Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) akimueleza jambo Afisa Kurugenzi ya Usimamizi wa sarafu BoT, Bw. Shadrack Mapunda, wakati alipotembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu ya "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania", yanayofanyika katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

CHAMA cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kimeipongeza Tume ya Ushindani (FCC) kwa kuendelea kutoa elimu kuhusu utambuzi wa bidhaa bandia na ulinzi wa biashara kwa wajasiriamali, kikisema mafunzo hayo yameongeza uelewa na kusaidia kulinda biashara halali nchini.

Akizungumza baada ya darasa la elimu leo Julai 10, 2026 katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa Ushirikiano wa TWCC, Nelson Clevary, amesema ushirikiano kati ya TWCC na FCC umeendelea kuzaa matunda kwa kuwajengea wajasiriamali uwezo wa kutambua bidhaa bandia pamoja na namna ya kulinda bidhaa na biashara zao dhidi ya vitendo vya udanganyifu.

Alisema mwaka huu ni wa tatu mfululizo kwa TWCC kushirikiana na FCC kuendesha mafunzo hayo, huku matokeo yakionyesha kuwa wajasiriamali wengi wameanza kuelewa athari za bidhaa bandia na umuhimu wa kushirikiana na mamlaka husika zinapotokea changamoto zinazohusiana na bidhaa hizo.

"Leo tumepata darasa zuri ambalo limewasaidia wajasiriamali kutambua bidhaa halisi na bidhaa bandia, lakini pia wamefundishwa namna ya kulinda biashara zao ili zisidhurike kutokana na watu wanaoiga au kutengeneza bidhaa bandia kwa kutumia majina ya biashara zao," amesema Clevary.

Amebainisha kuwa ingawa mafunzo yanayotolewa wakati wa maonesho huwafikia washiriki wachache, bado kuna haja ya kupanua wigo wa elimu hiyo ili kuwafikia wajasiriamali wengi zaidi nchini.

Clevary amesema TWCC ina wanachama zaidi ya 22,000 nchini, hivyo ushirikiano wa karibu na FCC utawezesha elimu hiyo kuwafikia wengi zaidi na kuongeza uwezo wa wafanyabiashara kulinda bidhaa zao na haki za biashara.

Aidha, amewataka wajasiriamali kuendelea kutumia fursa ya mafunzo hayo kujifunza namna ya kutambua bidhaa bandia na kuripoti vitendo vya ukiukwaji vinavyoweza kuhatarisha biashara zao.

Kwa upande wake Mjasiriamali kutoka mkoani Mwanza, Praxeda Mgyabuso, amesema elimu inayotolewa na Tume ya Ushindani (FCC) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) imewasaidia wafanyabiashara na wananchi kutambua tofauti kati ya bidhaa halisi na bidhaa bandia, pamoja na umuhimu wa kulinda biashara zao kupitia usajili wa alama na nembo za biashara.

Amesema awali alikuwa hana uelewa wa kutosha kuhusu madhara ya bidhaa bandia na namna ya kuzitambua, hali iliyowafanya watumiaji wengi kununua bidhaa zisizo halisi bila kufahamu athari zake kwa afya na uchumi.

Amesema elimu hiyo imewafungua macho wafanyabiashara kutambua kuwa pamoja na kuzingatia ubora wa bidhaa, ni muhimu pia kusajili majina na nembo za biashara ili kuzuia watu wengine kuiga bidhaa zao na kutumia utambulisho wao kinyume cha sheria.

"Kwa kweli tumepata elimu kubwa. Wengi wetu tulikuwa tunanunua bidhaa kwa kuangalia bei ya chini bila kujua kuwa baadhi yake ni bandia na zinaweza kuhatarisha afya zetu. Sasa tumeelewa namna ya kutambua bidhaa halisi na umuhimu wa kulinda biashara zetu kupitia usajili wa nembo na majina ya biashara," amesema.

Nae Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa FCC, Roberta Feruzi, amesema kuwa maonesho hayo yameipa tume hiyo fursa ya kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwaelimisha kuhusu haki zao pamoja na huduma zinazotolewa na taasisi hiyo.

Pamoja na hayo amesema mbali na kutoa elimu, FCC pia inatoa huduma za moja kwa moja kwa wananchi wanaotembelea banda lake, ikiwemo kupokea na kushughulikia malalamiko, usajili wa mikataba na huduma nyingine zinazotolewa na tume hiyo.

Na. Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC), Dkt. Aggrey Mlimuka, ametembelea banda la FCC katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Maonesho hayo yamewakutanisha washiriki mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, wakiwemo kampuni binafsi, taasisi na mashirika ya Serikali, yakitoa fursa ya kutangaza bidhaa, huduma na uwekezaji.

Akiwa katika banda la FCC, Dkt. Mlimuka ameipongeza Tume hiyo kwa kazi kubwa inayofanya katika kulinda ushindani wa haki sokoni na kuimarisha mapambano dhidi ya bidhaa bandia, hatua inayochangia kulinda maslahi ya walaji na kukuza mazingira bora ya biashara nchini.

Pia amempongeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, Menejimenti pamoja na watumishi wote wa Tume hiyo kwa kujituma, weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao na kuhakikisha taasisi hiyo inatimiza malengo yake kwa mafanikio.

FCC ina jukumu la kulinda na kuhimiza ushindani wa haki katika biashara, kulinda maslahi ya walaji, kupokea na kushughulikia malalamiko yanayohusu ukiukwaji wa sheria za ushindani, pamoja na kudhibiti uingizaji, usambazaji na uuzaji wa bidhaa bandia nchini.

Mbali na kutembelea banda la FCC, Dkt. Mlimuka pia alitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara ili kujionea shughuli na huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yenye kaulimbiu "Sabasaba Fahari ya Tanzania," yalianza rasmi Juni 28, 2026, na yanatarajiwa kuhitimishwa Julai 13, 2026 katika Viwanja vya Maonesho vya Julius Nyerere (Sabasaba Grounds), Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC) akipata maelezo kutoka kwa Bi. Roberta Feruzi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano - FCC wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa  yanayoendelea viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa FCC wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa  yanayoendelea viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Tanzania imepata heshima ya kutunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya WSIS Prizes 2026 kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano ulioongeza upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya vijijini na ambayo hayakuwa na huduma ya mawasiliano nchini.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Bw. Rashid Kassim Mchatta, amesema chanjo zinazozalishwa na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) zimeendelea kuthibitisha ubora wake kwa kusaidia kudhibiti magonjwa mbalimbali ya mifugo na kuongeza tija kwa wafugaji nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar.

Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar ambapo wamejadili kuhusu ushirikiano katika maeneo ya uwekezaji, ajira na maendeleo ya ujuzi.

Aidha, katika mazungumzo yao Mhe. Sangu alitumia fursa hiyo kumueleza Mwenyekiti wa Al Mansour Holding dhamira ya Serikali ya Tanzania katika kuendelea kuweka mazingira bora na rafiki kwa wawekezaji pamoja na kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Qatar.

Vilevile, Waziri Sangu ameipongeza kampuni ya Al Mansour Holding kwa kuendelea kuongeza wigo wa uwekezaji katika Mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania Bara na Zanzibar. Pia, amehamasisha kampuni hiyo kutumia wataalamu na nguvu kazi ya Watanzania katika shughuli zake nchini Qatar na katika masoko mengine ya kimataifa.

Kadhalika, ameihakikishia kampuni hiyo ushirikiano katika kukuza maendeleo ya rasilimali watu kupitia mafunzo, uhamishaji wa teknolojia na ujuzi ili kuchochea ajira na ukuaji wa uchumi.

Katika ziara hiyo, Waziri Sangu ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na wataalamu wengine kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar.

Mimi nilikuwa naishi na maumivu ya tumbo kwa muda mrefu sana. Kila siku nilikuwa naanza siku nikiwa sijisikii vizuri, na wakati mwingine maumivu yalikuwa yanazidi baada ya kula. Ilifika wakati nilianza kuogopa hata kula chakula kwa sababu sikujua kama nitapata maumivu tena.

Hali hii ilinifanya nipungue nguvu na hata uzito wangu ukaanza kushuka.
Nilitembelea vituo vya afya mara kadhaa, nikapewa dawa tofauti, lakini nafuu ilikuwa ya muda mfupi tu. Baada ya muda maumivu yalirudi tena kama kawaida.

Hali hii ilinichosha sana. Nilianza kukata tamaa na kuona kama nitakuwa na tatizo hili maisha yangu yote. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Baada ya miaka mingi ya majaribio bila mafanikio, Neema (si jina lake halisi) alikuwa amekata tamaa kuhusu ndoto yake ya kuwa mama. Licha ya kutafuta msaada katika vituo mbalimbali vya afya, changamoto ya kushika mimba iliendelea kuwa mzigo mkubwa kwake na familia yake.

Katika harakati za mwisho za kutafuta suluhisho, Neema alisikia kuhusu Kiwanga Doctors—wataalamu wa tiba za asili na jadi wanaosaidia watu kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiafya. Akiwa na matumaini kidogo yaliyosalia, aliamua kuwafikia na kupata ushauri wao.

Baada ya tathmini ya kina, Neema alipatiwa mwongozo na tiba za asili zilizolenga kuimarisha afya yake ya uzazi kwa ujumla. Kulingana na maelekezo aliyopatiwa, alianza kufuata matibabu hayo kwa nidhamu huku akizingatia pia ushauri wa mtindo bora wa maisha. SOMA ZAIDI.