Na WMJJWM- Mbeya

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Mhe.Mhandisi Maryprisca Mahundi ametembelea Kituo cha Tumaini la Wazee kilichopo Kata ya Majengo Jijini Mbeya kwa lengo la kuwapa tabasamu na kuwatia moyo kwa kutoa zawadi mbalimbali.

Akiongea na Wazee zaidi ya hamsini wa Kata ya Majengo Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweka mkakati mzuri kwa ajili ya kuwasaidia wazee hususani katika huduma za afya.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mbeya Salum Manyendi amesema Serikali imedhamiria kuanza kutoa huduma za afya kwa wazee kwa kuwafuata majumbani ili kuwaondolea kadhia ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya katika zahanati, vituo vya afya na hospitali.

Mwenyekiti wa Tumaini la Wazee Moses Sanga mbali ya kushukuru kupokea msaada huo hakusita kubainisha baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee zikiwemo za baadhi ya wazee kushindwa kwenda hospitali kutokana na ukata wa fedha unaotokana na kukosa wategemezi.

Kwa sasa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Makundi Maalum ikiongozwa na Waziri Dkt. Dorothy Gwajima na Naibu wake Mhandisi Maryprisca Mahundi wanafanya ziara nchi nzima kwa lengo la kutoa faraja kwa Makundi mbalimbali wakiwemo wazee na kubaini changamoto zinazowakabili ili Serikali iweze kuzitatua.












 


Na.Ashura Mohamed -Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Bw.Joseph  Modest  Mkude amewataka wananchi wa Wilaya ya Arusha Mjini kuhakikisha kuwa wanajenga tabia ya kufanya Usafi wa mazingira katika Maeneo yao wanayoishi.

Mkude amesema kuwa ikiwa kila mwananchi atafanya Usafi katika Maeneo yake ni wazi kuwa Maeneo mengi ya Wilaya ya Arusha yatakuwa safi na Jiji la Arusha litaendelea kung'ara kitaifa kwenye eneo la Usafi wa Mazingira.

Ameyasema hayo leo katika muendelezo wa kampeni ya Usafi wa Mazingira yenye kauli mbiu isemayo," Ng'arisha  Jiji la Arusha"iliyozinduliwa na Mstahiki meya wa Jiji la Arusha mnamo Januari 02 na kuendelea leo katika hospital ya Wilaya ya Arusha iliyopo kata ya Engutoto.

"Usafi ni tabia ya mtu sasa tukianzia kufanya Usafi katika Maeneo yetu ni wazi kuwa itakuwa rahisi kwa mitaa yetu kuwa safi, hivyo kila mtu ajijengee mazoea haya ili Maeneo yake yawe safi tukiweza hivyo ni rahisi sana Maeneo ya Umma yatakuwa Safi tu"Amesisitiza Mkude

Aidha amesema kuwa Jiji lina uwezo wa kutosha kuhakikisha kuwa Halmshauri hiyo inashika nafasi ya kwanza kitaifa,katika Usafi wa mazingira,ambapo itakuwa Ajenda Mahususi kwa kuwa ni Jiji lenye Vivutio Vikubwa vya Utalii.

Pia amesisitiza kuwa swala la Usafi liende kwenye kata na kufanywa kwa Ushindani mkubwa ili kuwa na Matokeo chanya,ndani ya jamii kwa kuwa Usafi wa mazingira una faida kubwa ndani ya Jamii.

"Maeneo yasiwe hospitali tu  kama hapa hapana,kuna Maeneo ya Umma kama mito,makorongo,Masoko haya yasisahaulike tupange muda tushirikishe watu ili kila kitu kuwa sawa nimefurahi pia mmesema mtaenda nyumba kwa nyumba"Amesema Mkude

Nae James Lobikoki ni Mkuu wa kitengo Cha Uthibiti wa Taka,na Usafi wa Mazingira Jiji letu la Arusha amesema kuwa kampeni hiyo ya Usafi  ni muendelezo kuhakikisha kuwa Jiji linaendelea kung'ara,na kuhamasisha wananchi kwa kuona swalaa Usafi wa mazingira ni la kila mwananchi.

Hata hivyo ametoa rai kwa wazoa taka wa Jiji la Arusha kuendelea kufanya kazi hiyo kwa nguvu haswa katika kipindi hiki cha mvua za Vuli ili Maeneo ndani ya kataa yaendelee kuwa Safi na Salama.

Mratibu wa Kampeni hiyo ambaye ni diwani wa Viti Maalum bi.Aminata Salesh Toure,amesema awamu ya kwanza imeanza katika kata ya sokoni One katika eneo la Soko la dampo,Engutoto katika hospitali ya Wilaya na Kisha kumalizika katika soko la mbauda lililopo kata ya Sombetini kesho Januari 04,2025.

Bi.Salesh amesema kuwa madiwani wa Viti Maalum wamejipanga vema na kampeni hiyo itakwenda majumbani ili kuhakikisha wananchi wanashiriki zoezi kampeni hiyo na kuifanya Arusha kuwa salama na Safi.

Bw.Hamza Juma  Njiku ni diwani wa kata ya Engutoto amesema kuwa kila Jumamosi watakuwa wanafanya Usafi katika Maeneo mbali mbali ndani ya kata hiyo kwa kuwa Usafi wa mazingira ni Ajenda ya Serikali inayoongizwa na Raisi daktari Samia Suluhu Hassan.

 


Na.Ashura Mohamed– ARUSHA

Wananchi  zaidi 1,000 wa Jiji la Arusha na maeneo ya jirani wamenufaika na huduma za upimaji na uchunguzi wa afya bure, hususan magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo, kupitia Mpango wa Tiba Mkoba wa Dkt. Samia Suluhu Hassan (Outreach Program).

Akizungumza wakati wa zoezi hilo leo Jan 3,2025, Dkt. Kisenge amesema kambi hiyo imelenga kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa kuwapatia huduma muhimu za uchunguzi wa afya mapema,hatua ambayo itasaidia kuzuia madhara makubwa ya kiafya yanayotokana na kuchelewa kugundua magonjwa.

Huduma hizo zimetolewa na timu ya madaktari bingwa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiongozwa na Mkurugenzi wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge, ambaye ni bingwa wa magonjwa ya moyo, ambapo zoezi hilo litafanyika mkoani Arusha kwa kipindi cha siku kadhaa kuanzia tarehe 3 hadi 7.

Dkt.Kisenge amesema huduma zilizotolewa ni pamoja na vipimo vya moyo vya Echo na ECG, pamoja na vipimo vingine muhimu, vyote vikifanyika bila malipo yoyote, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya kwa wakati na kwa usawa.

“Upimaji wa mapema humsaidia mtu kugundua tatizo kabla halijawa kubwa na kuepusha madhara makubwa kama kushindwa kwa moyo, figo au kupata kiharusi,” alisema Dkt. Kisenge.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wananchi kadhaa wamebainika kuwa na matatizo mbalimbali ya moyo, ambapo wagonjwa 36 wamepatiwa rufaa ya kwenda Hospitali ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu ya kibingwa zaidi. 

Alisema baadhi yao wanahitaji kufanyiwa uchunguzi maalum wa mishipa ya damu ya moyo kwa kutumia mtambo wa Cath Lab, huku wengine wakihitaji upasuaji wa kuziba matundu ya moyo au kuanza matibabu ya shinikizo la damu.

Aidha, wananchi waliogundulika kuwa na shinikizo la damu bila wao kufahamu wamepatiwa elimu ya lishe bora, ushauri wa kitaalamu na kuanzishiwa dawa, hatua inayolenga kuwakinga dhidi ya madhara makubwa ya baadaye kama figo kushindwa kufanya kazi au moyo kuchoka.

Dkt. Kisenge amewahimiza wananchi wa Jiji la Arusha na mikoa ya pembezoni katika Kanda ya Kaskazini kuendelea kujitokeza kupata huduma za uchunguzi wa afya katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC),na vituo vingine vilivyobainishwa, akisisitiza umuhimu wa kupima afya mara kwa mara hata pale mtu anapoonekana kuwa mzima.

Katika hatua nyingine muhimu, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeingia makubaliano na Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre, ambapo hospitali hiyo itatoa huduma za magonjwa ya moyo chini ya usimamizi wa JKCI kwa kipindi cha miaka 20, huku huduma zote za upasuaji wa kibingwa zikiendelea kusimamiwa na JKCI.

Uamuzi huo umetokana na umuhimu wa Mkoa wa Arusha kama kitovu cha utalii pamoja na maandalizi ya mashindano ya AFCON, hatua itakayosaidia kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi bila ulazima wa kusafiri umbali mrefu.

Kwa sasa, wananchi wote wenye matatizo ya moyo na magonjwa mengine yasiyoambukiza wanahimizwa kufika katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre, ambayo sasa inatoa huduma hizo chini ya usimamizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete.

Nilianza kuhisi mabadiliko kwa mwenzi wangu, lakini sikuweza kueleza mara moja. Hisia za wasiwasi na shaka zilianza kunitawala kila siku. 

Nilijaribu kuzungumza mara kwa mara, lakini kila mazungumzo yalikuwa magumu na mara nyingine yaligeuka malalamiko ya kutokuelewana.

Nilisalia nikijilaumu kwa nini ningeweza kuwa na uhusiano wa amani na furaha kama wengine.
Nilijaribu njia za kawaida kama kuzungumza mara kwa mara na marafiki, lakini hakuna kilichobadilika. 

Hofu ya kupoteza mpenzi wangu na hofu ya kuumiza uhusiano ilizidi kuongezeka. Soma Zaidi..........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilihisi-mpenzi-wangu-ananisaliti-jinsi-ukweli-ulivyojitokeza-bila-kelele/
Nilijihisi nimeangushwa kabisa. Mtu ambaye nilimwamini sana aliniacha nikihisi ni mdogo, na mara kadhaa niliumizwa sana kimawazo na kimoyo.

Kila wakati nilipokumbuka kilichotokea, hasira ilinijaza, na mara nyingi nilifikiria kulipiza kisasi.

Nilijaribu kuzunguka mawazo haya, lakini kila jaribio lilishindwa. Nilipoona kuwa kulipiza kisasi kungeleta madhara zaidi kuliko faida, niliamua kutafuta njia nyingine ya kurejesha heshima yangu. Soma Zaidi.....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/niliumizwa-sana-lakini-sikuchagua-kulipiza-kisasi-njia-niliyotumia-kurejesha-heshima-yangu/
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa. Nilipanga bidhaa vizuri, nikahakikisha bei zangu ni za ushindani, lakini bado siku zilipita bila mabadiliko. Wateja walikuwa wachache sana, na wakati mwingine siku nzima ilipita bila hata mauzo moja.

Nilianza kujilaumu, nikidhani labda eneo ni baya au labda mimi sina bahati kwenye biashara.
Nilijaribu matangazo madogo madogo, nikabadili mpangilio wa duka, hata nikapunguza bei, lakini wateja walikuwa wanapita tu.Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara jirani zikiwa na wateja wengi ilhali mimi nikiwa mtupu. 

Hapo ndipo niligundua kuwa biashara si bidhaa peke yake, kuna nguvu nyingine huifanya isonge au isimame.. Soma Zaidi.......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nafungua-duka-kila-asubuhi-bila-wateja-nilichofanya-kikaanza-kuvutia-mauzo/
Kwa muda mrefu nilikaa kimya nikidhani ni mimi peke yangu niliyepitia hali hii. Kila ilipofika wakati wa tendo la ndoa, mwili wangu haukuitikia kama awali. 

Kulikuwa na ukavu uliosababisha maumivu, hofu, na wakati mwingine kuepuka kabisa ukaribu na mwenzi wangu.

Sikujua nianzie wapi kueleza kilichokuwa kinaendelea ndani yangu. Nilijilaumu, nikahisi kama nimemwangusha mwenzi wangu, na taratibu kujiamini kwangu kukapungua.
Nilidhani labda ni uchovu, mawazo, au mabadiliko ya kawaida tu.

Nilijaribu kujisaidia kwa kusoma na kusikiliza ushauri wa hapa na pale, lakini hali haikubadilika. Kadri siku zilivyopita, ndoa yetu nayo ilianza kuwa baridi. 

Nilipofikia hatua ya kuchoka kimya kimya, niliamua kutafuta msaada wa kuelewa chanzo cha tatizo, si kulifunika. Soma Zaidi.....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilianza-kukauka-wakati-wa-tendo-la-ndoa-nilipoelewa-chanzo-afya-yangu-ilibadilika/
Siku ile sitoisahau. Alitoka nyumbani kama kawaida, akaacha simu, na hakurudi tena. Masaa yakageuka siku, siku zikawa wiki. 

Nilizunguka hospitali, vituo vya polisi, na kwa marafiki bila majibu. Kila mtu alikuwa na nadharia yake, lakini hakuna aliyekuwa na uhakika.

Hofu ilinivamia, usingizi ukaisha, na kila sauti ya simu ilifanya moyo kuniruka. Nilijaribu kila njia ya kawaida. 
Polisi walifanya walichoweza, lakini hakuna dalili ya mwelekeo alikokwenda. Soma Zaidi........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilimpoteza-mtu-wangu-bila-maelezo-hatua-niliyofanya-ilimrudisha-nyumbani/

 





*Autaja mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kuhifadhi maji ya Mvua eneo la Kidete.

WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amezungumza na wakazi wa Tindiga wilaya ya kilosa mkoani Morogoro ambao wameathirika na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Mheshimi wa Dkt. Mwigulu amewaeleza wakazi hao kuwa Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ilishaanza mikakati ya kukabiliana na athari za mvua katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa morogoro kwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa Mabwawa eneo la Kidete.

Amesema kuwa ujenzi wa mabwawa hayo ya maji yatakuwa ni suluhisho la kudumu ya mafuriko katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Morogoro.

Ameongeza kuwa kwa sasa mpango huo upo katika hatua za kitalaam ikiwemo kumpata mkandarasi. ”Fedha imepatikana kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa kwa sasa tunaendelea na taratibu za kitaalam, Wizara zinazohusika hakikisheni mnakamilisha taratibu hizo ili ujenzi uanze”

 Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda lililopo Mkoani Morogoro.


Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Dkt. Mwigulu amesema kuwa mradi huo unaakisi maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nchi inakabiliana na changamoto ya upungufu wa maji hasa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Pia, ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi huo hausimami na unakamilika kwa wakati ili uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi.










 


Mbunge wa Jimbo la Lushoto Prof. Riziki  Shemdoe ameishukuru Taasisi ya The Sunshine Muslims Volunteers (SMV) yenye makazi yake jijini Dar es Salaam kwa kufadhili matibabu ya macho kwa wananchi 811 wa Lushoto, mkoani Tanga, yaliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto kuanzia tarehe 29 hadi 31 Disemba, 2025.

Miongoni mwa wananchi hao 811 wa Jimbo la Lushoto waliopatiwa huduma ya uchuguzi wa macho, 104 walifanyiwa upasuaji wa macho, 312 walipatiwa miwani ya macho na 267 walipatiwa miwani ya kujikinga na mionzi ya jua.

Kutokana na huduma hiyo, Prof. Shemdoe ameishukuru taasisi hiyo  leo Januari 01, 2026 jimboni Lushoto, wakati akizungumza na Mweka Hazina wa taasisi hiyo Dkt. Juma Mzimbiri ambaye ni Daktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili MOI.

Aidha, Mhe. Prof. Shemdoe ametoa shukrani zake za dhati kwa Daktari Bingwa wa macho na timu yake  kwa kuendesha kambi hiyo ya matibabu kwa kushirikiana wa Mganga Mkuu wa Wilaya pamoja na madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo ya wilaya ya Lushoto.

Akizungumzia diplomasia ya mashirikiano, Prof. Shemdoe amemshukuru  Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutengeneza diplomasia ya mashirikiano na nchi mbalimbali, ambayo imewezesha wananchi wa majimbo ya Lushoto, Mlalo na Bumbuli kunufaika na huduma hiyo.

“Ninawaomba wadau hawa waendelee kutoa udhamini huu wa huduma ya matibabu ya macho,   natamani uwe endelevu kila mwaka ili wananchi wengi zaidi wanufaike,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, ana imani kuwa wadau hao wataendelea kuona umuhimu wa kusaidia watu, kama ambavyo kauli mbiu yao inavyosema kuwa We Serve to Please Allah yaani wanasaidia ili kupata radhi ya Mwenyezi Mungu.

Naye, Mweka Hazina wa SMV  Dkt. Juma Mzimbiri amesema kuwa, kambi ya matibabu imekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi ambao wamejitokeza kwani wamepatiwa huduma ya uchuguzi wa macho,  upasuaji wa macho, na kupatiwa miwani za macho pamoja na za kujikinga na mionzi ya jua.

Kuhusiana na jitihada za kutafuta wadau wengine, Dkt. Mzimbiri   kumshukuru Prof. Shemdoe kwa kuendelea kushirikiana na taasisi yake ya SMV katika kutafuta wadau ambapo mdau YERYUZ DOKTORLARI alipatikana na kushiriki kutoa huduma katika kambi ya matibabu.

Kwa miaka kadhaa, Januari ilikuwa mwezi wa mateso kwangu. Nilikuwa naumwa karibu kila mwanzo wa mwaka mafua ya mara kwa mara, maumivu ya mwili, homa zisizoeleweka, na uchovu uliokataa kuisha.

Nilianza kuamini kuwa labda mwili wangu hauwezi kuvumilia mabadiliko ya msimu au presha ya mwanzo wa mwaka. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba hali hii ilinifanya nipoteze siku nyingi za kazi na kuvuruga mipango yangu.

Nilijaribu kila nilichojua. Nilikunywa dawa za kawaida, nikabadilisha mlo, na nikajaribu kupumzika zaidi. Kulikuwa na afueni ya muda mfupi, lakini Januari iliyofuata hali ilijirudia. Nilipoona hali hii inakuwa mzunguko, nilijua nilihitaji kufanya mabadiliko ya kweli, si ya kubahatisha.

Ndipo nilipopata ushauri wa kutafuta mwongozo tofauti. Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/januari-kila-mwaka-nilikuwa-naumwa-sana-nilichobadilisha-kikaanza-kunilinda/
Kupoteza kazi kulinivunja moyo zaidi kuliko nilivyotarajia. Nilikuwa na majukumu, familia iliyonitegemea, na mipango mingi ya maisha. Siku ile niliyoitwa ofisini nikaambiwa huduma zangu hazihitajiki tena, nilitoka nikiwa na kichwa kizito.

Nilipoteza amani, usingizi ukaanza kunikimbia, na hofu ya kesho ikatawala mawazo yangu.
Siku zilivyoendelea, nilijaribu kuonekana imara mbele ya watu, lakini moyoni nilikuwa nimechoka.

Kuomba kazi kuligeuka kuwa mzigo nikakataliwa mara kwa mara. Nilianza kujiuliza thamani yangu iko wapi, na kwa nini milango yote ilionekana kufungwa kwa wakati mmoja. Presha ilizidi, na nilihisi kama nimekwama mahali pamoja.

Ndipo nilipogundua kuwa nilihitaji si juhudi pekee, bali pia mwelekeo sahihi.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-amani-baada-ya-kupoteza-kazi-nilichojifunza-kilinisaidia-kuendelea-bila-kukata-tamaa/
Januari ilinipata nikiwa sina hata fedha za mahitaji ya msingi. Sikukuu zilikuwa zimepita, pesa zilikuwa zimeisha, na madeni yalikuwa yananikumbusha kila siku.

Niliamka kila asubuhi nikijiuliza nitapata wapi ya chakula, na nitashughulikaje kodi na gharama zingine zilizokuwa zinanifuata kwa kasi. Ilikuwa hali ya kuchosha kiakili na kihisia.

Nilijaribu kila nilichoweza kwa njia za kawaida. Niliomba kazi za vibarua, nikapiga simu kwa marafiki na jamaa, na hata nikajaribu kuuza vitu vidogo nyumbani. Kilichopatikana hakikutosha.

Kadri siku zilivyopita, hofu iliongezeka na kujiamini kulipungua. Nilihisi kama Januari ilikuwa inanimeza taratibu. Ndipo nilipoamua kutafuta ushauri tofauti.Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilianza-januari-bila-pesa-ya-mahitaji-hatua-moja-ilinisaidia-kusimama-tena/
Nilianza kugundua jambo lisilo la kawaida pale nilipoanza kuchoka kila siku bila sababu ya kueleweka. Niliamka asubuhi nikiwa nimechoka kama sikuwa nimelala, mchana nilihisi kulemewa na jioni sikuwa na nguvu hata za kuzungumza.

Awali nilidhani ni kazi nyingi au msongo wa mawazo wa kawaida wa maisha, lakini hali iliendelea kwa miezi. Kila nilipojaribu kupumzika zaidi, haikusaidia.

Nilianza kutumia dawa za kuongeza damu na nguvu nikiamini huenda ni upungufu wa lishe, lakini bado nilijikuta nikiwa dhaifu. Watu waliniona nikikaa kimya sana, nikiepuka mikusanyiko, na wengine wakaanza kudhani nina chuki au kiburi.

Ukweli ni kwamba mwili wangu haukuwa na nguvu, na akili yangu pia ilikuwa imechoka. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba hata vipimo vya kawaida havikuonyesha tatizo kubwa.
Siku moja niliamua kutafuta ushauri tofauti. Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nachoka-kila-siku-bila-sababu-nilipoelewa-chanzo-nguvu-zikarudi-polepole/
Kwa miezi kadhaa, nilihisi wasiwasi kila nikimuangalia mtoto wangu. Wenzake walikuwa tayari wanatembea, wanazungumza maneno ya kwanza, na kuonyesha maendeleo ya kawaida ya watoto wa umri wake, lakini wangu alionekana kuchelewa.

Kila mara nilipomuuliza kitu, alitabasamu tu bila kujibu kwa maneno, na kila hatua ndogo ya kujisimamia alikosa kufanya. Nilijawa na hofu kuwa kuna kitu kilikuwa kimekwama kwenye ukuaji wake.

Nilijaribu kumchochea kwa michezo na maneno, nikajitahidi kuzungumza naye kila siku na kumfundisha maneno mapya. Lakini maendeleo hayakuonekana kwa kasi niliyokuwa natarajia. Nilianza kuogopa kuwa huenda tatizo hili litaendelea kumzuia maisha yote yake ya awali, na hofu hiyo ilinifanya nikae usingizi mchana usiku.

Siku moja, nilipata ushauri kutoka Kiwanga Doctors. Nilipowaeleza hali yetu, walinisikiliza kwa makini na kuniuliza maswali ili kuelewa mtoto na mazingira yake vizuri.

Walinionyesha njia ya asili ya kusaidia mtoto kufikia maendeleo yake, ikijumuisha mazoezi rahisi ya kila siku, maneno ya kumtia moyo, na mbinu za kumsaidia kuimarisha misuli na mazoezi ya akili.

Nilifuata mwongozo wao kwa nidhamu na kwa usahihi. Ndani ya wiki chache, nilianza kuona tofauti. Mtoto wangu alianza kutembea hatua ndogo ndogo bila msaada, akaanza kusema maneno ya kwanza, na tabia yake ya kila siku ilibadilika.

Nilijisikia furaha isiyoelezeka kuona maendeleo yake yanapanuka hatua kwa hatua. Leo, nimefurahi kuona mtoto wangu akipata mwendo wake wa kawaida na kuonyesha vipaji vyake. Soma Zaidi..…https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mtoto-wangu-alichelewa-kutembea-na-kuongea-hatua-moja-iliibua-maendeleo-yake/

 WANANCHI Kijiji cha Laja katika Halmashauri ya Wilaya ya Karatu mkoani Arusha wameishukuru TASAF kukubali Mradi wa kupunguza Umaskini (OPEC) kutekelezwa katika Kiji hicho na kutoa fedha kutekelezwa mradi wa ujenzi wa mpya ya Shule ya Sekondari ambao umesaidia wanafunzi kuondokana na changamoto ya kutembea umbali wa kilometa nane kuisaka elimu.


Wakizungumza wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) Shedrack Mziray aliyekuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo,wananchi wa Kijiji hicho wamesema kupitia Mfuko huo wamepata shule hiyo ambayo imeondoa changangamoto wanafunzi waliokuwa wanachaguliwa kujiunga Sekondari kutembea umbali mrefu.

Mkazi wa Kijiji cha Laja Christina Lucas amesema wakati shule haijajengwa katika maeneo hayo wanafunzi walikuwa wanateseka haswa watoto wa kike ambao ndio kundi lililokuwa linaathirika kwasababu wanakutana na adha nyingi.

“Uwepo wa shule hii imepunguza utoro usio wa lazima kwasababu kwa vyovyote vile mtoto akitoka nyumbani kilometa nane njiani anakutana na changamoto nyingi ,mara nyingine wanasindikizwa na bodaboda ambao baadhi yao ni hatari kwa usalama wa wanafunzi Wetu.

“Baada ya kupata mradi huu na shule kujengwa hivi sasa watoto wanakaa katika mabweni hivyo wanakuwa salama na ndio maana mpaka sasa hakuna mwanafunzi ambaye amepata ujauzito kwani wazazi tunafuatilia sana ,watoto wako salama.

Kuhusu TASAF amesema wananchi wa Kijiji cha Laja wanaipongeza na kuishukuru lakini wanatoa ombi la kujengewa majengo ya maabara pamoja na kuongezwa nyumba za walimu kwani zilizopo hazitoshi.

“Tunatamani kama itawezekana basi Rais wetu Dk.Samia Suluhu Hassan kupitia TASAF atuone tena kwa kutujengea Maktaba,mabweni na nyumba za walimu.Pia namshukuru Rais wangu kwa kuliona hili kwani hii shule hatukutegemea ingejengwa katika maeneo haya.

“Rais wetu ni msikivu ameangalia mpaka huku kwetu ambako tulisahaulika lakini sasa ametujengea shule ya kifahari ambayo pengine ilitakiwa ijengwe hata Karatu ila kwa sasa iko kijijini kwetu.”

Kwa upande wake Andrea Mtupa amesema wanafunzi wanaofaulu kwenda kidato cha kwanza walikuwa wanatembea umbali wa kilometa nane kwenda na kilometa nane wakati wa kurudi kila siku lakini hivi sasa TASAF kupitia mradi wa OPEC wamejengewa shule ya Sekondari ya kisasa.

Awali Ofisa Mtendaji Kijiji cha Laja Daniel Mpigachai amesema mradi wa ujenzi wa shule hiyo umegharimu Sh.774,946,675, ambapo TASAF kupitia OPEC awamu ya Nne walitoa fedha Sh. 659,505,275 na fedha Sh.115,441,400 ni mchango wa jamii ambao umejumuisha mchanga,Kokoto ,mawe,maji na nguvu kazi wakati wa ujenzi.

Kuhusu manufaa ya mradi amesema shule hiyo iliyosajiliwa Novemba 2023 ilianza rasmi mwaka 2024 kwa kupokea wanafunzi 26 wa Kidato cha kwanza, kwa sasa shule ina Jumla ya wanafunzi 63 ambao ni kidato cha kwanza na cha pili na wote wanakaa Bweni.

“Uwepo wa mradi huu umeondoa tatizo la utoro shuleni, wanafunzi kuongeza morali ya kusoma tofauti na awali walipokuwa wanasoma shule ya kata iliyo na umbali wa Zaidi ya kilometa 8 kutoka kijini kwetu, shule imepokea pia watoto wanaotoka viji vya jirani.

Aidha amesema kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji cha Laja wanatoa ombi kwa TASAF kama fursa nyingine itajitokeza wanaomba mradi wa ujenzi Majengo mengine yaliyosalia kama Maabara, Maktaba, Nyumba nyingine za walimu na Madarasa.

Wakati huo huo Mkuu wa Shule ya Sekondari Laja Daniel Panga amesema shule hiyo iliyojengwa kisasa mbali kuondoa changamoto wanafunzi kutembea umbali mrefu imeleta hamasa kwa wanafunzi wanaosoma elimu ya msingi wanaamini ipo siku watajiunga na shule hiyo.






Kila mwaka Januari ilinipokea kwa hofu nzito. Siku za mwanzo za mwaka zilikuwa na changamoto zisizoelezeka, na kila jaribio la kupata mwongozo au bahati nzuri lilibebwa na vikwazo vipya.

Nilihisi kama nyota yangu ilizimika, kila jambo nzuri nililokuwa nalo likiisha haraka. Hii haikuwa tu hisia; kwa kweli nilihisi nikiwa na mizigo ya kifedha, familia, na afya ambavyo viliniondoa mwelekeo.

Nilijaribu kila njia za kawaida za kuboresha mwaka: kuomba ushauri, kupanga bajeti, hata kufanya maombi ya haraka. Lakini kila kitu kilionekana kudumu kwa muda mfupi tu, na hatimaye hali yangu ikawa mbaya zaidi.

Usiku nililala na mawazo ya hofu, na kila asubuhi nikiamka, moyo wangu ulikuwa unitetemeka kwa kuogopa changamoto zilizokuwa zikisubiri.

Nilipofikia hatua ya kukata tamaa, niligundua kwamba nilihitaji msaada wa kipekee. Soma Zaidi...
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilihisi-nyota-yangu-inazimika-kila-januari-kilichonisaidia-kuilinda-mwaka-huu/
Nilipoingia mwaka mpya, kilichoninyima amani zaidi haikuwa sherehe wala barua za matokeo mazuri, bali deni la kodi lililonisubiri. 

Nilikuwa nimetumia pesa nyingi wakati wa sikukuu, nikidhani ningeweza kuanza Januari kwa urahisi, lakini hali haikukubaliana na mipango yangu.

Mwenye nyumba alianza kunikumbusha kila wiki, na hofu ya kufungiwa nje ikawa sehemu ya mawazo yangu ya kila siku. Nilijaribu kila njia: niliomba marafiki, ndugu, nikatafuta kazi za muda, hata kuuza vitu vidogo, lakini pesa haikutosha.

Kila kitu kilionekana kunipinga. Nilihisi nimekwama, na muda ukienda mbio, nikawa na wasiwasi mkubwa kuhusu familia yangu na mustakabali wa watoto wangu. 

Usiku usingizi haukuja; kila saa nilipokuwa na macho, moyo wangu ulikuwa ukitetemeka na hofu. Soma Zaidi..
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilianza-mwaka-mpya-nikiwa-na-kodi-imenifuata-hatua-nilizochukua-kuepuka-kufungiwa-nyumbani/
Nilipoingia mwaka mpya, nilikuwa nimejaa hamasa. Niliandika malengo yangu yote; kazi, biashara, akiba, hata maendeleo binafsi. Niliahidi mwaka huu utakuwa tofauti. Lakini wiki zilipopita, hakuna kilichosogea.

Nilijitahidi, nilijipanga, nilijaribu nidhamu kali, lakini kila nilichogusa kilionekana kukwama. Nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa mimi au kuna kitu kingine kilikuwa kinanizuia.

Kadiri siku zilivyopita, nilipoteza morali. Kila nilipoangalia orodha ya malengo yangu, nilihisi mzigo moyoni. Niliona watu wakisonga, wakipata mafanikio mapema mwaka, nami nikabaki palepale.

Nilianza hata kuacha baadhi ya mipango niliyokuwa nimejipangia kwa sababu ya kuchoka moyo. Nilipotafakari kwa kina, niligundua kuwa nilikuwa nafanya kila kitu kwa nguvu nyingi lakini bila mwelekeo.

Nilihitaji msaada wa kunifanya nione kile ambacho macho yangu yalikuwa hayakioni. Soma Zaidi.........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilijiwekea-malengo-ya-mwaka-mpya-lakini-kila-kitu-kilikwama-nilipobadilisha-njia-mambo-yalisonga/