NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Mkutano wa kimataifa wa siku tatu wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere umezinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kujadili masuala ya siasa za kimataifa (geopolitics), maendeleo na mwelekeo mpya wa Afrika katika mazingira ya dunia yanayobadilika kwa kasi.
Jaji Mwambegele ameyasema
hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika
Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani
Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya
Juni 1, 2026.
Jaji Mwambegele pia
amewasisistiza watendaji hao kuishi
kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha
na upendeleo wa aina yoyote.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo
hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni,
miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi
.
Naye Msimamizi wa Uchaguzi
wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa
asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.
Uchaguzi huo utafanyika
sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni
iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo,
Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa,
Halmashauri ya Mji wa Kasulu.
Nyingine ni kata ya Kala
iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga;
Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya
Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya
Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena, akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 28,2026 katika Mako Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kuhusu wito wa vijana waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kwa mwaka 2026 kujiunga na mafunzo ya JKT.
Na.Alex Sonna-CHAMWINO
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajab Mabele amewataka Vijana waliohitimu kidato cha Sita kwa Mwaka 2026 ambao wamechaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa sheria kujiunga na mafunzo hayo katika makambi waliyochaguliwa kuanzia juni mosi, hadi juni 7, 2026.
Hayo yamesemwa leo Mei 28,2026 katika Mako Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT, Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema majina ya vijana wote waliohitimu kidato cha sita kwa Shule za Sekondari Tanzania Bara na Visiwani waliochaguliwa wanatakiwa kujiunga na mafunzo hayo. Amesema orodha kamili ya majina ya vijana hao, makambi JKT waliyopangiwa, Maeneo ya Makambi hayo yalipo na vifaa wanavyotakiwa kwenda navyo inapatikana katika tovuti ya JKT ambayo ni www.jkt.mil.tz. Amesema ilikufahamu kambi kijana aliyopangiwa atatakiwa kuingiza jina la shule au namba ya shule aliyohitimu kidato cha sita, mbele ya jina la shule ataona neno lililoandikwa waliochaguliwa ambapo akichagua neno hilo ataona majina ya waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2026 na kambi aliyopangiwa. Amesema ili kuona majina yote ya vijana na kambi walizopangiwa mtumiaji atapakua JKT PDF 2026 iliyopo juu kulia katika ukurasa huo. Ameongeza kuwa Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele anawakaribisha vijana wote waliohitimu kidato cha sita kwa mwaka 2026 ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujengewa uzalendo, kufundishwa nidhamu, ukakamavu, umoja wa kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na utayari wa kulijenga na kulitumikia taifa. Katika hatua nyingine amebainisha kuwa kwa wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho wataripoti katika kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miondombinu ya kuwahudumia watu hao.
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amewataka viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kutambua kuwa Uongozi ni utumishi wa kuwatumikia watu na si kutumikiwa, kwani kazi ya kiongozi ni kuwa tayari muda wote kutatua changamoto mbalimbali.
Mapesa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwapisha viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kwa mwaka 2026/27 pamoja na mambo mengine amepongeza Uongozi wa Serikali iliyomaliza muda wake iliyokuwa ikiongozwa na Magashi Magina kuwa walizingatia Weledi wa hali ya Juu.
Mkuu huyo wa Taasisi ameitaka Serikali mpya kuzingatia misingi ya Uongozi, na kuwa na namna bora ya kutatua changamoto ikiwa ni pamoja na kushirikiana vyema na Serikali ya Wanafunzi ambayo imemaliza muda wake, huku akiwaahidi ushirikiano wa dhati kutoka kwa Uongozi wa Chuo.
Kwa upande wake, Rais aliyemaliza muda wake Magashi Magina ameishukuru Menejimenti ya chuo kwa ushirikiano alioupata katika kipindi chote cha uongozi wake, ameeleza kuwa mafanikio yote yaliyopatikana yalitokana na uwazi na utayari wa Menejimenti kusikiliza na kutatua Changamoto mbalimbali za Wanafunzi jambo lililorahisisha utendaji kazi wa serikali yake.
Nao, Viongozi wapya walioapishwa kuiongoza Serikali ya Wanafunzi , Rais ni Samir Naseer na Makamu wa Rais Julieth Mandia wametoa shukrani za dhati kwa Wanafunzi wote kwa kuonyesha imani kwao na kuwachagua kuongoza Serikali ya wanafunzi ambapo wameahidi kuongozi kwa Uadilifu, Amani, mshikamano kwa kushirikiana na Menejimenti ya Chuo pamoja na Serikali ya Wanafunzi iliyomaliza muda wake.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE
28.05.2026
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Maryprisca Mahundi amesema maonyesho ya Mbeya City Expo yameendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa Mkoa wa Mbeya kwa kuwakutanisha wananchi, taasisi na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Akizungumza baada ya kutembelea mabanda mbalimbali katika maonyesho hayo yanayofanyika katika viwanja vya Uhindini, Jijini Mbeya, Eng. Mahundi amesema ameridhishwa na namna shughuli za kijamii na kiuchumi zinavyooneshwa kupitia maonyesho hayo.
Amesema Mbeya City Expo imekuwa jukwaa muhimu la kutoa elimu, kutangaza huduma na bidhaa pamoja na kuhamasisha fursa za maendeleo kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na maeneo ya jirani.
Aidha, amepongeza waandaaji wa maonyesho hayo kwa kutoa nafasi kwa wananchi kupata elimu na huduma mbalimbali zinazochochea maendeleo ya jamii pamoja na kukuza uchumi.
Katika hatua nyingine, Eng. Mahundi amesisitiza wananchi, hususan makundi maalum, kutumia vizuri mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na halmashauri ili kujikwamua kiuchumi na kuongeza kipato cha familia zao.
Wengine walikuwa wakiniambia siwezi kufanikiwa, huku wengine wakinifanya nijihisi mdogo bila sababu. Kwa kweli iliniumiza sana. Polepole nilianza kujifungia ndani ya dunia yangu mwenyewe.
Nilianza kuogopa kuzungumza mbele za watu, kujaribu opportunities mpya, au hata kuvaa vile nilivyopenda kwa sababu nilihofia watu wangesema nini.
Kulikuwa na siku nilijiangalia kwenye kioo na kushindwa kuona kitu kizuri kuhusu mimi mwenyewe.
Mwanzoni nilidhani ni makosa ya kawaida. Lakini kadri wiki zilivyopita, hasara ilianza kuongezeka. Mara napoteza mahindi yaliyokuwa tayari kuvunwa, mara vifaa vya kazi vinatoweka.
Kwa kweli nilichanganyikiwa. Nilianza kufanya ulinzi wa usiku mara kadhaa lakini bado sikuweza kumkamata mtu yeyote.
Nilikuwa karibu kuvunjika moyo. Watu wengine waliniambia niache kupambana kwa sababu huenda singepata anayehusika. Lakini moyoni sikuwa tayari kuona jasho langu linaendelea kupotea.SOMA ZAIDI.
Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda sawa, na nilikuwa na matumaini makubwa ya kuona biashara yangu ikikua. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.
Biashara nyingine iliyokuwa karibu yangu ilianza kunizidi kwa namna ambayo sikuielewa. Wateja wangu wa kawaida wakaanza kupungua. Wengine walikuwa wanaenda upande mwingine ghafla bila maelezo.
Kilichoniumiza zaidi ni kusikia maneno yaliyokuwa yanaenezwa. Kulikuwa na watu waliokuwa wakisema biashara yangu haikuwa nzuri, bidhaa zangu hazikuwa na ubora, na huduma yangu haikuridhisha wakati nilikuwa najua nilikuwa najitahidi sana.
Polepole nilianza kuhisi kama mshindani wangu alikuwa akifanya kila kitu kuhakikisha ninapoteza wateja. Kwa kweli nilivunjika moyo.
Kulikuwa na siku nilikosa pumzi ghafla usiku, nikaanza kukohoa sana, na familia yangu ikalazimika kunikimbiza hospitalini. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.
Nilikuwa naogopa hata mabadiliko ya hali ya hewa. Vumbi, baridi, moshi, au harufu kali vilikuwa vinanifanya niwe na wasiwasi. Wakati mwingine nilishindwa kushiriki shughuli za kawaida kwa sababu niliogopa kupata shida ya kupumua.
Kilichoniumiza zaidi ni kulazwa hospitalini mara kwa mara. Kulikuwa na nyakati nilihisi kama maisha yangu yalikuwa yamesimama.
Kulikuwa na kipindi nilianza kukata tamaa. Nilikuwa najiuliza kama ningewahi kuishi maisha ya kawaida bila hofu ya kushindwa kupumua ghafla.SOMA ZAIDI.
Tuliamini kila kitu kilikuwa sawa kwa sababu tulikuwa tunajua historia ya ardhi ile tangu zamani. Lakini ghafla mambo yalibadilika pale mtu mmoja alipojitokeza akidai sehemu ile ilikuwa yake.
Mwanzoni nilidhani ni misunderstanding ya kawaida. Lakini baada ya muda, jambo lile likafika hadi mahakamani.
Kwa kweli nilichanganyikiwa. Miaka ilianza kupita. Kila hearing ilikuwa inanipa stress kubwa. Mara kesi inaahirishwa, mara lawyer anahitaji gharama nyingine, mara napewa matumaini halafu mambo yanabadilika tena.
Wakati mwingine nilirudi nyumbani nikilia kimya nikihofia familia yangu ingepoteza kila kitu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wakianza kunizungumza vibaya.SOMA ZAIDI.
📌Yawasha umeme ukanda wa Nyasa kitongoji cha Nkanda
📌Yapongezwa kufikisha umeme kwenye mazingira magumu Njombe
📌Bodi ya REA yasisitiza wananchi kuchangamkia fursa uwepo wa nishati ya umeme
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijni (REA), unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa na watakaopewa zabuni ya kutekeleza miradi ili kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi.
Hayo yamebainishwa leo Mei 25, 2026 na Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), wakati wa hafla ya kukagua miradi, kutembelea na kuwasha umeme kitongoji cha Nkanda kilichopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe mradi uliokuwa unatekelezwa na Suma Jkt Electric Company Ltd.
Mha. Ahmed Chinemba amesema kuwa, mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji vya mwambao wilayani Ludewa unatekelezwa na mkandarasi M/S SUMAJKT ELECTRIC COMPANY LTD kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2 ili wananchi wa mwambao wapate huduma ya umeme.
"Mradi huu umelenga kuongeza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa kitongoji cha nkanda ukiwa na chachu ya kutoa fursa za kibiashara kwa kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kurahisiha upatikanaji wa huduma za kijamii na uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo kama mashine za kusaga, mashine za kuchana mbao pamoja na mashine za kuchomelea," Amesema Mha. Chinemba.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Suma JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi, ameishukuru REA kwa kuwapatia kazi hiyo ya kufikisha umeme katika maeneo ya mwambao kikiwemo kitongoji hicho cha Nkanda ambapo kazi imekamilika kwa ubora.
"Sisi Suma JKT tumefanisha kufikisha umeme kwenye mazingira magumu kama haya ambayo yalikuwa na changamoto nyingi lakini tumefanikiwa na sasa tunaona matunda yake, " Amesema Brigedia Jenerali Lupi.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mha. Deogratius Nagu amesema katika kitongoji cha Nkanda takribani shilingi milioni 450 zimetolewa na Serikali kupitia REA ili kufikisha huduma ya umeme katika kitongoji hicho.
Aidha, amewataka wananchi wa Nkanda kuchangamkia fursa ya uwepo wa umeme kwa kuhakikisha wanafanya wiring katika nyumba zao na kuunganisha umeme kwa wingi ili wanufaike na umeme huo katika kitongoji chao.
Naye, Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo hilo Bw. Stanslaus Gowele amesema ujio wa umeme maeneo ya mwambao yanakwenda kuongeza chachu ya Maendeleo kiuchumi na kijamii kwa wananchi hao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa lei Mei 25, 2026 akipanda mti aina ya mwembe katika eneo la Shule ya Sekondari ya Ndaoya, Mtaa wa Chongoleani jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026
....
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa amezitaka halmashauri, taasisi binafsi, mashirika mbalimbali pamoja na wananchi kuendelea kushirikiana na na Serikali katika kuhakikisha maeneo yanakuwa safi na salama.
Ametoa rai hiyo wakati akizungumza na wananchi mara baada ya kuongoza zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira jijini Tanga leo Mei 25, 2026 kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.
Mhe. Kwagilwa alisema kuwa katika suala la usafi wa mazingira sekta binafsi ina nafasi kubwa ya kuwekeza katika teknolojia na mifumo bora ya usimamizi wa taka na urejelezaji ili kupunguza athari za taka kwa mazingira.
Alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha mazingira yanakuwa safi kuanzia nyumbani, maeneo ya biashara, taasisi, masoko hadi maeneo ya wazi huku akiwataka wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya mifumo ya ukusanyaji na utupaji wa taka pamoja na kuepuka vitendo vya uchafuzi wa mazingira.
“Mazingira machafu yana athari kubwa kwa afya na uchumi wa jamii. Uwepo wa taka ovyo, mifereji iliyoziba na uchafuzi wa mazingira huchangia kuenea kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu, malaria na magonjwa ya mlipuko. Hivyo, shughuli ya leo isiwe ya siku moja tu, bali iwe sehemu ya utamaduni wetu wa kila siku,” alisistiza.
Halikadhalika, Mhe. Kwagilwa alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa zitokanazo na taka ikiwemo uzoaji na urejelezaji wa taka ili kuzalisha mbolea, vyakula vya mifugo na bidhaa za viwandani.
Aliwapongeza wadau mbalimbali ambao wamebadilisha changamoto za taka kuwa fursa na kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika viwanda vya kurejeleza taka akisema kuwa hatua hiyo inachangia upatikanaji wa ajira, kuongeza kipato na kukuza uchumi kwa wananchi.
Pamoja na jitihada hizo za wadau, Naibu Waziri huyo alisema Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kupambana na uchafuzi wa mazingira kwa kuandaa na kutekeleza Mwongozo wa Usimamizi wa Taka Ngumu (Punguza, Tumia Tena na Rejeleza) wa Mwaka 2021.
Aliongeza kuwa sekta binafsi na asasi za kiraia zimeendelea kutekeleza mwongozo huo ambapo baadhi ya viwanda vinavyozalisha bidhaa zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki vimeungana pamoja katika kutekeleza Mpango wa Wajibu wa Wazalishaji wa Kusimamia Taka zinazotokana na bidhaa za wanzozalisha kwa kuondosha taka hizo kwenye Mazingira.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Dadi Kolimba Mhe. Dadi Kolimba alisema mkoa huo umeendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kufanya usafi katika maeneo yao.
Alisema kuwa wananchi wa Jiji la Tanga kila mwisho wa mwezi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hushiriki zoezi la usafi wa mazingira na kuondoa uchafu unaozalishwa katika mitaa ya jiji hilo.
Pia, Mhe. Kolimba alitumia nafasi hiyo kupongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuratibu shughuli za usafi na uhifadhi wa mazingira kupitia zoezi la upandaji wa miti hususan kwa kila halmashauri kupanda miti milioni moja na nusu kila mwaka.
Itakumbukwa kwamba kilele cha Siku ya Mazingira kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026 na kaulimbiu ni ‘‘Dira 2050, Tuwajibike Kukijanisha Tanzania’’ ikilenga kuhamasisha jamii kushirki kikamilifu katika kuleta mageuzi na kuwajibika katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akiongoza zoezi la usafi wa mazingira lililohusisha uokotaji wa taka na kusafisha mifereji ya maji machafu katika eneo la Taifa Road ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa lei Mei 25, 2026 akipanda mti aina ya mwembe katika eneo la Shule ya Sekondari ya Ndaoya, Mtaa wa Chongoleani jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akizungumza na wananchi katika uwanja wa Tangamaano jijini Tanga mara baada ya zoezi la usafi wa mazingira lililohusisha uokotaji wa taka na kusafisha mifereji ya maji machafu katika eneo la Taifa Road ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian alipowasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa kabla ya zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.


