KAMPUNI ya Oryx Gas imekabidhi mitungi ya gesi ya kupikia 600 kwa makundi mbalimbali ya wajasiriamali wakimo mama lishe huku Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Subira Mgalu akieleza kuwa uamuzi wa Oryx kugawa mitungi hiyo kunakwenda kuondoa kabisa athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa.
Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amesema kilimo cha bangi katika Mkoa wa Mara kimepungua kwa takribani asilimia 80 kutokana na operesheni endelevu zinazotekelezwa na Serikali katika kukabiliana na uzalishaji wa dawa za kulevya.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Hussein Mohamed Omar,  akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Bustani (hawapo pichani) alipotembelea shule hiyo na kukagua maabara mbili za Sayansi zilizojengwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).

 

Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.

Ndoa yetu ilianza kwa amani na matumaini makubwa ya kujenga familia yenye furaha. Hata hivyo, miaka ilipozidi kusonga bila kupata mtoto, furaha hiyo ilianza kutoweka taratibu. 

Kila mwezi ulivyopita bila majibu ya matumaini, ndivyo simanzi na huzuni zilivyozidi kutanda nyumbani kwetu.

Baada ya miaka minane ya ndoa, tulikuwa tumetembelea hospitali na zahanati mbalimbali, tukafanya vipimo vyote vilivyowezekana, lakini madaktari walizidi kutuambia hakuna tatizo la kibiolojia linaloonekana.

​Aibu na maneno ya kejeli kutoka kwa baadhi ya ndugu na majirani yalianza kutuandama. Wengi walimnyooshea mke wangu kidole, na hata wengine walinishauri nimfukuze na kuoa mwanamke mwingine.

Mke wangu alilia kila usiku, na mimi nilijikuta nikiwa sina la kufanya huku nikishuhudia amani na matumaini ya familia yetu yakiporomoka. SOMA ZAIDI.

 

Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.

Baba yangu mzazi kabla ya kufariki dunia, aliniachia eneo kubwa la shamba la urithi kama mtoto wake wa pekee wa kiume ili liwe msingi wa maisha yangu na familia yangu.

Hata hivyo, baada tu ya mazishi yake kuisha, wajomba na ndugu wa karibu walianza kuweka mpango wa kuninyang’anya haki hiyo.

Walitengeneza nyaraka za uongo, wakadai kuwa baba hakuwahi kumiliki eneo hilo peke yake, na kunifungulia kesi iliyodumu mahakamani kwa miaka kumi mtawalia.

​Kwa miaka hiyo yote kumi, nilitumia akiba yangu yote kulipa mawakili na gharama za kesi. Kila mara tulipokaribia kufanya maamuzi, kesi iliahirishwa au nyaraka muhimu zilipotea kimiujiza.

Ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuninyanyasa, huku mimi nikibaki maskini wa kutupwa na mwenye msongo mkubwa wa mawazo. Nilihisi kutengwa na kudhulumiwa jasho la marehemu baba yangu.SOMA ZAIDI.

 


Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.

Binti yangu alikuwa mtoto mwenye bidii na mwenye kuonyesha uwezo mkubwa wa akili darasani wakati wa vipindi vya kawaida. Walimu walimsifu kwa ustahimilivu na uwezo wake wa kuelewa masomo kwa haraka.

Hata hivyo, kuanzia alipoingia darasa la sita, kulizuka mtihani mzito uliotatiza maisha ya familia yetu. Kila siku ya mtihani ilipofika, binti yangu alipata homa kali ya ghafla, maumivu makali ya tumbo, na kupoteza kuona vizuri kiasi cha kushindwa hata kushika kalamu.

​Tulitembelea hospitali mbalimbali na kufanya vipimo vya kila aina, lakini madaktari walithibitisha kuwa mwili wake haukuwa na ugonjwa wowote wa kimatibabu.

Hali hii ilipojirudia kwa miaka miwili mtawalia, matokeo yake ya shule yaliporomoka vibaya mno, na alianza kuogopa hata kwenda shule. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, Oryx Gas Tanzania imetoa mafunzo ya matumizi salama na sahihi ya gesi ya kupikia kwa makundi ya wajasiriamali mbalimbali yakiwemo mama na baba lishe.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus C. Sangu, akizungumza na waandishi wa habari mjini Sumbawanga, Mkoa wa Rukwa, leo Julai 23, 2026,kuhusu Tanzania kushiriki katika maonesho ya Wajasiliamali Wadogo (Juakali) ya Afrika Mashariki yatakayofanyika Kigali Rwanda mwezi Oktoba mwaka huu. 

Na: Mwandishi Wetu, SUMBAWANGA

Serikali imetangaza kuwa Tanzania itashiriki Maonesho ya 26 ya Wajasiriamali Wadogowadogo, Wadogo na wa Kati (MSMEs) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, maarufu kama Nguvu Kazi/Jua Kali, yatakayofanyika jijini Kigali, Rwanda kuanzia Oktoba 30 hadi Novemba 8, 2026.

Akitoa taarifa kwa umma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, amesema Tanzania itawakilishwa na wajasiriamali 250 kati ya washiriki wapatao 1,000 wanaotarajiwa kutoka nchi nane wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Amesema kaulimbiu ya maonesho ya mwaka huu ni "Kuendeleza Mnyororo wa Thamani kwenye Sekta ya Ngozi na Kilimo cha Bustani (Matunda na Mbogamboga) katika Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki."

 "Maonesho hayo yanalenga kuwawezesha wajasiriamali kurasimisha shughuli zao za biashara, kutangaza bidhaa na huduma, kubadilishana uzoefu, kuongeza ujuzi wa uzalishaji pamoja na kupanua masoko ya bidhaa na teknolojia za uzalishaji."amesema Waziri Sangu 

Ameongeza kuwa ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha sekta ya ujasiriamali, kukuza biashara za ndani na nje ya nchi, pamoja na kuongeza fursa za ajira zenye staha kwa Watanzania.

Aidha, Waziri Sangu amewataka wajasiriamali wenye sifa kutumia fursa hiyo kwa kujisajili kushiriki maonesho hayo kuanzia sasa hadi Septemba 30, 2026 kupitia mfumo rasmi wa usajili uliotengwa kwa ajili ya washiriki.

Maonesho ya Nguvu Kazi/Jua Kali ni miongoni mwa majukwaa makubwa ya biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki yanayowakutanisha wajasiriamali, wawekezaji na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kuongeza ushindani wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda huo.


Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.

Mwanangu wa kiume alikuwa akiongoza darasani tangu anaanza shule. Alikuwa mtoto mwenye akili nyingi, mwenye bidii, na fahari kubwa ya familia yetu. Hata hivyo, alipoingia kidato cha tatu, mambo yalibadilika ghafla.

Ripoti zake za shule zilianza kuonyesha maksi za chini sana, alipoteza hamu ya kusoma, na walimu wake walianza kulalamika kuwa anakaa darasani akiwa amezubaa na kukosa ushirikiano.

​Nilitumia fedha nyingi kumlipia walimu wa ziada (tuition) na kununua vitabu vya kila aina, lakini hakuna kilichobadilika. Kila mtihani uliporudi, matokeo yalikuwa mabaya zaidi kuliko ya nyuma.

Nilianza kuchanganyikiwa na kuhisi kuwa siku za usoni za mwanangu zinasambaratika mbele ya macho yangu. SOMA ZAIDI.
Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.

Urafiki wa miaka mingi unaweza kukudanganya ukadhani unamjua mtu kwa undani. Rafiki yangu wa karibu, niliyemwamini na kushirikiana naye kwa kila jambo, alinigeuka kwa namna mbaya zaidi.

Siku moja nilipokea simu kutoka kwa taasisi ya mikopo wakinidai fedha nyingi ambazo sikuwahi kuzikopa. Baada ya kufuatilia, nilipata mshtuko mkubwa.

Baada ya kugundua kuwa rafiki yangu alitengeneza nyaraka za uongo na kutumia kitambulisho changu kukopa mamilioni ya fedha, kisha akatoweka na kukata mawasiliano.

​Riba zilianza kuongezeka, na watoa mikopo walianza kunitishia kunipiga mnada na kunichukulia hatua za kisheria. Nilipoteza amani ya moyo, sikuweza kulala usiku, na jina langu lilikuwa hatarini kuchafuka kabisa kwa kosa ambalo sikufanya. SOMA ZAIDI.
Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.

Kwa miaka saba mtawalia, nilikuwa mfanyakazi wa mfano kwenye kampuni yetu. Nilijitolea kwa moyo wote, nikifanya kazi hadi usiku wa manane na kuacha familia yangu nyuma ili kuhakikisha kampuni inapata faida.

Hata hivyo, uaminifu wangu haukuthaminiwa. Siku moja niliitwa ofisini kwa Mkurugenzi na kupewa barua ya kufukuzwa kazi mara moja, kisa ikiwa ni fitina zilizotengenezwa na bosi mpya aliyekuwa ananionea wivu.

​Nilipoteza kila kitu kwa sekunde moja. Bado nilikuwa na madeni ya benki, kodi ya nyumba ilikuwa inakaribia kuisha, na watoto wangu walihitaji ada za shule. Kwa miezi miwili ya mwanzo, maisha yaligeuka kuwa usiku mnene.

Nilihisi kuchezewa akili, kupotezewa muda wangu, na kukatishwa tamaa na mfumo mzima wa maisha.SOMA ZAIDI.



Na Mwandishi Wetu - Pwani.


Serikali imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana na utendaji wa mazoea na kujielekeza katika uongozi unaozingatia matokeo, ubunifu, uwajibikaji na ushirikiano wa karibu na sekta binafsi ili kuharakisha utekelezaji wa DIRA ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Wito huo ulitolewa Jumanne jioni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, wakati akifungua Mafunzo Elekezi kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali yanayoratibiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.


Mafunzo hayo ya siku nne yanafanyika chini ya kaulimbiu "Kutoka Maono mpaka Matokeo: Kufungamanisha Utendaji wa Mashirika ya Umma na DIRA 2050."

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mkumbo alisema Tanzania imeweka lengo la kufikia uchumi wa kati wa juu na kukuza Pato la Taifa (GDP) kutoka dola za Marekani bilioni 85 hadi dola trilioni 1 ifikapo mwaka 2050 kupitia DIRA 2050.

Alisema mafanikio ya DIRA hiyo hayatategemea ubora wa sera na mipango iliyoandaliwa pekee, bali uwezo wa viongozi wa Taasisi za Umma kutafsiri maono hayo kuwa matokeo yanayoonekana katika maisha ya wananchi.

“Jukumu mlilonalo ni kubwa. Tunahitaji viongozi wenye maono, uwajibikaji, ubunifu na uadilifu watakaoweza kutafsiri DIRA 2050 kuwa matokeo yanayopimika,” alisema.

Prof. Mkumbo alisema dunia ya sasa inabadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya teknolojia, ushindani wa kimataifa wa kuvutia uwekezaji, mabadiliko ya tabianchi na mabadiliko ya masoko ya dunia, hivyo Taasisi za Umma hazina budi kubadilika ili ziwe sehemu ya suluhisho la changamoto za maendeleo.

Alisisitiza kuwa Serikali haitapima mafanikio ya taasisi kwa idadi ya vikao vinavyofanyika au taarifa zinazoandaliwa, bali kwa matokeo yanayopatikana kupitia utoaji wa huduma bora, ongezeko la tija, uwekezaji, ajira na mapato ya Serikali.

Aidha, aliwataka Watendaji Wakuu kuhakikisha mipango ya kimkakati ya taasisi zao, bajeti, mipango ya mwaka, mikataba ya utendaji na viashiria vya utendaji vinaendana na DIRA 2050 ili kila taasisi iwe na mchango unaopimika katika utekelezaji wa malengo ya Taifa.

Alisema DIRA hiyo imebainisha sekta za kimageuzi zitakazochochea ukuaji wa uchumi, zikiwemo kilimo, viwanda, utalii, ujenzi, madini, uchumi wa buluu, michezo na ubunifu, huduma za kifedha pamoja na sekta ya huduma, huku Taasisi za Umma zikipewa jukumu la kuwezesha ukuaji wa sekta hizo.

Prof. Mkumbo alisema utekelezaji wa DIRA 2050 unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, sekta binafsi, wananchi na wadau wa maendeleo.

Alieleza kuwa sekta binafsi ndiyo injini ya uwekezaji, ubunifu, uzalishaji na uundaji wa ajira, hivyo Taasisi za Umma zinapaswa kujiona si wadhibiti wa maendeleo pekee, bali pia wawezeshaji wa uwekezaji kwa kuweka mazingira rafiki ya biashara na kuvutia mitaji.

“Tunapaswa kujenga mazingira yatakayowezesha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa DIRA 2050. Ushirikiano huo ndio utakaoharakisha ukuaji wa uchumi na kufikia malengo ya Taifa,” alisema huku akionya taasisi za umma kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji.


Aliongeza: “Ninyi mmepewa dhamana ya kuongoza mageuzi ya Taasisi za Umma. Watanzania wanatarajia kuona matokeo kupitia uongozi wenu. Fanyeni kazi kwa bidii, uadilifu na ubunifu ili taasisi mnazoziongoza ziwe chachu ya kufanikisha DIRA ya Taifa ya Maendeleo 2050.”
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, alisema kaulimbiu ya mwaka huu inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha DIRA ya Taifa ya Maendeleo 2050 haitabaki kuwa maono ya muda mrefu, bali inageuzwa kuwa matokeo yanayopimika kupitia utendaji wa Taasisi za Umma.

“Hatutaifikia Tanzania tunayoitamani kwa kutegemea sera pekee. Tunahitaji taasisi zenye viongozi wanaoweza kutafsiri maono ya Taifa kuwa matokeo yanayopimika katika kila sekta,” alisema.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, alisema Watendaji Wakuu wana wajibu wa kuhakikisha taasisi wanazoongoza zinakuwa chachu ya kuvutia uwekezaji, kuongeza ushindani wa uchumi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisisitiza kuwa uongozi wenye maono, unaozingatia uwajibikaji na matumizi bora ya rasilimali za umma ni nguzo muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kuharakisha maendeleo endelevu ya nchi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, alisema mafunzo hayo ya siku nne ni sehemu ya utekelezaji wa sera za maendeleo ya rasilimali watu na uongozi katika Utumishi wa Umma, yakilenga kuwawezesha Watendaji Wakuu kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Alisema matarajio ya Serikali ni kwamba maarifa na ujuzi watakaoupata washiriki kupitia mafunzo hayo yataakisiwa katika utendaji wao wa kila siku, hivyo kuimarisha ufanisi wa taasisi wanazoongoza na kuchangia kwa kiwango kikubwa kufanikisha utekelezaji wa Dira 2050.

“Matarajio yetu ni kuwa maarifa na ujuzi mtakaoupata kupitia mafunzo haya vitaonekana katika utendaji wenu wa kila siku na hatimaye kuchangia kwa kiwango kikubwa kufanikisha utekelezaji wa Dira 2050,” alisisitiza Bw. Mkomi.

Akihitimisha, aliwataka washiriki kuwasilisha mapendekezo kuhusu mahitaji ya rasilimali watu yatakayowezesha taasisi wanazoongoza kuwa chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Kwa mujibu wa Msajili wa Hazina, ndiyo sababu Ofisi ya Msajili wa Hazina, kwa kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI, imeendelea kuwekeza katika maendeleo ya uongozi kupitia mafunzo elekezi kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali.

Alisema tangu programu hiyo ilipoanzishwa mwaka 2024, zaidi ya Watendaji Wakuu 187 wamepatiwa mafunzo hayo, huku viongozi wapatao 57 wakishiriki katika awamu ya mwaka huu.

Bw. Mchechu alisema mafunzo hayo yanawajengea viongozi uelewa wa matarajio ya Serikali, utawala bora, uwajibikaji, usimamizi wa uwekezaji wa umma, matumizi bora ya rasilimali na uongozi unaozingatia matokeo.

Alisema uwekezaji huo katika maendeleo ya viongozi tayari umeanza kuleta matokeo chanya, ambapo makusanyo ya gawio na michango yameongezeka kutoka Sh637 bilioni mwaka wa fedha 2020/21 hadi Sh1.327 trilioni mwaka 2025/26, sawa na ongezeko la asilimia 108.

“Matokeo haya yanaonesha kuwa uwekezaji katika uongozi ni uwekezaji katika uchumi wa Taifa. Kadiri tunavyojenga viongozi wenye uwezo, ndivyo tunavyojenga taasisi zenye tija na kuongeza mchango wake katika mapato ya Serikali,” alisema.

Alisema katika kipindi cha utekelezaji wa DIRA 2050, Ofisi ya Msajili wa Hazina imeainisha maeneo matano ya kimkakati yatakayoongoza mageuzi ya Taasisi za Umma.

Maeneo hayo ni kuimarisha utawala bora, kuendeleza uongozi na rasilimali watu, kuimarisha usimamizi wa utendaji unaotegemea viashiria na ushahidi, kuwezesha upatikanaji wa rasilimali kupitia ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), masoko ya mitaji na mifuko ya uwekezaji, pamoja na kuongeza tija, faida na thamani ya uwekezaji wa Serikali.

Aliongeza kuwa mafanikio ya maeneo hayo yanategemea pia ushirikiano wa karibu kati ya Taasisi za Umma na sekta binafsi, ili kuongeza uwekezaji, matumizi ya teknolojia, ubunifu, ushindani wa uchumi na ajira.

Naye Bw. Kadari Singo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, alisema kuwa mafanikio ya utekelezaji wa Dira 2050 yatategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa mfumo imara wa uongozi.

Alisema ni muhimu kujenga mifumo ya kutambua na kuendeleza vipaji vya uongozi, kuhakikisha viongozi wanawekwa katika nafasi zinazolingana na uwezo wao, kuweka mipaka ya wazi ya mamlaka na majukumu yao, pamoja na kuimarisha uwajibikaji katika ngazi zote za uongozi.

"Masuala haya yanapaswa kupewa kipaumbele na kuzingatiwa kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," alisema.

Katika mafunzo hayo ya siku nne, washiriki watapata mada kuhusu afya na ustawi wa viongozi, kufungamanisha mipango ya taasisi na DIRA 2050, uongozi wa kimkakati, usimamizi wa migogoro, usimamizi wa uwekezaji wa Serikali, utawala bora, usimamizi wa vihatarishi, ESG, fedha, ukaguzi pamoja na zoezi la kuandaa ahadi binafsi za utekelezaji wa DIRA 2050.

>
Kuanzia chini kabisa ni mtihani ambao watu wengi wanauogopa, lakini kwangu haikuwa hiari. Miaka michache iliyopita, nilijikuta kwenye hali ngumu sana ya kiuchumi. Mfukoni nilikuwa na shilingi elfu kumi tu, fedha iliyobaki baada ya kupoteza kazi na kukataliwa kila kona. TAZAMA VIDEO HAPA.

Badala ya kukata tamaa na kuitumia kwa chakula cha siku mbili, niliamua kuchukua hatua ya kipekee nilinunua bidhaa ndogo za viungo na kuanza kuzitembeza mtaani nyumba kwa nyumba.

​Maisha ya biashara ya mtaji mdogo hayakuwa mepesi. Nilitembea umbali mrefu chini ya jua kali, nilipatwa na dharau na kukatishwa tamaa na watu wengi.

Kwa miezi kadhaa, biashara ilikuwa ikienda kwa kusua sua mno; faida niliyopata ilikuwa ndogo sana kiasi cha kushindwa hata kukuza mtaji wangu. Nilijihisi kama ninazunguka kwenye duara lile lile bila kupiga hatua.
Maisha yangu kwa miaka mingi yalikuwa kama mduara usio na mwisho wa kufeli. Kila jambo jema nililojaribu kuanzisha liliporomoka dakika za mwisho. Kama ni biashara, ilikufa ghafla pindi tu nilipoweka Mtaji.TAZAMA VIDEO HAPA.

Kama ni mahusiano, yalivunjika bila sababu ya msingi; na hata nilipopata fedha, zilipotea bila kufanya la maana. Nilikabiliwa na mikosi mfululizo kiasi cha kuanza kuamini kuwa labda nilizaliwa chini ya nyota ya nuksi na bahati mbaya tu.

​Ndugu na marafiki walizoea kuniona kama mtu wa mikosi. Kila nilipoomba msaada au ushauri, nilionekana kama mzigo. Msongo wa mawazo ulinisonga sana, na matumaini ya kufanikiwa maishani yalianza kutoweka kabisa.
Kuwekeza akiba yangu yote kwenye duka la bidhaa za jumla ilikuwa hatua kubwa ya kimaisha. Hata hivyo, biashara hiyo iligeuka kuwa chanzo cha maumivu makubwa. Ndani ya miezi sita tu, wezi walivamia duka langu mara tatu mtawalia....TAZAMA VIDEO HAPA.

Kila mara walivunja kufuli na kubeba bidhaa za thamani kubwa pamoja meza ya fedha. Nilipata hasara ya mamilioni ya fedha, na ripoti za polisi hazikuzaa matunda yoyote.

​Nilishindwa kulala usiku kwa hofu na wasiwasi. Nilikopa fedha tena ili kujiweka sawa, lakini mawazo ya kuvamiwa tena yalinikosesha amani. Nilijua wazi kuwa uvamizi mwingine mmoja ungekuwa mwisho wa biashara yangu na mwanzo wa umaskini wa kutupwa. 

Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.



📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi.

📌 Amuagiza mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji na kuzingatia masharti ya mkataba.

📌 Aelekeza hatua stahiki kuchukuliwa iwapo maendeleo ya mradi hayataboreshwa kabla ya Septemba 30, 2026.

📌 Mradi wa kV 220 utaiunganisha Mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye Gridi ya Taifa na kuimarisha upatikanaji wa umeme Kusini mwa Tanzania.


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameonesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Songea hadi Masasi kupitia Tunduru na kuagiza mkandarasi kuongeza juhudi ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo leo Julai 22, 2026, Mhe. Ndejembi amesema Serikali haitakuwa tayari kuona miradi ya kimkakati inayogusa maisha ya wananchi ikicheleweshwa bila sababu za msingi.

Amesema mradi huo ni miongoni mwa miradi muhimu ya Sekta ya Nishati inayopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na mchango wake katika kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Kusini.

“Maendeleo ya mradi huu hayaridhishi ukilinganisha na muda uliopita tangu utekelezaji wake uanze. Serikali inatarajia kuona kasi kubwa zaidi ya utekelezaji katika kipindi kilichobaki. Nimemuagiza Katibu Mkuu kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maelekezo haya na kuhakikisha hatua stahiki zinachukuliwa iwapo hakutakuwa na maboresho yanayoonekana,” amesema Mhe. Ndejembi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mhe. Boniface Magiri, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, amesema Mkoa utaendelea kushirikiana na Serikali Kuu katika kufuatilia utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha unakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi kwa wakati.

Naye Mhe. Sikudhani Chikambo kwa niaba ya wabunge wa Mkoa wa Ruvuma, viongozi hao wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya umeme ambayo itachochea ukuaji wa uchumi, uwekezaji na kuboresha huduma za kijamii katika maeneo ya Kusini mwa Tanzania.

Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Songea kupitia Tunduru hadi Masasi unatekelezwa na Mkandarasi Kalpataru Power kutoka India. Mradi huo unatarajiwa kuiunganisha Mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye Gridi ya Taifa pamoja na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Wilaya ya Tunduru na maeneo jirani.












 


📌Ni baada ya kukamilika kwa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 33 Masasi - Mtwara

📌Mradi umeimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa Wilaya ya Newala na maeneo jirani.

📌MD Twange asema thamani ya mradi ni takribani shilingi bilioni 4.65


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amezindua rasmi mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 33 kutoka Masasi hadi Newala, akieleza kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi na kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika Wilaya ya Newala.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa njia hiyo, Mhe. Ndejembi amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuwekeza katika miradi ya kimkakati ya umeme ili kuhakikisha huduma ya nishati inawafikia wananchi wengi zaidi na kuwa chachu ya maendeleo.

"Njia hii ya umeme ni msingi wa kukuza uchumi, kuongeza uzalishaji, kuvutia uwekezaji na kuboresha upatikanaji wa umeme kwa Wilaya ya Newala," amesema Mhe. Ndejembi.

Aidha, Waziri Ndejembi amesema Serikali itaendelea kuhakikisha Mikoa ya Lindi na Mtwara inapata umeme wa uhakika ikiwa ni pamoja na kuiunganisha Mikoa hiyo na umeme wa gridi ya Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Donald Msengi amesema miradi mbalimbali imeendelea kutekelezwa Mkoa wa Mtwara.

"Mheshimiwa Waziri niipongeze Serikali kwani Vijiji vyote vya Mkoa wa Mtwara 785 vinapata huduma ya umeme". Amesema Kanali Msengi.

Ameongeza kuwa katika kuboresha huduma kwa wateja mkoa wa Mtwara umepokea vitendea kazi yakiwemo magari kumi na moja, bajaji nne na pikipiki tisa.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema Serikali imekuwa ikiboresha uwekezaji na upatikanaji wa umeme Mikoa ya  Mtwara na Lindi.

"Mahitaji ya Lindi na Mtwara yameendelea kuongezeka na Serikali imewekeza kwenye uzalishaji na hivi sasa Mkoa wa Mtwara tunazalisha zaidi ya megawati 50". Amesema Mha. Mramba.

Awali akitoa taarifa za utekelezaji wa mradi Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Bw. Lazaro Twange amesema ujenzi wa njia hiyo umetekelezwa kwa shilingi bilioni 4.56 kwa umbali wa Kilometa 76 kutoka Masasi hadi Newala.

"Mheshimiwa mgeni rasmi kabla ya mradi huu kutekelezwa Wilaya ya Newala ilikuwa ikipata umeme kutokea Mtwara kupitia Nanyumbu umbali wa kilometa 170, hali iliyochangia tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara". Amesema Bw. Twange.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa njia hiyo ya umeme kumeimarisha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme kwa Wilaya hiyo.

Aidha, Serikali kupitia TANESCO imetenga takribani shilingi bilioni 5.27 kwa ajili ya kujenga kituo cha kubadilishia umeme (Switching Station) kitakacho saidia kuboresha upatikanaji wa umeme na kukidhi mahitaji ya sasa na ya badaye ya wananchi na wawekezaji wa Wilaya ya Newala. 

Mbunge wa Newala Vijijini Dkt. Yahaya Nawanda kwa niaba ya Wabunge wa Mkoa wa Mtwara ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme Mkoa wa Mtwara.













.




NA DENIS CHAMBI TANGA.


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt.Batilda Burian amewasisitiza watumishi wa umma, watendaji wa taasisi pamoja na wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo kutambua thamani ya fedha zinazoteolewa na serikali kwaajili utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kuhakikisha kuwa wanazuia ubadhilifu fedha na mianya yote ya rushwa ambayo inaweza kuwa kikwazo katika utoaji wa huduma kwa wananchi.


Akitoa rai hiyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Tanga, mkuu wa wilaya ya Handeni Salum Nyamwese katika warsha ya wadau wa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoa wa Tanga iliyoandaliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU amewataka kuonyesha uzalendo uwajibikaji pamoja na kutokuwa sababu ya kuzuia maendeleo kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa mkoani humo.


"Rushwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya Taifa lolote, kuhujumu matumizi sahihi ya rasilimali za umma, kudhoofisha ubora wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupunguza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi na kuondoa imani kwa wananchi , taasisi za serikali serikali kwa ujumla"


"Hatuwezi kufikia malengo ya maendeleo ambayo tumejiwekea kufikia kwenye dira ya maendeleo ya mwaka 2050 ikiwa tutaruhusu rushwa, ubadhilifu , ufisadi na ukiukwaji wa taratibu kuendelea" amesema Nyamwese


"Mapambano dhidi ya rushwa sio jukumu la TAKUKURU pekee mapambano haya ni ya kwetu sisi sote ambao tuna wajibu Kila kiongozi na Kila mtishi kwenye eneo lake kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa na hii inaakisi kaulimbiu ya kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu tutimize wajibu wetu" amesisitiza.

Amesema serikali inautazama mkoa wa Tanga kama kitomvu cha biashara na utakaowavutia wawekezaji mbalimbali kutoka nje ya nchi kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo bomba la mafuta , ujenzi wa barabara inayotoka Tanga Hadi Dar es salaam pamoja na uboreshaji wa bandari ambapo kupitia fedha zilizoletwa ndani ya miaka mitano takribani Trillion 3.17 hazitokuwa na maana kama watendaji wa wasimamizi wa miradi hiyo hawatawajibika kikamilifu kwenye nafasi zao.


"Rais ametuamini na kutukabidhi dhamana ya kusimamia rasilimali za umma kwa niaba ya wananchi, hizo fedha zinazokuja na kupelekwa kwenye miradi hatuna budi kuonyesha kwamba imani hiyo hajaiweka mahali pasipo sahihi Kila moja wetu awajinike kikamilifu katika kufanya kazi kwa weledi ubadhilifu na uzalendo wa hali ya juu sisi kama watendaji kazi kubwa tuliyonayo ni kidaiwa matokeo" ameongeza Nyamwese.


Awali akizungumza mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa Tanga 'TAKUKURU' Ramadhani Ndwatah amesema kuwa wamefanikiwa kufanya tahmini na kupitia miradi yote inayotekelezwa ndani ya mkoa ambapo wamebaini baadhi ya changamoto zilizochangiwa na usimamizi mbovu, ucheleweshwaji wa miradi na matumizi yasiyosahihi ya fedha zilizotolewa kwenye miradi husika ambapo iliweza kuchukua hatua kisheria .


" Licha ya mafanikio yaliyopatikana kwenye miradi ya maendeleo lakini bado kuna changamoto ya udhaifu katika utekelezaji wa miradi ucheleweshwaji wa miradi kwa baadhi ya wadau wenye dhamana, kuongeza gharama zisizo za lazima na kupunguza manufaa yanahotarajiwa kwa wananchi"


"Kutokana na changamoto hizo zilizojitoleza tumeona ni vyema kukaa na wadau wa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili tuweze kukumbuahana kuhusu wajibu wao katika usimamizi na utekelezaji wa programu na miradi inayotekelezwa katika maeneo yetu" amesema Ndwatah.


Amewataka wadau wote wenye dhamana ya usimamizi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kushirikiana kikamilifu na TAKUKURU ili kuweza kutimiza adhima ya serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo kupitia miradi inayotekelezwa kwenye maendeleo mbalimbali.


Akizungumza katika warsha hiyo mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Tanga mhandishi Juma Hamsini ameiomba serikali kupitia mamlaka za serikali tawala za mikoa na serikali za mitaa 'TAMUSEMI' mara wanapopeleka BOQ za ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo madarasa kuzingatia thamani halisi ya vifaa vinavyotumika kwenye miradi husika.











Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid , ameshiriki Mkutano Mkuu wa Chama cha Botswana National Front (BNF) unaofanyika mjini Jwaneng, Botswana, akiwakilisha Chama Cha Mapinduzi.




Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Rabia amesisitiza kuwa kila chama tawala kina wajibu wa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, kuimarisha misingi ya utawala bora, na kuendelea kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wananchi bila kuchoka.




Aidha, amekisii Chama cha BNF kuendelea kuzingatia maslahi ya wananchi katika utekelezaji wa sera na maamuzi yake, pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna mwananchi anayebaki nyuma katika mchakato wa maendeleo ya taifa.


Aidha,Ndg. Rabia amempongeza Rais wa Chama cha Botswana National Front (BNF) na Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Duma Gideon Boko kwa ushindi wa Chama chake na kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Jamhuri ya Botswana.

Ameeleza kuwa kuchaguliwa kwa Rais Boko na Chama cha BNF ni kielelezo cha imani waliyopewa na wananchi wa Botswana na amewatakia mafanikio katika kuwaletea maendeleo na ustawi wao.
Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu akipata Maelezo kutoka kwa msimamizi wa mradi wa ujenzi wa madarasa Noble Helium ambayo Inafanya shughuli za utafiti na uchimbaji wa gesi ya helium Christian Temba (20 Julai 2026) alipokuwa akikagua miradi ya Maendeleo katika Kijiji cha Kinambo Kata ya Milepa Wilaya ya Sumbawanga.