📌Bima ya afya kwa wote yaguswa

Na Augusta Njoji

KAMATI ya Ushauri ya Wilaya ya Handeni (DCC) imepitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti ya Sh. bilioni 35 kwa mwaka wa fedha 2026/27 ya Halmashauri ya Mji Handeni, huku miongoni wa vipaumbele vilivyotajwa ni pamoja na kugharamia Bima ya Afya kwa Wote kwa wananchi wasio na uwezo kwa kutumia mapato ya ndani.

Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichofanyika leo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewaagiza Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wahudumu wa Afya kutoa elimu kwa wananchi kwa lugha rahisi ili wahamasike kujiunga na mpango huo wa bima ya afya.

Amesema serikali tayari imetangaza kuanza utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hivyo ni wajibu wa viongozi na watendaji kuhakikisha wananchi wanaelewa umuhimu wake ili wawe na uhakika wa matibabu wanapohitaji huduma za afya.

“Ni lazima wananchi waelimishwe kwa lugha wanayoielewa ili wajue faida za bima hii, kwani itawasaidia kupata huduma za matibabu kwa uhakika,” amesema Mhe. Nyamwese.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kubaini kama inatekelezwa kwa kuzingatia thamani halisi ya fedha, sambamba na kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema rasimu ya mpango na bajeti imeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi na mikakati ya maendeleo ya Halmashauri.

Ametaja vipaumbele vingine vitakavyotekelezwa kwa kutumia mapato ya ndani kuwa ni pamoja na kutenga Sh milioni 176 kwa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ujenzi wa fremu za maduka ili kuongeza vyanzo vya mapato, utekelezaji wa afua za lishe, ujenzi wa maabara katika shule moja ya sekondari pamoja na kuboresha miundombinu ya mifugo.

Awali, Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt. Hudi Muradi, amesema kwa mwaka wa fedha 2026/27 Sh milioni 30 zimetengwa katika mapato ya ndani kwa ajili ya kugharamia bima ya afya kwa wananchi wasio na uwezo na kwamba kwasasa serikali inaendelea na zoezi la uhakiki wa wananchi hao.

Ameongeza kuwa serikali imeimarisha miundombinu ya afya na kuajiri watumishi wapya 58 ili kuboresha utoaji wa huduma katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali imekwishabainisha na kufanya utafiti wa maeneo mbalimbali yanayofaa kuendelezwa kwa ajili ya miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo na jua, ikiwa ni pamoja na Zuzu-Dodoma, Same-Kilimanjaro na Manyoni-Singida.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Februari 05, 2026 bungenini jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mwera, Mhe. Suleiman Mohamed Rashid aliyehoji juu ya mpango wa Serikali wa kutumia vyanzo vya umeme na upepo juu vilivyopo nchini.

" Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 150 katika Wilaya ya Kishapu, Shinyanga ambapo awamu ya kwanza ya mradi huo wenye megawati 50 imekamilika na hatua za kuingiza umeme huo katika Gridi ya Taifa zimeanza," Amesema Mhe. Salome.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe Esther Malleko aliyehoji mkakati wa Serikali katika kumaliza usambazaji wa umeme kwenye vitongoji vilivyosalia mkoani humo, Mhe. Salome amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na kazi za utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro ambapo hadi kufikia Januari 2026 jumla ya vitongoji 2,032 kati ya 2,258 sawa na asilimia 90 vilipatiwa umeme na kusalia vitongoji 226 ambavyo vitapelekewa umeme kupitia miradi mbalimbali.





 



Na. Peter Haule. na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma


Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa mageuzi ya uchumi yataendelea kuwa ajenda ya muda mrefu yakilenga si tu kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi bali kuhakikisha ukuaji huo unachangia katika upatikanaji wa ajira na ustawi wa wananachi kwa ujumla.


Amebainisha hayo wakati wa kikao na Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa ya Moody’s Investor Service ikiongozwa na  Bw. John Walsh, kilichofanyika Ofisi za Treasury Square, jijini Dodoma.

 

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa uchumi wa nchi umeendelea kuimarika licha ya matukio kadhaa yaliyokwaza ustawi wa uchumi wa dunia ukiwemo uviko 19 ambapo katika kipindi cha mwaka jana uchumi ulikua kwa asilimia 5.4 na unatarajiwa kukua zaidi mwaka huu wa fedha 2025/26 hadi kufikia asilimia 6.

 

Aidha, alibainisha kuwa mahitaji ya uwekezaji yanaendelea kuwa makubwa hususani kwenye miundombinu ya kimkakati kama Bandari, Viwanja vya Ndege, Reli na mtandao wa Barabara ili kuchochea maendeleo.

 

Alieleza kuwa nchi inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli iendayo Kasi -SGR, Bwawa la uzalishaji wa umeme la Julius Nyerere na uimarishaji wa sekta nyingine za kijamii na kiuchumi hatua itakayochochea zaidi ukuaji na uimara wa uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.

 

Akizungumzia Mfumuko wa bei amesema kuwa, hali imeendelea kuwa tulivu ambapo kiwango cha mfumuko wa bei kimeendelea kubaki chini ya asilimia tano kwa miaka kadhaa, kikiwa kati ya asilimia 2.9 na 3.4.

 

Kwa upande wake Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya kimataifa inayojihusisha na tathmini ya nchi kukopesheka katika masoko ya mitaji ya kimataifa Moody’s,  Bw. John Walsh, alisema kuwa uamuzi wa kupandisha hadhi ya uwezo wa nchi kukopesheka na kuipa alama B1 yenye mtazamo thabiti ulitokana na uthabiti wa kiuchumi na kifedha ambao nchi imeuonesha licha ya changamoto za uchumi za dunia katika miaka ya karibuni.


Alisema kuwa Tanzania iliendelea kurekodi ukuaji thabiti wa uchumi licha ya athari za janga la UVIKO-19, mfumuko wa bei wa kimataifa na kupanda kwa viwango vya riba duniani.


“Uamuzi wa kupandisha hadhi kwa kiwango cha B1 ulitokana na uthabiti wa sera za uchumi jumla na mageuzi ya Serikali yanayotekelezwa chini ya Mpango wa Shirika la Fedha la Kimatafa (IMF), unaokaribia kukamilika”, alisema Bw. Walsh.


Alisema kuwa Serikali imepiga hatua muhimu katika kushughulikia changamoto za muda mrefu, ikiwemo ukusanyaji mdogo wa mapato ya ndani na mapungufu ya utekelezaji wa sera, hivyo Tathmini ya sasa inalenga kufuatilia mafanikio, changamoto zilizopo, na mwelekeo wa mageuzi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.


Aidha alieleza kuwa tathmini hiyo inalenga kupata taswira ya kina ya hali ya sasa ya uchumi wa Tanzania, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha ukuaji endelevu na uthabiti wa kifedha kwa muda mrefu.

Matokeo ya mapitio ya hivi karibuni ya Kampuni za Moody’s na Fitch ziliipa Tanzania daraja la B1 (stable outlook) na B+ (stable outlook), mtawalia ambayo yanaonesha kwamba Tanzania ni nchi salama kwa wawekezaji.

 


Serikali imetoa wito kwa wadau kutoka sekta ya fedha nchini kuanzisha huduma na bidhaa za kifedha zitakazowezesha ajenda ya nishati safi ya kupikia kusambaa zaidi, hususan kwa kuwawezesha wajasiriamali wadogo katika maeneo ya pembezoni na vijijini pamoja na wabunifu wa teknolojia za matumizi ya nishati hiyo.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba  tarehe 4 Februari 2026 wakati akimwakilisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi katika uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika shule ya sekondari Bunge Wasichana iliyopo mkoani Dodoma.

"Tanzania imepiga hatua kubwa katika ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, matumizi ya nishati hii yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 na kufikia asilimia 23.2 mwaka 2025. Hata hivyo, bado takribani asilimia 77 ya kaya nchini zinatumia nishati isiyo safi ya kupikia, hivyo natoa wito kwa sekta binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma ajenda hii kwa kuwezesha upatikanaji wa nishati mbalimbali safi za kupikia katika maeneo ya pembezoni na yale ya vijijini." Amesema Mhe. Salome

Aidha, Mhe. Salome amewasisitiza Wasambazaji wa gesi za mitungi kuongeza vituo vya usambazaji na ujazaji wa gesi za mitungi ili kurahisisha upatikanaji wake kwa watumiaji wengi zaidi, pia Wabunifu na vijana walioko vyuoni kufanya tafiti na kubuni nyenzo na teknolojia zitakazowezesha ajenda hii kusambaa na kuwafikia watu wengi. 

Kuhusu mradi wa nishati safi ya kupikia aliouzindua Mhe. Salome amesema kuwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali kwa taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za binadamu na kutunza mazingira.

Ameongeza kuwa mfumo huo  uliozinduliwa  utawezesha chakula kupikwa kwa usafi, kwa haraka, kwa ufanisi, kwa gharama nafuu na bila madhara ya moshi kwa wapishi na wanafunzi huku mazingira  yakiendelea kustawi.

Mhe. Salome ameeleza kuwa kuzinduliwa kwa mradi huo ni sehemu ya juhudi za kitaifa zinazoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034 ambapo mpaka sasa tayari asilimia 23.2 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia huku taasisi 1,136 zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku zikihamia katika matumizi ya nishati hiyo.

Akiwa katika shule hiyo ya Wasichana Bunge, Naibu Waziri amezindua pia Klabu ya Nishati Safi ya Kupikia  yaani Clean Cooking School Club ambayo ni ya kwanza kuzinduliwa kwa Tanzania ambayo itakuwa mfano wa kuigwa na shule nyingine nchini katika kueneza elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.

Wanafunzi watakaojiunga na klabu hiyo watakuwa Vinara  wa Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Champions) na watashirikiana na Wizara ya Nishati na wadau wengine katika kutoa elimu mashuleni na katika jamii pamoja na kubuni teknolojia za nishati safi ya kupikia zitakazolinda afya na mazingira.

Awali Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bunge Wasichana, Richard Msana  alisema shule hiyo yenye wanafunzi 555 imefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za nishati ya kupikia baada ya kuachana na matumizi ya kuni na kuhamia katika gesi.

Amesema kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2022, shule ilikuwa ikitumia takribani shilingi milioni 10.5 kwa kila miezi mitatu kununua kuni. Baadaye walipoanza kutumia mkaa mbadala, gharama zilishuka hadi kufikia shilingi milioni 2.7 na hivi sasa, kupitia mradi wa matumizi ya gesi, shule imenunua tani moja ya gesi iliyotumika kwa miezi miwili, ambapo matumizi ni wastani wa shilingi milioni 1.3 kwa mwezi, kiwango ambacho ni nafuu zaidi kiuchumi.








 


𝘼𝙞𝙩𝙖𝙠𝙖 𝙨𝙚𝙧𝙞𝙠𝙖𝙡𝙞 𝙠𝙪𝙬𝙚𝙠𝙖 𝙢𝙞𝙥𝙖𝙣𝙜𝙤 𝙢𝙞𝙯𝙪𝙧𝙞 𝙮𝙖 𝙠𝙪𝙬𝙖𝙞𝙣𝙪𝙖 𝙫𝙞𝙟𝙖𝙣𝙖 𝙠𝙖𝙩𝙞𝙠𝙖 𝙠𝙪𝙟𝙞𝙠𝙬𝙖𝙢𝙪𝙖 𝙠𝙞𝙪𝙘𝙝𝙪𝙢𝙞.

𝘼𝙨𝙝𝙖𝙪𝙧𝙞 𝙆𝙤𝙣𝙜𝙖𝙣𝙞 𝙯𝙖 𝙑𝙞𝙬𝙖𝙣𝙙𝙖 𝙠𝙪𝙬𝙚𝙠𝙬𝙖 𝙠𝙞𝙡𝙖 𝙨𝙚𝙝𝙚𝙢𝙪.

"𝙈𝙥𝙖𝙣𝙜𝙤 𝙝𝙪𝙪 𝙬𝙖 𝙠𝙤𝙣𝙜𝙖𝙣𝙞 𝙯𝙖 𝙫𝙞𝙬𝙖𝙣𝙙𝙖 𝙪𝙨𝙞𝙬𝙚 𝙢𝙥𝙖𝙣𝙜𝙤 𝙬𝙖 𝙢𝙖𝙚𝙣𝙚𝙤 𝙛𝙪𝙡𝙖𝙣𝙞 𝙝𝙖𝙡𝙖𝙛𝙪 𝙢𝙖𝙬𝙖𝙯𝙤 𝙮𝙖𝙠𝙖𝙬𝙖 𝙩𝙪𝙩𝙖𝙛𝙞𝙠𝙞𝙧𝙞𝙖 𝙠𝙪𝙬𝙚𝙠𝙖 𝙠𝙖𝙩𝙞𝙠𝙖 𝙠𝙞𝙡𝙖 𝙬𝙞𝙡𝙖𝙮𝙖 𝙗𝙖𝙡𝙞 𝙠𝙬𝙖𝙠𝙪𝙬𝙖 𝙝𝙪𝙤 𝙣𝙞 𝙢𝙥𝙖𝙣𝙜𝙤, 𝙣𝙞𝙣𝙜𝙚𝙤𝙢𝙗𝙖 𝙩𝙪𝙟𝙞𝙚𝙡𝙚𝙠𝙚𝙯𝙚 𝙠𝙪𝙬𝙚𝙠𝙖 𝙠𝙤𝙣𝙜𝙖𝙣𝙞 𝙯𝙖 𝙫𝙞𝙬𝙖𝙣𝙙𝙖 𝙠𝙬𝙚𝙣𝙮𝙚 𝙠𝙞𝙡𝙖 𝙚𝙣𝙚𝙤"

Hayo yameswa na Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mkoani Iringa, Mhe. 𝗗𝗶𝗰𝗸𝘀𝗼𝗻 𝗟𝘂𝘁𝗲𝘃𝗲𝗹𝗲 (𝗩𝗶𝗹𝗹𝗮) wakati akichangia kuhusiana na mpango wa serikali katika kujenga kongani za viwanda.

Mhe. Lutevele ameeleza kuwa ni muhimu kujenga kongani za viwanda kwa kila eneo kwa kile alichodai kuwa katika sekta ya viwanda wapo watu wengi walioajiriwa kufanya kazi na huwenda bado kama serikali haijawafikia.

Akitolea mfano jambo hilo, Mhe. Lutevele amesema "..𝘬𝘸𝘢 𝘮𝘧𝘢𝘯𝘰 𝘬𝘢𝘵𝘪𝘬𝘢 𝘯𝘤𝘩𝘪 𝘺𝘦𝘵𝘶 𝘩𝘢𝘵𝘢 𝘶𝘬𝘪𝘵𝘰𝘬𝘢 𝘯𝘫𝘦 𝘩𝘢𝘱𝘢 𝘴𝘢𝘴𝘢 𝘩𝘪𝘷𝘪 𝘶𝘵𝘢𝘬𝘶𝘵𝘢 𝘬𝘪𝘭𝘢 𝘣𝘢𝘢𝘥𝘢 𝘺𝘢 𝘮𝘵𝘢𝘢 𝘬𝘶𝘯𝘢 𝘨𝘦𝘳𝘦𝘫𝘪, 𝘷𝘪𝘫𝘢𝘯𝘢 𝘸𝘢𝘯𝘢𝘵𝘦𝘯𝘨𝘦𝘯𝘦𝘻𝘢 𝘮𝘢𝘨𝘢𝘳𝘪, 𝘷𝘪𝘫𝘢𝘯𝘢 𝘸𝘢𝘯𝘢𝘧𝘢𝘯𝘺𝘢 𝘬𝘢𝘻𝘪 𝘻𝘢 𝘶𝘧𝘶𝘯𝘥𝘪 𝘴𝘦𝘭𝘦𝘮𝘢𝘭𝘢, 𝘸𝘢𝘮𝘰 𝘩𝘶𝘮𝘰 𝘭𝘢𝘬𝘪𝘯𝘪 𝘩𝘢𝘸𝘢 𝘷𝘪𝘫𝘢𝘯𝘢 𝘩𝘢𝘵𝘶𝘫𝘢𝘸𝘢𝘬𝘶𝘴𝘢𝘯𝘺𝘢 𝘴𝘦𝘩𝘦𝘮𝘶 𝘮𝘰𝘫𝘢"

Akiwekea msisitizo jambo hilo, Mhe. Lutevele amelieleza Bunge kuwa kwa serikali kutofanya hivyo kunaathiri mambo makubwa mawili ambayo amesema ni kutokuwa na mpangilio mzuri katika miji Pamoja na kushindwa serikali kushindwa kukusanya mapato kwakuwa vijana hao hawajekewa mpango mzuri wa kurudi kuangalia maendeleo yao.

Aidha, ameeleza namna ambavyo mpango wa BBT ulivyoshindwa kufuzu katika kuleta matokeo chanya kwa ukubwa kwenye kuwainua vijana katika kujikwamua kiuchumi na kushauri namna bora ya kufanya.

#KaziNaUtuTunasongaMbele

Nilikuwa kwenye ndoa ambayo kwa nje ilionekana ya kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, hakukuwa na kelele. Lakini kulikuwa na tatizo moja lililonisumbua kimya kimya kila aliponikaribia, mwili wangu ulikataa kabisa.

Sikuwa najifanya, wala sikuwa namchukia. Ilikuwa ni kama mwili wangu na moyo wangu havikuelewana tena. Nilitembea hospitali kadhaa. Vipimo vikafanywa, majibu yakarudi yale yale: uko sawa.

Lakini nilijua ndani yangu kuna kitu hakiko sawa. Nilihisi hatia, huzuni, na hofu kuwa ndoa yangu ingeangamia kwa jambo ambalo sikuweza kulieleza vizuri hata kwa maneno.

Kadri siku zilivyopita, ukimya ukaingia kati yangu na mume wangu. Nilijitenga, nikajilaumu, na wakati mwingine nikajikuta nikilia peke yangu usiku. Madaktari walikuwa wamesema niko sawa, lakini kwa nini basi mwili wangu ulikataa?

Ndipo nilipopata ushauri wa kumtafuta mtu anayeelewa mahusiano, nafsi, na mizizi ya matatizo ya ndani. Soma Zaidi.
Baada ya harusi yangu, nilikuwa na furaha kubwa. Ndoa ilikuwa mpya, maisha yalionekana kuanza upya, na kila mtu alinitakia heri. Lakini baada ya wiki chache, kitu cha ajabu kilianza kutokea.

Nilianza kuota ndoto ileile mara kwa mara. Kila wiki, ndoto hiyo ilirudi bila kubadilika mandhari ileile, hisia ileile, na hofu ileile. Mwanzoni nilipuuzia.

Nilijiambia labda ni mawazo mengi au uchovu wa maandalizi ya harusi. Lakini ndoto zilipoendelea, nilianza kuona athari zake hata nikiwa macho.

Nilikuwa mchovu kila siku, moyo haukuwa na amani, na ndoa yangu ilianza kuingia ukimya usio wa kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, lakini furaha ile ya mwanzo ilianza kupotea polepole.

Nilipomweleza mume wangu, alicheka na kusema ni kawaida. Lakini moyoni nilijua kuna kitu hakiko sawa. Ndipo nikaanza kutafuta ushauri wa busara.Soma Zaidi.

Maisha yangu nyumbani yalikuwa hatari. Kila usiku, nilihisi kama kuna mtu anakuja. Hatua zisizoelezeka zilisikika nje ya mlango wangu. Wakati mwingine, niliona kivuli kisichoelezeka karibu na dirisha.

Familia yangu ilikuwa katika hofu. Hatukuwa na njia ya kujua ni lini hatari ingeibuka. Nilijaribu kuziba milango, kuacha kufanya kelele, na hata kulala na tahadhari. Lakini kila kitu kilionekana kushindwa.

Usiku ulikuwa mzito, na mawazo mabaya yalikuwa sehemu ya kila siku yangu. Nilihisi kama hatimaye maisha yangu yatakuwa hatarini.Soma Zaidi.
Nilipoteza kazi yangu ghafla. Hakukuwa na onyo, na hakuna kilichokuwa tayari. Kila njia niliyojaribu kupata pesa ili kuendesha maisha ilishindikana. Nilihisi kuwa na mzigo mkubwa usiopunguka.

Nyumbani, wasiwasi uliongezeka. Nilijaribu kila njia ya kawaida: kutafuta kazi nyingine, kuuza vitu madogo, hata kuuliza familia. Lakini kila kitu kilishindikana.

Siku moja nilihisi nimekosa suluhisho. Nilikaa usiku kucha nikihisi huzuni na hofu. Nilijua kama hali hii ingeendelea, maisha yangu yote yangekwama. Nilihitaji msaada wa kweli, suluhisho ambalo lingebadilisha hali yangu haraka na kwa uhakika.Soma Zaidi.
Kwa muda mrefu, nilihisi maisha yangu hayakuwa na furaha ya kweli. Nilijaribu kila njia ya kawaida kurejesha amani moyoni, lakini hakuna kilichobadilika. Kila siku ilinipita nikiwa na huzuni na mawazo yasiyoisha.

Nilijaribu kucheka mbele ya watu, lakini ndani yangu kulikuwa tupu. Nilijaribu mazoezi, kusoma vitabu, na kuzungumza na marafiki. Lakini kila hatua ilikuwa ya muda mfupi tu, na furaha haikurudi.

Nilihisi kama kuna kitu kilikuwa kimenifungia kutoka ndani. Nilihitaji njia ya kipekee kurejesha amani ya kweli.Soma Zaidi.

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta neema ya maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Arusha kwa kuanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 127 kwa gharama ya shilingi bilioni 19.5.

Mradi huo unatekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika awamu ya Pili B na unatarajiwa kuwanufaisha wateja 4,086 katika wilaya za Arusha DC, Meru, Karatu, Ngorongoro, Longido na Monduli.

Akizungumza Februari 4, 2026 mkoani Arusha wakati wa hafla ya kumtambulisha mkandarasi aliyeshinda zabuni, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina, amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza rasmi Februari 2, 2026 na mkandarasi mzawa Kampuni ya NAKUROI Investment Co. Ltd.

“Tunamshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia utekelezaji wa mradi huu muhimu. Tumewaelekeza wakandarasi kuepuka rushwa, kutumia vibarua wa maeneo husika kwa kazi zisizo za kitaalamu na kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ubora na kwa wakati,” amesema Mhandisi Mhina.

Mhandisi Mhina ameongeza kuwa hadi sasa vitongoji 368 kati ya 1,505 mkoani Arusha vimefikishiwa umeme, huku jitihada zikiendelea kufikisha nishati hiyo katika vitongoji vilivyobaki.

“Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa umeme. REA imejipanga kikamilifu kutekeleza dhamira hiyo kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati,” amefafanua Mhandisi Mhina.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makala, ameipongeza REA kwa kutekeleza kwa vitendo maelekezo na dira ya Rais Samia ya kuwaletea wananchi maendeleo.

“Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itatoa ushirikiano wa kutosha kwa mkandarasi na REA kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa mafanikio,” amesema Mhe. Makala.

Naye Meneja wa Mradi kutoka Kampuni ya NAKUROI Investment Co. Ltd, Mhandisi Selestine Egongo, ameishukuru Serikali kwa kuwaamini na kuahidi kutekeleza mradi kwa ufanisi kwa kushirikiana na viongozi na wananchi wa maeneo husika.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo,akizungumza wakati wa kikao cha kumtambulisha rasmi Mkandarasi wa Mradi huo Burhani Engineers limited atakaye hudumia Vitongoji 415 vya Mkoani wa Simiyu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha.

Na.Mwandishi Wetu-SIMIYU

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anamringi Macha ametoa rai kwa Wanachi Mkoani Simiyu kuchangamkia fursa ya umeme Vitongojini wenye thamani ya kiasi cha Shil Bil. 4.8 unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Bi. Kayombo pia amewataka wananchi kutokuhujumu miradi hio kwani lengo lake ni kukuza na kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla.

Ameyasema hayo leo tarehe 04/02/2026 Ofisini kwake wakati wa kikao cha kumtambulisha rasmi Mkandarasi wa Mradi huo Burhani Engineers limited atakaye hudumia Vitongoji 415 vya Mkoani wa Simiyu.

Aidha, Bi. Kayombo amewasisitiza wananchi wa Mkoa huo kutoa ushirikiano kwasababu mradi huo unakwenda kupelekea Maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa huo.

"Mradi huu utakwenda kusaidia uendeshaji wa viwanda vidogo, Umeme utakwenda kurahisisha uchimbaji wa Dhahabu na kusaidia katika viwanda vya uchakataji wa zao la Pamba na mafuta ya kupikia ya Alizeti.

“Hii Miradi ni Miradi ya Maendeleo hivyo Wananchi mtoe ushirikiano kwa asilimia kubwa. Lakini sisi pia ni wakulima wazuri wa zao la alizeti na pamba, nahakika umeme huu utasaidia katika viwanda vitakavyo tengeneza mafuta yakupikia yatokanayo na alizeti” amesisitiza Bi. Kayombo.

Kwa upande wake, Mhandisi Seif Abduli, Mhandisi wa Miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amesema kwa Mkoa wa Simiyu Jumla ya Vitongoji 415 vitaanza kufikishiwa Umeme huku taratibu zingine zikiendelea ili kabla ya 2030 Vitongoji Vilivyo bakia 1026 vinafikiwa na Umeme

Mhandisi Seif ameeleza kuwa Vitongoji hivyo Vitahusisha kuunga Wateja 13292 na Mradi utatekelezwa kwa Muda wa Miaka Mitatu hivyo ametoa wito kwa Wananchi kuhakikisha kwamba wanachangamkia Fursa ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo vitongojini kwani transformer zitakazo fungwa zitakuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji ya viwanda.

Mhandisi Seif amesema kuwa Serikali inatumia gharama kubwa ya kufikisha huduma ya umeme kwa wananchi wake, hivyo akawataka kila mwananchi awe mlinzi wa miundombinu hiyo ili malengo ya kuwainua wananchi vijijini kiuchumi na kijamii yaweze fikiwa.

 

Maisha yangu nyumbani yalikuwa hatari. Kila usiku, nilihisi kama kuna mtu anakuja. Hatua zisizoelezeka zilisikika nje ya mlango wangu. Wakati mwingine, niliona kivuli kisichoelezeka karibu na dirisha.

Familia yangu ilikuwa katika hofu. Hatukuwa na njia ya kujua ni lini hatari ingeibuka. Nilijaribu kuziba milango, kuacha kufanya kelele, na hata kulala na tahadhari. Lakini kila kitu kilionekana kushindwa.

Usiku ulikuwa mzito, na mawazo mabaya yalikuwa sehemu ya kila siku yangu. Nilihisi kama hatimaye maisha yangu yatakuwa hatarini.Soma Zaidi.
Baada ya harusi yangu, nilikuwa na furaha kubwa. Ndoa ilikuwa mpya, maisha yalionekana kuanza upya, na kila mtu alinitakia heri. Lakini baada ya wiki chache, kitu cha ajabu kilianza kutokea.

Nilianza kuota ndoto ileile mara kwa mara. Kila wiki, ndoto hiyo ilirudi bila kubadilika mandhari ileile, hisia ileile, na hofu ileile. Mwanzoni nilipuuzia.

Nilijiambia labda ni mawazo mengi au uchovu wa maandalizi ya harusi. Lakini ndoto zilipoendelea, nilianza kuona athari zake hata nikiwa macho.

Nilikuwa mchovu kila siku, moyo haukuwa na amani, na ndoa yangu ilianza kuingia ukimya usio wa kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, lakini furaha ile ya mwanzo ilianza kupotea polepole.

Nilipomweleza mume wangu, alicheka na kusema ni kawaida. Lakini moyoni nilijua kuna kitu hakiko sawa. Ndipo nikaanza kutafuta ushauri wa busara.Soma Zaidi.
Nilikuwa kwenye ndoa ambayo kwa nje ilionekana ya kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, hakukuwa na kelele. Lakini kulikuwa na tatizo moja lililonisumbua kimya kimya kila aliponikaribia, mwili wangu ulikataa kabisa.

Sikuwa najifanya, wala sikuwa namchukia. Ilikuwa ni kama mwili wangu na moyo wangu havikuelewana tena. Nilitembea hospitali kadhaa. Vipimo vikafanywa, majibu yakarudi yale yale: uko sawa.

Lakini nilijua ndani yangu kuna kitu hakiko sawa. Nilihisi hatia, huzuni, na hofu kuwa ndoa yangu ingeangamia kwa jambo ambalo sikuweza kulieleza vizuri hata kwa maneno.

Kadri siku zilivyopita, ukimya ukaingia kati yangu na mume wangu. Nilijitenga, nikajilaumu, na wakati mwingine nikajikuta nikilia peke yangu usiku. Madaktari walikuwa wamesema niko sawa, lakini kwa nini basi mwili wangu ulikataa?

Ndipo nilipopata ushauri wa kumtafuta mtu anayeelewa mahusiano, nafsi, na mizizi ya matatizo ya ndani.Soma Zaidi.
Maumivu ya mgongo na misuli yalikuwa sehemu ya kila siku yangu. Kila asubuhi niliamka nikiwa nimechoka, na kila hatua ilinichosha. Nilijaribu dawa za maduka, lakini matokeo yalikuwa madogo.

Nilihisi kama hakuna suluhisho lolote, na kila siku ilikuwa ni vita mpya ya kuhimili maumivu. Nilijaribu mazoezi madogo na kupumzika mara kwa mara. Lakini maumivu hayakupungua.

Nilihisi kama mwili wangu ulikuwa unanikataa. Hisia za hofu na wasiwasi zilikuwepo kila wakati. Nilijua lazima nifate suluhisho ambalo lingefanya mabadiliko ya kweli.Soma Zaidi.
Nilihisi moyo wangu umevunjika. Aliondoka ghafla, bila kueleza sababu yoyote. Kila siku niliamka nikihisi huzuni na upweke. 

Nilijaribu kuwasiliana, kumwambia maneno mazuri, na kujaribu kurekebisha mahusiano.

Lakini kila jaribio lilishindikana. Nilihisi tamaa na kuhisi kuwa upendo wangu ulikosa nguvu. Nilijaribu kufanya kila kitu ili kumfanya arudi: zawadi, maneno mazuri, na hata kujaribu kubadilisha tabia yangu.

Lakini hakuonekana. Nilihisi kuwa na shida kubwa zaidi kuliko nilivyoweza kushughulikia peke yangu. Nilihitaji msaada wa kweli, suluhisho lililo na nguvu na linaloweza kurejesha upendo wa kweli.Soma Zaidi.

 


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OWM- TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na uwakilishi wa Benki ya NMB na kujadili namna wanavyoweza kufanya maboresho katika mchakato wa kutoa fedha za mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi kupitia taasisi hiyo ya kifedha.

Prof. Shemdoe amekutana na ujumbe huo leo Februari 03, 2026 ofisini kwake jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa Serikali kutafuta namna bora ya kurahisisha utolewaji wa mikopo hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha makundi yote lengwa ya Wanawake, Vijana na wenye Ulemavu yananufaika na mikopo hiyo.

Msisitizo wa Prof. Shemdoe kwa ujumbe huo ulioongozwa na Mkuu wa Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo umekuwa ni kuhakikisha vikundi vya wanufaika vyenye sifa stahiki vinapata mikopo hiyo kwa wakati.

Sanjali na hilo, Prof. Shemdoe ameipongeza na kuishukuru Benki ya NMB kwa kuiunga mkono Serikali katika uboreshaji wa miundombinu ya afya msingi na elimu msingi pamoja na kurahisisha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa walengwa. 

Akitoa ufafanuzi kuhusu hoja ya walengwa kutakiwa kuweka dhamana ili kupata mikopo ya asilimia 10, Bi. Bishubo amesema kuwa, hoja hiyo si ya kweli kwani mikopo hiyo ni nafuu na inatolewa bila dhamana yoyote, hivyo amewataka walengwa kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo. 

Katika hatua nyingine, uwakilishi huo wa Benki ya NMB umekutana na Naibu Waziri OWM- TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, pamoja na Naibu Waziri, OWM - TAMISEMI, anayeshughulikia Afya, Mhe. Dkt. Jafal Seif kama sehemu ya Kuimarisha mahusiano baina ya Benki hiyo na OWM- TAMISEMI.



Na Mwandishi Wetu - DODOMA


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta aina ya petroli zitakazotumika hapa nchini kwa mwezi kuanzia tarehe 4 Februari 2026, zikionesha kushuka maradufu kwa bei ya dizeli kwa mafuta yaliyopokelewa bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mtwara.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule, leo 4 Februari 2026, imebainisha kuwa, bei ya rejareja ya petroli dizeli imepungua kwa shilingi 90 kwa mafuta yaliyopokelewa Dar es Salaam, 25 kwa Tanga na shilingi 24 kwa bandari ya Mtwara. Aidha, bei ya mafuta ya taa nayo imepungua kwa shilingi 17, 14 na 93 kwa mafuta yaliyopokelewa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia ikilinganishwa na bei za mwezi Januari 2026.

Hivyo basi, bei za reja reja za bidhaa za mafuta kwa mwezi huu, zitakuwa shilingi 2,788, 2,849 na 2881 kwa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia. Na bei ya dizeli, Dar es Salaam ni shilingi 2,701, Tanga 2,762 na Mtwara 2,807 huku bei ya mafuta ya taa kwa Dar es Salaam ikiwa ni shilingi 2,881, Tanga 2794 na Mtwara 2,838.

Aidha, kwa mwezi Februari 2026, gharama za kuagiza mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam ziliongezeka kwa wastani 1.88% kwa mafuta ya petroli na 1.65% kwa mafuta ya taa na kupungua kwa wastani wa 5.10% kwa mafuta
ya dizeli. Kwa bandari ya Tanga zimepungua kwa 1.62% kwa petroli na dizeli; huku bandari ya Mtwara zikipungu kwa 9.24% kwa mafuta ya petroli. Vilevile, wastani wa gharama za kubadilisha fedha za kigeni umeongezeka kwa 1.86%.

EWURA inawahimiza wauzaji wa mafuta nchini kutoa stakabadhi za mauzo kwa wanunuzi zinazoonesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita.

Aidha,vituo vyote vya mafuta nchini vichapishe bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana kwani kutokufanya hivyo ni kosa na atakayekiuka atapata adhabu kali kwa mujibu wa sheria.