NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) imewahimiza wananchi na wadau wa maendeleo kutembelea banda lake katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) ili kupata huduma mbalimbali na elimu kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake.
Na Mwandishi Wetu

NDOTO za vijana wa Tanzania wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali nje ya nchi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 zimeingia hatua muhimu baada ya Global Education Link kuwakutanisha wanafunzi hao pamoja na wazazi na walezi wao kwa ajili ya kuhakiki nyaraka na kukamilisha maandalizi ya safari.
Siku nilipogundua kwamba mume wangu alikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine, nilihisi dunia yangu imeporomoka. 

Tulikuwa tumekaa kwenye ndoa kwa miaka kadhaa na niliamini tulikuwa tunajenga maisha mazuri pamoja. Kugundua ukweli huo kuliniacha na maumivu makubwa, hasira, na maswali mengi ambayo sikuwa na majibu yake.

Mwanzoni nilitaka kukabiliana nao kwa hasira.
Nilifikiria kumpigia simu mwanamke huyo na hata kwenda kumtafuta ili tuzungumze. Lakini kila nilipotulia, niliona kwamba ugomvi usingeweza kujenga ndoa yangu upya. Nilihitaji suluhisho ambalo lingeokoa familia yangu.SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha kampuni yangu, nilikuwa na ndoto ya kuifanya ikue na kushindana na kampuni kubwa zilizokuwa sokoni. 

Tulifanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kila mteja anapata huduma bora. Hata hivyo, ili kampuni iweze kupiga hatua kubwa, tulihitaji kupata zabuni kubwa ambayo ingetupa nafasi ya kukua. Haikuwa rahisi.

Mara kadhaa niliwasilisha maombi ya zabuni katika taasisi mbalimbali, lakini kila mara nilipokea taarifa kwamba kampuni nyingine ndiyo ilikuwa imechaguliwa. 

Kila kushindwa kuliniongezea maumivu na kunifanya nipoteze matumaini. Baada ya muda, hali ya kifedha ya kampuni ilianza kuwa mbaya.

Mapato yalipungua na baadhi ya miradi ilisimama kutokana na ukosefu wa fedha. Nilianza kuogopa kwamba ningelazimika kufunga kampuni ambayo nilikuwa nimeijenga kwa miaka mingi. Nilikuwa karibu kukata tamaa. SOMA ZAIDI.

Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kufanikiwa. Nilichagua eneo zuri, nikahakikisha bidhaa zangu zina ubora, na nilihudumia kila mteja kwa heshima. Mwanzoni biashara ilikuwa inaenda vizuri, lakini baada ya muda idadi ya wateja ilianza kupungua.

Kila siku nilifungua duka nikiwa na matumaini.
Lakini mara nyingi nilimaliza siku bila kuuza chochote cha maana. Wakati mwingine nilikaa kwa saa nyingi nikisubiri mteja mmoja tu aingie dukani. Gharama za kodi, umeme na bidhaa ziliendelea kuongezeka huku mapato yakizidi kushuka.

Nilijaribu kila nilichoweza. Nilitangaza biashara yangu, nikapunguza bei za bidhaa na hata nikaanzisha ofa maalumu, lakini bado hali haikubadilika. Nilianza kufikiria kufunga biashara kwa sababu hasara zilikuwa zimekuwa nyingi. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miaka sita, niliishi nikipigania ardhi ambayo nilijua ilikuwa yangu halali. Nilikuwa nimeinunua kwa fedha nilizozitafuta kwa jasho, lakini muda mfupi baadaye watu wengine walianza kuidai. 

Kila nilipofikiri mgogoro umeisha, changamoto mpya iliibuka. Nilizunguka katika ofisi mbalimbali nikitafuta haki yangu, lakini sikuona mwisho wa matatizo hayo.

Hali hiyo ilininyima amani. Sikuweza kuendeleza mipango yangu ya kujenga nyumba kwa sababu sikuwa na uhakika kama ningebaki na ardhi hiyo. 

Watu wengi walinishauri niikate tamaa na nitafute sehemu nyingine, lakini moyo wangu haukukubali kupoteza mali yangu. SOMA ZAIDI.
Dada yangu alikuwa mtu wa karibu sana katika maisha yangu. Tulikulia pamoja, tukashirikiana katika kila hatua ya maisha, na tuliamini hakuna jambo ambalo lingeweza kututenganisha. Lakini baada ya kutokea mgogoro wa kifamilia, kila mmoja alichukua upande wake na mawasiliano yakakatika kabisa.

Mwaka mmoja ukawa miwili. Miaka miwili ikawa mitano, na kabla hatujagundua, miaka kumi ilikuwa imepita bila kuonana wala kuzungumza. Kila mmoja aliendelea na maisha yake kana kwamba mwenzake hakuwahi kuwepo. Nilikuwa nikimuona kwenye sherehe za kifamilia mara chache.

Lakini kila mmoja aliepuka mwenzake. Hakukuwa na salamu, hakukuwa na mazungumzo, na hali hiyo iliwaumiza hata wazazi wetu ambao walitamani kutuona tukipatana tena. Kadri miaka ilivyozidi kusonga, nilianza kuona pengo kubwa lililokuwa limejitokeza ndani ya familia yetu. SOMA ZAIDI.

 


Awataka kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa wanafunzi walioshiriki mashindano ya UMISSETA mwaka 2026 kuendeleza vipaji vya michezo na Sanaa walivyonavyo kwani vitawasaidia katika maisha yao ya baadaye, huku akiwataka kuzingatia nidhamu na kusoma kwa bidii ili  kufikia ndoto zao na kutoa mchango katika maendeleo ya taifa.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa wanafunzi leo Juni 28, 2026 mjini Iringa katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Lugalo, wakati akifunga mashindano ya UMISSETA kwa mwaka wa 2026.

“Nina wasihi muendelee kuwa na nidhamu, kujituma katika masomo yenu na kuendeleza vipaji vyenu vya michezo na sanaa, msiviache vipaji vyenu kwani hata mimi juzi tulipokuwa tunapokea Mwenge wa Uhuru Lushoto nilijikuta nikikumbushia kipaji changu cha kupiga ngoma za utamaduni na kuimba kwa umahiri,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amewahakikishia wanafunzi hao kuwa, Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kuhakikisha vipaji vya wanafunzi vinaibuliwa, vinatambuliwa, vinakuzwa ili kuwanufaisha na kulinufaisha taifa kupitia ushiriki wao katika kuliwakilisha taifa kwenye mashindano ya michezo na Sanaa ndani na nje ya nchi.

Aidha, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu, michezo, sanaa na maendeleo ya vijana kwenye ajenda kuu ya taifa na kuongeza kuwa, uwekezaji huo unaendelea kuweka msingi imara wa kuibua na kuendeleza vipaji vya watoto na vijana wa Tanzania.

 Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Bw. Atupele Mwambene amesema kuwa, ushiriki wa wanafunzi katika michezo mbalimbali ya UMITASHUMTA na UMISSETA umeendelea kuwa jukwaa muhimu la kitaifa la kuibua vipaji, kuimarisha afya, kujenga urafiki na kuendeleza umoja wa kitaifa miongoni mwa wanafunzi. 

Naye Mwakilishi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Leah Kihimbi amemuhakikishia Prof. Shemdoe kuwa wizara yake itatekeleza ipasavyo jukumu la kuibua kuendeleza vipaji na vipawa vinavyotokana na mashindano hayo ya sanaa na michezo shuleni. 

Mwakilishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ambaye ni Afisa Mdhamini Bw. Mohamed Nassoro Salimu amesema Zanzibar inakwenda kujipanga ili kuleta ushindani mkubwa katika mashindano ya mwakani, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kufanya mageuzi katika sekta ya michezo.

Akitoa neno la shukrani, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru amewashukuru maafisa elimu, wakuu wa shule, walimu, waratibu wa michezo na walezi wa wanafunzi, kwa kazi kubwa walioifanya ya kuwaandaa na kuwaleta wanafunzi katika mashindano ambayo yamewawezesha kujifunza thamani ya nidhamu, ushindani wa haki, uvumilivu, uzalendo na mshikamano wa kitaifa.















NAIBU Waziri wa Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Longido Mkoani Arusha, Dkt Steven Kiruswa amewataka wananchi wa jimbo hilo kujenga umoja  na wananchi wa nchi jirani ya Kenya kwani viongozi wa juu ya nchi hizo wanamahusiano mazuri na hivyo nao wanapaswa kufuata nyayo hizo. 

Kiruswa alisema hayo juzi katika kijiji cha Kimwat kilichopo kata ya Sinonik wilayani Longido ambacho kipo mpakani mwa Kenya wakati akizindua miradi miwili ya maendeleo ikiwemo mradi wa Zahanati na mradi wa maji vyote vikiwa na gharama ya zaidi ya shilingi milioni 188.3 miradi hiyo imetekelezwa kwa mchango wa Mbunge Kiruswa , nguvu za wananchi,shirika lisilo la kiserikali la Pingo's na fedha kutoka serikali kuu.

Alisema kijiji hicho na kata kwa ujumla walikuwa wakipata huduma ya maji ,elimu na afya katika nchi jirani ya Kenya kutokana na mahusiano mazuri waliyajenga na wananchi wa nchi hizo lakini awamu ya sita ya uongozi wa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan huduma hiyo inapatikana nchini na sasa wananchi wa Kenya wanakuja kupata huduma hizo hapa nchini.

Kiruswa alisema kutokana na uhusiano mzuri na wananchi wa Kenya na Tanzania ndio màana Uzinduzi wa miradi hiyo umehudhuriwa wananchi wa nchini humo wakiongozwa na viongozi wao akiwemo  Afisa Mtendaji Kijiji cha Meto,Peter Milia na Joseph Kink Afisa Mtendaji wa Kata ya Meto.

Alisema mradi wa Zahanati ulianza kujengwa june 2023 na kukamilika mwaka huu yeye binafsi amechangia kiasi cha shilingi milioni 5,michango ya wananchi sh milioni 11 na fedha toka serikali kuu zilipelekwa shilingi milioni 80 na sasa Zahanati hiyo inahudumia wananchi wa Kijiji cha Kimwat na wananchi wa nchi jirani.

Naibu Waziri kiruswa aliipongeza Pingo’s kwa kusimamia na kutoa fedha shilingi milioni 70 ,michango ya wananchi shilingi milioni 2.3 na Mbunge shilingi milioni 20 na kusema kuwa mradi huo utasaidia wananchi na wananchi na mifugo na utekelezaji huo ni kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) kufikisha huduma karibu na wananchi.

Naye Mkuu wa wilaya ya Longido ,Salumu Kally amewaomba wananchi wa Longido kumpa ushirikiano Mbunge Kiruswa kwani kiongozi mwenye upendo na wananchi wake na amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha huduma zote muhimu ikiwemo miradi ya Maji ,Afya ,elimu ,umeme na Barabara inakamilika kwa maslahi ya wananchi wake hivyo hapasŵi kupotezwa katika uongozi wake.

Naye Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kimwat Rosemary Mbogho wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi Kiruswa alisema kijiji kinakabiliwa na changamoto ikiwemo upungufu wa watumishi wa Zahanati,nyumba za watumishi ,madarasa ,barabara na umeme katika vitongoji na Mbunge Kiruswa aliahidi yeye na marafiki zake kujenga nyumba ya watumishi na suala la barabara alimwagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini(TARURA) kutekeleza hilo kwani bajeti fedha hizo zipo.