Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.
Na.Mwandishi Wetu-MOSHI
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameielekeza VETA Moshi kuimarisha ushirikiano na makampuni na viwanda ili kuongeza fursa za ajira kwa wahitimu na kukuza matumizi ya teknolojia mpya, sambamba na uelekeo wa taifa uliobainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, sera za kisekta na miongozo mbalimbali ya kitaifa.
Mhe. Ameir ametoa maelekezo hayo Januari 07, 2026, alipotembelea chuo hicho, amesisitiza kuwa ushirikiano huo unaboresha mafunzo na kulingana na mahitaji ya soko la ajira.
Aidha, amesema kuwa utekelezaji wa mafunzo ya sekta ya madini kupitia programu jumuishi ya ufundi wa teknolojia ya uchimbaji madini kwa kushirikiana na Chemba ya Madini Tanzania utawezesha utoaji wa mafunzo yanayoakisi mahitaji halisi ya sekta hiyo muhimu kwa taifa.
"Serikali itaendelea kuwekeza katika kuongeza fursa na kuinua ubora wa mafunzo ya ufundi stadi kwa kununua vifaa vya kisasa, kuimarisha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na ujenzi wa vyuo vipya vya VETA 64 nchini."amesema Mhe. Ameir
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore, amesema kuwa Chuo cha VETA Moshi kimeendelea kuwa mfano wa mafanikio ya elimu ya ufundi stadi kwa kuimarisha ushirikiano na viwanda na migodi, hatua inayowezesha mafunzo yanayotolewa kuendana na mahitaji ya soko.
CPA Kasore amesema ushirikiano huo umewezesha vijana kupata ajira kwa haraka kutokana na ujuzi wa vitendo wanaopata wakati wa mafunzo, na kwamba baadhi ya wahitimu kutoka VETA Moshi wamefanikiwa kupata ajira nje ya nchi, jambo lililosaidia kuboresha uchumi wa familia zao na kuchangia pato la taifa.
Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, zinazotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na wadau katika kuimarisha Elimu Amali, Mbunge wa Moshi Mjini, Mhe. Ibrahim Shayo, ameahidi kufadhili masomo ya vijana 10 kila mwaka katika Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akizungumza mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore,akielezea mafanikio yaliyopatikana katika Chuo cha VETA Moshi mara baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, kutembelea Chuo cha VETA Moshi.
































.jpg)
.jpg)
.jpg)