Kila nilipomwona, nilihisi furaha ambayo sikuweza kuelezea kwa maneno. Alikuwa mchangamfu, mwenye heshima, na mtu ambaye nilifurahia kuwa karibu naye. Tatizo pekee lilikuwa kwamba hakujua nilivyokuwa najisikia.
Kwa kweli nilikuwa mwoga.
Mara nyingi nilitaka kumwambia ukweli, lakini kila nilipopata nafasi, nilikosa ujasiri. Niliogopa kukataliwa na kuharibu urafiki uliokuwepo kati yetu. Miezi iligeuka miaka.
Kadri muda ulivyopita, nilianza kuamini kwamba huenda nafasi yangu ilikuwa imepita.
Nilijaribu kujisahaulisha na kuendelea na maisha, lakini kila nilipokutana naye, hisia zile zilikuwa zinarudi tena. SOMA ZAIDI.
Kila niliposimama kuzungumza mbele ya watu, moyo wangu ulianza kwenda mbio. Mikono ilitetemeka na wakati mwingine nilisahau hata kile nilichotaka kusema.
Mimi nilibaki nyuma kwa sababu ya hofu iliyokuwa ndani yangu. Kadri miaka ilivyopita, confidence yangu ilizidi kupungua.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua uwezo nilikuwa nao. Lakini uwezo ule ulikuwa umefichwa nyuma ya hofu na kutojiamini. SOMA ZAIDI.
Tatizo lilikuwa moja.
Hakukuwa na ushahidi. Kila nilipoamka asubuhi na kukuta kuku wamepungua, nilianza kuwashuku watu tofauti. Lakini sikuwa na namna ya kuthibitisha tuhuma zangu.
Hasara ilikuwa inaongezeka, na kila nilipoongeza ulinzi, mwizi alionekana kupata njia nyingine ya kuendelea na wizi wake.
Watu wengi walianza kuniambia nikubali hasara na kuendelea na maisha. Lakini sikuwa tayari kufanya hivyo.
Kuku wale walikuwa sehemu ya chanzo changu cha kipato, na nilijua lazima siku moja ningepata ukweli.SOMA ZAIDI.
Kwa hiyo haikuwa rahisi. Kila siku nilifungua biashara yangu mapema na kusubiri wateja. Wakati mwingine nilikaa kwa saa nyingi bila kufanya mauzo ya kuridhisha.
Kulikuwa na nyakati nilijiuliza kama nilifanya makosa kuanzisha biashara ile. Nilikuwa najituma kwa bidii, lakini matokeo hayakuwa yale niliyotarajia.
Nilisikiliza maoni yao na kujitahidi kufanya maboresho pale nilipoweza. Polepole baadhi ya watu walianza kugundua tofauti. Lakini bado ushindani ulikuwa mkubwa.SOMA ZAIDI.
Kila siku niliishi kwa tahadhari. Mabadiliko ya hali ya hewa, vumbi, moshi, au hata harufu kali zingeweza kunisababishia matatizo ya kupumua.
Usiku ndiyo ulikuwa wakati mgumu zaidi.
Mara nyingi nilishtuka usingizini nikihangaika kupata hewa ya kutosha. Wakati familia yangu ilikuwa imelala kwa amani, mimi nilikuwa nimekaa kitandani nikijaribu kutuliza pumzi zangu. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kuogopa kufanya baadhi ya shughuli nilizozipenda. Nilihofia kwamba pumu ingeanza ghafla na kunifanya nishindwe kuendelea na nilichokuwa nikifanya. Miaka ilipita katika hali hiyo. Nilitafuta ushauri wa wataalamu wa afya na kujifunza namna ya kudhibiti hali yangu.
Ingawa kulikuwa na nyakati nilizopata nafuu, bado kulikuwa na vipindi ambavyo pumu ilinisumbua sana.SOMA ZAIDI

Wathibiti Ubora wa Shule nchini wametakiwa kusimamia kwa weledi matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) ili kuhakikisha manunuzi yote ya Serikali yanafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.
Rai hiyo imetolewa Juni 11, 2026 jijini Arusha na Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Fredrick Salukele, akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, katika ufunguzi wa mafunzo kuhusu matumizi ya Mfumo huo.
Dkt. Salukele amesema mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kutumia mfumo huo kwa ufanisi katika usimamizi wa fedha za uchangiaji, ununuzi wa bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na malipo ya shughuli za tathmini za shule.
Amewasisitiza washiriki kusimamia kwa ufanisi rasilimali zilizopo, ikiwemo rasilimali watu na miundombinu, sambamba na kuimarisha huduma bora za elimu.
Aidha, Dkt. Salukele amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri na Wathibiti Ubora wa Shule kuhakikisha taasisi za elimu zinazingatia taratibu zote za uendeshaji ikiwemo masuala ya malazi, chakula na usalama wa wanafunzi.
Naye, Miurugenzi wa Uthibiti Ubora wa Shule kutoka Wizara hiyo Dkt. Ephrahim Simbeye amesisitiza uzingatiaji wa miongozo ya elimu, akitaka kukomeshwa kwa adhabu zisizokubalika na kuhakikisha kuna mazingira bora ya ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.
Wakizungumza kuhusu mafunzo hayo, Bi. Lilian Kasenga Mthibiti Ubora kutoka Manispaa ya Temeke pamoja na Emmanuel Hangaya kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, wametaja mbinu wanazotumia kufikia malengo huku wakisema mafunzo hayo yatakwenda kuwaongezea ufanisi kazini.










Na; Mwandishi Wetu - Chato
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Mohammed Ali Sheikh, Ametoa wito kwa wataalam kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu kuwa na mbinu bora za kiutendaji zitakazowezesha programu hiyo kutekelezeka kwa kasi zaidi.
Ameyasema hayo Wilayani Chato Mkoani Geita Tarehe 12 Juni 2026 alipozungumza na wataalam wa programu wanaofanya kazi ya utekelezaji ya mapitio ya programu mara baada ya ziara yake maalum ya kutembelea kituo cha kuendeleza Ukuzaji viumbemaji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani chato.
“Niwapongeze sana kwa kuchukua hatua za haraka baada na maagizo ya kikao cha Mawaziri kukaa pamoja kama wataaalamu na kuyafanyia kazi maagizo yale. Hii ni hatua muhimu sana inayoonesha ni kwa namna gani mnaweza kuwajibika kiutaalamu, mnapewa maelekezo na mnayatekeleza” Alisema.
Naibu Katibu Mkuu Sheikh alibainisha kuwa, kukutana kwa wataalamu hao ni hatua muhimu sana ya kukaa pamoja na kujaribu kujitathmini kuona kila kinachofanyika kinakwenda sawa ama vinginevyo, ‘’Niipongeze sana timu ya Uratibu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kuitisha kikao kazi hiki “Mnapoona kitu hakiendi hebu muitane muone namna ya kukifanyia kazi sisi kama watekelezaji wa Programu hii ni familia moja, Serikali ni moja na tunachotaka ni kufikia malengo na kumsaidia mtanzania katika kilimo na uvuvi kwa ukubwa wake” Alisisitiza
Alibainisha kuwa, kwa kufanya tathmini kunasaidia kujua wapi ulikwama na wapi pa kuboresha. Zaidi aliendelea alisema kuwa, kukua na kubadilika kwa teknolojia kufanya tathmini kunaweza kusaidia kwenda mbele zaidi, “lazima tusaidianae tuje na mbinu bora za utekelezaji katika utendaji wa mradi msione aibu kushauri na kutoa mapendekezo ya kiutendaji kuhusiana na Programu.” Alisema
Akizungumza katika kikao kazi hicho, Mhandisi Enock Nyanda, Mkurugenzi msaidizi sehemu ya Sekta za Uchumi na Uzalishaji Idara ya Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) alisema lengo mahususi ya wataalam kukutana katika kikao kazi hicho ni kuongeza kasi ya utekelezaji wa Programu ili kufikia malengo.
Na Mwandishi Wetu
Baraza la Ushindani Halali Zanzibar (ZFCT) limefanya ziara ya mafunzo katika Tume ya Ushindani ya Haki (FCC) kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya ushindani wa biashara, udhibiti wa bidhaa bandia pamoja na usimamizi wa mashauri yanayohusiana na ushindani.
Ziara hiyo iliyofanyika katika ofisi za FCC Juni 10, 2026 Jijini Dar es Salaam, imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuhakikisha mazingira ya biashara yanakuwa ya haki kwa wadau wote.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa alisema kuwa kubadilishana uzoefu na taasisi za ndani ya nchi ni muhimu katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa ushindani na kulinda maslahi ya watumiaji dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria za ushindani na biashara.
Alisema ujumbe wa ZFCT unapata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kudhibiti vitendo vya ushindani usio wa haki, kukabiliana na biashara ya bidhaa bandia pamoja na mifumo ya uchunguzi na uendeshaji wa mashauri mbalimbali yanayofikishwa mbele ya taasisi hiyo.
Kwa upande wake, ujumbe wa ZFCT ukiongozwa na Msajili wa Baraza, Bi. Fatma Yahya alieleza kuridhishwa na mafunzo na uzoefu uliopatikana katika ziara hiyo, ukibainisha kuwa utaisaidia taasisi hiyo kuimarisha utendaji wake katika kushughulikia rufaa na mashauri yanayohusiana na ushindani wa biashara Zanzibar.
ZFCT ni chombo kinachoshughulikia mashauri na rufaa zinazotokana na maamuzi ya mamlaka za ushindani, ambapo wadau wasiokubaliana na maamuzi yaliyotolewa huwasilisha kesi zao kwa ajili ya kusikilizwa na kutolewa uamuzi.
Ziara hiyo pia ilitoa nafasi kwa wataalamu kutoka pande zote mbili kujadiliana changamoto na fursa zilizopo katika usimamizi wa ushindani wa biashara, huku wakisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika kujenga uwezo wa kitaasisi na kuimarisha utekelezaji wa sheria zinazolinda ushindani wa haki katika soko.

Wakulima wa zao la pamba kutoka vijiji vya Mbutu, Iyogelo, Ilambakuki, Imalanguzu na Mwamakoma vilivyopo katika Wilaya ya Igunga, Mkoa wa Tabora, wamehamasika kufungua akaunti za benki na kusajili laini za simu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea malipo ya mazao yao kwa njia ya kidijitali. Hatua hiyo inalenga kuongeza uwazi, usalama na uharaka wa malipo kwa wakulima.
Wakulima hao wamefungua akaunti kupitia Benki ya NMB pamoja na kusajili laini kupitia mtandao wa simu wa Mixx by Yas, hatua itakayowawezesha kupokea fedha zao kwa urahisi kupitia mifumo ya benki na huduma za kifedha za simu za mkononi.
Zoezi hilo limefanyika kwa kushirikiana na AMCOS za Ngw'ajojabi, Ngw'asabi na Mwamakoma AMCOS, likitekelezwa kufuatia waraka wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika unaoelekeza malipo ya wakulima wa pamba kufanyika kupitia akaunti za benki na huduma za fedha kwa njia ya simu badala ya kutegemea fedha taslimu. Lengo ni kuhakikisha wakulima wanapata malipo yao kwa wakati, kwa uwazi na kwa usalama zaidi.
Mwitikio wa wakulima umeendelea kuongezeka siku hadi siku kufuatia juhudi za uhamasishaji zinazoendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali. Hadi kufikia Juni 10, 2026, jumla ya wakulima 506 wamejitokeza na kufungua akaunti pamoja na kujiunga na huduma za kifedha za simu, hatua inayoonesha uelewa na utayari mkubwa wa wakulima kupokea mabadiliko ya mfumo wa malipo ya kidijitali.
Aidha, uhamasishaji wa zoezi hilo umefanywa na Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Tabora, Peja Mhoja pamoja na Mrajis Msaidizi (Uhamasishaji), Ibrahim Kadudu, ambao wamekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wakulima kujiunga na mifumo rasmi ya kifedha ili kunufaika na malipo ya kisasa, salama na yenye tija.


Mkuu wa Tawi la Operation na Mafunzo wa JKT, Brigedia Jenerali Peter Mnyani,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 12,2026 katika Mako Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kuhusu wito wa kuripoti makambini vijana waliochaguliwa kujiunga na mafaunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria 2026.
Na.Alex Sonna-CHAMWINO
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajab Mabele amewataka Vijana waliohitimu kidato cha Sita kwa Mwaka 2026, Tanzania Bara na Visiwani ambao wamechaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa sheria ambao hawajaripoti kwenye kambi waliyopangiwa, kwenda kuripoti kwenye makambi yaliyokaribu nayo kuanzia juni 12 hadi Juni 15, 2026.





