Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir (hayupo pichani) wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

......

Serikali imewataka watumishi wa sekta ya elimu nchini kuimarisha mshikamano, uwajibikaji na ubunifu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu bora inayokidhi mahitaji ya karne ya 21.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir wakati akifunga Mkutano wa Pili wa Baraza la 37 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Mhe.Ameir  amesisitiza kuwa mafanikio ya sekta ya elimu yanategemea kwa kiasi kikubwa ushirikiano kati ya wafanyakazi, menejimenti pamoja na wadau wote wa elimu, akibainisha kuwa mshikamano huo ni chachu ya kuleta mageuzi chanya na endelevu.

Ametoa pongezi kwa uongozi wa Wizara, ukiongozwa na Waziri Adolf Mkenda, kwa kuendelea kusimamia mageuzi ya elimu ikiwemo maboresho ya sera na mitaala inayolenga kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia duniani.

Aidha, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake unaoendelea kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu, hususan katika kukuza ubora wa elimu, ubunifu na tafiti.

" Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha elimu, ikiwemo uzinduzi wa Mkakati wa Kisayansi wa Kuimarisha Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) pamoja na mpango wa kuunganisha taasisi za elimu na waajiri."amesema Mhe.Ameir

Ameeleza kuwa mipango hiyo inalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na hivyo kuongeza ushindani wao kitaifa na kimataifa.

Hata hivyo amewataka wajumbe wa baraza hilo kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, akisisitiza umuhimu wa kuwa na maadili, nidhamu na uwajibikaji kazini.

Amebainisha kuwa baraza la wafanyakazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la majadiliano, ushauri na maamuzi yanayochangia kuboresha utendaji kazi pamoja na ustawi wa watumishi.

Katika mkutano huo, mada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo bajeti ya wizara, usimamizi wa rasilimali watu, maadili ya utumishi wa umma na afya ya akili mahali pa kazi.

Ameir amesema  mada hizo zina mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza tija kwa watumishi, hivyo kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Aidha Ameir ametoa wito kwa watumishi wote kuendelea kudumisha mshikamano, uzalendo na uadilifu, pamoja na kuwa mabalozi wa kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof.Carolyne Nombo, amesema kuwa utekelezaji wa kaulimbiu ya mkutano wa wafanyakazi ya “Ushirikishwaji na Mshikamano wa Wafanyakazi ni Chachu ya Kuimarisha Elimu Inayochochea Ubunifu” ni muhimu katika kufanikisha malengo ya sekta ya elimu nchini.

Prof. Nombo amesisitiza kuwa mshikamano na ushirikiano kazini ni msingi wa kuleta mabadiliko ya kweli katika sekta ya elimu.

Ameeleza kuwa kaulimbiu hiyo inalenga kuwajenga watumishi kuwa na utamaduni wa kufanya kazi kwa pamoja, kwa bidii na kwa uwajibikaji, hali ambayo itachochea mageuzi makubwa yanayohitajika katika kuboresha ubora wa elimu nchini.

“Tunaposhirikiana na kufanya kazi kwa bidii kama timu moja, tunaweka msingi imara wa kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya elimu, yanayoakisi dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2050,” amesema Prof. Nombo.

Ameongeza kuwa juhudi hizo zinapaswa kuendana na utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 (toleo la 2023), pamoja na kuzingatia mabadiliko mbalimbali yaliyofanyika katika mitaala iliyoboreshwa.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa watumishi kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya serikali katika kutekeleza majukumu yao, akibainisha kuwa nidhamu na uwajibikaji ni nguzo muhimu za kufanikisha malengo ya wizara.

 Na Mwandishi Wetu, Ilala

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, mkoani Dar es Salaam, Edward Mpogolo, ametoa onyo kali kwa wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya ujenzi wa barabara wilayani humo, akiwataka kuzingatia mikataba na kukamilisha kazi kwa wakati.

Onyo hilo amelitoa wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya barabara, aliyoifanya kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya, ambapo alitembelea miradi inayotekelezwa na wakandarasi, wengi wao wakiwa makampuni ya wazawa.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mpogolo aliwakosoa baadhi ya wakandarasi kwa kuchelewesha miradi kwa visingizio visivyo na msingi, hali inayosababisha usumbufu kwa wananchi huku Serikali ikiwa tayari imeshatoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa kazi hizo.

Aidha, alionya tabia ya baadhi ya wakandarasi kukaidi maelekezo ya wasimamizi wa miradi kutoka TARURA na TANROADS, wakitumia mwanya wa kufahamiana na baadhi ya viongozi wa juu. Alisisitiza kuwa vitendo hivyo havitavumiliwa, hasa pale vinapoambatana na ujenzi wa barabara chini ya viwango vilivyokubaliwa kwenye mikataba.

Mpogolo, pia alieleza wasiwasi wake juu ya wakandarasi wanaochukua miradi mingi kwa wakati mmoja bila kuwa na uwezo wa kutosha wa rasilimali na vifaa, jambo linalosababisha baadhi yao kutelekeza miradi au kuchelewesha utekelezaji wake.

Kutokana na hali hiyo, aliagiza taasisi zote zinazohusika na usimamizi na uchunguzi wa miradi kuchukua hatua kali dhidi ya wakandarasi wanaokiuka taratibu na kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo katika Wilaya ya Ilala.

Katika ziara hiyo, Mpogolo, alitaja baadhi ya barabara zilizokaguliwa kuwa ni pamoja na Halisi na Kimanga, zilizogharimu shilingi bilioni 1.7 zilizotolewa mwaka 2024.

Barabara nyingine ni Mafia, Masasi, Magila, Bondi na Muhonda, zilizogharimu shilingi bilioni 1.8 zilizotolewa mwaka 2025.

Pamoja na barabara za Mwanza, Livingstone, Nyamwezi, Kipati, Msikitini, Sharifushamba, Kigoma na Tunduru, zilizogharimu shilingi bilioni 1.9.

Mpogolo alisisitiza kuwa Serikali haitavumilia uzembe wowote utakaoathiri ubora na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha miundombinu na maisha ya wananchi.












Benki ya Ushirika (Coop Bank) imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kukuza uchumi jumuishi kwa kuongeza kiwango cha mikopo kwa sekta ya kilimo, hususan kwa wakulima, ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kupanua huduma za kifedha kwa makundi ambayo hayajafikiwa kwa urahisi.

 Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), kupitia Mkurugenzi Mkuu wake, Ephraim Mafuru, imepokea ugeni maalum kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Prof. Abel Makubi, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika kukuza utalii wa matibabu nchini Tanzania na kushiriki katika Maadhimisho ya Miaka 10, tarehe 15 July 2026 ambapo pia Hospitali itakuwa ianzindua mfuko wa kusaidia huduma za Upandikizaji Uloto kwa Watoto na Upandikizaji Figo. 

Katika kikao hicho, taasisi hizo mbili zimejadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano na kukubaliana kuendelea kuhamasisha utalii wa Matibabu kama moja ya mazao ya kipekee ya utalii nchini. Hatua hiyo inakuja wakati Hospitali ya Benjamin Mkapa ikiendelea kujipambanua kwa kutoa huduma za kibingwa na ubobezi wa hali ya juu, na kuifanya kuwa miongoni mwa hospitali bora za rufaa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Akizungumza katika kikao hicho, Mafuru amesema Bodi ya Utalii imevutiwa sana na huduma sita za kibingwa zinazotolewa na hospitali hiyo, huku huduma mbili zikiwa za kipekee zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

“Ni jambo la kujivunia Hospitali ya Benjamin Mkapa kuwa hospitali pekee Afrika Mashariki na Kati yenye utaalamu wa kupandikiza uloto kwa watoto waliozaliwa na selimundu (Sickle Cell), lakini pia huduma ya upandikizaji figo,” amesema Mafuru.

Ameeleza kuwa upekee wa hospitali hiyo unaweza kuinua taswira nzuri ya Tanzania katika sekta ya utalii wa tiba, sambamba na kuboresha maisha ya Watanzania kwa kuwapatia huduma za kibingwa ndani ya nchi badala ya kusafiri nje kutafuta matibabu.

Mafuru pia ametoa wito kwa wadau wote wa sekta ya utalii nchini kushiriki harambee ya kuanzisha mfuko maalum wa kusaidia matibabu ya wagonjwa wa selimundu na figo kwa wananchi wasio na uwezo. Harambee hiyo inatarajiwa kufanyika Julai 15, 2026, sambamba na maadhimisho ya miaka kumi tangu kuanzishwa kwa Hospitali ya Benjamin Mkapa.

Kwa upande wake, Prof. Makubi ameahidi kushirikiana kikamilifu na Bodi ya Utalii Tanzania katika kukuza zao hili la utalii wa tiba nchini, akisisitiza kuwa taasisi zote mbili zipo chini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuimarishwa kwa utalii wa tiba kutaiwezesha Tanzania kujijengea nafasi kubwa zaidi kama kitovu cha huduma za afya za kibingwa katika ukanda wa Afrika, huku pia ikichangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Ushirikiano huu unaendelea kufungua ukurasa mpya wa kuitangaza Tanzania si tu kama kivutio cha wanyamapori, fukwe na urithi wa utamaduni, bali pia kama kitovu cha huduma za afya za ubora wa kimataifa.



 


Na Munir Shemweta

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imempokea mjumbe maalum kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani (UN-Habitat) kwa ajili ya kukagua maandalizi ya kufunguliwa kwa ofisi za shirika hilo nchini.

Mjumbe huyo maalum, Bw. Grace Lubale, yupo nchini kwa ziara ya siku tatu inayolenga kutembelea na kukagua ofisi zilizotolewa na Serikali ya Tanzania kwa UN-Habitat, ambazo zipo katika jengo la Wizara hiyo lililopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano yaliyosainiwa tarehe 7 Juni 2023 kati ya Serikali ya Tanzania na UN-Habitat, yakilenga kuimarisha ushirikiano katika sekta ya makazi na maendeleo ya miji.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo tarehe 28 April 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Deogratius Kalimenze, amesema Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha ofisi hiyo inaanza kazi kwa ufanisi, ikiwa ni pamoja na kutoa vitendea kazi na wataalam wanne watakaosaidia uendeshaji wake.

‘’Serikali ina matarajio makubwa kutokana na uwepo wa ofisi hii, hususan katika kuimarisha juhudi za kushughulikia changamoto mbalimbali katika sekta ya makazi, ikiwemo maendeleo ya miji, matumizi ya nishati jadidifu, ustahimilivu wa miji, pamoja na uboreshaji wa makazi yasiyopangwa’’. ameeleza Bw. Kalimenze.

Kwa upande wake, Bw. Grace Lubale amesema UN-Habitat inaendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Tanzania ili kuhakikisha malengo ya ushirikiano huo yanatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya shirika hilo.

‘’Kupitia ushirikiano huu, maeneo yatakayopatiwa kipaumbele ni pamoja na uboreshaji wa makazi, ujenzi wa nyumba za gharama nafuu pamoja na nishati safi katika majengo’’. amesema,

Ushirikiano kati ya pande hizo mbili pia unalenga kuwezesha upatikanaji wa wadau wa maendeleo na mifumo ya Umoja wa Mataifa katika kusaidia utekelezaji wa miradi ya makazi, pamoja na kuanzisha mifumo madhubuti ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, hususan lengo namba 11 linalohusu miji na makazi endelevu.

Hatua ya kufunguliwa kwa ofisi ya UN-Habitat nchini Tanzania inatarajiwa kuwa chachu ya kuimarisha maendeleo ya sekta ya makazi na miji, na kuongeza ushirikiano wa kimataifa katika kutatua changamoto za makazi nchini.

Timu ya Mpira wa Miguu ya Mashtaka imeshindwa kuonesha ubabe wake baada ya kukubali kichapo cha mabao 4-2 kutoka kwa TCDC Sports Club katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Venite, Mji Mwema mkoani Njombe.

Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa, TCDC Sports Club ilianza kwa kasi na kuonyesha kiwango bora tangu dakika za mwanzo. Kipindi cha kwanza kilishuhudia TCDC ikienda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-1, huku Mashtaka wakijitahidi kusawazisha bila mafanikio makubwa.

Kipindi cha pili kiliendelea kuwa na ushindani mkali, lakini TCDC waliendelea kutawala mchezo kwa kuongeza mabao mawili zaidi, wakionyesha umakini mkubwa katika safu yao ya ushambuliaji.

Mashtaka walifanikiwa kupata bao moja la kufutia machozi, lakini halikutosha kuzuia ushindi wa TCDC, na hivyo mchezo kumalizika kwa mabao 4-2.

Ushindi huo unaipa TCDC Sports Club morali kubwa wanapoendelea na maandalizi yao kupitia mechi za kirafiki dhidi ya timu mbalimbali za Wizara na Taasisi.

Mechi hizo ni sehemu ya kujiandaa kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) mwaka 2026, yatakayofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Kwa upande wao, Mashtaka watalazimika kujipanga upya na kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza ili kuimarisha kikosi chao katika michezo ijayo.



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa 21 wa Baraza la Mawaziri wa Nishati wa Ukanda wa Mashariki mwa Afrika, uliofanyika Aprili 29, 2026 jijini Cairo, Misri, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya umeme.

Katika mkutano huo wa nchi wanachama wa Umoja wa Nishati Mashariki mwa Afrika (EAPP), uamuzi muhimu umefikiwa wa kuichagua rasmi Jamhuri ya Kiarabu ya Misri kuwa mwenyeji wa kudumu wa kituo cha uendeshaji wa soko la umeme la pamoja  kwa nchi wanachama.

Mkutano huo uliongozwa na Waziri wa Umeme na Nishati Jadidifu wa Misri, Mhe. Dkt. Mahmoud Esmat, ambaye pia ni mwenyekiti anayemaliza muda wake,  uliwakutanisha Mawaziri wa Nishati kutoka nchi 13 wanachama kwa lengo la kukamilisha mfumo wa kiutawala na kiuendeshaji wa soko la umeme la pamoja na endelevu.

Mbali na kuichagua Misri, Baraza hilo pia limepitisha nyongeza ya muda wa miezi miwili kwa nchi wanachama kukamilisha mchakato wa kuridhia hati za makubaliano ya ushirikiano baina ya serikali na mashirika ya umeme.

Aidha, mkutano huo umeridhia Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasi ya Ethiopia kuchukua nafasi ya uenyekiti wa Baraza la Mawaziri, kufuatia kumalizika kwa muda wa uongozi wa sasa, kwa mujibu wa katiba ya umoja huo inayotaka uongozi kuzunguka kwa wanachama kila mwaka.

Akihitimisha mkutano huo, Mwenyekiti wa EAPP, Mhe. Dkt. Esmat, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza umoja, ushirikiano, uwazi na kuheshimiana miongoni mwa nchi wanachama ili kufikia malengo ya kuwa na soko la umeme la kikanda lenye tija.

Akizungumza kuhusu mkutano, Mhe. Salome amesema maazimio yaliyofikiwa ni hatua muhimu katika kuleta mageuzi makubwa katika biashara ya umeme na kuimarisha soko la nishati la pamoja kwa nchi za ukanda huo.

Katika mkutano huo, Mhe. Makamba ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Misri, Meja Jenerali Richard Makanzo, Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO anayeshughulikia uzalishaji umeme, Mhandisi Anthony Mbushi, pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati, TANESCO na EWURA.














Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza wakati akifungua  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza wakati akifungua  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda (hayupo pichani) wakati wa  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema utekelezaji wa mageuzi ya elimu unaoendelea nchini ni sehemu ya dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha vijana wanapatiwa ujuzi, maarifa na uwezo unaowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa taifa.

Ameyasema hayo leo  Aprili 29, 2026 katika Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo, Prof. Mkenda amesisitiza kuwa sekta ya elimu inabeba wajibu mkubwa katika maendeleo ya nchi na kwamba, wajibu wa Wizara ni kuhakikisha mipango yote inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kasi.

Waziri Mkenda ameongeza kuwa kuanzishwa kwa Wizara maalum ya maendeleo ya vijana ni uthibitisho wa umuhimu wa kundi hilo katika maendeleo ya taifa na kuwa elimu ya ufundi kupitia VETA, ni msingi wa kuwaandaa vijana kuzalisha na kushiriki katika uchumi wa kisasa.  "Utekelezaji wa elimu ya miaka 10 ya lazima na uimarishaji wa shule za Sekondari na shule za amali unatekelezwa kwa ushirikiano wa karibu na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, na hata sekta binafsi hasa katika kuhakikisha upatikanaji wa shule karibu na makazi ya wananchi na ununuzi wa vifaa vya kisasa kwa ajili ya mafunzo ya ufundi."amesema Prof. Mkenda Katika kuhimiza ubunifu na uwajibikaji, Prof. Mkenda amewataka watumishi wa Wizara kuendeleza kasi ya utendaji na kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa kuhusu utekelezaji na mafanikio ya serikali katika maeneo ya sekta ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,amesema Serikali inaendelea kuimarisha usimamizi wa ajira na rasilimaliwatu kwa kuzingatia malengo na maono ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hususan katika utekelezaji wa Kifungu cha 73 cha Sheria ya Ajira kinachohusu uhusiano kazini.

Prof. Nombo amesema kuwa kupitia mkutano huo, wajumbe watapitia mpango na bajeti ya wizara pamoja na masuala ya utawala na usimamizi wa rasilimali watu pamoja na kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuboresha afya na usalama mahali pa kazi. Prof. Nombo amesisitiza kuwa mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ubora na uaminifu katika utendaji kazi,  "Dhamira ya Wizara ni kuona watumishi wanafanya kazi kwa bidii, kwa uadilifu na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuendeleza mageuzi yanayoendelea katika elimu."amesema Prof. Nombo Aidha, amewashukuru wajumbe wa Baraza hilo kwa ushirikiano wao na amewataka kuendekeza juhudi za kuimarisha mifumo ya usimamizi ndani ya Wizara.