Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rosemary Senyamule, ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma kwa kusimamia vizuri upatikanaji wa fursa za Ununuzi wa Umma kwa makundi maalum, hususan wanawake, hatua ambayo imeendelea kuwasaidia kiuchumi na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo.
Akizungumza leo Machi 8, 2026 katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Mbande, Wilayani Kongwa Mkoa wa Dodoma, Bi. Senyamule amesema kuwa usimamizi mzuri wa PPRA umewezesha makundi ya wanawake kunufaika na zabuni mbalimbali za serikali kupitia mfumo wa kielektroniki wa Usimamizi wa Ununuzi -NeST.
Amesema kuwa hadi sasa vikundi vya wanawake vimefanikiwa kupata zabuni za serikali zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 16, hatua inayodhihirisha kuwa sera ya kutoa kipaumbele kwa makundi maalum inaleta matokeo chanya katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa zaidi ya vikundi 500 vya wanawake vimesajiliwa kwenye mfumo wa NeST, jambo linaloonesha mwitikio wa wanawake katika kutumia fursa za ununuzi wa umma zinazotolewa na Serikali.
Aidha, Bi. Senyamule amewataka wanawake wote nchini kuendelea kuunda vikundi vingi zaidi ili waweze kunufaika na fursa hizo za zabuni za serikali, akisisitiza kuwa serikali imeweka mazingira rafiki yanayowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa nchi.
“Ni muhimu wanawake mkajiunga katika vikundi na kujisajili katika mfumo wa NeST ili mpate nafasi ya kushiriki katika zabuni za serikali.
Fursa hizi zipo kwa ajili yenu na zinaweza kuwasaidia kukuza biashara na kuinua kipato chenu,” amesema.
Ameongeza kuwa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana katika kuwawezesha wanawake na kuhamasisha juhudi zaidi za kuhakikisha wanawake wanapata nafasi sawa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Msimizi wa Kituo cha Msaada wa Kitaalam kwa Wateja wa NeST - PPRA ( NeST Customer Technical Support Center) Bi. Asifiwe Makweta amesema Mamlaka ina shauku kuona vikundi vya kina Mama vonaongezeka siku hadi siku ili kuhakikisha fursa hizi za serikali zinawafikia walengwa kiyakinifu kwa makundi yote ikiwemo Wanawake ili kuleta uhai wa ushiriki wa makundi maalum bila kubaki nyuma kwa kundi lolote.
"Pamoja na kufikia idadi ya kusajili makundi 500 ya Wanawake kwenye mfumo wa NeST bado haijafikia idadi ya makundi tunayotamani kusajili kwenye Mfumo wa NeST ili kushiriki katika fursa hii ya asilimia 30 ya zabuni kwa makundi hayo ambayo ni Vijana, wanawake, Wazee na watu wenye ulemavu"amesema Bi. Makweta.

Bi.Kaswaga amebainisha kuwa kabla ya kutoa msaada huo, walitembelea baadhi ya vituo vya watoto yatima ili kubaini mahitaji yaliyopo na kuamua kuchagua vituo vyenye uhitaji mkubwa zaidi.
Kwa upande wake, Katibu wa Kituo cha Rahman, Abdallah Said, amewapongeza na kuwashukuru wanawake kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa kutoa msaada huo kwa ajili ya kusaidia watoto wenye uhitaji, akibainisha kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka hasa katika kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. 








































Na Mwandishi Wetu