Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Serikali inaendelea kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na upatikanaji wa umeme nchini, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka 2026/2027. 

Amesema hayo Aprili 23, 2026  Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja za wabunge mara baada ya kuwasilishwa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati ya Mwaka 2026/2027.

Akijibu hoja hizo amesema Rais wa Jamuhurinya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia, akilenga kufikisha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia  ifikapo mwaka 2034 huku akifafanua kuwa matumizi hayo yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi zaidi ya asilimia 28 kwa sasa, huku jitihada hizo zikilenga kulinda mazingira na afya za wananchi.

Aidha, ameeleza kuwa Serikali imesambaza zaidi ya kilomita 56.4 za mabomba ya gesi asilia, mitungi ya gesi zaidi ya laki tatu, majiko ya gesi zaidi ya elfu 49 na majiko ya umeme zaidi ya elfu saba ambapo  zaidi ya taasisi 55 zimepatiwa majiko ya nishati safi, huku mpango ukiwa kufikia taasisi zaidi ya 400.

Katika kuhakikisha upatikanaji wa umeme vijijini  zaidi ya visiwa 120 kati ya 143 tayari vimepata umeme wa sola kwa ruzuku ya asilimia 45 hadi 75  hatua inayolenga kuwaondoa wananchi katika matumizi ya vibatari na kuboresha maisha yao kwa ujumla.








Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) pamoja na Menejimenti ya NEEC, tarehe 23 Aprili 2026 walifanya ziara maalum ya kutembelea mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) katika maeneo ya Ntondo mkoani Singida na Sojo mkoani Tabora.

 


📌Ni shilingi trilioni 2.53

📌Serikali kuja na mradi wa kuunganisha umeme kwa sh.27,000 katika maeneo ya Mjini yenye sura ya Vijiji

📌Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2000 kwa makaa ya mawe mbioni

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha kwa kishindo shilingi trilioni 2.53 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Nishati 2026/2027.

Kati ya fedha hizo, Shilingi trilioni 2.46 sawa na asilimia 97.5 ya bajeti yote  imeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 2.5 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Akihitimisha hoja kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2026/2027 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi alilieleza Bunge kuwa Wizara ya Nishati itaendelea kuhakikisha kwamba maono ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi na mwelekeo uliowekwa kwenye Dira 2050 yanatekelezwa kwa vitendo na kwa haraka.

Kutokana na hilo alieleza kuwa lengo lililowekwa kwa Wizara la kuzalisha umeme  wa megawati 8000 ifikapo 2030 litatekelezwa kwani Wizara ya Nishati imeshajipanga kuzalisha kiasi hicho cha umeme huku ikidhamiria kuzalisha megawati 70,000 ifikapo 2050.

"Ili kutekeleza lengo hili tutatumia vyanzo vyote vinavyopatikana kwenye Taifa letu ikiwemo vyanzo vya maji kama vile Malagarasi (49.5MW), Kakono (87MW), Ruhudji (358), Rumakali (222MW),  Jeothemo na makaa ya mawe.." Alisema Mhe. Ndejembi

Akifafanua kuhusu mradi wa uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe, Mhe. Ndejembi alisema Tanzania ina hifadhi kubwa ya makaa hayo na sasa Serikali inashirikiana na Sekta binafsi ili kuhakikisha kuwa inaanza uzalishaji wa megawati zaidi ya 2000 kwa kutumia nishati hiyo.

Aliongeza kuwa miradi mingine  itakayowezesha kufikia lengo la uzalishaji wa megawati 8000 ifikapo 2030 ni pamoja na miradi ya umeme Jua ikiwemo  ya Kishapu, Manyoni, Zuzu, miradi ya upepo ya Same, Makambako pamoja na kuzalisha umeme kwa kutumia urani.

Aidha, Mhe. Ndejembi aligusia suala la kufikisha umeme kwenye maeneo ya wananchi akieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha umeme unatoka kwenye vyanzo vya uzalishaji na kufikia maeneo ya wananchi na ya uzalishaji kama vile migodi viwanda n.k

Katika jitihada hizo za kufikisha umeme kwa wananchi alisema mradi wa kufikisha umeme wa gridi mikoa ya Mtwara na Lindi  kupitia ujenzi wa njia ya umeme ya kV 220 ya Songea- Tunduru- Masasi-Mahumbika unaendelea huku mkandarasi akiwa ameshalipwa shilingi bilioni 83 kwa ajili ya kuendelea na kazi.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Nishati aliiagiza TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) kuwasiliana na Wabunge wote ambao wana maeneo ambayo ni Manispaa/Majiji/ Halmashauri za Mji lakini yana sura ya vijiji ambayo wananchi wake wanalipa zaidi ya shilingi 27,000  kuunganisha umeme ili kuvitambua vijiji hivyo na kuja na mradi utakaohakikisha  wananchi katika vijiji hivyo wanaunganishiwa umeme kwa shilingi 27,000 tu ndani ya mwaka mmoja. 

" Serikali hii ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu na haiwezi kuweka matabaka ya wananchi, mtu amekaa ng'ambo moja analipa 27,000 na ng'ambo nyingine analipa 320,000 hili halikubaliki, Serikali imesikia changamoto hii na inaifanyia kazi, tutahakikisha umeme unawaka katika vijiji ambavyo vipo ndani ya miji." Alisema Mhe. Ndejembi

Kuhusu suala la kufikisha umeme kwenye Taasisi kama vile shule, zahanati n.k aliitaka REA kufanya tathmini ili kutambua taasisi ambazo hazijapelekewa umeme katika vijiji vyenye umeme ili ziweze kuunganishiwa.

Aidha, kuhusu suala la mafuta alisema kufungwa kwa mlango  bahari wa Hormuz kunaleta changamoto kubwa ya upatikanaji mafuta duniani kwani asilimia 20 ya nishati ya mafuta inatoka katika mlango bahari huo lakini kutokana na Serikali ya Tanzania kujali wananchi wake, nchi ina mafuta ya kutosha na hakuna kituo ambacho kimefungwa kwa kukosa nishati hiyo tofauti na baadhi ya maeneo mengine duniani.

Vilevile kuhusu bei ya mafuta alieleza kuwa Serikali inafanya kila jitihada ili ziwe himilivu huku ikihakikisha mafuta yanapatikana muda wote na  hifadhi mpya ya mafuta inayojengwa jijini Dar es Salaam eneo la Kigamboni ikitoa hakikisho la uhifadhi wa mafuta.

Vilevile alieleza kuwa, ili kurahisisha upatikanaji wa mafuta katika maeneo mbalimbali  nchini Serikali inajenga bomba la kusafirisha mafuta safi kutoka Dar es Salaam hadi Ndola, Zambia litakokuwa na matoleo na matenki ya kuhifadhi mafuta katika mikoa ya Morogoro, Njombe na Songwe na hivyo kupunguza msongamano jijini Dar es Salaam na kuondoa mzigo barabarani.

Katika Gesi Asilia, Mhe. Ndejembi alisema Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linafanya kazi kubwa kuhakikisha Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia inazidi kuimarika na sasa Shirika hilo linaendelea na miradi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa bomba la gesi la km 34 kutoka Ntorya hadi Madimba, wanachimba kisima kingine cha gesi katika eneo la Mnazi Bay ambacho kimeonekana kina hifadhi kubwa ya gesi mara mbili ya makisio ya awali, vilevile Shirika hilo linaendelea na  utafutaji wa mafuta katika kitalu cha Eyasi Wembere.

Aidha kuhusu mradi mkubwa wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika ( LNG)  alisema kuwa kwa sasa Serikali imefikia hatua za mwisho kuweza kuanza mradi na kwamba makubaliano ya kibiashara na kikodi yamekamilika na hatua inayoendelea sasa ni makubaliano ya kisheria.

Aliongeza kuwa, katika mradi wa LNG tayari  kuna kazi ambazo tayari zimeshaanza kama vile ulipaji fidia na ujenzi wa shule ya Likong'o.

Ili kuhakikisha wazawa wanashiriki ipasavyo katika mradi wa LNG alisema Serikali imeielekeza TPDC  kwenda mkoa wa Lindi kutoa elimu ya fursa zitakazopatikana huku Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) ikitakiwa kuwajengea uwezo wazawa ili mradi utakapoanza waweze kushiriki katika nyanja  mbalimvali ikiwemo utoaji wa huduma. ‎<This message was edited>

 


-Moshi, Kilimanjaro

Katika hatua kubwa inayolenga kuleta mapinduzi kwenye soko huria na kumlinda Mlaji. Mamlaka ya Ushindani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCA) zimekutana Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro leo Aprili 23, 2026 na kuwaapisha rasmi wajumbe wapya wanne kutoka Nchi za Tanzania, Somalia, Uganda na DRC ambao watasimamia mazingira mazuri ya ushindani wa biashara na walaji kwa Jumuiya hiyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewataka waajiri na wafanyakazi nchini kuyatazama upya mazingira ya kazi ili kuhakikisha yanakuwa salama na rafiki kwa afya, hususan afya ya akili.

Na Oscar Assenga, Tanga

Katika kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia duniani, Shule ya Sekondari Coastal High School imetangaza mpango kabambe wa kuanzisha programu ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) ifikapo Januari 2027.

Mpango huo unalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kisasa utakaowawezesha kushindana katika soko la ajira la Kimataifa.

Akizungumza wakati wa mahafali ya Kidato cha Sita yaliyofanyika jijini Tanga, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Isack Dastan Kifwete  alisema kuwa tayari wameanza kuchukua hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa mpango huo.


Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kufanikisha upatikanaji wa huduma ya intaneti kupitia Kampuni ya TTCL, pamoja na kuwepo kwa mtaalamu wa TEHAMA shuleni hapo.

Hata hivyo, alibainisha kuwa bado kuna changamoto kadhaa zinazokwamisha utekelezaji wa mpango huo kwa ufanisi unaohitajika.

Alizitaja changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vifaa muhimu kama kompyuta za kisasa, ubao janja (smart board), pamoja na miundombinu ya chumba maalumu kitakachotumika kufundishia programu ya AI.

Mbali na hilo, shule pia ina mpango wa kuanzisha programu ya Habari na Mawasiliano ya Umma, unaolenga kuwajengea wanafunzi uwezo wa uandishi wa habari, mawasiliano, pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa katika tasnia ya habari.

Tayari maandalizi ya awali, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya studio, yameanza kufanyika.

Pamoja na jitihada hizo, Mwalimu Mkuu alieleza kuwa shule bado inahitaji vifaa muhimu ili kukamilisha studio hiyo.

Vifaa vinavyohitajika ni pamoja na kamera za kisasa, meza ya matangazo, vifaa vya kuzuia kelele, vinasa sauti, vipaza sauti pamoja na kompyuta zenye uwezo wa kisasa.

Aidha, alitaja changamoto nyingine zinazoikabili shule kuwa ni pamoja na baadhi ya wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati kutokana na hali ngumu ya kiuchumi, pamoja na ushiriki mdogo wa wazazi na walezi katika masuala ya kitaaluma na malezi ya wanafunzi.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule umetoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia jitihada hizo ikiwemo kuwaomba wadau msaada wa vifaa kwa ajili ya kuanzisha studio ya habari, pamoja na kuunganishwa na taasisi au watu binafsi wanaoweza kusaidia upatikanaji wa kompyuta za kisasa.

Kwa ujumla, mpango huu unaonesha dhamira ya dhati ya shule katika kuwajengea wanafunzi msingi imara wa elimu ya kisasa ili kuwaandaa kukabiliana na dunia inayoendeshwa na teknolojia kwa kasi kubwa.

Awali, akizungumza katika mahafali hayo,Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar (CCM), Ussi Salum Pendeza, alisema kuwa atashirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha baadhi ya changamoto zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka.

Alisema kuwa ataanza mwenyewe kuchangia upatikanaji wa baadhi ya vifaa muhimu, ikiwemo kompyuta za kisasa na ubao janja, sambamba na kuhamasisha wadau wengine kushiriki.

“Katika hili la ubao janja na baadhi ya kompyuta, nitaanza mimi mwenyewe. Pia nitahakikisha michango inapatikana na kuwashirikisha wengine. Nachukua nafasi hii kuwashukuru walimu na Bodi ya Shule ya Coastal kwa ushirikiano wao katika kuhakikisha shule inafanya vizuri na matokeo yanakuwa mazuri,” alisema.

Ussi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Taasisi ya Pendeza Foundation, alisema anajivunia kuiongoza shule hiyo na ameahidi kuendelea kuisimamia ili iweze kufanya vizuri zaidi na kujulikana kitaifa.

Baraza kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) limekutana kujadili na kuweka mwelekeo wa vipaumbele vya Mamlaka kuelekea mwaka wa fedha 2026/2027, likilenga kuimarisha utoaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi.
Naibu Katibu Mkuu (Taaluma) Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt. Mwanakhamis Ameir (kulia) na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha (kushoto) wakisaini mkataba maalum kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya elimu visiwani Unguja na Pemba.

 



#Ataka kazi zikamilike ifikapo Mei 2027

Arusha

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara zinazoingia katika uwanja utakaotumika kwa mashindano ya AFCON jijini Arusha.

Mhandisi Seff amesema kwamba ziara hiyo imelenga kujionea hatua za utekelezaji wa mradi wa barabara zenye urefu wa kilomita 21.4 ambapo kazi tayari zimeanza katika sehemu ya barabara ya Essuri.

Amesema serikali imejipanga kuhakikisha miundombinu hiyo inakamilika kwa wakati na kuongeza kuwa maeneo ambayo bado hayajaanza yanasubiri kukamilisha taratibu za fidia kwa wananchi watakaoathiriwa na mradi huo huku mkakati ukiwa ni kuendelea kuzungumza nao ili kutoa ushirikiano na kuruhusu kazi ziendelee bila vikwazo.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha barabara hizi zinakamilika ifikapo Mei mwaka 2027 ili ziwe tayari kabla ya mashindano ya AFCON,” amesema Mhandisi Seff.

Aidha, amesema mradi huo unatekelezwa kwa utaratibu wa Sanifu na Jenga (Design and Build) unaotumika pale ambapo muda ni mchache huku hatua zote za ununuzi tayari zikikamilika.

Ameeleza kuwa TARURA itaendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha mkandarasi anakamilisha kazi kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa sanjari na ratiba ya mashindano hayo makubwa ya Mataifa ya Afrika.

Ameongeza kuwa kwa sasa Mkandarasi M/s China Railway Construction Engineering Group tayari ameanza kazi ambapo ameanza na barabara ya Essuri yenye urefu wa kilomita 2.45 pia kutajengwa daraja lenye urefu wa mita 100.

Kwa upande wa barabara ya Lendita yenye kilomita 2.75, Mhandisi Seff amesema barabara hiyo itajengwa pamoja na daraja katika awamu ya pili ya mradi huku barabara hiyo ikitarajiwa kuwa ya njia nne.

Ameongeza kusema pia barabara ya Mateves yenye kilomita 6.5 itajengwa kwa sehemu mbili ambapo kilomita 5.5 zitakuwa njia mbili na kilomita 1 itakuwa njia nne.

Mtendaji Mkuu huyo amesema kukamilika kwa mradi huo kutaleta mafanikio makubwa kwa Taasisi hiyo kwa kupata uzoefu wa kusimamia miradi ya Sanifu na Jenga, huku wananchi wakinufaika kwa kuondokana na changamoto ya miundombinu katika maeneo hayo.

Vilevile, amesema wakazi wa maeneo yanayozunguka mradi huo watapewa kipaumbele cha ajira na amewataka vijana kujitokeza kupata ajira na kutumia fursa hiyo kujiongezea kipato pamoja na uzoefu wa kazi.

Kwa upande mwingine amewataka wasimamizi wa mradi huo kusimamia kwa karibu utekelezaji wake kwani mashindano hayo yanatarajiwa kuanza Julai mwakani.

Naye, Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya M/s Afrisa Construction Engineering Group Bw. Idephonce Karol amesema mradi huo ulianza rasmi tarehe 1 Aprili, 2026 na kwa sasa hatua za awali zinaendelea vizuri.

Amesema tayari wamehamasisha timu ya wataalamu, kufanya upimaji wa maeneo yote matatu ya barabara, uchunguzi wa udongo, tathmini ya vifaa vya ujenzi pamoja na kusafisha sehemu ya barabara ya Essuri urefu wa kilomita 1.8.

“Tumejipanga kikamilifu na tunafahamu umuhimu wa mradi huu hivyo tutafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha unakamilika kwa wakati,” amesema Karol.














Na Oscar Assenga,TANGA

MKURUGENZI wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani Segule Segule amewataka wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kauli hiyo ameitoa baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.



Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.



Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.



Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.



Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.

Wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Onyo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Segule Segule, baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.

Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.

Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekabidhi tuzo kwa Mkoa wa Njombe ikiwa ni Mshindi wa Jumla wa Shindano la Afya na Usafi wa Mazingira kwa Mwaka 2024.

WITO umetolewa kwa viongozi wa Serikali za Mitaa nchini kuimarisha ushirikiano na Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mifuko ya Elimu ya Halmashauri ili kuongeza kasi ya maendeleo ya sekta ya elimu.
Afisa Masoko wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Bw. Fihiri Mbawala, akitoa ufafanuzi kwa Bi. Rauhya Omary, muuzaji wa duka la pembejeo za mifugo la Manispaa ya Lindi, tarehe 22 Aprili 2026, kuhusu mbinu bora za kuhakikisha mazingira ya uhifadhi wa chanjo yanazingatia viwango vinavyotakiwa ili kudumisha ubora na ufanisi wake, wakati wa ziara ya utoaji elimu ya matumizi sahihi ya chanjo zilizofanyika mikoa ya Lindi na Mtwara.