
Na. Mwandishi Wetu
Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC), Dkt. Aggrey Mlimuka, ametembelea banda la FCC katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Maonesho hayo yamewakutanisha washiriki mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, wakiwemo kampuni binafsi, taasisi na mashirika ya Serikali, yakitoa fursa ya kutangaza bidhaa, huduma na uwekezaji.
Akiwa katika banda la FCC, Dkt. Mlimuka ameipongeza Tume hiyo kwa kazi kubwa inayofanya katika kulinda ushindani wa haki sokoni na kuimarisha mapambano dhidi ya bidhaa bandia, hatua inayochangia kulinda maslahi ya walaji na kukuza mazingira bora ya biashara nchini.
Pia amempongeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, Menejimenti pamoja na watumishi wote wa Tume hiyo kwa kujituma, weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao na kuhakikisha taasisi hiyo inatimiza malengo yake kwa mafanikio.
FCC ina jukumu la kulinda na kuhimiza ushindani wa haki katika biashara, kulinda maslahi ya walaji, kupokea na kushughulikia malalamiko yanayohusu ukiukwaji wa sheria za ushindani, pamoja na kudhibiti uingizaji, usambazaji na uuzaji wa bidhaa bandia nchini.
Mbali na kutembelea banda la FCC, Dkt. Mlimuka pia alitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara ili kujionea shughuli na huduma zinazotolewa kwa wananchi.
Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yenye kaulimbiu "Sabasaba Fahari ya Tanzania," yalianza rasmi Juni 28, 2026, na yanatarajiwa kuhitimishwa Julai 13, 2026 katika Viwanja vya Maonesho vya Julius Nyerere (Sabasaba Grounds), Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC) akipata maelezo kutoka kwa Bi. Roberta Feruzi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano - FCC wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa yanayoendelea viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa FCC wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa yanayoendelea viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar.
Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar ambapo wamejadili kuhusu ushirikiano katika maeneo ya uwekezaji, ajira na maendeleo ya ujuzi.
Aidha, katika mazungumzo yao Mhe. Sangu alitumia fursa hiyo kumueleza Mwenyekiti wa Al Mansour Holding dhamira ya Serikali ya Tanzania katika kuendelea kuweka mazingira bora na rafiki kwa wawekezaji pamoja na kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Qatar.
Vilevile, Waziri Sangu ameipongeza kampuni ya Al Mansour Holding kwa kuendelea kuongeza wigo wa uwekezaji katika Mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania Bara na Zanzibar. Pia, amehamasisha kampuni hiyo kutumia wataalamu na nguvu kazi ya Watanzania katika shughuli zake nchini Qatar na katika masoko mengine ya kimataifa.
Kadhalika, ameihakikishia kampuni hiyo ushirikiano katika kukuza maendeleo ya rasilimali watu kupitia mafunzo, uhamishaji wa teknolojia na ujuzi ili kuchochea ajira na ukuaji wa uchumi.
Katika ziara hiyo, Waziri Sangu ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na wataalamu wengine kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na Mwenyekiti wa Al Mansour Holding, Mhe. Sheikh Mansour, leo tarehe 10, 2026 jijini Doha, Qatar.

Hali hii ilinifanya nipungue nguvu na hata uzito wangu ukaanza kushuka.
Nilitembelea vituo vya afya mara kadhaa, nikapewa dawa tofauti, lakini nafuu ilikuwa ya muda mfupi tu. Baada ya muda maumivu yalirudi tena kama kawaida.
Hali hii ilinichosha sana. Nilianza kukata tamaa na kuona kama nitakuwa na tatizo hili maisha yangu yote. Siku moja nilimweleza rafiki yangu wa karibu hali yangu. SOMA ZAIDI.
Katika harakati za mwisho za kutafuta suluhisho, Neema alisikia kuhusu Kiwanga Doctors—wataalamu wa tiba za asili na jadi wanaosaidia watu kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiafya. Akiwa na matumaini kidogo yaliyosalia, aliamua kuwafikia na kupata ushauri wao.
Baada ya tathmini ya kina, Neema alipatiwa mwongozo na tiba za asili zilizolenga kuimarisha afya yake ya uzazi kwa ujumla. Kulingana na maelekezo aliyopatiwa, alianza kufuata matibabu hayo kwa nidhamu huku akizingatia pia ushauri wa mtindo bora wa maisha. SOMA ZAIDI.

