Na Anangisye Mwateba, Zanzibar
MRADI wa Mifumo ya Chakula, Matumizi ya Ardhi na Urejesho wa Mandhari ya Misitu nchini Tanzania (FOLUR), unatarajia kutoa mafunzo maalum kwa viongozi wa serikali za vijiji na shehia mbalimbali visiwani Zanzibar. Hatua hiyo inalenga kujenga uwezo wa kiutendaji na kuhakikisha jamii inatekeleza shughuli za mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.
Akifungua mafunzo hayo kwa maafisa ugani wa kilimo na misitu upande wa Zanzibar, Mratibu wa mradi huo, Bi. Miza Suleiman Khamis, alisema dhumuni kubwa ni kuwawezesha watendaji hao kubaini, kuepuka au kupunguza athari hasi zinazoweza kujitokeza kabla hazijaletea madhara wanajamii na mazingira yao.
Kwa upande wake, Msimamizi wa Kitengo cha Jinsia, Usalama wa Mazingira na Jamii wa mradi huo, Bw. Revocatus Kadoshi, alibainisha kuwa viongozi wa shehia na maafisa ugani watafundishwa miongozo minne mikuu.
Miongoni mwa miongozo hiyo ni Mpango wa Usimamizi wa Mazingira na Jamii (ESMP), unaohusu udhibiti wa matumizi ya rasilimali na kuzuia uhamishaji wa watu usio wa hiari.
Bw. Kadoshi alifafanua kuwa mwongozo huo unalenga kudhibiti na kupunguza athari za kimazingira na kijamii wakati wa utekelezaji wa mradi. Aliongeza kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na matakwa ya Mwongozo wa Sera na Taratibu Jumuishi za Ulinzi wa Kijamii za Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF).
"Viongozi hawa pia watafundishwa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Visumbufu. Huu unalenga kulinda afya na usalama wa jamii kwa kudhibiti athari zitokanazo na matumizi ya viuatilifu na mbolea," alisema Bw. Kadoshi.
Aidha, mafunzo hayo yatahusisha mbinu za usimamizi wa mazingira zinazohakikisha ustawi wa jamii, usalama mahali pa kazi, pamoja na usafi wa mazingira wakati wote wa utekelezaji wa shughuli za mradi huo.
Vilevile Aliongeza kuwa, ili kuhakikisha usalama wa jamii, mradi umeweka utaratibu maalumu wa kupokea nakufanyia kazi malalamiko kutoka kwa mwanajamii au kikundi cha kijamii kuhusiana na shughuli zinazotekelezwa na mradi. Hii inalwnga kuhakikisha jamii inashiriki vema kwenye shighuli za mradi na wanakuwa na nafasi ya kutoa dukuduku au lalamiko wakati wowote.
![]() |
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo, ameielekeza Bodi mpya ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kusimamia kwa ukaribu ukusanyaji wa mapato na madeni ya Shirika, akisisitiza kuwa hakuna mdaiwa anayepaswa kupewa upendeleo katika kulipa fedha zinazodaiwa na taasisi hiyo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi ya NHC uliofanyika jijini Arusha tarehe 3 Juni 2026 , Dk. Akwilapo alisema mafanikio ambayo Shirika limeyafikia katika kujiendesha kibiashara na kuendelea kuwa imara kifedha yanapaswa kulindwa kwa kuimarisha nidhamu ya mapato na usimamizi wa rasilimali zake.
“Msitishike linapokuja suala la kudai malipo yenu halali. Hakuna mdaiwa anayepaswa kuogopwa. Wote wapeni ankara zao za madeni kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo,” alisema Dk. Akwilapo.
Waziri huyo wa Ardhi alisema NHC ni miongoni mwa mashirika ya umma yaliyoendelea kuonesha uimara katika biashara zake, tofauti na baadhi ya taasisi ambazo zilishindwa kujiendesha kwa ufanisi na hatimaye kupoteza nafasi yake katika uchumi wa taifa.
Alieleza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ina matarajio makubwa kwa NHC katika kuendeleza agenda ya makazi bora, miji endelevu na uwekezaji wa kimkakati unaochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Dk. Akwilapo pia aliitaka Bodi mpya kusimamia kwa karibu maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa Shirika utakaokwenda sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo pamoja na malengo ya kimataifa ya maendeleo endelevu yanayohusiana na makazi na maendeleo ya miji.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, alisema Shirika limeendelea kuimarisha utendaji wake kupitia uwekezaji katika miradi ya makazi, biashara na matumizi ya mifumo ya kidijitali inayorahisisha utoaji wa huduma na usimamizi wa shughuli zake.
Alisema NHC imeendelea kuimarisha vyanzo vya mapato kupitia upangishaji wa majengo, mauzo ya nyumba na viwanja pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo tofauti nchini.
Bw. Hamad alibainisha kuwa Menejimenti ya Shirika itaendelea kushirikiana kwa karibu na Bodi mpya ili kuhakikisha maelekezo ya Serikali yanatekelezwa kwa ufanisi na NHC inaendelea kuwa taasisi ya mfano katika sekta ya makazi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC, Dk. Sophia Kongela, alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini Bodi hiyo na kuwapa wajumbe dhamana ya kuiongoza taasisi hiyo katika kipindi kingine cha utekelezaji wa majukumu yake.
Dk. Kongela alisema Bodi imepokea kwa uzito maelekezo yaliyotolewa na Waziri na iko tayari kuyafanyia kazi kwa kushirikiana na Menejimenti ya Shirika.
Alisema moja ya vipaumbele vya Bodi ni kuimarisha usimamizi wa mali za Shirika, kuongeza tija ya uwekezaji, kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kusimamia miradi ya makazi nafuu na kuhakikisha NHC inaendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya makazi nchini.
“Tunatoa hakikisho la ushirikiano wa karibu na Serikali pamoja na Menejimenti ya Shirika ili kuhakikisha NHC inafikia malengo yake na kuendelea kuwa chachu ya maendeleo ya sekta ya makazi Tanzania,” alisema Dk. Kongela.
Uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi ya NHC umeashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi unaotarajiwa kuimarisha zaidi ukuaji wa Shirika, kuongeza uwekezaji na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya makazi bora kwa manufaa ya Watanzania.
Bodi hiyo mpya inaongozwa na Mwenyekiti, Dk. Sophia Kongela na wajumbe wake wakiwa ni Eliud Sanga, Profesa Wilbard Kombe, Ali Hussein Laay, Doroth Mwanyika, Ayoub Omari Kasui, Vupe Ligate na Elias Kisamo
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo, ametembelea banda la Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika Maonesho ya Kimataifa ya Mbeya City Expo 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Uhindini, jijini Mbeya, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo katika kulinda maslahi ya walaji na kuimarisha ushindani wa biashara nchini.
Katika maonesho hayo, FCC imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusu haki za mlaji, namna ya kutambua na kuepuka bidhaa bandia pamoja na umuhimu wa ushindani wa haki katika shughuli za biashara.
Elimu hiyo imevutia mamia ya wananchi waliojitokeza kutembelea banda hilo na kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu biashara, ushindani na ulinzi wa walaji.
Akizungumza wakati akifunga Maonesho hayo yaliyodumu kwa siku tisa Mei 30, 2026 jijini Mbeya, Naibu Waziri Londo alisisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya bidhaa bandia, akieleza kuwa bidhaa hizo zinaathiri afya za watumiaji, kudhoofisha biashara halali na kupunguza mapato ya Serikali.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kanda wa FCC - Nyanda za Juu Kusini Bw. Dickson Mbanga, amesema taasisi hiyo imejipanga kuendelea kuimarisha kampeni za utoaji elimu kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kutambua bidhaa halisi na kuepuka kununua au kutumia bidhaa zisizo na viwango vinavyotakiwa.
Mbanga alisema Maonesho ya Mbeya City Expo yamekuwa jukwaa muhimu la kuifikia jamii kwa karibu na kutoa elimu inayolenga kuongeza uelewa kuhusu sheria za ushindani na hatua zinazochukuliwa dhidi ya wafanyabiashara wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa bandia.
“Tunatumia maonesho haya kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwaelimisha kuhusu hatari za bidhaa bandia na kumlinda mlaji. Lengo letu ni kuhakikisha watumiaji wanakuwa na taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi bora wanaponunua bidhaa mbalimbali sokoni,” alisema Mbanga.
Aliongeza kuwa FCC itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa biashara na vyombo vya usalama katika kudhibiti bidhaa bandia zinazoingia sokoni, huku ikiendelea kuhamasisha wananchi kutoa taarifa wanapobaini uwepo wa bidhaa zinazotiliwa shaka.
Maonesho ya Mbeya City Expo 2026 yamewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za uchumi, biashara na uwekezaji, huku yakitoa fursa kwa taasisi za umma na binafsi kuonesha huduma, bidhaa na mafanikio yao kwa wananchi. Kupitia ushiriki wake, FCC imeendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya kulinda walaji na kujenga mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki kwa


Kulikuwa na matatizo ya kifamilia, presha za kifedha, na mambo mengine mengi yaliyokuwa yakinifanya nifikirie kupita kiasi kila siku. Mwanzoni nilijaribu kuvumilia.
Nilijiambia kwamba hali ile ingepita yenyewe. Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kugundua kwamba sikuwa yule mtu niliyemzoea zamani. Kwa kweli nilibadilika. Nilianza kupoteza hamu ya kufanya mambo niliyokuwa napenda.
Mara nyingi nilikuwa nataka kukaa peke yangu. Furaha yangu ilipungua, na hata kuzungumza na watu wa karibu kulianza kuwa jambo gumu. Kilichoniumiza zaidi ni kupoteza kujiamini. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningepokea oda kutoka sehemu ambazo sijawahi hata kufika. Mwanzoni biashara yangu ilikuwa ndogo sana.
Nilikuwa na wateja wachache kutoka eneo nililoishi, na mauzo yalitosha tu kuendesha shughuli za kila siku. Ingawa nilikuwa na ndoto kubwa, ukweli ni kwamba biashara ilikuwa inakua polepole kuliko nilivyotarajia.
Kwa kweli kulikuwa na wakati nilikata tamaa. Nilikuwa nikijitahidi kutangaza bidhaa zangu, kuboresha huduma, na kuwahudumia wateja vizuri, lakini matokeo hayakuwa makubwa. Wakati mwingine nilijiuliza kama biashara yangu ingeweza kufika kiwango nilichokuwa nikiota.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara nyingine zikikua kwa kasi huku yangu ikibaki pale pale. SOMA ZAIDI.
Ndiyo maana niliamua kukiuza. Mwanzoni niliamini isingechukua muda mrefu kupata mnunuzi. Eneo lilikuwa zuri, nyaraka zilikuwa sawa, na bei niliyoweka ilikuwa ya kawaida kulingana na soko.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Watu wengi walikuwa wanapiga simu kuuliza maswali. Wengine walifika hata kukiona. Kila nilipofikiri nimepata mnunuzi, mazungumzo yalivunjika dakika za mwisho.
Kwa kweli nilichoka. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa nahitaji fedha hizo kwa jambo muhimu sana. Kadri miezi ilivyopita, nilianza kuona kama kiwanja kile kingebaki mikononi mwangu milele.
Marafiki wengine walinishauri nipunguze bei sana. Lakini kufanya hivyo kungeleta hasara kubwa kwangu. Nilijikuta nikiwa kwenye hali ya kuchanganyikiwa, sijui nichukue hatua gani. SOMA ZAIDI.
Tulizungumza kila siku, tulicheka pamoja, na nilikuwa nikiamini kwamba hakuna jambo ambalo lingeweza kututenganisha. Lakini kadri miaka ilivyopita, mambo yalianza kubadilika.
Migogoro ya kifamilia ilianza kujitokeza. Mwanzoni ilikuwa ni kutokuelewana kwa kawaida, lakini polepole ikageuka mabishano makubwa yaliyoacha majeraha ya kihisia kwa pande zote mbili.
Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona siku zikigeuka wiki na wiki zikigeuka miezi bila kuzungumza naye. Kila nilipoona wazazi wengine wakifurahia ukaribu wa watoto wao, moyo wangu ulijaa huzuni.SOMA ZAIDI.
Maumivu yalikuwa yanarudi mara kwa mara, hasa nilipokaa muda mrefu bila kula au nilipokula baadhi ya vyakula. Kwa kweli hali ile ilianza kunichosha.
Wakati mwingine nilihisi moto tumboni, maumivu makali, na kutokuwa na raha baada ya kula. Nilianza kuogopa baadhi ya vyakula kwa sababu nilihisi vinaweza kuongeza maumivu.
Kilichoniumiza zaidi ni jinsi hali ile ilivyoathiri maisha yangu ya kila siku. Kulikuwa na siku nilishindwa kufurahia chakula nilichokipenda. Wakati mwingine nilikosa usingizi kwa sababu ya maumivu na usumbufu uliokuwa ukijirudia mara kwa mara.
Nilianza kutafuta msaada. Nilipata ushauri wa kitabibu na nikajifunza umuhimu wa kufanyiwa uchunguzi ili kubaini chanzo halisi cha tatizo.
Lakini kipindi kile kilikuwa kigumu kwangu kihisia. SOMA ZAIDI.
KATIBU Mkuu wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Doyo Hassan Doyo, amewataka baadhi ya wanasiasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuonyesha nia ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2030 kuelekeza nguvu zao katika kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi badala ya kuanza harakati za kisiasa mapema.
Akizungumza jijini Tanga mara baada ya kuhitimisha ziara ya kichama mkoani humo, Doyo alisema taifa kwa sasa linahitaji mjadala unaolenga maendeleo, ustawi wa wananchi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kuliko mijadala ya urais ambayo muda wake bado haujafika.
Alisema kuwa ingawa Katiba na sheria za nchi zinatoa haki kwa kila mwananchi mwenye sifa kugombea nafasi yoyote ya uongozi, ikiwemo urais, si jambo la busara kwa viongozi kuanza kujinadi kisiasa wakati wananchi bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za maendeleo.

“Ni haki yao kikatiba na kisheria kugombea nafasi yoyote ya uongozi. Hata hivyo, kwa mtazamo wetu, si jambo lenye afya kwa taifa kuanza mijadala ya urais miezi michache tu baada ya uchaguzi mkuu kumalizika,” alisema Doyo.
Doyo alidai kuwa katika siku za hivi karibuni baadhi ya wabunge wa CCM wamekuwa wakitoa kauli ndani ya Bunge na kwenye mikutano ya hadhara ambazo, kwa tafsiri yake, zinaashiria kuanza kwa harakati za kuwania urais wa mwaka 2030.
Alisema viongozi waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wanapaswa kutumia nafasi zao kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuibua hoja zenye tija na kuishauri serikali katika masuala yatakayoboresha maisha ya Watanzania.

“Wananchi waliwachagua wabunge wao kwa matarajio ya kuona changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi. Tungetarajia kuona nguvu nyingi zikielekezwa katika kujadili maendeleo, uchumi, huduma za jamii na ustawi wa wananchi kuliko kujenga mazingira ya kampeni za uchaguzi ambao bado uko mbali,” alisisitiza.
Kwa mujibu wa Doyo, kuanza kwa siasa za urais mapema kunaweza kuathiri umakini wa viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao na kupunguza kasi ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.
Aidha, aligusia kauli mbalimbali zilizowahi kutolewa na baadhi ya viongozi wa serikali kuhusu watu wanaotamani nafasi ya urais mapema, akisema hali hiyo inaonyesha dalili za kuanza kujitokeza kwa makundi ya kisiasa ndani ya chama tawala kabla ya wakati wake.
Pamoja na hayo, Doyo alisisitiza kuwa viongozi wa vyama vyote vya siasa wanapaswa kuweka mbele maslahi ya taifa kwa kushirikiana kutafuta suluhisho la changamoto zinazowagusa wananchi katika maisha yao ya kila siku.
Atoa Wito wa Kumuunga Mkono Rais Samia
Katika hatua nyingine, Doyo aliwataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi zake za kusimamia maendeleo ya nchi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
“Sasa ni wakati wa kushughulikia changamoto za wananchi, kuimarisha huduma za kijamii na kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya taifa. Wakati wa siasa za urais ukifika, kila mwenye sifa na nia atapata nafasi ya kujitokeza,” alisema.
Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akipata maelezo mbalimbali wakati akitembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.


Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukagua banda la Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.


aibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akiangalia jiko la kunyomea nyama linalotumia nishati ya gesi badala ya mkaa alipotembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama akiangalia gari linalotumia mfumo wa gesi asilia kupunguza matumizi ya mafuta yanasababisha uzalishaji wa gesijoto alipotembelea banda la Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) wakati wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Switbert Mkama (wa tatu kushoto) akipata maelezo kuhusu uzalishaji wa miche alipotembelea banda la Wizara ya Kilimo kwenye Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais inaratibu maonesho hayo kuelekea Siku ya Mazingira Duniani Juni 05, 2026. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Baraka Luvanda.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania - TEMESA, Bw. Kheri Mahimbali, leo tarehe 02 Juni 2026 amekutana na viongozi wa kampuni ya TOYOTA Tanzania katika ofisi zao eneo la Posta, jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili kuhusu jitihada za Serikali katika kuendelea kuboresha huduma za matengenezo ya magari hapa Nchini.

Akizungumza katika kikao hicho, Bw. Mahimbali amesema TEMESA imejipanga kuhakikisha huduma za ufundi na matengenezo ya magari ya Serikali zinatolewa kwa viwango vya juu kwa kutumia teknolojia za kisasa na za viwango vya kimataifa.

“TEMESA inaona fursa kubwa katika kuimarisha ushirikiano na TOYOTA kupitia miradi ya pamoja itakayowezesha taasisi hizi mbili kubadilishana utaalamu kwa mafundi na kuongeza ufanisi wa huduma zinazotolewa kwa wadau wetu,” amesema Mtendaji Mkuu.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa TOYOTA Tanzania, Bw. Jatin Pandya amehakikisha utayari wa kampuni hiyo kuendelea kushirikiana na TEMESA katika mafunzo ya kitaalamu kwa mafundi, ushauri wa kiufundi, matumizi ya teknolojia mpya na kuimarisha mifumo ya usalama wa magari.

“Sisi TOYOTA tunatanguliza usalama wa watumiaji wa magari na ubora wa huduma. Tunaamini ushirikiano huu utachangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha huduma za matengenezo ya magari nchini na kujenga uwezo wa wataalamu wa ndani,” amesisitiza Pandya.
Aidha, mara baada ya kikao hicho, Mtendajji mkuu pia alipata fursa ya kufanya ziara fupi katika karakana za TOYOTA ili kujionea teknolojia mpya zinazotumika katika matengenezo ya magari.
Miongoni mwa mambo waliyojadili katika kikao hicho ni pamoja na uwezekano wa kuanzisha ushirikiano kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi - PPP. Hatua inayotarajiwa kuimarisha uwezo wa karakana na kuongeza ufanisi wa huduma katika sekta ya matengenezo ya magari.
Kikao hicho kimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano kati ya TEMESA na TOYOTA, huku kikitarajiwa kuwa chachu ya mageuzi makubwa katika sekta ya ufundi wa magari nchini.
Watumiaji wa petroli wamepata afueni mwezi Juni 2026 baada ya bei ya mafuta hayo kushuka ikilinganishwa na mwezi uliopita. Kwa Dar es Salaam, petroli sasa itauzwa kwa bei kikomo ya shilingi 4,086 kwa lita, hatua inayotarajiwa kupunguza gharama kwa watumiaji wa kawaida na baadhi ya shughuli za usafiri.
Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo.
Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu kama usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii.
Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli na Irani. Mgogoro huo umeathiri uzalishaji, uhifadhi na usafirishaji wa mafuta duniani, huku kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz kukiongeza gharama za usafirishaji na bima za meli za mafuta.









