Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase,akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.
....
Serikali imewataka wakulima nchini kuhakikisha wanapeleka kakao yenye ubora sokoni ili kulinda bei nzuri inayoendelea kupatikana kwa sasa.
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi (Mb), wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo, .
DC Manase amesisitiza kuwa kuingiza kakao isiyo na viwango katika masoko kutasababisha bei kuporomoka, jambo ambalo litawaathiri wakulima kiuchumi. Amesema kuwa uaminifu wa mkulima katika kuzingatia vigezo vilivyowekwa ndiyo njia pekee ya kuhakikisha zao hilo linaendelea kuwa na ushindani na kupata masoko yenye tija ndani na nje ya nchi.
Aidha, DC Manase amewahimiza wakulima wa Kyela kuendelea kupanda miti kama mbinu madhubuti ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi na kulinda mazingira ya kijani. Amebainisha kuwa utunzaji wa mazingira ni kigezo muhimu kinachowezesha mazao ya wakulima kukubalika katika ngazi ya kimataifa, huku akisisitiza kuwa juhudi hizo pia zinasaidia wakulima kupata uaminifu wa kibenki na huduma nyingine za kifedha.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, ameeleza umuhimu wa utaratibu wa kukagua mizigo ghalani kabla ya kuifikisha mnadani. Akifafanua kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha kile kinachouzwa kinafahamika kwa usahihi, jambo linalosaidia kuondoa migogoro kati ya wanunuzi na wauzaji.
Vilevile, amesema utaratibu huo wa ukaguzi umeleta matokeo chanya kwani hivi sasa hakuna malalamiko yanayotolewa na pande zote mbili katika mnyororo wa biashara.
Naye Naibu Msajili wa Udhibiti wa Vyama vya Ushirika, Bw. Collins Nyakunga, ameeleza kuwa vipaumbele vya sasa vya ushirika ni kuwekeza katika ujenzi wa viwanda ili kuongeza thamani ya mazao, hatua inayolenga kubadilisha taswira ya vyama vya ushirika ili viweze kutoa mchango mkubwa zaidi kwa wakulima kwa kuhakikisha wanapata faida kubwa kutokana na kazi yao.

Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase,akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu,akielezea umuhimu wa utaratibu wa kukagua mizigo ghalani kabla ya kuifikisha mnadani wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

Naibu Msajili wa Udhibiti wa Vyama vya Ushirika, Bw. Collins Nyakunga,akielezea vipaumbele vya sasa vya ushirika ni kuwekeza katika ujenzi wa viwanda ili kuongeza thamani ya mazao, wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.
