Na Mwandishi wetu- Dar es salaam


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza Watu Wenye Ulemavu kuwa mabalozi wazuri wa kudumisha amani nchini.


Mhe. Nderiananga alieleza hayo wakati wa kikao chake na Wajumbe wa Bodi ya Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) kilichofanyika mwishoni mwa wiki  katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu uliopo Magogoni jijini Dar es salaam.

Alisema kwamba, ili shughuli za kiuchumi ziweze kufanyika ni lazima iwepo amani kwani wananchi watakuwa na uhuru wa kufanya shughuli zao bila vurugu zozote hatua itakayochagiza ukuaji wa uchumi wao binafsi  hata taifa.

“Tunafahamu yanapotokea madhara watu wa kwanza kuathirika ni watu wenye ulemavu basi tunawashukuru kwa umoja wenu nasi tunawaahidi kuendelea kushirikiana,” alisema Mhe. Nderiananga.


Pia, aliongeza kwamba ipo haja ya Viongozi wa dini kukutana na wakundi ya watu wenye ulemavu kuendelea kuwajenga imani hatua itakayodumisha upendo na mshikamano kama  taifa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu katika Ofisi hiyo Dkt. Jim Yonazi alisema, Ofisi hiyo imedhamiria kuwahudumia watu wenye ulemavu pamoja na kusikiliza kero zao ili kuzitafutia ufumbuzi.


“Ofisi ya Waziri Mkuu ni ya utekelezaji wa shughuli za serikali  hivyo niwakaribishe katika familia hii naamini tutaendelea kushirikiana na kuhakikisha kila mmoja wetu anafaidika na hadhi ya kuwa mtanzania bila kujali hali yake,”alieleza Dkt. Yonazi.

Naye Makamu Mwenyekiti  wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bi. Tungi Mwanjala  aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna inavyojali watu wenye ulemavu.

Aidha Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi Wasiiona (TASODEB) Bw. David Shaba ambaye pia ni mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo  alishauri watu wenye ulemavu kutokubali kutumiwa na watu wenye nia ovu akisema mahali popote zinapotokea vurugu kundi hilo huathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na kukosa msaada wa haraka.

“Niwaombe wenye ulemavu wenzangu tuwe makini sana tusishawishike hovyo, haya mambo ni ya hatari sana tuzingatie hali zetu hatuwezi kukabiliana na fujo vitakapotokea vita  sisi ndio tutaathirika sana zaidi ya hao wanaotuchochea tuwe na msimamo,” alieleza Mwenyekiti huyo.


MWISHOOO

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imewahakikishia Watanzania kuwa itaendelea kuboresha huduma zake kwa kuboresha miundombinu, kupanua mtandao wa usambazaji, ili kutekeleza ajenda ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa ajili ya afya bora, mazingira safi, na maendeleo endelevu.

Ofisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Esther Herman,akizungumza na wananchi leo Disemba Mosi,2025 katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika katika kata ya Msasa mjini Handeni.

Na Mwandishi Wetu, Handeni

Halmashauri ya Mji Handeni imehamasisha jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora kama nguzo muhimu katika kudhibiti maambukizi na kuimarisha afya, hususan kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU).

Akizungumza na wananchi Desemba mosi, 2025, katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika katika kata ya Msasa mjini Handeni, Ofisa Lishe wa Halmashauri hiyo, Esther Herman, amesema lishe bora ina mchango mkubwa katika kuongeza uimara wa kinga ya mwili na kusaidia watumiaji wa dawa za kufubaza Virusi vya UKIMWI (ARV) kustahimili matibabu kwa ufanisi zaidi.

“Lishe bora si suala la hiari, ni msingi wa afya kwa kila mtu, lakini kwa watu wanaoishi na VVU ina umuhimu wa pekee. Ulaji wa mlo kamili huongeza nguvu, hupunguza makali ya magonjwa nyemelezi na kuimarisha mwili kupambana na maambukizi,” amesema

Amesema Halmashauri imetoa mafunzo kuhusu matumizi sahihi ya vyakula vyenye virutubisho, mbinu za kuboresha afya ya mwili, pamoja na uelewa juu ya nafasi ya lishe katika kupunguza hatari za kudhoofika kwa kinga.

Katika maadhimisho hayo yenye Kauli mbiu: “ Imarisha Mwitikio, Tokomeza UKIMWI.” yameandaliwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali wa afya, yakilenga kuongeza mwamko wa wananchi kujua hali zao, kuzingatia kinga, na kushiriki kikamilifu kwenye mapambano dhidi ya UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

Wananchi wamepata huduma mbalimbali ikiwemo ushauri nasaha, vipimo vya hiari vya VVU, elimu ya afya ya uzazi, na uhamasishaji kwa vijana kuongeza ushiriki katika kampeni za kutokomeza UKIMWI nchini.

 


Katika jitihada za kuimarisha utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Wizara ya Nishati kupitia kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia kimetoa mafunzo kwa watumishi 133 wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Akiwasilisha taarifa ya Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya nishati safi ya kupikia, Mhandisi Anitha Ringia kutoka Wizara ya Nishati ameeleza kuwa mafunzo hayo yamelenga kuongeza uelewa juu ya faida za nishati safi, ikiwemo kupunguza athari za kiafya na kimazingira zinazotokana na matumizi ya kuni na mkaa katika kupikia huku akiwaeleza Watumishi kuwa matumizi ya nishati safi ni sehemu ya ajenda ya kitaifa ya kulinda mazingira na kuboresha ustawi wa wananchi.

“Mafunzo haya yanaonesha dhamira ya Serikali katika kuhakikisha Taasisi za Umma zinakuwa mfano wa kuigwa katika matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupitia ninyi watumishi mtafanya uhamasishaji utakaoleta mwamko mpana zaidi kitaifa katika matumizi ya nishati safi na hatimaye kupunguza utegemezi wa nishati zisizo rafiki kwa mazingira." Amesema Ringia

Amesema  Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha nishati safi inapatikana kwa urahisi, na inawanufaisha Watanzania wote ili kuhakikisha ifikapo 2034 asilimia 80% ya Watanzania  wanatumia nishati safi ya kupikia.

Aidha Kupitia mafunzo hayo Mha. Ringia ametoa wito kwa  watumishi wote wa umma kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha jamii kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia huku akiwahimiza kutumia uelewa walioupata kuwa mabalozi katika maeneo yao ya kazi na jamii wanazoishi.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Nishati Bi. Neema Mbuja ameeleza kuwa kupitia Mkakati wa Taifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia wa Mwaka 2024 uliundwa Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia lengo likiwa  ni kuongeza uelewa wa umma na taasisi kuhusu umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupika ili kufanikisha malengo ya Taifa ya kuhakikisha wananchi wanapika kwa  kutumia nishati safi, salama na rafiki wa mazingira.

" Mkakati wa mawasiliano umetokana na Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na lengo lake ni kutoa elimu na kuwawezesha watanzania  kupata taarifa sahihi  juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia,  elimu hii wanaipata kupitia njia mbalimbali ikiwemo  redio, televisheni, mitandao ya kijamii na maonyesho ya wazi, pia kupitia mkakati huu tumeendelea kuhamasisha umma na kufanya kampeni mbalimbali sambamba na kauli mbiu isemayo Nishati Safi ya Kupikia Okoa Maisha na Mazingira." Amesema Bi. Mbuja

Aidha Bi. Mbuja ameongezea kuwa Mkakati wa Mawasiliano umelenga kufikisha ujumbe kwa jamii kupitia vyombo vya habari, mikutano ya hadhara na mafunzo mbalimbali lakini pia kushirikisha  kila mtanzania kulingana na rika na nafasi ya kila mtu mmojammoja  kwa lengo la kuhakikisha ujumbe uliokusudiwa unawafikia Watanzania wote.

Naye Mhandisi Mwandamizi wa Utafiti kutoka Shirika la Umeme Tanzania( TANESCO) Mha. Catherine Mwegoha ameeleza kuwa TANESCO imeendelea kutoa elimu juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia hususani nishati ya umeme kwani ni salama na nafuu kwa watumiaji  hususani kwa kutumia majiko kama “Pressure Cooker” na “Induction cooker” (Jiko Janja ) kwani majiko haya yamefanyiwa utafiti na hupika vyakula vya asili kama vile ugali maharage makande na ndizi kwa kutumia umeme kidogo ukilinganisha na majiko mengine.

Akifunga Mafunzo hayo Mwakilishi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi wa uendelezaji Sera wa Ofisi hiyo Bw. Cyrus Kapinga amesisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kuongeza kasi ya matumizi ya teknolojia bora na rafiki kwa mazingira kwa kuendelea kuchangia juhudi za Serikali katika kupunguza hewa ukaa na kulinda afya za wananchi.

“Sisi kama watumishi wa Umma ni sehemu ya jamii tunaopaswa kuhakikisha  tunatekeza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati safi ya kupikia kwani kila Wizara ina jukumu la kuhakikisha watumishi wanatumia nishati safi hivyo katika kutekeleza hilo tutaanzisha mkakati wa ndani wa namna tutakavyopata majiko ya positive cooker kama Taasisi na kuhakikisha kila Mtumishi anapatiwa jiko hilo ili kila Mtumishi aweze kuendana na mabadiliko hayo.”Amesisitiza Bw. Kapinga

Katika mafunzo hayo Watumishi walipata fursa ya kuona namna jiko janja (Induction Cooker) linavofanya kazi kwa ufaisi na kuokoa muda bila kutumia gharama kubwa.

PRETORIA, AFRIKA KUSINI

Kilele cha utambuzi wa uandishi wa habari za kidijitali nchini Tanzania kimethibitishwa baada ya Bi. Veronica Mrema, Mwanzilishi wa chombo cha habari cha M24 TANZANIA MEDIA na mwanachama mahiri wa Tanzania Bloggers Network (TBN), kuingia rasmi kwenye jopo la mdahalo katika Mkutano wa 13 wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025) unaofanyika jijini Pretoria. 

Hili si tu fahari kwa Mrema binafsi, bali ni heshima kubwa kwa TBN na tasnia nzima ya habari nchini, ikionesha kuwa kazi ya uandishi wa kidijitali inatambulika katika majukwaa makuu duniani.

Mrema yuko Afrika Kusini kuhudhuria mkutano huo mkuu unaotarajiwa kudumu hadi Desemba 5, 2025, baada ya kukabidhiwa udhamini maalum wa safari (Travel Grant) na Wizara ya Sayansi, Teknolojia, na Ubunifu ya Afrika Kusini (DSTI). Udhamini huu ulikuja kama matunda ya utambuzi wa utendaji wake wa kipekee katika uandishi wa habari za kisayansi na afya, akibainishwa kuwa miongoni mwa wachache barani Afrika waliochaguliwa kwa heshima hiyo. Uwepo wake kwenye jopo la mdahalo unampa fursa adhimu ya kushiriki moja kwa moja katika kuunda mwelekeo wa mustakabali wa habari za sayansi duniani.

Akiwa anahutubia jukwaa la WCSJ2025 ambalo linakutanisha waandishi, watafiti, na wataalamu mashuhuri kutoka kote duniani, Veronica Mrema anatarajiwa kusisitiza kuwa tasnia ya habari za sayansi na afya barani Afrika inakua kwa kasi na kwa hivyo inahitaji sasa zaidi ya wakati mwingine uandishi wa weledi wa hali ya juu, ubunifu, na ushahidi wa ki-sayansi ili kufikisha ujumbe sahihi na wa kuaminika kwa jamii. 

Lengo lake kuu ni kuhakikisha uelewa sahihi wa sayansi unakuza maamuzi yanayoleta maendeleo, huku akitumia uzoefu wake kama kiongozi, ikiwemo nafasi yake kama Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DAR-PC) na Afisa Habari wa Jumuiya ya Watu Wanaoishi na Selimundu Tanzania (SCDPCT), kutetea uandishi wenye tija.

Kutambulika huku kwa Mwanachama wa TBN kunaimarisha nafasi ya Tanzania katika uwanja wa uandishi wa habari za kisasa, kuashiria kwamba mchango wake katika upashanaji habari ni wa kiwango cha kimataifa.



Na Oscar Assenga,TANGA


Historia ya usafirishaji baharini imeendelea kuandikwa upya katika Bandari ya Tanga baada ya meli ya mizigo ya makontena, MV Pioneer yenye uzito wa tani 13,000 kutoka Iran, kutia nanga moja kwa moja bandarini hapo ikiwa ni mara ya kwanza kwa safari ya moja kwa moja kutoka Iran hadi Tanga.

Tukio hilo lilielezewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, kama hatua muhimu inayoweza kuongeza fursa za kiuchumi hasa kwa vijana na kuimarisha ushindani wa kanda.



Meli hiyo iliwasili ikiwa na makontena 463—ambapo 261 yameelekezwa Tanzania na 182 kwenda Malawi, Zambia, Uganda na nchi nyingine za SADC—yakibeba vifaa vya viwandani, malighafi ya uzalishaji na bidhaa za kiteknolojia. Ujio huo umewezeshwa na kampuni ya Seven Seas Shipping Agency, ambayo inaendesha safari za baharini kati ya Iran na Tanga.


Akizungumza wakati wa kuipokea meli hiyo iliyoongozwa na Nahodha Ahmadjoo, Dkt. Burian alisema ujio huo unafungua mwanya mpya kwa vijana wa Tanga kunufaika na teknolojia ndogo na za kisasa kutoka Iran.


“Iran ina teknolojia za kisasa katika uchakataji wa viungo, viwanda vidogo na bidhaa za dawa,” alisema. “Haya ni maeneo ambayo vijana wa Tanga wanaweza kuwekeza na kuzalisha bidhaa zitakazopata masoko. Meli hii si mizigo tu—ni fursa.”


Alisema Serikali ya Mkoa ipo katika mazungumzo na mamlaka za Iran kuanzisha ushirikiano kati ya miji na mikoa (Sister City na Sister Region) kwa lengo la kuharakisha uhamishaji teknolojia, mafunzo ya viwandani na upatikanaji wa masoko kwa wazalishaji wa ndani.



Pia alisema wafanyabiashara sasa wanaweza kuagiza bidhaa kutoka Iran na kuzipokea ndani ya siku nane. “Tunaweza kuifanya Tanga kuwa kitovu cha biashara ya jumla ya bidhaa kutoka Iran na kuongeza kipato chetu,” alisema.

Dkt. Burian alibainisha kuwa maendeleo makubwa ya Bandari ya Tanga—ambayo sasa inavutia meli kubwa za safari ndefu—ni matokeo ya uwekezaji wa Sh bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan katika maboresho na upanuzi wa bandari hiyo.



“Bandari hii inakua kwa sababu tumewekeza ipasavyo. Kuongezeka kwa meli kunamaanisha ajira, viwanda na fursa za kuuza bidhaa nje. Lakini yote haya yanahitaji amani,” alisema. “Bila amani, fursa tunazoshuhudia leo zisingekuwepo.”



Aliongeza kuwa mkoa wa Tanga una mazao mengi yakiwemo mkonge, kahawa, viungo na mazao ya baharini ambayo yanaweza kubadilisha maisha ya vijana kiuchumi.

Alisisitiza kuwa uvurugaji wa amani unaweza kuathiri si Tanzania pekee bali pia nchi zote zinazotegemea bandari za Tanzania kwa shughuli zao za kiuchumi.



Kwa upande wake, Meneja wa Uendeshaji wa Seven Seas Shipping Agency, Athumani Kimaro, alisema ujio wa MV Pioneer unaashiria mwanzo wa njia ya kudumu ya usafirishaji kati ya Iran na Tanga.



“Huu ni mwanzo wa hatua mpya ya biashara ya baharini,” alisema. “Kwa mara ya kwanza tunapokea safari za moja kwa moja kutoka bandari za Iran hadi Tanga. Tunatarajia meli tatu au nne kwa mwezi.”



Alisema tayari meli nyingine zimepangwa kuja, ambapo meli inayofuata inatarajiwa kuwasili Desemba 8, na nyingine Desemba 14. Safari kati ya Iran na Tanga huchukua siku 7–8 pekee, hivyo kuwa moja ya njia za haraka kwa wafanyabiashara wa Afrika Mashariki.




Dkt. Burian aliwataka wafanyabiashara na wazalishaji wa ndani kutumia fursa hiyo ipasavyo.




“Hii ni nafasi muhimu. Lazima kuhakikisha meli zinarejea kwa kujaza makontena ya kusafirisha bidhaa kwenda Iran—viungo, bidhaa za asili, mazao yaliyoongezwa thamani na mengine.”


Nahodha Ahmadjoo aliishukuru bandari ya Tanga kwa mapokezi mazuri na ufanisi, akisema ana matarajio ya kuifanya Tanga kuwa moja ya kituo cha mara kwa mara cha meli zao.



Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba, aliwataka vijana kuchangamkia fursa zilizofunguliwa na safari hizo mpya.



“Uhusiano huu wa biashara ya baharini una maana kubwa kwetu kwa sababu makontena haya yatasafirishwa kwa njia ya barabara, jambo ambalo linatoa ajira kwa vijana,” alisema.

 


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Reuben Kwagilwa amesema kitendo cha Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa fedha za ujenzi wa miundombinu ya Shule ya watoto wenye Mahitaji malumu ya Mlandizi, kinadhihirisha namna anavyoiishi kwa vitendo kauli mbiu yake ya KAZI NA UTU kwa kuwajali watoto wenye uhitaji maalum.

Mhe. Kwagilwa ameyasema hayo leo Novemba 29, 2025 katika ziara yake ya kikazi mkoani Pwani, iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ukiwepo mradi wa ujenzi wa miundombinu ya Shule ya watoto wenye Mahitaji malumu ya Mlandizi. 

Mhe. Kwagilwa amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka watoto wenye uhitaji maalum kwa kutoa milioni 506.5 za ujenzi wa miundombinu rafiki katika shule hiyo Maalum ya Mlandizi ambayo itawahudumia watoto wenye uhitaji maalum.

“Kitendo cha Mhe. Rais kutoa milioni 506.5 kwa ajili ya watoto wenye uhitaji maalum, kinaenzi kaulimbiu yake ya KAZI NA UTU ambayo alizunguka kuinadi nchi nzima,” Mhe. Kwagilwa amesisitiza.

Mhe. Kwagilwa amefafanua kuwa, fedha hizo zitawezesha kukamilisha ujenzi wa jengo la utawala, madarasa sita kwa ajili ya watoto wenye uhitaji maalum, madarasa mawili ya mfano, nyumba ya mwalimu na mabweni.

Aidha, Mhe. Kwagilwa amesema Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI imejipanga kuwapokea watoto wote wanaotarajiwa kuanza masomo ya shule za awali na msingi mnamo mwezi Januari, hivyo amewataka wasimamizi wa mradi huo wa ujenzi wa shule maalum pamoja na miradi mingine ya shule inakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Bi. Regina Bieda amesema, mradi unatarajiwa kukamilika Disemba 30, 2025 na mkandarasi ameahidi kukabidhi mradi huo Januari 5, 2025 hivyo watoto watakaopangwa katika shule hiyo watapokelewa na kuanza masomo.

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kutekeleza jukumu lake la kisheria na kijamii la kutoa elimu kuhusu ulinzi na usalama wa miundombinu ya gesi asiliakwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopitiwa na bomba la gesi nchini.

Lengo la kampeni hii ni kuongeza uelewa wa jamii juu ya umuhimu wa kulinda rasilimali za taifa, kuzuia uharibifu wa miundombinu, na kuimarisha ushirikishwaji wa wananchi katikamasuala ya usalama.

Kampeni hii endelevu inatekelezwa katika vijiji na mitaa 140 vinavyopatikana mikoa yaMtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam.

Katika Mkoa wa Lindi, elimu hiyo iliendeleakutolewa katika kijiji cha Kilangala kupitia mkutano wa hadhara ulioandaliwa na TPDC, nakuhudhuriwa na wananchi, viongozi wa vijiji, viongozi wa serikali pamoja na mkuu waWilaya ya Lindi, Mhe. Victoria Mwanziva, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutanohuo, alisisitiza wajibu wa wananchi katika kulinda miundombinu ya taifa.

“Tunapolinda bomba la gesi, tunalinda uchumi wetu, usalama wetu na mustakabali wa vizazivijavyo. Ninaishukuru TPDC kwa jitihada hizi za kuendelea kuelimisha jamii, na nawasihiwananchi wote tushiriki kikamilifu kuripoti na kuzuia vitendo vyote vinavyoweza kuhatarishamiundombinu hii muhimu,” alisema Mhe. Mwanziva.

Kupitia kampeni hii, TPDC inaendelea kuhimiza wananchi kuacha kufanya shughuli zozotezinazoweza kuhatarisha usalama wa bomba la gesi, kama vile uchimbaji holela, kilimo karibuna miundombinu, au uvamizi wa maeneo ya hifadhi ya bomba.

Vilevile, shirikalinahamasisha wananchi kuwa mabalozi wa kulinda miundombinu ya gesi katika maeneoyao, ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa mara moja wanapohisi au kuona viashiria vyauharibifu.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Afisa Maendeleo ya Jamii wa TPDC, Bw. Oscar Mwakasege, alieleza jinsi TPDC inavyotekeleza wajibu wake wa kuchangia maendeleo yajamii kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (Corporate Social Responsibility).

“TPDC imejikita katika kuboresha huduma za jamii kupitia miradi ya afya, elimu, maji nautawala bora. Tumekuwa tukitekeleza miradi inayogusa maisha ya wananchi moja kwa mojakama ujenzi wa zahanati, maboresho ya shule, miradi ya upatikanaji wa maji safi na ujenziwa serikali za mitaa. Lengo letu ni kuhakikisha jamii zinazoishi karibu na miundombinu yagesi zinanufaika na uwepo wa rasilimali hii,” alisema Bw. Oscar

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Lindi , Mhe. Victoria Mwanziva, alielezaumuhimu wa kampeni hii kwa ustawi wa taifa na kuipongeza TPDC kwa jitihada zake.

“Mradi wa gesi asilia ni kichocheo cha uchumi wa taifa. Ni muhimu kwa TPDC kuendeleakutoa elimu hii mara kwa mara ili kuhakikisha wananchi wanauelewa wajibu wao na athariza uharibifu wa miundombinu. Kama serikali, tunaunga mkono kikamilifu jitihada hizi,”Alisema Mhe. Mwanziva.
Waziri wa TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, amewataka madereva wa mabasi ya mwendokasi na yale ya kawaida kutumia lugha nzuri wanapotoa huduma kwa abiria ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima barabarani na kuepusha ajali.

Wito umetolewa kwa Watendaji walipo ngazi za halmashauri nchini kuhakikisha wanakusanya taarifa na takwimu za watu wenye ulemavu ili waingia katika mfumo wa utambuzi ili kurahisha utambulisho wao kwenye huduma mbalimbali.

Hatua hiyo inajiri baada wa uwepo wa changamoto kwa baadhi ya watu wenye ulemavu ikiwemo Viziwi kushindwa kuwa na mawasiliano mazuri na watoaji wa huduma za msingi.

Akizungumza kwa Niaba ya mkurugenzi wa kitengo cha watu wenye ulemavu wakati wa ufunguzi wa kongamano la ujumuishaji wa watu wenye ulemavu kwenye fursa za kiuchumi ,afisa Ustawi wa Jamii kutoka ofisi ya Waziri Mkuu,Sera,Bunge,Uratibu na Watu wenye ulemavu Bruno Mwakibibi amesema kuwa
Aidha ametoa rai kwa jamii kuendelea kuwaibua watu wenye ulemavu walipo kwenye jamii na kuhakikisha wanasajiliwa huku Viongozi wa serikali za mitaa wakitakiwa kuwajumuisha watu wenye ulemavu katika ushiriki wa shughuli za ujenzi wa taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa SHIVYAWATA mkoa wa Dodoma Mwl Omary Lubuva ameiomba serikali kuelekeza Viongozi wa serikali ngazi za mitaa na kata kuhakikisha wanatoa uelewa wa kutosha kwa watu wenye ulemavu kufahamu fursa zinazopatikana ikiwemo mikopo na lengo lake ili kuondoa dhana ya kuwakatisha tamaa baadhi ya walishindwa kupata mikopo hiyo licha ya kuomba katika ngazi za Halmashauri.

Awali akielezea lengo Mamlaka ya udhibiti wa Ununuzi wa umma PPRA kuwesha mafunzo hayo kwa makundi maalum Meneja uhusiano na mawasiliano Remija Salvatory amesema sheria inazitaka taasisi zote za serikali kuwezesha makundi maalum ikiwa ni utekelezaji sheria ya PPRA ya kutaka taasisi hizo kutenga asilimia 30 ya bajeti ya ununuzi wa umma kwa ajili ya makundi hayo ikiwemo Wanawake,Vijana ,Wazee na Watu wenye Ulemavu.

Remija amesema serikali imetanga zaidi ya trilioni 1 kwa ajili ya tenda kwa makundi maalum hivyo amewataka kujiunga na mfumo Nest ili kuweza kupata zabuni mbalimbali.

Amesema kundi la Watu wenye ulemavu wananafasi pana ya kuingia katika kila kundi hivyo ni wajibu wao kuchangamkia fursa hiyo ambayo ipo kwa mujibu wa sheria.

Nae Beatus Nzogela ni Afisa Masoko kutoka shirika la madini la taifa (STAMICO) amesisitiza umuhimu wa utimiaji wa nishati safi ya kupikia kwa makundi ya watu wenye ulemavu.

Ametaja fursa zilizopo STAMICO ambazo Watu wenye Ulemavu kupitia shirikisho lao la SHIVYAWATA wanaweza kuzichangamkia kwa makundi tofauti Hasa wachimbaji wadogo,shughuli za uchorongaji,Kuuza Mkaa rafiki Briquettes ikiwa ni Nishati safi ya kupikia,Makarasha ya Migodi

Amesema watu wenye ulemavu wanaweza kuwa mawakala wa kuuza mkaa huo ikiwa ni fursa ambapo STAMICO wameweka fursa kwao kuchangamkia fursa hiyo.

Pamoja na hayo ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Mchango mkubwa katika kuhakikisha STAMICO wanakuwa sehemu ya kufanikisha azma ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


CHUO Kikuu Mzumbe, Ndaki ya Mbeya, kimekamilisha ujenzi wa zahanati ya kisasa iliyogharimu shilingi 465,706,251.70, ambayo sasa imeanza kutoa huduma za afya kwa wana-Mzumbe pamoja na wakazi wa jamii inayozunguka chuo hicho.



Na Oscar Assenga, Tanga

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman ametangaza kuunda kamati maalumu itakayochunguza sababu zilizosababisha uwanja wa CCM Mkwakwani kufungiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutokuchezewa mechi.

Akizungumza na waandishi wa habari siku baada ya uwepo wa Taarifa za kufungiwa uwanja huo na TFF,Rajabu alisema kwamba tume hiyo itajumuisha kamati ndogo kutoka CCM,Maafisa wa TFF na baadhi ya wadau soka mkoa wa Tanga.




Alisema kwamba wameamua kufanya hivyo kutokana na kwamba waanaamini kuna uzembe ulijitokeza kwa wale ambao walipewa jukumu la kusimamia uwanja huo na kupelekea kukumbana na rungu hilo la TFF.

Aidha alisema kwamba ameshangazwa na hatua ya TFF kufungia uwanja huo kutokana na hivi karibuni waliufanyia marekebisho makubwa na kujiridhisha kwamba unaweza kutumika kwa ajili ya mashindano mablimbali ya ndani na nje ya hicho hivyo walishangazwa kuona taarifa hiyo.

“Nilikuwa nimesafiri nje ya mkoa wa Tanga kikazi lakini nimelazimika kuhairisha safari yangu ili niweze kushughulika tatizo hilo na ndio maana leo hiii nimefika hapa uwanja kujionea na kuzungumza nanyi wanahabari na kukubaliana na uamuzi wa TFF kwamba zipo dosari ambazo zinapaswa kurekebishwa na hili tutalifanyia kazi”Alisema

Katika hatoba yake fupi iliyojaa hekima alionyesha kutokuwa na imani na viongozi ambao wamepewa dhamana ya kusimamia uwanja hatua iliyopelekea kuwaita mbele ya wanahabari na wadau wengine watoe maelezo.

Awali akizungumza kabla ya mkaribisha Mwenyekiti huyo,Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Mfaume Kizito alisema kwamba uwanja huo ulikuwa kwenye hali nzuri lakini alishtushwa na uamuzi ambao ulichukuliwa na TFF kuufungia uwanja huo.

Pamoja na kauli hiyo Mwenyekiti wa CCM Mkoa alimtaka Meneja wa Uwanja wa CCM Mkwakwani Akida Machai aeleze nini ambacho kimepelekea uwanja huo kufungiwa licha ya kufanyiwa maboresho makubwa katika siku zilizopita.

Ambapo Meneja huyo alidai kuwa moja ya changamoto iliysababisha hali hiyo ni kutokuwepo na maji ya kutosha kutokana na chanzo cha maji kwenye uwanja huo kukauka na kupelekea nyasi za uwanja kukauka.

Alisema kwamba changamoto nyengine ni uwepo wa mchwa katika eneo lenye majani na hivyo kuwalazimu kutumia dawa ya kumwagilia na kufanikiwa kuwaondosha


Mwisho.
Tarehe 27 Novemba 2025, Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Mbeya kimesheherekea Sherehe ya Mahafali ya 24. Ikiwa ni siku muhimu ya kuwapongeza wahitimu wa Ndaki hiyo kwa juhudi na uwajibikaji kitaaluma na kusherehekea mafanikio kwa wanafunzi na watumishi kwa ujumla.

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme kwa ufanisi mkubwa, hatua inayoliwezesha taifa kusonga mbele katika kujenga mfumo madhubuti wa upatikanaji wa nishati ya umeme.

Mhe. Ndejembi amesema hayo Novemba 27, 2025, wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma, ambapo ametaka kuona kazi inakamilika kwa wakati na viwango vinavyotakiwa.

Mhe. Ndejembi amebainisha kuwa mradi huo mkubwa unatekelezwa kwa fedha za ndani, na hadi kukamilika kwake utagharimu takribani shilingi bilioni 556.

“Niwaagize TANESCO kuendelea kumsimamia Mkandarasi kuhakikisha kazi inakamilika kulingana na ratiba. Hatutaki kufika mwisho wa utekelezaji na kukuta mradi umekabidhiwa bila kukamilika,” amesisitiza Waziri Ndejembi.

Ameongeza kuwa TANESCO imeelekezwa kukutana na Mkandarasi ili kuandaa mpango kazi mpya utakaoonesha mikakati ya ufuatiliaji wa hatua kwa hatua katika ukamilishaji wa mradi huo muhimu kwa taifa.

Aidha, Waziri Ndejembi amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatoa msukumo mkubwa kuhakikisha umeme unawafikia wananchi kote nchini kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Tanzania ina umeme wa kutosha kutoka kwenye vyanzo vyake vya uzalishaji, na kazi kubwa inayoendelea sasa ni kuutoa umeme huo katika maeneo ya uzalishaji na kuufikisha kwa wananchi na wawekezaji.

Bw. Twange ameeleza kuwa Serikali imekamilisha ujenzi wa vituo vikubwa vya kupokea na kupoza umeme katika Dodoma na Chalinze, ambavyo vitakuwa kitovu cha kusafirisha umeme kutoka Mradi wa Julius Nyerere (JNHPP) na vyanzo vingine kwenda maeneo mbalimbali ya nchi.

“Kituo cha kupokea umeme cha Dodoma ni njia panda muhimu inayopokea umeme kutoka maeneo mbalimbali, na pia ndicho kinachotuunganisha na wenzetu nchini Kenya,” amesema BW. Twange

Ameongeza kuwa hatua hizi zote ni muhimu katika kulifanya taifa kuwa na mfumo imara wa umeme unaokidhi mahitaji ya sasa na ya vizazi vijavyo.

 


Na Munir Shemweta, Mtwara

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewataka watumishi wa sekta ya ardhi kuhakikisha wanazingatia utu wakati wa kuwahudumia wanachi.

Aidha, amewataka watumishi hao Kufanya kazi kwa umakini, uadilifu pamoja na kuzingatia miongozo ya utumishi wa umma wakati wote wa kutekeleza majukumu yao.

Mhe. Dkt Akwilapo amesema hayo leo tarehe 27 Novemba 2025  wakati alipotembelea Kliniki ya Ardhi inayoendeshwa katika mtaa wa Mbae Mashariki na Likombe katika Halmashuari ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara.

Amesema, dhamira ya wizara yake ni kutoa huduma bora na kwa wakati  zenye nia ya  kumaliza migogoro yote ya ardhi sambamba na kuagalia chanzo cha migogoro hiyo. 

"Falasafa ya Mhe Rais ni kuwaacha wananchi kuwa na furaha kwa kuondoa migogoro ya ardhi". amesema 

Amewataka wananchi wa Mtwara kuhakikisha wanamilikishwa maeneo yao kwa kupata hati milki za ardhi pamoja na kuwa na vibali vya ujenzi  wanapotaka kuendeleza maeneo yao ili kuepuka migogoro.

Mhe. Dkt. Akwilapo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuitumia wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi.

Kwa upande wake kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Mtwara Bw. Fredrick Mrema amemueleza Waziri wa Ardhi kuwa, katika zoezi la Kliniki ya ardhi linaloendelea katika halmashauri ya Mtwara Mikindani takriban hati milki za ardhi 503 zimetolewa kwa wananchi wa mitaa ya Mbae na Likombe.

"Zoezi hili la kliniki ya ardhi ni endelevu na lengo letu tumepanga kuhudumia wananchi 10,984 katika kata nne za halmashauri hii ya mtwara mikindani" amesema Bw. Mrema.

Naye mkuu wa wilaya ya Mtwara Bw. Abdallah Mwaipaya aliyemuwakilisha mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala amewahimiza wananchi wa wilaya yake kuhakikisha wanamiliki maeneo yao kwa kupatiwa hati milki za ardhi.

" Ndugu wananchi nawaombeni mmiliki maeneo yenu kwa kuwa na hati milki, hati ya ardhi inakupa uhakika wa milki na kilichofanywa na wizara katika kliniki hii ya ardhi  kuwapatia wananchi hati  ni jambo kubwa na ka kihistoria na niishukuru wizara ya ardhi" amesema.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo ametembelea ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Mtwara na kukutana na wafanyakazi wa ofisi hiyo.

Akiwa katika ofisi hiyo Mhe. Dkt Akwilapo amewapongeza watumishi wa ofisi hiyo kwa kazi kubwa wanayofanya na kuwaeleza azma ya wizara hiyo katika kumaliza migogoro ya ardhi katika mkoa huo.


 


Na Munir Shemweta, Mtwara

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amezitaka taasisi za umma kuhakikisha zinalinda mipaka ya maeneo yake ili kuepuka uvamizi unaoweza kuzalisha migogoro ya ardhi nchini.

Mhe Dkt Akwilapo ametoa rai hiyo mapema leo tarehe 27 Novemba 2025 mkoani Mtwara alipozungumza wakati wa kikao na uongozi wa mkoa katika ziara yake mkoani humo.

"Tuhakikishe tunazuia uvamizi ili kuepuka migogoro ya baadaye hii itatusaidia sana kama wizara kushughulika na masuala ya jamii, migogoro ya ardhi ni mingi" amesema

Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Mtwara Bw. Fredrick Mrema ameeleza katika kikao hicho kuwa, mkoa wa Mtwara kwa sasa unakabiliwa na migogoro mikubwa saba ya ardhi katika maeneo mbalimbali mkoani humo.

Ameitaja baadhi ya migogoro hiyo kuwa, ni ile inayohusisha wananchi wa Mbae na  Mayanga na jeshi la wananchi, mgogoro wa wananchi wa eneo la uwanja wa ndege-Mngamba na halmashauri ya mtwara mikindani pamoja na ule wa wananchi wa kijiii cha Nakada kata ya Katere na mwekezaji kampuni ya Sugar-Tanzania.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameuahidi uongozi wa mkoa wa Mtwara kuunda timu maalum kutoka makao makuu ya wizara kwenda mkoani humo kushughukia migogoro hiyo ya ardhi.

Ameeleza kuwa, kwa sasa Wizara yake  imejipanga vyema kukabiliana na migogoro ya ardhi nchini kwa lengo la kuwaacha wananchi na furaha.

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (Mb), ametembelea na kushuhudia utekelezaji wa utafiti wa kina wa madini kwa kutumia teknolojia ya ndege nyuki (drone) katika Kata ya Basotu, Wilaya Hanang, mkoani Manyara. Utafiti huo wa jiofizikia unalenga kubainisha maeneo yenye hifadhi ya madini utakaopelekea kuanzishwa kwa mgodi mkubwa wa dhahabu wilayani humo.

Ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa wakati akihutubia Bunge Oktoba 13, 2025 ambapo alitaja utafiti wa madini kama kipaumbele kwa mwaka 2025 - 2030 utakaopelekea kufikia angalau asilimia 50 ya utafiti wa kina wa madini nchini ifikapo mwaka 2030.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Waziri Mavunde amesema utafiti huo ni hatua muhimu kwa maendeleo ya wananchi wa Hanang na Mkoa wa Manyara kwa ujumla, kwani matokeo yake yanatarajiwa kuongeza ajira, kuvutia uwekezaji na kuchochea utekelezaji wa miradi ya kijamii kupitia leseni za uchimbaji madini.

“Tunatarajia utafiti huu utaleta matokeo chanya yatakayobadilisha maisha ya wananchi. Serikali itaendelea kusimamia sekta hii ili iwe chachu ya maendeleo kwa wote,” amesema Mavunde.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mhe. Almish Hazal, amemshukuru Waziri Mavunde kwa kutembelea eneo la mradi huo na kuendelea kusisitiza umuhimu wa tafiti za madini katika wilaya yake pia, ameiomba Wizara ya Madini kuendeleza kasi hiyo katika maeneo mengine ya Hanang yenye uwezekano wa kuwa na madini.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Cobra Resources Ltd, Bw. Amos Nzungu amempongeza Waziri Mavunde kwa ushirikiano na uzalendo anaouonesha kwa kufuatilia utekelezaji wa miradi ya utafiti wa madini na kuahidi kukabidhi matokeo ya utafiti mara tu yatakapokamilika.

Kwa upande wa Meneja wa Kampuni ya SkyPM Solution inayofanya utafiti huo, Bw. Paul Madata amesema matumizi ya teknolojia ya ndege nyuki yamerahisisha na kuongeza ufanisi wa utafiti wa awali, kwani inaweza kupima hadi zaidi ya kilomita tatu chini ya uso wa ardhi kwa muda mfupi.

Awali, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Manyara, Mhandisi Godfrey Nyanda ametoa taarifa ya maendeleo ya sekta ya madini mkoani hapo, akibainisha kuwa hadi kufikia robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/26 (Julai–Oktoba), wamekusanya asilimia 35.21 ya lengo la makusanyo ya Shilingi Bilioni 2.2 lililopangwa kwa mwaka mzima.

“Tutaendelea kusimamia kikamilifu maagizo ya Mhe. Rais na ya Waziri wetu Mhe. Mavunde ili kuhakikisha sekta ya madini inaendelea kukua na kuimarika hapa Manyara,” amesema Mha. Nyanda.



Na Mwandishi wetu -Dodoma


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kupitia  Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) imeendelea kuiishi kauli mbiu ya "Kazi na Utu" kwa kufanya ziara maalum ya kuwatembelea wanafunzi wenye mahitaji maalum waliopo vyuo vikuu Nchini kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi ili kuwasaidia wanafunzi hao kutimiza malengo yao.

Hayo yalisemwa na  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga kwenye ziara yake alipotembelea wanafunzi wenye ulemavu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mhe. Nderiananga amesema kuwa Serikali ipo tayari kushirikiana na wanafunzi wenye ulemavu kutatua changamoto zinazowakabili ili kuhakikisha wanafikia malengo yao ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi itakayowezesha kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2025-2050.


Aidha, Nderiananga ametoa wito kwa vijana wenye ulemavu kuwaelimisha watu wengine juu ya dhima ya kutunza amani, kwa sababu amani ikikosekana watu wenye ulemavu wanaathirika zaidi kutoka na kukosa uwezo wa kujiokoa.

Awali, Mkurugenzi wa Elimu Maalum Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Magreth Matonya aliwaambia wanafunzi wenye ulemavu kuwa kupata mkopo asilimia 100 ni haki yao hivyo watashirikiana na Bodi ya Mikopo (HESLB) ili kuhakikisha wanafunzi wenye ulemavu ambao hawajapata mikopo wanapata kwa wakati.


"Serikali imekuwa ikitoa fedha kila mwaka kwa ajili ya kununulia vifaa vya wanafunzi wenye mahitaji maalum, uhitaji bado upo lakini si mkubwa kama ilivyokuwa hapo awali kutokana na juhudi zinazofanywa na Serikali. Ameongeza Dkt. Matonya



Kwa upande wake Bi. Grace Daniel mwanafunzi mwenye ulemavu wa Ngozi  katika Chuo Kikuu cha DODOMA ameiomba Serikali na Sekta binafsi kuendelea kutoa kipaumbele cha ajira kwa watu wenye ulemavu wenye sifa.


Naye Bw. Jackson James mwanafunzi mwenye ulemavu wa viungo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kutoa vifaa kama vile Viti mwendo  vinavyowawezesha kuhudhuria vipindi kwa urahisi huku akiiomba Seriklai kuwafiki wanafunzi wenyeulemavu Vijijini.


 


= MWISHO=