Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana,akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza,ili  kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara yaliyoandaliwa na Baraza la Ushindani wa Soko (FCT).

Na.Mwandishi Wetu-MWANZA

 BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara.

Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

“Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Baraza la Ushindani na nafasi yake katika kulinda haki za mlaji pamoja na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”Alisema Bw.Elikana

Akizungumza katika mafunzo hayo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Bw. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza lipo kwa ajili ya kulinda masuala yote yanayohusu ushindani wa soko na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini. Alieleza kuwa utekelezaji wa majukumu ya Baraza unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha sheria za ushindani zinatekelezwa kikamilifu, kwa haki na kwa uwazi.

Aidha, aliongeza kuwa Baraza huhakikisha mamlaka za udhibiti zinazingatia taratibu na kanuni za ushindani wakati wa utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kutoa majibu sahihi na ya haraka katika migogoro ya kibiashara. Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kumlinda mlaji dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha ushindani, hivyo kuchangia katika ujenzi wa uchumi shindani, jumuishi na wenye tija kwa Watanzania.

Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa Chemba ya Wafanyabiashara, Bw. Hassan Karambi, alisema kuwa amepata elimu yenye manufaa makubwa kupitia programu ya Baraza ya kuwajengea uwezo wadau.

Alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia wafanyabiashara kufahamu kuwa endapo hawataridhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti kama LATRA, TCRA, TCAA, EWURA, PURA pamoja na Tume ya Ushindani (FCC), wana haki ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yao.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa, Bi. Imelda Salumu, alifafanua utaratibu wa Baraza katika kupokea rufaa kutoka kwa wadau.

Alisema kuwa malalamiko huanza kwa mtoa huduma husika, na endapo hayatapatiwa ufumbuzi, hufikishwa katika mamlaka ya udhibiti kama hatua ya kwanza ya rufaa. Aliongeza kuwa iwapo mlalamikaji hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hiyo, utaratibu humruhusu kuwasilisha rufaa katika Baraza la Ushindani kwa hatua zaidi za kisheria.


Kijiji kilishuhudia tukio la kushtua. Daktari mmoja aliyekuwa akijitangaza kama mtaalamu wa upasuaji alinaswa akifanya kazi hatari mtaani. Watu walishangaa kuona kuwa huduma aliyoitoa ilikuwa hatari na haikufuata taratibu za afya.

Wagonjwa walikuwa wakijiingiza hatarini kila siku. Familia za wagonjwa walikuwa na hofu na wasiwasi. Hakukuwa na mamlaka ya kudhibiti kitendo hicho mara kwa mara, na tukio hili lilitokea bila kutarajiwa.

Baada ya tukio, watu walihisi wamesalia na mashaka na hofu kubwa. Familia na marafiki walijaribu kusaidia wagonjwa waliopata matatizo. Wengi walijua kuwa suluhisho la haraka lilihitajika.Soma Zaidi.
Mwanamke huyu alishangaza kijiji chote. Alidai kuwa nyumba ya jirani ni yake na akaanza kujaribu kuiuza. Wajirani walishangaa na kushangilia kwa hofu. Familia ya jirani ilihisi kutoamini kilichotokea.

Tukio hili lilipelekea kesi ya kisheria. Wajirani walijaribu kulinda haki yao. Kila hatua ilichukua muda na hofu ilikuwa kubwa. Mwanamke huyo alijikuta akishindwa kuelezea kitendo chake mbele ya mamlaka.

Baada ya tukio, watu walihisi wamesalia na mashaka. Wengi walihitaji mwongozo wa kisaikolojia na kiroho.Soma Zaidi.
Mume huyu alishangaza wakewe na familia yake. Alimfumania pastor kitandani kwake. Tukio hili liliibua hofu, hasira, na mshangao mkubwa. Familia ilijikuta ikitafuta njia ya kuelewa kilichotokea.

Pastor alidai kuwa alifanya yote kwa ajili ya kutoa pepo na kusaidia kuondoa dhambi. Wengine walishangaa na kushangilia. Watu walijikuta wakiwa kwenye mgongano wa hisia: kuamini au kushuku.

Hali iliendelea kuwa ngumu. Mume na wakewe walijikuta kwenye hofu ya kijamii na kiroho. Wote walihitaji mwongozo sahihi wa kuelewa na kushughulikia tukio hili lisiloeleweka.Soma Zaidi.
Mama huyu alishangaza kijiji chote kwa kitendo chake. Alidaiwa kuiba mtoto wa jirani kwa lengo la kumridhisha mumewe. Tukio hili liliibua hofu, hasira, na mshangao mkubwa.

Familia za watoto walihisi kushikwa na hofu. Marafiki walijaribu kuingilia kati, lakini hali ilikua ngumu. Kila siku ilikuwa changamoto kubwa kwa jamii kuona usalama wa watoto.

Waliopata madhara walihitaji mwongozo wa kisaikolojia na kiroho. Soma Zaidi.
Kijiji kilishuhudia tukio lisilo la kawaida. Binti mmoja aligundulika akihifadhi nguo za ndani za jirani kwenye kamba yake. Wajirani walishangaa na kushutumiwa.

Familia na marafiki walijikuta wakitafuta suluhisho la haraka. Tukio hili liliibua hasira na hofu ya jamii. Kila mmoja alihisi hofu na aibu. Hali ilikua ngumu kwa sababu hakukuwa na mwongozo wa haraka wa kushughulikia kitendo hicho.

Baada ya tukio, waliothirika walihitaji msaada wa kisaikolojia na kiroho. Soma Zaidi.


Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimeendelea kutoa wahitimu mahiri wenye ujuzi wa kitaaluma, maadili na uwezo wa kiuongozi, wenye uwezo wa kuleta mabadiliko chanya katika taasisi na jamii wanazozihudumia.

Akizungumza Februari 6, 2026, wakati wa mahafali ya 27 ya wahitimu wa Shahada ya Uzamili ya mwaka 2025 yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ngurdoto mkoani Arusha, Mkuu wa Chuo Profesa Eliamani Sedoyeka, amesema maboresho yanayoendelea katika huduma za ufundishaji na ujifunzaji yameiwezesha IAA kuandaa wataalamu wanaokidhi mahitaji ya taifa na soko la ajira.

Prof. Sedoyeka amewasisitiza wahitimu kuzingatia misingi ya uwajibikaji, uadilifu na uzalendo wanapotekeleza majukumu yao huku akiwataka kutumia ujuzi wa kisayansi, tafiti na maadili katika kufanya maamuzi katika maeneo watakayoaminiwa kuyahudumia.

“Mmeandaliwa kuwa viongozi wenye maarifa, maadili na uwezo wa kuongoza mabadiliko chanya katika taasisi na jamii mnazozihudumia, Ni wajibu wenu kuzingatia uwajibikaji, uadilifu na uzalendo katika kila jukumu mtakalotekeleza,” amesema Prof. Sedoyeka.

Akizungumzia mchango wa tafiti zilizofanywa na wahitimu, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, Dkt. Mwamini Tulli, amesema tafiti hizo ni msingi muhimu katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi, kuboresha utoaji wa huduma na kuchochea ukuaji wa uchumi endelevu.

Dkt. Tulli amesisitiza kuwa matokeo ya tafiti zilizofanywa na wahitimu hazipaswi kubaki kwenye makabati bali yatumike kutatua changamoto halisi zinazolikabili taifa na taasisi zake.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula, ameupongeza uongozi wa IAA kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya kisasa inayoendana na mabadiliko ya teknolojia duniani, hali iliyowawezesha kuzalisha wahitimu wenye uwezo wa kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Naibu Waziri amethibitisha kuwa hatua hiyo ni ishara ya dhamira ya huo katika kuhakikisha mifumo ya ufundishaji na ujifunzaji inaendana na mahitaji ya dunia ya sasa na ya baadaye.












Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar(Mb), amekipongeza Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwa kufanya mageuzi ya kidigitali, ufanyaji wa tafiti, maendeleo pamoja na mipango na mikakati ya kuboresha na kuongeza ufanisi kwenye utoaji wa mafunzo, na ushauri wa kitaalam, ambazo ni miongoni mwa vichocheo vya kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050.


Hayo yasemwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), wakati akihutubia kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), katika Mahafali ya 27 (Duru ya Pili) ya Chuo hicho, yaliyofanyika katika Hoteli ya Ngurdoto, mkoani Arusha.

Mhe. Luswetula alisema kuwa mchango wa IAA katika uchumi wa Taifa ni mkubwa kwa kuwa kimeendelea kuzalisha wataalam wa fedha, uhasibu, uchumi, kodi, utalii, usimamizi biashara, benki, ununuzi na ugavi, masoko, bima, TEHAMA na nyingine nyingi.

 Alisema kuwa Wataalam hao wamekuwa mhimili muhimu katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, usimamizi wa fedha za umma, sekta binafsi, taasisi za kifedha na miradi ya maendeleo.

Aliongeza kuwa Kupitia wahitimu wake, Chuo kimechangia kwa vitendo katika kukuza uwajibikaji, uwazi na nidhamu ya kifedha nchini.

“Niwapongeze IAA mmeendelea kudhihirisha umahiri mkubwa katika kuandaa rasilimali watu mahiri, wanaokidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa Taifa letu” alisema Mhe. Luswetula.

Aidha, Mhe. Luswetula alikisifu Chuo cha IAA kwa kuwa kinara katika kuboresha mifumo ya ufundishaji na ujifunzaji kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa sambamba na kuimarisha tafiti na ushauri wa kitaalam.

“Mageuzi ya kidigitali ni kichocheo muhimu cha maendeleo hususan katika kuboresha ukuaji wa uchumi na kuimarisha huduma za jamii ikiwemo elimu. Serikali inatambua na kupongeza juhudi za IAA katika kuwekeza kwenye mifumo ya kidigitali na katika kuimarisha ufanisi wa utoaji wa elimu kwa njia bunifu,” aliongeza Mhe. Luswetula.

Mhe. Luswetula alitumia fursa hiyo pia kuwasihi wanafunzi na wahitimu wa Shahada ya Uzamili kutumia tafiti zao kutoa majibu ya changamoto halisi zinazolikabili Taifa kama vile usimamizi wa fedha za umma, ukuaji wa uchumi jumuishi, ajira, ubunifu na matumizi sahihi ya teknolojia.

“Tafiti zenu ziwe chachu ya sera bora, maamuzi sahihi na maendeleo endelevu kwa wananchi na Taifa letu,” alisisitiza.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya ukuaji wa uchumi na maendeleo jumuishi yanayomgusa kila Mtanzania, huku sekta za fedha, uhasibu, uchumi, benki, usimamizi wa biashara na miradi zikiwa nguzo muhimu katika kuhakikisha rasilimali za Taifa zinakusanywa, zinapangwa, zinatumika na zinadhibitiwa kwa ufanisi, uwazi na uwajibikaji.

Aidha, alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha, itaendelea kuhimiza na kuunga mkono Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyoendana na dira ya Taifa ya kujenga uchumi wa kisasa unaotegemea maarifa na ujuzi.

“Wizara itaendelea kushirikiana na vyuo hivi katika kuweka mazingira wezeshi ya kifedha na kisera yatakayowezesha kuimarishwa kwa kozi za kimkakati, tafiti zenye tija, na maandalizi ya wataalam wanaokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.” Alisema Mhe. Luswetula

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Dkt. Mwamini Tulli, alisema kuwa Chuo hicho kimejipanga kuendelea kutoa wahitimu mahiri kwa kuwekeza katika rasilimali watu, hususani wahadhiri wenye sifa, uzoefu wa kitaaluma na kitaalam, pamoja na kuimarisha mbinu shirikishi za ufundishaji na ujifunzaji.

Alisema kuwa IAA imejipambanua kama Taasisi inayozalisha wahitimu mahiri, wabunifu, na wenye uwezo wa kuchambua na kutatua changamoto za jamii inayowazunguka, maeneo wanayofanyia kazi zao na Taifa kwa ujumla.

Wahitimu wa Shahada ya Uzamili wa IAA wanatambulika kwa ubora wa taaluma, maadili, na weledi wa kitaaluma katika sekta mbalimbali.

“Ubora huu unatokana na mitaala inayozingatia mahitaji ya sasa ya soko la ajira, maendeleo ya teknolojia, na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii. IAA imeendelea kuhakikisha kuwa programu zake za Uzamili zinawajengea wanafunzi ujuzi wa kina, fikra pevu, na uwezo wa uongozi” alisema Dkt. Tulli.

Aliongeza kuwa Baraza la Uongozi wa Chuo litaendelea kusimamia kwa karibu mipango na kimkakati ya Chuo, ili kuhakikisha IAA inaendelea kuwa Taasisi kinara katika elimu ya juu, tafiti, na ushauri wa kitaalamu nchini na nje ya nchi.

Naye Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka, alisema kuwa kwa kutambua mabadiliko ya kasi katika mahitaji ya soko la ajira na uongozi wa kitaifa, Chuo hicho kinaendelea kuimarisha huduma za ufundishaji na ujifunzaji kwa kuboresha mitaala, mbinu za kufundishia, na mifumo ya tathmini ili kuendana na sera, mikakati, na dira ya maendeleo ya Taifa 2025-2050.

Alisema kuwa IAA imeweka mkakati mahususi wa kuwawezesha wahadhiri wengi zaidi kusomea Shahada ya Uzamivu ndani na nje ya nchi, ili kukidhi ongezeko la idadi ya wanafunzi wa Uzamili linaloendelea kushuhudiwa kila mwaka ambapo katika mwaka wa masomo 2025/2026 jumla ya wahadhiri 115 wamepelekwa kusoma Shahada ya Uzamivu (PhD) katika vyuo mbalimbali nchini na nje ya nchi.

“Mkakati huu unalenga kuhakikisha uwiano sahihi kati ya wanafunzi na wahadhiri, kuimarisha usimamizi wa tafiti, na kuongeza uwezo wa Chuo katika uzalishaji wa wataalam wanaokidhi mahitaji ya kitaifa na kimataifa” alisema Prof. Sedoyeka.

Mahafali ya 27 (Duru ya Pili) ya IAA, imewahusisha jumla ya wahitimu 2,250 kati yao wanaume wakiwa 1,369 sawa na asilimia 60.8 na wanawake 881 sawa na asilimia 39.2 ambao wametunukiwa Shahada ya Uzamili katika fani kumi na tano (15) .

Fani hizo ni (Accountancy), Uhasibu na Fedha (Accounting and Finance), Fedha na Benki (Finance and Banking), Fedha na Uwekezaji (Finance and Investment), Usimamizi wa Miradi (Project Planning Management), Usimamizi wa Taarifa (Information Management), Uchumi na Fedha (Economics and Finance), Usimamizi wa Elimu (Education Management), Usimamizi wa Rasilimali watu (Human Resource Management) na Amani na Usalama (Peace and Security ). Fani nyingine ni Usimamizi wa Biashara (Master of Business Administration in Corporate Management), Usimamizi wa Biashara katika Teknolojia ya Habari (MBA-Information Technology), Usimamizi wa Biashara katika Uandaaji na Utekelezaji wa Sera (MBA-Policy Development and Execution), Usimamizi wa Biashara katika Uongozi (MBA-Leadership and Governance), Usimamizi wa Biashara katika Ununuzi na Ugavi (MBA-Procurement and Supply Chain Management).














Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Handeni, Amiri Mwaliko,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju,akizungumza katika mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa,akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese,wakati wa  mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Sehemu ya Madiwani wakifuatilia mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata za Halmashauri ya Mji Handeni uliofanyika leo Februari 7, 2026.

Na Augusta Njoji

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Mji Handeni, Mhe. Amiri Mwaliko, amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kibali cha ajira kilichowezesha kupatikana kwa watumishi 82 wa kada mbalimbali na hivyo kupunguza uhaba wa watumishi katika halmashauri hiyo.

Akifungua mkutano wa kupokea na kujadili taarifa za kata wa Halmashauri hiyo uliofanyika Februari 7, 2026 mjini hapa, Mhe. Mwaliko amesema serikali imeendelea kuchukua hatua za kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi.

“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kutatua changamoto ya watumishi. Tunafurahia hatua hii kwa kuwa lengo la serikali ni kuondoa uhaba wa watumishi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema.

Aidha, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, kwa kuhakikisha wilaya hiyo inaendelea kudumisha amani na utulivu.

Mhe. Mwaliko amewataka viongozi na watumishi kushirikiana katika kujenga halmashauri yenye mshikamano na kutatua changamoto zinazojitokeza.

Ameongeza kuwa ni muhimu kusimama pamoja na watumishi na kushughulikia changamoto kwa njia ya mazungumzo ili kujenga timu imara ya utendaji kwa maendeleo ya halmashauri.

Kadhalika, amesisitiza kuendelea kuchukuliwa hatua za kudhibiti utoro wa wanafunzi kwa kushirikiana na madiwani wa maeneo husika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 serikali imeajiri watumishi 82 wakiwemo walimu wa shule za msingi na sekondari pamoja na wauguzi.

Amesema changamoto ya upungufu wa watumishi inaendelea kupatiwa ufumbuzi kadri serikali inavyoendelea kutoa ajira, huku halmashauri ikiendelea kutenga bajeti kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya kata, ikiwemo ununuzi wa madawati.