Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Dkt. Evaline Munisi amesema kuwa Mafanikio ya utekelezaji wa Dira 2050 yanategemea Mahusiano mema kwa kuwa ndio matokeo ya Utawala bora, Amani, Usalama na Maendeleo endelevu.
Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imebainisha kuwa mwaka 2025 ilikamata tani 31.76 na lita 183,500 za kemikali bashirifu, huku ikizuia tani 734 kuingia nchini kinyume cha sheria, ikisema waandishi wa habari wanapaswa kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya uhalifu huo kupitia utoaji wa taarifa sahihi kwa umma.
 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Na. Veronica Mwafisi-Dar ES Salaam 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ina nafasi ya kipekee katika kujenga na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji wa majukumu ya Serikali kila siku.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2026 wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya TPSC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kikwete amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka kipaumbele katika uimarishaji wa Utumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye tija. 

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania si tu taasisi ya mafunzo, bali ni nguzo muhimu ya Serikali katika kujenga rasilimaliwatu yenye maarifa, stadi, maadili na uzalendo unaohitajika katika kutumikia umma kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatutaka kuwa na Taifa lenye uchumi wa kisasa, ushindani wa kimataifa, matumizi makubwa ya teknolojia, na huduma za umma zenye ufanisi wa hali ya juu. Hivyo, mafanikio ya Dira hiyo yatategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo. 

“Chuo hiki kina wajibu mkubwa wa kuhakikisha  Watumishi wa Umma wanapata maarifa na stadi zinazolingana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja ili kuwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo,” amesema Waziri Kikwete.

Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza watangulizi wake kwa usimamizi mzuri ambao umechangia mafanikio makubwa ya Chuo hicho huku akimshukuru Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Juma Mkomi kwa kuendelea kusimamia Chuo hicho kiutendaji. 

Vilevile, Waziri Kikwete ameipongeza Bodi ya Ushauri ya TPSC, Menejimenti, Watumishi, Wanafunzi na wadau wote kwa mchango wao katika safari ya kutimiza miaka 25 ya mafanikio ya chuo hicho.

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mhe. Waziri kuzungumza na wadau katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa waajiri kutumia Kampasi za TPSC zilizo katika kanda zao ili kuwawezesha watumishi ikiwemo waajiriwa wapya kupata mafunzo ya awali.

“Kampasi katika Kanda hizo zimewekwa kimkakati ili kusogeza huduma za chuo katika mikoa mbalimbali, hivyo Waajiri wazitumie kikamilifu kwa watumishi kupata mafunzo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.” Amesisitiza Katibu Mkuu Mkomi.

Amezitaja Kampasi hizo kuwa ni Dar es Salaam, Mbeya, Tanga, Singida, Tabora na Mtwara na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na TPSC za kumiliki majengo yao ambapo Kampasi ya Singida inaendelea na ujenzi wa majengo 30 na Kampasi ya Tanga majengo 15.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TPSC, Dkt. Florens Turuka amesema Bodi itaendelea kutoa ushauri ili Chuo kiendelee kuwa kinara katika masuala mbalimbali ikiwemo kujenga rasilimaliwatu yenye maadili, na yenye tija kwa taifa.

Akiwasilisha taarifa ya miaka 25 ya TPSC, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho amesema tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo taaluma, rasilimaliwatu na miundombinu.


Kamati ya Sera ya Fedha ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imepandisha kiwango cha Riba yaBenki Kuu (CBR) kutoka asilimia 5.75 hadi asilimia 6.25 katika robo ya tatu ya mwaka inayoanza Julai hadi Septemba 2026.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kuanzisha Kijiji cha Mazingira, jukwaa maalum linalowakutanisha wananchi, wadau wa mazingira na taasisi mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu, kuonesha ubunifu na teknolojia rafiki kwa mazingira, pamoja na kuhamasisha uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira.
Na. Mwandishi Wetu - Arusha

Tanzania ipo tayari kwa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) ikiwa mwenyeji kwa kushirikiana na Kenya na Uganda ambapo maandalizi yamefikia hatua nzuri kwa kuzingatia viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) vinavyotakiwa.


Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam.


Kadri Maonesho ya 56 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanavyoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeendelea kuthibitisha kuwa teknolojia ya nyuklia siyo teknolojia ya kutumika kwenye uzalishaji wa nishati pekee, bali ni nyenzo muhimu inayochochea maendeleo ya kiuchumi, biashara, uwekezaji na ustawi wa jamii kupitia matumizi yake katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Leo ikiwa ni siku ya sita tangu kuanza kwa maonesho hayo yaliyofunguliwa rasmi tarehe 28 Juni na yanayotarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Julai 2026, banda la TAEC limeendelea kuwa moja ya maeneo yanayovutia idadi kubwa ya wananchi, wanafunzi, watafiti, wawekezaji, wafanyabiashara na wadau kutoka ndani na nje ya nchi wanaotaka kupata uelewa kuhusu nafasi ya teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya Tanzania.

Ushiriki wa TAEC katika maonesho haya unaendana na dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu sahihi kuhusu matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia pamoja na mchango wake katika kukuza uchumi wa taifa kupitia uzalishaji wenye tija, huduma bora za afya, usalama wa chakula, maendeleo ya viwanda, utafiti na uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza katika banda la TAEC lililopo ndani ya Banda Kubwa la China, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TAEC, Bwana Peter Ngamilo, amesema maonesho ya Sabasaba ni jukwaa muhimu linaloiwezesha TAEC kuwasiliana moja kwa moja na wananchi na wadau mbalimbali, kuwaelimisha kuhusu majukumu ya Tume pamoja na fursa zinazotokana na matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya Taifa.

“Lengo letu kubwa ni kuhakikisha wananchi wanafahamu kuwa teknolojia ya nyuklia ni nyenzo muhimu ya maendeleo. Kupitia maonesho haya tunaendelea kutoa elimu kuhusu matumizi salama ya mionzi, wajibu wa TAEC katika usimamizi na udhibiti wa matumizi ya mionzi nchini, pamoja na namna teknolojia hii inavyochangia kukuza biashara, kuongeza tija katika uzalishaji na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Bwana Ngamilo.

Ameeleza kuwa wananchi wengi wamekuwa wakitembelea banda la TAEC kwa lengo la kupata ufafanuzi kuhusu teknolojia ya nyuklia na matumizi yake katika sekta mbalimbali, hali inayoonyesha kuwa uelewa wa jamii kuhusu teknolojia hiyo unaendelea kuongezeka siku hadi siku.

Katika sekta ya afya, TAEC imekuwa ikiendelea kutoa elimu kuhusu matumizi ya mionzi katika uchunguzi wa magonjwa, tiba ya saratani, tiba za nyuklia na uchunguzi wa kitaalamu unaowezesha madaktari kutoa huduma zenye usahihi zaidi kwa wagonjwa. Matumizi haya yameendelea kuboresha ubora wa huduma za afya nchini na kuongeza uwezo wa taasisi za tiba kutumia teknolojia za kisasa katika kuokoa maisha ya wananchi.

Kwa upande wa kilimo, wananchi wanaelimishwa namna teknolojia ya nyuklia inavyosaidia kuboresha mbegu za mazao, kuongeza uzalishaji, kudhibiti wadudu waharibifu wa mazao, kuhifadhi chakula baada ya kuvunwa na kuongeza usalama wa chakula. Teknolojia hizi zinachangia kuongeza ushindani wa bidhaa za kilimo katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Katika sekta ya mifugo, TAEC inaendelea kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika utambuzi wa magonjwa ya mifugo, kuboresha uzalishaji wa mifugo, kuimarisha lishe ya wanyama na kusaidia programu za uzalishaji zinazoongeza tija kwa wafugaji.

Sekta ya viwanda nayo ni miongoni mwa maeneo yanayonufaika kwa kiwango kikubwa kupitia matumizi ya teknolojia ya nyuklia. Kupitia teknolojia za mionzi, viwanda vinaweza kufanya ukaguzi wa ubora wa bidhaa bila kuziharibu (Non-Destructive Testing), kupima unene wa bidhaa mbalimbali, kufanya vipimo vya ubora wa miundombinu, kutambua hitilafu katika mitambo na kuongeza usalama wa uzalishaji. Teknolojia hizi husaidia kupunguza gharama za uzalishaji, kuongeza ubora wa bidhaa na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Aidha, katika sekta ya nishati na utafiti, TAEC inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa kujenga uwezo wa matumizi ya teknolojia za nyuklia katika tafiti zinazolenga kutatua changamoto za maendeleo, usimamizi wa rasilimali za maji, ulinzi wa mazingira na matumizi bora ya maliasili.

Kwa mujibu wa Bwana Ngamilo, elimu inayotolewa katika maonesho haya pia inalenga kuondoa dhana potofu ambazo baadhi ya wananchi wamekuwa nazo kuhusu teknolojia ya nyuklia.

“Wananchi wengi walikuwa wakihusisha teknolojia ya nyuklia na silaha pekee, lakini wanapofika katika banda letu wanajionea ushahidi kuwa teknolojia hii inagusa maisha yao ya kila siku kupitia huduma za afya, uzalishaji wa chakula, maendeleo ya viwanda, utafiti, usimamizi wa mazingira na sekta nyingine nyingi zinazochochea maendeleo ya uchumi wa Taifa.”

Maonesho ya Sabasaba yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha taasisi za Serikali, sekta binafsi, wawekezaji na wananchi katika kuonesha bidhaa, huduma na ubunifu unaochochea biashara na maendeleo ya uchumi wa Tanzania. Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha teknolojia ya nyuklia inatumika kwa amani, usalama na manufaa ya wananchi wote huku ikichangia utekelezaji wa dira ya maendeleo ya taifa kupitia sayansi, teknolojia na ubunifu.

TAEC inaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake lililopo ndani ya Banda Kubwa la China, Vyumba Na. 60 na 61, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam, ili kujionea teknolojia mbalimbali zinazotumiwa nchini na kupata elimu kuhusu mchango wa teknolojia ya nyuklia katika kujenga uchumi imara, kuongeza ushindani wa biashara na kuharakisha maendeleo endelevu ya Tanzania.



Nilijua wazi kuwa ardhi ile ilikuwa yangu kihalali. Niliinunua kwa jasho langu mwenyewe baada ya miaka mingi ya kufanya kazi ndogo ndogo, kujiwekea akiba, na hatimaye kupata kipande hicho cha ardhi kando ya mto katika kijiji cha baba yangu. Ilikuwa sehemu niliyoipenda sana, na ndoto yangu ilikuwa ni kujenga nyumba ndogo ya kupumzikia baada ya kustaafu kazi ya ualimu.

Lakini mambo yalibadilika nilipopata taarifa kwamba kijana mmoja wa ukoo, ambaye sikuwa hata na ukaribu naye, alikuwa ameweka uzio na kuanza kulima kwenye ardhi yangu kana kwamba ni yake. Nilipokwenda kumhoji, alinikaripia na kusema kuwa hiyo ardhi ni ya familia, na mimi sina haki nayo kwa sababu sikuishi kijijini kwa muda mrefu.

Nilichanganyikiwa, nikamuonyesha stakabadhi za umiliki halali lakini bado alikataa kuondoka.
Nilifikisha suala hilo kwa uongozi wa kijiji, lakini hata hapo hakukuwa na msaada wowote wa maana. Kila mtu alionekana kumwogopa au kumfurahia kwa sababu ya pesa zake. Nikaamua kufungua kesi mahakamani, nikiwa na imani kwamba haki itatendeka.

Lakini niligundua kuwa hata kwenye mchakato wa kisheria, si kila kitu ni haki na uwazi. Mtu huyo alianza kutumia mbinu chafu, akijaribu kushawishi mashahidi wangu na hata kutoa rushwa kwa baadhi ya maafisa.SOMA ZAIDI.
Siku hiyo siwezi kuisahau, hata kama nitazeeka. Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, majira ya saa mbili asubuhi, niliporudi nyumbani mapema kutoka sokoni baada ya kusahau mkoba wangu. Nilipoingia chumbani kwangu, sikutegemea kabisa kuona kile nilichokiona.

Mume wangu aliyekuwa ameniahidi uaminifu wa milele, alikuwa kitandani na bosi wangu wa kazi mwanamke ambaye nilimwamini sana, ambaye alikuwa kama dada yangu mkubwa.
Nilishtuka, nikakosa hata nguvu ya kuhema. Waliposhtuka kuniangalia, waliruka kitandani na kuanza kutoa visingizio visivyokuwa na kichwa wala miguu.

Nilihisi kama dunia imeanguka juu yangu. Machozi yalinibubujika kwa uchungu na hasira. Niliwageukia na kusema kwa sauti ya chini lakini yenye uzito, “Mmeharibu kila kitu.” Baada ya tukio hilo, maisha yangu yalibadilika. Nilikuwa na hasira, huzuni, na chuki ndani yangu. Kazini sikuweza tena kustahimili kumuona bosi wangu, hivyo nikaandika barua ya kuacha kazi.

Nyumbani hali ilikuwa mbaya zaidi mume wangu alianza kujitetea kwa kunilaumu eti nilikuwa nikimnyima haki zake za ndoa. Alisema nilikuwa mbali kihisia, na kuwa hiyo ndiyo sababu ya yeye kutafuta “faraja” kwingine.
Nikiwa nimevurugika kiakili na kihisia, rafiki yangu wa karibu alinitembelea na kunikuta katika hali ya unyonge mkubwa.SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miezi mitatu, usingizi haukuwahi kuwa wa amani katika familia yetu. Kila usiku, hasa saa sita kamili, mtoto wetu mchanga alikuwa akiamka kwa vilio vya ajabu, vilivyokuwa na sauti ya hofu, maumivu, na mshtuko.

Mwanzo tulidhani ni ndoto za kawaida au labda tatizo la kiafya la mtoto, lakini tulipojaribu kumpeleka hospitali, madaktari hawakugundua tatizo lolote.

Kila mara alipoamka kwa vilio hivyo, hakuwa na homa, hakulalamika maumivu ya tumbo, na mara nyingi alitulizwa haraka lakini baada ya dakika chache, kilio kilianza tena. 

Kama mzazi, ni jambo la kutisha kuona mtoto wako akiteseka na huwezi kuelewa sababu. Nilianza kuchunguza mazingira ya chumba chetu. Nikahakikisha hakuna mbu, baridi kali wala kelele za usiku zinazoweza kumsumbua.

Lakini hakuna kilichobadilika. Tulijaribu kulala chumba kingine kwa wiki moja, na cha kushangaza mtoto alilala kwa utulivu kabisa. 

Lakini mara tu tuliporudi kwenye chumba chetu cha kawaida, vilio vilirejea saa hiyo hiyo saa sita usiku. Siku moja, nikiwa nimemchukua mtoto chumbani kumtuliza, nilihisi baridi kali ikipita miguuni mwangu kana kwamba mtu alikuwa amepita. SOMA ZAIDI.
Mara ya kwanza niliposikia mume wangu akisema kwa utani kuwa mimi ni kama friji, nilicheka tu. Lakini baadaye maneno hayo yalianza kuniuma. Hakusema moja kwa moja, lakini kila wakati tulipokuwa karibu, nilihisi kama kuna kitu kinamkera. Hakuwa akifurahia tendo la ndoa kama zamani, na mara nyingi alinitafuta visingizio.

Kama mwanamke, nilianza kujihisi duni. Ushawishi wangu wa kimapenzi ulizidi kupungua, na hali hiyo ilianza kuathiri ndoa yetu kwa ujumla. Nilipojaribu kumkabili, alinikwepa. Lakini siku moja nilimsikia akiongea na rafiki yake akisema kuwa mimi “sijui kumfurahisha mume,” na kwamba nilikuwa kama barafu kitandani.

Machozi yalinibubujika usoni mwangu. Nilimpenda sana mume wangu, na sikutaka kumpoteza. Lakini kwa hali ile, nilijua ni suala la muda tu kabla hajaanza kutoka nje ya ndoa au kuniacha kabisa. Nilianza kutafuta suluhisho. Niliangalia YouTube, nilisoma blogu, nikajaribu hata zile chai za mitishamba zinazouzwa mitandaoni lakini hakuna kilichosaidia.

Nilijaribu kujifunza mbinu mpya za kimapenzi, lakini bado hakukuwa na mabadiliko. Mume wangu alikuwa baridi zaidi yangu sasa. Hatukuwa tukiongea sana, hatukushiriki mapenzi kwa wiki kadhaa, na chumba chetu kiligeuka kuwa kama hosteli ya watu wawili wasiojuana.SOMA ZAIDI.
Wakati mwingine, maisha ya biashara yanaweza kuwa magumu kuliko tunavyoweza kuyakubali. Ndivyo ilivyokuwa kwa biashara yangu. 

Nilikuwa na biashara ya kuuza bidhaa maarufu mjini kwetu, na ingawa mwanzoni nilikuwa na mafanikio makubwa, hali ilianza kubadilika kwa haraka. Wateja walikuwa wanakuja kwa wingi, lakini walikuwa wanapungua kwa kila mwezi uliopita.

Hali ilionekana kuwa mbaya sana. Nilikuwa nimejitolea kwa bidii na kuongeza juhudi, lakini kila nilipokuwa najaribu kuboresha hali, biashara yangu iliendelea kuporomoka. Kwa kweli, kila nilichofanya kilionekana kuwa hakileti matokeo mazuri. Hata nilipotafuta njia mpya za kuvutia wateja, hakukuwa na mabadiliko yoyote.

Nilikuwa nikiingia kwenye madeni, wateja walikuwa wanakimbia, na hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya. Huo ndio ulikuwa wakati mgumu zaidi maishani mwangu. Nilijua kuwa kama sitapata suluhisho haraka, biashara yangu ingeweza kufa kabisa. Nikiwa katika huzuni na shinikizo, nilijua kuwa nilikuwa nikikosa kitu. SOMA ZAIDI.

 

Na Munir Shemweta

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania (IST), ambapo pande hizo zilijadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya taaluma ya Upimaji Ardhi na sekta ya ardhi nchini.

Ujumbe wa IST ulioongozwa na Rais wa taasisi hiyo, Dkt. Julian Magezi Ijumulana na Upande wa Wizara ya Ardhi uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Upimaji Ardhi ambaye ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansoor, ulimtembelea Waziri Dkt. Akwilapo kwa lengo la kujitambulisha.

Aidha, ujumbe huo ulimuelezea Mhe Dkt Akwilapo mikakati ya taasisi hiyo, ikiwemo maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 45 ya kuanzishwa kwake pamoja na Mkutano Mkuu wa Mwaka unaotarajiwa kufanyika Novemba 2026 katika Mkoa wa Mwanza.

Akizungumza katika kikao hicho, Julai 2, 2026 jijini Dar es Salaam Dkt. Akwilapo alisema ameyapokea mawazo na mapendekezo yaliyowasilishwa na Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania na kuahidi kuwa serikali itayafanyia kazi kwa kuzingatia maslahi ya sekta ya ardhi na maendeleo ya nchi.

Aidha, Waziri Dkt. Akwilapo alisisitiza kuwa swala la sheria ya Upimaji ardhi sura 324 na usajili wa Wapima ardhi sura 270 amelipokea na atafanyia kazi kwa haraka kwani Wapima Ardhi wana nafasi muhimu katika  kupunguza na kuondoa migogoro ya ardhi nchini kupitia upimaji sahihi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, akihutubia waumini na wageni mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Kumbukizi ya Damu ya Yesu (C.PP.S) ya Provinsi ya Tanzania yaliyofanyika katika Viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida .

Na: OWM (KAM), Manyoni - Singida

Serikali imesema inatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii, kudumisha amani na kukuza maadili nchini, huku ikizitaka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza malezi bora kwa watoto na vijana ili kujenga taifa lenye ustawi na mshikamano.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu Amesema hayo  alipomwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Kumbukizi ya Miaka 60 ya Uwepo wa Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania iliyofanyika katika viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana, Manyoni, Mkoani Singida.

Amesema, maendeleo ya taifa hayawezi kupatikana kwa juhudi za Serikali pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo taasisi za dini, sekta binafsi na wananchi, hivyo alibainisha kuwa maadhimisho hayo ya miaka 60 Uwepo wa Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania ni ishara ya urafiki, mshikamano na dhamira ya pamoja ya kujenga Tanzania yenye amani na matumaini.

“Ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini umeendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa kwa kusaidia utoaji wa huduma za kijamii, kuimarisha maadili na kujenga jamii yenye amani,” amesema

Kwa upande wake, Mhe. Sangu ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuwa sauti ya matumaini kwa waliokata tamaa, chanzo cha upatanisho katika jamii na daraja la kuunganisha wananchi pale panapojitokeza migawanyiko. Ameongeza kuwa, kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo na kwamba Watanzania wanapaswa kuendelea kuilinda na kuirithisha kwa vizazi vijavyo.

Vilevile, Alisisitiza kuwa vijana wanapaswa kutumia vipaji na maarifa yao bila kuacha misingi ya imani, akieleza kuwa maendeleo ya kweli yanahitaji kizazi kinachounganisha elimu, maadili na hofu ya Mungu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego amesema, Serikali itaendelea kuzifanyia kazi changamoto zilizowasilishwa na viongozi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania, ikiwemo ushirikiano katika sekta ya afya na huduma za kijamii ili shirika hilo liendelea kutoa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu, Padre Vedasto Ngowi ameshukuru Serikali kwa ushirikiano uliopo na kueleza matumaini yao ya kuendelea kushirikiana katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kiroho na kijamii.

Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu limesajiliwa na Serikali ya Tanzania kama (The Society of the Precius Blood) ambapo linajishughulisha na kazi za kitume kwa Mapadre na Mabruda kwa lengo la kueneza upendo wa Kristo aliouonesha alipomwaga Damu yake msalabani kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano Mhe.Deus Sangu akisalimiana na Baba Askofu Mkuu wa Jimbo la Singida Katoliki Mhashamu Edward Mapunda katika Kumbikizi ya Damu ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania iliyofanyika katika Viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana, Wilaya ya Manyoni, Singida.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, akihutubia waumini na wageni mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Kumbukizi ya Damu ya Yesu (C.PP.S) ya Provinsi ya Tanzania yaliyofanyika katika Viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

 


•Aitaka kamati iliyoshiriki majadiliano ya awali kujadiliana tena

Na OWM - TAMISEMI, Kibaigwa


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Kampuni ya Barrick - Twiga Minerals kwa kupeleka tabasamu mashuleni kupitia majadiliano waliyoyafanya ambayo yalipelekea Barrick kuchangia zaidi ya shilingi bilioni 70 za kitanzania ambazo zimewezesha ujenzi wa madarasa, mabweni na matundu ya vyoo katika shule za sekondari 132 nchini. 

Prof. Shemdoe ametoa pongezi hizo kwa Mhe. Rais na Kampuni ya Barrick - Twiga Minerals Julai 02, 2026 akiwa katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibaigwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa miundombinu ya shule za kidato cha tano na sita, ambao unaofadhiliwa kupitia ushirikiano wa Serikali na Kampuni ya Barrick - Twiga Minerals. 

“Nampongeza sana Mhe. Rais kwa kuwaona Barrick kama wadau muhimu, na nawashukuru na kuwapongeza Barrick kwa kuleta fedha za kuwekeza kwenye sekta hii muhimu ya elimu,” ameeleza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, ni chini ya uongozi makini wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndipo yalipoanzishwa majadiliano kati ya Serikali na Kampuni ya Barrick ya kuimarisha ushirikiano katika kuchangia maendeleo ya jamii kupitia uwekezaji wa sekta ya elimu, na kuongeza kuwa majadiliano hayo yalipelekea kupatikana kwa zaidi ya bilioni 70 za kitanzania ziloizotumika kwenye ujenzi wa madarasa, mabweni na matundu ya vyoo.

Aidha, Prof. Shemdoe ameelekeza kamati iliyoshiriki kwenye majadiliano ya awali ya mwaka 2023 na Kampuni ya Barrick - Twiga Minerals kurejea tena kwenye majadiliano mengine na kampuni hiyo, ili awamu awamu ya pili ya mradi huo ikikamilika zipatikane fedha nyingine za kuendelea kujenga miundombinu bora ya elimu.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Kampuni ya Barrick - Twiga Minerals Bi Penina Kituku ambaye ni Meneja wa Fedha amesema kuwa, uwekezaji wa zaidi ya shilingi bilioni 70 za kitanzania walioufanya una maana kubwa kwa jamii na unakwenda moja kwa moja kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji, ikiwa ni pamoja kutoa fursa kwa wanafunzi kusoma katika mazingira bora na salama.

Naye, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia elimu Bw. Atupele Mwambene,amesema kwamba mradi huo ulianzishwa kwa lengo la kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi wenye ufaulu mzuri ambao wanajiunga na kidato cha tano, na kuongeza kuwa afua ambazo zimetekelezwa nchi nzima mpaka hivi sasa ni ujenzi wa madarasa 1090, mabweni 270 na matundu ya vyoo 1640.

Akizungumza kwa niaba ya wakazi wa Kibaigwa, Bw. Alex Sailemi amesema kuwa, wakazi wa Kibaigwa wanayo sababu ya kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan  pamoja na Kampuni ya Barrick kwa kujengewa miundominu ya madarasa, mabweni na matundu ya vyoo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibaigwa.















 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma. Kushoto ni Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizindua jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa sita na mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Muonekano wa sehemu ya majengo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, akiwa pamoja na ujumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na viongozi wa Mkoa wa Dodoma, wakikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa na mabweni katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliozinduliwa Kibaigwa, mkoani Dodoma, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akipeana mkono na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program unaotekelezwa nchini kote kwa lengo la kuboresha miundombinu katika shule za sekondari zenye madarasa ya Kidato cha Tano na Sita.
Meneja wa Fedha wa Barrick nchini, Penina Kituku, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa, mkoani Dodoma.

***
Kampuni ya Barrick, inayofanya shughuli zake kwa ubia na Serikali kupitia Twiga Minerals, imeahidi kwamba kupitia programu yake ya Barrick-Twiga Future Forward Education Program itaendelea kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Sita kwenye sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu ya elimu, kuwezesha mazingira rafiki ya kusomea kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya taifa kwenye sekta hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa kitaifa wa mradi huo wa awamu ya pili, Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido, amesema kwamba baada ya makubaliano na Serikali mwaka 2023, kampuni hiyo ya Barrick ilikubali kutoa zaidi ya Tsh bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, mabweni na matundu ya vyoo katika shule za sekondari nchini kote.

“Mradi huu wa Barrick-Twiga Future Forward Education Program unalenga kuwekeza kwa Watanzania kwa kuweka mbele maslahi ya jamii kwa kutoa kipaumbele kwenye uboreshaji wa miundombinu kwenye sekta ya elimu ambayo itatengeneza mazingira bora zaidi ya kujifunza na kufundishia kwa pande zote, walimu na wanafunzi,” amesema Dkt. Ngido.

Aliongeza kwamba programu hiyo leo imezinduliwa kwa kujengwa madarasa sita na mabweni mawili ambayo yote kwa pamoja yana madawati na vitanda kwa ajili ya wanafunzi wa kike wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibaingwa, mkoani Dodoma.

Amesema kwamba mradi huo unalenga kujenga madarasa 1,090, majengo ya maliwato na vyoo 1,640 na mabweni 270 katika shule 161 nchini kote ili kusaidia kuwapatia malazi wanafunzi takribani 190,000 wa Kidato cha Tano na Sita.

Alifafanua kwamba kampuni hiyo ya Barrick ni mdau mkubwa kwenye sekta ya elimu baada ya hivi karibuni kuingia makubaliano na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na kutoa ufadhili wa Tsh bilioni 25 kwa ajili ya kufanya tafiti, uzalishaji wa wanataaluma na kuwezesha sekta ya madini kupata wataalamu wa kutosha wenye maarifa.

“Tangu mwaka 2020, baada ya Twiga Minerals kuundwa, Barrick imekuwa ikishirikiana na Serikali katika kuendeleza sekta ya madini ili iweze kuleta tija na maendeleo endelevu kwa nchi yetu,” amesema Dkt. Ngido.

Naye, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, amesema kwamba sekta ya elimu ina mchango mkubwa sana kwenye maendeleo ya taifa na ustawi wa watu wake, na ni muhimu miundombinu hiyo itunzwe na kulindwa kwa maslahi ya vizazi vijavyo.

“Nachukua nafasi hii kuwashukuru sana kampuni ya Barrick kwa fedha hizi za uwekezaji kwenye sekta ya elimu na nina imani yangu wataendelea kutusaidia baada ya awamu hii ya pili kukamilika, na ni kwa sababu mazungumzo ya awali aliyafungua Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, na mimi jukumu langu ni kuendeleza tu juhudi za Rais,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa Fedha wa Barrick, Penina Kituku, amesema kwamba uwekezaji huo kwenye sekta ya elimu ni muhimu kwa ajili ya kufungua milango ya elimu kwa Watanzania kwa kuboresha mazingira ya kusomea na kujifunzia.

“Tunajivunia kama Barrick kuwa kwenye safari hii ya maendeleo ya elimu hapa nchini na ni ahadi tutaendelea kushirikiana na Serikali katika kufanikisha watoto wa Kitanzania wanapata elimu katika mazingira bora na rafiki zaidi,” amesema Kituku.

Kampuni hiyo ya Barrick inaendesha migodi ya Bulyanhulu uliopo Kahama, Shinyanga, North Mara uliopo Tarime, Mara, na Buzwagi uliopo Kahama ambao upo kwenye hatua za mwisho za kufungwa.

Kampuni hiyo ya Barrick wiki hii ilitoa gawio la Serikali la Tsh 221,907,320,687 kwa Serikali ya Tanzania na kutunukiwa tuzo ya nafasi ya kwanza kwa kuongoza kutoa gawio kubwa mwaka huu kwa makampuni ambayo Serikali ina hisa, pamoja na kupata Tuzo ya Rais ya Mlipa Kodi Bora nchini.


Back To Top