Nilibaki nikijiuliza ni kwa nini wenzangu niliosoma nao au kuanza nao maisha walikuwa wakifanikiwa kwa urahisi, wakati mimi kila mlango niliotamani kuufungua ulikuwa ukijifunga kwa kishindo.
Nilianza kujiona kama mtu aliyelaaniwa. Nilibadili kazi zaidi ya mara tano na kujaribu Biashara tofauti tofauti kuanzia kilimo, uuzaji wa nguo, hadi usafirishaji lakini zote ziliishia kwenye madeni na msongo mkubwa wa mawazo.
Nilihisi kabisa kuwa kuna kitu kikubwa kilichokuwa kimefichika kuhusu maisha yangu ambacho nilikuwa sikijui, lakini sikuwahi kupata mtu wa kunifungua macho na kunionyesha njia sahihi ya kufuata ili nitoke kwenye giza hilo la umaskini na mahangaiko. SOMA ZAIDI.
Kila siku ilikuwa ni vita ya kupata mlo mmoja tu wa jioni, huku madeni yakiniandama kutoka kila pembe. Nilibaki nikikopa hapa ili kulipa kule, lakini badala ya afadhali, mzunguko wa umaskini na madeni ulizidi kunisonga na kuninyima kabisa usingizi wa usiku.
Kazi zozote nilizojaribu kufanya au biashara ndogo ndogo nilizozianzisha ziliishia kupata hasara na kufilisika ndani ya muda mfupi sana.
Nilibaki nikitazama watoto wangu wakikosa ada za shule na mahitaji ya msingi, huku majirani na ndugu wengine wakianza kunitenga na kunidharau kama mtu asiyekuwa na msaada wowote.
Hakuna maumivu makubwa kama kuona familia yako ikiteseka huku ukiwa huna uwezo wa kubadilisha hali hiyo, ukijua wazi kuwa unatia juhudi zote lakini matokeo yanakuwa ni sifuri. SOMA ZAIDI.
Kila mwezi ulipopita bila kuona dalili za ujauzito, ndivyo matumaini yangu na mume wangu yalivyozidi kufifia. Tulitembea kwenye hospitali mbalimbali na kuonana na madaktari bingwa wa uzazi.
Nilitumia dawa za kila aina za kuweka homoni sawa na kusafisha kizazi, huku mume wangu naye akifanyiwa vipimo vilivyoonyesha hana tatizo lolote. Pamoja na vipimo vyote kuonyesha tuko salama, mimba haikutokea.
Nilianza kuona mabadiliko kutoka kwa ndugu wa mume wangu maneno ya chini chini, kebehi, na dharau zilianza kuelekezwa kwangu wakidai mimi ni “tumbo lisilobeba.”
Nilibaki nikilia usiku kucha, nikijifungia ndani kwa aibu na msongo mkubwa wa mawazo, nikihofia ndoa yangu ingevunjika muda wowote. SOMA ZAIDI.
Na John Walter -Babati
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Hamidu Aweso, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Maji wa Vijiji vya Endamagay na Gidaboshka, uliopo katika Jimbo la Babati Vijijini. Mradi huo wenye thamani ya Shilingi bilioni 1.099 unalenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi 3,766 wa vijiji hivyo na maeneo ya jirani.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Mhe. Aweso alisema Serikali inaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maji ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.
Alibainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 30, 2026, huku utekelezaji wake ukiwa umefikia asilimia 87.
Katika ziara hiyo, Waziri Aweso aliambatana na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Baran Sillo.
Kufuatia hatua iliyofikiwa na mradi huo, Mhe. Aweso alitoa maelekezo kwa Wizara ya Maji kuhakikisha ndani ya kipindi kifupi inapatikana Shilingi 508,300,000 kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizosalia, ili mradi ukamilike kwa wakati na wananchi waanze kunufaika na huduma ya maji safi na salama kama ilivyopangwa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, amefurahishwa na uelewa mkubwa ulioonyeshwa na wanafunzi waliopata elimu ya vipimo katika banda la Wakala wa Vipimo - (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane.
Akizungumza leo Agosti 6, 2026 baada ya kuzungumza na wanafunzi hao aliowakuta katika Banda la WMA, Viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, Dodoma, Naibu Waziri ambaye pia alikuwa katika ziara ya kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho, alisema ni hatua nzuri kwa WMA kuanza kuwafundisha watoto umuhimu wa vipimo sahihi wakiwa wadogo.
“Nimefurahishwa sana. Watoto hawa wameelewa kuwa kipimo sahihi ni haki ya kila mtu. Hawa ndio Maafisa Vipimo wa kesho,” alisema.
Awali, Naibu Waziri Chande alipowakuta wanafunzi hao bandani aliwauliza maswali mbalimbali kuhusu vipimo na waliweza kujibu kwa ufasaha.
Wanafunzi hao wa Shule ya Msingi Blessed Mabuba iliyopo jijini Dodoma, ambao waliongozana na mwalimu wao Irene Ketta, ambaye pia alipongeza WMA kwa kujielekeza katika utoaji elimu ya vipimo mashuleni hatua ambayo alisema imewawesha wanafunzi kueleza tofauti ya kipimo sahihi na kisicho sahihi, umuhimu wa kusoma lebo na jinsi ya kutumia mizani.
“Niwape pongezi WMA. Kama tutaendelea kuwapa elimu hii watoto wetu, tunajenga Taifa la wafanyabiashara waaminifu na walaji wenye ufahamu. Huu ndio msingi wa uchumi imara,” alisema Mwalimu Ketta.
WMA imeahidi kuhakikisha elimu ya vipimo inaenea kwa jamii nzima kupitia utoaji elimu kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameupongeza Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kwa maboresho makubwa ya utoaji wa huduma, hususan matumizi ya teknolojia yanayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Dkt. Msonde amesema hayo leo, Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la TEMESA katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.
Dkt.Msonde Amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofikiwa na TEMESA, akieleza kuwa uimarishaji wa huduma za kidijitali pamoja na ongezeko la ubora wa mafundi umeongeza ufanisi wa wakala huo.
“Kilichonifurahisha zaidi ni uimarishaji wa mafundi. Sasa wanafanya kazi kwa weledi mkubwa na wanatengeneza magari kwa ubora. Kwa kweli TEMESA mmenifurahisha sana,hongereni sana” amesema Dkt. Msonde.
Aidha, amesema Serikali na wananchi wanaiamini TEMESA kutokana na mchango wake katika kulinda usalama wa magari ya Serikali na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za umma. Amewataka viongozi na watumishi wa wakala huo kuendelea kubuni na kuboresha huduma kwa kutumia teknolojia.
Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma- TEMESA, Bi. Martha Joachim, amesema miongoni mwa maboresho yaliyofanywa ni kuhuisha huduma ya ukodishaji wa mitambo kupitia Mfumo wa TIMIS, ambapo wateja sasa wanaweza kuwasilisha maombi ya ukodishaji kwa njia ya kidijitali, hatua iliyopunguza urasimu na muda wa kupata huduma.
Maonesho hayo yenye kauli mbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050”, yanatarajiwa kuadhimishwa tarehe 8 Agosti, 2026.
Na.Mwandishi Wetu.
Serikali imewataka wawekezaji binafsi na taasisi mbalimbali nchini kutumia fursa zinazotolewa kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuwekeza katika ujenzi wa nyumba, majengo ya umma na makazi ya kisasa kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa makazi bora na kuharakisha maendeleo ya miundombinu nchini.
Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, baada ya kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, jijini Dodoma.Amesema Serikali imefanya maboresho ya sheria na kanuni zinazoiongoza TBA ili kuipa mamlaka mapana ya kushirikiana na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hatua itakayowezesha taasisi hiyo kuvutia mitaji na kuongeza kasi ya utoaji wa huduma.
Dkt. Msonde amesema tangu kuanzishwa kwake, TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi jukumu la kujenga na kusimamia majengo ya Serikali kwa viwango vya juu vya ubora, huku ikichangia kupunguza gharama za ujenzi na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya umma. Alisema majengo mengi ya Serikali yaliyopo nchini ni ushahidi wa uwezo na weledi wa taasisi hiyo katika sekta ya ujenzi.
Ameongeza kuwa pamoja na mafanikio hayo, TBA sasa ina nafasi kubwa zaidi ya kushiriki katika kutatua changamoto ya makazi kwa kujenga nyumba bora kwa gharama nafuu. Alisema taasisi hiyo inaweza kubuni na kutekeleza miradi ya makazi inayokidhi mahitaji ya wananchi wa kipato cha chini na cha kati, huku ikitumia maeneo yake ya kimkakati kuvutia uwekezaji na kuendeleza miradi ya kisasa.
Dkt. Msonde, amesema ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi kupitia TBA utaongeza uwekezaji, ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya ujenzi, huku ukiwezesha ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma, makazi ya biashara na miradi mingine ya maendeleo. Amewahimiza wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa hizo mapema kwa kuwa Serikali imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji na milango iko wazi kwa wote wenye nia ya kushirikiana na TBA.
Aidha, Dkt. Msonde ameipongeza TBA kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini, akisema utendaji wake umeendelea kuijengea Serikali imani kutokana na ubora wa kazi zake. Alisisitiza kuwa matarajio ya Serikali ni kuona taasisi hiyo ikitumia kikamilifu mamlaka mapya iliyopewa kupanua wigo wa huduma, kuongeza miradi ya kimkakati na kuwa chachu ya kuvutia uwekezaji utakaobadilisha sekta ya makazi na miundombinu nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano, Mh.Deus Sangu (MB) (wanne kushoto), akipokea zawadi toka kwa Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Jafari Merai Mgala, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini, Viwanja vya Nganga Mkoani Lindi Agosti 5, 2026.
Wananchi wakiwa kwenye banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, alipokuwa akizungumza kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini kwenye Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026
Lindi, Agosti 5, 2026
Mhe. Sangu ameyasema hayo Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi, ambapo alizungumza na wanachama, wastaafu na wananchi waliotembelea banda hilo.
"Wastaafu wengine wanashangaa kuona fedha zimeingia kwenye akaunti zao mara tu wanapotoka kazini na kujiuliza, 'Hizi fedha ni zangu kweli?' Hilo linaonesha wazi ukwasi wa Mfuko wa PSSSF na utekelezaji wa kaulimbiu ya Tunalipa Jana," amesema Mhe. Sangu.
Ameongeza kuwa hata wastaafu wanaopokea pensheni za kila mwezi hulipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi, na wakati mwingine hupokea malipo yao kabla ya watumishi walio bado kazini kupokea mishahara yao.
Serikali, kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.
Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.
Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.
“Mafuta yanapowasili nchini, Wakaguzi wa Mafuta hufuatilia hatua mbalimbali za upakuaji ili kuhakikisha yanakidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa,” amesema Mhandisi Makembe.
Ameeleza kuwa ufuatiliaji huo huanza mafuta yakiwa ndani ya meli na kuendelea wakati wa upakuaji na usafirishaji kupitia miundombinu maalumu, hadi yanapofikishwa kwenye maghala yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.
Kwa mujibu wa Mhandisi Makembe, Baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuidhinisha ubora wa bidhaa za mafuta kabla Meli haijaanza zoezi la Upakuaji ,Wakaguzi wa Mafuta wanajukumu la kuhakikisha kuwa taratibu za usalama na masharti ya upakuaji yanazingatiwa katika mchakato mzima wa upakuaji wa mafuta hayo. Hatua hiyo inalenga kulinda ubora wa mafuta na kuhakikisha shughuli za upakuaji zinafanyika kwa usalama.
Aidha, ukaguzi huo unalenga kubaini mapema changamoto zozote zinazoweza kuathiri ubora wa mafuta wakati wa upakuaji, usafirishaji au uhifadhi. Hatua hiyo husaidia kuhakikisha mafuta yanayopokelewa yanaendelea kuwa katika hali inayokubalika na TBS hadi yanapofikishwa kwenye maghala husika.



















.jpg)















.jpg)

