Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Akiongoza Kikao Maalum cha Halmashauri  Kuu ya CCM Taifa  kilichofanyika Zanzibar Jumatano tarehe 29 Julai, 2026.











Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Dar es Salaam imeandika historia mpya katika harakati za kuboresha huduma za afya baada ya Mkoa wa Manyara kufanikisha zoezi kubwa la kuchangisha fedha lililowezesha kupatikana kwa zaidi ya Shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa njiti na kuimarisha huduma za afya katika mkoa huo.


Fedha hizo zilikusanywa kupitia hafla maalumu ya chakula cha jioni cha hisani (Manyara Tanzanite Marathon Dinner Gala) iliyofanyika Julai 24, 2026 katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya Hatua Moja Okoa Maisha ya Mtoto, ambayo inalenga kuongeza upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa, kuboresha huduma za watoto wachanga na kupunguza vifo vinavyotokana na kuzaliwa njiti.


Jumla ya Shilingi 1,356,900,000 zilipatikana kupitia ahadi za michango na fedha taslimu kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo, taasisi za fedha, makampuni binafsi, viongozi wa Serikali, wabunge, wafanyabiashara na wananchi waliojitokeza kuunga mkono kampeni hiyo.



Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa kitaifa na kikanda pamoja na wadau wa sekta ya afya, ambapo mshikamano mkubwa ulionekana katika jitihada za kuhakikisha watoto wanaozaliwa njiti wanapata huduma bora na salama.


Akizungumza baada ya harambee hiyo, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Babati Vijijini, Mhe. Daniel Baran Sillo, aliyekuwa mgeni rasmi, alisema mafanikio hayo yanaonesha moyo wa uzalendo na mshikamano wa Watanzania katika kusaidia sekta ya afya.


Alisema lengo la kampeni hiyo ni kufikisha zaidi ya Shilingi bilioni 1.5, huku akiwakaribisha Watanzania kushiriki Manyara Tanzanite Marathon itakayofanyika Agosti 22, 2026 mkoani Manyara.





“Tunawashukuru wadau wote waliojitokeza na kuchangia. Kila mchango una maana kubwa katika kuokoa maisha ya watoto wetu. Tunataka kuhakikisha hospitali zetu zinakuwa na vifaa vinavyohitajika kuwahudumia watoto njiti kwa kiwango cha kisasa,” alisema Mhe. Sillo.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, alisema kampeni hiyo imeibuka kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha nguvu za Serikali na sekta binafsi katika kuboresha huduma za afya kwa mama na mtoto.


Aliwataka wananchi, taasisi na wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kuchangia ili kufanikisha lengo lililowekwa, akisisitiza kuwa uwekezaji katika afya ya watoto ni uwekezaji katika mustakabali wa taifa.







“Kila mtoto ana haki ya kuishi. Tunapowekeza katika vifaa tiba na huduma za watoto njiti, tunaokoa familia, tunaimarisha jamii na tunajenga taifa lenye nguvu,” alisema Mhe. Sendiga.


Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method, alieleza kuwa mkoa huo unakabiliwa na changamoto kubwa ya watoto wanaozaliwa njiti, ambapo kati ya watoto 3,000 hadi 3,200 huzaliwa njiti kila mwaka.


Alisema idadi hiyo inaweka shinikizo kubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya, hasa katika upatikanaji wa mashine za kusaidia watoto kupumua, incubators, vifaa vya ufuatiliaji wa afya za watoto wachanga na miundombinu ya huduma maalumu.



“Watoto njiti wanahitaji uangalizi wa karibu na vifaa maalumu. Bila uwekezaji wa kutosha, tunakuwa katika hatari ya kupoteza maisha ambayo yangeweza kuokolewa,” alisema Dkt. Method.


Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, kuzaliwa njiti ni miongoni mwa sababu kuu zinazochangia vifo vya watoto wachanga duniani, na huduma bora katika saa na siku za mwanzo baada ya kuzaliwa ndiyo huamua kwa kiasi kikubwa uwezekano wa mtoto kuendelea kuishi.


Wadau waliohudhuria hafla hiyo walieleza kuwa kampeni hiyo imeonesha mfano wa namna matukio ya michezo yanaweza kutumika kama nyenzo ya kuchangisha fedha kwa ajili ya miradi ya kijamii na maendeleo.



Mbio za Manyara Tanzanite Marathon zimekuwa zikikua kwa kasi na sasa zinatajwa kuwa moja ya matukio makubwa ya michezo na hisani nchini Tanzania, yakilenga kuhamasisha afya, utalii na maendeleo ya jamii kwa wakati mmoja.


Waandaaji wa marathon hiyo walisema fedha zitakazopatikana zitaelekezwa katika ununuzi wa vifaa tiba, uboreshaji wa huduma za watoto wachanga na kuimarisha uwezo wa hospitali za Mkoa wa Manyara kuhudumia watoto njiti kwa ufanisi zaidi.


Kampeni hiyo pia inaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambazo zimekuwa zikilenga kuboresha huduma za afya, kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuimarisha ustawi wa jamii na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora katika maeneo yote ya nchi.




Waandaaji wameendelea kutoa wito kwa Watanzania kushiriki mbio hizo au kuchangia kupitia akaunti maalumu za kampeni, wakisisitiza kuwa kila mchango ni hatua muhimu katika kuokoa maisha ya mtoto mmoja au zaidi.


Michango inaendelea kupokelewa kupitia CRDB Lipa Namba 113069180 na CRDB Account No. 10401215064 (Manyara Tanzania Marathon).


Kwa mafanikio yaliyopatikana katika usiku huo wa kihistoria, Mkoa wa Manyara umeonesha kuwa mshikamano wa jamii unaweza kuwa nguvu kubwa ya kuokoa maisha, huku kampeni ya Hatua Moja Okoa Maisha ya Mtoto ikiendelea kuwa mwanga wa matumaini kwa maelfu ya watoto wanaozaliwa njiti kila mwaka nchini Tanzania.



 

Kazini, kutengwa au kupuuzwa na bosi wako ni moja kati ya mambo yanayoweza kukatisha tamaa na kurudisha nyuma maendeleo yako. Kwa miezi mingi, nilikuwa nikifanya kazi kwenye kampuni moja kubwa, nikijituma kwa uwezo wangu wote.

Lakini bosi wangu alikuwa ananipita kama siioni; hakuwa hata anaitikia salamu zangu. Kila fursa ya kupandishwa cheo au kupata nafasi za kusimamia miradi mikubwa ilipojitokeza, alikuwa akiwapa watu wengine hata wale waliokuwa wageni na walio na uzoefu mdogo kuliko mimi.

​Nilibaki nikijihisi sina thamani, nikiwaza kuacha kazi kila siku. Nilibaini kuwa hata ningefanya kazi kwa bidii vipi, bila nyota yangu kung’aa na kupata kibali mbele ya viongozi, juhudi zangu zote zingepotea bure na ningebaki palepale. SOMA ZAIDI.

 


Kutoa jasho lako kwa miezi kadhaa bila kupata haki yako ni moja ya mateso makubwa zaidi kisaikolojia. Kwa zaidi ya miezi sita, nilifanya kazi kwa bidii na uaminifu mkubwa katika kampuni moja ya kibinafsi, nikijituma usiku na mchana ili kuhakikisha kazi zinaenda vizuri.

Hata hivyo, siku za malipo zilipowadia, mwajiri wangu alianza kutoa visingizio visivyoeleweka. Siku zikawa wiki, na wiki zikawa miezi bila kuona hata senti moja kwenye akaunti yangu.

​Nilipojaribu kumfuata kwa heshima na kudai stahiki zangu, alinijibu kwa dharau na kejeli kubwa, akinitishia kunifuta kazi na hata kuniingiza kwenye matatizo iwapo ningeendelea kumsumbua.

Nilibaki sina la kufanya, nikiwa nimelemewa na madeni ya kodi ya nyumba, ada za watoto, na mahitaji ya kila siku ya familia. Uchungu na kukata tamaa viliniletea msongo mkubwa wa mawazo. SOMA ZAIDI.

 

Kwa miaka mingi nikiwa msichana wa umri wa kuolewa, swali kubwa lililokuwa likisumbua akili yangu usiku na mchana lilikuwa ni nafasi ya nani atakayejiunga na mimi kujenga familia. Nilipita kwenye mahusiano kadhaa yaliyojaa ahadi hewa, kukatishwa tamaa, na maumivu ya moyo.

Kila mwanamume niliyekutana naye alionekana kuwa sahihi kwa nje, lakini haikuchukua muda mrefu kabla ya tabia zao halisi kujitokeza na kuniacha nikiwa nimevunjika moyo. Nilianza kuogopa kuwa huenda nisingeolewa kabisa au ningeingia kwenye mtego wa kuolewa na mtu asiye sahihi.

​Urafiki na mahusiano ya mashaka vilinichosha sana. Nilitamani kujua hatma ya maisha yangu ya mapenzi na kumpata mume wangu halali wa maisha bila kuendelea kupoteza muda na watu wasio na nia njema. SOMA ZAIDI.

 

Shamba langu lilikuwa ndiyo nguzo pekee ya uchumi na tegemeo la maisha ya familia yangu. Niliwekeza jasho na akiba yangu yote kwenye eneo hilo kwa miaka mingi, nikilima na kuendeleza miradi mbalimbali.

Hata hivyo, siku moja nikiwa kwenye shughuli zangu za kila siku, nilipokea taarifa iliyonishtua na kunipiga na butwaa: mtu mmoja mwenye fedha na ushawishi mtaani alikuwa amevamia eneo langu na kudai kuwa yeye ndiye mmiliki halali.

​Nilipojaribu kufuatilia kwenye mamlaka husika, nilipata pigo kubwa zaidi. Hati halisi za umiliki wa shamba langu zilikuwa zimebadilishwa kimyakimya, na jina langu lilikuwa limefutwa kabisa kwenye mfumo!

Kila ofisi niliyotembea kutafuta msaada, niligonga mwamba kwa sababu mpinzani wangu alitumia fedha kufunika ukweli na kunifanya nionekane tapeli. Nilibaki sina la kufanya, nikilia usiku na mchana huku nikishuhudia jasho langu likiporwa mchana kweupe. SOMA ZAIDI.

 

Kwa miaka mingi, nyumba ya familia yetu ilikuwa imepoteza kabisa amani na utulivu. Sehemu iliyopaswa kuwa hifadhi ya upendo na furaha iligeuka kuwa uwanja wa mapambano, migogoro, na chuki zisizo na msingi.

Ndugu wa tumbo mmoja tulikuwa tukitazamana kama maadui wakubwa; maneno ya shombo, majununu, na migogoro ya mara kwa mara kuhusu mali ndogo ndogo vilikuwa vitu vya kawaida kila siku. Hata watoto wetu walianza kuathirika kisaikolojia na kujitenga.

​Kila mara wazee wa familia na viongozi wa kijamii walipoketi ili kutusuluhisha, mazungumzo yaliishia kwenye matusi na ugomvi mkubwa zaidi. 

Kila mtu alihisi analogwa au kuchukiwa na mwenzake, na amani ilionekana kuwa kitu kisichoweza kurejea tena kwenye ukoo wetu. SOMA ZAIDI.

 


Mimi ni mfanyabiashara na mmiliki wa kampuni ndogo ya kandarasi. Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikuwa nikitumia muda mwingi, nguvu, na kiasi kikubwa cha fedha kuandaa nyaraka za zabuni (tenders) mbalimbali za serikali na makampuni binafsi.

Kila mara nilipowasilisha maombi yangu, nilikuwa na matumaini makubwa kwa sababu kampuni yangu ilikuwa na vigezo vyote vilivyohitajika na gharama zetu zilikuwa na ushindani mzuri.

Lakini matokeo yalikuwa yale yale kila siku jina langu halikujitokeza hata mara moja. Kila maombi yalipokataliwa, nilijikuta nikipoteza mtaji na kuingia kwenye madeni makubwa.

Wafanyikazi wangu walizoea kukosa mishahara kwa wakati, na marafiki wengi wa kibiashara waliaza kunikimbia wakiamini kuwa sikuwa na nyota ya mafanikio au uwezo wa kusimamia miradi mikubwa. Msongo wa mawazo ulinikosesha amani ya moyo na usingizi usiku. SOMA ZAIDI.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limekutana na wadau wa sekta ya vipodozi nchini kwa lengo la kutoa elimu kuhusu matakwa ya viwango, ubora na usalama wa bidhaa hizo zinazotumika kwa kiasi kikubwa na Watanzania.
Na Abduly Madenge, WAF – Dar es Salaam

Tanzania imeandika historia mpya katika sekta ya afya baada ya wataalamu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kufanikisha kwa mara ya kwanza upasuaji wa kupandikiza mashine za usikivu (Cochlear Implant) kwa kutumia wataalamu wa ndani pekee, bila kutegemea wataalamu kutoka nje ya nchi.
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

GLOBAL Education Link (GEL) imesema jumla ya wanafunzi, wazazi na walezi 1,113 wamefikiwa na kupatiwa huduma kupitia maonesho ya Global Education Fair 2026 yaliyofanyika Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam.




Na Mwandishi Wetu, Tanga

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Muheza mkoani Tanga kimesema hakihusiki na vitendo vinavyodaiwa kufanywa na aliyekuwa Katibu wa chama hicho wilayani humo, Joseph Mwakidasi, huku kikiwataka wanachama kuendelea kudumisha mshikamano na kuepuka makundi yanayoweza kukigawa chama.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Katibu wa CHADEMA Jimbo la Muheza, Michael Mhina, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio yaliyojitokeza ndani ya chama katika siku za hivi karibuni.

Mhina alisema Julai 8 mwaka huu viongozi wa chama waliona kupitia vyombo vya habari taarifa za Mwakidasi akimtuhumu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, kutumia vibaya fedha zinazochangwa na wanachama kupitia kampeni ya "Tone Tone".

Alisema kutokana na uzito wa tuhuma hizo, Kamati Tendaji ya Wilaya ilikutana kwa dharura Julai 9 na kumuita Mwakidasi ili afafanue chanzo cha madai yake, lakini hakufika wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa m hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki kwenye kikao hicho wala kutoa maelezo.

Mhina alidai kuwa Julai 20, Mwakidasi aliwasili katika ofisi za CHADEMA Wilaya ya Muheza akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi kutoka wilaya nyingine pamoja na watu ambao, kwa mujibu wa chama hicho, si viongozi wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa mweka hazina wa chama.

Kwa mujibu wa Mhina, watu hao walifanya kikao ndani ya ofisi hizo na baadaye kurekodi na kusambaza taarifa mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii, jambo alilodai lilisababisha taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

"Baada ya matukio hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki na yaliyofanywa na watu hao," alisema Mhina.

Alisema viongozi wa chama wilayani humo wanaendelea kumuunga mkono Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, pamoja na Mwenyekiti wa chama, Tundu Lissu.

Pia aliomba vyombo vya dola kuchunguza madai ya kuwahamasisha wananchi kuhudhuria mkutano kwa ahadi ya kulipwa fedha, akisisitiza kuwa CHADEMA haina utaratibu wa kuwalipa wanachama kushirikiio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa shughuli za chama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Ally Mahanyu, alisema chama kinapinga vitendo vinavyodaiwa kufanywa na Mwakidasi kwa madai kuwa vilikiuka taratibu za chama.

Mahanyu alisema viongozi walimuita Mwakidasi mara kadhaa kwenye vikao vya Kamati Tendaji ili kutoa maelezo, lakini hakuitikia wito huo.

Aidha, alivitaka vyombo vya dola kuchunguza matukio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

Aliwataka wanachama wa CHADEMA kuendelea kuwa watulivu, kuwaamini viongozi wao na kushiriki shughuli za ujenzi wa chama kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA Wilaya ya Muheza, Isa Mwaikani, alisema baraza hilo pia lilimuita Mwakidasi kutoa maelezo kuhusu tuhuma alizozielekeza kwa Heche, lakini hakuitikia wito huo.

Mwaikani alisema viongozi wa chama walishangazwa na tuhuma hizo kwa kuwa, kwa mujibu wa muundo wa uongozi wa chama, Makamu Mwenyekiti hahusiki na usimamizi wa fedha.

"Hatuelewi amepata wapi ujasiri wa kumtuhumu kiongozi wa juu wa chama bila kuwasilisha ushahidi kwenye vikao halali vya chama," alisema.

Aliongeza kuwa wanachama wengi wa CHADEMA Muheza wameendelea kubaki ndani ya chama na hali ya kisiasa wilayani humo ni tulivu.



Akijibu tuhuma hizo, aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Joseph Mwakidasi, alisema madai yanayotolewa dhidi yake hayana ukweli na kwamba anaendelea kutetea nafasi yake ndani ya chama.

Alisema hana mpango wa kuhamia chama kingine cha siasa na anasubiri maamuzi ya vikao vya chama kuhusu nafasi yake.

Kuhusu tuhuma alizomwelekeza John Heche, Mwakidasi alisema suala hilo linatokana na mijadala iliyofanyika katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika Dodoma, akidai baadhi ya taarifa zilizokuwa siri zilivuja kutoka ndani ya chama.


Mkuu wa wilaya ya Bahi Mhe. Joachim Thobias Nyingo amekabidhi gari jipya aina ya ‘Toyota Pickup’ kwa Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa wilaya hiyo Mha. Hopeness Liundi huku akitoa wito wa kutumia vizuri kitendea kazi hicho kwa kuongeza kasi ya utendaji kazi kwa tija ili kufikia lengo la kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwafikishia huduma ya Majisafi ya bomba wananchi wa wilaya hiyo.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika ofisi ya Meneja RUWASA Mkoa wa Dodoma Julai 27, 2026 na kuhudhuriwa na Meneja wa Mkoa huo Mha. Beatrice Kasimbazi pamoja na watumishi wengine wa mkoa huo.

Akizungumza kabla ya kuzindua na kukabidhi gari hilo, Mhe. Nyingo aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuiwezesha RUWASA na kuboresha utendaji wao wa kazi ikionesha dhamira ya dhati ya serikali kuwafikishia wananchi huduma muhimu ya majisafi ya bomba.

Hivi karibuni, Serikali kupitia RUWASA ilinunua na kugawa magari 22 katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kuboresha na kuimarisha utendaji wa taasisi katika kusimamia na kufuatilia miradi na huduma ya maji katika maeneo ya vijijini.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa wilaya Nyingo amemkaribisha Meneja mpya wa RUWASA wa mkoa wa Dodoma Mha. Beatrice Kasimbazi ambaye amehamishiwa mkoani humo akitokea mkoa wa Pwani, huku akitoa wito kwa watumishi wa wilaya hiyo kumpokea na kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya serikali na kuwahudumia wananchi.