📌Yawasha umeme ukanda wa Nyasa kitongoji cha Nkanda
📌Yapongezwa kufikisha umeme kwenye mazingira magumu Njombe
📌Bodi ya REA yasisitiza wananchi kuchangamkia fursa uwepo wa nishati ya umeme
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijni (REA), unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa na watakaopewa zabuni ya kutekeleza miradi ili kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi.
Hayo yamebainishwa leo Mei 25, 2026 na Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), wakati wa hafla ya kukagua miradi, kutembelea na kuwasha umeme kitongoji cha Nkanda kilichopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe mradi uliokuwa unatekelezwa na Suma Jkt Electric Company Ltd.
Mha. Ahmed Chinemba amesema kuwa, mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji vya mwambao wilayani Ludewa unatekelezwa na mkandarasi M/S SUMAJKT ELECTRIC COMPANY LTD kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2 ili wananchi wa mwambao wapate huduma ya umeme.
"Mradi huu umelenga kuongeza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa kitongoji cha nkanda ukiwa na chachu ya kutoa fursa za kibiashara kwa kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kurahisiha upatikanaji wa huduma za kijamii na uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo kama mashine za kusaga, mashine za kuchana mbao pamoja na mashine za kuchomelea," Amesema Mha. Chinemba.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Suma JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi, ameishukuru REA kwa kuwapatia kazi hiyo ya kufikisha umeme katika maeneo ya mwambao kikiwemo kitongoji hicho cha Nkanda ambapo kazi imekamilika kwa ubora.
"Sisi Suma JKT tumefanisha kufikisha umeme kwenye mazingira magumu kama haya ambayo yalikuwa na changamoto nyingi lakini tumefanikiwa na sasa tunaona matunda yake, " Amesema Brigedia Jenerali Lupi.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mha. Deogratius Nagu amesema katika kitongoji cha Nkanda takribani shilingi milioni 450 zimetolewa na Serikali kupitia REA ili kufikisha huduma ya umeme katika kitongoji hicho.
Aidha, amewataka wananchi wa Nkanda kuchangamkia fursa ya uwepo wa umeme kwa kuhakikisha wanafanya wiring katika nyumba zao na kuunganisha umeme kwa wingi ili wanufaike na umeme huo katika kitongoji chao.
Naye, Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo hilo Bw. Stanslaus Gowele amesema ujio wa umeme maeneo ya mwambao yanakwenda kuongeza chachu ya Maendeleo kiuchumi na kijamii kwa wananchi hao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa lei Mei 25, 2026 akipanda mti aina ya mwembe katika eneo la Shule ya Sekondari ya Ndaoya, Mtaa wa Chongoleani jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026
....
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa amezitaka halmashauri, taasisi binafsi, mashirika mbalimbali pamoja na wananchi kuendelea kushirikiana na na Serikali katika kuhakikisha maeneo yanakuwa safi na salama.
Ametoa rai hiyo wakati akizungumza na wananchi mara baada ya kuongoza zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira jijini Tanga leo Mei 25, 2026 kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.
Mhe. Kwagilwa alisema kuwa katika suala la usafi wa mazingira sekta binafsi ina nafasi kubwa ya kuwekeza katika teknolojia na mifumo bora ya usimamizi wa taka na urejelezaji ili kupunguza athari za taka kwa mazingira.
Alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha mazingira yanakuwa safi kuanzia nyumbani, maeneo ya biashara, taasisi, masoko hadi maeneo ya wazi huku akiwataka wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya mifumo ya ukusanyaji na utupaji wa taka pamoja na kuepuka vitendo vya uchafuzi wa mazingira.
“Mazingira machafu yana athari kubwa kwa afya na uchumi wa jamii. Uwepo wa taka ovyo, mifereji iliyoziba na uchafuzi wa mazingira huchangia kuenea kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu, malaria na magonjwa ya mlipuko. Hivyo, shughuli ya leo isiwe ya siku moja tu, bali iwe sehemu ya utamaduni wetu wa kila siku,” alisistiza.
Halikadhalika, Mhe. Kwagilwa alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa zitokanazo na taka ikiwemo uzoaji na urejelezaji wa taka ili kuzalisha mbolea, vyakula vya mifugo na bidhaa za viwandani.
Aliwapongeza wadau mbalimbali ambao wamebadilisha changamoto za taka kuwa fursa na kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika viwanda vya kurejeleza taka akisema kuwa hatua hiyo inachangia upatikanaji wa ajira, kuongeza kipato na kukuza uchumi kwa wananchi.
Pamoja na jitihada hizo za wadau, Naibu Waziri huyo alisema Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kupambana na uchafuzi wa mazingira kwa kuandaa na kutekeleza Mwongozo wa Usimamizi wa Taka Ngumu (Punguza, Tumia Tena na Rejeleza) wa Mwaka 2021.
Aliongeza kuwa sekta binafsi na asasi za kiraia zimeendelea kutekeleza mwongozo huo ambapo baadhi ya viwanda vinavyozalisha bidhaa zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki vimeungana pamoja katika kutekeleza Mpango wa Wajibu wa Wazalishaji wa Kusimamia Taka zinazotokana na bidhaa za wanzozalisha kwa kuondosha taka hizo kwenye Mazingira.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Dadi Kolimba Mhe. Dadi Kolimba alisema mkoa huo umeendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kufanya usafi katika maeneo yao.
Alisema kuwa wananchi wa Jiji la Tanga kila mwisho wa mwezi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hushiriki zoezi la usafi wa mazingira na kuondoa uchafu unaozalishwa katika mitaa ya jiji hilo.
Pia, Mhe. Kolimba alitumia nafasi hiyo kupongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuratibu shughuli za usafi na uhifadhi wa mazingira kupitia zoezi la upandaji wa miti hususan kwa kila halmashauri kupanda miti milioni moja na nusu kila mwaka.
Itakumbukwa kwamba kilele cha Siku ya Mazingira kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026 na kaulimbiu ni ‘‘Dira 2050, Tuwajibike Kukijanisha Tanzania’’ ikilenga kuhamasisha jamii kushirki kikamilifu katika kuleta mageuzi na kuwajibika katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akiongoza zoezi la usafi wa mazingira lililohusisha uokotaji wa taka na kusafisha mifereji ya maji machafu katika eneo la Taifa Road ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa lei Mei 25, 2026 akipanda mti aina ya mwembe katika eneo la Shule ya Sekondari ya Ndaoya, Mtaa wa Chongoleani jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akizungumza na wananchi katika uwanja wa Tangamaano jijini Tanga mara baada ya zoezi la usafi wa mazingira lililohusisha uokotaji wa taka na kusafisha mifereji ya maji machafu katika eneo la Taifa Road ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa leo Mei 25, 2026 akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian alipowasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa kabla ya zoezi la upandaji miti na usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitafanyika jijini Dodoma Juni 05, 2026.
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amewataka Wafanyakazi wa MNMA kuendelea kufanya kazi kwa furaha, Uadilif na kuweka maslahi ya Taasisi mbele kwa kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa Wanafunzi na Watumishi kwa moyo na kufanya hivyo ni utumishi kama ilivyo utumishi wa Mungu, kwani kila kazi unayoifanya kwa ajili ya watu basi hiyo ni kazi ya Mungu.
Prof.Mapesa ameyasema hayo leo wakati wa kuwapongeza Watumishi hodari katika uwajibikaji wa utumishi wa umma kwa mwaka 2025/2026 kwa wale wote waliopata fursa ya kuwa Wafanyakazi bora, na kusisisitiza kuwa Watumishi waendelee kufanya kazi kwa kuzingatia Misingi ya utumishi wa umma na huo ndiyo uwe utamaduni wa kila siku.
Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaaluma Prof. Richard Kangalawe amesema Ushindi ni heshima huku akiwataka watumishi wengine kuendeela kuwajibika katika nafasi zao kwa lengo la kutimiza malengo ya Taasisi.
Naye Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Mipango, Fedha na Utawala Prof.Evaristo Haulle alisema mchakato wa kupata Mfanyakazi bora ulikuwa ni wa huru na haki ambapo vigezo mbalimbali vilizingatiwa ikiwemo Nidhamu ya mtumishi , Utendaji kazi wa mtumishi,(PEPMIS) na Mienendo mbalimbali, hivyo dosari zote zilizojitokeza zilishughulikiwa ipasavyo.
Nao viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Debora Donati wa THTU na kwa upande wa RAAWU Hashimu Mtongola kwa pamoja wameipongeza Menejimenti kwa hafla hiyo fupi ambayo inatoa motisha na kuongeza morali ya kazi kwa Wafanyakazi na pia wameomba uongozi ufikirie kujumuisha Wafanyakazi wote kwa hafla ya namna hiyo wakati mwingine.
Wafanyakazi bora wa Taasisi kwa mwaka huu Filbert Nyakasi upande wa Wanataaluma na Amedeus Mchau upande wa Waendeshaji wameshukuru uongozi kwa kutambua jitihada zao na mchango wao katika kutimiza majukumu ya kila siku na wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa Uadilifu, Nidhamu kwa kushirikiana na Wafanyakazi wengine.
Wafanyakazi wote hodari wamentunukiwa vyeti vya kutambuliwa na zawadi ya fedha, ambapo zoezi limejumuisha Wafanyakazi wote bora wa Kampasi ya Kivukoni, Karume na Pemba.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
ChUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE
25.05.2026
Washiriki zaidi ya 300 wameshiriki mbio fupi za kilomita 5 katika bonde la Olduvai Ngorongoro kwa lengo la kutangaza vivutio vya asili vya Olduvai na Laetoli ambapo historia ya Binadamu wa Kale ilianzia.
Akizungumza kwa Niaba ya Kamishna wa Uhifadhi kwenye tukio hilo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za Utalii na Masoko Mariam Kobelo ameeleza kuwa
Ngorongoro kwa kushirikiana na Cape to Cairo Marathon imefanya mbio hizo ili kuonesha utajiri wa utalii wa asili, historia, urithi wa utamaduni na mambo kale uliopo Olduvai na Laetoli kama Nyumbani kwa asili ya Binadamu. Ameongeza kuwa Ngorongoro ni Nyumbani kwa Nyumbu wanaohama kwa kuwa pumzi ya kwanza ya ndama kupigwa mhuri kabla ya kuhamia maeneo mengine safari yao huanzia Ndutu Ngorongoro.
"Ngorongoro ni Nyumbani kwa asili ya binadamu kisayansi, Ni nyumbani kwa Nyumbu wanaohama kila mwaka, ni nyumbani kwa Spinshi ya Ndege zaidi ya 500, ni nyumbani kwa Wanyama wakubwa watano, kiufupi eneo la Ngorongoro ni Nyumbani kwa mkusanyiko wa Vitu vingi ndio maana tunawaambia wadau wote ndani na nje ya Nchi kuwa Wonders Are Calling" ameongeza Kamishna Kobelo.
Mkurugenzi wa Cape to Cairo Arusha International Marathon, Timothy Mdinka ameeleza kuwa lengo la mbio hizo ni kutangaza mazao mapya ya Utalii yaliyopo Tanzania na Bara la Africa kwa Ujumla kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo Michezo kama mbio ambayo imefanyika leo Olduvai pamoja na marathon ya Cape to Cairo itakayofanyika tarehe 31 Mei, 2026.
Mbio hizo zimejumuisha wadau mbalimbali wakiwepo Ngorongoro, Cape to Cairo international Marathon, Karatu Runners, Amani Collection, CRDB, UNDP, NHIF, Diplomatic and Tourism Police Arusha
Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Isack Joseph Copriano amesimamisha uuzaji wa ardhi katika kata ya Esilale huku akita maeneo yote ya malisho kuhakikiwa upya na idara ya ardhi wilaya ya Monduli.
Yote hayo yanajiri mara baada kundi la wamama zaidi 200 kutoka majumbani kwao na kwenda kukaa eneo la Losirwa lililouzwa kinyemela na kupaza sauti zao kuiomba serikali kuingilia kati na ili kurejeshewa eneo lao muhimu la malisho.
Mhe.Isack amesisitiza kuwa amefanya hivyo kwasababu yeye ni mwakilishi wa wananchi nani mtu namba moja anayetetea maslahi ya wananchi wake wa jimbo la Monduli.
“Ili kujiridhisha eneo hili ni mali ya wanakijiji kesho nendeni na wekeni Vibao vitakavyo onyesha eneo hili ni eneo la Malisho na ogopa matapeli eneo hili haliuzwi!.
Nae Mwenyekiti wa sasa wa kijiji hicho Bwana Yamat amesema anatambuq kuwa eneo hilo kama eneo la malisho na kuwataka wananchi kijiji hicho kuwachukia watu waliouza eneo hilo la Malisho.
Hata hivyo wanachi hao walifikisha kero yao kwa Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Isack Joseph Copriano na kumuomba awasaidie kurejesha eneo lililouzwa na watu wasio julikana.
Katika ziara hiyo Mbunge wa jimbo la Monduli amembatana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Monduli Mhe. Kisioki Moitiko.
WANAUME 300 WATEMBELEA MAKUMBUSHO YA JIOPAKI YA NGORONGORO -LENGAI,WAVUTIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA
Kumekuwa na mwitikio mkubwa wa watalii wa ndani kutembelea hifadhi ya Ngorongoro hii ikimaanisha wanarudi nyumbani eneo ambalo ndilo pekee lenye ushahidi wa kisayansi usiotiliwa shaka kuwa ndio chanzo cha binadamu wa kale.
Safari hii ni zamu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT ) chini ya Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo Usharika wa Kijitonyama jijini Dar es Salaam Rev, Dr. Elliona Kimaro aliyeongoza kundi la wanaume 300 kutoka mikoa mbalimbali nchini kutembea Makumbusho ya Jiopaki ya Ngorongoro-Lengai (Urithi Geopark) na vituo vya hifadhi vilivyopo Ngorongoro
Akiwa na Ujumbe huo Dkt. Kimaro amesema makundi mbalimbali kuhamasika kufanya utalii wa Ndani wanavutiwa na vitu mbalimbali ikiwemo kushuhudia uumbaji wa Mungu, kuona na kujifunza Chanzo cha asili ya Mwanadamu katika bonde la Olduvai na Laetoli, kuona Ikolojia ya hifadhi pamoja na utunzaji wa Mazingira kama vitabu vitakatifu vinavyohimiza.
"Tumekuja Nyumbani Ngorongoro kwenye asili ya Mwanadamu tukiwa na kundi la wanaume 300, tumeshuhudia uumbaji wa Mungu, utunzaji wa Ikolojia, Mazingira, Misitu Wanyama wa kila aina ya vyote vilivyoumbwa kwa mfano wa Mungu" alisema Dkt. Kimaro.
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inawarudisha nyumbani binadamu wote ili kushuhudia asili yao ambapo binadamu alianza kutembea na kufanya shughuli zake kwa miguu miwili.
Dar es Salaam
Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Jubilei ya Dhahabu ya miaka 50 ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), mwaka huu wadau wa biashara, wawekezaji, wabunifu na wananchi wanatarajiwa kushuhudia tukio la kipekee la kihistoria litakalojulikana kama “Sabasaba Golden Night”, Usiku wa Tuzo utakaofanyika tarehe 6 Julai 2026, usiku huu maalum wa dhahabu unalenga kusherehekea mafanikio, ubunifu na mchango wa maonesho hayo katika kukuza biashara na uchumi wa Tanzania kwa zaidi ya nusu karne.
Aidha,Uzinduzi wa Sabasaba Golden Night umebeba taswira mpya ya Maonesho ya Sabasaba ya mwaka 2026, ukiahidi burudani ya kiwango cha juu, mwangaza wa kipekee, maonesho ya kisasa, kutambua wadau waliotoa mchango mkubwa katika safari ya miaka 50 pamoja na kuunganisha sekta za biashara, uwekezaji na ubunifu chini ya jukwaa moja. Tukio hilo linatarajiwa kuwa moja ya vivutio vikubwa ndani ya Maonesho ya 50 ya Jubilei ya Dhahabu, yakiyotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 28 Juni hadi 13 Julai, 2026.
Akizungumza Mgeni Rasmi Mhe. Dennis Londo amesema Tuzo hizo zitakazotolewa Mwaka huu zinalenga kuonesha ni kwa namna gani Sekta ya Biashara imekua kupitia maonesho ya Biashara ya Sabasaba na namna ambavyo Maonesho haya yamekuza maelfu ya wafanyabiashara amba sasa ni wakubwa.
Aidha Dkt.Latifa Mohammed Khamis Mkurugenzi Mkuu wa Maendeleo ya Biashara Tanzania ameeleza kuwa “Usiku wa Dhahabu” si burudani pekee, bali ni ishara ya heshima kwa safari ya mafanikio ya Sabasaba tangu kuanzishwa kwake, sambamba na kufungua ukurasa mpya wa fursa za biashara, teknolojia na ushirikiano wa kimataifa. Wageni watakaohudhuria watapata nafasi ya kushuhudia historia ikikutana na ubunifu wa kizazi cha sasa katika mazingira yatakayobeba hadhi ya Jubilei ya Dhahabu. “Sabasaba 2026 KUBWA KULIKO


>Sheria Isichague Chama
NA OSCAR ASSENGA, TANGA
Katibu Mkuu wa Chama cha NLD, Doyo Hassan Doyo, amesema mjadala unaoendelea kuhusu hatua zinazochukuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa umeonyesha jinsi baadhi ya Watanzania wanavyotoa hukumu za haraka bila kutafakari misingi ya sheria.
Doyo alisema kumekuwa na mtazamo kwamba Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inalenga zaidi vyama vya upinzani, huku ukweli ukiwa ni kwamba taasisi hiyo inasimamia sheria bila kuangalia itikadi ya chama husika.

Akizungumza wakati wa ziara ya chama hicho mkoani Tanga, alisema hatua zilizochukuliwa hivi karibuni dhidi ya baadhi ya viongozi wa kisiasa zinatokana na matamshi yaliyotafsiriwa kuwa na viashiria vya uvunjifu wa sheria za vyama vya siasa.
“Sheria iko wazi. Chama au kiongozi anayekiuka taratibu anaweza kupewa adhabu ya faini, kusimamishwa shughuli au hata kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria. Hii siyo kwa chama fulani pekee,” alisema.

Alieleza kuwa baada ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoa kauli zilizozua mjadala, Ofisi ya Msajili iliwaandikia barua ya kutaka maelezo. Hatua hiyo, kwa mujibu wa Doyo, ilitafsiriwa vibaya na baadhi ya wananchi pamoja na wanaharakati waliodai kuwa upinzani unaonewa.
Hata hivyo alisema hali hiyo imebadilika baada ya mmoja wa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) naye kuandikiwa barua kufuatia matamshi yake ya kisiasa.
“Watu walidhani sheria inafanya kazi kwa upande mmoja, lakini sasa imeonekana wazi kuwa anayevunja sheria ndiye anayechukuliwa hatua, bila kujali anatoka chama gani,” alisema.
Doyo alisema vyama vya siasa vinapaswa kutambua kuwa vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria na hivyo vina wajibu wa kuendesha shughuli zake ndani ya mipaka ya kisheria.
Alionya kuwa siasa zisizo na nidhamu zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani na kuhatarisha usalama wa Taifa.
“Ukianza kufanya siasa nje ya sheria, maana yake unaondoka kwenye misingi ya kisiasa na kinachofuata ni migogoro na vurugu. Taifa haliwezi kujengwa kwa misingi ya shinikizo na vitisho,” alisema.

Aidha, aliitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuendelea kusimamia sheria kwa uthabiti bila kuogopa presha za kisiasa kutoka kwa wanasiasa au wanaharakati.
Kwa mujibu wa Doyo, uwepo wa taasisi imara zinazotekeleza sheria kwa haki ndiyo msingi wa kulinda amani na utulivu wa nchi.
Katika ziara hiyo ya NLD iliyoanzia Pangani na kuelekea Lushoto, chama hicho kimesema kinaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria, taratibu na kanuni za kisiasa ili kuimarisha demokrasia na mshikamano wa Taifa.













.jpeg)












