Na Mwandishi Wetu

Halmashauri ya Mji Handeni imetoa mafunzo maalum ya Mfumo wa Kidigitali wa Taarifa za Shule (School Information System – SIS) kwa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi, Wakuu wa Shule za Sekondari pamoja na baadhi ya walimu, huku ikielezwa kuwa mfumo huo utasaidia kuongeza uwajibikaji kwa walimu na kudhibiti tatizo la utoro shuleni.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Januari 9, 2026, mjini Handeni, Kaimu Afisa Elimu Idara ya Sekondari ambaye pia ni Afisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Halmashauri ya Mji Handeni, Montan Mathew, amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo Walimu Wakuu wa Shule za Msingi, Wakuu wa Shule za Sekondari pamoja na mwalimu mmoja kutoka kila shule ili waweze kutumia mfumo huo kwa ufanisi.

Amesema mfumo wa SIS utatumika kukusanya, kuhifadhi na kuchambua taarifa zote muhimu za shule na kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI imeelekeza mfumo huo kuanza kutumika rasmi mara shule zitakapofunguliwa Januari 13, 2026.

“Walimu hawa wanapaswa kuanza kutumia mfumo huu mara moja ili kuweka taarifa za shule zao. Sisi kama Halmashauri ya Mji Handeni tuna wajibu wa kuhakikisha mfumo unatumika kama ilivyoelekezwa, na tutafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara,” amesema Mathew.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mshikamano, Beatrice Chaeka, amesema mfumo huo utasaidia kuwa na takwimu zenye mpangilio mzuri ikilinganishwa na awali walipokuwa wakitumia karatasi ambazo wakati mwingine zilipotea au kuharibika.

Ameongeza kuwa mfumo wa SIS utakuwa suluhisho la changamoto mbalimbali ikiwemo utoro wa wanafunzi na walimu.

“Katika mfumo huu, mwanafunzi anapowekewa alama ya hayupo mara tatu mfululizo, ujumbe hutumwa moja kwa moja kwa mzazi. Hii itawasaidia wazazi kufuatilia mahudhurio na maendeleo ya watoto wao, kwani kuna baadhi ya wanafunzi wanatoka nyumbani lakini hawafiki shuleni,” amesema Chaika.

Naye, Mkuu wa Shule ya Sekondari Kwenjugo, John Rajabu, amesema hapo awali kulikuwa na changamoto katika mipangilio ya taarifa za shule, lakini ujio wa mfumo wa SIS utaboresha usimamizi wa shule kwa ujumla.

Amesema mfumo huo utaongeza uwajibikaji kwa walimu katika ufundishaji pamoja na kuwahusisha wazazi kikamilifu katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao kielimu.

Na Mwandishi Wetu, Handeni

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, ametoa wiki tatu kwa Halmashauri ya Mji Handeni kufanya maboresho mbalimbali katika Soko la Chogo, ikiwamo kurekebisha mageti ya kuingilia sokoni, ili kudhibiti tatizo la wizi wa bidhaa za wafanyabiashara.

Mhe. Nyamwese ametoa agizo hilo Januari 9, 2026, baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika soko hilo na kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katika eneo hilo.

Amesema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya shughuli zao katika mazingira safi, salama na rafiki, ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi bila hofu ya usalama wa mali zao.

Aidha, katika ziara hiyo, Mhe. Nyamwese ameelekeza Halmashauri ya Mji Handeni kufanya marekebisho ya haraka ya mageti ya kuingilia sokoni hapo ili kudhibiti wizi wa mara kwa mara wa bidhaa za wafanyabiashara, jambo ambalo limekuwa likisababisha hasara kwao.

“Hali ya usafi katika lile dampo hairidhishi. Mrundikano wa taka uliopo unahatarisha afya za wananchi na wafanyabiashara. Naiagiza Halmashauri kwa kushirikiana na viongozi wa soko kuangalia namna bora ya kuhakikisha taka zinaondolewa kwa haraka pindi zinapokusanywa,” ameagiza.

Naye, Afisa Biashara wa Halmashauri wa Mji Handeni, Paul Lusinde, ameahidi kufanyia kazi maagizo ya Mkuu huyo.

Na.Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM

Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) imesema imeendelea kuhimiza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za nchi, ili kuhakikisha wananchi wananufaika na shughuli za uchimbaji na utafutaji.

Akizungumza jijini Dar es salam jana katika mahojiano maalum,Katibu Mtendaji wa TEITI, Bi. Mariam Mgaya, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi 57 zinazotekeleza viwango vya kimataifa vya uwazi na uwajibikaji vinavyosimamiwa na EITI.

Amesema Tanzania ilijiunga na EITI mwaka 2009, hatua iliyolenga kuimarisha usimamizi bora wa rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia kwa maslahi ya maendeleo endelevu.

“Asasi hii inahamasisha wananchi kuelewa hatua zote za mnyororo wa thamani wa rasilimali hizi, ikiwemo ukusanyaji na ufuatiliaji wa mapato,” amesema Bi.Mgaya

Bi. Mgaya amebainisha kuwa utekelezaji wa majukumu ya TEITI unasimamiwa na Sheria ya TEITA ya mwaka 2015 ambayo imeainisha jukumu la kuboresha uwazi na uwajibikaji, hasa katika uvunaji wa rasilimali hizo.

Aidha, ameeleza kuwa mpaka sasa TEITI imechapisha ripoti 15 zinazolinganishwa kati ya malipo ya kampuni za madini, mafuta na gesi na mapato ya Serikali, kuanzia Julai 1, 2008 hadi Juni 30, 2023.

“Uwekaji wazi wa ripoti hizi ni sehemu ya utekelezaji wa viwango vya kimataifa ambapo nchi wanachama hutakiwa kufichua takwimu zote za mnyororo wa thamani,” ameongeza.

Hata hivyo Bi. Mgaya ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Madini kwa kuendelea kuiwezesha TEITI kifedha na kimiongozo ili kuhakikisha rasilimali za madini, mafuta na gesi zinaendelea kunufaisha wananchi na kukuza uchumi wa taifa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Uwazi na Uwajibikaji, Bw. Erick Ketagory, amesema TEITI inaendelea kutoa elimu kwa umma ili kuongeza uelewa kuhusu taarifa zinazochapishwa kwenye ripoti hizo na namna zinavyoweza kutumika kuibua mijadala kuhusu manufaa ya rasilimali za nchi.

Amesema Serikali kupitia Wizara ya Madini imeweka wazi huduma 20 muhimu zinazotakiwa kutolewa na kampuni zinazomilikiwa na Watanzania kwa asilimia 100 katika migodi, akitoa wito kwa Watanzania kuchangamkia fursa hizo.

Ketagory ameongeza kuwa TEITI ina wajibu wa kuhakikisha kampuni za uchimbaji na utafutaji zinatoa taarifa za shughuli zao kwa mujibu wa sheria, sambamba na kujenga uwezo wa wananchi kutumia takwimu hizo kuhoji na kufuatilia uwajibikaji.

“Ripoti za TEITI ni nyaraka muhimu sana kwa sababu zinaweka wazi malipo ya kodi na tozo mbalimbali zinazolipwa serikalini,” amesisitiza.

KITUO cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ( PPP Centre), kimeendesha mafunzo kwa wafanyabiashara, wawekezaji na maafisa kutoka taasisi za kiserikali katika Halmashauri za Mkoa wa Tanga, kikielimisha juu ya kazi zinazofanywa na kituo hicho.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na watumishi Umma wa Halmashauri ya Mji na babati vijijini wakati akiwa wa ziara yake ya kikazi Mkoani Manyara, tarehe 8 January, 2026.

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao na watumishi hao, tarehe 8 Januari, 2026 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Ayalagaya.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Emmanuela Kaganda kwa ziara ya kikazi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwasili katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Babati wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Manyara, tarehe 8 Januari, 2026.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wa pili kulia) akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Emmanuela Kaganda baada ya kuwasili katika Ofisi hiyo iliyopo Mkoani Manyara, tarehe 8 Januari, 2026

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Emmanuela

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (watatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali mara baada ya kikao na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, tarehe 8 Januari, 2026. Wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Muhaji.


Na Antonia Mbwambo - Manyara


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amewataka watumishi wa Umma kutambua wajibu wao katika kutekeleza majukumu ya kila siku ili kufanya kazi kwa uwezo, maarifa na ujuzi walio nao kwa lengo la kuboresha huduma ikiwa ni mojawapo ya njia ya kuwatumikia wananchi kwa ustawi wa Taifa.

Mhe. Qwaray ameyasema hayo tarehe 8 Januari, 2026 Mkoani Manyara wakati akizungumza na watumishi wa umma ngazi ya Mkoa, Halmashauri ya Mji wa Babati na Hamashauri ya Wilaya ya Babati wakati alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ambapo ni ziara ya kwanza Mkoani hapo tangu alipoteuliwa tarehe 17 Novemba, 2025 na Mhe Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Amesema Waajiri wote wa Taasisi za Umma lazima waweke kipaumbele katika kushugulikia changamoto zinazowakumba watumishi waliopo chini yao ikiwemo madai ya kupandishwa vyeo na malimbikizo ya mishahara ili kuongeza dhana ya uwajibikaji na kupunguza malalamiko ya watumishi hao.

“Ukiona mtumishi wa umma anakuja hadi Wizarani kwa ajili ya kufuatilia utatuzi wa changamoto zake za kiutumishi, ujue wewe kama msimamizi hujawajibika ipasavyo”,Mhe. Qwaray alisema.

Pia Mhe. Qwaray amewataka watumishi kuzingatia Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma ambazo zinaelekeza tabia na mienendo ambayo mtumishi anapaswa kuwa nayo anapokuwa anatoa huduma katika eneo lake la kazi.

“Mtumishi anapokuwa eneo la kazi hana budi kuachana na masuala binafsi na kujikita katika utoaji wa huduma kwa mwananchi ili kutumia vizuri rasilimali za Serikali katika kuhakikisha kila anayefika kupata huduma anaipata kwa wakati”, Mhe. Qwaray alisema.

Aidha amesisitiza matumizi ya mifumo iliyopo na inayotumika katika kushughulikia masuala mbalimbali ya kiutumishi ikiwemo maombi ya uhamisho na likizo ili kuendana na teknolojia iliyopo kwa lengo la kuwa na utendaji unaozingatia muda na usawa.

Mhe. Qwaray alihitimisha kwa kutoa wito kwa watumishi wa umma kuwa wazalendo na wenye kutanguliza Maslahi ya Taifa mbele katika kulinda na kuimarisha Amani ya nchi kwa kutoa huduma bora, kuzingatia maadili ya kazi na kuepuka vitendo vinavyoweza kuleta mgawanyiko katika jamii.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akimsikiliza Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (kulia) wakati akizungumza nae alipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Kibele, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini, Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026

Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akisisitiza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Mbweni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026.

Mama Sitti Mwinyi, mke wa Hayati Ali Hassan Mwinyi (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (wa kwanza kulia) akisisitiza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kulia) wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) baada ya kuzungumza nae nyumbani kwake Mbweni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026.

Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono (wa kwanza kushoto) akizungumza jambo wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipomtembelea Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (hayupo pichani). Wengine ni wake wa Dkt. Bilal

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (katikati) baada ya kuzungumza nae nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar alipomtembelea kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (watatu kutoka kulia). Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mama Sitti Mwinyi, mke wa Hayati Ali Hassan Mwinyi (kushoto) baada ya kuzungumza nae alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (watatu kutoka kulia). Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mama Sitti Mwinyi (wa tatu kutoka kushoto), mke wa Hayati Ali Hassan Mwinyi wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake. Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.


Na. Veronica Mwafisi-Zanzibar


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amefikisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu ambaye ameahidi kuendelea kuwatunza Viongozi na Wenza wao kwa kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni zilizopo.

Salamu hizo zimefikishwa Januari 8, 2026 kwa nyakati tofauti alipomtembelea Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein nyumbani kwake Kibele Mkoa wa Kusini Unguja, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal nyumbani kwake Mbweni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini na Mwenza wa Hayati Ali Hassan Mwinyi-Mama Sitti Mwinyi nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini.

Mhe. Kikwete amesema, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ina jukumu la kutunza Viongozi Wakuu Wastaafu Kitaifa na Wenza wao, hivyo yuko tayari kuendelea kutekeleza jukumu hilo alilopewa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia kwa salaamu na kumpongeza Mhe. Kikwete kwa kupanga ziara ya kuwatembelea Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu. Ziara hiyo inawapa faraja, heshima na inaonesha thamani ya mchango wao kwa taifa.

Aidha, Dkt. Shein ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa watumishi wa umma kufanya kazi kwa kupendana, ushirikiano na kuzingatia mipaka ya kazi zao kwa kuwa watumishi hao wanamsaidia Rais ambaye anawajibika kwa wananchi.

Naye, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal ameishukuru Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kwa kuwajali na kuwahudumia vyema kwa mujibu wa taratibu


Kwa upande wake, Mama Sitti Mwinyi amemshukuru Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wenza wa Viongozi Wastaafu na ameomba moyo huo uendelee.
8 Januari, 2026

Hayo yamesemwa leo tarehe 08 Januari, 2026 na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu – ADEM Dkt. Maulid J. Maulid alipokuwa akifunga rasmi mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa yanayoendeshwa na ADEM kwa Maafisa Elimu Kata 101 wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Picha ya Pamoja ya baadhi ya viongozi watendaji wa Kata na Tarafa, waliohudhuria semina iliyotolewa na Mamlaka  ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, leo Januari 8,2026

.....

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, leo Januari 8,2026 ilitoa elimu kwa watendaji wa Serikali za Mitaa mkoani Njombe kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko na migogoro, mchakato wa kupata leseni za kuanzisha vituo vya mafuta vijijini pamoja na matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia majumbani.

Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Kanda hiyo, Mhandisi Mwandamizi wa Maji na Usafi wa Mazingira kutoka EWURA, Bw. Dikson Semkuyu, alisema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo viongozi hao ili waweze kuwafikishia wananchi elimu sahihi kuhusu huduma zinazodhibitiwa na EWURA.

“Tunatarajia elimu tuliyotoa itawafikia wananchi mnaowaongoza, ikiwemo mwongozo wa kutambua na kuchangamkia fursa mbalimbali za uwekezaji zinazotolewa na EWURA,” alisema Mhandisi Semkuyu.

Kwa upande wake, Katibu Kata wa Idamba, Bw. Ibrahim Ilomo, aliishukuru EWURA kwa kutoa mafunzo hayo, akisema yamewasaidia kufahamu matumizi salama ya gesi ya kupikia na kugundua kuwa zipo fursa za uwekezaji katika vituo vya mafuta vya gharama nafuu vijijini.

Mwakilishi wa Meneja wa EWURA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambaye ni Mhandisi Mwandamizi wa Maji na Usafi wa Mazingira, Dickson Semkuyu, akiwasilisha mada juu ya kazi na wajibu wa EWURA.

Ofisa za Huduma kwa Wateja Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Francis Mhina, akiwasilisha mada ya namna EWURA inavyosikiliza na kutatua migogoro na malalamiko ya wateja kwa watoa huduma zinazodhibitiwa wakati wa semina hiyo leo.

Mhandisi Mwandamizi Mkaguzi wa Mafuta ya Petroli EWURA Nyanda za Juu Kusini, Raphael Nyamamu, akiwasilisha mada wakati wa semina hiyo, leo.

Picha ya Pamoja ya baadhi ya viongozi watendaji wa Kata na Tarafa, waliohudhuria semina iliyotolewa na Mamlaka  ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, leo Januari 8,2026

 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Na.Mwandishi Wetu-MOSHI

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameielekeza VETA Moshi kuimarisha ushirikiano na makampuni na viwanda ili kuongeza fursa za ajira kwa wahitimu na kukuza matumizi ya teknolojia mpya, sambamba na uelekeo wa taifa uliobainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, sera za kisekta na miongozo mbalimbali ya kitaifa.

Mhe. Ameir ametoa maelekezo hayo Januari 07, 2026, alipotembelea chuo hicho, amesisitiza kuwa ushirikiano huo unaboresha mafunzo na kulingana na mahitaji ya soko la ajira.

Aidha, amesema kuwa utekelezaji wa mafunzo ya sekta ya madini kupitia programu jumuishi ya ufundi wa teknolojia ya uchimbaji madini kwa kushirikiana na Chemba ya Madini Tanzania utawezesha utoaji wa mafunzo yanayoakisi mahitaji halisi ya sekta hiyo muhimu kwa taifa.

 "Serikali itaendelea kuwekeza katika kuongeza fursa na kuinua ubora wa mafunzo ya ufundi stadi kwa kununua vifaa vya kisasa, kuimarisha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na ujenzi wa vyuo vipya vya VETA 64 nchini."amesema Mhe. Ameir 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore, amesema kuwa  Chuo cha VETA Moshi kimeendelea kuwa mfano wa mafanikio ya elimu ya ufundi stadi kwa kuimarisha ushirikiano na viwanda na migodi, hatua inayowezesha mafunzo yanayotolewa kuendana na mahitaji ya soko.

CPA Kasore amesema  ushirikiano huo umewezesha vijana kupata ajira kwa haraka kutokana na ujuzi wa vitendo wanaopata wakati wa mafunzo, na kwamba baadhi ya wahitimu kutoka VETA Moshi wamefanikiwa kupata ajira nje ya nchi, jambo lililosaidia kuboresha uchumi wa familia zao na kuchangia pato la taifa.

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, zinazotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na wadau katika kuimarisha Elimu Amali, Mbunge wa Moshi Mjini, Mhe. Ibrahim Shayo, ameahidi kufadhili masomo ya vijana 10 kila mwaka katika Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akizungumza mara baada ya  kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore,akielezea mafanikio yaliyopatikana katika Chuo cha VETA Moshi mara baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.