
Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM — Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema uhuru wa uhariri ni nguzo muhimu katika taaluma ya habari na unapaswa kulindwa ili vyombo vya habari viweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwajibikaji na kwa maslahi ya umma.
Akizungumza Mei 26, 2026 katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, Wakili Kipangula alisema hakuna mtu anayepaswa kuingilia maamuzi ya uhariri wa chombo cha habari, awe ni chanzo cha taarifa, mmiliki wa chombo, mwanasiasa au mtu mwingine yeyote mwenye maslahi binafsi.
Alisema uhuru huo unapaswa kuendana sambamba na uwajibikaji wa kitaaluma, huku akisisitiza kuwa maadili ya taaluma ya habari yanamtaka mwandishi kufanya kazi kwa uadilifu, bila upendeleo na kuhakikisha taarifa zote zinathibitishwa kabla ya kuchapishwa au kurushwa.
“Ukweli ndio mlinzi wa taaluma ya habari. Mwandishi anatakiwa kutoa taarifa ambazo amezithibitisha na ana uhakika nazo kwa sababu jamii inategemea kupata taarifa sahihi na kwa wakati ili iweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo,” amesema Wakili Kipangula.
Aidha, alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye uelewa, mshikamano na maendeleo, hivyo ni muhimu kutumia uhuru wa habari kwa kuzingatia sheria, maadili ya taaluma pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wengine kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.
Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri, Bw. Deodatus Balile, alisema uhuru wa vyombo vya habari utakuwa na maana halisi pale vyombo hivyo vitakapokuwa na uwezo wa kiuchumi wa kujiendesha bila kutegemea ushawishi wa nje.
“Uhuru wa vyombo vya habari utakuwa uhuru wa kweli pale vyombo vya habari vitakapokuwa na nguvu ya kiuchumi,” amesema Balile.
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kuonesha nafasi yake katika kuchochea maendeleo ya viwanda na kukuza ubunifu wa vijana kwa kutoa elimu ya viwango na ubora wa bidhaa katika Maonesho ya Fursa za Kazi na Ubunifu kwa Vijana (Career Fair 2026), hatua inayolenga kuwajengea vijana uwezo wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani katika soko la ndani na kimataifa.
Baadhi ya matukio katika picha wakati wa kutangazwa kwa dirisha la udahili mwaka wa masomo 2026/2027.
Na Benny Mwaipaja, Congo Brazzaville
Tanzania imeelezea msimamo wake wa kuunga mkono mbinu za fedha za mseto (blended finance) zitakazosaidia kuimarisha sekta za usafiri wa anga na afya barani Afrika, akieleza kwamba hakuna chanzo kimoja kitakachoweza kuziba mapungufu ya miundombinu ya bara hilo.
Akizungumza kama Gavana Mbadala wa Tanzania kwenye mkutano ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kuhusu “Platform solutions to Africa’s Transformation: De‑risking Aviation and Health systems through Innovative Financing”, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba alisema suluhisho linalopendekezwa ni la vitendo, nafuu na linaendana na vipaumbele vya kitaifa vya Tanzania.
“Tunasisitiza matumizi ya rasilimali za umma na binafsi pamoja na dhamana na msaada kutoka kwa washirika. Hatuwezi kutegemea chanzo kimoja pekee,” alisema Dkt. Mwamba, akiongeza kuwa ni muhimu kuzingatia udhibiti wa deni linalozidi kukua katika nchi za Afrika.
Katika Mkutano huo, Dkt. Mwamba alisisitiza kuwa usafiri wa anga ni kichocheo cha biashara, utalii, uwekezaji na ukuaji wa kikanda na kwamba Tanzania inakaribisha uwekezaji wa ubunifu kwa ajili ya uboreshaji wa viwanja vya ndege, uimarishaji wa usalama, utengenezaji wa mifumo ya usafirishaji na kuunganisha safari za kikanda kwa ufanisi. Lengo ni kuifanya Tanzania kuwa kituo cha usafiri kwa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Vilevile, kuhusu huduma za afya, Dkt. Mwamba alibainisha kuwa mifumo thabiti ya afya ni nguzo ya uzalishaji, raslimali watu na ustahimilivu wa kiuchumi inayohitaji fedha za kuaminika na nafuu kwa ajili ya dawa muhimu, vifaa vya kisasa na miundombinu ya afya inayoweza kustahimili mabadiliko ya tabianchi na mazingira.
Dkt. Mwamba alieleza mahitaji ya Tanzania kwa AfDB: kuendeleza msaada kwa ajili ya maandalizi ya miradi ili kuibua miradi inayoweza kuvutia wawekezaji, hususan kutoka sekta binafsi, upatikanaji wa dhamana na kuwa na masharti nafuu zaidi ya mikopo kutoka Taasisi za Fedha, ikiwemo AfDB.
“Tanzania iko tayari kushirikiana na AfDB na wadau wote kwa uwekezaji wa matokeo dhahiri kwa wananchi wetu,” alisema Gavana huyo.
Mkutano huo uliofunguliwa na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, uliwaleta pamoja Wadau wa maendeleo, Mawaziri wa Fedha, Magavana wa Benki Kuu, wawekezaji na viongozi wa Serikali kuzungumza kuhusu njia za kuondoa vikwazo vinavyoweka hatari kwa wawekezaji na kuleta mbinu za upatikanaji wa fedha zenye tija kwa miradi ya usafiri na afya barani Afrika.
Na. Peter Haule na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Nsubili Joshua amewataka watumishi wa Wizara hiyo kudumisha mshikamano, nidhamu, weledi na uzalendo katika kutekeleza majukumu ya kila siku ili kuwezesha kufikia malengo ya Wizara na Taifa kwa ujumla.
Rai hiyo imetolewa jijini Dodoma wakati akifunga kikao cha 39 cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha kilichofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 28 hadi 29 Mei 2026.
Alisema kuwa wajumbe wa Baraza hilo wanatakiwa kuwa mabalozi wazuri katika kuhakikisha maazimio na mapendekezo yote yaliyotokana na mijadala iliyokuwepo inazingatiwa kikamilifu na kufanyiwa kazi kwa wakati ili kuendelea kuimarisha ufanisi, uwajibikaji na mazingira bora ya kazi kwa watumishi wote wa Wizara.
Aidha, amewapongeza wajumbe wa Baraza hilo kwa mijadala yenye tija, maoni ya kujenga na michango yenye hekima, busara na mtizamo wa kuboresha utendaji wa wizara.
Alisema mada zote zilizowasilishwa zimegusa maeneo muhimu yanayohusu utendaji wa Wizara, ustawi wa watumishi pamoja na utekelezaji wa majukumu ya msingi ya kusimamia uchumi na fedha za umma.
Kwa upande mwingine Afisa Habari wa Wizara hiyo, Bw. Joseph Mahumi, amewataka wajumbe wa Baraza kutumia akaunti rasmi za mitandao ya kijamii ya Wizara ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu mafanikio na mikakati mbalimbali ya Wizara, Sera na masuala ya uchumi na fedha.
“Kwa upande wa Akaunti ya LinkedIn Wizara imefanya vizuri si tu kwa Wizara na Taasisi za Serikali lakini pia kwa taasizi binafsi zikiwemo Benki na mashirika binafsi, jambo ambalo si la kubeza”, alisema Bw. Mahumi.
Amesema pia Wizara inafanya vizuri katika mitandao ya Instagram (urtmof), Facebook (MofURT), Youtube (Hazina TV), LinkedIn (Ministry of Finance Tanzania), Whatsapp Channel (Wizara ya Fedha Tanzania) na Threads (urtMof).
Amewataka watanzania kwa ujumla kufuatilia kwa karibu mitandao hiyo ili kupata taarifa muhimu za masuala ya Sera, fedha na programu mbalimbali zitakazowasaidia kufanya maamuzi sahihi katika kukuza maendeleo binafsi na ya Taifa kwa Ujumla.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga (Mb), ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kushirikiana kikamilifu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Taasisi nyingine husika katika kushughulikia na kuondoa kero zote zinazosababishwa na mifumo ya utoaji vibali kwa shehena zinazoingia nchini.
Waziri Kapinga ametoa agizo hilo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Waziri Salum alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi na ujumbe wake Mei 29, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, kufuatia kuibuka kwa changamoto zilizojitokeza wakati wa kuunganisha mfumo wa TANeSW wa TRA na mfumo wa OAS wa TBS na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wafanyabiashara.
Aidha, Waziri Kapinga amepongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa baina ya TBS pamoja na TRA katika kuunganisha mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha taratibu na kuongeza ufanisi wa utoaji wa vibali kwa shehena za mizigo inayoingia nchini.

Nilijituma, niliheshimu kazi yangu, na nilikuwa naamini uaminifu ndio ulikuwa unanifanya nisogee mbele. Ndiyo maana siku mambo yalipoanza kubadilika, sikuamini kabisa. Ghafla nilianza kusikia uvumi.
Mwanzoni nilipuuzia nikidhani ni maneno ya kawaida ya kazini. Lakini kadri siku zilivyopita, nilianza kugundua baadhi ya wafanyakazi walikuwa wakiniepuka. Wengine walikuwa wakinitazama tofauti kana kwamba kuna jambo baya nilikuwa nimefanya.
Kwa kweli nilichanganyikiwa. Siku moja niliitwa ofisini kwa meneja. Nilishtuka kusikia nikihusishwa na jambo ambalo sikuwa nimefanya kabisa. Kulikuwa na madai yaliyokuwa yanaenea kwamba nilikuwa nimehusika kwenye kosa lililoharibu imani ya kampuni.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona hata baadhi ya watu niliokuwa na ukaribu nao wakianza kuniamini vibaya. Nilijaribu kujitetea, lakini ilionekana kama tayari watu walikuwa wameamua ukweli wao kuhusu mimi.SOMA ZAIDI.
Niliona watu wengi wakibadilisha maisha yao baada ya kuhamia nje, na moyoni nilikuwa na tumaini kuwa siku moja na mimi ningefanikiwa. Lakini safari haikuwa rahisi.
Kila nilipoanza mchakato wa application, changamoto zilikuwa zinajitokeza. Mara documents zinaonekana hazijakamilika, mara application inachelewa, mara napokea majibu ya kukataliwa bila kuelewa nilikosea wapi.
Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu nilioanza nao process wakifanikiwa huku mimi nikibaki pale pale. Wakati mwingine nilianza kujiuliza kama ndoto ile ilikuwa kubwa sana kwangu.
Kulikuwa na kipindi nilianza kukata tamaa. Nilikuwa nimechoka emotionally na financially kutokana na process za mara kwa mara ambazo zilionekana kutokwenda popote. Watu wengine walikuwa wakiniambia niache kupoteza muda na nikubali hali ilivyo.SOMA ZAIDI.
Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri wateja walikuwa wanakuja, mapato yalikuwa yanaongezeka, na nilikuwa na matumaini makubwa kuhusu future ya biashara yangu. Lakini ghafla mambo yakabadilika.
Nilianza kuona idadi ya wateja ikipungua. Mwanzoni nilidhani ni msimu mbaya tu wa biashara, lakini kadri wiki zilivyopita, hali ilianza kuwa mbaya zaidi. Siku moja nilipoangalia reviews za online, moyo wangu ulivunjika.
Kulikuwa na reviews nyingi mbaya. Baadhi ya watu walilalamika kuhusu huduma, wengine wakasema mazingira hayakuwa mazuri kama walivyotarajia. Kilichoniumiza zaidi ni kuona baadhi ya comments ambazo nilihisi hazikuwa fair kabisa.SOMA ZAIDI.
Ndiyo maana siku alipoamua kuondoka, nilihisi kama dunia yangu imevunjika vipande vipande. Kwa kweli iliniumiza sana. Mwanzoni nilidhani ni ugomvi wa kawaida ambao ungeisha baada ya muda.
Lakini siku zikapita, wiki zikageuka miezi, na hatimaye mawasiliano yakakatika kabisa. Kilichoniumiza zaidi ni kuona akiwa anaendelea na maisha yake huku mimi nikibaki na maumivu na maswali mengi.
Kulikuwa na kipindi nilipoteza furaha. Nilikuwa nikijiuliza nilikosea wapi. Wakati mwingine nilikosa hamu ya kutoka, kuzungumza na watu, au hata kujaribu uhusiano mwingine. Nilihisi kama moyo wangu ulikuwa umechoka kupenda. SOMA ZAIDI.
Lakini siku moja kila kitu kilibadilika ghafla. Nilituhumiwa kwa jambo ambalo sikuwa na uhusiano nalo kabisa.
Lakini badala yake, hali ilizidi kuwa mbaya. Watu walianza kunitazama tofauti, baadhi ya marafiki wakaanza kunikwepa, na hata watu wa karibu walionekana kuwa na mashaka nami. Kwa kweli iliniumiza sana.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona jina langu likiharibika kwa jambo ambalo sikulifanya. Kulikuwa na wakati nilihisi kama kila mtu tayari alikuwa amenihukumu bila kusikia upande wangu.
Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa najiuliza kama kweli ningewahi kupata haki yangu au kama maisha yangu yangekuwa vile milele. Hofu ya kupoteza heshima, kazi, na future yangu ilinifanya niishi kwa mawazo mengi sana.SOMA ZAIDI.
Na Mwandishi Wetu Ruangwa, Lindi
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema kwamba Tanzania inajipanga kuwa mmoja ya wazalishaji wakubwa Duniani wa madini kinywe(𝙂𝙧𝙖𝙥𝙝𝙞𝙩𝙚) kupitia Kampuni 30 zinazomiliki Leseni za kati na kubwa za uchimbaji wa madini hayo na hivyo kutoa ushindani wa kiuzalishaji kwa nchi ya China ambayo ndio inaongoza kwa uzalishaji wa madini hayo duniani kwa kuzalisha tani milioni 1.2 kwa mwaka.
Mhe Mavunde ameyasema hayo leo Mei 28, 2026 Wilayani Ruangwa, Lindi aliposhiriki katika hafla ya utiaji saini wa mikataba wa ubia baina ya Serikali na Kampuni ya Lindi Jumbo Limited kwa ajili ya mradi mkubwa wa uchimbaji madini kinywe na kubainisha kuwa kuanza kwa uchimbaji mkubwa wa madini mkakati ya kinywe (graphite) kunaiweka Tanzania kwenye dira ya duniani kama Nchi ya kimkakati katika uzalishaji wa madini hayo muhimu kwenye utengenezaji wa betri za magari ya umeme.

"Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuijenga na kuifanya nchi yetu ya Tanzania kama Taifa lenye dira wazi ya kiuchumi, mazingira rafiki ya uwekezaji na usimamizi imara wa rasilimali zake," amesema Waziri Mavunde
Amesema tukio la leo ni matokeo ya dira na maono hayo thabiti ya Mhe Rais ambayo yameendelea kuifanya Tanzania kuwa sehemu salama ya wawekezaji ambayo ina sera na Sheria zinazoeleweka na kutabirika.
Pia, Mhe.Mavunde amefafanua kwamba kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya sita Duniani kwa uzalishaji wa madini kinywe ambapo kwa mwaka uzalishaji wa Tanzania ni tani 25,000 kwa kampuni mbili tu zilizoanza uzalishaji mkubwa za Lindi Jumbo na God Mwanga-Tanga huku zingine 28 zikiwa katika hatua mbalimbali za kuanza uzalishaji.
Mhe Mavunde amewataka wamiliki wa Leseni 28 za uchimbaji madini kinywe kuhakikisha wanaanza uzalishaji mapema kama sheria inavyoelekeza ili kuepuka kufutuwa leseni hizo.
Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa dunia kwa sasa inapita kwenye mageuzi makubwa ambapo madini kinywe ni msingi wa kesho kwani upatikanaji wake ni kichocheo kikubwa katika uzalishaji wa nishati safi kwa kusaidia utengenezaji betri za magari ya umeme.
Mradi huo wenye thamani ya zaidi ya Dola za Kimarekani Milioni 82 unataraji kuzalisha madini kinywe tani 40,000 kwa mwaka katika kipindi cha uhai miaka 24 ya mgodi ambapo zaidi ya ajira 300 zimezalishwa hadi sasa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye sekta ya madini, Prof. Sifuni Mchome ameeleza kuwa miongoni mwa faida ambazo Serikali itapata kupitia kusaini mikataba hiyo ya ubia ni pamoja na udhibiti wa fedha na uhakika wa mapato kutokana na uwekezaji huo na fursa za ajira kwa watanzania.
Prof. Mchome amebainisha kuwa kupitia
makubaliano hayo yaliyotiwa saini, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itamiliki asilimia 16 ya hisa huru zisizohafifishwa thamani (non-dilutable free carried interest shares), huku Kampuni ya Lindi Jumbo Limited ikimiliki asilimia 84 ya hisa katika kampuni ya ubia.
Awali, akieleza maendeleo ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Lindi Jumbo Limited, Bw. Andrew Cunningham amebainisha kuwa pamoja na upanuzi wa uzalishaji wa mgodi huo, wataendelea kufanya utafiti ili kubaini mashapo zaidi ambayo yatarefusha maisha ya mgodi na kuongeza manufaa zaidi kwenye uchumi wa Tanzania.
Naye mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuvutia wawekezaji ambayo wamekuwa ni chachu ya maendeleo ya Mkoa wa Lindi na kuahidi kwamba Serikali ya Mkoa wa Lindi itaendelea kuwapa ushirikiano wawekezaji wote ili wafikie malengo yao na kuchochea uchumi wa Nchi yetu.





-Naibu Waziri Kwagilwa aahidi kufanya ziara katika halmashauri 184 kukagua zoezi hilo
Na Ashura Mohamed - ARUSHA
Serikali imesema haitamuonea haya mtu yeyote atakayefanya maigizo katika zoezi la upandaji miti nchini, ikieleza kuwa zoezi hilo ni muhimu kwa mustakabali wa mazingira.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Reuben Nhamanilo Kwagilwa, wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Jamii cha Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi - CCRC, kilichopo Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru - TICD.
Mhe. Kwagilwa amesema baada ya kumalizika kwa Bunge la Bajeti ataomba idhini kwa Waziri wa Mazingira kufanya ziara ya kukagua utekelezaji wa upandaji miti katika halmashauri zote 184 nchini ili kujionea hali halisi.
“Bunge hili likiisha nitataka kama serikali kwenda kuangalia hali halisi ya upandaji miti. Kwa kuwa kila mkurugenzi anayeulizwa anasema tumepanda miti milioni 5, milioni 2, lakini ukikagua eneo hilo miti hutaiona kabisa. Maigizo haya ndugu zangu kwenye mazingira ni hatari,” alisema.
Aliongeza kuwa serikali itamchukulia hatua mtu yeyote atakayethibitika kuendeleza shughuli za uharibifu wa mazingira baada ya kupewa taarifa.
Naibu Waziri ameeleza kuwa chanzo kikubwa cha mabadiliko ya tabia nchi ni uharibifu wa vyanzo vya maji, ukataji miti, kilimo kisichozingatia uhifadhi wa ardhi, pamoja na shughuli za viwanda, uvuvi na uchimbaji wa madini usiozingatia utaratibu.
Hali hiyo imesababisha ukame usioelezeka, mvua zisizo na majira, mafuriko, mito kubadilisha mikondo, maziwa kuingia kwenye makazi ya watu, dhoruba na vimbunga.
“Chanzo kikubwa cha uharibifu wa mazingira ni uchafuzi wa vyanzo vya maji, ukataji misitu, kilimo ambacho hakiipi ardhi yetu ikolojia,hali inayochangia ongezeko la gesi joto kwenye ikolojia ya uso wa dunia na kupelekea mabadiliko ya tabia nchi ambayo tunayaona leo,” alisema Kwagilwa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii TICD, Dkt. Bakari George amesema kituo hicho kitashirikiana na jamii na wadau mbalimbali kuandaa sera na kufanya tafiti za kusaidia jamii kuondokana na janga la mabadiliko ya tabia nchi.
Meneja wa CCRC, Dkt. Agnes Kapinga amesema uanzishwaji wa kituo hicho umefuata uchafuzi mkubwa wa mazingira unaopelekea ongezeko la taka kila siku na mifumo kushindwa kustahimili.
“Uwepo wa kituo hicho kwa kushirikiana na taasisi zingine utakujia na majibu ya changamoto mbalimbali zitakazosaidia jamii na taifa kwa ujumla kuwa na ustahimilivu kwa maendeleo endelevu,” alisema Dkt. Kapinga.
Kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM inamtaka kila Mkurugenzi wa Halmashauri nchini kuhakikisha anapanda miti milioni 1.5 ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Mkutano wa kimataifa wa siku tatu wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere umezinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kujadili masuala ya siasa za kimataifa (geopolitics), maendeleo na mwelekeo mpya wa Afrika katika mazingira ya dunia yanayobadilika kwa kasi.



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
