Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mhe. Timontheo Mnzava, amewataka madiwani na wenyeviti wa vijiji kushirikiana kwa karibu katika kutatua migogoro ya ardhi ili kulifanya jimbo hilo kuwa mfano wa matumizi sahihi ya ardhi na kuimarisha amani kwa wananchi.

Mbunge Mnzava ametoa wito huo wakati akiendelea na ziara zake za kukutana na makundi mbalimbali ya jamii, kwa kushirikiana na viongozi wa Chama pamoja na Halmashauri. Katika kikao maalum alichokaa na madiwani pamoja na wenyeviti wa vijiji, walijadili masuala mbalimbali yenye lengo la kuimarisha utawala bora na maendeleo ya wananchi.

Katika kikao hicho, Mhe. Mnzava aliwapongeza madiwani kwa ushindi wao katika uchaguzi na kuwashukuru wenyeviti wa vijiji kwa kushiriki kikamilifu katika kulinda amani wakati wote wa zoezi la uchaguzi, Alisisitiza kuwa mchango wao ulikuwa mkubwa katika kuhakikisha maeneo yao yanabaki salama na yenye mshikamano.

Aidha, aliwakumbusha viongozi hao majukumu yao ya msingi, hususan kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kwa vitendo, kwa kuzingatia maslahi ya wananchi waliowachagua.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mnzava alikemea vikali vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya mihuri katika maeneo yao, akisisitiza kuwa vitendo hivyo vinadhoofisha uaminifu wa wananchi kwa viongozi wao na kukwamisha haki. Akihitimisha kikao hicho, aliwataka madiwani na wenyeviti wa vijiji kuwa mstari wa mbele katika kulinda na kuitunza amani iliyopo, akisisitiza kuwa amani ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu ya jimbo na taifa kwa ujumla.

 


Na Benny Mwaipaja, Zanzibar


Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, itaendelea kuboresha huduma za jamii ikiwemo sekta ya afya kwa wananchi wake.

Mhe. Balozi Omar ametoa kauli hiyo wakati akizindua Kituo cha Afya cha Kisasa cha Kinduni, kilicho gharimu shilingi bilioni 3.77, kilichokojengwa katika Wilaya ya Kaskazini B mkoa wa Kaskazini Unguja, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Alisema kuwa uwepo wa Kituo hicho cha Afya inathibitisha mafanikio makubwa katika sekta ya afya chini ya Uongozi wa Raisi wa Zanzibar wa Awamu ya nane, Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya katika ngazi zote za kijamii. 

“Serikali imeshajenga na kuweka vifaa katika  hospital 10 za wilaya katika wilaya za Unguja na Pemba, baada ya kuimarisha huduma katika ngazi ya wilaya zote, kuanzia mwaka 2023/2024 ambapo imeweka kipaombele katika kuimarisha miundombinu ya Afya ya msingi ili kutoa huduma bora zaidi ya Afya kwa jamii” alisema Mhe. Balozi Omar.

Alisema kuwa amefarijika kuona miundombinu ya afya inazidi kuimarika zaidi katika awamu ya nane ya Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na kuwataka wananchi wakitunze  Kituo hicho ili kiwe chenye ubora na cha kuvutia siku zote ili kiendelee kutoa huduma bora za afya kwa muda mrefu na kuwahudumia Wananchi wengi zaidi.

Alisema kuwa Kituo hicho kitahudumia zaidi ya watu 19,546 wakiwemo watoto wenye umri wa chini ya mwaka mmoja 782, watoto wenye umri chini ya miaka mitano 2,834 na wanawake wenye umri wa kuzaa 5,336 kutoka shehia nne za Kinduni, Mkataleni, Mahonda na Mnyimbi pamoja na maeneo Jirani.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa Kituo hicho cha afya Kinduni, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Mgereza Mzee Miraji, alisema kuwa Mradi huo unajengwa kwa fedha za Serikali kwa gharama ya shilingi za Tanzania bilioni 3.77 chini ya Mkandarasi Mazrui Building Contractors Ltd na unasimamiwa na Mshauri elekezi, Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA).

Alisema Ujenzi wa kituo hicho unahusisha jengo moja la gorofa moja (G+2) na baada ya kukamilika kwake kitakuwa kinafanya kazi saa 24, kitakuwa na uwezo wa kulaza wagonjwa 30 kwa wakati mmoja na kitakuwa kikitoa huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo huduma za Kliniki na wagonjwa wa nje (OPD), huduma za Kliniki za mama na mtoto, maradhi ya pua, koo, masikio na macho, klinik ya magonjwa ya shinikizo la damu, kisukari, Ngozi, kinywa na meno.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Bw. Cassian Galoss Nyimbo, alisema kuwa Kitu cha Afya Kundini, ni cha kisasa kilichojengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa fedha zake za ndani, ambacho kitatoa huduma za afya karibu na wananchi na kwamba hawatakwenda umbali wa zaidi ya kilometa 5 kupata huduma hizo.

Nao wananchi wa Kundini na Mahonda, waliishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuwasogezea huduma za afya karibu nao kwa kuwajengea Kituo hicho kitakachotoa huduma za afya kwa mfumo wa kidigitali kwani tayari vifaa vya uchunguzi, matibabu na TEHAMA, vimeshafungwa.










Magesa Magesa ,Arusha .



Arusha .Mkuu wa mkoa wa Arusha ,CPA Amos Makalla amewataka wananchi kuhakikisha kuwa wanajiunga na bima ya afya kwa wote ili waweze kupata vipimo,matibabu,na dawa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Ameyasema hayo jijini Arusha leo wakati akizindua sehemu maalumu ya kupokelea wagonjwa wa dharura pamoja na magonjwa yasiyoambukiza katika hospitali ya ALMC (Selian ) iliyopo jijini hapa .

Sehemu hiyo maalumu ya kupokelea wagonjwa hao imekarabatiwa na kuweka vifaa tiba na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)  ambapo ukarabati pamoja na vifaa tiba umegharimu kiasi cha shs 200 milioni .


CPA Makalla aliwapongeza wananchi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani kujitokeza kwa wingi kupata huduma ya upimaji wa magonjwa ya moyo yanayotolewa na Tasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete ambayo imeweka kambi ya matibabu hospitalini hapo .


"kila binadamu ni mgonjwa mtarajiwa hivyo nawapongeza wananchi kwa kuwahi kukua afya zenu, kwani kwa kufanya hivyo mtaweza kupata matibabu ya haraka na kuepukana na magonjwa hayo yasiyoambukiza."amesema CPA Makalla. 


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dokta Peter Kisenge amesema kuwa , Taasisi hiyo imekwisha  kufungua vituo sita katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo kituo hiki.cha hapa  Arusha ambacho kitahudumia mikoa ya kaskazini na mikoa jirani .

Dkt Kisenge amesema kuwa , kambi hiyo ya  uchunguzi wa magonjwa ya moyo ilianza desemba 29 na inatarajiwa kifikia tamati  januari 9, na kusema kuwa hadi sasa zaidi ya wagonjwa 1,200 wameshahudumiwa na walioonekana na tatizo kubwa walipewa rufaa ya kwenda makuu ya Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. 


Amesema kuwa, mwitikio wa wananchi ni mkubwa hali inayoonyesha kuwa wananch9 wengi wanakabiliwa na tatizo la moyo na kuwataka wananchi kuendelea kujitokeza kwa siku hizo chache zilizobakia .


"Bado tatizo la magonjwa yasiyoambukiza yamekuwa ni tishio kubwa kwa uhai wa mwanadamu hivyo umefika wakati sasa kwa wananchi kuchunguza afya zao mapema ili kuweza kutambua afya zao badala ya kusubiri  hadi dalili za ugonjwa husika kujitokeza kitendo ambacho kinakuwa ni changamoto kwenye suala la matibabu ."amesema Dkt Kisenge .

 Aidha ameshukuru hospitali hiyo ya ALMC (Selian) inayomilikiwa na kanisa la Kiinjili la.kilutheri Tanzania (KKKT)  pamoja na uongozi  wa kanisa hilo kwa kuwakubalia kuweka kituo cha kutoa huduma ya matibabu ya moyo katika hospitali hiyo kwani lengo la JKCI  ni kutaka kuona wananchi hawapotezi maisha  yao kwa tatizo la moyo.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Ngarenaro, Abdulaziz  Chande (Dogo Janja) amemshukuru Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha JKCI ili kuweza kuja kutoa huduma hiyo kwa siku zote hizo kwa  wananchi wa Arusha  na mikoa ya jirani.

"Mimi.nina mfano ulio hai baba yangu mzazi anasumbuliwa na tatizo la moyo na ilikuwa nikitakiwa kumpeleka  jijini Dar es Salaam mara mbili kwa mwezi ,lakini kufunguliwa kwa kituo hiki mkoani Arusha kimeleta faraja sio kwangu tu ila kwa wananchi wote wanaosumbuliwa na matatizo ya moyo kwani imewapunguzia gharama za kwenda kufuata huduma hiyo jijini Dar es Salaam. "amesema Dogojanja.

Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa (Kushoto) akiwa katika mazungumzo na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango ya Zanzibar, Dkt. Afua Khalfan Mohamed (Katikati) alipotembelea ofisi hizo Zanzibar leo ( 6.1.2025). Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasimali Watu, Bi.Maryam Ukki.

 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Gugu, amewahimiza wafanyakazi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo iliyowekwa katika usajili na utambuzi wa wananchi.

Gugu alitoa wito huo tarehe 3 Januari, 2025, alipokuwa akifungua rasmi mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa NIDA uliofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.

“Nawapongeza kwa utendaji mzuri wa kazi, lakini nawasisitiza muendelee kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za usajili, kwani NIDA ni taasisi muhimu sana katika maendeleo ya taifa,” alisema Gugu.

Alisisitiza kuwa NIDA inatekeleza majukumu nyeti yenye maslahi makubwa kwa taifa, hivyo wafanyakazi wanapaswa kuonesha uzalendo na uadilifu katika kulinda na kusimamia vyema taarifa binafsi za wananchi walizokabidhiwa.

Aidha, aliwahimiza wananchi ambao bado hawajachukua vitambulisho vyao vya taifa kufika katika ofisi za NIDA za wilaya ili kuvichukua, akibainisha kuwa vitambulisho hivyo ni nyaraka muhimu za utambulisho na kwamba serikali imetumia gharama kubwa kuvizalisha.

Vilevile, Gugu aliipongeza NIDA kwa kuanzisha huduma ya Msimbo Mfupi (Short Code) inayowawezesha wananchi kupata mrejesho wa huduma za vitambulisho kupitia simu za mkononi bila malipo.

Alisema huduma hiyo itanufaisha zaidi wakazi wa maeneo ya vijijini kwa kuwawezesha kupata taarifa kuhusu hali ya usajili wao na taarifa binafsi wakiwa maeneo yao, bila ya kusafiri umbali mrefu hadi ofisi za wilaya.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, James Kaji, alieleza kuwa zaidi ya vitambulisho vya taifa 300,000 bado havijachukuliwa katika ofisi za NIDA za wilaya mbalimbali.

“Natumia fursa hii kuwasihi wananchi kwenda kuchukua vitambulisho vyao, kwani serikali imetumia fedha nyingi katika uzalishaji wake,” alisema Kaji.

Aidha, aliwashauri wananchi wenye makosa katika taarifa zao binafsi kutumia kibali maalum cha mwaka mmoja kurekebisha taarifa hizo, akisisitiza kuwa baada ya kibali hicho kuisha, hakutakuwa na muda wa nyongeza.

Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase,akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

....

Serikali imewataka wakulima nchini kuhakikisha wanapeleka kakao yenye ubora sokoni ili kulinda bei nzuri inayoendelea kupatikana kwa sasa.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi (Mb), wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo, .

 DC Manase amesisitiza kuwa kuingiza kakao isiyo na viwango katika masoko kutasababisha bei kuporomoka, jambo ambalo litawaathiri wakulima kiuchumi. Amesema kuwa uaminifu wa mkulima katika kuzingatia vigezo vilivyowekwa ndiyo njia pekee ya kuhakikisha zao hilo linaendelea kuwa na ushindani na kupata masoko yenye tija ndani na nje ya nchi.

Aidha, DC Manase amewahimiza wakulima wa Kyela kuendelea kupanda miti kama mbinu madhubuti ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi na kulinda mazingira ya kijani. Amebainisha kuwa utunzaji wa mazingira ni kigezo muhimu kinachowezesha mazao ya wakulima kukubalika katika ngazi ya kimataifa, huku akisisitiza kuwa juhudi hizo pia zinasaidia wakulima kupata uaminifu wa kibenki na huduma nyingine za kifedha.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, ameeleza umuhimu wa utaratibu wa kukagua mizigo ghalani kabla ya kuifikisha mnadani. Akifafanua kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha kile kinachouzwa kinafahamika kwa usahihi, jambo linalosaidia kuondoa migogoro kati ya wanunuzi na wauzaji.

Vilevile, amesema utaratibu huo wa ukaguzi umeleta matokeo chanya kwani hivi sasa hakuna malalamiko yanayotolewa na pande zote mbili katika mnyororo wa biashara.

Naye Naibu Msajili wa Udhibiti wa Vyama vya Ushirika, Bw. Collins Nyakunga, ameeleza kuwa vipaumbele vya sasa vya ushirika ni kuwekeza katika ujenzi wa viwanda ili kuongeza thamani ya mazao, hatua inayolenga kubadilisha taswira ya vyama vya ushirika ili viweze kutoa mchango mkubwa zaidi kwa wakulima kwa kuhakikisha wanapata faida kubwa kutokana na kazi yao.

Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase,akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu,akielezea umuhimu wa utaratibu wa kukagua mizigo ghalani kabla ya kuifikisha mnadani wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

Naibu Msajili wa Udhibiti wa Vyama vya Ushirika, Bw. Collins Nyakunga,akielezea  vipaumbele vya sasa vya ushirika ni kuwekeza katika ujenzi wa viwanda ili kuongeza thamani ya mazao, wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase, kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase (hayupo pichani) ,akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua uendeshaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) wilayani humo kwa niaba ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi.

   

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir (katikati) akimsikiliza Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia Professa Maulilio Kipanyula,(kulia) akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Bweno katika taasisi hiyo mara baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike yenye jumla ya vyumba 184 katika Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

.....

SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeeleza kuridhishwa na hatua ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), kufuatia ziara ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, iliyofanyika jana katika Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri alikagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike yenye jumla ya vyumba 184, mradi unaolenga kuongeza ushiriki wa wanawake na watu wenye ulemavu katika elimu ya juu, hususan katika fani za sayansi, teknolojia na ubunifu ambazo ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa.

Aidha, Mhe. Wanu alipokea taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa Samia Scholarship Extended (DS/AI+), unaodhamini wanafunzi 50 wanaosoma fani za Sayansi ya Takwimu, Akili unde  (Artificial Intelligence—AI) na Sayansi Shirikishi. Mpango huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuandaa rasilimali watu wenye ujuzi wa kisasa unaokidhi mahitaji ya soko la ajira sambamba na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mhe. Naibu Waziri aliipongeza NM-AIST kwa usimamizi mzuri na hatua iliyofikiwa katika kutekeleza miradi hiyo, akisisitiza kuwa miradi hiyo ni muhimu katika kuimarisha elimu ya juu, kukuza utafiti na kuandaa wataalamu watakaoharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia Professa Maulilio Kipanyula, alisema awamu ya kwanza ya ujenzi wa mabweni imefikia asilimia 80 na inatarajiwa kukamilika Februari 2026.

Kukamilika kwa mradi huo kunatarajiwa kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuishi kwa wanafunzi wa kike na kuongeza motisha kwao kushiriki kikamilifu katika masomo ya sayansi na teknolojia.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir (katikati) akimsikiliza Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia Professa Maulilio Kipanyula,(kulia) akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Bweno katika taasisi hiyo mara baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike yenye jumla ya vyumba 184 katika Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akizungumza mara baada ya   kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike yenye jumla ya vyumba 184 katika Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia Professa Maulilio Kipanyula,akizungumza mara baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir kufanya ziara katika taasisi hiyo  ya  kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike yenye jumla ya vyumba 184 katika Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Sehemu ya wanafunzi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir (hayupo pichani),akizungumza baada ya   kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike yenye jumla ya vyumba 184 katika Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Kwa muda mrefu nilijihisi kuwa kila juhudi niliyoweka ili kupata utajiri ilishindikana. 

Biashara zangu ziligonga mwamba, akaunti yangu ya benki ilionekana kuwa na nambari ndogo kila siku, na marafiki waliokuwa na mafanikio yalionekana kuwa mbali sana.

Nilijaribu kila njia, kutoka kwa mikopo, ushauri wa biashara, hadi kufanya kazi nyingi, lakini kila mara niliishia na hasara na kuchoka. Hali hii ilinifanya niwe na huzuni na wasiwasi mkubwa.

Nilijisikia ningeendelea kuwa maskini bila mwisho. Kila mtu aliniuliza ni nini kilikuwa chanzo cha matatizo yangu, lakini sijui ni kitu gani kilinizuia kufanikisha malengo yangu. 

Nilijaribu njia nyingi za kawaida za kuongeza kipato, lakini hakuna kilichobadilika kwa muda mrefu. Soma Zaidi...

Kwa miaka mitatu ya ndoa yangu, kila siku ilionekana kuwa changamoto isiyoisha. Nilikuwa na furaha ya ndoa na mume wangu, lakini jambo moja liliendelea kunichosha na kunisababisha wasiwasi mkubwa siku moja hakuwezi kuzaa mtoto.

Nilijaribu kila njia ya kisasa: mitihani ya hospitali, dawa za uzazi, na hata mabadiliko ya mtindo wa maisha. Lakini matokeo yalibaki hafifu, na huzuni ilianza kuathiri uhusiano wetu.
Hali hii ilinifanya niwe na aibu na kushindwa kueleza hisia zangu.

Nilijisikia kuwa kitu kiko vibaya kwangu, na mara nyingine nilihisi hofu kuwa ndoa yangu ingeathirika. Kila mtu aliniuliza ni nini kilikuwa chanzo, lakini sijui ni nini kilikuwa kimenizuia kupata mtoto. Nilijaribu mbinu za kawaida, lakini matokeo yalibaki hafifu na moyo wangu ukijaa huzuni.

Baada ya muda, nilijua kuwa lazima nipate msaada wa kina.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikaa-miaka-mitatu-kwa-ndoa-bila-mtoto-lakini-njia-hii-ya-kienyeji-ilinipa-suluhisho/

Msiba wa mzazi wangu ulikuwa kama kimbunga kilichinikumba ghafla. Nilihisi maisha yameniacha, kila siku ilikuwa ya huzuni na upweke. 

Nilijaribu kuendelea na kazi na shughuli za kila siku, lakini kila hatua ilionekana bure.

Nguvu za mwili na akili zilibaki chini, na mara nyingi nilijikuta nikilala masaa mrefu bila kufanya lolote. 

Hali hii ilinifanya niwe na wasiwasi na huzuni isiyoisha. Nilijaribu kuzungumza na marafiki na familia, lakini walishindwa kuelewa uzito wa maumivu yangu.

Mara nyingine nilijihisi nitaanguka ndani ya giza la mawazo hasi, nikidhani maisha hayatabadilika kamwe. 

Nilijaribu mbinu za kawaida za kujiponya, kama kufanya mazoezi, kula vizuri, na kujitenga na mawazo hasi, lakini matokeo yalibaki hafifu.

Baada ya muda, nilijua kuwa lazima nipate msaada wa kina.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-mwelekeo-baada-ya-msiba-safari-ya-kujiponya-ilianza-polepole/

Kwa muda mrefu nilijihisi kuwa na tatizo lisilo la kawaida. Kila nikikutana na mume wangu au fikiria tendo la ndoa, hamu yangu ilikuwa chini sana. 

Nilijaribu kuzungumza naye, lakini mara nyingi nilihisi aibu au hasira kwa sababu sijui tatizo lilitoka wapi.

Nilijaribu kubadilisha mtindo wa maisha, kula vizuri, hata kupumzika zaidi, lakini hakuna kilichobadilika. 

Hali hii ilinifanya nijihisi kuchoshwa na kuanza kujilaumu. Nilijisikia kuwa si mzuri tena, na kuishi kwa hofu ya kuvunja uhusiano wangu kulikuwa kawaida.

Nilijaribu kupata ushauri kutoka kwa madaktari wa kawaida, lakini walieleza tu kuwa ni jambo la kawaida la kiakili au la kihembe. 

Nilihisi kama ningeendelea hivi, ndoa yangu ingepoteza maisha yake ya furaha na unyenyekevu.

Hatua ya mabadiliko ilikuja nilipokuwa nikiwa tayari kutafuta suluhisho la kina. Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nikikosa-hamu-ya-ndoa-bila-kuelewa-kwa-nini-nilipoangalia-afya-yangu-majibu-yakapatikana/

Kwa muda mrefu, nilijaribu kufanikisha maisha yangu kila jambo lilionekana kunizidi. Biashara zangu hazikua, kazi zangu hazikuleta matokeo, na kila mara nilihisi nimekumbwa na vizuizi visivyoonekana.

Nilianza kujiuliza kama kuna nguvu fulani inanikwamisha, nikishindwa kuelewa ni kwa nini jitihada zangu hazina matokeo. Hali hii ilinifanya niwe na hofu na wasiwasi kila siku.

Nilijikuta nikiishi kwa kujihisi chini, nikiwa na mashaka yasiyoisha kuhusu kila hatua ninayochukua. Kila napata fursa, huwa nahisi kama inakwamishwa kwa njia fulani. Nilijaribu mbinu za kawaida kusoma, kufanya kazi kwa bidii, na kuuliza ushauri lakini mafanikio yalionekana mbali.

Hatua ya mabadiliko ilikuja nilipokuwa nikiwa tayari kutafuta suluhisho la kina. Soma Zaidi...

 


Na. Joseph Mahumi, WF, Arusha


Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi Khamis Mussa Omar (MB), ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuendelea kufanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, hatua iliyochangia kuimarika kwa uchumi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Ametoa Pongezi hizo wakati akifungua Mkutano wa Kutathmini Utendaji Kazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa Nusu Mwaka wa Fedha 2025/26 (Mid-Year Performance Review Meeting), uliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), jijini Arusha.

Mhe. Balozi Khamis, alisema kuwa Mamlaka hiyo imeendelea kuonesha ufanisi mkubwa katika ukusanyaji wa mapato ambapo katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2025 ilikusanya shilingi trilioni 18.77 sawa na ufanisi wa asilimia 103.7 ya lengo la kukusanya trilioni 18.10.

“Mwezi Desemba pekee, TRA mmeweka rekodi mpya kwa kukusanya shilingi trilioni 4.13 kiwango cha juu zaidi kuwahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa Mamlaka hii, mafanikio haya ni kiashiria tosha kwamba TRA ipo katika mwelekeo mzuri wa kufanikisha na hata kuvuka lengo la mapato lililopangwa kwa mwaka wa fedha 2025/26. Hongereni sana kwa jitihada zenu,” alisema Mhe. Balozi Khamis.

Aidha, aliongeza kuwa mafanikio hayo yanatokana na sera na miongozo madhubuti inayowekwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hasa uwekezaji wa mifumo ambao umeleta mapinduzi katika makusanyo ya kodi.

“Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha uchumi kupitia mageuzi ya mifumo ya mapato, sera bora za kodi na matumizi ya teknolojia za kisasa katika ukusanyaji wa mapato na yameiwezesha TRA kufanya vizuri zaidi mwaka hadi mwaka,” alisema Mhe. Balozi Khamis.

Mhe. Balozi Khamis, aliitaka TRA kuhakikisha Mfumo Mpya wa IDRAS unafanya kazi kwa ufanisi mara tu baada ya kuzinduliwa rasmi, ili kuongeza uwazi, ufanisi na usimamizi bora wa ukusanyaji wa mapato sambamba na kuendelea kupanua wigo wa kodi, hasa katika sekta isiyo rasmi, biashara mtandaoni na uchumi wa kidijitali, pamoja na kutumia mbinu rafiki na zenye kuzingatia utu wa mlipakodi ili kujenga uhusiano wa kuaminiana kati ya TRA na walipakodi.

Kwa upande wao Naibu Mawaziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) na Mhe. Laurent Luswetula, wameahidi kutoa ushirikiano kwa Mhe. Waziri wa Fedha, ili kuhakikisha wanaisimamia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili iweze kuendelea kutimiza malengo yake ya muda mfupi na mrefu ya kukusanya mapato, na kuboresha zaidi uhusiano wake na walipa kodi.

Akizungumza kwa Niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dkt. Albina Chuwa, alisema kuwa wataendelea kuhakikisha wanapanua zaidi wigo wa walipa kodi kutoka milioni 7 waliopo hivi sasa hadi milioni 21 ili kuwa na mapato mengi zaidi kusaidia ujenzi wa miradi ya wananchi.

Kwa upande wake Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Bw. Yusuph Mwenda, aliwapongeza wafanyabiashara kwa namna walivyotimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari na kuwezesha kufikia malengo waliyofikia katika Nusu Mwaka wa Fedha 2025/26.

Bw. Mwenda alisema kuwa kupitia Mkutano huo TRA itatathmini miezi sita ijayo, maeneo ya kuboresha zaidi ili kufikia malengo ya makusanyo ya mapato ifikapo Juni 2026 baada ya TRA imeweza kurekodi Ukuaji chanya wa asilimia 13.6 katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2025, hali inayoonesha matokeo chanya kwa Mamlaka kusimamia mapato ya Serikali, pamoja na juhudi za Serikali kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi nchini.

“Ufanisi wa makusanyo uliofikiwa na TRA kwa miezi ya Julai hadi Desemba 2025 ni kiashiria chanya katika kuhakikisha kuwa lengo la makusanyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 la Shilingi trilioni 36.06 linafikiwa” aliongeza Bw. Mwenda

Aliongeza kuwa Mamlaka hiyo imeweka lengo la kuhakikisha sehemu ya makusanyo ya mapato kwenye Pato la Taifa (revenue to GDP ratio) kwa mwaka 2025/26 inakuwa ni zaidi ya asilimia 14.1, toka kwenye kiwango cha asilimia 13.7 kilichorekodiwa mwaka 2024/25 ambapo katika kufanikisha hilo, Menejimenti ya TRA imeendelea kutekeleza kikamilifu mikakati iliyojiwekea, ikiwemo kuhakikisha kuwa Mfumo wa Usimamizi wa Kodi za Ndani Uliohuishwa (IDRAS) unaanza kutumika kuanzia Mwaka huu 2026.

 


Na James Mwanamyoto - Tanga

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekabidhi hundi yenye thamani ya Bilioni 2.761 kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vilivyonufaika na mkopo wa asilimia 10, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hasan aliyoitoa kwa wananchi kuwa ataitekeleza ndani ya siku 100 za uongozi wake.

Prof. Shemdoe amekabidhi hundi hiyo leo Januari 05, 2026 kwa vikundi hivyo jijini Tanga katika Uwanja wa Tangamano, mara baada ya kukagua shughuli za wajasiriamali walionufaika na mikopo ya asilimia 10 mkoani Tanga.

“Leo tumetoa Bilioni 2.761 kwa vikundi vya halmashauri ya jiji la Tanga, Korogwe Mji,  Korogwe wilaya , Lushoto, na Pangani, ambazo zitanufaisha vikundi vya wanawake 155, vijana 71 na wenye ulemavu 19 ambapo jumla ya ajira 1,715 zimetengenezwa,” amefafanua Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe, Balozi Dkt. Batilda Burian, kwa kusimamia vema utoaji wa mikopo ya asilimia 10 pamoja na kuandaa maonesho ya shughuli za vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo, na kuwaelekeza Wakuu wa Mikoa mingine kuandaa maonesho kama Mkoa wa Tanga ulivyofanya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian amesema katika kutekeleza ahadi hiyo ya Mhe. Rais, kwa Tanga jiji pekee Prof. Shemdoe amekabidhi hundi ya Bilioni 2 kwa vikundi 137 ambapo wanufaika ni wananchi 686.

Naye mmoja wa wanufaika wa mikopo hiyo ya asilimia 10, Bi. Zainab Abdallah ambaye ni mlemavu amesema yeye na mwenzie Mariam Siafu wamenufaika na mikopo hiyo ambapo wameweza kununua bajaji nne (4), awamu ya kwanza walipata  Shilingi Milioni 17 zilizowawesha kununua bajaji mbili (2) na awamu ya pili walipata Milioni 22 zilizowawezesha kununua bajaji (2) nyingine na hatimaye wamefanikiwa kuajiri madereva wanne (4).



Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amemtaka mkandarasi anayesimamia ujenzi wa bweni la wasichana katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole, Jijini Mbeya, kuhakikisha anakamilisha mradi huo kwa wakati uliopangwa ili kuendana na malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto wa kike.

Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi ametoa maagizo hayo wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni hayo, ambayo yamefikia zaidi ya asilimia 90 ya utekelezaji wake huku akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na matumizi sahihi ya fedha za umma katika miradi ya maendeleo.

“Serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni tano katika ujenzi wa bweni hili, hivyo ni wajibu wa mkandarasi, msimamizi wa mradi na uongozi wa Chuo kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana na mradi huu unakamilika kwa ubora na kwa wakati,” amesema Mhe. Mahundi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Mbeya Edina Mwaigomole amesema ujenzi wa bweni hilo ni hatua muhimu katika kumlinda na kumwezesha mtoto wa kike kielimu, hasa kwa wanafunzi wanaotoka maeneo ya mbali.

“Bweni hili ni suluhisho la changamoto nyingi zilizokuwa zinawakabili wasichana, ikiwemo ukosefu wa makazi salama. UWT tunaipongeza Serikali kwa kuendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowasaidia wasichana kusoma kwa utulivu na kujiendeleza,” amesema Mwenyekiti Edina.

Naye Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole, Silvester Mwambene, amesema kukamilika kwa mabweni hayo kutakuwa na mchango mkubwa katika kuongeza udahili wa wanafunzi wa kike pamoja na kupunguza changamoto za kijamii zilizokuwa zikijitokeza awali.

“Mabweni haya yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 600 na yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa changamoto ya mimba zisizotarajiwa kwa wanafunzi wa kike, kwani yatatoa mazingira salama na rafiki kwa masomo,” amesema Mwambene.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa mabweni hayo, Latoi Mollel, amesema maandalizi ya mwisho yanaendelea na mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba mwaka huu kama ilivyopangwa.








Kwa muda mrefu nilijihisi kuwa kila juhudi niliyoweka ili kupata utajiri ilishindikana. Biashara zangu ziligonga mwamba, akaunti yangu ya benki ilionekana kuwa na nambari ndogo kila siku, na marafiki waliokuwa na mafanikio yalionekana kuwa mbali sana.

Nilijaribu kila njia, kutoka kwa mikopo, ushauri wa biashara, hadi kufanya kazi nyingi, lakini kila mara niliishia na hasara na kuchoka. Hali hii ilinifanya niwe na huzuni na wasiwasi mkubwa.

Nilijisikia ningeendelea kuwa maskini bila mwisho. Kila mtu aliniuliza ni nini kilikuwa chanzo cha matatizo yangu, lakini sijui ni kitu gani kilinizuia kufanikisha malengo yangu.

Nilijaribu njia nyingi za kawaida za kuongeza kipato, lakini hakuna kilichobadilika kwa muda mrefu. Soma Zaidi..........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/pete-ya-ajabu-iliyoniletea-utajiri-na-fursa/

Kila nilipojaribu kubashiri mechi za AFCON, matokeo yalikuwa dhahiri: hasara na kuchanganyikiwa. Nilijisikia kama kila mbinu ya kawaida niliyoitumia haikuwa na maana. Kila beti niliyoweka ilikuwa hatari, na pesa zangu zilikuwa zikipotea kila siku.

Marafiki walinipigia simu, wakiuliza ni mbinu gani ninatumia, lakini sikuweza kuelezea. Nilijihisi kama mtu aliyechoshwa na kuwa na bahati mbaya isiyoisha.

Nilijaribu mikakati mbalimbali: kuangalia takwimu, kujaribu kupata ushauri kutoka kwa marafiki wenye uzoefu, hata kutumia mbinu za kawaida mtandaoni. Lakini kila beti ilimalizika kwa hasara.

Nilihisi kuchoshwa, kushindwa, na kuanza kujiuliza kama ninafaa tena kubashiri au hata kuendelea na ndoto yangu ya kupata kipato kwa njia hii.Soma Zaidi.............
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-nilivyoshinda-beti-ya-afcon-baada-ya-kupata-usaidizi-wa-kimaajabu/
Msiba wa mzazi wangu ulikuwa kama kimbunga kilichinikumba ghafla. Nilihisi maisha yameniacha, kila siku ilikuwa ya huzuni na upweke. Nilijaribu kuendelea na kazi na shughuli za kila siku, lakini kila hatua ilionekana bure.

Nguvu za mwili na akili zilibaki chini, na mara nyingi nilijikuta nikilala masaa mrefu bila kufanya lolote. Hali hii ilinifanya niwe na wasiwasi na huzuni isiyoisha. Nilijaribu kuzungumza na marafiki na familia, lakini walishindwa kuelewa uzito wa maumivu yangu.

Mara nyingine nilijihisi nitaanguka ndani ya giza la mawazo hasi, nikidhani maisha hayatabadilika kamwe. Nilijaribu mbinu za kawaida za kujiponya, kama kufanya mazoezi, kula vizuri, na kujitenga na mawazo hasi, lakini matokeo yalibaki hafifu.

Baada ya muda, nilijua kuwa lazima nipate msaada wa kina. Soma Zaidi...
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-mwelekeo-baada-ya-msiba-safari-ya-kujiponya-ilianza-polepole/
Kwa muda mrefu nilijihisi kuwa na tatizo lisilo la kawaida. Kila nikikutana na mume wangu au fikiria tendo la ndoa, hamu yangu ilikuwa chini sana. Nilijaribu kuzungumza naye, lakini mara nyingi nilihisi aibu au hasira kwa sababu sijui tatizo lilitoka wapi.

Nilijaribu kubadilisha mtindo wa maisha, kula vizuri, hata kupumzika zaidi, lakini hakuna kilichobadilika. Hali hii ilinifanya nijihisi kuchoshwa na kuanza kujilaumu. Nilijisikia kuwa si mzuri tena, na kuishi kwa hofu ya kuvunja uhusiano wangu kulikuwa kawaida.

Nilijaribu kupata ushauri kutoka kwa madaktari wa kawaida, lakini walieleza tu kuwa ni jambo la kawaida la kiakili au la kihembe. Nilihisi kama ningeendelea hivi, ndoa yangu ingepoteza maisha yake ya furaha na unyenyekevu.

Hatua ya mabadiliko ilikuja nilipokuwa nikiwa tayari kutafuta suluhisho la kina. Soma Zaidi.......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nikikosa-hamu-ya-ndoa-bila-kuelewa-kwa-nini-nilipoangalia-afya-yangu-majibu-yakapatikana/
Kwa muda mrefu, nilijaribu kufanikisha maisha yangu kila jambo lilionekana kunizidi. Biashara zangu hazikua, kazi zangu hazikuleta matokeo, na kila mara nilihisi nimekumbwa na vizuizi visivyoonekana.

Nilianza kujiuliza kama kuna nguvu fulani inanikwamisha, nikishindwa kuelewa ni kwa nini jitihada zangu hazina matokeo. Hali hii ilinifanya niwe na hofu na wasiwasi kila siku.

Nilijikuta nikiishi kwa kujihisi chini, nikiwa na mashaka yasiyoisha kuhusu kila hatua ninayochukua. Kila napata fursa, huwa nahisi kama inakwamishwa kwa njia fulani. Nilijaribu mbinu za kawaida kusoma, kufanya kazi kwa bidii, na kuuliza ushauri lakini mafanikio yalionekana mbali.

Hatua ya mabadiliko ilikuja nilipokuwa nikiwa tayari kutafuta suluhisho la kina. Soma Zaidi...........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilihisi-kuna-kitu-kinazuia-maendeleo-yangu-baada-ya-kufunguliwa-mambo-yalisonga-2/