Viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii leo, Agosti 4, 2026, wamehitimisha Mkutano wao wa Kimkakati (Retreat) kwa kufanya ziara maalumu ya kutembelea vivutio vya utalii ndani ya Hifadhi ya Taifa Nyerere kupitia Game Drive na utalii wa boti, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi.


 


Katibu wa NEC, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kitaifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Rabia Abdalla Hamid, leo Agosti 4, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Kitengo cha Siasa kutoka Ubalozi wa Marekani nchini, Ndugu Garvey Pierre, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba, Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo ni sehemu ya kuendeleza ushirikiano na kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa na uhusiano wa kimataifa.
Afya njema ndiyo msingi wa kila mafanikio na furaha maishani. Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka mitatu, maisha yangu yaligeuka kuwa mfululizo wa maumivu makali yasiyovumilika.

Kila siku nilitawaliwa na maumivu makali ya miguu na mgongo yaliyokuwa yakinichoma kama sindano za moto au kuniunguza kwa ndani. Nilibaki siwezi kukaa kwa muda mrefu, siwezi kutembea umbali mfupi, wala siwezi kulala kwa amani kitandani.

​Tulitembea kwenye hospitali kubwa na za kisasa zaidi nchini. Nilifanyiwa vipimo vya kila aina kuanzia MRI, X-ray, hadi vipimo vya damu kwa madaktari bingwa wa mifupa na neva.

Hata hivyo, kila vipimo viliporudi, majibu yalikuwa yale yale ya kushangaza: vipimo vilionyesha kuwa mimi niko salama kabisa na sina tatizo lolote linaloweza kusababisha maumivu hayo! Nilipewa dawa kenda za kutuliza maumivu (painkillers), lakini hazikusaidia kitu zaidi ya kuniongezea kizunguzungu.

Akiba yangu yote ilisha kwa kulipa bili za hospitali, huku kazi na biashara zangu zikiwa zimesimama kabisa na kunifanya nionekane kama mtu aliyepooza na aliyetengwa na ulimwengu. SOMA ZAIDI.

 ​

Usingizi ni zawadi ya pekee inayomwezesha mwanadamu kupumzika na kupata nguvu mpya baada ya mahangaiko na uchovu wa mchana. 

Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka miwili, kwangu mimi usiku ulikuwa ni wakati wa hofu, mateso, na jinamizi lisiloelezeka.

Kila mara nilipoweka kichwa changu kitandani na kufumba macho, badala ya kupata mapumziko, nilitawaliwa na ndoto mbaya na za kutisha sana. ​

Nilitawaliwa na ndoto za kufukuzwa na wanyama wa ajabu niliokuwa sijawahi kuwaona sura zao zilikuwa za kutisha, zenye macho ya moto na pembe zisizo za kawaida.

Katika ndoto hizo, nilikuwa nikikimbia kwa kasi kubwa huku nikipiga yowe bila sauti kutoka, nikijikwaa na kuanguka huku wanyama hao wakiniingia na kunitishia maisha.

Nilikuwa niamka katikati ya usiku nikiwa nimeloa jasho mwili mzima, moyo ukienda mbio kama unataka kutoka kifuani, na mwili mzima ukiwa umechoka kana kwamba nilikuwa nikikimbia kweli barabarani.

Nilianza kuogopa hata kulala, nikibaki macho usiku kucha huku afya yangu ya mwili na akili ikizorota kwa kasi. SOMA ZAIDI.

 

Kutafuta fedha ni kazi ngumu inayohitaji jasho, muda, na akili nyingi, lakini hakuna maumivu makubwa kama kuona matunda ya kazi yako yakitoweka mikononi mwako kama moshi.

Kwa miaka kadhaa, nilikuwa nikifanya kazi kwa bidii na kupata mshahara pamoja na faida nzuri kwenye biashara zangu ndogo ndogo. Hata hivyo, maisha yangu ya kifedha yaligeuka kuwa fumbo la kutisha.

Kila pesa iliyoingia kwenye mikono yangu au akaunti yangu ya benki ilikuwa ikipotea kihasara na kwa njia za ajabu sana bila mimi kufanya la maana.

​Nikipokea fedha leo, kesho yake zingeibuka dharura zisizoelezeka simu au kifaa cha gharama kinaharibika ghafla, ugonjwa usiotarajiwa unaingia nyumbani, au kosa dogo linalogharimu fedha nyingi.

Hata pale nilipojaribu kuficha pesa taslimu kwenye kabati au pochi, nilikuta zimepungua bila mtu yeyote kugusa! Nilikuwa nikikaa na kuhesabu fedha zangu jioni, lakini kufika asubuhi nakuta kiasi kikubwa kimetoweka.

Nilibaki nikiwa na madeni yasiyotibika, nikikopa hapa na kurejesha pale, huku wenzangu niliowaingiza kwenye biashara wakipiga hatua na kujenga maisha yao. SOMA ZAIDI.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amekutana na kuagana na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Christine Grau, kufuatia kukamilika kwa muda wake wa uwakilishi nchini.



Na Oscar Assenga, TANGA

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Rashid Mchatta amefungua kikao kazi cha Wakurugenzi na Mameneja wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini huku akisisitiza matumizi teknolojia ya kisasa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao.

Wito huo umetolewa jijini Tanga na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, wakati akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Sekta ya Maji nchini.

Kikao hicho kinafanyika chini ya kaulimbiu “Huduma Janja: Matumizi ya Teknolojia kwa Huduma Bora kwa Wateja”, kikilenga kuwawezesha wakurugenzi na mameneja hao kubadilishana uzoefu na kujadili mbinu mbalimbali za kuboresha huduma kwa wananchi.

Mchatta aliipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini na kuiwezesha Wizara ya Maji kutekeleza miradi na programu mbalimbali zinazolenga kuboresha upatikanaji wa maji safi na huduma za usafi wa mazingira nchini.

Pia aliipongeza uongozi wa Wizara ya Maji unaoongozwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, Naibu Waziri, Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Rose Ambrose, kwa juhudi wanazofanya katika kusimamia utekelezaji wa majukumu ya wizara hiyo.

Alisema mafanikio yanayoonekana katika sekta ya maji, kuanzia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati hadi uboreshaji wa huduma kwa wananchi, yanaonesha kuwa uongozi wa wizara hiyo umejikita katika kuhakikisha huduma zinaboreshwa kila siku.

“Viongozi hawa wameonesha weledi, uzoefu na uthubutu katika kusimamia sekta ya maji. Ushirikiano wao umeendelea kuleta mafanikio yanayoonekana na wananchi wanaendelea kushuhudia mabadiliko katika huduma za maji na usafi wa mazingira,” alisema Mchatta.

Alisema kikao hicho ni fursa muhimu kwa wakurugenzi na mameneja wa huduma kwa wateja kujifunza, kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza katika utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa Mchatta, mafunzo hayo pia yanahusu ufanisi wa biashara katika mamlaka za maji pamoja na mbinu za uwekezaji binafsi, ambapo wataalamu kutoka UTT-AMIS wanashiriki kutoa elimu kwa washiriki.

Aliwataka washiriki kutumia kikamilifu fursa hiyo kujifunza mbinu mpya, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma kwa wateja.

“Ninaamini mafunzo haya yatakuwa chachu ya kuboresha ufanisi mtakaporudi katika vituo vyenu vya kazi na hivyo kuongeza ubora wa huduma mnazozitoa kwa wananchi,” alisema.


JUKWAA LA WAKURUGENZI LAZIDI KUKUA

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini, Alawi Ahmad, alisema jukwaa hilo ni sehemu muhimu ya uongozi katika sekta ya maji, kwa kuwa linawapa nafasi wakurugenzi na mameneja kukutana, kujadiliana na kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma.

Alisema jukwaa hilo limekuwa likifanya vikao kila mwaka na kwa sasa lina takribani miaka 10 tangu kuanzishwa kwake.

“Jukwaa hili limekuwa likitusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utoaji wa huduma kwa wateja na pia limetumika kama sauti ya pamoja ya wakurugenzi wa huduma kwa wateja katika sekta ya maji,” alisema Ahmad.

Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Abbas Muslim Pyarali alisema kikao hicho kinawakutanisha wakurugenzi wa mamlaka za maji wanaojikita katika utoaji wa huduma kwa wateja.

Abbas ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Maji alisema kikao hicho kitakachodumu kwa siku tatu kitawapa washiriki nafasi ya kupata mafunzo maalumu na kubadilishana uzoefu kuhusu namna bora ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Wizara ya Maji za kuhakikisha huduma za maji safi na usafi wa mazingira zinaendelea kuboreshwa nchini.








Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza hekari 3,117.9 za mashamba ya bangi na kukamata watuhumiwa 12 katika operesheni maalum ya siku 16 iliyofanyika katika vijiji vinne vya Kata ya Kandawale na Kipatimo, Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi.

 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mkutano mkuu wa wanahisa wa Afrika50 na jukwaa la miundombinu Afrika, Agosti 03, 2026, Ofisi za Wizara ya Fedha, jijini Dar es salaam.

TANZANIA itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), yatakayofanyika Agosti 5 na 6, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Dar es Salaam.

Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mwenyeji na mwenyekiti wa hafla ya ufunguzi wa mkutano huo, ambao pia utahusisha taasisi mbalimbali za umma na sekta binafsi nchini, benki za biashara na maendeleo, taasisi za hifadhi ya jamii, masoko ya mitaji na wadau wa sekta za nishati, uchukuzi, reli, bandari, usafiri wa anga, maji, afya, madini, mafuta na gesi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, leo Septemba 03, 2026  Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, amesema mkutano huo wa kimataifa unafanyika wakati Africa50 inatimiza miaka 10 tangu kuanza shughuli zake mwaka 2016, huku ukitarajiwa kukutanisha washiriki zaidi ya 1,200 kutoka Afrika na maeneo mbalimbali duniani.

Balozi Omar amesema Africa50 ilianzishwa mwaka 2013 kwa ushirikiano wa Serikali za Afrika na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ikiwa na lengo la kuharakisha maandalizi, uendelezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya miundombinu kupitia ubia kati ya Serikali na sekta binafsi katika sekta za nishati, uchukuzi, afya, elimu, TEHAMA na huduma za kifedha.

Amesema Tanzania ilijiunga rasmi na Africa50 Februari 14, 2023 kama mwanahisa wa kundi la “A” (African Sovereign States), hatua iliyopanua fursa za nchi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na ufadhili wa miradi mikubwa ya miundombinu.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, tangu kujiunga na taasisi hiyo, Tanzania imeanza kunufaika kupitia maandalizi ya miradi ya kimkakati ikiwemo maendeleo ya Bandari ya Mangapwani Zanzibar, Mradi wa Mini Liquefied Natural Gas (Mini LNG), miundombinu ya usafirishaji wa umeme na upanuzi wa huduma za usafishaji wa figo (dialysis) kupitia ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP).

Mkutano wa mwaka 2026 unafanyika chini ya kaulimbiu isemayo “A Decade of Economic Impact: From Ambition to Delivery.”

Balozi Omar amesema katika kipindi cha siku mbili za mkutano kutakuwa na Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50, Jukwaa la Miundombinu Afrika na hafla za kusaini makubaliano mbalimbali ya maandalizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya miundombinu.

Amesema kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo, Tanzania itapata fursa ya kuendelea kujitangaza kama kitovu cha uwekezaji na maendeleo ya miundombinu Afrika Mashariki, kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na taasisi za fedha za kimataifa, pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika miradi ya kimkakati yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

“Serikali inawahakikishia wananchi kuwa maandalizi yote yanaendelea vizuri kwa ushirikiano na Africa50 pamoja na taasisi mbalimbali za Serikali ili kuhakikisha mkutano huo unafanyika kwa mafanikio makubwa,” amesema Balozi Omar.

Ameongeza kuwa Serikali inawakaribisha wananchi kuendelea kutoa ushirikiano na kuwapokea wageni watakaofika nchini kwa ajili ya mkutano huo, ambao unatarajiwa kuwa miongoni mwa mikutano mikubwa ya kimataifa itakayofanyika nchini mwaka 2026.


 

Kusoma kwa miaka mingi na kupata shahada ya chuo kikuu ni hatua inayokupa matumaini makubwa ya kupata ajira nzuri na kujenga maisha yako. Baada ya kumaliza masomo yangu miaka mitano iliyopita, nilianza harakati za kuomba kazi za serikali na kwenye taasisi kubwa.

Nilikuwa na sifa zote zilizohitajika, viwango vya juu vya taaluma, na uwezo mkubwa wa kujieleza. Hata hivyo, maisha yangu ya utafutaji yaligeuka kuwa mfululizo wa maumivu na kukata tamaa kulikoingia akilini.

​Kila mara nilipoomba kazi, nilipita kwenye usahili wa mchujo (interview) kwa alama za juu sana. Lakini ajabu ni kwamba, ilipofika hatua ya mwisho ya kutoa majina ya waliopata ajira, jina langu lilipotelea hewani au kutupwa kimyakimya!

Watu niliowazidi uwezo na alama walikuwa wakichukuliwa, huku mimi nikibaki mtaani nikichekwa na kusaidiwa chakula na wazazi wangu.

Nilifanya usahili zaidi ya mara kumi na tano katika miaka hiyo mitano, lakini kila mara nilibaki ukingoni mwa mafanikio. Nilibaki nikijiuliza ni kwanini elimu na juhudi zangu hazikuwa zikizaa matunda.SOMA ZAIDI.

 

Kujenga nyumba ya kifahari na kuweka msingi imara wa maisha ni hatua inayompa kila mtafutaji heshima kubwa. 

Baada ya kufanya kazi kwa bidii ughaibuni na kuwekeza akiba yangu yote, nilipata kiwanja kizuri na kuanza ujenzi wa nyumba kubwa ya ghorofa moja kwa ajili ya familia yangu.

Mwanzo kila kitu kilienda kwa kasi na matumaini makubwa. Hata hivyo, mara tu kuta zilipoinuka na kuanza kuonekana kwa majirani na ndugu, vita vya chini kwa chini vilianza bila mimi kutarajia.

​Ujenzi ulianza kukumbana na ajali na mikosi isiyoelezeka. Mafundi bora niliowakodi walianza kuugua ghafla pindi tu walipokanyaga kwenye eneo la mradi, wengine wakipata majeraha ya ajabu na kukimbia kazi.

Vifaa vya ujenzi kama simenti na nondo vilikuwa vikiharibika au kupotea kimyakimya, na pesa nilizokuwa nikituma zilipotea kwenye dharura zisizotabirika.

Kumbe bila mimi kujua, baadhi ya ndugu zangu wa damu waliokuwa wakijifanya kunipongeza kwa nje, ndio waliokuwa wakizunguka usiku kufanya fitina na matambiko ya giza ili mradi wangu ufe na nifilisike!SOMA ZAIDI.

 


Kila mwanamume anapofikisha umri fulani na kufanikiwa kijamii, hamu yake kubwa ni kupata mke mwema wa kujenga naye familia na kuendeleza maisha.

Nikiwa na umri wa miaka 32, nikiwa na kazi nzuri na nyumba yangu mwenyewe, nilijiona nipo tayari kabisa kuoa.

Hata hivyo, maisha yangu ya mahusiano yaligeuka kuwa fumbo la kutisha na lenye kuumiza moyo kwa zaidi ya miaka minne.

Kila mara nilipompata binti mstaarabu, mwenye tabia njema na tukakubaliana kuoana, mambo yalianza kubadilika ghafla pindi tu alipokanyaga mlangoni kwangu.

Binti ambaye jioni tulikuwa na amani na furaha tele, ikifika usiku alipatwa na hofu isiyoelezeka, ndoto za kutisha za kuingiliwa na majitu, au maumivu makali ya mwili.

Ndani ya siku chache au wiki moja pekee, kila binti alifunganya virago vyake na kukimbia nyumba yangu huku akisema hawezi kuendelea kuishi pale.

Zaidi ya wasichana sita tofauti waliondoka kwa mtindo huo huo bila mimi kufanya kosa lolote, jambo lililonifanya nianze kuonekana kama mwanamume aliyelaaniwa au mwenye nuksi ya ajabu. SOMA ZAIDI.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ametembelea Banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) akiwa ameambatana na Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mhe. John Malechela, Nzuguni – Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafadh Ameir, amesisitiza nafasi muhimu ya wanawake wanataaluma katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026, Naibu Waziri amesema kuwa kauli mbiu ya hafla hiyo, “The Contribution of Women Professionals to the Implementation of Tanzania Development Vision 2050”, imeakisi mchango wa wanawake katika kujenga uchumi wa maarifa, ubunifu na teknolojia.

Ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu. Hatua zilizotekelezwa ni pamoja na maboresho ya sera na sheria, ujenzi wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika ufundishaji na ujifunzaji.

Aidha, amesisitiza kuwa mchango wa wanawake hauwezi kupuuzwa na kwamba Serikali ikiendelea kuimarisha usawa wa kijinsia, kuongeza ushiriki wa wanawake katika fani za STEM, kuzuia ukatili wa kijinsia na kuwekeza katika maendeleo ya kitaaluma ya walimu na wahadhiri kupitia mafunzo endelevu na tafiti.

Naibu Waziri ametoa wito kwa walimu, wakufunzi na wahadhiri kuendelea kuwa chachu ya mabadiliko ya Taifa kwa kuandaa kizazi chenye maadili, maarifa na ubunifu.

“Mustakabali wa Taifa upo mikononi mwa vijana na wanafunzi,” amesisitiza, akiwataka kutumia kikamilifu fursa za elimu zinazotolewa na Serikali ili kuleta suluhisho kwa changamoto za kijamii na kiuchumi." amesema Naibu Waziri

Naye Mbunge Viti Maalum Mwakilishi wa Vyuo Vikuu, Mhe. Asha Feruzi, amesema kuwa hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026 ni jukwaa la kujadili mustakabali wa elimu, ubunifu na teknolojia katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mhe. Feruzi amebainisha kuwa matokeo yanayotarajiwa kupitia ushirikiano huo ni kuimarika kwa tafiti, ubunifu na matumizi ya teknolojia za kisasa, hususan akili unde (Artificial Intelligence). Ameongeza kuwa vyuo vikuu na sekta binafsi vitaunganishwa ili kuzalisha suluhisho, bidhaa na huduma zinazochochea ukuaji wa uchumi shindani na endelevu.