Kila kitu kuanzia mashamba, nyumba, hadi akaunti za benki kilikabidhiwa kwa ndugu zangu na mke wake mdogo. Nilifukuzwa kama mtu baki kwenye mali ambazo mimi mwenyewe nilisumbuka kuzitafuta pamoja na baba yangu.
Ndugu walinitenga na kuniona sifai. Nilijaribu kwenda mahakamani, lakini kesi iligonga ukuta kwa sababu wosia ulikuwa umegongwa muhuri rasmi.
Nilijikuta nikiwa maskini wa kutupwa, ninaishi kwa dhiki, huku wale waliochukua urithi wangu wakicheka na kunisimanga kila siku. Nilijawa na kinyongo, upweke, na sonona kali. SOMA ZAIDI.
Miezi tisa ya mwanzo ilikuwa jehanamu ya kiuchumi. Siku zote zilifanana; nilikaa kwenye kiti kuanzia asubuhi hadi jioni nikitazama mlango, lakini hakuna mtu aliyeingia.
Kila mwezi ulikuwa wa maumivu, vilio vya chini kwa chini, na maswali yasiyokuwa na majibu kutoka kwa ndugu na marafiki. Tulijaribu kila njia ya hospitali. Tulitumia gharama kubwa kufanya vipimo na kununua dawa mbalimbali, lakini majibu yalibaki yale yale hakuna mabadiliko.
Upendo wetu ulianza kuingia kwenye majaribu makubwa, na matumaini yalianza kutoweka kabisa. Nilikua nikishuhudia wenzangu wakibeba mimba na kujifungua, huku mimi nikibaki na upweke na masikitiko moyoni. SOMA ZAIDI.
•Uwekezaji huo ni sehemu ya zaidi ya Shilingi Bilioni 100 zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita katika wilaya hiyo
Na. OWM–TAMISEMI, Gairo
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza Shilingi bilioni 2.8 katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kituo cha Afya Chanjale, Barabara ya Confort Pub–Magoweko na Shule ya Amali Kwipipa, hatua iliyoboresha upatikanaji wa huduma za afya, kurahisisha usafiri na usafirishaji pamoja na kupanua fursa za elimu ya amali kwa wananchi wa wilaya ya Gairo.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 17, 2026 katika kijiji cha Kwipipa, kata ya Rubeho, wilaya ya Gairo, baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma.
Prof. Shemdoe amesema miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo wanayoishi kupitia uwekezaji unaogusa maisha yao ya kila siku.
"Leo nimekagua miradi mitatu muhimu. Mradi wa Kituo cha Afya Chanjale wenye thamani ya Shilingi Milioni 680, Barabara ya Confort Pub–Magoweko yenye thamani ya Shilingi Milioni 470 na Shule ya Amali Kwipipa yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.6. Miradi hii ni matokeo ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi," amesema Prof. Shemdoe.
Akizungumzia Shule ya Amali Kwipipa, Prof. Shemdoe amesema shule hiyo imebobea katika mafunzo ya uhandisi na itakuwa chachu ya kuandaa wataalamu wenye ujuzi watakaoshiriki katika ujenzi wa taifa na maendeleo ya sekta mbalimbali za uzalishaji na amewataka wanafunzi wa shule hiyo kuitunza miundombinu yake ili idumu kwa muda mrefu na kuendelea kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.
Prof. Shemdoe ameainisha kuwa, uwekezaji huo ni sehemu ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita, akieleza kuwa tangu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aingie madarakani, Halmashauri ya Wilaya ya Gairo imepokea zaidi ya Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Gairo, Mhe. Ahmed Shabiby, amewapongeza wananchi wa kijiji cha Kwipipa kwa kujitolea eneo lililowezesha ujenzi wa shule ya Amali, yenye manufaa kwa wananchi wa Gairo na taifa kwa ujumla, Aidha ameipongeza TAMISEMI kwa kutenga bajeti ya chakula kwa wanafunzi wa shule hiyo, hatua itakayochangia kuboresha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia.
Naye, Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Josephine Kapoma, amesema Shule ya Amali Kwipipa itasaidia taifa kupata wahandisi wazawa wenye ujuzi na tija kwa taifa, hivyo amemuomba Prof. Shemdoe amfikishie salamu Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa wananchi wa Kwipipa wameipokea shule hiyo kwa furaha kutokana na mchango wake katika kuinua elimu ya ufundi nchini.
Wazazi wametakiwa kutimiza wajibu wao katika malezi na ulinzi wa mtoto ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama yasiyo na vitendo vya ukatili.
Wito huo umetolewa na Mkaguzi Msaidizi Emmanuel Kisiri, ambaye ni Polisi wa Kata ya Ikoma, Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara,alipokuwa akitoa elimu ya Polisi Jamii katika nyumba ya Abwire Thomas hivi karibuni.
Mkaguzi Msaidizi Kisiri amesema wazazi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwalea, kuwafuatilia na kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuhatarisha ustawi wao.
Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya wazazi, jamii na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kujenga mazingira bora ya malezi na kuhakikisha haki za watoto zinazingatiwa.

Kwa muda mrefu maisha yangu yaligeuka kuwa uwanja wa mateso makali. Nilikuwa nikishuhudia mambo ya ajabu ambayo sikuwahi kufikiria yangeweza kunipata.
Usiku nilipokuwa nikilala, nilisikia mizigo mizito ikinikandamiza kifua, nikashindwa kupumua na kushindwa hata kupiga kelele kuomba msaada.
Wakati mwingine nilikuwa nikiona vivuli vikizunguka chumbani kwangu, vikicheka kwa sauti ya kutisha, na mara nyingine nilihisi kama kuna mikono isiyoonekana ikinishika shingoni.
Wakati wa mchana hali haikuwa tofauti sana, nilikuwa nikihangaishwa na hofu isiyo na sababu, uchovu uliokithiri na migogoro isiyoisha katika maisha yangu.
Nilijua wazi kwamba haya yote yalikuwa matokeo ya uchawi uliokuwa unanifuata kila mahali. Kazi yangu ilianza kudorora kwa sababu nilikosa nguvu ya kufanya chochote. Ndugu na marafiki walianza kunitazama kama mtu asiye na msaada, na wengine walidhani nimechanganyikiwa.
Nilijitahidi kutafuta msaada wa kawaida kwa madaktari na hata kwa maombi yangu ya binafsi, lakini mambo yaliendelea kuwa mabaya zaidi. Usiku ulipokuwa ukiingia nilikuwa nikiingiwa na hofu kubwa, kwa sababu nilijua mzimu au nguvu mbaya ingenisumbua tena.
Nilijiona kama nimefungwa minyororo isiyoonekana ambayo haikuniruhusu kuishi maisha ya kawaida. Siku moja nilipokuwa nikisoma mtandaoni, nilikutana na ushuhuda wa watu waliokuwa wamepitia hali kama yangu lakini wakapata msaada. SOMA ZAIDI.
Niliona maisha yangu yote yakiporomoka ghafla, nikajua heshima yangu imefutwa milele. Mwanamke aliyenishitaki alijua fika hakuwa na ushahidi wowote. Lengo lake lilikuwa kunilazimisha nimpe pesa nyingi ili kunyamazisha kesi.
Alijua jina la ubakaji lingetisha na kunifanya nikubali masharti yake. Nilipoambiwa nitoe fedha ili nisionekane kortini, nilikataa. Nilihisi moyoni kuwa ningepoteza kila kitu iwapo ningekubali uongo huo.
Nilipoamua kusimama mahakamani, wengi waliniona kama mtu wa kujitakia maafa. Hata hivyo nilijua ukweli ulikuwa upande wangu. Nilichohitaji ni nguvu ya kusimama imara wakati huu mgumu. SOMA ZAIDI.
Usiku mmoja uliokuwa umesheheni giza na ukimya mzito, mjini kulizuka taharuki kubwa baada ya wezi kuvamia na kuvunja maduka yote kwenye barabara tuliyokuwa tunafanya biashara.
Kelele za kufuli zikivunjwa na milango ikipigwa ziliwafanya wenye maduka waliokuwa majumbani mwao kuamka kwa hofu, lakini hakuna aliyeweza kufika eneo la tukio kwa sababu wezi walikuwa wengi na wamejihami.
Asubuhi ilipofika, hali ya simanzi na hasira ilitanda miongoni mwa wafanyabiashara. Maduka yalikuwa yameachwa yakiwa wazi, rafu tupu, na hasara kubwa ikawa imewakumba.
Nilipofika dukani kwangu, majirani walikuwa wamejaa pale wakiwa na macho ya mshangao. Walidhani mimi pia ningekumbwa na masaibu yale yale. Lakini cha kushangaza ni kwamba lango langu lilikuwa limefungwa vilevile nilivyoacha jana usiku.
Hakuna kufuli lililovunjwa, hakuna mlango ulioguswa, na mali yangu yote ilikuwa salama kabisa. Wengine walishangaa wakajiuliza ni kwa nini wezi walipita kila duka lakini langu hawakuweza kulivunja.
Wengine walidhani nilikuwa nimeajiri mlinzi wa siri, kumbe ukweli ulikuwa tofauti kabisa. Siku chache kabla ya tukio hilo, nilikuwa nikipitia changamoto kubwa. Hali ya wizi katika eneo letu ilikuwa imeongezeka kwa kasi.
Wafanyabiashara wengi walikuwa wanalalamika kwamba kila wiki kulikuwa na duka lililoporwa. Mimi mwenyewe nilikuwa na wasiwasi mkubwa, hasa kwa sababu sikuwa na uwezo wa kumlipa mlinzi kila mwezi.
Ndipo nilipoamua kutafuta msaada wa kiroho ambao nilikuwa nimesikia watu wengi wakizungumza.SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi wetu, Lushoto
Wananchi wa Jimbo la Lushoto Julai 16, 2026 wamemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa Barabara ya Malibwi–Kwekanga–Ngwelo, wakisema hatua hiyo imeondoa kero ya muda mrefu iliyokuwa ikikwamisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa mazao, na kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Lushoto Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, kwa kuifikisha Serikalini changamoto hiyo ambayo imepatiwa ufumbuzi.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kwekanga, Bw. Salim Khamis Nyongo, amesema barabara hiyo inayojengwa inaunganisha Kata za Malibwi, Kwekanga, Kilole na Ngwelo pamoja na Jimbo la Mlalo, hivyo ni mhimili muhimu wa uchumi kwa wananchi wa eneo hilo ambao ni wakulima wa nyanya, viazi na karoti.
“Kwa miaka mingi tumeshindwa kusafirisha mazao yetu kwa urahisi kutokana na ubovu wa barabara, hivyo tunamshukuru Rais Samia kwa kututatulia kero yetu ya barabara na tunampongeza Prof. Shemdoe kwa kuwasilisha kero yetu na hatimaye imetatuliwa,” amesema Bw. Nyongo.
Bi. Rukia Selemani, Mkazi wa Kijiji cha Kwekanga amesema kuwa kabla ya kuanza kwa ujenzi wa barabara hiyo walikuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kusafirisha mazao yao, lakini hata wakati ujenzi ukiendelea tayari wameanza kuona manufaa yake kwani imewarejeshea matumaini na kuwaletea tabasamu, hivyo wanamshukuru Prof. Shemdoe kwa kuhakikisha changamoto hiyo inafanyiwa kazi.
Kwa upande wake, Bi. Fadhila Salehe ambaye pia ni mkazi wa kijiji cha Kwekanga amesema hapo awali magari yalikuwa yakiishia Malibwi, jambo lililowalazimu wananchi kubeba mizigo kichwani au kutumia pikipiki kwa gharama kubwa, hivyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa barabara hiyo na kumpongeza Mhe. Prof. Riziki Shemdoe kwa ufuatiliaji na usimamizi mzuri wa mradi huo.
Naye Bi. Biasina Shaban Mtari, Mkazi wa Kijiji cha Kwekanga amesema anashukuru kwa sasa magari kutoka Dar es Salaam, Arusha na Tanga yanafika kwenye makazi ya wananchi pasipo na kikwazo chochote, tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Mkazi Mwingine wa Kijiji cha Kwekaga, Bi. Shekela Ramadhan Mohamed amesema ujenzi wa barabara hiyo umeboresha pia maisha ya watoto wanaokwenda shule, kwani zamani walikuwa wakirejea nyumbani wakiwa wamechafuka kutokana na ubovu wa barabara, lakini sasa wanakwenda shuleni na kurejea nyumbani wakiwa wasafi.
Akizungumzia utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi wa TARURA Wilaya ya Lushoto, Bi. Brand Joseph Nyaki, amesema Barabara ya Malibwi–Kwekanga–Ngwelo inarekebishwa kwa kiwango cha zege na Mkandarasi Ms. Broader Construction Company Ltd, ikihusisha tabaka la zege lenye unene wa milimita 150 kwa urefu wa kilomita 1.5.
Bi. Nyaki ameongeza kuwa, mradi huo umeleta manufaa ya kiuchumi kwa vikundi vya Songambele, Inuka na Mkombozi vinavyonufaika na miradi ya vikundi kwa huduma wakati wa utekelezaji wa ujenzi huo wa mradi wa barabara, huku akimshukuru Mhe. Prof. Shemdoe kwa kuendelea kusimamia upatikanaji wa miundombinu bora ya barabara inayofungua fursa za maendeleo na kuboresha maisha ya wananchi wa Jimbo la Lushoto.
Nilipopata nyumba nyingine, nilianza kuugua mara kwa mara bila sababu iliyoeleweka. Nilikwenda hospitalini, nikapimwa mara kadhaa, lakini madaktari hawakuona tatizo kubwa. Nilihama tena nikidhani labda mazingira ya pale hayakuwa mazuri.
Lakini hata nilipohamia nyumba ya tatu, mambo yalikuwa yale yale. Biashara yangu ilianza kushuka, vifaa vya umeme vilikuwa vikiharibika mara kwa mara, na nilikuwa nikipata ndoto za kutisha karibu kila usiku. Nilianza kuishi kwa hofu na wasiwasi.
Miaka ilivyopita, nilihama nyumba ya nne, ya tano na hatimaye ya sita. Nilikuwa nimetumia fedha nyingi kwa kuhama, lakini mikosi haikuisha. Watu wa karibu walinishangaa. Wengine walisema nilikuwa nakimbia matatizo badala ya kuyatatua, lakini mimi nilijua kulikuwa na jambo lisilo la kawaida.
Siku moja nilimweleza mjomba wangu kila kitu kilichokuwa kinanitokea. Alikaa kimya kwa muda kisha akaniambia, “Inawezekana tatizo si nyumba unazoishi, bali kuna kizuizi kinachokufuata popote unapoenda.” SOMA ZAIDI.
Mwanzoni kila kitu kilionekana kwenda vizuri. Nilipata wateja wachache na niliamini mafanikio yalikuwa karibu. Lakini baada ya mwezi mmoja tu, matatizo yalianza.
Ndani ya miezi mitatu, mtaji wote ulikuwa umeisha. Nilibaki na deni kubwa la benki, simu za wadai kila siku na familia iliyokuwa imekata tamaa. Nilishindwa hata kulala usiku kwa mawazo. Nilifikiria kuuza nyumba niliyokuwa nimejenga ili kulipa sehemu ya deni.
Nilitembea kwa wataalamu wa biashara kutafuta ushauri. Wote walinielekeza namna ya kuboresha usimamizi wa fedha, lakini hata nilipofuata ushauri wao, mambo hayakubadilika. Nilianza kuamini kuwa kulikuwa na kizuizi kisichoonekana kilichokuwa kinaharibu kila nilichokifanya. SOMA ZAIDI.
Mara ya kwanza nilidhani nilikosea katika maandalizi. Nilijipanga upya na kusoma kwa bidii zaidi. Lakini nilipofanya mtihani wa pili, matokeo yalikuwa mabaya kuliko ya kwanza. Nilihisi aibu kubwa. Wenzangu waliendelea na masomo, huku mimi nikirudia mitihani.
Nilipopata nafasi ya tatu, niliahidi nafsi yangu kwamba lazima nifaulu. Nilitumia fedha nyingi kwa tuition, nikanunua vitabu vipya na nikajitenga na marafiki ili nisome kwa utulivu. Lakini nilipata matokeo yale yale nilifeli tena.
Nilianza kuamini labda sikuumbwa kwa ajili ya masomo. Familia yangu ilivunjika moyo, na baadhi ya watu waliniambia nitafute kazi za mikono badala ya kuendelea kupoteza muda darasani. Maneno hayo yalinichoma moyo, lakini sikuwa tayari kukata tamaa.
Siku moja nilikutana na mwalimu wangu wa zamani ambaye alinishangaa kuniona bado nikipambana na mitihani. Baada ya kusikiliza simulizi yangu, aliniambia kuna wakati vikwazo vya mafanikio haviwezi kuelezeka kwa juhudi pekee. SOMA ZAIDI.























