Na Alex Sonna, Dodoma

WAZAZI jijini Dodoma wamesema elimu ya vipimo inayotolewa kupitia Klabu za Vipimo katika shule za msingi imeanza kuleta mabadiliko ndani ya familia, baada ya watoto waliopatiwa mafunzo na Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) kuanza kuwafundisha wazazi wao namna ya kutambua vipimo sahihi na kujilinda dhidi ya upunjaji katika manunuzi.

Wazazi wameyasema hayo  Septemba 18,2026  wakati wa mahafari ya wanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Mtemi Mazengo jijini Dodoma ambapo  wanafunzi wa klabu ya vipimo walikuwa wakitoa elimu ya vipimo kwa wazazi na watu wengine mbalimbali waliohudhuria akiwemo Mgeni Rasmi.

Mzazi wa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mtemi Mazengo, Bertha Paulo Chipaga, amesema mtoto wake, Gloria Elisha Enock, amekuwa akimsaidia kuelewa matumizi sahihi ya mizani ya chakula, mita ya maji na vipimo vingine, jambo ambalo limempa uelewa na kujiamini zaidi kama mlaji.

Bi.Chipaga amesema awali hakuwa na uelewa mpana kuhusu namna ya kutambua kama kipimo kinachotumika katika biashara ni sahihi, lakini tangu mtoto wake ajiunge na Klabu ya Vipimo amekuwa akipata elimu hiyo nyumbani na sasa anaelewa umuhimu wa kuhakikisha bidhaa anayonunua inalingana na kiasi cha fedha anacholipa.

"Hatua hiyo inaonesha kuwa elimu inayotolewa kwa watoto haiishii shuleni, bali inasambaa hadi kwenye familia na jamii, hivyo akawataka wazazi wengine kutumia fursa hiyo kuwaelimisha watoto wao kuhusu haki za mlaji na matumizi sahihi ya vipimo."amesema Bi.Chipaga

Akizungumza kuhusu umuhimu wa kuwaandaa watoto na elimu hiyo, mkazi wa Makao Mapya jijini Dodoma, Peter Daudi Mponzi, amesema mafunzo ya vipimo kwa wanafunzi ni uwekezaji muhimu kwa jamii kwa sababu yanawajengea uwezo wa kutambua mizani na vipimo visivyo sahihi wanapokuwa katika mazingira ya biashara.

Amesema mtoto anayeelewa vipimo anaweza kwenda dukani na kuangalia kama mzani unaotumika umehakikiwa, hivyo kupunguza uwezekano wa yeye au familia yake kupunjwa na wakati huo huo kueneza elimu hiyo kwa watu wengine.

Mponzi amesema kuanzia elimu hiyo katika umri mdogo kunaweza kujenga kizazi chenye uelewa mpana wa masuala ya vipimo na haki za walaji, kwa kuwa watoto wanakuwa na nafasi ya kutumia maarifa hayo katika maisha yao ya kila siku.

 "Watoto wanapotoka shuleni na kwenda majumbani, dukani na katika maeneo mengine ya jamii, wanakuwa sehemu ya mnyororo wa elimu unaoweza kuwafikia wazazi, ndugu na wananchi wengine, hivyo kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi."amesema

Mwanafunzi wa Klabu ya Vipimo katika Shule ya Msingi Mtemi Mazengo, Gloria Elisha Enock, amesema WMA imewajengea uwezo wa kuelewa maana na umuhimu wa vipimo pamoja na jukumu la Wakala la kumlinda mlaji.

Amesema wamefundishwa kuwa WMA huhakiki vipimo mbalimbali, ikiwemo mizani, mita za maji na umeme, pamoja na bidhaa zilizofungashwa, huku mlaji akitakiwa kuangalia alama ya WMA kwenye mizani ili kuhakikisha kipimo  hicho kimehakikiwa na kinafanya kazi kwa usahihi.

Kwa upande wake, mwanafunzi mwenzake, Venosa Michael Simba, amesema elimu hiyo imemsaidia kubadilika kutoka kuwa mtoto anayekwenda dukani bila kuzingatia usahihi wa vipimo hadi kuwa mfuatiliaji na mtoa elimu kwa jamii.

Amesema baada ya kupata mafunzo hayo aligundua hata nyumbani kwao kuwa mita ya maji ilikuwa haijahakikiwa na akaweza kutoa elimu kwa watu waliokuwa hawajui umuhimu wa kuhakiki vipimo.

 "kabla ya kupata elimu hiyo alikuwa akienda dukani bila kuangalia chochote, lakini sasa anaelewa kuwa mlaji ana wajibu wa kuhakikisha anapata kiasi sahihi cha bidhaa anayolipia."amesema

Kwa ujumla, Klabu za Vipimo za WMA zimeanza kuwa darasa la vitendo la kuwaandaa watoto kuwa mabalozi wa ulinzi wa mlaji, huku elimu hiyo ikitoka shuleni na kuingia moja kwa moja katika familia na jamii.

Mpango huo unaongeza uelewa wa wananchi kuhusu matumizi ya vipimo sahihi, unasaidia kujenga utamaduni wa kuhoji na kuthibitisha vipimo vinavyotumika katika biashara na, kwa muda mrefu, unaweka msingi wa kizazi kinachothamini uadilifu, usawa na uwazi katika shughuli za kiuchumi.

 

ZANZIBAR, Septemba 19, 2026 — Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amewataka Wakuu wa Taasisi za Muungano kuimarisha ushirikiano na utekelezaji wa majukumu yao ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora bila kujali wanaishi upande gani wa Muungano.
Na Mwandishi Wetu

Mkururugenzi wa shule ya Green Acres ya Mbezi Beach Salasala jijini Dar es Salaam, Jacklline Rushaigo ameelezea namna shule hiyo ilivyoanza kufundisha Teknojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA ili kwenda sanjari na ulimwengu kidijitali.
Mfanyabiashara maarufu nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi, akizungumza katika Jukwaa la Nne la Biashara la Watendaji Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum).
Mfanyabiashara maarufu nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi, akizungumza katika Jukwaa la Nne la Biashara la Watendaji Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum)
Mfanyabiashara maarufu nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi, akiwa katika Jukwaa la Nne la Biashara la Watendaji Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum)

***
Mfanyabiashara maarufu nchini na kanda ya Afrika na Mwenyekiti wa Taifa Group , Rostam Azizi, amehimiza uwepo wa uongozi imara, taasisi madhubuti, sera nzuri na uwazi wa mifumo ili kufungua zaidi fursa za uwekezaji na mitaji ya kimataifa katika nchi za kanda ya Afrika Mashariki.

Akiongea kwenye Jukwaa la nne la Biashara la Watendaji wakuu 200 (200 CEOs Business Forum) linalowakutanisha pamoja wafanyabiashara na wawekezaji nchini, alisema ushirikiano wa kweli kati ya wawekezaji, wafanyabiashara na Serikali utajengwa kwenye misingi ya mifumo mathubuti ya kikodi, kisera kikanuni na sheria nchini na kwenye nchi nyinginezo za Afrika Mashariki.

Rostam alisema wadau wote wanapaswa kujikita kuangalia ni kwa namna ipi tunaweza kuifanya Afrika Mashariki kuwa chaguo kuu la uwekezaji wa mitaji ya mitajiya kimataifa.

“Nianze kwa kuwapongeza waandaaji wa Kongamano la Biashara la Wakurugenzi Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum) kwa kuwaleta pamoja viongozi wa Serikali, Sekta binafsi na wawekezaji na suala la msingi la kujadili ni jinsi gani tuanaweza kuifanya Afrika Mashariki kuwa chaguo kuu la mitaji wa kimataifa”, alisema Rostam Azizi.

Alisema rasilimali nyingi za asili, idadi ya watu na eneo la kijiografia havitoshi kuhakikisha uwekezaji wa muda mrefu kutoka kwa wawekezaji wa kimataifa kuja kuwekeza bali pia kunatakiwa uwepo mazingira ya kuwakikishia uhakika,utulivu ,ukuaji na kuwajengea imani.

Alisisitiza jukwaa hili kutoka na maamuzi yenye kuleta athari kubwa kwa utekelezaji wa mitaji na pamoja na mambo mengine kujua sekta zinazokua na ajira jinsi ya utengenezaji wa ajira mpya ndani ya Afrika Mashariki sambamba na kujua taasisi za kifedha zinazowezesha biashara na ufadhili, viwanda vinavyoongeza thamani ya fedha, makampuni ya madini yanayofungua fursa za rasilimali na makampuni ya mawasiliano yanayofanya vizuri ili kuwaunganisha mamilioni ya watu ndani ya Ukanda wa Afrika Mashariki.
“Niruhusuni kuzungumza kutokana na uzoefu wangu, katika kipindi cha zaidi ya miaka thelathini, kupitia Taifa Group pamoja na washirika wetu mbalimbali, nimepata fursa ya kuwekeza katika sekta za mawasiliano, madini, nishati, usafiri wa anga, vyombo vya habari na miundombinu,” amesema Rostam Azizi.

Aliongeza kwamba watu wengi hudhani kuwa uwekezaji unaanza na uchambuzi wa kifedha ambapo si kweli bali wawekezaji wengi wanataka imani na mwelekeo wa nchini husika pamoja na makubaliano kuheshimiwa na sera ambazo zinaweza kutabirika.

Pamoja na mambo mengine alilisitiza umuhimu wa kuwa na taasisi imara na zenye kuaminika na kanuni zilizo wazi na mazingira mazuri ya uwekezaji na madhubuti yanayoweza kutabirika kisheria na kitaasisi ambayo yataleta matokeo chanya.

Alisema Afrika Mashariki si eneo la matarajio pekee ni fursa halisi ambayo inahitaji mageuzi ya haraka ya kidigitali, na mikakati kabambe ya kufikia njia kuu za biashara za dunia ili kufugua milango ya fursa ya mitaji ya kimataifa.

“Ari ya ujasiriamali ndani ya Afrika mashariki na ukauaji wa soko la walaji ni fursa ya kipekee wa wanajumuiya wa kuunganisha nguvu pamoja ili kuleta mapinduzi ya kweli kwenye uwekezaji. Tanzania iko katikati ya fursa hiyo na bandari zetu zinaunganisha uchumi wetu pamoja na nchi jirani zisizo na bandari na dunia tambayo hutoa fursa ya kufikia masoko ya kikanda na kimataifa,”alisisitiza.
Aliongeza kwamba uwekezaji katika bandari, reli ya Standard Gauge Railway (SGR) , nishati , mifumo ya usafirishaji na mawasiliano ya kidigitali unaimarisha nafasi hiyo kwa kupunguza gharama za biashara na kuongeza tija.

Alisema kwa pamoja , nchi za Afrika Mashariki zinawakilisha soko la zaidi ya watu milioni 300, ikiwa na rasilimali nyingi za asili , idadi kubwa ya vijana na miundombinu inayozidi kuimarika.

“Hakuna nchi moja katika ukanda wetu yenye kila faida ya ushindani , hakuna uchumi mmoja wenye kila rasilimali, hakuna soko moja linaloweza kufikia uwezo wake kamili likiwa peke yake,” alisisitiza.

Rostam Azizi alisema ni muhimu kwa serikali za Afrika Mashariki kuanza mchakato wa kuimarisha miumdombinu inayovuka mipaka , kupunguza vikwazo vya kibiashara , kuimarisha ushirikiano wa kifedha na kurahisisha usafirishaji wa mitaji, bidhaa na wataalamu wenye ujuzi ndani ya ukanda huo.

Aliongeza kuwa jukumu la serikali, ni kuendelea kujenga mazingira bora na yanayotabirika kwa uwekezaji na biashara na inajumuisha kudumisha uthabiti wa uchumi wa jumla, kuimarisha miundombinu, kuboresha mazingira ya udhibiti, kuwezesha uwekezaji, kuongeza upatikanaji wa mitaji na kuimarisha taasisi za umma.

Alitoa rai kwa sekta binafsi kuhakikisha zinaongeza tija huku zikiimarisha utawala bora katika biashara zao na kutumia teknolojia za kisasa pia ziendeleze rasilimali watu na zijenge biashara zinazoweza kushindana ndani ya Tanzania, Afrika Mashariki na kwingineko.


Jina langu ni Asha. Kupenda kwa dhati kisha ukawa unagawana mpenzi wako na mchepuko wa kila aina ni mateso yanayoweza kukuondolewa amani na furaha ya maisha.

Kwa muda mrefu, mimi na mpenzi wangu tulikuwa kwenye mahusiano, lakini tabia yake ya umalaya na tamaa za nje ilikuwa ikiniliza kila siku.

Kila nilipomfumania au kumuonya kuhusu tabia yake ya kutembea na wanawake wengine, alikuwa akiahidi kubadilika lakini baada ya siku chache alirudia pale pale.

Nilibaki nikiumia sana moyoni, nikikosa amani na kufikiria jinsi gani alivyokuwa akichukua pesa na pendo letu na kwenda kuwapa watu wa nje, huku mimi nikiambulia dharau na maumivu.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na nikitafuta njia ya kuokoa pendo langu na kuzuia asitoke nje tena, rafiki yangu wa karibu alinitembelea.

Baada ya kumsimulia machozi na mateso niliyokuwa nakumbana nayo, alinieleza kwa huruma kuwa wapo wataalamu wa kiasili wanaoweza kumfunga mpenzi ili asione wala kutamani mtu mwingine yeyote zaidi yako. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Neema. Kufikisha umri wa ukubwani bila kuwa na mpenzi wa dhati wala matumaini ya kuanzisha familia ni jaribu linaloweza kumvunja mtu moyo na kumpa msongo mkubwa wa mawazo.

Kwa miaka mingi, nilikuwa nikitamani sana kupata mwanamume mwenye mapenzi ya kweli ili tujenge maisha na familia ya pamoja, lakini kila mahusiano niliyoyaanzisha yalikuwa yakiishia njiani bila sababu za msingi.

Wanaume walikuwa wakitokea, wanaonyesha kunipenda kwa muda mfupi, lakini ghafla walibadilika, kunikimbia, na kutoweka kabisa wakiniacha na maumivu na maswali mengi yasiyo na majibu.

Nilibaki nikishinda na huzuni huku wenzangu wote wakiolewa na kupata watoto, mimi nikionekana kama mtu aliyeandikiwa kuishi kwa upweke maisha yangu yote.

​Nikiwa kwenye simanzi nzito na kuanza kukata tamaa kabisa ya kupata mume wa ndoto zangu, shangazi yangu aliyekuwa akitambua mateso yangu alinitembelea.

Baada ya kumueleza jinsi nilivyokuwa nikidhulumiwa kimapenzi na kuachwa kila mara, alinieleza kwa huruma kuwa mara nyingi mikosi ya kukataliwa au kukosa bahati ya ndoa hutokana na vifungo vya kishirikina na nuksi zilizowekwa ili kufunika nyota yako ya mapenzi. SOMA ZAIDI.
Jina langu ni Mwajuma. Kukosa usingizi wa amani na kuota ndoto za kutisha kila siku ni mateso makubwa yanayoweza kumnyima mtu furaha ya maisha na kumfanya aishi kwa hofu masaa yote.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilikuwa nikiteseka sana kila nikienda kulala usiku. Nilikuwa nikiota ndoto za kufukuzwa na wanyama wakali, kuogelea kwenye maji machafu, au kulishwa vitu visivyoeleweka usiku wa manane.

Siku zingine nilishtuka usiku nikiwa nimebanwa pumzi na kuhisi kama kuna mtu mzito aliyekuwa amenikalia kifuani.

Hali hii ilinifanya niogope hata kufumba macho usiku, nikawa naamka asuhi nikiwa nimechoka sana mwilini, nina maumivu ya kichwa, na sina nguvu za kufanya kazi zangu za kila siku.

​Nikiwa kwenye simanzi na msongo mkubwa wa mawazo baada ya kwenda hospitali na kuambiwa sina ugonjwa wowote wa kimwili, mama yangu mdogo alinitembelea.

Baada ya kumueleza jinsi ndoto hizo za kutisha zilivyokuwa zikininyima amani na kunirudisha nyuma kimaisha, alinieleza kwa huruma kuwa ndoto za namna hiyo mara nyingi hutokana na vifungo vya kishirikina, kulishwa uchawi ndotoni, au mikosi iliyowekwa na maadui ili kuharibu nyota yako. SOMA ZAIDI.



Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amewaagiza Makamishna wa Ardhi Wasaidizi katika mikoa yote nchini kufanya ukaguzi wa maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali kwa lengo la kubaini maeneo yasiyoendelezwa na kutoa taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe

Dkt. Akwilapo ametoa agizo hilo Septemba 18, 2026, mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika maeneo ya uwekezaji ya Kongani ya Viwanda ya KAMAKA pamoja na kiwanda cha Nondo cha Gain Company Limited kilichopo Mlandizi, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.

Amesema Wizara ya Ardhi, imebaini kuwepo kwa maeneo ambayo yalipewa wawekezaji kwa ahadi ya kuanzisha viwanda au shughuli nyingine za uzalishaji, lakini hayajaendelezwa kwa muda uliokubaliwa.

“Tuna taarifa kuna waliochukua maeneo wakasema watatengeneza viwanda lakini bado hawajafanya hivyo. Natoa maelekezo makamishna kufanya ukaguzi na kuwasilisha taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe kwa maeneo yasiyoendelezwa kadri ya mikataba waliyoingia,” amesema Dkt. Akwilapo.

Aidha, Waziri huyo amewataka wamiliki wote wa ardhi ambao hawazingatii masharti ya uendelezaji maeneo waliyopewa kuhakikisha wanayaendeleza kwa wakati, vinginevyo wizara itachukua hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

Amesisitiza kuwa, hatua hizo zitawahusu wawekezaji wazawa na wa kigeni, akieleza kuwa kwa wawekezaji wazawa hatua inaweza kujumuisha kubadilisha milki za ardhi walizopewa, huku kwa wawekezaji wa kigeni wizara ikishirikiana na taasisi husika, ikiwemo TISEZA, katika kushughulikia masuala ya umiliki na uwekezaji.

Dkt. Akwilapo amesema, hatua hiyo inalenga pia kujibu malalamiko kutoka kwa wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa ajili ya uwekezaji, lakini baadaye hayakuendelezwa.

Ameeleza kuwa, hali hiyo imekuwa ikisababisha wananchi kuhoji sababu za maeneo kutolewa kwa wawekezaji ambao hawajaanza shughuli za maendeleo kwa muda mrefu.

Awali Mhe Dkt Akwilapo alielezwa kuwa eneo la Kongani ya Viwanda Mlandizi wilayani Kibaha mkoa wa Pwani linakabiliwa na changamoto kadhaa kama vile upatikanaji wa maji na ubovu wa barabara hali waliyoieleza kuwa inayosababisha kero katika usafirishaji bidhaa na malighafi.

Hata hivyo, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wameeleza kuanza  kuchukua hatua za dharura kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi wa muda mfupi na mrefu

Ziara ya Dkt. Akwilapo katika Mkoa wa Pwani imelenga kujionea kwa karibu shughuli za uwekezaji na matumizi ya ardhi katika maeneo hayo, pamoja na kutathmini namna bora ya kuendeleza maeneo ya uwekezaji kwa kuzingatia mipango ya matumizi ya ardhi na maendeleo endelevu.

Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi za kutambua fursa na changamoto zinazohusiana na ardhi na uwekezaji, kwa lengo la kuimarisha matumizi bora ya ardhi, kuvutia uwekezaji na kuchochea maendeleo ya wananchi

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano la Sita la Jumuiya ya Taasisi za Mitaala Afrika (ACA), litakalofanyika Septemba 22 hadi 25, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.
TAASISI ya Tanzania Pathways Initiative (TPi) imeungana na jamii ya Kawe Ukwamani jijini Dar es Salaam katika zoezi la usafi wa mazingira, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha jiji linakuwa safi na salama.

 

Na Mwandishi Wetu.

Washiriki wa mafunzo kwa Waandishi wa Habari kutoka Wasafi Media wameeleza kuwa mada zilizotolewa katika mafunzo hayo zimewasaidia kutambua makosa yaliyokuwa yakijirudia katika utekelezaji wa majukumu yao na kuwapatia mwongozo wa kuboresha utendaji.

Wakizungumza wakati wa tathmini ya mafunzo hayo yaliyofanyika Septemba 17 na 18, 2026, katika Ofisi za Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) jijini Dar es Salaam, Gerald Hando, Aggai Kifumu na David Rwenyagira wameeleza kuwa mafunzo yamewaongezea uelewa kuhusu sheria, maadili na uzalendo katika uandishi wa habari.
Wamebainisha kuwa miongoni mwa changamoto zinazowakabili Waandishi wa Habari na wazalishaji wa maudhui ni shinikizo la kuongeza idadi ya wafuasi katika majukwaa ya kidijitali, kukidhi matakwa ya hadhira pana na kasi ya mabadiliko katika mazingira ya kidijitali kuwa kubwa kuliko maboresho ya baadhi ya sheria zinazoongoza shughuli zao.

Kwa mujibu wa washiriki hao, mazingira hayo yanaweza kusababisha baadhi ya Waandishi wa Habari kufanya kazi kwa mazoea au kujikuta wakifanya makosa ya kisheria na kimaadili bila kuwa na uelewa wa kutosha.
Wamesema mafunzo hayo yamewajenga kitaaluma, yamewafungua kutoka katika utendaji wa mazoea na kuwapatia mwongozo wa kufanya maamuzi sahihi katika majukumu yao ya kila siku.

Aidha, wameiomba JAB kuendelea kutoa mafunzo hayo kwa Waandishi wa Habari kutoka vyombo vingine, huku kipaumbele kikitolewa kwa wanaofanya kazi na kuzalisha maudhui kupitia majukwaa ya kidijitali, ambako changamoto za uzingatiaji wa sheria na maadili zimeendelea kujitokeza.
Wamesema kasi ya uzalishaji na usambazaji wa maudhui katika majukwaa hayo imeongeza uwezekano wa kutokea kwa makosa ya kisheria na kimaadili, hivyo elimu endelevu inahitajika ili kuimarisha weledi na uwajibikaji.

Mafunzo hayo yalihusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya uandishi wa habari na uzalendo, yakilenga kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari na watangazaji wa Wasafi Media kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, viwango vya taaluma na maslahi ya jamii.
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas imekabidhi mitungi ya gesi 600 na vifaa vyake kwa wananchi wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wanapata fursa ya kutumia nishati safi, salama na rafiki kwa mazingira.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza kuchukua tahadhari kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño, baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kueleza kuwa mvua hizo zinatarajiwa kuimarika katika maeneo mbalimbali nchini kuanzia wiki ya nne ya Septemba hadi Oktoba mwaka huu.




Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amewaonya wananchi wanaovamia maeneo kwa nguvu na kuunda vikosi vya ulinzi kwa ajili ya kulinda maeneo hayo, akisema Serikali haitavumilia vitendo hivyo na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Dkt. Akwilapo ametoa onyo hilo leo Sept 17, 2026 wakati akizungumza na wananchi katika Kliniki ya Ardhi iliyofanyika Kata ya Zingiziwa, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Amesema, wananchi hawapaswi kujichukulia sheria mkononi kwa kuvamia maeneo yanayomilikiwa na watu wengine na kuanzisha vikosi vya ulinzi kwa lengo la kuyadhibiti kwa nguvu.

“Serikali haitavumilia vitendo vya watu kujichukulia sheria kwa kuvamia maeneo ya wananchi wengine na kuunda vikosi vya ulinzi kwa lengo la kulinda maeneo hayo kwa nguvu,” amesema Dkt. Akwilapo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bw. Elihuruma Mabelya, amesema hadi sasa jumla ya hati miliki 545 zimetolewa kwa wananchi kupitia Kliniki hiyo ya Ardhi.

Mabelya ameeleza kuwa, timu ya wataalamu itaendelea kuwepo katika eneo hilo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za ardhi kwa urahisi na kwa wakati, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Wizara.

Baadhi ya wananchi, kupitia Diwani wa Kata hiyo, wameipongeza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kusogeza huduma za ardhi karibu na maeneo yao.

Wameielezea hatua hiyo kuwa  imewapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu pamoja na gharama kubwa walizokuwa wakitumia ili kufuata huduma hizo



 


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Mark Kihula, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Septemba 18, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO, kuhusu utekelezaji wa Taasisi hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa 2026/27.


Na Mwandishi Wetu - DODOMA


Wakala wa Vipimo Nchini (WMA), umeonya wafanyabiashara wanaotumia vipimo visivyo sahihi au kuuza bidhaa kwa vipimo visivyokidhi viwango kwamba wanakabiliwa na adhabu kali kwa mujibu wa sheria, ikiwemo faini na kifungo

Akizungumza na waandishi wa habari Septemba 18, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Mtumba jijini Dodoma, Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Bw. Alban Kihulla, amesema mtuhumiwa anayekubali kosa anaweza kutozwa faini ya Shilingi 100,000 hadi 20,000,000 kwa kosa moja, huku anayekataa kosa na kupatikana na hatia anapelekwa Mahakamani na kutozwa faini ya Shilingi laki tatu hadi milioni 50, au faini na kifungo kisichozidi miaka miwili.

Amesema kwa mkosaji wa mara kwa mara, faini inaweza kuwa kati ya Shilingi 500,000 na milioni 100 kwa kosa moja, hatua inayolenga kuhakikisha wafanyabiashara wanazingatia matumizi ya vipimo sahihi na kulinda haki za walaji.

Bw. Kihulla amewataka wakulima kuachana na matumizi ya magunia, madebe, makopo, mafungu na vipimo vingine visivyo rasmi katika biashara ya mazao, akisisitiza matumizi ya mizani kwa kuwa kilo ndiyo kipimo kinachotambulika katika biashara kote duniani.

Amesema matumizi ya vipimo visivyo rasmi yanaweza kusababisha kutokuwepo kwa usawa katika biashara, hivyo wananchi wanapaswa kudai kupimiwa bidhaa kwa mizani ili kuhakikisha wanapata kiasi halisi wanacholipia.

“Madebe, makopo, visado na mafungu siyo vipimo, wafanyabiashara tumieni mizani,” amesisitiza Kihulla, akieleza kuwa WMA inahakikisha kilo moja inakuwa kilo moja na vipimo vyote vinazingatia viwango vinavyotambulika.

Aidha, amesema WMA haisimamii vipimo vya bidhaa pekee, bali inahakikisha usahihi wa vipimo katika sekta mbalimbali kwa mujibu wa sheria za kitaifa, kikanda na kimataifa.

Bw. Kihulla ametoa mfano wa sekta ya afya, ambako vipimo vya uzito vimekua vikihakikiwa ili kuhakikisha mgonjwa anapata uzito halisi, jambo linalomsaidia daktari kuamua kiwango sahihi cha dawa kinacholingana na uzito wa mgonjwa.

Amewataka wananchi kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya matumizi ya vipimo visivyo sahihi kwa kutoa taarifa wanapobaini au kuhisi kuwa vipimo vinavyotumika au walivyopimiwa si sahihi kwa kuwasiliana na WMA kupitia namba 08001197 ili kutoa taarifa na kupata msaada na kuwezesha hatua stahiki kuchukuliwa.



Na Mwandishi Wetu, Kibaha.

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Mashariki, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Bohari ya Dawa (MSD), imetoa mafunzo maalum kwa Waganga Wafawidhi, Wafamasia, Wauguzi na Wakaguzi wa dawa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Manispaa ya Kibaha Mjini, September 18, 2026.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yusuf Masauni, amezindua na kukabidhi magari matano kwa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), hatua inayolenga kuimarisha shughuli za ukaguzi, ufuatiliaji na upimaji wa mazingira nchini.
Naitwa James kutoka Nyandarua. Kwa muda mrefu nilikuwa mfanyabiashara mdogo nikijitahidi kujenga maisha yangu kupitia duka la bidhaa za kila siku. Mwanzoni biashara yangu ilikuwa ikienda vizuri, lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Bidhaa zilianza kukwama sokoni, wateja wakapungua, na mara nyingine nilikuwa napata hasara bila kuelewa chanzo.
Nilijaribu kubadilisha bidhaa, kupunguza bei, na hata kubadili eneo la mauzo, lakini bado hali haikubadilika. Kila wiki ilikuwa kama napoteza zaidi kuliko ninavyopata.

Hali hiyo ilinifanya niingie kwenye msongo wa mawazo. Nilianza kujiuliza kama biashara siyo sehemu yangu kabisa. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu changamoto zangu. SOMA ZAIDI.

Fatuma Juma, mkazi wa Mombasa, alikuwa amezoea maisha ya upweke kwa karibu miaka mitatu baada ya mume wake kumwacha bila maelezo. Kila siku alijikuta akijiuliza ni wapi alikosea katika ndoa yao iliyodumu kwa miaka saba kabla ya matatizo kuanza.

Kwa mujibu wa Fatuma, mume wake alianza kubadilika ghafla. Alianza kuchelewa kurudi nyumbani, mawasiliano yakapungua na hatimaye akaondoka kabisa bila kuaga. Jaribio la kuwasiliana naye lilikuwa gumu kwani mara nyingi hakuwa akipokea simu zake.

“Nilibaki na watoto wawili na maswali mengi kichwani. Nilijaribu kuomba msamaha hata bila kujua kosa langu lakini hakutaka kunisikiliza,” alisema Fatuma. SOMA ZAIDI.