Na.Mwandishi Wetu-Babati, Manyara

 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kaskazini imeendesha semina ya kuwajengea uwezo Maafisa wa Huduma kwa Wateja, Mahusiano na Sheria kutoka TANESCO na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira za Kanda ya Kaskazini kuhusu huduma kwa wateja na uzingatiaji wa matakwa ya kisheria.

Akifungua semina hiyo katika Hoteli ya White Rose, Babati, Meneja wa EWURA Kanda ya Kaskazini, Bw. George Mhina, aliwasisitiza washiriki kuyafahamu vyema majukumu yao ili waweze kutoa majibu sahihi, ya wakati na yanayozingatia sheria, hivyo kuboresha huduma kwa wateja.

Kwa niaba ya washiriki, Bi. Devotha Mayala kutoka Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tanga na Bw. Samwel Mandari kutoka TANESCO waliishukuru EWURA kwa mafunzo hayo, wakieleza kuwa yamewaongezea uelewa na uwezo wa kuwahudumia wateja kwa weledi zaidi.

Semina hiyo ni sehemu ya juhudi za EWURA za kuimarisha uwezo wa watoa huduma na kulinda haki za watumiaji wa huduma za nishati na maji kupitia Udhibiti wa Haki kwa Matokeo Chanya.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa mwaka 2026, yatakayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24 katika viwanja vya michezo vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga.

.......

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametangaza maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa mwaka 2026, yatakayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24 katika viwanja vya michezo vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga.

Akitangaza maadhimisho hayo amesema yatawakutanisha wadau kutoka wizara mbalimbali, vyuo vya elimu ya juu, vyuo vya ufundi na ufundi stadi, mashirika ya utafiti na sekta binafsi kwa ajili ya maonesho na mijadala ya kimkakati katika kuimarisha elimu, ujuzi na ubunifu nchini.

Prof. Mkenda amebainisha kuwa wananchi watapata fursa ya kushuhudia bunifu zilizobuniwa na vijana wa Kitanzania, ambazo zikovkatika hatua mbalimbali ikiwemo zilizo sokoni akitoleta mfano mashine ya kukamua mafuta ya parachichi (Avomero), mabegi ya shule yenye mfumo wa umeme jua (Soma Bags), na mita janja za maji (Smart Prepaid Water Meter).

Amesisitiza kuwa bunifu hizo ni ushahidi wa jitihada za serikali kuendeleza wabunifu na kuwezesha uwepo wa bidhaa hizo za ndani zinazotatua changamoto za kijamii na kiuchumi.

Aidha, Waziri Mkenda amesema zaidi ya bunifu 70 zipo katika hatua mbalimbali za kukuzwa ili ziwe biashara halisi na kuchangia uchumi wa taifa. Ameongeza kuwa Serikali imeanzisha mfuko maalum wa kusaidia wabunifu kupunguza gharama za uzalishaji na kuharakisha ukuaji wa biashara zao.

Pia ameeleza kuwa katika wiki ya ubunifu kutakuwa na Mashindano ya Kitaifa ya Ujuzi ambapo ni vigego vyake vya ushindani ni vya kimataifa na ikiwa ni maandalixi ya Nchi kushiriki katika mashindano ya kimataifa (World Skills Competition)

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, amesema serikali ipo katika hatua za kuhuisha Sera ya Taifa ya Sayansi, Teknolojia ili iendane na mabadiliko ya kidunia na mahitaji ya sasa.

Ameeleza kuwa sera mpya itakuwa mwongozo wa namna masuala yote ya sayansi, teknolojia na ubunifu yatakavyoshughulikiwa nchini, ikiwemo mashindano ya kitaifa ya ubunifu.

Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, Prof. Ladislus Mnyone, amesema serikali imekamilisha mkakati wa kuongeza ushiriki wa Watanzania wanaoishi nje ya nchi (diaspora) katika kuendeleza bunifu na teknolojia za ndani.

Aidha, amebainisha kuwa katika kuendelea kuibua wabunifu halmashauri 90 tayari zimeanzisha madawati ya sayansi na ubunifu, hatua inayowawezesha wabunifu kuwasilisha mawazo yao na kuunganishwa na taasisi ya COSTECH kwa ajili ya urndelezaji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, amepongeza jitihada za serikali katika kuhamasisha ubunifu nchini. Amesema banda maalum litakuwepo Tanga kuonyesha bunifu zilizofanikiwa kuingia sokoni ili kutoa ushuhuda wa mafanikio ya wabunifu wa Kitanzania.

Amesisitiza kuwa ushirikiano wa serikali, wadau na wananchi ni muhimu katika kuendeleza ubunifu na kuchochea maendeleo ya taifa.

Kauli mbiu ya mwaka huu: “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050”

Na Mwandishi Wetu

Hospitali ya Medinova Specialized Polyclinic imezindua rasmi huduma ya Tibamazoezi (Physiotherapy) ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupanua huduma za kibingwa na kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imesema imeendelea kuimarisha nafasi yake katika kufadhili sekta ya kilimo nchini baada ya mtaji wake kuongezeka kutoka Sh bilioni 60 hadi Sh bilioni 452.16, hatua iliyowezesha kupanua utoaji wa mikopo na huduma za kifedha kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.

 


Kupambana kwenye korido za sheria bila kupata haki ni moja ya mateso makubwa zaidi yanayoweza kukatisha tamaa na kuua roho ya mtu. 

Kwa zaidi ya miaka mitano, nilikuwa nikipambana mahakamani kutafuta haki yangu iliyopora na watu wenye fedha na ushawishi mkubwa.

Kila mara nilipowasilisha ushahidi na kufungua kesi, matokeo yalikuwa yale yale hukumu zilipotoshwa, ushahidi wangu ulipingwa, au kesi ilitupiliwa mbali kwa sababu zisizoeleweka.

Nilipoteza Rufaa baada ya Rufaa, huku nikitazama mali na jasho langu vikichukuliwa mchana kweupe. Gharama za mawakili na ada za mahakama zilitumia akiba yangu yote na kuniingiza kwenye madeni makubwa.

Watu wengi walianza kunidhiaki na kunipuuza, wakiamini kuwa nilikuwa nikipoteza muda kupambana na watu waliokuwa wameshikilia mfumo na kuwa na bahati isiyotikisika. Wasiwasi na msongo wa mawazo vilinikosesha amani na usingizi usiku. SOMA ZAIDI.

 

Kujituma kazini na kuonyesha matokeo bora ni lengo la kila mfanyikazi anayetaka kukua kitaaluma. Kwa zaidi ya miaka mitano, nilikuwa mfanyikazi wa mfano katika kampuni yetu.

Nilikuwa wa kwanza kuwasili ofisini, wa mwisho kuondoka, na miradi yote niliyopewa nilitekeleza kwa ufanisi wa hali ya juu. Hata hivyo, kila mwaka ulipowadia muda wa tathmini na kupandishwa vyo (promotions), jina langu lilipitwa kimyakimya.

Walikuwa wakipandishwa cheo watu niliowafundisha kazi au wale waliokuwa na uzoefu mdogo kabisa. Kila nilipojaribu kumuuliza mkurugenzi au idara ya rasilimali watu (HR), nilipewa ahadi hewa za “mwaka ujao ni zamu yako.”

Nilibaki nikijihisi nimekwama, nikiwa na majuto na msongo mkubwa wa mawazo huku nikiona juhudi zangu zote zikienda bure. SOMA ZAIDI.
Familia ndiyo kila kitu katika maisha ya mwanamume, na inapovunjika, unahisi kama dunia yote imekuporomokea. Kwa miaka mingi tulikuwa tukilinda na kuijenga ndoa yetu, tukipitia mengi na kupata watoto wazuri.

Hata hivyo, taratibu migogoro midogo midogo ilianza kuingia ndani ya nyumba yetu. Kila siku kulikuwa na maneno ya shombo, kutokuelewana, na hasira zisizo na msingi.

Siku moja baada ya ugomvi mkubwa, nilirudi nyumbani jioni na kukuta nyumba ipo tupu mke wangu alikuwa amebeba kila kitu, akachukua watoto, na kutoweka bila kuniambia anakokwenda.

​Nilibaki peke yangu kwenye nyumba iliyokuwa na baridi na ukimya wa kutisha. Nilijaribu kumtafuta kwa simu lakini alikuwa ameniziba (blocked) kila mahali, na ndugu zake walipokea simu zangu kwa dharau na kejeli wakidai kuwa sitamuona tena.

Wasiwasi, upweke, na maumivu ya kuwakosa watoto wangu viliniletea msongo mkubwa wa mawazo. Nilianza kujiona kama mwanamume niliyefeli kabisa. SOMA ZAIDI.

 

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, Julai 29, 2026

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza rasmi kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, yakilenga kuimarisha weledi, maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari wa Bongo FM jijini Dar es Salaam, redio dada ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya JAB, Tido Mhando, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kuelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, kwa kuzingatia weledi, maadili na uwajibikaji.

“Mafunzo haya ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari. Leo tumeanza rasmi na waandishi wa habari wa Bongo FM, tutaendelea kwa vyombo vingine pia kwa sababu, kutakuwa na mafunzo ya muda mfupi na ya muda mrefu. Hivyo, mafunzo haya yawe fursa ya kujenga uwezo na kuweka msingi imara wa kukuza na kulinda taaluma ya uandishi wa habari kwa kuongeza maarifa na weledi,” amesema Wakili Kipangula.

Akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, historia na uanzishwaji wake, katika mafunzo hayo yaliyoanza leo tarehe 29 Julai, 2026 katika ukumbi wa Bodi, Wakili Kipangula amesema sheria hiyo imeweka msingi wa kuimarisha taaluma ya habari kwa kubainisha viwango vya weledi, maadili na uwajibikaji

Amesisitiza kuwa JAB itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo kwa kuzingatia haki, uwazi na kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari, huku ikihakikisha taaluma ya habari inalinda maslahi ya umma..

Aidha, amewataka waandishi wa habari kuzingatia sheria na maadili katika kila hatua ya ukusanyaji, uchakataji na usambazaji wa habari ili kujiepusha na madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na ukiukaji wa taaluma.

Amesema kuzingatia misingi hiyo kunajenga weledi, kunalinda heshima ya taaluma na kuimarisha imani ya jamii kwa vyombo vya habari.
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.

Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

"Mafunzo haya yametupatia maarifa muhimu yatakayotusaidia kutekeleza majukumu yetu kwa kuzingatia maadili, sheria na viwango vya taaluma ya uandishi wa habari. Tunaamini yatachangia kuboresha utendaji wetu na kuongeza uwajibikaji katika kuhabarisha umma," wamesema washiriki hao.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.



📌PPRA Yatambua Ubora na Usimamizi .

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Tanga imeibuka miongoni mwa taasisi zilizofanya vizuri zaidi nchini katika usimamizi wa ununuzi wa umma baada ya kutwaa tuzo mbili katika Kongamano la 10 la Ununuzi wa Umma la mwaka 2026 linaloendelea jijini Arusha.

Tuzo hizo zilizotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) zinatokana na mafanikio ya TARURA Tanga katika kuzingatia kikamilifu matakwa ya Sheria ya Ununuzi wa Umma pamoja na kuonyesha ufanisi mkubwa katika utoaji wa mikataba.

Katika tuzo ya kwanza TARURA Tanga ilitambuliwa kwa kutekeleza kwa kiwango cha juu matakwa ya sheria yanayotaka asilimia 30 ya bajeti ya ununuzi kutengwa kwa ajili ya vikundi vya kijamii hatua iliyotajwa kuwa mfano bora wa utekelezaji wa sera za Serikali za kuwainua makundi yenye mahitaji maalum kiuchumi.

Tuzo ya pili ilitokana na mafanikio ya Wakala huo katika usimamizi wa mikataba baada ya kufanikisha utoaji wa mikataba 106 katika mwaka wa fedha 2025/2026, jambo lililoiweka miongoni mwa taasisi zilizofanya vizuri zaidi nchini.

Mafanikio hayo yanaendelea kuithibitisha TARURA kuwa miongoni mwa taasisi zinazosimamia kwa ufanisi matumizi ya fedha za umma kupitia uzingatiaji wa sheria, uwazi na uwajibikaji katika mchakato wa ununuzi nchini.







 

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeshiriki Kongamano la 10 la Ununuzi wa Umma mwaka 2026 linaloendelea jijini Arusha, limewakutanisha wadau wa ununuzi pamoja na viongozi wa Serikali kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kuimarisha Sekta ya ununuzi na ugavi nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando, Mkuu wa Sehemu ya Huduma za Sheria PPAA, Bi. Agnes Sayi amewahimiza wadau wa ununuzi wa umma kutembelea banda la Mamlaka ya Rufani kupata uelewa juu ya majukumu na huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo hususan matumizi ya Moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST.

PPAA imeshiriki maonesho yanayofanyika pembezoni mwa Kongamano hilo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uamuzi juu ya rufaa zinazotokana na mchakato wa ununuzi wa umma, uamuzi juu ya rufaa zinazotokana na kufungiwa kushiriki katika michakato ya ununuzi wa umma pamoja na uamuzi juu ya malalamiko yanayotokana na kushindwa kwa Afisa Masuuli kutoa uamuzi ndani ya muda uliowekwa.

Awali, akifungua Kongamano hilo kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, (Mb.), Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila amesema sekta ya ununuzi wa umma inahusisha sehemu kubwa ya matumizi ya fedha za serikali, hivyo kuna ulazima wa kuhakikisha fedha zote zinazotengwa zinasimamiwa kwa umakini mkubwa ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

Dkt. Nguvila amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika mfumo wa ununuzi wa umma ili kuongeza uwazi, kupunguza gharama za ununuzi, kuharakisha mchakato na kurahisisha ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma.

"Ununuzi wa umma na ugavi ni nyenzo ya kisera na kimkakati ya Serikali katika kuchochea uzalishaji, ukuaji wa viwanda, kuongeza ajira, kuimarisha kampuni za ndani, kukuza ubunifu, na kuhakikisha maendeleo yanayopatikana yanawanufaisha Watanzania wengi zaidi," amesema Dkt. Nguvila.

Kongamano hilo la siku tatu limeanza tarehe 29 - 31 Julai, 2026 limewakutanisha wadau wa ununuzi zaidi ya 1,500. Aidha, limewakutanisha Wakuu wa Taasisi, Maafisa Masuuli, Maafisa Ununuzi, Idara Tumizi, Maafisa Sheria, Wazabuni na Taasisi binafsi.





Mlezi wa APSP na Kamishna Mstaafu wa Sera za Ununuzi wa Umma, Dkt. Fredrick Asumile Mwakimbinga,

 Mkutano Mkuu wa Tano wa Chama cha Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi Tanzania (APSP) umefanyika jijini Arusha ukiwa na lengo la kupokea taarifa za uongozi, kujadili utekelezaji wa maazimio, fedha na bajeti, pamoja na kuweka mikakati ya kuongeza ushiriki wa makundi maalum na biashara ndogo na za kati (SMEs) katika fursa za ununuzi wa umma.


Akifungua mkutano huo, Mlezi wa APSP na Kamishna Mstaafu wa Sera za Ununuzi wa Umma, Dkt. Fredrick Asumile Mwakimbinga, alisema zaidi ya asilimia 70 ya fedha za Serikali hupitia katika shughuli za ununuzi, hivyo aliwataka wataalamu wa sekta hiyo kufanya kazi kwa uadilifu, kuzingatia maadili ya taaluma na kulinda heshima ya taasisi zao.

Dkt. Mwakimbinga pia aliwahimiza wanachama kuendelea kuimarisha taaluma ya ununuzi na ugavi kwa kuzingatia sheria na matumizi ya teknolojia, kushiriki kutoa elimu kwa umma, kusimamia migogoro ya mikataba, kufanya ukaguzi wa bidhaa na kuzuia bidhaa bandia ili kuhakikisha fedha za umma zinatumika kwa ufanisi na miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa wakati.

Alisema kaulimbiu ya mkutano huo, inayohusu kuimarisha ushiriki wa kitaaluma na kuwezesha makundi maalum pamoja na SMEs kunufaika na fursa za ununuzi wa umma, inalenga kuwafanya wataalamu kuwa kiungo muhimu kati ya sheria, urasimishaji wa biashara na utekelezaji wa maendeleo nchini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya APSP, Dkt. Emmanuel Urembo, alisema mustakabali wa taaluma hiyo unategemea uwezo wa wataalamu kuendana na maendeleo ya teknolojia, kuzingatia maadili na kutoa ushauri wa kimkakati. Alibainisha kuwa chama kina wanachama zaidi ya 2,200 na kimepata mafanikio ikiwemo kusaini mikataba ya ushirikiano, kulipa deni la kiwanja la shilingi milioni 134 na kusajili nembo ya chama kupitia BRELA.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria na Uzingatiaji kutoka BRELA, Wakili Lamecky Nyangi Samson, alisema wataalamu wa ununuzi wana mchango mkubwa katika kuhamasisha urasimishaji wa biashara kwa kuzingatia sheria na kuunganisha wafanyabiashara na fursa zinazotokana na ununuzi wa umma.

Akifunga mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa PPRA, Bw. Denis Kwame Simba, aliwataka washiriki kutumia mifumo ya kielektroniki kwa ufanisi, kuzingatia uwazi, ushindani na thamani ya fedha, kutenga asilimia 30 ya zabuni kwa makundi maalum, kusimamia vihatarishi, kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa wakati na kuzingatia masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika utekelezaji wa shughuli za ununuzi wa umma.

 




Tanga, Julai 28, 2026


Katika kuendeleza dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSI) chini ya kampeni yake ya #PSSSFKaribuNaJamii, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umekabidhi rasmi mradi wa miundombinu wenye thamani ya Shilingi milioni 25 katika Shule ya Msingi Majani Mapana iliyopo mkoani Tanga.


Mradi huo unahusisha ujenzi wa chumba cha darasa, chumba cha mapumziko pamoja na vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bw. Kwame Temu alieleza kuwa msaada huo unalenga kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum wanapata haki yao ya msingi ya elimu. Alisisitiza kuwa hatua hiyo itawasaidia wanafunzi hao kujifunza katika mazingira yanayowawezesha kujifunza kwa ufanisi, kushiriki katika michezo na kukuza vipaji vyao mbalimbali.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Kata ya Nguvumali, Bi. Lilian Shetui, aliishukuru PSSSF kwa mchango huo akieleza kuwa miundombinu hiyo itaongeza ubora wa huduma za elimu shuleni hapo. Kwa niaba ya Afisa Elimu Shule za Awali na Msingi wa mkoa huo, Bi. Lilian alipongeza PSSSF kwa kuona umuhimu wa kundi hilo na kutoa msaada utakaokuwa na tija kubwa kwa watoto hao.

Kupitia mchango huo, jumla ya wanafunzi 71 wenye mahitaji maalum na usonji katika Shule ya Majani Mapana wanatarajiwa kunufaika na mazingira rafiki ya kujifunzia, kupumzika na kucheza, hatua inayochochea elimu jumuishi na kuwajengea msingi bora wa maisha ya baadaye.




 


Na OWM – TAMISEMI, Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Bw. Sospeter Mtwale, ameongoza kikao kazi kati ya ofisi yake na Shirika lisilo la Kiserikali la World Vision Tanzania, kilicholenga kujadili Mkakati wa Jubilee 2026–2030 uliowasilishwa na World Vision Tanzania wa kuboresha ustawi wa watoto nchini.

Mkakati huo uliofanyika leo Julai 29, 2026 unalenga kuwafikia watoto moja kwa moja kupitia programu za afya, lishe, elimu, ulinzi wa mtoto, huduma za maji safi na usafi wa mazingira (WASH), pamoja na kuimarisha kipato cha kaya. 

Akifafanua kuhusu lengo la mkakati huo, Mkurugenzi wa Ubora na Mikakati wa World Vision Tanzania Bw. Simon Moikan amesema, mpango huo  unakusudia kushughulikia changamoto tatu zinazoendelea kuathiri mamilioni ya watoto nchini ambazo ni utapiamlo, utoro wa shule na ukatili dhidi ya watoto.

Mara baada ya Mkakati huo kuwasilishwa, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI Bw. Sospeter Mtwale alitoa fursa kwa wataalamu kutoka idara mbalimbali za Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI zinazoshughulikia masuala ya ustawi wa watoto pamoja na wataalamu kutoka World Vision Tanzania, kujadiliana kuhusu namna bora ya kuratibu ushirikiano katika utekelezaji wa mkakati huo iwapo mamlaka itaridhia, pindi utakapowasilishwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kwa hatua za uidhinishaji.

Majadiliano hayo  yanaakisi dhamira ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa maendeleo katika kuhakikisha watoto wa Tanzania wanapata huduma bora na mazingira salama yanayowezesha ukuaji, maendeleo na ustawi wao.