Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameupongeza Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kwa maboresho makubwa ya utoaji wa huduma, hususan matumizi ya teknolojia yanayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Dkt. Msonde amesema hayo leo, Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la TEMESA katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.
Dkt.Msonde Amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofikiwa na TEMESA, akieleza kuwa uimarishaji wa huduma za kidijitali pamoja na ongezeko la ubora wa mafundi umeongeza ufanisi wa wakala huo.
“Kilichonifurahisha zaidi ni uimarishaji wa mafundi. Sasa wanafanya kazi kwa weledi mkubwa na wanatengeneza magari kwa ubora. Kwa kweli TEMESA mmenifurahisha sana,hongereni sana” amesema Dkt. Msonde.
Aidha, amesema Serikali na wananchi wanaiamini TEMESA kutokana na mchango wake katika kulinda usalama wa magari ya Serikali na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za umma. Amewataka viongozi na watumishi wa wakala huo kuendelea kubuni na kuboresha huduma kwa kutumia teknolojia.
Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma- TEMESA, Bi. Martha Joachim, amesema miongoni mwa maboresho yaliyofanywa ni kuhuisha huduma ya ukodishaji wa mitambo kupitia Mfumo wa TIMIS, ambapo wateja sasa wanaweza kuwasilisha maombi ya ukodishaji kwa njia ya kidijitali, hatua iliyopunguza urasimu na muda wa kupata huduma.
Maonesho hayo yenye kauli mbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050”, yanatarajiwa kuadhimishwa tarehe 8 Agosti, 2026.
Na.Mwandishi Wetu.
Serikali imewataka wawekezaji binafsi na taasisi mbalimbali nchini kutumia fursa zinazotolewa kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuwekeza katika ujenzi wa nyumba, majengo ya umma na makazi ya kisasa kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa makazi bora na kuharakisha maendeleo ya miundombinu nchini.
Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, baada ya kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, jijini Dodoma.Amesema Serikali imefanya maboresho ya sheria na kanuni zinazoiongoza TBA ili kuipa mamlaka mapana ya kushirikiana na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hatua itakayowezesha taasisi hiyo kuvutia mitaji na kuongeza kasi ya utoaji wa huduma.
Dkt. Msonde amesema tangu kuanzishwa kwake, TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi jukumu la kujenga na kusimamia majengo ya Serikali kwa viwango vya juu vya ubora, huku ikichangia kupunguza gharama za ujenzi na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya umma. Alisema majengo mengi ya Serikali yaliyopo nchini ni ushahidi wa uwezo na weledi wa taasisi hiyo katika sekta ya ujenzi.
Ameongeza kuwa pamoja na mafanikio hayo, TBA sasa ina nafasi kubwa zaidi ya kushiriki katika kutatua changamoto ya makazi kwa kujenga nyumba bora kwa gharama nafuu. Alisema taasisi hiyo inaweza kubuni na kutekeleza miradi ya makazi inayokidhi mahitaji ya wananchi wa kipato cha chini na cha kati, huku ikitumia maeneo yake ya kimkakati kuvutia uwekezaji na kuendeleza miradi ya kisasa.
Dkt. Msonde, amesema ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi kupitia TBA utaongeza uwekezaji, ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya ujenzi, huku ukiwezesha ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma, makazi ya biashara na miradi mingine ya maendeleo. Amewahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa hizo mapema kwa kuwa Serikali imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji na milango iko wazi kwa wote wenye nia ya kushirikiana na TBA.
Aidha, Dkt. Msonde ameipongeza TBA kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini, akisema utendaji wake umeendelea kuijengea Serikali imani kutokana na ubora wa kazi zake. Alisisitiza kuwa matarajio ya Serikali ni kuona taasisi hiyo ikitumia kikamilifu mamlaka mapya iliyopewa kupanua wigo wa huduma, kuongeza miradi ya kimkakati na kuwa chachu ya kuvutia uwekezaji utakaobadilisha sekta ya makazi na miundombinu nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano, Mh.Deus Sangu (MB) (wanne kushoto), akipokea zawadi toka kwa Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Jafari Merai Mgala, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini, Viwanja vya Nganga Mkoani Lindi Agosti 5, 2026.
Wananchi wakiwa kwenye banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, alipokuwa akizungumza kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini kwenye Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026
Lindi, Agosti 5, 2026
Mhe. Sangu ameyasema hayo Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi, ambapo alizungumza na wanachama, wastaafu na wananchi waliotembelea banda hilo.
"Wastaafu wengine wanashangaa kuona fedha zimeingia kwenye akaunti zao mara tu wanapotoka kazini na kujiuliza, 'Hizi fedha ni zangu kweli?' Hilo linaonesha wazi ukwasi wa Mfuko wa PSSSF na utekelezaji wa kaulimbiu ya Tunalipa Jana," amesema Mhe. Sangu.
Ameongeza kuwa hata wastaafu wanaopokea pensheni za kila mwezi hulipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi, na wakati mwingine hupokea malipo yao kabla ya watumishi walio bado kazini kupokea mishahara yao.
Serikali, kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.
Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.
Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.
“Mafuta yanapowasili nchini, Wakaguzi wa Mafuta hufuatilia hatua mbalimbali za upakuaji ili kuhakikisha yanakidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa,” amesema Mhandisi Makembe.
Ameeleza kuwa ufuatiliaji huo huanza mafuta yakiwa ndani ya meli na kuendelea wakati wa upakuaji na usafirishaji kupitia miundombinu maalumu, hadi yanapofikishwa kwenye maghala yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.
Kwa mujibu wa Mhandisi Makembe, Baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuidhinisha ubora wa bidhaa za mafuta kabla Meli haijaanza zoezi la Upakuaji ,Wakaguzi wa Mafuta wanajukumu la kuhakikisha kuwa taratibu za usalama na masharti ya upakuaji yanazingatiwa katika mchakato mzima wa upakuaji wa mafuta hayo. Hatua hiyo inalenga kulinda ubora wa mafuta na kuhakikisha shughuli za upakuaji zinafanyika kwa usalama.
Aidha, ukaguzi huo unalenga kubaini mapema changamoto zozote zinazoweza kuathiri ubora wa mafuta wakati wa upakuaji, usafirishaji au uhifadhi. Hatua hiyo husaidia kuhakikisha mafuta yanayopokelewa yanaendelea kuwa katika hali inayokubalika na TBS hadi yanapofikishwa kwenye maghala husika.


Na OWM – TAMISEMI, Morogoro
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wakulima, wafugaji na wavuvi kwa mchango wao mkubwa uliowezesha Tanzania kufikia utoshelevu wa chakula wa zaidi ya asilimia 120, hatua inayodhihirisha mafanikio ya uwekezaji unaoendelea kufanywa na Serikali katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.
Dkt. Mwigulu aliwasilisha pongezi hizo za Mhe. Rais Agosti 4, 2026, alipotembelea Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Nane Nane mkoani Morogoro.
Katika ziara hiyo alijionea shughuli na ubunifu wa wakulima, wafugaji na wavuvi kutoka mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam, Pwani na Tanga.
Amesema maonesho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, "Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050," ambayo inawahimiza Watanzania kuzalisha kwa kuzingatia mahitaji ya soko, kutumia teknolojia za kisasa, kuongeza ubora wa bidhaa na kuimarisha mnyororo wa thamani ili kufanya kilimo kuwa biashara yenye tija na mchango mkubwa katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
"Kwa nilichojionea kupitia maonesho ya mwaka huu, ninaziona dalili zote kwamba ifikapo mwaka 2050 malengo ya Dira ya Taifa tuliyojiwekea yatakuwa yamefikiwa, kwa kuwa tuko kwenye hatua nzuri ya utekelezaji katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi," amesema Dkt. Mwigulu.
Ameongeza kuwa ameridhishwa na ubora wa mazao mbalimbali yaliyooneshwa, ikiwemo nyanya, bilinganya na bidhaa nyingine zinazokidhi viwango vya masoko ya kimataifa, yakiwemo ya Marekani na Ulaya, jambo linaloashiria kuwa Tanzania ipo kwenye mwelekeo sahihi wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani duniani.
Akizungumzia sekta ya mifugo na uvuvi, Dkt. Mwigulu amesema zimeendelea kuwa nguzo muhimu za uchumi wa taifa, akibainisha kuwa mchango wa sekta ya mifugo katika pato la taifa umeongezeka kutoka asilimia 2.3 hadi asilimia 6.2.
Ametoa mfano wa mafanikio ya wanaonufaika na sekta hiyo kwa kumtaja kijana mmoja mhitimu anayejihusisha na ufugaji wa kisasa, ambaye ameonesha ng'ombe mwenye uzito wa zaidi ya kilogramu 1,000 mwenye thamani ya takribani Shilingi Milioni 20. Aidha, amesema kijana huyo anafuga zaidi ya ng'ombe 200 na alipoulizwa na Waziri wa TAMISEMI kama anahitaji mkopo, alieleza kuwa hana uhitaji huo kutokana na mafanikio ya shughuli zake.
Awali, akitoa neno la utangulizi kabla ya Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi pamoja na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, alisema Waziri Mkuu alimpa jukumu la ulezi wa Mkoa wa Morogoro, hivyo alimkaribisha rasmi kama waziri mwenyeji wa mkoa huo, ambao ni mmoja wa mikoa inayounda Kanda ya Mashariki katika Maonesho ya Nane Nane.







.jpg)















.jpg)














