Kwa muda mrefu maisha yangu yaligeuka kuwa uwanja wa mateso makali. Nilikuwa nikishuhudia mambo ya ajabu ambayo sikuwahi kufikiria yangeweza kunipata.
Usiku nilipokuwa nikilala, nilisikia mizigo mizito ikinikandamiza kifua, nikashindwa kupumua na kushindwa hata kupiga kelele kuomba msaada.
Wakati mwingine nilikuwa nikiona vivuli vikizunguka chumbani kwangu, vikicheka kwa sauti ya kutisha, na mara nyingine nilihisi kama kuna mikono isiyoonekana ikinishika shingoni.
Wakati wa mchana hali haikuwa tofauti sana, nilikuwa nikihangaishwa na hofu isiyo na sababu, uchovu uliokithiri na migogoro isiyoisha katika maisha yangu.
Nilijua wazi kwamba haya yote yalikuwa matokeo ya uchawi uliokuwa unanifuata kila mahali. Kazi yangu ilianza kudorora kwa sababu nilikosa nguvu ya kufanya chochote. Ndugu na marafiki walianza kunitazama kama mtu asiye na msaada, na wengine walidhani nimechanganyikiwa.
Nilijitahidi kutafuta msaada wa kawaida kwa madaktari na hata kwa maombi yangu ya binafsi, lakini mambo yaliendelea kuwa mabaya zaidi. Usiku ulipokuwa ukiingia nilikuwa nikiingiwa na hofu kubwa, kwa sababu nilijua mzimu au nguvu mbaya ingenisumbua tena.
Nilijiona kama nimefungwa minyororo isiyoonekana ambayo haikuniruhusu kuishi maisha ya kawaida. Siku moja nilipokuwa nikisoma mtandaoni, nilikutana na ushuhuda wa watu waliokuwa wamepitia hali kama yangu lakini wakapata msaada. SOMA ZAIDI.
Niliona maisha yangu yote yakiporomoka ghafla, nikajua heshima yangu imefutwa milele. Mwanamke aliyenishitaki alijua fika hakuwa na ushahidi wowote. Lengo lake lilikuwa kunilazimisha nimpe pesa nyingi ili kunyamazisha kesi.
Alijua jina la ubakaji lingetisha na kunifanya nikubali masharti yake. Nilipoambiwa nitoe fedha ili nisionekane kortini, nilikataa. Nilihisi moyoni kuwa ningepoteza kila kitu iwapo ningekubali uongo huo.
Nilipoamua kusimama mahakamani, wengi waliniona kama mtu wa kujitakia maafa. Hata hivyo nilijua ukweli ulikuwa upande wangu. Nilichohitaji ni nguvu ya kusimama imara wakati huu mgumu. SOMA ZAIDI.
Usiku mmoja uliokuwa umesheheni giza na ukimya mzito, mjini kulizuka taharuki kubwa baada ya wezi kuvamia na kuvunja maduka yote kwenye barabara tuliyokuwa tunafanya biashara.
Kelele za kufuli zikivunjwa na milango ikipigwa ziliwafanya wenye maduka waliokuwa majumbani mwao kuamka kwa hofu, lakini hakuna aliyeweza kufika eneo la tukio kwa sababu wezi walikuwa wengi na wamejihami.
Asubuhi ilipofika, hali ya simanzi na hasira ilitanda miongoni mwa wafanyabiashara. Maduka yalikuwa yameachwa yakiwa wazi, rafu tupu, na hasara kubwa ikawa imewakumba.
Nilipofika dukani kwangu, majirani walikuwa wamejaa pale wakiwa na macho ya mshangao. Walidhani mimi pia ningekumbwa na masaibu yale yale. Lakini cha kushangaza ni kwamba lango langu lilikuwa limefungwa vilevile nilivyoacha jana usiku.
Hakuna kufuli lililovunjwa, hakuna mlango ulioguswa, na mali yangu yote ilikuwa salama kabisa. Wengine walishangaa wakajiuliza ni kwa nini wezi walipita kila duka lakini langu hawakuweza kulivunja.
Wengine walidhani nilikuwa nimeajiri mlinzi wa siri, kumbe ukweli ulikuwa tofauti kabisa. Siku chache kabla ya tukio hilo, nilikuwa nikipitia changamoto kubwa. Hali ya wizi katika eneo letu ilikuwa imeongezeka kwa kasi.
Wafanyabiashara wengi walikuwa wanalalamika kwamba kila wiki kulikuwa na duka lililoporwa. Mimi mwenyewe nilikuwa na wasiwasi mkubwa, hasa kwa sababu sikuwa na uwezo wa kumlipa mlinzi kila mwezi.
Ndipo nilipoamua kutafuta msaada wa kiroho ambao nilikuwa nimesikia watu wengi wakizungumza.SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi wetu, Lushoto
Wananchi wa Jimbo la Lushoto Julai 16, 2026 wamemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa Barabara ya Malibwi–Kwekanga–Ngwelo, wakisema hatua hiyo imeondoa kero ya muda mrefu iliyokuwa ikikwamisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa mazao, na kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Lushoto Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, kwa kuifikisha Serikalini changamoto hiyo ambayo imepatiwa ufumbuzi.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kwekanga, Bw. Salim Khamis Nyongo, amesema barabara hiyo inayojengwa inaunganisha Kata za Malibwi, Kwekanga, Kilole na Ngwelo pamoja na Jimbo la Mlalo, hivyo ni mhimili muhimu wa uchumi kwa wananchi wa eneo hilo ambao ni wakulima wa nyanya, viazi na karoti.
“Kwa miaka mingi tumeshindwa kusafirisha mazao yetu kwa urahisi kutokana na ubovu wa barabara, hivyo tunamshukuru Rais Samia kwa kututatulia kero yetu ya barabara na tunampongeza Prof. Shemdoe kwa kuwasilisha kero yetu na hatimaye imetatuliwa,” amesema Bw. Nyongo.
Bi. Rukia Selemani, Mkazi wa Kijiji cha Kwekanga amesema kuwa kabla ya kuanza kwa ujenzi wa barabara hiyo walikuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kusafirisha mazao yao, lakini hata wakati ujenzi ukiendelea tayari wameanza kuona manufaa yake kwani imewarejeshea matumaini na kuwaletea tabasamu, hivyo wanamshukuru Prof. Shemdoe kwa kuhakikisha changamoto hiyo inafanyiwa kazi.
Kwa upande wake, Bi. Fadhila Salehe ambaye pia ni mkazi wa kijiji cha Kwekanga amesema hapo awali magari yalikuwa yakiishia Malibwi, jambo lililowalazimu wananchi kubeba mizigo kichwani au kutumia pikipiki kwa gharama kubwa, hivyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa barabara hiyo na kumpongeza Mhe. Prof. Riziki Shemdoe kwa ufuatiliaji na usimamizi mzuri wa mradi huo.
Naye Bi. Biasina Shaban Mtari, Mkazi wa Kijiji cha Kwekanga amesema anashukuru kwa sasa magari kutoka Dar es Salaam, Arusha na Tanga yanafika kwenye makazi ya wananchi pasipo na kikwazo chochote, tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Mkazi Mwingine wa Kijiji cha Kwekaga, Bi. Shekela Ramadhan Mohamed amesema ujenzi wa barabara hiyo umeboresha pia maisha ya watoto wanaokwenda shule, kwani zamani walikuwa wakirejea nyumbani wakiwa wamechafuka kutokana na ubovu wa barabara, lakini sasa wanakwenda shuleni na kurejea nyumbani wakiwa wasafi.
Akizungumzia utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi wa TARURA Wilaya ya Lushoto, Bi. Brand Joseph Nyaki, amesema Barabara ya Malibwi–Kwekanga–Ngwelo inarekebishwa kwa kiwango cha zege na Mkandarasi Ms. Broader Construction Company Ltd, ikihusisha tabaka la zege lenye unene wa milimita 150 kwa urefu wa kilomita 1.5.
Bi. Nyaki ameongeza kuwa, mradi huo umeleta manufaa ya kiuchumi kwa vikundi vya Songambele, Inuka na Mkombozi vinavyonufaika na miradi ya vikundi kwa huduma wakati wa utekelezaji wa ujenzi huo wa mradi wa barabara, huku akimshukuru Mhe. Prof. Shemdoe kwa kuendelea kusimamia upatikanaji wa miundombinu bora ya barabara inayofungua fursa za maendeleo na kuboresha maisha ya wananchi wa Jimbo la Lushoto.
Nilipopata nyumba nyingine, nilianza kuugua mara kwa mara bila sababu iliyoeleweka. Nilikwenda hospitalini, nikapimwa mara kadhaa, lakini madaktari hawakuona tatizo kubwa. Nilihama tena nikidhani labda mazingira ya pale hayakuwa mazuri.
Lakini hata nilipohamia nyumba ya tatu, mambo yalikuwa yale yale. Biashara yangu ilianza kushuka, vifaa vya umeme vilikuwa vikiharibika mara kwa mara, na nilikuwa nikipata ndoto za kutisha karibu kila usiku. Nilianza kuishi kwa hofu na wasiwasi.
Miaka ilivyopita, nilihama nyumba ya nne, ya tano na hatimaye ya sita. Nilikuwa nimetumia fedha nyingi kwa kuhama, lakini mikosi haikuisha. Watu wa karibu walinishangaa. Wengine walisema nilikuwa nakimbia matatizo badala ya kuyatatua, lakini mimi nilijua kulikuwa na jambo lisilo la kawaida.
Siku moja nilimweleza mjomba wangu kila kitu kilichokuwa kinanitokea. Alikaa kimya kwa muda kisha akaniambia, “Inawezekana tatizo si nyumba unazoishi, bali kuna kizuizi kinachokufuata popote unapoenda.” SOMA ZAIDI.
Mwanzoni kila kitu kilionekana kwenda vizuri. Nilipata wateja wachache na niliamini mafanikio yalikuwa karibu. Lakini baada ya mwezi mmoja tu, matatizo yalianza.
Ndani ya miezi mitatu, mtaji wote ulikuwa umeisha. Nilibaki na deni kubwa la benki, simu za wadai kila siku na familia iliyokuwa imekata tamaa. Nilishindwa hata kulala usiku kwa mawazo. Nilifikiria kuuza nyumba niliyokuwa nimejenga ili kulipa sehemu ya deni.
Nilitembea kwa wataalamu wa biashara kutafuta ushauri. Wote walinielekeza namna ya kuboresha usimamizi wa fedha, lakini hata nilipofuata ushauri wao, mambo hayakubadilika. Nilianza kuamini kuwa kulikuwa na kizuizi kisichoonekana kilichokuwa kinaharibu kila nilichokifanya. SOMA ZAIDI.
Mara ya kwanza nilidhani nilikosea katika maandalizi. Nilijipanga upya na kusoma kwa bidii zaidi. Lakini nilipofanya mtihani wa pili, matokeo yalikuwa mabaya kuliko ya kwanza. Nilihisi aibu kubwa. Wenzangu waliendelea na masomo, huku mimi nikirudia mitihani.
Nilipopata nafasi ya tatu, niliahidi nafsi yangu kwamba lazima nifaulu. Nilitumia fedha nyingi kwa tuition, nikanunua vitabu vipya na nikajitenga na marafiki ili nisome kwa utulivu. Lakini nilipata matokeo yale yale nilifeli tena.
Nilianza kuamini labda sikuumbwa kwa ajili ya masomo. Familia yangu ilivunjika moyo, na baadhi ya watu waliniambia nitafute kazi za mikono badala ya kuendelea kupoteza muda darasani. Maneno hayo yalinichoma moyo, lakini sikuwa tayari kukata tamaa.
Siku moja nilikutana na mwalimu wangu wa zamani ambaye alinishangaa kuniona bado nikipambana na mitihani. Baada ya kusikiliza simulizi yangu, aliniambia kuna wakati vikwazo vya mafanikio haviwezi kuelezeka kwa juhudi pekee. SOMA ZAIDI.
NEEC YAHITIMISHA MAFUNZO YA FURSA ZA MITAJI NA PROGRAMU ZA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI MKOANI RUKWA
📌 Ukaguzi wa miundombinu wabaini hakuna changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara
📌 Wafanyabiashara waipongeza TANESCO kwa utatuzi wa haraka wa hitilafu
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limebaini kuwa huduma ya umeme katika Jengo la Kituo cha Mabasi cha Mwenge inaendelea kuwa ya uhakika baada ya kufanya ukaguzi wa miundombinu kufuatia taarifa zilizosambaa zikidai kuwepo kwa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara katika eneo hilo.
Ukaguzi uliofanywa Julai 15, 2026, ulihusisha tathmini ya miundombinu ya umeme pamoja na mazungumzo na wafanyabiashara wanaofanyia shughuli zao katika jengo hilo. Matokeo ya ukaguzi yameonesha kuwa hakuna changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara kama ilivyodaiwa, huku hitilafu chache zinazojitokeza zikishughulikiwa kwa wakati.
Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kinondoni Kaskazini, Mhandisi Jeremiah Jahulula, amesema shirika lilichukua hatua ya kufika eneo hilo ili kujiridhisha na hali halisi ya huduma na kusikiliza maoni ya wateja.
“Tumekagua miundombinu na kuzungumza na wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao hapa. Tulichobaini ni kwamba huduma ya umeme ni ya uhakika, na pale hitilafu chache zinapojitokeza, hupatiwa ufumbuzi kwa wakati ili shughuli za wananchi zisiathirike,” amesema Mhandisi Jahulula.
Ameongeza kuwa TANESCO imeendelea kuimarisha mawasiliano na wateja kupitia makundi maalumu ya WhatsApp pamoja na namba ya huduma kwa wateja 180, hatua inayorahisisha upokeaji wa taarifa za hitilafu na kuzifanyia kazi kwa haraka.
Kwa upande wao, wafanyabiashara wanaofanyia shughuli zao katika jengo hilo wameeleza kuridhishwa na huduma ya umeme inayotolewa, wakisema imewawezesha kuendesha biashara zao bila usumbufu.
Mmoja wa wafanyabiashara hao, Bi. Latifa Tuli, anayemiliki saluni katika jengo hilo, amesema hajawahi kushuhudia changamoto ya muda mrefu ya kukatika kwa umeme inayoweza kusimamisha biashara yake.
“Biashara yangu inategemea umeme kwa kiwango kikubwa. Kwa uzoefu wangu, sijawahi kukwama kufanya kazi kutokana na kukosekana kwa umeme kwa muda mrefu. Changamoto zinapotokea na kutoa taarifa TANESCO hufika kwa haraka na kuzitatua, jambo linalotupa utulivu wa kuendelea na biashara,” amesema Bi. Latifa.
Ukaguzi huo unaendelea kudhihirisha dhamira ya TANESCO ya kusimamia ubora wa huduma zake kwa karibu, kusikiliza maoni ya wateja na kuchukua hatua kwa wakati pale changamoto zinaporipotiwa.
NAIBU Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya, amezungumzia umuhimu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), kushirikiana na sekta binafsi na taasisi za elimu ya uhandisi katika kuendesha maabara zake za kisasa.
Hatua hiyo itaiwezesha TANROADS kuongeza mapato, kuimarisha huduma za kitaalamu na kuifanya Taasisi hiyo kuwa kitovu cha umahiri katika upimaji wa vifaa vya ujenzi wa barabara nchini na ukanda wa Afrika Mashariki.
Eng. Kasekenya amesema hayo leo wakati wa ziara yake kukagua maendeleo ya ujenzi wa Makao Makuu ya TANROADS jijini Dodoma.
Ameitaka TANROADS kuhakikisha viongozi wake wakuu na watumishi wanaopaswa kuhamia Makao Makuu ya nchi wanakamilisha uhamisho wao ifikapo mwisho wa Agosti mwaka huu.
Amemtaka Mkandarasi CRJE East Africa Ltd. anayejenga jengo hilo ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 85 kuongeza kasi ili likamilike kwa wakati.
"Tunapoelekea katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ni muhimu Taasisi za umma kuangalia namna ya kushirikiana na sekta binafsi ili kuongeza tija kwa umma hivyo TANROADS ina maabara za kisasa ambazo zinaweza kutumika kutoa huduma za kibiashara na kitaalamu kwa taasisi mbalimbali ndani na nje ya nchi," amesisitiza Naibu Waziri Kasekenya.
Aliongeza kuwa ushirikiano, ubunifu, uadilifu na moyo wa kujituma kutaifanya TANROADS kuwa kituo cha umahiri katika upimaji wa vifaa vya ujenzi wa barabara na kuongeza uwezo wa wataalamu wa ndani kupitia ubadilishanaji wa uzoefu na teknolojia.
Eng. Kasekenya amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejidhatiti kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa ili kuimarisha uwezo wa Taasisi za Serikali kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
"Serikali imehakikisha TANROADS inapata eneo kubwa pamoja na majengo na maabara za kisasa zinazokwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia duniani," amesema Eng. Kasekenya.
Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma, Eng. Zuhura Amani, amesema mradi huo wenye thamani ya Shilingi bilioni 49.72 unatekelezwa na kampuni ya CRJE East Africa Limited chini ya usimamizi wa Tanzania Building Agency (TBA)
▪️Tanzania yajipanga kuwa kitovu cha huduma bora za Maabara ya madini kusini mwa Jangwa la Sahara
■ Waziri Mavunde amshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia kwa uamuzi wa ujenzi wa maabara
■ Amtaka Mkandarasi kukamilisha ujenzi kwa wakati
■ Ujenzi wa Maabara kugharimu zaidi ya Bilioni 14.3
Kufuatia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa maabara ya kisasa ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), hatua hiyo inakwenda kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za maabara ya madini kusini mwa Jangwa la Sahara.
Hayo yamesemwa leo tarehe 15 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maabara ya GST uliopo Kizota, Jijini Dodoma.
"Tunamshukuru Rais wetu Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha za utekelezaji wa mradi huu wa kisasa, unaokwenda kuifanya Nchi yetu kuwa kinara na mahiri katika utoaji wa huduma za maabara za madini", amesema.
"Mradi huu pia unakwenda kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za maabara kwa Nchi za Afrika ya Mashariki na Kati, kutokana na ubora wa huduma hizo kuwa za kimataifa" ameeleza Waziri Mavunde.
Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa kwa muda mrefu wachimbaji wadogo wamekuwa wakipata changamoto ya upimaji wa sampuli zao kwenye maabara, hali iliyopelekea kushindwa kufanya shughuli zao kiufanisi.
Mavunde amesitiza kuwa ujio wa maabara hiyo ya kisasa unakwenda kuwa mwarobaini wa changamoto za wachimbaji ikiwa ni pamoja na kuhudumia wachimbaji wengi zaidi kwa ubora wa kimataifa.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Madini Tanzania, Mhandisi Ally Samaje ameeleza kuwa ujenzi wa mradi huo wa maabara unagharimu shilingi bilioni 14.3 na upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji ambapo unataraji kukamilika ifikapo Mwezi Septemba, 2027.
Aidha, ameongeza kuwa maabara hiyo ikikamilika itakuwa ni ya kisasa na inakwenda kuhudumia wateja wengi wa ndani na nje ya Nchi.





































