Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii leo Agosti 18, 2026 Bungeni Jijini Dodoma, imeipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Taasisi yake ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania(TAWIRI)

Kwa namna inavyofanya jitihada za kugundua mbinu mbalimbali za kupambana na kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu.

Pongezi hizo zimetolewa wakati kamati hiyo ikipokea  na kujadili taarifa ya Wizara ya Maliasili na Utalii ya utendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI). 

“ tunaona na kuthamini kazi nzuri ya Wizara kupitia TAWIRI kwa kufanya tafiti zilizosaidia kupata njia bora zinazoonesha matokeo chanya katika kudhibiti wanyama wakali na waharibifu” amesema Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Timotheo Mnzava

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameihakikishia Kamati kuwa , Wizara hiyo itaendelea kuziwezesha taasisi zake ili ziendelee kufanya kazi kwa  ufanisi na kufikia malengo yanayotarajiwa, 

“ Wizara na wataalamu wake wapo kazini kila wakati kuhakikisha changamoto zinazojitokeza zinapatiwa ufumbuzi wa haraka ili kuifanya Sekta ya Maliasili na Utalii kuendelea kuwa na mchango mkubwa katika ustawi wa wananchi na taifa kwa ujumla” amebainisha Dkt. Kijaji

Ikumbukwe mbali na jukumu la Kufanya, Kuratibu na Kusimamia tafiti za wanyamapori hapa nchini, TAWIRI inajukumu la kuishauri serikali juu ya masuala yote ya sayansi ya wanyamapori kwa uhifadhi endelevu, ustawi wa jamii na kukuza utalii.







Mkurugenzi Mtendaji wa BODI ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) , Bw. Asangye Bangu, akizungumza wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA

BODI ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imesema itaendelea kushirikiana kwa karibu na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri nchini ili kuimarisha utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS), kuongeza tija kwa wakulima na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, ameyasema hayo leo Agosti 18, 2026, wakati akizungumza na Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.

Bw. Bangu amesema utekelezaji wenye tija wa mfumo huo katika mikoa na halmashauri unahitaji ushiriki wa karibu wa Maafisa Biashara, hususan katika usimamizi wa shughuli zinazohusiana na maghala pamoja na minada ya mazao inayofanyika katika maeneo yao.

Amesema Maafisa Biashara wana nafasi muhimu katika kuhakikisha taarifa sahihi kuhusu mahitaji ya maghala katika maeneo yao zinapatikana, sambamba na kufuatilia hali, matumizi na uhitaji wa maghala katika halmashauri na mikoa ili kuwezesha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kutekelezwa kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano kwa Umma na Mawasiliano wa WRRB, Bw. Dionis Musseru, amesema utoaji wa elimu kwa umma umeendelea kuongeza uelewa na ushiriki wa wadau katika mfumo huo, ambapo hadi sasa mazao 11 yanauzwa kupitia WRS.

 


📌 Umeme wa JNHPP kufika Dodoma kupitia Chalinze

📌 SGR kupata njia yake maalum ya umeme, kuimarisha uhakika wa huduma


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, amesema Njia ya Kusafirisha Umeme ya Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma imekamilika hatua itakayowezesha umeme unaozalishwa katika Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) kufika Dodoma kupitia Chalinze.

Mramba ameyasema hayo leo, Agosti 18, 2026, wakati akikagua hatua za mwisho za utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Chalinze–Dodoma yenye urefu wa kilomita 345, pamoja na upanuzi wa Vituo vya Kupoza na Kusambaza Umeme vya Chalinze mkoani Pwani na Zuzu jijini Dodoma.

Amesema ujenzi wa njia hiyo umefikia asilimia 99, huku upanuzi wa Kituo cha Zuzu ukiwa umefikia asilimia 98 na kwamba wataalamu wamekamilisha maandalizi ya kuanza kuwasha njia hiyo.

“Kituo cha Zuzu kipo tayari katika hatua za mwisho kabisa. Wataalamu wamenieleza waatanza kuwasha kwa majaribio katika kituo. Umeme utaanza kufika Dodoma kutoka Bwawa la Julius Nyerere kupitia Chalinze hadi kufika Dodoma,” amesema Mramba.

Amesema kukamilika kwa njia hiyo ya kV 400 ni hatua muhimu katika kuimarisha mfumo wa usafirishaji wa umeme nchini, kwa kuwa itapokea umeme unaozalishwa katika Bwawa la Julius Nyerere na kuusafirisha kutoka Chalinze hadi Dodoma, ambako utaingizwa kwenye Gridi ya Taifa na kusambazwa kwenda maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Mramba amesema wanufaika wakubwa wa mradi huo ni Reli ya SGR, akifafanua kuwa njia ya umeme inayotumika kwa ajili ya SGR ilikuwa ikitumika pia kwa matumizi ya watumiaji wengine ambapo kukamilika kwa njia hiyo kutawezesha watumiaji wengine kuondolewa kwenye njia inayotumiwa na SGR, hivyo reli hiyo kuwa na njia yake ya umeme kwa matumizi yake.

Aidha, Mramba amesema utatuzi wa changamoto kama iliyotokea hivi karibuni ya kuzimika kwa Gridi ya Taifa ni kukamilika kwa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Chalinze hadi Dodoma, ambayo itawezesha kuwepo kwa utulivu na kuimarisha ubora wa umeme katika Gridi ya Taifa kwa kuwepo kwa umeme wa kutosha.

Amesema kwa sasa mradi huo ni miongoni mwa miradi muhimu kwa nchi, ambapo unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100 kwa takribani Shilingi bilioni 600, ukiwa ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kusafirisha umeme inayotekelezwa nchini.

Mramba ameeleza kuwa maeneo yatakayonufaika na njia hiyo ya umeme ni pamoja na mikoa ya Kanda ya Ziwa, ikiwemo Mwanza, Shinyanga, Tabora na Kigoma, pamoja na Singida upande wa magharibi. upande wa kaskazini, mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro itanufaika na umeme utakaosafirishwa kupitia njia hiyo.

Mramba amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha utekelezaji wa mradi huo pamoja na usimamizi wa Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi akieleza kuwa kukamilika kwake kutaongeza uwezo wa mfumo wa usafirishaji wa umeme nchini na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme yenye ubora na uhakika kwa wananchi.















NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeweka Viwango vya Chini vya Ufanisi wa Nishati (MEPS) kwa vifaa vinavyotumia umeme, hatua inayolenga kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya nishati na kuwasaidia wananchi kupata vifaa bora na vyenye ufanisi mkubwa.

 




 Na Mwandishi wetu- IRINGA

Naibu  Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amewataka watu wenye ulemavu kutumia mikopo inayotolewa na Serikali kama fursa ya kujikwamua kiuchumi na kubadili maisha yao, badala ya kuichukulia kama msaada au hisani.


Naibu Waziri aliyasema  hayo katika Ofisi za Mkoa wa Iringa, wakati wa ziara yake ya kutoa elimu kwa watu wenye ulemavu kuhusu fursa mbalimbali zinazopatikana kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi na kijamii.

Amesemalisema  Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa watu wenye ulemavu kupata mikopo na fursa nyingine za kiuchumi, huku akibainisha kuwa kiasi kikubwa cha fedha tayari kimetolewa kwa wanufaika nchini.



“Hadi sasa watu wenye ulemavu Nchi nzima  wameshakopa shilingi Bilioni 26.8 huvyo tunapaswa kushukuru na kuipongeza Serikali kwa mikakati mizuri kuhakikisha Kundi hili linafikiwa na sisi kama watu wenye ulemavu tuchangamkie fursa hihi ya mikopo tujiinue kiuchumi na tuwe waaminifu kurejesha ili kuwawezesha na wengine,”Alieleza Mhe. Ummy.

Mhe. Ummy Alieleza kwamba  ongezeko hilo ni ishara kuwa watu wenye ulemavu wameanza kutambua na kutumia fursa zinazotolewa kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi, hivyo kuwataka kuendelea kujitokeza na kutumia fursa hizo .

"Mafanikio ya baadhi ya watu wenye ulemavu waliopata mikopo yanapaswa kutumika kama mfano na kuwahamasisha  wengine kuchangamkia fursa hii ya mikopo kwani wapo wenye ulemavu wengi wamenufaika hatimaye kupungua wimbi la utegemezi katika familia hata Taifa," Alisisitiza.


Aidha Waziri Ummy aliitaka  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kujitathmini katika utoaji wa mikopo kwa watu wenye ulemavu akibainisha kuwa kiwango kilichotolewa katika manispaa hiyo

bado ni kidogo ikilinganishwa na mahitaji yaliyopo huku akiwapongeza watu wenye ulemavu wanaofanya shughuli zao kama vile kiwanda cha kufyatua matofali Kata ya Nduli, duka la jumla la mahitaji ya nyumbani, mnufaika wa mikopo aliyenunua bajaji ya baishara na wafanyabiashara wadogo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

“Serikali za mitaa zinapaswa kuhakikisha fursa za mikopo zinawafikia walengwa, huku wakitenga pia maeneo maalumu ambayo watu wenye ulemavu watafanya  shughuli za uzalishaji na biashara biashara zao bila kusumbuliwa,” Alibainisha.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Benjamini Sitta alisema Serikali imefanya jitihada kubwa kuhakikisha inatatua changamoto ya mikopo kwa wenye ulemavu kutoka utaratibu wa kukopa kwa vikundi wa awali  hadi mtu mmoja mmoja.

Awali akitoa taarifa ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ya Utoaji wa mikopo kwa vijana, wanawake na wenye ulemavu  kwa kipindi cha mwaka 2024/2025 hadi 2025/2026, Afisa Maendeleo ya Jamii ambaye ni Mratibu wa mikopo Bi. Sunday Mtamakaya alieleza kuwa vikundi 183 vimepatiwa mikopo wakiwemo wanawake, vijana na wenye ulemavu.

“ Halmashauri imefanikiwa kuwawezesha wenye ulemavu mitaji, wana vikundi kuboresha hali za maisha yao na baadhi ya wanavikundi kuwaajiri watu wengine katika biashara zao. Licha ya mafanikio hayo bada ya kurejeshwa utaratibu wa mikopo bado kuna changamoto ya baadhi yao kushindwa kuejesha mikopo hiyo kwa uaminifu,” Alisema Afisa Maendeleo huyo.


Naye  Mnufaika wa mikopo hiyo mwenye ualbino  Bwa. Issa Iddi Sogoi ambaye anamiliki duka la jumla la mahitaji ya nyumbani  katika Halmashauri hiyo alimshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoonyesha upendo, kujali na kuwaunga mkono watu wenye ulemavu kupitia mikopo hatua inayomsaidia kumudu mahitaji ya familia na kujiongezea kipato ambapo pia ametoa ajira kwa vijana wengine.






NA DENIS CHAMBI, TANGA.


WASHINDI  kupitia maonesho ya  Elimu ujuzi na ubunifu yanayoendelea kufanyika  kitaifa mkoani Tanga  wanatarajiwa kuiwakilisha Tanzania katika maonesho ya kidunia  kwenda kuonesha ujuzi ,ubunifu na maarifa yao.


Hayo yameelezwa na  katibu mtendaji kutoka baraza la Taifa la elimu  ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET) Mwajuma Lingwanda wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho hayo ambapo amesema jumla ya washiriki 49  waliopatikana kwenye mchujo uliofanyika katika ngazi ya Kanda watashindanishwa  kwenye vipengele 9 ambapo kila  mshidi atakata tiketi ya kwenda kuiwakilisha Tanzania kimataifa.

"Mashindano haya yalianza katika ngazi ya Kanda ambapo tulikiwa na washiriki  katika maeneo 9 ya ujuzi  na baada ya hapo tumefikia kwenye maonesho ya kitaifa na tuna washiriki 49 kutoka kwenye taasisi mbalimbali waamuzi wako tayari  wale watakaofanikiwa kufaulu na kuwa washindi wa kwanza  watapata nafasi ya kushiriki kwenye mashindano ya kimataifa  mwaka huu"amesema Lingwanda.


Fani hizo zitakazoshindaniwa ni pamoja na mapishi , mekatroniksi, ujenzi, ujuzi wa mitandao,  uchomeleaji wa vyuma , uhandisi, ushonaji wa nguo, na urembo.

Akizungumza Mkurugenzi  mdhibiti ubora kutoka NACTVET Geoffrey Oleke amesema kuwa  ujuzi katika nyanja mbalimbali ni una umuhimu husasani kwa rika la vijana ambao ndio tegemeo na Taifa la kesho hivyo Taifa linapaswa kuwekeza katika elimu ya sayansi.


Amesema mchakato wa kuwapata washiriki wa maonesho hayo ulianza juni 2026 ambapo vyuo vyote vya sayansi vilishiriki katika mchakato katika fani 15 ambapo kati ya hizo  fani 9 zilipata washiriki wengi hivyo kupewa kipaumbele kwa washiriki wa mwaka huu kitaifa ambapo kila fani ina washiriki watano watakaochuana kuonyesha maarifa na ujuzi wao.


"Bila ujuzi kwa Hakika hakuna nchi inaweza ikaendelea kwahiyo na sisi kama nchi tunashiriki kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunakuza ujuzi wa vijana wetu katika shule za sekondari na vyuo ili tupate nguvu kazi iliyo imara ambayo itaisaidia nchi yetu katika kuchochea maendeleo yake" amesema  Oleke.


Maonesho hayo ambayo kwa mwaka huu wa 2026 yamebebwa na kauli mbiu isemayo Elimu ujuzi na ubunifu , njia ya kufikia dira 2050 yameanza kufanyika August 16 yakifunguliwa  rasmi na waziri wa elimu Prof. Adolfu Mkenda huku yakitarajiwa kufungwa August 24 na waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba




NA DENIS CHAMBI, TANGA.


TAASISI za elimu zilizopo hapa nchini zimetakiwa kuendana na  dira ya Taifa ya 2050  katika kupitia masomo tafiti na ujuzi mbalimbali wanaoutoa kwa wanafunzi  wanaosoma ngazi mbalimbali ili kuendana na maendeleo ya teknolojia..


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani wakati alipotembelea na kukagua maandalizi ya maonesho ya wiki ya kitaifa ya Elimu ujuzi na ubunifu yanayoendelea katika viwanja ya shule ya sekondari Usagara ambapo yanayotarajiwa kuzinduliwa rasmi na waziri wa elimu Prof Adolfu Mkenda  17 august 2026.


Dkt.Buriani amesema kuwa Kila taasisi  za elimu Zina wajibu wa kuwaelimisha wananchi juu ya mwelekeo wa kitaifa wa dira ya 2050 ili kutoa ufahamu juu ya malengo ya serikali katika maendeleo  kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo za kielimu.


kaimu mkuu wa kitengo Cha mawasiliano na masoko kutoka katika chuo cha maji  kilichopo mkoani Dar es salaam chini ya wizara ya maji Godfrey Kituli wakati akizungumza na Msumba Blog katika maonesho ya Elimu , sayansi na ubunifu yanayoendelea kufanyika kitaifa mkoani Tanga ambapo ameeleza kuwa katika kuunga mkono jitihada za serikali juu ya umuhimu wa utunzaji wa vyanzo vya maji wameweza kupanda miti zaidi ya 1500 katika chuo hicho.


"Kumekuwa na uharibifu wa vyanzo mbalimbali vya maji  kutokana na shughuli za kibinadamu  tunaendelea kufanya tafiti na kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha vyanzo vya maji  vinalindwa na kutunzwa, tunaiunga mkono moja kwa moja  serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu juu ya utunzaji wa mazingira hususani vyanzo vya maji vinavyowazunguka katika maeneo yao". Amesema Kituli.


Maonesho hayo ambayo yanajumuiaha zaidi ya taasisi 300  kwa mwaka 2026 yamebebwa na kauli mbiu isemayo Elimu , ujuzi na ubunifu njia  ya kufikia dira ya 2050 yanatarajiwa kufungwa rasmi august 24 na waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba.

Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS, Bw.Habakuki Kalebo,akiwasilisha mada wakati wa kikao kilichoandaliwa na BRELA cha Maafisa Biashara pamoja na Wakuu wa Idara za Viwanda na Biashara kinachofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA 

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limesisitiza umuhimu wa kusajili maeneo yote yanayohusika na uuzaji, usambazaji na uhifadhi wa bidhaa za chakula na vipodozi, likieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na bora, kulinda afya zao.

Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS, Bw.Habakuki Kalebo, amesema hayo wakati wa kikao kilichoandaliwa na BRELA cha Maafisa Biashara pamoja na Wakuu wa Idara za Viwanda na Biashara, akieleza kuwa TBS inashirikiana na Ofisi ya Rais–TAMISEMI kupitia mamlaka za serikali za mitaa katika kusimamia usajili wa maeneo hayo.

Kalebo amesema usajili huo unalenga kuhakikisha bidhaa zinazouzwa, kusambazwa au kuhifadhiwa ni salama, bora na zimethibitishwa na TBS, huku mazingira yanayotumika kuhifadhi na kuuza bidhaa yamekidhi masharti ya usalama na usafi. Amesema kwa bidhaa za chakula, hatua hiyo inasaidia kuzuia uchafuzi kwa kuhakikisha chakula hakihifadhiwi au kuchanganywa na bidhaa nyingine zinazoweza kuhatarisha ubora wake.

Aidha, amesema usajili huo unasaidia kudhibiti usalama wa vipodozi vinavyoingizwa sokoni, kwa kuhakikisha havina viambata vyenye madhara kwa watumiaji. Ameongeza kuwa ukaguzi katika maeneo hayo pia husaidia kubaini na kuondoa bidhaa zilizomaliza muda wake kabla hazijawafikia wananchi, hivyo kupunguza hatari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya bidhaa zisizofaa.

 "Mfumo wa usajili pia una umuhimu katika ufuatiliaji wa bidhaa sokoni, kwani pale changamoto inapojitokeza, TBS inaweza kubaini bidhaa husika zilipo, kiasi kilichopo na kuchukua hatua za haraka za kuziondoa sokoni. Amesema utaratibu huo unaimarisha udhibiti wa bidhaa na kuongeza uwezo wa Serikali kulinda afya na usalama wa wananchi."amesema Bw.Kalebo 

Amesema ushirikiano kati ya TBS, Maafisa Biashara na Mamlaka za serikali za mitaa ni muhimu katika kuhakikisha wafanyabiashara wanaelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria na Viwango vya bidhaa. 

Kalebo amesisitiza kuwa ulinzi wa afya ya wananchi unapaswa kuwa sehemu muhimu ya usimamizi wa biashara, akieleza kuwa mtu mwenye afya njema ana uwezo mkubwa wa kushiriki katika shughuli za uzalishaji na kuchangia uchumi wa taifa.

Amesema matumizi ya bidhaa salama hupunguza hatari za magonjwa na gharama za matibabu, hivyo usajili na udhibiti wa maeneo ya biashara ya chakula na vipodozi ni hatua muhimu katika kulinda afya ya jamii na kuongeza tija ya Taifa.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, amesema ushirikiano kati ya Serikali, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania na wadau mbalimbali ni muhimu katika kugeuza ubunifu, teknolojia na utafiti kuwa chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Dkt. Kida amesema hayo kuelekea Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026, inayotarajiwa kufanyika Agosti 31 hadi Septemba 4, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.



Amesema jukwaa hilo litasaidia kuunganisha mawazo bunifu, utafiti, teknolojia, sera, mitaji, masoko na uwekezaji, ili kuchochea suluhisho zenye kuongeza tija, kuzalisha ajira na kuboresha maisha ya wananchi.

“Hatuhitaji ubunifu unaobaki katika mawazo au maabara. Tunahitaji kuugeuza kuwa bidhaa, huduma na suluhisho zinazoongeza tija, kuzalisha ajira, kuvutia uwekezaji na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Dkt. Kida.

Aidha, Amesema ushirikiano wa Serikali, sekta binafsi, taasisi za elimu na utafiti, wabunifu, wajasiriamali, wawekezaji na washirika wa maendeleo utakuwa muhimu katika kujenga mazingira yatakayowezesha mawazo bunifu kufikia hatua ya utekelezaji na soko.

Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026, yenye kaulimbiu “Kutoka Kwenye Matarajio hadi Mabadiliko; Kutumia Ubunifu katika Kuelekea Tanzania yenye Ustawi wa Pamoja,” itajumuisha mijadala ya kisera, maonesho ya ubunifu, shughuli za vijana na majadiliano ya uwekezaji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo anatarajiwa kuzindua Jukwaa hilo, litakalohusisha mjadala wa Mawaziri kuhusu Ubunifu na Utekelezaji, utakaojadili namna ubunifu na teknolojia vinavyoweza kuimarishwa katika mipango na utekelezaji wa maendeleo ya Taifa.

Unaweza kujisajili sasa kupitia https://summitpoint.co.tz/events/iwtz-2026




SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeteketeza tani 39 za bidhaa za chakula zisizokidhi matakwa ya viwango, zenye thamani ya takribani Sh milioni 149, ikiwa ni hatua ya kuwalinda wananchi dhidi ya matumizi ya bidhaa zisizo salama.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kugungua Mkutano wa Kati ya Wizara na Wakuu wa Sehemu na Idara za Viwanda,Biashara na Uwekezaji katika Sekretariet za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kinachofanyika kuanzia leo Agosti 17 hadi 18 jijini Dodoma.

............

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amewataka Maafisa Biashara nchini kutumia nafasi zao kikamilifu kuibua fursa za uwekezaji, kuongeza thamani ya mazao na kuboresha mazingira ya biashara katika halmashauri, hatua inayolenga kuchochea maendeleo ya kiuchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Londo ametoa kauli hiyo leo Agosti 17,2026 jijini Dodoma  wakati wa Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara nchini, kilicholenga kuimarisha utekelezaji wa majukumu yao katika kukuza biashara, viwanda na uwekezaji.

Amesema Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchumi wa viwanda katika Afrika Mashariki na Kati, ikiwamo kufikia uchumi wa dola trilioni moja na kuongeza kipato cha Mtanzania hadi dola 7,000. Amesema kufikia malengo hayo kunahitaji uchumi imara, jumuishi na shindani unaotegemea sekta binafsi, sayansi na teknolojia, uwekezaji, utafiti pamoja na nguvu kazi yenye ujuzi.

"Maafisa Biashara wana jukumu la kuhakikisha halmashauri zinakuwa vituo vya uzalishaji, uwekezaji na biashara kwa kutambua fursa zilizopo, kuwaunganisha wazalishaji na masoko na kuhakikisha mazao yanaongezwa thamani. "amesema Mhe.Londo

Hata hivyo ametolea mfano wa mahindi, amesema wakulima wanapaswa kusaidiwa kuondokana na kuuza mazao ghafi na badala yake kuzalisha bidhaa kama unga wenye chapa na kuufikisha kwenye masoko, hatua itakayoongeza kipato na kuchangia kupunguza umaskini.

Aidha, amesema utekelezaji wa Dira 2050 unahitaji vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kushirikishwa kikamilifu katika uzalishaji, uwekezaji na biashara kupitia fursa za mikopo na uwezeshaji. Amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026, viwanda vikubwa vipya 25 vilijengwa katika sekta mbalimbali na kutoa ajira 39,000, zikiwamo ajira 7,600 za moja kwa moja na 31,000 zisizo za moja kwa moja.

Katika kuimarisha mazingira ya uwekezaji, Londo amezitaka mikoa kuhuisha kanzidata za viwanda, biashara, masoko, leseni, wawekezaji na maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kiuchumi, huku kila halmashauri ikiandaa wasifu wa fursa za uwekezaji unaoonyesha upatikanaji wa malighafi, miundombinu, masoko na maeneo ya uwekezaji. Pia amewataka Maafisa Biashara kuhakikisha Mabaraza ya Biashara yanafanya kazi kikamilifu na hoja za sekta binafsi zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Londo amewataka Maafisa Biashara kuharakisha urasimishaji wa biashara zisizo rasmi kwa kutoa elimu kuhusu usajili wa biashara, leseni, TIN, viwango, vipimo na taarifa za umiliki.

Amesema urasimishaji utawawezesha wafanyabiashara kupata huduma za uwezeshaji, mitaji na masoko, huku akieleza kuwa halmashauri zimetengewa asilimia tano ya mapato ya ndani, yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 72 kwa mwaka wa fedha 2026/2027, kwa ajili ya kuwekeza katika miundombinu ya masoko, maeneo ya biashara na ujasiriamali.

Amesisitiza fedha hizo zitumike kwa ufanisi kwa kushirikisha sekta za ardhi, maji, nishati na barabara ili kuongeza tija kwa wafanyabiashara na kuvutia wawekezaji. Aidha, amewataka Maafisa Biashara kutumia nafasi zao kuboresha huduma na kuifanya Tanzania kuwa na mazingira bora zaidi ya biashara na uwekezaji, hatua ambayo ni muhimu katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum, amewataka Maafisa Biashara kuongeza udhibiti wa bidhaa feki na viwanda visivyo rasmi katika maeneo yao, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda afya na usalama wa wananchi, watumiaji pamoja na wazalishaji wanaofuata sheria.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa, amesema Maafisa Biashara ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wafanyabiashara katika kuhakikisha sera, sheria na kanuni za biashara zinatekelezwa na kuleta mabadiliko chanya katika mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Amesema kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, BRELA imeendelea kuboresha mifumo na sheria zinazosimamia usajili na utoaji wa leseni kwa lengo la kupunguza muda na gharama za kuanzisha na kuendesha biashara. Amesema kupitia BRELA Online System (ORS), huduma za wakala zimeunganishwa katika mfumo mmoja, huku mfumo huo ukiwezesha pia utoaji na usimamizi wa leseni za biashara kundi A na B.

Amesema mfumo huo unatoa fursa kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoa na kusimamia leseni za kundi B bila kuathiri mapato yao, kwani malipo yanayofanywa na mfanyabiashara yanaingia moja kwa moja katika akaunti ya halmashauri husika.

Aidha, ORS imeunganishwa na mifumo ya taasisi nyingine za Serikali ikiwamo NIDA na TRA, hatua inayowezesha taarifa muhimu kupatikana moja kwa moja bila mfanyabiashara kuwasilisha nyaraka ambazo tayari zipo kwenye mifumo hiyo.

Nyaisa,amesema kuwa  maboresho hayo yameongeza uwazi na ufanisi, kupunguza urudufu wa taarifa, muda na gharama za kupata huduma, pamoja na kupunguza mianya ya uzembe katika utoaji wa huduma.

"BRELA itaendelea kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara, Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI, sekretarieti za mikoa na halmashauri katika kuwajengea uwezo Maafisa Biashara."amesema Nyaisa

Amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, BRELA imepanga kutoa mafunzo kwa Maafisa Biashara wote nchini kupitia kanda nne, yatakayolenga matumizi ya mifumo, utoaji na usimamizi wa leseni pamoja na utekelezaji wa sheria.

Pia amesema BRELA itaendelea kuboresha miunganiko ya mifumo ya kidijitali na kushirikiana na vyama vya Maafisa Biashara katika kutatua changamoto zao, huku akisisitiza kuwa maafisa hao ni mawakala muhimu wa uwekezaji nchini na wanapaswa kutambua kuwa jukumu lao ni kuwezesha biashara, si kuikwamisha, ili kujenga mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji.