Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (kulia) akizungumza na Mwakilishi Maalumu wa Uingereza nchini Mongolia Bi. Ruth Davis, mara baada ya kikao kilichofanyika katika ubalozi wa Uingereza nchini Mongolia, Agosti 26, 2026.




✅Asisitiza Sheria ya Uhifadhi hairuhusu utafiti, uchimbaji madini mengine isipokuwa Urani, Gesi Asilia na Mafuta


✅Aeleza Sheria Ya Madini inamtaka Mmiliki wa Leseni Kupata Ridhaa ya Maandishi toka Mamlaka za Hifadhi ya Misitu


Serikali imesema itaendelea kutoa Vibali vya Uchimbaji wa Madini katika maeneo ya Hifadhi yanayoruhusiwa Kisheria kwa wananchi na wawekezaji watakaokidhi masharti husika na kupata vibali kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TSF), Mamlaka ya usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) na   Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)  kadri maombi yanavyowasilishwa.

Hayo yamebainishwa Agosti 26, 2026 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Kiruswa wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Josephine Kapoma aliyetaka kujua ni lini Serikali itaruhusu wananchi kupewa vibali vya kuchimba madini kwenye hifadhi.

 Dkt. Kiruswa amefafanua kuwa, kwa mujibu wa kifungu cha 26 cha Sheria ya Misitu, Sura ya 323, uchimbaji wa madini ndani ya Hifadhi za Misitu zinazosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na unaruhusiwa pale ambapo mwombaji amepewa leseni au kibali kwa mujibu wa Sheria hiyo huku akitakiwa kuwa amekamilisha Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA).

"Kwa upande wa Mapori ya Akiba yanayosimamiwa TAWA, vifungu vya 20(2) na 20(3) vya Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, vinazuia utafutaji au uchimbaji wa madini ndani ya Pori la Akiba, isipokuwa mafuta, gesi asilia na madini ya urani, baada ya kufanyika kwa EIA, kulipwa gharama za ulinzi wa eneo, ada ya leseni, na Serikali kuwa mwanzilishi wa mradi husika," amesema Dkt. Kiruswa.

Pia, ameeleza kuwa, kifungu cha 120 (1)(c) cha Sheria ya Madini, Sura ya 123, kinamtaka mmiliki wa leseni ya madini kupata ridhaa ya maandishi ya mamlaka zinazosimamia Hifadhi ya Misitu, Pori la Akiba, eneo la hifadhi ya malisho au eneo jingine la hifadhi kabla ya kutumia haki zake za madini katika eneo husika.


 


Na. John Masele na Martha Mbena, WF – Dodoma.


Serikali imesema inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kisera na kiusimamizi ili  kuwezesha benki za biashara kutoa mikopo kwa riba nafuu zaidi ikiwemo kuendelea kutekeleza sera ya fedha inayolenga kudhibiti mfumuko wa bei.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Haidary Hemed Sumry, Mbunge wa Mpanda mjini aliyetaka kujua mpango wa Serikali kupunguza riba za mikopo ya biashara katika benki ili kuwawezesha wafanyabiashara kulipa mikopo kwa wakati.

Mhe. Luswetula alisema kuwa Serikali haiingilii moja kwa moja upangaji wa viwango vya riba za mikopo katika benki za biashara zinazofanya shughuli zake nchini bali huamuliwa kwa kuzingatia misingi ya soko, ikiwamo kiwango cha mfumuko wa bei, vihatarishi vya mikopo kutolipwa, gharama za uendeshaji wa benki husika pamoja na kiwango cha faida wanacholenga kupata.

“Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kisera na kiusimamizi na kuwezesha benki za biashara kutoa mikopo kwa riba nafuu zaidi ikiwemo kuendelea kutekeleza sera ya fedha inayolenga kudhibiti mfumuko wa bei, ambao ni moja ya kiashiria muhimu kinachotumika katika kukokotoa na kuamua riba inayotozwa kwenye mikopo na benki hizi za biashara’’, alifafanua Mhe. Luswetula.

 Alisema kuwa katika kufanikisha azma hiyo, Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kufanya mabadiliko katika kiwango cha Riba ya Benki Kuu (Central Bank Rate - CBR) kuendana na mwelekeo wa kiuchumi ili kuhakikisha kuwa mfumuko wa bei unabaki ndani ya wigo, huku ikiendelea kuhakikisha uwepo wa kiwango cha kutosha cha ukwasi kwenye uchumi ili kuchagiza upatikanaji wa mikopo kwa gharama nafuu.

Mhe. Luswetula aliongeza kuwa Serikali imeanzisha mfumo wa ulinganishi wa bei unaojulikana kama Price Comparator System unaongeza uwazi kuhusu viwango vya riba na gharama zinazotozwa na taasisi mbalimbali za kifedha, na hivyo kuwasaidia wakopaji kufanya maamuzi sahihi kuhusu huduma za mikopo wanazozihitaji. Vilevile, mfumo huo unachochea ushindani miongoni mwa benki za biashara, jambo linaloweza kuchangia kupungua kwa gharama za mikopo kwa wananchi.

Mhe. Luswetula alisema kuwa hatua nyingine zilizochukuliwa ni pamoja na kuendelea kuhimiza benki na taasisi za fedha kutumia kanzidata ya taarifa za wakopaji (Credit Reference Bureau), ambayo hutoa taarifa za historia ya ukopaji na ulipaji wa madeni ya wakopaji. Mfumo huu hupunguza wasiwasi wa benki kuhusu vihatarishi vya mikopo kutolipwa, hivyo kusaidia kupunguza gharama za tathmini ya mikopo.



 Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa Tanzania ina dhamira ya kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo na Serikali ya Jamhuri ya Comoro, ili kuleta manufaa ya pamoja kwa wananchi wa nchi hizo mbili.

Mhe.  Balozi Omar, amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Bajeti na Sekta ya Benki wa Comoro, Mheshimiwa Moussa Abderemane, kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha Jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa ushirikiano wa kiuchumi unapaswa kuwa kitovu cha juhudi za kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Comoro na kuyataja maeneo yenye fursa kubwa za ushirikiano kuwa ni pamoja na biashara na uwekezaji, huduma za kifedha na kibenki, usimamizi wa fedha za umma, maendeleo ya miundombinu, nishati, utalii na kilimo.

Mhe. Balozi Omar alisisitiza umuhimu wa kuweka mazingira rafiki yatakayorahisisha usafirishaji wa bidhaa, huduma, mitaji na wafanyabiashara kati ya nchi hizo mbili na kwamba  hatua hiyo inaweza kusaidia kuongeza biashara, uwekezaji na ajira.

Pia, alisema kuwa kikao hicho kilikuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu na mbinu bora katika usimamizi wa uchumi, fedha za umma, ukusanyaji wa mapato ya ndani na ujenzi wa uchumi imara unaojumuisha wananchi wote.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha, Bajeti na Sekta ya Benki wa Comoro Mheshimiwa Moussa Abderemane, aliishukuru Tanzania kwa kuwa mshirika muhimu wa maendeleo ya nchi yake katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Alisema kuwa lengo la ziara yake nchini Tanzania, akiambatana na ujumbe wake, lilikuwa kujifunza namna Tanzania ilivyopiga hatua kubwa ya matumizi ya mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya Serikali.

Aliahidi kuwa watayatumia matokeo ya ziara yake hapa nchini kuboresha mifumo yao ya ukusanyaji mapato ya Serikali kwa kutumia TEHAMA na mifumo ya kodi hatua itakayochochea zaidi ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Balozi wa Comoro nchini Tanzania,Mhe. Ahamada Elbadaoul Mohamed fakih, Mkurugenzi wa Masoko wa Kanda wa Kampuni ya SoftNet Technologies Bw. Maharage Chande, na viongozi wengine kutoka Tanzania na Comoro.









Pasi na shaka, kupata ajira katika nyakati za leo ni hatua inayotoa matumaini makubwa ya kujenga maisha na kujikimu kimaisha. 

Hata hivyo, pale ambapo kila kazi unayopata inaingia mkosi na kukatika ghafla kabla hata hujakamilisha miezi mitatu, maisha hugeuka kuwa mfululizo wa aibu, simanzi, na mahangaiko yasiyo na majibu.

Kwa zaidi ya miaka minne, nilipitia mtihani huu mgumu na wa ajabu katika ulimwengu wa ajira. 

Nilibahatika kupata kazi katika makampuni na taasisi mbalimbali, lakini kila nilipoanza kufanya kazi, mambo yalibadilika ghafla na kuwa meusi pindi tu mwezi wa tatu ulipowadia.

​Bila kufanya kosa lolote la nidhamu au uzembe wa kazi, mabosi wangu walianza kunichukia bila sababu, kunipazia sauti mbele ya wafanyakazi wenzangu, na hatimaye kunikabidhi barua za kufukuzwa kazi au kusitishiwa mkataba ghafla.

Nilibaki nikishangaa na kulia kwa uchungu, kwani hata pale nilipojitahidi kufanya kazi kwa juhudi kubwa kuliko kila mtu, matokeo yalikuwa ni kuonyeshwa mlango wa kutokea.

Ndugu na marafiki walianza kunitenga na kuniona kama mtu mwenye gundu au asiye na nidhamu, huku nikibaki bila kipato chochote na nikikabiliwa na madeni kila mwezi. SOMA ZAIDI.
Kusoma kwa bidii, kupata shahada ya chuo kikuu, na kuwa na sifa zote za taaluma ni hatua kubwa ya kujenga maisha, lakini pale unapoingia kwenye usaili wa kazi (interview) zaidi ya mara kumi kisha unafeli kila mara, moyo hukata tamaa kabisa.

Kwa miaka mitatu baada ya kumaliza masomo yangu, nilikuwa nikisaka ajira bila mafanikio. Kila nilipotuma maombi ya kazi, niliingia kwenye orodha ya wasailiwa (shortlist), lakini kila nilipofika kwenye chumba cha usaili, mambo yote yalibadilika na kuwa meusi.

​Ingawa nilikuwa na uwezo mkubwa wa kujibu maswali na vyeti vyangu vilikuwa na ufaulu wa juu, jopo la wasaili lilinichukulia kwa dharau na kuonyesha kutonipenda kabisa bila sababu ya msingi.

Nilipitia usaili zaidi ya mara kumi kwenye makampuni na mashirika tofauti, lakini kila matokeo yalipotoka, jina langu halikuwepo.

Nilibaki nikitazama wenzangu waliokuwa na ufaulu mdogo wakipata kazi za mshahara mkubwa, huku mimi nikibaki mtaani nikichekwa, nikitegemea pesa za wazazi, na kupata msongo mkubwa wa mawazo.SOMA ZAIDI.
Fugaji wa mifugo ni nguzo kuu ya uchumi wa familia nyingi, na ng’ombe wa maziwa mara nyingi ndio tegemeo la pekee la kuingiza kipato cha kila siku na kulipa ada za watoto.

Hata hivyo, pale unapoamka asubuhi na kukuta banda lako lipo wazi, nyayo za ng’ombe zikielekea kusikojulikana, maisha hugeuka kuwa simanzi na mshangao mkubwa.

Kwa miaka mitano, nilikuwa msumbufu wa kujenga mradi wangu wa ng’ombe wanne wa maziwa waliokuwa wananiingizia kiasi kizuri cha fedha kila siku.

​Usiku mmoja wa mvua kubwa, majambazi na wezi wa mifugo walivunja kufuli za banda langu na kuondoka na ng’ombe wote wanne bila mtu yeyote kusikia kishindo. Asubuhi nilipofika bandani, nilikuta patupu.

Nilibaki nikilia kwa uchungu na kupiga yowe, kwani hiyo ndiyo ilikuwa tegemeo langu pekee la maisha. Nilitoa taarifa kituo cha polisi na kuzunguka minada mbalimbali ya mifugo kwa siku tatu bila mafanikio yoyote.

Ndugu na majirani wote walianza kunipiga msiba, wakiamini ng’ombe hao tayari walikuwa wameshachinjwa au kuuzwa mbali mno. SOMA ZAIDI.


JUHUDI za wananchi wa kitongoji cha Lailupa katika Kijiji cha Meirugoi Kata ya Gelai-Meirugoi wilayani Longido Mkoani Arusha za kujitoa na kujenga darasa la shule ya awali {chekechea} kwa gharama ya shilingi milioni 12 kumemuibua Mbunge wa Jimbo hilo Dkt Steven Kiruswa kuamua kumalizia ujenzi wa darasa hilo kwa gharama zake binafsi za kiasi cha shilingi milioni 6.

Akizungumza nasi ,Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nailupa Ndung’anak  Mepukor alisema wananchi wa Kitongoji hicho walimsimamisha Kiruswa ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini aliyekuwa akielekea kata nyingine kukagua miradi ya maendeleo kutembelea darasa hilo na kujionea mwenye watoto wakipata elimu chini ya mti bila kujali jua wala mvua.

Mepukor alisema jitihada za ushawishi wa akina mama ,vijana ,viongozi wa Milla maarufu kwa jina la Laigwanani ulimfanya Mbunge kwenda kutembelea darasa hilo ambalo bado lilikuwa halijakamilika kwa kukosekana mlango mmoja,madirisha sita ,bati 60 ,madawati 20,mbao,madawati 20 na umaliziaji wa kupiga Plasta hatua iliyomfanya mbunge kubeba gharama hiyo kwa gharama ya kiasi hicho cha fedha cha shilingi milioni 6

Mwenyekiti alisema ujenzi wa darasa hilo uliofanywa na wananchi hao umetokana na michango ya kila kaya kwa fedha taslimu na uuzwaji wa mifugo kwa kila kaya na kujitoa kwa uchimbaji wa msingi na ujenzi wa darasa sambamba na ubebaji wa matofali kwa kila mwananchi wa kitongoji hicho ili watoto waweze kusoma ndani ya darasa hilo wakiwa wameketi kwenye madawati.    

‘’Tulijitahidi hadi kufikia hatua hiyo na Mbunge Kiruswa kukubali tu kufika kuona hali halisi ya watoto kusomea chini ya mti na kuona jitihada za wananchi katika ujenzi wa darasa hilo ameamua kumalizia kila kitu kwa gharama zake’’alisema Mepukor

Akizungumza katika mara baada ya kuahidi kumalizia hatua iliyobaki ,Kiruswa alisema kwa kuwashukuru wananchi hao kwa kujitoa na kufanikisha ujenzi wa darasa hilo na kusema kuwa hatua hiyo imempa faraja kubwa sana na yeye kuamua kuchangia na kumamilisha ujenzi wa darasa ili watoto waweze kusoma karibu na makazi na kuondoka na kutembea umbalim mrefu kufuata elimu.

Kiruswa alisema jukumu la kutaka watoto kusoma na kupata elimu bora ni la kila mwananchi wa Jimbo la Longido na sehemu kubwa inayofanywa na serikali inapaswa kuungwa mkono na wananchi na kilichofanyika katika kitongoji cha Lailupa ni kitendo kinachopaswa kupongezwa na kuungwa mkono na yeye na Halmashauri ya wilaya ya Longido.

Alisema jukumu lake la pili ni kuhakikisha shule hiyo ya awali inasajiliwa na kupata mwalimu mwenye sifa tofauti na sasa mwalimu anayewafundisha ni wa kujitolea na asiyekuwa na sifa na jukumu hilo linabebwa na yeye na hadi mwakani januari kila kitu kinapaswa kukamilika ili watoto wasomeshwe na mwalimu mwenye sifa shule kutambuliwa na serikali.

Naye Diwani wa Kata ya Gelai Meirugoi,Daniel Nasinda alisema kuwa watoto wa Kitongoji cha Lailupa hutembea umbali wa zaidi ya km 10 kwenda na kurudi kusaka elimu hatua ambayo ni hatari kwao kwa kuwa na eneo hilo lina wanyama wakali na ndio maana wazazi walijitoa kujenga darasa ili iwe salama kwa watoto wao kwenda shule.














Amani ya akili na hisia za usalama ndizo zinazomfanya mwanadamu aishi kwa furaha, lakini pale unapoanza kuhisi unachunguzwa, kufuatiliwa, au kutazamwa na viumbe au watu usioshuhudia kwa macho, maisha hugeuka kuwa ndoto ya kutisha.

Kwa zaidi ya miezi sita, nilipitia mateso makubwa ya kisaikolojia na kiroho. Kila nilipokuwa nyumbani peke yangu, chumbani, au hata nikitembea barabarani, nilihisi uwepo wa mtu au kitu kilichokuwa kikinitazama kwa karibu sana.

​Nilianza kusikia sauti za kunong’ona masikioni, vishindo vya hatua za watu usiku wa manane mlangoni, na hisia za mtu kusimama nyuma yangu kila nilipokuwa nikifanya kazi zangu.

Hofu ilitawala maisha yangu; nilishindwa kulala usiku, nikakosa amani ya kula, na hata kufanya kazi zangu za kila siku ikawa mtihani mkubwa.

Nilitembelea madaktari wa afya ya akili na kutumia dawa mbalimbali za kutuliza mfadhaiko, lakini hazikunipa matokeo yoyote. 

Kila siku iliyopita, hofu ilizidi kunisonga, nikihisi kama ninaenda kurukwa na akili au kifo kipo jirani kinanisubiri, huku ndugu zangu wakidhani nimeanza kupata wazimu. SOMA ZAIDI.
Kila mzazi anatamani kuona mtoto wake anafanya vizuri shuleni, anapata alama za juu, na kujenga msingi bora wa maisha yake ya baadaye. 

Hata hivyo, pale mtoto wako anapojitahidi kusoma lakini anashindwa kabisa kuelewa chochote darasani, maisha hugeuka kuwa chanzo cha msongo mkubwa wa mawazo kwa familia.

Kwa zaidi ya miaka miwili, mwanangu wa kiume alikuwa akipitia kipindi kigumu mno kielimu. Kila mtihani uliporudi, alikuwa akishika nafasi ya mwisho kabisa darasani, huku akipata alama za sifuri kwenye kila somo.

​Walimu walianza kunipigia simu kila mara wakidai mtoto hana akili na hawezi kuendelea na masomo. Nilitumia fedha nyingi kumlipia walimu wa ziada (tuition) na kumnunulia vitabu vyote vya gharama kubwa, lakini hakuna kilichobadilika.

Kila alipokaa chini kusoma, alilalamika kupata maumivu makali ya kichwa, Usingizi mzito ulimshika, au akili yake ilipotea kabisa na kutosikia kile mwalimu anachofundisha.

Nilibaki nikilia kwa uchungu, nikiona ndoto na siku zijazo za mwanangu zikitokomea, huku nikipata aibu kubwa mbele ya wazazi wenzangu waliokuwa wakijivunia maendeleo ya watoto pao. SOMA ZAIDI.
Ndoa ni safari ya upendo na kupeana furaha, lakini pale ambapo nyumba yenu inageuka kuwa uwanja wa vita na kelele za kila siku bila sababu ya msingi, amani ya nafsi hutoweka kabisa. Kwa zaidi ya miaka mitatu, mimi na mume wangu tuliaishi kwenye mateso makubwa ya migogoro.

Tulianza kugombana kwa vitu vidogo sana visivyo na msingi; jambo dogo tu liligeuka kuwa ugomvi mkubwa wa kutukanana, kuvunja vyombo vya ndani, na hata kupigana mbele ya watoto wetu na majirani.

​Furaha na upendo tuliokuwa nao mwanzoni mwa ndoa yetu vilitoweka ghafla na kubaki chuki nzito. Kila mume wangu aliporudi nyumbani, nilisikia uchungu na hasira mwilini mwangu bila kujua sababu, na yeye pia alikuwa akinitazama kwa jicho la udharau na ukali.

Njaa ya amani ilitutawala, watoto wetu walianza kuishi kwa hofu na msongo wa mawazo, na ndoa yetu ilikuwa ikielekea kwenye kuvunjika kabisa huku kila mtu akitafuta wanasheria wa kututenganisha.SOMA ZAIDI.

 


Na: OWM – TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara zinazoingia kwenye viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michezo na mazoezi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) jijini Dar es Salaam, huku wananchi wakifurahia hatua hiyo na kuipongeza Serikali kwa ujenzi wa miundombinu  itakayosaidia kutatua changamoto ya usafiri katika maeneo hayo.

Prof. Shemdoe amesema hayo Agosti 24, 2026, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu hiyo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, ikiwemo Kigamboni, Uwanja wa Taifa (Benjamin Mkapa), Leaders Club pamoja na eneo la Mbweni kuelekea Uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo.

Amesema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, akieleza kuwa ujenzi wa barabara za Kigamboni umefikia asilimia 75, barabara za Uwanja wa Taifa asilimia 20, Leaders Club asilimia 70, huku barabara za Mbweni kuelekea Uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo zikifikia asilimia 20. Kwa ujumla, Prof. Shemdoe amesema utekelezaji wa ujenzi wa barabara hizo umefikia wastani wa asilimia 50.

Prof. Shemdoe amesema ametoa maelekezo kwa wakandarasi katika maeneo yote yanayotekeleza miradi hiyo kuhakikisha wanaongeza kasi ya ujenzi na kufanya kazi kwa saa 24, ili kuongeza ufanisi na kuhakikisha ifikapo Agosti 30, 2026, utekelezaji unafikia wastani wa zaidi ya asilimia 60. 

Kwa upande wake, Mkazi wa Mbweni jijini Dar es Salaam na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Malindi Estate, Bi. Maria Bilia, amesema wananchi wa Mbweni wamefarijika kuona ujenzi wa barabara hizo ukiendelea, kwa kuwa utasaidia kupunguza changamoto ya usafiri katika eneo hilo.

Bi. Bilia amemuomba Prof. Shemdoe kufikisha salamu za pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuboresha miundombinu ya barabara kuelekea AFCON 2027.

Ameongeza kuwa ameshuhudia wakandarasi wakifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, hatua ambayo amesema inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Malindi Estate, Kata ya Mbweni, Manispaa ya Kinondoni, Bi. Selina Mkonye, amesema wananchi wa eneo hilo wanaunga mkono jitihada za Serikali kwa vitendo, ikiwemo kuwa na mpango mkakati wa miaka mitano wa ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 30 kwa kiwango cha lami na kilomita 60 kwa kiwango cha changarawe.

Bi. Mkonye amesema ujenzi wa barabara zinazotekelezwa kwa ajili ya maandalizi ya AFCON 2027 umekuja kuchagiza na kuimarisha mpango mkakati huo wa wananchi wa kuboresha miundombinu katika eneo lao.

Ujenzi wa barabara hizo unalenga kuboresha upatikanaji na mtiririko wa usafiri kuelekea viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michezo na mazoezi ya Fainali za AFCON 2027 jijini Dar es Salaam, sambamba na kuboresha miundombinu kwa manufaa ya wananchi.

Kwa sasa, miradi minne (4) inatekelezwa, ambayo ni ujenzi kwa kiwango cha zege wa Barabara ya Taifa yenye urefu wa kilomita 1.3, Litapwasi kilomita 0.43 na Sotele kilomita 0.2; ujenzi kwa kiwango cha zege wa Barabara ya Yanga yenye urefu wa kilomita 0.7; ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Dahomey yenye urefu wa kilomita 0.5; ujenzi wa Barabara ya Mbalizi yenye urefu wa kilomita 0.8, pamoja na uboreshaji wa maegesho ya VVIP katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo.


















Na Oscar Assenga, TANGA

BENKI ya NMB imesema uwekezaji katika elimu, ujuzi wa vitendo na ubunifu unaowawezesha Watanzania kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili nchi ni muhimu katika kufikia uchumi wa kipato cha juu.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Meneja Mwandamizi wa Maabara ya Ubunifu ya NMB, Maria Mwamyalla, alipokuwa akitoa salamu za wadhamini kwa niaba ya wadhamini wote katika maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yaliyofanyika mkoani Tanga.

Mwamyalla alisema kaulimbiu ya mwaka huu, “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” inaendana na mkakati wa NMB wa kuwekeza katika teknolojia, ubunifu, vijana na ujumuishaji wa kifedha.

Alisema kupitia Agenda 2030, benki hiyo imeweka teknolojia, ubunifu, uwekezaji kwa vijana na ujumuishaji wa kifedha kuwa sehemu muhimu ya mkakati wake wa ukuaji.

“Mwelekeo huo unaendana moja kwa moja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kujenga uchumi wa ushindani unaotumia maarifa, ujuzi na teknolojia,” alisema.

Alisisitiza kuwa teknolojia pekee haiwezi kuleta matokeo yanayotarajiwa bila kuwapo kwa watu wenye maarifa na ujuzi wa kuitumia ipasavyo.


NMB yawekeza Sh bilioni 2 kwa vijana

Mwamyalla alisema kupitia NMB Foundation, benki hiyo imeendelea kuwekeza katika elimu na malezi ya uongozi kwa vijana, hususan wanaotoka katika familia zenye uwezo mdogo kiuchumi.

Alisema kupitia programu ya Nuru Yangu Scholarship and Mentorship, NMB imewekeza zaidi ya Sh bilioni mbili tangu mwaka 2022, kwa ajili ya kuwafadhili wanafunzi 121 katika vyuo vikuu 11 nchini.

Kwa mujibu wa Mwamyalla, wanafunzi hao wamekuwa wakisaidiwa mahitaji mbalimbali yakiwamo ada, malazi na vitendea kazi kama kompyuta mpakato.

Alisema wanafunzi 21 tayari wameingia katika soko la ajira, huku wengine 42 wakitarajiwa kuhitimu mwaka huu.

“Tunatarajia kufungua dirisha la tatu la programu hii mwezi Septemba mwaka huu,” alisema.
Wabunifu wanufaika

Aidha, Mwamyalla alisema NMB inaendelea kutekeleza programu ya SEP kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Save the Children pamoja na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Alisema programu hiyo inalenga kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa kuwapatia vijana elimu ya vitendo katika maeneo mbalimbali, ikiwamo mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa na vyuo vya VETA.

Katika eneo la teknolojia na ubunifu, alisema NMB imewekeza zaidi ya Sh bilioni 232, huku sehemu kubwa ya suluhisho za kiteknolojia zikitengenezwa na wataalamu wazawa.

Alisema uwekezaji huo unalenga kujenga utaalamu wa Watanzania, kuimarisha usalama wa mifumo pamoja na kupunguza muda wa kupeleka bidhaa za kidijitali sokoni.

Alitaja miongoni mwa suluhisho hizo kuwa ni huduma ya NMB Mkononi, inayowawezesha wateja kupata huduma mbalimbali za kibenki kupitia simu zao za mkononi, ikiwamo kutuma na kupokea malipo ya kielektroniki.

Kwa mujibu wa Mwamyalla, huduma hizo zimechangia kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa zaidi ya wateja milioni 10 wa NMB.

Alisema kupitia programu ya PesaTek, iliyoanzishwa mwaka 2022, benki hiyo imezindua Innovation Sandbox na kuendelea kuwawezesha vijana pamoja na wabunifu katika sekta ya teknolojia kupima na kuendeleza suluhisho zao.

Mwamyalla alisema NMB itaendelea kushirikiana na Serikali na taasisi za elimu kuhakikisha elimu, ujuzi na ubunifu vinageuzwa kuwa suluhisho zinazochochea biashara na kuchangia maendeleo ya Taifa.

 


Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimeandika historia mpya mkoani Manyara kwa kuzindua rasmi utoaji wa programu Shahada (Degree) katika Kampasi ya Babati. 

Hafla hiyo ya uzinduzi wa 'Bachelor of Accountancy with Information Technology' na "Bachelor of Computer Science' imeongozwa leo Agosti 24, 2026 na Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo.

Mhe. Sillo amesema wahitimu wa programu hizo watakuwa sehemu ya kizazi kipya cha wabunifu watakaosadia kuimarisha matumizi ya Teknolojia katika sekta ya fedha, elimu, afya,biashara, kilimo, utalii, viwanda na utoaji wa huduma za serikali.

Mkuu wa Chuo IAA, Prof. Eliamani Sedoyeka amesema" hatua hii ni mkakati wa IAA kuunga mkono juhudi za Serikali kusogeza elimu bora kwa wananchi na kuhakikisha wanapata elimu inayokidhi mahitaji ya dunia ya sasa na baadaye".

Aidha, Prof. Eliamani Sedoyeka ametangaza kuwa wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza watapatiwa huduma ya hosteli bure  hatua inayolenga kupunguza gharama kwa wazazi na kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira salama na tulivu.

Kampasi ya Babati ilianza mwaka 2014 ikiwa na wanafunzi 272, sasa ina wanafunzi 728 na IAA  inalenga kuongeza idadi ya wanafunzi Babati hadi 6,000 ifikapo mwaka 2031.

Aidha, IAA inaandaa mkakati wa kuanzisha programu za  elimu inayozingatia ujuzi (skills-based curriculum) katika maeneo kama Kilimo biashara, Uchakataji wa chakula,Uchakataji wa ngozi,Uhandisi wa uchomeleaji.Lengo ni kuwaandaa vijana wenye ujuzi wa vitendo, kuongeza fursa za kujiajiri na kuajiriwa, na kuendana na mahitaji ya soko la ajira.