✅ Viwanda vya KEDA, GoodWill Vyachochea Kasi
✅ Wilaya yatenga Hekari 15 ujenzi wa Bandari Kavu
✅ Dkt.Kiruswa Ahimiza uzingatiaji Bei Elekezi za Madini
Kutokana na kuongezeka kwa Kasi ya uwekezaji ya shughuli za uongezaji thamani madini nchini huku ikizidi kujifungamanisha zaidi na sekta nyingine za uchumi, Sekta ya Madini imeendelea kuweka Msingi wa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kujenga uchumi wa Dola Trilioni 1, kupitia viwanda.
Hayo yalibainishwa Agosti 19, 2026 wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, Wilayani Mkuranga iliyolenga kufuatilia shughuli za madini, kubaini changamoto na kutoa maelekezo muhimu.
Katika ziara hiyo , Dkt. Kiruswa alitembelea viwanda vikubwa vya KEDA Tanzania Float Glass kinachozalisha vioo kwa ajili ya maghorofa, magari na matumizi mbalimbali, pamoja na Kiwanda cha GoodWill Ceramic Co.Ltd kinachozalisha vigae vya sakafu na ukutani pamoja na vifaa vya usafi wa majumbani na vyooni na kueleza kuwa, ni jambo la kujivunia kuona Tanzania inaweza kuzalisha bidhaa zinazoweza kuuzwa kwenye mataifa makubwa duniani kama Marekani.
Dkt.Kiruswa alisisitiza uzingatiaji wa bei elekezi zinazotolewa na Serikali kwa madini yanayotumika viwandani, pamoja na kumuagiza Afisa Madini Mkazi Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kwa kushirikiana na Wilaya hiyo kuandaa semina kwa wamiliki wa viwanda na leseni za uchimbaji kuhusu uwajibikaji kwa jamii, utunzaji wa mazingira na masuala mengine ya msingi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mhe. Hadija Nasri Ally, alisema Wilaya hiyo inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa uwekezaji, ikiwemo kutenga ekari 15 kwa ajili ya ujenzi wa Bandari Kavu itakayorahisisha uhifadhi na usafirishaji wa bidhaa zinazozalishwa wilayani humo,
Alisema Mkuranga ina viwanda 275, ambapo 39 vinatumia madini kuzalisha bidhaa mbalimbali, huku shughuli za madini zikichangia shilingi bilioni 3.2 katika mwaka wa fedha 2025/26.
Naye, Meneja Biashara wa KEDA Tanzania, Ruby Zhu, alieleza kuwa, asilimia 98 ya malighafi ya kiwanda hicho inatoka Mkuranga, huku kiwanda kikizalisha takribani tani 600 za vioo kwa siku, vinavyosafirishwa katika masoko mbalimbali duniani ikiwemo Marekani.
Kwa upande wake, Meneja Biashara wa GoodWill, Justin Xie alieleza kwamba, asilimia 90 ya malighafi zinazotumiwa na kiwanda hicho zinatoka Tanzania na kuongeza kuwa, kampuni hiyo imepanua uzalishaji wa bidhaa za majumbani, ikiwemo sinki za kunawia, vifaa vya vyooni na bafu huku bidhaa zao zikiuzwa mataifa mbalimbali ikiwemo nchi za Ulaya na Marekani.
Kuhusu ajira, Xie alisema kiwanda kimetoa ajira za moja kwa moja kwa watanzania zipatazo 3,000 na zisizo za moja kwa moja 12,000.
"Tumeweka mizizi nchini Tanzania, tunaweza kujitolea kubadilisha rasilimali za madini za ndani kuwa bidhaa za usafirishaji nje zenye thamani kubwa, na kuleta ajira zaidi na kodi na kushiriki na idara zote kuzungumzia vizuizi katika mnyororo wa usambazaji wa madini, na kwa pamoja kuendeleza ujenzi wa viwanda nchini Tanzania," alisema Justin Xie.
Kwa mujibu wa Afisa Madini wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, Mhandisi Lameck Gabote, Mkuranga ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa madini ya ujenzi na viwandani yanayohudumia kwa kiasi kikubwa Mkoa wa Dar es Salaam na mikoa jirani.

Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) inaendelea kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga, ikitumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya mionzi na fursa zinazotokana na teknolojia ya nyuklia katika kuchochea maendeleo ya Taifa.
Maonesho hayo, yanayoratibiwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, yanawakutanisha taasisi za Serikali, taasisi za elimu na utafiti, wabunifu, wanafunzi, wataalamu pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu, sayansi na teknolojia.
Katika banda la TAEC, wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali wanaendelea kupata elimu kuhusu jukumu la Tume la kusimamia na kudhibiti matumizi salama ya mionzi nchini, pamoja na mchango wa teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, kilimo, mifugo, maji, viwanda, migodi, utafiti na nishati.
Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo pia unatoa fursa kwa wanafunzi na vijana kufahamu taaluma mbalimbali zinazohusiana na teknolojia ya nyuklia na umuhimu wa kujikita katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM) ili kujenga kizazi cha wataalamu kitakachosaidia Taifa kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Akifungua rasmi maonesho hayo Agosti 18, 2026, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisisitiza umuhimu wa elimu, ujuzi, sayansi, teknolojia na ubunifu katika kujenga uchumi wa kisasa na kuongeza uwezo wa Taifa kutumia maarifa na teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo.
Katika muktadha huo, ushiriki wa TAEC unaunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha sayansi na teknolojia zinatumika moja kwa moja katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Teknolojia ya nyuklia ina matumizi mapana yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo katika uchunguzi na tiba ya magonjwa, kuongeza tija katika kilimo na mifugo, usimamizi wa rasilimali za maji, shughuli za viwandani na migodini, utafiti wa kisayansi pamoja na sekta ya nishati.
Wananchi wanaotembelea banda la TAEC pia wanapata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na wataalamu, kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu usalama wa mionzi, udhibiti wa vyanzo vya mionzi na matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa madhumuni ya amani na maendeleo.
TAEC itaendelea kutoa elimu na kuhamasisha matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia kwa maendeleo endelevu ya Taifa.
“Mionzi kwa Matumizi Salama na Teknolojia ya Nyuklia kwa Maendeleo ya Taifa.”








Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
Msimamizi wa Mradi wa Tanzania FAST Health, Japhet Daud, akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Honoratha Rutatinisibwa, akizungumza wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tanzania FAST Health unaotekelezwa na THPS katika Manispaa ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga, Agosti 19, 2026.












.jpeg)





















































