Na James  Mwanamyoto - Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameulekeza uongozi wa Shirika la Masoko kuhakikisha zoezi la upangishaji wa vizimba na vyumba kwa wafanyabishara wa Soko la Kariakoo unazingatia bei ya soko ili mradi huo wa Soko la Kariakoo uwanufaishe wafanyabiashara kama ilivyokusudiwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo leo Disemba 24, 2025 Jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ukarabati wa soko, ambao ulianza kutekelezwa Januari 7, 2022 na kukabidhiwa katika Shirika la Masoko ya Karikakoo  Agosti 25, 2025.

“Mpangishe vizimba na vyumba kwa kuzingatia bei ya soko kwani Mhe. Rais alitoa Shilingi Bilioni 28 za ukarabati wa soko ili wafanyabishara wanufaike, hivyo kusiwe na ujanja ujanja wa baadhi ya watu kufanya udalali,” Prof. Shemdoe amesisitiza.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ameusisitiza uongozi wa Soko la Kariakoo kuhakikisha wafanyabishara wa awali wanapewa kipaumbele kupewa vizimba na vyumba kabla ya kuwapatia wafanyabiashara wapya, ili kuondokana na malalamiko.

Pia, Prof. Shemdoe ameusisitiza uongozi wa Soko la Karikaoo kutoruhusu watu kupata vizimba au vyumba kinyume na utaratibu katika soko jipya, wakati tayari wapo wafanyabiashara waliokwishapata vizimba na vyumba kupitia mfumo wa TAUSI.

Aidha, Prof. Shemdoe ameuhimiza uongozi wa Kariakoo kuhakikisha majengo ya Soko la Kariakoo yanakatiwa bima, na kuendelea kutoa elimu ya umuhimu wa bima kwa wafanyabiashara ili nao wakate bima kwa ajili ya kulinda mitaji yao pindi wanapokabiliana na changamoto zitakazoweza kuwarudisha nyuma kibiashara.

Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, ujenzi wa Soko la Kariakoo umeongeza chachu kwa sekta binafsi kufanya uwekezaji katika kujenga majengo ya kibiashara kulizunguka soko hilo, hivyo amewapongeza  na kuwahimiza kukamilisha majengo hao ili  kuimarisha sekta ya biashara na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi (Miundombinu), Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhandisi Aman Mafuru amesema kuwa, ukarabati wa soko la Karikaoo umezingatia uwekaji wa miundombinu mbalimbali ikiwemo  mifumo imara ya kukabiliana na ajali za moto, lifti za kubeba bidhaa, wafanyabiashara na wanunuzi wa bidhaa.





Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, akiwa ameongoza na Kikosi cha Usalama Barabarani wilayani humo kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika barabara kuu ya Dar es Salaam–Tanga, eneo la Segera, ambapo jumla ya madereva 60 walibainika kukiuka makosa mbalimbali ya usalama barabarani.

Na Mwandishi Wetu, Handeni

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, ameongoza Kikosi cha Usalama Barabarani wilayani humo kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika barabara kuu ya Dar es Salaam–Tanga, eneo la Segera, ambapo jumla ya madereva 60 walibainika kukiuka makosa mbalimbali ya usalama barabarani.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mhe. Nyamwese amesisitiza umuhimu wa madereva kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani, hususan katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, ili kuepusha ajali na kulinda maisha ya abiria pamoja na watumiaji wengine wa barabara.

“Ninatoa wito kwa madereva wote; huu ni msimu wa sikukuu, tafadhali epukeni kabisa matumizi ya vilevi mnapokuwa barabarani. Tuko macho saa 24. Dereva yeyote atakayekamatwa akiendesha gari akiwa amelewa katika barabara yetu hatapata msamaha, leseni yake itafutwa,” amesema Mhe. Nyamwese.

Ameeleza kuwa ukaguzi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Wilaya ya Handeni katika kuhakikisha usalama wa wananchi unaimarishwa na ajali za barabarani zinapungua, hasa katika kipindi cha sikukuu.

Nilikuwa nikijaribu bahati yangu kwa muda mrefu. Kila siku nilikuwa nikinunua tiketi za lottery, nikijaribu hesabu tofauti, na hata kuzingatia nasaha za marafiki.

Lakini kila mara matokeo yalikuwa sawa kushindwa. Wakati mwingine nilihisi ningeweza kuacha, lakini ndani yangu kulikuwa na tamaa ya kuona maisha yamebadilika mara moja kwa bahati moja.

Marafiki na familia walidhani sitaweza kushinda, wakiwemo watu waliokuwa karibu sana nami. Hali hiyo ilinifanya nijihisi peke yangu na kujiuliza kama jackpot inaweza kuwa kweli kwangu. Nilijua lazima nifate njia sahihi zaidi, njia ambayo ingekuwa tofauti na mbinu za kawaida ambazo hazikuleta matokeo.Soma Zaidi..............
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/wote-walidhani-jackpot-haingewezekana-lakini-hatimaye-nilipata-bahati-kubwa-na-hii-njia-ya-kienyeji/
Nilihisi maisha yangu ya shule yamegeuka kuwa giza la kila siku. Marafiki walikuwa hawajali, walimu walikosa kujua au kushughulikia, na mimi niliishi kwa hofu isiyoelezeka. Kila hatua nilipochukua, nilijihisi nikiwa hatarini, huku heshima yangu ikinyamazishwa kila mara.

Mara nyingi nilijihisi peke yangu, na kuanza kuamini kuwa maisha yangu ya shule hayangeweza kubadilika. Nilijaribu kuzungumza na watu wazima, walimu, na hata familia yangu, lakini mara nyingi waliniambia subiri au kujaribu kusahau.

Lakini huzuni na hofu vilikuwa vikibakia. Nilihisi kila siku kama ngome ya ukatili haingeweza kuondolewa bila msaada wa kina zaidi. Soma Zaidi......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipitia-unyanyasaji-wa-kijinsia-shuleni-hatua-moja-ilinilinda-na-kubadilisha-maisha-yangu/
Nilikuwa nimefika hatua ya kuchoka kimawazo na kihisia. Ndani ya ndoa yangu kulikuwa na maswali mengi kuliko majibu. Mabadiliko ya tabia, simu zilizokuwa zikifichwa, kuchelewa kurudi nyumbani na ukimya usioelezeka vilianza kunipa mawazo mengi.

Kama mwanamke wa Kitanzania, nilijaribu kuvumilia nikiamini muda ungeweka sawa mambo. Lakini kadri siku zilivyopita, hali ilizidi kuwa nzito moyoni. Soma Zaidi.........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-nilivyopata-ukweli-wa-ndoa-yangu-kupitia-tiba-asili-ya-kiwanga-doctor-na-kurejesha-amani-ya-maisha-tanzania-leo-tu/
Mimi ni mwanamke wa kawaida kutoka Dodoma. Kwa muda mrefu nilikuwa nikijaribu kubashiri kama njia ya kujiongezea kipato. Sio kwa tamaa, bali kwa matumaini.

Nilikuwa napiga bet kwa nidhamu, nikichagua timu kwa uangalifu, lakini bahati ilikuwa inanipita kila wakati. Nilipoteza pesa kidogo kidogo mpaka nikaanza kujiuliza kama tatizo ni akili au bahati.

Nilipochoka, niliamua kusimama kabisa. Ndipo rafiki yangu akanisimulia hadithi yake ya kubadilika kwa bahati baada ya kupata msaada wa tiba asili.Soma Zaidi........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/jinsi-mwanamke-wa-dodoma-alivyoshinda-jackpot-kubashiri-baada-ya-kusaidiwa-kwa-tiba-asili-ya-kiwanga-doctor-leo-hii-tu/
Nilihisi moyo wangu umesalia kwenye hatua moja, huku mpenzi wangu akionekana mbali zaidi kila siku. Tulikuwa tumepitia changamoto nyingi, lakini mara nyingi nilihisi kama hakuna njia ya kumfanya arudie kuamini hisia zangu.

Nilijaribu maneno, zawadi, hata makosa yangu kuonyesha nia, lakini hakuwa tayari. Kila jaribio lilikuwa dogo na kuisha haraka. Hali ilizidi kuwa ngumu nilipoona rafiki zangu wakifurahia mapenzi yao wakati wangu ulishindikana.

Nilijua lazima kuna kitu nilikuwa nakosa kuelewa. Nilihisi kuna kizuizi kisichoonekana kinazuia mpenzi wangu kumkaribia moyo wangu tena. Nilijua lazima nitafute msaada wa kina zaidi kuliko vile nilivyokuwa nikijaribu peke yangu. Soma Zaidi...........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mpenzi-wangu-alikuwa-kizuizi-hatua-moja-ilinisaidia-kumwinua-moyo-wake/

Watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), leo 23 Desemba 2025, wamekutana na kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa utendaji hususani katika usimamizi wa masuala ya kikodi yanayotokana na huduma zinazodhibitiwa na EWURA.

 

 


Na Ashrack Miraji

Waziri wa Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka, amewataka viongozi wa Mikoa, Wilaya, Halmashauri na Kata kuacha tabia ya kukaa ofisini na badala yake kushuka chini kuwafuata vijana ili kuwaeleza fursa mbalimbali za kimaendeleo zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuwainua kiuchumi.

Akizungumza na vijana wa Jimbo la Same Mashariki mkoani Kilimanjaro, Waziri Nanauka alisema viongozi hao wana wajibu wa kuwafikia vijana moja kwa moja kwenye maeneo yao na kuwapatia taarifa sahihi kuhusu fursa za mikopo, mafunzo, ajira na miradi mbalimbali ya kiuchumi inayotolewa na Serikali.

Alisema katika ziara zake tangu ateuliwe kuwa Waziri wa wizara hiyo, amebaini kuwa idadi kubwa ya vijana hawana taarifa za fursa za maendeleo zinazotolewa na Serikali, hali inayosababisha fursa hizo kuwafikia vijana wachache huku wengi wakibaki nyuma kwa kukosa taarifa.


“Nimegundua taarifa nyingi za fursa za vijana hubaki kwa makundi machache. Serikali ya Awamu ya Sita inataka kila kijana, bila kujali itikadi au eneo alipo, apate taarifa na kunufaika na fursa hizi,” alisema Waziri Nanauka.

Aliongeza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameagiza fursa zote zinazohusu vijana zitolewe kwa uwazi na usawa, huku viongozi wa ngazi zote wakihamasishwa kuhakikisha vijana wanapata elimu ya namna ya kuzitumia fursa hizo kwa maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.


Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anne Kilango, alisema kundi la vijana ni kubwa kuanzia ngazi ya dunia, Taifa hadi jimbo lake, akieleza kuwa takribani asilimia 64 ya wakazi wa jimbo hilo ni vijana, hivyo linahitaji mikakati madhubuti ya kuwawezesha kiuchumi.

Kilango alisema miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya jimbo hilo imeongeza imani ya vijana kwa Serikali, ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara ya Mkomazi–Kisiwani Same yenye urefu wa kilomita 101 inayojengwa kwa kiwango cha lami, ambayo imefungua fursa za kiuchumi na kijamii kwa vijana wa eneo hilo.

Naye Waziri Nanauka aliahidi kushughulikia changamoto zilizowasilishwa na vijana, hususan miundombinu ya umwagiliaji, akisema Serikali inaendelea kutenga rasilimali ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji kwa mazao ya kimkakati yanayolimwa na vijana ili kuongeza tija na kipato.

Kwa upande wao, vijana waliohudhuria mkutano huo, wakati wakiwasilisha risala yao kwa Waziri, walisema wanakabiliwa na changamoto ya miundombinu ya umwagiliaji katika kilimo cha tangawizi kwenye kata za milimani pamoja na kilimo cha mpunga katika kata za tambarare, wakiiomba Serikali kuharakisha upatikanaji wa miradi ya maji kwa ajili ya kilimo.






 

 


 

·       Waziri Akwilapo Ataka Kukamilisha malipo ifikapo Desemba 31, 2025

 

·       Aagiza Vituo vya Makusanyo ya Kodi kutoa huduma bora

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameelekeza wadaiwa wote wa Kodi ya Pango la Ardhi nchini wawe wamekamilisha malipo ya madeni yao kufikia  Desemba 31, 2025.

 

Akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Masasi mkoani Mtwara leo tarehe 23 Desemba 2025 Mhe. Dkt Akwilapo amesema, kuchelewa kulipwa kodi ya pango la ardhi kutasababisha wamiliki wa ardhi kuwa na malimbikizo ya madeni pamoja na riba. 

 

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, madhara mengine yanayoweza kutokea kwa wamiliki ambao hawajalipa kodi ya pango la ardhi kwa wakati ni pamoja na kufikishwa mahakamani na kufutiwa umiliki wa ardhi. Hatua hiyo ni kwa mujibu wa sheria ya ardhi Sura ya 113 Fungu la 48 (1), 50,  51 na 52.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ameelekeza vituo vyote vya makusanyo ya kodi ya pango la ardhi katika ofisi za ardhi za mikoa na halmashauri nchini kuhakikisha vinatoa huduma bora za kuwasaidia wananchi wanaopata changamoto za kulipa kodi hiyo kwa kuzingatia utu pale wanapotekeleza majukumu yao

Katibu Mtendaji wa Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika wa Kujitathmini kwa Vigezo vya Utawala Bora (APRM) Tanzania, Bw. Lamau Mpolo, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini.

Lengo la kikao hicho lilikuwa kujadili nafasi ya vijana katika kukuza dhana ya Utawala Bora kama nguzo muhimu ya kuimarisha amani na usalama nchini Tanzania.

Katika kikao hicho, Bw. Mpolo alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vijana katika masuala ya utawala, akieleza kuwa vijana ni rasilimali muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji, uwazi na maamuzi jumuishi.

Kikao hicho cha siku moja kilifanyika Desemba 22, 2025, katika Ofisi za APRM zilizopo katika jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi ,akizungumza wakati wa ziara yake katika Baraza la Ushindani (FCT) Jijini Dar es Salaam.

....

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi (Mb), ameliagiza Baraza la Ushindani (FCT) kuendelea kusimamia na kulinda ushindani wa haki ili kuondoa vitendo vya ukiritimba, hususan katika suala la kupandisha bei za bidhaa na huduma.

Ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Baraza la Ushindani Desemba 22, 2025 Jijini Dar es Salaam akisisitiza kuwa ushindani wa haki ni msingi muhimu wa ukuaji wa biashara, kwani vitendo vya ukiritimba vimekuwa vikiathiri biashara nyingi na walaji.

Ameeleza kuwa biashara zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia ulinzi wa walaji, ambapo bei za bidhaa na huduma ziwe za haki, bidhaa ziwe na ubora, na uchunguzi wowote ufanyike kwa haki na kwa kuzingatia misingi ya kisheria.

Mhe. Katambi amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji kwa kuboresha sera rafiki, kufanya marekebisho ya sheria na kuendelea na maboresho ya mazingira ya biashara ili kuhakikisha Tanzania inakuwa mahali salama na rafiki kwa kufanya biashara bila kuweka vikwazo kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.

Amesisitiza kuwa haki katika utatuzi wa migogoro ni kipaumbele, kwa kulinda muda, heshima na maslahi ya wawekezaji na kusimamia sheria za ushindani, ndani na nje ya nchi, kwa lengo la kumlinda mlaji ili awe mnufaika mkuu wa shughuli za kibiashara.

Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani Jaji Rose Ibrahim, Dkt. Onesmo Kyauke amesema Baraza la Ushindani lina nafasi ya kipekee katika kuhakikisha malengo ya sera ya ushindani nchini yanatekelezwa kwa ufanisi, hususan kupitia usikilizaji wa rufaa na mashauri yanayotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani pamoja na mamlaka za udhibiti wa soko.

Amesema hatua hiyo inasaidia kujenga mazingira bora ya biashara, kuvutia uwekezaji na kulinda maslahi ya walaji na washiriki wote wa soko.