Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

JIJI la Dar es Salaam limezindua Jukwaa la Mifumo ya Chakula litakalokuwa chombo cha kuunganisha wadau mbalimbali katika kuboresha upatikanaji wa chakula salama, bora na chenye lishe kwa wakazi wa jiji hilo.

Na.Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani ya Somali  imefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza uzoefu na mbinu zinazotumiwa na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika kusimamia ushindani wa kibiashara, kudhibiti bidhaa bandia na kulinda maslahi ya walaji.

Ziara hiyo imefanywa na Mkurugenzi wa Masuala ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na Kamishna wa Mamlaka ya Ushindani ya Afrika Mashariki (EACA), Bw. Ahmed Warsame pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Upatikanaji wa Masoko wa Wizara ya Biashara na Viwanda ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Bw. Abdihalim Osman.

Katika ziara hiyo, ujumbe huo umekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, pamoja na uongozi wa Tume, ambapo walipata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kukuza na kulinda ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, uongozi wa ujumbe wa Somalia umepongeza utendaji wa FCC, ukieleza kuwa uzoefu wa Tanzania katika kusimamia ushindani na kulinda mlaji ni muhimu kwa Somalia katika kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa soko na kukuza mazingira bora ya biashara.

Ujumbe huo umeeleza kuwa kujifunza kutoka FCC kutasaidia kuongeza uelewa na uwezo wa taasisi za Somalia katika kukabiliana na changamoto zinazohusu ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwadhuru walaji.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema  kuwa Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na taasisi za Somalia na nchi nyingine katika kubadilishana uzoefu, maarifa na mbinu bora za usimamizi wa ushindani na ulinzi wa walaji.

Ziara hiyo ya siku moja imekuwa fursa muhimu kwa Somalia kujifunza uzoefu wa Tanzania katika eneo la ushindani wa kibiashara, udhibiti wa bidhaa bandia na ulinzi wa mlaji, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi na kuchangia katika ujenzi wa masoko yenye ushindani wa haki na biashara endelevu.

 


Ukosefu wa Mawasiliano na taarifa sahihi miongoni mwa wamiliki wa leseni za uchimbaji madini unaweza kuchochea migogoro isiyo ya lazima na kudhoofisha shughuli za uchimbaji, hasa kwa wachimbaji wadogo.

Hayo yamebainishwa leo Septemba 15, 2026 jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, wakati akiongoza kikao cha kutatua mgogoro uliowahusisha wachimbaji wadogo jijini humo.


Dkt. Kiruswa amesema mgogoro huo umetokana kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa taarifa sahihi na mawasiliano baina ya wabia wanaomiliki kwa pamoja leseni 33, ambapo upande mmoja uliamini kuwa baadhi ya wabia wanafanya uzalishaji bila kumshirikisha na bila kumpatia stahiki zake, huku upande mwingine ukieleza kuwa katika leseni hizo bado haujaanza uzalishaji.

Baada ya kusikiliza pande zote, Dkt. Kiruswa amewataka wamiliki hao kuweka mfumo wa wazi na wa pamoja wa mawasiliano, huku wakihakikisha kila mmoja anatambua mipaka na maeneo ya leseni wanazomiliki ili kuondoa sintofahamu zinazoweza kusababisha migogoro.

Aidha, amewataka wachimbaji wadogo kujenga utamaduni wa kuaminiana, kushirikiana na kuheshimiana, akisisitiza kuwa chuki na kutokuelewana miongoni mwa wabia kunaweza kuchelewesha maendeleo na kupunguza manufaa yanayopaswa kupatikana kutokana na rasilimali madini.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa ametoa angalizo kwa wamiliki wa leseni nchini kuhakikisha wanazifanyia kazi leseni walizopewa na Serikali, akieleza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kwa leseni ambazo hazijaendelezwa kwa mujibu wa masharti yake.

Amesema leseni ambazo zitabainika kutotumika kwa shughuli za uchimbaji kwa mujibu wa taratibu zitafutwa na maeneo hayo kutolewa kwa wachimbaji wenye uwezo na nia ya kuendeleza shughuli za uchimbaji.

Dkt. Kiruswa amesema Serikali, chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa wachimbaji wadogo ili waweze kushiriki kikamilifu katika sekta ya madini na kunufaika na rasilimali zilizopo nchini.

Katika ziara hiyo, Dkt. Kiruswa pia ametembelea na kukagua shughuli za Soko la Madini la Mkoa wa Mwanza, akijionea namna shughuli za biashara ya madini zinavyoendeshwa na kusisitiza umuhimu wa masoko hayo katika kuwawezesha wachimbaji kupata soko rasmi na kuongeza mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.


Dkt. Kiruswa amesema mgogoro huo umetokana kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa taarifa sahihi na mawasiliano baina ya wabia wanaomiliki kwa pamoja leseni 33, ambapo upande mmoja uliamini kuwa baadhi ya wabia wanafanya uzalishaji bila kumshirikisha na bila kumpatia stahiki zake, huku upande mwingine ukieleza kuwa katika leseni hizo bado haujaanza uzalishaji.

Baada ya kusikiliza pande zote, Dkt. Kiruswa amewataka wamiliki hao kuweka mfumo wa wazi na wa pamoja wa mawasiliano, huku wakihakikisha kila mmoja anatambua mipaka na maeneo ya leseni wanazomiliki ili kuondoa sintofahamu zinazoweza kusababisha migogoro.

Aidha, amewataka wachimbaji wadogo kujenga utamaduni wa kuaminiana, kushirikiana na kuheshimiana, akisisitiza kuwa chuki na kutokuelewana miongoni mwa wabia kunaweza kuchelewesha maendeleo na kupunguza manufaa yanayopaswa kupatikana kutokana na rasilimali madini.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa ametoa angalizo kwa wamiliki wa leseni nchini kuhakikisha wanazifanyia kazi leseni walizopewa na Serikali, akieleza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kwa leseni ambazo hazijaendelezwa kwa mujibu wa masharti yake.

Amesema leseni ambazo zitabainika kutotumika kwa shughuli za uchimbaji kwa mujibu wa taratibu zitafutwa na maeneo hayo kutolewa kwa wachimbaji wenye uwezo na nia ya kuendeleza shughuli za uchimbaji.

Dkt. Kiruswa amesema Serikali, chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa wachimbaji wadogo ili waweze kushiriki kikamilifu katika sekta ya madini na kunufaika na rasilimali zilizopo nchini.

Katika ziara hiyo, Dkt. Kiruswa pia ametembelea na kukagua shughuli za Soko la Madini la Mkoa wa Mwanza, akijionea namna shughuli za biashara ya madini zinavyoendeshwa na kusisitiza umuhimu wa masoko hayo katika kuwawezesha wachimbaji kupata soko rasmi na kuongeza mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.


 



Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amemtaka Mkandarasi anayetekeleza miradi ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara katika Jiji la Dodoma kuongeza kasi ya ujenzi ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuwanufaisha wananchi.

Mhe. Senyamule ametoa agizo hilo, Septemba 14, 2026, wakati akikagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi na uboreshaji wa barabara katika maeneo ya katikati ya Jiji la Dodoma.

Amesema uboreshaji wa miundombinu ya barabara ni muhimu katika kuboresha mazingira ya biashara, kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Aidha, Mhe. Senyamule ameiagiza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kabla ya Novemba 2026, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua za El Niño zinazotarajiwa.

Amesema kukamilika kwa wakati kwa miradi hiyo ni muhimu zaidi katika maeneo ambayo shughuli za biashara zinaendelea pembezoni mwa barabara zinazoendelea kujengwa, kwa kuwa kuchelewa kwa miradi kunaweza kuongeza usumbufu kwa wananchi na wafanyabiashara, hususan wakati wa msimu wa mvua.

“Ni lazima tujiandae kwa mvua hizi kwa kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati ili kupunguza usumbufu na athari zinazoweza kujitokeza kwa wananchi,” amesema Mhe. Senyamule.

Katika ziara hiyo, Mhe. Senyamule alikagua mradi wa uboreshaji wa barabara nane kwa kiwango cha Lami (Asphalt Concrete), wenye urefu wa jumla ya kilomita 1.06 katika maeneo ya katikati ya Jiji la Dodoma.

Mradi huo unatekelezwa na M/S Msekwa General Enterprises Co. Ltd., ikiwa ni sehemu ya juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuboresha miundombinu ya barabara na kujenga mazingira bora na rafiki kwa shughuli za mijini.

Kaimu Mhandisi wa Jiji la Dodoma, Mhandisi Ally Yusuph Bellah, amesema Halmashauri inaendelea kuwekeza katika maendeleo ya miundombinu kwa kutumia mapato yake ya ndani, ambapo asilimia 10 ya mapato hayo hutengwa kwa ajili ya miundombinu ya barabara.

Amesema fedha hizo zinatumika kutekeleza miradi mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa barabara za lami, vivuko vya waenda kwa miguu, taa za barabarani pamoja na mifumo ya mifereji ya maji ya mvua.

Mhandisi Bellah amesema uwekezaji huo unalenga kuboresha mtandao wa barabara za Jiji, kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za umma na kuweka mazingira salama na rafiki kwa wananchi na wafanyabiashara.

Ziara ya Mhe. Senyamule ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhakikisha inakamilika kwa wakati, inazingatia viwango vinavyotakiwa na kukidhi mahitaji ya wananchi.

 

Makandarasi wanaotekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara za kuingia viwanja vya mazoezi na uendelezaji wa barabara ya uwanja wa Taifa ambayo itatumika wakati wa michuano ya AFCON wametakiwa kufanyia kazi maelekezo yote wanayopatiwa na Wakala ya Barabara za Vijini na Mijini (TARURA) kabla ya kuanza kwa mvua za El Nino.

Msisitizo huo umetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TARURA Mhandisi Florian Kabaka wakati wa ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara hizo jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Kabaka amesema kwamba Makandarasi hawapaswi kuzungumza tu bali kutekeleza kwa kufanyia kazi yale yote wanayoshauriwa na kuelekezwa na Wakala huo ili mvua zitakavyoanza kunyesha iwakute wamemaliza ujenzi wa mitaro ya maji na hivyo kuepusha maeneo muhimu kutokupata changamoto za maji na kuathiri miundombinu mingine.

Aidha, Mwenyekiti huyo amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi unaoendelea na kuwapongeza kwa kufanya kazi usiku na mchana, pia kuwepo kwa wataalam, mitambo na vifaa vingine inatoa matumaini ya kufikia hatua nzuri hadi kufikia mwisho wa mwezi huu.

Amesema miradi yote inayotekelewa Dar es Salaam imefikia 50% na kuwasisitiza kuongeza kasi zaidi.

Pamoja na hayo, Mhandisi Kabaka aliwatoa hofu wananchi kwamba TARURA watahakikisha wanaboresha barabara zote muhimu wakati wa El Nino ili wananchi wasikwame katika kupata huduma muhimu.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff amesema miradi hiyo inaendelea vizuri na wao kama wasimamizi wataendelea kuwafuatilia kwa karibu ili kuhakikisha kazi zinamalizika kwa wakati ifikapo Desemba mwaka huu.

Pia amesema kwa hatua iliyofikiwa ana uhakika barabara zote zitakamilika kwa viwango na kufikiwa masharti yaliyowekwa.

 Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa Malaigwanani ,wazee na kina mama maarufu wapatao 33 kutoka kata 11 za ndani ya eneo la hifadhi Ngorongoro ili kuwajengea uwezo wa kutambua fursa mpya za kiuchumi.


Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kamishina Msaidizi Mwandamizi anayeshughulikia huduma za jamii bi Gloria Bideberi amesema lengo la semina hiyo ni kuhakikisha Malaigwanani na wazee hao wanapata elimu ya kutosha kuhusu ujasiriamali na namna ya kutumia fursa zinazopatikana katika maeneo yao.

Bi. Gloria alieleza kwamba elimu hiyo itakwenda sambamba na ziara za kujifunza kwa vitendo, ambapo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ikiwemo kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za maziwa Tanga Fresh kilichopo Mkoani Tanga ili kujifunza namna bidhaa zinavyozalishwa, kuendelezwa na kufikishwa katika masoko.

“Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha kuwa wananchi hawa wanapata elimu ya kutosha na kuwawezesha kutembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ili kujifunza kwa vitendo zaidi,” alisema Gloria

Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuimarisha ushiriki wa jamii katika maendeleo endelevu ya eneo la Hifadhi Ngorongoro.









Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Yusuf Masauni, amelitambua na kulipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa nafasi yake muhimu kama Mlezi na mdau wa kitaasisi wa Tanzania Green Summit.





Na; Mwandishi Wetu- Dar es Salaam

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Makatibu Wakuu kutoka katika Wizara zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), Wakuu wa Taasisi pamoja na Wakurugenzi wa Sekta, pamoja na wataalam kutoka katika sekta hizo na Ujumbe Kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mtaa wa Magogoni Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Septemba 2026.

Kikao hicho kimefanyika baada ya ziara maalumu ya wataalamu kutoka IFAD na AFDP kukamilisha ziara ya kutembelea maeneo yanayotekeleza Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi ya kupima matokeo utekelezaji wa program ya muda wa kati (MTR)


Pamoja na mambo mengine IFAD wamepongeza Serikali kwa Kusimamia vyema Shughuli za Programu kwa kuleta matokeo chanya kwa wananchi..Aidha kikao hicho kimepokea wasilisho la dondoo lnayoainisha hoja za makubaliano yaliyopendekezwa kuhusiana na mwenendo wa utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP).



 Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashiriki katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la Maadili ya Akili Unde linaloendelea mjini Riyadh, Saudi Arabia, likiwakutanisha wawakilishi kutoka nchi mbalimbali duniani kujadili namna ya kuhakikisha maendeleo na matumizi ya akili unde yanaongozwa na maadili, uwajibikaji na kuhudumia maslahi ya jamii.

Jukwaa hilo linatoa nafasi kwa nchi na wadau mbalimbali kubadilishana uzoefu na kujadili masuala yanayohusu mustakabali wa akili unde, ikiwemo namna ya kuimarisha mifumo ya sera na utawala, kujenga uwezo na kuhakikisha teknolojia hiyo inatumika kwa kuzingatia haki za binadamu, usalama, usawa na uwajibikaji.

Kwa Tume ya Taifa ya UNESCO, ushiriki huo ni sehemu ya kuendelea kuunganisha Tanzania na UNESCO katika mijadala na ajenda za kimataifa zinazohusu sayansi, teknolojia, elimu, utamaduni na maendeleo ya jamii.

Tume inawakilishwa katika jukwaa hilo na Bi Fides Mallya, Afisa Programu kutoka Sekta ya Sayansi Jamii ya Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anayeshiriki katika shughuli na mijadala mbalimbali inayoendelea katika jukwaa hilo.

TUME YASHIRIKI MJADALA WA AFRIKA

Katika jukwaa hilo, Tume ya Taifa ya UNESCO inashiriki pia katika mjadalawa viongozi na wadau kutoka Afrika unaolenga kujadili namna bara hilo linavyoweza kuwezeshwa ili kunufaika kikamilifu na maendeleo ya teknolojia ya akili unde.

Mjadala huo unaangazia umuhimu wa Afrika kuimarisha uwezo wake katika sayansi, teknolojia, utafiti, ubunifu na ujuzi wa kidijitali, pamoja na kujenga mazingira bora ya kisera na kitaasisi yatakayowezesha matumizi salama na yenye tija ya akili unde.

Kwa kushiriki katika mjadala huo, Tume inaendelea kufuatilia mwelekeo wa kimataifa kuhusu akili unde na kuchangia katika mijadala inayolenga kuhakikisha maendeleo ya teknolojia hiyo yanazingatia mahitaji ya jamii na yanachangia maendeleo jumuishi na endelevu.

USHIRIKI WA TUME WAIUNGANISHA TANZANIA NA UNESCO

Ushiriki wa Tume katika jukwaa hilo unaonesha nafasi yake muhimu kama kiungo kati ya Tanzania na UNESCO, kwa kuwezesha ushiriki wa nchi katika mijadala, programu na ajenda za UNESCO katika ngazi ya kimataifa.

Kupitia majukwaa hayo, Tume inaendelea kufuatilia maendeleo na mwelekeo wa kimataifa katika maeneo ya UNESCO, kubadilishana uzoefu na nchi nyingine na kutafuta fursa za ushirikiano zinazoweza kuchangia maendeleo ya Tanzania.

Katika eneo la akili unde, ushiriki huo unaipa Tume fursa ya kufuatilia mijadala kuhusu maadili, utawala na matumizi yanayowajibika ya teknolojia hiyo, huku ikiendelea kuhusisha mijadala ya kimataifa na mahitaji ya maendeleo ya Tanzania.

UJUMBE WA TUME WAKUTANA NA BALOZI

Katika mwendelezo wa ushiriki wa Tume katika jukwaa hilo, ujumbe wa Tanzania unaoshiriki katika shughuli za jukwaa umepata fursa ya kufanya kikao na Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia.

Kikao hicho kimekuwa fursa ya kubadilishana taarifa kuhusu ushiriki wa Tanzania katika jukwaa hilo na kuimarisha uratibu kati ya ujumbe wa Tanzania na Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia katika masuala yanayohusu shughuli za kimataifa.

Jukwaa la Nne la Kimataifa la Maadili ya Akili Unde linaendelea mjini Riyadh likiwa sehemu ya juhudi za kimataifa za kuimarisha ushirikiano katika kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanaenda sambamba na maadili, uwajibikaji, haki za binadamu na maendeleo jumuishi.