Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akifuatilia maelezo ya Mhandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Rashid Mtamila (wa tatu kutoka kushoto) walipotembelea uwanja wa Sokoine leo Septemba 17, 2025, kukagua maandalizi ya uwanja huo kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Na; Mwandishi wetu- Mbeya
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus amekagua maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zitakazofanyika jijini Mbeya.
Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mkoa kuhusu maandalizi leo 17 Septemba 2025, Naibu Katibu Mkuu Zuhura Yunus alieleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi na kuipongeza kamati ya Mkoa kwa kuendelea kusimamia na kuratibu vyema shughuli hiyo.
Katika ziara hiyo, Naibu Katibu Mkuu huyo aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo kukagua uwanja wa Uhindini kutakapofanyika maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa, uwanja wa Sokoine kwa ajili ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na kukagua mazoezi ya vijana wa halaiki.
Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa mwaka 2025 zinaongozwa na kauli mbiu isemayo “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa waka 2025 kwa Amani na Utulivu”.
Mbio hizo zilizinduliwa rasmi Aprili 2, 2025 Kibaha, Mkoani Pwani na kilele chake kitafanyika Mkoani Mbeya Oktoba 14, 2025, ambapo Mwenge wa Uhuru unakimbizwa katika mikoa 31 na Halmashauri 195 zikiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Mkoa wa Mbeya wakati wa ziara yake Septemba 17, 2025 ya kukagua maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru zitakazofanyika jijini Mbeya.
Wajumbe wa Kamati Elekezi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakifuatilia taarifa ya mkoa wa Mbeya kuhusu maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025.
Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo akieleza hatua zilizofikiwa na mkoa kuhusu maandalizi ya Wiki ya Vijana Kitaifa na shughuli za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akikagua moja ya mabango ya hamasa kuhusu kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru yaliyaondaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya leo Septemba 17, 2025, jijini Mbeya.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akikagua maeneo mbalimbali katika uwanja wa Sokoine wakati wa ziara yake ya kufuatilia Maendeleo ya maandalizi ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo Septemba 17, 2025, jijini Mbeya.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Zuhura Yunus akifuatilia maelezo ya Mhandisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Rashid Mtamila (wa tatu kutoka kushoto) walipotembelea uwanja wa Sokoine leo Septemba 17, 2025, kukagua maandalizi ya uwanja huo kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.