📌 Miradi mipya ya kusafirisha umeme kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar
📌 Serikali yawekeza Dola za Marekani milioni 282 kuongeza upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Katika ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, Mhe. Dkt. Mwinyi alipata fursa ya kujionea miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme, teknolojia za matumizi bora ya umeme ikiwemo majiko sanifu yanayotumia umeme kwa ufanisi, huduma ya Luku Janja pamoja na mfumo wa Smart House unaomwezesha mtumiaji kufuatilia matumizi ya umeme kupitia simu ya mkononi.
Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa kujenga njia mpya tatu za kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar kupitia nyaya zitakazopita chini ya bahari.
Ameeleza kuwa njia hizo zitajumuisha Dar es Salaam–Unguja, Tanga–Pemba na Kisiju–Mafia, na kwamba kukamilika kwake kutaongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na uwezo wa kuhudumia ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ukuaji wa viwanda, sekta ya utalii, uwekezaji na shughuli nyingine za kiuchumi visiwani Zanzibar.
Bw. Twange amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 282, ambapo Dola milioni 6 zimetengwa mahsusi kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).
“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea katika sekta ya umeme. Kupitia mradi huu wa Dola za Marekani milioni 282, tunaendelea kuimarisha miundombinu ya umeme, huku sehemu ya fedha hizo ikielekezwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na ZECO,” amesema Bw. Twange.
Aidha, amesema TANESCO imeendelea kuleta ubunifu wa kidijitali kupitia mfumo wa Smart House, unaomwezesha mwananchi kufuatilia matumizi ya umeme wa nyumba yake kupitia simu ya mkononi, hatua inayosaidia matumizi bora na yenye tija ya umeme.
Vilevile, Bw. Twange amesema mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme umefikia mafanikio makubwa, ambapo zaidi ya asilimia 90 ya wananchi waliopata majiko hayo wanaendelea kuyalipia kwa utaratibu wa makato kupitia ununuzi wa umeme wa LUKU, hatua inayorahisisha wananchi kumudu gharama za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Jitihada hizo ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme ya uhakika na kutumia nishati safi katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, ikiwemo katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115, umeendelea kuweka msingi wa upatikanaji wa umeme wa kutosha unaowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amemkabidhi mfanyabiashara mwenye ulemavu, Bi.Esther Mashaka Msengi, mashine ya kusagia viungo ili kuongeza uzalishaji, kupunguza gharama za biashara na kuboresha kipato chake.
Akikabidhi mashine hiyo katika Viwanja vya Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), amesema aliguswa na changamoto za Esther aliyekuwa akitumia muda na fedha nyingi kusafirisha viungo kwenda kusagwa kabla ya kuvifungasha na kuviuza.
Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi zake kuhakikisha anaimarisha biashara yake, huku akiitaka BRELA kukamilisha usajili wa nembo ya bidhaa zake, TBS kumsaidia kupata ithibati ya ubora na SIDO kuendelea kumjengea uwezo.
Aidha, amelishukuru Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania TEMDO kwa kuwezesha upatikanaji wa mashine hiyo na kueleza kuwa hatua hiyo inaunga mkono maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha wajasiriamali kuongeza tija.
Kwa upande wake, Bi. Esther Msengi amesema mashine hiyo itapunguza gharama za uzalishaji na kumwezesha kupanua biashara yake.
Mwakilishi wa Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO), Mhandisi. Elisante Mjema, amesema mashine hiyo inaweza kusaga kilo 10 za viungo kwa saa moja na kuongeza uzalishaji hadi kufikia mauzo ya takribani shilingi milioni 1.5 kwa siku endapo kutakuwa na malighafi za kutosha.

Na OWM–TAMISEMI, Sumbawanga
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amempongeza Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa juhudi zake za kuwaunganisha wadau mbalimbali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, uongozi wa mkoa wa Rukwa na halmashauri zake, hatua iliyowezesha kufanyika kwa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi mkoani Rukwa.
Prof. Shemdoe ametoa pongezi hizo Julai 13, 2026 katika Ukumbi wa Country Hotel mjini Sumbawanga wakati akifungua mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, mafunzo ambayo yameratibiwa na Mbunge huyo kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).
Prof. Shemdoe amesema kuwa, anaamini mafunzo hayo yatafungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa, akiwataka washiriki kutumia elimu watakayopata kuanzisha biashara mpya, kuimarisha biashara walizonazo, kuongeza uzalishaji na kuongeza thamani ya bidhaa na mazao wanayozalisha, na kuongeza kwamba mafunzo hayo yameandaliwa kwa lengo la kuwafikia wananchi wa makundi yote, wakiwemo watu wenye ulemavu.
Aidha, Prof. Shemdoe amezielekeza ofisi za mikoa na halmashauri nchini kutenga nafasi za ofisi kwa ajili ya vituo vya uwezeshaji kiuchumi vitakavyohudumia vijana, wanawake, watu wenye ulemavu na makundi mengine maalum yanayojishughulisha na kilimo, ufugaji, uvuvi, umachinga, bodaboda, ufundi na ujasiriamali, ili kujenga taifa lenye uchumi imara, shindani na jumuishi.
"Ninazielekeza ofisi zote za mikoa na halmashauri nchini kuiga mfano wa mkoa wa Rukwa kwa kutenga ofisi za vituo vya uwezeshaji kiuchumi, vitakavyowawezesha wananchi kupata taarifa, ushauri na kuunganishwa na fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji ili wananchi wajikwamue kiuchumi," amesema Prof. Shemdoe.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhe. Makongoro Nyerere, amemshukuru Prof. Shemdoe kwa kukubali kumwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika ufunguzi wa mafunzo hayo, akisema uwepo wake unaonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha kiuchumi vijana, wanawake, watu wenye ulemavu na makundi mengine maalum.
Kwa upande wake, Mhe. Mzindakaya amesema uwepo wa Prof. Shemdoe akimuwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika ufunguzi wa mafunzo hayo, ni ishara ya namna Serikali inavyothamini jitihada za kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Naye Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bw. Gwakisa Bapala, amesema mafunzo hayo yatawawezesha wananchi kunufaika na huduma za mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji kwa ajili ya kuanzisha miradi mipya, kukuza biashara zilizopo, kuongeza thamani ya mazao na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Rukwa na Taifa kwa ujumla.
Mafunzo hayo yanayofanyika katika halmashauri zote nne za mkoa wa Rukwa kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026, yamelenga kuwafikia wananchi zaidi ya 1,000 na kuwapa maarifa yatakayowawezesha kutumia kikamilifu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji kwa maendeleo yao na ya Taifa, fursa ambazo zinatoka katika mifuko na taasisi 15 ikijumuisha NMB, CRDB, Azania Bank, TADB, AGITF, Self MF, BOT, Machinga Fund, YDF, SIDO, Pass Trust, Pass Leasing, EFTA, TaFF na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa.








Usiku mmoja nilipata ndoto ya ajabu sana. Niliota nimesimama kando ya mto mkubwa uliokuwa karibu na kijiji chetu.
Nilipoamka asubuhi, moyo wangu ulikuwa mzito. Sikuwa na amani kabisa. Saa chache baadaye nilipigiwa simu na kaka yangu aliyekuwa akiishi mjini.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Kila biashara niliyoanzisha ilianguka bila sababu ya kueleweka. Niliwahi kufungua duka la jumla, likafungwa baada ya miezi sita. Nikajaribu biashara ya mazao, nikapata hasara kubwa.
Hata nilipoingia kwenye biashara ya usafirishaji, gari langu liliharibika mara kwa mara hadi nikauza kwa hasara. Kilichonishangaza ni kwamba watu waliokuwa wanaanza biashara baada yangu walikuwa wakifanikiwa, lakini mimi nilikuwa narudi nyuma kila mwaka.
Madeni yaliongezeka, amani ikatoweka nyumbani, na mara kwa mara nilijikuta nikigombana na mke wangu. Miaka saba ilipita katika hali hiyo.
Siku moja, mke wangu alisafiri kwenda kumtembelea mama yake. Alisahau begi lake nyumbani. Nilipokuwa nikitafuta kitabu cha watoto ndani ya begi hilo, niliona bahasha ndogo iliyokuwa imefungwa.
Ndani yake kulikuwa na vitu vya ajabu picha yangu ndogo, vipande vya kitambaa nilivyokuwa nimevaa zamani na karatasi zilizoandikwa maneno nisiyoyafahamu. Nilishtuka sana. Mke wangu aliporudi, nilimuuliza kuhusu vitu hivyo.
Alianza kulia na baada ya muda mrefu alikiri ukweli. Aliniambia kwamba miaka mingi iliyopita, kabla hatujaoana, alienda kwa mganga kwa sababu aliogopa nitamuacha. Alipewa vitu hivyo na kuambiwa avihifadhi ili nibaki karibu naye milele.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.
Mwanzoni nilidhani ni uchovu wa kawaida kwa sababu nilikuwa nafanya kazi ya useremala. Lakini kadri miezi ilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.
Nilitumia pesa nyingi kutafuta matibabu. Wakati mwingine nililala chini kwa sababu sikuweza kupanda kitandani kutokana na maumivu.
Mke wangu ndiye aliyekuwa akinisaidia kwa karibu kila kitu. Kuna siku nilishindwa hata kumbeba mwanangu mdogo kwa sababu mgongo wangu ulikuwa unauma sana. Nilijikuta nikipoteza matumaini na kuanza kuamini kwamba ningekaa na maumivu hayo maisha yangu yote.
Siku moja nilikutana na rafiki yangu wa zamani ambaye nilikuwa sijamuona kwa miaka kadhaa. Alinishangaa kuniona nikitembea kwa shida.Endelea Kusoma Kwa Kubofya Hapa.
Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.
Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.
“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
.jpeg)





























.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


