Na Saidina Msangi na Asia Singano, WF - Dodoma

Wizara ya Fedha imeendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhakikisha wananchi wanapata ufafanuzi kuhusu masuala ya kodi, uchumi na sera mbalimbali za fedha na mchango wa kodi katika kugharamia huduma muhimu za kijamii kama vile miundombinu, elimu, afya, maji nishati na huduma nyingine muhimu.

Hayo yamebainishwa na Afisa Usimamizi wa Fedha Mkuu, Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. Abdul Dachi, wakati akitoa elimu kwa wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026, yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Bw. Dachi alisema kupitia Maonesho hayo, Idara imekuwa ikitoa taarifa kwa wananchi kwa lugha rahisi na inayoeleweka ili kuwawezesha kufahamu mchango wa Sera za Kodi na Uchumi katika maendeleo ya Taifa na ustawi wa jamii.

‘‘Miongoni mwa maeneo yanayotolewa elimu ni kuhusu mwenendo wa uchumi wa Taifa na namna Sera za Uchumi zinavyosaidia kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza fursa za ajira na kukuza uchumi kwa ujumla pamoja na namna hizo zinavyoandaliwa ili kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kwa ufanisi na kwa kuzingatia maslahi ya Taifa,’’, alisema Bw. Dachi.

Aliongeza kuwa Serikali inatumia taarifa za takwimu na tafiti mbalimbali zinazosaidia katika upangaji wa bajeti na utekelezaji wa mikakati ya maendeleo ya muda mfupi na mrefu pamoja na usimamizi wa mikataba ya kikodi kati ya Tanzania na mataifa mengine na ushirikiano wa kikanda na kimataifa unaolenga kulinda maslahi ya Taifa katika sekta ya kodi.

Alifafanua kuwa wananchi wanapatiwa elimu kuhusu namna Wizara inavyofanya tafiti za kisera na kuandaa mapendekezo ya kitaalamu yanayosaidia Serikali kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya nchi pamoja na namna Serikali inavyoshughulikia masuala ya kodi za kimataifa.

‘’Tumetumia fursa hii kueleza wananchi umuhimu wa sera za kodi na fedha katika kukuza uchumi na ustawi wa wananchi, mchango wa kodi katika maendeleo ya Taifa, pamoja na umuhimu wa uwazi na uwajibikaji katika mchakato wa utungaji wa sera nafasi ya Tanzania katika uchumi wa dunia na manufaa yanayotokana na ushirikiano wa kiuchumi na mataifa na taasisi mbalimbali za kimataifa’’, alifafanua Bw. Dachi.

Alisema kuwa ili kuhakikisha ujumbe unawafikia wananchi wengi zaidi, idara pia inatoa vipeperushi, vitabu vya elimu pamoja na mazungumzo ya ana kwa ana na wageni wanaotembelea Banda hatua inayochangia kuongeza uelewa wa umma na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wananchi katika maendeleo ya Taifa.

Tume ya Ushindani (FCC) imesema imeanza mpango wa kuanzisha klabu za elimu ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia katika shule za msingi, sekondari na taasisi za elimu ya juu ili kujenga kizazi chenye uelewa wa masuala hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari Juni 20, 2026, katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema mpango huo utatekelezwa kupitia klabu zitakazojulikana kama Ushindani School Club. 

Amesema lengo la mpango huo ni kuwafikia wanafunzi mapema na kuwajengea uelewa kuhusu ushindani, haki za mlaji na namna ya kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa au kupata huduma.

Feruzi amesema elimu hiyo itawasaidia wananchi kutambua bidhaa bandia, kulinda soko dhidi ya udanganyifu na kuwawezesha watumiaji kuchagua bidhaa salama na zenye ubora.

Ameeleza kuwa uelewa wa masuala ya ushindani na ulinzi wa mlaji utasaidia wananchi kufanya uchaguzi bora wa bidhaa na huduma, huku sekta binafsi ikiendelea kuchangia katika uzalishaji na ukuaji wa uchumi.

Aidha, amesema utoaji wa elimu hiyo utaendelea kupitia ofisi za kanda za FCC zilizopo Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma na Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha wananchi katika mikoa yote ya Tanzania Bara wanapata elimu hiyo.



Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.

Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.

Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.




Kwa miaka mingi, nilikuwa na ndoto ya kusafiri kwenda Marekani. Nilitaka kutembelea nchi hiyo kwa sababu mbalimbali zilizokuwa muhimu kwangu. 

Kila nilipofikiria kuhusu safari hiyo, nilijawa na matumaini kwamba siku moja ndoto yangu ingetimia. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Nilipotuma maombi yangu ya kwanza ya visa, niliamini kila kitu kilikuwa sawa. Nilikuwa nimeandaa nyaraka zote nilizohitaji na nilijitokeza kwenye mahojiano nikiwa na matumaini makubwa. Hata hivyo, maombi yangu yalikataliwa. Nilihuzunika sana.

Baada ya muda, nilijaribu tena. Safari hii nilijitayarisha zaidi na kuhakikisha kila kitu kiko sawa. Lakini kwa mshangao wangu, nilikataliwa tena. Mara ya pili ilinivunja moyo zaidi. Nilianza kuamini kwamba labda safari ya kwenda Marekani haikuwa sehemu ya maisha yangu. SOMA ZAIDI.

Maisha yangu yalibadilika ghafla siku mume wangu alipoondoka nyumbani. Mwanzoni nilidhani alikuwa amekasirishwa na migogoro ya kawaida ya ndoa na angerudi baada ya siku chache. 

Lakini siku zikageuka kuwa wiki, na wiki zikageuka kuwa miezi. Baadaye niligundua kwamba alikuwa ameanza kuishi na mwanamke mwingine.

Habari hiyo ilinivunja moyo. Tulikuwa tumejenga maisha pamoja kwa miaka mingi na tulikuwa na watoto ambao walimhitaji baba yao. Kila nilipowaona watoto wakimuulizia, moyo wangu ulizidi kuumia.

Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa.
Wakati mwingine alipokea simu zangu, wakati mwingine hakujibu kabisa. Nilimwomba afikirie kuhusu familia yetu, lakini alionekana kuwa amefanya uamuzi wake. Kadri miezi ilivyopita, matumaini yangu yalianza kupungua.

Watu wengi walinishauri nikubali hali na kuendelea na maisha yangu. Ingawa nilisikiliza ushauri wao, bado nilitamani kuona familia yetu ikiungana tena. SOMA ZAIDI.

 WANAFUNZI wanaofanya ubunifu wa matumizi ya teknolojia mbalimbali katika chuo cha ufundi Arusha (ATC), wametakiwa kusoma Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kuielewa na kuona fursa zilizopo ndani yake na kufanya bunifu zao kutokana na malengo ya dira hiyo.


Hayo yameelezwa Juni 19, 2026 na Mkuu wa chuo cha ufundi Arusha Profesa Musa Chacha katika hotuba yake ya kufungua wiki ya maonyesho ya ubunifu yanayoandaliwa kila mwaka chuoni hapo.

Profesa Chacha amesema dira ya Taifa 2050 imeainisha maeneo ambayo yanapaswa kuendelezwa kwaajili ya Maendeleo ya Watanzania hivyo wanafunzi wanaofanya bunifu chuoni hapo wanapaswa kuyasoma na kuyajua na kuyafanyia ubunifu.

Amesema kutokana na kazi nzuri ya ubunifu ambayo imekuwa ikifanywa na wanafunzi chuoni hapo, chuo kimepanga kujenga jengo maalum la ghorofa nne ambalo litatumika kwaajili ya shughuli za ubunifu.

“ Kwa kushirikiana na Serikali ya Italia hivi karibuni tunatarajia kujenga jengo kubwa la ghorofa nne ambalo litatumika kwaajili ya shughuli za ubunifu( innovation), hapa chuoni hatutaki hivi vipaji vyenu vipotee,” amesema.

Aidha Profesa Chacha amesema chuo kinaendelea na ujenzi wa karakana ( industrial workshop), ambayo itatumika kutengeneza mitambo bunifu itakayokuwa ikigunduliwa na wanafunzi chuoni hapo kwaajili ya kuuzwa na kwamba tayari mashine zitakazotumika katika karakana hiyo zipo njiani kufika chuoni hapo.

“ Hivi sasa tumeamua kuendeleza bunifu zote zitakazobuniwa na wanafunzi Kwa kuzizalisha na kuziingiza sokoni, tutakuwa na kiwanda hapa hapa chuoni na wote mnaofanya ugunduzi huu tutaendelea kuwafuatilia na kuona namna mnafaidika na bunifu zenu, tutawashika mkono popote mtakapoenda,” amesema Profesa Chacha.

Aidha amesema chuo kinakamilisha jengo la hospitali itakayokuwa ikitibia wanafunzi chuoni hapo lakini pia chuo kipi kwenye mikakati ya kujenga jengo litakalojulikana kama innovation center ambalo litakuwa maalum kwaajili ya ugunduzi na uzalishaji wa vifaa tiba vya hospitalini ( biomedical engineering).

Awali akimkaribisha mgeni rasmi Makamu mkuu wa chuo, Dkt Yusuph Mhando alisema katika maonyesho ya mwaka huu ambayo ni awamu ya tatu tangu kuanzishwa, jumla ya bunifu 75 ziliingia kwenye ushindani.

Amesema kati ya bunifu hizo, bunifu 20 zilihusiana na teknolojia ya habari na mawasiliano(Tehama), umeme 15, mitambo na magari 19, sayansi timizi 8, ujenzi na barabara13 na kwamba baada ya majaji kupitia bunifu hizo jumla ya bunifu 19 pekee ziliweza kuingia fainali.

Amesema mshindi wa kwanza ametoka katika fani ya mitambo aliyegundua mashine inayojulikana kama ( Energy trauma kit), akifuatiwa na Tehama ambaye amegundua mashine ya kupima uoni wa macho ( VR acute test),

Aidha amesema maonyesho hayo ni muhimu Kwa Taifa Kwa kuwa yamekuwa yakikuza ujuzi wa wanafunzi chuoni hapo Kwa kuweza kuonyesha Kwa vitendo kile ambacho wamekuwa wakifundishwa darasani.

“ Katika bunifu hizi, Kuna vijana wametengeneza mfumo wa kupiga kura wakati wa uchaguzi ukiwa nyumbani, teknolojia hii ikiweza kuboresha itaweza kusaidia sana katika eneo hili,” amesema.

Amesema ni tegemeo la chuo kuwa bunifu hizo zitafikia jamii na kutatua kero mbalimbali inazizikabili na hivyo chuo kitaendelea kuimarisha na kuendeleza vipaji vya wanafunzi hao.

Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa za kufanikiwa na kubadilisha maisha ya familia yangu. Nilifanya kazi kwa bidii kila siku. 

Niliamka mapema, nilikutana na wateja, na nilijitahidi kuhakikisha kila huduma niliyotoa ilikuwa ya kiwango cha juu. Licha ya juhudi zote hizo, faida niliyokuwa napata haikutosha kufikia malengo yangu.

Miaka ilipita katika hali hiyo. Biashara yangu ilikuwa ikiendelea kuwepo, lakini haikuwa inakua kwa kasi niliyokuwa nimeitarajia. 

Wakati mwingine nilipata faida ndogo, na wakati mwingine nilihangaika hata kulipa baadhi ya gharama za kawaida za biashara.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona washindani wangu wakipata mikataba mikubwa huku mimi nikibaki nikisubiri fursa ambazo hazikuonekana kuja.

Nilijaribu kuboresha huduma zangu na kutafuta masoko mapya. Ingawa kulikuwa na mabadiliko madogo, bado sikuweza kupata nafasi ambayo ingeibadilisha biashara yangu kwa kiwango kikubwa. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miezi sita, nilikuwa nikipata hasara ambazo sikuweza kuzielewa. Nilimiliki duka la jumla ambalo lilikuwa likifanya vizuri katika eneo letu. Hata hivyo, nilianza kugundua kwamba baadhi ya bidhaa zilikuwa zinapotea mara kwa mara. Mwanzoni nilidhani ilikuwa ni makosa ya kawaida ya hesabu.

Lakini kadri muda ulivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya. Kila wiki nilikuwa nikikuta bidhaa zimepungua bila maelezo ya kuridhisha. Nilipohesabu mauzo na kulinganisha na bidhaa zilizobaki, kulikuwa na tofauti kubwa ambayo sikuweza kuieleza. Nilianza kuwa na wasiwasi mkubwa.

Nilizungumza na wafanyakazi wangu na kuwauliza kama kuna jambo walilokuwa wamegundua. Wote walikana kujua chochote. Hata wateja wa kawaida hawakuonekana kuwa na taarifa yoyote kuhusu kilichokuwa kinaendelea. Hasara iliendelea kuongezeka.

Wakati mwingine nililala nikiwa nawaza jinsi biashara yangu ingeendelea kama wizi ule usingekoma. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba mwizi huyo hakuacha ushahidi wowote nyuma.
Nilijaribu njia mbalimbali za kumgundua. SOMA ZAIDI.


Kwa miaka mingi, ndoto yangu kubwa ilikuwa kuwa mama. Nilikuwa nikitamani siku ambayo ningeshika mtoto wangu mikononi na kusikia akiniita mama. Baada ya kuolewa, mimi na mume wangu tulikuwa na matumaini makubwa kwamba tungepata watoto ndani ya muda mfupi.

Lakini mambo hayakwenda kama tulivyotarajia.

Mwaka wa kwanza ulipita bila kupata ujauzito. Kisha mwaka wa pili nao ukapita. Kadri miaka ilivyoendelea, watu wa karibu walianza kuuliza maswali ambayo yaliniumiza moyo. Nilijaribu kutabasamu mbele za watu, lakini ndani yangu nilikuwa nikiteseka.

Kila nilipoona familia nyingine zikifurahia watoto wao, nilijikuta nikitamani siku yangu ifike. Wakati mwingine nililia peke yangu usiku nikijiuliza kwa nini safari yangu ilikuwa ngumu kiasi hicho. Baadaye nilianza kutafuta ushauri kutoka sehemu mbalimbali.

Ingawa nilijitahidi kubaki na matumaini, kulikuwa na nyakati ambazo nilihisi kama ndoto yangu ilikuwa ikizidi kuwa mbali. Kilichoniumiza zaidi ni pale baadhi ya watu waliponiambia nisijiwekee matumaini makubwa. Maneno hayo yaliniumiza sana. SOMA ZAIDI.

  


Na. Farida Ramadhani na Chedaiwe Msuya, WF, Dodoma.

Serikali imeendelea kutumia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), kama nyenzo muhimu ya kuharakisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi, kuboresha huduma kwa wananchi na kuvutia uwekezaji nchini.

Hayo yameelezwa na Mchumi Mwandamizi wa Kitengo cha Ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi, Wizara ya Fedha, Bi. Josephina Melkiol wakati akizungumza na wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

Alisema katika kufanikisha hilo Serikali imefanya maboresho ya Sera, Sheria na Kanuni za PPP ili kuimarisha mazingira ya uwekezaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambapo hadi kufikia Juni 2026, jumla ya mikataba tisa (9) ya PPP imesainiwa katika sekta mbalimbali za maendeleo.

“Miradi iliyosainiwa ni pamoja na Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (DART) Awamu ya Kwanza na ya Pili wenye jumla ya mikataba minne, Mradi wa Ukaguzi wa Lazima wa Vyombo vya Moto, Mradi wa Ujenzi na Uendeshaji wa Jengo la Biashara Kariakoo, Mradi wa Ukarabati na Uendeshaji wa Reli ya TAZARA pamoja na miradi ya uboreshaji na uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam kupitia Kampuni za DP World na ADAN,” alibainisha Bi. Josephina.

Alieleza kuwa Serikali ilianzisha utekelezaji wa Programu ya PPP kupitia Sera ya Taifa ya PPP ya mwaka 2009, iliyolenga kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika utoaji wa huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha, alisema Sheria ya PPP ya mwaka 2010 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2011 ziliweka msingi wa mfumo wa kisheria na kitaasisi wa kusimamia miradi hiyo, huku marekebisho yaliyofanyika mwaka 2014, 2018 na 2023 yakilenga kuongeza ufanisi katika maandalizi ya miradi na mchakato wa kupata wabia.

Bi. Josephina alisema Serikali itaendelea kuimarisha matumizi ya mfumo wa PPP ili kuongeza uwekezaji katika sekta za kimkakati, kuboresha miundombinu na kuharakisha utekelezaji wa miradi yenye manufaa kwa wananchi.

Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi unaendelea kuwa chachu muhimu ya maendeleo kwa kuwezesha upatikanaji wa rasilimali, teknolojia na utaalamu unaohitajika katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kitaifa.






 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa vijana wa vyuo vikuu kuwa waadilifu na wazalendo pindi watakapoajiriwa Serikalini kuwatumikia wananchi au kupata fursa za uongozi wa kulitumikia taifa.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa vijana hao Juni 20, 2026, wakati akifungua Kongamano la Vijana (Youth Uongozi Forum) kwa niaba ya Mhe. Prof. Palamagamba John Aaidan Kabudi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) ambalo linalofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro, lililoandaliwa na taasisi ya Tanzania Leadership Foundation (TLF).

“Vijana wangu, watoto wangu, wadogo zangu mjitahidi sana kuwa waadilifu na wazalendo kwani mkishindwa kuwa waadilifu na wazalendo hamtaweza kudumu katika nafasi mtakazoaminiwa kuzitumikia,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka vijana hao kuwa wanyenyekevu watakapopata fursa ya kuwahudumia wananchi kwani haitowagharimu chochote kumsikiliza na kumuhudumia vizuri mwananchi anayefuata huduma, na kuongeza kuwa hakutakuwa na tija yoyote kwa kijana kuwa na majivuno pindi akipata nafasi ya kuutumikia umma.

Aidha, Prof. Shemdoe amewahimiza vijana wote nchini kutokata tamaa, kutokatishwa tamaa, kuchukua hatua mapema (pro-active) kwa jambo lolote wanaloliona linaweza kuwasaidia badala kusubiri kuambiwa walifanye na kuongeza kuwa, vijana wanapaswa kuilinda nchi kwa hali na mali kwani hakuna taifa lingine ambalo watajivunia zaidi ya taifa mama ambalo ni Tanzania.

Prof. Shemdoe amewahikikishia vijana kuwa, Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwajengea vijana mazingira bora kwa kuimarisha miundombinu ya elimu, mafunzo ya ujuzi pamoja na kuwawezesha kujikomboa kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri nchini, hivyo amewataka vijana kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo huku wakiwa wanaendelea na masomo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amewaasa vijana hao kutotegemea akili za watu wengine katika kujenga uwezo wao wa kufikiri bali watumie akili na uwezo wao binafsi katika kutafakari, kuchambua na kufanya maamuzi yenye mantiki, ili kujijenga na kuwa watu bora zaidi katika jamii.

Naye, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Taasisi ya Tanzania Leadership Foundation Mhe. Jabiri Makame ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe  amesema kuwa, msingi na dira ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni kutengeneza kizazi cha vijana viongozi ambao ni wazalendo, wenye maono, uwezo wa kujiongoza, kutoa uongozi katika taasisi za umma na sekta binafsi.












Katika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ili kuwawezesha wananchi, hususan vijana, kumudu kumiliki makazi.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TBA, Bi. Amina Lumuli, amesema kuwa TBA tayari imeanza kutekeleza miradi ya nyumba za gharama nafuu katika mkoa wa Dar es Salaam.

Bi. Lumuli ametaja Mradi wa Temeke Kota kuwa ni miongoni mwa miradi hiyo, akibainisha kuwa utekelezaji wa mpango huo utaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

"Tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi ili kwa pamoja tuweze kufanikisha lengo la Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 la kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu," amesema Bi. Lumuli.

Aidha, Bi. Lumuli amesema utekelezaji wa mradi huu unatokana na dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na yenye gharama nafuu.

Amesema TBA itaendelea kuhakikisha makundi yote, yakiwemo makundi maalum, yanafikiwa na kunufaika na programu hii ya nyumba za gharama nafuu.
Nilipoamua kugombea nafasi ya uongozi, watu wengi hawakunichukulia kwa uzito. Wapinzani wangu walikuwa na majina makubwa, uzoefu wa muda mrefu, na ushawishi mkubwa katika jamii. 

Wengi waliniambia nilikuwa napoteza muda wangu kwa kuingia kwenye uchaguzi ambao tayari ulikuwa umeamuliwa.

Lakini sikukata tamaa. Nilijua nilikuwa na maono ya kuwaletea watu maendeleo na nilitaka kuwapa sababu ya kuamini kwamba mabadiliko yanawezekana. 

Hata hivyo, kadri kampeni zilivyoendelea, changamoto ziliongezeka. Kulikuwa na maneno mengi ya kunikatisha tamaa.

Baadhi ya watu walieneza uvumi kwamba sikuwa na uwezo wa kuongoza. Wengine walisema sina mtandao wa watu wenye ushawishi wa kunisaidia kushinda. 

Wakati mwingine nilirejea nyumbani nikiwa nimechoka na kujiuliza kama kweli nilikuwa nimefanya uamuzi sahihi. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miaka mitano, nilikuwa nimejenga biashara yangu kwa juhudi kubwa. Nilijitahidi kuwahudumia wateja wangu vizuri na kuhakikisha biashara yangu inakua mwaka baada ya mwaka. Lakini ghafla mambo yalianza kubadilika kwa njia ambayo sikuweza kuielewa.

Kila nilipoanzisha ofa mpya au mpango wa biashara, washindani wangu walionekana kujua kila kitu kabla hata sijaanza kuutekeleza. Mwanzoni nilidhani ilikuwa bahati mbaya. Lakini kadri hali ilivyoendelea kujirudia, nilianza kupata mashaka.

Wakati mwingine nilikuwa nazungumza mipango yangu na wafanyakazi wachache tu wa ndani, lakini baada ya siku chache washindani walikuwa tayari wamechukua hatua zinazofanana na zangu. Biashara yangu ilianza kupata hasara.

Wateja waliokuwa wakinifuata kwa muda mrefu walikuwa wakivutiwa na washindani waliokuwa wakionekana kujua kila hatua niliyopanga kuchukua. Nilihisi kama kuna mtu alikuwa akivujisha siri muhimu za biashara yangu.

Nilijaribu kuchunguza mwenyewe.

Nilifuatilia mawasiliano mbalimbali na kuangalia mienendo ya wafanyakazi wangu, lakini sikuweza kupata ushahidi wa kutosha. SOMA ZAIDI.
Hakuna jambo linaloumiza mzazi kama kuwaona watoto wake wakiteseka. Kwa muda mrefu, watoto wangu walikuwa wakiugua mara kwa mara.

Mwezi mmoja hawakuwa sawa, na kabla hawajapona kabisa, tatizo jingine lilikuwa limeanza. Safari za hospitali zikawa sehemu ya maisha yetu ya kawaida. Nilikuwa na wasiwasi mkubwa.

Mbali na matatizo ya afya, amani nyumbani pia ilikuwa imepotea. Watoto walikuwa wakigombana mara kwa mara, kulikuwa na hali ya huzuni ambayo sikuweza kuieleza, na kila mtu ndani ya nyumba alionekana kuwa na mawazo mengi. Nilijaribu kufanya kila nilichoweza kama mzazi.

Nilihakikisha watoto wanapata matibabu wanapohitaji, wanakula vizuri, na wanapata mapumziko ya kutosha. Hata hivyo, nilihisi kama bado kulikuwa na jambo lililokuwa likinisumbua moyoni. Kadri miezi ilivyopita, uchovu na wasiwasi vilianza kunizidi. SOMA ZAIDI.
Baada ya kuhitimu masomo yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kupata kazi nzuri na kuanza kujitegemea.

Nilituma maombi kwa kampuni mbalimbali na kuhudhuria mahojiano mengi. Kila nilipoitwa kwenye interview, niliamini safari hii ningepata nafasi niliyokuwa nikiiota. Lakini mara nyingi majibu yalikuwa yale yale.

“Sikuchaguliwa.” Kadri miezi ilivyogeuka kuwa miaka, hali ilianza kuniumiza sana. Niliona marafiki zangu wakipata kazi na kuendelea na maisha huku mimi nikiendelea kutuma maombi kila wiki bila mafanikio. Wakati mwingine nilifika hatua ya kujiuliza kama kulikuwa na kitu nilichokuwa nikifanya vibaya.

Nilijitahidi kuboresha wasifu wangu, kujifunza ujuzi mpya, na kujiandaa vizuri kwa mahojiano. Hata hivyo, kila nilipokuwa karibu kupata matumaini, nilipokea ujumbe mwingine wa kukataliwa. Familia yangu ilinipa moyo, lakini ndani yangu nilikuwa nimeanza kukata tamaa. SOMA ZAIDI.
Ndoa yangu ilikuwa imejengwa juu ya upendo, heshima, na matumaini makubwa ya maisha ya pamoja. Kwa miaka kadhaa mambo yalikuwa mazuri. Mimi na mume wangu tulielewana na tulifanya kila kitu kwa ushirikiano. Lakini hali ilianza kubadilika taratibu.

Mume wangu alianza kurudi nyumbani akiwa amechelewa, akawa mbali kihisia, na muda aliokuwa akitumia na familia ukapungua.
Mwanzoni sikutaka kuamini kwamba kulikuwa na tatizo. Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa, lakini kila nilipouliza kuhusu mabadiliko yake, alinipa majibu mafupi au kubadilisha mada.

Kadri miezi ilivyopita, niligundua kwamba kulikuwa na mwanamke mwingine katika maisha yake. Habari hiyo ilinivunja moyo. Nilihisi hasira, huzuni, na kuchanganyikiwa kwa wakati mmoja.

Wakati mwingine nilitaka kuondoka kabisa, lakini nilikuwa bado na matumaini kwamba familia yetu ingeweza kuokolewa. SOMA ZAIDI.


Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam


Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la International Media Support (IMS), umeahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano na vyombo vya habari pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya habari nchini ili kukuza uandishi wa habari zenye maslahi kwa umma.

Akizungumza wakati wa semina iliyowakutanisha wawakilishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, Mkurugenzi wa UTPC, Kenneth Simbaya, alisema ushirikiano kati ya wadau wa sekta ya habari ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na zenye manufaa kwa maendeleo yao.

Alisema kuna haja ya kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari, mamlaka za usimamizi wa sekta hiyo na wadau wengine ili kuleta mabadiliko chanya yatakayochochea upatikanaji wa habari zinazolenga maslahi ya wananchi.

“Tunao wajibu wa kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha tunajenga jamii yenye taarifa sahihi. Kila mmoja anatakiwa kutimiza wajibu wake ili kufikia malengo ya kuimarisha sekta ya habari nchini,” alisema Simbaya.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanzania Media Foundation Dastan Kamanzi (TMF), alisema waandishi wa habari wanapaswa kuweka kipaumbele katika kuandaa na kuchapisha habari zinazogusa maisha ya wananchi, haki zao pamoja na uhuru wao.

Alieleza kuwa kufanya hivyo kutasaidia kuitendea haki taaluma ya uandishi wa habari na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya jamii.

Wakichangia mjadala huo, baadhi ya wawakilishi wa vyombo vya habari walieleza kuwa utekelezaji wa habari za maslahi kwa umma unahitaji uwezeshaji zaidi kupitia mafunzo na upatikanaji wa vitendea kazi vya kisasa.

Walisema baadhi ya vyombo vya habari bado vinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa wataalamu wenye ujuzi wa kutumia mbinu za kisasa katika kuandaa na kuandika habari za maslahi kwa umma.


Semina hiyo iliyoandaliwa na UTPC ililenga kufanya tathmini ya pamoja kuhusu changamoto zinazoathiri upatikanaji wa habari za maslahi kwa umma na kujadili mikakati ya kuzitatua. Semina hiyo ilifanyika Juni 19, 2026 katika Hoteli ya Mbezi Garden, jijini Dar es Salaam.