Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Na.Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Mazungumzo ya Viongozi hao yamelenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar katika sekta ya kazi na ajira, hususan eneo la kukuza maendeleo ya rasilimali watu, ulinzi na haki za wafanyakazi pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania.
Vilevile, wamejadili kuhusu Mkutano wa Uhamaji wa Wafanyakazi (Labour Mobility Dialogue) utakaowakutanisha nchi wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Nchi za Ghuba (GCC), Jordan, Lebanon na nchi za Afrika zinazotuma wafanyakazi nje ya nchi chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika (African Union). Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Oktoba 2026 Tanzania, jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na kupanua fursa za ajira salama na zenye staha kwa wananchi wa nchi shiriki.
Katika kikao hicho, Waziri Sangu aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Jane Songoro.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akimkabidhi tuzo Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, tuzo ya kutambua ushirikiano katika ya Tanzaniana Qatar katika masuala ya Ajira, leo Julai 8, 2026, katika Ofisi za Wizara hiyo ya Kazi Jijini Doha, nchini Qatar.















