Na: OWM - TAMISEMI


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeanza rasmi vikao vyake jijini Dodoma kwa kukutana na watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, kujadili utekelezaji wa shughuli za Serikali, hususan miradi ya miundombinu na utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa Nne wa Bunge unaotarajiwa kuanza Agosti 25, 2026.

Katika kikao hicho, Kamati imepokea na kujadili taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhusu ukarabati wa barabara zilizoharibiwa na mvua za masika nchini, pamoja na maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya BRT na mpango wa kuboresha huduma za usafirishaji zinazotolewa na UDART.

Katika vikao hivyo, Kamati pia inatarajia kupitia masuala mbalimbali yanayohusu utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwemo uimarishaji wa huduma za maji na lishe shuleni, utunzaji wa mazingira, ujenzi wa viwanja vya michezo pamoja na ajira za walimu wa michezo katika shule za msingi na sekondari.

Aidha, ratiba ya Kamati inaonesha kuwa itajadili masuala ya elimu, afya na mazingira, ikiwemo ujenzi wa shule na miundombinu yake, mikakati ya kukabiliana na viuadudu katika halmashauri, pamoja na mahitaji ya walimu na maandalizi ya utekelezaji wa mabadiliko ya mtaala wa elimu.













 



▪️ Lengo ni kurahisisha huduma kwa wateja

▪️ Kamati ya Bunge yaishauri Serikali kupunguza tozo zinazowaumiza wachimbaji wadogo

▪️ Dhahabu tani 67.8 zenye thamani ya Sh trilioni 18.4 zazalishwa kwenye viwanda vya usafishaji

▪️Waziri Mavunde aeleza mkakati wa kukuza biashara ya Tanzanite


Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameiagiza Tume ya Madini kuongeza muda wa uendeshaji wa masoko ya madini mpaka saa 3:00 usiku, hatua inayolenga kuongeza fursa za biashara na kuwahudumia wafanyabiashara na wauzaji wa madini kwa muda mrefu zaidi ili kuendana na mahitaji ya wadau na kuongeza ufanisi katika biashara ya madini.

Mavunde ametoa agizo hilo Agosti 11, 2026, wakati akijibu maswali ya Wabunge katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini jijini Dodoma, ambapo Wizara imewasilisha taarifa kuhusu hali halisi na maendeleo ya sekta ya madini nchini.

Mavunde amesema Serikali pia inaendelea kuimarisha udhibiti wa biashara ya madini na utoroshaji, huku ikisisitiza uongezaji thamani ndani ya nchi. Ameeleza kuwa katika eneo la Mirerani, serikali itatekeleza mkakati ambao imejiwekea wa kukuza biashara hiyo ya madini ya Tanzanite kwa kuhakikisha mfumo wa biashara ya madini hayo unapitiwa ili kusaidia kuchochea ukuaji wa biashara ya madini ya Tanzanite.

Kuhusu uwekezaji, amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua dhidi ya wenye leseni wanaoshikilia maeneo makubwa bila kuyaendeleza, akisisitiza kuwa maeneo yasiyoendelezwa kwa mujibu wa sheria yanaweza kuchukuliwa hatua, ikiwemo kufutwa kwa leseni. Aidha, Serikali inaendelea kushirikiana na Wizara ya Nishati kuhakikisha maeneo ya migodi yanapata umeme wa uhakika pamoja na kuzingatia miundombinu ya kimkakati katika mipango ya maendeleo.

Amesema Serikali pia inaendelea kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika uchumi wa madini kupitia mpango wa MBT unaolenga vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalum. Kwa upande mwingine, Serikali imesaini hati za makubaliano 14 na wawekezaji ambao miradi yao bado haijaanza uzalishaji, huku ikiendelea kuweka mazingira wezeshi kwa taasisi za fedha kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo wenye sifa.

Akitoa taarifa ya hali ya sekta hiyo, Kamishna wa Madini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, amesema madini yanaendelea kuwa sekta muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika mwaka wa fedha 2025/26, dhahabu iliongoza kwa uzalishaji baada ya kufikia tani 67.8 zenye thamani ya Sh trilioni 18.4. Aidha, kilogramu 28,701 za dhahabu ziliuzwa katika viwanda vitano vya kusafisha dhahabu nchini, ambapo kilogramu 21,710, sawa na asilimia 75.64, zilinunuliwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara kwa hatua zinazochukuliwa kuimarisha sekta hiyo, huku akisisitiza umuhimu wa kudhibiti utoroshaji wa madini na kupunguza tozo katika mnyororo wa biashara ya madini na kuitaka Serikali iangalie upya tozo kwa wachimbaji wadogo ambazo zimekuwa ni mzigo mkubwa.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amesema Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) na kuhakikisha shughuli za madini zinawanufaisha wananchi wanaozunguka maeneo ya migodi.

 


Na. Josephine Majura na Asia Singano, WF- Dodoma

Serikali imesema uchumi wa Tanzania unaendelea kuimarika na kwamba uwekezaji katika sekta mbalimbali, hususani madini, gesi, nishati, kilimo na miundombinu, unatarajiwa kutoa msukumo mkubwa kwa ukuaji wa uchumi.

Hayo yalielezwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akifungua mkutano na wataalamu wa Kampuni ya Kimataifa ya Tathmini ya Madeni ya (Fitch Ratings), uliofanyika kwa njia ya mtandao, ikiwa ni sehemu ya mchakato wa kufanya mapitio ya hali ya uchumi wa Tanzania.

Alisema Serikali imeendelea kuchukua hatua za kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, ikiwa ni pamoja na kufanyia kazi mapendekezo ya Tume ya Mageuzi ya Kodi iliyoundwa na Serikali, jambo ambalo limeendelea kukuza uchumi wa nchi.

‘’Upande wa ukuaji wa uchumi tumetoka asilimia 5, mwaka mwaka 2024, tumekwenda asilimia 5.9 mwaka jana, mwaka huu tunategemea uchumi utakuwa kwa asilimia 6.3 hatujafikia viwango ambavyo vilikuwa kabla ya COVID 19 lakini tunaendelea vizuri’’ alisema Mhe. Balozi Omar.

Alisema kuwa, moja ya maeneo muhimu yaliyojadiliwa na Fitch ni maendeleo makubwa yanayoendelea katika sekta ya madini na uchakataji wa madini, huku akieleza kuwa Tanzania ina miradi mikubwa ambayo ipo katika hatua mbalimbali za maandalizi na ikitekelezwa itakuwa na mchango mkubwa katika uchumi.

‘’Kuna miradi mingine mikubwa ukiwemo wa Nyanzaga wa uchimbaji wa dhahabu Mwanza ambao unatarajiwa kuwekeza zaidi ya dola milioni 500, kuna miradi mingine ambayo inaendelea upande wa aluminiam – Songea, Chuma- Liganga, Chuma -Dodoma, na miradi mingine kwa hiyo kwa ujumla kwenye sekta hii kuna uwekezaji mkubwa ambao unatarajiwa kuleta msukumo mkubwa katika uchumi wetu’’ Alisema Mhe. Balozi Omar (Mb).

Aliongeza kuwa kwa ujumla sekta ya madini inaendelea kuwa na nafasi kubwa katika kuchochea ukuaji wa uchumi, hasa kutokana na ongezeko la uwekezaji unaotarajiwa katika uchimbaji na uchakataji wa madini hapa nchini.

Alisema Mradi mkubwa wa gesi asilia iliyosindikwa (LNG), ni miongoni mwa miradi inayotarajiwa kuleta msukumo mkubwa katika uchumi, pamoja na mradi wa madini ya niobium ambao tayari umesainiwa na unatarajiwa kuvutia uwekezaji wa takribani dola milioni 442.

Aidha, alibainisha kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kupunguza athari za mabadiliko ya bei za mafuta na bidhaa nyingine muhimu kwa kutumia sera na mifumo mbalimbali ya kiuchumi.

Kwa upande wa Fitch, majadiliano yaliongozwa na mchambuzi Mkuu anayeshughulikia Tanzania, Bw. José Mantero, ambapo majadiliano hayo yalilenga kuwapa wachambuzi hao fursa ya kupata taarifa za kina kuhusu mwenendo wa uchumi wa Tanzania, utekelezaji wa sera za kibajeti na fedha, pamoja na mikakati ya Serikali katika usimamizi wa deni la Taifa.

Aidha, wachambuzi hao walijikita katika kutathmini athari za vita kati ya Iran katika uchumi wa Tanzania, hususan mwenendo wa bei za mafuta na mbolea, pamoja na hatua na mikakati inayochukuliwa na Serikali kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, Kamishna Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Deni la Taifa, Nuru Ndile, kwa njia ya mtandao.



 Na. Josephine Majura na Asia Singano, WF – Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, ameongoza Ujumbe wa Serikali ya Tanzania kwa niaba ya Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, katika kikao na Ujumbe wa Benki ya Dunia kilicholenga kuhitimisha maandalizi ya kitaalamu ya Programu ya Uendelezaji wa Ushoroba wa Kati wa Maendeleo ya Kiuchumi Utakaoongeza Ajira kwa Vijana (CATALYZING JOBS AND RESILIENT GROWTH IN THE CENTRAL CORRIDOR MULTIPHASE PROGRAMMATIC APPROACH 
(KAZI MPA).

Kikao hicho kilifanyika kwa lengo la kuwasilisha na kujadili matokeo ya maandalizi yaliyofanywa kwa pamoja kati ya Serikali na Benki ya Dunia, pamoja na kukubaliana hatua zinazofuata kuelekea kukamilisha maandalizi ya Programu hiyo, kilichofanyika, Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, pande hizo zilijadili kwa kina maeneo muhimu ya utekelezaji wa KAZI MPA, huku zikisisitiza umuhimu wa programu hiyo katika kuchochea mageuzi ya kiuchumi, kuongeza uwekezaji na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika kuchangia maendeleo ya uchumi wa Tanzania.

Aidha, KAZI MPA inalenga kuongeza fursa za ajira, hususan kwa vijana, pamoja na kuimarisha ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa kupitia kuendeleza miundombinu na mazingira wezeshi ya shughuli za kiuchumi katika Ushoroba wa Kati.

Utekelezaji wa programu hiyo unatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya jitihada za Serikali katika kutafsiri kwa vitendo malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, hususan katika kujenga uchumi wenye tija, jumuishi na stahimilivu, unaotoa fursa kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na biashara.

Ujumbe wa Serikali katika kikao hicho uliwahusisha pia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Bw. Adolf Ndunguru, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvivu Bi. Agness Meena, Kaimu Katibu Mkuu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubil Joshua, Naibu Makatibu Wakuu Wizara ya Kilimo, Prof. Peter Msoffe na Mhandisi Athumani Kilundumya pamoja na Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Taifa ya Mipango Bw. Sosthenes Kewe.

Kwa upande wa Ujumbe wa Benki ya Dunia ukiongozwa na Meneja wa Benki ya Dunia, Kitengo cha Utekelezaji wa Sekta ya Usafiri, Afrika Mashariki na Kusini, (Practice Manager for Transport in Eastern and Southern Africa), Bw. Binyam Reja.

Kikao hicho ni hatua muhimu kuelekea kukamilisha maandalizi ya KAZI MPA na kuweka msingi wa utekelezaji wa programu inayolenga kuchochea shughuli za kiuchumi, kuongeza fursa za ajira kwa vijana na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika uchumi wa kikanda na kimataifa.

 


Na. Benny Mwaipaja


Tanzania na Marekani zimeendelea kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika sekta mbalimbali zikiwemo madini adimu, nishati, afya, uwekezaji na maendeleo ya kiuchumi, pamoja na dhamira ya kuendeleza mazungumzo na ushirikiano wa kitaalamu kwa manufaa ya nchi hizo mbili.

Hayo yameafikiwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, walipokutana na kufanya mazungumzo ya katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo pia walieleza umuhimu wa kuendelea kutumia majadiliano ya kitaalamu na ushirikiano wa Serikali kwa Serikali katika kushughulikia maeneo yenye umuhimu wa kimkakati, ikiwemo maendeleo ya sekta ya Nishati ya Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas (LNG).

Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, alisisitiza kuwa mawasiliano ya karibu na ushirikiano kati ya wataalamu wa pande zote ni muhimu katika kuwezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

Aidha, walijadili fursa za kuendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini, ikiwemo miradi mikubwa ya madini na kuongeza thamani ya rasilimali nchini, ambapo walikubaliana kuhusu umuhimu wa kuwa na uratibu mzuri wa Serikali na wawekezaji ili kuhakikisha miradi ya kimkakati inatekelezwa kwa ufanisi na kutoa manufaa kwa uchumi na wananchi.

Kwa upande wa afya, alisema kuwa hivi karibuni, Marekani na Tanzaniaa zimesaini makubaliano ya kuendeleza sekta ya afya yatakayogharimu dola za Marekani bilioni 3.1 katika kipindi cha miaka mitano ijayo kwa ajili ya  kuimarisha mifumo ya afya, kukabiliana na magonjwa mbalimbali na kujenga uwezo wa ndani, kuelekea kwenye mifumo endelevu ya afya inayoongeza uwezo wa Tanzania kugharamia na kusimamia huduma za afya kwa muda mrefu, sambamba na kuimarisha uwezo wa kitaifa katika kinga, ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa.

“Tunatambua umuhimu wa uwekezaji katika miundombinu ya afya, uzalishaji wa bidhaa za afya nchini na kuimarisha taasisi zinazohusika na afya ya umma na Ushirikiano huu unalenga kuongeza uwezo wa Tanzania kukabiliana na changamoto za kiafya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu” alisema Mhe. Balozi Lentz

Kwa upande wake Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema kuwa kuna nafasi kubwa ya kubadilishana uzoefu kuhusu namna Serikali hizo zinavyoweza kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, kifedha na kitaalamu, na Serikali inatambua juhudi zinazoendelea za wataalamu wa pande zote mbili katika kuimarisha mifumo ya kifedha, ikiwemo maendeleo ya soko la dhamana za Serikali, ambazo zinatajwa kama mfano wa ushirikiano wa kitaalamu unaoweza kutoa manufaa ya muda mrefu kwa uchumi wa Tanzania.

“Kwa ujumla, mkutano huu umeonesha dhamira ya Tanzania na Marekani ya kuendeleza ushirikiano wa karibu katika maeneo ya kimkakati, na msisitizo mkubwa ukiwa katika kuimarisha uwekezaji, kujenga uwezo wa ndani, kuongeza thamani ya rasilimali na kuhakikisha ushirikiano huo unaleta matokeo chanya na endelevu kwa wananchi” alisema Mhe. Balozi Omar.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria Wizara ya Fedha, Bi. Mwantumu Sultan, Mshauri wa Siasa na Uchumi Ubalozi wa Marekani Nchini,  Bi. Rebecca Hunter, na wataalamu wengine wa Wizara ya Fedha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda, akifungua mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa wakaguzi wa Tume hiyo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama naAfya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwajengea uelewa wakaguzi hao wenye jukumu la kukagua uzingatiaji wa sheria na miongozo mbalimbali katika sekta ya umma.
Serikali imekusudia kukomesha uuzaji wa mazao ghafi kwani mfumo huo unamnyima mkulima zaidi ya nusu ya faida halisi na kubainisha kuwa mkakati uliopo ni kuongeza thamani ya mazao kama korosho kabla ya kuyaweka sokoni, hatua itakayoinua kipato cha wajasiriamali na wakulima wadogo mkoani humo.
Serikali imetoa agizo kwa wakandarasi na wasimamizi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji wa Masasi kuhakikisha miradi yote inakamilika ndani ya muda uliopangwa, na kusisitiza kuwa utamaduni wa kuongeza muda wa utekelezaji (extension) hauleti tija wala maendeleo kwa Taifa.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka watendaji wa Serikali na taasisi za udhibiti kuwa wawezeshaji wa biashara badala ya kufungia biashara, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kulinda mitaji na maslahi ya wananchi.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

WATANZANIA wameanza kunufaika na huduma za matibabu ya kibingwa zinazopatikana nchini, hali inayopunguza gharama na ulazima wa kusafiri nje ya nchi kutafuta matibabu.

 

Mimi naitwa Elizabeth, natokea mkoani Dodoma, maeneo ya Area D. Maisha yangu ya ndoa yalikuwa kwenye kilele cha mafanikio kwa nje kwa sababu mume wangu ni mwanasiasa anayejulikana nchi nzima. Lakini siri iliyokuwa ndani ya nyumba yetu ilikuwa ni ya kusikitisha.

Kwa muda mrefu, nilikuwa napitia changamoto ya kukosa hamu ya tendo la ndoa na kuwa mkavu kiasi kwamba nikawa naogopa kumuona mume wangu akirudi nyumbani.

Ili kukwepa unyumba, nilianza tabia ya kujifanya nimevamiwa na “pepo la usingizi”, nikifika tu chumbani, najilaza sakafuni au kitandani na kuanza kukoroma kwa nguvu hata kama sijalala, ili tu mume wangu asiniguse.

Mume wangu alianza kuchoka na tabia yangu. Alisema, “Elizabeth, mbona kila nikirudi unakuwa umechoka kiasi hiki? Unafanya kazi gani Dodoma nzima mpaka ukorome kama trekta?”. 

Nilianza kukosa amani maana nilijua mume wangu anaweza kuanza kutafuta mwanamke mwingine nje, na hali hiyo ingeharibu sifa yetu kama familia ya kiongozi.

Nilienda kwa madaktari bingwa hapa Dodoma wakaniambia nina upungufu wa damu, lakini dawa walizonipa hazikurudisha hamu wala kuondoa ukavu uliokuwa unanichoma kama moto wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.

 

Naitwa Zaituni, mkazi wa jijini Arusha, maeneo ya mtaa wa Njiro. Maisha yangu ya ndoa yalifika mahali yakawa ni ya aibu na siri nzito ambayo ilikaribia kunivunjia heshima yangu mbele ya mume wangu na jamii inayotuzunguka.

Mume wangu ni mfanyabiashara mkubwa wa vito vya thamani kama Tanzanite, hivyo maisha yetu yalikuwa ni ya anasa, lakini ndani ya chumba chetu cha kulala, kulikuwa na “jangwa” la kutisha.

Kwa takriban miaka minne, nilipoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa na mwili wangu ukawa mkavu kiasi cha kutisha. Kila mume wangu alipojaribu kunigusa, nilihisi maumivu makali kama ninasuguliwa na msasa butu.

Katika hali ya kukata tamaa na kuogopa mume wangu asije kunitupa nje, nilianza kufanya kitendo cha hatari. Nilikuwa naiba mafuta ya kulainisha mashine (lubricants) kutoka kwenye gereji ya mume wangu na kuyaweka kwenye kopo la ‘lotion’ ili tu kumlainisha mume wangu wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.

 

Mimi naitwa Rehema, mkazi wa jijini Dar es Salaam, eneo la Sinza. Kwa miaka mingi, maisha yangu yalikuwa ni mzunguko wa maumivu na masikitiko.

Licha ya kuwa na kazi nzuri na mwonekano unaovutia, suala la ndoa lilikuwa kama ndoto ya mchana.

Kila mwanaume aliyekuja kwangu alikuwa akitafuta starehe tu na kisha kutokomea. Nilifikisha umri wa miaka 38 nikiwa bado nipo nyumbani kwa wazazi, huku mdogo wangu wa mwisho akishabeba mtoto wake wa pili.

Kila sherehe ya kifamilia ilikuwa ni kero kwangu; ndugu walikuwa wakinitazama kwa jicho la huruma lililochanganyika na dhihaka. “Rehema, mbona hutuletei wifi?” au “Umri unaenda, utazaa lini?” yalikuwa maswali ya kila siku.

Nilijaribu kila mbinu, kuanzia mitandao ya kijamii hadi kuomba marafiki waniunganishe na watu, lakini wapi! Nilianza kuamini kuwa labda nimezaliwa kuwa mpweke maisha yangu yote. Hofu ya kukosa watoto ilinitesa sana usiku, nilikuwa nalia hadi mto unaloa maji. SOMA ZAIDI.

 


📌 Ahimiza wananchi kuunganishiwa huduma ya umeme na kuitumia kuongeza tija

📌 Shule, zahanati na maeneo mengine ya huduma za kijamii kupewa kipaumbele

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasha umeme katika Kitongoji cha Mwanubi mkoani Shinyanga na kusema kuwa huduma ya umeme ni hitaji la msingi kwa Watanzania na nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuwasha umeme katika kitongoji hicho, Mhe. Ndejembi amesema kufikishwa kwa umeme vijijini kunapaswa kwenda sambamba na matumizi yenye tija, ikiwemo kuongeza thamani ya mazao, kuendeleza biashara na shughuli za uzalishaji pamoja na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii.

Amesema Serikali inaendelea kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma ya umeme, hususan katika maeneo ya vijijini, ili nishati hiyo iwe kichocheo cha uzalishaji, ongezeko la kipato na uboreshaji wa maisha ya wananchi.

Mhe. Ndejembi amewahimiza wananchi ambao miundombinu ya umeme imewafikia kuchangamkia fursa hiyo kwa kuunganishiwa huduma kwa gharama nafuu ya shilingi 27,000, na kutumia umeme katika shughuli mbalimbali za uzalishaji na kujiletea maendeleo.

Aidha, ameiagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kufanya tathmini ya maeneo ambayo bado hayajafikiwa na miundombinu ya umeme ili yaingizwe katika mipango ya utekelezaji na kufikishiwa huduma hiyo.

Pia, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme kuongeza kasi ya kusimika nguzo na kujenga miundombinu katika maeneo yaliyosalia ili wananchi wengi zaidi waweze kufikiwa na kuunganishiwa huduma ya umeme.

Amesisitiza kuwa shule, zahanati na maeneo mengine muhimu ya kutolea huduma za kijamii yanapaswa kupewa kipaumbele katika kufikishiwa umeme ili kuongeza ufanisi na kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Aidha Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wanapata nishati ya uhakika.

Ameeleza kuwa uwekezaji huo unalenga kuwezesha wananchi kutumia umeme katika shughuli za uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao, kukuza biashara, kuongeza fursa za ajira na kuboresha huduma za kijamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote vya Mkoa wa Shinyanga, akieleza kuwa hatua hiyo imefungua fursa mbalimbali za maendeleo kwa wananchi.

Amesema upatikanaji wa umeme katika maeneo ya vijijini umeendelea kubadilisha maisha ya wananchi kwa kuchochea shughuli za kiuchumi, kuongeza fursa za uzalishaji na ajira pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.

Naye, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Herini Mhina, amesema Wakala unaendelea kutekeleza miradi ya kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji mbalimbali nchini ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi, hususan katika maeneo ya vijijini, wanapata huduma hiyo.

Mha. Mhina amesema REA itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hiyo ili kupanua wigo wa upatikanaji wa umeme na kuwawezesha wananchi kutumia nishati hiyo katika shughuli za kiuchumi, uzalishaji na utoaji wa huduma za kijamii.

Nao wananchi wa Kitongoji cha Mwanubi wameishukuru Serikali kwa kuwafikishia huduma ya umeme katika kitongoji chao, wakieleza kuwa hatua hiyo itachochea shughuli za kiuchumi na kijamii na kuboresha maisha yao.

Wamesema ujio wa umeme utafungua fursa mpya za biashara na uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu katika eneo hilo.

Hafla ya kuwasha umeme katika Kitongoji cha Mwanubi ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia REA za kupanua wigo wa upatikanaji wa umeme vitongojini na kuhakikisha nishati hiyo inakuwa kichocheo cha maendeleo endelevu ya wananchi.

 Katika sehemu nyingi za burudani, mazungumzo ya marafiki siku hizi hayaishii kwenye muziki au mpira pekee. Mara kwa mara kuna anayemuuliza mwenzake kama tayari ameionja ORIJIN na anaionaje ladha yake.


Kinywaji hicho kimeleta mjadala kutokana na mchanganyiko wa herbs, roots na fruits za Kiafrika unaotoa ladha ya uchungu na utamu. Hilo limewafanya baadhi ya watumiaji kulinganisha uzoefu wao na kuwahamasisha wengine kujaribu ili wajipatie maoni yao binafsi.

Kwa sasa ORIJIN inapatikana katika aina tofauti zikiwemo Bitters na Mixed (RTD), jambo linalompa mtumiaji nafasi ya kuchagua kulingana na anachokipendelea.



Sehemu ya barabara iliyowekwa lami katika Mradi wa Barabara ya Kahama–Bulyanhulu Jct–Kakola, unaowezeshwa na migodi ya Barrick-Twiga nchini Tanzania.
Waziri wa Nishati na Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, Mhe. Deogratius Ndejembi akiongozana na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita na viongozi wengine wa serikali kukagua mradi wa barabara ya Kahama–Bulyanhulu Jct–Kakola unaowezeshwa na migodi ya Barrick-Twiga nchini.
Waziri wa Nishati na Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, Mhe. Deogratius Ndejembi akiongea na waandishi wa habari baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akiongea na waandishi wa habari wakati wa ziara hiyo.

**

Waziri wa Nishati na Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, Mhe. Deogratius Ndejembi, amemtaka Mkandarasi wa ujenzi wa Barabara ya Kahama–Bulyanhulu Jct–Kakola, M/s China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC), kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ili ukamilike kwa wakati na kuwawezesha wananchi kuanza kunufaika na miundombinu hiyo.

Na Mwandishi Wetu

WANAFUNZI 85 wanatarajia kwenda masomoni kwenye vyuo vikuu mbalimbali nchini India kuanzia wiki ijayo kupitia Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL).

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imeibuka kinara miongoni mwa Taasisi za Elimu katika Maonesho ya 33 ya Kilimo, Mifugo na Sherehe za Nanenane Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha.

Akizungumzia ushindi huo, Prof. Maulilio Kipanyula, Makamu Mkuu wa NM-AIST, amesema bidhaa bora zinahitaji utafiti na NM-AIST kama Taasisi inayotanguliza ubunifu, imeendelea kubadilisha matokeo ya tafiti kuwa teknolojia zinazotoa suluhisho kwa changamoto za wakulima na wafugaji.

Amesema teknolojia mbalimbali zinazooneshwa na Taasisi, ikiwemo Mfumo wa Ng’ombe Smart, zinalenga kuongeza tija katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kwa kuwezesha ufuatiliaji wa uzalishaji wa maziwa na taarifa muhimu za mifugo.

Aidha, Prof Kipanyula amesema mwaka huu NM-AIST imekuja na teknolojia zinazolenga kuongeza thamani ya mazao, yakiwemo tumbaku, mazao ya chakula pamoja na vyakula vya mifugo kama kuku na ng’ombe.

Prof. Kipanyula amesisitiza kuwa NM-AIST inaendelea kujipanga kuwa kinara katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hususan katika maeneo ya utafiti na maendeleo, sayansi, teknolojia na ubunifu, pamoja na mabadiliko ya kidijitali.

“Ushindi huu ni chachu ya kuendelea kufanya vizuri zaidi. Mwaka ujao tutakuja na teknolojia mpya kabisa. Mwaka huu tumefanikiwa kuzalisha takribani patent 40, jambo tunalojivunia na linalotupa nguvu ya kuendelea kuzalisha teknolojia na bunifu zenye tija kwa sekta ya kilimo na mifugo.”

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla, ameipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) kwa tafiti na bunifu mbalimbali zinazolenga kuongeza tija katika sekta za kilimo na mifugo.

Mhe. Makalla amesema kuwa ametembelea banda la NM-AIST na kujionea teknolojia mbalimbali za kilimo na mifugo, pamoja na bunifu zinazolenga kuongeza thamani ya mazao na bidhaa za mifugo.

Amesisitiza kuwa mapinduzi ya kweli hayawezi kufanyika bila utafiti, teknolojia na ubunifu, akieleza kuwa NM-AIST imekuwa ikifanya vizuri katika kuibua na kuendeleza teknolojia zinazolenga kutatua changamoto za jamii.

“Kilimo bila utafiti, teknolojia na dhana za kisasa hakiwezi kuleta mabadiliko makubwa. Taasisi za utafiti zinatuelekeza na kutupeleka kwenye kilimo na ufugaji wenye tija,” amesema Mhe. Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amesema maendeleo ya sekta za kilimo, mifugo na uvuvi hayapaswi kupimwa kwa kuongezeka kwa uzalishaji pekee, bali pia kwa uwezo wa kuzalisha kwa tija, ubora na kuzingatia mahitaji ya soko, kama inavyosisitizwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Ameeleza kuwa Dira hiyo inalenga kujenga uchumi shindani unaoongozwa na maarifa, teknolojia, ubunifu na uongezaji wa thamani, hivyo taasisi za utafiti kama NM-AIST zina nafasi muhimu katika kufanikisha azma hiyo.

Mhe. Makalla ameyasema hayo wakati akihitimisha Maonesho ya 32 ya Kilimo, Mifugo na Sherehe za Nanenane Kanda ya Kaskazini, yaliyofanyika katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Baraza la Ushindani (FCT limeendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kutumia teknolojia za kidijitali, likiwataka wananchi na wadau kutumia mfumo wa kielektroniki kuwasilisha mashauri na rufaa zao kwa urahisi na kwa wakati.
Msajili wa Baraza la Ushindani, Mbegu Kaskasi, amesema Baraza hilo lililo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara lina jukumu la kusikiliza na kutatua migogoro ya ushindani wa biashara na udhibiti wa soko inayotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na mamlaka za udhibiti zikiwemo TCRA, EWURA, LATRA, TURA na TCAA.
Kaskasi amesema Baraza hilo linaundwa na Jaji wa Mahakama Kuu pamoja na wajumbe sita, huku likitumia fursa mbalimbali kuwaelimisha wananchi kuhusu majukumu yake, namna ya kupata huduma na utaratibu wa kuwasilisha mashauri, ikiwemo kupitia mfumo wa kielektroniki wa usikilizaji wa mashauri.
Amesema mfumo huo umewekwa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, ambapo kwa sasa wanaweza kuwasilisha mashauri na rufaa zao kwa njia ya kielektroniki bila kulazimika kufika ofisini, hatua inayokwenda sambamba na mabadiliko ya kidijitali nchini.
Kwa upande wake,Afisa Sheria wa baraza hilo ,Hafsa Said, amesema mchakato wa rufaa huanza kwa mhusika kuwasilisha notisi ya rufaa pamoja na kuwapatia nakala wahusika wanaopaswa kujibu rufaa hiyo. Baada ya hapo, mhusika anatakiwa kuwasilisha sababu za rufaa pamoja na kumbukumbu zinazohusiana na shauri hilo.
Amesema baada ya mjibu rufaa kuwasilisha majibu yake, shauri hukamilika kwa ajili ya kusikilizwa, huku Baraza likiwa na utaratibu wa kuhakikisha rufaa inayowasilishwa kikamilifu inasikilizwa na kutolewa uamuzi ndani ya kipindi kisichozidi miezi sita.
Naye Afisa TEHAMA wa Baraza hilo Bw.Athumani Kanyegezi  amewataka wananchi na wadau kutumia mfumo wa kielektroniki unaopatikana kupitia tams.fct.or.tz au tovuti ya Baraza fct.or.tz, akieleza kuwa mfumo huo ni rafiki kwa mtumiaji na umeundwa kuendana na mahitaji ya sasa ya utoaji huduma kwa njia ya kidijitali.
Amesema matumizi ya teknolojia hiyo ni sehemu ya juhudi za Baraza kwenda sambamba na mabadiliko ya kidijitali na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, huku akiwataka wananchi kutumia fursa hiyo kupata huduma kwa urahisi.
Aidha, imeelezwa kuwa uwepo wa Baraza la Ushindani unawapa wananchi fursa ya kukata rufaa pale wanapokuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya mamlaka zinazodhibiti sekta mbalimbali. Kwa mfano, mwananchi mwenye malalamiko dhidi ya kampuni ya simu anaweza kwanza kuyawasilisha katika mamlaka husika na, endapo hataridhishwa na uamuzi, anaweza kutumia fursa ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani.
Naye Mdau Vendeline Shekifu,ameeleza kufurahishwa na uwepo wa taasisi hiyo umewapa fursa ya kujifunza kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi za Serikali, ikiwemo Baraza la Ushindani.
Awali Diwani wa Kata ya Tamkaleli Clinton Manzi  amesema maadhimisho hayo yamekuwa na manufaa kwa wakazi wa Dodoma kutokana na muda walioupata kujifunza huduma na fursa mbalimbali, huku akimshukuru Rais kwa kuwezesha maadhimisho hayo kufanyika jijini Dodoma.