Na.Ashura Mohamed - Arusha.
Maonesho ya Karibu- KiliFair yamefunguliwa rasmi Jijini Arusha ambapo pamoja na kuchangia ukuaji wa pato la taifa Jukwaa hilo linatahwa kama kitovu cha kukutanisha wauzaji na waonenyeshaji kutoka mataifa mbali mbali barani Afrika
Maonesho hayo ambayo ambayo yanazidi kukua mwaka hadi mwaka yanawakutanisha wadau wa sekta ya utalii barani Afrika na Dunia kwa Ujumla kwa lengo la kutangeneza mnyororo wa Uchumi ndani ya sekta hiyo ili kuendelea kufanya vizuri zaidi,ambapo jukwaa hilo huwakutanisha wadau wa ndani na nje ya nchi ambao wameendelea kuwekeza na kuchagiza ongezeko la watalii katika Hifadhi za Taifa nchini.
Akifungua Maonesho hayo Juni 05, 2026 katika Viwanja vya Magereza jijini Arusha, Mkurugenzi wa Utalii Dkt. Thereza Mugobi kwa niaba ya Waziri waMaliasili na Utalii alisema kuwa Karibu-KiliFair ni zaidi ya maonesho,ambao ni uwekezaji wa kimkakati katika mustakabali wa utalii wa Tanzania.
Dkt.Mugobi amesema kuwa Uhusiano huo wa kibiashara ulioanzishwa katika jukwaa hilo la Karibu KiliFair umezalisha ushirikiano mpya, kuongeza idadi ya watalii wanaowasili nchini, kuvutia uwekezaji, kutengeneza ajira, na kuimarisha maisha ya jamii zinazotegemea utalii.
"Serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya utalii ikiwemo malazi, viwanja vya ndege, barabara ili kuboresha uzoefu wa watalii na kuwafikisha katika maeneo mbalimbali yenye vivutio kwa urahisi,pia Wizara itaendelea kutangaza vivutio vyake kupitia njia za kidijitali ili kuyafikia masoko mbalimbali duniani." Amesema Dkt. Mugobi.
Naye mwakilishi kutoka “TATO” Wilbard Chambulo, amesema kuwa maonesho haya ni daraja linalounganisha wadau wa ndani ambao ni mawakala wa utalii na waongoza watalii pamoja na mawakala wa kimataifa kutoka katika mabara yote duniani.
Mkurugenzi Mwenza wa Karibu-KiliFair, Dominic Shoo, amesema ongezeko la washiriki kutoka mataifa mbalimbali ni ishara kuwa Tanzania imeendelea kujijengea heshima kama kitovu muhimu cha biashara ya utalii katika ukanda wa Afrika Mashariki
Shoo ameongeza kuwa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi utaendelea kuwa nguzo muhimu katika juhudi za kuitangaza Tanzania na kuongeza mchango wa utalii katika uchumi wa taifa
Karibu-KiliFair imeendelea kuwa moja ya maonesho makubwa zaidi ya utalii katika Afrika Mashariki, yakitoa nafasi kwa wadau kutangaza vivutio vya utalii, kujenga mitandao ya biashara na kuibua fursa mpya za uwekezaji ndani ya sekta hiyo.
Maonesho haya yatamalizika kesho Jumapili June 07 ambapo mwaka huu yamekutanisha zaidi ya watu 1000 kutoka mataifa mbali mbali.
NA MWANDISHI WETU – SONGEA
Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki maghala ya kuifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hii kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.
Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,
Ambao umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga
Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.

Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.
‘Mkoa hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.
Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.
✅️ Sawa na Asilimia 105.8, Zikiwa Zimebaki siku 26 Kufunga Mwaka wa Fedha 2025/26
✅️ Watumishi Watakiwa Kuongeza Weledi Kufikia Sh Trilioni 1.4 Mwaka 2026/27
✅️ Watumishi Watakiwa kuhudumia wananchi bila ubaguzi
WIZARA ya Madini imevuka lengo la ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 baada ya kukusanya Sh trilioni 1.27 hadi Juni 5, 2026, dhidi ya lengo la Sh trilioni 1.2, huku ikitarajia kufikia Sh trilioni 1.3 ifikapo Juni 30, 2026.
Kutokana na mafanikio hayo, watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake wametakiwa kuondokana na uzembe, kuongeza bidii na kufanya kazi kwa weledi ili kufikia lengo jipya la ukusanyaji wa Sh trilioni 1.4 lililowekwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Akizungumza katika kikao cha watumishi wote wa Wizara ya Madini na taasisi zake ambazo ni GST, TEITI, Tume ya Madini, STAMICO na TGC, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, amesema mafanikio yaliyopatikana yanapaswa kuwa chachu ya kuongeza juhudi katika usimamizi wa Sekta ya Madini kwa kuzingatia Sera, miongozo, kanuni na Sheria zilizowekwa.
Amesema watumishi wanapaswa kutambua kuwa wanapowahudumia wananchi wanatekeleza wajibu wenye thamani kubwa kwa taifa, hivyo wanapaswa kuwahudumia watu wote kwa usawa bila kujali itikadi, dini wala uraia wao.
“Wachache tuliokabidhiwa jukumu la kuhudumia sekta ya madini tunapaswa kuhakikisha watu wote wanahudumiwa kwa haki na uzalendo mkubwa ili kuendelea kujenga taifa letu,” amesema.
Amesema watumishi ndiyo injini ya Serikali katika sekta ya madini na kwamba mchango wao una nafasi muhimu katika kukuza uchumi wa nchi kupitia usimamizi bora wa rasilimali madini.
“Wito wangu ni kufanya kazi kwa bidii, weledi na kusimamia sera, miongozo, kanuni na sheria zilizowekwa ili sekta hii iendelee kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa,” amesema.
Katibu Mkuu huyo amesema watumishi wanapaswa kujiepusha na vitendo vya rushwa, uvivu na uzembe ambavyo vinaweza kuharibu imani ya wananchi kwa wizara, taasisi zake na Serikali kwa ujumla.
“Tusiharibu imani ya wananchi kwa rushwa, uvivu na uzembe. Mtu mmoja anayepokea rushwa anaweza kuchafua kazi za watumishi wengi waadilifu. Tufanye kazi kwa uzalendo mkubwa ili kuhakikisha hakuna mtu au wachache miongoni mwetu wanaochafua taswira ya wizara, taasisi zetu na Serikali kwa ujumla,” amesema.
Amesema watumishi wanapaswa kuchagua kuwa mwangaza badala ya kuwa kivuli na kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya wizara na taasisi zake kwa kuwa wote ni timu moja yenye malengo yanayofanana.
“Kazi ya mwenzako ikichelewa, mafanikio yako pia yanachelewa. GST ikichelewa kutekeleza majukumu yake, Tume ya Madini nayo itaathirika. Tusaidiane kwa pamoja kufikia malengo yetu,” amesema.
Katika salamu za Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, watumishi wamepongezwa kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Aidha, imeelezwa kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini imepangiwa kukusanya Sh trilioni 1.4, lengo ambalo linahitaji watumishi kuongeza uwajibikaji, uadilifu na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Siku hiyo ilikuwa ya kawaida sana. Biashara haikuwa ikifanya vizuri kama nilivyotarajia. Wateja walikuwa wachache, na nilikuwa nikihangaika kutafuta njia za kuongeza mauzo. Katikati ya siku, mtu mmoja aliingia dukani kwangu.
Alinunua bidhaa chache na kuuliza maswali machache. Nilimhudumia kwa heshima kama nilivyowahudumia wateja wengine wote. Baada ya hapo aliondoka, na sikuendelea kufikiria sana kuhusu tukio lile.
Kwa kweli nilimsahau kabisa. Miezi ilipita. Biashara iliendelea kupambana na changamoto zile zile. Wakati mwingine nilijiuliza kama juhudi zangu zote zilikuwa na maana. Kulikuwa na siku nilifikiria hata kufunga biashara na kuanza kitu kingine.
Lakini siku moja nilipokea simu ya kushangaza. Mtu aliyekuwa upande wa pili wa simu alijitambulisha, na baada ya muda mfupi niligundua alikuwa yule mteja wa dakika tano.
Nilishangaa sana. Aliniambia alikuwa amevutiwa na namna nilivyomhudumia siku ile. Alikuwa amekumbuka jinsi nilivyokuwa mkarimu, mvumilivu, na mtaalamu katika kazi yangu.
Kisha alinipa habari ambayo sikuitarajia. Alikuwa na fursa ambayo aliamini ingeweza kusaidia biashara yangu kukua. Kwa kweli sikuamini nilichokuwa nikisikia.
Lakini mara nyingi matokeo yalikuwa tofauti. Biashara ndogo niliyoanzisha ilikwama. Baadhi ya mipango yangu muhimu ilivunjika dakika za mwisho. Hata katika mahusiano, mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Kadri miaka ilivyopita, nilianza kusikia watu wakisema labda nilikuwa na mkosi. Mwanzoni sikuyachukulia maneno hayo kwa uzito.
Kwa kweli hali hiyo ilinivunja moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa nimeanza kupoteza furaha.
Nilikuwa naishi kwa hofu na mashaka. Watu wa karibu waliniona nikibadilika. Nilicheka mara chache, nilijitenga zaidi, na nilianza kupoteza matumaini kuhusu maisha yangu ya baadaye. Kulikuwa na kipindi nilihisi nimechoka kabisa.
Watu ambao awali walionyesha kuniamini ghafla walibadilisha mtazamo wao. Baadhi ya marafiki walianza kuwa mbali nami bila sababu ya wazi. Mwanzoni nilidhani ilikuwa bahati mbaya.
Lakini kadri miaka ilivyopita, nilianza kugundua kuwa hali ile ilikuwa inajirudia mara nyingi sana kiasi kwamba haikuonekana kuwa ya kakawaida. Kwa kweli iliniumiza sana.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba sikujua chanzo cha tatizo. Nilijikuta nikitetea jina langu mara kwa mara dhidi ya maneno ambayo hata sikujua yalitoka wapi.
Wakati mwingine nilisikia uvumi kuhusu mimi ambao sikuamini kwamba watu wangeweza kuuamini. Nilianza kupoteza imani kwa baadhi ya watu.
Katikati ya majonzi yale, nilipewa bahasha ndogo na mmoja wa ndugu wa marehemu. Aliniambia kitu kimoja tu. “Usiifungue sasa.
Nilihifadhi bahasha ile mahali salama. Miezi ikapita. Kisha miaka ikaanza kupita. Mara kwa mara nilikuwa nikiiona lakini sikuwahi kuifungua. Kwa kweli, baada ya muda nilianza hata kusahau kilichokuwa ndani yake.
Lakini siku moja kila kitu kilibadilika. Nilipokuwa nikipanga baadhi ya vitu vya zamani nyumbani kwangu, macho yangu yaliangukia bahasha ile. Nilikaa kwa dakika kadhaa nikiiangalia.
Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitano, nilihisi ni wakati wa kujua ukweli. Kwa kweli nilikuwa na mchanganyiko wa hofu na hamu ya kujua. Nilipoifungua, sikukuta fedha wala hati za mali kama nilivyokuwa nimewahi kuhisi.
Kilichokuwa ndani kilikuwa ujumbe ambao sikuwahi kuutarajia. Maneno yale yalinigusa sana. Yalinifanya nitafakari maisha yangu, maamuzi yangu, na mwelekeo ambao nilikuwa nimeuchukua kwa miaka yote hiyo. SOMA ZAIDI.
Mara nyingi alikuwa akitumia muda mwingi nje ya nyumba, na nilihisi kama umakini wake ulikuwa umehamia sehemu nyingine. Kwa kweli hali ile iliniumiza sana.
Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa nikijitahidi kufanya kila niwezalo kuifanya ndoa yetu iwe na furaha. Nilizungumza naye mara kadhaa, lakini mambo hayakuonekana kubadilika kwa kiwango nilichotarajia.
Polepole confidence yangu ilianza kushuka. Nilianza kujiuliza kama bado nilikuwa muhimu kwake kama zamani. Wakati mwingine nilijikuta nikilia peke yangu usiku nikifikiria mustakabali wa ndoa yetu. SOMA ZAIDI.

KONDOA, DODOMA
Mbunge wa Jimbo la Kondoa ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amesisitiza kuwa nyumba za ibada zinapaswa kuwa sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja na amani miongoni mwa wananchi na si kuwa chanzo cha migawanyiko katika jamii.
Dkt. Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua rasmi Msikiti wa Filimo uliopo Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kijaji amesema kuwa nyumba za ibada zina nafasi kubwa katika kujenga maadili mema, kuimarisha upendo na kukuza mshikamano wa kijamii, hivyo zinapaswa kutumika kwa malengo hayo kwa manufaa ya Taifa.
“Msikiti huu uwe chachu ya mshikamano ndani ya jamii yetu. Nawapongeza viongozi wa dini kwa kusimama katika haki na kuendelea kuhubiri amani na umoja miongoni mwa wananchi,” alisema Dkt. Kijaji.

Aidha, aliongeza kuwa kila mtu ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu katika jamii na mbele za Mungu, akibainisha kuwa maendeleo yanayopatikana katika Jimbo la Kondoa yanalenga kuwanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.
"Ninachokifanya ndani ya jimbo letu ni kwa ajili ya maendeleo ya Wakondoa wote. Tunapaswa kuendelea kushirikiana na kuishi kwa upendo ili kuleta maendeleo endelevu,” alisisitiza.

Vilevile , Dkt. Kijaji alitumia fursa hiyo kuwahamasisha waumini na wananchi wa eneo hilo kuendelea kujenga na kuendeleza nyumba za ibada ili zitumike katika kukuza maadili mema na kuimarisha imani katika jamii.
Katika hatua nyingine, amewataka vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vingine vinavyohatarisha mustakabali wao, huku akiwataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pia amesisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto na vijana, akiwataka wazazi na walezi kuwajenga katika misingi ya maadili mema ili kuwa raia wema na wenye mchango chanya kwa maendeleo ya Taifa.














