Wamiliki wa shule zisizo za serikali nchini wamezitaka mamlaka za serikali za mitaa kuacha kutoza ushuru na tozo ambazo wanadai tayari zilisamehewa na Serikali Kuu, wakisema hali hiyo inaongeza gharama za uendeshaji na kuhatarisha utoaji wa huduma za elimu.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, viongozi wa Shirikisho la Wamiliki na Mameneja wa Shule na Vyuo Visivyo vya Serikali Tanzania (TAMONGSCO) wamesema shule zisizo za serikali zinakabiliwa na zaidi ya tozo na makato mbalimbali, ikiwemo ushuru wa huduma unaotozwa na halmashauri kwa taasisi zinazotoa huduma, ada za mitihani, leseni za mabango ya shule pamoja na michango ya michezo na taaluma.

Mtendaji Mkuu wa TAMONGSCO, Benjamin Nkonya, alisema pamoja na mzigo wa makusanyo hayo, kinachowasumbua zaidi ni namna baadhi ya halmashauri zinavyotekeleza ukusanyaji wake.

Alidai kuwa katika baadhi ya matukio, askari mgambo huingia shuleni kufuatilia madeni ya ushuru na tozo, jambo ambalo kwa mujibu wake huathiri mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

“Tunachohoji si suala la kulipa wajibu wa kisheria pekee, bali ni matumizi ya nguvu katika ukusanyaji wa fedha hizo na kuendelea kudai baadhi ya tozo ambazo tunaamini tayari ziliondolewa au kutolewa mwongozo wake na Serikali Kuu,” alisema Nkonya.

Amesema shirikisho hilo limekuwa na mahusiano mazuri na mamlaka ya Mapato nchini TRA wakati wote wanapohitaji ushirikiano wao tofauti na halmashauri ambao wamekuwa wakitumia ubabe kukusanya tozo hizo wakati taasisi hizo zikiwa zimesamehewa ushuru huo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAMONGSCO Kanda ya Kaskazini, Leonard Mao, Malalamiko hayo yameelekezwa zaidi kwa baadhi ya halmashauri, hususan, ambazo zinadaiwa kuendelea kukusanya ushuru na tozo mbalimbali kutoka kwa shule zisizo za serikali licha ya kuwepo kwa maelekezo ya serikali kuhusu baadhi ya makusanyo hayo.

“Tunaamini mwongozo wa wazi utasaidia kuondoa migogoro isiyo ya lazima na kuweka mazingira bora ya uwekezaji katika sekta ya elimu,” alisema Mao.

Naye Wakili Mshauri wa TAMONGSCO, Pascal Temba, alisema iwapo kuna ushuru au tozo zinazodaiwa baada ya kufutwa na Serikali Kuu, mamlaka husika zinapaswa kuweka wazi msingi wa kisheria unaoruhusu makusanyo hayo.

Kutokana na hali hiyo, TAMONGSCO imesema tayari imewasilisha barua kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikiomba ufafanuzi wa kisheria kuhusu mamlaka ya halmashauri kuendelea kukusanya baadhi ya ushuru na tozo zinazolalamikiwa.

Shirikisho hilo linaeleza kuwa majibu yatakayopatikana yatasaidia kutoa mwongozo kwa wadau wote na kuondoa mkanganyiko uliopo.

Wakati wakisubiri ufafanuzi huo, wamiliki wa shule zisizo za serikali wanaonya kuwa endapo changamoto hiyo haitapatiwa ufumbuzi, gharama za uendeshaji wa shule zinaweza kuongezeka na hatimaye kuathiri upatikanaji wa elimu kwa wazazi na wanafunzi.

Kwa wadau wa elimu, mjadala huu unafungua swali muhimu: Je, mazingira yaliyopo yanasaidia kukuza uwekezaji katika sekta ya elimu au yanaongeza mzigo ambao mwisho wake hubebwa na mzazi na mwanafunzi.


Siku gari langu lilipoibiwa, nilihisi kama sehemu ya maisha yangu imeondoka pamoja nalo. Nilikuwa nimelifanyia kazi kwa miaka mingi. Halikuwa tu chombo cha usafiri, bali pia lilikuwa sehemu muhimu ya shughuli zangu za kila siku.

Ndiyo maana nilishtuka sana nilipoamka asubuhi na kugundua kwamba halikuwepo pale nilipoliacha usiku. Kwa kweli nilichanganyikiwa. 

Nilianza kulitafuta mara moja. Niliwapigia simu marafiki, majirani, na watu wengine ambao wangeweza kuwa na taarifa.

Kadri saa zilivyopita bila habari yoyote, matumaini yangu yalianza kupungua. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba sikuwa na wazo lolote la mahali lilipokuwa.

Baadhi ya watu waliniambia nikubali kwamba huenda nisingeliona tena. Wengine waliniambia magari mengi yaliyoibiwa hayapatikani kirahisi. Nilianza kuamini kwamba nilikuwa nimelipoteza milele. SOMA ZAIDI HAPA.
Kwa miezi mingi, nilikuwa nikikabiliwa na tatizo ambalo lilikuwa linaninyima amani. Kila baada ya wiki chache, mali zangu zilikuwa zinapotea kwa njia ya ajabu. 

Wakati mwingine zilikuwa fedha, wakati mwingine vifaa vya kazi, na mara kadhaa mazao kutoka shambani mwangu.

Mwanzoni nilidhani ni bahati mbaya. Lakini kadri matukio yalivyozidi kujirudia, niligundua wazi kuwa kulikuwa na mtu aliyekuwa akiniibia kwa makusudi. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba sikuwa na ushahidi wa kumtambua.

Nilijaribu kila njia. Niliimarisha ulinzi, nikawa makini zaidi, na hata kuwaomba watu wa karibu wanisaidie kufuatilia kinachoendelea. Lakini kila mara mwizi huyo alionekana kutoweka bila kuacha alama yoyote. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilianza kuamini kwamba bahati ilikuwa imenikimbia. Haikuwa kwamba sikujitahidi. Kinyume chake, nilikuwa nafanya kila niwezalo kufanikisha malengo yangu.

Nilipanga biashara, niliomba kazi, na nilitumia muda mwingi kujenga maisha bora kwa familia yangu. Lakini jambo la kushangaza lilikuwa moja. Kila nilipokaribia kufanikiwa, kitu kilitokea dakika za mwisho na kuharibu kila kitu.

Nilipata wateja wakubwa waliobadilisha mawazo yao ghafla. Nilipata nafasi za kazi ambazo zilionekana kuwa zangu, lakini mwishowe zikaenda kwa mtu mwingine. Hata baadhi ya mipango ya kifamilia ilivunjika wakati nilikuwa tayari nimeanza kusherehekea mafanikio. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi kama ndoa yangu ilikuwa ikiteleza kutoka mikononi mwangu. Mimi na mume wangu tulikuwa tumeishi pamoja kwa miaka kadhaa. SOMA ZAIDI/TAZAMA VIDEO.

Tulikuwa tumepitia changamoto nyingi pamoja na kujenga familia ambayo nilikuwa naiona kama baraka kubwa maishani mwangu. Lakini mambo yalianza kubadilika.

Mume wangu alianza kuwa tofauti. Alitumia muda mwingi nje ya nyumba, mawasiliano yetu yakapungua, na ukaribu tuliokuwa nao ukawa kama umepotea ghafla.

Mwanzoni nilijaribu kupuuza hali ile. Nilijiambia labda alikuwa na presha za kazi au changamoto nyingine za maisha. Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kugundua kuwa kulikuwa na jambo kubwa zaidi nyuma ya mabadiliko yale.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kusikia uvumi kwamba kulikuwa na mwanamke mwingine aliyekuwa karibu sana na maisha ya mume wangu. Kila niliposikia taarifa hizo, moyo wangu ulivunjika zaidi.

Kulikuwa na usiku nililia peke yangu. Nilikuwa nikijiuliza kama ndoa yangu ilikuwa imefika mwisho. Wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa karibu kupoteza kila kitu nilichokuwa nimekijenga kwa miaka mingi.
Nilipoanza biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa kuliko uwezo wangu wa wakati huo. Nilikuwa na duka dogo tu, lakini ndani yangu niliona siku moja nikiwa na matawi mengine, nikihudumia wateja wengi zaidi, na kuifanya biashara yangu ikue hadi kiwango kikubwa.SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO

Lakini mwanzo haukuwa rahisi. Miezi ya kwanza ilikuwa ya mapambano. Wateja walikuwa wachache, faida ilikuwa ndogo, na mara nyingine nililazimika kutumia akiba yangu ili kuendeleza biashara. Watu wengine waliniona na kuniambia wazi kwamba nilikuwa napoteza muda wangu.

Kwa kweli maneno yale yaliniumiza. Kilichoniumiza zaidi ni kuona baadhi ya biashara nilizoanza nazo wakati mmoja zikikua haraka zaidi huku yangu ikionekana kusimama sehemu moja. Nilianza kujiuliza kama nilichagua njia sahihi.

Lakini sikukata tamaa. Niliendelea kujituma kila siku. Nilijifunza namna ya kuwahudumia wateja vizuri zaidi, niliboresha bidhaa zangu, na kuhakikisha kila anayenunua anarudi tena.

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajia kuadhimisha Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu kuanzia Juni 9 hadi 11, 2026, katika Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere, huku Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akitarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Maadhimisho hayo yatakayowakutanisha watafiti, wabunifu, wanafunzi, sekta binafsi, taasisi za umma na wadau wa maendeleo, yanalenga kuonesha mchango wa utafiti na ubunifu katika kuharakisha maendeleo ya taifa na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Utafiti, Profesa Nelson Boniface, alisema maadhimisho ya mwaka huu yataongozwa na kaulimbiu isemayo: "Kutumia Utajiri wa Madini wa Tanzania katika Kukuza Nishati Jadidifu, Mageuzi ya Kidijitali na Usalama wa Jamii."

Alisema kaulimbiu hiyo imechaguliwa kutokana na umuhimu wa madini katika maendeleo ya teknolojia za kisasa ikiwemo Akili Mnemba (AI), vituo vya kuhifadhi taarifa (Data Centres), magari ya umeme na nishati jadidifu.

“Tunataka kuonesha namna Tanzania inaweza kutumia rasilimali zake za madini kuchochea mageuzi ya kidijitali, kuimarisha usalama wa nishati na kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” alisema Profesa Boniface.

Aliongeza kuwa maadhimisho hayo yatahusisha maonesho ya tafiti na ubunifu, mawasilisho ya kitaaluma, makongamano pamoja na majadiliano ya ushirikiano wa kimkakati yatakayowawezesha washiriki kubadilishana maarifa na kujenga mitandao ya kitaaluma na kibiashara.

Kwa mujibu wa UDSM, maadhimisho hayo yatatoa nafasi kwa watafiti na wabunifu kuonesha suluhisho mbalimbali za kisayansi na kiteknolojia zinazolenga kukabiliana na changamoto za maendeleo nchini katika sekta za madini, nishati, kilimo, afya na uchumi wa kidijitali.

Profesa Boniface alisema chuo kinaendelea kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuunganisha taaluma, ubunifu na maendeleo ya taifa kwa kuwafikia wananchi, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo.

"Utafiti na ubunifu ni msingi wa maendeleo endelevu. Tunawaalika Watanzania wote kushiriki katika Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu UDSM 2026 ili kujionea kazi na mafanikio ya watafiti na wabunifu wetu," alisema.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amesema dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa ni fursa muhimu ya kukuza sekta ya viwanda, kuongeza thamani ya malighafi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza katika kikao cha mawaziri kilichofanyika jijini Istanbul nchini Uturuki, Juni 5, 2026, kilichobeba mada ya Mageuzi ya Kijani ya Viwanda: Mtazamo wa taka sifuri na urejeshaji bidhaa, Kapinga amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta ya viwanda huku ikisisitiza matumizi bora ya rasilimali na uhifadhi wa mazingira. Ameeleza kuwa dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa inatoa fursa kwa nchi zinazoendelea kupitia matumizi endelevu ya malighafi, kupunguza upotevu baada ya mavuno, kupunguza uzalishaji wa taka na kuongeza thamani ya bidhaa zinazotengenezwa viwandani. Kapinga amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kuunganisha masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sera na mipango ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ufanisi wa nishati na teknolojia rafiki kwa mazingira. Aidha, amesisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi ya kijani yanategemea uwekezaji wa kutosha, upatikanaji wa teknolojia za kisasa pamoja na ushirikiano madhubuti kati ya serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo. Amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuendeleza viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali, kudhibiti taka na kuvutia uwekezaji huku akiwakaribisha wafanyabiashara kuwekeza nchini kwa lengo la kujenga uchumi imara na shindani.

Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Uturuki kupitia taasisi ya Zero Waste Foundation inayosimamiwa na Mwenza wa Rais wa Uturuki Bibi Emine Erdoğan na umeleta pamoja washiriki zaidi ya 3,000 kutoka nchi zote duniani, pamoja na taasisi za kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Mataifa, Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu na Shirika la Maendeleo na Biashara la Umoja wa Mataifa (UNCTAD).

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu ametoa onyo kali kwa watu wanaojihusisha na udanganyifu na uchakachuaji wa taarifa katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kusisitiza itaendelea kuchukua hatua ili kuhakikisha misingi ya uadilifu na uwazi inazingatiwa ipasavyo.

Bangu,ametoa onyo hilo baada ya kufanya kikao kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro, kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Amesema mfumo huo unaendelea kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya uadilifu na uwazi, huku WRRB ikiendelea kushirikiana na mamlaka za mikoa, wilaya na halmashauri kusimamia utekelezaji wake.

“Moja ambalo nataka kuliweka wazi kwa Watanzania ni kwamba mfumo huu unafanya kazi kwa kuzingatia uadilifu. Kuna maeneo mengi mfumo unafanya vizuri, lakini tumeanza kuona baadhi ya watu wakiingiza taarifa zisizo sahihi kwenye mfumo kwa lengo la kujipatia fedha. Nataka nitoe onyo kali kwao kwamba tunasimamia mfumo huu kwa karibu na hatua stahiki zitachukuliwa,” amesema Bangu.

Ameeleza kuwa WRRB imeweka utaratibu wa kufanya uhakiki wa bidhaa zilizopo maghalani kabla ya kutolewa kwa katalogi za mauzo ili kuhakikisha wanunuzi wanapata taarifa sahihi kuhusu kiasi cha mazao yaliyopo.

Bangu pia amewahamasisha wakulima wa ufuta kuendelea kuuza mazao yao kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kupata masoko yenye ushindani na kuongeza kipato chao.

Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha mazingira ya biashara ya mazao kupitia mfumo huo, jambo linalowezesha wakulima kunufaika zaidi na jasho lao.

“Wilaya ya Malinyi imeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mfumo huu. Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto, lakini sasa tumeridhishwa na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wakulima wananufaika na mapato yao yanaongezeka,” amesema.

Katika hatua nyingine, WRRB imekabidhi msaada wa vifaa vya usafi na vyakula kwa Hospitali ya Wilaya ya Malinyi ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za uwajibikaji kwa jamii.

Akikabidhi msaada huo katika Wodi ya Wazazi ya hospitali hiyo, Bangu amesema WRRB itaendelea kushirikiana na jamii sambamba na kutekeleza majukumu yake ya kusimamia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala nchini.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Dk. Julius Nyasongo, aliyepokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Wakili Sebastian Waryuba, ameishukuru WRRB kwa msaada huo akisema utasaidia kuboresha ustawi wa akina mama wanaopata huduma hospitalini hapo.

“Msaada huu utakuwa na mchango mkubwa kwa akina mama wanaopata huduma katika hospitali yetu. Tunawashukuru WRRB kwa kuendelea kushirikiana na sekta ya afya na jamii kwa ujumla,” amesema Dk. Nyasongo.

     
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb) amelitaja Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa ni nguzo kuu ya kulinda afya za walaji na kuchochea ustawi wa viwanda nchini.

 



Na Oscar Assenga,TANGA


SERIKALI imekipongeza Chama cha Washauri wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TACOGA) kwa kuendelea kuandaa mafunzo yanayolenga kuimarisha uwezo wa kitaaluma na kiutendaji wa washauri wa wanafunzi, wanasihi na viongozi wa serikali za wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali nchini.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Tanga,Mkurugezi wa Maendeleo ya Jinsia kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Badru Abdnur alisema mafunzo hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kuwajengea washiriki uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanafunzi katika taasisi za elimu ya juu.

Alisema katika kipindi cha mafunzo hayo, washiriki walipata nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao, pamoja na kupata mbinu mpya zitakazowawezesha kuboresha huduma wanazozitoa kwa wanafunzi.

"Nawapongeza viongozi wa TACOGA kwa ubunifu na maono yao ya kuhakikisha mafunzo haya yanafanyika kila mwaka. Bila uongozi imara, kuandaa mafunzo ya aina hii si jambo rahisi," alisema.

Aliongeza kuwa hatua hiyo inaonesha utambuzi wa umuhimu wa maendeleo endelevu ya kitaaluma kwa watendaji wanaohusika na huduma za wanafunzi pamoja na viongozi wa serikali za wanafunzi.

Badru alibainisha kuwa mada zilizowasilishwa zimegusa maeneo nyeti yanayoathiri ustawi na maendeleo ya wanafunzi, ikiwemo afya ya akili, maadili, matumizi ya teknolojia na uongozi bora.

Alisema dunia ya sasa inabadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia, hali inayowafanya vijana kuwa miongoni mwa makundi yanayoathirika zaidi na mabadiliko hayo.

"Vijana wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo afya ya akili, matumizi mabaya ya teknolojia, matumizi ya dawa za kulevya na mmomonyoko wa maadili. Hivyo, kuna haja ya kuendelea kuwajengea uwezo na kuwapa mwongozo sahihi ili wawe raia wema na wazalendo," alisema.

Aidha, aliwakumbusha washiriki kuwa serikali na jamii kwa ujumla zinategemea sana mchango wa washauri na wanasihi katika kuwajenga wanafunzi. 

Alisema wazazi na walezi wana matumaini makubwa kwa maafisa hao kwa kuwa vijana wengi wanaojiunga na vyuo vikuu bado wana umri mdogo na wanahitaji mwongozo, uangalizi na malezi ya karibu.

Kwa mujibu wake, kutokana na nafasi hiyo muhimu, TACOGA ina wajibu mkubwa wa kuchangia mageuzi ya maendeleo ya taifa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Alitoa wito kwa chama hicho kuwekeza zaidi katika mifumo ya kiteknolojia ili kuendana na mazingira ya sasa ya kidijitali. Alisema ni muhimu kuanzisha mifumo ya kimtandao na programu za simu zitakazowezesha wanafunzi kupata huduma za ushauri kwa haraka na kwa urahisi bila kuathiri muda wao wa masomo.

Pia aliwataka kuendelea kujenga uwezo wa wanachama wao kupitia mafunzo endelevu ya saikolojia, unasihi na mbinu mpya za utoaji wa huduma ili kuwawezesha washauri na wanasihi kutoa suluhisho stahiki na la kisasa kwa changamoto zinazowakabili wanafunzi.

Vilevile, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha viashiria vya kupima matokeo ya kazi zinazofanywa na TACOGA kwa kuwekeza katika tafiti ndogo ndogo za kutathmini kama huduma zinazotolewa zinaleta matokeo chanya katika ufaulu wa wanafunzi na maendeleo yao ya kijamii na kitaaluma.

Mgeni rasmi huyo pia alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya ofisi za washauri wa wanafunzi na madawati ya jinsia pamoja na vitengo vya kuzuia ukatili wa kijinsia katika vyuo vikuu. Alisema kuna muunganiko mkubwa wa majukumu kati ya taasisi hizo, hivyo ushirikiano ukiimarishwa utasaidia kupunguza mzigo wa kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wanafunzi.

Alisema maarifa na stadi zilizopatikana kupitia mafunzo hayo zinatarajiwa kuwafanya washiriki kuwa mabalozi wa mabadiliko katika taasisi zao na kuchangia kufikiwa kwa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TACOGA, Sophia Nchimbi, alisema chama hicho kimeendelea kuandaa mafunzo hayo kwa lengo la kuwawezesha maafisa wa ofisi za washauri wa wanafunzi katika vyuo vikuu kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi.

Alisema washiriki walipata mafunzo yaliyohusu nidhamu chanya, usimamizi wa tabia, unasihi, matumizi salama ya mitandao ya kijamii, afya ya akili, malezi ya wanafunzi, uongozi bora na usimamizi wa madawati ya jinsia katika vyuo vikuu.

"Mafunzo haya yanatusaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbalimbali tunazokutana nazo katika maeneo yetu ya kazi. Maarifa tunayopata yanatupa uwezo wa kuwahudumia wanafunzi kwa ufanisi zaidi," alisema Nchimbi.

Alisema mada kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii zimewawezesha washiriki kuelewa namna bora ya kuwaelekeza wanafunzi kutumia teknolojia kwa manufaa ya elimu badala ya matumizi yasiyofaa.

Nchimbi alisema pia washiriki walipata elimu kuhusu namna ya kusimamia madawati ya jinsia ili kuhakikisha wanafunzi wanaokumbana na changamoto mbalimbali wanapata msaada kwa wakati na kwa usahihi.

Aliongeza kuwa TACOGA imekuwa ikifanikiwa kuendesha mafunzo hayo kutokana na ushirikiano mkubwa wa wanachama na wadau mbalimbali wanaochangia maendeleo ya huduma za ushauri kwa wanafunzi.

Jumla ya washiriki 94 kutoka vyuo mbalimbali nchini walishiriki mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Tanga.







Kwa zaidi ya miezi sita, nilikuwa nikikabiliana na tatizo ambalo lilikuwa linaninyima Amani. Mazao yangu yalikuwa yanipotea usiku. Mwanzoni nilidhani ni wanyama wa porini waliokuwa wanaingia shambani. SOMA ZAIDI/TAZAMA VIDEO.

Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kugundua kuwa baadhi ya mazao yalikuwa yanavunwa kwa utaratibu ambao haukuonyesha kazi ya wanyama. Mtu alikuwa anaiba. Kwa kweli iliniumiza sana.

Nilikuwa nimewekeza muda, nguvu, na fedha nyingi kwenye shamba lile. Kila nilipoenda kuvuna, niligundua sehemu ya mazao imepungua. Hasara iliongezeka mwezi baada ya mwezi. Nilijaribu kulinda shamba.

Niliweka walinzi mara kadhaa, nikabadilisha ratiba za kutembelea shamba, na hata kuwaomba majirani wanisaidie kufuatilia hali ya eneo hilo. 
Kwa muda mrefu, nilikuwa mfanyakazi ambaye kila mtu alijua kuwa mwenye Bidii. Nilifika kazini mapema, nilitimiza majukumu yangu kwa umakini, na nilijitahidi kuhakikisha kila kazi niliyopewa inakamilika kwa wakati. Niliamini kwamba juhudi zangu zingetambuliwa siku moja.SOMAZAIDI'TAZAMA VIDEO HAPA.

Lakini miaka ilipita bila mabadiliko. Kila mara nafasi mpya zilipofunguka, nilikuwa na matumaini kwamba safari hii ningechaguliwa. Badala yake, niliona wafanyakazi wengine wakipandishwa vyeo huku mimi nikibaki pale pale.

Kwa kweli iliniumiza Sana. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba baadhi ya watu waliokuwa wakitangulia walikuwa wamefika kazini muda mfupi kuliko mimi. Wakati mwingine nilijikuta nikijiuliza kama kazi yangu ilikuwa inaonekana au kama juhudi zangu zilikuwa zinapotea bure.

Polepole nilianza kupoteza hamasa. Nilikuwa bado nafanya kazi zangu, lakini moyo wangu haukuwa na furaha kama zamani. Nilihisi kama nilikuwa nimekwama katika sehemu moja huku miaka ikiendelea kusonga mbele.

Kulikuwa na kipindi nilifikiria kuacha Kazi. Lakini nilijua kwamba kufanya hivyo kwa hasira kungeweza kunigharimu zaidi. Nilihitaji sababu mpya ya kuendelea kupambana.
Kwa miaka mingi, nilitamani kupata mtu ambaye angenipenda kwa dhati na kunikubali jinsi nilivyo. Lakini safari yangu ya mapenzi haikuwa rahisi. SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO HAPA.

Kila nilipoingia kwenye uhusiano, nilikuwa na matumaini makubwa. Niliamini kwamba safari hii mambo yangekuwa tofauti. Cha kusikitisha ni kwamba mara nyingi mahusiano yale yaliishia kwenye maumivu, ahadi zilizovunjwa, na kuvunjika moyo.

Kwa kweli nilichoka. hKadri miaka ilivyopita, nilianza kupoteza imani katika mapenzi. Niliona marafiki zangu wakipata wenza, wakifunga ndoa, na kujenga familia, huku mimi nikiendelea kuanza upya kila baada ya kuvunjika moyo.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kuamini kuwa labda sikuwa nimekusudiwa kupata upendo wa kweli. Nilijitahidi kuonekana mwenye furaha mbele za watu, lakini moyoni nilikuwa na huzuni.

Wakati mwingine nilijiuliza kama kuna mtu ambaye angeniona wa thamani na kutaka kubaki maishani mwangu kwa dhati. Kulikuwa na kipindi nilikata tamaa kabisa.

Niliacha kutafuta mahusiano na kuamua kujikita kwenye shughuli zangu za kila siku. Nilijaribu kujikubali na kuendelea na maisha, ingawa sehemu ya moyo wangu bado ilitamani kupata mtu sahihi.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo sikuweza kukumbuka siku ambayo sikuwa nikikohoa. Mwanzoni nilidhani ilikuwa mafua ya kawaida ambayo yangepita yenyewe baada ya muda mfupi.TAZAMA VIDEO HAPA/ SOMA ZAIDI.

Lakini wiki zilipita, kisha miezi. Kikohozi kilibaki, na mara kwa mara nilikuwa nahisi maumivu kwenye kifua yaliyokuwa yananifanya niwe na wasiwasi. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Wakati mwingine niliamka usiku nikikohoa. Nilipozungumza kwa muda mrefu, koo lilichoka haraka. Watu wa karibu walikuwa wakiniuliza kwa nini sikuwa napona, lakini hata mimi sikuwa na jibu.

Kilichoniumiza zaidi ni kutokuwa na uhakika. Kila nilipohisi nafuu kidogo, dalili zilikuwa zinarudi tena. Nilianza kuogopa kwamba huenda kulikuwa na tatizo kubwa kuliko nilivyokuwa nikifikiria.

Hatimaye niliamua kutafuta msaada wa kitabibu. Nilifanyiwa uchunguzi na kupewa ushauri wa wataalamu wa afya. Pia nilielekezwa kuhusu umuhimu wa kufuata matibabu, kupumzika vya kutosha, na kuepuka vitu ambavyo vingesababisha hali yangu kuwa mbaya zaidi.

Lakini safari ya kupona haikuwa rahisi. Kulikuwa na siku nilihisi nimekata tamaa kwa sababu mabadiliko hayakuja haraka kama nilivyotarajia.
Kwa miaka minane, maisha yangu yalizunguka kesi moja ambayo ilinitesa kuliko jambo lolote nililowahi kupitia. Ilikuwa ni kesi ya ardhi ya familia yetu. Ardhi hiyo haikuwa tu kipande cha shamba. Ilikuwa sehemu ya historia yetu.  SOMA ZAIDI/ TAZAMA VIDEO.

Hapo ndipo wazazi wetu walilelewa, na hapo ndipo tulikuwa tumejenga matumaini ya vizazi vijavyo. Lakini siku moja mgogoro ulizuka. Kilichoanza kama kutokuelewana kidogo kiligeuka kuwa kesi kamili mahakamani.

Kila upande ulikuwa na madai yake, na ghafla familia yetu ikajikuta katika vita ya kisheria ambayo haikuonekana kuwa na mwisho. Kwa kweli ilikuwa safari ngumu sana.

Miaka ilipita huku kesi ikiendelea. Kulikuwa na vikao, nyaraka, na kusubiri maamuzi mbalimbali. Kila nilipoondoka mahakamani, nilibeba mzigo wa hofu moyoni mwangu.

Hofu ya kupoteza kila kitu. Kilichoniumiza zaidi ni kuona wazee wa familia wakihangaika. Walikuwa wamewekeza matumaini yao yote kwenye ardhi hiyo, na kila siku waliishi kwa wasiwasi kuhusu hatima yake.

Kulikuwa na wakati nilikata tamaa. Baadhi ya watu waliniambia nikubali matokeo yoyote na kuacha kupambana. Wengine waliniambia kesi ile ingeendelea milele bila suluhisho.

Lakini moyoni sikuwa tayari kuacha. Siku moja rafiki yangu alinieleza kuhusu Kiwanga Doctors. Aliniambia waliwahi kumpa moyo wakati alikuwa akipitia changamoto kubwa iliyomfanya ahisi amefika mwisho wa safari.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

 


Na.Ashura Mohamed - Arusha.

Maonesho ya Karibu- KiliFair yamefunguliwa rasmi Jijini Arusha ambapo pamoja na kuchangia ukuaji wa pato la taifa Jukwaa hilo linatahwa kama kitovu cha kukutanisha wauzaji na waonenyeshaji kutoka mataifa mbali mbali barani Afrika

Maonesho hayo ambayo ambayo yanazidi kukua mwaka hadi mwaka yanawakutanisha wadau wa sekta ya utalii barani Afrika na Dunia kwa Ujumla kwa lengo la kutangeneza mnyororo wa Uchumi ndani ya sekta hiyo ili kuendelea kufanya vizuri zaidi,ambapo jukwaa hilo  huwakutanisha wadau wa ndani na nje ya nchi  ambao wameendelea kuwekeza na kuchagiza ongezeko la watalii katika Hifadhi za Taifa nchini.

Akifungua Maonesho hayo  Juni 05, 2026 katika Viwanja vya Magereza jijini Arusha, Mkurugenzi wa Utalii Dkt. Thereza Mugobi kwa niaba ya Waziri waMaliasili na Utalii alisema kuwa Karibu-KiliFair ni zaidi ya maonesho,ambao ni  uwekezaji wa kimkakati katika mustakabali wa utalii wa Tanzania. 

Dkt.Mugobi amesema kuwa Uhusiano huo wa kibiashara ulioanzishwa katika jukwaa hilo la Karibu KiliFair umezalisha ushirikiano mpya, kuongeza idadi ya watalii wanaowasili nchini, kuvutia uwekezaji, kutengeneza ajira, na kuimarisha maisha ya jamii zinazotegemea utalii. 

"Serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya utalii ikiwemo malazi, viwanja vya ndege, barabara ili kuboresha uzoefu wa watalii na kuwafikisha katika maeneo mbalimbali yenye vivutio kwa urahisi,pia Wizara itaendelea kutangaza vivutio vyake kupitia njia za kidijitali ili kuyafikia masoko mbalimbali duniani." Amesema Dkt. Mugobi.

Naye  mwakilishi kutoka “TATO” Wilbard Chambulo, amesema kuwa maonesho haya ni daraja linalounganisha wadau wa ndani ambao ni mawakala wa utalii na waongoza watalii pamoja na mawakala wa kimataifa kutoka katika mabara yote duniani.

Mkurugenzi Mwenza wa Karibu-KiliFair, Dominic Shoo, amesema ongezeko la washiriki kutoka mataifa mbalimbali ni ishara kuwa Tanzania imeendelea kujijengea heshima kama kitovu muhimu cha biashara ya utalii katika ukanda wa Afrika Mashariki

Shoo ameongeza kuwa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi utaendelea kuwa nguzo muhimu katika juhudi za kuitangaza Tanzania na kuongeza mchango wa utalii katika uchumi wa taifa

Karibu-KiliFair imeendelea kuwa moja ya maonesho makubwa zaidi ya utalii katika Afrika Mashariki, yakitoa nafasi kwa wadau kutangaza vivutio vya utalii, kujenga mitandao ya biashara na kuibua fursa mpya za uwekezaji ndani ya sekta hiyo.

Maonesho haya yatamalizika kesho Jumapili June 07 ambapo mwaka huu yamekutanisha zaidi ya watu 1000 kutoka mataifa mbali mbali.







Mradi wa uchorongaji wa visima vitatu vya gesi asilia unaoendelea katika Kitalu cha Mnazi Bay kilichopo Mkoani Mtwara umeleta manufaa makubwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kufuatia utekelezaji wenye mafanikio.