Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema jukumu kuu la Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na wanapatiwa taarifa kwa wakati pindi changamoto zinapojitokeza.

Mhe. Makamba ameyasema hayo leo, tarehe 01 Septemba 2026, wakati akijibu Swali lanMhe. Exaud Silaoneka Kigahe, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, aliyetaka kufahamu lini Serikali itabadilisha mkataba wa usambazaji wa umeme kwa wananchi kutoka Mwenga Power kwenda TANESCO, ili Mwenga Power ibaki kuwa mzalishaji wa umeme.

Akijibu swali hilo, Mhe. Makamba amesema utoaji na usimamizi wa leseni za uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini ni jukumu la kisheria la Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), kwa mujibu wa Sheria ya Umeme ya mwaka 2008 na taratibu za utoaji wa leseni hizo.

“Jukumu namba moja la Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na wanapata taarifa kwa wakati kunapotokea changamoto,” amesema Mhe. Makamba.

Ameeleza kuwa uamuzi wowote wa kubadili muundo wa leseni ya usambazaji umeme katika eneo hilo unapaswa kuzingatia matakwa ya sheria na taratibu zilizowekwa.

Hata hivyo, Mhe. Makamba amesema Serikali, kwa kutambua kuwa kumekuwa na malalamiko kuhusu ubora wa huduma inayotolewa na Mwenga Power, tayari taasisi zake za EWURA, TANESCO na REA zimeanza kufanya tathmini ya kina ili kubaini uwezekano wa kufanya mabadiliko hayo bila kuathiri uwekezaji uliopo.

Amesema tathmini hiyo itafanyika kwa haraka ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme yenye uhakika na inayokidhi mahitaji yao.

Aidha, akihitimisha, Mhe. Makamba amesema yupo tayari, pindi Vikao vya Bunge vitakapokamilika, kuongozana na Mhe. Exaud Silaoneka Kigahe, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, kwenda kusikiliza na kufahamu kwa kina changamoto zinazowakabili wananchi katika eneo hilo.

 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

Na.Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amewapongeza watumishi wa wizara hiyo kwa kazi kubwa na mafanikio waliyoyapata katika mwaka wa fedha uliopita, huku akiwataka kuendelea kuyasema kwa ujasiri mafanikio hayo yaliyoiwezesha sekta ya elimu kung’aa kitaifa na kimataifa.

Prof. Nombo amesema mafanikio hayo yametokana na uongozi imara wa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, na Naibu Waziri, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, pamoja na ushirikiano wa Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na watumishi wote.

Prof. Nombo amesema hayo Septemba 1, 2026 jijini Dodoma wakati alipoongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara. Amewashukuru watumishi kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano katika kufikia malengo ya wizara.

Aidha, Prof. Nombo amesema mabadiliko makubwa yanayoendelea katika sekta ya elimu yanatokana na utekelezaji wa sera mpya ya elimu, ambayo inalenga kuandaa wahitimu wenye ujuzi, kuboresha matokeo ya kujifunza na kuimarisha mfumo mzima wa elimu nchini. Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imewekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu kupitia ujenzi wa miundombinu, ajira za walimu, mafunzo ya watumishi na fursa mbalimbali za kitaaluma.

Katika kikao hicho, Katibu Mkuu amekumbusha wajibu mkubwa wa Wizara katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, akieleza kuwa takribani asilimia 40 ya masuala yaliyomo kwenye dira hiyo yanahusu sekta ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu. Ameongeza kuwa utekelezaji wa elimu ya lazima kwa miaka 10 na maandalizi ya kupokea kundi la wanafunzi la double cohort mwaka 2028 ni miongoni mwa majukumu makubwa yanayohitaji maandalizi ya mapema na ushirikiano wa pamoja.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano, weledi, nidhamu na uadilifu, akisema misingi hiyo ni muhimu katika kuimarisha utendaji kazini. Prof. Mushi amesema hayo Septemba 1, 2026 jijini Dodoma wakati akifunga kikao cha tafakuri cha watumishi wa wizara hiyo.

Amesema mafanikio ya wizara yanatokana na mchango wa kila mtumishi, hivyo kuna umuhimu wa kuongeza ubunifu katika utendaji huku sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma ikizingatiwa. Pia amesisitiza umuhimu wa kuzingatia usalama wa taarifa za Serikali na kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kwa furaha, ufanisi na weledi, huku akiwataka watumishi kutumia mafunzo waliyopata kuongeza tija na kuhamasisha utamaduni wa kuendelea kujifunza katika kila ngazi ya utumishi.

Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Edith Rwiza, amesema kikao cha uongozi na watumishi kimetoa fursa ya kutafakari kwa pamoja, kujenga mshikamano na kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi.

Amesema kikao hicho pia kililenga kutafakari mafanikio, changamoto na mafunzo yaliyopatikana katika utekelezaji wa mipango na majukumu ya wizara katika mwaka uliopita.

Dkt. Rwiza amesema kikao hicho kimewapa watumishi nafasi ya kujitathmini kwa kuzingatia uhalisia wa utendaji kazi na kujadili namna bora ya kuhakikisha malengo ya wizara yanafikiwa kwa ufanisi.

Ameongeza kuwa washiriki wamepata fursa ya kutazama kwa pamoja changamoto za rasilimali na kubaini namna ya kuongeza ufanisi ili kupata matokeov makubwa zaidi kwa kutumia rasilimali zilizopo, huku wakielekezwa kuimarisha mshikamano na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

  

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

 

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

  

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

 

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.        
 

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei za bidhaa za mafuta kwa mwezi Septemba 2026. Bei ya petroli imeshuka kwa Shilingi 102 kwa lita, huku bei ya dizeli ikishuka kwa Shilingi 101 kwa lita. Bei hizo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 2 Septemba 2026, saa 6:01 usiku.

EWURA inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia, ambapo mabadiliko ya bei yanaendelea kuathiriwa pamoja na mambo mengine na hali ya kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati.

Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015, bei za mafuta zinaendelea kupangwa kwa kuzingatia mfumo wa soko. Wafanyabiashara wote wa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zisizozidi bei elekezi, na wananchi wanashauriwa kutoa taarifa EWURA kwa kituo chochote cha mafuta kitakachouza zaidi ya bei elekezi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

Na.Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amewapongeza watumishi wa wizara hiyo kwa kazi kubwa na mafanikio waliyoyapata katika mwaka wa fedha uliopita, huku akiwataka kuendelea kuyasema kwa ujasiri mafanikio hayo yaliyoiwezesha sekta ya elimu kung’aa kitaifa na kimataifa.

Prof. Nombo amesema mafanikio hayo yametokana na uongozi imara wa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, na Naibu Waziri, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, pamoja na ushirikiano wa Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na watumishi wote.

Prof. Nombo amesema hayo Septemba 1, 2026 jijini Dodoma wakati alipoongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara. Amewashukuru watumishi kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano katika kufikia malengo ya wizara.

Aidha, Prof. Nombo amesema mabadiliko makubwa yanayoendelea katika sekta ya elimu yanatokana na utekelezaji wa sera mpya ya elimu, ambayo inalenga kuandaa wahitimu wenye ujuzi, kuboresha matokeo ya kujifunza na kuimarisha mfumo mzima wa elimu nchini. Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imewekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu kupitia ujenzi wa miundombinu, ajira za walimu, mafunzo ya watumishi na fursa mbalimbali za kitaaluma.

Katika kikao hicho, Katibu Mkuu amekumbusha wajibu mkubwa wa Wizara katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, akieleza kuwa takribani asilimia 40 ya masuala yaliyomo kwenye dira hiyo yanahusu sekta ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu. Ameongeza kuwa utekelezaji wa elimu ya lazima kwa miaka 10 na maandalizi ya kupokea kundi la wanafunzi la double cohort mwaka 2028 ni miongoni mwa majukumu makubwa yanayohitaji maandalizi ya mapema na ushirikiano wa pamoja.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano, weledi, nidhamu na uadilifu, akisema misingi hiyo ni muhimu katika kuimarisha utendaji kazini. Prof. Mushi amesema hayo Septemba 1, 2026 jijini Dodoma wakati akifunga kikao cha tafakuri cha watumishi wa wizara hiyo.

Amesema mafanikio ya wizara yanatokana na mchango wa kila mtumishi, hivyo kuna umuhimu wa kuongeza ubunifu katika utendaji huku sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma ikizingatiwa. Pia amesisitiza umuhimu wa kuzingatia usalama wa taarifa za Serikali na kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kwa furaha, ufanisi na weledi, huku akiwataka watumishi kutumia mafunzo waliyopata kuongeza tija na kuhamasisha utamaduni wa kuendelea kujifunza katika kila ngazi ya utumishi.

Naye, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Edith Rwiza, amesema kikao cha uongozi na watumishi kimetoa fursa ya kutafakari kwa pamoja, kujenga mshikamano na kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi.

Amesema kikao hicho pia kililenga kutafakari mafanikio, changamoto na mafunzo yaliyopatikana katika utekelezaji wa mipango na majukumu ya wizara katika mwaka uliopita.

Dkt. Rwiza amesema kikao hicho kimewapa watumishi nafasi ya kujitathmini kwa kuzingatia uhalisia wa utendaji kazi na kujadili namna bora ya kuhakikisha malengo ya wizara yanafikiwa kwa ufanisi.

Ameongeza kuwa washiriki wamepata fursa ya kutazama kwa pamoja changamoto za rasilimali na kubaini namna ya kuongeza ufanisi ili kupata matokeov makubwa zaidi kwa kutumia rasilimali zilizopo, huku wakielekezwa kuimarisha mshikamano na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.

Sehemu ya Watumishi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara.




Na Denis Chambi, Tanga


SERIKALI ya mkoa wa Tanga imewaagiza wamiliki wote wa Mabasi yanayosafirisha abiria kwenda nje ya mkoa huo na maeneo mbalimbali ya nchi kuhakikisha kuwa ifikapo September 8,2026 Magari yote yanaanza na kumaliza safari zake katika kituo kikuu cha Mabasi kilichopo Kange.


Agizo hilo linatokana na maadhimio yaliyotolewa na ofisi ya Waziri mkuu, Kamati ya Bunge inayoshughulika na Ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 'TAMISEMI' pamoja na wamiliki na wadau wa usafirishaji kwa lengo la kuhakikisha huduma ya usafirishaji inaimarika pamoja na kuchangia maendeleo ya mkoa huo hususani kwa kwa Halmashauri ya jiji la Tanga kupitia kituo hicho ambacho kinatarajia kuwa kitomvu cha uchumi kwa wananchi .

Akizungumza katika kikao cha pamoja na wadau wa usafirishaji wakiwemo wamiliki wa Mabasi, Baraza la madiwani na ofisi ya halmashauri ya jiji la Tanga Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani amesema kuwa utekelezaji wa agizo hilo umezingatia utekelezaji wa Sheria ndogo ya Halmashauri 'by laws' ya mwaka 2019 huku akiitaka Halmashauri kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau wote wa usafirishaji.

"Baada ya kupitia mapendekezo na ushauri ulioyotolewa na wadau wa usafirishaji na viongozi mbalimbali kwa kuzingatia Sheria ndogo ya Halmashauri 'by laws' ya mwaka 2019 Magari yote yatapaswa kuanza na kumaliza safari zake katika kituo kikuu cha Mabasi Kange wamiliki wote wanapaswa kuzingatia Sheria hizi na tumekubaliana suala hili lianze rasmi tarehe 8,2026" amesema Dkt Buriani.

Amesema kuwa agizo hilo limeambatana na mapendekezo ambayo yanatakiwa kutekelezwa ikiwa ni pamoja na kuitaka mamlaka ya udhibiti wa usafiri ardhini 'LATRA' kwa kushirikiana na Wakala wa Barabara za vijijini na mijini kuanzisha njia za safari za Daladala zinazotoka maeneo mbalimbali ya jiji kwenda katika kituo hicho cha Kange, kuwepo kwa gari la Zimamoto na uokoaji, kukaguliwa kwa vituo vyote vya Mabasi vilivyopo katikati ya jiji kama vinakidhi vigezo.

Aidha kabla ya kutekelezwa kwa agizo hilo Balozi Dkt. Buriani ameiagiza Halmashauri ya jiji la Tanga kuhakikisha kuwa katika kituo hicho kunakuwa na maeneo maalumu kwaajili ya maegesho la Daladala, Bodaboda, Magari binafsi na kuweka mabango ili kuwarahisishia abiria na wananchi kuweza kuendelea na safari zao.

Amewataka wamiliki wote wa Mabasi mkoani humo kuhakikisha wanakuwa na maeneo maalumu kwaajili ya kupaki Magari yao ambayo yatakuwa yakisubiri safari tofauti na sasa ambapo baadhi yao hutumia barabara zilizopo katikati ya jiji hilo na kusababisha msongamano.

"Wale wenye terminal zao huko itabidi sasa terminal hii ya Kange iwe ndio inafanya kazi lakini hatuwakatazi kuwa na terminal zenu hiyo lazima iwe imezungushiwa ukuta ambapo gari linaweza kwenda kufanyiwa marekebisho wakati likisubiri safari" amesisitiza Dkt Buriani.

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Mstahiki Meya wa Halmashauri ya jiji la Tanga Khalid Hamza amepongeza maadhimio hayo na kuahidi kuendelea kusimamia uboreshaji wa kituo hicho ambacho mbali na kuwa kituo kikuu cha Mabasi kinatarajia kuwa kitomvu cha uchumi kwa wananchi na Serikali kuendelea kukusanya mapato.

"Tunaendelea kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani kwa miradi mikubwa ya kimkakati ambayo inaletwa katika mkoa wetu hususani jiji letu la Tanga sisi kama halmashauri tuko tayari kupokea maelekezo na kwenda kuyafanyia kazi kuhakikisha stendi yetu inafanya kazi kwaajili ya mapato ya Halmashauri yetu" amesema Hamza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama Cha wamiliki wa Mabasi Mkoa wa Abdi Awadhi amepongeza kutekelezwa kwa baadhi ya mapendekezo ambayo waliyatoa hapo awali huku akiiomba Serikali Mabasi yote kuendelea kushusha na kupakia abiria wake nyakati za usiku katika terminal zao za siku zote wakati ambapo bado miundombinu inaendelea kuboreshwa katika kituo hicho cha Kange.

"TABOA mkoa wa Tanga tumeridhia maelekezo yote ambayo umeyatoa mkuu wa mkoa na kamati uliyoiunda kwaajili ya maboresho ya mpito yaliyotolea sisi tunaomba turuhusiwe kushusha na kupakia abiria Tanga mjini nyakati za usiku kutokana na kituo chetu hali ya usalama bado hijakuwa sawa" amesema Awadhi.

Kikao hicho pia kimeadhimia kuwa mara tu baada ya kuanza kutekelezwa kwa agizo hilo wadau wote wa usafirishaji, wamiliki wa Mabasi pamoja na Serikali kila baada ya mwezi kuweza kukutana kufanya tathmini ya mkakati huo na kufanyika kazi mapungufu ambayo yanatakiwa kuboreshwa ili kutoa huduma iliyo bora kwa wananchi.












The ICT Transforming Education in Africa – Phase III Project is designed to go beyond providing teachers with basic digital skills by building a sustainable culture of technology-enabled teaching and continuous professional development, Project Coordinator Gabriela Lucas has said.

Ms Lucas, who coordinates the project at UNESCO, said the KFIT-supported initiative was focused on strengthening teachers’ ability to use ICT purposefully to improve teaching and learning while ensuring that the skills acquired could continue to benefit other educators and learners beyond the training period.


“UNESCO aspires to see every teacher able to use ICT for learning and teaching,” she said.

She explained that the project uses the ICT Competency Standards for Teachers in Tanzania (ICT-CSTT) as a structured framework for helping teachers progressively develop their digital competencies according to their existing levels of knowledge and skills.


The framework comprises 15 modules, with the Arusha training focusing on the Beginner and Intermediate levels, covering 10 modules, while participants are also being introduced to five modules under the Advanced level.

Ms Lucas said the training covers practical areas including ICT integration in teaching and assessment, digital learning platforms, Open Educational Resources (OER), online information-search skills, digital content development and the use of Artificial Intelligence (AI) in education.

She stressed that the objective was not simply to teach teachers how to use digital devices, but to enable them to integrate technology effectively into classroom practice, develop relevant learning resources and create more engaging learning experiences for students.





Ms Lucas said the project had adopted a cascade training model, whereby teachers who receive specialised training are expected to share their knowledge and skills with colleagues in their respective schools.

“This approach enables us to reach more teachers and expand the impact of the training beyond those participating directly in the programme,” she said.

She explained that the approach would allow trained teachers to become multipliers of digital knowledge, helping to extend the benefits of the programme from individual participants to entire schools and, ultimately, to more learners.

The Arusha training follows a similar programme conducted in Morogoro, while the wider project is being implemented in Tanzania, Namibia and Uganda.

Ms Lucas said the project was also leveraging existing Government digital systems to ensure that teacher professional development continued beyond face-to-face training.

Through the TIE Teachers Continuous Professional Development Learning Management System (TCPD LMS), linked to the Government’s MEWAKA system, teachers can access learning materials and continue strengthening their professional skills.

She said continuous professional development was increasingly important as digital technologies, including AI, continued to change the way teaching and learning were conducted.

Ms Lucas said the long-term ambition of the project was to contribute to a digitally capable teaching workforce in which teachers could confidently use technology, support their colleagues, develop relevant educational content and prepare learners with the knowledge and competencies required for an increasingly technology-driven society and economy.

She said investing in teachers’ digital capacity was therefore an investment in the future of education and in the human capital needed to drive sustainable development in Africa.