Jina langu ni Bakari. Kwa muda mrefu, nilikuwa mtu wa kufanikiwa katika biashara na mambo yangu ya kifamilia, lakini ghafla mambo yote yalianza kuporomoka bila sababu za msingi.

Afya yangu ilianza kudhoofika kwa magonjwa ya ajabu yasiyorekodiwa vipimo vya hospitali, biashara yangu ikapoteza wateja wote, na migogoro isiyoisha ikaanza kuibuka nyumbani kwangu.

Nilijua wazi kuwa kuna maadui waliokuwa wakinitazama kwa jicho la husuda na kunirushia mishale ya kishirikina ili kunidondosha kabisa na kuniharibia maisha.

​Nikiwa kwenye majuto na hofu kubwa ya kupoteza kila kitu nilichochuma kwa jasho langu, mzee mmoja wa heshima katika kijiji chetu alinitembelea.

Baada ya kumsimulia mateso na majanga yaliyokuwa yakiniandama, alinieleza kwa huruma kuwa ulinzi wa kawaida hautoshi pale unapokabiliwa na maadui wenye roho mbaya na uchawi wa waziwazi. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Juma. Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikuwa nikiamka usiku wa manane nikiwa na jasho jingi na hofu kubwa baada ya kuota nikifukuzwa na wanyama wakali, watu waliojifunika nguo nyeusi, au kutumbukia kwenye mashimo marefu.

Mateso haya hayakuishia ndotoni pekee; mchana nilikuwa nikihisi uzito mkubwa mabega, maumivu ya kichwa yasiyoonekana hospitali, na kila mpango wangu wa maendeleo ulikuwa ukiharibika ghafla.

Nilibaki nikijitenga na watu, nikiteseka na vifungo vya kishirikina vilivyotaka kuniangamiza. Nikiwa kwenye majuto na kukata tamaa kabisa, ndugu yangu mmoja aliyekuwa akijua hali yangu alinitembelea.

Baada ya kushuhudia jinsi nilivyokuwa nikidhoofika kwa kukosa usingizi na amani, alinieleza kwa huruma kuwa maumivu na ndoto za namna hiyo ni ishara za wazi za vifungo vya giza na uchawi uliotegwa ili kuniharibia maisha. SOMA ZAIDI.
Kuhisi kuwa mpenzi wako anacheat huku akikana kwa sauti ya juu na kukuona kama unamsingizia ni jambo linaloumiza roho na kukosesha amani ya nafsi.

Kwa miezi mingi, nilikuwa nikiona mabadiliko makubwa kwa mwenzangu; simu zilifungwa maneno ya siri, alirudi nyumbani usiku wa manane akiwa na visingizio visivyo na msingi, na mapenzi yote na heshima kwangu vilipungua.

Kila nilipojaribu kumuuliza kwa ukweli, alipandisha hasira, kunifokea, na kunifanya nionekane mwenye wivu usio na maana. Hali hii iliniletea msongo mkubwa wa mawazo, nikiishi kwa hofu na wasiwasi huku nikitazama mahusiano yetu yakitumbukia kwenye shimo la usaliti.

​Nikiwa kwenye simanzi na nikitafuta njia ya kupata ukweli bila kuendelea kudanganywa na kuonekana mjinga, rafiki yangu wa karibu alinishauri kutafuta suluhisho la kienyeji badala ya kuendelea kugombana bila ushahidi.

Alinieleza kuwa wapo wataalamu wa kiasili wenye uwezo wa kufanya visomo vinavyoweza kumfanya mtu anayecheat afumanishe mwenyewe au kunaswa papo kwa papo bila kukana. SOMA ZAIDI.


Kizimkazi, Kusini Unguja — Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Hamisi Masanja Malebo, ameungana na viongozi wengine wa Wizara katika kumtembelea na kumpa pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 11 Septemba 2026 nyumbani kwa Rais Samia, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo ujumbe huo ulifika kutoa pole na faraja kwa Rais pamoja na familia yake katika kipindi hiki cha maombolezo.

Prof. Malebo, akiwa sehemu ya ujumbe huo wa viongozi, aliungana na viongozi wengine wa Wizara kuwasilisha salamu za pole kwa Rais Samia na familia yake kufuatia msiba wa Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 7 Septemba 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar.



Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaungana na Rais Samia, familia, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huo katika kipindi hiki cha huzuni na maombolezo.

Tume inatoa pole kwa Rais Samia na familia yake, huku ikiwaombea nguvu, faraja na moyo wa subira katika kipindi hiki cha majonzi.

Tume ya Taifa ya UNESCO inaendelea kuungana na familia katika kuomboleza msiba huo na kuenzi kumbukumbu ya Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.




GEITA: Kwa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu, kukosa ajira si lazima kuwe na maana ya kukosa kabisa fursa za kufanya kazi; wakati mwingine changamoto kubwa ni kukosa maarifa na ujuzi unaowawezesha kuzitambua na kuzitumia fursa zilizopo.

Hilo ndilo linalolenga kushughulikiwa na Mradi wa BRIDGE Tanzania, unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini, kwa kuwapatia vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu elimu ya msingi na ujuzi wa vitendo unaoweza kuwawezesha kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, vijana 210 tayari wamepatiwa mafunzo kupitia mradi huo, huku baadhi yao wakianza kutumia ujuzi walioupata katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, zikiwemo sabuni za miche, sabuni za maji na vyakula vya mifugo.


Mafunzo hayo pia yanahusisha kusoma, kuandika, kuhesabu na ujasiriamali, yakilenga kuwajengea vijana uwezo unaoweza kutumika katika maisha yao na katika mazingira ya soko.

Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya (District Steering Committee) ya Mradi wa BRIDGE Tanzania kilichofanyika Nzera, Geita, Mratibu Msaidizi wa Kitaifa wa mradi huo, Adriano Adrian Hyera, alisema hadi sasa vijana 210 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita wamepatiwa mafunzo.

Alisema mradi huo unaweka mkazo katika kuwapa vijana fursa ya kupata maarifa na ujuzi ambao unaweza kuwasaidia kujenga uwezo wa kujitegemea.


“Lengo si kuwapa vijana mafunzo pekee, bali kuwajengea uwezo ambao wataweza kuutumia baada ya mafunzo ili kujipatia kipato na kujitegemea,” alisema Hyera.

Kwa mujibu wa muundo wa mradi, vijana ambao hawakupata fursa ya kukamilisha elimu ya msingi hupewa nafasi ya kujenga uwezo katika kusoma, kuandika na kuhesabu, kabla ya kuendelea na mafunzo ya ujuzi wa vitendo unaoendana na mazingira yao na fursa zinazopatikana katika soko.

Mtazamo huo unaweka msisitizo katika kuunganisha elimu na ujuzi wa vitendo, ili kijana anapomaliza mafunzo asiishie kuwa na maarifa ya darasani pekee, bali awe na uwezo wa kutumia ujuzi huo katika shughuli za uzalishaji na kujiajiri.

Katika utekelezaji wake Geita, mradi unawawezesha vijana kujifunza kwa vitendo na pia unatoa vifaa na mahitaji muhimu kwa ajili ya mafunzo, ili kuwapa nafasi ya kufanya mazoezi ya uzalishaji wakati wa kujifunza.

Baadhi ya vijana walionufaika na programu hiyo wamesema mafunzo yamewajengea uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji na kuwapa mtazamo mpya kuhusu namna wanavyoweza kutumia ujuzi wao kama njia ya kujipatia kipato.

Ujuzi huo unawapa pia nafasi ya kutengeneza bidhaa ambazo zinaweza kutumika katika jamii na, kwa kuzingatia ubora na mahitaji ya soko, kuwa sehemu ya shughuli zao za kiuchumi.

Kutoka elimu ya msingi hadi ujuzi wa soko

Kwa mtazamo wa mradi, elimu na ujuzi haviwekwi katika maeneo mawili tofauti, bali vinaunganishwa ili kumjengea kijana uwezo wa kutumia maarifa yake katika mazingira halisi.

Baada ya kujenga msingi wa kusoma, kuandika na kuhesabu, kijana hupewa ujuzi wa vitendo unaozingatia eneo analotoka na fursa zinazopatikana katika soko.

Hii inalenga kuwapa vijana ambao hawakumaliza elimu rasmi nafasi ya kupata ujuzi unaoweza kuwasaidia kushindana katika shughuli za kiuchumi pamoja na vijana wengine waliopitia njia rasmi za elimu na mafunzo ya ufundi.

Kwa maana hiyo, BRIDGE Tanzania inalenga kujenga daraja kati ya elimu, ujuzi na soko, badala ya kuishia katika utoaji wa mafunzo pekee.

Vijana wahimizwa kutumia fursa za mikopo

Akizungumzia hatua zinazofuata baada ya mafunzo, Hyera aliwashauri vijana kujiunga katika vikundi vya watu watano ili waweze kuchangamkia fursa za mikopo zinazotolewa na Halmashauri.

Alisema ushiriki katika vikundi unaweza kuwasaidia vijana kutumia ujuzi walioupata katika shughuli za kiuchumi na kutafuta fursa za kukuza shughuli zao.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa mafunzo wanayopata vijana yanaunganishwa na fursa za mitaji na uzalishaji, ili kuongeza uwezekano wa ujuzi huo kuleta matokeo katika maisha yao.

Majaribio yenye matarajio ya kupanuka

BRIDGE Tanzania ni mpango wa majaribio unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Kaskazini A Unguja.

Mradi una lengo la kuwafikia vijana 3,000 katika kipindi cha miaka mitano, sawa na takribani vijana 600 kila mwaka.

Majaribio hayo yanatoa nafasi ya kutathmini namna ya kuwaunganisha vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu na elimu ya msingi, ujuzi wa vitendo na fursa za kiuchumi.

Matokeo na uzoefu unaopatikana katika maeneo ya utekelezaji utasaidia katika kutathmini namna mfumo huo unavyoweza kuimarishwa na, baada ya tathmini, kupanuliwa katika maeneo mengine nchini.

Tume ya UNESCO katika utekelezaji

Utekelezaji wa BRIDGE Tanzania unaenda sambamba na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuwawezesha vijana kupata maarifa, ujuzi na fursa za kushiriki katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa.

Kupitia Tume ya Taifa ya UNESCO, ushirikiano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini umegeuzwa kuwa fursa ya kuwafikia vijana ambao kwa sababu mbalimbali hawapo katika mfumo rasmi wa elimu.

Tume ya Taifa ya UNESCO, kwa jukumu lake la kuratibu, kutathmini na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za UNESCO nchini, inaendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kuhakikisha programu zinazotekelezwa zinachangia mahitaji na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania.

Kwa BRIDGE Tanzania, msisitizo ni kuhakikisha kijana aliye nje ya mfumo rasmi hapotezi fursa ya kujenga uwezo. Badala yake, anapewa nafasi ya kujifunza, kupata ujuzi na kuutumia katika kujenga maisha yake.

Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya kilichofanyika Nzera, Geita, kilitoa nafasi kwa wadau kupitia utekelezaji wa mradi, mafanikio, changamoto na hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kuongeza manufaa yake kwa vijana.

Kwa vijana hao 210 wa Geita, safari inaanzia katika kujenga msingi wa elimu na ujuzi; lakini lengo kubwa ni kuwawezesha kutumia uwezo huo katika ulimwengu halisi wa kazi, uzalishaji na kujitegemea. https://www.instagram.com/reel/DczGOqpqA74/?igsi=ZHVqMjQwemwyYTU=


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salumu, akiongoza ujumbe wa jumuiya hiyo kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Septemba 2026, kufuatia kufiwa na mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar, tarehe 7 Septemba 2026.
WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, ameshiriki utiaji saini mikataba ya kiutendaji kati ya Wizara ya Maji na Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), hatua inayolenga kubadili utendaji kutoka mazoea hadi mfumo unaopimika na wenye uwajibikaji.


KAMPUNI ya Kimataifa ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Barrick Gold kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Kiseriani kata ya Engikaret wilyani Longido Mkoani Arusha,Mbunge wa Jimbo hilo,Dkt Steven Kiruswa na serikali wamefanikiwa kujenga shule shikizi kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 230.

Akizungumza katika uzinduzi wa shule hiyo Kijiji hapo ,Meneja Mkazi wa Barrick{Country Manager} Tanzania ,Melkiory Ngido alisema uamuzi wa kampuni hiyo kuchangia msaada ni kufuatia maombi ya Kiruswa ambaye ni Naibu Waziri wa Madini na kujionea wenyewe hali ya changamoto za wanafunzi kutembea km 32 kwenda na kurudi shule  hali inayoleta hatari kwa wanafunzi hao kwa wanyama wakali.

Ngido aliwaahidi wananchi Kiseriani na Longido kwa ujumloa kuwa Barrick Gold itashirikiana na wananchi katika kujenga miundombinu ya elimu kwa kuwa wananchi wameonyesha nia ya dhati na ushirikiano na uadilifu mkubwa katika ujenzi wa madarasa mawili na 0fisi ya mwalimu kwani kampuni hiyo imechangia zaidi ya shilingi milioni 180 na zimetumika kama ilivyokusudiwa.

Alisema elimu ni msingi wa maisha na wananchi wa Kijiji cha Kiseriani ambao wengi wao ni wa jamii ya kifugaji ya Kimasai kuamua wenye kujitoa na kujenga madarasa mawili na ofisi ya mwalimu ni uamuzi unaopaswa kuungwa mkono kwa kuwa jamii hiyo imeamua kujitoa na kuwajali wanafunzi wa jamii hiyo na kujali elimu zaidi na sio vinginevyo.

‘’Barrick Gold Mining imeaamua kujitoa zaidi Longido kuhakikisha elimu inasogezwa zaidi katika maeneo ya makazi ya watu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miundombinu ya elimu ikiwemo madarasa,ofisi na nyumba za walimu zinajengwa kwa maslahi ya watoto wa jamii hiyo’’alisema Ngido

Naye Kiruswa aliishukuru kampuni hiyo kwa uamuzi wa ujenzi wa madarasa na ofisi ya mwalimu na kuahidi ushirikiano zaidi na kusema kuwa uamuzi huo unapaswa kupongezwa na wananchi wote wa Longido na kusema kuwa uadilifu ni jambo muhimu katika kuwashawishi wafadhili wengine kujitoa katika kutoa misaada ya miundombinu ya elimu,maji na barabara.

Alisema uamuzi wa ujenzi wa madarasa mengine mawili ulioazwa na wananchi kwa kusomba mawe,mchanga na kokote ni uamuzi wenye busara kubwa na yeye ataunga mkono kwa hilo kwa kutoa mifuko 100 ya simenti na kumalizia upauaji.

Waziri Kiruswa alisema na kuwaomba wana Kiseriani na Longido kwa ujumla kujitoa katika shughuli za kijamii ikiwemo ujenzi wa miundoimbinu ya elimu na kusema kuwa yeye kwa hilo atakuwa mstrari wa mbele katika kuchangia na kusaka wafadhili zaidi .

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi{CCM} wilaya ya Longido ,Papa Nakuta amempongeza Kiruswa kwa jinsi anavyojitoa kwa maendeleo ya wananchi wa longido na kuwataka wananchi kumuunga mkono mbunge huyo ambaye ameenda bungeni kufanya kazi na sio kulala kwani kila mradi mchango wake upo kama sio yeye basi analeta marafiki zake na kufanya ushawishi kwa serikali kuendelea kupeleka fedha za miradi Jimbo hapo.














Shirika la Viwango Tanzania (TBS) imekabidhi cheti cha ubora wa huduma kwa wakala wa maji na usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ikiwa ni Ishara ya utoaji huduma bora ya maji nchini.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb), ametembelea kiwanja kinachotarajiwa kujengwa Viwango House eneo la Mateves, Mkoani Arusha.

 



OWM –TAMISEMI, Dar es Salaam  


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi leo Septemba 11, 2026 amezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika na majanga kuchukua hatua za haraka kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba hadi Desemba 2026. 

 

Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo kwa taasisi hizo katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam, ambapo kwa upande wa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI yamepokelewa na Waziri Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, mara baada ya ofisi yake na taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka, kuwasilisha taarifa ya utayari na maandalizi ya Serikali katika kukabiliana na madhara ya mvua hizo, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.


Katika kikao kazi hicho, Makamu wa Rais, Mhe. Ndejembi ameagiza wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo kuhakikisha zinafanya kampeni maalum ya usafi katika miundombinu ya barabara na mifereji ya maji.


“Ifanyike kampeni ya haraka, mikondo na mifereji ya maji izibuliwe, na barabara ziandaliwe,” amesisitiza Makamu wa Rais.

 

Aidha, Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi, ameelekeza taka, tope na udongo unaotolewa baada ya kuzibua mitaro na mifereji katika maeneo mbalimbali kuondolewa mara moja na kutupwa katika maeneo yaliyotengwa, badala ya kuachwa kandokando ya barabara ambako taka, tope na udongo huo zinaweza kurejea kwenye mifereji wakati mvua zinapoanza.

 

Makamu wa Rais pia amezitaka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo, kufanya kazi kwa pamoja ya kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.



Akipokea maagizo hayo kwa ajili ya utekelezaji, Waziri wa Nchi, OWM – TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemueleza Mhe. Makamu wa Rais kuwa ofisi yake imeshaanza kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha usafi wa mazingira katika majiji aliyoyatoa Septemba 02, 2026 wakati akiwaapishwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.


Prof. Shemdoe amemtaarifu Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi kuwa, Septemba 07, 2026 alifanya kikao kazi na Wakuu wa Mikoa yenye majiji, viongozi wa majiji na manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka kuhakikisha wanatekeleza kampeni maalum ya wiki mbili ya usafi wa mazingira katika majiji ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais.


Akianisha namna ofisi yake itakavyotekeleza maelekezo ya Makamu wa Rais ya kujiandaa na kukabiliana na athari za mvua za El Niño, Prof. Shemdoe amewasilisha kwa Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi, mkakati wa ofisi yake kupitia TARURA ulioandaliwa kwa ajili ya kujiaanda, kuzuia na kupambana na madhara ya uharibifu wa miundombinu ya barabara unaoweza kutokana na mvua za El Niño, ambao umeanisha namna utakavyotekelezwa.

Kariakoo, 11 Septemba, 2026

Wafanyabiashara wa vipodozi katika Mtaa wa Vipodozi Kariakoo, Dar es Salaam, wamepata elimu kuhusu masuala ya kodi na huduma zinazotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia ziara ya maafisa wa mamlaka hiyo iliyoongozwa na Kaimu Meneja wa Mkoa wa Kodi Kariakoo, Edson Issanya.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), akichangia hoja kuhusu uwekezaji katika sekta ya afya wakati wa Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya, linalofanyika jijini Nairobi, Kenya.
Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, ndugu Saddy Sevingi akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua mafunzo kuhusu uelewa wa usalama wa kimtandao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Tanzania imepata nafasi 150 za ufadhili wa masomo nchini Algeria kwa wanafunzi waliofanya vizuri, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuongeza fursa za elimu ya juu nje ya nchi.
Mimi nilikuwa kwenye mahusiano ambayo yalinivunja moyo vibaya sana. Nilimpenda mtu kwa dhati, nikajitoa kwa kila hali, lakini mwisho wake niligundua nilikuwa natumiwa tu. Alikuwa ananihitaji pale tu alipokuwa na shida.

Nilipokuwa nikihitaji upendo au msaada, hakuwa karibu. Hilo liliniumiza sana, lakini nilivumilia kwa sababu nilikuwa na matumaini mambo yangebadiika.

Baada ya muda, ukweli ulijitokeza wazi. Nilijikuta nimeachwa na maumivu makubwa ya moyo.

Ilikuwa ngumu sana kuamini tena au hata kufikiria kuanza upya. Nilikaa kwa muda mrefu nikiwa peke yangu. Nilikuwa na hofu ya kuingia kwenye mahusiano mengine. Nilihisi kama kila mtu angeweza kuniumiza tena. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.

Mimi nilikuwa kwenye kesi ambayo ilinichukua karibu miaka mitano. Ilianza kama jambo dogo, lakini baadaye ikageuka kuwa vita kubwa ya kisheria iliyokuwa inaninyima amani kila siku.

Kila nilipoenda kusikilizwa kwa kesi, nilirudi nyumbani nikiwa nimechoka na kukata tamaa.

Ilionekana kama haki haikuwa upande wangu, hata pale nilipojua ukweli uko wazi. Gharama ziliongezeka, muda ulienda, na nilianza kupoteza matumaini kabisa. Ilifika wakati nilihisi kama nitaacha kila kitu na kukubali kushindwa. SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kufikiria kama siku moja ningepitia tukio ambalo lingebadilisha maisha yangu kwa sekunde chache tu. Ilianza kama siku ya kawaida kabisa, nikiwa nimechoka baada ya shughuli za mchana. Nilirudi nyumbani mapema bila kumpa taarifa yoyote.

Nilipoingia, nilihisi kuna hali ya tofauti ukimya usio wa kawaida na mlango ambao haukuwa katika hali niliyoacha asubuhi. Nilipoelekea ndani, nilianza kusikia sauti ndogo kutoka chumbani. Moyo wangu ulianza kupiga kwa kasi bila kuelewa kinachoendelea. Kila hatua niliyopiga iliongeza wasiwasi na mashaka.

Nilipofika mlangoni, niliganda kwa muda. Nilichokishuhudia kilikuwa kitu ambacho sikuwahi kukitarajia kutoka kwa watu wawili niliowaamini zaidi maishani mwangu. Mke wangu na rafiki yangu wa karibu walikuwa katika hali iliyonifanya nisemeze chochote kwa muda mrefu.

Ukimya mzito uliingia chumbani mara moja baada ya kuniona. Hisia zilichanganyika hasira, maumivu, na mshangao mkubwa. Sikuweza kuendelea kubaki pale kwa muda mrefu, hivyo niliondoka nikiwa nimevurugika kabisa kiakili.

Siku zilizofuata zilikuwa ngumu sana kwangu. Nilijikuta nikifikiria sana kilichotokea, nikikosa amani na hata mwelekeo wa maisha. SOMA ZAIDI.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) akisalimiana na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

Na William Bundala-Kahama Shinyanga

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kata ya Majengo manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga imeishukuru na kuipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya barabara katika kata hiyo.