Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa umeme kwenye vitongoji ni chachu ya kuinua uchumi wa wananchi vijijini.

Mhe. Sendiga ameyabainisha hayo leo Mkoani Manyara wakati wa kikao na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kilicholenga kumtambulisha Mkandarasi Mzawa aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 267 kwa mkoa huo, Kampuni ya SAGEM COM ENERGY.

Mradi huo unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 45.8 unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu ambapo Vitongoji katika Wilaya za Babati, Hanang, Mbulu, Kiteto, na Simanjiro vitanufaika na mradi huo.

“Tunamshkuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo zinazowezesha kutekelezwa kwa mradi huu muhimu unaokwenda kuendelea kuinua uchumi wa maisha wa wananchi wetu hasa wa vijijini,” amesema Mhe. Sendiga.

Mkuu huyo wa Mkoa pia amewataka wakandarasi kufanya kazia kwa bidii na weledi na kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa huku akitoa rai kwa viongozi wa serikali pamoja na wananchi kutoka ushirikiano kwa mkandarasi wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

“Nikiwa kama Mkuu wa Mkoa natoa maelekezo kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya kuhakikisha kuwa wanashirikiana na wanaenda kumtambulisha mkandarasi kwa wananchi. Lakini pia nitoe rai kwa wananchi, miradi hii ya kijamii ambayo inakwenda kutupatia faida kubwa tuipokee, tupunguze vikwazo,” amesisitiza Mhe. Sendiga.

Awali akizungumza kuhusu utekelezwaji wa mradi huo, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina amesema kuwa Mkoa wa Manyara unajumla ya Vitongoji 1946 na vitongoji 1113 tayari vimefikishiwa umeme.

Mhandisi Mhina ameongeza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.

Kwa muda mrefu, maisha yake yalikuwa magumu. Kila mwezi alijikuta akikabiliwa na madeni makubwa. Benki, wamiliki wa biashara, na marafiki walikuwa wanamshinikiza. Kila alipojaribu kupata suluhisho, njia zote zilifungwa.

Simu zake zililia kila siku. Alilala usingizi mchache. Kila hatua ilionekana kuzidiwa na changamoto. Familia ilianza kuogopa. Marafiki walipotea. Alijikuta akitafuta suluhisho kila mahali lakini kila kitu kilishindikana.

Mara moja, alisikiliza ushauri wa mtu wa karibu. Alielezwa atafute msaada wa hekima. Soma Zaidi.
Mchungaji huyu alisimulia maisha yake kwa huzuni na mshangao. Kwa miaka 15, alidai kuwa kila jaribio la kuoa lilipotea bila sababu. Kila mwanamke aliyekaribishwa kwenye maisha yake aliondoka au matatizo yalitokea ghafla.

Watu walimchukulia kama mtu mwenye bahati mbaya. Familia na waumini walijaribu kumfariji. Wengine walidhani ni kama mtazamo wa kijamii. Lakini alijua kulikuwa na kitu cha ndani kilichomzuia.

Hakuwahi kuacha kujaribu, lakini kila wakati alishindwa. Hatimaye, aliamua kufuata mwongozo wa kina. Alijua kuna nguvu za ndani na vizuizi visivyoonekana.Soma Zaidi.
Mwanamke huyu alishiriki hadithi yake kwa huzuni kubwa. Alidai kuwa amefunga ndoa mara tatu, lakini kila ndoa ilidumu siku 30 tu. Kila mara alikuwa na matumaini mapya, lakini kila mwisho ulikuwa wa ghafla na maumivu.

Familia na marafiki walishangaa.

Wengine walidhani alikuwa na bahati mbaya. Wengine walidhani ni yeye aliye na tabia zisizoeleweka. Lakini alijua kuwa kuna kitu kilichomzuia kupata amani ya ndoa.

Kila alipojaribu kuelezea hofu yake, wengine walimkemea. Soma Zaidi.
Miaka minane iliyopita, kijana huyu aliondoka nyumbani bila kusema neno. Familia ilimtafutia kila mahali. Polisi walifanya uchunguzi, lakini hakuna aliyetambua hatima yake. Kila siku ilikuwa changamoto kwa wazazi wake.

Wazazi walilala kwa wasiwasi kila usiku. Marafiki walijitahidi kuangalia kama kuna ishara ya kupona. Kila jaribio la kumtafutia lilishindikana. Kila mwaka, matumaini yalipungua.

Kila mtoto wa jirani alijua hadithi yake, lakini hakuna aliyetaka kuamini kuwa angeweza kurudi. Ghafi ya shaka na hofu, kijana huyo alionekana ghafla nyumbani. Hakukosa mshangao, machozi, na hofu ya familia.

Hakuna aliyekuwa tayari kwa tukio hilo. Familia ilijikuta ikipumua kwa shida na furaha kwa wakati mmoja. Kijana huyo alieleza kuwa alikabiliwa na changamoto nyingi misituni.

Alipata ushauri mdogo kutoka kwa watu wachache waliomkumbatia, lakini bado hakukuwepo mwongozo wa kina. Soma Zaidi.
Jamaa huyu alishiriki hadithi yake kwa mshangao na shukrani. Kwa miaka mingi, aliishi kwa msaada wa wengine.

 Kila kitu kilimpatia hofu: nyumba, chakula, na hata mahitaji ya kila siku. Alijikuta akitumia kila nguvu ili kuishi kwa heshima.

Familia na marafiki walimfariji, lakini alijua kwamba changamoto zake zilikuwa kubwa. Kila siku ilikuwa mapambano ya kuishi. Kila mwezi alikosa suluhisho la kudumu. Hali yake ilimfanya kuhisi aibu na kushindwa.

Hatimaye, aliamua kutafuta mwongozo wa kina.Soma Zaidi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya muundo wa Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji ambapo amemteua Dkt. Tausi Mbaga Kida kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango.

 


Imeelezwa kuwa mradi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Awamu ya Pili B (HEP 2B) unakwenda kuongeza  na kuchocchea uchakataji wa mazao ambayo kwa kiasi kikubwa wananchi wa mkoa wa Katavi wanazalisha mazao katika mkoa huo. 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi,  Mhe. Mwanamvua Mrindoto leo tarehe 6 Februari, 2026 mara baada ya kutambulishwa kwake mkandarasi Kampuni ya M/s ETDCO Ltd atakayetekeleza mradi wa HEP 2B wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 358 kwa wakazi zaidi ya 11,536 mkoani Katavi. 

"Kwa sasa  badala ya kuuza mazao ghafi tutaiza bidhaa, suala hili la kupatikana kwa umeme litakwenda kuipandisha bei za mazao kwa sababu yatachakatwa katika hali nzuri na zitauzwa bidhaa badala ya kuuza malighafi," Amesema RC. Mrindoto. 

Vilevile, ameongeza kuwa upatikanaji wa umeme wa uhakika kupitia mradi wa HEP 2B utakwenda kukuza uchumi, kukuza uwekezaji na kuleta ajira kwa vijana, wanawake, wazee na makundi mbalimbali katika mkoa huo.

"Nimsisitize mkandarasi kujipanga sawasawa uingie kazini kwa miguu yote miwili ukiwa na kasi kubwa kwa sababu wanachohitaji wananchi ni umeme wala sio maneno au ahadi, sio ratiba, sio michakato," Amesema RC Mrindoto. 

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Mussa Muze amesema lengo kuu la utekelezaji wa mradi wa HEP 2B ni kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi katika vitongoji vya mkoa wa Katavi na kusaidia maendeleo jumuishi ya kijamii na kiuchumi. 

Naye, Msimamizi wa Miradi ya REA mkoa wa Katavi, Mha. Gilbert Furia amesema, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kushiriki vema katika utekelezaji wa mradi, na kutumia fursa ya kuletewa umeme  kuweza kujiinua kiuchumi.

Pia, Mkandarasi kutoka Kampuni ya M/s ETDCO Ltd, Mha. Abdalah Mitenda amemueleza RC Mrindoto kuwa katika mradi huo wakandarasi watapewa kipaumbele kufanya shughuli mbalimbali zitakazokuwa zinafanyika katika mradi huo na kuwataka kuchangamkia fursa.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi,akizungumza wakati wa mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo.

Na.Mwandishi Wetu- KARIAKOO

Wafanyabiashara wameukubali mfumo wa Usimamizi wa Kodi za ndani (IDRAS) ,huku wakijiandaa kuupokea Jumatatu ya tarehe 9 Februari mwaka huu.

Akizungumza leo 6.2.2026 jijini Dar es salaam katika mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi amesema wapo tayari kuanza kuutumia mfumo huo kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mwenyekiti huyo amesema kupitia mafunzo ambayo wamepatiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanaamini mfumo utakuwa msaada kwao na kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo.

Amesema mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa yameondoa hofu iliyokuwepo awali na kuwapa uelewa wa pamoja kuhusu matumizi ya mfumo huo.

Bw. Mushi amesema wamejiandaa kuupokea mfumo wa IDRAS, akieleza kuwa jambo lolote jipya huwa linaogopesha kwa wanaolipokea.

Amebainisha kuwa mabadiliko ya kiteknolojia hayaepukiki katika dunia ya sasa, hivyo wafanyabiashara wanapaswa kuendana nayo ili kuboresha ufanisi wa ulipajikodi.

Hata hivyo, Mushi ametoa rai kwa TRA kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutatua changamoto ya mtandao katika baadhi ya maeneo ya biashara, hususani Kariakoo ili kuleta ufanisi wa matumizi mazuri ya mfumo mpya wa IDRAS kwa walipakodi.

Aidha, ametoa wito kwa wafanyabiashara wote kuwa tayari kuupokea mfumo wa IDRAS na kushirikiana na Serikali pamoja na TRA kwa karibu, akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kuhakikisha ulipaji wa kodi unakuwa rahisi na wenye tija.

“Tumejiandaa kuupokea mfumo kuanzia Jumatatu ya tarehe 9 mwezi huu Kikubwa ni kushirikiana na Serikali kuhakikisha tunalipa kodi na mifumo ya ulipaji iwe rahisi,” amesema Bw. Mushi.

Aidha,Mwenyekiti huyo amependekeza kuwepo kwa kipindi cha mpito cha mafunzo ili kuwapa wafanyabiashara nafasi ya kuuelewa mfumo huo Zaidi na kuleta ufanisi sahihi wa utekelezaji wake.

“Angalau miezi mitatu ya mwanzo iwe ni ya mafunzo na kuwaelimisha watu namna ya kutumia mfumo, watakapokuwa wameuelewa, tutakwenda pamoja,”- Bw. Mushi.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Frank Nkinda amekabidhi Hundi ya zaidi ya Bilioni moja kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu fedha zinazotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. 

Aidha, amekabidhi pia vitendea kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ambavyo ni cherehani pamoja na vifaa vya uchomeleaji.

Akizungumza wakati wa kukabidhi Hundi hiyo, DC Nkinda amevitaka vikundi hivyo kuitumia mikopo hiyo vizuri ili iweze kuwakwamua kiuchumi pamoja na kuhakikisha wanarudisha mikopo hiyo kwa wakati ili na wengine waweze kunufaika.

“Fedha hizi zimeletwa kwa lengo la kuwasaidia na kuwakwamua wananchi kiuchumi, fedha hizi zisiwe chanzo cha ugomvi miongoni mwenu, nendeni mkazitumie vizuri ili muweze kufikia malengo mliyojiwekea kama wanakikundi “ Amesema DC Nkinda

DC Nkinda amevitaka pia vikundi hivyo kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika Halmashauri hiyo ili pia ziweze kuwasaidia katika urejeshaji wa mikopo hiyo pamoja na kuvitaka vikundi hivyo kuhakikisha wanarudisha mikopo hiyo kwa wakati ili iweze kuwasaidia na wengine wanaohitaji.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Mhe. Ibrahim Six amevitaka vikundi hivyo kutumia fedha hizo vizuri ili viwe mfano kwa jamii inayowazunguka 

Bi. Rose Manumba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala amewasisitiza wanufaika hao wa Mkopo wa asilimia 10 kurejesha fedha kwa wakati kusudi waweze kukopa tena na kuweza kujikwamua zaidi.

Afisa Maendeleo ya jamii (W) Bw. Judica Sumari akisoma taarifa ya utoaji wa mikopo hiyo amesema mgawanyo wa fedha hizo ambao ni kiasi cha Shilingi 464,959,101 kimeenda kwa Wanawake, Shilingi 469,959,101 kwa vijana na watu wenye ulemavu ni Shilingi 232,479,550 

Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kupitia mikopo ya Asilimia 10 imeweza kutengeneza ajira 462 ikiwa wanawake ni 296, vijana 155 na  watu wenye ulemavu 11.









Habari zilianza kama uvumi. Watu hawakuamini. Lakini tiketi zilipoonyeshwa, ukimya ulitawala. Mwanamume huyo alidai kushinda bet mara 12 mfululizo. Sio siku moja. Sio wiki moja.

Bali kwa kipindi kilichowashangaza wengi. Kabla ya hapo, maisha yake hayakuwa mazuri. Alikuwa akifanya kazi ndogo ndogo. Mapato hayakuwa ya uhakika. Mara nyingi alikopa.

Alikuwa mmoja wa wale waliokuwa wakijaribu bahati bila mafanikio. Wengi walimjua kama mtu wa kawaida tu.
Ghughuli zilianza baada ya ushindi wa tatu mfululizo.

Marafiki waliinua nyusi. Baada ya ushindi wa sita, swali likaanza. Ilipofika ushindi wa kumi na mbili, mjadala ukalipuka. Wengine walimwonea wivu. Wengine walimshuku. Wengine walitaka kujua siri yake.

Alipoulizwa, hakutoa jibu la moja kwa moja. Alisema tu kuwa kulikuwa na kipindi aligundua mambo hayako sawa katika maisha yake. Kila alichogusa kilikuwa kinakwama.

Alijua tatizo halikuwa maarifa ya michezo. Kulikuwa na kitu kingine.
Ndipo aliposema alitafuta ushauri wa kina. Sio wa kubahatisha. Soma Zaidi.
Kwa muda mrefu, jina lake lilikuwa mfano wa kushindwa. Alikuwa na deni la zaidi ya Ksh2M. Benki zilikuwa zimemkataa. Marafiki walijitenga. Simu zilimlia kila siku. Alilala kwa mawazo. Aliamka kwa hofu.

Biashara yake ilikuwa imeanguka. Miradi ilifeli moja baada ya nyingine. Kila alipojaribu kuinuka, kitu kilimrudisha chini. Alianza kuuza mali zake. Alipoteza gari. Alipoteza heshima mbele ya familia.

Wengine walimshauri akubali kuwa ni mwisho. Wiki moja kabla ya mabadiliko, alitangaza wazi kuwa amechoka. Alisema hana tena la kufanya. Aliomba muda zaidi kwa wadai. Hakupata. Alikaa kimya.

Aliangalia maisha yake yakimponyoka.
Ndipo jambo lisilotarajiwa lilipotokea. Jamaa huyo alikutana na rafiki wa zamani. Walizungumza kwa kina. Alisimulia mzigo wa deni. Alisimulia kukwama kwake.

Rafiki alimshauri atafute usaidizi wa busara. Sio wa papara. Sio wa haraka.Soma Zaidi.
Kilio chake kilikatiza kimya cha mkutano wa ukoo. Machozi hayakuweza kuzuilika. Kwa miaka saba, alisema amebeba lawama nzito. Lawama ambazo hakuziomba. Lawama ambazo ziliharibu jina lake.

Alidaiwa kumroga mume wake. Bila ushahidi. Bila kusikilizwa. Mume wake alianza kubadilika taratibu. Biashara ikaanguka. Hasira ikaongezeka. Afya ikaanza kuyumba.

Kila jambo baya liligeuzwa lawama kwake. Ndugu wa mume wakaanza kunong’ona. Majirani wakaanza kujitenga. Amani ya nyumba ikapotea.
Alipelekwa kwa wazee wa ukoo mara kadhaa.

Alituhumiwa hadharani. Hakuna aliyesikiliza upande wake. Kila kilio chake kilichukuliwa kama mchezo. Alianza kuishi kwa hofu. Alianza kujilaumu. Ndoa ikawa gereza la kimya.

Kwa miaka yote hiyo, mume hakuwahi kupelekwa hospitali ya kina. Hakukuwa na uchunguzi wa kweli. Kila mtu aliridhika na jibu rahisi. Lawama zilipata mahali pa kukaa. Mwanamke akabaki na alama moyoni.

Hatimaye, baada ya hali kuwa mbaya zaidi, jamaa wa mbali aliingilia kati. Aliwashauri watafute msaada wa busara. Soma Zaidi.
Ilikuwa mwaka 2013 alipotea bila kuacha dalili yoyote. Jamaa huyo aliondoka nyumbani asubuhi kama kawaida. Hakurudi tena. Simu yake ilizimwa. Hakukuwa na ujumbe. Hakukuwa na maelezo.

Familia ilianza kumsaka kila mahali. Polisi walihusishwa. Marafiki waliulizwa. Miaka ikapita bila majibu.
Kadri siku zilivyogeuka kuwa miaka, matumaini yalififia. Mama yake aliugua kwa msongo wa mawazo.

Watoto wake walikua bila kumjua baba yao. Wengine walianza kusema huenda alikufa. Wengine walidai alikimbia kwa makusudi. Familia ilibaki katikati ya maumivu na maswali yasiyo na majibu.

Ghafla, mwaka huu, kilio kilisikika nyumbani. Jamaa huyo alisimama mlangoni. Alikuwa amechoka. Amebadilika sana. Lakini alikuwa hai. Familia ilishindwa kuamini macho yao. Wengine walilia.

Wengine walimkumbatia. Ilionekana kama ndoto. Lakini furaha ilichanganyika na maswali mengi mazito. Baada ya siku chache, ukweli ukaanza kujitokeza. Jamaa huyo alidai maisha yake yalivurugika ghafla.

Kila alipojaribu kurejea nyumbani, mambo yalizidi kuwa magumu. Alipoteza kumbukumbu kwa vipindi. Alijikuta akihama maeneo bila mpangilio.

Alisema nguvu zisizoeleweka zilikuwa zinamfanya ashindwe kurudi. Hapo ndipo familia ilipotafuta msaada wa nje. Soma Zaidi.
Tukio hili lililazua hofu na mshangao kiliibuka kijijini mmoja wa viongozi wa kanisa. Mchungaji maarufu aliopendwa na wengi alipatikana amekufa chooni. Habari hizo zilienea haraka, na kila mtu alikuwa na mashaka na maswali yasiyo na jibu.

Hali ilianza baada ya uvumi kuhusu msichana wa miaka 21 aliyehusishwa na matukio yasiyoeleweka ndani ya kanisa. Watu walijiuliza ni kweli au ni uvumi tu. Familia na waumini walikusanyika, lakini hofu ilitawala.

Hakuna aliyesema lolote kwa ujasiri.
Uchunguzi wa awali ulionyesha kuwa mchungaji alikula uroda iliyokuwa imechanganywa na kitu kisichoeleweka.

Sababu ya matokeo hayo bado haikuwa wazi. Polisi walipiga ripoti. Wanaume na wanawake walikaa wakitazama, wakiwa na hofu kubwa. Jamii ilikosa amani. Waumini walijilaumu kwa kushindwa kutambua hatari.

Familia ya mchungaji ililia kimya. Wengine waliogopa kuzungumza. Nyumba ya mchungaji ikawa kimya.Soma Zaidi.

 

Mbunge wa Jimbo la Kilombero, Abubakari Asenga, ameibua mjadala mzito bungeni baada ya kutoa kauli kali akiwataka Watanzania kuacha tabia ya kumkosoa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na familia yake kwa lugha ya kejeli kwenye mitandao ya kijamii. 

Kauli hiyo imekuja wakati ambapo mijadala mikali imekuwa ikiibuka mtandaoni, ikihusisha hata watu wa karibu na Rais, jambo lililoibua hisia tofauti miongoni mwa wananchi.

Akichangia hotuba ya Rais wakati wa ufunguzi wa Bunge la Kumi na Tatu, Asenga alisema wazi kuwa baadhi ya maneno yanayozungumzwa mitandaoni hayalengi kujenga Taifa. Kusoma Zaidi, bonyza hapa.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameongoza maelfu ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tabora, Munde Tambwe, yaliyofanyika Februari 4, 2026, nyumbani kwao Kata ya Cheyo, Manispaa ya Tabora. Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi wa Serikali, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wabunge, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi waliokuja kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi huyo.

Munde Tambwe alifariki dunia Februari 2, 2026, jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Baada ya taratibu za kitaifa na kifamilia kukamilika, mwili wake ulisafirishwa hadi mkoani Tabora na kuzikwa katika makaburi ya Sheikh Yahaya yaliyopo Kata ya Kidongo Chekundu.Kusoma Zaidi, Bonyza hapa.

Wakala wa Maendeleo ya Usimamizi wa Elimu (ADEM) kwa kushirikiana na VVOB – Education for Development umefikia hatua muhimu katika kuimarisha uongozi wa shule nchini Tanzania kufuatia utekelezaji wenye mafanikio wa Mradi wa LIT-LEAD.

 


Na OWM – TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe.  Tone Tinnes na kufanya mazungumzo ya namna ya kuboresha ushirikiano katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, ili kuikinga jamii dhidi ya majanga yanayoweza kuwakumba kutokana na mabadiliko ya tabianchi.

Prof. Shemdoe amekutana na Balozi Tinnes leo Februari 05, 2026 Jijini Dodoma katika ofisi ndogo za Wizara na kujadiliana masuala mbalimbali ili kuimarisha mahusiano ya kiutendaji baina ya OWM-TAMISEMI na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania.

Katika mzungumzo hayo wamekubaliana kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuwezezesha utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika sekta za afya na elimu msingi, miundombinu ya barabara na huduma nyinginezo za kijamii, ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Aidha, Prof. Shemdoe ameishukuru Serikali ya Norway kwakuwa mmoja wa wadau wa maendeleo katika kuimarisha mabadilikoyatabianchi, na kuiomba nchi hiyo kuendelea kuchangia maendeleo nchini kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inagusa maisha ya Watanzania.

Kwa upande wake, Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe.  Tinnes ameishukuru na kuipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Norway na Tanzania, ushirikiano ambao una tija katika maendeleo ya wananchi.

Katika kikao  hicho, Balozi huyo wa Norway aliambatana na Msaidizi wake Dkt. Lutgart Lenaerts pamoja na Mshauri Mwandamizi Dkt. Yassin Mkwizu.

📌Bima ya afya kwa wote yaguswa

Na Augusta Njoji

KAMATI ya Ushauri ya Wilaya ya Handeni (DCC) imepitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti ya Sh. bilioni 35 kwa mwaka wa fedha 2026/27 ya Halmashauri ya Mji Handeni, huku miongoni wa vipaumbele vilivyotajwa ni pamoja na kugharamia Bima ya Afya kwa Wote kwa wananchi wasio na uwezo kwa kutumia mapato ya ndani.

Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichofanyika leo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewaagiza Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wahudumu wa Afya kutoa elimu kwa wananchi kwa lugha rahisi ili wahamasike kujiunga na mpango huo wa bima ya afya.

Amesema serikali tayari imetangaza kuanza utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hivyo ni wajibu wa viongozi na watendaji kuhakikisha wananchi wanaelewa umuhimu wake ili wawe na uhakika wa matibabu wanapohitaji huduma za afya.

“Ni lazima wananchi waelimishwe kwa lugha wanayoielewa ili wajue faida za bima hii, kwani itawasaidia kupata huduma za matibabu kwa uhakika,” amesema Mhe. Nyamwese.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kubaini kama inatekelezwa kwa kuzingatia thamani halisi ya fedha, sambamba na kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema rasimu ya mpango na bajeti imeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi na mikakati ya maendeleo ya Halmashauri.

Ametaja vipaumbele vingine vitakavyotekelezwa kwa kutumia mapato ya ndani kuwa ni pamoja na kutenga Sh milioni 176 kwa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ujenzi wa fremu za maduka ili kuongeza vyanzo vya mapato, utekelezaji wa afua za lishe, ujenzi wa maabara katika shule moja ya sekondari pamoja na kuboresha miundombinu ya mifugo.

Awali, Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt. Hudi Muradi, amesema kwa mwaka wa fedha 2026/27 Sh milioni 30 zimetengwa katika mapato ya ndani kwa ajili ya kugharamia bima ya afya kwa wananchi wasio na uwezo na kwamba kwasasa serikali inaendelea na zoezi la uhakiki wa wananchi hao.

Ameongeza kuwa serikali imeimarisha miundombinu ya afya na kuajiri watumishi wapya 58 ili kuboresha utoaji wa huduma katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.