Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Yusuf Masauni, amelitambua na kulipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa nafasi yake muhimu kama Mlezi na mdau wa kitaasisi wa Tanzania Green Summit.





Na; Mwandishi Wetu- Dar es Salaam

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Makatibu Wakuu kutoka katika Wizara zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), Wakuu wa Taasisi pamoja na Wakurugenzi wa Sekta, pamoja na wataalam kutoka katika sekta hizo na Ujumbe Kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mtaa wa Magogoni Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Septemba 2026.

Kikao hicho kimefanyika baada ya ziara maalumu ya wataalamu kutoka IFAD na AFDP kukamilisha ziara ya kutembelea maeneo yanayotekeleza Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi ya kupima matokeo utekelezaji wa program ya muda wa kati (MTR)


Pamoja na mambo mengine IFAD wamepongeza Serikali kwa Kusimamia vyema Shughuli za Programu kwa kuleta matokeo chanya kwa wananchi..Aidha kikao hicho kimepokea wasilisho la dondoo lnayoainisha hoja za makubaliano yaliyopendekezwa kuhusiana na mwenendo wa utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP).



 Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashiriki katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la Maadili ya Akili Unde linaloendelea mjini Riyadh, Saudi Arabia, likiwakutanisha wawakilishi kutoka nchi mbalimbali duniani kujadili namna ya kuhakikisha maendeleo na matumizi ya akili unde yanaongozwa na maadili, uwajibikaji na kuhudumia maslahi ya jamii.

Jukwaa hilo linatoa nafasi kwa nchi na wadau mbalimbali kubadilishana uzoefu na kujadili masuala yanayohusu mustakabali wa akili unde, ikiwemo namna ya kuimarisha mifumo ya sera na utawala, kujenga uwezo na kuhakikisha teknolojia hiyo inatumika kwa kuzingatia haki za binadamu, usalama, usawa na uwajibikaji.

Kwa Tume ya Taifa ya UNESCO, ushiriki huo ni sehemu ya kuendelea kuunganisha Tanzania na UNESCO katika mijadala na ajenda za kimataifa zinazohusu sayansi, teknolojia, elimu, utamaduni na maendeleo ya jamii.

Tume inawakilishwa katika jukwaa hilo na Bi Fides Mallya, Afisa Programu kutoka Sekta ya Sayansi Jamii ya Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anayeshiriki katika shughuli na mijadala mbalimbali inayoendelea katika jukwaa hilo.

TUME YASHIRIKI MJADALA WA AFRIKA

Katika jukwaa hilo, Tume ya Taifa ya UNESCO inashiriki pia katika mjadalawa viongozi na wadau kutoka Afrika unaolenga kujadili namna bara hilo linavyoweza kuwezeshwa ili kunufaika kikamilifu na maendeleo ya teknolojia ya akili unde.

Mjadala huo unaangazia umuhimu wa Afrika kuimarisha uwezo wake katika sayansi, teknolojia, utafiti, ubunifu na ujuzi wa kidijitali, pamoja na kujenga mazingira bora ya kisera na kitaasisi yatakayowezesha matumizi salama na yenye tija ya akili unde.

Kwa kushiriki katika mjadala huo, Tume inaendelea kufuatilia mwelekeo wa kimataifa kuhusu akili unde na kuchangia katika mijadala inayolenga kuhakikisha maendeleo ya teknolojia hiyo yanazingatia mahitaji ya jamii na yanachangia maendeleo jumuishi na endelevu.

USHIRIKI WA TUME WAIUNGANISHA TANZANIA NA UNESCO

Ushiriki wa Tume katika jukwaa hilo unaonesha nafasi yake muhimu kama kiungo kati ya Tanzania na UNESCO, kwa kuwezesha ushiriki wa nchi katika mijadala, programu na ajenda za UNESCO katika ngazi ya kimataifa.

Kupitia majukwaa hayo, Tume inaendelea kufuatilia maendeleo na mwelekeo wa kimataifa katika maeneo ya UNESCO, kubadilishana uzoefu na nchi nyingine na kutafuta fursa za ushirikiano zinazoweza kuchangia maendeleo ya Tanzania.

Katika eneo la akili unde, ushiriki huo unaipa Tume fursa ya kufuatilia mijadala kuhusu maadili, utawala na matumizi yanayowajibika ya teknolojia hiyo, huku ikiendelea kuhusisha mijadala ya kimataifa na mahitaji ya maendeleo ya Tanzania.

UJUMBE WA TUME WAKUTANA NA BALOZI

Katika mwendelezo wa ushiriki wa Tume katika jukwaa hilo, ujumbe wa Tanzania unaoshiriki katika shughuli za jukwaa umepata fursa ya kufanya kikao na Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia.

Kikao hicho kimekuwa fursa ya kubadilishana taarifa kuhusu ushiriki wa Tanzania katika jukwaa hilo na kuimarisha uratibu kati ya ujumbe wa Tanzania na Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia katika masuala yanayohusu shughuli za kimataifa.

Jukwaa la Nne la Kimataifa la Maadili ya Akili Unde linaendelea mjini Riyadh likiwa sehemu ya juhudi za kimataifa za kuimarisha ushirikiano katika kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanaenda sambamba na maadili, uwajibikaji, haki za binadamu na maendeleo jumuishi.


 

Mratibu wa Mafunzo ya Kidijitali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Eng. Joyce Baravuga, amesema mafanikio ya Mradi wa Kuziba Pengo la Kidijitali: Kuhakikisha Elimu ya Ujuzi wa Kidijitali Inayozingatia Usawa wa Kijinsia kwa Wanawake na Wasichana (Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls) yatategemea kwa kiasi kikubwa utayari wa shule kuendeleza mafunzo na shughuli za Klabu za TEHAMA (ICT Clubs) baada ya kumalizika kwa Kambi ya Mafunzo (Boot Camp).

Eng. Baravuga amewapongeza wakuu wa shule zilizochaguliwa kushiriki katika programu hiyo, akisema utayari na uthubutu wa shule ni miongoni mwa vigezo vilivyozingatiwa katika uteuzi.

Amesema shule hizo zinapaswa kuwa wadau muhimu wa programu hiyo kwa kuhakikisha maarifa na ujuzi unaopatikana kupitia mafunzo unaendelea kutumika shuleni na kuwafikia wanafunzi wengine.

Amewataka walimu na wakuu wa shule kuhakikisha Klabu za TEHAMA zinaendelea baada ya wanafunzi kurejea shuleni, ili kuwapa wasichana nafasi ya kuendelea kujifunza, kufanya mazoezi na kuendeleza ubunifu wao katika teknolojia.

Aidha, amewataka walimu, hususan wanaohusika na TEHAMA, kushiriki kikamilifu katika mafunzo hayo na kuhakikisha maarifa yanayopatikana hayabaki kwa wanafunzi walioshiriki pekee, bali yanawafikia wanafunzi wengine shuleni.

Eng. Baravuga pia amesisitiza umuhimu wa kukusanya taarifa za utekelezaji wa shughuli za mafunzo kila siku, akisema taarifa hizo zitasaidia kupima mafanikio ya programu, kubaini changamoto na mapungufu, pamoja na kuweka msingi wa kuboresha utekelezaji katika hatua zijazo.

Amesema ukusanyaji wa taarifa kwa wakati utasaidia pia kutambua maeneo yanayohitaji kupewa msukumo zaidi na kuhakikisha malengo ya programu yanafikiwa.

Vilevile, amesisitiza umuhimu wa wanafunzi kuchaguliwa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa bila upendeleo, ili kuhakikisha fursa zinazotolewa kupitia programu hiyo zinawafikia walengwa kwa usawa.

Eng. Baravuga amesema ushiriki wa shule, walimu na viongozi wa shule ni muhimu katika kuhakikisha Kambi ya Mafunzo haibaki kuwa tukio la muda mfupi, bali inakuwa mwanzo wa kujenga mazingira endelevu ya kujifunza, kutumia na kubuni kupitia TEHAMA miongoni mwa wanafunzi.

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeonya wananchi kuhusu matumizi ya vipodozi visivyo salama, likisema bidhaa hizo zinaweza kusababisha madhara makubwa kiafya, ikiwemo magonjwa sugu kama saratani.

MOROGORO: Wasichana kutoka shule 10 za Mkoa wa Morogoro kesho wanaingia katika Kambi ya Mafunzo (Boot Camp) ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), wakiwa na lengo la kujifunza, kubuni na kutumia teknolojia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika maisha ya kila siku.

Kambi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuziba Pengo la Kidijitali: Kuhakikisha Elimu ya Ujuzi wa Kidijitali Inayozingatia Usawa wa Kijinsia kwa Wanawake na Wasichana (Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls), unaotekelezwa na UNESCO kwa ufadhili wa Chuo Kikuu cha Beijing Normal (BNU), kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo, leo wadau wa mpango huo wamekutana katika Ukumbi wa Odema Hotel, Morogoro, kwa kikao cha maandalizi kilicholenga kuweka mikakati ya kuhakikisha mafunzo hayo yanaacha matokeo yanayoendelea hata baada ya wanafunzi kurejea shuleni.

Mradi huo unalenga kuongeza fursa kwa wasichana kupata ujuzi wa kidijitali, kuwajengea hamasa na uelewa kuhusu masomo na taaluma za TEHAMA, pamoja na kukabiliana na mitazamo ya kijinsia inayoweza kuwafanya wasichana kuona teknolojia kama eneo linalohusishwa zaidi na wavulana.

Miongoni mwa maeneo muhimu ya utekelezaji wa mradi huo ni kuimarisha uwezo wa walimu, kuongeza fursa kwa wasichana kujifunza ujuzi wa kidijitali, pamoja na kuanzisha na kuimarisha Klabu za TEHAMA (ICT Clubs), malezi na ushauri wa kitaalamu (mentorship) na shughuli za ubunifu.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Faith Shayo amesema msisitizo wa mafunzo hayo si kuwapatia wasichana maarifa ya TEHAMA kwa muda mfupi, bali kuwajengea hamasa na shauku ya kuendelea kujifunza na kutumia teknolojia.

Amesema hatua hiyo ni muhimu katika kuwafanya wasichana waone kwamba TEHAMA inaweza kuwa sehemu ya maisha yao, masomo yao na njia ya kutengeneza suluhisho kwa changamoto zinazowazunguka. “Lengo ni kuwajengea hamasa watoto wa kike ili waweze kupenda masomo ya sayansi na kuona uwezo wa TEHAMA katika teknolojia,” amesema Dkt. Shayo.

Amesema jumla ya wasichana 500 wanalengwa kunufaika na mpango huo, huku akisisitiza kuwa Kambi ya Mafunzo ya wiki hii si mwisho wa programu.

Baada ya mafunzo, wanafunzi watarudi katika shule zao na kuendelea na shughuli za Klabu za TEHAMA, huku wataalamu wakiendelea kuzifuatilia shule hizo na walimu pamoja na wakuu wa shule wakitarajiwa kusimamia mwendelezo wa klabu hizo.

Kwa kuzingatia nafasi kubwa ya kilimo katika Mkoa wa Morogoro, wanafunzi watatumia ujuzi watakaoupata kubuni suluhisho linalolenga sekta hiyo.

Miongoni mwa ubunifu unaotarajiwa kuwasilishwa ni Mkulima Mahiri (Smart Farmer), mfumo unaolenga kutumia Akili Bandia (Artificial Intelligence – AI) kumsaidia mkulima kutambua tatizo linaloweza kuikabili mimea.

Kupitia mfumo huo, mkulima ataweza kupiga picha ya mmea kwa kutumia simu, kisha mfumo kuchambua picha hiyo na kumsaidia kubaini tatizo linaloweza kuwa limeathiri mmea.

Ubunifu mwingine utahusu mfumo wa kuripoti matukio na changamoto zinazowakabili wananchi, ikiwemo matatizo ya maji, barabara na huduma nyingine muhimu katika jamii.

Kwa kufanya hivyo, Kambi hiyo inalenga kuwatoa wanafunzi katika nafasi ya kuwa watumiaji wa teknolojia pekee na kuwajengea uwezo wa kuwa wabunifu na watatuzi wa changamoto kupitia TEHAMA.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia amesema Wizara ina jukumu la kuandaa sera na miongozo, lakini utekelezaji wa sera hizo unahitaji ushirikiano wa wadau mbalimbali.

Ameishukuru UNESCO, BNU, wawezeshaji kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) pamoja na viongozi wa shule kwa kushiriki katika mpango huo, akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha wasichana wanapata fursa sawa za kujifunza na kutumia TEHAMA.

Amesema jamii inapaswa kuacha mitazamo inayoweza kuwafanya watoto wa kike waachwe nyuma katika matumizi ya teknolojia na badala yake kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika masomo ya sayansi na TEHAMA.

Kwa upande wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Eng. Joyce Baravuga, Mratibu wa Mafunzo ya Kidijitali (E-Learning Coordinator), amesema programu hiyo ni hatua muhimu katika kuimarisha elimu ya kidijitali nchini.

Amepongeza wakuu wa shule zilizochaguliwa kushiriki, akisema utayari na uthubutu wa shule ni miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika uteuzi huo.

Eng. Baravuga amewataka walimu na wakuu wa shule kuwa wadau wakuu wa mpango huo kwa kuhakikisha Klabu za TEHAMA zinaendelea baada ya wanafunzi kurejea shuleni na kwamba maarifa yanayopatikana yanawafikia wanafunzi wengine.

Aidha, amewataka walimu na wawezeshaji kukusanya taarifa za utekelezaji wa shughuli za mradi kila siku ili kuwezesha kupima mafanikio, kubaini mapungufu na kutoa msingi wa kuboresha programu katika hatua zijazo.

Amesisitiza pia umuhimu wa wanafunzi kuchaguliwa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa bila upendeleo, ili kuhakikisha fursa zinazotolewa zinawafikia walengwa kwa usawa.

Mradi wa Kuziba Pengo la Kidijitali unalenga pia kuongeza uelewa wa walimu, wazazi, viongozi wa shule na jamii kuhusu umuhimu wa ushiriki wa wasichana katika elimu na taaluma zinazohusiana na TEHAMA.

Morogoro ni miongoni mwa maeneo yanayolengwa katika utekelezaji wa shughuli za mradi huo, pamoja na Dodoma.

Kesho, macho yanaelekezwa Shule ya Sekondari Kilakala, ambako wasichana kutoka shule 10 wataanza rasmi Kambi ya Mafunzo, wakibeba si tu matarajio ya kujifunza TEHAMA, bali pia nafasi ya kuonesha kwamba teknolojia inaweza kuwa nyenzo ya kubadili maisha na kutatua changamoto za jamii.

Kwa mradi huu, kuziba pengo la kidijitali hakumaanishi kuwapa wasichana teknolojia pekee, bali kuwapa maarifa, ujasiri na nafasi ya kuitumia teknolojia kuunda mustakabali wao.

MOROGORO, September 14, 2026: The journey to equip girls with the digital skills, confidence and opportunities they need to participate in the technology-driven future has moved to Morogoro.

Following the official launch of the UNESCO-BNU ICT Clubs programme in Dodoma on September 7, 2026, UNESCO, in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, today launched the Morogoro phase of the initiative, which will run from September 14 to 18, 2026.

The programme is being implemented under the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls,” aimed at addressing the gender gap in digital education and expanding opportunities for women and girls to participate meaningfully in the digital economy and technology sector.

The Morogoro phase builds on the experience gained in Dodoma, where participating students were introduced to practical digital learning and innovation through ICT Clubs.

Rather than limiting technology education to theory, the programme gives girls opportunities to learn by doing—developing skills in coding, computational thinking, problem-solving, digital creativity, visual and audio content production, and the safe and responsible use of technology.

The experience in Dodoma demonstrated the value of creating spaces where girls can explore technology, ask questions, experiment with ideas and develop solutions to real-life challenges.

More importantly, the initiative seeks to nurture confidence and aspiration, enabling girls to see technology not simply as something they consume or use, but as a field in which they can create, innovate and build careers.

Speaking during the Morogoro launch, UNESCO Tanzania Head of Education Sector, Dr Faith Shayo, encouraged girls to take advantage of the opportunities provided through the ICT Clubs and to challenge perceptions that technology-related learning and careers are primarily for boys.

She emphasized the importance of creating learning environments where girls feel confident to experiment, make mistakes, ask questions and develop their abilities in technology.

The message is clear: girls should not only be users of technology; they should also be creators, innovators and future leaders in the digital world.

FROM LEARNING TO CREATING

Through the ICT Clubs, students are expected to gain practical experience while developing creativity, collaboration, problem-solving and leadership skills.

The programme will also connect girls with women ICT professionals through mentorship, giving them opportunities to learn from their experiences and gain a broader understanding of education, employment and career pathways in the technology sector.

For a girl writing her first line of code, developing a digital idea or using technology to solve a community problem, such experiences can represent more than a new skill.

They can be the beginning of a new ambition.

The ambition to become a programmer, engineer, developer, digital creator, entrepreneur, innovator—or a future leader in technology.

ICT INNOVATION BOOTCAMP STARTS TOMORROW

The Morogoro programme continues tomorrow, September 15, 2026, with an ICT Innovation Bootcamp at Kilakala Secondary School, a girls’ school.

The Bootcamp will provide participants with hands-on opportunities to strengthen their digital skills, develop innovative ideas and work collaboratively on technology-based solutions to real-life challenges in their communities.

The activities will reinforce the programme’s emphasis on practical learning, creativity and innovation, while encouraging girls to explore their potential in ICT.

The Morogoro activities will continue through September 18, 2026.

A SHARED COMMITMENT

The initiative is being implemented in collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), and the Tanzania Institute of Education (TIE).

Across Dodoma and Morogoro, the programme is expected to strengthen ICT Clubs in 20 public schools, directly benefiting 500 girls and 40 teachers.

The ICT Clubs are intended to provide safe, inclusive and supportive learning environments where students can develop digital skills, creativity, leadership and collaboration, while gaining greater awareness of opportunities in ICT-related education and careers.

As the programme moves from Dodoma to Morogoro, the goal remains the same: to ensure that girls are not left behind in the digital transformation.

They must have the opportunity to learn technology.

They must have the confidence to use it.

They must have the freedom to create with it.

And they must have the opportunity to build their future through it.

From Dodoma to Morogoro, the journey continues—one girl, one skill and one digital opportunity at a time.

The future of technology needs girls. Let us give them the skills, confidence and opportunity to build it.

#UNESCO #BNU #GirlsInICT #ICTClubs #DigitalSkills #DigitalEducation #GirlsInTechnology #ClosingTheDigitalDivide #Morogoro #Tanzania

Jina langu ni Halima. Kuingia kwenye ndoa na kuishi miaka nenda rudi bila kupata mtoto ni jaribu zito linaloweza kumvua mwanamke amani, heshima, na furaha ya moyo wake.

Kwa zaidi ya miaka saba tangu niolewe, tulikuwa tukihangaika usiku na mchana mimi na mume wangu kutafuta mtoto wa kulea na kumpa upendo wetu, lakini tumbo langu lilibaki tupu.

Maneno ya chini chini kutoka kwa ndugu, kejeli za majirani, na mabadiliko ya taratibu kutoka kwa mume wangu yalianza kuninyonga nafsi.

Kila nilipotembea mtaani nilionekana kama mtu mwenye mikosi, na hofu ya ndoa yangu kuvunjika au mume wangu kuamua kuoa mke mwingine ilikuwa ikinikesha usiku kucha na machozi.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na kupoteza matumaini ya kuwahi kuitwa “mama”, bibi yangu mzaa mama alinitembelea kijijini.

Baada ya kunikuta nikiwa nimejikunyata kwa huzuni, alinishika mkono na kunieleza kwa dhati kuwa matatizo mengi ya uzazi na vifungo vya tumbo hutibiwa na kupona kabisa kwa kutumia tiba za asili na mitishamba ya babu zetu. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Hassan. Kufanya kazi kwa bidii na kujitoa kwa moyo wote katika kampuni au asasi kwa miaka mingi bila kuonekana thamani yako ni jambo linalokata tamaa na kuua morali ya maisha.

Kwa zaidi ya miaka nane, nilikuwa nikijituma usiku na mchana katika nafasi yangu ya kazi, nikitimiza wajibu wangu kwa uaminifu mkubwa na hata kufanya kazi za ziada ili kuleta matokeo mazuri.

Hata hivyo, kila fursa ya kupandishwa cheo au kuongezwa mshahara ilipowadia, mabosi wangu walinipita na kuwapa nafasi hizo watu wapya au wale waliokuwa na majungu na fitina.

Nilibaki nikitazama wenzangu wakipiga hatua, huku mimi nikiishia kupokea mshahara mdogo usiotosheleza hata mahitaji ya msingi ya familia yangu.

​Nikiwa kwenye majuto na msongo mkubwa wa mawazo nikifikiria kuacha kazi, kaka yangu mkubwa alinitembelea.

Baada ya kumsimulia dhuluma na kusahaulika huko kazini, alinieleza kwa huruma kuwa mara nyingi hali ya kuziba kwa nyota ya mafanikio na kutoonekana thamani kazini hutokana na fitina za kishirikina au vifungo kutoka kwa wafanyakazi wenzako wenye wivu. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Asha. Kufikisha miaka ya ukubwani bila kuwa na mwenzi wa maisha wala dalili za kuanzisha familia ni jaribu linaloweza kukuletea simanzi na kukuondolea furaha ya nafsi.

Kwa miaka mingi, nilikuwa nikitamani kupata mtu mwenye mapenzi ya dhati wa kujenga naye maisha ya ndoa, lakini kila mahusiano niliyoyaanzisha yalikuwa yakiishia njiani bila sababu za msingi.

Wanaume walijitokeza na kuahidi mambo makubwa, lakini punde tu walipopata walichotaka, walipoteza hamu na kutoweka kabisa, wakiniacha na maumivu moyoni na maswali yasiyo na majibu.

Nilibaki nikishinda na huzuni huku marafiki zangu wote wakifunga ndoa na kupata watoto, mimi nikionekana kama mtu aliyeandikiwa kuishi peke yake.

​Nikiwa kwenye majuto na kuanza kukata tamaa kabisa ya kupata mume wa ndoto zangu, shangazi yangu aliyekuwa akitambua mateso yangu ya muda mrefu alinitembelea.

Baada ya kumweleza jinsi nilivyokuwa nikidhulumiwa kimapenzi na kuachwa, alinieleza kwa huruma kuwa mara nyingi mkosi wa kukataliwa au kukosa bahati ya ndoa hutokana na vifungo vya kishirikina na mikosi ya kimaisha iliyowekwa ili kukuharibia nyota yako. SOMA ZAIDI.
CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Mwaka wa 2026 wa Alliance for African Partnership (AAP), utakaowakutanisha viongozi wa vyuo vikuu, wanazuoni, watunga sera, wabunifu, sekta binafsi na washirika wa maendeleo kutoka Afrika na sehemu mbalimbali duniani.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kimeanzisha programu mbili mpya za shahada zinazolenga kuwaandaa vijana kuwa wataalamu wenye ujuzi wa kimataifa, teknolojia na uwezo wa kutatua changamoto za kiuchumi na kijamii.

 


Na: OWM – TAMISEMI, Kilwa – Lindi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amezielekeza Wilaya na Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinafanya kazi ya kuzibua mitaro na mifereji ya maji ili kujiandaa na kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kunyesha kuanzia mwezi Oktoba 2026 hadi Februari 2027, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Septemba 13, 2026 akiwa Somanga, wilaya ya Kilwa, katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Lindi, yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhimiza uwajibikaji kwa viongozi na watumishi wa umma katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Prof. Shemdoe amewataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Mameneja wa TARURA Wilaya nchini kote, kuhakikisha wanashirikiana na taasisi nyingine katika kujiandaa na kuwa na utayari wa kukabiliana na athari za mvua za El Niño kwa kuhakikisha miundombinu ya kupitisha maji inakuwa katika hali nzuri na inakidhi mahitaji.

“Nimuelekeze Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kushirikiana na wananchi kuzibua mifereji ya maji iliyoziba ili kipindi cha mvua za El Niño maji yasipate nafasi ya kuchepuka na kuvamia makazi ya wananchi na kuleta madhara,  Mkuu wa Wilaya ya Kilwa simamia jambo hili,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Katika hatua nyingine, akijibu ombi la wananchi wa kata ya Kinjumbi la kujengewa kwa kiwango cha lami 

barabara ya Kinjumbi yenye urefu wa kilomita 30, Prof. Shemdoe amesema ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami utachukua muda mrefu, hivyo amemuelekeza Meneja wa TARURA kufanya tathmini ya gharama za kuikarabati kwa kiwango cha changarawe na kuwasilisha gharama hizo ofisini kwake ili bajeti ya fedha za matengenezo itumike kuikarabati na kuiwezesha kutumika muda wote.

Maelekezo ya Prof. Shemdoe kwa wilaya na halmashauri kujiandaa kukabiliana na athari za mvua za El Niño ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa katika kikao kazi  Septemba 11, 2026 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, aliyezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka za kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba 2026.

Aidha, maelekezo hayo ya Prof. Shemdoe kwa wilaya na halmashauri kujiandaa kukabiliana na athari za mvua za El Niño ni muendelezo wa hatua za utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha usafi wa mazingira katika miji na majiji, aliyoyatoa Septemba 2, 2026 wakati akiwaapisha Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Somanga, mkazi wa kata ya Somanga, wilaya ya Kilwa, Bw. Hashimu Omary Changadua, ameishukuru na kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mbili za sekondari, soko la kimkakati na kituo cha afya, pamoja na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.

Mara baada ya kuzungumza na wananchi wa Somanga, Prof. Shemdoe aliendelea na ziara yake kwa kutembelea na kukagua ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao linalojengwa na halmashauri ya Kilwa, pamoja na ujenzi wa soko la wajasiriamali wadogo katika kijiji cha Njianne, kata ya Tingi, katika halmashauri hiyo.
















Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imekabidhi pikipiki kwa Kamati ya Watumia Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO) ya MIMAKI, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji na usimamizi wa huduma za maji kwa wananchi.

 Ikiwa taifa liko katika juhudi za kujenga jamii yenye maadili, amani, mshikamano na uwajibikaji, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limetakiwa kuendelea kutumia nafasi yake katika kuimarisha misingi hiyo na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rose Mary Senyamule, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 6 wa Wachungaji wa KKKT unaofanyika katika Ukumbi wa Chimwaga, jijini Dodoma.

Senyamule amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa KKKT katika maendeleo ya taifa, ikieleza kuwa kwa miaka mingi kanisa hilo limekuwa mshirika muhimu katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii.

Amesema huduma hizo ni pamoja na elimu, afya, malezi ya vijana, huduma kwa watu wenye mahitaji maalum pamoja na misaada ya kijamii na juhudi za kupambana na umaskini.

 Senyamule amesema pamoja na huduma za kijamii, KKKT imeendelea kuwa mdau katika shughuli za kiuchumi na uwekezaji, huku viongozi wa dini wakiwa na nafasi ya kipekee katika kujenga maadili mema, kudumisha amani na kuimarisha umoja wa kitaifa.

“Viongozi wa dini tunatambua kuwa mnaaminika sana na wananchi kuliko taasisi na watu wengine. Kwa sababu hiyo, mafundisho na matendo yenu yanaweza kuleta mabadiliko makubwa katika familia, jumuiya na taifa kwa ujumla,” amesema.

Amesema taifa linahitaji viongozi wa dini wanaoweza kuwa sauti ya matumaini na faraja kwa wananchi, hususan wale wanaopitia changamoto mbalimbali za maisha.

Senyamule amewataka wachungaji na viongozi wa dini kwa ujumla kuendelea kuwa sauti ya faraja kwa wenye huzuni, matumaini kwa waliokata tamaa na msaada kwa watu walio katika mazingira magumu.

Katika eneo la malezi, amesema kuna umuhimu wa kuimarisha malezi ya kiroho na kimaadili, hasa kwa watoto na vijana, ili kuwaandaa kuwa kizazi chenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.

Aidha, amewataka wachungaji kuendelea kutoa elimu inayowajenga wananchi katika nyanja za kiroho, kijamii na kiuchumi, huku wakihimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, kutumia fursa zilizopo na kushiriki katika shughuli halali za maendeleo.

“Imani iendelee kusambaa sambamba na matendo yanayoleta ustawi wa mtu binafsi, jamii na taifa kwa ujumla,” amesema.

Mkutano Mkuu wa 6 wa Wachungaji wa KKKT umehusisha wachungaji kutoka Dayosisi 28 za KKKT na umefunguliwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Alex Malalusa.

Mkutano huo unatarajiwa kuendelea hadi Septemba 17, 2025, ukiwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayohusu huduma ya kanisa, malezi ya kiroho na nafasi ya kanisa katika jamii na maendeleo ya taifa.



Mashindano  ya Soka ya Kiruswa Jimbo Cup yanayoandaliwa kila mwaka na Naibu Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Longido Mkoani Arusha,Dkt Steven Kiruswa yameingia msimu wa sita na kuendelea kufana kila mwaka na mwaka huu timu 51 zimeshiriki mashindano hayo kutoka katika tarafa nne wa wilaya hiyo yenye wakazi wengi vijana wa jamii ya kifugaji ya Kimasai.

Naibu Waziri huyo alisema hayo baada ya uzinduzi rasmi wa mashindano ya Kiruswa Jimbo Cup mwaka huu na kusema kuwa mwaka  yatafanikiwa zaidi kwani waandaji wamejipanga kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa na  vijana kuchukuliwa kwenda katika ligi za madaraja mengine ya juu timu za huko ili waweze kuiwakilisha vema Longido.

"Sasa mwakani ntakuja kivingine  nataka iwatoe vijana wa kiume na kike wa hapa  Longido kwenda kupata fursa za kimaisha kupitia michezo na kujikita katika michezo zaidi na kuacha mara moja kujikita katika ujambazi, madawa na ulevi"alisema Kiruswa

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Wilaya ya Longido(LDFA) Obeid Mollel amesema Kiruswa Jimbo Cup ni mashindano yanayokuwa mwaka hadi mwaka na vijana wengi wamefanikiwa kusajili katika timu za ngazi mbalimbali Mkoa na ligi daraja la pili na kwanza baada kuonyesha vipaji vyao katika mashindano hayo. 

Mollel alisema timu zote shiriki zimepewa seti moja ya jezi na mpira na washindi watapata zawadi ya fedha taslimu na medali ila mwakani utaratibu utabadilika kwa kuongeza zawadi ya fedha kuwa nono na timu zilizoshika nafasi tatu za juu zitapewa jezi na mpira na sio timu zote kama ilivyokuwa sasa hiyo ni kuongeza ushindani katika soka.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Longido ,Salumu Kally amesema kuwa Kiruswa Jimbo Cup ni mashindano muhimu katika wilaya yake kwani yanawapa ubize vijana kujikita katika soka na kuacha kujikita katika uhalifu,madawa na ulevi hivyo Mbunge anastahili pongezi na kuungwa mkono kwa hali na mali.

Naye Maenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Papa Nakuta amesema michezo ni ilani ya chama hicho inayosisitiza kuendeleza michezo na anachofanya Kiruswa ni utekelezaji wa ilani ya chama katika kukuza michezo katika Jimbo la Longido na vijana wanafurahia mashindano hayo ambayo yanaonyesha ushindani mkubwa mwaka hadi mwaka.













Mimi nilipitia tukio ambalo liliniumiza sana. Mtu niliyemwamini alinisaliti na kuniharibia mambo yangu muhimu. Ilikuwa ni hali iliyonifanya nijisikie kudharauliwa na kupoteza heshima yangu mbele ya wengine.

Nilikuwa na hasira kubwa ndani yangu. Wakati mwingine nilifikiria kulipiza kisasi kwa njia za haraka, lakini nilijua hilo lingeweza kuniletea matatizo makubwa zaidi, hasa ya kisheria. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu kuhusu hali hiyo. SOMA ZAIDI.
Mimi nilikuwa naishi na maumivu ya kuona ardhi ya familia yetu ikichukuliwa bila haki. Ilikuwa ni mali ya wazazi wetu, lakini kwa sababu ya migogoro na ukosefu wa nyaraka kamili, tulijikuta tukiipoteza.

Tulijaribu kupambana kwa njia mbalimbali kwa miaka mingi, lakini hakuna kilichobadilika. Kila hatua tuliyochukua ilionekana kugonga mwamba. Hali hii ilinichosha sana. Ilikuwa sio tu kupoteza mali, bali pia historia na heshima ya familia yetu.

Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali hiyo. SOMA ZAIDI.
Nilikuwa na kazi ambayo nilikuwa naiweka kama sehemu muhimu ya maisha yangu. Ilikuwa chanzo cha matumaini na heshima yangu mbele ya jamii na familia. Lakini ghafla mambo yalibadilika.

Nilishutumiwa kwa makosa ambayo sikuwa nimeyafanya, na bila nafasi ya kujitetea kwa ufasaha, nikafukuzwa kazi kwa aibu kubwa. Siku ile nilihisi kama dunia imenigeuka. Niliondoka kazini nikiwa na maswali mengi kichwani na maumivu makubwa moyoni.

Watu waliokuwa wananijua walishangaa na wengine walianza kunidharau. Siku zilizofuata zilikuwa ngumu sana. Nilianza kujifungia ndani, nikikosa hamu ya kufanya chochote. Nilihisi kama maisha yangu yamefikia mwisho wa safari. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Bakari. Kwa muda mrefu, nilikuwa mtu wa kufanikiwa katika biashara na mambo yangu ya kifamilia, lakini ghafla mambo yote yalianza kuporomoka bila sababu za msingi.

Afya yangu ilianza kudhoofika kwa magonjwa ya ajabu yasiyorekodiwa vipimo vya hospitali, biashara yangu ikapoteza wateja wote, na migogoro isiyoisha ikaanza kuibuka nyumbani kwangu.

Nilijua wazi kuwa kuna maadui waliokuwa wakinitazama kwa jicho la husuda na kunirushia mishale ya kishirikina ili kunidondosha kabisa na kuniharibia maisha.

​Nikiwa kwenye majuto na hofu kubwa ya kupoteza kila kitu nilichochuma kwa jasho langu, mzee mmoja wa heshima katika kijiji chetu alinitembelea.

Baada ya kumsimulia mateso na majanga yaliyokuwa yakiniandama, alinieleza kwa huruma kuwa ulinzi wa kawaida hautoshi pale unapokabiliwa na maadui wenye roho mbaya na uchawi wa waziwazi. SOMA ZAIDI.