Maisha yetu yalikuwa ya kawaida lakini yenye amani. Mimi na mume wangu tulikuwa tunajitahidi pamoja kujenga familia yetu. Haikuwa maisha ya utajiri mkubwa, lakini tulikuwa tunatosheka na kile tulichokuwa nacho.

Kisha ghafla kila kitu kilibadilika. Siku moja mume wangu alirudi nyumbani akiwa kimya sana. Nilijua kuna kitu hakikuwa sawa.

Baadaye alinieleza kuwa alikuwa amepoteza kazi. Kwa kweli ilikuwa habari nzito kwetu.
Mwanzoni tulijaribu kujipa moyo kuwa ni kipindi tu kingepita haraka. Nilimfariji na kumwambia tutapambana pamoja. Lakini kadri wiki zilivyopita bila kazi mpya, mambo yakaanza kuwa magumu. Pesa zilianza kuwa shida.

Bills zilianza kujikusanya, kodi ikaanza kutusumbua, na mahitaji ya watoto yalikuwa yanaendelea kuongezeka. Polepole msongo wa mawazo ukaanza kuingia ndani ya nyumba yetu.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona mume wangu akibadilika. Mtu ambaye zamani alikuwa mchangamfu alianza kuwa mkimya sana.

Mara nyingine alikuwa anakasirika kwa mambo madogo. Alianza kujitenga, na wakati mwingine alikuwa anakaa peke yake kwa muda mrefu bila kuzungumza na mtu. Nyumbani kulianza kupoteza furaha. Tulianza kugombana mara kwa mara kwa sababu ya pressure ya maisha.

Wakati mwingine nilijikuta nikilia kimya usiku nikihofia familia yetu ingeanza kuvunjika kwa sababu ya hali ile. Ilifika hatua nikaanza kukata tamaa. SOMA ZAIDI.
Share To:

Post A Comment: