Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na Menejimenti ya watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)

Mwenyekiti wa wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Joyce Mapunjo, akizungumza katika kikao kazi kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu , Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na Menejimenti ya watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu, akiwa katika picha ya pamoja na ,Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na Menejimenti ya watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)

...

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu (Mb) leo (Jumanne, Jan. 20, 2026) amekutana Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na kusisitiza umuhimu wa Mfuko kuwekeza katika miradi inayozalisha ajira kwa vijana wa kitanzania.

Katika mkutano huo uliofanyika katika Makao Makuu ya PSSSF jijini Dodoma, Mhe. Sangu amekumbusha kuwa kwa sasa Serikali inatekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo (DIRA 2025) ambayo, Pamoja na mambo mengine, inasisitiza uwekezaji katika miradi inayozalisha ajira na kuchochea Uchumi.

“Bodi ihakikishe mambo makubwa mawili katika utekelezaji wa miradi – kwanza kuzalisha ajira na pia ajira hizo ziwafikie vijana wa kitanzania kama DIRA 2050 na mipango ya Serikali inavyoelekeza,” amesema Waziri Sangu katika mkutano huo wake wa kwanza na Bodi ya Wadhamini ya PSSSF.

Katika mkutano huo, Menejimenti ya PSSSF nayo ilihudhuria ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Bw. Fortunatus Magambo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSSSF Bi. Joyce Mapunjo, kwa niaba ya Bodi, alimuhakikishia Waziri Sangu kuwa utekelezaji wa majukumu ya Mfuko unaongozwa na Mpango Mkakati uliohuishwa kwa kuzingatia DIRA 20250 na miongozo ya Serikali.

“Tumepokea maelekezo na tutazingatia katika utekelezaji … nikuhakikishie kuwa tuna Mpango Mkakati mpya (2026/2027 - 2030/2031) unaozingatia mipango ya kitaifa na pia tunatumia utaalam na uzoefu wetu kuhakikisha malengo ya Mfuko yanatimia na unaendelea kuwa stahimilivu,” amesema Bi. Mapunjo ambaye ni Katibu Mkuu mstaafu aliyehudumu kwenye Wizara mbalimbali.

Mfuko wa PSSSF ulianzishwa mwaka 2018 kufuatia kuunganishwa kwa iliyokuwa Mifuko ya GEPF, LAPF, PSPF na PPF. Kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Mfuko, PSSSF ina majukumu manne ya kusajili wanachama, kukusanya michango, kuwekeza ili kutunza thamani ya fedha na kulipa mafao mbalimbali kwa wanachama wake.

Na Mwandishi wetu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amefanya ziara ya kikazi katika Tume ya Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar (ZFCC) ikiwa ni hatua ya kuimarisha mashirikiano kati ya taasisi hizo mbili katika masuala ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Bi. Ngasongwa alipokelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZFCC, Bi. Aliya Juma ambapo viongozi hao walifanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ustawi wa taasisi hizo na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika ziara hiyo iliyofanyika tarehe 14 Januari, 2026 katika ofisi za ZFCC - Zanzibar, Bi. Ngasongwa alisema ushirikiano kati ya taasisi hizo unaendelea kuimarika kupitia utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MoU) yaliyokwisha sainiwa.

"FCC na ZFCC tayari zimeanza kutekeleza kwa vitendo maeneo ya ushirikiano ikiwemo kujengeana uwezo, kubadilishana uzoefu na kufanya ukaguzi wa pamoja ili kudhibiti bidhaa bandia na kulinda haki za watumiaji wa bidhaa au huduma."alisema Bi. Ngasongwa

Katika ziara hiyo, Bi. Ngasongwa pia alikutana na kuzungumza na menejimenti ya ZFCC ambapo walijadili namna ya kuendeleza mpango wa pamoja wa kuboresha mifumo ya utendaji kazi na kubadilishana taarifa.

Kikao hicho cha siku moja kilihitimishwa kwa pande zote mbili kuahidi kuendeleza juhudi za pamoja ili kuhakikisha mazingira ya biashara yanaendelea kuwa shindani, salama na rafiki kwa mlaji.

 

Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga, ametembelea Kata za Mkako na Kihangimahuka katika mwendelezo wa ziara yake ya kuwashukuru wananchi kwa ushindi mkubwa waliompatia yeye na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lihale, Mhe. Kapinga aliahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Wilaya pamoja na taasisi husika ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi, hususan katika sekta za miundombinu, maji na umeme.

“Serikali ipo pamoja nanyi, na mimi kama Mbunge wenu nitaendelea kushirikiana na viongozi wa wilaya na taasisi zote kuhakikisha changamoto zenu zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu".

Katika kuonesha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya elimu, Mhe. Kapinga alitoa msaada wa bati 50 za geji 28 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 1.7 pamoja na kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya ununuzi wa kenchi, kwa ajili ya ujenzi wa chumba kimoja cha darasa katika Shule ya Msingi Liale.

Aidha, alitembelea Shule ya Sekondari Kihangimahuka ambapo alikabidhi kompyuta moja yenye thamani ya shilingi milioni 2.5 pamoja na mifuko 50 ya saruji yenye thamani ya shilingi laki tisa, ikiwa ni jitihada za kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji. Vilevile, aliahidi kuipatia shule hiyo mashine ya fotokopi kabla ya kumalizika kwa mwezi Februari 2026.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Vijijini alisema Serikali itaendelea kuleta miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Mbinga Vijijini, hususan katika sekta ya afya, alieleza kuwa jumla ya wahudumu wa afya 100 wameanza kuwasili katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri, wakiwemo madaktari zaidi ya 10, manesi wenye shahada zaidi ya 30 pamoja na wataalamu wengine wa afya.

Aidha, alimpongeza Mhe. Kapinga kwa mchango wake katika kuboresha huduma za afya, ikiwemo kuwasaidia kupata gari la wagonjwa (ambulance) ambalo limekuwa likisaidia kwa kiasi kikubwa kusafirisha wagonjwa, pamoja na ahadi yake ya kukarabati jengo la kinamama katika Zahanati ya Lihale.

Kwa upande wa wananchi wa Kata za Mkako na Kihangimahuka walimpongeza na kumshukuru Mbunge wao kwa kuendelea kutoa michango yake binafsi katika miradi ya maendeleo, wakieleza kuwa hatua hizo zimeongeza mshikamano na ari ya wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii.

Ziara hiyo ni sehemu ya mkakati wa Mbunge huyo wa kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi, viongozi na taasisi za serikali kwa lengo la kuleta maendeleo endelevu katika Jimbo la Mbinga Vijijini.

 

Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akizungumza na Waandishi wa Habari  leo Januari 20,2026  Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya MKUU wa JKT.

Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akisisitiza jambo kwa  Waandishi wa Habari  leo Januari 20,2026  Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya MKUU wa JKT .

Na.Alex Sonna-DODOMA

JESHI la Kujenga Taifa JKT limetangaza nafasi za kujitolea kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mwaka 2026, vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wenye sifa za kujiunga na Jeshi  hilo  huku watakaopata nafasi hizo wametakiwa kuripoti katika kambi za JKT kuanzia February 27 hadi Machi 4, mwaka huu.

Akizungumza leo Januari 20,2026  na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya MKUU wa JKT,Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema usaili utaanza Januari 26, mwaka huu kupitia Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema utaratibu wa vijana kuomba mafunzo hayo unaratibiwa chini ya ofisi za wakuu wa mikoa na wilaya na vijana wenye elimu ya kuanzia darasa la saba hadi chuo kikuu wanazo sifa za kuomba, akisema watakaochaguliwa wataanza kujiunga katika kambi mbalimbali za JKT kuanzia February 27 hadi Machi nne mwaka huu.

"Mafunzo haya ni bure wazazi au walezi wasikubali kurubuniwa kutoa fedha ili vijana wao wapate nafasi za kujiunga na mafunzo hayo," amesema Brigedia Jenerali  Mabena.

Brigedia Jenerali Mabena, amesema  Jeshi hilo limeweka mkazo maalumu kwa vijana wenye ujuzi wa masomo ya kompyuta kuanzia ngazi ya Stashahada hadi Shahada ili kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia duniani.

“Kipaumbele kitakuwa kwa vijana wenye taaluma za Stashahada ya Teknolojia ya Habari, Stashahada ya Mifumo ya Taarifa za Biashara, Stashahada ya Sayansi ya Kompyuta, Stashahada ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Stashahada ya Usalama Mtandaoni na Forensics ya Kidigitali,” amesema Brigedia Jenerali Mabena.

Aidha, ametoa wito kwa vijana wenye sifa kujitokeza katika maeneo yao ya vijiji, kata na tarafa kujiandikisha, akisisitiza kuwa nafasi hizo haziuziwi na kwamba kumekuwa na matapeli wanaojaribu kutumia mwanya huo kuwaibia wananchi.

“Nafasi hizi hazihitaji malipo yoyote. JKT Makao Makuu haina jukumu la kuandikisha, kila kitu kimepelekwa kwenye halmashauri, wilaya na mikoa. Wananchi wajihadhari na utapeli,” amesisitiza

Amesema kutokana na matumizi makubwa ya mitandao ya kidigitali nchini, JKT imeendelea kuwaandaa vijana kuielewa na kuitumia kwa maendeleo, ikiwemo kuongeza kipato kupitia ubunifu na fursa za kidigitali.

Brigedia Jenerali Mabena ameongeza kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa amewakaribisha vijana wote wa Tanzania Bara na Visiwani kujiunga na mafunzo hayo ya kujitolea kwa mwaka 2026.

Aidha amesema sifa za mwombaji awe raia wa Tanzania.Kwa Vijana wenye elimu ya darasa la saba kutoka Tanzania Bara na Vijana wenye elimu ya kidato cha Pili kutoka Zanzibar.

Amesema umri ni kuanzia miaka 16 hadi 18, waliomaliza kuanzia Mwaka 2022,2023, 2024, 2025 na awe na cheti halisi cha kumaliza elimu ya msingi na Kidato cha Pili. Vijana wenye elimu ya kidato cha nne umri usiwe zaidi ya miaka 20, waliomaliza Elimu ya Sekondari kuanzia Mwaka 2022,2023, 2024, 2025 na awe na cheti halisi cha kumaliza elimu ya sekondari  na cheti halisi cha matokeo 

Pia awe na ufaulu wa daraja la Kwanza hadi daraja la nne. Kijana mwenye daraja la nne awe na ufaulu waalama kuanzia 26 hadi 32.

Amesema kuwa vijana wenye elimu ya Kidato cha Sita umri usiwe zaidi ya miaka 22,waliomaliza elimu ya Sekondari kuanzia mwaka 2022, 2023,2024, 2025 na awe na cheti halisi cha kumaliza Elimu ya Sekondari na cheti halisi cha matokeo

Pia awe na ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi daraja la Nne. Vijana wenye elimu ya Stashahada umri usiwe zaidi ya miaka 25,awe na vyeti vya Sekondari na cheti cha Chuo. Vijana wenye Elimu ya Shahada umri usiwe zaidi ya miaka 26,awe na vyeti vya Sekondari na cheti cha Chuo

Aidha vijana wenye elimu ya Shahada ya Uzamili umri usiwe zaidi ya miaka 27, awe na vyeti vya Sekondari na cheti cha Chuo. Awe na afya njema,  akili timamu na asiwe na alama yoyoteya michoro mwilini (Tattoo).


Written by Alex Sonna

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akizungumza wakati wa kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika leo Januari 20, 2025, Jijini Dodoma

Na Alex Sonna, Dodoma

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imezitaka taasisi za elimu ya juu nchini kuhakikisha kampasi mpya zinazoendelea kujengwa katika maeneo mbalimbali zinajielekeza katika kutoa mafunzo ya ujuzi (Amali), ili kuandaa wahitimu wenye uwezo wa kujitegemea na kushindana katika soko la ajira.

Agizo hilo limetolewa leo Januari 20,2026  jijini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, wakati wa kikao kazi cha kimkakati kati ya Wizara na Wakuu wa Taasisi zilizo chini yake, kilicholenga kujadili utekelezaji wa majukumu na malengo ya sekta hiyo.

Prof. Mkenda amesema Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023 inaelekeza kwa nguvu zote kuandaliwa kwa wahitimu wenye ujuzi, hivyo ni muhimu kampasi mpya zikabeba dhana ya mafunzo ya amali kama ufundi na ufundi stadi.

“Haya ni maagizo ya Sera. Tunapopanua miundombinu ya elimu ya juu, lazima tuhakikishe tunapanua pia ujuzi kwa vitendo. Kampasi hizi mpya zisigeuke kuwa za kufundisha nadharia pekee, zizingatie mafunzo ya amali kwa lengo la kuongeza tija kwa Taifa,” amesema Prof. Mkenda.

Aidha Prof.Mkenda amesema kuwa serikali imeanza kuchukua hatua mahsusi za kutatua changamoto ya upatikanaji wa ufadhili wa masomo nje ya nchi baada ya kubaini kuwa wanafunzi wengi wa Kitanzania wanakosa fursa hizo kutokana na kushindwa kuziomba ipasavyo.

Prof. Mkenda amesema Serikali imefanikiwa kupata nafasi 127 za ufadhili wa masomo nchini Saudi Arabia, lakini bado idadi ya wanafunzi wanaoomba na kunufaika na fursa hizo ni ndogo, hali iliyosababisha Wizara kuanza kushughulikia vikwazo vinavyowafanya wanafunzi wengi kushindwa kuomba masomo nje ya nchi.

Amesema Wizara imeanza mchakato wa haraka wa kufanya tathmini ili kubaini sababu zinazofanya Watanzania kutozitumia kikamilifu fursa za masomo nje ya nchi pindi zinapojitokeza, akisisitiza kuwa hali hiyo haikubaliki ikizingatiwa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, la kuongeza idadi ya Watanzania wanaopata elimu katika vyuo vya nje ya nchi.

“Ni muhimu kubaini kwa nini fursa zinapopatikana hazichangamkiwi na Watanzania, ili Serikali iweze kuchukua hatua sahihi na kuongeza ushiriki wa wanafunzi wetu katika masomo ya kimataifa,” amesema Prof. Mkenda.

‎Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, amesema kuwa kikao hicho ni fursa muhimu ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujenga uelewa wa pamoja kuhusu mwelekeo wa utekelezaji wa sera na mipango ya Wizara.

‎Aidha amebainisha kuwa Wizara itaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya viongozi wa Wizara, taasisi zake na wataalamu wa sekta ya elimu ili kuhakikisha mageuzi yanayopangwa yanatekelezwa kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya kwa Taifa.

Naye ,Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, amesema  kikao hicho cha kimkakati kimewaleta pamoja viongozi wa wizara na taasisi  ili kupitia utekelezaji wa malengo ya mwaka 2025/26 na kupanga mikakati itakayowezesha kufikiwa kwa Dira 2050 katika sekta za Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Amesema mikakati hiyo inajumuisha utekelezaji wa elimu ya lazima ya miaka 10, uimarishaji wa mafunzo ya amali katika ngazi ya sekondari, kuimarisha fursa za elimu ya juu pamoja na masuala ya ufadhili.

“Tutajadili pia programu nyingine muhimu zenye lengo la kuboresha sekta ya elimu, kuimarisha ubora, usawa na upatikanaji wa huduma kwa Watanzania wote,” amesema Prof. Nombo.

Kikao hicho kinatarajiwa kutoa mwongozo mpya wa utekelezaji wa vipaumbele vya Serikali katika sekta ya elimu kuelekea kufikiwa kwa malengo ya muda mfupi na mrefu.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akizungumza wakati wa kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika leo Januari 20, 2025, Jijini Dodoma

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir akizungumza wakati wa kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika leo Januari 20, 2025, Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika leo Januari 20,2026 jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Hussein Omary,akifuatilia mada mbalimbali ambazo zilikuwa zikitolewa wakati wa kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika leo Januari 20,2026 jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi,akifuatilia mada mbalimbali ambazo zilikuwa zikitolewa wakati wa kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika leo Januari 20,2026 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  kikao kazi na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kilichofanyika Januari 20, 2025, Jijini Dodoma.

Kwa muda mrefu nilikuwa mtu wa kulaumiwa kwa kila jambo. Kila kitu kikiharibika, macho yaligeuka kwangu. Kazi ikiyumba, familia ikagombana, biashara ikishindwa jina langu lilitajwa.

Niliambiwa ni mkosi, ninaleta bahati mbaya, na niwe mbali. Nilivumilia kimya kimya, nikijilaumu, nikijiuliza kosa langu ni nini.

Kilichonichanganya ni kwamba, nilipokuwa peke yangu mambo yalikaa sawa kidogo. Lakini kila nilipozingirwa na watu fulani, matatizo yalizidi. Nilipoteza pesa bila sababu, nilikosa usingizi, na nilijihisi mzito kila mara.

Nilianza kujiuliza maswali mazito: je, kweli mimi ndiye mkosi, au kuna watu wanaobeba mikosi wanayonipachika bila kujua? Nilikaa muda mrefu nikihofia kusema ukweli. Kuwaambia watu kuwa huenda wanachangia kuanguka kwangu kulionekana kama kukosa adabu.

Lakini hali ilipozidi, nilijua nikikaa kimya nitaangamia. Niliamua kuchunguza maisha yangu kwa umakini. Ndipo nikagundua mfanano wa kushangaza watu wachache tu walikuwepo karibu nami kila jambo lilipoharibika.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nachukuliwa-kama-mkosi-siku-watu-wenye-mikosi-walipoondolewa-maisha-yangu-yakabadilika/

Kwa muda mrefu nilikuwa nikiishi maisha ambayo hayakuwa yangu. Kila jambo lilikuwa linaanza vizuri lakini linaisha vibaya bila sababu ya kueleweka. 

Nilikuwa na afya njema jana, leo naamka nikiwa dhaifu. Nilikuwa na furaha asubuhi, jioni huzuni nzito inanielemea.

Nilihisi kama kulikuwa na mkono usioonekana uliokuwa unanisukuma chini kila nilipojaribu kuinuka. Nilianza kuona ishara zisizo za kawaida. 

Ndoto mbaya zilikuwa za kurudia rudia, usingizi haukuwa usingizi, na nyumbani kwangu hapakuwa na amani.

Watu wa karibu waliniona nimebadilika, lakini hawakujua nini kinaniandama. Nilijaribu kupuuza nikidhani ni msongo wa mawazo, lakini moyoni nilijua kuna zaidi ya hilo. Kilichonishtua ni pale matatizo yalipoanza kuingia kwa kasi.

Kazi ikaanza kuyumba, fedha zikapotea ovyo, na migogoro ikaibuka bila chanzo cha wazi. Nilianza kujiuliza, “Kwa nini mambo haya yote kwa wakati mmoja?” Ilikuwa kana kwamba mtu alitamani niharibikiwe kila upande.

Ndipo nikaanza kuamini kuwa labda kuna uchawi mbaya umeelekezwa kwangu kwa siri.
Nilikaa kimya kwa muda kwa sababu ya hofu na aibu. Sikutaka kuonekana nikiamini mambo ambayo watu wanacheka.

Lakini hali ilipozidi kuwa mbaya, nilijua nikikaa kimya zaidi ningeangamia. Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/walinitakia-mabaya-kwenye-giza-lakini-nuru-ilipowaka-walikimbia/
Kwa muda mrefu nilikuwa mtu wa “kujitahidi sana bila kuona matokeo.” Nilifanya kazi kwa bidii kuliko wengi, nikaamka mapema, nikarudi nyumbani usiku, lakini kila nilichoshika hakikukaa. Mapato yalipotea, fursa zilipita mikononi, na kila nilipokaribia kufanikiwa, kitu fulani kilivuruga mambo.

Nilianza kujiuliza kama nilizaliwa bila bahati.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu niliowazidi juhudi wakipiga hatua kubwa. Wengine walipata ajira, wengine walipanua biashara, nami nilibaki palepale. 

Kila mtu alinipa ushauri wake badilisha kazi, hama mji, soma tena lakini nilipofanya hayo, bado hakuna kilichobadilika.

Nilihisi kama kuna pazia zito lililokuwa limetandikwa mbele ya maisha yangu.
Nilipoanza kukata tamaa, nilikaa kimya nikijitathmini.

Ndipo nikatambua jambo moja la ajabu: kila nikipata wazo zuri au fursa, niliingiwa na wasiwasi usioelezeka, mambo yalivurugika ghafla, au nilipoteza motisha bila sababu. Sikuweza kulieleza, lakini nilijua hili halikuwa la kawaida. Bahati yangu ilikuwa imefungwa mahali.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilijitahidi-bila-mafanikio-mpaka-bahati-yangu-ilipofunguliwa-ghafla/
Kwa muda mrefu nilikuwa mtu wa ajabu machoni pa wengine. Nilifanya kazi kwa bidii, lakini kila nilichopata kilipotea ghafla. Nilipojaribu kuanzisha jambo jipya, lilivurugika kabla halijakomaa.

Kilichonichanganya ni kwamba, watu waliokuwa karibu nami walikuwa wakinitabasamia kila siku, wakinionyesha upendo wa juu juu, huku nyuma ya pazia mambo yangu yakianguka moja baada ya jingine.

Nilipoanza kuchunguza maisha yangu kwa makini, niliona mfanano wa ajabu. Kila niliposhiriki habari njema mpango, hatua, au mafanikio madogo ndani ya muda mfupi kulikuwa na tatizo. Ama pesa zinapotea, ama migogoro inaibuka, ama ninajikuta nimechoka bila sababu.

Nilijiuliza maswali mengi, lakini sikuthubutu kusema wazi kuwa labda nilizingirwa na adui waliovaa mavazi ya marafiki. Nilikaa kimya kwa muda mrefu kwa sababu sikuwa na ushahidi. Watu wale wale walikuwa wanakuja nyumbani kwangu, wanakula nami, wanacheka nami.

Lakini ndani yangu kulikuwa na sauti iliyokuwa ikiniambia, “Si kila tabasamu ni la heri.” Niliendelea kuvumilia hadi pale nilipofikia mwisho. Usiku mmoja, niliketi peke yangu nikahisi presha nzito isiyoelezeka. Ndipo nikajua nilihitaji msaada.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/adui-zangu-walikuwa-wananitabasamia-siku-nilipowafunga-kimya-kimya-wakaanza-kujitenga/
Kwa miaka nane, maisha yangu yalizunguka neno moja tu subira. Niliolewa nikiwa na matumaini makubwa ya kuwa mama mapema, kama wanawake wengi. 

Mwaka wa kwanza ulipita, wa pili pia, nikijifariji kwamba labda ni wakati tu. Lakini kadri miaka ilivyoongezeka, shinikizo nalo liliongezeka.

Kila sherehe ya mtoto wa mtu ilinifanya nijifungie chumbani na kulia kimya kimya.
Nilizunguka hospitali nyingi. 

Vipimo vilifanyika mara kwa mara, majibu yalikuwa yale yale: “Hakuna tatizo kubwa.” Maneno hayo yaliuma zaidi kuliko majibu mabaya, kwa sababu hayakunipa suluhisho.

Nilimeza vidonge, nikafuata ratiba kali, nikabadili chakula, hata nikapunguza stress kwa makusudi. Lakini kila mwezi ulipoisha bila mabadiliko, moyo wangu ulizidi kupasuka.
Kilichoniumiza zaidi ni maneno ya watu. Wengine walinionea huruma, wengine walinidharau bila kujua.

Nilianza kujitenga na familia na marafiki. Niliishi na hofu ya kuulizwa, “Mbona bado?” Nilimpenda mume wangu, naye alinipa moyo, lakini nilijilaumu mwenyewe kila siku. Nilianza kuamini labda uzazi haukuwa sehemu ya hatima yangu.

Siku moja, katika mazungumzo ya kawaida tu, mwanamke niliyekuwa simjui sana alinisimulia safari yake ya miaka ya kutafuta mtoto. Alizungumza kwa utulivu, bila kujisifu, lakini kulikuwa na amani kwenye sauti yake.

Alipotaja kuwa kuna wakati matatizo ya uja uzito hayawi ya kitabibu pekee, bali yanahitaji kufunguliwa kwa njia ya kiroho, nilitetemeka.

Ilikuwa ni hofu niliyokuwa najaribu kuikimbia kwa miaka. Baada ya tafakari ndefu, niliamua kujaribu kitu ambacho nilikuwa nakiogopa kuomba msaada wa kiroho.Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/miaka-nane-ya-kutafuta-mtoto-iliisha-baada-ya-hatua-moja-niliyokuwa-nikiogopa-kuijaribu/
 

SHIRIKA la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) limebuni, kusanifu na kutengeneza mtambo wa kuchakata zao la miwa ili kupata sukari kwa kiwango cha mjasiriamali wa kati, ikiwa ni jitihada za kupunguza uhaba wa sukari nchini pamoja na kuwaongezea wakulima wa miwa soko la uhakika.

Hayo yalisemwa Januari 19, 2026 na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb.), wakati wa Ziara yake TEMDO jijini Arusha ambapo amelishauri Shirika hilo kuzalisha mitambo hiyo ya Sukari pamoja na mitambo mingine katika kanda zote nchini kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za ndani ikiwemo TAMISEMI na nje ya nchi, ili kufikia Malengo yanayotarajiwa.

Aidha, aliiagiza TEMDO kuzalisha mitambo inayoendana na kasi ya teknolojia ili kuhakikisha teknolojia zinazozalishwa zinaingia sokoni na kutoa fursa zaidi za kiuchumi na kuondokana na umaskini kwa Wajasiliamali na Wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TEMDO, Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia, alisema Shirika hilo linaendelea kuweka mikakati madhubuti ya mageuzi ya viwanda kwa kuzalisha mitambo itakayotatua changamoto za wakulima na kuwawezesha kupata masoko ya uhakika ili kuongeza uzalishaji viwandani na kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Profesa Frederick Kahimba alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kupunguza pengo la uzalishaji wa sukari nchini sambamba na kuongeza thamani ya zao la miwa kwa wakulima wadogo na wa kati ambapo hadi sasa Shirika hilo limepokea maombi sita kutoka kwa Wajasiliamali wa kati wanaotaka kufungiwa mitambo hiyo ya Sukari kutoka Dodoma, Same, Manyara, Busega, Kilosa na Morogoro.

Temdo inazalisha bidhaa zaidi ya 16 ikiwemo vifaa tiba vya hospitali kama majokofu ya kuhifadhia maiti, vichomea taka hatarishi, vitanda vya aina mbalimbali vinavyohitaji kufika soko la Zanzibar ili kuongeza pato la Taifa, kukuza uchumi na kupunguza uagizaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi. Alifafanua Kahimba.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango wa wizara hiyo, Audax Bahweitama akimwalikilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo alisema Serikali improvises Sera na Sheria mbalimbali zinazohusu Maendeleo ya Viwanda ili kufikia uchumi jumuishi kupitia viwanda kwa kuzalisha bidhaa zenye ushindani na ubora sokoni, kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.