>Agawa vifaa vya michezo kwa timu zote zinazoshiriki Ligi ya wilaya ya Mkinga

Na Oscar Assenga, MKINGA

Mbunge wa Jimbo la Mkinga mkoani Tanga, Twaha Mwakioja, ameahidi kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo kuinua kiwango cha soka wilayani humo kwa kuwekeza katika elimu na maendeleo ya waamuzi pamoja na makocha.

Akizungumza wakati wa mchezo wa Ngao ya Jamii uliokwenda sambamba na uzinduzi wa Ligi ya Wilaya ya Mkinga, uliofanyika katika Uwanja wa Chamazi, Kata ya Matamba, Mwakioja alisema lengo lao ni kuwekeza katika michezo kwa vijana ili kuwapatia ajira, kuboresha afya zao, pamoja na kuimarisha amani, mahusiano mema na ushirikiano miongoni mwao.

Alieleza kuwa dhamira yao ni kuwashika mkono vijana ili waweze kupiga hatua kutoka ngazi ya wilaya, kwenda mkoa, kanda na hatimaye ligi za juu, huku yeye akiwa bega kwa bega nao kuhakikisha wanafikia malengo yao.

Mbunge huyo alibainisha kuwa wamepata taarifa ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali, ikiwemo uhaba wa makocha na waamuzi wenye sifa. Hivyo, wamejipanga kuwekeza katika mafunzo ya makocha ili kila kata iwe na angalau kocha mmoja mwenye ujuzi na mafunzo rasmi, pamoja na kuandaa waamuzi wenye vyeti ili kuboresha usimamizi wa michezo.

Alisisitiza kuwa uwekezaji huo utaenda sambamba na ushirikiano na Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga katika kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana.

Aidha, alisema mpango wao ni kuhakikisha kila kata na kijiji kinakuwa na timu ya mpira wa miguu inayoshiriki ligi ya wilaya. Aliongeza kuwa watawekeza zaidi ili kuibua timu imara zitakazoweza kushiriki ligi za ngazi ya mkoa, kanda na hatimaye Ligi Kuu, hatua itakayosaidia kuitangaza Mkinga katika ramani ya soka nchini.

Katika kuonyesha dhamira hiyo, Mwakioja alikabidhi jezi na mipira kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha na kusaidia maendeleo ya michezo wilayani humo.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga, Fadhili Habibu, alisema ratiba ya ligi hiyo imeanza Mei 4 katika kituo cha Mkinga, huku kituo cha Maramba kikitarajiwa kuanza Mei 6 (Jumatano), ambapo kutakuwa na vituo vinne vitakavyochezwa katika Kijiji cha Maramba, ikiwa ni pamoja na mechi kati ya Viva Dynamo na Maramba FC.

Habibu alisema lengo la ligi hiyo ni kusimamia na kuibua vipaji vya vijana, pamoja na kuwapa mwelekeo wa maendeleo yao kisoka. Alimshukuru mbunge kwa kujitoa na kushirikiana nao katika kufanikisha malengo hayo.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga, Hassan Zumo, alimpongeza mbunge kwa juhudi zake za kuendeleza michezo wilayani humo, akieleza kuwa hatua hiyo imeongeza hamasa na matarajio ya ushindani mkubwa katika ligi hiyo, hasa baada ya timu kukabidhiwa vifaa.

Zumo aliongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 2008, wamekuwa wakipeleka vilabu katika mashindano ya ngazi ya mkoa lakini wamekuwa wakikwama kutokana na changamoto za kifedha. Hata hivyo, alisema kupitia uongozi wa Mbunge Mwakioja, wana matumaini ya kupata timu itakayoweza kufika hadi Ligi Kuu.

Aidha, timu zinazoshiriki mashindano hayo zimeahidi kujituma na kupambana kwa juhudi zote ili kuhakikisha ligi hiyo inaleta mafanikio na tija kwa vijana wa Wilaya ya Mkinga.




Na Mwandishi Wetu, Kibaha-Pwani.


Imeelezwa kuwa Tume ya Taifa ya Mipango imekamilisha nyenzo zote za utekelezaji wa Dira 2050 ambazo ni Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051 (LTPP 2050), Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2026/27 – 2030/31 (FYDP IV) na Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2026/2027 kuelekea Julai 1, 2026 ambapo utekelezaji wa Dira hiyo utaanza rasmi.

Hayo yameelezwa leo Mei 4, 2026 na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida alipofungua mafunzo kwa Wakurugenzi wa Sera na Mipango, Wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini, na Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali yanayofanyika katika Chuo cha Uongozi Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha - Pwani.

Dkt. Kida amewaambia washiriki wa mafunzo hayo kuwa, baada ya kukamilisha Dira 2050 na nyenzo zake, mafunzo hayo ni utekelezaji wa mkakati mahususi wa Serikali wa kujipanga kufanya utekelezaji wa Dira hiyo kwa kuhakikisha kunakuwepo na uelewa wa pamoja na utekelezaji unaolingana katika ngazi zote za Wizara, Taasisi za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuhakikisha mipango ya Kitaifa inatekelezwa kwa tija.

“ Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Mipango inakamilisha Miongozo ya Upangaji (NPGs), Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Programu na mirado ya Maendeleo (NF-MEDeP) na Mfumo wa Kidigitali uitwao E-Delivery. Mfumo huu na miongozo hiyo italetwa kwenu na mafunzo stahiki yanaandaliwa kwa ajili yenu” Amesisitiza Dkt. Kida.

Aidha, Dkt. Kida amesema kupitia mafunzo hayo, washiriki watapata fursa ya kujifunza kwa vitendo (i.e. case studies), kubadilishana uzoefu, na kujenga uwezo katika hatua zote za mzunguko wa miradi ya maendeleo kuanzia uibuaji, upangaji, uchambuzi, uidhinishaji hadi utekelezaji na ufuatiliaji.








Kutoka Pemba, Unguja, Mji mkongwe, Bagamoyo, Kondoa, Magofu ya kilwa, paa la mlima kilimanjaro na maeneo mengine ya Tanzania, wadau wa urithi wa dunia wamekutana katika Makumbusho ya Urithi Geopark Karatu Mkoani Arusha yanayosimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro  kwa lengo la kuadhimisha   Urithi wa Dunia Afrika yaliyoanza leo tarehe 04/05/2026 hadi tarehe 05/05/2026.

Wakiwa katika jengo la makumbusho ya Urithi Geopark Wadau hao wameelezwa jinsi Ngorongoro ilivyo ni utajiri wa urithi wa dunia kutokana na uumbwaji wake uliotokana na mlipuko wa volcano zaidi ya miaka milioni mbili iliyopita na kutengeneza kasoko iliyokusanya asili, uhai wa binadamu, mifumo ya ikolojia, na ustawi wa viumbe mbalimbali.

Katika  taarifa yake kwa vyombo vya habari Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Bw. Abdul-Razaq Badru amewashukuru wadau wote hasa Shirika la Umoja wa Mataifa la  Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)   kwa kuipa fursa Ngorongoro kuandaa na kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo kwa mwaka huu.

Wadau wa urithi wa duania wakiwa katika Makumbusho ya Urithi Geopark walipata fursa ya kuelezewa kuhusu uthibitisho wa wasomi unaoeleza wazi historia ya chimbuko la binadamu wa kale aliyepatikana katika bonde la olduvai  takribani milioni  2 iliyopita na ushahidi wa Nyanyo za binadamu wa kale  katika eneo la Laetoli takribani miaka  3.6 iliyopiTa ambapo binadamu hao walitembea kwa miguu miwili.

Taasisi zinazoshiriki maadhimisho hayo ambazo zinasimamia maeneo ya urithi wa dunia ni pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Mamlaka ya Uzimamizi wa Wanyamapori (TAWA), Wakala wa Huduma za misitu Tanzania (TFS), pamoja na wawakilishi wa maeneo ya urithi wa dunia kutoka Zanzibar.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAHITIMU wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) (alumni) wametakiwa kutumia nafasi zao kuchangia maendeleo ya taifa kupitia taaluma, uzoefu na rasilimali walizonazo.
Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) imemtangaza Irene Luoga, Afisa Ushirika Mwandamizi kutoka Ofisi ya Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Mbeya, kuwa mfanyakazi hodari kwa mwaka 2025/2026.
Tuzo hiyo imetolewa kufuatia mchango wake mkubwa katika kusimamia na kuendeleza shughuli za ushirika, ikiwa ni pamoja na kuhamasisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi katika Sekta ya ushirika.
Katika kipindi hicho, Irene ameonyesha weledi wa hali ya juu katika utekelezaji wa majukumu yake, akisimamia vyema shughuli mbalimbali za maendeleo ya Ushirika na kutoa msaada wa kitaalamu kwa wanachama na viongozi wa vyama. Juhudi zake zimechangia kuimarika kwa utendaji wa vyama vingi pamoja na kuongeza imani ya wanachama katika sekta ya ushirika nchini.
Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Irene alieleza shukrani zake kwa Uongozi wa TCDC kwa kutambua mchango wake, akiahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii zaidi.
 “Ninawashukuru sana TCDC kwa kunichagua kuwa mfanyakazi hodari wa mwaka huu.Hii ni heshima kubwa kwangu na inanipa motisha ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na ufanisi zaidi ili kuleta maendeleo chanya katika sekta ya ushirika nchini na Taifa kwa ujumla,” alisema Irene.
 

 


Ripoti ya Tume iliyoongozwa na Jaji Mohamed Chande Othman ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 imeendelea kuzua mjadala mkubwa nchini, huku mchambuzi wa masuala ya uongozi, uchumi na siasa Tanzania, Dk Netho Ndilito (PhD), akiitaja kama nyaraka muhimu iliyofichua mambo makubwa matano yenye maslahi kwa taifa.

Akizungumza kuhusu ripoti hiyo, Dk Ndilito amesema baada ya kupitia maoni ya Watanzania, wanamitandao na wachambuzi mbalimbali, amebaini kuwa taarifa hiyo imeleta mwanga mpya kuhusu hali halisi ya taifa na changamoto zilizokuwa zikijadiliwa kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Dk Ndilito, jambo la kwanza ni kwamba ripoti hiyo imeliponya taifa kwa kueleza ukweli ambao kwa muda mrefu haukupata nafasi ya kujadiliwa waziwazi, ikifichuliwa pia kwa nia na dhamira ovu za baadhi ya watu waliotamani vurugu kabla, wakati na baada ya uchaguzi, jambo ambalo sasa limewekwa wazi kupitia uchunguzi huo.

Aidha, ameeleza kuwa ripoti hiyo imeweka bayana upotoshaji na taarifa zisizo sahihi zilizokuwa zikisambazwa na baadhi ya watu wasiolitakia mema taifa, huku wakitamani kuona nchi ikiingia kwenye machafuko.

Katika hoja ya nne, Dk Ndilito amesema ripoti hiyo imeonesha namna Watanzania wengi wanavyoipenda nchi yao, kuiamini serikali yao na kutokuwa tayari kushawishika kuivuruga amani, umoja na mshikamano wa taifa, huku pia ripoti hiyo ikionesha uimara wa serikali pamoja na ukomavu wa vyombo vya ulinzi na usalama katika kushughulikia masuala ya ndani kwa weledi na utulivu.

Dk Ndilito alitumia nafasi hiyo kuwapongeza Watanzania kwa kuendelea kudumisha umoja, upendo, mshikamano na amani, akisisitiza kuwa huo ndiyo utamaduni uliojenga heshima ya taifa kwa miaka mingi.

“Watanzania wameendelea kuonesha ukomavu mkubwa wa kisiasa na uzalendo. Hii ndiyo desturi yetu kama taifa,” alisema.

 


Yajipanga Kubeba Suluhu ya Uhaba wa Gesi hiyo Duniani

Helium One Global Yasema Akiba ya Songwe ina Thamani Kubwa Kijiolojia

Mradi Kuanza Kutekelezwa baada ya Miezi 18, Zaidi ya Dola Milioni 60 tayari Zimewekezwa

Serikali Kumiliki Asilimia 17 ya Hisa kupitia Kampuni ya Ubia ya Songwe Helium Limited


Tanzania imeanza rasmi Safari Mpya ya Kihistoria ikiingia kwenye ramani ya dunia kama Mzalishaji na Msambazaji wa kimkakati wa Gesi ya Helium. Hatua hiyo inafuatia baada ya kusainiwa kwa Mkataba wa Uchimbaji wa gesi hiyo baina ya Serikali na kampuni ya Helium One Global Limited kupitia Kampuni ya Ubia ya Songwe Helium Limited, katika hafla iliyofanyika Mei 2, 2026 Mkoani Songwe.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Madini  Dkt. Steven  Kiruswa wakati akizungumza katika hafla  hiyo na kueleza kuwa, uzalishaji wa helium duniani kwa sasa unatawaliwa na nchi chache, hususan Marekani na Qatar, zinazochangia zaidi ya asilimia 75 ya uzalishaji wote, huku Urusi, Algeria, Canada, China na Poland zikichangia kwa kiwango kidogo. Ameongeza kuwa mahitaji ya gesi hiyo tayari yamevuka futi za ujazo bilioni 6 kwa mwaka na yanatarajiwa kuongezeka hadi zaidi ya bilioni 8.5 ifikapo mwaka 2030 ambapo kwa Tanzania kampuni za Helium One Global Limited na Noble Helium zimepiga hatua kubwa katika shughuli za utafiti wa gesi hiyo.

Ameeleza kuwa, mradi wa Southern Rukwa ni wa kimkakati unaoiwezesha Tanzania kuingia kwenye soko lenye thamani kubwa na ushindani mdogo na kuiweka katika nafasi ya kuathiri mwelekeo wa soko la helium duniani, huku ikitarajiwa kuwa sehemu ya suluhisho la uhaba wa gesi hiyo duniani na kueleza kwamba, uchimbaji wa helium utakwenda sambamba na gesi ambata kama hydrogen ambapo manufaa yake kimapato yatatenganishwa.

Aidha, Dkt. Kiruswa  amefafanua kwamba kupitia mkataba huo, Serikali itamiliki asilimia 17 ya hisa katika kampuni ya ubia ya  Songwe Helium Limited, hatua inayoiwezesha kushiriki moja kwa moja katika maamuzi ya kimkakati na kunufaika na mapato ya mradi kwa manufaa ya Taifa na wananchi.

‘’Huu ni utekelezaji halisi wa falsafa ya Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa rasilimali za nchi lazima ziwe chanzo cha ustawi wa taifa,’’ amesema Dkt. Kiruswa.

Akizungumzia manufaa mengine ya mradi huo amesema  utachangia ajira kwa vijana wa eneo husika na taifa kwa ujumla, fursa za kibiashara kwa wazawa kupitia huduma za ugavi, uboreshaji wa miundombinu, mapato kwa Serikali na fedha za kigeni na uboreshaji wa miundombinu muhimu kama  barabara na huduma za kijamii.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Helium One Global Limited, Lorna Blaisse amesema utiaji saini huo ni hatua muhimu kwa Tanzania na soko la helium duniani, akibainisha kuwa mradi una akiba yenye thamani kubwa na unaelekea kwenye uzalishaji wa kibiashara baada ya mafanikio ya  uchimbaji kisima mwaka 2024 ambacho kilipelekea ugunduzi wa helium katika kisima cha Itambula West-1.

‘’Katika upimaji wa kisima uliopanuliwa robo ya tatu ya 2024, kisima cha ITW-1 kilirekodi helium yenye mkusanyiko wa asilimia 5.5 hadi juu ya ardhi, na hadi asilimia 7.6 kutoka miamba ya Karoo iliyovunjika na miamba ya Basement iliyopasuka,’’ amesema

Amesema baada ya utiaji saini wa leseni ya uchimbaji, kampuni ya Songwe Helium Ltd itaendelea na hatua za uendeshaji kuelekea uzalishaji wa kwanza wa kibiashara wa heliamu.  Amezitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kukamilisha mipango ya maendeleo; mfumo wa usimamizi wa tathmini ya athari za mazingira na jamii; kubuni miundombinu, na kununua vifaa vya uchakataji na usafirishaji wa bidhaa.

Pia, ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wake na kuridhia muundo wa ubia unaohakikisha nchi inanufaika na rasilimali zake, akibainisha dhamira ya kuzalisha helium ya Tanzania kwa uwajibikaji na ubora wa juu kwa soko la dunia.

Awali, akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Majadiliano ya Wizara ya Madini Prof. Sifuni Mchome amesema  kupitia utaratibu wa Serikali kumiliki hisa huru zisizohafifishwa thamani, Serikali inashiriki moja kwa moja katika miradi ya madini, inapata faida kupitia gawio, mrabaha,kodi  na tozo mbalimbali, inashiriki maamuzi ya kimkakati, kulinda mapato na maslahi ya wananchi kwa uwazi na uwajibikaji.

" Tulijadiliana kwa utaratibu mzuri bila kugombana na tumefika kwenye hatua ya kila mmoja apate, na leo tuko hapa kuweka wazi na kila mmoja ashuhudie," amesema Prof. Mchome.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Songwe  Mhe. Jabiri Makame amesema Mkoa huo ni wa kimkakati ukiwa na utajiri wa Madini mbalimbali yakiwemo ya rare earth elements ambao utafiti wake unaendelea.

" Tunaipongeza Wizara ya Madini kwa kutafsiri kwa vitendo. Kwetu sisi suala la kuwasaidia wawekezaji kutekeleza mradi Kwa mafanikio ni kipaumbele cha kwanza," amesema Mhe. Makame.

Helium ni gesi ya kipekee sana duniani kwa sababu haina mbadala wake na matumizi yake ni ya kimkakati kwa maisha ya kisasa ya binadamu; inatumika katika vifaa vya tiba kama MRI, uzalishaji wa vifaa vya kielektroniki na teknolojia za kidigitali;  sekta ya anga; ulinzi na tafiti za kisayansi, teknolojia za kisasa kama fibre optics  na quantum computing.

 Mradi huo unatekelezwa katika eneo la kilomita za mraba 480 ukiwa zaidi katika Mkoa wa Songwe Wilaya ya Momba na sehemu ndogo ikiingia Mkoa wa Rukwa.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji (Mb), ameongoza kikao kazi cha maandalizi ya bajeti ya Wizara hiyo inayotarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la bajeti la mwaka wa fedha 2026/2027 linaloendelea Jijini Dodoma.
Wafanyakazi wa Tume ya Ushindani (FCC) wameshiriki kikamilifu katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika Leo tarehe 1 Mei, 2026 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy, akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu kwa wananchi wa Kata ya Kibaya wilaya ya Kiteto, Mkoa wa manyara (hawapo pichani), mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Afisa Afya wa Wilaya ya Kiteto, Kennedy Mlapwa (kulia), akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyekaa kushoto) kwa ajili ya kufungua mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto, (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Emmanuel Haule, akiwasilisha mada ya utokeaji wa sumu kuvu na jinsi ya kudhibiti sumu kuvu nchini kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto, (hawapo pichani), katika mafunzo ya kuthibiti matukio ya sumukuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.

Washiriki wa mafunzo wakifuatilia mada katika mafunzo ya kuthibiti matukio ya sumu kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy, akiwasilisha mada ya namna ya kuepukana na matukio ya sumu mbalimbali katika jamii kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto (hawapo pichani), mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili29, 2026. 
Mshiriki akiuliza swali kwa Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyesimama kushoto), katika mafunzo ya kuthibiti matukio ya sumu-kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Emmanuel Haule, akiwasilisha wasilisho la hali ya matukio ya sumu nchini kwa wananchi wa Kata ya Kibaya Wilaya ya Kiteto wakati wa mafunzo ya udhibiti wa matukio ya sumu kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Washiriki wakiuliza maswali kwa Mtumishi wa Mamlaka, Emmanuel Haule (hayupo pichani), kuhusu hali ya matukio ya sumu nchini wakati wa mafunzo ya kudhibiti matukio ya sumu kuvu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.
Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy (aliyekaa katikati), akiwa pamoja na wananchi washiriki wa mafunzo hayo yakuthibiti matukio ya sumu kuvu nchini yaliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba, mkoani Manyara, Aprili 29, 2026.

Na Grace Msungu Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira, Mheshimiwa Kwagilwa Reuben Nhamanilo, amesema kuwa kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kunategemea kwa kiwango kikubwa uwekezaji wa kimkakati katika usimamizi endelevu wa mazingira pamoja na uwezeshaji wa wataalamu wazawa.




Na Mwandishi wetu- Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amewataka wataalamu ambao wamepatiwa mafunzo ya kukabiliana na maafa kuyatumia vyema katika  kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa.
Ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya siku nne  ya kujiandaa na kukabiliana na maafa  kwa  Kamati ya wataalamu , Timu ya kukabiliana na maafa na watumishi wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura  (REOCC) Mkoa wa Dodoma.

Brigedia Jenerali Ndagala ameeleza kuwa Awamu ya kwanza ya utekelezaji ilianza katika Mkoa wa Mwanza na Arusha, ambapo hatua za kuanzisha Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu ya kukabiliana na Maafa ilianza kutekelezwa Mikoay a Mwanza na Arusha huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yataendelea katika Mikoa yote Nchini.

Sambamba na hilo amebainisha kuwa mafunzo hayo ni  nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika na uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura.
Pia ameeleza  kuwa Uanzishwaji wa kituo hicho katika Mkoa wa Dodoma ni hatua muhimu  kwani kitawezeshaufuatiliaji  wa matukio kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma na Taifa kwa ujumla ili kuokoa maisha ya watu na mali zao.
Aidha Brigedia Jenerali Ndagala amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Senyamule kwa kukubali mafunzo hayo kutolewa katika timu hizo na kuanzisha Kituo  cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa ambacho kitaunganishwa na Kituo cha Taifa akisema uamuzi huo unaonyesha dhamira thabiti ya uongozi wa Mkoa wa  kuimarisha utayari, mwitikio wa haraka na uratibu madhubuti wakati wa dharura.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) pamoja na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Tabora, imefanya operesheni maalum katika hifadhi ya msitu wa Igombe river iliyopo wilaya ya Uyui na katika hifadhi ya msitu wa Nyahua iliyopo wilaya ya Skonge mkoani Tabora na kufanikiwa kuteketeza ekari 68 za mashamba ya bangi, kukamata gunia 133 za bangi huku watu saba (7) wakikamatwa katika operesheni hiyo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mfuko wa uwekezaji nchini, UTT AMIS, umehimiza wananchi kutumia fursa ya kuwekeza katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji wa pamoja ili kuongeza thamani ya fedha zao na kupata faida shindani.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

...

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.

Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.

Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.

Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.