Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw. Abdul-Razaq Badru ameongoza kikao cha kimkakati kilichojumuisha waheshimiwa Madiwani,  Viongozi wa Mila, watendaji wa kata, wenyeviti wa Vijiji na watendaji wa vijiji kwa lengo la kudumisha mahusiano na uboreshaji wa huduma za kijamii na uboreshaji wa shughuli  za Uhifadhi shirikishi.

Kamishna Abdul-Razaq Badru ameeleza kuwa kikao hicho ni sehemu ya mkakati wa Mamlaka hiyo kukutana na makundi mbalimbali kujadili uboreshaji wa shughuli za kijamii na huduma za wananchi kama Maji, shule, Malisho, barabara, mawasiliano, afya na mengineyo.

"Viongozi na Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro ni wadau muhimu katika hifadhi, tunakutana nao kama sehemu ya kuboresha uhusiano na kuwaeleza mikakati ya Serikali dhidi yao. 

 kwa sasa tunaboresha miundombinu ya huduma za maji, ujenzi wa Barabara kwa tabaka gumu kutoka Loduare hadi Golini, kujenga minara mipya ya mawasiliano 9 ndani ya hifadhi ili kufikisha huduma kwa wananchi na wadau mbalimbali" amefafanua Kamishna Badru.

Kwa upande wa Viongozi waheshimiwa Madiwani, viongozi wa Mila wameiomba Serikali kupitia Mamlaka hiyo kuendelea kuboresha mahusiano, huduma za kijamii kama  miundombinu ya Maji, barabara, ukarabati wa vituo vya afya na shule, mahitaji  ya baraza la wafugaji, chunvi za mifugo na mpango wa malisho ya mifugo hawa wakati wa kiangazi.











 

Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati) akiwa na viongozi wengine wa wa Serikali, Bunge, na Benki ya CRDB wakipata maelezo kutoka mwanzilishi wa kampuni ya Aquafresh iliyoshiriki katika maonesho ya biashara changa bunifu za vijana katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (katikati) akipokelewa na kikundi cha ngoma za asili vacati alipowasili katika uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Wengine pichana ni kushoto kwake ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wapili kushoto) akipata maelezo kutoka kampuni ya Kana Wine iliyoshiriki katika maonesho ya biashara changa bunifu za vijana katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (watatu kulia), Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Dkt. Donald Mmari (wapili kulia), Mwenyekiti wa CRDB Bank Foundation, CPA Osward Urassa (wakwanza kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.
Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wapili kushoto) akiwasili katika katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Alioongozana nao ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wakwanza kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Kitila Mkumbo, ameipongeza CRDB Bank Foundation pamoja na CRDB Bank kwa kuanzisha programu ya Go Green na IMBEJU, akisema ni hatua ya kimkakati inayounganisha ajenda ya Serikali ya uchumi wa kijani na uwezeshaji wa vijana nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, Profesa Mkumbo alisema mpango huo unaendana na Dira ya Taifa 2050 inayolenga kujenga uchumi jumuishi, shindani na himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, huku vijana wakitambuliwa kuwa nguvu kazi kuu ya maendeleo.

Alisema Serikali imeweka mkazo katika kukuza ubunifu wa vijana, uchumi wa kijani na ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi, akibainisha kuwa miradi ya vijana inayolinda mazingira ni utekelezaji wa moja kwa moja wa dira ya maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Abdulmajid Nsekela, alisema Go Green na IMBEJU ni daraja linalounganisha fedha za kimataifa za tabianchi na vijana wabunifu wanaokosa dhamana au historia ya mikopo katika mifumo ya kawaida ya kifedha. Alieleza kuwa kupitia programu ya TACATDP yenye thamani ya dola milioni 200 kwa ushirikiano na Green Climate Fund, zaidi ya Sh bilioni 100 tayari zimetolewa kufikia takribani wanufaika 600,000 kote nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Tully Esther Mwambapa, alisema maombi ya programu yatafanyika kidijitali kupitia jukwaa la FursaHub kuanzia Februari 12 hadi Machi 11, 2026, yakilenga kuchuja miradi yenye uwezo wa kujiendesha kibiashara na kurejesha mitaji nafuu. Alibainisha kuwa mitaji itatolewa kuanzia Sh 500,000 hadi Sh milioni 500, huku miradi bora zaidi ikipata ruzuku ya kati ya Sh 500,000 hadi Sh milioni 10 kuongeza kasi ya ukuaji.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Naibu Spika wa Bunge, Daniel Sillo, alisema Bunge limeweka msingi wa kisheria unaounga mkono ulinzi wa mazingira na uchumi wa kijani, akitaja programu hiyo kuwa mfano halisi wa kuunganisha sera, mitaji na ubunifu wa vijana.

Kwa niaba ya vijana wanufaika, Irene Vambi, mwanzilishi wa Mrembo Naturals, alisema programu ya IMBEJU imemwezesha kubadili wazo la biashara kuwa uzalishaji unaokua na kutoa ajira kwa vijana wengine, akiwahimiza vijana nchini kutumia fursa hiyo kujenga mustakabali wao kiuchumi.

Uzinduzi wa Go Green na IMBEJU unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa mitaji nafuu, kuimarisha biashara bunifu za vijana na kuchochea uchumi wa kijani nchini, huku ukiongeza mchango wa sekta binafsi katika maendeleo endelevu ya taifa.

Ukitaka, naweza pia kukuandalia kichwa cha habari kikali cha ukurasa wa mbele, au toleo fupi la mtandaoni.

 


Na Munir Shemweta, WANMM

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani mwaka huu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi itaendesha Kliniki Maalum ya Ardhi kwa ajili ya wanawake itakayojulikana kwa jina la "Samia Ardhi Week."

Kiniki hiyo itashughulikia changamoto za ardhi kwa wanawake na itafanyika kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026 katika mikoa yote ya Tanzania Bara ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake ambayo huadhimishwa tarehe 8 Machi kila mwaka ambapo kwa mwaka huu inaongozwa na Kaulimbiu "Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050"

Akizungumza jijini Dodoma tarehe 12 Februari 2026 wakati wa kuahirisha Kliniki Maalum ya Maombi ya Hati, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema, wanawake wote wenye changamoto za ardhi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi katika maeneo ambayo kliniki hizo zitafanyika.

"Wanawake wote wenye shida za masuala ya ardhi wanatakiwa kujitokeza katika mikoa ya Tanzania Bara ambayo kliniki hizo zitafanyika" amesema Mhe Dkt. Akwilapo.

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nia ya wizara yake kuanzisha kliniki za ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ni kuwafikia wananchi wenye shida zinazohusiana masuala ya ardhi.

Akizungumzia Kliniki Maalum ya Maombi ya Hati aliyoiahirisha, Mhe. Dkt Akwilapo amesema, kliniki hiyo imekuwa na mafanikio makubwa ambapo hadi kufikia tarehe 12 Februari 2026 wananchi 4,597 wamehudumiwa huku Hatimilki 3,878 zikiwa zimeandaliwa.

"Kumbe kupata hati inawezekana, katika hati 3,878 zilizoandaliwa jumla ya hati 1,508 zimechukuliwa na wahusika huku hati 2,370 zikiwa bado hazijachukuliwa", amesema Dkt. Akwilapo.

Ametoa rai kwa wananchi ambao wamepata huduma na hati zao zimekamilika wafike ofisi za ardhi kwa ajili ya kuzichukua kwa kuwa hati hizo za ardhi ni mali yao.

Kliniki Maalum ya Maombi ya hati ilianza januari 28, 2026 katika viwanja vya Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Dodoma na kuhitimishwa tarehe 12 Februari 2026.








Na Mwandishi Wetu Morogoro

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa, imefanya kikao kazi kinacholenga kuimarisha ushirikiano kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi za Elimu ya Juu na Taasisi za Utafiti katika eneo la usimamizi wa maafa leo tarehe 12 februari, 2026 Mkoani Morogoro.

Akifungua Kikao hicho Dkt. James Henry Kilabuko Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu kwa niaba ya Dkt. Jim Yonazi  Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo amesema;

Lengo kuu la kikao kazi hiki ni kuandaa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano na Mpango Kazi wa kuimarisha matumizi ya Sayansi, Teknolojia, Utafiti na Ubunifu katika usimamizi wa maafa kwa pamoja nchini ili kuweza kuwasaidia Wananchi katika kujiandaa, kuzuia na kukabiliana na maafa kipindi yanapotokea.

Aidha ameeleza kwamba, Serikali inadhamira ya kuimarisha mfumo wa taifa wa usimamizi wa maafa kwa kuzingatia mzingo mzima wa maafa unaojumuisha kuzuia na kupunguza madhara, kujiandaa, kukabiliana na maafa yanapotokea pamoja na kurejesha hali baada ya maafa. 

Amesema Mwelekeo huu, umeainishwa wazi katika Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2004, (Toleo la Mwaka 2025) inayosisitiza matumizi ya sayansi, teknolojia na tafiti katika kufanya maamuzi na utendaji wenye ufanisi.

"Katika utekelezaji wa sera na sheria, Ofisi ya Waziri Mkuu imeona umuhimu wa kuimarisha ushirikiano na Vyuo vya Elimu ya Juu na Taasisi za Utafiti nchini, Ushirikiano huu unalenga kuhakikisha kuwa tafiti, mafunzo na teknolojia zinajibu changamoto zinazokabili taifa letu" amesema Dkt. Kilabuko

Pamoja na hayo, Dkt. Kilabuko amesisitiza uunganishaji wa nguvu, maarifa na rasilimali tulizonazo,  utajenga Taifa lenye ustahimilivu dhidi ya maafa na lenye uwezo wa kufikia malengo ya maendeleo yaliyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Awali Mkurugenzi wa Idara ya Menejimentu ya Maafa Brg. Jenerali Hosea M. Ndagala alisema, kikao hiki kinatoa fursa ya kujenga uelewa wa pamoja kati ya wahadhiri, wataalamu wa kitaaluma na watendaji wa Serikali kuhusu mahitaji halisi ya shughuli za usimamizi wa maafa katika ngazi ya kitaifa, mkoa hadi wilaya kwa lengo la kuongeza ufanisi wa majibu wakati wa maafa na kuboresha mikakati ya kurejesha hali baada ya maafa. 




Na Mwandishi wetu -Dodoma


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Watu Wenye Ulemavu (SBUU) Mhe. Ummy Nderiananga amesema, Serikali itaendelea kuwaunga mkono watu wenye ulemavu ili wajikwamue kiuchumi.


Mhe. Nderiananga alisema  hayo wakati akikabidhi Cherehani kwa mkazi wa Mtaa wa Viwandani Bw. Eliah Ndayabunya mwenye ualbino  alipomtembelea Ofisini kwake Jijini Dodoma.

Alisema, amemkabadhi cherehani hiyo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Watu Wenye Ulemavu) ili kumrahisishia shughuli zake za ushonaji kwa lengo la kujipatia kipato na kupunguza utegemezi.


“Tumefurahi tumempokea kijana wetu, alifika katika Ofisi hii kueleza shida yake ambapo alitaka kusaidiwa cherehani, hivyo kupitia Ofisi ya Waziri wa Nchi Mhe. William Lukuvi nimemkabidhi kifaa hiki  hatua ambayo ni kuonyesha utu na kuwathamini watu wenye ulemavu,” alisema Mhe. Nderiananga.


Pia, aliongeza kuwa juhudi hizo ni kushiriki falsafa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha watu wenye ulemavu hawaachwi nyuma katika shughuli za maendeleo.


Aidha, akitoa shukrani zake kwa Serikali mara baada ya kukabidhiwa Cherehani hiyo Bw. Ndayabunya alimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Ofisi ya Waziri Mkuu inayoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu kwa kundi hilo katika nyanja zote  za kiuchumi, kisiasa hata kijamii.


“Cherehani hii inaongeza kipato kupitia shughuli zangu za ufundi, namshukuru Mheshimiwa Rais na Ofisi hii ya Waziri Mkuu kwa sababu  kifaa hiki kitanitoa katika hali ya utegemezi maana tayari nina ujuzi ambao naenda sasa kuufanyia kazi,”alipongeza Bw. Ndayabunya.


*MWISHO*

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Wanataaluma ya Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka (hawapo pichani) wakati alipokuwa akifunga kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Wanataaluma hao leo tarehe 12 Februari, 2026 Mjini Njombe.

Na Antonia Mbwambo, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora-Njombe

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka wanataaluma ya Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka kuzingatia maadili ya utendaji kazi kutokana na dhamana kubwa waliyonayo kwa maslahi mapana ya Taifa.

 Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 12, Februari, 2026 alipokuwa akifunga kikao kazi cha mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji wanataaluma ya Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka mkoani Njombe.

“Tambueni dhamana yenu ni kubwa sana kwa maslahi ya Taifa letu. Ni vizuri utaalamu wenu uzingatie maadili ya utendaji kazi ili kuepuka kuvuja kwa siri na kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na siri kuvuja,” amesisitiza Mhe. Kikwete.

 Amesema kaulimbiu ya kikao kazi hicho isemayo “Kumbukumbu Sahihi leo, Maamuzi Sahihi kesho; Tunza siri kwa heshima ya Taifa” inaakisi kikamilifu mwelekeo wa Serikali katika kusimamia rasilimaliwatu na mifumo ya utendaji kazi na umuhimu wa kutunza siri kwa heshima ya Taifa. Na kuongeza kuwa hilo halina ubishi kwamba siri za nchi hii zinatakiwa kulindwa kwa wivu mkubwa. Hivyo, wataalamu wa kada hiyo wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha kwa namna yoyote ile mtu yoyote haruhusiwi kuikanyaga taaluma hiyo wala kuvujisha siri.

Mhe. Kikwete amesema Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndio msimamizi wa Chama cha Wanataaluma hao (TRAMPA), hivyo itaendelea kuhakikisha Nyaraka za serikali zinabaki salama kwa kuendelea kutoa miongozo mbalimbali pamoja na kusimamia utekelezaji wake.

Amewapongeza waajiri waliotenga bajeti na kuwaruhusu watumishi wao kushiriki kikao kazi hicho huku akimuagiza Katibu Mkuu-UTUMISHI kuwaandikia barua waajiri wote serikalini kutenga bajeti ya ushiriki wa watumishi walio chini yao kwani vikao hivyo ni muhimu katika kukua kitaaluma.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na TRAMPA katika kutekeleza majukumu yake ya kitaaluma na kiutumishi ikiwemo kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali katika usimamizi wa Kumbukumbu na Nyaraka, hususani katika Ofisi za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ili kuongeza ufanisi, usalama wa taarifa,Uwajibikaji na upatikanaji wa kumbukumbu kwa wakati.

“Kwenye hili Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa ninakuagiza kushirikiana na TRAMPA kuzitambua na kuziorodhosha halmashauri ambazo zinazorota katika kukamilisha hili ili ziweze kupewa msukumo kwa maandishi,” ameongeza Waziri Kikwete.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Kikwete kuhitimisha kikao kazi cha wanataaluma hao, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka alimshukuru Mhe. Kikwete kwa kuwapa heshima wanataaluma hao na wenyeji wa Mkoa wa Njombe kwa kufika mwenyewe kuhitimisha kikao kazi hicho.

Mhe. Mtaka amewaasa watumishi hao kuthamini kazi walizo nazo kwa kutekeleza majukumu yao kwa bidii, nidhamu na uadilifu kwani watu wengi wanatafuta kazi usiku na machana lakini hawapati.

Naye Mwenyekiti wa TRAMPA, Bi. Devotha Mrope amesema mada mbalimbali zimewasilishwa katika kikao kazi hicho ili kuwajengea uwezo wa kiutendaji wanataaluma hao.

Amesema takribani wanataaluma wa Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka 1900 wameshiriki kikao kazi hicho cha siku 4.

Mwenyekiti wa chama cha TRAMPA Bi. Devotha Mrope akitoa taarifa fupi ya kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Wanataaluma ya Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka (hawapo pichani) kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kabla ya Waziri huyo kufunga kikao hicho leo tarehe 12 Februari, 2026 Mini Njombe.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka akitoa neno la shukrani kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kufunga kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Wanataaluma hao leo tarehe 12 Februari, 2026 Mini Njombe.

Wanataaluma ya Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) walipokuwa katika kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mjini Njombe leo tarehe12 Februari, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini Kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe alipokuwa akifunga kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Wanataaluma hao leo tarehe 12 Februari, 2026 Mjini Njombe.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka (kushoto) wakati waziri huyo akifunga kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Wanataaluma hao leo tarehe 12 Februari, 2026 Mini NjombeWaziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Usalama ya mkoa wa Njombe baada ya waziri huyo kufunga kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Wanataaluma hao leo tarehe 12 Februari, 2026 Mini Njombe.

Wanataaluma ya Menejimenti ya Taarifa, Kumbukumbu na Nyaraka wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) walipokuwa katika kikao kazi cha Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mjini Njombe leo tarehe12 Februari, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi amezitaka Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Wananchi kuhakikisha wanalinda miundombinu ya umeme pamoja na vifaa vitakavyatumikakutekeleza mradi wa Kupelekea Umeme katika Vitongoji 371 mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa maelekezo hayo leo Februari 12, 2026 Ofisini kwake wakati wa kikao na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kilicholenga kumtambulisha rasmi Mkandarasi wa Mradi huo, NAMIS Corporate L.t.d atakaye hudumia Vitongoji 371 vya Mkoani humo.

“Miradi hii inatekelezwa kwa fedha nyingi kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi na asitokee mtu yoyote akafanya ubadilifu wa kuharibu miundombinu ya umeme pamoja na wizi wa vifaa vya utekelezaji wa mradi huu na kukwamisha kutekelezwa kwa mradi huu.

Nitoe onyo kwa mtu yoyote aliyepanga kufanya uharibifu asijaribu katika Mkoa wa Mara hakika tutawakamata, na tukiwakamata tutawachukulia hatua kali za kisheria,” amesisitiza Kanali Mtambi.

Sambamba na hilo amemtaka Mkandarasi anayetekeleza mradi kuhakikisha anautekeleza mradi huo ndani ya muda wa miaka mitatu kama ulivyopangwa kwenye mkataba, na pia alimsisitiza kuzingatia ubora

Kwa upande wake, Mhandis Ernest Makale Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amesema kwa Mkoa wa Mara Jumla ya Shilingi Bilioni 38.2 itatumika kusambaza umeme katika Vitongoji 371 huku akiwasisitiza kutumia umeme kujikwamua kiuchumi.

“Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa na lengo la kuendelea kuboresha maisha ya wananchi vijijini. Lengo kuu likiwa Vitongoje vyote ifikapo 2030 viwe na huduma ya umeme

Tuendelee kutoa rai kwa wananchi kuanza kufanya maandalizi ya kupokea mradi huu kwa kuanza kufanya wiring kwenye nyumba zao pamoja na kutumia uwepo wa umeme kujikwamua kiuchumi kwa kufungua miradi mbalimbali vijijini,” amesema Mhandisi Makale.