Na Joseph Mahumi, WF

Kampuni ya tathmini ya nchi kukopa na kulipa mikopo ya Fitch Ratings, imeithibitisha Tanzania kuendelea kuwa ‘B+’ huku likidumisha mtazamo wa “Stable Outlook”. Hatua hiyo inaashiria imani ya Kampuni hiyo katika mwenendo wa uchumi wa nchi pamoja na uthabiti wake wa kifedha katika kipindi cha kati.

Kwa mujibu wa tathmini hiyo, Tanzania inaendelea kunufaika na ukuaji mzuri wa pato la taifa (GDP) , kiwango cha chini cha mfumuko wa bei, deni kuendelea kuwa himilivu ikilinganishwa na nchi nyingine zinazofanana.

Mwenendo mzuri wa uchumi umepelekea upatikanaji wa fedha za nje kupitia programu za Shirika la Fedha la Kimataifa - IMF ikiwemo Extended Credit Facility (ECF) inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii na Resilience Sustainability Facility (RSF) ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. 

Ripoti hiyo pia imeeleza kuwa ushindi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi wa Oktoba 2025 unatarajiwa kuendeleza sera za kiuchumi, jambo litakalosaidia utekelezaji wa mipango ya mageuzi ya uchumi na kuendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji.

Kwa upande wa ukuaji wa uchumi, Fitch inatarajia Tanzania kuendelea kuwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 6 mwaka 2026 na 2027, juu ya wastani wa nchi zilizo katika kundi la ‘B’ ambapo Ukuaji huo utachangiwa na sekta za kilimo na madini pamoja na uwekezaji mkubwa katika miundombinu, ikiwemo mradi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge Railway na bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).

Kwa upande wa sera za fedha za umma, Fitch inakadiria nakisi ya bajeti kubaki karibu asilimia 3 ya Pato la Taifa katika miaka ya fedha 2026 na 2027, huku ukusanyaji wa mapato ukiendelea kuimarika kutoka asilimia 14.2 ya Pato la Taifa mwaka wa fedha 2021 hadi asilimia 15.9 mwaka wa fedha 2025.

Ripoti hiyo inaonesha kuwa Mapato ya utalii (travel exports) yalifikia dola za Marekani bilioni 4.4 mwaka 2025, sawa na asilimia 25 ya mauzo yote ya bidhaa na huduma nje ya nchi. 

Hata hivyo, hali hii itafidiwa kwa kiasi na kuongezeka kwa thamani ya mauzo ya dhahabu ya Tanzania nje ya nchi, ambayo yalifikia dola za Marekani bilioni 4.7 mwaka 2025 (sawa na asilimia 27 ya jumla ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi).

Aidha, deni la serikali linatarajiwa kushuka hadi asilimia 47 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2027, likisaidiwa na ukuaji wa uchumi na nidhamu ya matumizi ya Serikali.

Tathmini hiyo pia imepongeza jitihada za Serikali katika kuboresha usimamizi wa fedha za umma, ikiwemo kupunguza madeni ya wazabuni na marejesho ya VAT katika miaka ya karibuni ambapo Kufikia Desemba 2025, kiasi kilichothibitishwa cha madeni hayo kilipungua hadi asilimia 0.2 ya Pato la Taifa (GDP), kutoka asilimia 1.2 mwishoni mwa Desemba 2022, hatua inayochangia kuongeza uwazi na ufanisi wa kifedha.

“Ninawapongeza Viongozi wa Wizara Taasisi zake zote waliofanikisha kazi ya kusimamia sekta hii ya uchumi na fedha, tunafarijika kuona matokeo haya ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu kwani tutaendelea kuaminika katika masoko ya fedha na dhamana ya Kimataifa” alisema Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha

Kwa ujumla, uthibitisho wa daraja la ‘B+’ na mtazamo thabiti unaashiria kuwa Tanzania inaendelea kujenga msingi imara wa uchumi, huku ikiongeza imani ya wawekezaji wa ndani na kimataifa katika uwezo wa nchi kusimamia uchumi wake na kukabiliana na mishtuko ya nje.

 Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) unatekeleza ujenzi wa barabara zenye urefu wa Kilomita 51.2 kwa kiwango cha lami na zege katika Kata zaidi ya nane (8) na mitaa isiyopungua 20 katika halmashauri ya Manispaa ya Temeke.‎


‎Hayo yamebainishwa na Meneja wa TARURA wilaya ya Temeke, Mhandisi Paul Mhere ambapo ameeleza kuwa wameingia mikataba ya ujenzi wa barabara kwa gharama ya shilingi Bilioni 97.176.

‎"TARURA wilaya ya Temeke tuna mtandao wa barabara Kilomita 648.45, tuna majimbo matatu (3) ambayo ni Temeke, Chamazi na Mbagala na kote miradi inaendelea utekelezaji wake upo zaidi ya asilimia 75 isipokuwa Mbagala na Yombo mikataba ilisainiwa mwezi wa Aprili 2025 utekelezaji wake upo asilimia 32", amesema.

‎Ameongeza kuwa zaidi ya Kilomita 166 za barabara wilayani humo ni lami na zege, barabara za zege zinahimili uzito wa aina yoyote na zinadumu muda mrefu huku zikipunguza matengenezo ya mara kwa mara na kuondolea gharama serikali.

‎‎"Wilaya yetu ina bandari kavu na pia tuna bandari ambayo inahudumia nchi za Afrika Mashariki na Kati, hivyo malori yanayopita katika barabara zetu ni mengi, barabara hizi za zege zitadumu kwa muda mrefu na wananchi wameanza kufurahia maboresho ya miundombinu hii", amesema.

‎Naye, Diwani wa Kata ya Chang'ombe Mhe. Caroline Henrich amesema wamepata barabara sita (6) ambazo ni Igombe-Yemen, Songambele, Majimaji, Basra, Diwani na Mwakalinga ambapo hapo awali kipindi cha mvua maji yalijaa kwenye makazi ya watu na kusababisha kero lakini kukamilika kwa ujenzi wa mitaro sasa maji hayatuami na kero imeondoka pia thamani ya nyumba imepanda.

‎"Namshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mradi huu, awali barabara zilikuwa korofi Kata yetu ni mtambuka barabara kubwa ya VETA na ile inayoelekea Uwanja wa Taifa zikiwa zina foleni hakuna njia nyingine ya kupita zaidi ya barabara zetu, lakini sasa barabara zimejengwa imara kwa kiwango cha zege wageni wengi wanakuja kwa ajili ya biashara", amesema.

‎Kwa upande wake, Mwenyekiti wa mtaa wa Bora, Bw. Pius Kapungu ameeleza kuwa awali kulikuwa na mashimo na kipindi cha mvua maji yalikuwa yanaingia mpaka kwenye makazi ya watu lakini sasa wanashukuru mitaro iliyowekwa imesaidia hakuna maji na taa zikiwekwa kutakuwa salama mitaa itapendeza na ulinzi utaimarika.

‎Aidha, Bi. Saada Salim mkazi wa mtaa wa Majimaji ameipongeza serikali kwa ujenzi wa barabara na mifereji kwani kipindi cha mvua watu walishindwa kupata wateja wa kupangisha lakini sasa wanapata wateja wengi uchumi unakua, mazingira yamekuwa mazuri, maduka yamekuwa mengi na magari yanafika.

‎‎Naye, Bw. Jimmy Mwakipesile mkazi wa Chang'ombe maduka mawili amesema barabara imewarahisishia kusafirisha abiria kwa usalama tofauti na awali walikuwa wanadondoka kwenye maji na matope, pia sasa abiria wameongezeka kwa siku walikuwa wanapata shilingi 15,000 hadi 20,000 lakini sasa wanaweza kupata hadi shilingi 40,000 mpaka 50,000 kwa siku.






 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Huduma za Maji (EWURA) kuendesha operesheni ya kuwabaini watu wanaojihusisha na vitendo vya kuficha mafuta kwa makusudi ili kusababisha uhaba katika maeneo mbalimbali.

Ameeleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanatumia mwanya wa hali iliyopo kwa kuchukua mafuta kutoka kwenye maghala (depots) kwa kiwango kikubwa kuliko mahitaji yao, kisha kuyahifadhi wakisubiri bei mpya zitangazwe ndipo wayauze kwa bei ya juu.

Amesisitiza kuwa vitendo hivyo ni kosa la uhujumu uchumi, na yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria. Hivyo, amewaonya wafanyabiashara wanaojihusisha na vitendo hivyo kuacha mara moja kwa kuwa vinachangia kuleta uhaba wa mafuta.

“Nimewaelekeza Ewura kuanzia leo, usimwonee mtu yoyote aibu kama mtu akikamatwa ameficha mafuta, kwakweli sisi hatutamvumilia na Kamshna msimamie hilo mafuta yanayopakiwa hapa Dar es salaam muhakikishe yanafika kwenye vituo kama inavyokuwa imepangwa” amesisitiza Matarajio.

Dkt. Mataragio amefafanua kuwa tayari wameanza kupokea taarifa za baadhi ya vituo kukosa mafuta, hali inayochangiwa na vitendo vya aina hiyo ambapo mafuta yanapochukuliwa Dar es Salaam hayafiki katika vituo kama inavyotakiwa.

Kwa upande wake, Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima, amesema Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa usafirishaji na uuzaji wa mafuta nchini, ili kuhakikisha mafuta yote yanayopakiwa kutoka kwenye matenki yanafika katika vituo husika na wananchi wanaendelea kupata huduma bila usumbufu wowote.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na Tume ya Ushindani (FCC) wamekutana na wadau wa bidhaa za pombe nchini kwa lengo la kuwajengea uelewa juu ya matakwa ya sheria, kanuni na viwango vinavyosimamia sekta hiyo.

Naibu Waziri wa Nishati Mh. Salome Makamba amekabidhi vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kutatua changamoto zao kwa haraka.

Akizungumza leo tarehe 27, Machi 2026 wakati wa hafla ya kukakabidhi vitendea kazi hivyo iliyofanyika katika Manispaa ya Kahama Mkaoni Shinyaga Mhe. Salome amesema  hatua hiyo ya kukabidhi vitendea kazi hivyo ni kuyaishi maono ya Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma za Umeme wa uhakika.

Amesema vitendea kazi  hivyo vinakwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi kwa watumishi wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga na kuwawezesha kutatua changamoto za wateja kwa wakati. 

“Kupitia vyombo hivi vya usafiri vitakwenda kuleta mabadiliko makubwa katika kumfikia mteja kwa haraka na kumhudumia, niwaombe mvitumie kutatua changamoto zao kwa wakati “ amesema Salome.

Aidha Mhe. Salome ametumia nafasi hiyo kuwataka wakazi wa Manispaa ya Kahama kuchangamkia matumizi ya Nishati safi ya umeme kupikia kwani Nishati ya umeme ni nafuu salama na rafiki kwa mazingira.

“Niwaombe wakina mama wa Kahama tuchangamkie matumizi ya nishati safi ya kupikia ya umeme, TANESCO wameleta majiko hapa unapika kwa urahisi na haraka zaidi”.

Hata hivyo Mhe. Salome amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme TANESCO inaendelea kwa kasi kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika Manispaa ya Kahama kutokana na kuendelea kukua kwa Mji huo ambapo mpaka sasa tayari zaidi ya  Shilingi milioni 600 zimetengwa kwa ajili ya kujenga laini mpya ya umeme itakayo wahudumia wakazi wa Manispaa ya Kahama.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Benson Mbigili amesema wamepokea vitendea kazi mbalimbali ikiwemo Magari manne (4), Bajaji moja (1)  pamoja na Pikipiki nne (4). 

Mha. Benson ameipongeza Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kwa kuwezesha vitendea kazi hivyo ambavyo kwa sasa wanakwenda kuvitumia kufikisha huduma kwa wananchi kwa haraka zaidi.

Amesema kupitia Magari hayo sasa yatawasaidia kuwafikia wateja wapya katika maeneo yote hasa yale korofi ambapo kabla ya Magari hayo ilikuwa changamoto kuwafikia na kuwaahidi wananchi kuendelea kutoa huduma bora na ya uhakika kila wakati.

“Tunaishukuru Serikali kupitia Shirika la umeme Tanzania TANESCO kwa kutupa vitendea kazi hivi ambavyo kwa sasa tunakwenda kuvitumia kufikisha huduma kwa wananchi kwa haraka zaidi.

Aidha amesema TANESCO Mkoa wa Shinyanga inaendelea kwa kasi kubwa kuhamasisha matumizi ya Nishati safi ya kupikia kwa umeme ili wananchi waweze kuelewa umuhimu wa kutumia nishati hiyo kupikia.











 


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla amewataka watendaji wa Wakala hiyo kuanza ukaguzi wa mazao ya shamba na kupambana zaidi na ufungashaji wa mazao hayo kwa mtindo wa lumbesa.

Akifungua Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa WMA, Machi 27, 2026 jijini Dodoma, Kihulla amewasisitiza wajumbe wa Baraza hilo kufikisha ujumbe huo kwa watumishi wote katika maeneo yao kuanza kutekeleza jukumu hilo kikamilifu.

“Lakini tunapotekeleza majukumu haya, tuhakikishe haki katika biashara na kulinda mapato ya Serikali,”ametahadharisha.

Amesema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai 2025 hadi Machi 2026, WMA imepata mafanikio mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yake ya kumlinda mlaji kupitia uhakiki wa vipimo lakini pia kumekuwepo na changamoto kadhaa.

Akidadavua, amesema mafanikio yaliyopatikana yametokana na juhudi, weledi na ushirikiano wa watumishi wote wa Wakala hivyo amewapongeza kwa kazi nzuri wanayoendelea kufanya.

“Pamoja na mafanikio hayo, bado tunakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ongezeko la wigo wa majukumu yetu katika kumlinda mtoa huduma pamoja na mpokea huduma,” ameeleza.

Mtendaji Mkuu Kihulla amebainisha baadhi ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na jukumu la uhakiki wa vipimo vinavyotumika kupima muda wa maongezi pamoja na uhakiki wa mita za maji na vilevile lumbesa; suala ambalo liliungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Sekta ya Afya (TUGHE), Ngazi ya Taifa, Rugemalira Rutatina ambaye pia alishiriki mkutano huo, akisema yako malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi katika maeneo hayo hivyo yanapaswa kushughulikiwa.

Kihulla amesisitiza kuwa hata viongozi wakuu wa Wizara akiwemo Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga wameielekeza WMA kupambana na ufungashaji mazao ya shamba kwa mtindo wa lumbesa ili kuwalinda wakulima.

Katika hatua nyingine, Mtendaji Mkuu amewahimiza wafanyakazi wote wa WMA kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uzalendo akiwataka kutambua kuwa kazi wanayofanya ina mchango mkubwa katika kulinda haki za wananchi pamoja na kukuza biashara ya ushindani na haki, ikiwemo pia kuongeza mapato ya Serikali.

“Kwahiyo, niwaombe sana mkawasisitize watumishi waliopo katika vituo vyenu kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na weledi na kubwa zaidi kujiepusha na vitendo vya rushwa.”

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la WMA, Isaac Birahi aliushukuru Uongozi wa Wakala hiyo kwa kuendelea kuweka mazingira mazuri ya ufanyaji kazi kwa watumishi na kuomba hali hiyo iendelee kwa viwango vya juu zaidi.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Sera na Mipango, Nelson Ruturagala, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 16, 2026 alisema kuwa Wakala imefanikiwa kutekeleza Mpango Kazi wake kwa wastani wa zaidi ya asilimia 91.62

Akidadavua, aliyataja maeneo ya utekelezaji yaliyochangia kufikia wastani huo kuwa ni katika usimamizi wa vipimo, ukaguzi, uhakiki wa bidhaa zilizofungashwa zinazoingia nchini pamoja na ada kutokana na utolewaji wa huduma.

Katika kikao hicho cha 37, wajumbe wa baraza walipata pia fursa ya kujadili Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

 


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, leo Machi 27, 2026 ameshiriki katika ibada ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Watu Wenye Ulemavu), marehemu Mhe. William Vangimembe Lukuvi.

Ibada hiyo imefanyika katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na Serikali, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba.

Katika tukio hilo, Prof. Shemdoe aliambatana na wasaidizi wake akiwemo Naibu Waziri anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagwila, Naibu Waziri anayeshughulikia Afya, Dkt. Mhe. Jafar Seif, Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Bw. Adolf Ndunguru pamoja na Naibu Katibu Mkuu Bw. Sospeter Mtwale.

Marehemu William Lukuvi ataendelea kukumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika Utumishi wa Umma na maendeleo ya taifa kwa ujumla, kutokana na uzoefu wake wa kulitumia taifa katika nafasi mbali mbali za uongozi.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewataka walimu 150 wa Amali za Kihandisi wanaokwenda India kuongeza umahiri kuhakikisha wanajifunza kwa bidii ili watakaporejea wawajengee uwezo walimu wengine, na hatimaye kutoa mchango utaokuwa na tija katika kuharakisha mageuzi ya elimu nchini.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo Machi 26, 2026 kwa walimu hao waliopata fursa ya kwenda nchini India kuongeza umahiri, wakati wa hafla ya kuwaaga walimu hao iliyofanyika Jiji Dar es Salaam.

“Nendeni mkajifunze kwa bidii na nidhamu, mkazingatie maadili, jifunzeni mbinu mpya na muwe tayari kuzitumia mtakaporejea, hivyo tunatarajia mtakaporejea mtakuwa nguzo ya kuboresha elimu ya amali katika shule zenu na chanzo cha maarifa kwa walimu wengine,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesisitiza kuwa mpango wa mafunzo hayo ni utekelezaji wa sera ya elimu ya lazima ya miaka 10, unaolenga kujenga umahiri wa ufundishaji na kuandaa kizazi cha wataalamu wenye ushindani wa kimataifa, huku akiwataka walimu hao kutambua nafasi yao kama daraja kati ya sera na utekelezaji darasani.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia walimu hao fursa ya mafunzo, akisisitiza kuwa ni ishara ya dhamira ya dhati ya kuendeleza mageuzi ya elimu, huku akipongeza mshirikiano wa viongozi wa wizara za kisekta katika kulitekeleza kwa ufanisi.

Wanufaika wa mafunzo hayo, akiwemo Mwalimu Judith Faustine wa Uhandisi Ujenzi katika Shule ya Sekondari Mwadui Ufundi na Mwalimu Jacob Mwalyego wa fani ya Uashi katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Mbogwe, wameishukuru Serikali kwa kuwapatia nafasi hii ya kipekee. Wamesema ni heshima kubwa na fursa ya kuongeza maarifa yatakayowawezesha kuendeleza mageuzi ya elimu nchini.

Kamishna wa Elimu Dkt. Lyabwene Mtahabwa ameeleza kuwa mafunzo hayo ya mwezi mmoja yamewahusisha walimu kutoka mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na viongozi wa ngazi ya elimu mkoa kutoka mikoa tisa, hivyo

kuiwezesha Tanzania kuandika ukurasa mpya katika historia ya elimu ya ufundi kwa kupeleka walimu 150 wa Amali za Kihandisi nchini India ambao wakirejea watasimamia kikamilifu uendelevu wa mafunzo nchini.

Tanzania imeandika ukurasa mpya katika historia ya elimu ya ufundi kwa kupeleka walimu 150 wa Amali za Kihandisi nchini India.

Hatua hii kubwa ya kimkakati siyo tu safari ya mafunzo, bali ni uwekezaji wa kitaifa katika mustakabali wa elimu na uchumi wa viwanda, ikilenga kuongeza umahiri wa walimu na kuandaa kizazi cha wataalamu watakaoshindana kimataifa katika nyanja za teknolojia na uhandisi.

Katika hafla ya kuwaaga walimu hao Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesisitiza kuwa mpango wa mafunzo hayo ni utekelezaji wa sera ya elimu ya lazima ya miaka 10, unaolenga kujenga umahiri wa ufundishaji na kuandaa kizazi cha wataalamu wenye ushindani wa kimataifa. Ameeleza kuwa safari ya mageuzi ya elimu inaendelea na haitarudi nyuma, huku akiwataka walimu watambue nafasi yao kama daraja kati ya sera na utekelezaji darasani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe amewataka walimu hao kudumisha nidhamu na maadili, kujifunza kwa bidii na wakirudi wasambaze maarifa kwa wenzao ili kuharakisha mageuzi ya elimu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia walimu hao fursa ya mafunzo, akisisitiza kuwa ni ishara ya dhamira ya dhati ya kuendeleza mageuzi ya elimu, huku akipongeza mshirikiano wa viongozi wa wizara za kisekta katika kulitekeleza kwa ufanisi.

Kamishna wa Elimu Dkt. Lyabwene Mtahabwa ameeleza kuwa mafunzo hayo ya mwezi mmoja yamewahusisha walimu kutoka mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na viongozi wa ngazi ya elimu mkoa kutoka mikoa tisa ili kusimamia kikamilifu uendelevu wa mafunzo warudipo nchini.

Wanufaika wa mafunzo hayo, akiwemo Mwalimu Judith Faustine wa Uhandisi Ujenzi katika Shule ya Sekondari Mwadui Ufundi na Mwalimu Jacob Mwalyego wa fani ya Uashi katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Mbogwe, wameishukuru Serikali kwa kuwapatia nafasi hii ya kipekee. Wamesema ni heshima kubwa na fursa ya kuongeza maarifa yatakayowawezesha kuendeleza mageuzi ya elimu nchini.

 


Na Oscar Assenga, TANGA

BODI ya Wakurugenzi ya Bonde la Pangani leo wamefanya ziara ya kukagua maeneo vyanzo vya maji ikiwemo Bwawa la Mabayani na Mtambo wa Kutibu Maji wa Mowe na kujiridhisha kuhusiana na kazi zinazotelezwa na menejimenti pamoja na wateja wao namna wanavyopokea huduma.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bonde la Pangani,Mhandisi Ruth Koya alisema kwamba bodi hiyo na menejimenti wamefanya ziara hiyo kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa maelekezo na majukumu wanayowalekeza menejimenti kwamba wanayafuatilia na kuyafanya kwa uhakika.



Katika ziara hiyo Bodi hiyo wametembelea Bwawa la mabayani wamejionea shughuli Zinazofanyika ikiwemo utunzwaji wa Bwawa la mabayani pamoja na kumtembelea mteja wao mkubwa Tanga Uwasa wameona yupo vizuri na kazi inafanyika kwa waledi

Alisema kwamba wameona bwawa limewekwa alama na wameipokea taarifa kwamba wananchi nao wanashirikishwa kutokana na uwepo wa jumuiya za watumia maji ambao wamekuwa chachu kubwa kuhakikisha vyanzo hivyo vinalindwa na kutunzwa.

Aidha alitoa wito kwa watumishi na kusisitiza kuwasimamia wadau wao wakiwemo Tanga Uwasa ili kuendelea kutunza chanzo cha maji kikubwa ambacho ni muhimu kwa ajili ya Jiji la Tanga na kushirikiana na wadau Tanga Uwasa na wengineo .

Alisema kwamba lakini wamepata taarifa Tanga Uwasa wanazidi kupanua uzalishaji maji hadi kufikia lita milioni 70 ina maana utunzaji ni nzuri ndio maana wameweza kuwekeza zaidi kupitia hat fungani yao walioipata hivi karibuni.

Awali akizungumza Mkurugenzi wa Bonde la Pangani Segule segule alisema kwamba ziara ya Bodi hiyo ni kutembelea maeneo ya uwandani na kukakgua maeneneo mbalimbali na kujiridhisha kuhusiana na kazi zinazotekelzwa na menejimenti lakini kupata kujua kuhusu wateja wao mbalimbali wanavyopokea huduma zao.

Alisema kwamba bodi imeona ipite kwenye eneo la mnufaika mkubwa wa maji Mto Zigi ambao ni wenzao wa Tanga Uwasa ambapo wametembelea maeneo mbalimbali ambayo Tanga Uwasa wanafaidika nayo wamenza ikiwemo Bwawa la Mabayani ambalo wao ndio wamiliki na yeye ndio mteja wao.

Aidha alisema kwamba wamejionea mazingira yanavyotunzwa na wametumia fursa hiyo kupata maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Tanga Uwasa kuhusiana na mradi wa Hati Funfani ambao unatumia chanzo kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji Tanga .

Alieleza kwamba na ziara ilitoa fursa kwa wajumbe wa bodi,menejimenti kuona mchango wao kama bonde mchango wao kwenye mradi Hatifungani kwamba wakitunza vyanzo vyema wenzao wa Tanga Uwasa wataweza fikia matarajio yao na kwa gharama walizokadiria.

Aliongeza kwamba bwawa hilo wanalitunza na moja walishaanza kuweka alama za mipaka kuainisha mita 500 na kama sheria za usimamizi rasilimali za maji zinaelekeza mita 60 za chanzo lakini wanatoa mamlaka kwa taasisi na wao kama mabonde kuomba nyongeza kwa bwawa la mabayani wamehifadhi mita 500 .

Alieleza kwa sasa hiyo inatoa fursa hata nyongeza za miradi kutokana na mahitaji ya maji wanaweza kuhifadhi hivyo mkakakati wao ni kuendelea kuimraisha baada ya kuweka alama za mipaka katika yale maeneo walioweka mipaka watu wasifanye shughuli za kibinadamu ili kupunguza uchafuzi kwenda kwenye bwawa.

Aliongeza kwamba lakini upande wa juu wa bwawa wanaendelea kuimarisha utunzaji wa jumuiya za watumiaji maji ambao wote wanakuwa watumiaji maji na mkakati wa kuziimarisha huku wenzao Tanga Uwasa wameimarisha utunzaji wa vyanzo vya maji .

Hata hivyo alisema kwamb hali ya vyanzo vya maji ukilinganisha na miaka ya nyuma ni nzuri changamoto zipo lakini hawajafika wakati wa kusema hali iliyopo imehataraisha vyanzo kukauka na kushindwa kuwahudumua watu.

Aliongeza kwamba lazima waendelee kuimarisha na shughuli zinaongezeka kutokana na mahitaji ya ardhi kuna jitihada kubwa za watu kutokana na uhaba wa ardhi na watu wanaongezeka na kutaka kusogelea vyanzo wao wanaendelea kuimarisha jumuiya za watumiaji maji ili kuweza kuhakikisha vyanzo vya maji vilivyopo vinatunzwa na kuvilindwa.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly alisema kwamba ameshiriki katika ziara hiyo ya Bodi ya Bonde la Pangani ambao wanatembelea kuangalia vyanzo vya maji vinavyotunzwa ikiwemo bwawa la mabayani ambalo ndio chanzo kikubwa wanachotumia Tanga Uwasa katika kusambaza maji kinahudumia Tanga, Muheza na Mkinga .

Mhandisi Hilly alisema wameongeza uzalishaji wa maji kuhakikisha wanawafikia vema wananchi ili kutekeleza malengo yao mbalimbali ya nchi ifikapo 2030 watu wote wawe wamepata maji mijini na Tanga Uwasa na wenzao Ruwasa wananchi waweze kupata maji.

Alisema kwa hiyo mahitaji na matumizi ni makubwa wao kwa kushirikiana na Bodi la Bonde la Mto Pangani wanaweka juhudi kubwa katika utunzaji chanzo cha maji kutokana na kuwa wanufaika wakubwa wa bonde hilo.

Alieleza hivyo wana wajibu kuhakikisha chanzo hicho kinalindwa na kutunzwa wanashirikiana kwenye maeneo mbalimbali ya mto,bwawa la mabayani wana mpaka kamati za uhifadhi na utunzaji wa mazingira ikiwemo uwamakizi kuhakikisha vinaendelea kuwa imara.

“Kwa mfano mradi wa hati fungani miongoni mwa fedha zinakwenda kwenye chanzo cha maji na sasa wana mkakati wa kupanda miti laki moja katika maeneo hayo na mpaka sasa wamepanda miti zaidi 50,000”Alisema

Hata hvyo alieleza pia wameendelea na mradi wa hati fungani kuongeza uzalishaji maji huku wakieleza mipango yao ni kuongeza uwezo bwawa tuta eneo la kupita utoro wa maji na kazi za mazingira zitafanyika na hivyyo itawasadia kuwa na uhakika wa usambazaji wa maji hata ikitokea mabadiliko ya tabia ya nchi na wakati wa ukame.

TUME  ya Ushindani (FCC) kupitia Kanda ya Ziwa imeendelea kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kutoa elimu ya ulinzi wa mlaji kupitia Kliniki ya Mlaji inayofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo, Manispaa ya Musoma.

Katika kuimarisha uelewa wa wadau mbalimbali, FCC haikuishia kwa wananchi pekee bali pia ilifanya ziara maalum kwa baadhi ya taasisi zinazotoa huduma ndogo za fedha katika manispaa hiyo, kwa lengo la kuzielimisha juu ya wajibu wao wa kuzingatia sheria na kanuni katika utoaji wa huduma.

Akiongoza zoezi hilo, Mkuu wa Kanda ya Ziwa,Bw. Frank Mdimi, akishirikiana na Afisa Biashara wa Manispaa ya Musoma, Joshua Mlole pamoja na maafisa wengine, walitembelea taasisi za Enokwe, Pongeza na Ohura na kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na watoa huduma hao.

Katika ziara hiyo, maafisa wa FCC wamesisitiza umuhimu wa kuandaa mikataba ya huduma kwa uwazi na haki, wakielekeza taasisi hizo kuzingatia matakwa ya  Sheria ya Ushindani inasimamia na kudhibiti Mikataba ya Mlaji inayoandaliwa na watoa huduma

Watoa huduma kutoka taasisi hizo walionesha utayari mkubwa wa kupokea maelekezo hayo, wakieleza kufurahishwa kwao na hatua ya FCC kuwafuata na kuwapatia elimu kwa vitendo. Wamesisitiza kuwa elimu hiyo itawasaidia kuboresha huduma zao na kujenga uaminifu kwa wateja wao.

Aidha, taasisi hizo zimeahidi kushirikiana kwa karibu na FCC kwa kuhakikisha zinazingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali, pamoja na kudumisha mawasiliano ya mara kwa mara ili kuboresha zaidi sekta ya huduma ndogo za fedha.

Zoezi la utoaji elimu kupitia Kliniki ya Mlaji linaendelea Machi 27, ambapo wananchi wataendelea kupatiwa elimu kuhusu haki zao, wajibu wao na namna bora ya kujilinda wanapotumia huduma mbalimbali sokoni.