Na. OWM (KAM), Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema mahusiano mema, mazungumzo ya kujenga na mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu katika kuimarisha demokrasia, amani na maendeleo endelevu nchini.
-DODOMA

Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua rasmi Awamu ya Pili ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC II) Juni 20,2026 katika Viwanja vya Maonesho Dole, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi wote.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026  jijini Dodoma leo, Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera, amesema  kampeni hiyo inalenga kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa huduma za msaada wa kisheria, elimu ya sheria na ushauri wa kisheria ili kuongeza uelewa wa haki na wajibu wao katika jamii.

Dkt. Homera amesema kampeni hiyo ni utekelezaji wa maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha huduma za sheria na haki zinapatikana kwa wananchi wote bila ubaguzi, hususan makundi maalumu na wananchi wa maeneo ya pembezoni ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto za kupata huduma hizo.

Amefafanua kuwa Awamu ya Pili ya kampeni hiyo itaendelea kutumia kaulimbiu ya “Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo,” ambayo inaakisi dhamira ya Serikali ya kuimarisha utawala wa sheria, usawa na maendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, mafanikio ya Awamu ya Kwanza ya kampeni iliyotekelezwa kuanzia Aprili 2023 hadi Juni 2025 ndiyo yamechochea kuanzishwa kwa awamu mpya. Katika kipindi hicho, kampeni ilitekelezwa katika mikoa yote 31 ya Tanzania Bara pamoja na mikoa yote mitano ya Zanzibar.

Amesema Zanzibar pekee, jumla ya wananchi 422,908 walinufaika na huduma mbalimbali za msaada wa kisheria, ambapo wanaume walikuwa 213,723 huku wanawake wakifikia 209,185.

“Matokeo haya yanaonesha wazi umuhimu wa kampeni hii katika kuwajengea wananchi uelewa wa sheria, haki na wajibu wao pamoja na kusaidia kutatua migogoro mbalimbali ya kisheria inayowakabili,” amesema Dkt. Homera.

Katika awamu mpya, wananchi watapata huduma zinazohusu masuala ya ndoa na talaka, mirathi, migogoro ya ardhi, haki za watoto, ukatili wa kijinsia, haki za wafanyakazi pamoja na usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala.

Huduma nyingine zitakazotolewa ni pamoja na usajili wa matukio muhimu ya maisha, upatikanaji wa nyaraka za utambulisho, uandaaji wa nyaraka za kisheria na utoaji wa elimu ya sheria kwa wananchi.

Dkt. Homera amesema maandalizi yote ya uzinduzi wa kitaifa yamekamilika na kwamba zaidi ya washiriki 15,000 wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo, wakiwemo viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, viongozi wa dini, vyama vya siasa, mashirika ya kiraia, wataalamu wa sheria na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

Ameongeza kuwa sambamba na uzinduzi huo, huduma za msaada wa kisheria zitatolewa kupitia mabanda katika wilaya za Mjini, Magharibi A na Magharibi B, huku timu za wataalamu zikitembelea shehia mbalimbali kutoa elimu ya sheria, ushauri na utatuzi wa migogoro.

Waziri huyo ametumia fursa hiyo kupongeza ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika utekelezaji wa kampeni hiyo, akisema ni mfano halisi wa manufaa ya Muungano katika kuwahudumia wananchi.

Aidha, amewataka wananchi wa Zanzibar kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi huo na kutumia fursa ya kupata huduma mbalimbali za kisheria zitakazotolewa bila malipo.

“Ushiriki wa wananchi katika kampeni hii utasaidia kuongeza uelewa wa haki zao za kisheria, kuimarisha amani na utulivu katika jamii pamoja na kuchochea maendeleo ya Taifa,” amesema 

Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imeendelea kuwa miongoni mwa programu muhimu za Serikali zinazolenga kusogeza huduma za haki karibu na wananchi na kujenga jamii inayozingatia sheria, usawa na utawala bora.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Na Mwandishi Wetu-DODOMA
Wizara ya Viwanda na Biashara imewahimiza wananchi, hususan vijana na wajasiriamali, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na taasisi zake ili kukuza biashara, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.
Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2026 na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Saidi Msabimana, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Msabimana amesema wizara hiyo, ambayo ni miongoni mwa taasisi muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imeshiriki maonesho hayo pamoja na taasisi nane zilizo chini yake kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi pamoja na kutoa elimu kuhusu biashara, viwanda na uwekezaji.
Amesema jukwaa hilo limetumika kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa taarifa za huduma zinazotolewa na kuwaelekeza namna ya kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla.
“Tunatumia jukwaa hili kuwafikia wananchi moja kwa moja, kuwaeleza huduma tunazotoa na kuwahamasisha kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa kwa ujumla,” amesema Msabimana.
Katika maonesho hayo, taasisi zilizo chini ya wizara hiyo zimeendelea kutoa huduma mbalimbali, ikiwemo huduma za usajili wa biashara kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni Tanzania (BRELA), ambapo wananchi wamewezeshwa kupata huduma za usajili wa kampuni, majina ya biashara na alama za biashara kwa njia ya kidijitali.
Kwa upande wa Mamlaka ya Usajili wa Maghala Tanzania (ZAGARA), wananchi wanaomiliki au wanaotarajia kuendesha maghala wamepata elimu na huduma za usajili pamoja na leseni zinazotakiwa kisheria.
Aidha, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE ) kimetumia maonesho hayo kutoa taarifa za udahili na programu mbalimbali za masomo zinazolenga kuwaandaa vijana kuwa wataalamu na wajasiriamali wenye ushindani sokoni.
Vilevile, Wakala wa Vipimo umeendelea kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo katika biashara ili kulinda haki za walaji na kuimarisha uaminifu katika shughuli za kibiashara nchini.
Msabimana amesema kupitia maonesho hayo, zaidi ya wananchi 365 wamepata huduma za kuboresha mifumo ya biashara zao pamoja na taratibu za usajili wa lebo za bidhaa, hatua inayosaidia kuongeza ubora na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Kwa upande mwingine, Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), limeendelea kutoa taarifa kuhusu miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Liganga, Mchuchuma na Soda Ash, inayotarajiwa kuwa kichocheo cha mapinduzi ya viwanda, ajira na ukuaji wa uchumi.
Msabimana amewahimiza wananchi kutembelea mabanda ya wizara hiyo katika maonesho hayo ili kupata huduma, elimu na taarifa sahihi zitakazowawezesha kuboresha maisha yao na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi shindani wa Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.

...

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.

Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.

Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.

Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.

“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.

Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuongeza vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya  umeme ili kuongeza wigo wa utoaji huduma hiyo ambayo imeonekana kuleta mageuzi katika matumizi ya nishati safi.

Mhe. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma.

Waziri huyo mwenye dhamana ya Utumishi ametumia nafasi hiyo kuipongeza TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati safi kwa ajili ya  kupikia na katika vyombo vya usafiri.

‘’ TANESCO mnafanya kazi kubwa nawapongeza kwa mageuzi ya matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, natoa rai muongeze Vituo vya kuchajia vyombo hivyo ili kuongeza wigo wa utoaji huduma,’’ alisisitiza Mhe. Ridhiwani

Naye Meneja Masoko Bw. Fredrick Kalinga amesema TANESCO inashiriki katika Maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika ikiwemo maendeleo ya miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme, maboresho makubwa yaliyofanywa na Shirika kwenye mifumo ya kidigitali ya utoaji huduma kwa wateja pamoja na kuhamasisha jamii kutumia nishati safi ya umeme kupikia na katika vyombo vya usafiri kama magari, bajaji, guta, na pikipiki.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026  yenye kauli mbiu isemayo ‘’Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa huduma Endelevu’’ yameanza rasmi Juni 16, 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026










 


Serikali imeendelea kuimarisha jitihada za kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia upatikanaji wa mitaji, mafunzo na masoko ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya Taifa. 

Hayo yameelezwa leo Juni 17, 2026 bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga (Viti Maalum) aliyetaka kufahamu mipango maalum ya Serikali katika kuwawezesha wanawake.

Akijibu swali hilo, Mhe. Mahundi amesema Serikali inatumia mifumo mbalimbali ya uwezeshaji inayotekelezwa kupitia Wizara za kisekta pamoja na mamlaka za serikali za mitaa ikiwa na lengo la kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kujenga uwezo wa kiuchumi, kuongeza kipato na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Amefafanua kuwa miongoni mwa mipango hiyo ni utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri pamoja na Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake huku kabla ya kunufaika na mikopo hiyo, wanawake hupatiwa mafunzo ya kuongeza thamani ya bidhaa wanazozalisha kupitia ushirikiano kati ya Serikali, SIDO, VETA na taasisi mbalimbali zinazojihusisha na maendeleo ya wanawake.

Naibu Waziri huyo pia amesema Serikali inaendelea kutekeleza Programu ya Jenga Kesho Yako (BBT) katika sekta za kilimo, mifugo na ufugaji nyuki, ambayo imekuwa ikitoa fursa kwa wanawake kujikita katika shughuli za uzalishaji mali ambayo imeendelea kuwajengea uwezo wa kiufundi na kuwasaidia kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na sekta hizo muhimu.

Katika sekta ya madini, Mhe. Mahundi amesema Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) linaendesha programu maalum zinazowawezesha wanawake kushiriki katika shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa kuwapatia mafunzo, maarifa na kuwaunganisha na fursa mbalimbali za uwekezaji. Hatua hiyo inalenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta hiyo yenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

Aidha, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kuimarisha huduma jumuishi za kifedha zinazowawezesha wanawake kupata mitaji kupitia SACCOS na kuboresha mazingira ya uwezeshaji wa wanawake ili kuhakikisha wanapata mitaji, mafunzo na masoko ya uhakika yatakayowasaidia kukuza biashara zao na kuchangia kwa kiwango kikubwa zaidi katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.


















 


‎Wkala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia mradi wa RISE imeendelea kuimarisha ushiriki wa wananchi katika shughuli za matengenezo ya barabara kwa kutumia vikundi vya Kijamii vya Matengenezo ya Kawaida ya Barabara (CBRM) hatua inayolenga kuongeza ajira, kukuza uchumi wa wananchi na kuhakikisha barabara zinabaki katika hali nzuri mwaka mzima.

‎Akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu yanayoendelea jijini Arusha, Mtaalamu wa masuala ya  kijamii kutoka TARURA Makao Makuu, Bi. Mwanamisi Abdallah amesema mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa takwa la kisheria linaloelekeza asilimia 30 ya bajeti ya kazi za barabara kutengwa kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya barabara.

‎Amesema TARURA kupitia Mradi wa RISE imeamua kutumia fursa hiyo kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuunda na kuimarisha vikundi vya kijamii vyenye wanachama kati ya watano hadi ishirini ambavyo vitashiriki katika utekelezaji wa kazi mbalimbali za matengenezo ya barabara.

‎"Vikundi hivi vitapatiwa mikataba ya kufanya kazi za kusafisha mitaro, kuziba mashimo madogo, kuondoa vikwazo vinavyokatiza njia, kufyeka majani pamoja na shughuli nyingine ambazo hazihitaji matumizi ya mitambo mikubwa. Hii ni fursa kwa wananchi kupata ajira, kuongeza kipato na kushiriki moja kwa moja katika kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo yao", amesema Bi. Mwanamisi.

‎Kwa upande wake, Mratibu wa Kitaifa wa Programu kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. Dampu Ndenzako amesema ushirikiano kati ya ILO na TARURA unalenga kujenga uwezo kwa wataalamu na kuhakikisha vikundi vya kijamii vinatumika kikamilifu katika matengenezo ya barabara huku vikitoa manufaa ya kiuchumi kwa wananchi.

‎Amesema uzoefu unaonesha kuwa ushiriki wa wananchi katika matengenezo ya barabara hususan maeneo ya vijijini huongeza umiliki wa miundombinu hiyo, huimarisha huduma za usafiri na usafirishaji na kuhakikisha barabara zinapitika katika misimu yote ya mwaka huku wananchi wakinufaika kwa kupata ajira na kuongeza kipato.

‎Naye, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kongwa Mhandisi Peter Johnson, amesema wilaya hiyo imeanza kutekeleza mpango huo katika mwaka wa fedha 2025/26 ambapo imefanikiwa kuunda vikundi 34 vya CBRM, kati ya hivyo vikundi 31 tayari vimeanza kazi huku vingine vikiendelea kukamilisha taratibu za kuingia mikataba.

‎Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Bi. Hidaya Abdallah amesema mafunzo hayo yatawawezesha wataalamu wa maendeleo ya jamii kutambua, kuunda, kusajili na kuvijengea uwezo vikundi kwa kuzingatia miongozo na taratibu zilizowekwa huku wananchi wakipata fursa za ajira, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya miundombinu na uchumi wa jamii kwa ujumla.

‎Mafunzo hayo ya siku sita yanawakutanisha Wahandisi na Wataalamu wa Mazingira na Jamii kutoka TARURA Makao Makuu, Ofisi za Mikoa na Wilaya pamoja na Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi za Wakurugenzi wa Wilaya kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kusimamia utekelezaji wa mpango huo katika mwaka wa fedha 2026/27.











Nilipoolewa, niliamini ndoa yangu ingekuwa mahali pa furaha, amani, na upendo. Kwa miaka ya mwanzo mambo yalikuwa mazuri. 

Mimi na mume wangu tulikuwa karibu sana na tulifurahia muda wetu pamoja. Lakini kadri miaka ilivyopita, hali ilianza kubadilika taratibu.

Mazungumzo yetu yalipungua.

Tulianza kugombana kwa mambo madogo madogo. Wakati mwingine tungekaa siku nzima bila kuzungumza vizuri. 

Upendo ambao zamani ulikuwa wazi ulianza kupoa kiasi kwamba nilianza kuhisi kama tunaishi pamoja kama marafiki tu. Kwa kweli jambo hilo liliniumiza sana.

Nilijaribu kufanya kila nilichoweza ili kuboresha hali. Nilizungumza naye mara kadhaa kuhusu hisia zangu, lakini mazungumzo mengi yaliishia kwenye mabishano. Kadri muda ulivyopita, nilianza kuogopa kwamba ndoa yetu ilikuwa ikielekea mahali pabaya...SOMA ZAIDI.
Kwa muda fulani nilianza kuhisi mabadiliko katika ndoa yangu. Mke wangu ambaye zamani alikuwa mchangamfu na mkarimu alianza kubadilika. 

Alianza kutumia muda mwingi nje ya nyumba, simu yake ikawa na siri zaidi, na mazungumzo yetu yakapungua sana. Mwanzoni nilijaribu kujipa moyo.

Nilijiambia labda ni uchovu wa kazi au majukumu ya kawaida ya maisha. Lakini kadri siku zilivyopita, hisia zangu za wasiwasi zilianza kuongezeka. 

Nilianza kuona dalili ambazo zilinifanya nijiulize maswali mengi. Wakati mwingine alikuwa akirudi nyumbani akiwa na visingizio visivyoeleweka.

Simu yake ilikuwa haipatikani kwa muda mrefu, na mara nyingi alionekana kukasirika nilipomuuliza maswali madogo. 

Kwa kweli hali ile ilinichanganya sana. Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa, lakini hakutoa majibu ya kuridhisha. Badala yake, mazungumzo yetu yaligeuka kuwa mabishano. SOMA ZAIDI.
Sikuwahi kuwa mtu wa kuamini sana katika ishara za hatari. Kwa miaka mingi nilikuwa nikiendesha gari na kusafiri mara kwa mara bila matatizo makubwa. 

Nilichukulia usalama kama jambo la kawaida ambalo halikuhitaji kufikiriwa sana. Lakini mwezi mmoja ulifika na kubadilisha mtazamo wangu kabisa.

Tukio la kwanza lilitokea nilipokuwa nikirejea nyumbani usiku. Gari moja lilitoka ghafla kwenye barabara ndogo bila kutoa ishara. Kwa sekunde chache nilidhani mgongano haukuwa unaweza kuepukika. Kwa bahati, nilifanikiwa kulikwepa.

Wiki moja baadaye, nilikuwa ndani ya gari la abiria lililopata hitilafu ya ghafla barabarani. Watu wengi walipata hofu, lakini dereva alifanikiwa kulisimamisha kabla ya kutokea madhara makubwa. Nilishukuru na kuendelea na maisha....SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu, nilikuwa nikiishi na tatizo ambalo sikuwa na ujasiri wa kulizungumzia na mtu yeyote. Mwanzoni nilidhani lilikuwa jambo la kawaida ambalo lingepita lenyewe. 

Lakini kadri miezi ilivyopita, niligundua hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya. Nguvu na hamu yangu ya mapenzi zilianza kupungua, jambo ambalo lilianza kuathiri mahusiano yangu.

Kwa kweli nilihangaika sana. Nilianza kupoteza kujiamini na nilikuwa nikiepuka mazungumzo yanayohusiana na suala hilo. 

Kila nilipoona hali haibadiliki, nilihisi wasiwasi zaidi. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mpenzi wangu akianza kuhisi kwamba simjali kama zamani.

Ingawa nilijaribu kueleza kwamba nilikuwa napitia changamoto, haikuwa rahisi kuelezea hisia nilizokuwa nazo. Hali ile ilianza kuleta umbali kati yetu na mara kwa mara kulikuwa na mabishano yaliyotokana na kutokuelewana.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kutafuta suluhisho. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kufanikiwa. Nilijituma kila siku kuhakikisha wateja wanapata huduma nzuri na bidhaa bora. 

Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda vizuri, lakini baada ya muda hali ilianza kubadilika. Washindani wapya waliingia sokoni.

Walikuwa na mitaji mikubwa, matangazo mengi, na ofa zilizovutia wateja. Polepole nilianza kuona idadi ya wateja wangu ikipungua. Mauzo yangu yakashuka mwezi baada ya mwezi. 

Kwa kweli nilihuzunika sana. Kulikuwa na siku ambazo biashara yangu ilikaa karibu tupu huku maduka ya washindani wangu yakiwa yamejaa watu.

Kila jioni nilihesabu mauzo na kuona jinsi faida ilivyokuwa ikizidi kupungua. Miezi kadhaa ilipita katika hali hiyo. Watu wengi waliniambia biashara yangu isingeweza kushindana na zile zilizokuwa zimejijengea nguvu sokoni. Baadhi walinishauri nifunge biashara na kutafuta kazi nyingine.

Lakini sikuwa tayari kukata tamaa. Nilijua nilikuwa nimewekeza muda, nguvu, na fedha nyingi katika biashara hiyo. Nilihitaji njia ya kuirudisha kwenye mafanikio....SOMA ZAIDI.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, amevutiwa na mfumo wa Kupanga na Kusimamia miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA). 

Mhe. Kikwete ameipongeza REA kwa kuja na mfumo huo mara baada ya kutembelea banda hilo kwenye ufunguzi wa Maadhimiaho ya Wiki ya Utumishi kwa Umma 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. 

Mfumo huo (*REA DIGITAL PLATFORM*) unaonyesha miradi yote inayotekelezwa na REA na kuweza kuisimamia kidijitali na kuwapa taarifa wadau popote walipo duniani kuhusiana na miradi ya Nishati vijijini.

Akimueleza Mhe. Kikwete, Afisa Upimaji Mwandamizi wa REA, Bw. Hussein Shamdas ameeleza kuwa kupitia mfumo huo mwananchi anaweza kujua mipango ya Wakala kwenye eneo lake na kufuatilia miradi inayotekelezwa na Wakala katika eneo husika.

 


Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwan Kikwete ameipongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi kwa Wananchi pamoja na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za nishati nchini.

Kikwete amesema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Aidha, amesisitiza Wizara pamoja na Taasisi zake kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ili Kila mmoja aifahamu kwa kina kwa manufaa ya kulinda Afya na mazingira.

" Hongerani Sana Nishati kwa kuendelea kuwasha Umeme na kuangaza Maisha ya Wananchi, tunaona Umeme upo wa kutosha" Alisema Kikwete 

Sambamba na hilo amesisitiza kuendelea kutangaza fursa zilizopo katika Sekta ya Nishati nchini kwa wananchi.

Ametembelea Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati ambazo ni TANESCO, REA, TPDC, EWURA, PURA,PBPA na EWURA CCC ambapo alipata fursa ya kujionea huduma zinazotolewa na taasisi hizo pamoja na mafanikio ya miradi mbalimbali inayotekelezwa.