Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, ameipongeza Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kwa mchango wake katika kuwawezesha wakulima kupata masoko yenye ushindani kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Mhe. Chande ameyasema hayo leo Agosti 6, 2026, baada ya kutembelea banda la WRRB katika Maonesho ya 88 yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, jijini Dodoma.

Amesema WRRB imeendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha biashara ya mazao kwa kuwawezesha wakulima kupata masoko yenye ushindani, kuongeza thamani ya mazao yao na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Aidha, ameipongeza WRRB kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na kutoa wito kwa wadau wa sekta ya kilimo kuendelea kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya Maonesho ya Nane Nane ya mwaka 2026 isemayo, "Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," kwa kuimarisha mifumo ya masoko, kuongeza tija katika uzalishaji na kuhakikisha wakulima wananufaika na fursa zilizopo katika mnyororo wa thamani wa mazao.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu Huduma ,Bw. Mwita Thomas ameeleza kuwa WRRB itaendelea kuboresha huduma zake, kuimarisha usimamizi wa mfumo huo kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha sekta ya kilimo inakuwa chachu ya maendeleo ya uchumi na ustawi wa wananchi.

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (wa pili kutoka kushoto), akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Japhet Nkangaga kuhusu huduma zinazotolewa na TVLA, wakati alipotembelea banda la TVLA lililopo kwenye banda jumuishi la Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Kilimo ya NaneNane 2026 yanayoendelea kwenye Viwanja vya John Malecela, Nzuguni jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Prof. Mohammed Ali Sheikh.
DODOMA

Mfumo wa kuagiza mafuta kwa ajili ya matumizi ya miezi miwili inayofuata umeiwezesha Tanzania kuendelea kuwa na bidhaa za mafuta za kutosha, licha ya vita na changamoto nyingine zinazoathiri soko la dunia.

Mkurugenzi wa Uthibiti Ubora wa Shule, Dkt. Ephraim Simbeye,akizungumza wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali na visivyo vya Serikali pamoja na Waratibu wa Taaluma jijini Dodoma, leo Agosti 6, 2026, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,

Na.Mwandishi wetu-

Serikali imesisitiza kuwa ubora wa walimu wanaoandaliwa katika vyuo vya ualimu ndio utakaoamua mustakabali wa elimu nchini katika miaka ijayo.

Akifungua kikaokazi cha Wakuu wa Vyuo vya Ualimu vya Serikali na visivyo vya Serikali pamoja na Waratibu wa Taaluma jijini Dodoma, Agosti 6, 2026, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mkurugenzi wa Uthibiti Ubora wa Shule, Dkt. Ephraim Simbeye, amewataka Wakuu wa vyuo kuimarisha usimamizi wa mafunzo ili kuhakikisha wahitimu wanakuwa na umahiri, maadili na stadi zinazokidhi mahitaji ya Taifa.

Ameongeza kuwa vyuo vya Ualimu vina jukumu kubwa katika utekelezaji wa mtaala kwa kuhakikisha walimu wanaohitimu wanakidhi viwango hitajika.

Dkt. Simbeye ameeleza kuwa kikaokazi hicho kimefanyika katika kipindi muafaka baada ya kukamilika kwa mzunguko wa kwanza wa wahitimu wa Mtaala Ulioboreshwa wa Elimu ya Ualimu ulioanza kutekelezwa mwaka 2023 na kusema kuwa hatua hiyo inatoa nafasi ya kutathmini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji maboresho.

Kiongozi huyo amesema kuwa Wakuu wa Vyuo wanapaswa kuwa wabunifu katika matumizi ya rasilimali. Ushirikiano na sekta binafsi pamoja na kuanzisha miradi ya uzalishaji mali bila kuathiri utoaji wa elimu.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuzingatia miongozo ya Serikali katika utekelezaji wa mtaala, mafunzo kwa vitendo na utoaji wa mafunzo kwa njia ya masafa, ili kuhakikisha nchi inapata walimu wenye viwango vinavyofanana vya umahiri, maadili na uzalendo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu ya Ualimu na Mafunzo, Mathias Mvula, amesema lengo la kikao kazi hicho ni kubadilishana uzoefu uliopatikana katika utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa wa Elimu ya Ualimu.

Serikali imewataka wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali nchini kutumia elimu ya ushindani wa haki na ulinzi wa mlaji kama nyenzo ya kuongeza thamani ya bidhaa zao, kupanua masoko na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, alipotembelea banda la Tume ya Ushindani (FCC) katika Maonesho ya 33 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea jijini Nzuguni Dodoma.

Mhe Chande amesema elimu inayotolewa na FCC imekuwa na mchango mkubwa katika kuwajengea uwezo wazalishaji na wafanyabiashara kuzalisha bidhaa zenye ubora unaoweza kushindana katika soko la ndani na la kimataifa.

 "Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kujenga mazingira rafiki ya biashara yanayozingatia ushindani wa haki, fursa sawa kwa washiriki wa soko na ulinzi wa maslahi ya walaji. Msingi huo unachochea uwekezaji, huongeza tija katika uzalishaji na kuimarisha mchango wa sekta mbalimbali katika kukuza uchumi wa Taifa."amesema Mhe.Chande

Hata hivyo amewahimiza wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali kutumia kikamilifu elimu inayotolewa na FCC kwa kuzingatia sheria za ushindani, kuepuka vitendo vinavyopotosha soko na kujikita katika uzalishaji wa bidhaa bora zenye kukidhi mahitaji ya walaji.

"Hatua hiyo itaongeza thamani ya mazao, kuinua kipato cha wazalishaji na kufungua fursa zaidi za biashara ndani na nje ya nchi."amesema 

Aidha, Naibu Waziri huyo ameipongeza FCC kwa kuendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali katika kutoa elimu kwa umma kuhusu haki za walaji na ushindani wa haki, akieleza kuwa juhudi hizo zinaimarisha mazingira ya biashara yenye uwazi na usawa kwa manufaa ya wazalishaji na watumiaji wa bidhaa na huduma.

Amesisitiza kuwa Maonesho ya Nanenane yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwafikia wananchi moja kwa moja na kuwapa maarifa yatakayowawezesha kuongeza ubora wa mazao na bidhaa zao.

Ametoa rai kwa FCC kuendeleza kampeni za elimu nchini kote ili Watanzania wengi zaidi wanufaike na fursa zinazotokana na soko lenye ushindani wa haki na hivyo kuchangia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya uchumi wa Taifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Lindi tarehe 5 Agosti, 2026. Waziri Sangu aliwahakikishia wazee hao kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inathamini na kujali maslahi yao.
Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan na Yoweri Museveni wa Uganda wameshuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano (MoU) ya kuendeleza ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta na Kitovu cha Nishati cha Kikanda Jijini Tanga, mradi unaotarajiwa kubadili taswira ya sekta ya nishati Afrika Mashariki.
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewataka vijana wanaoshiriki mpango wa Kujenga kesho bora (Building a Better Tomorrow (BBT) kutumia fursa ya urasimishaji wa biashara ili kuongeza thamani ya shughuli zao za kilimo na ufugaji, hatua itakayowawezesha kushindana katika masoko ya ndani na nje ya nchini.

Wito huo umetolewa leo Agosti 6,2026 jijini Dodoma na Afisa Usajili wa BRELA, Bw. Yusuph Mwasakafyuka,wakati akitoa mafunzo kwa vijana wa BBT, wanaoshiriki katika Maonesho ya 33 ya Kimataifa ya Kilimo (nanenane) Nzuguni jijini Dodoma. “Urasimishaji wa biashara ni nguzo muhimu ya kuwajengea uwezo wa kufanya kilimo cha kisasa kinachozalisha tija, badala ya kuendelea na mifumo ya jadi isiyo na ushindani wa kibiashara”. Amesema Mwasakafyuka.

Aidha amewaeleza vijana hao kuwa; wanapaswa kutambua kuwa mradi wa BBT hauwalengi tu kuwapa ujuzi wa uzalishaji wa mazao na mifugo, bali pia kuwajengea msingi wa kuwa wajasiriamali wenye biashara rasmi zinazotambulika kisheria. Alieleza kuwa kuongeza thamani ya mazao huanza kwa kusajili biashara au kampuni ili kuwapa nafasi ya kupanua shughuli zao na kuvutia masoko pamoja na wawekezaji.

Amefafanua kuwa BRELA imewapatia washiriki hao elimu kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo, ikiwemo usajili wa majina ya biashara, usajili wa makampuni, upatikanaji wa leseni pamoja na usajili wa alama za biashara, hatua ambazo zitawawezesha kulinda bidhaa na huduma zao dhidi ya matumizi yasiyo halali.

Aongeza kuwa elimu hiyo inalenga kuwahamasisha vijana kuanza mapema urasimishaji wa biashara wanazotaka kushughulika nazozao ili wanapohitimu mafunzo na kuanza uzalishaji wa kibiashara wawe tayari kushiriki kikamilifu katika uchumi rasmi, kupata fursa za mikopo, masoko na ushirikiano na taasisi mbalimbali za kifedha. Kwa upande wake Afisa Usajili Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bw. Nassoro Mtavu, amewahimiza vijana wajasiriamali kutambua umuhimu wa kusajili alama za biashara na huduma ili kulinda bidhaa na huduma zao dhidi ya matumizi yasiyo halali.

Amesema usajili wa alama za biashara pamoja na ulinzi wa hataza ni nyenzo muhimu zinazowezesha wabunifu na wajasiriamali kunufaika na kazi zao, kuongeza ushindani sokoni na kujenga chapa zenye kuaminika ndani na nje ya nchi.

Aidha, amewasisitiza vijana hao kutumia huduma zinazotolewa na BRELA mapema ili kuhakikisha bunifu na biashara zao zinalindwa kisheria, hatua itakayochochea ukuaji wa biashara, kuvutia uwekezaji na kuongeza thamani ya bidhaa za Kitanzania. Aidha, BRELA imeeleza itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo na programu mbalimbali za kuwawezesha vijana ili kuhakikisha elimu ya urasimishaji wa biashara inawafikia wananchi wengi zaidi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kujenga uchumi shindani unaochochewa na biashara rasmi, ubunifu na ongezeko la thamani katika sekta ya kilimo.