Mbunge wa Jimbo la Kwela na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi,Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lwanji Tarafa ya Kipeta Sumbawanga ambapo amewasihi kuendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo jana. Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ephraim Konta
( Picha na OWM- KAM)
Na: OWM (KAM), Sumbawanga
Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amewataka vijana wa Mkoa wa Rukwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa za ajira zinazozalishwa na mradi wa kimkakati wa uchimbaji wa gesi ya helium katika Bonde la Ziwa Rukwa.
Sangu alitoa wito huo Julai 20, 2026 alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kinambo Kata ya Milepa Wilaya ya Sumbawanga akisema mradi huo una nafasi kubwa ya kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi hususan vijana wa maeneo yanayouzunguka.
Alisema Serikali imeingia makubaliano na kampuni ya Marekani ya Noble Helium kufanya shughuli za utafiti na uchimbaji wa gesi ya helium katika ukanda wa Bonde la Ziwa Rukwa, ambapo shughuli hizo tayari zimeanza na kuendelea kuzalisha nafasi mbalimbali za ajira.
Waziri Sangu ambaye ndiye mwenye dhamana na masuala ya ajira nchini alisema tayari amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo ili kuhakikisha vijana wa Kijiji cha Kinambo kilicho jirani na mradi huo wa gesi na Mkoa wa Rukwa wanapewa kipaumbele katika nafasi za ajira zinazopatikana kupitia mradi huo.
“Fursa za ajira katika mradi huu ni nyingi. Lengo letu ni kuona vijana wa maeneo haya wananufaika moja kwa moja kwa kupata ajira zitakazowaongezea kipato na kuboresha maisha yao,” alisema.
Mbali na kutoa ajira kampuni ya Noble Helium imeanza kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii kwa kujenga madarasa mawili katika Shule ya Msingi Kinambo hatua inayolenga kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto wa eneo hilo.
Akizungumza kwa niaba ya kampuni hiyo msimamizi wa mradi wa ujenzi wa madarasa Christian Temba alisema ujenzi huo ni sehemu ya mchango wa kampuni katika kuunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na wananchi na Serikali katika sekta ya elimu.
Katika ziara hiyo Sangu pia alikabidhi madawati 20 kwa Shule ya Msingi Msia iliyopo Kata ya Milepa. Madawati hayo yametolewa kwa ufadhili wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na yanatarajiwa kunufaisha wanafunzi zaidi ya 60 kwa kuboresha mazingira ya kujifunzia.
Aidha, aliwahakikishia wananchi wa Jimbo la Kwela kuwa ataendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutafuta misaada na rasilimali za kuchangia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa utekelezaji wa ahadi zake za uchaguzi wa mwaka 2025 unaendelea kwa vitendo.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ephraim Konta, alimpongeza Waziri Sangu kwa mchango wake katika miradi ya maendeleo akisema msaada wake wa vifaa vya ujenzi umechangia kukamilika kwa ujenzi wa madarasa katika Shule za Msingi Lwanji na Kanyala hatua iliyotoa unafuu kwa wananchi wengi.
Jumuiya ya Afya ya Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini (ECSA-HC), kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Tanzania na wadau mbalimbali, imeandaa kambi maalum ya huduma za madaktari bingwa na bobezi iliyoanza Julai 20 hadi 30 mwaka huu katika Hospitali ya Rufaa ya Arusha Mount Meru na Hospitali ya Kanda ya Kusini ya Mtwara.
Akizungumza Jijini Arusha kuhusu kambi hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ECSA-HC, Dkt. Ntuli Kapologwe, amesema kambi hizo zinalenga kuwahudumia wananchi wenye mahitaji mbalimbali ya upasuaji na huduma za kitabibu, huku ECSA ikitoa shilingi milioni 211 kufanikisha zoezi hilo.
Amesema kati ya fedha hizo, shilingi milioni 52 zitatumika kununua vifaa tiba, dawa na mahitaji mengine muhimu, huku shilingi milioni 158 zikielekezwa kugharamia wataalamu pamoja na madaktari bingwa na bobezi watakaotoa huduma kwa takribani siku 10.
Dkt. Kapologwe ametoa shukrani kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Waziri Mohammed Mchengerwa na Katibu Mkuu Dkt. Grace Maghembe kwa ushirikiano mkubwa walioutoa katika maandalizi ya zoezi hilo na wadau mbalimbali, wakiwemo mabenki, kwa michango yao iliyowezesha kufanikisha utekelezaji wa kambi hizo.
Amesema mbali na kupunguza maumivu na kuwasaidia wananchi wenye uhitaji wa huduma za kibingwa, lengo kuu la mpango huo ni kuwawezesha wagonjwa kurejea katika hali yao ya kawaida ili waendelee kushiriki katika shughuli za uzalishaji na kuchangia maendeleo pamoja na pato la Taifa.
Ameongeza kuwa zoezi hilo ni sehemu ya programu ya ECSA inayotekelezwa katika nchi mbalimbali, baada ya kufanyika Lesotho na Uganda, huku Tanzania na Malawi zikitekeleza kambi hizo kwa kipindi na tarehe zinazofanana.
Halikadhalika, Dkt. Kapologwe amewataka wananchi wenye uhitaji wa huduma za upasuaji kujitokeza kwa wingi kupata huduma hizo ili warejee katika katika afya njema na maisha yao ya kawaida.
Nikiwa nimevalia shela langu la harusi, nikisubiri kuingia kanisani, mlango wa chumba changu ulifunguka kwa nguvu. Alikuwa ni bwana harusi mtarajiwa, akiwa na uso wa baridi, na kuniambia maneno yaliyosimamisha moyo wangu: “Siwezi kufanya hivi. Harusi imefutwa.”
Saa moja tu kabla ya kiapo, aliondoka na kuniacha nikiwa nimechanganyikiwa, nikilia kwa uchungu na aibu kubwa mbele ya wazazi wangu. Ndoto yangu ya miaka minne ilisambaratika kwa sekunde chache.
Ndugu walibaki wameduwaa, na sherehe iligeuka kuwa msiba wa kihisia. Nilihisi sitaweza kamwe kuinua uso wangu mbele ya jamii tena. SOMA ZAIDI.
Hata hivyo, ukweli wa mitaani ulikuwa tofauti kabisa. Miaka minne ilipita nikiwa nazurura na bahasha ya vyeti chini ya jua kali, nikituma maombi ya kazi kila kona bila mafanikio yoyote.
Kila usaili niliompata uliishia kwa kuambiwa “tutakutafuta,” maneno ambayo yalikuwa ishara ya kukataliwa.
Simu yake ilianza kuwekwa nenosiri (password) kali, safari za kikazi za ghafla zilipishana, na upendo wake kwangu ulianza kupoa. Kila nilipomuuliza, alinituhumu kwa kuwa na wivu usio na msingi. Niliumia moyoni na kukosa amani ya nafsi.
Kilele cha sintofahamu hii kilikuja kudhihirika siku tuliyofanya sherehe kubwa ya kifamilia nyumbani kwetu, tukiwa tumewaalika ndugu, jamaa, na marafiki zetu wa karibu.
Na.Mwandishi Wetu
Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela ( NM- AIST) inatumia mbio za marathon kama moja ya mikakati ya kupata fedha za kutoa ufadhili wa masomo kwa wanawake na wasichana ili kuongeza ushiriki wao katika masomo ya Sayansi, Teknolojia, Hisabati na Ubunifu (STEM).
Hayo yamebainishwa Julai 19, 2026 Jijini Arusha wakati wa Maadhimisho ya Mbio za Taasisi hiyo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila ambapo amesema kuwawezesha wanawake na wasichana katika masuala ya Sayansi si hisani bali ni uwekezaji wa kimkakati wa Maendeleo ya Taifa
Dkt. Nguvila ameeleza kuwa Dira ya Taifa 2050 inalenga kujenga uchumi wa maarifa unaotegemea ujuzi, utafiti na teknolojia hivyo ametoa wito kwa Taasisi za Elimu ya Juu hususan NM- AIST kuhakikisha tafiti zinazofanyika katika Taasisi hiyoziwe ni zile zizotatua changamoto za wananachi katika sekta za Kilimo, mifugo, madini na viwanda.
Akizungumza awali katika tukio hilo Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula amesema kuwa mbio hizo zilianzishwa mwaka 2024 kuhamasisha wasichana kusoma masomo ya sayansi na kutimiza ndoto zao za kuwa madaktari, wahandisi na watafiti.
"Kwa sasa, Mbio za Mandela zimekuwa alama ya mkoa wa Arusha kwa kuchangia ukuaji wa sekta za michezo, elimu, sayansi, afya na utalii. Tukio hili limeweka msingi imara wa kujenga taifa lenye ujumuishi, mshikamano, na kuandaa kizazi kipya cha wanasayansi na wabunifu wasichana na wanawake," amesema Prof Kipanyula
Mbio hizo zilizohusisha umbali wa kilomita 2.5, 5 10 na 21 zimevuta ushiriki mkubwa wa jamii kutoka ndani na nje ya nchi, na kufanya azma ya kuifanya Arusha kitovu cha sayansi na ubunifu barani Afrika kuwezekana.
Mbio za NM- AIST za Mwaka 2026 zina kauli mbiu isemayo Jitihada kwa Sayansi Hatua kwa Mafanikio.

Hata hivyo, miezi michache baada ya kuanza, nilikumbana na mtihani mzito uliotishia kufunga biashara yangu na kuniazima deni kubwa la benki.
Kila wiki, mashine zilikuwa zinaharibika bila sababu yoyote ya msingi. Mara mota ziungue, mara vipuri vikatike, au mifumo ya umeme ivurugike kabisa. Mafundi walikuja na kubadilisha vifaa vipya, lakini baada ya siku mbili au tatu, mtambo ule ule unajifunga tena.
Nilikuwa nikipoteza mamilioni ya fedha kwa ajili ya matengenezo na kununua vipuri, huku wateja wangu wakiondoka kwa kukosa bidhaa kwa wakati. Nilikuwa naingia hasara kila kukicha, na amani ya moyo ilitoweka kabisa. SOMA ZAIDI.
Tangu siku hiyo, hakurudi, na mawasiliano yalikatika kabisa. Tulimtafuta kila kona hospitalini, vituo vya polisi, na hata kwenye vyombo vya habari lakini hatukupata hata chembe ya matumaini.
Mama yetu alizeeka kwa majonzi, kila kukicha akilia na kutazama mlangoni akihisi labda mwanaye angerudi. Miaka 18 ya upweke, sintofahamu, na simanzi ilianza kutufanya tuamini kuwa labda kaka yetu hayuko hai tena duniani. Furaha ilitoweka kabisa kwenye familia yetu. SOMA ZAIDI.
Licha ya kujitetea kwa nguvu zote na kuonyesha ushahidi, uongozi ulikataa kunisikiliza na kunifukuza kazi mara moja bila hata kiinua mgongo.
Maisha yalibadilika ghafla kuwa magumu mno. Ndani ya miezi sita, nilishindwa kulipa kodi ya nyumba, nikashindwa kuhudumia familia yangu, na marafiki niliokuwa nao kazini walinitenga wakiniogopa kama mhalifu.
Msongo wa mawazo ulinisonga sana nikijua sifa yangu ya miaka mingi imechafuka kwa uongo uliotengenezwa na maadui zangu wa kazini waliokuwa wakionea wivu mafanikio yangu. SOMA ZAIDI.
•Prof. Shemdoe atoa wito kwa sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za watumishi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wananchi wa mvomero la kujengewa shule mbili za Sekondari katika Halmashauri ya Mvomero, ombi ambalo liliwasilishwa kwa niaba yao na Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe. Sara Msafiri pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro Mhe. Josephine Kapoma wakilenga kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji katika Halmashauri hiyo.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 18, 2026 katika kijiji cha Mkindo, kata ya Mkindo, Halmashauri ya Mvomero Mkoa wa Morogoro, mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Mkindo, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma mkoani Morogoro.
"Mhe. Sara Msafiri akishirikiana na pacha wake Mhe. Josephine Kapoma waliniomba tujenge shule nne, nilipokea ombi hilo na kuliwasilisha kwa Mhe. Waziri Mkuu naye akaliwasilisha kwa Mhe. Rais ambaye ameridhia ombi hilo kwa kutoa Shilingi Bilioni 1.1 za kujenga shule mbili, na tayari fedha hizo zimeshaingizwa kwenye akaunti ya Halmashauri," amesema Prof. Shemdoe.
Katika kuhakikisha wananchi waliopo kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa wananufaika na shule hizo, Prof. Shemdoe ameelekeza zijengwe kwenye kata ya Dakawa na Mzumbe kama alivyoomba Mbunge wa Jimbo la hilo la Mvomero, Mhe. Msafiri, huku akitoa wito kwa sekta binafsi kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za walimu nchini.
Aidha, Prof. Shemdoe amesema kabla ya kufika shuleni hapo amekagua, ameweka jiwe la msingi na kuzindua huduma ya upasuaji katika jengo jipya la upasuaji la Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero lenye vifaa tiba vya kisasa, hatua itakayowawezesha wakazi wapatao 459,304 wa wilaya ya Mvomero na maeneo jirani kuwa na uhakika wa kupata huduma ya upasuaji katika hospitali hiyo.
Katika hatua ya kuboresha miundombinu ya elimu Mvomero, Prof. Shemdoe amesema pia ametembelea na kuzindua vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Miembeni yenye thamani ya Shilingi Milioni 115 ambayo imejengwa katika kijiji cha Mvomero, kata ya Mvomero wilayani Mvomero.
“Na sasa nipo hapa na nimeshiriki nanyi katika kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Mkindo katika kijiji hiki cha Mkindo kilichopo kata ya Mkindo, shule ambayo imejengwa baada ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa Shilingi Milioni 528 za ujenzi wa shule hii,” ameeleza Prof. Shemdoe.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Mhe. Sara Msafiri, amemuomba Prof. Shemdoe kufikisha salamu za shukrani za wananchi wa Mvomero kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha ujenzi wa shule ya Sekondari ya Sayansi Mkindo, akisema shule hiyo itazalisha madaktari, wahandisi pamoja na walimu wa masomo ya sayansi.
Naye, Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Josephine Kapoma, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi wa miundombinu ya elimu katika maeneo ya vijijini hususani kwenye kijiji hicho cha Mkindo.
Kila kitu kuanzia mashamba, nyumba, hadi akaunti za benki kilikabidhiwa kwa ndugu zangu na mke wake mdogo. Nilifukuzwa kama mtu baki kwenye mali ambazo mimi mwenyewe nilisumbuka kuzitafuta pamoja na baba yangu.
Ndugu walinitenga na kuniona sifai. Nilijaribu kwenda mahakamani, lakini kesi iligonga ukuta kwa sababu wosia ulikuwa umegongwa muhuri rasmi.
Nilijikuta nikiwa maskini wa kutupwa, ninaishi kwa dhiki, huku wale waliochukua urithi wangu wakicheka na kunisimanga kila siku. Nilijawa na kinyongo, upweke, na sonona kali. SOMA ZAIDI.
Miezi tisa ya mwanzo ilikuwa jehanamu ya kiuchumi. Siku zote zilifanana; nilikaa kwenye kiti kuanzia asubuhi hadi jioni nikitazama mlango, lakini hakuna mtu aliyeingia.








