Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akifuatilia maelezo ya Mhandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Rashid Mtamila (wa tatu kutoka kushoto) walipotembelea uwanja wa Sokoine leo Septemba 17, 2025, kukagua maandalizi ya uwanja huo kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.

Na; Mwandishi wetu- Mbeya

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus amekagua maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zitakazofanyika jijini Mbeya.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mkoa kuhusu maandalizi leo 17 Septemba 2025, Naibu Katibu Mkuu Zuhura Yunus alieleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi na kuipongeza kamati ya Mkoa kwa kuendelea kusimamia na kuratibu vyema shughuli hiyo.

Katika ziara hiyo, Naibu Katibu Mkuu huyo aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo kukagua uwanja wa Uhindini kutakapofanyika maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa, uwanja wa Sokoine kwa ajili ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na kukagua mazoezi ya vijana wa halaiki.

Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa mwaka 2025 zinaongozwa na kauli mbiu isemayo “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa waka 2025 kwa Amani na Utulivu”.

Mbio hizo zilizinduliwa rasmi Aprili 2, 2025 Kibaha, Mkoani Pwani na kilele chake kitafanyika Mkoani Mbeya Oktoba 14, 2025, ambapo Mwenge wa Uhuru unakimbizwa katika mikoa 31 na Halmashauri 195 zikiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Mkoa wa Mbeya wakati wa ziara yake Septemba 17, 2025 ya kukagua maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru zitakazofanyika jijini Mbeya.

Wajumbe wa Kamati Elekezi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakifuatilia taarifa ya mkoa wa Mbeya kuhusu maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025.

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo akieleza hatua zilizofikiwa na mkoa kuhusu maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akikagua moja ya mabango ya hamasa kuhusu kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru yaliyaondaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya leo Septemba 17, 2025, jijini Mbeya.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akikagua maeneo mbalimbali katika uwanja wa Sokoine wakati wa ziara yake ya kufuatilia Maendeleo ya maandalizi ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025, jijini Mbeya.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akifuatilia maelezo ya Mhandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Rashid Mtamila (wa tatu kutoka kushoto) walipotembelea uwanja wa Sokoine leo Septemba 17, 2025, kukagua maandalizi ya uwanja huo kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.

 

Sikuwahi kufikiria siku moja ningefutwa kazi bila hata kupewa sababu. Ilikuwa siku ya Ijumaa asubuhi nilipoitwa ghafla ofisini kwa meneja. Nilipofika, nilikabidhiwa barua na kuambiwa huduma zangu hazihitajiki tena. Nilihisi dunia inazunguka, moyo ukasita kupiga kwa sekunde kadhaa. Nilishindwa hata kuuliza kwa nini. Niliondoka ofisini nikiwa na machozi yakinitiririka, nikihisi aibu na huzuni kubwa.

Wiki ya kwanza nyumbani ilikuwa mbaya zaidi. Niliamka kila asubuhi nikijiuliza kosa langu lilikuwa lipi. Niliogopa kukutana na majirani au marafiki kwani sikutaka kuulizwa maswali. Kila usiku nililala nikiwa na mawazo mazito, nikijiuliza maisha yangu yangeendeleaje bila kipato.

\Nilikuwa nimezoea maisha yenye ratiba na mshahara wa kila mwezi. Mara ghafla nikawa sina kazi, sina mpango, na sina uhakika wa kesho.

Nilijaribu kutuma maombi ya kazi mtandaoni na kwa rafiki zangu lakini sikupata majibu yoyote. Hali yangu ya kiakili ilianza kuwa mbaya.

Nilianza hata kufikiria pengine nililaaniwa au kuna mtu alikuwa hanitakii mema. Ilikuwa kama kila kitu kilikuwa kikinipita, na wenzangu wa zamani kazini walionekana kufurahia maisha. Hapo ndipo nilipoamua sitakaa chini nione maisha yangu yakiharibika. Soma zaidi hapa 

 


 Na; Mwandishi Wetu - Kilindi 

 Vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mkuu nchini mwaka 2025,katika Jimbo la Kilindi vimetakiwa kufanya kampeni za kistaarabu ili kuendeleza utulivu na amani iliopo nchini. 

Wito huo umetolewa na Afisa mwandamizi kutoka ofisi ya msajili wa vyama vya siasa Bi. Edna Assey katika kikao cha mafunzo na vyama vya siasa vyenye wagombea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, katika jimbo la Kilindi kilichofanyika tarehe 17/09/2025 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya wilaya ya Kilindi. 

 “wakati wa kufanya kampeni zenu acheni sera ziongee” alisema Afisa mwandamizi Bi Assey na kuvitaka vyama vya siasa kunadi sera zao ili zieleweke kwa wananchi na kuacha kutumia maneno na vitendo ambavyo vinaweza kuhatarisha kuvunjika kwa amani na utulivu. 

 Aliongeza kusema kuwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ina majukumu mbalimbali ikiwemo kusimamia utekelezaji wa sheria ya vyama vya siasa sura ya 258 na kuvitaja vitendo vinavyokatazwa na sheria ya vyama vya siasa kuwa ni pamoja na Kunadi sera zinazopingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Katiba ya Zanzibar na Sheria nyingine za nchi, Kuunda kikundi cha ulinzi na usalama cha aina yeyote au kuwa na taasisi inayolenga kufanya majukumu ya jeshi la polisi au vikosi vingine vya ulinzi na usalama wa nchi.

 Kuratibu,kuendesha au kufadhili mafunzo yeyote ya kutumia nguvu au silaha kwa wananchama wake au kwa mtu yeyote Kuhamasisha udini,ukabila na ukanda ,kuhamasisha kuvunjika kwa Muungano wa Tanzania au kuwa na lengo la kufanya siasa upande mmoja wa Muungano Vitendo vingine vinavyokatazwa na sheria ya vyama vya siasa ni kuruhusu au kuhamasisha matumizi ya nguvu kama njia ya kufikia malengo ya kisiasa.

 Kuruhusu viongozi au wananchama wake kutumia maneno ya matusi,dhihaka,kashfa na uchochezi yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani Kupeperusha bendera ya chama,kufanya siasa au kufungua tawi katika maeneo ya kazi,shule,vyuo,ibada
,majengo ya serikali au umma Kutoa matamshi,kuandaa machapisho,kuharibu au kufanya kitendo chochote chenye dhamira ya kudhalilisha au kudhihaki bendera ya chama kingine na kufanya mikutano au maandamano bila kufuata utaratibu wa kisheria.


 Kwa upande wao viongozi wa vyama vya siasa Wilayani Kilindi waliipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kwa maandalizi mazuri ya uchaguzi na kuomba kuendeleza ushirikiano mzuri kati ya serikali na vyama vya siasa. 




 


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa Watanzania kudumisha amani na utulivu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa uchaguzi siyo vita bali ni tendo la demokrasia.

Akihutubia leo, Jumatano Septemba 17, 2025, katika kijiji cha Kajengwa, Makunduchi, Visiwani Zanzibar, Dkt. Samia amesema amani ni msingi wa maendeleo ya Taifa na inapaswa kulindwa kwa gharama yoyote, hususan wakati huu wa uchaguzi.

“Ndugu zangu, tunaingia kipindi cha uchaguzi. Mwanzo nilipokuja kujitambulisha, ahadi kubwa niliyoitoa ni kuifanya Tanzania iwe na amani na utulivu. Sasa tunapoelekea Uchaguzi Mkuu, nawaomba sana tudumishe amani na utulivu. Uchaguzi si vita, ni tendo la demokrasia. Nenda weka kura yako, kisha rudi nyumbani ukatulie ili nchi ibaki salama,” amesema Dkt. Samia.

Dkt. Samia ameonya dhidi ya vitendo vya vurugu na matumizi ya silaha za aina yoyote, akisema havileti suluhisho la maana kwa Taifa. Amesisitiza kuwa utulivu na mshikamano wa kitaifa unapaswa kupewa kipaumbele na kila Mtanzania.

Aidha, Dkt. Samia amesema vyombo vya ulinzi na usalama nchini vimejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira salama na ya amani, Bara na Visiwani.

KIGODA Cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere katika Taaluma za Umajumui wa Afrika (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam) kwa kushirikiana na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP Centre), limeandaa kongamano kubwa la kujadili Uchumi Jumuishi kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

 

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeandaa kikao cha Waratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 15–19 Septemba 2025  ambacho kimeshirikisha taasisi 22 kwa lengo la kujadili maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimeshiriki kama moja ya taasisi nufaika ya mradi huu.

Akifungua kikao hicho Mratibu wa Mradi wa HEET KitaifaDkt. Kenneth Hosea amewataka waratibu hao kutumia kikao hicho kubadilishana uzoefu katika kuboresha utekelezaji wa mradi huo, ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 74.3 hali inayoonesha kasi nzuri ya shughuli zilizopangwa kutekelezwa katika mradi huo

 Akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Mratibu wa Mradi HEET IAA, Mratibu Msaidizi wa Mradi wa HEET IAABw. Emmanuel Pallangyo amesema, IAA kupitia mradi huu IAA inaendelea na ujenzi wa majengo ya TEHAMA, taaluma, utawala, maktaba na maabara ya kompyuta katika kampasi za SongeaBabati na Arusha ambayo yatachangia kuboresha mazingira ya ufundishaji, ujifunzaji na kuongeza udahili wa wanafunzi.

Aidha, Pallangyo amesema ujenzi wa majengo hayo umezingatia miundombinu wezeshi kwa watu wenye mahitaji maalum, huku akibainisha kuwa jumla ya wananchi 1055 wamepata ajira za muda katika ujenzi unaoendelea  ikiwemo ujenzi, utoaji wa huduma za chakula na ufundi mbalimbali, ambazo zinawasaidia kujipatia kipato kwa ajili ya kujikimu kimaisha. 

Pamoja na ujenzi wa miundombinu, Pallangyo amesema mradi wa HEET umewezesha IAA kuhuisha jumla ya mitaala 08 ili kuendana na mahitaji ya soko la ajira, kutoa mafunzo ( Shahada ya Uzamivu) kwa watumishi 22 , kuimarisha ushirikiano wa kisekta katika ya Chuo na wadau ikiwemo sekta binafsi na kuongeza uelewa wa masuala ya jinsia na elimu jumuishi katika utoaji wa elimu.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mradi huu  imetenga jumla ya shilingi bilioni 48 kwa  ajili ya IAA ili kuwezesha ujenzi na uboreshaji wa miundombinu, mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa watumishi, kuimarisha ushirikiano wa kisekta na kuimarisha masuala ya jinsia na elimu jumuishi.













 


Baadhi yao waliniambia waziwazi kuwa hawawezi kuwa na mwanamke mwenye ulemavu. Nilipita katika aibu nyingi za hadharani na mara nyingine nililia usiku kucha nikiuliza Mungu kwa nini mimi.

Niliona marafiki zangu wakiolewa mmoja baada ya mwingine, wengine wakiposti mitandaoni maisha ya kifahari wakiwa na wake zao. Mimi nilibaki peke yangu, moyo wangu umevunjika. Nilipoteza imani kwamba ningepata mwanaume atakayenipenda kwa dhati.

Nilikuwa nimekubali kuishi maisha ya upweke hadi rafiki yangu mmoja aliniambia nisiache kupigania furaha yangu. Aliniambia kuna suluhisho na akanipendekeza nimtafute Doctor Kashiririka.

Nilipiga simu huku nikiwa na mashaka, nikamweleza yote niliyopitia. Nilishangazwa na jinsi alivyonisikiliza kwa upole na kunipa moyo. Aliniambia kuwa haijalishi hali yangu, bado naweza kuvutia upendo wa kweli.

Aliniandalia dawa za mitishamba maalum za kuvutia mapenzi ya kweli na kuondoa laana ya kukataliwa. Nilifuata maagizo yake kwa makini, nikiweka matumaini yangu yote kwenye tiba hiyo. Soma zaidi hapa 

  


Nilikuwa mtu mwenye furaha, kazi nzuri na familia yenye upendo, lakini ghafla maisha yangu yalibadilika. Nilianza kupoteza kila kitu bila sababu ya kueleweka. Kwanza nilifutwa kazi ghafla bila kosa lolote. Baada ya hapo, biashara ndogo niliyokuwa nimewekeza ikaanguka.

Ndoa yangu nayo ikayumba, mume wangu akaanza kuwa mkali na hatimaye akaniacha. Watu waliokuwa marafiki zangu wakaanza kuniepuka kana kwamba mimi ndiye nilikuwa chanzo cha matatizo yote. Nilihisi dunia imenipoteza na sikujua la kufanya.

Nilipojaribu kuanza upya, kila hatua ilikuwa inakwama. Nilikuwa nikipata kazi mpya, lakini ndani ya miezi michache nilifutwa tena. Afya yangu nayo ilianza kudorora, nilikuwa mgonjwa kila mara bila madaktari kupata tatizo maalum.

Nilijikuta nikiwa mpweke, sina msaada, na sina cha kutegemea. Nilihisi kama kuna nguvu isiyoonekana inayonifuatilia na kuhakikisha sipigi hatua yoyote ya kimaisha. Woga na huzuni vilinifanya nisiamini tena mtu yeyote, na nilikaribia kukata tamaa kabisa. Soma zaidi hapa 

 

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza leo  Septemba 16, 2025, wakati wa ziara yake ya kukagua athari za moto uliotokea alfajiri ya Septemba 15 katika soko la Kawe.

...

SERIKALI  imetenga shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa soko la muda kwa wafanyabiashara waliokumbwa na janga la moto katika soko la Kawe, huku ikiahidi kukamilisha ujenzi huo ndani ya wiki mbili.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo, ametoa  kauli hiyo leo  Septemba 16, 2025, wakati wa ziara yake ya kukagua athari za moto uliotokea alfajiri ya Septemba 15 katika soko hilo.

Dkt.Jafo amesema kuwa  ujenzi wa soko hilo la muda utafanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers, na kumtaka Mhandisi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha kazi hiyo inakamilika kwa muda uliopangwa ili wafanyabiashara waweze kurejea kazini.

“Serikali imejipanga kuhakikisha shughuli za biashara zinaanza tena haraka. Wafanyabiashara wataendelea kutumia soko la muda wakati Serikali ikiendelea na mpango wa kujenga soko la kudumu la kisasa litakalokuwa na miundombinu bora na bima dhidi ya majanga,” amesema  Dkt. Jafo.

Aidha, ametoa  onyo kali dhidi ya kuingilia mchakato wa upangaji wa maeneo katika soko la muda, akisisitiza kuwa ni wafanyabiashara halali pekee ndio watakaopangiwa nafasi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Saad Mtambule, amethibitisha kuwa mbali na shilingi milioni 400 zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko la muda, Serikali pia imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara walioathirika na moto huo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Bi Hanifa Hamza, amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) imedhamiria kujenga soko jipya la kisasa litakalokuwa na mpangilio bora, uzio, na miundombinu ya kisasa ikiwemo bima ya majanga.