Miti imekuwa muhimili muhimu katika ukuaji wa sekta ya viwanda na biashara kwani kupitia miti, viwanda hupata malighafi, biashara hukua, na uchumi huimarika.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb.), Januari 27, 2026, akiwa ameambatana na Naibu Waziri,Mhe. Dennis Londo pamoja na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Needpeace Wambuya kushiriki zoezi la kupanda miti katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma. 

Zoezi hilo ni sehemu ya kusherehekea kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Mwanamazingira namba moja hapa nchini, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye aliazimisha siku yake 27 Januari, 1960 kwa kupanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026.

Aidha, Waziri Kapinga wakati akiongea na Watumishi wa Wizara hiyo baada ya kupanda mti, Altria rai kwa watumishi wa wizara kuhakikisha kila mmoja anashiriki kikamilifu katika upandaji miti ili kusaidia uhifadhi wa mazingira na kuibadili Dodoma kuwa ya kijani.

Uhifadhi na utunzaji wa miti unachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ndogo ya uchakataji wa mazao ya misitu, hususan utengenezaji wa mbao na samani, ambayo ni moja ya nyanja muhimu katika kukuza maendeleo endelevu ya sekta ya viwanda na biashara nchini

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akiwa ameshiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 26 Januari, 2026.

Na: OWM (KAM) – Riyadh, Saudi Arabia

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuongeza fursa za ajira kwa vijana nchini ikiwemo kushirikiana na sekta binafsi pamoja na wadau wa maendeleo.

Aidha, Mhe. Sangu amesema ushirikiano huo umewezesha wadau wa Maendeleo na sekta binafsi kutoa nafasi mbalimbali za ajira kwa vijana wa Tanzania nje ya nchi, kutokana na uwezo na ujuzi walionao.

Amesema hayo wakati aliposhiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia Januari 26, 2026.

Amesema, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefungua vyuo vya ufundi stadi, ambavyo vinatoa mafunzo ya ujuzi kulingana na mahitaji ya soko la ajira. Ameongeza kuwa, Vyuo hivyo vimekuwa chachu ya kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa vitendo, kukuza ubunifu kuongeza ajira.

Vilevile, Waziri Sangu ameseema Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Ukuzaji Ujuzi ambapo kupitia Programu hiyo vijana wamekuwa wakipatiwa mafunzo kwa njia ya Uanagenzi yanayolenga kuwajengea uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji, kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira, kuongeza kipato cha mtu binafsi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Kadhalika, Mhe. Sangu ameshukuru viongozi wa nchi mbalimbali kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa kuongeza fursa zaidi za ajira kwa Watanzania.

Mkutano huo unawakutanisha Mawaziri wa Kazi kutoka nchi zaidi ya 45 duniani na wameweza kujadili na kuweka mikakati ya kushirikiana katika soko la ajira, kuongeza kazi za staha kwa Vijana kwa kuzingatia mchango wa sayansi na teknolojia.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akiwa ameshiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia tarehe 26 Januari, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

 


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 mkoani Lindi.

Meneja Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme wa REA, Mhandisi Deogratius Nagu amebainisha hayo Januari 27, 2026 mkoani Lindi wakati wa kumtambulisha Mkandarasi Mzawa aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Jaitech Co Ltd kwa ofisi ya mkuu wa mkoa huo.

“Tunamshukuru Rais Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi cha shilingi 25,826,594,700.00 kitumike kusambaza umeme katika vitongoji 159 mkoani hapa na leo hii tumefika hapa kumtambulisha Mkandarasi na maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi yameanza,” amesema Mhandisi Nagu.

Akizungumzia hali ya usambazaji umeme mkoani humo, Mhandisi Nagu amesema kuwa,vijiji vyote 523 vimefikishiwa umeme na kwamba hadi sasa vitongoji 1,831 vimefikishiwa umeme kati ya vitongoji 2,402.

“REA inaendelea na utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyobaki, hivi tunavyozungumza Wakandarasi wanaendelea na kazi na hadi sasa katika vitongoji hivyo vilivyobaki vitongoji 378 vipo kwenye mpango wa kufikishiwa umeme,” amebainisha.

Amesema, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.

Aidha,Mhandisi Nagu ametoa wito kwa wananchi watakaopitiwa na mradi kuhakikisha wanatoa ushirikiano ili kumuwezesha Mkandarasi kutekeleza kazi ndani ya muda na kwa ubora unaopaswa na kwamba mradi huo unazo faida lukuki kuanzia hatua za awali za utekelezaji hadi hapo utakapokamilika.

Pia, Mhandisi Nagu ameiomba Ofisi ya Mkoa kushirikiana na REA kufikisha elimu na taarifa sahihi kwa wananchi kuwa hakutokuwa na fidia kwa wananchi ambao maeneo yao yatapitiwa na mradi hasa ikizingatiwa kuwa umeme ni fursa ya kiuchumi na kijamii.

“Tunaomba ushirikiano kutoka katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kurahisisha utekelezaji wa mradi ikiwemo kuruhusu mradi kukatiza katika baadhi ya maeneo ya misitu sambamba na kuwa na miundombinu wezeshi kuruhusu kusafirisha vifaa vya mradi maeneo mbalimbali atakapokuwa mkandarasi,” amesema Mha. Nagu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Katibu Tawala wa mkoa huo, Zuwena Omari ameipongeza REA kwa kuendelea kuenzi kwa vitendo dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kufikisha maendeleo kwa wananchi.

Amesema, Ofisi ya Mkoa wa Lindi itatoa ushirikiano kwa Mkandarasi muda wote wa utekelezaji wa mradi na alimtaka Mkandarasi kuhakikisha anatoa taarifa endapo atakutana na changamoto yoyote.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Jaitech Co Ltd, Isihaka Kibode ameishukuru Serikali kwa kupata kazi na ameahidi kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwamba atashirikiana karibu na viongozi na wananchi wa maeneo ya mradi.

 



Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo na Naibu wake Mhe. Kaspar Mmuya leo Januari 27, 2026 wamewaongoza watumishi wa Wizara katika zoezi la upandaji miti kwenye Ofisi za Wizara zilizopo eneo la Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni siku ya kitaifa ya kuhamasisha upandaji miti.

Zoezi hilo linaongozwa na Kaulimbiu “Kesho yetu inaanza na mti unaopandwa leo, Panda mti kwa maendeleo endelevu ya makazi.”

Katika kufanikisha zoezi hilo, Viongozi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi, Vyuo vya Ardhi Morogoro (ARIMO) na kile cha Tabora (ARITA) pamoja na Ofisi za Ardhi za Mikoa zimeelekezwa kushiriki zoezi hilo kwa kupanda miti kwenye maeneo yao.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema, wizara yake inashiriki zoezi la upandaji miti kuunga mkono juhudi za Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwana mazingira namba moja kutunza mazingira hasa ikizingatiwa kuwa, leo Januari 27, 2026 ni siku yake ya kuzaliwa.

Waziri huyo wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amewahamasisha watumishi wa sekta ya ardhi nchini pamoja na wananchi kwa ujumla kukumbuka kuwa miti ni uhai hivyo wapande miti na kuitunza kwa lengo la kumuunga mkono Rais akiwa mwanamazingira namba moja.

”Wakati tunasherekea siku ya kuzaliwa ya Mhe. Rais, yeye ni mwana mazingira namba moja tunamuunga mkono kwa vitendo kwa kuhakikisha tunapanda miti ikiwa ni juhudi za kutunza mazingira’’ amesema.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa watanzania kuendelea kujenga utamaduni wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa hiari wakitambua kuwa ulinzi wa mazingira ni msingi wa uhai, maendeleo na Usalama wa taifa.

Zoezi hili ni ishara ya uwajibike na linatoa fursa kwa kila mmoja kwa nafasi na mahali alipo kushiriki katika kulinda na kuenzi mazingira kwa manufaa ya sasa na kizazi kijacho.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (kulia) akipanda mti katika eneo la Ofisi za Wizara ya Ardhi Mtumba Jijini Dodoma tarehe 27 Januari 2026 ikiwa ni siku ya kitaifa ya kuhamasisha upandaji miti. Kushoto ni Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga.Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya akipanda mti kwenye eneo la Ofisi ya Wizara ya Ardhi lililopo katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma tarehe 27 Januari 2026 ikiwa ni siku ya kitaifa ya kuhamasisha upandaji miti. 
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga (Kushoto) akishiriki zoezi la kupanda miti lililoongozwa na Waziri wa Ardhi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo katika ofisi za Wizara katika mji wa Serikali Mtumba tarehe 27 Januari 2026. Kulia ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Ardhi Dkt. Netho Ndilito.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemera (Kushoto) akishiriki zoezi la kupanda miti lililoongozwa na Waziri wa Ardhi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo katika ofisi za Wizara katika mji wa Serikali Mtumba.

Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Makao Makuu, wakiwa katika zoezi la upandaji miti lililoongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika Ofisi za Wizara katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

 


NA.MWANDISHI WETU – NKASI

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. James Kilabuko amezindua nyaraka za usimamizi wa maafa katika Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa huku akisisistiza nyaraka hizo kutekelezwa kwa vitendo.

Dkt. Kilabuko amesema hayo leo 27 Januari, 2026 wakati wa uzinduzi huo na kusema kuwa, hatua hiyo ni mwanzo wa kuanza kazi rasmi endapo kutatokea janga lolote, na kutoa wito kwa idara, vitengo na taasisi ngazi ya wilaya kuzingatia nyaraka hizo kwa kuhakikisha zinakuwa chachu ya kuongeza ushirikishwaji wa jamii na wadau katika masuala ya menejimenti ya maafa.

Ameongeza kuwa, hatua hiyo itasaidia kujenga uelewa wa jamii kuhusu masuala ya usimamizi wa maafa, kuimarisha mfumo wa utoaji wa tahadhari awali, kujenga uwezo wa kuzuia, kupunguza madhara na kujiandaa na kurejesha hali pindi maafa yanapotokea.

 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mkeli Mbossa, ametunukiwa Cheti cha Heshima kwa usimamizi wake ikiwa ni kutambua na kuthamini mchango wangu wake mkubwa na utoaji huduma wa kipekee kwa jumuiya ya kimataifa ya Forodha, katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Forodha 2026.

Cheti hicho cha kimetolewa na Shirika la Forodha Duniani ( WCO) kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), katika maadhimisho yaliyofanyika tarehe 26 Januari, 2026, jijini Dar es Salaam, chini ya kaulimbiu isemayo: 

“Forodha inalinda jamii kupitia umakini na uwajibikaji.”

Cheti hicho cha heshima kimetolewa ikiwa ni kuthamini huduma ya kipekee ya TPA chini ya usimamizi wa Bw. Mbossa na mchango mkubwa katika kuunga mkono na kuimarisha jumuiya ya kimataifa ya Forodha, hususan kupitia uboreshaji wa mifumo, taratibu na ushirikiano wa taasisi.

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Forodha 2026 yalilenga kutambua na kuenzi mchango wa sekta ya forodha katika kukuza biashara halali, kulinda uchumi wa taifa, kuongeza makusanyo ya mapato ya serikali, pamoja na kuimarisha uwajibikaji na ushirikiano kati ya TRA na wadau wake wakuu, wakiwemo taasisi zinazosimamia bandari na biashara ya kimataifa.

Akizungumza kabla ya kukabidhi cheti hicho, Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Yusuph Juma Mwenda, aliipongeza TPA kwa ushirikiano wake wa karibu na wa muda mrefu na TRA, uliosaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha ufanisi wa shughuli za forodha bandarini, kurahisisha biashara na kuimarisha udhibiti wa mapato ya serikali.

Bw. Mwenda alieleza kuwa TPA imeendelea kuwa mdau muhimu na mfano wa kuigwa, kwa kuzingatia misingi ya weledi, uwajibikaji na uadilifu, huku ikiendelea kushirikiana kwa karibu na TRA katika utekelezaji wa maboresho ya mifumo na taratibu za forodha kwa manufaa ya taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Bw. Plasduce Mkeli Mbossa, ameishukuru TRA na Utawala wa Forodha wa Tanzania kwa kutambua mchango wake binafsi na wa taasisi ya TPA kwa ujumla, na kuahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo ili kuongeza ufanisi wa bandari na kuchangia zaidi katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Bw. Mbossa amesema kuwa tuzo hiyo ni chachu kwa TPA kuendelea kuboresha huduma zake, kuimarisha matumizi ya teknolojia ya kisasa, pamoja na kudumisha misingi ya uwajibikaji, uwazi na uadilifu katika utoaji wa huduma za bandari na forodha.

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Forodha yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kutathmini mafanikio ya sekta ya forodha, kuimarisha mahusiano na wadau wa biashara, pamoja na kuweka mwelekeo wa pamoja wa kuboresha mazingira ya biashara na maendeleo ya taifa kwa ujumla.











Na Mwandishi Wetu


Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mha. Wolta Kirita amewataka Mameneja wa Mikoa na Wilaya katika mikoa yote 25 inayohudumiwa na taasisi hiyo kuelekeza nguvu zaidi za kiutendaji katika kuvisimamia na kuvijengea uwezo Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) ili viimarishe utoaji wa huduma hiyo kwa wananchi waishio vijijini na kuchangia uchumi wa nchi.

Mkurugenzi Mkuu Kirita ametoa maelekezo hayo Januari 26, 2026 wakati akizungumza na watumishi wa RUWASA mkoa wa Mara ambako ameanza ziara ya kukagua shughuli za CBWSO na hali ya utoaji huduma ya maji vijijini katika mikoa ya Mara na Mwanza.

Ziara hiyo ni muendelezo wa zoezi la kukagua kazi za vyombo katika kuwahudumia wananchi ambapo Menejimenti ya RUWASA ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu huyo inapita mikoani kutambua na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizopo katika kuwahudumia maji safi ya bomba wananchi wa vijijini.

Akizungumza na watumishi hao wakiongozwa na Meneja wa RUWASA mkoa wa Mara Mha. Charles Pambe na Mameneja wa wilaya za mkoa huo, Mkurugenzi Mkuu Kirita aliwataka kuweka na mpango wa kudumu wa mara kwa mara kuzitembelea CBWSO na kuzisadia pale zinapohitaji msaada wa kiufundi na kitaalamu ili kuzijengea uwezo wa kujua na kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria na kuondoa changamoto ndogondogo katika kuwahudumia wananchi.

Alisema tangu kuanzishwa kwake mwaka 2019, RUWASA imeshajenga miradi zaidi ya 3,000 ya maji vijijini na kwamba sasa ni wakati muafaka wa kuhakikisha miradi hiyo inakuwa endelevu na unahudumia wananchi maji kwa ufanisi.

Awali, akitoa taarifa ya hali ya huduma ya maji vijijini katika mkoa wa Mara kwa Mkugugenzi Mkuu aliyeambatana na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti, Meneja wa mkoa huo Mha. Pambe alisema wastani wa utoaji wa huduma umefikia asilimia 75 na kwamba ipo miradi inayoendelea kujengwa na itainua zaidi hali ya huduma.

Katika siku ya kwanza ya zoezi la ukaguzi wa CBWSO, Mkurugenzi Mkuu Kirita aliongoza ukaguzi huo katika CBWSO ya Bulisumakwi wilayani Musoma na Kokwe wilayani Rorya.






Kwa miaka mingi, nilijaribu kupata kazi kwenye makampuni makubwa na ya kimataifa, lakini kila jaribio lilishindikana. Kila maombi yangu ya kazi yalipokelewa kwa kukanushwa au bila jibu kabisa.

Nilijikuta nikihisi kuchoshwa, kudharauliwa, na hata kuanza kujiuliza kama nilikuwa na thamani ya kufanya kazi katika kampuni yoyote. 

Hali hii ilinifanya nihisi huzuni kubwa, shauku yangu ya kukua kitaaluma ikipotea kidogo kidogo.

Kila siku ilikuwa changamoto. Nilijaribu kurekebisha CV yangu, kujifunza ujuzi mpya, na kujitahidi kushirikiana na watu wenye nafasi ya uongozi, lakini matokeo yalikuwa hafifu.

Kila kukanushwa kunaniumiza na kuongezea woga kwamba ndoto yangu ya kufanya kazi kwenye kampuni ya kimataifa ingekufa bila kutimia.Soma Zaidi.

Rafiki yangu alikuwa akipitia mateso makubwa kwa miaka mingi. Alikabiliwa na fibroids ambazo zilikuwa zinamsumbua kila siku, zikileta maumivu makali na kumfanya asiweze kuzaa.

Kila jaribio la kupata mtoto lilishindikana, na kila wakati alikuwa akijikuta akilia, akihisi kutokuwa na matumaini. Hali hii ilinifanya nihisi huzuni kubwa kwake, kwani kila siku nilimuona akiteseka bila msaada wa kudumu.

Alijaribu dawa mbalimbali, madawa ya kupunguza maumivu, na hata vipimo vya kimatibabu, lakini hakuna kilichomsaidia kwa hakika.

Mateso yake yalionekana kuendelea kila siku, na hofu ya kutoweza kuwa mama ilimuumiza zaidi. Familia yake na marafiki walikuwa wakiangalia kwa wasiwasi, wakidhani labda hakuna suluhisho la kudumu kwa tatizo lake.Soma Zaidi.

Nilijikuta katika hali ya mshtuko mkubwa siku ile nilipogundua kuwa mume wangu alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na kijana wa jirani yetu. 

Nilihisi dunia yangu imevunjika, moyo wangu ukachanika, na hofu kubwa ikajaza kila kona ya maisha yangu.

Kila kitu kilionekana kuharibika, na heshima yangu kama mke ilikuwa kwenye hatari kubwa.

Kwa muda, nilijaribu kuficha huzuni yangu na kujaribu kuepuka mzozo, lakini kila mara nilipoona mume wangu nikijikuta nikiwa na hasira na maumivu yasiyo na mwisho.

Nilijua lazima nichukue hatua, lakini pia nilihitaji busara; hatua ya ghafla au uhasama inaweza kuharibu ndoa yetu kabisa. Soma Zaidi.

Kwa muda mrefu, nilijikuta nikiteseka kimoyo na kiroho. Ndoto zangu za kufanikisha maisha yangu, kupata amani ya ndani, na kufanikisha familia yangu zilionekana kutokuwepo.

Kila siku nilijaribu, lakini kila jaribio lilishindikana; nilihisi huzuni isiyo na mwisho na kuanza kujiuliza kama maisha yangu yangeweza kamwe kubadilika.

Nilijaribu suluhisho kadhaa: kuomba, kujitahidi kiroho, na hata kuzungumza na watu mbalimbali wa kuelimisha, lakini kila kitu kilikuwa hafifu. Hisia za kukata tamaa, kuchanganyikiwa, na hofu ya kudumu zilinijaza.

Nilijua lazima nifanye kitu tofauti, lakini sikuwahi kujua ni njia gani ya kweli ya kufanikisha ndoto zangu za kiroho. Soma Zaidi.
Siku ile nilipokuwa nikijaribu kurudi kwenye maisha ya kawaida baada ya ajali mbaya, nilijikuta nikiwa na maumivu yasiyoisha na mwili wangu ukidhaniwa kukosa nguvu kabisa.

Kila hatua nilipokuwa nikifanya ilikuwa changamoto, na mara nyingi nilijikuta nikikata tamaa, nikiwa na woga kwamba huenda sitawahi kurudi kwenye hali ya kawaida.

Miaka mitano ilipita nikiwa nikiteseka kimwili na kiakili. Nilijaribu madaktari mbalimbali, tiba za jadi na za kisasa, lakini hakuna kitu kilichokuwa na matokeo ya kudumu.

Nilijikuta nikijihisi mgonjwa wa kudumu, huku wengine wakiendelea na maisha yao kama kawaida. Hali hii ilinifanya nijisikie kukosa thamani na kushindwa kabisa. Soma Zaidi.

 


Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amempongeza Dkt. Rose Mbwete aliyekuwa Mkurugenzi wa kamapsi ya Karume –Zanzibar kwa kufanya kazi nzuri iliyozingatia kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma kwa kipindi cha miaka saba (2018- 2025) akiwa Mkurugenzi wa kampasi ya karume Zanzibar.

Profesa mapesa ameyasema hayo leo wakati wa kikao kazi cha Menejimenti cha kumuaga Dkt. Mbwete na Kumkaribisha Mkurugenzi mpya Dkt. Sifuni Lusiru, ambapo pamoja na mambo mengine Dkt Mbwete amepongezwa kwa kujenga mahusiano mazuri kati ya Chuo na Taasisi nyingine za Serikali zilizopo Zanzibar, pia amekuwa mvumilivu , amejenga umoja na mshikamano miongoni mwa Wafanayakazi wa kampasi ya karume.



Prof. Mapesa amemsihi Mkurugenzi mpya Dkt. Lusiru kuhakikisha anayaendeleza  na kudumisha yale yote ambayo Dkt. Mbwete aliyasimamia kwa maslahi mapana ya Taasisi, ametakiwa pia kushirikisha Menejimenti ya Chuo na Watumishi anawaowasimia pale inapobidi.

Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Richard Kangalawe amesema kwa sasa Kampasi ya karume imekuwa huwezi kulinganisha na miaka ya nyuma kwa maana  kozi zinazofundishwa zimeongezeka, idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa imeongezeka, idadi ya wanafunzi wanaohitimu imeongezeka na  hata idadi ya Watumishi imeongezeka.

Kwa upande wa Naibu Mkuu wa Chuo, Mipango, Fedha na Utawala Prof. Evaristo Haulle amesema ni jambo la kufurahia pamoja kumpongeza Dkt. Mbwete kwa utumishi wake mwema, ulioleta tija kwa Taasisi hivyo kukutana pamoja na kumpongeza anaponaliza muda wake kunatoa fursa kwa viongozi wengine kufanya tafakuri ya kina ya namna bora ya kuendeleza Taasisi.

Dkt.Rose Mbwete Mkurugenzi aliyemaliza muda wake amekiri kuwa kufanikiwa kwake kutimiza majukumu ya taasisi ni pamoja na ushirikiano wa dhati aliupata kutoka kwenye bodi ya Chuo, Menejimenti na Watumishi aliokuwa anawasimami, hivyo anaamini kuwa ushirikiano ni jambo la muhimu, Uvumilivu, Hekima na kuzingatia Tamaduni za aneo husika.

Mbwete amesema changamoto zipo lakini lazima kuwe na namna bora ya kuzitatua. Kwa kuweka maslahi ya Taasisi mbele Umoja Ndiyo nguvu yetu na umoja ni ushindi.

Naye Dkt. Sifuni Lusiru ameahidi kuendeleza yale yote ambayo Dkt Mbwete aliyasimamia kwa mustakbali wa Taasisi, ameahidi kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, taratibu, sheria na miongozo ya Utumishi wa umma.

Imetolewa na ;

Kitengo cha mawasiliano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

26.01.2026