Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Bi. Khadija Ngasongwa,akizungumza na wadau wakati wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.

DURBAN - AFRIKA KUSINI

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amezishauri nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuwekeza zaidi katika maendeleo ya viwanda na miundombinu ili kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji.

Bi. Ngasongwa ametoa wito huo jijini Durban, Afrika Kusini, wakati akishiriki Mkutano wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC unaoendelea nchini humo.

"Ushiriki wa FCC katika wiki hii unalenga kuhakikisha sera na miongozo ya ushindani wa haki inazingatiwa katika maendeleo ya viwanda. Tunataka kuona viwanda vya ukanda wetu vinakuwa na ushindani, vinatoa fursa kwa wanawake na vijana, na vinatoa bidhaa zenye ubora kwa walaji," alisema Bi. Ngasongwa.

Ameongeza kuwa uwekezaji katika viwanda vya kuongeza thamani ya malighafi utasaidia kuwainua kiuchumi wanawake na vijana, kupanua masoko ya bidhaa za nchi za SADC na kuongeza mapato ya fedha za kigeni.

Akizungumzia ushiriki wa Tanzania, Bi. Ngasongwa amesema mkutano huo unaendana na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania hususan katika sekta za madini, kilimo, bidhaa za afya, miundombinu na ubunifu.

"Ushiriki wa Tanzania una umuhimu mkubwa kwa sababu unajikita katika kuimarisha mnyororo wa thamani. Ni maeneo muhimu katika safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa viwanda na kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," alisema.

Bi. Ngasongwa pia amewataka wadau wa fedha waliopo katika mkutano huo ikiwemo TIB, Exim Bank, BADEA na Nedbank kushirikiana katika kuhamasisha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya miradi ya maendeleo na uwekezaji nchini.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa na madini ya kimkakati na rasilimali nyingine. Hivyo ni muhimu kuyachakata ndani ya nchi badala ya kuuza malighafi ili kuongeza thamani, kuzalisha ajira na kuchochea ukuaji wa viwanda.

Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC ulifunguliwa rasmi Julai 27, 2026 na ulihitimishwa Julai 31, 2026 na umetoka na maazimio ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika biashara, uwekezaji na maendeleo ya viwanda kama sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa 46 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2026 Jijini Durban, Afrika Kusini.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Bi. Khadija Ngasongwa, akizungumza na wadau wakati wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki kutoka Tanzania wakati wa Mkutano wa 9 wa Wiki ya Viwanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Industrialisation Week), unaofanyika jijini Durban, Afrika Kusini.

 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma, Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na FCC kwa baadhi ya wadau waliotembelea Banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.

 

Kushuhudia mtoto wako wa pekee akiteseka bila kupata msaada ni jambo linaloweza kumvunja moyo mzazi yeyote. Kwa zaidi ya miaka miwili, binti yetu mwenye umri wa miaka kumi na mbili alipatwa na hali ya kutatanisha sana.

Alianza kulalamika maumivu makali ya kichwa na tumbo kila ilipofika jioni, na mwili wake ulipoteza nguvu kabisa hadi kushindwa kutembea au kwenda shuleni. Usiku uliingia akiwa anapiga makelele ya kutisha, akidai kuona watu waliovaa nguo nyeusi wakimnyonya damu na kumtishia maisha.

​Nilimtembeza kwenye hospitali kubwa na za kifahari nchini. Madaktari walifanya vipimo vya kila aina kuanzia vipimo vya damu, MRI, hadi Scan za kichwa lakini majibu yote yalikuja kuwa yuko salama na hana ugonjwa wowote wa kibinadamu!

Pamoja na majibu hayo, mtoto alizidi kukonda na kudhoofika siku hadi siku. Tilitumia akiba yetu yote kununua dawa za kutuliza maumivu ambazo hazikusaidia kitu.

Nilibaki nikilia usiku na mchana, nikitazama binti yangu akipotea mikononi mwangu huku tukiamini alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa nadra usio na tiba. SOMA ZAIDI.

 

Nyumba yenye furaha na amani inaweza kubadilika ghafla na kuwa uwanja wa dhiki na mateso pindi janga la uraibu linapoingia. Kwa zaidi ya miaka mitatu, mume wangu alitumbukia kabisa kwenye mtego wa michezo ya bahati nasibu (gambling).

Kila mwezi alipopokea mshahara wake, badala ya kuleta nyumbani kwa ajili ya chakula, kodi ya nyumba, na ada za watoto, alielekeza pesa zote kwenye kubashiri matokeo ya mpira na kucheza michezo ya mtandaoni kwa matumaini ya kupata faida ya haraka.

​Matokeo yake yalikuwa ni maafa makubwa kwa familia yetu. Aliuza vifaa vya nyumbani kimyakimya, alikopa fedha kwa majirani na taasisi za mikopo, na kila mara alirudi nyumbani akiwa na hasira, dharau, na migogoro mikubwa baada ya kupoteza kila senti.

Watoto wetu walifukuzwa shule mara kwa mara kwa kukosa ada, na madeni yalitukabili kila kona. Nilibaki nikilia usiku kucha nikiwa na hofu kwamba tungeshia mtaani bila makazi wala chakula, huku mume wangu akionekana kupoteza kabisa akili ya uongozi wa familia. SOMA ZAIDI.

 

Kusafiri kwenda nje ya nchi kwa ajili ya masomo au kazi ndoto ambayo kila kijana anayepambana anatamani kuitimiza. 

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikuwa nikihangaika usiku na mchana kupata fursa ya kwenda kufanya kazi Ulaya baada ya kupata mwaliko rasmi kutoka kwa kampuni moja kubwa.

Kila kitu kilikuwa kikienda vizuri upande wa waajiri wangu, lakini ajabu ni kwamba kila nilipofika kwenye hatua za mwisho za kukamilisha pasipoti na mchakato wa Visa, vikwazo visivyoeleweka vilianza kujitokeza.

​Nyaraka zangu zilikuwa zikipotea kimyakimya maofisini, majina yangu yalikosewa mara kwa mara kwenye mifumo, au maombi yangu yalikataliwa bila sababu za msingi. Nilibaki nikishangaa na kuumia moyoni huku nikishuhudia fursa zangu za dhahabu zikiyeyuka.

Kumbe bila mimi kujua, baadhi ya ndugu zangu wa karibu waliokuwa wakionyesha kunifurahia kwa nje, ndio waliokuwa mstari wa mbele kufanya fitina chini kwa chini ili nisifanikiwe kutoka kimaisha! SOMA ZAIDI.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Mark Kihulla amewatembelea na kuzungumza na watumishi wa Wakala huo Mkoa wa Arusha tarehe 31 Julai 2026.

Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa kusikiliza changamoto za watumishi, kuwapongeza kwa utendaji wao, na kuwapa mwelekeo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wakala.

Akizungumza na watumishi hao, Afisa Mtendaji Mkuu aliipongeza Ofisi ya Mkoa kwa kazi nzuri ya uhakiki wa vipimo wanayoendelea kufanya.

Alisema mafanikio ya WMA yanategemea uadilifu, umahiri na nidhamu ya kila mtumishi.

Aidha, aliwataka watumishi kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi na kuzingatia maadili ya kazi. “Tuwe mabalozi wazuri wa WMA. Kila mteja tunayemhudumia ni fursa ya kujenga taswira nzuri ya Wakala,” alisisitiza.

Kwa upande wao, watumishi wa Mkoa wa Arusha walimshukuru Mtendaji Mkuu kwa uongozi wake wenye 'kuonesha njia' na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Katika ziara hiyo ya Afisa Mtendaji Mkuu, watumishi walipata nafasi ya kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali ya kuboresha utoaji huduma ya vipimo katika Mkoa huo.


 

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi, akizungumza wakati wa semina maalum ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.


*Mmoja atoa ushuhuda wa ‘Tunalipa Jana’


*Bunge: tunawashukuru PSSSF kwa elimu


Morogoro, Julai 31, 2026


Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.

Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.

“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Bi. Angelina Sanga.

Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.

Katika semina hiyo Mtumishi Mstaafu wa Bunge Bw. Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.


Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Bw. Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine

“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Bw. Hajji Moshi.

Kwa upande wake, Bw. Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.

Mtumishi kutoka Ofisi ya Bunge, Bi. Angelina Sanga (kushoto), akiwa na Afisa Matekelezo kutoka PSSSF, Bi. Upendo Chilewa, wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bi. Sanga alipokuwa akijisajili kaaika huduma ya mifumo ya kidijitali.

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi (kushoto), akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto (kulia), mara baada ya kuhitimishwa kwa semina ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto, akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa ajili ya Makatibu wa Kamati za Bunge mjini Morogoro.

Mtumishi Mstaafu wa Bunge, Bw. Gerald Magili, akitoa ushuhuda wake wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bw. Magili aliipongeza PSSSF kwa kulipa mafao yake kwa wakati
Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kwa umakini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajj Moshi (kulia), wakati wa semina ya kujenga uelewa wa Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Denis Londo, amesema ubora wa bidhaa ni nguzo muhimu katika kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kwenye soko la kimataifa na kufanikisha azma ya nchi ya kujenga uchumi wenye thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050.
Kariakoo, 31 Julai, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeendelea kuimarisha ushirikiano na walipakodi kupitia mikutano ya ana kwa ana (Outreach) inayolenga kusikiliza, kutatua changamoto na kutoa elimu ya kodi ili kuwawezesha walipakodi kutekeleza wajibu wao kwa hiari.
Kuingia kwenye ndoa ni matumaini ya kila mwanamke kwamba atapata mume atakayempenda, kumheshimu, na kuilinda familia yao. Hata hivyo, mara tu baada ya harusi yetu, ndoa yangu iligeuka kuwa uwanja wa maumivu na dharau kubwa.

Mume wangu alibadilika ghafla na kuanza kuendesha nyumba yetu kwa maelekezo ya mama yake mzazi pekee. Kila uamuzi uliotakiwa kufanywa kuanzia matumizi ya fedha, chakula kinachopikwa, hadi malezi ya watoto ulipaswa kupitishwa na mama mkwe wangu kwanza.

​Kila nilipojaribu kutoa maoni yangu au kushauri kama mke wa ndani, mume wangu alinisukuma pembeni, kunitusi, na kuniambia kuwa mimi ni mgeni tu aliyetoka mbali ambaye sina haki ya kupinga kauli ya mama yake.

Mama mkwe alitumia fursa hiyo kunidharau waziwazi na kunifanyia vitimbi vya kila aina ili nionekane sifai. Nilibaki nikiwa sina sauti wala thamani kwenye nyumba yangu mwenyewe, nikilia usiku kucha kwa uchungu wa kuonekana kama mjakazi na sio mke halali.SOMA ZAIDI.

 

Kwa zaidi ya miaka minne, nilikuwa nikimiliki duka kubwa la vifaa vya ujenzi na bidhaa za nyumbani katika mji wetu. Biashara hii ilikuwa ndiyo tegemeo langu kuu na chanzo cha rizki kwa familia na wafanyikazi wangu sita.

Niliwekeza mamilioni ya fedha na mtaji wangu wote ili kuhakikisha duka langu linakuwa na kila aina ya bidhaa zenye ubora wa hali ya juu. Hata hivyo, kuanzia katikati ya mwaka jana, mambo yalianza kubadilika ghafla kwa njia ya kutatanisha sana.

​Duka langu lilikuwa katikati ya mji ambapo watu wengi wanapita, lakini ajabu ni kwamba wateja walikuwa wakipita mlangoni na kuingia kwenye maduka ya jirani yaliyokuwa na bidhaa chache kuliko zangu.

Siku zilipita bila kuuza hata bidhaa moja ya maana. Akiba yangu ya benki ilisha kabisa, madeni ya wauzaji wa jumla yalianza kunilundikia, na wafanyikazi wangu walishindwa kupata mshahara kwa miezi mitatu mfululizo.

Nilibaki nikiketi dukani kuanzia asubuhi hadi jioni nikiwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikitazama biashara yangu ya mamilioni ikiporomoka kuelekea kufilisika kabisa. SOMA ZAIDI.

 

Jina langu ni Baraka. Kuna siku moja katika maisha yangu ambayo sitaisahau kamwe.

Ilikuwa siku ambayo kosa dogo la kutuma pesa lilibadilisha maisha ya familia yangu.

Mama yangu alikuwa amelazwa hospitalini katika hali mbaya sana. Madaktari walihitaji malipo ya haraka ili kuendelea na matibabu yake.

Nyumbani kulikuwa na hofu kubwa. Kila mtu alikuwa akipiga simu kutafuta msaada. Ndugu walichangia walichoweza.

Baada ya kuhangaika kwa muda, hatimaye nilifanikiwa kupata TSh 1,850,000. Kwangu mimi, hiyo haikuwa pesa tu.

Ilikuwa matumaini. Ilikuwa nafasi ya kumuokoa mama yangu. SOMA ZAIDI.

Takribani wakulima wadogo 1,000 kutoka mikoa ya Morogoro, Dodoma na Arusha wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kuondokana na matumizi ya viuatilifu hatarishi katika shughuli zao za kulimo. Idadi hiyo ya wakulima itawagusa moja kwa moja wakulima wa mbogamboga, vitunguu, mbogamboga na pamba waliopo kwenye wilaya za Karatu, Chamwino, Mvomero na Meru. Hatua hiyo inayolenga kuwahamasisha wakulima kuachana na matumizi ya viuatilifu hatarishi ili kupunguza madhara ya kiafya yanayosababishwa na kemikali hizo kuanzia kwa mkulima mpaka kwa mlaji.

Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa Asasi Isiyo ya Kiserikali ya AGENDA For Environment and Responsible Development, Dorah Swai, mkoani Morogoro wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa kilimo bora na mazingira kutoka katika taasisi za serikali na binafsi. Bi. Swai amesema kuwa mradi huo uliofadhiliwa na mfuko wa Global Frame Work (GFC) unahusisha nchi tatu za ukanda wa Mahariki mwa Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya na Ethiopia na kila nchi imejiwekea malengo ya kufikia angalau wakulima 1000. Amesema dhamira kuu ya mradi huo wa kuondoa viuatilifu hatarishi ukanda wa Mashariki mwa Afrika una lengo la kuangalia namna bora ya kuwawezesha wakulima wadogo 3,000 watakaokuwa vinara wa mabadiliko katika matumizi ya viuatilifu mbadala kwa wenzao.

Katika warsha hiyo, Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Joseph Kiwango, amesema serikali iko tayari kushiriukiana na wadau wote wenye nia ya kuwainua Watanzania kupitia sekta ya kilimo kinachozingatia utunzaji wa mazingira na afya za binadamu. Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya Mwavuli wa Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Bakari Mongo, pamoja na Afisa Programu Mkuu wa Agenda, Silvani Mng’anya, kila mmoja kwa nyakati tofauti amesema suala la kupambana na viuatilifu hatarishi halipaswa kuwa la mtu mmoja au kikundi Fulani, kwani madhara ya viuatilifu hatarishi hayaishii kwa mtu mmoja. “Jukumu la kuondoa viuatilifu hatarishi halipaswa kuwa la mtu mmoja, ni jukumu letu sote katika kuhakikisha mlaji wa mwisho analindwa dhidi ya madhara yatokanayo na viuatilifu hatarishi.”amesema Mongo.

 

 

Na. Mtemi Sona

Dodoma. Mwenyekiti wa Ujenzi Sports Club, Arch. Ibrahim Chatila, amesema uongozi mpya umejipanga kuijenga timu hiyo kuwa ya kisasa, imara na yenye ushindani mkubwa katika mashindano yote itakayoshiriki.

Akizungumza kuhusu mikakati ya kuiboresha klabu hiyo iliyo chini ya Wizara ya Ujenzi, Chatila amesema lengo kuu ni kuunda kikosi chenye ubora wa hali ya juu kitakachokuwa na uwezo wa kushindana na timu mbalimbali nchini.

Amesema hatua za awali zitahusisha usajili wa wachezaji bora pamoja na kuimarisha benchi la ufundi kwa kuwashirikisha makocha wenye uwezo na sifa zinazohitajika ili kuongeza ushindani wa timu.

"Tunataka kuunda timu yenye wachezaji watakaoweza kuleta ushindi na ambao watazingatia weledi, nidhamu na taaluma katika kila mashindano tutakayoshiriki," amesema Chatila.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa uongozi mpya uliochaguliwa umeazimia kuijenga upya Ujenzi Sports Club kwa misingi ya umoja, utawala bora na uwajibikaji kuanzia kwa viongozi, benchi la ufundi, wachezaji hadi wanachama.

Kwa mujibu wa Chatila, mafanikio ya timu hayatategemea ubora wa kikosi pekee, bali pia uimara wa mifumo ya uendeshaji wa klabu.

Mbali na masuala ya kiufundi, amesema uongozi wake umeweka mkazo katika kuimarisha uchumi wa klabu kwa kutafuta wadhamini na wadau mbalimbali watakaosaidia kuiendesha timu kwa kiwango cha kisasa.

"Lengo letu ni kuwa na klabu inayojitegemea kiuchumi, yenye uwezo wa kujiendesha na kushiriki mashindano kwa ushindani mkubwa," amesema.

Arch. Ibrahim Chatila ni Mbunifu Majengo kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ambayo ni moja ya taasisi zinazounda Ujenzi Sports Club. Pia ni kocha mwenye leseni ya CAF na amewahi kuwa mjumbe wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Singida kwa kipindi cha miaka minne.

Yeye ni miongoni mwa viongozi wapya waliochaguliwa hivi karibuni kuiongoza Ujenzi Sports Club, klabu inayoundwa na taasisi 10 zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi.

Klabu hiyo hushiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, netiboli, riadha, kuvuta kamba na michezo mingine ya ushindani.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Takribani watoto 10,000 nchini wanahusishwa na shughuli za uchimbaji mdogo wa dhahabu zinazotumia zebaki  hali inayowaweka katika hatari  ya kupata madhara ya kiafya kutokana na sumu ya kemikali hiyo. Mbali na watoto, wanawake  kati ya asilimia 20 hadi 30  katika sekta ya uchimbaji mdogo wa madini pia wanakabiliwa na athari kubwa za kiafya zinazotokana na matumizi ya zebaki, ikiwemo madhara ya mfumo wa fahamu na afya ya uzazi. Hali hiyo imechochea wadau wa mazingira kutaka biashara ya zebaki duniani ikomeshwe na matumizi yake katika uchimbaji mdogo kusitishwa ifikapo mwaka 2032. Akizungumza leo Julai 30, 2026 jijini Dodoma katika Warsha ya Mradi wa Marekebisho ya Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki unaotekelezwa na AGENDA kwa kushirikiana na IPEN,Afisa Programu wa AGENDA, Angel Shaniva amesema mbali na kuhusisha watoto, sekta ya uchimbaji mdogo wa dhahabu (ASGM) inakadiriwa kuajiri moja kwa moja zaidi ya watu milioni 1.2 huku zaidi ya watu milioni 7.2 wakitegemea shughuli zake kwa njia zisizo za moja kwa moja. Shaniva amesema jamii inapaswa kuachana na matumizi ya zebaki (mercury) ili kuwalinda wanawake na watoto dhidi ya athari za kiafya na kimazingira.  Amesema mradi huo unalenga kuongeza uelewa na kujenga ushirikiano kati ya wadau wote ili kuharakisha utekelezaji wa Mkataba wa Minamata na kuunga mkono marekebisho yanayolenga kukomesha biashara ya zebaki duniani pamoja na kuweka tarehe rasmi ya kusitisha matumizi yake katika uchimbaji mdogo wa dhahabu. Amesema AGENDA imekuwa ikifanya kazi katika maeneo ya mazingira, mabadiliko ya tabianchi, elimu na jinsia, ambapo kupitia zaidi ya miradi 140 iliyotekelezwa imeendelea kukuza ushirikiano na kuongeza uelewa kuhusu masuala ya maendeleo endelevu. Kwa upande wake Afisa Program wa AGENDA, Clara Benjamin, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi 153 wanachama wa Mkataba wa Minamata unaolenga kulinda afya ya binadamu na mazingira dhidi ya madhara ya zebaki, lakini bado biashara ya kemikali hiyo inaendelea huku kukiwa hakuna tarehe rasmi ya kusitisha matumizi yake katika uchimbaji mdogo wa dhahabu. Amesema takwimu zinaonyesha biashara ya zebaki duniani imeongezeka kutoka tani 1,200 mwaka 2017 hadi tani 1,700 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 40, huku sekta ya uchimbaji mdogo wa dhahabu ikiendelea kutumia zaidi ya tani 2,000 za zebaki kila mwaka bila dalili za kupungua. Kwa mujibu wake, maeneo yenye matumizi makubwa ya zebaki nchini ni Geita, Shinyanga, Mbeya na Mara ambako kemikali hiyo hutumika kutenganisha dhahabu, lakini matumizi hayo yameendelea kusababisha uchafuzi wa ardhi, mito na samaki pamoja na madhara makubwa ya kiafya ikiwemo uharibifu wa mfumo wa fahamu na kuhatarisha usalama wa chakula. Amesema matumizi ya zebaki pia yanahusishwa na biashara haramu ya dhahabu, kuikosesha Serikali mapato na kudhoofisha usimamizi wa sekta ya madini. Amesema marekebisho yanayopendekezwa katika Mkataba wa Minamata yanataka biashara ya kimataifa ya zebaki ipigwe marufuku isipokuwa kwa matumizi yanayokubalika kimazingira pamoja na kuweka mwaka 2032 kuwa mwisho wa matumizi ya zebaki katika uchimbaji mdogo wa dhahabu. Kwa upande wake, Afisa Mazingira Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Ahmad Hassan Mbwana, amesema Serikali kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na wadau wengine imeendelea kutekeleza miradi ya kupunguza matumizi yasiyo salama ya zebaki kupitia utoaji wa elimu katika mikoa saba ikiwemo Mwanza na Geita. Amesema wachimbaji wadogo wameendelea kuelimishwa kuhusu madhara ya zebaki, matumizi ya teknolojia salama na umuhimu wa kufanya tathmini za athari kwa mazingira kabla na wakati wa shughuli za uchimbaji. Mbwana amesema elimu hiyo imechangia kuongeza uelewa kuhusu uhifadhi wa mazingira na pia kuongeza tija ya uzalishaji kwa wachimbaji wanaotumia teknolojia salama, huku uratibu wa wadau na mapitio ya sheria mbalimbali ukiendelea kuboreshwa. Hata hivyo amesema bado ipo changamoto ya baadhi ya wachimbaji kutokuwa na anuani rasmi za maeneo yao ya kazi, hali inayofanya kuwa vigumu kuwafikia kwa ajili ya ukaguzi wa usalama, utoaji wa elimu na ufuatiliaji wa matumizi ya kemikali hatarishi. Naye Mkaguzi wa Usalama Mahali pa Kazi (OSHA), Thadei Mwasamila, amesema ni muhimu kuimarisha ukaguzi wa mara kwa mara katika migodi midogo, kubaini vihatarishi na kuhakikisha wachimbaji pamoja na waajiri wanazingatia viwango vya afya na usalama kazini. Amesema OSHA itaendelea kusisitiza matumizi sahihi ya vifaa vya kinga binafsi, uhifadhi salama wa kemikali na usimamizi wa taka zenye zebaki ili kupunguza madhara ya muda mrefu kwa wachimbaji na jamii zinazozunguka maeneo ya migodi. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NESODO, Alfred Lugela, amesema kupanda kwa bei ya dhahabu duniani kumeongeza matumizi ya zebaki katika uchimbaji mdogo, huku akieleza kuwa udhibiti wa biashara ya kemikali hiyo unaweza kuhamasisha matumizi ya teknolojia mbadala zilizo salama. Kutokana na hayo Mhandisi wa Migodi kutoka Wizara ya Madini, Yusuf Yusufu, amesema usimamizi madhubuti wa shughuli za uchimbaji mdogo pamoja na matumizi ya teknolojia mbadala kama gravity concentration na borax ni muhimu katika kulinda afya za wananchi, mazingira na kuongeza tija katika sekta ya madini. Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Tawfiq Halfan, amesema mafanikio ya kupunguza matumizi ya zebaki yatategemea ushirikiano wa Serikali, wadau wa mazingira, wachimbaji na jamii kwa ujumla ili kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika bila kuhatarisha afya za wananchi na mazingira. Kwa mujibu wa wadau hao, kuungwa mkono kwa marekebisho ya Mkataba wa Minamata kutaiwezesha Tanzania kupunguza matumizi ya zebaki, kuimarisha usimamizi wa sekta ya madini na kulinda afya za wachimbaji, wanawake, watoto na vizazi vijavyo.
            
 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza Julai 31, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua Kikao cha Kamati Elekezi ya Programu ya Pili ya Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi (ESPJ II)

Na.Mwandishi Wetu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema Programu ya Pili ya Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi (ESPJ II) ni hatua ya kimkakati inayolenga kuongeza ajira zenye tija na kuimarisha ustawi wa jamii.

Akizungumza Julai 31, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua Kikao cha Kamati Elekezi ya Programu hiyo, Prof. Nombo amesema kuwa programu hiyo inalenga kuzalisha rasilimali watu wenye umahiri wa kisasa kwa sekta za viwanda, teknolojia, ubunifu na sekta binafsi, ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Prof. Nombo amebainisha kuwa Programu imeandaliwa katika misingi ya Mkakati wa Pili wa Taifa wa Kuendeleza Ujuzi, Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023, pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa matokeo makuu yanayotarajiwa ni kuongeza fursa za mafunzo kwa vijana wasio na ajira na wanaotoka katika mazingira magumu, kuimarisha mfumo wa kusimamia Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (TVET), na kushirikisha sekta binafsi katika kuboresha ubora wa mafunzo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Programu ya Pili ya Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi, Dkt. Erick Mgaya, amesema utekelezaji wa Programu hiyo ni wa miaka sita wenye thamani ya Shilingi bilioni 780 sawa na Dola za Kimarekani milioni 300 unatarajiwa kunufaisha zaidi ya Watanzania milioni moja.

Amefafanua kuwa programu hii inatekelezwa na Taasisi 19 pamoja na wizara mbalimbali ikiwemo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Afya, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, pamoja na taasisi za mafunzo zikishirikiana na Sekta binafsi.