
Chama cha Wafanyakazi Serikali za Mitaa (TALGWU), tawi la RUWASA, kimefanya mkutano mkuu wa uchaguzi wa viongozi wapya ambapo Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Mhandisi Rashid Abdallah, amefanikiwa kutetea nafasi yake ya uenyekiti.
Uchaguzi huo ulifanyika Aprili 24, 2026 jijini Dodoma, katika mazingira ya uwazi na ushirikishwaji mpana wa wanachama, waliotekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kuchagua viongozi watakaoongoza tawi hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Katika uchaguzi huo, viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Rashid Abdallah (Mwenyekiti wa Tawi), Ibrahim Fungo (Katibu wa Tawi), Tumaini Gwatalile (Mwenyekiti wa Makundi Maalum – Wanawake), Ashura Nkunya (Katibu wa Makundi Maalum – Wanawake), Victoria Charles (Mjumbe wa Makundi Maalum – Vijana), na Adam Suleiman (Mjumbe wa Makundi Maalum – Watu wenye Ulemavu).
Uongozi huo mpya unatarajiwa kuimarisha mshikamano miongoni mwa wanachama, kulinda na kutetea maslahi yao, pamoja na kuendeleza maendeleo ya chama katika tawi la RUWASA.









NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
SERIKALI imewahimiza wawekezaji wazawa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya viwanda, ikisisitiza kuwa imeendelea kuboresha na kurahisisha mazingira ya biashara ili kuongeza uwekezaji wa ndani.
Na Augusta Njoji
Timu ya wataalamu wa afya kutoka Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni imeanza rasmi mpango wa utoaji elimu kwa jamii ili kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa na kuboresha ustawi wa wananchi.
Utoaji wa elimu hiyo imejikita katika afua za kuzuia malaria, lishe bora, bima ya afya kwa wote pamoja na huduma za mama na mtoto, ikiwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha jamii inakuwa na afya bora.
Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Ofisa Afya wa Halmashauri na Mratibu wa Elimu ya Afya kwa Umma, Jonas Mkondya, amesema wamejipanga kutembelea kila mtaa katika kata zote 12 za Halmashauri ya Mji Handeni ili kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapatia elimu sahihi ya afya.
Ameeleza kuwa elimu hiyo itasaidia kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na magonjwa, kuboresha lishe pamoja na umuhimu wa kujiunga na bima ya afya kwa wote ili kupata huduma kwa urahisi.
Kata zitakazofikiwa katika ziara hiyo ya wataalamu wa afya ni Konje, Mabanda, Kwenjugo, Malezi, Chanika, Mlimani, Mdoe, Vibaoni, Kwediyamba, Kideleko, Msasa na Kwamagome.

Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sports Club imeonyeshana ubabe na Timu ya Mpira wa miguu ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT) baada ya kutoka sare ya goli mbili kwa mbili katika mechi ya kirafiki iliyochezwa leo Aprili 24, 2026 katika viwanja vya Chai mkoani Njombe.
Hapo Aprili 22, 2026 TCDC Sports Club ilikubali kipigo cha bao moja bila 1- 0 kutoka Timu ya Mpira wa miguu ya TANWART katika mechi ya kirafiki iliyochezwa viwanja vya Kibena mkoani humo.
TCDC Sports Club inaendelea kushiriki Michezo ya kirafiki mkoani humo baada ya kushindwa kuvuka hatua za makundi kwenye Mashindando ya Michezo ya Meimosi inayoendelea mkoani humo.

Katika kuelekea Kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani ( Meimosi) ambayo kitaifa inafanyika mkoani Njombe, Timu ya Pooltable ya TCDC Sports Club imeshiriki mashindando ya mchezo huo Aprili 23, 2026 ndani ya African Club mjini humo.
Mchezaji Mbasso John ameiwakilisha TCDC Sports Club katika mchezo huo huku akishinda mechi ya kwanza kati ya TCDC na Ulinzi na ,mechi ya pili akicheza na Arusha DC na kutoka moja moja na kupoteza mchezo wa mwisho baada ya kufungwa na timu ya Mahakama.
Kwa hatua hiyo TCDC Sports Club haijafanikiwa kuingia nusu fainali katika mchezo wa Pooltable katika Mashindando ya Michezo ya Meimosi.

Wanamichezo wa TCDC Sports Club wameshiriki mashindano ya riadha (mbio) katika Michezo ya kitaifa Meimosi inayoendelea mkoani Njombe.
Wachezaji walioshiririki mbio hizo ni Mbaso John aliyekimbia Mita 100 na kuibuka mshindi wa tatu (3) katika round ya kwanza, na baadae kupoteza nafasi ya ushindi katika hatua ya nusu fainali.
Mchezaji mwingine ni William Valentine aliyeshiriki riadha mbio za Mita 800 na kutofaninikiwa kupata ushindi baada ya kuzidiwa na wanariadha kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI na Wizara ya Mambo ya ndani.
Kwa upande wake Noel Steven ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCDC Sports Club ameshiriki mchezo wa Draft ambapo kwa mzunguko wa kwanza TCDC Sports Club ilishinda mechi mbili na mzunguko wa pili kupata draw na hivyo kutofanikiwa kuvuka hatua za makundi baada ya kuzidiwa kete na TRA na Wizara ya Kilimo.
Michezo hiyo yote imechezwa Aprili 21, 2026 katika viwanja vya Njombe Sekondari na Viwanja vya sabasaba (77) mkoani humo.

Na Mwandishi Wetu, Lusaka
WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unashiriki Kongamano la Kimataifa la Nishati Endelevu ya Kuni na Mkaa (Sustainable Woodfuel Forum) linaloendelea Lusaka, Zambia, likiwa jukwaa la kimataifa la kubadilishana uzoefu na mbinu bora za usimamizi wa misitu na nishati ya miti.
Kongamano hilo linafanyika chini ya Programu ya Dryland Sustainable Landscapes Impact Programme (DSL-IP) kwa ufadhili wa Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF) na kuratibiwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa kushirikiana na Serikali ya Zambia.
Akizungumza katika kongamano hilo, Mhifadhi Mkuu TFS, Kassim Ally, amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati ya kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Amesema hatua hiyo ni sehemu ya azma ya Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ifikapo mwaka 2034.
Ally amesema juhudi hizo zinajumuisha utekelezaji wa sera, uwekezaji katika nishati mbadala na kampeni za elimu kwa umma ili kubadilisha tabia ya matumizi ya nishati.
Ameeleza kuwa hatua hizo zitasaidia kupunguza ukataji miti hovyo, kulinda misitu na kuboresha afya za wananchi dhidi ya athari za moshi wa majumbani.
Kwa mujibu wa Ally, ushiriki wa TFS unafanyika kupitia mradi wa Integrated Landscape Management in Dry Miombo Woodlands of Tanzania unaolenga kurejesha mifumo ikolojia na kupunguza upotevu wa bioanuwai.
Amesema mradi huo pia unalenga kuimarisha ustahimilivu wa uzalishaji katika maeneo ya Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame katika Mkoa wa Tabora (Wilaya za Kaliua, Sikonge na Urambo) na Wilaya ya Mlele mkoani Katavi kupitia usimamizi shirikishi wa misitu.
Ameongeza kuwa kupitia mradi huo, jamii zinashirikishwa moja kwa moja katika uhifadhi huku zikipewa fursa za kunufaika kiuchumi kupitia matumizi endelevu ya rasilimali.
Kongamano hilo linawakutanisha wadau kutoka nchi mbalimbali za ukanda wa Miombo-Mopane kujadili mahitaji ya nishati ya kuni na mkaa hadi mwaka 2050 na athari zake kwa uchumi na mazingira.
Katika maonesho yanayoambatana na kongamano hilo, TFS imewasilisha teknolojia za nishati safi ya kupikia na mbinu mbadala za matumizi ya kuni na mkaa.
Maji ya kimataifa ni moja ya rasilimali inayoleta amani katika nchi mbalimbali zinazonufaika na wananchi wake.
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso ( Mb) akifungua kikao cha 13 cha Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (ZAMCOM) jijini Dar es salaam amesema maji hayana mpaka na yanakusanya watu kwa maendeleo yao.
Mhe. Aweso ambaye katika mkutano huo ni Mwenyekiti ameainisha kuwa umoja wa wananchi na nchi walizopo umeletwa na maji ya kimataifa, maji yanayovuka mipaka ya nchi zao.
Amesema ni muhimu kuwa na rasilimali za kutosha ili kuleta maendeleo na wananchi wanashirikishwa kutunza rasilimali za maji ili kuleta maendeleo katika sekta nyingine za uchumi.
Mhe. Aweso amesisitiza kwa wajumbe wa mkutano huo kuwa maji ni muhimu na yanahitajika kuleta maendeleo kwa wananchi.
ZAMCOM inagusa maisha ya kila wananchi zaidi ya milioni 51 na imekusanya nchi za Tanzania, Angola, Zambia, Malawi, Namibia, Botswana, Zimbabwe, na Msumbiji.
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff, amefungua mafunzo ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uelewa wataalamu wa TARURA kutoka TAMISEMI, ofisi ya Makao Makuu, Mikoa, Wilaya, Mhandisi Mshauri pamoja na Mkandarasi katika kutekeleza mradi wa Sanifu na Jenga wa barabara zinazoingia uwanja wa AFCON jijini Arusha.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhandisi Seff alisema lengo kuu ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa miradi ya sanifu na jenga ili kuimarisha uzingatiaji wa taratibu, kushughulikia changamoto kwa wakati na kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa mafanikio.
Alifafanua kuwa mafanikio hayo yanapaswa kuzingatia misingi ya usalama, masuala ya kijamii na kimazingira, muda, gharama, thamani, ubora pamoja na mahitaji ya kiutendaji.
Mhandisi Seff alibainisha kuwa tangu kuanzishwa kwa TARURA, Wakala huo haujawahi kupata mradi mkubwa kama huo, hivyo mafunzo hayo ni fursa muhimu ya kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani ili wawe tayari kushughulikia miradi mikubwa zaidi ijayo.
Aliwataka washiriki wa mafunzo kujifunza kwa umakini na kuuliza maswali yatakayowaongezea uelewa, akisisitiza kuwa jukumu walilonalo ni kubwa na linahitaji umakini wa hali ya juu katika kila hatua ya utekelezaji.
Aidha, aliwakumbusha wasimamizi wa mradi kuzingatia muda akieleza kuwa barabara hizo zinatakiwa kukamilika ifikapo Mei 2027 bila nyongeza ya muda.
“Serikali imeiamini TARURA kwa kuipatia jukumu hilo kwa manufaa ya Taifa hivyo hamna budi kufanya kazi usiku na mchana”.
Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Serikali inaendelea kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na upatikanaji wa umeme nchini, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka 2026/2027.
Amesema hayo Aprili 23, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja za wabunge mara baada ya kuwasilishwa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati ya Mwaka 2026/2027.
Akijibu hoja hizo amesema Rais wa Jamuhurinya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia, akilenga kufikisha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034 huku akifafanua kuwa matumizi hayo yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi zaidi ya asilimia 28 kwa sasa, huku jitihada hizo zikilenga kulinda mazingira na afya za wananchi.
Aidha, ameeleza kuwa Serikali imesambaza zaidi ya kilomita 56.4 za mabomba ya gesi asilia, mitungi ya gesi zaidi ya laki tatu, majiko ya gesi zaidi ya elfu 49 na majiko ya umeme zaidi ya elfu saba ambapo zaidi ya taasisi 55 zimepatiwa majiko ya nishati safi, huku mpango ukiwa kufikia taasisi zaidi ya 400.
Katika kuhakikisha upatikanaji wa umeme vijijini zaidi ya visiwa 120 kati ya 143 tayari vimepata umeme wa sola kwa ruzuku ya asilimia 45 hadi 75 hatua inayolenga kuwaondoa wananchi katika matumizi ya vibatari na kuboresha maisha yao kwa ujumla.










