NA DENIS CHAMBI, TANGA.


JUMLA ya miradi  ya maendeleo 73 iliyopo mkoani  Tanga yenye thamani  zaidi ya shilingi Bilioni 27.7 inatarajiwa kupitia na mwenge  wa Uhuru kwa mwaka 2026 katika halmashauri 11.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian amesema kuwa Mwenge huo  utakimbizwa kwa umbali wa kilomita 1,340  ambapo , miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, miradi 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, miradi 11  itakaguliwa na baadaye kukabidhiwa mkoani Kilimanjaro junior 28,2026 katika viwanja vya shulen ya msingi Hedalu wilayani Korogwe.


Aidha Balozi Dkt Burian ameongeza kuwa kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu huku Shilingi bilioni 15.47 zikiwa ni kutoka katika mchango wa wahisani.


Akizungumzia kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema,  "Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo amewasisitiza wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi na kushiriki shughuli zote za Mwenge huo ikiwa ni ishara ya kuonyesha uzarendo kwa Taifa 


"MWENGE huu wa Uhuru ukiwa mkoani Tanga utafanya kazi katika miradi 73 ambapo  utaweka mawe ya msingi jumla ya miradi 34, utafungua na kizindua jumla ya miradi 26 na utatembelea na kukagua jumla ya miradi 11 ya shughuri za vijana na miradi miwili ya maendeleo ya sekta ya maji, miradi hii yote ina jumla ya thamani ya shilingi Bilioni 27,764, 390,480.01." amesema Dkt Burian.


"Fedha ambazo zimetoka katika nguvu za wananchi ni shilingi Million 300,638,449.32, fedha kutoka halmashauri ni shilingi Bilioni 1,79,673,076.72, fedha kutoka serikali ni shilingi Bilioni 10, 707,064,607.76 na fedha kutoka kwa wahisani ni shilingi milioni 15, 477, 014" amebainisha.


Aliongeza kuwa baadhi ya  wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja wa kitaifa na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.


Mbali na kuhamasisha maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na umuhimu wa lishe bora kwa jamii.


Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru na kufaidika na ujumbe wake.


Alisema mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi vya sanaa vitakavyoshiriki katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka (Mb), amewataka wataalamu wa maendeleo ya jamii nchini kutumia taaluma, mbinu na uzoefu wao kuwaelimisha wananchi kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ili kuhakikisha kila Mtanzania anaielewa na kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.

Mhe. Nanauka ametoa wito huo, alipokuwa akifungua Kongamano na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (CODEPATA), uliofanyika katika Ukumbi wa Kwatunza Beach Arena, jijini Mwanza, leo Juni 17, 2026.

“Nyinyi mnazo mbinu na maarifa ya kuijenga jamii. Nendeni kwa wananchi mkawape elimu na uelewa kuhusu Dira ya Taifa 2050 ili wawe sehemu ya safari ya maendeleo ya nchi yetu,” amesema Mhe. Nanauka.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju, amewahimiza wataalamu wa maendeleo ya jamii kuendelea kujiendeleza kitaaluma kwa kujiunga na programu ya Shahada ya Uzamili kwa njia mseto (Blended/Online) inayotolewa na Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD), ambayo hukamilika ndani ya mwaka mmoja.

Aidha, Wakili Mpanju ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa wataalamu wa maendeleo ya jamii kupitia utoaji wa vitendea kazi, kuboresha maslahi ya kada hiyo na kuendelea kutoa ajira kwa wataalamu nchini.

Mkutano huo wa siku tatu unaendelea kesho kwa uwasilishaji wa mada mbalimbali zitakazotolewa na wataalamu na wadau wa maendeleo ya jamii, zikiwa na lengo la kuimarisha taaluma na mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya Taifa.
















Na. OWM (KAM), Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema mahusiano mema, mazungumzo ya kujenga na mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu katika kuimarisha demokrasia, amani na maendeleo endelevu nchini.
-DODOMA

Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua rasmi Awamu ya Pili ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC II) Juni 20,2026 katika Viwanja vya Maonesho Dole, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi wote.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026  jijini Dodoma leo, Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera, amesema  kampeni hiyo inalenga kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa huduma za msaada wa kisheria, elimu ya sheria na ushauri wa kisheria ili kuongeza uelewa wa haki na wajibu wao katika jamii.

Dkt. Homera amesema kampeni hiyo ni utekelezaji wa maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha huduma za sheria na haki zinapatikana kwa wananchi wote bila ubaguzi, hususan makundi maalumu na wananchi wa maeneo ya pembezoni ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto za kupata huduma hizo.

Amefafanua kuwa Awamu ya Pili ya kampeni hiyo itaendelea kutumia kaulimbiu ya “Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo,” ambayo inaakisi dhamira ya Serikali ya kuimarisha utawala wa sheria, usawa na maendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, mafanikio ya Awamu ya Kwanza ya kampeni iliyotekelezwa kuanzia Aprili 2023 hadi Juni 2025 ndiyo yamechochea kuanzishwa kwa awamu mpya. Katika kipindi hicho, kampeni ilitekelezwa katika mikoa yote 31 ya Tanzania Bara pamoja na mikoa yote mitano ya Zanzibar.

Amesema Zanzibar pekee, jumla ya wananchi 422,908 walinufaika na huduma mbalimbali za msaada wa kisheria, ambapo wanaume walikuwa 213,723 huku wanawake wakifikia 209,185.

“Matokeo haya yanaonesha wazi umuhimu wa kampeni hii katika kuwajengea wananchi uelewa wa sheria, haki na wajibu wao pamoja na kusaidia kutatua migogoro mbalimbali ya kisheria inayowakabili,” amesema Dkt. Homera.

Katika awamu mpya, wananchi watapata huduma zinazohusu masuala ya ndoa na talaka, mirathi, migogoro ya ardhi, haki za watoto, ukatili wa kijinsia, haki za wafanyakazi pamoja na usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala.

Huduma nyingine zitakazotolewa ni pamoja na usajili wa matukio muhimu ya maisha, upatikanaji wa nyaraka za utambulisho, uandaaji wa nyaraka za kisheria na utoaji wa elimu ya sheria kwa wananchi.

Dkt. Homera amesema maandalizi yote ya uzinduzi wa kitaifa yamekamilika na kwamba zaidi ya washiriki 15,000 wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo, wakiwemo viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, viongozi wa dini, vyama vya siasa, mashirika ya kiraia, wataalamu wa sheria na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

Ameongeza kuwa sambamba na uzinduzi huo, huduma za msaada wa kisheria zitatolewa kupitia mabanda katika wilaya za Mjini, Magharibi A na Magharibi B, huku timu za wataalamu zikitembelea shehia mbalimbali kutoa elimu ya sheria, ushauri na utatuzi wa migogoro.

Waziri huyo ametumia fursa hiyo kupongeza ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika utekelezaji wa kampeni hiyo, akisema ni mfano halisi wa manufaa ya Muungano katika kuwahudumia wananchi.

Aidha, amewataka wananchi wa Zanzibar kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi huo na kutumia fursa ya kupata huduma mbalimbali za kisheria zitakazotolewa bila malipo.

“Ushiriki wa wananchi katika kampeni hii utasaidia kuongeza uelewa wa haki zao za kisheria, kuimarisha amani na utulivu katika jamii pamoja na kuchochea maendeleo ya Taifa,” amesema 

Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imeendelea kuwa miongoni mwa programu muhimu za Serikali zinazolenga kusogeza huduma za haki karibu na wananchi na kujenga jamii inayozingatia sheria, usawa na utawala bora.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 17,2026 jijini Dodoma  kuhusu uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya msaada wa kisheria itakayofanyika Juni 20 mwaka huu, Zanzibar.

Na Mwandishi Wetu-DODOMA
Wizara ya Viwanda na Biashara imewahimiza wananchi, hususan vijana na wajasiriamali, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na taasisi zake ili kukuza biashara, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.
Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2026 na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Saidi Msabimana, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Msabimana amesema wizara hiyo, ambayo ni miongoni mwa taasisi muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imeshiriki maonesho hayo pamoja na taasisi nane zilizo chini yake kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi pamoja na kutoa elimu kuhusu biashara, viwanda na uwekezaji.
Amesema jukwaa hilo limetumika kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa taarifa za huduma zinazotolewa na kuwaelekeza namna ya kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla.
“Tunatumia jukwaa hili kuwafikia wananchi moja kwa moja, kuwaeleza huduma tunazotoa na kuwahamasisha kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa kwa ujumla,” amesema Msabimana.
Katika maonesho hayo, taasisi zilizo chini ya wizara hiyo zimeendelea kutoa huduma mbalimbali, ikiwemo huduma za usajili wa biashara kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni Tanzania (BRELA), ambapo wananchi wamewezeshwa kupata huduma za usajili wa kampuni, majina ya biashara na alama za biashara kwa njia ya kidijitali.
Kwa upande wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB)wananchi wanaomiliki au wanaotarajia kuendesha maghala wamepata elimu na huduma za usajili pamoja na leseni zinazotakiwa kisheria.
Aidha, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE ) kimetumia maonesho hayo kutoa taarifa za udahili na programu mbalimbali za masomo zinazolenga kuwaandaa vijana kuwa wataalamu na wajasiriamali wenye ushindani sokoni.
Vilevile, Wakala wa Vipimo umeendelea kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo katika biashara ili kulinda haki za walaji na kuimarisha uaminifu katika shughuli za kibiashara nchini.
Msabimana amesema kupitia maonesho hayo, zaidi ya wananchi 365 wamepata huduma za kuboresha mifumo ya biashara zao pamoja na taratibu za usajili wa lebo za bidhaa, hatua inayosaidia kuongeza ubora na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Kwa upande mwingine, Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), limeendelea kutoa taarifa kuhusu miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Liganga, Mchuchuma na Soda Ash, inayotarajiwa kuwa kichocheo cha mapinduzi ya viwanda, ajira na ukuaji wa uchumi.
Msabimana amewahimiza wananchi kutembelea mabanda ya wizara hiyo katika maonesho hayo ili kupata huduma, elimu na taarifa sahihi zitakazowawezesha kuboresha maisha yao na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi shindani wa Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.

...

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.

Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.

Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.

Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.

“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.

Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuongeza vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya  umeme ili kuongeza wigo wa utoaji huduma hiyo ambayo imeonekana kuleta mageuzi katika matumizi ya nishati safi.

Mhe. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 alipotembelea Banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma.

Waziri huyo mwenye dhamana ya Utumishi ametumia nafasi hiyo kuipongeza TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati safi kwa ajili ya  kupikia na katika vyombo vya usafiri.

‘’ TANESCO mnafanya kazi kubwa nawapongeza kwa mageuzi ya matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, natoa rai muongeze Vituo vya kuchajia vyombo hivyo ili kuongeza wigo wa utoaji huduma,’’ alisisitiza Mhe. Ridhiwani

Naye Meneja Masoko Bw. Fredrick Kalinga amesema TANESCO inashiriki katika Maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika ikiwemo maendeleo ya miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji umeme, maboresho makubwa yaliyofanywa na Shirika kwenye mifumo ya kidigitali ya utoaji huduma kwa wateja pamoja na kuhamasisha jamii kutumia nishati safi ya umeme kupikia na katika vyombo vya usafiri kama magari, bajaji, guta, na pikipiki.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2026  yenye kauli mbiu isemayo ‘’Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa huduma Endelevu’’ yameanza rasmi Juni 16, 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026










 


Serikali imeendelea kuimarisha jitihada za kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia upatikanaji wa mitaji, mafunzo na masoko ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya Taifa. 

Hayo yameelezwa leo Juni 17, 2026 bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga (Viti Maalum) aliyetaka kufahamu mipango maalum ya Serikali katika kuwawezesha wanawake.

Akijibu swali hilo, Mhe. Mahundi amesema Serikali inatumia mifumo mbalimbali ya uwezeshaji inayotekelezwa kupitia Wizara za kisekta pamoja na mamlaka za serikali za mitaa ikiwa na lengo la kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kujenga uwezo wa kiuchumi, kuongeza kipato na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Amefafanua kuwa miongoni mwa mipango hiyo ni utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri pamoja na Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake huku kabla ya kunufaika na mikopo hiyo, wanawake hupatiwa mafunzo ya kuongeza thamani ya bidhaa wanazozalisha kupitia ushirikiano kati ya Serikali, SIDO, VETA na taasisi mbalimbali zinazojihusisha na maendeleo ya wanawake.

Naibu Waziri huyo pia amesema Serikali inaendelea kutekeleza Programu ya Jenga Kesho Yako (BBT) katika sekta za kilimo, mifugo na ufugaji nyuki, ambayo imekuwa ikitoa fursa kwa wanawake kujikita katika shughuli za uzalishaji mali ambayo imeendelea kuwajengea uwezo wa kiufundi na kuwasaidia kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na sekta hizo muhimu.

Katika sekta ya madini, Mhe. Mahundi amesema Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) linaendesha programu maalum zinazowawezesha wanawake kushiriki katika shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa kuwapatia mafunzo, maarifa na kuwaunganisha na fursa mbalimbali za uwekezaji. Hatua hiyo inalenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta hiyo yenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

Aidha, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kuimarisha huduma jumuishi za kifedha zinazowawezesha wanawake kupata mitaji kupitia SACCOS na kuboresha mazingira ya uwezeshaji wa wanawake ili kuhakikisha wanapata mitaji, mafunzo na masoko ya uhakika yatakayowasaidia kukuza biashara zao na kuchangia kwa kiwango kikubwa zaidi katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.


















 


‎Wkala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia mradi wa RISE imeendelea kuimarisha ushiriki wa wananchi katika shughuli za matengenezo ya barabara kwa kutumia vikundi vya Kijamii vya Matengenezo ya Kawaida ya Barabara (CBRM) hatua inayolenga kuongeza ajira, kukuza uchumi wa wananchi na kuhakikisha barabara zinabaki katika hali nzuri mwaka mzima.

‎Akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu yanayoendelea jijini Arusha, Mtaalamu wa masuala ya  kijamii kutoka TARURA Makao Makuu, Bi. Mwanamisi Abdallah amesema mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa takwa la kisheria linaloelekeza asilimia 30 ya bajeti ya kazi za barabara kutengwa kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya barabara.

‎Amesema TARURA kupitia Mradi wa RISE imeamua kutumia fursa hiyo kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuunda na kuimarisha vikundi vya kijamii vyenye wanachama kati ya watano hadi ishirini ambavyo vitashiriki katika utekelezaji wa kazi mbalimbali za matengenezo ya barabara.

‎"Vikundi hivi vitapatiwa mikataba ya kufanya kazi za kusafisha mitaro, kuziba mashimo madogo, kuondoa vikwazo vinavyokatiza njia, kufyeka majani pamoja na shughuli nyingine ambazo hazihitaji matumizi ya mitambo mikubwa. Hii ni fursa kwa wananchi kupata ajira, kuongeza kipato na kushiriki moja kwa moja katika kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo yao", amesema Bi. Mwanamisi.

‎Kwa upande wake, Mratibu wa Kitaifa wa Programu kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. Dampu Ndenzako amesema ushirikiano kati ya ILO na TARURA unalenga kujenga uwezo kwa wataalamu na kuhakikisha vikundi vya kijamii vinatumika kikamilifu katika matengenezo ya barabara huku vikitoa manufaa ya kiuchumi kwa wananchi.

‎Amesema uzoefu unaonesha kuwa ushiriki wa wananchi katika matengenezo ya barabara hususan maeneo ya vijijini huongeza umiliki wa miundombinu hiyo, huimarisha huduma za usafiri na usafirishaji na kuhakikisha barabara zinapitika katika misimu yote ya mwaka huku wananchi wakinufaika kwa kupata ajira na kuongeza kipato.

‎Naye, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kongwa Mhandisi Peter Johnson, amesema wilaya hiyo imeanza kutekeleza mpango huo katika mwaka wa fedha 2025/26 ambapo imefanikiwa kuunda vikundi 34 vya CBRM, kati ya hivyo vikundi 31 tayari vimeanza kazi huku vingine vikiendelea kukamilisha taratibu za kuingia mikataba.

‎Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Bi. Hidaya Abdallah amesema mafunzo hayo yatawawezesha wataalamu wa maendeleo ya jamii kutambua, kuunda, kusajili na kuvijengea uwezo vikundi kwa kuzingatia miongozo na taratibu zilizowekwa huku wananchi wakipata fursa za ajira, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya miundombinu na uchumi wa jamii kwa ujumla.

‎Mafunzo hayo ya siku sita yanawakutanisha Wahandisi na Wataalamu wa Mazingira na Jamii kutoka TARURA Makao Makuu, Ofisi za Mikoa na Wilaya pamoja na Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi za Wakurugenzi wa Wilaya kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kusimamia utekelezaji wa mpango huo katika mwaka wa fedha 2026/27.