Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amewaagiza Makamishna wa Ardhi Wasaidizi katika mikoa yote nchini kufanya ukaguzi wa maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali kwa lengo la kubaini maeneo yasiyoendelezwa na kutoa taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe

Dkt. Akwilapo ametoa agizo hilo Septemba 18, 2026, mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika maeneo ya uwekezaji ya Kongani ya Viwanda ya KAMAKA pamoja na kiwanda cha Nondo cha Gain Company Limited kilichopo Mlandizi, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.

Amesema Wizara ya Ardhi, imebaini kuwepo kwa maeneo ambayo yalipewa wawekezaji kwa ahadi ya kuanzisha viwanda au shughuli nyingine za uzalishaji, lakini hayajaendelezwa kwa muda uliokubaliwa.

“Tuna taarifa kuna waliochukua maeneo wakasema watatengeneza viwanda lakini bado hawajafanya hivyo. Natoa maelekezo makamishna kufanya ukaguzi na kuwasilisha taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe kwa maeneo yasiyoendelezwa kadri ya mikataba waliyoingia,” amesema Dkt. Akwilapo.

Aidha, Waziri huyo amewataka wamiliki wote wa ardhi ambao hawazingatii masharti ya uendelezaji maeneo waliyopewa kuhakikisha wanayaendeleza kwa wakati, vinginevyo wizara itachukua hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

Amesisitiza kuwa, hatua hizo zitawahusu wawekezaji wazawa na wa kigeni, akieleza kuwa kwa wawekezaji wazawa hatua inaweza kujumuisha kubadilisha milki za ardhi walizopewa, huku kwa wawekezaji wa kigeni wizara ikishirikiana na taasisi husika, ikiwemo TISEZA, katika kushughulikia masuala ya umiliki na uwekezaji.

Dkt. Akwilapo amesema, hatua hiyo inalenga pia kujibu malalamiko kutoka kwa wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa ajili ya uwekezaji, lakini baadaye hayakuendelezwa.

Ameeleza kuwa, hali hiyo imekuwa ikisababisha wananchi kuhoji sababu za maeneo kutolewa kwa wawekezaji ambao hawajaanza shughuli za maendeleo kwa muda mrefu.

Awali Mhe Dkt Akwilapo alielezwa kuwa eneo la Kongani ya Viwanda Mlandizi wilayani Kibaha mkoa wa Pwani linakabiliwa na changamoto kadhaa kama vile upatikanaji wa maji na ubovu wa barabara hali waliyoieleza kuwa inayosababisha kero katika usafirishaji bidhaa na malighafi.

Hata hivyo, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wameeleza kuanza  kuchukua hatua za dharura kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi wa muda mfupi na mrefu

Ziara ya Dkt. Akwilapo katika Mkoa wa Pwani imelenga kujionea kwa karibu shughuli za uwekezaji na matumizi ya ardhi katika maeneo hayo, pamoja na kutathmini namna bora ya kuendeleza maeneo ya uwekezaji kwa kuzingatia mipango ya matumizi ya ardhi na maendeleo endelevu.

Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi za kutambua fursa na changamoto zinazohusiana na ardhi na uwekezaji, kwa lengo la kuimarisha matumizi bora ya ardhi, kuvutia uwekezaji na kuchochea maendeleo ya wananchi

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano la Sita la Jumuiya ya Taasisi za Mitaala Afrika (ACA), litakalofanyika Septemba 22 hadi 25, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.
TAASISI ya Tanzania Pathways Initiative (TPi) imeungana na jamii ya Kawe Ukwamani jijini Dar es Salaam katika zoezi la usafi wa mazingira, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha jiji linakuwa safi na salama.

 

Na Mwandishi Wetu.

Washiriki wa mafunzo kwa Waandishi wa Habari kutoka Wasafi Media wameeleza kuwa mada zilizotolewa katika mafunzo hayo zimewasaidia kutambua makosa yaliyokuwa yakijirudia katika utekelezaji wa majukumu yao na kuwapatia mwongozo wa kuboresha utendaji.

Wakizungumza wakati wa tathmini ya mafunzo hayo yaliyofanyika Septemba 17 na 18, 2026, katika Ofisi za Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) jijini Dar es Salaam, Gerald Hando, Aggai Kifumu na David Rwenyagira wameeleza kuwa mafunzo yamewaongezea uelewa kuhusu sheria, maadili na uzalendo katika uandishi wa habari.
Wamebainisha kuwa miongoni mwa changamoto zinazowakabili Waandishi wa Habari na wazalishaji wa maudhui ni shinikizo la kuongeza idadi ya wafuasi katika majukwaa ya kidijitali, kukidhi matakwa ya hadhira pana na kasi ya mabadiliko katika mazingira ya kidijitali kuwa kubwa kuliko maboresho ya baadhi ya sheria zinazoongoza shughuli zao.

Kwa mujibu wa washiriki hao, mazingira hayo yanaweza kusababisha baadhi ya Waandishi wa Habari kufanya kazi kwa mazoea au kujikuta wakifanya makosa ya kisheria na kimaadili bila kuwa na uelewa wa kutosha.
Wamesema mafunzo hayo yamewajenga kitaaluma, yamewafungua kutoka katika utendaji wa mazoea na kuwapatia mwongozo wa kufanya maamuzi sahihi katika majukumu yao ya kila siku.

Aidha, wameiomba JAB kuendelea kutoa mafunzo hayo kwa Waandishi wa Habari kutoka vyombo vingine, huku kipaumbele kikitolewa kwa wanaofanya kazi na kuzalisha maudhui kupitia majukwaa ya kidijitali, ambako changamoto za uzingatiaji wa sheria na maadili zimeendelea kujitokeza.
Wamesema kasi ya uzalishaji na usambazaji wa maudhui katika majukwaa hayo imeongeza uwezekano wa kutokea kwa makosa ya kisheria na kimaadili, hivyo elimu endelevu inahitajika ili kuimarisha weledi na uwajibikaji.

Mafunzo hayo yalihusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya uandishi wa habari na uzalendo, yakilenga kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari na watangazaji wa Wasafi Media kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, viwango vya taaluma na maslahi ya jamii.
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas imekabidhi mitungi ya gesi 600 na vifaa vyake kwa wananchi wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wanapata fursa ya kutumia nishati safi, salama na rafiki kwa mazingira.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza kuchukua tahadhari kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño, baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kueleza kuwa mvua hizo zinatarajiwa kuimarika katika maeneo mbalimbali nchini kuanzia wiki ya nne ya Septemba hadi Oktoba mwaka huu.




Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amewaonya wananchi wanaovamia maeneo kwa nguvu na kuunda vikosi vya ulinzi kwa ajili ya kulinda maeneo hayo, akisema Serikali haitavumilia vitendo hivyo na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Dkt. Akwilapo ametoa onyo hilo leo Sept 17, 2026 wakati akizungumza na wananchi katika Kliniki ya Ardhi iliyofanyika Kata ya Zingiziwa, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Amesema, wananchi hawapaswi kujichukulia sheria mkononi kwa kuvamia maeneo yanayomilikiwa na watu wengine na kuanzisha vikosi vya ulinzi kwa lengo la kuyadhibiti kwa nguvu.

“Serikali haitavumilia vitendo vya watu kujichukulia sheria kwa kuvamia maeneo ya wananchi wengine na kuunda vikosi vya ulinzi kwa lengo la kulinda maeneo hayo kwa nguvu,” amesema Dkt. Akwilapo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bw. Elihuruma Mabelya, amesema hadi sasa jumla ya hati miliki 545 zimetolewa kwa wananchi kupitia Kliniki hiyo ya Ardhi.

Mabelya ameeleza kuwa, timu ya wataalamu itaendelea kuwepo katika eneo hilo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za ardhi kwa urahisi na kwa wakati, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Wizara.

Baadhi ya wananchi, kupitia Diwani wa Kata hiyo, wameipongeza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kusogeza huduma za ardhi karibu na maeneo yao.

Wameielezea hatua hiyo kuwa  imewapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu pamoja na gharama kubwa walizokuwa wakitumia ili kufuata huduma hizo



 


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Mark Kihula, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Septemba 18, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa Taasisi hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.


Na Mwandishi Wetu - DODOMA


Wakala wa Vipimo Nchini (WMA), umeonya wafanyabiashara wanaotumia vipimo visivyo sahihi au kuuza bidhaa kwa vipimo visivyokidhi viwango kwamba wanakabiliwa na adhabu kali kwa mujibu wa sheria, ikiwemo faini na kifungo

Akizungumza na waandishi wa habari Septemba 18, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Mtumba jijini Dodoma, Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Bw. Alban Kihulla, amesema mtuhumiwa anayekubali kosa anaweza kutozwa faini ya Shilingi 100,000 hadi 20,000,000 kwa kosa moja, huku anayekataa kosa na kupatikana na hatia anapelekwa Mahakamani na kutozwa faini ya Shilingi laki tatu hadi milioni 50, au faini na kifungo kisichozidi miaka miwili.

Amesema kwa mkosaji wa mara kwa mara, faini inaweza kuwa kati ya Shilingi 500,000 na milioni 100 kwa kosa moja, hatua inayolenga kuhakikisha wafanyabiashara wanazingatia matumizi ya vipimo sahihi na kulinda haki za walaji.

Bw. Kihulla amewataka wakulima kuachana na matumizi ya magunia, madebe, makopo, mafungu na vipimo vingine visivyo rasmi katika biashara ya mazao, akisisitiza matumizi ya mizani kwa kuwa kilo ndiyo kipimo kinachotambulika katika biashara kote duniani.

Amesema matumizi ya vipimo visivyo rasmi yanaweza kusababisha kutokuwepo kwa usawa katika biashara, hivyo wananchi wanapaswa kudai kupimiwa bidhaa kwa mizani ili kuhakikisha wanapata kiasi halisi wanacholipia.

“Madebe, makopo, visado na mafungu siyo vipimo, wafanyabiashara tumieni mizani,” amesisitiza Kihulla, akieleza kuwa WMA inahakikisha kilo moja inakuwa kilo moja na vipimo vyote vinazingatia viwango vinavyotambulika.

Aidha, amesema WMA haisimamii vipimo vya bidhaa pekee, bali inahakikisha usahihi wa vipimo katika sekta mbalimbali kwa mujibu wa sheria za kitaifa, kikanda na kimataifa.

Bw. Kihulla ametoa mfano wa sekta ya afya, ambako vipimo vya uzito vimekua vikihakikiwa ili kuhakikisha mgonjwa anapata uzito halisi, jambo linalomsaidia daktari kuamua kiwango sahihi cha dawa kinacholingana na uzito wa mgonjwa.

Amewataka wananchi kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya matumizi ya vipimo visivyo sahihi kwa kutoa taarifa wanapobaini au kuhisi kuwa vipimo vinavyotumika au walivyopimiwa si sahihi kwa kuwasiliana na WMA kupitia namba 08001197 ili kutoa taarifa na kupata msaada na kuwezesha hatua stahiki kuchukuliwa.



Na Mwandishi Wetu, Kibaha.

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Mashariki, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Bohari ya Dawa (MSD), imetoa mafunzo maalum kwa Waganga Wafawidhi, Wafamasia, Wauguzi na Wakaguzi wa dawa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Manispaa ya Kibaha Mjini, September 18, 2026.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yusuf Masauni, amezindua na kukabidhi magari matano kwa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), hatua inayolenga kuimarisha shughuli za ukaguzi, ufuatiliaji na upimaji wa mazingira nchini.
Naitwa James kutoka Nyandarua. Kwa muda mrefu nilikuwa mfanyabiashara mdogo nikijitahidi kujenga maisha yangu kupitia duka la bidhaa za kila siku. Mwanzoni biashara yangu ilikuwa ikienda vizuri, lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Bidhaa zilianza kukwama sokoni, wateja wakapungua, na mara nyingine nilikuwa napata hasara bila kuelewa chanzo.
Nilijaribu kubadilisha bidhaa, kupunguza bei, na hata kubadili eneo la mauzo, lakini bado hali haikubadilika. Kila wiki ilikuwa kama napoteza zaidi kuliko ninavyopata.

Hali hiyo ilinifanya niingie kwenye msongo wa mawazo. Nilianza kujiuliza kama biashara siyo sehemu yangu kabisa. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu changamoto zangu. SOMA ZAIDI.

Fatuma Juma, mkazi wa Mombasa, alikuwa amezoea maisha ya upweke kwa karibu miaka mitatu baada ya mume wake kumwacha bila maelezo. Kila siku alijikuta akijiuliza ni wapi alikosea katika ndoa yao iliyodumu kwa miaka saba kabla ya matatizo kuanza.

Kwa mujibu wa Fatuma, mume wake alianza kubadilika ghafla. Alianza kuchelewa kurudi nyumbani, mawasiliano yakapungua na hatimaye akaondoka kabisa bila kuaga. Jaribio la kuwasiliana naye lilikuwa gumu kwani mara nyingi hakuwa akipokea simu zake.

“Nilibaki na watoto wawili na maswali mengi kichwani. Nilijaribu kuomba msamaha hata bila kujua kosa langu lakini hakutaka kunisikiliza,” alisema Fatuma. SOMA ZAIDI.
Mimi ni Ashura, natokea mkoani Dodoma, makao makuu ya nchi. Maisha yangu ya mapenzi yalikuwa ni simulizi la kusikitisha ambalo liliwafanya watu wanicheke badala ya kunionea huruma. 

Nilikuwa nafikisha miaka 40, lakini kila mwanaume aliyekuwa akitaka kunioa, mwishowe alikuwa anaghairi dakika za mwisho.

Nilivishwa pete za uchumba zaidi ya mara nne, lakini zote ziliishia kwa wanaume hao kutoweka au kupata matatizo yanayofanya ndoa isifungwe.

Watu kijijini kwetu walianza kusema nina nuksi, wengine wakidai nina jini mahaba anayenizuia kuolewa. Nilijisikia mnyonge, nikawa najifungia ndani nalia tu. Nilikuwa naogopa hata kwenda kwenye harusi za wenzangu maana kila mtu alikuwa ananitazama kwa dhihaka. 

Nilikuwa nishakata tamaa kabisa ya kuitwa “mke” au kubeba mwanangu mkononi. Niliona bora nijiue kuliko kuendelea na aibu hii ya kuzeekea nyumbani. SOMA ZAIDI.
KATIBU Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji wa Mkoa wa Njombe, Gumbo Mvanda, amesisitiza kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Halmashauri za mkoa huo katika kudhibiti ubora na usalama wa chakula na vipodozi kwa ajili ya kulinda afya za wananchi.

 


Na Shua Ndereka, Morogoro


Serikali mkoani Morogoro imeanza kuchukua hatua za kukabiliana na migogoro ya wakulima na wafugaji, huku Mkuu wa Mkoa huo, Queen Sendiga, akitangaza kipindi cha siku 60 cha kushughulikia changamoto hiyo na kutafuta suluhisho la kudumu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Sendiga amesema katika kipindi hicho Serikali itafanya utambuzi wa maeneo yenye migogoro, kusikiliza pande zote zinazohusika na kuhakikisha maamuzi yatakayofikiwa kwa lengo la kuleta amani na usalama yanatekelezwa.

Amesema moja ya hatua zitakazochukuliwa ni kufanya zoezi la utambuzi wa mifugo yote iliyopo mkoani humo, hatua inayolenga kupata takwimu sahihi kuhusu idadi ya mifugo, maeneo inayotumia pamoja na kusaidia katika kupanga matumizi bora ya ardhi.


Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, zoezi hilo linatarajiwa kuanza Septemba 18, 2026, na litaendelea kwa siku 60 huku Serikali imejipanga kuhakikisha migogoro ya wakulima na wafugaji inapata suluhisho la kudumu kwa kuzingatia kanuni na sheria zilizopo.

“Serikali mkoani Morogoro haitasita kumchukulia hatua mfugaji yeyote anayevunja sheria mahali popote, ikiwa ni pamoja na kuhuisha kamati za amani na usalama katika kata na mabaraza ya kutatua migogoro kwenye kata kama ilivyokuwa zamani,” amesema Sendiga.

Aidha, amesema viongozi watakaobainika kutumia nafasi zao kuchochea migogoro kati ya wakulima na wafugaji watachukuliwa hatua kali, akieleza kuwa vitendo hivyo vinaweza kuhatarisha amani na kuvuruga shughuli za uzalishaji.

Amewataka wananchi kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa sahihi na kufuata taratibu zilizowekwa katika utatuzi wa migogoro, badala ya kuchukua sheria mkononi.

 


Na Shua Ndereka, Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Queen Sendiga, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mussa Kilakala, Shirika la Reli Tanzania (TRC) pamoja na wataalamu wa Manispaa ya Morogoro kukutana mara moja ili kutafuta suluhisho la mafuriko yanayowaathiri wakazi wa Kata za Lukobe na Kihonda.

Sendiga ametoa agizo hilo akiwa katika ziara yake ya kwanza mkoani Morogoro tangu aanze majukumu hayo, ambapo ametembelea na kukagua baadhi ya maeneo yanayokumbwa mara kwa mara na mafuriko.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mafuriko hayo yanatokana na ujenzi wa tuta la reli ya SGR katika eneo la Kihonda Azimio.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Serikali kupitia wataalamu wake inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha usalama wa wananchi, ikiwemo kuchimba mifereji itakayosaidia kupitisha maji na kupunguza athari za mafuriko.

Hatua hizo pia zinakuja wakati Mkoa ukijiandaa kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua za El Niño zinazotarajiwa kunyesha mwaka huu.

Sendiga amewataka wananchi kutojenga makazi katika maeneo ambayo ni njia za maji, huku akiwataka wale wanaoishi pembezoni mwa mito, kwenye mikondo ya maji na maeneo ya mabondeni kuondoka katika maeneo hayo kwa kuwa ni hatarishi.

Kwa upande wao, wakazi wa Kata ya Lukobe, akiwemo Anateti Mkola, wamepongeza ziara ya Mkuu wa Mkoa na kuiomba Serikali kuchukua hatua zaidi, ikiwemo kufukuliwa kwa Mto Ngerengere na kuondolewa matope ili maji yaweze kupita kwa urahisi.

Mkola amesema ziara hiyo imewapa matumaini kutokana na hatua zinazochukuliwa mapema na Serikali katika kukabiliana na changamoto zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.

Kwa ujumla, hatua hizo zinaonyesha msisitizo wa Serikali mkoani Morogoro katika kushughulikia changamoto zinazogusa moja kwa moja usalama wa wananchi, matumizi ya ardhi, shughuli za uzalishaji pamoja na athari za mafuriko.

 

Mkuu wa Wilaya ya Tarime, (DC) Meja Edward Gowele, akizungumza na wakazi wa vijiji vya Matongo na Nyangoto kuhusu mradi huo wa TSF.
Mkurugenzi wa Shirika la Sheria na Haki za Binadamu la Tuwakombowe Paralegal (TPO) linalofanya shughuli zake katika wilaya za Tarime na Rorya, Bonny Matto (aliyevaa kofia ya kaki), akizungumza na wananchi katika eneo la uthamini huo. Kulia mbele aliyevaa kofia nyeusi ni Mkuu wa Wilaya, Meja Edward Gowele.
Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Francis Uhadi, akizungumza katika mkutano wa kuelimisha wakazi wa Matongo na Nyangoto kuhusu mradi wa ujenzi wa Bwawa la Kuhifadhi Mabaki ya Uchimbaji TSF.
Muonekano wa sehemu ya eneo linalofanyiwa uthamini kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa TSF.

**

#Wakazi zaidi ya 350 wafanyiwa uthamini kupisha ujenzi wa Bwawa la kuhifadhi taka sumu

Wananchi zaidi ya 350 wa vijiji vya Matongo na Nyangoto vilivyopo Kata ya Matongo Wilayani Tarime  Mkoani Mara wamefanyiwa uthamini kwa ajili ya kupisha ujenzi wa Bwawa la Kuhifadhi Taka -Sumu (Tailings Storage Facility – TSF) jipya la Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara.

 Akizungumza na waandishi wa habari Septemba 16,2026 wilayani Tarime, Mkuu wa Wilaya ya hiyo , Meja Edward Gowele (DC) amesema mwitikio wa wananchi ni mkubwa kwa ajili ya kazi ya kufanyiwa uthamini wa mali zao ili waweze kupisha ujenzi wa bwawa hilo na kufungua milango kwa ajili ya kulipwa fidia.

 “Mwitikio ni mkubwa na unaridhisha, hadi leo watu 350 wafamefanyiwa uthamini kazi hii ni kubwa kwa ajili ya watu watakaopisha ujenzi wa bwawa hili na shughuli hii inaendelea vizuri,”alisema Meja Edward Goweley.

 Alisema  uthamini unafanyika katika vijiji vya Matongo na Nyangoto vilivyopo Kata ya Matongo Wilayani, Tarime ili kuwezeshwa mgodi huo kuanza ujenzi wa bwawa hilo kwenye eneo hilo.

 Aliongeza kwamba kazi hiyo ilianza Agosti 24, mwaka huu na inatarajiwa kukamilika ndani ya siku 60, ambapo eneo lenye ukubwa wa ekari 419 linahitajika ili kujenga mradi huo mkubwa wa kuhifadhi taka sumu.

 Aidha, alisema kwamba katika kuhakikisha haki, uwazi, usawa, sheria na uwajibikaji vinazingatiwa kwa pande zote zinazohusika, Barrick imewashirikisha watetezi wa haki za binadamu kutoka mashirika ya ndani kama waangalizi wa uthamini huo.

 “Uwazi ni mkubwa na hata kuna watu wa haki za binadamu na vyombo vingine vya serikali, ikiwemo TAKUKURU ili kuhakikisha haki inatendeka kwa pande zote,” alisisitiza Meja Gowele.

 Wakati uthamini huo unaanza Agosti 24, mwaka huu, Mkuu wa Wilaya, Meja Gowele alitangaza katazo la serikali kwa wananchi kutofanya uendelezaji wowote katika eneo hilo ambalo lipo katika leseni ya mgodi huo wa Barrick North Mara.

 “Uzuri ni kwamba kazi hii ya uthamini imekuwa shirikishi kuanzia ngazi ya vijiji, kata hadi wilaya,” alisema Meja Gowele.

 Alitoa onyo kwa wakazi wa Tarime na vitongoji vyake hasa vikundi vya watu maarufu kama Tegesha wanaofanya mchezo wa kuweka miradi , nyumba na mazao sehemu ambayo zimefanyiwa uthamini kuacha mchezo huo mara moja.

 Onyo hilo la Mkuu wa Wilaya wa Tarime , Meja Gowele lilikwenda mbali mpaka kwa taasisi za serikali ambazo zinaendeleza baadhi ya miradi au shughuli kama vile Tanesco kwa kupeleka umeme kwenye nyumba ambazo zipo tayari kwenye uthamini kuondoa mara moja.

 Aidha, aliwataka wataalamu na wasimamizi wa mradi huo kutenda haki na kuhakikisha hakuna udanganyifu wowote unaofanyika hadi hatua ya malipo ya fidia.

 Pamoja na mambo Shughuli hiyo ya uthamini inatekelezwa na wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

 Kabla ya kuanza uthamini huo, Serikali ilishirikiana na Mgodi wa  Barrick North Mara kuendesha mikutano ya kuelewesha na kuhamasisha wananchi wa maeneo hayo kuhusu ujio wa mradi huo.
 
Mgodi wa  Barrick North Mara unaendeshwa na Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia Kampuni ya Twiga Minerals.

 Mradi wa ujenzi wa TSF ni muhimu katika upanuzi na uendelevu wa shughuli za mgodi huo kwa manufaa ya kijamii na kiuchumi. Kwa mujibu wa Barrick, utafiti wa kitaalamu unaonesha kwamba maisha ya Mgodi wa Dhahabu wa  Barrick North Mara yameongezeka kutoka mwaka 2030 hadi 2041. Unalenga kuendana na uendelevu wa mgodi huo baada ya tafiti za Barrick kurefusha maisha ya Mgodi wake.

 Mabwawa ya kuhifadhi Taka-Sumu (Tailings facilities), ambayo ni miundombinu mikubwa iliyosanifiwa kitaalamu kwa ajili ya kuhifadhi mabaki yanayotokana na uchakataji wa madini, ni miongoni mwa maeneo yenye hatari kubwa zaidi za kiusalama katika migodi.

 Barrick inatumia mfumo madhubuti wa viwango vya kimataifa wa usimamizi wa mabaki ya uchimbaji unaotanguliza usalama wa watu na mazingira hupewa kipaumbele katika kuchagua maeneo, usanifu, ufuatiliaji, uendeshaji na hatimaye kufungwa kwa miundombinu ya kuhifadhi mabaki ya uchimbaji.

 Kama ilivyo katika shughuli zake za uendelevu, Barrick imekuwa ikishirikiana kwa karibu na jamii zinazozunguka migodi yake ili kuhakikisha uwekezaji wao unaleta manufaa ya kudumu kwa jamii.

 Katika Mgodi wa Barrick North Mara nchini imewekeza takribani Dola za kimarekani 65  milioni kujenga mitambo miwili ya kisasa ya kutibu maji katika maeneo ya kuhifadhi mabaki ya uchimbaji.

 Kampuni ya Barrick imeendelea kuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wanaozunguka migodi yake na Taifa kwa ujumla, huku ikiongoza kwa ulipaji wa Gawio, mrahaba , kodi mablimbali na mapato yasiyotokana na kodi serikalini.

 Tangu Ubia wa Barrick na Twiga uanze mwaka 2019, Barrick imewekeza zaidi ya  Dola za Kimarekani bilioni 4.79 katika uchumi wa Tanzania, kwa mujibu wa takwimu zilizopo.

 Kampuni ya Barrick pia imekuwa ikitekeleza Sera ya Ushurikishwaji Watanzania katika mnyororo wa sekta ya madini (Local Content) kwa vitendo, ambapo inafanya ununuzi wa bidhaa za uzalishaji kwa asilimia zaidi ya 90 kutoka kwa wazabuni wa ndani, huku asilimia 96 ya wafanyakazi wake wakiwa Watanzania, wakiwemo wanaotoka maeneo ilipo migodi yake ya North Mara na Bulyanhulu.
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekutana na kufanya Mafunzo ya siku mbili yanayolenga kubadilishana uzoefu na kuimarisha uelewa kuhusu majukumu na utekelezaji wa Sheria katika sekta ya usafiri.