Nilipoolewa, nilikuwa na matumaini makubwa ya kuanzisha familia yenye watoto na furaha.

Mimi na mume wangu tulikuwa na ndoto za muda mrefu kuhusu jinsi tutakavyolea watoto wetu na kujenga maisha ya pamoja yaliyojaa upendo. Hata hivyo, miezi iligeuka kuwa miaka bila kupata ujauzito.

Miaka miwili ya kwanza tulichukulia kama kawaida. Lakini kadri muda ulivyoendelea, maswali kutoka kwa watu wa karibu yalianza kuongezeka. 

Kila mara tulikuwa tukikumbushwa jambo ambalo tayari lilikuwa linatugusa moyoni kwa kina. Nilijikuta nikikumbwa na huzuni kila nilipoona familia nyingine zikifurahia watoto wao.

Tulianza kutafuta ushauri wa kitabibu na njia mbalimbali za kupata msaada. Tulipitia vipimo, tukapata ushauri tofauti, na kila mara tulijaribu kubaki na matumaini. 

Hata hivyo, miaka ilizidi kwenda bila mabadiliko. Baada ya miaka saba, tulikuwa karibu kukata tamaa kabisa. Kulikuwa na siku ambazo nilijitenga kabisa na watu. SOMA ZAIDI.

Kwa muda mrefu, maisha yangu yalibadilika kutokana na tatizo ambalo sikulielewa vizuri.

Kila usiku nilikuwa nikienda kulala nikiwa na matumaini ya kupumzika, lakini mara nyingi nilikuwa naamka katikati ya usiku nikiwa na hofu kubwa. Nilikuwa naota ndoto za kutisha zilizokuwa zikijirudia mara kwa mara.

Kadri muda ulivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.
Nilianza kukosa usingizi wa kutosha. Kila asubuhi nilikuwa nimechoka, kichwa kikiwa kizito na mwili hauna nguvu. Kazini nilianza kushindwa kuzingatia kazi zangu na mara nyingi nilifanya makosa ambayo hayakuwa ya kawaida kwangu.

Hali hiyo ilinifanya niwe na wasiwasi mkubwa.
Nilijaribu njia mbalimbali za kawaida ili kupata usingizi, lakini hazikusaidia kwa muda mrefu. Wakati mwingine nililala kwa muda mfupi tu kisha nikashtuka tena nikiwa na hofu isiyoelezeka. Familia yangu ilianza kugundua mabadiliko yangu.SOMA ZAIDI.

Kwa muda mrefu, ndoa yangu ilionekana kuwa ya kawaida kwa watu wa nje. Lakini ndani ya nyumba yetu, kulikuwa na changamoto ambazo zilikuwa zikiongezeka polepole. 

Mawasiliano yalipungua, migogoro midogo ikawa mikubwa, na kila mmoja wetu alianza kuishi kama mtu aliyechoka kihisia.

Siku moja niligundua kwamba mume wangu alikuwa amebadilika kabisa. Alianza kuwa mkimya zaidi, akitoka nyumbani mara kwa mara bila maelezo ya kutosha, na wakati mwingine hakutaka hata kuzungumza nami. Nilihisi kama kuna kitu kilikuwa kinaendelea ambacho sikukijua.

Baada ya wiki kadhaa, aliniambia jambo lililonishtua sana. Alisema alikuwa amefikiria kwa muda kuhusu kuondoka kwenye ndoa yetu. 

Maneno hayo yaliniumiza sana na kuniacha nikiwa sina uhakika wa mustakabali wa familia yangu. Nilijaribu kumwomba tuzungumze. SOMA ZAIDI.
Nilinunua kipande cha ardhi kwa jasho langu baada ya kufanya kazi kwa miaka mingi. Nilikuwa na ndoto ya kujenga nyumba ya familia yangu kwenye eneo hilo. 

Nilihifadhi nyaraka zote muhimu na niliamini hakuna mtu ambaye angeweza kuninyang’anya mali yangu.

Lakini siku moja jirani yangu alianza kudai kwamba sehemu ya ardhi hiyo ilikuwa yake.
Mwanzoni nilidhani ilikuwa ni kutokuelewana tu. 

Nilijaribu kukaa naye chini ili tuzungumze na kutafuta suluhisho la amani, lakini alikataa kusikiliza. Badala yake, alianza kuweka alama ndani ya eneo langu na kuwaambia watu kwamba mimi ndiye nilikuwa nimevamia ardhi yake.

Tatizo hilo liliendelea kwa zaidi ya miaka mitano.
Nilizunguka katika ofisi mbalimbali nikitafuta msaada. Nilitoa nyaraka nilizokuwa nazo na kueleza ukweli mara nyingi, lakini mgogoro haukuisha. Wakati mwingine nilihisi kama ningepoteza ardhi ambayo nilikuwa nimeitafuta kwa jasho langu.SOMA ZAIDI.

Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto ya kuifanya ikue na kuwa moja ya biashara kubwa katika eneo letu. Nilifanya kazi kwa bidii kila siku. 

Nilihakikisha wateja wanapata huduma nzuri na bidhaa zenye ubora. Ingawa biashara iliendelea kuwepo, mapato yake yalitosha tu kulipa gharama za kawaida.

Nilihitaji mteja mkubwa ambaye angebadilisha hali yangu ya kifedha, lakini sikufanikiwa kumpata. Miaka miwili ilipita bila mafanikio.

Nilituma mapendekezo kwa kampuni mbalimbali na kuhudhuria mikutano mingi ya biashara. Mara nyingi niliahidiwa kwamba ningepigiwa simu, lakini majibu hayakuwahi kufika.

Wakati mwingine nilikaribia kupata mkataba, lakini dakika za mwisho nafasi hiyo ilipewa mtu mwingine. Nilianza kukata tamaa. Nilifikiria hata kufunga biashara na kuanza shughuli nyingine. 

Nilihisi juhudi zangu zote zilikuwa zimepotea bure. Hata hivyo, ndani yangu bado kulikuwa na matumaini kwamba siku moja mambo yangenibadilika. SOMA ZAIDI.



Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA) imepokea ugeni wa viongozi wa kanda na wawakilishi kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) ukiongozwa na Katibu Mtendaji wa Mfuko huo Bw. Pradeep Kurukulasuriya uliolenga kutembelea na kujionea maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji huduma ya maji Tanga awamu ya tatu kupitia ufadhili wa Hatifungani ya Kijani ambapo UNCDF ni miongoni mwa wadau muhimu walioshiriki katika hatua za awali za kufanikisha mradi huo.

Katika ziara hiyo, Katibu Mtendaji na wageni walipokea taarifa ya mradi na mwenendo wa magawio kwa wawekezaji pamoja na kutembelea eneo la mradi na kujionea kasi ya utekelezaji wa shuguli mbalimbali zinazolenga kuongeza na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji ya uhakika kwa wakazi wa maeneo ya kihuduma ya Tanga UWASA unaotarajiwa kukamilika mapema mwezi Agosti, 2026.

Katibu Mtendaji pamoja na wageni walipata pia fursa ya kufanya kikao na sehemu ya wanufaika wa mradi wa Hatifungani katika Hospiali ya Jiji iliyopo kata ya Masiwani ambapo awali walikuwa wakipata changamoto katika kutoa huduma kutokana na adha ya upatikanaji wa huduma ya maji ya uhakika na kupitia mradi wa Hatifungani wameboreshewa miundombinu hivyo kuimarisha upatikanaji wa uhakika wa huduma ya majisafi.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Katibu Mtendaji wa UNCDF Bw. Pradeep Kurukulasuriya  ameipongeza Tanga UWASA kwa uthubutu huo na kwa maendeleo mazuri ya utekelezaji wa mradi lengwa sambamba na kuonesha nia ya kuongeza wigo wa kuendelea kushirikiana.


" Tunajivunia kuwa sehemu ya mchango katika kufanikisha Hatifungani ya Kijani ya Tanga na matarajio yetu ni kwamba mradi huu utaboresha maisha ya jamii na kupitia hili Tanga UWASA imedhihirisha kuwa inawezekana kuhamasisha uwekezaji ndani ya nchi kwani takriban asilimia 65 ya uwekezaji ulitoka kwa wawekezaji wa Kitanzania, na kwa kupitia mpango huu, tumedhihirisha kuwa mitaji ya ndani inaweza kuhamasishwa ili kufadhili miradi muhimu ya maendeleo na kwa sasa tunasoma mfano huu kwa karibu, tunatafuta kuelewa ni nini kilifanya kazi vizuri, changamoto zipi zilizojitokeza, na ni somo gani tunaweza kujifunza ili tuweze kuiga mafanikio ya Hatifungani ya Tanga si tu ndani ya Tanzania bali katika nchi nyingine pia", alisema Bw. Kurukulasuriya.

Awali kabla ya ziara hiyo, Katibu Mtendaji wa UNCDF na wageni wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Tanga UWASA, Eng. Salum Ngumbi walifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kutoa salamu na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Dadi Kolimba aliyetoa salamu za Mkoa kwa niaba ya Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Buriani Mkuu wa Mkoa wa Tanga






 


Serikali imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha ustawi wa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kwa kuratibu vikao shirikishi vya kijamii vinavyowapa elimu wazazi na walezi kuhusu wajibu wao wa malezi, matunzo na ulinzi wa watoto, hususan yatima na watoto wenye ulemavu. 

Hayo yameelezwa na  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, Bungeni jijini Dodoma leo, Juni 26, 2026, alipokuwa akijibu hoja mbalimbali za wabunge.

Waziri Dkt. Gwajima amewataka wazazi kutoruhusu migogoro yao ya kifamilia kuwa chanzo cha watoto kukosa malezi na kuishia kuishi mitaani katika mazingira hatarishi. 

"Wazazi niwasihi pale ambapo migogoro ya wazazi itakuwa imefikia hatua ya kushindwa kuwalea watoto kwa wakati, ni vyema mkakawapeleka watoto hao katika vituo vya ustawi wa jamii ili wapate malezi na ulinzi stahiki kwa muda, badala ya kuwaacha wakitelekezwa." amesema Dkt. Gwajima

Akijibu swali la msingi  la Mbunge wa Msalala, Mhe. Mabula Johnson Magangila Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema kuwa katika kipindi cha Julai 2025 hadi Mei 2026, jumla ya wazazi na walezi 469,634 walifikiwa kupitia elimu hiyo, wakiwemo wanaume 178,343 na wanawake 288,025, huku watu wenye ulemavu waliofikiwa wakiwa 3,266 lengo ni kuwajengea uwezo wazazi na walezi ili kuhakikisha watoto wanapata malezi bora na ulinzi stahiki ndani ya familia na jamii. 

"Utoaji wa elimu hii ni endelevu na unafanyika kupitia programu na kampeni mbalimbali za Serikali, ikiwemo kampeni ya "Familia Bora, Taifa Imara", inayolenga kuimarisha malezi bora, mshikamano wa familia na ustawi wa watoto nchini."amesema Mhe. Mahundi

Aidha Mhe. Mahundi amesisitiza kuwa ushiriki wa wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ni nguzo muhimu katika kuhakikisha watoto wote, hususan walio katika mazingira magumu, wanapata haki zao za msingi, ulinzi na fursa za kukua katika mazingira salama yatakayowajengea maisha bora ya baadaye.








Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, ametoa mafunzo kwa watoa huduma katika mnyororo wa thamani wa utalii ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027 ambayo Tanzania itaandaa kwa ushirikiano na Kenya na Uganda.

 


📌Imepunguza kodi kwenye vifaa vya Nishati Safi

📌Lengo ni kuwafikia wananchi wa aina zote.


Imeelezwa kuwa Serikali  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka dhamira  ya dhati  katika kuleta  mapinduzi ya matumizi ya Nishati  Safi ya kupikia yanayoongozwa na mkakati wa taifa wa Nishati Safi ya kupikia  kwa mwaka 2024-2034 unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia Nishati Safi ya kupikia ifikapo 2034.

Ameyasema hayo Naibu Waziri wa Nishati  Mhe. Salome Makamba alipokuwa akifunga kongamano la kuhamasisha na kuelimisha juu ya matumizi ya Nishati  safi ya kupikia Juni 25, 2026 lilokuwa likifanyika katika Ukumbi  wa East  Africa Commercial Logistic Center uliopo Jijini  Dar es Salam.

Mhe. Salome amesema kuwa ni muda wa kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na matumizi ya Nishati Safi  ya Kupikia ili kuweza kulinda afya pamoja na kutunza Mazingira hali itakayosaidia Nchi kuingia kwenye mapinduzi  makubwa ya Matumizi ya Nishati  Safi.

"Katika kuhakikisha tunafikia lengo la asilimia 80 mwaka 2034 Serikali  imefanya maamuzi mbalimbali  ya kisera  na kiutendaji  ikiwa ni pamoja na kuondoa au kupunguza kodi mbalimbali kwenye vifaa vya Nishati safi ili kupunguza gharama ya vifaa hivyo kwa mtumiaji wa mwisho" alieleza Mhe. Salome.

Naye Meneja wa Masoko kutoka Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Fredrick Kalinga ameeleza kuwa TANESCO  imejipanga kikamilifu katika kuhakikisha inawafikia wananchi wote kwa kuwaelimisha na kuwahamisisha juu ya matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kwa umeme ili kuweza kutengeneza uchumi endelevu kwa mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

"Tutaendelea kuhakikisha tunapata miradi ambayo itatuwezesha kusambaza majiko mengi zaidi kwa wananchi na wateja wetu ili wote tuweze kutumia Nishati Safi ya Kupikia kwa umeme ambayo sisi kama shirika tunazalisha na tunapenda wateja wetu waendelee kutumia"

Aliongeza kuwa tofauti na Nishati Safi ya kupikia kwa Umeme TANESCO  imeendelea kuimarika  kwa maana ya huduma kwa wateja kwa kuhakikisha wateja wote wanapata taarifa rasmi na sahihi wakati wote.

FCC YAONGEZA NGUVU KATIKA KUDHIBITI BIDHAA BANDIA

Serikali imetoa wito kwa wazalishaji, waingizaji bidhaa, wasambazaji, wafanyabiashara, vyombo vya habari, vyombo vya dola, mamlaka za forodha, Taasisi za umma, asasi mbalimbali pamoja na wananchi kwa ujumla kuendelea kushirikiana kwa karibu na Tume ya Ushindani (FCC) katika kubaini na kudhibiti bidhaa bandia.

Vilevile, ameipongeza FCC kwa kuendelea kuimarisha juhudi katika kukabiliana na changamoto ya bidhaa bandia na kulipa uzito unaostahili katika mipango ya baadaye ili kuendelea kuboresha mazingira ya biashara Nchi

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Sixtus Mapunda, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani (WACD) 2026.

Aidha, amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuunga mkono FCC kupitia maboresho ya sera, sheria na mifumo ili kuhakikisha masoko salama na ushindani wa haki ili kukabiliana na athari zake kwa afya za wananchi na uchumi wa taifa.

Mapunda pia amesema FCC inapaswa kupanua matumizi ya teknolojia katika uchunguzi, ufuatiliaji na udhibiti wa bidhaa bandia, hususan katika masoko ya kidijitali na mipaka ya nchi ili kuziba mianya inayotumiwa na wahalifu wa kiuchumi.

Akizungumzia kaulimbiu isemayo, “Linda Maisha na Masoko Dhidi ya Pombe, Vilainishi na Sigara Bandia,” amesema bidhaa bandia zina madhara kwa afya, hupunguza mapato ya Serikali na kudhoofisha biashara halali.

Naye, Kamishna wa Tume Bw. Said Tunda ambaye alimwakilisha Mwenyekiti wa FCC Dkt. Aggrey Mlimuka amesema kampeni za elimu kwa umma na mijadala ya kitaalamu zimeendelea kuongeza uelewa kuhusu athari za bidhaa bandia kwa afya, uchumi na maendeleo ya biashara halali nchini.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema maadhimisho yanalenga kuongeza uelewa wa umma kuhusu madhara ya bidhaa bandia na kuimarisha ushirikiano wa wadau.

 




Na Oscar Assenga, Pangani

SERIKALI imeanza rasmi kulipa fidia kwa wananchi 474 wa vijiji vya Mseko na Kigurusimba, Kata ya Masaika, Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kupisha utekelezaji wa mradi mkubwa wa kilimo cha miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari wenye thamani ya dola za Marekani milioni 350.

Hatua hiyo inaashiria mwanzo wa utekelezaji wa moja ya miradi mikubwa ya uwekezaji nchini inayotarajiwa kuzalisha maelfu ya ajira, kuongeza uzalishaji wa sukari na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Wilaya ya Pangani na taifa kwa ujumla.

Akizindua rasmi zoezi la ulipaji fidia, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Batilda Burian, alisema Serikali imeanza kuwalipa wananchi wote waliokamilisha taratibu zinazohitajika ili kuondoa vikwazo vya utekelezaji wa mradi huo.

Alisema zaidi ya wananchi 400 tayari wamekamilisha kusaini nyaraka zinazowaruhusu kupokea malipo yao, huku akibainisha kuwa waliojitokeza mapema watapewa kipaumbele na wengine wataendelea kuhudumiwa kadri watakavyokamilisha taratibu.

"Tunataka zoezi hili lifanyike kwa uwazi, haki na kwa wakati. Serikali imejipanga kuhakikisha kila mwananchi aliyestahili analipwa fidia yake bila kuchelewa," alisema Dkt. Burian.

Aidha, aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana na mamlaka zinazoratibu zoezi hilo ili kuhakikisha mradi unaanza kwa wakati na kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa jamii na taifa.

Awali, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), Remigius Reverius alisema malipo yanafanyika moja kwa moja kupitia akaunti za benki za wanufaika waliokamilisha uhakiki wa nyaraka zao.

Alisema zoezi hilo limeanza katika Kijiji cha Kigurusimba na litaendelea kwa awamu hadi wananchi wote waliothibitishwa kulipwa fidia watakapopokea stahiki zao.

"Tunawashukuru wananchi kwa ushirikiano wao. Serikali kupitia TISEZA imejipanga kuhakikisha kila aliyefanyiwa tathmini analipwa haki yake. Zoezi hili litaendelea hadi Juni 30 mwaka huu," alisema Reverius.

Aliongeza kuwa wataalamu wanaendelea kuhakiki taarifa za akaunti za benki pamoja na nyaraka mbalimbali ili kuhakikisha malipo yote yanafanyika kwa usahihi na bila dosari.

Mwakilishi wa wakulima wa Kigurusimba, Biligita Batilimeo, alisema kuanza kwa ulipaji wa fidia ni hatua muhimu inayoonyesha dhamira ya Serikali ya kutekeleza mradi huo huku ikilinda maslahi ya wananchi.

Alisema pamoja na fidia, mradi huo unatarajiwa kufungua fursa nyingi za ajira na biashara ambazo zitainua uchumi wa wakazi wa Pangani.

Naye mkazi wa Kigurusimba, Benard Mhagama, aliwasihi wananchi watakaopokea fidia kutumia fedha hizo kwa busara kwa kuwekeza katika shughuli za maendeleo zitakazowanufaisha wao na familia zao kwa muda mrefu.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Masaika, George Mariano, alisema uwekezaji huo utabadilisha sura ya uchumi wa Pangani kwa kuongeza ajira, kuchochea shughuli za biashara na kuongeza mapato ya Serikali.

Mradi huo wa kilimo cha miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari unatekelezwa na TISEZA katika eneo la ekari 22,000 kwa gharama ya dola za Marekani milioni 350, na unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi mikubwa itakayochangia kuongeza uzalishaji wa sukari nchini pamoja na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa wa Tanga.

Mwisho.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akizungumza katika Mkutano Mkuu wa 67 wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) uliofanyika leo Juni 25, 2026 katika hoteli ta Serena Jijini Dar es Salaam.
Kariakoo, 25 Juni, 2026

Kuelekea maadhimisho ya Tuzo za Rais kwa Walipakodi Bora, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kariakoo imewapongeza walipakodi kwa mchango wao mkubwa katika ulipaji wa kodi na uzingatiaji wa sheria za kodi, hali iliyowezesha baadhi yao kutambuliwa kama walipakodi bora wa mwaka.

Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na wawekezaji wa sekta ya viwanda ili kutatua changamoto zinazokwamisha uzalishaji na kuweka mazingira bora yatakayochochea ukuaji wa uchumi wa viwanda nchini.

Kauli hiyo imetolewa  na  Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe.Judith Kapinga mara baada ya kufanya ziara katika kiwanda kikubwa cha kuchakata na kuzalisha mafuta ya kula cha Mainland Group Agro Process Tanzania  jijini Dodoma, ambapo amejionea shughuli mbalimbali za uzalishaji na kiwango cha uwekezaji kilichofanyika katika kiwanda hicho.

Akizungumza baada ya kutembelea mitambo ya uzalishaji, Waziri Kapinga amesema   Serikali inatambua mchango mkubwa wa sekta binafsi katika kukuza uchumi, kuongeza ajira na kuimarisha mapato ya Taifa, hivyo itaendelea kuhakikisha changamoto zinazowakabili wawekezaji zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Amesema ameoneshwa kuvutiwa na uwekezaji mkubwa uliofanyika katika kiwanda hicho na kusisitiza kuwa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya ndani vina nafasi muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo ya Taifa pamoja na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Tunataka kuona mazao yanayozalishwa na wakulima wetu yanaongezewa thamani hapa hapa nchini. Hii ndiyo njia sahihi ya kuongeza tija kwa mkulima, mfanyabiashara, mwekezaji na Serikali kwa ujumla,” amesema Kapinga

Amebainisha kuwa licha ya Tanzania kuwa miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa mazao ya mafuta, bado uzalishaji wa mafuta ya kula haujakidhi mahitaji ya ndani, hali inayolazimu nchi kuagiza sehemu ya mafuta kutoka nje.

Kutokana na hali hiyo, amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo maboresho ya sera, sheria na mifumo ya kodi ili kuvutia uwekezaji zaidi katika viwanda vya mafuta ya kula na kuongeza uzalishaji wa ndani.

Waziri huyo amesema Serikali inalenga kuona nchi inafikia kujitosheleza kwa mafuta ya kula katika miaka ijayo kwa kuongeza uzalishaji wa malighafi na kuimarisha uwezo wa viwanda vilivyopo.

Katika mazungumzo yake na viongozi wa kiwanda hicho, ameelezwa kuwa changamoto kubwa inayokikabili ni upatikanaji mdogo wa malighafi, hususan mbegu za mazao ya mafuta, jambo linalofanya kiwanda kufanya kazi chini ya uwezo wake licha ya uwekezaji mkubwa uliowekwa.

Aidha, Serikali imeanza kushirikiana na Wizara ya Kilimo pamoja na taasisi zake kuweka mikakati ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya mafuta ili kuhakikisha viwanda vinapata malighafi za kutosha na kutumia uwezo wake kikamilifu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Jiaweli Chen, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na kutoa ushirikiano unaowezesha viwanda kufanya kazi kwa ufanisi na kuchangia maendeleo ya uchumi wa nchi.

Amesema kuwa sera na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali zimeongeza imani kwa wawekezaji, jambo ambalo limechangia ukuaji wa shughuli za uzalishaji na kuongeza ajira kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.

Bw. Chen pia ameishukuru Serikali kwa kutembelea mradi huo na kusikiliza changamoto zinazowakabili, akieleza kuwa hatua hiyo inaonesha utayari wa viongozi kushirikiana na sekta binafsi katika kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa shughuli za uzalishaji.

Hatahivyo amesema kuwa kiwanda hicho kitaendelea kushirikiana na Serikali katika kuongeza uzalishaji, kuimarisha ubora wa bidhaa na kuchangia jitihada za taifa za kukuza sekta ya viwanda, huku akieleza matumaini yake kuwa changamoto zilizowasilishwa zitapatiwa ufumbuzi kwa manufaa ya wawekezaji na wananchi kwa ujumla.