Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amemtaka Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma, kuhakikisha anasimamia kwa karibu malipo ya wakulima wa kahawa ili kuwalinda dhidi ya ucheleweshaji wa fedha zao unaofanywa na baadhi ya kampuni zinazonunua zao hilo.

Mhe. Kapinga, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, ametoa maelekezo hayo mapema wiki hii alipokuwa akizungumza katika kikao na viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Amesisitiza kuwa zao la kahawa ni uti wa mgongo wa uchumi wa Wilaya ya Mbinga na chanzo kikuu cha maisha ya wananchi wengi, hivyo Serikali haitavumilia kuona watu wachache wanaitia doa kutokana na uzembe au kushindwa kusimamia ipasavyo sheria na kanuni ili wakulima walipwe fedha zao za mauzo ya kahawa kwa wakati.

Katika maelekezo yake, Waziri Kapinga amemwagiza Afisa Ushirika wa wilaya hiyo, kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha wakulima wanalipwa fedha zao kwa wakati bila visingizio, huku akiwataka watumishi kutotumia masuala ya ukomo wa malipo kama kisingizio cha kuwakandamiza wakulima.

Kwa upande mwingine, Waziri Kapinga amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, kufanya tathmini upya ya kampuni ya Mamba Coffee ili kubaini kama inastahili kuendelea kupewa kibali cha kununua kahawa, kutokana na malalamiko ya ucheleweshaji wa malipo kwa wakulima, amesema kuchelewesha malipo ni sawa na kuwarudisha nyuma wakulima na maendeleo yao.

Vilevile, amewahimiza viongozi wa vyama vya ushirika kukaa vikao na kufanya maamuzi muhimu mapema kabla ya kuanza kwa msimu wa kilimo, ili kuzuia migogoro inayoweza kuepukika.

Pia ametoa onyo kali dhidi ya matumizi mabaya ya fedha za ushirika, akisisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kutumia fedha hizo kwa maslahi binafsi hatavumiliwa.

 



Tanga, Januari 21, 2026


Baada ya kustaafu nilishuhudia kitu kimoja, nilistaafu tarehe 1/7/2012 na baada ya wiki moja niliweza kupata Mafao yangu.


Hayo ni maneno ya Mzee Ndibalema Kisheru, mstaafu anayepokea pensheni kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

Mzee Kisheru ambaye alitumikia nafasi mbalimbali serikali akimalizia ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, ameyasema hayo kwenye banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Tano ya Wiki ya Huduma ya Fedha, ambayo yamefunguliwa rasmi leo Januari 21, 2026 na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) kwaniaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamisi Mussa Omar, kwenye viwanja vya Usagara jijini Tanga.

Aidha, mzee Kisheru amesema, “Miaka 13 imepita nimeendelea kupata Mafao yangu bila kusita” Alisisitiza.

Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga amechangia vifaa vya ujenzi kwa Shule ya Msingi Ugano iliyopo Kata ya Kambarage na Shule ya Msingi Kibandai A iliyopo Kata ya Maguu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma, kwa lengo la kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Mchango huo umehusisha bati 100 za geji 28 zenye thamani ya shilingi milioni 3.5 kwa ajili ya kuezeka vyumba viwili vya madarasa, mbao za kenchi zenye thamani ya shilingi milioni 1, pamoja na mifuko ya saruji na nondo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba katika Shule ya Msingi Ugano.

Akiwa katika Kijiji cha Kibandai A, Kata ya Maguu, Mhe. Kapinga amesema anatambua changamoto za uchakavu wa miundombinu ya shule ikiwemo madarasa, nyumba za walimu, nyumba ya mganga pamoja na ofisi za shule, na ameahidi kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuzitatua changamoto hizo, Katika hatua hiyo, Mhe. Kapinga amechangia mifuko 50 ya saruji pamoja na shilingi laki tano kwa ajili ya ununuzi wa mchanga, ili kuharakisha ukamilishaji wa miradi ya ujenzi.

Wakati huo huo, Mhe. Kapinga amewakumbusha wananchi wa jimbo hilo umuhimu wa kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa kutumia kinga na kuwa waaminifu katika mahusiano yao na kujiepusha na vitendo vyote vinavyoweza kuchangia maambukizi. Amesema haikubaliki kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuendelea kutajwa miongoni mwa maeneo yenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya UKIMWI kila ripoti za kitaifa zinapotolewa.

Amesisitiza umuhimu wa wananchi kuchukua hatua binafsi na za kijamii ikiwemo kupima afya mara kwa mara, kutumia kinga, na kuepuka kuwaambukiza wengine, akibainisha kuwa maambukizi ya UKIMWI hayawezi kutambulika kwa kumuangalia mtu kwa sura.

Mhe. Kapinga amemshukuru Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa miradi ya maendeleo inayoendelea katika Jimbo la Mbinga vijijini mkoani Ruvuma.

Akizungumza Dkt Salemani Jumbe Kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, amesema zaidi ya madawati 2,000 yamekamilika kutengenezwa na yako katika hatua za mwisho za kusambazwa, na yatapelekwa katika shule zote zenye upungufu wa madawati ikiwemo Shule ya Msingi Ugano, ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Dkt. Jumbe, ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, amesema Kijiji cha Kibandai A tayari kimefungua zahanati kwa ushirikiano na Mhe. Kapinga, ambaye alichangia kwa kiasi kikubwa vitanda na vifaa tiba, ameeleza kuwa kwa sasa watumishi wa afya 100 tayari wamewasili wilayani kwa ajili ya kupangiwa vituo vya kazi.

Kwa ujumla, mchango wa Mhe. Judith Kapinga umepokelewa kwa furaha na wananchi wa Kata ya Kambarage na Maguu, ambao wameeleza kuwa hatua hiyo itaongeza hamasa ya elimu, kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi, na kuonesha dhamira ya dhati ya serikali katika kuimarisha sekta ya elimu na afya.

 



Na Mwandishi wetu, Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, kupitia Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali, imesaini Hati za Mashirikiano (MoU) na Vyuo Vikuu vinne ambavyo ni Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Mzumbe, Chuo Kikuu cha Usimamizi wa Fedha na Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa lengo la kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji na tathmini unaotumia ushahidi katika kupanga na kutekeleza sera, mipango, programu na miradi ya maendeleo.  

Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo Januari 21, 2026 jijini Dodoma, Katibu Mkuu Ofisi Waziri Mkuu (SBUU) Dkt. Jim Yonazi amesema kupitia mashirikiano hayo, Serikali na Vyuo Vikuu vitashirikiana katika kuimarisha uwezo wa wataalamu wa ufuatiliaji na tathmini, kufanya tathmini za pamoja za miradi ya maendeleo, kuendeleza tafiti bunifu na kuhakikisha maarifa yanayozalishwa vyuoni yanatumika kuboresha utendaji wa Serikali. 

"Serikali imesisitiza kuwa, mafanikio ya MoU hizo yatapimwa kwa utekelezaji wake, kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, yenye msisitizo wa matokeo yanayopimika na manufaa halisi kwa wananchi" ameongeza Dkt. Yonazi.

 


Licha ya kuongezeka kwa gharama za vifaa vya umeme ikiwemo nguzo, waya na mita, Serikali imeendelea kuhakikisha gharama za matumizi ya umeme kwa wananchi hazipandi kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2016.

Akizungumza Januari 21, 2026 jijini Dodoma katika kikao cha pili kati ya Wizara ya Nishati, taasisi zake na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema hatua hiyo imelenga kila mwananchi apate  huduma ya umeme kwa gharama nafuu.

Amesema kiwango cha uunganishaji wa umeme nchini kimefikia asilimia 52, huku Serikali ya Awamu ya Sita ikiweka lengo la kufikia asilimia 75 ifikapo mwaka 2030 linalotekelezwa kupitia Mpango wa Nishati uliosainiwa Januari 2025 wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika.

Akizungumzia suala la mita janja, Waziri Ndejembi amesema kuwa zoezi la uunganishaji wa mita hizo linaendelea nchi nzima na zitamwezesha mwananchi kupata umeme mara moja baada ya kununua token bila kutumia kifaa cha ziada cha kuingiza namba (CIU), hatua itakayopunguza changamoto zilizokuwepo katika mfumo wa awali.

Kuhusu upatikanaji wa umeme wa Gridi mkoani Rukwa, Waziri Ndejembi amesema mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa kilovoti 400 unaendelea kutekelezwa kupitia mkandarasi TBEA na itawezesha mkoa huo kupata umeme wa uhakika na wa kuaminika.

Aidha, ametaja mradi wa kuimarisha upatikanaji wa umeme katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Tabora na Simiyu, unaotekelezwa na mkandarasi Kalpataru.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, amepongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya umeme ya uhakika.

Amesema mafanikio hayo yametokana na maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa ya uzalishaji umeme ikiwemo Mradi wa Julius Nyerere (JNHPP) wa megawati 2,115, mradi wa umeme wa jua wa Kishapu unaotarajiwa kuanza kuzalisha megawati 50, pamoja na mradi wa Malagarasi wa megawati 49 unaoendelea kutekelezwa.

Mhe. Mgalu ameongeza kuwa kuimarika kwa upatikanaji wa umeme kumechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi na ongezeko la mapato ya Serikali, hususan katika sekta za viwanda na migodi, hali iliyoisaidia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuvunja rekodi ya makusanyo kwa kufikia Sh.trilioni 4.13 mwezi uliopita.

Vilevile, amepongeza REA kwa kuwapa kipaumbele wakandarasi wa ndani katika miradi ya usambazaji umeme pamoja na kampeni ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, akisisitiza umuhimu wa elimu hiyo kufika hadi ngazi ya shule za awali.














Serikali ya Tanzania na  Marekani zimeendelea kuimarisha ushirikiano wa kikazi katika sekta ya madini, hususan kwenye utafiti wa kina wa madini ya kimkakati yakiwemo madini ya kinywe, kwa lengo la kuimarisha usimamizi,  tija, ajira na mchango wa sekta hiyo katika pato la Taifa.

Akizungumza leo Januari 21, 2025 jijini Dodoma wakati wa kikao kilichohusisha ujumbe maalum kutoka Ubalozi wa Marekani ulioongozwa na Mhe. Andrew Lentz, Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini pamoja na wataalamu wa Wizara ya Madini, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amesema ushirikiano huo unatekelezwa kupitia Wizara ya Nishati na Madini ya Marekani (US Department of States Enegry and Mineral Governance Program) na unalenga kuinua uwezo wa kitaifa katika utafutaji wa madini (Mineral exploration) na usimamizi wa Sekta kwa ujumla.

Aidha, Waziri Mavunde kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, ameshukuru Serikali ya Marekani ambayo kwa miongo kadhaa sasa imekuwa mshirika mkubwa wa maendeleo ya Tanzania kupitia misaada mbalimbali ya kiufundi na kifedha, Mhe. Waziri amebanisha kuwa serikali ya Marekani imekuwa ikishirikiana kwa karibu na Serikali ya Tanzania katika miradi mbalimbali inayohusu  sekta za elimu, kilimo, miundombinu, afya, masuala ya utawala bora na demokrasia na mengine mengi.

Waziri Mavunde amesema kuwa misaada ya kiufundi inayotolewa na Serikali ya Marekani, ikiwemo  vitendea kazi kama vishikwambi na zana nyingine za kisasa za ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa za jiosayansi, ni kielelezo cha dhamira ya dhati ya Serikali ya Marekani ya kuimarisha usimamizi wa Sekta ya Madini na hivyo  kuunga mkono ajenda muhimu ya maendeleo ya nchi yetu.

Ameeleza kuwa ni wakati muafaka kwa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) pamoja na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kutumia fursa hiyo kikamilifu kwa kuongeza ujuzi na uwezo katika ukusanyaji, utunzaji, uchakataji na usambazajiwa taarifa za utafiti wa jiosayansi (Geo-data) kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Aidha, Waziri Mavunde amesema ushirikiano huo wa kuimarisha shughuli za utafiti za pamoja unatarajiwa kusaidia kubaini na kuibua migodi mikubwa ya madini ya kinywe katika mikoa ya Mtwara na Lindi. Hatua hii itaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa madini ya kinywe duniani. Waziri Mavunde alibainisha kuwa ifikapo mwaka 2050, uhitaji wa madini ya kinywe duniani utakuwa takriban tani milioni 4.5. Hii inathibitisha uhitaji mkubwa wa madini hayo kulinganisha na hali halisi ya upatikanaji wake kwa sasa.

Vilevile, Waziri amesema kupitia ushirikiano huu wataalamu wetu wa GST na STAMICO, watapata mafunzo yatakayowajengea uwezo wa kuweza kufanya utafutaji madini kwa njia za kisasa zaidi (state of art technologies) na pia kuongeza weledi kwa ujumla katika masuala yote yanayohusu usimamizi na uendelezaji miradi ya madini.

Kwa upande wake, Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Balozi Andrew Lentz, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano wa kikazi unaolenga matumizi ya teknolojia za kisasa, hususan katika sekta ya nishati safi na salama zitokanazo na vyanzo jadidifu, kuanzia madini ya kimkakati hadi yale muhimu kwa ajili ya maendeleo ya viwanda.

Balozi Lentz ameongeza kuwa msaada wa kiufundi unaotolewa katika eneo la utafutaji wa madini utaboresha kwa kiwango kikubwa matumizi ya mbinu nateknolojia za kisasa zaidi katika utafiti, usimamizi na uhifadhi wa taarifa a za jiosayansi, hivyo kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha tafiti za madini katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.

Serikali imekitaka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kuelekeza nguvu katika kuzalisha wataalamu wabunifu na wenye ujuzi wa hali ya juu watakaoweza kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya utalii, ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kauli hiyo imetolewa  na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Dennis Londo (Mb.) akiwa ameambatana na Viongozi mbalimbali wakati wa ziara yake ya kukagua eneo linalotarajiwa kujengwa Kampasi ya CBE Kilimanjaro lililopo wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro.

Amesema kampasi hiyo inatarajiwa kuwa sehemu ya majibu ya changamoto za kimuundo na kitaalamu zinazokabili sekta ya utalii, kwa kuandaa wataalamu watakaobobea katika biashara ya utalii na shughuli zote zinazohusiana, ikiwemo ukarimu, ujasiriamali, masoko ya utalii na usimamizi wa biashara za utalii.

“Tunatambua umuhimu mkubwa wa sekta ya utalii katika mapato ya Taifa na ajira, ndio maana tunataka CBE izalishe wataalamu watakaosaidia kuongeza thamani ya sekta hii, siyo kama waajiriwa pekee bali pia kama wamiliki na wabunifu wa makampuni na miradi ya utalii,” amesema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Profesa Edda Tandi Lwoga, amesema kampasi ya Kilimanjaro itakuwa kampasi ya tano ya chuo hicho nchini na itachangia kuongeza udahili wa wanafunzi wa sekta ya biashara.

Amesema kuwa kwa sasa wana Wanafunzi 24,657 na chuo hicho kikikamilima itaongeza zaidi ya Wanafunzi 2000.

Amesema usanifu wa majengo matatu ya awali tayari umeanza ikijumuisha madarasa yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,000, hoteli ya nyota tatu yenye uwezo wa kulaza wageni 52 kwa wakati mmoja pamoja na mabweni ya wanafunzi.

Amesema mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Mageuzi ya Elimu ya Juu (Higher Education Transformation Project) una thamani ya Sh bilioni 17.4, na baada ya taratibu za kifedha kukamilika, ujenzi wa kampasi unatarajiwa kuanza baadaye mwaka huu.

Nilipoolewa, nilijua ninaingia kwenye familia yenye ukaribu. Mume wangu alikuwa karibu sana na mama yake, jambo ambalo wengi waliniambia ni la kawaida. 

Alisema ni mapenzi ya mama na mwanawe, na kwamba hakuna cha kushangaza.

Nilijitahidi kuelewa, nikajipa moyo, na nikamwambia nafsi yangu kwamba labda mimi ndiye nilikuwa na wivu usio na msingi.

Lakini kadri siku zilivyopita, kulikuwa na vitu vilivyonifanya nikose amani.

Uamuzi wa mume wangu ulionekana kuongozwa zaidi na mama yake kuliko familia yetu. Kila jambo ninalopendekeza lilipingwa, kila mpango ulivunjwa, na mara nyingi nilijikuta nipo pembeni kana kwamba mimi si sehemu ya maisha yake.

Nilipojaribu kuzungumza naye, alisisitiza kuwa mama yake ananipenda na anataka mema yangu pia. Usiku mmoja, tukio lilitokea ambalo lilibadilisha kila kitu. 

Nilishuhudia jambo lililonionyesha kuwa kulikuwa na ushawishi mkubwa na usio wa kawaida juu ya mume wangu.

Haikuwa suala la mapenzi ya kawaida ya kifamilia, bali nguvu ya ajabu ya kumdhibiti, kumfanya ashindwe kusimama kwa uamuzi wake mwenyewe. Ndipo moyo wangu uliponiambia wazi: hapa kuna kitu kisicho cha kawaida.

Nilianza kudhoofika kihisia. Ndoa yangu ilikuwa baridi, mawasiliano yakakatika, na nilihisi kama kuna ukuta mkubwa kati yetu. 

Nilijaribu kushauriana na watu, lakini hakuna aliyenielewa kikamilifu. Wengi waliniambia nivumilie, wengine wakasema labda ninaruhusu mawazo kunitawala. Soma Zaidi.....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/alisema-ni-mapenzi-ya-mama-na-mwanawe-lakini-moyo-wangu-haukuamini-kilichotokea-usiku-moja-kilishangaza-wengi/

Nilianza kucheza betting kwa sababu nilitaka kuongeza kipato. Awali, kila kitu kilionekana rahisi kumbuka mechi, bet kidogo, na furaha ya kupata matokeo chanya. Lakini hatimaye, kila bet niliyofanya iligeuka hasara.

Nilijaribu mikakati tofauti, kuangalia takwimu, kusoma taarifa, na hata kuomba ushauri kutoka kwa marafiki, lakini kila wakati nilishindwa.
Baada ya miezi kadhaa, nilianza kuhisi uchovu mkubwa. Nilipoteza fedha, muda, na tumaini.

Nilijiona kama kila kitu kilikuwa kimekataa. Kila bet ilivyoshindwa ilikuwa kama kizuizi kipya kwenye maisha yangu, na moyo wangu ukaanza kuchoka. Nilihisi nimekosa bahati kabisa na labda nilitakiwa kuacha kabisa.

Hali ilizidi kuwa mbaya. Marafiki wangu walishangaa mimi kuendelea kucheza huku nikishindwa kila wakati. Nilihisi kushitakiwa na dunia, nikijua kuwa kila njama yangu ilikuwa ikibatilika. Nilianza kuuliza ndani yangu: Je, kuna njia yoyote ya kubadilisha hali hii? Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilijaribu-betting-lakini-nikafeli-kila-wakati-ila-nilipopata-huu-usaidizi-niliibuka-na-jackpot/

Haikuanza kama hadithi ya kutisha. Ilianza taratibu, kana kwamba maisha yalikuwa yanajifunga yenyewe. 

Kila nilichogusa kiliharibika. Kazi ilianza kunichosha bila sababu, pesa zilipotea ghafla, na afya yangu ikaanza kuyumba.

Nilikuwa nikijitahidi mara mbili zaidi, lakini matokeo yalizidi kuwa mabaya. Ndani yangu nilihisi kama kuna kitu kilikuwa kinanivuta chini kimya kimya. Nilijaribu kujilinda kwa njia nilizozifahamu. Niliomba, nilinyamaza, nilijiepusha na watu niliodhani wananiletea mkosi.

Lakini haikusaidia. Kila usiku nililala nikiwa na mawazo mazito, nikiamka nikiwa nimechoka kana kwamba sikulala. Ndoto zangu zilikuwa nzito na za kurudia. Nilihisi wazi kuwa kulikuwa na shambulio lisilo la kawaida.

Kadri siku zilivyosonga, nilianza kukata tamaa. Nilijiuliza kama kuna njia yoyote ya kutoka kwenye giza hilo. Nilihisi hakuna anayeweza kuelewa kilichokuwa kinanitokea. Watu waliniona kama mtu aliyeshindwa, lakini hawakujua nilikuwa napambana na kitu kisichoonekana.

Iliniumiza zaidi kuona juhudi zangu zote zikiishia patupu. Ndipo mtu wa karibu akanifungulia macho. Aliniambia wazi kwamba huenda nilikuwa nimetumiwa uchawi mbaya na mtu wa karibu niliyemwamini. Habari hiyo ilinistua, lakini pia ilinipa mwelekeo.

Niligundua kuwa nilikuwa nikijaribu kujilinda kwa nguvu zangu mwenyewe, lakini nilihitaji msaada sahihi. Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/alinitumia-uchawi-mbaya-nilijaribu-kujilinda-lakini-nilishindwa-nilihisi-hakuna-njia-suluhisho-hili-lilirudisha-amani-yangu/