Na Oscar Assenga, Lushoto

Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kujipambanua kama kinara wa usambazaji wa gesi nchini Tanzania, ikiwa na takribani asilimia 51 ya ujazo wa gesi yote inayopatikana nchini.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Meneja wa Masoko wa kampuni hiyo, Oscar Shelukindo, amesema kuwa mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya kuhifadhi na kusambaza gesi, pamoja na dhamira ya dhati ya kuwahudumia Watanzania.

Ameeleza kuwa lengo kuu la kampuni hiyo ni kusaidia juhudi za taifa za kuhamasisha matumizi ya nishati safi, kwa kuwahamasisha wananchi kuachana na matumizi ya kuni na mkaa, ambayo yamekuwa na athari kubwa kwa afya na mazingira.

Kwa mujibu wa takwimu, zaidi ya Watanzania 33,000 hufariki kila mwaka kutokana na magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya nishati zisizo safi. Hali hiyo imeifanya Taifa Gesi kuongeza juhudi za kuhakikisha gesi inapatikana kwa urahisi na kwa gharama nafuu.

Katika hatua hiyo, kampuni hiyo inatoa mitungi ya gesi ya kilogramu 6 na 15 kwa bei nafuu, pamoja na huduma ya kujaza mitungi kwa wateja waliokwisha kuwa nayo, hatua inayolenga kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Aidha, Taifa Gesi kwa kushirikiana na NMB Bank wanatarajiwa kushiriki katika Tamasha la Kijiji Day, ambapo watatoa huduma mbalimbali pamoja na elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi.

Juhudi hizi zinatajwa kuwa chachu ya mabadiliko chanya, zikilenga kuboresha afya za Watanzania na kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Share this

Serikali itahakikisha vipaumbele vya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) vinaakisi uhalisia wa mchango wa Sekta Binafsi, inayotarajiwa kuchangia takribani 70% ya Pato la Taifa (GDP) ifikapo mwaka 2050.

Hatua hiyo imebainishwa na Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dr. Blandina Kilama leo Aprili 13, 2026, wakati akifungua Warsha mahususi inayolenga kutoa fursa ya kujadili kwa kina, kukusanya maoni, uzoefu na mapendekezo ya wadau kutoka Sekta ya Umma, na Sekta Binafsi kuhusu maeneo sita (6) ya kipaumbele ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano, sambamba na mwelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“majadiliano haya yanalenga kuhakikisha kuwa mchango wa Sekta Binafsi unatambuliwa, unathaminiwa na kuingizwa kikamilifu katika uundaji na utekelezaji wa vipaumbele pamoja na mikakati ya maendeleo, ili kuimarisha ufanisi, kuongeza kasi ya utekelezaji wa FYDP IV, na kufikia matokeo yenye tija na endelevu kwa taifa” Amesema Dkt. Kilama.

Aidha, katika Warsha hiyo, washiriki watajadili mada mahususi zilizomo katika FYDP IV, ikiwemo Kujenga Uwezo wa Watu na Maendeleo ya Jamii, Kutumia Vichocheo vya Maendeleo, Mageuzi ya Sekta muhimu, Uadilifu wa Mazingira na Uhimilivu wa Tabianchi, Uchumi Imara, Jumuishi na Shindani na Kuimarisha Misingi ya Uendelevu wa Taifa.

Dkt. Kilama amesisitiza kuwa, matokeo ya warsha hiyo hayatabaki kuwa nadharia pekee, bali yatatumika katika kuboresha sera, mipango na mikakati ya maendeleo ya taifa.

▪︎ Asisitiza Vijana kuomba udahili na ufadhili*

▪︎ Asisitiza Uwazi na Ushindani*

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametangaza rasmi kutolewa kwa ufadhili kupitia Samia Scholarship Exender AI/DS wa masomo ya Uzamili (Masters) katika Sayansi ya Data, Akili Unde na fani zinazohusiana.

Akizungumza Aprili 13, 2026 jijini Dar es Salaam amesema kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika kuandaa rasilimali watu wenye uwezo wa kushindana kimataifa katika sayansi na teknolojia na kuwashawishi vijana wenye vigezo kuomba udahili na ufadhili.

Prof. Mkenda ameeleza kuwa Samia Scholarship extended DS/AI+ ilianza kufadhili wanafunzi wa shahada ya kwanza waliobobea katika sayansi, uhandisi, tiba na hisabati, ambapo tayari wanafunzi 16 wamepelekwa nchini Afrika Kusini na wengine 34 watakwenda nchini Ireland.

Ameongeza kuwa ufadhili wa sasa unalenga kuongeza idadi ya vijana wa kitanzania wenye ujuzi na taaluma katika maeneo hayo.

"Ufadhali huu ni kwa waombaji watakaosoma shahada ya Uzamili katika Taasisi ya Indian Institute of Technology (IIT) Madras – Kampasi ya Zanzibar," amesisitiza Prof. Mkenda

Waziri Mkenda amesema kuwa masharti ni ya wazi ambapo mwombaji awe Mtanzania, mwenye umri usiozidi miaka 35, awe na daraja la kwanza katika masomo ya sayansi ya kidato cha sita, GPA ya angalau 3.8 katika shahada ya kwanza, na awe amepata udahili katika IIT Madras, Zanzibar.

Amesisitiza kuwa hatua ya kwanza ni kuomba udahili chuoni kabla ya Aprili 15, kisha kuwasilisha maombi ya ufadhili kuanzia Juni 1 hadi Juni 30 na kwamba Kamati huru itapitia maombi kwa uwazi na ushindani, kuhakikisha wanafunzi bora zaidi wanapata nafasi.

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikiwa kukamata kilogramu 101.2 za dawa za kulevya aina ya mirungi katika eneo la Tabata Kibo jijini Dar es Salaam, zikiwa zimefichwa ndani ya basi la abiria.

 


 Mbunge wa Jimbo la Hanang Mkoani Manyara ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mhe. Asia Halamga, amekabidhi mifuko ya mbegu za dengu kwa viongozi na wananchi mbalimbali wilayani Hanang  ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha sekta ya kilimo na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa mbegu hizo Mbunge huyo amesema kuwa lengo la kutoa mbegu hizo ni kuongeza tija kwa wakulima na kuinua kipato chao kupitia kilimo cha kisasa hususani baada ya mvua nyingi za mwaka huu kuharibu mazao ya maharage shambani

Asia ameendelea kueleza kuwa  kuwa utoaji wa mbegu hizo utasaidia kurejesha uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula kwa wakazi wa Hanang kwani mbegu za dengu ni mkakati wa kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara yenye soko la uhakika ndani na nje ya nchi.

Kwa upande Mkuu wa Wilaya ya Hanang Almishi Issa Hazali amemshukuru Mbunge Asia Halamga kwa kuwakumbuka wananchi wa Jimbo hilo na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi

“Hatua hii ni ya kupongezwa kwani inaenda moja kwa moja kugusa maisha ya wananchi wetu na sisi kama Serikali tutaendelea kushirikiana na Mbunge sambamba na viongozi wengine wote wenye nia njema ya kuleta maendeleo katika Jimbo letu hili,” Amesema Almishi

Hata hivyo wananchi hao wamemshukuru sana Mbunge huyo kwa msaada huo ambao utaleta mapinduzi makubwa katika sekta ya kilimo.




 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali katika mwaka wa fedha 2025/26 imetenga bajeti kwa ajili ya malipo ya fidia yenye thamani ya Sh Bilioni 5.1 kwa wananchi 1, 730 wanaopisha njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa Kilovoti 220 kutoka Masasi hadi Mahumbika.

Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Aprili 13, 2026 wakati akijibu swali la Mbunge wa Ndanda, Mhe. Faraji Buriani Nandala aliyehoji ni lini Wananchi wa Kata za Chikukwe, Chigugu, Chigundi, Mwena, Ndanda na Nanganga ambao wamepitiwa na Mradi wa Grid ya Taifa watalipwa fidia.








 Timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (NJE Sports) imepoteza kwa mabao 3–2 dhidi ya timu ya Ubalozi wa Umoja wa Ulaya katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Aprili 11, 2026, kwenye Uwanja wa John Merlin, jijini Dodoma.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa James Milya (Mb), amezipongeza timu zote mbili kwa kuonesha ushindani wa kirafiki na kudumisha mshikamano. Amesema michezo ya aina hiyo ina mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano, urafiki na diplomasia kati ya taasisi na mataifa.

Ameongeza kuwa mechi hiyo ni sehemu ya juhudi za kukuza diplomasia ya michezo, sambamba na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo kati ya Wizara na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya.

Mchezo huo pia ulihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa, ambaye amesema kuwa pamoja na ushindani uliokuwepo uwanjani, lengo kuu la mchezo huo lilikuwa kuimarisha uhusiano kati ya pande husika, akisisitiza kuwa huo ndio ushindi mkubwa zaidi kuliko mabao.

Kwa upande wake, kiongozi wa timu ya Ubalozi wa Umoja wa Ulaya, Bw. Ally Mwinchade, amesema ameridhishwa na kiwango cha ushindani kilichooneshwa na timu zote mbili, akieleza kuwa mchezo huo umeimarisha zaidi uhusiano wa kirafiki kati ya pande hizo.

Ameongeza kuwa ushindi huo si matokeo ya uwanjani pekee, bali pia ni ishara ya mshikamano, ushirikiano na dhamira ya kuendeleza diplomasia kupitia michezo. Aidha, ameipongeza timu ya NJE Sports kwa kuonesha mchezo mzuri na kuahidi kuendeleza ushirikiano huo katika michezo ijayo.













Baraza la Wafanyakazi la Nne la Tume ya Ushindani (FCC) limehitimisha kikao chake cha siku mbili kwa kuazimia kuunga mkono rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Miaka Mitano 2026/27-2030/31 unaolenga kutekeleza moja kwa moja Dira ya Taifa ya 2050.

Na Oscar Assenga,Tanga

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman  ameanza jitihada za kuinusuru Klabu ya African Sports ambayo ipo hatarini kushuka daraja kufuatia matokeo mabaya katika Ligi ya Championship.

Rajab aliyasema hayo baada ya kukutana na wachezaji pamoja na viongozi wa klabu hiyo, ambapo alieleza kuwa hali ya timu si ya kuridhisha, akifananisha na mgonjwa aliye katika chumba cha mahututi.

Alibainisha kuwa kwa sasa African Sports inashika nafasi ya 15 kati ya timu 16, hali inayoiweka katika hatari kubwa ya kushuka daraja endapo haitafanya vizuri katika mechi zilizobaki.

Akizungumzia historia ya klabu hiyo, alisema ni moja ya timu zenye heshima kubwa nchini na mshindani wa jadi wa Coastal Union, hivyo ni muhimu kurejesha ushindani wa soka la Tanga.

Katika hatua ya kuokoa timu hiyo, Mwenyekiti huyo  alitangaza kuchangia Shilingi milioni 20 ambazo tayari alikwisha kuziweka kwenye akauti, huku Mbunge wa Jimbo la Tanga akiahidi kutoa milioni tano na mdau mwingine kuahidi milioni 20, ikiwa ni sehemu ya kufikia lengo la kukusanya milioni 45 zinazohitajika kuiwezesha timu kumaliza msimu salama.

Alisema atahakikisha fedha hizo zinapatikana ili kutatua changamoto zinazoikabili klabu hiyo na kuwawezesha wachezaji kucheza kwa utulivu.

Aidha, aliwataka wachezaji kujituma katika mechi zilizobaki ili kuinusuru timu, akisisitiza kuwa wana dhamana ya kulinda heshima ya klabu hiyo.

Kwa upande mwingine, aliwashauri viongozi wa klabu kuweka mikakati ya muda mfupi na mrefu, ikiwemo kutovunja kambi mara baada ya msimu kumalizika ili kuboresha maandalizi ya msimu ujao.

Aliongeza kuwa mabadiliko ya mara kwa mara ya kikosi na maandalizi hafifu yamekuwa yakichangia kushuka kwa kiwango cha timu, na kusisitiza kuwa kwa mipango madhubuti wanaweza kurejea Ligi Kuu katika msimu ujao.