Na Mwandishi Wetu,Kwimba

WATUMISHI wa idara ya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza wamepatiwa mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia sambamba ba kuelezea kwa kina madhara yanayotokana na matumizi ya kuni na mkaa kiafya.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetangaza kuanza kwa kampeni maalum ijulikanayo kama “Samia Ardhi Kliniki” itakayofanyika katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026, kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayoadhimishwa tarehe 8 Machi 2026.Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Lucy Kabyemera, amesema kliniki hiyo itaendeshwa na watumishi wanawake kutoka Ofisi za Ardhi za Mikoa yote nchini kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi.
“Kupitia Samia Ardhi Kliniki tunalenga kuwafikia wanawake wengi zaidi kwa kuwapatia elimu kuhusu haki zao za umiliki wa ardhi, kuwasaidia kitaalamu na kutoa hati miliki kwa waliokamilisha taratibu,” amesema Kabyemera.
Ameongeza kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Samia Suluhu Hassan ya kuwataka watumishi wa umma kuwafuata wananchi na kuwapatia huduma bora kwa kuzingatia utu. “Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,’ na tunawahimiza wanawake wote kujitokeza kutumia fursa hii muhimu,” amesisitiza.
Kwa mujibu wa Kabyemera, serikali inalenga kuongeza idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi kwani kwa sasa ni takribani asilimia 28 tu ya wanawake nchini ndio wanamiliki. “Tunaamini kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi ni kuimarisha familia na Taifa kwa ujumla,” amesema.
 

Na. Joyce Ndunguru, Mara.

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Grumeti Reserve Ltd imekabidhi vifaa mbalimbali yakiwemo Madawati 3,015, Kompyuta 21, Vitanda vya hospital 24, UPS 8 pamoja na Printa 2 vyenye thamani ya takribani shilingi za kitanzania Milioni 362 kwa Wilaya za Serengeti na Bunda zilizopo Mkoani Mara.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano yaliyofanyika Februari 27,2026, Mwakilishi wa Kamishna wa Uhifadhi ambaye pia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Kitengo cha Jamii, Utafiti na Ujirani Mwema, Omary Msangi alisema vifaa hivyo vilivyokabidhiwa ni utekelezaji wa Mkataba wa Uwekezaji Mahiri (SWICA) baina ya TAWA na Kampuni ya Grumeti Reserve Ltd kwa ajili ya shughuli za Uhifadhi katika Hifadhi za Ikorongo na Grumet.

Aidha , Kamishna Msangi aliongeza kuwa miongoni mwa matakwa ya Mkataba huo ni kuongeza mapato na kuhakikisha jamii zinazoishi pembezoni mwa hifadhi hizo zinanufaika na uwepo wa rasilimali Wanyamapori katika maeneo yao.

Sambamba na hilo, Kamishna Msangi, alitoa rai kwa wananchi kuendelea kuunga mkono shughuli za uhifadhi na utalii zinazofanyika sehemu mbalimbali ili kuhakikisha kuwa manufaa yaliyoonekana leo yanaendelea kupatikana.

Naye, Kamanda wa Uhifadhi anayesimamia Kanda ya Ziwa, Mark Chuwa alisema TAWA imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali katika ulinzi wa maeneo ya hifadhi, Aidha, mashirikiano hayo pia yanajikita katika kuhakikisha wananchi wananufaika na rasimali za Taifa.

Kamanda Chuwa aliongeza kuwa vifaa hivi vilivyokabidhiwa vitaenda kupunguza changamoto za madawati zilizokuwepo katika mashule na kuboresha utendaji kazi katika Zahanati zinazopatikana katika Wilaya za Serengeti na Bunda.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Mhe. Angelina Lubela aliwashukuru TAWA pamoja na Kampuni ya Grumeti kwa kuwakabidhi vifaa hivi ambavyo vitaenda kupunguza changamoto katika Sekta ya Elimu na Afya katika Wilaya ya Serengeti.

Pia, Mhe. Lubela aliongeza kuwa madawati haya yataenda kuweka mazingira mazuri kwa wanafunzi na kuwahamasisha wanafunzi kuhudhuria masomo yao hivyo kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mhe. Aswege Kaminyonge aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji ambazo faida za wawekezaji hao zinagusa jamii moja kwa moja.

Kadhalika, Mhe.Kaminyonge aliishukuru TAWA pamoja na Kampuni ya Grumeti kwa vifaa hivyo yakiwemo madawati kwani yataenda kupunguza upungufu wa madawati kwa wanafunzi takribani 4,600 wa Wilaya ya Bunda.

Kwa upande wake, Mwakilishi kutoka Kampuni ya Grumeti Reserve Ltd, Frida Mollel alisema , Grumeti wataendelea kuhakikisha jamii zinazoishi pembezoni mwa Hifadhi ya Ikorongo na Grumet wanafaidika na uwepo wao kama wawekezaji.

Aidha, alisema kuwa vifaa hivi vilivyotolewa kwa wananchi vikawe chachu katika kuendelea kuhamasisha wananchi kutunza maeneo ya hifadhi.

 

Na Munir Shemweta, KITETO

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameahidi kupelewa kwa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Kiteto mkoani Manyara.

Dkt Akwilapo alitoa ahadi hiyo leo tarehe 26 Februari 2026 kufuatia kuwasilishwa kwa malalamiko na mwananchi mmoja aliyemueleza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba aliyeko katika ziara mkoani Manyara kuwa, katika wilaya ya kiteto wananchi wamekuwa wakipata shida ya kushughulikiwa mashauri yao ya ardhi kupitia Baraza la Ardhi kutokana na kukosekana kwa mwenyekiti wa Baraza.

Kwa sasa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Kiteto linahudumiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba kutoka Dodoma jambo lililoelezwa kuwa limechangia mashauri kuchukua muda mrefu.

Dkt Akwilapo amesema, suala la Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba Wilaya katika wilaya ya Kiteto tayari limeshamfikia na analifanyia kazi na muda wowote mwenyeikiti atapatikana ndani ya muda mfupi.

‘’Nimemuagiza katibu mkuu aliyefanyie kazi na muda wowote tutapata mwenyekiti mahsusi kwa ajili ya eneo hili’’. Amesema Dkt Akwilapo

Akigeukia suala la migogoro ya ardhi katika wilaya ya Kiteto, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema, migogoro mingi katika wilaya ya Kiteto imesababishwa na ukosefu wa mipango ya matumizi ya ardhi.

Kwa mujibu wa Dkt Akwilapo, wilaya ya Kiteto ina jumla ya vijiji 63 na kati ya hivyo vijiji 33 ndivyo vilivyofanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi huku vijiji 22 mpango wake ukiwa umeisha muda wake jambo alilolieleza kuwa, sasa jumla ya vijiji 52 vinahitaji kufanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi.

Amesema, Wizara yake inalifanyia kazi suala hilo na katika mpango wa Bajeti ijayo ya 2026/2026 wameomba fedha na itakapofanikiwa Wizara yake itatekeleza mpango huo kwa kushirikiana na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMA). Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza katika mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kiteto mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba akiwa pamoja na viongozi wengine wakati wa ziara yake mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Wa pili kulia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo. Sehemu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara katika ziara ya Waziri Mkuu Wilayani Kiteto mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba akisalimiana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri alipowasili wilayani Kiteto wakati wa ziara yake mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

 



Pongezi hizo zimetolewa katika taarifa ya Kamishna Mkuu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa Volker Turk wakati wakutoa taarifa inayoangazia maeneo yaliyokumbwa na changamoto ya vita na migogoro duniani katika kikao cha 61 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Geneva, Uswisi.

Akizungumza katika kikao hicho,
Kamishna Turk alisema hatua iliyochukuliwa na Tanzania kuanzisha Tume ya kuchunguza kilichojiri Oktoba 29, kama hatua muhimu inayojali haki za binadamu


Tume ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea Oktoba, 2025 ilianza rasmi majukumu yake Desemba 2025, kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.


Wizara ya Afya imewataka wananchi kuendela kuchukua tahadhari na kufuatilia ushauri wa kitaalam ili kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali kama ilivyoelezwa katika taarifa kwa umma  ya   Mganga Mkuu wa Serikali hivi karibuni

 

Hayo yamebainishwa Februari 27, 2026 Jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa alipofanya ziara ya kimakakati katika hospitali ya Rufaa Mkoa Amana kwa lengo la kukagua utolewaji wa huduma za afya pamoja na maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu ya hospitali hiyo

 

Aidha amesema, Serikali bado inaendelea kufuatilia kwa ukaribu juu ya mienendo  ya  magonjwa mbalimbali kama kipindu pindu, Dengue na UVIKO-19 hususani katika kipindi hiki cha mvua  huku akisistiza kwamba hakuna kisa chochote UVIKO, cha mgonjwa aliyelazwa katika hospitali nchini

 

“Napenda kuwahakikishia wananchi na Watanzania wote Serikali yenu ipo makini na inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa maambukizi ya UVIKO-19 nchini na kimataifa, lakini pia tunasisitiza umuhimu wa kila mmoja kuendelea kuchukua tahadhari na kuzingatia ushauri wa kitaalamu unaotolewa na wataalamu wa afya ili kulinda afya binafsi na ya jamii kwa ujumla,” amesema Mhe. Mchengerwa.

 

Mhe. Mchengerwa amewataka Watanzania kujiandikisha na kulipia bima ya afya kwa wote sababu gharama za matibabu zinaweza kuwa kikwazo kwa wananchi wa hali ya chini hasa wanapohitaji kufanyiwa huduma za kibingwa na kibingwa bobezi

 

Waziri Mchengerwa amesema kuwepo kwa bima ya afya kwa wote kuendana sanjari na upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya na hospitali ili kukamilisha dhamira ya serikali katika kurahisisha huduma za afya kwa wananchi 

 

Katika ziara hiyo, Mhe. Mchengerwa ameambatana na Katibu Mkuu Dkt. Seif Shekalaghe pamoja na menejimenti ya Wizara ya Afya, ambapo alikagua hali ya upatikanaji wa huduma, kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi na wagonjwa, na kueleza mikakati madhubuti ya serikali katika kuimarisha ubora na ufanisi wa huduma za afya kwa wananchi.

 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio amesema Tanzania sasa itakuwa na jumla ya vitalu vitatu vinavyozalisha gesi asilia kufuatia uzinduzi wa uchimbaji wa visima vya kuongeza uzalishaji pamoja na bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka Ntorya hadi Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba.

Dkt. Mataragio ameyasema hayo leo, Februari 27, 2026, wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi, mkoani Mtwara katika maeneo ya vitalu vya uchimbaji wa gesi asilia.

Dkt. Mataragio amemshkuru Waziri wa Nishati kwa kuzindua mradi huo wa kimkakati katika maendeleo ya sekta ya mafuta na gesi asilia nchini na kusema hatua hiyo itaongeza uzalishaji wa gesi na kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati nchini.

Akizungumzia umuhimu wa mradi wa Ntorya, amesema kuwa ukikamilika utaongeza upatikanaji wa gesi asilia na kufungua fursa kwa miradi mingine inayohitaji nishati hiyo, ikiwemo miradi ya uzalishaji wa mbolea ambayo kwa sasa inakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa gesi.

‘Ongezeko la uzalishaji wa gesi unatarajiwa kuchochea matumizi yake katika uzalishaji wa umeme, viwanda, taasisi mbalimbali, vyombo vya usafiri pamoja na matumizi ya majumbani, na hivyo kuimarisha utekelezaji wa agenda ya matumizi ya nishati safi nchini’ amesisitiza Dkt. Mataragio.

Mradi wa uchimbaji wa visima vya kuongeza gesi asilia pamoja na ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Ntorya hadi Madimba unasimamiwa kwa karibu na Shirika la Maendeleo ya Petrolu Tanzania (TPDC) kwa kutumia wataalamu wake wa ndani, hali inayoonesha mafanikio ya uwekezaji wa Serikali katika kuandaa wataalamu wa sekta ya mafuta na gesi nchini.











Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, akimkabidhi cheti cha ushiriki wa Mafunzo ya Usimamizi wa Kimkakati wa Elimu Mwalimu Dennis John Otieno, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) na pia Mkuu wa Shule ya Sekondari Ilboru mkoani Arusha.

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amelitaka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kumsimamia kikamilifu Mkandarasi anayetekeleza mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka eneo la ugunduzi la Ntorya hadi Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba ili kuhakikisha unakamilika ifikapo Septemba 2026

Amesema hayo, leo tarehe 27 Februari 2026 mkoani Mtwara mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa bomba la gesi asilia Ntorya–Madimba ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 35 akieleza kuwa mradi huo utachangia kuongeza matumizi ya gesi asilia na kuchochea ukuaji wa uchumi

“Tumeweka ‘taget’ ya mwezi wa tisa kuhakikisha visima hivi vinazalisha gesi na kuunga kwenye bomba kuu la Madimba, ikifika muda huo kusiwe na hadisi nyingine, ili haya yasitokee tunahitaji usimamizi wa hali ya juu kuhakikisha TPDC mnakuwa site muda wote, Watanzania wanataka wanataka kuona maendeleo,” amesisitiza Ndejembi

Aidha, Ndejembi amewataka wataalamu wa TPDC kuhakikisha shughuli zote zinafanyika kwa ubora na kwa kuzingatia muda uliokubaliwa kwenye mkataba huku akibainisha kuwa mradi huo utachochea ukuaji wa sekta ya gesi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme kuvutia uwekezaji na kukuza viwanda vitakavyozalisha ajira kwa Watanzania

Ameihimiza TPDC kuongeza kasi ya utafutaji na uendelezaji wa visima vipya ili kuhakikisha upatikanaji wa gesi ya kutosha hususan ikizingatiwa kuwa miundombinu ya usafirishaji tayari ipo nchini pamoja na kutekeleza kikamilifu miradi ya uwajibikaji kwa jamii katika maeneo ya mradi kwa kushirikiana na wananchi kutatua changamoto kama ujenzi wa vyumba vya madarasa uchimbaji wa visima vya maji na miradi mingine kulingana na mahitaji ya eneo husika

Vilevile, Waziri Ndejembi amesema Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 imelenga kuongeza upatikanaji na matumizi ya gesi asilia hatua itakayowezesha kufikiwa kwa lengo la kuzalisha megawati 8000 za umeme ifikapo mwaka 2030

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt. James Mataragio amesema kitalu cha Ntorya kitaongeza upatikanaji wa gesi asilia huku akibainisha kuwa mahitaji ya gesi hiyo yanaongezeka kila siku na wawekezaji wa viwanda wamekuwa wakiwasilisha maombi ya gesi hiyo

Mradi wa bomba la kusafirisha gesi asilia ghafi kutoka kitalu cha Ntorya ulisainiwa tarehe 3 Julai 2025 kati ya TPDC na mkandarasi wa kampuni za China Petroleum Pipeline Engineering Co. Ltd. na China Petroleum Technology & Development Corporation kwa thamani ya Dola za Marekani Milioni 46.8 na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Septemba 2026.












  


Na Mapuli Kitina Misalaba

Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, tawi la Tanzania (MISA Tanzania), kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imeendesha warsha ya tathmini ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na wahariri, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya mafunzo yaliyofanyika Juni 16, 2025.

Akizungumza katika warsha hiyo leo Februari 27, 2026 jijini Dar Es Salaam, Mwenyekiti wa MISA TAN, Edwin Soko, ameishukuru EWURA kwa kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo katika kuwawezesha waandishi wa habari kuandika kwa weledi kuhusu masuala ya uthibiti wa nishati na maji.

Amesema tangu mafunzo ya awali kufanyika, jumla ya habari 103 zimeandikwa na kurushwa kupitia vyombo mbalimbali vya habari, hatua inayodhihirisha mafanikio ya ushirikiano huo.

Ameongeza kuwa MISA TAN inaishukuru EWURA kwa kuwaamini na kuahidi kuwa waandishi waliopata mafunzo wataendelea kuwa mabalozi wazuri wa taasisi hiyo popote walipo.

Katika wasilisho lake, Mwenyekiti huyo amesisitiza matarajio ya kuona habari zenye weledi, zinazozingatia maadili ya taaluma na zenye kuleta suluhisho kwa jamii huku akiwasisitiza washiriki kuendelea kuandika kwa ufasaha kuhusu majukumu ya EWURA baada ya kuifahamu vyema mamlaka hiyo, pamoja na kufanya kazi kwa karibu na ofisi za kanda za EWURA ili kupata taarifa sahihi.

Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA amesema jukumu la EWURA ni kuelimisha umma kuhusu masuala ya uthibiti wa huduma za nishati na maji, na kwamba kupitia vyombo vya habari wanaamini wakielimisha waandishi wa habari wanakuwa wameuelimisha umma kwa ujumla.

Ameeleza kuwa katika sekta ya nishati, kwa takwimu zilizopo nchini, huduma zinaendelea vizuri na ubora wake umeimarika ambapo amewaomba waandishi kuendelea kuwa mabalozi wazuri kwa kuandika habari za kuelimisha umma kwa kuzingatia maadili na misingi ya taaluma ya uandishi wa habari.

Aidha, amebainisha kuwa EWURA imekuwa ikitoa ushirikiano kwa waandishi wa habari na itaendelea kufanya hivyo, ili kuhakikisha wananchi wanapata elimu sahihi kuhusu haki na wajibu wao katika matumizi ya huduma za nishati na maji.

Kuhusu changamoto zilizopo, amesema baadhi ya watumiaji wa huduma hizo wamekuwa na mazoea yanayochangia malalamiko yasiyo rasmi, akiwataka waandishi kusaidia kuelimisha wananchi kuchukua hatua stahiki kwa kufikisha malalamiko yao katika ofisi za EWURA.

Ametolea mfano changamoto zinazowakabili baadhi ya wamiliki wa magari wakati wa kununua mafuta, pamoja na bili bandikizi za maji au umeme, akisisitiza kuwa malalamiko hayo yakifikishwa katika ofisi za EWURA hushughulikiwa bila gharama yoyote.

Mhandisi Long’idu amesisitiza kuwa EWURA itaendelea kushirikiana na vyombo vya habari katika juhudi za kuwafikishia wananchi elimu juu ya wajibu wao na namna bora ya kunufaika na huduma za nishati na maji.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Wilfred Mwakalosi, amesema bado wananchi wengi hawafahamu haki na wajibu wao katika huduma za nishati na maji, hali inayochangia baadhi yao kushindwa kudai haki zao au kutotimiza wajibu wao ipasavyo.

Amesema uelewa mdogo kwa wananchi unasababisha malalamiko mengi kutowasilishwa katika mamlaka husika kwa wakati, huku wengine wakishindwa kufuata taratibu sahihi za kupata huduma au kuwasilisha changamoto zao.

Ameongeza kuwa wananchi wakifahamu haki zao pamoja na wajibu wao, itasaidia watoa huduma kutekeleza majukumu yao kwa wakati na kwa ufanisi zaidi, sambamba na kuimarisha uwajibikaji katika sekta ya nishati na maji.

Warsha hiyo imehusisha majadiliano ya wazi, maswali na majibu kati ya washiriki na wataalamu wa EWURA, pamoja na kufikiwa kwa maazimio ya pamoja yaliyolenga kuimarisha uandishi wa habari za sekta ya nishati na maji kwa weledi na uwajibikaji. Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi endelevu za kuimarisha ushirikiano kati ya MISA Tanzania na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, zenye kuelimisha na kuchochea uwajibikaji katika matumizi ya huduma za nishati na maji.

Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA 

Mwenyekiti wa MISA TAN, Edwin Soko, akiishukuru EWURA kwa kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo. 

Mwenyekiti wa MISA TAN, Edwin Soko, akiishukuru EWURA kwa kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo.