Na Mwandishi Wetu - DODOMA


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta aina ya petroli zitakazotumika hapa nchini kwa mwezi kuanzia tarehe 4 Februari 2026, zikionesha kushuka maradufu kwa bei ya dizeli kwa mafuta yaliyopokelewa bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mtwara.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule, leo 4 Februari 2026, imebainisha kuwa, bei ya rejareja ya petroli dizeli imepungua kwa shilingi 90 kwa mafuta yaliyopokelewa Dar es Salaam, 25 kwa Tanga na shilingi 24 kwa bandari ya Mtwara. Aidha, bei ya mafuta ya taa nayo imepungua kwa shilingi 17, 14 na 93 kwa mafuta yaliyopokelewa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia ikilinganishwa na bei za mwezi Januari 2026.

Hivyo basi, bei za reja reja za bidhaa za mafuta kwa mwezi huu, zitakuwa shilingi 2,788, 2,849 na 2881 kwa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia. Na bei ya dizeli, Dar es Salaam ni shilingi 2,701, Tanga 2,762 na Mtwara 2,807 huku bei ya mafuta ya taa kwa Dar es Salaam ikiwa ni shilingi 2,881, Tanga 2794 na Mtwara 2,838.

Aidha, kwa mwezi Februari 2026, gharama za kuagiza mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam ziliongezeka kwa wastani 1.88% kwa mafuta ya petroli na 1.65% kwa mafuta ya taa na kupungua kwa wastani wa 5.10% kwa mafuta
ya dizeli. Kwa bandari ya Tanga zimepungua kwa 1.62% kwa petroli na dizeli; huku bandari ya Mtwara zikipungu kwa 9.24% kwa mafuta ya petroli. Vilevile, wastani wa gharama za kubadilisha fedha za kigeni umeongezeka kwa 1.86%.

EWURA inawahimiza wauzaji wa mafuta nchini kutoa stakabadhi za mauzo kwa wanunuzi zinazoonesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita.

Aidha,vituo vyote vya mafuta nchini vichapishe bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana kwani kutokufanya hivyo ni kosa na atakayekiuka atapata adhabu kali kwa mujibu wa sheria.





 

Na Mwandishi Wetu, Tabora

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara,John Mongella, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, ameshiriki katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa mstaafu, Ndugu Nassor Hamdani.

Mazishi hayo yamefanyika leo Februari  3,2026 katika makaburi ya Mihogoni, Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora mkoani Tabora. 

Akizungumza katika ibada hiyo,Mongella amewasilisha salamu za rambirambi kutoka Chama Cha Mapinduzi, akimuelezea marehemu ndugu Nassor Hamdani kuwa alikuwa mshauri mwema wa Chama kwa kipindi chote cha uhai wake, sambamba na mchango wake mkubwa wa kujitolea kwa jamii.

Amesema CCM itaendelea kumkumbuka marehemu kwa uadilifu, hekima na mchango wake katika kukijenga Chama pamoja na ustawi wa jamii kwa ujumla.












 Veronica Simba - WMA 

Wakala wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa kuhakiki dira za maji katika jengo la makao yake makuu lililopo jijini Dodoma.

Meneja Uhakiki wa Vipimo na Viwango wa WMA Makao Makuu, Magesa Biyani amesema usimikaji mtambo huo uliogharimu takribani shilingi milioni 400, utawezesha uidhinishaji na uhakiki wa dira za maji kwa muda mfupi na kwa usahihi zaidi kupitia miradi mingi ya maji inayoendelea kutekelezwa nchini ikiwemo Mkoa wa Dodoma na mikoa mingine jirani.

Akizungumza na wanahabari wa WMA Februari 3, 2026, Biyani amesema kuwa “Mtambo huu umekuja kwa wakati mwafaka kuwezesha wafanyabiashara pamoja na Mamlaka za Maji kuzingatia kwamba dira za maji zote ambazo wanawafungia wateja katika maeneo yao ziwe zimehakikiwa na WMA ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma kulingana na thamani ya fedha wanazolipa.”

Akifafanua zaidi, amesema kuwa mtambo huo una uwezo wa kuhakiki dira za maji nyingi zaidi kwa wakati mmoja kwa kutumia muda mfupi zaidi tofauti na mitambo ya awali ambayo ni ya ki-makenikali (Mechanical Test Bench) yenye uwezo wa kuhakiki dira za maji 10 kwa wakati mmoja ikitumia dakika 20 hadi 30.

Amesema kuwa mtambo huo pamoja na mingine miwili ya aina hiyo iliyoko katika Kituo cha Uhakiki Vipimo, Misugusugu mkoani Pwani, kwa pamoja imeleta faida kubwa ikiwemo kupima dira za maji nyingi zaidi, kwa usahihi zaidi na kwa muda mfupi tofauti na awali kabla ya uwepo wake.

Akitoa mfano, Biyani amesema mathalani kwa Kituo cha Misugusugu ambako mitambo ya aina hiyo ilitangulia kusimikwa kabla ya Dodoma, dira za maji kati ya laki mbili hadi laki tatu zimekuwa zikipimwa kwa mwaka kutegemea na uhitaji kutokana na kuongezeka kwa miradi ya kimkakati.

“Kwahiyo imeleta faida kubwa sana na kusaidia thamani ya fedha iweze kuonekana kwa wateja/wananchi, Mamlaka za Maji na wafanyabiashara na hata kwa uchumi wa nchi,” ameeleza Biyani.

 Akidadavua zaidi namna WMA inavyohusika katika uidhinishaji na uhakiki wa dira za maji, ameeleza kuwa hilo ni mojawapo ya majukumu yake ya uhakiki wa vipimo vya aina mbalimbali nchini kwa lengo la kumlinda mlaji.

Amesema kuwa, WMA huidhinisha na kuhakiki vipimo kwa niaba ya Serikali ambapo kwa upande wa dira za maji, mfanyabiashara yeyote binafsi au kampuni kabla ya kuagiza au kuzalisha bidhaa hizo anatakiwa awasilishe sampuli yake WMA ili kuhakiki muundo wake na baada ya kuidhinishwa anatakiwa kuziwasilisha bidhaa zote alizoagiza au kuzalisha ili zihakikiwe kwa kila moja kujiridhisha kuhusu usahihi wake.

Biyani amefafanua zaidi kuwa zoezi hilo hulenga kuzilinda pande zote mbili yaani mteja na muuzaji ili yeyote kati yao asipunjwe. Dira za maji zilizohakikiwa humuwezesha mteja kulipia kiwango stahiki kulingana na matumizi yake ilhali kwa upande wa muuzaji humwezesha kupata malipo stahiki kulingana na huduma anayotoa.

Akijibu swali la mwandishi kuhusu mipango ya WMA kufikisha huduma hiyo nchi nzima, Biyani ameeleza kuwa Mpango Mkakati wa Wakala wa miaka mitano ijayo kuanzia mwaka huu wa 2026 ni kusimika mitambo ya aina hiyo katika Kanda zote zilizosalia nchini ambazo amezitaja kuwa ni Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Magharibi pamoja na Kanda ya Kusini.

Hata hivyo, ameweka bayana kuwa kutokuwepo kwa mitambo ya kisasa katika Kanda tajwa haimaanishi kuwa kazi hiyo haifanyiki katika maeneo hayo, la hasha, inafanyika kwa kutumia mitambo ya ki-makenikali pamoja na ile midogo inayobebeka (Portable Test Kit) ambayo amesema Maafisa Vipimo kote nchini huibeba mikononi na kwenda nayo katika maeneo mbalimbali kuhakiki dira za maji.

Katika hatua nyingine, Biyani ametoa hamasa kwa wadau wa vipimo mkoani Dodoma na mikoa ya jirani hususani katika sekta ya maji kutumia fursa ya uwepo wa mtambo huo wa kisasa kupeleka dira za maji WMA zikahakikiwe na kuidhinishwa.

Biyani ameonya kwamba ni kosa kisheria kwa mtu yeyote kufunga na/au kutumia dira ya maji ambayo haijahakikiwa na Wakala wa Vipimo huku akibainisha kuwa adhabu yake huanzia kutozwa faini ya shilingi laki moja hadi milioni 20 kwa kosa la kwanza na shilingi milioni 20 hadi milioni 50 kwa kosa la pili kutegemea na aina ya kosa.

Ametaja gharama za kuhakiki dira za maji kwa mujibu wa sheria kuwa ni shilingi elfu kumi tu kwa kila moja na kwa uidhinishaji wa muundo ni shilingi elfu hamsini.

Sheria ya Vipimo, Sura Namba 340 kupitia kanuni zake mbalimbali inaielekeza WMA kuhakiki dira za maji walau mara moja kila mwaka lakini pia Wakala hufanya kaguzi mbalimbali za kushtukiza ili kubaini endapo kuna udanganyifu na kuchukua hatua.

Wakala imeendelea kutoa elimu kwa wadau wa vipimo na umma kwa ujumla katika maeneo mbalimbali ikiwemo namna ya kutambua kipimo ambacho kimehakikiwa ambapo kwa upande wa dira za maji, utambuzi kuwa dira husika imehakikiwa ni kwa kuona lakiri iliyofungwa pamoja na muhuri wa WMA ukionesha tarehe, mwezi na muda ambao kifaa hicho kimehakikiwa. Dira yoyote ambayo haina lakiri na muhuri wa WMA inamaanisha kuwa haijahakikiwa.

Mtambo wa kisasa unaotumika kuhakiki dira za maji. Mtambo huu wa kidijitali umefungwa katika Jengo la Makao Makuu ya Wakala wa Vipimo (WMA), Dodoma.
Sehemu ya Mtambo wa kisasa unaotumika kuhakiki dira za maji. Mtambo huu wa kidijitali umefungwa katika Jengo la Makao Makuu ya Wakala wa Vipimo (WMA), Dodoma.
Jengo lenye mitambo ya kuhakiki dira za maji, lililopo katika Kituo cha Uhakiki Vipimo Misugusugu, Mkoa wa Pwani.

Afisa Vipimo kutoka Wakala wa Vipimo (WMA), akihakiki dira za maji.
     

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 376 vya mkoa huo utawezesha uongezaji thamani wa mazao ya kilimo kupitia uanzishwaji na uendelezaji wa viwanda vidogo vidogo katika maeneo ya wananchi.

Mhe. Dendego aliyasema hayo wakati wa hafla ya kumtambulisha rasmi mkandarasi wa mradi huo, Kampuni ya China Railway No. 4 Engineering Group Ltd kutoka Jamhuri ya Watu wa China, kampuni iliyoshinda zabuni ya kusambaza umeme katika vitongoji hivyo na kuongeza kuwa mradi huo unatarajiwa kufikia kaya 13,259 mara utakapokamilika.

Amesema kuwa upatikanaji wa umeme si anasa bali ni nyenzo muhimu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, na kwamba Mkoa wa Singida umeendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo kutokana na uwepo wa viwanda vidogo hadi ngazi ya vitongoji.

“Upatikanaji wa umeme utaongeza thamani ya mazao ya kilimo kupitia viwanda vidogo vidogo. Wananchi wa Mkoa wa Singida wana mahitaji makubwa ya umeme, hivyo idadi ya awali ya wananchi 13,000 ni mwanzo tu, na tunatarajia mahitaji yataongezeka zaidi,” amesema Mheshimiwa Dendego.

Aidha, Mkuu wa Mkoa huyo amemtaka mkandarasi kuhakikisha anatoa kipaumbele cha ajira za muda mfupi kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yatakayopitiwa na mradi huo.

Mhe. Dendego alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kipaumbele katika upatikanaji wa nishati ya umeme vijijini kwa kuidhinisha jumla ya shilingi bilioni 45.6 kwa ajili ya kusambaza umeme katika vitongoji 376 vya Mkoa wa Singida.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Umeme Vijijini (REA), Mhandisi, Thomas Mmbaga, amesema kuwa Serikali kupitia REA imemtambulisha rasmi mkandarasi ili kuanza utekelezaji wa mradi huo kwa mkataba wa miaka mitatu. Ameeleza kuwa wateja wa awali 13,259 wanatarajiwa kuunganishwa na huduma ya umeme katika wilaya za Ikungi, Mkalama, Itigi, Iramba, Singida na Manyoni.

Naye mwakilishi wa Kampuni ya China Railway No. 4 Engineering Group Ltd, Mhandisi, Baraka Mhagama, amesema kuwa kampuni hiyo imejipanga kutekeleza mradi ndani ya kipindi cha miaka miwili licha ya mkataba kuruhusu utekelezaji kwa miaka mitatu. Ameahidi kushirikiana kwa karibu na REA, TANESCO pamoja na viongozi wa Mkoa wa Singida ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kuleta tija iliyokusudiwa.

  


Na. Chedaiwe Msuya na Jordan Mbwambo WF, Dodoma.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti mikopo yenye riba kubwa ili kulinda wananchi dhidi ya mikopo hatarishi, ikiwemo kuimarisha usimamizi wa sekta ya fedha kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mhe. Munde alitoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Mhe. Nyakisa Sanga, aliyetaka kufahamu hatua zinazochukuliwa na Serikali kuhakikisha wananchi, hususan wafanyakazi, hawabebeshwi mzigo wa riba kubwa za mikopo.

Alieleza kuwa Serikali kwa kushirikiana na BoT imeendelea kusimamia kwa karibu taasisi za fedha ili kuhakikisha zinazingatia sheria, kanuni na miongozo ya utoaji wa mikopo.

Akijibu swali la msingi lililoulizwa kuhusu wakati ambao wafanyakazi wa Tanzania watapunguziwa riba za mikopo na kufikia asilimia 7 au 8, Mhe. Munde alisema kuwa kwa mujibu wa sera za uchumi wa nchi, riba za mikopo zinazotolewa na taasisi za fedha huamuliwa na nguvu za soko, hivyo Serikali haiwezi kuelekeza moja kwa moja taasisi hizo kuweka viwango maalum vya riba kwa kundi fulani la wakopaji.

“Riba za mikopo nchini huamuliwa na soko. Serikali ikielekeza taasisi za fedha kuweka kiwango maalum cha riba kwa wafanyakazi au mkopaji yeyote, itakuwa inakinzana na mwelekeo wa sera ya soko huria,” alisema Mhe. Munde.

Mhe. Munde alifafanua kuwa taasisi za fedha zina uhuru wa kuweka viwango vya riba vya chini ikiwemo asilimia 7 au pungufu endapo zitaona inafaa kufanya hivyo.

Aidha, wafanyakazi binafsi au kupitia waajiri wao wana fursa ya kufanya majadiliano na benki husika ili kukubaliana juu ya viwango vya riba vinavyoweza kutolewa.

Mhe. Munde alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kifedha nchini kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu na yenye tija kwa wananchi, huku ikilinda misingi ya sera ya soko huria inayotumika nchini
Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dar es Salaam Dalmia Mikaya amezindua rasmi mradi wa Elimu ya Mirathi Mashuleni ulio chini ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Mirathi Tanzania (MITA)lengo likiwa kuipeleka elimu hiyo kwa jamii ya Wilaya hiyo na Watanzania kwa ujumla.

Na Job Karongo

HALMASHAURI ya Mji Handeni imeendelea kuonyesha mafanikio katika utekelezaji wa mpango wa lishe shuleni baada ya jumla ya wanafunzi 28,047 kati ya 30,898, sawa na asilimia 91, wanaosoma shule za msingi na sekondari kuendelea kupata chakula wakiwa shule.

Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Handeni, Esther Herman, wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe kwa Robo ya Pili ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za lishe kilichohudhuriwa na viongozi wa halmashauri pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Amesema kuwa mpango huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha afya za wanafunzi, kuongeza mahudhurio shuleni pamoja na kuinua kiwango cha ufaulu kutokana na wanafunzi kuwa na umakini zaidi darasani.

Amebainisha kuwa utoaji wa chakula shuleni ni sehemu ya mkakati wa halmashauri wa kuboresha lishe kwa watoto wa umri wa shule, huku ukilenga pia kupunguza tatizo la utoro na kuongeza motisha ya wanafunzi katika masomo.

Kwa mujibu wa Afisa Lishe huyo, mafanikio ya mpango huo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya halmashauri, uongozi wa shule, wazazi na wadau wa maendeleo ambao kwa pamoja wamekuwa wakichangia upatikanaji wa chakula shuleni.

Hata hivyo, ametoa wito kwa shule na jamii kwa ujumla kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha wanafunzi wote waliosalia wanafikiwa na huduma ya chakula shuleni, kwa lengo la kufikia asilimia 100 ya wanafunzi wote katika halmashauri hiyo.

 



📌Mradi unatekelezwa kwa Miaka Mitatu


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi kabambe wa shilingi bilioni 69 wa kusambaza umeme katika vitongoji 634 utakaonufaisha wateja wa awali 20,328 Mkoani Ruvuma.


Meneja Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme wa REA, Mhandisi Deogratius Nagu amebainisha hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy Februari 02, 2026 Mkoani Ruvuma wakati wa kuwatambulisha Wakandarasi watakaotekeleza mradi Kampuni ya mzawa ya Energy Services Ltd na Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Kusafirisha na Kusambaza Umeme (ETDCO) kwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Brigedia Jenerali Ahmed Abasi Ahmed.


“Tunamshukuru Rais Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi cha shilingi 69,134,982,657.9576 kitumike kusambaza umeme katika vitongoji 634 mkoani hapa na leo hii tumefika hapa kumtambulisha Mkandarasi na maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi yameanza,” amesema Mhandisi Nagu.


Akizungumza wakati wa utambulisho wa wakandarasi hao, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Ahmed ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza dhamira na maono ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vitendo na kuwataka wakandarasi hao kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.


Amesema umeme unakwenda kuongeza chachu ya maendeleo na kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi na metoa wito kwa wananchi maeneo ya mradi kuchangamkia fursa zitokanazo na mradi lakini pia kuwa waadilifu kwa kulinda na kutunza miundombinu ya umeme na pia kuwapatia ushirikiano wakandarasi.


“Tuwahakikishie Mkoa unao wataalam walio tayari kufanya kazi muda wowote, hivyo tunawahakikishia ushirikiano wa kutosha na ni wajibu wetu kuhakikisha ulinzi na usalama lakini pia wkandarasi mnapaswa kuwa waadilifu na mjikague wenyewe kwa wenyewe,” ameelekeza Brigedia Jenerali Ahmed.


Akizungumzia hali ya usambazaji umeme mkoani humo, Mhandisi Nagu amesema kuwa vijiji vyote 551 vimefikishiwa umeme na kwamba hadi sasa vitongoji 2,107 vimefikishiwa umeme kati ya vitongoji 3,691 na kwamba kazi inaendelea ya kusambaza umeme katika vitongoji 731.


Mha. Nagu amefafanua kuwa ETDCO atatekeleza mradi kwenye vitongoji 262 katika Wilaya za Mbinga na Nyasa kwa gharama ya shilingi bilioni 37.9 na huku Energy Services akitekeleza kwenye vitongoji 372 kwa gharama ya shilingi bilioni 31.2 katika Wilaya za Songea, Namtumbo na Tunduru


Amesema, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.


Pia, Mhandisi Nagu amesema mradi unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu na ameiomba Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kushirikiana na REA kufikisha elimu na taarifa sahihi kwa wananchi sambamba na kuhamasisha wananchi kuunganishiwa umeme.


Aidha, kwa upande wao wakandarasi wa mradi huo walimhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa watatekeleza mradi kwa uaminifu, uadilifu na uzalendo kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za Serikali. 






 

Stakeholders Laud Transparent Indicative Pricing System as Small Scale Output Soars


Singida

Mineral sector stakeholders in Singida Region have hailed the Singida Mineral Market as a game changer, citing significant improvements in transparency, fairness and efficiency driven by the adoption of a digital indicative pricing system.

Artisanal miners, mineral processors and traders operating in the region say the market has revolutionized mineral trade by safeguarding miners against price exploitation and quality manipulation, while strengthening trust among sector players.

Speaking at the market, a geologist from the Singida Resident Mines Office,  Mbeleye David, said the establishment of the mineral market has yielded substantial benefits for small-scale miners and traders by introducing systems that protect them from fraud related to gold quality and unfair pricing.

 David noted that before the establishment of mineral markets, Singida Region was recording very low volumes of officially traded mineral production between 100 and 200 grammes. However, through the operational mineral markets, the region is now coordinating between 50 and 60 kilogrammes of mineral output from small-scale miners, reflecting increased efficiency and stakeholder confidence in the system.

He explained that the government has put in place a robust indicative pricing mechanism aimed at protecting artisanal miners from selling minerals at undervalued prices.

“The market is equipped with a modern X-Ray Fluorescence (XRF) machine for testing gold purity, ensuring that minerals are traded based on accurate quality standards and their true market value,” said David.

He added that unlike in the past, when indicative prices were provided only for raw gold, the current system uses a digital display board showing indicative prices for various minerals, including gold, copper and silver an innovation that has enhanced transparency and eliminated loopholes for malpractice in mineral trade.

“This technology has streamlined market operations, including mineral valuation and the issuance of mineral transportation permits for both domestic and international markets, which are now processed faster and more efficiently,” he said.

Meanwhile, mineral trader   Abubakari Omary said that despite the notable progress, continuous education on the use of indicative prices is essential for miners and traders to avoid misunderstandings and disputes during transactions.

“Education remains critical to ensure every stakeholder understands their rights and obligations and conducts business based on actual market prices,” said Omary.

Stakeholders also commended the new mineral market framework for allowing unlicensed artisanal miners to register and sell their minerals directly at the markets without being required to use a trader’s licence a move that has removed a major barrier that previously limited participation in the formal mineral trade.

Overall, the Singida Mineral Market has been described as a key driver of growth in the region’s mineral sector by enhancing transparency, improving trade security and increasing government revenue through the control and prevention of mineral smuggling.