Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith  Kapinga (Mb), ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kushirikiana kikamilifu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Taasisi nyingine husika katika kushughulikia na kuondoa kero zote zinazosababishwa na mifumo ya utoaji vibali kwa shehena zinazoingia nchini.

Waziri Kapinga ametoa agizo hilo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Waziri Salum alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi na ujumbe wake Mei 29, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, kufuatia kuibuka kwa changamoto zilizojitokeza wakati wa kuunganisha mfumo wa TANeSW wa TRA na mfumo wa OAS wa TBS na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wafanyabiashara.

Aidha, Waziri Kapinga amepongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa baina ya TBS pamoja na TRA katika kuunganisha mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha taratibu na kuongeza ufanisi wa utoaji wa vibali kwa shehena za mizigo inayoingia nchini.

Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi maisha yangu yote yalikuwa yanaanguka mbele ya macho yangu. Nilikuwa nafanya kazi kwa bidii sana kwenye kampuni niliyokuwa nimeajiriwa.

Nilijituma, niliheshimu kazi yangu, na nilikuwa naamini uaminifu ndio ulikuwa unanifanya nisogee mbele. Ndiyo maana siku mambo yalipoanza kubadilika, sikuamini kabisa. Ghafla nilianza kusikia uvumi.

Mwanzoni nilipuuzia nikidhani ni maneno ya kawaida ya kazini. Lakini kadri siku zilivyopita, nilianza kugundua baadhi ya wafanyakazi walikuwa wakiniepuka. Wengine walikuwa wakinitazama tofauti kana kwamba kuna jambo baya nilikuwa nimefanya.

Kwa kweli nilichanganyikiwa. Siku moja niliitwa ofisini kwa meneja. Nilishtuka kusikia nikihusishwa na jambo ambalo sikuwa nimefanya kabisa. Kulikuwa na madai yaliyokuwa yanaenea kwamba nilikuwa nimehusika kwenye kosa lililoharibu imani ya kampuni.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona hata baadhi ya watu niliokuwa na ukaribu nao wakianza kuniamini vibaya. Nilijaribu kujitetea, lakini ilionekana kama tayari watu walikuwa wameamua ukweli wao kuhusu mimi.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa na ndoto ya kuanza maisha mapya nje ya nchi. Nilikuwa naamini kupata uraia wa nje kungefungua milango mipya ya opportunities kwa maisha yangu na familia yangu.

Niliona watu wengi wakibadilisha maisha yao baada ya kuhamia nje, na moyoni nilikuwa na tumaini kuwa siku moja na mimi ningefanikiwa. Lakini safari haikuwa rahisi.

Kila nilipoanza mchakato wa application, changamoto zilikuwa zinajitokeza. Mara documents zinaonekana hazijakamilika, mara application inachelewa, mara napokea majibu ya kukataliwa bila kuelewa nilikosea wapi.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu nilioanza nao process wakifanikiwa huku mimi nikibaki pale pale. Wakati mwingine nilianza kujiuliza kama ndoto ile ilikuwa kubwa sana kwangu.

Kulikuwa na kipindi nilianza kukata tamaa. Nilikuwa nimechoka emotionally na financially kutokana na process za mara kwa mara ambazo zilionekana kutokwenda popote. Watu wengine walikuwa wakiniambia niache kupoteza muda na nikubali hali ilivyo.SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi kama ndoto yangu ilikuwa karibu kuanguka mbele ya macho yangu. Nilikuwa nimewekeza kila kitu nilichokuwa nacho kufungua hoteli yangu ndogo. Ilikuwa ndoto ambayo nilikuwa nimeibeba kwa miaka mingi.

Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri wateja walikuwa wanakuja, mapato yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu future ya biashara yangu. Lakini ghafla mambo yakabadilika.

Nilianza kuona idadi ya wateja ikipungua. Mwanzoni nilidhani ni msimu mbaya tu wa biashara, lakini kadri wiki zilivyopita, hali ilianza kuwa mbaya zaidi. Siku moja nilipoangalia reviews za online, moyo wangu ulivunjika.

Kulikuwa na reviews nyingi mbaya. Baadhi ya watu walilalamika kuhusu huduma, wengine wakasema mazingira hayakuwa mazuri kama walivyotarajia. Kilichoniumiza zaidi ni kuona baadhi ya comments ambazo nilihisi hazikuwa fair kabisa.SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kufikiria ningemuona tena mpenzi wangu wa zamani akirudi maishani mwangu. Tulikuwa tumekuwa pamoja kwa muda mrefu, tukijenga ndoto za maisha ya baadaye pamoja. 

Nilimpenda kwa moyo wangu wote na nilikuwa naamini uhusiano wetu ungeishia kwenye ndoa.

Ndiyo maana siku alipoamua kuondoka, nilihisi kama dunia yangu imevunjika vipande vipande. Kwa kweli iliniumiza sana. Mwanzoni nilidhani ni ugomvi wa kawaida ambao ungeisha baada ya muda.

Lakini siku zikapita, wiki zikageuka miezi, na hatimaye mawasiliano yakakatika kabisa. Kilichoniumiza zaidi ni kuona akiwa anaendelea na maisha yake huku mimi nikibaki na maumivu na maswali mengi.

Kulikuwa na kipindi nilipoteza furaha. Nilikuwa nikijiuliza nilikosea wapi. Wakati mwingine nilikosa hamu ya kutoka, kuzungumza na watu, au hata kujaribu uhusiano mwingine. Nilihisi kama moyo wangu ulikuwa umechoka kupenda. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambacho nilihisi kama dunia yote imenigeuka. Sikuwahi kufikiria siku moja ningejikuta matatani kwa kosa ambalo sikulifanya. Maisha yangu yalikuwa ya kawaida. Nilikuwa najituma kazini na kujali familia yangu.

Lakini siku moja kila kitu kilibadilika ghafla. Nilituhumiwa kwa jambo ambalo sikuwa na uhusiano nalo kabisa. 

Mwanzoni nilidhani ukweli ungejulikana haraka. Nilikuwa na uhakika kuwa watu wangenielewa na mambo yangerudi sawa.

Lakini badala yake, hali ilizidi kuwa mbaya. Watu walianza kunitazama tofauti, baadhi ya marafiki wakaanza kunikwepa, na hata watu wa karibu walionekana kuwa na mashaka nami. Kwa kweli iliniumiza sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona jina langu likiharibika kwa jambo ambalo sikulifanya. Kulikuwa na wakati nilihisi kama kila mtu tayari alikuwa amenihukumu bila kusikia upande wangu.

Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa najiuliza kama kweli ningewahi kupata haki yangu au kama maisha yangu yangekuwa vile milele. Hofu ya kupoteza heshima, kazi, na future yangu ilinifanya niishi kwa mawazo mengi sana.SOMA ZAIDI.

 


Na Mwandishi Wetu Ruangwa, Lindi


Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema kwamba Tanzania inajipanga kuwa mmoja ya wazalishaji wakubwa Duniani wa madini kinywe(𝙂𝙧𝙖𝙥𝙝𝙞𝙩𝙚) kupitia Kampuni 30 zinazomiliki Leseni za kati na kubwa za uchimbaji wa madini hayo na hivyo kutoa ushindani wa kiuzalishaji kwa nchi ya China ambayo ndio inaongoza kwa uzalishaji wa madini hayo duniani kwa kuzalisha tani milioni 1.2 kwa mwaka.

Mhe Mavunde ameyasema hayo leo Mei 28, 2026 Wilayani Ruangwa, Lindi aliposhiriki katika hafla ya utiaji saini wa mikataba wa ubia baina ya Serikali na Kampuni ya Lindi Jumbo Limited kwa ajili ya mradi mkubwa wa uchimbaji madini kinywe na kubainisha kuwa kuanza kwa uchimbaji mkubwa wa madini mkakati ya kinywe (graphite) kunaiweka Tanzania kwenye dira ya duniani kama Nchi ya kimkakati katika uzalishaji wa madini hayo muhimu kwenye utengenezaji wa betri za magari ya umeme.

"Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuijenga na kuifanya nchi yetu ya Tanzania kama Taifa lenye dira wazi ya kiuchumi, mazingira rafiki ya uwekezaji na usimamizi imara wa rasilimali zake," amesema Waziri Mavunde

Amesema tukio la leo ni matokeo ya dira na maono hayo thabiti ya Mhe Rais ambayo yameendelea kuifanya Tanzania kuwa sehemu salama ya wawekezaji ambayo ina sera na Sheria zinazoeleweka na kutabirika.

Pia, Mhe.Mavunde amefafanua kwamba kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya sita Duniani kwa uzalishaji wa madini kinywe ambapo kwa mwaka uzalishaji wa Tanzania ni tani 25,000 kwa kampuni mbili tu zilizoanza uzalishaji mkubwa za Lindi Jumbo na God Mwanga-Tanga huku zingine 28 zikiwa katika hatua mbalimbali za kuanza uzalishaji.

Mhe Mavunde amewataka wamiliki wa Leseni 28 za uchimbaji madini kinywe kuhakikisha wanaanza uzalishaji mapema kama sheria inavyoelekeza ili kuepuka kufutuwa leseni hizo.

Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa dunia kwa sasa inapita kwenye mageuzi makubwa ambapo madini kinywe ni msingi wa kesho kwani upatikanaji wake ni kichocheo kikubwa katika uzalishaji wa nishati safi kwa kusaidia utengenezaji betri za magari ya umeme.

Mradi huo wenye thamani ya zaidi ya Dola za Kimarekani Milioni 82 unataraji kuzalisha madini kinywe tani 40,000 kwa mwaka katika kipindi cha uhai miaka 24 ya mgodi ambapo zaidi ya ajira 300 zimezalishwa hadi sasa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye sekta ya madini, Prof. Sifuni Mchome ameeleza kuwa miongoni mwa faida ambazo Serikali itapata kupitia kusaini mikataba hiyo ya ubia ni pamoja na udhibiti wa fedha na uhakika wa mapato kutokana na uwekezaji huo na fursa za ajira kwa watanzania.

Prof. Mchome amebainisha kuwa kupitia
makubaliano hayo yaliyotiwa saini, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itamiliki asilimia 16 ya hisa huru zisizohafifishwa thamani (non-dilutable free carried interest shares), huku Kampuni ya Lindi Jumbo Limited ikimiliki asilimia 84 ya hisa katika kampuni ya ubia.

Awali, akieleza maendeleo ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Lindi Jumbo Limited, Bw. Andrew Cunningham amebainisha kuwa pamoja na upanuzi wa uzalishaji wa mgodi huo, wataendelea kufanya utafiti ili kubaini mashapo zaidi ambayo yatarefusha maisha ya mgodi na kuongeza manufaa zaidi kwenye uchumi wa Tanzania.

Naye mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuvutia wawekezaji ambayo wamekuwa ni chachu ya maendeleo ya Mkoa wa Lindi na kuahidi kwamba Serikali ya Mkoa wa Lindi itaendelea kuwapa ushirikiano wawekezaji wote ili wafikie malengo yao na kuchochea uchumi wa Nchi yetu.




 -Naibu Waziri Kwagilwa aahidi kufanya ziara katika halmashauri 184 kukagua zoezi hilo


Na Ashura Mohamed - ARUSHA

Serikali imesema haitamuonea haya mtu yeyote atakayefanya maigizo katika zoezi la upandaji miti nchini, ikieleza kuwa zoezi hilo ni muhimu kwa mustakabali wa mazingira.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Reuben Nhamanilo Kwagilwa, wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Jamii cha Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi - CCRC, kilichopo Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru - TICD.

Mhe. Kwagilwa amesema baada ya kumalizika kwa Bunge la Bajeti ataomba idhini kwa Waziri wa Mazingira kufanya ziara ya kukagua utekelezaji wa upandaji miti katika halmashauri zote 184 nchini ili kujionea hali halisi.

“Bunge hili likiisha nitataka kama serikali kwenda kuangalia hali halisi ya upandaji miti. Kwa kuwa kila mkurugenzi anayeulizwa anasema tumepanda miti milioni 5, milioni 2, lakini ukikagua eneo hilo miti hutaiona kabisa. Maigizo haya ndugu zangu kwenye mazingira ni hatari,” alisema.

Aliongeza kuwa serikali itamchukulia hatua mtu yeyote atakayethibitika kuendeleza shughuli za uharibifu wa mazingira baada ya kupewa taarifa.

Naibu Waziri ameeleza kuwa chanzo kikubwa cha mabadiliko ya tabia nchi ni uharibifu wa vyanzo vya maji, ukataji miti, kilimo kisichozingatia uhifadhi wa ardhi, pamoja na shughuli za viwanda, uvuvi na uchimbaji wa madini usiozingatia utaratibu.

Hali hiyo imesababisha ukame usioelezeka, mvua zisizo na majira, mafuriko, mito kubadilisha mikondo, maziwa kuingia kwenye makazi ya watu, dhoruba na vimbunga.

“Chanzo kikubwa cha uharibifu wa mazingira ni  uchafuzi wa vyanzo vya maji, ukataji misitu, kilimo ambacho hakiipi ardhi yetu ikolojia,hali inayochangia ongezeko la  gesi joto kwenye ikolojia ya uso wa dunia na kupelekea mabadiliko ya tabia nchi ambayo tunayaona leo,” alisema Kwagilwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii TICD, Dkt. Bakari George amesema kituo hicho kitashirikiana na jamii na wadau mbalimbali kuandaa sera na kufanya tafiti za kusaidia jamii kuondokana na janga la mabadiliko ya tabia nchi.

Meneja wa CCRC, Dkt. Agnes Kapinga amesema uanzishwaji wa kituo hicho umefuata uchafuzi mkubwa wa mazingira unaopelekea ongezeko la taka kila siku na mifumo kushindwa kustahimili.

“Uwepo wa kituo hicho kwa kushirikiana na taasisi zingine utakujia na majibu ya changamoto mbalimbali zitakazosaidia jamii na taifa kwa ujumla kuwa na ustahimilivu kwa maendeleo endelevu,” alisema Dkt. Kapinga.

Kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM inamtaka kila Mkurugenzi wa Halmashauri nchini kuhakikisha anapanda miti milioni 1.5 ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi.

Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Mkuu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh.Reuben Nhamanilo Kwagila akizungumza katika hafla hiyo
Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira akikata Utepe wakati wa Uzinduzi wa kituo Cha Jamii Cha Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi
Mkuu wa chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD),Dkt.Bakari George akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika chuoni hapo

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa mchango wake katika kuwawezesha wakulima, wafugaji na wavuvi kupitia utoaji na usimamizi wa mikopo, hatua aliyoeleza kuwa inaendelea kuchochea maendeleo ya sekta za uzalishaji na ukuaji endelevu wa uchumi wa Taifa.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mkutano wa kimataifa wa siku tatu wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere umezinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kujadili masuala ya siasa za kimataifa (geopolitics), maendeleo na mwelekeo mpya wa Afrika katika mazingira ya dunia yanayobadilika kwa kasi.

SERIKALI imezindua rasmi Mpango wa Mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa Elimu kwa Wakuu wa Shule za Sekondari na Maafisa Elimu Kata nchini, hatua inayolenga kuimarisha ufanisi wa uongozi wa shule, usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji pamoja na kuimarisha ubora wa elimu nchini.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa  Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani  waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa  Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani  waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa  Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na utaratibu wakati wa uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.

Jaji Mwambegele ameyasema hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Jaji Mwambegele pia amewasisistiza  watendaji hao kuishi kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha na upendeleo wa aina yoyote.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi .

Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi  huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.

Uchaguzi huo utafanyika sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.


Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa  Bi. Nuru Sovella akizungumza wakati wa mafunzo hayo. 
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno akizungumza na kusema kua maandalizi ya uchaguzi  huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.

Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena, akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 28,2026 katika Mako Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kuhusu wito wa  vijana waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kwa mwaka 2026 kujiunga na mafunzo ya JKT.

Na.Alex Sonna-CHAMWINO

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajab Mabele amewataka Vijana waliohitimu kidato cha Sita kwa Mwaka 2026 ambao wamechaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa sheria kujiunga na mafunzo hayo katika makambi waliyochaguliwa kuanzia juni mosi, hadi juni 7, 2026.

Hayo yamesemwa leo Mei 28,2026  katika Mako Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT, Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema majina ya vijana wote waliohitimu kidato cha sita kwa Shule za Sekondari Tanzania Bara na Visiwani waliochaguliwa wanatakiwa kujiunga na mafunzo hayo. Amesema orodha kamili ya majina ya vijana hao, makambi JKT waliyopangiwa, Maeneo ya Makambi hayo yalipo na vifaa wanavyotakiwa kwenda navyo inapatikana katika tovuti ya JKT ambayo ni www.jkt.mil.tz. Amesema ilikufahamu kambi kijana aliyopangiwa atatakiwa kuingiza jina la shule au namba ya shule aliyohitimu kidato cha sita, mbele ya jina la shule ataona neno lililoandikwa waliochaguliwa ambapo akichagua neno hilo ataona majina ya waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2026 na kambi aliyopangiwa. Amesema ili kuona majina yote ya vijana na kambi walizopangiwa mtumiaji atapakua JKT PDF 2026 iliyopo juu kulia katika ukurasa huo. Ameongeza kuwa Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele anawakaribisha vijana wote waliohitimu kidato cha sita kwa mwaka 2026 ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujengewa uzalendo, kufundishwa nidhamu, ukakamavu, umoja wa kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na utayari wa kulijenga na kulitumikia taifa. Katika hatua nyingine amebainisha kuwa kwa wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho wataripoti katika kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miondombinu ya kuwahudumia watu hao.

 

 


Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni  Mapesa amewataka viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kutambua kuwa Uongozi ni utumishi wa kuwatumikia watu na si kutumikiwa, kwani kazi ya kiongozi ni kuwa tayari muda wote kutatua changamoto mbalimbali.

Mapesa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwapisha viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi (MASO) kwa mwaka 2026/27 pamoja na mambo mengine amepongeza Uongozi wa Serikali  iliyomaliza muda wake iliyokuwa ikiongozwa na Magashi Magina  kuwa walizingatia Weledi wa hali ya Juu.

Mkuu huyo wa Taasisi ameitaka Serikali mpya kuzingatia misingi ya Uongozi, na kuwa na namna bora ya kutatua changamoto ikiwa ni pamoja na kushirikiana vyema na Serikali ya Wanafunzi ambayo imemaliza muda wake, huku akiwaahidi ushirikiano wa dhati kutoka kwa Uongozi wa Chuo.

Kwa upande wake, Rais aliyemaliza muda wake Magashi Magina ameishukuru Menejimenti ya chuo kwa ushirikiano alioupata katika kipindi chote cha uongozi wake, ameeleza kuwa mafanikio yote yaliyopatikana yalitokana na uwazi na utayari wa Menejimenti kusikiliza na kutatua Changamoto mbalimbali za Wanafunzi jambo lililorahisisha utendaji kazi wa serikali yake.

Nao, Viongozi wapya walioapishwa kuiongoza Serikali ya Wanafunzi , Rais ni Samir Naseer na Makamu wa Rais  Julieth Mandia  wametoa shukrani za dhati kwa Wanafunzi wote kwa kuonyesha imani kwao na kuwachagua kuongoza Serikali ya wanafunzi ambapo wameahidi kuongozi kwa Uadilifu, Amani, mshikamano kwa  kushirikiana na Menejimenti ya Chuo pamoja na Serikali ya Wanafunzi iliyomaliza muda wake.

 

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

28.05.2026

 


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Maryprisca Mahundi amesema maonyesho ya Mbeya City Expo yameendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa Mkoa wa Mbeya kwa kuwakutanisha wananchi, taasisi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Akizungumza baada ya kutembelea mabanda mbalimbali katika maonyesho hayo yanayofanyika katika viwanja vya Uhindini, Jijini Mbeya, Eng. Mahundi amesema ameridhishwa na namna shughuli za kijamii na kiuchumi zinavyooneshwa kupitia maonyesho hayo.

Amesema Mbeya City Expo imekuwa jukwaa muhimu la kutoa elimu, kutangaza huduma na bidhaa pamoja na kuhamasisha fursa za maendeleo kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na maeneo ya jirani.

Aidha, amepongeza waandaaji wa maonyesho hayo kwa kutoa nafasi kwa wananchi kupata elimu na huduma mbalimbali zinazochochea maendeleo ya jamii pamoja na kukuza uchumi.

Katika hatua nyingine, Eng. Mahundi amesisitiza wananchi, hususan makundi maalum, kutumia vizuri mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na halmashauri ili kujikwamua kiuchumi na kuongeza kipato cha familia zao.

Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa najiona sifai kabisa. Nilikuwa mtu mwenye ndoto nyingi, lakini kadri muda ulivyopita nilianza kupoteza kujiamini. Kila nilipojaribu jambo jipya, kulikuwa na watu waliokuwa tayari kunikosoa au kunicheka.

Wengine walikuwa wakiniambia siwezi kufanikiwa, huku wengine wakinifanya nijihisi mdogo bila sababu. Kwa kweli iliniumiza sana. Polepole nilianza kujifungia ndani ya dunia yangu mwenyewe.

Nilianza kuogopa kuzungumza mbele za watu, kujaribu opportunities mpya, au hata kuvaa vile nilivyopenda kwa sababu nilihofia watu wangesema nini. 

Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wa rika langu wakisonga mbele huku mimi nikihisi kama nimesimama sehemu moja.

Kulikuwa na siku nilijiangalia kwenye kioo na kushindwa kuona kitu kizuri kuhusu mimi mwenyewe. 

Confidence yangu ilikuwa imeshuka sana kiasi kwamba hata watu walikuwa wanaanza kunichukulia kawaida. Nilianza kuamini maneno mabaya ya watu.SOMA ZAIDI.


Kulikuwa na kipindi ambacho nilikuwa karibu kukata tamaa kabisa kuhusu shamba langu. Nilikuwa nimewekeza nguvu nyingi sana kwenye kilimo. 

Kila siku nilikuwa naamka mapema kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Lakini ghafla nilianza kugundua mazao na vifaa vidogo vidogo vinaanza kupotea kwa njia isiyoeleweka.

Mwanzoni nilidhani ni makosa ya kawaida. Lakini kadri wiki zilivyopita, hasara ilianza kuongezeka. Mara napoteza mahindi yaliyokuwa tayari kuvunwa, mara vifaa vya kazi vinatoweka. 

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba kila nilipojaribu kuuliza watu wa karibu, hakuna aliyekuwa na taarifa yoyote.

Kwa kweli nilichanganyikiwa. Nilianza kufanya ulinzi wa usiku mara kadhaa lakini bado sikuweza kumkamata mtu yeyote. 

Wakati mwingine nilifika shambani asubuhi na kukuta dalili kuwa mtu alipita usiku lakini hakuna clue ya kueleweka.

Nilikuwa karibu kuvunjika moyo. Watu wengine waliniambia niache kupambana kwa sababu huenda singepata anayehusika. Lakini moyoni sikuwa tayari kuona jasho langu linaendelea kupotea.SOMA ZAIDI.


Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa karibu kufunga biashara yangu kwa maumivu makubwa. 

Nilikuwa nimeanzisha biashara yangu kwa juhudi nyingi sana. Nilikuwa naamka mapema kila siku, nikijituma kuhakikisha wateja wanapata huduma nzuri.

Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda sawa, na nilikuwa na matumaini makubwa ya kuona biashara yangu ikikua. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Biashara nyingine iliyokuwa karibu yangu ilianza kunizidi kwa namna ambayo sikuielewa. Wateja wangu wa kawaida wakaanza kupungua. Wengine walikuwa wanaenda upande mwingine ghafla bila maelezo.

Kilichoniumiza zaidi ni kusikia maneno yaliyokuwa yanaenezwa. Kulikuwa na watu waliokuwa wakisema biashara yangu haikuwa nzuri, bidhaa zangu hazikuwa na ubora, na huduma yangu haikuridhisha wakati nilikuwa najua nilikuwa najitahidi sana.

Polepole nilianza kuhisi kama mshindani wangu alikuwa akifanya kila kitu kuhakikisha ninapoteza wateja. Kwa kweli nilivunjika moyo. 

Kulikuwa na siku nilikaa dukani kwa masaa mengi bila mteja wa maana. Bills zilianza kuongezeka, stock ilianza kukaa sana, na nilianza kujiuliza kama ndoto yangu ilikuwa inaisha.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, maisha yangu yalikuwa ya hofu na wasiwasi kwa sababu ya pumu. Mwanzoni nilidhani ni hali ambayo ingeisha kadri muda ulivyopita. Lakini kadri nilivyokuwa nakua, mashambulizi ya pumu yakaanza kuwa ya mara kwa mara.

Kulikuwa na siku nilikosa pumzi ghafla usiku, nikaanza kukohoa sana, na familia yangu ikalazimika kunikimbiza hospitalini. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Nilikuwa naogopa hata mabadiliko ya hali ya hewa. Vumbi, baridi, moshi, au harufu kali vilikuwa vinanifanya niwe na wasiwasi. Wakati mwingine nilishindwa kushiriki shughuli za kawaida kwa sababu niliogopa kupata shida ya kupumua.

Kilichoniumiza zaidi ni kulazwa hospitalini mara kwa mara. Kulikuwa na nyakati nilihisi kama maisha yangu yalikuwa yamesimama. 

Nilifuata dawa nilizopewa hospitalini na kutumia inhaler kama nilivyoelekezwa, lakini bado nilikuwa napata changamoto za mara kwa mara.

Kulikuwa na kipindi nilianza kukata tamaa. Nilikuwa najiuliza kama ningewahi kuishi maisha ya kawaida bila hofu ya kushindwa kupumua ghafla.SOMA ZAIDI.