Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Christine Grau, Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, katika Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yamefanyika jana Juni 30,2026, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kumuaga Balozi Grau anayehitimisha kipindi chake cha uwakilishi nchini Tanzania. Viongozi hao walitathmini ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya na kujadili namna ya kuuendeleza kwa manufaa ya pande zote mbili.

Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu umuhimu wa kuimarisha misingi ya utawala bora, amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa kama nguzo ya maendeleo endelevu ya Taifa. Katika muktadha huo, CCM ilisisitiza dhamira yake ya kuendelea kujenga Taifa linaloongozwa kwa misingi ya haki, uwajibikaji na utulivu wa kisiasa.

Pia, ilitambua changamoto zilizojitokeza nchini katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu uliopita na umuhimu wa hatua ambazo Serikali inaendelea kuzichukua katika kuimarisha imani ya wananchi, ikiwemo kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi, Tume ya Upelelezi wa Jinai na hatua nyingine za kisheria zinazolenga kuhakikisha ukweli, uwajibikaji na haki vinaendelea kutawala katika kulinda amani na mshikamano wa Taifa.

Aidha, ilielezwa kuwa ajenda ya kuendelea kuimarisha demokrasia nchini, ikiwemo mchakato wa Katiba Mpya ambao umeainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, inabaki kuwa sehemu muhimu ya maono ya muda mrefu ya kuimarisha utawala bora na mshikamano wa Taifa.

Viongozi hao pia walitambua nafasi ya vijana katika mustakabali wa maendeleo ya Tanzania na umuhimu wa kuhakikisha kizazi hicho kinaendelea kuwa sehemu ya safari ya Taifa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na ujenzi wa uchumi wenye ushindani na maendeleo jumuishi.

CCM inathamini ushirikiano wake na Umoja wa Ulaya na inaamini kuwa ushirikiano huo utaendelea kuimarika kwa kuzingatia misingi ya kuheshimiana, maslahi ya pamoja na dhamira ya pamoja ya kuendeleza maendeleo endelevu ya Tanzania.







 

 


HALMASHAURI za Wilaya, Miji na Jiji mkoani Tanga, zimeagizwa kuzuia vyanzo vinavyosababisha hoja zinazoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). 

Agizo hilo limetoa leo Juni 30, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt Batilda Burian, alipozungumza kwenye vikao maalum vya kujadili hoja za CAG katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri za Lushoto na Bumbuli.

Amesema, taarifa za CAG kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, inaonesha halmashauri hizo zimefanikiwa kupata hati inayoridhisha, ikiwa ni Ishara ya ufanisi, weledi na kujituma kwa watumishi na watendaji.

Amesema, hali hiyo inapaswa kuendelezwa ili kufikia malengo msingi ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa wananchi.


Hata hivyo, Mhe. Balozi Dkt Batilda amesema, pamoja na mafanikio hayo, halmashauri hizo zinatakiwa kudhibiti vitendo vinavyosababisha hoja za ukaguzi.

Awali, taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Nje, Mkoa wa Tanga, Hamu Mwakasola, ilieleza kuwa kutolewa hati inayoridhisha haimaanishi kuwepo mifumo mizuri ya udhibiti wa ndani, bali kutokuwepo dosari kubwa wakati wa ukaguzi.

“Inamaanisha hapakuwa dosari kubwa zilizobainika wakati wa ukaguzi ambazo zingemzua Mkaguzi kutoa maoni, au kumlazimu kutoa hati yenye mashaka au hati mbaya,” amesema

Naye Katibu Tawala Mkoa (RAS) wa Tanga, Rashid Mchatta, pamoja na mambo mengine, amewahimiza watumishi na umma, kuendeleza mahusiano mema ili kuongeza ufanisi na tija mahali pa kazi.

Amesema, viongozi, watendaji na watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wanapaswa kutambua ‘uzito’ wa hadhi ya Ofisi ya CAG katika ukaguzi wa hesabu uliopo katika ngazi za kimataifa.

Mchatta amesema utambuzi wa ubora huo utachangia kuboresha utendaji kazi na kupunguza kwa kiasi kikubwa hoja za ukaguzi, hali itakayoifanya CAG kutekeleza vema wajibu wake wa ushauri wa kitaalamu kwa taasisi husika.  


 


📌 Waziri Ndejembi asema mradi utaimarisha Gridi ya Taifa na kuongeza uwezo wa kusafirisha umeme

📌 Mradi unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026

📌 MD TANESCO asema Shirika limevunja rekodi kwa kuunganisha wateja zaidi ya laki nane mwaka 2025/26


Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma wenye urefu wa kilometa 345 umefikia asilimia 89 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026, hatua itakayoongeza uwezo wa kusafirisha umeme na kuimarisha uthabiti wa Gridi ya Taifa.

Akikagua maendeleo ya Mradi huo Julai 1, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amesema mradi huo ni miongoni mwa uwekezaji wa kimkakati wa Serikali unaolenga kuimarisha miundombinu ya usafirishaji wa umeme nchini na kuongeza uwezo wa Gridi ya Taifa kuhudumia mahitaji yanayoendelea kuongezeka.

Amesema njia hiyo ya kusafirisha umeme ina umuhimu mkubwa kutokana na kuwezesha usafirishaji wa umeme unaozalishwa na Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere chenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115.

Aidha, Waziri Ndejembi amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika miradi ya umeme ili kuhakikisha huduma ya umeme wa uhakika inaendelea kuwafikia Watanzania na kukidhi mahitaji ya sekta mbalimbali za uzalishaji.

“Serikali imeona mahitaji ya umeme nchini yanazidi kuongezeka, hivyo ujenzi wa njia hii ya umeme ni muhimu sana kwani utaleta uthabiti katika Gridi ya Taifa,” amesema Mhe. Ndejembi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Razalo Twange, amesema ongezeko la uwekezaji katika miundombinu ya umeme limechangia kuongezeka kwa idadi ya wateja wanaounganishiwa huduma, ambapo katika mwaka wa fedha 2025/26 Shirika limeandika historia kwa kuwaunganishia umeme zaidi ya wateja laki nane.

“Haijawahi kutokea tangu Tanzania ipate uhuru. Hii inaonesha mahitaji ya umeme yameongezeka, na hivyo sisi tunaendelea kuongeza miundombinu ya umeme,” amesisitiza Bw. Twange.

Awali, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa Mradi, Mha. Newton Mwakifamba, amesema kazi zinaendelea vizuri na zinatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026, kwa mujibu wa ratiba ya mkataba.
















Na Mwandishi Wetu- Dodoma

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Bi. Debora Charwe amesema, Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa Mpango wa Muda Mrefu wa Lishe wa Taifa (NN-LTP) ili kuongeza jitihada za sekta mtambuka katika kuboresha utekelezaji wa lishe kwa kipindi cha miaka 25 ijayo

Bi. Debora ameyasema hayo leo tarehe 30 Juni, 2026 wakati akifungua Warsha ya mafunzo kuhusu kuandaa mpango wa muda mrefu wa lishe wa Taifa (National Nutrition Long Term Plan 2026-2050) ambayo inafanyika jijini Dodoma kwa siku tatu kuanzia Juni 30 hadi Julai 02, 2026



Amesema, mafunzo hayo yanatolewa kwa Wataalam kutoka ngazi ya Wizara mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu uandaaji wa mipango ya muda mrefu wa lishe inayojumuisha sekta mtambuka pamoja na kubadilishana uzoefu kusaidia katika usanifu, muundo na taratibu za utekelezaji wa Mpango wa muda mrefu wa Lishe wa Taifa.




















Vilevile Bi. Debora amefafanua kuwa, mpango huo unaandaliwa chini ya usimamaizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) na wadau wengine wa maendeleo kwa kuzingatia haja ya kuifanya lishe kuwa moja ya kichocheo na kipimo katika kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania kufikia 2050.

Aidha, warsha hiyo imehusisha Afisa viungo wa lishe kutoka Wizara mbalimbali zikiwemo Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) pamoja na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Wizara ya Maji na Wizara ya Mambo na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Baada ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzindua Dira 2050, Julai 17, 2025 jijini Dodoma, hatimaye leo tarehe 1 Julai, 2026, Tanzania imeanza rasmi utekelezaji wa Dira hiyo.

Kuanza kwa utekelezaji wa Dira 2050 kunahitimisha safari ndefu ya utekelezaji wa DIRA 2025 na kuanza kwa safari nyingine ya robo karne (miaka 25) inayolenga kubadilisha sura ya kiuchumi, kijamii, na kiteknolojia ya taifa letu.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi M. Kida, Dira ya 2050 imejengwa juu ya misingi ya ushiriki wa moja kwa moja wa mwananchi. Kuanzia kwa mkulima wa kijijini hadi kwa mbunifu wa teknolojia mjini, kila mmoja leo anaanza kuhesabiwa kama injini ya mabadiliko haya.

"Huu ni wakati wa kuangalia jinsi kila sekta, (binafsi na ya umma) inavyoingiza vipaumbele vya Dira 2050 kwenye utendaji wake wa kila siku, kwa kuwa mafanikio ya utekelezaji wake yanategemea ushiriki wa kila mmoja wetu" amesema Dkt. Kida.

Dira hiyo, inatarajiwa kujenga Taifa jumuishi lenye ustawi, haki na linalojitagemea, Taifa litakalokuwa na uchumi imara, jumuishi na wenye Pato la thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo 2050.

Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA, Mha. Ngosi Mwihava (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Ndg. Gerald Maganga (Kulia) wakimkabidhi Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mfano wa hundi kama ishara ya kukabidhi Hazina mchango wa kisheria wa taasisi hiyo wa Sh. 10.6 bilioni, kwa mwaka wa Fedha 2025/26, kwenye hafla iliyofanyika Ikulu jana.

 

 


● Yaligunduliwa kwa mara ya kwanza duniani mwaka 1959 katika Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma.

● Yana thamani kubwa katika elimu, utafiti wa kisayansi na utalii wa jiolojia.

● Ni sehemu ya urithi wa asili wa Tanzania.


Imeelezwa kuwa kuna umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti za kuhifadhi na kulinda madini adimu aina ya Yoderite yanayopatikana katika eneo la Mlima wa Mautia, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, ili kuhakikisha urithi huo wa kipekee wa kijiolojia unabaki salama kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Hayo yalisemwa Juni 30, 2026 na Meneja wa Jiolojia kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Solomon Maswi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea eneo hilo kwa ziara maalumu.

Maswi alisema kuwa uhifadhi wa Yoderite unaweza kuiwezesha Tanzania kuwa kitovu cha kimataifa cha tafiti kuhusu madini adimu, sambamba na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea maeneo yenye urithi wa jiolojia.

Aliongeza kuwa Yoderite ni miongoni mwa madini adimu yanayoifanya Tanzania kutambulika duniani kutokana na historia yake ya kugunduliwa kwa mara ya kwanza katika Mlima wa Mautia.

Aidha, alifafanua kuwa madini hayo yana mchango mkubwa katika tafiti za kisayansi kwa kusaidia kuelewa mchakato wa uundaji wa miamba na mazingira yenye shinikizo na joto la juu ndani ya ganda la dunia. Pia yana umuhimu mkubwa katika elimu ya jiolojia, maendeleo ya utalii wa jiolojia na uhifadhi wa urithi wa asili duniani.

Maswi alibainisha kuwa, kutokana na uchache wake na kupatikana katika maeneo machache sana duniani, madini ya Yoderite hayachimbwi kwa matumizi ya viwandani wala biashara. Badala yake, yanahifadhiwa kama urithi wa kipekee wa kijiolojia unaovutia watafiti, wanafunzi, wataalamu wa sayansi na watalii kutoka ndani na nje ya nchi. Hali hiyo inaipa Tanzania fursa ya kujijengea hadhi kama kitovu cha tafiti za kimataifa na utalii wa jiolojia unaotegemea urithi wa asili.

Taasisi za utafiti wa madini na vyuo vya Madini vimeshauriwa kutumia eneo hilo kwa mafunzo endelevu ya utafiti wa madini.

Madini ya Yoderite yaligunduliwa kwa mara ya kwanza duniani mwaka 1959 katika Milima ya Mautia, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma.

Kutokana na kuendelea kwa tafiti baada ya miaka 35 watafiti wa miamba na madini walifanikiwa kugundua aina hiyo ya madini nchini Zimbambwe.

Jina la Yoderite lilipewa kwa heshima ya mwanajiolojia mashuhuri wa Marekani, Hatten Yoder Jr., kutokana na mchango wake mkubwa katika tafiti za miamba na madini.







Nilipokuwa mdogo, nilikuwa na ndoto ya kuolewa na mwanamume mwenye huruma, anayejali, anayesikiliza na kunipa heshima kama mke.

Lakini kadri nilivyokua, niliingia kwenye uhusiano ambao ulivunja kabisa ndoto zangu. Nikiwa na umri wa miaka 23, nilipenda kwa moyo wangu wote, nikajitoa kwa mwanaume ambaye nilidhani ni mpenzi wa maisha yangu.

Tulikaa naye kwa miaka miwili, lakini kwa kipindi chote hicho nilijikuta nikilia kila siku.
Alininyima mapenzi ya kweli si tu kimwili bali hata kwa maneno. 

Hakuwa akinipa muda, hakuwahi kunipa sifa wala heshima, na mara nyingi aliniongelea vibaya mbele ya watu.

Nilivumilia kwa sababu nilidhani labda siku moja atabadilika. Lakini siku zilisonga, na mateso yakawa kawaida yangu. 

Nilijiona sifai, sina thamani, na sikustahili kupendwa. Wakati mwingine nilikuwa nikilala nikiwa nimejifunika na mto ili watoto wasisikie nikilia. Nilikuwa naumia sana, hasa kwa sababu sikuwahi kumkosea. SOMA ZAIDI.
Siku hiyo nilikuwa peke yangu nyumbani. Ilikuwa siku ya Jumamosi saa mbili usiku, nilikuwa nimekamilisha kazi za siku na nikajipumzisha kwenye kochi langu la sebuleni. 

Kama ilivyo kawaida yangu, nikachukua simu yangu kupiga picha ya selfie kwa ajili ya kupakia kwenye WhatsApp status.

Nilitabasamu kidogo na kupiga picha moja tu, halafu nikaangalia matokeo yake kabla sijaiweka hadharani. 

Ndipo nikaona jambo la kushangaza ambalo lilinifanya nitetemeke ghafla. Kwenye picha hiyo, nyuma yangu, kulionekana watu watatu wakiwa wamesimama karibu na mlango wa chumba cha kulala.

Wote walionekana ni marefu na walikuwa wamevaa mavazi meusi, lakini cha kutisha zaidi ni kwamba nyuso zao zilikuwa zimefunikwa kwa kitambaa cheusi kama mazishi. 

Hakukuwa na mtu mwingine nyumbani, milango yote ya chumba na nyumba ilikuwa imefungwa, na mimi mwenyewe nilikuwa nimehakikisha hilo kabla sijapiga selfie.

Moyo wangu ulianza kwenda mbio. Nilitetemeka mikono, nikahisi baridi kali ghafla licha ya kuwa ilikuwa jioni ya joto. 

Niliinuka taratibu, nikawasha taa zote za nyumba, nikafungua mlango wa nje na kutoka nje kwa haraka. Nilikaa kwa muda mrefu nje nikiwa sijaelewa kilichokuwa kimetokea.SOMA ZAIDI.
Niliwahi kuamini kuwa ndoa yetu ilikuwa imejengwa juu ya misingi ya upendo wa kweli. Tulikutana tukiwa chuoni, tukapendana kwa dhati, na baada ya miaka miwili ya uhusiano, tuliamua kuoana. Harusi yetu ilikuwa ya kupendeza sana, tulipendeza mbele ya watu, na kila mtu alitupongeza.

Lakini ndani ya miezi sita tu baada ya harusi, maisha yangu yakabadilika ghafla. Mke wangu alianza kuwa mtu tofauti kabisa na yule niliyempenda. 

Alianza kuwa mkali, mgumu kuelewana naye, na mara kwa mara alinituhumu kwa mambo ambayo hayakuwa ya kweli.

Mara nyingi alirudi nyumbani akiwa mlevi au aliingia chumbani akiwa mnyamavu kana kwamba hakutaka hata kuzungumza nami. Ilifikia hatua hata kula pamoja ilikuwa shida. Nilihisi kuna kitu kibaya, lakini sikuweza kukieleza.

Kilichonitatiza zaidi ni ndoto ambazo nilianza kupata nilikuwa naota moto, maiti, na mara nyingine nilimuona mke wangu akiwa na wanaume wengine. 

Hali hiyo ilinizidi nguvu. Nilipojaribu kuzungumza naye kuhusu hali yetu, alikasirika na kusema sina imani naye.

Niliendelea kuvumilia kwa matumaini kuwa labda ni msimu mgumu tu wa maisha ya ndoa, lakini hali ilizidi kuwa mbaya. 

Siku moja nilipokwenda kijijini kumtembelea babu yangu, nilikutana na mzee mmoja ambaye ni jirani yao. Baada ya kuzungumza naye kwa muda, aliniuliza maswali ya kushangaza kuhusu maisha yangu ya ndoa. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu familia yetu ilikuwa ikikumbwa na misukosuko isiyoelezeka. Kila aliyekuwa anafanikiwa kwao ghafla alianza kudorora. 

Watoto walifukuzwa shule kwa sababu zisizoeleweka, biashara za kaka zangu zilikufa ghafla, na hata afya ya mama yetu ilianza kuzorota pasipo ugonjwa halisi kujulikana.

Tulisali, tulifunga, lakini hali ilizidi kuwa mbaya.
Kila mtu alikuwa anahisi hali hiyo si ya kawaida. Hata wageni waliokuja nyumbani walihisi hali ya baridi na uzito wa ajabu mara tu walipoingia mlangoni. 

Mmoja wa marafiki wa karibu wa familia yetu alituambia wazi kuwa huenda kuna mtu ametuloga au ametutendea jambo la kichawi.

Nilikuwa miongoni mwa watu ambao zamani nilikuwa siamini mambo haya lakini kilichokuwa kinaendelea kilinifanya nibadili msimamo wangu. Kwa mara ya kwanza, niliamua kutafuta msaada wa kitaalamu wa asili. SOMA ZAIDI.
Hakuna kitu kilichokuwa kinaniumiza kama mume wangu kuonyesha dalili za kutojali mara baada ya kujifungua mtoto wa pili wa kike. 

Nilihisi kama sipendwi tena, hata kama hakuwahi kusema wazi. Alianza kuchelewa kurudi nyumbani, alikosa furaha nyumbani, na kila mara alipokuwa akizungumza na marafiki zake, alitaja jinsi anavyotamani kuwa na mtoto wa kiume.

Nilijaribu kulazimisha mazungumzo naye kuhusu hali hiyo, lakini alinijibu kwa maneno ya baridi, “Watoto wote ni baraka.” 

Ndiyo, nilielewa hilo, lakini moyo wa mwanamke unajua ukweli wa mambo. Nilijikuta nikianza kuishi kwa hofu na mashaka. Nilianza kujiona duni. Nilijiuliza kama ndoa yangu ingesalia imara bila kumpatia mtoto wa kiume.

Nilianza kusaka suluhisho kila mahali kwa madaktari wa kawaida, mitandaoni, na hata kupitia marafiki wa karibu. Lakini kila nilichopewa kilikuwa ushauri wa jumla tu. Hakuna kilichokuwa na uhakika.SOMA ZAIDI.
Wizara ya Afya imewataka waandishi wa habari na wadau wa mitandao ya kijamii kuendelea kutoa taarifa sahihi, kwa wakati na kutoka katika vyanzo rasmi ili kuimarisha uelewa wa wananchi na kuimarisha utayari wa taifa dhidi ya ugonjwa wa Ebola na dharura nyingine za afya ya umma.



Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amezindua rasmi Mfuko wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika Jimbo la Mtwara Mjini (UWEZO Program) na kusema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za uwezeshaji wa wanawake.

Akizungumza katika hafla hiyo Juni 30, 2026, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila kuyawezeaha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana.

Amesema ushiriki wa makundi maalum katika shughuli za kiuchumi ni hatua ya kujivunia na kuongeza kuwa mafanikio yatapatikana kwa makundi hayo kupatiwa mafunzo stahiki.

"Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila wananchi wake kuwa na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na hii ndiyo sababu kuwndelea kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake na vijana kupata fursa za kiuchumi kupitia sera na programu mbalimbali," alisema Naibu Waziri Mahundi.


Aidha, ameeleza kuvutiwa kwake na  Programu ya UWEZO kwa kuanza kutoa mikopo na kuwajengea wanawake uwezo kupitia mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, utunzaji wa kumbukumbu za biashara na uundaji wa vikundi, akieleza kuwa msingi huo utasaidia kuhakikisha mikopo inazalisha matokeo chanya na kuongeza maendeleo ya wanawake pamoja na familia zao.

Awali akitoa maelezo kuhusu Programu ya UWEZO, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, amesema wazo la kuanzisha mfuko huo limetokana na ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ya kuwawezesha wananchi kiuchumi. 

Amesema kupitia mfuko huo wenye mtaji wa shilingi milioni 150, wanawake zaidi ya 5,000 walitambuliwa kutoka kata zote 18 za jimbo hilo, wanawake 300 walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali na wanawake 81 wamekabidhiwa mikopo katika awamu ya kwanza.

"Mikopo hiii haina riba kutokana na ushirikiano kati ya Joel Nanauka Foundation na Benki ya Ushirika (Coop Bank), sababu lengo la programu hii si kutoa fedha pekee bali kujenga wanawake wajasiriamali wenye uwezo wa kujitegemea, kuongeza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Mtwara Mjini na Taifa kwa ujumla". alisema 
Waziri Nanauka.

Nao baadhi ya wanufaika wa Mkopo huo wameipongeza Serikali na kumpongeza Waziri Nanauka kwa maono na kutekeleza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni zake ambapo kwa sasa wataweza kujiendesha kiuchumi na kupunguza makali ya ugumu wa maisha na kuingizia taifa mapato.