MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mhe. Deodatus Mwanyika, akizungumza  katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.

......

MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mhe. Deodatus Mwanyika, ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara kwa hatua inazoendelea kuchukua katika kuanzisha na kuendeleza kongani za viwanda kupitia taasisi zake, hatua inayochochea fursa za ajira na ukuaji wa uchumi nchini.

Akizungumza katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma, Mhe. Mwanyika,amesema  usimamizi madhubuti wa Wizara katika miradi ya kimkakati na miradi kielelezo kuwa kinaonyesha dhamira ya dhati ya serikali kubadili sura ya sekta ya viwanda.
  "Miradi hiyo inapaswa kutekelezwa mapema iwezekanavyo kwa kuwa ina mchango muhimu katika kuongeza ajira, kukuza pato la taifa na kuimarisha uchumi wa viwanda kwa ujumla."amesema Mhe.Mwanyika
Aidha, ameisisitiza Wizara kuendelea kuboresha sera na sheria ili ziendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, na hivyo kuweka msingi wa uchumi shindani, jumuishi na shindanishi.
Kwa upande wao, Wajumbe wa Kamati hiyo wamepongeza juhudi za Wizara na kutoa mapendekezo mbalimbali ya kuboresha zaidi maendeleo ya sekta ya viwanda na biashara, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na Wizara hiyo kuhakikisha mageuzi yanayolenga ukuaji wa kasi wa sekta yanatekelezwa ipasavyo.
 
Awali, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, akijibu hoja na maoni ya wajumbe , ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Wizara itaendeleza ushirikiano makini katika kuimarisha sekta ya viwanda na biashara, ikijikita katika uanzishaji wa kongani mpya za viwanda zinazochochea ajira, ufufuaji wa viwanda vilivyokuwa vimesimama, kuongeza uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa, pamoja na kuboresha mfumo wa utoaji leseni za biashara.
Ameongeza kuwa Wizara imeweka kipaumbele katika usimamizi wa miradi ya kimkakati na miradi kielelezo kwa weledi, ubunifu na umakini mkubwa, ikiwemo Mradi wa Liganga na Mchuchuma ambao una mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya viwanda, ujenzi wa uchumi wa taifa na kupunguza utegemezi wa uagizaji wa malighafi za chuma kutoka nje ya nchi.

MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mhe. Deodatus Mwanyika, akizungumza  katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Mariam Ditopile Mzuzuri,akichangia mada  katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.
Wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo,wakichangia mada mbalimbali wakati wa  kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.
Wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo,wakichangia mada mbalimbali wakati wa  kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.
Wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo,wakichangia mada mbalimbali wakati wa  kikao cha kwanza cha Kamati hiyo cha kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, akijibu hoja na maoni ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo mara baada ya kamati hiyo kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, akitoa  maoni ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo mara baada ya kamati hiyo kupokea taarifa ya wizara kuhusu muundo, majukumu, sera na sheria kilichofanyika Januari 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma.

 


Na Munir Shemweta, WANMM

 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii imeahidi kutoa ushirikiano kwa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati wote wa kutekeleza majukumu yake.

 

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 15 Januari, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Timetheo Mnzava wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge na Wizara ya Ardhi kilichokuwa na lengo la kuifahamu wizara ya ardhi na taasisi zake.

 

Pamoja na kuifahamu wizara na taasisi zake, Kamati za Kudumu za Bunge zinatakiwa kufahamu baadhi ya sera na sheria kulingana na majukumu ya kila kamati kama ilivyofafanuliwa kwenye nyongeza ya 8 ya Kanuni za Kudumu za Bunge chini ya Kanuni ya 140 ya Kanuni za Bunge inayoelekeza Kamati kupitishwa kwenye majukumu yake ya msingi na Kamati ya Bajeti kufanya maandalizi ya Hoja zitakazojadiliwa na Bunge.

 

Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ambaye ni Mbunge wa jimbo la Korogwe vijijini amesema, kelele ni nyingi katika masuala ya ardhi lakini wao kama kamati wataendelea kuwa pamoja na wizara kuhakikisha migogoro ya ardhi inatatuliwa na kazi ya kushughulikia changamoto za sekta ya ardhi inakuwa nyepesi.

 

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo aliwashukuru wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii kwa michango yao aliyoieleza kuwa ina lengo la kuboresha sekta ya ardhi nchini.

 

"Sisi wizara tutahakikisha tunapokea ushauri na maoni yenu na kuyafanyia kazi ili tuwe na matokeo chanya katika sekta ya ardhi" amesema mhe Dkt Akwilapo.

 

Vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge ni kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa 2 wa Bunge la 13 unaotarajiwa kuanza Jumanne, tarehe 27 Januari, 2026.

 

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Kaspar Mmuya, Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga, Naibu Katibu Mkuu Bi Lucy Kabyemera, wajumbe wa Menejimeti pamoja na Wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo




📌Kituo cha Kupoza Umeme Mtera

📌Mradi wa Kusambaza umeme katika vitongoji 9,009

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuzindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera na Kusaini Mikataba ya kutekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 katika Mikoa yote Tanzania Bara.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy amesema hayo Jijini Dodoma Januari 15, 2026 katika mkutano maalum na wanahabari  alipokuwa akitambulisha matukio hayo mawili yatakayoshuhudiwa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ambaye atakuwa mgeni rasmi.

“Tarehe 16 Januari, 2026 Kituo cha Kupoza Umeme cha Mtera kitazinduliwa rasmi na tarehe 17 Januari, 2026 tutasaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji zaidi ya 9,000,” amefafanua Mha. Saidy

Amebainisha kuwa Kituo cha Mtera kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 9.2 na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa ushirikiano na Serikali za Sweden na Norway.

Aidha, Mhandisi Saidy amesema REA itasaini mikataba 30 na Wakandarasi 21 wazawa na wakandarasi 9 kutoka nje ya nchi lakini wamesajiliwa nchini kwa ajili ya kutekeleza mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu ndani ya Mikoa yote Tanzania Bara.

Amewataka wananchi kuchangamkia fursa zitakazopatikana wakati wote wa utekelezaji wake ikiwemo ajira, biashara na huduma mbalimbali zitakazohitajika na pia kuhakikisha wanachangamkia kutumia umeme kuzalisha mali na kuboresha huduma za kijamii.

“Tunatekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan; mradi huu unakwenda kufungua nchi kiuchumi ni wa kipekee na mradi mkubwa kuwahi kutekelezwa na REA kwa viwango vya gharama na idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa,” amesema Mha. Saidy.


📌Kituo cha Kupoza Umeme Mtera

📌Mradi wa Kusambaza umeme katika vitongoji 9,009

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuzindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera na Kusaini Mikataba ya kutekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 katika Mikoa yote Tanzania Bara.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy amesema hayo Jijini Dodoma Januari 15, 2026 katika mkutano maalum na wanahabari  alipokuwa akitambulisha matukio hayo mawili yatakayoshuhudiwa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ambaye atakuwa mgeni rasmi.

“Tarehe 16 Januari, 2026 Kituo cha Kupoza Umeme cha Mtera kitazinduliwa rasmi na tarehe 17 Januari, 2026 tutasaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji zaidi ya 9,000,” amefafanua Mha. Saidy

Amebainisha kuwa Kituo cha Mtera kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 9.2 na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa ushirikiano na Serikali za Sweden na Norway.

Aidha, Mhandisi Saidy amesema REA itasaini mikataba 30 na Wakandarasi 21 wazawa na wakandarasi 9 kutoka nje ya nchi lakini wamesajiliwa nchini kwa ajili ya kutekeleza mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu ndani ya Mikoa yote Tanzania Bara.

Amewataka wananchi kuchangamkia fursa zitakazopatikana wakati wote wa utekelezaji wake ikiwemo ajira, biashara na huduma mbalimbali zitakazohitajika na pia kuhakikisha wanachangamkia kutumia umeme kuzalisha mali na kuboresha huduma za kijamii.

“Tunatekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan; mradi huu unakwenda kufungua nchi kiuchumi ni wa kipekee na mradi mkubwa kuwahi kutekelezwa na REA kwa viwango vya gharama na idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa,” amesema Mha. Saidy.

 


▪️ Kipaumbele kikubwa ni leseni za uchimbaji kwa wachimbaji wadogo

▪️ Waziri Mavunde aelezea mkakati wa kuwawezesha kimtaji

▪️ Kamati ya Bunge yaipongeza BoT kwa ununuzi wa tani 16.4 za dhahabu

▪️ Kamati yasisitiza kuongezwa kwa eneo la utafiti madini kutoka asilimia 16 ya sasa

Serikali imeainisha mkakati mahsusi wa kuwaendeleza wachimbaji wadogo wa madini nchini, kwa kuweka kipaumbele katika utoaji wa leseni, upatikanaji wa mitaji, teknolojia, masoko ya uhakika pamoja na maeneo yenye taarifa za utafiti.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, wakati wa kikao cha kwanza cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kilichofanyika leo Januari 15, 2025 katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mavunde amesema kuwa shughuli zote za utafutaji, uchimbaji, uongezaji thamani na biashara ya madini zinatekelezwa kwa mujibu wa Sera ya Madini ya mwaka 2009 na Sheria ya Madini, Sura ya 123, kwa lengo la kuhakikisha wachimbaji wadogo wananufaika ipasavyo na rasilimali za madini kwa tija na uendelevu.

Ameeleza kuwa utekelezaji wa Sera na Sheria hizo umeleta mageuzi makubwa katika sekta ya madini, ambapo mchango wake katika Pato la Taifa umeongezeka kutoka asilimia 2.7 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 10.1 mwaka 2024.

Ameongeza kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na kuimarika kwa usimamizi, uwazi na uwajibikaji, hali iliyosababisha makusanyo ya maduhuli ya Serikali kuongezeka kutoka shilingi bilioni 173.7 mwaka wa fedha 2012/13 hadi kufikia shilingi trilioni 1.071 mwaka 2024/25.

Waziri Mavunde amesema, Serikali imeendelea kuwapa kipaumbele wachimbaji wadogo kwa kuwatengea maeneo yenye taarifa za utafiti na kuwapatia leseni za uchimbaji mdogo katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Nyanhwale, Simanjiro, Mbogwe na Chunya, hatua inayolenga kuongeza tija, usalama na mapato yao.

Aidha, amesema Wizara ya Madini imeanzisha mkakati wa Mining For A  Brighter Tomorrow (MBT) unaolenga kuwawezesha wachimbaji wadogo katika nyanja za mitaji, teknolojia na taarifa za kijiolojia, ili waweze kujitegemea badala ya kutegemea wadhamini kutoka nje ya nchi. Mpaka sasa, zaidi ya wachimbaji wadogo 12,000 wamenufaika na mpango huo.

Kwa upande wa biashara ya madini nje ya nchi, Waziri Mavunde amesema mauzo ya madini yameongezeka kutoka dola za Marekani bilioni 1.94 mwaka 2013 hadi dola bilioni 4.12 mwaka 2024. Aidha, Serikali imeanzisha masoko 44 ya madini na vituo 114 vya ununuzi na uuzaji wa madini, hatua iliyoboresha upatikanaji wa masoko ya uhakika na bei shindani kwa wachimbaji.

Katika eneo la ajira, amesema ajira za moja kwa moja katika kampuni za madini zimeongezeka kutoka ajira 7,280 mwaka 2011 hadi ajira 19,371 mwaka 2024. Sambamba na hilo, ununuzi wa bidhaa na huduma za ndani umeongezeka kutoka shilingi trilioni 1.85 mwaka 2018 hadi shilingi trilioni 4.41 mwaka 2024, sawa na ongezeko la asilimia 88.

Akizungumzia kuimarishwa kwa akiba ya fedha za kigeni, Waziri Mavunde amesema kuanzia Oktoba 1, 2024, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilianza kununua dhahabu kupitia viwanda vya ndani vya kusafisha dhahabu, na hadi kufikia Desemba 2025 ilikuwa imenunua tani 16.4 za dhahabu zenye thamani ya dola za Marekani bilioni 2.2. Hatua hiyo imeifanya Tanzania kuingia katika orodha ya nchi kumi bora barani Afrika kwa hifadhi ya dhahabu.

Ameongeza kuwa Sera ya Madini pia inasisitiza uwajibikaji wa kampuni za madini kwa jamii (CSR), ambapo miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule, miradi ya maji, barabara, huduma za afya na kilimo inaendelea kutekelezwa katika maeneo yanayozunguka migodi.

Kwa upande wao, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, Makamu Mwenyekiti Mhe. Simon Songe na Wajumbe wa Kamati hiyo wameipongeza Wizara ya Madini kwa mafanikio yaliyofikiwa, pamoja na kuipongeza Benki Kuu ya Tanzania kwa kununua zaidi ya tani 16 za dhahabu ndani ya kipindi kifupi.

Aidha, Kamati imesisitiza haja ya Wizara ya Madini kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuongeza wigo wa utafiti wa madini kutoka asilimia 16 ya sasa ili kuongeza fursa za ushiriki wa Watanzania katika sekta ya madini.

Akiwasilisha taarifa kuhusu Sera na Sheria zinazosimamia Wizara ya Madini, Kamishna wa Madini, Dkt. AbdulRahman Mwanga, amesema utekelezaji wake umewezesha kuanzishwa kwa viwanda 16 vya kuyeyusha madini na viwanda sita vya kusafisha madini, pamoja na migodi miwili ya kati na migodi mikubwa miwili iliyo katika hatua mbalimbali za kuanza uzalishaji.

Awali, Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Madini, Festus Mbwiro, aliwasilisha taarifa ya muundo na majukumu ya Wizara hiyo, akieleza kuwa uimarishaji wa rasilimali watu na mifumo ya usimamizi umechangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa ufanisi na tija katika sekta ya madini.









 



Dar es Salaam, Januari 2026.
KAMPUNI ya Airtel Tanzania leo imezindua kampeni ya Wese ni Bure ambayo inatokana na kampeni mama Inayoitwa Mwaka umenyooka na My airtel money app, Kampeni hii inalenga kuhamasisha matumizi ya miamala ya kidigital kupitia huduma ya Lipa namba kila unapoweka mafuta kwenye vituo vya mafuta zaidi ya 62 kote nchini ambavyo ni Mount Mero, ACER, Zebra Station na Bavuai.

Kampeni ya Wese ni Bure ni sehemu ya juhudi endelevu za Airtel Tanzania za kuwazawadia wateja wake, ikithibitisha dhamira ya kampuni ya kurahisisha malipo ya kila siku kwa njia salama na rahisi. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara wa Airtel Money, Bw. Emmanuel Moshi, alisisitiza umuhimu wa malipo ya kidijitali katika maisha ya kila siku akisema: “Kwa kuunganisha Airtel Lipa Namba kwenye malipo ya mafuta, tunaongeza thamani ya huduma za fedha kidijitali kwenye huduma moja muhimu sana ya kila siku, huku tukiwazawadia wateja wetu kwa kuchagua miamala salama na rahisi isiyotumia fedha taslimu.”

Akisisitiza dhamira hiyo kwa ngazi ya jamii, Meneja wa Malipo kwa Wafanyabiashara wa Airtel Money, Bw. Ismail Simanga, alieleza manufaa ya moja kwa moja ya kampeni ya Mwaka Umenyooka na My Airtel Money kwa wateja akisema: “Kampeni hii inaleta thamani halisi kwa wateja wetu kwa kubadilisha ununuzi wa kawaida wa mafuta kuwa fursa ya kupata zawadi, huku ikichochea matumizi ya malipo salama, ya haraka na rahisi ya kidijitali”

Kupitia kampeni hii, wateja watakaonunua mafuta katika vituo hivyo na kulipia kupitia Airtel Lipa Namba watapata nafasi ya kushinda lita 10 za mafuta bure kila wiki katika kipindi cha mwezi mmoja. Ili kushiriki, mteja anatakiwa kununua mafuta yenye thamani ya Shilingi 10,000 au zaidi na kulipa kupitia Airtel Lipa Namba, ambapo ataingizwa moja kwa moja kwenye droo ya kila wiki. Washindi watatangazwa kila wiki katika kipindi chote cha kampeni. Airtel Tanzania inaendelea kuonesha namna suluhisho za kifedha kupitia simu zinavyoweza kuongeza urahisi, ufanisi na ujumuishaji wa kifedha kwa kuziunganisha na mahitaji ya kila siku ya wateja.

 Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeshiriki mkutano mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii na kuimarisha ushirikiano kati ya Ngorongoro na Mahakama.


Mkutano huo uliofunguliwa tarehe 13 januari, 2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan unaendelea hadi tarehe 16 Januari, 2026 ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya sheria kutoka maeneo tofauti ya nchi wanashiriki kujadili masuala mbalimbali yanayohusu haki, utawala wa sheria na maendeleo ya mfumo wa utoaji haki nchini.

Ujumbe wa Ngorongoro uliongozwa na Kamishna msaidizi mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya utalii na Masoko Mariam Kobelo pamoja na Afisa Uhifadhi mwandamizi-Sheria Usaje Mwambene ambapo mada mbalimbali kuhusu vivutio vya utalii, fursa za uwekezaji, huduma zinazotolewa na upekee wa Ngorongoro kama kivutio bora cha utalii barani afrika kwa mwaka 2023 na 2025.

Aidha, NCAA imetumia mkutano huo kujenga uelewa kwa wadau wa sheria kuhusu misingi ya kisheria inayosimamia uhifadhi wa rasilimali za asili ili kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ikiwemo Kreta za Ngorongoro, Empakai, Olmoti, maporomoko yaa maji endoro, Ndutu ambalo ni maarufu kwa mazalia ya nyumbu wanaaohama, mchanga unaohama, makumbusho ya olduvai, makumbusho na jiopaki na vingine vingi.





 Na Mwandishi Wetu, WMTH – Dodoma


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb), amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ili kuwawezesha wadau wa sekta ya sanaa kufanya kazi zao kwa ubora na tija.

Waziri Kairuki ameyasema hayo tarehe 14 Januari 2026, alipofanya mazungumzo na mtengeneza maudhui ya mtandaoni, Bw. Vicent Pendael Njau maarufu kama KIREDIO, aliyefika katika ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, masuala yaliyojadiliwa ni pamoja upatikanaji wa huduma ya intaneti ya uhakika, fursa za kujipatia kipato kupitia mitandao ya kijamii, pamoja na uwepo wa sera na mifumo ya kiserikali ikiwemo ya kikodi inayogusa sekta ya ubunifu na maudhui ya mtandaoni.

Waziri Kairuki alimpongeza Bw. Njau (Kiredio) kwa kazi nzuri anayofanya na kutoa wito kwa watengeneza maudhui pamoja na wasanii kwa ujumla kuzingatia maadili, mila na desturi za Kitanzania pindi wanapotengeneza maudhui yao na kabla ya kuyaweka mtandaoni.

Kwa upande wake, Kiredio ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasikiliza vijana na kutambua mchango wao katika uchumi wa kidijitali, huku akiwasilisha changamoto mbalimbali zinazokabili sekta ya utengenezaji wa maudhui ili zifanyiwe kazi kwa wakati na kuiwezesha sekta hiyo kuendelea kukua.

Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Mohammed Abdulla pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.








 


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amekagua ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum pamoja na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa nyumba ya mlezi (matroni) katika Shule ya Msingi Segese, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Miradi hiyo ina thamani ya zaidi ya shilingi milioni 490 na inalenga kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu kwa kundi hilo muhimu katika jamii.

Mhe. Mhita alifanya ukaguzi huo Januari 14, 2025, alipokuwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi katika Kijiji cha Segese, Kata ya Segese.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Mkuu wa Mkoa aliipongeza Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya elimu, hususan kwa watoto wenye mahitaji maalum, akisema miradi hiyo itasaidia kuongeza usalama, malezi bora na mazingira rafiki ya kujifunzia kwa wanafunzi hao.

Ujenzi wa bweni la wanafunzi umegharamiwa kupitia fedha kutoka Serikali Kuu pamoja na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Msalala. Aidha, ujenzi wa uzio wa bweni hilo umefadhiliwa na Kampuni ya Bulyanhulu Gold Mine (BARRICK) kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa gharama ya shilingi milioni 238, huku ujenzi wa nyumba ya mlezi ukigharimu shilingi milioni 79.2.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Frank Nkinda ameshukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya Elimu na kuwataka kuitunza na kuitumia vyema ili iweze kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Bi. Rose Manumba amesema ataendelea kuhakikisha miradi inasimamiwa vyema na kukamilika kwa wakati katika Halmashauri hiyo kusudi wananchi waweze kupata huduma bora na nzuri.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mkuu wa Shule ya Msingi Segese, Ndg. Alpha Matambo, amesema ujenzi wa majengo hayo utachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza usalama, uangalizi na malezi bora kwa watoto wenye mahitaji maalum, tofauti na ilivyokuwa awali kabla ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutaongeza ari ya wanafunzi kuhudhuria masomo na kuwapa wazazi na walezi imani ya kuwapeleka watoto wao shule katika mazingira salama na rafiki.










Biashara yangu ilikuwa ikipata mapato mazuri kwa miaka kadhaa, lakini ghafla kila kitu kilibadilika. Wateja wangu walianza kupungua kwa kasi, mapato yangu yalishuka, na siku moja niligundua kuwa nimepoteza wateja wote wa kawaida.

Nilihisi kukosa udhibiti wa biashara yangu, na hofu ilianza kunishika. Nilijua kwamba ikiwa sitafanya kitu haraka, kila kitu nilichojenga kitakuwa kimeharibika. Nilijaribu njia mbalimbali kupiga matangazo.

Kutoa punguzo, hata kuwasiliana moja kwa moja na wateja waliokuwa wanarudi mara kwa mara lakini matokeo yalikuwa hafifu. Hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba siku moja nikakaa tu nikijaribu kuelewa ni wapi nilikosea.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-wateja-wangu-wote-ghafula-lakini-njia-moja-niliyojaribu-iliwarudisha-kwa-kasi-isiyotarajiwa/