Maisha yanaweza kuwa katili sana, hasa unapoona wadogo zako uliowasomesha wanakupita kimaendeleo wakati wewe umeshikilia karatasi za chuo zinazoliwa na mchwa. Mimi naitwa Mariam, mzaliwa wa Ilemela, jijini Mwanza.

Nilihitimu shahada yangu ya Uhasibu (Accounting) kwa kiwango cha juu, lakini mtaani niligeuka kuwa mtu wa dharau. Nilifikia hatua ya kukaa pembeni ya barabara nikisaidia mama yangu mdogo kushona viatu vya kimasai ili tu nipate mlo wa mchana.

Kila usaili niliokwenda, nilikuwa naonekana sifai, au nafasi inachukuliwa na mtu mwenye kujuana na wakubwa. Umri wangu wa kuelekea miaka 30 ulinifanya nikose amani; kila ndugu aliyeniona aliniuliza “Lini unaolewa?” au “Kazi mbona hupati?”. SOMA ZAIDI.
Naitwa Erick, mkazi wa jiji la Mbeya. Kwa miaka saba, nilikuwa nikipambana na biashara ya kuuza vifaa vya kielektroniki kama TV, redio, na pasi pale mtaa wa uhuru. 

Nilikuwa na duka lililopambwa kwa vioo na taa za kuvutia, lakini mfukoni nilikuwa nakauka kama jangwa la Sahara.

Kila asubuhi nilikuwa nawasha redio kubwa dukani kwangu ili kuvutia wateja, lakini watu walikuwa wakipita na kusikiliza muziki tu kisha wanaenda kununua kwa jirani yangu ambaye duka lake lilikuwa dogo na chafu.

Hali hii ilinitesa sana kisaikolojia. Nilianza kuonekana mwanaume niliyefeli mbele ya mke wangu na ndugu zangu, kwani kila mwezi nilikuwa nakopa pesa ya kulipa kodi ya pango. Nilihisi nina nuksi ya ajabu inayowafukuza watu wenye pesa na kuvuta watazamaji tu.

Nilijaribu kila mbinu; nilishusha bei hadi ya hasara, nilifanya matangazo kwa gari la spika mitaani, na hata kutoa zawadi kwa kila aliyenunua bidhaa, lakini wapi! Duka langu lilikuwa kama limepakwa dawa ya kufukuza watu. Nilikaribia kukata tamaa na kuuza kila kitu nikawe kondakta wa daladala.

Siku moja nilisafiri kwenda kijijini kwetu kwa ajili ya mazishi ya ndugu. Nikiwa nimekaa na wazee wa busara chini ya mwembe, tulianza kuzungumzia changamoto za kimaisha mjini. Mzee mmoja ambaye alikuwa ni rafiki wa marehemu, alinifuata pembeni na kuniambia, “Erick, kijana wangu, unahangaika bure na mbinu za kizungu. SOMA ZAIDI.
Maisha ya mtaani yanaweza kukufanya uonekane kama kiumbe usiye na thamani, hasa unapokuwa na akili lakini kila unachogusa kinaharibika. Naitwa Suleiman, kijana ambaye nilipoteza miaka saba mtaani nikitafuta mpenyo wa kimaisha bila mafanikio.

Nilijitosa kwenye michezo ya kubashiri (betting) nikiamini ndiyo njia pekee ya kuninasua kwenye umaskini, lakini badala yake niliishia kuwa ombaomba. Nilifikia hatua ya kulala kwenye mabenchi ya stendi ya mabasi baada ya kufukuzwa kwenye chumba nilichokuwa nimepanga kwa kukosa kodi ya miezi sita.

Kila nikiangalia umri wangu ukikaribia miaka 35, nilihisi moyo wangu unapasuka. Nilikuwa naona vijana wadogo wakishinda mamilioni kwenye betting, lakini mimi hata nikiweka mkeka wa timu mbili tu, lazima moja ingeharibu.

Nilihisi kuna kitu kimejifunga kwenye maisha yangu, maana hata bahati ndogo ya kuokota shilingi mia barabarani haikuwahi kunitokea. Nilikata tamaa kabisa na kuanza kuhisi labda nimerogwa na ndugu zangu wasiotaka nifanikiwe.SOMA ZAIDI.

 

MBUNGE Viti Maalum Mkoa wa Pwani Mariam Ibrahim, amechangia Sh. milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi Kisutu iliyopo Jimbo la Bagamoyo mkoani humo. 

Ametoa mchango huo wakati aliposhiriki katika  tukio la upandaji wa miti 300 lililofanyika katika eneo la shule hiyo.
Akizungumza na wananchi, Mbunge Mariam amesema mchango huo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na wananchi pamoja na wadau mbalimbali katika kuhakikisha shule hiyo inakamilika. 

Pia amempongeza Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo CPA Subira  Mgalu, kwa juhudi zake za kusimamia maendeleo ya elimu na kuendelea kushirikiana na wananchi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha, amempongeza  Diwani wa Kata ya Kisutu Awesu Muhidini, kwa uongozi wake na namna anavyoshirikiana na wananchi kuipambania shule hiyo hadi kufikia hatua ya sasa.

Mbunge Mariam pia amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwezesha upatikanaji wa eneo lililojengwa shule hiyo, hatua ambayo imefungua fursa ya kuboresha huduma za elimu kwa watoto wa Kata ya Kisutu.

Katika hafla hiyo,amekabidhi sh. milioni 3 papo hapo, huku akiahidi kuwa Sh. milioni mbili zilizobaki atazikabidhi kupitia Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo CPA Mgalu, ili kukamilisha ahadi yake ya mchango wa Sh.Milioni 5.




Na OWM–TAMISEMI, Lilongwe, Malawi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri wa Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe (SONGWECOM) kilichofanyika Julai 10, 2026 jijini Lilongwe, Malawi, kwa lengo la kujadili kuharakisha utekelezaji wa Mradi wa Maendeleo wa Bonde la Mto Songwe.

Mradi huo unatarajiwa kujengwa kwa pamoja na Serikali za Tanzania na Malawi na kuzalisha umeme wa megawati 180.2, huku ukiwa na manufaa makubwa katika sekta za umwagiliaji, usambazaji wa maji, uvuvi, utalii pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa nchi hizo mbili.

Kikao hicho kilijadili hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi, ikiwemo kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati, kwa manufaa ya wananchi wa pande zote za Bonde la Mto Songwe.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria kikao hicho ni Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde, Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola, pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Kasper Kasper Mmuya, na wataalamu mbalimbali kutoka Serikali za Tanzania na Malawi.

Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe (The Joint Songwe River Basin Commission – SONGWECOM) linaundwa na Mawaziri kumi kutoka Tanzania na Malawi wanaowakilisha sekta tano muhimu ambazo ni Maji, Nishati, Kilimo cha Umwagiliaji, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), pamoja na Ardhi, ndilo chombo cha juu cha maamuzi kinachosimamia shughuli za Kamisheni hiyo. 

Kupitia kikao hicho, Tanzania na Malawi zimeendelea kudhihirisha dhamira ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika usimamizi endelevu wa rasilimali za Bonde la Mto Songwe, kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa nishati, kuimarisha usalama wa maji na chakula, na kuchochea maendeleo endelevu ya wananchi wa mataifa hayo mawili.











 


Mawaziri wa Nishati kutoka nchi wanachama wa Soko la Pamoja la Nishati Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP) wameazimia kuharakisha utekelezaji wa soko la pamoja la umeme ili kuimarisha upatikanaji wa nishati, kuongeza biashara ya umeme kati ya nchi wanachama na kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa umeme katika ukanda huo.

Azimio hilo limefikiwa wakati wa Mkutano wa 22 wa Baraza la Mawaziri wa EAPP uliofanyika Julai 9 hadi 10, 2026 jijini Addis Ababa, Ethiopia ambapo Tanzania iliwakilishwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb), kwa niaba ya Waziri wa Nishati.

Mkutano huo uliwakutanisha Mawaziri wa Nishati, wakuu wa taasisi za umeme na wawakilishi wa sekta ya nishati kutoka nchi wanachama wa EAPP kujadili hatua za kuimarisha ushirikiano wa kikanda kupitia biashara ya umeme, uunganishaji wa gridi za taifa na matumizi bora ya rasilimali za nishati.

Maazimio yaliyofikiwa yanatarajiwa kuweka mfumo madhubuti utakaowezesha nchi wanachama kuuziana umeme kwa ufanisi, kuimarisha uhakika wa upatikanaji wa nishati, kuchochea ukuaji wa uchumi, kuvutia uwekezaji na kuimarisha maendeleo ya kijamii katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Mhe. Salome Makamba amesema maazimio hayo yatachangia kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme, kupunguza changamoto za upungufu na kukatika kwa umeme katika nchi wanachama, pamoja na kuimarisha ushindani na ufanisi wa taasisi za umeme kupitia kubadilishana uzoefu na teknolojia.

Amesema upatikanaji wa umeme wa uhakika utaongeza kasi ya ukuaji wa viwanda vidogo, vya kati na vikubwa, hali itakayochochea uzalishaji, kuvutia uwekezaji na kuzalisha ajira zaidi kwa vijana, ikiwemo kuwapa Watanzania fursa za kushiriki katika shughuli mbalimbali za kitaalamu ndani ya EAPP.

Akihitimisha mkutano huo, Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la EAPP ambaye pia ni Waziri wa Maji na Nishati wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Habtamu Itefa, amesema ushirikiano na mshikamano wa kikanda ni msingi muhimu katika kufanikisha uunganishaji wa mifumo ya umeme na kuhakikisha wananchi wa nchi wanachama wanapata huduma ya umeme salama, ya uhakika na endelevu.











 



 Asilimia 10 ya mapato ya sekta ya madini kuelekezwa kwenye utafiti

MBT kuwanufaisha wachimbaji Mundarara


Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amesimamisha kwa muda uchaguzi wa Viongozi wa Mabroka wa Madini katika Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha, akisisitiza kuwa uchaguzi huo hautafanyika hadi pale wapiga kura watakapopatiwa elimu ya kutosha kuhusu haki, wajibu na taratibu za uchaguzi kwa mujibu wa  Katiba ya Mabroka.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi, haki na ushirikishwaji wa wadau wote, huku ukiepusha migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na kutokuelewa taratibu za uchaguzi.

Akizungumza leo Juni 10, 2026 na wachimbaji, wafanyabiashara wa madini na viongozi wa Serikali wakati wa ziara yake wilayani humo, Dkt. Kiruswa amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejidhatiti kujenga sekta ya madini yenye uwazi, uwajibikaji na ushiriki mpana wa Watanzania katika shughuli zote za mnyororo wa thamani wa madini.

"Nataka uchaguzi huu ufanyike kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zote. Kwanza tutoe elimu kwa wapiga kura ili kila mshiriki ajue haki na wajibu wake. Tukifanya hivyo tutapata viongozi wenye uhalali, wanaokubalika na watakaoweza kuwatumikia wadau wa sekta ya madini kwa ufanisi," amesema Dkt. Kiruswa.

Ameelekeza Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania (CHAMMATA), Jeremiah Kituyo, kwa kushirikiana na viongozi wa kitaifa wa chama hicho, kuhakikisha elimu hiyo inatolewa kwa wakati na uchaguzi mpya unaratibiwa mara baada ya zoezi hilo kukamilika bila kucheleweshwa.

Naibu Waziri huyo amewakumbusha mabroka wote wa madini kuzingatia matakwa ya Sheria ya Madini kwa kuhakikisha wanakuwa na leseni halali za ubroka pamoja na vitambulisho vinavyoonesha namba za leseni zao wakati wote wanapotekeleza shughuli zao.

Amesema Serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayejihusisha na ubroka wa madini bila leseni halali, akibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kulinda maslahi ya wafanyabiashara, kuongeza uwajibikaji na kuhakikisha Serikali inakusanya mapato yote yanayostahili.

Aidha, amewataka viongozi wa vijiji, viongozi wa sekta ya madini na wananchi kushirikiana kwa karibu katika kulinda rasilimali za madini na kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa mujibu wa sheria na zinawanufaisha wananchi wa maeneo husika.

Katika kuimarisha sekta ya madini, Dkt. Kiruswa amesema Serikali imeanza kutekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kurejesha sehemu ya mapato yanayotokana na sekta ya madini katika maendeleo ya sekta hiyo, ambapo asilimia 10 ya makusanyo ya sekta itaelekezwa kwenye shughuli za utafiti wa madini.

Amesema hatua hiyo itaiwezesha Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kufanya tafiti zaidi za kijiolojia, kuongeza upatikanaji wa taarifa za kisayansi kuhusu maeneo yenye madini na kuwasaidia wachimbaji wadogo kufanya uwekezaji wenye tija.

"Utafiti ni msingi wa mafanikio ya sekta ya madini. Tunataka wachimbaji wetu waondokane na uchimbaji wa kubahatisha na badala yake watumie taarifa sahihi za kijiolojia zitakazoongeza uzalishaji, kupunguza hasara na kuongeza kipato chao," amesema.

Ameongeza kuwa uwekezaji katika tafiti za madini utaongeza ugunduzi wa maeneo mapya yenye rasilimali, kuchochea uwekezaji, kuongeza ajira na kuimarisha mchango wa sekta ya madini katika Pato la Taifa.

Dkt. Kiruswa amesema Serikali kupitia Wizara ya Madini inatekeleza Programu ya Mining For A Brighter Tomorrow (MBT), inayowalenga wachimbaji wadogo, wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum ili washiriki kikamilifu katika shughuli za utafiti, uchimbaji, uchakataji, uongezaji thamani na biashara ya madini.

Kutokana na fursa hizo, amewahamasisha wananchi wa Kijiji cha Mundarara kuunda vikundi na kujiandikisha katika programu hiyo ili kunufaika na mafunzo, teknolojia, mitaji na fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kukuza shughuli za madini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania (CHAMMATA), Jeremiah Kituyo, amesema uchaguzi wa mabroka katika ngazi ya wilaya utasimamiwa na viongozi wa mkoa kwa mujibu wa Katiba na mwongozo wa chama.

Amesema mwanachama atakayeshiriki uchaguzi atalazimika kuwa na kitambulisho hai cha chama pamoja na leseni halali ya biashara ya madini, huku akibainisha kuwa viongozi wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi huchaguliwa kila mwaka ili kuimarisha uwajibikaji, uwazi na uwakilishi wa wadau wa sekta hiyo.

Kituyo amesema chama kitaendelea kushirikiana na Wizara ya Madini kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa amani, uwazi na kuzingatia sheria, hatua itakayochangia kuimarisha mazingira ya biashara ya madini nchini.














Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ametembelea Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Addis Ababa, Ethiopia, na kufanya mazungumzo na Mhe. Balozi. Innocent Shiyo.

Ziara hiyo imefanyika wakati Mhe. Salome akiwa nchini humo kushiriki Mkutano wa 22 wa Baraza la Mawaziri la Soko la Pamoja la Nishati Mashariki mwa Afrika (Eastern African Power Pool – EAPP), mkutano unaotarajiwa kuhitimishwa leo kwa kupitisha maamuzi muhimu kuhusu biashara ya pamoja ya umeme na uimarishaji wa gridi za taifa kati ya nchi wanachama.

Katika ziara hiyo, Mhe. Salome aliambatana na Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mipango, Utafiti na Uwekezaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mha. HenryFried Byabato, aliyemuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Nishati.