Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy, akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu kwa wananchi wa Kata ya Kibaya wilaya ya Kiteto, Mkoa wa manyara (hawapo pichani), mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Afisa Afya wa Wilaya ya Kiteto, Kennedy Mlapwa (kulia), akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyekaa kushoto) kwa ajili ya kufungua mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto, (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Emmanuel Haule, akiwasilisha mada ya utokeaji wa sumu kuvu na jinsi ya kudhibiti sumu kuvu nchini kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto, (hawapo pichani), katika mafunzo ya kuthibiti matukio ya sumukuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.

Washiriki wa mafunzo wakifuatilia mada katika mafunzo ya kuthibiti matukio ya sumu kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy, akiwasilisha mada ya namna ya kuepukana na matukio ya sumu mbalimbali katika jamii kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto (hawapo pichani), mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili29, 2026. 
Mshiriki akiuliza swali kwa Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyesimama kushoto), katika mafunzo ya kuthibiti matukio ya sumu-kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Emmanuel Haule, akiwasilisha wasilisho la hali ya matukio ya sumu nchini kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto wakati wa mafunzo ya udhibiti wa matukio ya sumu kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Washiriki wakiuliza maswali kwa Mtumishi wa Mamlaka, Emmanuel Haule (hayupo pichani), kuhusu hali ya matukio ya sumu nchini wakati wa mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyekaa katikati), akiwa pamoja na wananchi washiriki wa mafunzo hayo yakuthibiti matukio ya sumu kuvu nchini yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.

Na Grace Msungu Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira, Mheshimiwa Kwagilwa Reuben Nhamanilo, amesema kuwa kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kunategemea kwa kiwango kikubwa uwekezaji wa kimkakati katika usimamizi endelevu wa mazingira pamoja na uwezeshaji wa wataalamu wazawa.




Na Mwandishi wetu- Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amewataka wataalamu ambao wamepatiwa mafunzo ya kukabiliana na maafa kuyatumia vyema katika  kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa.
Ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya siku nne  ya kujiandaa na kukabiliana na maafa  kwa  Kamati ya wataalamu , Timu ya kukabiliana na maafa na watumishi wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura  (REOCC) Mkoa wa Dodoma.

Brigedia Jenerali Ndagala ameeleza kuwa Awamu ya kwanza ya utekelezaji ilianza katika Mkoa wa Mwanza na Arusha, ambapo hatua za kuanzisha Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu ya kukabiliana na Maafa ilianza kutekelezwa Mikoay a Mwanza na Arusha huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yataendelea katika Mikoa yote Nchini.

Sambamba na hilo amebainisha kuwa mafunzo hayo ni  nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika na uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura.
Pia ameeleza  kuwa Uanzishwaji wa kituo hicho katika Mkoa wa Dodoma ni hatua muhimu  kwani kitawezeshaufuatiliaji  wa matukio kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma na Taifa kwa ujumla ili kuokoa maisha ya watu na mali zao.
Aidha Brigedia Jenerali Ndagala amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Senyamule kwa kukubali mafunzo hayo kutolewa katika timu hizo na kuanzisha Kituo  cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa ambacho kitaunganishwa na Kituo cha Taifa akisema uamuzi huo unaonyesha dhamira thabiti ya uongozi wa Mkoa wa  kuimarisha utayari, mwitikio wa haraka na uratibu madhubuti wakati wa dharura.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) pamoja na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Tabora, imefanya operesheni maalum katika hifadhi ya msitu wa Igombe river iliyopo wilaya ya Uyui na katika hifadhi ya msitu wa Nyahua iliyopo wilaya ya Skonge mkoani Tabora na kufanikiwa kuteketeza ekari 68 za mashamba ya bangi, kukamata gunia 133 za bangi huku watu saba (7) wakikamatwa katika operesheni hiyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mfuko wa uwekezaji nchini, UTT AMIS, umehimiza wananchi kutumia fursa ya kuwekeza katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji wa pamoja ili kuongeza thamani ya fedha zao na kupata faida shindani.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

...

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.

Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.

Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.

Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Wahitimu 12 wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamehitimu mafunzo ya awali ya lugha ya Kijapani, hatua inayolenga kuongeza ujuzi na ushindani wao katika soko la ajira la ndani na kimataifa.

 


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) Alban Kihulla ametuma ujumbe wa shukrani na pongezi kwa wafanyakazi wa Wakala hiyo, siku ya maadhimisho ya siku ya Mei Mosi, 2026.

Katika Andiko hilo, Mtendaji Mkuu ameielezea siku ya Mei Mosi kuwa ni sehemu ya kutambua mchango mkubwa wa wafanyakazi hao katika kujenga uchumi imara kupitia matumizi sahihi ya Vipimo vilivyo katika usahihi unaokubalika kimataifa.

"Ninajivunia kujituma kwenu, uadilifu, na weledi mnaouonesha kila siku katika uhakiki na ukaguzi wa Vipimo pamoja na ukaguzi wa bidhaa zilizofungashwa. 

Kazi yenu ina mchango mkubwa katika kuimarisha biashara yenye haki, kuongeza imani kwa walaji, na kukuza maendeleo ya taifa letu."

Aidha, ameongeza kuwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya teknolojia na ukuaji wa sekta mbalimbali, anawiwa zaidi kuwapongeza kwa kuendelea kujifunza, kuboresha ufanisi, na kuendana na mahitaji mapya ya kazi.

Amewasisitiza kuendelea kushikamana, kudumisha nidhamu ya kazi, na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Kiulla ameweka bayana kuwa Uongozi wa Wakala unatambua na kuthamini mchango wa wafanyakazi, na utaendelea kuboresha mazingira ya kazi ili kuwawezesha  kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.



Wakala wa Vipimo (WMA) imeungana na wafanyakazi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali nchi nzima kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani.

Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kila Mwaka tarehe 1 Mei na kaulimbiu ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mwaka 2026 ni *"Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".

Wakala imeshiriki katika maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Njombe ambapo watumishi wa Mkoa huo wameongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA Bw. Alban Kihulla.

Pamoja na ushiriki wa Kitaifa kadharika, WMA imeshiriki kuadhimisha siku ya Wafanyakazi katika ngazi za Mikoa kupitia ofisi za Mikoa za Kivipimo.

Uongozi wa WMA unaendelea kuwahimiza watumishi wake kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wananchi kwa kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo katika sekta mbalimbali.





Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imesema mkakati wake ni kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia huku pia ikisisitiza umuhimu wa elimu ya mara kwa mara kwa watumiaji ili wawe na uelewa namna bora ya kutumia nishati safi ya kupikia.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir (hayupo pichani) wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

......

Serikali imewataka watumishi wa sekta ya elimu nchini kuimarisha mshikamano, uwajibikaji na ubunifu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu bora inayokidhi mahitaji ya karne ya 21.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir wakati akifunga Mkutano wa Pili wa Baraza la 37 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Mhe.Ameir  amesisitiza kuwa mafanikio ya sekta ya elimu yanategemea kwa kiasi kikubwa ushirikiano kati ya wafanyakazi, menejimenti pamoja na wadau wote wa elimu, akibainisha kuwa mshikamano huo ni chachu ya kuleta mageuzi chanya na endelevu.

Ametoa pongezi kwa uongozi wa Wizara, ukiongozwa na Waziri Adolf Mkenda, kwa kuendelea kusimamia mageuzi ya elimu ikiwemo maboresho ya sera na mitaala inayolenga kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia duniani.

Aidha, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake unaoendelea kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu, hususan katika kukuza ubora wa elimu, ubunifu na tafiti.

" Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha elimu, ikiwemo uzinduzi wa Mkakati wa Kisayansi wa Kuimarisha Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) pamoja na mpango wa kuunganisha taasisi za elimu na waajiri."amesema Mhe.Ameir

Ameeleza kuwa mipango hiyo inalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na hivyo kuongeza ushindani wao kitaifa na kimataifa.

Hata hivyo amewataka wajumbe wa baraza hilo kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, akisisitiza umuhimu wa kuwa na maadili, nidhamu na uwajibikaji kazini.

Amebainisha kuwa baraza la wafanyakazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la majadiliano, ushauri na maamuzi yanayochangia kuboresha utendaji kazi pamoja na ustawi wa watumishi.

Katika mkutano huo, mada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo bajeti ya wizara, usimamizi wa rasilimali watu, maadili ya utumishi wa umma na afya ya akili mahali pa kazi.

Ameir amesema  mada hizo zina mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza tija kwa watumishi, hivyo kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Aidha Ameir ametoa wito kwa watumishi wote kuendelea kudumisha mshikamano, uzalendo na uadilifu, pamoja na kuwa mabalozi wa kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof.Carolyne Nombo, amesema kuwa utekelezaji wa kaulimbiu ya mkutano wa wafanyakazi ya “Ushirikishwaji na Mshikamano wa Wafanyakazi ni Chachu ya Kuimarisha Elimu Inayochochea Ubunifu” ni muhimu katika kufanikisha malengo ya sekta ya elimu nchini.

Prof. Nombo amesisitiza kuwa mshikamano na ushirikiano kazini ni msingi wa kuleta mabadiliko ya kweli katika sekta ya elimu.

Ameeleza kuwa kaulimbiu hiyo inalenga kuwajenga watumishi kuwa na utamaduni wa kufanya kazi kwa pamoja, kwa bidii na kwa uwajibikaji, hali ambayo itachochea mageuzi makubwa yanayohitajika katika kuboresha ubora wa elimu nchini.

“Tunaposhirikiana na kufanya kazi kwa bidii kama timu moja, tunaweka msingi imara wa kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya elimu, yanayoakisi dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2050,” amesema Prof. Nombo.

Ameongeza kuwa juhudi hizo zinapaswa kuendana na utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 (toleo la 2023), pamoja na kuzingatia mabadiliko mbalimbali yaliyofanyika katika mitaala iliyoboreshwa.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa watumishi kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya serikali katika kutekeleza majukumu yao, akibainisha kuwa nidhamu na uwajibikaji ni nguzo muhimu za kufanikisha malengo ya wizara.