Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kufanya mageuzi makubwa katika kuboresha upatikanaji wa  huduma ya umeme nchini hatua ambayo imeongeza imani na fursa mbalimbali za kiuchumi kwa wananchi.

Mhe. Ndejembi ameyasema hayo Novemba 22, 2025, mkoani Dodoma katika kikao chake na viongozi wa TANESCO chenye lengo la kufanya tathmini na kukumbushana majukumu muhimu ya kuwahudumia wananchi. Ameutumia mkutano huo kuwataka watendaji wa TANESCO kuongeza kasi na ubunifu katika kuwaunganishia wananchi umeme kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Misheni 300.

Amesema kuwa ili mpango huo utekelezeke ipasavyo, ni lazima kuwachukulia  hatuaza kisheria  wakandarasi wote watakaobainika kuwa wazembe au kushindwa kuendana na kasi ya serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na huduma ya umeme.

“Nawapongeza TANESCO kwa kazi kubwa na nzuri ya kuwafikishia wananchi huduma ya umeme, lakini bado tuna kazi kubwa mbele yetu. Ongezeni ubunifu na mbinu bora za kuwaunganishia wananchi umeme kwa haraka. Ninaamini tukishirikiana na wadau wetu, tutafikia lengo la kuwaunganishia wateja milioni 1.7 kwa mwaka,” alisema Mhe. Ndejembi.

Naye Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba amemshukuru Rais.  Dkt.  Samia Suluhu Hassan kwa kuwekeza katika miradi ya umeme ambayo imekuwa na dhamira ya dhati ya  kuhakikisha wananchi wote mijini na vijijini wanafikiwa na huduma ya umeme.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhe. Felchesmi Mramba, amesema TANESCO imekuwa ikitekeleza miradi yake kwa viwango vya kimataifa, hatua inayofanya Tanzania kuwa kielelezo kwa mataifa mengine katika ujenzi na usimamizi wa miradi ya umeme.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, Mhe. Balozi Zuhura Bundala, amesema  Shirika hilo lina watendaji wazalendo na wenye kujituma, ambao wanaendelea kufanya kazi kwa bidii  ambapo amesisitiza bodi hiyo itaendelea kushirikiana na Shirika ili kufikia malengo yaliyowekwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema  katika kipindi cha siku 100 za utendaji wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Shirika litakamilisha miradi ya umeme  kwa kasi zaidi, ukiwemo mradi wa kuzalisha umeme wa jua wa Kishapu ambao kwa sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji.

“Katika kipindi cha siku 100 za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, tumejipanga kuhakikisha baadhi ya miradi ya umeme inakamilika, ukiwemo mradi wa umeme wa jua wa Kishapu. Pia tunaendelea na mkakati wa kuwaunganishia wananchi umeme  lengo ni kuwafikia wateja milioni 1.7 kwa mwaka,” alieleza Bw. Twange.

Kikao kazi hicho  kimehusisha viongozi wa ngazi ya juu wa TANESCO, wakurugenzi wa kanda, mameneja wa mikoa na wilaya, na kilifunguliwa rasmi na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius  Ndejembi ambaye aliambatana na Naibu waziri wa nishati Mhe. Salome Makamba











 


Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Prof Eliamani Sedoyeka amefungua Kongamano la uwasilishwaji wa machapisho ya kitaaluma kwa wanafunzi wa Masters linalofanyika kwa siku mbili katika Kampasi za Arusha, Dodoma na Dar es salaam

Akizungumza katika ufunguzi wa Kongamano hilo Prof Eliamani Sedoyeka amesema Chuo kimekuwa na desturi ya kuandaa jukwaa la uwasilishwaji wa tafiti za wanafunzi wa Masters mbele ya watu “Demokrasia ya Kitaaluma” kwa lengo la kupata maoni na maboresho ili machapisho hayo yaweze kuwa rasmi, na kwa mwaka huu wanatarajia mawasilisho ya wahitumu takribani “Elfu mbili miatano” kwa kampasi zote

Kwa upande wake Meneja wa Kampasi ya Arusha Dkt. Joseph Daudi amesema jukwaa hili limekuwa likiwanufaisha wahitimu na jamii kwa ujumla kutokana na machapisho hayo kutumika kutatua changamoto mbalimbali katika jamii hasa baada ya uwasilishwaji wake na kuwa machapisho rasmi

Janeth Obedi moja ya wanafunzi wanawasilisha machapisho haya ambae anasoma “Masters of Leadership and Governance” ameushukuru uongozi wa IAA kwa kuwaandalia jukwaa hili ambalo limesaidia machapisho yao kuonekana na wadau katika jamii hivyo kuwatengenezea fursa za kimaendeleo

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof Eliamani Sedoyeka, amesema chuo hicho kimejipanga kuja na tafiti zitakazo saidia kuleta matokeo chanya katika jamii ambazo zitafanywa na wanafunzi.
NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA

Taasisi ya HakiElimu Tanzania imefanya mafunzo kwa wadau wake ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa SAUTI ZETU ambao umejikita katika kusisitiza ujumuishaji wa masuala ya kijinsia katika mambo mbalimbali ya kijamii.






Na Oscar Assenga, MKINGA

WAVUVI na Wakulima wa Mwani 800 wilayani Mkinga mkoani Tanga wanatarajiwa kupatiwa elimu ya utendaji wa shughuli zao kwa usalama ili kuwaepusha na changamoto za baharini zinazotokana na uwepo wa mwigiliano wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Shirika la Uwashem Hussein Msagati wakati wa kikao cha wavuvi na wakulima wa mwani katika kata ya Boma wilayani humo ikiwa ni kutambulisha mradi wa kujenga uwezo kwa matumizi bora ya rasilimali za bahari ngazi ya Kata .

Mradi huo unaendeshwa na Shirika la Umoja wa Wasaidizi wa Sheria wilayani Mkinga (Uwashem) ukifadhiliwa na Shirika la 4 H Tanzania pamoja na We World ambapo sasa utasaidia kuwaweka kwenye hali ya amani ili waweze kushirikiana kwa pamoja kufanya kazi zao na kutokuwepo kwa mivutano ya hapa na pale.

Alisema kwamba umuhimu wa elimu hiyo ni mkubwa kutokana na changamoto za baharini zinazotokana na kuwepo kwa mwingiliano wa maeneo kwa sababu wavuvi wanaotumia makokoro wanaingia kwenye maeneo yanayolimwa mwani kufanya shughuli za uvuvi.

Aidha alisema kwamba hatua hiyo inapelekea kuharibu mazao ya mwani jambo ambalo sio zuri hivyo ikiwezekana washirikiane kwa pamoja ili kuepusha migongano katika shughuli zao za kila siku.

Awali akizungumza Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Mkinga Hilda Muro alilipongeza Shirika hilo kwa kuandaa vikao kati ya wavuvi na wakulima wa mwani akieleza kwamba itasaidia kuleta tija kwa kuwaepusha na migogoro au kuitatua pindi inapotokea baina yao wakati wa utekelezaji wa majukumu yao baharini.

Alisema kwamba wanapotokea wadau kama hao kuwaletea elimu ya kutatua migigoro kwa njia za mazungumzo inapendeza zaidi hivyo wanalishukuru shirika hilo kuwapelekea elimu na wanaamini kupitia elimu hiyo kwa wananchi itakuwa ni mwanzo wa amani kwa jamii za pwani.

“Kutokana na kila mtu atafanya shughuli zake bila kukutana na vikwazo au kubuguziwa na mtu mwengine yoyote na hivyo kutengeneza amani na mazingira ya uzalishaji kuwa bora kuanzia sasa”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba elimu itasaidia uzalishaji mwani na wavuvi kutokana na kwamba watakuwa wakitekeleza majukumu yao wakiwa kwenye hali ya usalama baharini.


Hata hivyo mmoja wa Wavuvi wilayani humo Yasin Baraza alisema kwamba midahalo hiyo inayoendeshwa na Shirika hilo itawasaidia kuweza kutatua migogoro kati ya wavuvi na wakulima wa mwani na tatizo hilo liweze kuondoka moja kwa moja .


Ferdinand Shayo ,Arusha .


Benki ya NCBA imeshiriki zoezi la kupanda miti ya asili 11000 katika eneo la Olkokola Wilayani Arumeru Mkoani Arusha kwa kushirikiana na shirika la Kijani Pamoja kwa lengo la kuhakikisha uoto wa asili unarejea na kutimiza adhma ya Benki hiyo kupanda miti milioni 10 ifikapo mwaka 2030.

Akizungumza katika Zoezi la kupanda miti hiyo,Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NCBA Tanzania Alex Mziray amesema wamezindua mradi wa kupanda miti 11000 kwa lengo la kutunza mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.

“Kwa kushirikiana na shirika la Kijani Pamoja wametupa njia ya kuhakikisha kuwa mradi huishii tu kwenye kupanda miti bali kuangalia jinsi ya kuendeleza miti na kuhakikisha inakua na hata ikifika miaka 10 ijayo uweze kuiona hiyo miti” Anaeleza Mziray.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kijani Pamoja Sarah Scott ameeleza furaha yake baada ya benki ya NCBA kuunga mkono mradi wa kupanda miti na kukuza miti na amekua akitumia mbinu ya “lipa ukue” inayolenga kuhamasisha wananchi kutunza miti huku wakijipatia kipato na tayari wataanza kupanda miti 11000 katika msimu huu wa mvua.

“Kupanda miti ni rahisi lakini kutunza miti iweze kukua ni ngumu sana lakini pia kupata miti sahihi na eneo sahihi kunasaidia kuleta matokeo chanya ya kuhakikisha kuwa tunarejesha uoto wa asili na mfumo wa ekolojia kwa ujumla” Alisema Sarah

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mwinyi Ahmed akizindua mradi huo kwa kupanda mti kama ishara ya uzinduzi amepongeza juhudi za benki ya NCB katika kutunza mazingira na kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi na kuwataka wadau wengine wa maendeleo kuiga mfano wa benki hiyo.

Mkuu wa Kitengo cha Mikakati Benki ya NCBA Tanzania Charles Mbatia amesema mpaka sasa wameshapanda miti 16000 ili kufikia lengo la kupanda miti milioni 10 ifikapo 2030.

Hata hivyo Mkuu wa Idara ya Mazingira Shirika la Kijani Pamoja ,Samwel Simon kazi yetu kubwa ni kuotesha miti ya asili kwenye maeneo yaliyoharibika ,vyanzo vya maji ,mito tukishirikiana na wadau mbali mbali kama ilivyo leo tumeshirikiana na benki ya NCBA.







 


Na. Benny Mwaipaja, Dodoma 


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa Wizara ya Fedha imebeba matumaini ya Serikali na Wananchi katika kuhakikisha kuwa inatafuta fedha za kuendeleza ujenzi wa miradi ya maendeleo itakayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi.

Mhe. Balozi Omar, amesema hayo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi za Wizara ya Fedha (Treasury Square), jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na Menejimenti na Wafanyakazi wa Wizara hiyo, baada ya kuwasili katika Ofisi hizo akiambatana na Naibu Mawaziri wake wawili, Mhe. Mshamu Ali Munde na Mhe. Laurent Deogratius Luswetula.

Alisema kuwa Wizara inatakiwa kuweka mikakati na mipango madhubuti ya kutafuta rasilimali za ndani kwa ajili ya kuendeleza na kukamilisha miradi mbalimbali pamoja na kuweka sera bora za fedha zitakazosaidia kuyawezesha makundi mbalimbali wakiwemo ya  vijana kupata ajira na kufanya biashara.

Alisema kuwa Wizara ya Fedha ndio moyo wa Serikali kwa maendeleo ya nchi hivyo Menejimenti na Wafanyakazi wote wanapashwa kujipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa fedha zinapatikana lakini pia kwa kuyasikiliza makundi mbalimbali yenye changamoto zinazokwaza ustawi wao wakati nchi ikianza kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wao, Naibu Mawaziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), na Mhe. Laurent Deogratius Luswatula, wameshukuru kwa mapokezi makubwa waliyoyapata kutoka kwa Menejimenti na Wafanyakazi wa Wizara na kuahidi kutoa ushirikiano na kuwa chachu ya mafanikio ya kuwaletea wananchi maendeleo kama walivyoaminiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Awali, akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara,  Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, alisema kuwa Wizara ya Fedha, ina wafanyakazi wachapakazi ambao wako tayari kuhakikisha kuwa kuna usimamizi mzuri wa uchumi na sekta ya fedha kwa ujumla kwa manufaa ya wananchi kiuchumi na kijamii.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, na Naibu Mawaziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Ali Munde na Mhe. Laurent Deogratius Luswetula, waliapishwa jana na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kushika nyadhifa hizo, Ikulu-Chamwino, mkoani Dodoma.

Waziri wa  Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi  amewaagiza Watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kutimiza Vipaumbele vya Serikali katika Sekta ya Nishati ikiwemo kufikia Megawati 8000 ifikapo 2030.

Mhe. Ndejembi ameyasema hayo tarehe 18 Novemba 2025 wakati akizungumza na watumishi wa Wizara mara baada ya kuwasili Katika Wizara  Mji  wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. 

Amesema watumishi wa Wizara ya Nishati ndio watendaji wakuu na wenye dhamana ya kuhakikisha kwamba malengo ya Serikali yaliyowekwa yanatimia kwa kufanya kazi kwa bidii , kuwataka watumishi kuchambua kwa kina  hotuba ya Mhe   Rais ili kuweza kufikia vipaumbele kwa wakati  na kuyoa huduma bora kwa wananchi wa Tanzania.

Pia amesisitiza watumishi kutumia siku mia moja za Mhe. Rais kama kipimo na  kielelezo cha kutathmini uelekeo wa malengo ya Serikali.

“Sisi kama viongozi wenu tunategemea zaidi ushirikano kutoka kwenu ninyi wataalamu wa hapa Wizara ya Nishati  ili tuweze kukamilisha Vipaumbele vya Mhe. Rais alivyoviweka katika sekta yetu  kwasababu tunatakiwa tuanze kwa kukimbia na sio kutembea“ amesema Mhe. Ndejembi.

Nae Naibu Waziri wa  Nishati Mhe. Salome Makamba amewataka watumishi kushirikiana kwa pamoja na viongozi wa Wizara hiyo ili kuendesha Sekta ya Nishati kwa pamoja, na kuongeza kuwa anatambua kwamba maswala mengi ya sekta ya Nishati yameshafanyika tayari mpaka sasa.

Amesema  Serikali imeshafikisha Megawat 4000 za kiwango cha kuzalisha Umeme, hivyo ni jukumu letu kukamilisha miradi iliyokuwa inaendelea na kuongeza vyanzo vingine vya uzalishaji umeme ili kufikia megawati 8,000 ifikapo 2030.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mha. Felchesmi Mramba amewashukuru viongozi hao na amewataka watumishi wa Wizara ya Nishati kutoa ushirikiano kwa viongozi hao sambamba na kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kuweza kutekeleza Vipaumbele vya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2030.












 


Waziri wa Madini Anthony Mavunde amewataka Watumishi wa Wizara ya Madini  na Taasisi zake kutambua kwamba maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Hassan kuhusu kutumia fedha za ndani zinazotokana  na rasilimali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo  ni agizo  linaloigusa  Wizara ya Madini moja kwa moja.

Ameyasema hayo Novemba 18, 2025 wakati akizungumza na Watumishi wa Wizara ya madini na taasisi zake Makao Makuu ya Wizara Mtumba, mapema baada ya kuapishwa Ikulu ya Chamwino Dodoma na Rais  Dkt. Samia Hassan.

‘’Mapato ya ndani aliyoyaelekeza Mhe.  Rais yanatugusa sisi Sekta ya Madini moja kwa moja. Dkt. Samia anataka uongozi unaogusa watu hivyo tuendelee kuongeza kasi. Lakini Katibu Mkuu nitapenda maelekezo aliyoyasema wakati akihutubia Bunge, haya ya leo na yale yaliyoahidiwa kwenye Ilani ya Uchaguzi yamfikie kila mtumishi,’’ amesisitiza Mavunde.

Mhe. Mavunde ameeleza kuwa Rais. Dkt.Samia Suluhu Hassan amekuwa na imani kubwa na Wizara ya Madini hususan kutokana na mapato yanayotokana na  rasilimali madini kuendesha uchumi wa nchi  na hivyo kumtaka kila mtumishi kutumia nafasi yake kuhakikisha sekta ya madini inagusa maisha ya kila mwananchi kwa manufaa ya jamii na taifa.

Akielezea kuhusu programu ya Mining for A Brighter Tommorrow (MBT), Mhe. Mavunde amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kikamilifu kama ulivyopangwa kwa lengo la kuwawezesha wachimbaji vijana na wanawake kuchimba kwa tija. Kupitia mradi wa MBT Wizara imepanga kuwawezesha vijana na wanawake kwa kuwapatia maeneo ya kuchimba na teknolojia ili kuwarahisishia shughuli zao.

Pia, ametumia fursa hiyo kumshukuru Dkt. Samia kwa kumuamini na kumrejesha tena kuitumika wizara hiyo pamoja na kuwashukuru watumishi wote na wadau wote wa Sekta ya madini  kwa ushirikiano mkubwa waliompatia katika kipindi cha miaka miwili aliyohudumu katika wizara hiyo na kueleza kwamba, kwake mlango uko wazi kwa  ajili ya kupokea maoni na mapendekezo yanayojenga kwa lengo la kuendelea kuboresha Sekta ya Madini.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa Dkt. Kiruswa ameshukuru Rais Samia kwa kumuamini kuendelea kuhudumu katika Wizara ya Madini na kuwashukuru watendaji wote kwa ushirikiano waliompatia na kuwapongeza watumishi kwa kazi wanayofanya hususan kuendelea na ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali.

‘’Mhe. Rais ametoa mwelekeo, hivyo tunapaswa  kutekeleza yale  tuliyoagizwa,  tuliwaacha na mchango wa asilimia 10.1 matamanio ni kufikia  asilimia 15 – 20  ifikapo mwaka 2030’’ amesema Dkt. Kiruswa.

Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng. Yahya Samamba amewapongeza viongozi hao kwa kuchaguliwa tena katika Wizara ya Madini na kuahidi kuendelea kuwapa ushirikiano wa utendaji kazi  kuanzia ngazi ya chini mpaka juu.

Pamoja na mambo Kamishna wa Madini Dkt.AbdulRahman Mwanga kwa pamoja  amewapongeza  hao  kwa kuchaguliwa tena na kuahidi  ushirikiano

*#Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri*

 


Na WAF, Dodoma

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amewataka watendaji wa Wizara ya Afya kufanya kazi kwa bidii, weledi na uadilifu  na kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kuleta tija na ufanisi kwa wananchi.

Mhe. Mchengerwa ametoa wito huo leo, Novemba 18, 2025, alipokutana na Menejimenti ya Wizara mara baada ya kuwasili rasmi kuanza majukumu yake mapya ya kazi kwenye wizara hiyo.

Amesema huu ni wakati wa watumishi kuongeza juhudi na kuto bweteka, ili kuendelea kusukuma maendeleo ya Sekta ya  Afya mbele.

“Nawasisitiza watumishi wote kuacha kufanya kazi kwa mazoea Tubadilike na kutekeleza majukumu kwa ufanisi ili kuhakikisha Taifa letu linasonga mbele katika Sekta ya Afya,” amesema Mhe. Mchengerwa.

Aidha, Waziri Mchengerwa amewataka watumishi wote kufuata maadili ya kazi na kusimamia kwa umakini maelekezo yanayotolewa, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya.







Wajumbe wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya Tuzo za Uhifadhi na Utalii 2025 wakiongozwa na Mkurugenzi Msaidizi Utalii Richie Wandwi wameendelea na zoezi la uhamasishaji na utoaji elimu kwa wadau wa utalii na uhifadhi juu ya tuzo za Serengeti zinazotarajiwa kufanyika mwezi Desemba 2025.

Zoezi hilo linalolenga kuwajengea uelewa wadau juu mambo muhimu ikiwemo, kategoria za tuzo na namna ya kujisajili na kuwa mshiriki wa tuzo hizo limefanyika Jumatatu Novemba 17 Jijini Arusha kwa Kanda ya Kaskazini.