Nilikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho chuoni na nilikuwa nimebakiza wiki moja tu kufanya mitihani yangu ya mwisho.

Nilikuwa nimehangaika kwa miaka mitatu, nikifanya kazi ndogo ndogo ili kujilipia ada na mahitaji mengine. Ndoto yangu ilikuwa moja tu kuhitimu na kuibadilisha maisha ya familia yangu.

Siku moja nilipokuwa nikitoka darasani, niliitwa katika ofisi ya utawala. Nilidhani ni jambo la kawaida, lakini nilipoingia, nilikabidhiwa barua iliyosema kuwa nilikuwa nimefukuzwa chuo kutokana na deni la ada na madai ya ukiukaji wa kanuni za chuo.

Nilishangaa sana. Kwanza, nilikuwa nimebakiza kiasi kidogo sana cha ada ambacho nilikuwa nimeahidi kulipa baada ya mitihani. Pili, sikuwahi kuvunja sheria za chuo. Nilijaribu kujitetea lakini hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza.

Nilitoka ofisini nikiwa nimevunjika moyo. Nililia sana usiku huo. Niliona ndoto zangu zote zikifutika mbele ya macho yangu. Nilijiuliza ningewaambia nini wazazi wangu ambao walikuwa wamejitolea kila kitu ili nisome.

Rafiki yangu mmoja aliponiona katika hali hiyo, aliniambia nisikate tamaa. SOMA ZAIDI.
Share To:

Post A Comment: