Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo aibu ilikuwa rafiki yangu wa karibu. Nilikuwa nikikopa hata chakula cha jioni. Nilijua majina ya watu wanaoweza kunisaidia, na nilijua pia namna ya kujitetea kwa maneno ili nisijisikie mdogo sana.

Kila siku ilikuwa hesabu ya kuishi, si kuota. Nilijilaumu, nikajilinganisha, na nikaanza kuamini kuwa umaskini ulikuwa sehemu yangu ya kudumu.

Nilifanya kazi ndogo ndogo, nikajaribu biashara ambazo hazikudumu, na mara nyingi nilikata tamaa kabla hata ya kuanza upya. Kilichonivunja zaidi haikuwa kukosa pesa pekee, bali kukosa matumaini.

Nilijikuta nikihofia kuomba msaada tena, huku nikijua bila msaada ningeendelea kudidimia.
Mabadiliko hayakuja ghafla. Yalianza pale nilipokubali kuwa nilihitaji mwelekeo, si huruma.Soma Zaidi...........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nikikopa-hata-chakula-leo-nawasaidia-wengine-kuanzia-mwanzo/
Kwa muda mrefu nilihisi kama uzito wangu ulikuwa mzigo nilioubeba kila siku. Sio tu kimwili, hata kiakili. Nilijaribu njia nyingi kwa haraka kuacha kula ghafla, kufanya mazoezi bila mpangilio, na kujilinganisha na wengine.

Kila jaribio lilipoisha bila matokeo, nilizidi kuvunjika moyo. Nilianza kuamini kuwa labda mwili wangu hauwezi kubadilika. Kilichonikwamisha zaidi haikuwa chakula pekee, bali mawazo.

Kila niliposhindwa, nilijilaumu. Kila nilipoanza upya, hofu ya kushindwa ilinitangulia. Nilielewa baadaye kuwa mabadiliko ya kweli huanza akilini. Nilihitaji kuacha vita na mwili wangu na kuanza kushirikiana nao.

Hatua ya kwanza ilikuwa ndogo. Nilijifunza kula kwa uelewa, si kwa adhabu. Kutembea dakika chache kila siku kulinisaidia kujenga nidhamu. Badala ya kupima mafanikio kwa mizani pekee, nilianza kuyapima kwa nguvu niliyokuwa nayapata, usingizi mzuri, na hali ya kujiamini iliyokuwa inarudi taratibu. Soma Zaidi.......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/uzito-ulionekana-kunizidi-nguvu-hatua-moja-baada-ya-nyingine-zilileta-mabadiliko/
Nilipojeruhiwa, haikuwa kwa kisu wala ngumi. Ilikuwa kwa maneno. Maneno kutoka kwa mtu niliyemwamini, niliyemheshimu, na niliyefungua moyo wangu kwake. Kila alichosema kilikaa akilini mwangu kama ukweli, na taratibu nikaanza kujiuliza kama nilikuwa wa thamani kweli.

Kujiamini kulipotea, sauti yangu ya ndani ikawa ya lawama. Kwa muda nilijifungia. Niliepuka mazungumzo, nikajifunza kunyamaza ili nisiongeze maumivu. Nilidhani ukimya ungeponya.

Badala yake, nilibeba mzigo mzito wa hasira na huzuni. Kila nilipokumbuka, nilihisi nimekwama kati ya kusamehe na kuondoka kabisa.
Hatua ya kwanza ya kupona ilianza nilipokubali kuwa kuumizwa hakumaanishi udhaifu.Soma Zaidi......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilijeruhiwa-na-maneno-ya-niliyekuwa-ninamwamini-safari-ya-kujiponya-ilinisaidia-kuamua-hatua-ijayo/

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Mchemba leo Desemba 21, 2025 amekagua hali ya bandari ya Barazani mkoani Lindi na kuiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania kukamlisha kwa haraka michakato ya awali ya kitaalam ya ujenzi wa mradi wa Bandari ya Ngongo wilayani Lindi mkoani Lindi.

Amesema kukamilika kwa bandari ya Ngongo kutasaidia kuwaondolea adha watumiaji wa bandari inayotumika sasa ya Barazani ambayo hali yake haiendani na mahitaji ya sasa.

Dkt. Mwigulu ameongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa bandari ya Ngongo kutaleta chachu ya maendeleo mkoani humo kwani bandari ya Lindi imeanza kuchangamkiwa na wafanyabiashara, wakiwemo wa nchi jirani.

 





Babati, Manyara Desemba 19, 2025: Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, leo Desemba 19, 2025 amezindua rasmi na kuhamasisha utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote (NHIF) katika Mkoa wa Manyara, akisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kuwa na bima ya afya ili kupata huduma za matibabu kwa urahisi na kwa gharama nafuu.


Uzinduzi huo umefanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) mjini Babati, na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wataalamu wa afya, wawakilishi wa mpango wa kitaifa wa Bima ya Afya kwa Wote pamoja na wananchi mbalimbali.


Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Sendiga amesema mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutimiza ahadi ya siku 100 za kuanzisha mfumo utakaohakikisha kila Mtanzania anakuwa na bima ya afya.




“Mfumo huu unalenga kumwondolea mwananchi mzigo wa gharama kubwa za matibabu na kuhakikisha kila mmoja, bila kujali kipato chake, anapata huduma bora za afya kwa wakati,” amesema Mhe. Sendiga.


Aidha, amewaelekeza Wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya mkoani Manyara kuhakikisha mpango wa Bima ya Afya kwa Wote unatekelezwa kwa kuzingatia miongozo, kanuni na taratibu zilizowekwa, ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali.


Sambamba na hilo, Mhe. Sendiga amesisitiza kuwa ni wajibu wa viongozi na watendaji wote kwenda kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujiunga na mpango huo, ili waweze kunufaika na huduma za afya kwa uhakika.


Kwa upande wake, Bi. Janeth Kibambo, Mwakilishi wa Timu ya Kitaifa ya Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, amesema lengo kuu la mfumo huo ni kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na uwezo wa kupata huduma za afya katika vituo vyote vya umma na binafsi vilivyosajiliwa, bila kikwazo cha kifedha.


Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method, ameeleza kuwa mkoa umejipanga kikamilifu kutekeleza mpango huo, akibainisha kuwa changamoto ya wananchi kushindwa kugharamia matibabu imekuwa kubwa, hivyo kuanzishwa kwa Bima ya Afya kwa Wote ni mwarobaini muhimu katika kuboresha sekta ya afya.


Dkt. Method ameongeza kuwa Mkoa wa Manyara uko tayari kuupokea na kuutekeleza mpango huo kikamilifu, kwa kushirikiana na vituo vyote vya afya na wadau mbalimbali, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu.


Uzinduzi wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote mkoani Manyara unatarajiwa kuongeza wigo wa upatikanaji huduma za afya, kupunguza vifo vinavyotokana na ukosefu wa matibabu kwa wakati, na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla.

   


Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Arusha, wametembelea vivutio vya utalii katika Hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti sambamba na kupata mafunzo ya namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo mahali pa kazi.

Akizungumza na watumishi, Meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha Mhandisi Nicholas Francis amesema hiyo ni katika kutekeleza moja ya malengo ya Taasisi hiyo lengo (A) linalohusu jinsi ya kukabiliana na HIV/AIDS, magonjwa yasiyoambukiza, ikiwa ni hatua ya kuboresha ustawi wao na kuboresha ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao wawapo kazini.

Semina hiyo ililenga kuwaeleza hali halisi ilivyo ya maambukizi, njia ya kujikinga, umuhimu wa kupima kwa hiari na kwa usiri na kuondoa ile dhana za maambukizi zinazoathiri juhudi za kukabiliana na kudhibiti na kuenea kwa maambukizi ya VVU.

Aidha, washiriki walikumbushwa kuzingatia maadili, kujilinda na kuchukua tahadhari za kujikinga na maambukizi ya VVU katika maisha yao ya kila siku.

Vile vile Mhandisi Nicholas aliwataka washiriki hao kuchukua tahadhari na kujenga tabia ya kuchunguza afya zao mara kwa mara jambo ambalo litawasaidia kutambua afya zao, vile vile itawaepushia msongo wa mawazo.















NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA

TAASISI ya HakiElimu Tanzania inaendelea na juhudi mahsusi za kushirikisha wadau wa elimu nchini ili kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa mtoto wa kike, hatua inayolenga kukabiliana na ongezeko la wasichana wanaokatisha masomo kutokana na vikwazo vya kijinsia.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid Maulid (wa pili kulia) na Bi. Bertha Mwaihojo (wa kwanza kulia) wakionesha Mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi pamoja mbele ya Vyombo vya habari, katika Ukumbi wa Mikutano, hoteli ya Stella Maris. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB) na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (SLADS) Dkt. Mboni Ruzegea, wa pili kushoto ni Mgeni Rasmi wa Mahafali ya 31 ya SLADS Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Shaibu Ndemanga wakishuhudia tukio hilo.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, amewatoa hofu wazazi na walezi nchini kuwa Serikali imejipanga kikamilifu  kuwapokea wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kuanzia Januari 2026, kwani imeandaa  miundombinu ya kutosha itakayowahudumia wanafunzi wote watakaopokelewa.

Mhe. Kwagilwa ametoa kauli hiyo mkoani Lindi wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambapo alitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Msingi Likong’o, iliyopo katika Manispaa ya Lindi.

“Shule hii inakwenda kuongeza na kutimiza idadi ya shule 567 zilizojengwa nchini. Ukiacha shule hii, tayari zipo shule 566 zilizojengwa nchi nzima, na kwa hapa mkoa wa Lindi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta Shilingi Bilioni 114 kwa ajili ya kuimarisha sekta ya Elimu,” amesema Mhe. Kwagilwa.

Ujenzi wa Shule ya Msingi Likong’o ni sehemu ya miradi ya kijamii inayotekelezwa kupitia sera ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) chini ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kwa kushirikiana na kampuni za Equinor na Shell, ambazo ni wadau wa maendeleo katika sekta ya mafuta na gesi.

Mhe. Kwagilwa amesema mradi huo umelenga kuboresha miundombinu ya elimu kwa watoto wa shule za msingi kwa kutoa mazingira salama, ya kisasa na bora ya kujifunzia, ikizingatiwa kuwa awali eneo hilo lilikuwa likikabiliwa na changamoto ya miundombinu ya elimu.

Ujenzi huo unahusisha vyumba vya madarasa na miundombinu ya kusaidia utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi, ambapo thamani ya mradi huo inakadiriwa kufikia Shilingi Bilioni 1.2 za Kitanzania na Serikali imesisitiza kuwa hatua hii ni sehemu ya jitihada za kuwekeza katika elimu kwa maendeleo endelevu ya taifa.


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi ya Lindi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika eneo la Ngongo mkoani Lindi na kusema kwamba huo ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya kupanua fursa za elimu ya juu nchini.

“Uwekezaji huu ni utekelezaji wa vitendo wa nguzo ya pili ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika kujenga uwezo wa watu kifikra, kiubunifu, kufanya uchambuzi, kutatua changamoto, pamoja na kuwa na utaalamu na umahiri katika nyanja mbalimbali za maisha,” amesema.

Akizungumza na viongozi na mamia ya wananchi wa mkoa wa Lindi waliofika kushuhudia uzinduzi huo leo (Jumamosi, Desemba 20, 2025), Waziri Mkuu amewapongeza viongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuamua kutekeleza maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupanua huduma za elimu ya juu katika maeneo ya kimkakati kama vile Mkoa wa Lindi.

“Maono haya ni ya kwake mwenyewe Mheshimiwa Rais. Zilipotolewa fedha za mradi huu kwa vyuo vikuu kama vya Dar es Salaam na Mzumbe, alisema ujenzi uelekezwe katika kupeleka kampasi za vyuo vikuu kwenye mikoa yote ambayo haikuwa na vyuo vikuu.”

Amesema Mkoa wa Lindi, kama ilivyo kwa mikoa mingine ya Kusini mwa Tanzania una ardhi yenye rutuba, rasilimali watu na mazingira rafiki kwa kilimo cha kisasa na biashara ya mazao.

“Kampasi hii ya kilimo itasogeza huduma ya elimu karibu na wananchi wa Kanda ya Kusini na kuendeleza utafiti na ubunifu katika sekta ya kilimo ambayo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa letu. Uwekezaji huu utachangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha sekta ya kilimo kupitia maarifa, teknolojia na tafiti za kisasa zitakazojibu changamoto halisi za wakulima wetu,” amesisitiza.

Dkt. Mwigulu amesema ujenzi wa Kampasi ya Kilimo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mkoani Lindi ni ushahidi mwingine wa dhamira ya dhati ya Serikali ya kuifanya elimu ya juu kuwa chombo cha mageuzi ya kiuchumi na kijamii. “Kupitia Kampasi hii, Serikali inalenga kuandaa wataalamu wabobezi wa kilimo, utafiti na biashara ya kilimo watakaosaidia kuongeza uzalishaji, thamani ya mazao, ajira kwa vijana na mapato ya wakulima.”

Sambamba na ujenzi wa chuo hicho, Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025, Serikali itahakikisha inafanya ukarabati wa barabara katika maeneo ya Nane Nane (Ngongo), ujenzi wa barabara zenye urefu wa km. sita kwa kiwango cha lami katika Kampasi za Chuo Kikuu (Ngongo na Ruangwa); ujenzi wa barabara za lami za Kilambo (km 1.5); Mtange – Kinengene - Kibaoni na barabara ya Mahakama – Mitwero (km 1.2).

Mapema, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete alimpongeza Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba kwa sababu yeye ni zao la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. “Shahada zako zote tatu umezipatia pale chuo kikuu. Tunajivunia kwani wewe ni miongoni mwa mabalozi wema wa chuo chetu,” alisema. 

Akielezea uwekaji wa jiwe la msingi la Kampasi ya Lindi, Dkt. Kikwete alisema anaamini iko siku kampasi ya Lindi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nayo pia itakuwa chuo kikuu kamili.

Alisema chuo hicho kinatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi wa kwanza ifikapo Oktoba, mwakani. “Mwaka ujao wa masomo utakaoanza Oktoba, 2026 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam - Kampasi ya Lindi kitapokea wanafunzi wa kwanza; vivyo hivyo kwa kampasi za Bukoba na kule Zanzibar,” alisema.

Alitumia fursa hiyo kumshukuru Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa kwa kusaidia upatikanaji wa ardhi wilayani Ruangwa ambako Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimejenga tayari kituo cha utafiti wa kilimo.

Naye, Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anayesimamia Fedha, Utawala na Mipango, Prof. Bernadeta Killian alisema ujenzi wa chuo hicho unafuata masterplan ya miaka 20 (2025-2045) kutegemea na uwezo wa Serikali na uwepo wa bajeti. “Mradi wote utagharimu sh. bilioni 14.8 na kati ya hizo, sh. bilioni 13.7 ni za mkandarasi ambaye tayari amelipwa sh. bilioni 5.9. Shilingi bilioni moja ni za kumlipa mshauri mwelekezi.” 

Akitoa maelezo ya ujenzi huo mbele ya Waziri Mkuu, Prof. Killian ambaye pia ni msimamizi wa mradi wa kuendeleza elimu ya juu kwa mageuzi ya kiuchumi (HEET) alisema majengo mengi yanaendelea yakiwemo ya utawala, vyumba vya mikutano, madarasa sita yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 60 kila moja, karakana ya mafunzo na maabara yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 125 kwa wakati mmoja.

Alisema kampasi hiyo pia ina mabweni mawili yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 200 lakini kuna nafasi ya kuongeza ghorofa tatu kila moja na hivyo kuweza kuchukua wanafunzi 800.

 



Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mh. Anthony Mavunde ametoa rai kwa jamii kuwajali na kuwakumbuka yatima na wajane katika utatuzi wa changamoto zao mbalimbali na kuwapa faraja.

Mh. Mavunde ameyasema hayo leo wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na Taasisi ya Joy of Giving ya kugawa mahitaji kwa wajane na yatima ikiwemo vyakula na mahitaji ya shule kwa watoto.

“Nawapongeza Joy of Giving Foundation kwa kuwajali na kuwakimbilia wahitaji mara zote.

Mmekuwa mfano mzuri kwenye jamii na hivyo mnatuma ujumbe kwa Jamii nzima juu ya kuwajali na kuwakumbuka wajane na yatima huku tukijua kwamba hii ni ibada kubwa.

Nitaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuwahudumia wajane na yatima na kwasasa tunatarajia kuwa na Tamasha kubwa la wahitaji la kila mwaka ili kutengeneza msingi wa utatuzi wa changamoto zao”Alisema Mavunde

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Joy of Giving Bi. Jackline Nitwa Machoke amesema Taasisi yake imejipanga kufanya tukio la mara moja kila mwaka la kuwahusu wajane na yatima na kutoa rai kwa wadau kuiwezesha Taasisi hiyo ili kuweza kutimiza malengo yake hasa katika huduma za kila siku za kuwahudumia watu wenye ugonjwa mbalimbali na upatikanaji wa bima ya Afya kwa wananchi wanaoishi katika mazingira magumu.

Hafla hiyo imehusisha watoto yatima na wajane takribani 200 ambao wote wamepatiwa mahitaji mbalimbali kutoka kwa Mbunge Mavunde na Taasisi ya Joy of Giving.







 


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Mwigulu Nchemba amepongeza Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa ujenzi wa shule bora ya Awali na Msingi katika Kijiji cha Likong'o mkoani Lindi inayojengwa kupitia mradi wa uzalishaji na usindikaji wa Gesi Asilia kuwa kimiminika ( LNG). .

Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo tarehe 20 Desemba 2025 wakati akikagua ujenzi wa shule hiyo itakayokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 400 katika Kijiji cha Likong'o, Kata ya Mbanja, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.


" Nawapongeza TPDC kwa hatua hii ya kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kupitia mradi huu wa LNG, shule hii ni bora ya kisasa na imezingatia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuwa na miundombinu inayokidhi watu wenye mahitaji maalum na watoto wa kike." Amesema Mhe. Nchemba

Katika hatua nyingine Dkt. Nchemba ametoa msisitizo kwa Wizara ya Nishati kuhakikisha kuwa shule hiyo inafungwa miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia kuunga mkono utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo kinara wake ni Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kutokana na uwepo wa shule hiyo, Waziri Mkuu amewaasa wananchi kuchangamkia fursa kwa kuwasomesha watoto wao na hivyo kuunga mkono jitihada anazofanya Rais Rais Samia za ujenzi shule katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwawezesha watoto wote kupata elimu.


Kwa upande wake Mhe. Salome Makamba ambaye ni Naibu Waziri wa Nishati, amesema mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Likong'o unatekelezwa kama sehemu ya kurudisha fadhila kwa wananchi waliotoa ardhi kwa ajili ya utekelezaji mradi wa LNG.

Ameeleza kuwa ujenzi wa Shule hiyo ambao umefikia asilimia 70 unaonesha jinsi kaulimbiu ya kazi na utu inavyotekelezwa kwa vitendo na Serikali ya Awamu ya Sita.

Katika hatua nyingine, Mhe. Salome ameeleza kuwa agizo la Waziri Mkuu la shule hiyo kuwekewa miundombinu ya nishati safi ya kupikia litatekelezwa na kuongeza kuwa ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan taasisi 52 zitasambaziwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia.

Naye, Mbunge wa Lindi, Mohamed Utaly amemshukuru Rais Samia kwa uwekezaji huo wa mradi wa LNG ambao amesema unaleta chachu ya elimu mkoani Lindi.

Amepongeza pia TPDC kwa kuhakikisha kuwa miradi ya uwajibikaji kwa jamii imeanza kutekelezwa mapema kupitia mradi huo wa LNG.

Awali, Mhandisi Msimamizi wa mradi wa shule ya Awali na Msingi Likong'o, Upendo Mahavanu kutoka TPDC alisema mradi huo unagharimu Sh .bilioni 1.27 ambapo shule itakuwa na Madarasa 9; saba yakiwa ni ya shule msingi na mawili ni ya awali. Pia kutakuwa na ofisi na nyumba za walimu.

Utekelezaji wa mradi wa LNG unatarajiwa kuwa na manufaa mbalimbali nchini ikiwemo mapato ya Serikali yatakayotokana na uuzaji wa LNG kwenye soko la kimataifa, fursa za ajira, fursa kwa wazawa kuuza bidhaa, uhaulishaji wa teknolojia mbalimbali ili kuwajengea uwezo wataalam wa ndani n.k