Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

.... Zaidi ya shilingi bilioni 127.7 zimetumika kupeleka huduma ya nishati safi Vijijini Mkoa wa Mwanza hali iliyochochea ukuaji wa uchumi na kuboreka kwa huduma za kijamii vijijini.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) ambapo Wakala huo uliwasilisha mpango kazi pamoja na bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027.

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkoa wa Mwanza pekee imetoa jumla ya shilingi Bilioni 127.7 ili kutekeleza miradi ya kupeleka umeme hadi vitongojini. Mafanikio haya makubwa yamechangiwa pia na wabia wa maendeleo, tunawapongeza na kuwashukuru sana.

Niendelee kuwataka wananchi waendelee kulinda miundombinu ya umeme kwa kuwa serikali na wabia hawa wa maendeleo wanaweka fedha nyingi sana. Lakini pia niendelee kuwahimiza wabia wa maendeleo pamoja na REA kuendelea kuwekeza zaidi katika nishati safi ya kupikia,” amesema Mhe. Mtanda.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu amesema kuwa wabia hao wa maendeleo wamekuwa na imani kubwa na fedha wanazotoa katika utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini na ndio maana wanaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia REA katika utekelezaji wa miradi hiyo huku akiahidi kuwa Bodi yake itaendelea kuhakikisha kunakuwa na thamani ya fedha katika miradi inayotekelezwa na REA.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy amesema kuwa Wakala umewasilisha mipango na vipaumbele vyake kwa mwaka ujao wa fedha ili wabia hao waweze kuona maeneo wanayoweza kuendelea kushirikiana na Serikali kupitia REA katika kuendelea kuboresha maisha ya Wananchi.

“Pamoja na kazi kubwa inayofanyika katika kujenga miundombinu ya umeme, lakini lengo la msingi ni mwananchi wa kawaida aweze kuunganishiwa umeme na aweze kupata manufaa ya upatikanaji wa umeme.

Tumewasilisha mipango pamoja na vipaumbele katika bajeti yetu ijayo ambapo ni kuharakisha upatikanaji wa umeme kwenye vitongoji. Tumewapitisha pia wenzetu katika mpango wetu maalum wa kuwezesha na kuharakisha uunganishaji umeme majumbani,” amebainisha Mhandisi Saidy.

Mhandisi Saidy pia ameongeza baadhi ya mipango mingine iliyopangwa kutekelezwa na Wakala kwa mwaka ujao wa fedha ni pamoja na kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia vijijini, kuwezesha miradi ya nishati jadidifu na kuongeza ufanisi katika matumizi ya umeme na utumiaji wa umeme katika shughuli za maendeleo.

Mwenyekiti wa Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG), Robert Hovde ameipongeza Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa kufikisha umeme vijijini.

“Katika kipindi cha miongo kadhaa nyuma, Tanzania imekuwa na maendeleo makubwa katika kufikisha umeme vijijini yaliyotekelezwa na REA. Miundombinu ya umeme inaonekana hali inayotia matumaini kufikiwa kwa mpango wa kuunganisha umeme wananchi wote. Tunawatakia kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema Hovde.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG), Robert Hovde,akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

 

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

 

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (hayupo pichani) akizungumza  wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy,akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda,mara baada ya kumalizika kwa  kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) kilichofanyika jijini Mwanza.

 

Na OWM - TAMISEMI, Bahi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amemuarifu kuwa, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wananchi wa Kata ya Chifutika lililowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Bahi Mhe. Kenneth Nollo la kupatiwa shilingi milioni 544 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Chifutuka ambayo itakidhi uhitaji wa wananchi wa kata hiyo. 

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Aprili 17, 2026 wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa darasa la nne, darasa la saba, kidato cha pili na kidato cha nne wilayani Bahi, iliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Chiona wilayani humo. 

“Mhe. Mbunge alinifuata kabla sijasimama kuzungumza, akiomba shule ya sekondari ijengwe Kata ya Chifutika, nikawasiliana na Mhe. Waziri Mkuu na kuliwasilisha ombi hilo kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ameridhia milioni 544 ziletwe kujenga shule ya sekondari,” amesema Prof. Shemdoe.

Kutokana na kuridhiwa kwa kiasi hicho cha fedha, Prof. Shemdoe kwa niamba ya wananchi wa Kata ya Chifutuka Wilayani Bayi amemshukuru kwa moyo wa dhati Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchema kwa upendo mkubwa waliouonesha kwa wananchi wa Kata hiyo Chifutuka.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, fedha hizo zimeridhwa na Mheshimiwa Rais kwasababu lengo la Serikali ni kuendelea kuimarisha elimu nchini, ikizingatiwa kuwa Bahi imeonesha juhudi kubwa na kuwa Halmashauri ya kwanza kitaifa kwenye ufaulu wa mitihani ya darasa la saba kwa mwaka 2025.











Na Mwandishi Wetu.


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula , amesema uandishi wa habari usiozingatia maadili unaweza kuhatarisha umoja wa kitaifa, amani na utulivu wa jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari ambao ni wanachama wa JUMIKITA, TADIO na TBN, Aprili 17, 2026 jijini Dar es Salaam, Kipangula alisema waandishi wa habari wanapaswa kutambua uzito wa nafasi yao katika jamii, hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi, ambapo taarifa wanazozitoa zina athari kubwa kwa mwenendo wa jamii.

Alifafanua kuwa amani ni hali ya kutokuwepo kwa migogoro au vurugu, huku utulivu ukimaanisha usalama na uhakika wa maisha ya wananchi bila hofu, akibainisha kuwa hali hizi mbili haziwezi kudumu bila uwepo wa umoja wa kitaifa unaojengwa juu ya mshikamano wa wananchi bila kujali tofauti zao.


“Pale ambapo uandishi hauzingatii maadili, unaweza kuchochea migawanyiko, kupotosha ukweli na hatimaye kuvuruga mshikamano wa kitaifa. Hivyo, ni muhimu kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji,” alisema Kipangula.

Alibainisha kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa msingi wa kukusanya, kuchakata na kusambaza taarifa sahihi, pamoja na kusaidia kuunda mitazamo ya wananchi kwa njia inayochangia maridhiano na maendeleo ya jamii.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia Kanuni za Maadili ya Taaluma ya Uandishi wa Habari, akibainisha kuwa maadili hayo yanahimiza ukweli, usawa, uwazi na heshima kwa haki za binadamu, mambo ambayo ni msingi wa kulinda amani, kuimarisha utulivu na kukuza umoja wa kitaifa.






Serikali imepanga kufanya mageuzi makubwa katika mfumo wa mafunzo na uendelezaji wa watumishi wa umma kupitia Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) katika mwaka wa fedha 2026/27, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utoaji wa huduma bora na kuongeza ufanisi serikalini.

Timu ya Mpira wa miguu ya TCDC Sports Club imechukua alama tatu (3) baada cha kuifunga Timu ya Mpira wa miguu ya Wizara ya Kilimo goli mbili (2) kwa moja (1) katika mechi iliyochezwa leo Aprili 17, 2026 saa 2:30 3:45 katika viwanja vya Venite mkoani Njombe.

Timu hizo zimekutana katika mashindano ya Michezo ya Wafanyakazi (Meimosi) yanayoyafanyika kitaifa mkoani Njombe.

Hapo Kesho Aprili 18, 2026 Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sport Club inatarajia kukutana na Timu ya Mpira wa miguu ya TAMISEMI saa10:15 jioni katika viwanja vya Kibena mkoani humo.


**********

Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre), kwa kushirikiana na Jukwaa la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), kimewakutanisha wadau kwa sekta binafsi jijini Dar es Salaam katika mafunzo maalum ya kujenga uwezo kuhusu miradi ya ubia (PPP).