Tanzania na Oman zimeendelea kuonyesha dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira ili kuongeza ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kukuza uchumi wa mataifa yote mawili.
Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi wa Oman, Dkt. Mahad bin Said bin Ali Baawain walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.
Aidha, katika kikao hicho Waziri Sangu alielezea umuhimu wa kukamilishwa na kutiwa saini kwa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira (MoU) kati ya nchi hizo mbili, ili kuweka mfumo rasmi na endelevu wa usimamizi wa masuala ya ajira, ulinzi wa haki za wafanyakazi na utatuzi wa changamoto za kiutendaji zinazojitokeza.
Vilevile, Waziri Sangu ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa fursa za ajira kwa Watanzania katika sekta mbalimbali. Pia, amesema idadi ya Watanzania wanaofanya kazi nchini Oman imeendelea kuongezeka , jambo linaloonesha kuimarika kwa mahusiano ya ajira kati ya mataifa hayo mawili.
Kwa upande mwingine, nchi hizo zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kwa kuendelea kupanua wigo wa ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kijamii kati ya mataifa yetu mawili.
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026 Jiji la Dodoma.
.....
Waziri Wa Maji Mhe. Jumaa Aweso amewataka wakurugenzi wa bodi za maji za mabonde nchini kuonyesha umuhimu wa taasisi hizo kwa wananchi kwa vitendo kwa kutoa huduma sahihi.
Waziri Aweso ametoa maelekezo hayo katika kikao cha Bodi za maji za mabonde nchini katika ukumbi wa Jiji la Dodoma.
Aweso ambaye ndiye mgeni rasmi katika kikao hicho amewataka viongozi wa mabonde hayo kutambulika kwa utoaji wa huduma na si kutambulika kwa sifa mbaya kwa wananchi na serikali ikiwemo utozaji wa Kodi zisizi halali.
Aidha Serikali bado inaendelea na mpango mkakati iliyojiwekea katika kujenga mabwawa ya kimkakati kuendelea kupanda miti rafiki wa maji kwa mazingira Ili kuboresha vyanzo vya maji na kutoa huduma ya uhakika kwa wananchi.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewataka wakurugenzi na wenyeviti wa Bodi za maji za mabonde nchini kuendelea kutunza vyanzo vya maji Ili kuwa na uhakika wa huduma ya Maji kwa mwananchi.
Ameeleza kuwa vyanzo vya maji nchini ni muhimu katika kikao mabonde yanakuwa na maji ya kutosha kutoa huduma kwa wananchi.
Kadhalika Ili kuwe na uhakika wa utunzwaji wa vyanzo vya maji, amezitaka Bodi hizo kushirikiana na jamii na wadau wa mazingira ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI pamoja na taasisi zinazojihusisha na mazingira, Ili kuweka mipango mikakati ya Pamoja katika utunzwaji wa vyanzo vya maji.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026 Jiji la Dodoma.
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026 Jiji la Dodoma.
Serikali imesema haina haja ya kuweka sharti la kisheria linalowalazimisha watoto kuwahudumia wazazi wao wasiojiweza, ikieleza kuwa suala hilo tayari linashughulikiwa kupitia misingi ya kifamilia na kijamii.
Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa kinondoni Mhe. Tarimba Gulam Abbas lililohoji "Je Serikali haioni haja ya kuweka sharti la kisheria la watoto wakubwa kutunza wazazi wao wasiojiweza"?
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inatambua umuhimu wa familia na jamii katika kuchukua jukumu la kulea na kuwahudumia wazee, akisisitiza kuwa huo ni msingi wa mila na desturi za Watanzania.
Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuimarisha huduma na matunzo kwa wazee kupitia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003, Toleo la mwaka 2024, ambayo inasisitiza wajibu wa familia na jamii katika kuwahudumia wazee wao.
“Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa familia na jamii katika kuchukua jukumu la kulea na kutunza wazee, kwani huu ndio msingi wa mila na desturi za Kitanzania na nguzo muhimu katika kujenga mshikamano wa kijamii. Katika kuimarisha huduma na matunzo kwa wazee, Serikali imefanikiwa kufanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003 na kuandaa toleo la mwaka 2024, ambalo linaeleza bayana wajibu wa familia na jamii katika kusimamia matunzo ya wazazi na wazee kwa ujumla, Sera hiyo pia imeweka msisitizo wa kuimarisha mifumo ya kisheria utakaolinda na kuendeleza ustawi wa wazee pamoja na watoto wanaowatunza. Kwa sasa Serikali ipo katika hatua ya kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kutoa maoni juu ya masuala muhimu ya kuzingatiwa katika sheria hiyo.”amesema Mhe. Mahundi
Hata hivyo, amebainisha kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha maadili ya uwajibikaji wa kifamilia na kuimarisha mifumo ya kijamii inayosaidia ustawi wa wazee nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa onyo kwa Watumishi wa Umma dhidi ya matumizi ya baruapepe binafsi katika mawasiliano ya shughuli za Serikali.
Amesema kuwa, watumishi wote wa Umma wanapaswa kutumia baruapepe rasmi za Serikali ili kulinda usalama wa taarifa Serikalini, kuongeza uwajibikaji, kuimarisha mifumo rasmi ya mawasiliano ya Serikali sambamba na kuzuia kuvuja kwa taarifa za Serikali.
Akizungumza mapema hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Pili ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Mhe. Kikwete amesema, matumizi ya barua pepe zisizo za Serikali yamekuwa chanzo cha hatari ya uvujaji na upotevu wa taarifa nyeti za Serikali.
Alibainisha kuwa, Serikali imewekeza katika miundombinu ya TEHAMA inayokidhi viwango vya usalama na inapaswa kutumiwa ipasavyo katika mawasiliano ya shughuli zote za Serikali, ili kudhibiti na kulinda usalama wa taarifa muhimu za nchi.
“Kuanzia sasa, serikali itakuwa na jicho la karibu sana kuangalia namna watumishi wa Umma wanavyopeana taarifa za Serikali kupitia baruapepe rasmi za Serikali na si vinginevyo, nitoe wito kwa viongozi na watumishi wote wa umma kutumia anuani za baruapepe rasmi kwa ajili ya mawasiliano ya shughuli zote za Serikali, alisisitiza Waziri Kikwete.
Alibainisha kuwa, barua pepe za Serikali zinatoa mazingira salama ya kuhifadhi kumbukumbu, kudhibiti hatari ya kuvuja kwa taarifa za serikali, usalama na ulinzi wa taarifa hizo kwa mujibu wa sheria na miongozo mbalimbali inayohusu usalama na utunzaji wa taarifa za Serikali, sambamba na uwajibikaji kwa watumishi wa umma katika kuzingatia misingi ya utunzaji wa taarifa za Serikali.
“Matumizi ya baruapepe zisizo rasmi yamesababisha baadhi ya nyaraka za Serikali kupotea na wakati mwingine kuhatarisha usalama na usiri wa taarifa hizo ndani ya serikali, tukiwa kama watumishi wa umma sote tunawajibika kulinda usalama wa taarifa za Serikali kwa kutumia baruapepe rasmi za Serikali”, alisema Mhe.Kikwete.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Eng. Benedict Ndomba, alisema kuwa e-GA itaendelea kutoa ushirikiano kwa taasisi za umma ili kuzijengea uwezo katika matumizi ya mfumo wa Buruapepe Serikalini (GMS).
Alisema kuwa, takriban zaidi ya miaka 10 sasa, tangu kuanza kutumika kwa mfumo wa GMS na kuleta matokeo chanya ikiwemo kurahisisha mawasiliano ndani na nje ya taasisi pamoja na kuwezesha utekelezaji wa maamuzi kwa wakati.
“e-GA tunatoa msaada wa kiufundi kwa saa 24 kwa watumiaji wa mifumo mbalimbali ukiwemo GMS na tutaendelea kufanya hivyo, ili kuhakikisha mawasiliano ya Serikali yanakuwa imara muda wote kupitia mfumo huu wa GMS”, alisema Ndomba.


Na Oscar Assenga,TANGA
MSTAHIKI Meya wa Jiji la Tanga Seleboss Mustapha amewataka vijana wataopata fursa ya ajira nje ya nchi katika Falme za Kiarabu kufanya kazi kwa uadilifu na kuitangaza vizuri sifa na fursa ya nchi jambo ambalo litafungua milango kwa wengine kuendelea kuaminiwa.
Seleboss aliyasema hayo wakati akizungumza na vijana zaidi ya 200 waliojitokeza kufanyiwa usaili kwa ajli ya kwenda nchi za falme za Kiarabu kwa shughuli za udereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda.
Alisema kufanya kazi kwa uaminifu sambamba na kuyaishi maadili ya kitanzania katika nchi za kigeni itasaidia kuleta taswra njema ya kutangaza nchi kwa mazuri badala ya kuwa kinyume chake.
Aidha alisema watakaofanikiwa kupita kwenye mchujo wakawe mabalozi wazuri kwa kufanya kazi lea ajil ya maendeleo yao ikiwemo kutokusahau kuwekeza nyumbani ikiwemo wawwe waaminifu
Meya huyo aliwataka kuhakikisha wanazingatia sheria na tararubu na miongozo ya nchi wanazokwenda ili waweze kufanya shughuli vizuri lakini kwa kujenga imani kwa wengine kuweza kuvutika na vijana kutoka nchni.

Awali akizungumza Ofisa Kazi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Mahusiano Peter Ugata alisema kwamba Serikali imekuwa ikiendelea kuratibu fursa za ajira nje ya nchi kwa kuhakiisha wanawasimamia vijana wao kupata ajira zao.
Alisema kuwa hiyo ni dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana na hivyo ni muhimu vijana kuchangamkia fursa hizo zinapojitokeza.
Alisema miongoni mwa majukumu yao ni kuhakikisha wanapata vijana wenye sifa na vigezo ambao wataweza kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu za nchi husika.
Naye kwa upande wake mmoja wa vijana wanaoshiriki kwenye usaili huo ,Juma Haki waliishukuru Serikali kwa fursa hiyo kuweza kufika hadi ngazi ya mikoa na hivyo kuweza kushiriki nao.
Hata hivyo alisema kwamba wanaishukuru Serikali kwa fursa hiyo ambayo itasaidia kumaliza changamoto za ajira lakini itawapa mwamko wa kujipanga kwa ajili ya kuwa na sifa za kufanya kazi nje ya nchi .
Mwisho.
Siku nyingi nilijisikia mgonjwa wa moyo, nikihisi kuanguka kimwili na kihisia, huku nikikosa msaada wa kweli wa kisheria na kiroho. Kesi ya malezi ilikua changamoto isiyo na kifani.
Kila mtu alidhani sina nafasi ya kushinda, kwa sababu hali ya kifedha na hofu yangu ilionekana kuendelea kudhoofisha hoja zangu.
Nilijua kuwa lazima nifanye kitu tofauti, kitu cha busara na cha hekima, la sivyo watoto wangu wangepotea mikononi mwa hofu na udhaifu wangu.Soma Zaidi.
Nilijisalimisha kwa kuamini maneno yake, lakini bila kujua, nilidanganywa na alichukua KSh 200,000 zangu kwa udanganyifu. Baada ya tukio hilo, nilihisi aibu kubwa, huzuni, na hasira isiyo na kipimo.
Nilijikuta nikijua kwamba fedha hizi siyo tu zilipotea bali pia hakika ya usalama wa wengine ilikuwa hatarini ikiwa mtu kama huyu angeendelea. Nilijua lazima nifanye kitu, la sivyo wengine wangeendelea kujeruhiwa na wajasusi hawa wa uongo.Soma Zaidi.
Kila siku ilikuwa changamoto mpya, na hisia za huzuni, aibu, na kukata tamaa zilianza kunikumba. Hali hii ilileta mabadiliko makubwa nyumbani.
Mke wangu alianza kunitenga kidogo kidogo, na siku moja nikagundua kuwa amepata mwanamume mwingine. Hatimaye, alichukua hatua ya kuoa mzee tajiri, huku akibeba watoto wetu naye.
Hii ilinifanya nijisikie kupoteza heshima, familia, na kila kitu niliyekipenda. Nilihisi maisha yangu yamevunjika na kila mtu karibu nami alidhani sitawahi kurejea.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mke-wangu-alinitenga-na-watoto-wetu-na-akaoa-mzee-tajiri-baada-ya-kupoteza-kazi-na-kupata-ugumu-wa-kimaisha/
Lakini baada ya kujiingiza kwenye uhusiano wa siri na mke wa mtu mwingine katika mtaa wao, maisha yake yalibadilika ghafla kwa namna ambayo hakuwahi kufikiria.
Siku ya pili baada ya tukio hilo, alianza kuhisi tumbo lake limekaza isivyo kawaida. Alidhani ni tatizo la chakula tu. Lakini siku zilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.
Alishindwa kabisa kujisaidia haja kubwa kwa siku moja, mbili, tatu… hadi ikafika wiki nzima. Tumboni kulivimba, maumivu yaliongezeka, na jasho jingi lilianza kumtoka usiku.
Aliamua kwenda hospitali, akapewa dawa za kawaida za kuharisha na kusafisha tumbo, lakini hakuna kilichofanya kazi. Madaktari walishangaa kwa sababu vipimo vyote vilionyesha hakuna tatizo la kawaida la kiafya.
Maumivu yaliendelea, akashindwa hata kula vizuri, na usingizi ukawa shida.
Hapo ndipo alipoanza kuogopa. Alianza kukumbuka maneno ya watu wazima waliokuwa wakisema kuna mambo mengine hayatibiki kwa dawa za hospitali pekee.
Kwa hofu na kukata tamaa, alimweleza rafiki yake wa karibu siri yote. Rafiki huyo alimshauri atafute msaada wa kipekee kabla hali haijawa mbaya zaidi.Soma Zaidi.
Siku moja, baada ya vipimo vya hivi karibuni, daktari mmoja alituambia kwa maneno mabaya sana: “Ana siku mbili tu za kuishi.” Hisia zetu zilivunjika moyo kabisa.
Nilihisi hofu isiyoelezeka, huzuni, na kuchanganyikiwa. Tukijaribu madawa ya kisasa, kudhibiti chakula, na matibabu ya kawaida, hakuna kilichokuwa na matokeo ya kudumu.
Baba yangu aliendelea kupoteza nguvu, na kila siku ilikuwa changamoto kubwa. Nilijua lazima nifanye kitu tofauti kabla ya maisha yake kupotea kabisa. Soma Zaidi.
Miti imekuwa muhimili muhimu katika ukuaji wa sekta ya viwanda na biashara kwani kupitia miti, viwanda hupata malighafi, biashara hukua, na uchumi huimarika.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb.), Januari 27, 2026, akiwa ameambatana na Naibu Waziri,Mhe. Dennis Londo pamoja na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Needpeace Wambuya kushiriki zoezi la kupanda miti katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma.
Zoezi hilo ni sehemu ya kusherehekea kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Mwanamazingira namba moja hapa nchini, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye aliazimisha siku yake 27 Januari, 1960 kwa kupanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026.
Aidha, Waziri Kapinga wakati akiongea na Watumishi wa Wizara hiyo baada ya kupanda mti, Altria rai kwa watumishi wa wizara kuhakikisha kila mmoja anashiriki kikamilifu katika upandaji miti ili kusaidia uhifadhi wa mazingira na kuibadili Dodoma kuwa ya kijani.
Uhifadhi na utunzaji wa miti unachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ndogo ya uchakataji wa mazao ya misitu, hususan utengenezaji wa mbao na samani, ambayo ni moja ya nyanja muhimu katika kukuza maendeleo endelevu ya sekta ya viwanda na biashara nchini

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akiwa ameshiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 26 Januari, 2026.
Na: OWM (KAM) – Riyadh, Saudi Arabia
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuongeza fursa za ajira kwa vijana nchini ikiwemo kushirikiana na sekta binafsi pamoja na wadau wa maendeleo.
Aidha, Mhe. Sangu amesema ushirikiano huo umewezesha wadau wa Maendeleo na sekta binafsi kutoa nafasi mbalimbali za ajira kwa vijana wa Tanzania nje ya nchi, kutokana na uwezo na ujuzi walionao.
Amesema hayo wakati aliposhiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia Januari 26, 2026.
Amesema, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefungua vyuo vya ufundi stadi, ambavyo vinatoa mafunzo ya ujuzi kulingana na mahitaji ya soko la ajira. Ameongeza kuwa, Vyuo hivyo vimekuwa chachu ya kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa vitendo, kukuza ubunifu kuongeza ajira.
Vilevile, Waziri Sangu ameseema Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Ukuzaji Ujuzi ambapo kupitia Programu hiyo vijana wamekuwa wakipatiwa mafunzo kwa njia ya Uanagenzi yanayolenga kuwajengea uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji, kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira, kuongeza kipato cha mtu binafsi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Kadhalika, Mhe. Sangu ameshukuru viongozi wa nchi mbalimbali kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa kuongeza fursa zaidi za ajira kwa Watanzania.
Mkutano huo unawakutanisha Mawaziri wa Kazi kutoka nchi zaidi ya 45 duniani na wameweza kujadili na kuweka mikakati ya kushirikiana katika soko la ajira, kuongeza kazi za staha kwa Vijana kwa kuzingatia mchango wa sayansi na teknolojia.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akiwa ameshiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 26 Januari, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.












