Na John Walter -Babati

Mahakama ya Mwanzo Babati imewahukumu kifungo cha miezi miwili gerezani vijana wawili, Abubakari Semburi (18) na Abdul Hamza (18), wakazi wa Maisaka, kwa kosa la kuharibu mali ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA).

Washitakiwa hao walikutwa na hatia ya kuharibu mita za maji za BAWASA na kuziuza kama chuma chakavu katika kesi iliyowasilishwa na mlalamikaji, Sebastian Honorath, ambaye ni Meneja wa Ufundi wa BAWASA. 

Hukumu hiyo ilitolewa Januari 10, 2025, na Mheshimiwa Hakimu Kangida Kalembo, kwa mujibu wa kifungu cha 326(1) cha Sheria ya Kanuni za Adhabu, sura ya 16, marejeo ya mwaka 2022.

Wawili hao walikutwa na mita hizo  Desemba 24, 2024, majira ya saa saba mchana, katika maeneo ya Maisaka, mjini Babati.

Meneja wa Huduma kwa Wateja wa BAWASA, Rashidi Chalahani, amesema wamekuwa wakifuatilia kwa muda mrefu visa vya wizi wa mita za maji kutoka kwa wateja wao ambapo uchunguzi walioufanya ulipelekea kugundua mita hizo zikiwa zimeuzwa kwenye eneo la biashara ya chuma chakavu, hatua iliyosababisha kufunguliwa kwa kesi hiyo mahakamani.

Bw. Chalahani ametoa wito kwa jamii kutambua kuwa mita za maji ni mali ya umma na zinapaswa kuheshimiwa na kutunzwa. 

Aidha, amewataka wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika endapo wataona uharibifu au uhujumu wa miundombinu ya maji. 

Amesema vitendo kama hivyo vinakwamisha juhudi za serikali za kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi wote.

Hukumu hii ni onyo kwa wale wanaojihusisha na uharibifu wa miundombinu ya umma, huku ikisisitiza umuhimu wa kushirikiana katika kulinda rasilimali za taifa.

 

Katika kutafuta mke wa kumuoa kuna wakati nilifikia kipindi na kusema huwenda nina mikosi katika maisha yangu, hiyo ni kutokana kila mwanamke ambaye nilikuwa namtongoza alikuwa akinikatalia ombo langu.

Sikujua sababu ni nini hasa maana kama ni mvuto wa sura ninao, nina kazi ya kunipa kipato kizuri tu cha kijikimu na kuendeleza maisha yangu na hata kumuhudumia mwanamke ambaye nitakuwa naye katika mahusino.

Jina langu ni Yona toka Dodoma mkoani Tanzania, nina miaka 30 sasa nikiwa ni Baba wa watoto wawili na mke mmoja ambaye na mpenda sana na yeye ameonyesha kunipenda tangu siku ya kwanza tunaanza mahusiano yetu.

Mke wangu ni raia wa Marekani, alikuja Tanzania kutalii na ndipo aliweza kukutana na mimi na kuanzisha mahusiano, kukutana kwetu kulikuja baada ya mimi kuhaingaika sana kutafuta dawa za mvuto wa kimapenzi ambazo nilikuja kuzipata kwa mtu aitwaye Dr Bokko.

Mtu huyu nilikutana naye kupitia mitandao ya kijamii ambapo kwenye group moja la Facebook linalohusu mambo ya uchumba, dada mmoja alituma namba zake +255618536050 na kueleza Dr Bokko alifanikiwa lengo lake la kupata mume.

Nikiwa katika hali ya kukata tamaa, niliamua kupiga moyo konde na kumtumia Dr Bokko ujumbe mrefu kupitia WhatsApp nikimueleza kuhusu shida yangu.

Haikuchukua muda ujumbe wangu ukawa umejibiwa na mchakato wa kutumiwa dawa ukawa umeanza.

Baada ya kupata dawa zangu nilianza kuzitumia nikiwa na matumaini tele, sasa siku moja nikiwa nakatiza maeneo ya mjini nilikutana na dada mmoja wa kizungu ambaye alikuwa anahitaji nyumba ya kufikia wageni, kutokana mimi nilikuwa ni mwenyeji wa pale, nilimsaidia kupata nyumba hiyo mara moja.

Aliniomba namba yangu ya simu na kuniambia atanitafuta siku inayofuata, sikuwa na mawazo kuwa anaweza kuja kuwa mpenzi wangu, nilikuwa najua tu anaweza kunipa kazi za hapa na pale na baadaye kupata fedha.

Basi akanipigia tukakutana na kuzungumza sana, tukala na kunywa, tuliendelea kuzoeana hadi ikafika hatua za yeye kuonyesha dalili kuwa ananipenda.

Nilisita kumwambia kuhofia kuwa naweza kuharibu urafiki wetu, mwenyewe uvumilivu ulimshinda na kunitumia SMS kuwa ananipenda ana angependa niwe mume wake.

Hatimaye tulianza mahusiano hadi kuja kufunga ndoa na sasa tumejaliwa kupata watoto wawili wa kiume, maisha ni mazuri sana, nashukuru kwa tiba ya Dr Bokko ambaye ameweza kubadilisha maisha yangu kabisa.

 


Wataalam sekta za Wanyamapori na Misitu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Wizara ya Maliasili na Utalii  na Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakutana Jijini Arusha, kujadili utekelezaji wa mashirikiano baina ya pande mbili kwa ustawi wa uhifadhi na kukuza utalii nchini.

Wakizungumza wakati wa kikao hicho viongozi wa pande zote mbili, Bi. Kay Kagaruki, Mkurugenzi Msaidizi Matumizi Endelevu ya Wanyamapori , Kutoka Wizara ya Malisili na Utalii, Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Bw. Said Juma Ali Mkurugenzi wa Misitu, Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamesema  mashirikiano hayo yameleta tija katika sekta ya uhifadhi wa wanyamapori, Misitu na Utalii.

Aidha, Miongoni mwa mada zilizojadiliwa katika kikao  kazi hicho ambacho kimefanyika makao Makuu ya TAWIRI, ni pamoja na utekelezaji wa Mikataba ya Kikanda na Kimataifa, udhibiti wa ujangili, utoroshwaji wa nyara, usimamizi wa rasilimali za misitu, nyuki na wanyamapori, utafiti na biashara katika sekta za misitu, nyuki na wanyamapori na uendelezaji Utalii.









Wananchi wanaotumia barabara ya Same – Mkomazi wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa haraka wa daraja lililovunjika katika kijiji cha Mpirani, Same mapema mwezi huu kutokana na mvua. 

Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti, wananchi hao wameeleza kwamba kukatika kwa daraja hilo kulikata mawasiliano ya barabara kati ya Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro hadi Mkomazi kulisababisha usumbufu mkubwa kwao.

“Tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa kumtuma Waziri wa Ujenzi kuja hapa kuangalia hali na kutoa maelekezo. Tunashukuru kwamba daraja linapitika na tunaweza kuendelea na kazi zetu kama kawaida,” alisema Hassan Mkayanda ambaye ni mkazi wa Same.

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, alitembelea eneo hilo wiki iliyopita na kuagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kujenga daraja hilo usiku na mchana ili liweze kupitika tena na kuruhusu shughuli za kijamii na kiuchumi zirejee katika hali ya kawaida.

Barabara hiyo muhimu katika upande wa Kaskazini mwa Tanzania ni miongoni mwa zilizoathiriwa na mvua ambazo Waziri Ulega alizifanyika ukaguzi katika maeneo tofauti nchini katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.






Hakimu mkazi mkuu mfawidhi mkoa wa Lindi Consolata Singano akizungumza wakati kuwaapisha watendaji wa mkoa wa Lindi na kuwataka kila mtendaji anatakiwa kusimamia zoezi hilo kwa uadilifu uliotukuka.
Watendaji wa ngazi ya Mkoa katika mkoa wa Lindi wamekula Kiapo na kupewa mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.
Watendaji wa ngazi ya Mkoa katika mkoa wa Lindi wamekula Kiapo na kupewa mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.


Na Fredy Mgunda, Lindi.

Watendaji wa ngazi ya Mkoa katika mkoa wa Lindi wamekula Kiapo na kupewa mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.


Watendaji hao wamekula kiapo cha kutokuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa katika zoezi zima la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Watendaji hao wamekula kiapo cha kuzingatia maadili katika zoezi hilo kama walivyoapa kwenye maadili ya utumishi wa umma.

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha, Hakimu mkazi mkuu mfawidhi mkoa wa Lindi Consolata Singano alisema kila mtendaji anatakiwa kusimamia zoezi hilo kwa uadilifu uliotukuka.

Akitoa hotuba kwa watendaji hao,Makamu Mwenyekiti wa tume huru ya taifa ya uchaguzi, Mheshimiwa Jaji (R) (MST.) Mbarouk Mbarouk, aliwataka watendaji hao kuwafundisha kwa umahiri wasimamizi wa uandikishaji wa wapiga kura.

Jaji Mbarouk alisema kuwa kila mmoja anatakiwa kufanya kazi kwa weledi na kutumia uzoefu wao kufanikisha malengo ya tume.

Alimalizia kwa kusema kuwa Mawakala wa vyama vya siasa wanaruhusiwa kushiriki zoezi la kuandikisha wapiga kura lakini hawataki wa kuingilia majukumu ya watendaji wa tume ya uchaguzi.

 


Wananchi  wa Loliondo wilayani Ngorongoro na Simanjiro Mkoa wa Manyara wanatarajia kunufaika na huduma za mawasiliano kutoka kampuni ya Yas ambapo awali mawasiliano yalikuwa shida maeneo hayo ya pembezoni.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Januari 16, 2025 Ofisa Mkuu wa Biashara kutoka YAS, Isack Nchunda  amesema mabadiliko ya chapa ya kampuni hiyo yanakwenda sanjari na uboreshaji wa huduma za mawasiliano.

Amesema amesema hatua hiyo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake Kanda ya Kaskazini amesema upelekeaji wa mawasiliano hayo haswa maeneo ya Loliondo na Simanjiro ni kuboresha huduma bora za mawasiliano.

“Tumefika maeneo yenye changamoto ya mawasiliano kwa kasi ya 4G na 5G lakini pia huduma zetu za tigo pesa sasa zinajulikana kwa Mixx by Yas ikiwemo kampeni yetu ya magift ya kigift ambayo wateja wetu wanashinda zawadi mbalimbali za fedha taslim pamoja na gari ”

Wakati huo huo, Kaimu Mkurugenzi wa Yas Kanda ya Kaskazini, Daniel Mainoya ameongeza kuwa kampeni ya “magifti ya kugift” bado inaendelea huku washiriki wakiendelea kujishindia zawadi za kila siku na kila wiki ikiwemo zaidi ya sh, milioni 156 na simu janja 172 zilizobakia.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma leo tarehe 16 Januari, 2025.





Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) na Mkewe Salma Kikwete (kulia) wakielekea kupanda Treni ya Mwendo kasi ya SGR wakati wakielekea Jijini Dodoma kushiriki Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao utafanyika Januari 18 hadi 19, 2025. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa.


Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

WAJUMBE 600 wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiongozwa na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wametia fora kwa kusafiri na treni ya Mwendo kasi ya SGR kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Dodoma kushiriki mkutano huo utakaoanza Januari 18 na 19, 2025.

Hali hiyo imeonekana leo asubuhi Januari 15, 2025 katika Stesheni ya Treni ya Magufuli Dar es Salaam ambapo kuanzia saa 12 hadi saa 2: 30 asubuhi wajumbe hao makundi kwa makundi walifika katika stesheni hiyo na saa 3: 30 waliondoka kwa treni maalumu  kuelekea jijini Dodoma.

Mbali ya wajumbe hao watu wengine walioondoka na treni hiyo kwenda kwenye mkutano huo ni wasanii mbalimbali wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Nyerere na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali,

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa tukio hilo alisema jumla ya wajumbe 600 watasafiri kwa usafiri huo wa treni hiyo pamoja na wattu wengine jumla yao itakuwa ni 900.

“ Shirika letu limepewa heshima kubwa ya kuwasafirisha wajumbe hawa kwani wangeweza kusafiri kwa ndege, mabasi na magari yao binafsi lakini kazi hiyo tumepewa sisi,” alisema Kadogosa.

Alisema kwao kusafirisha wajumbe hao sio mara ya kwanza kwani walishawahi kusafirisha wajumbe kutoka mikoa ya kanda ya ziwa  na kuwa kwa kuaminiwa huko na kutumi usafiri wao kwao ni fursa kibiashara.

Alisema wajumbe ambao watatumia treni hiyo kusafiri kwenda Dodoma ni kutoka Zanzibar, Mtwara, Lindi, Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani.

“ Treni hii maalumu kwa ajili ya kusafirisha wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM haitaathiri  ratiba za safari za treni za kila siku ambazo zitaendelea kama kawaida,” alisema Kadogosa. 



Kila mmoja anapenda kuona maisha yake yanapiga hatua kila siku, hakuna mtu ambaye hapendi kuona maendeleo yake binafsi ingawa vikwazo ni vingi hasa upande wa utafuta riziki.

Jina langu ni Wangechi toka Nairobi nchini Kenya, nimeajiriwa kwenye kampuni kubwa ya usambazaji vinywaji baridi, nimefanya kazi hii kwa miaka zaidi ya 12 sasa.

Miaka mitatu iliyopita nilifanikiwa kupandishwa cheo na kuongezewa mshahara baada ya kufanya kwa miaka tisa bila kupata fursa hiyo ambayo kila mfanyakazi huwa anaitamani.

Sababu ya kuikosa kwa muda mrefu sio kwamba sikuwa na vigezo au ofisi yangu haikuwa na uwezo, laah hasha!, bali ni fitna za kikazi ambazo baadhi ya wafanyakazi wenzangu walikuwa wanazifanya kwa kushirikiana na uongozi.

Nasema hivyo kwa sababu nilishuhudia vijana wengie wakitoka katika Vyuo na kuja kuanza kazi wakiwa hawana uzoefu wowote lakini baada ya miaka miwili au mitatu wanapandishwa vyeo na mishahara huku mimi nikisaliwa mtupu.

Siku moja nilitembelewa nyumbani na rafiki yangu ambaye nilisoma naye miaka mingi iliyopita, nilimueleza kuhusu changamoto hiyo, aliniambia mbona sikumpa taarifa toka awali kwani ningekuwa tayari nimeshapata ufumbuzi.

Alichukua simu yake na kunipa namba ya Dr Bokko ambazo +255618536050 na kusema mtu huyu amekuwa msaada mkubwa kwa watu wote wenye changamoto kama yangu.

Basi tuliendelea na stori za hapa na pale na yule rafiki yangu, alipoondoka niliamua kupiga namba ile na kueleza shinda yangu kwa undani zaidi.

Dr Bokko alinialika Ofisi kwake pande za Kericho ili kupata huduma zaidi, nilifika na kuzungumza naye tena, kisha akanifanyia matambiko yake ambayo nakiri ndio hasa yamenisadia.

Tangu nilipotoka kwa Dr Bokko nilikaa nyumbani kwa muda wa wiki mbili bila kwenda kazini kwani nilikuwa likizo, baada ya likizo kuishi nilirejea kazi na kukutana na barua ya kunitaarifu kuwa nimepandishwa cheo na mshahara.

Siwezi kusahau jinsi siku hiyo nilikuwa na furaha kubwa, nilijua kuwa dawa ya Dr Bokko tayari imeshafanya maajabu yake ambayo yule rafiki yangu aliniambia.

Tangu wakati huo nimekuwa naishi maisha yangu vizuri kwani kipato ninachopata kinanitosheleza kabisa mimi na familia yangu tofauti na ilivyokuwa hapo awali kabla ya kupanishwa cheo. Shukrani za kipekee kwako Dr Bokko wangu.

Ukiachana na hayo, kumbuka Dr Bokko anaweza kukuwezesha kushinda bahati nasibu, kukuondolea migogoro ya mashamba, migogoro ya mapenzi, kuikinga biashara yako na kukupa mvuto wa kimapenzi.

 Na. Saidina Msangi na Asia Singano, WF, Dodoma


Serikali imesema kuwa itaendelea kushirikiana na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), na kuhakikisha Fedha zote za maendeleo zinazotolewa na Shirika hilo zinatumika kukamilisha azma ya kukuza uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), jijini Dodoma wakati akimuaga Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa Tanzania, Bw. Charalambos Tsangarides, aliyemaliza muda wake baada ya kuhudumu kwa zaidi ya miaka mitatu na nusu.

Alisema Serikali itaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuwaletea wananchi maendeleo na kukuza uchumi kwa ujumla kupitia juhudi mbalimbali inazofanya ikiwemo kutafuta fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati.

‘Kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, napenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kujitolea kwako katika kusaidia safari ya maendeleo ya kiuchumi ya nchi yetu, ninawahakikishia kwamba Timu yangu itawapa ushirikiano wote unaohitajika, kwa upande mwingine, nina furaha kuwajulisha kwamba tunaendelea vyema na hatua zetu za mageuzi chini ya program mpya ya Serikali ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia dirisha la Resilient and Sustainable Fund (RSF),’’ alisema Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba, mbali na kumuaga Kiongozi huyo wa IMF nchini, alitumia fursa hiyo kumkaribisha Kiongozi mpya anayechukua nafasi hiyo Bw. Nicolas Blancher, huku akimuahidi ushirikiano kutoka Serikali ya Tanzania.

‘’Napenda kuchukua fursa hii kumkaribisha rasmi Bw. Nicolas Blancher, kama Kiongozi wetu mpya wa “Mission” kwa Tanzania na tunafurahi kupata nafasi ya kushuhudia mwongozo kutoka kwa mtaalamu mwingine kama tulivyofanya na Kiongozi wa “Mission”anayemaliza muda wake katika kufanikisha maendeleo yetu endelevu ya kiuchumi’’ alisema Dkt. Nchemba.

Kwa upande wake Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa Tanzania, anayemaliza muda wake, Bw. Charalambos Tsangarides, ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa alioupata wakati akitekeleza majukumu yake nchini.

Aidha, ameipongeza Serikali kwa juhudi za kusimamia maendeleo ya kiuchumi na kuahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha ustawi wa wananchi wake hata baada ya kumaliza muda wake wa kuhudumu.

Naye Kiongozi Mpya wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Nicolas Blancher, ameahidi kushirikiana kikamilifu na Serikali ya Tanzania na kumhakikishia Dkt. Nchemba kuwa ataendeleza ushirikiano na kazi zilizofanywa na mtangulizi wake huku akisisitiza dhamira ya kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanatimia.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akimkabidhi zawadi Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, anayemaliza muda wake wa kuisimamia Tanzania baada ya kuhudumu kwa zaidi ya miaka mitatu na nusu, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiagana na Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, anayemaliza muda wake wa kuisimamia Tanzania, wakati alipofika kuagana na Waziri Mhe. Dkt. Nchemba pamoja na kumtambulisha Kiongozi mpya wa Shirika hilo anayechukua nafasi yake, Bw. Nicolas Blancher, katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akisalimiana na Kiongozi Mpya wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Nicolas Blancher, anayeshuhudia ni Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, aliyemaliza muda wake na Mwakilishi Mkazi wa IMF, Bw. Sebastian Acevedo, katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akizungumza wakati wa kikao kifupi akiagana na Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, anayemaliza muda wake nchini Tanzania na kumkaribisha Kiongozi Mpya wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Nicolas Blancher, katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.








Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamisi Shaaban, katika kikao chake na ujumbe wa IMF, katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.


Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, anayemaliza muda wake nchini Tanzania akizungumza wakati wa kikao kifupi na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati alipofika kwa ajili ya kumuaga pamoja na kumtambulisha Kiongozi Mpya wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Nicolas Blancher, katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.

Kiongozi Mpya wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Nicolas Blancher, akizungumza wakati wa kikao kifupi na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati alipofika kwa ajili ya utambulisho, katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Kiongozi wa Timu ya Wataalam ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Charalambos Tsangarides, anayemaliza muda wake, akifuatiwa na Kiongozi mpya wa IMF Bw. Nicolas Blancher, na Mwakilishi Mkazi wa IMF, Bw. Sebastian Acevedo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Amina Khamis Shaaban, Kamishna wa Idara ya Sera Bw. Johnson Nyella, na Kamishna Msaidizi idara ya Fedha za Nje Bw. James Msina. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Mhe. Waziri wa Fedha, jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa tume huru ya taifa ya uchaguzi, Mheshimiwa Jaji (R) ( MST.) Mbarouk Mbarouk alisema kuwa ni kosa la jinai mwananchi kujiandikisha zaidi ya mara moja
kaimu mkurugenzi tume ya uchaguzi Giveness Aswile alisema kuwa Mkoa wa Lindi kutumia vituo 1308 kuandika wapiga kura katika daftari la kudumu la mpiga kura ikiwa ni ongezeko 


NA Fredy Mgunda, Lindi.

Mkoa wa Lindi unatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 121,187 sawa na ongezeko la asilimia 18.7 ya wapiga kura 645,644 waliopo kwenye daftari la kudumu la wapiga kura hivyo mkoa wa Lindi unatarajia kuandikisha wapiga 768,641.

Akizungumza wakati wa mkutano wa tume na wadau wa uchaguzi wa kuhusu uboreshaji wa daftari la wapiga kura,kaimu mkurugenzi tume ya uchaguzi Giveness Aswile alisema kuwa Mkoa wa Lindi kutumia vituo 1308 kuandika wapiga kura katika daftari la kudumu la mpiga kura ikiwa ni ongezeko 

Awali akifungua mkutano huo, makamu Mwenyekiti wa tume huru ya taifa ya uchaguzi, Mheshimiwa Jaji (R) ( MST.) Mbarouk Mbarouk alisema kuwa ni kosa la jinai mwananchi kujiandikisha zaidi ya mara moja.


Jaji Mbarouk alisema kuwa ukibainika unaweza fungwa jela miezi sita au miaka miwili ili kujiepusha na kadhia hii hakikisha unajiandikisha mara moja tu.


Alisema kuwa Kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 10 Cha sheria ya Uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani Na.1 ya mwaka 2024,wafuatao hawana sifa za kuandikishwa kwenye Daftari,Iwapo mtu yupo chini ya kiapo Cha utii wa nchi nyingine tofauti na Tanzania,Hana akili timamu.

Aidha Jaji Mbarouk alisema mwananchi yoyote yule aliyewekwa kizuizini kama muhalifu mwenye ugonjwa wa akili,Amewekwa kizuizini kwa ridhaa ya Rais,Ametiwa hatiani kwa kosa ambalo adhabu yake ni kifo na anatumikia kifungo kwa kosa ambalo adhabu yake inazidi miezi sita iliyotolewa na mahakama.

"KUJIANDISHA KUWA MPIGA KURA NI MSINGI WA UCHAGUZI BORA"

 


Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amewataka wachimbaji kote nchini kuhakikisha wanazingatia sheria na kanuni ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima.

Mh Mavunde ameyasema hayo jana Jijiji Dodoma wakati wa kikao cha kutatua mgogoro wa mipaka ya Leseni uliyopo kati ya Kampuni ya Njake na Ndg. Patrick Miroshi, ambapo alizikutanisha pande zote mbili zenye mgogoro huo na kujadili kwa pamoja namna ya kutatua mgogoro huo na mwishoni kufikia muafaka wa kila mmoja kuendelea na uchimbaji katika eneo la leseni yake kwa amani.

“ Serikali inatamani kuona Sekta ya Madini inaendelea kukua na kutoa mchango wa ukuaji wa uchumi wa nchi yetu,migogoro siku zote inaturudisha nyuma katika jitihada za kuongeza uzalishaji na kuchochea Uchumi.

Ni maelekezo ya Mh. Rais Dkt. Samia Hassan juu ya utatuzi wa haraka wa migogoro kwenye sekta ya madini ili kuchochea ukuaji wake.

Niwatake maafisa Madini wote nchini kusimamia sheria na kanuni ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima na pia niwatake wachimbaji wote kuzingatia sheria katika shughuli zao za kila siku”, alisema Mavunde. 

Baada ya Taarifa ya Timu ya wataalamu iliyoundwa na Waziri Mavunde ilielekezwa nankuridhiwa kuwa Pande mbili hizo kila mmoja kurejea kwenye eneo la mipaka ya Leseni yake na Kampuni ya Njake kumfidia Ndg. Miroshi gharama alizoingia awali za uchimbaji.

Kikao hicho cha usuluhishi kilihudhuriwa na viongozi wa Wizara akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Mhandisi Yahya Samamba na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwamo.







MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi {CCM} Mkoa wa Arusha Thomas Roy Ole Sabaya amewataka wabunge wote Mkoani Arusha katika Majimbo yao kujifunza kwa Mbunge wa Jimbo la Longido ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini,Dkt Steven Kiruswa kwani amekuwa akifanya shughuli za kuwaletea maendeleo wananchi na kutatua changamoto zao bila makeke.

Sabaya alisema hayo disemba 3 mwaka huu mara baada ya Kiruswa kusoma kwa kifupi taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM katika kipindi cha miaka mitano {2020/25} aliyokuwa Mbunge mara baada ya wajumbe hao kuonyeshwa kwa video wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wa Wilaya ya Longido miradi yote iliyotekelezwa katika kipindi hicho.

Alisema Kiruswa ni Mbunge wa aina yake katika Mkoa wa Arusha,ni mbunge asiyekuwa na makundi,mwenye heshima ,hana dharau,munyenyekevu na hana makeke hivyo wabunge wengine wanapaswa kujifunza kutoka kwake kitabia na kiutendaji hiyo itasaidia kurahishisha CCM kushinda katika kipindi cha uchaguzi ujao.

Mwenyekiti huyo alisema sifa alizonazo Mbunge Kiruswa ndio  zimemsukuma Rais Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa Naibu Waziri wa Madini na ni Waziri pekee Mkoani Arusha hivyo alistahili kuteuliwa kwani amemsaidia sana Rais kusukuma maendeleo Longido.

‘’Wabunge Mkoani Arusha acheni makeke igeni tabia ya Kiruswa mtaisaidia kwa kiasi kikubwa CCM kufanya kazi yake kwa urahisi katika uchaguzi ujao ,majivuno,makundi na dharau kwa wengine haitawasaidia ’’alisema Sabaya

Aidha Mwenyekiti huyo aliwataka Madiwani katika kata zote 18 za jimbo la Longido kuhakikisha na wao wanasoma taarifa za utekelezaji wa ilani ya CCM katika Mkutano Mkuu wa Kata ili kuwaeleza wanaowaongoza shughuli walizofanya katika kipindi cha miaka mitano.

‘’Hii sio ombi ni kwa mujibu wa kanuni ya katiba ya CCM inaeleza hivyo kutoka kwa Mbunge,diwani na Rais lazima wazungumze walichokifanya katika kipindi hicho’’alisema Sabaya

Naye Mkuu wa Wilaya ya Longido,Salumu Kalli mbali ya kumpa maua yake Kiruswa kwa kazi nzuri ya utekelezaji wa ilani ya CCM Katika Jimbo la Longido aliwataka wanachama wa chama hicho kumpa ushirikiano Mbunge kwani ndio njia pekee ya kuleta maendeleo Longido.

Kalli alisema kuna baadhi ya watu bado ni vipofu na wanajifanya hawaoni kilichofanywa na Kiruswa na Rais katika jimbo la Longido hivyo aliwaasa kuacha fitina hizo kwani hazitawasaidia kwa sasa kwa kuwa watu wote wanaona tofauti ya sasa na miaka ya nyuma katika Jimbo hilo.

Alisema penye ukweli panapaswa kusemwa ukweli na kutofanya hivyo ni kuwakosea Mbunge na Rais mamilioni ya fedha yaliyopelekwa Longido anastahili kupongezwa Rais na hilo halina kificho.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido,Saimon Oteseu alisema Mbunge na Madiwani wamekuwa wakishirikiana kwa hali na mali katika kutatua changamoto za wananchi wa Jimbo la Longido na kuwaletea maendeleo na sio vinginevyo.

Alisema fedha zote zilizopelekwa Longido na Rais zimetumika kama zilivyokusudiwa kwa usimamizi madhubuti wa Mbunge na Madiwani katika kila kata na ndio maana wananc