
Nilikuwa na sifa zote zilizohitajika, viwango vya juu vya taaluma, na uwezo mkubwa wa kujieleza. Hata hivyo, maisha yangu ya utafutaji yaligeuka kuwa mfululizo wa maumivu na kukata tamaa kulikoingia akilini.
Kila mara nilipoomba kazi, nilipita kwenye usahili wa mchujo (interview) kwa alama za juu sana. Lakini ajabu ni kwamba, ilipofika hatua ya mwisho ya kutoa majina ya waliopata ajira, jina langu lilipotelea hewani au kutupwa kimyakimya!
Watu niliowazidi uwezo na alama walikuwa wakichukuliwa, huku mimi nikibaki mtaani nikichekwa na kusaidiwa chakula na wazazi wangu.
Nilifanya usahili zaidi ya mara kumi na tano katika miaka hiyo mitano, lakini kila mara nilibaki ukingoni mwa mafanikio. Nilibaki nikijiuliza ni kwanini elimu na juhudi zangu hazikuwa zikizaa matunda.SOMA ZAIDI.
Mwanzo kila kitu kilienda kwa kasi na matumaini makubwa. Hata hivyo, mara tu kuta zilipoinuka na kuanza kuonekana kwa majirani na ndugu, vita vya chini kwa chini vilianza bila mimi kutarajia.
Ujenzi ulianza kukumbana na ajali na mikosi isiyoelezeka. Mafundi bora niliowakodi walianza kuugua ghafla pindi tu walipokanyaga kwenye eneo la mradi, wengine wakipata majeraha ya ajabu na kukimbia kazi.
Vifaa vya ujenzi kama simenti na nondo vilikuwa vikiharibika au kupotea kimyakimya, na pesa nilizokuwa nikituma zilipotea kwenye dharura zisizotabirika.
Kumbe bila mimi kujua, baadhi ya ndugu zangu wa damu waliokuwa wakijifanya kunipongeza kwa nje, ndio waliokuwa wakizunguka usiku kufanya fitina na matambiko ya giza ili mradi wangu ufe na nifilisike!SOMA ZAIDI.
Kila mwanamume anapofikisha umri fulani na kufanikiwa kijamii, hamu yake kubwa ni kupata mke mwema wa kujenga naye familia na kuendeleza maisha.
Hata hivyo, maisha yangu ya mahusiano yaligeuka kuwa fumbo la kutisha na lenye kuumiza moyo kwa zaidi ya miaka minne.
Kila mara nilipompata binti mstaarabu, mwenye tabia njema na tukakubaliana kuoana, mambo yalianza kubadilika ghafla pindi tu alipokanyaga mlangoni kwangu.
Binti ambaye jioni tulikuwa na amani na furaha tele, ikifika usiku alipatwa na hofu isiyoelezeka, ndoto za kutisha za kuingiliwa na majitu, au maumivu makali ya mwili.
Ndani ya siku chache au wiki moja pekee, kila binti alifunganya virago vyake na kukimbia nyumba yangu huku akisema hawezi kuendelea kuishi pale.
Zaidi ya wasichana sita tofauti waliondoka kwa mtindo huo huo bila mimi kufanya kosa lolote, jambo lililonifanya nianze kuonekana kama mwanamume aliyelaaniwa au mwenye nuksi ya ajabu. SOMA ZAIDI.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafadh Ameir, amesisitiza nafasi muhimu ya wanawake wanataaluma katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Akizungumza jijini Dar es Salaam katika hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026, Naibu Waziri amesema kuwa kauli mbiu ya hafla hiyo, “The Contribution of Women Professionals to the Implementation of Tanzania Development Vision 2050”, imeakisi mchango wa wanawake katika kujenga uchumi wa maarifa, ubunifu na teknolojia.
Ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu. Hatua zilizotekelezwa ni pamoja na maboresho ya sera na sheria, ujenzi wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika ufundishaji na ujifunzaji.
Aidha, amesisitiza kuwa mchango wa wanawake hauwezi kupuuzwa na kwamba Serikali ikiendelea kuimarisha usawa wa kijinsia, kuongeza ushiriki wa wanawake katika fani za STEM, kuzuia ukatili wa kijinsia na kuwekeza katika maendeleo ya kitaaluma ya walimu na wahadhiri kupitia mafunzo endelevu na tafiti.
Naibu Waziri ametoa wito kwa walimu, wakufunzi na wahadhiri kuendelea kuwa chachu ya mabadiliko ya Taifa kwa kuandaa kizazi chenye maadili, maarifa na ubunifu.
“Mustakabali wa Taifa upo mikononi mwa vijana na wanafunzi,” amesisitiza, akiwataka kutumia kikamilifu fursa za elimu zinazotolewa na Serikali ili kuleta suluhisho kwa changamoto za kijamii na kiuchumi." amesema Naibu Waziri
Naye Mbunge Viti Maalum Mwakilishi wa Vyuo Vikuu, Mhe. Asha Feruzi, amesema kuwa hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026 ni jukwaa la kujadili mustakabali wa elimu, ubunifu na teknolojia katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Mhe. Feruzi amebainisha kuwa matokeo yanayotarajiwa kupitia ushirikiano huo ni kuimarika kwa tafiti, ubunifu na matumizi ya teknolojia za kisasa, hususan akili unde (Artificial Intelligence). Ameongeza kuwa vyuo vikuu na sekta binafsi vitaunganishwa ili kuzalisha suluhisho, bidhaa na huduma zinazochochea ukuaji wa uchumi shindani na endelevu.

Akizungumza kuhusu fursa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa BMT, Bw. Aminiel Aligaesha, amesema AFCON 2027 ni tukio la kihistoria litakalofanyika kwa mara ya kwanza Ukanda wa Afrika Mashariki na likiwa linatimiza miaka 70 mwakani tangu kuanzishwa kwake.
Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, fursa ya kwanza ni kuongezeka kwa biashara na shughuli za kiuchumi, ambapo hoteli, nyumba za kulala wageni, migahawa, maduka pamoja na wauzaji wa bidhaa zenye nembo za mashindano watanufaika kutokana na ongezeko la wageni na mashabiki.
Aidha, amesema sekta ya benki na huduma za kifedha itanufaika kupitia ongezeko la miamala ya kifedha, huduma za kubadilisha fedha za kigeni, udhamini wa matukio na utoaji wa bidhaa maalum za kifedha kwa wafanyabiashara watakaohudumia wageni.
Katika upande wa ajira, Bw. Aligaesha amesema vijana watapata nafasi za kazi katika sekta za ukarimu, usafiri, utalii, teknolojia, uandishi wa habari, uzalishaji wa maudhui na huduma nyingine, hali itakayowaongezea uzoefu wa kufanya kazi katika mazingira ya kimataifa.
Pia ametaja sekta ya usafiri kuwa miongoni mwa zitakazonufaika kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya usafiri wa anga, nchi kavu na majini, ikiwemo safari za ndani, huduma za teksi, mabasi, usafiri wa mtandaoni na vifurushi maalum vya safari za AFCON vinavyoweza kujumuisha utalii na malazi.
Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, AFCON 2027 pia itachochea maendeleo ya soka nchini kwa kuhamasisha uwekezaji katika akademi za vijana, ukocha, urefa na ukuzaji wa vipaji, huku sekta ya afya ikitarajiwa kunufaika kupitia utoaji wa huduma kwa wageni na kukuza utalii wa afya kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali.
Amesema mashindano hayo yatatoa jukwaa la kutangaza utamaduni wa Tanzania kupitia muziki, vyakula, sanaa, mavazi na lugha ya Kiswahili, sambamba na kuitangaza Tanzania (national branding) kwa mamilioni ya watazamaji duniani kupitia televisheni, mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya kimataifa.
Kuhusu sekta ya utalii, Bw. Aligaesha alisema wageni watakaokuja kushuhudia mashindano hayo watapata nafasi ya kutembelea vivutio mbalimbali ikiwemo Serengeti, Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro na Zanzibar, jambo litakaloongeza mapato ya sekta hiyo.
Ameongeza kuwa maandalizi ya AFCON tayari yamechochea maboresho makubwa ya miundombinu ikiwamo ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, ujenzi wa viwanja vipya Arusha na kule Zanzibar, pamoja na uboreshaji wa barabara, viwanja vya mazoezi na mifumo ya huduma za kidijitali ambayo itaendelea kutumika hata baada ya mashindano hayo kumalizika.
Kwa mujibu wa Bw. Aligaesha, mafanikio ya maandalizi na uendeshaji wa AFCON 2027 yataifanya Tanzania kuwa kitovu cha michezo barani Afrika, huku yakifungua milango ya kuandaa mashindano mengine ya kimataifa, kuvutia wawekezaji na kukuza uchumi wa michezo.
Aidha, amesema mashindano hayo yataimarisha diplomasia ya michezo na ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na kuimarisha uhusiano wa kikanda katika biashara, utalii, utamaduni na uwekezaji.
Akihitimisha, Bw. Aligaesha amewataka Watanzania kuendelea kufuatilia taarifa za BMT, akieleza kuwa utaratibu rasmi wa namna wananchi na wadau watakavyoweza kushiriki na kunufaika kupitia fursa hizo utatangazwa baadaye mwaka huu.
"Tunatoa wito kwa wananchi, wafanyabiashara na wadau wote kuanza kujiandaa mapema. AFCON 2027 ni mwanzo wa ukurasa mpya wa maendeleo ya michezo na uchumi wa michezo nchini, na muda si mrefu tutatangaza utaratibu wa namna fursa hizi zitakavyopatikana," amesisitiza Bw. Aligaesha

.jpeg)

.jpeg)



















































































