Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umeeleza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja umeendelea kuhakikisha Tanzania inapata bidhaa za mafuta kwa uhakika, kwa wakati na kwa gharama shindani.

Akizungumza katika Maonesho ya Nne ya Kitaifa ya Utamaduni yanayoendelea mkoani Morogoro, Mchumi wa PBPA, Bw. Henry Kilenga, amesema mfumo huo unahusisha ukusanyaji wa mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta nchini kabla ya kutangazwa kwa zabuni za kimataifa.

Amesema PBPA hukusanya mahitaji hayo na kuyaunganisha ili mafuta yaagizwe kwa pamoja kwa kiwango kikubwa. Utaratibu huo huiwezesha nchi kunufaika na ununuzi wa pamoja na kupata gharama shindani za uagizaji na usafirishaji.

“PBPA hukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, huandaa zabuni na kuwashindanisha wazabuni waliokidhi vigezo. Utaratibu huu unasaidia kuhakikisha nchi inapata mafuta kwa uhakika na kwa gharama shindani,” amesema Kilenga.

Amefafanua kuwa zabuni hizo hushirikisha kampuni za kimataifa zilizohakikiwa na kukidhi vigezo vilivyowekwa na PBPA. Wazabuni hushindanishwa kwa uwazi, huku tathmini ikizingatia bei zilizowasilishwa, uwezo wa kusambaza mafuta na masharti mengine ya zabuni.

Kwa mujibu wa Kilenga, baada ya kukamilika kwa tathmini, kampuni zilizokidhi vigezo na kuwasilisha bei nzuri huchaguliwa kuleta mafuta nchini kulingana na kiasi na muda uliopangwa.

Kilenga amesema uwazi na ushindani katika uendeshaji wa zabuni unalenga kulinda maslahi ya taifa, kuongeza ufanisi na kuhakikisha bidhaa za mafuta zinaendelea kupatikana kwa ajili ya wananchi na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Amesisitiza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja una mchango mkubwa katika kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Katika umri wa utu uzima, utulivu wa ndoa na furaha ya mke na mume ni nguzo kuu ya amani ya familia. 

Hata hivyo, pale uwezo wa kutimiza tendo la ndoa unapotoweka ghafla na kukuacha ukiwa huna nguvu wala uwezo wa kumridhisha mwenza wako, heshima na kujiamini kama mwanamume husambaratika kwa kasi kubwa.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia maumivu makubwa ya nafsi na fedheha ya siri ndani ya nyumba yangu. 

Mwanamume niliyestahiwa na jamii na kupata mafanikio ya kimaisha, nilijikuta ghafla nikishindwa kabisa kutimiza wajibu wangu wa ndoa.

Kila nilipojaribu kusogelea kitanda cha mke wangu, mwili ulilegea na kukosa ushirikiano kabisa. Mke wangu, ambaye mwanzoni alijitahidi kuwa mvumilivu, alianza kubadilika taratibu; alianza kunionyesha dharau, kunipazia sauti kwa mambo madogo, na mara kwa mara kunipigia pasi za maskhara zilizoniumiza sana chembe za moyo.

Nilitumia dawa mbalimbali za viwandani na hospitali zilizokuwa zikaniongezea tu mapigo ya moyo bila kutoa suluhu ya kudumu. Nilibaki nikikabiliwa na msongo mkubwa wa mawazo na hofu ya kuachwa au kusalitiwa. SOMA ZAIDI.
Katika umri wa utu uzima, furaha kuu ya mzazi ni kushuhudia watoto uliowalea kwa shida na tabu wakikua kwa nidhamu, heshima, na kuwa nguzo ya familia.

Hata hivyo, pale mtoto wako wa kwanza ambaye ndiye tegemeo na mfano kwa wadogo zake anapogeuka ghafla, kuanza kukudharau, na kutumbukia kwenye matumizi ya dawa za kulevya, amani ya nyumba hutoweka kabisa.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia maumivu makubwa ya nafsi kutoka kwa mwanangu mkubwa aliyekuwa na umri wa miaka 24.

​Kijana aliyekuwa na nidhamu ya hali ya juu na aliyefaulu masomo yake kwa kiwango kizuri, alianza kubadilika kwa kasi ya ajabu.

Alijiunga na makundi mabaya ya mtaani, akaanza kuvuta bangi na kutumia dawa kali za kulevya. Kila nilipojaribu kukaa naye na kumshauri kama mzazi, alinijibu kwa matusi makali, kunipazia sauti, na hata kutishia kunipiga.

Numba yetu iligeuka kuwa chumba cha mateso; alipoteza kazi yake, akaanza kuiba vitu vya nyumbani na kuuza ili apate fedha za kununulia dawa hizo.

Nilibaki nikilia usiku na mchana, nikiona maisha ya mwanangu yakisambaratika na heshima ya familia yetu ikipotea mbele ya jamii. SOMA ZAIDI.
Uwekezaji katika majengo ya kupanga na biashara za nyumba ni miongoni mwa malengo makubwa ya kiutu uzima yanayotoa uhakika wa kipato na usalama wa kimaisha katika uzee.

Hata hivyo, pale unapoweka akiba zako zote za maisha na kujenga jengo la kifahari, kisha linakaa wazi miaka miwili bila mpangaji hata mmoja kujitokeza, maisha hugeuka kuwa chanzo cha msongo mkubwa wa mawazo na madeni yasiyolipika.

Baada ya kustaafu na kumaliza ujenzi wa jengo langu la ghorofa lenye vyumba vya biashara na makazi, nilikuwa na matumaini makubwa ya kuanza kuvuna matunda ya jasho langu.

​Hata hivyo, mambo yalikwenda tofauti kabisa na matarajio yangu. Kwa zaidi ya miaka miwili, hakuna mpangaji aliyetaka kupanga kwenye jengo hilo. 

Watu wengi walikuwa wakipita na kuangalia, wengine wakiulizia bei na kuahidi kurudi, lakini walipotoka tu hapo hawakurejea tena.

Wakati huo huo, majengo mengine ya majirani yaliyokuwa ya kizee na yasiyo na miundombinu mizuri yalikuwa yakipata wapangaji kila siku.

Nilibaki nikilipa kodi za ardhi na ulinzi kutoka mfukoni mwangu bila kuingiza hata sarafu moja, huku madeni ya benki yakianza kunisonga na kutishia kupiga mnada uwekezaji wangu wote. SOMA ZAIDI.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Dkt. Evaline Munisi (wa tatu kutoka kushoto) akizindua rasmi Ughaibuni Loan wakati wa hafla ya kuwaaga Watanzania wanaokwenda kufanya kazi nje ya  nchi, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya CRDB, Palm Beach Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Agosti, 2026.
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar imeupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kazi kubwa inayofanya katika kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za bima ya afya nchini, pamoja na ushirikiano wake na Mfuko wa Huduma za Afya Zanzibar (ZHSF).

Pongezi hizo zimetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mariam Hamis Said, wakati Kamati hiyo pamoja na Menejimenti za ZHSF na NHIF ilipotembelea Makao Makuu ya NHIF kwa ajili ya kujifunza namna Mfuko huo unavyoendesha na kutoa huduma kwa wanachama.

Mhe. Mariam amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa, kwa kuwa Kamati imepata fursa ya kuelezwa na kujionea kwa vitendo mifumo na huduma zinazotolewa na NHIF, kupitia ziara kwenye Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH).

Pamoja na kutoa pongezi kwa NHIF, Kamati hiyo ilipata fursa ya kutaka kufahamu kwa kina masuala mbalimbali yanayohusu uendeshaji na maendeleo ya Mfuko, ikiwemo namna NHIF inavyopambana na udanganyifu, utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wanachama wanapata huduma bora na kwa wakati.

Aidha, Kamati ilitaka kufahamu namna matumizi ya TEHAMA yameboresha utendaji wa NHIF na kusaidia kupunguza gharama za uendeshaji, pamoja na namna uwekezaji unavyosaidia kuimarisha Mfuko.

Masuala mengine yaliyotiliwa mkazo ni pamoja na vyanzo vya mapato ya Mfuko, viashiria vinavyotumika kupima mafanikio na uendelevu wa NHIF, pamoja na mafunzo na uzoefu ambao Mfuko umeupata katika kipindi cha miaka 25 ya utekelezaji wa majukumu yake.

Amesema ushirikiano kati ya NHIF na ZHSF umeleta matokeo makubwa katika hatua mbalimbali za uanzishaji na uendelezaji wa ZHSF, huku akieleza kuwa uzoefu na msaada uliotolewa na NHIF umeiwezesha Zanzibar kuanza na kuendelea vizuri katika safari ya kuimarisha huduma za bima ya afya.

“Kamati inapongeza NHIF na ZHSF kwa mashirikiano makubwa wanayoyafanya ambayo yamewezesha ZHSF kuanza na kuendelea vizuri,” amesema Mhe. Mariam.

Ameongeza kuwa kazi iliyofanywa na NHIF katika kusaidia uanzishaji wa ZHSF ilihitaji uvumilivu na kujitolea kwa kiwango kikubwa, akieleza kuwa Zanzibar imenufaika na uzoefu wa NHIF katika kujenga mfumo wa bima ya afya.

“Kazi iliyofanywa na NHIF ni kazi iliyofanyika kwa uvumilivu mkubwa, lakini kwa kutubeba Zanzibar katika uanzishaji wa Mfuko wetu,” amesema.

Aidha, Mhe. Mariam ameipongeza Menejimenti ya NHIF kwa kuwawezesha kutembelea Hospitali ya Benjamin Mkapa, ambako wamejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa.

Amesema ziara hiyo imewapa fursa ya kuona kwa vitendo ubora wa huduma zinazotolewa, hususan huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, ambayo ni mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha huduma za afya nchini.

“Tumejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa. Hakika kazi hii ni kubwa na nzuri ambayo kwa ujumla tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, ambapo huduma za kibingwa na kibingwa bobezi zinapatikana hapa nchini,” amesema. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, amesema Mfuko utaendelea kushirikiana kwa karibu na ZHSF ili kuhakikisha wananchi na wanachama wanapata huduma bora za afya kwa wakati na kwa ufanisi.

Dkt. Isaka amesema NHIF itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa ZHSF, hususan katika maeneo ya uzoefu, mifumo ya utoaji huduma na masuala mengine ya kitaalamu, kwa lengo la kuimarisha huduma za bima ya afya kwa wananchi wa Zanzibar.

Amesema ushirikiano huo ni sehemu ya dhamira ya NHIF ya kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa wananchi popote walipo nchini, huku mifuko hiyo ikiendelea kujifunza na kubadilishana uzoefu katika kuboresha huduma kwa wanachama.

Ziara hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu baina ya taasisi zinazohusika na utoaji wa huduma za bima ya afya Tanzania Bara na Zanzibar.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!

Na Mwanaheri Jazza

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dkt. Elizabeth Myema, ameipongeza Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kutoa huduma bora kwa jamii huku akiitaka Mamlaka kuendelea kuwajengea uwezo wadau wanaojihusisha na Tiba Asili kwa kuzalisha dawa zenye ubora kwa kuwa sehemu kubwa ya watanzania wanatumia dawa hizo.
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umetoa elimu kwa wafanyabiashara wa mazao ya misitu katika eneo la Mbezi Kwa Msuguli, jijini Dar es Salaam, kuhusu sheria na taratibu zinazopaswa kuzingatiwa katika shughuli hizo.


Na Lusungu Helela, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini.

Mhe. Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi Jama Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo.

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mhe. Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao.

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho, Mhe.Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia.

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira.

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.








Hakuna jaribu zito kimaisha kama kukabiliwa na tuhuma za uongo mahakamani, ambazo si tu kwamba zinatishia kukupotezea uhuru wako, bali pia zinaharibu kabisa heshima na hatima ya familia yako.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia mateso makubwa ya kisheria na kisaikolojia. Jirani yangu mmoja aliyekuwa na wivu na chuki binafsi alishirikiana na watu wenye ushawishi kutunga kesi nzito ya bandia dhidi yangu, wakinituhumu kwa makosa ya ujambazi wa kutumia silaha na uharibifu wa mali.

​Kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani, mashahidi wa uongo walipangwa kwa umahiri mkubwa na ushahidi wa kughushi uliwasilishwa ili kuhakikisha ninahukumiwa kifungo cha miaka ishirini jela.

Kila nilipohudhuria vipindi vya mahakama, niliona jinsi haki yangu ilivyokuwa ikikandamizwa. Nilitumia fedha nyingi kulipa mawakili mbalimbali, lakini kila hatua tuliyopiga, hakimu na waendesha mashitaka walionekana kupendekeza upande wa walionishtaki.

Nilibaki nikikabiliwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikishindwa kulala usiku, huku mke wangu na watoto wangu wakilia kila siku wakihofia kunipoteza kwa miaka mingi jela. SOMA ZAIDI.
Kila mwanamke anapoingia kwenye ndoa, tamani lake kubwa ni kubeba mtoto wake mwenyewe mkononi na kushuhudia furaha ya familia ikikua. Hata hivyo, pale miaka inapopita bila kupata mtoto, ndoa hugeuka kuwa chungu na chenye machozi yasiyoisha.

Kwa zaidi ya miaka kumi ndani ya ndoa yangu, nilipitia mateso makubwa ya kisaikolojia na kijamii. Nilitengwa na ndugu wa mume wangu, wakinibeza na kunipa majina ya kejeli kama “tasa” na “mwanamke asiye na faida.”

​Kila mkutano wa familia ulipofanyika, nilionekana kama kiumbe kisicho na thamani. Mume wangu, ambaye mwanzoni alikuwa akinipenda sana, anza kubadilika taratibu; alianza kuchelewa kurudi nyumbani, kunipazia sauti, na hata kutishia kumleta mwanamke mwingine nyumbani ili amzalie watoto.

Nilitembelea madaktari bingwa mbalimbali wa afya ya uzazi na kutumia dawa nyingi za hospitali, lakini vipimo vyote vilionyesha sina tatizo lolote linaloonekana. Nilibaki nikilia usiku kucha na kuomba miracle, nikiona ndoa yangu ya miaka kumi ikienda kuvunjika kabisa. SOMA ZAIDI.
Kujenga maisha na mume wako kwa miaka mingi ni safari inayohitaji juhudi, uvumilivu, na upendo wa dhati. 

Hata hivyo, pale msiba unapotokea na mume wako kufariki dunia, kisha ndugu zake wanapogeuka kuwa maadui na kukuvua kila kitu ulichokipigania, maisha hugeuka kuwa jehanum ya papo hapo.

Baada ya mume wangu kufariki ghafla, nilijikuta kwenye mateso makubwa yasiyoelezeka. Wajomba na kaka zake walipanga safu ya kunivua haki zote za ujane.

​Siku chache tu baada ya mazishi, ndugu hao walivamia nyumba yetu ya familia, wakachukua nyaraka zote za viwanja, magari, na kadi za benki, kisha wakaniamuru niondoke mimi na watoto wangu wawili wadogo bila kubeba kitu chochote.

Kila nilipojaribu kutafuta msaada wa kisheria na serikali za mitaa, ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuziba mianya yote na kunitishia maisha yangu na ya watoto wangu.

Nilibaki nikilia kwa uchungu na simanzi nzito, nikiwa hana hifadhi wala kipato cha kulisha watoto wangu, huku nikitazama jasho la mume wangu likifaidiwa na watu waliomtelekeza wakati wa uzima wake. SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Viongozi wapya wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) wameapishwa rasmi jijini Dar es Salaam, huku wakitakiwa kusimamia Katiba ya chama, kulinda maslahi ya wanachama na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uwajibikaji na mshikamano.

Uapisho huo umefanyika leo, Agosti 26, 2026, katika hafla iliyowakutanisha viongozi wa chama, wanachama pamoja na wageni mbalimbali, ikiwa ni hatua muhimu ya kuanza rasmi kwa kipindi kipya cha uongozi wa TAPSEA.

Akizungumza wakati wa kuwaapisha viongozi hao, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, aliwataka viongozi hao kuzingatia Katiba ya TAPSEA na kuitumia kama msingi wa kuwaongoza wanachama pamoja na kufanya maamuzi yenye maslahi kwa chama.
Mhe. Kiswaga amesema uongozi wa chama unahitaji umakini, hekima na uwezo wa kusimamia tofauti zinazoweza kujitokeza miongoni mwa wanachama, akisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuhakikisha changamoto zinatatuliwa kwa kufuata Katiba na taratibu zilizowekwa.

Amesema TAPSEA ni chama kikubwa chenye wajibu wa kuwatumikia wanachama wake, hivyo viongozi wapya wanapaswa kuwa imara katika kutetea na kusimamia maslahi yao, huku wakihakikisha chama kinaendelea kukua na kufikia malengo yaliyowekwa.

“Niwaombe viongozi mnapotoka hapa mkasimamie vyema Katiba yenu ili kuweza kuondoa migogoro itakayojitokeza,” amesema Kiswaga.
Aidha, Mhe. Kiswaga amewataka viongozi hao kuwa mfano kwa wanachama katika utekelezaji wa majukumu yao, akieleza kuwa uongozi bora hujengwa kupitia uwazi, ushirikishwaji na kuheshimu taratibu zinazokubalika ndani ya chama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa TAPSEA, Leah Mwamba, amewashukuru wanachama kwa kumpa dhamana ya kuwaongoza na kuahidi kufanya kazi kwa kushirikiana nao ili kuhakikisha chama kinafikia malengo yake.

Mwamba amesema tukio la uapisho ni hatua muhimu katika safari ya uongozi wa TAPSEA na kwamba dhamana waliyopewa viongozi hao inahitaji ushirikiano wa wanachama pamoja na wadau mbalimbali.
“Ninatoa shukrani zangu za pekee kwa wote walioungana nasi katika historia hii. Jambo hili la uapisho ni kubwa sana, hivyo tunaomba mzidi kutuombea tufanye vyema katika uongozi,” amesema Mwamba.

Amesema uongozi mpya utaendelea kusikiliza maoni ya wanachama na kutafuta njia zitakazosaidia kuimarisha umoja, mshikamano na maendeleo ya chama, huku ukizingatia majukumu na wajibu uliowekwa kupitia Katiba ya TAPSEA.

Naye Katibu Mkuu wa TAPSEA, Hellen Magati, amewashukuru wageni na wadau waliohudhuria hafla hiyo, akiahidi kuwa uongozi mpya utashirikiana na wanachama katika kutekeleza majukumu yake.
Magati amesema ushirikiano wa viongozi na wanachama ni muhimu katika kuhakikisha mipango ya chama inatekelezwa kwa ufanisi na changamoto zinazojitokeza zinapata ufumbuzi kwa wakati.

Amesisitiza kuwa uongozi mpya utazingatia misingi ya ushirikiano katika kuendeleza shughuli za TAPSEA na kuhakikisha wanachama wanapata nafasi ya kutoa maoni na kushiriki katika masuala yanayohusu maendeleo ya chama.

Viongozi wengine walioapishwa ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Halima Twaha Mgulo, Makamu Mwenyekiti, Zainab Ibrahim Ally, Mweka Hazina, Nyanza Msongela, pamoja na wajumbe wengine waliochaguliwa katika uongozi huo.
Uapisho huo unatajwa kuwa hatua ya kukamilisha mchakato wa uchaguzi na kuweka rasmi uongozi mpya katika nafasi zao za kuwahudumia wanachama, huku matarajio yakiwa ni kuona chama kinaendelea kuimarisha umoja na kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Viongozi hao walioapishwa leo, Agosti 26, 2026, walichaguliwa katika Mkutano Mkuu wa 13 wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) uliofanyika mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Ngurdoto, mkoani Arusha.