Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa utendaji kazi mzuri, maendeleo na mabadiliko makubwa yanayoonekana katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 16 Januari, 2026, katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), baada ya Kamati kupokea Taarifa ya Muundo na Majukumu ya BRELA iliyowasilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa.

Mhe. Mwanyika amesema kuwa, licha ya kazi nzuri inayoendelea kufanywa na BRELA, bado kuna changamoto ya wafanyabiashara na wamiliki wa kampuni wengi kutohuisha taarifa za kampuni zao kupitia mfumo wa BRELA. Ameeleza kuwa tatizo hilo ni kubwa, lakini wananchi wengi hawalitambui ipasavyo.

“Hili tatizo ni kubwa lakini wengi hawalielewi; wengi wana kampuni lakini hawajahuisha taarifa za kampuni hizo,” amesema Mhe. Mwanyika.

Kutokana na hali hiyo, Mhe. Mwanyika ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara kufanya utafiti na kutathmini namna ya kuboresha mfumo wa uhuishaji wa taarifa za biashara na kampuni, ili kuja na mfumo wezeshi, unaoongeza ufanisi na kuharakisha utoaji wa huduma.

Aidha, Mwenyekiti huyo amesisitiza umuhimu wa kuhuisha taarifa za biashara na kampuni, akitoa wito kwa wafanyabiashara kuchukua hatua hiyo kwa hiari na kwa wakati.

“Kuhuisha taarifa ni jambo jema, na ni muhimu tukalifanye,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa, amesema kuwa Wakala itaendelea kutoa elimu kwa Waheshimiwa Wabunge kupitia Kamati hiyo ili kuwajengea uelewa mpana kuhusu majukumu ya BRELA pamoja na mifumo ya kidijitali inayotumika katika utoaji wa huduma.

Bw. Nyaisa ameeleza kuwa, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu matumizi ya mifumo ya kidijitali bado ni miongoni mwa changamoto zinazokwamisha urasimishaji wa biashara na utoaji wa leseni.

Amefafanua kuwa mfumo wa BRELA ni rafiki kwa mtumiaji na unajieleza wenyewe, hivyo kumwezesha mwananchi kujisajili moja kwa moja bila usumbufu.

“Mfumo wa BRELA ni rafiki kwa mtumiaji na unajieleza wenyewe, hivyo humwezesha mtu kuingia moja kwa moja na kusajili kampuni yake bila usumbufu,” amesema Bw. Nyaisa.

Ameongeza kuwa BRELA inaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuwahamasisha kufahamu kuwa mchakato wa usajili wa biashara, kampuni na utoaji wa leseni si mgumu kama inavyodhaniwa.

Amebainisha kuwa katika mapitio ya sheria yanayoendelea, BRELA inapendekeza kutambuliwa rasmi kwa Mawakala wa Usajili wa Kampuni, ili kusaidia wananchi wanaokutana na changamoto wakati wa usajili.

“Lengo ni kuhakikisha mwananchi akikwama, anapata msaada kutoka kwa watu wanaotambulika na kuaminika,” amesisitiza Bw. Nyaisa.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mheshimiwa Petro Magoti akiwa kwenye picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid J. Maulid, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe pamoja na Mwakilishi wa Madiwani wa Mkoa wa Pwani, mara baada ya kufunga mafunzo kwa Waheshimiwa Madiwani.
Nilikuwa nikilala kwa amani ya kawaida, lakini siku moja mambo yakaanza kuwa tofauti. Kila usiku, sikitazama saa, nilisikia nyayo zisizo za kawaida zikitembea karibu na kitanda changu. Sauti za kupiga kelele, kuomba, na kunialika zikiningia, nikitishiwa bila kuona mtu yeyote.

Nilijaribu kupumzika, kuacha kufikiria, lakini hofu haikupungua. Kila siku ilipita, hali ikawa mbaya zaidi. Nilianza kuhofia kuendelea kuishi kama kawaida. Ndoa yangu ilianza kushindwa, usingizi wangu ukawa wa usiku tu.Soma Zaidi........https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-nilivyopata-pete-ya-ulinzi-baada-yakusikia-nyayo-zikitembea-na-sauti-zikiniita-usiku-bila-kuona-mtu/
Kwa muda mrefu nilikuwa nikiishi maisha ya kawaida juu juu. Kila kitu kilionekana sawa. Lakini nyuma ya pazia, kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa hayapigi kelele. Familia yetu ilikuwa imegubikwa na migogoro isiyoeleweka. Chuki zisizo na chanzo.

Wagonjwa wa mara kwa mara. Watoto waliokuwa na hofu bila sababu. Nilidhani ni mikosi ya kawaida ya maisha. Kadri nilivyokua, nilianza kuona muingiliano wa ajabu. Kila aliyekuwa anajaribu kusonga mbele, alirudi nyuma. Ndoa zilikuwa hazidumu.

Biashara zilikuwa zinafungwa ghafla. Kila sherehe ilimalizika kwa machozi. Nilipouliza wazee, walinyamaza. Kulikuwa na siri nzito iliyokuwa haizungumzwi. Ukweli ulianza kujitokeza taratibu. Ndoto zilianza kunijia. Ndoto zilizojaa sura za watu niliowajua.

Majina ya waliokufa yakitajwa. Ahadi za zamani nilizokuwa sizijui. Hapo ndipo nilipoanza kuogopa. Nilihisi kama kuna kitu kinatutawala kimya kimya bila sisi kujua. Nilipokutana na Kiwanga Doctors ndipo nilianza kuelewa nilichokuwa nikikabiliwa nacho.

Walinieleza kuwa familia yetu ilikuwa imefungwa katika mzunguko wa ushirikina wa kizazi. Soma Zaidi........https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipofahamu-ushirikina-usioonekana-kwenye-familia-yangu-kila-nilichojuwa-kilikuwa-kinaogopesha/
Kila mara nilipopata pesa, ndoto zangu za kuishi kwa utulivu zilikuwa zikidhoofika. Nilijaribu kuokoa kila shilingi, lakini mara zote zilikuwa zikitoweka kwa sababu ambazo sikuwa nafahamu.

Nilijikuta nikiwa nimeshikwa na hofu isiyoelezeka kila nikipokea kipato changu. Hii haikuwa maisha niliyotarajia, na kila siku nilipita nilijiona nikishindwa. Nilijaribu njia mbalimbali za kifedha.

Nilipanga bajeti, nilijitahidi kuepuka madeni, hata hivyo, kila kitu kilikwama. Nilijitahidi kufanyia biashara ndogo ndogo, lakini mara nyingi matokeo yalikuwa hafifu.

Nilihisi kama kila kitu kilikuwa kimefungwa kimya kimya. Kulikuwa na wakati nilifikiri nilikuwa nimeshaanza kushindwa kabisa.
Ndipo nilipoona sina budi kutafuta msaada wa kiroho. Soma Zaidi........https://kiwangadoctor.com/kiswahili/kila-nilipopata-pesa-zilikuwa-zikitoweka-sababu-nilizoigundua-ilinishtua/
Nilikuwa nimekaa mbali na mume wangu kwa muda, kwa sababu ya kazi. Nilifikiria kuwa uhusiano wetu ungeendelea kama kawaida, kila mmoja akijali nafasi ya mwingine. Lakini siku moja, taarifa zisizotarajiwa zilisogea kwangu kama radi.

Nilipogundua ukweli, moyo wangu ukatetemeka na hofu ilijaa ndani ya nafsi yangu. Nilihisi kutetema kila sehemu ya mwili wangu, na akili zangu hazikuamini kilichokuwa kikiendelea.

Kila hatua niliyopiga kujaribu kupata ukweli, ilikuwa kama kuingia kwenye giza.

Nilijaribu kuzungumza na watu wa karibu, lakini walinipa maoni tofauti. Nilihitaji msaada wa dhahiri, suluhisho linaloweza kurekebisha hali hii kabla ya kuharibu kila kitu tulichojenga.Soma Zaidi........https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mwanamke-alifichuliwa-akifanya-mapenzi-na-mume-wangu-nikiwa-niko-mbali-kilichofuata-kilinishtua/

Siku hiyo nilifikiria kuwa ni ya kawaida. Nilikuwa nimechoka na masuala ya familia na kazi, nikihitaji muda wa kupumzika na kutulia. Nilipofika kwenye lodging, hakuwa na dalili yoyote ya kile kilichokuwa kikiwasubiri.

Nilifungua mlango, na macho yangu hayakuamini kile nilichokiona. Kwa kinyume cha matarajio yangu, mama yangu alikuwa pale, na kilichonivunja moyo zaidi, alikuwa anakutana kimapenzi na babake binti yangu.

Mwili wangu ukatetemeka, moyo ukalia ndani ya kifua changu, na uso wangu ukajaa hofu na mshtuko. Nilihisi dunia kuzunguka na kila kitu kilionekana kisicho halisi. Nilijaribu kusema kitu, lakini sauti haikutoka.

Siku zote niliamini familia yetu ilikuwa salama na ya amani, lakini sasa nilijikuta katika hadithi ya kushangaza, isiyo ya kawaida na isiyokuwa ya kufikirika. 

Nilihitaji suluhisho haraka, njia ya kurekebisha hali bila kuharibu kila kitu zaidi ya kile kilichokuwa kimedhoofisha familia. Soma Zaidi......https://kiwangadoctor.com/kiswahili/drama-yatokea-baada-ya-mama-kumfumania-bintiye-na-babake-kwenye-lodging/


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika  la Uwakala wa Meli Tanzania- TASAC Bw. Mohamed Salum leo tarehe 16 Januari, 2026 amehitimisha  rasmi mafunzo kwa watumisi wapya 25 yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. 

Wakati akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Mkuu amewaasa watumishi hao kuzingatia maadili ya utumishi wa umma,  nidhamu ya kazi, ushirikiano na ubunifu katika kazi. 

“Ndugu watumishi, napenda kuwakumbusha na kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kuzingatia maadili katika utumishi wa umma, nidhamu kazini, ushirikiano na kuendelea kujifunza kwakuwa Sekta ya usafiri kwa njia ya maji inakuwa kwa kasi sana  kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia” amesema Bw. Salumu.

Pia, amewasihi kuzingatia kanuni na miongozo katika kutekeleza majukumu yao. 


“Napenda mtambue yakuwa mmepewa dhamana kubwa na serikali hivyo ni vema kuzingatia Kanuni, Sheria, Taratibu na Miongozo mbalimbali inayosimamia utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kutunza siri, nidhamu na utii kwa viongozi wa serikali, kuendeleza mashirikiano, kutoa huduma bora kwa wateja, kulinda mali za Shirika pamoja na kufuata sheria na miongozo inayoongoza utekelezaji wa majukumu ya TASAC.  

Mwisho Mkurugenzi Mkuu aliwakaribisha watumishi wapya TASAC na kuwatakia utekelezaji mwema wa Majukumu yao.

Mafunzo yalikuwa ya siku 14 ambapo watumishi hao wali kabidhiwa vyeti vya ushiriki na kukaribishwa katika utumishi wa umma.










 

KAMATI  ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imezipongeza Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) na Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) kwa utendaji kazi mzuri na mafanikio makubwa yanayoendelea kuonekana katika maeneo mbalimbali ya utoaji huduma.

Pongezi hizo zimetolewa Januari 16, 2026 bungeni jijini Dodoma na Mwenyekiti wa kamati hiyo , Mhe. Deodatus Mwanyika, baada ya taasisi hizo kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu yake katika kikao cha kamati hiyo.

Mhe.Mwanyika, ameongoza kikao cha kamati hiyo, pia amezitaka taasisi hizo kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kutoa huduma bora na kuongeza nguvu katika utoaji wa elimu kwa wananchi ili kuchochea ushindani na ukuaji wa sekta ya viwanda na biashara nchini.

Aidha, wajumbe wa kamati hiyo walipata fursa ya kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali yaliyolenga kuboresha utendaji kazi wa NDC, TBS, BRELA na TIRDO ili ziweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kushughulikia changamoto zinazoibuka katika utoaji wa huduma kwa wananchi, pamoja na kusimamia miradi ya kimkakati ya maendeleo kwa weledi.

Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, akiwa ameambatana na Naibu Waziri wake, Mhe. Dennis Londo , Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Suleiman Serera, Menejimenti ya wizara na wakuu wa taasisi zilizo chini ya wizara yake, ameihakikishia kamati hiyo kuwa wizara yake itayafanyia kazi maoni na mapendekezo yote yaliyotolewa na kuahidi kushirikiana na kamati hiyo katika kuziwezesha taasisi hizi kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili kupata matokeo chanya yanayotarajiwa katika kuendeleza sekta ya viwanda na biashara na kukuza uchumi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mwendeshaji wa NDC, Dkt. Nicolaus Shombe, ameeleza kuwa shirika hilo limepiga hatua katika usimamizi wa miradi ya kimkakati na kielelezo, uendekezaji wa kongani za viwanda na uendeshaji wa kiwanda cha viuadudu na uzalishaji wa mbolea ya viuatilifu.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa, Mkurugenzi mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi na Kaimu mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Ramson Mwilangali, wakiwasilisha taarifa za utekelezaji wa majukumu ya taasisi zao kwa kamati hiyo, walibainisha kuwa taasisi zao zinalenga kutoa huduma bora kwa urahisi kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla ili kukuza uchumi wa nchi.