Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imeibuka kinara miongoni mwa Taasisi za Elimu katika Maonesho ya 33 ya Kilimo, Mifugo na Sherehe za Nanenane Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha.

Akizungumzia ushindi huo, Prof. Maulilio Kipanyula, Makamu Mkuu wa NM-AIST, amesema bidhaa bora zinahitaji utafiti na NM-AIST kama Taasisi inayotanguliza ubunifu, imeendelea kubadilisha matokeo ya tafiti kuwa teknolojia zinazotoa suluhisho kwa changamoto za wakulima na wafugaji.

Amesema teknolojia mbalimbali zinazooneshwa na Taasisi, ikiwemo Mfumo wa Ng’ombe Smart, zinalenga kuongeza tija katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kwa kuwezesha ufuatiliaji wa uzalishaji wa maziwa na taarifa muhimu za mifugo.

Aidha, Prof Kipanyula amesema mwaka huu NM-AIST imekuja na teknolojia zinazolenga kuongeza thamani ya mazao, yakiwemo tumbaku, mazao ya chakula pamoja na vyakula vya mifugo kama kuku na ng’ombe.

Prof. Kipanyula amesisitiza kuwa NM-AIST inaendelea kujipanga kuwa kinara katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hususan katika maeneo ya utafiti na maendeleo, sayansi, teknolojia na ubunifu, pamoja na mabadiliko ya kidijitali.

“Ushindi huu ni chachu ya kuendelea kufanya vizuri zaidi. Mwaka ujao tutakuja na teknolojia mpya kabisa. Mwaka huu tumefanikiwa kuzalisha takribani patent 40, jambo tunalojivunia na linalotupa nguvu ya kuendelea kuzalisha teknolojia na bunifu zenye tija kwa sekta ya kilimo na mifugo.”

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla, ameipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) kwa tafiti na bunifu mbalimbali zinazolenga kuongeza tija katika sekta za kilimo na mifugo.

Mhe. Makalla amesema kuwa ametembelea banda la NM-AIST na kujionea teknolojia mbalimbali za kilimo na mifugo, pamoja na bunifu zinazolenga kuongeza thamani ya mazao na bidhaa za mifugo.

Amesisitiza kuwa mapinduzi ya kweli hayawezi kufanyika bila utafiti, teknolojia na ubunifu, akieleza kuwa NM-AIST imekuwa ikifanya vizuri katika kuibua na kuendeleza teknolojia zinazolenga kutatua changamoto za jamii.

“Kilimo bila utafiti, teknolojia na dhana za kisasa hakiwezi kuleta mabadiliko makubwa. Taasisi za utafiti zinatuelekeza na kutupeleka kwenye kilimo na ufugaji wenye tija,” amesema Mhe. Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amesema maendeleo ya sekta za kilimo, mifugo na uvuvi hayapaswi kupimwa kwa kuongezeka kwa uzalishaji pekee, bali pia kwa uwezo wa kuzalisha kwa tija, ubora na kuzingatia mahitaji ya soko, kama inavyosisitizwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Ameeleza kuwa Dira hiyo inalenga kujenga uchumi shindani unaoongozwa na maarifa, teknolojia, ubunifu na uongezaji wa thamani, hivyo taasisi za utafiti kama NM-AIST zina nafasi muhimu katika kufanikisha azma hiyo.

Mhe. Makalla ameyasema hayo wakati akihitimisha Maonesho ya 32 ya Kilimo, Mifugo na Sherehe za Nanenane Kanda ya Kaskazini, yaliyofanyika katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Baraza la Ushindani (FCT limeendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kutumia teknolojia za kidijitali, likiwataka wananchi na wadau kutumia mfumo wa kielektroniki kuwasilisha mashauri na rufaa zao kwa urahisi na kwa wakati.
Msajili wa Baraza la Ushindani, Mbegu Kaskasi, amesema Baraza hilo lililo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara lina jukumu la kusikiliza na kutatua migogoro ya ushindani wa biashara na udhibiti wa soko inayotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na mamlaka za udhibiti zikiwemo TCRA, EWURA, LATRA, TURA na TCAA.
Kaskasi amesema Baraza hilo linaundwa na Jaji wa Mahakama Kuu pamoja na wajumbe sita, huku likitumia fursa mbalimbali kuwaelimisha wananchi kuhusu majukumu yake, namna ya kupata huduma na utaratibu wa kuwasilisha mashauri, ikiwemo kupitia mfumo wa kielektroniki wa usikilizaji wa mashauri.
Amesema mfumo huo umewekwa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, ambapo kwa sasa wanaweza kuwasilisha mashauri na rufaa zao kwa njia ya kielektroniki bila kulazimika kufika ofisini, hatua inayokwenda sambamba na mabadiliko ya kidijitali nchini.
Kwa upande wake,Afisa Sheria wa baraza hilo ,Hafsa Said, amesema mchakato wa rufaa huanza kwa mhusika kuwasilisha notisi ya rufaa pamoja na kuwapatia nakala wahusika wanaopaswa kujibu rufaa hiyo. Baada ya hapo, mhusika anatakiwa kuwasilisha sababu za rufaa pamoja na kumbukumbu zinazohusiana na shauri hilo.
Amesema baada ya mjibu rufaa kuwasilisha majibu yake, shauri hukamilika kwa ajili ya kusikilizwa, huku Baraza likiwa na utaratibu wa kuhakikisha rufaa inayowasilishwa kikamilifu inasikilizwa na kutolewa uamuzi ndani ya kipindi kisichozidi miezi sita.
Naye Afisa TEHAMA wa Baraza hilo Bw.Athumani Kanyegezi  amewataka wananchi na wadau kutumia mfumo wa kielektroniki unaopatikana kupitia tams.fct.or.tz au tovuti ya Baraza fct.or.tz, akieleza kuwa mfumo huo ni rafiki kwa mtumiaji na umeundwa kuendana na mahitaji ya sasa ya utoaji huduma kwa njia ya kidijitali.
Amesema matumizi ya teknolojia hiyo ni sehemu ya juhudi za Baraza kwenda sambamba na mabadiliko ya kidijitali na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, huku akiwataka wananchi kutumia fursa hiyo kupata huduma kwa urahisi.
Aidha, imeelezwa kuwa uwepo wa Baraza la Ushindani unawapa wananchi fursa ya kukata rufaa pale wanapokuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya mamlaka zinazodhibiti sekta mbalimbali. Kwa mfano, mwananchi mwenye malalamiko dhidi ya kampuni ya simu anaweza kwanza kuyawasilisha katika mamlaka husika na, endapo hataridhishwa na uamuzi, anaweza kutumia fursa ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani.
Naye Mdau Vendeline Shekifu,ameeleza kufurahishwa na uwepo wa taasisi hiyo umewapa fursa ya kujifunza kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi za Serikali, ikiwemo Baraza la Ushindani.
Awali Diwani wa Kata ya Tamkaleli Clinton Manzi  amesema maadhimisho hayo yamekuwa na manufaa kwa wakazi wa Dodoma kutokana na muda walioupata kujifunza huduma na fursa mbalimbali, huku akimshukuru Rais kwa kuwezesha maadhimisho hayo kufanyika jijini Dodoma.
Wajasiriamali na wananchi wanaoshiriki Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Kusini wamepata elimu kuhusu umuhimu wa kuzingatia viwango, kuthibitisha bidhaa na kutumia Alama ya Ubora ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), hatua inayolenga kuongeza uaminifu wa bidhaa na kufungua fursa zaidi za masoko ndani na nje ya nchi.

Soko la vinywaji linaendelea kubadilika kadri watumiaji wanavyotafuta uzoefu mpya. Ndiyo sababu ORIJIN imeendelea kuvutia macho ya wengi tangu ilipozinduliwa rasmi nchini wiki moja iliyopita.



Na Munir Shemweta, Bariadi, Simiyu

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amesema Wizara yake iko tayari kushirikiana na mikoa inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki pamoja na Wizara ya Kilimo na wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kuandaa ramani ya uwanja ikiwemo mpangilio kulingana na mahitaji ya eneo la Viwanja vya Maonesho Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu.

Mikoa inayounda kanda ya Ziwa Mashariki katika maonesho ya Wakulima (Nanenane) ni mkoa wa Simiyu, Mara Pamoja na Shinyanga.

Dkt. Akwilapo ameyasema hayo Agosti 8, 2026 wakati akifunga Maonesho na Sherehe za Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) Kanda ya Ziwa Mashariki, yaliyofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu.

Amesema, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pia itasaidia kutoa muongozo wa umiliki wa eneo la uwanja na kuandaa mpango endelevu wa matumizi yake

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, upangaji mzuri wa eneo ni msingi muhimu katika kuhakikisha shughuli na miundombinu inayotekelezwa katika viwanja hivyo inakuwa ya kudumu, inatumika kwa ufanisi na inaepusha migongano ya matumizi ya ardhi hapo baadaye.

“Wizara yetu iko tayari kushirikiana na mikoa inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki, Wizara ya Kilimo pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kutayarisha ramani na mpangilio wa matumizi ya eneo hili kulingana na mahitaji yaliyopo na yajayo,” amesema Dkt. Akwilapo.

Akigeukia upande wa Maonesho ya Wakulima (Nane nane) katika kanda ya Ziwa Mashariki aliyoyafunga rasmi, Dkt Akwilapo ambaye alikuwa mgeni rasmi ametoa wito maonesho hayo kufanyika kuanzia ngazi za Vijiji, Kata, Mitaa na Halmashauri alizozieleza kuwa huko ndiko wananchi wanakoishi.

‘’Kufanyika kwa maonesho kuanzia ngazi hizo itasaidia kuwawezesha waliokusudia kuona na kujifunza teknolojia mbalimbali katika maeneo yao huko waliko’’. Amesema.

Amezishauri mamlaka za serikali za mitaa kuratibu ili maonesho hayo yaweze kufanyika katika ngazi za vijiji, kata, mitaa na wilaya kwa lengo la kuleta mapinduzi katika kilimo, mifugo na uvuvi.

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha amesema maonesho na sherehe za wakulima (Nane nane) katika mkoa wake yalilenga kutoa fursa kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kujifunza, kubadilishana uzoefu, kujenga ushirikiano na kutangaza bidhaa wanazozalisha katika maeneo yao.

Amewashukuru washiriki wa maonesho hayo kwa kuonesha mbinu mbalimbali alizozieleza kuwa zimesaidia wananchi kujifunza teknolojia bora katika mnyonyoro wa thamani ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Akwilapo alitembelea Banda la Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Simiyu ambapo alipata fursa ya kukabidhi hati miliki za ardhi kwa baadhi ya wananchi wa Bariadi mkoani Simiyu waliokamilisha taratibu za kumilikishwa maeneo yao.

Akizungumza baada ya kukabidhi hati hizo, Dkt. Akwilapo aliwataka wananchi waliopokea hati hizo kuhakikisha wanazingatia masharti yote yanayoambatana na umiliki wa ardhi zao.

Maonesho na Sherehe za Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) Kanda ya Ziwa Mashariki, yamefungwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo kwenye Viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu

 

 



Serikali imetangaza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia utoaji wa kiasi cha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kufanikisha mpango wa kupima vijiji vyote nchini ili kumaliza migogoro ya ardhi.

Hayo yameelezwa leo Julai 1, 2026 katika viwanja vya Sokoni Mugumu Wilaya ya Serengeti mkoani Mara na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya alipokuwa akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambaye yuko katika ziara ya kikazi ya siku tano mkoani humo.

Katika hatua ya haraka ya kusogeza huduma kwa wananchi, Mhe. Mmuya amemuagiza Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Mara pamoja na timu yake, kuhakikisha wanaratibu na kuanzisha kliniki za ardhi katika kila kata.

"Hakikisheni mnaratibu uwepo wa kliniki za ardhi katika kila kata ili muwasikilize wananchi hawa na msione kila changamoto mpewazo ni ya mazoea. Hapana, amekuja kwako kwa sababu ana jambo la kusikilizwa na litatuliwe," alisema Naibu Waziri Mmuya.


Mhe. Mmuya alieleza kuwa wizara ya Ardhi iliwasilisha mpango na maombi ya fedha bungeni kufuatia maelekezo ya awali ya Waziri Mkuu, na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akaidhinisha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kupima jumla ya vijiji 12,333 vya Tanzania.


"Mpaka hivi ninavyoongea, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kipindi chake kifupi tu ameweza kupima vijiji 4,873. Na ametupatia maelekezo kuwa ndani ya kipindi chake, vijiji vyote vilivyobakia tuvipime." Aliongeza Naibu Waziri Kaspar Mmuya 



Katika hatua nyingine Mhe. Mmuya amesema Wizara ya Ardhi itashirikiana bega kwa bega na Ofisi ya Rais - TAMISEMI ili kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa kikamilifu katika vijiji vyote vilivyosalia nchini.


Aidha, Mhe. Mmuya alieleza kuwa Wilaya ya Serengeti ina kata 30 na vijiji 78. Ameuhakikishia uongozi wa wilaya hiyo kuwa vijiji vyote 78 vimeshaingizwa kwenye mpango wa upimaji ndani ya kipindi cha miaka mitano ya Rais Samia Suluhu Hassan.


"Kupima vijiji hivi ndiyo dawa kubwa ya kutatua changamoto ya mipaka kati ya kijiji na kijiji. Lakini ni dawa kubwa ya kutatua changamoto ya kugombania matumizi ya ardhi ya mtu mmoja mmoja, taasisi na taasisi, au serikali na wananchi," alisema Naibu Waziri Kaspar Mmuya.

 


​Kusikilizwa, kuheshimiwa, na kuwa na mvuto mbele ya jamii ni jambo la msingi sana kwa mtu yeyote anayetaka kupiga hatua maishani, iwe kwenye uongozi, sanaa, biashara, au shughuli za kijamii.

Hata hivyo, kwangu mimi, kila nilipojaribu kusimama na kuzungumza mbele ya watu au kutoa mawazo yangu kwenye mikutano, nilijikuta nikidharaulika, kupuuzwa, na kutoonekana wa maana kabisa.

Maneno yangu yalionekana hayana uzito wowote, na mara nyingi watu walikuwa wakikatisha mazungumzo yangu au kuonyesha kutoipenda sauti yangu bila sababu yoyote ya msingi.

​Hali hii iliniletea unyonge mkubwa, hofu ya kuzungumza mbele za watu, na kuninyima fursa nyingi za uongozi na mafanikio ambazo nilikuwa na uwezo nazo kabisa.

Nilibaki nikitazama wenzangu wakipewa heshima na kibali kikubwa hata wakati wao walipotoa mawazo ya kawaida sana, hali mimi wangu ukionekana kama kelele.

Nilianza kujitenga na jamii na kujiona sina thamani wala bahati yoyote ya kupendwa na kuheshimiwa na watu. SOMA ZAIDI.

 


Kipande cha ardhi au kiwanja cha mirathi ni kumbu kumbu na urithi muhimu unaoacha msingi wa maisha na maendeleo kwa familia.

Hata hivyo, kwangu mimi, kiwanja nilichoachiwa na wazazi wangu kiligeuka kuwa chanzo cha vita kali, vitisho, na msongo mkubwa wa mawazo.

Ndugu wa karibu pamoja na watu wenye pesa na ushawishi mtaani walianza kuweka mipango ya kunitapeli na kunipora kiwanja hicho, wakidai kuwa sina nyaraka halali na kwamba sina uwezo wa kupambana nao.

​Nilibaki nikihangaika kwenye mabaraza ya ardhi na serikali za mitaa bila kupata msaada wowote. Kila nilipojaribu kusimamia haki yangu, rushwa na maneno ya uongo vilipindisha ukweli na kunifanya nionekane mimi ndiye mvunjaji wa sheria.

Vita hiyo ilianza kuvuka mipaka ya kawaida na kuingia kwenye vitisho vya ushirikina na kunipigia simu za usiku kucha wakiniahidi kunipoteza au kunifanya nilete ukichaa kama sitajiondoa kwenye kiwanja hicho.

Nilibaki na hofu kubwa ya kupoteza urithi wa familia yangu na kuacha watoto wangu wakiwa hawana mahali pa kushika. SOMA ZAIDI.

 


▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini 

▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko

▪️Waziri Mavunde aelekeza uchunguzi kuwabaini na kukamata wahusika zaidi

▪️Mgeni mmoja kutoka nje ya nchi ahusishwa na utoroshaji

▪️Madini,fedha na vitendea kazi vyashilikiwa na serikali


Ikiwa ni sehemu ya usimamizi thabiti wa sekta na kuhakikisha Serikali inapata mapato yake ipasavyo kupitia mfumo rasmi wa masoko ya madini nchini, soko bubu la madini lagunduliwa jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb) ameyasema hayo  leo tarehe 09 Agosti, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam na kubainisha kuwa zaidi ya watuhumiwa 14 wamekamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya utoroshaji wa madini na watafikishwa kwenye vyombo vya sheria hivi karibuni.

"Hawa wenzetu pamoja na Serikali kuwezesha masoko na vituo vya ununuzi vilivyosambaa Nchi nzima, wao wameona waje kupanga nyumba na kuigeuza soko la madini ambapo ni kinyume na Sheria.

Natoa rai kwa wenye nyumba wote kuhakikisha wanafahamu shughuli za msingi za wapangaji wao ili kutojiingiza kwenye matatizo haya.

Tutafanya ukaguzi maalum kwenye baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es salaam na mikoa mingine kubaini hizi nyumba zinazotumika kama soko la madini na kuwa chanzo cha utoroshaji madini”Alisema Mavunde

Aidha, Waziri Mavunde amesema kwa taarifa za awali, raia mmoja wa kigeni anahusishwa na kitendo hicho cha kuwezesha utoroshaji wa madini nje ya mfumo rasmi na amedhibitiwa.

Vilevile, Mhe. Mavunde ameelekeza vyomba vya dola kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini na kuwakamata wahusika wote kwenye mnyororo huo wa vitendo vya utoroshaji wa madini.

Madini gram 174 yaliyokutwa katika soko hilo bubu pamoja na   mashine mbili za XRF aina ya NITON DXL 800, Mizani ya kupimia uzito, Mitungi ya gas, vyungu vya kuchomea dhahabu, borax, pipeza gas, legis za kutengenezea umbo la dhahabu Pamoja na jumla ya pesa taslimu TZS. 54,705,000 vyote vinashikiliwa na serikali.









 

Kujenga au kupata nyumba ya familia ni moja ya hatua kubwa zaidi maishani, lakini kuilinda dhidi ya majanga na hofu ya kupoteza kila kitu ni mtihani mwingine mzito.

Kwa miaka kadhaa, mtaa na eneo tulilokuwa tukiishi lilianza kukumbwa na matukio ya ajabu na ya kutisha ya majanga ya moto yaliyotokea ghafla, ajali za mara kwa mara, na upepo wa ajabu uliokuwa ukiezua mabaraza na kuezua nyumba za majirani zetu moja baada ya nyingine.

​Kila mara janga lilipotokea mtaani, nilijikuta nikipatwa na hofu kubwa na msongo wa mawazo. Nilitazama familia yangu na mali tulizozitolea jasho kwa miaka mingi.

Nikihofia kuwa usiku wowote au siku yoyote, nyumba yetu nayo ingeweza kukumbwa na majanga hayo ya giza na kutuacha mtaani bila chochote. Hofu hiyo ilitunyima amani na usingizi.

Kila sauti ya ajabu au upepo ulipovuma usiku, nilikuwa nikiamka kwa mshtuko mkubwa nikihisi nyumba yetu ipo hatarini kuungua au kupata maafa. SOMA ZAIDI.

 Na Munir Shemweta, Itilima


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameitaka mikoa na wilaya nchini kuhakikisha zinatenga na kuandaa maeneo maalumu yatakayotumika kwa ajili ya kuanzisha kongani za viwanda.

Amesema upangaji mzuri wa matumizi ya ardhi ni muhimu katika kuvutia wawekezaji kwa kuwa mwekezaji anahitaji eneo lililotengwa na kutambuliwa kwa matumizi husika kabla ya kuanzisha shughuli zake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati alikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa shule ya awali na msingi katika Kitongoji cha Mwankola, Kata ya Lagangabilili pamoja na kusikiliza kero za wananchi katika Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilayani itilima mkoa wa Simiyu tarehe 7 Agosti 2026 Dkt.  Akwilapo amesema hatua hiyo pia inalenga kuzuia migogoro ya matumizi ya ardhi kati ya makazi, shughuli za kilimo, viwanda na matumizi mengine yanayohitaji maeneo maalumu.

Aidha, Waziri huyo wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameeleza kuwa,  Wizara yake   imejipanga kuimarisha usimamizi wa sekta hiyo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na maeneo yao yanasimamiwa kwa kuzingatia sheria.

Amewataka wananchi wa Itilima kufuata sheria, kanuni na taratibu zinazohusu umiliki na matumizi ya ardhi ili kupunguza migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na migogoro ya ardhi.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha ameeleza kuwa, mkoa wa Simiyu hususan wilaya ya Itilima wanatambua umuhimu wa ardhi hasa katika kumilikisha wananchi, taasisi na vijiji lengo likiwa kuepuka migogoro ya ardhi.

Wakiwasilisha kero yao mbele ya Waziri wa Ardhi, wananchi wa Itilima wameiomba serikali kuwawekea uzio utakaowasaidia kuepukana na uvamizi wa mara kwa mara wa tembo wanaotoka hifadhini kwenda katika maeneo yao.

‘’Tunashukuru kwa ahadi ya kuwekewa uzio wa umeme kwa ajili ya kuzuia tembo kuvamia maeneo yetu ila tunaomba ahadi hiyo iwe ya kweli’. Amesema mkazi wa Itilima’

Hata hivyo, Mkuu wa mkoa wa Simiyu amewaambia wananchi hao kuwa serikali tayari imejipanga kuhakikisha inajenga uzio wa umeme kwa ajili ya kuzuia tembo kuingia katika maeneo ya wananchi.

‘’Niwaase wananchi kutoenda katika maeneo ya hifadhi kwa ajili ya kufanya uharibifu na mtoe ushirikiano wa kulinda uzio wa umeme pale utakaojengwa’’. Amesema

Mkuu wa wilaya ya Itilima Bi. Anna Gidarya amesema halmashauri ya wilaya ya Itilima ina lengo la kuandaa hati milki za viwanja vyote 1,604 vilivyopangwa ambapo hadi kufikia juni 2026 jumla ya hati milki 506 zimeandaliwa na kusajiliwa.

‘’Hati za viwanja vilivyosalia havijamilkishwa kwa vile wamiliki hawajalipia gharama za uandaaji wa milki hizo’’. Amesema Bi. Gidarya.

Katika hatua nyingine, Dkt. Akwilapo amewataka wananchi wa Wilaya ya Itilima kuendelea kulinda amani na utulivu uliopo nchini kwa kuwa ndiyo msingi wa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.

Amesema, hakuna uwekezaji unaoweza kufanyika kwa ufanisi katika mazingira yasiyo na amani, hivyo ni jukumu la wananchi kuendelea kuthamini na kulinda utulivu uliopo Tanzania.

Ameeleza kuwa maendeleo katika sekta mbalimbali, ikiwemo elimu, viwanda, biashara na miundombinu, yanahitaji mazingira tulivu yanayowawezesha wananchi na wawekezaji kufanya shughuli zao bila hofu.

“Uwekezaji wowote unategemea amani na utulivu na maendeleo yatakayopatikana yatatokana na amani. Hivyo amani inaiweka nchi katika nafasi nzuri ya kupokea wawekezaji,” amesema Dkt. Akwilapo.

Amesema uwepo wa amani unaifanya nchi kuwa na mazingira yanayovutia miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo baadaye inaweza kutoa ajira, kuongeza mapato na kuboresha maisha ya wananchi.

Ziara ya Dkt Akwilapo wilayani Simiyu ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuwapeleka mawaziri katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali iliyoahidiwa kwa wananchi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akiomba kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akilakiwa na wananchi wa Itilima alipowasili Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilayani itilima mkoa wa Simiyu kusikiliza kero za wananchi wakati wa ziara yake mkoani humo.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akikabidhiwa Zawadi ya kuku na wananchi wa Kijiji cha Simiyu kata ya Migato mara baada ya kuzungumza nao wilayani Itilima mkoa wa Simiyu tarehe 7 Agosti 2026. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akipata maelezo ya mradi wa ujenzi wa Daraja katika Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilaya ya Itilima mara baada ya kusikiliza kero za wananchi tarehe 7 Agosti 2026. Kulia kwa Dkt Akwilapo ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu mhe. Anamringi Macha na kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Itilima Bi. Anna Gidarya.

Sehemu ya wananchi wa Itilima waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo uliofanyika katika Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilayani Itilima mkoa wa Simiyu tarehe 7 Agosti 2026.
Muonekano wa Daraja lililopo Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilaya ya Itilima.(PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI) 



 Na. Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.


Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, amehitimisha ziara yake nchini Tanzania na kuagwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Jukwaa hilo la siku mbili lililofunguliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, liliipatia Tanzania fursa ya kusaini hati tatu za makubaliano ikiwemo hati ya makubaliano ya kujenga kituo kipya cha huduma za usafishaji wa figo, mradi wa kuchakata gesi asilia kuwa gesi kimiminika na makubaliano kati ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Africa50 ya kuendeleza miundombinu ya usafirishaji wa umeme.

Aidha, Mikutano hiyo iliyokutanisha washiriki wapatao 1,200, imeipatia Tanzania fursa ya kutangaza vivutio vya utalii, uwekezaji na miradi ya kimkakati kwa lengo la kuvutia mitaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika maendeleo ya miundombinu na hivyo kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Kitaifa wa Miaka Mitano (FYDP IV) na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

 


Na. Asia Singano na Josephine Majura, WF - Dodoma


Serikali imezitaka taasisi zote za umma nchini kuimarisha usimamizi wa mali za Serikali kwa kuhakikisha taarifa zote za mali zinaingizwa na kutunzwa katika Mfumo wa Serikali wa Usimamizi wa Mali (GAMIS), ili kuongeza uwajibikaji, kuimarisha matumizi ya rasilimali za umma na kupunguza hoja za ukaguzi.

Maagizo hayo yalitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nanenane), yaliyofanyika katika Uwanja wa Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.  

Alisema Serikali imetumia fedha nyingi kuwekeza katika miradi ikiwemo ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere -JNHPP (takribani sh. trilioni 6), ujenzi wa Reli ya kisasa-SGR (takribani sh. trilioni 10.6), ununuzi wa ndege, ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi (takribani sh. bilioni 716.3) pamoja na utekelezaji wa miradi ya maji mijini na vijijini (takribani sh. bilioni 457.4), huku akisisitiza umuhimu wa miradi hiyo.

“Mali za umma ni rasilimali muhimu zinazowezesha Serikali kutoa huduma kwa wananchi na kutekeleza miradi ya maendeleo, huku wastani wa asilimia 70 ya bajeti za taasisi za umma ukitumika katika ununuzi unaozalisha mali hizo, usimamizi wake unapaswa kuzingatia uwajibikaji, ufanisi na utii wa sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa’’ alisema Bw. Sendo.

Alisisitiza kuwa kutokana na uwekezaji mkubwa na wingi wa rasilimali nchini ni muhimu kuwa na mikakati madhubuti ya kuzisimamia mali hizo ili ziweze kutumika kwa matumizi yaliyokusudiwa na kuiwezesha Serikali kupata manufaa ya uwekezaji uliokusudiwa kwa kipindi kirefu. 

‘’Kwa upande wa Wizara ya Fedha ikiwa na dhamana ya Usimamizi wa Mali za umma nchini imefanya jitihada mbalimbali katika kuongeza ufanisi wa Usimamizi wa Mali za umma nchini kwa Kusimika na kuwezesha matumizi ya mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Mali za Serikali 

“Government Assets Management Information Systems - (GAMIS) ambao unatumika kutunza na kuchakata taarifa za mali za Taasisi zote za Umma hapa nchini’’, alisema Bw. Sendo.
Aliongeza kuwa, Wizara ya Fedha imefanya maboresho katika Sheria ya Fedha za Umma sura 348 pamoja na kuandaa Kanuni mahususi za Usimamizi wa Mali za Umma za mwaka 2024 ikiwa ni utekelezaji wa azma ya kuimarisha Mifumo ya Usimamizi wa Mali za Umma nchini.

Alisisitiza Maafisa Masuuli kuwa na mifumo thabiti ya uwajibikaji na kuwa mfano bora kwa wengine kwa kuzingatia misingi ya uadilifu, uwajibikaji, uwazi, na ufanisi katika kuonyesha kwamba mali za umma ni amana ambayo wamekabidhiwa kwa niaba ya Watanzania wote. 
Aidha, taasisi hizo zimetakiwa kuhakikisha mali chakavu, sinzia, ziada na zilizokwisha muda wa matumizi zinaondoshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo ili kuimarisha ufanisi wa matumizi ya mali za umma.

Katika hatua nyingine Bw. Sendo amezitaka taasisi za umma kuwasilisha taarifa za ajali, hasara na upotevu wa mali kwa Mlipaji Mkuu wa Serikali ndani ya siku 30 tangu tukio litokee na mali zilizopata ajali au uharibifu zifanyiwe matengenezo mara baada ya kupata kibali husika.

 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, ameshiriki kilele cha Maonesho ya 33 ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane, yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt.John Malecela Nzunguni Jijini Dodoma yakilenga kuimarisha tija, uzalishaji na upatikanaji wa masoko kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wadau wa sekta ya kilimo nchini.

Maonesho hayo yaliyoongozwa na kaulimbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya 2050”, yamefungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, huku yakitoa fursa kwa taasisi za Serikali, sekta binafsi na wadau mbalimbali kuonesha huduma, bidhaa na fursa zinazolenga kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo.

Akizungumza mara baada ya kushiriki kilele hicho, Bi. Ngasongwa amesema ushiriki wa FCC katika maonesho hayo ulikuwa sehemu ya jitihada za kuifikisha elimu ya ushindani kwa wananchi, wazalishaji na wafanyabiashara ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika shughuli za kiuchumi.

Amesema FCC imeendelea kutumia majukwaa mbalimbali kama Nane Nane kutoa elimu kuhusu madhara ya bidhaa bandia na umuhimu wa wananchi kuwa makini wakati wa kununua bidhaa, kwa kuwa matumizi ya bidhaa zisizo halisi yanaweza kuathiri usalama wa watumiaji, ubora wa uzalishaji na ushindani wa biashara.

Bi.Ngasongwa amesisitiza kuwa elimu kwa wananchi ni muhimu katika kujenga soko lenye ushindani wa haki, ambapo wazalishaji na wafanyabiashara wanapata mazingira bora ya kushindana huku watumiaji wakilindwa dhidi ya vitendo vinavyoweza kuathiri maslahi yao.

Amesema FCC itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuimarisha uelewa wa sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.

Ushiriki wa FCC katika Maonesho ya Nane Nane unaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kujenga uchumi shindani na wenye tija, kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu na uelewa unaowawezesha kufanya maamuzi sahihi katika soko, huku wafanyabiashara wakihimizwa kuzingatia sheria, ubora wa bidhaa na ushindani wa haki.