Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga shilingi milioni 273.6 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme wa jua katika visiwa saba vya Wilaya ya Musoma ikiwemo Nyasaungu, Muroba, Kagongo, Nyamasanje, Rukuba na Iriga, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais, Mhe. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya umeme bila kujali eneo analoishi.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kutatua kero za wananchi katika Jimbo la Musoma Vijijini.

 Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa umeme ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo tayari vimefikiwa na huduma hiyo, huku hatua zinazofuata zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyosalia.

 Amebainisha kuwa kati ya vitongoji 374 vilivyopo, takribani 100 pekee ndivyo bado havijafikiwa na umeme huku zaidi ya vitongoji 50 vikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme.

Aidha, amesema Serikali imepokea maombi ya Mbunge wa Musoma Vijijini ya kuhakikisha vitongoji vyote ambavyo havina umeme vinafikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2027, akieleza kuwa lengo hilo linaendana na dhamira ya Serikali inayolenga kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.

Sambamba na hilo, Mhe. Salome amesema Wizara ya Nishati imeendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya uzalishaji mali, ikiwemo maeneo ya wachimbaji wa migodi wilayani Musoma Vijijini.

 Kuhusu  baadhi ya wananchi ambao miundombinu ya umeme imepita karibu na makazi yao lakini hawajaunganishwa na huduma hiyo,  amemuelekeza Meneja wa TANESCO Wilaya ya Musoma kuhakikisha wananchi hao wanaunganishiwa umeme.

Katika hatua nyingine, amewahimiza wananchi wa Musoma Vijijini kutumia nishati safi ya kupikia, akibainisha kuwa Serikali imetoa ruzuku ya zaidi ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ili kuyawezesha kupatikana kwa gharama nafuu.













 


Imeelezwa kuwa Serikali inaendelea na maandalizi ya kuufanya Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, kuwa mfano wa matumizi ya nishati safi kupitia mradi wa usambazaji wa gesi asilia.

Miundombinu hiyo itaunganisha  gesi asilia katika majengo ya Wizara, ofisi za Ubalozi, taasisi za Serikali, majengo ya biashara, hoteli, migahawa pamoja na makazi ya eneo la Mtumba.

Hayo yameelezwa na Mjiolojia kutoka Wizara ya Nishati, Nuru Helambili  wakati akitoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba). 

Helambili amesema mradi huo unalenga kujenga kituo cha kupokelea gesi (Gas receiving terminal) itakayokuwa ikisafirishwa kwa magari maalum kutoka Kituo Mama cha CNG kilichopo Mlimani City, Dar es Salaam.

Amefafanua kuwa mradi huo utahusisha pia ujenzi wa kituo cha kupunguza mgandamizo wa gesi, mtandao wa usambazaji na kituo cha kujazia gesi asilia kwenye magari. 

Helambili ameeleza kuwa  katika mwaka 2026/2027  Serikali itakamilisha tathmini ya athari kwa mazingira na jamii na kuanza taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo, huku Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) likitenga shilingi bilioni 14.40 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli hizo.

 



Akagua miradi ya maendeleo, ahimiza ikamilike kwa wakati.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu, amewaletea wananchi wa Mlimba kiasi cha Shilingi Bilioni 1.2 za kitanzania kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili za msingi zitakazoongeza fursa za elimu na kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.

Prof. Shemdoe amesema hayo Julai 3, 2026 katika Uwanja wa Tandare, Kata ya Igima, wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi hao, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji wa watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba.

"Leo nimekuja na habari njema kutoka kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaletea Shilingi 

Bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa Shule za Msingi Mgeta na Nganyangira. Nimejiridhisha kuwa fedha hizo tayari zimeingizwa kwenye akaunti ya halmashauri ili utekelezaji uanze mara moja," ameeleza Prof. Shemdoe.

Katika ziara hiyo, Prof. Shemdoe amezindua mabasi mawili ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, amefungua Shule ya Msingi Ngajengwa na kukabidhi vipaza sauti kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii ili kuimarisha utoaji wa elimu kwa wananchi katika maeneo yao.

Aidha, Prof. Shemdoe amekagua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba saba za watumishi, kukagua ujenzi wa wodi mbili za upasuaji katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, pamoja na kutembelea barabara inayojengwa ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikisababisha usumbufu kwa wananchi.

"Nimetembelea daraja kubwa linalojengwa katika Kata ya Mgeta ambalo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Shilingi Bilioni 1.7 kwa ajili ya ujenzi wake. Vilevile, kuna daraja lingine limepatiwa 

Shilingi Bilioni 1.7. Huu ni uwekezaji mkubwa unaoonyesha dhamira ya Mhe. Rais ya kuwaletea wananchi maendeleo," amesema Prof. Shemdoe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima amesema Wilaya ya Mlimba ndiyo kinara wa uzalishaji katika mkoa huo, huku akibainisha kuwa mapato ya halmashauri hiyo yanaendelea kuongezeka kwa kasi kuliko halmashauri nyingine kutokana na kuimarika kwa shughuli za uzalishaji na ukusanyaji wa mapato.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Mlimba, Mhe. Dkt. Kellenrose Rwakatare amesema Serikali inaendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kujenga na kuimarisha miundombinu ya shule, ikiwemo kukamilisha majengo yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi, hatua inayochangia kuwapatia wanafunzi mazingira bora ya kujifunzia.













Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeelekeza kuwa wananchi wote ambao wamepitiwa na miundombinu ya umeme lakini bado hawajaunganishiwa huduma hiyo waunganishiwe  kwa gharama ya Shilingi 27,000 tu.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Julai 3, 2026, katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Butiama, mkoani Mara, katika ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Mwigulu Nchemba.

Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Salome amemuelekeza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara pamoja na Meneja wa TANESCO Wilaya ya Butiama kubaini maeneo yote ambayo nyaya za umeme zimepita juu ya kaya za wananchi lakini bado hawajaunganishwa na huduma husika ili hatua stahiki zichukuliwe, ikiwemo kufunga transfoma katika maeneo yenye uhitaji.

Amesisitiza kuwa umeme ni nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi, akieleza kuwa unachochea ukuaji wa uchumi, huboresha huduma za afya na kuinua ustawi wa wananchi, hivyo Serikali itaendelea kuhakikisha wananchi wote wanaostahili wanafikiwa na huduma hiyo.

Aidha, amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga zaidi ya Shilingi bilioni 38 kwa ajili ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini katika Mkoa wa Mara. Fedha hizo zitawezesha kuendelea kusambaza umeme katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Ameongeza kuwa, kufuatia maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali itahakikisha vitongoji 51 ambavyo havina umeme  mkoani Mara vinafikiwa na nishati hiyo.

Kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, Mhe.Salome amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

 Amesema katika Mkoa wa Mara tayari Serikali imesambaza majiko ya gesi zaidi ya 19,000 na majiko banifu zaidi ya 8,000 ili kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kulinda afya za wananchi na kuhifadhi mazingira.

Katika mkutano huo wa hadhara, wananchi waliwasilisha jumla ya kero sita, ambapo kero tatu zilipatiwa ufumbuzi papo hapo, huku hatua za kushughulikia kero zilizobaki zikiendelea kuchukuliwa na Serikali.







Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Dkt. Evaline Munisi amesema kuwa Mafanikio ya utekelezaji wa Dira 2050 yanategemea Mahusiano mema kwa kuwa ndio matokeo ya Utawala bora, Amani, Usalama na Maendeleo endelevu.
Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imebainisha kuwa mwaka 2025 ilikamata tani 31.76 na lita 183,500 za kemikali bashirifu, huku ikizuia tani 734 kuingia nchini kinyume cha sheria, ikisema waandishi wa habari wanapaswa kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya uhalifu huo kupitia utoaji wa taarifa sahihi kwa umma.
 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Na. Veronica Mwafisi-Dar ES Salaam 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ina nafasi ya kipekee katika kujenga na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji wa majukumu ya Serikali kila siku.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2026 wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya TPSC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kikwete amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka kipaumbele katika uimarishaji wa Utumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye tija. 

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania si tu taasisi ya mafunzo, bali ni nguzo muhimu ya Serikali katika kujenga rasilimaliwatu yenye maarifa, stadi, maadili na uzalendo unaohitajika katika kutumikia umma kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatutaka kuwa na Taifa lenye uchumi wa kisasa, ushindani wa kimataifa, matumizi makubwa ya teknolojia, na huduma za umma zenye ufanisi wa hali ya juu. Hivyo, mafanikio ya Dira hiyo yatategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo. 

“Chuo hiki kina wajibu mkubwa wa kuhakikisha  Watumishi wa Umma wanapata maarifa na stadi zinazolingana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja ili kuwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo,” amesema Waziri Kikwete.

Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza watangulizi wake kwa usimamizi mzuri ambao umechangia mafanikio makubwa ya Chuo hicho huku akimshukuru Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Juma Mkomi kwa kuendelea kusimamia Chuo hicho kiutendaji. 

Vilevile, Waziri Kikwete ameipongeza Bodi ya Ushauri ya TPSC, Menejimenti, Watumishi, Wanafunzi na wadau wote kwa mchango wao katika safari ya kutimiza miaka 25 ya mafanikio ya chuo hicho.

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mhe. Waziri kuzungumza na wadau katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa waajiri kutumia Kampasi za TPSC zilizo katika kanda zao ili kuwawezesha watumishi ikiwemo waajiriwa wapya kupata mafunzo ya awali.

“Kampasi katika Kanda hizo zimewekwa kimkakati ili kusogeza huduma za chuo katika mikoa mbalimbali, hivyo Waajiri wazitumie kikamilifu kwa watumishi kupata mafunzo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.” Amesisitiza Katibu Mkuu Mkomi.

Amezitaja Kampasi hizo kuwa ni Dar es Salaam, Mbeya, Tanga, Singida, Tabora na Mtwara na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na TPSC za kumiliki majengo yao ambapo Kampasi ya Singida inaendelea na ujenzi wa majengo 30 na Kampasi ya Tanga majengo 15.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TPSC, Dkt. Florens Turuka amesema Bodi itaendelea kutoa ushauri ili Chuo kiendelee kuwa kinara katika masuala mbalimbali ikiwemo kujenga rasilimaliwatu yenye maadili, na yenye tija kwa taifa.

Akiwasilisha taarifa ya miaka 25 ya TPSC, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho amesema tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo taaluma, rasilimaliwatu na miundombinu.


Kamati ya Sera ya Fedha ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imepandisha kiwango cha Riba yaBenki Kuu (CBR) kutoka asilimia 5.75 hadi asilimia 6.25 katika robo ya tatu ya mwaka inayoanza Julai hadi Septemba 2026.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kuanzisha Kijiji cha Mazingira, jukwaa maalum linalowakutanisha wananchi, wadau wa mazingira na taasisi mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu, kuonesha ubunifu na teknolojia rafiki kwa mazingira, pamoja na kuhamasisha uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira.
Na. Mwandishi Wetu - Arusha

Tanzania ipo tayari kwa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) ikiwa mwenyeji kwa kushirikiana na Kenya na Uganda ambapo maandalizi yamefikia hatua nzuri kwa kuzingatia viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) vinavyotakiwa.


Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam.


Kadri Maonesho ya 56 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanavyoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeendelea kuthibitisha kuwa teknolojia ya nyuklia siyo teknolojia ya kutumika kwenye uzalishaji wa nishati pekee, bali ni nyenzo muhimu inayochochea maendeleo ya kiuchumi, biashara, uwekezaji na ustawi wa jamii kupitia matumizi yake katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Leo ikiwa ni siku ya sita tangu kuanza kwa maonesho hayo yaliyofunguliwa rasmi tarehe 28 Juni na yanayotarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Julai 2026, banda la TAEC limeendelea kuwa moja ya maeneo yanayovutia idadi kubwa ya wananchi, wanafunzi, watafiti, wawekezaji, wafanyabiashara na wadau kutoka ndani na nje ya nchi wanaotaka kupata uelewa kuhusu nafasi ya teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya Tanzania.

Ushiriki wa TAEC katika maonesho haya unaendana na dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu sahihi kuhusu matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia pamoja na mchango wake katika kukuza uchumi wa taifa kupitia uzalishaji wenye tija, huduma bora za afya, usalama wa chakula, maendeleo ya viwanda, utafiti na uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza katika banda la TAEC lililopo ndani ya Banda Kubwa la China, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TAEC, Bwana Peter Ngamilo, amesema maonesho ya Sabasaba ni jukwaa muhimu linaloiwezesha TAEC kuwasiliana moja kwa moja na wananchi na wadau mbalimbali, kuwaelimisha kuhusu majukumu ya Tume pamoja na fursa zinazotokana na matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya Taifa.

“Lengo letu kubwa ni kuhakikisha wananchi wanafahamu kuwa teknolojia ya nyuklia ni nyenzo muhimu ya maendeleo. Kupitia maonesho haya tunaendelea kutoa elimu kuhusu matumizi salama ya mionzi, wajibu wa TAEC katika usimamizi na udhibiti wa matumizi ya mionzi nchini, pamoja na namna teknolojia hii inavyochangia kukuza biashara, kuongeza tija katika uzalishaji na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Bwana Ngamilo.

Ameeleza kuwa wananchi wengi wamekuwa wakitembelea banda la TAEC kwa lengo la kupata ufafanuzi kuhusu teknolojia ya nyuklia na matumizi yake katika sekta mbalimbali, hali inayoonyesha kuwa uelewa wa jamii kuhusu teknolojia hiyo unaendelea kuongezeka siku hadi siku.

Katika sekta ya afya, TAEC imekuwa ikiendelea kutoa elimu kuhusu matumizi ya mionzi katika uchunguzi wa magonjwa, tiba ya saratani, tiba za nyuklia na uchunguzi wa kitaalamu unaowezesha madaktari kutoa huduma zenye usahihi zaidi kwa wagonjwa. Matumizi haya yameendelea kuboresha ubora wa huduma za afya nchini na kuongeza uwezo wa taasisi za tiba kutumia teknolojia za kisasa katika kuokoa maisha ya wananchi.

Kwa upande wa kilimo, wananchi wanaelimishwa namna teknolojia ya nyuklia inavyosaidia kuboresha mbegu za mazao, kuongeza uzalishaji, kudhibiti wadudu waharibifu wa mazao, kuhifadhi chakula baada ya kuvunwa na kuongeza usalama wa chakula. Teknolojia hizi zinachangia kuongeza ushindani wa bidhaa za kilimo katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Katika sekta ya mifugo, TAEC inaendelea kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika utambuzi wa magonjwa ya mifugo, kuboresha uzalishaji wa mifugo, kuimarisha lishe ya wanyama na kusaidia programu za uzalishaji zinazoongeza tija kwa wafugaji.

Sekta ya viwanda nayo ni miongoni mwa maeneo yanayonufaika kwa kiwango kikubwa kupitia matumizi ya teknolojia ya nyuklia. Kupitia teknolojia za mionzi, viwanda vinaweza kufanya ukaguzi wa ubora wa bidhaa bila kuziharibu (Non-Destructive Testing), kupima unene wa bidhaa mbalimbali, kufanya vipimo vya ubora wa miundombinu, kutambua hitilafu katika mitambo na kuongeza usalama wa uzalishaji. Teknolojia hizi husaidia kupunguza gharama za uzalishaji, kuongeza ubora wa bidhaa na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Aidha, katika sekta ya nishati na utafiti, TAEC inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa kujenga uwezo wa matumizi ya teknolojia za nyuklia katika tafiti zinazolenga kutatua changamoto za maendeleo, usimamizi wa rasilimali za maji, ulinzi wa mazingira na matumizi bora ya maliasili.

Kwa mujibu wa Bwana Ngamilo, elimu inayotolewa katika maonesho haya pia inalenga kuondoa dhana potofu ambazo baadhi ya wananchi wamekuwa nazo kuhusu teknolojia ya nyuklia.

“Wananchi wengi walikuwa wakihusisha teknolojia ya nyuklia na silaha pekee, lakini wanapofika katika banda letu wanajionea ushahidi kuwa teknolojia hii inagusa maisha yao ya kila siku kupitia huduma za afya, uzalishaji wa chakula, maendeleo ya viwanda, utafiti, usimamizi wa mazingira na sekta nyingine nyingi zinazochochea maendeleo ya uchumi wa Taifa.”

Maonesho ya Sabasaba yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha taasisi za Serikali, sekta binafsi, wawekezaji na wananchi katika kuonesha bidhaa, huduma na ubunifu unaochochea biashara na maendeleo ya uchumi wa Tanzania. Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha teknolojia ya nyuklia inatumika kwa amani, usalama na manufaa ya wananchi wote huku ikichangia utekelezaji wa dira ya maendeleo ya taifa kupitia sayansi, teknolojia na ubunifu.

TAEC inaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake lililopo ndani ya Banda Kubwa la China, Vyumba Na. 60 na 61, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam, ili kujionea teknolojia mbalimbali zinazotumiwa nchini na kupata elimu kuhusu mchango wa teknolojia ya nyuklia katika kujenga uchumi imara, kuongeza ushindani wa biashara na kuharakisha maendeleo endelevu ya Tanzania.



Nilijua wazi kuwa ardhi ile ilikuwa yangu kihalali. Niliinunua kwa jasho langu mwenyewe baada ya miaka mingi ya kufanya kazi ndogo ndogo, kujiwekea akiba, na hatimaye kupata kipande hicho cha ardhi kando ya mto katika kijiji cha baba yangu. Ilikuwa sehemu niliyoipenda sana, na ndoto yangu ilikuwa ni kujenga nyumba ndogo ya kupumzikia baada ya kustaafu kazi ya ualimu.

Lakini mambo yalibadilika nilipopata taarifa kwamba kijana mmoja wa ukoo, ambaye sikuwa hata na ukaribu naye, alikuwa ameweka uzio na kuanza kulima kwenye ardhi yangu kana kwamba ni yake. Nilipokwenda kumhoji, alinikaripia na kusema kuwa hiyo ardhi ni ya familia, na mimi sina haki nayo kwa sababu sikuishi kijijini kwa muda mrefu.

Nilichanganyikiwa, nikamuonyesha stakabadhi za umiliki halali lakini bado alikataa kuondoka.
Nilifikisha suala hilo kwa uongozi wa kijiji, lakini hata hapo hakukuwa na msaada wowote wa maana. Kila mtu alionekana kumwogopa au kumfurahia kwa sababu ya pesa zake. Nikaamua kufungua kesi mahakamani, nikiwa na imani kwamba haki itatendeka.

Lakini niligundua kuwa hata kwenye mchakato wa kisheria, si kila kitu ni haki na uwazi. Mtu huyo alianza kutumia mbinu chafu, akijaribu kushawishi mashahidi wangu na hata kutoa rushwa kwa baadhi ya maafisa.SOMA ZAIDI.
Siku hiyo siwezi kuisahau, hata kama nitazeeka. Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, majira ya saa mbili asubuhi, niliporudi nyumbani mapema kutoka sokoni baada ya kusahau mkoba wangu. Nilipoingia chumbani kwangu, sikutegemea kabisa kuona kile nilichokiona.

Mume wangu aliyekuwa ameniahidi uaminifu wa milele, alikuwa kitandani na bosi wangu wa kazi mwanamke ambaye nilimwamini sana, ambaye alikuwa kama dada yangu mkubwa.
Nilishtuka, nikakosa hata nguvu ya kuhema. Waliposhtuka kuniangalia, waliruka kitandani na kuanza kutoa visingizio visivyokuwa na kichwa wala miguu.

Nilihisi kama dunia imeanguka juu yangu. Machozi yalinibubujika kwa uchungu na hasira. Niliwageukia na kusema kwa sauti ya chini lakini yenye uzito, “Mmeharibu kila kitu.” Baada ya tukio hilo, maisha yangu yalibadilika. Nilikuwa na hasira, huzuni, na chuki ndani yangu. Kazini sikuweza tena kustahimili kumuona bosi wangu, hivyo nikaandika barua ya kuacha kazi.

Nyumbani hali ilikuwa mbaya zaidi mume wangu alianza kujitetea kwa kunilaumu eti nilikuwa nikimnyima haki zake za ndoa. Alisema nilikuwa mbali kihisia, na kuwa hiyo ndiyo sababu ya yeye kutafuta “faraja” kwingine.
Nikiwa nimevurugika kiakili na kihisia, rafiki yangu wa karibu alinitembelea na kunikuta katika hali ya unyonge mkubwa.SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miezi mitatu, usingizi haukuwahi kuwa wa amani katika familia yetu. Kila usiku, hasa saa sita kamili, mtoto wetu mchanga alikuwa akiamka kwa vilio vya ajabu, vilivyokuwa na sauti ya hofu, maumivu, na mshtuko.

Mwanzo tulidhani ni ndoto za kawaida au labda tatizo la kiafya la mtoto, lakini tulipojaribu kumpeleka hospitali, madaktari hawakugundua tatizo lolote.

Kila mara alipoamka kwa vilio hivyo, hakuwa na homa, hakulalamika maumivu ya tumbo, na mara nyingi alitulizwa haraka lakini baada ya dakika chache, kilio kilianza tena. 

Kama mzazi, ni jambo la kutisha kuona mtoto wako akiteseka na huwezi kuelewa sababu. Nilianza kuchunguza mazingira ya chumba chetu. Nikahakikisha hakuna mbu, baridi kali wala kelele za usiku zinazoweza kumsumbua.

Lakini hakuna kilichobadilika. Tulijaribu kulala chumba kingine kwa wiki moja, na cha kushangaza mtoto alilala kwa utulivu kabisa. 

Lakini mara tu tuliporudi kwenye chumba chetu cha kawaida, vilio vilirejea saa hiyo hiyo saa sita usiku. Siku moja, nikiwa nimemchukua mtoto chumbani kumtuliza, nilihisi baridi kali ikipita miguuni mwangu kana kwamba mtu alikuwa amepita. SOMA ZAIDI.
Mara ya kwanza niliposikia mume wangu akisema kwa utani kuwa mimi ni kama friji, nilicheka tu. Lakini baadaye maneno hayo yalianza kuniuma. Hakusema moja kwa moja, lakini kila wakati tulipokuwa karibu, nilihisi kama kuna kitu kinamkera. Hakuwa akifurahia tendo la ndoa kama zamani, na mara nyingi alinitafuta visingizio.

Kama mwanamke, nilianza kujihisi duni. Ushawishi wangu wa kimapenzi ulizidi kupungua, na hali hiyo ilianza kuathiri ndoa yetu kwa ujumla. Nilipojaribu kumkabili, alinikwepa. Lakini siku moja nilimsikia akiongea na rafiki yake akisema kuwa mimi “sijui kumfurahisha mume,” na kwamba nilikuwa kama barafu kitandani.

Machozi yalinibubujika usoni mwangu. Nilimpenda sana mume wangu, na sikutaka kumpoteza. Lakini kwa hali ile, nilijua ni suala la muda tu kabla hajaanza kutoka nje ya ndoa au kuniacha kabisa. Nilianza kutafuta suluhisho. Niliangalia YouTube, nilisoma blogu, nikajaribu hata zile chai za mitishamba zinazouzwa mitandaoni lakini hakuna kilichosaidia.

Nilijaribu kujifunza mbinu mpya za kimapenzi, lakini bado hakukuwa na mabadiliko. Mume wangu alikuwa baridi zaidi yangu sasa. Hatukuwa tukiongea sana, hatukushiriki mapenzi kwa wiki kadhaa, na chumba chetu kiligeuka kuwa kama hosteli ya watu wawili wasiojuana.SOMA ZAIDI.
Wakati mwingine, maisha ya biashara yanaweza kuwa magumu kuliko tunavyoweza kuyakubali. Ndivyo ilivyokuwa kwa biashara yangu. 

Nilikuwa na biashara ya kuuza bidhaa maarufu mjini kwetu, na ingawa mwanzoni nilikuwa na mafanikio makubwa, hali ilianza kubadilika kwa haraka. Wateja walikuwa wanakuja kwa wingi, lakini walikuwa wanapungua kwa kila mwezi uliopita.

Hali ilionekana kuwa mbaya sana. Nilikuwa nimejitolea kwa bidii na kuongeza juhudi, lakini kila nilipokuwa najaribu kuboresha hali, biashara yangu iliendelea kuporomoka. Kwa kweli, kila nilichofanya kilionekana kuwa hakileti matokeo mazuri. Hata nilipotafuta njia mpya za kuvutia wateja, hakukuwa na mabadiliko yoyote.

Nilikuwa nikiingia kwenye madeni, wateja walikuwa wanakimbia, na hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya. Huo ndio ulikuwa wakati mgumu zaidi maishani mwangu. Nilijua kuwa kama sitapata suluhisho haraka, biashara yangu ingeweza kufa kabisa. Nikiwa katika huzuni na shinikizo, nilijua kuwa nilikuwa nikikosa kitu. SOMA ZAIDI.

 

Na Munir Shemweta

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania (IST), ambapo pande hizo zilijadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya taaluma ya Upimaji Ardhi na sekta ya ardhi nchini.

Ujumbe wa IST ulioongozwa na Rais wa taasisi hiyo, Dkt. Julian Magezi Ijumulana na Upande wa Wizara ya Ardhi uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Upimaji Ardhi ambaye ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansoor, ulimtembelea Waziri Dkt. Akwilapo kwa lengo la kujitambulisha.

Aidha, ujumbe huo ulimuelezea Mhe Dkt Akwilapo mikakati ya taasisi hiyo, ikiwemo maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 45 ya kuanzishwa kwake pamoja na Mkutano Mkuu wa Mwaka unaotarajiwa kufanyika Novemba 2026 katika Mkoa wa Mwanza.

Akizungumza katika kikao hicho, Julai 2, 2026 jijini Dar es Salaam Dkt. Akwilapo alisema ameyapokea mawazo na mapendekezo yaliyowasilishwa na Taasisi ya Wapima Ardhi Tanzania na kuahidi kuwa serikali itayafanyia kazi kwa kuzingatia maslahi ya sekta ya ardhi na maendeleo ya nchi.

Aidha, Waziri Dkt. Akwilapo alisisitiza kuwa swala la sheria ya Upimaji ardhi sura 324 na usajili wa Wapima ardhi sura 270 amelipokea na atafanyia kazi kwa haraka kwani Wapima Ardhi wana nafasi muhimu katika  kupunguza na kuondoa migogoro ya ardhi nchini kupitia upimaji sahihi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, akihutubia waumini na wageni mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Kumbukizi ya Damu ya Yesu (C.PP.S) ya Provinsi ya Tanzania yaliyofanyika katika Viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida .

Na: OWM (KAM), Manyoni - Singida

Serikali imesema inatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii, kudumisha amani na kukuza maadili nchini, huku ikizitaka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza malezi bora kwa watoto na vijana ili kujenga taifa lenye ustawi na mshikamano.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu Amesema hayo  alipomwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Kumbukizi ya Miaka 60 ya Uwepo wa Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania iliyofanyika katika viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana, Manyoni, Mkoani Singida.

Amesema, maendeleo ya taifa hayawezi kupatikana kwa juhudi za Serikali pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo taasisi za dini, sekta binafsi na wananchi, hivyo alibainisha kuwa maadhimisho hayo ya miaka 60 Uwepo wa Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania ni ishara ya urafiki, mshikamano na dhamira ya pamoja ya kujenga Tanzania yenye amani na matumaini.

“Ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini umeendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa kwa kusaidia utoaji wa huduma za kijamii, kuimarisha maadili na kujenga jamii yenye amani,” amesema

Kwa upande wake, Mhe. Sangu ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuwa sauti ya matumaini kwa waliokata tamaa, chanzo cha upatanisho katika jamii na daraja la kuunganisha wananchi pale panapojitokeza migawanyiko. Ameongeza kuwa, kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo na kwamba Watanzania wanapaswa kuendelea kuilinda na kuirithisha kwa vizazi vijavyo.

Vilevile, Alisisitiza kuwa vijana wanapaswa kutumia vipaji na maarifa yao bila kuacha misingi ya imani, akieleza kuwa maendeleo ya kweli yanahitaji kizazi kinachounganisha elimu, maadili na hofu ya Mungu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego amesema, Serikali itaendelea kuzifanyia kazi changamoto zilizowasilishwa na viongozi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania, ikiwemo ushirikiano katika sekta ya afya na huduma za kijamii ili shirika hilo liendelea kutoa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu, Padre Vedasto Ngowi ameshukuru Serikali kwa ushirikiano uliopo na kueleza matumaini yao ya kuendelea kushirikiana katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kiroho na kijamii.

Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu limesajiliwa na Serikali ya Tanzania kama (The Society of the Precius Blood) ambapo linajishughulisha na kazi za kitume kwa Mapadre na Mabruda kwa lengo la kueneza upendo wa Kristo aliouonesha alipomwaga Damu yake msalabani kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano Mhe.Deus Sangu akisalimiana na Baba Askofu Mkuu wa Jimbo la Singida Katoliki Mhashamu Edward Mapunda katika Kumbikizi ya Damu ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania iliyofanyika katika Viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana, Wilaya ya Manyoni, Singida.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, akihutubia waumini na wageni mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Kumbukizi ya Damu ya Yesu (C.PP.S) ya Provinsi ya Tanzania yaliyofanyika katika Viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.