Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) limetangaza kuwa Maonesho yake ya Tano ya Kitaifa yanatarajiwa kufanyika Oktoba 21 hadi 30, 2026 katika Uwanja wa Magufuli uliopo Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga, yakilenga kuinua uchumi wa wajasiriamali wadogo nchini.
📌Bilioni 12.1 yatumika kusambaza umeme vitongojini
📌Dkt. Homera awasha Umeme kwenye vitongoji
📌Aipongeza REA kwa utekelezaji miradi ya nishati vitongojini
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.
Hayo yamezungumzwa na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Juma Homera mara baada ya kuwasha umeme rasmi katika kitongoji cha Ujamaa na Kisutu vilivyopo wilaya ya Namtumbo mkoani humo.
Dkt. Homera amesema, uwashaji wa umeme katika vitongoji hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha upatikanaji wa umeme vijijini unawafikia wananchi wote ifikapo mwaka 2030
"Nampongeza sana Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy na timu yake kwa kuwezesha vijiji vyote 66 vya jimbo langu kupata huduma ya umeme na kama mnavyoona kasi bado inaendelea ya kupeleka umeme katika vitongoji 79 vilivyobakia vya jimbo hili," Amesema Dkt. Homera.
Halikadhalika Dkt. Homera ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi wa vitongoji hivyo kuchangamkia fursa kwa kufanya wiring ya umeme katika nyumba zao ili waweze kunufaika na huduma ya umeme ambayo imeletwa kwao kwa bei ya ruzuku ya shilingi 27,000 tu.
Kwa upande wake, Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme kutoka REA, Mha. Deogratius Nagu amesema kuwa Serikali imeweka jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya umeme wilayani Namtumbo kupitia miradi ya Ujazilizi na upanuzi wa miundombinu ya umeme ikiwemo miradi ya Densificationi 2C, HEP 2A na HEP 2B.
Ameongeza kuwa, Serikali kupitia REA imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya umeme kwa mafanikio makubwa ambapo vijiji vyote 66 vimefikiwa na huduma ya umeme wilayani Namtumbo.
"Kati ya vitongoji 424 vilivyopo, vitongoji 307 tayari vina umeme, na vitongoji 79 vipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na vinapatiwa umeme pindi miradi hii itakapokamilika, hali itakayofikisha upatikanaji wa umeme hadi takribani asilimia 91 ya vitongoji vyote, " Amesema Mha. Nagu.
Naye, Msimamizi wa Miradi Mkoa wa Ruvuma Mha. Hamis Mrope amesema kuwa umeme huo utachochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa kuongeza fursa za biashara, kuimarisha huduma za afya na elimu pamoja na kuboresha maisha ya wananchi.
Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameelekeza hatua za haraka zichukuliwe kuwarejesha wafanyabiashara wa Soko la Mawasiliano (Simu 2000) ili kuendelea na shughuli za biashara katika soko hilo ambalo lilipata ajali ya moto iliyoteketeza soko hilo Aprili 04, 2026.
Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Aprili 10, 2026 alipolitembelea soko hilo na kuridhishwa na utekelezaji wa Maelekezo ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba aliyoyatoa Aprili 6, 2026, alipofika kukagua madhara ya tukio hilo la moto na kuelekeza soko hilo kusafishwa mara moja ili kuruhusu wafanyabiashara kuanza taratibu za kurejesha shughuli zao.
“Nimeridhishwa na utekelezaji wa maelekezo aliyotupatia Mhe. Rais na Mhe. Waziri Mkuu, hivyo naelekeza haraka iwezekanavyo wafanyabiashara warejeshwe kuendelea na shughuli zao lakini wasijenge vibanda na badala yake waweke meza pamoja na miamvuli ili kujikinga dhidi ya jua na mvua,” amesisitiza Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila kusimamia kikamilifu maelekezo aliyoyatoa, huku akimtaka Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando kufanya ufuatiliaji wa kila siku ili wafanyabiashara wa soko hilo warejee haraka kuendelea na shughuli zao.
Aidha, katika hatua nyingine Prof. Shemdoe ameilekeza DART na Mkandarasi anayejenga soko jipya la Mawasiliano kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango ndani ya miezi minne badala ya sita ili wafanyabiashara hao wanaorejeshwa kwa kutumia meza wapate vibanda vya kufanyia biashara.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando kwa usimamizi mzuri wa utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu ambayo yanayowezesha urejeshwaji wa haraka wa wafanyabiashara hao walioathirika na ajali ya moto katika soko hilo la mawasiliano (simu 2000).
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando amesema, ameelekeza ndani ya siku tatu kuanzia leo kufanyike zoezi la utambuzi wa wafanyabishara wote kwa majina matatu na vitambulisho ili kuepuka changamoto ya watu kuchukua vibanda na kuwapangisha wafanyabiasharana kuongeza kuwa atahakikisha wafanyabiashara watakaopata mikopo ni wale waliothirika na janga la moto na wenye sifa na stahiri ya kupata mikopo.
Na Mwandishi wetu ..Arusha
Baada ya kupita miaka 42 tangu kufariki kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Hayati Edward Moringe Sokoine, wananchi mkoani Arusha wameendelea kukumbuka na kuthamini mchango wake, wakisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, mapambano dhidi ya rushwa na kilimo cha kufa na kupona.
Wakizungumza wakati wa maandalizi ya misa ya kumbukizi itakayofanyika Aprili 12 katika eneo la Monduli Juu, wananchi hao walisema Sokoine alijitofautisha kwa uongozi wa vitendo ulioweka mbele maslahi ya taifa.
Baadhi ya viongozi wa chama cha wazee wanaume Tanzania Joseph Laitatei makamu wa Rais wa chama hicho alisema Sokoine alikuwa kiongozi aliyesimamia haki bila kuyumba na hakuvumilia vitendo vya rushwa. Kwa upande wake, Cloud Gwangu alieleza kuwa kiongozi huyo alihamasisha kwa nguvu sera ya kilimo cha kufa na kupona, akilenga kujenga taifa linalojitegemea kwa uzalishaji.
Naye Abel Mollel Mwenyekiti wa wilaya wa chama hicho alisisitiza kuwa uwajibikaji wa Sokoine unapaswa kuwa somo kwa viongozi wa sasa, huku Geoge Mwakalukwa akimtaja kama mfano wa uongozi wa uadilifu usio na hofu.
Aidha viongozi wa Chama cha Wazee Wanaume Tanzania wameipongeza familia ya Sokoine kwa kuendelea kuuenzi na kuudumisha kumbukumbu ya kiongozi huyo kila mwaka, wakieleza kuwa hatua hiyo inasaidia kizazi cha sasa na kijacho kujifunza misingi ya uongozi bora.
Katika kuenzi uzalendo wa Hayati Edward Moringe Sokoine, baadhi ya wananchi wameeleza namna walivyoguswa na uongozi wake wa kujitolea kwa taifa.
Akizungumza, Cloud Gwandu, mkazi wa Arusha, amesema Sokoine alikuwa kiongozi wa vitendo aliyethamini maslahi ya wananchi kuliko yake binafsi.
“Uzalendo wake ulikuwa wa kweli, alipambana na rushwa bila kuogopa na alihakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha wananchi wote. Viongozi wa sasa wanapaswa kujifunza kutoka kwake,” amesema Gwandu.
Ameongeza kuwa msisitizo wa Sokoine kwenye kilimo cha kufa na kupona ulikuwa sehemu ya uzalendo wake, kwani aliamini taifa lenye chakula cha kutosha lina uhuru wa kweli.
Kwa mujibu wa Gwandu, mfano wa Sokoine unaendelea kuwa somo muhimu kwa kizazi cha sasa katika kujenga uongozi wenye uwajibikaji na uadilifu.
Hayati Sokoine alifariki dunia Aprili 12 mwaka 1984 kufuatia ajali ya gari iliyotokea Dumila mkoani Morogoro.
Wananchi hao wameeleza kuwa licha ya kupita kwa muda mrefu, bado taifa lina kila sababu ya kuuenzi na kuutumia urithi wa Sokoine kama mwongozo wa kujenga uongozi bora, unaozingatia uwajibikaji, kupinga rushwa na kukuza kilimo kwa maendeleo endelevu.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele, akihutubia wadau mbalimbali wa Sekta ya Mifugo, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma.

Mtaalam wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, ambaye ni Mchumi Mwandamizi Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Bw. Tumsime Mutta (aliyesimama), akielezea Mpango Mkakati wa Mradi, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi huo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma.

Mtaalam wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, ambaye ni Mchumi Mwandamizi Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Bw. Tumsime Mutta (aliyesimama), akielezea Mpango Mkakati wa Mradi, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi huo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma.

Mchungaji wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ndg. Jeremia Nyato (aliyesimama), akitoa Ushauri wa namna ya kuwashawishi vijana kukimbilia fursa za unenepeshaji Mifugo, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele (katikati), akijibu hoja mbalimbali za wadau wa Sekta ya Mifugo, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma, kulia ni Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa ambaye ni Afisa Tarafa ya Kongwa, Bw. Jerimia.

Picha ni baadhi ya wadau wa Sekta ya Mifugo wakimsikiliza Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele (hayupo pichani), wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele (aliyekaa katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa Sekta ya Mifugo, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo, uliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) - Kongwa, Aprili 9, 2026 Dodoma.
....
Wizara ya Mifugo na Uvuvi inayotekeleza Mradi wa miaka mitano wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo katika eneo la Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyopo Wilayani Kongwa, imepanga kuwawezesha vijana 200 wa Kitanzania kupata Mafunzo hayo ikiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa vijana na wanawake katika ujasiliamali wa Biashara ya Mifugo.
Akizungumza leo Aprili 9, 2026 Wilayani Kongwa Jijini Dodoma kwa Niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa warsha ya utambulisho wa Mradi huo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele, amesema mradi huo wenye thamani ya takribani shilingi Billioni 81, unalenga kuwawezesha vijana kupitia shughuli za unenepeshaji wa mbuzi na kondoo kibiashara, uzalishaji wa malisho na mbegu za malisho, uchakataji wa vyakula vya mifugo, pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa.
"Walengwa wakuu wa mradi huu ni vijana, ambao kupitia utekelezaji wake watapata ujuzi na uzoefu wa vitendo katika mnyororo mzima wa thamani wa mazao ya mifugo, hususan mbuzi, na kupitia mafunzo haya, vijana wetu watajengewa uwezo wa kuingia kwenye biashara za kisasa za mifugo na hivyo kujiongezea kipato pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa." Amesema Dkt. Madele
Aidha, Dkt. Madele amesema baada ya vijana kupata ujuzi huo, matarajio ya Serikali ni kuwa vijana wataweza kujiajiri wenyewe, kuanzisha biashara zao, na kuwa sehemu ya suluhisho la changamoto ya ajira nchini, ambapo vijana watakaonufaika watakuwa na fursa ya kupatiwa mikopo isiyo na dhamana kwa ajili ya kuendeleza biashara zao baada ya mafunzo.
Vilevile, Dkt. Madele amebainisha kuwa matokeo ya kuwepo kwa Mradi huo ni kutokana na uongozi madhubuti wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi mahiri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutambua kwa kina changamoto ya ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana, ndiyo maana Mheshimiwa Rais amechukua juhudi za makusudi kuhakikisha fedha hizo zinapatikana kwa ajili ya kuboresha maisha ya vijana kupitia miradi yenye tija kama huo wa BBT.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Daudi Mayeji, amesema Mradi huo hautaishia kwa vijana waliopo Dodoma tu bali kwa vijana kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, ambapo Mpango huo utamuwezesha kijana kuhudumia Mbuzi 100 kwa pamoja.
Pia, Ndg. Mayeji amesema Mradi huo unategemea ndani ya miaka mitano kutoa Mafunzo kwa vijana takriban 1750 na Serikali tayari imeshatenga eneo la hekta 2000 kwa ajili ya kupanda Malisho ya Mifugo.
Naye, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, ambaye ni Afisa Tarafa ya Kongwa, Ndg. Jeremiah Kabebwa ameishukuru Wizara kwa kuwaletea Mradi wenye fursa kwa vijana ambapo ameihakikishia Wizara kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itahakikisha vijana wote wanaichangamkia fursa hiyo ili kuweza kujikwamua kiuchumi.
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya mazungumzo na Kampuni ya Equinor Tanzania AS pamoja na Shell Exploration and Production Tanzania Ltd kuhusu utekelezaji wa uchimbaji wa gesi ya LNG katika mikoa ya kusini, leo tarehe 10 Aprili 2026, jijini Dar es Salaam.
Katika kikao hicho, Waziri alikutana na viongozi wa makampuni hayo, akiwemo Menno Bax, Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa Shell Exploration and Production Tanzania Ltd, pamoja na Hilde Merete Nafstad, Makamu wa Rais na Meneja wa Nchi wa Utafutaji na Uzalishaji wa Kimataifa (EPI) wa Equinor Tanzania AS.
Mazungumzo hayo pia yaliwashirikisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, na Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka Wizara ya Nishati, Goodluck Shirima.
Makampuni haya yanajihusisha na utafiti, uchimbaji na uendelezaji wa gesi asilia baharini, pamoja na kushiriki katika maandalizi na utekelezaji wa mradi wa gesi iliyoyeyushwa (LNG) nchini Tanzania.
















































