Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali katika mwaka wa fedha 2025/26 imetenga bajeti kwa ajili ya malipo ya fidia yenye thamani ya Sh Bilioni 5.1 kwa wananchi 1, 730 wanaopisha njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa Kilovoti 220 kutoka Masasi hadi Mahumbika.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Aprili 13, 2026 wakati akijibu swali la Mbunge wa Ndanda, Mhe. Faraji Buriani Nandala aliyehoji ni lini Wananchi wa Kata za Chikukwe, Chigugu, Chigundi, Mwena, Ndanda na Nanganga ambao wamepitiwa na Mradi wa Grid ya Taifa watalipwa fidia.








 Timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (NJE Sports) imepoteza kwa mabao 3–2 dhidi ya timu ya Ubalozi wa Umoja wa Ulaya katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Aprili 11, 2026, kwenye Uwanja wa John Merlin, jijini Dodoma.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa James Milya (Mb), amezipongeza timu zote mbili kwa kuonesha ushindani wa kirafiki na kudumisha mshikamano. Amesema michezo ya aina hiyo ina mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano, urafiki na diplomasia kati ya taasisi na mataifa.

Ameongeza kuwa mechi hiyo ni sehemu ya juhudi za kukuza diplomasia ya michezo, sambamba na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo kati ya Wizara na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya.

Mchezo huo pia ulihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa, ambaye amesema kuwa pamoja na ushindani uliokuwepo uwanjani, lengo kuu la mchezo huo lilikuwa kuimarisha uhusiano kati ya pande husika, akisisitiza kuwa huo ndio ushindi mkubwa zaidi kuliko mabao.

Kwa upande wake, kiongozi wa timu ya Ubalozi wa Umoja wa Ulaya, Bw. Ally Mwinchade, amesema ameridhishwa na kiwango cha ushindani kilichooneshwa na timu zote mbili, akieleza kuwa mchezo huo umeimarisha zaidi uhusiano wa kirafiki kati ya pande hizo.

Ameongeza kuwa ushindi huo si matokeo ya uwanjani pekee, bali pia ni ishara ya mshikamano, ushirikiano na dhamira ya kuendeleza diplomasia kupitia michezo. Aidha, ameipongeza timu ya NJE Sports kwa kuonesha mchezo mzuri na kuahidi kuendeleza ushirikiano huo katika michezo ijayo.













Baraza la Wafanyakazi la Nne la Tume ya Ushindani (FCC) limehitimisha kikao chake cha siku mbili kwa kuazimia kuunga mkono rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Miaka Mitano 2026/27-2030/31 unaolenga kutekeleza moja kwa moja Dira ya Taifa ya 2050.

Na Oscar Assenga,Tanga

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman  ameanza jitihada za kuinusuru Klabu ya African Sports ambayo ipo hatarini kushuka daraja kufuatia matokeo mabaya katika Ligi ya Championship.

Rajab aliyasema hayo baada ya kukutana na wachezaji pamoja na viongozi wa klabu hiyo, ambapo alieleza kuwa hali ya timu si ya kuridhisha, akifananisha na mgonjwa aliye katika chumba cha mahututi.

Alibainisha kuwa kwa sasa African Sports inashika nafasi ya 15 kati ya timu 16, hali inayoiweka katika hatari kubwa ya kushuka daraja endapo haitafanya vizuri katika mechi zilizobaki.

Akizungumzia historia ya klabu hiyo, alisema ni moja ya timu zenye heshima kubwa nchini na mshindani wa jadi wa Coastal Union, hivyo ni muhimu kurejesha ushindani wa soka la Tanga.

Katika hatua ya kuokoa timu hiyo, Mwenyekiti huyo  alitangaza kuchangia Shilingi milioni 20 ambazo tayari alikwisha kuziweka kwenye akauti, huku Mbunge wa Jimbo la Tanga akiahidi kutoa milioni tano na mdau mwingine kuahidi milioni 20, ikiwa ni sehemu ya kufikia lengo la kukusanya milioni 45 zinazohitajika kuiwezesha timu kumaliza msimu salama.

Alisema atahakikisha fedha hizo zinapatikana ili kutatua changamoto zinazoikabili klabu hiyo na kuwawezesha wachezaji kucheza kwa utulivu.

Aidha, aliwataka wachezaji kujituma katika mechi zilizobaki ili kuinusuru timu, akisisitiza kuwa wana dhamana ya kulinda heshima ya klabu hiyo.

Kwa upande mwingine, aliwashauri viongozi wa klabu kuweka mikakati ya muda mfupi na mrefu, ikiwemo kutovunja kambi mara baada ya msimu kumalizika ili kuboresha maandalizi ya msimu ujao.

Aliongeza kuwa mabadiliko ya mara kwa mara ya kikosi na maandalizi hafifu yamekuwa yakichangia kushuka kwa kiwango cha timu, na kusisitiza kuwa kwa mipango madhubuti wanaweza kurejea Ligi Kuu katika msimu ujao.









Na Oscar Assenga, Lushoto

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, ameishukuru Benki ya NMB Bank Plc kwa kuandaa tukio la kipekee la Kijiji Day, akisema ni hatua muhimu katika kuwafikia wananchi vijijini na kuwapatia elimu ya kifedha.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM), alisema kuwa wizara ina malengo mahsusi ya miaka mitano, likiwemo kuhakikisha wananchi wanapata uhuru wa kiuchumi.

 



MAKAMU wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, John Samuel Malecela amesema kuwa, swala la Utalii kokote Duniani linaenda sambamba na swala la Amani na Utulivu na kuwaomba wananchi kuhakikisha wanalinda Amani ili kukuza Utalii nchi na kuendelea kujinufaisha kupitia sekta hiyo. 


Malecela alitoa kauli hiyo jana wakati wa Uzinduzi wa tamasha la Same Utalii festival lililofanyika katika viwanja vya stendi wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambapo alisema kuwa, utalii ni kite ambacho huchangia kuleta fedha za kigeni. 


Alisema kuwa, baadhi ya nchi ulimwenguni serikali zinaendeshwa kwa fedha za Utalii na kuwataka kulichukulia swala hilo kwa umakini mkubwa. 

Kiongozi huyo alidai kuwa, misingi ya Utalii ni ukarimu kwa wageni na kuwataka wananchi wa wilaya ya Same kuwa mfano katika ukarimu ili kukuza Utalii wa wilaya ya Same. 

"Hata sehemu kukiwa na njiwa 10,000  wamejaa lakini jiwe likigonga tu wote wanakimbia kwa hiyo na sisi utalii wetu uanze na sisi wenyewe Watanzania kuwa na Amani ni jambo la msingi sana kwani Amani ndio italeta na kuwakaribisha watalii na ndio itatufanya tuendelee kukua kiuchumi" Alisema Malecela. 


Na kuongeza "Swala la ukarimu kwa wageni ni kitu muhimu sana mahali pengine watu hawaendi kwa sababu hakuna moyo wa kuwapokea wageni lakini kwetu same tuwe na moyo wa kuwapokea wageni ili kukuza utalii wetu".


Alisema kuwa, kinachotuunga pamoja ni Amani na kuwasihi Watanzania kuendelea kuitunga na mambo mengine yatafuata. 


"Ili Utalii wa same uweze kukua ni lazima uanze na sisi wenyewe wanasama kuwa na moyo dhabiti wa ukarimu ili wanapokuja na kurudi wakatoe sifa ni kweli wataenda kuona wanyama lakini mkiwakaribisha kwa moyo upande hawatarudi tena" Alisema Malecela.



SAME. 

MAKAMU wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, John Samuel Malecela amesema kuwa, swala la Utalii kokote Duniani linaenda sambamba na swala la Amani na Utulivu na kuwaomba wananchi kuhakikisha wanalinda Amani ili kukuza Utalii nchi na kuendelea kujinufaisha kupitia sekta hiyo. 

Malecela alitoa kauli hiyo jana wakati wa Uzinduzi wa tamasha la Same Utalii festival lililofanyika katika viwanja vya stendi wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambapo alisema kuwa, utalii ni kite ambacho huchangia kuleta fedha za kigeni. 

Alisema kuwa, baadhi ya nchi ulimwenguni serikali zinaendeshwa kwa fedha za Utalii na kuwataka kulichukulia swala hilo kwa umakini mkubwa. 

Kiongozi huyo alidai kuwa, misingi ya Utalii ni ukarimu kwa wageni na kuwataka wananchi wa wilaya ya Same kuwa mfano katika ukarimu ili kukuza Utalii wa wilaya ya Same. 

"Hata sehemu kukiwa na njiwa 10,000  wamejaa lakini jiwe likigonga tu wote wanakimbia kwa hiyo na sisi utalii wetu uanze na sisi wenyewe Watanzania kuwa na Amani ni jambo la msingi sana kwani Amani ndio italeta na kuwakaribisha watalii na ndio itatufanya tuendelee kukua kiuchumi" Alisema Malecela. 

Na kuongeza "Swala la ukarimu kwa wageni ni kitu muhimu sana mahali pengine watu hawaendi kwa sababu hakuna moyo wa kuwapokea wageni lakini kwetu same tuwe na moyo wa kuwapokea wageni ili kukuza utalii wetu".

Alisema kuwa, kinachotuunga pamoja ni Amani na kuwasihi Watanzania kuendelea kuitunga na mambo mengine yatafuata. 

"Ili Utalii wa same uweze kukua ni lazima uanze na sisi wenyewe wanasama kuwa na moyo dhabiti wa ukarimu ili wanapokuja na kurudi wakatoe sifa ni kweli wataenda kuona wanyama lakini mkiwakaribisha kwa moyo upande hawatarudi tena" Alisema Malecela.






 


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema kuwa, zoezi la kubadilisha tahasusi na kozi za vyuo vya kati kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha nne mwaka 2025 limeanza rasmi leo Aprili 11, 2026 na litahitimishwa  Mei 10, 2026. 

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Aprili 11, 2026 jijini Dodoma, wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu wahitimu wa kidato cha nne mwaka 2025 kufanya mabadiliko ya Tahasusi za kidato cha tano na kozi za vyuo vya kati kwa njia ya mtandao kwenye mfumo wa kielektroniki wa uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha tano na Vyuo mwaka 2026.

“Ninawahimiza wanafunzi, wazazi na walezi kushauriana kikamilifu ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa kitaalam na kitaaluma kabla ya kufanya mabadiliko ya tahasusi au kozi,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka wahitimu kufanya marekebisho ya machaguo ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao, kwa kuingia kwenye Mfumo wa Uchaguzi wa Wanafunzi (Student Selection MIS) unaopatikana kupitia kiunganishi cha selform.tamisemi.go.tz. 

Aidha, Prof. Shemdoe amewataka wahitimu kuzingatia muda uliotolewa wa kufanya marekebisho ili ratiba ya kuwachagua na kuwapangia shule na vyuo iweze kuendelea kwa muda uliopangwa, kwani mara baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo hakutakuwa na fursa ya kufanya mabadiliko tahasusi na kozi.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, huduma ya kubadilisha tahasusi ni bure na endapo wanafunzi watapata changamoto, wawasiliane na dawati la huduma la kwa mteja kupitia barua pepe: huduma@tamisemi.go.tz au kuwasiliana moja kwa moja na kituo cha huduma kwa wateja kwa simu +255 262 160 210 na +255 735 160 210 na kuongeza kuwa, mwanafunzi, mzazi au mlezi atakayekuwa na suala linalohitaji maelezo au ufafanuzi zaidi aende katika Ofisi za Elimu za Mikoa na Halmashauri.





Na Oscar Assenga, Tanga

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeeleza kuwa suluhisho la kudumu la kuboresha eneo la kuchezea katika Uwanja wa CCM Mkwakwani ni uwekaji wa nyasi bandia, huku wakipanga kushirikiana na wadau wa soka kufanikisha mpango huo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua uwanja huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurahman, alisema uwekaji wa nyasi bandia unakadiriwa kugharimu kati ya shilingi milioni 400 hadi 500.

Ziara hiyo ni sehemu ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo, ikiwemo ile inayotekelezwa kwa fedha zinazotolewa na Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kupunguza kero kwa wananchi.

Abdurahman aliwataka viongozi wa CCM, ambao ni wamiliki wa uwanja huo, kutumia ubunifu na kushirikiana na wadau wa soka ili kuhakikisha wanapata fedha za kuweka nyasi bandia.

“Tutawaomba wadau wa soka nchini watakapohitajika kutusaidia, kwani dhamira yetu ni njema. Kama ambavyo wamekuwa wakitusaidia hapo awali, tunaamini watashiriki nasi kuhakikisha tunakuwa na uwanja wa kisasa zaidi,” alisema.

Alieleza kuwa maboresho ya uwanja huo yatasaidia kuinua uchumi wa Mkoa wa Tanga, kwani utaweza kutumika kwa mashindano ya kitaifa na kimataifa, ikiwemo CECAFA na michuano mingine ya Afrika.

“Tunapokuwa na uwanja mzuri, hata timu za nje zitakuja kucheza hapa Tanga. Hii itaongeza mzunguko wa fedha na kukuza uchumi wa mkoa wetu,” aliongeza.

Aidha, alikumbusha kuwa uwanja huo uliwahi kufungiwa kutokana na kutokidhi vigezo, hasa ubora wa eneo la kuchezea, akisisitiza kuwa hatua zinazochukuliwa sasa zinalenga kuhakikisha viwango vinazingatiwa kwa usalama wa wachezaji na ubora wa mchezo.

“Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linapofungia uwanja si kwa kupenda, bali kuhakikisha viwango vinazingatiwa. Ndiyo maana tumekuwa wepesi kuchukua hatua za maboresho,” alisema.

Katika hatua nyingine, Abdurahman alieleza kuridhishwa na maendeleo ya ufungaji wa viti 6,500 vilivyotolewa na TFF chini ya Rais wake, Wallace Karia, licha ya kuwepo kwa ucheleweshaji mwanzoni.

Amesema tayari ameagiza kazi hiyo ikamilike ndani ya mwezi mmoja, na kwa sasa inaendelea vizuri chini ya usimamizi wa Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa, Nasoro Makau.

Kwa mujibu wa mpango huo, maeneo ya kipaumbele ni jukwaa kuu pamoja na sehemu za mashabiki wa klabu za Coastal Union na African Sports. Pia wameomba viti vingine 2,500 ili kukamilisha uwanja mzima.

Abdurahman aliishukuru Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, inayoongozwa na Waziri Paul Makonda na Naibu wake Hamisi Mwinjuma, pamoja na Rais wa TFF Wallace Karia, kwa ushirikiano wao katika kuboresha uwanja huo.

Alisisitiza kuwa maboresho hayo yanalenga kuhakikisha klabu za Coastal Union na African Sports zinaendelea kucheza mechi zao za nyumbani mkoani Tanga badala ya kuhamishiwa maeneo mengine.

Aidha, aliwataka mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi uwanjani kuunga mkono timu zao.

“Haileti maana kuwa na uwanja mzuri halafu mashabiki wanabaki nyumbani kuangalia mechi,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa Uwanja wa Mkwakwani, Nasoro Makau, alisema hadi sasa wamefikia asilimia 40 ya ufungaji wa viti na wana uhakika wa kukamilisha kazi hiyo ndani ya mwezi mmoja.