Na. Jordan Mbwambo, WF, Dodoma.

Serikali imeanza kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, hatua inayolenga kufungamanisha na kuboresha usimamizi wa shughuli za Mnyororo wa Ugavi nchini ili kuongeza ufanisi, matumizi bora ya rasilimali na kupata thamani halisi ya fedha za umma.

Hayo yalibainishwa na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Usimamizi wa Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi. Anne Swila, wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yenye Kaulimbiu ya “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Alisema kuwa Sera hiyo inalenga maeneo sita makuu, yakiwemo Ununuzi wa Umma, Ugomboaji na Uondoshaji wa Mizigo ya Serikali, Upokeaji na Urejeshaji, Utunzaji na Uhifadhi, Usambazaji, pamoja na uhifadhi wa Mazingira na Utawala Bora.

‘‘Kwa miaka mingi tumekuwa na sheria nzuri za ununuzi, lakini hazikuwa zimeunganishwa kwa msingi mmoja wa kisera, Sera hii sasa inakwenda kuziba pengo hilo na kuhakikisha kila shilingi ya umma inatumika kwa thamani yake halisi, kwa kuhakikisha mikakati ya utekelezaji inajumuisha kuimarisha udhibiti wa bei, uchaguzi wa wazabuni, na kuendeleza Kada ya Ununuzi na Ugavi Serikalini " alieleza Bi. Swila.

Alisisitiza kuwa ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wa Sera hii itaongeza ushindani na kuwapa fursa wazabuni wazawa, sekta binafsi na makundi maalum ya kijamii, hatua itakayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi na kuchochea ukuaji wa ajira.

Bi. Swila alisema Sera hiyo pia inatarajiwa kuimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki na rasilimali za ndani, kuvutia uwekezaji katika miundombinu ya uhifadhi na usambazaji, na hivyo kuifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

‘‘Miongoni mwa mafanikio yanayotarajiwa ni kuongezeka kwa ufanisi, udhibiti bora wa gharama, kuimarika kwa ubora wa huduma kwa wananchi, ongezeko la ajira, uzingatiaji wa uhifadhi wa mazingira, na kuwa na mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini utakaohakikisha utekelezaji wa sera unaleta tija iliyokusudiwa’’, alifafanua Bi Swila.

Aidha, alisema kuwa Sera hiyo itawezesha kuwepo kwa mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini, hatua itakayoifanya sekta ya mnyororo wa ugavi kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kuchangia kupunguza umasikini nchini.

Sera hiyo inatarajiwa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2026 hadi 2036 na tathmini ya utekelezaji itafanyika kila baada ya miaka mitano ya utekelezaji


 


“Sasa najua ni nini ninapaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua sukari au hata ninaponunua gesi ya kupikia.” Ni kauli ya Bw. Bilson Vedastus, mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Viwanja vya Chinangali Park, Dodoma.

Banda hilo limekuwa kitovu cha msongamano siku ya tatu ya maonesho, Juni 18, 2026 huku wananchi wakijitokeza kwa wingi kujifunza jinsi Serikali kupitia WMA inavyohakikisha kila kipimo kinachotumika kibiashara na katika huduma ni sahihi. Maonesho yalianza tarehe 16 Juni na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 23 Juni 2026.

Baada ya kupata maelezo ya hatua kwa hatua kutoka kwa wataalamu, wengi wameahidi kuwa mabalozi wa Wakala wa Vipimo katika maeneo yao. 

“Tumeona jinsi pampu, mizani na vifaa vingine vinavyohakikiwa kuhakikisha vinapima kwa usahihi. Sasa hatuwezi kukaa kimya tukiona mteja anadhulumiwa. Tutawaeleza jirani zetu na kuripoti udanganyifu popote tutakapouona,” alisema Bi. Asha Siyaya.

Wataalamu wa WMA, Albogast Kajungu, Mbwana Amani na Said Ibrahim waliwaeleza wananchi kuwa uhakiki wa vipimo unagusa sekta zote zinazowahusu moja kwa moja kila siku. Katika sekta ya mafuta, pampu zote huhakikiwa na kuwekewa stika ya uthibitisho. Sokoni na madukani, mizani inayotumika kupimia sukari, mchele na mboga hufanyiwa ukaguzi ili mteja asipoteze pesa.

Sekta ya maji na umeme nayo haikuachwa nyuma. Mita za maji na umeme zinazotumika nyumbani na kwenye biashara ndogo huhakikiwa na kuthibitishwa ili kuhakikisha mteja analipia matumizi halisi na si makadirio au idadi isiyo sahihi. Vile vile mitungi ya gesi ya kupikia, bidhaa zilizofungashwa kama unga na sabuni, pamoja na mizani za barabarani zote huhakikiwa mara kwa mara.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Meneja Mawasiliano wa Wakala wa Vipimo, Bi Veronica Simba amesema lengo ni moja: kuhakikisha mwananchi anapata thamani kamili ya kila shilingi anayolipa, na amewahamasisha wananchi wengi zaidi kutembelea banda hilo kabla ya maonesho kuhitimishwa.






NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA

SERIKALI imesema Tanzania bado haina mgonjwa wa Ebola na hali ya usalama wa afya nchini inaendelea kuwa nzuri, huku ikieleza kuwa imeimarisha hatua mbalimbali za kuzuia ugonjwa huo kuingia nchini kutokana na mlipuko unaoendelea katika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uganda.

Biashara yangu ilianza vizuri sana. Mwanzoni nilikuwa napata wateja kila siku na mauzo yalikuwa yakiongezeka. Lakini baada ya muda, mambo yalibadilika ghafla. Wateja wakapungua, bidhaa zikaanza kukaa muda mrefu bila kununuliwa, na gharama zikaanza kunizidi.

Nilijaribu kila njia niliyoweza kupunguza bei, kubadilisha bidhaa, hata kubadilisha eneo la biashara. Lakini bado hakuna kilichobadilika. Kila siku nilikuwa nikikumbana na hasara zaidi, na polepole nikaanza kupoteza matumaini.
Ilifika hatua nikaanza kufikiria kufunga kabisa biashara.

Ilikuwa vigumu kukubali kushindwa, lakini hali ilikuwa inanilazimisha kuona ukweli. Baada ya muda wa mawazo mengi, niliamua kutafuta mwongozo wa ziada. SOMA ZAIDI.
Maisha yetu yalibadilika ghafla pale ndugu yangu alipoanza kubadilika tabia. Alikuwa mtu mchangamfu, mwenye ndoto na malengo, lakini polepole akaanza kujitenga, kupoteza mwelekeo, na hatimaye kuingia kwenye matumizi mabaya ya dawa za kulevya.

Mwanzoni tulidhani ni hatua ya muda tu, lakini hali ilizidi kuwa mbaya. Alianza kupoteza heshima, afya yake ilidhoofika, na hata mawasiliano ndani ya familia yakavunjika. Kila tulipojaribu kumshauri, alionekana kama hataki kusikiliza.

Ilinivunja moyo kumuona akizama zaidi kila siku. Nilihisi kama tunampoteza polepole, na hakuna aliyekuwa na jibu la kumsaidia. Familia ilianza kukata tamaa, lakini mimi sikuweza kuacha kuamini kwamba bado kulikuwa na njia ya kumrudisha. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi nilikata tamaa kabisa na masomo. Nilikuwa nimeanza vizuri, lakini kadri muda ulivyopita, nikapoteza mwelekeo. Alama zilianza kushuka, motisha ikaisha, na hatimaye nikajikuta nimeacha kabisa kile nilichokuwa nimeanza.

Watu wengi walinishauri nirudi shuleni, lakini ndani yangu sikuwa na nguvu wala hamasa ya kuanza tena. Nilihisi kama nimechelewa, na hata nikirudi, singeweza kufanikiwa kama mwanzo. Hali hiyo ilinifanya nibaki pale pale bila maendeleo.

Kadri siku zilivyopita, nilianza kuona athari za uamuzi wangu. Maisha yalikuwa yanakwama, na nilianza kujilaumu kwa kuacha masomo. Ndani yangu kulikuwa na sauti ndogo iliyoniambia bado naweza kubadilisha hali hiyo, lakini sikuwa najua nianzie wapi. SOMA ZAIDI.

Maumivu ya usaliti yameendelea kuwa moja ya changamoto kubwa inayotikisa mahusiano mengi katika jamii ya sasa. 

Watu waliowahi kuamini kwa dhati hujikuta wakibeba huzuni, hasira na maswali mengi baada ya kugundua kuwa walisalitiwa na wale waliowapenda. Kutokana na hali hiyo, wengi sasa wameanza kutafuta njia salama za kujijenga upya na kulinda mapenzi yao yasivunjike tena.

Wataalamu wa mahusiano wanasema uponyaji wa penzi lililoumizwa huanza kwa mazungumzo ya kweli. Kukaa chini na kueleza hisia bila kuficha jambo husaidia kuondoa mizigo ya moyoni. Wenzi wanaoweza kuzungumza kwa uwazi kuhusu kilichotokea, sababu zake na matarajio ya baadaye huwa na nafasi kubwa ya kurejesha uelewano. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu nilikuwa naingia kwenye mahusiano yaliyoanza vizuri lakini yakavunjika ghafla. Kila mara ilikuwa ni hadithi ile ile mwanzo mzuri, matumaini makubwa, halafu mwisho usioeleweka. Nilijikuta nikibaki na maumivu na maswali mengi yasiyo na majibu.

Nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa kwangu.

Nilijaribu kubadilika, kuwa mvumilivu zaidi, na kujitahidi kuelewa wenzi wangu. Lakini licha ya jitihada hizo zote, matokeo hayakubadilika. Ilikuwa kama mzunguko unaojirudia bila mwisho. Kadri muda ulivyopita, nilianza kupoteza imani na mahusiano kabisa.

Nilihisi kama upendo haukuwa na nafasi katika maisha yangu. Hali hiyo ilinifanya nijitenge kihisia ili kuepuka maumivu zaidi.SOMA ZAIDI.


‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imewakutanisha wahandisi na wataalamu wa sekta ya barabara katika mafunzo maalum yanayolenga kuimarisha usalama wa watumiaji wa barabara wakati wa usanifu, ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara nchini.

‎Mafunzo hayo yanayofanyika mkoani Morogoro yanalenga kuongeza uelewa na uwezo wa wataalamu katika kuzingatia viwango vya usalama barabarani ili kupunguza ajali na kulinda maisha ya watumiaji wote wa barabara.

‎Akizungumza katika mahojiano maalum, Mratibu Msaidizi wa Mradi wa RISE, Mhandisi Lwitiko Mwandobo, amesema mafunzo hayo yameandaliwa mahsusi kuwajengea uwezo wahandisi na kuwakumbusha wajibu wao wa kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara unazingatiwa tangu hatua ya usanifu hadi utekelezaji wa miradi.

‎"Tunataka kuhakikisha kwamba kila mradi wa barabara unazingatia usalama kwa kuweka alama zote muhimu, miundombinu rafiki kwa watumiaji na hatua nyingine za kinga zitakazosaidia kupunguza ajali zinazoweza kuepukika. Hii ni sehemu ya juhudi za kulinda maisha ya wananchi na mali zao", amesema Mhandisi Mwandobo.

‎Kwa upande wake, Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema usalama wa watumiaji wa barabara ni jukumu la pamoja linalohitaji ushirikiano wa wadau wote ili kufikia lengo la kupunguza kwa kiwango kikubwa ajali za barabarani na pia kuna umuhimu wa kuendelea kuimarisha mifumo ya kisheria na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya barabara.

‎"Tukizingatia usalama katika kila hatua ya ujenzi wa barabara, kuimarisha elimu kwa umma na kuhakikisha miundombinu inakidhi viwango vinavyotakiwa, tutapunguza kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani na madhara yake kwa jamii",  amesema Mhandisi Mkinga.

‎Naye, Mratibu wa Masuala ya Usalama Barabarani kutoka (TARURA), Mhandisi Faizer Mbange, amesema mwelekeo wa sasa katika ujenzi wa barabara unalenga kuhakikisha mahitaji ya makundi yote ya watumiaji wa barabara yanazingatiwa ikiwemo waenda kwa miguu, waendesha baiskeli, bodaboda, bajaji pamoja na watumiaji wa vyombo vingine vya usafiri.

‎Amesema tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo usanifu wa barabara ulijikita zaidi katika magari, sasa miundombinu ya barabara inapaswa kuwa jumuishi na salama kwa kila mtumiaji bila kujali aina ya usafiri anaotumia.

‎Mafunzo hayo yamewakutanisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za sekta ya barabara na usafiri zikiwemo Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Ofisi ya Waziri Mkuu– TAMISEMI, TARURA na Mfuko wa Barabara (Road Fund).






Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Jakaya Kikwete (Mb), amefungua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, yanayofanyika kuanzia Juni 16 hadi 23, 2026 yakibeba kaulimbiu isemayo, "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu."

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, ameipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa huduma mbalimbali inazotoa kwa wananchi na kuitaka kuongeza juhudi za kuelimisha umma kuhusu hatua na mafanikio ya Serikali katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Ridhiwani alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la Mamlaka ya Elimu Tanzania katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, ambapo alipata fursa ya kujionea huduma na shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo.

Akizungumza alipotembelea banda hilo la TEA, Ridhiwani alisema taasisi hiyo ina mchango mkubwa katika maendeleo ya elimu nchini kupitia usimamizi wa Mfuko wa Elimu wa Taifa, hivyo ni muhimu wananchi wakaendelea kupata taarifa sahihi kuhusu miradi na mafanikio yanayotekelezwa kwa manufaa yao.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania, Eliafile Solla, alisema ushiriki wa TEA katika maadhimisho hayo unalenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu na shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na mamlaka hiyo kupitia Mfuko wa Elimu wa Taifa.

Ametaja majukumu makuu mawili yya TEA ambayo ni kutafuta rasilimali fedha na vifaa kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo na kisha kugawa rasilimali hizo katika shule na taasisi za elimu kwa lengo la kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia nchini.

“Tunatumia maonesho haya kuwafikia wananchi moja kwa moja ili waelewe namna TEA inavyoshirikiana na wadau mbalimbali katika kuimarisha sekta ya elimu kwa kutoa rasilimali zinazosaidia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu pamoja na upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia,” amesema Solla.

Ameongeza kuwa watumishi wa TEA walioshiriki maonesho hayo wamejipanga kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo, sambamba na kuendelea kutekeleza jukumu la kutafuta rasilimali fedha na vifaa vitakavyosaidia kuimarisha juhudi za Serikali za kuboresha mazingira ya elimu nchini.

Serikali ya Tanzania imefafanua uamuzi wake wa kuweka akiba ya fedha za kigeni ikiwemo dola za Marekani na dhahabu, ikieleza kuwa hatua hiyo inatokana na mabadiliko ya kiuchumi yanayoendelea kuikumba dunia.


Kauli hiyo imetolewa leo bungeni Dodoma na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, aliyetaka ufafanuzi kuhusu sera ya serikali ya ununuzi na uuzaji wa dhahabu pamoja na maslahi mapana ya taifa.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa dhahabu sasa imejumuishwa rasmi katika mfumo wa akiba ya fedha za kigeni, kama ilivyo kwa dola za Marekani, na si bidhaa ya biashara ya kawaida inayotumika kwa matumizi ya kila siku ya kiuchumi.

Amefafanua kuwa mpango wa ununuzi wa dhahabu umeendelea vizuri na hadi sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na takribani tani 27 za dhahabu kama sehemu ya akiba yake ya taifa.

Aidha, Waziri Mkuu huyo amesisitiza kuwa dhahabu ya taifa haiuzwi kiholela, na akabainisha kuwa utaratibu wa uuzaji wake, pale inapobidi, hufanywa kupitia taasisi rasmi za fedha au kwa tangazo la umma kupitia magazeti ya serikali, si kwa watu binafsi.

Dkt. Mwigulu amewahakikishia wabunge kuwa hakuna uuzaji holela wa dhahabu unaofanyika, bali mfumo uliowekwa unalenga kulinda maslahi ya taifa na kuimarisha uthabiti wa uchumi wa nchi.


 NA DENIS CHAMBI, TANGA.


JUMLA ya miradi  ya maendeleo 73 iliyopo mkoani  Tanga yenye thamani  zaidi ya shilingi Bilioni 27.7 inatarajiwa kupitia na mwenge  wa Uhuru kwa mwaka 2026 katika halmashauri 11.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian amesema kuwa Mwenge huo  utakimbizwa kwa umbali wa kilomita 1,340  ambapo , miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, miradi 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, miradi 11  itakaguliwa na baadaye kukabidhiwa mkoani Kilimanjaro junior 28,2026 katika viwanja vya shulen ya msingi Hedalu wilayani Korogwe.


Aidha Balozi Dkt Burian ameongeza kuwa kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu huku Shilingi bilioni 15.47 zikiwa ni kutoka katika mchango wa wahisani.


Akizungumzia kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema,  "Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo amewasisitiza wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi na kushiriki shughuli zote za Mwenge huo ikiwa ni ishara ya kuonyesha uzarendo kwa Taifa 


"MWENGE huu wa Uhuru ukiwa mkoani Tanga utafanya kazi katika miradi 73 ambapo  utaweka mawe ya msingi jumla ya miradi 34, utafungua na kizindua jumla ya miradi 26 na utatembelea na kukagua jumla ya miradi 11 ya shughuri za vijana na miradi miwili ya maendeleo ya sekta ya maji, miradi hii yote ina jumla ya thamani ya shilingi Bilioni 27,764, 390,480.01." amesema Dkt Burian.


"Fedha ambazo zimetoka katika nguvu za wananchi ni shilingi Million 300,638,449.32, fedha kutoka halmashauri ni shilingi Bilioni 1,79,673,076.72, fedha kutoka serikali ni shilingi Bilioni 10, 707,064,607.76 na fedha kutoka kwa wahisani ni shilingi milioni 15, 477, 014" amebainisha.


Aliongeza kuwa baadhi ya  wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja wa kitaifa na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.


Mbali na kuhamasisha maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na umuhimu wa lishe bora kwa jamii.


Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru na kufaidika na ujumbe wake.


Alisema mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi vya sanaa vitakavyoshiriki katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka (Mb), amewataka wataalamu wa maendeleo ya jamii nchini kutumia taaluma, mbinu na uzoefu wao kuwaelimisha wananchi kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ili kuhakikisha kila Mtanzania anaielewa na kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.

Mhe. Nanauka ametoa wito huo, alipokuwa akifungua Kongamano na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (CODEPATA), uliofanyika katika Ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, jijini Mwanza, leo Juni 17, 2026.

“Nyinyi mnazo mbinu na maarifa ya kuijenga jamii. Nendeni kwa wananchi mkawape elimu na uelewa kuhusu Dira ya Taifa 2050 ili wawe sehemu ya safari ya maendeleo ya nchi yetu,” amesema Mhe. Nanauka.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju, amewahimiza wataalamu wa maendeleo ya jamii kuendelea kujiendeleza kitaaluma kwa kujiunga na programu ya Shahada ya Uzamili kwa njia mseto (Blended/Online) inayotolewa na Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD), ambayo hukamilika ndani ya mwaka mmoja.

Aidha, Wakili Mpanju ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa wataalamu wa maendeleo ya jamii kupitia utoaji wa vitendea kazi, kuboresha maslahi ya kada hiyo na kuendelea kutoa ajira kwa wataalamu nchini.

Mkutano huo wa siku tatu unaendelea kesho kwa uwasilishaji wa mada mbalimbali zitakazotolewa na wataalamu na wadau wa maendeleo ya jamii, zikiwa na lengo la kuimarisha taaluma na mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya Taifa.
















Na. OWM (KAM), Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema mahusiano mema, mazungumzo ya kujenga na mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu katika kuimarisha demokrasia, amani na maendeleo endelevu nchini.
-DODOMA

Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua rasmi Awamu ya Pili ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC II) Juni 20,2026 katika Viwanja vya Maonesho Dole, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi wote.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026  jijini Dodoma leo, Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera, amesema  kampeni hiyo inalenga kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa huduma za msaada wa kisheria, elimu ya sheria na ushauri wa kisheria ili kuongeza uelewa wa haki na wajibu wao katika jamii.

Dkt. Homera amesema kampeni hiyo ni utekelezaji wa maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha huduma za sheria na haki zinapatikana kwa wananchi wote bila ubaguzi, hususan makundi maalumu na wananchi wa maeneo ya pembezoni ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto za kupata huduma hizo.

Amefafanua kuwa Awamu ya Pili ya kampeni hiyo itaendelea kutumia kaulimbiu ya “Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo,” ambayo inaakisi dhamira ya Serikali ya kuimarisha utawala wa sheria, usawa na maendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, mafanikio ya Awamu ya Kwanza ya kampeni iliyotekelezwa kuanzia Aprili 2023 hadi Juni 2025 ndiyo yamechochea kuanzishwa kwa awamu mpya. Katika kipindi hicho, kampeni ilitekelezwa katika mikoa yote 31 ya Tanzania Bara pamoja na mikoa yote mitano ya Zanzibar.

Amesema Zanzibar pekee, jumla ya wananchi 422,908 walinufaika na huduma mbalimbali za msaada wa kisheria, ambapo wanaume walikuwa 213,723 huku wanawake wakifikia 209,185.

“Matokeo haya yanaonesha wazi umuhimu wa kampeni hii katika kuwajengea wananchi uelewa wa sheria, haki na wajibu wao pamoja na kusaidia kutatua migogoro mbalimbali ya kisheria inayowakabili,” amesema Dkt. Homera.

Katika awamu mpya, wananchi watapata huduma zinazohusu masuala ya ndoa na talaka, mirathi, migogoro ya ardhi, haki za watoto, ukatili wa kijinsia, haki za wafanyakazi pamoja na usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala.

Huduma nyingine zitakazotolewa ni pamoja na usajili wa matukio muhimu ya maisha, upatikanaji wa nyaraka za utambulisho, uandaaji wa nyaraka za kisheria na utoaji wa elimu ya sheria kwa wananchi.

Dkt. Homera amesema maandalizi yote ya uzinduzi wa kitaifa yamekamilika na kwamba zaidi ya washiriki 15,000 wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo, wakiwemo viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, viongozi wa dini, vyama vya siasa, mashirika ya kiraia, wataalamu wa sheria na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

Ameongeza kuwa sambamba na uzinduzi huo, huduma za msaada wa kisheria zitatolewa kupitia mabanda katika wilaya za Mjini, Magharibi A na Magharibi B, huku timu za wataalamu zikitembelea shehia mbalimbali kutoa elimu ya sheria, ushauri na utatuzi wa migogoro.

Waziri huyo ametumia fursa hiyo kupongeza ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika utekelezaji wa kampeni hiyo, akisema ni mfano halisi wa manufaa ya Muungano katika kuwahudumia wananchi.

Aidha, amewataka wananchi wa Zanzibar kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi huo na kutumia fursa ya kupata huduma mbalimbali za kisheria zitakazotolewa bila malipo.

“Ushiriki wa wananchi katika kampeni hii utasaidia kuongeza uelewa wa haki zao za kisheria, kuimarisha amani na utulivu katika jamii pamoja na kuchochea maendeleo ya Taifa,” amesema 

Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imeendelea kuwa miongoni mwa programu muhimu za Serikali zinazolenga kusogeza huduma za haki karibu na wananchi na kujenga jamii inayozingatia sheria, usawa na utawala bora.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Na Mwandishi Wetu-DODOMA
Wizara ya Viwanda na Biashara imewahimiza wananchi, hususan vijana na wajasiriamali, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na taasisi zake ili kukuza biashara, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.
Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2026 na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Saidi Msabimana, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Msabimana amesema wizara hiyo, ambayo ni miongoni mwa taasisi muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imeshiriki maonesho hayo pamoja na taasisi nane zilizo chini yake kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi pamoja na kutoa elimu kuhusu biashara, viwanda na uwekezaji.
Amesema jukwaa hilo limetumika kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa taarifa za huduma zinazotolewa na kuwaelekeza namna ya kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla.
“Tunatumia jukwaa hili kuwafikia wananchi moja kwa moja, kuwaeleza huduma tunazotoa na kuwahamasisha kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa kwa ujumla,” amesema Msabimana.
Katika maonesho hayo, taasisi zilizo chini ya wizara hiyo zimeendelea kutoa huduma mbalimbali, ikiwemo huduma za usajili wa biashara kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni Tanzania (BRELA), ambapo wananchi wamewezeshwa kupata huduma za usajili wa kampuni, majina ya biashara na alama za biashara kwa njia ya kidijitali.
Kwa upande wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB)wananchi wanaomiliki au wanaotarajia kuendesha maghala wamepata elimu na huduma za usajili pamoja na leseni zinazotakiwa kisheria.
Aidha, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE ) kimetumia maonesho hayo kutoa taarifa za udahili na programu mbalimbali za masomo zinazolenga kuwaandaa vijana kuwa wataalamu na wajasiriamali wenye ushindani sokoni.
Vilevile, Wakala wa Vipimo umeendelea kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo katika biashara ili kulinda haki za walaji na kuimarisha uaminifu katika shughuli za kibiashara nchini.
Msabimana amesema kupitia maonesho hayo, zaidi ya wananchi 365 wamepata huduma za kuboresha mifumo ya biashara zao pamoja na taratibu za usajili wa lebo za bidhaa, hatua inayosaidia kuongeza ubora na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Kwa upande mwingine, Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), limeendelea kutoa taarifa kuhusu miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Liganga, Mchuchuma na Soda Ash, inayotarajiwa kuwa kichocheo cha mapinduzi ya viwanda, ajira na ukuaji wa uchumi.
Msabimana amewahimiza wananchi kutembelea mabanda ya wizara hiyo katika maonesho hayo ili kupata huduma, elimu na taarifa sahihi zitakazowawezesha kuboresha maisha yao na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi shindani wa Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.

...

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.

Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.

Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.

Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.

“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.

Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuongeza vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya  umeme ili kuongeza wigo wa utoaji huduma hiyo ambayo imeonekana kuleta mageuzi katika matumizi ya nishati safi.

Mhe. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma.

Waziri huyo mwenye dhamana ya Utumishi ametumia nafasi hiyo kuipongeza TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati safi kwa ajili ya  kupikia na katika vyombo vya usafiri.

‘’ TANESCO mnafanya kazi kubwa nawapongeza kwa mageuzi ya matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, natoa rai muongeze Vituo vya kuchajia vyombo hivyo ili kuongeza wigo wa utoaji huduma,’’ alisisitiza Mhe. Ridhiwani

Naye Meneja Masoko Bw. Fredrick Kalinga amesema TANESCO inashiriki katika Maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika ikiwemo maendeleo ya miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme, maboresho makubwa yaliyofanywa na Shirika kwenye mifumo ya kidigitali ya utoaji huduma kwa wateja pamoja na kuhamasisha jamii kutumia nishati safi ya umeme kupikia na katika vyombo vya usafiri kama magari, bajaji, guta, na pikipiki.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026  yenye kauli mbiu isemayo ‘’Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa huduma Endelevu’’ yameanza rasmi Juni 16, 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026