Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisafiri kwa Treni ya Kisasa ya Umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam kuelekea Morogoro leo tarehe 21 Machi 2026.

Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Maji, yatakayofanyika mkoani Morogoro, kesho tarehe 22 Machi 2026.



 


Serikali ya Tanzania imetangaza uwepo wa fursa kubwa za uwekezaji katika sekta ya nishati zenye thamani ya dola za Marekani bilioni 12.9, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukuza uchumi na kuboresha upatikanaji wa huduma za nishati nchini.

Akizungumza katika mjadala kuhusu ushirikiani wa Marekani na Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa mkutano wa Powering Africa Summit leo Machi 20, 2026 jijini Washington DC, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema uwekezaji huo unahitajika katika maeneo mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa umeme, usafirishaji, usambazaji pamoja na nishati safi ya kupikia.

Ameeleza kuwa katika sekta ya uzalishaji wa umeme, miradi 13 imepangwa kutekelezwa ndani ya miaka mitano ijayo, ikihitaji uwekezaji wa dola bilioni 2.77, hatua itakayowezesha kuongeza megawati 1,421 za umeme nchini.

Kwa upande wa miundombinu ya usafirishaji wa umeme, amesema jumla ya miradi 23 yenye thamani ya dola bilioni 1.21 inapangwa kujengwa, ikiwemo kilomita 1,350 za njia za kusafirisha umeme pamoja na vituo vya kupozea umeme.

Aidha, Mhe. Salome amebainisha kuwa kuna fursa nyingi katika sekta ya gesi asilia, akieleza kuwa Tanzania ina zaidi ya futi za ujazo trilioni 57 za gesi ambazo bado hazijatumika kikamilifu. 

Amesisitiza umuhimu wa uwekezaji katika uchimbaji, usindikaji na matumizi ya gesi hiyo katika uzalishaji wa umeme na shughuli za viwandani.

Katika hatua nyingine, amesema Serikali inaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikilenga kufikia asilimia 75 ya matumizi hayo ifikapo mwaka 2030. Mpango huo unahusisha usambazaji wa majiko bora, gesi pamoja na teknolojia nyingine rafiki kwa mazingira.

Mhe. Salome amewahimiza wawekezaji walioshiriki mkutano huo kutumia fursa zilizopo kuwekeza nchini, huku Serikali ikiendelea kuboresha mazingira ya biashara na kuweka sera rafiki kwa uwekezaji.

Katika Mkutano huo Naibu Waziri Salome ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Else Sia Kanza na wataalam kutoka Wizarani, TANESCO, REA pamoja na PURA. 

 


Na OWM - TAMISEMI, Bumbuli

  

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM -TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema kuwa amezindua madarasa matatu katika Shule ya Sekondari Kilivicha wilayani Bumbuli ambayo yataondoa changamoto ya msongamano wa wanafunzi madarasani, uliokuwa ukiikabili shule hiyo kwa muda mrefu.

Prof. Shemdoe ameongeza kuwa madarasa hayo pia ni sehemu ya maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2028 ambao watakuwa wamehitimu darasa ya sita na la saba kwa pamoja na kutakiwa kujiunga na kidato cha kwanza kutokana na mabadaliko ya mtaala mpya wa elimu unaotekelezwa na Serikali.

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Machi 21, 2026 wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa madarasa hayo matatu yaliyojengwa kwa ufadhiri wa taasisi ya VUGA DELOPMENT INITIATIVE kwa gharama ya Shilingi Milioni 84,086,600/=.

“Ni ukweli usiopingika kwamba, ujenzi wa madarasa haya utaondoa msongamano wa wanafunzi madarasani na ni maandalizi ya kupokea wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza mwaka 2028,  mara baada ya kumaliza darasa la sita na la saba kwa pamoja kwa mujibu wa mtaala mpya wa elimu,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amemshukuru Bw. Rama Kaoneka ambaye ni Meneja wa Miradi wa Taasisi ya A BETTER WORLD CANADA ambaye pia ni kiongozi wa Taasisi ya VUGA DEVELOPMENT INNITIATIVE ambazo zimeshirikiana kufadhili ujenzi wa madarasa hayo matatu katika shule hiyo ya Sekondari Kilivicha.

Akizungumzia jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya Elimu, Prof. Shemdoe amesema, Serikali inayongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mwaka huu wa fedha imeleta Bumbuli Shilingi Bilioni 3.2 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Shule za Msingi na Shilingi Bilioni 2.1 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Shule za Sekondari. 

Aidha, Prof. Shemdoe amemuelekeza Katibu Mkuu wa Ofisi yake kuhakikisha anatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya fizikia na biolojia katika Shule ya Sekondari Kilivicha kwenye Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/27 ambayo maandalizi yake yanaendelea.

Kwa upande wake  Bw. Kaoneka amesema kuwa, wamefadhili ujenzi wa madarasa hayo ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na ufundishaji shuleni hapo.

Mwanafunzi wa shule hiyo Bw. Emmanuel Francis Michael amesema kwamba miundombinu hiyo ya madarasa iliyojengwa itamuwezesha kufikia ndoto yake ya kuwa rubani, na kuongeza kuwa jamii itegemee ufaulu mzuri kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kilivicha.

Naye, Mkazi wa Kijiji cha Kivilicha Bw. Moses Thomas amemshukuru Prof. Shemdoe kwa kuzindua madarasa hayo matatu ambayo yatawawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira bora, na kuongeza kuwa madarasa hayo yataleta tabasamu kwa wanafunzi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kilivicha Bi. Sophia Dossa ameshukuru kwa kujengewa madarasa mapya na kuahidi kwamba madarasa hayo yatainua kiwango cha taaluma katika shule hiyo ya Sekondari ya Kilivicha.

 


Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameungana na waumini wa dini ya Kiislamu katika Baraza la Sikukuu ya Eid lililofanyika jijini Mbeya.

Baraza hilo limefanyika katika ukumbi wa City Garden, likiwakutanisha viongozi wa serikali, viongozi wa dini pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo kusherehekea sikukuu ya Eid kwa pamoja.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhandisi Mahundi amewapongeza waumini wa Kiislamu kwa kumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuwataka kuendelea kudumisha amani, mshikamano na upendo katika jamii.

Amesema serikali inaendelea kuthamini mchango wa viongozi wa dini katika kuimarisha maadili mema na umoja wa kitaifa, huku akisisitiza umuhimu wa kushirikiana katika kuleta maendeleo endelevu.

Kwa upande wao, baadhi ya viongozi wa dini wameeleza kufurahishwa na ushiriki wa viongozi wa serikali katika matukio ya kijamii na kidini, wakisema hatua hiyo inaimarisha uhusiano mzuri kati ya serikali na wananchi.

Baraza hilo limehitimishwa kwa dua maalum za kuliombea taifa amani, umoja na maendeleo.



WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa{TAMISEMI}Professa  Riziki Shemdoe amesema kuwa fedha za mradi wa shilingi Bilioni 82.5 za ujenzi wa Miundombinu ya barabara inayozunguka uwanja wa AFCON ni fedha za mapato ya ndani hivyo wananchi wa Mkoa wa Arusha wametakiwa kuitunza miundombinu hiyo.

Professa Shemdoe alisema hayo jana Jijini Arusha wakati wa utiaji saini kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini{TARURA} na Mkandarasi wa mradi huo kampuni ya CRJE ya Nchini China shughuli iliyofanyika eneo la karibu ya uwanja na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi{CCM}ngazi ya kata hadi Mkoa,viongozi wa serikali,viongozi wa dini na wananchi wa Mkoa wa Arusha.

Alisema mashindano ya AFCON ni mashindano muhimu sana Afrika na yanaangaliwa na mamia ya watu wengi Duniani na hivyo basi Miundombinu yeke ya kuzunguka uwanja huo yanapaswa kuwa yenye ubora mzuri wenye kuwafutia watu wote wataokwenda kuangalia mashindano hayo na ndio maana Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia utolewaji wa fedha hizo kutoka mapato ya ndani.

Waziri alisema kutokana na umuhimu ulionyeshwa na Rais wa kutoa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa  Miundombinu inayozunguka uwanja huo,wananchi wote wa Mkoa wa Arusha wanapaswa kuwa walinzi wa Miundombinu hiyo kwa maslahi ya Umma na mradi huo unapaswa kukamilika mapema mwezi Mei mwakani na kusiwe na visingizio.

Alisema viongozi wa Chama,serikali na wananchi wa Mkoa wa Arusha wanapaswa kumshukuru Rais kwa  kujitoa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo ambao kwa sasa ujenzi wake umefikia asilimia 75 na pia kutoa fedha nyingine kwa ajili ya Mindombinu ya Barabara inayozunguka uwanja hyuo kwani uamuzi huo unapaswa kupongezwa na kila mmoja.

''Utekelezaji wa mradi huu ni jitihada za serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan za kutaka mashindano ya AFCON kuchezwa katika mazingira mazuri na yenye mvuto sambamba na Miundombinu ya barabara kuwa katika hali ya ubora na kuvutia''alisema Shemdoe

''Wananchi wote wote Mkoani Arusha na Mikoa ya jirani wanatakiwa kuwa wasimamizi wa mradi huu na maradi unaposuasua wanapaswa kutoa taarifa sehemu husika ili hatua ziweze kuchukuliwa kwani mradi huu ni wetu sote''alisema 

Naye Mtendaji Mkuu wa Tarura,Mhandisi Victor Seif alisema ujenzi wa Miundombinu ya Barabara za kuelekea na kuzunguka uwanja wa mpira utakaotumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2027 katika Jiji la Arusha umegharimu kiasi hicho cha fedha na Barabara ya km 19.9  ambayo itakuwa na njia nne na mbili.

Mhandisi Seif alisema kuwa ujenzi wa uwanja umefikia zaidi ya asilimia 75 sambamba na ujenzi wa Miundombinu muhimu yenye umbali wa zaidi ya km 19.9 kwa kiwango cha lami kuelekea kwenye uwanja huo kutokea Barabara Kuu ya Arusha-Babati na Arusha Bypass na kuzunguka uwanja huo Mateves-Bondeni km 6.5,Km 1.5 njia nne na km 5 njia mbili kutoka barabara kuu Arusha -Babati,barabara ya Lendita km 2.75 njia nne ,barabara ya Essari km 2.45 2.45 njia nne zote kutoka barabara kuu ya Arusha Bypass na km 1.5 barabara kuzunguka uwanja.

Alisema baada ya mchakato wa ununuzi kukamilika,Kampuni ya M/s China Railway Construction Engineering Group kushinda zabuni na kupewa kazi hiyo ya ujenzi wa barabara kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 82.5 kwa muda wa miezi 13 na kazi inapaswa kuanza aprill mosi mwaka huu na usimamizi wa ujenzi wa barabara hiyo utasimamiwa na kampuni ya M/s Afrisa Consulting ya Jijini Dar es Salaam kwa mkataba wenye thamani ya shilingi Bilioni 1.4

Naye Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini na Waziri wa Habari,Sanaa ,Michezo na Utamaduni,Poul Makonda alisema kuwa Jiji la Arusha lina kiu kubwa na barabara za lami kwani ni Jiji la mwisho kuwa na barabara za lami kwani Majiji yote Tanzania yana barabara za lami hivyo aliiomba Tarura kuhakikisha inafanya kila jitihada kutekeleza ahadi zake za ujenzi wa barabara za kiwango cha lami ili wananchi waweze kupitia kwa nyakati zote.

Makonda alisema na kumshukuru Rais kwa uamuzi wake wa kuridhia kutoa fedha shilingi Bilioni 82.5 kwa ajili ya Miundombinu ya kuzunguka uwanja wa AFCON na kusema kuwa uamuzi huo unapaswa kupongezwa na kuwataka wakazi wa Arusha kushukuru kwa hilo na kuwasihi wananchi watakaolipwa fidia kupokea fedha hizo bila kuleta manung'uniko.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla ameahidi kuwasimamia wakandarasi wa ujenzi wa Miundombinu ya kuzunguka uwanja huo ili waweze kuimaliza kwa wakati na kuwataka wananchi kuwa mstari wa mbele kutoa taarifa pindi mkandarasi atakaonekana anafanaya kazi kwa kusuasua katika kutekeleza majukumu yake.















  

 

 

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa mkono wa Eid kwa wazee wanaoishi katika Kata ya Ilemi, jijini Mbeya, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Eid al-Fitr.

Akiwasililisha zawadi hizo Kwa niaba ya Rais, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali inayoongozwa na Rais Samia katika kuwajali wazee na makundi maalum, hususan katika nyakati za sikukuu.

“Mheshimiwa Rais amewakumbuka wazee wa Ilemi katika kipindi hiki cha Eid, na ameona ni vyema kuwafikishia mkono wa upendo ili nao waweze kusherehekea kwa furaha kama Watanzania wengine,” amesema Mahundi.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuthamini mchango wa wazee katika jamii na kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha ustawi wao unaimarika siku hadi siku.

Baadhi ya wazee waliopokea msaada huo wamemshukuru Rais Samia pamoja na Naibu Waziri Mahundi kwa kuwajali, wakisema msaada huo umewaletea faraja na kuwatia moyo katika kipindi hiki cha sikukuu.

Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi wa serikali za mitaa pamoja na wananchi wa eneo hilo.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

TUME ya Ushindani (FCC) kanda ya Nyanda za Juu Kusini  imetoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa mpana ili waweze kufanya maamuzi sahihi wanaponunua na kutumia bidhaa mbalimbali  ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Akitoa elimu hiyo Mkoani Njombe, Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) Nyanda za Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga, amesisitiza umuhimu wa kila mlaji kufahamu haki zake za msingi.alieza kuwa haki hizo ni pamoja na kupata bidhaa bora, kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa, pamoja na haki ya kulalamika pale mlaji anapodhulumiwa.

Aidha, Bw. Mbanga ameeleza madhara makubwa yatokanayo na matumizi ya bidhaa bandia, akibainisha kuwa bidhaa hizo zinaweza kusababisha athari za kiafya, kupoteza fedha, na kudhoofisha uchumi wa nchi. Amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii zao ili kupunguza matumizi ya bidhaa hizo hatarishi.

“FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi.”amesema Bw. Mbanga

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameacha alama chanya kwa wanafunzi wa FDC Njombe, ambapo wengi wao wameeleza kuwa elimu hiyo imewafungua macho na kuwapa nguvu ya kusimamia haki zao kama walaji, huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia nchini.

Kupitia mafunzo hayo, walikumbushwa kuwa mlaji ana nafasi kubwa katika kulinda afya yake na uchumi wa taifa kwa kuchagua bidhaa zilizo salama na zenye ubora unaokubalika.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) Mkoani Njombe wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia yaliyotolewa  na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

 

Na WMA – Dodoma

Watumishi wa Wakala wa Vipimo (WMA), wameitikia wito wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaowataka watanzania kupitia makundi mbalimbali kupanda miti katika maeneo yao ili kuhifadhi mazingira.

Akiongoza zoezi la upandaji miti katika eneo ilipo Ofisi Kuu ya WMA Medeli jijini Dodoma, mapema leo Machi 20, 2026 Meneja Utawala na Rasilimali Watu, Charles Mavunde amewasisitiza watumishi wa Wakala hiyo nchi nzima kuzingatia maelekezo ya Serikali kwa kupanda miti na kuitunza ili kulinda mazingira.

Amesema kuwa, Mheshimiwa Rais Samia amekuwa akisisitiza mara kwa mara kuhusu upandaji miti katika maeneo mbalimbali na kwamba yeye mwenyewe ameonyesha mfano kwa kuwa kinara wa upandaji miti, hivyo WMA imeona ni vyema pia iitikie wito huo.

“Mtakumbuka kwamba, hata Mheshimiwa Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimwakilisha Mhe. Rais katika maadhimisho ya siku ya upandaji miti duniani na maadhimisho ya upandaji miti kitaifa, jana Machi 19, 2026 kule Lindi aliagiza kuwa makundi mbalimbali ya watanzania waendeleze utamaduni wa kupanda miti,” ameeleza Mavunde na kuhitimisha kuwa WMA imeyachukulia kwa uzito maelekezo ya viongozi hao na itayatekeleza kikamilifu.

Viongozi na watumishi mbalimbali wa WMA Makao Makuu wameshiriki zoezi hilo la upandaji miti akiwemo Mkurugenzi wa Huduma za Biashara Phanuel Mtuki, Meneja Sehemu ya Fedha, CPA Ibrahim Mbinga, Meneja Mkoa wa Dodoma Said Ibrahim na Meneja Mawasiliano Veronica Simba.

Wengine walioshiriki ni watumishi kutoka Idara mbalimbali wakiwemo maafisa, maafisa usafirishaji na wasaidizi wa ofisi.

WMA ni wakala ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara yenye jukumu kuu la kumlinda mlaji kupitia usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo katika sekta mbalimbali.

 




Na Mwandishi wetu- DAR ES SALAAM


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambaye pia ni Mbunge wa

Arumeru Magharibi Mhe. Johannes Lukumay ameipongeza  Serikali kuendelea kusaidia kundi la Watu waishio na Maamubikizi Virusi vya 

UKIMWI kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Lukumay ameyasema  hayo tarehe 19 Machi 2026 mara baada ya ziara ya kutembelea Baraza la Watu waishio na maambukizi ya Virusi vya  UKIMWI akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika ( Konga ya Jiji) iliyofanyika   katika Viwanja vya Pugu Mnadani Jijini Dar es Salaam.

 Amesema kuwa watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni sawa na watu wengine hivyo yapaswa kuwapa kipaumbele katika fursa mbalimbali za kimaendeleo.

Pia Mwenyekiti huyo amelipongeza kundi hilo kwa namna

wanavyojituma katika kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini hivyo  kuziagiza  sekta husika kusaidia katika kuwatafutia masoko kwa ajili ya bidhaa zao.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wataendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuongeza nguvu zaidi kwa Wanakonga ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Nderiananga amempongeza Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Wilaya pamoja na Katibu Tawala wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na timu nzima kwa kuwawezesha Wanakonga katika fursa mbalimbali na kuwataka kuendelea na desturi hiyo ya kuwawezesha kwani mwaka huu wa fedha bado haujamalizika.

Aidha  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Elihuruma Mabelya amesema kuwa moja ya eneo waliloliwekea nguvu ni Konga hiyo kwa kuunga mkono shughuli zao za  kiuchumi ili kuhakikisha

wanainuka na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo.