Serikali imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kujipanga kikamilifu katika maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, hususan katika kuhakikisha wageni watakaofika nchini wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo.

Agizo hilo limetolewa l na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Florence Samizi (Mb.) ambaye amesema NHIF ina jukumu muhimu la kuratibu suala la bima ya afya wakati wa mashindano hayo ili kuhakikisha wageni wanapata huduma za matibabu kwa urahisi pindi wanapohitaji huduma hizo.

“Tuwape uhakika wa huduma bora ili waone fahari kuwapo hapa nchini katika kipindi chote cha mashindano hayo,” amesema Dkt. Samizi.

Amesema maandalizi ya huduma za matibabu yanapaswa kuzingatia pia huduma za dharura pamoja na huduma maalum, ikiwemo za moyo na mifupa, ili kukidhi mahitaji mbalimbali ya afya yatakayoweza kujitokeza wakati wa mashindano.

Aidha alidokeza kuwa tayari Wataalamu kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wamekagua Vituo vya kutolea huduma kwa alengo la kujiridhisha na wamefurahishwa na utayari unaoonyeshwa katika maandalizi ya huduma za matibabu jambo linaloonesha kuwa Tanzania inajiandaa kuhakikisha AFCON 2027 inafanyika katika mazingira salama na yenye huduma bora.

Ameitaka NHIF kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya, vituo vya kutolea huduma na wadau wengine kuhakikisha mfumo wa huduma za matibabu wakati wa mashindano hayo unakuwa imara, unaopatikana kwa wakati na unaokidhi viwango vinavyohitajika.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi Mkuu waa NHIF, Dkt. Irene Isaka alisema kuwa tayari Mfuko umeshajipanga na umeandaa kifurushi maalumu kwa ajili ya wageni wote watakaokuja nchini kwa ajili ya mashindano hayo.

“Tayari tumejipanga na tuna kifurushi ambacho tutakileta Wizarani ili tupate baraka ya Wizara hivyo tunashukuru sana kwa maelekezo haya ambayo yanaboresha na kuhakikisha tunajipanga vyema,” alisema Dkt. Isaka. ‎

‎NAIBU Waziri wa Afya, Mhe Dkt. Florence George Samizi (Mb), amelipongeza Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuwa moja ya mabaraza bora nchini. Amelitaka baraza kuhakikisha ajenda ya Bima ya Afya kwa wote inawafikia wananchi wengi zaidi.

Nimefurahi kusikia kwamba katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 Mfuko umeweza kufikia 10.7% ya Wananchi toka 8% ya wananchi iliyodumu kwa takriban miaka 10. Pamoja na pongezi hizo Mh. NAIBU WAZIRI ameutaka Mfuko kutumia TEHAMA na kusajili wanachama wengi zaidi ili kutimiza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wote huduma za bima ya afya. Hii itasaidia wananchi kuondokana na umaskini pale wanapopata maradhi. ‎Dkt. Samizi ametoa maelekezo Hayo wakati wa mkutano wa nne wa wa Baraza la 4 wafanyakazi NHIF, Jijini Arusha, na kusisistiza menejimenti ya wafanyakazi wa NHIF kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu, weledi na uwajibikaji, huku wakisikiliza na kutatua kwa wakati kero za wananchi. ‎Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya. Kutoa huduma bora na kuwa na mfumo wa kupokea mrejesho toka kwa wananchi. ‎Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa NHIF, Dkt. Samizi amesema ni muhimu mfuko huo kuonesha mafanikio yaliyopatikana. Kuwepo kwa NHIF kumesaidia kuboresha huduma za Afya kwa kulipa madai na kutoa mikopo kwa vituo vya afya. Ni vema wanachi wakajulishwa hatua kubwa iliyofikiwa katika huduma za Afya na mchango wa NHIFkatika Sekta hii muhimu. Mlianza na vituo vichache sana mwaka 2001 hivi sasa yaani mwaka wa Fedha 2025/26 mmesajili zaidi ya vituo 10,600 nchi nzima. Ni vema kuonesha namna mlivyokabiliana na changamoto za wakati ule na namna zilivyowasaidia kuboresha Mfuko katika utoaji wa huduma. ‎Amesema mafanikio hayo yanadhihirishwa na kujituma, ushirikiano, umoja na mshikamano miongoni mwa watumishi wa NHIF ili kufikia malengo ya mfuko kwa lengo la kutekeleza jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata bima ya Afya. ‎Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, ameeleza mafanikio yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa kilipa madai toka zaidi ya siku 90 hadi wastan wa siku 50 kwa mwaka wa Fedha 2025/2026. Vile vile alieleza kwamba Mfuko umeendelea kuimarika ambapo ziada imeongezeka kwa 57% Mfuko umepunguza matumizi kwa asilimia13% na uwekezaji umeongezeka kwa 106%.

Hii imewezesha Mfuko kuendeleza kifurushi cha wanafunzi, Toto Afya. Mfuko kusajili kifurushi cha tarangire, Mikumi, Ngorongoro, Serengeti Tanzanite na kifurushi cha vikundi yaani Umoja Afya ambacho ni sh. 60, 000 kwa matibabu ya mwaka mzima.

Vile vile alielezea mikakati inayotekelezwa na mfuko huo katika kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na matumizi ya TEHAMA kwenye usajili, uchakataji madai na kupambana na udanganyifu. Mfuko pia unashirikisha Sekta Binafsi katika usajili wa wanachama na katika huduma za matibabu. ‎Mwakilishi wa chama Cha wafanyakazi TUGHE, Bw.Paul wamepongeza baraza Hilo kuzingati misingi ya Kazi stahiki za wafanyakazi kwenye taasisi hiyo. ‎Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki semina elekezi ya siku mbili wamesema wamepata maarifa na mwelekeo mpya ambao utawasaidia kuboresha utendaji wao wa kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bima ya Afya kwa wote! Jiunge sasa!

Kushikwa na matatizo ya vidonda vya tumbo ni jaribu gumu linaloweza kubadili maisha yako kuwa kero ya kila siku na kukosesha amani mwilini. 

Kwa zaidi ya miaka mitano, nilipitia maumivu makali mno ya tumbo yaliyokuwa yakiniuma kama vile nimechomwa na moto au visu kwa ndani.

Kila nilipojaribu kula chakula, hata kiwe kidogo au chepesi vipi, tumbo lilikuwa likijaa gesi, nikipatwa na kiungulia kikali kinachopanda koo, na maumivu yanayotoboa hadi mgongoni.

Nilitumia fedha nyingi hospitalini kununua dawa za kutuliza asidi na maumivu, lakini zote zilikuwa zikituliza kwa muda mfupi tu na baadaye maumivu yakirudi kwa kasi kubwa zaidi, yakinifanya nikonde sana na kukata tamaa ya kuishi.

​Nikiwa kwenye mateso hayo bila kupata suluhu ya kudumu, jirani yangu aliyetazama jinsi nilivyokuwa nikiteseka alinifuata na kunishauri nisijikate tamaa.

Alinieleza kuwa magonjwa mengi sugu ya tumbo yanayoshindikana hospitalini yanaweza kutibiwa kikamilifu kwa kutumia mitishamba asilia inayotibu chanzo cha tatizo na kuponya majeraha ya ndani.SOMA ZAIDI.
Kuishi na mke unayempenda kwa dhati huku ukijua fika kuwa anakusaliti na kutoka nje ya ndoa ni mateso makubwa yanayoweza kumvua mwanamume heshima na amani ya nafsi.

Kwa miezi mingi, nilipitia maumivu makali ya moyo baada ya kugundua kuwa mke wangu alikuwa na mchepuko wa siri aliyekuwa akikutana naye mara kwa mara.

Kila nilipojaribu kumuuliza au kumkanya kwa wema, alikuwa akiruka kimanga, kuniletea kiburi, na hata kunidharau ndani ya nyumba yangu mwenyewe.

Nilibaki nikikosa raha, nikishindwa kufanya kazi zangu za kila siku kwa umakini huku hofu ya kuletewa magonjwa au kuvunjika kwa familia yangu ikinitesa usiku na mchana.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na nikifikiria kumfukuza na kuvunja ndoa yetu, rafiki yangu wa karibu alinifuata na kunishauri nisichukue maamuzi ya kukurupuka.

Alinieleza kuwa tabia za usaliti na tamaa zilizopitiliza mara nyingi hutokana na upepo mchafu au vifungo vya kishirikina vinavyoharibu amani ya ndoa. SOMA ZAIDI.
Kuanzisha huduma ya kiroho na kufungua kanisa ni ndoto inayobeba maono makubwa ya kuongoza jamii na kutoa huduma kwa jamii.

Hata hivyo, pale unapotumia miaka mingi ukihubiri kwenye viti vitupu bila waumini kujitokeza, maisha ya utumishi hugeuka kuwa chanzo cha simanzi, aibu, na umaskini mkubwa.

Kwa zaidi ya miaka mitatu tangu nilipofungua kanisa langu, nilipitia nyakati ngumu mno. Kila siku ya ibada nilifika mapema na kuweka vyombo vizuri vya muziki, lakini waumini walikuwa hawazidi watu watano, huku makanisa mengine yaliyo jirani yakifurika na kupasuka na watu.

Nilibaki nikidharaulika mtaani, nikishindwa hata kulipa kodi ya eneo la kanisa na kununua mahitaji ya msingi ya familia yangu.

​Nikiwa kwenye majuto makubwa na nikifikiria kufunga kanisa na kukimbia mji kwa aibu, mchungaji mwandamizi kutoka mji mwingine alinitembelea.

Baada ya kushuhudia jinsi kanisa langu lilivyokuwa likifia sokoni, alinieleza ukweli kwamba mara nyingi ukosefu wa waumini na kukosa kibali kwenye huduma hutokana na nyota yako ya uongozi kufunikwa na giza au kuwekewa ukungu wa kishirikina na maadui wanaochukia maendeleo yako. SOMA ZAIDI.
Na; Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Serikali inatoa wito kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji kuhakikisha kuwa wanaweka utaratibu wa kusimamia utekelezaji wa maelekezo ya kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kuwa siku ya usafi wa Mazingira Kitaifa kwa kuzingatia maslahi ya makundi mbalimbali.
Na; Mwandishi wetu – Babati

Wakulima wa vijiji vya Endakiso na Orng'adida vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wameeleza kunufaika na Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kushirikina na Serikali na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, na wenye Ulemavu.


Na; Mwandishi wetu – Babati


Wakulima wa vijiji vya Endakiso na Orng'adida vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wameeleza kunufaika na Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kushirikina na Serikali na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, na wenye Ulemavu.

Kwa nyakati Tofauti wakulima kutoka vijiji hivyo wameyasema hayo tarehe 4 Septemba wakati wa ziara ya timu kutoka IFAD inayotathimini maendeleo ya utekelezaji  Programu ya  muda wa kati  (MTR).

Wakulima hao waliweka bayana kuwa, Programu hiyo imeweza kuwaletea teknolojia ya kisasa ya Kilimo Mseto kwa kutumia Mbegu himilivu zinazoweza kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.


Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Bw. Ramadhani Iddi Mfumbilo mkulima kutoka katika kijiji cha Mkombozi Kata ya Endasiko alisema, kupitia Programu hii wakulima wameweza kupata mbegu za mahindi aina ya situka na mbegu za lishe ambazo zimepandwa mashambani pamoja na mazao mengine kama vile labulabu ambayo yanaweza kurutubisha ardhi na kuzuia Mmomonyoko wa udongo.



“Majani hayo pia siyo rafiki kwa mifugo kama vile ng’ombe hivyo mifugo itakapovamia shamba la Mkulima si rahisi kuweza kula au kuharibu mazao, na yanakimbiza wadudu waharibifu wa mazao.” Aliendekea kufafanua.

Alibainisha kuwa, Mbegu hizi za Lishe zina uwezo mkubwa wa Kurutubisha Afya ya Familia hasa kwa watoto, kinamama wajazito, wazazi na wazee na pia zimesaidia kupunguza magonjwa ya Utapiamlo kwa watoto.

Aidha, Akiongelea mbegu za Jamii ya Mikunde yaani Maharage aina ya Jesca, alisema, Mbegu hizo zina virutubisho muhimu na vya kipekee hasa kwa watoto.



Kwa upande wake Bi Naseriani Joseph kutoka katika Kijiji cha Orng'adida Kata ya Qash mkulima wa mazao ya Lishe yanayolimwa katika bustani nyumbani maarufu kama '_Kitchen gardens_', alisema kuwa, kupitia Programu ya AFDP wakulima hao waliweza kupata Elimu na Mbegu bora za mazao ya lishe ambayo wanalima Nyumbani na wamepata manufaa mengi kama vile kuwepo kwa mboga nyumbani pamoja na kuwasaidia watoto shule na familia kwa ujumla pamoja na kuimarisha Afya ya familia na kuongeza kipato

“Wanawake tunapata mahitaji yetu muhimu kupitia kilimo hiki kwa upande wa mboga mboga na mazao ya mikunde, tumepata elimu ya maharage lishe tumepata mbegu na tumeyatumia, Maharage yale yameboreshwa yana viini lishe na madini chuma, hivyo afya za familia zinaimarika, natoa tuu wito kwa serikali kuongeza mbegu hizi maana ni adimu na zinazalishwa kwa uchache katika kata yetu. Alisema”


Wataalam hao wanaendelea na ziara hiyo kwa kutembela maeneo tofauti yanayotekeleza programu nchini katika sekta za Kilimo na Uvuvi.




 Na WMA - MWANZA


 Wakala wa Vipimo (WMA) umesisitiza kuwa ni rafiki wa muuzaji na mnunuzi na kwamba sheria ya vipimo haikuundwa kuwakomoa wafanyabiashara bali kuwasaidia kufanya biashara ya haki.

 Kauli hiyo imetolewa leo Septemba 4, 2026 katika Siku ya Nane ya Maonesho ya 21 ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.

Wakiizungumza kwa nyakati tofauti na wageni waliotembelea banda la WMA, Wataalamu wa Wakala wamesema lengo la uhakiki wa vifaa vya vipimo ni kulinda pande zote mbili.

"Muuzaji akitumia kipimo sahihi anajenga imani kwa mteja wake na kupata soko la uhakika. Na mlaji naye anapata thamani kamili ya fedha yake. Hapa hakuna mshindi na mshindwa. Sheria ya Vipimo ni msaada, sio adhabu" wamewaeleza wananchi.

Katika siku ya nane ya maonesho hayo, banda la WMA limeendelea kuwa kivutio kwa wafanyabiashara, wazalishaji na wananchi wa kawaida ambapo Wataalamu wameendelea kutoa elimu ya vipimo hususan jinsi ya kutambua vipimo halali pamoja na umuhimu wa kuhakiki vipimo mbalimbali ili kuepuka hasara katika biashara. 

WMA imesema ushiriki wake katika maonesho hayo ni sehemu ya mkakati wa kusogezwa kwa huduma kwa umma na kusikiliza changamoto za moja kwa moja kutoka kwa wadau. 

Wakala wa Vipimo umewahakikishia wananchi kuwa unaendelea kutoa huduma za uhakiki wa haraka katika Ofisi zao zilizopo mikoa yote ya Tanzania Bara na umewakaribisha kuendelea kutembelea banda lao katika Maonesho hayo hadi Septemba 6, 2026 yatakapofungwa.

ARUSHA, Septemba 4, 2026 — Mafunzo ya siku nne ya Umahiri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Walimu Tanzania (ICT Competency Standards for Teachers in Tanzania - ICT CSTT) yameahirishwa leo jijini Arusha, huku walimu wakihimizwa kutumia maarifa na stadi walizojifunza kuboresha ufundishaji, ujifunzaji, tathmini pamoja na kuwawezesha waalimu wenzao.

Mafunzo hayo yaliyofanyika Gold Crest Hotel kuanzia Septemba 1 hadi 4, 2026, yamewajengea washiriki uwezo wa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Akili Bandia (AI), rasilimali za kidijitali na mifumo ya kujifunzia kwa njia ya mtandao katika kazi za kila siku za mwalimu.


Akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Bw. Mathias Innocent Mvula, amebainisha kuwa kukamilika kwa mafunzo hayo kunapaswa kuwa mwanzo wa utekelezaji wa maarifa na stadi hizo katika shule za na za jirani.

Kwa mtazamo wake, thamani ya uwekezaji huo itaonekana kupitia mabadiliko katika ufundishaji na ujifunzaji, badala ya kuishia kwenye vyeti. Amewataka washiriki kutekeleza mipango kazi waliyoandaa wakati wa mafunzo na kuonesha hatua watakazochukua katika utekelezaji wanaporejea shuleni.

Akieleza mazingira mapya ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Toleo la mwaka 2023, Bw. Mvula amebainisha kuwa maendeleo ya teknolojia, hususan Akili Unde, yamebadilisha namna watu wanavyopata taarifa na maarifa, hali inayohitaji walimu kuongeza uwezo wa kutumia zana hizo kwa malengo ya kuinua ubora wa elimu.


Amebainisha pia kuwa simu za mkononi na vifaa vingine vya kidijiti vinaweza kuwa nyenzo muhimu za kujifunzia na kufundishia vinapotumiwa kwa usahihi. Hata hivyo, matumizi ya teknolojia yanapaswa kwenda sambamba na mabadiliko ya sera na mitaala yanayolenga kujenga umahiri wa mwanafunzi.

Kwa mujibu wa Bw. Mvula, elimu ya sasa inalenga kumwandaa mwanafunzi kutumia maarifa na stadi katika maisha halisi, kukabiliana na changamoto na kutumia fursa za kiuchumi, badala ya kutegemea ajira pekee. Ameeleza kuwa kuimarishwa kwa mikondo ya amali ni miongoni mwa hatua zinazolenga kuongeza uwezo huo.



Katika kuendana na mabadiliko hayo, Bw. Mvula ametoa wito kwa walimu kuendelea kutumia fursa za Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA), akibainisha kuwa ujifunzaji kwa njia ya mtandao unawapa nafasi ya kuongeza uwezo kitaaluma na kitaalamu bila kulazimika kurejea chuoni mara kwa mara.

Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuweka mifumo endelevu ya kuimarisha umahiri wa walimu, ikiwemo utaratibu wa kutambua mafunzo kabilishi mbalimbali ya kuwajengea uwezo walimu ili kuboresha elimu nchini. 

MKOA WATAKA UJUZI UONEKANE SHULENI

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Elimu Mkoa wa Arusha, Bw. Vicent Boniface Kayombo, amewataka walimu walioshiriki katika mafunzo hayo kuwa kiungo cha kusambaza maarifa kwa walimu wenzao na kuhakikisha ujuzi walioupata unatafsirika katika vitendo vya ufundishaji na ujifunzaji shuleni.

Kayombo ameeleza kuwa Mkoa wa Arusha una mpango wa utekelezaji wa MEWAKA katika shule za msingi na sekondari, hivyo walimu walioshiriki katika mafunzo hayo wana nafasi muhimu ya kusaidia kufanikisha mpango huo kwa kushirikisha wenzao na kuchochea matumizi yenye tija ya TEHAMA katika shule zao.


Na John Mapepele – WAF

Washington, D.C.

Serikali ya Tanzania imekubaliana na Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C na Serikali ya Marekani kufanya utekelezaji wa kimkakati wa mkataba wa sekta ya afya ulioingiwa hivi karibuni ili kuzinufaisha pande zote mbili,huku wakiifanya Tanzania kuwa muhimili wa uzalishaji na usambazaji dawa na vifaa tiba katika bara la Afrika.
Mimi nilianza kuona mabadiliko kwenye ndoa yangu taratibu. Kila kitu kilionekana sawa mwanzoni, lakini baada ya muda, migogoro midogo midogo ikaanza kujitokeza mara kwa mara.

Mazungumzo ya kawaida yakawa mabishano. Kila jambo dogo lilikuwa linaishia kwa hasira au kutoelewana. Nilianza kuchoka kihisia na kujiuliza nini kilikuwa kikiendelea.

Nilijaribu kuzungumza na mwenzi wangu kwa utulivu, lakini wakati mwingine hali ilizidi kuwa ngumu kuliko ilivyokuwa awali. Ilikuwa kama kila hatua ya kutatua tatizo inaleta lingine jipya.

Nilianza kuhisi kama kuna kitu hakiko sawa kabisa, si tu kwenye mawasiliano bali hata kwenye mtiririko wa maisha yetu ya kila siku. Siku moja nilikuwa Facebook nikakutana na simulizi za watu waliopitia migogoro ya ndoa inayojirudia na jinsi walivyopata mwongozo wa kuelewa chanzo cha matatizo yao na kurejesha utulivu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa na ndoa ambayo nilidhani ni imara. Tulianza vizuri, tukijenga maisha pamoja kwa matumaini makubwa. Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningekutana na ukweli ambao ungegeuza kila kitu. Dalili zilianza polepole.

Mume wangu alianza kubadilika tabia. Alikuwa kimya zaidi, simu yake haikuwa mbali naye, na wakati mwingine alitoa visingizio visivyoeleweka. 

Nilihisi kuna kitu hakiko sawa, lakini sikuwa na uthibitisho. Nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu wasiwasi wangu. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa sina kazi ya kudumu kwa muda mrefu. Nilitegemea vibarua vya hapa na pale, na maisha yalikuwa magumu sana kwangu na familia yangu.

Nilikuwa na wazo la kuanzisha biashara ndogo, lakini nilikosa mtaji na hata ujasiri wa kuanza. Kila nilipofikiria kujaribu, nilihisi kama ningeanguka tena.

Siku moja nilimweleza rafiki yangu hali yangu. SOMA ZAIDI.
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imewaalika waajiri na wamiliki wa viwanda nchini kuendelea kushirikiana na mamlaka hiyo katika kuandaa na kuendeleza wataalamu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchochea maendeleo ya Taifa.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, alitoa kauli hiyo jana jijini Dodoma wakati wa hafla ya kusaini Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya VETA na Kampuni ya Van Mo, inayolenga kuimarisha ushirikiano katika kuwaendeleza vijana wenye ujuzi na kuwawezesha kupata ajira mara baada ya kuhitimu mafunzo yao.

Makubaliano hayo yaliyosainiwa katika Ukumbi wa Mikutano wa VETA Makao Makuu yalihusisha CPA Kasore kwa upande wa VETA na Meneja Mkuu wa Van Mo, Fathi Ahmed Ally. Kampuni hiyo inajihusisha na shughuli mbalimbali zikiwemo usafirishaji, uchukuzi, uuzaji wa mafuta, umiliki wa majengo na ardhi, kilimo, utalii pamoja na shughuli za uzalishaji viwandani.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, pande hizo zinalenga kuongeza upatikanaji wa wahitimu wenye umahiri, tija, ubunifu, maadili na wanaozingatia usalama kazini, huku Van Mo ikitoa fursa za ajira kwa wahitimu wa VETA wenye sifa zinazohitajika.

Aidha, ushirikiano huo utasaidia kuoanisha programu za mafunzo ya ufundi stadi na mahitaji halisi ya sekta ya viwanda na biashara pamoja na kuwawezesha wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo katika maeneo ya kazi.

Maeneo ya ushirikiano yaliyoainishwa katika MoU hiyo ni pamoja na mafunzo ya udereva wa magari makubwa, usimamizi wa vyombo vya usafiri, uchukuzi na uhifadhi wa mizigo, usimamizi wa mnyororo wa ugavi, ukaguzi na ukarabati wa magari pamoja na mifumo ya umeme na elektroniki ya magari. Maeneo mengine ni uendeshaji wa maghala na usimamizi wa stoo, uendeshaji wa vituo vya mafuta, ujenzi, usimamizi wa majengo na miundombinu, utalii na ukarimu pamoja na kilimo na uhifadhi wa mazao.

Akizungumza baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo, Kasore alisema ushirikiano huo pia utasaidia kuwajengea uwezo wakufunzi na kuhakikisha mafunzo yanayotolewa na VETA yanaendana na mahitaji ya soko la ajira.

Alisema VETA itaendelea kushirikiana na waajiri na wamiliki wa viwanda ili kutambua fursa zilizopo na kuhakikisha wahitimu wanapata nafasi za ajira katika viwanda na maeneo mengine yenye uhitaji wa wataalamu wenye ujuzi.

“Tutahakikisha pia wenzetu wa Van Mo wanapohitaji wataalamu wenye ujuzi mbalimbali, sisi VETA tuweze kusaidia kuwapata. Sambamba na hilo, ushirikiano huu una maslahi mapana kwa wananchi katika kupata fursa za ajira,” alisema Kasore.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Van Mo, Fathi Ahmed Ally, alisema kampuni hiyo imelenga kutoa ajira kwa takribani vijana 500 wenye ujuzi mbalimbali waliohitimu katika vyuo vya VETA.

Alisema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na VETA kutokana na ubora wa ujuzi unaopatikana kwa wahitimu wake, hususan katika fani zinazohusiana na shughuli za usafirishaji ambazo ni muhimu katika utekelezaji wa shughuli za kampuni hiyo.

“Kilichotuvutia kuja VETA ni kutokana na wahitimu kutoka katika vyuo hivi kuwa na ujuzi ambao sisi tunauhitaji katika kampuni yetu, hususan shughuli za usafirishaji. Hivyo tumeona hapa ndipo mahali sahihi pa kuwapata vijana wenye ujuzi huo,” alisema Fathi.

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeandaa kliniki ya viwango katika maeneo ya Soko Kuu la Biashara Kariakoo na Mwenge jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kusogeza huduma za kitaalamu karibu na wafanyabiashara wa bidhaa za chakula na vipodozi ili kuwawezesha kuendesha biashara zinazokidhi viwango.
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeibuka mshindi wa pili katika kundi la Taasisi za Udhibiti wakati wa Maonesho ya 21 ya Biashara Afrika Mashariki (MEATF), yanayofanyika katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.



ZANZIBAR, Septemba 3, 2026 — Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania imeshiriki katika uzinduzi wa Mwongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi (Parent-Child Communication – PCC Toolkit), unaolenga kuimarisha mawasiliano ndani ya familia na kusaidia kulinda afya na ustawi wa watoto na vijana Zanzibar.

Mwongozo huo unazinduliwa leo katika Hoteli ya Verde Zanzibar na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar, Mheshimiwa Zawadi Amour Nassor, katika hafla iliyowakutanisha viongozi na wadau mbalimbali wanaohusika na afya, ulinzi na ustawi wa watoto.


Mwongozo huo umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar na UNESCO, ukiwa na lengo la kuwasaidia wazazi na walezi ku

anzisha mazungumzo sahihi na yenye kujenga na watoto kuhusu afya ya uzazi, mabadiliko ya ukuaji, usalama na namna ya kujilinda dhidi ya mazingira yanayoweza kuhatarisha afya na ustawi wao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mheshimiwa Zawadi anasema Serikali ya Zanzibar imejizatiti kuhakikisha watoto wanakulia katika mazingira salama, wanasikilizwa na hawabaki nyuma, akisisitiza kuwa malezi na ulinzi wa mtoto ni jukumu la pamoja.

Anasema afya ya uzazi ni sehemu ya afya na ustawi wa mtoto, hivyo wazazi, walezi, taasisi na jamii wanapaswa kushirikiana katika kuwapatia watoto taarifa sahihi na mazingira yanayowawezesha kukua kwa usalama.


“Mtoto ni kama mbegu; ukimlea vizuri atakuwa na afya bora,” anasema.

Naibu Waziri pia anawataka wadau kuimarisha ushirikiano katika kukabiliana na changamoto zinazochangia ukatili na udhalilishaji wa watoto, akisisitiza umuhimu wa kuzuia matukio hayo kabla hayajatokea.

Anasema changamoto hizo zinahitaji ushirikiano wa karibu baina ya taasisi, jamii na wadau mbalimbali, huku akigusia pia umuhimu wa wanaume kushiriki kikamilifu katika juhudi za kuzuia na kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.

“Tuzuie matukio yanayosababisha udhalilishaji ili tuweze kupata taifa bora,” anasisitiza.

Kwa upande wa UNESCO, Mr Mathias Luhanya, National Project Officer, anasema mwongozo huo umefanyiwa kazi tangu mwaka 2020, na kufikia hatua ya kuzinduliwa rasmi ni matokeo ya uvumilivu, juhudi na ushirikiano wa wadau mbalimbali.

Anasema mwongozo huo unalenga kumsaidia mzazi kuelewa namna bora ya kuzungumza na mtoto kuhusu afya ya uzazi, kumsaidia kuelewa mabadiliko anayopitia na kutambua mazingira yanayoweza kuhatarisha afya na usalama wake.

Ushiriki wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania katika uzinduzi huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya UNESCO, Serikali ya Zanzibar na wadau wa kitaifa katika kuendeleza programu zinazolenga elimu, afya, ulinzi na ustawi wa watoto na vijana.

Hatua hiyo pia inaendana na juhudi za UNESCO za kuwawezesha watoto na vijana kupata maarifa na mazingira salama yanayowasaidia kulinda afya zao na kufikia uwezo wao.

Akizungumza kuhusu ushirikiano huo, Mheshimiwa Zawadi anaishukuru UNESCO kwa kushirikiana na Serikali ya Zanzibar katika kufanikisha uzinduzi wa mwongozo huo, akisisitiza kuwa mafanikio katika kumlinda mtoto yanahitaji dhamira na ushirikiano wa pamoja.

“Penye nia pana njia.”

Uzinduzi wa mwongozo huo unaweka msisitizo kwamba kumlinda mtoto ni jukumu la pamoja la mzazi, familia, jamii, Serikali, taasisi na wadau wa maendeleo, ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama, wanasikilizwa na wanapata fursa ya kuwa na afya bora na maisha yenye ustawi.
Kufikisha umri wa uzee ni baraka kubwa, lakini pale mwili unapovamiwa na magonjwa sugu yasiyokwisha, furaha ya kuishi hutoweka na badala yake unakuwa mtumwa wa vidonge na maumivu ya kila siku.

Kwa miaka mingi, nilipitia mateso makubwa ya kiafya baada ya kukabiliwa na shinikizo la juu la damu pamoja na kisukari vilivyokuwa vikipanda kila uchao. Kila mwezi nilikuwa nikitumia kiasi kikubwa cha fedha kununua dawa za hospitali, lakini afya yangu iliendelea kuzorota siku hadi siku.

Miguu ilianza kufa ganzi, mwili ukawa dhaifu bila nguvu, na macho yalianza kupoteza uwezo wa kuona vizuri. Nilibaki nikilala kitandani kwa maumivu makali, nikihisi kabisa kuwa siku zangu za kuishi hapa duniani zilishafika mwisho.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na nikionekana kupoteza matumaini ya kupona, ndugu yangu wa karibu alinitembelea na kunishauri nisikate tamaa kwani kuna tiba za kiasili zinazoweza kusaidia kuweka mwili sawa na kuondoa maumivu hayo kabisa. SOMA ZAIDI.
Kujitoa mhanga kwa miaka mingi kuwasomesha watoto, kuwauguza, na kujinyima kila kitu ili wapate maisha mazuri ni jukumu ambalo kila mzazi analibeba kwa upendo na matumaini ya kutunzwa uzeeni.

Hata hivyo, pale watoto hao wanapofanikiwa, wakapata kazi nzuri na maisha ya kifahari mjinikisha wakakusahau kabisa na kukutelekeza kwenye uzee wako, maumivu yake ni makali mno kuliko ugonjwa wowote.

Nilipambana sana kulea watoto wangu watatu baada ya kufiwa na mume wangu; niliuza shamba na kukopa ili kuhakikisha wote wanahitimu elimu ya chuo kikuu. Cha kusikitisha, baada ya kupata kazi zenye mishahara mikubwa, walibadilika kabisa.

Hawakuwa wakinipigia simu, hawakutuma hata fedha za chakula au dawa, na kila nilipowatafuta walidai wapo busy au kukata simu zangu, wakiniaacha nikiteseka na uzee na umaskini kijijini.

​Nilibaki nikilia peke yangu nyumbani, nikihangaika kupata hata mlo mmoja kwa siku huku majirani wakinicheka kuwa nilisomesha watoto ili wanitelekeze.

Rafiki yangu mzee wa rika langu alinitembelea na kunieleza ukweli kwamba watoto kuwasahau wazazi waliowatesekea mara nyingi hutokana na vifungo vya kishirikina kutoka kwa watu wenye wivu waliowafunga akili zao ili wasile matunda ya jasho langu. SOMA ZAIDI.