Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa nimekata tamaa kabisa kuhusu mapenzi. Nilikuwa nimepitia mahusiano mengi yaliyoniacha nikiwa na maumivu makubwa.

Kila mara nilipoanza kumpenda mtu, mwishowe mambo yalikuwa yanaishia kuvunjika moyo. Nilianza kuamini labda mapenzi ya kweli hayakunihusu tena. Kwa kweli iliniumiza sana.

Nilikuwa nimejenga ukuta wa kujilinda. Sikutaka tena kuumizwa, na nilianza kuwa na hofu ya kuingia kwenye uhusiano mpya. Wakati mwingine hata nilipoona watu wakiwa na furaha kwenye mahusiano yao, nilihisi kama mimi niko tofauti.

Kulikuwa na siku nilijihisi mpweke sana. Nilianza kujitenga, nikapunguza kutoka, na hata kuacha kuamini kwamba ningepata mtu ambaye angenipenda kweli. Nilianza kufikiria labda niishie peke yangu tu.SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi biashara yangu ilikuwa karibu kuanguka kabisa. 

Nilikuwa nimeanzisha duka langu kwa juhudi nyingi sana. Nilijinyima mambo mengi ili nipate mtaji, nikajituma kuhakikisha biashara inakua.

Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri wateja walikuwa wanakuja, mauzo yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Nilianza kugundua pesa hazilingani. Kila nilipofanya hesabu za mwisho wa siku, kulikuwa na upungufu ambao sikuuelewa.

Mwanzoni nilidhani labda ni makosa ya kawaida ya biashara. Lakini kadri wiki zilivyopita, hasara ilianza kuongezeka kwa namna iliyonipa hofu kubwa. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa naishi na maumivu ambayo ni vigumu kuelezea. Baada ya kuolewa, mimi na mume wangu tulikuwa na ndoto ya kuwa wazazi. Kila mwaka ulivyopita bila kupata mtoto, pressure ilianza kuongezeka.

Mwanzoni tuliamini muda wetu ungefika, lakini kadri miaka ilivyosonga mbele, matumaini yangu yalianza kupungua. Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni maneno ya watu.

Kila harusi, family gathering, au sherehe ilikuja na maswali yale yale “Mtoto lini?” Wakati mwingine nilitabasamu mbele za watu lakini nikilia peke yangu usiku. Nilijaribu kutafuta msaada wa kitabibu.

Nilifanya checkups na kupata ushauri wa hospitali ili kuelewa hali yangu vizuri. Kulikuwa na wakati niliambiwa safari ya kupata mimba ingeweza kuwa ngumu na ningehitaji uvumilivu pamoja na matibabu sahihi. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi ndoa yangu ilikuwa karibu kuvunjika kabisa. Mwanzoni mume wangu alikuwa mtu wa furaha, mwenye kujali familia, na aliyekuwa karibu sana nasi. Lakini polepole mambo yakaanza kubadilika.

Kile kilichoanza kama kunywa mara moja moja kiligeuka tabia ya kila siku. Kwa kweli hali iliniumiza sana. 

Alianza kurudi nyumbani usiku sana, wakati mwingine akiwa amelewa kiasi cha kutoweza hata kuzungumza vizuri. Migogoro nyumbani ikaongezeka.

Watoto walikuwa wanaanza kumuogopa, na amani ya familia yetu ikaanza kupotea. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtu niliyemjua akibadilika mbele ya macho yangu.

Kulikuwa na siku hakutokea nyumbani kabisa, na nilikesha nikijiuliza maisha yetu yalikuwa yanaelekea wapi. Wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa nimebaki peke yangu kubeba kila jukumu la familia.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa naishi maisha ya kutafuta kazi kila siku bila mafanikio ya maana. Baada ya kumaliza masomo, nilikuwa na matumaini makubwa kwamba ningepata kazi nzuri haraka.

Nilikuwa na ndoto ya kusaidia familia yangu, kujitegemea, na kuishi maisha bora. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Nilianza kutuma applications kila mahali.

Mara nyingine nilikuwa nikiitwa interviews, lakini mwisho wa siku sikupata nafasi. Wakati mwingine hata sikupigiwa simu kabisa. Miezi iligeuka miaka, na nilijikuta nikifanya vibarua vya hapa na pale ili kujisitiri.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu niliomaliza nao shule wakisonga mbele huku mimi nikihangaika. Wakati mwingine nilianza kujiuliza kama nilikuwa nimekosea njia maishani. SOMA ZAIDI.


Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM- TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi mbalimbali chini ya Mradi wa TACTIC kuzingatia viwango vya ubora vilivyoainishwa katika mikataba yao.

Mhandisi Mativila ametoa agizo hilo Mei 29,2026 wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya miundombinu inayotekelezwa na TACTIC katika mkoa wa Mara, ambapo amesisitiza kuwa ubora wa kazi ni jambo lisilopaswa kufanyiwa mzaha.

“Katika ziara hii, moja ya mambo muhimu tunayoyaangalia ni ubora wa miradi kwa kuzingatia maelezo yaliyopo kwenye mikataba, hivyo wakandarasi wote mnapaswa kuhakikisha mnatekeleza kazi kwa viwango vilivyokubaliwa,” amesema Mhandisi Mativila.

Ameeleza kuwa wakandarasi wanaposaini mikataba ya utekelezaji wa miradi, wanakuwa wamekubali kutekeleza kazi kwa ubora unaotakiwa, hivyo ni wajibu wao kujisimamia na kuhakikisha wanazingatia masharti yote ya mikataba bila kushurutishwa.

Aidha, Mhandisi Mativila amesema kuwa utekelezaji wa miradi kwa ubora ni sehemu ya kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa akisisitiza umuhimu wa kujenga miradi yenye viwango bora ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, Mhandisi Mativila amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa chini ya Mradi wa TACTIC, ikiwemo ujenzi wa soko, jengo la Ofisi ya TARURA pamoja na Stendi ya Bweli iliyopo mkoani humo.

Serikali imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ili kuipa nafasi pana sekta binafsi kushiriki katika ukuaji wa uchumi na uzalishaji wa ajira kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameagiza Menejimenti ya Kiwanda cha Kuzalisha Bidhaa za Kibaolojia Tanzania (TBPL) kinachomilikiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kuongeza uzalishaji na kuimarisha mikakati ya masoko ili kunufaika na mahitaji makubwa yaliyopo sokoni, kuhakikisha kiwanda kinaendelea kujiendesha kwa ufanisi wa kibiashara


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika ustawi wa wazee na uwezeshaji wa vijana kupitia utekelezaji wa programu mbalimbali zinazolenga kuboresha maisha yao na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo ya taifa.

Mhe. Mahundi ameyasema hayo tarehe 30 Mei, 2026 wakati akizungumza na wageni kutoka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Maryprisca Women Foundation wakiongozana na Machifu kutoka Mkoa wa Mbeya waliowasili mkoani Dodoma kwa ziara ya mafunzo na kujionea maendeleo yaliyofikiwa katika Mji wa Serikali Mtumba pamoja na shughuli zinazotekelezwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Amesema Serikali inaendelea kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki ikiwemo bima ya afya na kuishi katika mazingira salama na bora, huku ikiimarisha mikakati ya kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia fursa za mikopo, mafunzo ya ujasiriamali na programu mbalimbali za maendeleo.

Katika ziara hiyo, wageni hao walipata fursa ya kutembelea Mji wa Serikali Mtumba na kujionea majengo ya kisasa ya Wizara na Taasisi mbalimbali yaliyojengwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mMhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, hatua ambayo imeendelea kuifanya Dodoma kuwa kitovu cha shughuli za Serikali.

Aidha, walijifunza kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Wizara katika kuimarisha ustawi wa jamii, hususan kwa makundi maalum yakiwemo wazee, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Kwa upande wao, baadhi ya machifu walioshiriki ziara hiyo wameipongeza Serikali kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba na kwa kuendelea kutoa kipaumbele katika masuala ya maendeleo ya jamii. 


Pia wamempongeza Mhe. Mahundi kwa juhudi zake katika kusimamia utekelezaji wa mipango inayolenga kuboresha maisha ya wananchi, hususan makundi maalum.


MWISHO


Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Mwigulu Nchemba amepongeza kiwanda darasa cha kubangua korosho kilichoanzishwa na kituo cha zana za kilimo na teknolojia vijijini (CAMARTEC) wilayani manyoni mkoani singida na kuitaka sekta binafsi kuchangamkia fursa ya kuanzisha viwanda vipya vya kubangua korosho ili kuwawezesha wakulima kupata bei nzuri na kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

Akizungumza mara baada ya kutembelea Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho kilichoanzishwa na CAMARTEC ambapo amejionea shughuli za ubanguaji wa korosho.Dr.Mwigulu Nchemba amesema kiwanda hicho ni utekelezaji wa Ilani ya CCM pamoja na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050 hivyo ameitaka sekta binafsi kuanzisha viwanda vya kubangua korosho.

Kaimu mkurugenzi Mkuu wa CAMARTEC Mhandisi Godifrey Mwinama amesema iwapo korosho zitabanguliwa nchini zaidi ya ajira 36000 zitazalishwa na pia ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dr.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa kiwanda darasa hicho kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wa korosho na wananchi kwa ujumla.

kwa upande wake mbunge wa jimbo la manyoni Dr.Pius Chaya ameitaka serikali kuanzidha kongani ya viwanda huku meneja wa bodi ya korosho tawi la manyoni wanaeleza hali ya uzalishaji ilivyo









 



Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde ameielekeza Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye Sekta ya Madini (GNT) kuwaita na kufanya nao majadiliano wamiliki wote wa leseni za uchimbaji madini kinywe nchini Tanzania kujadiliana kuhusu ubia wa serikali katika Kampuni hizo na kuwataka kuanza utekelezaji wa uchimbaji kwa mujibu wa masharti ya leseni na Sheria ya Madini Sura ya 123.

Ameyasema hayo leo tarehe 30 Mei, 2026 Wilayani Ruangwa aliposhiriki zoezi la utiaji saini na Kampuni za Grafica Resources na Eminent Minerals Limited zenye ubia wa uwekezaji wa hisa asilimia 83 na Serikali asilimia 17 kwa kila kampuni. 

"Sisi sekta ya madini tunamshukuru kwa dhati Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotupa maelekezo na kutuwezesha kusimamia sekta kikamilifu kwa maendeleo ya Taifa letu"

"Na ndiyo maana Kampuni zote ambazo hazijaanza uzalishaji kwa mujibu wa masharti ya leseni zao tumeziandikia hati ya makosa (Default Notice) kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura ya 123. Kusaini kwetu mikataba siku ya leo, hakutoi unafuu kwa wawekezaji hawa kutotekeleza uwekezaji wao kwa mujibu wa Sheria yetu ya madini" amesisitiza Mhe. Mavunde.

Waziri Mavunde amesema hatua ya Timu ya GNT kuwaita na kuwataka wamiliki wa leseni za uchimbaji madini kinywe kufuata masharti ya Sheria na kuanza uzalishaji kutapelekea ufikiaji wa lengo la kuifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa kwanza duniani wa madini kinywe ifikapo mwaka 2030.

Vilevile, Waziri Mavunde ametoa wito kwa wawekezaji wa miradi hiyo kutoa fursa ya kipaumbele cha ajira kwa watanzania hususan wanaozunguka miradi hiyo. Kwa kufanya hivyo kutachochea uchumi wa Vijiji, Wilaya ya Ruangwa hususan kupitia wajibu wa uwekezaji kwa jamii (CSR) na kupelekea maendeleo ya uchumi wa Nchi yetu.

Aidha, Waziri Mavunde amebainisha kuwa miradi hiyo itakapoanza kuzalisha kikamilifu, itakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 101,048 za kinywe kila mwaka kwa upande wa mradi wa Grafica na tani 15,930 za kinywe kila mwaka kwa upande wa mradi wa Eminent mtawalia, hali inayoifanya Ruangwa sasa kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani wa teknolojia za kisasa duniani.

Waziri Mavunde pia ameeleza kuwa bado Tanzania ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika uzalishaji wa madini mbalimbali duniani, na ndiyo maana tunaendelea kuweka mkazo kwenye ufanyaji wa utafiti wa kina ili kubaini mashapo zaidi yatakayoongeza uchimbaji hususan kupitia wachimbaji wadogo wenye mchango mkubwa katika uchumi wetu.

Awali, akieleza mchakato wa kufikia makubaliano hayo, Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye sekta ya Madini, Prof. Sifuni Mchome amebainisha kuwa, majadiliano hayo yalifanyika kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi yetu na hayakuwa na lengo la kutafuta mshindi, hali iliyopelekea Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupata hisa zisizofifishwa za asilimia 17 kwenye kila mradi wa ubia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Grafica Resources, Bw. Vikas Bardiya ameeleza kuwa kampuni yao inaishukuru Serikali kwa ushirikiano iliyowapa mpaka kufikia makubaliano ya kuwekeza na kuahidi kwamba watahakikisha wanatekeleza uwekezaji huo kwa mujibu wa mkataba ili uweze kuleta manufaa kwa wananchi wa Ruangwa na Taifa kwa ujumla.

Pia, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Eminent Minerals Limited, Bw. Shafiqali Khaki ameeleza kufarijika kwao kuwa kampuni ya kizawa kuingia ubia na Serikali katika uwekezaji kwenye mradi huo wa uchimbaji madini kinywe na kwamba wao kama wazawa watahakikisha sehemu kubwa ya zaidi ya ajira 250 zitakazozalishwa katika uwekezaji huo zinachukuliwa na watanzania ili kuinua uchumi wa Taifa letu. 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack alimshukuru Mhe. Rais kwa kuwa kiongozi mahiri katika kusimamia uchumi na kuhakikisha rasilimali zetu zinanufaisha watanzania.

 Aidha, alisisitiza kuwa Serikali ya Mkoa wa Lindi itaendelea kuwapa ushirikiano wawekezaji hao ili waweze kuendesha shughuli zao kwa kasi na kunufaisha wananchi wa Lindi na Taifa kwa ujumla.
Jumla ya wafugaji wadogo 92,831 na wadau wa mnyororo wa thamani wa maziwawa Tanzania Bara na Visiwani-Zanzibar wamenufaika na Mradi Shirikishi waWasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P) tangu ulipoanzishwa mwezi Machi mwaka 2022, ambapo asilimia 30 ya wanufaika hao ni wanawake.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi biashara yangu ilikuwa karibu kufungwa kabisa. 

Nilikuwa nimejenga biashara yangu kwa miaka ya juhudi na kujituma. Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri.

Wateja walikuwa wanakuja kila siku, mauzo yalikuwa yanaenda vizuri, na nilianza kuona matumaini ya maisha bora kupitia biashara ile. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Nilianza kuona wateja wangu wa kawaida wakipungua mmoja baada ya mwingine. Mwanzoni nilidhani ni hali ya kawaida ya biashara, lakini kadri wiki zilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona wengi wakihamia kwa competitor aliyekuwa karibu. Mara kwa mara nilikuwa nasikia watu wakisema huko kulikuwa na huduma nzuri zaidi au offers ambazo zilikuwa zinawavutia. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi ambacho nilianza kuhisi kama uhusiano wangu ulikuwa unabadilika polepole. Mwanzoni mimi na mpenzi wangu tulikuwa karibu sana. 

Tulizungumza kila siku, tulicheka pamoja, na kila kitu kilionekana kwenda vizuri. Nilikuwa naamini tulikuwa tunaelekea kwenye maisha mazuri pamoja.

Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika. Mpenzi wangu alianza kuwa tofauti. Alianza kurudi akiwa kimya, mazungumzo yetu yakapungua, na mara nyingi alikuwa anashika simu yake kwa siri. Wakati mwingine nilipomuuliza nini kinaendelea, alikuwa anakasirika au kubadilisha mada.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtu ambaye zamani alikuwa karibu sana nami akianza kuwa distant. 

Nilianza kujiuliza kama kuna kitu nilikuwa nimekosea au kama kulikuwa na mtu mwingine kwenye maisha yake.

Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa na mawazo mengi sana kuhusu future ya relationship yetu. Wakati mwingine nilijikuta nikilia kimya kwa sababu sikuwa nataka kupoteza mtu niliyempenda sana.

Lakini sikutaka kufanya maamuzi ya haraka. Nilijaribu kuzungumza naye kwa utulivu mara kadhaa, lakini ilikuwa ngumu kupata maelezo ya wazi. Polepole nilianza kupoteza furaha na confidence yangu. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi ambacho nilianza kuishi na wasiwasi mkubwa kuhusu maendeleo ya mtoto wangu. Nilikuwa namwangalia akikua vizuri kwenye mambo mengi, lakini kulikuwa na jambo moja lililoniumiza moyo.

Wakati watoto wa rika lake walikuwa wanaanza kusema maneno mengi na kuwasiliana vizuri, wangu alikuwa bado anapata ugumu wa kujieleza. Mwanzoni nilijipa moyo.

Nilijua watoto hukua kwa tofauti, hivyo niliamini labda muda wake ulikuwa bado. Lakini kadri miezi ilivyopita, nilianza kupata pressure kutoka kwa watu wa karibu.

Wengine walikuwa wakiuliza kwa nini bado haongei vizuri, jambo lililonifanya nizidi kuwa na mawazo. Kwa kweli nilihuzunika sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtoto wangu akijaribu kueleza kitu lakini ashindwe.

Wakati mwingine alikuwa anakasirika au kulia kwa sababu hatukuelewa alichotaka kusema. Nilianza kutafuta msaada. 

Nilizungumza na walimu na nikatafuta ushauri wa kitaalamu ili kuelewa kama kulikuwa na changamoto ya maendeleo ya lugha au kitu kingine kilichohitaji attention mapema. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu nilikuwa nikihangaika kukuza biashara yangu bila mafanikio makubwa. Nilikuwa nauza bidhaa mtandaoni na wakati mwingine dukani, lakini ukweli ni kwamba mambo hayakuwa rahisi.

Nilikuwa napost bidhaa kila siku, nikijitahidi kutangaza kwa watu, lakini wateja walikuwa wachache sana. Kulikuwa na siku nilikaa bila kuuza kitu chochote. Kwa kweli nilianza kukata tamaa.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara nyingine zikikua kupitia social media huku yangu ikionekana kusimama sehemu moja. 

Nilikuwa najitahidi kurecord videos, kupost picha, na hata kufanya offers, lakini hakuna kilichokuwa kinabadilika sana. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu nilikuwa na ndoto ya kufanya kazi Gulf ili nibadilishe maisha yangu na kusaidia familia yangu. Nilikuwa nikiona watu wakirudi kutoka nje wakiwa wamejenga nyumba, kuanzisha biashara, na kusaidia familia zao.

Moyoni nilijua na mimi nilitaka nafasi kama hiyo. Lakini safari yangu haikuwa rahisi hata kidogo. Nilianza kutuma applications kupitia agencies mbalimbali.

Mwanzoni nilikuwa na matumaini makubwa. Nilihakikisha documents zangu zimekamilika, nikafanya interviews, na hata mara nyingine nikatoa pesa za process nikiamini safari yangu ilikuwa karibu.

Lakini kila mara kulikuwa na disappointment. Mara application inakataliwa, mara nafasi inaenda kwa mtu mwingine, mara naambiwa nisubiri bila majibu ya kueleweka. 

Kadri muda ulivyopita, madeni yalianza kuniongezea pressure kwa sababu nilikuwa nimetumia pesa nyingi kufuatilia process ile.

Kwa kweli nilianza kuchoka. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu nilioanza nao process wakifanikiwa kusafiri huku mimi nikibaki nyuma. Watu wengine walianza kuniambia labda safari ile haikuwa ya kwangu.SOMA ZAIDI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu leo ameongoza watumishi, mawakili na wananchi kumuaga aliyekuwa mtumishi wa Ofisi hiyo, marehemu Wakili Msomi Charles Boaz Swai aliyefariki jana jijini Dodoma.






Na Mwandishi Wetu


DAR ES SALAAM — Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema uhuru wa uhariri ni nguzo muhimu katika taaluma ya habari na unapaswa kulindwa ili vyombo vya habari viweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwajibikaji na kwa maslahi ya umma.


Akizungumza Mei 26, 2026 katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, Wakili Kipangula alisema hakuna mtu anayepaswa kuingilia maamuzi ya uhariri wa chombo cha habari, awe ni chanzo cha taarifa, mmiliki wa chombo, mwanasiasa au mtu mwingine yeyote mwenye maslahi binafsi.


Alisema uhuru huo unapaswa kuendana sambamba na uwajibikaji wa kitaaluma, huku akisisitiza kuwa maadili ya taaluma ya habari yanamtaka mwandishi kufanya kazi kwa uadilifu, bila upendeleo na kuhakikisha taarifa zote zinathibitishwa kabla ya kuchapishwa au kurushwa.


“Ukweli ndio mlinzi wa taaluma ya habari. Mwandishi anatakiwa kutoa taarifa ambazo amezithibitisha na ana uhakika nazo kwa sababu jamii inategemea kupata taarifa sahihi na kwa wakati ili iweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo,” amesema Wakili Kipangula.


Aidha, alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye uelewa, mshikamano na maendeleo, hivyo ni muhimu kutumia uhuru wa habari kwa kuzingatia sheria, maadili ya taaluma pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wengine kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.


Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri, Bw. Deodatus Balile, alisema uhuru wa vyombo vya habari utakuwa na maana halisi pale vyombo hivyo vitakapokuwa na uwezo wa kiuchumi wa kujiendesha bila kutegemea ushawishi wa nje.


“Uhuru wa vyombo vya habari utakuwa uhuru wa kweli pale vyombo vya habari vitakapokuwa na nguvu ya kiuchumi,” amesema Balile.

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kuonesha nafasi yake katika kuchochea maendeleo ya viwanda na kukuza ubunifu wa vijana kwa kutoa elimu ya viwango na ubora wa bidhaa katika Maonesho ya Fursa za Kazi na Ubunifu kwa Vijana (Career Fair 2026), hatua inayolenga kuwajengea vijana uwezo wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani katika soko la ndani na kimataifa.