Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amezipa siku 20 Viwanda vya saruji vya Tanga Cement na Twiga Cement kukutana na wanachama wa ushirika wa wachimbaji wa madini ya jasi (gypsum) kutoka Kijiji cha Makanya, Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, ili kufikia muafaka wa utaratibu wa biashara ya malighafi inayotumika viwandani humo.

Akizungumza Januari 28, 2026 wakati wa kikao cha pamoja kati ya wawekezaji hao na Serikali kupitia Wizara ya Madini, Dkt. Kiruswa alisema Serikali inalenga kuona biashara ya madini ya jasi inanufaisha pande zote, kuhakikisha viwanda vinapata malighafi kwa uendelevu huku wachimbaji na jamii zinazozunguka migodi zikinufaika kiuchumi na kimazingira. 

Alisisitiza kuwa anatoa siku 20, kufikia tarehe 20 Februari 2026, uongozi wa Kampuni inayomiliki viwanda hivyo na ushirika wa wachimbaji hao kukaa pamoja na kukubaliana namna bora ya uratibu wa biashara hiyo bila kuathiri upande wowote na kwamba kikao hicho kihusishe uongozi wa kijiji hicho na vyama vya wachimbaji ili kuweka misingi ya uwazi, haki, uhusiano na uendelevu.

Katika kuhakikisha shughuli za uchimbaji na usafirishaji wa jasi zinafanyika kwa kuzingatia Sheria na maslahi ya jamii, Naibu Waziri alielekeza kampuni hiyo kutekeleza hatua zafuatazo ambazo ni Utunzaji wa Mazingira: Kupitia upya mikataba yote waliyoingia na wachimbaji, na kuhakikisha utunzaji wa mazingira unazingatiwa ipasavyo wakati wa uchimbaji wa madini ya jasi sambamba na kufukia mashimo yaliyoachwa wazi.

Hatua nyingine ni barabara inazoelekea maeneo ya uchimbaji ambayo kwa sasa ni mbovu inapaswa ifanyiwe ukarabati wa haraka ili kurahisisha usafirishaji na kupunguza athari kwa jamii ikiwemo vumbi kali pamoja  kuagiza mizigo ya madini ya jasi kununuliwa kwa watu wanaotambulika na kuthibitishwa na uongozi wa kijiji husika, ili kudhibiti migogoro na kuongeza uwajibikaji.

Pia, Dkt. Kiruswa alielekeza viwanda hivyo kutekeleza kikamilifu Miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa kuwa vinachukua malighafi kutoka katika kijiji hicho na kwamba wanapaswa kuchangia huduma za jamii kama elimu, afya na maji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ununuzi (Procurement Director) wa Kanda ya Afrika Mashariki anaesimamia Tanzania, DRC, Msumbiji na Afrika Kusini chini ya Heidelberg Materials, ambao ni wamiliki wa viwanda hivyo Ahmed Ali, alisema kuwa uongozi wa viwanda hivyo utaitisha kikao cha pamoja na wachimbaji hao wa jasi sambamba na wadau muhimu kwa ajili ya kushughulikia suala hilo na kwamba Kampuni italeta mrejesho Serikalini kama ilivyoelekezwa kufanyika ndani ya siku 20.

Mbunge wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiuliza swali la nyongeza leo Januari 29,2026 bungeni jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna, Dodoma

Mbunge wa Jimbo la  Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amehoji mpango wa Serikali wa kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mlandizi–Mzenga–Maneromango kwa kiwango cha lami, akisisitiza kuwa ni barabara muhimu kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni, Dkt. Jafo amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 70.2 inaanzia Mlandizi kupitia Mzenga hadi Maneromango, na kwamba tayari upembuzi yakinifu umekamilika.

Ameeleza kuwa kwa sasa mkandarasi ameanza kazi katika kipande cha Mzenga chenye urefu wa mita 300, hali iliyomfanya kuihoji Serikali kuhusu mpango wake wa kuongeza fedha katika bajeti ya mwaka huu ili kufungua kipande cha Mlandizi hadi Mzenga.

“Nini mpango wa Serikali katika bajeti ya mwaka huu kuongeza fedha ili kuhakikisha barabara hii muhimu inaanza kujengwa kuanzia Mlandizi hadi Mzenga?” amehoji Dkt. Jafo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema Serikali tayari imeonesha nia ya dhati ya kuijenga barabara hiyo, akibainisha kuwa kutokana na ukubwa na umuhimu wake, lazima ijengwe kwa kiwango cha lami.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutenga na kuongeza fedha kadri zinavyopatikana, ili kuhakikisha ujenzi wa barabara hiyo unaendelea hadi kukamilika kwa kiwango kilichokusudiwa.



Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Mwanza unaendelea na utekelezaji wa miradi 71 inayoendelea kujengwa katika wilaya mbalimbali ambapo ikikamilika inatarajiwa kupandisha wastani wa huduma ya maji vijijini mkoani humo kutoka wastani wa asilimia 73 ya sasa hadi kufikia asilimia 88 hivyo kuendelea kuimarisha uchumi wa mtu mmoja na jamii kwa ujumla.

Miradi hiyo inatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 151 kutoka vyanzo mbalimbali vya fedha ikiwemo Serikali Kuu, Programu ya lipa kwa matokeo (PforR) na Mfuko wa Taifa wa Maji.

Hayo yameelezwa na Meneja wa RUWASA mkoa wa Mwanza Mha. Godfrey Sanga wakati wa ziara ya timu ya Menejimenti ya taasisi hiyo kutoka Makao Makuu inayofanya tathimini ya uendeshaji wa huduma ya maji vijijini inayotolewa na Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) kote nchini.

Mha. Sanga alisema miradi hiyo ipo katika hatua tofauti za ujenzi ikiwemo mradi wa maji wa Ukiriguru wenye vijiji 19, na Ilujamahate-Buhingo utakaohudumia vijiji 16, na kwamba itakapokamilika itainua huduma kufikia vijiji vingi zaidi mkoani humo na kuendelea kukamilisha dhamira ya serikali ya kumtua mama wa kijijini ndoo kichwani.
Katika siku ya kwanza mkoani Mwanza, timu ya Menejimenti ya ukaguzi na tathimini ya kazi za CBWSO ilitembelea Chombo cha Nyamwaki kilichopo wilayani Magu na Miswaso kilichopo wilaya ya Kwimba ambapo zoezi hilo litaendelea katika wilaya za Misungwi na Segerema.





 -Rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri ipo Tayari : Dkt. Kiruswa

Na Wizara ya Madini, Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Madini inaendelea na mchakato wa kuanzisha Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania (Tanzania Geoscientists Registration Board – TGRB), ambapo kwa sasa ipo katika hatua ya kukusanya maoni na mapendekezo ya wadau kabla ya kuanzishwa rasmi kwa bodi hiyo.

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amesema hayo leo Januari 28, 2026, Bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Bukene, Mhe. Stephano Luhende, aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanzisha bodi hiyo ili kuongeza ufanisi katika sekta ya madini nchini.

Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa baadhi ya taratibu tayari zimekwisha tekelezwa, ikiwemo uandaaji wa rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri kuhusu kuanzishwa kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania.

Amefafanua kuwa kwa sasa Wizara ya Madini inaendelea na zoezi la kukusanya na kuchambua maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu masuala yatakayowezesha bodi hiyo kuanzishwa na kujiendesha kwa ufanisi, ikiwemo masuala ya uendeshaji na vyanzo vya fedha.

Ameongeza kuwa mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ukusanyaji na uchambuzi wa maoni, Wizara itawasilisha waraka huo katika ngazi za maamuzi za Serikali, ambazo ni kikao cha kitaalamu cha Makatibu Wakuu na kikao cha Baraza la Mawaziri, kwa ajili ya kujadiliwa na kupata ridhaa ya kuanzishwa rasmi kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania.

Nilijikuta katika wakati mgumu wa ndoa yangu baada ya tofauti kubwa kibiashara. Nilipoteza mwelekeo mzuri na mke wangu kutokana na migongano ya mali, mapato, na maamuzi ya kifedha.

Kila siku ilikuwa vita ya maneno, huzuni, na hata kukata tamaa. Nilihisi kuwa upendo wetu ulikuwa ukipotea, na kwa mara ya kwanza nilijisikia kutokuwa na maana nyumbani mwangu.

Nilijaribu kuzungumza naye, kujaribu suluhisho la kawaida, na hata kuomba msamaha kwa mambo madogo, lakini hila zetu za kibiashara zilikuwa kubwa na hazikubadilika.

Ndoa yetu ilianza kuathirika, na hofu ya kuachana kweli ilianza kuibuka kila siku. Nilijua lazima nifanye kitu tofauti, cha hekima na busara, la sivyo upendo wetu ungeharibika kabisa.Soma Zaidi.
Siku zote nimeamini kuwa mtu anaweza kupotea kwa muda na kurudi bila shida. Lakini nilipokabiliana na hali halisi, niligundua kuwa kupotea kwa mpendwa wangu kulileta hofu isiyoelezeka.

Rafiki yangu wa karibu alitoweka ghafla, bila onyo au ujumbe wowote. Kila siku ilikuwa changamoto, nikijaribu kumtafuta kwa marafiki, polisi, na hata mitandao ya kijamii, lakini kila njia ilishindikana.

Maumivu na hofu vilipanda kila siku. Nilihisi kuchanganyikiwa, kuumizwa kiasili, na aibu kubwa. Nilijua kwamba ni lazima nifanye kitu kisicho cha kawaida, kitu cha busara na hekima, la sivyo labda ningepoteza tumaini kabisa.Soma Zaidi.
Rafiki yangu alikuwa akiteseka kwa muda mrefu kutokana na asthma. Kila pumzi ilikuwa changamoto, kila mchango wa hewa ulileta maumivu, na maisha yake yalikuwa magumu.

Mara nyingi alikuwa amekosa usingizi wa kutosha, kuondoa uchovu, na hata kushiriki kikamilifu katika shughuli za kila siku. Hali hii ilimfanya kuwa na huzuni na kutokuwa na matumaini, na familia yake walihisi uchungu mkubwa kumwona akiteseka.

Tumejaribu kila njia ya kawaida dawa za hospitali, masharti ya kula vizuri, na mbinu za kawaida za kupumua lakini hakuna kilichofanikisha kupona. Nilijua lazima tufanye kitu tofauti, kitu cha hekima na busara, la sivyo mateso yake yangekuwa endelevu.Soma Zaidi.
Nilipokumbuka jinsi tulivyokutana na ex wangu, nilijua tulikuwa na historia ndefu ya upendo, lakini hatimaye tulitengana kwa sababu za tofauti za maisha.

Nilijaribu kuendelea na maisha yangu, lakini moyo wangu haukuweza kupumzika. Mara kadhaa tulijaribu kurudi pamoja, lakini nilikataa kwa sababu nilihisi ni bora kuendelea na maisha yangu bila marudio ya makosa ya zamani.

Hata hivyo, moyo wangu haukuweza kuacha tamaa ya kuwa naye tena. Nilijisikia huzuni, uchungu, na hasira kwa kila siku niliyokuwa mbali naye.

Nilijua lazima nifanye kitu, la busara na hekima, la sivyo nilijua nafasi yangu ya kumrejesha ingepotea milele.Soma Zaidi.
Kwa muda wa miaka mingi, nilikuwa nikitafuta mpenzi ambaye angeweza kunikubali na kunielewa. Nilijaribu kila njia ya kawaida mitandao ya kijamii, marafiki wa karibu, hata familia lakini kila mara nilishindwa.

Hali hii ilinifanya nijisikie kukosa thamani, huzuni, na uchungu wa pekee. Nilijua kwamba siyo tu moyo wangu unaumia, bali pia maisha yangu ya kila siku yalikuwa magumu bila upendo.

Nilijaribu kusahau, lakini kila siku nilijikuta nikitafuta matumaini. Nilijua lazima nifanye kitu cha tofauti, jambo la hekima na busara, la sivyo miaka yangu ya kutafuta mpenzi yangekuwa bure.Soma Zaidi.

 



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameshiriki katika mdahalo wa Mawaziri kuhusu uwekezaji na uimarishaji wa ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya mafuta na gesi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India (India Energy Week – IEW 2026) yanayoendelea kufanyika Goa, India.

Akizungumza katika mdahalo huo uliofanyika leo Januari 28, 2026, Mhe. Makamba ameeleza kuwa Tanzania inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwa kuzingatia fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya mafuta na gesi.

Amebainisha kuwa tafiti za kuchukua taarifa za mitetemo zinaendelea kufanyika katika vitalu vya Eyasi–Wembere, Lindi na Mtwara, sambamba na kukamilisha majadiliano na wawekezaji mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo Mradi wa Gesi Asilia Kimiminika (LNG).

Aidha, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika miradi ya usambazaji wa gesi kwa matumizi ya viwandani, uzalishaji wa umeme, matumizi ya majumbani pamoja na kuendesha magari.

“Sekta ya mafuta na gesi ni sekta muhimu na wezeshi katika kukuza uchumi wa taifa. Tanzania, kama zilivyo nchi nyingine zenye rasilimali za gesi asilia na mafuta, imeweka msisitizo mkubwa katika ushirikiano na sekta binafsi ili kunufaika na teknolojia na mitaji,” amesema Mhe. Makamba.

Amefafanua kuwa mahitaji ya nishati nchini yanaendelea kuongezeka kutokana na ukuaji wa kasi wa uchumi, hali inayoongeza uhitaji wa nishati ya uhakika na endelevu.

Pia, amesema jiografia ya Tanzania inaipa nchi fursa ya kuhudumia nchi jirani kupitia bandari zake pamoja na kuunganisha mifumo ya umeme na nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara, huku ikizingatia ulinzi wa mazingira.

Vilevile, Mhe. Makamba amesema Serikali inasisitiza kuwa mpito kuelekea matumizi ya nishati safi na rafiki kwa mazingira lazima uwe wa haki, usiomwacha mwananchi yeyote nyuma, kwa kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya gharama nafuu, salama na ya uhakika.

Maadhimisho ya Wiki ya Nishati ya India (IEW 2026) yanaendelea kutoa fursa kwa Tanzania kujitangaza katika majukwaa ya kimataifa, kuvutia wawekezaji zaidi na kuchochea ukuaji wa uchumi unaoendana na maendeleo ya teknolojia. 

Tanzania na Oman zimeendelea kuonyesha dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira ili kuongeza ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kukuza uchumi wa mataifa yote mawili.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi wa Oman, Dkt. Mahad bin Said bin Ali Baawain walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Aidha, katika kikao hicho Waziri Sangu alielezea umuhimu wa kukamilishwa na kutiwa saini kwa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira (MoU) kati ya nchi hizo mbili, ili kuweka mfumo rasmi na endelevu wa usimamizi wa masuala ya ajira, ulinzi wa haki za wafanyakazi na utatuzi wa changamoto za kiutendaji zinazojitokeza.

Vilevile, Waziri Sangu ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa fursa za ajira kwa Watanzania katika sekta mbalimbali. Pia, amesema idadi ya Watanzania wanaofanya kazi nchini Oman imeendelea kuongezeka , jambo linaloonesha kuimarika kwa mahusiano ya ajira kati ya mataifa hayo mawili.

Kwa upande mwingine, nchi hizo zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kwa kuendelea kupanua wigo wa ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kijamii kati ya mataifa yetu mawili.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

.....

Waziri Wa Maji Mhe. Jumaa Aweso  amewataka wakurugenzi wa bodi za maji za mabonde nchini kuonyesha umuhimu wa taasisi hizo kwa wananchi kwa vitendo kwa kutoa huduma sahihi.

Waziri Aweso ametoa maelekezo hayo katika kikao cha Bodi za maji za mabonde nchini katika ukumbi wa Jiji la Dodoma.

Aweso ambaye ndiye mgeni rasmi katika kikao hicho amewataka viongozi wa mabonde hayo kutambulika kwa utoaji wa huduma na si kutambulika kwa sifa mbaya kwa wananchi na serikali ikiwemo utozaji wa Kodi zisizi halali.

Aidha Serikali bado inaendelea na mpango mkakati iliyojiwekea katika kujenga mabwawa ya kimkakati kuendelea kupanda miti rafiki wa maji kwa mazingira Ili kuboresha vyanzo vya maji na kutoa huduma ya uhakika kwa wananchi.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewataka wakurugenzi na wenyeviti wa Bodi za maji za mabonde nchini kuendelea kutunza vyanzo vya maji Ili kuwa na uhakika wa huduma ya Maji kwa mwananchi.

Ameeleza kuwa vyanzo vya maji nchini ni muhimu katika kikao mabonde yanakuwa na maji ya kutosha kutoa huduma kwa wananchi.

Kadhalika Ili kuwe na uhakika wa utunzwaji wa vyanzo vya maji, amezitaka Bodi hizo kushirikiana na jamii na wadau wa mazingira ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI pamoja na taasisi zinazojihusisha na mazingira, Ili kuweka mipango mikakati ya Pamoja katika utunzwaji wa vyanzo vya maji.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso,akizungumza wakati wa Mkutano wa Tisa wa mwaka wa Bodi  za Maji za Mabonde nchini uliofanyika leo Januari 28,2026  Jiji la Dodoma.

 


Serikali imesema haina haja ya kuweka sharti la kisheria linalowalazimisha watoto kuwahudumia wazazi wao wasiojiweza, ikieleza kuwa suala hilo tayari linashughulikiwa kupitia misingi ya kifamilia na kijamii.

Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa kinondoni Mhe. Tarimba Gulam Abbas lililohoji "Je Serikali haioni haja ya kuweka sharti la kisheria la watoto wakubwa kutunza wazazi wao wasiojiweza"?

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inatambua umuhimu wa familia na jamii katika kuchukua jukumu la kulea na kuwahudumia wazee, akisisitiza kuwa huo ni msingi wa mila na desturi za Watanzania.

Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuimarisha huduma na matunzo kwa wazee kupitia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003, Toleo la mwaka 2024, ambayo inasisitiza wajibu wa familia na jamii katika kuwahudumia wazee wao.

“Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa familia na jamii katika kuchukua jukumu la kulea na kutunza wazee, kwani huu ndio msingi wa mila na desturi za Kitanzania na nguzo muhimu katika kujenga mshikamano wa kijamii. Katika kuimarisha huduma na matunzo kwa wazee, Serikali imefanikiwa kufanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003 na kuandaa toleo la mwaka 2024, ambalo linaeleza bayana wajibu wa familia na jamii katika kusimamia matunzo ya wazazi na wazee kwa ujumla, Sera hiyo pia imeweka msisitizo wa kuimarisha mifumo ya kisheria utakaolinda na kuendeleza ustawi wa wazee pamoja na watoto wanaowatunza. Kwa sasa Serikali ipo katika hatua ya kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kutoa maoni juu ya masuala muhimu ya kuzingatiwa katika sheria hiyo.”amesema Mhe. Mahundi

Hata hivyo, amebainisha kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha maadili ya uwajibikaji wa kifamilia na kuimarisha mifumo ya kijamii inayosaidia ustawi wa wazee nchini.











Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa onyo kwa Watumishi wa Umma dhidi ya matumizi ya baruapepe binafsi katika mawasiliano ya shughuli za Serikali.

Amesema kuwa, watumishi wote wa Umma wanapaswa kutumia baruapepe rasmi za Serikali ili kulinda usalama wa taarifa Serikalini, kuongeza uwajibikaji, kuimarisha mifumo rasmi ya mawasiliano ya Serikali sambamba na kuzuia kuvuja kwa taarifa za Serikali.

Akizungumza mapema hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Pili ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Mhe. Kikwete amesema, matumizi ya barua pepe zisizo za Serikali yamekuwa chanzo cha hatari ya uvujaji na upotevu wa taarifa nyeti za Serikali.

Alibainisha kuwa, Serikali imewekeza katika miundombinu ya TEHAMA inayokidhi viwango vya usalama na inapaswa kutumiwa ipasavyo katika mawasiliano ya shughuli zote za Serikali, ili kudhibiti na kulinda usalama wa taarifa muhimu za nchi.

“Kuanzia sasa, serikali itakuwa na jicho la karibu sana kuangalia namna watumishi wa Umma wanavyopeana taarifa za Serikali kupitia baruapepe rasmi za Serikali na si vinginevyo, nitoe wito kwa viongozi na watumishi wote wa umma kutumia anuani za baruapepe rasmi kwa ajili ya mawasiliano ya shughuli zote za Serikali, alisisitiza Waziri Kikwete.

Alibainisha kuwa, barua pepe za Serikali zinatoa mazingira salama ya kuhifadhi kumbukumbu, kudhibiti hatari ya kuvuja kwa taarifa za serikali, usalama na ulinzi wa taarifa hizo kwa mujibu wa sheria na miongozo mbalimbali inayohusu usalama na utunzaji wa taarifa za Serikali, sambamba na uwajibikaji kwa watumishi wa umma katika kuzingatia misingi ya utunzaji wa taarifa za Serikali.

“Matumizi ya baruapepe zisizo rasmi yamesababisha baadhi ya nyaraka za Serikali kupotea na wakati mwingine kuhatarisha usalama na usiri wa taarifa hizo ndani ya serikali, tukiwa kama watumishi wa umma sote tunawajibika kulinda usalama wa taarifa za Serikali kwa kutumia baruapepe rasmi za Serikali”, alisema Mhe.Kikwete.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Eng. Benedict Ndomba, alisema kuwa e-GA itaendelea kutoa ushirikiano kwa taasisi za umma ili kuzijengea uwezo katika matumizi ya mfumo wa Buruapepe Serikalini (GMS).

Alisema kuwa, takriban zaidi ya miaka 10 sasa, tangu kuanza kutumika kwa mfumo wa GMS na kuleta matokeo chanya ikiwemo kurahisisha mawasiliano ndani na nje ya taasisi pamoja na kuwezesha utekelezaji wa maamuzi kwa wakati.

“e-GA tunatoa msaada wa kiufundi kwa saa 24 kwa watumiaji wa mifumo mbalimbali ukiwemo GMS na tutaendelea kufanya hivyo, ili kuhakikisha mawasiliano ya Serikali yanakuwa imara muda wote kupitia mfumo huu wa GMS”, alisema Ndomba.

 


Na Oscar Assenga,TANGA

MSTAHIKI Meya wa Jiji la Tanga Seleboss Mustapha amewataka vijana wataopata fursa ya ajira nje ya nchi katika Falme za Kiarabu kufanya kazi kwa uadilifu na kuitangaza vizuri sifa na fursa ya nchi jambo ambalo litafungua milango kwa wengine kuendelea kuaminiwa.

Seleboss aliyasema hayo wakati akizungumza na vijana zaidi ya 200 waliojitokeza kufanyiwa usaili kwa ajli ya kwenda nchi za falme za Kiarabu kwa shughuli za udereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda.

Alisema kufanya kazi kwa uaminifu sambamba na kuyaishi maadili ya kitanzania katika nchi za kigeni itasaidia kuleta taswra njema ya kutangaza nchi kwa mazuri badala ya kuwa kinyume chake.

Aidha alisema watakaofanikiwa kupita kwenye mchujo wakawe mabalozi wazuri kwa kufanya kazi lea ajil ya maendeleo yao ikiwemo kutokusahau kuwekeza nyumbani ikiwemo wawwe waaminifu

Meya huyo aliwataka kuhakikisha wanazingatia sheria na tararubu na miongozo ya nchi wanazokwenda ili waweze kufanya shughuli vizuri lakini kwa kujenga imani kwa wengine kuweza kuvutika na vijana kutoka nchni.

Awali akizungumza Ofisa Kazi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Mahusiano Peter Ugata alisema kwamba Serikali imekuwa ikiendelea kuratibu fursa za ajira nje ya nchi kwa kuhakiisha wanawasimamia vijana wao kupata ajira zao.

Alisema kuwa hiyo ni dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana na hivyo ni muhimu vijana kuchangamkia fursa hizo zinapojitokeza.

Alisema miongoni mwa majukumu yao ni kuhakikisha wanapata vijana wenye sifa na vigezo ambao wataweza kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu za nchi husika.

Naye kwa upande wake mmoja wa vijana wanaoshiriki kwenye usaili huo ,Juma Haki waliishukuru Serikali kwa fursa hiyo kuweza kufika hadi ngazi ya mikoa na hivyo kuweza kushiriki nao.

Hata hivyo alisema kwamba wanaishukuru Serikali kwa fursa hiyo ambayo itasaidia kumaliza changamoto za ajira lakini itawapa mwamko wa kujipanga kwa ajili ya kuwa na sifa za kufanya kazi nje ya nchi .


Mwisho.
Maisha yangu yalikuwa mgumu sana baada ya talaka na mke wangu. Mke wangu alitaka kudai malezi ya watoto wetu wote, na nilijikuta nikiwa na hofu kubwa kwamba maisha yangu ya kifamilia yangeisha kabisa.

Siku nyingi nilijisikia mgonjwa wa moyo, nikihisi kuanguka kimwili na kihisia, huku nikikosa msaada wa kweli wa kisheria na kiroho. Kesi ya malezi ilikua changamoto isiyo na kifani.

Kila mtu alidhani sina nafasi ya kushinda, kwa sababu hali ya kifedha na hofu yangu ilionekana kuendelea kudhoofisha hoja zangu.

Nilijua kuwa lazima nifanye kitu tofauti, kitu cha busara na cha hekima, la sivyo watoto wangu wangepotea mikononi mwa hofu na udhaifu wangu.Soma Zaidi.
Siku ile haikuwa ya kawaida kabisa. Nilikuwa na haja ya haraka ya kufanya malipo ya simu na huduma nyingine, ndipo nikakutana na agent wa Safaricom ambaye alionekana mwaminifu na mwenye heshima.

Nilijisalimisha kwa kuamini maneno yake, lakini bila kujua, nilidanganywa na alichukua KSh 200,000 zangu kwa udanganyifu. Baada ya tukio hilo, nilihisi aibu kubwa, huzuni, na hasira isiyo na kipimo.

Nilijikuta nikijua kwamba fedha hizi siyo tu zilipotea bali pia hakika ya usalama wa wengine ilikuwa hatarini ikiwa mtu kama huyu angeendelea. Nilijua lazima nifanye kitu, la sivyo wengine wangeendelea kujeruhiwa na wajasusi hawa wa uongo.Soma Zaidi.
Nilijikuta katika giza la maisha baada ya kupoteza kazi yangu. Siku za furaha na amani zilianza kutoweka, na hali ya kifedha ilizidi kuwa mbaya. Nilijaribu kila njia kurekebisha hali, lakini kila jaribio lilishindikana.

Kila siku ilikuwa changamoto mpya, na hisia za huzuni, aibu, na kukata tamaa zilianza kunikumba. Hali hii ilileta mabadiliko makubwa nyumbani.

Mke wangu alianza kunitenga kidogo kidogo, na siku moja nikagundua kuwa amepata mwanamume mwingine. Hatimaye, alichukua hatua ya kuoa mzee tajiri, huku akibeba watoto wetu naye.

Hii ilinifanya nijisikie kupoteza heshima, familia, na kila kitu niliyekipenda. Nilihisi maisha yangu yamevunjika na kila mtu karibu nami alidhani sitawahi kurejea.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mke-wangu-alinitenga-na-watoto-wetu-na-akaoa-mzee-tajiri-baada-ya-kupoteza-kazi-na-kupata-ugumu-wa-kimaisha/
Haikuwa rahisi kwa mwanaume huyu kusimulia kilichompata, kwani kilikuwa cha aibu na cha kutisha. Alikuwa mtu mwenye afya nzuri, akifanya kazi zake kawaida bila shida yoyote.

Lakini baada ya kujiingiza kwenye uhusiano wa siri na mke wa mtu mwingine katika mtaa wao, maisha yake yalibadilika ghafla kwa namna ambayo hakuwahi kufikiria.

Siku ya pili baada ya tukio hilo, alianza kuhisi tumbo lake limekaza isivyo kawaida. Alidhani ni tatizo la chakula tu. Lakini siku zilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.

Alishindwa kabisa kujisaidia haja kubwa kwa siku moja, mbili, tatu… hadi ikafika wiki nzima. Tumboni kulivimba, maumivu yaliongezeka, na jasho jingi lilianza kumtoka usiku.

Aliamua kwenda hospitali, akapewa dawa za kawaida za kuharisha na kusafisha tumbo, lakini hakuna kilichofanya kazi. Madaktari walishangaa kwa sababu vipimo vyote vilionyesha hakuna tatizo la kawaida la kiafya.

Maumivu yaliendelea, akashindwa hata kula vizuri, na usingizi ukawa shida.
Hapo ndipo alipoanza kuogopa. Alianza kukumbuka maneno ya watu wazima waliokuwa wakisema kuna mambo mengine hayatibiki kwa dawa za hospitali pekee.

Kwa hofu na kukata tamaa, alimweleza rafiki yake wa karibu siri yote. Rafiki huyo alimshauri atafute msaada wa kipekee kabla hali haijawa mbaya zaidi.Soma Zaidi.