika mwaka wa fedha 2025/26, ili kuanzisha Kituo cha Ujasiriamali, Ubunifu na Uhawilishaji wa Teknolojia kupitia Mradi wa TELM II.

Kumbuka, Mradi huo wa miaka miaka mitano (2025/2030) unatekelezwa kwa bajeti ya Euro milioni 19.79 (sawa na Sh. Bilioni 54). Fedha hizo ni mkopo nafuu kutoka Serikali ya Italia kwa Serikali ya Tanzania kupitia makubaliano rasmi.

Taasisi zingine zinazonufaika na Mradi wa TELMS II, ni Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) na Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST).

Katika duru ya kwanza ya mahafali hayo, Waziri Mkenda amewatunuku vyeti jumla ya wahitimu 1,341 katika ngazi za Astashahada, Stashahada, Shahada na Shahada ya Uzamivu katika nyanja za Sayansi na Teknolojia. Kati ya hao, wanaume ni 1,003 na wanawake 338.



Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imefanikisha kuendesha mafunzo ya kitaifa ya siku nne kuhusu usalama wa mionzi ya mashine za X-Ray na vyanzo vingine vya mionzi vinavyotumika katika upigaji picha za kitabibu kwa binadamu.

Mafunzo hayo yalifanyika kuanzia Jumatatu, tarehe 1 hadi Alhamisi, tarehe 4 Desemba 2025, katika ofisi za TAEC Kanda ya Kaskazini jijini Arusha, na yalihusisha takribani washiriki 50 kutoka sekta mbalimbali muhimu nchini.

Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na kufungwa na Dkt. Denis Mwalongo, Mkuu wa Kanda ya Kaskazini wa TAEC, aliyesimamia hafla hizo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TAEC, Prof. Najat Kassim Mohammed.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Dkt. Mwalongo alisisitiza umuhimu wa usalama wa mionzi katika kulinda wafanyakazi, wagonjwa, umma na mazingira.

Alibainisha kuwa mafunzo hayo ni kielelezo cha dhamira ya TAEC ya kuendelea kujenga uwezo wa kitaifa katika matumizi salama ya vifaa vya nyuklia.

“Mafunzo haya si suala la kufuata taratibu pekee; ni kuhusu kukuza utamaduni wa uwajibikaji na uelewa miongoni mwa wataalamu wanaofanya kazi na vifaa vinavyotoa mionzi,” alisema Dkt. Mwalongo.

Mafunzo yalilenga kuwapatia washiriki ujuzi wa nadharia na vitendo kuhusu usalama wa mionzi. Mada kuu zilizojadiliwa ni pamoja na: Utangulizi wa mionzi ayonisha, Vipimo na viwango vya mionzi, Matumizi ya mionzi ionizishi, Athari za kibaolojia za mionzi, Muhtasari wa mionzi isiyo ionizishi, Udhibiti wa kisheria wa vyanzo vya mionzi Tanzania, Mfumo wa kimataifa wa ulinzi wa mionzi, Vipengele vya udhibiti wa mionzi kazini, Hatua za ulinzi wa mionzi kwa wafanyakazi, Uboreshaji wa ulinzi wa mionzi katika ICT, Ubunifu wa majengo na vipengele vya usalama, Mpango wa uthibitisho wa ubora kwa mionzi ya kitabibu, Uboreshaji wa ulinzi wa mionzi kwa watoto, Uundaji wa programu za ulinzi wa mionzi, Upimaji na ufuatiliaji wa mionzi, Mionzi ya kitabibu na usimamizi wa dozi kwa wagonjwa, Uboreshaji wa ulinzi wa mionzi katika radiografia, Vipengele vya ulinzi wa mionzi katika radiografia ya kidigitali, Majukumu ya Maafisa Usalama wa Mionzi (RSOs)
Aidha, washiriki walitembelea Maabara ya Dosimetry na Maabara ya Secondary Standard Dosimetry Laboratory (SSDL) ya TAEC, ambapo walipata nafasi ya kutekeleza taratibu za usalama wa mionzi kwa vitendo.

Mafunzo haya yalilenga kuongeza uelewa, kuboresha ujuzi wa kiufundi, na kuhamasisha matumizi salama ya vyanzo vya mionzi katika sehemu za kazi. Kupitia mafunzo haya, TAEC inaendelea kuimarisha uwezo wa kitaifa katika usalama wa mionzi.

TAEC ina jukumu kubwa la kudhibiti na kuendeleza matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia nchini Tanzania. Hatua zake zinaendana na viwango vya kimataifa na zinachangia katika malengo ya maendeleo ya taifa, kuhakikisha kuwa sayansi na teknolojia ya nyuklia zinatumika kwa uwajibikaji na usalama katika sekta ya afya.

Akitoa ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu, Dkt. Mwalongo alieleza shukrani za Prof. Najat Kassim Mohammed kwa washiriki na kusisitiza maono ya TAEC kwa siku zijazo:

“Usalama wa mionzi ni kiini cha dhamira yetu ya kulinda maisha huku tukisonga mbele na teknolojia ya kitabibu. Kupitia uwekezaji katika mafunzo na ujenzi wa uwezo, TAEC inathibitisha upya kujitolea kwake kuhakikisha Tanzania inabaki mstari wa mbele katika matumizi salama na yenye uwajibikaji ya teknolojia ya nyuklia,” alisema Prof. Najat Kassim Mohammed.

Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) ndiyo mamlaka ya kitaifa yenye jukumu la kudhibiti, kuendeleza, na kuhakikisha matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia nchini.


Kupitia mafunzo, utafiti, na udhibiti wa kisheria, TAEC inalinda afya, usalama na mazingira huku ikisaidia maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia ya taifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Watendaji na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa) kuzungumza na Watendaji hao walipokuwa kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Bw. Shadrack Mziray akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za TASAF kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifuatilia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Bw. Shadrack Mziray (wa kwanza kulia) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe. Regina Qwaray mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa lengo la kufanya ziara ya kikazi ili kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (Wa kwanza kulia) akizungumza jambo na Viongozi na Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika ofisi hizo kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (meza kuu kushoto) na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe. Regina Qwaray wakifuatilia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (aliyesimama) wakati wa ziara ya kikazi ya Viongozi hao iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Wengine ni Watendaji na Menejimenti ya TASAF.

Sehemu ya Watendaji na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji wa Watumishi wa ofisi hiyo.


Na Veonica Mwafisi-Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameielekeza Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kufanya tathmini na ufuatiliaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ili kuona ni kwa kiwango gani malengo ya Mpango huo yanafikiwa, kubainisha changamoto na kuzishughulikia ili kuboresha utendaji kazi na matokeo yanayotarajiwa.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 05 Disemba, 2025 alipokuwa akizungumza na Menejimenti ya TASAF wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa TASAF jijini Dar es Salaam.

Amesema kufanya tathmini kutafichua mambo mengi ambayo yalikuwa hayajulikani katika utekelezaji ambapo itasaidia kuboresha awamu nyingine ya Mpango.

“Tufanye tathmini tuangalie kwanini kunakuwa na utofauti katika mafanikio ili tuone tunasaidiaje, je wasimamizi wa eneo fulani wana ubunifu zaidi kuliko wa eneo lingine? Amejiuliza, na kuongeza kuwa haya mambo ni vizuri yakawa shirikishi ili kuboresha zaidi tutakapoingia kwenye awamu nyingine ya Mpango,” Mhe. Kikwete ameongeza

Aidha, ameitaka TASAF kuzungumza mafanikio na changamoto za utekelezaji wa mradi huo kwa walengwa na wananchi. “Tutoke, tuseme mafanikio na changamoto kwanini wamekosa, watu waambiwe ukweli, TASAF imefanya mambo makubwa, tuwaonyeshe waliohitimu, wamefanya nini mpaka kufanikiwa na walioshindwa kufanikiwa wanatakiwa kufanya nini.” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Mhe. Kikwete ameipongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa uendelea kuhawilisha ruzuku kwa kaya maskini zinazokidhi vigezo vya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye Sekta za Afya, Elimu, Maji, Mazingira na ujasiriamali.

Pamoja na pongezi hizo ameitaka TASAF kuendelea kuboresha shughuli za kuwezesha utekelezaji wa Miradi ya Jamii ya kutoa Ajira ya muda ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa Ajira, kuwezesha jamii kutekeleza miradi ya kuendeleza miundombinu ya huduma za jamii katika Sekta za Afya, Elimu, Maji, Mazingira na ujasiriamali na uendelea kufungamanisha mikakati mbalimbali ya kuwezesha wananchi kiuchumi ili kuhakikisha matokeo yanayopatika kwenye kila mkakati yanaharakisha kasi ya kuondoa umaskini wa wananchi.

Vile vile ameitaka Taasisi hiyo kuimarisha miundombinu ya mifumo ili kulinda usalama wa taarifa za walengwa na kuungamanisha mifumo wa walengwa na mifumo mingine ya Serikali pamoja na kuongeza idadi ya walengwa wanaolipwa kwa njia za kielekitroniki ili kupunguza dosari za malipo ya ruzuku.

Mhe. Kikwete amesema malengo makubwa ya yeye na Naibu Waziri Mhe. Mhe. Regina Qwaray kutembelea TASAF leo ni kujitambulisha na kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufikia malengo ya TASAF yaliyokusudiwa.

“Mimi sio mgeni katika Ofisi hii, hivyo ninawaahidi tutaendelea kushirikiana kama ambavyo tulikuwa tukifanya siku zote nilipokuwa hapa kwa nafasi ya Naibu Waziri. Kuletwa kwangu katika Ofisi hii ni kuja kuongeza nguvu ili kupata matokeo chanya ikiwemo ubunifu katika maeneo mbalimbali. Tufanye kazi tuliyopangwa kufanya tukiongozwa na misingi yetu ya utendaji kazi. Lengo ni kujenga na kumsaidia Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupunguza kaya masikini katika taifa letu.

Pia Mhe. Kikwete amesema dhana ya ushirikishwaji wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ni nzuri kwani imewasaidia kubuni miradi mbalimbali na imepunguza changamoto nyingi ikiwemo za miundo mbinu, afya na elimu.

Amesisitiza kuwajengea uwezo wa kifikra walengwa, fedha ziwafikie kwa wakati, usimamizi mzuri huku wakitambua kuwa msingi mkubwa wa Mpango huo walengwa wake ni wananchi na si vinginevyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mhe. Regina Qwaray ameipongeza TASAF kwa kazi nzuri wanayoifanya. “Mimi ni mgeni katika Ofisi hii, lakini napenda niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya, TASAF sio ngeni masikioni mwangu, hii inaonyesha ni kwa jinsi gani mnatekeleza majukumu yenu vizuri, naombeni ushirikiano ili tufanye kazi kwa pamoja na kuwa na matokeo chanya,” amesema Mhe. Qwaray.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Shadrack Mziray amesema Mfuko huo ulianzishwa na Serikali mwaka 2000 kama mojawapo ya mikakati katika kupambana na umaskini kwa kutumia dhana ya ushirikishaji jamii na imetekelezwa kwa awamu tatu tangu kuanzishwa kwake.

 


Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Bwana Abdul-Razaq Badru amezipongeza timu za Mamlaka hiyo zinazoshiriki mashindano ya Shirikisho la Mashirika ya serikali na Taasisi Binafsi (SHIMMUTA) yanayoendelea mkoani Morogoro kwa kuendelea kulinda na kutangaza taswira ya taasisi hiyo kupitia sekta ya Michezo.

Akitoa salamu  alipotembelea timu hiyo kwa niaba  Kamishna Badru, Kaimu Meneja wa Uhusiano kwa umma bwana Hamis Dambaya amesema menejimenti ya Ngorongoro imeridhishwa na kazi kubwa iliyofanywa na timu hizo katika mashindano hayo na kulitangaza shirika kupitia utalii wa michezo (sport tourism) 

Katika mashindano hayo Ngorongoro imefanikiwa kutwaa Medali saba huku ikidhihirisha upekee wake kimataifa na kuendelea kuwa _Premium Safari Destination._

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Na Veonica Mwafisi-Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameielekeza Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kufanya tathmini na ufuatiliaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ili kuona ni kwa kiwango gani malengo ya Mpango huo yanafikiwa, kubainisha changamoto na kuzishughulikia ili kuboresha utendaji kazi na matokeo yanayotarajiwa.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 05 Disemba, 2025 alipokuwa akizungumza na Menejimenti ya TASAF wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa TASAF jijini Dar es Salaam.

Amesema kufanya tathmini kutafichua mambo mengi ambayo yalikuwa hayajulikani katika utekelezaji ambapo itasaidia kuboresha awamu nyingine ya Mpango. “Tufanye tathmini tuangalie kwanini kunakuwa na utofauti katika mafanikio ili tuone tunasaidiaje, je wasimamizi wa eneo fulani wana ubunifu zaidi kuliko wa eneo lingine? Amejiuliza, na kuongeza kuwa haya mambo ni vizuri yakawa shirikishi ili kuboresha zaidi tutakapoingia kwenye awamu nyingine ya Mpango,” Mhe. Kikwete ameongeza

Aidha, ameitaka TASAF kuzungumza mafanikio na changamoto za utekelezaji wa mradi huo kwa walengwa na wananchi. “Tutoke, tuseme mafanikio na changamoto kwanini wamekosa, watu waambiwe ukweli, TASAF imefanya mambo makubwa, tuwaonyeshe waliohitimu, wamefanya nini mpaka kufanikiwa na walioshindwa kufanikiwa wanatakiwa kufanya nini.” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Mhe. Kikwete ameipongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa uendelea kuhawilisha ruzuku kwa kaya maskini zinazokidhi vigezo vya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye Sekta za Afya, Elimu, Maji, Mazingira na ujasiriamali.

Pamoja na pongezi hizo ameitaka TASAF kuendelea kuboresha shughuli za kuwezesha utekelezaji wa Miradi ya Jamii ya kutoa Ajira ya muda ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa Ajira, kuwezesha jamii kutekeleza miradi ya kuendeleza miundombinu ya huduma za jamii katika Sekta za Afya, Elimu, Maji, Mazingira na ujasiriamali na uendelea kufungamanisha mikakati mbalimbali ya kuwezesha wananchi kiuchumi ili kuhakikisha matokeo yanayopatika kwenye kila mkakati yanaharakisha kasi ya kuondoa umaskini wa wananchi.

Vile vile ameitaka Taasisi hiyo kuimarisha miundombinu ya mifumo ili kulinda usalama wa taarifa za walengwa na kuungamanisha mifumo wa walengwa na mifumo mingine ya Serikali pamoja na kuongeza idadi ya walengwa wanaolipwa kwa njia za kielektroniki ili kupunguza dosari za malipo ya ruzuku.

Mhe. Kikwete amesema malengo makubwa ya yeye na Naibu Waziri Mhe. Mhe. Regina Qwaray kutembelea TASAF leo ni kujitambulisha na kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufikia malengo ya TASAF yaliyokusudiwa.

“Mimi sio mgeni katika Ofisi hii, hivyo ninawaahidi tutaendelea kushirikiana kama ambavyo tulikuwa tukifanya siku zote nilipokuwa hapa kwa nafasi ya Naibu Waziri. Kuletwa kwangu katika Ofisi hii ni kuja kuongeza nguvu ili kupata matokeo chanya ikiwemo ubunifu katika maeneo mbalimbali. Tufanye kazi tuliyopangwa kufanya tukiongozwa na misingi yetu ya utendaji kazi. Lengo ni kujenga na kumsaidia Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupunguza kaya masikini katika taifa letu.

Pia Mhe. Kikwete amesema dhana ya ushirikishwaji wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ni nzuri kwani imewasaidia kubuni miradi mbalimbali na imepunguza changamoto nyingi ikiwemo za miundo mbinu, afya na elimu.

Amesisitiza kuwajengea uwezo wa kifikra walengwa, fedha ziwafikie kwa wakati, usimamizi mzuri huku wakitambua kuwa msingi mkubwa wa Mpango huo walengwa wake ni wananchi na si vinginevyo. 

Kwa upande wake Naibu Waziri Mhe. Regina Qwaray ameipongeza TASAF kwa kazi nzuri wanayoifanya. “Mimi ni mgeni katika Ofisi hii, lakini napenda niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya, TASAF sio ngeni masikioni mwangu, hii inaonyesha ni kwa jinsi gani mnatekeleza majukumu yenu vizuri, naombeni ushirikiano ili tufanye kazi kwa pamoja na kuwa na matokeo chanya,” amesema Mhe. Qwaray.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Shadrack Mziray amesema Mfuko huo ulianzishwa na Serikali mwaka 2000 kama mojawapo ya mikakati katika kupambana na umaskini kwa kutumia dhana ya ushirikishaji jamii na imetekelezwa kwa awamu tatu tangu kuanzishwa kwake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Watendaji na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa) kuzungumza na Watendaji hao walipokuwa kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Bw. Shadrack Mziray akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za TASAF kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifuatilia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Bw. Shadrack Mziray (wa kwanza kulia) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe. Regina Qwaray mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa lengo la kufanya ziara ya kikazi ili kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (Wa kwanza kulia) akizungumza  jambo na Viongozi na Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika ofisi hizo kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (meza kuu kushoto) na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe. Regina Qwaray wakifuatilia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (aliyesimama) wakati wa ziara ya kikazi ya Viongozi hao iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Wengine ni Watendaji na Menejimenti ya TASAF.

Sehemu ya Watendaji na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji wa Watumishi wa ofisi hiyo.


NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WAHITIMU wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kusimamia masuala mtambuko ikiwemo kupinga vitendo vya rushwa, ukatili wa kijinsia, utoaji wa elimu jumuishi, lishe shuleni, na mapambano dhidi ya dawa za kulevya pamoja na maambukizi mapya ya VVU.

Wito huo umetolewa leo Desemba 5, 2025 wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Omary, wakati wa mahafali ya 33 ya ADEM ambapo jumla ya wahitimu 785 wa kozi zaStashahada ya Uongozi, Usimamizi na Utawala katika Elimu -DELMA, Stashahada ya Uthibiti Ubora wa Shule - DSQA na Astashahada ya Uongozi, Usimamizi na Utawala katika Elimu -CELMA wamehitimu.

Dkt. Omary amesema masuala hayo yakiwa hayapatiwi uzito unaostahili yanaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa sekta ya elimu na maendeleo ya taifa kwa ujumla. Ameongeza kuwa serikali inawategemea wahitimu hao kwa kuwa ujuzi walioupata ni muhimu kwa mustakabali wa elimu nchini.

“Mtakaporudi katika vituo vyenu vya kazi, hakikisheni mnashirikiana na uongozi wa ngazi zote pamoja na jumuiya za shule ili kuhakikisha shule zinafanya vizuri kitaaluma na katika nidhamu,” alisema.

Akizungumzia changamoto ya ukosefu wa rasilimali fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi na utoaji wa mafunzo, Dkt. Omary alisema Serikali kupitia wizara itaendelea kushirikiana na ADEM kupunguza changamoto hizo na, inapowezekana, kuondoa kabisa.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid Maulid, alisema wahitimu wote wa ngazi mbalimbali ni wataalam mahiri wanaohitajika katika sekta ya elimu, na mchango wao ni muhimu katika kukuza rasilimali watu.

“Hii inaonesha kuwa chuo kinaendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya taifa kupitia uzalishaji wa wataalam wa uongozi na usimamizi wa elimu,” alisema.

Aidha, Dkt. Maulid alibainisha changamoto ya kukosekana kwa bajeti ya kuendesha mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi wa elimu, wakiwemo walimu wakuu, wakuu wa shule, maafisa elimu ngazi ya kata hadi mkoa, wathibiti wa shule na viongozi waandamizi wa wizara.

Amesema ili kukabiliana na changamoto hizo, chuo kitaimarisha ushirikiano na taasisi binafsi pamoja na mashirika ya kimataifa ili kuongeza rasilimali fedha na kuendeleza mafunzo.

“Tutaongeza nguvu kupitia ushirikiano wa ‘Public Private Partnership’ na ‘Tanzania Investment Centre’ ili kubainisha wadau wanaoweza kuwekeza katika maeneo ya ardhi tunayomiliki,” alieleza.

Aidha, aliwasihi wahitimu kutumia maarifa waliyopata kuelimisha jamii kuhusu athari za uvunjifu wa amani, mmomonyoko wa maadili na ukosefu wa uzalendo.

“Wahitimu wakasimamie ipasavyo maeneo yao kwa kutoa maarifa kwa walimu na wanafunzi ili watambue thamani ya amani, uzalendo na maadili,” alisema Dkt. Maulid.