Na Oscar Assenga, TANGA



BONANZA la Michezo maarufu kama Michezo Plus limekuwa na mvuto wa aina yake huku likifanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Tanga Ufundi kwa kushirkisha wanafunzi zaidi ya 500.


Wanafunzi hao kutoka shule 50 Jijini Tanga ambao walishiriki katika Michezo ya Mpira wa Miguu,Pete na Wavu huku wakionyesha vipaji vya hali ya juu hatua iliyoshangiliwa na wadau wa michezo ambao walijitokeza kushuhudia bonanza hilo


Akizungumza baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Afisa Michezo wa Jiji la Tanga na Mratibu wa Michezo Plus katika mradi unaotekelezwa na Jiji hilo ukifadhiliwa nan a Botnar Foundation chini ya Programu ya Tanga Yetu Lucy Michael alisema kwamba waliliandaamaalumu kwa ajili ya kujenga mahusiano na kuwajenga kiakili.

Alisema kwamba bonanza hilo litakuwa linafanyika kila mwaka mara mbili ambapo hilo limeanza kwa kufungua mwaka na kukaribisha wanafunzi na watafanya bonanza la vijana.



Awali akizungumza Mratibu wa Bonanza hilo Haji Milao alisema kwamba nia na madhumuni yake ni kuwaweka watoto sawa kwa ajili ya michezo ya Umistashumta mwaka huu 2026 ikiwemo kutengeneza afya za watoto ili waweze kuwa sawa na watoto wakiwa vizuri kwenye michezo hata darasani watakuwa vizuri.



Naye kwa upande wake Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Makorora Zuhuru Ally alisema michezo hiyo ina faida kubwa sana kwao kutokana na kwamba inawafanya wakutana na wenzao na kubadilisha mawazo jambo ambalo linawapa fursa.
Maisha yangu ya ndoa yalikuwa changamoto kubwa. Nilipata hisia kuwa upendo na uaminifu vilikuwa vimepotea baada ya mke wangu kuanza kuonyesha tabia zisizo za kawaida.

Mara nyingi nilihisi huzuni, kuchanganyikiwa, na hata kujiuliza ikiwa bado tupo kwenye ndoa ya kweli. Hali ilizidi kuwa mbaya nilipoona ishara kuwa mke wangu alikuwa akitengeneza uhusiano wa siri na gateman wa nyumba.

Nilijaribu kuzungumza naye, kujaribu kuelewa, na hata kujaribu kusahau alichokuwa akifanya, lakini kila hatua ilishindwa. Hali hii ilinifanya nijisikie kukosa nguvu, huzuni, na hasira. Nilijua lazima nifanye kitu cha hekima na busara, la sivyo ndoa yangu ingeishia kudorora kabisa.Soma Zaidi.
Nilipokutana na mpenzi wangu wa sasa, nilijua moyo wangu ulikuwa umepotea kwake. Tulianza mahusiano yetu kwa upendo wa kweli, lakini nilijaribu kumtambulisha kwa familia yake na kumpa heshima ya kulipa mahari, ila alikataa kabisa.

Nilihisi hasira, huzuni, na mara nyingine kuchanganyikiwa kwa sababu nilihisi upendo wetu ulikuwa hatarini kusambaratika.

Kila siku nikiwa naye nilijisikia huzuni kidogo, nikijua kwamba familia yake ilikataa kumpa ruhusa ya kuishi pamoja bila sababu halisi.

Nilijaribu kuongea, kujaribu suluhisho, na hata kuacha kujaribu mara kadhaa, lakini kila hatua ilikuwa imefungwa na kuta zisizoonekana.

Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo upendo wetu ungeendelea kudorora.Soma Zaidi.
Siku zote nilikuwa na shauku ya vitu vya ajabu na nguvu zisizo za kawaida, lakini sikuwa na wazo lolote kuwa kitambaa ndogo kilichopewa kama zawadi kinaweza kubadilisha maisha yangu kwa namna isiyotarajiwa.

Nilipokipata, nilihisi furaha ndogo tu, lakini ghafla mambo yasiyokuwa ya kawaida yalianza kutokea katika maisha yangu. Kila siku niliona mabadiliko madogo, lakini makubwa.

Familia yangu, ambao tulikuwa tukikabiliana na migongano ya muda mrefu, alianza kuonyesha mabadiliko ya kushangaza.

Hatimaye, niligundua kuwa kitambaa hiki kilikuwa na nguvu ya kipekee, kilichoweza kufichua siri zilizofichwa, kuleta amani, na kubadilisha hatma ya familia.

Nilijaribu kutumia hekima yangu mwenyewe, lakini mambo yalikuwa magumu kuelewa. Soma Zaidi.
Nilihisi maumivu makali siku nilipopata habari kwamba mume wangu aliniambukiza ugonjwa baada ya kuhusiana na wanawake wengine bila tahadhari yoyote.

Hii ilikuwa dhihaka kubwa kwangu; si tu kwa sababu ya ugonjwa, bali pia kwa uaminifu na heshima yetu ya ndoa. Kila siku nilihisi huzuni, hasira, na kuchanganyikiwa, nikijiuliza ni jinsi gani ningeweza kumrejesha bila kuharibu maisha yangu.

Nilijaribu njia za kawaida zungumza naye, kujaribu kumuelewa, na hata kumtetea lakini hakuna kilichofanya mabadiliko. Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo mateso yangu yangeendelea na heshima yangu ingepotea milele.Soma Zaidi.
Nilipokuwa nikicheza michezo ya kubeti, nilijua hatari ilikuwa kubwa, lakini sikuwa na wazo kwamba bet moja ingeweza kunipotezea kila kitu nilichokuwa nacho.

Nilipoteza pesa zangu zote, na ghafla maisha yangu yaligeuka kuwa mateso yasiyo na mwisho. Hali hii ilinifanya nijisikie huzuni kubwa, hasira, na kushindwa kuelewa ni jinsi gani ningeweza kurekebisha hali hiyo.

Nilijaribu njia za kawaida kujaribu kubeti tena, kuomba msaada wa rafiki, na hata kuacha michezo ya kubeti lakini kila jaribio lilishindikana. Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo maisha yangu yangeendelea kuwa magumu bila mwisho.Soma Zaidi.

 


Na Mwandishi Wetu ,RUVUMA.


 


CHAMA cha National League For Democracy (NLD) kimempitisha Mhagama Hamisi Yusufu kuwania Ubunge Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma ambayo ataipeperusha Bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mdogo kufuatia Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Jenista Mhagama.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,Katibu wa NLD Doyo Hassan Doyo ambapo aliwaambia kwamba siku hiyo ni muhimu kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho kufanya maamuzi ya kiongozi wanayemtaka .

Alisema kwamba kiongozi ambaye anaweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo ni mgombea wao kutokana na uongozi uliopita kwa miaka mingi umeshindwa kuwapa maendeleo na mabadiliko katika Jimbo hilo.


Katibu huyo aliwataka wananchi hao kutokufanya makosa katika uchaguzi huo wa marudio kutokana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kufariki dunia hivyo aliwataka kumchagua mgombea anayetokana na NLD ili aweze kuwapa maendeleo makubwa.

Katika uchaguzi huo Mhagama Hamis Yusuf wa NLD atachuana na wagombea wengine akiwemo Yusuf Rashid Rai wa Chama cha AAFP,Abdallah Boniface Ngonyani wa Chama cha Makini,Hanifa Sembe Mohamed wa Chama cha UMD,Beatrice Omari Muya wa UPDP,Mapunda wa Chama cha DP,Dastan Frolian Pili wa CCK,Morice Thomas Nkongo wa TLP na Mtemi Pachoto wa UDP.


 


Mwisho.


Wadau na wawekezaji mbalimbali wameonesha nia ya kuwekeza katika sekta ya mafuta nchini Tanzania, uwekezaji ambao utachangia ukuaji wa uchumi wa nchi na kuboresha huduma ya bidhaa za nishati kwa wananchi.

Miongoni mwa wawekezaji hao ni Kampuni ya Mafuta ya India (Indian Oil Corporation Limited), yenye uzoefu mkubwa katika usambazaji wa mafuta na gesi, ambayo imeonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kampuni hiyo imeonesha nia hiyo katika kikao kilichofanyika kati yao na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba pembezoni mwa Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanayoendelea Jimbo la Goa, nchini India.

Katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa kampuni hiyo, Suman Kumar, amesema Tanzania ni soko la bidhaa nyingi ikiwemo bidhaa za nishati.

Amesema kutokana na ongezeko la mahitaji ya bidhaa kama mafuta, gesi ya mitungi na nishati linalotokana na ukuaji wa uchumi, idadi ya watu inayoongezeka na miji kukua haraka, inatoa fursa kwa kampuni za nishati kushirikiana katika usambazaji, uchakataji na huduma za nishati.

Kwa upande wake Mhe. Salome amesema “Serikali ya Tanzania inawakaribisha wawekezaji wote na ipo wazi kwa uwekezaji wa kimataifa katika sekta ya nishati, ikiwa ni pamoja na usambazaji wa mafuta na gesi ya mitungi kuendana na msukumo wa Serikali wa kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia."

Aidha Mhe. Salome amewahimiza wawekezaji hao kuona umuhimu wa kufungua matawi nchini Tanzania na kushiriki katika ununuzi wa pamoja wa bidhaa za mafuta ili kuongeza ushindani na uhakika wa upatikanaji wa mafuta ya gharama nafuu nchini.

 "Hivyo tunawakaribisha wadau wote kuja kuwekeza nchini Tanzania kupitia makubaliano ya kibiashara na kampuni zetu za ndani kulingana na sera za Tanzania na mapendekezo ya wawekezaji” amesema Mhe. Salome.

Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 30, 2026 na yamewakutanisha washiriki kutoka nchi zaidi ya 125, yakivutia wawekezaji wengi wa kigeni katika sekta ya nishati. 

Kupitia Maadhimisho hayo yamefungua fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya nishati kwa wadau na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani.










 


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 73.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 527 mkoani Tanga.

Hayo yamebainishwa leo Januari 29, 2026 Jijini Tanga na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi waliuoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

“Leo tuko hapa kwako kutambulisha Wakandarasi ambao watakuja kutekeleza mradi mkubwa wa kupeleka umeme katika vitongoji 527 katika Mkoa wa Tanga.

Wakati tunafanya nao majadiliano kuna maagizo mahususi tuliwapa na tungependa kama kiongozi wetu wa Mkoa uyafahamu. Moja tumewaelekeza wawe na timu ya kufanya kazi karibu kila Wilaya,” ameainisha Mhandisi Saidy.

Ameongeza pia, Wakandarasi hao wanatakiwa kujiepusha na vitendo vya kutoa lugha chafu, pamoja na vitendo vya rushwa wakati wanatekeleza miradi hiyo kwa wananchi.

“Ukifanya kazi kwenye mradi wa serikali unatakiwa kufanya kama mtumishi wa umma. Lugha chafu hazikubaliki. Kurubuni wanakijiji ni kitu ambacho kitapelekea kuvunja mkataba wako,” amessisitiza Mhandisi Saidy.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dadi Kolimba ameipongeza serikali kwa utekelezwaji wa mradi huo na kusema kuwa utakwenda kufungua zaidi fursa za uchumi vijijini.

“Ukiangalia kwa wakandarasi hawa wawili ambao wametambulishwa leo ambao wanaenda kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 527, jumla ya shilingi Bilioni 73.8. Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutoa fedha za kuwezesha kutekelezwa kwa mradi huu,” amesema Mhe. Kolimba huku akiwataka Wakandarasi hao kuhakikisha wanamaliza mradi huo ndai ya muda uliopangwa.

Aidha, Mhe. Kolimba ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao pindi watakapoanza kutekeleza mradi huo ili malengo yaliyowekwa na serikali yaweze kufikiwa.








Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

.....

Tanzania na Jamhuri ya Serbia zimejadili fursa za kuimarisha ushirikiano wa masuala ya kazi, ajira na maendeleo ya rasilimali watu, hususan katika Sekta ya Ujenzi na maeneo mengine muhimu ya kiuchumi.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski, walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Sangu amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kufanya mageuzi makubwa yanayolenga kukuza ajira zenye staha, kuongeza ujuzi kwa nguvu kazi na kupanua fursa za ajira kwa wananchi.

Vilevile, Mhe. Sangu alitumia fursa hiyo kueleza wataalamu na uwezo wa wafanyakazi katika nyanja mbalimbali zikiwemo uhandisi, afya, elimu, uhasibu, utawala wa biashara, uchumi, sheria, utalii na ukarimu, kilimo, TEHAMA, biashara ya kilimo na usindikaji wa mazao, anga na usafiri, ufundi mitambo, usafirishaji huduma za majumbani pamoja na fani nyingine nyingi, hivyo amesema Watanzania wanatambulika kwa bidii, unyenyekevu, maadili mema ya kazi na mtazamo chanya kazini.

Kadhalika, Waziri Sangu amemwalika Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski kutembelea Tanzania ili kujionea mikakati inayotekelezwa na Serikali katika kuimarisha soko la ajira pamoja na sera za ajira. Pia, amemkaribisha kutembelea vivutio vya utalii nchi ya Tanzania.

Kwa upande wake, Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski, amesema nchi ya Serbia ipo katika mchakato wa kufungua ubalozi nchini Tanzania ili kuendelea kukuza ushirikiano kati ya mataifa hayo. Pia alimwalika Waziri Sangu kutembelea nchi ya Serbia ili kujadili kuhusu masuala ya kazi na ajira ikiwemo fursa za ajira zilizopo nchini humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akisalimiana na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu alipokutana na kuzungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

 


Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amezipa siku 20 Viwanda vya saruji vya Tanga Cement na Twiga Cement kukutana na wanachama wa ushirika wa wachimbaji wa madini ya jasi (gypsum) kutoka Kijiji cha Makanya, Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, ili kufikia muafaka wa utaratibu wa biashara ya malighafi inayotumika viwandani humo.

Akizungumza Januari 28, 2026 wakati wa kikao cha pamoja kati ya wawekezaji hao na Serikali kupitia Wizara ya Madini, Dkt. Kiruswa alisema Serikali inalenga kuona biashara ya madini ya jasi inanufaisha pande zote, kuhakikisha viwanda vinapata malighafi kwa uendelevu huku wachimbaji na jamii zinazozunguka migodi zikinufaika kiuchumi na kimazingira. 

Alisisitiza kuwa anatoa siku 20, kufikia tarehe 20 Februari 2026, uongozi wa Kampuni inayomiliki viwanda hivyo na ushirika wa wachimbaji hao kukaa pamoja na kukubaliana namna bora ya uratibu wa biashara hiyo bila kuathiri upande wowote na kwamba kikao hicho kihusishe uongozi wa kijiji hicho na vyama vya wachimbaji ili kuweka misingi ya uwazi, haki, uhusiano na uendelevu.

Katika kuhakikisha shughuli za uchimbaji na usafirishaji wa jasi zinafanyika kwa kuzingatia Sheria na maslahi ya jamii, Naibu Waziri alielekeza kampuni hiyo kutekeleza hatua zafuatazo ambazo ni Utunzaji wa Mazingira: Kupitia upya mikataba yote waliyoingia na wachimbaji, na kuhakikisha utunzaji wa mazingira unazingatiwa ipasavyo wakati wa uchimbaji wa madini ya jasi sambamba na kufukia mashimo yaliyoachwa wazi.

Hatua nyingine ni barabara inazoelekea maeneo ya uchimbaji ambayo kwa sasa ni mbovu inapaswa ifanyiwe ukarabati wa haraka ili kurahisisha usafirishaji na kupunguza athari kwa jamii ikiwemo vumbi kali pamoja  kuagiza mizigo ya madini ya jasi kununuliwa kwa watu wanaotambulika na kuthibitishwa na uongozi wa kijiji husika, ili kudhibiti migogoro na kuongeza uwajibikaji.

Pia, Dkt. Kiruswa alielekeza viwanda hivyo kutekeleza kikamilifu Miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa kuwa vinachukua malighafi kutoka katika kijiji hicho na kwamba wanapaswa kuchangia huduma za jamii kama elimu, afya na maji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ununuzi (Procurement Director) wa Kanda ya Afrika Mashariki anaesimamia Tanzania, DRC, Msumbiji na Afrika Kusini chini ya Heidelberg Materials, ambao ni wamiliki wa viwanda hivyo Ahmed Ali, alisema kuwa uongozi wa viwanda hivyo utaitisha kikao cha pamoja na wachimbaji hao wa jasi sambamba na wadau muhimu kwa ajili ya kushughulikia suala hilo na kwamba Kampuni italeta mrejesho Serikalini kama ilivyoelekezwa kufanyika ndani ya siku 20.

Mbunge wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiuliza swali la nyongeza leo Januari 29,2026 bungeni jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna, Dodoma

Mbunge wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amehoji mpango wa Serikali wa kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mlandizi–Mzenga–Maneromango kwa kiwango cha lami, akisisitiza kuwa ni barabara muhimu kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni, Dkt. Jafo amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 70.2 inaanzia Mlandizi kupitia Mzenga hadi Maneromango, na kwamba tayari upembuzi yakinifu umekamilika.

Ameeleza kuwa kwa sasa mkandarasi ameanza kazi katika kipande cha Mzenga chenye urefu wa mita 300, hali iliyomfanya kuihoji Serikali kuhusu mpango wake wa kuongeza fedha katika bajeti ya mwaka huu ili kufungua kipande cha Mlandizi hadi Mzenga.

“Nini mpango wa Serikali katika bajeti ya mwaka huu kuongeza fedha ili kuhakikisha barabara hii muhimu inaanza kujengwa kuanzia Mlandizi hadi Mzenga?” amehoji Dkt. Jafo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema Serikali tayari imeonesha nia ya dhati ya kuijenga barabara hiyo, akibainisha kuwa kutokana na ukubwa na umuhimu wake, lazima ijengwe kwa kiwango cha lami.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutenga na kuongeza fedha kadri zinavyopatikana, ili kuhakikisha ujenzi wa barabara hiyo unaendelea hadi kukamilika kwa kiwango kilichokusudiwa.



Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Mwanza unaendelea na utekelezaji wa miradi 71 inayoendelea kujengwa katika wilaya mbalimbali ambapo ikikamilika inatarajiwa kupandisha wastani wa huduma ya maji vijijini mkoani humo kutoka wastani wa asilimia 73 ya sasa hadi kufikia asilimia 88 hivyo kuendelea kuimarisha uchumi wa mtu mmoja na jamii kwa ujumla.

Miradi hiyo inatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 151 kutoka vyanzo mbalimbali vya fedha ikiwemo Serikali Kuu, Programu ya lipa kwa matokeo (PforR) na Mfuko wa Taifa wa Maji.

Hayo yameelezwa na Meneja wa RUWASA mkoa wa Mwanza Mha. Godfrey Sanga wakati wa ziara ya timu ya Menejimenti ya taasisi hiyo kutoka Makao Makuu inayofanya tathimini ya uendeshaji wa huduma ya maji vijijini inayotolewa na Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) kote nchini.

Mha. Sanga alisema miradi hiyo ipo katika hatua tofauti za ujenzi ikiwemo mradi wa maji wa Ukiriguru wenye vijiji 19, na Ilujamahate-Buhingo utakaohudumia vijiji 16, na kwamba itakapokamilika itainua huduma kufikia vijiji vingi zaidi mkoani humo na kuendelea kukamilisha dhamira ya serikali ya kumtua mama wa kijijini ndoo kichwani.
Katika siku ya kwanza mkoani Mwanza, timu ya Menejimenti ya ukaguzi na tathimini ya kazi za CBWSO ilitembelea Chombo cha Nyamwaki kilichopo wilayani Magu na Miswaso kilichopo wilaya ya Kwimba ambapo zoezi hilo litaendelea katika wilaya za Misungwi na Segerema.





 -Rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri ipo Tayari : Dkt. Kiruswa

Na Wizara ya Madini, Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Madini inaendelea na mchakato wa kuanzisha Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania (Tanzania Geoscientists Registration Board – TGRB), ambapo kwa sasa ipo katika hatua ya kukusanya maoni na mapendekezo ya wadau kabla ya kuanzishwa rasmi kwa bodi hiyo.

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amesema hayo leo Januari 28, 2026, Bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Bukene, Mhe. Stephano Luhende, aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanzisha bodi hiyo ili kuongeza ufanisi katika sekta ya madini nchini.

Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa baadhi ya taratibu tayari zimekwisha tekelezwa, ikiwemo uandaaji wa rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri kuhusu kuanzishwa kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania.

Amefafanua kuwa kwa sasa Wizara ya Madini inaendelea na zoezi la kukusanya na kuchambua maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu masuala yatakayowezesha bodi hiyo kuanzishwa na kujiendesha kwa ufanisi, ikiwemo masuala ya uendeshaji na vyanzo vya fedha.

Ameongeza kuwa mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ukusanyaji na uchambuzi wa maoni, Wizara itawasilisha waraka huo katika ngazi za maamuzi za Serikali, ambazo ni kikao cha kitaalamu cha Makatibu Wakuu na kikao cha Baraza la Mawaziri, kwa ajili ya kujadiliwa na kupata ridhaa ya kuanzishwa rasmi kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania.

Nilijikuta katika wakati mgumu wa ndoa yangu baada ya tofauti kubwa kibiashara. Nilipoteza mwelekeo mzuri na mke wangu kutokana na migongano ya mali, mapato, na maamuzi ya kifedha.

Kila siku ilikuwa vita ya maneno, huzuni, na hata kukata tamaa. Nilihisi kuwa upendo wetu ulikuwa ukipotea, na kwa mara ya kwanza nilijisikia kutokuwa na maana nyumbani mwangu.

Nilijaribu kuzungumza naye, kujaribu suluhisho la kawaida, na hata kuomba msamaha kwa mambo madogo, lakini hila zetu za kibiashara zilikuwa kubwa na hazikubadilika.

Ndoa yetu ilianza kuathirika, na hofu ya kuachana kweli ilianza kuibuka kila siku. Nilijua lazima nifanye kitu tofauti, cha hekima na busara, la sivyo upendo wetu ungeharibika kabisa.Soma Zaidi.
Siku zote nimeamini kuwa mtu anaweza kupotea kwa muda na kurudi bila shida. Lakini nilipokabiliana na hali halisi, niligundua kuwa kupotea kwa mpendwa wangu kulileta hofu isiyoelezeka.

Rafiki yangu wa karibu alitoweka ghafla, bila onyo au ujumbe wowote. Kila siku ilikuwa changamoto, nikijaribu kumtafuta kwa marafiki, polisi, na hata mitandao ya kijamii, lakini kila njia ilishindikana.

Maumivu na hofu vilipanda kila siku. Nilihisi kuchanganyikiwa, kuumizwa kiasili, na aibu kubwa. Nilijua kwamba ni lazima nifanye kitu kisicho cha kawaida, kitu cha busara na hekima, la sivyo labda ningepoteza tumaini kabisa.Soma Zaidi.
Rafiki yangu alikuwa akiteseka kwa muda mrefu kutokana na asthma. Kila pumzi ilikuwa changamoto, kila mchango wa hewa ulileta maumivu, na maisha yake yalikuwa magumu.

Mara nyingi alikuwa amekosa usingizi wa kutosha, kuondoa uchovu, na hata kushiriki kikamilifu katika shughuli za kila siku. Hali hii ilimfanya kuwa na huzuni na kutokuwa na matumaini, na familia yake walihisi uchungu mkubwa kumwona akiteseka.

Tumejaribu kila njia ya kawaida dawa za hospitali, masharti ya kula vizuri, na mbinu za kawaida za kupumua lakini hakuna kilichofanikisha kupona. Nilijua lazima tufanye kitu tofauti, kitu cha hekima na busara, la sivyo mateso yake yangekuwa endelevu.Soma Zaidi.