Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Zanzibar
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Na.Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.
Mazungumzo ya Viongozi hao yamelenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar katika sekta ya kazi na ajira, hususan eneo la kukuza maendeleo ya rasilimali watu, ulinzi na haki za wafanyakazi pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania.
Vilevile, wamejadili kuhusu Mkutano wa Uhamaji wa Wafanyakazi (Labour Mobility Dialogue) utakaowakutanisha nchi wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Nchi za Ghuba (GCC), Jordan, Lebanon na nchi za Afrika zinazotuma wafanyakazi nje ya nchi chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika (African Union). Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Oktoba 2026 Tanzania, jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na kupanua fursa za ajira salama na zenye staha kwa wananchi wa nchi shiriki.
Katika kikao hicho, Waziri Sangu aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Habibu Awesi Mohamed, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji Zanzibar, Khalid Masoud Waziri, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Rashid Ali Salim, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Jane Songoro.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, leo Julai 8, 2026, jijini Doha, nchini Qatar.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akimkabidhi tuzo Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Samikh Al Marri, tuzo ya kutambua ushirikiano katika ya Tanzaniana Qatar katika masuala ya Ajira, leo Julai 8, 2026, katika Ofisi za Wizara hiyo ya Kazi Jijini Doha, nchini Qatar.
Munir Shemweta, Misungwi
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo amewatahadharisha viongozi wa vijiji nchini kuacha kujihusisha moja kwa moja na uuzaji wa ardhi bila kufuata taratibu za kisheria, akisema tabia hiyo imekuwa chanzo kikubwa cha migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini.
Dkt. Akwilapo ametoa onyo hilo Julai 6, 2026 wilayani Misungwi mkoani Mwanza wakati wa hafla ya kukabidhi hati 668 za hakimiliki za kimila kwa wananchi wa vijiji vya Ndinga na Lubuga. Alisisitiza kuwa viongozi wa vijiji, wakiwemo wenyeviti, ni wasimamizi wa ardhi na si wauzaji, hivyo maamuzi ya kuuza ardhi ya kijiji yanapaswa kufanywa kwa kufuata sheria kupitia mikutano ya vijiji na kupata ridhaa ya halmashauri husika.
"Mnapotaka kuuza ardhi kwa watu lazima kijiji kupitia mikutano ya kijiji na halmashauri kikubaliane na hilo. Asije akawa mwenyekiti anaingia kwenye makubaliano peke yake. Tunapiga vita suala hilo kwa sababu limetuingiza kwenye matatizo mengi katika maeneo mbalimbali," alisema Dkt. Akwilapo, akibainisha kuwa kauli hiyo inawahusu viongozi wa vijiji kote nchini na si Misungwi pekee.
Waziri huyo pia alisisitiza kuwa Serikali haitavumilia ubaguzi wa aina yoyote katika umiliki wa ardhi, ikiwemo ubaguzi wa kijinsia, kikabila au kwa misingi mingine. Alieleza kuwa sera na sheria za ardhi zinatambua haki sawa kwa wananchi wote kumiliki ardhi, huku wataalamu wa sekta hiyo wakitakiwa kuendelea kuzisimamia ipasavyo ili kuhakikisha haki inatendeka kwa kila Mtanzania.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Bi. Johari Simizi alisema wilaya hiyo kwa sasa ndiyo eneo linalopokea kasi kubwa ya ukuaji wa makazi kutoka maeneo mengine ya Mkoa wa Mwanza, hali inayohitaji upangaji bora wa matumizi ya ardhi.
Alisema wananchi wa Misungwi wanahitaji mji uliopangwa vizuri kupitia umilikishwaji rasmi wa ardhi ili kuondoa makazi holela na kuifanya wilaya hiyo kuwa na mwonekano unaovutia.
Naye Mbunge wa Jimbo la Misungwi, Mhe. Silvery Salvatory aliitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuongeza elimu kwa wananchi kuhusu matumizi na umuhimu wa nyaraka za umiliki wa ardhi, akisema baadhi ya wanufaika wa hati bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu haki na wajibu unaoambatana na nyaraka hizo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Mwanza, Bw. Wilson Luge aliwapongeza wananchi wa Misungwi kwa mwitikio mkubwa wa kushiriki zoezi la urasimishaji wa ardhi, akisema hatua hiyo imeifanya wilaya hiyo kuwa mfano wa kuigwa na maeneo mengine katika juhudi za kupunguza migogoro ya ardhi kupitia upimaji na utoaji wa hati za umiliki.
Kwa niaba ya wanufaika, Bw. Shije Mashaka aliishukuru Serikali kwa kuwawezesha wananchi kumiliki ardhi kwa hati za hakimiliki za kimila, akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa migogoro ya mipaka iliyokuwa ikiwasumbua kwa muda mrefu.
Katika utekelezaji wa mradi wa upangaji na upimaji ardhi, Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoa wa Mwanza iliipa kampuni ya GMS Geo Tech Consultancy Co. Ltd kazi ya kupima vijiji vya Ndinga na Lubuga, ambapo jumla ya hati 668 zilitolewa kwa wananchi katika awamu ya kwanza ya mradi huo.
Na.Ashura Mohamed-Arusha
Maonesho ya Sanaa ya Kazi za Ufundi,Uchoraji na Uchongaji yanatarajia kukutanisha zaidi ya wasanii 1500 duniani lengo likiwa ni kutangaza na kukuza saana ya Ufundi nchini ikiwa ni pamoja na kuwafungulia Masoko ya kimataifa wasanii hao.
Akizungumza Jijini Arusha na Waandishi wa Habari kuhusiana na Maonesho hayo,Makurugenzi mwenza wa Tanzania International Tourism Festival bwana Ibrahim Jama amesema wanalenga kutangaza utalii na utamaduni pamoja na vivutio vilivyo ndani ya nchi ya Tanzania.
"Katika kudumisha utalii,sanaa na utamaduni Wetu ni maonyesho haya yatakuwa yenye vivutio vya sanaa ya uchongaji na pia kutakuwa na warsha ya kuelekeza kuhusu sanaa nzima ya uchongaji yenye maelekezo ya elimu na Maendeleo na kulinda sanaa ya uchongaji."Alisisitiza Ibrahim
Pia amesema kuwa wasanii hao watapata fursa ya kupata ya kupata elimu kuhusu sanaa nzima mwenendo halisi wa soko la sanaa ndani ya nchi katika uchongaji na uchoraji na michezo kujua wajibu wao katika kuingiza kipato kikubwa haswa fedha za. kigeni.
Aidha Wadau ambao watashiriki mkutano huo watapata fursa ya kutembelea vivutio vilivyopo katika Mkoa wa Arusha ili kuendelea kuiunga Mkono serikali katika kuendeleza utalii wa ndani pamoja na maonyesho ya bidhaa za Uchoraji na Uchongaji yatakayofanyika kwa siku tatu.
Bi Rukia Walele ni Raisi wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA ) amesema kuwa Shirikisho hilo linaundwa na wachoraji,wachongaji,wasusi,wanaofuma vitambaa,Wanamitindo na wabunifu wa Mavazi na Viatu ambapo lengo ni kutoa elimu Maalum ya sekta ya Utalii ili kutumia majukwaa hayo kupata elimu zaidi na ushiriki wa kundi hilo bado sio wa kuridhisha.
Kupitia maonyesho hayo watawezeshwa kuingia katika mfumo rasmi wa kupata kipato na kupata Maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na kuliingizia Taifa fedha za kigeni.
Na OWM–TAMISEMI, Ifakara
Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ifakara wanatarajia kunufaika na huduma za kulaza wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Ifakara mara baada ya Serikali kuahidi kutoa Shilingi Milioni 700 ndani ya mwezi Julai, 2026 kwa ajili ya kukamilisha miundombinu muhimu itakayowezesha hospitali hiyo kuanza kutoa huduma hiyo kwa wagonjwa.
Ahadi hiyo ya Serikali imetolewa na Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Julai 6, 2026 akiwa kata ya Kiberege, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo, ambapo alipokea taarifa za utekelezaji wa miradi ya nyumba nne za Wakuu wa Idara, majengo matatu ya Hospitali ya Wilaya na Soko la Kiberege na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo.
Prof. Shemdoe amesema Serikali itapeleka Shilingi Milioni 700 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la utawala, chumba cha kuhifadhia maiti pamoja na njia za kupita (walkways) katika Hospitali ya Wilaya ya Ifakara, ili kuwezesha hospitali hiyo kuanza rasmi huduma za kulaza wagonjwa na kupunguza adha iliyokuwa ikiwakabili wananchi kutafuta huduma hizo mbali na maeneo yao.
Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, fedha hizo zinaakisi dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuimarisha huduma za afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na makazi yao na kuongeza kuwa, wananchi wanapaswa kuendelea kulinda amani na utulivu uliopo ili Serikali iendelee kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya umma na taifa.
"Fedha hizi ni ishara ya upendo wa Rais Samia kwa wananchi wa Ifakara. Anawapenda na ameazimia kuona huduma za afya zinaboreshwa na maisha ya wananchi yanabadilika kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo," amesema Prof. Shemdoe.
Mbali na sekta ya afya, Prof. Shemdoe amesema Serikali itatoa Shilingi Milioni 330 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mkasu kama ilivyotoa Shilingi Milioni 191 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa soko la Kiberege, miradi inayolenga kuboresha huduma ya usafiri na usafirishaji, biashara pamoja na kuinua uchumi wa wananchi.
Akizungumzia utekelezaji wa ujenzi wa barabara zenye urefu kilomita 10, Prof. Shemdoe amemuelekeza Mhe. Sultan Kwanja, Diwani wa Kata ya Kiberege kuweka kipaumbele katika ujenzi wa barabara zinazoelekea kwenye maeneo yenye shughuli za kilimo ili kurahisisha usafirishaji wa mazao na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi.
Kwa upande wake, Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, amesema ziara ya Mhe. Prof. Shemdoe imelenga kutatua changamoto za wananchi na si kufanya ziara zenye mlengo wa kuwahadaa wananchi.
"Waziri wa TAMISEMI hajaja kufanya sanaa; amekuja kushughulikia changamoto za wananchi, ndiyo maana aliposikia changamoto ya barabara ameambatana na Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro pamoja na Meneja wa TARURA Wilaya ya Ifakara ili kuhakikisha suala hilo linapatiwa ufumbuzi," amesema Mhe. Malima.
Naye, Mhe. Abubakari Asenga, Mbunge wa Jimbo la Ifakara, amewahakikishia wananchi kuwa ujenzi wa barabara za mitaa utasimamiwa kwa karibu chini ya uongozi wa Prof. Shemdoe, akibainisha kuwa mafanikio yaliyopatikana katika upatikanaji wa fedha za soko la Kiberege yanaonesha dhamira ya Serikali ya kutekeleza pia miradi mingine ya maendeleo.
Akiwa wilayani Ifakara, Prof. Shemdoe amekagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo nyumba nne za wakuu wa idara, majengo matatu ya hospitali ya wilaya ya Ifakara na soko la Kiberege, ikiwa ni pamoja na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma.
Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu na Ubora wa WRRB, Bw. Mwita Thomas,akizungumza wakati wa ufungaji mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika Morogoro.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.
Na.Mwandishi Wetu-MOROGORO
Watumishi na wasimamizi wa shughuli za ghala nchini wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji ili kuimarisha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuongeza ufanisi katika biashara ya mazao ya kilimo.
Wito huo umetolewa na Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, alipokuwa akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo.
Bi. Chatta amesema uadilifu wa watendaji wa mfumo ni msingi wa kujenga imani kwa wakulima, wanunuzi na taasisi za fedha, huku akisisitiza kuwa Mfumo huo umeendelea kuwa nyenzo muhimu ya kuhakikisha biashara ya mazao inafanyika kwa uwazi, ubora na ushindani.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhimiza matumizi ya Mfumo huo pamoja na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) ili kuongeza thamani ya mazao, kupanua fursa za masoko yenye ushindani na kuongeza manufaa kwa wakulima.
Aidha, amewataka washiriki kutumia maarifa waliyoyapata kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kuendana na mabadiliko ya teknolojia na kuhakikisha taarifa za mazao zinakuwa sahihi na kwa wakati.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu na Ubora wa WRRB, Bw. Mwita Thomas, amewataka wahitimu wa mafunzo hayo kuzingatia sheria, kanuni na taratibu walizofundishwa ili kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji, pamoja na kulinda hadhi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.
Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na WRRB yamefanyika kwa siku tano na yamehudhuriwa na washiriki 103 kutoka kampuni za uendeshaji wa ghala na wadau mbalimbali wa Mfumo huo.
Siku zote alikuwa miongoni mwa wale wanaopinga imani yoyote inayohusiana na mambo ya kiroho au usaidizi wa kipekee nje ya hospitali na sheria za kawaida.
Lakini maisha ni walimu wakubwa kuliko vitabu. Na wakati mwingine, hata wasioamini, hupata sababu ya kufikiri upya. Brian alikuwa kwenye uhusiano wa muda mrefu na msichana aitwaye Hellen. Walikuwa kama mfano wa wapenzi bora mitandaoni. Picha za mapenzi, safari, zawadi ilikuwa ni hadithi ya kisasa ya upendo.
Hata hivyo, mambo yalianza kubadilika mwaka jana, pale Brian alipogundua kwamba Hellen alikuwa akiongea kwa karibu sana na jamaa mmoja wa kazini kwake. Awali alipuuzia, akiamini ni wivu tu wa kawaida. Lakini alipoanza kuona ujumbe mfupi wa siri, mazungumzo ya sauti usiku wa manane, na safari za ghafla zisizoelezeka, alijua kuna jambo. SOMA ZAIDI.
Nilijaribu njia nyingi za kujitibu, nikitembelea madaktari na kutumia dawa za hospitali, lakini hakuna kilichobadilika. Nilikuwa nikikosa usingizi na kujikuta nikiishi na hofu ya kila wakati. Hali hii ilianza kuathiri maisha yangu ya kila siku, hata kazi yangu.
Nilikuwa mchovu, mwenye huzuni, na nashindwa kuendelea mbele. SOMA ZAIDI.
Nilijaribu kila njia. Nilihudhuria kliniki za kibingwa, nikatumia dawa za gharama kubwa, nilijaribu hata mashine maalum za mazoezi ya nyonga. Madaktari walinitia moyo kuwa inaweza kuisha kwa muda, lakini mwaka ulipita baada ya mwingine, hali haikubadilika.
Nilijiepusha na mahusiano ya karibu, nikaacha safari za usiku, na hata kazi zilizoitaji kulala nje niliziacha all kwa sababu ya haya. Mara moja nikiwa kazini, niliitwa kwenye kikao cha wafanyakazi cha kusafiri nje ya jiji. Kwa kisingizio cha afya, niliomba nisiende.
Lakini macho ya baadhi ya wenzangu yalinielekea kwa mashaka. Nilihisi kama watu walikuwa wakianza kugundua kuwa kuna kitu kisicho cha kawaida kwangu. Ukweli ni kwamba nilikuwa nimechoka kujificha. Nilihitaji mabadiliko. SOMA ZAIDI.
Wafugaji nchini wanatarajiwa kunufaika na biashara ya kisasa ya mifugo baada ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kuanza kuingiza mifugo katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, utakaounganisha taarifa za mifugo kidijitali na kuwawezesha wanunuzi kushindana kwa uwazi kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).
Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema baada ya mafanikio ya kusimamia bidhaa 18 za mazao ya kilimo kupitia mfumo huo, sasa bodi imepanua huduma zake kwa kujumuisha mifugo.
Amesema hatua hiyo inatokana na mahitaji ya wafugaji waliokuwa wakihoji kwa nini mfumo huo unawanufaisha wakulima pekee huku sekta ya mifugo ikibaki nje.
"Tumekuja na bidhaa mpya ambazo zimeongezwa kwenye mfumo, na kubwa zaidi tumewafikia wafugaji. Tulikuwa tunasimamia bidhaa 18 za mazao ya kilimo, lakini sasa tumeingia rasmi kwenye bidhaa za mifugo," amesema.
Bw. Bangu amesema WRRB inalenga kuunganisha biashara ya mifugo na TMX, ambapo taarifa za kila mnyama zitawekwa kidijitali ili wanunuzi waweze kuzifikia kwa urahisi, kushindana kwa uwazi na kufanya maamuzi ya ununuzi kwa kutumia taarifa sahihi badala ya makadirio.
Ameeleza kuwa mfumo huo utatumia taarifa zinazopatikana kupitia hereni za utambuzi wa mifugo zilizozinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ambazo zina namba maalumu zinazobeba taarifa za kila mnyama.
"Tunafahamu Mheshimiwa Rais Samia miaka miwili iliyopita alizindua uwekaji wa hereni kwenye mifugo. Sisi kama WRRB tunapiga hatua zaidi kwa kutumia taarifa zilizopo kwenye hereni hizo kuingiza mifugo kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala. Hereni hiyo ndiyo itakuwa msingi wa stakabadhi kwa kuwa ina namba na taarifa zote za mnyama," amesema.
Amefafanua kuwa mfumo huo utawanufaisha wafugaji wanaojishughulisha na unenepeshaji wa mifugo kwa kuwa mifugo yao itahifadhiwa katika maeneo maalumu yatakayokuwa yanatambulika kama ghala, huku wafugaji wakipewa stakabadhi zitakazowawezesha kupata mikopo kutoka taasisi za fedha.
Kwa mujibu wa Bangu, WRRB tayari imefikia makubaliano na Benki ya NBC ambayo imekubali kutoa mikopo kwa wafugaji watakaoweka mifugo yao kwenye ghala.
"Wengi wanauliza ghala litakuwaje. Kwa upande wa mifugo, zizi ndilo litakuwa ghala. Mifugo itatunzwa katika maeneo maalumu yenye chakula na huduma za matibabu, huku mfugaji akiwa na stakabadhi inayomwezesha kupata fedha bila kulazimika kuuza mifugo yake mapema," amesema.
Bangu amesema hatua nyingine muhimu ni kuondoa utaratibu wa kupanga bei kwa kutazama mwonekano wa mnyama pekee, badala yake mifugo itapimwa kwa uzito ili bei iweze kuamuliwa kwa kuzingatia kilo halisi za mnyama.
"Leo hii kwenye minada mingi ng'ombe anapimwa kwa macho, anaonekana mnene au mwembamba ndipo bei inawekwa. Sisi tunataka mifugo ipimwe kwa uzito ili bei iwe ya haki kwa mfugaji na mnunuzi. Hii itakuwa mkombozi mkubwa kwa wafugaji na pia itarahisisha upatikanaji wa taarifa zinazohitajika katika masoko ya ndani na kimataifa," amesema.


Serikali imewaagiza wazalishaji wote nchini kutumia alama ya 'Made in Tanzania' ili kuongeza imani kwa bidhaa zinazozalishwa nchini na kuimarisha ushindani wake katika masoko ya kimataifa.
Agizo hilo limetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Immanuel Nchimbi, kwenye kilele cha Usiku wa Jubilei ya Dhahabu (Miaka 50) ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), uliofanyika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam. Sherehe hizo zilienda sambamba na utoaji wa tuzo kwa washirika muhimu wa mamlaka hiyo. Udhibiti wa Viwango na Huduma za Kifedha.
Aidha, Makamu wa Rais amezitaka taasisi zinazosimamia viwango na huduma za kifedha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha bidhaa za Tanzania zinakidhi viwango vya kimataifa. Alisema matumizi ya alama ya 'Made in Tanzania' yataongeza utambulisho wa bidhaa zenye ubora na kuimarisha heshima ya taifa katika biashara za kimataifa.
"Nazipongeza taasisi za fedha kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa viwanda vidogo na vya kati, akisema hatua hiyo imeendelea kupunguza changamoto za upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali na kuchochea ukuaji wa uzalishaji nchini."amesema Balozi Nchimbi
Amesema Serikali itaendelea kuweka sera rafiki, kuboresha miundombinu na kuimarisha sekta binafsi ili kujenga uchumi wa viwanda wenye ushindani. Ameongeza kuwa maadhimisho ya Jubilei ya Dhahabu ya TANTRADE ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana, ikiwemo kuongezeka kwa viwanda, uzalishaji, ajira na upanuzi wa masoko ya bidhaa za Tanzania duniani.
Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga (Mb), amesisitiza kuwa manufaa makubwa ya rasilimali zilizopo nchini yatapatikana Tanzania itakapowekeza katika kuchakata na kuzalisha bidhaa za mwisho zenye ubora wa juu badala ya kuuza malighafi ghafi nje ya nchi.
Waziri Kapinga amebainisha kuwa hatua hiyo itafungua masoko mapya, itaongeza thamani ya mauzo ya nje, na kuinua uchumi wa wananchi kwa ujumla.
Mhe. Kapinga ameeleza kuwa, ili kujenga uchumi imara wa viwanda na wenye ushindani, kuna haja ya kubadili mtazamo wa kibiashara kwa kuhakikisha mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi, misitu na madini yanageuzwa kuwa bidhaa zilizofungashwa vizuri na kukidhi viwango vya kimataifa.
Amesisitiza kuwa uwekezaji mkubwa katika teknolojia za kisasa una mchango mkubwa katika kuongeza kiwango cha uzalishaji, kuboresha ubora wa bidhaa zinazotengenezwa nchini, kupunguza gharama za uendeshaji, na kuzipa bidhaa za Tanzania uwezo mkubwa wa kushindana katika soko la kimataifa.













