Na Munir Shemweta, WANMM MUHEZA

 

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Leonard Akwilapo amewaongoza Mawaziri wenzake wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na Ofisi ya Raisi Mipango na Uwekezaji katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

 

Kikao hicho kimefanyika tarehe 18 Februari 2026 katika ofisi ya Mkuu wa wilaya Muheza mkoa wa Tanga ikiwa ni utekelezaji wa masuala yaliyojitokeza wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

 

Mawaziri hao ni Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa TAMISEMI na Dkt. Pius Chaya, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji ambao kupitia kikao hicho, kilichohusisha pia wataalamu, viongozi hao walipata fursa ya kuwahoji wananchi walioguswa na migogoro hiyo ya mashamba ya uwekezaji ambayo yaliyofutiwa umiliki mwaka 2016.

 

Mashamba hayo ni Azimio/ Kilapula Geiglitz, Bwembwera, Kibaranga, Kihuhwi, Lewa pamoja na Saguras yaliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.




Na OWM-TAMISEMI, Dodoma

Serikali imezitaka Halmashauri zote nchini kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuwezesha utekelezaji wa mipango mikubwa ya maendeleo inayoanza Julai 2026, ikiwemo Dira ya Taifa ya 2050 na Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2026/27–2030/31).

Akifungua Kikao Kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Wakuu wa Vitengo vya Fedha na Uhasibu kilichofanyika Ukumbi wa Mabeyo jijini Dodoma leo Februari 19, 2026, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Bw. Sospeter Mtwale, amesema mafanikio ya mipango ya Serikali yanategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kukusanya na kusimamia mapato yao ipasavyo.

“Kama Serikali haitakusanya mapato ya kutosha, hatutaweza kuwapatia wananchi huduma bora wala kufikia malengo ya kitaifa tuliyojiwekea,” amesema.

Kikao hicho cha siku mbili kitajadili hali ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na maandalizi ya makadirio ya mwaka 2026/27.

Bw. Mtwale amesisitiza kuwa ukusanyaji wa mapato si suala la hiari bali ni wajibu wa kimfumo unaohitaji nidhamu, uwazi na uwajibikaji.

 Amesema bado kuna maeneo yanayohitaji maboresho, hasa katika upangaji wa malengo ya ukusanyaji, usimamizi wa vyanzo vipya vya mapato na ufuatiliaji wa karibu wa utekelezaji wake.

“Ni lazima tuandae makadirio ya mapato kwa uhalisia, tukizingatia uwezo wa kiuchumi wa maeneo yetu na fursa zilizopo,” ameeleza.

Katika hatua ya kuimarisha ukusanyaji, Serikali imeelekeza matumizi makubwa ya mifumo ya kidijitali katika usimamizi wa mapato.
Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu huyo, matumizi sahihi ya TEHAMA yatasaidia kupunguza mianya ya upotevu wa mapato, kuongeza uwazi na kuwezesha maamuzi ya haraka ya kiutendaji kwa kuzingatia takwimu sahihi.

Ameelekeza Halmashauri zote kuboresha vyanzo vya mapato vilivyopo kwa kuwekeza katika mifumo ya makusanyo, kuandaa mipango na bajeti inayozingatia uhalisia wa rasilimali na vipaumbele vya Taifa, kutumia takwimu sahihi katika kupanga malengo ya ukusanyaji na kuimarisha ufuatiliaji wa mikoa na Halmashauri ili malengo yafikiwe kwa wakati.

Kwa muktadha huo, viongozi wa fedha katika ngazi za Serikali za Mitaa wametakiwa kujitathmini kwa kina kuhusu utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2025/26 na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha utendaji kwa mwaka ujao wa fedha.

“Kikao hiki kitumike kubadilishana uzoefu na kuibua mbinu bunifu zitakazosaidia kuongeza mapato ya ndani kwa manufaa ya wananchi,” amesema Bw. Mtwale.

Serikali imeweka wazi kuwa nidhamu ya matumizi ya fedha za umma ni msingi wa mafanikio ya mipango ya maendeleo. Wasimamizi wa fedha wametakiwa kuhakikisha kunakuwa na uwazi na uwajibikaji katika kila hatua ya ukusanyaji na matumizi ya mapato.












 


📌 Yapongeza kasi ya Serikali ujenzi wa vituo vya CNG

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, kupitia Mwenyekiti wake Mhe. Subira Mgalu, imetoa wito kwa wawekezaji kuunga mkono Serikali katika ujenzi wa  vituo vya gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi katika Jiji la Dar es Salaam na mikoa mingine ikiwemo Morogoro na Dodoma.

Wito huo umetolewa  tarehe 19 Februari 2026 wakati Kamati hiyo ilipotembelea Kituo Mama cha Gesi Asilia Iliyoshindiliwa (CNG) kilichopo eneo la Mlimani jijini Dar es Salaam.

“Tumeona Serikali tayari ina mpango wa kuongeza ujenzi wa vituo hivi kutokana na uhitaji wa wananchi kuendelea kuongezeka pamoja na unafuu unaopatikana ukitumia CNG kwenye vyomvbo vya usafiri kama vile magari na bajaji, kwani gharama zinapungua kwa asilimia 40 ukilinganisha na mafuta. Hii hii ni fursa kwa sekta binafsi kushirikiana na Serikali kujenga vituo vingi zaidi,” amesema Mhe. Mgalu

Aidha, kamati hiyo imetoa wito kwa Serikali kufunga mfumo wa CNG katika magari yake,  jambo litakalosaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa vyombo hivyo vya usafiri.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini pia imeipongeza Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)  kwa uwekezaji inaoufanya katika ujenzi wa vituo vya CNG na kupelekea vyombo vya usafiri vipatavyo 15,000 kutumia CNG.

Vilevile, imepongeza  shughuli za utafiti na uendelezaji wa gesi asilia zinazoendelea; ikisema kuwa upatikanaji wa gesi asilia ya kutosha  utawezesha kuendelea kuboresha huduma nyinginezo ikiwemo kupikia majumbani na viwandani.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema tangu kuanza kwa vituo vya CNG nchini, Serikali imekuwa ikiona tija yake na ndiyo maana  inaongeza kasi ya usogezaji wa huduma  hiyo kwa wananchi kwa kuhusisha pia sekta binafsi mfano ukiwa ni uzinduzi wa hivi karibuni wa kituo cha CNG cha Puma kilichopo Salasala ambacho kwa Afrika ndicho kituo kikubwa.

Amesema Serikali pia katika mwaka huu wa fedha imeagiza magari makubwa matano yatakayobeba gesi asilia iliyoshindiliwa na kuisambaza katika vituo vilivyopo katika maeneo ya mbali  ikiwemo Dodoma, Morogoro, Arusha na Tanga, lengo likiwa ni kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kutoka eneo moja kwenda jingine.

Kuhusu kubadilisha mfumo wa magari ya Serikali kwenda kwenye CNG, ameeleza kuwa, tayari Serikali imeanza kufanyia kazi suala hilo na moja ya vielelezo ni mabasi mapya ya mwendo kasi ambayo yote yanatumia mfumo wa CNG, jambo ambalo limefanya utoaji wa huduma kwa abiria kuboreka.

Kituo cha CNG Mlimani kina uwezo wa kujaza gesi asilia kwenye magari 1,200 kwa siku huku kikiwa na pampu maalum tatu kwa ajili ya kujaza magari maalum ya kusafirisha CNG kwenda kwenye vituo vidogo vya kujaza gesi kwenye magari (Offline CNG Filling Stations), viwandani, katika taasisi na majumbani.








Na Oscar Assenga, TANGA

MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Kassim Amar Makubel ameanza kugawa madaftari kwa wanafunzi wa shule za Msingi ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuinua sekta ya elimu hapa nchini.

Makubel aliyasema hayo wakati wa halfa ya kuzindua zoezi la kugawa Madaftari kwa wanafunzi wa Shule za Msingi Pongwe kupitia Mpango wa Daftari la Mama Samia kwa kushirikiana na Taasisi ya Watoto Foundation ambapo mpango huo utazifikia shule zote kwenye Jimbo hilo.

Mbunge huyo alisema kwamba mpango huo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali na Rais Dkt Samia Suluhu katika sekta ya elimu kutokana na mabadiliko na mageuzi makubwa yaliyofanyika.

Alisema kwamba wakati alipoingia madarakani alikaa na kubaini vijana wengi wa shule ya msingi wanapitia changamoto nyingi hivyo akaona ni bora kila kila mzazi wa mtoto wa Jimbo hilo anayesoma shule ya msingi walau aguse maisha yake kwa kutoa madaftari matano 5 ili kuwapunguzia makali kwenye baadhi ya mahitaji.


Alieleza madaftari hayo ni sehemu ya mchango wake kurejesha shukrani kwa kumchagua katika uchaguzi mkuu uliopita na wameanza rasmi uzinduzi ambapo wataanza kugawa madaftari hayo Tarafa ya Pongwe na kasha kuelekea kwenye kata nyengine.

Aidha alisema kwamba Tarafa hiyo inayojumuisha Kata za Marungu,Kirare na Pongwe na baadae wataenda kwenye Tarafa nyengine ili kuhakikisha shule zote za misngi zinafikiwa na kuwagusa.



Alisema keamba mabadiliko hayo yaliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika sekta ya elimu wakati alipoingia madarakani ni kuona elimu walionayo haikizi mahitaji ya sasa na wanatakiwa kuendana na mabadiliko kwenye mitaa ya elimu ya sasa na sasa watoto watasoma darasa la kwanza mpaka la sita.



Aidha alisema mabadiliko hayo machache ikiwemo mkondo wa amali ambao ni muhimu kwa ajili ya kuwapatia ujuzi watoto wanapomaliza shule jambo ambalo litasaidia kuongeza wataalamu mbalimbali ambao watakuwa na mchango mkubwa wa kuweza kujiajiri na kuweza kujiendeleza kwenye vyuo vya kati

“Kutokana na mabadiliko hayo makubwa ya kielimu hapa nchi na hakuna malipo hivyo tuwahimize watoto waende shule pamoja na kufuatilia maendeleo yao na tuhudhurie vikao”Alisema .



Awali akizungumza Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule ya Pongwe Mchanganyiko Abubakari Sadik alimshukuru Mbunge huyo kwa kuwapelekea msaada huo madaftari ambayo yamekuja kutatua changamoto ya watoto ambao hawana uwezo wa kununua madaftari kwa wakati .

"Ukosefu wa daftari ni kwamba wanafunzi asipokuwa na madaftari anakosa kumbukumbu ya kusoma kipindi anapofikia kwenye mtihani yake hivyo msaada huu umeenda kutatua changamoto ya kila mmoja kutokana na wazazi wa watoto wengine wako mbali na inakuwa vigumu kuwa na madaftari kila wakati”Alisema

Alisema kwamba shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika taaluma na wamekuwa na mwendelezo mzuri wa wanafunzi katika madarasa ya mitihani ya darasa la nne.

Aliongeza kwamba changamoto ambazo zinawakabili ni upungufu wa madarasa unaotokana na ongezeo la uandikishaji wanafunzi kila mwaka na wale wanaohamia kutoka maeneo mengine huku akieleza jambo linguine ni bima za afya kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

“Tunamshukuru Mhe Mbunge Wetu kwa kutupelekea wadau wenye kuwasaidia madaftar mchango huo umewapa faraja kubwa na matumaini motisha mpya kwa watoto wao kuonyesha dhamira ya kweli kujenga jamii inayojali na kuthamini kila mtoto bila ubaguzi”Alisema

Hata hiyo alitoa shukrani zake kwa Rais Dkt Samia Suluhu katika kukuza na kutoa kipaumbeme kwenye elimu jumuishi na kupitia uongozi wake fursa za elimu zinaendelelea kuimarishwa na kuwafikia hata wenye mahitaji maalumu.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Watoto Foundation Ally Yakub Pingizi alisema taasisi hiyo imezindua mpango unaoitwa Daftari la Mama Soma na Samia ikiwa ni kipaumbele kuhakikisha wanafunzi hawana sababu ya kutoroka shule ikiwa hana vitendea kazi cha shule.

Alisema kwamba wao wamekuja na mpango wa daftari la mama soma na samia ikiwa ni kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika kuboresha sekta ta elimu na amefanya maboresho makubwa kwa kujenga miundombinu ya elimu, nyumba za walimu,mabweni na vyoo.


Alisema kwamba taasisi hiyo kupitia mpango huo wameona wao waunge mkono kwa kutoa vifaa hivyo vitendea kazi na kuwatia moyo watoto wa kike waweze kusoma kwa hari na moyo ili kuepuka kujiingiza kwenye vishawishi na watoto wa kike na hivyo kusoma kwa bidii pamoja na kupunguza utoro shuleni hatua itakayochochea ufaulu.
 






Na. OWM-KAM Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano imewapiga msasa Washiriki kutoka katika Wizara pamoja na Taasisi za Serikali kuhusu Mfumo wa Kielektroniki wa Taarifa za Soko la Ajira (NLMIS) yanayofanyika leo Februari 18, 2026 katika Jengo la OSHA, Jijini Dodoma.

Serikali ya India imeshatumia Dola za Kimarekani milioni 600 sawa na fedha za kitanzania Bilioni 1.4 katika kuwekeza miradi ya maendeleo hapa nchini ikiwa ni jitihada za kuiunga mkono serikali katika kuwaletea maendelea wananchi wake.

Fedha hizo ni kutoka na serikali ya India kutenga katika bajeti yake ya mwaka 2026/27 dola Bilioni 1.1 sawa na fedha za kitanzania  shilingi Trioni 2.7 kwa ajili ya miradi yote ya maendeleo hapa nchini.

Fedha hizo Dola milioni 600 ni kwa ajili ya  miradi ya maendeleo ikiwemo Afya,elimu,maji na barabara ikiwa ni njia mojawapo ya kuunga mkono utendaji kazi wa Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha uongozi wake.

Hayo yalisemwa na Balozi wa India hapa nchini ,Bishwadip Dey katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama toka chanzo cha chemchem ya tono,Kijiji cha Losirwa kata ya Iloirienito Tarafa ya Ketumbeine Wilayani Longido Mkoani Arusha ambapo serikali ya India ilitoa shilingi milioni 125 katika mradi huo na watu zaidi ya 2000 kunufaika.

Balozi Dey alisema yeye hakwenda Longido kama mtalii bali ameenda Longido kama mwanafamilia kwa kwenda kuangalia miradi iliyoanzishwa na kumalizwa na nchi ya India kupitia wawekezaji wa nchi hiyo.

Alisema serikali ya India inaunga mkono jitihada za serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea wananchi wake maendeleo katika sekta zote na kwa kutambua hilo ndio maana serikali ya India imetenga fedha hizo ikiwa ni njia mojawapo ya  kumuunga mkono kazi ya Rais kwa kupeleka fedha katika miradi  sehemu mbalimbali kote nchini.

‘’Serikali ya India imepitisha bajeti kwa ajili ya miradi ya maendeleo kote nchini na tayari dola milioni 600 zimeshatumika katika miradi hiyo ikiwemo miradi iliyopo Longido hiyo ni kumsaidia Rais kwa kazi nzuri anayoifanya kwa wananchi wake’’ alisema Balozi Dey

Aidha ameishukuru kampuni ya Dar Solution inayomilikiwa na mwekezaji kutoka nchini India kwa kuchangia vifaa vya Tehama vyenye thamani ya shilingi milioni 15 na kuwezesha ukamilishaji wa majengo ya shule shikizi katika kata ya Engikaret,Noondoto na Ketumbeine vyneye thamani ya shilingi milioni 30 na kusema kuwa hayo yote ni matunda ya serikali yao katika kuwahimiza wawekezaji kushirikiana na serikali ya Tanzania.

Balozi alisema na kuwaeleza wananchi wa kata ya Iloirienito juu ya mahitajitaji ya shule ya katika Kata hiyo na kusema kuwa watakwenda kuyafanyia kazi  ili kata hiyo iwe na shule ya karibu kuondoa usumbufu kwa watoto kwenda umbali mrefu kusaka elimu huku wakikutwa na vikwazo vingi.

Naye Naibu Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Longido ,Dkt Steven Kiruswa alisema mradi wa maji uliozinduliwa na Balozi Dey umewezeshwa kwa nguvu za wananchi wakishirikiana na yeye pamoja na wahisani toka kampuni ya kihindi ya Dar Solution ambayo ndio iliyonunuwa mabomba yote na matanki yaliyotumika kukusanya na kusambaza maji ya chemchem ya tono katika vitongoji vya Kisambi na Olomuki.

Kiruswa alisema na kuishukuru serikali ya India kwa ushirikiano mkubwa wanaoutoa kwa serikali na wananchi wa Longido na kusema kuwa wao kama serikali ya Tanzania na wananchi wa Longido watashirikiana kwa hali na mali katika kufanikisha miradi ya manedeleo katika Jimbo hilo iliyoanzishwa na nchi hiyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Longido,Salumu Kally pamoja na kumshukuru Balozi Dey pia aliwaomba wananchi wa Longido kutunza miradi hiyo ili iwajengee heshima kwa wahisani wawqeze kuendelea kusaidia miradi mingine wilayani huo.