Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 26, 2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam kuhusu kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Akizungumza na wanafunzi hao,Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bi.Techla Kitosi,amesisitiza umuhimu wa watumiaji kuwa na uelewa wa haki zao wanaponunua bidhaa au huduma. Ameeleza kuwa mlaji ana haki ya kupata bidhaa bora, salama na zenye ubora unaokubalika.

Aidha ameonya dhidi ya ununuzi wa bidhaa bandia ambazo zinaweza kuhatarisha afya na usalama wa mtumiaji.

“Ni muhimu sana kwa kila mmoja wenu kujifunza kutambua bidhaa halisi na bandia. Msikubali kudanganywa na bei ndogo bila kuangalia ubora wa bidhaa,” amesema Bi.Kitosi

Kwa upande wake, Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi, Magdalena Hall, ameeleza wajibu wa mlaji kuwa ni pamoja na kusoma maelekezo ya matumizi ya bidhaa, kuhifadhi stakabadhi za manunuzi na kutoa taarifa pale wanapokutana na bidhaa zisizo na viwango.

Hata hivyo Bi.Hall ,amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wa ulinzi wa mlaji katika jamii zao kwa kutoa elimu kwa familia na marafiki kuhusu madhara ya bidhaa bandia.

Wanafunzi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali na kupewa majibu ya kina, jambo lililosaidia kuongeza uelewa wao kuhusu masuala ya ulinzi wa mlaji.

Elimu  hiyo ni sehemu ya jitihada za Tume ya Ushindani kuendelea kutoa elimu kwa umma, hususan vijana, ili kujenga jamii yenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi wanaponunua bidhaa na huduma.

Mafunzo hayo ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi kutoka FCC, Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja iliyopo jijini Dar es Salaam iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Wanafunzi Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ikiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), imeridhia Randama ya mpango wa bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2026/2027 Machi 26, 2027 Bungeni jijini Dodoma

Katika michango yao, Wajumbe wa Kamati hiyo walionyesha kuridhishwa na vipaumbele vya Mpango wa Bajeti hiyo ya mwaka 2026/2027, huku wakimpongeza Waziri Kapinga kwa uwasilishaji wenye maono mapana yanayolenga kukuza sekta ya viwanda na biashara nchini. Pamoja na pongezi hizo, Kamati ilitoa miongozo na ushauri wa kimkakati uliolenga kuboresha mazingira ya biashara, na viwanda nchini.

Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), alibainisha kwa kina kuwa vipaumbele vya kimkakati vitakavyopewa uzito katika Mpango wa bajeti wa 2026/2027, pamoja na mchanganuo wa fedha zinazohitajika kutekeleza majukumu hayo.

Uidhinishaji wa makadirio hayo unafungua milango kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kuanza maandalizi ya mwisho ya Hotuba ya Bajeti itakayowasilishwa rasmi na katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Mkutano wa bajeti.

       

  


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) Alban Kihulla amewaelekeza wajumbe wa 

menejimenti ya Wakala hiyo kuwa na majadiliano ya wazi na yenye tija yanayolenga kuboresha zaidi huduma kwa wananchi hivyo kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kujenga nchi.

Ametoa wito huo mapema leo Machi 26, 2026 wakati akifungua   kikao kazi cha Menejimenti kilichoketi kupitia utekelezaji wa mpango na bajeti ya mwaka 2025/26 na kupitia mpango na bajeti wa mwaka wa fedha 2026/27.

"Majadiliano yetu yawe ya wazi na kila mmoja atoe mchango wenye tija kwa manufaa ya Taifa letu," amesisitiza.

Aidha, Mtendaji Mkuu Kihulla amewataka wajumbe wa kikao hicho kinachofanyika katika ukumbi wake wa Makao Makuu, eneo la Medeli Dodoma, kuhakikisha wanaudadavua na kuuchambua kwa kina mpango na bajeti ya mwaka wa fedha ujao ili kuwezesha utekelezaji wenye tija.

Wakala wa Vipimo iko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara na ina jukumu kuu la kumlinda mlaji kupitia uhakiki na usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, amefanya kikao kazi na watumishi wa taasisi hiyo kutoka kampasi zote, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, umoja na mshikamano katika kufanikisha malengo ya taasisi.

WATUMISHI  wa Tume ya Ushindani Ofisi ya Kanda ya Ziwa wametoa elimu kwa wadau mbalimbali, wakiwemo wanafunzi, waandishi wa habari na wafanyabiashara, walipotembelea Banda la Kliniki ya Walaji katika Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.

Banda hilo limegeuka kuwa kitovu cha maarifa, likiwavutia wengi waliotaka kuelewa kwa undani haki zao kama walaji pamoja na namna bora ya kushiriki katika soko kwa uadilifu na uelewa mpana.

Akitoa elimu hiyo, Mkuu wa Kanda ya Ziwa FCC, Bw. Mdimi, amesisitiza umuhimu wa walaji kuwa na uelewa wa haki zao ili kujilinda dhidi ya bidhaa duni, huduma zisizo na viwango na vitendo vya udanganyifu vinavyoweza kujitokeza sokoni.

"Amebainisha kuwa elimu kwa walaji ni silaha muhimu katika kujenga uchumi imara unaozingatia haki na usawa kwa wote."amesema Bw.Mdimi

Kwa upande wa wafanyabiashara, wamekumbushwa umuhimu wa kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia sheria za ushindani wa haki, wakielezwa kuwa uaminifu kwa wateja ni msingi wa mafanikio ya biashara yoyote endelevu.

Elimu hiyo imewajengea uelewa mpya kuhusu wajibu wao katika kulinda maslahi ya walaji.

Wanafunzi  wameahidi kuwa mabalozi wa elimu hiyo katika jamii zao, huku waandishi wa habari wakiahidi kueneza ujumbe huo kwa umma kupitia vyombo vyao.

Elimu hiyo  ni sehemu ya maandalizi kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026, yakilenga kuendelea kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kulinda haki za walaji na kuimarisha ushindani wa haki sokoni.

Kwa ujumla, juhudi hizi zinaakisi dhamira ya Tume ya Ushindani kuhakikisha kuwa kila mlaji anakuwa na sauti, analindwa na anapata huduma bora, huku biashara zikikua katika mazingira ya haki na uwazi.

 


Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, ameshiriki mafunzo maalum kwa waandaaji wa maudhui (content creators) yanayofanyika leo Machi 24, 2026 mkoani Dar es Salaam, yakilenga kuwajengea uwezo waandaaji hao wa maudhui ili kuboresha ubunifu na kuongeza tija ya kazi zao.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wawezeshaji.


Uwezeshaji wa Wizara ya Nishati katika mafunzo hayo ni kielelezo cha kutambua kazi zinazofanywa na waandaaji hao wa maudhui ambao ni daraja muhimu la kutoa elimu na kuhamasisha kupitia majukwaa yao kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Mafunzo yanayotolewa leo yanalenga kuwasaidia watengeneza maudhui kuboresha kazi zao kupitia kubiasharisha maudhui mtandaoni (Content Monetization & Sustainability), kujiongezea thamani binafsi na chapa (Personal Branding na Channel Optimization), pamoja na masuala ya hakimiliki.

Aidha, waandaji hao wa maudhui watapata elimu ya namna ya kufikia masoko ya kimataifa, maadili na miongozo ya utoaji huduma mtandaoni, pamoja na usalama wa taarifa binafsi katika utengenezaji wa maudhui.

 


Dubai, Machi 2026
KAMPUNI ya Airtel Africa kwa kushirikiana na SpaceX wametangaza kufanikiwa kwa majaribio ya huduma za data na ujumbe (SMS) kupitia Starlink Mobile nchini Kenya, hatua muhimu inayofungua njia ya kuleta mawasiliano ya satelaiti moja kwa moja kwenye simu za mkononi kwa mamilioni ya wananchi katika nchi 14 ambako Airtel inafanya kazi barani Afrika.

Majaribio hayo yalifanyika katika maeneo yasiyokuwa na mtandao wa kawaida wa simu, yaani maeneo ambayo minara ya mawasiliano ya ardhini haikuwa na mawimbi. Katika maeneo hayo, huduma ya Starlink Mobile iliwezeshwa moja kwa moja na kuruhusu simu janja zinazotumia teknolojia ya 4G kuunganishwa na mtandao wa satelaiti zaidi ya 650 zilizokwisha kurushwa angani, hivyo kuwezesha watumiaji kuendelea kuwa na mawasiliano hata katika maeneo ya mbali kabisa.

Katika kipindi cha majaribio, huduma hiyo iliweza kusaidia matumizi ya data nyepesi kama vile kupiga na kutuma ujumbe kupitia WhatsApp, kutumia ramani, Facebook Messenger pamoja na kufanya miamala ya kifedha kupitia programu ya Airtel App. Watumiaji waliweza kuendelea kutumia huduma muhimu hata walipokuwa katika maeneo ambayo kwa kawaida hayana mtandao wa simu.

Akizungumzia mafanikio hayo, Mtendaji Mkuu wa Airtel Africa, Sunil Taldar, alisema hatua hiyo inaonesha utekelezaji wa vitendo baada ya tangazo la ushirikiano kati ya Airtel Africa na SpaceX. Alisema majaribio yaliyofanyika nchini Kenya yanaonesha dhamira ya kampuni hiyo kupanua upatikanaji wa mawasiliano kwa watu wengi zaidi barani Afrika.

Aliongeza kuwa kwa kuunganisha teknolojia ya Starlink Mobile, Airtel Africa inahakikisha wateja wake wanaendelea kuwa na mawasiliano hata wanaposafiri nje ya maeneo yenye mtandao wa kawaida wa simu.

Baada ya majaribio hayo nchini Kenya, Airtel Africa na Starlink Mobile wanatarajia kutumia uzoefu walioupata kupanua huduma hiyo katika nchi zote 14 ambako Airtel inafanya kazi, kulingana na vibali vya mamlaka za mawasiliano za kila nchi. Aidha, kampuni hizo zinapanga kuanzisha huduma za kupiga simu kwa sauti pamoja na huduma za data zenye uwezo mkubwa zaidi kupitia teknolojia ya Starlink Mobile V2, ambayo itawawezesha watumiaji kupata huduma ya intaneti ya kasi moja kwa moja kwenye simu zao bila kutegemea minara ya kawaida ya mawasiliano.

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ametoa wito kwa wadau na waandaaji wa majukwaa mbalimbali ya wanawake nchini kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, pamoja na kutoa elimu itakayosaidia kuwaokoa wanawake dhidi ya changamoto zitokanazo na matumizi ya nishati isiyo safi.

Salome Makamba ameyasema hayo leo, tarehe 25 Machi 2026, katika hafla ya maadhimisho ya miaka 10 ya Malkia wa Nguvu Legacy Mark 2026 iliyoandaliwa na Clouds Media Group, inayofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.

Ameitaka pia Jukwaa la Malkia wa Nguvu kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ni mhamasishaji namba moja barani Afrika wa ajenda hiyo.

“Malkia wa Nguvu Levels isimuache Mwanamke wa Kitanzania akaendelea kuteketea kwa kutumia Nishati isiyo safi. Wizara ya Nishati tunacho kipaumbele cha kuhakikisha kufikia mwaka 2030 Watanzania zaidi ya asilimia 80 wawe wanatumia nishati safi ya kupikia” amesema Salome Makamba.

Aidha, Salome ameeleza kuwa juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali zinahitaji kuungwa mkono na majukwaa mengine kama Malkia wa Nguvu, ambayo yana nafasi muhimu ya kuwa sehemu ya suluhisho kwa kuweka kipaumbele katika utoaji wa elimu kuhusu matumizi ya nishati safi.

Amesisitiza kuwa nishati safi inaleta mapinduzi makubwa katika maisha ya mwanamke kwa kuondoa madhara yatokanayo na moshi wa kuni na mkaa, kufungua fursa za biashara, kuongeza kipato, pamoja na kupunguza hatari na unyanyasaji unaoweza kujitokeza wakati wa kutafuta nishati katika maeneo hatarishi.

“Tukiamua kwa pamoja, tunaweza kuhakikisha hakuna mwanamke anayebaki nyuma kimaendeleo. Tushirikiane na kuwezeshana ili siku moja tujivunie jitihada hizi za kumkomboa mwanamke na kuona matunda yake yakinufaisha jamii nzima,” amesisitiza Mhe. Salome.

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amewasili katika hafla ya maadhimisho ya miaka 10 ya Malkia wa Nguvu Legacy Mark 2026 iliyoandaliwa na Clouds Media Group, inayofanyika katika Serena Hotel. Leo tarehe 25 Machi 2026.

Mhe. Salome ndiye mgeni rasmi katika hafla hiyo, ambapo ameambatana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Nishati, Nteghenjwa Hosseah.

Jukwaa la Malkia wa Nguvu ni mpango maalum unaolenga kuwawezesha wanawake katika nyanja za kiuchumi, kijamii na maendeleo binafsi. Kupitia jukwaa hili, wanawake hupata fursa ya kujifunza, kushirikishana uzoefu na kujenga mitandao itakayowasaidia kukua katika biashara, uongozi na maisha kwa ujumla.

 Aidha, jukwaa hilo huibua mijadala ya masuala muhimu yanayowagusa wanawake na kuwapa motisha ya kujitambua, kujiamini na kutumia fursa zilizopo ili kufikia mafanikio.