Na.Mwandishi Wetu
Tume ya Ushindani ya Somali imefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza uzoefu na mbinu zinazotumiwa na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika kusimamia ushindani wa kibiashara, kudhibiti bidhaa bandia na kulinda maslahi ya walaji.
Ziara hiyo imefanywa na Mkurugenzi wa Masuala ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na Kamishna wa Mamlaka ya Ushindani ya Afrika Mashariki (EACA), Bw. Ahmed Warsame pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Upatikanaji wa Masoko wa Wizara ya Biashara na Viwanda ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Bw. Abdihalim Osman.
Katika ziara hiyo, ujumbe huo umekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, pamoja na uongozi wa Tume, ambapo walipata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kukuza na kulinda ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, uongozi wa ujumbe wa Somalia umepongeza utendaji wa FCC, ukieleza kuwa uzoefu wa Tanzania katika kusimamia ushindani na kulinda mlaji ni muhimu kwa Somalia katika kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa soko na kukuza mazingira bora ya biashara.
Ujumbe huo umeeleza kuwa kujifunza kutoka FCC kutasaidia kuongeza uelewa na uwezo wa taasisi za Somalia katika kukabiliana na changamoto zinazohusu ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwadhuru walaji.
Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema kuwa Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na taasisi za Somalia na nchi nyingine katika kubadilishana uzoefu, maarifa na mbinu bora za usimamizi wa ushindani na ulinzi wa walaji.
Ziara hiyo ya siku moja imekuwa fursa muhimu kwa Somalia kujifunza uzoefu wa Tanzania katika eneo la ushindani wa kibiashara, udhibiti wa bidhaa bandia na ulinzi wa mlaji, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi na kuchangia katika ujenzi wa masoko yenye ushindani wa haki na biashara endelevu.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa Malaigwanani ,wazee na kina mama maarufu wapatao 33 kutoka kata 11 za ndani ya eneo la hifadhi Ngorongoro ili kuwajengea uwezo wa kutambua fursa mpya za kiuchumi.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kamishina Msaidizi Mwandamizi anayeshughulikia huduma za jamii bi Gloria Bideberi amesema lengo la semina hiyo ni kuhakikisha Malaigwanani na wazee hao wanapata elimu ya kutosha kuhusu ujasiriamali na namna ya kutumia fursa zinazopatikana katika maeneo yao.
Bi. Gloria alieleza kwamba elimu hiyo itakwenda sambamba na ziara za kujifunza kwa vitendo, ambapo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ikiwemo kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za maziwa Tanga Fresh kilichopo Mkoani Tanga ili kujifunza namna bidhaa zinavyozalishwa, kuendelezwa na kufikishwa katika masoko.
“Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha kuwa wananchi hawa wanapata elimu ya kutosha na kuwawezesha kutembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ili kujifunza kwa vitendo zaidi,” alisema Gloria
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuimarisha ushiriki wa jamii katika maendeleo endelevu ya eneo la Hifadhi Ngorongoro.

Na; Mwandishi Wetu- Dar es Salaam
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Makatibu Wakuu kutoka katika Wizara zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), Wakuu wa Taasisi pamoja na Wakurugenzi wa Sekta, pamoja na wataalam kutoka katika sekta hizo na Ujumbe Kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mtaa wa Magogoni Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Septemba 2026.
Kikao hicho kimefanyika baada ya ziara maalumu ya wataalamu kutoka IFAD na AFDP kukamilisha ziara ya kutembelea maeneo yanayotekeleza Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi ya kupima matokeo utekelezaji wa program ya muda wa kati (MTR)

Pamoja na mambo mengine IFAD wamepongeza Serikali kwa Kusimamia vyema Shughuli za Programu kwa kuleta matokeo chanya kwa wananchi..Aidha kikao hicho kimepokea wasilisho la dondoo lnayoainisha hoja za makubaliano yaliyopendekezwa kuhusiana na mwenendo wa utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP).


Jukwaa hilo linatoa nafasi kwa nchi na wadau mbalimbali kubadilishana uzoefu na kujadili masuala yanayohusu mustakabali wa akili unde, ikiwemo namna ya kuimarisha mifumo ya sera na utawala, kujenga uwezo na kuhakikisha teknolojia hiyo inatumika kwa kuzingatia haki za binadamu, usalama, usawa na uwajibikaji.

Kwa Tume ya Taifa ya UNESCO, ushiriki huo ni sehemu ya kuendelea kuunganisha Tanzania na UNESCO katika mijadala na ajenda za kimataifa zinazohusu sayansi, teknolojia, elimu, utamaduni na maendeleo ya jamii.
Tume inawakilishwa katika jukwaa hilo na Bi Fides Mallya, Afisa Programu kutoka Sekta ya Sayansi Jamii ya Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anayeshiriki katika shughuli na mijadala mbalimbali inayoendelea katika jukwaa hilo.


























.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

