Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam kinaendesha semina ya siku tatu inayohusu uvumbuzi katika matumizi ya akili mnemba kwenye sekta ya usafirishaji na usimamizi wa mizigo. Semina hiyo imezinduliwa Desemba 16, 2025 na Rasi wa Ndaki hiyo, Prof. Cyriacus Binamungu, katika kituo cha Upanga.
Nilizoea kudharauliwa. Kwa miaka mingi, jina langu lilikuwa likitajwa sambamba na umaskini, kushindwa, na ndoto zisizo na mwelekeo. Nilitembea mitaani nikiwa sina kitu cha kujivunia zaidi ya matumaini ambayo hata yenyewe yalikuwa yanapotea taratibu. Watu walinitazama kama mfano wa kile ambacho hawakutaka kuwa.

Nilituma maombi ya kazi, nilijaribu biashara ndogo ndogo, na nilijitosa kwenye miradi iliyoshindikana mara kwa mara. Kila nilipoanguka, waliokuwa karibu nami waliongeza dharau.

“Huyu hatawahi kufika popote,” walisema. Nilikuwa na mawazo, nilikuwa na bidii, lakini kila nilichogusa kilionekana kukwama bila maelezo ya kueleweka.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba hata nilipopata fursa ndogo, zilivunjika ghafla. Zabuni zilipotea dakika za mwisho, mikataba ilibadilishwa, na mara zote nilibaki mikono mitupu. Ndipo nilipoanza kujiuliza kama tatizo lilikuwa zaidi ya juhudi na mipango kama kulikuwa na kitu kilichokuwa kimefungwa katika safari yangu ya mafanikio. Soma Zaidi..................
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/walimdharau-kwa-miaka-kwa-sababu-ya-umaskini-leo-anasaini-contracts-za-serikali-zenye-thamani-ya-mabilioni/

Niliingia ndani ya jengo la mahakama asubuhi ile nikiwa na mzigo mzito moyoni. Nilikuwa mtuhumiwa katika kesi nzito iliyotikisa maisha yangu kwa miezi kadhaa.

Kila mtu aliyekuwa ukumbini alionekana kunitazama kama tayari ana jibu juu ya hatma yangu. Nilitembea taratibu, nikihisi hofu, aibu, na kukata tamaa vikichanganyika ndani yangu.

Kabla ya siku hiyo, maisha yangu yalikuwa yameporomoka. Jina langu lilichafuliwa, marafiki walijitenga, na familia yangu iliishi kwa hofu ya kile ambacho kingetokea.

Nilijua moyoni sina hatia, lakini bila ushahidi wa wazi, ukweli wangu haukuwa na nguvu mbele ya mashtaka. Usiku mwingi nilikesha nikijiuliza kama ningewahi kuishi maisha ya kawaida tena.

Niliposimama kizimbani, upande wa mashtaka uliongea kwa kujiamini sana. Kila sentensi ilionekana kunizidi uzito. Nilihisi kama tayari nimeshahukumiwa hata kabla ya hukumu kutolewa. Ndani yangu nilikuwa nimevunjika kabisa, hadi pale nilipokumbuka uamuzi nilioufanya wiki chache kabla ya kesi. Soma Zaidi..............
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/aliingia-mahakamani-kama-mtuhumiwa-lakini-alitoka-akiwa-huru-baada-ya-ushahidi-mmoja-kubadili-kila-kitu/
Nilianza kuishi na maumivu ambayo sikuweza kuyaeleza kwa urahisi. Kila siku niliamka nikiwa nimechoka, mwili mzito, na maumivu yaliyokuwa yakija bila onyo. Nilitembea kutoka hospitali moja hadi nyingine nikitafuta majibu, lakini majibu niliyopata yalikuwa yale yale hali yangu haikuwa na tiba ya kudumu. Madaktari waliniambia nijifunze kuishi na maumivu milele.

Maneno hayo yaliniangamiza kisaikolojia. Nilijaribu dawa mbalimbali, nikafuata maelekezo yote, lakini nafuu ilikuwa ya muda mfupi. Nilianza kukosa usingizi, kazi ikawa ngumu, na hata tabasamu langu lilipotea taratibu.

Watu waliniona kama mzigo kwa sababu sikuweza kufanya mambo kama zamani. Ndani yangu nilikuwa napambana na hofu kwamba maisha yangu yangeishia kwenye maumivu yasiyoisha. Soma Zaidi........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/madaktari-walimwambia-ataishi-na-maumivu-milele-lakini-ndani-ya-miezi-sita-kila-kitu-kilibadilika/






Na Oscar Assenga, KOROGWE.

SERIKALI imemtaka Mkandarasi anayesimamia mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji la Mkomazi wilayani Korogwe unao gharimu kiasi cha Bilioni 18.6 kuongeza nguvu kazi ya kutosha ikiwemo kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha unakamilika kwa wakati uliopangwa.

Maagizo hayo yalitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian wakati alipofanya ziara ya kutembelea mradi huo akiwa na kamati ya ulinzi na usalama kwa lengo la kujionea hali ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Bwawa hilo kuhakikisha mradi huo wa kimkakati unatekelezwa kwa viwango na kwa kasi inayostahili.

Bwawa la Umwagiliaji la Mkomazi linajengwa katika Kijiji cha Manga Mtindilo wilayani ya Korogwe ambalo linatarajiwa kuwa mkombozi mkubwa kwa Kilimo cha Umwagiliaji mkoani Tanga na mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi China Sichuan International Cooperation Co.LTD.


Hatua hiyo ilitokana na kutokuridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi wa bwawa hilo kutokana na namna unavyotekelezwa hasa kwa kazi ambazo zingepaswa kutekelezwa kwa haraka zaidi .

Aidha alisema kwamba wamekuja kutembelea Bwawa hili ambalo ni muhimu kutokana na kwamba mkoa wa Tanga unatarajiakuwa kitovu cha uzalishaji wa chakula kwa mikoa ya Kilimanjaro,Manyara na Arusha kupitia mradi huo mkubwa pindi utakapokamilika

Mkuu huyo wa mkoa alimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa maono yake na kuamua kutenga zaidi ya Bilioni 18.2 kwa ajili ya mradi huo mkubwa na kuongeza tena Milioni 400 hivyo kufikia Bilioni 18.6 ikiwa ni dhamira ya kweli kuhakikisha kilimo cha umwagliaji kinakuwa nguvu ya usalama wa chakula.

Alisema kwamba mradi huo ni muhimu kutokana na kwamba mabadiliko ya tabia ya nchi mvua ambazo zilitarajiwa kunyesha mkoa wa Tanga hazikunyesha kwa wakati wala kwa kiwango kilichokusudiwa hivyo hiyo ni ishara kwamba hawawezi kutegemea kilimo cha mvua pekee ndio maana wanasisitiza kilimo cha uhakika ni cha umwagiliaji.

Awali akizungumza Mhandisi kutoka kwa Mkandarasi Andrew Magungu alisema kwamba wamepokea maelekezo ya kiongozi huyo na kuhaidi kuyafanyia kazi ili kuhakikisha malengo ya mradi huo yaliyowekwa ya kukamilisha mradi huo kwa wakati.
Naye kwa upande wake Meneja wa Mradi huo ,Mhandisi Leonard Someke maendeleo ya kazi mpaka sasa ipo asilimia 84.9 na mradi huo utakapokamilika unatarajiwa kuwanufaisha zaidi ya wananchi 20,000 kutoka Kata saba ambapo ni jumla ya vijiji 28 kutoka wilaya ya Korogwe kwa kuwawezesha kulima mara mbili hadi tatu kwa mwaka tofauti na awali .

Eneo ambalo litakapomwagiliwa litakuwa ni Hekta 9000 sawa na Ekari 22,500 huku faida za mradi huo zikielezw kupunguza athari ya mafuriko yanayokumba mashamba ya wakulima .

Na John Mapepele, New Delhi.

Waziri wa Afya  Mheshimiwa  Mohamed Omary Mchengerwa amezikaribisha jumuiya za kimataifa na wadau mbalimbali wa Sekta  ya Afya duniani kushirikiana na Tanzania katika  kufanya  tafiti,  ubunifu na uhamishaji wa teknolojia,  pamoja na biashara ya kimaadili ya tiba asili ili kuboresha  huduma  ya tiba asili kwa kuwa tiba asilia inaweza kuwa nguzo muhimu ya afya bora na maendeleo endelevu ya kiuchumi duniani.

Mhe. Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo wakati akiwasilisha uzoefu wa Tanzania kwenye mada ya tatu iliyohusu “kufikiria upya mifumo ya afya  kwa usawa, usalama na ustahimilivu katika eneo la  Tiba Asili” kwenye  Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu Tiba Asilia, unaoendelea jijini New Delhi nchini India.

“Tanzania inaendelea kubadilisha tiba asilia kutoka katika mfumo wa jadi Kwenda katika mfumo wa tiba yenye ushahidi wa kisayansi, inayodhibitiwa kitaalamu, inalindwa kidijitali, na yenye mchango wa kiuchumi. Kwa sasa takribani asilimia 60 ya watanzania hutegemea tiba asilia, huku zaidi ya waganga 60,000 na vituo zaidi ya 2,000 vikisajiliwa rasmi nchini”. Amefafanua Waziri Mchengerwa.

Ameongeza kuwa Serikali ya Tanzania inaweka mkazo katika utafiti wa gharama nafuu unaozingatia jamii, pamoja na uthibitishaji wa usalama, ubora na ufanisi wa tiba asili, sambamba na utekelezaji wa Mkakati wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wa Tiba Asili wa mwaka 2025–2034 ambapo amesisitiza kuwa Tanzania hailegezi udhibiti wa tiba asilia, bali inaiboresha kitaaluma kupitia mifumo imara ya sheria na taasisi za udhibiti.

Akizungumzia ujumuishaji wa tiba asilia katika mifumo ya afya, Waziri Mchengerwa ameeleza kwamba, Tanzania imeanza kutumia huduma za tiba asili katika vituo vya afya, ambapo hadi sasa bidhaa 27 za tiba asilia zimetumika katika utoaji wa huduma za afya tangu mwaka 2023 huku akisisitiza  kuwa ujumuishaji wa tiba asili katika mifumo ya afya si ushindani, bali ni ushirikiano, unaolenga kufanikisha Bima ya Afya kwa Wote.

Katika eneo la maendeleo ya kiuchumi, Mheshimiwa Mchengerwa amebainisha kuwa Tanzania imesajili bidhaa 141 za tiba asilia, ambapo zaidi ya asilimia 90 huzalishwa na wazalishaji wadogo wa ndani, hatua inayochangia ajira na kukuza uchumi na kwamba  Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kuhimiza ubia kati ya sekta ya umma na binafsi, kilimo cha mimea tiba, usindikaji, na upatikanaji wa masoko ya ndani na ya kimataifa.

Pia amesisitiza umuhimu wa kulinda haki miliki na maarifa ya jadi ya jamii, pamoja na matumizi ya akili mnemba (AI) na teknolojia za kidijitali kuhifadhi, kuthibitisha, na kulinda maarifa ya tiba asili. Vilevile, alieleza kuwa teknolojia haitachukua nafasi ya waganga wa jadi, bali itaongeza na kulinda hekima yao.

Mkutano huo wa siku tatu unatarajiwa kufungwa na leo na  Waziri Mkuu wa India, Mheshimiwa Narendra Modi, jambo linaloonesha uzito na umuhimu mkubwa wa mkutano huo katika ngazi ya juu ya kisera.

NDEGE ya Shirika la Ndege Tanzania (Air Tanzania) imefanya first touch down katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Victoria Falls, Zimbabwe, leo mchana tarehe 18 Desemba 2025, hatua inayozidi kuimarisha ushirikiano wa usafiri wa anga kati ya Tanzania na Zimbabwe.
 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akikabidhi  cherehani za umeme kwa vikundi viwili vya akinamama wa Kata ya Kazimzumbwi ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ikiwa ni  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kisarawe, inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia viwanda vidogo na vya kati.

Na.Alex Sonna- Kisarawe

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ametekeleza ahadi yake ya kutoa cherehani za umeme kwa vikundi viwili vya akinamama wa Kata ya Kazimzumbwi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kisarawe, inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia viwanda vidogo na vya kati.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi cherehani hizo, Dkt. Jafo amesema kuwa wakati wa kampeni aliahidi kuwawezesha akinamama wanaojishughulisha na viwanda vidogo, hususan shughuli za ushonaji, na leo ametimiza ahadi hiyo kwa kukabidhi cherehani vinavyotumia umeme kwa vikundi hivyo viwili vya akinamama.

“Leo nimepata fursa ya kutoa cherehani za umeme kwa vikundi vya akinamama; kikundi cha Darajani na kikundi cha Sanze vya Kata ya Kazimzumbwi ” amesema Dkt. Jafo.

Ameeleza kuwa ana imani kubwa kuwa cherehani hizo zitatumika ipasavyo katika kujenga uchumi wa akinamama hao na jamii kwa ujumla, ikiwemo kushona sare za wanafunzi, nguo za sherehe na mavazi mengine.

“Imani yetu kubwa ni kwamba cherehani hizi zitawasaidia akinamama hawa kujiongezea kipato na kuchangia maendeleo ya familia zao na jamii kwa ujumla,” ameongeza.

Aidha, amesema hatua hiyo inalenga kuhamasisha jamii kutumia na kuendeleza viwanda vidogo vilivyopo katika maeneo yao kama njia ya kukuza uchumi wa ndani.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kazimzumbwi, Mhe. Siza Juma Dilunga, amemshukuru Mbunge Dkt. Jafo kwa kutekeleza ahadi yake kwa akinamama hao, akisema uwezeshaji huo utawasaidia kujikwamua kiuchumi. Ameahidi kuwasimamia wanufaika hao ili kuhakikisha cherehani zilizotolewa zinatumika kwa tija na kuleta manufaa chanya kwa jamii.

Naye, Afisa Miradi kutoka Shirika la Sustainable Planet Foundation, ndugu Aloyce Kamando, amesema shirika hilo limekabidhi cherehani hizo za kisasa kupitia Ofisi ya Mbunge wa Kisarawe kwa lengo la kuchochea maendeleo ya wananchi na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akikabidhi  cherehani za umeme kwa vikundi viwili vya akinamama wa Kata ya Kazimzumbwi ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ikiwa ni  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kisarawe, inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia viwanda vidogo na vya kati.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza mara baada ya kukabidhi  cherehani za umeme kwa vikundi viwili vya akinamama wa Kata ya Kazimzumbwi ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ikiwa ni  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kisarawe, inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia viwanda vidogo na vya kati.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi  cherehani za umeme kwa vikundi viwili vya akinamama wa Kata ya Kazimzumbwi ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa wakati wa Kampeni ikiwa ni  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kisarawe, inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia viwanda vidogo na vya kati.

 Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Joel Nanauka ametoa rai kwa Maafisa Maendeleo ya Vijana nchini kuhakikisha wana takwimu sahihi na changamoto zinazowakabili vijana katika maeneo yao ili kuwa rahisi kuwafikia pamoja na kuhakikisha wanawaunganisha vijana hao na program na fursa zote za Kitaifa zinazohusu ajira,ujuzi na uwezeshaji kiuchumi.

Waziri Nanauka ameyasema hayo leo Jijini Dodoma Desemba 17,2025 wakati akifungua kikao kazi cha Maafisa Maendeleo ya Vijana wa Mikoa na Halmashauri zote nchini.

Na kuwataka pia kuimarisha ushirikiano na wadau wa masuala ya vijana waliopo katika maeneo yao kwa kuwaunganisha na vijana ili kuleta matokeo ya haraka na endelevu huku wakizingatia uwajibikaji,uadilifu na matumizi sahihi ya rasilimali zinazotolewa kwaajili ya vijana zitakazokuja katika maeneo yao.

"Natoa Rai kwenu,katika kutekeleza majukumu yenu hakikisheni mnakuwa na takwimu sahihi za vijana waliopo katika maeneo yenu na changamoto wanazokabiliana nazo pia hakikisheni mnawaunganisha vijana hao na program na fursa zote za Kitaifa na zinazopatikana katika maeneo yenu zinazohusi ujuzi,ajira na uwezeshaji wa kiuchumi"

Aidha Waziri Nanauka amesema kuwa pamoja Serikali ya awamu sita kufanya kila jitihada za kutaka kuwapa sauti vijana lakini bado vijana hao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji majibu ya kimkakati na majibu pamoja kwani wapo waliokosa ajira zenye tija,mitaji,masoko kwa shughuli wanazofanya,fursa za kiuwekezaji na pengo kati ya ujuzi wanaopata vijana na mahitaji ya soko la ajira.

Ambapo pia amesema ili kuwafikia vijana wengi zaidi ni lazima wakae kwa pamoja ili kujadiliana na kukubaliana kutokana na yale ambayo wanayafanya na kuyajua katika mazingira ya kazi ili kujua namna wanavyoweza kuunda mkakati wa pamoja.

"Ni muhimu kutambua kuwa vijana wetu bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinahitaji majibu ya kimkakati na majibu ya pamoja,na changamoto hizo ni pamoja na ukosefu wa ajira au kukosa ajira zenye tija zaidi lakini pia tunakabiliwa na pengo kati ya ujuzi wanaopata vijana katika mifumo yetu ua Kielemu na mahitaji ya soko la ajira".

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ya Maendeleo ya Vijana Jenifer Omoro amesema kuwa Maafisa Maendeleo wa Vijana ni kiungo muhimu kati ya Serikali kuu na Serikali za Mitaa katika kushughulikia masuala ya ya Maendeleo ya vijana na ndio watekelezaji wa Sera,Miongozo,Mikakati,Program na Afua mbalimbali za maendeleo ya vijana hapa nchini.

Na ndio maana kikao kazi hiki kimeandaliwa si tu kwaajili ya kujadiliana bali pia kama jukwaa la kupata mawazo yao wakati ambao pia Wizara inaandaa muundo na mpango mkakati utakaowezesha Wizara na Maafisa Maendeleo ya vijana katika ngazi zote za Mkoa na Halmashauri kutekeleza majukumu ya kuwahudumia vijana kwa ufanisi.

Hiki ni kikao kazi cha kwanza tangu kuanzishwa kwa Wizara hii mpya ya Maendeleo ya Vijana chini ya Ofisi ya Rais ambacho kimewakutanisha Maafisa Maendeleo ya Vijana kutoka mikoa yote 26 na Halmashauri 184 za hapa nchini.



Nilikuwa mtu wa kawaida kabisa. Kila siku nilienda kazini, kulipa bili, na kurudia maisha yale yale. Watu waliniona kama mtu anayepitia maisha bila bahati yoyote. 

Nilijua ndoto zangu hazingeishi, lakini moyo wangu bado ulikuwa na tumaini dogo kuwa labda siku moja jambo kubwa lingeweza kutokea.

Siku ile ya kipekee, nilipata tangazo la shindano la jackpot. Nilijaribu kufikiria kwa makini, nikajiuliza kama ni kweli kwamba mtu kama mimi anaweza kushinda. 

Watu walinicheka pale nilipoanza kujaza fomu; waliona ni bahati kidogo, labda hata ya kupoteza pesa. Hata mimi nilijisikia sina uhakika, lakini nilijaribu kwa moyo mmoja. Soma Zaidi.............
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/hakuna-aliyeamini-angeweza-kushinda-jackpot-mpaka-siku-akaingia-benki-akiwa-mtu-tofauti/
Siku ile nilihisi dunia imenishusha. Tulikuwa tumeandaa kila kitu kwa harusi yetu, watu walikuwa wamefika, sherehe ilikuwa karibu, na ndoto zangu zote zilikuwa tayari kutimia.

Kisha ghafla, mpenzi wangu alinieleza kuwa hataki kuendelea na harusi. Nilishangaa, kuchanganyikiwa, na haswa kulia ndani ya moyo wangu. Hakuna mtu aliyeweza kuelewa maumivu niliyohisi.

Ilikuwa kama ndoto mbaya. Familia yangu, marafiki, na hata wageni walikuwa wameshuhudia huzuni yangu. Nilijaribu kuuliza sababu, lakini hakutoa majibu ya kweli.

Nilihisi kila kitu kilichojengwa kwa upendo na imani kiliporomoka kwa sekunde chache. Nilipoteza usingizi, hamu ya kula, na hata uwezo wa kuamka asubuhi kwa furaha. Soma Zaidi..........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/aliachwa-na-mpenzi-wake-siku-moja-kabla-ya-harusi-miezi-michache-baadaye-dunia-ilimshangaa/
Huyu ni Ally, kijana mchapa kazi anayekuja kutoka Ilala, Dar es Salaam. Kwa muda mrefu alikuwa akijishughulisha na biashara ndogo ndogo ikiwemo uuzaji wa vifaa vya simu na bidhaa za matumizi ya kila siku. 

Licha ya juhudi zake kubwa, biashara zake zilikuwa zikileta faida ndogo sana kiasi kwamba wakati mwingine hakuwa hata na uhakika wa kulipa kodi ya pango au kugharamia mahitaji ya msingi. Kila alipohesabu mapato na matumizi, alijikuta anarudia pale pale bila maendeleo ya maana.

Changamoto hiyo ilimfanya Ally akate tamaa mara kadhaa. Alijaribu kubadilisha aina ya bidhaa, kuboresha huduma kwa wateja, na hata kuongeza muda wa kazi, lakini matokeo yalibaki kuwa yale yale. 

Wateja walikuja na kuondoka bila ongezeko la faida, na mitaji ilionekana kuyeyuka taratibu. Alianza kujiuliza kwa nini biashara zake hazikui ilhali aliona watu wengine wakifanikiwa kwa kufanya vitu vinavyofanana na vyake.

Msongo wa mawazo ulimzidi, hasa alipoona marafiki zake wakipiga hatua kimaisha huku yeye akibaki nyuma. Wakati mwingine alifikiria kuacha kabisa biashara na kutafuta kazi ya kuajiriwa, lakini moyoni alijua ana ndoto ya kuwa mfanyabiashara mkubwa. Kilichomuumiza zaidi ni kuona bidii yake haizai matunda yanayolingana na juhudi alizoweka. Soma Zaidi...........................
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/unavyoweza-kuibadilisha-biashara-yako-na-kukupa-faida/
Leo hii kutana na Emmanuel ambaye ni kijana kutoka jiji la Arusha, kijana mwenye bidii, nidhamu na ndoto kubwa maishani. 

Kwa muda mrefu alikuwa akitamani sana kupata mke wa maisha yake na kuanzisha familia yenye upendo na heshima. Licha ya kuwa na kazi, tabia njema na moyo wa kujituma, upande wa mapenzi ulikuwa ni chanzo kikubwa cha maumivu kwake. 

Kila msichana aliyekuwa akimpenda mwanzoni, baada ya muda mfupi alikuwa akibadilika ghafla na kuondoka bila maelezo ya kuridhisha.

Emmanuel alijikuta akiishi katika msongo wa mawazo, akijiuliza kosa lake ni nini. Marafiki zake walikuwa wakimuona kama mtu mzuri na walishangaa kwa nini kila alipokaribia kufikia hatua ya ndoa, mahusiano yalivunjika. 

Wengine walimwambia labda hakuwa na bahati katika mapenzi, huku wengine wakimshauri apumzike kwanza. Lakini ndani ya moyo wake, Emmanuel alihisi kulikuwa na jambo lisilo la kawaida lililokuwa likimkwamisha.

Kadri muda ulivyopita, maumivu ya mapenzi yalizidi. Alikuwa akitamani sana kuwa na mwenzi wa maisha, mtu wa kushirikiana naye furaha na changamoto za maisha. Endelea Kusoma........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/kila-mwanamke-mzuri-alimuacha-kabla-ya-kupata-msaada-huu/
Nilihisi kila siku inakuwa nzito kuliko ile ya jana. Kila mara nilipowasilisha maombi ya kazi, majibu yalikuwa ndiyo ile ile: “Hatuwezi kukuchagua.” Mara 15 niliyenyimwa kazi hiyo moja, na kila kinyume kilinifanya nijihisi mdogo na kutokuwa na thamani. Marafiki walinipatia ushauri, lakini hakuna kilichokuwa na nguvu ya kubadilisha hali yangu.

Nilijaribu kila kitu: kuboresha CV yangu, kujifunza ujuzi mpya, hata kutumia mawasiliano ya mtu wa karibu. Lakini kila wakati nilipokaribia kupata nafasi, kitu kilishindikana. Nilianza kujiuliza kama maisha yangu yalikuwa yamefungwa, kama kila juhudi yangu ingekuwa bure. Endelea Kusoma....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/alinyimwa-kazi-mara-15-mfululizo-lakini-uamuzi-mmoja-ulimweka-ofisini-ambayo-aliomba-kazi-zamani/

 


Na James K. Mwanamyoto - Arusha

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewataka Wakuu wa Shule za Sekondari nchini kutokuwa kikwazo cha utendaji kazi wa walimu wanaowasimamia, akisisitiza kuwa jukumu lao la msingi ni kuweka mazingira wezeshi yatakayowawezesha walimu kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi.

Prof. Shemdoe wito huo leo kwa Wakuu hao wa shule nchini, wakati akifungua Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA), unaofanyika Jijini Arusha katika Ukumbi wa Tanzania Convention Center (Ngurudoto Mountain Lodge).

“Walimu wakuu mmepewa hizi nafasi za uongozi ili muwaongoze na kuwasaidia walio chini yenu, hivyo msiwe vikwazo kiutendaji katika shule mnazozisimamia,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amesema, haipendezi kwa Mkuu wa shule unapoonekana mwalimu wa taaluma anatafuta njia tofauti ya kupita ili kukukwepa, wakati mwalimu mkuu anapaswa kuwa na mahusiano mazuri na walimu, mahusiano ambayo yatajenga umoja na ari ya walimu katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi.

Prof. Shemdoe amewataka Wakuu wa Shule nchini, kuhakikisha wana vilinda vyeo vyao kwa kufanya kazi vizuri na kwa ushirikiano na watumishi walio chini yao, wakiwemo wanafunzi pamoja na wazazi ili wasiwe sababu ya walimu, wanafunzi na wazazi kukosa tabasamu.

Aidha, Prof. Shemdoe amewaasa Wakuu hao wa shule nchini kutogeuza huduma ya elimu kuwa chanzo cha kujiingizia kipato kwa njia ya rushwa, akitoa mfano wa suala la uhamisho wa walimu na wanafunzi kutokuwa chanzo walimu wao kuomba au kushawishiwa kupokea rushwa. 

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Prof. Shemdoe kufungua mkutano huo, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI anayeshughulikia elimu Bw. Atupele Mwambene amesema kuwa, wakuu wa shule waliohudhuria mkutano huo wako 3500 ambao wanajukumu la msingi la kusimamia malezi ya walimu zaidi ya 100,000 ambao ndio wenye jukumu la kupeleka tabasabu kwa wanafunzi zaidi ya bilioni 5 kote nchini, kupitia utekelezaji wa majukumu yao hususani jukumu la usimamizi wa malezi na ujifunzaji kwa wanafunzi hao.

Kwa upande wake, Rais wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) Bw. Denis Otieno amesema kwamba, wanatambua na kuthamini mchango na azma ya Serikali kuleta maendeleo katika Sekta ya Elimu, miundombinu na afya, hivyo Wakuu wa shule wataendelea kuunga mkono jitahada za Serikali kwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili kuleta mapinduzi katika sekta ya elimu.

Kaulimbiu ya Mkutano Mkuu huo wa 20 wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania Bara wa mwaka 2025 unaofanyika jijini Arusha kwa siku tatu inavyosema: “Teknologia na mafunzo wa ufundi stadi katika kuimarisha ujasiliamali mjini”.

 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewaomba wananchi wa Kisarawe na watanzania kwa ujumla kumuombea Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa ana maono makubwa ya kuwatumikia Watanzania na kulisukuma Taifa mbele kimaendeleo.

Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza katika kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe, kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

“Niwaombe wajumbe wa Halmashauri Kuu kuhakikisha tunamuombea Rais Dkt. Samia kwa kuwa ana kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo Watanzania na kuhakikisha Taifa letu linaendelea kusonga mbele,” amesema Dkt.Jafo

Ameongeza kuwa amani na usalama ni nguzo muhimu za maendeleo ya kiuchumi, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kumuombea Rais na Taifa kwa ujumla.

“Bila amani na usalama, nchi yetu haiwezi kupata mafanikio ya kiuchumi. Nawaomba wananchi wa Kisarawe na Watanzania kwa ujumla tuendelee kumuombea Rais wetu na Taifa letu, kwa sababu kiongozi wetu mwenye maono ni Rais Samia, na lazima tumuombee ili nchi yetu iendelee kusonga mbele,” amesema Dkt. Jafo

Awali, amesema baada ya ushindi huo, chama na serikali vimeanza rasmi awamu mpya ya kazi kwa kipindi cha miaka 5, huku akiendelea na utekelezaji wa majukumu ya maendeleo jimboni kupitia mkakati wao wa ‘Chaka kwa chaka’.

“Tumeanza kazi kwa mara nyingine katika msimu wa 2025–2030. Tumeendelea na kazi za jimboni, tukikutana na viongozi wa kada mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa, watendaji wa halmashauri, madiwani pamoja na wenyeviti wa vijiji na vitongoji vya Wilaya ya Kisarawe,” amesema Dkt. Jafo.

Ameeleza kuwa kikao hicho na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ni cha muhimu sana kwa kuwa ni timu inayobeba jukumu la kuimarisha uhai wa chama pamoja na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Aidha, Dkt. Jafo ametumia mkutano huo kueleza mikakati ya maendeleo ndani ya Wilaya ya Kisarawe, ikiwemo kuboresha sekta za afya, elimu, barabara, maji, umeme pamoja na ujenzi wa viwanda vya kati na vikubwa kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao na kutoa ajira kwa vijana.

“Wilaya ya Kisarawe ipo na mtazamo mpya wa maendeleo, kuhakikisha tunasonga mbele kwa kasi zaidi katika kuboresha maisha ya wananchi,” amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kisarawe, Khalfan Sika, amesema jukumu la wanachama wa CCM ni kuipa ushirikiano Serikali ili kuhakikisha Ilani ya Uchaguzi inatekelezwa kikamilifu.

“Ilani tuliyowapa Mhe. Rais, Mbunge na Madiwani ni Ilani ya CCM. Utekelezaji wake ndio mafanikio na suluhisho la kero za wananchi. Huu ni mkataba kati ya wananchi na CCM,” amesema.

Ameongeza kuwa Ilani hiyo ni maelekezo ya chama ambayo Serikali imepewa dhamana ya kuyatekeleza kwa vitendo, huku akimpongeza Rais Samia na Mbunge Jafo kwa maono makubwa waliyonayo ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Kadhalika, Mwenyekiti huyo amempongeza Dkt. Jafo kwa uungwana wake wa kukutana na Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya mara baada ya kumalizika kwa shughuli za uchaguzi.

“Mara nyingi baada ya uchaguzi, watu waliobeba mzigo mkubwa wa kampeni hawakumbukwi kushukuriwa. Nimpongeze sana Mbunge Jafo kwa kuona umuhimu wa kukutana na wajumbe hawa na kuwashukuru,” amesema.

Amefafanua kuwa katika Wilaya ya Kisarawe, kampeni zilifanyika katika vijiji vyote 84 na mikutano 105 ilifanyika katika ngazi ya vijiji na vitongoji, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanaielewa Ilani ya CCM na sababu za kuchagua chama hicho.

Amesema katika matokeo ya uchaguzi, Rais Samia alipata ushindi wa asilimia 98 huku Mbunge Jafo akipata asilimia 95, hali inayoonesha imani kubwa ya wananchi wa Kisarawe kwa viongozi wao na Chama Cha Mapinduzi.

“Jukumu letu sasa ni kusimamia utekelezaji wa Ilani, kwa sababu uchaguzi mwingine utafanyika mwaka 2030, na wananchi watataka kuona ni kwa kiasi gani tumetekeleza ahadi tulizotoa,” amesema.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwasili katika ukumbi  kwa ajili ya kuzungumza na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kisarawe Khalfan Sika,wakati ,akizungumza   na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Katibu  wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kisarawe Bi.Josephine Mwanga wakati akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare wakati akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

 

Wajumbe wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo (hayupo pichani) wakati,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.