DAR ES SALAAM

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeendelea kuthibitisha ubora wake barani Afrika baada ya kutwaa tuzo mbili muhimu katika Tuzo za Kampuni Bora za Mwaka Afrika (Africa Company of the Year Awards - ACOYA).
Na: OWM-KAM, Mwanza

Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa kuendeleza mshikamano, umoja na amani kwa kuwa ni nguzo muhimu zinazowezesha taifa kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.
Kwa miaka mingi, kulikuwa na msichana mmoja ambaye sikuwahi kumuondoa moyoni mwangu.....................TAZAMA VIDEO.

Kila nilipomwona, nilihisi furaha ambayo sikuweza kuelezea kwa maneno. Alikuwa mchangamfu, mwenye heshima, na mtu ambaye nilifurahia kuwa karibu naye. Tatizo pekee lilikuwa kwamba hakujua nilivyokuwa najisikia.
Kwa kweli nilikuwa mwoga.

Mara nyingi nilitaka kumwambia ukweli, lakini kila nilipopata nafasi, nilikosa ujasiri. Niliogopa kukataliwa na kuharibu urafiki uliokuwepo kati yetu. Miezi iligeuka miaka.

 Niliendelea kumtazama kwa mbali huku nikificha hisia zangu. Wakati mwingine niliona watu wengine wakimkaribia na hilo liliniumiza, lakini bado sikuweza kupata nguvu za kusema kile kilichokuwa moyoni mwangu.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kuamini kwamba huenda nafasi yangu ilikuwa imepita.
Nilijaribu kujisahaulisha na kuendelea na maisha, lakini kila nilipokutana naye, hisia zile zilikuwa zinarudi tena. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu, nilikuwa mtu ambaye alipenda kukaa kimya. Kila nilipojikuta kwenye mkutano, darasani, au sehemu yenye watu wengi, niliepuka kuzungumza....TAZAMA VIDEO.

Nilikuwa na mawazo mazuri kichwani, lakini nilikosa ujasiri wa kuyasema mbele ya wengine. Tatizo hilo lilianza kunisumbua tangu nikiwa mdogo.

Kila niliposimama kuzungumza mbele ya watu, moyo wangu ulianza kwenda mbio. Mikono ilitetemeka na wakati mwingine nilisahau hata kile nilichotaka kusema. 

Kwa kweli hali ile ilinifanya nijisikie duni. Niliona watu wengine wakizungumza kwa kujiamini, wakitoa maoni yao na kupata fursa mbalimbali maishani.

Mimi nilibaki nyuma kwa sababu ya hofu iliyokuwa ndani yangu. Kadri miaka ilivyopita, confidence yangu ilizidi kupungua. 

Nilianza kuamini kwamba labda sikuumbwa kuwa mtu wa kuonekana au kusikilizwa. Hata kwenye kazi na mahusiano yangu, nilikuwa na tabia ya kujishusha na kuhisi kwamba watu wengine walikuwa bora kuliko mimi.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua uwezo nilikuwa nao. Lakini uwezo ule ulikuwa umefichwa nyuma ya hofu na kutojiamini. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja, nilikuwa nikiishi kwa hasira na kuchanganyikiwa. Kila baada ya wiki chache, niligundua kuwa kuku wangu walikuwa wanapungua.....TAZAMA VIDEO.

Mwanzoni nilidhani ni wanyama wa porini au makosa ya kuhesabu, lakini kadri muda ulivyopita, ilibainika wazi kwamba kulikuwa na mtu aliyekuwa akiwaiba.

Tatizo lilikuwa moja.

Hakukuwa na ushahidi. Kila nilipoamka asubuhi na kukuta kuku wamepungua, nilianza kuwashuku watu tofauti. Lakini sikuwa na namna ya kuthibitisha tuhuma zangu. 

Mwizi alikuwa akifanya kazi yake kwa ustadi mkubwa na hakuacha alama yoyote nyuma. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Hasara ilikuwa inaongezeka, na kila nilipoongeza ulinzi, mwizi alionekana kupata njia nyingine ya kuendelea na wizi wake. 

Wakati mwingine nilikesha usiku nikisubiri, lakini hakutokea.
Watu wengi walianza kuniambia nikubali hasara na kuendelea na maisha. Lakini sikuwa tayari kufanya hivyo.

Kuku wale walikuwa sehemu ya chanzo changu cha kipato, na nilijua lazima siku moja ningepata ukweli.SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa sana. Nilitaka kuona biashara yangu ikikua na kuvutia wateja wengi, lakini ukweli ulikuwa tofauti.....TAZAMA VIDEO.

Eneo nililokuwa nafanyia biashara lilikuwa tayari na wafanyabiashara wakubwa waliokuwa wamejijengea jina kwa miaka mingi.

Kwa hiyo haikuwa rahisi. Kila siku nilifungua biashara yangu mapema na kusubiri wateja. Wakati mwingine nilikaa kwa saa nyingi bila kufanya mauzo ya kuridhisha

Wakati huo huo, nilikuwa nikiona maduka ya washindani wangu yakiwa yamejaa watu. Kwa kweli iliniumiza.

Kulikuwa na nyakati nilijiuliza kama nilifanya makosa kuanzisha biashara ile. Nilikuwa najituma kwa bidii, lakini matokeo hayakuwa yale niliyotarajia. 

Badala ya kukata tamaa, niliamua kuboresha huduma zangu. Nilihakikisha kila mteja anahudumiwa kwa heshima.

Nilisikiliza maoni yao na kujitahidi kufanya maboresho pale nilipoweza. Polepole baadhi ya watu walianza kugundua tofauti. Lakini bado ushindani ulikuwa mkubwa.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, pumu ilikuwa sehemu ya maisha yangu ambayo sikuweza kuikwepa.

TAZAMA VIDEO.

Kila siku niliishi kwa tahadhari. Mabadiliko ya hali ya hewa, vumbi, moshi, au hata harufu kali zingeweza kunisababishia matatizo ya kupumua. 

Wakati mwingine nilihisi kama kifua changu kilikuwa kizito kiasi kwamba kuvuta pumzi ya kawaida ilikuwa kazi ngumu.

Usiku ndiyo ulikuwa wakati mgumu zaidi.
Mara nyingi nilishtuka usingizini nikihangaika kupata hewa ya kutosha. Wakati familia yangu ilikuwa imelala kwa amani, mimi nilikuwa nimekaa kitandani nikijaribu kutuliza pumzi zangu. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kuogopa kufanya baadhi ya shughuli nilizozipenda. Nilihofia kwamba pumu ingeanza ghafla na kunifanya nishindwe kuendelea na nilichokuwa nikifanya. Miaka ilipita katika hali hiyo. Nilitafuta ushauri wa wataalamu wa afya na kujifunza namna ya kudhibiti hali yangu.

Ingawa kulikuwa na nyakati nilizopata nafuu, bado kulikuwa na vipindi ambavyo pumu ilinisumbua sana.SOMA ZAIDI

Wathibiti Ubora wa Shule nchini wametakiwa kusimamia kwa weledi matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) ili kuhakikisha manunuzi yote ya Serikali yanafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

Rai hiyo imetolewa Juni 11, 2026 jijini Arusha na Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Fredrick Salukele, akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, katika ufunguzi wa mafunzo kuhusu matumizi ya Mfumo huo.

Dkt. Salukele amesema mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kutumia mfumo huo kwa ufanisi katika usimamizi wa fedha za uchangiaji, ununuzi wa bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na malipo ya shughuli za tathmini za shule.

Amewasisitiza washiriki kusimamia kwa ufanisi rasilimali zilizopo, ikiwemo rasilimali watu na miundombinu, sambamba na kuimarisha huduma bora za elimu.

Aidha, Dkt. Salukele amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri na Wathibiti Ubora wa Shule kuhakikisha taasisi za elimu zinazingatia taratibu zote za uendeshaji ikiwemo masuala ya malazi, chakula na usalama wa wanafunzi.

Naye, Miurugenzi wa Uthibiti Ubora wa Shule kutoka Wizara hiyo Dkt. Ephrahim Simbeye amesisitiza uzingatiaji wa miongozo ya elimu, akitaka kukomeshwa kwa adhabu zisizokubalika na kuhakikisha kuna mazingira bora ya ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.

Wakizungumza kuhusu mafunzo hayo, Bi. Lilian Kasenga Mthibiti Ubora kutoka Manispaa ya Temeke pamoja na Emmanuel Hangaya kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, wametaja mbinu wanazotumia kufikia malengo huku wakisema mafunzo hayo yatakwenda kuwaongezea ufanisi kazini.









Na: OWM (KAM) – Geneva, Uswisi

Ujumbe wa Tanzania umeunga mkono Mkataba mpya wa Kimataifa unaolenga kulinda haki, usalama na ustawi wa Wafanyakazi wa Mtandaoni ikiwa ni dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha maendeleo ya teknolojia na majukwaa ya kidijitali yanakwenda sambamba na ulinzi wa utu wa mfanyakazi, usawa na haki za msingi za kazi.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Tume ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imezindua filamu ya “Kifurushi” itakayooneshwa katika mabasi yanayosafiri mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuongeza uelewa wa jamii kuhusu mbinu zinazotumiwa kusafirisha dawa za kulevya na madhara yatokanayo na vitendo hivyo.

 

Na; Mwandishi Wetu - Chato

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Mohammed Ali Sheikh, Ametoa wito kwa wataalam kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu kuwa na mbinu bora za kiutendaji zitakazowezesha programu hiyo kutekelezeka kwa kasi zaidi.

Ameyasema hayo Wilayani Chato Mkoani Geita Tarehe 12 Juni 2026 alipozungumza na wataalam wa programu wanaofanya kazi ya utekelezaji ya mapitio ya programu mara baada ya ziara yake maalum ya kutembelea kituo cha kuendeleza Ukuzaji viumbemaji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani chato.

“Niwapongeze sana kwa kuchukua hatua za haraka baada na maagizo ya kikao cha Mawaziri kukaa pamoja kama wataaalamu na kuyafanyia kazi maagizo yale. Hii ni hatua muhimu sana inayoonesha ni kwa namna gani mnaweza kuwajibika kiutaalamu, mnapewa maelekezo na mnayatekeleza” Alisema.

Naibu Katibu Mkuu Sheikh alibainisha kuwa, kukutana kwa wataalamu hao ni hatua muhimu sana ya kukaa pamoja na kujaribu kujitathmini kuona kila kinachofanyika kinakwenda sawa ama vinginevyo, ‘’Niipongeze sana timu ya Uratibu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kuitisha kikao kazi hiki “Mnapoona kitu hakiendi hebu muitane muone namna ya kukifanyia kazi sisi kama watekelezaji wa Programu hii ni familia moja, Serikali ni moja na tunachotaka ni kufikia malengo na kumsaidia mtanzania katika kilimo na uvuvi kwa ukubwa wake” Alisisitiza

Alibainisha kuwa, kwa kufanya tathmini kunasaidia kujua wapi ulikwama na wapi pa kuboresha. Zaidi aliendelea alisema kuwa, kukua na kubadilika kwa teknolojia kufanya tathmini kunaweza kusaidia  kwenda mbele zaidi, “lazima tusaidianae tuje na mbinu bora za utekelezaji katika utendaji wa mradi msione aibu kushauri na kutoa mapendekezo ya kiutendaji kuhusiana na Programu.” Alisema


Akizungumza katika kikao kazi hicho, Mhandisi Enock Nyanda, Mkurugenzi msaidizi sehemu ya Sekta za Uchumi na Uzalishaji Idara ya Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) alisema lengo mahususi ya wataalam kukutana katika kikao kazi hicho ni kuongeza kasi ya utekelezaji wa Programu ili kufikia malengo.


Na; Mwandishi Wetu - Chato

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Mohammed Ali Sheikh, Ametoa wito kwa wataalam kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu kuwa na mbinu bora za kiutendaji zitakazowezesha programu hiyo kutekelezeka kwa kasi zaidi.

Na Mwandishi Wetu

Baraza la Ushindani Halali Zanzibar (ZFCT) limefanya ziara ya mafunzo katika Tume ya Ushindani ya Haki (FCC) kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya ushindani wa biashara, udhibiti wa bidhaa bandia pamoja na usimamizi wa mashauri yanayohusiana na ushindani.

Ziara hiyo iliyofanyika katika ofisi za FCC Juni 10, 2026 Jijini Dar es Salaam, imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuhakikisha mazingira ya biashara yanakuwa ya haki kwa wadau wote.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa alisema kuwa kubadilishana uzoefu na taasisi za ndani ya nchi ni muhimu katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa ushindani na kulinda maslahi ya watumiaji dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria za ushindani na biashara.

Alisema ujumbe wa ZFCT unapata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kudhibiti vitendo vya ushindani usio wa haki, kukabiliana na biashara ya bidhaa bandia pamoja na mifumo ya uchunguzi na uendeshaji wa mashauri mbalimbali yanayofikishwa mbele ya taasisi hiyo.

Kwa upande wake, ujumbe wa ZFCT ukiongozwa na Msajili wa Baraza, Bi. Fatma Yahya alieleza kuridhishwa na mafunzo na uzoefu uliopatikana katika ziara hiyo, ukibainisha kuwa utaisaidia taasisi hiyo kuimarisha utendaji wake katika kushughulikia rufaa na mashauri yanayohusiana na ushindani wa biashara Zanzibar.

ZFCT ni chombo kinachoshughulikia mashauri na rufaa zinazotokana na maamuzi ya mamlaka za ushindani, ambapo wadau wasiokubaliana na maamuzi yaliyotolewa huwasilisha kesi zao kwa ajili ya kusikilizwa na kutolewa uamuzi.

Ziara hiyo pia ilitoa nafasi kwa wataalamu kutoka pande zote mbili kujadiliana changamoto na fursa zilizopo katika usimamizi wa ushindani wa biashara, huku wakisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika kujenga uwezo wa kitaasisi na kuimarisha utekelezaji wa sheria zinazolinda ushindani wa haki katika soko.

Wakulima wa zao la pamba kutoka vijiji vya Mbutu, Iyogelo, Ilambakuki, Imalanguzu na Mwamakoma vilivyopo katika Wilaya ya Igunga, Mkoa wa Tabora, wamehamasika kufungua akaunti za benki na kusajili laini za simu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea malipo ya mazao yao kwa njia ya kidijitali. Hatua hiyo inalenga kuongeza uwazi, usalama na uharaka wa malipo kwa wakulima.

Wakulima hao wamefungua akaunti kupitia Benki ya NMB pamoja na kusajili laini kupitia mtandao wa simu wa Mixx by Yas, hatua itakayowawezesha kupokea fedha zao kwa urahisi kupitia mifumo ya benki na huduma za kifedha za simu za mkononi.

Zoezi hilo limefanyika kwa kushirikiana na AMCOS za Ngw'ajojabi, Ngw'asabi na Mwamakoma AMCOS, likitekelezwa kufuatia waraka wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika unaoelekeza malipo ya wakulima wa pamba kufanyika kupitia akaunti za benki na huduma za fedha kwa njia ya simu badala ya kutegemea fedha taslimu. Lengo ni kuhakikisha wakulima wanapata malipo yao kwa wakati, kwa uwazi na kwa usalama zaidi.

Mwitikio wa wakulima umeendelea kuongezeka siku hadi siku kufuatia juhudi za uhamasishaji zinazoendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali. Hadi kufikia Juni 10, 2026, jumla ya wakulima 506 wamejitokeza na kufungua akaunti pamoja na kujiunga na huduma za kifedha za simu, hatua inayoonesha uelewa na utayari mkubwa wa wakulima kupokea mabadiliko ya mfumo wa malipo ya kidijitali.

Aidha, uhamasishaji wa zoezi hilo umefanywa na Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Tabora, Peja Mhoja pamoja na Mrajis Msaidizi (Uhamasishaji), Ibrahim Kadudu, ambao wamekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wakulima kujiunga na mifumo rasmi ya kifedha ili kunufaika na malipo ya kisasa, salama na yenye tija.

Mkuu wa Tawi la Operation na Mafunzo wa JKT, Brigedia Jenerali Peter Mnyani,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 12,2026 katika Mako Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kuhusu wito wa kuripoti makambini vijana waliochaguliwa kujiunga na mafaunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria 2026.

Na.Alex Sonna-CHAMWINO 

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajab Mabele amewataka Vijana waliohitimu kidato cha Sita kwa Mwaka 2026, Tanzania Bara na Visiwani ambao wamechaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa sheria ambao hawajaripoti kwenye kambi waliyopangiwa, kwenda kuripoti kwenye makambi yaliyokaribu nayo kuanzia juni 12 hadi Juni 15, 2026.

Akizungumza Wilayani Chamwino Mkaoni Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT, Mkuu wa Tawi la Operation na Mafunzo wa JKT, Brigedia Jenerali Peter Mnyani amesema awali Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele alitoa wito kwa vijana hao kuanza kuripoti kuanzia juni mosi hadi juni 7 ambapo baadhi ya vijana walishindwa kuripoti kwenye makambi waliyopangiwa kutokana na changamoto mbalimbali.
Amesema vijana hao wanatakiwa kuripoti kwenye kambi yoyote iliyokaribu nao, isipokuwa kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani, JKT Makutupora iliyopo Mkoani Dodoma na Chuo Cha uongozi Cha JKT (CUJKT) kilichopo Kimbiji Jijini Dar es salaam.
Ameongeza kuwa Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele anawakaribisha vijana wote waliohitimu kidato cha sita kwa mwaka 2026 ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujengewa uzalendo, kufundishwa nidhamu, ukakamavu, umoja wa kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na utayari wa kulijenga na kulitumikia taifa.
Katika hatua nyingine amebainisha kuwa kwa wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho wao wataripoti katika kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miondombinu ya kuwahudumia watu hao.