Na Oscar Assenga, TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amewataka wananchi wa mkoa wa Tanga ambao wamepanga kutumia matairi kuchoma moto barabarani kama njia ya kusheherekea sikuuu ya mwaka mpya wasithubutu kufanya hivyo.

Dkt Batilda aliyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mkesha wa mwaka mpya ambao unatarajiwa kufanyika kwenye viwanja vya Urithi Jijini Tanga ambapo alisema kutokana huo ni uharibifu wa miundombinu ya barabara na hatari kwa Taifa.

Alisema kwamba ndio maana Ofisi ya Mkoa huo kwa kushirikiana na Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Mbunge wa Jimbo la Tanga wameamua kufanya shughuli ya wana Tanga kwenye uwanja wa Burudani wa Uhuru Park.

Alisema kwamba kutakuwa na sanaa mbalimbali taarabu na miziki mbalimbali ikiwemo mashindano ya kupika maandazi ,vitumbua na watakaokuwa mabingwa wa kupika sambusa lakini watachoma samaki na mbuzi watu watakula bila gharama yoyote ili kuendeleza umoja,amani na ukarimu wa wana Tanga.

Aidha alisema kwamba baada ya hapo usiku watawasha mafataki watakayowashwa na wataalamu maalumu ya viwango maalumu hivyo kuliko kuchoma matairi waje kwenye uwanja wa uhuru ili kuona burudani mbalimbali ikiwemo mafataki.

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wana Tanga kwenda uwanja wa Urithi ili kuweza kuomba dua kumshukuru Mungu kuuona mwaka na baada ya hapo mtu kurudi nyumbani ni eneo ambalo litakuwa salama.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akikabidhiwa Jarida la “Hazina Yetu” Toleo la Tano, na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja, katika ofisi ndogo za Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam, ambapo ameipongeza kitengo hicho kwa uandaaji mzuri wenye ubunifu, ubora na kwa kuendelea kuboresha mawasiliano na uelimishaji kwa umma katika masuala ya fedha na uchumi wa Taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja, baada ya kukabidhiwa Jarida la “Hazina Yetu” Toleo la Tano, katika ofisi ndogo za Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam, ambapo ameipongeza kitengo hicho kwa uandaaji mzuri wenye ubunifu, ubora na kwa kuendelea kuboresha mawasiliano na uelimishaji kwa umma katika masuala ya fedha na uchumi wa Taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akisoma Jarida la “Hazina Yetu” Toleo la Tano, baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja (hayupo pichani), katika ofisi ndogo za Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam, ambapo ameipongeza kitengo hicho kwa uandaaji mzuri wenye ubunifu, ubora na kwa kuendelea kuboresha mawasiliano na uelimishaji kwa umma katika masuala ya fedha na uchumi wa Taifa.

Katibu wa Waziri wa Fedha, Bw. Geoffrey Kesase na Katibu wa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Fatma Shaaban, wakifurahia Jarida la “Hazina Yetu” Toleo la Tano, katika ofisi ndogo za Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WF, Dar es Salaam)


Na. Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam


Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amepongeza ubunifu na ubora wa Jarida la Hazina Yetu Toleo la Tano ambalo limeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha Wizara ya Fedha.

Ametoa pongezi hizo wakati akipokea Jarida hilo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mwamba alisema Jarida hilo ambalo limeendela kuwa bora na kufika kila mahali duniani kwa njia ya kidigitali ni nyenzo muhimu katika kuwasilisha taarifa sahihi, za wazi na kwa lugha inayoeleweka kuhusu shughuli, mafanikio na mipango ya Wizara ya Fedha.

Dkt. Mwamba alipongeza jitihada za Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kwa kuendelea kuboresha mawasiliano na uelimishaji kwa umma pamoja na ubunifu na weledi unaooneshwa katika uandaaji wa Jarida hilo, akibainisha kuwa limeendelea kuwa chombo muhimu cha kuimarisha uwazi, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya fedha na uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake, Bw. Benny Mwaipaja alisema kuwa Jarida la Hazina Yetu linalenga kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Fedha pamoja na mchango wake katika maendeleo ya Taifa, akiahidi kuendelea kuliboresha ili liwe chombo chenye tija zaidi katika mawasiliano ya serikali.

Jarida la “Hazina Yetu Toleo la Tano” limesheheni maarifa mbalimbali kupitia Makala bora kabisa, habari, matukio ya picha na matangazo mbalimbali na linapatikana kwa njia ya nakala ngumu (hard copies) na nakala tete (soft copies) kupitia mitandao ya kijamii ya Wizara na wadau wengine wa habari pamoja na Tovuti ya Wizara ya Fedha www.mof.go.tz



Na Mwandishi wetu- KILIMANJARO

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga ametoa wito kwa jamii kuwapenda, kuwajali na kuwahudumia makundi ya wenye mahitaji maalumu ili kukuza umoja na mshikamano katika Jamii.


Mhe. Nderiananga alisema hayo leo Disemba 31, 2025  akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa utaratibu wa utoaji zawadi za sikukuu mbalimbali kuelekea Sikukuu ya Mwaka Mpya wa 2026, zawadi hizo  zimeenda kwa watoto 190 wakiwemo wenye ulemavu na wasio na ulemavu wanaolelewa na Shirika la The Creator Share Foundation lililopo Kata ya Kirua, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani  Kilimanjaro.

Alisema, ndani ya siku 100 za uongozi wake ameendelea kuleta faraja, upendo, tumaini na umoja kwa watanzania huku akisema kuwa kitendo hicho ni ishara ya upendo mkubwa kwa wananchi bila kujali hali zao.


“Naomba nitumie fursa hii kuwatakia kheri ya sikukuu ya mwaka mpya  wa  2026 twende tukasherehekee kwa amani  na tukiwa na faraja kwa sababu Mhe. Rais ametukumbuka sisi ni watoto wake hivyo tudumishe upendo huu miongoni mwetu kila mmoja amuone mwenzake ni wa muhimu katika jamii,” alisema Mhe. Nderiananga.

Akitaja vitu alivyovikabidhi kwa watoto hao alisema, ni pamoja na Mchele kilo 100, Ngano kilo 50, Mbuzi wawili, sabuni, mafuta ya kupikia, madaftari, sukari kilo 25 na vinywaji



" Nitoe wito kwa jamii kuwa, kila mmoja ana wajibu wa kuwahudumia watoto na watu wenye mahitaji maalum, siyo tu kwa siku za sikukuu, bali kwa muda wote ili kuwapa faraja na huo ndio upendo tunaotakiwa kuwaonesha," aliongeza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Moshi Bw. Godfrey Mnzava  alibainisha kuwa,  ili kuwa na ustawi wa maisha ya kijamii ni lazima kuwajali watu wenye uhitaji  ili waweze kukidhi mahitaji muhimu ya kila siku.


Naye,Diwani wa Viti Maalum Tarafa ya Vunjo Magharaibi ambaye pia ana mtoto mwenye ulemavu anayelelewa katika Shirika hilo Bi. Pamela Chuwa alipongea hatua hiyo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikia watu wenye ulemavu hatua inayowaganya kujisikia kuwa ni sehemu ya jamii.



“Mimi kama mama mwenye mtoto wa mahitaji maalum nimejisikia furaha kwa kupewa kipaumbele na tumefurahi sana Naibu Waziri Ummy kutufikia ukizingatia baadhi yetu tumefukuzwa katika familia  tukionekana kama kuzaa watoto wenye ulemavu ni mkosi na laana katika familia,” alipongeza Bi. Diwani huyo.



Vilevile Afisa Rasilimali Watu katika Shirika hilo Bi. Judith Shio mara  baada ya kupokea zawadi hizo alimshukuru Mhe. Rais Dkt.  Samia  Suluhu Hassan kwa moyo wa upendo na kuwajali watu wenye mahitaji Maalum huku akitoa wito kwa wadau mbalimbali kujitolea ili kuendelezwa moyo wa upendo na faraja kwa makundi hayo.



“Kwa niaba ya Shirika tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa upendo huu na mwaka huu tunauanza kipekee sana na watoto wamefurahi hivyo kwetu imekuwa faraja kubwa na imegusa jamii,” alishukuru Bi. Judith.


 Nao baadhi ya watoto wanaolelewa katika Shirika hilo wameishukuru Serikali kwa kuwakumbuka wakisema ujio huo kwao umekuwa ni historia na furaha kubwa ya kuuanza mwaka mpya kwa matumaini huku wakimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa upendo huo wa the kuwashika mkono watoto wenye mahitaji maalum.


MWISHO

 


Imeelezwa kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia yameendelea kufungua fursa nyingi za ajira kwa Watanzania, hususani katika uzalishaji wa mkaa mbadala na utengenezaji wa mashine za kuzalishia mkaa huo.

Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay amesema hayo wakati wa ziara yake ya kutembelea Taasisi ya Wazalendo Movement inayojishughulisha na utengenezaji wa mashine za kuzalisha mkaa mbadala pamoja na uzalishaji wa mkaa huo wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Bw. Mlay amesema kuwa taasisi nyingi zinazohudumia watu kuanzia 100 na kuendelea zimeanza kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia, jambo linaloongeza kwa kiasi kikubwa mahitaji ya mkaa mbadala na hivyo kuhitaji uzalishaji wa kasi zaidi.

“Niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuzalisha mkaa mbadala pamoja na mitambo ya kutengenezea mkaa huo. Hii ni fursa kubwa kwa Watanzania kwani mahitaji ni makubwa, lakini ni muhimu kuhakikisha mkaa huu unaozalishwa ni wa ubora wa hali ya juu na unaodumu hata ukisafirishwa kwa umbali mrefu,” amesisitiza Bw. Mlay

Kwa upande wake, Mhandisi Mwandamizi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Deusdedit Malulu amesisitiza umuhimu wa kushirikisha Shirika la Viwango Tanzania (TBS) katika utengenezaji wa mkaa mbadala ili kuhakikisha bidhaa zinakidhi viwango vinavyotakiwa.

Aidha, amewahimiza wazalishaji kujisajili kwenye mfumo wa NEST ili kupata fursa mbalimbali na kubainisha kuwa REA ina mpango wa kutoa fursa kwa wananchi katika utengenezaji wa mashine kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa vifaa vya kuzalisha mkaa mbadala.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wazalendo Movement,Bw. Saidi Malema amesema kuwa taasisi hiyo, katika kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, imeanzisha kikundi cha nishati safi ya kupikia kinachojihusisha na uzalishaji wa mkaa mbadala unaotengenezwa kutokana na magunzi ya mahindi na nyasi kavu.

Amesema taasisi hiyo hutengeneza mashine za kuzalishia mkaa zinazotumia umeme na zisizotumia umeme.

Ameongeza kuwa taasisi hiyo pia imeanzisha kikundi cha Nishati Safi Sanaa Group, kinacholenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia sanaa ya maigizo na nyimbo.

Amesema Taasisi ya Wazalendo Movement imefanikiwa kuuza mashine zake kwa wadau katika mikoa ya Tabora, Singida na Pwani. Aidha, imekuwa ikigawa mashine ndogondogo kwa wananchi wa vijiji vya Wilaya ya Mkuranga ambako umeme bado haujafika ili kuwahamasisha kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Katika ziara hiyo, Bw. Nolasco Mlay pia alitembelea kampuni ya Matima Investment inayojishughulisha na utengenezaji wa majiko ya kuchomea nyama yanayotumia gesi, kwa lengo la kujionea namna majiko hayo yanavyosaidia kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.






 


Na Angela Msimbira, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha hakuna mtoto anayezuiwa kuanza au kuendelea na masomo kwa sababu ya kukosa sare, wakati shule zote nchini zikitarajiwa kufunguliwa rasmi Januari 13, 2025.

Prof. Shemdoe amesema kuwa agizo hilo linapaswa kusimamiwa kikamilifu katika maeneo yote ya nchi ili kuhakikisha kila mtoto anapokelewa shuleni bila masharti yanayokiuka miongozo na sera za elimu.

Amesisitiza kuwa mara mtoto anapopokelewa shuleni, masuala mengine ikiwemo sare, yataendelea kushughulikiwa akiwa tayari anaendelea na masomo, hatua itakayosaidia kuondoa vikwazo vinavyowafanya baadhi ya watoto kukosa haki yao ya msingi ya elimu.

Aidha, Prof. Shemdoe amekemea tabia ya baadhi ya shule za Serikali kuweka michango mingi kwa wazazi, ikiwemo kuwalazimisha kununua sare shuleni, akieleza kuwa hatua hiyo ni kinyume na taratibu na miongozo ya Serikali.

Ameelekeza walimu wakuu, walimu na viongozi wa shule kusoma, kuelewa na kuzingatia miongozo ya elimu iliyopo, pamoja na kutoa elimu sahihi kwa wazazi na walezi ili kuondoa sintofahamu zisizo za lazima.

“Lengo la Serikali ni kuona watoto wote wanakwenda shule bila vikwazo vyovyote, na kuhakikisha hakuna mtoto anayenyimwa haki yake ya elimu kwa sababu ya changamoto za kiuchumi au maamuzi yasiyo sahihi,” amesisitiza Prof. Shemdoe.




 Zaidi ya Shilingi milioni mia moja na mchango wa vifaa vya ujenzi, ikiwemo saruji zimepatikana katika harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa ofisi mpya ya kisasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tunduru, mradi unaotarajiwa kugharimu Shilingi milioni 200.


Harambee hiyo imewaleta pamoja wadau mbalimbali wa maendeleo, wanachama na viongozi wa chama, ikiwa ni jitihada za pamoja za kuboresha miundombinu ya chama na kuimarisha mazingira ya utendaji katika ngazi ya wilaya.

Akizungumza wakati wa harambee hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Denis Masanja, amesema Serikali inatambua na kutoa baraka za kiserikali kwa harambee hiyo, akieleza kuwa ni sehemu ya uzalendo na mchango wa wananchi katika kujenga misingi imara ya taasisi za kisiasa na kijamii.

Mkuu huyo wa Wilaya ameongeza kuwa Serikali haina pingamizi lolote mradi harambee hiyo izingatie taratibu zilizopo, huku akisisitiza kuwa ushiriki wa wananchi na wadau wa maendeleo ni nyenzo muhimu katika kufanikisha miradi ya maendeleo wilayani humo.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya amekemea vikali tabia za baadhi ya watu na viongozi wanaojaribu kufubaza jitihada hizo za kizalendo, akisema vitendo hivyo vinachochewa na maslahi binafsi na siasa chafu zisizolenga maendeleo ya Wilaya ya Tunduru na wananchi wake.

Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini, Mhandisi Fadhili Chilombe, amesema uamuzi wa kujenga ofisi mpya umetokana na hali ya uchakavu wa ofisi ya zamani ya CCM, iliyojengwa mwaka 1965 na kuzinduliwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambayo kwa sasa ina zaidi ya miaka 60 na haikidhi mahitaji ya kiutendaji ya chama.

Akisisitiza hoja ya maendeleo, Mkuu wa Wilaya amesema Tunduru ni miongoni mwa wilaya kongwe nchini Tanzania, iliyoanzishwa mwaka 1905, lakini maendeleo yake hayajaendana na historia na kongwe wa wilaya hiyo. Amesema hali hiyo inapaswa kuwa chachu kwa wananchi wa Tunduru kuungana, kuweka tofauti zao pembeni na kuunga mkono jitihada za kizalendo, ikiwemo ujenzi wa ofisi ya kisasa ya CCM, ili kuibadilisha wilaya hiyo na kuisukuma mbele kimaendeleo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tunduru, Abdallah Mtila, amesema ujenzi wa ofisi mpya utaimarisha mazingira ya kazi, kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya chama na kuimarisha mshikamano wa wanachama, huku akitoa wito kwa wadau zaidi kujitokeza kuchangia ili kukamilisha mradi huo kwa wakati.




Sikukuu zilipofika, nilijipa ruhusa ya kufurahia kama wengine. Nilicheka, nilisafiri, nilinunua zawadi na kuandaa sherehe nyumbani. Kila kitu kilionekana sawa hadi likizo ilipokwisha.

Nilipoanza kuandaa watoto kurudi shuleni, ukweli ulinigonga ghafla ada haikuwepo. Nilijilaumu kwa kimya, nikijua nilienda mbali kuliko uwezo wangu.

Nilianza kutafuta suluhisho la haraka. Nilipiga simu kwa marafiki, nikauza vitu vidogo, nikajaribu kazi za muda mfupi. Kila nilichopata kilikuwa kidogo sana kuliko kilichohitajika.

Hofu ikaongezeka, hasa nilipofikiria watoto wangu wakikaa nyumbani kwa kosa lisilokuwa lao. Usiku usingizi haukunijia, mawazo yakinizidi. Soma Zaidi....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilicheka-sikukuu-sasa-nalipa-bei-suluhisho-la-haraka-la-kupata-ada-ya-shule/
Baada ya shamrashamra za sikukuu kuisha, ukweli ulinikuta nikiwa nimechoka na mifuko mitupu. Desemba ilinifurahisha, lakini iliniacha nikiwa na madeni, ada za shule, na majukumu ambayo hayakuwa yanasubiri.

Nilipoanza Januari, kila mpango niliokuwa nimejiwekea ulionekana mzito. Nilihisi kama mwaka mpya ulikuwa unanivuta chini badala ya kunipa mwanzo mpya.

Nilikaa nikitazama makadirio yangu ya mapato na matumizi, nikagundua tatizo halikuwa pesa pekee bali maamuzi niliyokuwa nikiyafanya bila mwelekeo. Nilijilaumu, lakini lawama hazikubadilisha hali.

Nilihitaji hatua ya haraka, tofauti, na yenye mwelekeo. Ndipo nikaamua kutafuta ushauri uliojikita kwenye kupanga upya njia zangu za kifedha na kufungua nafasi mpya. Soma Zaidi........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/sikukuu-zilinimaliza-kifedha-nilichofanya-desemba-mwisho-kikabadilisha-januari-yangu/
Siku ya kurudi shule ilipokaribia, nilikuwa nimebaki na shilingi chache mfukoni. Likizo ilikuwa ndefu na matumizi yalionekana madogo kila siku, lakini mwishowe ada ya shule ilikuwa imeisha kabisa.

Nilijaribu kujiweka imara mbele ya watoto wangu, lakini ndani nilikuwa ninaumia. Nilihofia walimu wakiwaita kando kwa sababu ya ada, na watoto wangu wakauliza kwa nini wanachelewa kurudi darasani.

Nilipiga hesabu kila asubuhi nikitafuta pa kuanzia. Niliomba kazi za mkono, nikaomba ndugu, nikauza vitu vidogo vya nyumbani lakini pesa iliyopatikana haikutosha.

Kila jioni nilihisi aibu na lawama zikiongezeka. Nilijua nikikosa suluhisho la haraka, watoto wangekaa nyumbani bila kosa lao. 

Nilibadilisha mkakati. Badala ya kukimbizana na ahadi hewa, niliamua kutafuta ushauri ulio na mwelekeo. Soma Zaidi.....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/watoto-waliporudi-shuleni-nilikuwa-sifuri-uamuzi-mmoja-ulininusuru-na-aibu-ya-ada/
Krismasi ilipopita, kilichobaki mezani kwangu hakikuwa furaha bali orodha ya madeni. Nilikuwa nimekopa ili kusafiri, kula vizuri na kufurahisha familia kama ilivyo desturi.

Nilipoamka siku za kwanza za Januari, simu zilianza kupiga kutoka kwa watu waliotaka kurudishiwa pesa. Kila sauti iliniongezea presha, na nilihisi mwaka mpya unaanza vibaya kabla hata haujapiga hatua.

Nilijaribu kupanga upya. Niliketi nikahesabu ninachodaiwa, nikatafuta njia za kulipa kidogo kidogo. Tatizo lilikuwa chanzo cha pesa. Kazi yangu haikuwa inalipa kwa wakati, na biashara ndogo niliyokuwa nayo ilikuwa imesimama.

Nililala na wasiwasi, nikiamka na mzigo ule ule moyoni. Nilijua nikibaki hapo, hata afya yangu ingeathirika. Ndipo nilipobadilisha mtazamo. Niliona kuwa nilihitaji ushauri wa kina, sio kukimbizana na mikopo mingine.

Kupitia rafiki, niliwasiliana na Kiwanga Doctors. Mazungumzo ya kwanza yalikuwa tofauti; niliombwa nieleze historia yangu ya kifedha, maamuzi ya zamani, na matarajio ya mwaka mpya.

Nilihisi nimesikilizwa kwa mara ya kwanza bila kuhukumiwa. Baada ya kufuata maelekezo niliyopata, nilipata uthubutu wa kufanya maamuzi mapya.

Nilifungua njia niliyokuwa nikiihofia, nikapanga malipo kwa nidhamu, na fursa ya ziada ya kipato ikanijia ghafla. Ndani ya wiki chache, nilianza kupunguza madeni. Simu za madai zikapungua, usingizi ukarudi.

Leo naanza mwaka mpya bila mzigo ule wa moyoni. Nimejifunza kuwa msongo hauondoki kwa bahati, unaondoka kwa hatua sahihi. Soma Zaidi..
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/baada-ya-krismasi-nilikuwa-na-madeni-pekee-hatua-nilizochukua-kuanza-mwaka-mpya-bila-msongo/

Nilipoangalia kalenda wiki ya mwisho ya likizo, moyo wangu ulizama. Ada ya shule ilikuwa imekwisha, iliyeyuka taratibu kwenye safari za Krismasi, zawadi za familia, na sherehe nilizodhani “hazitakuwa nyingi.”

Nilijilaumu kimya kimya, nikikumbuka ahadi niliyotoa kwa watoto wangu kwamba Januari haitakuwa ya vilio. Lakini ukweli ulinikuta nikiwa sifuri, shule zikifungua ndani ya siku chache.

Nilikimbia kila kona ya kawaida. Niliomba kazi ya muda, nikaomba mkopo mdogo, nikajaribu kuuza vitu ambavyo tayari vilishuka thamani. Kila nilipojaribu, majibu yalikuwa yale yale: subiri, rudi kesho, au hapana.

Usiku usingizi haukuja. Nilihisi nimewaangusha watoto wangu, na hilo liliniumiza zaidi kuliko deni lenyewe. Siku moja niliamua kubadilisha mbinu. Badala ya kukimbizana na suluhisho za haraka zisizo na mwelekeo, nilitafuta ushauri wa mtu aliyekuwa ameona hali kama yangu mara nyingi. Soma Zaidi.......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilitumia-ada-ya-shule-wakati-wa-sikukuu-njia-niliyopata-fedha-haraka-kabla-ya-shule-kufunguliwa/

Na Mwandishi Wetu

Maboresho ya huduma za afya katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni yameanza kuleta matokeo chanya baada ya idadi ya wagonjwa wanaohudumiwa kwa siku kuongezeka kutoka wagonjwa 100 hadi kufikia 175.

Akizungumza kuhusu maboresho hayo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Handeni, Dkt.Hudi Muradi, amesema ongezeko hilo limetokana na kuboreshwa kwa miundombinu ya hospitali, upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa pamoja na kuimarika kwa utoaji wa huduma za uchunguzi na matibabu.

Ameeleza kuwa kwa sasa huduma zote muhimu za uchunguzi wa magonjwa zinapatikana hospitalini hapo, huku huduma za kibingwa zikiendelea kutolewa muda wote, hatua inayowapunguzia wananchi gharama na usumbufu wa kufuata huduma hizo nje ya halmashauri.

Aidha, amesema Serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa, jambo lililochangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma na kuimarisha imani ya wananchi kwa hospitali hiyo.

Mganga Mkuu huyo ameongeza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora na za uhakika kupitia utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, ambao unalenga kuweka usawa katika upatikanaji wa huduma za afya kati ya wananchi wenye kipato kikubwa na wale wa kipato cha chini.

Amesisitiza kuwa hospitali itaendelea kuboresha huduma ili kukidhi mahitaji ya wananchi na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya afya nchini.

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI imepokea taarifa ya awali ya Kamati ya Mapitio ya Sheria ya Elimu, Sura ya 353.  

Akizungumza Dodoma, Desemba 30, 2025 katika kikao cha Kisekta cha kupokea taarifa hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, amesema Sheria ya Elimu ya mwaka 1978 imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara lakini bado ina mapungufu makubwa yanayohitaji maboresho ili kuendana na mageuzi ya kisera na kiutendaji.  

Prof. Nombo alieleza mapungufu hayo ni pamoja na umri wa kuanza shule ya awali na darasa la kwanza, muda wa masomo ya elimu ya lazima na elimu ya awali, kutokuwepo kwa vifungu vinavyotambua wanafunzi wenye mahitaji maalum, ulinzi wa mtoto akiwa shuleni, uimarishaji wa vyombo vya uongozi na usimamizi wa sekta ya elimu pamoja na ushirikiano kati ya sekta binafsi na Serikali katika utoaji wa huduma za elimu.  

Aidha, amebainisha kuwa Kamati iliyoundwa na Wizara Mei 2024 chini ya Prof. Saudin Mwakaje imekusanya maoni ya wadau mbalimbali na kuandaa taarifa ya awali ambayo sasa inawasilishwa kwa uhakiki na maboresho na kisha kwa wadau kama rasimu na hatimae Baraza la Mawaziri.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mapitio ya Sheria ya Elimu, Prof. Saudin Mwakaje amesema kuwa Kamati ilifanya uchambuzi wa kina wa matamko ya sera ili kubaini yapi yanahitaji kuwekewa misingi ya kisheria ili kuondoa mgongano kati ya Sera na Sheria. 

Prof. Mwakaje ameongeza kuwa uchambuzi huo ulihusisha wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo wakuu wa taasisi za elimu, vyama vya wamiliki wa Shule na Vyuo binafsi, vyama vya kitaaluma, wazazi, walimu, wanafunzi, vyama vinavyoshughulika na Watu wenye welemavu pamoja na wadau wa maendeleo.