Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akipata maelezo mbalimbali wakati akitembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukagua banda la Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.

aibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akiangalia jiko la kunyomea nyama  linalotumia nishati ya gesi badala ya mkaa alipotembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akiangalia gari linalotumia mfumo wa gesi asilia kupunguza matumizi ya mafuta yanasababisha uzalishaji wa gesijoto alipotembelea banda la Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama (wa  tatu kushoto) akipata maelezo kuhusu uzalishaji wa miche alipotembelea banda la Wizara ya Kilimo kwenye Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Baraka Luvanda.



Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania - TEMESA, Bw. Kheri Mahimbali, leo tarehe 02 Juni 2026 amekutana na viongozi wa kampuni ya TOYOTA Tanzania katika ofisi zao eneo la Posta, jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili kuhusu jitihada za Serikali katika kuendelea kuboresha huduma za matengenezo ya magari hapa Nchini.



Akizungumza katika kikao hicho, Bw. Mahimbali amesema TEMESA imejipanga kuhakikisha huduma za ufundi na matengenezo ya magari ya Serikali zinatolewa kwa viwango vya juu kwa kutumia teknolojia za kisasa na za viwango vya kimataifa.



“TEMESA inaona fursa kubwa katika kuimarisha ushirikiano na TOYOTA kupitia miradi ya pamoja itakayowezesha taasisi hizi mbili kubadilishana utaalamu kwa mafundi na kuongeza ufanisi wa huduma zinazotolewa kwa wadau wetu,” amesema Mtendaji Mkuu.


Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa TOYOTA Tanzania, Bw. Jatin Pandya amehakikisha utayari wa kampuni hiyo kuendelea kushirikiana na TEMESA katika mafunzo ya kitaalamu kwa mafundi, ushauri wa kiufundi, matumizi ya teknolojia mpya na kuimarisha mifumo ya usalama wa magari.



“Sisi TOYOTA tunatanguliza usalama wa watumiaji wa magari na ubora wa huduma. Tunaamini ushirikiano huu utachangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha huduma za matengenezo ya magari nchini na kujenga uwezo wa wataalamu wa ndani,” amesisitiza Pandya.



Aidha, mara baada ya kikao hicho, Mtendajji mkuu pia alipata fursa ya kufanya ziara fupi katika karakana za TOYOTA ili kujionea teknolojia mpya zinazotumika katika matengenezo ya magari.

Miongoni mwa mambo waliyojadili katika kikao hicho ni pamoja na uwezekano wa kuanzisha ushirikiano kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi - PPP. Hatua inayotarajiwa kuimarisha uwezo wa karakana na kuongeza ufanisi wa huduma katika sekta ya matengenezo ya magari.

Kikao hicho kimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano kati ya TEMESA na TOYOTA, huku kikitarajiwa kuwa chachu ya mageuzi makubwa katika sekta ya ufundi wa magari nchini.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tanzania na Malaysia zimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika elimu ya juu kupitia ubia wa vyuo vikuu, tafiti za pamoja, ubadilishanaji wa wanafunzi na wahadhiri, ufadhili wa masomo pamoja na ushirikiano katika sayansi na teknolojia.

Watumiaji wa petroli wamepata afueni mwezi Juni 2026 baada ya bei ya mafuta hayo kushuka ikilinganishwa na mwezi uliopita. Kwa Dar es Salaam, petroli sasa itauzwa kwa bei kikomo ya shilingi 4,086 kwa lita, hatua inayotarajiwa kupunguza gharama kwa watumiaji wa kawaida na baadhi ya shughuli za usafiri.

Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo.

Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu kama usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii.

Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli na Irani. Mgogoro huo umeathiri uzalishaji, uhifadhi na usafirishaji wa mafuta duniani, huku kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz kukiongeza gharama za usafirishaji na bima za meli za mafuta.

 Mbunge wa Tunduru Kaskazini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Ado Shaibu, amewataka wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuepuka kuingiza siasa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2030 katika mijadala ya Bunge, akisema hali hiyo inaweza kuathiri ubora wa majadiliano na utekelezaji wa majukumu muhimu ya chombo hicho.


Akichangia hoja ya Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha 2026/2027 leo Juni 2, 2026, Bungeni jijini Dodoma, Ado amesema Bunge ni taasisi muhimu inayopaswa kujadili masuala ya maendeleo kwa umakini bila kuruhusu ushindani wa kisiasa kutawala kila mjadala.

"Nafahamu siasa zinaendeshwa na siasa, na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni sehemu ambayo siasa haziwezi kuepukika. Hata hivyo, nawaomba wabunge wa CCM, homa ya kuelekea mwaka 2030 isiharibu mijadala ya Bunge hili," alisema.

Ameongeza kuwa ingawa siasa zina nafasi yake, kuzidisha mijadala ya kisiasa mapema kunaweza kuondoa mwelekeo wa Bunge katika kushughulikia masuala ya msingi yanayogusa maendeleo ya wananchi.

"Kuna ladha katika siasa, lakini tukizidisha chumvi mapema kiasi hiki, tutafika mahali ambapo hakuna wizara itakayoweza kujadiliwa kwa utulivu ndani ya Bunge. Mwenendo huo si mzuri kwa ustawi wa Bunge la Muungano wa Tanzania," alisisitiza.

Katika hatua nyingine, mbunge huyo aliipongeza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa kazi iliyoifanya katika kupitia masuala ya fedha za Serikali, sambamba na kupongeza Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kuendelea kusimamia uwajibikaji na matumizi sahihi ya fedha za umma.

Ado amesema mafanikio ya maendeleo ya taifa yanategemea uwajibikaji na usimamizi madhubuti wa rasilimali za umma, hivyo akaishauri Serikali kuendelea kuipatia Ofisi ya CAG rasilimali na fedha za kutosha ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.

"Endapo tutaamua kuwa makini na kutekeleza wajibu wetu ipasavyo, nchi inaweza kufikia hatua kubwa zaidi za maendeleo. Ni muhimu Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

(CAG)ikawezeshwa vya kutosha ili iendelee kufanya kazi yake kwa uhuru na ufanisi," amesema.

Kauli za Ado zimekuja wakati Bunge likiendelea kujadili bajeti za wizara mbalimbali kuelekea mwaka wa fedha 2026/2027.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema vijana wanapaswa kutumia fursa zinazotolewa na Serikali kwa kukuza ubunifu, kuongeza bidii katika kazi, kutumia teknolojia na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi hususan zilizo rafiki kwa Mazingira.

 Serikali kupitia Wizara ya Fedha imetangaza vipaumbele vinane (8) vya kimkakati kwa mwaka wa fedha 2026/27, vyenye lengo la kukuza uchumi, kuimarisha nidhamu ya matumizi ya rasilimali za umma, na kulipa madeni.


Vipaumbele hivyo vimewasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akisoma mapendekezo ya mpango na bajeti ya wizara hiyo.Sera na mikakati hiyo mikuu imegawanyika katika maeneo yafuatayo:

1. Ukuaji wa Uchumi na Kudhibiti Mfumuko wa BeiWizara imepanga kusimamia uchumi jumla ili ufikie ukuaji wa asilimia 6.3 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2026. Aidha, jitihada zitawekwa ili kudhibiti mfumuko wa bei ubaki kwenye viwango vya tarakimu moja (wastani wa asilimia 3.0 hadi 5.0), huku akiba ya fedha za kigeni ikitunzwa kukidhi uagizaji wa bidhaa na huduma kwa angalau miezi minne (4).

2. Nidhamu ya Matumizi na Ukusanyaji MapatoIli kuhakikisha thamani halisi ya fedha za umma inaonekana, serikali itaimarisha nidhamu ya bajeti (fiscal discipline). Hatua hii itahusisha usimamizi madhubuti wa ununuzi wa umma na kupunguza tabia ya kuhamisha fedha kutoka fungu moja kwenda jingine (reallocation between votes).

3. Kuvunja Rekodi ya Mapato (Tsh Bilioni 55,200.75)Katika bajeti kuu ya serikali ya jumla ya shilingi bilioni 62,334.19, Wizara ya Fedha inalenga kuboresha mifumo ya kodi, misaada, na mikopo ili kuchangia shilingi bilioni 55,200.75 kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina. Hii ni sawa na asilimia 88.6 ya bajeti yote.

4. Kulipa Madeni na Kuaminika KimataifaSerikali imetenga shilingi bilioni 15,102.80 kwa ajili ya kulipa kwa wakati riba na mitaji ya madeni yanayotarajiwa kuiva. Hatua hii inalenga kulinda mikataba na kuendelea kujenga imani kwa wawekezaji katika masoko ya fedha ya kikanda na kimataifa.

5. Mabilioni ya Kulipa Watumishi na WakandarasiHabari njema kwa wadau wa ndani ni kwamba serikali itakuwa ikitoa shilingi bilioni 100.00 kila mwezi. Fedha hizi zitasaidia kulipa madeni ya watumishi wa umma, wakandarasi, wazabuni, na watoa huduma mbalimbali ili kuchochea mzunguko wa fedha.

6. Usawa wa Mgawanyo wa Fedha kwa HalmashauriKutakuwa na maboresho makubwa kwenye ugawaji wa rasilimali fedha kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa (Halmashauri). Mgawanyo huo utazingatia tafiti za kitaalamu ili kuondoa urudufu wa majukumu na kuleta uwiano wa kimaendeleo nchini.

7. Mageuzi ya Mfumo wa Bajeti (PBB)Serikali itafanya tathmini ya kina ya usimamizi wa bajeti kwa kutumia Mfumo wa Programu (Programme Based Budgeting – PBB). Lengo ni kuwezesha maamuzi sahihi ya kimabadiliko katika upangaji wa bajeti unaoleta matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi.

8. Matumizi ya Akili Unde (AI) na Utawala BoraKatika kwenda na wakati, wizara itajenga uwezo wa watumishi wake kuhusu masuala ya Mazingira, Jamii na Utawala Bora (ESG). Kubwa zaidi, serikali itaanza kuingiza matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) katika usimamizi wa fedha za umma na uchumi ili kuongeza ufanisi na uwazi.

 



Na Mwandishi Wetu, Dodoma


Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, leo tarehe 2 Juni, 2026 amekutana na Balozi wa Australia nchini Tanzania anayemaliza muda wake wa uwakilishi, Mhe. Jenny Da Rin, kwa mazungumzo ya kumuaga yaliyofanyika jijini Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kiruswa amempongeza Mhe. Jenny Da Rin kwa kumaliza muda wake wa uwakilishi nchini kwa mafanikio makubwa, huku akitambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Australia, hususan katika maendeleo ya Sekta ya Madini.

Amesema Tanzania na Australia zimeendelea kushirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo imekuwa na matokeo chanya katika kukuza sekta ya madini na kuchangia maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla.


Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa Serikali ya Tanzania imeendelea kuhakikisha wananchi wanapata manufaa ya rasilimali madini kwa kuwashirikisha kikamilifu katika shughuli za madini, huku ikitambua mchango wa wawekezaji wa kimataifa, wakiwemo kutoka Australia, katika maendeleo ya sekta hiyo.


Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano na Australia katika maeneo ya utafiti wa madini, uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na maendeleo ya rasilimali watu ili kuongeza uzalishaji na kuifanya sekta ya madini kuwa na tija zaidi kwa Taifa.


“Sekta ya madini inaendelea kukua kwa kasi na inahitaji uwekezaji wa kutosha katika teknolojia, ujuzi na tafiti ili kuongeza uzalishaji na manufaa ya kiuchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla,” amesema Dkt. Kiruswa.




Kwa upande wake, Mhe. Jenny Da Rin ameishukuru Serikali ya Tanzania na Wizara ya Madini kwa ushirikiano mkubwa alioupata katika kipindi chote cha utumishi wake nchini.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa Watanzania kutumia kikamilifu fursa za elimu, mafunzo na semina zinazotolewa na Australia, akibainisha kuwa maarifa na ujuzi unaopatikana kupitia programu hizo unachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sekta mbalimbali, ikiwemo Sekta ya Madini.


Mhe. Jenny Da Rin ameongeza kuwa moja ya malengo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Australia ni kuhamasisha wawekezaji na wafanyabiashara wa Australia kuja kuwekeza nchini Tanzania pamoja na kuendeleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa pande zote mbili.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutatua changamoto zinazoweza kuathiri mazingira ya uwekezaji ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kukuza maendeleo ya nchi hizo mbili.




WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema vijana wanapaswa kutumia fursa zinazotolewa na Serikali kwa kukuza ubunifu, kuongeza bidii katika kazi, kutumia teknolojia na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi hususan zilizo rafiki kwa Mazingira.

Mhe. Masauni amesema hayo katika Kongamano la Vijana lililofanyika jijini Dar es Salaam, Juni 2, 2026 ambalo ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambapo kilele chake kitaifa yanafanyika Juni 5, 2026 mkoani Dodoma.

Amesema, kongamano hilo ni jukwaa muhimu linalowaunganisha vijana na maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kwa kuwapa nafasi ya kushiriki katika mijadala, kujifunza kutoka kwa wataalam, kubadilishana uzoefu na kuibua suluhisho bunifu zinazoweza kutekelezwa kwa vitendo katika jamii zao.

“Ninyi ndio nguvu kazi ya Taifa na nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, vijana ni zaidi ya asilimia 64 ya nguvu kazi ya Taifa. Hii ina maana kuwa mchango wenu ni muhimu sana katika kulinda mazingira, kukuza uchumi wa kijani na kuhakikisha maendeleo endelevu ya Taifa letu.”

Aidha ameongeza kuwa ni vyema vijana wakatambua changamoto za kimazingira pia zinaweza kuwa fursa kubwa za kiuchumi, takwimu za kimataifa zinaonesha kuwa mpito kuelekea uchumi wa kijani unaweza kuzalisha ajira milioni 8.4 kwa vijana duniani ifikapo mwaka 2030.

Aidha, amesema uchumi endelevu duniani unakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola trilioni 12 na uwezo wa kuzalisha zaidi ya ajira milioni 380 duniani kote.

“Hii inaonesha dhamira ya pamoja ya Taifa katika kulinda mazingira na kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho”.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi, amesema kuwajengea uwezo vijana kupitia programu za kujitolea ni mkakati muhimu wa kuandaa kizazi kitakachosimamia agenda za maendeleo endelevu, uhifadhi wa mazingira na uchumi wa kijani.

Amesema programu za kujitolea zinawawezesha vijana kupata uzoefu wa kazi unaohitajika katika soko la ajira, huku zikizisaidia taasisi kupata kundi la vijana wenye maarifa, ubunifu na uwezo wa kutumia teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo.

“Afrika ina hazina kubwa ya rasilimali watu, ambapo takribani asilimia 40 ya vijana wa dunia wanaishi katika bara hilo, jambo linalotoa fursa kubwa ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kiteknolojia endapo vijana hao watapatiwa elimu, ujuzi na nafasi za kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.” Amesema Dkt. Muyungi.

 

Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Suzan Mkangwa (kulia), Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda na Mkurugenzi wa CMA, Usekelege Mpulla wakifuatilia agenda mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi leo Juni 2, 2026 ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaofanyika Jijini Geneva, Uswisi.

Na: OWM (KAM)

Tanzania imeshiriki kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi kinachoendelea jijini Geneva, Uswisi, ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).

Katika kikao hicho kilichifanyika leo Juni 2, 2026 wajumbe wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa viwango vya kazi, ikiwemo mjadala wa jumla kuhusu ripoti kuu ya Kamati ya Mkutano na maadhimisho ya miaka 100 ya ajenda ya Kazi zenye Staha, Tathmini ya Jumla, pamoja na wajibu wa nchi wanachama katika kuwasilisha taarifa na kutekeleza majukumu mengine yanayohusiana na viwango vya kazi.

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho ulijumuisha Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Kazini, Suzan Mkangwa, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), Khadija Mwenda, pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Usekelege Mpulla.

Tanzania, ambayo ni mwanachama wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) na mjumbe wa Bodi ya Magavana inayowakilisha nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki, inaendelea kushiriki Mkutano Mkuu wa 114 wa shirika hilo unaowakutanisha wawakilishi wa Serikali, Waajiri na Wafanyakazi kutoka nchi wanachama 187.

Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Suzan Mkangwa (kulia), Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda na Mkurugenzi wa CMA, Usekelege Mpulla wakifuatilia agenda mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi leo Juni 2, 2026 ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaofanyika Jijini Geneva, Uswisi.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina akifuatilia agenda mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi leo Juni 2, 2026 ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaofanyika Jijini Geneva, Uswisi.


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetangaza kuwa jumla ya walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Nne la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Awali na Msingi pamoja na Shindano la Pili la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Sekondari Tanzania Bara,ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuendelea kuimarisha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 2, 2026, jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, amesema kuwa hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo itafanyika Juni 6, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Amesema mashindano hayo yanatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao wa kitaaluma, ubunifu na matumizi ya mbinu bora za ufundishaji darasani, huku yakitumika pia kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA).

"Kati ya walimu 3,153 waliosajiliwa kupitia Mfumo wa National Teaching Skills Competition System (TSCS), walimu 1,263 walitimiza masharti yote ya ushiriki kwa kuwasilisha video za ufundishaji pamoja na maandalio ya masomo kwa ajili ya tathmini."amesema Mhe.Ameir

Amesema mchakato wa tathmini umekamilika na tayari orodha teule ya walimu watano bora imepatikana katika kila eneo la ushindani, huku mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa zawadi akitarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.

Mhe. Ameir ameeleza kuwa mshindi wa kwanza katika kila kundi atazawadiwa Shilingi milioni 2.5, cheti cha pongezi, cheti cha ushindi pamoja na kompyuta mpakato. Aidha, shule anayofundisha mshindi huyo itapatiwa projekta kwa ajili ya kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.

Katika hatua nyingine, amesema shule zitakazotoa washindi wa kwanza katika maeneo ya Kusoma kwa Darasa la Awali, Kiingereza kwa Darasa la Kwanza na Ufaraguzi wa Zana kwa Darasa la Pili zitapatiwa vibao vya kielektroniki 100 vyenye thamani ya Shilingi milioni tano.

Serikali inaendelea kutumia mashindano hayo kama nyenzo ya kuhamasisha ubunifu, kuongeza ari ya utendaji kwa walimu na kuibua mbinu bora za ufundishaji zitakazochangia kuinua viwango vya elimu nchini.

Kaulimbiu ya shindano la mwaka huu ni “UFUNDISHAJI BORA, TAIFA IMARA.

 
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Shirika la Viwango Tanzania limeandaa Jukwaa la Biashara la Viwango (Viwango Business Forum) litakalofanyika Juni 5, 2026 katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, likiwa sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo mwaka 1975 na kuanza utekelezaji wake mwaka 1976.
Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imewahukumu kifungo cha maisha jela Suleiman Thabit Ngulangwa na Farid Hamis Said baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 15.19.
Na: OWM (KAM)

Tanzania imeshiriki kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi kinachoendelea jijini Geneva, Uswisi, ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Nilipofikisha miaka 40, nilikuwa nimeanza kukubaliana na wazo kwamba huenda nisingeolewa tena. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Kwa miaka mingi nilikuwa nimeota kuwa na familia yangu mwenyewe. Niliona marafiki na ndugu wakifunga ndoa, wakijenga familia, na kuendelea na maisha yao.

Mimi pia nilitamani furaha hiyo, lakini kila uhusiano niliouanzisha uliishia njiani. Kwa kweli iliniumiza sana. 

Kadri miaka ilivyopita, maswali kutoka kwa watu yaliongezeka. Kila sherehe ya familia ilikuja na swali lile lile: “Wewe lini?”

Wakati mwingine nilicheka mbele za watu, lakini moyoni nilikuwa na huzuni kubwa. Kilichoniumiza zaidi ni kuona matumaini yangu yakipungua mwaka baada ya mwaka.

Nilijaribu mahusiano mbalimbali, lakini hayakudumu. Baadhi yaliishia kwenye kuvunjika moyo, mengine yalikufa kabla hata hayajafika mbali.

Polepole nilianza kuamini kwamba ndoa haikuwa sehemu ya hatima yangu.
Hakuna kitu kinachoumiza mzazi kama kuona mtoto wake akijitahidi lakini matokeo yake yaendelee kuwa mabaya. Hivyo ndivyo nilivyokuwa nikihisi kuhusu mwanangu. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Kwa miaka kadhaa alikuwa akirudi nyumbani na matokeo ambayo hayakuwa mazuri. Walimu walikuwa wakisema hakuwa makini darasani, wengine wakisema hakupenda kusoma. Kadri muda ulivyopita, watoto wengine walikuwa wakimpita huku yeye akibaki nyuma.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kusikia baadhi ya watu wakimuita mzembe. Mimi nilijua alikuwa mtoto mwenye akili, lakini nilikuwa nashindwa kuelewa kwa nini hakufanya vizuri kama wengine.

Matokeo yalipozidi kushuka, hali ikawa ngumu zaidi. Mtoto wangu alianza kupoteza confidence. Wakati mwingine alikuwa anakataa hata kuonyesha report form yake. Nilimuona akianza kuamini maneno mabaya aliyokuwa akiyasikia kutoka kwa watu.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo kila siku nilifungua biashara yangu bila kujua kama ningepata faida au hasara. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Nilikuwa nimewekeza fedha nyingi kwenye biashara yangu nikiamini ingeweza kubadilisha maisha yangu na ya familia yangu.

Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda vizuri, lakini baada ya muda hali ilianza kubadilika. Wateja walipungua.

Mauzo yakaanza kushuka mwezi baada ya mwezi. Nilijaribu matangazo mbalimbali, offers, na hata kupunguza bei za bidhaa zangu, lakini matokeo hayakuwa mazuri kama nilivyotarajia.

Kwa kweli nilianza kuchoka. Kilichoniumiza zaidi ni kuona madeni yakiongezeka huku mapato yakipungua.

Kulikuwa na wakati nilishindwa hata kulipa baadhi ya bili kwa wakati. Watu wa karibu walianza kuniambia nifunge biashara kabla sijapata hasara kubwa zaidi.
Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningejikuta nikituhumiwa kwa kosa ambalo sikuwahi kulifanya. Nilikuwa nikiishi maisha ya kawaida kijijini kwetu.SOMA ZAIDI/TAZAMA VIDEO

Watu walinifahamu kama mtu mtulivu, mwenye bidii, na asiye na ugomvi na mtu yeyote. Nilikuwa na marafiki wengi na niliheshimika katika jamii.

Lakini siku moja kila kitu kilibadilika. Kulitokea tukio la wizi katika eneo letu, na ghafla jina langu likaanza kutajwa. 

Mwanzoni nilidhani ilikuwa ni tetesi za kawaida ambazo zingeisha haraka. Lakini kadri siku zilivyopita, watu wengi zaidi walianza kuamini kwamba mimi ndiye nilihusika.

Kwa kweli nilivunjika moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu ambao walikuwa wakinisalimia kila siku wakianza kuniepuka. 

Baadhi yao walikuwa wakininyoshea vidole kwa siri, huku wengine wakizungumza kunihusu nyuma yangu.

Nilijaribu kueleza ukweli. Lakini ilionekana kama hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza. Watu walikuwa tayari wameunda maoni yao kuhusu mimi. Hata baadhi ya ndugu zangu walionekana kuwa na mashaka.

Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini jambo lile lilikuwa limenitokea. Nilihofia kupoteza kabisa heshima niliyokuwa nimeijenga kwa miaka mingi. Kulikuwa na wakati nilitaka kuondoka kijijini.