Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Winfred Mahundi, amewataka wazazi, walezi, walimu na jamii kuimarisha ushirikiano katika malezi na makuzi ya watoto, akisisitiza kuwa malezi bora ni msingi wa kujenga kizazi chenye maadili, nidhamu, uwajibikaji na uwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali katika jamii ya sasa.

Ameyasema hayo Septemba 19, 2026, jijini Arusha wakati wa Mahafali ya 12 ya Darasa la Saba na Mahafali ya 8 ya Kidato cha Nne katika Shule ya St. Monica Moshono.

Mhe. Mahundi amesema malezi ya mtoto hayapaswi kuangalia mafanikio ya kitaaluma pekee, bali yanapaswa kuzingatia makuzi na  ukuaji wa kimwili, kiroho, kitabia na kitaaluma, huku akisisitiza kuwa mafanikio ya mtoto yanahitaji ushirikiano wa familia, shule, jamii na Serikali.

Amesema wazazi na walezi wana wajibu wa kuwa karibu na watoto wao, kuwafuatilia, kuwasikiliza na kuwapatia mwongozo unaofaa ili kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo katika maisha.

“Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum inaendelea kutekeleza wajibu wake wa kushirikiana na jamii katika kujenga mazingira yenye ulinzi, haki, usalama na fursa kwa watoto, Aidha,  mabadiliko ya teknolojia yameleta fursa mbalimbali kwa watoto katika kujifunza na kupata taarifa, lakini pia yameibua changamoto zinazohitaji uangalizi wa karibu kutoka kwa wazazi, walezi na walimu hivyo wazazi na walezi wanapaswa kuwaongoza watoto katika matumizi sahihi ya teknolojia na kuwajengea uwezo wa kutambua taarifa na maudhui yenye manufaa na yale yanayoweza kuwa na madhara katika maisha yao, pamoja na kuhakikisha matumizi ya teknolojia hayaathiri maadili, nidhamu na mwenendo wa watoto.” Alisesema Naibu Waziri Mahundi 

Awali, akisoma taarifa ya shule hiyo, Mkuu wa shule hiyo Sr. Yuster Andrea Mbilinyi amesema shule imeendelea kuweka mkazo katika elimu, malezi na makuzi ya wanafunzi ili kuwajenga kuwa watu wenye nidhamu, maadili na uwajibikaji katika jamii.

 Sr. Yuster   ameongeza kwamba pamoja na kufanya vizuri kitaaluma, shule imeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na malezi kwa wanafunzi kwa kuweka miundombinu ya kujifunzia na mazingira ya shule 

Amesema ushirikiano wa wazazi na shule ni muhimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata malezi na matunzo yanayowawezesha kukua katika mazingira salama, huku akiwataka wazazi kuendelea kufuatilia maendeleo ya watoto wao na kushirikiana na walimu katika kutatua changamoto zinazowakabili.

Serikali itaendelea kushirikiana na jamii katika kuimarisha mazingira yanayolinda na kukuza ustawi wa watoto, ili kuhakikisha wanapata malezi, elimu na fursa zinazowawezesha kukua na kuwa raia wenye mchango katika maendeleo ya familia, jamii na Taifa.













 




Serikali kupitia Wizara ya Madini imesema inatambua mchango wa wachimbaji wadogo katika kukuza uchumi wa nchi, na itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha kupata huduma na fursa mbalimbali zinazohitajika katika shughuli zao.

Akifunga Maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Lindi kwa mwaka 2026, yaliyofanyika katika Wilaya ya Ruangwa leo Septemba 19, 2026, Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa, amesema Wizara itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wachimbaji wadogo ili kuongeza uzalishaji na tija katika sekta ya madini.

“Ninawaomba wachimbaji kutumia fursa zinazotolewa na Serikali na taasisi zake ili kuboresha shughuli zao na kuongeza tija katika uzalishaji,” amesema Dkt. Kiruswa.

Aidha, Dkt. Kiruswa amewahimiza wachimbaji wa madini kuzingatia Sheria ya Madini, sheria za mazingira, afya na usalama mahali pa kazi, pamoja na taratibu na miongozo inayotolewa na Serikali katika shughuli za uchimbaji.

Ametoa wito kwa taasisi zinazohusika, ikiwemo OSHA, NEMC, Tume ya Madini na Halmashauri, kuendelea kutoa elimu na kusimamia shughuli za uchimbaji ili kuhakikisha zinafanyika kwa usalama na kwa kuzingatia misingi ya uendelevu

Pia, Dkt. Kiruswa amesema maonesho hayo yamekuwa fursa kwa wananchi kujifunza na kutambua fursa zilizopo katika sekta ya madini, huku akiwahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuutazama Mkoa wa Lindi kama eneo lenye fursa za uwekezaji katika utafiti, uchimbaji, uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini.

“Mkoa wa Lindi unaendelea kujenga nafasi muhimu katika sekta ya madini nchini kutokana na uwepo wa madini mbalimbali. Kwa hiyo, ninawahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuendelea kuutazama Mkoa wa Lindi kama eneo lenye fursa za uwekezaji,” amesema Dkt. Kiruswa.

Sambamba na hayo, Dkt. Kiruswa amesema Serikali ina dhamira ya kuhakikisha Mkoa wa Lindi unakuwa na kiwanda cha kuchakata madini ya nikeli, pamoja na kuimarisha masoko ya madini ili kuwawezesha wachimbaji kupata masoko ya uhakika na kupunguza changamoto za uuzaji wa madini yao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Adam Malima, amesema mkoa huo unatambua mchango mkubwa wa sekta ya madini katika maendeleo ya Mkoa wa Lindi, na umejipanga kuendelea kuweka mazingira mazuri kwa wachimbaji na wawekezaji.

Naye Mwakilishi wa Wabunge wa Mkoa wa Lindi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Fadhili Ally Liwaka, ameiomba Serikali kuongezan viwanda vya uchenjuaji wa madini ya nikeli na shaba ili kuongeza thamani na tija ya madini hayo katika Mkoa wa Lindi.


Meneja Mauzo wa Taifa Gas Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Joseph Richard (kulia) akikabidhi cheti kwa mmoja wa washiriki wa mafunzo.
Meneja Mauzo wa Mkoa wa Dar es Salaam wa Taifa Gas, Enock Ngulwa , akitoa maelezo na ufafanuzi ya jinsi ya matumizi sahihi ya gesi kwenye semina ya siku moja kwa wawakilishi wa Umoja wa Ulinzi Shirikishi Tanzania (USHITA) kwa Mkoa wa Dar es Salaam
Meneja Mauzo wa Mkoa wa Dar es Salaam wa Taifa Gas, Enock Ngulwa , akitoa maelezo na ufafanuzi ya jinsi ya matumizi sahihi ya gesi kwenye semina ya siku moja kwa wawakilishi wa Umoja wa Ulinzi Shirikishi Tanzania (USHITA) kwa Mkoa wa Dar es Salaam
Washiriki wa mafunzo wakionesha vyeti vyao baada ya kukamilisha mafunzo ya matumizi sahihi ya gesi na udhibiti wa ujazaji haramu wa gesi.
Washiriki wa mafunzo wakionesha vyeti vyao baada ya kukamilisha mafunzo ya matumizi sahihi ya gesi na udhibiti wa ujazaji haramu wa gesi.
Washiriki wa mafunzo ya Taifa Gas na wawakilishi wa USHITA wakipiga picha ya pamoja baada ya kukamilisha mafunzo.
****

Afisa Mahusiano ya Jamii kutoka Barrick Bulyanhulu, Stella Kuyonga (katikati) akingalia zoezi la ufungaji jenereta katika kituo cha afya cha Bugarama ambalo limekabidhiwa na mgodi kusaidia kukabiliana na changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na kuathiri utoaji huduma kwa wananchi.

 MAKAMISHNA Wasaidizi Waandamizi wa Uhifadhi wanawake kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) wapo nchini Indonesia kushiriki mkutano wa mtandao wa wanawake maafisa waandamizi wa Polisi na vyombo vingine vya usalama unaofanyika nchini humo.

Makamishna hao wanaongozwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Rasilimali Watu na Utawala, Salma Chisonga, ambapo wanatarajiwa kushiriki katika majadiliano na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya ulinzi, uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.

Mkutano huo wa siku tano umewakutanisha wanawake kutoka vyombo mbalimbali vya usalama kutoka nchi tofauti duniani kwa lengo la kujadili fursa na changamoto zinazowakabili wanawake katika vyombo vya usalama pamoja na taasisi zinazolinda rasilimali za nchi.

Aidha, ushiriki wa makamishna hao unatarajiwa kutoa fursa kwa Tanzania kubadilishana uzoefu na mataifa mengine kuhusu namna ya kuimarisha ushiriki wa wanawake katika ulinzi, uhifadhi wa rasilimali na usimamizi wa maeneo ya utalii.

Mkutano huo pia unalenga kuimarisha ushirikiano na mitandao ya wanawake katika vyombo vya usalama duniani, huku ukitoa nafasi ya kujifunza mbinu na uzoefu mbalimbali katika kukabiliana na changamoto za kiusalama na uhifadhi.


 


MWENGE wa uhuru unatarajiwa kuzindua, kukagua, kutembelea na kuweka jiwe la msingi, kwenye miradi ya thamani ya shilingi bilioni 4.1 Wilayani Nzega Mkoani Tabora.

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Naitapwaki Tukai ameeleza hayo wakati akikabidhiwa mwenge wa uhuru na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Uyui Pendo Wella ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Tabora.

DC Tukai amesema ukiwa Wilayani Nzega, mwenge wa uhuru utakimbizwa umbali wa kilometa 223 na kupitia miradi ya thamani ya shilingi bilioni 4.1 ambapo Nzega DC thamani yake ni shilingi bilioni 1.2 na Nzega mji shilingi bilioni 2.9.

Amewapongeza na kuwashukuru wananchi wa maeneo ambayo yamepitiwa na mwenge kwani wamekuwa na hamasa kubwa na mwamko pindi ukipita na kujitokeza kwa wingi kwenye mkesha kata ya Nata.

"Tangu niteuliwe na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa DC Nzega miaka minne iliyopita sijawahi kuwaona pamoja wabunge wa majimbo ya Nzega vijijini na Bukene wakiwa pamoja ila leo nimewaona na nimefurahi mno," amesema DC Tukai.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2026 Wazo Michael Mwangonda amempongeza DC wa Nzega Naitapwaki Tukai kwa namna alivyosimamia maendeleo ya eneo hilo.

"Leo tumeingia Nzega DC kutoka Uyui na tangu tulivyoanza mradi wa kwanza hadi wa mwisho yote ni mizuri na kesho Nzega mji nasikia mambo ni mazuri huko hongera sana Mkuu wetu wa Wilaya," amesema Mwangonda.

Amewaasa wana Nzega waendelee kumpa ushirikiano wa kutosha mkuu wao wa Wilaya ambaye anamwakilisha Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwenye eneo hilo.

Mkimbiza mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2026 kutoka mkoa wa Manyara, Inyasi Amsi amempongeza DC Naitapwaki Tukai kwa namna anavyosimamia maendeleo na ushirikiano kwa wana Nzega.

"Hakika Mheshimiwa DC unatuheshimisha wana Manyara kwani watu wa hapa Nzega wanakupenda kutokana na namna unavyowaongoza na kuwasimamia," amesema Inyasi.

 MWENGE wa uhuru umezindua mradi wa Nkuba hotel (Pride of Nzega) iliyopo mjini Nzega Mkoani Tabora wenye thamani ya shilingi 274,000,000.

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Mhe Naitapwaki Tukai akizungumza mbele ya kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2026 Wazo Michael Mwang'onda amesema wanampongeza mmiliki wa hoteli hiyo Ndongo Mabula kwa uwekezaji huo.

Amesema mradi huo ni ishara ya sekta binafsi kuunga mkono juhudi za Serikali kukuza uchumi, kuvutia wageni, kuongeza matumizi yenye tija ya ardhi na kutoa ajira kwa wananchi.

"Mradi huu utaboresha mazingira ya upatikanaji wa huduma za hoteli na ukumbi wa kisasa wa mji wa Nzega, wageni watapata sehemu ya kupumzika na halmashauri ya mji itapata kodi," amesema DC Tukai.

Edina Eliberatus akisoma taarifa ya ujenzi kwa niaba ya mmiliki wa hoteli hiyo Ndongo Mabula amesema ujenzi wa mradi ulianza rasmi Machi mosi mwaka 2025 na kukamilika Septemba 4 mwaka 2026.

Amesema gharama za mradi huo wa hoteli ni shilingi 24,000,000 unahusisha vyumba 12 vya kulala wageni na ukumbi mmoja wa mikutano.

"Tunaishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais DKt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira bora ya uwekezaji kwa sekta binafsi," amesema Mabula.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2026 Wazo Michael Mwang'onda amempongeza mwekezaji wa hoteli hiyo Ndongo Mabula kwa ujenzi wa mradi huo.

Mwang'onda amesema mwekezaji amejenga bila kuwekewa mikwamo hivyo Serikali ya Wilaya ya Nzega inastahili pongezi kubwa.

"Mwekezaji anapotaka kuwekeza mradi asiwekewe mikwamo na vikwazo wapeni kipaumbele kwani hata Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza sekta binafsi kupewa kipaumbele hivyo Nzega hongereni sana," amesema


 MKUU wa Wilaya ya Ilala, Edward Jonas Mpogolo, amezindua rasmi Kampeni ya “Safisha Mazingira, Linda Afya” katika Kata ya Kisutu, huku akimpongeza Diwani wa kata hiyo, Tousif Mohammedali Bhojani, kwa kuwa diwani wa kwanza wilayani humo kuanzisha kampeni hiyo.

Mbali na uzinduzi huo, Diwani Bhojani alimkabidhi Mkuu wa Wilaya vifaa mbalimbali vya usafi vilivyotolewa na wadau kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za usafi na utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wengine, ya kuhakikisha Jiji la Dar es Salaam linakuwa safi.

Uzinduzi huo ulifanyika katika Soko la Baba na Malishe, Kisutu, na kuendelea katika mitaa mbalimbali ya kata hiyo, ukiongozwa na DC Mpogolo akishirikiana na wananchi na wadau wa maendeleo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mpogolo alimpongeza Diwani Bhojani kwa kuwa diwani wa kwanza katika Jimbo na Wilaya ya Ilala kuzindua kampeni hiyo.

Alisema Wilaya ya Ilala ina jumla ya kata 36 na kwamba Kata ya Kisutu, chini ya uongozi wa Diwani Bhojani, imeonesha dhamira ya dhati ya kutekeleza kwa vitendo kampeni hiyo muhimu ya usafi.

Mpogolo alisema wilaya imeandaa mikakati ya kuzishindanisha kata na mitaa yote ya maeneo ya katikati ya jiji (CBD) katika suala la usafi, huku kata na mitaa itakayofanya vizuri ikitarajiwa kupewa zawadi.

“Katika kuhamasisha suala la usafi, tumeandaa zawadi ambazo zitatolewa kwa kata na mitaa ya mjini, yaani CBD, itakayofanya vizuri katika usafi. Lengo ni kuhamasisha kampeni hii ya usafi katika wilaya yetu. Kisutu mmeonesha mfano kwa kuwa kata ya kwanza kuzindua kampeni hii muhimu,” alisema Mpogolo.

Aidha, alisema Wilaya ya Ilala itaendelea kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuhakikisha usafi unakuwa sehemu ya utamaduni wa wananchi, kuanzia ngazi ya mtu mmoja, familia hadi jamii nzima.

“Tunaenda kutekeleza sheria zetu ndogo kwa wananchi watakaokiuka sheria za usafi. Wale watakaovunja sheria tutawakamata na kuwafikisha katika Mahakama ya Jiji. Akipatikana na hatia atalipishwa faini au kifungo,” alisema.

Aliwataka wananchi wa Kata ya Kisutu na Wilaya ya Ilala kwa ujumla kuhakikisha wanazingatia kanuni za usafi, ikiwemo kuwa na vifaa vya kuhifadhia taka na kufuata sheria na taratibu zinazohusu usafi wa mazingira.

Kwa upande wake, Diwani Bhojani alisema kata hiyo imejipanga kikamilifu kuhakikisha inadumisha usafi, ikieleza kuwa usafi hautakuwa shughuli ya Jumamosi pekee au wakati wa kampeni, bali utakuwa sehemu ya maisha ya kila siku.

“Hivi karibuni Rais Dk. Samia alitamka kuwa Jiji ni chafu. Tamko lile lilikuwa ni ujumbe kwetu. Tuko tayari kutekeleza kwa vitendo agizo hilo,” alisema.

Alisema tangu Rais alipotoa kauli hiyo, Kata ya Kisutu imeendelea kufanya usafi na kuwataka wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kushiriki katika kampeni hiyo.






 MWENGE wa Uhuru umezindua mradi wa upanuzi wa mfumo wa kusafisha na kutibu maji unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Nzega Mjini (NUWASA), huku ukielezwa kuwa utasaidia kuimarisha upatikanaji wa maji kwa wananchi.


Mradi huo umezinduliwa leo, Septemba 19, 2026, na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai, mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2026, Wazo Michael Mwang'onda.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Tukai amesema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama, sambamba na kupunguza magonjwa ya mlipuko yanayoweza kusababishwa na ukosefu wa maji.

Amesema mradi huo pia umewawezesha wananchi wa Mji wa Nzega kupata huduma ya maji kulingana na mahitaji na uwezo wao wa kulipia.

“Wananchi wa Mji wa Nzega wanatumia maji kadiri wanavyohitaji kupitia mradi huu. Wananchi wanaweza kulipia kiasi wanachohitaji; wakitaka maji ya Shilingi 3,000 wanapata na wakitaka ya Shilingi 100,000 pia wanapata,” amesema.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi huo, Mhandisi Salum Yasin Ikinda, amesema mradi umetekelezwa kwa kipindi cha miezi 36 na umejengwa na kampuni ya FABEC Investment Ltd.

Amesema mradi huo umetekelezwa kwa gharama ya Shilingi 620,103,998.30, ambapo hadi sasa mkandarasi ameshalipwa Shilingi 290 milioni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026, Wazo Michael Mwang'onda, ameipongeza Nzega kwa utekelezaji na ubora wa mradi huo.

“Kutokana na ubora wa mradi huu, hapa panapaswa kulindwa kwa wivu mkubwa ili kuhakikisha unakuwa endelevu kwa maslahi mapana ya jamii ya eneo hili,” amesema Mwang'onda.


 MBUNGE wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. CPA Subira Khamisi Mgalu, ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bagamoyo kwa ubunifu na mipango madhubuti inayolenga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.


Mhe. Mgalu aliyasema hayo wakati wa ziara yake katika Ofisi za TRA Bagamoyo, ambapo alipata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na Meneja wa TRA Bagamoyo, Mariam Omari.

Katika mazungumzo hayo, walijadili masuala mbalimbali yanayohusu ongezeko la mapato, ukusanyaji wa kodi, mikakati ya kuvuka malengo ya ukusanyaji pamoja na umuhimu wa kuendelea kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi kuhusu ulipaji wa kodi.

Mhe. Mgalu ameipongeza TRA Bagamoyo kwa kazi inayofanyika katika kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unaendelea kuimarika, akisema hatua hizo ni muhimu katika kuchochea maendeleo ya Taifa na Jimbo la Bagamoyo.

Aidha, ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa TRA na kuhamasisha wananchi kupitia mikutano yake mbalimbali kuhusu umuhimu wa kulipa kodi kwa wakati ili kuwezesha Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo.

Mbunge huyo pia amempongeza Meneja wa TRA Bagamoyo, Mariam Omari, kwa moyo wa kujitolea na kushirikiana na jamii, hususan katika kuchangia uboreshaji wa miundombinu katika Shule ya Msingi Ukuni.

Amesema ushiriki wa taasisi na watendaji katika shughuli za kijamii ni mfano mzuri wa ushirikiano kati ya Serikali, taasisi na wananchi, hivyo unapaswa kuungwa mkono na kuendelezwa.

Mhe. Mgalu ameahidi kuwa balozi wa kuhamasisha ushirikiano kati ya wananchi, taasisi na wadau mbalimbali katika kuhakikisha juhudi za maendeleo ya Bagamoyo zinaendelea kuimarika.

Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya viongozi, taasisi na wananchi ni muhimu katika kuongeza uelewa kuhusu ulipaji wa kodi, kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kuchochea kasi ya maendeleo.


 


Na WMA  - DODOMA

Wazazi jijini Dodoma wamesema elimu ya vipimo inayotolewa kupitia Klabu za Vipimo katika shule za msingi imeanza kuleta mabadiliko ndani ya familia, baada ya watoto waliopatiwa mafunzo na Wakala wa Vipimo (WMA) kuanza kuwafundisha wazazi wao namna ya kutambua vipimo sahihi na kujilinda dhidi ya upunjaji katika manunuzi.

Wazazi wameyasema hayo  Septemba 18,2026  wakati wa mahafari ya wanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Mtemi Mazengo jijini Dodoma ambapo  wanafunzi wa klabu ya vipimo walikuwa wakitoa elimu ya vipimo kwa wazazi na watu wengine mbalimbali waliohudhuria akiwemo Mgeni Rasmi.

Mzazi wa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mtemi Mazengo, Bertha Paulo Chipaga, amesema mtoto wake, Gloria Elisha Enock, amekuwa akimsaidia kuelewa matumizi sahihi ya mizani ya chakula, mita ya maji na vipimo vingine, jambo ambalo limempa uelewa na kujiamini zaidi kama mlaji.

Bi.Chipaga amesema awali hakuwa na uelewa mpana kuhusu namna ya kutambua kama kipimo kinachotumika katika biashara ni sahihi, lakini tangu mtoto wake ajiunge na Klabu ya Vipimo amekuwa akipata elimu hiyo nyumbani na sasa anaelewa umuhimu wa kuhakikisha bidhaa anayonunua inalingana na kiasi cha fedha anacholipa.

"Hatua hiyo inaonesha kuwa elimu inayotolewa kwa watoto haiishii shuleni, bali inasambaa hadi kwenye familia na jamii, hivyo akawataka wazazi wengine kutumia fursa hiyo kuwaelimisha watoto wao kuhusu haki za mlaji na matumizi sahihi ya vipimo."amesema Bi.Chipaga

Akizungumza kuhusu umuhimu wa kuwaandaa watoto na elimu hiyo, mkazi wa Makao Mapya jijini Dodoma, Peter Daudi Mponzi, amesema mafunzo ya vipimo kwa wanafunzi ni uwekezaji muhimu kwa jamii kwa sababu yanawajengea uwezo wa kutambua mizani na vipimo visivyo sahihi wanapokuwa katika mazingira ya biashara.

Amesema mtoto anayeelewa vipimo anaweza kwenda dukani na kuangalia kama mzani unaotumika umehakikiwa, hivyo kupunguza uwezekano wa yeye au familia yake kupunjwa na wakati huo huo kueneza elimu hiyo kwa watu wengine.

Mponzi amesema kuanzia elimu hiyo katika umri mdogo kunaweza kujenga kizazi chenye uelewa mpana wa masuala ya vipimo na haki za walaji, kwa kuwa watoto wanakuwa na nafasi ya kutumia maarifa hayo katika maisha yao ya kila siku.

 "Watoto wanapotoka shuleni na kwenda majumbani, dukani na katika maeneo mengine ya jamii, wanakuwa sehemu ya mnyororo wa elimu unaoweza kuwafikia wazazi, ndugu na wananchi wengine, hivyo kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi."amesema

Mwanafunzi wa Klabu ya Vipimo katika Shule ya Msingi Mtemi Mazengo, Gloria Elisha Enock, amesema WMA imewajengea uwezo wa kuelewa maana na umuhimu wa vipimo pamoja na jukumu la Wakala la kumlinda mlaji.

Amesema wamefundishwa kuwa WMA huhakiki vipimo mbalimbali, ikiwemo mizani, mita za maji na umeme, pamoja na bidhaa zilizofungashwa, huku mlaji akitakiwa kuangalia alama ya WMA kwenye mizani ili kuhakikisha kipimo  hicho kimehakikiwa na kinafanya kazi kwa usahihi.

Kwa upande wake, mwanafunzi mwenzake, Venosa Michael Simba, amesema elimu hiyo imemsaidia kubadilika kutoka kuwa mtoto anayekwenda dukani bila kuzingatia usahihi wa vipimo hadi kuwa mfuatiliaji na mtoa elimu kwa jamii.

Amesema baada ya kupata mafunzo hayo aligundua hata nyumbani kwao kuwa mita ya maji ilikuwa haijahakikiwa na akaweza kutoa elimu kwa watu waliokuwa hawajui umuhimu wa kuhakiki vipimo.

 "kabla ya kupata elimu hiyo alikuwa akienda dukani bila kuangalia chochote, lakini sasa anaelewa kuwa mlaji ana wajibu wa kuhakikisha anapata kiasi sahihi cha bidhaa anayolipia."amesema

Kwa ujumla, Klabu za Vipimo za WMA zimeanza kuwa darasa la vitendo la kuwaandaa watoto kuwa mabalozi wa ulinzi wa mlaji, huku elimu hiyo ikitoka shuleni na kuingia moja kwa moja katika familia na jamii.

Mpango huo unaongeza uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya vipimo sahihi, unasaidia kujenga utamaduni wa kuhoji na kuthibitisha vipimo vinavyotumika katika biashara na, kwa muda mrefu, unaweka msingi wa kizazi kinachothamini uadilifu, usawa na uwazi katika shughuli za kiuchumi.

Na Alex Sonna, Dodoma

WAZAZI jijini Dodoma wamesema elimu ya vipimo inayotolewa kupitia Klabu za Vipimo katika shule za msingi imeanza kuleta mabadiliko ndani ya familia, baada ya watoto waliopatiwa mafunzo na Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) kuanza kuwafundisha wazazi wao namna ya kutambua vipimo sahihi na kujilinda dhidi ya upunjaji katika manunuzi.

Wazazi wameyasema hayo  Septemba 18,2026  wakati wa mahafari ya wanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Mtemi Mazengo jijini Dodoma ambapo  wanafunzi wa klabu ya vipimo walikuwa wakitoa elimu ya vipimo kwa wazazi na watu wengine mbalimbali waliohudhuria akiwemo Mgeni Rasmi.

Mzazi wa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mtemi Mazengo, Bertha Paulo Chipaga, amesema mtoto wake, Gloria Elisha Enock, amekuwa akimsaidia kuelewa matumizi sahihi ya mizani ya chakula, mita ya maji na vipimo vingine, jambo ambalo limempa uelewa na kujiamini zaidi kama mlaji.

Bi.Chipaga amesema awali hakuwa na uelewa mpana kuhusu namna ya kutambua kama kipimo kinachotumika katika biashara ni sahihi, lakini tangu mtoto wake ajiunge na Klabu ya Vipimo amekuwa akipata elimu hiyo nyumbani na sasa anaelewa umuhimu wa kuhakikisha bidhaa anayonunua inalingana na kiasi cha fedha anacholipa.

"Hatua hiyo inaonesha kuwa elimu inayotolewa kwa watoto haiishii shuleni, bali inasambaa hadi kwenye familia na jamii, hivyo akawataka wazazi wengine kutumia fursa hiyo kuwaelimisha watoto wao kuhusu haki za mlaji na matumizi sahihi ya vipimo."amesema Bi.Chipaga

Akizungumza kuhusu umuhimu wa kuwaandaa watoto na elimu hiyo, mkazi wa Makao Mapya jijini Dodoma, Peter Daudi Mponzi, amesema mafunzo ya vipimo kwa wanafunzi ni uwekezaji muhimu kwa jamii kwa sababu yanawajengea uwezo wa kutambua mizani na vipimo visivyo sahihi wanapokuwa katika mazingira ya biashara.

Amesema mtoto anayeelewa vipimo anaweza kwenda dukani na kuangalia kama mzani unaotumika umehakikiwa, hivyo kupunguza uwezekano wa yeye au familia yake kupunjwa na wakati huo huo kueneza elimu hiyo kwa watu wengine.

Mponzi amesema kuanzia elimu hiyo katika umri mdogo kunaweza kujenga kizazi chenye uelewa mpana wa masuala ya vipimo na haki za walaji, kwa kuwa watoto wanakuwa na nafasi ya kutumia maarifa hayo katika maisha yao ya kila siku.

 "Watoto wanapotoka shuleni na kwenda majumbani, dukani na katika maeneo mengine ya jamii, wanakuwa sehemu ya mnyororo wa elimu unaoweza kuwafikia wazazi, ndugu na wananchi wengine, hivyo kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi."amesema

Mwanafunzi wa Klabu ya Vipimo katika Shule ya Msingi Mtemi Mazengo, Gloria Elisha Enock, amesema WMA imewajengea uwezo wa kuelewa maana na umuhimu wa vipimo pamoja na jukumu la Wakala la kumlinda mlaji.

Amesema wamefundishwa kuwa WMA huhakiki vipimo mbalimbali, ikiwemo mizani, mita za maji na umeme, pamoja na bidhaa zilizofungashwa, huku mlaji akitakiwa kuangalia alama ya WMA kwenye mizani ili kuhakikisha kipimo  hicho kimehakikiwa na kinafanya kazi kwa usahihi.

Kwa upande wake, mwanafunzi mwenzake, Venosa Michael Simba, amesema elimu hiyo imemsaidia kubadilika kutoka kuwa mtoto anayekwenda dukani bila kuzingatia usahihi wa vipimo hadi kuwa mfuatiliaji na mtoa elimu kwa jamii.

Amesema baada ya kupata mafunzo hayo aligundua hata nyumbani kwao kuwa mita ya maji ilikuwa haijahakikiwa na akaweza kutoa elimu kwa watu waliokuwa hawajui umuhimu wa kuhakiki vipimo.

 "kabla ya kupata elimu hiyo alikuwa akienda dukani bila kuangalia chochote, lakini sasa anaelewa kuwa mlaji ana wajibu wa kuhakikisha anapata kiasi sahihi cha bidhaa anayolipia."amesema

Kwa ujumla, Klabu za Vipimo za WMA zimeanza kuwa darasa la vitendo la kuwaandaa watoto kuwa mabalozi wa ulinzi wa mlaji, huku elimu hiyo ikitoka shuleni na kuingia moja kwa moja katika familia na jamii.

Mpango huo unaongeza uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya vipimo sahihi, unasaidia kujenga utamaduni wa kuhoji na kuthibitisha vipimo vinavyotumika katika biashara na, kwa muda mrefu, unaweka msingi wa kizazi kinachothamini uadilifu, usawa na uwazi katika shughuli za kiuchumi.