Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametambuliwa kuwa kinara katika kuimarisha huduma za afya ya msingi kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana nchini, hususan katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto. 

Akifungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Aya ya Msingi (IPHC) kwa niaba ya Rais Samia katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Jijini Arusha (AICC), Septemba 9, 2026, Waziri Mkuu amesema mafanikio hayo yameiwezesha Tanzania kutambulika kimataifa, ikiwemo Rais Samia kutunukiwa Goalkeeper Award mwaka 2025 na kuteuliwa kuwa kinara wa Umoja wa Afrika wa huduma za afya ya mama na mtoto mwaka 2026.

“Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya, na sasa Serikali inaelekeza nguvu zaidi katika kuboresha ubora na ufanisi wa huduma hizo,” amesema Waziri Mkuu. Ameeleza kuwa vifo vitokanavyo na uzazi duniani vimepungua kutoka takribani 328 hadi 197 kwa kila vizazi hai 100,000 kati ya mwaka 2000 na 2023, hali inayoonesha kuwa malengo ya afya yanaweza kufikiwa kwa kuongeza uwekezaji na kutekeleza mipango madhubuti.

Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kuimarisha sekta ya afya kwa kuongeza miundombinu, wataalamu na rasilimali nyingine muhimu, huku zaidi ya watumishi 16,000 wa sekta hiyo wakiajiriwa kati ya Desemba 2025 na mwaka 2026. Aidha, Serikali imejenga nyumba zaidi ya 430 za watumishi wa afya na inapanga kujenga takribani nyumba nyingine 2,000 kuelekea mwaka 2030. Amesisitiza kuwa utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote utawezesha wananchi, wakiwemo wenye kipato duni, kupata huduma bora kwa gharama nafuu na bila ubaguzi wa kipato.

Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema kati ya mahudhurio milioni 32.3 ya wagonjwa wa nje yaliyorekodiwa katika vituo vya afya vya umma, mahudhurio milioni 27.8, sawa na asilimia 86, yalikuwa katika vituo vya afya ya msingi. Aidha, kati ya vituo 8,288 vya afya vya Serikali nchini, vituo 7,946, sawa na asilimia 95.8, ni vya ngazi ya afya ya msingi vinavyomilikiwa na halmashauri. Ameongeza kuwa asilimia 96.6 ya vituo hivyo vimeunganishwa na mfumo wa GoTHOMIS na asilimia 87.6 vimeunganishwa na GePG, hatua inayoongeza ufanisi, uwazi na usimamizi wa mapato na huduma.

upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla, amesema Mkoa huo umepokea zaidi ya Sh bilioni 94 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ya msingi. Uwekezaji huo umechangia kuongezeka kwa vituo vya kutolea huduma za afya kutoka 382 hadi 450, kuajiriwa kwa watumishi wapya 823 wa kada za afya na kupatikana kwa magari 27 ya kuhudumia wananchi, hatua zilizosaidia kupunguza vifo vya akina mama na watoto.

Akizungumza kwa niaba ya asasi za kiraia zinazoshughulikia masuala ya afya nchini, Bw. Amson Mwendamake amependekeza kuimarishwa kwa ushiriki wa jamii katika kupanga, kutekeleza na kufuatilia mipango na bajeti za afya ya msingi. Pia, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ufadhili wa ndani, kuwalinda wananchi walio katika mazingira hatarishi dhidi ya gharama kubwa za matibabu na kuimarisha uwajibikaji pamoja na ushirikiano kati ya Serikali na wadau.

Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Afya ya Msingi unafanyika jijini Arusha kuanzia Septemba 9 hadi 11, 2026, ukiwakutanisha wataalamu wa kada mbalimbali za afya kwa ajili ya kujadili na kutathmini masuala ya afya ya msingi. Mkutano huo unaongozwa na kaulimbiu isemayo: “Kuelekea upatikanaji wa huduma za afya kwa wote: Kuimarisha ugharamiaji endelevu wa huduma za afya, ufanisi na uboreshaji wa huduma katika ngazi ya msingi.”













 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Tanzania inalenga kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme hadi kufikia megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030, hivyo kuna fursa kubwa kwa wawekezaji kushiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya nishati nchini.

 Amesema Serikali inakaribisha wawekezaji wenye uwezo wa kifedha, kiteknolojia na kitaalamu ili kushirikiana katika kufikia lengo hilo.

Mhe.Salome ameyasema hayo leo jijini Dodoma, katika Mji wa Serikali Mtumba, wakati alipofanya mazungumzo na watendaji kutoka kampuni ya PowerChina,  wakiongozwa na Makamu wa Rais anayesimamia Afrika Mashariki na Kusini, Bw. Yu Haian, waliofika Wizara ya Nishati kwa lengo la kujadili fursa za uwekezaji na ushirikiano katika sekta ya nishati nchini.

"Serikali inalenga kufikia ongezeko hili la uzalishaji kwa kutumia mchanganyiko wa vyanzo mbalimbali vya nishati, ikiwemo maji, jua, upepo na jotoardhi, hatua itakayosaidia kuwa na vyanzo mchanganyiko vya umeme vitakavyoimarisha usalama wa nishati na kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme kwa wananchi na shughuli za kiuchumi."  Amesema Mhe. Salome

. Amesisitiza kuwa ushiriki wa sekta binafsi ni muhimu katika kuongeza uzalishaji wa umeme na kuimarisha miundombinu ya nishati nchini.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa PowerChina anayesimamia Afrika Mashariki na Kusini, Bw. Yu Haian, amesema kampuni hiyo imevutiwa na fursa za uwekezaji zilizopo Tanzania, hususan katika maeneo ya uzalishaji, usafirishaji, usambazaji na uhifadhi wa umeme.

Bw. Yu amesema Tanzania ina rasilimali kubwa za maji, jua, upepo na jotoardhi ambazo zinaweza kutumika kuongeza uzalishaji wa umeme na kuimarisha usalama wa nishati.

 Ameeleza kuwa PowerChina imefanya utafiti kuhusu mipango ya Tanzania katika sekta hiyo na kuona fursa kubwa za ushirikiano na Serikali.

Ameongeza kuwa PowerChina ina uzoefu katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya nishati duniani, ikiwemo uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji, jua, upepo na jotoardhi, ujenzi wa njia za kusafirisha umeme pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa za kuhifadhi nishati.

Vilevile, Bw. Yu amesema PowerChina iko tayari kushirikiana na Serikali katika miradi ya nishati jadidifu, ikiwemo nishati ya jua, upepo na jotoardhi, pamoja na mifumo ya kuhifadhi umeme kwa kutumia betri na teknolojia ya pumped storage, ambayo inaweza kusaidia kuimarisha uthabiti wa gridi ya taifa




Serikali imesisitiza kuwa inaendea kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa vifaa tiba katika ngazi ya Afya ya Msingi,  ikiwa ni hatua muhimu ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya kwa wakati.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe (Mb.), wakati akitoa salamu za ofisi yake katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Afya ya Msingi unaofanyika Arusha jijini Arusha katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC).

Prof. Shemdoe amesema takwimu za mwaka 2025 zinaonesha umuhimu mkubwa wa vituo vya Afya ya Msingi, ambapo kati ya wajawazito milioni 2.09 waliojifungulia katika vituo vya afya vya umma, milioni 2 sawa na asilimia 95.6 walipata huduma katika ngazi hiyo.

Aidha, amefafanua kuwa kati ya mahudhurio milioni 32.3 ya wagonjwa wa nje katika vituo vya umma, milioni 27.8 sawa na asilimia 86 yalifanyika katika vituo vya Afya ya Msingi.

Amesema kati ya vituo 8,288 vya afya vya Serikali nchini, vituo 7,946 sawa na asilimia 95.8 ni vya ngazi ya Afya ya Msingi vinavyomilikiwa na Halmashauri.

Kwa upande wa TEHAMA, Prof. Shemdoe amesema asilimia 96.6 ya vituo hivyo vimeunganishwa na mfumo wa GoTHOMIS, huku asilimia 87.6 vikiwa vimeunganishwa na GePG, hatua inayosaidia kuongeza ufanisi, uwazi na usimamizi wa mapato na huduma.

"Ninaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuimarisha sekta ya Afya nchini kwa uwekezaji mkubwa unaondelea katika ngazi ya Afya ya Msingi," ameeleza  Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, Serikali inaendelea kuboresha mifumo ya usimamizi wa dawa na bidhaa za afya ili kuhakikisha upatikanaji wake unaimarika katika vituo vya kutolea huduma.

Prof. Shemdoe ameahidi kuimarisha usimamizi na uwajibikaji kupitia Mikoa, Wilaya na Halmashauri ili kuhakikisha uwekezaji unaofanywa na Serikali unaleta matokeo yanayoonekana kwa wananchi.

Mkutano huo unaofanyika Septemba 09 hadi 11, 2026 umefunguliwa na Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu, umelenga kujadili namna ya kuimarisha huduma za Afya ya Msingi, ugharamiaji endelevu, ufanisi, ubora wa huduma na mifumo imara ya afya ili kufikia lengo la  Afya kwa Wote.














 Na Martha Mbena na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma

Watumishi wa Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma na wa Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar, Idara ya Usimamizi Sera za Umma, wamebadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya Daftari la Kielektroniki la Taarifa za Maafisa Ununuzi na Ugavi Serikalini.

Watumishi hao wamekutana jijini Dodoma kwa ajili ya kujifunza namna ya usanifu na ujenzi wa  Daftari la Kielektroniki la Taarifa za Maafisa Ununuzi na Ugavi Serikalini (Procurement and Supplies Personnel Information System – PSPIS) ambalo hutumika kama zana ya utekelezaji wa matakwa ya Kifungu  cha  7(j) cha Sheria ya Ununuzi wa Umma Na. 10 ya Mwaka 2023, kinachoipa Wizara jukumu la kushauri kuhusu muundo, uteuzi wa Wakuu wa Vitengo vya Usimamizi wa Ununuzi na Ugavi, na kupendekeza uhamisho wa watumishi wa ununuzi na ugavi.

Akizungumza wakati wa kikao kazi hicho, Kaimu Kamishna wa Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bw. Alex Haraba, amesema kuwa Mfumo wa PSPIS ni nyenzo muhimu inayosaidia Serikali kuwa na taarifa sahihi za watumishi wanaotekeleza majukumu ya ununuzi wa umma na ugavi.

“Matumizi ya Mfumo huo yanawezesha taarifa za maafisa wa ununuzi na ugavi kukusanywa na kusimamiwa kwa ufanisi, hatua inayosaidia Serikali kufanya maamuzi kwa kuzingatia taarifa sahihi na zinazopatikana kwa wakati,” amesema Bw. Haraba.

Amesema taarifa hizo ni muhimu katika kupanga rasilimali watu, kutambua mahitaji ya kada, kujenga uwezo wa watumishi na kutoa ushauri wa kisera na kiutendaji.

Aidha, daftari la watumishi wanaofanya kazi za ununuzi na ugavi katika Vitengo vya Usimamizi wa Ununuzi (PMUs) ni nyenzo ya kiutawala inayolenga kuiwezesha Serikali kuwa na kumbukumbu sahihi, zilizohakikiwa na zinazosasishwa kuhusu watumishi hao.

Pia, katika kikao kazi hicho, wataalamu wa Idara ya Usimamizi wa Mifumo ya Kifedha na huduma za ndani, Wizara ya Fedha, walitoa maelezo kuhusu matumizi ya Mfumo wa PSPIS na namna ulivyounganishwa na Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) kama mbinu ya kuhakikisha mifumo hii inabadilishana taarifa kwa usahihi.

 

Kikao kazi hicho kimekuwa chachu ya kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu na maarifa kati ya Tanzania Bara na Zanzibar katika usimamizi wa Kada ya Ununuzi wa Umma na Ugavi, pamoja na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utendaji wa Serikali.

 


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameitaka Afrika kujenga uwezo wake wa ndani wa kugharamia, kusimamia na kuzalisha mahitaji muhimu ya huduma za afya, badala ya kutegemea misaada na mifumo ya nje kwa muda mrefu.


Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo, Jumatano Septemba 09, 2026, wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi unaofanyika jijini Arusha, ukiwakutanisha zaidi ya washiriki 2,700 kutoka mataifa 27.

Amesema Afrika inapaswa kubadili namna inavyoelewa na kutekeleza dhana ya kujenga uwezo, akisisitiza kuwa haipaswi kuishia katika miradi midogo isiyojenga uwezo wa kudumu, bali iwekeze katika uzalishaji wa dawa, vifaa tiba, teknolojia na wataalamu.

“Enzi zile nikiwa Waziri wa Fedha nilikuwa nawaambia nchi za Afrika zimeshashuhudia muda mrefu sasa wa maisha ya misaada na misaada inayoelekezwa pengine katika maeneo ambayo yanatofautiana na malengo ya ndani ya nchi kwa jina la capacity building. Capacity building. Capacity building. Na ndio tunaishia chapati, mandazi, sambusa. Hatuwekezi kitu kitakachodumu na kikawa endelevu.”

Dkt. Mwigulu amesema malengo ya ndani ya nchi yanayokwenda sambamba na malengo ya maendeleo endelevu yanapaswa kuheshimiwa na washirika wa maendeleo, ili misaada na uwekezaji viweze kuacha matokeo ya kudumu katika maisha ya Waafrika.

Amesema Tanzania inaendelea kuweka nguvu katika kuimarisha huduma za afya, ikiwemo kuongeza miundombinu, rasilimali watu na utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, ambayo Serikali imeanza kutekeleza mwaka 2026.

“Tunapozungumza kuhusu afya ya msingi, tusizungumzie tu kujenga vituo vya afya. Tujenge pia uwezo wa nchi zetu kugharamia huduma hizo, kuzalisha mahitaji yake na kutumia teknolojia zetu wenyewe,” amesema.

Aidha, amesema Tanzania imeanza kuwekeza katika uwezo wa ndani wa uzalishaji wa dawa ili kupunguza utegemezi wa misaada na kuhakikisha upatikanaji wa dawa unaendelea kuwa wa uhakika hata wakati dunia inapokumbwa na changamoto zinazoathiri minyororo ya usambazaji.

Amesema Serikali pia itaendelea kuboresha mazingira ya watumishi wa afya, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za watumishi na kuongeza ajira katika sekta hiyo.

Dkt. Mwigulu amesema mkutano huo unapaswa kuzaa hatua mahsusi zinazoweza kutekelezwa na kupimwa, badala ya kuishia katika mijadala na maazimio.

Kwa upande wake,Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya, amesema Afrika ya mwaka 2026 si Afrika ya mwaka 1960 na kwamba wakati umefika kwa washirika wa maendeleo kubadili namna wanavyoshirikiana na serikali za Afrika.

Dkt. Kaseya amesema serikali za Afrika zinapaswa kuwa na umiliki na uelewa wa rasilimali zinazotolewa kwa ajili ya afya, huku fedha za washirika zikiendana na mipango ya kitaifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa WHO, Profesa Mohammed Janabi, amesema changamoto kubwa si kukosa suluhisho, bali ni kukosa ujasiri wa kuyafadhili, nidhamu ya kuyatekeleza na uwajibikaji wa kuyadumisha.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, amesema Serikali itaendelea kuongeza uwekezaji katika afya ya msingi kwa kuwa ndiyo ngazi inayohudumia wananchi wengi zaidi.

Amesema asilimia 95.6 ya wajawazito wanaojifungua nchini wanapata huduma katika ngazi ya afya ya msingi, huku asilimia 86 ya mahudhurio ya wagonjwa wa nje katika vituo vya umma yakihudumiwa katika ngazi hiyo.

Profesa Shemdoe amesema kati ya vituo 8,288 vya afya vinavyomilikiwa na Serikali, vituo 7,946 sawa na asilimia 95.8 ni vya ngazi ya afya ya msingi, hivyo uwekezaji katika ngazi hiyo ni uwekezaji wa moja kwa moja kwa wananchi wengi.

Mkutano huo wa siku tatu unajadili namna ya kuimarisha huduma za afya ya msingi kuelekea upatikanaji wa huduma za afya kwa wote, kupitia ufadhili endelevu, ufanisi, ubora wa huduma, ubunifu, ushirikiano wa kikanda na kujenga mifumo ya afya inayostahimili majanga.















Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amemshukuru Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa uongozi, malezi na ushirikiano alioutoa katika kipindi cha zaidi ya miezi kumi walichofanya kazi pamoja katika Wizara ya Nishati.

Mhe. Salome ameyabainisha hayo leo Septemba 09,2026 wakati akizungumza waati wa kumuaga Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi mbaye awali alikuwa Waziri wa Nishati iliyofanyika katika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma.

Amesema katika kipindi cha uongozi wake amejifunza umuhimu wa upendo, kuthaminiana na kushirikiana katika kutekeleza majukumu ya Serikali, akieleza kuwa kupitia Mhe. Ndejembi ameweza kuwa moja ya Manaibu Waziri bora katika Bunge na Baraza la Mawaziri.

"Katika kipindi cha uongozi wako nimejifunza mambo matatu ikiwemo upendo na kuthaminiana  na kuwa na mahusiano mazuri, kufanya kazi kwa ushirikiano pamoja na kuwa na uthubutu wa kufanya maamuzi kwa kuangalia maslahi ya Taifa bila kujali maslahi binafsi hivyo sisi kama familia ya Nishati tunaendelea kukuombea katika majukumu yako mapya uendelee kuwa na utii na hekima katika ufanyaji kazi wako". Amesisitiza Mhe. Salome.

Amesema kupitia Uongozi wa Mhe Ndejembi viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati wataendelea kusimamia misingi iliyowekwa  katika kuendeleza Sekta ya Nishati huku akisisitiza kukamilisha kwa wakati miradi ya maendeleo aliyoicha katika uongozi wake kipindi alichokua Waziri wa Nishati.

Sambamba na hilo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini Mhe. Deogratius Ndejembi na kumpa nafasi ya kulitumikia Taifa katika ngazi za juu za uongozi, jambo lililoendelea kuimarisha uaminifu na imani kwa Wizara ya Nishati katika utekelezaji wa majukumu yake kwa maslahi ya Taifa.

Mhe. Salome ameongeza kuwa, pamoja na kuwa Mhe. Ndejembi umeondoka katika Wizara ya Nishati, tunaomba uendelee kuwa sehemu ya familia ya Wizara ya Nishati, uwe mlezi wetu na tutakapohitaji ushauri, tunaomba utupokee  na kuwaongoza, napale tunapokosea utukosoe ili tuweze kujirekebisha na kuendelea kuijenga na kuiimarisha Sekta ya Nishati nchini






 
.


 

The room comes alive as the girls settle into their groups.

Around the tables, conversations begin.

One idea leads to another as the students share their views, listen to their colleagues and work together to understand the challenges they have been given.

As part of the UNESCO-BNU project, this is learning by participation.


The girls are not sitting back and waiting for answers.

They are thinking for themselves, exchanging ideas and challenging one another as they work towards a common solution.

You can see the teamwork taking shape.


Some students speak. Others listen carefully. Ideas are added, discussed and refined.

What looks like a simple classroom discussion is becoming something much bigger—a practical exercise in critical thinking, collaboration and confidence.


And gradually, each group begins to shape its ideas into something they can share.

The discussions continue, the ideas become clearer, and the girls prepare for the next moment.

It is time to stand up and let the whole class hear what they have created together.