Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na taasisi zake kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake, huku ikizitaka kuongeza kasi ya utekelezaji wa mikakati ya kukuza uchumi wa taifa.

Pongezi hizo zimetolewa jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deodatus Mwanyika (picha ya kwanza), wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za wizara kupitia taasisi zake ambazo ni Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Tume ya Ushindani Tanzania (FCC), Wakala wa Vipimo (WMA) na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mwanyika amesema juhudi zinazofanywa na wizara hiyo zimeanza kuleta matokeo chanya katika kuimarisha mazingira ya biashara na uzalishaji nchini. Aidha, ameielekeza wizara kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia na hafifu zinazoingia sokoni, akieleza kuwa bidhaa hizo husababisha hasara kwa wazalishaji wa ndani na kuhatarisha afya pamoja na usalama wa watumiaji. Pia ameagiza hatua kali kuchukuliwa dhidi ya matumizi ya vipimo visivyo sahihi katika biashara, hususan lumbesa, ambalo limekuwa likilalamikiwa na wananchi katika maeneo mbalimbali nchini kutokana na matumizi ya vipimo visivyo rasmi. Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amesema wizara imepokea maelekezo na ushauri uliotolewa na kamati hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi kwa lengo la kuboresha huduma na kuongeza ufanisi katika sekta ya viwanda na biashara nchini. Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Ashura Katunzi, pamoja na viongozi wengine wa taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, wamesema wanaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha usimamizi wa bidhaa na huduma nchini. Hatua hizo ni pamoja na kufanya operesheni maalumu za ukaguzi wa bidhaa bandia na kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu matumizi sahihi ya vipimo vinavyotambulika kisheria.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Bi. Erica E. Yegella amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fursa ya ajira mpya takriabani 259 katika kipindi cha mwezi Januari na Mei 2026.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeendelea kutoa mafunzo kupitia kozi ndefu 49 zinazolenga kuzalisha wataalam mahiri watakaosaidia utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali nchini.

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata lita 66,048 za kemikali bashirifu zilizokuwa zikiingizwa na kusafirishwa nchini kinyume cha sheria, katika operesheni maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwezi Aprili mwaka huu.
Na Mwandishi Wetu, Arusha

HOSPITALI ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) chini ya menejimenti ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wamefanikuwa kutoa huduma za matibabu bure kwa zaidi ya watu 2,000 kuelekea kilele cha maadhimisho ya wauguzi duniani.
NA EMMANUEL MBATILO

Serikali imeanza rasmi kutoa mafunzo ya urubani kupitia Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), hatua inayotajwa kuwa utekelezaji wa maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ya kuimarisha sekta ya usafiri wa anga nchini.



Serikali ya Tanzania ndani ya kipindi cha Miezi Mitatu ijayo inatarajiwa kuanza rasmi utekelezaji wa Mradi wa Kimkakati wa Liganga na Mchuchuma wenye uwekezaji wa Dola za Marekani Bilioni 2 hadi 3 baada ya mazungumzo kati ya Serikali na Mwekezaji kufikia   zaidi ya asilimia 90.

Hayo yalibainishwa Mei 9, 2026 na Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika Shamba la Parachichi la Havira Farm Mkoani Njombe, pembeni mwa Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini, kinachotumika kama sehemu ya tathmini na kujipanga.

Alisema hatua hiyo inaashiria mwanzo wa utekelezaji wa mradi huo uliosubiriwa kwa miaka mingi ukitarajiwa kuongeza mapato ya Seikali, ajira kwa wananchi, kukuza sekta ya viwanda vya chuma na ustawi wa jamii inayozunguka mradi na taifa.

Aliongeza kwamba,  mradi huo unatarajiwa kuzalisha tani milioni 2.9 za chuma ghafi kwa mwaka pamoja na tani milioni 1.1 za bidhaa za chuma kwa mwaka, huku ukitarajiwa kutoa zaidi ya ajira rasmi 6,500 na ajira zisizo rasmi zipatazo 26,000

‘’ Katika kipindi cha miaka 25 ya kwanza ya mradi, jumla ya mapato ya dola za Marekani 1,990,489,585,000 zinatarajiwa kupatikana ambapo kwenye miradi ya makaa ya mawe kiasi cha dola za Marekani 92,593,820; uchimbaji chuma kiasi cha dola za Marekani 910,781,519 na kiwanda cha chuma kiasi cha dola za Marekani 987,114,246,’’ alisema Msigwa.

Pia, aliongeza kwamba utekelezaji wa mradi huo utahusisha ujenzi wa msongo wa umeme wa Kilovoti 220 kati ya mchuchuma na  na liganga na barabara kutoka Mchuchuma na Liganga ukiwemo mgodi wa makaa ya mawe  mchuchuma wenye uwezo wa kuzalisha tani milioni 3 kwa mwaka na Kituo cha kufua umeme kwa megawati 600.

 Msigwa alisema tayari Serikali imelipa zaidi ya shilingi bilioni 15 za fidia kwa wananchi ili kupisha utekelezaji wa mradi huo, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali kuhakikisha mradi huo unaanza kwa vitendo baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu.

Utekelezaji wa mradi wa Liganga na Mchuchuma unaashiria safari ya kuelekea Dira 2050 ambapo kupitia Sekta ya Madini imejipanga kufikia Uchumi wa Dola trilioni Moja ukiwa ni miongoni mwa miradi kielelezo iliyoanishwa kwenye mpango wa muda mrefu wa wa dira hiyo unaotarajiwa kuchochea sekta ya viwanda nchini.

Mbali na Sekta ya Madini, alisema Serikali inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Njombe ikiwemo barabara, maji na umeme kwa lengo la kuufungua zaidi mkoa huo kiuchumi na kijamii.

#LigangaMchuchuma #Madini ni Maishana Utajiri #TanzaniaSteelHub

#NjombeMpya #SafariyaViwanda #InvestInTanzania #MiningSector

#Mining4Development #MineralForGrowth

Viongozi mbalimbali wa Chama cha mapinduzi Mkoa na Wilayani wakiambatana na Viongozi wa Serikali mkoa wa Dodoma wameanza safari ya Kikazi kuelekea mkoani Mtwara kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Ushirika vya Msingi.

Viongozi hao wakingozana na Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma Ndg Joseph Chitinka na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Dodoma Bibi Theresia Nyoka wameanza ziara hiyo leo Mei 12, 2026 kutokea mkoani Dodoma kuelekea mkoani humo.

Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma ameeleza lengo la ziara hiyo ni kuwajengea uwezo, kujifunza utekelezaji wa Mfumo wa stakabadhi za ghala na kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Msingi Ushirika vya mkoa wa Mtwara na hivyo kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya kiushirika ndani ya Mkoa wa Dodoma.

Ziara hiyo inafanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Mei 13 hadi 14, 2026 na kuwahusisha Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa, Wenyeviti wa CCM Wilaya Mkoani Dodoma, Sekretariti ya Mkoa CCM, Baadhi ya Makatibu wa Chama wilaya na Wenezi,, Makatibu, Makatibu Tawala Uchumi na Uzalishaji Viwanda na Biashara na Kilimo.


 


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewasisitiza  washiriki wa Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Afua ya Uthibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, kuhakikisha suala usafi wa mazingira linakuwa ajenda ya kudumu katika vikao vyote vitakavyofanyika katika ngazi zote za Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuwezesha miji na majiji nchini kuwa masafi.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Mwaka wa Tathmini ya Afua ya Uthibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, unaofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Jiji- Mtumba, unaohudhuriwa na Maafisa Afya wa Mikoa, Maafisa Afya wa Halmashauri na Maafisa Mazingira wa Halmashauri.

“Nasisitiza suala la usafi wa mazingira liwe ajenda ya vikao vyenu. Vikao vya Kamati za Ushauri za Mikoa, Kamati za Ushauri za Wilaya, Kamati za Maendeleo za Kata, Mabaraza ya Madiwani, Kamati za Kudumu za Halmashauri pamoja na vya ALAT ngazi ya mkoa na taifa,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameainisha kuwa, usafi wa mazingira ukizingatiwa katika ngazi zote za Mamlaka ya Serikali za Mitaa utapunguza milipuko ya magonjwa na matumizi ya fedha kwa ajili ya ununuzi wa madawa, na fedha zitakazookolewa zitaelekezwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hivyo amewataka maafisa hao kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kupunguza milipuko ya magonjwa na matumizi ya ununuzi wa dawa.

“Namshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuanzisha vitengo vya udhibiti wa taka ngumu ambavyo vinasaidia kuboresha zoezi la usafi wa mazingira nchini,” Prof. Shemdoe ameeleza.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Prof. Tumaini Nagu amesema uthibiti wa taka kwenye halmashauri ni jambo muhimu katika kuhakikisha kunakuwa na usafi wa mazingira na udhibiti wa magonjwa ya milipuko na kuongeza kuwa, takwimu za kisayansi zinaeleza kwamba uthibiti madhubuti wa taka ngumu unapelekea kupungua kwa asilimia 30 hadi 40 za magonjwa kama Malaria na mengineyo ambayo yanadhibitiwa kwa usafi wa mazingira.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki, Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti taka ngumu wa Halmashauri ya wilaya Bahi Bw. William Mpangala amesema kuwa Serikali kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa inaendelea kushirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa afua za udhibiti wa taka ngumu kama za ukusanyaji na uchakataji wa taka ngumu, na kuongeza kuwa ushirikishwaji huo umeongeza ufanisi katika udhibiti wa taka kwenye halmashauri nchini.

Mkutano wa Mwaka huu una kaulimbiu isemayo “Taka ngumu ni Mali; tumia, rejeleza na Weka Miji katika hali ya usafi”.

Kampuni kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa kuwekeza nchini Tanzania katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia, hatua inayodhihirisha kuendelea kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji katika sekta ya nishati nchini.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wamepatiwa mafunzo maalum kuhusu masuala ya haki miliki, hatua inayolenga kuwajengea uwezo katika usikilizaji na utoaji wa maamuzi yanayohusu ubunifu, kazi za wasanii, wabunifu pamoja na wavumbuzi nchini.

Ujumbe wa wadau wa maendeleo ya elimu ukiwemo Global Partnership for Education (GPE) pamoja na Education Program for Results (EP4R) ukiongozwa na Morten Sigsgaard Mratibu wa Ushirika wa Nchi (GPE) umeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu inayotekelezwa katika Shule ya Msingi na Sekondari Buswelu, Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo Mei 11, 2026, Morten amesema miradi hiyo imeendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, hususan kwa wanafunzi wa elimu jumuishi.

Katika Shule ya Msingi Buswelu, inayohudumia wanafunzi 1,211 wakiwemo 176 wenye mahitaji maalumu, imefanikiwa kujenga bweni la wasichana wenye mahitaji maalumu kupitia ufadhili wa Serikali na GPE-LANES II.

Mradi huo9 umewezesha wanafunzi 80 kupata makazi salama ya bweni, huku huduma za bweni zikianza rasmi Mei 8, 2026 baada ya Serikali kuanza kutoa fedha za chakula.

Aidha, walimu na wanafunzi wameeleza mabadiliko chanya yaliyotokana na miradi hiyo, wakisema awali wanafunzi walikuwa wakisoma katika mazingira ya msongamano wa madarasa, lakini sasa wanapata nafasi ya kusoma katika mazingira bora na yenye nafasi ya kutosha, jambo lililoongeza umakini na ushiriki darasani.

Katika Shule ya Sekondari Buswelu, kupitia Programu ya EP4R, shule imepokea Shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa vyenye viti na meza 100, mradi ambao tayari umekamilika na unatumika.

Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wanasema awali walikuwa wakisoma wakiwa wamebanana kutokana na upungufu wa madarasa, hali iliyokuwa ikichangia usumbufu wakati wa masomo, lakini kwa sasa wanafurahia kusoma katika madarasa mapya yenye nafasi kubwa na mazingira rafiki ya kujifunzia.

Uongozi wa shule ulieleza kuwa miradi hiyo imechangia kuboresha ufaulu pamoja na kuongeza hamasa ya kujifunza.

Wadua wa maendeleo walitoa pongezi kwa Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya elimu na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kuboresha mazingira ya kujifunzia nchini.










Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea Mheshimiwa Noel Kaganda amepokelewa rasmi katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Seoul kuanza rasmi majukumu yake ya uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea.

 

📌 Vijana maeneo ya mradi wa umeme kwenye vitongoji kupewa kipaumbele kwenye ajira

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imetoa wito kwa wananchi kuwa walinzi wa kwanza wa miundombinu ya miradi ya kufikisha umeme vijijini inayotekelezwa na serikali, huku ikieleza kusikitishwa na matukio ya wizi wa vifaa vya umeme ikiwemo waya za mashine umba (transfoma) katika baadhi ya maeneo.

Wito huo umetolewa leo Mei 11, 2026 Mkoani Manyara na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu wakati akihitimisha ziara ya Bodi hiyo katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikiwa ni miradi ya nishati safi ya kupikia pamoja na miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji.

Balozi Kingu amesema serikali imetumia fedha nyingi kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda miundombinu hiyo dhidi ya vitendo vya hujuma na wizi vinavyoweza kuchelewesha maendeleo ya wananchi.

Katika ziara hiyo mkoani Manyara, Bodi ya REB imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji ambao ni kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom Tanzania pamoja na China Railway Seventh Group.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Msimamizi wa Miradi wa REA Mkoa wa Manyara, Mhandisi Geofrey Mkeni, amesema serikali kupitia REA imetenga zaidi ya shilingi bilioni 45.8 kwa ajili ya miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji 267 vya mkoa wa Manyara.

Mhandisi Mkeni amesema miradi hiyo inalenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme kwa wananchi wa vijijini ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Pia ametoa wito kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayofikiwa na miradi hiyo kuanza kufanya maandalizi ya miundombinu ya ndani ya nyumba ikiwemo wiring ili wawe tayari kuunganishiwa huduma ya umeme mara baada ya miradi hiyo kukamilika.

Kwa upande wao, wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo wameahidi kuhakikisha kazi zinakamilika kwa wakati huku wananchi wakinufaika kupitia ajira zinazotokana na utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom Tanzania, Afisa Mahusiano ya Jamii na Mazingira, Oliver Charles, amesema miradi hiyo imefungua fursa mbalimbali za ajira kwa vijana wanaoishi katika maeneo yenye miradi ili wawe sehemu ya maendeleo yanayoletwa na serikali.

Naye Mhandisi wa Miradi kutoka kampuni ya China Railway Seventh Group, Estheria Fumbuka, amesema kampuni hiyo itaendelea kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati ili malengo ya serikali ya kuwafikishia wananchi huduma ya umeme vijijini yaweze kutimia.