Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Mtumba, Antony Mavunde, amekabidhi jumla ya majiko 1,000 ya gesi kwa mama lishe na baba lishe wa Jimbo la Mtumba, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mavunde amesema mpango huo unalenga kuboresha afya za mama na baba lishe, kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku pamoja na kulinda mazingira kwa kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wajasiriamali wadogo ambapo ameahidi kuanzisha klabu za mama lishe katika kila kata za Jimbo la Mtumba zitakazosaidia kuwaunganisha mama lishe na kuwapatia elimu ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha pamoja na kuwawezesha kupata mikopo kwa urahisi ili waondokane na mikopo kandamizi maarufu kama kausha damu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Mafunzo kutoka kampuni ya Oryx Gas, Peter Ndomba, amewataka mama lishe na baba lishe kuacha kabisa matumizi ya mkaa na kuni akisema nishati hizo zimekuwa zikisababisha madhara makubwa ya kiafya ikiwemo magonjwa ya mfumo wa hewa, macho na moyo kutokana na moshi unaotokana na matumizi yake.

Kwa upande wao, mama lishe na baba lishe waliopokea majiko hayo wameishukuru Mbunge wao Antony Mavunde pamoja kwa msaada huo wakisema utawapunguzia adha ya kuni na mkaa, kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku.

Usiku ule ulikuwa wa hofu na mateso makubwa. Nilikuwa nikielekea nyumbani kutoka kazi, lakini ghafla nilishambuliwa na watu wasiojulikana. Walinipiga na kunijeruhi vibaya, wakidhani mimi ni rahisi.

Kila kipande cha mwili wangu kiliumia, na hofu ilijaa moyoni mwangu. Nilihisi kama maisha yangu yamekumbwa na giza lisilo na mwisho. Lakini walikosea zaidi ya kuelewa.

Hawakujua kuwa nilikuwa tayari nimejipanga kwa hekima na busara. Nilikuwa na mbinu ya kipekee, njia ambayo walidhani haikuwepo.

Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la busara na la hekima, la sivyo mateso yangu yangeendelea bila mwisho, na dhihaka lao lingedumu.Soma Zaidi.
Nilipokuwa nikitazama shamba langu lililojaa historia ya familia yetu, siku moja nilikumbana na hali ya kustaajabisha na ya kuhuzunisha. 

Watu fulani walitaka kuninyang’anya shamba langu, wakitumia uongo na hila kuonekana kama mali hiyo ni yao.

Nilijaribu kuzungumza, kuwasilisha shauri kwa wazee wa kijiji, na hata kutafuta msaada wa kawaida, lakini kila jaribio lilishindikana. 

Hali hii ilinifanya nijisikie huzuni, hasira, na hatari isiyoonekana, huku kila siku ikizidi kuwa changamoto.

Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo shamba langu lingeishia mikononi mwa watu wasiokuwa na haki.Soma Zaidi.
Maisha ya kijiji chetu yalijaa hadithi na hekima za kale, lakini siku ile, tukio lisilo la kawaida liligusa kila mtu. 

Marehemu alifariki kwa sababu zisizo za kawaida, na kulikuwa na utata mkubwa kuhusu sababu ya kifo chake.

Baada ya mazishi, watu walishuhudia taambiko ya kipekee, ikiwemo kuzikwa kwa tochi kama ilivyokuwa desturi ya kale. Hali hiyo ilisababisha hofu na mshangao miongoni mwa kila mmoja aliyehudhuria.

Lakini jambo lililokuwa la kushangaza zaidi ni kwamba, siku chache baada ya mazishi, yule aliyemuua marehemu alifariki ghafla, bila hatia yoyote iliyoonekana.

Hii ilisababisha hofu kubwa, wakazi wa kijiji wakijiuliza kama kweli hekima na nguvu za kiroho zipo. Tukio hili lilionyesha wazi kuwa matendo mabaya hayana amani, na kwamba uharibifu unaweza kuja kwa haraka bila onyo.

Nilijaribu kuelewa sababu za hili, na baada ya kushauriana na wazee wa kijiji, niliambiwa kuna hekima maalum za kiroho zinazoweza kusaidia kulinda maisha, kutunza familia, na kuondoa hatari zisizotarajiwa.Soma Zaidi.
Nilipokuwa nikitazama sherehe ya mavuno ya maembe kijijini, nilishangaa kuona jamaa mmoja akijaribu kuiba maembe mengi haramu. Kila mmoja alishangaa, lakini hatimaye jambo hilo liligeuka tukio la kusikitisha.

Baada ya kula maembe yote aliyoiba, jamaa huyo alifura tumbo kupita kiasi. Hali ilikuwa mbaya sana, watu walikuwa wameshangaa, na machozi yalikuwa karibu kutokana na tukio hilo la aibu.

Nilijaribu kumsaidia kwa njia za kawaida kumpeleka kwa daktari wa kijiji, kumtuliza, na kumsaidia kunyonyesha maji lakini hali ilizidi kuwa mbaya.

Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo mateso yake yangeendelea, na tukio hili lingekuwa mbaya zaidi kwa jamii yetu. Soma Zaidi.
Nilipokuwa na matumaini makubwa katika ndoa yangu, siku moja maisha yangu yaligeuka ghafla. Dada yangu mdogo, ambaye niliyekaribisha kuishi nami Nairobi kwa muda, alianza kuonyesha tabia zisizozingatia heshima na uaminifu.

Hatimaye, aliniiba mume wangu, akivuruga amani na furaha ya familia yetu. Hii ilikuwa dhihaka kubwa kwangu; si tu kwa sababu ya mume wangu, bali pia kwa uaminifu na heshima yetu ya ndoa.

Kila siku nilijisikia huzuni, hasira, na kuchanganyikiwa. Nilijaribu njia za kawaida kuongea naye, kumshawishi, hata kujaribu kuondoa misugu lakini kila jaribio lilishindwa.

Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo upendo wangu ungeishia kudorora milele. Soma Zaidi.

 


Na Oscar Assenga,

Kutokana na kuporomoka  mmomonyoko wa maadili katika jamii, wanawake wa Kiislamu mkoani Tanga wameanzisha majadiliano na mikakati maalum ya kutafuta suluhisho la changamoto hiyo, sambamba na maandalizi ya kuupokea mwezi mtukufu wa Ramadhani.


Kupitia Taasisi ya Subra na Nusra, wanawake hao wameandaa kongamano maalum litakalofanyika Jumamosi hii katika Ukumbi wa Simba Mtoto, jijini Tanga, likilenga kuwaandaa wanawake kiroho na kijamii ili kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW).


Mratibu wa kongamano hilo, Bi Mwanakombo Abdallah Kipanga, alisema lengo kuu ni kutoa elimu kwa jamii, hususan wanawake, kuhusu umuhimu wa maadili mema na maandalizi sahihi ya mwezi wa Ramadhani.



“Huu si mwezi wa kawaida. Tunataka wanawake wapate elimu itakayowasaidia kuimarisha imani, malezi ya watoto na maadili ndani ya familia na jamii kwa ujumla,” alisema.




Alisema Mufti Abubakar Bin Zuberi anatarajiwa kuwa mgeni wa heshima, huku Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk Batilda Burian, akiwa mgeni rasmi. Hili litakuwa kongamano la nne kufanyika chini ya taasisi hiyo.


Bi Kipanga aliongeza kuwa jitihada hizo zimeungwa mkono pia na wanawake wenye asili ya Tanga wanaoishi Dar es Salaam, walioungana kuimarisha maandalizi ya kongamano hilo.




Miongoni mwa mada zitakazojadiliwa ni maandalizi ya wanawake katika mwezi wa Ramadhani, kujenga hofu ya Mungu, malezi bora ya watoto pamoja na umuhimu wa kuzingatia maadili mema katika maisha ya kila siku.


Aliwataka wanawake wa Kiislamu pamoja na wa dini nyingine kujitokeza kwa wingi kushiriki kongamano hilo.
Naye mjumbe wa kamati ya maandalizi, Bi Shamsi Diwani kutoka Dar es Salaam, alisema kuna haja ya dharura kwa wanawake kuungana kupambana na kuporomoka kwa maadili kunakojitokeza katika jamii.


“Ni wakati wa kusaidiana kurejesha maadili mema. Inasikitisha kuona mienendo isiyofaa na burudani zinazokiuka maadili zikizidi kushika kasi katika jamii,” alisema.


Aliongeza kuwa wako tayari kukaa pamoja na wanawake na kujadili kwa kina chanzo cha changamoto hiyo ili kupata suluhisho la kudumu.


Bi Diwani pia alielezea wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa migogoro ya ndoa na kuvunjika kwa familia, akisema si jambo jema kushuhudia baadhi ya wanawake wakisherehekea talaka.


“Hili si jambo la kufurahia. Ingawa talaka inaruhusiwa, si tukio la kushangiliwa,” alisisitiza.
Kwa upande wake, Bi Kibibi Saidi Kibao aliwahimiza wanawake kuhudhuria ili kunufaika na mafunzo yatakayotolewa na Mashehe maarufu pamoja na mke wa Mufti wa Kwanza, Sheikh Jumaa.

Naye mjumbe mwingine wa kamati, Bi Hawa Mweri, alisisitiza umuhimu wa wanawake wa Kiislamu kudumisha maadili mema wakati wote, si kipindi cha Ramadhani pekee.
MWISHO

 



Na Oscar Assenga, TANGA



BONANZA la Michezo maarufu kama Michezo Plus limekuwa na mvuto wa aina yake huku likifanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Tanga Ufundi kwa kushirkisha wanafunzi zaidi ya 500.


Wanafunzi hao kutoka shule 50 Jijini Tanga ambao walishiriki katika Michezo ya Mpira wa Miguu,Pete na Wavu huku wakionyesha vipaji vya hali ya juu hatua iliyoshangiliwa na wadau wa michezo ambao walijitokeza kushuhudia bonanza hilo


Akizungumza baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Afisa Michezo wa Jiji la Tanga na Mratibu wa Michezo Plus katika mradi unaotekelezwa na Jiji hilo ukifadhiliwa nan a Botnar Foundation chini ya Programu ya Tanga Yetu Lucy Michael alisema kwamba waliliandaamaalumu kwa ajili ya kujenga mahusiano na kuwajenga kiakili.

Alisema kwamba bonanza hilo litakuwa linafanyika kila mwaka mara mbili ambapo hilo limeanza kwa kufungua mwaka na kukaribisha wanafunzi na watafanya bonanza la vijana.



Awali akizungumza Mratibu wa Bonanza hilo Haji Milao alisema kwamba nia na madhumuni yake ni kuwaweka watoto sawa kwa ajili ya michezo ya Umistashumta mwaka huu 2026 ikiwemo kutengeneza afya za watoto ili waweze kuwa sawa na watoto wakiwa vizuri kwenye michezo hata darasani watakuwa vizuri.



Naye kwa upande wake Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Makorora Zuhuru Ally alisema michezo hiyo ina faida kubwa sana kwao kutokana na kwamba inawafanya wakutana na wenzao na kubadilisha mawazo jambo ambalo linawapa fursa.
Maisha yangu ya ndoa yalikuwa changamoto kubwa. Nilipata hisia kuwa upendo na uaminifu vilikuwa vimepotea baada ya mke wangu kuanza kuonyesha tabia zisizo za kawaida.

Mara nyingi nilihisi huzuni, kuchanganyikiwa, na hata kujiuliza ikiwa bado tupo kwenye ndoa ya kweli. Hali ilizidi kuwa mbaya nilipoona ishara kuwa mke wangu alikuwa akitengeneza uhusiano wa siri na gateman wa nyumba.

Nilijaribu kuzungumza naye, kujaribu kuelewa, na hata kujaribu kusahau alichokuwa akifanya, lakini kila hatua ilishindwa. Hali hii ilinifanya nijisikie kukosa nguvu, huzuni, na hasira. Nilijua lazima nifanye kitu cha hekima na busara, la sivyo ndoa yangu ingeishia kudorora kabisa.Soma Zaidi.
Nilipokutana na mpenzi wangu wa sasa, nilijua moyo wangu ulikuwa umepotea kwake. Tulianza mahusiano yetu kwa upendo wa kweli, lakini nilijaribu kumtambulisha kwa familia yake na kumpa heshima ya kulipa mahari, ila alikataa kabisa.

Nilihisi hasira, huzuni, na mara nyingine kuchanganyikiwa kwa sababu nilihisi upendo wetu ulikuwa hatarini kusambaratika.

Kila siku nikiwa naye nilijisikia huzuni kidogo, nikijua kwamba familia yake ilikataa kumpa ruhusa ya kuishi pamoja bila sababu halisi.

Nilijaribu kuongea, kujaribu suluhisho, na hata kuacha kujaribu mara kadhaa, lakini kila hatua ilikuwa imefungwa na kuta zisizoonekana.

Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo upendo wetu ungeendelea kudorora.Soma Zaidi.
Siku zote nilikuwa na shauku ya vitu vya ajabu na nguvu zisizo za kawaida, lakini sikuwa na wazo lolote kuwa kitambaa ndogo kilichopewa kama zawadi kinaweza kubadilisha maisha yangu kwa namna isiyotarajiwa.

Nilipokipata, nilihisi furaha ndogo tu, lakini ghafla mambo yasiyokuwa ya kawaida yalianza kutokea katika maisha yangu. Kila siku niliona mabadiliko madogo, lakini makubwa.

Familia yangu, ambao tulikuwa tukikabiliana na migongano ya muda mrefu, alianza kuonyesha mabadiliko ya kushangaza.

Hatimaye, niligundua kuwa kitambaa hiki kilikuwa na nguvu ya kipekee, kilichoweza kufichua siri zilizofichwa, kuleta amani, na kubadilisha hatma ya familia.

Nilijaribu kutumia hekima yangu mwenyewe, lakini mambo yalikuwa magumu kuelewa. Soma Zaidi.
Nilihisi maumivu makali siku nilipopata habari kwamba mume wangu aliniambukiza ugonjwa baada ya kuhusiana na wanawake wengine bila tahadhari yoyote.

Hii ilikuwa dhihaka kubwa kwangu; si tu kwa sababu ya ugonjwa, bali pia kwa uaminifu na heshima yetu ya ndoa. Kila siku nilihisi huzuni, hasira, na kuchanganyikiwa, nikijiuliza ni jinsi gani ningeweza kumrejesha bila kuharibu maisha yangu.

Nilijaribu njia za kawaida zungumza naye, kujaribu kumuelewa, na hata kumtetea lakini hakuna kilichofanya mabadiliko. Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo mateso yangu yangeendelea na heshima yangu ingepotea milele.Soma Zaidi.
Nilipokuwa nikicheza michezo ya kubeti, nilijua hatari ilikuwa kubwa, lakini sikuwa na wazo kwamba bet moja ingeweza kunipotezea kila kitu nilichokuwa nacho.

Nilipoteza pesa zangu zote, na ghafla maisha yangu yaligeuka kuwa mateso yasiyo na mwisho. Hali hii ilinifanya nijisikie huzuni kubwa, hasira, na kushindwa kuelewa ni jinsi gani ningeweza kurekebisha hali hiyo.

Nilijaribu njia za kawaida kujaribu kubeti tena, kuomba msaada wa rafiki, na hata kuacha michezo ya kubeti lakini kila jaribio lilishindikana. Nilijua lazima nifanye kitu kingine, jambo la hekima na busara, la sivyo maisha yangu yangeendelea kuwa magumu bila mwisho.Soma Zaidi.

 


Na Mwandishi Wetu ,RUVUMA.


 


CHAMA cha National League For Democracy (NLD) kimempitisha Mhagama Hamisi Yusufu kuwania Ubunge Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma ambayo ataipeperusha Bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mdogo kufuatia Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Jenista Mhagama.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,Katibu wa NLD Doyo Hassan Doyo ambapo aliwaambia kwamba siku hiyo ni muhimu kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho kufanya maamuzi ya kiongozi wanayemtaka .

Alisema kwamba kiongozi ambaye anaweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo ni mgombea wao kutokana na uongozi uliopita kwa miaka mingi umeshindwa kuwapa maendeleo na mabadiliko katika Jimbo hilo.


Katibu huyo aliwataka wananchi hao kutokufanya makosa katika uchaguzi huo wa marudio kutokana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kufariki dunia hivyo aliwataka kumchagua mgombea anayetokana na NLD ili aweze kuwapa maendeleo makubwa.

Katika uchaguzi huo Mhagama Hamis Yusuf wa NLD atachuana na wagombea wengine akiwemo Yusuf Rashid Rai wa Chama cha AAFP,Abdallah Boniface Ngonyani wa Chama cha Makini,Hanifa Sembe Mohamed wa Chama cha UMD,Beatrice Omari Muya wa UPDP,Mapunda wa Chama cha DP,Dastan Frolian Pili wa CCK,Morice Thomas Nkongo wa TLP na Mtemi Pachoto wa UDP.


 


Mwisho.


Wadau na wawekezaji mbalimbali wameonesha nia ya kuwekeza katika sekta ya mafuta nchini Tanzania, uwekezaji ambao utachangia ukuaji wa uchumi wa nchi na kuboresha huduma ya bidhaa za nishati kwa wananchi.

Miongoni mwa wawekezaji hao ni Kampuni ya Mafuta ya India (Indian Oil Corporation Limited), yenye uzoefu mkubwa katika usambazaji wa mafuta na gesi, ambayo imeonesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kampuni hiyo imeonesha nia hiyo katika kikao kilichofanyika kati yao na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba pembezoni mwa Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanayoendelea Jimbo la Goa, nchini India.

Katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa kampuni hiyo, Suman Kumar, amesema Tanzania ni soko la bidhaa nyingi ikiwemo bidhaa za nishati.

Amesema kutokana na ongezeko la mahitaji ya bidhaa kama mafuta, gesi ya mitungi na nishati linalotokana na ukuaji wa uchumi, idadi ya watu inayoongezeka na miji kukua haraka, inatoa fursa kwa kampuni za nishati kushirikiana katika usambazaji, uchakataji na huduma za nishati.

Kwa upande wake Mhe. Salome amesema “Serikali ya Tanzania inawakaribisha wawekezaji wote na ipo wazi kwa uwekezaji wa kimataifa katika sekta ya nishati, ikiwa ni pamoja na usambazaji wa mafuta na gesi ya mitungi kuendana na msukumo wa Serikali wa kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia."

Aidha Mhe. Salome amewahimiza wawekezaji hao kuona umuhimu wa kufungua matawi nchini Tanzania na kushiriki katika ununuzi wa pamoja wa bidhaa za mafuta ili kuongeza ushindani na uhakika wa upatikanaji wa mafuta ya gharama nafuu nchini.

 "Hivyo tunawakaribisha wadau wote kuja kuwekeza nchini Tanzania kupitia makubaliano ya kibiashara na kampuni zetu za ndani kulingana na sera za Tanzania na mapendekezo ya wawekezaji” amesema Mhe. Salome.

Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 30, 2026 na yamewakutanisha washiriki kutoka nchi zaidi ya 125, yakivutia wawekezaji wengi wa kigeni katika sekta ya nishati. 

Kupitia Maadhimisho hayo yamefungua fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya nishati kwa wadau na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani.










 


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 73.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 527 mkoani Tanga.

Hayo yamebainishwa leo Januari 29, 2026 Jijini Tanga na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi waliuoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Giza cable industries pamoja na Energy service Limited katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

“Leo tuko hapa kwako kutambulisha Wakandarasi ambao watakuja kutekeleza mradi mkubwa wa kupeleka umeme katika vitongoji 527 katika Mkoa wa Tanga.

Wakati tunafanya nao majadiliano kuna maagizo mahususi tuliwapa na tungependa kama kiongozi wetu wa Mkoa uyafahamu. Moja tumewaelekeza wawe na timu ya kufanya kazi karibu kila Wilaya,” ameainisha Mhandisi Saidy.

Ameongeza pia, Wakandarasi hao wanatakiwa kujiepusha na vitendo vya kutoa lugha chafu, pamoja na vitendo vya rushwa wakati wanatekeleza miradi hiyo kwa wananchi.

“Ukifanya kazi kwenye mradi wa serikali unatakiwa kufanya kama mtumishi wa umma. Lugha chafu hazikubaliki. Kurubuni wanakijiji ni kitu ambacho kitapelekea kuvunja mkataba wako,” amessisitiza Mhandisi Saidy.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dadi Kolimba ameipongeza serikali kwa utekelezwaji wa mradi huo na kusema kuwa utakwenda kufungua zaidi fursa za uchumi vijijini.

“Ukiangalia kwa wakandarasi hawa wawili ambao wametambulishwa leo ambao wanaenda kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 527, jumla ya shilingi Bilioni 73.8. Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutoa fedha za kuwezesha kutekelezwa kwa mradi huu,” amesema Mhe. Kolimba huku akiwataka Wakandarasi hao kuhakikisha wanamaliza mradi huo ndai ya muda uliopangwa.

Aidha, Mhe. Kolimba ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao pindi watakapoanza kutekeleza mradi huo ili malengo yaliyowekwa na serikali yaweze kufikiwa.








Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

.....

Tanzania na Jamhuri ya Serbia zimejadili fursa za kuimarisha ushirikiano wa masuala ya kazi, ajira na maendeleo ya rasilimali watu, hususan katika Sekta ya Ujenzi na maeneo mengine muhimu ya kiuchumi.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski, walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Sangu amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kufanya mageuzi makubwa yanayolenga kukuza ajira zenye staha, kuongeza ujuzi kwa nguvu kazi na kupanua fursa za ajira kwa wananchi.

Vilevile, Mhe. Sangu alitumia fursa hiyo kueleza wataalamu na uwezo wa wafanyakazi katika nyanja mbalimbali zikiwemo uhandisi, afya, elimu, uhasibu, utawala wa biashara, uchumi, sheria, utalii na ukarimu, kilimo, TEHAMA, biashara ya kilimo na usindikaji wa mazao, anga na usafiri, ufundi mitambo, usafirishaji huduma za majumbani pamoja na fani nyingine nyingi, hivyo amesema Watanzania wanatambulika kwa bidii, unyenyekevu, maadili mema ya kazi na mtazamo chanya kazini.

Kadhalika, Waziri Sangu amemwalika Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski kutembelea Tanzania ili kujionea mikakati inayotekelezwa na Serikali katika kuimarisha soko la ajira pamoja na sera za ajira. Pia, amemkaribisha kutembelea vivutio vya utalii nchi ya Tanzania.

Kwa upande wake, Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic Stamenkovski, amesema nchi ya Serbia ipo katika mchakato wa kufungua ubalozi nchini Tanzania ili kuendelea kukuza ushirikiano kati ya mataifa hayo. Pia alimwalika Waziri Sangu kutembelea nchi ya Serbia ili kujadili kuhusu masuala ya kazi na ajira ikiwemo fursa za ajira zilizopo nchini humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akisalimiana na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, walipo kutana katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu alipokutana na kuzungumza na Waziri wa Kazi, Ajira na Ustawi wa Jamii wa Serbia, Mhe. Milica Djurdjevic, katika kikao cha pembeni (side meeting) kujadili ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.