Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Benezeth Lutege, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness K. Meena. Warsha hiyo imefanyika leo Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha.

Mkurugenzi Msaidizi wa Epidemiolojia na Magonjwa ya Mifugo Yanayovuka Mipaka (TADs) akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Habari II wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Chiku Makwai, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Sheria I wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Denis Ukaka, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Na Chiku Makwai – ARUSHA

Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo.

Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika.

Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapema kabla hayajasababisha athari kubwa kwa uzalishaji, biashara ya mifugo na afya ya jamii.

“Mkakati huu utaweka msingi wa kuwa na mfumo mmoja wa kitaifa wa mawasiliano ya dharura utakaoongoza utoaji wa taarifa, ushirikishwaji wa wadau na usimamizi wa mawasiliano wakati wa matukio ya milipuko ya magonjwa ya mifugo,” amesema Dkt. Lutege.

Aidha, amebainisha kuwa magonjwa mbalimbali ya mifugo, ikiwemo Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever), yanahitaji uratibu madhubuti wa mawasiliano ili kuhakikisha wananchi na wadau wanapata taarifa sahihi zitakazowawezesha kuchukua hatua stahiki kwa wakati.

Warsha hiyo imewakutanisha wataalamu wa mifugo, afya ya wanyama, mawasiliano na wadau wengine kutoka taasisi za Serikali pamoja na mashirika ya kimataifa kwa lengo la kujadili mbinu bora za mawasiliano ya hatari, usimamizi wa taarifa za dharura na mikakati ya kuimarisha mwitikio wakati wa milipuko ya magonjwa.

Washiriki pia wanatarajiwa kujadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa taarifa pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya afya ya wanyama na afya ya binadamu kwa kuzingatia dhana ya Afya Moja (One Health).

Kupitia warsha hiyo, Tanzania inatarajia kuwa na mkakati madhubuti wa mawasiliano ya dharura utakaosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema, kuongeza mwitikio wa haraka wakati wa matukio ya dharura na kulinda ustawi wa mifugo sambamba na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Dunia la Haki Miliki (WIPO) kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, wamezindua mradi wa miezi 12 utakaotumia teknolojia zilizopo kwenye kanzidata za kimataifa za hakimiliki kuongeza thamani ya mazao, kupunguza gharama za uzalishaji na kuimarisha sekta za kilimo na ufugaji nchini.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa sijitambui tena. Mwanzoni nilikuwa mtu mwenye furaha, confidence, na aliyependa kujitokeza mbele za watu. 

Nilipenda kuvaa vizuri, kuzungumza kwa uhuru, na kujiamini kwenye kila sehemu niliyokuwa.

Lakini kadri muda ulivyopita, mambo yalianza kubadilika. Nilipitia maumivu mengi ya mahusiano. Nilivunjwa moyo mara kadhaa na watu niliowaamini sana. 

Kila relationship ilipoisha vibaya, nilianza kupoteza sehemu ya confidence yangu. Polepole nilianza kuamini labda mimi ndiye nilikuwa tatizo.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wengine wakionekana wenye furaha kwenye mahusiano huku mimi nikijihisi kama sipendwi au sioni bahati kabisa. Wakati mwingine hata nikitaka kuzungumza na mtu mpya, nilikuwa najihisi sina mvuto wa kutosha.

Kulikuwa na siku nilijifungia ndani. SOMA ZAIDI.
Kwa miezi 18 maisha yangu yalizunguka jambo moja tu kutafuta kazi. Kila asubuhi nilikuwa naamka mapema, kufungua simu au laptop yangu, na kutafuta matangazo mapya ya ajira.

Nilikuwa na ndoto ya kupata kazi nje ya nchi ili niweze kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Niliamini elimu na uzoefu wangu vingefungua milango mingi. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Nilituma CV kwa kampuni nyingi sana. Kila nilipoona tangazo jipya, nilihakikisha nimetuma maombi yangu kwa wakati. Wakati mwingine nilikuwa natumia saa nyingi kurekebisha CV na cover letter ili ziendane na nafasi husika.

Kilichoniumiza zaidi ni kutopata majibu. Wiki zikageuka miezi. Nilikuwa naangalia email kila siku nikitarajia mwaliko wa interview, lakini hakuna kilichokuwa kinatokea. Wakati mwingine nilipokea ujumbe wa kukataliwa, na mara nyingi sikupata jibu lolote.

Kwa kweli nilianza kukata tamaa. Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na tatizo kwenye qualifications zangu au kama ndoto yangu ilikuwa kubwa sana. Watu wengine walinishauri niache kufikiria kazi za nje na nijikite kwenye nafasi za karibu. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilifikiri nimepoteza pesa zangu milele. Nilikuwa nimeweka akiba kwa muda mrefu nikitarajia kuanzisha biashara ambayo ingebadilisha maisha yangu. Nilitumia miezi mingi kujinyima mambo mengi ili kukusanya mtaji huo.

Ndiyo maana siku nilipopata nafasi iliyoonekana kuwa nzuri mtandaoni, niliona kama ndoto yangu ilikuwa karibu kutimia. Mwanzoni kila kitu kilionekana cha kawaida.

Mtu niliyekuwa nikizungumza naye alionekana mtaalamu na mwenye kuelewa biashara. Alikuwa na maelezo mazuri, ahadi za faida, na alijibu maswali yangu kwa kujiamini. Kadri mazungumzo yalivyoendelea, nilianza kumuamini.

Hatimaye nilituma pesa. Baada ya kufanya malipo, mambo yakaanza kubadilika. Simu zilianza kutopokelewa, ujumbe haukujibiwa kwa wakati, na maelezo yalikuwa yanabadilika kila siku. Hapo ndipo nilianza kutambua kuwa huenda nilikuwa nimetapeliwa.

Kwa kweli niliumia sana. Kilichoniumiza zaidi ni kujua kuwa sehemu kubwa ya akiba yangu ilikuwa imeenda kwa muda mfupi sana. 

Nilihisi hasira, huzuni, na aibu kwa wakati mmoja. Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi nikifikiria jinsi ningeeleza familia yangu kilichotokea. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa sana. Nilikuwa naamini kwamba bidhaa zangu zingepata soko haraka na maisha yangu yangeanza kubadilika. 

Nilitumia akiba yangu kununua bidhaa, nikafungua ukurasa wa Facebook, na kuanza kutangaza kila siku.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Kila nilipopost bidhaa zangu, watu walikuwa wanapenda picha na wakati mwingine kuacha comments, lakini hakuna aliyekuwa akinunua. Siku zikageuka wiki, wiki zikageuka miezi, na bado mauzo yalikuwa karibu sifuri.

Kwa kweli nilivunjika moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara nyingine zikikua kupitia Facebook huku mimi nikihangaika kupata hata mteja mmoja wa kweli. Wakati mwingine nilikuwa natumia pesa kutangaza posts lakini matokeo yalikuwa madogo sana.

Nilianza kujiuliza kama nilifanya makosa kuanzisha bibiashara. Kulikuwa na siku nilifikiria kuacha kabisa na kuuza bidhaa nilizokuwa nimebaki nazo. SOMA ZAIDI.
Siku ambayo nilipokea taarifa kwamba harusi yetu haitafanyika ndiyo siku niliyohisi moyo wangu ukivunjika zaidi kuliko wakati mwingine wowote maishani mwangu.

Mimi na mpenzi wangu tulikuwa tumepanga harusi kwa miezi mingi. Familia zote mbili zilikuwa zimejiandaa, wageni walikuwa wamealikwa, na mipango mingi ilikuwa imekamilika. Nilikuwa nikihesabu siku zilizobaki kabla ya kuanza maisha mapya ya ndoa.

Lakini wiki mbili kabla ya harusi, kila kitu kilibadilika. Mpenzi wangu aliniambia kuwa alihitaji kusitisha harusi. Nilihisi kama dunia ilisimama kwa sekunde chache. 

Sikuelewa kilichokuwa kinaendelea. Nilijaribu kuuliza maswali mengi, lakini majibu hayakuwa wazi vya kutosha kunipa amani.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuwaeleza ndugu, marafiki, na watu waliokuwa tayari wamepanga kuhudhuria harusi. Nilihisi aibu, huzuni, na kuchanganyikiwa kwa wakati mmoja. SOMA ZAIDI.



Na Mwandishi wetu, Iringa.

Wapiga Kura 222,218 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani lililopo Halamashauri ya Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.
 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Mei 31, 2026 Mkoani Iringa wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Juni 01, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 628 vya Kupigia Kura vitatumika.
 
“wapiga kura 89,753 wapo kwenye Jimbo la Ismani na wapiga kura 132,465 wapo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo na vituo 277 vipo kwenye Jimbo la Ismani na vituo 351 vipo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo.,”amesema Jaji Mwambegele.
 
Aidha, amesema Katika Uchaguzi huu, jumla ya wagombea 108 kutoka katika vyama vya siasa 17 wanawania nafasi wazi ya ubunge na udiwani katika maeneo niliyoyataja.

“Jimbo la Ismani lina wagombea 17 wa nafasi ya Ubunge ambapo kati ya wagombea hao wagombea nane (08) sawa na asilimia 47.06 ni wanaume na wagombea tisa (09) sawa na asilimia 52.94 ni wanawake. Kata 12 zinazofanya uchaguzi mdogo wa udiwani zina jumla ya wagombea 91 ambapo kati ya hao wagombea 61 sawa na asilimia 67.03 ni wanaume na wagombea 30 sawa na asilimia 32.97 ni wanawake.” alisema Jaji Mwambegele.

“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Juni 01, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
 
Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.
 
“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.
 
Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).

Kata 12 zitakazo fanya uchaguzi ni Mzimuni iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji Kasulu. 

Nyingine ni Kata ya Kala iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.

 

Na Mwandishi Wetu

Waandishi wa Habari watakaoshiriki Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo (Samia Kalamu Awards - SKA) 2026 wamelazimika kukidhi sharti la kuwa na ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), hatua inayolenga kuimarisha weledi, uwajibikaji na ushindani wa haki katika taaluma hiyo.

Akizindua rasmi mchakato wa kupokea kazi za kushindanishwa, Jumapili Tarehe 31 Mei, 2026, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa SKA, Mha. Peter Mwasalyanda, amesema maandalizi ya mwaka huu yanazingatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kutambua mchango wa Waandishi wa Habari za maendeleo nchini.
Mwasalyanda amesema ili kuhakikisha uadilifu, uwazi na ushindani wa haki, maandalizi ya tuzo hizo yanahusisha pia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kama mdau muhimu katika kusimamia weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

“Tuzo hizi zinalenga kutambua, kuthamini na kuhamasisha uzalishaji wa maudhui ya ndani yenye ubora, yanayochangia kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha, na kuimarisha taswira chanya ya Taifa kupitia habari za maendeleo,” amesema.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema tofauti na msimu wa kwanza wa tuzo hizo, mwaka huu washiriki wanapaswa kuhakikisha wamekidhi sharti la ithibati.

“Mtakumbuka Msimu wa kwanza wa Samia Kalamu mambo ya JAB hayakuwepo, kwa hiyo waandishi walishiriki wote bila kujali vigezo vya Ithibati lakini mwaka huu kuna hiki kigezo cha kuwa na ithibati kwa hiyo niwashauri basi wote wanaoshiriki kwenye hizi tuzo wahakikishe wanakuwa na ithibati, wamethibitishwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.” Amesema Wakili Kipangula na kuongeza;
“Ni muhimu sana kwa sababu ni takwa la kisheria na kitu ambacho hatuwezi kukikwepa. Nawahamasisha tushiriki wote kwa sababu isionekane ni tuzo za watu fulani tu, kila mmoja awasilishe kazi zake,” amesema Kipangula.

Kwa mujibu wa vigezo vya ushiriki vilivyotangazwa, Waandishi wa Habari wa Tanzania Bara wanatakiwa kuwa wamethibitishwa na JAB, huku kwa Zanzibar washiriki wakitakiwa kuwa na kitambulisho cha Mwandishi wa Habari (Press Card).

Tuzo hizo zimeanza kupokea kazi kuanzia Mei 31 hadi Juni 30, 2026 na zinatarajiwa kutolewa kati ya Oktoba na Desemba mwaka huu.

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limesema linaendelea kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa yanayofanyika mkoani Iringa kwa lengo la kutoa elimu kwa wadau wa sekta ya maziwa na wananchi kuhusu umuhimu wa kuzingatia viwango na ubora wa bidhaa za maziwa.
Na Mwandishi Wetu, Iringa

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Kakurwa, ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa utekelezaji wa Mradi Shirikishi wa Wasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P), akisema umekuwa chachu ya mageuzi katika sekta ndogo ya maziwa kwa kuongeza uzalishaji, kuimarisha mnyororo wa thamani na kuboresha maisha yawafugaji nchini.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa nimekata tamaa kabisa kuhusu mapenzi. Nilikuwa nimepitia mahusiano mengi yaliyoniacha nikiwa na maumivu makubwa.

Kila mara nilipoanza kumpenda mtu, mwishowe mambo yalikuwa yanaishia kuvunjika moyo. Nilianza kuamini labda mapenzi ya kweli hayakunihusu tena. Kwa kweli iliniumiza sana.

Nilikuwa nimejenga ukuta wa kujilinda. Sikutaka tena kuumizwa, na nilianza kuwa na hofu ya kuingia kwenye uhusiano mpya. Wakati mwingine hata nilipoona watu wakiwa na furaha kwenye mahusiano yao, nilihisi kama mimi niko tofauti.

Kulikuwa na siku nilijihisi mpweke sana. Nilianza kujitenga, nikapunguza kutoka, na hata kuacha kuamini kwamba ningepata mtu ambaye angenipenda kweli. Nilianza kufikiria labda niishie peke yangu tu.SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi biashara yangu ilikuwa karibu kuanguka kabisa. 

Nilikuwa nimeanzisha duka langu kwa juhudi nyingi sana. Nilijinyima mambo mengi ili nipate mtaji, nikajituma kuhakikisha biashara inakua.

Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri wateja walikuwa wanakuja, mauzo yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Nilianza kugundua pesa hazilingani. Kila nilipofanya hesabu za mwisho wa siku, kulikuwa na upungufu ambao sikuuelewa.

Mwanzoni nilidhani labda ni makosa ya kawaida ya biashara. Lakini kadri wiki zilivyopita, hasara ilianza kuongezeka kwa namna iliyonipa hofu kubwa. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa naishi na maumivu ambayo ni vigumu kuelezea. Baada ya kuolewa, mimi na mume wangu tulikuwa na ndoto ya kuwa wazazi. Kila mwaka ulivyopita bila kupata mtoto, pressure ilianza kuongezeka.

Mwanzoni tuliamini muda wetu ungefika, lakini kadri miaka ilivyosonga mbele, matumaini yangu yalianza kupungua. Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni maneno ya watu.

Kila harusi, family gathering, au sherehe ilikuja na maswali yale yale “Mtoto lini?” Wakati mwingine nilitabasamu mbele za watu lakini nikilia peke yangu usiku. Nilijaribu kutafuta msaada wa kitabibu.

Nilifanya checkups na kupata ushauri wa hospitali ili kuelewa hali yangu vizuri. Kulikuwa na wakati niliambiwa safari ya kupata mimba ingeweza kuwa ngumu na ningehitaji uvumilivu pamoja na matibabu sahihi. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi ndoa yangu ilikuwa karibu kuvunjika kabisa. Mwanzoni mume wangu alikuwa mtu wa furaha, mwenye kujali familia, na aliyekuwa karibu sana nasi. Lakini polepole mambo yakaanza kubadilika.

Kile kilichoanza kama kunywa mara moja moja kiligeuka tabia ya kila siku. Kwa kweli hali iliniumiza sana. 

Alianza kurudi nyumbani usiku sana, wakati mwingine akiwa amelewa kiasi cha kutoweza hata kuzungumza vizuri. Migogoro nyumbani ikaongezeka.

Watoto walikuwa wanaanza kumuogopa, na amani ya familia yetu ikaanza kupotea. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtu niliyemjua akibadilika mbele ya macho yangu.

Kulikuwa na siku hakutokea nyumbani kabisa, na nilikesha nikijiuliza maisha yetu yalikuwa yanaelekea wapi. Wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa nimebaki peke yangu kubeba kila jukumu la familia.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi nilikuwa naishi maisha ya kutafuta kazi kila siku bila mafanikio ya maana. Baada ya kumaliza masomo, nilikuwa na matumaini makubwa kwamba ningepata kazi nzuri haraka.

Nilikuwa na ndoto ya kusaidia familia yangu, kujitegemea, na kuishi maisha bora. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Nilianza kutuma applications kila mahali.

Mara nyingine nilikuwa nikiitwa interviews, lakini mwisho wa siku sikupata nafasi. Wakati mwingine hata sikupigiwa simu kabisa. Miezi iligeuka miaka, na nilijikuta nikifanya vibarua vya hapa na pale ili kujisitiri.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu niliomaliza nao shule wakisonga mbele huku mimi nikihangaika. Wakati mwingine nilianza kujiuliza kama nilikuwa nimekosea njia maishani. SOMA ZAIDI.


Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM- TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi mbalimbali chini ya Mradi wa TACTIC kuzingatia viwango vya ubora vilivyoainishwa katika mikataba yao.

Mhandisi Mativila ametoa agizo hilo Mei 29,2026 wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya miundombinu inayotekelezwa na TACTIC katika mkoa wa Mara, ambapo amesisitiza kuwa ubora wa kazi ni jambo lisilopaswa kufanyiwa mzaha.

“Katika ziara hii, moja ya mambo muhimu tunayoyaangalia ni ubora wa miradi kwa kuzingatia maelezo yaliyopo kwenye mikataba, hivyo wakandarasi wote mnapaswa kuhakikisha mnatekeleza kazi kwa viwango vilivyokubaliwa,” amesema Mhandisi Mativila.

Ameeleza kuwa wakandarasi wanaposaini mikataba ya utekelezaji wa miradi, wanakuwa wamekubali kutekeleza kazi kwa ubora unaotakiwa, hivyo ni wajibu wao kujisimamia na kuhakikisha wanazingatia masharti yote ya mikataba bila kushurutishwa.

Aidha, Mhandisi Mativila amesema kuwa utekelezaji wa miradi kwa ubora ni sehemu ya kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa akisisitiza umuhimu wa kujenga miradi yenye viwango bora ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, Mhandisi Mativila amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa chini ya Mradi wa TACTIC, ikiwemo ujenzi wa soko, jengo la Ofisi ya TARURA pamoja na Stendi ya Bweli iliyopo mkoani humo.

Serikali imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ili kuipa nafasi pana sekta binafsi kushiriki katika ukuaji wa uchumi na uzalishaji wa ajira kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameagiza Menejimenti ya Kiwanda cha Kuzalisha Bidhaa za Kibaolojia Tanzania (TBPL) kinachomilikiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kuongeza uzalishaji na kuimarisha mikakati ya masoko ili kunufaika na mahitaji makubwa yaliyopo sokoni, kuhakikisha kiwanda kinaendelea kujiendesha kwa ufanisi wa kibiashara


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika ustawi wa wazee na uwezeshaji wa vijana kupitia utekelezaji wa programu mbalimbali zinazolenga kuboresha maisha yao na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo ya taifa.

Mhe. Mahundi ameyasema hayo tarehe 30 Mei, 2026 wakati akizungumza na wageni kutoka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Maryprisca Women Foundation wakiongozana na Machifu kutoka Mkoa wa Mbeya waliowasili mkoani Dodoma kwa ziara ya mafunzo na kujionea maendeleo yaliyofikiwa katika Mji wa Serikali Mtumba pamoja na shughuli zinazotekelezwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Amesema Serikali inaendelea kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki ikiwemo bima ya afya na kuishi katika mazingira salama na bora, huku ikiimarisha mikakati ya kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia fursa za mikopo, mafunzo ya ujasiriamali na programu mbalimbali za maendeleo.

Katika ziara hiyo, wageni hao walipata fursa ya kutembelea Mji wa Serikali Mtumba na kujionea majengo ya kisasa ya Wizara na Taasisi mbalimbali yaliyojengwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mMhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, hatua ambayo imeendelea kuifanya Dodoma kuwa kitovu cha shughuli za Serikali.

Aidha, walijifunza kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Wizara katika kuimarisha ustawi wa jamii, hususan kwa makundi maalum yakiwemo wazee, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Kwa upande wao, baadhi ya machifu walioshiriki ziara hiyo wameipongeza Serikali kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba na kwa kuendelea kutoa kipaumbele katika masuala ya maendeleo ya jamii. 


Pia wamempongeza Mhe. Mahundi kwa juhudi zake katika kusimamia utekelezaji wa mipango inayolenga kuboresha maisha ya wananchi, hususan makundi maalum.


MWISHO